jarida litolewalo na; banana investments ltd · mhariri mkuu 0717 350 971 emanuel nevava mjumbe...
TRANSCRIPT
HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
TOLEO NAMBA 21 HALIUZWI APRIL— JUNE
Jarida litolewalo na;
Banana Investments Ltd
2 HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
BODI YA WAHARIRI
Beatha Anthony
Mhariri Mkuu
0717 350 971
Emanuel Nevava
Mjumbe
0756 601 830
Augustine Minja
Mwenyekiti
078 5451 004
Gerald Lyimo
Mjumbe
SALAMU ZA MHARIRI
YALIYOMO
WATU NA MATUKIO
Ilikua ni siku ya Alhamis tarehe 5/5/2011 yalisikika
matatumbeta katika kijiji cha Oloirien, pale Bi Tecla aki-
tokea nyumbani kwao kuelekea katika ukumbi wa kifahari wa Golden Rose ambapo wazazi wake alikua wamemuan-
dalia tafrija kwa ajili ya kumuaga kwenda kuanza maisha
ya kifamilia na Bw. Godbless Msuya wa Moshi. Baada ya sherehe hizo
siku ya Jumamosi tarehe
7/5/2011 ilifanyika ibada ya ndoa takatifu katika kanisa la
KKKT CKMC Moshi na
kufuatiwa na sherehe zilizo-
fanyika ukumbu wa chuo cha Ushirika hukohuko Moshi.
Bwana harusi ni Af-
isa masoko wa TBL na Bibi harusi ni Afisa Ugavi wa Ba-
nana Investments Ltd.
Imeandikwa na
Beatha Anthony.
Ni mara nyingine tena toleo la Mbiu ya Banana li-
natoka na kwa habari mbalimbali. Toleo hili
tumeweka habari kutoka mikoa mbalimbali ambayo
kampuni yetu inasambaza bidhaa zake. Hii ni
kuonyesha kwamba kampuni inawajali wateja wake
wote popote pale walipo. Tungependa sana kupokea
makala kutoka kwa wateja wetu. Pia tunashauri
kwamba makala hizo ziwe fupi na pia kwa namna
moja au nyingine zihusiane na kampuni.
Kwa wale wateja wetu ambao wataandika makala
yao wazitume kwa kupitia magereva wetu wa
Mauzo au wasambazaji. Pia unaweza kuleta hapa
kiwandani na ukakabidhi mapokezi.
Makala itakayochapishwa kwenye jarida mwandishi
atalipwa kiasi cha shilingi 10,000/=.
Tunatumia tena nafasi hii kuwakarisha katika kam-
puni ya Banana Investments Ltd watengenezaji na
wasambazaji wa mvinyo halisi wa Ndizi.
Kwa mawasiliano zaidi tumia namba za simu
zilizopo ukurasa wa mwisho wa Jarida hili.
1.MAONI YA MHARIRI…………………………………….02
2. HABARI KUTOKA SINGIDA …………………………...02
3. BANANA SPORTS CLUB YAJIPANGA UPYA ………..03
4. KAMPUNI YABORESHA MASOKO…………………….03
5. SAFARI YANGU YA LOLIONDO……………………….03
6. KAMPUNI YASHIRIKI MEI MOSI 2011………………...04
7. BOHARI MPYA YAFUNGULIWA MOROGORO ……...05
8 HABARI HUTOKA BOHARI YA DSM…………………..05
9. MPANGO WA KAMPUNI KUSAFISHA MAJI TAKA… 06
10. DONDOO MUHIMU ZA UNYAJI WA VILEO ……….. 06
11. AJIRA MPYA NGUVU MPYA…………………………..07
12. Y’S MEN ARUSHA WAPOKEA UGENI KUTOKA
GENEVA……………………………………………………...07
BI TECLA EDUARD, AFISA UGAVI APATA MWENZA
3 HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
Miongoni mwa wanafalsafa maarufu duniani ni Mgiriki Socrates.
Kwa wale wanaosoma na kufuatilia maisha ya wanafalsafa wa kale hapa duniani, huenda watakuwa wanajua kuhusu ndoa ya
mwanafalsafa huyu maarufu.
