fataawa za ad-dur an-nadhwiyd fiy ikhlaasw kalimaat at-tawhiyd - ´allaamah al-fawzaan

158
1 Mkusanyiko Wa Fataawa ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd Imaam Muhammad bin ´Aliy ash-Shawkaaniy (Rahimahu Allaah) ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah) Imefasiriwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

Upload: wanachuoni

Post on 30-Oct-2014

356 views

Category:

Documents


2 download

DESCRIPTION

Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd - ´Allaamah al-Fawzaan

TRANSCRIPT

Page 1: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

1

Mkusanyiko Wa Fataawa

ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy

Ikhlaasw Kalimaat

at-Tawhiyd

Imaam Muhammad bin ´Aliy

ash-Shawkaaniy (Rahimahu Allaah)

´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

(Hafidhwahu Allaah)

Imefasiriwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

2

Dibaji

Bismillaah, Alhamdulillaah. Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu

Muhammad na ahli zake na Maswahabah zake (Radhiya Allaahu ´anhum)

mpaka siku ya mwisho. Amma ba´ad:

Himidi zote ni Zake Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Aliyeniwezesha kufanya

kazi hii. Hizi ni Fataawa zilizokusanywa baada ya Duruus zote zilizotolewa

na Shaykh Fawzaan (Hafidhwahu Allaah) akisherehesha kitabu cha Imaam

ash-Shawkaaniy (Rahimahu Allaah) cha Tawhiyd kiitwacho “ad-Dur an-

Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd.”

Fataawa nyingi ni kuhusiana na masuala ya Tawhiyd na ´Aqiydah kwani

kitabu chenyewe ni cha Tawhiyd. Kuna baadhi ya Fataawa ni masuala ya Fiqh

na mengine ila si nyingi.

Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) kijitabu hichi kilichokusanya

Fataawa muhimu ziweze kutunufaisha sisi na nyinyi na kuleta faida kubwa

katika Ummah wetu wa Kiislamu. Tunamuomba Allaah Atuwafikishe sote

kwa Ayapendayo na Kuyaridhia.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra.

Swalla Allaahu ´alaa Muhammad, wa ´alaa aalihi wa Aswhaabihi wa sallam

Page 3: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

3

Fataawa zilizomo ni hizi zifuatazo:

01) Mwenye Maradhi Ya Kutokwa Na Ugonjwa Kuongoza Kuwa Imaam

02) Witr kabla Ya Swalah Ya Alfajiri Kwa Nusu Saa

03) Kuswalia Jeneza Mbili Bila Ya Kujua

04) Masikini Anafanya Shirki Kwa Ajili Ya Maisha Bila Ya Kuitakidi

Anachofanya

05) Kuna Tawassul Inayojuzu Kwa Mtume (´alayhis-Salaam) Baada Ya

Kufa?

06) Hukumu Ya Kutoka Msikitini Wakati Muadhini Anaadhini

07) Hekima Ya Kuwalingania Makafiri Kazini Kwake

08) Vipi Mtu Atawalingania Waabudu Makaburi?

09) Hekima Wakati Wa Kuwalingania Waabudu Makaburi

10) Kumpa Mtu Pesa Akuombee Du´aa

11) Hukumu Ya Kuwatolea Salaam Mashia Ismaa´iliyyah

12) Hukumu Ya Kunyama Makosa Ya Madu´aat Wanaokhalifu Sunnah

13) Makatazo Ya Kuwanasibishia Wanachuoni Na Mambo Yasiokuwa

Na Ushahidi

14) Lini Unaanza Huhesabu Muda Wa Kupangusa Juu Ya Soki?

15) Madu´aat Wa Ushirikina Katika Chaneli

16) Wanaodai Ni Wafasiri Wa Ndogo Katika Vyombo Vya Habari

17) Je, Maji Ya Zamzam Yakitoka Nje Ya Makkah Baraka Yake Bado

Yabaki?

18) Kurukuu Kabla Ya Kufika Katika Safu Kwa Ajili Ya Kudiriki Rakaa

19) ´Amali Za Kuweza Kumfanyia Maiti Zikamnufaisha

20) Je, Kila Maradhi Yasioweza Kutibiwa Na Madaktari Inakuwa Na

Uchawi, Kijicho Au Hasadi?

21) Kujuta Tu Baada Ya Kosa Yatosha Kuwa Ni Tawbah?

22) Je, ´Iysa (´alayhis-Salaam) Alipewa Utume Alipofikisha Miaka

Arubaini?

23) Kafiri Wanatana Kumsimamishia Hadd Akamtaka Shahaadah, Je

Atasaliwa?

24) Mzee Kakatwa Mguu Na Ana Maradhi Ya Kutokwa Na Akili, Mwaka

Mzima Haswali

Page 4: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

4

25) Nifanye Hijrah Kuhama Kutoka Europe Na Wakati Nadhihirisha

Dini?

26) Hafidh Wa Qur-aan Ambaye Si Mwarabu Anatumbukia Katika

Shirki, Je, Ana Udhuru?

27) Watu Watapewa Udhuru Katika Shirki Mpaka Lini?

28) Huyo Si Mke Hakufai, Tafuta Mwengine!

29) Mke Mkaidi Anafanya Ya Haramu Na Kusema Nisimwingilie Katika

Uhuru Wake

30) Kijana Ameoa Mnaswara, Mke Anataka Waende Nae Kanisani

31) Je Inajuzu Kuweka Mlio Wa Simu Sauti Ya Adhaana au Aayah

Tukufu?

32) Muislamu Katumbukia Katika Shirki Kubwa, Je Atoe Shahaadah

Upya?

33) Kuswali Kwenye Msikiti Uitwao Masjid Sayyid al-Badawiy Usio Na

Kaburi

34) Je, Kijusi Kikitoka Tumboni Hufanyiwa ´Aqiyqah?

35) Hukumu Ya Mtu Anaedai Kuwa Ni Muislamu Ila Haswali

36) Muislamu Ambaye Anafanya ´Ibaadah Zake Zote Kwa Kukhalifu

Sunnah

37) Hukumu Ya Muislamu Asietoka Zakaah

38) Hukumu Ya Mwanaume Mwenye Kulipa Swawm Ya Dhwihaar

Akamjamii Mke Wake Kabla Hajamaliza Swawm Yake

39) Mwanafunzi Anaehofia Mas-ala Ya Qadhwaa Na Qadar

40) Mwanamke Mjamzito Kafa Na Mtoto Tumboni, Mtoto Atolewe Na

Kuzikwa Mwenyewe?

41) Mwanamke Kafa Baba Yake Mdogo Kafiri

42) Mwanamke Mgonjwa Kafa Naye Hakufunga Ramadhaan

43) Hukumu Ya Kuzuia Mimba Moja Kwa Moja

44) Mwanamke Kwenda Sokoni Bila Mahram

45) Mwanamke Ambaye Yuko Katika Familia Yake Kutoka Bila Ya

Ruhusa Ya Mumewe

46) Inajuzu Kuwatolea Wanawake Salaam?

47) Mwenye Kuanguka Katika Bid´ah Moja Tu Ya Kiitikadi Anakuwa

Mubtadi´ah?

48) Daa´iy Anaetoa Fatwa Kujuzisha Ndoa Ya Mut´ah Kwa Vijana

49) Miongoni Mwa Masharti Ya Laa Ilaaha Illa Allaah

50) Je, Fuqahaa´ Murji-ah Ni Mubtadi´ah?

Page 5: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

5

51) Radd Kwa Mwenye Kusema Mzazi Kumchunguza Mtoto Wake Ni

Ujasusi

52) Waalimu Wasiofunza Tawhiyd Katika Madrasa

53) Nasaha Kwa Wanafunzi Wanaopondana Wao Kwa Wao

54) Wake Zangu Wawili Wameingia Katika Uislamu, Je Ni Wajibu Kwao

Kurudi Upya Ndoa Zao?

55) Ufafanuzi Kuhusu Kufuru Ya ´Amali (Ya Kimatendo)

56) Wajibu Wa Kumkata Ndugu Ambaye Anachukia Sunnah Na Watu

Wa Sunnah

57) Kufanya Jamaa´ah Nyingine Wakati Jamaa´ah Ya Kwanza Inapokuwa

Katika Tashahhud Ya Mwisho

58) Wafanyao Barnamiji Za Video Kwenye TV

59) Je Kutahadharisha Watu Dhidi Ya Maulamaa Wa Ahl-ul-Bid´ah Ni

Katika Kusengenya Na Kueneza Uvumi?

60) Radd Kwa Mwenye Kusema Kaburi La Mtume Liko Ndani Ya

Msikiti

61) Wanayomba Makaburi Kwa Hoja Eti ´Umar Alimuomba Abbaas

(Radhiyallaahu ´anhum)

62) Ribaa Ni Dhambi Ya Pili Baada Ya Dhambi Ya Ushirikina

63) Mwenye Kula Ribaa Pamoja Na Kujua Kuwa Ni Haramu

64) Risaalah Ya Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab Kwa Watu Wa

Europe

65) Jinsi Ya Kumtibu Aliemsibu Ndugu Yake Kwa Kijicho

66) Tawassul Na Sharti Zake

67) Sijdah at-Tilaawah Ndani Ya Gari

68) Sisi Tunawaua Washirikina Tu Na Hatuwaui Waislamu

69) Sunnah Ya Kuangalia Kidole Cha Shahaadah Wakati Wa Tashahhud

70) Sifa Ya Swalah Ya Istisqaa Ni Kama Swalah Ya `iyd

71) Aina Mbali Mbali Za Tawassul Na Hukumu Zake

72) Nyote Ni Wakoseaji Na Mbora Ni Yule Mwenye Kutubia

73) Tawhiyd-il-Ilaahiyyah Na Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah

74) Tawhiyd-ul-Khaaliqiyyah, Tawhiyd-ul-Raaziqiyyah Na Tawhiyd-ul-

Haakimiyyah

75) Tofauti Baina Ya Sanamu Na Wathan

76) Tofauti Ya Ujinga Na Upotevu

77) Usikae Na Mvuta Sigara!

78) ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Madu´aat Wanaohudhuria Katika

Maulidi

Page 6: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

6

79) Kuomba Kwa Nuru Ya Uso Wa Allaah Mambo Ya Kidunia Na

Aakhirah

80) Kuswalishwa Na Imaam Wa Kisufi Ambaye Msimamo Wake

Haujabainika

81) Shubuha Za Waabudu Makaburi

82) Waabudu Makaburi Lazima Wasimamishiwe Hoja!

83) Kila Aliye Fikiwa Na Qur-aan Hoja Imemsimamia

84) Qur-aan Yatosheleza Kuwa Hoja Kwa Kila Mtu!

85) Kufasiri Kwa Ajili Ya Taazia (Kutoa Ole Kwa Wafiwa)

86) Wanafunzi Wanaotoka Katika Miji Ya Kikafiri Na Kwenda Kusoma

Saudi Arabia Kisha Wanabaki Huko

87) Utata Wa Waabudu Makaburi

88) Wanaolilia Umoja Wa Uislamu Bila Kujali ´Aqiydah

89) Ni Kweli Kwamba Kuna Wenye Kuomba Kwenye Kaburi La Mtume?

90) Hukumu Ya Kuapa “Wallaahi Kwa Nyumba Aliyojenga Allaah”

91) Vipi Ntamlingania Baba Yangu Aingie Katika Uislamu?

92) Vipi Muislamu Kafiri Asieswali Atatubia?

93) Vipi Kumsimamishia Mtu Hoja?

94) Vipi Mtu Atamjua Mwanachuoni?

95) Jinsi Ya Kutangamana Na Makafiri Kazini

96) Wanafunzi Kupiga Radd Makundi Potevu Katika Miji Yao

97) ´Uzayr Ni Nani?

98) Aina Mbali Mbali Za Tawassul Na Hukumu Zake

99) Mzee ambaye Muusa Alikutana Naye Madyaan Ni Mtume Shu´ayb

(´alayhis-Salaam)?

100) Kuswali Nyuma Ya Mshirikina Kwa Kusoma Msikiti Wa Sunnah

101) Asiyeweza Kulipa Kafara Ya Yamini Kwa Kulisha Anafunga

102) Shaykh Muhammad ibn ´Abdil-Wahhaab Si Bora Kuliko

Wanavyuoni Wa Madhehebu Manne

103) Kupita Mbele Ya Mwenye Kuswali Kwa Nguvu

104) ´allaamah al-Fawzaan Kuhusu Answaar-us-Sunnah

105) Kuacha ´Amali Kwa Kukhofia Riyaa

106) Kumwita Mtu Bwana

107) Kumuambia Kafiri Ni Rafiki

108) Hukumu Unaposhtushwa Na Kitu Kuita “Ewe Mtume”

109) Hukumu Ya Kusema Mimi Ni Kwa Allaah Na Kwako

110) Anaepinga Hadiyth Ya Shafaa´ah Anakuwa Kafiri?

111) Hukumu Ya Kuapa Kwa Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

Page 7: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

7

112) Anataka Kumpa Alieingia Katika Uislamu Tafsiri Ya Qur-aan

113) Kumuomba Kafiri Msaada Kwa Ayawezayo

114) Kuomba Msaada Kwa Majini

115) Je, Kufuru Ya Kimatendo Yaweza Kuwa Kubwa?

116) Haijuzu Kuomba Maiti Kwa Kuwa Hana Anachokiweza

117) Sote Tuwaite Washirikina Kuwa Ni Washirikina

118) Je, Ni Kweli Kuwa Wengi Wa Washirikina Wa Leo Wanafanya Shirki

Kwa Kutokujua?

119) Nina Miaka 17 Wazazi Wangu Hawaswali Alfajiri, Unaninasihi Vipi?

120) Kulipa Swalah Za Rawaatib Kinyume Na Wakati Wake

121) Baada Ya Siku Tatu Ndo Kajua Kuwa Aliswahi Kinyume Na Qiblah,

Alipe?

122) Kuomba Viumbe Waliyo Hai Wakuombee Du´aa Ni Makosa Na

Udhaifu?

123) Hukumu Ya Kuambizana “Ijumaa Yenye Baraka” Siku Ya Ijumaa

124) Hukumu Ya Kutawassul Kwa Jaha Ya Mtume (´alayhhis-Salaam)

125) Hukumu Ya Kuwaombea Du´aa Watu Wa Bid´ah

126) Je, Kutamka Shahaadah Tu Bila ´Amali Inatosha?

127) Hukumu Ya Anaesema Laa Ilaaha Illa Allaah Ila Hakufuru

Vinavyoabudiwa Kinyume Na Allaah

128) Wana Ada Wakiona Maiti Usingizi Wanamchinjia Na Kualika Watu

Walimani

129) Kumuomba Allaah Kwa Kusem “Ewe Wa Allaah”

130) Hukumu Ya Mtoto Kushtushwa Na Kusema “Ewe Mama”

131) Watu Wataotoka Motoni Bila Ya Kufanya Kheri Yoyote

132) Hukumu Ya Wazazi Wasiofahamu Kiarabu Wanaita “Ewe Mtume Wa

Allaah!”

133) Mume Anamlingania Mke Wake Katika ´Aqiydah Ya Ash´ariyyah,

Mke Amtii?

134) Hukumu Mwanamke Kusoma Qur-aan Kwa Mashaykh Wanaume

135) Acheni Falsafa, Mwenye Kufanya Shirki Ni Mshirikina!

136) Hukumu Ya Kuweka Nadhiri Kwa Asiyekuwa Allaah

137) Hukumu Ya Kuitamidi Kwa Allaah Kisha Kwa Kiumbe

138) Hukumu Ya Kutosoma Kwa Tajwiyd

139) Kumuomba Mtu Ni Vibaya?

140) Nilikuwa Na Deni La Mtu Simjui Ama Sasa Nimejua, Nimpe Au

Nitoe Swadaqah?

141) Tahadhari Na Kundi La Qur-aaniyyah Linalopinga Sunnah!

Page 8: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

8

142) Makataza Ya Wanafunzi Kuwapa Zawadi Waalimu Zao

143) Imaam ash-Shawkaaniy Ni Imaam Wa Ahl-us-Sunnah

144) Ni nani ´Abdul-Qadir al-Jaylaaniy?

145) Waabudu Makaburi Wanaotumia Hoja Aayah Katika Suurat-ul-Kahf

146) Inajuzu Kusema Allaah Na Mtume Wake Ndio Wanajua?

147) Aliechelewa Swalah Ya Istisqaa Upi Wajibu Wake?

148) Nasaha Kwa Anaekhofia Riyaa

149) Imaam Kukariri Aayah Fulani Anaposalisha Jamaa´ah

150) Anamtangulia Kumsalia Maiti Kabla Ya Imaam Kusalisha

151) Kuelekea Kaburi La Mtume (´alayhis-Salaam) Msikitini Na

Kumuomba

152) Mgonjwa Anaepata Tabu Kutia Wudhuu Afanye Nini?

153) Msafiri Anaejua Lini Atarudi Kwao Hachukui Hukumu Za Msafiri

154) Anaemwendea Mpiga Ramli Kisha Akatubia Swalah Zake

Zitakubaliwa?

155) Lini Mtu Anaweza Kuingia Peponi Bila Ya ´Amali?

156) Je, Athari Ya Mtume (´alayhis-Salaam) Inapatikana Mpaka Hivi Leo?

157) Ni Sahihi Muadhini Kusema Haqqan Laa ilaaha illa Allaah?

158) Mgonjwa Anaruhusiwa Kujumuisha Swalah Na Haruhusiwi

Kuzifupisha

159) ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Tijaaniyyun Na Burda

160) Qaswiydah Ya Burda Ina Shirki Na Ghuluu

161) Kulingania Katika Tawhiyd Inatosha Kukataza Tu Kuabudu

Makaburi?

162) Tofauti Baina Ya Du´aa Ya Masuala Na Du´aa Ya ´Ibaadah

163) Eda Ya Mwanamke Aliyezaa Baada Ya Kufa Mumewe Kwa Saa Au

Dakika Kadhaa

164) Wanafunzi Wanadai Kwamba Kusoma “Suurat-ul-Ikhlaas Baada Ya

Kila Swalah Ni Bid´ah

165) Ghurabaa Ni Watu Gani?

166) Hukumu Ya Mafukara Wanaotumbukia Katika Shirki Kwa Ajili Ya

Kutafuta Riziki

167) Anadai Watu Hawana Haja Ya Kusoma Elimu Imejaa Kwenye

Internet Na Kwenye Mikanda

168) Hukumu Ya Kusema Washirikina Ni Ndugu Zetu

169) Anataka Kuacha Kupiga Punyeto Anashindwa, Ipi Nasaha Yako?

170) Haijuzu Kuomba Shafaa´ah (Uombezi) Kwa Maiti Sawa Mtume Au

Mwengine Yeyote

Page 9: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

9

171) Kuvaa Nguo Za Makafiri Za Kumalizia Masomo

172) Hukumu Ya Anaeacha Kufunga Ramadhaan Ila Hapingi Uwajibu

Wake

173) Anaetetea Ushirikina Sawa Hakimu Au Yeyote Yule Ni Mshirikina

174) Mwanaume Si Sawa Na Mwanaume

175) Daa´iy Mpotofu Anaewaponda Maswahaba (radhiya Allaahu

´anhum)

176) Anaejuzisha Kujengea Misikiti Makaburi Ni Mshirikina

177) Imaam Kujumuisha Maghrib Na ´Ishaa Wakati Wa Mvua Na Baridi

Kali

178) Ahl-ul-Kitaab Wa Zama Hizi Inajuzu Kuwaoa

179) Wazazi Haijuzu Kuwapeleka Watoto Katika Madrasah Ya Ahl-ul-

Bid´ah Kama Masufi

180) Itikafi Potofu Ya Kuogopa Kijicho Kwa Kutupa Kipande Cha

Chakula Chini

181) Allaah (Ta´ala) Ana Sifa Ya Nafsi

182) Allaah Yuko Kwenye Jiha Ya Juu

183) Je Al-Muhaasib Ni Jina La Allaah (Ta´aal)?

184) Khatari Ya Kumkufurisha Mtu Binafsi?

185) Maulamaa Waliopinda Wasiojua Tawhiyd

186) Maiti Hata Wakisikia Hawawezi Kukunufaisha Kwa Kitu

187) Picha Ni Haramu Sawa Za Digital Au Za Aina Yoyote

188) Usingizi Hauwajibishi Kustanji, Kinachowajibisha Ni Kutokwa Na

Kitu Tupuni

189) Kila Kivazi Cha Mwanaume Chenye Kuvuka Kongo Mbili Za Miguu

Ni Motoni

190) Tawassul Ni ´Ibaadah?

191) Kulisha Watu Watano Mara Mbili Ili Ihesabike Kalipa Kafara Ya

Yamini Kwa Watu Kumi

192) Aliyeuawa Na Usaamah Bin Zayd Ni Katika Maswahaba?

193) Kaweka Nadhiri Kuamka Kuswali Fajr La Sivyo Ataswali Rakaa

Kumi

194) Kufunga Safari Kwenda Kwenye Kaburi Ya Mtume Au Mwengine

Yoyote

195) Kila Jina La Allaah Linajenga Sifa Kinyume Na Matendo

196) Hukumu Ya Swalah Ambayo Wudhuu Haukushika Kidogo Cha

Mguuni

Page 10: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

10

197) Aliopigana Nao Abu Bakr (radhiya Allaahu ´anhu) Ilikuwa Ni Kwa

Ajili Ya Kufuru Yao

198) Kazi Ya Kuamrisha Mema Na Kukataza Mabaya Ni Ya Nani?

199) Mtazamo Wa Kwanza Kuiangalia Ka´abah Mtu Hukubaliwa Du´aa?

200) Hukumu Ya Kuapa Kwa Ahadi Ya Allaah

201) Kuchinja Kwa Ajili Ya Allaah Kwenye Kaburi La Walii Fulani

202) Kuchukua Mkopo Benki Kwa Ajili Ya Kuoa

203) Kufanya Mzaha (Maskhara) Na Hadiyth Za Mtume

204) Ruqyah Kwenye Maji Ya Zamzam Na Mti Wa Mzaituni

205) Tofauti Ya Kufuru Na Shirki

206) Kufanya Mjadala Na Ahl-ul-Bid´ah

207) Kuacha Nyumba Inasoma Qur-aan Na Hakuna Wakuisikiliza

208) Waitao “Ewe Yuma” Wanaposhtuliwa Na Kitu

209) Haijuzu Kuwanunulia Wanawake Simu Za Khatari Za Kisasa

210) Ni Haramu Kumpa Mwanamke Mwanamke Ajinabi

211) Kumpigia Simu Aliehai Na Kumuomba Akuombea Du´aa

212) Kuomba Rahma Na Kinga Ndani Ya Swalah

213) Kauli Sahihi Kuhusiana Na Thawabu Kumfikia Maiti

214) Haijuzu Kuomba Kwa Uso Wa Allaah Mambo Ya Kidunia

215) Kumwambia Mtu Unaefanya Kazi Kwake “Bwana Wangu”

216) Kuosha Mikono Mtu Anapoamka Kutoka Usingizini

217) Kutokataza Shirki Kwa Kukithiri Kwa Jambo Lile Kwa Watu

218) Nikiona mtu mwenye kumshirikisha Allaah na nisimbainishie

219) Kumsalia Mtume (´alayhis-Salaam) Ni Katika Sababu Za

Kukubaliwa Du´aa

220) Kutawassul Kwa Allaah Kwa Kukusanyika Msikitini Na Kufanya

Dhikr

221) Kutenga Siku Maalumu Kwa Ajili Ya Taazia

222) Tofauti Ya Kusimama Kwa Kumuadhimisha Mtu Na Kumpokea

Mgeni

223) Haijuzu Kuleta Adhkaar Maalumu Baada Ya Swalah Ambazo

Hazikuthibiti

224) Hakuna Haja Ya Kuchukua Elimu Kwa Mtu Mwenye Baadhi Ya

Bid´ah

225) Kuswali Nyuma Ya Imaam Anaevaa Herizi

226) Kunyunyizia Maji Ya Kisomo Kwenye Kuta Za Nyumbani Kuzuia

Madhara

227) Kuswali Na Nguo Yenye Damu

Page 11: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

11

��م ا�ر�ن ا�ر��م

01) Mwenye Maradhi Ya Kutokwa Na Ugonjwa Kuongoza Kuwa Imaam

Swali:

Ipi hukumu ya kwenye tatizo la kutokwa na mkojo wakati anapowaongoza

watu katika swalah - yaani anakuwa imaam, je inajuzu kwake kuwa imaam

ikiwa hawakupata mwengine awazae kuwasalisha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwenye tatizo la kutokwa na mkojo haijuzu kumuongoza mtu ila yule

nwenye tatizo kama yeye. Ama mtu salama [asiye na ugonjwa huu] haijuzu

kuswali nyuma yake. Kwa kuwa mtu kama huyu hata akitokwa na mkojo

[anaendelea] kuswali na swalah yake ni sahihi. Lakini haisihi swalah ya mtu

salama nyuma yake. Anaweza tu kumuongoza mwenye tatizo kama yeye,

mwenye hadathi daima [kama yeye].

