hotuba za kisasa...aya za kurani tukufu zimehimiza kufanya kazi na kuishi. likaja agizo la kutaka...
Post on 30-Dec-2019
7 Views
Preview:
TRANSCRIPT
Jamhuri ya kiarabu ya Misri
Wizara ya Wakfu
Hotuba za kisasa
Kutoka Wizara ya Wakfu ya Misri
Kimetolewa na kusimamiwa
Na
Profesa \Muhammad Mukhtar Juma Mabrook
Waziri wa Wakfu
Mkuu wa Baraza Kuu la masuala ya Kiisilamu
Na Mwanachama wa Jopu la Utafiti la Kiisilamu
Kimefasiriwa
Na
Profesa\ Ayman Ibrahim Alaasar
Kitivo cha Lugha na Ufasiri
Chuo Kikuu cha Alazhar
Kairo, Misri
6102 - 0341 H
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye
kurehemu
Utangulizi
Sukurani zote ni za Mwenyezi Mungu Mola wa ulimwengu, rehma
na amani zimshukie Mjumbe na Mtume wake wa mwisho, Mtume
Muhammad na watu wake na masahaba zake na waliowafuata
uongofu wake mpaka siku ya mwisho
Baada ya utangulizi:
Tuna furaha kubwa kwa kutoa kitabu hiki chenye mkusanyiko wa
hotuba za kisasa zilizochaguliwa kwa maimamu, wahadhiri,
wasomi na wenye kuhusika na masuala ya ulinganiaji ndani ya
Misri na katika ulimwengu wa kiarabu na wa kiisilamu. Kitabu
kilichoandaliwa na idara ya utafiti katika Wizara ya Wakfu chini
ya usimamizi na uhakiki wetu
Na tumezingatia kuwa hotuba za kidini ziwe katika muktadha wa usamehevu na
uadilifu wa dini ya kiisilamu ulio mbali na itikadi kali na kufanya inda na kuvuka
mipaka, na kwa ajili ya kufikisha ujumbe misikitini ambao utakuwa ukiwaweka
pamoja waumini na wala hauwatenganishi, na pia ukiwa na malengo ya kuleta
masilahi kwa waja kwa kuzingatia kuwa sheria ya Mwenyezi Mungu ipo kwa ajili
ya kusimamia masilahi haya. Na popote yawapo masilahi basi ni kwa kuwepo
sheria za Mwenyezi Mungu na kwa kufuatwa dini itakiwavyo na ipasavyo. Tuna
imani kuwa hotuba hizi zitakuwa ni maandalizi na marejeo kwa mwenye
kuhitaji hotuba kwa lugha ya kiswahili, sawa iwapo atakuwa anahutubu kwa
lugha mbili ya kiarabu na kiswahili au kwa kiswahili (pekee) na hii ni kwa mujibu
wa mazingira.
Mwenyezi Mungu ni mwafikishaji na ni mwenye kuombwa msaada…
Profesa: Muhammad Mukhtar Juma
Waziri wa Wakfu
Na Mkuu wa Baraza Kuu la masuala ya Kiisilamu
Uisilamu ni dini ya ujenzi na ya uimarishaji
32 Rabiu L awal 2548H. Sawa na 2 Januari 3127 A.D.
Imefasiriwa na profesa\ Ayman. I.Alasar
Kwanza: Vipengele
2. Kuimarisha ardhi ni jambo litakiwalo kisheria.
3. Wito wa uisilamu katika ujenzi na uimarishaji wa ardhi.
4. Kufanya vizuri kazi ni njia ya kuinuka kwa umma na raia
5. Uisilamu unakataa aina zote za uvivu.
6. Onyo la kubomoa na kufanya ufisadi katika ardhi.
Pili: Dalili
Ndani ya Kurani Tukufu
2. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: { Yeye ndiye aliye kuumbeni katika
ardhi, na akakuwekeni humo.}(Hud. 72)
3. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Yeye ndiye aliyedhalilisha ardhi kwa
faida yenu, basi tembeeni katika pande zake, na kuleni katika riziki zake. Na
kwake Yeye ndio kufufuliwa} (Almulk. 26)
4. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {na wengine wanasafiri katika ardhi
wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu} (Muzammil. 31)
5. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: { Na sema: Tendeni vitendo. Na
Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Waumini wataviona vitendo vyenu. Na
mtarudishwa kwa Mwenye kujua siri na dhaahiri; naye atakuambieni mliyo
kuwa mkiyatenda} (Taubah. 216)
6. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {wala msifanye uharibifu katika nchi
baada ya kuwa imekwisha tengenezwa.. na muombeni kwa kuogopa na kwa
kutumai. Hakika rehema za ya Mwenyezi Mungu iko karibu na wanaofanya
mema} (Al Aaraf. 67)
7. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Basi malipo ya wale wanao mpiga
vita Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakawania kufanya uchafuzi
katika nchi, ni kuuwawa, au kusalibiwa, au kukatwa mikono yao na miguu
yao kwa mabadilisho, au kutolewa nchi. Hii ndiyo hizaya yao katika dunia;
na katika Akhera watapata adhabu kubwa} (Al maidah. 44)
Ndani ya Hadithi za Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake)
2. Kutoka kwa Miqdam (Mwenyezi Mungu amwie radhi), kwamba Mtume
(Rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ Hakula mtu chakula bora
kuliko alichochuma kwa kazi ya mikono yake, na hakika Mtume wa
Mwenyezi Mungu Daudi (juu yake rehma na amani) alikuwa akila kutokana
na kazi za mikono yake. (Imepokewa na Bukhari)
3. Na kutoka kwa Abdalla bin Abbas (Mwenyezi Mungu awawie radhi)
amesema: amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukia juu yake) “ atakaepambazukiwa hali ya kuwa amejitosheleza
kutokana na kazi ya mkono wake basi amepambazukiwa hali ya kuwa
amesamehewa. (Muujam Alwasiyt).
4. Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukia juu
yake) kujifungia mmoja wenu mzigo wa kuni juu ya mgongo wake ni bora
kuliko kuomba mtu mwengine sawa ampe au amkatalie. (Imepokewa na
Bukhari)
5. Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukia juu
yake) “mwenye kumhudumikia mjane au masikini, hupata malipo sawa na
waipiganiao dini ya Mwenyezi Mungu, au anaesimama usiku kusali na
kufunga mchana. (Imepokewa na Bukhari)
6. Kutoka kwa Anas Bin Malik (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukia juu
yake) iwapo kitasimama kiama na kwenye mkono wa mmoja wenu ana
mche, kama ataweza kutosimama kabla ya kuipanda, basin a aipande.
(Imepokewa na Bukhari)
7. Kutoka kwa Ka`ab bin U`jrah (Mwenyezi Mungu amwie radhi). Kuna kijana
alipita mbele ya Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake), masahaba
wa Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) wakaona kwenye ngozi
yake ukakamavu na ucheshi wake kitu ambacho kiliwavutia. Wakasema: “
ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unaonaje lau kama kijana huyu
angelikuwa anapigania njia ya Mwenyezi Mungu!! Mtume (Rehma na amani
zimshukie juu yake) akasema: “ iwapo anawatafutia riziki watoto wake,
basi yupo katika njia ya Mwenyezi Mungu. Na iwapo ametoka kuwatafutia
riziki wazazi wake wawili watu wazima basi yupo katika njia ya Mwenyezi
Mungu. Na iwapo ametoka kwa ajili ya nafsi yake ili kujikinga na
haramu, basi yupo katika njia ya Mwenyezi Mungu, na ikiwa ametoka kwa
ajili ya kuitafutia familia yake riziki basi yupo katika njia ya Mwenyezi
Mungu. Na kama ametoka kutafuta riziki kwa ajili ya kujifaharisha na
kujilimbikizia basi atakuwa yupo katika njia ya shetani. (Imepokewa na
Attabari).
8. Kutoka kwa Anas bin Malik (rehma na amani zimshukia juu yake)
amesema: Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) alikuwa akisema
“Ewe Mola angu, hakika mimi ninajilinda kwako kutokana na kushindwa,
uvivu, woga, ukongwe, ubakhili. Na ninajikinga kwako na adhabu za kaburi
na fitina za uhai na umauti.” (Imepokewa na Muslim).
Maudhui
Hakika Mwenyezi Mungu amemuumba mwanadamu katika umbile bora zaidi,
akamtukuza kuliko viumbe wengine, na kumdhalilishia ulimwengu kila kilichopo
ulimwenguni. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {Na hakika tumewatukuza
wanaadamu, na tumewapa vya kupanda nchi kavu na baharini, na tumewaruzuku vitu
vizuri vizuri, na tumewafadhilisha kwa fadhila kubwa kuliko wengi miongoni mwa
tulio waumba} Al Israa, 81. Pia amesema: {Yeye ndiye aliye kuumbieni vyote
vilivyomo katika ardhi.} Al baqara 3:.
Na ikapelekea ukarimu huu na neema hii kuwa ndio sababu ya ukhalifa katika
ardhi. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {Na pale Mola wako Mlezi alipo
waambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi Khalifa (mfwatizi), wakasema:
Utaweka humo atakaye fanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi
tunakutakasa kwa sifa zako na tunakutaja kwa utakatifu wako? Akasema: Hakika
Mimi nayajua msiyo yajua} (Al baqara 41). Kisha Mwenyezi Mungu Mtukufu
akamwekea mwanadamu mipaka na kumpa jukumu kubwa kuhusu ibada nalo ni
kumtaka aiimarishe ardhi, na atowe hazina zake na vyenye thamani. Akasema {
Yeye ndiye aliye kuumbeni katika ardhi, na akakuwekeni humo. } (Hud, 72.) Ikiwa na
maana, amewatakeni kuijenga ardhi na kuiimarisha, na kuangalia vile alivyokupeni
katika kheri na katika vyakula.
Mwenyezi Mungu amemuamrisha mwanadamu atafute na awe na sababu ya
kutafutia riziki, na kuacha kujibweteka na kupiga uvivu kwa ajili hiyo Mwenyezi
Mungu amesema { Yeye ndiye aliyedhalilisha ardhi kwa faida yenu, basi tembeeni
katika pande zake, na kuleni katika riziki zake. Na kwake Yeye ndio kufufuliwa}
(Almulk.26).
Na katika kufanya kazi hakuna wakati maalumu, mwanadamu hana budi kufanya
kazi hadi mwisho wa pumzi zake, kuthibisha hilo, Mtume (Rehma na amani
zimshukie juu yake) anasema katika hadithi aliyoipokea Anas Bin Malik
(Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: amesema Mjumbe wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukia juu yake) Kutoka kwa Anas Bin Malik
(Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: amesema mjumbe wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukia juu yake) iwapo kitasimama kiama na kwenye
mkono wa mmoja wenu ana mche, kama ataweza kutosimama kabla ya kuipanda,
basi na aipande. (Imepokewa na Bukhari). Dini ya kiisilamu inatukuza sana ujenzi,
na kuimarisha na inalingania hasa vitu hivi, hata iwapo katika wakati wa dhiki,
kwani kuimarisha ni miongoni mwa sababu kuu za maendeleo ya umma na jamii.
Uisilamu unazingatia sana elimu na mafunzo yote yanayoshikamana na kuijenga
ardhi na kuimarisha dunia, ikawahimiza wafuasi wake kutembea katika pembe
zake, na kujitafutia riziki zao baharini na nchi kavu pia, pamoja na kuhimizwa
kufanya kazi. Inathibiti haya kutoka kwa hadithi ya Miqdam (Mwenyezi Mungu
amwie radhi), kwamba Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “
Hakula mtu chakula bora kuliko alichochuma kwa kazi ya mikono yake, na hakika
Mtume wa Mwenyezi Mungu Daudi (juu yake rehma na amani) alikuwa akila
kutokana na kazi za mikono yake”. (Imepokewa na Bukhari).
Uisilamu ni wito ulio wazi wa kufanya kazi ambazo zitapelekea kuimarisha na
kujenga ili manufaa yarudi kwa ulimwengu mzima.
Kwa ajili hiyo: Uisilamu umeingalia kazi kwa mtazamo usio na mzaha na
kuitukuza pia, na kunyanyua thamani ya kazi na kuifanya kuwa ndio sababu ya
maeneleo. Na pia kuifanya kuwa ni ibada ambayo mtu hupata malipo. Aya za
Kurani Tukufu zimehimiza kufanya kazi na kuishi. Likaja agizo la kutaka watu
watawanyike katika ardhi kwa ajili ya kutafuta riziki baada ya amri ya kusali.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {Na itakapokwisha sala, tawanyikeni katika
nchi mtafute fadhila za Mwenyezi Mungu, na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa
wingi ili mpate kufanikiwa} Jumaa, 21.
Na Sayyidna I`rak Bin Malik (Mwenyezi Mungu amwie radhi) akishasali sala ya
Ijumaa husimama mbele ya mlango wa msikiti, kisha husema “ewe Mola wangu
hakika nimeitikia wito wako na nimekishasali faradhi yako, na ninaondoka kama
ulivyoniamrisha, niruzuku katika fadhila zako kwani wewe ni mbora wa
wanaoruzuku.”
Na kwa kutokana na umuhimu wa kazi kwa ajili ya kuimarisha na kujenga, aya
nyingi ndani ya Kurani Tukufu zimezungumzia kuhusu kazi, vilevile hadithi za
Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) zipo nyingi zilizoweka wazi jambo
hili na kuhimiza na kutia shime kuhusu kazi, na kuacha kupiga uvivu na
kujibweteka. Na kuweka wazi kuwa kufanya kazi ni kijiondoshea udhalilifu na
kuwa na heshima na utukufu. Imepokewa na Abi Hurayra (rehma na amani
zimshukia juu yake) amesma: amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na
amani zimshukia juu yake) “kujifungia mmoja wenu mzigo wa kuni juu ya
mgongo wake ni bora kuliko kuomba mtu mwengine sawa ampe au amkatalie.
(Imepokewa na Bukhari). Na Sufyan Thawriy (Mwenyezi Mungu amrehemu)
akipita kwa baadhi ya watu wakiwa wamekaa ndani ya msikiti wa mtukufu,
huwaambia: “ ni nini kilichowafanya mukae? Nao hujibu: “Tufanye nini sasa!?
Nae husema: tafuteni fadhila za Mwenyezi Mungu na wala musiwe waombaji kwa
waisilamu.
Uisilamu umeweka wazi kuwa, yeyote atafutae maisha ya halali kwa ajili ya
wanawe anahesabiwa kuwa yupo katika mashahidi na aliyefungamana na njia ya
Mwenyezi Mungu. Imepokewa na Kutoka kwa Ka`ab bin U`jrah (Mwenyezi
Mungu amwie radhi). Kuna kijana alipita mbele ya Mtume (Rehma na amani
zimshukie juu yake), masahaba wa Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake)
wakaona kwenye ngozi yake ukakamavu na ucheshi wake kitu ambacho
kiliwavutia. Wakasema: “ ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unaonaje lau kama
kijana huyu angelikuwa anapigania njia ya Mwenyezi Mungu!! Mtume (Rehma na
amani zimshukie juu yake) akasema: “ iwapo anawatafutia riziki watoto wake,
basi yupo katika njia ya Mwenyezi Mungu. Na iwapo ametoka kuwatafutia riziki
wazazi wake wawili watu wazima basi yupo katika njia ya Mwenyezi Mungu. Na
iwapo ametoka kwa ajili ya nafsi yake ili kujikinga na haramu , basi yupo katika
njia ya Mwenyezi Mungu, na ikiwa ametoka kwa ajili ya kuitafutia familia yake
riziki basi yupo katika njia ya Mwenyezi Mungu. Na kama ametoka kutafuta riziki
kwa ajili ya kujifaharisha na kujilimbikizia basi atakuwa yupo katika njia ya
shetani. (Imepokewa na Attabari).
Na uisilamu haukutosheka kuwalingatia wafuasi wake kufanya kazi tu pekee kama
ndio njia ya maendeleo, bali pia umewataka wafanye kazi kama itakiwavyo –wawe
na ikhlasi- kwa ajili ya kupata mapenzi ya Mwenyezi Mungu na rehema zake.
Imepokewa kutoka kwa Aisha (rehma na amani zimshukia juu yake). Kwamba
Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ Hakika Mwenyezi
Mungu – Mtukufu – anapenda mmoja wenu akifanya kazi aifanye vizuri.”
(imepokewa na Tabbariy).
Kufanya kazi itakiwavyo na kuijali na kuihifadhi ni katika misingi ambayo
uisilamu unataka ifuatwe, nayo ni lengo miongoni mwa malengo ya dini,
humtukuza muisilamu kupata radhi za Mwenyezi Mungu, kwa sababu Mwenyezi
Mungu huwa hakubali kazi isipokuwa ile iliyofanywa kwa ajili yake, kwani
Mwenyezi Mungu ameumba kila kitu kwa uangalifu sana, Mwenyezi Mungu
Mtukufu anasema {Huo ndio ufundi wa Mwenyezi Mungu aliye tengeneza vilivyo kila
kitu. Hakika Yeye anazo khabari za yote myatendayo} (Annaml, 99).
Na uisilamu ukahimiza kufanya vizuri na ipasavyo na kukataza kufanya ufisadi,
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Na fanyeni wema. Hakika Mwenyezi Mungu
huwapenda wafanyao wema} (Al baqara.2:6). Na akasema {Nawe fanya wema
kama Mwenyezi Mungu alivyo kufanyia wema wewe. Wala usitafute kufanya ufisadi
katika ardhi. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi mafisadi.} (Al qasas.88).
Aya nyingi za Kurani Tukufu zimetaka mtu akifanya kazi basi aifanywe katika njia
sahihi hii kwa ajili ya kupata radhi za Mwenyezi Mungu, kusaidiana katia ya mtu
na jamii, na akaahidi malipo makubwa sana na kumsifia sifa njema hapa duniani
na kesho akhera. Na akaweka wazi kuwa mwanaadamu hatoacha kuwa anafanya
kazi ilivyokuwa yupo chini ya ulinzi wa Mwenyezi Mungu, mjuzi wa
vilivyofichikana kifuani, Naye kwake hakifichiki hata kilicho kidogo sana katika
matendo ya waja. Mwenyezi Mungu tawadhihirishia kwa kuwa amekisajili na
atawalipa kwa hicho siku ya watakayokutana. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema
{Na huwi katika jambo lolote, wala husomi sehemu yoyote katika Qur'ani, wala
hamtendi kitendo chochote ila Sisi huwa ni mashahidi juu yenu mnapo shughulika
nayo. Na hakifichikani kwa Mola wako Mlezi chenye uzito hata wa chembe katika
ardhi na katika mbingu, wala kidogo kuliko hicho wala kikubwa ila kimo katika
Kitabu kilicho wazi} (Yunus. 72).