Wanaofuatilia maisha ya wanafalsafa hao watakubaliana nami kuhusu mke wa Socrates. Watu au wenzake Socrates walipokuwa
wanamuuliza kuhusu mke wake, wakitegemea kusikia akila-
lamika, kwa sababu mama huyu alikuwa na ghubu sana, hawa-
kusikia malalamiko yoyote. Badala yake aliwauliza, ‘mnataka
kujua yukoje kwa kulinganisha na nini? Ni hivi, iwe ni kwa watu,
maeneo, hali, matukio, na hata hisia zetu vyote hivyo havina
maana yenye kulingana kwa watu wote. Vyote hivyo ni vizuri au
vibaya kwa viwango kwa kutegemea tunavilinganisha na nini.
Hebu tuchukue vikombe vya aina moja, kama kimoja kimeben-
duka, tunaweza kusema hakiko kamili. Ni rahisi kusema hivyo
kwa sababu, tuna mahali pa kulinganisha, ambapo ni kwenye vile
vikombe vingine vizima. Kwa binadamu hali ni tofauti kabisa,
kwa sababu wote ni tofauti.
Hebu fikiria kuhusu tukio fulani kwenye maisha yako. Lakini
bado kuna swali, kwa kulinganisha na tukio lipi? Kila tukio lina-
tokea mahali pake, muda wake na kwa sababu fulani ili maisha
yaendelee kuwepo. Kwa nini kama ni hivyo udhani tukio fulani ni baya au zuri? Huu ubaya au uzuri ni kwa kulinganisha na tukio
lipi wakati kila tukio lina mahali, muda,na sababu ya kutokea
kwake?
Tunaambiwa kwamba kila jambo ambalo linaingia kwenye
mfumo wetu wa kufikiri ni vizuri au vema likawa limepimwa
kwa mujibu wa tafsiri zetu ambazo hazipaswi kutuumiza. Unaona
jambo ambalo linataka kukuumiza kihisia, ni kwa nini usijiulize
kama jambo hilo ni baya, ni kwa kulinganisha na lipi?
Kumbuka ni lazima kuwe na mahali ambapo tunasimama ili
kupima uzuri au ubaya wa jambo kwa kulinganisha na mengine,
ambayo kwa kawaida hayatarajiwi kubadilika.
Kama yanabadilika, basi ni vigumu kusema kuwa ni mabaya au
mazuri, kwani hatuna mahali pa kuyalinganisha. Kama vikombe
vinavyofanana kabatini vingekuwa wakati mwingine kimoja ki-
nakuwa kirefu kingine kifupi au kinabadilika rangi, tusingeweza kuvilinganisha pia. Binadamu kila mmoja ana haiba yake, kila
mmoja ni yeye kwa tabia, mienendo na hata miili.
Na, Peter Mapunda.
Baada ya kimya kirefu sasa ile Club maarufu ya
Banana imeanza kujipanga upya ili kuendeleza
shughuli za michezo na utalii wa ndani na nje ya
nchi.
Ili kuhakikisha kuwa mipango yake yote
inafanikiwa Club hiyo inatarajia kufanya uchaguzi
wa viongozi katika ngazi za Mwenyekiti, Katibu,
Mweka hazina na wajumbe wane.
Viongozi hao wanatarajiwa kuwa wabunifu hasa
kwa kuanzisha miradi itakayoongeza kipato cha
Vlubu na kukusanya ada za wanachama kwa wa-
kati.
Pia Club hii inatarajia kuingia ubia na Club ya
Genuine Sports Club iliyopo maeneo ya Kijenge
Backdad kwaajili ya kufanya mazoezi ya viungo
ya kunyanyua vyuma na Aerobics.
Wanachama wanaombwa kuwa tayari kulipa ada
zao za mwezi ili kuwezesha mipango yote hii.
Imeandikwa na
Adrian Anthony
BANANA SPORTS CLUB YAJIPANGA UPYA KAMPUNI YADHAMIRIA KUBORESHA MASOKO
Katika kuhakikisha kwamba wateja wanapata huduma kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu, kampuni imesogeza
huduma zake kwa karibu zaidi katika mikoa ya Kilimanjaro,
Manyara na Dodoma.