02) Witr kabla Ya Swalah Ya Alfajiri Kwa Nusu Saa

Swali:

Mimi naswali witr kabla ya swalah ya alfajiri kwa nusu saa. Je kitendo changu

hichi ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 12: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

12

Umesali usiku hakuna ubaya. Witr inasaliwa usiku mzima ni sawa. Sawa ni

mwanzo wa usiku au mwisho wake.

03) Kuswalia Jeneza Mbili Bila Ya Kujua

Swali:

Tukiswalia jeneza msikitini, na wakati wakufika makaburini kukaletwa

jeneza. Sijui kama ni katika jeneza tuliyoiswalia [msikitini] au hapana.

´Allaamah al-Fawzaan:

Mswalie. Hata swalah ikikariri kwa maiti ni kheri kwake. Kwa kuwa du´aa ni

jambo jema kwake yeye na wewe pia. Mswalie!

04) Masikini Anafanya Shirki Kwa Ajili Ya Maisha Bila Ya Kuitakidi

Anachofanya

Swali:

Mwenye kulingania watu katika kuabudu makaburi ya watu wema kwa ajili

ya kupata riziki, naye anajua kuwa hii ni shirki na wala haamini kuwa

waliomo ndani ya kaburi wananufaisha au kudhuru...

Page 13: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

13

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu kakhasirika duniani na akhera - Allaah Atukinge. Riziki iko mikononi

mwa Allaah na si kwenye makaburi. Ikiwa ni mkweli katika kazi yake aombe

riziki kutoka kwa Allaah. Na si kwenye makaburi.

05) Kuna Tawassul Inayojuzu Kwa Mtume (´alayhis-Salaam) Baada Ya

Kufa?

Swali:

Je kuna masharti ya kujuzisha kutawassul kwa Mtume (swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) baada ya kufa kwake katika du´aa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Tawassul kwa kumfuata na kumpenda (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Kwa kuwa haya ni matendo mema. Kumfuata na kumpenda haya ni matendo

mema. Tawassul kwavyo. Ama kutawassul kwa dhati ya Mtume, haijuzu

kutawassul kwake. Wala kutawassul kwa jaha yake.

06) Hukumu Ya Kutoka Msikitini Wakati Muadhini Anaadhini

Swali:

Page 14: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

14

Ipi hukumu ya mwenye kutoka msikitini na muadhini anaadhini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa ni kwa dharurah na atarejea, hakuna ubaya. Kama kutawadha, kuongea

na mtu halafu atarejea, hakuna ubaya. Ama ikiwa hatorejea, hili ndo sehemu

ya kutazamwa. Anasema mmoja katika Maswahaba ´Umar bin Yaasir.

"Anaetoka msikitini baada ya adhaana, kamuasi Abal Qaasim [Mtume]

(swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)."

Alitoka mtu baada ya adhaana, akasema ama huyu kamuasi Abal Qaasim

(swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kutoka bila ya udhuru haijuzu. Ama kwa

udhuru hakuna neno.

07) Hekima Ya Kuwalingania Makafiri Kazini Kwake

Swali:

Ipi njia nzuri tunayotakiwa kuifuata katika kuwalingania makafiri ambao

wako pamoja nami kazini? Je naweza pia kula pamoja naona kuwapa

swadaqah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, hakuna neno. Waweza kula nao na wao wakala nawe katika [chakula]

mubaha. Kuwapa swadaqah ya zakaah haijuzu. Ama [swadaqah] ya kujitolea

Page 15: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

15

[ya kawaida] hakuna ubaya kwa hilo. Khasa ikiwa kwa hili walenga

kuwaingiza katika Uislamu.

08) Vipi Mtu Atawalingania Waabudu Makaburi?

Swali:

Je waabudu makaburi tuwawie wagumu na wanadiwe kabisa kwa kuambiwa

ewe fulani na fulani? Au tuwanasihi kwa uzuri [upole] na tuwalinganie kwa

uzuri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwenye kukubali nasaha, tunamnasihi kwa uzuri upole. Ama kwa yule

asiyekubali nasaha, huyu mtu awe mgumu kwake.

��ھد ا�����ر وا�������ن وا��ظ ���م ��� �� ا��� � �� أ�

“Ewe Nabii! Pambana na makafiri na wanaafiki, na kuwa mgumu kwao!”

(66:09)

Kuwa mgumu! Ikiwa hawakubali, hakuna njia ingine ila kuwa mgumu kwao.

Upole ni kwa yule mwenye kukubali [nasaha].

09) Hekima Wakati Wa Kuwalingania Waabudu Makaburi

Page 16: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

16

Swali:

Katika mji wangu kuna waabudu makaburi. Je ni lazima kwangu kuwawekea

wazi kuwa ni makafiri? Au badala ya hili niwalinganie?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, wabainishie kwa hekima na uzuri. Huenda wakakubali. Usiwaambie

nyinyi ni makafiri nyinyi ni washirikina. Watakukimbia na... Lakini waambie

Qur-aan Allaah Kasema kadha na Mtume Wake kasema kadha.Wabainishie

kwa uzuri na hekima.

10) Kumpa Mtu Pesa Akuombee Du´aa

Swali:

Mwenye kuwapa watoto wadogo pesa ili wamuombee du´aa. Je kitendo hichi

kinajuzu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, mtu hapewi ujira kwa ajili ya kumuombea mwengine. Akiomba kwa

ajili ya [kupewa] ujira haitokubaliwa du´aa yake. Kwa kuwa du´aa ni

´ibaadah, haichukuliwi ujira.

Page 17: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

17

11) Hukumu Ya Kuwatolea Salaam Mashia Ismaa´iliyyah

Swali:

Mimi nina ndugu katika Ismaa´iliyyah [kundi katika Mashia] na nafanya

juhudi kuwalingania waingie katika Uislamu. Je niwatolee salaam wakati

naenda kuwazuru kwenye manyumba yao kwa kusema "as-salaam

´alaykum"? Na ikiwa kufanya hivyo haijuzu, je ntakuwa mwenye kupata

madhambi nikiwatolea salaam hivi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hii salaam ni ya Kiislamu. Haitolewi kwa watu kama hawa. Lakini waweza

kuwaambia "as-Salaam ´alaa mani taba´al hudaa." Hili ndio alilolifanya

Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

12) Hukumu Ya Kunyama Makosa Ya Madu´aat Wanaokhalifu Sunnah

Swali:

Je wale wanyamazao na wala hawabainishi baadhi ya makosa ya wafuasi

wanaofuata mifumo, ambao wanafuata mifumo kinyume na mfumo wa

Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Je mwenye kunyamazia hilo

anaingia katika wale wenye kuficha aliyoteremsha Allaah [waliolaaniwa]?

Page 18: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

18

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Lazima abainishe kwa kila mkosaji. Sawa makosa yake ikiwa ni ya

shirki au kinyume na shirki au maasi au... Lazima abainishie watu. Wenye

kukaa kimya naye ana uwezo wa kubainisha, atakuwa ni mwenye kuficha

elimu. Au mtu mwenye makosa katika manhaj.

13) Makatazo Ya Kuwanasibishia Wanachuoni Na Mambo Yasiokuwa Na

Ushahidi

Swali:

Ni jambo lenye kujulikana kuwa Shaykh ibn Baaz alijibu kuwa wanachuoni

ambao wanawapata waabudu makaburi udhuru kwa ajili ya ujinga

wanafanya taawili na ni wajibu kuwawekea wazi. Lakini ikiwa wanachuoni

hawa watawapa udhuru watu hawa baada ya kuwawekea wazi hoja....

´Allaamah al-Fawzaan:

Ewe ndugu tuletee maneno hayo ya Shaykh ibn Baaz. Leta dalili tuisome hapa

halafu ndo tutaangalia maneno yako haya. Wanachuoni wana nafasi zao,

msiwanasibishie kitu ila kwa [kuleta] vyanzo kutoka katika maneno yao. Ili

uthibitishe ukisemacho. Ama kujisemea tu fulani kasema hivi kuhusu Shaykh,

au alisema fulani - ananukuu kutoka kwa Shaykh kuwa kasema kadha, hili

halijuzu.

Page 19: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

19

14) Lini Unaanza Huhesabu Muda Wa Kupangusa Juu Ya Soki?

Swali:

Lini unaanza kuhesabu muda wa kupangusa juu ya soki?

´Allaamah al-Fawzaan:

Unaanza unapopata hadathi baada ya kuzivaa. Utapotenguka wudhuu wako

uliouvaa juu yake, wudhuu wako unaanza muda ule [mpako wa kwanza]

ulioanza kupangusa. Ulipopata hadathi [ukapangusa] baada tu ya kuzivaa.

15) Madu´aat Wa Ushirikina Katika Chaneli

Swali:

Katoa Fatwa mmoja katika wale wanaodhiri katika chaneli mbovu kwamba

tawassul na kuomba au kutafuta kinga kwa mawalii na watu wema waliokufa

ni jambo linajuzu, bali ni jambo lina ujira mwingi. Je inajuzu kuchukua kutoka

kwake...

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu ni katika wao. Huyu ni katika wao waabudu makaburi. Anaejuzisha

mambo haya ni katika wao, usidanganyike kuwa anadhihiri katika wao

Page 20: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

20

mmoja wao katika madu´aat [walinganizi] wa makaburi. Lisikudanganye hili.

Hakuna mwanachuoni awazae kusema hili anamuogopa Allaah na kumcha.

16) Wanaodai Ni Wafasiri Wa Ndogo Katika Vyombo Vya Habari

Swali:

Katika siku zimezopita kumekithiri wafasiri wa ndoto, na imekuwa

wanajitokeza hata kwenye chaneli mbovu...

´Allaamah al-Fawzaan:

Wanatafuta pesa hao, wanatafuta pesa hao. Leo jambo hili imekuwa ni kama

biashara. Watu hawa wasifatwe na wala wasiangaliwe [kwenye hivyo

vyombo vyao vya habari].

17) Je, Maji Ya Zamzam Yakitoka Nje Ya Makkah Baraka Yake Bado

Yabaki?

Swali:

Yakipelekwa maji ya zamzam katika mji wowote, yatabaki kuwa na baraka

inayojulikana au yatapungua?

Page 21: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

21

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwanini [ipungue baraka]? Maji ya zamzam yana baraka sehemu yoyote

yawapo.

18) Kurukuu Kabla Ya Kufika Katika Safu Kwa Ajili Ya Kudiriki Rakaa

Swali:

Kuna mtu ameingia msikitini na imaam amerukuu, kwa ajili ya kutaka kudiri

rakaa akarukuu kabla ya kufika katika safu. Na baada ya kufika kwenye

rukuu akawa anatembea [kwa kusutama] kwa kupiga hatua kama kumi hivi

au zaidi ili afike kwenye safu. Ipi hukumu ya swalah yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili kalikataza Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Alilifanya Abu

Bakr (radhiya Allaahu ´anhu) na akamkataza.

Alimwambia:

"Allaah Akuzidishie juhudi, na wala usirudi. Halifanywi hili wala halijuzu.

Tembea taratibu kama alivyosema Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Mtazowahi swalini na zitazowapita timizeni au lipeni."

19) ´Amali Za Kuweza Kumfanyia Maiti Zikamnufaisha

Page 22: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

22

Swali:

Kuna mtu kafa ndugu yake. Ipi amali bora awezayo kumfanyia imnufaishe

kwayo huyo maiti?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kumtolea swadaqah, kumuombea du´aa, amhijie na amfanyie ´Umrah. Yote

haya imethibiti dalili zake.

20) Je, Kila Maradhi Yasioweza Kutibiwa Na Madaktari Inakuwa Na

Uchawi, Kijicho Au Hasadi?

Swali:

Je ni kila maradhi ambayo matabibu hawakuweza kuyatibu inakuwa ni

uchawi, au kijicho au hasadi? Na nini unaninasihi mimi ni mtu nimepatwa na

mfano wa maradhi haya, kwa kuwa watu wengi wananambia ni uchawi, na

hili [kuambiwa hivi] limenizidishia] pia maradhi.

[Mtume anasema]:

"Allaah Hakuteremsha ugonjwa ila Kateremsha dawa yake, mwenye kujua

amejua na asiyekuwa hakujua."

Kama hawakuyajua baadhi ya matabibu, kuna matatibu wengine wayajuayo

[maradhi hayo]. Usiishie kwa matatibu wawili watatu, maadamu unaweza

kupata wengine. Waulize huenda Allaah Akajaalia kupitia katika mikono yao

ponyo. Ama uchawi unatibiwa kwa Qur-aan au kwa du´aa mubaha. Hakuna

Page 23: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

23

makatazo ukatibiwa kwa Qur-aan na ukatibiwa kwa du´aa mubaha. Ama

kutibiwa kwa wachawi, hili halijuzu.

21) Kujuta Tu Baada Ya Kosa Yatosha Kuwa Ni Tawbah?

Swali:

Je kujuta baada ya kufanya maasi moja kwa moja inachukuliwa kuwa ni

[kama kufanya] tawbah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haitoshelezi kujuta tu. Lazima mtu aache dhambi hio na aazimie kuwa

hatorudi. Halafu ndo ajute kwa dhambi. Masharti matatu [ya tawbah].

22) Je, ´Iysa (´alayhis-Salaam) Alipewa Utume Alipofikisha Miaka

Arubaini?

Swali:

Je imethibiti kuwa Iysa (´alayhis-Salaam) kuwa alipewa Utume kabla ya

kufikisha miaka arubaini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 24: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

24

Allaah Ndiye Ajuae zaidi.

Swali La Pili:

Na je imethibiti kuwa katika mwisho wa dunia atapoteremka kwamba ataoa

na kuzaa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Litapodhihiri hilo tutawafunza, [msijali!]. Kuna mmoja alimuuliza Taabi´iyn,

akasema: "Iblisi ana watoto, nani mke wake?"

Akamwambia: "Halikudhihiri hili."

Kwanini maswali kama haya ya pumba, kwanini mnayauliza??!!

23) Kafiri Wanatana Kumsimamishia Hadd Akamtaka Shahaadah, Je

Atasaliwa?

Swali:

Je mwenye kusimamishiwa hadd (adhabu) kwa kuwa ni mchawi au mwenye

kuritadi akasema Laa ilaaha illa Allaah kabla ya kusimamishiwa hadd, je

atasaliwa na kuzikwa katika makaburi ya Waislamu?

Page 25: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

25

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, atafanyiwa anayofanyiwa alieritadi. Lakini ni baina yake yeye na

Allaah ikiwa tawbah yake ni sahihi - Allaah Ndiye Aijuae zaidi. Tunamwachia

hilo Allaah. Ama sisi tunamsimamishia hadd na tunamfanyia anayofanyiwa

alieritadi.

24) Mzee Kakatwa Mguu Na Ana Maradhi Ya Kutokwa Na Akili, Mwaka

Mzima Haswali

Swali:

Baba yangu ni mgonjwa sasa miaka 30, wakati fulani anakuwa bado yu na

akili na wakati mwingine haiwi hivyo. Mwaka ulopita alikatwa mguu wake

na wala hawezi kufanya kitu ila kwa msaada wa watoto, na mwaka mzima

haswali. Swali ni vipi ataswali baba yangu? Na je tumlipie swalah zake

zilizompita mwaka mzima au miwili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa akili zake bado zimebaki anaswali kwa kiasi cha hali yake.

�� ا$!ط"!م ��!��وا %�

”Basi mcheni Allaah kama mwezavyo.” (64:16)

Page 26: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

26

Aswali kwa wudhuu au kwa kutayamamu. Aswali hali ya kuwa amesimama

au amekaa au kwa ubavu nk - kadiri na atavyoweza.

�� ا$!ط"!م ��!��وا %�

”Basi mcheni Allaah kama mwezavyo.” (64:16)

Ama ikiwa akili zake zimeenda na hajui kitu kinachoendelea, hana juu yake

swalah.

25) Nifanye Hijrah Kuhama Kutoka Europe Na Wakati Nadhihirisha Dini?

Swali:

Mimi niko katika mji wa Europe, je ni wajibu kwangu kufanya Hijrah

[kuhama] pamoja na kuzingatia ya kwamba ninadhihirisha swawm, swalah

na adhaana?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ukiweza kufanya Hijrah hama - ukiweza. Na ikiwa huwezi wewe utakuwa

mwenye kupewa udhuru [ila] pamoja na kushikamana [bara bara] na dini

yako. Na huko si kudhihirisha dini. Kufunga kwako, kuswali nk na hawasemi

kitu [makafiri]. Sivyo hivyo kudhihirisha dini. Kudhihirisha dini ni kulingania

kwa Allaah, kulingania katika Tawhiyd, na katika kumuabudu Allaah na

katika dini ya Kiislamu. Huku ndo kudhihirisha dini.

Page 27: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

27

26) Hafidh Wa Qur-aan Ambaye Si Mwarabu Anatumbukia Katika Shirki,

Je, Ana Udhuru?

Swali:

Ikiwa mfanya shirki kahifidhi Qur-aan lakini sio mwarabu na wala hafahamu

maana ya Aayaat, je inaweza hili kuwa udhuru kwake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haitoshi kwake kuhifadhi tu Qur-aan. Lazima aulize maana yake na tafsiri.

Hili halitoshi, ni mpuuzaji. Kwanini asiulize?! Ila tu ikiwa hakuwa na uwezo

na wala hakupata wakati, huyu atapewa udhuru. Lakini ikiwa ni mwenye

kuweza kusomakiarabu na kufahamu Qur-aan, huyu hapewi udhuru. Kwa

kuwa ni mpuuzaji.

27) Watu Watapewa Udhuru Katika Shirki Mpaka Lini?

Swali:

Masuala ya kupewa udhuru kwa ajili ya ujinga yanachukuliwa ni katika

masuala naazilah hayaongelewi na yeyote ila wanachuoni wakubwa tu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 28: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

28

Kupewa udhuru kwa ajili ya ujinga - kwa hakika leo, udhuru kwa kila

anaetumbukia katika shirki na anatumbukia katika kufuru wanasema huyu ni

mjinga, pamoja na kuwa Qur-aan inasomwa usiku na mchana. Katika idhaa

zao wanasikia. Mpaka lini ujinga?

28) Huyo Si Mke Hakufai, Tafuta Mwengine!

Swali:

Kuna mtu Kamneemesha Allaah kwa kumpa msimamo naye kaoa lakini mke

wake hataki ajidhihirishe kama Salafiy - kama kufuga ndevu na kufupisha

nguo. Na wakatianapomuamrisha kuachana na mambo ya mchanganyiko

[wanaume na wanawake] na kwenda kwenye hafla za muziki anakataa.

Nimemsubiria na kumnasihi. Ipi nasaha yako kwa hilo kwa kuwa sina watoto

nae?

´Allaamah al-Fawzaan:

Alhamdulillaah huna nae watoto. Huyu ikiwa hasikii tengana nae na tafuta

mke mwengine.

29) Mke Mkaidi Anafanya Ya Haramu Na Kusema Nisimwingilie Katika

Uhuru Wake

Swali:

Page 29: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

29

Mke wangu anafupisha nywele zake na hajali katika kufupisha kwake.

Nimemnasihi kwa hilo na kuwa ni wajibu anitii ananijibu kuwa "Huu ni

uhuru wangu, na eti namwingilia katika mambo yake". Ipi nasaha yako

kwangu na kwake kwa hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, qadhia hii imeenewa kwa watu. Nayo ni kuhusu udhuru - uhuru wa

maoni, uhuru wa kutabiri, uhuru wa tabia. Nini maana ya uhuru? Uhuru ni

katika mipaka ya Shari´ah, uhuru ni katika mipaka ya Shari´ah. Ama uhuru

unaovuka mipaka ya Shari´ah umekatazwa na ni upotofu. Sisi ni waja wa

Allaah Waislamu. Tunatekeleza amri za Allaah (´Azza wa Jalla).

30) Kijana Ameoa Mnaswara, Mke Anataka Waende Nae Kanisani

Swali:

Mimi ni kijana nimemuoa mnaswara na anahudhuru pamoja nami ijumaa na

sikukuu kwa kutaka aongoke [awe mwislamu], lakini anataka nende nae

kanisani ili "Qissiysu" [mchungaji] aibariki ndoa yetu...

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Hapana! Hapana! Haijuzu kwenda nae. Wala hatokubariki huyo

Qissiysu. Ni Shaytwaan na si Qissiysu. Hana baraka. Baraka zinatoka kwa

Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Usende nae! Na ichukie dini yake. Ichukie

dini yake chuki kubwa kweli kweli.

Page 30: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

30

31) Je Inajuzu Kuweka Mlio Wa Simu Sauti Ya Adhaana au Aayah Tukufu?

Swali:

Je inajuzu kuweka mlio wa simu sauti ya adhaana au Aayah tukufu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Zisitumiwe adhkaar katika simu kwa ajili ya tanbihi ya maongezi.

Huu ni mtihani kwa dhikr - mtihani kwa Qur-aan.Weka mlio usiokuwa na ala

wala muziki wala... kwa jili tu ya kukushtua [kuwa kuna mtu anapiga].

32) Muislamu Katumbukia Katika Shirki Kubwa, Je Atoe Shahaadah Upya?

Swali:

Ukiona mtu anafanya kitendo cha shirki kisha nikambainishia kuwa hii ni

shirki akatubia. Je ni juu yake kutamka shahaadah [upya]?

´Allaamah al-Fawzaan:

Akiwa ni Muislamu naye anafanya shirki atatamka shahaadah. Ama ikiwa sio

Muislamu na ukambainishia huyu anaingia katika Uislamu upya, si kwamba

karitadi kisha akatubu.

Page 31: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

31

33) Kuswali Kwenye Msikiti Uitwao Masjid Sayyid al-Badawiy Usio Na

Kaburi

Swali:

Katika mji wetu nje ya mji huu [Saudia] kuna Suufiy kajenga msikiti na

akaupa jina "Masjid Sayyid al-Badawiy [msikiti wa bwana al-Badawiy]." Je

inajuzu kuswali katika msikiti huu kwa kuwa hauna kaburi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Jina litolewe na mtu aswali maadamu hakuna kaburi, mtu aswali na jina

litolewe. Wamnasihi kutoa jina.

34) Je, Kijusi Kikitoka Tumboni Hufanyiwa ´Aqiyqah?

Swali:

Je kijusi [mtoto mbichi sana tumboni] hufanyiwa ´aqiyqah au huchinjiwa

´aqiyqah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 32: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

32

Ndio, akifikisha siku arubaini anachukua hukumu za mtoto [wa kawaida].

Anaoshwa, anakafiniwa, anaswaliwa. Anazikwa kwenye makaburi ya

Waislamu na anapewa jina.

35) Hukumu Ya Mtu Anaedai Kuwa Ni Muislamu Ila Haswali

Swali:

Mtu ambae anajinasibisha na Uislamu lakini haswali...

´Allaamah al-Fawzaan:

Uislamu wake uko wapi? Asiyeswali sio Muislamu. Uislamu wa bila swalah?!

