lesson 3: maternal nutritioncaregroupinfo.org/docs/swahili_drc_flipchart2.docx · web viewni...
TRANSCRIPT
MATENDO YA LAZIMA YA MALISHO BORA KITABU KYA MAMA KIONGOZI WA KUNDI
LA AFIAKITABU KYA PILI
Module 2 of 6
1
SHUKRANI
Hanold, Mitzi J. na Wetzel, Carolyn (2009), matendo ya la-zima ya malisho bora.Washington DC. Chakula kwa ajili ya njaa, inawezekanisha kupitiya musaada yenye ilipewa na of-fisi ya chakula kwa ajili ya amani, offisi ya democratia, mi-zozano, musaada wa kibinadamu na chirika ya marekani kwa ajili ya maendeleo ulimwenguni chini ya namba FFP-A-00-08-00072-00
Maonyi yenye kuwa umu ni ya waandishi na haiusishi shirika ya marekani kwa ajili ya maendeleo ulimwenguni Shukrani kwa maitre Wabangu, Octavio Gonzales, na Petra Rohr-Rouendaal, na uwaziri wa afia wa serkali ya Congo ya ki democratia pamoja na UNICEF.Acknowledgements
2
Lesson 1: First Foods
Not Eating (Picture 1.1)
Mama Mubaya alifata ma shauri ya mama muzuri na akamnyonyesha mateso kwa maziwa yake tu hadi miezi sita na yeye mwenyewe alienda kwa mganga kupata vitamine A mu myezi mbili kisha kuzaa na yeye na mtoto wake mateso wanakuwa na afia bora.
Wakati mateso anaeneza miezi sita, mama mubaya anaaanza kumupa buyi na mateso amekataa kunywa ile buyi. Wajirani wana muhimiza ma-ma mubaya na kumueleza kama anamukunywisha mateso buyi mubaya. Mama mateso hadjuwi ginsi ya kufanya
? NI VIZURI KWA MTOTO KUKATAA CHAKULA MPYA ?
? NI WAKATI GANI TUNAHITAJI KUMUPA MTOTO CHAKULA MUPYA ?
3
Not Eating (Picture 1.1)
4
Breast Feeding (Picture 1.2)
Tangu miezi sita mama Muzuri anamupatiya Furaha chakula kusudi akomale vizuri
Anamupikiya buyi ama chakula ya kupondwa, kutiya amo mafuta kisha kuitosha ku moto
Kutiya mafuta yenye hayikutshamushiwa ku moto inaleta nguvu kuzidi ile mafuta ya kutshamushi-wa
Mu djuma ya kwanza yenyewe banaanza kumupa mtoto buyi, banamupa pao moja ao mbili ya buyi ya teketeke mara moja ao mara mbili kwa siku. Kumunyonyesha mtoto mbele ya kumupa buyi kwa kumuzoesha ku chakula mupya.
Mama Muzuri anapashwa kumunyonyesha mtoto wake Furaha mpaka miaka mbili ao kupita
Maziwa ya mama ndiyo chakula ya muhimu kwa watoto wa ile miezi
Inafaa kunyonyesha mtoto kila wakati anapohitaji chakula Maziwa ya mama inasaidiya kukinga mtoto kwa magonjwa
mbali mbali
? TUTAFANYA NINI KAMA MTOTO ANAKATALA KULA BUYI?
Kumusemecha vizuri na kumuhimiza akule ile buyi Kumuimbiya mimbo kwa kumuhimiza anywe ile buyi Kumulisha polepole na kuwa muvumilifu Kuongeza maziwa ya mama ndani ya buyi. Inasaidiya mtoto
kuzoeya chakula mupya. Atadjuwa harufu na utamu wake Tusimukaze mtoto ili akule kwani chakula inaweza kuingiya
ndani ya mafafa wakati mtoto analiya Kama unapata chakula yenye mtoto anapenda, inafaa
kumupatiya ayo
Breast Feeding (Picture 1.2)5
6
Adding New Foods (Picture 1.3)
Siku ine ya kwanza yenye wanamupa Furaha buyi, wana mupa tu buyi yenye inachanga bun-ga ya chakula yenye inakuliwa sana na mafuta. Kisha siku ine anaongeza amo chakula ingine
Anaweza kuongeza amo samaki ya kupondwa, maharagi ya kupondwa ama chakula ingine
Inafaa ma siku chache kwa butumbu ya mtoto kuzoeya ile chakula ya mupya
Kuongeza ingine chakula kasha siku ine kwa kuona kama butumbu tumbu inaizoweya
Kama hakuzoweya ile chakula mupya mu ile siku ine, inafaa kuibadirisha na kumuongezeya ingine
? NI CHAKULA GANI TUTAONGEZA KU BUYI DJU YA KUIFANYA IKUWE YA MALISHO BORA?