Hii ni pamoja na kuajiri wawakilishi wa masoko katika
mikoa hiyo. Wawakilishi hao ambao wameanza kazi ya rasmi mwezi wa tano, 2011 pamoja na mambo mengine wa-
tasikiliza na kutatua matatizo mbalimbali ya wateja, watatoa
fursa kwa wateja wapya watakaokua tayari kufanya biashara na kampuni yetu pia kuhakikisha kwamba bidhaa zetu zi-
nafika kwa wateja kwa wakati unaotakiwa.
Wawakilishi hao ni
1. MANYARA
Patrice B. Menda - Namba ya simu 0754 299529
0785 945067
2. DODOMA
Denis Kessy- Namba ya simu 0713 778958
0762 966988
3. KILIMANJARO
Tumaini A Mungete Namba ya simu 0754 299529
0688 299529
0715 229529 Kwa wateja wetu waliopo maeneo hayo wawasiliane na
hawa wawakilishi ili waweze kupata huduma kwa haraka
zaidi.
Imeandikwa na
Emanuel Nevava
NI M’BAYA KWA KULINGANISHWA NA NINI HASA?” Kuna mengi tusiyoyajua!
4 HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
KAMPUNI YASHIRIKI MAONESHO SIKUU YA WAFANYAKAZI MEI MOSI
Kampuni ya Banana Investments Ltd imekua iki-
shiriki maadhimisho ya sherehe za wafanyakazi za
Mei Mosi kwa miaka mingi. Na kila mwaka huibuka
na ushindi mnono. Mwaka huu vilevile kampuni
imejinyakulia makombe mawili ikiwa ni pamoja na
mashindano ya maandamano ya miguu na naonesho
ya bidhaa kwenye maandamano ya magari.
Katika kuhakikisha kwamba wafanyakazi wanapon-
geza uongozi wa kampuni uliandaa tafrija fupi iliyo-
fanyika katika ukumbi wa kampuni mara baada ya
sherehe ya uwanjani. Karika tafrija hiyo ambayo ili-
jumuisha wafanyakazi tu, mkurugenzi mkuu alitoa
hotuba fupi akiwashukuru wafanyakazi wote kwa
moyo wao wa utendaji pamoja na kushiriki katika
maonesho hayo. Pia aliahidi kuwa kampuni
itaendelea kutoa huduma mbalimbali kwa wafanya-
kazi kwa uaminifu na kuomba pia wafanyakazi won-
yeshe uzalendo na uaminifu katika kufanya kazi za
kampuni. Pia aliwatakia sherehe njema ingawa na
yeye pia alikuwepo mpaka mwisho wa tafrija.
Baada ya hotuba ya Mkurugenzi mtendaji wafanya-
kazi waliendelea kupata chakula na vinywaji na
baadae lilipigwa disco la nguvu na Dj Rogaa.
Sherehe iliisha salama na kila mfanyakazi kurejea
nyumbani.
Imeandikwa na
Beatha Anthony
Maandamono ya Magari yakiongozwa na Pikipiki za kampuni
Magari ya Maonesho ya kampuni yakipita mbele ya mkuu wa
Mkoa yakiwa yamepambwa vizuri.
Mkurugenzi msaidizi akikabidhiwa ngao ya ushindi na mkuu
wa Mkoa.
Wafanyakazi wakiburudika na kinywaji na Muziki.
5 HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
Maendeleo ni hatua. Banana Investsments Ltd imepiga
hatua moja kati ya hatua nyingi, ya kufungua bohari
mjini Morogoro ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa
wateja wake. Bohari hii ipo maeneo ya Kihonda Ma-
gorofani Polyester Club mkabala na Carmel/Kanisa
Katoliki.
Wateja wa mkoa wa Morogoro na mikoa ya jirani sasa
watahudumiwa vizuri kutokana na uwepo wa bohari
hii. Kampuni inakaribisha maoni, ushauri na mawa-
kala maeneo ya Turiani, Kilosa, Ifakara, Morogoro
vijijini, na Mahenge. Wasiliana na afisa masoko Mi-
chael Emanuel kwa maelezo zaidi.