Mwenyezi Mungu Mtukufu ndie anayemchunga mwanadamu katika kazi zake, na
humuona akiwa kiwandani, kondeni na hata katika biashara zake sehemu ambazo
hufanyia kazi. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Na sema: Tendeni vitendo. Na
Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Waumini wataviona vitendo vyenu. Na
mtarudishwa kwa Mwenye kujua siri na dhaahiri; naye atakuambieni mliyo kuwa
mkiyatenda.} (Tawbah. 216). Amri ya hapa ni kama walivyosema wafasiri: kuna
kuogopesha: ikiwa na maana: matendo yenu hayafichikani mbele ya Mwenyezi
Mungu na wala kwa Mtume wake wala kwa waumini, basi harakisheni kutenda
mema, na fanyeni kazi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Na pia kuna - katika aya hii
– bishara na kuhamasishwa, kwani iwapo mtu ataelewa kuwa matendo ayatendayo
sawa ni mabaya au mazuri Mwenyezi Mungu ndie ayaonae, basi atakuwa na shime
ya kuyakimbilia matendo mema, na kujiepusha na mabaya, na maneno mazuri
yaliyoje ya mshairi Zuhayri:
“Mtu akiwa na tabia ya aina yoyote * hata kama ataificha, basi watu wataijua”
Pia imekuja katika hadithi za Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) zenye
kuhimiza kufanya kazi kama itakiwavyo na kuimarisha kwa ajili ya kufikia kilicho
bora na kizuri. Kwa mfano katika upande wa kuabudu kupitia ibada ya sala
ambayo ninguzo kati ya mja na Mola wake, inatakiwa imamu wao awe mwenye
ujuzi kuliko wote na awe anaisoma Kurani Tukufu vizuri, pia awe anaisoma kwa
kuizingatia, ili ajumuike na wale waliobashiriwa na Mtume (Rehma na amani
zimshukie juu yake) kuwa atakuwapo pamoja na malaika wakarimu. Na vilevile
kwa asimamiaye masuala ya maiti, Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake)
anasema: “ Mmoja wenu akimveka sanda maiti basin a amvike vizuri”
(Imepokewa na Muslim).
Kutoka kwa A`swim Bin Kulayb Al jaramiy amesema: Baba yangu Kulayb
amenihadithia kwamba yeye amehudhuria jeneza pamoja na baba yake
alipokuwepo Mtume na mimi kipindi hicho ni mdogo mwenye akili na ufahamu,
wakamaliza kusalia jeneza wakaenda makaburini walipomlaza, akasema, Mtume
(Rehma na amani zimshukie juu yake) akawa anasema “uwekeni vizuri
mwanandani huu”. Mpaka watu kakadhania kuwa ni sunna, nikawageukia,
akasema: “ Ama huu haumfai maiti na wala haumdhuru, isipokuwa Mwenyezi
Mungu hupenda kwa mtenda kazi akifanya kazi basi aifanye vizuri.” (Imepokewa
na Bayhaqiy).
Kazi yoyote aitendayo mwanadamu ni lazima aifanye vile itakiwavyo, amchunge
Mwenyezi Mungu katika kazi hiyo, kwani Yeye Mwenyezi Mungu humuona mja
huyo na kilichomo ndani ya moyo wake na atawahesabu juu ya matendo yao
makubwa au madogo, mengi au machache.
Ama kwa wale ambao hawafanyi itakiwavyo kazi zao na wala hawamchungi
Mwenyezi Mungu, hupata madhambi mengi kwa kadiri ya madhara
atakayoyasababisha ya kupoteza mali na nguvu. Mfanya kazi ambaye hatimizi
wajibu wake na huzembea na wala hafanyi kazi kama alivyoagizwa na akatosheka
kujiridhisha yeye mwenyewe na akawa anapokea mshahara, huyu huwa anapokea
mshahara wa haramu na watu watakwenda kudai madai yao siku ya kiama. Na
yeyote ambae hii ndio sifa yake basi aelewe kuwa anabeba jukumu la
kutokuendelea kwa umma na kuonekana kuwa upo nyumba kimaendeleo.
Hatutoacha kumshtakia mbele ya Mwenyezi Mungu. Sayidna Omar (Mwenyezi
Mungu amwie radhi) anasema: “namshtakia Mwenyezi Mungu kutokana na
udhaifu wa kiongozi na ukhaini wa mwenye nguvu.”
Hakika uisilamu umepiga vita aina zote za kukata tama na uvivu ambao hausaidii
kitu katika kujenga na kuimarisha. Na ukaifanya sifa ya uvivu kuwa ni sifa chafu,
Mwenyezi Mungu amewakashifu wavivu kwenye kitabu chake kitukufu na kusema
kuwa ni sifa za wanafiki, akasema {wala hawaji kwenye Sala ila kwa uvivu, wala
hawatoi michango ila nao wamechukia} (Atawba. 65).
Uvivu ni njia mbaya na ni maafa makubwa yenye kuangamiza yenye kuharibu
taifa na raia zake na pia hupelekea kutoendelea na kuonekana taifa lililo nyuma
kimaendeleo. Nao ni ugonjwa hatari, mtu akiwa nao basi anaweza hata kupoteza
utu wake. Imamu Raghib amesema: “ajiewekae bila kazi hujivua ubinaadamu na
kujiweka kuwa mnyama, na hufikia pia kuwa kama maiti”.
Kwa ajili hiyo Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) akajikinga kwa
Mwenyezi Mungu kutokana na uvivu na unyongonyevu, imepokewa kutoka kwa
Anas bin Malik (rehma na amani zimshukia juu yake) amesema: Mtume (Rehma
na amani zimshukie juu yake) alikuwa akisema “Ewe Mola angu, hakika mimi
ninajilinda kwako kutokana na kushindwa, uvivu, woga, ukongwe, ubakhili. Na
ninajikinga kwako na adhabu za kaburi na fitina za uhai na umauti.” (Imepokewa
na Muslim).
Na Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) amelinganisha kati ya uvivu na
ukongwe kwa sababu kila moja katika hivi viwili humfanya mtu kuwa mzito wa
kutimiza wajibu aliotakiwa autimize.
Uvivu ni maafa yatokayo moyoni, na kizuizi chenye kuzuia kutimiza wajibu,
hudhoofisha utashi, hupelekea kwenye ufakiri, na ni vimelea vyenye kuua, maradhi
yenye kuangamiza, hudhoofisha ukuaji wa taifa na watu wake, na huzuia watu
wasifanye kazi kwa bidii na kuyatafuta manufaa.
Uisilamu umeutia dosari uvivu na kutahadharisha kutokuwa nao, kwani una
kuzembea katika mambo yasiyopasa kuzembewa, na kupelekea kujiweka mbali na
yaliyo muhimu na kuhisi kama kwamba ni sumu au kitu cha kuchukiza Mwenyezi
Mungu atuepushe nao. Na –uvivu- humfanya mtu achukie mazuri kutokana na
udhaifu wake wa kufuatilia, na humfanya aache yaliyo wajibu, kweli ni maafa
yasiyoleta mafanikio, humsambaratisha kila aliye nao, na humfanya mvivu kuwa
mwenye kutegemea wengine, asiye na uwezo wa kuchukua jukumu kama mtu
kamili. Na hatari yake huenea kwa mmoja moja na hata kwa jamii nzima. Imamu
Ali (Mwenyezi Mungu amwie radhi) anasema: “Kuzembea ni ufunguo wa kukatisha
tamaa, ulegevu na uvivu huleta maafa, na huzalisha maangamizo, asiyetafuta huwa
hapati na pia hupelekea katika maovu.”
Uvivu si katika mambo yatakiwayo katika uisilamu na wala hauna thamani, kwani
uisilamu hufukuzia mema na kuimarisha ulimwengu, ama wavivu wao hubomoa
ustaarabu na huharakisha kubomoa aina zote nyengine za ustaarabu.
Haya ni miongoni mwa mambo ambayo uisilamu umeyapiga vita, na ambayo katu
hayajengi na kuimarisha ulimwengu na huleta ufisadi katika ardhi na kuiharibu nayo
ni tabia yenye kudhalilisha iwapo atakuwa nayo mwanadamu. Tabia hii huwa hawawi
nayo isipokuwa wanafiki pekee ambao Mwenyezi Mungu amesema. {Na
wanajitahidi kuleta uharibifu katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi
waharibifu} (Al maida 75). Na anasema {wala msiasi katika nchi mkafanya
uharibifu} (Al baqara. 71).
Ufisadi upo wa aina nyingi, na ulio mbaya zaidi ni ule unaotumia jina la dini,
umma umefikwa na mitihani kwa sababu ya ufisadi hali ya kuwa dini haihusiki
kabisa. Huuwa, hujihalalishia mali na kuvunja heshima kwa jina la dini. Watu
hawa Mwenyezi Mungu amewakashifu ndani ya kitabu chake akasema {Na katika
watu yupo yule ambaye maneno yake kwa maisha ya kidunia hukufurahisha; naye
humshuhudisha Mwenyezi Mungu kwa yaliyomo moyoni mwake, na hali yeye ndiye
mkubwa wa ukhasimu 316. Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi
humo na kuteketeza mimea na viumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi. 317. Na
akiambiwa: Mwogope Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kutenda madhambi.
Basi huyo inamtosha Jahannam. Paovu mno hapo kwa mapumziko.} (Al baqara
315-317).
Ufisadi kwanamna zake zote huyumbisha ukuaji na maendeleo ya taifa, na hueneza
mabaya na kupelekea kutojali majukumu. Kwa ajili hiyo, hakuna budi kupinga
ufisadi na wafanyao ufisadi. Kuupinga ufisadi ni kwa manufaa ya jamii nzima. Na
kuzembea bila ya kuupinga ni maangamizo kwa jamii nzima. Imepokewa kutoka
kwa Nuuman Bin Bashir (Mwenyezi Mungu awawie radhi), kwamba Mtume
(Rehma na amani zimshukie juu yake) alikuwa akisema: “Mfano wa asimamiaye
mipaka ya Mwenyezi Mungu na aliyeivuka ni mfano wa watu waliojazana kwenye
marikebu, wengine wakawa wapo juu na wengine chini, wale waliopo chini
wakiwa wanataka maji huwafuata wale waliopo juu, kisha huwaambia lau kama
sisi tungelichukua fungu letu na wala tusingelikukereni mliopo juu. Iwapo –wa
juu- wangeliwaacha na kile watakacho basi wangelizama wote na wangeliwapa
watakacho basi wangeliokoka wote pamoja.” (Imepokewa na Bukhari).
Hakuna budi kusaidiana, kuwa pamoja na kushikamana kati ya waisilamu ili imani
ipatikane pamoja na undugu wa kiisilamu.
Kuisafisha ardhi na wafanyao ufisadi , na kulinda njia na taasisi ni katika mambo
mema na mazuri. Mwenyezi Mungu huwakinga wafanyao ufisadi kwa kuwepo
watu wema, amesema {Basi mbona hawakuwamo katika watu wa kabla yenu wenye
vyeo na wasaa wanao kataza uharibifu katika nchi, isipo kuwa wachache tu, ambao
ndio tulio waokoa? Na walio dhulumu walifuata starehe zao, na wakawa ni
wakosefu} (Hud. 227). Kwani ufisadi ni ubomoaji wa jamii na hakuna njia ya
kujiokoa nao isipokuwa kuuzuia.
Na umma wa kiisilamu kwa fadhila zake Mwenyezi Mungu una kheri nyingi
kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Kuna bahari, maziwa, mito mikubwa, ndani ya
ardhi muna madini yanayoitajika katika ulimwengu wetu wa kisasa, pia unamiliki
hazina kubwa ya mafuta ulimwenguni, ukizidisha thamanikubwa ya akili na fikira
na watendaji kazi. Kwa ajili hiyo umma hauna budi kuweka vitega uchumi vilivyo
bora, na pia kutumia wakati katika yenye kuleta manufaa kwa watu, na kwa njia ya
kuinua ustaarabu na maendeleo ya kielimu.
Umma wetu ni wa kazi na si wa kupiga uvivu, umma wa kujenga si wa kubomoa
na kuharibu, umma wenye ustaarabu, na kutoendelea si sifa isifikayo katu kwa
umma huu, ni juu ya kila muisilamu mwenye kuipenda dini yake na kujifaharishia
nayo atende kwa ajili ya kuiinua dini yake na kuliinua taifa lake.
Ubora wa maadili katika ujumbe wa Muhammad
25 Rabi`u awal 2548H. Sawa na 36 Disemba 3126 A.D
Kwanza :Vipengele
Uisilamu ni dini ya maadili mema.
Kuporomoka kwa maadili ni kuporomoka kwa umma.
Maadili ni matunda ya matendo sahihi.
namna gani tutatukuka kupitia maadili yetu?
Pili: Dalili
Katika Kurani Tukufu:
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema { Na hakika wewe una tabia tukufu. }
Alqalam, 5.
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema {Shikamana na kusamehe, na amrisha
mema, na jitenge na majaahili} Al aaraf, 2::.
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema {Na ni nani mbora wa kusema kuliko aitae
kwa Mwenyezi Mungu, na akasema: hakika mimi ni katika Waisilamu 45. Mema
na maovu hayalingani. Pinga uovu kwa lililo jema zaidi. Hapo yule ambaye baina
yako naye pana uadui atakuwa kama rafiki jamaa wa kukuonea uchungu. 46. lakini
hawapewi wema huu ila wanao subiri, wala hawapewi ila wenye bahati kubwa.}
Fuswilat 44 -46.
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema { Na waja wa Arrahman Mwingi wa
Rehema ni wale wanao tembea ulimwenguni kwa staha, na wajinga wakiwasemeza
hujibu: Salama! } Alfurqaan, 74.
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema { Ewe mwanangu! Shika Sala, na amrisha
mema, na kataza maovu, na subiri kwa yanayo kupata. Hayo ni katika mambo ya
kuazimiwa. 29. Wala usiwabeuwe watu, wala usitembee katika nchi kwa maringo.
Hakika Mwenyezi Mungu hampendi kila anaye jivuna na kujifakhirisha. 2: Na
ushike mwendo wa katikati, na teremsha sauti yako. Hakika katika sauti mbaya
zote bila ya shaka iliyo zidi ni sauti ya punda.} Luqman, 28-2:.
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema {Soma ulivyofunuliwa katika kitabu, na
ushike sala, hakika sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini
kumdhukuru Mwenyezi Mungu ni jambo kubwa kabisa. Na Mwenyezi Mungu
anayajua mnayoyatenda. 57. wala msijadiliane na watu wa kitabu ila kwa njia iliyo
nzuri kabisa, isipokuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni:
tumeyaamini yaliyo teremshwa kwetu nayaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu
wetu na Mungu wenu ni mmoja. Na sisini wenye kusilimi kwake. } Al ankabuut,
56-57.
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema {Hija ni miezi maalumu. Na anaye kusudia
kufanya Hija katika miezi hiyo, basi asiseme maneno machafu wala asifanye
vitendo vichafu wala asibishane katika Hija. Na kheri yoyote mnayo ifanya
Mwenyezi Mungu anaijua. Na jitengezeeni zawadi. Na hakika bora ya zawadi ni
uchamngu. Na nicheni Mimi, enyi wenye akili !} Al baqarah, 2:8.
Mwenyenzi Mungu Mtukufu anasema {Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa
kudharauliwa, 22. Wanatamani lau unge lainisha ili nao
wakulainishie. 23. Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa
madhambi, 24. Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu. 25. Ati kwa kuwa
ana mali na watoto! 26. Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za
uwongo za watu wa zamani! 27. Tutamtia kovu juu ya pua yake.} Alqalam 21-27.
Katika hadithi za Mtume (Saw)
Kutoka kwa Nawaas bin Sama`n Al-answaary (Mwenyezi Mungu amwie radhi)
kwamba yeye amesema: Nilimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na
amani zimshukie juu yake) kuhusu wema na ubaya? Akasema: “wema ni tabia
njema, na ubaya ni uliopo ndani ya moyo wako na ukachukia watu wengine
wasikione.” (Sahihi Muslim).
Kutoka kwa Abi Dardai (Mwenyezi Mungu amwie radhi), kwamba Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ Hakuna kitu
cha muumini ambacho kitakuwa kina uzito kwenye mizani yake siku ya kiyama
kuliko tabia njema, na hakika ya Mwenyezi Mungu anamchukia muovu mwenye
tabia chafu.” (kitabu cha Tirmidhy).
Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi), amesema: amesema
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) “ Hakika
mimi nimetumwa ili kutimiza matendo mema” (Imepokewa na Imam Ahmad).
Kutoka kwa Abi Durrin (Mwenyezi Mungu amwie radhi), amesema, Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) ameniambia: “ Mche
Mwenyezi Mungu popote ulipo, na fuatishia jema kwa baya ili ulifute, na ishi na
watu kwa tabia njema.” (Imepokewa na Tirmidhiy).
Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi), amesema: amesema
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) “Muumini
aliyekamilika imani ni yule mwenye tabia njema, na mbora wenu ni yule aliye
mbora kwa wake zake.” (Imepokewa na Ahmad).
Kutoka kwa Saa`d bin Hisham bin Amir Al answaari (Mwenyezi Mungu amwie
radhi), amesema: Nilisema “ewe mama wa waumini –yaani Aisha (Mwenyezi
Mungu amwie radhi), - nieleze kuhusu tabia za Mtume wa Mwenyezi Mungu
akasema “ kwani wewe si unasoma Kurani? Nikamwambia ndio, akasema: “Basi
hakika tabia ya Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) ilikuwa ni Kurani.”
(Imepokewa na Muslim).
Kutoka kwa Aisha (Mwenyezi Mungu amwie radhi), amesema: “ nilimsikia
Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema: “ hakika ya muumini hujulikana kwa uzuri
wa tabia zake na kwa vyeo vya kusimama usiku na kufunga mchana.” (Imepokewa
na Abu Daudi.)
Kutoka kwa Jabir (Mwenyezi Mungu amwie radhi), hakika ya Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ hakika ya
nimpendae kati yenu na atakaekuwa karibu nami kwenye kikao siku ya kiama ni
yule mwenye tabia njema, na hakika ya nimchukiae kati yenu na atakaekuwa mbali
nami kwenye kikao siku ya kiama wenye kuropokwa, wenye kusema sana na
wenye kujigamba” Masahaba wakamuuliza ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu
tumekwishamuelewa ni nani mropokwaji na msema sana lakini ni nani huyo
mwenye majigambo ? Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie
juu yake) akasema ni wenye kiburi.” (Amepokea Tirmidhy.)
Tatu: Maudhui
Hakuna shaka ya kuwa namna ya kuupata utukufu ndani ya uisilamu ipo za aina
tofauti, na katika utukufu wake ni kuwa ni dini ya sheria na tabia, inayokusanya
maadili na utu wa hali ya juu, ambau unaweka pamoja sura ya kipekee ya tabia
njema. Na dini hii inatukuka kwa kuwa imekusanya njanja zote za maisha,
haikuacha jema miongoni mwa mambo mema isipokuwa imekusanya na
kulilingania na kuhimiza kulishikilia, wakati huo huo haikuacha ovu isipokuwa
imeliweka wazi na kulitahadharisha na kuamrisha kuliepuka.
