ripoti ya kamati ya kuchunguza na kudhibiti hesabu …2. ndg. othman ali haji - katibu 3. ndg. asha...

129
1 RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU ZA SERIKALI NA MASHIRIKA (P.A.C) YA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR, 2014/2015 SEHEMU YA KWANZA 1.0 UTANGULIZI Kufuatia Mhe. Waziri wa iliyokuwa Wizara ya Utumishi wa Umma na Utalawa Bora, Mhe. Haji Omar Kheir, kuwasilisha ripoti mbili za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ambazo ni Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, zote za mwaka 2011/2012 katika kikao cha Bajeti ya mwaka 2013/2014, na kwa kuzingatia kuwa, Kamati ilizifanyia kazi ripoti hizo bila ya kuzimaliza na hatimae ilitoa taarifa yake mwaka jana. Kwa kuzingatia uwasilishwaji mwengine wa ripoti mbili za Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, za mwaka 2012/2013, kupitia kwa Mhe. Waziri, Dr. Mwinyihaji Makame Mwadini wa Wizara ya Nchi, Afisi ya Rais, Ikulu na Utawala Bora, katika Mkutano wa Baraza la Wawakilishi wa mwezi wa Oktoba 2014, Kamati pia ilikabidhiwa ripoti hizo na kutakiwa kuendelea nazo na hatimae, itoe taarifa yake katika Mkutano huu wa Baraza, Machi/Aprili, 2015 kwa ripoti zote nne. 1.1 WAJUMBE NA SEKRETARIETI YA KAMATI Kwa mwaka 2014/2015, Kamati inaundwa na Wajumbe 8 na Sekretarieti kama ifuatavyo: 1. Mhe. Omar Ali Shehe - Mwenyekiti. 2. Mhe. Fatma Mbarouk Said - Makamo Mwenyekiti. 3. Mhe. Mbarouk Wadi Mussa (Mtando) - Mjumbe 4. Mhe. Mwanajuma Faki Mdachi - Mjumbe 5. Mhe. Rufai Said Rufai - Mjumbe 6. Mhe. Salim Abdalla Hamad - Mjumbe 7. Mhe. Salma Mussa Bilali - Mjumbe 8. Mhe. Shamsi Vuai Nahodha - Mjumbe Sekretarieti ya Kamati iliongozwa na Makatibu wa Kamati, Afisa wa Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Maofisa kutoka Wizara ya Fedha kama wafuatao:- 1. Ndg. Nasra Awadh Salmin - Katibu 2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti, Wizara ya Fedha 5. Ndg. Khalid Bakar Hamrani - Afisa Sera, Wizara ya Fedha 6. Ndg. Mfaume Mohamed Mfaume - Afisa wa Afisi ya Mdhibiti 1.2 REJEA ZA KAMATI Kwa mwaka 2013/2014, Kamati ilifuatilia ripoti nne za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambazo ndio rejea za Kamati. Ripoti zenyewe ni hizi zifuatazo:

Upload: others

Post on 25-Sep-2020

2 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

1

RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI

HESABU ZA SERIKALI NA MASHIRIKA (P.A.C) YA BARAZA LA

WAWAKILISHI ZANZIBAR, 2014/2015

SEHEMU YA KWANZA

1.0 UTANGULIZI

Kufuatia Mhe. Waziri wa iliyokuwa Wizara ya Utumishi wa Umma na Utalawa Bora, Mhe.

Haji Omar Kheir, kuwasilisha ripoti mbili za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ambazo ni Ripoti ya

Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar na Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, zote za mwaka 2011/2012 katika kikao cha Bajeti ya mwaka 2013/2014, na kwa

kuzingatia kuwa, Kamati ilizifanyia kazi ripoti hizo bila ya kuzimaliza na hatimae ilitoa

taarifa yake mwaka jana.

Kwa kuzingatia uwasilishwaji mwengine wa ripoti mbili za Ukaguzi wa Hesabu kwa

Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Ripoti ya Ukaguzi

Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, za mwaka 2012/2013,

kupitia kwa Mhe. Waziri, Dr. Mwinyihaji Makame Mwadini wa Wizara ya Nchi, Afisi ya

Rais, Ikulu na Utawala Bora, katika Mkutano wa Baraza la Wawakilishi wa mwezi wa

Oktoba 2014, Kamati pia ilikabidhiwa ripoti hizo na kutakiwa kuendelea nazo na hatimae,

itoe taarifa yake katika Mkutano huu wa Baraza, Machi/Aprili, 2015 kwa ripoti zote nne.

1.1 WAJUMBE NA SEKRETARIETI YA KAMATI

Kwa mwaka 2014/2015, Kamati inaundwa na Wajumbe 8 na Sekretarieti kama ifuatavyo:

1. Mhe. Omar Ali Shehe - Mwenyekiti.

2. Mhe. Fatma Mbarouk Said - Makamo Mwenyekiti.

3. Mhe. Mbarouk Wadi Mussa (Mtando) - Mjumbe

4. Mhe. Mwanajuma Faki Mdachi - Mjumbe

5. Mhe. Rufai Said Rufai - Mjumbe

6. Mhe. Salim Abdalla Hamad - Mjumbe

7. Mhe. Salma Mussa Bilali - Mjumbe

8. Mhe. Shamsi Vuai Nahodha - Mjumbe

Sekretarieti ya Kamati iliongozwa na Makatibu wa Kamati, Afisa wa Afisi ya Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Maofisa kutoka Wizara ya Fedha kama wafuatao:-

1. Ndg. Nasra Awadh Salmin - Katibu

2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu

3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha.

4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti, Wizara ya Fedha

5. Ndg. Khalid Bakar Hamrani - Afisa Sera, Wizara ya Fedha

6. Ndg. Mfaume Mohamed Mfaume - Afisa wa Afisi ya Mdhibiti

1.2 REJEA ZA KAMATI

Kwa mwaka 2013/2014, Kamati ilifuatilia ripoti nne za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa

Hesabu za Serikali ambazo ndio rejea za Kamati. Ripoti zenyewe ni hizi zifuatazo:

Page 2: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

2

Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya

Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 2011/2012.

Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, ya mwaka 2011/2012.

Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya

Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 2012/2013.

Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, ya mwaka 2012/2013.

1.3 UTARATIBU WA KAZI ZA KAMATI

Kamati imefanya kazi kwa utaratibu wa kawaida kama unavyoelekezwa na kanuni ya 108(7)

ya Kanuni za Baraza la Wawakilishi toleo la 2012, juu ya uwezo wa Kamati kujipangia kazi

zake baada ya kushauriana na Spika. Katika kutekeleza majukumu yake, Kamati ilikutana na

Wizara na Taasisi za Serikali zilizohusika na kazi, na hatimae Kamati ilifanya ziara katika

maeneo mbali mbali kushuhudia uhalisia wa maelezo ya Wizara, Taasisi husika ama hoja ya

ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu. Aidha, Kamati kwa kuzingatia haja iliyokuwepo,

ilifanya ziara katika maeneo husika na baadae ilifanya mijadala ya hoja mbali mbali.

1.4 UPEO WA RIPOTI

Pamoja na kuzifanyia kazi ripoti nne za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kama

tulivyoeleza awali, kwa mwaka 2014/2015 na kwa kuzingatiwa kuwa, ripoti nne hizo

zimejumuisha Ukaguzi Maalum wa Viinua Mgongo, Ukaguzi Yakinifu wa Miradi mbali

mbali ya Wizara na Taasisi mbali mbali za Serikali, Ukaguzi Maalum wa Mazingira na

Ukaguzi wa kawaida wa Hesabu za Serikali kwa miaka ya 2011/2012 na 2012/2013. Aidha,

Kamati imeshindwa kuyafanyia kazi maeneo yafuatayo ya ripori hizo:

Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya SMZ,

kwa mwaka 2011/2012

Ukaguzi wa Viinua Mgongo kwa Baadhi ya Taasisi kama zifuatazo (uk-19, Hoja

Namba 14.2)

Wizara ya Kilimo na Maliasili

Kikosi cha Kuzuia Magendo (KMKM)

Kikosi cha Valantia (KVZ)

Kikosi cha Zimamoto na Uokozi

Wizara ya Afya

Wizara ya Fedha

Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Maendeleo ya Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2012/2013

Taarifa ya Ukaguzi wa Mazingira - Pemba

Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya SMZ,

kwa mwaka 2012/2013

Page 3: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

3

WIZARA YA NCHI (OR) TAWALA ZA MIKOA NA IDARA MAALUM ZA SMZ

Jeshi la Kujenga Uchumi

Chuo cha Mafunzo

Kikosi cha KMKM

Kikosi cha Zimamoto na Uokozi

Kikosi cha Valantia

Ofisi ya Kadi za Utambulisho

Mkoa wa Mjini Magharibi

Mkoa wa Kusini Unguja

Mkoa wa Kusini Pemba

Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “A”

Halmashauri ya Wilaya ya Magharibi

Halmashauri ya Wilaya ya Kusini

WIZARA YA NCHI OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS

Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais

Baraza la Wawakilishi

Tume ya Uchaguzi

WIZARA YA NCHI OFISI YA MAKAMO WA KWANZA WA RAIS

Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais

Tume ya UKIMWI

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Wizara ya Katiba na Sheria

Mahkama Kuu

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu

Tume ya Kurekebisha Sheria

WIZARA YA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI

Wizara Ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati

WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI UTALII NA MICHEZO

Wizara ya Habari, Utamaduni Utalii na Michezo

Kamisheni ya Utalii

MASHIRIKA YA UMMA

Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu

Pamoja na taarifa hii kuelezwa katika ripoti hii, Kamati ilimuarifu Mhe. Spika wa Baraza la

Wawakilishi kuhusiana na uwezekano mdogo wa kumalizwa kwa kazi hizo kupitia barua ya

tarehe 04 Febuari, 2015 yenye kumbu kumbu namba BLW/K.10/2 VOL.VII/49 ambayo pia

imenakiliwa kwa Katibu wa Baraza la Wawakilishi, ili kama Afisi ya Baraza la Wawakilishi

itaona ipo haja ya kumalizwa kwa kazi zote hizo ama nusu yake, iongeze muda wa ziada

kwa Kamati ili mapema kabla ya kutoa ripoti yake, kazi hizo ziweze kufanywa na taarifa

yake iweze kupatikana pamoja na taarifa hii. Hata hivyo, hadi tunaandika taarifa hii,

hakukuwa na majibu yoyote ya barua hiyo wala hakukuwa na muda wowote ulioengezwa,

pamoja na makubaliano ya Baraza hili kwa Kamati ya P.A.C kuongezewa muda wa kazi.

Page 4: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

4

1.5 MUUNDO WA RIPOTI

Ripoti hii ina sehemu tatu, Utangulizi, Maudhui na Hitimisho. Utangulizi umejumuisha

Utangulizi, Wajumbe wa Kamati na Sekretarieti, Rejea za Kamati, Utaratibu wa Kazi za

Kamati, Upeo na Muundo wa ripoti. Maudhui ya Ripoti yamejumuisha; Ripoti ya Ukaguzi

wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya

mwaka 2011/2012; Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya

Mapinduzi ya Zanzibar, ya mwaka 2011/2012; Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara,

Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 2012/2013 na Ripoti

ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ya

mwaka 2012/2013.

Katika kila ripoti tulizozitaja hapo juu, zimegusia mambo manne ambayo ni Hoja ya

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kama maudhui yake yalivyoripotiwa katika ripoti

tulizozitaja hapo juu, Majibu ya Wizara au Taasisi husika, Uchunguzi wa Kamati na mwisho

ni Mapendekezo ya Kamati.

Isipokuwa, katika ufafanuzi wa hoja za Ukaguzi Maalum wa Viinua Mgongo, mapendekezo

ya Kamati yamejumuishwa kwa hoja zote.

SEHEMU YA PILI

MAUDHUI YA RIPOTI

UFAFANUZI WA HOJA MBALI MBALI ZILIZOFANYIWA

KAZI NA KAMATI

RIPOTI YA UKAGUZI WA HESABU KWA MAWIZARA, MASHIRIKA NA

TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012

2.0 UKAGUZI MAALUM WA VIINUA MGONGO

Ukaguzi huu ulifanyika kwa miaka miwili, baina ya mwaka 2010 hadi Machi 2012, kwa

kupitia baadhi ya majalada na kubainika kasoro mbali mbali zikiwemo; kuongezwa kwa

muda wa utumishi wa mstaafu, kuongezwa mshahara wa mwisho ambao hutumiwa

kutayarisha malipo ya viinua mgongo na mstaafu kulipwa mara mbili kinyume na utaratibu.

Ukaguzi umebaini kuwa, kasoro hizi zimejitokeza zaidi katika Wizara ya Miundombinu na

Mawasiliano mara tu yalipofanywa mabadiliko ya mshahara mwezi wa Oktoba 2011. Aidha,

kasoro nyengine zimeonekana katika Chuo cha Mafunzo, Mkoa wa Mjini Magharibi, Wizara

ya Kilimo na Maliasili, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Kikosi Maalum cha Kuzuia

Magendo, Kikosi cha Valantia, Kikosi cha Zimamoto na Uokozi na Jeshi la Kujenga

Uchumi.

Kwa upande wa kuifanyia kazi hoja hii, Kamati ilianza mahojiano yake tokea mwaka

2013/2014 ilipokutana na Ofisi ya Mkoa wa Mjini Magharibi kwa hoja mbali mbali

zilizotokana na ripoti ya ukaguzi, na kuelezwa kuwa, hoja hii ingepaswa zaidi kufanywa kwa

kukutana na Wizara ya Fedha na taasisi mbali mbali zilizohusika. Hivyo, katika mwaka huu,

Kamati iliifanyia kazi hoja hii katika ratiba ya awali kwa kuipangia Wizara ya Fedha, lakini

kabla ya kazi, ilifanya kikao na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ambapo

Kamati ilipatiwa ufafanuzi pamoja na Mkuu wa Utawala wa Afisi ya Baraza la Wawakilishi

Page 5: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

5

na kubainika kuwa, hoja ingestahiki kufanyiwa kazi kwa Taasisi zilizohusika, ambapo

wakati huo Kamati ilifanya marekebisho ya ratiba na kutokana na uchache wa muda, Kamati

haikuweza kukutana na kila taasisi zilizotajwa katika ripoti, isipokuwa imefanikiwa

kukutana na taasisi zote muhimu zilizotajwa zaidi katika hoja hizo ambazo ni hizi zifuatazo:

2.1 CHUO CHA MAFUNZO

Hoja Namba 14.2 Ukaguzi Maalum kupitia mafaili 8 yaliyohusika na ukaguzi

Ukaguzi uliyapitia mafaili manane ya Chuo na kubaini kasoro za kuongezwa kwa muda wa

utumishi wa mstaafu, kuongezwa mshahara wa mwisho ambao hutumiwa kutayarisha malipo

ya viinua mgongo na mstaafu kulipwa mara mbili kinyume na utaratibu.

Majibu ya Chuo

Kwa bahati mafaili hayo hayakutaja wafanyakazi halisi waliohusika na ukaguzi, na hivyo

inakua tabu kuyatambua moja kwa moja. Waliomba Kamati iwapatie muda wa ziada

kuyatafuta na kuyatambua mafaili hayo na walileta taarifa za wastaafu 47 kwa mwaka

2010/2011.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imekubaliana na Chuo kuwa, hoja hii haikutaja wastaafu waliohusika na ukaguzi

moja kwa moja na hivyo inakuwa tabu kuwatambua wastaafu wanaotakiwa, pamoja na

ukweli kwamba, Chuo kilikabidhi kwa Kamati idadi kubwa zaidi ya wastaafu 47, badala ya

wastaafu 8 kama walivyoripotiwa. Aidha, Kamati kabla ya kukutana na Chuo kuhusiana na

hoja hii ilimtaka Afisa Mkaguzi anaefuatana na Kamati kufuatilia majina ya wastaafu hao

katika Afisi yake ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu, lakini alishindwa kupata majina

hayo na hivyo Kamati haikuwa na uhakika wa wastaafu waliohusika isipokuwa kwa

kutegemea majibu sahihi ya Taasisi husika.

Hoja Namba 14.2.1 Kuongezeka kwa malipo ya viinua mgongo, Tsh. 35,899,595

Ukaguzi umebaini kuwepo wastaafu watatu wa chuo walioongezewa mishahara yao kinyume

na taratibu, kwa lengo la kupata viinua mgongo vikubwa ambavyo hawastahiki kulipwa

kulingana na mishahara yao halisi. Wastaafu hao ni Ndg. Jaffar Silima Jaffar, Ndg. Abdu

Makame Vuai na Ndg. Rahma Mgeni Mzee.

Majibu ya Chuo

Chuo kinakubali kuwa na wastaafu wawili tu na sio watatu kama walivyoripotiwa. Ndg.

Jaffar Silima Jaffar na Ndg. Abdu ndio wastaafu halali, lakini Ndg. Rahma Mgeni Mzee, sio

mfanyakazi wao na hawakuwa na taarufa zozote za utumishi wake. Kuhusiana na wastaafu

hao wawili, Chuo kililazimika kuwastaafisha kutokana na maradhi na baada ya kupata

ushauri wa bodi ya madaktari kwa kutoweza kwao kuendelea na kazi.

Walipostaafu waliwalipa viinua vyao mgongo kwa kuzingatia mshahara halali na halisi wa

mwisho wa mwezi, na sio kweli kwamba Chuo kimewazidishia, lakini ni Afisi ya Mdhibiti

na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ndio iliyofanya hivyo na yenye dhamana ya kujibu suala hilo,

kwani viinua mgongo vyote vilipitiwa na Afisi hii na kuhakikiwa.

Kwa mfano, mshahara uliofanyiwa malipo kwa Ndg. Jaffar ni Tsh. 63,200 na Ndg. Abdu

Makame amefanyiwa kiinua mgongo kwa mshahara halali wa mwezi ambao ni Tsh. 61,400

na sio vyenginevyo.

Page 6: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

6

Aidha, Chuo kilikataa kuwalipa viinua mgongo wastaafu hao, na baada ya wao kulalamika

kwa barua, Chuo kilimuandikia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kuomba muongozo

wao, lakini kwa bahati hadi wanaripoti kwa Kamati, hawakujibiwa barua zao.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha na maelezo ya Chuo kuwa Ndg. Rahma Mgeni Mzee sio mfanyakazi

wao baada ya kupata taarifa za hakika kutoka kwa Afisa wa Wizara ya Fedha anaefuatana na

Kamati kuwa ni mstaafu wa Wizara ya Afya, na namba yake ya ajira ilikuwa 7105481 na

tarehe 22/3/2012 ndipo Mdhibiti alitoa barua ya mafao yake ya kiinua mgongo aliyolipwa ni

Tsh. 11,024,000/-.

Kuhusiana na taarifa za Ndg. Jaffar na Ndg. Abdu, Kamati ilipoangalia fomu za malipo

zilizotayarishwa na Chuo, ilijiridhisha kuwa, malipo halali waliyoombewa wastaafu hayo ni

mishahara yao ya mwisho kama walivyoeleza Chuo, kuwa Ndg. Jaffar ni Tsh. 63,200 na

Ndg. Abdu Tsh. 61,400, lakini kwa kuzingatia taarifa zao za mishahara (Service Record)

zinaonesha kuwa mshahara wa mwisho wa Ndg. Jaffar ulikuwa Tsh. 93,000/-(badala ya Tsh.

63,200/-) na Ndg. Abdu ni Tsh. 103,000/- (badala ya Tsh. 61,400/-).

Hata hivyo, suala hili halikuweza kuthibitishwa zaidi kwa Kamati kushindwa kupata fomu

kamili zilizotoka Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu na hata barua za

kuthibitisha malipo ya wastaafu hao. Aidha, kwa kuzingatia maelezo ya Afisi ya Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu katika kikao cha pamoja cha kupata uelewa wa hoja hii kuwa

Afisi ya Mdhibiti tayari ilipogundua mapungufu ya baadhi ya watendaji wake ilichukua

hatua na hivyo, hawana lolote la kusema ama kushirikishwa katika suala hili na kwa kuwa

Kamati ilikosa mashirikiano ya moja kwa moja kwa ufafanuzi kamili wa hoja hii, Kamati

pamoja na uchache wa muda, haikuweza kufuatilia kwa kina suala hili.

Hoja Namba 14.2.2 Wastaafu kulipwa mafao mara mbili, kinyume na utaratibu.

Ukaguzi umebaini kuwepo kwa tatizo la mstaafu, Ndg. Abdu Vuai Makame kulipwa kiinua

mgongo mara mbili kinyume na utaratibu. Mkataba wake wa ajira unaonesha ameanza kazi

tarehe 18/4/1994 na kumaliza tarehe 9/4/2002. Barua ya tarehe 24/7/2008 kutoka kwa

Kamishna wa Chuo inathibitisha kulipwa kiinua mgongo mara mbili baada ya kukatishwa

mkataba wa kazi ingawa alikuwa akidai malipo ya pencheni tu.

Aidha, barua ya tarehe 12/10/2006 kuliyotoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara wa Nchi (OR)

Tawala za Mikoa na Vikosi vya SMZ kwenda kwa msaafu na barua ya tarehe 01/08/2008

kutoka kwa Kamishna wa Chuo cha Mafunzo kwenda kwa mstaafu zote zinaeleza wazi

kuwa mstaafu alikuwa hastahiki kupata pencheni kutokana na muda wake wa utumishi.

Katika hatua nyengine ukaguzi umebaini kwamba, mstaafu huyo aliombewa malipo ya

kiinua mgongo kutoka Chuo cha Mafunzo kupitia barua ya tarehe 8/03/2012 yenye kumbu

kumbu namba MF/G.2/Vol.VI/2012 na analipwa kiinua mgongo kwa mara ya pili kupitia

hundi namba 112416 yenye thamani ya Tsh. 8,065,200

Majibu ya Chuo

Chuo kimemlipa kiinua mgongo mara moja tu kwa mshahara wa Tsh. 61,400 na hakijawahi

kulipa pencheni kwa mstaafu huyo, zaidi ya kupokea malalamiko yake ya kulipwa pencheni

ambapo Chuo iliyakataa na mwishowe kuomba muongozo wa kisheria na kihatua kutoka

Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ambapo hawajawahi kujibiwa barua yao.

Aidha, Mkaguzi aliegemeza hoja zake kwa kuangalia barua tu bila ya kufanya mahojiano ya

kina na kupatiwa ufafanuzi sahihi wa hoja hizo.

Page 7: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

7

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imepitia barua hizo zilizonukuliwa na hoja ya ukaguzi lakini haijajiridhisha kwamba,

Chuo cha Mafunzo kimelipa mara mbili kiinua mgongo cha Ndg. Abdu Vuai Makame.

Aidha, Kamati imejiridhisha kwamba, Chuo kiliomba ufafanuzi wa haki ya mstaafu huyo

kulipwa pencheni, lakini hakukuwa na majibu kutoka Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

wa Hesabu.

2.2 AFISI YA MKOA WA MJINI MAGHARIBI

Hoja Namba 14.2 Ukaguzi Maalum kupitia mafaili 5 yaliyohusika na ukaguzi

Katika Afisi ya Mkoa wa Mjini Magharibi, ukaguzi umeyapitia mafaili matano na kubaini

kasoro za kuongezwa kwa muda wa utumishi wa mstaafu, kuongezwa mshahara wa mwisho

ambao hutumiwa kutayarisha malipo ya viinua mgongo na mstaafu kulipwa mara mbili

kinyume na utaratibu.

Majibu ya Afisi ya Mkoa

Mafaili matano yaliyohusika na ukaguzi ni ya Ndg. Pili Salum Said, Ndg. Rehema Mwinyi

Zubeir, Ndg. Idrisa Iddi Siwamoja, Ndg. Salum Haji Haji na Ndg. Nassir Ali Kombo.

Watumishi wote hao wamekaguliwa lakini kasoro zilizoelezwa zilipatikana kwa mtumishi

mmoja tu, Ndg. Pili Salum Said, ambapo kwa upande wa Afisi, haukubaliani na hoja za

ukaguzi.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, kasoro zilizoelezwa na ukaguzi zinamhusu Ndg. Pili, ambapo

hoja yake itafafanuliwa katika hoja inayofuata baadae. Kuhusiana na wastaafu wanne

waliobakia, Kamati imekagua mafaili yao na kujiridhisha kuwa hayakuwa na tatizo.

Hoja Namba 14.2.2 Wastaafu kulipwa mafao mara mbili, kinyume na utaratibu

Ukaguzi umebaini kuwepo kwa kasoro ya mstaafu, Ndg. Pili Salum Saidi kulipwa kiinua

mgongo mara mbili kinyume na utaratibu. Aidha, kwa mujibu wa Mkataba wake wa kuingia

kazini, ameanza kazi tarehe 02/08/1999 na kumaliza utumishi wake tarehe 2/12/2011.

Kutokana na utaratibu wa ulipaji wa kiinua mgongo, wastaafu walioajiriwa baada ya mwezi

wa sita mwaka 1998, walitakiwa kulipwa na kupokelea mafao yao ya uzeeni katika Mfuko

wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) na sio Hazina. Hata hivyo, ukaguzi umebaini kwamba

Ndg. Pili alilipwa kiinua mgongo ZSSF kwa hundi namba 100144 yenye thamani ya Tsh.

3,137,391 na pia amelipwa Hazina kwa hundi namba 048665 yenye thamani ya Tsh.

8,210,400 ambapo hakustahiki kulipwa.

Majibu ya Ofisi ya Mkoa

Ofisi haina uhakika wa suala hilo lakini inawezekana limefanyika au halikufanyika kwani

alipostaafu Ndg. Pili Ofisi ilitakiwa na ilitayarisha fomu za kiinua mgongo kwa utaratibu

uliowekwa na kuziwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kwa ajili ya

kufanyiwa uchunguzi wa kisheria kama taratibu zilivyo.

Fomu ya kiinua mgongo kwa Ndg. Pili iliyotayarishwa na Ofisi ya Mkoa inaonesha malipo

ya Tsh. 2,906,107.60/- kwa mujibu wa „formula‟ iliyotumika baada ya masahihisho ya

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu imeonekana imekosewa na usahihi wake ukafanywa

na Mkaguzi kuwa Tsh. 3,907,200, ambapo Ofisi hii haikuwa na pingamizi dhidi ya

masahihisho hayo na ndiyo yaliyolipwa. Ofisi inashauri Kamati ifuatilie suala hili kwa

Page 8: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

8

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, kwa kuwa ndie aliehusika na nyongeza hiyo na

anajua usahihi wake. Pia Kamati ifuatile Wizara ya Fedha au Mfuko wa ZSSF.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imepitia faili la mstaafu huyu na kujiridhisha kuwa mshahara wake wa mwisho

ulikuwa Tsh. 132,000/- na ndio uliofanyiwa hesabu za kiinua mgongo chake na Ofisi ya

Mkoa. Pia, Ndg. Pili alizaliwa tarehe 2/12/1951 na ameajiriwa tarehe 9/7/1999 na kustaafu

kwa miaka 60, tarehe 2/12/2011, hivyo hakukuwa na muda wa ziada ya malipo yake.

Hata hivyo, kasoro kubwa iliyobainika na Kamati ni mstaafu huyo kufanyiwa hesabu ya

miezi 148 na sio 144 ambapo Afisa Utumishi alikiri mbele ya Kamati kukosea hesabu hizo,

ingawa anashangazwa na Ofisi ya Mdhibiti kukubali ziada ya miezi hiyo, na kuidhinisha

malipo zaidi. Vile vile, Kamati haikupata uthibitisho wa fomu ya malipo au barua kutoka

Afisi ya Mdhibiti inayoonesha kima halisi na fomula iliyotumika kumlipa mstaafu huyu, na

Kamati imejiridhisha kuwa, udhaifu ulioonekana katika hoja hii, Afisi ya Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu inahusika kwa namna moja ama nyengine.

2.3 JESHI LA KUJENGA UCHUMI (J.K.U)

Hoja Namba 14.2 Ukaguzi Maalum kupitia mafaili 8 yaliyohusika na ukaguzi

Ukaguzi uliyapitia mafaili manane ya J.K.U na kubaini kasoro za kuongezwa kwa muda wa

utumishi wa mstaafu, kuongezwa mshahara wa mwisho ambao hutumiwa kutayarisha malipo

ya viinua mgongo na mstaafu kulipwa mara mbili kinyume na utaratibu.

Majibu ya J.K.U

Ni kweli majalada yaliyohusika na ukaguzi yalikuwa manne, lakini ni majalada matatu

ambayo yalionekana na kasoro zilizohusika na hoja. Mafaili hayo ni ya wastaafu, Ndg.

Abdalla Moh‟d Khamis, Ndg. Kombo Adeeti Othman na Ndg. Zakia Abdalla Sleiman na

Uongozi wa J.K.U haukubaliani kuhusika na hoja za ukaguzi.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeyapitia mafaili yote manane yaliyohusika na hoja hii na kujiridhisha kuwa, ni

mafaili ya wastaafu watatu ndio yaliyohusika na hoja.

Hoja Namba 14.2.1 Kuongezeka kwa malipo ya viinua mgongo, Tsh. 35,899,595

Ukaguzi umebaini kuwepo wastaafu watatu wa J.K.U walioongezewa mishahara yao

kinyume na taratibu kwa lengo la kupata viinua mgongo vikubwa ambavyo hawastahiki

kulipwa kulingana na mishahara yao halisi. Wastaafu hao ni Ndg. Abdalla Moh‟d Khamis,

Ndg. Ndg. Kombo Adeeti Othman na Ndg. Zakia Abdalla Sleiman.

Majibu ya J.K.U

J.K.U hawakubalini kuhusika na hoja hiyo na badala yake anaehusika ni Afisi ya Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu. Kwa mfano, mstaafu Ndg. Abdalla Moh‟d Khamis, fomu

iliyotayarishwa ya kiinua mgongo chake na J.K.U inaonesha alistahiki kulipwa kiinua

mgongo cha Tsh. 20,013,600 lakini baada ya kuiwasilisha faili la mstaafu huyo kwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ndipo walipoelekezwa kwamba, mstaafu anatakiwa

alipwe Tsh. 21,627,600 kama inavyothibitika katika barua ya tarehe 06/02/2012 yenye

kumbu kumbu namba AUD/G.18/2/WF/VOL.XIV/41.

Page 9: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

9

Mstaafu, Ndg. Kombo Adeeti Othman fomu ya kiinua mgongo iliyotayarishwa na JKU kuwa

cha Tsh. 30,727,200 lakini baada ya kuiwasilisha faili la mstaafu huyo kwa Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ndipo walipoelekezwa kulipa Tsh. 32,792,200 kama

inavyothibitika katika barua ya tarehe 06/02/2012 yenye kumbu kumbu namba

AUD/G.18/2/WF/VOL.XIV/41.

Vile vile kwa mstaafu Ndg. Zakia Abdalla Sleiman, inathibitishwa kupitia fomu ya kiinua

mgongo iliyotayarishwa na J.K.U kuwa alistahiki kulipwa Tsh. 11,625,600 lakini baada ya

kuiwasilisha faili la mstaafu huyo kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ndipo

walipoelekezwa kwamba, mstaafu anatakiwa alipwe Tsh. 13,238,400 kama inavyothibitika

katika barua ya tarehe 06/02/2012 yenye kumbu kumbu namba

AUD/G.18/2/WF/VOL.XIV/41.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imepitia mafaili ya wastaafu hao pamoja na fomu zao za malipo ya viinua mgongo

vilivyotayarishwa na J.K.U na kuzipitia barua zilizotoka Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi

Mkuu wa Hesabu kama zilivyonukuliwa hapo juu na kujiridhisha usahihi wa maelezo ya

J.K.U. Hata hivyo, Kamati imehitaji uthibitisho wa malipo ya wastaafu hawa kwa mujibu wa

hesabu zilizotoka Afisi ya Mkaguzi Mkuu, lakini haikuweza kupatiwa. Aidha, J.K.U

wameshindwa kuwasilisha mbele ya Kamati fomu za malipo zilizotayarishwa na Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, kwa kueleza kuwa hawakuwahi kupewa, ingawa ni haki na

kitaratibu kupewa fomu hizo.

2.4 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI

Hoja Namba 14.2 Ukaguzi Maalum kupitia mafaili 22 yaliyohusika na ukaguzi.

Ukaguzi uliyapitia mafaili 22 ya Wizara na kubaini kasoro za kuongezwa kwa muda wa

utumishi wa mstaafu, kuongezwa mshahara wa mwisho ambao hutumiwa kutayarisha malipo

ya viinua mgongo na mstaafu kulipwa mara mbili kinyume na utaratibu.

Majibu ya Wizara

Kati ya majalada 22 yaliyofanyiwa ukaguzi, Wizara imefanikiwa kuyapata 18, lakini kwa

bahati hakukuwa na kasoro yoyote iliyoelezwa katika ripoti ya ukaguzi. Kwa mfano mstaafu

Ndg. Batuli Masoud, Ndg. Safia Ali na Ndg. Moh‟d Ali walirekebishiwa mishahara yao kwa

toleo la Serikali namba OR/UUU/M.140/1/VOL.I/58 la tarehe 17 Oktoba 2011, likitoka kwa

Katibu Mkuu (OR) Utumishi wa Umma Zanzibar. Ndg. Safia alilipwa kwa mshahara wa

Tsh. 231,000/- kwenye vocha ya mshahara wa mwisho, wakati kweye „salary register folio‟

kwa bahati mbaya umerekodiwa Tsh. 230,000/-

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imetaka uthibitisho wa toleo hilo na kupatiwa, ambalo linahusu marekebisho ya

mishahara. Kuhusiana na mstaafu Ndg. Safia Ali, Kamati imejiridhisha kuwa kalipwa kwa

mshahara wa Tsh. 230,000/- badala ya Tsh. 231,000/ ambazo ndizo mshahara halisi

aliostahiki kulipwa, na Kamati ikaridhika na maelezo kuwa Wizara ilikosea kumfanyia

hesabu, lakini tayari malalamiko yake yameshafikishwa sehemu inayohusika na yanafanyiwa

kazi.

Ndg. Batuli Masoud Juma kwa mujibu wa „salary register‟ alilipwa kwa mshahara wa Tsh.

254,000/- badala ya Tsh. 106,426 kama ilivyoelezwa na Wizara na kwa bahati Wizara

imekiri usahihi huo.

Page 10: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

10

Aidha, Ndg. Moh‟d Ali Abdalla alilipwa kwa Tsh. 229,000/- tofauti na ilivyoelezwa na

Wizara kuwa kalipwa kwa Tsh. 377,000/. Hata hivyo, ili kujiridhisha na usahihi wa

kiwango gani hasa kimelipwa kwa mishahara ya wastaafu hao, Kamati imeitaka Wizara

kuwasilisha kwa Kamati, fomu za viinua mgongo kutoka kwao kwenda kwa Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ama kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kwenda kwa

Wizara, ambapo fomu hizo nazo zilithibitisha malipo ya wastaafu hao kama tulivyoeleza

hapo juu.

2.5 WIZARA YA MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Hoja Namba 14.2 Ukaguzi Maalum kupitia mafaili 22 yaliyohusika na ukaguzi.

Ukaguzi uliyapitia mafaili 69 ya Wizara na kubaini kasoro za kuongezwa kwa muda wa

utumishi wa mstaafu, kuongezwa mshahara wa mwisho ambao hutumiwa kutayarisha malipo

ya viinua mgongo na mstaafu kulipwa mara mbili kinyume na utaratibu.

Majibu ya Wizara

Wizara katika kipindi cha Disemba 2011 na Febuari 2012, ilistaafisha kisheria baada ya

kutimia muda wao kustaafu kwa wafanyakazi wake 16 kwa upande wa Unguja na Pemba 37.

Kati ya wafanyakazi hao 53 waliotengenezewa mafao yao, ilibainika wafanyakazi 12

walitengenezewa mafao yao kwa makosa. Baada ya kugundua hilo, Watendaji wa Wizara

walifuatilia suala hilo kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, kutaka kujua

ukweli wa suala hilo walipowasiliana na watendaji wa Afisi ya Mdhibiti, waligundua kuwa

kosa hilo limefanyika kweli na wafanyakazi wawili kati ya hao 12 walikuwa wameshapokea

malipo hayo na waliwataka warejeshe fedha hizo kwa haraka.

Pamoja na kuwa watendaji wa Wizara ndio waliogundua kasoro hizo, watendaji wa Afisi ya

Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu walimuandikia barua Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais,

Utumishi wa Umma na Utawala Bora kumjuulisha juu ya suala hilo ambae nae alichukua

hatua za kuiandikia Wizara yao.

Wizara ilichukua hatua za kuwasimamisha kazi wafanyakazi wanne, mmoja wa Makao

Makuu na wengine watatu wa Ofisi Kuu Pemba. Aidha, Wizara iliunda Kamati Maalum ya

kuchunguza suala hilo na kutoa mapendekezo kwa uongozi wa Wizara ambao uliyafanyia

kazi mapendekezo hayo. Hivyo, wafanyakazi waliobainika kushiriki katika suala hili,

walichukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa makosa waliyoyafanya kama Sheria ya

Utumishi wa Umma ya mwaka 2011 inavyoelekeza.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha juu ya usahihi wa taarifa za Wizara kuwa chanzo halisi cha

udanganyifu uliofanyika kupitia viinua mgongo ni Ndg. Mgeni Ramadhan Suwed, mmoja

kati ya wastaafu katika mwaka uliofanyiwa ukaguzi. Ndg. Mgeni alistahiki kupokea kiinua

mgongo cha Tsh. 10,708,800 lakini wakati anakwenda kupokea kiinua chake mgongo

alitakiwa kulipwa Tsh. 21,964,800, na aliyesimamia malipo hayo ni Afisa Utumishi

aliyekuwepo wakati huo Ndg. Ali Hassan.

Dg. Mgeni kwa uchamunu wake na uaminifu aliokuwa nao, alieleza kuwa hastahiki fedha

hizo, lakini alinasihiwa sana na Ndg. Ali achukue kwani mgao huo (wa ziada ya kiinua

mgongo halali) pia unalipwa (kinyume na taratibu) kwa Mkurugenzi wa masuala ya

Utumishi, Ndg. Rajab Uweje. Hali hii ilimpelekea Ndg. Mgeni kufika kwa Mkurugenzi

Uweje na kumueleza hali ilivyo, lakini kwa bahati Ndg. Uweje akamhakikishia kuwa yeye

Page 11: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

11

hayumo katika udanganyifu huo na hana mgao wowote, na ndipo alipoanza kulifikisha suala

hilo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na hatimae suala hilo likafuatiliwa kama

ilivyoelezwa na Wizara.

Kamati pia imejiridhisha kuwa, suala hili lilifanywa zaidi na Afisa huyo Utumishi wa Wizara

ya Miundombinu na Mawasiliano, lakini kwa mashirikiano ya karibu na kuhusika kwa

baadhi ya Maofisa wa Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu pamoja na baadhi ya

Maofisa wa Wizara ya Fedha.

Hoja Namba 14.2.1 Kuongezeka kwa malipo ya viinua mgongo, Tsh. 35,899,595

Ukaguzi umebaini kuwepo wastaafu watano wa Wizara, waliongezewa mishahara yao

kiyume na taratibu kwa lengo la kupata viinua mgongo vikubwa ambavyo hawastahiki

kulipwa kulingana na mishahara yao halisi. Wastaafu wenyewe ni hawa wafuatao:

Nam Jina Malipo ya

awali

yaliyopangwa

kulipwa

Malipo

yaliyostahiki

kulipwa

Tofauti

1. Mgeni Ramadhan

Suwed

21,964,800 10,708,800 11,256,000

2. Moh‟d Ismail Moh‟d 20,428,800 10,188,800 10,240,000

3. Ibrahim Elius Kilundira 725,578 248,769.60 476,808

4. Khamis Ali Kombo 5,224,892.40 4,979,277 245,615

5. Ali Haji Mcha 5,046,263.60 4,912,292 133,972

Majibu ya Wizara

Wizara inakiri juu ya ukweli wa hoja hii na wao waliwahi kuwalipa Ndg. Mgeni na Ndg.

Moh‟d Ismail, lakini baada ya kugundua mwenyewe na kwa khiari yake, Ndg. Mgeni

alizirejesha fedha hizo na kwa hivyo, alilipwa fedha alizostahiki na fedha za ziada alizolipwa

Tsh. 11,256,000/- zilirejeshwa Wizara y Fedha kwenye akaunti namba 9928161504.

Ndg. Moh‟d Ismail alilipwa Tsh. 20,428,800 kwa makosa, wakati anastahiki kulipwa Tsh.

10,240,000/. Hatua ambazo Wizara ilizichukua baada ya kugundua ilimwita na kumtaka

arejeshe fedha za ziada alizolipwa kwa makosa. Kwa bahati alikuwa tayari ameshazitumia

zote na Wizara ilimtaka azirejeshe fedha hizo na Ndg. Moh‟d aliahidi kuzirejesha mara tu

atakapozipata. Kwa hivi sasa mhusika amesimamishwa kulipwa pencheni ya kila mwezi

kufidia deni hilo.

Aidha, wastaafu waliobakia wote walilipwa viinua vyao mgongo sahihi wala hakukuwa na

udanganyifu wowote uliotokea, baada ya kufanyiwa uhakiki hesabu za awali ambazo kweli

hapo mwazo zilikosewa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeridhishwa na majibu ya Wizara kuhusiana na ukweli wa hoja hii. Na

imejiridhisha kuwa, kasoro zilizojitokeza zilichangiwa na kusababishwa na Afisi ya Mdhibiti

na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Wizara ya Fedha.

Page 12: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

12

Hoja Namba 14.2.3 Malipo ya Viinua Mgongo yaliyobainika kuwa na udanganyifu

ambayo hayakuwahi kulipwa, Tsh. 48,570,917

Fedha hizo ni ziada ya fedha ambazo zilitarajiwa zilipwe kwa wastaafu mbali mbali, lakini

kutokana na kasoro iliyobainika ya kuongezwa muda wa utumishi wa wastaafu hao, fedha

hizo hazijawahi kulipwa.

Nam Jina Malipo ya

awali

yaliyopangwa

kulipwa

Malipo

yaliyostahiki

kulipwa

Tofauti

1. Fasihi Mtumweni Ali 12,000,000 7,000,000 5,000,000

2. Bogo Isabu Khamis 12,304,000 6,592,600 5,712,000

3. Jongo Juma Mtwana 12,672,000 7,392,000 5,280,000

4. Mzee Khamis Mzee 11,857,200 5,492,833 6,364,367

5. Simai Makame Pandu 11,785,600 6,705,600 5,080,000

6. Kassim Haji Ameir 19,401,200 10,389,400 9,011,800

7. Fatma Rashid Said 12,000,000 7,336,000 6,136,000

8. Hamad Saleh Hamad 12,240,000 7,140,000 5,100,000

9. Ramadhan Khatib Ali 2,678,250 319,500 2,358,750

JUMLA KUU 106,938,850 58,367,933 48,570,917

Majibu ya Wizara

Kama walivyoeleza awali kuwa, wastaafu hao hawakuwahi kulipwa kwa udanganyifu

kutokana na juhudi za Wizara yenyewe baada ya kugundua kupitia kwa Mstaafu mwaminifu,

Ndg. Mgeni na kulifanyia kazi suala hili ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za

kinidhamu waliohusika.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeridhishwa na usahihi wa maelezo ya Wizara ispokuwa imehoji juu ya Wizara

kutowachukulia hatua za kijinai watendaji wake waliohusika, wakati suala hili sio tu la

kuchukuliwa kwa hatua za kinidhamu wakati kosa lililofanyika linahusika na wizi na

kuvunja uaminifu.

Mapendekezo ya Kamati (kwa hoja zote zinazohusiana na Ukaguzi wa Kiinua

Mgongo)

Ni kweli Kamati imejiridhisha kuwepo kwa udanganyifu uliotajwa katika ripoti ya Mkaguzi

kuhusiana na suala zima la Viinua Mgongo na udanganyifu huo ulitokea baina ya Maofisa

Utumishi wa Taasisi husika kwa mashirikiano na Maofisa wa Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi

Mkuu wa Hesabu za Serikali na Wizara ya Fedha. Hivyo, Kamati inapendekeza ifuatavyo:

Wale wote waliohusika na udanganyifu huo wachukuliwe hatua za kinidhamu na

kisheria.

Serikali iimarishe „database‟ ya wafanyakazi, ili iwe rahisi kuzipata taarifa za

wafanyakazi wote.

Serikali iunde Kamati Maalum ya kufuatilia hatua sahihi zilizochukuliwa na Afisi ya

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano

dhidi ya watendaji wao waliohusika na udanganyifu huo na ambao tayari

walikwishachukuliwa hatua kabla ya ukaguzi wa Kamati ya P.A.C.

Page 13: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

13

Kamati inamshauri Mdhibiti kuweka wazi taarifa za hoja anazoziripoti, ili ziwe ni

taarifa za wazi na kujitosheleza na kuiwezesha Kamati kuzifuatilia hoja hizo kwa

urahisi.

3.0 UKAGUZI WA HESABU WA MAWIZARA NA TAASISI ZA SERIKALI

KWA MWAKA 2011/2012

3.1 WIZARA YA FEDHA

Hoja Namba 15.1 Matokeo ya Hesabu za mwisho wa mwaka.

Taarifa za mapato na matumizi.

Wizara ya Fedha iliidhinishiwa kukusanya Tsh. 248,260,661,000 kwa mwaka 2011/2012.

Hadi kufikia Juni 2012, mapato yaliyokusanywa yalikuwa Tsh. 286,962,675,000.44 ambayo

ni sawa na asilimia 115 ya makadirio.

Kwa upande wa matumizi ya kawaida, fedha zilizoainishwa ni Tsh. 47,020,000,000/- na

fedha halisi zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 33,912,500,000/- ikiwa ni pungufu ya Tsh.

13,107,500,000 sawa na asilimia 27.9 ya makadirio. Aidha, matumizi ya maendeleo, Wizara

iliidhinishiwa kutumia Tsh. 7,240,000,000/-, lakini mwisho wa mwaka ulipofika, fedha

zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 6,144,663,000, sawa na asilimia 85 ya makadirio.

Majibu ya Wizara

Taarifa za makisio ya makusanyo ni sahihi, isipokuwa taarifa ya fedha zilizopatikana

hazikuwa Tsh. 286,962,675,000.44 na usahihi ni Tsh. 240,339,913,699.44. Kufanikiwa

kuongeza makusanyo kunatokana na kupata baadhi ya mapato ambapo vyanzo vyake

havikukadiriwa kukusanywa katika upangaji wa bajeti.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji sababu zinazopelekea Wizara hii kuvuka lengo la makusanyo wakati Wizara

nyengine na taasisi za Serikali hazifikii, wakati kwa kiasi kikubwa makisio yao ya

makusanyo yanaongozwa na Wizara hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuwa na vigezo sahihi vya makusanyo ya mapato, ili Taasisi zote

ziwe na rikodi nzuri za kiwango cha mafanikio ya makusanyo halisi.

Hoja Namba 15.4 Malipo yasiyokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu), Tsh.

295,977,000

Fedha hizo zimelipwa kwa matumizi mbali mbali lakini vielelezo husika havikupatikana kwa

ukaguzi, na hivyo, uhalali wa malipo hayo haukuweza kuthibitishwa.

Majibu ya Wizara

Ni kweli wakati wa ukaguzi vielelezo hivyo havikuwepo kutokana na matumizi husika

yanayohusu safari za viongozi kuwa na taratibu tofauti na safari za kawaida. Hata hivyo,

wakati Mkaguzi anafanya mkutano wa kuingia na kutoka (entry and exit meeting), Wizara

ilimuandikia kuwa vielelezo vipo, arudi kwa ajili ya ukaguzi. Lakini Mkaguzi huyo hajaja

hadi leo Kamati ipofika kwa ukaguzi wake.

Page 14: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

14

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imetaka ushahidi wa maandishi wa barua ambayo Wizara iliiandikia Afisi ya

Mkaguzi kuhusiana na vielelezo hivyo, ambapo Wizara haikuweza kutoa kwa maelezo kuwa

waliwasiliana kwa mazungumzo tu, bila ya maandishi. Hata hivyo, Kamati imejiridhisha

kuwa matumizi hayo yalihusu viongozi wa Kitaifa ambapo taarifa za safari zao huwa siri

kwa maslahi ya usalama, lakini haikubaliani kukiukwa kwa sheria kwa sababu hiyo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuzingatia sheria kwa matumizi ya fedha za Serikali pamoja na

matumizi hayo kuwahusu viongozi wa kitaifa.

3.2 WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, UTALII NA MICHEZO

Hoja Namba 15.2 Ujenzi wa uzio wa maeneo ya Chumbuni na Bungi, Tsh.

474,810,000

Ukaguzi umebaini kuwa Wizara ya Fedha imefanya malipo ya fedha hizo kwa Katibu Mkuu

Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo kupitia Kitengo cha Madeni ya Serikali

(Public Debt) kwa hati namba P/D 05/11/2011 yenye hundi namba 048084 ya tarehe 2

Novemba, 2011 na katika malipo hayo, Tsh. 281,041,000 ni kwa ajili ya ujenzi wa uzio

eneo la Chumbuni na Tsh. 193,769,000 kwa ajili ya ujenzi wa uzio eneo la Bungi.

Aidha, ukaguzi umebaini kuwa, fedha zilizotumika katika ujenzi huo hazilingani na hali

halisi ya uzio huo. Wizara ilijenga uzio kwa kutumia waya (senyenge) wakati fedha

zilizoingizwa zilikuwa na uwezo wa kujenga ukuta utakaokuwa madhubuti na utakaodumu

kwa muda mrefu.

Majibu ya Wizara

Ni kweli fedha hizo ziliingizwa na kutumiwa kwa ujenzi wa uzio wa waya kama

ulivyolelezwa, lakini sio sahihi kuwa fedha hizo zingelitosha kujengea uzio wa ukuta. Eneo

la Chumbuni lina ukubwa wa hekta 17 na lenye mzunguko wa kilomita 3.5 sawa na mita

3500. Aidha, makisio ya Wakandarasi walio wengi walioandikiwa kutoa makisio ya kazi

hiyo walithibitisha kuwa, ujenzi wa ukuta wa tofali ungeligharimu Tsh. 640,500,000/-,

gharama ambazo bado hazijajumuisha kazi za uwekaji wa msingi, uwekaji wa zege kwenye

nguzo na usafishaji wa eneo husika.

Eneo la Bungi linaukubwa wa hekta 14 na mzunguko wa mita 2700, ambapo ujenzi wa ukuta

ungeligharimu Tsh. 494,100,000/, gharama ambazo hazijajumuisha uchimbaji wa msingi,

uwekaji wa zege kwenye nguzo na usafishaji wa eneo. Aidha, gharama za ukuta kama huo

wenye mzunguko wa kilomita 3.5 kwa ujenzi wa kuta za zege unahitaji Tsh. 300,000 kwa

mita moja ya mraba na kwa kuzidisha mita za mraba 8,100, zitakuwa Tsh. 2,430,000,000/-,

na sio kama zilivyoelezwa na Mkaguzi.

Kuhusiana na taratibu za kupatikana kwa mjenzi, Wizara imetumia kifungu cha 146(3) cha

Kanuni ya Manunuzi na 67(1)(ii) na kutumia Idara ya Majenzi ya Serikali kwa kufuata

kifungu cha 63 cha Kanuni za Manunuzi.

Sababu kuu za ujenzi huo ni wa uharaka wa kuondoshwa mnara wa redio medium wave ni

kunusuru hatari iliyotolewa na Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA) ya mnara huo

uliokuwepo Chumbuni, kuhatarisha urukaji na utuaji wa ndege za Kimataifa, hali ambayo

ingelipelekea kuanguka kwa uchumi na kudhoofika kwa sekta ya utalii Zanzibar.

Page 15: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

15

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, msingi wa ujenzi huo ni barua ya tarehe 17 Machi, 2011

kutoka Mamlaka ya TCAA na baada ya kupokelewa kwa barua hiyo, Idara ya Habari kwa

muongozo wa Wizara ilipeleka Waraka Serikalini na kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu

wa kufuatilia suala hilo ambapo baada ya utafiti, walipeleka taarifa yao Baraza la Mapinduzi

na kuangizwa kuhamishiwa kwa mnara huo, kujengwa uzio wa Chumbuni na eneo jipya

lililohamishiwa mnara huo, Bungi pamoja na ujenzi wa nyumba za wafanyakazi na walinzi

huko Bungi, kama Kamati ilivyojiridhisha kupitia barua ya tarehe 11/08/2011 yenye kumbu

kumbu namba BLM/30/M/C.6/VOL.VI/13. Na ndipo Wizara ya Habari ilitekeleza ujenzi

huo kufuatia agizo hilo.

Pamoja na usahihi wa ujenzi wa uzio kufuatia kupokea maelekezo ya Baraza la Mapinduzi,

kwa mujibu wa gharama zilizoainishwa katika barua husika, Kamati hairidhishwi na

kutokuwepo kwa juhudi zozote za kujengwa ukuta wa matofali, ambao ndio madhubuti, na

inaamini ujenzi wa uzio hautafikia lengo, kwa kukosa umadhubuti, pamoja na usahihi kuwa,

ukuta wa tofali una gharama kubwa kuliko wa senyenge.

Kuhusiana na hatua za kisheria zilizofuatwa kwa ujenzi huo, Kamati imehoji iwapo njia hiyo

ilipata idhini ya Bodi ya Zabuni kama inavyoelezwa na kifungu cha 32 cha Sheria ya

Manunuzi na iwapo ilifuatiliwa na Kamati ya Tathmini kama inavyotakiwa kuundwa na

kutekeleza majukumu yake kisheria, mambo ambayo kwa ujumla wake yametekelezwa na

Kamati ya Wataalamu iliyoundwa.

Pia, kifungu cha 67 kilichotumiwa na Wizara kinahusiana na bidhaa „goods‟ na sio kazi za

ujenzi husika, na hivyo, bado haikidhi kuthibitisha kuwa, taratibu sahihi za manunuzi

zimefuatwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuzingatia sana ujenzi utakaodumu kwa muda mrefu na sio kufanya

matumizi ambayo kudumu kwake ni kwa muda mfupi. Aidha, Kamati inaishauri Wizara

kufuata ipasavyo taratibu za manunuzi katika matumizi yoyote ya fedha za Serikali.

Hoja Namba 15.3 Ujenzi wa nyumba pamoja na kutengeneza mnara wa matangazo

eneo la Bungi, Tsh. 1,021,790,000

Ukaguzi umebaini kuwa Wizara ya Fedha imefanya malipo ya fedha hizo kwa Katibu Mkuu

Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo kupitia Kitengo cha Madeni ya Serikali

(Public Debt) kwa hati namba P/D 05/11/2011 yenye hundi namba 048084 ya tarehe 2

Novemba 2011 na hati namba P/D 23/12 yenye hundi namba 048335.

Ukaguzi umebaini kuwa, kazi za ujenzi wa mnara huo zilifanyika kwa kuhamisha vifaa vya

mnara wa zamani uliokuwepo Chumbuni na kuupeleka Bungi. Aidha, ukaguzi umebaini hata

gharama za kutengeneza mnara ni kubwa, kwani fedha hizo zimeingizwa na kutumika kwa

kujenga mnara mpya kwa kutumia vifaa vipya.

Majibu ya Wizara

Sio kweli kuwa Tsh. 398,000,000 ambazo zimeainishiwa kutumika kwa kuhamishia mnara

huo zingelitosha kujengea mnara mpya wa redio wa medium wave. Kuna tofauti kubwa ya

ujenzi wa mnara huo na minara mengine ya redio za FM, mawasiliano ya simu au kuongozea

meli. Mnara huo uliohamishiwa Bungi, una urefu wa mita 150 na ulijengwa 1971 na

Page 16: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

16

kampuni ya Hurish Tower Co. Ltd ya Ujerumani kwa USD 1,527,000 na mnara kama huo

haupo popote Afrika ya Mashariki na Kati.

Sweden kwa mfano mwaka 1985 walijenga kwa sawa na gharama USD 3,125,000. Hivyo,

Tsh. 398,000,000 hazingelitosha kujenga mnara mpya. Hata hivyo, Wizara imetafuta vifaa

vingi vipya vinavyohusu usimamizi wa mnara huo isipokuwa viunzi (sections) 21 vyenye

urefu wa mita 7 kila kimoja, ndivyo vilivyorejeshwa wakati wa kuusimamisha tena.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imezingatia hoja hii ya ukaguzi lakini imeshindwa moja kwa moja kulinganisha na

bei halisi ya mnara mpya, ambapo ripoti haijaonesha mlingano wa bei hiyo. Aidha,

ilipohitaji kuelezwa bei ya mnara mpya kama huo, ilielezwa na Wizara kuwa ungeligharimu

kwa bilioni 2 na nusu.

Aidha, pamoja na kuelezwa kuwa fedha zilizotumika katika hoja hii ni Tsh. 1,021,790,000

lakini ripoti hiyo inathibitisha kuwa, Tsh. 398,000,000 zimetumika kwa ajili ya kuhamishia

mnara kutoka Chumbuni hadi Bungi, na Tsh. 623,790,000 zimetumika kwa ujenzi wa

nyumba za wafanyakazi na walinzi eneo la Bungi, lakini ukaguzi haukuhoji matumizi ya

ujenzi wa nyumba, jambo ambalo lilipaswa nalo kutolewa ufafanuzi wake.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Afisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu kutoa ufafanuzi wa

kutosha katika ripoti zake na anapohoji ukubwa wa gharama za suala lolote, ni vyema

akaainisha gharama ndogo zilizofanyiwa utafiti wa kitaalamu.

