taarifa kwa vyombo vya habari zanzibar
TRANSCRIPT
-
7/23/2019 Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Zanzibar
1/3
30 Oktoba, 2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ndugu waandishi,tumewaita hapa ili kuzungumza nanyi juu ya jambo moja muhimu linalohusu nchi yetu.
Kama mnavyojua kuwa juzi tarehe 28 Oktoba, 2015 alikaririwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi BwanaJecha Salim Jecha kupitia vyombo vya Habari kuwa matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar
yamefutwa na kwamba kuna haja ya kufanyika Uchaguzi mwengine.
Ndugu Waandishi,Tamko hilo limekuja wakati Tume ikiwa inaendelea na zoezi la Kufanya Majumuisho ya
Kura za Urais na Jamii ya Wazanzibari na wadau wengine ndani na nje ya Nchi wakiwa wanasubiria
kutangazwa kwa Mshindi wa kiti cha Urais katika uchaguzi uliofanyika Tarehe 25 Oktoba. 2015. Katika
Tamko lake, Mwenyekiti alitoa sababu 9 zilizopelekea kuchelewa kwa utoaji wa Matokeo hayo na ambazo
ndio zilizomfanya Mwenyekiti Huyo kuufuta Uchaguzi huo.
Sisi, Kama Chama Cha Wanasheria Zanzibar tumefadhaishwa na uamuzi huo hasa kwa kuzingatia mamlaka
aliyonayo Mwenyekiti huyo kisheria katika kufikia Uamuzi kama huo. Chama cha Wanasheria kimepitia
kwa umakini Katiba ya Zanzibar ya 1984 na Sheria ya Uchaguzi Nambari 11 ya 1984 ili kujiridhisha kama
Mwenyekiti anao uwezo wa Kufuta matokeo ya Uchaguzi kama alivyoeleza kwenye tamko lake na kama
sababu zilizoelezwa zinakidhi kufutwakwaUchaguzi Nchi nzima.
Ndugu Waandishi,Kwa Mujibu wa Ibara ya 119 (1) ya Katiba ya Zanzibar ya 1984, Tume ni Mwenyekiti
pamoja na Wajumbe wengine Sita kama walivyoanishwa na ibara hiyo na kwamba maamuzi yoyote ya
Tume lazima yaungwe Mkono na wajumbe waliowengi. Taarifa iliyotolewa na wajumbe wawili wa Tume
Ndugu Nassor Khamis na Ndugu Ayoub Bakari kwa Waandishi wa Habari kuwa hakukuwa na kikao
chochote kilichokaa na kufikia maamuzi ya Kufuta Uchaguzi wa Zanzibar kauli ambayo haijapingwa mpaka
sasa na wajumbe wengine wa Tume, kinaleta taswira ya wazi kuwa Maamuzi hayo hayakuwa ya Tume balini ya Mtu mmoja ambaye ni Mwenyekiti, Hivyo kuyafanya kuwa ni Batili mbele ya macho ya Sheria.
Ndugu Waandishi, Kanuni ya 41(1) imeweka wazi utaratibu kufutwa kwa siku ya uchaguzi na kutangazwa
siku nyengine na namna uamuzi huo utakavyofikiwa na sio kufuta matokeo ya Uchaguzi au Uchaguzi
wenyewe. Ni kwa bahati mbaya sana Mwenyekiti katika Tamko lake hakueleza kama utaratibu umefatwa.
Huu ni ukiukwaji mkubwa wa Sheria.
-
7/23/2019 Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Zanzibar
2/3
Ndugu Waandishi,katika Tamko lake Mwenyekiti ameeleza kufuta matokeo yote ya Uchaguzi wa Zanzibar
jambo ambalo ni kinyume na Sheria na Katiba. Kwa mfano katika ngazi ya Majimbo kwa uchaguzi wa
Wajumbe wa Baraza la wawakilishi na Madiwani, Tume inawakilishwa na Msimamizi wa Uchaguzi ngazi
ya Wilaya ambae kwa Mujibu wa Sheria ndio mwenye mamlaka ya kutangaza Mshindi katika Uchaguzi
wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani na Kwa Mujibu wa Sheria Tume haina uwezo wala
Mamlaka ya kufuta matokeo yaliyokwisha tangazwa na ambapo mgombea ameshapewa shahada ya
kuchaguliwa. Wajibu wa Tume ni kuchapisha matokeo hayo kwenye gazeti la serikali kama kanuni ya 59
(4) na kifungu cha 88 (c) cha Sheria ya Uchaguzi vinavyoeleza na kama kuna Mgombea ambae hajaridhika
na matokeo au maamuzi ya Msimamizi wa Uchaguzi basi anatakiwa kwenda Mahakama Kuu kwa mujibu
wa kifungu cha 86 cha Sheria ya Uchaguzi na Ibara ya 72 (1) ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 ambayo ndio
yenye Mamlaka ya kufuta uchaguzi na matokeo yake kwa Mujibu.
Ndugu waandishi,athari ya Tamko la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar yanaweza kuiingiza Nchi
katika mgogoro wa Mkubwa wa Kikatiba katika maeneo yafuatayo:-
1.