Na katika mambo mazuri ambayo yamelinganiwa na kupendezeshwa kwa kuwa
nayo ni: Kujipamba na tabia njema kama subira, upole, huruma, ukweli uaminifu,
kutimiza ahadi, ukarimu, haya, kunyenyekea, ushujaa, uadilifu, wema, kusaidia,
kuweka macho chini, kuondoa uchafu, ubashasha wa uso, maneno mazuri, dhana
nzuri, kumheshimu mkubwa, kusuluhisha kati ya watu, athari njema, kuchunga
hisia za wengine na tabia njema nyenginezo. Na haya yote ni kama ilivyoashiriwa
katika aya ya Kurani Tukufu {Hakika hii kuran inaongoa kwenye yaliyo nyooka
kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata
malipo makubwa.) Al israa :.
Na kwa jambo hili kuna aya na hadithi za Mtume wa Mwenyezi Mungu nyingi
sana, kwa mfano Mwenyezi Mungu anamuamrisha Mtume wake kwa kusema
{Shikamana na kusamehe, na amrisha mema, na jitenge na majaahili} Al a`raf 2::.
Pia anasema {na semeni na watu kwa wema} Al baqara 94. Anaongeza kusema
tena { Hakuna kheri katika mengi ya wanayo shauriana kwa siri, isipo kuwa kwa
yule anaye amrisha kutoa sadaka, au kutenda mema, au kupatanisha baina ya watu.
Na mwenye kufanya hayo kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi tutakuja
mpa ujira mkubwa} Alnisa 255. Na aya zenye ujumbe kama huu ziko nyingi.
Na kwa kila mwenye kuzingatia aya a Kurani na akachuguza kwa kina atagundua
ya kuwa muna aya nyingi sana zenye kulingania katika tabia njema na kuhimiza
watu wawe nazo. Na si kwa chochote zaidi ya kuwa tabia ni kama mizani ya
kisheria yenye kumpima mtu na kumpandisha mtu daraja za ukamilifu.
Na kama hadithi za Mtume wa Mwenyezi Mungu zilivyosisitiza juu ya umuhimu
wa tabia katika maisha ya mwanadamu. Kwa kuweka wazi malipo kwa mwenye
kuwa nazo, kwa mfano Mtume wa Mwenyezi Mungu anasema: “wema ni tabia
njema” (imepokewa na Imam Muslim.) na wema ni neno lenye kumaanisha kila
lililo zuri. Na hadithi nyengine ya Mtume wa Mwenyezi Mungu: “ Hakuna kitu
cha muumini ambacho kitakuwa kina uzito mkubwa kwenye mizani kushinda tabia
njema” na katika mapokezi mengine: “ Hakuna kitu cha muumini ambacho
kitakuwa kina uzito mkubwa kwenye mizani siku ya kiyama kuliko tabia njema, na
hakika ya Mwenyezi Mungu anamchukia muovu mwenye tabia chafu.”
(imepokewa na Tirmidhy katika kitabu chake kutoka kwa Abi Dardai.)
Na hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa akihimiza watu wawe na tabia
njema, kwani baadhi ya wakati huwa anasema “Muumini aliyekamilika imani ni
yule mwenye tabia njema, na mbora wenu ni yule aliye mbora kwa wake zao.”
(Imepokewa na Ahmad).
Na akaulizwa Mtume wa Mwenyezi Mungu: “ Ni muumini gani aliye bora?
Akasema: “ Mwenye tabia njema kuliko wote” (imepokewa na Ib Maajah.
Na Mtume wa Mwenyezi Mungu alipoulizwa kuhusu kitu ambacho kitawaingiza
kwa wingi watu peponi akasema: “ucha Mungu na tabia njema.” (Kitabu cha
Tirmidhy.)
Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake)
akafanya kuwa miongoni mwa mapenzi ya kumpenda yeye ni kuwa na tabia
njemaakasema: “hakika ya nimpendae kati yenu na atakaekuwa karibu nami
kwenye kikao siku ya kiama ni yule mwenye tabia njema.” (Kitabu cha Tirmidhy.)
Maadili yana nafasi yake kubwa sana ndani ya uisilamu, kwani ni kiini cha dini na
johari yake. Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake)
alipoulizwa: “ dini ni nini? akasema: “tabia njema” (Imepokewa na Muslim.)
Si hivyo tu bali pia Mtume wa Mwenyezi Mungu amezipa tabia umuhimu wa hali
ya juu pale alipotangaza kwa kusema kuwa, lengo kuu la kutumwa kwake na la
ujumbe wake ni kutimiza maadili mema akasema: “ hakika nimetumwa kwa ajili
ya kutimiza tabia njema.” (Imam Buhkari.)
Na hata kabla utume watu walikuwa wakimuita mkweli muaminifu. Hizo ndizo
tabia njema za kiisilamu ambazo zinakwenda sambamba na imani ya ukweli,
kwani Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake)
alikuwa ni mfano wa hali ya juu kabisa wa tabia njema, kwa ajili hiyo Mwenyezi
Mungu Mtukufu Mola wake akamsifu kwa kusema {Na hakika wewe una tabia
tukufu} Al qalam 5.
Na huu ni ushahidi mkubwa sana kutoka kwa Mkuu Alietukuka kwa Mtume wake
(Rehma na amani zimshukie juu yake), kwa uzuri wa tabia yake na wema wa
maadili yake. Hakika ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani
zimshukie juu yake) alikuwa ni mwenye tabia njema kuzidia wote, kwani tabia ya
Kurani yote aliikusanya yeye na akawa anaifuatisha na kujiepusha na makatazo
yake, hapo ubaora ndipo ulipojikusanya na haya yanathibitishwa na mama wa
waumini Aisha (Mwenyezi Mungu amwie radhi), alipoulizwa kuhusu tabia ya
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) akasema: “
tabia yake ilikuwa ni Kurani.”
Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa ni mfano wa kimatendo katika kuifuata
Kurani, alikuwa ni mwenye tabia bora zaidi kuliko watu wote, na pia alikuwa na
upendo, huruma, ucheshi, msamaha kuzidi wote, mkweli anapozungumza,
anapotoa ahadi, na mkarimu kwenye familia, na ni mfano katika unyenyekuvu
pamoja ya kuwa yeye ni bwana wa viumbe, amuonae ni lazima amtukuze,
ukiungana nae basi utampenda.
Mama wa waumini Khadija (Mwenyezi Mungu amwie radhi), amemtakasa Mtume
wa Mwenyezi Mungu kwa kumwambia: “ hakika wewe utaunga koo, utavumilia
vishindo, utampata asiyekuwepo na utakuwa ni mwenye kuwarudisha watu katika
haki.”
Na Mola wake pia akamsifu kwa kusema {Basi ni kwa sababu ya rehema itokayo
kwa Mwenyezi Mungu ndio umekuwa laini kwao. Na lau ungeli kuwa mkali,
mwenye moyo mgumu, bila ya shaka wangeli kukimbia. Basi wasamehe, na
waombee maghfira, na shauriana nao katika mambo. Na ukisha kata shauri basi
mtegemee Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanao
mtegemea} Al imraan 26:. Na kwa tabia hii basi Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Rehma na amani zimshukie juu yake) ameweza kuathiri nyoyo na akili.
Mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) aliwalea masahaba zake katika tabia
njema na kuwaamrisha kujipamba nayo na kuishikilia, na haya ni kama alivyosema
kumambia Abi Dhari (Mwenyezi Mungu amwie radhi), “ mche Mwenyezi Mungu
popote ulipo na fuatishia jema kwa baya ili ulifute, na ishi na watu kwa tabia
njema.” Wakajifunza upole, msahama na hisani na kujiepusha na maasi na hasira
wakawa ni wema na wavumilivu, wakawa pia ni mfano wa hali ya juu katika tabia
na muamala na ukarimu sawa kwa mtu mmoja mmoja au kwa pamoja.
Mtume wa Mwenyezi Mungu alipohama kutoka Makka kwennda Madina na
kuwaunganisha undugu kati ya muhajirina na Maanswari, Ansari alikuwa
akimuunga mkono ndugu yake muhajirina kwa nusu ya mali yake, kwani tabia ya
mwanadamu hujulikana kwa kadir ya utoaji wake, na kurani metupa mfano mzuri
ambao haukusudii kumlenga mtu maalumu, isipokuwa ni sifa kwa waumini wote,
Mwenyezi Mungu anasema {bali wanawapendelea kuliko nafsi zao ingawa
wenyewe ni wahitaji} Al hashri :.
Kwa ajili ya tabia hizo umma ukaongoza, ukawa unaangaliwa kuwani igezo kwa
kule kushikamana na tabia njema iliyotukuka. Na watu walikuwa wakiingia katika
dini ya Mwenyezi Mungu kwa makundi kwa kuona tabia na muamala mzuri, na
maadili mema. Ama wakati tabia zilipoanza kubadilika na maadili ya watu kuanza
kupotea; kigezo chema kikatoweka na ufahamu ukabadilika, hakika amesema
kweli imamu Malik (Mwenyezi Mungu amwie radhi), aliposema “Umma huu wa
mwisho hautopata kuwa mzuri isipokuwa kwa kufuata umma wa mwanzo.”
Maadili ni kitu bora ambayo jamii kujikinga na upotovu, na kuihifadhi na
misukosuko na kupotea, amani ya umma na nguvu za ujenzi wake na kuimarika
nafasi yake ipo katika maadili mema. Na kama ilivyo kuwa kuenea kwa uchafu na
maovu ni kwa sababu ya kujiweka mbali na maadili mema na vitendo vizuri.
“Tengeneza tabia yako kwa matendo mazuri * ijenge nafsi yako kwa maadili ili
isiyumbe.
Ipe nafsi ubora naa fya njema * kwani nafsi kwa maovu huwa duni.
Kwa ajili hiyo, kuwa na hadhari juu ya kuporomoka kwa maadili ni jambo la
kusisitizwa. Kutoka kwa Sahli bin Saa`d Saa`idi (Mwenyezi Mungu amwie radhi),
kwamba yeye amemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani
zimshukie juu yake) akisema: “ Hakika ya Mwenyezi Mungu ni Mkarimuna
anawapenda wakarimu na hupenda tabia njema na huchukia mambo machafu.”
Maadili hulifanya taifa kukua na athari zake hubakia milele, na kwa kutokuwa na
maadili mema taifa husambaratika na huanguka. Ni Staarabu ngapi zimeporomoka
na si kwa sababu ya hali mbaya ya kiuchumi au nguvu zake za kijeshi lakini ni
kwa sababu ya kuwa na maadili maovu. Mwenyezi Mungu amrehemu kiongozi wa
mashairi. Aliposema:
Hakika umma utabakia kwa kubaki maadili * wakikosa maadili basi na umma
hutoweka.
Na ukizingatia ibada ndani ya kurani na hadithi za Mtume tutagundua kuwa
malengo hasa makuu ni: kuijenga tbia njema ya muisilamu na kumpamba kwa
maadili, hakuna ibada ambayo Mwenyezi Mungu ameiamrisha mfano; sala,
saumu, zaka, na kuhiji isipokuwa ina athari ambayo inaonekana ndani ya tabia ya
mtu, si hivyo tu, bali tabia hii huathiri mtu hadi jamii kwa ujumla. Uisilamu si
kufanya ibada zisizo na natija ndani ya msikiti ambazo hazina mfungamano na
maisha ya nje (ya msikiti), ikawa aliyesali baada ya sala atoke kisha afanye ghoshi,
adanganye, amuudhi jirani yake, si hivyo. Lakini ibada zimeletwa kwenye dini
zote ili mwanadamu awe na utu na tabia iwe njema. Kwa mfano sala, Mwenyezi
Mungu ametuwekea wazi hekima yakusaliwa. Akasema {Soma ulivyofunuliwa
katika kitabu, na ushike sala. Hakika sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na
kwa yakini kumdhukuru Mwenyezi Mungu ndio jambo kubwa kabisa. Na
Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyatenda.} Al ankabuut 56. kujiepusha na maovu
na kujitakasa na kauli chafu na matendo mabaya hivi ndivyo sala itakiwavyo.
Kutoka kwa Ibn Abass (Mwenyezi Mungu awawie radhi), amesema: Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “amesema
Mwenyezi Mungu Mtukufu: hakika ninaikubali sala kwa anaenyenyeyekea kwa
utukufu wangu, na akawa hajitukuzi mbele ya waja wangu, na wala haendelei
kuniasi, na akawa naumaliza mchana wake kwa kunitaja, na kuwahurumia
masikini, na wapiti njia na wajane, na kuwahurumia wenye matatizo..”
(Imepokewa na Bazaz.)
Na kutoka kwa Ib Masu`ud (Mwenyezi Mungu amwie radhi): “ Yule ambaye sala
yake haimuamrishi kutenda mema na wala haimkatazi kuacha mabaya
hatozidishiwa kwa Mwenyezi Mungu isipouwa kutengwa mbali.” (Imepokewa na
Twabari). Basi yule ambaye sala yake haimuweki mbali na maovu sawa iwe ya
maneno au matendo, mtu huyu basi sala yake itakuwa haimfikishi katika lengo
miongoni mwa malengo makubwa ya sala.
Na namna hiyo hiyo kwa upande wa utoaji wa zaka, kufunga, kuhiji na kwa
upande wa ibada nyengine, utaona kuwa zimewekwa kwa kuitakasa nafsi na
kumfanya mja atukuke kimaadili, na Mwenyezi Mungu anasema khusu zaka:
{Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo, na uwaombee
rehema. Hakika maombi yako ni utulivu kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye
kusikia Mwenye kujua.} Al taubah 214.
Hivyo basi Mtume wa Mwenyezi Mungu akalipambanua zaidi neno sadaka
ambayo ni inampasa muisilamu kuitoa, imepokewa kwa Abi Dhari (Mwenyezi
Mungu amwie radhi) amesema, amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (Rehma
na amani zimshukie juu yake) “kutabasamu mbele ya uso a mwenzako ni sadaka,
na kuiweka tupu ndoo yako na kuijaza ya mwenzako ni sadaka, kuamrisha mema
na kukataza mabaya pia huandikiwa sadaka, kuondoa mwiba na jiwe njiani ni
sadaka, kumuongoza aliyepotea njia pia ni sadaka.” (Imepokewa na Bazaz).
Na swaumu ni ibada miongoni mwa ibada alizozifaradhisha Mwenyezi Mungu
kwa ajili ya kufanikisha uchamungu, matunda na malengo ambayo Mwenyezi
Mungu anayataka yafikiwe na mja ni uchaji Mungu, akasema Mwenyezi Mungu
Mtukufu: {Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, kama waliyo andikiwa walio
kuwa kabla yenu ili mpate kuchamngu} Albaqara 294.
Kwa kupitia funga utashi wa muumini huwa na nguvu na anakuwa na uwezo wa
kuidhibiti nafsi yake na matamanio yake, kwani imepokewa kutoka kwa Abi
Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi), hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu
amesema: “ Funga ni kinga, basi asisema maneno mabaya wala kutenda mabaya,
na iwapo mtu amempiga au kumtusi basin a aseme; mimi nimefunga.”
(Imepokewa na Bukhari). Hii inamaanisha kuwa funga yake inabidi imlinde na
kuwa na tabia chafu na matendo maovu, funga ni lazima iache athari za tabia
njema kwa muisilamu na katika maadili yake.
Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: {Hija ni miezi maalumu. Na anaye kusudia
kufanya Hija katika miezi hiyo, basi asiseme maneno machafu wala asifanye
vitendo vichafu wala asibishane katika Hija. Na kheri yoyote mnayo ifanya
Mwenyezi Mungu anaijua. Na jitengezeeni zawadi. Na hakika bora ya zawadi ni
uchamngu. Na nicheni Mimi, enyi wenye akili!} Albaqara 2:8. Na kutoka kwa Abi
Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi), amesema: amesema mjumbe wa
Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake): “ atakaeijia nyumba hii
akawa hajanena upuuzi, na wala kufanya uchafu basi atakuwa amerejea kama
kwamba amezaliwa na mama yake”. (Imepokewa na Muslim.)
Kwa upande wa ibada ni lazima iache athari njema kwa mtu na kwa jamii, na
iwapo ibada hazitoleta athari yoyote kwa mtu na maadili yake na nyenendo zake
huwa haina thamani yoyote siku ya kiyama, kwa sababu matendo maovu hula zile
ibada na mema kama ambavyo moto unavyokula kuni. Imepokewa na Abi Hurayra
(Mwenyezi Mungu amwie radhi), Kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma
na amani zimshukie juu yake) amesema: “ Munamjua ni nani muflisi? Wakamjibu,
mtu aliyefilisika miongoni mwetu ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni yule asiye
na dirhamu wala starehe, akasema (Rehma na amani zimshukie juu yake) “ Mtu
aliyefilisika katika umma wangu ni yule atakaekuja siku ya kiama na sala zake,
funga zake, na zaka zake, na atakuja hali ya kuwa kamtukana huyu, kamzulia
huyu, amekula mali ya huyu na kumwaga damu ya huyu na amempiga huyu,
atakaa na kupunguzwa katika mema yake, n kwa huyu yatachukuliwa mema yake,
na yatakapomalizika mema yake, kabla ya kumaliza kuhesabiwa huchukuliwa
madhambi yao na kupewa yeye kisha hutumbukizwa motoni.” (Imepokewa na
Tirmidhy.)
Na alipoulizwa (Rehma na amani zimshukie juu yake) ewe mjumbe wa Mwenyezi
Mungu; “ hakika ya fulani hutajwa kwa kuwa anasali sana, anafunga sana, na
anatoa sadaka sana isipokuwa anawakera majirani zake kwa ulimi wake, akasema;
“yeye ataingia motoni”. Akasema: “ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika ya
fulani hutajwa kuwa ni mchache wa kufunga, na sadaka zake, na sala zake naye
hutoa sadaka kwa, isipokuwa hawakeri majirani zake kwa ulimi wake; akasema
“yeye ataingia peponi.” (Imepokewa na Ahmad).
Hakika tabia njema (maadili mema) inakusanya kwa viumbe vyote, hakuna tafauti
kati ya muisilamu na asiye muisilamu, wote ni ndugu kwa ubinaadamu, Mwenyezi
Mungu Mtukufu anasema {Na hakika tumewatukuza wanaadamu, na tumewapa
vya kupanda nchi kavu na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na
tumewafadhilisha kwa fadhila kubwa kuliko wengi miongoni mwa tulio waumba}
Israa 81.
Na Mtume wa Mwenyezi Mungu aliposimama lilipopitishwa, akaambiwa: ni
jeneza la Myahudi, mtume (Rehma na amani zimshukie juu yake) “je kwani si
nafsi? (imepokewa na Bukhari).
Na Mwenyezi Mungu {wala msijadiliane na watu wa Kitabu ila kwa njia iliyo
nzuri kabisa, isipokuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni:
Tumeyaamini yaliyo teremshwa kwetu na yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu
wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake.} Al ankabuut
57. Na kutoka kwa Mujahid, kwamba Abdallah bin Amru (Mwenyezi Mungu
amwie radhi), amechinjiwa mbuzi na familia yake, alipofika akasema: je
mumempa jirani yetu myahudi? Je mumempa jirani yetu myahudi? Nimemsikia
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) akisema: “
Jibrilu hakuacha kuniusia kuhusu jirani mpaka nikadhani kuwa anaweza kumrithi”
(Imepokewa na Tirmidhy.)
