tathmini ya mafunzo ya sam ukerewe: kuanzia tarehe 3- 10 … · 2013-01-18 · stadi zao...

14
1 Tathmini ya Mafunzo ya SAM Ukerewe: Kuanzia tarehe 3- 10 Septemba 2012 Weka Alama ya √ (tick) katika mabano kwa kila swali hapo chini: Swali 1 Kwa ujumla umeyaonaje mafunzo haya? 1=Safi 2=Safi sana 3=Mbaya 4=Mbaya Sana Jedwali 1 Evaluation Response Total response % 1- Safi 5 14 35.7% 2- Safi Sana 9 14 64.3% 3-Mbaya 14 4- Mbaya Sana 14 Matokeo: Kwa upande wa maoni juu ya mafunzo haya asilimia 64.3 % ya washiriki wamesema mafunzo haya ni safi sana wakati 35.7% ya washiriki wote wamesema mafunzo haya ni safi.Hii inamaanisha kwamba mafunzo haya SAM yanaumuhimu mkubwa kwa jamii hususani katika kuwawezesha kufanya ufuatiliaji juu ya matumizi ya rasilimali za jamii katika utoaji huduma unaolenga kustawisha jamii. Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki: Mafunzo yametuongezea uelewa wa kutosha kuanza kuhoji,kufuatilia,na kuishawishi jamii iweze kuamka Mafunzo yamekwenda vizuri kutokana na kupangiliwa vyema na wawezeshaji wazuri Mafunzo yanasisimua nakutupa fursa ya ufuatiliaji Mafunzo ni mazuri sana kwani ni somo ambalo ni muhimu na tunaomba liwe endelevu Mafunzo ni mazuri kwani yamenijengea uwezo mkubwa katika mfumo wa ufuatiliaji wa uwajibikaji kwa jamii o Wawezeshaji walikuwa wanafundisha vizuri na walieleweka vizuri ,mada zilikuwa nzuri na za kuvutia ila mda wamafunzo ulikuwa mdogo sana Mafunzo ni mazuri sana kwa sababu tumeweza kujifunza mambo ya msingi ya haki za binadamu Mafunzo haya ni safi sana kwa sababu yanalenga upatikanaji wa haki za binadamu kwa kuzingatia uwezo wao katika jamii husika kuanzia ngazi ya chini kabisa.

Upload: others

Post on 08-Feb-2020

14 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

1

Tathmini ya Mafunzo ya SAM

Ukerewe: Kuanzia tarehe 3- 10 Septemba 2012

Weka Alama ya √ (tick) katika mabano kwa kila swali hapo chini:

Swali 1

Kwa ujumla umeyaonaje mafunzo haya? 1=Safi 2=Safi sana 3=Mbaya 4=Mbaya Sana

Jedwali 1

Evaluation Response Total response %

1- Safi 5 14 35.7%

2- Safi Sana 9 14 64.3%

3-Mbaya 14

4- Mbaya Sana 14

Matokeo: Kwa upande wa maoni juu ya mafunzo haya asilimia 64.3 % ya washiriki wamesema

mafunzo haya ni safi sana wakati 35.7% ya washiriki wote wamesema mafunzo haya ni safi.Hii

inamaanisha kwamba mafunzo haya SAM yanaumuhimu mkubwa kwa jamii hususani katika

kuwawezesha kufanya ufuatiliaji juu ya matumizi ya rasilimali za jamii katika utoaji huduma

unaolenga kustawisha jamii.

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Mafunzo yametuongezea uelewa wa kutosha kuanza kuhoji,kufuatilia,na kuishawishi jamii iweze

kuamka

Mafunzo yamekwenda vizuri kutokana na kupangiliwa vyema na wawezeshaji wazuri

Mafunzo yanasisimua nakutupa fursa ya ufuatiliaji

Mafunzo ni mazuri sana kwani ni somo ambalo ni muhimu na tunaomba liwe endelevu

Mafunzo ni mazuri kwani yamenijengea uwezo mkubwa katika mfumo wa ufuatiliaji wa

uwajibikaji kwa jamii

o Wawezeshaji walikuwa wanafundisha vizuri na walieleweka vizuri ,mada zilikuwa nzuri

na za kuvutia ila mda wamafunzo ulikuwa mdogo sana

Mafunzo ni mazuri sana kwa sababu tumeweza kujifunza mambo ya msingi ya haki za binadamu

Mafunzo haya ni safi sana kwa sababu yanalenga upatikanaji wa haki za binadamu kwa

kuzingatia uwezo wao katika jamii husika kuanzia ngazi ya chini kabisa.