Fika ofisini au: Simu:
0713791119/0788791119/0759980851
Email: [email protected]
RAHA: RAHISI: HALISI. BIDHAA BORA YA BANANA
INVESTMENTS LTD - ARUSHA
BOHARI MPYA YAFUNGULIWA MOROGORO
HABARI KUTOKA SINGIDA
Picha: Jengo ambalo linatumika kama bohari kabla
ya marekebisho. Polyester Club Kihonda.
Baada ya kampuni kuanzisha utaratibu wa kutoa huduma
mojakwa moja kwa wateja wake, sasa wananchi wa Mkoa
wa Singida wanafurahia huduma hiyo kwani wanapata bid-
haa yetu hususani Raha kwa bei nzuri inayo wawezesha
kupata faida nono.
Kampuni kwa kushirikiana na wasambazaji
wake wanefanya upatikanaji wa kinywaji cha RAHA ku-
wepo na pia kuhakikisha kwamba bei yake inamuwezesha
hata mwananchi ya kawaida kuweza kununua.
Kampuni kupitia muwakilishi wake aliyeko
mkoani Singida Ndg Frank Joseph Urio inakaribisha
ushauri,maoni, kutoka kwa wateja mbalimbali katika
kuboresha biashara yake kwa faida ya wateja na kampuni
kwa ujumla. Mwakilishi wetu sasa anapatikana kwenye
ofisi iliyoko eneo la Shule ya Msingi Mughanga chumba
namba 23, Au wasiliana nae kwa simu namba 0754
607715, 0786 607718.
Imeandikwa na
Frank Joseph Urio
TANZIA
Kampuni ya Banana Investments Ltd unasikitika kutan-
gaza vifo vya wafanyakazi wawili wafuatao:-
Bi. Editha Joachim alifariki tarehe 03.02.2011 na
kuzikwa tarehe 08.02.2011 nyumbani kwake Moshono - Arusha. Bi Editha ali-
yekuwa anafanya kazi katika Idara ya
Uzalishaji ameacha mtoto mmoja na waju-
kuu wawili. Mungu ailaze roho ya Mare-
hemu Editha mahala pema peponi Amina.
Bw. Uhuru Kawiche alifariki tarehe 15.05.2011 na
kuzikwa tarehe 19.05.2011 nyumbani kwake Marangu
Mamba mkoa wa Kilimanjaro. Bw.
Uhuru alikuwa anafanya kazi katika
Idara ya Uzalishaji. Bw. Uhuru ameacha
mke pamoja na watoto. Mungu ailaze roho ya Marehemu Uhuru mahala pema
peponi Amina.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA
BWANA LIHIMIDIWE
Imeandikwa na Joan Mrema
6 HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
DONDOO MUHIMU ZA UNYWAJI SALAMA WA KILEO “ALCOHOL”
Kileo ni kitu chochote kinacholevya kilicho katika
mfumo wa bia, mvinyo, ama spirits. Jamii yote
duniani iwe Africa, Ulaya, Asia na hata Amerika, ime-
kuwa na aina yake ya kileo kulingana na utamaduni
wake. Wengi wameathirika kutokana na kutozingatia
njia nzuri za unywaji salama. Umri wako unaruhusu?
Kama una miaka chini ya miaka 18, USIJARIBU NA
ACHA KILEO. Hapa chini ni dondoo muhimu ku-
husu unywaji ulio salama:
Uhalali wa kinywaji chenyewe; Kila kinywaji kina
utaalamu wake unaokubalika kwa mnywaji ku-
toka kwa mamlaka husika. Tanzania tuna mam-
laka inayoitwa TBS-hawa ni wataalamu wa vi-
wango nchini na TFDA ni wataalamu wa vya-
kula na madawa. Kinywaji chako hakikisha ki-
meruhusiwa na kupewa nembo ya TBS kwa
usalama wa afya yako
Fahamu kiwango chako. Kama wewe ni mnywaji wa
Raha kwa mfano, kwanini leo unywe Raha + bia
+ viroba? Ni hatari kuzidisha kiwango cha kileo.