Na tabia njema si kwa wanaadamu tu pekee, isipokuwa inakusanya hata wanyama
pia, kwani Mwenyezi Mungu amemuingiza kijana peponi kwa sababu ya mbwa
aliyemyweshelezea maji. Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie
radhi), “hakika ya kijana alimuona mbwa anakula mchanga kutokana na kiu, kijana
akachukua khofu yake akawa anamchotea kwayo maji mpaka akamywesha,
akamshukuru Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu akamuingiza peponi”
(Imepokewa na Bukhari). Na namna kama hiyo Mwenyezi Mungu amemuingiza
mtu motoni kwa sababu ya paka, imepokewa na Ibn Umar (Mwenyezi Mungu
awawie radhi), hakika ya Mwenyezi Mungu amesema “mwanamke ameadhibiwa
kwa sababu ya paka amemfunga na wala hakumuacha huru akila masalia ya
ardhini.” (Imepokewa na Bukhari).
Iwapo tunataka kujiimarisha kitabia na kuinuka kwa jamii yetu hatuna budi kufuata
vigezo vyema. Vigezo ni kitendea kazi muhimu katika kujenga maadili, Mwenyezi
Mungu anasema {Hakika nyinyi mnayo ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi
Mungu kwa anaye mtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na
akamkumbuka Mwenyezi Mungu sana } Al Ahzab 32. Kwani mzazi anatakiwa
kuwa ni kigezo kwa mwanawe, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani
zimshukie juu yake) ametueleza kwamba ya mtoto huzaliwa katika maubile safi,
maumbile ya Mwenyezi Mungu aliyowaumbia watu, kisha tena kigezo ndicho
kitakachombadilisha ima kizuri au kibaya. Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi
Mungu amwie radhi), amesema, amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (Rehma
na amani zimshukie juu yake) “ hakuna kizaliwacho isipokuwa huzaliwa katika
maumbile (uisilamu), ima baba yake humfanya kuwa myahudi, au mnasara au
mmajusi...” Kisha akaendelea kusema Abu Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie
radhi), {Basi uelekee uso wako sawasawa kwenye dini – ndilo umbile la
Mwenyezi Mungu alilowaumbia watu. Hapana mabadiliko katika uumbaji wa
Mwenyezi Mungu. Hiyo ndiyo dini iliyoonyoka sawa.} Ruum 41. (Imepokewa na
Bukhari).
Vile vile mwalimu ni kigezo kwa wanafunzi kwa mwenendo wake na tabia zake,
wanafunzi inabidi wawe kama yeye kitabia. Siku moja imam Shafii ameingia kwa
Harun Rashid pamoja na kijana Siraj, akawakaribisha na kuwaambia wakae kitako
mbele ya Abdul-swamad ambae ni mwalimu wa watoto wa Rashid. Siraj akasema
kumwambia Shafii: ewe Abu Abdallah! Hawa ni watoto wa Amir Muuminina,
naye ni wanafunzi wake, unaonaje lau kama ungeliwausia.. Imam Shafii
akamwelekea Abi Abdul-swamad akamwambia, “iwe kwako ewe kiongozi wa
waumini ukitaka kuwarekebisha wanao ni itakubidi kuirekebisha nafsi yako
kwanza, kwani macho yao yanaangalia macho yako, zuri kwao ni lile
utakalolipenda wewe, na baya kwao ni lile uliachalo…” (Kitabu cha Hilliya
Awliyaa. Abi Na`im).
Na jambo lililo muhimu kukumbushia ni kwamba, tabia za mtu binafsi ambazo
hujilazimisha kuacha na kujikataza na kitu, n.k. na kuna tabia za kifamilia kati ya
mtu na mkewe na kati ya mtu na wanawe na wazazi wake na watu wa karibu nae
na ukoo wake na mfano wake. Pia kuna tabia za kijamii kwa mfano katika kuuza,
kununua, ujirani, urafiki, kazini, … n.k. na pia kuna tabia za kimataifa kati ya nchi
na nchi, na tabia za wakati wa vita na wakati wa usalama.
Na katika mambo ambayo humsaidia mja katika kuwa na tabia njema ni: kufanya
kitu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kisha kuomba awe na tabia njema, na pia
kujitahidi ndani ya nafsi yake ili ashinde matamanio, na kuihesabu nafsi kila siku
pamoja na kuzingatia mwisho wa kuwa na tabia mbaya na kwa yaliyowafika watu
walioishi kwenye jamii mbaya.
Miongoni mwa aliyokirimiwa Mtume Muhammad
(Saw)
1 Rabiul awwal, 0341 H. Sawa na 01 Disemba 6102 A.D.
Kwanza: Vipengele
1. Kukirimiwa kwake Mtume Muhammad (Saw) tangu mwanzo wa
kuumbwa.
2. Kukirimiwa kwake Mtume Muhammad (Saw) kabla ya kuzaliwa.
3. Kukirimiwa kwake Mtume Muhammad (Saw) kwa kuwemo katika na
familia njema.
4. Kutajwa jina lake Mtume Muhammad (Saw) kunaendana sambamba
na utukufu wa utume na ubora wa risala.
5. Wajibu wa kumpenda na kumtii Mtume Muhammad (Saw).
6. Kukirimiwa kwake Mtume Muhammad (Saw) kwa kupata ulinzi
utokao kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
7. Ujumbe wake ni kwa walimwengu wote.
8. Ujumbe wake ni rehem kwa walimwengu wote.
Pili: Dalili
Dalili ndani ya Kurani Tukufu
1. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Na pale Mwenyezi Mungu alipo
chukua ahadi kwa Manabii: Nikisha kupeni Kitabu na hikima, kisha
akakujieni Mtume mwenye kusadikisha mliyo nayo, ni juu yenu mumuamini
na mumsaidie. Akasema: Je, mmekiri na mmekubali kushika agizo langu juu
ya hayo? Wakasema: Tumekubali. Akasema: Basi shuhudieni, na Mimi ni
pamoja nanyi katika kushuhudia.} (Al Imraan aya ya 81).
2. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: { Ewe Mola Mlezi wetu! Waletee
Mtume anaye tokana na wao, awasomee Aya zako, na awafundishe Kitabu
na hikima na awatakase. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye
hikima.} Albaqarah aya 129.
3. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: { Na Isa bin Mariamu alipo sema: Enyi
Wana wa Israili! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu,
ninaye thibitisha yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati, na mwenye
kubashiria kuja Mtume atakaye kuja baada yangu; jina lake ni Ahmad!
Lakini alipo waletea hoja zilizo wazi, walisema: Huu ni uchawi ulio
dhaahiri! } Assa`f aya 2.
4. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Mwenye kumt'ii Mtume basi ndio
amemt'ii Mwenyezi Mungu. Na anaye kengeuka, basi Sisi hatukukutuma
wewe uwe ni mlinzi wao } Al nisaa aya 11.
5. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: { Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda
Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na
atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta
madhambi na Mwenye kurehemu.} Al Imraa aya 31.
6. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Ewe Mtume! Fikisha uliyo
teremshiwa kutoka kwa Mola wako Mlezi. Na ikiwa hukufanya hayo basi
hukufikisha ujumbe wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu. Hakika
Mwenyezi Mungu hawaongoi watu makafiri} Al maidah aya 21.
7. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Na hatukukutuma ila kwa watu
wote, uwe mbashiri, na mwonyaji. Lakini watu wengi hawajui } Sabaa 61.
8. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Nasi hatukukutuma ila uwe ni
Rehema kwa walimwengu wote} Al anbiyaa aya011.
9. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika
wake wanamsalia Nabii. Enyi mlio amini! Msalieni na mumsalimu kwa
salamu } Al ahzaab 22.
11. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Msifanye wito wa Mtume baina yenu
kama wito wa nyinyi kwa nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu anawajua
miongoni mwenu wanao ondoka kwa uficho. Basi nawatahadhari wanao
khalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu} Al
nuur aya 24.
Dalili ndani ya hadithi
1. Kutoka kwa Waathila bin Asqa`a (Mwenyezi Mungu amwie radhi)
amesema: nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema: “ hakika ya
Mwenyezi Mungu amechagua Kabila la Kinana kutoka katika kizazi cha
Ismaili, na akawachagua Maquraishi kuwa ndio kutoka kwa Kabila la
Kinana, na katika maquraishi ukachagulia ukoo wa bani Hashim, na katika
ukoo wa bani hashim akanichaguwa mimi”. (Imepokewa na Muslim).
6. Kutoka kwa Irbaadh bin Saariya Salamiy amesema: nimemsikia Mtume
wa Mwenyezi Mungu akisema: “ … mimi ni kutokana na maombi ya baba
yangu Ibrahim, na bishara ya Isa kwa watu wake, na nikutokana na ndoto
ya mama yangu ambaye ameona nuru imechomoza na kuangaza
majumba ya Sham.” (Kitabu cha Imam Ahmad).
4. Kutoka kwa Abi Saaed (Mwenyezi Mungu amwie radhi), kutoka kwa
Mtume (Saw) kwamba yeye amesema: “Jibrilu alinijia akaniambia: hakiak
mola wako na mola wangu anasema: Ni namna gani nimenyanyua utajo
wako? Mtume akajibu: Mwenyezi Mungu ndie ajuae: Jibrilu akasema:
nitajwapo mimi nawe hutajwa pamoja nami”) (Kitabu cha Zawaed cha
Imam Haytham).
4. Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema,
hakika mjumbe wa Mwenyezi Mungu amesema “yeyote atakaenitii mimi
basi kwa hakika amemtii Mwenyezi Mungu, na atakaeniasi basi kwa
hakika amemuasi Mwenyezi Mungu” (Imepokewa na Muslim na
Bukhari).
5. Kutoka kwa Anas (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema, amesema
mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie) “hatoamini
mmoja wenu mpaka niwe ananipenda zaidi kuliko wazazi wake watoto
wake na watu wote.” (Imepokewa na Muslim na Bukhari).
6. Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema,
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie),
“hakika mimi ni rehema yenye kuongoa” (Imepokewa na Imam Hakim
katika kitabu cha Mustadrik).
1. Kutoka kwa Jabir bin Abdi Llah (Mwenyezi Mungu awawie radhi
amesema: amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie): “ nimepewa mambo matano hakuna nabii yeyote aliyepewa
kabla yangu: nimepewa ushindi wa kuwahofisha maadui kwa mwendo wa
mwezi, nikafanyiwa ardhi kuwa ni msikiti na ipo safi na mtu yeyote katika
umma wangu akifikwa na swala basi na aswali, na nimehalalishiwa
ngawira, na ilikuwa nabii akipelekwa (akitumwa) kwa watu wake
maalumu, ama mimi nimetumwa kwa watu wote, na nimepewa uombezi.
((Imepokewa na Bukhari).
Tatu: Maudhui
Hakika Mwenyezi Mungu amemkirimu mtume wake, ukarimu ambao
hajawahi kumpa yeyote katika waja wake, mwanzo wa kuumbwa kwake
(rehma na mani ziwe juu yake), kabla ya kuzaliwa kwake (rehma na amani
ziwe juu yake), baada ya kuzaliwa kwake (rehma na amani ziwe juu yake),
dani ya maisha yake na baada ya kufariki kwake (rehma na amani ziwe juu
yake).
Ama ukarimu aliokirimiwa na Mwenyezi Mungu mwanzo wa kuumbwa ni;
Mwenyezi Mungu ameuinua utajo wake kwa waliotangulia (umma wa
mwanzo) na waliochelewa (umma wa mwisho), kwani hakuna Mtume yeyote
aliyetumwa na Mwenyezi Mungu – kabla yake (rehma na amani ziwe juu
yake) isipokuwa amechukua ahadi na utiifu iwapo atakutana na Mtume
rehma na amani ziwe juu yake) basi atamuamini na kumnusuru, Mwenyezi
Mungu mtukufu anasema: {Na pale Mwenyezi Mungu alipo chukua ahadi
kwa Manabii: Nikisha kupeni Kitabu na hikima, kisha akakujieni Mtume
mwenye kusadikisha mliyo nayo, ni juu yenu mumuamini na mumsaidie.
Akasema: Je, mmekiri na mmekubali kushika agizo langu juu ya hayo?
Wakasema: Tumekubali. Akasema: Basi shuhudieni, na Mimi ni pamoja nanyi
katika kushuhudia} (Al imraan aya 81). Mwenyezi Mungu Mtukufu
akamzidishia Mtume wake rehma na amani ziwe juu yake) ubora na heshima
kwa ahadi hii ambayo imeshuhudiwa na Mitume wengine pia.
Na mitume waliotangulia pia walimbashiria, kutoka kwa Irbaadh bin sariyata
Salamiy amesema: nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema: “mimi
ni kutokana na maombi ya baba yangu Ibrahim, na bishara ya Issa kwa watu
wake, na nikutokana na ndoto ya mama yangu ambaye ameona nuru
imechomoza na kuangaza majumba ya Sham.” (Kitabu cha Imam Ahmad).
Na maombi ya sayidna Ibrahim (A.S) ni pale aliposema { Ewe Mola Mlezi
wetu! Waletee Mtume anaye tokana na wao, awasomee Aya zako, na
awafundishe Kitabu na hikima na awatakase. Hakika Wewe ndiye Mwenye
nguvu, Mwenye hikima.} Albaqara 061. Ama bishara ya sayidna Isa (A.S) ni
pale aliposema Mwenyezi Mungu { Na Isa bin Mariamu alipo sema: Enyi
Wana wa Israili! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu, ninaye
thibitisha yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati, na mwenye kubashiria kuja
Mtume atakaye kuja baada yangu; jina lake ni Ahmad! Lakini alipo waletea
hoja zilizo wazi, walisema: Huu ni uchawi ulio dhaahiri} Assa`f 6).
Na kuhusu kukirimiwa kwake Mtume Muhammad (rehma na amani ziwe juu
yake) na Mwenyezi Mungu kabla ya kuzaliwa kwake, ni kule kuitwa
Muhammad. Amina bint Wahab alipokuwa akielezea namna alivyomzaa
Mtume (rehma na amani ziwe juu yake). Nimewasikia waliokuwa
wakimbwambia; “ wewe umebeba mamba ya bwana wa umma huu,
utakapomzaa tu basi sema: ninamrudisha kwa aliye Mmoja na aepukane na
kila shari ya mwenye husuda, kisha umpe jina la Muhammad, kwani jina lake
ndani ya kitabu cha Taurati ni Ahmad, atashukuriwa na wakazi wa ardhini na
wa mbinguni. Na jina lake ndani ya kitabu cha Injili ni Ahmad atashukuriwa
na wakazi wa ardhini na wa mbinguni.. na jina lake ndani ya Kurani ni
Muhamad basi umwite kwa jina hilo. (Imam Bayhaqiy).
Hivyo basi, ukoo wake katika koo njema zaidi ya koo nyengine, kwani yeye
rehma na amani ziwe juu yake) ni katika kizazi cha familia iliyo bora zaidi,
imesemwa hayo na Mwenyezi Mungu { Na mageuko yako kati ya wanao
sujudu } Ashuaraa aya 601, amesema Ibn Abbas, kinachokusudiwa ni katika
migongo ya mababu, Sayidna Adam (A.S), Sayidna Nuh (A.S) na Sayidna
Ibrahim (A.S) mpaka akazaliwa mtume wetu rehma na amani ziwe juu yake).
(Tafsiri Ibn kathir).
Familia yake ni bora, na ni nyumba njema katika nyumba za waarabu, kwani
Mwenyezi Mungu ameihifadhi na maovu ya kijahilia, na akamtoa katika
migongo mitukufu mpaka kwenye tumbo jema kutoka kizazi hadi kizazi.
Mwenyezi Mungu amechagua Kabila la Kinana kutoka katika kizazi cha
Ismaili, na akawachagua Maquraishi kuwa ndio kutoka Kinana, na katika
maquraishi ukachaguliwa ukoo wa bani Hashim, naye Mtume (rehma na
amani ziwe juu yake) ni katika uchaguzi ulio bora na mwema. Imepokewa na
Waathila bin Asqa`a (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: nimemsikia
Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema: “ hakika ya Mwenyezi Mungu
amechagua Kabila la Kinana kutoka katika kizazi cha Ismaili, na akawachagua
Maquraishi kuwa ndio kutoka Kinana, na katika maquraishi ukachagulia ukoo
wa bani Hashim, na katika ukoo wa bani hashim akanichaguwa mimi”.
(Imepokewa na Muslim).
Ama kukirimiwa kwake na Mwenyezi Mungu katika maisha yake rehma na
amani ziwe juu yake). Jina na utajo wake umenyayuliwa duniani na akhera,
kwani jina la Mwenyezi Mungu huwa halitajwi isipokuwa na jina la Mtume
rehma na amani ziwe juu yake) hutajwa pamoja nae. Hakika amesema kweli
Mwenyezi Mungu: {tukaunyajua utajo wako}.
Kutoka kwa Abi Saaed (Mwenyezi Mungu amwie radhi), kutoka kwa Mtume
(Saw) kwamba yeye amesema: “Jibrilu alinijia akaniambia: hakika mola wako
na mola wangu anasema: Ni namna gani nimenyanyua utajo wako? Mtume
akajibu: Mwenyezi Mungu ndie ajuae: Jibrilu akasema: nitajwapo mimi nawe
hutajwa pamoja nami”) (Kitabu cha Zawaed cha Imam Haytham).
Na Mwenyezi Mungu ameliweka pamoja jina lake na jina la Mtume wake
rehma na amani ziwe juu yake) katika sehemu nyingi, kwani hata shahada ya
anaesilimu huwa haikubaliwi mpaka amshuhudie kuwa yeye ni mjumbe
mtume na upweke wa Mwenyezi Mungu.
Amesema Hassan bin Thabit (Mwenyezi Mungu amwie radhi):
Jina la Mwenyezi Mungu lipo na la mtume * pindi Muadhini akisoma adhana.
Hutaja jina hilo kwa utukufu * kwenye arshi ni Mahmud na huyu hapa ni
Ahmad.
Jina la Mtume (rehma na amani ziwe juu yake) hutajwa atajwapo Mwenyezi
Mungu kwenye shahada mbili, kwenye hutuba ya Ijumaa, ndani ya Kurani
Tukufu. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ameweka sambamba utiifu wa
mtume kua ndio utiifu wa Mwenyezi Mungu, akasema: {Mwenye kumt'ii
Mtume basi ndio amemt'ii Mwenyezi Mungu. Na anaye kengeuka, basi Sisi
hatukukutuma wewe uwe ni mlinzi wao} Al nisaa 11.
Ibnu Abbas (Mwenyezi Mungu awawie radhi) alikuwa akisema: Aya tatu
zimeteremshwa na kuambatana sambamba na aya tatu, hakuna aya hata
moja yenye kukubalika bila ya aya nyengine (iliyo sambamba nae).