Muulizaji:

Je inajuzu kula katika kichinjo chake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Hapana haijuzu kula katika kichinjo chake. Ikiwa anaacha swalah

kwa kukusudia, huyu sio Muislamu wala sio halali kichinjo chake.

Page 33: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

33

36) Muislamu Ambaye Anafanya ´Ibaadah Zake Zote Kwa Kukhalifu

Sunnah

Swali:

Mwenye kusema Laa ilaaha illa Allaah, lakini haswali swalah ya Waislamu,

hafungi swawm yao na wala hatoa zakaah yao bali anatekeleza ´ibaadah zote

hizi kwa mfumo unaokhalifu Sunnah.

´Allaamah al-Fawzaan:

Sio Muislamu huyu. Mwenye kukhalifu sifa ya swalah na zakaah ya

Kishari´ah na anazileta kwa sura tu, huyu sio Muislamu.

37) Hukumu Ya Muislamu Asietoka Zakaah

Swali:

Kuna wanaotamka Laa ilaaha illa Allaah na wanaswali, lakini hawatoi zakaah

iliyofaradhishwa. Je mtu huyu, mtu atasema ni Muislamu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Anaweza kuwa amekataa kwa ajili ya ubakhili na hapingi. Huyu anasihiwe na

ichukuliwe kutoka kwake hata kama itakuwa kwa kutumia mabavu na

mtawala wa Waislamu. Wala hahukumiwi ukafiri, bali huyu ni bakhili.

Page 34: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

34

38) Hukumu Ya Mwanaume Mwenye Kulipa Swawm Ya Dhwihaar

Akamjamii Mke Wake Kabla Hajamaliza Swawm Yake

Swali:

Ipi hukumu lau mwanaume kafanya dhwihaar kwa mke wake, akamjamii

katikati ya swawm ya kafara. Je ataanza swawm upya au atajengea juu yayo

[ataendelea]?

´Allaamah al-Fawzaan:

Bila shaka ataanza, kwa kuwa kabatilisha swawm yake. Kwa kuwa Allaah

Kasema. [Kwa mwanaume aliyefanya dhwihaar]afunge miezi miwili

mfululizo. Na huyu kaikata. Ataanza upya [mwanzo].

39) Mwanafunzi Anaehofia Mas-ala Ya Qadhwaa Na Qadar

Swali:

Mimi ni katika watafutaji elimu, lakini ninakhofia kusoma maudhui ya

Qadhwaa [yaliyopangwa na Allaah] na Qadar. Ipi nasaha yako kwangu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 35: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

35

Amini Qadhwaa na Qadar. Ni lazima kuamini Qadhwaa na Qadar. Ama

kuingia katika hayo na kukithirisha kuyauliza, hili kuliacha ni bora kwako na

litakuweka mbali na mashaka. Amini Qadhwaa na Qadar na muachie mambo

haya Allaah (´Azza wa Jalla). Allaah Hakukukalifisha kwa haya.

40) Mwanamke Mjamzito Kafa Na Mtoto Tumboni, Mtoto Atolewe Na

Kuzikwa Mwenyewe?

Swali:

Mwanamke kafa na tumboni mwake kuna mtoto, je apasuliwe kutolewa

mtoto na kuzikwa sehemu yake kwa hoja akibaki mtoto tumboni mwake

atazikwa kwa kutokielekea Qiblah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana ataachwa mtoto tumboni mwake.Azikwe yeye na [mtoto] yu tumboni

mwake. Haifai kumpasua. Qiblah cha mtoto tumboni ndio Qiblah cha mama

yake. Maadamu mama yake kaelekea Qiblah anamfuata.

41) Mwanamke Kafa Baba Yake Mdogo Kafiri

Swali:

Page 36: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

36

Kuna baba mdogo wa mwanamke kafa ambaye alikuwa ni kafiri. Je inajuzu

kwa mwanamke kuhudhuria janaza yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, watahudhuria makafiri! Watamsimamia makafiri na si Waislamu.

Lakini kukiwa hakuna mtu katika makafiri, anaweza kumsimamia - yaani

akamuosha akamkafini na akamzika mahala pa mbali na si katika makaburi

ya Waislamu. Haifai kumuosha kwa kuwa kuosha ni ´ibaadah na haifai kwa

kafiri. Mzingire kwenye kitu na amzike mahala mbali na njia [manyumba].

42) Mwanamke Mgonjwa Kafa Naye Hakufunga Ramadhaan

Swali:

Mwanamke kasibiwa na maradhi akafa naye hakufunga Ramadhaan na wala

hakulipa, je alipiwe?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa aliacha kufunga kwa ajili ya maradhi na akafa kwayo, hana juu yake

kitu.

43) Hukumu Ya Kuzuia Mimba Moja Kwa Moja

Swali:

Page 37: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

37

Dada kutoka Holland anasema, ipi hukumu ya mwanamke kuzuia mimba

kabisa ikiwa kuna matatizo baina ya wanandoa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Asizuie mimba ila kwa maradhi, wakithibitisha hilo matatibu kuwa hafai

kushika mimba kwa ajili inaweza kumuua au itamfanya mgonjwa. Hivyo

ataakhirisha na si kukata uzazi moja kwa moja, bali ataakhirisha. Haijuzu

kwake kuzuia uzazi.

44) Mwanamke Kwenda Sokoni Bila Mahram

Swali:

Inajuzu kwa mwanamke kuingia sokoni bila mahram?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mahram ni katika safari, ama mjini mwake hahitajii mahram. Akiwa ni

mwenye kujiheshimu, kavaa Hijaab na hatochanganyika na wanaume na

akaenda sokoni kwa haja [dharurah]; hana haja ya mahram. Mahram ni

wakati wa safari.

Page 38: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

38

45) Mwanamke Ambaye Yuko Katika Familia Yake Kutoka Bila Ya Ruhusa

Ya Mumewe

Swali:

Je inajuzu kwa mwanamke ikiwa kakaa katika familia yake, inajuzu kwake

kutoka na familia yake bila kumuomba ruhusa mume wake na bila kujerea

kwake [kuomba ruhusa]?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mume wake ndiyo kamruhusu kwenda kuwazuru. Ataenda nao kwa kuwa

hili pia [kuwafuata] linaingia katika ruhusa.

46) Inajuzu Kuwatolea Wanawake Salaam?

Swali:

Ipi hukumu ya kuwatolea salaam wanawake, mwanaume kuwatolea salaam

wanawake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna neno. Wasalimie wanawake kwa maneno na si kwa kupeana mikono.

Page 39: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

39

47) Mwenye Kuanguka Katika Bid´ah Moja Tu Ya Kiitikadi Anakuwa

Mubtadi´ah?

Swali:

Anayetumbukia katika bid´ah ya Kiitikadi (´Aqiydah) huku alikuwa

akijulikana ni mwenye kushikamana na mfumo wa Ahl-ul-Sunnah katika kila

kitu lakini katumbukia tu katika bid´ah hii, anachukuliwa ni mubtadi´ah au

kuangaliwe mfumo wake wote?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, huchukuliwa ni mubtadi´ah. Ikiwa hatotubia na kuacha bid´ah ni

mubtadi´ah hata kama bid´ah yake ni moja tu.

48) Daa´iy Anaetoa Fatwa Kujuzisha Ndoa Ya Mut´ah Kwa Vijana

Swali:

Baadhi ya wanaojiita maulamaa wanadhihiri sana katika TV wanawapa vijana

Fatwa za kujuzisha [ndoa ya] mut´ah na kuwa ni afadhali kuliko kuzini...

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 40: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

40

Jitu hili ni shia. Isichukuliwe Fatwa yake. Wanachuoni wamekubaliana wote

uharamu wa ndoa ya mut´ah, baada ya kufutwa wamekubaliana uharamu

wake. Mwenye kuiruhusu ni kafiri.

49) Miongoni Mwa Masharti Ya Laa Ilaaha Illa Allaah

Swali:

Mwenye kusema laa ilaaha illa Allaah na asifanye mambo mengine, si swalah

wala swawm. Lakini anakiri nguzo zote za Uislamu lakini hayafanyii kazi. Je

itamfaa [laa ilaaha illa Allaah]?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Akiacha amali naye ni muweza; haswali, hatoi zakaah, hafungi na

wala hahiji na yeye ni muweza. Haitomfaa laa ilaaha illa Allaah. Kwa kuwa

hakuifanyia kazi muqtadhwa yake, hakuifanyia kazi haki yake. Ama lau

ataisema kwa ikhlaasw kisha akafariki kwa hali moja au nyingine au akauawa

na hakuweza kufanya amali, huyu itamfaa kwa idhini ya Allaah. Mithili

Hadiyth ya bitwaaqah, yule aliyesilimu kisha akauawa akaingia Peponi.

Mithili kijana wa kiyahudi aliyekuwa mgonjwa akamzuru Mtume (´alayhis-

Salaam) akamlingania katika Uislamu akasilimu, akaingia Peponi. Hawa

hawakuweza kufanya amali. Ama kwa mtu aliyeweza kufanya amali akaacha

bila ya udhuru wa Kishari´ah huyu si muumini na wala haimtomfaa kitu laa

ilaaha illa Allaah.

Kulisemwa kwa Wahbiy bin Munabeh (rahimahu Allaah):

"Je laa ilaaha illa Allaah si ndiyo funguo ya Pepo?" Akasema "ndiyo!", ila

hakuna funguo ila huwa na meno. Ukija na funguo ya meno utafunguliwa, la

sivyo hutofunguliwa”.

Page 41: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

41

Laa ilaaha illa Allaah ndio funguo ya Pepo sahihi, lakini ina meno. Na meno

yake ni amali [matendo]. Ukija na laa ilaaha illa Allaah na amali utafunguliwa

Pepo. La sivyo hutofunguliwa Pepo.

50) Je, Fuqahaa´ Murji-ah Ni Mubtadi´ah?

Swali:

Yapi maoni yako kwa mwenye kusema Fuqahaa´ Murji-ah ni mubtadi´ah, na

mwenye kusema ni katika Ahl-ul-Sunnah kauli yake ni upotofu. Je mtu

huyu...

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa kuwa hajui mubtadi´ah na wala hajui upotofu. Huyu ni masikini.

Anataka kusema Hanafiyyah ni mubtadi´ah? Hakuna waliyo katika Ahl-ul-

Sunnah? Nani awezae kusema Hanafiyyah si katika Ahl-ul-Sunnah?! Haya ni

maneno ya mjinga.

51) Radd Kwa Mwenye Kusema Mzazi Kumchunguza Mtoto Wake Ni

Ujasusi

Swali:

Page 42: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

42

Kuna baadhi ya watu wasemao kitendo hichi cha baba [kuwachunguza

watoto] ni katika ujasusi uliokatazwa, vipi kauli hii?

´Allaamah al-Fawzaan:

Maneno haya ni maneno batili. Mzazi kaamrishwa kuwalea watoto wake,

kuwaangalia na kuwakemea, hili ni wajibu kwake. Na si ujasusi, bali hili ni

kusimama na la wajibu aliyomuwajibishia Allaah juu yake. Lakini leo watu

wamekuwa na fikra mbovu wanasema "msiwapeleleze watoto wenu wala

wake zenu na wala mabanati zenu, waacheni wafanye wapendalo ni uhuru

wao msiwaingilie." Wanataka pasiwe yeyote atayesimama na la wajibu

kwake, na kila mmoja afanye akipendacho.

52) Waalimu Wasiofunza Tawhiyd Katika Madrasa

Swali:

Baadhi ya ndugu wanaosomesha katika madrasah hawafunzi Tawhiyd, bali

wanafunza Fiqh, Tafsiri na Hadiyth. Je una nasaha katika hili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nasaha haitowafaa kitu, watu hawa wafikishiwe wasimamizi wao.

Wasiwaweke wakafunza Tawhiyd, wawatoe na waweke waalimu wenye

kupenda Tawhiyd na wanaifunza kwa sura itakikanayo.

53) Nasaha Kwa Wanafunzi Wanaopondana Wao Kwa Wao

Page 43: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

43

Swali:

Muulizaji kutoka Europe anasema, ipi nasaha yako kwa watafutaji elimu na

madu´aat ambao wanasusana wao kwa wao na wanapigana radd wao kwa

wao bila ya hoja wala dalili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili halijuzu. Maadamu wao ni madu´aat na ni watafutaji elimu haijuzu

kusasana wao kwa wao. Watu hawawakubali, isitoshe wao kwa wao waanze

tena kujengeana uadui na kukatana wao kwa wao?! Ni lazima ndugu

wasaidizana na wawe kitu kimoja. Na watanabahishane makosa baina yao,

wapeane nasaha. Na wala wasidhihirishe ikhtilaf mbele ya makafiri. Kwa

kuwa makafiri watawatawanyisha na wala hawatokubali da´wah yao.

54) Wake Zangu Wawili Wameingia Katika Uislamu, Je Ni Wajibu Kwao

Kurudi Upya Ndoa Zao?

Swali:

Wake zangu wawili wameingia katika Uislamu, je ni wajibu kwao kurudi

upya ndoa zao?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 44: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

44

Kama wameingia katika Uislamu wote, hapana [kufanya ndoa upya]!

Watabaki katika ndoa yao. Washirikina walikuwa wakisilimu wakati wa

Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wala hawaamrishi kurudi

kufunga ndoa zao upya. Lakini lau mwanamume atasilimu na akachelewa

mwanamke kuingia katika Uislamu mpaka akatoka katika eda, ni lazima

kufunga ndoa upya. Ama lau atasilimu mmoja wao na akasilimu mwengine

ndani ya eda pia ndoa inabaki na haina haja kufunga ndoa upya.

55) Ufafanuzi Kuhusu Kufuru Ya ´Amali (Ya Kimatendo)

Swali:

Ni ipi kufuru ya amali? Na je, inamtoa mtu katika Uislamu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kufuru ya amali ni ile iliyoitwa kufuru na haijafika katika kiwango cha shirki

kubwa. "Kama kumtukana Muislamu ni ufaasiq, na kumuua ni kufuru."

Kumuua Muislamu ni dhambi kubwa miongoni mwa madhambi makubwa na

ni kufuru, lakini ni kufuru ndogo. Na dalili ya hilo ni katika Qur-aan:

وإن ط�)�!�ن �ن ا��ؤ���ن ا&!!�وا

”Na ikiwa makundi mawili katika Waumini yanapigana.” (49:09)

Angalia kawaita waumini na wao wanapigana.

Page 45: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

45

إ*داھ�� 3� ا12رى ������ �/ن �.ت وإن ط�)�!�ن �ن ا��ؤ���ن ا&!!�وا �,+�*وا

”Na ikiwa makundi mawili katika Waumini yanapigana, basi yapatanisheni.

Na likiwa moja la hao linamdhulu mumwenzie.” (49:09)

Mpaka Aliposema:

�� ا��ؤ��ون إ1وة �,+�*وا ��ن أ1و��م إ��

”Hakika Waumini ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu.” (49:10)

Ni dalili ya kuwa kumuua Muislamu ni dhambi kubwa na kufuru ndogo,

haifiki katika kiwango cha kufuru kubwa.

56) Wajibu Wa Kumkata Ndugu Ambaye Anachukia Sunnah Na Watu Wa

Sunnah

Swali:

Niko na ndugu anachukia Sunnah na watu wa Sunnah, mpaka rafiki zangu

wanamwita adui wa Sunnah na mimi nimemkata na simuongeleshi na wala

simsalimii kiasi cha miaka mitano. Je mimi nina haki katika amri hii?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio! Wewe wafanya sawa na uko katika haki. Na kumkata ni wajibu mpaka

atubu kwa Allaah (´Azza wa Jalla).

Page 46: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

46

57) Kufanya Jamaa´ah Nyingine Wakati Jamaa´ah Ya Kwanza Inapokuwa

Katika Tashahhud Ya Mwisho

Swali:

Ninapoingia katika swalah na imaam kakaa katika tashahhud ya mwisho,

naona watu wananiita wafanye jamaa´ah nyingine. Sahihi ni kujiunga nao au

niingie na imaam?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kutokana na kauli sahihi kuwa jamaa´ah haipatikana ila kwa rakaa moja.

Hivyo akitoa salaam imaam salini. Msisali na imaam hajatoa salaam. Akitoa

salaam salini jamaa´ah.

58) Wafanyao Barnamiji Za Video Kwenye TV

Swali:

Barnamiji za dini mubashara kwa sauti na picha kwenye TV zinazorushwa

baada ya kuziremba, je zinajuzu au nazo ni katika picha ambazo ni haramu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 47: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

47

Hili liko katika dhima ya wafanyao hivyo. Liko katika dhima yao.

59) Je Kutahadharisha Watu Dhidi Ya Maulamaa Wa Ahl-ul-Bid´ah Ni

Katika Kusengenya Na Kueneza Uvumi?

Swali:

Utahadharisho dhidi ya maulamaa potofu na watu wenye fikra potofu na Ahl-

ul-Ahwaa, huchukuliwa ni katika usengenyaji na kueneza uvumi? Na ipi

dhwaabit ya hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Utahadharisho - ikiwa uko na elimu na baswiyrah katika Kitabu na Sunnah,

na una ujuzi wa kosa hilo na upi usawa na upotofu, na una uwezo wa

kubainisha ni lazima kubainisha na hili si katika usengenyaji na kueneza

uvumi; hili ni katika [kupeana] nasaha. Lakini ukaanza kuwajeruhi watu na

kuwaponda, fulani hana khayr na fulani ni hivi - hili halijuzu na halileti khayr

hili. Hili linazidisha shari juu ya shari. Hili haliwi ila kwa wanachuoni na

wenye baswirah wanaokataza kwa njia sahihi na kupiga radd. Si kwa kila

mtu.

60) Radd Kwa Mwenye Kusema Kaburi La Mtume Liko Ndani Ya Msikiti

Swali:

Page 48: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

48

Vipi kumpiga radd shubuha za mwenye kusema kaburi la Mtume (swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) liko ndani ya msikiti wa Mtume na anashikamana

na hili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haipo ndani ya msikiti, ipo ndani ya chumba cha ´Aaishah na si ndani ya

msikiti. Na ilikuwa nje ya msikiti katika uongozi wa makhalifah waongofu, na

uongozi wa Mu´aawiyah na uongozi wa ´Abdul-Maalik bin Marwaan.

Alipokuja Waliyd ibn ´Abdil-Maalik baada ya baba yake ´Abdul-Maalik na

wakaupanua msikiti, hivyo wakawa wameingiza chumba cha Mtume ndani,

kwa rai yake yeye na hakushauriana na maulamaa. Maulamaa

hawakukubaliana na hili. Lakini mtu hawezi kusema kaburi la Mtume liko

ndani ya msikiti, iko ndani ya chumba. Na chumba kimeingizwa msikitini.

61) Wanayomba Makaburi Kwa Hoja Eti ´Umar Alimuomba Abbaas

(Radhiyallaahu ´anhum)

Swali:

Tukiwakumbusha washirikiana katika mji wetu kuwa kuyaomba makaburi ni

shirki, wanaturadi na kusema ´Umar alikuwa akimuomba ´Abbaas.

´Allaamah al-Fawzaan:

´Abbaas alikuwa hai na hakuwa maiti. Na ´Umar alimuomba ´Abbaas

[amuombee] du´aa. Inajuzu kuomba mtu aliyehai akuombee du´aa. Wala

Page 49: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

49

hakumuomba, tamko hili "aliomba" hapana! Kilichothibiti ni kuwa alitaka

kutoka kwa ´Abbaas amuombe Allaah Awanyeshelezee mvua.

62) Ribaa Ni Dhambi Ya Pili Baada Ya Dhambi Ya Ushirikina

Swali:

Ulisema katika khutbah ya ijumaa iliopita kuwa kula ribaa ni dhambi kubwa

baada ya kumshirikisha Allaah, je kula ribaa ni dhambi kubwa kuliko kuuwa

mtu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Allaah Katoa makemeo makali kwa mla riba makemeo ambayo hajatoa

kwa mwengine. Makemeo makali sana. Ni dhambi kubwa.

63) Mwenye Kula Ribaa Pamoja Na Kujua Kuwa Ni Haramu

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kusema mimi najua kuwa ribaa ni haramu, lakini

pamoja na hivyo nitakula na nitaifanyia kazi. Je mtu huyu anachukuliwa

kaihalalisha?

Page 50: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

50

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu hakuhalalisha lakini hatoacha kula ribaa. Huyu anakula ribaa na anajua

kuwa ni haramu.

�� 6 ��و�ون إ �ط�ن �ن ا��س7 �6 ��� ��وم ا��ذي �!1��ط9 ا��ذ�ن �,��ون ا�ر7 ا�>�

“Wale walao riba hawasimami ila kama anavyo simama aliyezugwa na

shaytwaan kwa kumgusa.” (02:275)

Siku ya Qiyaamah aliyekuwa akila ribaa duniani litavimba tumbo lake kwa

ribaa, hatoweza kusimama na watu watapotoka kwenye makaburi yao na

kutaka kwenda kwenye uwanja wa hesabu atakuwa akitaka kusimama

anaanguka. Kwa kuwa tumbo lake linamtia uzito - Allaah Atukinge. Itakuwa

ni fedheha kuwa kwake mbele ya umati. Haijuzu kula ribaa.

64) Risaalah Ya Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab Kwa Watu Wa

Europe

Swali:

Je Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab ana risaalah (ujumbe) kwa watu

wa magharibi na Qairawaan akiwalingania katika Tawhiyd?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 51: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

51

Ndiyo. Ana risalah aliwatumia watu wa magharibi. Inapatikana katika risalah

zake.

65) Jinsi Ya Kumtibu Aliemsibu Ndugu Yake Kwa Kijicho

Swali:

Vipi atajiosha mwenye kudhani kuwa kamsibu ndugu yake kwa kijicho? Je

atatawadha au atajiosha ndani ya...

´Allaamah al-Fawzaan:

Yote ni sawa. Anaweza kumtawadhia, akamuoshea nguo yake, akamsomea.

Yote ni sawa inshaa Allaah.

66) Tawassul Na Sharti Zake

Swali:

Sura ya pili uliyotaja katika sura za tawassul imenitatiza kwa kuwa tulisoma

kwako katika kitabu cha "Tawassul" kuwa kutawassul kwa mtu mwema kwa

kusema kwa mfano "ewe fulani niombee kwa Allaah anisamehe" kuwa ni...

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 52: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

52

Hili ni sahihi ila ni katika uhai wake. Katika uhai wake unaweza kumwambia

mtu mwema niombee kwa Allaah anisamehe. Ama kuliendea kaburi na kudai

eti ni mtu mwema - Allaah ndiye Mwenye Kujua [wema wake], na

kumwambia "ewe fulani maiti niombee kwa Allaah", hili halijuzu. Kuna

tofauti baina ya aliyehai na maiti. Na kuna tofauti baina ya aliyehudhuria na

asiyeonekana. Hata aliyehai ikiwa haonekani, [haifai] kumuomba kitu.

Utamuomba tu aliyehai na kahudhuria. Sharti ya tatu pia ni kuwa uwe

unamuomba kitu akiwezacho. Sharti tatu. Sharti ya kwanza awe hai, ya pili

kahudhuria na sharti ya tatu awe ni muweza wa unachomuomba.

67) Sijdah at-Tilaawah Ndani Ya Gari

Swali:

Nikiwa ndani ya gari na mimi niko nasoma Qur-aan kisha nikakutana na

Aayah yasajdah, je naweza kusujudu sehemu ya kiti kilichoko mbele yangu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna ubaya ukasujudu sehemu ya kiti, au ikiwa unaweza kusujudu katika

ardhi kwenye gari fanya hivyo.

68) Sisi Tunawaua Washirikina Tu Na Hatuwaui Waislamu

Swali:

Page 53: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

53

Tunapowanasihi waabudu makaburi wanasema "nyinyi ni Makhawaarij",

mnawaua Waislamu na mnawaacha waabudu masanamu.

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndiyo, wangelikuwa ni Waislamu tusingeliwaua. Thibitisheni kama kweli ni

Waislamu?! Ilihali mnaabudu asiyekuwa Allaah, mnachinja kwa asiyekuwa

Allaah na mnatazamia kwa asiyekuwa Allaah. Nyinyi sio katika Waislamu.

