kilimo na ufugaji - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.ufugaji wa kuku wa kienyeji ....

63
Smart agro business KILIMO NA UFUGAJI Mbinu za ujasiliamali SMART AGRO BUSINESS PUBLISHER /www.smartagrobusiness.wordpress.com/

Upload: doancong

Post on 28-Aug-2019

361 views

Category:

Documents


22 download

TRANSCRIPT

Page 1: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

1

1

Smart agro business KILIMO NA UFUGAJI

Mbinu za ujasiliamali

SMART AGRO BUSINESS PUBLISHER

/www.smartagrobusiness.wordpress.com/

Page 2: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 2 Tanzania.

YALIYOMO

1.MISINGI MITANO(5) MUHIMU YA KUFANIKIWA KWENYE UJASILIAMALI NA BIASHARA.

2.NJIA TANO ZA KUWA MWAJIRI BORA NA KUFANIKISHA KWENYE BIASHARA YAKO.

3. FURSA 150 ZA UJASILIAMALI NA BIASHARA TANZANIA.

4.UTAMBUZI WA MAGONJWA YA KUKU KUPITIA KINYESI.

5.JINSI YA KULEA VIFARANGA VYA NDEGE(mf Kuku)

6.USINDIKAJI WA VIAZI VITAMU.

7.NGUZO 7 ZA MAFANIKIO KATIKA ELIMU YA BIASHARA.

8.HATUA 26 ZA KUFANIKIWA KATIKA BIASHARA

9.KILIMO CHA MATIKITIMAJI.

10.KILIMO CHA MANANASI.

11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI

12.KILIMO BORA CHA NYANYA

Page 3: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 3 Tanzania.

(1)

Misingi Mitano(5) Muhimu Ya Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali na Biashara

Katika ulimwengu wa sasa ambao ajira zimekuwa ngumu na shida kupatikana, ujasiriamali na biashara vimekuwa ndio kimbilio la wengi. Watu wengi wanaingia kwenye biashara kama njia kuu ya kujipatia kipato.Pamoja na biashara kuonekana kuwa kimbilio la wengi sio wote wanaoingia kwenye biashara wanafanikiwa. Tafiti zinaonesha kwamba asilimia tisini ya biashara zinazoanzishwa zinakufa mwaka mmoja baada ya kuanzishwa. Na hata hizo zinazovuka mwaka mmoja asilimia tisini hufa baada ya miaka mitano. Hivyo kama mwaka huu zimeazishwa biashara mia moja basi miaka mitano ijayo ni biashara moja tu itakayokuwa bado inadumu.Kwa nini biashara nyingi zinashindwa kudumu?

Page 4: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 4 Tanzania.

Biashara nyingi zinakufa kutokana na ukosefu wa elimu muhimu kuhusiana na biashara na ujasiriamali. Watu wengi wanaoingia kwenye biashara wanaingia kwa kuangalia tu ni kitu gani watu wengine wanafanya na wao kufanya hivyo hivyo.

Biashara ni rahisi sana kufanya ila ni ngumu kuendesha na kuikuza mpaka iweze kukupa faida kubwa sana. Ili uweze kuendesha na kukuza biashara itakayokupa faida kubwa ni muhimu kuchukua muda na kujifunza vitu vya muhimu vinavyohusiana na biashara.

Leo tutajifunza misingi mitano muhimu ya biashara ambayo kila biashara inatakiwa kuizingatia. Wewe kama mjasiriamali una jukumu la kujifunza na kufuata misingi hii ili uweze kufikia malengo yako kwenye ujasiriamali na biashara.

Misingi mitano muhimu ya biashara.

Ili biashara yoyote iweze kudumu na kukua inahitaji kufuata misingi ifuatayo.

1. Kutengeneza thamani/ubunifu.

Ili biashara iweze kukua na kutengeneza faida ni lazima itengeneze bidhaa au huduma ambayo ni ya thamani kwa wateja. Ni lazima utoe bidhaa au huduma ambayo watu wanaihitaji sana ili kuboresha maisha yao. Kama hujaanza biashara fikiria ni kitu gani cha thamani ambacho watu wanakihitaji ila wanakikosa, kisha anza kuwapatia na utajenga biashara kubwa. Kama tayari unafanya biashara angalia ni kitu gani cha thamani unachotoa kwa watu na angalia jinsi unavyoweza kuboresha ili kupata wateja wengi zaidi.

2. Soko.

Kuwa na kitu chenye thamani pekee bado haikutoshi kutengeneza biashara kubwa, ni lazima kuwe na soko linalohitaji bidhaa au huduma hiyo. Hata kama soko lipo bado sio rahisi kwa kila mtu kujua kwamba unatoa huduma muhimu. Hivyo ni muhimu kutafuta soko la biashara yako kwa njia mbalimbali zikiwemo matangazo. Inakubidi uhakikishe watu wanajua uwepo wa biashara yako na utengeneze uteja ili watu waje kupata thamani unayotoa. Kukosa soko la uhakika ni chanzo cha kufa kwa biashara nyingi.

Page 5: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 5 Tanzania.

3. Kuuza.

Ili biashara ikue ni lazima uweze kuuza thamani uliyotengeneza. Ni muhimu uweze kuwashawishi watu wanunue bidhaa au huduma unayotoa. Kuuza ndio moyo wa biashara ambapo kama usipokuwa makini ni rahisi kwa biashara kufa.

4. Kufikisha thamani.

Kama umewaahidi wateja wako kwamba bidhaa ama huduma unayotoa itaboresha maisha yao basi hakikisha hicho ndio kitu kitakachotokea kwa wateja. Ni lazima uweze kufikisha thamani uliyoahidi kwa wateja. Kwa kushindwa kufanya hivi wateja watakuona wewe ni tapeli na hawatanunua tena bidhaa yako. Kama biashara itashindwa kutengeneza wateja wanaojirudia ni lazima itakufa.

5. Fedha(mapato na matumizi).

Usimamizi wa fedha ni muhimu sana kwenye biashara. Ili biashara iweze kudumu ni lazima iweze kutengeneza mapato makubwa kuliko matumizi na uzalishaji. Ni lazima iweze kuzalisha fedha za kutosha kuiendesha na ibaki faida. Ukosefu wa fedha unaotokana na mauzo kidogo na matumizi makubwa ndio chanzo cha kufa kwa biashara nyingi.

Misingi hii mitano ni muhimu sana kwa biashara. Hakuna msingi ambao unaweza kusema ni muhimu zaidi ya mwingine, yote inategemeana. Ili biashara yoyote iweze kudumu ni muhimu kuzingatia misingi hiyo.

Page 6: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 6 Tanzania.

(2)

Njia Tano Za Kuwa Mwajiri Bora Na Kufanikiwa Kwenye Biashara Yako.

Huwezi kuendesha biashara kubwa na yenye mafanikio kama unafanya kila kitu peke yako. Unahitaji watu wengi sana wa kukusaidia kufikia ndoto kubwa ulizonazo kwenye biashara yako.Lakini pia sio kila mtu unayemwajiri anaweza kukusaidia kukuza biashara yako. Hivyo ni muhimu sana kuwa na wafanyakazi ambao wanaweza kuwa msaada mkubwa kwako.

Pamoja na kuwa na wafanyakazi wazuri, bado mambo hayatakwenda yenyewe kama unavyoweza kufikiri. Wewe kama mmiliki wa biashara unahitaji kuwa mwajiri au bosi mzuri ili uweze kwenda vizuri na wafanyakazi hawa. Kama utashindwa kwenda nao vizuri, haijalishi wana uwezo mzuri kiasi gani, bado utashindwa kufaidi uwezo huo.

1. Tengeneza utamaduni wa kufanya kazi kama timu.

Kuna faida kubwa sana kwenye timu, kwa sababu watu wote hatulingani au kufanana, basi tunahitaji kusaidiana kwa hali ya juu. Kuna mtu ambaye ni mzuri kwenye jambo fulani na mbovu kwenye jambo jingine. Mtu huyu anapokutana na mwingine ambaye anafukia mapungufu yake, biashara yako inakwenda vizuri sana.

Page 7: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 7 Tanzania.

Hakikisha wafanyakazi wako wanafanya kazi kwa kushirikiana na wanajua wote lengo lao ni moja ambalo ni mafanikio ya biashara. Kwa kushirikiana huku pamoja na wewe mnaweza kuleta mabadiliko makubwa.

2. Tambua michango ya wafanyakazi kwenye ukuaji wa biashara yako.

Pamoja na kutoa kipato kizuri, binadamu hawavutiwi na kipato pekee, bali wanapenda kuona wakithaminiwa kwa kile wanachofanya. Tambua michango ya wafanyakazi wako kwenye ukuaji wa biashara yako, na wapongeze na kuwashukuru kwa juhudi zao. Unaweza kufanya hivi kwa kuweka nao malengo pamoja na yanapofikiwa wakapata zawadi fulani au hata kutambuliwa kwa kazi yao bora. Kwa vyovyote vile hakikisha wanajisikia ufahari kuweka juhudi zaidi.

3. Wasaidie wafanyakazi kujiongoza wenyewe.

Ni kawaida kwa mmiliki wa biashara kutaka kumsimamia mfanyakazi kwa karibu sana. Unaweza kufanya hivi ila hii itakuchukulia muda wako mwingi na hivyo utashindwa kukuza biashara yako. Pia wafanyakazi wako ni watu wazima, na hakuna mtu mzima anayependa kuona anafuatiliwa kwa kila kitu.

Badala ya kuwafuatilia wafanyakazi wako kwa kila kitu, kubaliana nao majukumu wanayotakiwa kutekeleza kisha wasaidie waweze kujisimamia mwenyewe na kutekeleza majukumu yao. Kwa njia hii watu watafurahia uhuru huu na watakuwa na uzalishaji mkubwa sana.

4. Wajengee wafanyakazi kujiamini na sio hofu.

Waajiri wengi wamekuwa wanajenga hofu kubwa kwa wafanyakazi wao. Watu wanahofia wakifanya jambo fulani au wakishindwa kufanya jambo fulani watafukuzwa kazi. Hii inawafanya watawaliwe na hofu na hivyo kushinda kufanya mambo makubwa na mazuri.

Kamwe usiwatishie wafanyakazi kwamba utawafukuza kama ndio njia ya kuwafanya watekeleze majukumu yao, hivyo unawajengea hofu. Kama kuna wafanyakazi ambao hawatimizi majukumu yao, kaa nao na ujue tatizo ni nini. Wakati mwingine hawana uelewa halisi wa kazi yao. Wajengee kujiamini na kuamini kwamba wanaweza na watakufanyia kazi nzuri sana.

Page 8: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 8 Tanzania.

5. Makosa ni sehemu ya kujifunza.

Jambo jingine muhimu sana unalotakiwa kufanya wewe kama mwajiri ni kuchukulia makosa wanayofanya wafanyakazi wako kama sehemu yao ya kujifunza. Usitoe adhabu kubwa kwa wafanyakazi wanaokosea, ila jua hilo ni darasa zuri kwao na wakati mwingine hawatarudia tena.

Wasaidie waone kwamba kosa wanalofanya wanatakiwa kujifunza ili wasilirudie tena na hii itawafanya kuwa bora. Ila kama utawatishia kwamba wakifanya kosa ni dhambi kubwa, watakazana kuepuka makosa na hivyo kuzuia ukuaji wa biashara yako

Page 9: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 9 Tanzania.

(3)

Fursa 150 za ujasiriamali, biashara na miradi nchini Tanzania

1. Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha. 2. Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha. 3. Kutengeneza na kuuza tofali 4. Ufundi, Website updating/ Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na Makampuni mbalimbali. 5. Kuanzisha kituo cha redio na televisheni 6. Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na vifaa vya compyuta na mawasiliano. 7. Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k 8. Kushona na kuuza nguo.