2

Maada zilizotolewa zilikuwa zinalenga uhalisia wa uwajibikaji wa shughuli za umma,

wawezeshaji walikuwa na uwezo wa kutosha katika ufundishaji hata mifano iliyotolewa ilikaribia

na mazingira halisi.

Mafunzo haya ni mazuri kwasababu yanaelekeza jamii kutambua wajibu wake na wajibu wa

wasimamizi na watoa huduma ili kufikia lengo la kupata huduma bora zinazozingatia haki za

binadamu

Ni safi sana kwa sababu nimeelewa kuwa tatizo au kitu chochote kinavyoanza lazima kuanzia

kwa jamii kwanza ndo kuenda ngazi za juu

Kwa sababu yamenijengea uwezo wa uwajibikaji jamii kwa kuangalia haki za msingi za binadamu

ili zitimizwe lazima watoa huduma wazingatie uadilifu

Mafunzo haya yamenijengea uelewa wa mfumo wa uwajibikaji katika jamii

Swali 2

Je wawezeshaji walikuwa wanaeleweka wakati wa kufundisha? 1=Ndio Kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 2

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 9 14 64.3%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

5 14 35.7%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: Kwa upande wa uelewa kwa wawezeshaji 64.3% wamesema walikuwa na uelewa wa

kiwango kikubwa wakati 35.7% ya washiriki wamesema walikuwa na uelewa wa kiwango cha

kawaida

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Wawezeshaji walionyesha kutoa mafunzo walikuwa na uhakika na kile wanachokifundisha

Mpangilio wa mada na uwasilishaji, ufahamu wao mkubwa.

Wamekuwa waungwana na wanafuata mda na wanajali watu

Mwezeshaji ametoa mafunzo kwa umakini mzuri na amezingatia haki za msingi za binadamu

3

Walitumia mbinu mbalimbali kuhakikisha ninaelewa kinachowezeshwa i.e majadiliano na

kutumia mifano halisi

Walikuwa wanaweza kushirikisha wawezeshwaji kwa kiwango cha kutosha

Maelezo yao na ufafanuzi wao ulikuwa ni wa kina pia walitumia lugha rahisi

Kwa sababu wamefundisha na kuweza kuelewa japokuwa masomo yalikuwa mengi muda mfupi

Wadau wa mafunzo hawakuonyesha kuchoka pindi mafunzo yanatolewa

Mafunzo ni mazuri sana yalihitaji muda zaidi kwa muda huu wawezeshaji imewalazimu

kufukuzana na muda ili angalau mada zote zipitiwe hivyo wameeleweka kiasi

Mafunzo ni mazuri kwa maoni yangu mafunzo sikunyingine yaongezwe muda

Maana kila mada imefundishwa kwa vitendo na maelekezo ya kina zaidi

Kwa sababu tulienda nao sambamba bila kutuacha nyuma na walituelewesha pale ambapo

hatujui lakini kitu kingine tulibadilishana uzoefu

Swali 3

Je mifano iliyotumika ilikuwa na uhusiano na mada na ili saidia kuelewa mada? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 3.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 11 14 78.57%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

3 14 21.43%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: Kwa upande wa uhusiano wa mifano na mada 78.57% ya washiriki wamesema mifano

iliyotumika inauhusiano kwa kiwango kikubwa na mada zinazotolewa wakati 21.43% wamesema

inauhusiano kwa kiwango cha kawaida.