Ya kwanza: { Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na inameni pamoja na wanao
inama } Albaqarah 34.
Ya pili : { Nishukuru Mimi na wazazi wako} Luqman 14.
Ya tatu: {Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume} Al
nisaa 59. kwani atakaemtii Mwenyezi Mungu na kuacha kumtii Mtume
(rehma na amani ziwe juu yake) mtu huyo haikubaliwi ibada yake.
Pia Mwenyezi Mungu ameweka sambamba uteuzi (uchaguzi) wa kumteua
mtume (rehma na amani ziwe juu yake) kuwa sana na kumteua Yeye
Mwenyezi Mungu. Amesema {Bila ya shaka wanao fungamana nawe, kwa
hakika wanafungamana na Mwenyezi Mungu.} Al fathi aya 01. a kufanya
kuwa, kumtii Mtume (rehma na amani ziwe juu yake) kuwa ni moja ya
mafanikio ya kuingia peponi, akasema { Na anaye mt'ii Mwenyezi Mungu na
Mtume wake, bila ya shaka amefanikiwa mafanikio makubwa.} Al ahzaab
aya 10. Na aya nyenginezo.
Na imekuja katika hadithi kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie
radhi) hakika mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani ziwe juu yake)
amesema: “ watu wote katika umma wangu wataingia peponi isipokuwa
atakaekataa”, akaulizwa: na ni nani atakaekataa ewe mjumbe wa Mwenyezi
Mungu? Akasema: “ atakaenitii mimi ndie atakaeingia peponi, na atakaeniasi
mimi huyo ndie aliyekataa.” ( imepokewa na Bukhari).
Na hadithi ya Umar (Mwenyezi Mungu amwie radhi), wakati alipoliendea
jiwe jeusi na kulibusu akasema: “hakika mimi ninaelewa wazi kuwa hili ni jiwe
halidhuru wala halinufaishi, na lau kama nisingelimuona Mtume anakubusu
basi nisingelikubusu”. (Imepokewa na Bukhari). Utiifu kwa Mwenyezi Mungu
hautokamilika katu isipokuwa kwa kumtii mtume wake (rehma na amani
ziwe juu yake).
Na vile vile katika kukirimiwa kwake Mtume (rehma na amani ziwe juu yake)
na Mwenyezi Mungu ni kufanywa mapenzi yake kuwa ni sehemu ya imani ya
kumuamini Mwenyezi Mungu, namapenzi a Mwenyezi Mungu ni mapenzi ya
Mtume wake (rehma na amani ziwe juu yake). Kumfuata Mtume (rehma na
amani ziwe juu yake) ni alama ya upendo kwake, Mwenyezi Mungu
amesema: { Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni
mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu. } Al
Imraan 31. Kumpenda mtume (rehma na amani ziwe juu yake) ni jambo la
lazima kwa kila muisilamu. Imekuja katika hadithi Kutoka kwa Anas
(Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema, amesema mjumbe wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukie) “hatoamini mmoja wenu mpaka niwe
ananipenda zaidi kuliko wazazi wake watoto wake na watu wote.”
(Imepokewa na Muslim na Bukhari).
Si hivyo tu, bali hata imani ya mja huwa ni pungufu ndani ya moyo wake
iwapo hatotanguliza mapenzi ya Mtume (rehma na amani ziwe juu yake)
zaidi ya nafsi yake, wazazi wake, na watu wote kwa ujumla.
Imepokewa na Abdallah Bin Hisham (Mwenyezi Mungu amwie radhi),
amesema: “ tulikuwa pamoja na Mtume (rehma na amani ziwe juu yake)naye
ameushika mkono wa Umar bin Khatwab akasema kumwambia Umar: ewe
mjumbe wa Mwenyezi Mungu hakika wewe ninakupenda sana isipokuwa
nafsi yangu ninaipenda zaidi, Mtume (rehma na amani ziwe juu yake)
akasema: “ hapana, naapa kwa yule ambae nafsi yangu ipo mikononi mwake
mpaka niwe unanipenda kuliko nafsi yako”. Umar kamwambia Mtume
(rehma na amani ziwe juu yake) “ hakika kuanzia hivi sasa na ninaapa kuwa
wewe ninakupenda zaidi kuliko nafsi yangu, Mtume (rehma na amani ziwe
juu yake) akamwambia: “ Hivi sasa ewe Umar.” (Imepokewa na Bukhari).
Na inatosha kwa ampendae Mtume (rehma na amani ziwe juu yake)
Kuwa na ubora na bahati ya kufufulia pamoja nae mpenzi wake Mtume
(rehma na amani ziwe juu yake) siku ya kiama, na nii ni fadhila kubwa sana na
ukarimu wa hali ya juu. Imepokewa na Anas Ibn Malik (rehma na amani ziwe
juu yake) amesema: “tulipokuwa mimi na Mtume (rehma na amani ziwe juu
yake) tunatoka msikitini tukakutana na mtu kwenye mlango wa msikitini,
akasema: ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kiama kitakuwa lini? Mtume
(rehma na amani ziwe juu yake) akasema “ je umejiandaa nacho? Kama
kwamba yule mtu alikuwa amejawa na unyenyekevu “kisha akasema: ewe
mjumbe wa Mwenyezi Mungu sikujiandaa kwa kufunga sana, wala kwa
swala, wala kwa sadaka lakini mimi ninampena mwenyezi mungu na Mtume
wake, akasema: ‘ wewe basi utakuwa na umpendae”. (Imepokewa na
Bukhari).
Na katika hali ya juu zaidi ya kukirimiwa Mtume (rehma na amani ziwe juu
yake) ni kuwa Mwenyezi Mungu anapomzungumzia huwa hamtaji jina lake
kikawaida kama anavyowataja mitume wengine wa kabla yake. Mitume
wengine walikuwa wakiitwa majina yao kikawaida tu, mfano kauli yake
Mwenyezi Mungu Mtukufu: { Na tulisema: Ewe Adam! Kaa wewe na mkeo
katika Bustani,} Al baqarah 42.
{Ewe Isa! Mimi nitakufisha, na nitakunyanyua kwangu,} Al Imraan aya 22.
{Ewe Nuhu! Shuka kwa salama itokayo kwetu } Hud aya 31.
{Ewe Musa! Hakika Mimi ni Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu
wote } Al qaswas 41.
{ Ewe Yahya! Kishike Kitabu kwa nguvu!} Maryam 06.
{ Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Musa! 12. Hakika Mimi ndiye Mola wako
Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la T'uwa.} Taha
00-06.
{ Tulimwita: Ewe Ibrahim! 115. Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo
tunavyo walipa wanao tenda mema. } Aswaafat 013-012.
{(Akaambiwa): Ewe Zakariya! Hakika Sisi tunakubashiria mwana; jina lake ni
Yahya. Hatujapata kumpa jina hilo yeyote kabla yake.} Maryam aya 1.
Lakini anapomzungumzia mtume wa mwisho (rehma na amani ziwe juu yake)
anamtaja kwa cheo chenye kujuulisha utukufu wake na nafasi yake na
ukubwa wa risala yake, Mwenyezi Mungu anasema {Ewe Nabii! Hakika Sisi
tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na mwonyaji,} Al ahzaab 32.
Pia anasema {Ewe Mtume! Fikisha uliyo teremshiwa kutoka kwa Mola wako
Mlezi. Na ikiwa hukufanya hayo basi hukufikisha ujumbe wake. Na Mwenyezi
Mungu atakulinda na watu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu
makafiri} Al maidah aya 21.
Si hivyo tu, bali pia Mwenyezi Mungu amewakataza wafuasi wa umma huu
kutomwita jina lake kikawaida kama walivyokuwa wakiita wafuasi wa umma
ziliizopita mitume yao. Na akaahidi kumpa adhabu kali atakaehalifu agizo
hili. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu { Msifanye wito wa Mtume baina
yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu anawajua
miongoni mwenu wanao ondoka kwa uficho. Basi nawatahadhari wanao
khalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu. } Al
nuur aya 24.
Vile vile kukirimiwa kwa Mtume (rehma na amani ziwe juu yake) ni wajibu wa
kumfanya kuwa ni kigezo, Mwenyezi Mungu amesema { Hakika nyinyi mnayo
ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anaye mtaraji
Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Mwenyezi Mungu
sana } Al ahzaab 60.
Aya hii ina umuhimu mkubwa sana kwani chimbuko la wajibu wa kumfuata
Mtume (rehma na amani ziwe juu yake) kimaneno, kivitendo na kihali, je,
tunamfuata na kuigiza kama alivyokuwa (rehma na amani ziwe juu yake).?
Na pia katika kukirimiwa kwake na Mwenyezi Mungu ni kuwa. Mwenyezi
Mungu Mtukufu amemtakia rehema ndani ya kitabu chake pia na malaika
wakamtakia rehema na kuwahimiza waumini nao wamswalie (wamuombee
rehma), Mwenyezi Mungu amesema { Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika
wake wanamsalia Nabii. Enyi mlio amini! Msalieni na mumsalimu kwa
salamu} Al ahzaab aya 22.
Na pia katika kukirimiwa kwake ni kwamba Mwenyezi Mungu mwenyewe
ndie aliyeshika jukumu la kumlinda (rehma na amani ziwe juu yake), tna
mitume wengine, wao ilikuwa wakituhumiwa kwa tuhuma sizo huwa
wanajitetea wenyewe, mfano nabii Nuh (A.S.), watu wake wamemtuhumu
kwa upotofu kama inavyosimulia Kurani Tukufu, inasema {Wale watukufu
katika kaumu yake wakasema: Hakika sisi tunakuona wewe umo katika
upotofu ulio dhaahiri.} Al aaraf 21. Naye anajitete mwenyewe kwa kusema
{Akasema: Enyi watu wangu! Mimi simo katika upotofu, lakini mimi ni
Mtume nitokaye kwa Mola Mlezi wa viumbe vyote. 62. Nakufikishieni
Ujumbe wa Mola Mlezi wangu, na ninakunasihini; na ninayajua kwa
Mwenyezi Mungu msiyo yajua nyinyi} Al aaraf 20-26.
Mfano mwengine nabii Hud (A.S.) watu wake walimtuhumu kwa uzembe na
wendawzimu na uongo walipomwambia {Wakasema watukufu wa wale walio
kufuru katika kaumu yake: Sisi tunakuona umo katika upumbavu, na hakika
sisi tunakufikiria kuwa wewe ni katika waongo} Al aaraf aya 22. Naye
anajitetea mwenyewe kwa kusema. {Akasema: Enyi watu wangu! Mimi sina
upumbavu. Lakini mimi ni Mtume niliye toka kwa Mola Mlezi wa viumbe
vyote. 68 Nakufikishieni ujumbe wa Mola wangu Mlezi. Na mimi kwenu ni
mwenye kukunasihini, muaminifu} Al aaraf 21-21.
Lakini kwa mtume wa mwisho (rehma na amani ziwe juu yake) kila
anaposingiziwa uongo na kumzushia uzushi Mwenyezi Mungu ndiye
anaesimama kumtetea, watu wake walimtuhumu kuwa yeye ni mshairi, {
Lakini wao walisema: Hizo ni ndoto za ovyo ovyo, bali amezizua tu, bali huyo
ni mtunga mashairi. Basi atuletee miujiza kama walivyo tumwa wale wa
mwanzo.} Al anbiya 2. Mwenyezi Mungu akawarudi kwa kusema { Wala
hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo.
Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha} Yasin 21.
Wakamwambia kuwa yeye ni kuhani, anayasema aambiayo na shetani…
Mwenyezi Mungu akawarudikwa kusema { Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa
neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.} Al Twuur 61.
Na Mwenyezi Mungu anaapa kiapo – na hakuna kiapo kikuba kkuliko cha
Mwenyezi Mungu - kwa ajili ya kumlinda mtume wake (rehma na amani ziwe
juu yake) na kuthibitisha ukweli wa wahyi na kurani na kuvunja hoja na
uzushi wao, Mwenyezi Mungu anasema { Basi naapa kwa mnavyo viona
41. Na msivyo viona, 31. Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe
mwenye hishima. 30. Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana
mnayo yaamini. 36. Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo
yakumbuka. 34. Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu
wote.} Al haqah aya 41-34.
Baadhi ya nyakati walikuwa wakimwambia kuwa yeye ni mchawi. Mwenyezi
Mungu akawajibu { Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila
walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.} Al dhariyaat 26. Na baadhi
ya nyakati walikuwa wakimwambia amerogwa, Mwenyezi Mungu akawajibu
aliposema { Au akaangushiwa khazina juu yake, au akawa na bustani ale
katika hiyo? Wakasema madhaalimu: Nyinyi hamumfuati ila mtu aliye rogwa
9. Tazama jinsi wanavyo kupigia mifano. Basi wamepotea, wala
hawataiweza Njia.} Al furqan 1-1.
Wakasema ni mwendawazimu, nae Mwenyezi Mungu akawarudi kwa
kusema {Au wanasema: Ana wazimu? Bali amewajia kwa Haki, na wengi wao
wanaichukia Haki.} Al muuminuun aya 11. Na kauli yake aliposema { Nuun.
Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo. 6. Kwa neema ya Mola wako
Mlezi wewe si mwendawazimu. 4. Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo
katika. 3. Na hakika wewe una tabia tukufu.} Al qalam aya 0-3.
Wakamtuhumu kwa upotofu na kuchanganyikiwa , naye Mwenyezi Mungu
akawajibu, aliposema {0. Naapa kwa nyota inapo tua . 6. Mwenzenu huyu
hakupotea, wala hakukosea. 4. Wala hatamki kwa matamanio. 3. Hayakuwa
haya ila ni ufunuo ulio funuliwa.} An najm 0-3.
Si hivyo tu bali Mwenyezi Mungu amejitolea kumkinga na kumlinda juu ya
washirikina, akasema, {Ewe Mtume! Fikisha uliyo teremshiwa kutoka kwa
Mola wako Mlezi. Na ikiwa hukufanya hayo basi hukufikisha ujumbe wake.
Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu. Hakika Mwenyezi Mungu
hawaongoi watu makafiri.} Al maidah 21.
Na vile vile katika kukirimiwa kwa Mtume (rehma na amani ziwe juu yake)
kwa kule kupewa ujumbe kwa walimwengu wote na si kwa kizazi maalumu
au watu maalumu, ulinganio wake ni kwa watu wote. Kwani Mwenyezi
Mungu aliwatuma kila mtume kwa watu wake ama Mtume (rehma na amani
ziwe juu yake) yeye ni kwa watu wote. Kurani tukufu imeweka wazi jambo
hili, Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema { Na hatukukutuma ila kwa watu
wote, uwe mbashiri, na mwonyaji. Lakini watu wengi hawajui} Saba`a 61.
Na Kutoka kwa Jabir bin Abdi Llah (Mwenyezi Mungu awawie radhi
amesema: amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie): “ nimepewa mambo matano hakuna nabii yeyote aliyepewa
kabla yangu: nimepewa ushindi wa kuwahofisha maadui kwa mwendo wa
mwezi, nikafanyiwa ardhi kuwa ni msikiti na ipo safi na mtu yeyote katika
umma wangu akifikwa na swala basi na aswali, na nimehalalishiwa ngawira,
na ilikuwa nabii akipelekwa (akitumwa) kwa watu wake maalumu, ama mimi
nimetumwa kwa watu wote, na nimepewa uombezi. ((Imepokewa na
Bukhari).
Na miongoni mwa kukirimiwa ni kufadhilishwa kwake (rehma na amani ziwe
juu yake) na Mwenyezi Mungu zaidi ya mitume wengine, Mtume (rehma na
amani ziwe juu yake) amepewa ubora zaidi na hii ni kama ilivyoeleza Kurani
Tukufu { MITUME hao tumewatukuza baadhi yao juu ya wengineo. Katika
wao wapo ambao Mwenyezi Mungu alisema nao, na wengine
akawapandisha vyeo} Al baqara aya 624. Na kama walivyoeleza baadhi wa
wafasiri pale aliposema { Katika wao wapo ambao Mwenyezi Mungu alisema
nao, na wengine akawapandisha vyeo..} anaekusudiwa hapa ni mtume wetu
(rehma na amani ziwe juu yake), kwani yeye ndie mwenye vyeo vya juu, na ni
mwenye mwujiza wa kudumu nayo ni Kurani Tukufu na ni mwenye risala
iliyokusanya mambo yote mazuri yaliyotajwa katika umma zilizotangulia.
Na katika hadithi ambayo imepokewa na imam Muslim na Tirmidhy kutoka
kwa hadithi ya Abu Hurayra, kwamba Mtume (rehma na amani ziwe juu
yake) amesema, “ nimefadhilishwa zaidi ya mitume wengine kwa mambo
sita: nimepowa ufupisho wa maneno, nimenusuriwa kwa kuwapa hofu
maadui – na katika mapokezi ya ya Bukhari: nimpewa nusura ya
kuwaogopesha maadui kwa mwendo wa mwezi – na nimehalalishiwa
ngawira, na ardhi ikafanywa kwangu kuwa ni msikiti na ni safi, n nimetumwa
kwa viumbe wote na unabii ukaishia kwangu.”
Na katika kukirimiwa kwake (rehma na amani ziwe juu yake) ni kuwa
Mwenyezi Mungu akiapa basi huapa kwa kupitia jina lake na wala hatumii
jina la viumbe vyake, na Mwenyezi Mungu akiapia juu ya vitu basi ni kwa
kuvitilia mkazo, na anaapia vitu vingi mbali mbali, kama visivyo na uhai,
wanyama, malaika, maeneo, nyakati, na hali ya kilimwengu. Mwenyezi
Mungu hakupa ndani ya Kurani kumuapia mwanadamu isipokuwa Mtume
(rehma na amani ziwe juu yake), aliposema { Naapa kwa umri wako! Hakika
hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo} Al hajar 16. akikusudia,
kupitia uhai wako ewe Muhamad hakika wao wamo katika upotofu mkubwa,
na wamo katika kutojua njia wala haki wala uongofu… Na washirikina
waliposema kuwa Mwenyezi Mungu amemuacha mkono Mtume Mtume
(rehma na amani ziwe juu yake), na amemtenga, Mwenyezi Mungu Mtukufu
akapa kuwa yeye hakumuacha na wala hakumuacha mkono, akasema
{0. Naapa kwa mchana! 6. Na kwa usiku unapo tanda! 4. Mola wako Mlezi
hakukuacha, wala hakukasirika nawe. 3. Na bila ya shaka wakati ujao
utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia. 2. Na Mola wako Mlezi atakupa
mpaka uridhike.} Adhuha 0-2.
Na kwa upande wa kukirimiwa kwake (rehma na amani ziwe juu yake) baaya
ya kufariki, ni kuwa Mwenyezi Mungu amempa uombeaji mkubwa siku ya
kiama. Kwani katika hadithi mbayo ameipokea Bukhari na Muslim kutoka
kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi), hakika mtume (rehma na
amani ziwe juu yake) amesema, “ mimi ni bwana kati ya watoto wa Adam
siku ya kiama, na ni wa mwanzo atakaepasukiwa na kaburi na ni mwombezi
wa mwanzo na wa mwanzo atakae ekubaliwa maomi yake.”