3.3 WIZARA YA NCHI (OR) TAWALA ZA MIKOA NA IDARA MAALUM ZA

S.M.Z

3.3.1 KIKOSI CHA VALANTIA

Hoja Namba 20.1 Hesabu za mwisho wa mwaka

Taarifa za mapato na matumizi

Kwa mwaka 2011/2012, Kikosi kiliidhinishiwa kutumia Tsh. 2,802,616,659 kwa kazi za

kawaida na fedha halisi iliyoingizwa ni Tsh. 2,802,616,659, sawa na 100% ya makadirio.

Kwa upande wa matumizi ya maendeleo, Kikosi kiliidhinishiwa kutumia Tsh. 100,000,000

na fedha halisi zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 90,000,000 sawa na wastani wa 90% ya

makadirio.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati imetaka kujua iwapo kuna athari zozote zilizopatikana kwa Kikosi kushindwa

kuingiziwa Tsh. 10,000,000 kwa kazi za maendeleo, na Kikosi kilithibitisha kuathirika

katika baadhi ya miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kushindwa kukamilisha ujenzi wa

mesi yao. Hata hivyo, Kamati imetaka kujua iwapo ujenzi huo umefuata taratibu za kisheria

na kuelezwa kuwa, msimamizi wa Ujenzi huo anatoka katika Kikosi cha Zimamoto na

Uokozi, na kwa hatua hiyo Kikosi kimefuata taratibu za sheria.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Kikosi kutafuta Mjenzi na Mshauri Elekezi wa Ujenzi kwa kuzingatia

Sheria ya Manunuzi na Ugavi na sio kuzingatia urahisi na uhusiano wa kikosi kimoja na

chengine.

Page 17: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

17

Hoja Namba 20.2 Malipo yasiyokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu), Tsh.

90,000,000

Fedha hizo zimetumika kwa matumizi mbali mbali lakini vielelezo havikupatikana kwa

ukaguzi.

Majibu ya Kikosi

Ni kweli wakati wa ukaguzi vielelezo hivyo havikupatikana. Na Kikosi kilipotambua kasoro

hiyo, walijikuta tayari wamesharipotiwa katika ripoti ya Mkaguzi. Hata hivyo, juhudi

waliyoichukua ni kwenda Ofisini bila ya kuwa na maandishi yoyote ya barua.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati haikuridhika na hoja ya Kikosi, na kwa mujibu wa Kanuni za Fedha, kutokuwa na

risiti mara tu matumizi ya fedha za Serikali yanapofanyika, ni kosa la kisheria. Aidha,

majibu ya Kikosi kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu, hayakufuata taratibu. Hata

hivyo, Kamati imeshuhudia kuwepo kwa vielelezo hivyo, lakini haiwezi kukubaliana na

ilichokifanya Kikosi wala haikuwa na uwezo wa kufanya ukaguzi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Kikosi kufuata ipasavyo Sheria na Kanuni za Fedha wakati inapotumia

fedha za Serikali.

Hoja Namba 20.3 Malimbikizo ya madeni, Tsh.252,625,000

Fedha hizo zinadaiwa na wafanyabiashara pamoja na taasisi mbali mbali kwa ajili ya utowaji

wa huduma kwa Kikosi, lakini madeni hayo ni ya muda mrefu na kuwepo kwake ni kwenda

kinyume na mfumo sahihi wa kiuhasibu unaotambua mapato na matumizi kwa fedha taslim

ambao unatumika kwa Mawizara ya Serikali.

Majibu ya Kikosi

Ni kweli walikuwa na madeni hayo kwa muda mrefu, lakini tayari yamechukuliwa hatua ya

kulipwa, ingawa bado hayajamalizika. Kwa mfano deni la Regalia, Kikosi kimepokea barua

kutoka Wizarani kuwa tayari ameshalipwa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imetaka kuthibitishiwa kwa kupewa barua ya malipo hayo ya deni la Regalia, lakini

Kikosi kimeshindwa kuthibitisha kwa barua. Aidha, Kamati imetaka ushahidi mwengine

wowote wa kulipwa kwa deni hilo, ambao nao haukuweza kupatikana, zaidi ya Kikosi

kuahidi kufuatilia Wizarani na kuijuulisha Kamati.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Kikosi kuhakikisha kuwa kinafuatilia madeni yake kwa uhakika na

kinayalipa kama yanavyotakiwa.

Hoja Namba 20.4 Taarifa ya ukusanyaji wa mapato

Kikosi kinatoa huduma ya ulinzi kwa taasisi mbali mbali za Serikali na binafsi na kujipatia

mapato, lakini taratibu za ukusanyaji wa mapato hayo hazifuatwi kisheria. Aidha, kasoro

zilizopo katika ukusanyaji huo ni kukosekana kwa vitabu vya stakabadhi za mapato,

kutotayarishwa kwa daftari la fedha taslim (Cash Book) na kutokuwepo kwa hesabu ya

mapato ya Kikosi.

Page 18: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

18

Vile vile Kikosi hakikufungua hesabu juu ya ukusanyaji wa mapato yake ya ndani na

kupelekea uvujaji wa mapato na matumizi mabaya ya fedha za Umma. Aidha, ukaguzi

umeshindwa kupata taarifa za mapato na matumizi kutokana na kutayarishwa kwa daftari la

mapato na matumizi, ambalo lingelitoa taarifa za fedha zilizokusanywa na zilizotumiwa. Pia

ukaguzi umebaini Tsh. 64,674,000 zimekusanywa lakini taarifa za fedha iliyowasilishwa

kwa ukaguzi ilikuwa ni Tsh. 6,270,000, huku tofauti ya Tsh. 58,404,000/- hazijuulikani

taarifa zake.

Majibu ya Kikosi

Ni kweli taarifa za Mdhibiti na takriban taarifa zote za mapato zimebaki Kikosini. Aidha,

kuhusiana na risiti zinazotumiwa na Kikosi kwa ajili ya malipo, hapo awali zilikuwa za

Kikosi lakini kasoro hiyo imerekebishwa na hivi sasa wanatumia risiti za Serikali.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji hali ilivyo sasa ya utowaji wa huduma kwa Kikosi na kuelezwa kuwa,

Kikosi kinatoa huduma kwa taasisi za Serikali pekee na wala hakitoi huduma za ulinzi kwa

watu binafsi. Kuhusiana na hoja, Kamati imejiridhisha kuwepo kwa kasoro zilizoelezwa na

Mdhibiti.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imewataka Viongozi wa Kikosi kufanya marekebisho ya haraka kwa kufungua

akaunti kwa mujibu wa sheria ili mapato yote yanayokusanywa yaingizwe katika akaunti

hiyo, kutumia risiti za Serikali kwa kukusanya mapato na kuwa na daftari kama

alivyoelekeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

Hoja Namba 20.5 Matumizi yaliyofanyika kinyume na vifungu, Tsh. 21,529,660

Kuna baadhi ya malipo yamefanyika kinyume na vifungu vilivyoidhinishwa na Baraza la

Wawakilishi, huku taratibu za uhaulishaji hazikufuatwa kinyume na maelekezo ya Sheria.

Majibu ya Kikosi

Ni kweli wamefanya uhaulishaji kinyume na kufuata taratibu za Sheria kutokana na taratibu

hizo zinachukua muda mrefu na zina urasimu mwingi. Hata hivyo, Kikosi kimefanya kosa

hilo kwa kutokujua lakini sasa wamesharekebisha kasoro hizo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwua, Kikosi kimeshindwa kufuata taratibu za uhaulishaji kama

zinavyoelekezwa na Sheria na kupelekea kwa Kikosi kufanya matumizi kinyume na

maelekezo ya Baraza la Wawakilishi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imekitaka Kikosi kufuata ipasavyo Sheria za uhaulishaji ili kuepuka kufanya

matumizi kinyume na makusudio.

3.4 OFISI YA MAKAMO WA KWANZA WA RAIS

Hoja Namba 49.1 Hesabu za Mwisho wa mwaka. Taarifa kuhusu mapato na

matumizi ya kazi za kawaida na kazi za maendeleo

Mapato yanayotokana na ada za hifadhi mazingira na ada za ukaguzi wa mazingira,

yalikadiriwa kukusanywa kwa Wizara hii Tsh. 9,000,000 kwa mwaka 2011/2012, lakini

mapato yaliyopatikana ni Tsh. 5,978,000 sawa na 66.4 asilimia ya makadirio. Matumizi ya

Page 19: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

19

kazi za kawaida ni Tsh. 1,493,000,000 lakini matumizi halisi yalikuwa Tsh. 1,830,250,655

sawa na asilimia 122.6 ya makadirio.

Aidha, kwa upande wa matumizi ya maendeleo, Ofisi ilikadiriwa kutumia Tsh. 155,000,000,

lakini matumizi halisi yalikuwa Tsh. 140,000,000/- sawa na asilimia 90.3 ya makadirio.

Majibu ya Ofisi

Baada ya kueleza vyanzo vyao vya mapato, Ofisi ilieleza kuwa haikuridhika kama

ilivyokuwa kwa Kamati, hawajaridhika na kasi ndogo ya ukusanyaji wa mapato. Wizara

itakabiliana na changamoto hii kwa kupitia Sheria mpya ya Mazingira iliyopitishwa karibuni

na Baraza la Wawakilishi.

Kuhusu matumizi ya kawaida, Ofisi ilisema yameongezeka kutokana na kuongezeka kwa

kima cha mshahara, na athari za kutokamilika kwa bajeti ya matumizi ya maendeleo

kumeathiri shughuli kadhaa, ikiwa ni pamoja na kulazimika kukatisha matumizi ya gari

Pemba pamoja na matumizi mengine.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwa kuzingatia uhaba wa mapato kuwa, miradi mingi inayotakiwa

kufanyiwa ukaguzi wa kimazingira huwa haifanyiwi. Aidha, Kamati inahoji Serikali kuwa

na miradi mingi wakati mmoja ambayo inashindwa kutekelezeka, na kwa nini kusiwe na

miradi michache ambayo utekelezaji wake utakuwa fanisi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Ofisi kuangalia zaidi suala la ukaguzi wa kimazingira kwa miradi mbali

mbali inayopitishwa na Serikali na kulifanya hilo pia kwa azma ya kuongeza mapato. Aidha,

kuhusiana na suala zima la uandaaji na utekelezaji wa miradi, Kamati inaishauri Serikali

kuwa na miradi michache inayotekelezeka kuliko kuwa na miradi mingi ambayo inaachwa

njiani.

3.4.1 TUME YA UKIMWI

Hoja Namba 50.1 Hesabu za Mwisho wa mwaka. Taarifa ya matumizi ya kazi za

kawaida na kazi za maendeleo.

Kwa mwaka 2011/2012, Tume ilikadiriwa kutumia Tsh. 472,000,000 kwa kazi za kawaida

na fedha halisi iliyoingizwa ni Tsh. 518,535,274 sawa na asilimia 109.9 ya makadirio.

Kwa upande wa matumizi ya maendeleo, Tume ilikadiriwa kutumia Tsh. 90,000,000 na

fedha hizo hizo zimeingizwa na kutumika, sawa na asilimia 100.

Majibu ya Tume

Ongezeo la matumizi ya kazi za kawaida linatokana na kuongezwa kwa mishahara.

Ongezeko hilo lilikuwa ni la Tsh. 6,083,414.00 kwa mwezi.

Uchunguzi wa Kamati

Ongezeko la matumizi ya kazi za kawaida linalotokana na ongezeko la mishahara,

limeshuhudiwa kujirejea katika Taasisi mbali mbali za Serikali, na hili linatokana zaidi na

Serikali kutoainisha matumizi hayo katika bajeti husika, huku ikifahamu wazi kuwa, katika

mwaka kunakuwa na ongezeko la mishahara.

Mapendekezo ya Kamati

Page 20: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

20

Kamati inaishauri Serikali kuhakikisha inajipanga mapema katika ongezeko la mishahara,

ambalo takriban huathiri matumizi ya kazi za kawaida za taasisi zake.

3.5 OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS

Hoja Namba 13.1 Uwasilishaji wa hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya ukaguzi

Kifungu cha 24(2) cha Sheria ya Fedha namba 12 ya mwaka 2005, inakitaka taasisi zote za

Serikali zitayarishe na kufunga hesabu zao za mwisho wa mwaka na kuziwasilisha kwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa ajili ya ukaguzi. Hata hivyo,

uwasilishaji huo usizidi tarehe 30 ya mwezi wa Septemba ya kila mwaka, lakini Ofisi hii

imechelewa kwa kuwasilisha hesabu zao tarehe 3 Octoba, 2012.

Majibu ya Ofisi

Ni kweli Ofisi ilichelewa kuwasilisha hesabu hizo kwa wakati, lakini sasa wamechukua

hatua za kutorejea tena kosa hilo, na tokea lilipotokezea awali, kasoro hiyo haikutokezea

tena katika miaka iliyofuata.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imesikitishwa na Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais kuchelewa kuwasilisha hesabu

zao za mwisho wa mwaka kwa wakati, kutokana na umuhimu wa Ofisi hii kuwa kioo kwa

taasisi nyengine za Serikali.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, kufanya haraka marekebisho ya kasoro

hii, kwani Ofisi hii ndio kioo na kigezo kwa taasisi nyengine za Serikali.

Hoja Namba 51.1 Hesabu za Mwisho wa mwaka

Taarifa kuhusu mapato na matumizi ya kazi za kawaida na kazi za maendeleo

Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais imekusanya Tsh. 9,374,100 na matumizi ya kawaida

yalikadiriwa kuwa Tsh. 2,611,000,000 na fedha zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh.

3,118,818,842 sawa na asilimia 119.4 ya makadirio. Aidha, kwa upande wa matumizi ya

maendeleo, Ofisi ilikadiriwa kutumia Tsh. 715,000,000, na fedha zote hizo ziliingizwa na

kutumiwa, sawa na asilimia 100 ya makadirio.

Majibu ya Ofisi

Makusanyo hayakuwa makubwa kutokana na mapato yake kutegemea huduma za uchapaji

zinazotolewa chini ya Idara ya Uchapaji, ambapo mashine za uchapaji zimechakaa. Hata

hivyo, makusanyo hayo yameongezeka kutokana na kuhamishiwa kiwanda hicho Maruhubi

na kuwepo kwa baadhi ya vifaa vipya vya uchapaji. Aidha, kazi ya mwanzo ni kuchapisha

bajeti za Serikali, hali inayopelekea kuokoa fedha nyingi za Serikali.

Kuhusiana na ongezeko la matumizi ya kawaida, linatokana na ongezeko la mishahara

ambayo hapo wakati wa kuandaa bajeti haikuweza kuzingatiwa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati haikukubaliana na maelezo ya Ofisi kwa kuzingatia makusanyo ya mwaka

2010/2011 ambayo yalikuwa 18%, mwaka 2011/2012 ni 17% na mwaka 2012/2013

yalikuwa 43%, hali ambayo haioneshi hoja ya uchakavu wa mitambo kuwa hoja madhubuti,

huku Kamati inaona ni kukosekana kwa mipango madhubuti ya ukusanyaji wa mapato.

Page 21: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

21

Aidha, Kamati imehoji juu ya malipo yanayofanywa na taasisi za Serikali zinazopatiwa

huduma katika Idara ya Upigaji Chapa, na Ofisi ilijibu kuwa, fedha zote kwa ajili ya bajeti

kwa kuchapisha vitabu vya bajeti zinafikia Tsh. 74,000,000/- . Aidha, Ofisi huiandikia

Wizara ya Fedha kwa taasisi zote za Serikali ambazo hazilipi, ili wakatwe moja kwa moja

katika bajeti zao.

Pia, kuhusiana na ongezeko la matumizi, Kamati inahoji kwa nini taasisi hizi zisiandae

nyongeza husika tokea wakati wa kuandaa bajeti, na kushindwa kufanya hivyo hupelekea

ongezeko kubwa la matumizi kinyume na idhini ya nyongeza hiyo kufahamika.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais kuhakikisha inakuwa na fedha za

kutosha za matengenezo ya mashine za uchapishaji. Aidha, Kamati inaishauri Serikali

kuangalia uwezekano wa kuipa Idara ya Uchapaji mamlaka kamili ya kujiendesha

kibiashara. Vile vile, Kamati inaishauri Serikali kuwa na mipango mizuri yenye kufahamika

kwa mwaka mzima, ili kuepusha kuongezeka kwa matumizi kwa sababu ya mishahara.

3.5.1 IDARA YA MAAFA

Hoja Namba 51.2.1 Malipo ya fidia kwa waathirika wa ajali ya MV. Spice Islander 1.

Malipo ya fidia kwa waathirika wa ajali ya Mv. Islander, kati ya 1429 waliofariki na 941

waliopona, walilipwa Tsh. 1,267,661,287 kwa ajili ya fidia. Hata hivyo, katika ulipaji huo,

kuna kasoro kadhaa zilijitokeza ambazo ni fomu za malipo kukosa namba, kutumika tarehe

moja tu wakati ulipaji uliendelea kwa zaidi ya miezi mitatu, kukosekana kwa idadi sahihi ya

wanaopaswa kulipwa fidia hiyo, kutofanywa marejesho ya fedha ilobakia baada ya ulipaji

huo kufanyika, kukosekana kwa baadhi ya sahihi za waliopokea fedha hizo na kutokuwa na

idadi sawa ya walioathirika katika maafa hayo na kupelekea hadi leo hii kuna baadhi ya watu

wanakwenda kudai fedha hizo.

Majibu ya Ofisi

Idadi halisi ya maathirika inatofautiana katika orodha tatu tofauti. Mara tu ilipotokea ajali,

Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais iliwataka Masheha wa Shehia zote kuwasilisha majina ya

walioathirika na baadae kuyakabidhi kwa Wakuu wa Wilaya. Kulikuwa na orodha ya pili

ambayo waathirika walipewa kujaza na kuziwasilisha Wizarani na orodha ya tatu ni ile

iliyopatikana kutokana na Tume iliyoundwa na Mhe. Rais ambayo inasema waliohai ni 941

na waliofariki ni 1529 na kufanya idadi yote kuwa waathirika 2470, ambao Ofisi inaamini

ndio sahihi zaidi.

Aidha, walipopata orodha ya Tume wamezunguuka Wilaya zote na kuwalipa waathirika.

Kati ya waliohai 941, waliowapata ni 640 tu na kati ya 1529 waliofariki, waliwapata 1328 tu,

ila walitangaza katika vyombo vya habari, na kwa malalamiko yaliyoletwa kwa waliohai 53,

wamewalipa 14.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imezipitia fomu zilizowasilishwa na Ofisi hii na kugundua kuwa hazikuwa na

nambari. Kuhusiana na kutumiwa kwa tarehe moja, Kamati imeihoji Ofisi na kueleza kuwa,

wao walitumia orodha, kwa mtu ambae hakulipwa tarehe ya siku, alilipwa kwa tarehe

iliyofuata.

Page 22: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

22

Aidha, malipo ya fidia kwa waliofariki ilikuwa Tsh. 550,000/- na waliohai ilikuwa Tsh.

412,500/-. Na kwa upande wa Pemba, walilipa kwa mkupoa mmoja na „cheque‟ ilisainiwa

siku moja ila uvunjaji wa „cheque‟ hiyo ulifanywa siku tofauti.

Ofisi inakiri kuwa, wakati alipokuja Mkaguzi hakukuwa na baadhi ya marejesho kwa baadhi

ya Wilaya, ila sasa marejesho hayo yapo, hali inayoipelekea Kamati kuthibitisha usahihi wa

hoja ya Mdhibiti. Vile vile, Kamati imehoji kukosekana kwa baadhi ya sahihi, ambapo

ilielezwa kuwa baadhi ya waliohusika na malipo hawajui kusaini na hivyo kutilishwa dole

gumba. Aidha, Kamati imeelezwa kuwa, fedha iliyobakia imependekezwa kubakia katika

akaunti ya Idara ya Maafa kwa kusaidia matukio mbali mbali ya maafa kwa namna

yanavyojitokeza. Aidha, Tsh. 100,000,000 zimetengwa kwa ujenzi wa fance ya eneo

walikozikwa waliofariki, ili iwe kumbu kumbu na eneo tengefu kuwazika wengineo. Hivyo,

fedha zote zilizochangwa ni Tsh. 1,256,603,688/, fedha zilizotumika kwa malipo mbali

mbali ya fidia ni Tsh. 1,107,975,000/- na fedha zilizobakia ni Tsh. 148,628,688/-.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuwa makini na masuala ya malipo ya fidia kwa matukio mbali

mbali, kwa kuwa na utambulisho sahihi wa wanaostahiki kulipwa fidia hiyo, lakini pia

ihakikishe fedha za michango ya namna kama hiyo zinalipwa na kuwafikia walengwa.

3.5.2 TUME YA UCHAGUZI

Hoja Namba 52.1 Hesabu za Mwisho wa mwaka. Taarifa kuhusu matumizi ya kazi za

kawaida za Tume ya Uchaguzi

Tume ya Uchaguzi ilikadiriwa kutumia jumla ya Tsh. 761,000,000 kwa kazi za kawaida kwa

mwaka 2012/2013. Aidha, hadi kufikia Juni 2013, Tume iliingiziwa Tsh. 910,506,569 kwa

kazi hizo za kawaida na kufanya nyongeza ya fedha hizo za matumizi kuwa Tsh.

149,506,569.

Majibu ya Tume

Ni kweli fedha hizo ndizo zilizoingizwa na kutumiwa, huku kukiwa na nyongeza iliyotajwa.

Nyongeza hiyo imesababishwa na kuongezeka kwa mabadiliko ya viwango vya mishahara

kwa wafanyakazi mbali mbali wa Tume.

Uchunguzi wa Kamati

Kwa mwaka huu, Kamati imeshuhudia taasisi mbali mbali za Serikali zikiwa na ongezeko la

matumizi ya fedha walizoomba katika Baraza la Wawakilishi. Aidha, Kamati imekuwa

inashuhudia majibu hayo hayo ya kuongezeka kwa matumizi hayo kutokana na ongezeko la

mishahara. Hata hivyo, Kamati inashangazwa sana na Serikali kwa kutoona mabadiliko hayo

na kuzingatiwa mapema katika bajeti za taasisi hizo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuangalia mapema mabadiliko ya mishahara katika bajeti ya

mwaka, kabla ya kutangazwa kwa mabadiliko hayo, ili kuweka sawa taarifa za hesabu.

3.6 WIZARA YA BIASHARA, VIWANDA NA MASOKO

Hoja Namba 60.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012 na 2012/2013

Taarifa ya Mapato na Matumizi:

Page 23: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

23

Jumla ya Tsh. 30,000,000 zilikadiriwa kukusanywa kwa mwaka 2011/2012, na mwaka

ulipomalizika Wizara ilikusanya Tsh. 33,583,600 ambayo ni sawa na asilimia 112 ya

makadirio, ikiwa ni ongezeko la Tsh. 3,583,600 sawa na asilimia 12 ya makadirio.

Aidha, matumizi ya kazi za kawaida, yalikuwa Tsh.2,362,000,000/- na fedha halisi

zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 2,327,069,314, sawa na asilimia 98.5 ya makadirio,

ikiwa ni pungufu ya Tsh. 34,930,686 sawa na asilimia 1.5 ya makadirio. Aidha, matumizi ya

maendeleo, Wizara iliidhinishiwa kutumia Tsh. 300,000,000/-, lakini mwisho wa mwaka

ulipofika, fedha zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 298,985,100 sawa na asilimia

99.76 ya makadirio.

Majibu ya Wizara

Ongezeko la ukusanyaji wa mapato kwa Wizara hii limetokana na ufuatiliaji mzuri wa

vianzio vya mapato ikiwemo vituo vya mafuta na kuzikagua mizani za wafanyabiashara.

Uchunguzi wa Kamati

Katika kufanya uchunguzi wa suala hili, Kamati ilibaini kuwa ukusanyaji wa mapato wa

Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko hauridhishi kwa kuwa inaonekana kuna vianzio

vyengine vya mapato havijafikiwa. Aidha, Kamati iliwataka Wizara kuwasilisha vianzio

vyao vya mapato kwa Kamati, lakini hadi tunaandika taarifa hii, taarifa hiyo haijapatikana

kwa Kamati.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuongeza mikakati ya ukusanyaji wa mapato na ifanye matumizi

kwa kuzingatia mahitaji halisi ya Wizara na taratibu za kisheria. Aidha, Kamati inazitaka

taasisi za Serikali kuheshimu maelekezo ya Kamati ya kupatiwa taarifa mbali mbali

inazozihitaji.

Hoja Namba 60.2 Malipo yasiyokuwa na Vielelezo (Nyaraka Pungufu Tsh.

46,018,985)

Fedha hizo zimelipwa kwa matumizi mbali mbali lakini vielelezo husika havikupatikana kwa

ukaguzi, kinyume na taratibu za kisheria. Hali ambayo haikuweza kuthibitisha uhalali wa

malipo hayo. Malipo hayo yaligawika katika hesabu mbili, ya kawaida kwa Tsh. 46,018,985

alizolipwa Harisini Enterprises kwa ajili ya ukarabati wa banda la maonesho ya saba saba

Dar es Salaam na hesabu ya maendeleo ya Tsh. 140,855,100 alizolipwa Cris and

Infrastructure Solution Ltd kwa ajili ya utafiti wa kuifanya Zanzibar kuwa bandari kuu.

Majibu ya Wizara

Wizara iliieleza Kamati hii kuwa kwa upande wa hesabu za kawaida, kasoro hiyo

imesharekebishwa kwa kuwa malipo hayo hivi sasa yamelipwa kwa mujibu wa vielelezo

husika. Aidha, kuhusiana na Hesabu ya Maendeleo Wizara ilikiri kuwa ni kweli wakati wa

ukaguzi kielelezo cha ithibati cha uhaulishaji fedha (Bank Transfer) hakikuwepo. Hali hii

ilitokana na utaratibu uliotumika wa kumlipa Mshauri Elekezi ambapo Wizara ya Fedha

ilifanya uhaulishaji huo moja kwa moja na kusawazisha katika bajeti ya Wizara ya Bishara,

Viwanda na Masoko kwa kukata uhaulishaji uliofanyika katika matumizi ya eneo husika.

Hivyo, risiti kwa ajili ya ithibati hiyo ilikuwepo Wizara ya Fedha na tayari Wizara hii

imeshapokea nakala ya ithibati.

Page 24: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

24

Uchunguzi wa Kamati

Katika kufuatilia hoja hii Kamati ya PAC imebaini kuwa kasoro hii imejitokeza kwa kuwa

Kampuni iliyopewa shughuli hii ilishindwa kuwasilisha nyaraka husika kwa wakati. Ingawa

Wizara ilikuwa inahitaji kukarabatiwa banda la maonyesho ya sabasaba kwa uharaka, hata

hivyo, Wizara haikupaswa kuilipa Kampuni hii fedha za awamu ya pili kwa kuwa Kampuni

ilishindwa kutoa nyaraka kwa malipo ya awali yaliyofanyika jambo ambalo limeondosha

uaminifu wake.

Aidha, Kamati hii imebaini kuwa upatikanaji wa Mshauri Elekezi haukufuata taratibu za

kisheria. Suala hili hulitia mashaka Kamati hii na kuhisi kuwa kuna mchezo mchafu

ulifanyika wakati zoezi hili linafanyika. Aidha, kuhusiana na hesabu ya maendeleo Kamati

iliridhika na majibu yaliyotolewa na Wizara kuhusiana na suala hili.

Mapendekezo ya Kamati:

Kamati imeitaka Wizara kuwa wabunifu pamoja na kutafuta wataalamu ili iweze

kukusanya mapato mengi zaidi.

Waendelee kutoa taaluma kwa wananchi juu ya umuhimu wa kukaguliwa mizani

wanazozitumia katika shughuli zao za biashara.

Watekeleze majukumu yao kwa mujibu wa Sheria za nchi.

Mengineyo

Kamati ilielezwa kuwa Shirika la Viwango Zanzibar (ZBS) limeanza kutekeleza shughuli

zake, hata hivyo, kutokana na ukosefu wa maabara (Laboratory) Shirika hili hupeleka bidhaa

zake kwa ajili ya kuangaliwa ubora wa viwango katika Shirika la Viwango la Tanzania

(TBS). Hivyo basi, Kamati hii inaitaka Serikali iliongezee nguvu Shirika la ZBS, ili

kuhakikisha kuwa Shirika linatekeleza majukumu yake ipasavyo.

Kamati inaishauri Serikali kuipa mamlaka ya kushughulikia vibali vya kuingizwa gari

Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano badala ya Mamlaka ya Kukusanya Mapato (TRA)

na kuwa Taasisi hii ndio hasa inayohusika na masuala ya usafiri.

Kwa upande wa ZBS, Kamati ilishauri kuwa iajiri Kampuni itakayoshughulikia masuala ya

ubora wa viwango kwa bidhaa za hapa nchini ili kuongeza mapato ya nchi.

Vile vile, Kamati inaishauri Serikali kuhakikisha kuwa Shirika hili muhimu linapewa

kipaumbele kwani Sheria yake imeanzishwa tokea mwaka 2011 lakini utekelezaji wake bado

unasuasua.

3.7 WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI NA

USHIRIKA

Hoja Namba 63.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012

Taarifa ya Mapato na Matumizi

Wizara iliidhinishiwa kukusanya Tsh. 68,500,000 kwa mwaka 2011/2012. Hadi kufikia Juni

2012, mapato yaliyokusanywa yalikuwa Tsh. 123,277,000 ambayo ni sawa na asilimia 180

ya makadirio.

Kwa upande wa matumizi ya kawaida, fedha zilizoainishwa ni Tsh. 1,545,000,000/- na fedha

halisi zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 1,939,037,749/- sawa na asilimia 122.5 ya

makadirio. Aidha, matumizi ya maendeleo, Wizara iliidhinishiwa kutumia Tsh. 90,000,000/-,

lakini mwisho wa mwaka ulipofika, fedha zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh.

Page 25: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

25

70,000,000, sawa na asilimia 77.8 ya makadirio, kukiwa na upungufu wa Tsh.20,000,000

sawa na asilimia 22.2 ya makadirio.

Majibu wa Wizara:

Wizara hii iliieleza Kamati kuwa ongezeko la mapato hayo limetokana na kuongezeka kwa

idadi ya Vyama vya Ushirika vilivyoandikishwa, uchunguzi wa vibali vya katika Hoteli na

sehemu mbali mbali.

Aidha, walizidi kueleza kuwa kupanga makadirio ya mapato kuna changamoto kubwa kwani

kunategemea mazingira ya wakati; kwa mfano katika mwaka uliopita walikusanya fedha

nyingi kwenye eneo la vibali vya kazi (Work Permit), lakini mwaka uliofata walishindwa

kufikia malengo kutokana na malalamiko yaliyotolewa juu ya ongezeko la fedha katika eneo

hili. Ongezeko la matumizi ya kazi za kawaida limetokana na Serikali kupandisha mishahara

ya watendaji wake.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na maelezo hayo ya Wizara, Kamati hii inaona kuwa bado kuna changamoto

Serikalini katika kupanga makadirio ya mapato.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuwa makini wakati wa kuandaa makadirio hayo. Kwani

imefahamika wazi kuwa, nyongeza hiyo ya mishahara huwa haionekani katika bajeti za

Wizara na taasisi zake, inapopitishwa na Baraza.

3.7.1 IDARA YA MIKOPO

Hoja Namba 63.2.1 Malimbikizo ya madeni ambayo hayajalipwa ya (JK na AK) hadi

kufikia tarehe 30 juni, 2012 tsh. 877,877,910.6

Idara imekopesha fedha hizo kwa ajili ya watu binafsi SACCOS na vikundi mbali mbali vya

kiuchumi, lakini hadi kufikia 30 Juni, 2012, jumla ya Tsh. 740,197,007.09 zilikopeshwa

bado hazijarejeshwa. Fedha hizo zimekopeshwa kwa mikoa yote ya Unguja na Pemba.

Majibu ya Wizara

Wizara iliieleza Kamati kuwa usimamizi wa Mfuko huo ulikuwa na changamoto ambazo

ziliathiri urejeshaji wa mikopo iliyotolewa. Changamoto hizo ni kama zifuatazo;

i. Mfuko wa AK na JK ulikuwa ukiendeshwa na Taasisi mbili yaani Benki ya Watu wa

Zanzibar na Wizara inayohusika na masuala ya uwezeshaji. Hata hivyo, Benki ya

Watu wa Zanzibar ndio iliyokuwa na jukumu la utoaji wa mikopo pamoja na

ufuatiliaji wake wakati jukumu la Idara ya Mikopo lilikuwa ni kuratibu na

kuhakikisha mikopo inawafika wananchi wote waliostahiki;

ii. Kulikuwa na upungufu wa vitendea kazi, hasa usafiri kwa Idara ya Mikopo; na

iii. Tatizo la kuhamahama kwa wakopaji bila ya kutoa taarifa kwa Masheha wa Shehia

zao.

Ingawa jukumu la Idara ya Mikopo lilikuwa ni kuratibu tu, hata hivyo baada ya kubaini

kuwa kuna tatizo la ucheleweshaji wa malipo ya mikopo hiyo, ilikubaliana na Uongozi wa

Benki kusaidia ufuatiliaji na ukusanyaji wa fedha hizo.

Page 26: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

26

Tangu zoezi hilo lilivyoanza deni lililobaki ni kama ifuatavyo;-

MKOA DENI LILILOBAKI HADI SEPT, 2014

Mkoa wa Kaskazini Unguja Tsh. 104,954,619.50

Mkoa wa Kusini Unguja Tsh. 69,019,483.45

Mkoa wa Mjini/Magharibi Tsh. 277,804,214.24

Mkoa wa Kaskazini Pemba Tsh. 114,227,335.65

Mkoa wa Kusini Pemba Tsh. 110,126,947.70

JUMLA = Tsh. 676,132,600.54

Walizidi kueleza kuwa hivi sasa fedha zote zilizokuwa kwenye Mfuko wa JK/AK

zimejumuishwa kwenye Mfuko wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ambao ulizinduliwa na

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi mnamo mwezi wa Disemba,

2013.

Katika mwezi wa Septemba, 2014 Wizara hii ilipokea kutoka PBZ jumla ya Tsh.

600,000,000.00 zilizokuwa kwenye Mfuko huo pamoja na orodha ya wadaiwa ambao

hawajamaliza madeni yao. Hivyo, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana,

Wanawake na Watoto inaendelea kufuatilia madeni hayo.

Mapendekezo ya Kamati

Kwa kuwa deni lililobaki ni kubwa na kwa kuwa wadaiwa wakilipa madeni yao, fedha

zitakazopatikana zitawawezesha wananchi wengine kupata mikopo hiyo, Kamati hii

inaishauri Wizara kuendelea kufuatilia madeni hayo na kuwachukulia hatua wale wote

ambao hawatolipa madeni yao.

3.8 WIZARA YA NCHI (OR) UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA

Hoja Namba 43.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012

Taarifa ya Matumizi ya kawaida na maendeleo

Iliyokuwa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka

2011/2012 ilikadiriwa kutumia Tsh. 1,997,000,000 kwa kazi za kawaida na fedha halisi

zilizoidhinishwa na kutumika ni Tsh. 2,180,494,994 sawa na asilimia 109.3 ya makadirio,

kukiwa na ongezeko la Tsh. 183,494,994 sawa na asilimia 9.3 makadirio. Aidha, matumizi

ya kazi za maendeleo yalikisiwa kuwa Tsh. 360,000,000 na fedha hizo hizo ziliingizwa na

kutumiwa, sawa na asilimia 100 ya makadirio.

Majibu ya Wizara

Taarifa hizo ni sahihi na kuhusiana na matumizi ya maendeleo, Wizara ilikuwa na shughuli

mbali mbali za utekelezaji wa miradi iliyohusika, ikiwa ni pamoja na utungaji wa Sheria za

Utumishi wa Umma na kanuni zake, miradi ambayo hapo awali ilikuwa inategemea „World

Bank‟ lakini hivi sasa Wizara inapata fedha kutoka Serikalini pekee. Hivyo, Wizara

inakabiliwa na changamoto kubwa ya kukosa wafadhili wa mradi huu isipokuwa Serikali.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati imehoji muda mrefu wa utekelezaji miradi ya Wizara na kuamini kuhusiana na

kukosa wafadhili kuwa, suala hilo lingestahiki kufanywa na Serikali na sio kutegemea

Wafadhili.

Page 27: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

27

Hoja Namba 43.2 Malipo yaliyofanywa kinyume na utaratibu, Tsh. 89,232,000

Fedha hizo zimelipwa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Utawala wa Umma (IPA), lakini

stakabadhi zinazoonesha kupokelewa kwa malipo hayo hazikubaliki kwa mujibu wa Sheria.

Majibu ya Wizara

Suala hili liliwahi kujitokeza kwa mkandarasi wa ujenzi wa Chuo hicho (Chuo cha Mafunzo)

ila tatizo hilo liliwahi kuelezwa kwa Chuo cha Mafunzo kuhusiana na kasoro ya risiti

wanazotoa kuthibitisha mapokezi ya fedha za umma.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati inafahamu kuwa bado baadhi ya Vikosi vya SMZ vinatumia stakabadhi zao badala

ya stakabadhi za Serikali na Kamati imekuwa inalitolea taarifa suala hili takriban kila

mwaka.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo cha Mafunzo kutumia risiti za Serikali, kwa huduma wanazozitoa

kwa taasisi za Serikali na watu binafsi.

3.8.1 IDARA YA NYARAKA

Hoja Namba 43.3.1 Kuwepo kwa nyumba binafsi ndani ya uzio wa Idara

Ukaguzi umebaini kuwepo kwa nyumba ya mtu binafsi ambae hutumia mlango mkubwa wa

Idara ya Nyaraka ili aweze kufika ndani ya nyumba yake. Tatizo hili husababisha mlango wa

Idara kuwa wazi kwa muda mrefu kwa matumizi ya mtu binafsi. Hali hii hupelekea

kudhoofika kwa mfumo mzima wa kiusalama wa mali na nyaraka muhimu za Serikali. Suala

hili ni la muda mrefu linahitaji kutafutiwa ufumbuzi.

Majibu ya Wizara (Idara)

Ni kweli hoja hiyo na Idara kwa mashirikiano na Wizara wamechukua hatua kubwa na ya

muda mrefu kulieleza suala hilo na kulitafutia ufumbuzi, lakini hakuna mafanikio yoyote

yaliyopatikana. Nyumba hiyo imo ndani ya eneo hilo kwa zaidi ya miaka 10 sasa. Mmiliki

wa nyumba hiyo amekubali kuondoka hapo kwa kulipwa Tsh. 800,000,000 fedha ambazo ni

nyingi sana na hazina uhalisia wa thamani ya nyumba yake hiyo.

Aidha, pendekezo jengine ni mwenye nyumba atumie mlango wa mbele uliopo katika

barabara kuu ya Kilimani iendayo Uwanja wa Ndege na geti la nyuma lizibwe, lakini kwa

bahati mwenye nyumba hajaridhia au imegwe sehemu ya ardhi ya aneo la Idara ili kujenga

ukuta utakaowacha nafasi ya upana wa kupandisha gari yake, lakini bado pendekezo hili

linahitaji ushauri zaidi wa kitaalamu. Hata hivyo, Wizara inawasiliana na Wizara ya ardhi ili

kuwasilikiliza ushauri wao kuhusiana na suala hili.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati inaamini suala hili bado Serikali haijawa tayari kulifanyia kazi. Kama inaathirika

kweli, ina uwezo wa kulifanyia kazi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kulitafutia ufumbuzi suala hilo.

Page 28: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

28

3.9 WIZARA YA USTAWI WA JAMII MAENDELEO YA VIJANA

WANAWAKE NA WATOTO

Hoja Namba 13.1 na 12 Uwasilishaji wa Hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya

ukaguzi (mwaka 2011/2012 na 2012/2013)

Kifungu cha 24(2) cha Sheria ya Fedha namba 12 ya mwaka 2005, inakitaka taasisi zote za

Serikali zitayarishe na kufunga hesabu zao za mwisho wa mwaka na kuziwasilisha kwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa ajili ya ukaguzi. Hata hivyo,

uwasilishaji huo usizidi tarehe 30 ya mwezi wa Septemba ya kila mwaka, lakini Wizara hii

ilichelewa kwa kuwasilisha 01/10 kwa miaka yote miwili, mwaka wa 2011/2012 na

2012/2013.

Majibu ya Wizara

Mhasibu wa Wizara aliieleza Kamati kuwa, ripoti zote mbili ziliwasilishwa Masjala ya

Wizara kabla ya tarehe iliyotajwa na ukaguzi. Kwa mfano, ripoti ya mwaka 2011/2012

iliwasilishwa kwa Mdhibiti kama saa 9 hivi, lakini watendaji wao walipofika Ofisini hapo

kwa Mdhibiti walikuta Ofisi imeshafungwa na walimkuta mlinzi aliyewaambia warudi nayo

na waende siku ya pili yake.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji sababu zilizowapelekea Wizara kuchelewa hadi siku ya mwisho ambayo

ndiyo imetajwa kisheria, na kuelezwa kuwa, kulikuwa na mafunzo mafupi kutoka kwa

Mhasibu Mkuu wa Serikali, na hivyo walisubiri mafunzo hayo. Hata hivyo, Kamati

imejiridhisha kwamba, Wizara hawakuwajibika ipasavyo kwa kuandaa na kuwasilisha

hesabu zao kwa wakati na matokeo yake kuripotiwa usahihi wa kuchelewa kwao.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kurekebisha kasoro hiyo kwa miaka inayofuata.

Hoja Namba 64.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012

Taarifa ya Matumizi ya Kawaida na Maendeleo

Wizara iliidhinishiwa kufanya matumizi ya kawaida ya Tsh. 1,540,000,000 na fedha halisi

zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 1,754,310,000 sawa na asilimia 114 ya makadirio, ikiwa

ni ongezeko la Tsh. 214,310,000 sawa na ongezeko la asilimia 14 ya makadirio. Aidha,

matumizi ya maendeleo, Wizara iliidhinishiwa kutumia Tsh. 230,000,000/-, lakini mwisho

wa mwaka ulipofika, fedha zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh.224,450,000, sawa na

asilimia 97.6 ya makadirio, kukiwa na upungufu wa Tsh. 5,550,000 sawa na asilimia 2.4 ya

makadirio.

Majibu ya Wizara

Wizara hii iliieleza Kamati kuwa ongezeko la matumizi haya yametokana na kupandishwa

mishahara ya watendaji. Pia Kamati ilielezwa na Wizara kuwa upungufu wa fedha hizo

umetokana na Wizara ya Fedha kwa kuingiza fedha kinyume na makadirio ya Wizara hii.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kuwa kasoro ya uingizaji wa fedha ilisababishwa na Wizara ya Fedha

na inasikitishwa na utoaji wa fedha hizo kwa kutokuzingatia vipaumbele vya Wizara na

majukumu ama nafasi yao katika ujenzi wa taifa.

Page 29: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

29

Mapendekezo ya Kamati

Ingawa bajeti ya nchi hii ni „cash budget‟ bado Kamati inaitaka Serikali kuziingizia Taasisi

zake fedha za matumizi kwa mujibu wa makadirio ya Taasisi hizo hasa ikizingatiwa kuwa

Wizara ya Fedha ndio inayotoa ukomo „ceiling‟ ya makadirio hayo.

Hoja Namba 64.2 Malipo yasiokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu) Tsh. 5,152,000

Fedha hizo zimelipwa kwa matumizi mbali mbali lakini vielelezo vyake havikupatikana kwa

ukaguzi, kitendo ambacho kinakwenda kinyume na sheria ya Fedha na Kanuni zake.

Majibu ya Wizara

Vielelezo vyote vya matumizi yaliyotajwa kwenye hoja hii ikiwa ni pamoja na stakabadhi za

malipo vimeonekana baadae, isipokuwa kwamba hakukuwa na mawasiliano ya maandishi

baina ya Wizara husika na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Kufuatia kasoro hiyo Kamati ya Uongozi ya Wizara ilitoa maagizo yafuatayo kwa watendaji

wa Wizara hii:

i. Kujenga utamaduni wa kudai stakabadhi za malipo mara tu malipo yanapofanyika;

ii. Kuviimarisha Vitendo vya Manunuzi na Ukaguzi wa ndani ili viweze kutekeleza

majukumu yao ipasavyo kwa mujibu wa sheria;

iii. Kuimarisha mashirikiano ya kikazi kati ya Kitengo vya Manunuzi, Ukaguzi wa

Ndani na Uhasibu ili kuwe na uratibu mzuri wa masuala ya manunuzi;

iv. Ripoti za Ukaguzi wa Ndani zifanyiwe kazi ipasavyo ili kurekebisha kasoro

zinazojitokeza;

v. Wizara isimamie utaratibu wa kukagua “voucher; kabla ya malipo ili kuepuka hoja

zisizokuwa za lazima wakati wa ukaguzi;

vi. Uwekaji wa kumbu kumbu za hesabu uimarishwe, ikiwa pamoja na Vitengo vya

Uhasibu na Ununuzi kuweka namna bora ya uwekaji wa kumbu kumbu ili

kurahisisha shughuli za ukaguzi;

vii. Kamati ya Uchunguzi ihakikishe inafuatilia kwa karibu masuala yote yanayohusu

hesabu za Wizara na Kumshauri Katibu Mkuu ipasavyo, pamoja na kuhakikisha

kuwa inapatiwa na kupitia ripoti kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya Wakaguzi

wa Hesabu;

viii. Idara ya Uendeshaji na Utumishi iandae mafunzo kwa Wakurugenzi wote na Maafisa

Waandamizi wa Wizara juu ya sheria na kanuni za manunuzi na usimamizi wa fedha;

na

ix. Kuvitumia ipasavyo vikao vya “Entry Meeting” na “Exit Meeting” vinavyoitishwa na

wakaguzi ili kuepusha hoja zisizokuwa za msingi.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati imejiridhisha kuwa, Wizara haikufuata taratibu katika kuhifadhi vielelezo

vilivyotakiwa katika matumizi haya, kama Sheria ya Fedha ya mwaka 2005 inavyoelekeza.

Hivyo, Kamati inaitaka Wizara kufuata taratibu za kisheria inapofanya matumizi ya fedha za

Umma.

3.10. WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

3.10.1 OFISI YA MKURUGENZI WA MASHTAKA 2011/2012

Page 30: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

30

Hoja Namba 13.1: Uwasilishaji wa Hesabu kwa ajili ya Ukaguzi

Ukaguzi umebaini kuwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka haikuwasilisha hesabu za

mwaka, zinazojumuisha Mapato na Matumizi kama vifungu vya 24(2) na 8 vya Sheria ya

Fedha Namba 12/2005 vinavyoelekeza.

Majibu ya Ofisi

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ilikiri kosa la kutowasilisha hesabu kwa ajili ya ukaguzi

kwa kuwa Mhasibu aliyekuwepo wakati ule hakuwajibika ipasavyo katika kutekeleza

majukumu yake. Baada ya kupata Mhasibu mpya tatizo hilo limeondoka na kwa kuthibitisha

hilo katika mwaka wa fedha 2012/2013 Ofisi hii iliwasilisha hesabu hizo kwa wakati.

Uchunguzi wa Kamati:

Kamati ya P.A.C ilikubaliana na maelezo yaliyotolewa na Ofisi na hasa ikizingatiwa kuwa

kwa mwaka wa fedha uliofuata Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka iliwasilisha hesabu zake

kwa wakati.

Mapendekezo ya Kamati:

Kamati imewashauri Watendaji kuhakikisha kuwa wanatekeleza majukumu yao kama sheria

za nchi zinavyoelekeza.

Hoja Namba 46.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012

Taarifa ya Matumizi ya Kazi za Kawaida na Maendeleo

Ukaguzi umebaini kuwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ilitumia kwa kazi za kawaida

ongezeko la Tsh. 115,044,697/- sawa na asilimia 14.9 ya makadirio, kutokana na kukadiriwa

kutumia Tsh. 774,000,000 na hatimae ilipofikia Juni 2012, ilitumia Tsh. 889,044,697 sawa

na asilimia 114.9 ya makadirio. Kwa kazi za kawaida, ukaguzi umebaini kuwa Ofisi ya

Mkurugenzi wa Mashtaka ilitumia kwa kazi za maendeleo asilimia 100 ya makadirio ambazo

ni Tsh. 250,000,000.

Majibu ya Ofisi

Ofisi hii imeongeza matumizi ya ziada kwa kazi za kawaida kutokana na ongezeko la

mishahara na posho kwa watendaji. Ingawa kulikuwa na ongezeko hilo bado mishahara ya

Watendaji wa Ofisi hii ni midogo ukiliganisha na uzito wa majukumu yao. Jambo hili

linapelekea watendaji wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kuhama na kuisababishia Ofisi

hii kukosa watendaji waandamizi. Kuhusiana na tatizo ililolipata Ofisi kutokana na

kutokamilika kwa bajeti ya matumizi, Ofisi imeiarifu Kamati kuathiriwa kwa shughuli zake

mbali mbali ikiwa ni pamoja na kushindwa kuitumia Ofisi yao ya Makunduchi kwa kukosa

fedha, kama ilivyo tatizo la kutopewa OC kwa wakati.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ya PAC ilikubaliana na maelezo yaliyotolewa na Ofisi hii. Hii ni kutokana na kuwa

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka imebakiwa na mtendaji mmoja tu kati ya watendaji

waanzilishi wa Ofisi hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuyazingatia upya maslahi ya Watendaji wa Ofisi hii ili

wasiendelee kuhama ovyo pamoja na kuwaepusha kutenda vitendo viovu ikiwemo kupokea

rushwa.

Page 31: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

31

Hoja Namba 46.2 Malimbikizo ya Madeni Tsh. 93,637,950

Fedha hizo zinadaiwa na wafanyabiashara na taasisi mbali mbali kwa kutoa huduma zao kwa

Ofisi. Ukaguzi umebaini kuwa, madeni hayo ni ya muda mrefu na kuwepo kwake ni

kinyume na mfumo sahihi wa kiuhasibu unaotambua mapato na matumizi kwa fedha taslim

ambao unatumiwa na Mawizara ya Serikali.

Majibu ya Ofisi

Ni kweli Ofisi kutokana na kazi zake na umuhimu wa kazi zake imebidi iingie katika madeni

hayo. Hii ni kutokana na ufinyu wa bajeti inayotengewa Ofisi hii. Hata hivyo, Ofisi ya

Mkurugenzi wa Mashtaka imejitahidi kupunguza madeni hayo ingawa imeshindwa

kuyamaliza lakini kila hali inaporuhusu inajitahidi kupunguza kulipa madeni hayo kwa kiasi

kikubwa. Afisi hii hivi sasa imeondoa utaratibu wa kununua kwa mkopo na badala yake

imeamua kununua kwa fedha taslimu.

Jadweli lifuatalo linaonesha madeni yaliyosalia;

S/NO. MDAI MAELEZO KIASI KILICHOSALIA

1. Al Hilal Work Shop Ununuzi wa AC Tsh. 1,125,000

2. Majid Store Ununuzi wa Stationaries Tsh. 1,395,000

3. Masomo Book Shop Ununuzi wa Magazeti Tsh. 2,694,720

4. Masomo Book Shop Ununuzi wa Dictionary Tsh. 140,000

5. Penguin Refrigarator Matengenezo ya

Viyoyozi

Tsh. 349,000

6. Patel Import Export Ununuzi wa Mashine Tsh.290,000

7. Fire Rescue Force Ukaguzi wa Usalama wa

Moto

Tsh. 840,000

8. Moh‟d Ngweshani Ununuzi wa Vifaa vya

Gari

Tsh. 260,000

9. Omar S. Mtwana Kutengeneza Samani Tsh. 698,800

10. Abdulrahman Khamis

Juma

Matengenezo ya

Nyumba ya Naibu

Mkurugenzi wa

Mashtaka

Tsh. 6,800,000

11. Ramadhan S.

Abdallah

Utengenezaji wa Meza

na Viti

Tsh. 2,514,000

12. KMKM Ujenzi wa Jengo la

Maktaba

Tsh. 36,000,000

13. Hassan & Sons Ununuzi wa Vipasola Tsh. 4,000,000

14. Arkam Household

and Office Furniture

Ununuzi wa Samani Tsh. 2,800,000

JUMLA YA DENI LILILOSALIA NI TSH. 59,906,520

Uchunguzi wa Kamati

Tatizo kubwa la madeni la Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka linachangiwa na bajeti ndogo

wanayopatiwa na Serikali. Kamati imeelezwa kuwa, OC huingizwa kati kati ya mwezi na

hukabidhiwa katika mazingira magumu, hali inayokwamisha na kukosesha ufanisi wa

utekelezaji wa majukumu ya Ofisi hasa inapokuja Mahakama ya Rufani, kwa Ofisi

kushindwa kupata fedha za kutosha za maandalizi ya kesi zake mbele ya Mahakama hiyo.

Page 32: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

32

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuangalia kipaumbele cha kuwapa fedha kamili Ofisi hii ili iweze

kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa.

3.10.2 AFISI YA MRAJIS MKUU WA SERIKALI (WAKALA WA USAJILI WA

BIASHARA NA MALI)

Hoja Namba 44.3.1 Malimbikizo ya madeni, Tsh. 29,984,800

Fedha hizo zinadaiwa na wafanya biashara pamoja na taasisi mbali mbali kwa ajili ya

utowaji wa huduma tofauti kwa Afisi ya Mrajis Mkuu wa Serikali, lakini ukaguzi umebaini

kuwa madeni hayo ni ya muda mrefu na kuwepo kwake ni kinyume na mfumo sahihi wa

kiuhasibu unaotambua mapato na matumizi kwa fedha taslmi ambao unatumika kwa

Mawizara ya Serikali. Aidha, madeni hayo yanatokana na Tsh. 6,000,000 kwa ajili ya

uchapaji wa fomu za kuhaulisha, Tsh. 18,000,000 kuhusiana na uchapishaji wa vyeti vya

uzazi na Tsh. 5,984,800 kwa ununuzi wa zulia

Majibu ya Afisi

Ni kweli deni hilo lilikuwepo, ila sasa tayari Afisi imeshalipa. Aidha, deni la Tsh. 6,000,000

halikuwa halali kutokana na ukweli kuwa, hawakuzihitaji fomu hizo kutokana na suala la

uhaulishaji kuhamishiwa kwa Bodi ya Uhaulishaji wa Ardhi. Vile vile deni la Tsh. 5,984,800

ambalo kimsingi lingelipaswa lilipwe na Wizara ya Fedha kwa kuwa suala la ununuzi wa

zulia lilihitajika kutokana na kuhamishiwa kutoka jengo lao la awali la Mambo Msiige, hadi

jengo la sasa la zamani la Benki ya Watu wa Zanzibar. Hata hivyo, hivi sasa wamekubaliana

kuwa deni hilo litalipwa na Wizara ya Katiba na Sheria.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji iwepo Afisi imeshawasiliana na Idara ya Uchapaji kuhusiana na deni hilo

wanalosema hawalikubali, na kuelezwa na Afisi hii kuwa, deni hilo lilikuja baada ya miaka

miwili tokea walipowataka wawafanyie fomu hizo kwa Idara kuleta barua yenye „Invoice‟ ya

deni hilo. Aidha, Kamati imewataka Afisi wathibitishe iwapo nao walijibu kwa barua na

kuelezwa kuwa hawana hakina kama walijibu kwa barua, ila mawasiliano yalikuwepo baina

yao.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati iliitaka Afisi kuandika barua kwa Idara ya ya Upigaji Chapa kuwaeleza kuhusiana na

deni hilo na nakla ya barua hiyo iwasilishwe kwa Kamati.

Aidha, Kamati inaitaka Wizara au hata Afisi ihakikishe deni lililobakia la ununuzi wa zulia

linalipwa.

3.11 WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI

Hoja Namba 65.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012

Taarifa ya Makadirio ya Mapato na Matumizi

Mapato yaliyokadiriwa kukusanywa na Wizara hii kwa mwaka 2011/2012 ni Tsh.

240,000,000 na fedha halisi iliyokusanywa ni Tsh. 539,752,000 sawa na asilimia 225 ya

makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 299,752,000 sawa na asilimia 125 ya makadirio.

Aidha, Wizara iliidhinishiwa kufanya matumizi ya kawaida ya Tsh. 6,923,000,000 na fedha

halisi zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 8,456,604,481 sawa na asilimia 122.2 ya

makadirio, ikiwa ni ongezeko la Tsh.1,533,604,481 sawa na oasilimia 22.2 ya makadirio.

Vile vile, matumizi ya maendeleo, yaliidhinishiwa kwa Tsh. 3,600,000,000/-, lakini fedha

Page 33: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

33

zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 3,313,552,544, sawa na asilimia 92 ya makadirio,

kukiwa na upungufu wa Tsh. 286,447,456 sawa na asilimia 8 ya makadirio.

Majibu ya Wizara

Wizara hii iliieleza Kamati kuwa ongezeko la mapato hayo yametokana na kufanyika kwa

mapitio kwa vianzio vyake pamoja na Wizara kubaini mashamba mapya ya mikarafuu na

minazi baada ya kupata taarifa kutoka Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati na hatimae

mashamba hayo kukodishwa kwa wananchi. Aidha, Wizara iliongeza bei kwa baadhi ya

vianzio vyake.

Majibu wa Wizara

Kamati ya PAC ilielezwa na Wizara ya Kilimo na Maliasili kuwa, Wizara hii ililazimika

kutumia zaidi ya makadirio iliyokadiriwa kutokana na ongezeko la mishahara na maposho ya

Watendaji wake baada ya Serikali kuongeza mishahara hiyo.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati hii iliridhika na majibu ya Wizara, hata hivyo, pamoja na kuridhika kwake imeitaka

Wizara kuendelea kuchukua juhudi za makusudi za kufuatilia mashamba ya Serikali ili

kuweza kujua idadi halisi ya mashamba yake jambo ambalo litasaidia kuongezeka kwa

mapato ya nchi.