Page 10: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 10 Tanzania.

9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali, 10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Kuku, Bata, na wengine. 11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo. 12. Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu. 13. Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza popcorn na kuziuza. 14. Kusajili namba za simu na kuuza vocha 15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta 16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika. 17. Kuuza Mitumba 18. Kusimamia miradi mbalimbali 19. Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali 20. Kufungua banda la chakula na chips 21. Kukodisha turubai viti na meza 22. Kufungua Supermarket 23. Kufungua Saluni 24. Kufungua Bucha 25. Video Shooting & Editing. 26. Kufungua Internet cafe 27. Duka la kuuza matunda 28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline. 29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement, vifaa vya umeme, duka la mabati 30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi

Page 11: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 11 Tanzania.

ya ICT 31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k 32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor) 33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k 34. Kuuza maji kwa jumla na rejaleja. 35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora. 36. Kukodisha Music 37. Kuanzisha Mradi wa Taxi 38. Kuanzisha mradi wa Daladala 39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters, HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa vingine. 40. Kununua magenerator na kukodisha 41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu 42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP) 43. Kuuza mabati na vigae 44. Kujenga apartments 45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote 46. Kufungua Duka la samaki 47. Kufungua Duka la nafaka 48. Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo. 49. Kujenga hostel 50. Kuuza vocha na ving’amuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental. 51. Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda na wananchi.

Page 12: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 12 Tanzania.

52. Ufundi simu 53. Kufungua Hospitali, Zahanati. 54. Maabara ya Macho, Meno 55. Kuchimba/Kuuza Madini 56. Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na fax 57. Kuuza miti na mbao 58. Kufungua Grocery, bar 59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha 60. Kucharge simu/battery 61. Duka la TV na vifaa vingine 62. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na tamasha mbalimbali (catering). 63. Banda la kupigisha simu 64. Kuuza na kushona Uniform za shule 65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla. 66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari 67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe 68. Kuuza fanicha 69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi ya magari na mitambo. 70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel) 71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium. 72. Kuuza vioo 73. Kushona na kukodisha nguo za harusi 74. Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari 75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine). 76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site

Page 13: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 13 Tanzania.

(boots, helmets etc) 77. Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi 78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya redio na televisheni 79. Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games) 80. Kufungua benki 81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga 82. Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k 83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali 84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane) 85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu. 86. Kuanzisha viwanda mbalimbali 87. Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali zinazoendana na mawasiliano ya Vodacom, TTCL, AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k. 88. Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe, mikutano mbalimbali 89. Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa barabara na kukodisha 90. Kutengeneza antenna na kuuza 91. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao 92. Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo 93. Biashara ya kuagiza magari 94. Kufanya biashara za Jukebox 95. Kukodisha matenki ya maji 96. Kufungua duka la kuuza Asali 97. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha 98. Kufungua Duka la vinyago, batiki

Page 14: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 14 Tanzania.

99. Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZY PESA 100. Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym). 101. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi. 102. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy). 103. Kufungua Kampuni ya Ulinzi 104. Kufungua kampuni ya "Clearing and fowarding" 105. Kuchezesha vikaragosi 106. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki 107. Kuuza baiskeli 108. Kuuza magodoro 109. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe, vijiko, 110. Kuuza marumaru (limestones) 111. Kuuza kokoto 112. Kuuza mchanga 113. Kufundisha Tuisheni 114. Biashara za bima 115. Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya anga (ndege) 116. Biashara za kitalii 117. Biashara za meli na maboti. 118. Kampuni ya kuchimba visima 119. Kufungua ofisi ya wakili/ mawakili wa kujitegemea 120. Kuuza mkaa 121. Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali 122. Kampuni ya kupima ardhi 123. Kampuni ya magazeti 124. Kuchapa (printing) magazeti 125. Kuuza magazeti

Page 15: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 15 Tanzania.

126. Kuchimba mafuta 127. Kiwanda cha kutengeneza mabati 128. Kiwanda cha kutengeneza fanicha 129. Kiwanda cha kutengeneza matairi 130. Kutengeneza vitanda vya chuma 131. Kununua nyumba katika Maghorofa (Apartments) na kuzikodisha. 132. Kukodisha makapeti 133. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe. 134. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka. 135. Kazi ya ususi na kusafisha kucha. 136. Kuuza Gypsum 137. Malori ya kubeba mafuta na Mizigo 138. Duka la kuuza mboga za majani 139. Duka la kuuza maua. 140. Kampuni ya kuzoa takataka 141. Kampuni ya kuuza magari 142. Kuuza viwanja 143. Uvuvi 144. Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea fensi 145. Uchoraji wa mabango. 146. Duka la kuuza silaha 147. Ukumbi wa kuonesha mpira 148. Biashara ya mlm (network marketing) 149. Yadi kwa ajili ya kupaki magari 150. Mradi wa trekta za kukodisha.

Page 16: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 16 Tanzania.

(4)

Utambuzi wa magonjwa ya kuku kupitia rangi ya kinyesi

Kuku kama jamii nyingine za ndege nawao pia wanasumbuliwa sana na magonjwa mbalimbali,ndugu mfugaji tunakupa njia bora ya kugundua magonjwa hayo kwa kutumia kinyesi chao.Yafuatayo ni magonjwa hatari na pia uwakumba sana kuku;

1. Mharo mweupe(pullorum bacilary diarrhoea) ugonjwa huu huathiri zaidi vifaranga kabla ya wiki nne huharisha mharo mweupe, TIBA kuu ni usafi pekee kwenye banda na kuepusha maji yasimwagike ovyo.

2.Kipindupindu cha kuku(fowl cholera) kinyesi cha kuku ni njano tumia dawa za salfa, eg Esb3 au amprollium

3.Coccidiosis mwanzo kinyesi cha kijivu na baadae huharisha damu iliyochanganyika Tumia dawa ya VITACOX au ANTICOX 4.Mdondo(Newcastle)

Page 17: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 17 Tanzania.

kuku hunya kinyesi cha kijani sio kila kijani ni Newcastle na hakuna tiba ila kuna kinga.

5.Typhoid Kinyesi cheupe kinagandia sehemu za nyuma au hulowana sehemu za haja dawa ni Eb3 6.Gumboro

Huathiri zaidi vifaranga kinyesi huwa ni majimaji Dawa hakuna tumia vitamini na antibiotic kwa kalenda ya chanjo kama ifuatanyo. 1week- Marek's vaccine 2week- Newcastle vaccine 3week- Gumbolo vaccine 4week- Gumbolo vaccine tena pumzisha chanjo kisha endelea ikifika wiki ya nane 8week-Fowl pox vaccine 9week-Newcastle vaccine pumzika tena mpaka wiki ya kumi na name 18week- Fowl typhoid vaccine

Baada ya kumaliza chanjo hizi endelea kumpa chanjo ya Newcastle vaccine kila baada ya miezi mitatu au minne.Ukifanya hivi kuku wako wote hawataumwa na magonjwa nyemelezi tena

Page 18: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 18 Tanzania.

(5)

Jinsi ya kulea vifaranga vya ndege mfano vifaranga vya kuku

Hakikisha banda la vifaranga pamoja na vyombo umepuliza dawa ya kuua bakteria kwa kutumia dawa ya VRID nk kabla hujaingiza vifaranga.

Hakikisha unavifaa vya joto (a) kama unatumia umeme au solar tumia Balbu, heater, modules nk. (b) kama umeme huna tumia chemli, karabai, jiko la mkaa, vidumu vya maji ya moto, vyungu vya joto.

Baada ya hapo kuanzia siku ya 1-5 wape Grucose(glocovent ya ndege) + Otc plus/chicken plus + vitamin either ununue Multivitamin/vitalstress au ununue molasses ya unga 1kg +40litre za maji wape kila siku ni nzur.

Wakitimiza siku ya 7 wape chanjo ya Newcastle deases(mdondo) kisha uendelee kuwapa maji ya molasses baada ya kutoa maji ya mdondo masaa 2 yakipita.

wakitimiza wiki 2 yaan siku 14 zikiisha wape chanjo ya gomboro(uendelee na maji ya molases.

wakitimiza wiki 3 utarudia chanjo ya mdondo na kuwapa antibiotics kama Otc 20% or otc 50% +Amprolium kwa muda wa siku 4-8 na utaendelea na maji ya molases.

Wakitimiza wiki ya 4 wape chanjo ya Ndui(fowlpox) pamoja na dawa ya minyoo kama Ascaress( piperazine)

KUMBUKA:Chanjo zote utarudia kila baada ya miezi 3.

Page 19: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 19 Tanzania.

Chakula cha vifaranga kuanzia siku ya 1 mpaka wiki ya 8 wape either sterter / chick mash na kuanzia miezi 3-4 wape Chakula aina Growers /finisher nk.

Wakifisha miezi 5 nashauri anza kuwapa Chakula aina ya Layers mash 50 kg +1 kg ya G.L.P so G.L.P ni aina ya virutubisho vyenye kuongeza wingi wa utagaji wa mayai kwa ndege. wakifikisha wiki ya 16 kata midomo kisha wape Neoxyvital mfululizo kwa muda wa siku 4-6

usafi wa banda na vyimbo ndo nguzo ya msingi hakikisha kila baada ya miezi 3 unapuliza dawa kuuwa bakteria kama VRID pia zingatia muda sahihi wa madawa kwa magonjwa yote ya kuku iwe ya Virus, Bakteria nk pia maji safi ni muhimu kitaalamu kuku mmoja hunywa maji robo litre na gram 125/150 za chakula per day so ukizingatia hvyo hakika utaona mafanikio ya ufugaji acha kufuga fuga kibiashara nitaendelea kuwafahamisha Faida za Mlonge(moringe) pamoja na DCP(Dicalcium Phosphate ) kwa jamii za na wanyam

Page 20: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 20 Tanzania.

(6)

Usindikaji wa viazi vitamu

Ingawaje viazi vitamu vinatumiwa kama kiazi kilicho chemshwa, katika maeneomengine ya Afrika mashariki vinatumika kutengeneza chipsi na unga kwa ajili ya kuhifandi chakula na kwa ajili ya kuuza katika masoko madogo madogo vijijini na hata mijini.

Pamoja na faida ya kuhifadhi, utengenezaji wa chipsi na unga wa kuanika una faida zifuatazo:

1. Hurahisisha utunzaji na usafirishaji 2. Kupunguza ukubwa wa viazi na upotevu wa viazi kwa sababu viazi uharibika haraka na kama viazi vikiachwa ardhini wadudu (fukuzi) huweza kushambulia 3. Huongeza muda wa kuhifadhika 4. Unga na chipsi vina virutubisho vingi kwa vile kiwango kikubwa cha maji kwenye kiazi kinakuwa kimetolewa kwa hiyo kiwango cha protini, wanga, pectini, mafuta na chumvichumvi huongezeka 5. Huongeza chanzo cha mapato kwa wakulima kama vile upatikanaji wa masoko na chanzo kipya cha kipato

Njia mbalimbali za utengenezaji wa kienyeji kama vile kuanika juani viazi na nyinginezo kuna mapungufu yake ikiwemo:

1. Njia hizi hutegemea sana hali ya hewa (kama mvua ikinyesha inabidi kuanua na kwenda kuhifadhi sehemu kavu)

Page 21: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 21 Tanzania.

