kuwait

4
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA Simu: 255-22-2114615, 211906-12 Barua pepe: [email protected] Barua pepe: [email protected] Tovuti : www.foreign.go.tz Nukushi: 255-22-2116600 20 KIVUKONI FRONT, P.O. BOX 9000, 11466 DAR ES SALAAM, Tanzania. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Tanzania kufungua Ubalozi nchini Kuwait Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepanga kufungua Ubalozi nchini Kuwait kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha wa 2014/2015. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) alipokutana na Mtukufu Sheikh Sabah Al-Khalid Al- Sabah, Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait nchini Kuwait siku ya Jumanne tarehe 14 Aprili, 2015.

Upload: ngabwe

Post on 21-Dec-2015

68 views

Category:

Documents


5 download

TRANSCRIPT

Page 1: Kuwait

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Simu: 255-22-2114615, 211906-12

Barua pepe: [email protected] pepe: [email protected] : www.foreign.go.tzNukushi: 255-22-2116600

20 KIVUKONI FRONT, P.O. BOX 9000,

11466 DAR ES SALAAM, Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania kufungua Ubalozi nchini Kuwait

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepanga kufungua

Ubalozi nchini Kuwait kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa

fedha wa 2014/2015.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano

wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) alipokutana na

Mtukufu Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah, Naibu Waziri Mkuu

ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait nchini Kuwait

siku ya Jumanne tarehe 14 Aprili, 2015.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wawili walisifu ushirikiano

uliopo baina ya nchi hizi mbili ambao ni wa kidugu na unalenga

kuwanufaisha wananchi wa nchi hizi.

“Kwa kufungua ofisi za Ubalozi, Kuwait ushirikiano huu wa kidugu

utaongezeka kwenye nyanja zote muhimu na utazaa matunda

Page 2: Kuwait

yatakayo wanufaisha watu wetu, kwa nchi hizi mbili” alisisitiza

Waziri Membe katika mazungumzo yake na kiongozi huyo.

Kwa upande wa Kuwait, Serikali yao ilifungua ubalozi nchini

Tanzania Februari 2015 na Mhe. Jassem Ibrahim Al Najem kuwa

Balozi wake wa kwanza nchini Tanzania, mwenye makazi yake

Jijini Dar es salaam.

Aidha, kwa sasa Tanzania inawakilishwa nchini Kuwait kupitia

Ubalozi wake uliopo Riyadh, Saudi Arabia.

Katika mkutano huo, Mtukufu Sabah Al-Khalid Al Sabah alisifu

jitihada za Tanzania kwenye kulinda na kuleta amani Barani Afrika

hasusan kwenye maeneo yenye migogoro. Alisema kuwa Serikali

yake itaendelea kushirikiana na Tanzania sio tu kwenye maeneo

muhimu ya maendeleo lakini pia hata kwenye ulinzi wa amani

kwani ndio changamoto kubwa inayoikabili dunia kwa sasa.

Kuhusu misaada Barani Afrika, viongozi hao walijadili suala la

uratibu wa misaada mbalimbali ya Serikali ya Kuwait Barani humo

ambapo waliangalia uwezekano wa kuanzisha kituo maalum

nchini Tanzania kwa ajili ya kusimamia shughuli za uratibu wa

misaada hiyo.

Kwa sasa Serikali ya Kuwait kupitia Mfuko wake wa Maendeleo –

Kuwait Fund- imetoa Dola za Kimarekani Bilioni moja kwenye

Umoja wa Afrika kwa ajili ya usalama wa chakula Barani Afrika.

Page 3: Kuwait

Awali Waziri Membe alikutana na Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader,

Mkurugenzi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait na kumshukuru

kwa misaada mbalimbali ya kimaendeleo wanayoendelea kuitoa

nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.

Aidha Waziri Membe alielezea kuwa maandalizi ya miradi mitano

ya umwagiliaji nchini Tanzania ambayo inayofadhiliwa na mfuko

huo yamekamilika, na kwamba sasa iko tayari kuanza. Aidha

Waziri Membe na Mhe. Al-Bader walizungumzia uwezekano wa

mfuko huo kuikopesha Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) ili iweze

kuendesha shughuli zake kikamilifu.

Waziri Membe yuko nchini Kuwait kwa ziara ya siku moja na

anatarajiwa kuondoka kesho kuelekea nchini Oman. Ujumbe wa

Mhe. Membe nchini Kuwait unamjumuisha Bw. Peter Noni,

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Uwekezaji Tanzania, Balozi Simba

Yahya, Mkuregenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya

Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bi. Mindi Kasiga,

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo

ya Nje.

-Mwisho-

Imetolewa na:Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es Salaam15 Aprili 2015.

Page 4: Kuwait