Kuongeza mafuta na lutuba ya kalanga ndani ya buyi Kuongeza bipande ya nyama yenye kupondewa, mayayi na
mboka ya majani yenye kuponde-wa Kuongeza chakula ya mizizi ao matunda yenye na rangi ya
manjano ao ya mwekunda ndani ya buyi kwa kumuongezeya mtoto vitamine A ndani ya mwili
Kuongeza matunda, chakula ya mizizi ao mboka ya majani yenye kutwangiwa
7
Adding New Foods (Picture 1.3)
8
Quantity of Food for Each Feeding (Picture 1.4)
Tangu miezi sita hadi munane, analisha mtoto wake mara tatu kwa siku (busubuy, kisha midi na mangaribi)
Tangu miezi sita hadi munane, mama anamupa mtoto wake kopo ya buyi yenye kuwa mapawo ine ya supu kwa kila chakula. Ndani ya ko-po ya plastic, buyi inapasha kuwa ku mustari wa pili kuanziya chini na ndani ya kopo ya musaada buyi inapashwa kuwa kati ya kuanziya chini na mukono wa kopo kwa kila chakula
Tangu miezi kenda hadi kumi na moja, analisha mtoto wake mara ine kwa siku
Tangu miezi kenda hadi kumi na moja, mama anamupa mtoto wake ndani ya kopo ya plastic, buyi inapasha kuwa ku mustari wa pili kuan-ziya chini, na ndani ya kopo ya musaada buyi inapashwa kuwa ku mukono wa chini wa ile kopo kwa kila chakula
Mama anaanza kumupa mtoto wa miezi kenda hadi kumi na moja ma chakula ingine kidogo kidogo kati ya ma chakula
Mama anaikala karibu na mtoto wake na anamufundisha namna ya kula Mama anaweka akili yake yote kwa mtoto wake Ginsi mtoto eko anakomala ndjo ginsi mama muzuri ana muongezeya
chakula kwa kiasi na mara ya kula Tangu miezi kenda hadi kumi na moja, anamupa mtoto chakula yenye mtoto
anaweza kula yeye mwenyewe kwa mikono yake kama vile papayi, hembe, bitika, chungwa
Kuendeleye kumunyonyesha mtoto wakati wote mwenye anahitaji hadi miaka mbili na kupita
Maziwa ya mama ina maji yote yenyewe mtoto wa chini ya mwaka moja anahitaji. Kama mtoto analomba maji ya kunywa, inafaa kumupa-tiya maji ma safi yenye kuwa na dawa ya kuisaficha
Kumupa mtoto buyi mu kopo ama mu sahani kwa kujuwa kiasi gani anakula
KAZI : KUONESHA GINSI YAKUPIKA BUYI YA KWANZA YA
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
9
Quantity of Food for Each Feeding (Picture 1.4)
10
Lesson 2: Feeding During the Second Year (12-23 months)Still Hungry (Picture 2.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Saa kidogo kisha kula, mateso anasikiya tena ndjala. Ma-ma mubaya anamupikiya mateso kila siku buyi mingi mara tatu. Hawezi kumaliza ile buyi yote kwa mara moja. Kisha saa kidogo, mateso anasikiya tena ndjala. Mama muba-ya anasilika na anapenda meteso akule chakula mingi kwa mara moja sababu hana na wakati wakupiga saa yote. Hana na wakati wakupiga chakula mara tano kwa siku ? MUNAWAZA KAMA MAMA MUBAYA ANA SHERIYA YA
KUMUKASIRIKIYA MATESO? ? MARA NGAPI KWA SIKU TUNAWEZA KUMUPATIYA MTOTO WA
MWAKA MOJA HADI MBILI CHAKULA ? ? KIASI GANI MUNAWEZA KUWAPA KWA KILA CHAKULA ?