Na katika aya tukufu, Mwenyezi Mungu Mtukufu amemfanya (rehma na
amani ziwe juu yake) kuwa ni rehema kwa walimwengu wote, amesema {
Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.} Al anbiyaa
117.
Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema,
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie),
“hakika mimi ni rehema yenye kuongoa”. Na katika mapokezi mengine
nimetumwa kuwa ni rehema yenye kuongoa.
Wajibu wetu kwa upande wa Kurani tukufu
3 jamad-Awal 7331H. / 71-1-1172AD
Kwanza: Vipengele
Kurani Tukufu ni miujiza wa kiisilamu wa milele.
Nafasi ya Kurani Tukufu na fadhila zake.
Nafasi za wenye kuitendea Kurani Tukufu hapa duniani na akhera.
Wajibu wa waisilamu kwa upande wa Kurani Tukufu.
a. kuitukuza na kuisoma na kuzingatia aya zake.
b. Adabu tuwapo na Kurani Tukufu na kujiweka kitabia za Kurani Tukufu.
c. kuzifanyia kazi amri zake na makatazo yake.
Pili: dalili ndani ya Kurani Tukufu na hadithi
Dalili ndani ya Kurani Tukufu
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {Mwenyezi Mungu ameteremsha hadithi
nzuri kabisa, Kitabu chenye kufanana na kukaririwa; husisimua kwacho ngozi za
wenye kumkhofu Mola wao Mlezi. Kisha ngozi zao na nyoyo zao hulainika kwa
kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Huo ndio uwongofu wa Mwenyezi Mungu, na
kwa huo humwongoa amtakaye. Na ambaye ameachwa na Mwenyezi Mungu
kupotea, basi hapana wa kumwongoa }Zumar. 13.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Lau kuwa tumeiteremsha hii Qur'ani juu ya
mlima, basi bila ya shaka ungeli uona ukinyenyekea, ukipasuka kwa khofu ya
Mwenyezi Mungu. Na hiyo mifano tunawapigia watu ili wafikiri }Al hashri. 17.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {Na namna hivi tumekufunulia Qur'ani kwa
amri yetu. Ulikuwa hujui Kitabu ni nini, wala Imani. Lakini tumekifanya kuwa ni
Nuru ambayo kwayo tunammwongoa tumtakaye katika waja wetu. Na hakika
wewe unaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka 35. Njia ya Mwenyezi Mungu ambaye
ni vyake Yeye tu viliomo mbinguni na katika ardhi. Jueni kuwa mambo yote
yanarudi kwa Mwenyezi Mungu }Ash shuraa 21-23.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye ya
yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya
kwamba watapata malipo makubwa }Al israa. 3.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Hakika Sisi ndio tulio teremsha
Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda }Al hijri.3.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani
iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka? }Al qamar. 71.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Na tunateremsha katika Qur'ani yaliyo ni
matibabu na rehema kwa Waumini. Wala hayawazidishii madhaalimu ila khasara.
}Al israa. 21.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyo
mteremshia mja wetu basi leteni sura moja ya mfano wake, na muwaite mashahidi
wenu badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa mnasema kweli }Al baqara.13.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe,
kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.} S`aad. 13.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema { Sema: Wangeli kusanyika watu na majini
ili walete mfano wa hii Qur'ani basi hawaleti mfano wake, hata wakisaidiana wao
kwa wao }Al Isaraa. 22
Dalili ndani ya hadithi
Kutoka kwa Aisha (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) alipoulizwa kuhusu
tabia za mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “Tabia zake
zilikuwa ni kurani.” (Imam Ahmad).
Kutoka kwa Aisha (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) kutoka kwa mtume
(rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ambae husoma kurani naye
anaijua vyema basi huwa na malaika wema, na ambaye huisoma kurani hali ya
uzito basi ana malipo mara mbili.” (Imam Abi Daudi)
Kutoka kwa Anas bin Malik (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema;
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake)
“Mwenyezi Mungu ana watu wa aina mbili, wakasema, ni akina nani hao ewe
mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “hao ni watu wa kurani, watu wa
Mwenyezi Mungu na ndio aliowatenga maalumu.” (Ibn Majah)
Kutoka kwa Ibn Masuud (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema;
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu(rehma na amani zimshukie juu yake)
“mwenye kusoma herufi moja ndani ya kitabu basi atapatwa kwayo jema, na jema
moja ni huzidishwa mfano wake mara kumi, sisemi Alif Laam miim ni herufi,
lakini Alif ni herufi, Laam ni herufi na Miin ni herufi. (Imam Tirmidhy)
Kutoka kwa Ibn Masuud (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema;
mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) ameniambia: “Nisomee” akasema:
nikamwambia nikusomee na kwako imeteremshwa? Akasema “ hakika mimi
ninapenda kuisikia ikisomwa na mwengine. Akasema: nikasoma Annisai mpaka
nilipofika: { itakuwaje tutakapouleta kila umma na shahidi, kisha ukaja wewe
kama ni shahidi wa hawa} akaniambia inatosha. Nikayaona macho yake
yanatokwa na machozi.” (Imam Bukhari na Muslim)
Kutoka kwa Abi Malik Al ashaariy (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake)
amesema: amesema mjumbe (rehma na amani zimshukie juu yake) “… kurani ima
ni hoja kwako au dhidi yako… (Imam Muslim)
Na kutoka kwa Abi Mussa Al ashariy (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake)
amesema: amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu
yake) “mfano wa muumini asomae kuran ni mfano wa mtunda harufu yake ni
nzuri na ladha yake ni nzuri. Na mfano wa muumini ambae hasomi kurani ni
mfano wa tende, haina harufu (lakini) ladha yake ni tamu. Na mfano wa mnafiki
ambae anasoma kurani ni mfano wa mrehani harufu yake ni nzuri na ladha yake ni
chungu. Na mfano wa mnafiki ambae hasomi kurani ni sawa na mfano wa mtango
mwitu halina harufu na ladha yake ni chungu.” (Bukhari na Muslim)
Na kutoka kwa Ukubah bin Amir Aljuhaymiy amesema: mtume wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake) alitujia tulipokuwa tumekaa kivulini
akasema: “ hivyo ni nani kati yenu angependa kwenda Kuthan au Al akiyk
akachukua ngamia wawili walio wazuri bila ya kupata madhambi kutoka kwa
Mwenyezi Mungu na wla kukata ukoo?” wakasema: sote tunataka ewe mjumbe wa
Mwenyezi Mungu. Akasema: “ aendapo mmoja wenu msikitini kila siku
akajifunza aya mbili ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu ni bora kwake kuliko
ngamia wawili, na akisoma aya tatu (basi bora kwake) kuliko ngamia watatu na
mfano wa idadi za aya kwa idadi za ngamia.” (Abi Daudi)
Kutoka kwa Abi Umamah (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema:
nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi Mungu akisema: “Kurani italetwa siku ya
kiyama na watu wake ambao walikuwa wakiitendea, itatangulia sura ya Al baqara
na Al imran.” Na mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) akazipigia mfano
sitoisahau milele, akasema: mfano wake (hizo sura) ni kama mawingu mawili au
vivuli viwili vyeusi kati yao ni mwanga kama kwamba ni makundi ya ndege
waliopiga safu zitamuombea shifaa waliokuwa wakizisoma.” (Muslim)
Na kutoka kwa maneno ya wanazuoni (waliotangulia)
Abu Abdulrahman Assalamiy (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake)
anasema: “tulikuwa tukijifunza aya kumi za kurani na wala hatukuwa tukijifunza
aya kumi (nyengize) zijazo isipokuwa baada ya kujifunza halali zake na haramu
zake na amri zake na makatazo yake.” (Utunzi wa Abdu Razak)
Tatu: Maudhui
Kurani Tukufu ni mwujiza mkubwa wa kiisilamu kwa nyakati zote, majini na
wanadamu walishindwa kuileta kama hiyo. Akasema Mwenyezi Mungu { Sema:
Wangeli kusanyika watu na majini ili walete mfano wa hii Qur'ani basi hawaleti
mfano wake, hata wakisaidiana wao kwa wao }Al Isaraa. 22. bali pia
wameshindwa kuleta sura kumi tu mfano wake au sura moja mfano wake,
Mwenyezi Mungu amesema {Au wanasema: Ameizua? Sema: Basi leteni Sura
kumi zilizo zuliwa mfano wa hii, na waiteni muwawezao badala ya Mwenyezi
Mungu, ikiwa mnasema kweli.} Hud.73. na akasema Mwenyezi Mungu { Na
ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyo mteremshia mja wetu basi leteni sura moja ya
mfano wake, na muwaite mashahidi wenu badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa
mnasema kweli }Al baqara.35.
Mwenyezi Mungu Mtukufu ameiteremsha ndani ya moyo wa mtume (rehma na
amani zimshukie juu yake) iwe ni uongofu kwa watu katika njia iliyonyooka,
iwaangazie maisha, na kuongoa wasiokuwa na uongofu. Ni katiba ya waislamu
kwani kwayo nyoyo huuishwa pia nafsi hufanywa kuwa safi na kwayo tabia huwa
njema, Mwenyezi Mungu anasema {7. Alif Lam Mim. 1. Hiki ni Kitabu
kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wachamungu 3. Ambao
huyaamini ya ghaibu na hushika Sala, na hutoa katika tuliyo wapa} Albaqara. 7-3.
na Mwenyezi Mungu anasema { Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye ya yaliyo
nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba
watapata malipo makubwa }Al israa. 3. mwenye kushikamana nayo ataokoka na
fitina, kwani ni mwanga kwa waumini na ni roho ya uongofu wake. Mwenyezi
Mungu anasema {Na namna hivi tumekufunulia Qur'ani kwa amri yetu. Ulikuwa
hujui Kitabu ni nini, wala Imani. Lakini tumekifanya kuwa ni Nuru ambayo kwayo
tunammwongoa tumtakaye katika waja wetu. Na hakika wewe unaongoa kwenye
Njia Iliyo Nyooka 23. Njia ya Mwenyezi Mungu ambaye ni vyake Yeye tu viliomo
mbinguni na katika ardhi. Jueni kuwa mambo yote yanarudi kwa Mwenyezi
Mungu }Ash shuraa 21-23.
Na kutokana na uzuri wake kundi la majini walipoisikia waliiamini na kuitukuza,
wakapata uongofu wa njia iliyonyooka, kisha wakaenda kuwaonya wenziwao, na
hivi ni kama alivyosimulia Mwenyezi Mungu Mtukufu, {Na wakati tulipo waleta
kundi la majini kuja kwako kusikiliza Qur'ani. Basi walipo ihudhuria walisema:
Sikilizeni! Na ilipo kwisha somwa, walirudi kwa kaumu yao kwenda kuwaonya.
31. Wakasema: Enyi kaumu yetu! Sisi tumesikia Kitabu kilicho teremshwa baada
ya Musa, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake, na kinacho ongoza kwenye
Haki na kwenye Njia Iliyo Nyooka. 37. Enyi kaumu yetu! Muitikieni Mwenye
kuitia kwa Mwenyezi Mungu, na muaminini, Mwenyezi Mungu atakusameheni, na
atakukingeni na adhabu chungu. 31. Na wasio mwitikia Mwitaji wa Mwenyezi
Mungu basi hao hawatashinda katika ardhi, wala hawatakuwa na walinzi mbele
yake. Hao wamo katika upotovu ulio dhaahiri.} Al ahqaf 13-31.
Na iwapo hii ndio ilivyokuwa hali ya majini juu ya Kurani Tukufu basi na malaika
ni hivyo hivyo. Kutoka kwa Usayd bin Hudhayr, amesema: alipokuwa yeye
akisoma usiku sura albaqara na farasi wake amemfunga pembeni mwake, farasi
wake akataharaki naye akanyamaza (kusoma), akaendelea kusoma, farasi wake
akataharaki, akanyamaza kusoma naye (farasi) akaacha kutaharaki, kisha
akaendelea kusoma nae farasi akataharaki baadae akaondoka zake. Na mwanawe
yahya alikuwa karibu naye akaogopa asijwe kufikwa na tatizo na alipocheua (farasi
wake) alinyanyua kichwa chake juu kuangalia. Ilipofika asubuhi nikamueleza
mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) akasema: Soma ewe ibn Hudhayr,
akasema niliogopa ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu asije kumkanyaga yahya
kwani alikuwa nae karibu, nikanyanyua kichwa changu na kumuondoa kisha
nikanyanyua kichwa juu mbinguni, tahamaki mfano wa kivuli mifano ya taa,
nikaondoka ili nisiendelee kutazama, akasema “Unafahamu hicho kilikuwa ni kitu
gani?” akasema: “hapana”. Akasema “ hao ni malaika walikaribia kwa sababu ya
sauti yako na lau kama ungeliendelea basi watu wangeliwaona bila ya kificho.”
(Bukhari). Na namna hii ndio huwa athari ya kurani inaposomwa.
Ni maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ambae maajabu yake hayapungui, naye
amedhamini kuitunza kuepukana na kuharibiwa na kubadilishwa, akasema : {
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda
}Al hijri.3.
Asemae kupitia kurani basi amesema kweli, aitendeaye basi hulipwa, afanyae
hukumu kupitia kurani basi hufanya uadilifu, na ailinganiaye basi huongozwa
katika njia iliyonyooka nae Mwenyezi Mungu ameifanya kuwa ni tiba na rehema
akasema: { Na tunateremsha katika Qur'ani yaliyo ni matibabu na rehema kwa
Waumini. Wala hayawazidishii madhaalimu ila khasara. }Al israa. 21.
Kutoka kwa Abdillah (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) kutoka kwa
mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “hakika kurani hii ni
karamu ya Mwenyezi Mungu basi ipokeeni karamu hii kadiri muwezavyo, hakika
kurani hii ni kamba ya Mwenyezi Mungu, na nuru iliyo wazi na matibabu yenye
manufaa na ngao kwa wanaoshikamana nayo, uokovu kwa waifuatayo, haipotoshi
na wala haiendi kombo na maajabu yake hayaishi na wala haina majibizano.
Isomeni kwani Mwenyezi Mungu hukulipeni kwa kuisoma kwake kwa kila herufi
thawabu kumi kwani mimi sisemi Ali Laam Miin ni herufi lakini Alif ni herufi
Laam ni herufi na Miim ni herufi. (Alhakim)
Mwenyezi Mungu ameinyanyua cheo na kuisifu kwa sifa njema na kuitaja kwa
majina mazuri sana ili watu waelewe nafasi na cheo chake, Mwenyezi Mungu
akaisifia kwa kusema { Hiki ni Kitabu ambacho Aya zake zimewekwa wazi, kisha
zikapambanuliwa, kilicho toka kwa Mwenye Hikima na Mwenye Khabari} Hud. 7.
na aliposema { na haya bila ya shaka ni Kitabu chenye nguvu na utukufu.
23. Hautakifikia upotovu mbele yake wala nyuma yake. Kimeteremshwa na
Mwenye hikima, Msifiwa.} Fusilat37-31. na sifa nyengineze zenye kujuulisha
cheo na nafasi yake iliyotukuka.
Na mtume wetu (rehma na amani zimshukie juu yake) ametueleza fadhila nyingi
sana juu ya Kurani Tukufu ambazo manufaa yake humrudia yeye mwenyewe
mwanadamu hapa duniani na kesho akhera, na katika fadhila hizo ni:-
Ubora kwa mwenye kuisoma: Hadithi ya Othmani Bin Affan (radhi za Mwenyezi
Mungu ziwe juu yake) kutoka kwa mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
amesema: “mbora wenu ni mwenye kujifundisha kurani na kuifundisha”
(Bukhari?)
Kupandishwa cheo: imepokewa hadithi kutoka kwa Amru (Mwenyezi Mungu
awawie radhi) amesema, amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie juu yake) “itasemwa kuambiwa msomaji wa kurani: soma na panda
cheo, na soma kama ulivyokuwa ukiisoma duniani, kwani cheo chao ni mwisho wa
aya utakayoisoma) (Abi Daudi)
Kumuombea msomaji: imepokewa hadithi kutoka kwa Umama Albahiliy (radhi
za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake) akisema: “ someni kurani kani hiyo
itakuja siku ya kiyama kama ni mwombezi kwa wasomaji wake” (Muslim)
Malipo makubwa kwa msomaji wake: imepokewa hadithi kutoka kwa Ibn Mas
uud (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: amesema mjumbe wa
Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake) “Mwenye kusoma herufi
moja ndani ya kitabu basi atapatwa kwayo jema, na jema moja ni huzidishwa
mfano wake mara kumi, sisemi Alif Laam miim ni herufi, lakini Alif ni herufi,
Laam ni herufi na Miin ni herufi.” (Imam Tirmidhy)
Kuhifadhiwa nyumba zisomwazo kurani: imepokewa na Abi Hurayra (radhi za
Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) kwamba mtume (rehma na amani zimshukie juu
yake) amesema: “ musizifanye nyumba zenu makaburi, hakika ya shetani hukimbia
nyumba ambayo husomwa ndani yake sura ya Albaqara.” (Muslim) na fadhila
nyenginezo ambazo hazimaliziki. Kwa mfano hadithi ya Ibn Siyriyn, amesema:
“nyumba ambayo husomwa ndani yake kurani malaika huwa wanahudhuria na
mashetani hutoka, na wasomi wake huombewa na kheri zake huzidi. Na nyumba
ambayo kurani haisomwi, huhudhuria mashetani na malaika hutoka na huwapo
katika simanzi waktu wake na kheri zake huwa ni chache.” (Ibn Abi Shaybah)
Na tukizingatia hali za masahaba wakarimu (Mwenyezi Mungu awawie radhi)juu
ya kurani tukufu tutaona kuwa wao hawakutosheka kuisoma tu na kuisikiliza,
lakini waliisoma na kuizingatia nyonyo na nafsi zao zikashikamana nayo, wakawa
wanaitekeleza kimaneno na kimatendo na kufuata amri zake na kujiepusha na
makatazo yeke. Kwa ajili hiyo wakafikia vyeo vikubwa sana walivyofikia kwa
sababu ya kuitikia wito wa Kurani Tukufu. Sayidna Omar aliihifadhi sura ya
Albaqara kwa muda wa miaka minane si kwa sababu ya uzito wa kuhifadhi
isipokuwa alikuwa na pupa ya kupata elimu na kuitendea elimu hiyo. Abu Abdu
rahman As salamiy (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) anasema:
“tulikuwa tunapojifunza aya kumi ndani ya Kurani Tukufu huwa hatujifunzi aya
kumi nyengine zijazo mpaka (tunahakikisha) tumejifundisha halali yake na haramu
na amri zake na makatazo yake” (Abdu Razzak)
Na kwa kuwa masahaba (Mwenyezi Mungu awawie radhi) walikuwa
wakijielimisha na kisha kuitendea kwa ajili hiyo wakawa wako mbele katika
kumtii Mwenyezi Mungu Mtukufu na kujiepusha na makatazo yake. Na wakati
zilipoteremshwa aya za makatazo ya kunywa ulevi, muitaji akaita: “ Tambueni
kuwa ulevi umeharamishwa”, basi wote wakaitikia wito wa kurani. Aliyekuwa na
ulevi mkononi basi akaurembea, na aliyekuwa ulevu imo kinywani akaucheua, na
aliyekuwa na ulevi kwenye chombo akaumwaga hii yote ni kwa ajili ya kuitikia
wito wa Mwenyezi Mungu, - na mpaka njia za mji wa Madina zilijaa pombe-
wakawa wanasema “tumeacha ewe Mola wetu”. Na kwa namna hiyo ilipoteremka
aya { Kabisa hamtafikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyo vipenda. Na kitu
chochote mnacho kitoa basi hakika Mwenyezi Mungu anakijua} Al imran 31.