2. Zinahitaji watenda kazi wengi kwa ajili ya kumenya, kukatakata, kuanika juani, kugeuza geuza unga wakati wa kuanika, kulinda unga ili usiliwe na mifugo, kuanua unga kama mvua ikinyesha nk 3. Kuto kuwa na udhibiti wa vimeng’enyo wakati wa kuanika husababisha kuwa na unga unaotoa harufu na wenye rangi ya kizambarau 4. Ukubwa wa chipsi hutofautiana 5. Ukosefu wa uwiano katika ukubwa wa vipande vyake 6. Kutokuwa na usawa na kiwango cha rangi

7. Uharibifu wa ngozi ya viazi 8. Kuwepo kwa mchanganyiko usiotakiwa.

Ni muhimu kujua kuwa chipsi na unga kutokana na aina mbalimbali ya viazi utofautiana katika tabia kama vile vionjo na rangi. Hivyo, ni muhimu kuonja, kutambua na kutenganisha aina mbalimbali ya viazi wakati wakutengeneza chipsi kavu , unga na mlamba ili kupata unga wa viazi wenye rangi, harufu nzuri na virutubisho bora. Kwa vile inahusisha gharama ni bora teknolojia hii ikatumiwa na vikundi vya wakulima. Njia bora za utengenezaji wa viazi zinalenga kuboresha zile za kienyeji.

Hatua za kufuata ili kutengeneza chipsi na unga bora wa viazi vitamu ni kama zifuatazo:

1.Uchaguzi wa malighafi

Chagua viazi vizuri kwa ajili ya utayarishaji

2.Kuosha/ kusafisha kiazi

Kiazi kisafishwe kwa maji na kuhakikisha udongo wote umeondolewa na sehemu zilizoharibika zitolewe ili kupata kiazi safi Pipa lakuoshea limetengenezwa kwa ajili ya kusaidia uoshaji. Pipa hilo lina dramu la lita 200 lililofungwa kwenye mpingo wa sambamba. Pipa hilo limekatwa kwa urefu ili kutoa mlango ambao unaweza kufungwa na kufunguliwa wakati wa uwekaji na utoaji viazi wakati wa kuosha. Ndani ya pipa hilo kuna brashi zilizofungwa kwa mkabala. Pembeni imefungwa kuwezesha kuzungusha pipa hilo na kuosha viazi hivyo. Upande mmoja wa pipa unaweza kufunguliwa ili kutoa maji machafu baada ya uoshaji. Pipa hilo linaweza kutumika kuosha hadi kilo 40 za viazi vitamu kwa dakika 10-20

Page 22: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 22 Tanzania.

kwa kutumia lita 30 za maji masafi. Kama mapipa hayapatikani, mabeseni makubwa yanaweza kutumika. Baada ya kuosha pitisha viazi kwenye maji masafi.

3. Ukataji

Baada ya kusafishwa viazi vitamu inabidi vianikwe kwa muda kwenye sehemu safi juani kwa dakika 10 kuondoa maji kwenye gozi. Mashine ya mkono au motor inaweza kutumika kukata viazi vitamu katika vipande vinavyolingana ukubwa.

4.Kuweka majini

Vipande vilivyokatwa vya viazi vyeupe viwekwe ndani ya maji kwa dakika 15-30 ili kuzuia upotevu wa rangi lakini angalizo visikae muda mrefu kwenye maji maana utapoteza vitamin A. Kiasi cha maji kiwe ni mara mbili ya uwingi wa vipande vya viazi na yawe ni ya kutosha kasha funika vipande hivyo.

5.Uanikaji

Vipande vya viazi kisha huanikwa juani kwenye kitalu kilichoinuliwa kwa muda wa masaa 4-6 kama hali ya hewa ni nzuri au kwenye vyombo vya kuanikia kutumia kuni au mkaa kama chanzo cha joto. Matrei ya kuanikia yawe yameinuliwa juu ya udongo kuzuia vumbi na uchafu mwingine. Kama uanikaji sio wa kutosha, chipsi zitakuwa na hatari ya kupata ukungu wakati wa kuhifadhi. Muda wa kuanika utategemea ukubwa wa vipande vya viazi, kugeuzwa geuzwa wakati wa kuanika, na kiasi cha chipsi kilichowekwa ndani ya trei. Ni vizuri kuanza uanikaji wakati wa asubuhi.

6.Uchambuaji

Viazi vitamu vilivyoanikwa vifanyiwe uchambuzi ili kupata vyenye ukubwa sawa kabla ya kufunga kwenye maboksi au kufanyiwa utengenezaji mwingine, kwa vile inaweza kuharibu ubora au matumizi yaliyokusudiwa au bei yake.

7.Kusaga

Viazi vilivyoanikwa vinaweza kusagwa ili kupata unga.

Page 23: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 23 Tanzania.

8.Ufungaji

Unga wa viazi vitamu unaweza kufungwa kwenye mifuko ya nailoni, ndoo au makopo. Chipsi zinaweza kutunzwa kwenye magunia safi ya katani au magunia ya visalfeti au mifuko ya nailoni. Uwekaji wa nailoni nyeusi ndani ya mifuko ya kuhifadhia husaidia kupunguza upotevu wa vitamini A (ambayo huweza kuharibiwa na jua) wakati wa kuhifadhi.

Kuhifadhi

1. Viazi hivyo viwekwe kwenye sehemu nyenye ubaridi na kavu 2. Yenye hewa ya kutosha. 3. Mabanzi ya mbao yanaweza kutumika kubania mifuko yenye viazi ili kuzuia unyevu usiingie toka sakafuni. 4. Ukaguzi wa mara kwa mara ufanywe ili kubaini muda wa kuhifadhi viazi kabla ya kuharibika kwenye vyombo vya kuhifadhia vya aina mbalimbali na kuzuia wadudu na panya waharibifu. 5. Mifuko ni lazima iandikwe majina ya mkulima aliyezalisha na mtengenezaji, tarehe ya kutengenezwa, jina la kiazi; na muda wa mwisho kutumika.

Utambulisho

Muda wa matumizi hutofautiana kutegemea aina ya viazi kwa hiyo jaribio lifanywe ili kupata muda kwa kila aina. Kama aina ya virutubisho inahitajika kuonyeshwa kwenye mifuko basi sampuli zichukuliwe kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi. Ili kulinda ubora wa chipsi kavu zilizohifadhiwa, unapaswa kufanya ufuatiliaji wa: kiwango cha unyevu (kiwe chini ya asilimia 10-15). Kupima unyevu, uma kipande kwenye meno mpaka usikie kiinapasuka bila kunata mdomoni

Page 24: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 24 Tanzania.

(7)

Nguzo 7 za Mafanikio Katika Elimu, Biashara

Utangulizi Mafanikio ni hali ambayo kila mtu anapenda kuwa nayo na kuyafikia kila mara. Mafanikio humfanya mtu afarijike, ajisikie yuko salama, afurahi na kusonge mbele kwa ujasiri zaidi. Mafanikio humfanya mhusika kuwapenda wengine na kuwa mkarimu. Ukikosa mafanikio unaweza kuwa na hasira, kukata tamaa, kutawaliwa na mfadhaiko wa akili, ulevi wa kupindukia, uzinzi na kwa ujumla kuwa na tabia mbaya. Mtu anayeshindwa kufanikiwa huwa hana ujasiri na kila mara ametawaliwa na kushindwa, Ushirika mdogo na wenzake na sio mshauri mzuri kwa wengine Tafsiri ya Mafanikio Mafanikio ni ile hali ya kuweza kuyafikia kusudi au lengo lako la maisha

ambalo Mwenyezi Mungu alikuumbia nalo. Kila mtu ameumbwa kwa kusudi na hilo kusudi ni wewe peke yako unalo jukumu la kulifikia. Mwingine aliumbwa kuwa mchungaji na mwingine kuwa mwalimu, kuna wengine wafanyabiashara na wengine wanasiasa nk. Ukiweza kufikia hilo kusudi au lengo ndipo tunasema mtu fulani kafanikiwa.

Haitoshi tu kusema kuwa mtu ana majumba, mashamba, magari au pesa

nyingi benki ndio kafanikiwa. Inategemea ni kwa jinsi gani hizo pesa, majumba, mashamba, magari yana uhusiano kwanza na lengo kuu na pia umepataje hizo mali. Wengine wanapata kwa

Page 25: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 25 Tanzania.

kuua, kula rushwa, kuiba, kutapeli. Mafanikio ya namna hii sio mafanikio ya kweli.

Ili ufanikiwe unatakiwa angalau kuzingatia nguzo 7 hapa chini: 1. Kupanga 2. Kupenda 3. Kujiamini 4. Kuvumilia 5. Kuwa na mbadala 6. Kuwajibika 7. Kuweka vipaumbele

1) Kupanga Wahenga walisema usipopanga umepanga kushindwa Walisema pia usipokuwa na malengo kila lengo litakufikisha uendako Mipango ndio inaweka majukumu ya kufanya. Mfano kama hujapanga la kufanya asubuhi waweza kulala hata mpaka jioni bila kuona kama kuna shinda yeyote. Kupanga inaanzia kwa kuweka maono ya maisha yako. Unataka baada ya miaka 15/20 kuwa na mafanikio ya namna gani katika maeneo yafuatayo

1. Kiuchumi 2. Kiroho 3. Kielimu 4. Kisiasa 5. Kijamii

i) Kiuchumi Panga unatazamia kuwa na kampuni, ranchi, au ajira kwa ngazi ya mkurugenzi wa shirika, kampuni, taasisi ya serikali wenye mshahara mkubwa kulingana na wakati huo nk ii) Kiroho Upange kuwa maisha yako ya kiroho yatakuwaje baada ya muda huo, utakuwa mchungaji, mwinjiisti shekhe. Au hata kiroho utakuwa umepoa au umemuishia Mungu kwa undani zaidi nk iii) Kielimu Panga kama unategemea kuwa na digrii mbili au tatu baada ya miaka 15 au laa. iv) Kisiasa Kama unapendelea mambo ya siasa na upange kwamba baada ya miaka 15 utakuwa mbunge, rais wa nchi nk.

Page 26: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 26 Tanzania.

v) Kijamii Utakuwa na familia ya namna gani, mke, watoto, elimu yao,kujenga nyumba,uhusiano wa majirani na familia yako uweje nk. 2) Kupenda Upendo tunaouzungumzia hapa ni passion. Huu ni upendo wenye kujitoa na kuwajibika zaidi. Kile kitu unachokifanya jitahidi sana ukipende. Kama ni kozi ya udaktari hakikisha unakipenda na udaktari wenyewe unaupenda kiukweli. Kwa maana hii hakikisha unachagua vizuri njia unayopita.Penda pia na hali ya mafanikio unayotarajia, mfano penda kuwa bilionea au msomi kwa ngazi ya udaktari, kama ni mwanafunzi penda ile hali ya kupata alama ya “A” kwa masomo yako nk.Usijipeleke kwenye unesi wakati kazi za kuwahudumia wagonjwa inakupa kinyaa au unaona ni kama utumwa. Ukipenda kitu utakuwa tayari kuvumilia, kupambana na kukabiliana na changamoto zinazoambatana na eneo husika 3) Kujiamini (Kuwa mjasiri na kujiamini) Ujasiri unakupa mambo mengi. Kujiamini, kuchukua hatua, kuamua na kutenda hata kama wengi wanakupinga na kukubeza unaweza kufanya mambo makubwa ambayo hata wao hawakutegemea kama ungeweza. 4) Kuvumilia Kazi nyingi zina changamoto tena kubwa na nyingi. hakuna kazi rahisi duniani. Usipokuwa king’ang’anizi na mvumilivu hutakuwa unatangatanga mara leo mikaa mara kesho umachinga wa bango mara kesho kutwa mfanyakazi wa nyumbani mpaka uzee unakukuta hujafanya kitu. Uvumilivu unakusaidia wewe kuijua kazi yako na changamoto zake na hivyo kukufanya wewe kuwa mtaalamu na guru wa eneo au sekta husika. Hata kama imechukuwa muda mrefu huko mbeleni utatumia gharama na njia rahisi kufikia malengo kwa sababu ya uzoefu ulionao kwenye eneo husika ambao umesababishwa na kuvumilia. Kumbuka pia kuwa uvumilivu unaendana daima na kujifunza kutokana na changamoto unazokutana nazo njiani pamoja na kuweka mipango mbadala 5) Mpango mbadala (Kuwa na mpango mbadala) Wahenga walisema kuwa “Kushindwa ni dalili kuwa mpango wako wa kwanza haufanyi kazi hivyo weka mpango mwingine au mbadala” Pia wahenga wengine walienda mbali zaidi na kusema “Kushindwa ni fursa nzuri ya kufanya vizuri zaidi, safari hii kwa umakini zaidi”

Page 27: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 27 Tanzania.