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Mifano ilifanya darasa kuchangia kwamapana zaidi

Nimefumbuka macho hasa hatua 5 zilizo ndani ya mfumo wa uwajibikaji wa jamii

Kabisaa yaani we acha tuu

4

Iliendana na mafunzo yenyewe

Mifano yote iliendana na mada na hali halisi kwa ujumla

Kwa mfano mihimili ya dola ,serikali,bunge,mahakama,baraza la madiwani

Kwa sababu ya uelewa zaidi tumeweza kujibu maswali yaliyokuwa yakitolewa ndani ya vikundi

na mmoja mmoja

Sababu ililenga jamii kwa mifano halisia

Mifano halisi ya Halmashauri za wilaya pamoja na vyombo vya usimamizi zililenga kabisa mada

husika

Ufafanuzi ulinisaidia sana baada ya kutoa aina za mifano

Ilikuwa ya kiwango, maana ilikuwa na uhalisia wa kile kilichoongelewa

Kwa sababu mifano iliyotumika ilionyesha jinsi gani mfumo wa uwajibikaji katika jamii

unavyoweza kuzingatia utoaji wa huduma bora kwa kuzingatia misingi ya kazi

Swali4

Mada zilizowasilishwa zinaeleweka kwa ufasaha? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 4.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 6 14 42.86%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

8 14 57.14%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: Kwa upande wa mada kueleweka kwa ufasaha 42.86% ya washiriki wamesema mada

zilieleweka kwa ufasaha kiwango kikubwa wakati 57.14% wamesema mada zilieleweka kwa kiwango

cha kawaida.

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Mada zilieleweka kwa kiwango kikubwa kwani washiriki walitoa mifano mingi iliyo hai.

Mfumo mzima umejidhihirisha siku hadi siku

5

Zinaeleweka

Zinaeleweka ila kuna maeneo mengine yanahitaji muda zaidi kwa hali halisi ya jamii na mifumo

iliyopo

Mada ni nyingi muda ni mfupi hivyo kunakuwepo na changamoto za kuweza kuyamasta kwa

ufasaha

Kwa sababu tulikuwa na uwezo wa kujibu na kutambua yaliyokuwa yanaelezwa

Kwasababu bado elimu hii inahitajika kwa walengwa zaidi mfano wanajamii madiwani na

watendaji.

Mada za taratibu/somo la kamati ya ugavi na mkaguzi wa ndani

Mada zinaeleweka isipokuwa muda wa mafunzo uongezwe kwa sababu ni mada zinazohitaji

kuelewa kwa upana zaidi hususan miongozo ya kisheria

Ndiyo kwa pale pasipoeleweka mifano ilitolewa mpaka mtu akaelewa

Nimeweza kuelewa wajibu wa kila utawala na mipaka yake na unawajibika kwa nani ili nini

kitokee

Kwa sababu mada zote zinaonyesha umuhimu wa kuwepo kwa mfumo wa uwajibikaji katika

jamii

Swali 5

Mbinu zilizotumika kuwasilisha mada zilikuwa muafaka? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 5.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 9 14 64.29%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

5 14 35.71%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: Kwa upande wa mbinu muafaka zilizotumika kufundisha 64.29% ya washiriki wamesema

mbinu muafaka zilitumika kwa kiwango kikubwa wakati 35.71% wamesema zilitumika kwa kiwango

cha kawaida

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

6

Mbinu zilizotumika zilieleweka Kwa urahisi kwa washiriki.

Stadi zao wawezeshaji, nyenzo za kufaa zilizo zingatia elimu ya mtu mzima “adult learning”

Kungekuwepo na video za kutosha.

Zimeniwezesha kuelewa zaidi somo lililokuwa linafundishwa

Waliweza kushirikisha na kutoa mfano hai hivyo ilikuwa ni rahisi kueleweka

Zilikuwa zikizingatia muda

Kwa sababu tumefundishwa na kuelewa mapungufu yaliyopo hasa usimamizi wa uadilifu.