Sayidna Abu Dahdah alisimama kwenye bustani aipendayo zaidi akaitoa sadaka.
Kwa hivyo, masahaba (Mwenyezi Mungu awawie radhi) waliweza kuhifahi kitabu
cha Mwenyezi Mungu kwani kao hakikua kama kitabu cha kawaida, lakini ni
mwongozo wa kimalezi, kimaadili na kiimani iliyodhihiri katika maisha yao ya
kila siku na kwa wengine.
Kwa ajili hiyo cheo ambacho Mwenyezi Mungu amewapa wasomao Kurani
Tukufu na kuitendea kazi ni kikubwa mno. Imepokea kutoka kwa Anas bin Malik
(radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: amesema mjumbe wa
Mwenyezi Mungu ““Mwenyezi Mungu ana watu wa aina mbili, wakasema, ni
akina nani hao ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “hao ni watu wa
kurani, watu wa Mwenyezi Mungu na ndio aliowatenga maalumu.” (Ibn Majah).
Asomae Kurani Tukufu amenasibishwa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na ni
cheo kikubwa kilichoje!
Ama wajibu wetu kuhusu kurani inakusanya:-
* Kujifundisha na kuifundisha, na kuendelea kuisoma na kuifundisha, kwani walio
bora ni wale wenye kujifundisha na kuifundisha, imepokewa katika hadithi (mbora
wenu ni yule ajifundishae kurani kisha kuifundisha. Na mtume wetu (rehma na
amani zimshukie juu yake) ametuamrisha kuisoma na kuishikilia akasema:
“shikamaneni na kurani ninaapa kwa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi
mwake ni rahisi sana kuponyoka kuliko ngamia aliye katika kamba yake.”
(Bukhari)
Kurani Tukufu ni chanzo madhubuti chenye kutengeneza nafsi ya mwisilamu,
kupitia Kurani Tukufu hupata mafunzo na tabia njema. Hivyo basi, juu ya
muisilamu awe na pupa katika kuisoma vizuri, na jambo hili si gumu, kwani
tunakutia watu huwa wanajifunza lugha za kigeni, na hutumia juhudi za namna
tafauti ili wawe na maarifa mengi kwa ajili ya kupata kipato kingi. Itakuwaje basi
kuzembea katika kujifunza maneno ya Mwenyezi Mungu mtukufu iwe ndio tabu?
Imepokewa kutoka kwa Aisha (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) kutoka
kwa mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ambae husoma
kurani naye anaijua vyema basi huwa na malaika wema, na ambaye huisoma
kurani hali ya uzito basi ana malipo mara mbili.” (Imam Abi Daudi) na Mwenyezi
Mungu Mtukufu ametuahidi kuwa ametufanyia kuwa ni chepesi kwa kukisoma na
kwa kuabudia akasma { Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi
kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka? } Alqamar;71.
Kuzingatia aya zake kama kwamba bdio zinashuka kwa msomaji wake, kwani
katika wajibu wetu juu ya Kurani Tukufu isiwe ni kuisoma tu lakini hakuna budi
kuizingatia ili tupate ladha yake na kuihisi utukufu wake, Mwenyezi Mungu
anasema { Je! Hawaizingatii hii Qur'ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo
kufuli?}Muhhamad;13. na akasema pia, { Hebu hawaizingatii hii Qur'ani? Na lau
kuwa imetoka kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka wangeli kuta ndani
yake khitilafu nyingi} Anisaa;21.
Kwa wasomi wa Kurani Tukufu wanaopata malipo makubwa sana ni wale
waisomao kwa ndimi zao na kuzingatia nyoyoni mwao na akilini mwao,
Mwenyezi Mungu anasema, { Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe,
kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili } Saad;13. na
Mwenyezi Mungu amemsifu asomaye aya zake kwa kuzingatia zikawa
zinamzidishia imani akasema, { Hakika Waumini ni wale ambao anapo tajwa
Mwenyezi Mungu nyoyo zao hujaa khofu, na wanapo somewa Aya zake
huwazidisha Imani, na wakamtegemea Mola wao Mlezi }Al anfaal;1. Ibn Abbas
amesema: “Mwenyezi Mungu amechukua dhamana kwa aisomae Kurani Tukufu
kuwa hatapotea hapa duniani na wala hatokuwa na tabu kesho akhera, na dalili ya
hayo ni kauli yake Mwenyezi Mungu, {basi atakaye ufuata uwongofu wangu,
hatapotea wala hatataabika 432. Na atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi
kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya
kuwa kipofu 433. Aseme: Ewe Mola wangu Mlezi! Mbona umenifufua kipofu,
nami nilikuwa nikiona? 434. (Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo vivyo hivyo.
Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na kadhaalika leo unasahauliwa }
Taha;713-712.
Na mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) ametupigia mfano kwa mwenye
kuathirika na Kurani Tukufu na kutekeleza kama aya zake zisemavyo. Siku moja
alisema kumwambia Abdullah bin Masuud (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu
yake): “Kutoka kwa Ibn Masuud (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake)
amesema; mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) ameniambia: “Nisomee”
akasema: nikamwambia nikusomee na kwako imeteremshwa? Akasema “ hakika
mimi ninapenda kuisikia ikisomwa na mwengine. Akasema: nikasoma Annisai
mpaka nilipofika: {itakuwaje tutakapouleta kila umma na shahidi, kisha ukaja
wewe kama ni shahidi wa hawa} akaniambia inatosha. Nikayaona macho yake
yanatokwa na machozi.” (Imam Bukhari na Muslim). Fahari ya muumini ni kuenda
sambamba na neno la Mwenyezi Mungu Mtukufu, Mwenyezi Mungu anasema
{Mwenyezi Mungu ameteremsha hadithi nzuri kabisa, Kitabu chenye kufanana na
kukaririwa; husisimua kwacho ngozi za wenye kumkhofu Mola wao Mlezi. Kisha
ngozi zao na nyoyo zao hulainika kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Huo ndio
uwongofu wa Mwenyezi Mungu, na kwa huo humwongoa amtakaye. Na ambaye
ameachwa na Mwenyezi Mungu kupotea, basi hapana wa
kumwongoa}Azzumar;13.
Adabu (heshima) za kuwa na Kurani Tukufu na kujipamba kwa tabia zake,
miongoni mwa wajibu wa msomi wa Kurani Tukufu ni kuwa na heshima na
kujipamba kwa mwenendo wa Kurani Tukufu, ashikamane na mafunzo yake.
Kwani kupitia tabia za kurani mwanadamu anajikinga na ufuataji wa matakwa
yake na matamanio yake na nafsi yake huwa madhubuti katika maadili mema,
Mwenyezi Mungu anasema, { Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye ya yaliyo
nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba
watapata malipo makubwa }Al israa;3. na kigezo chetu juu ya hili ni bwana mtume
(rehma na amani zimshukie juu yake) kwani alikuwa kama kurani ikitembea juu ya
mgongo wa ardhi, alijipamba kitabia kama kurani itakavyo, akiridhia kile ambacho
Kurani Tukufu imeridhia,na kuchukia kile kilichochukiwa na Kurani Tukufu. Bibi
Aisha (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) aliulizwa kuhusu tabia za mtume
(rehma na amani zimshukie juu yake) akasema: “tabia zake ni kurani.” (Ahmad)
* kufuata maamrisho yake na makatazo yake, wajibu wetu juu ya Kurani
Tukufu hautakiwi uwe ni vifuani au hata kuizingatia pekee lakini itabidi kufuata
maamrisho yake na makatazo yake. Ili tabia na matendo yetu yaonekane kama
alivyokuwa mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) na masahaba wake.
Hivyo, wajibu wa muisilamu afuate amri za kurani na kuacha makatazo yake
kwani mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) anasema: “kurani ima ni
hoja kwako au dhidi yako.” (Muslim) Itakuwa ni hoja dhidi yako pindi iwapo
haitofika masikioni mwako na wala haitoathiri kitu katika mwenendo wa
maisha yako na huenda msomaji wake ikawa inamlaani.
* Na miongoni mwa wajibu wetu juu ya Kurani Tukufu ni kupambana na
wanaoipotosha na kuifasiri visivyo na kuizungumzia kisiasa au kiitikadi (sizo)
ili kupata manufaa na chumo. Kurani Tukufu inabidi ielezwe kimaneno na
kimaana kwa wasomi wake wa umma wenye kuamninika na waliobobea katika
fani hiyo, wawafundishe watu mafunzo sahihi na itikadi ndiyo ya kiisilamu ama
kwa wale wasioijua hawatakuwa na cha kufanya zaidi ya masilahi yao na
matamanio yao.
* Na ulimwengu wetu wa sasa unahitajia zaidi uongofu wa Kurani Tukufu,
matatizo yaliyopo sasa ni matatizo ya kimaadili na hakuna kitabu
kilicholingania maadili kwa watu wote mfano wa Kurani Tukufu. Na iwapo
kosa la waislamu kwa wakati huu kujiweka mbali na mwenendo wa Kurani
Tukufu sasa itawalazimu wairudie na kufuata mifano ya kivitendo ya Kurani
Tukufu na kwa aliyeteremshiwa hii kurani (mtume Muhammad rehma na amani
zimshukie juu yake). Kwani yeye ndiye aliyesifiwa na Mola wake kuwa ni
mwenye tabia njema kabisa kwakuwa tu ameifuata kurani kimarefu na mapana.
Alikuwa ni kiumbe mwenye tabia nzuri kwa kule kuifuata katika nyanya zote,
Mwenyezi Mungu anasema {Hakika wewe ni mwenye tabia nzuri} Alqalam,3.
na kama ilivyoelezwa katika hadithi ya Aisha (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe
juu yake) akasema “tabia zake ni kurani.”
* Nasi hatutoacha kuelezea Kurani Tukufu ili iwe ni mwongozo mwema
utakaotukinga siku ambayo hatutokuwa na mkingaji wala muokoaji,
imepokewa kutoka kwa Abi Umamah (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu
yake) amesema: “nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi Mungu akisema: “Kurani
italetwa siku ya kiyama na watu wake ambao walikuwa wakiitendea, itatangulia
sura ya Al baqara na Al imran.” Na mtume (rehma na amani zimshukie juu
yake) akazipigia mfano sitoisahau milele, akasema: mfano wake (hizo sura) ni
kama mawingu mawili au vivuli viwili vyeusi kati yao ni mwanga kama
kwamba ni makundi ya ndege waliopiga safu zitamuombea shifaa waliokuwa
wakizisoma.” (Muslim)
Waisilamu wakiendelea kuisoma, kuzingatia maana yake na kuitendea pia
kujifunza na kuifundisha watakuwa na manufaa makubwa sana, kwani rehema
na uadilifu utaenea, nyoyo zitakuwa njema kheri zitakuwa nyingi na shari na
maafa yatatoweka.
Wito wa Manabii na Mitume katika urekebishaji kwa
mtazamo wa kurani tukufu 71 Rabiu Akhar 7331H. 11 Januari 1172A.D
Kwanza: Vipengele
7. Uisilamu ni dini ya wema na marekebisho
1. mifano ya ulinganio wa Manabii na mitume katika kurekebisha kwa kupitia
Kurani Tukufu
3. Umuhimu wa kuzirekebisha nafsi zetu kwanza.
3. Athari ya marekebisho kwa mtu mmoja mmoja na kwa jamii
2. Madhara ya kuacha kujirekebisha.
Pili: Dalili
Ndani ya Kurani Tukufu
7. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema { Na hatuwatumi Mitume ila huwa ni
wabashiri na waonyaji. Na wenye kuamini na wakatenda mema haitakuwa khofu juu yao,
wala hawatahuzunika} [Al anaam; 24]
1. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema kwa kupitia ulimi wa Nabii Shuaib (
Rehema na amani zimshukie juu yake) {Akasema: Enyi watu wangu!
Mwaonaje ikiwa ninayo dalili wazi inayo tokana na Mola wangu Mlezi, na
ikawa Yeye ameniruzuku riziki njema kutoka kwake? Wala mimi sipendi
kukukhalifuni nikafanya yale ninayo kukatazeni. Sitaki ila kutengeneza kiasi
ninavyo weza. Na sipati kuwezeshwa haya ila na Mwenyezi Mungu. Kwake
Yeye ninategemea, na kwake Yeye naelekea} [Hud; 44]
3. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema kwa kupitia ulimi wa Nabii Shuaib (
Rehema na amani zimshukie juu yake) { Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe
katika wanao punja. 443. Na pimeni kwa haki iliyo nyooka; 445. Wala msiwapunje watu
vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi} [Ashuaraa; 444-445]
3. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema {Wala msifanye uharibifu katika nchi
baada ya kuwa imekwisha tengenezwa. Na muombeni kwa kuogopa na kwa
kutumai. Hakika rehema ya Mwenyzi Mungu iko karibu na wanao fanya
mema.} [Alaaraf; 34]
2. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema { Na Musa akamwambia nduguye
Haarun: Shika mahala pangu kwa watu wangu na utengeneze wala usifuate
njia ya waharibifu} [Al aaraf; 423]
2. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema {Sema: Njooni nikusomeeni aliyo
kuharimishieni Mola wenu Mlezi. Nayo ni kuwa, msimshirikishe Yeye na chochote. Na
wazazi wenu wafanyieni wema. Wala msiwauwe watoto wenu kwa sababu ya umasikini.
Sisi tunakuruzukuni nyinyi na wao. Wala msikaribie mambo machafu, yanayo onekana,
na yanayo fichikana. Wala msiuwe nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharimisha
kuiuwa, ila ikiwa kwa haki. Hayo amekuusieni ili myatie akilin} [Al anaam; 434]
7. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema { Wala hakuwa Mola wako Mlezi wa
kuihiliki miji kwa dhulma tu na hali watu wake ni watenda mema } [Hud;
447]
4. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema {Na Mola wako Mlezi haangamizi miji
mpaka ampeleke Mtume katika miji yake mikuu awasomee Ishara zetu. Wala
hatuiangamizi miji mpaka watu wake wawe madhaalimu.} [Al qasas; 35]
3. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema { Na kina Thamud tuliwapelekea ndugu
yao Saleh. Akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi
hamna Mungu ila Yeye. Yeye ndiye aliye kuumbeni katika ardhi, na
akakuwekeni humo. Basi mwombeni msamaha, kisha mtubu kwake. Hakika
Mola wangu Mlezi yupo karibu, anaitikia maombi.} [Hud; 44]
71. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema { Hakuna kheri katika mengi ya
wanayo shauriana kwa siri, isipo kuwa kwa yule anaye amrisha kutoa sadaka, au
kutenda mema, au kupatanisha baina ya watu. Na mwenye kufanya hayo kwa kutaka
radhi ya Mwenyezi Mungu, basi tutakuja mpa ujira mkubwa} [Nisaa; 442]
44. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema {Wanakuuliza juu ya Ngawira.
Sema: Ngawira ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume. Basi mcheni Mwenyezi
Mungu na suluhisheni mambo baina yenu, na mt'iini Mwenyezi Mungu na
Mtume wake ikiwa nyinyi ni Waumini} [Al anfaal; 4]
Dalili kwa hadithi za Mtume ( Rehema na amani zimshukie juu yake)
7. Kutoka kwa Zayd Bin Milha (Mwenyezi Mungu amwie radhi), hakika ya
mtume ( Rehema na amani zimshukie juu yake) amesema: (… hakika ya
dini imeanza ngeni na itarudi hali ya kuwa ni ngeni, basi uzuri ulioje kwa
wageni (nao ni) ambao wanarekebisha yale waliyoyaharibu watu baada
yangu katika mwenendo wangu (sunna zangu). (Tirmidhiy)
1. Kutoka kwa Abi Dardai (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu
yake), “Je nikuelezeni lililo bora kuliko thawabu za kufunga na s;a na
sadaka? Wakasema: “Ndio, akasema, kuwarekebisha jamaa , kwani
kuharibika kwa jamaaa ni kuifuta dini miongoni mwa watu . (Tirmidhy)
3. kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) alikuwa akisema: “ewe
Mola nirekebishie dini yangu ambayo ni hifadhi ya mambo yangu, na
unirekebishie dunia yangu ambayo ni maisha yangu, na unirekebishie
akhera yangu ambayo ni mareleo yangu, na nifanyie maisha kuwa na kila
la kheri, na nifanyie umauti wangu yawe ni starehe kwa kila ovu.”
(Muslim).
3. kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema;
amesema mtume wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu
yake) kila kiungo cha mwanadamu kina sadaka, kila siku ichomozayo
jua, akipatanisha kati ya watu waili ni sadaka, kumsaidia mtu katika
kumpandisha kipando cha mnyama wake ni sadaka au kumsaidia mtu
kupandisha mzigo wake juu ya mnyama ni sadaka, neno zuri ni sadaka,
na kila hatua apigayo kwenda kusali ni sadaka, kuondoa uchafu njiani ni
sadaka.” (Bukhari na Muslim)
2. Kutoka kwa Ubada Bin Umayr Bin Auf, amesema, Abu Ayubu
(Mwenyezi Mungu amwie radhi) aliniambia: Mtume (rehma na amani
zimshukie juu yake) aliniambia ewe Aba Ayubu, je nikujuulishe sadaka
ambayo Mwenyezi Mungu na mtume wake wanaipenda? Suluhisha kati
ya watu wakikasirikiana na kuharibiana.” (Muujam kabiir, Twabarani)
2. Kutoka kwa Anas Bina Malik amesema: amesema mtume wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake) “ iwapo kiama kitasimama
na kwenye mkono wa mmoja wenu ana mbegu basi akiweza kuipanda na
aipande.” (Bukhari)
Tatu: Maudhui
Miongoni mwa maadili ya uisilamu ambayo dini yetu imehimiza na kulingania
sana ni maadili ya wema na usuluhishaji (urekebishaji). Kwani ni tabia njema
ambayo nafsi ya mtu hupenda na kuitamani. Ni maadili ambayo kila mtu inapasa
awe nayo kwa ajili ya kuimarisha ulimwengu. Na ni kitu kitakiwacho katika sheria
kwa kuwa kinaondosha sababu za ufisadi na mipasuko, huharakisha uwepo wa
ukaribu kati ya watu kwa lengo la kuleta usawa wa hali zao ndani ya maisha.