Aliyegundua na kutengeneza taa alishindwa mara 10,000 na baadaye sana ndipo akagundua taa ambayo leo inatumulikia dunia nzima kuanzia majumbani, viwanja vya ndege na mpira pamoja na kwenye anga za juu Wahenga walisema kuwa “Kufanikiwa kupo kwa sababu kuna kushindwa na kushindwa kupo kwa sababu kuna kufanikiwa” 6) Kuwajibika (Kuwajibika na mafanikio au kushindwa

kwako) Daima watu wenye kufanikiwa wanawajibika kwa yale maeneo ambayo wanashindwa. Ukishindwa jisemee ni kwa sababu sikufanya vizuri kwenye eneo X na Y nk. Usianze kuwasingizia wenzako nk Mfano wa timu ya mpira Kama wewe ni mfungaji na ukashindwa kufunga bao la wazi, usiseme kuwa kiungo alikupa pasi mbovu au alipaiza juu sana Sema kuwa nilichelewa kuuwahi mpira ndio maana nikashindwa kufunga. Siku nyingine nitajitahidi kuwahi mpira kama huo” 7) Kufanya kwa vipaumbele Utekelezaji ndio hitimisho la mafanikio. Kama utapanga hata mipango 1,000 kama wewe hunatabia ya kutekeleza basi mafanikio sahau kabisa. Kuna mitego mingi kwenye kutekeleza mambo uliyoyapanga Sehemu ya I: Kuendesha biashara ndogo ndogo Sehemu ya I: Kuendesha biashara ndogo ndogo Maelezo ya utangulizi juu ya biashara ndogondogo na faida yake kwa wajasiriamali na taifa kwa ujumla 1.0 Biashara ndogo ndogo ni ile ambayo

o Inamilikiwa na kuendeshwa kibinafsi o Inafanya kazi katika eneo dogo la nyumbani o Haijaota mizizi katika utendaji o Ina mtaji mdogo.

2.0 Umuhimu wa Biashara ndogo ndogo o Inachangia mchango mkubwa sana katika uchumi o Ni rahisi kuifanya, kimtaji na kiuongozi o Ni rahisi kupata wateja

3.0 Faida ya biashara ndogo ndogo o Inakuza uchumi kwa haraka, ndio maana wachumi wengi

duniani wameipa umuhimu o Inazalisha sana kwani inahitaji wafanyakazi wachache o Ugunduzi wa technolojia mpya

Page 28: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 28 Tanzania.

o Inachangia ushindani wa kibiashara na kuleta ahueni kwa walaji.

4.0 Vikwazo kwa Wafanya biashara ndogo ndogo 1. Elimu ya biashara 2. Ufahamu wa soko 3. Utaalamu wa kiufundi 4. Mtaji wa kuanzia 5. Ufahamu wa biashara husika motisha 6. Aibu ya kijamii, kimila au kielimu nk. 7. Muda usiotosha 8. Vikwazo vya kisheria, sera nk

Page 29: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 29 Tanzania.

(8)

Hatua 26 za kufanikiwa katika biashara

Zifuatazo ni hatua 26 za kufuata katika kuanzisha biashara ndogondogo ambazo zitakuwezesha wewe kuanzisha biashara yeyote kwa uraisi zaidi.

Hatua ya kwanza ikiwa imebeba hatua zote kwani biashara inahitaji utayari (kuamua) zaidi ya vitu vingine kama mtaji nk

Hatua ya ya 1: Kuamua kuingia katika biashara

Kuamua kuingia katika biashara ni majumuisho ya utayari wa kisaikolojia, kiakili, kiuchumi na kukabiliana na hatari au vitisho vyote vitakavyojitokeza kwenye biashara

Maamuzi yako na hasa maamuzi magumu juu ya aidha kufanya hiyo biashara au la si ile hali ya kuamua kufanya biashara tu, bali pia ni ile hali ya kukubaliana na ups and downs za biashara husika na kuwa tayari kujitoa mhanga zaidi.

Hatua ya 2: Kuchanganua uwezo na udhaifu wako

Maeneo manne ni muhimu yapatiwe taarifa halisi na kuchukua hatua ili uweze kumudu kufanya biashara husika

Page 30: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 30 Tanzania.

Mazingira wezeshi Mazingira pingamizi

(Mambo yanayofanya biashara ikue na kusimama)

(Mambo yanayofanya biashara idumae na kufa)

Mazingira ya Ndani

(Mambo yaliyo ndani ya uwezo wa mhusika)

Uwezo

Uwezo wako katika kuendesha biashara mfano: utaalam, vitendea kazi, rasilimali kama kiwanja nk.

Udhaifu

Udhaifu wako katika kuendesha biashara mfano: ukosefu wa utaalam, ukosefu wa vitendea kazi, ukosefu wa rasilimali kama kiwanja nk.

Mazingira ya Nje

(Mambo yaliyo nje ya uwezo wa mhusika)

Fursa

Kuwepo kwa sera nzuri za nchi, kuwepo kwa katiba nzuri ya nchi, hali ya hewa nzuri, kuwepo mwitikio wa jamii kwenye biashara yako nk

Vitisho

Kutokuwepo kwa sera nzuri za nchi, kutokuwepo kwa katiba nzuri ya nchi, kutokuwepo kwa hali ya hewa nzuri, kutokuwepo kwa mwitikio wa jamii kwenye biashara yako nk

Hatua ya 3: Kupata mafunzo

Baada ya kujua udhaifu wako, pata mafunzo

Mfano:- Ya kupata mafunzo ya kiufundi katika biashara husika na au ya ya kubadili mitizamo,

Hatua ya 4: Kupeleleza mazingira utakayofanya biasha ili kujua:

i) Fursa nzuri zilizopo

ii) Vitisho au hatari zitakazoikabili biashara yako (vihatarishi vya biashara husika kama vile sera mbovu, barabara mbovu, hali ya hewa mbovu nk)

Page 31: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 31 Tanzania.

Hatua ya 5: Kuchagua biashara gani ufanye

i) Kutengeneza bidhaa (Manufacturing)

ii) Kuuza bidhaa (Trading)

iii) Kutoa huduma (Service)

Kutengeneza bidhaa (Manufacturing)

Kutengeneza bidhaa ni kutumia rasilimali watu na malighafi ili kutengeneza bidhaa ya kuuza kwa mlaji au mchuuzi. Bidhaa ni kama vyakula, vyombo, nk

Kuuza bidhaa (Trading)

Kuchuuza bidhaa zilizotengenezwa hapo juu no. A(a)

Kutoa huduma (Service)

Kutumia ujuzi wako au wa wengine katika kuwahudumia watu na shida zao kwa malipo. Mfano kufundisha, kutibu, kusafirisha, kutumbuiza nk

Hatua ya 6: Utafiti wa soko (Market Survey)

i) Washiriki wenza wa biashara katika soko

ii) Ukubwa wa soko

iii) Mgawanyo wa soko kati ya washiriki

iv) Aina ya soko/masoko

v) Tabia ya soko NK.

Hatua ya 7: Mfumo wa biashara

Fuatilia maelezo ya kila mfumo ukitilia maanani faida na hasara za kila mfumo. Unaweza pia kumtumia mshauri wa masuala ya biashara kukushauri kulingana na mazingira yako utakayofanyia biashara.

Hasa unatakiwa kujua zaidi mambo ya kisheria katika mfumo utakaoamua kuutumia kuendehsa baishara yako ili isije ikakuletea shida

Page 32: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 32 Tanzania.

huko mbeleni, maamuzi ya mfumo upi uuchukue inategemea zaidi sheria za ndani ya nchi husika, pia inategemea ukubwa wa mtaji wako nk.

Mtu mmoja (sole proprietor)

Faida yake

• Kuanzisha ni rahisi • Maamuzi hupitishwa kwa haraka kwa hiyo hakuna urasimu

Hasara yake

• Biashara ikipata shida mmiliki anahusika na hasara kama vile ya ufilisi nk

Ushirika (>watu wawili) (partnership)

Faida yake

• Kuanzisha ni rahisi • Maamuzi hupitishwa kwa haraka kwa hiyo hakuna urasimu

Hasara yake

• Biashara ikipata shida wamiliki wanahusika na hasara kama vile ya ufilisi nk

• Mikataba inayoingiwa na mmoja wa washirika huwabana na wengine wasiohusika

Kampuni ya umma (public companies)(zaidi ya watu wawili bila ukomo)

Faida yake

• Utambulisho wa kisheria • Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa • Ni rahisi kuvutia mitaji mikubwa kupitia masoko ya hisa

Hasara yake

Page 33: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 33 Tanzania.

• Haina usiri hivyo ni hatari kwani washindani wa biashara husika wanaweza kutumia taarifa hizo kujipanga

• Muda na rasilimali muda kupotea kwa shughuli za kihasibu na kazi za makaratasi

Kampuni ya binafsi yenye ukomo wa hisa

(private companies limited by shares) (watu wawili hadi 50)

Faida yake

• Utambulisho wa kisheria • Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa

• Kazi za makaratasi ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma

• Mlolongo wa taratibu za kisheria ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma

Hasara yake

• Gharama katika kuanzisha tofauti na biashara binafsi • Huruhusiwi kuuza hisa katika masoko ya hisa • Kampuni li lazima angalau iwe na wakurugenzi, katibu na mhasibu • Ni lazima ifanyiwe ukaguzi wa mahesabu kila mwaka

Kampuni ya binafsi yenye ukomo wa udhamini

(private companies limited by guarantees) (watu wawili hadi 50)

Faida yake

• Utambulisho wa kisheria • Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa • Kazi za makaratasi ni chache ukilinganisha na makampuni ya

umma • Mlolongo wa taratibu za kisheria ni chache ukilinganisha na

makampuni ya umma

Page 34: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 34 Tanzania.

Hasara yake

• Gharama katika kuanzisha tofauti na biashara binafsi • Huruhusiwi kuuza hisa katika masoko ya hisa • Kampuni li lazima angalau iwe na wakurugenzi, katibu na mhasibu • Ni lazima ifanyiwe ukaguzi wa mahesabu kila mwaka

Jumuiya (association)

Faida yake

• Utambulisho wa kisheria • Inavutia wahisani • Ni ya watu wachache waliokubaliana

Hasara yake

• Ukiritimba katika kupitisha maamuzi • Ugomvi wa mara kwa mara • Haina kinga kwa waazilishi

Vyama vya ushirika

Faida yake

• Utambulisho wa kisheria • Inavutia wahisani • Ni ya watu wachache waliokubaliana

Hasara yake

• Ukiritimba katika kupitisha maamuzi • Ugomvi wa mara kwa mara • Haina kinga kwa waazilishi

Hatua ya 8: Kuchagua sehemu ya biashara

Kama ni sheli itabidi iwekwe kando ya barabara yenye magari mengi

Page 35: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 35 Tanzania.

