warning for heavy rains/tahadhari ya mvua kubwa 20/01/2016 - 21/01/2016
DESCRIPTION
Warning for heavy rains/Tahadhari ya mvua kubwa 20/01/2016 - 21/01/2016.TRANSCRIPT
-
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Barua pepe: [email protected] DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 20 Januari, 2016
Taarifa kwa Umma: Vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa.
Taarifa Na. 201601-02
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki Saa 9:00 Alasiri
Daraja la Taarifa: Tahadhari
Kuanzia:
Tarehe 20 Januari, 2016 - Usiku
Mpaka:
Tarehe 21 Januari, 2016
Aina ya Tukio
Linalotarajiwa
Vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa
24 katika siku hizo vinatarajiwa.
Kiwango cha uhakika: Wastani (80%)
Maeneo yanayotarajiwa
kuathirika
Mikoa ya Lindi, Mtwara na kusini mwa mikoa ya Pwani na
Morogoro
Maelezo:
Hali hii inatokana na kuendelea kuimarika kwa ukanda wa
mvua katika maeneo yaliyotajwa hapo juu. Pia kutokana na
mvua kubwa zilizonyesha katika maeneo hayo, mvua
zinazotarajiwa zinaweza kusababisha mafuriko.
Angalizo:
Vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa kujitokeza pia
kwenye maeneo machache ya mikoa ya Arusha,
Kilimanjaro, Manyara na Mara.
Wakazi wa maeneo tajwa wanashauriwa kuendelea
kuchukua tahadhari na hatua stahiki.
Maelezo ya Ziada Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii
na itatoa mrejeo kila itakapobidi.
Imetolewa na
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.