Muda wa kushika madaraka yaUrais Kikatiba: Ibara ya 28 (2) ya Katiba ya Zanzibar ya 1984
inaeleza wazi kuwa Rais ataacha madaraka yake baada ya kumalizika miaka mitano kuanzia
tarehe alipokula kiapo cha uaminifu na kiapo cha kuwa Rais. Tafsiri yake yake nikuwatangu Rais
wa Zanzibar alipokula kiapo cha uaminifu na Kiapo cha kuwa Rais siku ya Tarehe 3 Novemba,
2010 atakuwa ametimiza miaka mitano siku ya Tarehe 3 Novemba, 2015. Hivyo akiendelea
kushikilia madaraka ya Urais zaidi ya Tarehe hiyo itakuwa kinyume na Katiba ya Nchi. Upo
mjadala katika jamii kuwa Rais anao uhalali wa kuendelea kuwa Rais chini ya Ibara ya 28 (1) (a).
Maoni ya Chama cha Wanasheria Zanzibar ni kuwa maudhui ya Ibara hiyo ni kumpa uwezo wa
Kikatiba Rais kuendelea ili kutoa nafasi ya maandalizi ya kula kiapo kwa Rais mpya(anaefuata) tu
na sio kuendelea kukaa madarakani bila ya kufanyika kwa Uchaguzi au kwa sababu ya Uchaguzi
kufutwa.
2.
Nchi kuendeshwa bila ya Baraza la Wawakilishi: Katika mazingira tuliyonayo ni wazi kuwa Nchi
itaendeshwa muda mrefu bila ya kuwepo kwa Baraza la Wawakilishi ambalo ni mhimili muhimu
katika uendeshaji wa Serikali. Katiba yetu imeruhusu hali ya kuendesha Nchi bila ya Baraza la
Wawakilishi kwa muda usiozidi siku tisini (90) tu kuanzia siku Baraza lilipovunjwa. Kwa mazingira
tuliyonayo, siku tisini (90) zinazokubalika kikatiba zinaishia tarehe 12 Novemba, 2015 kwa kuwa
Baraza la Wawakilishi lilivunjwa tarehe 13 Agosti, 2015.
3.
Hatari ya kuwa na Rais ambaye yuko juu ya Sheria na Katiba ya Nchi : Ibara ya 37 ya Katiba ya
Zanzibar ya 1984 inaipa Mamlaka Baraza la Wawakilishi kuondoa kinga ya Rais kutoshtakiwaanapokuwa madarakani kama inavyotolewa na Ibara ya 36 ya Katiba. Katika mazingira
tuliyonayo ambapo ifikapo tarehe 12 Novemba, 2015 ambapo Baraza la Wawakilishi
halitakuwepo na haliwezi kuitishwa kikatiba, ni wazi kuwa ikiwa Rais atafanya matendo yoyote
yenye kuvunja katiba ya Nchi na kukiuka Kiapo chake, hakutakuwa na Mamlaka nyengine yoyote
yenye uwezo wa kuhoji matendo ya Rais. Hii inatengeneza hatari ya kuwa na Serikali
inayoongozwa na Dikteta.
-
7/23/2019 Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Zanzibar
3/3
SULUHISHO:
Ndugu Waandishi,Chama cha Wanasheria Zanzibar kinaungana na wadau wengine wa ndani na nje ya
Nchi ya kutoa wito kwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar na wadau wengine kufanya yafuatayo:-
1.
Kufuta Tamko la Mwenyekiti wa Tume la kujaribu kufuta uchaguzi na matokeo ya uchaguzi Mkuu
wa Zanzibar kwa kuwa halina nguvu kisheria na linaweza kuhatarisha Amani ya nchi.
2.
Kuendelea kutoka pale ilipoishia katika kazi ya kufanya majumuisho ya Kura za Urais ili mshindi
halali wa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 apatikane na
kutangazwa kuwa Rais
3.
Rais aone haja ya kuunda Tume ya kumchunguza Mwenyekiti dhidi ya madai ya kushindwa
kufanya kazi zake na ikiwa madai hayo yakithibitika, basi amuondoe mara moja.
4.
Vyombo vya Dola vichunguze, wawakamate na hatimae kuwafikisha Mahakamani watu wote
waliohusika kumshinikiza Mwenyekiti kutoa tamko la kufuta uchaguzi na matokeo yake.
5.
Viongozi wote wa vyama vya siasa kujitathmini wajibu wao katika kuheshimu maamuzi ya
wananchi yanayofanywa kwa njia ya demokrasia ili kujenga misingi mizuri ya utawala bora.
MWISHO:
Ni matumaini ya Chama cha Wanasheria Zanzibar kuwa Rais wetu wa Zanzibar atangamua mtego huu
unaokusudia kumuweka katika Historia ya Rais wa Zanzibar aliewahi kuvunja Katiba ya Nchi na
kumuondolea rekodi nzuri aliyonayo ya kuheshimu sheria na Katiba ya Nchi na Utawala Bora.
AWADH ALI SAID
RAIS CHAMA CHA WANASHERIA ZANZIBAR