Hatua ya 9: Kuchagua technolojia

Teknolojia itasaidia kujua

a) Aina ya watumishi

b) Aina ya vitendea kazi mashine /mitambo

Mfano kilimo cha maksai na kukamua kwa mashine

Teknolojia nzuri ni lazima iwe na sifa zifuatazo

a) Ni rahisi kutumiwa

b) Iwe rahisi kupata msaada kama mafundi nk

c) Iwe inaendana na tamaduni husika

d) Iwe ni rafiki wa watu na mazingira

e) Iwe na gharama ndogo za uendeshaji

f) Inaendelezeka

Hatua ya10: Kununua mashine na vifaa

Mashine na mitambo mingine itategemea sana uchaguzi wa teknolojia hapo juu 9(a)

Mashine zote na mitambo ni lazima kuzingatia yaliyotajwa hapo juu 9(b)

Hatua ya 11: Usajili wa biashara

Hii hufanywa mara nyingi kwenye manispaa husika. Leseni kwa wafanya biashara ndogondogo ni bure (biashara ndogondogo ni ile ambayo mauzo yake hayazidi Shs 20 milioni kwa mwaka)

Hatua ya 12: Kuandika Mchanganuo wa Biashara

(Business Plan)

• Baada ya kufanya hayo yote sasa ni wakati mzuri wa kuandika mchanganuo wa biashara yako

Page 36: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 36 Tanzania.

• Mchanganuo wa biashara ni maelezo ya kina ambayo inaonyesha biashara yako ilikotoka, inakokwenda, hali ya masoko, sekta, kifedha na uongozi wa biahara yako. Ni taarifa muhimu ya kuwavutia wawekezaji na watoa mikopo kama mabenki

Mambo muhimu ya kujua katika kuandika Mchanganuo wa Biashara

1. Kasha la nje 2. Muhtasari wa biashara yako 3. Historia na maelezo ya biashara yako 4. Maelezo ya bidhaa au huduma ya biashara yako 5. Mchanganuo wa masoko

• Ukubwa wa soko • Mgawanyo wa soko • Aina ya soko/masoko • Watoa huduma au wauza bidhaa kama yako • Udhaifu wao • Uwezo wao • Uongozi na usimamizi wa kazi • Uchambuzi wa madhaifu, nguvu, fursa na hatari zinazokabili

biashara yako • Mkakati wa Uzalishaji • Mkakati wa kuuza

6.Mchanganuo wa ushindani

7.Mkakati wa utekelezaji

8. Mpango wa fedha

• Uchambuzi wa mahitaji ya mtaji • Wapi utatoa mtaji • Matumizi ya mtaji • Makisio ya Mauzo • Uchambuzi wa kurudisha gharama (break even analysis) • Makisio ya faida au hasara • Makisio ya mzunguko wa fedha katika biashara yako (cashflow) • Makisio ya oanisho la mali na madeni ya biashara yako (balance

sheet)

Page 37: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 37 Tanzania.

• Ulinganifu wa sehemu mbalimbali za biashara (business ratios) • viambatanisho

1. Lesseni 2. Cheti cha ulipaji kodi 3. TIN 4. Cheti cha usajili 5. Mikataba 6. Risiti za manunuzi hasa mali za Biashara 7. Taarifa zingine ambazo hazikupata nafasi ndani ya mchanganuo

huu 8. Taarifa zingine zinazoweza kuifanya biashara au kampuni

kuaminika zaidi

Hatua ya 13: Kupanga juu ya pesa.

Kutafuta mikopo kwa kufuata utaratibu wa taasisi za fedha husika

Taasisi nyingi huhitaji yafuatayo

1. Dhamana ya mkopo 2. Uzoefu wa biashara husika 3. Mchanganuo wa biashara 4. Maombi ya mkopo

Hatua ya 14: Ufahamu wa kiufundi.

Hii ifanywe ili mwenye biashara apate ufahamu wa kiufundi juu ya biashara yake hasa kutoka kwa taasisi husika au mshauri wa biashara (consultant).

Hatua ya 15: Kujua vyanzo vya nishati:

Kama ni umeme hakikisha iko sawa na umeme utakidhi matakwa ya biashara.

Kama ni mafuta uhakikishe mafuta inapatikana na bei haitaadhiri bei ya bidhaa

Page 38: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 38 Tanzania.

Hatua ya 16: Kuweka vifaa: (Machines installation)

Wataalam husika wafanye hii kazi tena wasiwe wababaishaji maana wanaweza kuwa ndio kikwazo

Hatua ya 17: Kuajiri wafanyakazi.

Wafanyakazi wako wengi mtaani, lakini kumpata mtu atakayekidhi matakwa ya biashara yako kwa maana ya ubora na kufikia lengo la uzalishaji inahitaji usambazaji wa taarifa kwa upana zaidi na kwa maeneo maalum ambayo unategemea wafanyakazi watoke. Mfano vyuoni, makanisani nk

Unashauriwa pia kutumia marafiki na ndugu wa karibu ili upate mfanyakazi ambaye ni bora zaidi

Hatua ya 18: Kujua upatikanaji wa malighafi

Malighafi bila ubishi ni kiungo muhimu kwa biashara yeyote inayohusisha bidhaa. Vyanzo vya kupata malighafi ni muhimu ijulikane na iwe ya uhakika.

Hatua ya 20: Kuhakikisha bidhaa yako hainakiliki/kukopiwa.

• Kama unatengeneza biadhaa hakikisha fomula na mbinu ulizotumia ni ngumu na zimefanywa siri kubwa

• Pia hakikisha unalinda hati miliki ya huduma au bidhaa husika katika ngazi husika za usajili na utambuzi

Hatua ya 21: Usalama wa biashara yako

Epuka majengo ambayo ni rahisi kuwaka moto, kubomolewa na wezi, wizi katika pesa za mauzo, utapeli wa bidhaa katika kununua na kuuza nk.

Hatua ya 22: Kuuza (Selling)

Kufikia wateja (fikiria utamfikiaje mteja wako wa kwanza – maelezo zaidi yatakuwepo katika mchanganuo wa biashara)

• Kusambasa huduma/bidhaa • Kuweka bei

Page 39: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 39 Tanzania.

• Kutangazia biashara • Promosheni nk. • Hii ifanywe kila mara ili kujua kama wateja wamebadilika au bado

Ili kujua kama wanapenda huduma/bidhaa zako au la. • Kujua biashara yako imekamata asilimia gani katika soko • Kupata maoni ya wateja ili kuboresha biashara/huduma/bidhaa

Hatua ya 23: Utafiti wa soko (Market Research)

Namna ya kufanya utafiti

Utafiti wa kuendelea

Kila mteja anaponunua bidhaa, ajaze fomu maalum ya maoni. Mfano ya jinsi alivyohudumiwa, bei ya bidhaa, usindikaji, ubora nk

Utafiti maalum

Huu ufanywe wakati wa kutoa vivutiuo maalum au promosheni maalum.

Mteja wa promosheni ajaze fomu maalum ya maoni. Mfano ya jinsi alivyohudumiwa, bei ya bidhaa, usindikaji, ubora nk

Hatua ya 24: Kusimamia na kuthibiti biashara:

Hii ni kuhakikisha kuwa biashara inakwenda kama ilivyobuniwa /pangwa.

Hatua ya 25: Kutathmini biashara.

Hii ni kujua kama biashara imekwenda kama ilivyobuniwa /pangwa.

Mambo ya kuangalia

1. Mapato na matumizi 2. Bajeti iliyiopita 3. Matokeo ya utaifit/wa soko

Hatua ya 26: Kufanya maboresho/mabadiliko

Unaweza kumuajiri au kumtumia mtaalam wa sekta hiyo kufanya taadhmini ya biashara yako.

Page 40: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 40 Tanzania.

Fanya sawa sawa na matokeo ya tathmini/utafiti.Mpango wa biashara wengine wanauita mchanganuo wa biashara sio kitu kigumu sana kama ukipenda kurahisisha.

Mpango wa biashara ni maelezo ya kina ambayo inaonyesha biashara yako ilikotoka, inakokwenda, hali ya masoko, sekta, kifedha na uongozi wa biashara yako. Ni taarifa muhimu ya kuwavutia wawekezaji na watoa mikopo kama mabenki

Mambo muhimu ya kujua katika kuandika Mpango wa Biashara au – Business Plan.Mpango wa biashara wengine wanauita mchanganuo wa biashara sio kitu kigumu sana kama ukipenda kurahisisha.

Fuatilia ngazi hizi nane (8), zitakusaidia:

1. Kasha la nje liwe na kichwa cha taarifa nzima, jina la biashara, muda wa mpango mara nyingi ni kati ya miaka 3 hadi 5

2. Muhstasari kwenye kurasa moja (Iandikwe mwishoni kwani huu ni maelezo kwa ufupi wa ulichokiandika)

3. Maelezo ya kampuni au biashara yako, historia ya kuanza, waazilishi, usajili, leseni za biashara, mali nk

4. Maelezo ya bidhaa au huduma unazotoa au utakazozitoa (Unatenegenezaje, au unaandaaje, usindikaji, ushahidi juu ya udhibiti wa viwango, bei, usambazaji na taarifa ya namna ya kutumia nk)

5. Maelezo juu ya soko na ushindani (ukubwa wa soko, watoa huduma au wauza bidhaa kama yako, udhaifu na nguvu yao, siri ya wewe/kampuni yako au biashara yako kufanikiwa zaidi yao)

6. Maelezo juu ya mkakati wa kutekeleza biashara yako (wafanyakazi na mgawanyo wa kazi, Ratiba ya usimamizi, machine, vifaa, mkakati wa kumfikia mteja, orodha ya watoa huduma, nk)

7. Makisio ya fedha (pesa za kianzio (Startup capital), mtaji (investment) wapi utatoa mtaji?, makisio ya mauzo (Sales forecast),ripoti ya faida na hasara (Profit and loss forecast), makisio ya mzunguko wa fedha katika biashara yako (cashflow forecast), Mchanganuo wa kurudisha gharama na kupata faida (Break even analysis) makisio ya oanisho la mali na madeni ya kampuni/biashara (balance sheet

Page 41: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 41 Tanzania.

forecast) na Ulinganifu wa sehemu mbalimbali za biashara (business ratios) nk

8. Viambatanisho muhimu kama Leseni, Cheti cha ulipaji kodi, Cheti cha usajili Mikataba, Risiti za mashine, mitambo, ununuzi wa mali za kudumu nk, taarifa mbalimbali za biashara yako ambazo hazikupata nafasi ndani ya mchanganuo huu. Nk

Page 42: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 42 Tanzania.

(9)

Kilimo bora cha matikiti maji

Tikiti maji ni mboga/tunda linalolimwa hasa katika maeneo ya joto lenye kiwango cha joto cha 22-28 0c na mvua 600 - 400mm kwa

mwaka.

Matikiti yanahitaji hali ya hewa yenye joto na mwangaza wa jua wa

kutosha . Kiwango kidogo cha unyevu kwa sababu unyevu mwingi unasababisha maradhi. Unyevunyevu mwingi unaadhiri ubora na utamu wa tunda. Vilevile, yanastawi vizuri katika aina mbalimbali za udongo wenye rotuba ya kutosha na wenye kupitisha maji vizuri.

• Aina ya matikiti maji • Arashani F1 - kutoka Syngenta • Sukari F1 - Kutoka East Africa seeds • Sugar king F1 - kutoka Africasia • Juliana F1 - kutoka Kiboseed • Zebra F1 - Kutoka Balton • Pato F1 - Kutoka Agrichem

• NEGRA F1

Aina hii ya matikiti maji ni ya mviringo yenye mazao na sifa nzuri” Ubora wake • Yana mazao mazuri, na uwezo wa kukupa tani 46 kwa kila ekari • Ni matamu sana na yenye wekundu wa kung’ara

Page 43: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 43 Tanzania.