Aidha, Kamati imeitaka Wizara kuzalisha miche mbali mbali ya mazao kwa kutafuta miche

bora ili kuepusha hasara za makusudi.

Pia, imeitaka Wizara kuwachukulia hatua wale wote wanaohujumu miti ya mikarafuu ili

kulinda hadhi ya mazao hayo

Hoja Namba 65.2 Mali hazikuoneshwa katika hesabu za mwaka Tsh. 29,886,000

Ukaguzi umebaini kuwepo kwa vyombo/magari ambayo yanamilikiwa na Wizara, lakini

hayakuoneshwa katika hesabu za mwaka (Financial Statement) wakati kufanya hivyo

kunaweza kusababisha upotevu wa mali za Serikali pia ni kwenda kinyume na Sheria na

Kanuni za ufungaji wa hesabu.

Majibu ya Wizara

Wizara hii ilikiri kwamba kuna baadhi ya vifaa, vyombo ambavyo vinamilikiwa na Wizara

havikuoneshwa katika Ripoti ya Hesabu za Fedha (Financial Statement) ya mwaka

2011/2012. Kadhia hii imechangiwa na kasoro ya uwekaji wa kumbukumbu, hata hivyo

hatua madhubuti tayari zimechukuliwa kwa kufanya mapitio ya vifaa vyote na kuviingiza

katika vitabu vya kumbukumbu (Asset Registry). Pamoja na hatua hiyo, Wizara imejipanga

kuwajengea uwezo watendaji wake wanaohusika na uwekaji wa kumbukumbu na usimamizi

madhubuti wa fedha na mali za Serikali kwa kuwapatia mafunzo.

Vile vile, Wizara ya Kilimo na Maliasili iliieleza Kamati kuwa gari aina ya Toyota Land

Cruiser SMZ 6927 haipo katika mamlaka yake na hivi sasa ipo chini ya Ofisi ya Makamu wa

Kwanza wa Rais na inatumiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo. Kitendo hiki

kimetokea baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo na Maliasili Ndg.

Islam Seif kuhamishiwa katika Ofisi hiyo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati katika kufuatilia suala hili imebaini kuwa vifaa hivyo ni kweli vimeingizwa baada ya

ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kufanyika. Hata hivyo,

Page 34: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

34

uingizwaji huo unakabiliwa na baadhi ya kasoro kama vile vifaa kukosa thamani halisi

nakadhalika.

Aidha, Kamati imebaini kuwa Serikali inazivunja sheria tulizozitunga wenyewe. Hii ni

kutokana na agizo la Katibu Mkuu Kiongozi Ndg. Abdulhamid Yahya Mzee la kuwataka

watendaji wa Wizara hii kuipeleka gari katika Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais bila ya

kuwepo kumbukumbu yoyote ya barua inayoonesha kuhamishiwa gari hilo katika Ofisi hiyo.

Vile vile, katika majibu ya Wizara, Kamati ilibaini kuwa kuna upungufu wa vespa moja

ukilinganisha na idadi ya vespa zilizoainishwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti.

Mapendekezo ya Kamati

Taasisi za Serikali zijitahidi kufuata sheria za nchi ili kuepusha kasoro zisizo za lazima.

Aidha, Wizara ya Kilimo na Maliasili ihakikishe kuwa kunakuwepo na kumbukumbu rasmi

zinazothibitisha kuwa gari aina ya Toyota Land Cruiser SMZ 6927 haipo katika mamlaka

yake na badala yake ipo chini mamlaka ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

3.12 WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Hoja Namba 57.2 Vifaa ambavyo havikuingizwa katika daftari la ghalani, Tsh.

61,717,700

Fedha hizo zimetumika kwa kununua vifaa mbali mbali kwa matumiszi ya Ofisi, lakini vifaa

hivyo havikuingizwa kwenye daftari la vifaa vya ghalani ili kuweza kuthibitisha uhalali wa

mapokezi pamoja na matumizi yake, kinyume na kanuni ya 198 ya Kanuni za Fedha za

mwaka 2005.

Majibu ya Wizara

Wizara inathibitisha kuwa vifaa vyote vyenye thamani iliyotajwa katika hoja hii,

vilinunuliwa na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa na vifaa hivyo vimeingizwa katika

daftari la ghalani. Aidha, fedha zote hizo zimetumika kwa usahihi na vifaa vyote

vimesharikodiwa katika daftari la ghalani na lipo tayari kwa ukaguzi wa Kamati.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kuwa hoja ya Mkaguzi inasimama katika usahihi wake, hata kama

Wizara itafanya masawazisho baada ya ukaguzi huo. Vile vile Kamati imejiridhisha baada ya

kuzipitia hati za malipo kuwemo na kasoro nyingi za kihesabu ikiwa ni pamoja na hati hizo

za malipo kukosa vielelezo vilivyokamilika, kama vile ilivyokuwa kwa baadhi ya risiti

zilizoambatanishwa kutokuwa na sifa zinazokubalika, ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa

namba ya usajili wa ZRB (Tin Number) na pia baadhi ya hati hizo za malipo hazina saini ya

Afisa Mhasibu.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kufuata taratibu za kuingiza taarifa za vifaa wanavyovinunua katika

daftari la ghalani. Aidha, Kamati inaitaka Wizara kufuata Sheria katika matumizi ya fedha za

Serikali, ikiwa ni pamoja na kufanya manunuzi kwa mujibu wa taratibu za Kisheria.

Hoja Namba 57.3.1 Mradi wa Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa

Pwani (MACEMP), Fedha zilizotumika kinyume na malengo, Tsh. 136,000,000

Tsh. 216,000,000 ziliingizwa kwa ajili ya kuendesha shughuli za mradi wa usimamizi wa

mazingira ya bahari na ukanda wa pwani kwa kipindi cha mwaka 2011/2012. Ukaguzi

Page 35: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

35

umebaini kuwa Tsh. 136,000,000 hazikutumika kwa lengo lililokusudiwa, hali iliyopelekea

malengo yaliyokusudiwa kutofikiwa.

Majibu ya Wizara

Mradi ulifanya matumizi ya fedha kwa mujibu wa malengo yaliyopangwa na mradi ulipokea

fedha hizo kutoka Wizarani kwa hati namba M10/1/2012 yenye thamani ya Tsh. 56,000,000,

kwa hati namba M20/2/2012 yenye thamani ya Tsh. 38,000,000 na hati namba M26/3/2012

yenye thamani ya Tsh. 42,000,000 ambazo zote zinafanya jumla ya Tsh. 136,000,000.

Aidha, Tsh. 56,000,000 zilitumika kwa ujenzi wa msingi wa jengo la ghorofa tatu la Ofisi ya

Wizara hii, badala ya ghorofa moja iliyokuwa katika bajeti ya awali na mchango kwa

„Marine Legacy Fund,‟ fedha ambazo ni mchango wa Serikali. Hivyo Tsh. 36,000,000

zilitumika kwa ujenzi wa jengo la Wizara, Unguja na Tsh. 20,000,000 zilitumika kama

mchango wa „Marine Legacy Fund‟ iliyoanzishwa, ili fedha hizo zitumike kuendeleza kazi

zilizofanywa na mradi wa MACEMP baada ya mradi kumalizika na sio Mamlaka ya Bahari

Kuu, kama ilivyoelezwa na Mkaguzi.

Vile vile, Tsh. 38,000,000 zilitumika kwa mgawanyo wa matumizi ya Tsh. 21,500,000

kutumika kwa ujenzi wa jengo la Wizara Unguja na Tsh. 16,500,000 kununuliwa samani za

majengo ya Wizara, Unguja na Pemba.

Katika matumizi ya Tsh. 42,000,000, jumla ya Tsh. 16,000,000 ilikuwa ni mchango wa

Serikali kwa ajili ya kuanzisha „Marine Legacy Fund‟, Tsh. 17,000,000 zilitumika kwa

manunuzi ya mashine na boti kwa ajili ya Idara ya Uvuvi (MCS) na Tsh. 9,998,966

zilitumika kwa ununuzi wa mafuta yaliyopelekwa Idara ya Uvuvi kwa ajili ya Doria.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na majibu ya Wizara, Kamati imekubaliana kuwa, kwa hoja hii ilivyo na majibu ya

Wizara yakitofautiana na maelekezo ya Mkaguzi, ni vyema Kamati ipatiwe ufafanuzi wa

kina kuhusu mradi huu na namna fedha zake zilivyotumika na sio kupata majibu ya jumla

jumla kama yalivyotolewa. Hivyo, pamoja na taarifa hizo zinazohitajika kwa Kamati,

Kamati pia imeelekeza kupatiwa maelezo ya Mradi kwa ukamilifu na ushahidi wa vielelezo

kwa kila maelezo yatakayotolewa, na baada ya kupatikana taarifa hizo, yawasilishwe kwa

Kamati. Hata hivyo, hadi tunaandika taarifa hii, maelekezo hayo ya Kamati yalikuwa bado

hayajatekelezwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuheshimu maelekezo ya Kamati kwa kuipatia taarifa inazozihitaji.

Aidha, Kamati inahitaji muda zaidi wa kuifanyia kazi hoja hii na kutoa taarifa yake.

3.13 AFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI –

BLM

Hoja Namba 17.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012

Taarifa ya Matumizi ya kawaida na maendeleo

Afisi iliidhinishiwa kufanya matumizi ya kawaida ya Tsh. 964,913,351 na fedha halisi

zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 964,997,151 sawa na asilimia 100 ya makadirio.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Katika kufuatilia hoja Kamati haikupata mashirikiano mazuri kutoka kwa Afisi husika

ingawa baadhi ya watendaji walihudhuria kikao hicho. Hii ni kutokana na kuwa Naibu

Page 36: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

36

Katibu Mkuu Ndg. Salmin Amour Abdalla ambaye ni Afisa Masuul alikuwa safarini na

alishindwa kutoa taarifa mbele ya Kamati hii. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu Ndg. Salum

Maulid Kibanzi, aliishauri Kamati hii kutoa majibu ya Afisi hiyo kwa niaba ya Naibu Katibu

Mkuu, hata hivyo, Kamati ya PAC iliukataa ushauri huo kwa kuwa Ndg. Salum sio Afisa

Mas ul wa Afisi hiyo. Baada ya majadiliano makubwa Kamati iliamua kupokea taarifa ya

Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora ingawa ratiba ya kazi ya siku hiyo, ilikuwa inaigusa

moja kwa moja Afisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Pamoja na kuwasilishwa kwa taarifa hiyo Kamati ya PAC iligundua kuwa Afisi hiyo

haikuwa na maandalizi mazuri kwani takriban masuala mengi yaliyoulizwa yalikosa majibu

ya uhakika na hivyo Kamati iliitaka Afisi hii kuwasilisha taarifa zake kwa maandishi kwa

yale maeneo ambayo yalikosa majibu. Kwa masikitiko makubwa hadi tunawasilisha taarifa

hii hakuna taarifa yoyote iliyowasilishwa mbele ya Kamati.

Kwa msingi huo hoja hiyo haikujibika, hivyo maafisa wanaohusika wafike mbele ya Kamati

kwa kujibu hoja hizo.

TAARIFA YA UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA NA MAMLAKA ZA

SERIKALI, KWA MWAKA 2011/2012

4.0 MAMLAKA YA MAJI (ZAWA)

Hoja Namba 74.1 Uwezo wa Mamlaka kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi

na uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Mamlaka ya Maji ilikuwa na mali za mpito za 6,462,608,268 na

dhima za mpito za 393,629,848 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 6,068,978,420 na uwezo wa

kulipa dhima kwa ratio ya 16.4:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa wengi

wa Malmaka na ikishauriwa kuongeza kukusanya mapato kutoka kwa wadaiwa.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 10,793,844,809 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 15,653,307,963 na hivyo kuendeshwa kwa hasara ya Tsh. 4,859,463,154

ambayo imepanda kwa tofauti ya Tsh. 392,305,263 sawa na 8.8% kwa mwaka

ikilinganishwa na mwaka 2010/2011.

Majibu ya Mamlaka

Wameupokea ushauri wa kuongeza mapato kwa kuongeza wigo wa ukusanyaji kupitia

wateja wakubwa kwa kuwafungia mita pamoja na wateja mbali mbali wanaopata huduma ya

maji. Aidha, imejipanga kuwaondoa katika orodha wateja wasiopata huduma ya maji katika

orodha ya wateja wanaotakiwa kulipia huduma hiyo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imegundua kuwa Mamlaka bado haijachukua hatua madhubuti za kukusanya mapato

kwa wateja wakubwa ikiwa ni pamoja na kuwafungia mita za matumizi ya maji, ingawa

imeanza kuchukua hatua hizo. Aidha, bado Mamlaka haijaweza kuwapatia wananchi wote

huduma ya maji.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kutekeleza kwa vitendo kwa kuwaondoa wananchi

wasiopata huduma ya maji katika orodha ya wateja wanaotakiwa kulipia huduma

hiyo.

Page 37: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

37

Kamati inawapongeza kwa kuchukua hatua za kuwakatia huduma ya maji wateja

wote ambao hawalipii maji na kuwataka waendeleze kuchukua hatua hizo na hata

taasisi za Serikali ambazo hazilipii huduma hiyo.

Kamati inaishauri Serikali kuisaidia Mamlaka katika kulipia deni la umeme.

Mamlaka liwe na mipango madhubuti ya kukusanya mapato, ili kuwa na uwezo wa

kujiendelesha.

Hoja Namba 74.2 Wadaiwa wa Mamlaka kwa deni la Tsh. 8,784,017,613.82

Ukaguzi umebaini kuwa, Mamlaka inadai watu binafsi na taasisi mbali mbali kwa kutoa

huduma ya maji bila ya kulipwa, kinyume na Sheria Namba 5 ya mwaka 2006 na kanuni za

Mamlaka za mwaka 2007.

Majibu ya Mamlaka

Kweli deni hilo limetokana na tokea kuanzishwa kwa Mamlaka. Hata hivyo, hivi sasa

wamechukua hatua ya kulipunguza deni hilo kwa kuchukua hatua mbali mbali za kuwakatia

maji wateja wasiolipa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imegundua kuwa, tatizo la Mamlaka kutofunga mita kwa wateja wake wote

wanaopata huduma ya maji, ikiwa ni pamoja na wateja wakubwa kunachangia sana

kulimbikizwa kwa madeni hayo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kuharakisha ufungaji wa mita kwa wateja wake na kuchukua hatua

za kuwakatia huduma ya maji wateja wote wenye madeni. Aidha, Kamati inaishauri Serikali

kulipa deni la umeme inalodaiwa Mamlaka.

4.1 SHIRIKA LA MELI NA UWAKALA

Hoja Namba 76.1 Uwezo wa Shirika kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Shirika lilikuwa na mali za mpito za 331,420,988.90 na dhima za

mpito za 326,189,256.08 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 5,231,732.90 na uwezo wa kulipa

dhima kwa ratio ya 1.01:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa deni la benki na deni la

taasisi nyengine.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 3,535,594,558.59 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 2,731,354,038.59 na hivyo kuendeshwa kwa faida ya Tsh. 804,240,520

ambayo imepanda kwa tofauti ya Tsh. 498,187,980.89 sawa na 163% kwa mwaka

ikilinganishwa na mwaka 2010/2011.

Majibu ya Shirika

Sababu kubwa iliyopelekea hali hiyo ni kulazimika kulipa madeni ya USD 150,000 kwa

Benki ya Watu wa Zanzibar na USD 65,000 walilokuwa wanadaiwa na GAPCO. Hata hivyo,

hivi sasa Shirika halina madeni ya namna hiyo , ila madeni ya mzunguko tu.

Kuhusiana na kupunguza gharama, Shirika limechukua hatua za kurekebisha muundo wake

kwa kuwapa kazi hiyo Chuo cha Uongozi wa Fedha kilichopo Chwaka kwa ajili ya kufanya

uchunguzi wa Shirika kujiendesha kibiashara, kuandaa mpango wa Shirika kujiendesha

kibiashara na kutayarisha mpango mkakati wa Shirika kwa miaka minne. Hata hivyo, Shirika

bado halijakabidhiwa ripoti hiyo.

Page 38: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

38

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, Shirika linadaiwa na Shirika la Bandari fedha nyingi na ni

deni la muda mrefu na limethibitishwa na Shirika la Bandari wakati Kamati ilipofika katika

Shirika hilo, ingawa wakati wa mjadala na Shirika la Meli uongozi wake ulieleza kuwa

hakuna uthibitisho wa deni hilo.

Kamati imehitaji kufanya ukaguzi angalau wa stakabadhi za karibuni za Shirika hili

kuwalipa Benki ya Watu wa Zanzibar, ingawaje mpaka tunaandika ripoti hii, hakuna

uthibitisho ulioletwa mbele ya Kamati. Aidha, Kamati ilipohitaji taarifa za matumizi ya

Kikao cha Bodi ya Wakurugenzi cha Shirika, imeelezwa kukutana kwake mara 4 kwa

mwaka kwa vikao vya kawaida lakini kuna zaidi ya vikao hivyo vinavyofanyika kwa njia ya

dharura na wajumbe wake wanafanya ziara ndani na nje ya Tanzania.

Mapendekezo ya Kamati

Shirika lisimamie ipasavyo ushauri wa kupunguza gharama za matumizi hasa katika

uendeshaji wa shughuli za Bodi ya Wakurugenzi kwa kupunguza wingi wa vikao na safari

zisizo za lazima.

Hoja Namba 76. 2 Kuajiriwa kwa Mfanyakazi wa Kigeni

Shirika limemuajiri Mfanyakazi wa Kigeni Ndg. Abdalla Moh‟d Mwakidudu kutoka Kenya

kwa mshahara wa USD 1,000 kwa mwezi. Mfanyakazi huyo ameajiriwa bila ya kuwepo

kibali cha ukaazi na kutokuwepo kwa ruhusa ya ajira yake kutoka Idara ya Kazi, aidha,

mshahara wake haukatwi kodi ya mapato.

Majibu ya Shirika

Ni kweli Shirika limeajiri mfanyakazi huyo kutokana na kuwa na matatizo ya breakdown ya

mara kwa mara katika meli zake na wamefanya hivyo ili kupunguza gharama za

matengenezo yake kutokana na kukosa mtaalamu wa aina hiyo hapa Tanzania. Shirika

limefunga mkataba na mfanyakazi huyo na tayari wameshachukua hatua za kumtaka alipe

kodi Serikalini.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imegundua kuwa, wafanyakazi hao sio mmoja kama ilivyoelezwa na ripoti ya

Ukaguzi, bali ni watatu ambao ni Ndg. Peter Oguti Wanyama, Ndg. Thomas Msemwa na

Ndg. Abdalla Moh‟d Mwakidudu.

Kamati imejiridhisha kupitia vocha zao za malipo kwamba sasa wanakwatwa kodi na pia

barua ya kuombewa kibali cha kazi kupitia barua ya tarehe 24/04/2014.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inayataka Mashirika ya Serikali kutoa kipaumbele zaidi kwa wafanyakazi wazalendo

na ikibidi kuajiriwa wageni, basi ni lazima wafuate ipasavyo taratibu za kisheria.

4.2 SHIRIKA LA BANDARI

Hoja Namba 75.1 Uwezo wa Shirika kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Shirika lilikuwa na mali za mpito za 10,089,038,751.26 na dhima

za mpito za 1,993,582,704.80 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 8,095,456,046.46 na uwezo wa

kulipa dhima kwa ratio ya 5:1, hali iliyochangiwa zaidi na uwekaji wa fedha benki katika

muda maalum (fixed deposit).

Page 39: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

39

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 15,714,578,510.11 na

matumizi yake yalikuwa Tsh. 14,742,721,238.21 na hivyo kuendeshwa kwa faida ya Tsh.

971,857,271.90 ambayo ni ongezeko la Tsh. 842,518,310.04 wastani wa 651 kwa mwaka.

Majibu ya Shirika

Katika kuhakikisha Shirika linaongeza mapato, juhudi mbali mbali zimechukuliwa ikiwa ni

pamoja na kudhibiti vianzio vya mapato. Shirika limefanya mapitio ya viwango vya tozo

(tariff) na kutoza kwa mujibu wa wakati, ambapo viwango hivyo vipya vimesaidia sana

kuongeza mapato.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalishauri Shirika kuongeza juhudi ya makusanyo na kupunguza gharama za

uendeshaji, ili liweze kujiendesha kwa faida.

Hoja Namba 75.1.1 Wadaiwa wa Shirika kwa Taasisi za Serikali, Tsh. 464,465,927 na

USD 843,756.82

Fedha hizo zinadaiwa na Shirika kwa Taasisi mbali mbali za Serikali pamoja na Kampuni na

watu binafsi kwa huduma mbali mbali zilizotolewa na Shirika, lakini madeni hayo

hayajalipwa kwa muda mrefu sasa.

Majibu ya Shirika

Madeni hayo ni ya muda mrefu na baadhi yao hayana vielelezo vya kuyathibitisha.

Waliandika barua kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, tarehe 30/07/2013 yenye kumbu

kumbu namba ZPC/MYS/C.16/VOL III/147, kuomba muongozo wa kisheria kwa ufutwaji

wake, lakini hawakupata majibu yoyote. Aidha, kwa kupitia Makamo wa Pili, waliweka

miadi ya kuonana nae na kujaribu kuwaandikia baadhi ya wadaiwa ikiwa ni pamoja na

KMKM, ila hakuna mafanikio.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha juu ya hatua walizozichukua Shirika katika kutafuta hatua za kusafisha

madeni hayo. Aidha, Kamati pia nayo ilichukua hatua ya kuishauri Serikali kuhusiana na

ufutwaji wa madeni ya namna hiyo kisheria, lakini mpaka leo hakuna hatua zilizochukuliwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuchukua hatua za makusudi na haraka kuyawasilisha madeni

yasiyolipika na ya muda mrefu Barazani kwa hatua za kuyafuta kabla ya Kikao cha Bajeti.

Hoja Namba 75.2 Ukiukwaji wa Sheria na Muongozo wa Manunuzi, Tsh.

856,264,185.92

Lishirika limefanya manunuzi ya vitu mbali mbali kwa matumizi ya Shirika lakini manunuzi

hayo hayajafuata taratibu za Sheria na muongozo wa manunuzi, kinyume na kifungu cha

6(1) na 73 cha Sheria ya Manunuzi ya mwaka 2005.

Majibu ya Shirika

Fedha hizo zimetumika kwa matengenezo ya „burgee‟ kubwa na wamevinunua vifaa vya

matengenezo yake kutoka Damen Shipyards, Kampuni ambayo ndiyo iliyotengeneza burgee

hiyo na wamefanya hivyo kwa sababu ni kampuni hii pekee ndiyo iliyohusika na burgee

hiyo.

Page 40: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

40

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imesikiliza hoja za Shirika na imeridhika kuwepo haja ya kununuliwa vifaa hivyo

kutoka Damen Shipyards, lakini Shirika linapaswa kufuata taratibu za kisheria ambazo nazo

zinaruhusu kwa mazingira maalumu kufanywa ununuzi kutoka kwa Kampuni ama mtoa

huduma mmoja. Aidha, kutokana na kuvunjwa kwa taratibu za sheria katika ununuzi huo,

Kamati haikuridhishwa na hatua hiyo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalitaka Shirika lifuate taratibu za kisheria katika kutumia fedha za umma.

Hoja Namba 75.3 Malipo yaliyofanywa kinyume na utaratibu , Tsh. 56,891,500

Fedha hizo zimelipwa kwa matumizi mbali mbali ya Shirika, lakini stakabadhi

zilizothibitisha kupokea malipo hayo hazikubaliki kwa mujibu wa Sheria.

Majibu ya Shirika

Shirika halioni kuwepo kwa kosa lolote katika stakabadhi hizo ambazo zinatoka Sami

Trader, ambaye katika risiti zake zimo Tin Numbers na Namba za ZRB kuonesha kuwa

mfanya biashara huyu analipa kodi.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati nayo imezipitia risiti hizo na kujiridhisha kuwa, zimo tin namba 104-704-603 na

namba za ZRB, ambazo ni ZRB/03/LCA/271.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inapendekeza kuwa hoja hii ifutwe.

4.3 BODI YA MAPATO YA ZANZIBAR (ZRB)

Hoja Namba 82.1 Uwezo wa Bodi kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

Uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Bodi ilikuwa na mali za mpito za 546,302,494 na dhima za mpito

za 208,718,033 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 337,584,461 na uwezo wa kulipa dhima kwa

ratio ya 2.6:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa pamoja na salio la benki na

hivyo ni faraja kwa Bodi.

Mapato ya Bodi kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 5,495,692,118 na matumizi yake

yalikuwa Tsh. 4,691,543,773 na hivyo kuendeshwa kwa faida ya Tsh. 804,148,345 ambayo

imeshuka kwa tofauti ya Tsh. 277,976,439 sawa na 25.7% kwa mwaka ikilinganishwa na

mwaka 2010/2011.

Majibu ya Bodi

Kuhusiana na takwimu zilizoelezwa na Mdhibiti kuhusiana na uwezo wa Bodi kujiendesha,

zinahitaji kupatiwa usahihi wake kwa kuwa Bodi imeeleza kuwa hazina usahihi.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imesikiliza maelezo ya Bodi na kumtaka Afisa wa Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi

Mkuu wa Hesabu za Serikali anaefuatana na Kamati kulifuatilia zaidi suala hili ili lipatiwe

usahihi wake.

Page 41: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

41

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inamshauri Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu kutayarisha vyema taarifa zake

ili ziweze kueleweka kwa wepesi na usahihi na Kamati iweze kuzifanyia kazi kwa uhakika.

Hoja Namba 82.2 Malipo ya ziada kwa ujenzi wa jengo jipya la Mazizini, Tsh.

2,387,492,229.85

Bodi ilifunga Mkataba na China Railways Co. Ltd kwa barua yenye kumbu kumbu namba

ZRB/C.3/VOL.1/48 kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo, huku bei ya ujenzi mpaka kukamilika

kwake ni Tsh. 6,216,820,414.69 kwa muda wa wiki 104 tokea tarehe ya kuanza kazi,

10/07/2009. Aidha, mpaka ilipofikia mwisho wa mwaka 2012, Bodi imeshalipa Tsh.

8,604,312,644.54 ikiwa ni ongezeko la Tsh. 2,387,492,229.85 zaidi ya makubaliano ya

mwanzo ya mkataba wa ujenzi ambapo bado malipo hayo yataendelea kulipwa katika

mwaka wa fedha 2012/2013 na kuongezeka kwa gharama za ujenzi.

Majibu ya Bodi

Uongozi wa Bodi ulilazimika kujenga jengo la Afisi zake katika eneo la Kilimani kwa

thamani ya Tsh. 6,488,171,072, na taratibu zote za tenda zilikuwa zimekamilika. Hata hivyo,

Mshauri Mwelekezi alishauri ujenzi huo usifanyike hapo kutokana na kupitishwa kwa mtaro

mkubwa wa kuondosha maji ya mvua, hatua iliyopeleka Serikali kupatiwa kiwanja chengine

Mazizini.

Hatua hii ililazimu kufanywa marekebisho katika ujenzi wa Mazizini kwa kuongeza ghorofa

moja katika sehemu ya nyuma ya jengo, kubadilisha „structure‟ za „patrons‟ (material and

designs) tofauti na mchoro wa awali, kubadilisha mfumo wa umeme, kuongeza na mambo

mengine.

Hivyo, ni kweli kuna ongezeko la Tsh. 2,387,492,229.85 na kufanya gharama hizo kuwa

Tsh. 8,604,312,644.45 badala ya Tsh. 6,216,820,414 zilizokisiwa awali kwa ujenzi

uliotarajiwa kufanyika Kilimani. Aidha, kiwango cha malipo alichokwishalipwa Mjenzi ni

Tsh. 8,392,755,072.87 na fedha zilizosalia kulipwa hadi kukabidhiwa jengo ni Tsh.

211,557,571.57 na Uongozi wa Bodi uliwasiliana na Bodi ya Wakurugenzi kuhusiana na

mabadiliko hayo ili kupata idhini iliyotakiwa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji taratibu za sheria ya manunuzi kama zimefuatwa katika upatikanaji wa

Mshauri Mwelekezi na Mjenzi. Na kwa upande wa upatikanaji wa Mshauri Mwenyekezi,

Ndg. Ramadhan Mussa Bakar (Rama China), Kamati imejiridhisha kwamba, haukufuatwa

utaratibu kwa sababu yeye sio Kampuni bali alielezwa kama mtu binafsi. Aidha, Kamati

imejiridhisha kuwa, Ndg. Rama China alikuwemo katika Kamati ya Tathmini na amealikwa

kama mataalamu wala sio kwamba, amepatikana kwa taratibu za kisheria kama Mshauri

Mwelekezi na badala yake, Bodi imetafuta Mtaalamu Mwelekezi mwengine.

Kuhusiana na ujenzi, Kamati ilihitaji kupatiwa Mkataba wa Mkandarasi wa ujenzi wa

Kilimani na taratibu za kupatikana kwake.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati iliutaka Uongozi wa Bodi kufuatilia ipasavyo Sheria na Kanuni za manunuzi, ili

kuepusha hasara kwa Serikali. Aidha, Kamati inaishauri Serikali kuwa makini na Washauri

Elekezi wa kigeni ambao baadhi yao huwa sio waaminifu na hushirikiana na Mjenzi katika

kuhujumu fedha za Umma.

Page 42: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

42

Hoja Namba 82.3 Vifaa vya Tsh. 21,529,000 ambavyo havikuingizwa katika Daftari

la ghalani.

Fedha hizo zimetumika kwa ununuzi wa vifaa mbali mbali lakini havikuingizwa katika

daftari la ghalani na kupelekea kushindwa kuthibitishwa uhalali wake.

Majibu ya Bodi

Ni kweli vifaa hivyo havikuingizwa kutokana na haja ya kuepuka gharama kwa kampuni

mbili tofauti kwa ajili ya ununuzi na kufanya „installation‟. Bodi iliona ni vyema kutumia

kampuni moja itakayofanya kazi zote mbili chini ya „guarantee‟ ya vifaa walivyowauzia,

kwani kampuni hizo ndizo zilizotumika kwa baadhi ya maeneo ya ujenzi.

Pia vifaa hivyo havikuingizwa katika daftari kutokana na uharaka uliojitokeza kwa wakati

huo ili kupata vifaa vitakavyosaidia kukwamua changamoto za dharura zilizojitokeza kipindi

hicho.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na fedha za ununuzi wa vifaa hivyo kupewa Mjenzi, vifaa hivyo vinatakiwa

kurikodiwa katika daftari la ghalani kama taratibu zilivyo, na zaidi kwa kuzingatia kuwa,hati

ya malipo iliyohusika na matumizi ya fedha hizo imejitegemea na ile iliyohusika na malipo

kwa Mjenzi.

Aidha, Kamati imejiridhisha kwamba, Bodi haikutekeleza maelekezo ya sheria kwa

kutofuata taratibu za manunuzi za matumizi ya fedha hizo na zaidi kwa kitendo cha Bodi

kumpa mjenzi huyo fedha zilizohusika na hoja hii, bila ya wao wenyewe kununua vifaa

hivyo na kumpatia mjenzi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati iliitaka Bodi kuzingatia sheria za manunuzi kwa matumizi yote ya fedha za Serikali.

Hoja Namba 82.4 malipo yasiyokuwa na vielelezo (Nyaraka pungufu) za Tsh.

915,788,712

Fedha hizo zimetumika kwa mahitaji mbali mbali ya Bodi, lakini vielelezo vya kuthibitisha

matumizi yake vimekosekana wakati wa ukaguzi.

Majibu ya Bodi

Viongozi wa Bodi wamekiri kuwa, wakati wa ukaguzi vielelezo hivyo havikuwepo na

vilikuwa „misplaced‟ lakini ilipofika Kamati vilipatikana na Kamati kuombwa kuvikagua na

kujiridhisha juu ya usahihi wake.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati haikuona haja ya kuvipitia na kuvikagua vielelezo hivyo, kwani Sheria ya Fedha na

Kanuni zake zinaelekeza kupatikana kwa vielelezo vya matumizi ya fedha za Serikali, mara

tu matumizi ya fedha hizo yanapofanyika.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuchukua hatua stahiki kama ilivyoelezwa katika Sheria na Kanuni

za Fedha za Umma za mwaka 2005.

Hoja Namba 82.5 Kitengo cha Magendo

Sheria Namba 36 ya Kodi ya Mafuta inamtaka mtu aliyekamatwa akijihusisha na upitishaji

ama uletaji wa mafuta kinyume na Sheria, awajibike kulipa faini isiyopungua Tsh. 1,000,000

Page 43: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

43

na isiyozidi Tsh. 10,000,000 ikiwa ni pamoja na kulipia gharama za usafirishaji na uwekaji

wa mafuta hayo, sambamba na utaifishwaji wa vyombo vilivyotumika kusafirishia mafuta

hayo.

Aidha, Ukaguzi ulibaini Kitengo hiki cha Magendo kilikamata vyombo mbali mbali katika

mwaka 2012 lakini vielelezo vinaonesha utaifishwaji wa vyombo hivyo havikupatikana kwa

ukaguzi.

Majibu ya Bodi

Ni kweli MV. Mashallah na MV. Burak 1 na Burak 2 pamoja na gari la mafuta (Tanker)

viliwahi kukamatwa na Bodi vikiwa vimepakia mafuta ya magendo na mafuta

yaliyokuwemo kwenye vyombo hivyo yalitaifishwa na kuuzwa. Hatua ya utaifishaji wa

mafuta yaliyokamatwa ilichukuliwa kwa sababu utaratibu upo na unaeleweka, lakini kwa

upande wa utaifishaji wa vyombo haikuchukuliwa, kutokana na changamoto zake zikiwa ni

pamoja na kukosekana kwa utaratibu wa kufuatwa katika utaifishaji wa vyombo vya aina

hiyo na bado wananchi, ikiwia ni pamoja na taasisi za Serikali na za watu binafsi, bado

hawajapewa taaluma ya kutosha kuhusiana na matakwa ya Sheria ya mafuta, Zanzibar na

utaratibu unaotakiwa kufuatwa katika kufanya biashara ya mafuta na nishati pamoja na athari

za biashara ya magendo.

Hata hivyo, Bodi imetayarisha utaratibu unaotakiwa wa kuondoa changamoto hizo kwa

kutayarisha utaratibu wa kufuatwa katika utaifishaji wa vyombo hivyo na kujipanga upya ili

kutoa elimu ya kisheria na utaratibu utakaotumika katika utaifishaji wake.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati inachukulia hoja za Bodi kama za kujitetea zaidi na hazikusudii kutekeleza

majukumu yao waliyopangiwa kisheria. Aidha, Kamati imehoji iwapo ZRB inatumia kanuni

zozote katika kuendesha zoezi la kukamata mafuta ya magendo na kuelezwa kuwa, kanuni

zimeshatungwa ila zinasubiri saini ya Mhe. Waziri kwa ajili ya kuwa na nguvu kisheria.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeitaka Bodi kufuata taratibu za ukamataji kisheria na kuharakisha utiwaji saini wa

kanuni zao ili waweze kuzitumia katika majukumu yao.

4.4 MAMLAKA YA VITEGA UCHUMI ZANZIBAR (ZIPA)

Hoja Namba 13 Kuwasilisha hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya ukaguzi

Mamlaka imeshindwa kuwasilisha hesabu zake za mwisho wa mwaka kwa Mkaguzi na

Mdhibiti Mkuu wa Hesabu na hivyo ameshindwa kutoa taarifa za ukaguzi za Taasisi hii.

Majibu ya Mamlaka

Hawakuweza kufunga hesabu kwa sababu hawana thamani ya mali zote na ili uweze

kufunga hesabu ni lazima ujue thamani ya mali zako zote. Wamewasiliana na Chuo cha

Ardhi kilichopo Tanzania Bara kwa ajili ya kuwafungia hesabu, lakini chuo hicho kilihitaji

Tsh. 30,000,000/ fedha ambazo ni nyingi na hawakuwa nazo. Aidha, wameshindwa hata

kupata muongozo kutoka Wizara ya Fedha ya Zanzibar juu ya ufungaji wa hesabu zao,

wakati Taasisi hii ni tofauti na Taasisi nyengine za Serikali.

Page 44: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

44

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, Mamlaka imeshindwa kufunga hesabu za mwaka wa

2011/2012, ingawaje ilipofanya ukaguzi wa mwaka uliofuata, ilithibitisha kwamba, hesabu

hizo zimefungwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imekemea tabia ya Mkurugenzi kushindwa kufunga hesabu kwa kusingizio cha

kutopata muongozo wa Wizara ya Fedha wakati muongozo huo ulikwisha toka zamani.

Kamati inamtaka Mkurugenzi wa Mamlaka kurekebisha kasoro hii.

4.5 CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR (SUZA)

Hoja Namba 72.1 Uwezo wa Mamlaka kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi

na uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Chuo kilikuwa na mali za mpito za 943,877,359 na dhima za mpito

za 112,138,600 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 831,738,759 na uwezo wa kulipa dhima kwa

ratio ya 8.4:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa pamoja na salio la benki

kwa hesabu za Chuo.

Aidha, kwa upande wa uwezo wa kujiendesha, ukaguzi umepima mapato ya Chuo kwa

mwaka 2011/2012 ambayo yalikuwa ni Tsh. 6,340,907,560 na matumizi yalikuwa Tsh.

6,785,849,432, huku kukiwa na upungufu wa Tsh. 444,941,872 ya matumizi ukilinganisha

na mapato.

Majibu ya Chuo

Ni kweli kama ilivyoelezwa na ukaguzi kuhusiana na mali za mpito ambazo zinajumuisha

akiba ya Chuo Benki, madeni ya ada za wanafunzi na madeni ya mikopo ya wafanyakazi.

Kuhusu uwezo wa kulipa kuwa mkubwa kuliko kiwango cha kawaida (cha 2:1), hali hii

imechangiwa na kuwa na salio la kiwango kikubwa wakati wa kifunga hesabu kutokana na

fedha za mradi. Kwa mfano Tsh. 783,354,609.23 kama akiba katika hesabu za benki za

Chuo, kati ya hizo, Tsh. 445,845,500 zilikuwa za mradi wa Sayansi na Teknolojia

unaofadhiliwa na Benki ya Dunia, Tsh. 69,576,096 zilikuwa ni za mradi wa „Building

Stronger Universities‟ unaofadhiliwa na Serikali ya Denmark na Tsh. 118,317,692 zilikuwa

ni mfuko maalum kwa ajili ya wanataaluma wa Chuo.

Kuhusiana na taarifa za mapato na matumizi, Chuo kiutaratibu kinatakiwa kioneshe mapato

yake yote kilichoyakusanya kwa mwaka unaohusika kutoka katika vyanzo vyake vyote,

ambavyo ni Ruzuku (Serikalini), mapato ya misaada au fedha za miradi na mapato

yaliyozalishwa na Chuo. Na matumizi nayo pia wanapaswa kuyaonesha na kuyajumuisha

katika vyanzo vya mapato vya Chuo.

Aidha, ukubwa wa matumizi umetokana na kutekeleza kazi za miradi kwa mwaka

2011/2012 kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na pesa walizozipokea. Ziada ya matumizi

ilitekelezwa kwa fedha zilizoletwa na kubaki katika mwaka wa fedha 2010/2011.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imetaka kufahamu iwapo hali ya upungufu ingeliendelea na kuelezwa kuwa, Chuo

kimejipanga kuongeza mapato yao kwa kuimarisha ukusanyaji wa ada za wanafunzi,

kuanzisha program za elimu kwa jamii, kushajihisha mafunzo ya Kiswahili kwa wageni na

kuwashajihisha wafanyakazi kuandaa miradi mbali mbali.

Page 45: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

45

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imekitaka Chuo kuchukua juhudi ya kuhakikisha kinaongeza mapato ili kukidhi

mahitaji yake.

Hoja Namba 72.1.1 Malipo yaliyofanywa kinyume na kanuni na taratibu za

manunuzi, Tsh. 74,084,000

Fedha hizo zimetumika kwa ajili ya ununuzi wa gari ya Makamu Mkuu wa Chuo, lakini

ununuzi huo haukufuata Sheria wala kanuni ya manunuzi.

Majibu ya Chuo

Ni kweli wamefanya matumizi ya fedha hizo kwa kununua gari kama ilivyoelezwa na ripoti,

lakini wamefuata taratibu za manunuzi kwa kutumia njia ya „Single Source‟, kama

inavyoelezwa na kifungu cha 38 cha Sheria ya Manunuzi.

Uchunguzi wa Kamati

Kifungu cha 38 kinachoelezea „Direct Procurement method‟, kinashurutisha kutumiwa njia

hii kwa kuwepo dharura ya kutolazimika kupatikana washindani zaidi ya mmoja katika

manunuzi, ikiwa ni pamoja na bidhaa inayonunuliwa kuwa haipatikani zaidi ya muuzaji

mmoja, kuwepo kwa haraka ya manunuzi yake ambayo haikupangwa kabla na masharti

mengine ambayo Chuo hawakuyafuata wala hawakuwa na sababu ya kulazimika kutumia

njia hii. Hata hivyo, wakati Kamati inakagua hati iliyohusika na manunuzi hayo, imegundua

kuwa Chuo kimetafuta wauzaji watatu, na kuchagua mmoja. Hivyo, fedha hizo ni nyingi na

walilazimika kufuata taratibu za tenda, angalau kufanya „quotation‟ kwa njia ya tenda, na

njia hiyo kupata idhini ya Bodi ya Zabuni, vitu ambavyo havikufanyika.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kufuata kikamilifu taratibu za manunuzi.

4.6 CHUO CHA UONGOZI WA FEDHA

Hoja Namba 70.1 Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha.

Chuo cha Uongozi wa Fedha kwa mwaka 2011/2012, kilikuwa na mali za mpito zenye

thamani ya Tsh. 956,583,572 na dhima za mpito za 63,900,594 kwa bakaa la thamani ya Tsh.

892,682,978 na uwezo wa kulipa dhima kwa ratio ya 15:1, hali iliyochangiwa zaidi na

kuwepo kwa wadaiwa pamoja na salio la benki kwa hesabu za Chuo.

Mapato ya Chuo kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 2,802,282,653 na matumizi yake

yalikuwa Tsh. 1,681,555,319 na hivyo kuendeshwa kwa faida ya Tsh. 1,120,727,333 ambayo

imeshuka kutoka Tsh. 1,409,434,625 kwa mwaka 2010/2011.

Majibu ya Chuo

Chuo hiki ni taasisi inayotoa huduma kwa umma na haifanyi biashara, hivyo haiwezi

kufanya faida. Fedha inayobakia katika akaunti yao, huwa wanaifanyia kazi katika maeneo

mengine. Aidha, kuhusiana na kuongezeka kwa dhima za mpito inatokana na mikato na wao

hawalipi mpaka wapate ruzuku. Pia wana deni ZSSF, ambapo hawawezi kulipa mpaka

waingiziwe fedha na Serikali, jambo linalowafanya wasubiri hiyo ruzuku kutoka Serikalini

ambayo kwa kawaida huchelewa.

Page 46: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

46

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji kuongezeka kwa dhima za mpito kwa mwaka 2011/2012 ukilinganisha na

mwaka 2010/2011, ambapo ilielezwa inatokana na deni walilokuwa wanadaiwa na China

Railways Jang Chang Engineering Ltd kutokana na ujenzi wa dahalia ya wanafunzi. Aidha,

kwa mwaka huo, pamoja na juhudi walizozichukua Wizara ya Fedha, bado walikuwa

wanawadai milioni 500 za ada ya wanafunzi wanaolipiwa na Wizara hiyo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imekitaka Chuo kuongeza kasi na umakini katika kukusanya mapato hasa kwa

kufuatilia ada za wanafunzi na kuhakikisha wanalipia gharama zinazowakabili.

Hoja Namba 70.1.1 Mfuko wa Mchango wa Wafanyakazi wa Chuo (ZIFA Deposit

Fund)

Wafanyakazi wa Chuo hukatwa mishahara yao ya kila mwezi na fedha hizo huhifadhiwa

katika hesabu ya Chuo. Idadi ya fedha hizo haikuwa inakaguliwa kutokana na kukosekana

kwa kumbu kumbu zinazohusiana na michango hiyo. Aidha, kuendelea kutumika hesabu ya

Chuo kwa kuingiza na kutoa fedha zinazotokana na michango ya wafanyakazi, kunaweza

kusababisha mwanya na upotevu wa fedha za Chuo na kupelekea kutokujua idadi halisi ya

fedha za Chuo na fedha za michango ya wafanyakazi.

Majibu ya Chuo

Ni kweli mchango huo upo ambapo walimu huchangia Tsh. 5000 na wafanyakazi wengine

huchangia Tsh. 3000 kwa mwezi, fedha ambazo zinawasaidia wafanyakazi wenyewe wakati

wanapopata mitihani ikiwa ni pamoja na majanga. Fedha hizo pia hugawana kwa mwaka

sawa sawa bila ya tofauti ya michango waliyoitoa.

Chuo kimechukua hatua za kupeleka nyaraka zao za Mfuko kwa Mkurugenzi anaehusika na

SACCOS, ili waunde SACCOS ya Chuo, lakini walielekezwa kuwa na mtaji usiopungua

Milioni 20, hali iliyopelekea ugumu wa kuanzisha SACCOS yao.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, Chuo kimeanzisha akaunti hiyo kwa nia njema na fedha hizo

zina msaada mkubwa kwa wafanyakazi wote wa Chuo. Hata hivyo, kuzichanganya fedha

hizo na account ya Chuo huenda kukaleta matatizo.

Kwa ajili ya kujiridhisha juu ya fedha hizo, Kamati ilihitaji kupatiwa taarifa za mikato

ambazo zililetwa na kukaguliwa na Kamati.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakishauri Chuo kutafuta utaratibu wa kuihifadhi fedha inayopatikana katika

michango ama mikato hiyo ya wafanyakazi, ili kuepusha utata ambao ungeliweza kujitokeza.

4.7 MAMLAKA YA KUSIMAMIA UVUVI WA BAHARI KUU

Hoja Namba 73.1.1 Kuwasilisha hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya ukaguzi

Mamlaka imechelewa kuwasilisha hesabu zake za mwisho wa mwaka kwa Mkaguzi na

Mdhibiti Mkuu wa Hesabu, kinyume na maelekezo ya Sheria ya Fedha za Mwaka ya mwaka

2005.

Page 47: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

47

Majibu ya Mamlaka

Mamlaka imekiri kuchelewesha hesabu hizo kutokana na tatizo la uchache wa wafanyakazi

wenye uwezo wa kufunga hesabu zao, na huku ikizingatiwa kuwa Mamlaka imeazishwa

karibuni, mwaka 2010.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na majibu ya Mamlaka, Kamati imehoji iwapo hesabu hizo kwa mwaka uliofuata

(2012/2013) zimewasilishwa kwa wakati na kuelezwa kuwa, pia imechelewa ingawa kwa

mwezi mmoja.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeitaka Mamlaka kurekebisha kasoro hiyo kwa haraka.

Hoja Namba 73.1 Uwezo wa Mamlaka kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi

na uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Mamlaka ya Maji ilikuwa na mali za mpito za 2,386,660,778 na

dhima za mpito za 24,536,873 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 2,362,123,906 na uwezo wa

kulipa dhima kwa ratio ya 97.2:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa salio kubwa

benki, la Tsh. 2,385,780,364 kwa hesabu za Mamlaka.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 2,337,056,151 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 539,443,728 na hivyo kuendeshwa kwa faida ya Tsh. 1,797,612,422.

Majibu ya Mamlaka

Mamlaka haina dhima kubwa za mpito kutokana na kwamba Mamlaka imeanzishwa

karibuni na haina madeni makubwa. Kwa mfano, wafanyakazi wote wanaofanya kazi katika

Mamlaka wameazimwa kutoka Wizara zinazohusika na Uvuvi, Tanzania Bara na Zanzibar,

hali inayofanya pia wasiwe na dhima ya kodi inayotokana na mishahara (payee).

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na majibu yao, Kamati ilitaka kufahamu kuhusu utaratibu wa vikao vya Bodi ya

Wakarugenzi ya Mamlaka, na ilielezwa kwamba, vikao hivyo havijawahi kuitishwa zaidi ya

vinne na hivyo hakuna matumizi makubwa ya vikao hivyo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeitaka Mamlaka kufanya vizuri zaidi katika uwiyano wa mali na dhima zao za

mpito, pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji na kuinua ufanisi, ili uwezo wa

Mamlaka uendelee kukua.

Hoja Namba 73.2 Malipo yasiyokuwa na vielelezo, Tsh. 178,460,370 na Pound 8,354

Fedha hizo zimetumika kwa ajili ya matumizi mbali mbali ya Mamlaka, lakini vielelezo vya

kuthbiitisha uhalali wa matumizi hayo havikupatikana kwa ukaguzi.

Majibu ya Mamlaka

Wakati wa ukaguzi vielelezo hivyo vilikuwepo na suala hili lilisababishwa na Mkaguzi

aliyekuja kufanya ukaguzi, hakuangalia mafaili yote, wakati mafaili hayo yalikuwepo na

walipogundua ilikuwa tayari Mdhibiti huyo ameshaandika ripoti yake.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na majibu hayo, Kamati haiwezi kukubaliana moja kwa moja na Mamlaka, kwa

sababu kwa kawaida ukaguzi hufanywa kwa kutolewa taarifa mapema na mashirikiano ya

Page 48: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

48

moja kwa moja, baina ya Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu na Taasisi

inayohusika na ukaguzi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeishauri Mamlaka kutekeleza vyema majukumu yake ili iweze kutoa taarifa kwa

wakati pale zinapohitajika.

4.8 BENKI YA WATU WA ZANZIBAR (P.B.Z)

Hoja Namba 71.1 Kuwasilisha hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya ukaguzi

Benki imeshindwa kuwasilisha hesabu zake za mwisho wa mwaka kwa Mkaguzi na Mdhibiti

Mkuu wa Hesabu na hivyo ameshindwa kutoa taarifa za ukaguzi za Taasisi hii.

Majibu ya Benki

Benki inafunga hesabu zake kila mwisho wa mwaka, kwa kuzingatia taratibu na maelekezo

ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ila tatizo lilikuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

alikua hahusishwi katika ukaguzi huo, wakati yeye Kikatiba na Sheria za Zanzibar ndie

mwenye mamlaka ya ukaguzi au kwa idhini yake.

Hata hivyo, tatizo hilo kwa mwaka 2012/2013 litakua limeshaondoka kwa sababu Serikali

kupitia Wizara ya Fedha imeshalishughulikia suala hili, kwa ukaguzi kufanywa kwa idhini

ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu na Mkaguzi atakaepewa kazi hiyo atatoa mashirikiano kwa

Maofisa wa Afisi hii.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati inakiri kupokea taarifa hiyo kutoka Afisi ya Mdhibiti na Serikali yenyewe na

imepongeza hatua hizo ambazo Kamati ililisimamia suala hilo kwa miaka ya nyuma.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kutoa mashirikiano makubwa kwa Taasisi hizi kwa kila mmoja

kutekeleza majukumu yake Kikatiba na Kisheria ili kuweza kupata ufanisi zaidi.

4.9 SHIRIKA LA MAGAZETI YA SERIKALI

Hoja Namba 66.1 Uwezo wa Shirika kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Shirika la Magazeti kwa mwaka 2011/2012, ilikuwa na mali za mpito za 383,326,865 na

dhima za mpito za 30,725,405 kwa bakaa ilikuwa na thamani ya Tsh. 352,601,460 na uwezo

wa kulipa dhima kwa ratio ya 12:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa wengi

wa Shirika pamoja na salio la benki.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 788,358,419 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 838,874,818, hali iliyopelekea kuendeshwa kwa hasara ya

Tsh.50,516,399 ambapo mwaka wa 2010/2011, Shirika liliendeshwa kwa hasara ya Tsh.

55,981,988, ingawaje imepungua kidogo kwa Tsh. 5,465,589.

Majibu ya Shirika

Shirika limekiri taarifa hiyo na kueleza kuwa, deni kubwa linatokana na gharama za

uchapishaji wa magazeti, kwa sababu mpaka leo Zanzibar haina kiwanda na mashine ya

Page 49: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

49

kuchapisha magazeti ya rangi, hali inayolifanya Shirika kupeleka magazeti yake

kuchapishwa Dar es Salaam ambako ni ghali sana.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji iwapo Shirika lina mkakati wowote wa kuondokana na tatizo la uchapishaji

huo na kuelezwa kuwa Shirika limekuwa likiandika mradi kwa kila mwaka na kuupeleka

Serikalini, lakini hilo bado halijafanikiwa.

Hata hivyo, hivi sasa Shirika limeamua kuiuza kwa Wafadhili miradi hiyo lakini nalo bado

halijafanikiwa. Shirika pia limezungumza na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Zanzibar

(ZSSF) kwa ajili ya kupatiwa mkopo wa Milioni 800 kwa ajili ya ununuzi wa mtambo wa

rangi wa kuchapisha magazeti, ambapo mtambo mpya haupungui Bilioni 2. Hata hivyo,

suala hili la kupatiwa mkopo huo linahitaji udhamini wa Serikali.

Kamati inahoji juu ya matumizi ya Tsh. 800 milioni kwa ununuzi wa mitambo iliyotumika,

ikizingatiwa pia Serikali sasa haitakiwi kununua vifaa ama mitambo kama hiyo iliyotumika.

Aidha, kuhusiana na uwezo wake wa kujiendesha, Kamati imepata maelezo na imeridhika

kwamba, Serikali imelianzisha Shirika hilo bila ya kulipatia nyenzo kamili za kufanyia kazi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imelitaka Shirika kufanya ununuzi wa mitambo mipya ya rangi kwa ajili ya

uchapishaji wa magazeti, lakini inaitaka Serikali na Shirika kusimamia kwa makini na kwa

misingi ya Sheria suala zima la ununuzi wa mitambo inayotakiwa na Shirika.

Hoja Namba 66.1.1 Kukosekana kwa mchanganuo wa samani (Assets) zenye thamani

ya Tsh. 443,845,155

Fedha hizo zimeoneshwa katika taarifa ya hesabu za mwisho wa mwaka za Shirika, bila ya

kuwepo mchanganuo wa orodha ya samani hizo, kinyume na taratibu za kufunga hesabu.

Majibu ya Shirika

Shirika limekiri kukosekana kwa mchanganuo huo wakati wa ufungaji wa hesabu hizo,

kasoro ambayo tayari wameshairekebisha.

Uchunguzi wa Kamati

Maelekezo ya Sheria ya Fedha ya mwaka 2005 na kanuni zake, zinaelekeza kuorodheshwa

kwa mchanganuo huo, katika taarifa za hesabu zinazotakiwa kuwasilishwa kwa Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu. Kukosekana wakati wa hesabu ni kwenda kinyume na

maelekezo ya sheria.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inautaka uongozi wa Shirika kuwa makini wakati wa kufunga hesabu, kwa

kuhakikisha taarifa zote zinazotakiwa katika hesabu hizo zinapatikana kwa wakati.

Hoja Namba 66.1.2 Madeni kwa Taasisi za Serikali, Tsh. 323,925,000

Fedha hizo zinadaiwa na Shirika kwa taasisi mbali mbali za Serikali kwa huduma za mauzo

ya magazeti pamoja na matangazo yaliyochapishwa katika gazeti la Zanzibar Leo. Fedha

hizo bado hazijalipwa.

Majibu ya Shirika

Shirika limechukua hatua mbali mbali kudai kulipwa kwa madeni hayo ikiwa ni pamoja na

kuziandikia taasisi zenye madeni, hatua ambazo zimeleta mafanikio kwa kupunguzwa kwa

Page 50: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

50

deni hilo, ambapo kwa sasa deni hilo limeshalipwa Tsh. 103,773,000 na limebakia

220,152,000/-. Aidha, Shirika wamelipeleka suala hilo Serikalini na Katibu Mkuu Kiongozi

aliwaandikia Makatibu Wakuu wanaohusika na deni kuwataka walipe madeni yao, hatua

ambayo ilileta mafanikio japo kwa kiasi kidogo.

Uchunguzi wa Kamati

Shirika limekuwa linatoa huduma kwa taasisi za Serikali bila ya kulipwa na hatimae deni

hilo huwa kubwa, kutokana na kukosekana kwa utaratibu imara wa Shirika kusimamia

malipo ya huduma wanayoitoa, na hatimae huwepo na ugumu mkubwa wa kudai madeni

hayo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kulisaidia Shirika katika kusimamia madeni yake, ili fedha

zinazodaiwa na taasisi za Serikali ziweze kulipwa. Na kama taasisi hizo zitashindwa kulipa

kwa khiari, basi zikatwe katika bajeti zao.

Hoja Namba 66.2 Gharama za uchapishaji, Tsh. 313,612,866

Kwa kawaida Shirika linapatiwa ruzuku ya Tsh 238,799,240 ili kukidhi kulipa mishahara ya

wafanyakazi wake. hata hivyo, ukaguzi umebaini kuwa, kutokana na gharama za uchapishaji

kuwa kubwa, Shirika linalazimika kukopa ruzuku hiyo na kuitumia kwa ajili ya uchapishaji

wa gazeti hilo na kuathiri ulipaji wa mishahara. Aidha, Shirika linalazimika kuwa na ukosefu

wa fedha kwa ajili ya kuendesha shughuli za Shirika kwa wakati unaotakiwa na kusababisha

wafanyakazi kutopata mishahara yao kwa wakati.