Still Hungry (Picture 2.1)
11
12
Feed First (Picture 2.2)
Mama muzuri na bwana yake wanamupatika mtoto wao Furaha chakula ndani ya sahani kwa kuweza kutambuwa kiasi kyenyewe anakula
Tangu mwaka moja mtoto anapata nguvu mingi ndani ya chakula kuliko ndani ya maziwa ya kifuwa ya mama yake
Tangu mwaka moja, mama Muzuri anapatiya mtoto wake Furaha mbele chakula kisha anamunyonyesha
Mama muzuri anamunyonyesha mtoto wake Furaha wakati wote, busiku na mchana wakati anahitaji. Na ataendeleya hivi hadi miaka mbili
Feed First (Picture 2.2)
13
14
Quantity and Frequency Increased (Picture 2.3)
Tangu mwaka moja hadi miaka mbili anamupatiya furaha mara tatu chakula ya jamaa
Anamuongezeya chakula ingine ya kidogo mara moja wakati Furaha ana miezi kumi na mbili hadi kumi na saba. Anamuongezeya chakula ingine ya kidogo mara mbili wakati
Furaha anakuwa na miezi ya kupita kumi na saba Anaendeleya kumusaidiya na kumuhimiza Furaha akule
chakula Anaongeza kiasi na mitindo ya chakula ? KAMA FURAHA ANAGONJWA, MAMA YAKE ATAELENDELEYA
KUMUPATIYA CHAKULA KWA KILE KILE KIASI?
Mama Muzuri atamulicha kwa kile kile kiasi, atamupatiya maji mingi na kumunyonyesha kupita wakati wa kawaida
Wakati mutoto ana gonjwa bwaki (ni kwa sababu hakupata chakula muzuri kwa wakati murefu) an-aweza kupoteza hamu ya kula chakula
Mama Muzuri anahitaji kumuhimiza Furaha kutumiya chakula na kumuongezeya chakula ingine
Wakati na kisha magonjwa mama Muzuri anapashwa kumupatiya mtoto chakula mingi kupita wa-kati wa kawaida kwa kumusaidiya mtoto kurudisha nguvu
15
Quantity and Frequency Increased (Picture 2.3)
16
Daily Nutrients Needed (Picture 2.4) ─ 5 minutes
Kwa kila chakula Furaha atakula kipande ya kopo ya plastic ama kopo ya musaada kati ya mikono yake
Kunakuwa vitu vya lazima vyenye mtoto wa mwaka moja hadi mbili anahitaji kula kama vile: maharagi, mandjekele, kunde, maboke, mboka ya majani ya rangi ya maji ya sombe.
Matunda kama vile chungwa, bitika, mahembe. Mafuta ama blue band. Nyama, mayayi, maziwa, samaki. Chakula ya rangi ya mwekunda ao manjano kama vile
mahembe, bitika, chungwa, papayi, ndizi; byote bya kuivya Chakula ingine kidogo kidogo sawa vile mikate, kalanga,
matunda ao mihindi
KAZI : KUONESHA KIASI KYA CHAKULA KYENYEWE MTOTO ANAHITAJI KULA KWA SIKU
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Uliza
Daily Nutrients Needed (Picture 2.4)
17
18
Lesson 3: Sanitary Food Preparation and Cleanup
Worms and Sickness (Picture 3.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Mama Mubaya anapima kufata ma shauri yenye alipewa na mama Muzuri. Anamupigiya Mateso buyi, chakula ya jamaa na ma chakula ingine kidogo kidogo, lakini Mateso eko wakati wote mugonjwa na an-agonda. Wakati moja Mateso anaharisha kwa masiku mingi na anapoteza hamu ya kula chakula. Wakati mwingine, mitchango inaonekana ndani ya choo kubwa ya mateso. Mama mukwe wa mama Mubaya na wengine wandugu yake wa jamaa wanamueleza kama asifazaike kwani watoto wote wanagonjwaka, na kuhara haina hatari. Asifazaike kabisa sababu ya hiyi vitu ? MUNAFIKIRI NINI KWA HIYI MASWALI YENYE MAMA MUKWE
WA MAMA MUBAYA ANASEMA?MUNAFIKIRI KAMA KUHARA NI SHIDA KUBWA?
? KUPITIYA HIYI PICHA, MUNAONA VITU VINGINE VYENYE VIN-AFANYA MATESO AUGUWE KILA SIKU?
19
Worms and Sickness (Picture 3.1)
20
21
Spoiled Foods and Hands (Picture 3.2)
Kuna njia mingi yenyewe mtoto anaweza kupata magonjwa ao kuhara
Njia ya kwanza ni kupitiya bitu byenyewe anatiya kukinywa Kula vitu vyenye havifinikwi, vya baridi vienyewe kufanya
zidi ya saa tatu inaweza kuleta magonjwa Kutumiya mikono michafu mbele ya kula ama mbele ya
kupika chakula inaweza kuleta magonjwa Hiyi mienendo inaweka mtoto ku hatari ya kutokukuwa
muzuri na kupata bwaki kwa urahisi. Vitu vichafu umuleteya mtoto kuhara na mitchango
? MUNAFIKIRI KAMA JAMAA INAWEZA KUFANYA KITU KWA KUEPUKI-SHA WATOTO WAO WAPATE MAGONJWA YA BWAKI? NAMNA GANI?