Kwa sababu huwezi kubaini kiasi ulichokunya
kwa urahisi.
Daima zingatia chakula kwanza kabla ya kileo/
pombe. Watalamu wanashauri ule vyakula
vyenye protini mfano nyama, samaki, jibini
’cheese’ kwa kuwa vyenyewe vinauwezo wa ku-
punguza kasi ya kileo kuingia katika mzunguko
wa damu kukuepusha na madhara.
Kubali kinywaji pale ukitakapo. Wengi wetu tume-
kuwa wataalamu wa ofa ya hapa na pale hata
kama mtu umetoka hospitalini leo ukiambiwa
“ebwana karibu tule vitu”, unavamia kileo. Je
nafsi yako ipo tayari? Kumbuka nafsi yako ni
muhimu sana kwenye maamuzi.
Epa kileo kama unatumia Dawa. Kama unaumwa na
unatumia dawa, acha kileo. Kama kuna umu-
himu sana wa kunywa, omba ushauri kwa
mtaalamu wa afya kwanza.
Epa unywaji ukiwa na njaa na kwenye joto kali
(juani). Wataalamu wanasema utapata kizungu-
zungu, udhaifu/legea, na kupoteza “mood” hali
iitwayo hypoglycemia,
Zingatia usalama wa maisha yako na wengine bara-
barani. Kama unajua utaendesha chombo cha
moto (gari, pikipiki hata baiskeli)
Zingatia unywaji wa maji. Kama ulipata kileo kiwe
kingi ama kidogo, shurti unywe maji mengi.
Unywaji wa kileo husababisha upotevu wa maji
mwilini kwa njia ya mkojo hivyo ukaribishaji wa
mning’inio “hang over” na kuumwa sana ki-
chwa. Dawa yake ni maji
Mwisho zingatia uchumi wako. Tunajua kuwa unap-
enda kunywa ila sasa uchumi wako unaruhusu?
Kinywaji unachotaka kunywa unamudu
kukinunua? Au unataka kunywa kwa mkopo,
upigwe, au kupewa ‘ofa’ daima huku familia
yako ikidhalilika?
Imeandikwa ma
Michael Massawe - Deport Incharge
Simu: 0713791119/0788791119/0759980851
Email: [email protected]
Morogoro
7 HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
Bw. Eliabu Joram –Machine Operator Bw. Eliabu ana cheti cha Technician in Mechanical Engineering
kutoka chuo cha Ufundi Arusha (ATC). Pia ame-
hitimu kidato cha IV katika shule ya Iyunga
Technical Secondary School. Ana uzoefu wa mi-aka 3 katika taasisi mbalimbali
Bw. Marko Andongolile – Machine Technician Bw. Marko ana Diploma ya Mechanical Engi-
neering katika chuo cha Ufundi Arusha (ATC).
Pia amehitimu kidato cha IV katika shule ya
Ifunda Technical iliyopo Iringa. Ana uzoefu
katika kazi hii kwa zaidi ya miaka 3 katika taasisi
mbalimbali.
Bw. Mohamed H. Luhindi – Auditing Technician Bw. Mohamed ana cheti cha Accountancy
Technician (ATEC II) kutoka National Board of
Accountancy and Auditing (NBAA). Pia na
Stashahada ya Elimu kutoka chuo cha Ualimu
Dar es Salaam. Na amehitimu kidato cha VI
katika shule ya Sekondari Union Islamic na
kidato cha IV katika shule ya Same Sekondari.
Bw. Tumaini A. Mungete – Marketing De-
velopment
Supervisor (Kilimanjaro Region) Bw. Tumaini ana Stashahada ya Biashara na utawala katika chuo cha Biashara (CBE). Pia
amehitimu kidato cha VI Kolila High School
Moshi na kidato cha IV Highlands Secondary
iliyoko Iringa. Ana uzoefu wa miaka 10 katika
taasisi mbalimbali.
Bw. Denis F. Kessy – Marketing Development
Supervisor (Dodoma Region) Bw. Denis ana Shahada ya juu ya biashara na
mahesabu kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Pia amehitimu kidato cha VI Minaki High School
na kidato cha IV Uru Seminary.