Majibu ya Shirika

Suala hilo halijawahi wala halitaweza kufanyika kutokana na utaratibu wa mishahara ya

wafanyakazi kuingizwa moja kwa moja benki na wafanyakazi huchukua fedha hizo kupitia

akaunti zao, wala hazipitii katika Shirika.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imemtaka Afisa Mdhibiti anaefuatana na Kamati kufuatilia zaidi suala hili, ili

uhakika wake uweze kupatikana.

Mapendekezo ya Kamati.

Kamati inahitaji muda zaidi na uhakika zaidi wa taarifa hii, ili iweze kuifuatilia kwa uhakika

wake.

4.10 SHIRIKA LA UTALII

Hoja Namba 68.1 Uwezo wa Shirika kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Shirika lilikuwa na mali za mpito za 62,262,419 na dhima za mpito

za 31,500,000 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 30,500,000 na uwezo wa kulipa dhima kwa

ratio ya 2:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa wengi wa Shirika.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 107,523,000 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 180,879,549 na hivyo kuendeshwa kwa hasara ya Tsh. 73,356,549.

Majibu ya Shirika

Wanakubaliana na maelezo ya ripoti, na hatua zilizochukuliwa na Serikali ni kulivunja

Shirika hilo, kupitia kikao cha Baraza la Mapinduzi cha tarehe 14/03/2013. Aidha, mali za

Page 51: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

51

Shirika zimeshakabidhiwa Wizara ya Fedha kupitia Idara ya Mitaji ya Umma na taarifa ya

kufungwa kwa Shirika hilo ilitolewa katika Baraza la Wawakilishi kupitia hotuba ya Bajeti

ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo ya mwaka 2013/2014.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeandika barua Serikali kutaka uthibitisho wa kuvunjwa kwa Shirika hilo, na

kuthibitishiwa kuwa limevunjwa kwa mujibu wa taraitub za Sheria.

Mapendekezo ya Kamati.

Kamati haikuweza kuendelea na hoja zilizobakia za Shirika kutokana na kutokuwepo kwake.

Aidha, Kamati inaitaka Serikali kuwa makini na uvunjaji wa Mashirika kwa kuzingatia

taratibu zilizopo na kuchunga upotevu wa mali za Mashirika hayo, ambapo bila ya

kusimamiwa ipasavyo, upotevu huo utatokea.

4.11 HOTELI YA BWAWANI

Hoja Namba 67.1 Uwezo wa Hoteli kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Mali za Mpito za Hoteli ya Bwawani kwa mwaka 2011/2012,zilifikia thamani ya Tsh.

356,429,176.65 na dhima za mpito zikifikia thamani ya Tsh. 37,975,888.38 na hivyo kufanya

hali halisi ya mali za mpito kuwa Tsh. 318,453,287.80 kwa ratio ya 9.38:1, hali

iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa pamoja na salio la benki Tsh. 240,436,414.68

kwa mwaka 2011/2012, fedha ambazo zingeliweza kutumika kwa kuiendeleza hoteli kwa

uwekezaji na kupunguza tatizo la upungufu wa mishahara ya wafanyakazi limaloikabili

hoteli kwa muda mrefu.

Aidha, Hoteli imekuwa na mapato ya Tsh. 1,100,632,772 na matumizi yakawa Tsh.

1,059,818,300.73 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa la Tsh. 40,814,471.27.

Majibu ya Hoteli

Uongozi wa hoteli umechukua hatua mbali mbali za kudai madeni kwa watu na taasisi mbali

mbali za Serikali na binafsi, hatua ambayo imesaidia sana kupunguza kwa kiasi kikubwa

kwa madeni hayo. Kwa upande wa uwezo wa kujiendesha, uongozi umechukua hatua za

kudhibiti vianzio vya mapato viliopo na kubuni vipya. Aidha, uongozi ulipitia viwango

vinavyotozwa kwa huduma mbali mbali na kubaini vingi vyao vimepitwa na wakati na kwa

kushirikiana na Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo, viwango hivyo

vimerekebishwa kwa kuendana na wakati.

Uchunguzi wa Kamati

Taasisi nyingi za Serikali zinazodaiwa na Hoteli huwa hazilipi huduma wanazopatiwa na

kuifanya hoteli kama sehemu inayotolewa huduma bure. Kamati imejiridhisha kwamba,

Wizara yenyewe ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo inadaiwa Tsh. 17,520,640 kwa

muda mrefu na wala hailipi. Hali hii inaifanya Kamati iamini kuwa, Wizara hii inaifanya

Hoteli kama kitega uchumi chake bila ya malipo yoyote ya huduma inayopatiwa. Aidha,

Kamati imepewa taaria ya barua mbali mbali zilizoandikwa na Hoteli kwa wadaiwa wake

kuwataka walipe madeni yao. Kamati imeridhishwa na hatua hiyo, lakini bado haitoshi kuwa

njia pekee ya kudai.

Page 52: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

52

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuangalia na kufanya maamuzi sahihi ya hatima ya Hoteli

ama iwe Shirika linalojitegemea, Idara iliyo chini ya Wizara au vyenginevyo, kuliko

hali iliyopo sasa.

Hoteli iundiwe chombo cha usimamizi wake badala ya kuwa chini ya Wizara.

Wizara ilipe deni inalodaiwa na Hoteli hii haraka iwezekanavyo ili Hoteli iweze

kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Hoteli ichukue hatua za kisheria kwa wadaiwa wote ambao hawatalipa madeni yao

badala ya kuwaandikia barua pekee.

Hoja Namba 67.1.1 Kukosekana kwa Mchanganuo wa samani (Assets) zenye thamani

ya Tsh. 6,137,266,383

Fedha hizo zimeoneshwa katika taarifa za hesabu za mwisho wa mwaka bila ya kuwepo

mchanganuo wa orodha ya samani za hoteli, kinyume na taratibu za ufungaji wa hesabu za

Serikali.

Majibu ya Hoteli

Ni kweli wameshindwa kuwasilisha mchanganuo huo katika ufungaji wao wa hesabu

waliouwasilisha kwa Mdhibiti, ingawaje taarifa hizo zipo.

Uchunguzi wa Kamati

Kutowasilisha mchanganuo huo ni kwenda kinyume na maelekezo ya Sheria na Kamati

haikubaliani na hoja za Hoteli za kuzipitia taarifa hizo wakati Sheria imeelekeza

kuwasilishwa kwake wakati wa ufungaji wa hesabu. Aidha, Kamati imeendelea kuhoji

kuhusu Cheo cha Kaimu Meneja wa Hoteli, ambae zaidi ya miaka mitatu sasa anaendelea

kukaimu nafasi hiyo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inautaka uongozi wa Hoteli ufanye marekebisho ya mara moja kwa kasoro za

kuwasilisha mchanganuo wa samani wakati wa uwasilishaji wa hesabu za mwisho wa

mwaka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu.

Aidha, kuhusiana na cheo cha Meneja, Kamati inaendelea na ushauri wake kwa Serikali

kufanya maamuzi ya haraka kuhusiana na mstakabali wa Hoteli.

4.12 MFUKO WA HIFADHI YA JAMII (ZSSF)

Hoja Namba 13.1 Uwasilishaji wa hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya ukaguzi

Kifungu cha 24(2) cha Sheria ya Fedha namba 12 ya mwaka 2005, kinazitaka taasisi zote za

Serikali zitayarishe na kufunga hesabu zao za mwisho wa mwaka na kuziwasilisha kwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa ajili ya ukaguzi. Hata hivyo,

uwasilishaji huo usizidi tarehe 30 ya mwezi wa Septemba ya kila mwaka, lakini Mfuko wa

Hifadhi ya Jamii haukuwasilisha hesabu zao kwa ukaguzi.

Majibu ya Mfuko

Mfuko ulikuwa haukaguliwi na Mdhibiti kutokana na wakati huo ulikuwa unakaguliwa moja

kwa moja na wakaguzi wa nje. Hivyo, sio sahihi kuelezwa kwamba haukuwasilisha kabisa,

badala yake ulichelewa kuwasilisha.

Page 53: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

53

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imetaka kujiridhisha iwapo Mfuko ulichelewa kuwasilisha na sio haukuwasilisha

kabisa kama ilivyoelezwa katika ripoti ya ukaguzi na kupatiwa ushahidi unaothibitisha

kuchelewa huko.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeridhika kwamba, Mfuko ulichelewa kwasilisha hesabu zake na kasoro hiyo sasa

imesharekebishwa.

4.13 CHUO CHA MAENDELEO YA UTALII

Hoja Namba 69.1 Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Chuo cha Maendeleo ya Utalii kilikuwa na mali za mpito za

221,549,527.39 na hakikua na dhima za mpito, huku hali halisi ya mali za mpito ilikuwa ni

Tsh. 221,549,527.39. Hali hii inaonesha kuwa, mali za mpito ni kubwa kutokana na

kutokuwepo kwa dhima za mpito, hali iliyochangiwa na kuwepo kwa wadaiwa pamoja na

salio la benki kwa hesabu za Chuo.

Aidha, mapato ya Chuo kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni 892,902,429 na matumizi yake

ni Tsh. 748,345,046 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa la Tsh. 144,557,383 ambayo

imeongezeka kwa tofauti ya Tsh. 134,312,716.90 sawa na 1311%.

Majibu ya Chuo

Sababu zilizopelekea hali hiyo ni kujipanga kwa Chuo kwa kutofautisha fedha za makusanyo

na fedha za ruzuku na kuzisimamia vizuri. Aidha, Chuo kimechukua hatua za makusudi

kupunguza matumizi ambayo sio ya lazima. Pia Chuo kimechukua hatua za kuboresha

huduma za Chuo kwa wanafunzi. Na kuhusiana na madeni, Chuo kilichukua hatua mbali

mbali za kulipa madeni hayo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji sababu zilizopelekea mafanikio hayo, na kuelezwa zaidi juhudi za

Mkurugenzi baada ya kufika katika Chuo hicho, akisaidiana na watendaji wengine.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakipongeza Chuo kwa maendeleo yake na kukitaka kuendelea na juhudi za

kuimarisha uwezo wake.

Hoja Namba 69.1.1 Kukosekana kwa mchanganuo wa samani (Assets) wa Tsh.

1,302,887,070

Fedha hizo zimeoneshwa katika taarifa za mwaka za Chuo, bila ya kuwepo mchanganuo wa

orodha ya samani za Chuo, kitendo ambacho kinapingana na maelekezo ya Sheria na taratibu

za ukaguzi na ufungaji wa Hesabu za mwaka.

Majibu ya Chuo

Ni kweli hilo lilikuwa tatizo wakati wa ufungaji wa hesabu za mwaka 2011/2012, lakini sasa

tayari wamesharekebisha kasoro hii kwa mwaka 2012/2013.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imefanya rejea ya maoni ya Ukaguzi yanayohusiana na Chuo, ambayo hayaoneshi

sura halisi na sahihi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa, na pamoja na

Page 54: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

54

kasoro nyengine, imesababishwa pia na kutoambatanishwa kwa mchanganuo huo katika

taarifa za hesabu.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kurekebisha mara moja kasoro hiyo, ili kukidhi matakwa ya Sheria

pamoja na kuweka vizuri hesabu zake kwa mujibu wa vigezo vya ukaguzi wa kitaifa na

kimataifa.

Hoja Namba 69.1.2 Malimbikizo ya madeni, Tsh. 113,694,750

Fedha hizo ni deni la wanafunzi wa fani mbali mbali katika Chuo, ambalo hadi ukaguzi

unafanyika, ilikuwa bado halijalipwa.

Majibu ya Chuo

Ni kweli kulikuwa na deni hilo. Hata hivyo, Kamati hii ilipokuja mwaka uliopita iliwataka

wafuatilie madeni hayo na uongozi umefanya hivyo ikiwa ni pamoja na kutoa matangazo

kwa wanaowadai, kufuatilia makazini, kwa wale ambao tayari wameshaajiriwa na hatua

nyengine, na kufanikiwa deni hilo kupungua na kufikia Tsh. 86,686,000/-.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, katika ufuatiliaji wa madeni hayo, Chuo hakiwajui wanafunzi

wote waliosoma na kudaiwa na hawana mawasiliano nao ya moja kwa moja.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kuendelea na juhudi na kuchukua hatua zaidi kuhakikisha deni hilo

linalipwa lote.

4.14 MAMLAKA YA UWANJA WA NDEGE

Hoja Namba 78.1 Uwezo wa Mamlaka kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi

na uwezo wa kujiendesha

Mamlaka ya Uwanja wa Ndege kwa mwaka 2011/2012, ilikuwa na mali za mpito za

989,929,435 na dhima za mpito za 496,752,012 na hali halisi ya mali hizo kuwa Tsh.

493,177,423, sawa na ratio ya 2:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa wengi

wa Mamlaka na salio la benki.

Kwa upande wa mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh.

2,275,561,428 na matumizi yake yalikuwa Tsh. 1,418,307,282 na hivyo kuendeshwa kwa

faida ya Tsh. 857,254,146.

Majibu ya Mamlaka

Mamlaka haifanyi biashara bali inatoa huduma, na kwa maana hii, haingeweza kufanya

faida. Aidha, Mamlaka ni wakala wa Serikali na fedha zote wanazozikusanya wanazipeleka

Serikalini na hali ya Mamlaka inaendelea kuwa mbaya siku hadi siku. Wameiomba Serikali

kwa muda mrefu sasa kupatiwa mgao wa wanachokikusanya, lakini hakuna mafanikio

yoyote.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeridhika kwamba, utekelezaji wa Sheria inayoanzisha Mamlaka unaiwezesha

Mamlaka kujinasua na hali waliyonayo sasa na kufikia hali wanayoitarajia.

Page 55: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

55

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kutekeleza ushauri waliopewa na Mdhibiti ya kuongeza juhudi ya

ukusanyaji na usimamizi wa vyanzo vyake vya mapato. Vile vile, Kamati inaishauri Serikali

kuipatia mgao wa fedha Mamlaka ili iweze kujienedesha kwa ufanisi

Hoja Namba 78.1.1 Malimbikizo ya madeni, Tsh. 73,285,940 na USD 273,317

Fedha hizo zinadaiwa na Mamlaka kwa wafanyabiashara na taasisi mbali mbali kutokana na

huduma walizowapatia, ambapo hadi ukaguzi unamalizika, fedha hizo bado hazijalipwa.

Majibu ya Mamlaka

Ni kweli Mamlaka inadai deni hilo na wamechukua hatua za kudai fedha hizo na kufanikiwa

kupungua. Utaratibu wanaoutumia ni kuwapelekea Ankara (Bill) wadaiwa wake wote tarehe

5 baada ya kutoa huduma, ambapo malipo hufanyika ndani ya siku 25 katika mwezi. Aidha,

kwa juhudi hizo, Mamlaka imelipunguza deni hilo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji iwapo mikataba inayohusika na huduma wanazozitoa Mamlaka, kama tayari

imesharekebishwa kama ilivyoelekezwa na Baraza la Wawakilishi. Aidha, imeipitia na

kujiridhisha kwamba, imerekebishwa katika eneo zaidi la kodi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka iendelee kufuatilia madeni yake ili kuhakikisha kuwa, wateja wote

wanaopatiwa huduma wanalipa ipasavyo kodi zao na wale ambao wanaendelea wachukuliwe

hatua za kisheria kwa mujibu wa mikataba yao.

Hoja Namba 78.2 Malipo yasiyokuwa na Vielelezo, Tsh. 11,200,000

Mamlaka imemlipa Moral Architectural and Engineering Consultancy Ltd kwa ajili ya

usimamizi wa Shopping Complex. Aidha, hadi ukaguzi unakamilika, ujenzi huo haujaanza

na hakukuwa na maelezo yoyote juu ya kuwepo uwezekano wa kufanyika kwa ujenzi huo.

Majibu ya Mamlaka

Ujenzi huo umefanywa na Msamaria mwema aliejitolea kujenga kwa kutumia fedha zake,

bila ya Mamlaka kutoa fedha yoyote. Aidha, baada ya kukamilika kwa ujenzi, Msamaria

huyo atakusanya 70% na Mamlaka 30%, na baada ya Msamaria mwema kurejesha fedha

zake za ujenzi, majengo hayo yatakuwa ya Mamlaka.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imefanya ziara katika eneo linalohusika na kugundua kuwa, ujenzi huo haukuwa

„Shopping Complex‟ bali ni ujenzi wa Ofisi mbali mbali zilizokodishwa kwa taasisi binafsi.

Ujenzi huo ulijengwa na Kampuni ya ASB Engineering na Mshauri wake ni Ndg. Abdu

Jindi, aliyechora ramani. Pamoja na msaada walioupata Mamlaka, Kamati imeona ujenzi huo

sio wa muda mrefu, kutokana na kuwa wa chini, wakati ingestahiki kujengwa kwa ghorofa

Aidha, kuhusiana na fedha Tsh. 11,200,000 zilizolipwa kwa Moral Architectural and

Engineering Consultancy Ltd, Kamati imejiridhisha kutumika bila ya vielelezo na zimelipwa

kwa Kampuni hiyo kwa ajili ya michoro na kutayarisha BOQ, kazi ambayo haikuiendeleza

na kuikamilisha.

Page 56: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

56

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kuhakikisha inatumia vizuri rasilimali zake kwa malengo ya muda

mrefu. Aidha, kuhusiana na fedha ambazo hazina vielelezo, Kamati inaitaka Mamlaka

kurekebisha mara moja kasoro hizo.

4.15 CHUO CHA UTAWALA WA UMMA

Hoja Namba 77.1 Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Chuo kilikuwa na mali za mpito za thamani ya Tsh. 406,206,983 kwa mwaka 2011/2012,

bila ya kuwa na dhima za mpito, hali iliyopelekea salio ama mali halisi za mpito kuwa Tsh.

406,206,983 hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa na salio la benki la chuo.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 1,397,161,548 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 935,745,286 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa la Tsh. 444,036,762.

Majibu ya Chuo

Ni kweli mpaka sasa hawana dhima, na mapato yao yanatokana na ada za wanafunzi wa fani

mbali mbali wanaosoma Chuoni hapo. Malipo ya ada hufanyika kwa njia ya hundi na fedha

taslim kupitia Benki ya Watu wa Zanzibar. Aidha, Chuo kinaiomba Serikali kuwamalizia

jengo la chuoni hapo kwa ajili ya kujiendesha kwa ufanisi zaidi.

Kuhusiana na deni kwa taasisi zinazoleta wafanyakazi wao kwa mafunzo, Uongozi wa Chuo

umefanya juhudi za kufuatilia ulipwaji wa madeni hayo, na mpaka sasa taasisi zote zimelipa

isipokuwa Mahakama.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, taasisi nyingi za Serikali zenye wanafunzi katika Chuo hiki,

zinahitaji msukumo ili waweze kulipa madeni yao.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kuongeza juhudi za ukusanyaji wa mapato yake kupitia ada za

wanafunzi na kuzifuatilia kwa karibu taasisi zote zenye wanafunzi, ili kuhakikisha madeni

yote yanalipwa ipasavyo.

Hoja Namba 77.1.1 Malimbikizo ya madeni, Tsh. 383,140,250

Fedha hizo zinadaiwa na Chuo cha Utawala wa Umma, kwa wanafunzi na taasisi mbali

mbali kutokana na huduma walizowapatia. Deni hilo halijalipwa

Majibu ya Chuo

Ni kweli kulikuwa na malimbikizo hayo ya madeni. Hata hivyo, baada ya kuchukua juhudi

wamefanikiwa kuondosha deni hilo kwa wadaiwa wote kulipa madeni yao, na hivyo, deni

hilo sasa halipo tena.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji juu ya wanafunzi wanaoakhirisha masomo katika semista husika, wakati

tayari wameshatumia huduma za Chuo angalau kwa mwezi mmoja au miwili, na kukitaka

Chuo kuwa makini sana na wanafunzi wa aina hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imepongeza juhudi zilizochukuliwa za kufuatilia na hatimae kulipwa kwa madeni

hayo na kuzitaka taasisi nyengine, hasa Vyuo, ziige mfano huu.

Page 57: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

57

4.16 CHUO CHA UANDISHI WA HABARI

Hoja Namba 79.1 Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2011/2012, Chuo kilikuwa na mali za mpito za 27,511,413 bila ya kuwa na

dhima za mpito, hali iliyopelekea bakaa kuwa kama mali za mpito. Hali hii imesababishwa

na kutokuwepo kwa madeni.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2011/2012 yalikuwa ni Tsh. 389,962,342 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 356,777,719.

Majibu ya Chuo

Ni kweli Chuo hakikuwa na dhima za mpito kwa mwaka 2011/2012 na kilichowasaidia

kuwa na mali za mpito ni ongezeko la wanafunzi 30. Aidha, kuhusiana na matumizi, Chuo

kilitumia Tsh. 356,777,719 badala ya Tsh. 395,458,994 zilizorikodiwa awali.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji iwapo Chuo kinamiliki jengo ambalo sasa ndio kipo Chuo chenyewe na

kujibiwa kuwa, jengo hilo sio mali ya Chuo na wao wanatumia ghorofa mbili, huku ghorofa

ya tatu ikitumiwa na Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Amali. Katika mahojiano ya Chuo

kuhusiana na mali, Kamati ilifahamishwa kwamba, Chuo kilinunua gari kwa Tsh.

39,000,000 lakini utaratibu wa manunuzi kama Sheria inavyoelekeza, haukufuatwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeutaka uongozi wa Chuo kuwa makini wakati wa kutumia fedha za umma kwa

kufuata ipasavyo Sheria zinazohusika.

Hoja Namba 79.1.1 Kukosekana kwa mchangauo wa samani (Assets) zenye thamani

ya Tsh. 119,460,550

Fedha hizo zimeoneshwa katika taarifa ya hesabu za mwaka za Chuo, lakini mchanganuo wa

orodha ya samani husika haukuwepo katika taarifa za hesabu za Chuo, kinyume na

maelekezo na matakwa ya Sheria zinazohusiana na ukaguzi na Sheria ya Fedha.

Majibu ya Chuo

Ni kweli wakati wa ukaguzi, mchanganuo huo haukuwemo katika taarifa ya hesabu za Chuo,

lakini kwa mwaka uliofuata walirekebisha kasoro hiyo.

Uchunguzi wa Kamati

Tatizo hili limeripotiwa sana kwa Vyuo, na majibu yake yamekuwa yanafanana.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kurekebisha kasoro hiyo kwa kutorejea tena kasoro iliyojitokeza.

4.17 CHUO CHA KILIMO, KIZIMBANI

Hoja Namba 13.1 Uwasilishaji wa Hesabu za mwisho wa mwaka kwa ukaguzi.

Chuo cha Kilimo Kizimbani kimeshindwa kuwasilisha hesabu zake za mwisho wa mwaka

wa 2011/2012, kinyume na maelekezo ya Sheria ya Fedha ya mwaka 2005.

Page 58: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

58

Majibu ya Chuo

Chuo kilishindwa kufunga hesabu zake, lakini kasoro hiyo tayari imeshafanyiwa kazi kwa

mwaka uliofuata. Aidha, kwa kawaida, baada ya Chuo kufunga hesabu zake, kwanza kabla

ya kuziwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, huziwasilisha kwanza kwa

Baraza la Chuo, ili wapate idhini ya kuziwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji iwapo Chuo kimeshakuwa na Daftari la kuhifadhia vifaa na kugundua kuwa,

daftari hilo halijahifadhiwa kwa pamoja, ni karatasi tu zilizowekwa pamoja. Hata hivyo,

Kamati iliwataka Chuo ndani ya wiki mbili kutayarisha Daftari hilo, ambalo baada ya muda

huo waliweza kulikabidhi kwa Kamati.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kufahamu kuwa, Sheria ya Fedha ya mwaka 2005 inawataka

wafunge na kuwasilisha hesabu zao za mwisho wa mwaka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

wa Hesabu za Serikali, suala ambalo haliwezi kuwekewa kipingamizi cha hesabu hizo

kwanza kukabidhiwa kwa Baraza la Chuo.

Hoja Namba 80.1 Malimbikizo ya madeni, Tsh. 2,350,000

Fedha hizo ni deni la wanafunzi wa fani mbali mbali katika Chuo, lakini hadi ukaguzi

unamalizika, deni hilo lilikuwa halijalipwa.

Majibu ya Chuo

Chuo kinakiri kuwepo kwa deni hilo wakati wa ukaguzi, lakini wamefanya juhudi ya

kulifuatilia na wakati ilipofika Kamati, ni wanafunzi wawili pekee walibakia kuwa na deni.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji wanafunzi ambao wameacha Chuo huku wakiwa wanadaiwa, mbali na

wanafunzi wanaodaiwa baada ya kuhitimu Chuo, na kuelezwa kuwa wapo baadhi ya

wanafunzi huakhirisha kwa sababu za msingi, kiasi ambacho kuwadai inakuwa tabu. Aidha,

Kamati imezipitia risiti za malipo na kujiridhisha kuwa zipo sawa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kuwa makini na kulichukulia kwa uzito wake suala la wanafunzi

wanaokatisha masomo, huku wakiwa hawajalipa miezi ambayo wamepata huduma hiyo,

ingawaje hawakuwahi kumaliza mitihani yao ya mihula husika.

4.18 SHIRIKA LA MAGARI

Hoja Namba 83.1 Rasilimali za Shirika kukodishwa bila ya kuzingatia thamani

halisi ya fedha

Ukaguzi umebaini kwamba, Shirika linamiliki majengo mbali mbali ambayo yamekodishwa

kwa mashirika mbali mbali na watu binafsi, lakini ukodishwaji huo haukuzingatia thamani

halisi ya majengo hayo kibiashara na muda wa ukodishwaji kwa lengo la kuleta tija kwa

Shirika kwa mujibu wa upandaji na ushukaji wa thamani ya fedha. Kwa mfano, benki ya

NMB imekodishwa jengo kwa miaka 33 tokea tarehe 31/12/2008, kwa mkataba kuanza kazi

tarehe 01/10/2008 hadi 30/09/2041, huku NMB wakilipa Tsh. 37,280.52 kwa mwaka.

Benki ya Posta imekodishwa jengo kwa mkataba wa tarehe 27/11/2007 kwa Tsh. 31,188,000

kwa mwaka, huku Mkataba huo ukimtaka Mkodishwaji kulipa kodi ya miaka miwili kwa

Page 59: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

59

mwaka wa mwanzo na kodi inayofuata kulipa kila mwaka, kwa sharti la ongezeko la asilimia

10 kila baada ya mwaka kuwa muda wote anaohitaji kulitumia jengo.

Ghala la Shirika liliopo Mchangani limekodishwa kwa Ndg. Bakia Ally Suleiman tarehe

9/2/2011 kwa malipo ya Tsh. 1,793,000 kwa mwaka. Tatizo zaidi ni kuwa, Mkodishwaji

amefariki na sasa linatumiwa na Ndg. Abubakar Pass Kajore na mkataba ulimalizika Januari

2012, bila ya kuingia mkataba mwengine, na hivyo Ndg. Abubakar anaendelea kulitumia

ghala hilo bila ya kulipa.

Majibu ya Shirika

Ni kweli wakati wa ukaguzi, majengo hayo yalikuwa yamekodishwa kwa kiwango kidogo

cha fedha , kutokana na hali mbaya na uchakavu wake. Hata hivyo, hivi sasa tatizo hilo

limesharekebishwa na bei zimefanyiwa marekebisho na ziko sawa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji mkataba wa Postal Bank na kugundua kuwa, hakuna marekebisho yoyote

yaliyofanywa. Aidha, Mkaguzi alishindwa kuupata mkataba wa benki hii kutokana na kuisha

muda. Kuhusiana na ghala, Kamati ilielezwa kuwa baada ya kumaliza muda wa ukodishwaji

kwa Ndg. Bakia Ally Suleiman, limerudi kwao na sasa wamekodisha kwa miaka miwili Tsh.

74,580.48.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalitaka Shirika kuhakikisha inafuatilia ipasavyo kodi za majengo yake kwa kufanya

marekebisho ya mikataba ili iendane na thamani halisi ya fedha kwa mujibu wa wakati

tulonao na sehemu ambayo majengo hayo yalipo.

Hoja Namba 83.2 Malimbikizo ya madeni, Tsh. 95,461,728

Fedha hizo zinadaiwa na Shirika la Biashara ya Magari kwa taasisi mbali mbali za Serikali

na watu binafsi, lakini hadi ukaguzi unakamilika, madeni hayo yalikuwa bado hayajalipwa

wakati yameshakaa muda mrefu.

Majibu ya Shirika

Ni kweli madeni hayo ni ya muda mrefu, mengine tokea Shirika lilipokuwa Bizanje. Aidha,

madeni ya taasisi nyingi yameshindwa kulipwa kutokana na baadhi yao kukosa vielelezo vya

ushahidi wa kuwepo kwake.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeshuhudia kuwa madeni hayo ni ya muda mrefu kutokana na sababu mbali mbali

ikiwa ni pamoja na kutokuwepo kwa usimamizi imara wa huduma iliyokuwa inatolewa na

Shirika kwa taasisi na watu mbali mbali. Aidha, ni kweli kuwa, baadhi ya vielelezo hasa vya

madeni ya muda mrefu sana, havipo kwenye Shirika kiasi ya kukwamisha juhudi za

kufuatilia ulipwaji wa madeni hayo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalitaka Shirika kuendelea kufuatilia madeni yake, ili kuongeza uwezo wa Shirika.

4.19 MAMLAKA YA MAFUNZO YA AMALI

Hoja Namba 54.6.1 Ruzuku ya Tsh. 60,000,000

Fedha hizo zikiwa ni ruzuku kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, hazikuingizwa

katika taarifa za hesabu za Mamlaka za mwisho wa mwaka, kinyume na taratibu za

Page 60: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

60

utayarishaji wa taarifa za hesabu, hali ambayo pia hupelekea taarifa za hesabu kutokuwa

sahihi. Fedha hizo zimelipwa kwa Mamlaka kupitia hundi namba 395303 ya tarehe

28/5/2012.

Majibu ya Mamlaka

Ni kweli viongozi wa Mamlaka wanakiri kutokea kwa kasoro hiyo, isipokuwa tayari

wamesharekebisha na kuahidi kutotokea tena kwa kasoro hiyo. Fedha hizo zimetumika na

uthibitisho wa vocha zake upo, isipokuwa kosa lililotokea ni la kibinaadamu.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ilipohoji sababu za msingi zilizopelea kasoro hiyo, imeelezwa kuwa ni sababu za

kibinaadamu. Aidha, Kamati imetaka kufahamu elimu ya Mhasibu wa Mamlaka, lakini kwa

bahati Mhasibu aliyepo sasa mwenye kiwango cha „Master‟ hakuwa yeye wakati Mamlaka

ilipokaguliwa.

Aidha, Kamati imejiridhisha pia, kosa hilo limejitokeza kutokana na kufungwa hesabu za

mwisho wa mwaka bila ya kukaguliwa na Mkaguzi wa Ndani wa Mamlaka, ambae iwapo

angeliona kasoro hizo mapema, angeliijuulisha Mamlaka inavyostahiki. Aidha, Kamati

imejiridhisha kurekebishwa kwa kasoro hiyo ikiwa ni pamoja na kuangalia „cash book‟ na

kuiona ipo sawa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kuhakikisha inarekebisha kasoro hiyo isitokezee tena.

Hoja Namba 54.6.2 Matumizi yaliyofanyika kinyume na vifungu husika, Tsh.

42,650,155

Fedha hizo zimetumika kinyume na vifungu vilivyoidhinishwa , kitendo ambacho kinakiuka

kanuni 41(4) ya Kanuni za Fedha za mwaka 2005.

Majibu ya Mamlaka

Ni kweli wamefanya matumizi hayo kinyume na vifungu vilivyoidhinishwa na Bodi ya

Mamlaka, isipokuwa matumizi hayo hayakuzidi bajeti ya Mamlaka na yamefuata taratibu

zote za kisheria. Imefahamishwa kuwa, pamoja na Mamlaka kupokea ruzuku Serikalini,

Mamlaka ina vituo vyake vya mafunzo ya amali vilivyopo Mwanakwerekwe, Mkokotoni na

Vitongoji, ambapo wamepewa idhini ya matumizi madogo madogo kwa usimamizi wa

Mkurugenzi.

Hapo mwanzo fedha hizo walikuwa hawazioneshi katika MTEF, ila sasa tayari

wamesharekebisha kasoro hiyo na fedha hizo za mapato zinaonekana katika MTEF na jumla

yake kuu ndio wanayoipangia matumizi. Aidha, fedha hizo zilitakiwa zipatiwe idhini ya

Bodi ya Mamlaka, ila viongozi wa Mamlaka wanakiri kasoro hiyo na tayari sasa kosa hilo

wameshalirekebisha.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na Mamlaka kushindwa kufanya matumizi kinyume na vifungu vilivyoidhinishwa na

Bodi, Kamati imejiridhisha kuwepo kwa tatizo kubwa la Wizara ya Fedha kutokutoa fedha

kwa wakati kwa taasisi husika, ili hatimae taasisi husika zipate muda mzuri wa kuzitumia

fedha hizo kwa kufuata taratibu za kisheria.

Page 61: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

61

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kurekebisha kasoro iliyobainika na kutorejea tena katika kufanya

kasoro hizo. Aidha, Kamati inaishauri Serikali, kupitia Wizara ya Fedha, kuhakikisha taasisi

zote za Serikali zinapatiwa fedha katika muda muafaka, ili taratibu za kisheria ziweze

kufuatwa ipasavyo.

Hoja Namba 54.6.3 Matumizi ya Ununuzi wa vifaa ambavyo havijapokelewa, Tsh.

46,960,800

Fedha hizo zimetumika kwa ajili ya manunuzi ya vifaa mbali mbali kwa matumizi ya vituo

vya Mamlaka vya Mwanakwerekwe na Mkokotoni, lakini hadi ukaguzi unakamilika vifaa

hivyo havikuonekana katika vituo husika na mapokezi ya vifaa hivyo hayakuonekana katika

kumbu kumbu ya vituo hivyo.

Majibu ya Mamlaka

Uongozi wa Mamlaka unakubaliana na hoja za Mkaguzi kwamba, baadhi ya taratibu

zimekiukwa kutokana na baadhi ya vifaa kupokelewa moja kwa moja na wakuu wa vituo,

lakini havikuingizwa katika daftari la ghalani. Tatizo hili limesababishwa na ugeni na hamu

ya kuvipata vifaa hivyo baada ya kuviomba kwa mufa mrefu. Uongozi unahakikisha

kwamba, vifaa hivyo vimenunuliwa na vilitumika kama vilivyokusudiwa. Aidha, wakati

huo, Mamlaka haikuwa na stoo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ilipohoji kuhusiana na upokelewaji wa vifaa hivyo kama umerikodiwa katika

„delivery note‟ ilijiridhisha kwamba, vifaa hivyo vinaonekana kupokelewa lakini

havijaingizwa katika „store ledger‟ na kulelezwa kuwa tatizo kama hili pia lipo Vitongoji.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inawataka Mamlaka kufuata utaratibu kama ulivyoelezwa katika Sheria.

Hoja Namba 54.6.4 Malipo ya Tsh. 58,320,800 yaliyofanywa kinyume cha Kanuni na

taratibu za manunuzi

Fedha hizo zimetumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa mbali mbali lakini ununuzi wake

haukufuata taratibu za zabuni, wakati thamani ya fedha hizo zinazidi kiwango kinachotakiwa

kuitishwa zabuni kwa mujibu wa Sheria.

Majibu ya Mamlaka

Ni kweli Mamlaka ilifanya manunuzi hayo kinyume na Sheria, kutokana na kutokuwepo

kwa Bodi ya Zabuni wakati huo. Aidha, vifaa hivyo vilivyonunuliwa ni vya mitihani na

Mamlaka inalazimika kuvinunua kwa muuzaji (supplier) mmoja ambae aliwahi kutoa

huduma kama hizo hapo awali. Hata hivyo, Mamlaka imesharekebisha kasoro hiyo.

Uchunguzi wa Kamati

Baada ya kujiridhisha kukiukwa kwa taratibu za manunuzi, Kamati imehitaji kupatiwa hati

za malipo ya fedha hizo na ilijiridhisha kwamba yalikuwa yanafanyika kidogo kidogo kwa

mujibu wa upatikanaji wa fedha. Aidha, Kamati pia imegundua kutokuwepo kwa maombi ya

fedha hizo kutoka kwa mtumiaji (user department) ndani ya Mamlaka, kosa ambalo Kamati

imeelezwa kuwa limesharekebishwa.

Page 62: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

62

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kufuata taratibu za kisheria katika manunuzi ya vifaa

vinavyohitajika.

Hoja Namba 54.6.5 Upotevu wa vitabu vya risiti

Mamlaka imechapisha vitabu vya risiti kwa ajili ya kukusanya mapato ya fedha kwa vituo

vyake mbali mbali. Kituo cha Mkokotoni vimepelekwa vitabu 40, vyenye risiti namba 6001

hadi 8000 kupitia barua yenye kumbu kumbu namba P33/MMA/18/42/VOL.I ya tarehe 31

Mei 2011, huku ukaguzi ukishindwa kuviona vitabu viwili vya risiti nambari 6701-6750 na

6901 – 6950, hali iliyopelekea kushindwa kupatikana ufafanuzi wa makusanyo ya fedha

kupitia vitabu hivyo.

Majibu ya Mamlaka

Ni kweli wakati wa ukaguzi vitabu hivyo havikuonekana kutokana na Mkuu wa Kituo hicho

kustaafu na aliviweka katika sehemu ambayo wao hawakuijua, ila baada ya kuvitafuta kwa

zaidi ya mwezi mmoja baada ya ukaguzi, ndipo walipoviona.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji utaratibu wa malipo katika Mamlaka, na kuelezwa kuwa wanafunzi

wanalipia Benki na baada ya kupewa „pay in slip‟ ndio Mamlaka hutoa risiti.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeitaka Mamlaka ifuate taratibu za kisheria katika kuweka kumbu kumbu zao.

4.20 AFISI YA MTAKWIMU MKUU WA SERIKALI

Hoja Namba 13.1 Uwasilishaji wa Hesabu kwa ajili ya Ukaguzi

Ukaguzi umebaini kuwa Afisi ya Mtakwimu Mkuu haikuwasilisha hesabu za mwaka,

zinazojumuisha Mapato na Matumizi kama vifungu vya 24(2) na 8 vya Sheria ya Fedha

Namba 12/2005 vinavyoelekeza.

Majibu ya Mtakwimu Mkuu

Afisi ya Mtakwimu Mkuu iliieleza Kamati kuwa haikuwasilisha hesabu hizo kwa kuwa

tangu Afisi hii inaanzishwa ilikuwa inawasilisha taarifa zake za hezabu kupitia Wizara ya

Fedha, isipokuwa kwamba ilipofika mwaka 2011 walipata agizo la kuandaa hesabu hizo

kupitia Ripoti ya Mdhibiti kwa kuwa ni taasisi inayojitegemea.

Kwa kuwa agizo hilo lilitolewa kipindi ambacho hesabu za mwaka zilikuwa zishawasilishwa

Afisi hii ililazimika kuwasilisha kwa wakati mmoja taarifa zake za mwaka wa fedha

2011/2012 na 2012/2013 mnamo mwezi wa Septemba, 2013.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ya PAC iliitaka Afisi hii kuthibitisha kauli yake hiyo kwa kuonesha nyaraka

zinazothibitisha maelezo yake hayo na baada ya kufanya hivyo Kamati ilikubaliana nayo na

kuifuta hoja hiyo ingawa kwa mwaka fedha 2012/2013 Afisi ya Mtakwimu Mkuu

haikuorodheshwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti kama imewasilisha taarifa za hesabu kwa

wakati au la.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati iliisisitiza Afisi hii kujitahidi kuwasilisha taarifa za hesabu kama Sheria

inavyoelekeza.

Page 63: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

63

Mengineyo

Kamati ilitaka kuona namna Afisi hii inavyoingiziwa fedha za matumizi ya kawaida na

maendeleo. Katika kufuatilia hili Kamati hii ilibaini kuwa uingizwaji wa fedha za matumizi

ya kawaida sio mbaya sana kinyume na upande wa kazi za maendeleo.

Aidha, Kamati ya PAC imebaini kuwa makadirio ya fedha kila mwaka yanashuka jambo

ambalo litadhoofisha utendaji wa Afisi hii.

WIZARA NA TAASISI MBALI MBALI ZA SERIKALI-PEMBA

5.0 KAMISHENI YA WAKFU NA MALI YA AMANA

Hoja Namba 44.2.1 Kiwango kidogo cha fedha za kodi za milango mbali mbali ya

Wakfu

Kamisheni inakodisha milango ya biashara kwa wafanya biashara mbali mbali lakini

kiwango cha kodi kinachotozwa ni kidogo kulingana na hali halisi ya thamani ya milango

hiyo katika maeneo hayo. Hali inayowapelekea Kamisheni kukosa mapato yanayostahiki.

Majibu ya Kamisheni

Milango hiyo ilikuwa katika hali mbaya sana ya ubovu na uchakavu na haikuwa ikileta faida

kwa Kamisheni wala wanufaika wa wakfu hiyo. Na kwa kuwa hakukuwa na fedha za

kuijenga upya, Kamisheni ilikubaliana na wapangaji wawekeze katika nyakfu hizo kwa

kutanguliza kima kikubwa cha fedha ili ijengwe kisha wapangishwe kwa mikataba nafuu na

ya muda mrefu, ambapo wanajilipa theluthi mbili na kulipa kodi theluthi moja, na utaratibu

huu ni maarufu katika utunzaji wa nyaraka ulimwenguni kote kwani kinachozingatiwa ni

wanufaika wa sasa na kutunza mali yenyewe ya wakfu ili idumu na iwe sadakatul jariya kwa

wajao.

Aidha, bei hizo huwa zinapitiwa na kupangwa upya kwa kila unapomalizika mkataba wa

miaka mitano kwa kuzingatia hali ya soko na kima alichowekeza mtumiaji. Hivyo, viwango

hivyo vilifanyiwa marekebisho mwaka 2012 na wale ambao mikataba yao haijamalizika,

Kamisheni itairekebisha kwa kuongeza kodi watakapopewa mikataba mipya.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehitaji kupatiwa chanzo cha kuharibika kwa nyumba hiyo ya wakfu na kuelezwa

kuwa imetokana na kuungua moto. Kamati ilipohoji iwapo kulikuwa na taarifa rasmi ya

Polisi au Kikosi cha Zimamoto kuhusiana na moto huo, ilishindwa kupata uthibitisho huo

zaidi ya kuelezwa kuwa, walipofika wao moto huo ulikuwa umeshazimwa.

Vile vile, Kamati imekosa uthibitisho wowote wa kuhusiana na hatua zilizochukuliwa katika

jengo hilo zaidi ya kuelezwa kuwa walimtafuta Engineer Bwana Suleiman Omar Hamad kwa

usimamizi wa ujenzi huo, lakini Kamati ilipohitaji uthibitisho wa upatikanaji wake ambapo

kwa mujibu wa mkataba alilipwa Tsh. 500,000/-, Kamati ilikosa uthibitisho wa upatikanaji

wake kisheria, lakini pia uthibitisho wa kupokea fedha hizo alizolipwa haukuweza

kupatikana kwa Kamati.

Hata hivyo, Kamati ilipofanya ziara katika maeneo hayo, ilishuhudia tofauti ya bei ya

milango kwa mnasaba wa hata eneo ilipo na ukubwa wake.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Kamisheni kuwa makini inaposhughulikia suala la ujenzi, kwani kama

hakutakuwa na usimamizi imara, watu wasiokuwa waaminifu watatumia mwanya huo na

kuifanya Kamisheni ishindwe kutimiza majukumu yake.

Page 64: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

64

MASHIRIKA YA SERIKALI - TANZANIA BARA

6.0 SHIRIKA LA BIASHARA LA TAIFA (ZSTC), TAWI LA DAR ES SALAAM

Hoja Namba 84.1.1 Rasilimali za Shirika

Nyumba ya Sinza

Shirika linamiliki nyumba namba 82 katika eneo la Sinza ambayo imekodishwa kwa Ndg.

Ramadhan Mwita kwa kodi ya Tsh. 500,000 kwa mwezi ni sawa na Tsh. 6,000,000 kwa

mwaka. Ukaguzi umebaini kuwa nyumba hiyo hairidhishi kutokana na kutofanyiwa

ukarabati kwa muda mrefu.

Majibu ya Shirika

Ni kweli hoja hiyo na Shirika linakiri kuwa kihalisia nyumba hiyo hairidhishi. Iwapo

inanyensha mvua, majo yote yanakwenda na kutuwama katika nyumba hiyo. Hata hivyo,

Shirika limechukuwa hatua ya kuamua kuivunja nyumba hiyo na kujenga jengo la ghorofa

tano kutokana na masharti ya ujenzi katika eneo hilo ni jengo lisilozidi ghorofa hizo tano,

vyenginevyo wangelizidisha zaidi ya ghorofa hizo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji gharama za kukodisha Tsh. 500,000 kama zina tija ukizingatia nyumba

pamoja na ubovu na uchakavu wake, kwa mazingira ya eneo la Sinza ingelikuwa na soko

zaidi, na kuelezwa ni kodi ya takriban miaka miwili sasa na hapo mwazo waliikodisha kwa

Shirika la Bima kwa Tsh. 350,000/- na kwa sasa hawana mpango wa kuzidisha kodi

kutokana na uchakavu wake na kutuwama kwa maji ya mvua.

Aidha, Kamati imeelezwa zaidi kuwa, mvua inaponyesha na maji kutuwama, wapangaji

hulazimika kuhama kwa takriban miezi mitatu na zaidi kipindi cha mvua za masika na

baadae Shirika hulazimika kutafuta gari la kufyonza maji ili maji hayo yaondoke.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeridhika kwamba, jengo hilo linahitaji matengenezo ya haraka na kwa kuwa

Shirika lina azma ya kujenga jengo jengine la ghorofa tano, ni vyema ujenzi huo ukaanza

mara moja ili kuepusha hasara inayoendelea kupatikana.

Kamati inalikumbusha Shirika kufanya ujenzi huo kwa kufuata taratibu za Sheria, ili

kuepuka kujengwa chini ya kiwango na kupoteza fedha za Serikali.

Tawi la Dar es Salaam

Ukaguzi umebaini kuwa, tawi la Shirika la Dar es Salaam halionekani kuwa na tija kwa

Shirika. Kuendelea kuwepo kwa tawi hilo ni kuongeza gharama za uendeshaji ambapo kuna

wafanyakazi wawili wanaoendesha shughuli za tawi hilo ambapo hulazimika kulipa gharama

za kukodi nyumba kwa ajili ya Ofisi na ghala kwa Tsh. 4,131,298 kwa mwezi ambapo ni

sawa na Tsh. 49,575,576 kwa mwaka.

Majibu ya Shirika

Tawi la Dar es Salaam ni sehemu ya Shirika na kwa sasa Shirika limo katika mageuzi

makubwa. Katika kuhakikisha tawi hilo linaleta tija, jambo la msingi ni kuhakikisha Shirika

linauziwa jengo liliopo tawi hilo kutoka kwa Shirika la Nyumba la Taifa, ambapo walifanya

juhudi ya kumuomba Makamo wa Pili wa Rais kuwasaidia kuwaomba Serikali ya Jamhuri

ya Muungano kuuziwa jengo hilo kwa Shirika.

Aidha, Shirika lilikiomba Chuo cha Utawala wa Fedha, Chwaka kulifanyia utafiti wa

kitaalamu (study) tawi hilo la Dar es Salaam, ili kujua faida na hasara ya kuwa na tawi hilo

na tayari Chuo kimeshakuja na kuliona na wanaendelea na kazi.

Page 65: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

65

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ilitaka kujiridhisha na kuthibitishiwa juhudi za kuomba kuuziwa kwa jengo hilo na

kupatiwa barua ya tarehe 29/12/2014 yenye kumbu kumbu namba SBT/BLW/52/36 VOL.III

inayotoa uthibitisho wa ufuatiliaji wa kuuziwa jengo hilo, ambapo uchambuzi wake ni huu

ufuatao.

Mnamo tarehe 16 August, 2004 Meneja wa Tawi Dar es Salaam, Ndg. Said M. Khamis

alimuandikia barua Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara, Viwanda, Masoko na Utalii yenye

kumbu kumbu namba ZSTC/DSM/36 VOL.2 kupendekeza hatua za kuuziwa kwa jengo hilo

ili Shirika, tawi la Dar es Salaam liweze kujitanua kibiashara kwa kuweza kupunguza

gharama za kodi zinazopanda mwaka hadi mwaka, na kopi ya barua hiyo ikapelekwa kwa

Katibu wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi na

Shirika la Nyumba la Taifa.

Tarehe 19 Augosti 2004, Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara, Viwanda, Masoko na Utalii

alimuandikia barua Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi yenye

kumbu kumbu namba WBVMU/M.120/C6 VOL.II/14 kumuomba kama Wizara, kuuziwa

kwa jengo hilo, na nakla ya barua hiyo ikapelekwa kwa Meneja Mkuu wa Shirika.

Mnamo tarehe 19 March 2009, Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara ya Utalii, Biashara na

Uwekezaji alimuandikia barua Meneja Mkuu wa Shirika yenye kumbu kumbu namba

WUBU/B.70/C2 VOL.IV/152 kumtaka afuatilie suala la kuuziwa kwa jengo hilo kwa

Shirika.

Tarehe 22 Oktoba 2010, Waziri wa Utalii, Biashara na Uwekezaji Zanzibar alimuandikia

barua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi ya Tanzania kumkukumbusha

juhudi alizofanya za kumuandikia barua kabla na watendaji wa Wizara pamoja na Shirika

kufuatilia suala la kuuziwa kwa jengo hilo kwa Shirika, bila ya kupata majibu yoyote.

Waziri huyo huyo mnamo tarehe 1/11/2012 alimuandikia barua nyengine Waziri wa Ardhi,

Nyumba na Maendeleo ya Makaazi yenye kumbu kumbu namba WBVU/M.120/C.8/43

akiomba kwa mara nyengine tena kuuziwa kwa jengo hilo huku akieleza gharama inazopata

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Shirika lakini hakuna mafanikio yoyote

yaliyofikiwa.

Kama hii haitoshi, Makamo wa Pili wa Rais, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, alimuandikia barua

nyengine Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi yenye kumbu kumbu namba

OMPR/MASH/TS.35/1 ya tarehe 26 Agosti 2013, kukumbushia barua zilizopita za Serikali

na kulalamikia tabia ya kutopata majibu yoyote na kueleza umuhimu wa jengo hilo kuuziwa

Shirika na nakla ya barua hiyo ikitumwa kwa Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko ya

Zanzibar na Mkurugenzi wa Shirika. Lakini hadi leo hakuna mafanikio yoyote.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeridhika kuwa Shirika limechukua hatua na juhudi za kutosha kuomba kuuziwa

jengo hilo lakini inashangazwa sana na Serikali ya Muungano kupitia Wizara ya Ardhi,

Nyumba na Maendeleo ya Makaazi kukaa kimya na kuonesha dharau kubwa kwa Serikali ya

Mapinduzi ya Zanzibar, jambo ambalo halikupaswa kufanywa.

Kamati inaitaka Serikali kusafiri hadi Tanzania bara kuonana na Mhe. Rais kuhusiana na

suala hili, ambae huenda akawa hajui kilichoendelea muda wote huo.

Page 66: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

66

RIPOTI YA UKAGUZI WA HESABU KWA MAWIZARA, MASHIRIKA NA

TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013

7.0 WIZARA NA TAASISI MBALI MBALI ZA SERIKALI

7.1 WIZARA YA FEDHA

Hoja Namba 19.1 Matokeo ya Hesabu za mwisho wa mwaka. Taarifa za mapato na

matumizi

Taarifa za mapato za Wizara ya Fedha za mwaka 2012/2013, zinathibitisha kuwa ilikadiriwa

kukusanya Tsh. 553,400,000/-, na ulipotimia mwaka, Wizara ilifanikiwa kukusanya Tsh.

956,918,000/. Kwa upande wa matumizi ya kawaida, fedha zilizoainishwa ni Tsh.

39,584,000,000/- na fedha halisi zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 37,277,912,000/- kukiwa

na upungufu ya Tsh. 2,306,088,000 sawa na asilimia 6 ya makadirio. Aidha, matumizi ya

maendeleo, Wizara iliidhinishiwa kutumia Tsh. 8,325,000,000/-, lakini mwisho wa mwaka

ulipofika, fedha zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 6,144,663,000, sawa na asilimia 74

ya makadirio.

Majibu ya Wizara

Taarifa za makisio ya makusanyo za mwaka huu haziko sawa, kwani inashindwa kujua kama

ni ya Wizara au ya Serikali, ukizingatia taarifa ya mwaka 2011/2012, ambapo makisio ya

makusanyo yaliyooneshwa katika taarifa yanathibitika kuwa ni ya Serikali kwa ujumla wake.

Uchunguzi wa Kamati

Ili kujiridhisha maelezo ya Wizara, Kamati ilihitaji ufafanuzi kutoka kwa Afisa Mdhibiti

aliefuatana na Kamati na kukubaliana kuwa, taarifa hizo hazioneshi uhalisia wa makusanyo

yaliyokusudiwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Afisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali,

kufafanua kwa uwazi na usahihi taarifa za ripoti zake, ili ziweze kufanyiwa kazi

kiurahisi na Kamati.

Kamati inaishauri Serikali kuwa na vigezo sahihi vya makusanyo ya mapato, ili

Taasisi zote ziwe na rikodi nzuri za kiwango cha mafanikio ya makusanyo halisi.

7.2 WIZARA YA AFYA

Hoja Namba 25.1.1 Matokeo ya hesabu za Mwisho wa Mwaka

Taarifa za mapato na matumizi

Wizara ya Afya ilikadiriwa kukusanya Tsh. 995,500,000 kwa mwaka 2012/2013, fedha

ambazo hazikuweza kufikiwa kama ilivyokisiwa kwa kukusanywa Tsh. 581,123,624 sawa na

asilimia 58.4 ya makadirio, kukiwa na upungufu wa Tsh. 414,376,376, sawa na asilimia 41.6

ya makadirio.

Aidha, matumizi ya kazi za kawaida yalikuwa Tsh. 18,229,000,000, na kutokana na hali

halisi ya kuingiziwa fedha hizo kwa ukamilifu wake, Wizara ilitumia kama ilivyokadiriwa.

Vile vile kwa kazi za maendeleo, Wizara ilikadiriwa kutumia Tsh. 21,982,205,000 kutoka

kwa Wahisani wa Maendeleo na Serikali, lakini fedha halisi iliyoingizwa na kutumika,

ilikuwa Tsh. 4,070,854,400.

Page 67: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

67

Majibu ya Wizara

Wizara inakiri hesabu hizo, ambapo uchache wa mapato kinyume na makadirio unatokana na

kuondoshwa kwa michango ya mama wajawazito. Aidha, kwa matumizi ya kawaida, Wizara

inashukuru kwa kupata asilimia mia moja, ingawaje hesabu hiyo inaakisi zaidi fedha za nje

ya nchi kwa matibabu, huku Wizara ikikosa fedha za matumizi kwa vifungu vyengine.

Aidha, kutokana na kukosa bajeti kamili ya maendeleo, Wizara imeshindwa kutekeleza

baadhi ya miradi kwa ukamilifu wake, kwa mfano, imeathirika katika mradi wa kupandisha

hadhi hospitali ya Mnazi mmoja na hospitali zilizotakiwa kuwa za Wilaya kutoka „Cottage‟

na kwa upande wa Mradi wa ujenzi wa jengo la Kitengo cha Macho, wameshindwa

kukarabati jengo hilo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imelipokea suala la usafirishwaji wa wagonjwa nje ye nchi kwa upekee, ambalo

linahitaji kuangaliwa tena, kwani Wizara huonekana inaingiziwa fedha hizo, wakati gharama

za usafirishaji na posho la kujikimu kwa watumishi wa Serikali, lingeliweza kufanywa na

Wizara ama Taasisi husika, huku Wizara ikabaki na jukumu la kugharamia matibabu tu.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuzingatia kipaumbele cha Wizara hii ya Afya kwa

kuingizia fedha kamili za matumizi ya kawaida na maendeleo.

Kamati inaishauri Serikali kupitia Wizara ya Fedha, kuzitaka Wizara na Taasisi za

Serikali, zitayarishe bajeti itakayoonesha malipo ya nauli na posho la kujikimu kwa

watumishi na viongozi mbali mbali wa Wizara na Taasisi husika, wanaosafirishwa

nje ya nchi kwa matibabu, huku jukumu la Wizara likabaki katika kugharamia

matibabu pekee.

Hoja Namba 25.1.2 Malipo yaliyofanywa kinyume na kanuni na taratibu za

manunuzi, Tsh. 54,425,500

Fedha hizo zimetumika kwa ununuzi wa madawa ya wodi ya wazazi, Unguja na Pemba,

lakini manunuzi hayo hayakufuata taratibu za kisheria.

Majibu ya Wizara

Dawa zilizonunuliwa kwa fedha hizo ni za kuwasaidia kina mama wajawazito na watoto.

Dawa hizo hununuliwa kila muda zinapopatikana fedha kwa awamu na sio kwa mara moja.

Vile vile hufuata taratibu za manunuzi ambapo kiwango kinachozidi USD 10,000 huitishwa

tenda na manununzi chini ya kiwango hicho hufuata utaratibu wa manunuzi kwa kuwasilisha

„Qoutation‟ na Kampuni yenye kiwango kidogo ndio wanayoitumia kununua dawa hizo.

Hivyo, Wizara imenunua dawa hizo kwa kutumia „Invoice System‟ kwa kufuata utaratibu wa

manunuzi.

Uchunguzi wa Kamati

Kwa kuzingatia fedha iliyotengwa kufanya manunuzi husika, Wizara haikuwa na sababu ya

kuzitumia fedha hizo kidogo kidogo (instalment) kwa lengo la kukwepa kufuata taratibu za

kisheria. Na kwa kuwa Wizara hutakiwa kuwa na Mpango wa Manunuzi, ambayo huonesha

matumizi ya fedha hizo kwa pamoja, kutumia kidogo kidogo kwa lengo hilo, haiifanyi

ulazima wa wa kufuatwa Sheria kubatilika.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuhakikisha inafanya manunuzi kwa kufuata taratibu za kisheria.

Page 68: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

68

7.3 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI

Hoja Namba 24.1.1 Matokeo ya hesabu za Mwisho wa Mwaka

Taarifa za mapato na matumizi

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ilikadiriwa kutumia Tsh. 71,050,000,000 kwa kazi za

kawaida kwa mwaka 2012/2013. Aidha, Wizara iliingiziwa na kutumia Tsh. 67,698,946,000

sawa na wastani wa asilimia 95, kukiwa na upungufu wa bajeti kamili ya Tsh. 3,351,054,000

sawa na asilimia 5 ya makadirio. Kwa matumizi ya kazi za maendeleo, Wizara ilikadiriwa

kutumia Tsh. 5,1000,000,000, lakini hali halisi ya uingizwaji na utumiaji wa fedha hizo

unaonesha kuwa ni Tsh. 3,016,700,000 sawa na asilimia 59 ya makadirio, kukiwa na

upungufu wa Tsh. 2,083,300,000 sawa na asilimia 41 ya makadirio.

Majibu ya Wizara

Ni kweli fedha hizo zimeingizwa na kutumika na athari zilizopatikana kwa upungufu wa

fedha za kawaida, ni kukosekana kwa vifaa vya kufanyia mitihani. Wizara pia ilipanga

kununua kompyuta kwa skuli za sayansi na kupelekea kushindwa kununua kompyuta hizo

kwa mwaka 2012/2013 na matokeo yake wamenunua kwa mwaka huu wa fedha. Wizara ina

limbikizo la deni linalotokana na ada ya mitihani ya Form IV na hawakuweza kulipa kwa

mwaka huo na wamelazimika kulibeba kwa miaka iliyofuata na sasa limeshafikia Tsh.

998,000,000/-

Kwa upande wa matumizi ya kazi za maendeleo, Wizara imeathirika katika maeneo mbali

mbali kwa kukosa bajeti kamili, ikiwa ni pamoja na kukamilisha ujenzi wa mradi wa

uimarishaji wa maktaba na kushindwa kukamilisha ujenzi wa mradi wa ukarabati wa taasisi

ya Karume pamoja na ujenzi wa msingi wa dahalia ya skuli ya sekondari ya Kengeja.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeelezwa kwamba, Wizara ya Fedha ina taarifa nyingi rasmi za madeni ya Wizara

ya Elimu na Mafunzo ya Amali, pamoja na kupokea mabadiliko ya mshahara na

malimbikizo yake kutoka Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma

kuhusu suala hilo na hakuna hatua ilizozichukuwa au kama ipo, basi hatua zilizochukuliwa

ni za kiwango kidogo na haziridhishi. Kwa mfano tokea 2012, Wizara ya Elimu Pemba

hakujafanyika mabadiliko ya mshahara wakati barua zimeshafika Wizara ya Fedha mapema.

Aidha, Wizara inakabiliwa na tatizo la kuchelewa kulipwa kwa walimu wanaosimamia

mitihani, huku Wizara ikitoa taarifa mapema za maombi hayo Wizara ya Fedha. Pia Kamati

imetaka ufafanuzi wa mradi wa usambazaji wa madawati katika Skuli za Zanzibar na

kuelezwa kuwa, Wizara inapewa kasma ya bilioni 2 kwa mwaka, lakini fedha wanayopata ni

milioni 300 pekee.

Kamati imesikitishwa na taarifa hii kutokana na fedha ya usambazaji wa madawati wakati

Serikali ilipandisha kodi ya Tsh. 1,000 kwa wasafiri wa njia ya boti wanaokwenda Dar es

Salaam, ili yanunuliwe madawati.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuwaingizia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, fedha zote

zinazotokana na kodi hiyo ili Wizara iweze kutekeleza malengo yaliyokusudiwa.

Page 69: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

69

7.4 WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

7.4.1 OFISI YA MKURUGENZI WA MASHTAKA

Hoja Namba 20.5.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Matumizi ya Kazi za Kawaida na Maendeleo

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ilikadiriwa kutumia kwa kazi za kawaida, Tsh.

979,000,000 kwa kazi za kawaida kwa mwaka 2012/2013. Aidha, fedha halisi zilizoingiziwa

na kutumia Tsh. 978,546,000 sawa na wastani wa asilimia 100 ya makadirio. Kwa matumizi

ya kazi za maendeleo, Wizara ilikadiriwa kutumia Tsh. 250,000,000, na fedha hizo hizo

ndizo zilizoingizwa na kutumika, sawa na asilimia 100 ya makadirio.

Majibu ya Ofisi

Ni kweli taarifa hizo na Ofisi imeshukuru kwa kuingiziwa lakini bado Ofisi inakabiliwa na

tatizo la mishahara na posho kwa watendaji. Ofisi pia inaendelea na tatizo la

kucheleweshewa kuingiziwa fedha za OC kiasi cha kukwamisha shughuli zake.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imepokea taarifa ya Ofisi kwa masikitiko makubwa na kuishangaa Serikali

kushindwa kutoa kipaumbele cha matumizi na mgawanyo wa fedha kwa Ofisi hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuzingatia mahitaji ya Ofisi hii na kuipatia fedha kwa wakati na

kwa ukamilifu, ili itekeleze majukumu yake kwa ufanisi.

7.4.2 KAMISHENI YA WAKFU NA MALI YA AMANA

Hoja Namba 20.2.1 Malimbikizo ya madeni kwenye nyumba za wakfu na mali ya

amana, Tsh. 205,125,700

Kumekuwa na ugumu kwa wananchi kulipia kodi ya upangaji katika nyumba za wakfu,

jambo ambalo linarejesha nyuma jitihada za Serikali katika ushughulikiaji wa nyumba hizo

kutokana na kuhitaji matengenezo tofauti na yanayohitaji gharama kubwa. Hivyo, fedha

zinazodaiwa kwa wapangaji hao ni Tsh. 205,125,700 na bado hazijalipwa na inashauriwa

kuandaliwa utaratibu wa kuwafanya wapangaji walipie kodi kwa wakati.

Majibu ya Kamisheni

Taarifa hiyo ni kweli, ingawaje Kamisheni imeshachukua hatua mbali mbali kama

ilivyoshauriwa na Mkaguzi. Miongoni mwa hatua hizo utoaji wa elimu juu ya dhana na

malengo ya wakfu, kuimarisha kumbu kumbu kwa kufanya uhakiki na kutambua wenye

madeni kila baada ya miezi sita, kukamilisha sulhu ya mzozo uliobuka baada ya

kupandishwa kwa kodi, kutayarisha na kuzifanyia kazi kanuni zilizotolewa kupitia Gazeti la

tarehe 9 Juni 2014, kuunda kikosi kazi cha watu watano kwa kufuatilia madeni na

kuwapangia baadhi ya watendaji kazi ya kudumu ya ukaguzi wa nyumba. Aidha, sasa deni

hilo la Tsh. 205,125,700 limelipwa na kubaki Tsh. 72,554,500/-

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji sababu zinazowapelekea wapangaji kutolipa wakati mikataba yao inaeleza

wanatakiwa kulipa. Aidha, kwa nini Kamisheni isiwachukulie hatua za kuwapeleka

Mahakamani ili kuwalazimisha kulipa. Kamati imefurahishwa na juhudi zilizochukuliwa na

Kamisheni za kupunguza deni, lakini imesikitishwa sana na baadhi ya wapangaji 31 ambao

hawajalipa kabisa na kuonesha dharau dhidi ya Kamisheni. Pia Kamati ilihitaji kupatiwa

Page 70: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

70

majina ya wapangaji waliokuwa hawakujaza mikataba mwaka 2014, na tarehe 24/02/2015

iliwasilishwa kwa Kamati orodha ya wapangaji 33 kupitia barua yenye kumbu kumbu namba

KWNMA/BW/85/VOL.I/11 inayoonesha majina yao, nyumba waliyopanfa na mtaa ambao

ipo nyumba husika.

Aidha, Kamati imehoji mkataba wa Aga Khan wa kukodishwa „Old Dispensary‟ kwa

gharama ndogo kabisa ya Tsh. 1,000 kwa mwezi tena kwa kodi ya miaka 80, wakati sheria

imeipa uwezo wa kuvunjwa kwa mikataba ya aina hiyo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Kamisheni kuhakikisha kuwa wapangaji 31 waliobainika kuwa hawajalipa

kabisa wafikishwe Mahakamani ili waweze kulipa madeni yao. Kuhusiana na wapangaji

ambao bado hawakujaza mikataba, Kamisheni inatakiwa kuhakikisha wapangaji hao

wanajaza mikata kwa mujibu wa Sheria, ili iweze kusimamia ipasvyo nyumba wanazokaa

wapangaji hao. Aidha, kuhusiana na mkataba wa Aga Khan, Kamati imeitaka Kamisheni

kulifuatilia suala hilo kwa hatua za kisheria.

Hoja Namba 20.2.2 Kuchukuliwa kwa shamba la wakfu.

Ukaguzi umebaini kuwa, shamba la wakfu la Ndg. Hamoud Ahmed liliopo Mfenesini

Unguja, limechukuliwa na watu mbali mbali kwa ajili ya shughuli za kilimo na kujenga

nyumba za kuishi, bila ya kibali kutoka kwa Kamisheni. Kamisheni inashauriwa kuchukua

hatua za kuyapitia mashamba ya wakfu pamoja na kuhakikisha kwamba, kunakuwa na

udhibiti mzuri wa mashamba hayo.

Majibu ya Kamisheni

Kamisheni imefanya uhakiki na uchambuzi wa kiutafiti kuhusiana na mashamba ya wakfu

juu ya namna bora ya kurejeshwa kwa mashamba ya wakfu na moja kati ya mambo

yaliyobainika ni kuwepo kwa utashi wa kisiasa (political will), kwani wakati Kamisheni

inaanzishwa mwaka 1980, mashamba ya wakfu yalikuwa tayari yameshavamiwa.

Shamba linalohusika na hoja hii liliasisiwa kuwa wakfu wa mawali (freed slave) mwaka

1875 na asili yake lilikuwa Saateni kwa Abass Hussein. Mwaka 1953 Serikali ya Zanzibar

ililichukua shamba hilo na kubadilishana na shamba la Mfenesini ambalo kwa sasa

limevamiwa kwa makaazi ya watu na shughuli za kilimo kwa zaidi ya miaka 40.

Hata hivyo, Kamisheni imechukua hatua za kufanya uhakiki na upembuzi wa wanufaika

pamoja na vikao tokea mwaka 2011 na wanufaika wa shamba na wanaolitumia. Pia

Kamisheni ilitoa barua tarehe 21/3/2013 kuwataka waliojenga nyumba za muda wahame na

wanaofanya shughuli za kilimo waendelee lakini wakati wowote wakitakiwa kuhama wasije

kudai fidia na uongozi wa Jimbo la Mfenesini kumuomba Mhe. Waziri wa Katiba na Sheria

kusitisha utekelezaji wa amri kwa muda ili kuliangalia upya suala hilo na kuomba Serikalini,

wakfu huo ufidiwe shamba jengine, ingawaje mazungumzo bado yanaendelea na kikao cha

mwisho kilitarajiwa kufanyika tarehe 7/11/2014.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na ufafanuzi huo, Kamati pia imeelezwa kuwa, wenye wakfu walikwishaongea na

Muzdalifa Charitable Association kwa ajili ya kujengwa chuo cha ufundi na dahalia, lakini

bado suala hilo lipo katika ngazi ya Wizara.

Page 71: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

71

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali pamoja na Kamisheni ya Wakfu kuharakisha kulitatua na

kulipatia mustakbali mwema suala hili kwa haraka.

7.5 WIZARA YA UWEZESHAJI, USTAWI WA JAMII, VIJANA,

WANAWAKE NA WATOTO

Hoja Namba 28.1.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa za matumizi ya kawaida na maendeleo

Wizara ilikadiriwa kutumia Tsh. 2,066,396,041 kwa kazi za kawaida kwa mwaka 2012/2013.

Aidha, Wizara iliingiziwa na kutumia Tsh. 2,034,175,011 sawa na wastani wa asilimia 98,

ikiwe ni upungufu wa Tsh. 32,221,030 sawa na asilimia 2 ya makadirio. Kwa matumizi ya

kazi za maendeleo, Wizara ilikadiriwa kutumia Tsh. 1,506,600,000, lakini hali halisi ya

uingizwaji na utumiaji wa fedha hizo unaonesha kuwa ni Tsh. 571,088,782 sawa na asilimia

38 ya makadirio, kukiwa na upungufu wa Tsh. 935,511,218 sawa na asilimia 62 ya

makadirio.

Majibu ya Wizara

Ni kweli kwamba Wizara hii iliingiziwa fedha hizo zikiwa na mapungufu hayo, hata hivyo,

Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto haina hatua za

kuchukua kwa kuwa inategemea kuingiziwa fedha kutoka Wizara ya Fedha. Kuhusiana na

nyongeza ya matumizi ya kazi za kawaida, Wizara imepata nyongeza hiyo kutokana na

nyongeza ya mishahara.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati hii imebaini kuwa ingawa kuna upungufu wa uingizwaji wa fedha za matumizi kwa

kazi za kawaida katika mwaka huu wa fedha, hata hivyo upungufu huo sio mkubwa sana

ukilinganisha na uingizwaji wa fedha kwa matumizi ya kazi za maendeleo. Hii ni kutokana

na kuwa kwa upande wa matumizi ya kazi za maendeleo kuna upungufu wa asilimia 62 ya

makadirio.

Mapendekezo ya Kamati

Serikali ifanye juhudi ya kuingiza kwa ukamilifu bajeti za Wizara na taasisi zake, ili Wizara

na taasisi hizo ziweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

7.6 WIZARA YA NCHI (OR) KAZI NA UTUMISHI WA UMMA

Hoja Namba 43.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2011/2012

Taarifa ya Matumizi ya kawaida na maendeleo

Makusanyo ya Wizara yalikadiriwa kuwa Tsh. 93,000,000 kwa mwaka 2012/2013 na hali

halisi ya makusanyo yalikuwa Tsh. 137,786,787. Kwa upande wa matumizi, Wizara

ilikadiriwa kutumia Tsh. 2,324,277,000 kwa kazi za kawaida na fedha halisi zilizoidhinishwa

na kutumika ni Tsh. 2,125,771,199. Aidha, matumizi ya kazi za maendeleo yalikisiwa kuwa

Tsh. 2,067,602,896 na fedha hizo hizo ziliingizwa na kutumiwa zilikuwa Tsh. 513,053,744.

Majibu ya Wizara

Taarifa hizo ni sahihi na kuhusiana na matumizi ya maendeleo, Wizara ilikuwa na shughuli

mbali mbali za utekelezaji wa miradi iliyohusika, ikiwa ni pamoja na utungaji wa Sheria za

Utumishi wa Umma na kanuni zake, miradi ambayo hapo awali ilikuwa inategemea „World

Page 72: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

72

Bank‟ lakini hivi sasa Wizara inapata fedha kutoka Serikalini pekee. Hivyo, Wizara

inakabiliwa na changamoto kubwa ya kukosa wafadhili wa mradi huu isipokuwa Serikali.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati imehoji muda mrefu wa utekelezaji miradi ya Wizara na kuamini kuhusiana na

kukosa wafadhili kuwa, suala hilo lingestahiki kufanywa na Serikali na sio kutegemea

Wafadhili.

Hoja Namba 16.1.2 malipo yasiyokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu), Tsh.

15,519,500

Fedha hizo zimelipwa kwa matumizi mbali mbali lakini vielelezo husika havikupatikana kwa

ukaguzi, kinyume na kanuni ya 95(4) ya Kanuni za Fedha za mwaka 2005 na kwa hali hii,

uhalali wa malipo haukuweza kuthibitishwa na Mkaguzi.

Majibu ya Wizara

Ni kweli wakati wa ukaguzi vielelezo hivyo havikuwepo, lakini hivi sasa tayari vipo tayari

kwa kukaguliwa na Kamati.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati inafahamu usahihi wa hoja ya Mkaguzi na maelezo ya Wizara hayawezi kufuta

maelekezo ya Sheria ya kupatikana kwa vielelezo hivyo, mara tu fedha za Serikali

zinapotumiwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara irekebishe kasoro hiyo.

7.6.1 KAMISHENI YA UTUMISHI WA UMMA

Hoja Namba 16.2.1 Taarifa ya Matumizi ya Kazi za Kawaida

Kamisheni ya Utumishi wa Umma ilikadiriwa kutumia Tsh. 856,484,000 kwa kazi za

kawaida kwa mwaka 2012/2013 na fedha halisi zilizopatikana na kutumika ni Tsh.

420,673,177, sawa na asilimia 49.12 ya makadirio, ikiwa kuna upungufu wa Tsh.

435,810,823 sawa na asilimia 50.88 ya makadirio.

Majibu ya Kamisheni

Ni kweli fedha hizo zimeingizwa na kutumika na athari kubwa zilizopatikana kwa

Kamisheni kutopatiwa fedha zote za makisio ya matumizi ni kushindwa kutekeleza

majukumu yake kisheria, ikiwa ni pamoja na kushindwa kutowa elimu ya Sheria za

Utumishi wa Umma na kutofanya shughuli mbali mbali. Kamisheni pia imeshindwa kutoa

uwezeshaji wa Miongozo ya Utumishi wa Umma na kufanya tathmini kwa taasisi mbali

mbali za Umma.

Aidha, Kamisheni haikuweza kununua gari iliyopanga kuinunua kwa Makamishna kwa ajili

ya kutembelea sehemu mbali mbali za umma na zaidi kwa hivi sasa ununuzi wa gari

hauhesabiki kuwa ni sehemu ya matumizi ya maendeleo, hivyo hulazimika kutumia OC kwa

matumizi hayo.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na maelezo ya Kamisheni, Kamati imejiridhisha kuwa Kamisheni inakabiliwa na

tatizo la kutokuwa na watendaji wa kutosha kwa kazi zake, jambo ambalo linawanyima pia

Page 73: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

73

fursa ya kuomba miradi ya maendeleo. Aidha, Kamisheni haina jengo lake na ililonalo sasa

linawagharimu USD 500 kwa kila mwezi kuwalipa Shirika la Bandari wamiliki wa jengo

hilo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuiwezesha Kamisheni kimatumizi na kuwapa miradi ya maendeleo

ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Hoja Namba 12. Uwasilishaji wa hesabu za mwisho wa mwaka kwa ukaguzi

Pamoja na kifungu cha 24(2) cha Sheria ya Fedha kuzitaka taasisi zote za Serikali

kuwasilisha hesabu zao za mwisho wa mwaka, Kamisheni imechelewa kwa kuwasilisha

tarehe 01/10/2013 kinyume na maelekezo ya Sheria ya kuwasilishwa hesabu hizo si zaidi ya

tarehe 30/09 ya kila mwaka.

Majibu ya Kamisheni

Si kweli kuwa Kamisheni imewasilisha hesabu zake tarehe iliyotajwa na mkaguzi na badala

yake imewahi na imewasilisha kwa wakati.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ilitaka kuthibitishiwa ukweli wa maelezo ya Kamisheni na kwa kupitia „Despatch‟,

ilijiridhisha kuwa waliwasilisha tarehe 30/09/2013 kupitia barua yenye kumbu kumbu namba

OR/KUU/F.47/VOL.1/010.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inapendekeza hoja hii ifutwe.

7.7 WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI

Hoja Namba 21.1.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Makadirio ya Mapato na Matumizi

Tsh. 426,000,000 zilikadiriwa kukusanywa kwa mwaka 2012/2013 na Wizara ya Kilimo na

Maliasili, na ulipotimia mwaka, Wizara ilifanikiwa kukusanya Tsh. 550,216,660 sawa na

asilimia 129 ya makadirio, ikiwa ni ongezeko la Tsh. 124,216,660 sawa na asilimia 29 ya

makadirio.

Kwa upande wa matumizi ya kawaida, fedha zilizoidhinishwa ni Tsh. 11,488,810,589/- na

fedha halisi zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 11,219,744,188/- sawa na asilimia 98 ya

makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 269,006,401 sawa na asilimia 2 ya makadirio. Aidha,

matumizi ya maendeleo, Wizara iliidhinishiwa kutumia Tsh. 11,507,116,000/-, lakini

mwisho wa mwaka ulipofika, fedha zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 3,250,832,104,

sawa na asilimia 28 ya makadirio, kukiwa na upungufu wa Tsh. 8,256,283,896 sawa na

asilimia 72 ya makadirio.

Majibu ya Wizara:

Wizara iliieleza Kamati kuwa ongezeko la mapato hayo yametokana na juhudi kubwa

zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara hii za kufuatilia vianzio vyake vya mapato. Aidha,

Wizara ilikiri kuingiziwa fedha zikiwa na upungufu. Hata hivyo, ilieleza kuwa tatizo hilo

limetokea Wizara ya Fedha kwani ndio taasisi yenye mamlaka ya kutoa fedha kwa Zanzibar.

Kutokana na upungufu huo Wizara ilishindwa kutekeleza baadhi ya shughuli zake kama

ilivyojipangia.

Page 74: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

74

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imebaini kuwa makisio ya mapato kwa mwaka wa fedha 2012/2013 ni madogo

ukilinganisha na mapato yaliyokusanywa kwa mwaka 2011/2012. Kutokana na hilo Kamati

hii ilielezwa kuwa Wizara haikuanzia kupanga kwenye makusanyo waliyoyapata katika

mwaka wa fedha 2011/2012 ambayo ni Tsh. 539,752,000.00 kwa kuwa katika mwaka

uliofuata mzao wa karafuu haukuwa mzuri. Kitendo hiki kimesababishwa na baadhi ya

wananchi kuikata mikarafuu jambo ambalo hupelekea mikarafuu kuwa michache na hivyo

kukosa mapato.

Kamati ya PAC haikukubaliana moja kwa moja na majibu hayo hasa ikizingatiwa kuwa

katika mwaka huo wa fedha (2012/2013) Wizara hii pia ilikusanya mapato kwa ongezeko la

Tsh.10,464,660.00.

Vile vile, Kamati imebaini kuwa uingizwaji wa fedha za maendeleo kwa Wizara hii sio wa

kuridhisha hata kidogo jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya Wizara hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kupitia Wizara ya Fedha kuhakikisha wanaipatia Wizara kiwango

kamili cha makisio ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Kwa upande wa

mapato, Kamati inaishauri Wizara kuongeza juhudi ya kukusanya, ili mapato ya Serikali kwa

ujumla yaweze kupatikana kwa uhakika.

7.8 WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Hoja Namba 23.1.1 Taarifa ya Mapato na Matumizi

Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilikadiriwa kukusanya Tsh. 213,000,000 kwa mwaka

2012/2013, na fedha halisi ya makusanyo hayo zilikuwa Tsh. 157,115,000 sawa na asilimia

74 ya makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 55,885,000 sawa na asilimia 26 ya makadirio.

Matumizi ya kawaida kwa Wizara hii, yalikadiriwa kuwa Tsh. 3,042,068,389, lakini fedha

halisi zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 3,007,524,535, sawa na asilimia 99 ya

makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 34,543,854, sawa na asilimia 1 ya makadirio. Aidha,

matumizi ya maendeleo ya Wizara, yalikadiriwa kuwa Tsh. 1,029,960,000, ingawa fedha

halisi zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 382,731,790 sawa na asilimia 37.2 ya

makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 647,228,210 sawa na asilimia 62.8 ya makadirio.

Majibu ya Wizara

Wizara inakusanya mapato yake kupitia Idara nne kati ya Idara sita zilizomo katika Wizara

hii. Sababu kuu ya kushindwa kufikia malengo ya makusanyo yaliyokusudiwa kwa mwaka

huu, inaokana na makusanyo yanayohusiana na Bahari Kuu, sasa yanakusanywa na

Mamlaka ya Bahari Kuu, ambayo hapo kabla yalizingatiwa kama mapato yanayokusanywa

na Wizara hii.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji sababu iliyotolewa na Wizara kuhusiana na makusanyo ya mapato, kwa

kuitaka kutoa maelezo ya sababu zilizowapelekea kuijumuisha Mamlaka ya Bahari Kuu

katika makisio ya mapato yao, wakati walijua kuwa haiko tena chini ya Wizara hii na

kuelezwa kuwa, wakati wa makisio ya mapato hayo, hawakujua kama ingeliondoshwa chini

ya Wizara na kuwa inajitegemea.

Page 75: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

75

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuhakikisha inaongeza juhudi za makusanyo ya mapato sambamba

na kufanya matumizi ya fedha zinazopatiwa kwa mujibu wa Sheria. Aidha, Wizara

inashauriwa kuwa na uhakika wa makisio ya mapato kwa uhakika wa vyanzo vyake vya

mapato.

Hoja Namba 23.1.2 Vifaa ambavyo havikuingizwa katika daftari la ghalani, Tsh.

19,918,450

Ukaguzi umebaini kufanyika kwa malipo kwa kununua vifaa mbali mbali kwa matumizi ya

Ofisi, lakini vifaa hivyo havikuingizwa kwenye daftari la vifaa vya ghalani ili kuweza

kuthbitisha uhalali wa mapokezi pamoja na matumizi yake, kinyume na kanuni ya 168 ya

Kanuni za Fedha za mwaka 2005.

Majibu ya Wizara

Wizara inathibitisha kuwa vifaa vyote vyenye thamani iliyotajwa katika hoja hii,

vilinunuliwa na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa na vifaa hivyo vimeingizwa katika

daftari la ghalani. Aidha, fedha zote hizo zimetumika kwa usahihi na vifaa vyote

vimesharikodiwa katika daftari la ghalani na lipo tayari kwa ukaguzi wa Kamati.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na majibu ya Wizara, Kamati imehoji sababu zilizopelekea kutokaguliwa wakati wa

ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ambapo Kamati inathibitisha kuwa, kwa

kutokaguliwa wakati wa ukaguzi ni wazi kuwa Sheria tayari ilikuwa imeshavunjwa. Pamoja

na hayo, Kamati ilipoangalia baadhi ya hati za malipo zinazohusika, imegundua baadhi ya

kasoro ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa maombi ya Katibu Mkuu wa Wizara kumuomba

fedha Mhasibu wa Wizara, badala ya yeye Afisa Mhasibu kuombwa fedha hizo. Aidha,

baadhi ya malipo hayakuombwa matumizi yake na Kitengo cha Mtumiaji, au Afisa mweye

hamitaji ya vifaa hivyo.

Vile vile baadhi ya hati hizo za malipo hazina vielelezo vilivyokamilika, kama vile

ilivyokuwa kwa baadhi ya risiti zilizoambatanishwa kutokuwa na sifa zinazokubalika, ikiwa

ni pamoja na kukosekana kwa namba ya usajili wa ZRB (Tin Number) na pia baadhi ya hati

hizo za malipo hazina saini ya Afisa Mhasibu.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kufuata taratibu za kuingiza taarifa za vifaa wanavyovinunua katika

daftari la ghalani. Aidha, Kamati inaitaka Wizara kufuata Sheria katika matumizi ya fedha za

Serikali, ikiwa ni pamoja na kufanya manunuzi kwa mujibu wa taratibu za Kisheria.

7.9 AFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI –

BLM

Hoja Namba 17.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Matumizi

Afisi iliidhinishiwa matumizi ya kawaida, ya Tsh. 3,750,000,000/- na fedha halisi

zilizoingizwa na kutumiwa ni Tsh. 3,102,320,000/- sawa na asilimia 83 ya makadirio, ikiwa

ni upungufu wa Tsh. 647,680,000 sawa na asilimia 17 ya makadirio. Aidha, matumizi ya

maendeleo, yaliidhinishwa kwa Tsh. 3,922,400,000/-, lakini mwisho wa mwaka ulipofika,

fedha zilizoingizwa na kutumika zilikuwa Tsh. 3,967,590,000, sawa na asilimia 100 ya

makadirio.

Page 76: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

76

Uchunguzi wa Kamati

Katika kufuatilia hoja ya Kamati haikupata mashirikiano mazuri kutoka kwa Afisi husika

ingawa baadhi ya watendaji walihudhuria kikao hicho. Hii ni kutokana na kuwa Naibu

Katibu Mkuu Ndg. Salmin Amour Abdalla ambaye ni Afisa Masuul alikuwa safarini na

alishindwa kutoa taarifa mbele ya Kamati hii. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu Ndg. Salum

Maulid Kibanzi, aliishauri Kamati hii kutoa majibu ya Afisi hiyo kwa niaba ya Naibu Katibu

Mkuu. Hata hivyo, Kamati ya PAC iliukataa ushauri huo kwa kuwa Ndg. Salum sio Afisa

Masuul wa Afisi hiyo. Baada ya majadiliano makubwa Kamati iliamua kupokea taarifa ya

Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora ingawa ratiba ya kazi ya siku hiyo ilikuwa inaigusa

moja kwa moja Afisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Pamoja na kuwasilishwa kwa taarifa hiyo Kamati ya PAC iligundua kuwa Afisi hiyo

haikuwa na maandalizi mazuri kwani takriban masuala mengi yaliyoulizwa yalikosa majibu

ya uhakika na hivyo Kamati iliitaka Afisi hii kuwasilisha taaifa zake kwa maandishi kwa

yale maeneo ambayo yalikosa majibu. Kwa masikitiko makubwa hadi tunawasilisha taarifa

hii hakuna taarifa yoyote iliyowasilishwa mbele ya Kamati.

Kwa msingi huo, hoja hii imebaki kama ilivyo na wahusika wanapaswa kufika mbele ya

Kamati ya PAC kuwasilisha majibu ya hoja hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakemea kitendo cha Afisa Mhasibu kutofika mbele ya Kamati, wakati Kamati

imeshatoa barua za kazi kwa Maofisa hao.

7.10 OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA IDARA MAALUM ZA SMZ.

7.10.1 TAARIFA ZA MIKOA, HALMASHAURI NA MABARAZA YA MIJI-

UNGUJA

7.10.2 MKOA WA KASKAZINI

Hoja Namba 15.9:1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Matumizi ya Kawaida

Kwa mwaka 2012/2013 Mkoa uliidhinishiwa kutumia Tsh. 1,108,400,000 kwa kazi za

kawaida ingawaje fedha zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 1,001,832,354 sawa na asilimia

90 ya makadirio ikiwa ni upungufu wa Tsh. 106,567,646 sawa na asilimia 10 ya makadirio.

Aidha, taarifa za fedha za maendeleo zinaonesha kuwa ziliingizwa Tsh. 60,000,000 ambazo

ndizo zilizokadiriwa.

Majibu ya Mkoa

Ni kweli taarifa hizo za ukaguzi wa hesabu ya matumizi ya kawaida, na athari kubwa

iliyopatikana kwa Mkoa kutokana na kushindwa kupata fedha hizo ni pamoja na kushindwa

kujenga ukuta wa Ofisi ya Mkoa na kujenga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ambayo ingelijengwa

kwa fedha za O.C. Aidha kuhusiana na fedha za maendeleo, Mkoa haukupata fedha za

maendeleo kwa mwaka 2012/2013 na fedha zilizoainishwa katika ripoti ya ukaguzi ni za

mwaka 2011/2012.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji juu ya usahihi wa majibu ya Mkoa na yale ya ripoti ya ukaguzi kuhusiana na

fedha za maendeleo, na kuhitaji kupatiwa „finantial statement‟ ambayo baada ya kuletwa na

kuipitia, Kamati ilijiridhisha kuwa, ripoti ya ukaguzi imekosewa na majibu ya Ofisi ya Mkoa

yapo sahihi. Aidha, Kamati pia imeshtushwa na taarifa ya Ofisi ya Wilaya kujengwa kupitia

Page 77: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

77

O.C za Mkoa na kuelezwa kuwa, baada ya Ofisi ya Mkoa kuona fedha za maendeleo

zimekatwa, ndipo walipoomba fedha hizo kupitia O.C.

Hata hivyo, Kamati ilipopitia bajeti ya Ofisi kwa mwaka huu, ilijiridhisha kuombwa Tsh.

30,000,000 kwa ajili ya ujenzi huo, lakini Ofisi ilieleza baadae kuwa, fedha hizo

hazikuingizwa zote na ndipo walipolazimika kukata kutoka O.C. Aidha, Kamati imetaka

kupatiwa „finantial statement‟ ya Ofisi ambayo Afisa Tawala na Mhasibu wa Ofisi hii

walishindwa kuiwasilisha kwa Kamati na hivyo, Kamati imeshindwa kuthibitisha uhalali wa

majibu ya Mkoa kuhusiana na fedha za ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Ofisi ya Mkoa kuwa makini na matumizi ya fedha za Ofisi kwa namna

ambayo imeidhinishwa na kuridhiwa na Baraza la Wawakilishi. Kitendo cha kutumia fedha

za O.C kwa ujenzi usiokudiwa bila ya kufuata taratibu za uhaulishaji, ni kukiuka Sheria.

Hoja Namba 15.9.2 Vifaa ambavyo havikuingizwa katika daftari la ghalani, Tsh.

14,180,000

Fedha hizo zimetumika kwa ununuzi wa vifaa mbali mbali kwa matumizi ya Ofisi, lakini

vifaa hivyo havikuingizwa kwenye daftari la vifaa vya ghalani ili kuweza kuthibitisha uhalali

wa mapokezi pamoja na matumizi yake, kinyume na kanuni ya 198 ya Kanuni za Fedha za

mwaka 2005.

Majibu ya Wizara

Ni kweli wakati wa ukaguzi hawakuingiza vifaa hivyo katika daftari. Hata hivyo, kasoro

hiyo sasa imesharekebishwa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji matumizi ya vifaa hivyo pamoja na kujiridhisha kuwa, hoja ya Mkaguzi iko

sahihi. Katika mahojiano hayo, Kamati ilipitia hati mbali mbali za malipo na kujiridhisha

kukiukwa kwa taratibu mbali mbali, ikiwa ni pamoja na kukosekana barua za maombi ya

fedha kwa Afisa Mhasibu na hata maombi ya vifaa hivyo kutoka kwa watumiaji, jambo

ambalo linatia shaka juu ya ufuataji wa taratibu za manunuzi. Aidha, hati hizo hazioneshi

kuwa vifaa vilivyonunuliwa vimerikodiwa na hata uingizwaji wa vifaa hivyo katika daftari,

hauko sahihi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Wizara kuipatia Mkaguzi wa Ndani Ofisi ya Mkoa wa Kaskazini, ili

aweze kuisaidia Ofisi kurekebisha kasoro mbali mbali zinazoendelea kufanyika Ofisini hapo.

7.10.3 BARAZA LA MANISPAA

Hoja Namba 15.12.1 Taarifa ya Mapato na Matumizi ya Kazi za Kawaida na

Maendeleo

Baraza la Manispaa lilikadiriwa kukusanya Tsh. 3,193,965,000 na mapato halisi

yaliyokusanywa yalikuwa Tsh. 2,839,200,094 sawa asilimia 89 ya makadirio, ikiwa ni

upungufu wa Tsh. 354,764,906 sawa asilimia 11 ya makadirio. Matumizi ya kazi za kawaida

yalikidiriwa kuwa Tsh. 4,300,409,302 na matumizi halisi yalikuwa Tsh. 2,890,440,095 sawa

na asilimia 67 ya makadirio, ikiwa ni pungufu ya Tsh. 1,409,969,207 sawa na asilimia 23 ya

makadirio.

Page 78: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

78

Kwa upande wa matumizi ya maendeleo makisio yalikuwa Tsh. 369,407,302 na fedha halisi

zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 59,039,500, sawa na asilimia 16 ya makadirio, ikiwa ni

upungufu wa Tsh. 310,367,802 sawa na asilimia 84 ya makadirio.

Majibu ya Baraza

Sababu kubwa iliyolifanya Baraza kushindwa kupata makisio halisi waliyoyakisia

kunatokana na kukosea kupanga makusanyo hayo, kushuka kwa vyanzo vya mapato

kutokana na sababu mbali mbali, mapungufu ya kisheria na kutegemea leseni za biashara

lakini maduka mengi hivi sasa wanakata leseni zao ZRB, Wizara ya Biashara, Viwanda na

Masoko na maeneo mengine. Hii ni kutokana na Baraza kukata leseni ndogo ndogo za

200,000 hadi 300,000 na leseni kubwa, wananchi hukimbilia ZRB. Na tatizo hilo lipo kwa

mkanganyiko wa Sheria kuwa kila taasisi kati ya hizi zinatumia Sheria zenye kutoa mamlaka

tofauti ya makusanyo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imepokea sababu hizo na kuhoji uhalisia wa makusanyo hayo na makisio na

kuelezwa kuwa, kuongezeka kwake kunatokana zaidi na agizo la Mhe. Waziri

anaeshughulikia Tawala za Mikoa kwa kuwataka lazima wafikie makusanyo ya bilioni 5,

wakati uwezo wa Baraza hauwezi kufikia makusanyo hayo, na hakuna vyanzo vyovyote

vipya vilivyoongezeka kinyume na vyanzo vilivyokuwepo kabla.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalitaka Baraza kuongeza juhudi katika makusanyo na lifanye matumizi yake kwa

kufuata taratibu za Sheria. Aidha, makisio ya makusanyo yawe halisi ili yaweze kufikiwa,

kuliko kukisia bila ya kuangalia uwezo halisi wa Baraza.

Hoja Namba 15.2.2 Malipo kwa ajili ya usafi, Tsh. 5,200,000

Baraza limefanya malipo ya usafi kwa kikundi cha Muwata, lakini makubaliano au mkataba

wa kazi hiyo haukuambatanishwa na kuweza kupatikana kwa ukaguzi na hivyo, Mkaguzi

ameshindwa kujua uhalali wa malipo hayo.

Majibu ya Baraza

Muwawata ni kikundi cha Muungano wa Wanajeshi Wastaafu Tanzania chenye namba ya

usajili S.A 17184 iliyotolewa tarehe 27/12/2010 chini ya Sheria ya Usajili wa Jumuiya

(Society Act), Cap 337 (R.E 2002) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na namba ya

usajili 934 ya tarehe 6/4/2011 chini ya Sheria ya Usajili wa Jumuiya (Society Act) namba 6

ya mwaka 1995 ya Zanzibar.

Kikundi hiki kiliomba na kupewa kazi ya kusimamia utekelezaji wa Sheria ndogo ndogo za

usafi na utunzaji wa mji na waliingia mkataba wa makubaliano na Baraza la Manispaa kwa

muda wa miezi mitatu kuanzia tarehe 01/06 hadi 31/08/2012. Kasoro iliyojitokeza ni

kutoambatanishwa mkataba huo katika kila hati ya malipo. Hata hivyo, Baraza linathibitisha

kwamba, mkataba huo upo na upo tayari kwa ukaguzi.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji kwa nini mkataba huo ambao ndio sasa unawasilishwa kwa Kamati,

haukuwepo wakati wa ukaguzi na kuelezwa kuwa, ulikuwepo katika hati za malipo ya awali

ambao ulikuwa ni mwisho wa mwaka (tarehe 1/6/2012), hivyo kasoro ilikuwa ni

kutoambatanishwa na hazi hizo za malipo. Hata hivyo, Kamati inatia mashaka majibu haya

Page 79: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

79

kwa sababu Mkaguzi hufanya kazi yake kwa mashirikiano makubwa na taasisi anayoikagua

na huwepo katika taasisi husika si chini ya wiki mbili za ukaguzi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalitaka Baraza la Manispaa kutoa mashirikiano mazuri na wakaguzi kwa kuwapatia

taarifa wanazozihitaji.

Hoja Namba 15.12.3 Malipo yasiyokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu), Tsh.

8,500,000

Fedha hizo zimetumika kwa matumizi mbali mbali lakini vielelezo husika havikupatikana

kwa ukaguzi, kinyume na kanuni ya 95(4) ya Kanuni za Fedha za mwaka 2005. Malipo hayo

ni kama ifuatavyo:

Hati

namba

Fedha

zilizolipwa

Aliyelipwa Maelezo

20/2 2,000,000 Pili Saidi

Ramadhani

Malipo ya usafi kwa mwezi wa

Januari 2013

21/2 2,000,000 Zacedy Malipo ya usafi kwa mwezi wa

Januari 2013

47/2 4,500,000 Mkurugenzi wa

Baraza la Manispaa

Fedha za maendeleo kwa wadi

tisa za Manispaa

Majibu ya Baraza

Ni kweli vielelezo hivyo vimekosekana kutokana na uhalisia na mazingira maalum ya

matumizi ya fedha hizo. Kwa mfano fedha zilizolipwa Ndg. Pili Saidi ni kwa ajili ya kikundi

cha usafi cha Glittering Volunteer Group kwa ajili ya huduma ya usafi, lakini kikundi hicho

hakikuwa na risiti wala akaunti ya benki na ndio maana akalipwa Mwakilishi wao.

Fedha za Zacedy nazo ni kama za awali, ni za kikundi za ZACEDY kwa ajili ya huduma ya

usafi, ambapo stakabadhi ilikuwepo lakini kwa bahati mbaya haikuambatanishwa na hati ya

malipo wakati ukaguzi unafanyika. Aidha, Tsh. 4,500,000 ni fedha za maendeleo kwa wadi

tisa ambazo wamepewa Waheshimiwa Madiwani ambapo kwa kuzingatia matumizi ya fedha

hizi, baadhi ya Waheshimiwa hawarejeshi marejesho kwa wakati. Hata hivyo, Baraza

linaendelea kutoa elimu kwa Waheshimiwa, ili waweze kutekeleza maelekezo ya Sheria.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na hoja za Baraza kuhusiana na hali halisi ya marejesho ya vielelezo vinavyohusiana

na hoja hii, Kamati haikubaliani kukiuikwa kwa Sheria kwa sababu hizo. Aidha, Kamati

imefanya mapitio ya hati za malipo zilizoelezwa kuwa vielelezo vyake vimekamilika wakati

wa kazi za Kamati na kujiridhisha kuwa kuna kasoro mbali mbali ikiwa ni pamoja na malipo

ya Tsh. 4,500,000 hayana risiti za malipo wala hati ya kuthbitisha malipo husika, na

Waheshimiwa Madiwani wamefanya wao maombi moja kwa moja kwa Mkurugenzi, badala

ya maombi yao kuombwa na watendaji wa Baraza.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalitaka Baraza kufuata taratibu za Sheria ya Fedha na Kanuni zake kwa kufanya

matumizi ya fedha za Umma kwa kufuata taratibu za matumizi yake na uthibitisho wa

vielelezo sahihi vya matumizi ya fedha hizo.

Page 80: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

80

Mengineyo yaliyojitokeza

Kamati imehoji Mradi wa ZUSP na kuelezwa kuwa una matatizo mengi katika utekelezaji

wake na Waheshimiwa Madiwani wa Baraza wamesema hawashirikishwi katika

utekelezwaji na upangaji wake. Hivyo, Kamati inahitaji kupata taarifa za kina kuhusiana na

mradi huu, namna ulivyoanza na utekelezaji wake pamoja na gharama zake.

Aidha, Kamati inaishauri Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, kufanya ukaguzi

wa mradi huu kwa sababu umeshakuwa na malalamiko mengi kutoka taasisi mbali mbali

zilizohusika na mradi huo.

7.10.4 HALMASHAURI YA WILAYA YA KASKAZINI “B”

Hoja Namba 17.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Makadirio ya Mapato na Matumizi

Taarifa ya mapato ya Halmashauri inaonesha kukadiriwa kukusanywa Tsh. 100,000,000 kwa

mwaka 2012/2013, ingawaje fedha halisi iliyokusanywa ni Tsh. 212,204,768 sawa na

asilimia 212 ya makadirio, ikiwa ni ongezeko la Tsh. 112,204,768 sawa na asilimia 12 ya

makadirio.

Matumizi ya kawaida, yalikadiriwa kuwa Tsh. 188,810,000 na fedha halisi zilizoingizwa na

kutumiwa ni Tsh. 211,000,100 sawa na asilimia 112 ya makadirio, ikiwa ni upungufu wa

Tsh. 22,190,100 sawa na asilimia 112 ya makadirio, ikiwa ni pungufu ya Tsh. 22,190,100

sawa na asilimia 12 ya makadirio.

Majibu ya Halmashauri

Halmashauri ilikadiriwa kukusanya Tsh. 275,600,000 na sio Tsh. 100,000,000 kama

ilivyoelezwa na Mkaguzi. Hadi kufikia Juni, 2013, fedha zilizokusanywa zilikuwa Tsh.

212,204,768, sawa na asilimia 78.20 ya makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 63,395,232,

sawa na asilimia 21.80 ya makadirio.

Matumizi yaliyokadiriwa kwa Halmashauri yalikuwa Tsh. 265,860,000 kwa kazi za kawaida

na za maendeleo na sio 188,810,000 kama ilivyoelezwa na ripoti ya ukaguzi. Aidha, Tsh.

211,000,100 zilitumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 79 ya makadirio, ikiwa ni

upungufu wa Tsh. 54,860,000 sawa na asilimia 20 ya makadirio.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na majibu ya Halmashauri, Kamati imehoji sababu zilizopelekea kushindwa kufikia

makisio ya makusanyo na kuelezwa kunatokana na kuwepo kwa mvua na kuadimika kwa

saruji, kulipekea kutopata mapato mengi, ikizingatiwa Halmashauri inategemea chanzo cha

mapato kupitia uchimbaji wa mchanga.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Halmashauri kuongeza vyanzo vya mapato, kwani kutegemea chanzo

kimoja tu tena kwa kinachotegemea mashamba ya watu binafsi kwa ajili ya uchimbaji wa

mchanga sio uhakika wa makusanyo ya mapato.

Hoja Namba 15.5.2 Kukosekana kwa kumbu kumbu za vifaa vilivyonunuliwa kwa

ajili ya utekelezaji wa miradi ya wananchi, Tsh. 10,500,000

Fedha hizo zimetumika kwa ununuzi wa vifaa mbali mbali, kwa ajili ya utekelezaji wa

miradi ya wananchi ya Halmashauri, lakini ukaguzi umeshindwa kupatiwa kumbu kumbu za

upokeaji, utoaji na utumiaji wa vifaa hivyo, kinyume na kanuni ya fedha ya 198 ya Kanuni

za Fedha za mwaka 2005.

Page 81: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

81

Majibu ya Halmashauri

Ni kweli kuwepo kwa upungufu huo katika uwekaji wa vifaa, hili linatokana na vifaa hivyo

kukabidhiwa moja kwa moja kwa waheshimiwa Madiwani na Kamati zao za Wadi kwa ajili

ya matumizi kutokana na mahitaji ya jamii kwa mazingira yao ya wakati huo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kuwa, matumizi ya vifaa hivyo ni kwa matumizi ya miradi ya

wananchi inayosimamiwa na Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri hiyo, na hivyo

kutaka kujua taratibu zinazotumika katika maombi ya matumizi hayo. Aidha Kamati

ilipofanya ukaguzi wa hati za malipo ya matumizi hayo, ilijiridhisha kuwa, baadhi ya hati

hizo hazina barua za maombi ya Waheshimiwa Madiwani hao. Pia hati hizo zinakosa saini

ya Afisa Mhasibu, ili kuthibitisha uhalali wa matumiz yaliyofanyika.

Aidha, kuhusiana na vifaa kuingizwa katika daftari, Kamati imejiridhisha kuwa, baadhi ya

vifaa tayari vimesharikodiwa katika daftari la ghalani, lakini vifaa vyengine bado

havijarikodiwa. Aidha, uingizwaji na utokaji wa vifaa hivyo hauoneshi usahihi na namna ya

vifaa hivyo vilivyotumika.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Halmashauri kuzingatia taratibu na maelekezo ya Sheria kwa kuingiza vifaa

katika daftari linalohusika. Aidha, Kamati inaitaka Halmashauri kuzingatia maelekezo ya

Sheria na Kanuni za Fedha kwa matumizi ya fedha za umma na khasa wanazopatiwa

Waheshimiwa Madiwani kwa miradi ya wananchi.

7.10.5 HALMASHAURI YA WILAYA YA KATI

Hoja namba 15.17.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Mapato na Matumizi ya Kazi za Kawaida

Halmashauri ilikadiriwa kukusanya mapato yake kwa ongezeko la Tsh. 200,000,000 kwa

mwaka 2012/2013 na fedha halisi iliyokusanywa ilikuwa Tsh. 167,979,183 sawa na asilimia

84 ya makadirio, kwa upungufu wa Tsh. 32,020,817 sawa na asilimia 16 ya makadirio.

Aidha, ilikadiriwa kutumia Tsh. 200,000,000 kwa kazi za kawaida na hatimae iliweza

kutumia Tsh. 161,383,499 sawa na asilimia 80 ya makadirio, kwa upungufu wa Tsh.

38,616,501 sawa na asilimia 19 ya makadirio.

Majibu ya Halmashauri

Mapato yalipungua katika kifungu namba 1200 ambacho kinakusanyiwa ada ya mauziano ya

Ushuru wa Forodha. Hali hii imesababishwa na Halmashauri kutaka kujiepusha na migogoro

ya ardhi kama alivyoagiza Mhe. Rais katika semina elekezi ya tarehe 4-5 Julai 2012.

Kifungu hiki kilikadiriwa kukusanya Tsh. 68,780,500 na kimeweza kukusanya Tsh.

17,219,000. Aidha, kulikuwa na upungufu mkubwa wa wafanyakazi wenye taaluma na

vitendea kazi na vyanzo vingi havina uhakika kutokana na kukosekana kwa takwimu sahihi,

jambo ambalo hivi sasa linafanyiwa kazi. Hivyo, na matumizi ya kazi za kawadia ya

Halmashauri nayo yaliathirika kwa namna hii.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kuwa, pamoja na makisio ya makusanyo yanayofanywa na

Halmashauri zetu, makusanyo hayo hayafanywi kwa uhakika wa vyanzo vya mapato na

Page 82: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

82

takwimu halisi ya uwezekano wa hakika wa kukusanywa kwake, hali inayopelekea kuwepo

kwa pengo kubwa baina ya makisio na uhalisia wa mapato.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Halmashauri iongeze juhudi za makusanyo kwa kufanya utafiti na kuwa na

taarifa za vyanzo vyake vya mapato kabla ya kufanya makisio, ili kuepusha kuwepo kwa

tofauti kubwa sana ya makisio ya makusanyo na uhalisia wake baada ya mwaka kukamilika.

Hoja Namba 15.17.2 Kukosekana kwa kumbu kumbu za vifaa vilivyonunuliwa kwa

ajili ya utekelezaji wa miradi ya wananchi, Tsh. 12,345,000

Fedha hizo zimetumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa mbali mbali kwa utekelezaji wa miradi

ya wananchi Wilaya ya Kati, lakini ukaguzi umeshindwa kupatiwa kumbu kumbu za

upokeaji, utoaji na utumiaji wa vifaa hivyo, kinyume na kanuni ya 198 ya Kanuni za Fedha

za mwaka 2005.

Majibu ya Halmashauri

Ni kweli Halmashauri ilifanya manunuzi ya vifaa hivyo vilivyotajwa na kweli kumbu kumbu

zake zilikosekana wakati wa ukaguzi, lakini marekebisho yamefanywa na sasa kumbu

kumbu zote zipo kamili na zipo tayari kwa ukaguzi.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kuwa, Halmashauri imekiri makosa yake, lakini hali hii haiifanyi

Kamati kuwavua makosa Halmashauri kwa sababu tu kumbu kumbu zilizokosekana wakati

wa ukaguzi sasa zipo tayari kwa Kamati. Kamati inasimamia Sheria kuwa ilikiukwa na

Halmashauri kwa kukosekana kwa kumbu kumbu hizo wakati wa ukaguzi.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Halmashauri kufanya marekebisho ya kasoro hii kwani haitoi sura nzuri kwa

utendaji wake.

WIZARA NA TAASISI MBALI MBALI ZA SERIKALI-PEMBA

8.0 OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA IDARA MAALUM ZA SMZ.

8.1 TAARIFA ZA MIKOA, HALMASHAURI NA MABARAZA YA MIJI-

PEMBA

8.1.1 MKOA WA KASKAZINI

Hoja Namba 15.11:1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Matumizi ya Kawaida

Kwa mwaka 2012/2013 Mkoa uliidhinishiwa kutumia Tsh. 1,254,010,723 kwa kazi za

kawaida ingawaje fedha zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 1,240,816,897 sawa na asilimia

99 ya makadirio ikiwa ni upungufu wa Tsh. 13,193,826 sawa na asilimia 1 ya makadirio.

Majibu ya Mkoa

Afisi hii iliidhinishiwa kutumia jumla ya Tsh. 1,384,000,000 kwa ajili ya matumizi ya kazi

za kawaida. Hata hivyo, kutokana na kuongezeka kwa mishahara ya watendaji Afisi ya

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini ililazimika kuomba kuidhinishiwa fedha za ziada ambazo ni

Tsh. 19,220,000 na kufanya fungu la mishahara na maposho kufikia Tsh. 581,220,000 badala

ya 562,000,000 ilizoidhinishiwa hapo kabla.

Page 83: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

83

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imebaini kuwa kuna mgongano wa taarifa juu ya ongezeko la matumizi ya fedha

baina ya Ripoti ya Mdhibiti na taarifa ya Mkoa iliyowasilishwa mbele ya Kamati. Aidha,

Kamati imebaini kuwa Mabaraza ya Miji hayaoneshi mapato yao yote ndani ya bajeti zao

zinazowasilishwa mbele ya Baraza la Wawakilishi. Kitendo hiki kimekitia mashaka Kamati

na hata kudhania kuwa baadhi ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya matumizi ya

Mabaraza ya Miji hupotea mikononi mwa wachache.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inayataka Mabaraza ya Miji kuonesha mapato yao yote wanayoyapata wakati wa

uwasilishwaji wa bajeti ndani ya Baraza la Wawakilishi.

Kamati inazitaka Taasisi za Serikali kutoa mashirikiano mazuri na taarifa sahihi kwa

wakaguzi, ili kuepusha usumbufu wa taarifa moja ya Taasisi kutofautiana na

inayowasilishwa kwa Mkaguzi.

Aidha, Kamati inaitaka Serikali kuacha tabia ya kuzishurutisha Taasisi zake kutumia fedha

za matumizi mengineyo kwa ajili ya kulipia mishahara ya watendaji wake endapo itaongeza

mishahara ili Taasisi hizo ziweze kutekeleza vyema majukumu yake.

Hoja Namba 15.11.2: Uchelewaji wa ujenzi wa ukuta (fence) Ofisi ya Wilaya Ndogo

Kojani kwa gharama ya Tsh. 83,308,500

Fedha hizo zimetumika kwa ujenzi wa ukuta wa ofisi ya ilaya ndogo Kojani ambapo ujenzi

wa ukuta huo ulichukua muda mrefu kumalizika na kazi iliyofanyika haikidhi viwango na

gharama zilizotumika. Aidha, mkataba wa ujenzi ulifungwa 2007 baina ya Mkoa wa

Kaskazini Pemba na El-Shally Construction Corperative Society tarehe 25/05/2007 ambapo

mkandarasi alitakiwa kujenga ukuta huo kwa muda wa mwaka mmoja kwa makubaliano ya

gharama ya Tsh. 83,308,500 ambapo Tsh. 81,500,000 zililipwa kwa mkandarasi huyo kwa

vpindi tofauti.

Mkandarasi alitakiwa kukamilisha ujenzi ndani ya kipindi cha mwaka mmoja kuanzia tarehe

ya mkataba, kutositisha kuendelea na ujenzi hata kama fedha za malipo zitachelewa na

kuzingatia vigezo vya ubora wa ujenzi huo. Aidha, baada ya ukaguzi kuufuatilia ujenzi huo,

mapungufu yafuatayo yalibainika:

Taratibu za kumpata mkandarasi hazikufuata sheria za manunuzi.

Ujenzi wa ukuta ulianza mwaka 2009 na kukabidhiwa Septemba 2013.

Hali halisi haioneshi ubora na umadhubuti wa ukuta huo, kwani baadhi ya

kuta tayari zimeshaanza kupasuka, baadhi ya sehemu za madirisha

zimeharibika na sehemu ya mbele ya ukuta huo haukukamilika.

Fedha zilizotumika hazilingani na hali halisi ya ukuta huo, na

Mkoa wa Kaskazini Pemba umeshindwa kuchukua hatua dhidi ya mkandarasi

huyo baada ya kukiuka makubaliano yaliyomo ndani ya mkataba.

Majibu ya Mkoa

Taratibu za kumpata mkandarasi hazikufuata Sheria za Manunuzi No. 9 ya mwaka

2005

Ofisi ya Mkoa wa Kaskazini – Pemba baada ya kupokea agizo la kujenga ukuta kutoka kwa

Waziri aliehusika na tawala za mikoa, ilimuandikia barua yenye kumbukumbu Namba

MKP/J.1/8/VOL.11/30 ya tarehe 15 Februari, 2007 Mjenzi wa ukuta huo ambaye ni El –

Sahaly Construction Cooperative Society iliyopo Wete na kumtaka kuandika barua ya ombi

la kukubali kujenga ukuta huo pamoja na kuambatanisha gharama za ujenzi huo. Mjenzi

Page 84: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

84

alilichukulia hatua suala hilo kama alivyoombwa na mnamo tarehe 2 Machi, 2007 Afisi ya

Mkuu wa Mkoa ilipokea barua ya Mjenzi inayokubali kujenga ukuta huo kwa gharama za

Tsh. 83,308,500. Baada ya mjenzi kukubali ombi hilo Afisi ya Mkoa ilifunga mkataba na

mjenzi tarehe 25 Mei, 2007 na kukubaliana kujenga ukuta huo ndani ya kipindi cha mwaka

mmoja.

Ujenzi wa Ukuta ulianza mwaka 2009 na kukabidhiwa Septemba, 2013

Ofisi ya Mkoa wa Kaskazini – Pemba haikukubaliana na Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi

Mkuu wa Hesabu za Serikali kuwa ujenzi wa ukuta ulianza mwaka 2009, isipokuwa kwamba

ujenzi huo ulianza mwaka 2007 mara baada ya kufunga mkataba. Ingawa ujenzi wa ukuta

ulianza mwaka 2007 Mjenzi alianza kulipwa fedha zake kwa awamu kuanzia mwaka 2012

hadi mwezi Agosti, 2013. Hii ni kutokana na uhaba wa fedha unaoukabili Mkoa huu.

Hali halisi haioneshi ubora na umadhubuti wa ukuta huo kwani baadhi ya kuta tayari

zimeanza kupasuka, baadhi ya sehemu ya madirisha zimeshaharibika na sehemu ya

mbele ya ukuta huo haikukamilika.

Nyufa ilizojitokeza ni nyufa ndogo ndogo za kawaida, hii ni kutokana na mazingira ya hali

ya hewa ya eneo husika. Aidha, wakati ukaguzi unafanyika ni miaka sita tokea ukuta huo

ulipojengwa.

Pia, Afisi ya Mkoa haikukubaliana na madai ya Mdhibiti kuwa sehemu ya madirisha

zimeshaharibika. Hii ni kutokana na kuwa ukuta huo haukutiwa madirisha bali umewekwa

venti. Baadhi ya venti hizo zimeharibika kutokana na watoto kucheza na kuparamia ukuta

kwa kuwa jengo la Afisi hii lipo karibu na uwanja wa mpira.

Ama kwa upande wa sehemu ya mbele Afisi ya Mkoa ilieleza kuwa sehemu hiyo

imekamilika kinyume na ilivyodaiwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa

Hesabu za Serikali.

Fedha zilizotumika hazilingani na hali halisi ya ukuta huo

Afisi ya Mkoa wa Kaskazini – Pemba ilikiri kuwa fedha zilizotumika hazilingani na hali

halisi ya ukuta huo kutokana na sababu zifuatazo;-

i. Ujenzi wa kwenye visiwa hususan kisiwa cha Kojani ni tofauti na ujenzi wa sehemu

nyengine zisizo za visiwa. Hii ni kutokana na kuwa vifaa vya ujenzi inabidi

visafirishwe kwa njia ya gari baadae kwa dau na hatimae vibebwe kwa kichwa hadi

katika eneo husika.

ii. Wakati ujenzi unafanyika hakukuwa na maji kwenye jengo na ililazimika maji hayo

kuchukuliwa ng‟ambo ya pili ya kisiwa.

Mkoa wa Kaskazini Pemba umeshindwa kuchukua hatua dhidi ya Mkandarasi huyo

baada ya kukiuka makubaliano yaliyomo ndani ya Mkataba

Afisi ya Mkoa ilishindwa kumchukulia hatua Mjenzi kwa kuwa Afisi yenyewe ilishindwa

kufuata matakwa ya mkataba kama vile kushindwa kumlipa Mjenzi kwa wakati.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati ya PAC haikuridhika na ujenzi wa ukuta wa Wilaya Ndogo Kojani kama

ilivyoelezwa na Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Kutokana na

kutoridhishwa kwake huko Kamati imeutaka Mkoa huu kufuata Sheria za nchi

zinavyoelekeza juu ya mambo mbali mbali ikiwemo ujenzi wa majengo, ununuzi wa vifaa

nakadhalika.

Page 85: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

85

Mengineyo

Kamati inawataka viongozi wa Taasisi za Serikali kuziheshimu ratiba za kazi za Kamati ili

Kamati hizo ziweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo na hasa ikizingatiwa kuwa Kamati

za Baraza la Wawakilishi hutekeleza majukumu yake ndani ya kipindi maalum. Kamati ya

PAC inatoa agizo hilo baada ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni kushindwa kuhudhuria

kikao cha Kamati kutokana na ziara ya Mheshimiwa Waziri, Wizara ya Nchi, (AR), Tawala

za Mikoa na Idara Maalum za SMZ, kitendo hiki kilikikosesha Kamati kupata taarifa za

Wilaya hiyo.

Aidha, Kamati ya PAC ilisikitishwa sana na kitendo cha Mahkama cha kuchelewa kutoa

maamuzi ya kesi ya Kituo cha Mafuta kinachomilikiwa na Mkoa huu na hasa ikizingatia

kuwa Mkodishwaji anaendelea kunufaika na kituo wakati Mkoa wa Kaskazini Pemba ndie

mmiliki wa Kituo na hanufaiki na chochote tokea mwaka 2013.

8.1.2 BARAZA LA MJI WETE

Hoja namba 15.13.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Mapato na Matumizi ya Kazi za Kawaida

Ukaguzi umebaini kuwa Baraza la Mji Wete lilikusanya mapato yake kwa ongezeko la Tsh.

1,100,000 sawa na asilimia 2 ya makadirio. Aidha, imetumia kwa kazi za kawaida ongezeko

la Tsh. 700,000 sawa na asilimia 1 ya makadirio.

Majibu ya Baraza la Mji Wete

Baraza la Mji Wete liliiieleza Kamati kwamba kwa mwaka wa fedha 2012/2013 ilikisia

kukusanya jumla ya Tsh. 50,125,000/- na sio Tsh. 53,200,000 kama ilivyoripotiwa na Ripoti

ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2012/2013. Hivyo, hadi

kufikia Juni, 2013 Baraza hili lilikusanya jumla ya Tsh. 55,578,641 ikiwa ni ongezeko la

Tsh. 5,453,641.

Ama kwa upande wa matumizi ya kazi za kawaida na maendeleo Baraza la Mji Wetet

liliomba idhini ya matumizi ya ziada ya Tsh. 5,453,641 kinyume na ilivyoripotiwa na

Mdhibiti.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na maelezo yaliyotolewa na Watendaji na Waheshimiwa Madiwani wa Baraza la Mji

Wete, Kamati ya P.A.C haikukubaliana na kauli hiyo. Hii ni kutokana na kuwa Ofisi ya

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa kawaida huwasilisha taarifa ya Hoja

hiyo na Baraza la Mji Wete haikuchukua hatua yoyote kuhusiana na Hoja hiyo.

Sambamba na hilo, katika kufuatilia matumizi ya kazi za maendeleo yaliyofanywa na Baraza

hili, Kamati ya PAC ilibaini kuwa ukarabati wa Ukumbi wa Jamhuri Hall haukufuata

taratibu za Sheria, pia Kamati haikuridhika na kiwango cha gharama ambacho kimetumika

(thamani ya matumizi halisi ya fedha hayakufikiwa). Vile vile, Kamati hii imegundua

kwamba Kamati ya Ujenzi ya Baraza la Mji Wete haikupata fursa ya kuupitia mkataba wa

ujenzi wa ukumbi huo jambo ambalo ni kinyume na utaratibu.

Mapendekezo ya Kamati:

Kwa kuwa Baraza la Madiwani ndio lenye dhamana na utendaji wa Baraza la Mji

Kisheria.

Kamati ya PAC imewataka Watendaji wa Baraza hili kuwapatia mafunzo kuhusiana

na Sheria ya Manunuzi Waheshimiwa Madiwani ili waweze kuyasimamia vyema

majukumu yao.

Page 86: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

86

Katika kuliongezea mapato Baraza hili, Kamati inaishauri Serikali kuifanyia

ukarabati bandari ya Wete ambayo ni kipindi kirefu haitumiki.

Mengineyo

Baraza la Mji Wete halifuati taratibu za kazi katika kutekeleza majukumu yake, jambo hili

limeipelekea Kamati hii kushindwa kupata baadhi ya nyaraka ikiwemo „Financial Statement‟

kwa kuwa Mhasibu aliyekuwepo hivi sasa hakukabidhiwa afisi rasmi na Mhasibu aliyepita

ingawa Mhasibu huyo aliondoka kwa ajili ya kwenda matibabuni nchini India.

Pia, Kamati ya PAC ilishindwa kupata taarifa za kiutendaji kwa kina kwa kuwa watendaji

waliokuwepo wakati Kamati inafanya shughuli zake ni wapya. Kwa kuwa mtendaji

aliyekuwa madarakani ndiye anayepaswa kujibu suala lolote kuhusiana na nafasi yake

aliyokuwepo, Kamati inawashauri watendaji kuchukua jitihada za makusudi za kufuatilia

masuala mbali mbali yaliyomo chini ya dhamana yake ili kuepusha migongano isiyo ya

lazima.

8.1.3 HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAKE CHAKE

Hoja Namba 15.19.1 Hesabu za mwisho wa mwaka, 2012/2013

Taarifa za mapato na matumizi

Kwa mwaka 2012/2013, makadirio ya makusanyo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Chake

Chake ilikua ni kukusanya Tsh. 33,217,860.17 na ilipofika Juni 2013, iliweza kukusanya

Tsh. 33,217,860.17 ikiwa ni sawa na asilimia 100 ya makadirio.

Kwa matumizi ya kazi za kawaida na maendeleo, Halmashauri hii ilikadiriwa kutumia Tsh.

33,217,860.17 na ilipofika Juni 2013, ilitumia Tsh. 33,217,860.17 sawa na asilimia 100 ya

makadirio.

Majibu ya Halmashauri

Halmashauri ya Wilaya ya Chake Chake iliieleza Kamati kuwa Makadirio ya bajeti

yaliyooneshwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti yanatofautiana na makadirio ambayo

Halmashauri hii inayafahamu. Aidha, matumizi yaliyofanywa na Halmashauri ambayo

yameripotiwa na Mdhibiti yanatofautiana na kumbukumbu za mahesabu walizokuwa nazo

Halmashauri. Jadweli liliopo chini linaonesha mchanganuo huo;

Maelezo Taarifa ya Halmashauri kwa

Mwaka wa fedha 2012/2013

Ripoti ya Mdhibiti kwa

Mwaka wa fedha 2012/2013

Makadirio ya

bajeti

Tsh. 36,000,000.00 Tsh. 33,217,860.17

Mapato

yaliyopatikana

Tsh. 33,217,860.17 Tsh. 33,217,860.17

Matumizi

yaliyofanyika

Tsh. 32,963,650.00 Tsh. 33,217,860.17

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ilihitaji kuangalia matumizi yaliyofanyika na imebaini kwamba Ripoti ya Mdhibiti

na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali imetoa taarifa zisizokuwa sahihi.

Aidha, Kamati ya PAC imebaini kuwa baadhi ya malipo (matumizi) yanafanywa kinyume na

utaratibu kwa mfano; fundi ameomba kazi ya kuweka vitasa vya milangoni tarehe 28 Agosti,

2012 wakati ombi la kununuliwa vitasa hivyo limefanyika tarehe 26 Agosti, 2012. Pia, barua

za safari za kikazi kwa mtu mmoja zimeandikwa tarehe moja ingawa ni safari mbali mbali

nakadhalika.

Page 87: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

87

Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeitaka Halmashauri ya Wilaya ya Chake Chake kutekeleza majukumu yake kama

Sheria zinavyoelekeza.

Aidha, Kamati ya PAC inaitaka tena Serikali kutoa elimu na semina kwa Waheshimiwa

Madiwani ili wafahamu majukumu yao.

Mengineyo na Mapendekezo ya Kamati

Kamati ya PAC imeishauri Serikali kuzishirikisha Halmashauri za Wilaya kwenye Miradi ya

TASAF hususan katika ujenzi wa masoko ili kuziwezesha Halmashauri hizo kuongeza

mapato yake sambamba na kuepusha migogoro isiyo ya lazima. Kamati imeshauri hili baada

ya kubaini kuwa baadhi ya masoko yaliyojengwa na TASAF kama vile Soko la Wesha

mapato yake yanasimamiwa na wananchi wenyewe. Kitendo hiki kimeifanya Halmashauri

hii kupewa asilimia 20 tu ya mapato yanayopatikana kwa mwezi na baadhi ya miezi

hawapewi chochote. Kiwango hicho cha fedha kinatofautiana kutoka Tsh. 40,000.00 hadi

Tsh. 100,000.00 hutegemea mapato yaliyokusanywa. Kwa kuwa Halmashauri hii haina

mtendaji wake anayesimamia ukusanyaji wa mapato hayo, Halmashauri haina uhakika na

kiwango halisi cha fedha inachopewa.

Aidha, Kamati imeitaka Halmashauri ya Wilaya ya Chake Chake pamoja na uhaba wa

watendaji unaoukabili kuteua mtendaji atakaefuatilia ukusanyaji wa mapato katika Soko la

Wesha ili kuwa na uhakika wa mapato inayopatiwa.

Kwa kuwa Halmashauri hii inakabiliwa na matatizo mbali mbali ikiwemo ya kuchukuliwa

rasilimali zake kama vile kifusi bila ya kupata kipato chochote na matatizo mengi

mengineyo, Kamati hii imeitaka Wizara ya Nchi (AR), Tawala za Mikoa na Idara Maalum za

SMZ kukaa pamoja na Afisi za Mikoa na Wilaya ili kutatua matatizo hayo.

8.2 WIZARA YA AFYA

Hoja Namba 25.2.1 Malimbikizo ya madeni ya shilingi 302,499,575

Fedha hizo zinadaiwa na wafanyakazi na taasisi za Serikali na bado madeni hayo hayalipwa

hadi ukaguzi unafanyika. Kufanya hivyo ni kinyume na mfumo sahihi wa kiuhasibu wa

IPSAS unaotambua mapato na matumizi kwa fedha taslmi na iaathiri bajeti ya miaka

inayofuata.

Majibu ya Wizara: Wizara ya Afya imekiri kuwepo kwa malimbikizo ya madeni hayo na uwezo wa Wizara hii

kulipa madeni hayo ni mdogo kutokana na bajeti ndogo sana wanayopatiwa ukilinganisha na

hali halisi ya mahitaji yake kwa mwaka pamoja na upatikanaji mdogo wa fedha. Kwa mfano

kwa mwaka wa fedha 2012/2013 Wizara hii ilikadiriwa kutumia jumla ya Tsh.

563,000,000.00 na hadi kufikia Juni, 2013 ilipokea jumla ya Tsh. 307,884,649.00 sawa na

asilimia 55 ya makadirio.

Hata hivyo, Wizara imechukua juhudi ya kulipa madeni hayo na hadi kufikia mwezi wa

Oktoba, 2014 inadaiwa kama ifuatavyo;

S/No. AINA YA DENI DENI HALISI

1. Umeme kwa hospitali tano za Pemba Tsh. 343,190,924.00

2. Maji kwa hospitali tano za Pemba Tsh. 16,620,000.00

3. Call za Madaktari Tsh. 47,980,000.00

4. Likizo za wafanyakazi Tsh. 39,900,000.00

JUMLA Tsh. 447,690,924.00

Page 88: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

88

Uchunguzi wa Kamati Ingawa Wizara ya Afya – Pemba imejaribu kulipa madeni hayo, hata hivyo, kiwango

kilichobaki ni kikubwa mno.

Aidha, Kamati ya PAC baada ya kuwahoji baadhi ya watendaji wanaodai fedha zao za likizo

imebani kuwa watendaji wa Taasisi hiyo hawana taaluma ya kutosha kuhusiana na stahiki

zao.

Mapendekezo ya Kamati:

Kwa kuwa deni la umeme ni kubwa sana, na kwa kuwa Wizara ya Afya haina uwezo

wa kulipa deni hilo kutokana na udogo wa bajeti yake, na kwa kuwa Shirika la

Umeme linahitaji kulipwa fedha hizo ili liweze kujiendesha, Kamati ya PAC

inaishauri Serikali kulibeba deni hilo ili lilipwe kupitia Mfuko Mkuu wa Hazina.

Kwa kuwa Hospitali zinalipa Tsh. 20,000.00 kwa mwezi kwa ajili ya malipo ya maji,

ingawa wakati mwengine huduma hiyo ya maji huwa haipatikani, Kamati imeishauri

Wizara hii kuomba kufungiwa mita za maji ili walipe gharama hizo kwa mujibu wa

matumizi yao.

Mamlaka ya Maji Zanzibar kuweka viwango tofauti vya fedha kati ya wale wanaotoa

huduma na watumiaji wa kawaida.

Ingawa fedha zinazoingizwa ni kidogo, hata hivyo, Kamati imeitaka Wizara hii

kuwalipa kwa wakati fedha za call madaktari kwa lengo la kuwatia moyo na

kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Wizara ya Afya iwapatie taaluma watendaji wake juu ya stahili zao ili kuondosha

malalamiko yasiyo ya lazima.

8.3 WIZARA YA MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Hoja Namba 27.2.1 Malipo yasiyokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu) shilingi

18,520,000.00

Fedha hizo zimelipwa kwa matumizi mbali mbali, lakini vielelezo vyake havikupatikana kwa

ukaguzi, jambo ambalo linakwenda kinyume na kanuni ya 95(4) ya Kanuni za Fedha za

mwaka 2005.

Majibu ya Wizara

Ni kweli kwamba baadhi ya vocha hizo zilikosa stakabadhi (receipts), ingawa kulikuwa na

sahihi za wapokeaji wa malipo hayo wakati Mkaguzi alipofanya marejeo ya hoja zake.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ya P.A.C imegundua kuwa hoja hiyo imeibuka baada ya Wizara ya Mindombinu na

Mawasiliano kukubali kuviajiri vikundi ambavyo havikuwa na usajili wala akaunti. Jambo

hili limepelekea vikundi hivyo kukosa stakabadhi ya malipo ingawa hutumiwa sana na

Wizara ya Kilimo na Maliasili kupitia Idara ya Misitu.

Katika kujiridhisha kama ni kweli vikundi hivyo vilitafutwa na Idara ya Misitu, Kamati

iliomba kupatiwa barua ya maombi iliyotumwa na Wizara ya Kilimo na Maliasili kwenda

kwa Idara ya Misitu, hata hivyo, Kamati ilishindwa kupata ushahidi wa suala hilo na

kuelezwa kuwa mawasiliano hayo yalifanywa kwa njia ya mdomo.

Sambamba na hilo, Kamati imebaini kuwa mikataba iliyofungwa baina ya vikundi

vilivyopanda miti na Wizara hii imewekwa saini na Msaidizi Mhasibu badala ya Mkuu wa

Taasisi jambo ambalo ni kinyume na utaratibu.

Page 89: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

89

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kufuata sheria za manunuzi katika matumizi ya fedha

zinazoidhinishwa kwake.

Hoja Namba 27.2.2 Magari machakavu ambayo hayafanyi kazi kwa muda mrefu

Ukaguzi umebaini kuwepo kwa magari 10 yanayomilikiwa na Wizara ya Miundombinu na

Mawasiliano Pemba, ambayo ni chakavu na hayafanyi kazi kwa muda mrefu. Magari hayo

yanahitaji matengenezo kwani kila yakiendelea kukaa bila ya kutengenezwa yanaendelea

kuharibika na kuna uwezekano wa kufa kabisa. Kuendelea kukaa kwa magari hayo bila ya

kuchukuliwa hatua muafaka, kunaweza kusababisha hasara kwa Serikali. Ukaguzi unashauri

hatua muafaka zichukuliwe kuhusiana na magari hayo.

Majibu ya Wizara

Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano ilikiri kuwa wakati wa ukaguzi yalikuwepo magari

machakavu Afisini hapo. Hata hivyo, magari hayo pamoja na vifaa vyengine vichakavu

vimeshauzwa na Idara ya Uhakiki Mali. Ingawa magari hayo na vifaa hivyo vilikuwa mali za

Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano, Wizara hii haijui gharama halisi ya mali hizo kwa

kuwa zoezi la uuzwaji wa mali hizo lilisimamiwa na Idara ya Uhakiki Mali.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati iliridhika na majibu ya Wizara hii kwa hoja ya pili, na kwa upande wa hoja ya

kwanza Kamati ya PAC haikuridhika na majibu ya Wizara na imeitaka Wizara ya

Miundombinu na Mawasiliano kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ili

kuepusha dhana ovu kwa watendaji wake. Kwa mfano, kuwepo na mawasiliano rasmi ya

maandishi baina ya Taasisi za Serikali na sio kutekeleza majukumu yake kwa njia ya

mdomo.

9.0 MASHIRIKA NA MAMLAKA MBALI MBALI ZA SERIKALI

9.1 BODI YA MAPATO

Hoja Namba 48.1 Taarifa ya Mapato na Matumizi kufuatia ufungaji wa Hesabu za

Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Bodi ilikadiriwa kukusanya Tsh. 7,397,684,066 kwa mwaka 2012/2013 na ulipomalizika

mwaka, ilikusanya Tsh. 7,358,500,788 sawa na asilimia 99.5 ya makadirio. Aidha, Bodi

ilikadiriwa kutumia Tsh. 5,616,214,100 kwa kazi za kawaida, na ilipofika tarehe 30 Juni,

2013, fedha zilizoingizwa na kutumika ni Tsh.6,061,166,430, sawa na asilimia 108 ya

makadirio, ikiwa ni ongezeko la Tsh. 444,952,330, sawa na asilimia 48 ya makadirio.

Majibu ya Bodi

Pamoja na maelezo hayo ya ukaguzi, taarifa sahihi za makadirio ya makusanyo kwa Bodi

yalikuwa Tsh. 162.02 bilioni na makusanyo halisi ni Tsh. 141.71 bilioni sawa na asilimia

87.46 ya makadirio. Aidha, matumizi yalikadiriwa kuwa Tsh. 7.358 bilioni na hali halisi ya

matumizi kwa kazi za kawaida yalikuwa bilioni 5.77 na Tsh. 1.39 bilioni kwa kazi za

maendeleo.

Tatizo kubwa lililipelekea kutofikia malengo ya makusanyo ni kushamiri kwa biashara ya

magendo ya mafuta, kuwepo kwa uwajibikaji mdogo kwa walipa kodi, kukosekana kwa

taaluma maalum kwa wafanyakazi wa Bodi, kukosa ufadhili kwa utekelezaji wa Mpango

Mkuu wa Miaka Mitano na viwango vidogo vya kutozea kodi kwa mfumo wa „package‟ kwa

hoteli kubwa zenye hadhi ya juu (transfer prising).

Page 90: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

90

Hata hivyo, Bodi inafanya juhudi za kuzishinda changamoto hizo kwa mikakati mbali mbali

ikiwa ni pamoja na kushirikiana na taasisi na vyombo vyengine kukabiliana na biashara ya

magendo ya mafuta, kuandaa mfumo wa kompyuta utakaosaidia kuhakikisha kuwa wanatoa

risiti wakati wa mauzo na kuimarisha elimu kwa walipa kodi na wananchi kwa ujumla kwa

lengo la kuongeza ufahamu juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji iwapo kuna utaratibu maalum na viegezo maalum vilivyowekwa katika

makisio ya makusanyo ya Bodi na kujiridhisha kuwa, makisio hayo hufanywa tu zaidi kwa

kuzingatia mafanikio yaliyofikiwa mwaka uliopita. Aidha, Kamati imejiridhisha kuwa,

kutokuwepo kwa mfumo wa utoaji wa risiti za electroniki kunachangia upotevu wa mapato,

na wakati sasa umefika kwa Serikali kuanzisha mfumo huo na zaidi mahotelini, ambako kwa

kushindwa kuwa na mfumo huo, kuna upotevu mkubwa wa mapato yatokanayo na kodi.

Kamati pia imeelezwa kuwa, kuna tatizo kubwa la kuwepo taasisi mbili (ZRB na TRA)

Zanzibar zinazokusanya kodi mbili ambazo zinategemeana katika kupata taarifa sahihi za

makusanyo ya aina moja. Ni vyema Serikali ikaliangalia hili kwa umakini na kulitafutia

ufumbuzi.

Mapendekezo ya Kamati

Serikali iagalie upya vigezo vya kufanya makisio ya makusanyo ili viwe wazi na kufahamika

kwa taasisi zake zote. Aidha, Kamati inaishauri Bodi kusimamia ipasavyo mikakati ya

kukusanya kodi ili izidi kuongeza mapato.

Uwezo wa Bodi kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na uwezo wa kujiendesha

Bodi ya Mapato kwa mwaka 2012/2013 ilikuwa na mali za mpito za thamani ya Tsh.

711,733,044.73, huku dhima za mpito zikiwa na thamani ya Tsh. 35,619,191, huku hali

halisi ya mali za mpito zikiwa na thamani ya Tsh. 676,113,853.73 sawa na 20:1, hali

iliyotokana na kuwepo kwa wadaiwa wengi kwa hivyo ni faraja kwa Bodi. Mapato ya

Mamlaka yalikuwa ni Tsh. 7,358,500,788.15 na matumizi yake yalikuwa Tsh.

6,061,166,429.72 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa ya Tsh. 1,297,334,358.43.

Majibu ya Bodi

Taarifa ni kweli na Bodi inaendelea na mikakati yake ya kuongeza mapato ya makusanyo na

kupunguza gharama za matumizi, ili iendelee kupata faida na kutekeleza kwa ufanisi

majukumu yake.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaipongeza Bodi kwa juhudi inazozichukua na kuitaka kukusanya mapato zaidi.

9.2 MAMLAKA YA UKUZAJI VITEGA UCHUMI ZANZIBAR (ZIPA)

Hoja Namba 47.1 Taarifa ya Mapato na Matumizi kufuatia ufungaji wa Hesabu za

Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Mamlaka imekadiriwa kukusanya Tsh. 371,762,500 kwa mwaka 2012/2013 na ulipomalizika

mwaka, Mamlaka iliweza kukusanya Tsh. 397,837,675 sawa na asilimia 107 ya makadirio,

kukiwa na ongezeko la Tsh. 26,075,175, sawa na asilimia 7 ya makadirio. Aidha, Mamlaka

ilikadiriwa kutumia Tsh. 776,174,312 kwa kazi za kawaida, na ilipofika tarehe 30 Juni, 2013,

fedha zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 452,134,513, sawa na asilimia 58 ya makadirio,

ikiwa ni pungufu ya Tsh.324,039,799, sawa na asilimia 42 ya makadirio.

Page 91: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

91

Majibu ya Mamlaka

Makadirio ya Mamlaka yaliangalia zaidi vyanzo vya ndani na fedha za ruzuku kutoka

Serikalini. Ni kweli mwaka huu walikuwa na mafanikio ya makusanyo, ingawaje mara

nyingi huanguka kwa makusanyo kutokana na kuanguka kwa shughuli za biashara kwa

wawekezaji.

Aidha, mwaka huu waliweza kuongeza kiwango cha makusanyo kutokana na kupata taarifa

ya Kampuni ya Zalu kuuza hisa zake kwa kampuni nyengine, ingawaje suala kama hili

halitokezei mara kwa mara.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji iwapo Mamlaka inafahamu suala la kuahamishwa kwa hisa za Kampuni ya

Zanteli, kufuatia pia kuelezwa kwamba, Kampuni zinazofika katika Mamlaka kufuatia kuuza

hisa, ni ile ambayo miradi yake imeidhinishwa na Mamlaka.

Aidha, Mamlaka imeeleza kutojua chochote kuhusiana na Kampuni ya Zanteli. Vile vile,

Mamlaka wameeleza kuwa, wajibu wa Mamlaka ni kurahishisha kwa Kampuni yoyote

inayotaka kuekeza Zanzibar, kuikabidhi kampuni hiyo kwa taasisi ya Serikali inayosimamia

uwekezaji wa kampuni hiyo na kuhakikisha miradi inaendelea na kutoa msaada kutoka hali

moja ya uekezaji kwenda katika hali bora zaidi ya kampuni hiyo.

Kuhusiana na matumizi ya kawaida kuwa chini ya makadirio, Kamati ilihoji athari

zilizopatikana kutokana na kutotimia kwa makadirio na kuelezwa athari hizo ni pamoja na

kushindwa kufanya utafiti, kushindwa kufanya makongamano ya kutoa elimu mbali mbali

ikiwa ni pamoja na kushindwa kurusha vipindi vya redio, kusita kwa ujenzi wa Afisi ya

Mamlaka Pemba, kushindwa kufanya matengenezo ya mitaro na kushindwa kutengeneza

maghala.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuwa wazi katika taarifa zake na ubia wa Kampuni ya Zanteli, ili

taasisi zake nyengine zinazohusika na uwekezaji ziwe na taarifa za kutosha na za uhakika ili

kukuza uekezaji nchini. Aidha, Kamati inaitaka Serikali kuhakikisha inatoa fedha kamili kwa

Mamlaka, ili iweze kutekeleza miradi na shughuli zake ilizojipangia kwa mwaka.

Uwezo wa Mamlaka kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na uwezo wa

kujiendesha

Kwa mwaka 2012/2013, Mamlaka ilikuwa na mali za mpito za thamani ya Tsh.

16,073,005,717.54, huku dhima za mpito zikiwa na thamani ya Tsh. 445,997,822.13, huku

hali halisi ya mali za mpito zikiwa na thamani ya Tsh. 15,627,007,895.41 sawa na 36.04:1,

hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa pamoja na salio la benki. Mapato ya

Mamlaka yalikuwa ni Tsh. 1,578,185,942.42 na matumizi yake yalikuwa Tsh.

2,191,039,830.69 na hivyo kuendeshwa kwa hasara kwa Tsh. 612,853,888.27.

Majibu ya Mamlaka

Mamlaka ni Wakala wa Serikali na sio Shirika la biashara kwamba lingefanya faida. Aidha,

tokea kuanzishwa kwa Mamlaka, Mfuko wa Mamlaka haujawahi angalau kupata fedha za

kutosha za kufanyia shughuli zake za msingi kama zilivyoelezwa katika Sheria, hivyo

haijapata kuwa na ziada. Aidha, ni sahihi kuwa Mamlaka haikufikia malengo yake kwa

mujibu wa mipango yake na makadirio ya mapato.

Page 92: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

92

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji suala zima la kuimarika kwa mipango ya maendeleo kama inavyotarajiwa

kusimamiwa na Mamlaka, na kuelezwa tatizo kubwa la nchi yetu ni kutokuwepo kwa

muendelezo wa mipango ya maendeleo (sustainability of development policy). Mfano

unatolewa kwa Waziri wa Fedha anapofuta msamaha wa kodi Fulani, bila ya kuwashirikisha

Mamlaka kunaleta tatizo na kurudisha nyuma maendeleo ya Mamlaka na Taifa.

Aidha, Kamati imesikitishwa sana na taarifa ya Serikali kufanya marekebisho ya Sheria ya

Mamlaka kwa baadhi ya vifungu vyake, huku viongozi wa Mamlaka hiyo wakiwa hawana

taarifa wala hawakushirikishwa katika mabadiliko hayo. Aidha, mfano unatolewa wa

kufanya marekebisho ya Sheria ya Fedha (Appropriation Bill) bila ya kufanya marekebisho

ya Sheria ya Uekezaji inayosimamiwa na Mamlaka, ni kufanya mambo kinyume nyume.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuwa na mipango endelevu ya maendeleo na kuachana na sera ya

kila kiongozi kuja na mipango yake ya maendeleo. Aidha, Kamati inaitaka Serikali

kuzishirikisha taasisi zinazohusika na usimamizi wa Sheria na sio kuzifanyia marekebisho

Sheria bila ya kuwashirikisha watendaji wakuu wa taasisi hizo.

9.3 MAMLAKA YA MAJI (ZAWA)

Hoja Namba 45.1 Uwezo wa Mamlaka kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Mamlaka ya Maji ilikuwa na mali za mpito zenye thamani ya Tsh. 6,920,333,649.63 na

dhima za mpito za 1,644,718,751.84 kwa mwaka 2012/2013 na kufanya uwezo halisi wa

mali za mpito kuwa Tsh. 5,275,614,897.79 kwa uwezo wa kulipa dhima 4.2:1,

kulikochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa wengi wa Malmaka na ikishauriwa kuongeza

kukusanya mapato kutoka kwa wadaiwa.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2012/2013 yalikuwa ni Tsh. 11,282,646,495.08 na

matumizi yake yalikuwa Tsh. 12,772,002,960.03 na hivyo kuendeshwa kwa hasara ya Tsh.

1,489,356,464.95, ingawaje imepungua ukilinganisha na mwaka 2011/2012, iliyokuwa Tsh.

4,859,463,154. Aidha, juhudi za makusudi zinahitajika za kuongeza ukusanyaji wa mapato

na kupunguza gharama za uendeshaji.

Majibu ya Mamlaka

Mamlaka inakubaliana na ushauri wa kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa mapato kutoka

kwa wadaiwa na miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni kutoa elimu kwa wananchi kupitia

vyombo vya habari na kufanya mikutano na wadau. Mamlaka pia imeanzisha zoezi maalum

la siku ya Alhamis kutoa huduma za maji ikiwa ni pamoja na kuwakatia huduma wale wote

wenye madeni zaidi ya miezi mitatu.

Mamlaka pia inaendelea na zoezi la uingizwaji wa taarifa za wateja katika mfumo wa kumbu

kumbu za Mamlaka (SBM), ili kuweza kuwajua wateja wepi wanaopata huduma ya maji na

wasiopata. Mamlaka inaendelea kuwafungia mita hususan katika maeneo ya utalii, ili

kuongeza ukusanyaji wa mapato.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji uwezo wa Mamlaka katika uhalisia wake na kuelezwa kuwa, bado Mamlaka

inasua sua kutokana na kuelemewa na madeni ambapo hivi sasa ina deni lifikalo Bilioni 1.8,

na kuna matarajio makubwa ya kuongezeka kwa deni hilo. Kamati pia imejiridhisha kuwepo

Page 93: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

93

kwa deni kubwa linalodaiwa na Shirika la Umeme dhidi ya Mamlaka na hali inayoikabili

Mamlaka kushindwa kuviendeleza visima na miradi yake mbali mbali ya uchimbaji wa

visima, kutokana na ukubwa wa gharama za umeme.

Aidha, Kamati imeelezwa kuwa Mamlaka hivi sasa ina visima 250 Unguja na Pemba,

ambapo ufanisi wake haupatikani kutokana na gharama za umeme. Aidha, deni la visima

hivyo inafikia milioni 400 kwa mwezi na kwa kujumuisha visima vipya vilivyochimbwa

lakini vimeshindikana kuendeshwa kwa kukosekana kwa uwezo wa kulipia huduma ya

umeme, gharama zake kwa mwezi zinatarajiwa kufikia milioni 500 hadi 600.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka iendelee na juhudi za kukusanya mapato na kupunguza gharama

za uendeshaji kwa kuiwezesha kujiendesha kwa faida.

9.4 MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE

Taarifa ya Mapato na Matumizi kufuatia ufungaji wa Hesabu za Mwisho wa Mwaka

2012/2013

Makusanyo ya Mamlaka kwa mwaka 2012/2013, yalikadiriwa kufikia 3,526,205,437, lakini

uhalisia wa makusanyo hayo ulikuwa Tsh. 3,431,996,398 sawa na asilimia 97 ya makadirio,

ikiwa kuna upungufu wa Tsh. 94,658,288 sawa na asilimia 3 ya makadirio.

Aidha, kwa ajili ya kuendesha shughuli za kawaida, Mamlaka ilikadiriwa kutumia Tsh.

3,526,654,686 na ulipotimia mwaka wa fedha, Mamlaka ilikwishatumia Tsh. 3,355,307,887,

sawa na asilimia 95 ya makadirio, ikiwa ni pungufu ya Tsh. 3,183,961,088 sawa na asilimia

5 ya makadirio.

Majibu ya Mamlaka

Mapato ya Mamlaka yanaathirika sana na huduma wanazozitoa ambazo zinastahiki kubebwa

na Serikali. Kwa mfano, Mamlaka inalipa 20,000,000/- kila mwezi kuwalipa KVZ kwa kutoa

huduma ya ulinzi ili kuwazuia watu wasichote mchanga na ulinzi mwengine unaohusika,

wakati jukumu hilo lingebebwa na Serikali. Aidha, Mamlaka inategemea mapato pekee ya

„airport service charge‟ ambayo ni wastani wa bilioni 12 kwa mwaka na ndio hizo hizo ni

mapato ya Serikali kuu.

Uzoefu walionao, „airport service charges‟ inayokusanywa na Bodi ya Mapato ya Tanzania

(TRA), kwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalim Julius K. Nyerere, Mamlaka ya

Uwanja wa Ndege ya Tanzania inarejeshewa asilimia 70 ya makusanyo hayo. Aidha, kwa

upande wa uwanja wa ndege wa Kilimanjaro, wa nchi ya Uganda na Kenya, Mamlaka za

Viwanja vya ndege hizo hupewa asilimia 100 ya makusanyo, kinyume na inavyofanyika

Zanzibar.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kuwa, Serikali bado haijawa tayari kuiacha kodi hii ya huduma ya

uwanja wa ndege moja kwa moja kwa Mamlaka, kutokana na Serikali yenyewe kutegemea

sana mapato hayo. Hata hivyo, kama tu Serikali ingeliangalia huduma bora zitakazopatikana

kutokana na kodi hiyo kusimamiwa na Mamlaka na huku faida ya maendeleo yake ikawa

ndio mafanikio ya Serikali, basi uchumi wa nchi ungelikuwa kwa kiwango kikubwa.

Page 94: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

94

Mapendekezo ya Kamati

Serikali iiwezeshe Mamlaka katika ukusanyaji wa mapato kwa kuwaongezea kiwango cha

mapato ya kodi ya uwanja wa ndege kwa Mamlaka, ili baada ya miaka miwili ijayo, kodi

hiyo moja kwa moja iwe kwa Mamlaka.

Uwezo wa Mamlaka kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na uwezo wa

kujiendesha

Kwa mwaka wa 2012/2013, Mamlaka ilikuwa na mali za mpito zenye thamani ya Tsh.

1,260,183,373 na dhima za mpito zilikuwa na thamani ya 680,743,469 na kufanya uwezo

halisi wa mali za mpito kuwa Tsh. 579,439,904 kwa uwezo wa kulipa dhima 1.9:1, hali

iliyochangiwa na kuwepo kwa wadaiwa na salio la benki.

Taarifa ya mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2012/2013 yalikuwa ni Tsh. 3,696,097,369 na

matumizi yalifikia Tsh. 5,764,876,672, hali iliyoifanya Mamlaka kuendeshwa kwa hasara ya

Tsh. 2,068,779,303, hasara ambayo inaweza kupungua iwapo Mamlaka itaongeza juhudi ya

ukusanyaji wa mapato na kupunguza gharama za uedeshaji.

Majibu ya Mamlaka

Mamlaka inatoa huduma kulingana na viwango vinavyotambulika na taasisi za kimataifa.

Kwa ujumla, Mamlaka ina mali za kudumu zenye thamani kubwa ambapo kwa mujibu wa

taratibu za kihasibu zimeoneshwa kama sehemu ya matumizi. Yaani, kwa mwaka huu,

uchakavu wa mali za kudumu ulifikia thamani ya Tsh. 2,650,041,479, ambapo gharama hizo

hazina uhalisia wa fedha bali ni njia ya kuweka kumbu kumbu za kimahesabu. Hivyo, kwa

kuzingatia gharama hizo za uchakavu na hasara iliyooneshwa katika ripoti, ya Tsh.

2,068,779,303, ni sawa kusema kuwa, Mamlaka ina ziada ya Tsh. 536,262,176.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji kwa Mamlaka kutoeleza ufafanuzi huo wakati wa ukaguzi, na hatimae

imekubaliana na Mamlaka kuwa, maelezo halisi ya taarifa hii ni kuonesha uhalisia wa

kimahesabu kwa Mamlaka.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kutoa ufafanuzi wa

kutosha katika ripoti kuhusiana na suala zima la uwezo wa Mashirika kumudu kulipa dhima

zao za muda mfupi na uwezo wa kujiendesha.

Hoja Namba 46.2 Malimbikizo ya Madeni, Tsh. 680,743,469

Fedha hizo zinadaiwa na wafanyabiashara, wafanyakazi pamoja na taasisi mbali mbali kwa

ajili ya utowaji wa huduma tofauti katika Mamlaka, deni ambalo limerithiwa kutoka Idara ya

Anga, ambalo hadi kuanzishwa kwa Mamlaka halijalipwa hadi sasa.

Majibu ya Mamlaka

Kweli madeni hayo ni ya muda mrefu. Aidha, deni la Tsh. 30,000,000 ni la TCAA kwa ajili

ya mafunzo ya wafanyakazi wa Mamlaka kutoka chuo cha Aviation CATC, deni ambalo

litalipwa mwaka wa fedha 2014/2015. Deni la Tsh. 34,018,986 ni la „salary in area‟ na hapo

awali lilikuwa kubwa sana lakini limelipwa na lililobaki litalipwa katika mwaka wa fedha

2014/2015. Aidha, deli lilobakia la Tsh. 467,333,708 ni deni endelevu la Shirika la Umeme

(ZECO), ambalo Mamlaka imelirithi kutoka Idara ya Anga. Deni hilo hadi Disemba 2014

lilikuwa Tsh. 639,643,389.40 ambapo Mamlaka imekubaliana na ZECO kupunguzwa kwa

Page 95: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

95

deni hilo kwa kila mwezi na ilipofikia Januari 2015, Mamlaka ilikwishalipunguza na kufikia

Tsh. 204,767,433.54.

Uchunguzi wa Kamati

Suala la madeni linahitaji kuekewa mikakati madhubuti ukizingatia kuwa, hakuna bajeti

inayowekwa kwa ulipaji huo, lakini ni jukumu la kila taasisi yenye madeni kuyalipa madeni

hayo, isipokuwa kwa yale madeni ambayo yangestahiki kubebwa na Wizara ya Fedha.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Mamlaka kukamilisha malipo ya deni lililobakia.

9.5 CHUO CHA UTAWALA WA UMMA

Hoja Namba 50.1 Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha.

Chuo cha Utawala wa Umma kilikuwa na mali za mpito zenye thamani ya Tsh.

968,455,883.58 kwa mwaka wa fedha wa 2012/2013 na hakukuwa na dhima za mpito, hali

iliyopelekea uwezo halisi ya mali za mpito kuwa na thamani ya Tsh.968,455,883.58 na

hivyo, mali za mpito kuwa kubwa kutokana na kutokuwepo kwa dhima za mpito.

Taarifa hizi pia zinaonesha mapato ya Chuo kuwa Tsh. 2,233,792,500 na matumizi yake

yakawa ni Tsh. 1,577,708,549.62, hali inayoonesha kuwa Chuo kinaendeshwa kwa bakaa ya

Tsh. 656,083,950.38, huku Chuo kikishauriwa kuongeza juhudi ya makusanyo na usimamizi

wa vyanzo vyake vya mapato.

Majibu ya Chuo

Suala la madeni yanayoikabili Chuo yanasababishwa zaidi na wanafunzi wanaochelewa

kulipia gharama za masomo kwa wakati unaotakiwa. Kwa kuzingatia sera ya Chuo na

Serikali ya kuwasaidia wanafunzi wanyonge kuweza kupata elimu, Chuo kinawasaidia

wanafunzi kwa kuhakikisha wanalipa madeni yao bila ya kuwazuilia kufanya mitihani.

Inapofikia mwanafunzi amelipa kidogo, Chuo kinamruhusu kufanya mitihani ila huzuia

matokeo yake na akishindwa kulipa, basi hatua ya mwisho ni kumzuia kupata cheti chake

mpaka amalize kulipa fedha zote.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji kuhusiana na nafasi ya Chuo kumueleza Mkaguzi wakati wa ukaguzi

kuhusiana na hali halisi inayowakabili na kuelezwa kuwa, Mkaguzi kwa kawaida huangalia

Ankara za malipo (invoice) na kuzihesabu kama deni.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kuongeza makusanyo ya mapato kwa kudhibiti ipasavyo uvujaji

wake.

Hoja Namba 50.2 Udhaifu katika ukusanyaji wa mapato

Chuo kilianzisha mfumo wa malipo ya ada za wanafunzi kulipiwa benki ya Watu wa

Zanzibar (PBZ) kupitia akaunti namba 021103000578 kuanzia tarehe 1/7/2012, ambapo

baada ya malipo mwanafunzi hupatiwa stakabadhi ya benki (pay in slip) na kuikabidhi

Chuoni kwa kupewa risiti.

Hata hivyo, ukaguzi umebaini kuwa baadhi ya wanafunzi walikuwa wanalipa bila ya kufuata

utaratibu huo kwa kumlipa Mshika Fedha wa Chuo, hali iliyokipelekea Chuo kukosa

Page 96: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

96

mapato. Aidha, ukaguzi umeshindwa kupata kiasi kamili cha fedha zilizopotea kutokana na

kukosa kumbukumbu za ukusanyaji wa mapato hayo, ambapo baadhi ya stakabadhi ziliweza

kupatikana na kujulikana fedha zilizokusanywa, lakini baadhi yao hazikuweza kupatikana na

kupelekea ukaguzi kushindwa kujua kiasi halisi cha fedha zilizokusanywa. Aidha,

kushindwa kwa ukaguzi kuendelea kulifuatilia suala hili, kunatokana na iliyokuwa Wizara ya

Nchi(OR) Utumishi wa Umma na Utawala Bora huingilia kati kadhia hiyo na baadhi ya

kumbu kumbu za mahesabu kuchukuliwa na Wizara husika ambapo ni kinyume na taratibu

za sheria ya fedha, kifungu namba 67(1) ya mwaka 2005.

Majibu ya Chuo

Wizara haijaingilia kati suala hilo ambalo ni Uongozi wa Chuo ulikuwa wa mwanzo

kugundua udhaifu huo na ililifikisha suala hilo kwa Bodi ya Chuo na kushauriwa

kuliwasilisha kwa Wizara kwa ajili ya ushauri na hatua zinazofaa. Chuo kiligundua udhaifu

huo baada ya kuwataka wanafunzi kuleta uthibitisho wa malipo, ambapo walileta risiti

zisizokubaliwa, ambazo kwa kiasi kikubwa zimefanana sana na risiti za Serikali wanazotoa

Chuo kutoka Wizara ya Fedha.

Baada ya kugundua, Chuo kilimpa fursa ya kujieleza Mshika Fedha huyo, Ndg. Hafidh Ali

Hassan kwa njia ya mazungumzo na maandishi na baada ya kujiridhisha kwamba, Ndg.

Hafidh amehusika, Chuo kilimpa likizo ya lazima la miezi mitatu kwa kumlipa nusu

mshahara na kuendelea na uchunguzi, kupitia barua ya tarehe 8/4/2013 yenye kumbu kumbu

namba IPA/OPF/H.18131/C/.

Chuo baadae kilitoa taarifa kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mhasibu Mkuu wa

Serikali tarehe 9/4/2013 kuhusiana na kadhia hiyo na kutokana na ushauri wa Baraza la

Chuo, hatua iliyofuata ni kumuagiza Mhusika kuzilipa fedha zote alizopokea kwa wanafunzi

kinyume na taratibu na Chuo kiliziwasilisha benki. Aidha, Mhusika alitekeleza agizo hilo

hadi kufikia Januari 2015 akiwa ameshalipa Tsh. 55,095,000/- sawa na asilimia 89% ya

fedha alizopokea (ambazo ni Tsh. 61,395,000/-) na fedha zilizobaki aliendelea kukatwa

katika mshahara wake kwa kiwango cha Tsh. 79,000/- kila mwezi.

Chuo kilitekeleza ushauri wa Baraza la Chuo na Wizara ya kwa kumrejesha Mhusika

Utumishi na kwa kipindi hiki, anaendelea na kazi katika kitengo cha Kalamazoo. Sambamba

na hilo, kadhia ya Ndg. Hafidh inashughulikiwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na

Uhujumu wa Uchumi Zanzibar.

Kuhusiana na hatua za kuimarisha Kitengo cha Fedha, Chuo kimeimarisha wafanyakazi wa

Kitengo hicho, wakiwemo Wahasibu watatu na Washika Fedha wawili, ambapo awali

Kitengo kilikuwa na Mhasibu mmoja pekee na Washika Fedha wawili. Vile vile Kitengo

kina kompyuta tatu na zote zimeunganishwa na mitandao inayoweza kugundua uwepo wa

stakabadhi bandia na udanganyifu.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na hatua ilizochukua Chuo, suala hili linaonekana lina mtandao mkubwa ambao

unapaswa kushughulikiwa ipasavyo na Serikali. Aidha, kulionekana kuwepo kwa udhaifu wa

udhibiti wa ndani, na Chuo kinatakiwa kuchukua hatua madhubuti zaidi katika kudhibiti

udanganyifu utakaoweza kutokea.

Page 97: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

97

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuchukua hatua za kudhibiti uvujaji wa fedha kwa kupitia risiti feki

zinazotumiwa na baadhi ya watendaji wasiokuwa waaminifu. Aidha, hatua madhubuti za

kisheria ziendelee kuchukuliwa kwa Mhusika, ili iwe funzo wa watu wengine.

Hoja Namba 50.3 Madeni ya wanafunzi, Tsh. 611,743,863

Fedha hizo deni la wanafunzi 1555 wa fani mbali mbali katika Chuo ambazo hazijalipwa na

wanafunzi hao. Hali hii inatokana na Uongozi wa Chuo kutokuwa na usimamizi madhubuti

wa ukusanyaji wa mapato yanayotkna na huduma mbali mbali zinazotolewa na Chuo.

Majibu ya Chuo

Ni kweli Chuo kina madeni hayo, ingawaje sasa kimechukua hatua madhubuti kuhakikisha

wanafunzi hawezi kumaliza masomo na kupewa cheti, bila ya kulipa deni lake lote.

Uchunguzi wa Kamati

Vyuo vingi vya Serikali vinakabiliwa na tatizo la malumbukizo ya madeni kutokana na vyuo

hivyo kujikita zaidi katika kutoa huduma na kuwasaidia wananchi wengi wenye kipato

kidogo. Pamoja na hali hii kuonekana kuwasaidia wananchi wengi, Serikali na Uongozi wa

vyuo husika, bado vina jukumu la kusimamia ukusanyaji wa malipo, ili vyuo hivyo viweze

kujiendesha.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kuhakikisha kuwa madeni hayo yanalipwa na yanapungua kila

mwaka na hatimae yamalizike kabisa.

9.6 CHUO CHA UANDISHI WA HABARI

Hoja Namba 51.1 Matokeo ya Hesabu za Mwisho wa Mwaka.

Taarifa za mapato na matumizi

Tsh. 80,800,000 zilikadiriwa kukusanywa na Chuo cha Uandishi wa Habari kwa mwaka

2012/2013, ambapo hali halisi ya makusanyo hayo yalikuwa Tsh. 105,710,000, sawa na

asilimia 131 ya makadirio ya makusanyo. Kwa upande wa matumizi ya kazi za kawaida,

Chuo kilikadiriwa kutumia Tsh. 305,000,000 na kuingiziwa Tsh. 216,000,000, sawa na

asilimia 71 ya makadio.

Majibu ya Chuo

Vyanzo vya mapato ni vile vile, lakini nyongeza ya makusanyo imetokana na ongezeko la

wanafunzi kwa mwaka 2012/2013. Hata hivyo, Chuo kinapanga kuongeza wanafunzi na

kufikia 600, lakini wanakabiliwa na tatizo la sehemu ya kuwaweka. Kuhusiana na gharama

za matumizi, Chuo kinatumia zaidi fedha zake kwa mitihani na gharama za Bodi, ambapo

kitendo cha kuwa na idadi kubwa ya walimu wa muda (part time), kinawalazimu kutumia

fedha nyingi, ili waweze kutoa elimu Chuoni hapo.

Kuhusiana na hasara ya Chuo, hali hiyo inatokana na utaratibu wa ufungaji wa hesabu

ambao unaelekeza kuzingatia kuingiza uchakavu wa thamani ya mali zilizopo katika taasisi

husika yaani (Depraciation) ambazo kwa kawaida huwa sio fedha taslim katika matumizi

(Non cash expenses). Kwa msingi huo, Chuo hakikutumia kwa hasara kwa mujibu wa

makusanyo na matumizi, ila hasara kama hiyo katika mahesabu huonekana kadri Chuo

kinapokuwa kinaongeza mali za mpito mwaka hadi mwaka kwa kuwa thamani za aina hiyo

hushuka.

Page 98: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

98

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imeridhishwa na juhudi za Chuo kuongeza idadi ya wanafunzi, lakini mabadiliko

hayo yaende sambamba na majengo ya kuwawezesha wanafunzi hao kusoma bila ya

usumbufu. Aidha, Kamati imejiridhisha kwamba, jengo walilonalo Chuo hivi sasa

wanatakiwa kuhama na jengo watakalohamia liliopo Kilimani Bar, ni dogo wala halitakidhi

mahitaji halisi ya Chuo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Chuo kutafuta mkopo Benki ya Kiislamu ya PBZ, kwa ajili ya kupata

mkopo utakaowawezesha kujenga majengo ya kisasa katika kiwanja cha Chuo kilichopo

Tunguu.

Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na uwezo wa kujiendesha.

Kwa mwaka 2012/2013, Chuo kilikuwa na mali za mpito za 26,972,422.50, bila ya kuwa na

dhima za mpito, hali iliyopelekea hali halisi ya mali za mpito kuwa sawa na mali zenyewe za

mpito, kutokana na kutokuwepo kwa madeni.

Mapato ya Chuo yalifikia Tsh. 358,335,000 na matumizi yake yakawa Tsh. 385,555,266, na

kukifanya Chuo kuendeshwa kwa upungufu wa Tsh. 27,220,266 na kumfanya Mkaguzi

ashauri kuongezwa kwa makusanyo na kuchukua hatua za kupunguza gharama za

uendeshaji.

Majibu ya Chuo

Pamoja na maelezo ya ripoti ya Mdhibiti, ni vyema ikafahamika kuwa, Chuo ni Taasisi ya

Serikali kinachotoa huduma na hivyo, hakina dhamira ya kupata faida. Hata hivyo, gharama

za matumizi kuzidi mapato, kunatokana na kushuka kwa thamani ya vifaa mwaka hadi

mwaka.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na ukweli kwamba, Chuo kama Taasisi ya Serikali huwa haifanyi faida, kuanzishwa

kwake kunatakiwa kukiwezesha kutoa huduma bora kwa wananchi, jambo ambalo

halitaweza kupatikana iwapo uwezo wa Chuo utapungua mwaka hadi mwaka.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kuongeza mapato na kupunguza gharama za uendeshaji zisizo za

lazima, ili kiweze kujiendesha na kutoa huduma bora iliyokusudiwa.

9.7 SHIRIKA LA BANDARI

Hoja Namba 38.1 Uwezo wa Bodi kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

Uwezo wa kujiendesha

Mali za mpito za thamani ya Tsh. 11,400,359,862.80 na dhima za mpito za thamani ya Tsh.

644,309,782.86 hufanya hali halisi ya mali za mpito kwa Shirika kuwa Tsh.

10,756,050,079.94 kwa mwaka 2012/2013, ambayo ni sawa na uwezo wa ration ya 18:1.

Mapato ya Shirika yalikuwa Tsh. 18,825,503,482.22 na matumizi yake yalikuwa Tsh.

16,454,104,373.42 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa la Tsh. 2,371,399,108.8, hali hii

itaimarika, iwapo Shirika litasimamia vyanzo vyake vya mapato na kupunguza gharama za

uendeshaji.

Page 99: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

99

Majibu ya Shirika

Jumla ya Tsh. 1,140,420,886 zilikadiriwa kukusanywa kwa mwaka 2012/2013, lakini fedha

halisi zilizokusanywa zilikuwa Tsh. 606,747,899.72 sawa na asilimia 53.20 ya makadirio.

Sababu kubwa iliyopelekea kutofikia lengo lililokusudiwa ni kwa Shirika kuandaa makadirio

makubwa kuliko hali halisi ilivyokuwa katika mwaka huo na kulitokana na viashiria mbali

mbali ikiwemo matarajio ya biashara kulingana na mwenendo pamoja na mabadiliko ya

thamani za sarafu mbali mbali zikilinganishwa na shilingi ya Kitanzania.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na juhudi za Shirika, Kamati imeendelea kujishuhudia tatizo la madeni ya muda

mrefu yanayoikabili Shirika, ambapo Kamati ilielezwa kuwa, hatua ambazo sasa zimefikiwa

na Shirika ni kushughulikiwa suala hili na Afisi ya Mwanasheria Mkuu kwa lengo la

kutafutwa taratibu za kutumika ili suala hilo liwasilishwe Baraza la Wawakilishi kwa hatua

za kufutwa.