Kutokana na dalili sahihi mutawaatir. Ama sisi tunajikinga kwa Allaah

kuwaua Waislamu. Sisi si kama Makhawaarij. Sisi tunamuua yule ambaye

imewajibika kumuua, waliyouawa na Maswahaba na Abu Bakr Asw-

Swiddiyq. Tunawaua!

69) Sunnah Ya Kuangalia Kidole Cha Shahaadah Wakati Wa Tashahhud

Swali:

Je ni katika Sunnah kuangalia mwenye kuswali kidole cha shahaadah katika

tashahhud ya mwisho na tashahhud ya kwanza?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, hili limepokelewa kuwa ataangalia katika kidole cha shahaadah.

Page 54: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

54

70) Sifa Ya Swalah Ya Istisqaa Ni Kama Swalah Ya `iyd

Swali:

Je kuna dalili ya kuwa swalah ya istisqaa wakati wake ni pale jua

linachomozapo, au inaswaliwa wakati wowote?

´Allaamah al-Fawzaan:

Imepokelewa kuwa ni kama swalah ya ´Iyd, inavyofanywa ni kama swalah ya

´Iyd - mahala pake sifa yake. Inachukua akhaam kama swalah ya ´Iyd.

71) Aina Mbali Mbali Za Tawassul Na Hukumu Zake

Swali:

Je tawassul bila ya kumfanyia chochote katika ´ibaadah [unayemfanyia

tawassul] ni shirki ndogo au ni bid´ah au?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nimeshawaambia hili, nilisema tawassul ni aina mbili. Tawassul iliyokatazwa

ni aina mbili:

Aina ya kwanza ni afanye kitu katika ´ibaadah kwa yule anayemfanyia

tawassul, hii ni shirki kubwa. Na hichi ni kitendo cha Ahl-ul-Jaahiliyyah.

Page 55: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

55

ھم و6 ���"�م و��و�ون �ھـؤ6ء >�"�ؤ�� �د % و�"�دون �ن دون % �� 6 �=ر

"Nao, badala ya Allaah, wanaabudu wasio wadhuru wala kuwanufaisha, na

wanasema: Hawa ndiowaombezi wetu kwa Allaah!" (10:18)

Aina ya pili ni kumfanya unayemfanyia tawasssul mkaakati (mpatanishi) tu

baina yako wewe na Allaah. Unadai kuwa anakukurubisha kwa Allaah tu, na

kuwa Allaah Atakuitikia kwa upatanishi wake, hii ni bid´ah na ni njia

inayopelekea katika shirki; Ikiwa hukumfanyia kitu katika ´ibaadah.

72) Nyote Ni Wakoseaji Na Mbora Ni Yule Mwenye Kutubia

Swali:

Ikiwa mtu ni Muwahhid anahifadhi nguzo za Uislamu, lakini ana madhambi

mengi kukiwemo makubwa na madogo. Je anachukuliwa ni katika wapotofu

na kuwa hakuna kinachomzuia kurudi katika haki?

´Allaamah al-Fawzaan:

[Mtume anasema]: "Nyote ni wakoseaji, na mbora wa kukosea ni wenye

kutubu. "Atubu kwa Allaah (´Azza wa Jalla) kwa madhambi na Allaah

Humsamehe mwenye kutubu. Na wala asiseme mimi ni katika wapotofu

akamtia wasiwasi shaytwaan. Aache fikra hizi na atubu kwa Allaah.

Page 56: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

56

73) Tawhiyd-il-Ilaahiyyah Na Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah

Swali:

Je kuna tofauti baina ya Tawhiyd-il-Ilaahiyyah na Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, zote maana yake ni moja. Tawhiyd-il-Ilaahiyyah na Tawhiyd-ul-

Uluuhiyyah. Tawhiy-il-´Ibaadah. Yote ni maana moja.

74) Tawhiyd-ul-Khaaliqiyyah, Tawhiyd-ul-Raaziqiyyah Na Tawhiyd-ul-

Haakimiyyah

Swali:

Je kunapatikana katika ´Aqiydah sahihi kitu kiitwacho Tawhiyd-ul-

Khaaliqiyyah, Tawhiyd-ul-Raaziqiyyah na Tawhiyd-ul-Haakimiyyah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ndio inayoitwa Tawhiyd-ul-Khaaliqiyyah,

Tawhiyd-ul-Raaziqiyyah; yaani ndio Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. Tawhiyd-ul-

Haakimiyyah inaingia katika Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Isitengwe!

Page 57: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

57

75) Tofauti Baina Ya Sanamu Na Wathan

Swali:

Kuna tofauti baina ya sanamu na wathan?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndiyo. Sanamu ni ile yenye sura ya mnyama. Tofauti ni ya kilugha tu, hakuna

tofauti Kishari´ah. Lakini kilugha [sanamu] ni ile yenye sura ima ya mtu au

mnyama. Na wathan ni ile isiyokuwa na sura, kama [mwenye kuabudu]

kaburi, mti na jiwe.

76) Tofauti Ya Ujinga Na Upotevu

Swali:

Je kuna tofauti ya ujinga na upotevu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ujinga ni kwa yule asiyejua haki, huyu ni mjinga. Ama upotevu ni kwa yule

mwenye kujua haki na akaicha, au akamuabudu Allaah pasina elimu kama

manaswara na Masufi. Wameisusa elimu.

Page 58: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

58

77) Usikae Na Mvuta Sigara!

Swali:

Kuna baadhi ya maasi yameenea sana kwa Waislamu na wamekuwa hawajali

kila mahala, kama kuvuta sigara. Je kwa mtu mmoja anaweza kukataza uovu

kama huu au aache kwa kukithiri kwake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, akataze kiasi atavyoweza. Akumbushe na kubainisha madhara ya

sigara na athari yake mbaya, awawekee wazi hili. Na ikiwa hawatokubali,

asikae nao. Jiweke nao mbali usikae nao.

78) ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Madu´aat Wanaohudhuria Katika

Maulidi

Swali:

Baadhi ya watu wa bid´ah Masufi na khasa Tijaaniyyah katika mji wetu wana

harakati mbali mbali kwa mnasaba wa kusherehekea Maulidi. Kunakuja

baadhi ya madu´aat na wanahudhuria nao na wanawaombea mwishoni siha

na afya na du´aa nyinginezo katika Mashaykh wa Kisuufiy walioandaa

mambo haya. Ipi hukumu ya mambo kama haya na kuhudhuria madu´aat

hao?

Page 59: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

59

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu anaafikiana nao na kuwasifia. Halijuzu hili, halijuzu hili. Isipokuwa tu

wakati tu pale unapohudhuria unawakataza na kuwabainishia kuwa hili

halijuzu na wasifanye mambo haya na si sawa. Walinganie kwa Allaah kabla

na la sivyo jendee zako waache. Usikae nao, unaafikiana, ukala nao chakula

ukapiga nao vicheko. Ukadai ni kuwalingania [Da´wah]! Hapana katu hii si

Da´wah.

79) Kuomba Kwa Nuru Ya Uso Wa Allaah Mambo Ya Kidunia Na Aakhirah

Swali:

Ulisema katika darsa iliopita kuwa haijuzu kuomba kwa Uso wa Allaah

[mambo] ya dunia. Vipi ikiwa nitamuomba Allaah kwa Nuru ya Uso Wake

jambo la dunia na Aakhirah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ukimuomba Allaah jambo katika mambo ya dunia na Aakhirah hakuna

ubaya. Kilichokatazwa ni kuomba cha dunia tu. Hilo ndo halijuzu.

80) Kuswalishwa Na Imaam Wa Kisufi Ambaye Msimamo Wake

Haujabainika

Page 60: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

60

Swali:

Kuna watu watatu, na aliyehifadhi Kitabu cha Allaah ndiye anaewasalisha. Ni

sahihi kwa kuwa kuna wanaosema ana taswawwuf pamoja na kuwa

hadhihirishi wazi katika ´Aqiydah ya Kisuufiy. Je tuswali nyuma yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa hamjabainikiwa na kitu, swalini nyuma yake. Ama mkibainikiwa na

kitu ni katika Masufi na mubtadi´ah, msiswali nyuma yake. Thibitisheni hilo.

81) Shubuha Za Waabudu Makaburi

Swali:

Katika utata wanaotaja waabudu makaburi wanasema sisi ni wapungufu,

wafanya madhambi na tunasikia haya kumuomba Allaah. Tunaomba kupitia

walii [kipenzi cha Allaah] kwa kuwa ana jaha na hadhi, vipi kuwapiga radd?

´Allaamah al-Fawzaan:

Waambie, je Allaah Kawaamrisha hili?! Leteni dalili kuwa Allaah

Kawaamrisha hili?! Hii ni sheria asiyoiruhusu Allaah. Ni bid´ah na wala

haijuzu. Allaah Kawaamrisha kumuomba moja kwa moja bila ya mkaakati.

Page 61: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

61

��م ادو� �أ$!�ب ��م و&�ل ر�

"Na Mola Wenu Anasema: Niombeni nitakuitikieni." (40:60)

Hakusema niombeni kwa kupitia kwa fulani. Wewe ni mwenye madhambi

kisha wewe unasikia haya?! Msikilie haya Allaah na umuombe Allaah

msamaha na utubu kwa Allaah na Allaah yu karibu Mwenye kujibu.

Ghafuuru Ar-Rahiym.

82) Waabudu Makaburi Lazima Wasimamishiwe Hoja!

Swali:

Baadhi ya mubtadi´ah na waabudu makaburi wanakataa ushirikina

unaofanywa kwenye makaburi; kama yafanywayo kwa al-Badawiy na

Karbala na sehemu zingine. Je nikiona video kwenye internet yenye mambo

kama hayo ya kishirki ili nimkinaishe na asadikishehilo, je nina makosa kwa

hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa atakinaika - Alhamdulillaah, lakini dhahiri ni kuwa hakinaiki. Lakini

wewe wajibu wako ni kumsimamishia hoja tu, aghlabu hawakinaiki ila -

Allaah Anajua zaidi, ni nadra sana.

Page 62: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

62

83) Kila Aliye Fikiwa Na Qur-aan Hoja Imemsimamia

Swali:

Kuna wanaosema ni lazima kuwasimamishia hoja waabudu makaburi, na

wala hawaisimamishi....

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndiyo, ni lazima [kwanza] kusimamisha hoja. Lakini hoja imesimamishwa

kwa Qur-aan Tukufu inayosomwa, wameiihifadhi, kuirudu na wanaisikiliza.

La sivyo, ipi faida ya Qur-aan?! Ingekuwa haisimamishi hoja. Ipi faida yake

baina ya watu?! Inasimamisha hoja.

C�� 9 و�ن�ھذا ا��رآن 2�ذر�م �� وأو*� إ�

“Na nimefunuliwa Qur-aan hii ili kwayo nikuonyeni nyinyi na kila

inayomfikia.” (06:19)

Aliye fikiwa na Qur-aan naye ni mwarabu, hoja imekwishamsimamia. Ama

akiwa siyo mwarabu, atarjumiwe maana ya Qur-aan mpaka imsimamikie hoja

na afahamu.

84) Qur-aan Yatosheleza Kuwa Hoja Kwa Kila Mtu!

Swali:

Page 63: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

63

Waabudu makaburi hawasimamishiwi hoja na mtu ni mtu, bali ni lazima awe

ni mwanachuoni na si kila mwanachuoni, bali ni lazima mjinga [huyo]

amsadikishe na amwamini. Je maneno haya ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hoja imekwishawasimamia - wa lillaahil hamd. Tangu iteremshwe Qur-aan

hoja imekwishasimama.

Muulizaji:

Na si mtu ni mtu atawasimamishia hoja, bali ni lazima awe ni mwanachuoni,

na si kila mwanachuoni.

´Allaamah al-Fawzaan:

Inatosheleza Qur-aan, inatosheleza Qur-aan. Yeye anasoma Qur-aan na ni

mwarabu, anafahamu maana ya lugha ya kiarabu; Anafahamu maana ya

kufuru, maana ya shirki. Anafahamu haya. Hoja imekwishawasimamia kwa

kufikiwa na Qur-aan, kwa lugha yake.

85) Kufasiri Kwa Ajili Ya Taazia (Kutoa Ole Kwa Wafiwa)

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 64: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

64

Safari kwa ajili ya kutoa pole, jambo hili halina asili. Mtoa pole hana haja ya

kusafiri, mtoa pole anaweza kuchukua simu na kumuongelesha kama

kwamba amehudhuria nao. Hakuna haja ya safari. Lakini akijikalifisha akenda

safari, huyu ni mgeni - huu ni ugeni na si utoaji pole. Huu ni ugeni kwa

walokuja.

86) Wanafunzi Wanaotoka Katika Miji Ya Kikafiri Na Kwenda Kusoma

Saudi Arabia Kisha Wanabaki Huko

Swali:

Baadhi ya wanafunzi wanakuja kutoka katika miji ya kikafiri na wanatafuta

elimu ya Kishari´ah kisha hawataki kurudi katika miji yao kwa ajili ya

Da´wah. Ipi nasaha zako kwa watu hawa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa wanaweza kuishi na kubaki hii ni Hijrah. Wamefanya Hijrah [kuhama].

Hili ni jambo zuri.

87) Utata Wa Waabudu Makaburi

Swali:

Wanapokumbushwa washirikina kuomba maiti, wanaturadi kuwa hakuna

tofauti kuomba maiti na aliye hai. Wanasema ni sababu katika sababu...

Page 65: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

65

´Allaamah al-Fawzaan:

Waulize, je kuna tofauti baina ya aliye hai na maiti au hapana? Je wanaweza

kweli kusema hakuna tofauti baina ya aliye hai na maiti?! Hawawezi kusema

hili. Waambie hivi. Je aliye hai na maiti ni sawa? Akisema ndiyo, atakuwa ni

mwenye kiburi. Akisema hawako sawa, aambiwe kuomba aliye hai si kama

kumuomba maiti. Kwa kuwa aliye hai anaweza kuombwa, na ama maiti

hawezi kuombwa. Hawezi hata kujiombea mwenyewe!!

88) Wanaolilia Umoja Wa Uislamu Bila Kujali ´Aqiydah

Swali:

Ipi hukumu ya kukimbiza watu kunako Da´wah katika Tawhiyd na kuali

"Watu wengi wanakubali kuwa hanapa mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila

Allaah."

´Allaamah al-Fawzaan:

Huku ni kukimbiza watu katika njia ya Allaah. Anakimbiza katika Da´wah ya

Allaah (Jalla wa ´Alaa). Haya ni mapote yamejitokeza [siku za] nyuma,

wanataka kuwafanya watu wawe wamoja bila ya kuangalia ´Aqiydah (itikadi)

zao. Na hili haliwezekani kamwe. Hawawezi watu kuwa wamoja ila kunako

´Aqiydah. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):

�م &وم �6 �"��ون !*$��م ���"� و&�و��م >!�3 ذ�ك �,��

Page 66: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

66

”Utawadhania kuwa wako pamoja, kumbe nyoyo zao ni mbali mbali. Hayo ni

kwa kuwa wao ni watu wasio na akili.” (59:14)

Hakuna kinachowafanya watu kuwa wamoja ila ´Aqiydah iliowajumuisha

Maswahaba, ikajumuisha mashariki na magharibi na ikajumuisha waarabu na

wasiyo kuwa waarabu. Chini ya Laa ilaaha illa Allaah. Haliwezekani hili. Kila

mmoja akibaki katika ´Aqiydah yake potofu, watafarakana hata wakiwa

pamoja kwa miili yao.

�م &وم �6 �"��ون !*$��م ���"� و&�و��م >!�3 ذ�ك �,��

”Utawadhania kuwa wako pamoja, kumbe nyoyo zao ni mbali mbali. Hayo ni

kwa kuwa wao ni watu wasio na akili.” (59:14)

89) Ni Kweli Kwamba Kuna Wenye Kuomba Kwenye Kaburi La Mtume?

Swali:

Mtu anaweza kuchukua kutoka katika kauli ya Mtume (swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) "Ee Allaah! Usiijalie kaburi yangu wathanan yenye kuabudiwa",

tunayoona leo wenye kuomba kwenye kaburi lake. Je, mtu anaweza kusema

kuwa wamemfanya wathanan...

´Allaamah al-Fawzaan:

Siyo kwenye kaburi lake, wanaofanya haya ni katika msikiti na si kwenye

kaburi lake Mtume. Kaburi la Mtume liko mbali nao kabisa limezuia na kuta

hawamuoni na wala hawajui alipo. Hili linafanywa msikitini.

Page 67: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

67

90) Hukumu Ya Kuapa “Wallaahi Kwa Nyumba Aliyojenga Allaah”

Swali:

Baadhi ya watu wanasema katika viapo vyao "Wallaahi, na nyumba

Aliyojenga Allaah." Je kauli hii ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu kuapa hivi. Asiape kwa nyumba. Siyo Allaah aliejenga nyumba!

Ilijenga Ibraahiym (´alayhis-Salaam) na waliokuja baada yake.

91) Vipi Ntamlingania Baba Yangu Aingie Katika Uislamu?

Swali:

Vipi ntamlingania baba yangu katika Uislamu, kwa kuwa hakubali nasaha

wala wito wa yeyote katika sisi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 68: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

68

Mchukue kwa urafiki, hekima na mawaidha yaliokuwa mazuri pole pole.

Huenda Allaah Akamuongoza. Usikatike moyo kwa kuongoka kwake. Jitahidi

kadiri na utavyoweza.

92) Vipi Muislamu Kafiri Asieswali Atatubia?

Swali:

Ikiwa mwenye kuacha swalah iliofaradhishwa kwa kukusudia inachukuliwa

ni ukafiri, vipi mwenye kufanya kitendo hichi atatubu kwa ukafiri huu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Asimamishe swalah. Atubu kwa Allaah na asimame kwa swalah katika

mustaqbal, ahifadhi swalah katika mustaqbal.

93) Vipi Kumsimamishia Mtu Hoja?

Swali:

Upi ufahamu wa kumsimamishia mtu hoja?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 69: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

69

Kusimamisha hoja ni kufikisha dalili kwa ufahamu wake, ikiwa ni katika wale

wenye kufahamu. Au kumtarjumia ikiwa hafamu kwa lugha yake.

94) Vipi Mtu Atamjua Mwanachuoni?

Swali:

Ulisema kuwa mtu aulize [dini yake] wanachuoni wanaojulikana

rabbaniyyuun na siyo wanachuoni wapotevu, vipi mtu atajua [kupambanua]

hawa na hawa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Watu wanawajua, elimu yao hujidhihirisha.Maneno yao, vitabu vyao,

hudhihiri hili. Pia mtu atajua kwa aliesoma kwake na kutakharaj kupitia

mikono yake, litajulikana hili. Hili lina msingi [chanzo] chake.

Muulizaji:

Je kule kuchaguliwa na kudhihiri, ni dalili [tosha] ya kuwa ni mwanachuoni

rabbaniy...

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Tunasema ni lazima kwanza ijulikane ni kwa nani alichukua elimu?

Wapi alisoma? Nani mashaykh wake? Pia tujue njia apitayo baada ya hapo. Je,

Page 70: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

70

anawafuata watu wa haki? Au ni mbabaishaji tu mwenye fikra mbovu? Ni

laziam tujue haya.

95) Jinsi Ya Kutangamana Na Makafiri Kazini

Swali:

Vipi ntatangamana na makafiri? Kwa kuwa wanachanganyika nami kazini

kila siku.

´Allaamah al-Fawzaan:

Ukipata kazi nyingine mbali nao ndio bora. La sivyo, fanya kazi yako na

waache katika kazi yao. Kila mmoja afanye kazi yake.

96) Wanafunzi Kupiga Radd Makundi Potevu Katika Miji Yao

Swali:

Mimi karibu nitaenda katika mji wakiarabu kumekithiri Masufi, je kuna

vitabu unaninasihi kuvisoma na kwenda navyo katika mji huo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 71: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

71

Chukua vya mukhtasari ambavyo vina radd kwa Masufi. Utavipata kwenye

maofisi.

97) ´Uzayr Ni Nani?

Swali:

Je ´Uzayr ni Mtume katika Mitume wa Banu Israaiyl, na kwa nini Mayahudi

walimuhusisha tu yeye kumtaja na hapana mwengine?

´Allaamah al-Fawzaan:

´Uzayr wametofautiana [wanachuoni] kuwa ni Mtume au ni katika watu

wema tu, kuna kauli mbili. Kauli yenye nguvu - Allaah Anajua zaidi - ni kuwa

si Mtume bali ni katika watu wema wa Banu Israaiyl. Alijishughulisha na

swalah na elimu mpaka wakampandisha. Bali yasemekana kuwa alikuwa

kahifadhi Tawrat ilihali Tawrat haiwezekani kuihifadhi. Lakini yeye Allaah

Alimpa uwezo na akaihifadhi.

98) Aina Mbali Mbali Za Tawassul Na Hukumu Zake

Swali:

Shaykh-ul-Islaam (rahimahu Allaah) katika kitabu chake "Tawassul wal-

Wasiylah" kataja katika maudhi kuwa tawasuli ni bid´ah, na katika maudhui

mengine kasema kuwa ni njia katika shirki na katika maudhui ya tatu kasema

kuwa ni shirki. Je hizi kauli zote ni zake?

Page 72: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

72

´Allaamah al-Fawzaan:

Mimi niliwawekea wazi hili. Niliwaambia kuwa mwenye kutawasali

ikimfanyia ´Ibaadah anaemtawasalia - kama kumchinjia, kumuwekea nadhiri

na kumuomba, hii ni shirki. Hii ni tawasuli ya shirki. Ama tawasuli isiyokuwa

na ´Ibaadah kwa huyo mwenye kumfanyia hio tawasuli, hii inachukuliwa ni

bid´ah. Na ni njia katika shirki.

99) Mzee ambaye Muusa Alikutana Naye Madyaan Ni Mtume Shu´ayb

(´alayhis-Salaam)?

Swali:

Mzee ambaye Muusa alienda kwake huko Madyaan ni Shu´ayb (´alayhis-

Salaam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijulikani - Allaah Ndiye Anajua zaidi. Baadhi ya watu wanasema kuwa

alikuwa ni Shu´ayb, lakini haikuwekwa wazi na sidhani kama ilikuwa ni

Shu´ayb. Allaah Hakusema kuwa ilikuwa ni Shu´ayb, bali ilikuwa ni mzee

mkubwa wakafanya na Muusa waliokubaliana. Ni mtu mwema katika watu

wa Madyaan.

100) Kuswali Nyuma Ya Mshirikina Kwa Kusoma Msikiti Wa Sunnah

Swali:

Page 73: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

73

Kwetu kumekithiri ushirikina wa sampuli mbalimbali na bid´ah na usomaji

wa burda misikitini na wanafunza wanafunzi, na tunapoongea nao

wanapinga. Ipi hukumu ya kuswali nyuma ya watu hawa kwa kuzingatia ya

kwamba hakuna msikiti wa Ahl-us-Sunnah mahala hapa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Usiswali nyuma yao. Usiswali nyuma ya mshirikina anaeabudu mawalii,

watu wema na Mtume usiswali nyuma yake. Swalah yako ni batili. Swali peke

yako nyumbani kwako au sehemu ingine. Na kama uko na ndugu zako

wengine au watu wa kawaida tafuteni mswalah mswali.

101) Asiyeweza Kulipa Kafara Ya Yamini Kwa Kulisha Anafunga

Swali:

Nina deni la kafara ya yamini, na nina baadhi ya mali ila niko nazo haja na

siwezi kuzitolea kafara. Je naweza kufunga au ni wajibu kwangu...

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio funga. Ikiwa huna kitu cha kutosheleza haja - kulisha, funga.

��� �� ��� ����م ��� أ��م

“Na asiyepata, afunge siku tatu.” (02:196)

Page 74: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

74

Na wewe hukupata kitu cha kutosheleza haja zako.