Vitu vyenye wenye kuusika na afya ya watoto katika ma jamaa wanaweza kufanya vina weza kuleta tafauti saana kwa maisha ya watoto
Kila maisha ni ya mafaa na inakuwa na lazima saana. Maisha ya mtoto inahitajika ku-kingwa na kila hatari
Kwa kuwa na usafi na kufanya vitu visafi tunaweza kusaidiya watoto kushinda ma-gonjwa na kuishi vizuri
Spoiled Food and Hands (Picture 3.2)
22
23
Preparing Hands, Foods and Utensils (Picture 3.3)
Kusafisha na maji na sabuni inatosha butchafu, mayayi ya mitchango na vitu vyenye kuleta magonjwa kupitiya chakula na vyombo vya kupikiya
Maji yenyewe haitoshi kusafisha mikono, mpaka sabuni ao majifu ndjo inaweza kuuwa vidudu vyenye kuleta magonjwa
Wenye kupika chakula wanapashwa kunawa maji na sabuni ama majifu mbele ya kupika chakula ao mbele ye kuokesha watoto
Wenyewe kuhudumiya watoto wanapashwa kusukula mikono ya watoto wao na maji na sabuni mbele ya kuwalisha chakula
Chakula yote ya kuliwa mubichi inapashwa kusafishiwa na sabuni na maji masafi kwa kusaidiya kuuwa mayayi ya mitchango yenye inaweza kuletewa na ile chakula
24
Preparing Hands, Foods and Utensils (Picture 3.3)
25
Cook Food Well and Cover (Picture 3.4)
Chakula yenyewe haipikiwe inaweza kuwa na mayayi ya mitchango. Ile mayayi inakufa kama chakula inapikiwa ku moto
Jamaa inapashwa kula chakula yenye kupikiwa na wakati ingali moto. Musiache buyi ao supu ipole mbele ya kuikula
Kufinika tchakula hadi wakati wa kuikula. Kisha kula, ile chakula inabaki inafaa kuifinika na mufuniko ama nguo kusudi ma inzi isiingiye ndani. Inzi inaleta ku chakula choo kubwa na uchafu kidogo saana yenye macho haiwezi kuona
Tuchunge chakula fasi muzuri na ya baridi, mbali na bulongo. Funika chakula na kipande kya nguo kisafi kwa kufanya ikuwe baridi
Kutchamusha kila siku chakula yenyewe tuliweka ili ikuwe moto mbele ya kuikula
Tuchunge chakula mu kabati ama kuifunika Kutupa chakula yenyewe ilibaki muda wa saa tatu Kutchamusha chakula ya maji maji kama vile buyi ama supu
yenye ili tchungiwa. Kama ile buyi ama supu ilisha fanya saa tatu inafaa kuitupa
Chakula ya nguvu kama vile ugali, wali, samaki, nyama, viazi inastahili kuliwa ata iko baridi. Lakini kama inaisha fanya saa ta-tu, tunastahili kuitupa.
KAZI : KUONESHA GINSI YA KUFIKA CHAKULA NA MITINDO YA MIFINIKO YENYEWE TU-NAWEZA KUTUMIYA
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Uliza
26
Cook Food Well and Cover (Picture 3.4)
27
28
Lesson 4: Vitamin A Too Expensive (Picture 4.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Mama Mubaya alisikiya mafundisho kutoka kwa wa ma-ma viongozi wa gundi la afya kama inafaa kuongeza chakula ya rangi mbali mbali kwa chakula yake. Anakutana muuzishadji mumoja anauzisha chakula ya rangi mbali mbali. Huyu muuzishadji anamueleza kama ile chakula inasaidiya mtoto kuwa na afia bora. Mama Mubaya anaangaliya ile chakula na anafazaika saana sababu hawezi kununuwa ile chakula yote kila djuma hata akipenda mtoto wake akuwe na afia bora.
Siwezi kununuwa hiyi chakula yote kasema mama Mubaya, akatoka karibu na yule muuzishadji kwani hana pesa nyingi. Angalipendeleya akuwe na pesa mingi.