• yanakomaa katika muda wa siku 100-120 • Ni mviringo na yenye rangi ya kijani kibichi na hutoa matunda

yenye mizani kati ya kilo 7-10 • Mmea hukua haraka na una mazao mazuri •Yamezungukwa na nyama ngumu, nzuri, yenye kukuwezesha

kusafirisha hadi sehemu za mbali • Yana kinga dhidi ya ugonjwa wa mnyauko unaosababishwa na

vimelea aina ya Fusari (Fusarium wilt)

• STINEL F1

Ni aina mpya ya matikiti ya mviringo marefu” Ubora wake • yanaweza kuzaa sana hadi tani 50 kwa kila ekari • Ni marefu, yameshiba na yana rangi ya pundamilia • ni tamu, yan wekundu uliokolea na nyama iliyo na maji mengi • Yanawezakutoa matunda ya kufanana na yaliyo na uzani kati kilo 11

- 14 • Matunda yana nyama nyingi na umbo inayokuwezesha kusafirisha

masafa marefu • yana kinga dhidi ya maradhi ya vimelea aina ya Fusari (Fusarium

wilt Race 1) • yanakua tayari katika muda wa siku 100 -120

Upunguzaji Wa Mimea Mimea ya mitikiti huanza kuota, baada ya kama wiki 2 hivi. Hivyo katika

mbegu mbili au tatu ulizopanda kata moja na uache ile miche yenye afya zaidi ndio uendelee kukua. Ni vizuri ukaacha miche miwili katika kila shimo.

Angalizo: Usinga’oe mche bali ukate ili kuzuia kusumbua mizizi ya mche

uliobaki. Vilevile unaweza kupandishia udongo kwenye mashina ili kusaidia kupunguza maji kutuama kwenye mimea yako, pia unaweza kuweka samadi badala ya kupandishia udongo ukiwa na nia ileile ya kuzuia maji yasituame na kuongeza rutuba. Kama una sehemu ndogo ya shamba unaweza kuyawekea matikiti waya wa kutambalia, ila inabidi uwe imara kwa sababu ya kuhimili uzito wa matunda. Wakati mimea inapo anza kutambaa kwenye waya ni lazima uifundishe (kuielekezea) kwenye waya na kuifungia.

Page 44: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 44 Tanzania.

Umwagiliaji Shamba linatakiwa limwagiliwe mara kwa mara wakati mvua

zinapokosekana au wakati wa mvua chache. Kipindi muhimu zaidi ambapo mimea hii huhitaji maji ni katika kipindi cha uotaji wa mbegu, wakati wa kutoa maua na siku takribani kumi kabla ya kuvuna. Iwapo kutakuwa na ukosefu wa maji kutasababisha kutengenezwa kwa matunda ambayo si mazuri na yenye umbo baya, pia kupungua kwa ukubwa wa tunda.

Angalizo: usimwagilie matikiti wakati wa jioni sana au usiku kwasababu

inaweza kusababisha magonjwa ya majani kutokana na unyevu kukaa muda mrefu. Vile vile usimwagilie juu ya maua wakati wa asubuhi au jioni kwasababu unaweza kuzuia wadudu kama nyuki ambao ni muhimu sana wakati wa uchavushaji.

Mahitaji ya Mbolea ya Matikiti Wakati wa kupanda tumia DAP weka gram 5 kwa kwa kila shimo (lenye

mbegu moja, na weka gram 10 au 15 kama kuna mbegu 2 au 3), hakikisha mbolea na mbegu havigusani. Wiki mbili baada ya miche yako kuota weka mbolea ya kiwandani NPK (Yaramila winner) gram 5 tena kwa kila mche, hakikisha unaichimbia chini na isigusane na mmea. Weka mbolea yenye Calcium kama Yaramila nitrabo au CAN gram 10 kwa kila shina unapoona matunda yameanza ili kusaidia kupata matunda makubwa na mazuri.

Kwa ekali 1 ya matikiti utahitaji mfuko mmoja wa DAP, mmoja wa NPK na

mmoja wa CAN ikiwa utabakiza miche miwili kwa kila shimo. Hivi ukiwa shambani unawezaje kupima gram 5 au 10 za mbolea? Ni

vigumu lakini kwa makadirio ya karibu ujazo wa kifuniko kimoja cha maji safi au soda take-away ni sawa na gram 5 hivyo ili upime gram 10 jaza vifuniko viwili vya maji safi

Matandazo (Mulches) Matandazo ina maana ya kutumia nyasi na mabaki ya mimea mingine

kufunika aridhi. Baada ya miche kutambaaa kwa kiasi unaweza kuweka matandazo (mulches) ambayo yaweza kuwa nyasi kavu kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu vile vile kupunguza uotaji wa magugu shambani kwako. Vile vile matandazo yakioza yanaongeza rutuba kwenye udongo na hulinda udongo dhidi ya mmomonyoko wa udongo.

Page 45: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 45 Tanzania.

Matikiti maji shambani

WADUDU NA MAGONJWA YA MATIKITI

Wadudu wa matikiti wako wa aina mbalimbali na wanaoshambulia sehemu za majani na maua, na wengine hushambulia matunda, pia kuna magonjwa ya fangasi ambayo hushambulia mimea.

Magonjwa kama ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy mildew) na mengine yathibitiwe kabla hayajaleta madhara kwenye mimea. Ili kujua dawa za magonjwa ni vizuri kuchukua sampuli na kwenda nayo kwenye duka la dawa na pembejeo za kilimo ili kupata dawa sahihi. Dawa aina ya Mancozeb inaweza kutumiwa kuthibiti magonjwa hayo hapo juu.

Vilevile matikiti hushambuliwa na wadudu ambao hukaa katika majani,

maua na matunda. Dawa aina ya KARATE itasaidia kuua wadudu wa majani, maua na matunda.

UVUNAJI NA UHIFADHI WA MATIKITI

Matikiti maji ni miongoni mwa mazao yanayochukua muda mfupi sana kukomaa. Kwa kawaida tikiki maji huwa tayari kwa kuvuna baada ya siku 80 hadi 100 baada ya kupanda. Vuna wakati tunda limeiva kabisa. Vuna kwa wakati unaofaa. Epuka kulijeruhi tunda. Hifadhi katika eneo lenye ubaridi nyuzi 15 hadi 20 C. Hifadhi vizuri, unyevua-anga (humidity) uwe 80 hadi 85%. Uza mara tu baada ya kuvuna shambani.

Page 46: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 46 Tanzania.

Jinsi ya kujua faida Katika maeneo mengi ya Tanzania bei ya tikiti maji lenye sifa nzuri ni

shilingi 2,000/= hadi 3,000/= kwa bei ya 2,000/= na mavuno ya 2000 matunda/ekari (Matunda

mazuri) Baada ya mavuno utajipatia kiwango cha chini kisichopungua jumla

ya Tsh.4,000,000/= kwa mwaka ni 12,000,000/= kwa mavuno ya mara tatu kwa mwaka kwa ekari.

Gharama hii itaenda juu zaidi ama itapungua kutegemea na idadi ya matunda uliyoyapata katika ekari mmoja na bei ya muuzaji. Hivyo unaweza ukapata faida kubwa zaidi ukiongeza uangalizi wa shamba lako na kufuata utaratibu katika ulimaji wa zao hili.

Mahitaji Tikiti maji linahitaji mbolea, maji, kemikali za kuua wadudu na

magonjwa pamoja na maandalizi mabali mbali ya shamba ambavyo gharama yake haizidi Tsh. 500,000/= katika uangalizi mkubwa

Faida Hivyo mkulima katika uangalizi wa mzuri ana uhakika wa kupata

faida ya Tsh. 3,500,000/= na zaidi kila baada ya miezi 3-4.

Ushauri: Kwa mafanikio mazuri na kuinuana kiuchumi wakulima wakiungana na kufanya kilimo bishara watakuwa na nafasi kubwa ya

Page 47: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 47 Tanzania.

mafanikio kwa maana kiuchumi wanataweza kusaidiana ili kuinua mtaji na kuweza kupata kiasi cha kuanzia shughuli zao za kilimo.

Page 48: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 48 Tanzania.

(10)

Kilimo bora cha mananasi

Zao la mananasi hulimwa sana hapa nchini maeneo ya Bagamoyo, Kibaha, Geita, Mwanza, Tanga, Mtwara, Lindi na maeneo mengine. Zao hili lina kiasi kikubwa cha vitamini A na B na kiasi kidogo cha vitamini C, pia kuna madini kama potasiam, kalsiam, chuma na magnesiam.... Hali ya hewa Manansi hustawi sana ukanda wa pwani usawa usiozini mita 900 toka usawa wa bahari ambapo kuna mvua nyingi kiasi cha milimita 1500 na unyevu wa kutosha, pia unaweza kupanda kwenye maeneo yenye mvua chache lakini kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji, Hali ya joto ni kuanzia sentigredi 15 - 32, huwa haya stahimili baridi Udongo Udongo wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji ndi unaofaa kwa ajili ya kilimo cha mananasi, unaweza kutumia samadi au mbole vunde ili kuongezea rutuba ya udongo wako. Msimu Kwa ukanda wa pwani wenye mvua mbili kwa mwaka upandaji wa mananasi huanza mara baada ya mvua za kwanza kuanza, ni vizuri kupanda kwa muda mfupi ili uzaaji usipishane sana na pia kusaidia kupata mvua za kutosha kabla ya msimu kuisha.

Page 49: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 49 Tanzania.

Upandaji Tumia miche ya aina moja na yenye umri sawa ili huduma zifanane na pia uzaaji uwe wa mpangilio, umbali toka mmea hadi mmea ni sentimeta 30 na mstari hadi mstari ni sentimeta 60, na umbali kila baada ya mistari miwili miwili ni sentimeta 90 Kwa ekari moja unaweza kupanda miche 25,200 na kwa hekta moja unaweza kupanda miche 44,000. ili mananasi yako yastawi vizuri basi tengeneza kama mtaro mdogo na kwenye mitaro ndio upande mananasi yako, hii husaidia kupata unyevu zaidi Mbolea Kwa wale wanaotumia mbolea za viwandani, ni vizuri kutumia NPK na DAP ambazo utaweka miezi miwili baada ya kupanda na miezi 12 baada ya kupanda baada ya hapo hautahitaji mbolea tena, lakini ni vizuri zaidi kama utatumia mbolea za asili Wadudu Wadudu wanaoshambulia mananasi ni aina ya mealybug ambao huondolewa kwa kupulizia dawa kama dume na karate. Ugonjwa wa kuoza moyo wa miche unaweza kuzuiwa kwa kupiga dawa za copper oxychloride au kwa kuzamisha miche kwenye dawa za fungasi (fungicides)kabla ya kupandwa shambani Uvunaji Mananasi huwa tayari kuvunwa miezi 18 mpaka 24 baada ya kupandwa kutegemeana na mbegu na matunzo ikiwemo kiasi cha mvua, mbolea na unyevu shambani, Uvunaji hufanyika kwa kutumia visu na vibebeo maalum kuhakikisha ubora wa zao hili.

Page 50: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 50 Tanzania.

(11)

Ufugaji wa kuku wa kienyeji

Mahitaji • Kuku(tetea) 10 na Jogoo 01 • Banda bora • Vyombo vya chakula na maji • Chakula bora • Madawa na chanjo kwajili ya magonjwa • Chanzo cha nishati joto na mwanga • Elimu na ujuzi wa malezi bora • Chombo au chumba cha kutunzia vifaranga • Mayai ya kuku wa kisasa/mayai mabovu(ambayo hayakuanguliwa) • Madaftari au kitabu cha kutunzia kumbukumbu • KUKU 10 Wakati wa kuanza mradi wako hakikisha una kuku 10 (matetea)

wenye umri sawa na hawajawai kutaga hata mara moja. Chagua kuku wenye rangi nzuri kutoka katika familia bora kutegemea malengo ya mradi wako. Mfano kama lengo lako ni kuzalisha kuku wa kienyeji kwajili ya nyama basi chagua mbegu ambayo inakuwa haraka na yenye uzito mkubwa. Au ikiwa lengo ni mayai basi ni vema kuchagua aina ya kuku yenye kukua haraka na kutaga mayai mengi.