Wawezeshaji wametumia lugha rahisi katika kuelekeza na katika kufafanua pia wametumia

mifano tete iliyo katika jamii zetu na kuelekeza namna ya kutatua au kufuatilia

Kwa sababu wawezeshaji waliweza kulisoma darasa /washiriki wanavyoielewa mada

Swali 6

Mada zilizowasilishwa zinauhusiano na hali halisi ya jamii yako? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 6.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 13 14 92.86%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

1 14 7.14%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: Kwa upande wa uhusiano wa mada na hali halisi ya jamii 92.86% ya washiriki wamesema

zinahusiana kwa kiwango kikubwa wakati 7.14% ya washiriki wamesema zihusiana kwa kiwango cha

kawaida

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Kuonyesha zinauhusiano washiriki walichangia wakati mwingine muda ulipungua.

Hakuna usimazi madhubuti wa mfumo wa uwajibikaji jamii iwe kijiji,kata na hata halmashauri

Saana tu.

Nilibaini kuwa hata sisi kama jamii tunapaswa kuwajibika na kukemea ubadhilifu

7

Mifumo ya utawala imesababisha uwajibikaji wa jamii kukosa nguvu hivyo yameakisi hali halisi

katika jamii zetu

Kwa mfano walipokuwa wanaulizana mafikiano kuhusu utendaji kazi wa halmashauri ni duni pia

wao walikiri kuwa bajeti imeandaliwa kwa lugha ngumu sana

Kwa sababu mambo muhimu yahusuyo jamii hayatekelezeki vizuri

Kwasababu mada zote zililenga kuitendea jamii haki ili kuweza kupata huduma bora

Kwa ujumla maada zilizotolewa zinaigusa jamii sehemu kubwa kwa upande wa viongozi

madiwani /wabunge na watendaji kwa pamoja

Kutokana na elimu hii kutokuwepo katika jamii mada hizi zimekuwa na uhusiano mkubwa mno

Usimamizi wa matumizi na rasilimali zinatumika ovyo na bila kujali kuwa mali ya wanajamii

wenyewe

Mada zilizowasilishwa kwenye jamii yangu zina uhusiano halisi .

Kwa kuzingatia mfumo wa ufuatiliaji na uwajibikaji ndo kutasababisha jamii ipate huduma iliyo

bora.

Swali 7

Wawezeshaji walikuwa na uelewa wa kile walichokuwa wanafundisha? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 7.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 12 14 85.71%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

2 14 14.29%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: Kwa upande wa uelewa wa wawezeshaji wa kile walichokuwa wanafundisha 85.71% ya

washiriki wamesema wanauelewa wa kiwango kikubwa wakati 14.29% wamesema wanauelewa wa

kiwango cha kawaida

8

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Kutotafuna maneno kutoa mifano ni ushahidi tosha kuwa na uelewa wa muwezeshaji.

Hakuna maelezo, wazuri, chamsingi walijitahidi sana “UWEZO WANAO”

Wanaeleweka wamesoma na kubobea vilivyo

Walikuwa makini pia waliheshimu wazo la kila mshiriki wa mafunzo

Walitoa ufafanuzi wakina kwa kila mada pia hawakuonyesha udhaifu katika kuwezesha

Waliweza kueleza vizuri na kueleweka kwa ufasaha

Mada zao zilieleweka vizuri sana na zililenga mahitaji ya jamii pia hata sisi tumeweza kujua

tufanye nini sasa baada ya mafunzo haya

Ndiyo kwa sababu mara kwa mara walikumbushia kuzingatia 3us ufafanuzi, uthibitisho na

uhalalisho

Wawezeshaji na mada zilizotolewa zinaweza kusema haya;walimu wa vyuo vikuu, maada pia

kwaajili ya watu wa diploma nk

Walijipanga kwa pamoja kwa kufundisha bila kutetereka

Walijiamini kutoa maelekezo pale walipokumbana na maswala tete (changamoto), walikuwa

wabunifu kwa kuibua mifano yenye utata nasi kuchangia kwa umakini zaidi.