Bw. Patrice M. Melley – Marketing Development Supervisor
(Manyara region) Bw. Patrice ana cheti cha Biashara katika chuo
cha Uchira Business College na cheti cha Auto
mechanics grade two VETA Dar es Salaam. Pia
amehitimu kidato cha IV Sarwatt Secondary
School na anao uzoefu wa miaka 10 katika
taasisi mbalimbali
.
AJIRA MPYA, NGUVU MPYA KAMPUNI YA BANANA
Y’S MEN ARUSHA WAPATA UGENI KUTOKA GENEVA
Klabu ya kimataifa ya Y’s Men imeendelea kujipatia umaarufu
mjini Arusha kutokana na shuhuli zao ya kijamii wanazofanya
kupitia wanachama wake waliopo mkoani hapo. Mnamo tarehe
12/04/2011 Klabu ya Y’s Men Arusha walipata ugeni mkubwa
kutoka makao makuu ya Taasisi hiyo iliyopo Geneva. Ugeni huo ulikua ni Mr Takao Nishimura ambae ni mtendaji mkuu wa
taasisi hiyo.
Pamoja na mambo mengine Mr Takao alitembelea kiwanda cha
kuzalisha Net aina ya Olyset cha A to Z ambao wanatengeneza
net zinazisambazwa na Y’s Men hii ni kufanikisha project ya
Y’s Men ya kuzuia Malaria (Roll Back Malaria). Pia katika
kuonyesha utendaji wake Mr Takao alishirikiana na wanachama wa Y’s Men wa Arusha kupanda miti katika eneo
la Mlima suye. Baadaye wanachama waliandaa chakula cha
jioni katika mgahawa wa Albero uliopo barabara ya Haille Sil-
las na kubadilishana mawazo na mgeni huyo.
Vilevile vijana hawakubaki nyuma kwani waliweza kutuma
muwakilishi katika Mkutano wa Jimbo la Y’s Men la kanda ya
Africa, kusini Mashariki. iliyofanyika Kitwe, Zambia na pia
walipokea ugeni kutoka Geneva ambae ni mtendaji mkuu Y’s
Youth Mami Hashikazi raia wa Japan. Katka Mkutano huu
Tanzania iliwakilishwa na Willy Kwayu wa Club ya Arusha.
Kutokana na changamoto zilizoonekana wakati wa mazun-
gunzo na wakeni hao Club ya Y’s Men Arusha pamoja na
Y’s Youth wamejipanga imara ili kuhakikisha wanatoa
huduma kwa jamii kulingana na mungu alivyowajalia.
Pia wanajipanga kuendesha mafunzo kuhusu TB na vilevile
kufungua rasmi club ya Y’s Youth ya Moshi. Kwa wale wata-
kaopenda kujiunga wawaliliane na Rais wa Club hiyo ambae ni
Miss Lucy Tesha Mob +255716395497 kwa upande wa vijana
na Mr Shanell Kavishe Mob +255717157128.
Na Beatha Anthon Mr Takao akipanda mti katika maeneo ya Mlima Suye.
8 HALIUZWI
Toleo la 21 April - June
Makao Makuu Kiwanja Na. 311, Kitalu jj Oloirien Village, P. O. Box 10123, Arusha TANZANIA S i m u : +255754224440,+255272506475 E-mail: [email protected] .banana.co.tz
Dar es Salaam Depot Ubungo Kibangu, S. L. P. 79407, Dar es Sa-laam TANZANIA Simu: +255 222 774 276, +255 756 707 983 Email: [email protected]
Tanga Depot Barabara ya 4, S. L. P. 5150, Tanga TANZANIA Simu: +255 272 646 134
Email:
Tunawakaribisha wafanyabiashara kujiunga na Kampuni yetu ya Banana Investments Ltd kusambaza kinywaji chetu kwenye mikoa am-bayo RAHA haijafika. Hali ya sasa katika usambazaji wa mvinyo wa Raha upo kama unavyoonyesha hapo juu kwenye Ramani
Morogoro Deport
Kihonda Area Simu +255713791119
+255788791119
+255759980851
Email: