sisal smallholders farmers training
TRANSCRIPT
SOKO LA MKONGE
YUNUS A. MSSIKA and Laddy Swai**Laddy Swai; ARI-Mlingano, Box 5088, Tanga, TanzaniaMobile phone: +255754921876JULAI, 2012**
YALIYOMO
Utangulizi
Uzalishaji wa Singa
Hali ya Soko la Mkonge
Nini kifanyike?
Hitimisho
1.0 UTANGULIZIKilimo cha Mkonge kwa Wakulima wadogo ni moja ya mikakati ya Bodi ya Mkonge Tanzania katika kuhakikisha kuwa umiliki wa Sekta hii unakuwa mikononi mwa wa Tanzania walio wengi.
Utekelezaji wake unazingatia sera na mikakati
mbalimbali ya kitaifa na unalenga katika kuongeza uzalishaji na tija kwa Sekta ya Mkonge nchini na hivyo kupunguza umasikini.
2.0 UZALISHAJI MKONGE
Tangu enzi za ukoloni na baada ya uhuru na hata sasa,
uzalishaji na mauzo ya Mkonge nchini kwa kiasi kikubwa
umekuwa ukitegemea wakulima wakubwa.
Kwenye miaka ya 1960-70 Sekta ya Mkonge ilikuwa ni
mhimili muhimu wa uchumi wa Tanganyika na baadaye
Tanzania huru.
Katika kipindi hicho, Sekta ilikuwa ikichangia zaidi ya
65% ya uzalishaji na mauzo ya mazao ya biashara nje ya
nchi.
UZALISHAJI….
Mfumo wa kwanza wa kilimo cha Mkonge kwa
wakulima wadogo nchini ulianzishwa miaka ya
1960 baada ya Azimio la Arusha katika kijiji cha
Kabuku, wilaya ya Handeni.
Mfumo huu ulidumu hadi miaka ya 1980 na ukafa
kutokana na sababu mbalimbali kubwa ikiwa ni
wananchi kutoandaliwa na kushirikishwa
kikamilifu kulima Mkonge kupitia mfumo huu.
UZALISHAJI…..
Baada ya muda mrefu kupita, mfumo wa kilimo cha Mkonge
kwa wakulima wadogo nchini ulianzishwa tena mwaka
1,998.
Mfumo wa Kilimo cha wakulima wadogo nchini
umegawanyika katika makundi mawili; .i.e kilimo cha
Mkataba chini ya skimu ya SISO ( Sisal Smallholders and
Outgrowers) na wakulima nje ya SISO.
Kwa sasa kuna jumla ya wakulima wadogo 5,828 nchini.
3.0 HALI YA SOKOHali ya soko la Mkonge duniani ni nzuri kutokana na ongezeko kubwa la mahitaji ya singa za Mkonge duniani kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa mpya kama Composite na masuala ya mazingira.
Masoko ya Mkonge wa Tanzania ni Uchina, Saudi Arabia, Uingereza, Uhispania, Ujerumani,Nigeria, Kenya na Uganda.
Hata hivyo, uzalishaji wetu bado ni mdogo kuweza kukidhi mahitaji hayo ya soko.
Ongezeko hilo la mahitaji limesababisha kupanda kwa bei za madaraja ya singa za Mkonge kwenye soko la ndani na nje ya nchi. Mfano,bei ya singa za daraja la UG kwa sasa ni Dola1,400/tani ikilinganishwa na Dola 1,250/tani mwaka 2011.
HALI YA SOKO….
Bei za Mkonge katika soko la dunia hupangwa na
Umoja wa Wazalishaji wa Singa Ngumu Duniani
(Inter-Govermental Group on Hard Fibre) ambao
hukutana kila mwaka kujadili masuala mbalimbali
yahusuyo maendeleo ya singa ngumu.
Bei hizo hubadilika kutokana na hali ya soko la
dunia ilivyo kwa kipindi husika.
HALI YA SOKO….
Mahitaji ya Mkonge ndani ya nchi ni makubwa
ikilinganishwa na kiasi kinachozalishwa kwa sasa.
Hali hii imesababisha kupanda kwa bei ya Mkonge
kwenye soko la ndani ya nchi.
Mathalani Bei elekezi ya Mkonge wa daraja la UG
kwa sasa ni wastani wa Shilingi 1,900,000/tani.
Wanunuzi wakubwa wa singa kwa soko la ndani ni
viwanda vya kusokota kamba pamoja na makampuni
na wafanyabiashara mbalimbali.
4.0 NINI KIFANYIKE…….
Ili mkulima wa Mkonge aweza kunufaika na bei
hizo nzuri za singa, hana budi kufuata kanuni
bora za kilimo cha Mkonge zitakazomwezesha
kuzalisha singa za daraja bora.
Lengo liwe kupata singa za madaraja ya juu na
hivyo kupata mapato zaidi na hatimaye kuboresha
maisha yake.
5.0 CHANGAMOTO
Mitaji midogo
Uhaba wa Korona ndogo za kusindikia majani
Ukosefu kwa hati miliki kwa wakulima walio chini ya mfumo wa SISO
Uelewa mdogo wa mfumo wa ukadiriaji bei kwa kwa wakulima hususan walio chini ya mfumo wa SISO
Uhaba wa huduma za ugani kwa wakulima walio nje ya SISO
6.0 HITIMISHO
Mkonge ni zao lenye matumizi mengi, kwenye nyanja
mbalimbali kama katika kilimo, nishati, ujenzi, famasia,
magari, meli, ndege,majumbani, ofisini na mazingira.
Ni zao ambalo kwa sasa soko lake ni la uhakika na mwelekeo
unaonesha litendelea kuwa hivyo kwa muda mrefu ujao na
hivyo kumuhakikishia mkulima kipato cha uhakika na kwa
muda mrefu.
Umuhimu wa zao la Mkonge kwa maendeleo ya nchi hasa
maeneo ya vijijini, sasa na baadaye unapaswa kupewa
kipaumbele kwani zao la Mkonge lina sifa za kustahimili hata
kwenye maeneo ambayo mazao mengine hayawezi kustawi.
MKONGE KWENYE MAGARI
MKONGE KWA UJENZI WA NYUMBA BORA
KORONA NDOGO ILIYOBORESHWA
AHSANTENI KWA
KUNISIKILIZA