Ili kupunguza gharama za manunuzi ya kuku na hivyo kuongeza faida kwa mfugaji ni vema kununua kuku wadogo ambao wametoka tu kuachishwa kulelewa na mama zao. Kuku hawa utawapata kwa bei ya chini, tena watafaa sana maana watakua na umri mmoja pia.

Page 51: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 51 Tanzania.

JOGOO Jogoo mmoja tu anatosha kuwahudumia kuku matetea yote kumi.

Hakikisha katika uchaguzi wa jogoo bora lililochangamka, rangi mzuri, upanga umesimama, macho angavu, uzito wa kutosha, rangi nzuri na uwezo mkubwa wa kuzalisha. Ni vema mfugaji akaelewa kwamba kuku wote watakaozalishwa watategemea ubora wa jogoo wake. Uwezo wa kutaga kwa kuku na upatikanaji wa mayai pia hutegemea kwa karibu ubora wa jogoo aliyechaguliwa.

BANDA BORA Miongoni mwa mambo mhimu naya kwanza kuzingatiwa katika

ufugaji wa kuku wa kienyeji kama mradi ni maandalizi ya banda bora. Kuku huhitaji banda bora ili wasiathirike na madhara mbalimbali. Mfugaji anatakiwa kuandaa banda lenye ukubwa wa mita 10 kwa mita 04. Yani urefu uwe mita 10 na upana upana wa mita 04. Kisha kata vyumba vya mita 2 urefu na upana mita 4 kutoka katika banda lako hivyo utakuwa na jumla ya vyumba vitano vyenye ukubwa unaolingana. Ujenzi uzingatie malighafi na vifaa vinavyopatikana kwa urahisi katika mazingira husika. Mfano katika maeneo ambayo fito zinapatikana kwa urahisi banda linaweza kuandaliwa kwa miti na kukandikwa kwa udongo. Au sehemu ambayo mabanzi hupatikana kwa urahisi basi banda laweza kujengwa kwa kutumia mabanzi. Vifaa vya kujengea banda vizingatie pia gharama na upatikanaji wake katika eneo husika. Baadhi ya vifaa hivyo ni kama ifuatavyo:-

• Sakafu: Saruji, udongo, mbao, mianzi au fito • Kuta: Fito, mabanzi, mbao, nguzo mianzi,udongo, matofali, mawe,

mabati na wavu • Paa: Nyasi, makuti, majani ya migomba, mabati na vigae. • Wigo: Matofali, mbao, fito nguzo, mabanzi, mianzi, matete, wavu

na mabati.

Banda bora la kuku linatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:- • Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya

hewa hatarishi kwa mfano jua kali, upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama hatari.

• Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi kufanyika kwa urahisi.

• Lijengwe sehemu yenye mwinuko isiyotuama maji, isiyo na upepo mkali na iwe mbali kidogo na nyumba ya kuishi watu.

Page 52: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 52 Tanzania.

• Liwe na vichanja kwa ajili ya kuku kupumzika na kulala. • Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji, kutagia, kuatamia na

sehemu ya kulelea vifaranga. • Liwe na nafasi ya kutosha kulingana na idadi ya kuku na kuweka

vyombo vya chakula na maji. • Kwenye mazingira ya joto banda liwe la ukuta mfupi na sehemu

kubwa wazi yenye wavu hadi kufikia kwenye paa. Kwenye mazingira ya baridi banda liwe na ukuta mrefu unaokaribia paa na sehemu ndogo tu iwe wazi yenye wavu ili kupitisha hewa na mwanga.

JINSI YA KUFANYA Wakuze kuku wako hadi watakapofikia muda wa kutaga. Wakianza

kutetea ni kiashiria kwamba wakati wa kutaga umekaribia hivyo andaa viota kwajili ya kutagia.

Viota vinapaswa viwe na ukubwa stahiki ili kumwezesha kuku kuyafunika mayai yote vizuri wakati wa kuetamia, viota viwe vinavyozuia mayai kutawanyika, viwe mahali pakavu na safi.

Hakikisha kuku wote wanataga katika viota tofauti. Kuku anapotaga mayai matatu unapashwa kuchukua mayai mawili na kumwachia yai moja ili kumfanya aendelee kutaga zaidi. Kuku akifikia yai la kumi na mbili anza kumwachia mayai matatu ili kumwandaa kwa kazi ya kuetamia. Kwa kufanya hivi, kuku atataga mayai 15 au zaidi na ikiwa atataga mayai 15 au chini ya hapo nakushauri utafute mayai mengine ujazilizie ili kufikisha mayai 20 kwa kila kuku. Zingatia kwamba mayai unayoyatoa kwa kila kuku, yanatunzwa sehemu salama, mahali pakavu, pasafi na penye joto la wastani.

Kuku wote wanapaswa kuanza kuetamia kwa siku moja. Ili kufanikisha hili inapasa uwe karibu na kuku wako. Kuku mmoja akianza kuetamia mwekee mayai ya kuku wa kisasa au mayai mabovu ya kuku wa kienyeji. Utafanya hivi hadi kuku wako wote watakapoanza kuetamia mayai. Kuweka mayai mabovu au mayai ya kuku yaliyotumika humfanya kuku aendelee kuetamia akijua ni mayai yake.

Baada ya kuona kwamba kuku wako wote wapo tayari kwa kuetamia mayai, waandalie banda maalumu kwajili ya kuetamia yani chumba kimoja katika lile banda letu. Ninashauri kwamba chumba kwajili ya kuetamia kiwe chumba cha kwanza au cha mwisho katika mfuatano wa vyumba vya banda lako. Andaa viota bora vya kuetamia, weka mayai 20 kwa kila kiota, ikiwa hayajatimia unaweza kununua kwa wafugaji wengine ili kuifikia idadi yako.

Waamishe kuku kutoka wanapotagia na kuwaweka katika chumba ulichokiandaa kwajili ya kuetamia. Ili ufanikiwe katika zoezi hili inafaa

Page 53: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 53 Tanzania.

lifanyike wakati wa usiku na unafanya katika giza. Mweke kuku katika kila kiota na asubuhi wajikute kila mmoja katika kiota chake. Wahudumie kwa chakula na maji ya kutosha. Wakati wa usiku waongezee joto la ziada kwa kuweka jiko au ndoo ya chuma yenye chengachenga za mkaa au kama una umeme weka taa za joto.

Baada ya siku 21-25 kuku wako wataanza kuangua vifaranga. Huu ndio wakati unaotakiwa kuwa karibu sana na kuku wako kuliko wakati wote. Watenge vifaranga mara tu baada ya kuanguliwa; waweke katika chumba chao maalumu mbali na kuku. Kama chumba cha kuetamia kilikuwa cha kwanza basi vifaranga wawe chumba cha mwisho n.k

Ukishawatenga vifaranga mbali na matetea wako, wawekee tena mayai mengine 20 kila tetea, mayai ambayo utayanunua kwa wafigaji wenzako. Hakikisha kuku waliotaga hayo mayai ni wazuri, hawana magonjwa na wanauzito/ukubwa unaofaa. Mayai yote yakaguliwe vizuri ili kujua kwamba yameharibika, yana nyufa au mabovu. Kabla ya kuweka mayai mengine hakikisha chumba chako ni kisafi na viota vimesafishwa, havina wadudu na uchafu wowote. Kuku wako bila kujijua wataanza kuetamia upya mayai uliowawekea.

Ukiwawekea mayai rudia mzunguko kama nilivyokwambia awali. Baada ya siku 21 hadi 25 tena utapata vifaranga wako wengine tena. Fuata kila hatua kama nilivyokwambia hapo awali. Lakini kwa awamu hii nashauri waache matetea wako wapumzike wala usiwapatie mayai mengine tena.

JINSI YA KULEA VIFARANGA Ikikaribia siku ya 20 tangu ulipowawekea matetea wako mayai katika

chumba cha kuetamia, andaa chumba kwa ajili ya kulea vifaranga. Safisha kwa kuondoa uchafu na wadudu wote.

Washa taa ya joto au weka chombo cha kutoa joto katika chumba cha vifaranga nusu saa kabla hujaanza kuingiza vifaranga wako. Weka pia chakula na maji ya kutosha katika vyombo vyenye umbile na ukubwa utakaowawezesha vifaranga kuvitumia. Tandaza magazeti, maboksi, makaratasi n.k katika sakafu ya chumba hicho. Hakikisha vifaranga wako hawajikusanyi sehemu moja maana wakifanya hivyo wengi wao watakufa ili ufanikiwe katika jambo hili, banda lako liwe la mduara katika kona zake.

Weka joto la kutosha. Joto la kutosha ni lile linalowafanya vifaranga watawanyike chini ya chanzo cha joto wakati kama joto limezidi vifaranya kukimbia mbali na chanzo cha joto na ikiwa joto halitoshi vifaranga hujukusanya chini ya chanzo cha joto.

Page 54: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 54 Tanzania.

Baada ya siku 3 utawapatia chanjo ya Gumboro na siku 7 wapatie chanjo ya New Castle, utarudia tena kuwapa chanjo hii baada ya mwezi mmoja kisha utafanya hivi kila baada ya miezi mitatu mitatu.

MAPATO YA MRADI WAKO Katika uzazi wa kwanza utapata vifaranga 150 kwa wastani wa

vifaranga 15 kwa kila kuku. Tuseme haujazingatia kanuni za ufugaji za makala hii ukapata vifaranga 100 yani wastani wa vifaranga 10 kwa kila kuku. Kisha baadaye wakakua wakafa kuku 50 yani watano kwa kila kuku utakuwa na jumla ya kuku 50.

Baada ya wiki 3 utapata tena kuku tufanye kwa mahesabu kama hayo hapo juu kwa hasara utakuwa na kuku wengine 50, na kufanya jumla ya kuku 100. Ikiwa kuku wako baada ya uzao wa pili uliwapumzisha kwa miezi miwili basi mwezi wa 3 utapata tena kuku vifaranga 100 na wiki 3 baadaye utapata wengine 100. Kwa mahesabu kama hayo awali wakikuwa utakuwa na kuku wengine 100 ambao watakuwa.

Baada ya miezi 6 utakuwa na kuku wakubwa wa uzao wa kwanza 50, uzao wa pili kuku 50 na utakuwa na kuku wenye umri wa miezi mitatu 50 wa uzao wa 3 na kuku wengine 50 wa uzao wa 4.

Katika kuku 100 wa uzao wa kwanza na pili, tufanye kuku 50 wawe matetea ukijumlisha na kuku 10 ulioanza nao mradi utakuwa na matetea 60. Ikiwa kila tetea atatotoa vifaranga 10 na vikakua vitano tu, mwishoni utakuwa na kuku 300 na baada ya miezi mitatu kuku wengine 900 toka katika kutoka kwa uzao wa kwanza, wapili na watatu. Hivyo mwaka wa pili utafunga na kuku si chini ya 1,200/= wanaotaga mayai.

Ukiuza majogoo yote 1,200/= kwa bei ya 8,000/= ili upate pesa ya kujenga miundombinu bora maana sasa utakuwa na kuku wengi wanaoendelea kuzaliana kwa kasi utapata pesa kiasi cha TZS 7,200,000/=. Sasa ongeza kuku wako wa kutaga hadi wafikie kuku 4,000 maana sasa utakuwa na pesa za kutosha kuendesha mradi wako.