102) Shaykh Muhammad ibn ´Abdil-Wahhaab Si Bora Kuliko Wanavyuoni

Wa Madhehebu Manne

Swali:

Je ni sahihi kuwa watu wa Najdiy na Hijaaz wanamuadhimisha Imaam

Muhammad ibn ´Abdil-Wahhaab (rahimahu Allaah) zaidi kuliko

wanavyowaadhimisha maimamu wanne na wengineo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nani kasema haya? Mwenyewe alikuwa akiwafuata maimamu wanne na ni

katika wafuasi wao. Na anawasifia, kuwaombea na kuwaiga. Yeye si bora

kuliko maimamu wanne.

103) Kupita Mbele Ya Mwenye Kuswali Kwa Nguvu

Swali:

Mtu anaswali mbele yake kukapita mwanaume akamzuia lakini akapita, je

swalah yake inabatilika kwa hilo?

Page 75: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

75

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, swalah yake haibatiliki. Lakini aliepita anapata dhambi kubwa. Na

mwenye kuswali hana juu yake kitu kwa kuwa alimzuia lakini akapita.

Dhambi ni za yule aliepita.

[Anasema Mtume]:

"Angelijua yule mwenye kupita mbele ya mwenye kuswali ana nini juu yake,

ingekuwa bora kwake kusimama arubaini kuliko kupita mbele yake."

Swali La Pili:

Akipita mwanamke mbele ya mwanaume katika swalah yake, je swalah yake

inabatilika kwa hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kauli sahihi ni kuwa swalah yake haibatiliki; sawa akipita mwanamke, mbwa

wala punda isipokuwa makusudio hapa ni kupungua thawabu na si

kubatilika. Madhehebu ya Imaam Ahmad ndio inabatilika kwa kupita vitu

hivi vitatu; mwanamke, mbwa mweusi na punda. Lakini jumhuri - na ni moja

ya upokezi wa Ahmad, kuwa makusudio kubatilika hapa ni kupungua

thawabu. Bali madhehebu ya Ahmad wanaona kuwa swalah inabatilika kwa

kupita mbwa mweusi tu. Haibatiliki kwa kupita mwanamke na punda, bali ni

mbwa mweusi tu.

104) ´allaamah al-Fawzaan Kuhusu Answaar-us-Sunnah

Swali:

Kusifia kwako Jamaa´at Answaar-us-Sunnah wa Misr na Sudan ni sifa ya

watu maalumu au ni kwa yale wayafanyayo kwa sifa ya ujumla?

Page 76: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

76

´Allaamah al-Fawzaan:

Mimi sikutaja watu maalumu. Mimi nilisema Answaar-us-Sunnah. Answaar-

us-Sunnah wa mahala popote, sawa ikiwa ni Egypt au sehemu zingine.

Mwenye kuinusuru Sunnah sisi tunamsifia. Na watu hawa wamesimama kwa

Da´wah ya Tawhiyd na kukataza shirki katika mji ambapo kuna shirki.

Allaah Awajaze kheri. Wana juhudi. Mimi sikutaja watu bali nilitaja kundi tu.

105) Kuacha ´Amali Kwa Kukhofia Riyaa

Swali:

Mimi nakhofia riyaa kwa daraja ambayo siwezi hata kuswali kwa mtu.

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana ewe ndugu. Haijuzu kuacha amali na kusema mimi nakhofia riyaa.

Hili linatokana na Shaytwaan. Fanya amali na yatakase kwa Allaah (´Azza wa

Jalla). Usiache amali kwa kukhofia riyaa. Hili ndo alitakalo Shaytwaan

anakudanganya na kukwambia usiswali watu watadhani kuwaunajionyesha

kwao, usisimame usiku kwa kwa kuwa ni kujionyesha. Muombe Allaah kinga

kwa riyaa na shirki na endelea kufanya amali njema.

106) Kumwita Mtu Bwana

Page 77: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

77

Swali:

Watu wengi wanapotaka kumwita mtu wanamwambia "Ewe bwana!".

Inajuzu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kujuzu inajuzu, lakini kuacha [kusema hivo] ni bora zaidi.

107) Kumuambia Kafiri Ni Rafiki

Swali:

Ipi hukmu ya neno “rafiki” kumwambia kafiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu. Haijuzu kumwambia kafiri rafiki. Rafiki maana yake ni kipenzi.

Haijuzu hili.

108) Hukumu Unaposhtushwa Na Kitu Kuita “Ewe Mtume”

Swaali:

Page 78: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

78

Baadhi ya watu wakistaajabishwa na kitu wanasema “Ewe swalah ya

Mtume!”. Ipi hukumu ya kusema hivi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu hili. Kwanini ewe swalah ya Mtume? Hii ni du´aa na wito. Haijuzu.

Kwanini hasemi Ewe Allaa! Na anasema ewe swalah ya Mtume? Haijuzu

kusema ewe Mtume! Anamuomba Mtume. Haijuzu hili. Vipi ataomba ewe

swalah ya Mtume, anamuoba.

109) Hukumu Ya Kusema Mimi Ni Kwa Allaah Na Kwako

Swali:

Katika mji wetu kuna neno linasemwa kwenye ndimi nyingi za watu, nalo ni

“Mimi ni kwa Allaah na kwako”. Inajuzu kusema hivi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Haijuzu kwa "na" - haijuzu. Aseme kwa Allaah kisha/halafu kwako,

anaweza kusema hivi. Kwa kuwa kaweka neno "kisha", na neno kisha halileti

maana ya ushirikiano bali linaleta maana ya mpangilio.

110) Anaepinga Hadiyth Ya Shafaa´ah Anakuwa Kafiri?

Page 79: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

79

Swali:

Tunaweza kusema kwa mwenye kupinga Hadiyth ya Shafaa´ah [maombezi]

kuwa ni kafiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Tunasema kuwa kapotea. Ikiwa anajua kuwa maombezi ni haki na kuwa

yamethibiti [katika hadiyth] kisha akakataa, anakufuru kwa hilo. Ama

akidhani kuwa haikuthibiti au akafahamu vibaya, huyu ni mpotofu wala

hakufurishwi.

111) Hukumu Ya Kuapa Kwa Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

Swali:

Baadhi ya watu wanapotaka kutoka kwa mtu mwengine kitu wanamwambia:

“Naapa kwa Mtume fanya hivi”, katika kauli hii kuna kitu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, huku ni kuapa kwa asiyekuwa Allaah. Naapa kwa Mtume huku ni

kuapa kwa asiyekuwa Allaah. Lakini yawezekana kakulia katika hili na wala

hakusudiii kuapa bali ni mazowea ya ulimi. Lakini kwa vyovyote ni wajibu

kujiepusha na kusema hivi na kumkataza anaesema hivo. Wanaosema hivi

wengi ni watu wa Egypt, naapa kwa Mtume, naapa kwa Mtume. Na kuna

mmoja anasema "Naapa mimi ni Muwahhid!".

Page 80: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

80

Swali La Pili:

Je nimkataze anaesema hivi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, mbainishie mfunze. Ikiwa ni mjinga hajui mbainishie hili. Huenda

kaona watu katika mji wake wanasema akaishi katika hilo akadhani kuwa

inajuzu.

112) Anataka Kumpa Alieingia Katika Uislamu Tafsiri Ya Qur-aan

Swali:

Siku moja nilimfanyia da´wah asiyekuwa mwarabu kuingia katika Uislamu

akakubali. Akaniomba kumpa tafsiri ya Qur-aan Tukufu kwa lugha yake,

inajuzu kwangu kumpa tafsiri hii ambayo iko katika lugha yake? Au nimpe

kitabu kingine chenye mafunzo ya Uislamu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mpe tarjum ya maana ya Qur-aan Tukufu na itume kwa madu´aat wa nje

wampe ili afahamu maana ya Qur-aan. Ama Qur-aan yenyewe haifasiriwi

wala haijuzu na wala haiwezekani. Lakini kutarjum maana yake tafsiri hakuna

neno. Mpe tarjum ya tafsiri. Hii huitwa tarjum ya maana ya Qur-aan Tukufu,

wala hakusemwi tarjum ya Qur-aan Tukufu.

Page 81: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

81

113) Kumuomba Kafiri Msaada Kwa Ayawezayo

Swali:

Inajuzu kuwaomba makafiri msaada kwa ayawezayo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wakati wa haja na dharurah hakuna ubaya. Unapokuwa katika safari na

wewe unahitajia msaada huwezi kumwambia nisaidie? Hili ni jambo linajuzu.

Hili ni jambo mubaha.

114) Kuomba Msaada Kwa Majini

Swali:

Inajuzu kuomba msaada kwa majini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Visivyoonekana na waliokufa na majini haijuzu kuwaomba msaada.

Haijuzu kuomba kinga wala kuomba msaada kwa visivyoonekana na

waliokufa. Hili ni kwa haki ya mtu aliehai kahudhuria.

115) Je, Kufuru Ya Kimatendo Yaweza Kuwa Kubwa?

Page 82: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

82

Swali:

Je yaweza kuwa baadhi ya kufuru ya amali [matendo] kufuru kubwa kama

kusujudia sanamu na kumchinjia asiyekuwa Allaah?

´Allaamah al-Fawzaan:

A´udhubi Allaah. Hii ni shirki ndogo? Kusujudia sanamu ni shirki ndogo?

Kumchinjia asiyekuwa Allaah ni shirki ndogo? Hii ni shirki kubwa. Hizi ni

kufuru kubwa. Ni za matendo lakini

ni kufuru kubwa. Si kila kufuru ya matendo inakuwa ndogo. Baadhi yazo ni

kubwa.

116) Haijuzu Kuomba Maiti Kwa Kuwa Hana Anachokiweza

Swali:

Katika kauli ya Imaam Shawkaaniy (rahimahu Allaah), kasema inajuzu

kuwaomba msaada viumbe kwa yale mambo wayawezayo. Je haingii aliye hai

na maiti katika neno viumbe?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa maiti anaweza! Nani anadai kuwa maiti anaweza? Maiti hawezi kitu ni

maiti. Amesagika tena ni udongo!

Page 83: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

83

�����ا ��� � �5�+ون �4+!�� و& �3,01 �/. -,�+ إن )�#�ھ� & �%���ا د#�ء!� و�� ����ا �� ا�و��م ا6���

“Mkiwaomba hawasikii maombi yenu; na hata wakisikia hawakujibuni. Na

Siku ya Qiyaamah watakataa ushirikina wenu. Na hapana atakayekupa

khabari vilivyo kama Yeye Mwenye khabari.” (35:14)

Maiti ni udongo hawezi... Hata akisia du´aa yako hawezi kukujibu kwa kuwa

si muweza. Unamuomba maiti?! Subhaana Allaah! Wewe ni hai unamuomba

maiti. Huu ni upumbavu!

117) Sote Tuwaite Washirikina Kuwa Ni Washirikina

Swali:

Hukumu kwa mtu kuwa ni mshirikina ni kwa wanachuoni tu au hata kwa

wasiyokuwa wanachuoni watapomuona anaetumbukia katika shirki

wamwambie kuwa ni kafiri mshirikina?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwenye kudhihirisha shirki ni mshirikina. Mwenye kuomba asiyekuwa

Allaah, akachinja kwa asiyekuwa Allaah na akaweka nadhiri kwa asiyekuwa

Allaah huyu ni mshirikina. Kwa watu wa kawaida na wanachuoni. Mwenye

kusema ewe ´Aliy, ewe Husayn n.k huyu ni mshirikina. Kila mtu anajua kuwa

ni mshirikina.

Swali La Pili:

Mmoja katika wanafunzi anasema kuwa mwenye kutumbukia katika shirki

Page 84: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

84

anakuwa kafiri, lakini akasema mwenye kuhukumiwa kuwa ni mshirikina na

karitadi si kwa kila mtu hata wanachuoni bali hili ni kwa Qaadhi tu kwa

kuwa...

´Allaamah al-Fawzaan:

Hii sio hukumu. Hukumu ya kuritadi inakuwa kwa Qaadhi kwa kuwa

anaweza kuuawa. Lakini kusema hii ni shirki hili kila mmoja analisema. Kila

mwenye imani anasema hii ni shirki na haihitajii Qaadhi tu.

118) Je, Ni Kweli Kuwa Wengi Wa Washirikina Wa Leo Wanafanya Shirki

Kwa Kutokujua?

Swali:

Watu wanajua kuwa shirki ni haramu, lakini hawajui kuwa wayafanyayo ni

shirki na hilo inatokana na ujinga wao.

´Allaamah al-Fawzaan:

Shirki iko wazi. Hakuna chakutokujua shirki. Shirki ni kumuomba asiyekuwa

Allaah. Kuchinja kwa asiyekuwa Allaah, kuweka nadhiri kwa asiyekuwa

Allaah, kumuomba du´aa asiyekuwa Allaah na kuwachinjia maiti, Haya yako

wazi. Kila mmoja anayajua haya.

Muulizaji:

Page 85: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

85

Na baadhi yao ni watu wa kawaida na wazee...

´Allaamah al-Fawzaan:

Watu wa kawaida na wazee wamesikia kuwa hii ni shirki kwa walinganizi,

katika vitabu, katika vyombo vya habari. Wamesikia hili. Lakini hawataki

kuachana nayo. Watu hawa imekwishawasimamikia hoja. Wewe wataka

kuwasimamishia hoja vipi, uiingize imani katika nyoyo zao?? Hapana! Hoja ni

wewe kuwafikishia. Wamekwishasimamishiwa hoja, lakini wamekataa.

Tuwafanye nini?

119) Nina Miaka 17 Wazazi Wangu Hawaswali Alfajiri, Unaninasihi Vipi?

Swali:

Mimi nina miaka kumi na saba na sina ndugu wakubwa kuliko mimi na

wazazi wangu hawaswali swalah ya alfajiri ila mara chache tu na wanaiswali

kabla ya kwenda kazini, na sina mtu ataeniamsha katika swalah ya alfajiri. Ipi

nasaha yako kwangu na kwa wazazi wangu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nasaha yangu kwao watubie kwa Allaah na wamuombe msamaha Allaah na

waswali swalah ya alfajiri. Hawana isipokuwa Allaah. Watakuwa wamebaki

na nini wakiacha swalah? Watakuwa wamebaki na nini katika dini?

Watakuwa hawakubaki na kitu. Wasaidie na uwakumbushe. Ama wewe swali

na jamaa´ah, swali uamke. Na ninakunasihi ikiwa utaweza kuhama na kuishi

nje yao ni wajibu kwako kuishi nje yao ikiwa hawatokubali nasaha.

Page 86: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

86

120) Kulipa Swalah Za Rawaatib Kinyume Na Wakati Wake

Swali:

Leo nilikuwa Hospitali na baba yangu alikuwa mgonjwa nami, nikaswali

dhuhr Hospitali na wala sikuswali Rawaatib [sunnah] si ya kablia wala baadia

kwa kushughulishwa na maradhi ya baba yangu. Je inajuzu kuzilipa hivi sasa

kwa kuwa mimi nimekuwa mwenye kuhifadhi sunnah hizi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Umekufutu wakati wake. Hizi ni naafilah na zimekufutu wakati wake.

Usizilipe.

121) Baada Ya Siku Tatu Ndo Kajua Kuwa Aliswahi Kinyume Na Qiblah,

Alipe?

Swali:

Kuna mtu kaswali kinyume na qiblah na kajua hilo baada ya kupita siku tatu,

je alipe swalah hizo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 87: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

87

Ikiwa yuko katika bari na wala hajui kilipo qiblah akajitahidi akaswali swalah

yake ni sahihi. Ama kama yuko katika mji na kuna misikiti na kuna watu

wakuuliza akaswali kinyume na qiblah alipuuza ni lazima azirudi [kuziswali].

122) Kuomba Viumbe Waliyo Hai Wakuombee Du´aa Ni Makosa Na

Udhaifu?

Swali:

Kuna mtu anaesema kuwa kuwaomba viumbe wakuombee du´aa ni udhaifu

wa kumtegemea Allaah na si katika ukamilifu wa kumtegemea na kuegemea

Kwake. Je kauli hii ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Yaani ´Umar (radhiya Allaahu ´anhu) ana udhaifu wa kumtegemea Allaah

alipomuomba ´Abbaas amuombee du´aa? Maswahaba (radhiya Allaahu

´ahum) walipomuomba Mtume awawaombee wana udhaifu wa kumtegemea?

Hapana! Hili ni kutokana na uwezeko mkubwa wa kujibiwa, kwa sababu

du´aa ya mja mwema kuna uwezekano mkubwa wa kujibiwa. Na si kuwa

unamtegemea yeye, bali ni kutokana tu na uwezekano mkubwa wa kujibiwa.

123) Hukumu Ya Kuambizana “Ijumaa Yenye Baraka” Siku Ya Ijumaa

Swali:

Page 88: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

88

Inajuzu kwa mtu kumwambia mwengine siku ya ijumaa kumwambia:

"Ijumaa yenye baraka"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, hili halikuthibiti kupeana hongera siku ya ijumaa. Wasipeane

pongezi siku ya ijumaa, halikuthibiti. Hata siku ya Idi hapakuthibiti chochote,

lakini ni kitu kimezoeleka tu na watu. Na imaam Ahmad anasema mimi sianzi

kwa kutoa hongera lakini kwa ataeanza kunipa nitamrudishia.

124) Hukumu Ya Kutawassul Kwa Jaha Ya Mtume (´alayhhis-Salaam)

Swali:

Je inajuzu kutawasuli kwa Allaah kwa jaha ya Mtume (swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili halikuthibiti ni bid´ah. Hii ni Hadiyth ya uongo kama mlivyoona katika

[kitabu] "Tawassul wal-Wasiylah" cha Shaykh-ul-Islaam ibn Taymiyyah.

Kutawasuli kwa jaha yake ni jambo halina dalili. Ni bid´ah.

125) Hukumu Ya Kuwaombea Du´aa Watu Wa Bid´ah

Page 89: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

89

Swali:

Je inajuzu kuwaombea du´aa watu wa bid´ah kwa rahmah, msamaha na

Pepo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa ni Waislamu na bid´ah zao hazikuwatoa katika Uislamu; wanasihiwe,

walinganiwe waache bid´ah na waombewe pamoja na Waislamu kwa ujumla

na watu wa Tawhiyd. Ama zikiwa bid´ah zao zimechanganyika na bid´ah na

shirki zinawatoa katika Uislamu, hapana [wasiombewe]. Kwa mfano du´aa

badala ya Allaah, kuabudu makaburi hizi ni bid´ah za shirki. Kujengea

makaburi kwa ajili ya kuyaabudu na kuyaadhimisha.

126) Je, Kutamka Shahaadah Tu Bila ´Amali Inatosha?

Swali:

Vipi kumradi ambae anatumia hoja Hadiyth ya Mtume (swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) nayo ni:

"Atakayesema Laa ilaaha illa Allaah [ataingia Peponi]"

Anasema muhimu ni kutamka tu na si matendo yanayostahiki.

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 90: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

90

Mtume (´alayhis-Salaam) hakusema Laa ilaaha illa Allaah akanyamaza.

"Atakayesema Laa ilaaha illa Allaah akiwa mkweli ndani ya moyo wake."

"Atakayesema Laa ilaaha illa Allaah na akakufuru kwa vinavyoabudiwa

kinyume ya Allaah."

"Allaah Kamharamishia Moto atakayesema Laa ilaaha illa Allaah akitafuta

kwa hilo Uso wa Allaah."

Vipi wewe ndugu utachukua Hadiyth moja na uache Hadiyth zingine zote?

127) Hukumu Ya Anaesema Laa Ilaaha Illa Allaah Ila Hakufuru

Vinavyoabudiwa Kinyume Na Allaah

Swali:

Katika kauli ya Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Atakayesema Laa ilaaha illa Allaah na akakufuru vinavyoabudiwa kinyume

na Allaah imeharamika kwake mali yake na damu yake."

Ina maana ya kwamba atakayesema Laa ilaaha illa Allaah na asikufuru

vinavyoabudiwa badala ya Allaah, mtu huyo haiharamiki kwake mali yake na

damu yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, liko wazi hili ni maneno ya Mtume. Kuwa atayesema Laa ilaaha illa

Allaah na wala asikufuru kwa vinavyoabudiwa badala ya Allaah, huyu

hakutoka katika shirki. Allaah (Jalla wa ´Alaa) Anasema:

Page 91: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

91

8�� �� ��� �5�+ ���>�;�ت و�9

“Basi anayemkufuru Shaytwaan na akamuamini Allaah.” (02:256)

Katanguliza kwanza kuyakufuru matwaghuut [mashaytwaan] kabla ya

kumuamini Allaah. Kwa kuwa imani ya kumaumini Allaah haisihi ila kwa

sharti mpaka uanze kukufuru mashaytwaan. Ni kama Laa ilaaha illa Allaah,

ni kukanusha na kuthibitisha.

128) Wana Ada Wakiona Maiti Usingizi Wanamchinjia Na Kualika Watu

Walimani

Swali:

Katika kabila yetu kuna ada nayo ni anapoona mmoja wetu ambae yu hai mtu

maiti usingizini, basi humchinjia maiti huyu na kuwaalika watu katika

waliymah huu kisha wanamuombea [du´aa] maiti. Ipi hukumu ya kitendo

hichi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili halijuzu, hili halijuzu. Na ndoto isizushiwe ahkam za Kishari´ah za

kuchinja, hii ni hukumu ya Kishari´ah. Haijuzu kuchinja kwa mujibu wa

ndoto au kwa yanayofanana na hayo. Haijuzu. Lakini kama kamuona maiti

[usingizini] na akakwambia kuwa ana deni la fulani na akamnasihi na umlipie

deni lake, hakuna ubaya. Au akakunasihi umuombee, hakuna ubaya. Ama

anakuomba umchinjie, hili halijuzu.

Page 92: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

92

129) Kumuomba Allaah Kwa Kusem “Ewe Wa Allaah”

Swali:

Ipi hukumu kauli baadhi ya watu "Ewe Uso wa Allaah!" Inajuzu kusema hivo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu kumuomba kwa Sifa. "Ewe rehema za Allaah!, ewe Uso wa Allaah!."

Inatakikana kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Ewe Allaah, na mtu

anatawasuli Kwake kwa Sifa au Jina Lake.

130) Hukumu Ya Mtoto Kushtushwa Na Kusema “Ewe Mama”

Swali:

Baadhi ya watu na khasa watoto wadogo wanapoona kitu kinachowatia khofu

wanamwita mama yao [Ee mama!] wala hakusudii hilo bali ni kitu

kinachomtoka tu kwenye ulimi na mama yake anaweza kuwa hayupo, je

huchukuliwa hii ni katika kuomba badala ya Allaah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu ni mtoto asikalifishwe. Na wala hamuoni mwengine anayeweza

kumwangalia kwa mambo mbalimbali zaidi ya mama yake. Haya ndio

makusudio yake.

Page 93: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

93

131) Watu Wataotoka Motoni Bila Ya Kufanya Kheri Yoyote

Swali:

Vipi kumpiga radd anaetumia hoja Hadiyth ya Shafaa´ah [maombezi] "Na

atatoka Motoni ambae hakufanya kheri yoyote."

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio ni katika watu wa Tawhiyd na kafa hakuweza kufanya amali. Alisema

Laa ilaaha illa Allaah akauawa au akafa kabla ya kuweza kufanya amali.

Huyu ni katika watu wa Tawhiyd na ni mwenye udhuru kwa kuacha amali

kwa kuwa hakuweza kufanya. Ama kwa yule aliyeweza kuishi miaka mia

haswali wala hafungi, kisha basi anasema tu Laa ilaaha illa Allaah. Kisha

wasema huyu ni katika watu wa Peponi? Na huyu eti atapata maombezi [ya

Mtume]? Nani anaedai hivi? Kama niwaambiavyo kila siku enyi ndugu

msichukue Hadiyth moja na mkaacha Hadiyth zingine zote. Lazima

zijumuishwe Hadiyth na zipeane nguvu. Huku ni kurejea [dalili] zisizo wazi

na kuacha zilizo wazi. Ama kuchukua Hadiyth moja isiyo wazi na ukaacha

Hadiyth zilizo wazi, huu ni mtindo wa watu wapotevu.