? MUNAWAZA KWA IYI SHIDA INAKUWA NA MAMA MUBAYA? ? KUKO WAKATI MUMOJA NA NYINYI MUNA KUWA NA SHIDA HIYI? ? SHAURI GANI MUNAWEZA KUMUPA MAMA MUBAYA?
29
Too Expensive (Picture 4.1)
30
Foods with Vitamin A (Picture 4.2)
Nyama ya mafuafua, minofu ya nyama ya rangi mwekunda, samaki, viazi ya kishenzi na papayi ina Vitamine A mingi
Mafuta ya ngazi, ndizi na mandjekele ina Vitamine A mingi lakini haizidi nyama ya mafuafua, minofu ya nyama ya rangi mwekunda, samaki, viazi ya kishenzi na papayi
Chakula ya majani sawa vile sombe, lenga lenga, matembele, kisinsa na ngai-ngai ina Vitamine A lakini haipiti mafuta ya ngazi, ndizi na mandjekele
Hembe ya kuivya ina Vitamine A lakini Haipiti iyi ma chakula yote tulitaja uku juu
Hii ma chakula yote ina Vitamine A yenye kusaidiya kukinga kwa magonjwa mbalimbali. Vitamine A inasaidiya mtoto kuwa na afia bora
Wazazi wanahitaji kuwapa watoto chakula yenye Vitamine A kwa wingi (sawa vile ile chakula yenye kuwa ku mustari wa kwanza) mara moja kwa juma. Iyi chakula iko na Vitamine A mingi na haistahili kuliwa kila siku
Wazazi wanaweza pia kuwapa watoto wao chakula yenye Vitamine A kidogo lakini wanahitaji kuwapa ayo kila siku ao mara mingi kwa juma
Chakula yenye rangi ya mwekunda ao ya manjano ndani na inje iko na Vitamine A mingi
Mboka ya majani ama mafuta ya ngazi inapoteza Vitamine A kama inatchamushwa kwa motomingi na muda mu-refu saana. Tunahitaji kuipika kwa muda kidogo
Kama ikiwezekana tukule mboka ya majani bila kupika inaweza kuwa vizuri saana kwani Vitamine A iko mingi
Matunda ya kuivya saana na inakuwa teketeke inaupungufu wa Vitamine A, inafaa kula matunda ya kuivya lakini apana ya kuivya saana.
31
Vitamin A (Picture 4.2)
32
Night Blindness (Picture 4.3)
Alama yenye kuonesha kama Vitamine A inakosa ku mwili ni upungufu wa kuona wakati busiku bunaanza kuingiya
Kama chakula yenye Vitamine A kwa uwingi ama vidonge vya Vitamine A havipewi kwa mtu mwenye kuonesha alama hiyi, anaweza kuwa kipofu
Ma nukta itatoka ku ile fasi mweupe ya macho Kama upungufu wa Vitamine A uki endeleya kwa mtoto ao mukubwa
atabakiliya kipofu lote Vitamine A inasaidiya ku kinga macho na kuiweka na afia njema Watoto wengi wanakuwa na upungufu wa Vitamine A lakini hawana alama
ya kutokuona muzuri wakati wa usiku kuingiya ama nukta kwa macho lakini wanakamatika na magonjwa saa yote na ma-gonjwa mbalimbali
? KWA NINI NI LAZIMA KWA WAZAZI KUTAFUTA MATUNZO KWA WATOTO WAO WAKATI WANA ONESHA HII MA ALAMA TUNATAJA HAPA JUU ?