Kuhusiana na vyanzo vya mapato vya Shirika, Kamati imehoji sababu zinanazokwamisha

kujengwa bandari mpya ya Mpiga Duri, kutaendelea kuzorotesha makusanyo ya Shirika na

wakati umefika kwa Serikali kutoa kauli ya kuanza kwa ujenzi wa bandari hiyo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kuharakisha taratibu za kuanza ujenzi wa bandari mpya ya Mpiga

Duri, ili kulifanya Shirika liongeze juhudi za makusanyo ya mapato na kuwa na uwezo

kamili wa kujiendesha. Kuhusiana na madeni ya muda mrefu ya Shirika, Kamati inaendelea

kuishangaa Serikali kwa kuchukua muda mrefu bila ya madeni hayo kuwasilishwa Barazani

kwa hatua za kufutwa, ikizingatiwa kuwa, Kamati ilifanya jihudi kubwa miaka iliyopita

kuhusiana na madeni ya namna kama hii, lakini bado Serikali haijafikia muafaka wa ufutwaji

wa madeni hayo. Inapendekezwa hatua ziharakishwe ili madeni yasiyolipika yafutwe

kisheria.

9.8 SHIRIKA LA MELI NA UWAKALA

Hoja Namba 36.1 Uwezo wa Bodi kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

Uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2012/2013, Shirika ilikuwa na mali za mpito za 151,850,572.7 na dhima za

mpito za 362,603,018.32 na kulifanya Shirika kuwa na hali halisi ya mali za mpito kwa

upungufu wa Tsh. 210,752,445.62 kwa ratio ya 0.42:1, hali iliyosababishwa na kuwepo kwa

deni la benki na madeni ya taasisi nyengine.

Mapato ya Shirika yalikuwa Tsh. 5,607,945,958.83 kwa mwaka 2012/2013 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 4,805,425,292.36 na hivyo kuendeshwa kwa faida ya Tsh.

802,520,666.47 ambayo imepungua kwa Tsh. 1,719,853.53 sawa na asilimia 0.2 kwa

mwaka. Hali hii itaimarika, iwapo Shirika litasimamia vyanzo vyake vya mapato na

kupunguza gharama za uendeshaji.

Majibu ya Shirika

Sababu kubwa ya kupungua kwa faida na kulifanya Shirika kujiendesha kunatokana na

uchakavu wa meli za Shirika. Kwa mfano Shirika lilizipeleka meli hizo chelezoni, hali

iliyolifanya Shirika kuathiriwa sana kiutendaji kwa sababu meli hizo zinapokuwepo

chelezoni, Shirika huwa halipati mapato yoyote ya kodi na ipomaliza kufanyiwa

matengenezo, Shirika hulazimika kutafuta mkodishwaji mwengine kwa ajili ya kuendelea

kujipatia mapato. Kwa ujumla, tatizo hili halitamaliza iwapo Shirika halitapata meli mpya,

kwa sababu meli walizonazo sasa tayari muda wake wa kufanya kazi umeshamaliza. Kwa

Page 100: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

100

mfano, meli hizi zina umri wa miaka 34, wakati umri halisi ulitakiwa usizidi miaka 20

mpaka 25.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji ufuatiliaji wa meli mpya ya Serikali na kwa nini Shirika limetumia mapato

yake kwa kuwasafirisha Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na

Mawasiliano wakati tayari bajeti ya ununuzi huo tayari imeshakatwa kutoka kwa Wizara na

Taasisi zote za Serikali.

Kamati pia imehoji ununuzi wa majereta mawili ambayo yameshatumika (second hand)

kununuliwa Singapore kwa USD 158,640, kwa mnasaba wa matumizi ya Shirika kama

umefuata taratibu za kisheria na kujiridhisha kwamba, ununuzi huo haukufuata taratibu za

kisheria kwa kukosekana Bodi ya Zabuni inayotakiwa kuundwa kwa mujibu wa Sheria,

ingawa kulifanyika vikao, kwa mfano, tarehe 7/8/2012, lakini kikao hicho hakina sifa ya

kuwa Bodi ya Zabuni.

Aidha, Bodi ya Wakurugenzi imechukua jukumu la kuidhinisha manunuzi ya majenereta

hayo, ambapo kazi hiyo inatakiwa kufanywa na Bodi ya Zabuni. Pia, hakukuwa na Kamati

yoyote ya tathmini iliyohusika na ununuzi wa majereta hayo, kinyume na taratibu za

kisheria.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inalitaka Shirika kuhakikisha matumizi yake yanakwenda sambamba na Sheria na

kufuata ipasavyo ushauri ya Mkaguzi wa kudhibiti matumizi yake na kuongeza makusanyo.

9.9 SHIRIKA LA UMEME (ZECO)

Kwa mwaka 2012/2013, Shirika ilikuwa na mali za mpito za 32,674,896,553 na dhima za

mpito za 45,641,826,646 na kulifanya Shirika kuwa na hali halisi ya mali za mpito kwa

upungufu wa Tsh. 12,966,930,093 kwa ratio ya 0.72:1, hali iliyosababishwa na kuwepo kwa

deni la benki na madeni ya taasisi nyengine.

Mapato ya Shirika yalikuwa Tsh. 15,965,004,949 kwa mwaka 2012/2013 na matumizi yake

yalikuwa Tsh. 18,218,538,557 na hivyo kuendeshwa kwa hasara ya Tsh. 2,253,533,608. Hali

hii inayoonesha haja kubwa ya Shirika kufanya juhudi za kupunguza gharama za uendeshaji

na kufuatilia wadaiwa mbali mbali wa Shirika ikiwezo taasisi za Serikali pamoja na watu

binafsi.

Hoja Namba 31.2 Wadaiwa ambao hawakuingizwa katika hesabu za mwaka (Financial

Statement), Tsh. 39,971,226

Ukaguzi umebaini Shirika limeshindwa kuingiza madeni ya wateja wanaodaiwa ambao

wamepata huduma za umeme katika hesabu ya mwaka ulioishia Juni, 2013 zilizowasilishwa

kwa ajili ya ukaguzi. Aidha orodha hiyo inaonesha idadi ya wateja 64 hawajaingizwa katika

hesabu ya mwaka.

Hoja Namba 31.3 Malimbikizo ya madeni, Tsh. 13,687,263,487.83

Fedha hizo zinadaiwa na Shirika kwa taasisi mbali mbali za Serikali. Ukaguzi umebaini

kuwa, madeni hayo ni ya muda mrefu na hakuna jitihada zozote zinazochukuliwa juu ya

taasisi za Serikali za kulipa madeni hayo kwa wakati, hali inayopelekea Shirika kushindwa

kujiendesha kutokana na fedha hizo kubakia katika mikono ya wadaiwa.

Page 101: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

101

Uchunguzi wa Kamati

Kamati haikufanya kazi na Shirika hili kwa kuwa tayari ilifanya kazi zinazohusiana na

udhaifu wa Shirika katika mwaka 2012/2013 kufuatia Hoja Binafsi ya Mhe. Hija Hassan

Hija ya kuundwa Kamati Teule ya kufuatilia Shirika hilo kwa rejea zilizotolewa, ambayo

hatimae kazi hiyo ya kufuatilia hoja hizo ilifanyiwa kazi na Kamati na kutoa ripoti yake

Barazani, ambayo hadi leo haijafanyiwa kazi kama ilivyopendekezwa na Kamati.

Hata hivyo, Kamati ilifanya kazi na taasisi zilizotajwa kuhusika na madeni hayo kwa upande

wa Pemba, ambazo zilikuwa Mamlaka ya Maji (ZAWA), Wizara ya Afya, Wizara ya Habari,

Utamaduni, Utalii na Michezo na Mahakama Kuu. Katika kufanya kazi na taasisi hizo,

Kamati iliwakutanisha na muwakilishi wa Shirika na kujiridhisha juu ya usahihi wa hoja hii

na taasisi zote ambazo zilikuwa hajizalikamilisha malipo ya madeni hayo, Kamati ilizitaka

zikamilishe madeni.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Serikali kufahamu kuwa, kasoro na udhaifu uliogundulika na Kamati hii

wakati ilipowasilisha ripoti yake ya Uchunguzi Maalum kwa Shirika hili, bado unaendelea

na utaendelea iwapo Serikali haitochukua hatua madhubuti za kutekeleza mapendekezo ya

Kamati hii kuhusiana na Shirika hili.

9.10 SHIRIKA LA BIMA

Shirika la Bima la Zanzibar halikuwa na hoja yoyote katika ripoti nne za Mdhibiti na

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za mwaka 2011/2012 na 2012/2013. Hata hivyo, kutokana na

mamlaka ya Kamati kama yanavyoelezwa na kifungu cha 118(2)(c) ya kanuni za Baraza la

Wawakilishi, toleo la 2012, Kamati imefanya ziara ya tawi la Shirika la Bima, Dar es

Salaam, Dodoma na Mbeya na ufafanuzi wake ni kama ufuatao:

Shirika la Bima Kanda ya Pwani (Dar es Salaam)

Shirika limefanikiwa kuongeza wigo wa biashara kwa kutanua huduma zake ikiwa ni pamoja

na kuongeza ofisi katika sehemu mbali mbali za Tanzania, ambapo Pemba mwaka 1985,

Kanda ya Pwani (Dar es Salaam) mwaka 2000, Kanda ya Ziwa Mwanza 2003, kanda ya

kaskazini, Arusha 2004, kanda ya nyanda za juu kusini, 2009, kanda ya Dodoma mwaka

2010 na kanda ya kusini Mtwara mwaka 2013.

Shirika pia limefanikiwa kuongeza mapato kupitia ofisi zake mbali mbali ambapo kwa

upande wa kanda ya pwani, Shirika kwa mwaka 2011 ilikusanya Tsh. 4,368,777,692/-,

mwaka 2012 ilikuwa Tsh. 4,032,934,917 na mwaka 2013 iliongezeka na kufikia Tsh.

5,185,146,746/-. Hata hivyo, Shirika linakabiliwa na changamoto nyingi ambapo kwa

upande wa kanda hii, pamoja na changamoto nyengine, Shirika halina ofisi yake mwenyewe

na hutumia kiasi kikubwa cha fedha kulipia kodi za ofisi zote za kanda hii na sehemu

nyengine Tanzania bara, ambapo kodi hizo ni kubwa na huongezeka mwaka hadi mwaka.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imetaka kufahamu sababu zilizopelekea Shirika kutoonekana katika ripoti ya

Mkaguzi kwa miaka takriban miwili sasa na kuelezwa kuwa Shirika linafunga hesabu zake

kila mwisho wa mwaka lakini na Uongozi wa Shirika unashangaa kutokuwemo katika taarifa

za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Kamati imehoji iwapo Shirika linalipia mgao Serikalini na kuelezwa kuwa, Serikali inadaiwa

zaidi ya 250 milioni na Shirika na Shirika limeshaiandikia Serikali kuomba kufidia mgao

huo kwa kusamehe deni hilo ili Shirika lisilipe gawiyo kwa mwaka 2012/2013.

Page 102: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

102

Kamati pia imejiridhisha kuwa, Serikali haikati bima kwa majengo yake, magari na hata

wafanyakazi wake, huku Mashirika pekee yanayokata bima kwa wafanyakazi wao ni Shirika

la Umeme na Shirika la Bandari ya Zanzibar, na hali mbaya zaidi Pemba, ambapo Serikali

haikati bima yoyote hata kwa magari ya Serikali kwa taasisi zake za Pemba, mpaka Shirika

lifanye ukaguzi maalum.

Kamati pia imeridhika na hatua za Shirika kuanzisha Bima inayofuata taratibu za Kiislamu

(Islamic Insuarence) ambapo tayari Shirika limeshalipitisha suala hilo katika Bodi yake ya

Wakurugenzi na sasa limo katika hatua za kufikishwa Bungeni.

Kamati imeshikitishwa na hatua zisizoridhisha za Kamisheni ya Utumishi kuzorotesha

„scheme of service‟ ya Shirika na kupelekea mishahara ya wafanyakazi wa Shirika

kutofanyiwa kazi na kuboreshwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaushauri uongozi wa Shirika kanda ya pwani kuongeza wigo wa kuhifadhi fedha

zao katika Benki ya Watu wa Zanzibar, ili kukuza biashara baina ya taasisi hizi za Serikali.

Aidha, Kamati inaitaka Serikali kukata bima za majengo na vyombo vyake mbali mbali vya

moto, pamoja na wafanyakazi wake.

Serikali isimamie Kamisheni ya Utumishi kushughulikia maslahi ya Shirika, kwani kinyume

chake kutaondosha motisha ya kufanya kazi kwa kujituma na kupunguza mapato ya Shirika.

Shirika la Bima Kanda ya Kati-Dodoma

Kanda ya Kati Dodoma inajumuisha mikoa wa Dodoma na wilaya zake, Tabora na wilaya

zake, Morogoro na wilaya zake, Singida na wilaya zake na baadhi ya maeneo katika mipaka

ya wilaya ya Kiteto. Kanda hii ina wafanyakazi wanne na imeanza biashara mwezi Mei 2011

na imefanikiwa kukusanya Tsh. 116,997,000 mwaka 2011, Tsh. 320,707,000/- mwaka 2012,

Tsh. 355,980,000 mwaka 2012 na Januari hadi Septemba ya mwaka 2014, imeweza

kukusanya Tsh. 324,758,000. Aidha, Kanda hii inashirikiana na Mawakala na Madalali

mbali mbali wanaopatikana Dodoma na maeneo mbali mbali ya mikoa ya jirani.

Pamoja na mafanikio hayo, Ofisi ya Shirika kanda ya Kati inakabiliwa na changamoto

kadhaa ikiwa ni pamoja na ugumu wa kuanzishwa kwa mawakala wapya ili kukuza biashara

kutokana na mji wa Dodoma kutokuwa na watu wengi wenye sifa ya kuruhusiwa na

Kamishna wa Bima kufungua Ofisi ya uwakala wa bima kama matakwa ya Sheria ya bima

yanavyohitaji. Aidha, soko la bima limeingiliwa na makampuni binafsi yasiyofuata kanuni

zilizopo kwa kutoa bima kwa bei ya chini sana kinyume na makubaliano na mikataba ya

mashirika ya bima.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imetaka kujua iwapo kanda hii inafanya juhudi za kutoa huduma kwa taasisi za

Serikali zilizopo Dodoma na kuelezwa kuwa, wamefanya juhudi ya kuonana na viongozi wa

Chuo Kikuu cha Dodoma, ingawaje bado wanahitaji nguvu za Kamati na Serikali ya

Mapinduzi ya Zanzibar kufanikisha hilo.

Pamoja na tatizo la ukosefu wa ofisi, Kamati imeridhishwa na juhudi zinazofanywa na

uongozi wa kanda na kushuhudia majengo tofauti ambayo yanaweza kupatikana kwa

kuuziwa Shirika, iwapo kutakuwa na umakini na juhudi za makusudi za kupatikana ofisi

hiyo ya kudumu.

Page 103: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

103

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri kanda hii kuongeza wigo wa kutoa huduma kwa taasisi mbali mbali za

Serikali zilizopo katika kanda hiyo. Aidha, Kamati inaushauri uongozi wa Shirika pamoja na

Serikali kununua jengo eneo litakaloonekana linafaa mjini Dodoma, kwa ajili ya kupatikana

ofisi ya kudumu ya Shirika.

Shirika la Bima Kanda ya Kusini-Mbeya

Ofisi ya nyanda za juu kusini, ilianzishwa rasmi mwezi July 2009 ikiwa na watendaji watatu

na sasa ina watendaji watano. Eneo hili la nyanda za juu kusini, lina mikoa ya Iringa,

Rvuma, Mbeya, Rukwa, Njombe na Katavi. Hali halisi ya makusanyo ya kanda hii kwa

mwaka 2010 ni Tsh. 723,554,746.50, mwaka 2011 ilikuwa Tsh. 911,398,481, mwaka 2012

iliongezeka kwa kufikia Tsh. 1,078,599,545 na kwa mwaka 2013 ni Tsh. 1,376,923,860.

Makusanyo ya kanda kwa mwezi Januari hadi Disemba 2014 yalikisiwa kuwa Tsh.

1,562,990,000/- na yameongezeka hadi kuwa Tsh. 2,036,107,038/- ikiwa ni ziada ya Tsh.

473,117,038/-. Matumizi kwa mwaka huo yalikisiwa kuwa Tsh 156,379,956/- kwa kazi za

kawaida, na halisi ikawa Tsh. 97,303,115.50 na Ofisi ya kanda imelipa Tsh. 256,654,023.30

kwa kulipia ujira wa mawakala.

Kanda hii ya kusini ni muhimu sana kwa mapato ya Shirika. Kwa mfano mwaka 2014,

Shirika la Bima la Zanzibar lilikusanya bilioni 17.7 ambapo, Kanda hii ilichangia kwa

asilimia 12.

Miongoni mwa changamoto kubwa inayoikabili kanda hii ya kusini ni „incentives‟ za

wafanyakazi. Ukimchukua Meneja wa Tawi na kumlinganisha na Mameneja wa mashirika

mengine binafsi na wafanyakazi wote kwa ujumla, kuna tofauti kubwa ambayo kama Shirika

na Serikali hawatolishughulikia kwa kupandisha maslahi yao, ni wazi kuwa, wafanyakazi

hao wanaweza kuchukuliwa na kuajiriwa na makampuni hayo. Hivyo, ni vyema Kamisheni

ya Utumishi wa Umma ikaharikisha maslahi ya watendaji wa Shirika, ili kuwatia moyo na

kuwawezesha kufanya kazi kwa bidii.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji juhudi za kanda za kuongeza makusanyo baina ya mwaka juzi na mwaka

uliopita na kuelezwa kuwa zinatokana na watendaji binafsi na mawakala wao kwa kufungua

mikataba mipya na kujitangaza kwa takriban wateja wote. Aidha, mabadiliko ya tozo ya

bima (tariff) iliyoanza mwaka jana, imewasaidia sana kuongeza mapato na kufanya juhudi ya

kudhibiti matumizi.

Kuhusiana na Kanda kukosa madalali na kuwa na mawakala pekee, Kamati imeelezwa kuwa

bado Mbeya watu hawajatanua wigo wa udalali wa bima lakini Kanda ina azma ya kuwanao

iwapo watatimiza masharti na vigezo vinavyotakiwa kuwa navyo. Kamati pia imehoji

kuhusiana na bima ya moto kwa wafanyabiashara mbali mbali na kuelezwa kuwa, kutokana

na wateja wengi kuhamia katika mabenki na kwa kuwa wao bado hawajaingia katika

makubaliano na mabenki maalum, kunachangia kwa kiasi kikubwa kushindwa kupata wateja

wa bima hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaushauri uongozi wa Kanda ya Kusini na Shirika kwa ujumla kuingia mahusiano

na mabenki ikiwa ni pamoja na Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), ili kutanua wigo wa

kutoa huduma ya bima ya moto kwa wafanyabiashara mbali mbali. Aidha, Kamisheni ya

Utumishi wa Umma ishughulikie „scheme of services‟ ya Shirika la Bima la Zanzibar, kwa

lengo la kufanya marekebisho ya mishahara yao ili kuwajengea motisha wa kufanya kazi

kwa kujituma na kuongeza mapato ya Shirika.

Page 104: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

104

9.11 SHIRIKA LA BIASHARA YA MAGARI

Hoja Namba 40.1 Matokeo ya Hesabu za mwisho wa mwaka. Taarifa za mapato na

matumizi

Shirika lilikadiriwa kukusanya Tsh. 673,548,183 kwa mwaka 2012/2013. Aidha, mwisho wa

mwaka ulipokamilika, Shirika lilifanikiwa kukusanya Tsh. 334,572,992, sawa na asilimia 50

ya makadirio, kukiwa na upungufu wa Tsh. 338,975,191 sawa na asilimia 50 ya makadirio.

Vile vile, Shirika lilikadiriwa kutumia Tsh. 603,276,210, lakini fedha haisi zilizoingizwa na

kutumiwa ni Tsh. 315,719,151, sawa na asilimia 61 ya makadirio.

Majibu ya Wizara ya Fedha na Shirika

Taarifa hizo ziko sawa, lakini wanapenda kuijuulisha Kamati kuwa, Shirika hilo sasa

limeshafungwan adhamana ya mali zake zipo katika Idara ya Uhakikimali iliyo chini ya

Wizara ya Fedha. Aidha, Serikali imetekeleza ushauri wa Mkaguzi unaopatikana katika

ripoti ya Ukaugi wa Hesabu ya mwaka huu (2012/2013), ukurasa wa 104.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imyari limeshafungwa na mali zake zinasimamiwa chini ya udhamini wa Wizara ya

Fedha kupitia Idara ya Uhakiki mali na wafanyakazi wake wameshapelekwa katika taasisi

mbali mbali za Serikali, kwa ajili ya kuendelea na utumishi wao.

Mapendekezo ya Kamati

Pamoja na Sheria ya Uekezaji wa Umma, Namba 4 ya mwaka 2002, kumpa Mhe. Rais

uwezo mkubwa wa kuvunja Mashirika ya Umma kwa amri ya kuyavunja, Kamati inaishauri

Serikali kutoa taarifa rasmi Baraza la Wawakilishi na kwa Kamati zinazohusika na Shirika

hilo, ili kuwe na uwazi na ufahamu wa kina juu ya kuvunjwa kwa Mashirika hayo.

9.12 SHIRIKA LA MAGAZETI YA SERIKALI ZANZIBAR

Hoja Namba 32.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Mapato na Matumizi

Shirika lilikadiriwa kukusanya Tsh. 500,000,000 kwa mwaka 2012/2013, lakini

kilichokusanywa halisi ni Tsh. 404,454,233 sawa na asilimia 81 ya makadirio, kukiwa na

upungufu wa Tsh. 95,545,767 sawa na asilimia 19 ya makadirio. Kwa upande wa matumizi,

Shirikalilikadiriwa kutumia kwa shughuli zake za kawaida, Tsh. 856,000,000 na fedha halisi

iliyoingizwa na kutumika ilikuwa Tsh. 598,280,421 sawa na asilimia 70 ya makadirio,

kukiwa na upungufu wa Tsh. 257,719,579 sawa na asilimia 30 ya makadirio.

Majibu ya Shirika

Ni kweli kuwa gharama za uchapaji ni kubwa na Shirika hulazimika kutumia zaidi ya

asilimia 70 ambazo ni sawa na Tsh. 334,974,490 kwa mwaka 2012/2013 na katika gharama

hizo pesa za makusanyo zilizotumiwa kwa matumizi hayo ni Tsh. 186,000,000.

Vile vile Tsh. 317,176,870 za ruzuku kwa mwaka 2011/2012 zilitumika kulipia gharama za

uchapishaji magazeti ambapo Tsh. 129,889,363 za makusanyo zilitumiwa katika gharama za

uchapishaji wa magazeti ya kila siku ya Zanzibar Leo, ambalo hugharamia zaidi ya Tsh.

36,000,000 kwa mwezi na Tsh. 432,000,000 kwa mwaka na gazeti la kila wiki la „Zaspoti‟

ambalo hugharimu Tsh. 42,000,000 kwa mwaka, malipo yake hupitia mapato ya Shirika kwa

vile hayatoshelezi, hata kama ruzuku itapatikana yote ambapo jambo hilo limetokana na

bajeti hiyo ya ruzuku kupangwa kwa mujibu wa ukomo (ceiling) ambayo Shirika limepewa

na Serikali ambayo hupatikana kwa asilimia ndogo na si kwa uhakika. Hali hii itaendelea

mpaka pale Shirika litakapopatiwa mitambo yake ya kuchapishia magazeti.

Page 105: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

105

Kuhusiana na posho la wafanyakazi halimo katika kuongeza gharama, kwani ni jambo la

kawaida kwa taasisi zinazozalisha magazeti duniani kutokana na maumbile ya kazi zenyewe

ambazo hazina muda maalum wala mapumziko kutokana na kuwa kazi ya kila siku. Na

hivyo, wafanyakazi hulazimika kuwepo kazini zaidi ya muda wa kawaida na haiwezekani

kuwapangia zamu.

Upungufu wa ukusanyaji wa mapato kwa Shirika hili umetokana na kutokuwa na kiwango

maalum cha uchapishaji wa magazeti, yaani, uchapishaji unategemea na kipindi wakati

wengine wanachapisha nakala nyingi na wakati mwengine nakala kidogo.

Aidha, walizidi kueleza kuwa kwa kawaida Mashirika ya Magazeti hupata faida kubwa

kutokana na matangazo yanayotangazwa, ingawa kwa Shirika hili mambo ni kinyume kwani

kuna taasisi nyingi hutoa matangazo yao bila ya kuyalipia kwa wakati, jambo ambalo

linalipelekea Shirika hili kushindwa kutekeleza shughuli zake kwa ufanisi unaotakiwa.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati ya PAC ilishindwa kufuatilia majibu ya hoja hizi kama ilivyopangwa baada ya

Watendaji wa Shirika hili kushindwa kutoa maelezo sahihi. Tatizo hili limejitokeza baada ya

watendaji wa Shirika la Magazeti kutoa majibu tofauti kwenye hoja, jambo ambalo

limeipelekea Kamati kushindwa kujua lipi jibu sahihi kati ya majibu hayo. Pamoja na hayo

walishindwa kujibu baadhi ya hoja za Wajumbe wa Kamati walizozihoji. Hatua hii imefikia

kwa kuwa Kaimu Mkurugenzi wa Shirika Ndg. Nasima kutokuwa na taarifa za kutosha

kuhusiana na Shirika analolikaimu.

Kutokana na kasoro hizo Kamati hii imehisi ni vyema ikatoa muda zaidi kwa Shirika ili

liweze kujiandaa vyema na hatimae kuwasilisha taarifa sahihi mbele ya Kamati kwa manufaa

ya Shirika na taifa kwa ujumla. Hata hivyo, Shirika liliwasilisha majibu yake tarehe

11/12/2014 kupitia barua yenye kumbu kumbu namba SMS/U/H/I/VOL.I/08, lakini majibu

hayo hayawezi kuchukuliwa sahihi bila ya kukaa tena na kujadiliana na Kamati. Hivyo,

Kamati hii haikubahatika kukutana tena na Shirika hili kutokana na majukumu mengi

iliyokuwa nayo. Kwa msingi huo, hoja za Shirika la Magazeti zimebaki kama zilivyo.

9.13 HOTELI YA BWAWANI

Hoja Namba 34.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Mapato na Matumizi

Ukaguzi umebaini kuwa Hoteli ya Bwawani ilikusanya mapato yake kwa upungufu wa Tsh.

73,046,378 sawa na asilimia 8 ya makadirio. Kwa upande wa matumizi, Hoteli ya Bwawani

iliingiziwa na kutumia jumla ya Tsh. 817,905,841 kwa kazi za kawaida ikiwa ni upungufu

wa Tsh. 8,261,675 sawa na asilimia 1 ya makadirio.

Majibu ya Hoteli

Hoteli ya Bawawani iliieleza Kamati kuwa upungufu huo wa ukusanyaji wa mapato

umetokea kutokana na uhaba wa wageni wanaofika hotelini kwa kuwa jengo la hoteli

linaendelea na ukarabati.

Walizidi kueleza kuwa ingawa hoteli hii inaendelea na ukarabati bado makisio ya ukusanyaji

wa mapato yameongezeka kutokana na mikakati waliojiwekea ikiwa ni pamoja na kufuatilia

madeni wanayodai. Katika kuthibitisha hili walizitaja baadhi ya Taasisi ambazo zilikuwa

zinadaiwa na Hoteli na hivi sasa zimepunguza kulipa madeni yao hayo na nyengine

zimekamilisha deni. Jadweli lifuatalo linaonesha namna baadhi ya Taasisi hizo zilivyolipa

madeni hayo;

Page 106: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

106

S/NO. JINA LA TAASISI KIWANGO CHA

FEDHA

ALICHOKUWA

ANADAIWA

KIWANGO CHA

FEDHA

ANACHODAIWA

1. Ofisi ya Rais, Fedha, Uchumi na

Mipango ya Maendeleo

Tsh. 2,340,648 -

2. Wizara ya Fedha Tsh. 12,437,200 -

3. Wizara ya Afya (Daktari wa

Kichina)

Tsh. 50,615,000 Tsh. 24,215,000

4. Hammy & Distributor Tsh. 3,360,000 -

5. National Marketing Co. Tsh. 75,000,000 -

6. Break Enterprise Tsh. 3,360,000 -

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ya PAC imesikitishwa sana na mwenendo wa uendeshaji wa Hoteli hii. Hii ni

kutokana na kuwa baadhi ya Taasisi za Serikali, Wanasiasa na Watendaji wa Serikali

huitumia Hoteli ya Bwawani kinyume na utaratibu. Jambo hili litapelekea Hoteli hii

kushindwa kujiendesha kutokana na ukosefu wa mapato.

Kutokana na kasoro hiyo, Kamati hii imebaini kuwa baadhi ya Taasisi za Serikali hutumia

fedha zao kinyume na walivyoidhinishiwa na Baraza la Wawakilishi

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inazitaka Taasisi zote pamoja na watu wote wanaodaiwa na Hoteli hii kuchukua

juhudi za makusudi za kulipa madeni yao ili kuiwezesha Hoteli ya Bwawani kutekeleza

majukumu yake ipasavyo.

Uwezo wa Hoteli ya Bwawani kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na uwezo wa

kujiendesha

Kwa mwaka 2012/2013, Hoteli ilikuwa na mali za mpito za Tsh. 488,785,177.16 na dhima

za mpito za Tsh. 20,171,218 kwa bakaa la thamani ya Tsh. 468,613,959.16 na uwezo wa

kulipa dhima kwa ratio ya 24.2:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa wa Tsh.

325,091,753 pamoja na salio la benki la Tsh. 163,693,424.16 kwa mwaka 2012/2013.

Mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2012/2013 yalikuwa ni Tsh. 1,136,279,917 na matumizi

yake yalikuwa Tsh. 986,417,431 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa la Tsh. 149,862,486.

Majibu ya Hoteli

Ni kweli kwamba Hoteli ni taasisi inayojiendesha kibiashara hivyo ni lazima itakuwa ina

wadaiwa. Katika kufuatilia madeni hayo Uongozi wa Hoteli imeunda Kamati ya Watu saba

ambao jukumu lao ni kuhakikisha wanafuatilia madeni ya Hoteli ili Hoteli iweze kutatua

tatizo la upungufu la mishahara kwa wafanyakazi wake ambalo linaikabili hivi sasa. Jumla

ya fedha inazodai ni Tsh. 325,091,753.

Pamoja na juhudi hizo Uongozi wa Hoteli imewasilisha tatizo hilo Wizara ya Fedha ili

kusaidiwa kulitafutia ufumbuzi suala hili na Wizara ya Fedha imekubali kushirikiana nao.

Aidha, kwa kipindi kirefu Hoteli ilikuwa inakabiliwa na changamoto ya gharama kubwa za

uendeshaji kibiashara. Kutokana na hilo Hoteli imechukua juhudi za makusudi ikiwa ni

pamoja na kudhibiti vianzio vya mapato na kudhibiti gharama za matumizi ya hoteli.

Aidha, Hoteli ilipitia viwango vinavyotozwa kwa huduma mbali mbali na kubaini viwango

vingi kati hivyo kuwa inahitaji kuongezwa. Hivyo, Hoteli kwa kushirikiana na Wizara ya

Page 107: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

107

Habari, Utamauni, Utalii na Michezo ilifanya mapitio ya viwango hivyo ili viendane na

wakati hatua ambayo itaongeza mapato ya Hoteli.

Mchanganuo wenyewe ni kama ifuatavyo;

S/NO. JINA LA UKUMBI BEI YA ZAMANI BEI YA SASA

1. Salama Hall – Promotion na

Biashara

Tsh. 1,000,000 Tsh.1,500,000

2. Salama Hall – Harusi na

Mahafali

Tsh. 600,000 Tsh. 1,000,000

3. Café Changu Restaurant -

Promotion na Biashara

Tsh. 500,000 Tsh. 1,000,000

4. Café Changu Restaurant –

Harusi na Mahafali

Tsh. 200,000 Tsh. 300,000

5. Roof Top – Semina Tsh. 200,000 Tsh. 300,000

6. Conference Hall above

Pemba Bar – Semina

Tsh. 250,000 Tsh. 300,000

Uchunguzi wa Kamati Kamati inaitaka Hoteli kuendelea kufuatilia madeni yake kwa inaowadai, pamoja na juhudi

walioionesha ya kuwasiliana kwa njia ya barua kwa wadaiwa, Kamati imejiridhisha kuwa,

taasisi nyingi za Serikali hazichukui hatua za kufuatilia madeni yao kisheria, hali

inayozifanya taasisi hizo kushindwa kusimamia ipasavyo mapato yake na kuendelea kutoa

huduma bila ya kulipwa chochote. Hivyo, Hoteli ichukue hatua za kisheria mbali na

kuandika barua, kwa wadaiwa wote watakaoshindwa kulipia madeni yao.

Mapendekezo ya Kamati

Serikali itoe toleo maalum kwa taasisi zake kutumia kumbi za Hoteli hii endapo zitakuwa na

shughuli kama vile semina, makongamano nakadhalika, jambo hili litalisaidia Hoteli kupata

mapato zaidi.

Aidha, inazitaka Taasisi za Serikali kulipia gharama za ukodishwaji wa kumbi kwa wakati ili

Hoteli iweze kutekeleza majukumu yake bila ya usumbufu wowote.

Hoja Namba 34.2 Kukosekana kwa mikataba kwa wasambazaji wa chakula

(Suppliers) Tsh. 27,139,300

Fedha hizo zilitumika kwa ununuzi wa vyakula kwa ajili ya wageni wa Hoteli ya Bwawani

kwa kununua bidhaa mbali mbali kwa ajili ya huduma za Hoteli bila ya kuwepo mikataba

maalum kuhusiana na manunuzi hayo, wakati kufanya hivyo ni kwenda kinyume na kifungu

cha 73 cha Sheria Namba 9 ya mwaka 2005.

Majibu ya Hoteli

Hoteli ya Bwawani ilikiri kutokufunga mikataba na wasambazaji wa vyakula, hii ni kutokana

na kuwa Hoteli kwa kupitia Serikali Kuu katika kipindi hicho chote imo katika mikakati ya

kutaka kumpa Mwekezaji ili kuiendeleza. Kutokana na malengo hayo Hoteli ilishindwa

kufunga mikataba ili kuepusha kujakutozwa fidia endapo itakatisha mikataba hiyo wakati

zoezi hilo litakapofanikiwa.

Kufuatia hoja hiyo ya Mdhibiti, Uongozi wa Hoteli umo katika mikakati ya kuwamalizia

madeni yao watoa huduma hiyo na baadae kutangaza zabuni kwa kumpata mzabuni ambae

atakaekidhi vigezo vyote kwa mujibu wa sheria.

Page 108: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

108

Uchunguzi wa Kamati Kamati ya PAC haiungi mkono suala la Hoteli hiyo kupewa Mwekazaji kutokana na uzoefu

uliopatikana kwa Hoteli hiyo kupewa Mwekezaji.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Hoteli kuwa na utamaduni wa kutoa zabuni kwa zile huduma

inazozihitaji ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima.

Vile vile, Kamati hii inaishauri Serikali kuendelea kuwaendeleza wafanyakazi wa

Hoteli ili waje wafaidike na ajira zao endapo Serikali atabaki kwenye msimamo wake

wa kuipatia Mwekezaji Hoteli hii.

Ili kulinda ajira za wananchi wake, Kamati ya PAC imeishauri Serikali kuwa

miongoni mwa masharti ya kupatiwa hoteli hiyo Mwekezaji huyo iwe ni uhakikisha

kuwa anawapa kipaombele watendaji wa Hoteli hii kwani mtu mwenye uzoefu

anaweza kufanya kazi nzuri kuliko mtu mwenye elimu kubwa.

9.14 MFUKO WA HIFADHI YA JAMII (ZSSF)

Hoja Namba 33.1 Uwezo wa Mfuko kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka 2012/2013, Mfuko ulikuwa na mali za mpito za Tsh. 5,950,764,431 na dhima

za mpito za Tsh. 141,637,269,148 kwa hasara ya Tsh. 135,686,504,717 na uwezo wa kulipa

dhima kwa ratio ya 0.04:1, hali iliyochangiwa zaidi na kuwepo kwa wadaiwa wengi wa

Mfuko.

Mapato ya Mfuko yalikuwa ni Tsh. 41,272,755,594 na matumizi yake yalikuwa Tsh.

10,360,040,228 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa la Tsh. 30,912,715,366.

Majibu ya Mfuko

Hesabu za dhima za mpito zimekosewa katika taarifa ya ukaguzi hali inayoonesha pia

maelezo yaliyotolewa hayana usahihi. Usahihi wa dhima kwa mwaka 2012/2013 ni Tsh.

310,159,732.81 na hali halisi ya mali za mpito ni Tsh. 5,640,604,699.00 na hivyo uwezo wa

kulipa dhima ni 19,186,128.36. aidha, kuhusiana na uwezo wa kujiendesha, uongozi wa

Mfuko umeeleza kuwa, Mfuko haufanyi faida na ziada yote inayopatikana inapelekwa moja

kwa moja kwa wanachama wake na wamefanikiwa kuwa na ongezeko kubwa kutokana na

kupunguza gharama za vikao vya bodi ya Wakurugenzi na kwa watendaji wa Mfuko. Pia

Mfuko umeongeza ufanisi wa kuwasomesha wafanyakazi wake, kiasi ya kufanya kazi kwa

juhudi kubwa ya kuendeleza Mfuko.

Uchunguzi wa Kamati

Kufuatia marekebisho yaliyoelezwa, Kamati ilimtaka Afisa Mkaguzi anaefuatana na Kamati

kutoa usahihi wa maelezo ya Mfuko na taarifa ya Mkaguzi na kueleza kuwa, anakubaliana

na maelezo ya Mfuko na kilichoandikwa katika taarifa ya ukaguzi kilikosewa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inamshauri Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar, kuandaa

vyema taarifa zake kwa usahihi, ili kuiwezesha Kamati kutekeleza vyema majukumu yake.

Page 109: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

109

9.15 SHIRIKA LA BIASHARA LA TAIFA (ZSTC)

Hoja Namba 12 Uwasilishaji wa hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya ukaguzi

Kifungu cha 24(2) cha Sheria ya Fedha namba 12 ya mwaka 2005, inakitaka taasisi zote za

Serikali zitayarishe na kufunga hesabu zao za mwisho wa mwaka na kuziwasilisha kwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa ajili ya ukaguzi. Hata hivyo,

uwasilishaji huo usizidi tarehe 30 ya mwezi wa Septemba ya kila mwaka, lakini Shirika

lilichelewa kwa kuwasilisha 9/04/2013.

Majibu ya Shirika

Shirika la Biashara la Taifa liliieleza Kamati kuwa linafunga hesabu za mwisho wa mwaka

katika mwezi wa Juni tofauti na Mashirika mengine. Pamoja na kufunga hesabu katika

mwezi huo limekiri kuwa limechelewa kufunga hesabu zake kutokana na mageuzi ya

kiutendaji i.e linabadilisha mfumo wa kiutendaji kutoka „manual‟ na kutumia „computer‟.

Hata hivyo, wameiahidi Kamati kuwa watajitahidi kufunga hesabu zao mapema ili

kuzipeleka kunakostahiki na kufanyiwa kazi kama ilivyotarajiwa.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ya PAC imebaini kuwa muda wa ufungaji wa hesabu za mwaka kwa Mashirika ya

Umma unatofautiana, jambo ambalo linaweza likaikosesha Serikali kujua mapato yake halisi

katika mwaka husika.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati ya PAC ililitaka Shirika kujitahidi kufunga hesabu za mwaka na kuziwasilisha kwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kama sheria inavyoelekeza.

Aidha, Kamati hii inaishauri Serikali kuwa na mfumo mmoja wa ufungaji wa hesabu kwa

Taasisi zake zote ili kujua mapato halisi ya nchi.

Hoja Namba 39.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013.

Taarifa ya Mapato na matumizi

Shirika la Biashara la Taifa lilikadiriwa kukusanya Tsh. 53,808,214,000 katika kipindi cha

mwaka 2012/2013, lakini hadi kufikia Juni 2013 lilikusanya jumla ya Tsh. 32,932,176,,000

sawa na asilimia 61 ya makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 20,876,038,0020 sawa na

asilimia 39 ya makadirio. Aidha, Shirika liliidhinishiwa kutumia Tsh. 53,753,050,000 na

kuingiziwa na kutumia Tsh. 32,535,901,100 sawa na asilimia 61 ya makadirio, ikiwa ni

pungufu ya Tsh. 21,217,148,900 sawa na asilimia 39 ya makadirio.

Majibu ya Shirika

Shirika lilikabiliwa na upungufu wa ukusanyaji wa mapato kwa mwaka huo, kutokana na

mzao wa karafuu kwa mwaka huo kuwa ni mdogo. Hii ni kutokana na kuwa kwa kawaida

mzao wa karafuu mwaka mmoja unakuwa mkubwa lakini mwaka unaofuata unakuwa

mdogo.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ya PAC iliridhika na majibu ya Shirika kwa upande wa ukusanyaji wa mapato. Ama

kwa matumizi ya kazi za kawaida, Kamati hii imebaini kuwa Shirika la Biashara la Taifa

hutumia fedha nyingi kwa ajili ya kukilipa Kikosi Kazi „Task Force‟ kilichoundwa kwa ajili

ya zoezi la ukamataji wa karafuu za magendo wakati katika zoezi hilo Shirika halinufaiki na

chochote ingawa Shirika lenyewe linahisi zoezi hilo lina tija.

Page 110: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

110

Aidha, Kamati ya PAC imeshangazwa na kitendo cha Kikosi cha Kuzuia Magendo (KMKM)

kulipwa fedha kwa kazi ya kuzuia magendo hayo ya karafuu kwa kuwa lengo kuu la

kuundwa kwa Kikosi hicho ni kuzuia magendo ndani ya nchi.

Sambamba na hilo, Kamati hii imebaini kuwa fedha zinazotumika kwa ajili ya Kikosi Kazi

hukabidhiwa kwa Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko na Shirika na huwa hazikaguliwi

na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kitendo ambacho kimekitia mashaka

Kamati hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati hii inamshauri Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuzikagua fedha

hizo kwa kuwa fedha zinazotumika ni nyingi. Kwa mfano; katika mwaka wa fedha

2012/2013 jumla ya Tsh, 420,000,000 zilitumika kwa ajili ya zoezi la ukamataji wa magendo

ya karafuu.

Ingawa Kikosi Kazi kipo kwa mujibu wa Sheria , Kamati ya PAC inawataka wakuu wa

Kikosi Kazi hicho kusitisha malipo kwa KMKM kwa kuwa kinatimiza jukumu lake kisheria.

9.16 SHIRIKA LA UTANGAZAJI LA ZANZIBAR (ZBC)

Hoja Namba 37.1 Taarifa ya Mapato na Matumizi kufuatia ufungaji wa Hesabu za

Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Shirika la ZBC lilikadiriwa kukusanya Tsh. 280,700,000 na makusanyo halisi yalikuwa Tsh.

210,326,283 sawa na asilimia 75 ya makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 70,373,717, sawa

na asilimia 25 ya makadirio. Aidha, matumizi ya kawaida yalikuwa Tsh. 2,016,224,000 na

fedha halisi zilizopatikana kwa matumizi zilikuwa Tsh. 1,611,857,366 sawa na asilimia 80

ya makadirio na upungufu wa Tsh. 404,366,634 sawa na asilimia 20 ya makadirio.

Majibu ya Shirika

Upungufu wa kutofikia makisio ya makusanyo unategemea na vyanzo vya mapato ya Shirika

kupungua kutokana na kukisia na kutegemea chanzo kimoja ambacho huathiri vyanzo

vyengine. Kwa mfano vipindi vya Baraza la Wawakilishi wanapotumia muda mwingi

takriban siku nzima kurusha vikao vya Baraza, huathiri kwa kukosa kurusha matangazo

mengine na hivyo hukosa biashara.

Shirika pia lina chanzo chengine ambacho ni minara ila kwa sasa makampuni mengi ina

minara hiyo. Na kuna taasisi zikikodi minara hiyo hazilipi wala haziingiliki, kwa mfano

Idara ya Usalama, Polisi. Hata hivyo, Shirika linajipanga kuwa na mikataba na taasisi hizo.

Aidha, changamoto nyengine ni kuzimwa kwa umeme kwa ghafla, kwani hukimbiza wateja

wa minara hiyo.

Kwa upande wa matumizi, Shirika linakabiliwa na ukata mkubwa na udogo wa mishahara ya

wataalamu wake kulipwa mishahara midogo, kwani hupunguza ari ya kufanya kazi kwa

kujituma.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imesikitishwa na taarifa ya udogo ya mishahara kwa wafanyakazi wa Shirika na hata

suala zima la kurushwa kwa vipindi vya Baraza la Wawakilishi bila ya malipo, wakati

Shirika linakosa uwezo wa kutoa huduma na kujipatia mapato katika wakati huo.

Mapendekezo ya Kamati

Baraza la Wawakilishi litenge bajeti ya huduma ya matangazo wanayopatiwa na Shirika na

ni vyema Baraza likanunua na kufunga mitambo yake ambayo itasaidia hata kuwepo kwa

Page 111: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

111

„storage’ ya vikao vya Baraza. Aidha, Serikali iangalie kwa karibu mishahara ya

wafanyakazi wa Shirika ili kuwaendeleza na kuwabakisha katika kulihudumia Shirika.

Uwezo wa Shirika kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na uwezo wa

kujiendesha

Kwa mwaka wa 2012/2013, Shirika lilikuwa na mali za mpito zenye thamani ya Tsh.

63,690,000 na dhima za mpito za Tsh. 587,727,614 na hali halisi ya uwezo wa kulipa dhima

za mpito kuwa 0.11:1, ambapo uwiyano wa mali za mpito ni mdogo kuliko dhima za mpito,

hali iliyosababishwa na kuwepo kwa deni kubwa.

Taarifa ya mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2012/2013 yalikuwa ni Tsh. 1,557,350,432 na

matumizi yalifikia Tsh.2,173,966,466 hali iliyoifanya Mamlaka kuendeshwa kwa hasara ya

Tsh. 616,616,034 kuonesha kuwepo uwezekano wa kuongezeka kwa hasara iwapo Shirika

halitochukua juhudi za makusudi za kupunguza gharama za uedeshaji.

Majibu ya Shirika

Deni kubwa wanalokabiliwa ni la Shirika la Umeme ambalo walilirithi kutoka Sauti ya

Tanzania Zanzibar na Televisheni ya Zanzibar, ambapo kila mara Shirika la Umeme

limekuwa linahoji na kutaka kulipwa. Shirika limejaribu kulilipa lakini kwa kiwango kidogo.

Shirika limechukua hatua ya kuwaomba viongozi mbali mbali kusamehewa kwa deni hilo,

lakini hakuna mafanikio, nab ado wanashauri ama deni hilo lilipwe na Serikali au lifutwe.

Uchunguzi wa Kamati

Kama zilivyo taasisi nyingi za Serikali, zimekuwa na deni kubwa la umeme ambalo huwa

mzigo mzito na kushindwa kulilipa. Kamati imejiridhisha kwamba, Shirika lilimuandikia

Mhe. Rais barua ya tarehe 23 May 2004 yenye kumbu kumbu namba ZBC/MUM/VOL.II

iliyoandikwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi kuomba ifuatiliwe ahadi ya Mhe. Rais ya

kusamehewa deni hilo.

Mapendekezo ya Kamati

Shirika liendelee kuchukua juhudi ya kufuatilia deni lake na kwa nafasi ya Kamati inaiomba

Serikali kutafakari namna ya kulilipa deni hilo ambalo limekuwa mzigo mzito kwa Shirika.

9.17 CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR (SUZA)

Hoja 43.1 Hesabu za Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Taarifa ya Mapato na Matumizi

Kwa mwaka 2012/2013 Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kilikadiriwa kukusanya jumla

ya Tsh. 6,936,252,920 hadi kufikia 30 Juni, 2013 kilifanikiwa kukusanya Tsh.

6,510,873,906 sawa na asilimia 94 ya makadirio ikiwa ni upungufu wa Tsh. 425,379,019

sawa na asilimia 6 ya makadirio. Aidha, kwa mwaka 2012/2013 Chuo hiki uliidhinishiwa

kutumia Tsh. 7,232,044,940 kwa kazi za kawaida ingawaje fedha zilizoingizwa na kutumika

ni Tsh. 6,527,987,637 sawa na asilimia 90 ya makadirio ikiwa ni upungufu wa Tsh.

704,057,303 sawa na asilimia 10 ya makadirio.

Majibu ya Chuo

Ni kweli kwamba kuna upungufu wa ukusanyaji wa mapato katika mwaka huo wa fedha. Hii

ni kutokana na upungufu wa Ruzuku kutoka Serikalini kwa asilimia 13, ambapo Chuo

kilitarajia kuingiziwa Ruzuku ya Tsh. 4,200,000,000.00 na badala yake kiliingiziwa jumla ya

Tsh. 3,646,331,000.00. Hata hivyo, vianzio vyengine vya mapato vilizidi malengo. Kamati

ya PAC ilielezwa na Chuo kuwa upungufu huo umetokea zaidi kwenye kipengele cha

Page 112: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

112

mishahara na matumizi mengineyo ambapo chimbuko lake ni kupatikana na upungufu kwa

fedha za Ruzuku.

Walizidi kueleza kuwa Chuo kilitumia zaidi kwa asilimia 10 kwenye fedha za misaada, hii ni

kutokana na utekelezaji wa miradi kwa kiwango kikubwa kwa kuwa fedha hizo zilikuwepo

tayari.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ilishtushwa na majibu ya Chuo ya upungufu wa mishahara kwa watendaji wake na

kuomba maelezo zaidi, ambapo ilijibiwa kuwa upungufu huo wa mishahara umetokana na

kuwepo kwa nafasi wazi (vacant posts) pamoja na kuwepo kwa Wahadhiri wa muda „Part

timer Lecturers‟ ambao malipo yao hutokana na fedha nyengine za mapato ya Chuo ukiacha

Ruzuku. Jambo ambalo hupelekea Chuo kushindwa kutekeleza baadhi ya shughuli ambazo

kimejipangia.

Aidha, Kamati imebaini kuwa Chuo hakiingiziwi fedha za matumizi ya kazi za Maendeleo

ingawa Chuo kinashirikiana na Serikali kutafuta washirika wa maendeleo.

Mapendekezo ya Kamati

Serikali ijitahidi kukipatia Chuo Ruzuku iliyokadiriwa ili kiweze kutekeleza

majukumu yake ipasavyo.

Serikali iwapatie Chuo hiki fedha za matumizi ya kazi za maendeleo kwa kuwa Chuo

kina mahitaji mengi kama vile ofisi ya kituo kinachohusiana na shughuli za

wanafunzi „student center‟, ofisi kwa watendaji, duka nakadhalika.

Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na Uwezo wa kujiendesha.

Mali za mpito za thamani ya Tsh. 1,223,541,312.43 na dhima za mpito za thamani ya Tsh.

73,572,882.20 hufanya hali halisi ya mali za mpito kwa Shirika kuwa Tsh. 1,149,968,430.23

kwa mwaka 2012/2013, ambayo ni sawa na uwezo wa ration ya 16:1.

Mapato ya Shirika yalikuwa Tsh. 6,510,873,906.48 na matumizi yake yalikuwa Tsh.

6,527,987,637.39 na hivyo kuendeshwa kwa hasara ya Tsh. 17,113,730.91, mwendo huo wa

hesabu hizo unaonesha kuwepo kwa uwezekano wa kupunguka kwa hasara iwapo Chuo

kitachukua juhudi za makusudi za kupunguza gharama za uendeshaji.

Majibu ya Chuo

Ni kweli kwamba mali za mpito zinazidi dhima ya mpito kwa kuwa mali za mpito

zinajumuisha Akiba za Benki, madeni ya ada za wanafunzi na madeni ya mikopo ya

wafanyakazi.

Aidha, uwezo wa kulipa umeonekana mkubwa kutokana na kiwango kikubwa cha salio

wakati wa kufunga hesabu kilichotokana na fedha za miradi ambapo, kwenye hesabu za

Benki kulikuwa na Tsh. 745,883,984.43. Aidha, hesabu za mapato na matumizi inaonesha

kuwa mapato yamezidiwa na matumizi kutokana na kutekeleza kazi za miradi kwa fedha

ambayo Chuo imeipokea kipindi cha nyuma.

Pia, Chuo kilizidi kueleza kuwa kiutaratibu kilitakiwa kwenye matumizi kijumuishe pia na

gharama za uchakavu wa mali za kudumu ambapo kwa mwaka wa fedha 2012/2013 gharama

hizo zilikuwa ni Tsh. 315,395,814.48.

Kiujumla Uongozi wa Chuo unazingatia sana matumizi ya Chuo, na umekuwa ukichukua

jitihada mbali mbali kuhakikisha kwamba matumizi yanafanywa kwa kuzingatia bajeti na

kazi zinaendana na Mpango Mkakati.

Page 113: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

113

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati:

Kamati imeridhika na majibu yaliyotolewa na Chuo hiki na inaiomba Serikali kukitengea

fedha za matumizi ya maendeleo Chuo, ili kiweze kufikia malengo yake kilichojipangia

ikiwa ni pamoja na kuongeza majengo ya madarasa hasa ikizingatiwa kuwa baadhi ya vijana

wanaoomba nafasi za mafunzo Chuoni hapo hukosa nafasi za kujiunga na masomo kutokana

na ufinyu wa madarasa.

9.18 CHUO CHA UONGOZI WA FEDHA ZANZIBAR

Hoja Namba 42.1 Hesabu za Mwaka 2012/2013

Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na Uwezo wa kujiendesha.

Mali za mpito za thamani ya Tsh. 1,002,066,951.54 na dhima za mpito za thamani ya Tsh.

39,023,967.70 hufanya hali halisi ya mali za mpito kwa Shirika kuwa Tsh. 963,042,983.84

kwa mwaka 2012/2013, ambayo ni sawa na uwezo wa ration ya 26:1. Kwa takwimu hizo,

uwiyano wa mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha na dhima za mpito, hali iliyochangiwa

zaidi na kuwepo kwa wadaiwa pamoja na salio la benki kwa hesabu za Chuo.

Mapato ya Shirika yalikuwa Tsh. 3,517,210,714.18 na matumizi yake yalikuwa Tsh.

2,559,665,672.8 na hivyo kuendeshwa kwa faida ya Tsh. 957,545,041.38, mwendo huo wa

hesabu hizo unaonesha kuwepo kwa uwezekano wa kuzidi kushuka kwa faida iwapo Chuo

hakitachukua juhudi za makusudi za kupunguza gharama za uendeshaji, sambamba na

kuwepo kwa mipango imara ya ukusanyaji wa mapato, kwa sababu takwimu zinaonesha

kwamba faida ya Chuo imeshuka kutoka Tsh. 1,120,727,333 kwa mwaka 2011/2012 hadi

kufikia Tsh. 957,545,041.38 kwa mwaka 2012/2013 ikiwa ni upungufu wa Tsh.

163,182,291.62 sawa na wastani wa asilimia 15 kwa mwaka, kwani upungufu huo

umetokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji ikiwemo gharama za kukodi majengo

ya watu binafsi.

Majibu ya Chuo

Chuo cha Uongozi wa Fedha kimeieleza Kamati ya PAC kuwa hakikubaliani na maelezo

yaliyotolewa kwenye Ripoti ya Mdhibiti kwa kuwa Mapato ya Chuo yaliongezeka kwa

asilimia 25 ukilinganisha na mwaka wa fedha uliopita, ongezeko hilo limechangiwa na

kuongezeka kwa mapato mengineyo kwa asilimia 48.2, kuongezeka kwa Ruzuku kutoka

Serikalini asilimia 47.2, kuongezeka kwa ada za wanafunzi asilimia 9.4 na kuongezeka kwa

fedha za maendeleo asilimia 6.3.

Aidha, gharama za matumizi zimeongezeka kwa asilimia 54.4, ongezeko hili

limesababishwa na kuongezeka kwa gharama za matunzo ya majengo na magari kwa

asilimia 157. Kwa upande wa majengo gharama zimeongezeka kutokana na uchimbaji wa

mashimo ya maji machafu na mfumo wake katika dahalia ya Chuo. Ama kwa upande wa

magari gharama imeongezeka kutokana na kuanza kuyakatia bima kubwa „Comprehensive‟

magari ya Chuo.

Walizidi kueleza kuwa kuongezeka kwa matumizi ya gharama za usafiri, malazi na chakula

kwa asilimia 94.8, kwa walimu wanasomeshwa na Chuo katika Shahada ya Uzamivu (PhD)

na Uzamili katika nje ya nchi.

Pia, gharama za uendeshaji zimechangia kuongezeka kwa matumizi kwa asilimia 67.7.

Gharama hizo zimeshababishwa na kuanza kulipa riba (Interest) ya shilingi 236,174,220.46

kwa ajili ya mkopo kutoka ZSSF uliotumika kwa ujenzi wa dahalia.

Page 114: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

114

Sambamba na hayo, kodi ya magari na madarasa ambayo imeongezeka kwa asilimia 10%

ukilinganisha na mwaka uliopita imechangia kuongezeka kwa matumizi ya Chuo. Aidha,

kuongezeka kwa huduma kwa mfano; kuwepo kwa dahalia, Chuo kimeanza kulipia huduma

za usafi na ulinzi kwa kampuni binafsi baada ya Bodi ya Chuo kushauri huduma hizi

zitolewe na kampuni binafsi ili kuweka uwiano wa walimu na wafanyakazi wengine kama

vyombo vya udhibiti wa ubora wa vyuo unavyotakiwa. Jadweli lifuatalo linaonesha namna

Mapato na Matumizi ya Chuo yalivyokuwa katika miaka husika.

Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012 - 2012/2013

2011/2012 2012/2013 Ongezeko/Upungufu

Mapato

Ruzuku, Ada ya

Masomo na Mapato

mengineyo

2,802,282,653.00 3,517,210,714.18 25.51

Matumizi

Mishahara na Posho 753,594,036.20 1,004,013,525.50 33.23

Gharama za

Uendeshaji

546,448,205.08 916,419,017.17 67.70

Gharama

Usafiri,Malazi na

Chakula

53,634,939.25 104,480,309.00 94.80

Matunzo ya

Majengo na Magari

63,286,060.00 162,852,090.00 157.33

Ziada ghafi 1,416,963,240.53 2,187,764,941.67 54.40

Ziada/Upungufu

baada ya kutoa

Uchakavu

1,120,727,333.02 957,545,041.38 (14.56)

Mapato Kwa Wanafunzi Waliokodishiwa Madarasa Nje ya Chuo

2011/2012 2012/2013

Mapato kwa wanafunzi waliokodiwa madarasa 445,350,000.00 400,050,000.00

Kodi 61,830,000.00 64,890,000.00

Mapato Halisi 383,520,000.00 335,160,000.00

Jadweli ilinaonesha gharama na mapato ya kukodi kwa madarasa ambayo yako nje ya chuo,

Katika mwaka wa fedha 2012/2013, uendeshaji wa mafunzo katika sehemu za kukodi

madarasa nje chuo kimeweza kuongeza mapato yaliyosaidia kutekeleza shughuli za mipango

yake. Chuo kiliweza kukusanya mapato ya jumla ya TZS 400,050,000 ikilinganishwa na

gharama ya TZS 64,890,000 na kukiwezesha Chuo kupata mapato halisi ya TZS

335,160,000.

Kwa hivyo, takwimu hizi hazioneshi kuwa zimeleta upungufu katika mapato ya Chuo kwa

kukodi majengo binafsi. Kwani Chuo kisingeweza kutoa mafunzo hayo katika majengo

yake, aidha, kupata fedha za zaidi ya milioni 335.

Gharama za uendeshaji zimekuwa zikiongezeka sambamba na kuongezeka kwa kutanuka

kwa shughuli za chuo zikiwemo za kuongezeka kwa programu mpya za masomo. Katika

Page 115: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

115

mwaka wa fedha 2015/2016 Chuo kimejipanga kuangalia kupunguza gharama za uendeshaji

bila kuathiri utekelezaji wa majukumu ya Chuo kama ilivyotajwa katika sheria.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati ya PAC iliridhika na majibu yaliyotolewa na Chuo na pamoja na mambo mengine

ilibaini na kupendekeza yafuatayo;

Kitendo cha wanafunzi kutokukaa katika dahalia za Chuo na badala yake kukodi

katika nyumba za watu binafsi kunakikosesha mapato Chuo. Hivyo, Kamati hii

inawashauri wanafunzi wa Chuo hicho kutumia dahalia za Chuo kwa usalama wao

na mali zao pamoja na kukipatia Chuo mapato.

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar hutoa asilimia tofauti ya fedha kwa fani

moja. Kwa mfano; kijana aliyeomba kusoma fani ya Teknohama na Uhasibu

(Computer with Accounting) ambaye amejiunga na Chuo cha Zanzibar basi hulipwa

asilimia ndogo ukilinganisha na kijana aliyeomba fani hiyo hiyo katika Chuo cha

Tanzania Bara. Jambo hili hupelekea vijana wengi wa Kizanzibari kuomba Vyuo vya

Tanzania Bara ili wapate fedha nzuri na kuvikosesha nafasi Vyuo vya Zanzibar.

Kutokana na changamoto hiyo Kamati ya PAC inaishauri Bodi hii kulifikiria kwa

makini suala hili ili Vyuo vya Zanzibar viweze kudahili wanafunzi kwa mujibu wa

uwezo wao na hatimae kupata mapato ambayo yatachochea kufikia malengo

waliyoyakusudia.

Kwa kuwa Chuo hiki kinadaiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF)

kutokana na ujenzi uliofanyika, na kwa kuwa Chuo hakina uwezo wa kulipa deni

hilo, Kamati ya PAC inaishauri Serikali kulilipa deni hilo ili Chuo kiweze kutekeleza

shughuli zake ipasavyo.

9.19 CHUO CHA MAENDELEO YA UTALII

Hoja Namba 41.1 Taarifa ya Mapato na Matumizi kufuatia ufungaji wa Hesabu za

Mwisho wa Mwaka 2012/2013

Chuo kilikadiriwa kwa 2012/2013 kukusanya Tsh. 262,000,000 na makusanyo halisi

yalikuwa Tsh. 295,000,700, sawa na asilimia 113 ya makadirio. Aidha, kwa ajili ya

kuendesha shughuli za kawaida, Chuo kilikadiriwa kutumia Tsh. 420,000,000 na ulipotimia

mwaka wa fedha, Chuo kiliidhinishiwa na kutumia Tsh. 382,635,777 sawa na asilimia 91 ya

makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 37,364,223 sawa na asilimia 9 ya makadirio, ikiwa ni

upungufu wa Tsh. 37,364,223 sawa na asilimia 9 ya makadirio.

Majibu ya Chuo

Matumizi ya fedha hizo yalikusudiwa kuendelea kujenga uzio wa Chuo, ununuzi wa samani

na ujenzi wa vibanda vya kusomea. Pia kufundishia walimu katika ngazi ya shahada ya

kwanza na afisa katika ngazi ya shahada ya pili. Chuo vile vile kilijipanga kutumia fedha

hizo kwa kushiriki mikutano mbali mbali ndani na nje ya Zanzibar na kuonesha shughuli

mbali mbali zinazotolewa na Chuo kwa wanafunzi katika wilaya za Zanzibar.

Pamoja na malengo hayo, kutokana na kutopatikana kwa ukamilifu fedha hizo, Chuo

kimeendelea kukabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo, kushindwa kutayarisha sera mbali

mbali za Chuo, kama vile sera ya mafunzo na sera ya fedha. Aidha, kushindwa kutayarisha

kanuni zinazosimamia wafanya kazi, wanafunzi, fedha, mitihani na utumishi, kama vile pia

walivyoshindwa kufanya marekebisho ya maslahi kwa wafanyakazi yakiwemo mishahara.

Page 116: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

116

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji msaada wanaupata Chuo kutoka NAUFIC wakisaidiwa mafunzo na masomo

kupitia NACTE lakini fedha na msaada wanaoupata hawauoneshi katika bajeti yao. Pamoja

na Chuo kueleza kuwa fedha hizo zinatoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Kamati

imeeleza bado ipo haja ya kuoneshwa katika bajeti ya Chuo ili ziweze kufuatiliwa.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inakitaka Chuo kuonesha fedha na misaada wanayoipata kupitia NAUFIC na

NACTE, katika bajeti na hesabu zake za mwisho wa mwaka, ili iweze kutambuliwa na

kufanyiwa ukaguzi.

Uwezo wa Chuo kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na uwezo wa kujiendesha

Kwa mwaka wa 2012/2013, Chuo kilikuwa na mali za mpito zenye thamani ya Tsh.

315,048,240 na hawakuwa na dhima za mpito na kufanya uwezo halisi wa mali za mpito

kuwa na mali zenyewe, hali iliyochangiwa na kuwepo kwa wadaiwa na salio la benki.

Taarifa ya mapato ya Mamlaka kwa mwaka 2012/2013 yalikuwa ni Tsh. 839,993,714 na

matumizi yalifikia Tsh. 796,871,499 hali iliyoifanya Mamlaka kuendeshwa kwa faida ya

Tsh. 43,122,215 na kuonesha kuwepo uwezekano wa kuongezeka kwa faida iwapo Chuo

kitaongeza juhudi ya kusimamia vyanzo vyake vya mapato na kupunguza gharama za

uedeshaji.

Majibu ya Chuo

Pamoja na maelezo ya ukaguzi, Chuo kinataraji kuongezeka kwa gharama za matumizi yake

kutokana na wanahitajika kutumia fedha kwa matumizi na kudumisha jengo lao walilonalo

sasa ambalo wamefunga huduma mbali mbali ikiwa ni pamoja na intaneti kuvutia

ukodishwaji na watu wanaokodi waweze kutumia intaneti. Aidha, Chuo kinakabiliwa na deni

la huduma ya umeme kutoka Shirika la Umeme.

Kuhusiana na uwezo wa kujiendesha utaongezeka iwapo kitapokea tenda za „catering‟

kutoka taasisi mbali mbali za Serikali, jambo ambalo hivi sasa wamelikosa khasa kutoka

Baraza la Mapinduzi ambapo hapo awali walikuwa wanatoa huduma kwao.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati pamoja na majibu ya Chuo imejiridhisha kuwa, Chuo kinatakiwa kuongeza juhudi ya

kukusanya malipo ya madeni yake inayowadai wanafunzi mbali mbali waliosoma Chuoni

hapo ambao bado wanadaiwa.

Kamati imesikitishwa na taarifa kuwa Baraza la Mapinduzi limekatisha huduma yake ya

vyakula na viburidhaji kutoka Chuoni hapo wakati ni njia moja ya taasisi moja ya Serikali

kuisaidia nyengine.

Mapendekezo ya Kamati

Chuo kinatakiwa kuendelea kuchukua juhudi za kudai madeni yake inayowadai wanafunzi

mbali mbali waliosoma na ambao hawajalipa madeni yao. Aidha, Kamati inaitaka Baraza la

Mapinduzi na taasisi za Serikali kwa ujumla kuzingatia sana kupatiwa huduma za „catering‟

kutoka Chuoni hapo.

9.20 BENKI YA WATU WA ZANZIBAR (P.B.Z)

Hoja Namba 49.1 Uwezo wa Benki kumudu kulipa dhima zake za muda mfupi na

Uwezo wa kujiendesha

Page 117: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

117

Mali za mpito za thamani ya Tsh. 257,538,000,000 na dhima za mpito za thamani ya Tsh.

260,074,000,000 hufanya hali halisi ya mali za mpito kwa Benki kuwa Tsh. 2,536,000,000

kwa mwaka 2012/2013, ambayo ni sawa na uwezo wa reshio‟ ya 0.990:1.

Mapato ya Benki yalikuwa Tsh. 28,224,473,000 na matumizi yake yalikuwa Tsh.

23,293,494,000 na hivyo kuendeshwa kwa bakaa la Tsh. 4,930,979,000. Aidha, mwenendo

wa hesabu hizo unaonesha kuwepo kwa uwezekano wa kuongezeka kwa faida iwapo Benki

itaendelea kuimarisha huduma na kupunguza gharama za uendeshaji.

Majibu ya Benki

Uongozi wa Benki hauna shaka na takwimu zilizotumika, lakini kutokana na mifumo ya

kihesabu ya kibenki, hakuna taarifa inayoelezea hali halisi ya uwiano wa mali za mpito

(current assets) na dhima za mpito (current liabilities). Kwa hivyo, ni vigumu kutoa uwiano

wa ukwasi (current ratio). Hali inayothibitisha kuwa, mtindo wa uwasilishwaji wa mahesabu

ya kibenki ni tofauti na mtindo unaotumika kuwasilisha mahesabu yasiyokuwa ya kibenki.

Kwa hivyo kuanisha uchambuzi wa mahesabu ya mitindo tofauti isingelikuwa sahihi.

Uongozi wa Benki unapendekeza kuwa, ingekuwa ni vyema kufanya uchambuzi wa

mahesabu ya kibenki katika kupima (liquidity) kwa kutotumia uwiano wa ukwasi (current

ratio) kwa sababu, vipo vigezo maalum vinavyopima ukwasi katika mabenki. Aidha,

mabenki hupimwa kwa namna mbili kuu; mali zenye ukwasi wa haraka (liquid assets) dhidi

ya jumla ya mali zote za taasisi (Total assets). Na aina ya pili mali zenye ukwasi zilizopo

(Available Liquid assets) dhidi ya dhima zitazohitajika kulipwa wakati wowote (Demand

liabilities).

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imepokea maelekezo ya Benki na imekuwa elimu kubwa kwa Kamati. Baada ya

maelezo yao, Kamati ilimtaka Afisa Mkaguzi anaefuatana na Kamati kutoa maelezo yoyote

kuhusiana na ripoti ya Afisi yake na usahihi wa maelekezo ya Benki, ambae alikubaliana

kuwa maelezo hayo ya Benki ni sahihi na yeye atayachukua na kuyawasilisha Afisini kwake.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kuongeza uelewa na

ufahamu wa namna ya mabenki yanavyofunga hesabu zao na vipimo vya mali na dhima za

mpito za mabenki husika.

Tawi la Dar es Salaam

Kwa mwaka 2012/2013, Benki haikuwa na hoja yoyote katika ripoti za Mkaguzi na Mdhibiti

Mkuu wa Hesabu, lakini kwa kuzingatia mamlaka ya Kamati ya kuchunguza kwa namna

yoyote inayoona inafaa hesabu zote za Serikali na taasisi zake, Kamati imetembelea Benki

ya Watu wa Zanzibar, Tawi la Dar es Salaam na kupata ufafanuzi wa masuala mbali mbali

kuhusiana na utekelezaji wa majukumu ya Benki.

Kama ilivyoripotiwa katika ripoti zilizopita za Kamati, Benki imefungua matawi mawili Dar

es Salaam tokea mwaka 2011. Tawi liliopo Kariakoo kati ya mtaa wa Mkunguni na Swahili

linatoa huduma za kawaida za kibenki na jengine liliopo mtaa wa Lumumba na Mahiwa

hutoa huduma za Kiislamu. Uanziswaji wa matawi haya ni miongoni mwa malengo

yaliyomo kwenye Mpango Mkakati wa Kibiashara (Business Plan) wa Benki 2008-2011.

Madhumuni ya kufungua matawi hayo ni kuingia ushindani wa soko dogo la wateja na

Benki, kuwafuata wateja wake waliopo na wanaokuja Tanzania bara kibiashara, kikazi,

kimasomo na wanaopita ambao huhitaji huduma za Benki, kutanua wigo wa wateja wa

Tanzania bara na kuongeza „market share‟ na kutimiza malengo ya kutoa huduma bora kwa

wananchi wote.

Page 118: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

118

Matawi haya yana wafanyakazi 30, 16 ni wa tawi linalotoa huduma za kawaida za kibenki na

14 wa tawi linalotoa huduma za Kiislamu. Miongoni mwao, wafanyakazi 16 ni wanaume na

14 ni wanawake. Pia Benki imeajiri kampuni za kutoa huduma za usafi, ulinzi, askari jeshi la

Polisi na kampuni ya kuchukua na kupeleka fedha. Aidha, Benki inaendelea na kukabiliana

na changamoto iliyopo kwa wananchi walio wengi juu ya kuzifahamu huduma za Kiislamu

zinazotolewa na Benki.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imepongeza juhudi za Benki na kufarajika kuelezwa kuwa, tawi la huduma za

Kiislamu limejipanga na tayari limeshaanzisha kutoa mikopo kwa wanafunzi mbali mbali

wanaojiunga na Vyuo Vikuu nchini. Kamati imehoji utanuzi kama huu wa matawi mbali

mbali ya Benki Tanzania bara na kuelezwa kuwa, Benki imejipanga kuongeza matawi yake

katika mikoa mbali mbali ya Tanzania bara, ikiwa ni pamoja na Mwanza na Arusha.

Kamati imesikitishwa na huduma za ulinzi zinazotolewa na Jeshi la Polisi kwani pamoja na

kulipwa na Benki na pamoja na askari wanaokuwa lindo usiku kugaiwa fedha kama motisha,

baadhi ya askari hao wamekuwa na tabia ya kukimbia kulinda na kumwacha askari mmoja

peke yake masaa 24 na siku nyengine hawaji kabisa, hali ambayo inahatarisha usalama wa

benki.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inautaka Uongozi wa Benki kukaa tena pamoja na Mkuu wa Polisi kwa ajili ya

kuzungumzia tena suala la huduma zao za ulinzi wanazozitoa kwa Benki. Aidha, Benki

iongeze juhudi katika kutekeleza mipango yake, ili kujiongezea mafanikio.

RIPOTI YA UKAGUZI YAKINIFU KWA MIRADI NA MAENDELEO YA

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012

10.0 WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI

Hoja Namba 10.1 Mradi wa Mpango wa Kuendeleza Huduma za Kilimo

(Agricultural Service Support Program-ASSP)

Mradi huu wa kuendeleza Huduma za Kilimo (Agricultural Service Support Program-

ASSP)ni mradi unaotoa huduma kwa wananchi, uliofadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, Mkopo kutoka Shirika la Kimataifa (IFAD) pamoja na nguvu za wananchi.

Malengo yake ni kuimarisha upatikanaji na utumiaji wa elimu na maendeleo ya kilimo kwa

wananchi wa vijijini pamoja na kushajiisha upatikanaji wa akiba ya chakula na kuongeza

pato la wananchi.

Mradi uliidhinishiwa kutumia Tsh. 805,845,452 lakini fedha zilizoingizwa na kutumika ni

Tsh. 680,354,274.92 sawa na wastani wa asilimia 84, hali inayoonesha upungufu wa

Tsh.125, 491,177.08, sawa na asilimia 16 ya makadirio.

Ukaguzi unashauri kuharakishwa uingizwaji wa fedha na utekelezwaji wa malengo

yaliyopangwa ili kuepuka uwezekano wa kuongezeka gharama kwa baadhi ya shughuli na

manunuzi ya vifaa vilivyokusudiwa.

Maelezo ya Wizara

Wizara inakiri mapungufu hayo ya fedha, lakini yametokana na wafadhili wa mradi

kutoingiza fedha kwa ukamilifu na kwa wakati, ikiwa ni pamoja na IFAD na Serikali. Hata

hivyo, Wizara inachukua juhudi za kuondosha kasoro nyengine za utekelezaji wa mradi huu

kwa ujumla, ili kusiwe na upungufu wowote.

Page 119: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

119

Uchunguzi wa Kamati

Kwa muda mrefu hoja hii hujirejea katika ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

na kwa ujumla majibu yanayojibiwa yanakuwa ya jumla jumla. Aidha, hata ripoti za ukaguzi

hazitoi ufafanuzi mkubwa na wa wazi kuhusiana na hoja hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Wizara kutoa majibu ya kina kuhusiana na hoja hii, ili iweze kufanyiwa

kazi na Kamati. aidha, Kamati inamshauri Mkaguzi kuendelea kufuatilia hoja hii kwa undani

na taarifa zake ziwe wazi na kufahamika, hasa katika maeneo yenye kasoro, ili kuwe na

wepesi wa ufuatiliaji wake.

Hoja Namba 10.2 Kuhusiana na Mpango wa Kuendeleza Huduma Sekta ya Ufugaji

(Agricultural Support Development Program-Livestock/ASDP-L)

Mradi huu wa kuendeleza Huduma sekta ya ufugaji ni mradi unaotoa huduma kwa wananchi,

uliofadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mkopo kutoka Shirika la Kimataifa

(IFAD) pamoja na nguvu za wananchi.

Malengo yake ni kuimarisha uwezo na kipato cha wafugaji wadogo wadogo; Kushajiisha

upatikanaji wa huduma za maendeleo kwa wafugaji wadogo wadogo na Kuimarisha

miundombinu ya masoko kwa wafugaji wadogo wadogo.

Kwa mwaka 2011/2012 mradi huu ulikadiriwa kupokea Tsh. 1,190,272,666 na fedha halisi

zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 1,393,833,583 sawa na wastani asilimia 117 ya makadirio,

ikiwa ni ongezeko la Tsh. 203,560,917 ya makadirio.

Maelezo ya Wizara

Wizara inakiri mapungufu hayo ya fedha, lakini yametokana na wafadhili wa mradi

kutoingiza fedha kwa ukamilifu na kwa wakati, ikiwa ni pamoja na IFAD na Serikali. Hata

hivyo, Wizara inachukua juhudi za kuondosha kasoro nyengine za utekelezaji wa mradi huu

kwa ujumla, ili kusiwe na upungufu wowote.

Uchunguzi wa Kamati

Kwa muda mrefu hoja hii hujirejea katika ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

na kwa ujumla majibu yanayojibiwa yanakuwa ya jumla jumla. Aidha, hata ripoti za ukaguzi

hazitoi ufafanuzi mkubwa na wa wazi kuhusiana na hoja hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Wizara kutoa majibu ya kina kuhusiana na hoja hii, ili iweze kufanyiwa

kazi na Kamati. aidha, Kamati inamshauri Mkaguzi kuendelea kufuatilia hoja hii kwa undani

na taarifa zake ziwe wazi na kufahamika, hasa katika maeneo yenye kasoro, ili kuwe na

wepesi wa ufuatiliaji wake.

10.1 WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Hoja Namba 11.2 Mradi wa ukarabati wa jengo la Beit el Ajaib, Zanzibar.

Mradi huu ulifandhiliwa na MACEMP na ulianza tarehe 16 Septemba 2010, ambapo Serikali

ilitiliana mkataba na Lucky Construction Ltd, ya Dar es Salaam, mkataba wenye namba

DFMRZ/MACEMP/CW/REH.2/10 na thamani ya mradi huo hadi unakamilika ni Tsh.

249,409,400. Aidha, Tsh. 83,202,633 zimetumika katika mwaka huu wa fedha na ukaguzi

umebaini kasoro ya kukosekana ubora wa ukarabati wa jengo hilo, ukilinganisha na fedha

zilizotumika. Vile vile, ukaguzi umebaini kasoro zifuatazo:

Page 120: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

120

Mkataba kushindwa kuonesha na kuthibitisha tarehe ya kuanza na kumalizika kwa

ujenzi huo.

Sehemu ya jengo bado haijakamilika kulingana na hati ya makisio ya ujenzi (BOQ),

hivyo kupelekea maji ya mvua kuingia ndani.

Utiaji wa umeme haujakamilika na kupelekea maharibiko makubwa katika baadhi ya

sehemu za ndani ya jumba hilo.

Baadhi ya sehemu zilizojengwa tayari zimeshaanguka chini.

Kengele ya usalama (security alarm) yenye thamani ya Tsh. 5,000,000 haijafungwa.

Taa za dharura zenye thamani ya Tsh. 500,000,000 bado hazijafungwa.

Power Generator 3 phase 380/50 KV na vifaa vyake vyenye thamani ya Tsh.

35,000,000 bado hazijafungwa.

Majibu ya Wizara

Wizara haikubaliani na maelezo ya ukaguzi na usahihi wa majibu ya hoja hii ni kuwa,

Mkataba uliofungwa unaonesha tarehe na maelezo ya kuanza na kumalizika ujenzi kama

inavyooneshwa katika mkataba husika. Na kuhusiana na kutokamilika kwa jengo kulingana

na makisio ya ujenzi (BOQ) na kupekeleka kukosekana baadhi ya athari, hii inatokana

kwamba, wakati wa ukaguzi, Mkandarasi basdo alikuwa anaendelea na kazi. Hata hivyo,

kazi hiyo ilisitishwa bada ya kuporomoka sehemu ya nyuma ya jengo hilo, na kupelekea

masuala yaliyobaki ya ujenzi kusitishwa pamoja na malipo yaliyobaki ya Tsh. 166,197,767

kama ripoti ya Mshauri Mwelekezi inavyoonesha.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati ilihoji juu ya taratibu za manunuzi kwa kuhoji namna alivyopatikana Mshauri

Elekezi na Mkandarasi wa ujenzi na kujiridhisha kuwa, Wizara ilitangaza zabuni tarehe

11/06/2010 na 12/06/2010 na kampuni 3 ziliingia katika zabuni hiyo ambapo Kampuni ya

Lucky ndio iliyopewa kazi hiyo. Na kwa upande wa Mshauri Elekezi walitoa zabuni kama

Mshauri Elekezi binafsi. Kuhusiana na hali halisi ya jengo hilo, Kamati ilijiridhisha kuwa

tayari liliporomoka, na Mamlaka ya Mji Mkongwe ilitoa taarifa ya kusitishwa kwa ukarabati

wake, huku Tsh. 83,202,633 tayari zilikwishalipwa kwa Mjenzi na tayari ameshazitumia kwa

ukarabati uliofanyika.

Kamati imejiridhisha kuwa Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 16/09/2010 na ujenzi

ulitakiwa uanze baada ya wiki mbili kutokea kusainiwa kwa mkataba na mkataba huo huo

unaonesha ujenzi ungelimalizika baada ya miezi 10 ya kuanza kwa ujenzi na jengo hilo

liliporomoka tarehe 1/12/2012, hali hii iliithibitishia Kamati kuwa, jengo liliporomoka muda

mrefu baada ya ujenzi, kinyume na Mkataba ulivyoelekeza.

Kamati pia ilijiridhisha kuwa, Mshauri Elekezi alitoa taarifa yake kwa Wizara kuhusiana na

hali hiyo, na Kamati iliarifiwa kuwepo kwa ripoti ya hali ya jengo kabla ya kufanyiwa

ukarabati, lakini Kamati haikuweza kupatiwa kwa kuelezwa kuwa haikuwepo wakati kikao

kinafanyika. Hata hivyo, Kamati imeelezwa kuwa Mradi huu ulikuwa na wadau sita wa

Taasisi za Serikali ikiwa ni pamoja na Wizara yenyewe, Tawala za Mikoa, Mamlaka ya Mji

Mkongwe, Wizara inayoshughulikia Utalii, Wizara inayoshughulikia mambo ya kale na

Idara yenyewe ya Uvuvi. Aidha, ilielezwa kuwa, Idara hii ya Uvuvi ilikuwa inatekeleza

maagizo ya Wizara na taasisi hizo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuwa makini katika kufanya ukarabati wa majengo yake na zaidi

haya ya zamani. Hata hivyo, Kamati nayo imeridhika, pamoja na sababu zilizoelezwa kuwa,

ukarabati wa jengo hilo haulingani na fedha zilizotumika.

Page 121: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

121

RIPOTI YA UKAGUZI YAKINIFU KWA MIRADI NA MAENDELEO YA

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013

11.0 WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI

Hoja Namba 10.1 Mradi wa Mpango wa Kuendeleza Huduma za Kilimo

(Agricultural Service Support Program-ASSP)

Mradi huu wa kuendeleza Huduma za Kilimo (Agricultural Service Support Program-

ASSP)ni mradi unaotoa huduma kwa wananchi, uliofadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, Mkopo kutoka Shirika la Kimataifa (IFAD) pamoja na nguvu za wananchi.

Malengo yake ni kuimarisha upatikanaji na utumiaji wa elimu na maendeleo ya kilimo kwa

wananchi wa vijijini pamoja na kushajiisha upatikanaji wa akiba ya chakula na kuongeza

pato la wananchi.

Mradi uliidhinishiwa kutumia Tsh. 807,534,540 lakini fedha zilizoingizwa na kutumika ni

Tsh. 762,134,868.59 sawa na wastani wa asilimia 94, hali inayoonesha upungufu wa

Tsh.45,599,671.41 sawa na asilimia 6 ya makadirio.

Maelezo ya Wizara

Wizara inakiri mapungufu hayo ya fedha, lakini yametokana na wafadhili wa mradi

kutoingiza fedha kwa ukamilifu na kwa wakati, ikiwa ni pamoja na IFAD na Serikali. Hata

hivyo, Wizara inachukua juhudi za kuondosha kasoro nyengine za utekelezaji wa mradi huu

kwa ujumla, ili kusiwe na upungufu wowote.

Uchunguzi wa Kamati

Kwa muda mrefu hoja hii hujirejea katika ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

na kwa ujumla majibu yanayojibiwa yanakuwa ya jumla jumla. Aidha, hata ripoti za ukaguzi

hazitoi ufafanuzi mkubwa na wa wazi kuhusiana na hoja hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Wizara kutoa majibu ya kina kuhusiana na hoja hii, ili iweze kufanyiwa

kazi na Kamati. aidha, Kamati inamshauri Mkaguzi kuendelea kufuatilia hoja hii kwa undani

na taarifa zake ziwe wazi na kufahamika, hasa katika maeneo yenye kasoro, ili kuwe na

wepesi wa ufuatiliaji wake.

Hoja Namba 10.2 Kuhusiana na Mpango wa Kuendeleza Huduma Sekta ya Ufugaji

(Agricultural Support Development Program-Livestock/ASDP-L)

Mradi huu wa kuendeleza Huduma sekta ya ufugaji ni mradi unaotoa huduma kwa wananchi,

uliofadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mkopo kutoka Shirika la Kimataifa

(IFAD) pamoja na nguvu za wananchi.

Malengo yake ni kuimarisha uwezo na kipato cha wafugaji wadogo wadogo; Kushajiisha

upatikanaji wa huduma za maendeleo kwa wafugaji wadogo wadogo na Kuimarisha

miundombinu ya masoko kwa wafugaji wadogo wadogo.

Kwa mwaka 2012/2013 mradi huu ulikadiriwa kupokea Tsh. 1,354,441,157 na ilipofikia

mwisho wa mwaka, fedha zilizoingizwa ni Tsh. 1,311,145,526.15, sawa na asilimia 97 ya

makadirio, ikiwa ni pungufu ya Tsh. 43, 295,630.85 sawa na asilimia 3 ya makadirio.

Maelezo ya Wizara

Wizara inakiri mapungufu hayo ya fedha, lakini yametokana na wafadhili wa mradi

kutoingiza fedha kwa ukamilifu na kwa wakati, ikiwa ni pamoja na IFAD na Serikali. Hata

Page 122: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

122

hivyo, Wizara inachukua juhudi za kuondosha kasoro nyengine za utekelezaji wa mradi huu

kwa ujumla, ili kusiwe na upungufu wowote.

Uchunguzi wa Kamati

Kwa muda mrefu hoja hii hujirejea katika ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

na kwa ujumla majibu yanayojibiwa yanakuwa ya jumla jumla. Aidha, hata ripoti za ukaguzi

hazitoi ufafanuzi mkubwa na wa wazi kuhusiana na hoja hii.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Wizara kutoa majibu ya kina kuhusiana na hoja hii, ili iweze kufanyiwa

kazi na Kamati. aidha, Kamati inamshauri Mkaguzi kuendelea kufuatilia hoja hii kwa undani

na taarifa zake ziwe wazi na kufahamika, hasa katika maeneo yenye kasoro, ili kuwe na

wepesi wa ufuatiliaji wake.

11.1 WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Hoja Namba 11.1 Mradi wa Kuimarisha Miundombinu ya Mifugo

Kwa mwaka 2012/2013 Wizara ilikadiriwa Tsh. 200,000,000 kwa ajili ya utekelezaji wa

ujenzi wa chinjio jipya eneo la Kisakasaka. Hadi kufikia Juni 30, 2013, fedha zilizoingizwa

ni Tsh. 17,537,700, sawa na asilimia 9 ya makadirio.

Ukaguzi umebaini kuwa mradi huo haukuweza kutekelezwa kutokana na kutoingiziwa fedha

zilizokadiriwa kwa ajili ya ujenzi wa chinjio jipya katika eneo la Kisakasaka. Wakaguzi

walitembelea eneo hilo na kutoona ujenzi wowote uliofanyika. Pia, imebainika kuwepo kwa

matumizi yaliyofanyika kwa baadhi ya shughuli za ujenzi wa chinjio hilo kwa malipo ya

uchoraji wa ramani, malipo kwa Mshauri Mwelekezi (Consultant) na malipo ya ujenzi.

Majibu ya Wizara

Fedha halisi zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 16,527,700 na sio Tsh. 17,537,700 kama

ilivyoripotiwa na Mkaguzi. Kuhusiana na maelezo ya kushindwa kutekelezwa mradi huo

kutokana na kutoingizwa fedha ni sahihi, na Wizara ilimuajiri Mshauri Mwelekezi kwa ajili

ya michoro tu, ingawaje walianza kwa hatua ya upimaji na ufuatiliaji wake. kwa ujumla,

mradi haukuweza kutekelezwa kutokana na kutopatikana kwa fedha.

Uchunguzi wa Kamati

Pamoja na kutoingizwa kwa fedha hizo, Kamati imehoji iwapo Wizara ina hatimiliki ya eneo

hilo la mradi na kuelezwa kuwa waliandika barua kwenda Wizara ya Ardhi kwa ajili ya

malipo ya hatimiliki hiyo. Hata hivyo, Kamati ilipokagua hati za malipo hayo, ilijiridhisha

kuwa yamekosekana maombi ya mahitaji yake. Aidha, hati namba 9/11 na 26/11 yenye

thamani ya Tsh. 1,500,000/- haina risiti wakati fedha zimelipwa kwa Wizara ya Ardhi,

Makaazi, Maji na Nishati nayo ni taasisi ya Serikali, bila ya shaka lazima itoe risiti.

Vile vile hati namba 10/3 ya tarehe 15/1/2013 haina saini ya Afisa Masuuli wala maombi

maombi ya fedha hizo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuhakikisha inafuata ipasavyo Sheria katika matumizi ya fedha za

Serikali.

Page 123: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

123

Hoja Namba 11.2 Mradi wa kudhibiti maradhi ya kichaa cha mbwa (Rabies Control

Project)

Mradi huu ulianza rasmi Agosti 2005 na unafadhiliwa na Jumuiya ya Kimataifa ya

kuwalinda wanyama (World Society for the Protection of Animals-WSPA) ambayo makao

makuu yake yapo nchini Uiengereza. Jumuiya hiyo imejitolea kuufadhili mradi huu kwa

kugharamia matumizi yote yanayohitajika katika mradi huu kwa kushirikiana na Serikali.

Mradi huu unatarajiwa kumalizika Disemba 2016.

Lengo la mradi ni kudhibiti na hatimae kutokomeza kichaa cha mbwa kwa lengo la

kutokomeza maambukizi ya kichaa kwa binaadamu pamoja na kuongeza muamko kwa

wafugaji ili kujali afya za wanyama wao.

Kwa mwaka 2012/2013 mradi huu ulikadiriwa kupokea Tsh. 158,166,790 kutoka kwa

Washirika wa Maendeleo wa WSPA kwa lengo la kudhibiti maradhi ya kichaa cha mbwa na

ilipofikia mwisho wa mwaka, Tsh. 158,166,790 ziliingizwa na kutumika, sawa na asilimia

100 ya makadirio.

Aidha, kwa upande wa mchango wa Serikali, mradi huu ulikadiriwa kupokea Tsh.

80,000,000 na fedha halisi zilizoingizwa na kutumika ni Tsh. 13,000,000 sawa na asilimia 16

ya makadirio, ikiwa ni upungufu wa Tsh. 67,000,000 sawa na asilimia 84 ya makadirio.

Ukaguzi uliweza kutathmini hali halisi ya utekelezaji wa mradi huu kama ifuatavyo:

Namba Utekelezaji Idadi ya mbwa Idadi ya paka

1. Waliochanjwa 14731 3989

2. Waliofungwa uzazi 560 617

3. Waliopatiwa dawa za minyoo 5318 369

4. Waliotibiwa maradhi ya aina

mbali mbali

1454 320

5. Waliokingwa na kupe 2212 256

Jumla 24275 5551

Aidha, ukaguzi umebaini kasoro zifuatazo katika utekelezaji wa mradi huo:

Baadhi ya wananchi wengi hushindwa kuwadhibiti mbwa wao kwa ajili ya

kuwapeleka na kupata huduma za matibabu.

Mbwa wanaozurura ovyo hata inapotumika mitego kwa lengo la kuwadhibiti

inakuwa ni vigumu kupatikana.

Baadhi ya wafugaji bado hawajaona umuhimu wa kupeleka mbwa wao katika chanjo

kutokana na kukosa taaluma.

Majibu ya Wizara

Changomoto hizo zipo na zinasababishwa na sababu mbali mbali. Kwa mfano kuhusiana na

wananchi kushindwa kuwadhibiti mbwa wao, pamoja na sababu nyengine kunachangiwa na

kutofahamu wafugaji kwamba wao ndio wenye dhamana ya mbwa wao. Hivyo

wanalazimika kuwalisha, kuwapatia makaazi na huduma nyengine. Aidha, kuzurura kwa

mbwa kunatokana zaidi na wamiliki wao kushindwa kuwadhibiti na kuwapa huduma

zinazotakiwa.

Vile vile kuna dhana potofu kwa wafugaji wengi, kwa mfano wengi wao huamini kuwa,

mbwa wanapochanjwa ni kuwafunga uzazi wakati sio kweli. Hata hivyo, Wizara inaendelea

kuzikabili changamoto hizo kwa kuendelea kuwaelimisha wafugaji na wananchi wote kwa

ujumla.

Page 124: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

124

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji mradi huu kuwa ni wa mbwa katika asili yake, lakini pia umehusisha paka

na kuelezwa kuwa, wanyama haswa waliokusudiwa ni mbwa lakini na paka pia wanaingia

katika lengo moja. Hiyo ni kwa sababu, kichaa cha mbwa pia kinaambukizwa kwa wanyama

wengine, ikiwa ni pamoja na paka.

Aidha, Kamati imeitaka Wizara kutayarisha na kuwasilisha kwa Kamati fedha zilizotumika

kwa mbwa na paka na mambo yaliyoikwaza Wizara kufikia malengo kwa kukosa fedha

katika bajeti yao ya mradi huu. Hata hivyo, Kamati haijawasilisha kwa Kamati taarifa hizo.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kusimamia utekelezaji wa miradi kwa kufuata taratibu za Sheria na

kuheshimu maelekezo ya Kamati ya kukabidhi taarifa mbali mbali zinazohitajika na Kamati.

11.2 WIZARA YA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI-PEMBA

Hoja Namba 13.1 Kutochukuliwa hatua ya utekelezaji wa ukarabati wa nyumba za

Maendeleo-Wete

Jumla ya Tsh. 110,080,000 ziliingizwa kwa ajili ya ukarabati wa jumba namba 4 lilioko

Wete Mtemani,Pemba. Ukaguzi umebaini kwamba, fedha hizo zilizoingizwa zilitumika kwa

matumizi mengine badala ya kufanya ukarabati wa jengo hilo. Jengo hilo lilikusudiwa

kufanyiwa ukarabati tangu mwaka 2011/2012 na fedha za ukarabati huo ziliingizwa na

kutumika kwa matumizi mengineyo kama ilivyoripotiwa katika ripoti ya ukaguzi ya mwaka

2011/2012. Jengo hilo limeshaanza kuporomoka na kusababisha hatari kwa wanaoishi

pamoja na wapita njia.

Aidha, ukaguzi unashauri hatua muafaka zichukuliwe ili kumaliza tatizo hilo kwa

kuyakarabati majengo ambayo yapo katika katika hali mbaya.

Majibu ya Wizara

Fedha hizo Tsh. 110,080,000/- zilitengwa kwa ajili ya shughuli zote za Idara ya Nyumba

Pemba ikiwa ni pamoja na matengenezo ya nyumba zote za Serikali (Nyumba za maendeleo,

za vijiji na za kutaifishwa) kwa Pemba nzima. Aidha, fedha zilizopatikana ni Tsh.

62,881,644 na zimetumika kwa ukarabati wa nyumba za maendeleo Block No.5 iliyoko

Mtemani Wete, nyumba Namba T. 17B iliyoko Kilimatinde Chake, matengenezo ya makaro

na mitandao ya maji machafu katika nyumba za maendeleo Micheweni, Machomanne Chake

na Mkoani na matengenezo ya nyumba Namba T.67 iliyopo Tibirinzi Chake Chake.

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imejiridhisha kwamba, hoja hii tayari imesharipotiwa mwaka uliopita na Kamati

ilifanya tena ziara katika eneo hilo la Mtemani na kushudia hali mbaya ya uchakavu wa

majengo hayo, bila ya kufanyiwa ukarabati wowote, pamoja na kuwahi kuahidiwa na Wizara

kuwa yatafanyiwa marekebisho.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaendelea kuitaka Wizara kufanya marekebisho majengo hayo sambamba na

Kamati kuitaka Serikali iipe fedha Wizara ili iweze kuyakarabati majengo hayo.

Page 125: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

125

11.3 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI

Hoja Namba 12.1 Mradi wa uimarishaji wa elimu ya Lazima (Zanzibar Basic

Education Improvement Project (ZABEIP))

Mradi huu unaoshughulikia huduma za elimu kwa ajili ya maendeleo ya elimu Zanzibar,

umehusika na ujenzi wa Maskuli, kutoa huduma za maabara, huduma za maktaba na huduma

nyenginezo. Mradi ni wa miaka mitano (Juni 2008 hadi Juni 2013) na umeripotiwa na

Kamati tokea uanze kutolewa taarifa zake katika ripoti ya ukaguzi na kwa mwaka wa

2012/2013, ukaguzi uliendelea kuuzungumzia kuwa umeonesha mafanikio makubwa kwa

wastani wa asilimia 90 ya utekelezaji wake wa awamu ya mwisho na kwa hivyo,

umefanikiwa kwa kiasi kikubwa, kwani majengo mengi ya skuli za sekondari kwa Unguja na

Pemba yamekamilika na tayari yameshaanza kutumika kwa ajili ya kutoa huduma ya elimu

kwa wanafunzi wa sekondari, na hali halisi iliyooneshwa katika ripoti hiyo ni skuli za

sekondari za Kiembe Samaki, Mpendae, Faraja, Forodhani, Hamamni, Tumekuja, Fidel

Castro, Uweleni na Utaani.

Majibu ya Wizara

Ni kweli taarifa za ukaguzi kuhusiana na mradi huo, na kuhusiana na skuli tatu za Kombeni,

Paje Mtule na Paje, ambazo Kamati iliziripoti kuwa wakandarasi wake walikimbia mwaka

uliopita, tayari ujenzi wake umefikia asilimia 99. Ujenzi wa skuli hizo ulichelewa kutokana

na mkandarasi aliyeanza ujenzi wake (Electrics International Limited) kushindwa

kuzimaliza.

Wizara iliamua kukatisha mkataba wake na kazi iliyobakia kumalizwa na Wakandarasi

wengine watatu ambao ni; Zeccon Company Ltd (kwa Skuli ya Kombeni Sekondari) kwa

Tsh. 296,850,000/; Quality Builders Contractor (kwa Skuli ya Sekondari ya Tunguu) kwa

Tsh. 299,061,360 na Rans Company Litd (kwa skuli ya Sekondari ya Paje Mtule) kwa Tsh.

299,943,000/- na jumla ya fedha zilizotumika kwa ujenzi huo ni Tsh. 895,854,360/-

Aidha, fedha zote hizo zilitolewa na Serikali na zimelipwa mwezi Oktoba 2014. Kwa upande

wa skuli za Kombeni na Tunguu zimeanza kutumika mwezi Septemba 2014 na skuli ya Paje

Mtule imeanza kutumika mwezi Januari 2015. Jambo jengine la msingi ni kuwa, Mkandarasi

aliyeshindwa awali (Electrics International Limited), hakukubaliana na uamuzi wa

kumalizwa kazi iliyomshinda kwa kupewa makampuni mengine na hivyo, amepeleka kesi

Mahakamani ambayo mpaka sasa bado haijatolewa uamuzi na anadai kulipwa fedha

zilizobakia kukamilisha ujenzi, ambazo ni Tsh. 152,741,412.12/-

Uchunguzi wa Kamati

Kamati imehoji sababu zilizopelekea Wizara kushindwa kumpeleka Mahakamani

mkandarasi huyo Electrics International Limited, ambae kwa makusudi amevunja mkataba

walioingia nao na Kamati ililishauri hilo awali, na kuelezwa kuwa, suala hilo halikuwa

uamuzi wa Wizara moja kwa moja kwani ni Serikali ndiyo iliyowapa maagizo ya kukaa

pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kwa lengo la kufungua kesi dhidi ya Mkandarasi

huyo, lakini kabla ya kumaliza, ndipo waliposhtukia mkandarasi huyo alitangulia kufungua

kesi hiyo.

Kamati imehoji taratibu zilizotumika kuwapata wajenzi hao waliomaliza skuli hizo na

ikizingatiwa kuwa fedha zilizotumika ni nyingi na kuelezwa kuwa, Wizara imezingatia

uteuzi wa wakandarasi ambao tayari wameshafanyakazi nao katika maskuli mengine.

Page 126: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

126

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaitaka Wizara kuzingatia taratibu za Sheria inapofanya ujenzi na matumizi ya

fedha za Umma.

11.4 WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, UTALII NA MICHEZO

11.4.1 JENGO LA KAMISHENI YA UTALII PEMBA

Hoja Namba 14.2 Jengo la Kamisheni ya Utalii Pemba, kutofanyiwa matengenezo

kwa muda mrefu

Kamisheni ya Utalii Pemba inamiliki jengo lililonunuliwa kutoka kwa Ndg. Ali Abeid Nassir

kwa Tsh. 30,000,000 tangu mwaka 1992 kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Kamisheni ya Utalii,

Pemba. Ukaguzi umebaini kwamba, jengo hilo bado halijafanyiwa matengenezo yoyote kwa

kipindi kirefu tokea liliponunuliwa. Kutokana na kutofanyiwa matengenezo kwa muda

mrefu, Kamisheni inaendelea kukodi jengo kwa matumizi ya Ofisi kwa muda mrefu na

kutumia gharama kubwa.

Majibu ya Kamisheni

Ni kweli kwamba jengo hilo halijafanyiwa matengenezo tokea liliponunuliwa na Kamisheni

ya Utalii na bado Kamisheni inaendelea kukodi jengo tokea mwaka 1992. Hii ni kutokana na

kuwa Wizara ilikusudia kupata tathmini ya kitaalamu juu ya hali halisi ya jengo lilivyo kwa

vile msingi wake umeshakaa karibu miaka 20.

Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni pamoja na Kamisheni kuiandikia barua Wizara ya

Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati mnamo tarehe 31 Mei, 2012 ili kuomba kufanyiwa tathmini

jengo hilo liliopo Chachani. Hata hivyo, hakukuwa na majibu yoyote ya barua hiyo na

mnamo tarehe 23 Aprili, 2013 Kamisheni ya Utalii iliiandikia tena barua ya ukumbusho

Wizara hiyo na tarehe 27 Februari, 2014 Kamisheni ilipokea barua kutoka Wizara ya Ardhi,

Makaazi, Maji na Nishati inayotoa maelekezo na ushauri baada ya kufanywa ukaguzi wa

kitaalamu kuwa ni vyema jengo hilo livunjwe na kujengwa upya badala ya kuliendeleza.

Kutokana na ushauri na maelekezo hayo Kamisheni ya Utalii imeona ni vyema kutafuta M-

bia wa kulijenga jengo hilo kutokana na ugumu wa upatikanaji wa fedha kutoka Hazina na

hivi sasa juhudi za kutafuta M-bia huyo zinaendelea.

Uchunguzi na Mapendekezo ya Kamati

Kamati imeunga mkono ushauri na maelekezo yaliyotolewa na Wizara ya Ardhi, Makaazi,

Maji na Nishati. Hata hivyo, imesikitishwa na kitendo cha Wizara hiyo cha kuchukua muda

mrefu kutoa ushauri na maelekezo hayo.

Kwa mnasaba huo, Kamati ya PAC inaishauri Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati

kuchukua hatua za haraka pale inapopelekewa jambo kwa kuwa Wizara hii ndio Taasisi

pekee inayotegemewa na Serikali kutoa ushauri na maelekezo juu ya majengo yake.

Vile vile, Kamati hii imeridhika na maamuzi ya Kamisheni ya Utalii ya kuendelea kutafuta

M-bia wa kujenga jengo hilo. Hii ni kutokana na kuwa Kamisheni inazalisha mapato mengi

lakini fedha zote inazokusanya huwasilishwa kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina na hakuna

mgao wowote wanaoupata katika mapato hayo zaidi ya kupewa Ruzuku. Hivyo, ni vigumu

kwa Kamisheni kuweza kujenga jengo hilo kwa nguvu zake mwenyewe.

Page 127: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

127

11.4.2 UTUNZAJI NA UDHIBITI WA MAENEO YA KIHISTORIA (WIZARA YA

HABARI, UTAMADUNI, UTALII NA MICHEZO-PEMBA)

Hoja Namba 14.2 Utunzaji na Udhibiti wa Maeneo ya Kihistoria

Ukaguzi umebaini kuwa baadhi ya sehemu za kihistoria ambazo ni vivutio vya wageni wa

ndani na nje, utunzaji na udhibiti wa maeneo hayo hauridhishi. Baadhi ya maeneo

yaliyokaguliwa ni magofu ya Rasi Mkumbuu, magofu ya Mkamandume Pujini, magofu ya

Chwaka Tumbe na magofu ya Jambangome Wambaa.

Kukosekana kwa utunzaji na udhibiti wa maeneo hayo kunaweza kusababisha uvamizi

pamoja na uharibifu na matumizi mabaya katika maeneo hayo. Aidha, maeneo hayo

hayajawekewa alama za utambulisho na kuonesha kwamba ni maeneo ambayo yako katika

hifadhi za kihistoria. Hali hii inaweza kupelekea kukosekana kwa mapato yatokanayo na

wageni wanaotembelea maeneo hayo muhimu ya kihistoria.

Mkaguzi anashauri hatua muafaka zichukuliwe ili kunusuru maeneo hayo ya kihistoria kwa

kuyaendeleza, kuyafanyia matengenezo, kuyawekea alama za utambulisho na kuweka

wataalamu wa uhifadhi wa historia, walinzi na wahudumu kwa ajili ya kuhifadhi, kutoa

huduma pamoja na kutoa maelezo kwa wageni wa ndani na nje wanaotembelea maeneo

hayo.

Majibu ya Wizara

Mabango

Wizara na Kamisheni ya Utalii imekiri kuwa hali ya Mabango iliyopo hivi sasa hairidhishi,

hii ni kutokana na gharama kubwa za kuyashughulikia Mabango hayo ambapo bango moja

kubwa linagharimu Tsh. 350,000.00 na Bango dogo Tsh. 300,000.00 wakati Mabango yote

ni 50 ambayo yatagharimu Tsh. 17,000,000.00. Mabango hayo yanahitaji kila baada ya

mwaka mmoja kuandikwa tena upya kutokana na kuharibika kwa mvua na kuwa kjaribu na

bahari.

Walizidi kueleza kuwa katika kuhami hali hiyo Kamisheni ina mpango wa kutayarisha

Mabango mapya ambayo yatatumia saruji. Ujenzi wa Mabango hayo utagharimu Tsh.

40,000,000.00.

Utunzaji wa maeneo

Utunzaji wa maeneo ya Kihistoria ni suala muhimu ambalo linahitaji nyenzo za kutosha

katika kuyatunza na kuyashughulikia maeneo hayo. Kwa sasa Idara ina wafanyakazi saba tu

ambao ndio wanaohudumia maeneo hayo 45 ya Kihistoria yaliyopo Pemba. Idadi hiyo ya

wafanyakazi ni ndogo sana na haikidhi haja. Hata hivyo, jitihada za kuajiri wafanyakazi

wapya zinachukuliwa ambapo nafasi 10 zimeshaombwa Idara ya Utumishi Serikalini ili

kuziba upungufu huo.

Kutokana na kasoro hiyo wameeleza kuwa Idara inachukua juhudi za makusudi za kuyaweka

maeneo hayo katika hali ya usafi, isipokuwa kwamba juhudi hizo zinakabiliwa na

changamoto ya ukosefu wa fedha hivyo, kasi ya kuyafanyia matengenezo maeneo hayo sio

kubwa sana.

Alama za maeneo

Alama katika maeneo ya Kihistoria zinafahamika kwa kuwa maeneo yote mipaka yake

imetangazwa katika Gazeti Rasmi la Serikali. Baadhi ya alama hizo zimo kwenye maeneo

husika isipokuwa kwamba alama za maeneo mengine zimeondolewa na wananchi

wanaolima katika maeneo hayo.

Aidha, tayari wameshapeleka maombi ya kupatiwa hati miliki ingawa hadi hivi sasa hati hizo

hazijapatikana.

Page 128: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

128

Nyumba za Ofisi katika maeneo ya kihistoria

Nyumba zilizopo katika maeneo ya Kihistoria zilijengwa kwa msaada wa Mradi wa TASAF

na MACEMP ambapo zilikabidhiwa Kamati za Jamii zilizoundwa na TASAF. Baada ya

Mradi wa MACEMP kumaliza muda wake nyumba hizo zimekabidhiwa Wizara na wakati

Mdhibiti anafanya ukaguzi maeneo hayo, nyumba hizo zilikuwa bado zipo chini ya udhibiti

wa Kamati za Jamii. Kwa sasa Idara imeanza kuzisimamia nyumba hizo na kuziweka katika

hali ya usafi.

Panga la Watoro

Panga la Watoro bado lipo chini ya udhibiti wa Serikali na liko huru kwa wananchi na

wageni kwenda kuliona wakati wowote. Pango hilo lipo karibu sana na ufukwe wa bahari,

ambapo mipaka aliyopewa Mwekezaji wa Hoteli ya Manta mita 20 kutoka ufukwe wa bahari

haingiliani kabisa na eneo la pango hilo.

Aidha, kwa upande wa kusini kwa Mwekezaji huyo ipo njia maalum ya wapitao kwa miguu

wanaohitaji kwenda katika pango hilo bila ya kupita ndani ya Hoteli hiyo.

Uchunguzi wa Kamati

Katika kufuatilia hoja hii Kamati ya PAC imeunga mkono maelezo yaliyotolewa na Mdhibiti

na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kupitia Ripoti yake ya Ukaguzi Yakinifu. Hii ni

kutokana na kuwa Wizara na Idara inayohusika na masuala ya Hifadhi ya maeneo ya

kihistoria, imeshindwa kusimamia vyema maeneo ya kihistoria kwa ujumla na kupelekea

baadhi ya sehemu za kihistoria kuanza kutoweka kwa mfano; katika eneo la Mkamandume

kisima kimeanza kuporomoka, ngazi ambazo zilikuwa zinatumika katika eneo hilo

zimejifukia, msikiti upo kwenye eneo la shamba la mtu binafsi nakadhalika.

Aidha, Kamati pia ilisikitika kwa taarifa kwamba, mmiliki wa hoteli iliyo karibu na pango la

Watoro, Kigomasha analitumia pango hilo kama sehemu yake na kujipatia makusanyo ya

fedha kwa wageni wanaofika hotelini hapo, lakini yote haya ni kwa sababu Wizara

imeshindwa kuyashughulikia maeneo hayo ya kihistoria.

Mapendekezo ya Kamati

Kamati inaishauri Serikali kuiwezesha kifedha Wizara ili iweze kuyatunza maeneo ya

kihistoria.

Wizara ifanye juhudi ambazo zipo katika uwezo wake katika kuhakikisha maeneo

hayo yanalindwa na kuhifadhiwa, ili iwe rahisi kuyaimarisha mara tu watakapopata

fedha.

SEHEMU YA TATU

HITIMISHO

Sehemu hii ya Ripoti inahusiana na Maoni ya Kamati na Mapendekezo yake kwa Baraza la

Wawakilishi, ili iiagize Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kutekeleza yale yote ambayo

Kamati imeyapendekeza. Kwa ujumla, Ripoti yetu inatofautiana sana na ripoti za Kawaida

za Kamati za Kudumu za Baraza la Wawakilishi. Kwa Kamati hizo inakuwa rahisi sana

kupendekeza Mapendekezo yote ya Kamati katika sehemu moja, lakini kwa kuwa Kamati ya

P.A.C inachunguza hoja moja baada ya moja inayotokana na Ripoti ya Mdhibiti na

Mkauguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, inakuwa kwa namna yoyote ile, lazima

mapendekezo ya Kamati yawe katika baada ya ufafanuzi wa Hoja husika.

Page 129: RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU …2. Ndg. Othman Ali Haji - Katibu 3. Ndg. Asha Foum Makame - Afisa Sera, Wizara ya Fedha. 4. Ndg. Hurina Said Mohamed - Afisa Bajeti,

129

Hii ina maana kwamba, katika ripoti hii tumeeleza vitu vinne kwa takriban kila hoja. Jambo

la kwanza tumeitaja Hoja yenyewe na kutoa maelezo yake kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

wa Hesabu alivyofanya katika Ripoti zake ; jambo la pili tulieleza maelezo ya Wizara.

Sehemu hii inamaanisha majibu yote ya Wizara iliyojibu mbele ya Kamati kuhusiana na

Hoja ya Mdhibiti. Maelezo ya tatu ni Uchunguzi wa Kamati. Sehemu hii inahusiana na

uchambuzi na ufafanuzi wa Kamati kuifafanua hoja ya Mdhibiti kwa namna ilivyokuwa

inaifanyia kazi na kwa kuzingatia uchunguzi wake mbele ya Taasisi husika ; na maelezo ya

mwisho ni Mapendekezo ya Kamati. Hapa panahusiana na maagizo na mapendekezo ya

Kamati kuhusiana na hoja ya Mdhibiti na Majibu yaliyotolewa na Taasisi husika.

Hivyo basi, katika kuifanyia kazi ripoti hii, mapendekezo ya Kamati yote yanapatikana

katika ripoti yenyewe na katika sehemu hii ya tatu ya Hitimisho, Kamati inaliomba Baraza la

Wawakilishi, iiagize Serikali kutekeleza maoni yote ya Kamati kama yalivyo katika ripoti

hii.

Baada ya maelezo hayo, Kamati inapenda kutoa shukurani za dhati kwa Wizara, Mashirika

na Taasisi zote za Serikali kwa mashikiano makubwa waliyoyaonesha wakati wote wa kazi

za Kamati. Shukurani pia ziwafikie Watendaji wote wa Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

wa Hesabu kwa mashirkiano mazuri waliyoipa Kamati wakati wote, aidha Kamati inatoa

shukurani za pekee kwa Afisi hii ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, Ofisi ya Rais,

Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo, Afisi ya Baraza la Wawakilishi, na Taasisi zote

zilizohusika kwa kuiandalia mafunzo kuhusu mada mbali mbali yanayohusiana na

majukumu yake, kwa lengo la kuiwezesha kutekeleza vyema majuku hayo.