� ا�=� �>� ?3� ?��4( ���,��ن �� A�ز �C��DE F� �

“Ama wale ambao nyoyoni mwao umo upotovu wanafuata zile za mifano

[zisizo wazi].” (03:07)

Mpaka Aliposema:

Page 94: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

94

� #3� ر�3� � .! ?� �3�ا��Jن �F ا��D� �6���ن آ وا�+

“Na wale waliobobea katika ilimu husema: Sisi tumeziamini ZOTE.” (03:07)

Zilizo wazi na zisizo wazi.

� #3� ر�3� � .!

“ZOTE zimetoka kwa Mola Wetu.” (03:07)

Vipi utachukua upande huu na uache upande mwingine? Kama huku

sikufuata matamanio ni nini? Na huu ndo mtindo wa watu wapotofu, Allaah

Atukinge. Hadiyth ni lazima zioanishwe na zinapeana nguvu na zinaweza

kufutwa kwa kuoanishwa hivyo. Ni lazima kufanya hivyo na hii ndio njia ya

wanachuoni waliobobea katika elimu. Ama wenye kujifunza hawajui mambo

kama haya.

� #3� ر�3� � .! ?� �3�ا��Jن �F ا��D� �6���ن آ وا�+

“Na wale waliobobea katika ilimu husema: Sisi tumeziamini ZOTE.” (03:07)

Lakini mwenye kujifunza hajui mambo haya masikini. Hali kadhalika kwa

yule mwenye matamanio hufuata yale yanayoafikiana na matamanio yake tu

na huacha yale yanayoenda kinyume na matamanio yake.

132) Hukumu Ya Wazazi Wasiofahamu Kiarabu Wanaita “Ewe Mtume Wa

Allaah!”

Page 95: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

95

Swali:

Wazazi wangu wanatoka Pakistan na wala hawafahamu lugha ya kiarabu na

mara nyingi wanasema "Ewe Mtume wa Allaah!". Je niwape udhuru kwa hili

au nifanye nao nini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu kuwapa udhuru kwa hili. Wabainishie kwa lugha yao. Kama

unafahamu lugha yao wabainishie kuwa hili halijuzu.

133) Mume Anamlingania Mke Wake Katika ´Aqiydah Ya Ash´ariyyah, Mke

Amtii?

Swali:

Ikiwa mume anamwita mke wake katika ´Aqiydah ya Ash´ariyyah na

anafanya siri kwa hilo. Upi wajibu wa mke na anakhofia ´Aqiydah yake na...

´Allaamah al-Fawzaan:

Wajibu kwake ni kumuasi. Ni wajibu kwake kwanza kumbainishia kuwa hili

ni kosa na kuwa Ashaa´irah wako katika makosa. Akikubali sawa la sivyo

usimtii kwa hilo. Baki katika ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah.

Page 96: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

96

134) Hukumu Mwanamke Kusoma Qur-aan Kwa Mashaykh Wanaume

Swali:

Je mwanamke anaweza kusoma Qur-aan kwa Shaykh mpaka afikie kiwango

cha kuweza kusoma?

´Allaamah al-Fawzaan:

Leo - Alhamduli Allaah, wanawake mahafidhi wanaojua kusoma ni wengi.

Asome kwa mwanamke.

135) Acheni Falsafa, Mwenye Kufanya Shirki Ni Mshirikina!

Swali:

Wanasema wanachuoni "sisi tunamhukumu mtu kwa uinje wake", vipi

tutajumuisha hili na mwenye kusema "mwenye kutafuta baraka udongoni

kwenye kaburi ni shirki kubwa akikusudia [akiamini] kuwa udongo huyo

unanufaisha la sivyo itakuwa ni shirki ndogo.

´Allaamah al-Fawzan:

Hizi ni falsafa. Mwenye kudhihirisha shirki tutamhukumu kwa hilo bila

falsafa kama hizi. Eti akiamini, akisema nadkhalika. Nani mwenye kudai hivi?

Page 97: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

97

136) Hukumu Ya Kuweka Nadhiri Kwa Asiyekuwa Allaah

Swali:

Mwenye kuweka nadhiri kwa asiyekuwa Allaah anakuwa mshirikina kwa

kauli yake hiyo au kwa kitendo chake hicho?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa yote mawili, kwa kauli yake na kwa kitendo chake. Kwa kuwa nadhiri ni

´Ibaadah na haiwekewi mtu mwengine ila Allaah (´Azza wa Jalla).

137) Hukumu Ya Kuitamidi Kwa Allaah Kisha Kwa Kiumbe

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kusema "mimi naitamidi kwa Allaah kisha kwako"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna ubaya. Naitamidi kwa Allaah kisha kwako, umemfanya ni

wakufuatia na hukumfanya akawa ni mshirika wa Allaah (´Azza wa Jalla).

Page 98: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

98

138) Hukumu Ya Kutosoma Kwa Tajwiyd

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kutochunga ahkaam za kisomo na Tajwiyd kama yule

asiyeleta muduud, inajuzu kuswali nyuma yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ewe ndugu kinachotakikana ni Tajwiyd ya nahwu, asilete kisomo ambacho

kitaenda kinyume na nahwu. Ama zaidi ya hapo ni katika kule kukamilisha tu

na hakudhuru. Ukikhalifu haidhuru. Muhimu ni kuchunga nahwu kwa lugha

ya Qur-aan iliotemreka kwayo. Achunge sehemu kama ya marfuu´, ahifadhi

majruur, manswuub na majzuum. Hili ndo muhimu. Hii ndio Tajwiyd

inayohitajika. Ama Tajwiyd kama ya Idghaam, Ghunnah na mduud hizi ni

kwa kukamilisha tu na si lazima.

139) Kumuomba Mtu Ni Vibaya?

Swali:

Nilikuwa nikimuomba mmoja katika watu, vipi nitubie kwa hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 99: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

99

Swali haliko wazi. Ikiwa anakusudia kuwa alikuwa anamuomba kwa mambo

ambayo anayaweza hakuna ubaya kwa hilo. Ama ikiwa alikuwa anamuomba

mambo ambayo hayawezi mwengine isipokuwa Allaah hili halijuzu. Ni juu

yake kufanya tawbah kwa Allaah na kuacha kitu hichi.

140) Nilikuwa Na Deni La Mtu Simjui Ama Sasa Nimejua, Nimpe Au

Nitoe Swadaqah?

Swali:

Baba yangu alikuwa na deni na wala sikuwa namjua mwenye deni hilo, kwa

sasa nimemjua. Nitoe swadaqah kwa mwenye deni hilo au nifanye nini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kama umemjua sasa mkabidhi kama yu hai. Na kama kishafariki, wape

warithi wake na usizitoe swadaqah. Isipokuwa tu kama hukumpata yeye na

hukupata mrithi wake, hapo utazitoa swadaqah.

141) Tahadhari Na Kundi La Qur-aaniyyah Linalopinga Sunnah!

Swali:

Page 100: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

100

Je yawezekana Qur-aan na Sunnah vikatofautiana na akasema mtu "Sichukui

kinachoenda kinyume na Qur-aan"? Je vipi kauli hii ni kufuru?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwenye kusema hivi hayuko mbali na kufuru. Kwa kuwa anampinga Mtume

(swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa kukataa Hadiyth zake. Na kuna pote

maarufu linaitwa Qur-aaniyyah wanakataa Sunnah. Na wakwanza wao

ilikuwa ni Makhawaarij, Makhawaarij wanapinga kuifanyia Sunnah kazi. Hili

halijuzu. Sunnah ya Mtume ni hoja baada ya Qur-aan. Anasema Allaah (Jalla

wa ´Alaa):

�C�اK�� ?3# �!�CK ����ل �J=وه و و�� آ)�!� ا�+

“ Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anachokukatazeni jiepusheni

nacho.” (59:07)

�C�D# 3�كD���ل �6� أط�ع هللا و�� )O�� ��� أر � �>S ا�+ ��U�5V

“Mwenye kumtii Mtume basi ndio amemtii Allaah. Na anayekengeuka, basi

Sisi hatukukutuma wewe uwe ni mlinzi wao.” (04:80)

��ل �� أC�� ا�=�� آ�3�ا أط���ا هللا وأط���ا ا�+

“Enyi mlioamini! Mtiini Allaah, na mtiini Mtume.” (04:59)

��واC( ه��وإن )>�

“Na mkimtii yeye mtaongoka.” (24:54)

��ل ��V+( ��D��ن وأط���ا هللا وا�+

Page 101: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

101

“Na mtiini Allaah na Mtume ili mpate kurehemewa.” (03:132)

Ni lazima kumtii Mtume na kuzifanyia kazi Hadiyth zake sahihi baada ya

Qur-aan Tukufu. Na Hadiyth za Mtume ndo zinaifasiri Qur-aan, zinaiweka

wazi na zinaitolea dalili. Zenyewe ndo zinaibainisha Qur-aan. Kwa kuwa

Allaah Kasema:

�C��ل إ XK ���,�� �3D�س � +! وأ3�XK� إ0�� ا�=

“Nasi tumekuteremshia wewe Ukumbusho ili uwabainishie watu yaliyo

teremshwa kwao.” (16:44)

Atabainisha kwa nini?

Atabainisha kwa Sunnah, Sunnah za Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam). Wapi tumetoa kuwa swalah ya dhuhr na ´asr ni raka nne na maghrib

ni tatu na fajr ni mbili, wapi tumetoa haya? Je ni katika Qur-aan?

Ni katika Sunnah. Wapi tumetoa kipimo na kiwango cha zakaah na mali

ambazo ni wajibu kutoa zakaah?

Tumetoa katika Sunnah. Qur-aan iko kwa jumla na inabaishwa na Sunnah.

Huyu anaesema maneno haya haifanyii hata Qur-aan kazi. Angekuwa

anaifanyia Qur-aan kazi, angechukua Kauli ya Allaah:

�C�اK�� ?3# �!�CK ����ل �J=وه و و�� آ)�!� ا�+

“Na anachokupeni Mtume chukueni, na anachokukatazeni jiepusheni nacho.”

(59:07)

Kasema Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Ee tambueni! Mimi nimepewa Qur-aan na mfano wake pamoja." Na Allaah

(Jalla wa ´Alaa) Kasema:

Page 102: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

102

OV�� FV�ى إن ھ� إ& وC�3>] #� ا� �� و

“Wala hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni ufunuo [wahyi] ulio

funuliwa.” (53:03)

Sunnah ni wahyi [utemremsho] kutoka kwa Allaah. Je unakadhibidha wahyi?

Jambo hili ni hatari sana.

142) Makataza Ya Wanafunzi Kuwapa Zawadi Waalimu Zao

Swali:

Kuna dada anauliza. Je inajuzu kwa wanafunzi wanawake kumpa zawadi

mwalimu baada ya kumaliza mwaka wa masomo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Wanafunzi wanawake wasimpe zawadi mwalimu. Kwa kuwa hili

lina tuhuma kwa mwalimu akikubali zawadi ina maana kutakuwepo

upendeleo fulani kwao. Hii ni katika rushwa, hili linangia katika rushwa.

143) Imaam ash-Shawkaaniy Ni Imaam Wa Ahl-us-Sunnah

Swali:

Page 103: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

103

Ipi sababu ya Zaydiyyah kumchukua imaam Shawkaaniy na kujinasibisha

kuwa ni katika wanachuoni wao?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana si katika maimamu wao. Ni katika wanachuoni wa Ahl-us-Sunnah. Ni

katika wanachuoni wa Ahl-ul-Hadiyth.

144) Ni nani ´Abdul-Qadir al-Jaylaaniy?

Swali:

Ni nani ´Abdul-Qadir al-Jaylaaniy?

´Allaamah al-Fawzaan:

´Abdul-Qadir al-Jaylaaniy ni imamu miongoni mwa maimamu wa Ki-

Hanbaliy, ni mtu mwema mcha Mungu. Lakini wanamdanganyia na

kumsingizia mambo ambayo alikuwa nayo mbali kabisa.

Swali La Pili:

Na ni nani al-Badawiy?

Page 104: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

104

´Allaamah al-Fawzaan:

Al-Badawiy kilicho dhahiri ni kuwa ni mtu wa Makkah alienda Egypt.

Inasemekana kwa alibaki muda mrefu msikitini siku ya ijumaa bila ya

kuchoshwa hivyo akawa walii, kwa kuwa mawalii ndo hawapati machovu

bila kujali wanachokifanya. Hivyo watu wakamuabudu badala ya Allaah.

145) Waabudu Makaburi Wanaotumia Hoja Aayah Katika Suurat-ul-Kahf

Swali:

Katika suurat-ul-Kahf Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Hakuwakataza

waliofanya makaburi kuwa misikiti. Vipi tutaradi shubuha [utata] huu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Subhaana Allaah! Hakukataza?

&�ل ا��ذ�ن ���وا 3� أ�ر

“Wakasema walioshinda katika shauri yao.” (18:21)

Haya ni makatazo, "walioshinda katika shauri yao". Wametumia nguvu zao

bila ya dalili wala hoja. Ni kushinda tu [kwa jeuri].

�دا&�ل $ 1ذن� ���م �� ا��ذ�ن ���وا 3� أ�رھم ��!�

Page 105: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

105

“Wakasema walioshinda katika shauri yao: "Bila ya shaka tutawajengea

msikiti juu yao." (18:21)

Wewe husomi tafsiri ya Qur-aan na wala hujui kitu.

146) Inajuzu Kusema Allaah Na Mtume Wake Ndio Wanajua?

Swali:

Akiulizwa mtu kitu fulani anasema "Allaah na Mtume Wake ndo wanajua."

Inajuzu kusema hivi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Kusema hivi ilikuwa wakati Mtume alikuwa bado yu hai (swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam), kulikuwa kukisemwa "Allaah na Mtume Wake

ndo wanajua. Ama baada ya kufa Mtume, kunasemwa "Allaah ndo Anajua

zaidi." Yatosha!

147) Aliechelewa Swalah Ya Istisqaa Upi Wajibu Wake?

Swali:

Page 106: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

106

Nikiingia kwenye mswallah [aina ya msikiti mdogo] na watu

wamekwishaswali swalah ya Istisqaa [ya kuomba mvua] na imaam anatoa

khutbah, nawajibika kufanya nini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Utakaa na kusikiliza khutbah. Yakutosheleza kufanya hivi Inshaa Allaah.

148) Nasaha Kwa Anaekhofia Riyaa

Swali:

Mimi mara nyingi nakhofia riyaa na huwa na shaka kunako amali zangu, ipi

nasaha zako kwangu kwa hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wasiwasi huu unatokana na shaytwaan. Fanya amali zako na itakase nia yako

kwa Allaah na wala usijali wasiwasi wa shaytwaan.

149) Imaam Kukariri Aayah Fulani Anaposalisha Jamaa´ah

Swali:

Page 107: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

107

Imaam msikitini kwetu anaposoma suurat-ul-Maa´uun, afikapo kwenye Kauli

ya Allaah (Ta´ala):

�و�ل �7��+��7ن

“Basi, ole wao wanaosali.” (107:04)

Anaikariri mara mbili, mara ya kwanza anasimama mwisho wake na mara ya

pili anafuatisha na aayah ya kufuata. Anafanya hivyo kila siku. Jambo hili

linafaa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Jambo hili halifai. Asome suurah bila ya kukariri.

150) Anamtangulia Kumsalia Maiti Kabla Ya Imaam Kusalisha

Swali:

Ipi hukumu ya kusimama baadhi ya watu kuwasalia maiti kabla hata imaam

hajasimama na kuanza kusalisha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 108: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

108

Hizi ni katika tabia mbaya. Haraka hizi hazifai. Haifai kwake kuja msikitini na

kumtangulia imaam akaanza kumsalia maiti, haifai. Amekuja msikitini

amfuate imaam. Subiri ndugu yangu, subiri! Mpaka atapokuja imaam uswali

nae.

151) Kuelekea Kaburi La Mtume (´alayhis-Salaam) Msikitini Na Kumuomba

Swali:

Nimeona mmoja wa waabudu makaburi anaomba kwenye kaburi la Mtume

(swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nikamkataza akasema "mimi namuomba

Allaah msikitini, nyumbani kwangu na kwenye kaburi la Mtume (´alayhis-

Salaam) na kila mahala.

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Kwenye kaburi la Mtume hapana usimuombe Allaah. Kaa msikitini

wa Mtume elekea Qiblah na umuombe Allaah (´Azza wa Jalla), hakuna

anaekukataza. Ama kuelekea kaburi na kuomba hili halijuzu. Ikiwa

unamuomba Mtume hii ni shirki, ikiwa unamuomba Allaah kwenye kaburi la

Mtume hii ni bid´ah na ni njia inayopelekea katika shirki.

152) Mgonjwa Anaepata Tabu Kutia Wudhuu Afanye Nini?

Swali:

Page 109: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

109

Mgonjwa mwenye maradhi awezae kuweka kutawadha na kujipangusa baada

ya kutia wudhuu lakini kwa kufanya hivyo anapata tabu, je anaweza

kutayamamu?

´Allaamah al-Fawzaa:

Ikiwa kuna ambaye anaweza kumsaidia ni wajibu kufanya hivyo, kwa kuwa

atamsaidia kutia wudhuu. Ama ikiwa hana wa kumsaidia na hawezi

kutawadha kwa maji, atayamamu.

153) Msafiri Anaejua Lini Atarudi Kwao Hachukui Hukumu Za Msafiri

Swali:

Mtu mwenye kuja Saudi Arabia kufanya kazi ana hukumu sawa na msafiri

kwa kuzingatia ya kuwa kazi yake imewekea muda mwaka mmoja?

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu si msafiri. Ni msafiri njiani - anapotoka na kule anapokwenda. Ama

muda wake wa kubaki Saudi Arabia kwa ajili ya kazi mwaka au zaidi huyu ni

mkazi na si msafiri. Atatimiza swalah, atafunga Ramadhaan. Ahkam zake zote

ni kama za wakazi.

Page 110: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

110

154) Anaemwendea Mpiga Ramli Kisha Akatubia Swalah Zake

Zitakubaliwa?

Swali:

Hadiyth ya Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Mwenye kumwendea mpiga bao (mpiga ramli) akamuuliza kuhusu jambo

lolote, kisha akamsadiki aliyoyasema, hazikubaliwi Swalah zake kwa siku

arubaini” [Muslim]

Je vipi mtu akitubia Allaah Atakubali swalah zake hizi au hukumu itabaki

kama ilivyo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Allaah Ndiye Mwenye kujua zaidi. Tunaichukulia Hadiyth kama ilivyokuja.

155) Lini Mtu Anaweza Kuingia Peponi Bila Ya ´Amali?

Swali:

Hadiyth ya al-Batwaaqah. Hii si dalili ya kuwa mwenye kusema Laa ilaaha

illa Allaah ataingia Peponi hata kama hakufanya amali yoyote njema?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 111: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

111

Ikiwa hakuweza kufanya amali. Akiisema kwa kuiamini na mwenye yakini na

hakuweza kufanya amali, kauawa au akafa kabla ya kupata fursa ya kufanya

amali ataingia Peponi. Ama akiacha amali kwa khiari yake na hakufanya

chochote, huyu si muumini. Kwa kuwa Laa ilaaha illa Allaah si kutamka tu

kwa ulimi, ina masharti yake na maana yake sahihi. Enyi ndugu! Msichukue

dalili moja ya jumla na mkaacha dalili zilizofafanua, za wazi na nyinginezo

zilizokuja kwenye Hadiyth nyingine, msifanya hivyo. Hadiyth kama hizi

lazima zirejelewe Hadiyth zilizoweka wazi suala hili. Ama kuchukua tu

Hadiyth moja na ukaacha Hadiyth zingine, hii ni njia ya watu wapotevu.

Ambao wanafuata [dalili] zisizowazi.

156) Je, Athari Ya Mtume (´alayhis-Salaam) Inapatikana Mpaka Hivi Leo?

Swali:

Athari ya Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) je, ipo mpaka hivi leo

kama nguo zake na nywele zake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wametoa wapi? Nani awezae kuthibitisha kuwa kweli ni nguo za Mtume na

nywele za Mtume nk? Nani awezae kuthibitisha hili? Huu ni ukhurafi

usiokuwa na asli.

157) Ni Sahihi Muadhini Kusema Haqqan Laa ilaaha illa Allaah?

Page 112: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

112

Swali:

Muda si mwingi nimesikia kwenye idhaa moja muadhini alipomaliza kutoa

adhaana akasema "Haqqan Laa ilaaha illa Allaah" [ni haki, hapana mungu

apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah]. Je kauli yake hii si makosa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana si makosa. Hapana mungu apasaye kuabidiwa kwa haki ila Allaah, ni

haki.

158) Mgonjwa Anaruhusiwa Kujumuisha Swalah Na Haruhusiwi

Kuzifupisha

Swali:

Baba yangu ana maradhi mazito hivyo anashindwa kuweka wudhuu katika

kila swalah, je anaweza kujumuisha swalah na kufupisha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kufupisha hapana, hakuna kufupisha [swalah] ila katika safari tu. Ama

kujumuisha akihitajia hilo mgonjwa anaweza kufanya hivyo.

Page 113: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

113

159) ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Tijaaniyyun Na Burda

Swali:

Katika mji wetu Tijaniyyuun [kipote cha mashia na masufi] wanamrehemu

Busiri [Gogo la Suufiy aliyetunga kaswiydah ya Burda, kaburi lake liko ndani

ya msikiti Misri] na wanamtakasa.

´Allaamah al-Fawzaan:

Si katika mji wenu tu, ni kila mahala. Baadhi yao wanasema Burda ni bora

kuliko hata Qur-aan. Hivyo ndo maana hawaipi umuhimu Qur-aan. Wanaipa

umuhimu Burda, wanaihifadhi, wanaiimba kila wakati. Huu ni upotevu -

A´udhubi Allaah. Huu ni mtihani khasa ukizingatia Burda ina baadhi ya

maneno maalumu, ya kupambia, kuimbika vizuri. Hii ni fitina - Allaah

Atukinge.

160) Qaswiydah Ya Burda Ina Shirki Na Ghuluu

Swali:

Ulisema katika darsa Burda ya Ahmad Shawqiy, je ndo ile Burda yenye

shirki?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 114: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

114

Ndio, ni kama ile ya Busiri. Zote ni moja tu. Zina ghuluu nakadhalika.

161) Kulingania Katika Tawhiyd Inatosha Kukataza Tu Kuabudu

Makaburi?

Swali:

Je kulingania watu katika Tawhiyd na kubainisha mfumo wa Mitume katika

Tawhiyd inatosheleza kukataza wanaoabudu makaburi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Awabainishie watu ´Aqiydah [itikadi] na kumkataza anaekwenda kinyume

nayo. [Waislamu wa leo] ukitaka kuwafunza Tawhiyd wanasema sisi

tunampwekesha Allaah na hatwendi kinyume na Tawhiyd. Lazima

uwabainishie na uwalinganie.

162) Tofauti Baina Ya Du´aa Ya Masuala Na Du´aa Ya ´Ibaadah

Swali:

Je kuna tofauti baina ya du´aa ya masuala na du´aa ya ´ibaadah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 115: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

115

Du´aa ya masuala ni haja yako wewe. na du´aa ya ´ibaadah ni

kumuadhimisha Allaah (´Azza wa Jalla).

�ك �$!"�ن �ك �"�د وإ�� إ��

“Wewe Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba msaada.” (01:05)

Unaposema:

راط ا��$!��م اھد�� ا�+7

“Tuongoze katika njia iliyonyooka.” (01:06)

Haya ni masuala.

9 رب7 ا�"����ن ﴿ *�م ﴿٢ا�*�د ��ـ� ن ا�ر� ـ �* �ن ﴿ ﴾ ���ك �وم ٣﴾ ا�ر� ﴾٤ا�د7

“Sifa Njema zote Anastahiki Allaah Mola wa al-‘Aalamiyn (walimwengu)

wote. Ar-Rahmaanir-Rahiym (Mwingi wa Rehma-Mwenye Kurehemu

Daima). Maalik (Mfalme) wa Siku ya Malipo.” (01:02-04)

Hii ni ´ibaadah. Ni kumsifia na kumuadhimisha Allaah (Jalla wa ´Alaa).