Upungufu wa kuona wenye unatokana na ukosefu ama upungufu wa Vitamine A inaonesha alama ya kusema kama mwili una hitaji musaada
Kama mwili haukupata ule musaada wa Viatmine A, mtoto atakua kipofu milele
Vitu sisi wazazi tutafanya inaweza kuleta faida na mabadiriko kwa afia na maisha ya watoto wetu
33
Night Blindness (Picture 4.3)
34
Vitamin A Supplements (Picture 4.4)
Mama mwenye kutoka kuzaa anahitaji kupata kidonge ya Vitamine A mu miezi mbili yenye kufata kuzaa, itamusaidiya kuwa na afia nzuri na kwa hiyo tutakuwa na uhakika kama mtoto wake atapata Vitamine A kupitiya maziwa ya mama yake
Wakati mtoto anaeneza miezi sita inafaa kumupatiya kidonge ya Vitamine A, na kisha iyo anahitaji kupata kidonge ya Vitamine A kila miezi sita hadi atafikisha miaka tano mtoto mwenye suluba, magonjwa ya nguvu ama bwaki anapashwa kwenda ku senta ya afia kwa kupewa vidonge ya Vitamine A
Watoto wagonjwa na wale wanaotoka mu magonjwa wanapashwa kula chakula yenye Vitamine A mingi kwa kuwasaidiya kurudisha kilo yao yenye walipoteza sababu ya magonjwa
Vitamine A inasaidiya kukinga kwa magonjwa zaidi ile ya nguvu na inasaidiya kufupisha muda wa magonjwa
KAZI : KUONESHA CHAKULA YENYE VITAMINE A KWA UWINGI
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
35
Vitamin A Supplements (Picture 4.4)
36
Lesson 5: Nutrition Rich Foods
Seeing is Believing (Picture 5.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Bwana wa mama Mubaya alitambua kama muke wake aliongeza chakula ingine nyingi ya mupya katika chakula ya jamaa, ijapokua mbele hakukubaliana na mke wake, lakini alitambua mabadiriko mingi katika afya ya mateso, na sasa mtoto mateso anakua na nguvu na afya nzuri. Jamaa nzima inakuwa na afia nzuri tangu wakati walianza kutumiya chakula mupia. Kumwanzo sikuwa nakubali kama hiyi chakula ya mupia inaweza kusaidiya watoto, Sasa nimeona na nimekubali kasema bwana yake ya mama mubaya.
Baba mateso anacheza na watoto wake Baba mateso anafurahi namna gani watoto wanaguwa na kukomala
vizuri Baba mateso anamupa moyo na kumueleza bibi yake aendeleye kwa ile
njia
? MUMEONA MABADIRIKO GANI MAZURI NDANI YA AFYA YA WATOTO WENU?
? CHAKULA GANI UNAWAZA INAWEZA KUONGEZEWA KATIKA CHAKULA YA MUTOTO WAKO KILA JUMA
37
Seeing is Believing (Picture 5.1)
39
Malnutrition (Picture 5.2)
Katika picha ya kwanza tunaona kama chakula ya mtoto ni ile ile moja. Chakula ile hamupatikani vifaa vingi vya afia kama vile maharagi, mandjekele ama mandizi.
Anapata magonjwa kwani mwili wake umekosewa vifaa vya afya ambavyo vinaweza kumusaidiya kujikinga
Chakula yenyewe haina vifaa vya afia vyenye anakula inamuweka muzaifu kwa magonjwa
Magonjwa ina fanya mtoto anapoteza hamu ya kula chakula Mtoto anapoteza kilo yake, mwili wake unashindwa kupikanisha magonjwa
na anende-leya kugonjwa na kula kidogo Mwisho anagonjwa saana na anakuwa mu hatari ya kufa Kula mubaya inafanya apoteze kilo na akuwe mu hatari ya kufa
? MUNAWAZA KAMA MAMA ANAPASHWA KUBADIRISHA NAMNA YA KUL-ISHA WATOTO WAKE? SABABU GANI?
Maisha ya mtoto ni ya lazima kubwa na inastahili Mupango wenyewe mama anakamata inaweza kuokowa maisha ya mtoto
40
Malnutrition (Picture 5.2)
41
42
Nutrient Rich Foods for Children Ages 12 to 23 Months (Picture 5.3)
Tupatiye watoto chakula yote yenye kuwa ndani ya miviringo yote. Kama hautaweza kumupa ile mitindo yote ya chakula mara moja, umupe ile ulisahau kama vile chakula kidogo kodogo muma wakati ingine mbele ya chakula ya jamaa. Ile itamusaidiya kuwa na afia na malisho bora
Chakula moja yenye inapatikana mu miviringo mingi iko na vifaa vingi vya afia. Kama ukitumiya ile chakula, si lazima uongeze tena ma chakula yenye kuwa mu miviringo in-gine
Mufano Figo ya nyama iko tajiri kwa Vitamine A na kiungo kya kuongeza damu (fer). Samaki iko tajiri kwa viungo vya kujenga (proteins), vitamine A na viungo vya kuongeza damu. Mboka ya majani ya rangi ya maji ya sombe iko tajiri kwa vitamine A na viungo vya kuongeza damu. Hembe iko tajiri kwa vitamine A na viungo vyenye kurahisisha utumivu wa viungo vya kuongeza damu mu mwili
? KUNA CHAKULA AMBAYO AINA VIUNGO VYA MAFAA YOYOTE NA AM-BAYO AISTAHILI KUWAPA WATOTO?