Sasa ukiwa na kuku 4000 wa kienyeji wa kutaga mayai, ikiwa kuku 3000 tu watataga ukauza yai moja kwa bei ya haraka haraka ya TZS 250 tu, utapata TZS 750,000/= kwa siku ambayo sawa na TZS 22,500,000/= kwa mwezi na TZS 270,000,000/= kwa mwaka sawa sawa na 128,572 USD. Kumbuka mwamba makadilio haya niya chini sana. Ukifata kanuni zote kwa makini na maombi huku ukimtanguliza Mungu utafikia hata TZS 500,000,000/= kwa mwaka.

Page 55: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 55 Tanzania.

Kumbuka unapofanikiwa kupata mapato ya kila aina, umtolee Mungu zaka(x10%) ya mapato yako, pia ukatoe sadaka ambayo ni kubwa kuliko zaka na uwasaidie masikini na wahitaji.

Page 56: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 56 Tanzania.

(12) KILIMO BORA CHA NYANYA

Utangulizi Nyanya ni zao la chakula na biashara. Kilimo cha zao hili hufanyika majira yote (masika na kiangazi), na faida hupatikana haraka na ni ya kuridhisha ikilinganishwa na mazao mengine. Pamoja na umuhimu wa zao hili, wadudu waharibifu na magonjwa huathiri uzalishaji na ubora wa matunda. Ili mkulima aweze kupata faida na kuongeza pato la kaya yake ni vema kuzingatia udhibiti wa magonjwa na wadudu wa zao hili. Kipeperushi hiki kinatoa maelezo ya udhibiti wa magonjwa na wadudu muhimu ya zao la Nyanya. MAGONJWA YA NYANYA Bakajani chelewa (Late blight) Ugonjwa huu huenenzwa na vimelea vya fangasi. Husababishwa na hali ya hewa hasa ya unyevunyevu, na huenezwa na upepo. Majani, shina, matunda hushambuliwa. Majani huwa na ukungu mweupe na kijivu, na baadaye hukauka. Matunda huwa na mabaka ya kikahawia na baadaye kuoza. Mashina pia huwa na mabaka ya kikahawia.

Page 57: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 57 Tanzania.

Udhibiti · Nyunyiza dawa ya kuzuia ukungu hasa wakati wa masika, Dawa zinazopendekezwa ni Ridomil, Dithane 45, Bravo, Funguran, milraz. · Fanya mzunguko wa mazao. Usipande nyanya sehemu moja kila msimu au palipolimwa mazao jamii ya nyanya km viazi mviringo, bilinganya, aina zote za pilipili na nyanya chungu. · Tumia mbegu safi · Panda aina za nyanya zinazovumilia ugomjwa Bakajani tangulia (Early blight) Huenezwa na vimelea vya fangasi. Husababishwa na kuenezwa na hali ya hewa pamoja na mbegu zenye ugonjwa. Mabaka ya kahawia yenye mistari ya mviringo huonekana kwenye majani na shina. Baka jeusi hutokea sehemu ya tunda inayoshikana na kikonyo. Udhibiti · Nyunyiza dawa ya Kocide, Funguran · Teketeza mabaka ya mazao baada ya kuvuna · Tumia mbegu safi na bora Mnyauko fusari (Fusarium wilt) Huenezwa na mbegu zenye ugonjwa. Husambazwa na vimelea vya fungasi vinavyoishi kwenye udongo. Ugonjwa hujitokeza zaidi wakati wa kiangazi. Vimelea hushambulia sehemu au mirija ya mmea ya kupitishia maji na chakula. Mmea hukosa maji na chakula na hatimaye hunyauka. Shina la mmea likipasuliwa ndani huonekana rangi ya kikahawia.

Udhibiti · Tumia mbegu safi na bora · Tumia mzunguko wa mazao. Nyanya zisizungushwe na mazao jamii

Page 58: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 58 Tanzania.

yake · Teketeza masalia ya mimea www.ariuyole.go.tz · Choma kitalu cha nyanya kabla ya kusia mbegu Mnyauko bacteria (Bacterial wilt) Ugonjwa husababishwa na vimelea vya bacteria vinavyoishi kwenye udongo. Huenezwa na kusambazwa na mbegu na udongo wenye vimelea. Mirija ya mimea ya kupitishia maji na chakula hushambulia na mimea hunyauka ghafla. Mmea hukauka na kufa. Udhibiti · Panda mbegu safi · Panda nyanya sehemu ambayo haijawahi kupandwa viazi mviringo, bilinganya au nyanya chungu · Tumia mzunguko wa mazao · Hakikisha mfereji wa maji ya kumwagilia hayapiti kwenye shamba lenye historia ya ugonjwa huu. · Choma kitalu cha nyanya kabla ya kusia mbegu Mnyauko vetisili (Verticillum wilt) Hakuna dawa inayozuia au kutibu ugonjwa huu kwa sasa. Ugonjwa husababishwa na ukungu (fangasi) kwenye udongo. Ukungu huu huishi kwenye udongo kwa muda mrefu bila kudhurika. Ugonjwa huongezeka ikiwa mizimizi ya nyanya imeshambuliwa na minyo fundo; au kukiwepo na hali ya ubaridi au ukame. Ugonjwa husababisha hasara kubwa. Ugonjwa hushambulia sehemu ya ndani ya shina na kusababisha sehemu hiyo kuwa na rangi ya kijivu. Majani hugeuka njano na mimea kunyauka na kufa. Udhibiti · Tumia mzunguko wa mazao usiopungua miaka mine · Ondoa mabaki ya nyanya shambani

Page 59: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 59 Tanzania.

· Tumia mbegu bora na safi Bakadoa (Bacterial spot) Ugonjwa huu huenezwa na vimelea vya bacteria vinavyoishi kwenye mbegu, pia kwenye hewa. Huenezwa kwa kasi sana wakati wa masika. Madoa ya rangi kahawia huonekana kwenye majani na matunda. Udhibiti · Panda mbegu bora na safi · Tumia mzunguko wa mazao · Teketeza masalia ya mazao · Nyunyizia dawa ya funguran, Kocide101, Cobox, Bravo Makovu bakteria (Bacterial canker) Ugonjwa huenezwa na vimelea vya bacteria vinavyoishi kwenye mbegu na hewani. Hutokea zaidi wakati wa masika. Majani hukauka nchani na makovu yaliyodidimia hutokea kwenye shina. Matunda huwa na makovu yenye rangi ya kahawia sehemu ya katikati. Udhibiti · Tumia mbegu bora na safi www.ariuyole.go.tz 2 · Teketeza masalia ya mazao · Tumia mzunguko wa mazao Rasta (Yellow leaf curl) Ugonjwa huu husababishwa na virusi na huenezwa na nzi wadogo weupe. Hutokea zaidi wakati wa kiangazi. Mimea hudumaa na majani yaliyoshambuliwa huwa na rangi ya manjano na pengine rangi ya zambarau. Nyanya hupasuka.

Udhibiti · Nyunyiza dawa za sumu za kuua wadudu (Selecron, Dursburn, Actelic) · Ng’oa mimea yenye ugonjwa · Tumia mzunguko wa mazao

Page 60: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 60 Tanzania.

· Weka shamba katika hali ya usafi Batobato (Tomato mosaic virus) Ugonjwa husababishwa na virusi na hueezwa na mbegu na kugusana. Majani huwa na mchanganyiko wa rangi hasa kijani kibichi na kijani kilichofifia (majano). Majani hujikunja na manjani machanga huwa na maumbile yasiyo kawaida. Ukifikisha jani huwa linavinjikavunjika. Udhibiti · Tumia mbegu bora na safi · Ng’oa mimea iliyoshambuliwa · Teketeza masalia ya mazao · Weka shamba katika hali ya usafi

WADUDU WAHARIBIFU Viwavi Matunda (Fruit worm) Viwavi hawa hutokana na wadudu nondo. Viwavi hutoboa matunda na kuacha matundu na hatimaye matunda huoza. Hupunguza ubora wa matunda. Udhibiti Nyunyizia dawa ya kuua wadudu. Dawa hizo ni pamoja na Actelic 50EC, Selectron, Dursbaan, Maji ya majani ya mwarobaini au utupa pia huua

Page 61: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 61 Tanzania.

wadudu. Utitiri wekundu (Red Spider mites) Hawa ni wadudu wekundu, wadogo sana wanaoweka utando chini ya majani, hasa wakati wa kiangazi. Wadudu hawa hufyonza utomvu kwenye majani na kusababisha majani kukauka. Udhibiti · Nyunyizia dawa za sumu. Dawa hizo ni pamoja na Actellic, Selecron, Dursbarn na Thionex · Mwagilia maji mara kwa mara · Weka shamba katika hali ya usafi www.ariuyole.go.tz 3 Inzi weupe (White flies) Hawa ni Inzi weupe wadogo sana. Hujitokeza sana wakati wa kiangazi. Hueneza ugonjwa wa virusi ujulikanao kama Rasta. Udhibiti Nyunyizia dawa za sumu za kuulia wadudu kama Selecron, Actellic, Dursban na thionex. Pia maji ya majani ya mwarobaini na utupa. Vidukari au Wadudu mafuta (Aphids) Ni wadudu wenye rangi nyeusi au kuijani au kahawia. Hukaa chini ya majani na kufyonza utomvu kwenye majani machanga. Hudumaza mmea na kushindwa kuzaa matunda Udhibiti Nyunyizia dawa za sumu za kuulia wadudu kama Rogor, Actellic, Selecron, Dursban maji ya majani ya mwarobaini na utupa, maji ya pilipili. Minyoo (Nematodes) Ni minyoo midogomidogo ambayo hushambulia mizizi na kuweka vifundo. Mizizi hushindwa kuchukua maji na chakula kwenye udongo. Mimea

Page 62: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 62 Tanzania.

hudumaa na kushindwa kuzaa Udhibiti · Tumia mzunguko wa mazao · Choma udongo wa kitalu kabla ya kusia mbegu kwa kutumia karatasi la plastiki jeusi na nishati ya jua · Choma masalia ya mazao Sota (Cutworms) Hushambulia miche ya nyanya hasa baada ya kupandikizwa shambani. Wakati wa mchana hujificha kwenye udongo na usiku hujitokeza na kukata miche kwenye shina usawa wa udongo. Udhibiti · Nyunyiza dawa za kuua wadudu kwenye shina usawa wa udongo · Hakikisha miche inapata maji ya kutosha.

MWISHO

Kama unataka kupata kitabu cha kilimo cha nyanya chenye magonjwa na dawa zake,kinapatikana.wasiliana nasi kwa email ni sh.2000/= tu.

KARIBU SANA!

(prepared by professor G. Mwangomile)

Page 63: KILIMO NA UFUGAJI - smartagrobusiness.files.wordpress.com · 11.UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI . 12.KILIMO BORA CHA NYANYA . Mbinu za ujasiliamali . smartagrobusiness Page 3 Tanzania

Mbinu za ujasiliamali

smartagrobusiness Page 63 Tanzania.

Smartagrobusiness na uongozi mzima tunapenda kutoa shukhrani kwa wale wote walioshiriki katika uandaaji wa

Kitabu hiki.Kitabu hiki kimeandikwa na watu wasio pungua 20 wakiwemo wajasiliamali,wataalamu wa kilimo

Na ufugaji,wanafunzi kutoka chuo cha sua na udsm pamoja na wadau wengine wa maendeleo.

ONYO;Hauruhusiwi kunakili au kuuza au kuchapisha nakala hii bila ruhusa kutoka kwa wahusika,endapo utagundulika unafanya hivyo hatua kali za kisheria zitafuata juu yako.

Tunawatakia usomaji mwema na utekelezaji madhubuti katika kulijenga taifa la Tanzania.Mungu ibariki Afrika Mungu ibariki Tanzania