�ك �"�د إ��

“Wewe Pekee tunakuabudu.” (01:05)

Hii ni du´aa ya ´ibaadah.

Page 116: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

116

�ك �$!"�ن وإ��

“Na Wewe Pekee tunakuomba msaada.” (01:05)

Mpaka mwisho wa suurah, hii ni du´aa ya masuala. Na ndio maana Allaah

Kasema nimeigawa suurah hii baina Yangu Mimi na mja Wangu. Kuanzia

Kauli Yake:

9 رب7 ا�"����ن ا�*�د ��ـ�

“Sifa Njema zote Anastahiki Allaah Mola wa al-‘Aalamiyn (walimwengu)

wote.

(Mpaka):

�ك �$!"�ن �ك �"�د وإ�� إ��

“Wewe Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba msaada.” (01:02-05)

Hii ni ya Allaah (Jalla wa ´Alaa).

(Akisema):

�ك �$!"�ن وإ��

“Na Wewe Pekee tunakuomba msaada.” (01:05)

Mpaka mwisho wa suurah, hii ni du´aa ya masuala. Hii ni du´aa ya mja.

Page 117: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

117

163) Eda Ya Mwanamke Aliyezaa Baada Ya Kufa Mumewe Kwa Saa Au

Dakika Kadhaa

Swali:

Mwanamke mjamzito kafa mume wake, mimba ikatoka baada ya kufa mume

wake kwa saa moja. Vipi eda yake imekwisha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Ikitoka baada ya kufa mume wake katoka kwenye eda hata ikiwa kwa

saa moja au dakika.

���ن� أن �="ن *���ن� وأو6ت ا2*��ل أ

“Na wenye mimba eda yao mpaka watakapo zaa.” (65:04)

164) Wanafunzi Wanadai Kwamba Kusoma “Suurat-ul-Ikhlaas Baada Ya

Kila Swalah Ni Bid´ah

Swali:

Baadhi ya watafutaji elimu wanasema "Kusoma suurat-ul-Ikhlaas baada ya

kila swalah ni bid´ah. Wanasema eti ni Fatwa ya Shaykh ibn Baaz?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 118: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

118

Yeye ndiye mubtadi´ah [mtu wa bid´ah], mwenye kusema hivi yeye ndiye

mubtadi´ah. Yaani yeye kila asichokijua anakikataa na kusema ni bid´ah?

Haijuzu. Je karejea Fatwa ya Shaykh vizuri au ni dhana zake tu? Namna ndo

wanavyokuwa baadhi ya wanafunzi, na wenye haraka. Shaykh ibn Baaz ni

imaam Jaliyl na hasemi ila yale alionayo yakini yana dalili.

165) Ghurabaa Ni Watu Gani?

Swali:

Yapi makusudio ya Ghurabaa ambao kasema Mtume (swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) kuhusu wao "Bishara nje kwa Ghurabaa [wageni]."

´Allaamah al-Fawzaan:

Kawabainisha Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). [Maswahaba]

walimuuliza "Ni kina nani Ghurabaa?” Akasema "Ni wale watengenezao

wanapoharibu watu." Katika riwaayah nyingine "Ni wale wenye kutengeneza

walioharibu watu." Hawa ndo Ghurabaa.

166) Hukumu Ya Mafukara Wanaotumbukia Katika Shirki Kwa Ajili Ya

Kutafuta Riziki

Swali:

Page 119: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

119

Sisi katika mji wetu Eritrea kuna makaburi watu wanayazuru.

´Allaamah al-Fawzaan:

Kila mahala siku hizi kuna makaburi.

Muulizaji:

Baadhi ya watu hawa [wanaozuru] ni mafukara na wanaenda wawasaidie

matumizi na njaa walonayo ili wale katika vichinjo hivi vinavyochinjwa huko.

Inajuzu kufanya hivyo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Yaani milango mingine yote ya riziki imefungwa mpaka aende makaburini

tu? Tafuta riziki kwa Allaah Allaah (´Azza wa Jala). Na Allaah yu Karibu

Mwenye kujibu. Na njia za kutafuta riziki ni nyingi na usende makaburini na

kula katika vichinjo vyao ni haramu kwa kuwa ni maiti hiyo mizoga. Kuchinja

kwenye makaburi ni shirki, vimechinjwa kwa asiyekuwa Allaah.

� �م �ذ�ر ا$م % �9� و6 !,��وا ���

“Wala msile katika wale wasio somewa jina la Allaah.” (06:121)

م ���م �� *ر� م و�*م ا�1�ز�ر و�� أھل� �9 �.�ر إ�� % ا���!N وا�د�

“Yeye Amekuharimishieni mzoga tu na damu na nyamaya nguruwe na

kilicho tajiwa - katika kuchinjwa kwake jina la asiyekuwa Allaah.” (02:173)

Page 120: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

120

Zimechinjwa kwa asiyekuwa Allaah, hivyo ni haramu kwenu.

167) Anadai Watu Hawana Haja Ya Kusoma Elimu Imejaa Kwenye Internet

Na Kwenye Mikanda

Swali:

Lipi jibu kwa anaesema leo watu hawana haja ya kwenda kwa mashaykh

misikitini, wanaweza kutosheka na elimu ya kwenye Internet na kusikiliza

mikanda na kusoma vitabu.

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu ni mpotevu, ni kama yule niliewaambia anasema msiwalinganie watu

katika Tawhiyd. Elimu haichukuliwi ila kwa wanachuoni. Si katika vitabu

wala mikanda. Inachukuliwa kwa wanachuoni. Kwanza nani aliyevifanya,

nani mwenye kuongea? Utamjuaje muongeaji? Utaijuaje ´Aqiydah yake?

Hujui ikuwa ni mwanachuoni au si mwanachuoni. Baadhi ya watu

wanayapamba maongezi, maneno yao lakini hawana elimu. Mtu kuongelea

kuwa na usulubu mzuri na tabia nzuri, si elimu. Ni kuiongelea elimu na Fiqh.

Fiqh imekuwa ndogo sana kwa watu leo. Wasomaji wamekuwa wengi na

wanachuoni wamekuwa wadogo kama alivyosema Mtume (swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Tunachoongelea ni Fiqh na si kusoma tu. Elimu

haichukuliwi kwenye vitabu. Vitabu vina haki na batili, vina upotevu, makosa

na kupatia. Na wala hakuna awezae kupambanua haya ila wanachuoni. Wewe

unajisomea tu na hujui kitu, utachukulia [kitabu] kama kilivyo. Na huenda

ukaitakidi upotevu na wewe hujui. Hili halijuzu katu. Na aliesema maneno

haya ima ni mjinga wakutupia au ni mpotevu. Anataka kuwakimbiza watu na

kutafuta elimu na kuchukua elimu kwa wanachuoni.

Page 121: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

121

168) Hukumu Ya Kusema Washirikina Ni Ndugu Zetu

Swali:

Je mwenye kumuomba Hasan na Husayn (radhi za Allaah ziwe juu yao) au

akatafuta baraka katika makaburi yao. Je mtu anaweza kusema kuwa ni

Waislamu au kusema ni ndugu zetu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Si ndugu zetu. Tunajiweka mbali na Allaah na mtu huyu na dini

yake. Naye ni mshirikina adui wa Allaah na ni adui wa Waislamu.

ون �ن *�د� %� � وا��وم ا1Oر �واد �P�� د &و�� �ؤ��ون�و ���وا آ��ءھم أو أ���ءھم أو إ1وا��م أو ور$و9� و� ا ! >�ر!�م

“Huwakuti watu wanaomuamini Allaah na Siku ya Mwisho kuwa

wanawapenda wanao mpinga Allaah Mtume Wake, hata wakiwa ni baba zao,

au watoto wao, au ndugu zao, au jamaa zao.” (58:22)

Hakuna mapenzi baina yetu sisi na baina ya washirikina na makafiri. Katu!

169) Anataka Kuacha Kupiga Punyeto Anashindwa, Ipi Nasaha Yako?

Page 122: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

122

Swali:

Kuna mtu Allaah Kampa mtihani wa kupiga punyeto, na mara nyingi anataka

kuacha lakini anashindwa. Anasema ipi nasaha yako kwake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakushindwa isipokuwa tu hana azima. Ana udhaifu wa azima. Aazimie,

awe na nia nzuri, amuombe Allaah Amsaidie na aache jambo hili. Kuna watu

wameacha mambo makubwa kuliko haya, wameyaacha nao wanayapenda

lakini wameyaacha kwa ajili ya Allaah (´Azza wa Jalla) na Allaah Kawasaidia

kuyaacha. Kuwa na nia nzuri kwa Allaah na azimia kuacha. Jambo lingine

jiweke mbali na watu wake wasije kukudanganya au kukuweka katika

mkumbo huo, jiweke nao mbali. Ikaa na watu wena na wenye msimamo.

170) Haijuzu Kuomba Shafaa´ah (Uombezi) Kwa Maiti Sawa Mtume Au

Mwengine Yeyote

Swali:

Ipi rai yako kwa mwenye kusema "Ewe bwana wangu niponye!", akikusudia

Mtume wa Allaah (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mtume kwa sasa haombwi shafaa´ah, ataombwa siku ya Qiyaamah

atapokuwa hai. Shafaa´ inaombwa kwa aliehai. Shafaa´ah inaombwa kwa

Page 123: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

123

aliehai. Kwa maana anamuomba Allaah. Inajuzu kuomba du´aa kwa aliehai.

Ama maiti haombwi shafaa´ah wala du´aa wala chochote.

171) Kuvaa Nguo Za Makafiri Za Kumalizia Masomo

Swali:

Sisi ni mjumuiko wa wanafunzi tunaenda thanawiy na karibu madrasah yetu

yatafanya hafla ya kumaliza madrasah na wametuomba kuvaa nguo za

kumaliza madrasah. Ni nguo zinazovaa watu wa magharibi wamalizapo

masomo. Je inajuzu kwangu kuvaa nguo hizi katika hafla hii?

´Allaamah al-Fawzaan:

Vaa nguo katika nguo za Waislamu na usivae nguo za makafiri. Vaa nguo za

Waislamu zenye kusitiri nzuri na usivae katika nguo za makafiri. Usiwaige

makafiri.

172) Hukumu Ya Anaeacha Kufunga Ramadhaan Ila Hapingi Uwajibu

Wake

Swali:

Mwenye kuacha swawm ya Ramadhaan lakini hapingi wajibu wake,

anakufuru kwa hilo?

Page 124: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

124

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Vipi ataacha kufunga naye hapingi? Vipi ataacha swawm ya

Ramadhaan naye hana udhuru wa Kishari´ah ikiwa kweli hapingi? Ameacha

kwa kuwa anaona si wajibu.

173) Anaetetea Ushirikina Sawa Hakimu Au Yeyote Yule Ni Mshirikina

Swali:

Hakimu anaetetea ´ibaadah ya makaburi, anayahami na kukataza kuyaharibu.

Ipi hukumu ya hilo na hukumu yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mnajua wenyewe hukumu ya mwenye kutetea shirki kuwa ni mshirikina na

karitadi akiwa anadai eti ni Muislamu.

174) Mwanaume Si Sawa Na Mwanaume

Swali:

Page 125: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

125

Kuna daa´iy [mfanya da´wah] kajitokeza na kusema kuwa hakuna tofauti

baina ya wanaume na wanawake isipokuwa tu wanaume...

´Allaamah al-Fawzaan:

Wanaume kama yeye hawana tofauti baina yao wao na wanawake. Ama

wanaume wakihakika si kama wanawake.

3Q�2�� �ر و��س ا�ذ�

“Na mwanamume si sawa na mwanamke.” (03:36)

175) Daa´iy Mpotofu Anaewaponda Maswahaba (radhiya Allaahu ´anhum)

Swali:

Baadhi ya watu wanasema kuwa haitupasi kwetu kuwasifia Maswahaba

(radhiya Allaahu ´anhum) wote, kwa kuwa kati yao kuna wanafiki na sisi

hatujui...

´Allaamah al-Fawzaan:

Huku ni kuwatia ila Maswahaba, huyu anataka kuwatia shubuha kwa

Maswahaba wa Mtume wa Allaah ( 9 و$�م��3 % �+ ). Huyu ni daa´iy mpotofu,

puuzeni maneno yake.

Page 126: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

126

176) Anaejuzisha Kujengea Misikiti Makaburi Ni Mshirikina

Swali:

Mwenye kujuzisha kutawassul kwa Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ) baada ya kufa

kwake na akapinga adhabu ya kaburi na akajuzisha kujengwa misikiti kwenye

makaburi. Je anakufuru kwa hayo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Bila shaka, akijuzisha kujenga misikiti kwenye makaburi naye anajua mwenye

kufanya hivyo kalaaniwa - haya yapo katika Hadiyth swahiyh. Mwenye

kujenga msikiti katika kaburi kalaaniwa na pia ni katika watu waovu sana

mbele ya Allaah (´Azza wa Jalla) kama ilivyo katika Hadiyth swahiyh. Ikiwa

anajua hilo basi anakufuru.

177) Imaam Kujumuisha Maghrib Na ´Ishaa Wakati Wa Mvua Na Baridi

Kali

Swali:

Je ni lazima kwa imaam anapotaka kujumuisha maghrib na ´ishaa kwa ajili ya

mvua atoke nje na kuangalia kama mvua bado yaendelea au yatosha

kuangalia waliotangulia waliopo msikiti [waliokuja wakati mvua ilikuwa

yanyesha]?

Page 127: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

127

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa wanaingia msikiti na mvua yanyesha na kuna matope na ni wakati wa

baridi, udhuru bado upo [wa kujumuisha]. Ama ikiwa ni mvua ni hafifu au

hajui kama bado kunaendelea kunyesha au hapana, ni lazima awe na uhakika.

178) Ahl-ul-Kitaab Wa Zama Hizi Inajuzu Kuwaoa

Swali:

Inajuzu kuoa mwanamke wa Ahl-ul-Kitaab [mayahudi na manaswara] katika

zama zetu hizi baada ya wao kutumbukia katika kumshirikisha Allaah

(Subhaanahu wa Ta´ala)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mpaka Qiyaamah inajuzu kuoa mwanamke mnaswara kwa sharti

[mwanamke huyo] awe si mzinifu, yaani awe mwema.

وا��*+��ت �ن ا��ذ�ن أو!وا ا��!�ب

“Na wanawake wema miongoni mwa walio pewa Kitabu.” (05:05)

Yaani ambaye si mzinifu. Allaah Anawajua vizuri manaswara tangu wakati

wa Mtume Qur-aan ilipokuwa ikiteremka, ila pamoja na hilo Akaruhusu hilo.

Hakuna yeyote awezae kupinga Aliloruhusu Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).

Page 128: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

128

179) Wazazi Haijuzu Kuwapeleka Watoto Katika Madrasah Ya Ahl-ul-

Bid´ah Kama Masufi

Swali:

Je niwasomeshe watoto wangu katika madrasah ya Masufi kwa kuwa hatuna

madrasah mengine katika mji wetu. Wanawafunza huku ya kwamba Allaah

Yuko kila mahala - Ametakasika Allaah na hilo. Na mimi nilisoma katika

madrasah haya na nnajua yaliomo. Je inajuzu kuwaingiza katika madrasah

haya?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Haijuzu kuwaingiza katika madrasah ya shirki na bid´ah na Itikadi

potofu. Wafunze wewe ukijuacho na inatosha hilo. Lau katika mji ulipo kuna

kundi la Waislamu wengine mnaweza kufungua madrasah ya kwenu kwa

watoto wenu tu. Huu ndo wajibu kwenu.

180) Itikafi Potofu Ya Kuogopa Kijicho Kwa Kutupa Kipande Cha Chakula

Chini

Swali:

Wanapotaka baadhi ya watu kula wanatupa [wanaweka] kwanza kipande

kidogo cha chakula chini, na wanasema wanakhofia kupatwa na kijicho?

Page 129: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

129

´Allaamah al-Fawzaan:

A´udhubi Allaah - hizi ni Itikadi potofu wala haijuzu kutupa chakula.Bali

Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kasema:

"Kitapoanguka [kipande] cha chakula cha mmoja wenu, akichukue [akiokote]

na akitoe maudhi [uchafu] uliokipata na akile naasimuachie nacho

shaytwaan."

181) Allaah (Ta´ala) Ana Sifa Ya Nafsi

Swali:

Kauli Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Iysa aliposema:

� و6 أ�م �� �� ��$ك $�� � !"�م �� �

“Wewe Unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo

katika Nafsi Yako.” (05:116)

Hii ina maana Allaah Anathibitishiwa Sifa ya kuwa na Nafsi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio bila shaka. Kuna uthibitisho wa Allaah kuwa na Nafsi.

ر�م % 9$�� و�*ذ7

Page 130: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

130

“Na Allaah Anakutahadharisheni Nafsi Yake.” (03:28)

Kasema hivyo mara mbili katika suurat-ul-´Imraan.

182) Allaah Yuko Kwenye Jiha Juu

´Allaamah al-Fawzaan:

Je wewe unaamini kuwa Allaah yuko katika kila jiha? Lazima uamini kuwa

Allaah Yupo katika jiha ya Juu. Kasema Mwenyewe kuwa Yuko katika Jiha ya

Juu.

183) Je Al-Muhaasib Ni Jina La Allaah (Ta´aal)?

Swali:

Je imethibiti kuwa katika Majina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ni al-

Muhaasib?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Sikumbuki kitu kuhusiana na hili. al-Muhaasib?!

Page 131: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

131

184) Khatari Ya Kumkufurisha Mtu Binafsi?

Swali:

Ipi hukumu ya kumlaani mtu binafsi, kama kusema "Laana ya Allaah iwe juu

ya fulani"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Yule ambaye laana yake imethibiti katika Qur-aan au Sunnah analaaniwa.

Ama yule ambaye laana yake haikuthibiti katika Qur-aan wala Sunnah hapa

ndo kuna khilaaf. Kauli yenye nguvu - na Allaah ndo Anajua zaidi - ni kuwa

asilaaniwe kwa kuwa hujui mwisho wake utakuwa vipi.

185) Maulamaa Waliopinda Wasiojua Tawhiyd

Swali:

Je kuna maulamaa wasioijua Tawhiyd?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni wengi. Maulamaa wengi hawaijui Tawhiyd. Wamebobea kunako lugha,

Fiqh, huenda pia Hadiyth. Lakini ´Aqiydah hakusoma. Unakuta yuko katika

Page 132: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

132

madhehebu ya Ashaa´irah au madhehebu ya wale wasiokataza ´ibaadah ya

wenye kuabudu makaburi.

186) Maiti Hata Wakisikia Hawawezi Kukunufaisha Kwa Kitu

Swali:

Lipi jibu la dalili ithibitishayo kuwa maiti anasikia? Na wameishikilia kweli

kweli waaburu makaburi.

´Allaamah al-Fawzaan:

Hata akisia ndo iweje!!. Allaah Kasema:

�$�"وا د�ء�م و�و $�"وا �� ا$!���وا ��م إن !دوھم 6

“Mkiwaomba hawasikii maombi yenu; na hata wakisikia HAWAKUJIBUNI.”

(03:14)

Hivyo hakuna faida ya kuwaomba nao HAWAKUJIBUNI. Lakini watu hawa

huchukia sehemu ya Aayah au katika Hadiyth na wanaacha... Wanachukua

yale ya kwao na wanaacha yale yaendao dhidi yao. Na hii ndio tabia ya watu

wapotevu. Kama Alivyosema Allaah (Jalla wa ´Alaa):

�"ون �� !>��9 9�� ا�!.�ء ا��!N� وا�!.�ء !,و�9� �!�� C��م ز��و& �� ا��ذ�ن � ��,�

“Basi wale ambao katika nyoyo zao mna upotevu, hufuata zile

zilizoshabihiana kutafuta fitnah na kutafuta tafsiri zake.” (03:07)

Page 133: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

133

Wanachukua yanayoenda sawa na madai yao na wanaacha yanayokwenda

kinyume nao. Na wanaacha yanayoweka wazi [kuponda] yake waliochukua

katika mujmal au zilizoshabihiana. Hii ndio njia ya watu wapotevu.

187) Picha Ni Haramu Sawa Za Digital Au Za Aina Yoyote

Swali:

Ninawanasihi wale wanaopiga picha kwa kutumia ala ya digital camera,

wananirudi kwa kusema "masuala haya wanachuoni wametofautiana". Ipi

dalili yenye nguvu katika masuala haya ya khilaaf?

´Allaaamah al-Fawzaan:

Waambie sisi hatujali eti wanachuoni wametofautiana. Sisi tunaangalia dalili.

Yule mwenye [kukhalif] kupinga kama yuko na dalili sahihi tunachukua. Ama

ikiwa hana dalili anapuuzwa. Hii ndio kanuni yetu katika masuala yote na si

picha tu.

188) Usingizi Hauwajibishi Kustanji, Kinachowajibisha Ni Kutokwa Na

Kitu Tupuni

Swali:

Page 134: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

134

Kuna mtu kalala usiku kisha akaamka, je ni wajibu kwake kustanji [kuosha

ima tupu ya mbele au ya nyuma]? Na akiswali kwa kutawadha tu bila ya

kustanji swalah yake ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Usingizi hauwajibishi kustanji, kinachowajibisha kustanji ni kutokwa na kitu

nje. Akitokwa na kitu atastanji au atastijmaar [kujisafisha kwa kutumia kama

mawe, karatasi nk]. Ama kulala tu hili haliwajibishi kustanji.

189) Kila Kivazi Cha Mwanaume Chenye Kuvuka Kongo Mbili Za Miguu

Ni Motoni

Swali:

Hadiyth ya Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Kilichoko chini ya kongo mbili za miguu katika izaar [nguo ya chini] ni

Motoni."

Je inaingia katika hukumu hii suruwali?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni chochote chenye kuvuka kongo mbili za miguu, ni jumla. Suruwali, izaar

vyote ni Motoni.

Page 135: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

135

190) Tawassul Ni ´Ibaadah?

Swali:

Tulisoma katika darsa iliopita kwamba kutawassul kwa maiti ni aina mbili.

Moja wapo mtu akitawassul bila ya kumfanyia ´ibaadah yoyote ni bid´ah,

kwani vipi tawassul sio ´ibaadah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Tawassul ni kuomba du´aa kutoka kwa maiti. Ikiwa hakumfanyia

aina yoyote ya ´ibaadah ni bid´ah na njia inayopelekea katika shirki.

191) Kulisha Watu Watano Mara Mbili Ili Ihesabike Kalipa Kafara Ya

Yamini Kwa Watu Kumi

Swali:

Mtu akiwa na deni la kafara ya yamini na akapata masikini watano, je

anawajibika kuwalisha mara mbili ili ihesabike kama kawalisha watu kumi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Hata ungelisha watu tano mara elfu, hukulisha ila watu watano na

kunabaki juu yako kulisha watu watano wengine.

Page 136: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

136

192) Aliyeuawa Na Usaamah Bin Zayd Ni Katika Maswahaba?

Swali:

Yule mtu aliyeuawa na Usaamah bin Zayd (radhiya Allaahu ´anhu) je, mtu

anaweza kusema ni katika Maswahaba wakamtakia radhi kwa kuwa kafa

baada ya kusema Laa ilaaha illa Allaah moja kwa moja?

´Allaamah al-Fawzaan:

Achana nalo, mtu huyu hakukutana na Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ). Swahaba ni

mtu ambaye alikutana na Mtume ( �+9�� % 3 akamuamini. Alikutana ( و$�م

naye akamuamini na akafa kwa hilo kwa sharti hizi. Ama aliekutana naye

ilihali si muumini huyu si katika Maswahaba. Abu Jahl alikutana nae na Abu

Lahab wala hawakuwa katika Maswahaba. Aliekutana nae akamuamini. Kwa

sharti hizi. Ama aliyemuamini na hakukutana naye si Swahaba kwa kuwa

hakukutana na Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ). Hata kama ni muumini. an-Najaashiy

(rahimahu Allaah) alimuamini Mtume lakini hakukutana nae na haihesabiki

ni mmoja katika Maswahaba bali ni Taabi´iyn. [Sharti ya pili] akafa juu ya

imani yake. Ama aliyekutana na Mtume ( 9�� % 3�+ و$�م ) akamuamini kisha

akaritadi, huyu si katika Maswahaba.