Watoto hawana lazima ya vinywaji vya sukari sawa vile chai, kahawa, soda.
Vinywaji vile havina vifaa vya kujenga na havipashwe kupewa kwa watoto.
43
Nutrient Rich Foods for Children Ages 12 to 23 Months (Picture 5.3)
44
45
Nutrient-Rich Meal Recipe (5.4)
Nyama nyekundu, maharagi na sombe viko tajiri kwa viungo vya kuongeza damu. Chakula hii ina-saidiya watoto kujikinga na ukosefu wa damu na inawapa watoto damu yenye nguvu
Chungwa, ndimu, papayi, na tomate viko tajiri kwa viungo vyenye kurahisisha mwili utumiye fer (Vitamine C). Hii chakula ina saidiya mwili kutumiya fer muzuri
Mafuta ya ngazi, ndimu, papayi na sombe viko tajiri kwa vitamine A. Chakula hii ina saidiya mtoto kujikinga na magonjwa mbalimbali piya na kuepuka kuwa kipofu
Nyama, samaki, maharagi viko tajiri kwa vifaa vya kujenga mwili. Vina saidiya watoto ku komala haraka na kurudisha haraka afia kisha magonjwa.
Chunvi yenye iode inasaidiya kukinga magonjwa ya limengu. Mafuta ya ngazi inasaidiya kuleta nguvu kwa mtoto. Maziwa ya mama inabaki njia ya kwanza kwa malisho bora
ya mtoto Kama mama anakula chakula nzuri na kuongezewa fer
itamusaidiya kuwa na nguvu wakati wa ku-nyonyesha pia itasaidiya maziwa kuwa na vifaa vya lazima kwa afia ya mtoto.
Mama akikula chakula yenye kuwa na vifaa vyote vya afia, atakuwa na afia nzuri wakati eko ana nyonyesha
KAZI : KUONESHA GINSI YA KUPITA CHAKULA YENYEWE INAPATIKANA VIFAA VYOTE VYA AFIA
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
46
Nutrient Rich Recipe (Picture 5.4)
47
Lesson 6: Growth MonitoringFour Children of the Same Age (Picture 6.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Mangaribi moja watoto wa mugini walikuwa wakicheza pamoja, jirani moja akaona kama kabla wale watoto walikuwa na miaka sawa, lakini ki-mo yao ilikuwa inaachana. Furaha alikuwa murefu na munene, watoto wengine waliku-wa wagonde lakini Mateso anaonekana kuwa na afia njema lakini eko na kimo mufupi saana kuliko furaha. Jirani akasema na mwenzake ; angaliya ginsi mungu alifanya. Bato-to betu batakuwa bafupi na bembamba kila siku mpaka tu Furaha ndjo atakuwa murefu na wa nguvu
Mtoto wa mama muzuri ni mrefu na anaonekana kuwa na kilo mingi na afia njema kuliko wale watoto wawili wa ile ngambo ya mwisho
Mtoto wa tatu na wa ine wana konda sana. Mateso ni mfupi na anaonekana kuwa na afia nzuri
? MUNAWAZA KAMA WATOTO WANATAFAUTI YA UREFU NAYA KILO? MUNAWAZA KAMA NI MUNGU ALIFANYA VILE ?
? MUNAWAZA KAMA BABA MUBAYA ANAWEZA KUFANYA TAFAUTI NDANI YA MAISHA NA AFIA YA MTOTO WAKE ?