Ndiyo kwasababu kile walichokuwa wanakifundisha wanauzoefunacho

Swali 8

Mafunzo haya yamekupa uelewa na dhana ya mfumo wa ufuatiliaji wa uwajibikaji wa kijamii na jinsi unavyofanya kazi? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 8.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 8 14 57.14%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

6 14 42.86%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

9

Matokeo: Kwa upande wa uelewa wa dhana ya mfumo wa ufuatiliaji wa uwajibikaji jamii na jinsi

unavyofanya kazi 57.14% ya washiriki wamesema wamepata uelewa kwa kiwango kikubwa wakati

42.86% ya washiriki wamesema wamepata uelewa kwa kiwango cha kawaida

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Kwa kiasi kikubwa

Nimegundua tofauti zilizopo kati ya mafunzo haya na niliyo tangulia kuyapata.

Katika sekta yangu mafunzo haya ni muafaka.

Nimepata ufahamu ya kuwa nina haki ya kufahamu na kusimamia rasilimali zetu.

Ndio kwani nina uwezo wa kupima mfumo wa uwajibikaji katika jamii yangu

Kwa sasa ninaweza kufuatisha taarifa za halmashauri /kijiji na kata yangu

Ninaweza kutambua niwajibikeje katika jamii

Mafunzo yameniwezesha kuelewa kwamba mfumo wa uwajibikaji uliopo hauzingatii haki za

binadamu ili kuweza kupata huduma bora

Kwa ufahamu nisawa lakini mifumo ya nchi bado haijaweka wazi sana uhuru wa kila raia kupewa

taarifa nyaraka.

Nitatumia 3us

Nilivyoelewa dhana nzima kama siku zingeongezeka uelewa wangu ungekuwa kwa asilimia

nyingi zaidi,lakini nimeelewa japo si kwa asilimia zote

Kwa sababu elimu niliyopata kutoka kwa wawezeshaji wetu imenijengea uelewa wa kawaida wa

namna ya ufuatiliaji na uwajibikaji katika jamii namna ya utoaji wa huduma bora

Swali 9 Ni mada ipi au zipi zimekuwia ugumu kuelewa?

Hakuna zote nimeelewa vizuri.

Mada ya uwajibikaji jamii lakini nimeelewa.

Hakuna.

Zote zimeeleweka vyema.

Kutokana na ufafanuzi wa wawezeshaji mad azote nilizielewa

Hakuna iliyokuwa ngumu kuielewa bali kwa kuwa mada zilikuwa nyingi hivyo ni vigumu kutunza

vipengele vyote kichwani

Kuhusu mgawanyo wa rasilimali Tanzania.

Vifupisho vya maneno ndivyo vinavyonisumbua kuelewa

Swali 10 Ni mada ipi au zipi umezielewa vizuri?

Ni mfumo mzima wa uwajibikaji kwa jamii.

Karibu zote.

Mada ya uchechemuzi

10

Mada ya uchechemuzi.

Uchechemuzi na ushawishi wake

Karibu zote

Mgawanyo wa rasilimali na mpango mkakati.

Nakubaliana na kitu au kukataliwa lazima mtu ajieleze kuzingatia afafanue,udhibitisho, na

uhalalisho

Mada ya mipango na mgawanyo wa rasilimali imeeleweka vizuri sana

Swali 11

Ukiwa kama raia wa kawaida au mwanaharakati, mafunzo haya yamekusaidia nini katika maisha

yako ya kila siku?

1. Yamenifumbua macho na kunipa uwezo wa kuanza kuhoji.

2. Nimezidisha uimara wa stadi za ufuatiliaji wa mfumo wa uwajibikaji wa kijamii

“NITAFUNDISHA KWA UZURI ZAIDI”

3. Yamenisaidia kujisahihisha na kuwabaini wala nchi.

4. Nimepata mwanga kuwa mimi nina nafasi ya kutoa ushawishi na utetezi

5. Yameniwezesha kutambua mfumo mzima wa uwajibikaji wa jamii pia mfumo wa

usimamizi wa fedha/mali ya umma

6. Ninao wajibu wa kushiriki katika kuwezesha mfumo wa uwajibikaji jamii ili kuhakikisha

huduma bora zinapatikana kwa mtizamo wa haki za binadamu

7. Ndiyo kwa sababu yameniongezea uelewa mkubwa wa masuala mbalimbali ya kijamii

8. Yamenifungua akili,Ninaweza kufanya kazi kwa uwezo mkubwa kulingana na

nilichokipata

9. Yameniongezea kuweza kujua haki zabinadamu zinazokiukwa

10. Kutambua haki na wajibu wa kupewa huduma kama kiongozi wa umma /asasi mbinu za

uwajibikaji

11. Mafunzo haya yamenisaidia kwenda kufanya ushawishi na uchechemuzi katika jamii ili

kufikia malengo ya upatikanaji wa huduma bora

12. Kwanza yamenijengea maamuzi mazuri kwenye familia yangu pamoja na jamii

inayonizunguka

13. Kuwajibika kusikokoma nikutanapo na vikwazo visivyo rasmi

14. Kwanza yamenifanya nizitambue haki zangu za msingi katika maisha ya kila siku ya

binadamu

11

Swali 12

Je mafunzo haya yamekujengea uwezo wa kuhoji na kuiwajibisha serikali yako au kiongozi wako katika eneo lako kama mwanaharakati wa kawaida? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 12.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 10 14 71.43%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

4 14 28.57%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 14

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: kwa upande wa kujenga uwezo wa kuweza kuhoji na kuiwajibisha Serikali au kiongozi

kama mwanaharakati 71.43% ya washiriki wamesema imewajengea uwezo kwa kiwango kikubwa

wakati 28.57% imewajengea uwezo kwa kiwango cha kawaida

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Ni kweli mafunzo haya yameniwezesha sasa kuanza kuifuatilia serikali na kuhoji.

Nimeimarika zaidi kuwajibisha au kuhoji kutaendelea kwa staili mpya.

Uwajibikaji unahusisha jamii nzima hivyo nitaihamasisha jamii kushiriki katika mfumo wa

uwajibikaji kwa hatua zote na hatimaye tunaweza kuwawajibisha watendaji wanaokwenda

kinyume.

Nimeweza kutambua namna ya kuandaa mpango mkakati na utekelezaji wake na pia sharia

mbalimbali na bajeti za halmashauri yangu, mkaguzi mkuu wa serikali anavyofanya kazi.

Kwa sababu sijapata elimu ya kujua sharia namba ngapi na vifungu vyake

Kama mwanaharakati nimeongeza ujuzi

Kwa kutumia miongozo na kanuni na taratibau nimeweza kutambua kwamba ni wajibu wangu

kufanya hivyo

Taarifa ya fedha ndani ya mwaka na mwisho wa mwaka halmashauli na kijiji change

Nimekuwa na uelewa uliokuwa umefichika kwa kutoelewa kuwa viongozi wako chini ya jamii

maana wao ndio waajiri

Kwa sababu ni moja ya majukumu yangu kama jamii

12

Swali 13

Mazingira ya kufanyia mafunzo na huduma zilizotolewa ni ya kuridhisha? 1=Ndio kwa kiwango kikubwa 2=Ndio kwa kiwango cha kawaida 3=Ndio kwa kiwango kidogo 4=Hapana kwa kiwango kikubwa 5=Hapana kwa kiwango cha kawaida 6= Hapana kwa kiwango kidogo

Jedwali 13.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio kwa kiwango kikubwa 3 14 21.43%

2- Ndio kwa kiwango cha

kawaida

8 14 57.14%

3- Ndio kwa kiwango kidogo 3 14 21.43%

4- Hapana kwa kiwango kikubwa 14

5- Hapana kwa kiwango cha

kawaida

14

6- Hapana kwa kiwango kidogo 14

Matokeo: Kwa upande wa mazingira 21.43% ya washiriki walisema yalikuwa ni ya kuridhisha kwa

kiwango kikubwa 57.14 % ya washiriki walisema mazingira ni ya kuridhisha kwa kiwango cha

kawaida na 21.43% walisema ni yakuridhisha kwa kiwango kidogo

Hapa chini ni sababu za matokeo hayo kama yalivyoandikwa na washiriki:

Kwakiasi cha kawaida yanaridhisha

Wakati mwingine kelele zilizidi kutokana na matumizi maalum ya maeneo yanayozunguka

ukumbi

Yametuwezesha kuwepo hapa kwa mda wote wa mafunzo

Ili kuweza kupata utulivu zaidi wa kujifunza ingefaa kubadilisha mazingira tuliyozoea

Chakula chai vilikuwa vizuri sana .chumba cha mafunzo kina madirisha makubwa hivyo

viliwasumbua wawezeshaji katika projection.choo cha hapa hakifai kikarabatiwe.