193) Kaweka Nadhiri Kuamka Kuswali Fajr La Sivyo Ataswali Rakaa Kumi

Swali:

Page 137: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

137

Kuna mtu kalala usiku na akaweka nadhiri kabla ya kulala ikiwa hatoamka

swalaat-ul-Fajr ataswali rakaa kumi siku hio hio, hakuamka na akasahau

kutekeleza nadhiri yake, kumeshapita mwezi au zaidi. Anawajibika nini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni juu yake kulipa kafara ya yamini. Kwa kuwa hakukusudia kujikurubisha

kwa Allaah kwa kuweka nadhiri hii, alichokusudia ilikuwa ni kuamka

mwenyewe. Alipe kafara ya yamini.

194) Kufunga Safari Kwenda Kwenye Kaburi Ya Mtume Au Mwengine

Yoyote

Swali:

Wanatumia hoja wale wanaofunga safari kuzuru kaburi ya Mtume ( 9�� % 3�+

?ni kama wale wanaofunga safari kwenda kutafuta elimu, vipi tujibie hili ( و$�م

´Allaamah al-Fawzaan:

Kufunga safari kwenda kutafuta elimu hili lakubalika.

�ن ��و6 ��ر �ن ��م طN�(R �7�!����وا �� ا�د7 7� N&�ل7 �ر

“Lakini kwanini hawatoki baadhi katika kila kundi miongoni mwao,

wakajifunze vyema Diyn.” (09:122)

Page 138: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

138

Kufunga safari kwenda kwenye kaburi ya Mtume si kutafuta elimu. Ni njia

inayopelekea katika shirki. Kuna tofauti baina ya kufunga safari kwenda

kwenye kaburi ya Mtume au nyingine yoyote na baina ya kufunga safari

kwenda kutafuta elimu.

195) Kila Jina La Allaah Linajenga Sifa Kinyume Na Matendo

Swali:

Je mtu anaweza kuchukua Majina ya Allaah (´Azza wa Jalla) ni katika

matendo Yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Kila Jina Lake linajenga Sifa ama matendo Yake hayachukuliwi Jina.

Usichukue Jina katika matendo Yake. Kwa mfano "Kaandika Allaah", je

utasema kuwa Allaah ni "Mwandishi"? Ukamwita "Mwandishi"? Hapana, si

kila kitendo [Chake] huchukuliwa Jina wala Sifa.

����ن ��"N� % 3� ا�ظ�

“Laana ya Allaah iwapate walio dhulumu.” (07:44)

Je waweza kusema Allaah Anaitwa "Mwenye kulaani"? Hapana.

Page 139: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

139

196) Hukumu Ya Swalah Ambayo Wudhuu Haukushika Kidogo Cha

Mguuni

Swali:

Kuna mtu mmoja kidole mguuni kilikuwa hakipati maji, na alifanya siku tatu

alikuwa akitawadha bila ya kuosha kidogo hichi kwa ujinga, je ana nini juu

yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni juu yake kurudi kuziswali kwa kuwa sehemu katika mwili haikupata maji,

ina maana arudi kutawadha na arudi kuswali. Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ )

alimuona mtu katika mguu wake kuliku sehemu ndogo imekosa maji,

akamuamrisha kurudi.

197) Aliopigana Nao Abu Bakr (radhiya Allaahu ´anhu) Ilikuwa Ni Kwa

Ajili Ya Kufuru Yao

Swali:

Je yaweza kufahamika kwa Abu Bakr asw-Swiddiyq (radhiya Allaahu ‘anhu)

kwa waliokataa kutoa zakaah kuwa aliwakufurisha na aliwaua kwa kufuru

yao?

Page 140: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

140

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, walisema hatutokupa ila Mtume tu Mtume wa Allaah ( 9 و$�م��3 % �+ ),

ina maana walipinga. Na Mwenye kupinga kutoa zakaah anakufuru. Ama

mwenye kukataa kwa ubakhili, huyu alazimishwe kutoa hata ikiwa ni kwa

kutumia nguvu.

198) Kazi Ya Kuamrisha Mema Na Kukataza Mabaya Ni Ya Nani?

Swali:

Kuna ambao wanasema kuwa kuamrisha mema na kukataza mabaya ni kazi

khasa ya wanaume [wanachuoni] wa al-Lajnah [ad-Daa´imah] na hairuhusiwi

kwa wengine, je kauli hii ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kuamrisha mwema na kukataza kwa kutumia nguvu ni khasa kwa wanaume

wa al-Lajnah. Ama kukataza kwa ulimi na kubainisha na kutoa nasaha na

kuwafikishia wasimamizi hili ni wajibu kwa kila mmoja awezae.

"Mwenye kuona munkari auondoshe kwa mkono wake."

"... na akiwa hawezi basi afanye hivyo kwa ulimi wake; na akiwa hawezi basi

afanye kwa moyo wake na huo ni udhaifu wa Imani." [Muslim]

Ni lazima kuondosha munkari hata ikiwa ni kwa moyo, lazima kuuondosha

munkari hata ikiwa ni kwa moyo ktiu cha mwisho.

Page 141: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

141

199) Mtazamo Wa Kwanza Kuiangalia Ka´abah Mtu Hukubaliwa Du´aa?

Swali:

Je imethibiti mtazamo wa kwanza kuiangalia al-Ka´abah, hukubaliwa du´aa

[ya mwenye kuomba]?

´Allaamah al-Fawzaan:

Sijui kitu kuhusiana na hili.

200) Hukumu Ya Kuapa Kwa Ahadi Ya Allaah

Swali:

Ipi hukumu ya kuapa kwa kusema: "[Naapa] kwa ahadi ya Allaah"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Halina asli hili. Mtu anaruhusiwa kuapa kwa Jina la Allaah au Sifa miongoni

mwa Sifa Zake.

Swali La Pili:

Page 142: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

142

Vipi pia kuapa kwa kusema "Naapa kwa dini"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna kuapa kwa dini, wala amaanah nk. "Mwenye kuapa aape kwa Allaah

au anyamaze."

201) Kuchinja Kwa Ajili Ya Allaah Kwenye Kaburi La Walii Fulani

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kuchinja kwa ajili ya Allaah kwenye kaburi la walii

miongoni mwa mawalii kwa kuamini baraka ya sehemu hio?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hii ni njia inayopelekea kunako shirki. Hii ni bid´ah. Kwa kuwa sehemu hii si

sehemu ya kuchinja. Na ni njia inayopeleka katika shirki.

202) Kuchukua Mkopo Benki Kwa Ajili Ya Kuoa

Page 143: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

143

Swali:

Ipi hukumu ya kuchukua sehemu [mkopo] katika benki kwa ajili ya kuoa au

kwa ajili ya kununua gari?

´Allaamah al-Fawzaan:

Unaweza kuchua maadamu ni mubaha [mkopo] hauna ribaa, chukua.

Wakikupa bila ya faida na bila ya kitu - sehemu nzuri, hakuna ubaya sawa

ikiwa kwa ajili ya kuoa au mengine. Ama kuchukua sehemu na faida juu hii

ni ribaa, haijuzu. Sawa ikiwa kwa ajili ya kuoa wala mengine.

203) Kufanya Mzaha (Maskhara) Na Hadiyth Za Mtume

Swali:

Ipi hukumu kwa mwenye kufanya mzaha na Hadiyth kisha anasema mwisho

wake "Hadiyth imepokelewa na Muslim." Anakusudia mzaha na hoja yake

anasema...

´Allaamah al-Fawzaan:

A´udhubi Allaah - tunamuomba Allaah kinga. Kasema Mtume ( 9 و$�م��3 % �+

): "Ataenisemea uongo kwa kukusudia, ajiandalie sehemu Motoni."Haijuzu

Page 144: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

144

mzaha kwa Hadiyth, Qur-aan au mengine ya dini. Haijuzu mzaha kwa haya.

Hii ni tabia ya wanafiki.

204) Ruqyah Kwenye Maji Ya Zamzam Na Mti Wa Mzaituni

Swali:

Ipi hukumu ya kusoma Qur-aan kwenye maji ya zamzam au mti wa mzaituni,

jambo hili lina asli?

´Allaamah al-Fawzaan:

Maji ya zamzam ni maji yenye baraka. Ikikusanyika ruqyah na maji ya

zamzam yenye baraka kunatarajiwa ponyo kwa idhini ya Allaah. Na mti wa

mzaituni pia ni mzuri. Mtu akitaka kufanya ruqyah kwa kuutimia baraka

inazidi kwa idhini ya Allaah (´Azza wa Jalla).

205) Tofauti Ya Kufuru Na Shirki

Swali:

Ipi tofauti kati ya kufuru na shirki? Na je kila kufuru ni shirki?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 145: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

145

Kufuru ni jumla. Mtu anaweza kuwa kafiri kwa kupinga kuwepo kwa Allaah,

mulhid. Hamuamini Allaah. Ama mshirikina yeye anaamini kuwepo kwa

Allaah. Anakubali Tawhiyd Rubuubiyyah lakini anamshirikisha Allaah katika

Tawhiyd Uluuhiyyah. Ama kafiri yeye haamini si hili wala hili.

206) Kufanya Mjadala Na Ahl-ul-Bid´ah

Swali:

Je ni katika njia ya Salaf na uongofu wao kufanya mjadala na Ahl-ul-Bid´ah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa mtu yuko na elimu na uwezo, bila shaka hii ni njia ya kufikisha haki na

kuiangamiza batili. Na haki haiwezi kuenezwa ila kwa njia hio. Lakini awe ni

mtu mwenye uwezo - uwezo wa elimu na kujua kujadili.

207) Kuacha Nyumba Inasoma Qur-aan Na Hakuna Wakuisikiliza

Swali:

Vipi kwa mwenye kuiacha Qur-aan inasoma wakati wa safari yake ili

aihifadhi nyumba?

Page 146: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

146

´Allaamah al-Fawzaan:

Isitumiwe Qur-aan namna hii. Aweke mlinzi nyumbani au afunge milango

vizuri nakadhalika. Ama kuiacha Qur-aan inasoma kwa ajili ya ulinzi, hii ni

katika kuiweka Qur-aan mtihanini.

208) Waitao “Ewe Yuma” Wanaposhtuliwa Na Kitu

Swali:

Ni jambo limeenea kwenye ndimi nyingi za watu, wakifikwa na jambo lenye

kushtua wanaita na kusema "Ee mama au yuma!" na wala hawakusidii hilo. Je

hili ni katika shirki?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna mkubwa asemae hivi, hakuna anaesema hivi ila mtoto. Si dhani kama

kuna mkubwa asemae "Ee Yuma!"

209) Haijuzu Kuwanunulia Wanawake Simu Za Khatari Za Kisasa

Swali:

Page 147: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

147

Nimruhusu mke wangu kushiriki na kaka zake kununua simu ya kaka yao

anaesoma darsa la pili, simu iitwayo blackberry. Je nimruhusu hilo na

kutumia simu hii?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, simu ambayo ni khatari kwa mtu isinunuliwe. Mtu anunue simu ya

maongezi tu, isiwe na ya zaidi ya kuongea. Simu zenye vitu vya haramu na

vitu vya khatari haijuzu kuziuza wala kuzinunua.

210) Ni Haramu Kumpa Mwanamke Mwanamke Ajinabi

Swali:

Ipi hukumu ya kumpa mkono mwanamke ajinabi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu kumpa mkono mwanamke ambae si mahram. Mtume ( 9 و$�م��3 % �+

) hakuwahi kumpa mkono wake katu mwanamke yeyote ambae si halali

kwake, bali alikuwa akiwabaay´ wanawake kwa maneno. Haijuzu kumgusa

au kumpa mkono mwanamke yeyote. Isipokuwa tu katika mahram zake.

211) Kumpigia Simu Aliehai Na Kumuomba Akuombea Du´aa

Page 148: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

148

Swali:

Inajuzu kumuomba aliehai akuombee du´aa ambae yuko nje ya mji nikimpigia

simu na kumuomba du´aa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna ubaya wa hilo kwa kuwa ukimpigia simu sio [kama kumuomba]

ghayb [jambo ambalo ni shirki].

212) Kuomba Rahma Na Kinga Ndani Ya Swalah

Swali:

Imaam akisoma Aayah yenye istighfaar, tasbiyh au takbiyr. Maamuma

anaweza akakabir, kuomba istighfaar au kusabihi?

´Allaamah al-Fawzaa:

Jambo lililothibiti ni kuwa Mtume ( % 3�+ 9 و$�م�� ) - tena ilikuwa ni katika

swalah ya usiku. Akifika katika Aayah ya Rahma, anamuomba Allaah

Amrehemu. Na akifika katika Aayah ya adhabu anamuomba Allaah kinga.

Hili ndo lililothibiti kwa Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ). Tunatosheka na haya.

Page 149: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

149

213) Kauli Sahihi Kuhusiana Na Thawabu Kumfikia Maiti

Swali:

Ipi kauli yenye nguvu katika masuala ya kumtumia thawabu maiti? Kuna

wanaosema inajuzu kumtumia thawabu aina yoyote ya ´ibaadah, na kuna

wanaoiwekea mpaka kwa yale yenye dalili tu katika ´ibaadah. Kauli yenye

nguvu katika hili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Sema kauli sahihi hapana kauli yenye nguvu. Kauli sahihi ni kuwa amali za

Muislamu ni zake mwenyewe tu, ispokuwa yale ambayo shari´ah imeruhusu

katika kumuombea du´aa, swadaqah ya kuendelea aliofanya au mtoto

anaemuombea baada ya kufa kwake. Du´aa yake [zao watoto] humfikia,

swadaqah wamtoleayo. Alipomuuliza mwanamke [Mtume], na alipomuuliza

Sa´ad bin ´Ubayd kumtolea swadaqah mama yake maiti. Kauli ya Allaah

(Ta´ala):

�$�ن إ�6 �� $"3 T� وأن ���س

“Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?” (53:39)

Yanabagua [tenga] yaliokuja katika dalili tu. Na waliobaki thawabu zao

hazimfikii maiti, kwa kuwa ni matendo ya mtu mwenyewe.

214) Haijuzu Kuomba Kwa Uso Wa Allaah Mambo Ya Kidunia

Page 150: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

150

Swali:

Ipi hukumu kwa mwenye kuomba kwa Uso wa Allaah na anasema

"nakuomba kwa Uso wa Allaah ufanye hivi na hivi."?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu hili kabisa. Hadiyth "Hakuombwi kwa Uso wa Allaah isipokuwa

Pepo tu." Wala hakuombwi kwa Uso wa Allaah mambo ya kidunia.

Hakuombwi kwa Uso wa Allaah ispokuwa Pepo au yanayomfikisha mtu

Peponi. Wala mtu haombwi mambo ya kidunia.

215) Kumwambia Mtu Unaefanya Kazi Kwake “Bwana Wangu”

Swali:

Ikiwa nafanya kazi kwa mtu na nikamwambia "Ewe bwana wangu!". Hili

linajuzu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa ni bwana wako hakuna neno. Wewe ni mtumwa wake? Ikiwa

anakumiliki waweza kusema "Ewe bwana wangu!".

Page 151: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

151

216) Kuosha Mikono Mtu Anapoamka Kutoka Usingizini

Swali:

Kuosha mikono miwili kwa mwenye kuamka kutoka katika usingizi wa usiku

ni khasa wakati mtu anataka kutia wudhuu tu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Hata wakati wa kula, kunywa nk. Lakini imewekewa nguvu wakati

wa kutia wudhuu.

217) Kutokataza Shirki Kwa Kukithiri Kwa Jambo Lile Kwa Watu

Swali:

Yule mwenye kusikia matamshi ya shirki kama kuapia kwa asiyekuwa Allaah

na asikataze jambo hilo kutokana na kukithiri kwa jambo hili, atakuwa mtu

huyu ni katika wale wenye kuificha elimu [waliolaaniwa na Allaah]?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kila afichae kitu katika wanayohitajia watu katike elimu basi ni mfichaji. Na

hili linatofautiana itategemea kaficha nini. Ila tu ikiwa hawezi, ikiwa hawezi

hilo atakuwa ni mwenye kupewa udhuru.

Page 152: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

152

218) Nikiona mtu mwenye kumshirikisha Allaah na nisimbainishie

Swali:

Nikiona mtu mwenye kumshirikisha Allaah na nisimbainishie kuwa

akifanyacho ni shirki, kwa kuwa katika mji wetu mwenye kufanya hivyo

anahukumiwa na serikali inayohukumu katika mji wetu nayo ni ya serikali ya

kinaswara. Ipi hukumu ya kunyamazia hili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kubainisha kuna daraja nyingi. Mbainishie baina yako wewe na yeye,

mbainishe siri, mpe nasaha siri kadiri na uwezavyo kwa kutumia njia

uwezazo. Serikali inaweza kuwa haikatazi ila jambo lililo dhahiri tu, ama

mambo yakujificha serikali haiyajui. Wewe fanya uwezavyo.

219) Kumsalia Mtume (´alayhis-Salaam) Ni Katika Sababu Za Kukubaliwa

Du´aa

Swali:

Je ni sahihi kuwa mtu akimuomba Allaah na asimalizie du´aa yake kwa

kumsalia Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ) kwamba du´aa yake haikubaliwi wala

kupandishwa?

Page 153: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

153

´Allaamah al-Fawzaan:

Imethibiti kuwa du´aa yake huzuiwa mpaka amsalie Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ).

Kwa kuwa kumsalia Mtume ni miongoni mwa sababu za kujibiwa [du´aa].

220) Kutawassul Kwa Allaah Kwa Kukusanyika Msikitini Na Kufanya

Dhikr

Swali:

Tukikubaliana katika mji wetu kukusanyika watu msikitini siku ya Ijumaa na

kusoma Qur-aan na kumuomba Allaah Atuteremshie mvua kwa hoja ya

kutawassul kwa Allaah kwa matendo mema walioyafanya, je kitendo hichi

kinajuzu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, hii ni bid´ah. Wanakusanyika na kusoma Qur-aan kwa ajili ya

kuomba mvua hili ni jambo la bid´ah. Kilichothibiti ni kuwa wanaswali

swalah ya istisqaa na imaam anakhutubu baada ya swalah na anaomba du´aa.

Kama alivyokuwa Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ) akifanya. Haikuthibiti kuwa

[watu] walikuwa wanakusanyika wanasoma Qur-aan kisha wanamuomba

Allaah mvua. Haikuthibiti.

221) Kutenga Siku Maalumu Kwa Ajili Ya Taazia

Page 154: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

154

Swali:

Ipi hukumu ya kutenga siku khasa kwa ajili ya kutoa pole [kwa wafiwa]?

Kama kukusanyika watu kwenye nyumba hivi na kukaletwa vyakula na

vinywaji hapo?’

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna dalili ya hilo. Bali hili ni jambo limezushwa na lina kujikalifisha na

kupoteza wakati na kupoteza mali na watu kukosa kufanya kazi. Mambo yote

haya hayajuzu. Watoa pole wasiwe ni wenye kukaa [hapo wakakusanyika],

unapokutana na ndugu yako [mfiwa] unampa pole au unaweza kumpigia

simu. Hakuna cha kujikalifisha.

222) Tofauti Ya Kusimama Kwa Kumuadhimisha Mtu Na Kumpokea Mgeni

Swali:

Wamezowea watu kumsimamia mgeni wakati wa kumpokea, ipi hukumu ya

kusimama kwa kuzingatia ya kwamba Mtume ( 9�� % 3�+ و$�م ) alikataza hilo

na alikuwa analichukia. Na je ni katika kumpandisha mtu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 155: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

155

Ewe ndugu yangu si hivyo. Kusimama kumsalimia na kumpokea mgeni

hakuna ubaya. Mtume ( 9 و$�م��3 % �+ ) aliwaambia Answaar "Simameni kwa

ajili ya bwana wenu", yaani Sa´ad bin Mu´aadh. Kumpokea mgeni na

kumsalimia hakuna ubaya. Alichokataza Mtume ni kusimama kwa ajili yake

nawe umekaa. Mtu anakuwa katika hali ya kukaa na watu wakamsimamia.

Hili halijuzu. Hivi ndivyo alivyokuwa akifanya Faaris wa Rome. Isipokuwa tu

ikiwa anahitajia ulinzi, ikiwa mtawala anahitajia ulinzi hakuna neno. Ama

kumsimamia yeye kwa ajili ya kumuadhimisha hili halijuzu.

223) Haijuzu Kuleta Adhkaar Maalumu Baada Ya Swalah Ambazo

Hazikuthibiti

Swali:

Inajuzu baada ya kumaliza kusoma adkhaar za swalah maarufu, je inajuzu

kuleta dhikr maalumu? Kama kuleta istighfaar mara mia na akadumu kwa

kufanya hivyo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni juu yako ewe ndugu yangu kurejea kunako adhkaar zilizothibiti katika

usahihi wake na idadi yake. Fanya hizo.

224) Hakuna Haja Ya Kuchukua Elimu Kwa Mtu Mwenye Baadhi Ya Bid´ah

Swali:

Page 156: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

156

Ipi hukumu ya kuchukua elimu kwa mtu ambae ana baadhi ya bid´ah katika

matendo, amali na si katika ´Aqiydah? Inajuzu kusoma katika mikono yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ewe ndugu maulamaa - Alhamdulillaah ni wengi. Na huna haja ya mtu wa

bid´ah ukachukua elimu kwake. Haijuzu kukaa na mtu wa bid´ah, vipi

kuchukua elimu kwake?!

225) Kuswali Nyuma Ya Imaam Anaevaa Herizi

Swali:

Je mtu mwenye kuandika katika karatasi suurah miongoni mwa suurah za

Qur-aan au Aayah na akajitundikia nayo na akategemea Aayah hii kuwa

inazuia madhara. Je inajuzu kuswali nyuma yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Abainishiwe kuwa hili halijuzu. Hii ni herizi. Haijuzu kwake hili. Anasihiwe.

Ikiwa hatoivua, ikiwa wako na uwezo kubadilisha na kuweka imaam

mwengine, ni wajibu kwao kufanya hivyo.

Page 157: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

157

226) Kunyunyizia Maji Ya Kisomo Kwenye Kuta Za Nyumbani Kuzuia

Madhara

Swali:

Je imethibiti kwa Mtume ( % 3�+9 و$�م�� ) kunyunyizia nguzo na kuta za

nyumbani kwa maji alioyasomea ili azuie kupatwa na kijicho na uchawi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kamwe! Hili halijuzu. Kunyunyizia kuta za nyumbani kwa Ruqyah. Baadhi ya

wengine wananyunyizia kwa [... sikufahamu neno alotumia Shaykh]. Yote

haya ni ukhurafi. Allaah Hakuteremsha chochote kuhusiana na hayo.

227) Kuswali Na Nguo Yenye Damu

Swali:

Ipi hukumu ya kuswali na nguo yenye damu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Aoshe damu na aiondoshe na mashaka. Aoshe kabla ya swalah. Na akiswali

nayo kwa kusahau au hakuona swalah yake ni sahihi, lakini baadae aioshe.

Page 158: Fataawa Za ad-Dur an-Nadhwiyd Fiy Ikhlaasw Kalimaat at-Tawhiyd -  ´Allaamah al-Fawzaan

158

Swali La Pili:

Anauliza tena, ikiwa ataiosha lakini rangi bado imebaki. Hilo laathiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haliathiri. Akiiosha na... akishindwa kuondosha rangi haliathiri. Na kwa hili

Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipomuamrisha mwanamke

kuosha damu ya hedhi kwenye nguo, akamwambia "wala haidhuru athari

yake."

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/alldroos?tid_1=252

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na Aali zake na

Maswahaba wake (Radhiya Allaahu ´anhum) na watakaowafuata kwa

wema mpaka hiyo siku ya Qiyaamah.