48
Four Children of the Same Age (Picture 6.1)
49
Growth Monitoring Activities (Picture 6.2)
Wazazi wanapashwa kupeleka watoto wao wa chini ya miaka tano ku kipimo ili wapate kujua nam-na gani afia ya watoto ikonaendeleya
Kwa watoto wa chini ya miaka mbili, tuwapeleke ku kipimo kila mwezi
Kwa watoto wa miaka mbili hadi tano, tuwapeleke ku kipimo kisha kila miezi tatu
Kisha kupima kilo na urefu wa mtoto, mganga atamueleza mzazi kama mtoto eko anakuwa muzuri
Mganga anamupatiya mama muzuri mashauri kuhusu nini anapashwa kufanya na mama Muzuri anamuuliza mganga vitu gani anahitaji kufanya
Malisho ya mtoto mu miaka tano tangu kuzaliwa kwake itasababisha kuguwa kwake na afia yake mu maisha yake yote
Mungu anaumba watu wa urefu na mufano mbalimbali lakini watoto wote wanapashwa kurefuka na kuongezeka kilo mu miaka tano tangu kuzaliwa. Kama watoto hawarefuki na kuongezeka kilo mu ile wakati, nilusema kuko kitu kimoja kyenyewe hakiendeki
Wazazi wanahitaji kusaidiya watoto wakati wanagonjwa na kufanya ginsi yote ya kuwasaidiya Mungu aliwapa wazazi mamalaka ya kuweza kufanya kitu kuhusu kutengeneza maisha ya watoto wao
50
Growth Monitoring Activities (Picture 6.2)
51
Growth Charts (Picture 6.3)
Kuguwa kwa mtoto kunapimiwa na mganga kupitiya mustari wa njia yake ya afia
Kwa kila kipimo, mganga anatiya nukta kwa ile fasi. kisha myezi mingi mganga anachanja kistari kienye kuunganisha vile vipimo vya myezi yote kwa kuonesha ginsi mtoto eko anaguwa
Kuna njia moja yenye kuonesha namna gani mtoto anahitaji kuguwa na ile njia inaanza tangu mwanzo wa kadi mpaka mwisho
Mustari wa njia ya kila mtoto unapashwa kubakiya ndani ya njia ya rangi ya maji ya sombe na kupanda kila mwezi
Kama mustari uko unapanda, ile ina onesha kama mtoto eko na guwa vizuri
Kama mustari haupandi kisha zidi ya mwezi moja ao kama unashuka, inaonesha kama mtoto haguwi mzu-ri na mama yake anahitaji kukamata hatuwa haraka saana
Katika ma kadi ya afia ya watoto wenye kuwa chini (Mateso na mwenzake), mistari ya njia ya afia yabo ni yenye kuwa mu ma rangi ya manjano ao ya mwekunda na ni ya kushuka. Ile inaonesha ma jamaa yao ka-ma hawaguwi muzuri
Kama mtoto haguwi muzuri, mganga atakupatiya mashauri ginsi mtoto aguwe muzuri
? WAKATI MTOTO WAKO ANAGONJWA AMA ANA MAGONJWA YENYEWE HAUJUWI GIN-SI YA KUITUNZA UTAFANYA NINI?
Omba mashauri kwa waganga, wao wanaweza kukupa madawa ama mashauri kwa kuweza kuboresha afia ya mtoto wako
Waganga wataweza kukueleza chakula bora kwa afia ya mtoto wako Kama mtoto ni mgonjwa saana, inafaa kumupeleka ku nyumba ya matunzo
ya mganga kule atapata mati-babu mazuriGrowth Charts (Picture 6.3)
52
More Activities (Picture 6.4) ─ 5 minutes
53
Kwenye kipimo kuna ma huduma ingine yenyewe waganga wataweza kuwafanyia
Kama inahitajika kumupa mtoto kinga, waganga watamupa kinga Kama inahitajika kumupa mtoto dawa ya kuuwa mitchango, waganga
watamupa Kama mama ni mudja muzito ao kama eko ananyonyesha, waganga
watamupa madawa yenye kufahi Waganga watamueleza kila mama namna mtoto wake eko anaguwa na
kumupa mashauri ginsi ya kuboresha kuguwa kwa mtoto wake Mganga atamweleza mama namna ya kukinga mtoto wake kwa magonjwa
na namna ya kumutunza wakati wa shida fulani
More Activities (Picture 6.4)
54
Our Responsibility (Picture 6.5)
55
Kwa watoto wa chini ya miaka mbili, tuwapeleke ku kipimo kila mwezi Kwa watoto wa miaka mbili hadi tano, tuwapeleke ku kipimo kisha kila
miezi tatu Mama (ao mama) wanasaidiya kukamata kichwa ya mtoto wakati mganga
anamupima urefu, anamu-hakikisha mtoto usalama wake, anasaidiya kukamata mtoto wakati mganga anamupatiya kinga
Ni wakati wenu wakuuuliza mganga kuusu afia ya watoto wenu Ni muzuri kuuliza na kusikiliza madjibu yenye munapewa Kwa kwenda wakati wote na mtoto ku kipimo, wazazi watadjuwa vizuri
ginsi watoto wao weko naguwa kulinganisha na wengine watoto Kama mtoto anaanza uzaifu, mganga atamueleza mama namna ya kufanya
KAZI : KUONESHA GINSI YA KUSAIDIYA MGANGA WAKATI ANAPIMA KILO NA UREFU WA WATOTO
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
56
Our Responsibility (Picture 6.5)
57