Nilitakiwa kuwa nje ya familia kwa maana ya kufuata ratiba jioni baada ya darasa kubadilishana

uzoefu na washiriki wengine.

Mafunzo yapewe muda wa kutosha pia yasiwe karibu na maeneo tunayoishi ili tuweze

kuhudhuria kwa kipindi chote mafunzo bila kutokatoka

Mahali pa mafunzo ni pakuridhisha /pametulia

Nimazingira yasiyo na kelele(tulivu)na salama

Kwa sababu huduma tuliyoihitaji kupewa tumepewa bila matatizo

13

Swali 14

Je ungependa kufanya zoezi la SAM baada ya mafunzo haya katika eneo lako? 1=Ndio 2=Hapana

Jedwali 14.

Evaluation Response Total response %

1- Ndio 12 14 85.75%

2- Hapana

14

0%

Fomu 2 hazikujazwa Swali

Nini matarajio yako baada ya mafunzo haya katika eneo lako?

1. Ni kusambaza elimu hii kadri ya uwezo wangu.

2. Ni uboreshaji wa shughuli za mfumo wa ufuatiliaji wa uwajibikaji wa umma.Ukusanyaji

taarifa za uwajibikaji wa umma katika sekta ya afya

3. Kuwa na uwezo wa kuhoji na kutafuta suluhu

4. Ufuatiliaji wangu kuhusu mali/fedha za umma sasa utakuwa wa kitaalamu sana

5. Kufanya ushawishi ili kubadilisha mifumo iliyopo

6. Kufanya uchechemuzi wa kina

7. Kufuatilia huduma kwenye idara ya afya

8. Kuwajibika kwa ukamilifu, kufuatilia mambo mbalimbali ambayo yanafanyika nje ya

utaratibu

9. Ninatarajia kufanya uchechemuzi ambao utaweza kuleta mabadiliko kutokana na

mapungufu yote yaliyopo

10. Kuelimisha jamii kuanzia kwenye familia /jamii inayonizunguka hadi watumishi wenzangu

11. Kufanya ushawishi na utetezi ili kuangalia kama mfumo wa ufuatiliaji na uwajibikaji katika

jamii unatakelezwa

14

Swali 16 Nini ungependa kiboreshwe kifanyike tofauti kuboresha mafunzo haya?

1. Nikuona tunafikia mwisho wa hatua zote za mafunzo haya naomba posho iongezwe.

2. Ukumbi peke yake

3. Yawepo maigizo na nyimbo za kutosha

4. Mafunzo haya yaendane na vifungu vya sheria namba 7 1982 na marekebisho yake na

memoranda ya 1997 vitatusaidia sana wakati wa kufuatilia kazi zetu

5. Mda uongezwe ,mda wa majadiliano uwe zaidi

6. Kuongeza posho ya chakula cha usiku na nauli

7. Muda wa mafunzo uongezwe na eneo la mafunzo liboreshwe

8. Mafunzo kufanyika ndani ya wilaya, mafunzo yawe nje ya wilaya, maslahi/posho

inayotolewa kwa siku ni kiasi kidogo kutokana na hali ya maisha ya sasa.

9. Muda wa mafunzo uongezwe,viambatanisho muhimu tuvipate kulingana na mada mfano

vitabu vya sheria ya utumishi, rushwa

10. Posho ningependa iboreshwe

11. Muda mchache.mafunzo ni mazuri yahitaji muda mrefu ili mada ziende kwa ufahamu zaidi

12. Ni kuzidi kutujengea uwezo wa kuelewa zaidi katika kuzitambua haki zetu za msingi