Hapana shaka kuwa wema na usuluhishaji ni upeo utakiwao kwa waja katika
ibada zao na katika kazi zao, bila ya wema ibada haikubaliki, kwa hivyo, hakuna
budi kwa mwanadamu awe mwema katika nafsi yake kimatendo na kimaneno
mwenye kusuluhisha matatizo ya wengine na kutenda kwa ajili ya kuwarekebisha.
Na mwenye kuzingatia aya za Kurani Tukufu ataona kuwa zimeweka mkazo
mkubwa sana katika suala hili – la maadili ya urekebishaji-. Neno kurekebisha
limetajwa ndani ya Kurani Tukufu karibuni mara mia moja na sabini, n kila
kinapotajwa kitu kwa wingi huwa ni dalili ya umuhimu wake na ukubwa na nafasi
yake. Hivyo neno hili (urekebishaji - usuluhishaji) limkuja kwa maana tafauti na
katika mana zote hizi inajulisha kuwa uisilamu ina lengo kusawaziha wanadamu
katika itikadi zao, ibada zao, matendo yao na nyanja nyengine za maisha yao.
Kurani Tukufu imeweka sambamba kati ya imani ya kumuamini Mwenyezi
Mungu na kurekebisha – kusuluhisha, katika aya nyingi, kama ni ishara ya mja
kuwa na imani ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anasema {Na wenye kuamini
na wakatenda mema haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika} [Al anaam; 32] na
amesema Mwenyezi Mungu {Wanakuuliza juu ya Ngawira. Sema: Ngawira ni ya
Mwenyezi Mungu na Mtume. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na suluhisheni mambo
baina yenu, na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume wake ikiwa nyinyi ni Waumini}
[Al anfaal;4]
Vile vile Kurani Tukufu imeweka sambamba kati ya uchaji Mungu na kurekebisha
– kusuluhisha, Mwenyezi Mungu amesema {basi watakao mchamngu na
wakatengenea haitakuwa khofu kwao, wala hawatahuzunika} [Al aaraf; 53]. Na pia
kufungamanisha kati ya kutubu na kurekebisha – kusuluhisha akasema Mwenyezi
Mungu { Ila wale walio tubu na wakatengeneza na wakabainisha,} [Al baqara;
441]. Na pia akasema { Na wakitubia wakatengenea }[Anisaa; 44]. Na akasema pia {
Isipo kuwa wale walio tubu baada ya hayo na wakatengenea; kwani bila ya shaka
Mwenyezi Mungu ni Msamehevu, Mwenye kurehemu} [Anuur; 3]. Hivyo basi,
kurekebisha – kusuluhisha ni matunda ya imani ya kumuamini Mwenyezi Mungu
Mtukufu na uchaji na ni toba ya kweli kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mola wa
walimwengu wote.
Na Kurani Tukufu imependezesha kurekebisha – kusuluhisha kwa kuwa kuna
malipo makubwa, Mwenyezi Mungu anasema { Hakuna kheri katika mengi ya wanayo
shauriana kwa siri, isipo kuwa kwa yule anaye amrisha kutoa sadaka, au kutenda mema, au
kupatanisha baina ya watu. Na mwenye kufanya hayo kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu,
basi tutakuja mpa ujira mkubwa} [Anisaa; 442].
Na tukifuatilia habari za manabii na mitume pamoja na watu wao tutaona kuwa
wametumwa kwa lengo la kurekebisha yale waliyoyaharibu watu katika dunia. Na
kwa ajili hiyo ujumbe wa kila nabii ulikuwa ni mmoja, nao ni kurekebisha
ulimwengu kutokana na maasi na magonjwa ambayo yameenea kati yao, na kila
mtume akapelekwa kwa watu wake ili kuondoa ufisadi ambao umeenea katika
zama zake, Mwenyezi Mungu akawatuma kwa waja wake ili wawe wabashiria
mema na waonyaji wa itikadi na sheria pamoja na maadili ya kuisawazisha nafsi na
kuiepusha na uchafu wa ushirikina. Mwenyezi Mungu anasema {Na hatukumtuma
kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipo kuwa Mimi. Basi
niabuduni Mimi tu.} [Al anbiya; 33] na wito wao mitume umekuja kwa ajili ya
kuwarekebisha waja duniani ili wakapate radhi za Mola wao huko akhera.
Mfano sayidna Nuh (rehma na amani zimshukie juu yake) hakika aliwalingania
watu wake kwa ajili ya kuwarekebisha ndani ya dini ya Mwenyezi Mungu ili
wapate kumuabudu Yeye (Mwenyezi Mungu) na wasimshirikishe na chochote na
waachane na ibada ya masanamu ambayo hayadhuru wala hayanufaishi, Mwenyezi
Mungu anasema { Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda
wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra 32. Na hao walikwisha
wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.} [Nuh; 35-32]. Na
akawa anawapenezeshea katika kujirekebisha ili wapate riziki nyingi, na
Mwenyezi Mungu awaneemeshe kwa mali na watoto. Mwenyezi Mungu anasema
{Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa
kusamehe. 44. Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo. 43. Na atakupeni mali na wana,
na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito. 45. Mna nini hamweki heshima ya
Mwenyezi Mungu?} [Nuh;41-45]
Na mfano mwengine ni nabii Shuaibu (rehma na amani zimshukie juu yake)
anatibu ufisadi wa itikadi na kila lililoambatana na uharibifu wa uchumi kwa watu
wake, akawa anawalingania waache kupunguza vipimo na mizani, na tabia hii
mbaya ilikuwa imeenea sana kati ya watu wake, akaja kuwalingania katika
marekebisho ya kuhifadhi haki ya muuzaji na mnunuzi. Mwenyezi Mungu
anasema kwa ulimi wa nabii Shuaib (rehma na amani zimshukie juu yake) { Na
kwa watu wa Madyana tuliwatumia ndugu yao Shua'ib. Akasema: Enyi watu wangu!
Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna Mungu ila Yeye, wala msipunguze
vipimo na mizani. Mimi nakuoneni mmo katika hali njema, nami nakukhofieni adhabu
ya Siku kubwa hiyo itakayo kuzungukeni. 43. Na enyi watu wangu! Timizeni vipimo
na mizani kwa uadilifu wala msiwakhini watu vitu vyao; wala msieneze uovu katika
nchi mkafanya uharibifu.} [Hud; 42-43]. Kisha akawawekea wazi kuwa lengo la
ulinganio wake ni kurekebisha akasema { Sitaki ila kutengeneza kiasi ninavyo weza.
Na sipati kuwezeshwa haya ila na Mwenyezi Mungu. Kwake Yeye ninategemea, na
kwake Yeye naelekea.} [Hud;44]. Na katika sehemu nyengine anasema kuwa
dhumuni ni kurekebisha tabia mbovu ya watu ya kupunguza mizani na vipimo
akawa anawaambia {Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja. 443. Na
pimeni kwa haki iliyo nyooka; 445. Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa
ufisad.} [Ashuaraa; 444-445].
Na tuzingatie kitu muhimu sana pale Sayidna Shuaib (rehma na amani zimshukie
juu yake) aliposema wakati anawalingania watu wake {Na sipati kuwezeshwa haya
ila na Mwenyezi Mungu. Kwake Yeye ninategemea, na kwake Yeye naelekea} [Hud;
44]. Hapa amebainisha kuwa pana dhumuni kubwa ambalo hapana budi
kuchungwa kwa kila mwenye kutaka kurekebisha, nalo ni kufanya marekebisho
kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee.
Nayo marekebisho hayahitaji masilahi na wala mapendekezo ya mtu binafsi, ni
marekebisho yenye kurekjelea manufaa yake kwa wana jamii wote na kwa kila
mtu.
Mfano mwengine ni Nabii Saleh (rehma na amani zimshukie juu yake) anawaita
watu wake kwa kusema {Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. 434. Wala msit'ii
amri za walio pindukia mipaka, 433. Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala
hawatengenezi} [Ashuaraa 431-433]
Na wakati sayidna Mussa (rehma na amani zimshukie juu yake) alipomachilia
madaraka mdogo wake sayidna Harun (rehma na amani zimshukie juu yake) juu ya
watu wake alimuusia kuwarekebisha na kuacha kufuata njia za waharibifu.
Mwenyezi Mungu amesema {Tulimuahidi Musa masiku thalathini na tukayatimiza
kwa kumi; ikatimia miadi ya Mola wake Mlezi masiku arubaini. Na Musa
akamwambia nduguye Haarun: Shika mahala pangu kwa watu wangu na utengeneze
wala usifuate njia ya waharibifu.}[Al aaraf 423].
Kisha akaja mtume wa waisilamu (rehma na amani zimshukie juu yake)
kukamilisha marekebisho katika nyanja zote za maisha ya kidunia, kijamii
kiuchumi na kisiasa ambayo hata watume waliomtangulia walilingania pia. Na kwa
kutazama kwa undani kabisa kuhusu maisha yake tutaona kuwa mtume (rehma na
amani zimshukie juu yake) ametengeneza tamaduni za kiisilamu zenye
kushikamana na maadili na tabia. Baada ya kuwa jamii ilikuwa imejaa uharibifu
wa kitabia kama uzinifu, wizi, mauaji, riba, kula mali za watu kwa dhuluma na
kula mali za mayatima na mengineyo katika maovu na mambo ya kuchukiza.
Lakini mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) aliyakabili haya yote kwa
mfumo wa kuyarekebisha, na wito wake ukawa ni wito wa urekebishaji wa mtu na
jamii. Mwenyezi Mungu anasema {Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na
Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele.}[Al anfaal 32]. Na kwa
upande wa dini, ulinganio wake umekuja kwa kuirekebisha nafsi kupitia dini,
akaweka wazi ya kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja na hana mshirika, na
akasimamisha dalili za kumpwekesha. Na pia kwa upande wa kurekebisha tabia
alilingania kuwa na tabii njema ambayo ndio chimbuko la ulinganiaji. Imepokewa
kutoka kwa Al bayhaqi (Mwenyezi Mungu amwie radhi) katika kitabu chake
kwamba mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ hakika mimi
nimetumwa kuja kukamilisha tabia njema.”
Na kama ambavyo mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) alilingania katika
misingi ya maadili mema ya kiutu ambayo kwayo jamii hutengenea, na huhifadhi
umoja wake na nguvu zake pia mshikamano wake kwa ajili ya kushi maisha yaliyo
salama na mazuri, yasiyo na machafuko wala mipasuko wala fujo na matendo ya
kigaidi kinyume na tuonavyo hivi sasa kuhusu mambo ya uharibifu, mauaji na
ubomoaji.
Na katika maadili ambayo sheria ya mbinguni imekusaya kuhusu urekebishaji ni
uadilifu, usamehevu, kutelekeza ahadi, kutimiza amana, ukweli katika maneno na
matendo, kuwafanyia wema wazazi wawili, kuacha mali ya mayatima, kuchunga
haki za jirani na maneno mazuri hii ni kwa sababu chimbuko la sheria za mbinguni
ni moja, na kwa ajili hii mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)amesema: “
manabii ni ndugu kwa aila za mama tafauti (lakini) dini yao ni moja.” (Bukhari).
Sheria zinaweza kutafautiana katika ibada na namna ya kuifanya kwa mujibu wa
zama na nyakati, lakini maadili na tabia za kiutu ambazo ni msingi wa kuishi hizi
huwa hazitafautiani katika sheria yoyote. Mtume (rehma na amani zimshukie juu
yake) “ katika yale waliyopata watu katika maneno ya mitume wa mwanzoni ni
kuwa utakapokuwa huna haya basi fanya utakacho.” Basi ni sheria gani
iliyohalalisha kuua nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameiharamisha kuuliwa
isipokuwa kwa haki au imehalalisha kuwatenga wazazi wawili, au kula haramu au
kula mali ya mayatima au kula mali za wafanyakazi?
Na ni sheria gani iliyohalalisha uongo, kuvunja ahadi, khiana, au kulipa mabaya
kwa wema? Yote haya ni kinyume, kwani sheria za mbinguni zimelingana na
kujikita katika maadili ya kiutu, na yeyote ambae ataziacha tabia hizi basi huwa
hajatoka tu katika sheria bali pia atakuwa ametoka katika mzunguko mzima wa
maadili na kujivua maumbile ya uanadamu wake ambayo Mwenyezi Mungu
amemuumbia.
Kwa ajili hiyo, Ibn Abas (rehma na amani ziwashukie juu yao) amesema kuhusu
kauli yake Mwenyezi Mungu {Sema: Njooni nikusomeeni aliyo kuharimishieni Mola wenu Mlezi.
Nayo ni kuwa, msimshirikishe Yeye na chochote. Na wazazi wenu wafanyieni wema. Wala msiwauwe
watoto wenu kwa sababu ya umasikini. Sisi tunakuruzukuni nyinyi na wao. Wala msikaribie mambo
machafu, yanayo onekana, na yanayo fichikana. Wala msiuwe nafsi ambayo Mwenyezi Mungu
ameharimisha kuiuwa, ila ikiwa kwa haki. Hayo amekuusieni ili myatie akilini. 026. Wala msiyakaribie
mali ya yatima ila kwa njia ya wema kabisa, mpaka afikilie utu-uzima. Na timizeni vipimo na mizani kwa
uadilifu. Sisi hatumkalifishi mtu ila kwa kadiri ya uwezo wake. Na msemapo semeni kwa uadilifu ingawa
ni jamaa. Na ahadi ya Mwenyezi Mungu itekelezeni. Hayo amekuusieni ili mpate kukumbuka 024. Na
kwa hakika hii ndiyo Njia yangu Iliyo Nyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine, zikakutengeni na
Njia yake. Haya amekuusieni ili mpate kuchamngu} [Al anaam 151-153]. Aya zenye
kuzungumzia hukumu hazikufuta chochote katika vitabu vyote, kwani nimambo
yaliyoharamishwa ka watu wote, nayo ni asili ya maandiko, yeyote atakayetenda
kwa mujibu wa aya hizo basi ataingia peponi na mwenye kuacha ataingia motoni.
Na mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) ametupigia mfano wa hali ya
juu katika kurekebisha – kusuluhisha kimaneno na kimatendo, na dua yake
ilikuwa ni kutaka marekebisho katika kila jambo, alikuwa akiomba ““ewe Mola
nirekebishie dini yangu ambayo ni hifadhi ya mambo yangu, na unirekebishie
dunia yangu ambayo ni maisha yangu, na unirekebishie akhera yangu ambayo
ni mareleo yangu, na nifanyie maisha kuwa na kila la kheri, na nifanyie umauti
wangu yawe ni starehe kwa kila ovu.” (Muslim).
Na alikuwa akisuluhisha kati ya watu, pia alikuwa na pupa ya kuondosha fitina
na hitilafu. Imepokewa kutoka kwa Sahli bin Saad (rehma na amani zimshukie
juu yake) “ kuwa watu wa Kubaa walipigana nakurembeana kwa mawe, mtume
akaelezwa jambo hilo, basi akasema: nipelekeni ili nikawasuluhishe.” (Bukhari)
Hakika ya wema na usuluhishaji ni nguzo madhubuti za kubaki kwa jamii na
kuendelea kwake, nasi tuna haja ya kurekebisha nafsi zetu kwanza na
kuzisafisha katika nyanja zote za kimasiha kama za kisiasa, kijamii kiuchumi na
kielimu pia. Kuirekebisha nafsi ni jambo litakiwalo na sheria na ni wajibu wa
kidini, na hasa katika wakati huu tulionao ambao imani imekuwa ni dhaifu na
uharibifu wa tabia na kupotea kwa haki na wajinu, watu wengi wakawa
hawaelewi haki ya mkubwa wala za jamaa, wazazi na za taifa.
Na katika kurekebisha ni kujichunga mtu juu ya haki yake na za wenzake,
asifnye uadui katika haki za wengine, na kila mtu aelewe wajibu wake na
autekeleze ipasavyo, kwani kufanya hivyo ni kutekeleza maadili mazuri na
kujiweka mbali na uharibifu na ufisadi katika ardhi na dhuluma na kuujaza
moyo chuki na hasada. Kwani hiki ni kiini cha urekebishaji, kila mtu
ajirekebishe yeye mwenyewe kwa ajili ya Mola wake na kwa ajili ya wenzake
na kwa ulimwengu mzima, kufanya hivyo atakuwa mtu mwema mwenye
kuweza kurekebisha na mwengine. Yaani kama kwamba kujirekebisha ni
kuitakasa nafsi kwa kuipamba kwa tabia njema na kuizuia na dhuluma na
madhambi na kutenda yaliyokatazwa na Mwenyezi Mungu, na kuiimarisha
ardhi pia kutoa hazina na siri zake ambazo manufa yake huwa kwa wote.
Kurekebisha huwa kwa mshikamano na si kwa mgawanyiko nao ni ule
unaolinganiwa na Kurani Tukufu, wema na usuluhishaji huakisi upendo na
usamehevu kati ya wana jamii kisha kwa umma mzima, na kwa kupitia
marekebisho vyanzo vya ugomvi hutoweka na chuki pamoja na husuda.
Nayo marekebisho hayana wakati maalumu, lakini mtu huwa hana budi
kuendeleza suluhisho hadi mwisho wa uhai wake na kwa ajili hiyo mtume
(rehma na amani zimshukie juu yake) ameashiria katika hadithi aliyoipokea
Anas bin Malik (Mwenyezi Mungu amwie radhi) “iwapo kiama kitasimama
na kwenye mkono wa mmoja wenu ana mbegu basi akiweza kuipanda na
aipande.” (Bukhari)
Na la muhimu kulitaja hapa ni kuwa suluhisho – marekebisho hayawezi
kuonekana mattund yake mpaka mtu aanze yeye mwenyewe kisha ndani ya
familia yake na kwa jamii yake. Marekebisho ni kitu cha lazima ili jamii iwe
sawa n taifa linufaike kwa usalama na kwa kazi na maendeleo na kueneza
upendo kati ya watu. Na yeyote afanyae juhudi kwa mali yake ili asuluhishe
kati ya watu waliohaimiana ajue kuwa mtume (rehma na amani zimshukie
juu yake) ameshamuombea dua akasema “hakika ya dini imeanza ngeni na
itarudi hali ya kuwa ni ngeni, basi uzuri ulioje kwa wageni (nao ni) ambao
wanarekebisha yale waliyoyaharibu watu baada yangu katika mwenendo
wangu (sunna zangu). (Tirmidhiy).
Suluhisho lina athari kubwa sana kwa mtu na kwa jamii, nazo: kuwezesha
maisha mazuri, Mwenyezi Mungu anasema {Mwenye kutenda mema,
mwanamume au mwanamke, naye akawa ni Muumini,tutamhuisha maisha
mema; na tutawapa ujira wao kwa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda.}
[Anahl; 57]
Pia, kuokoka na maangamizo na uharibifu, Mwenyezi Mungu anasema {
Wala hakuwa Mola wako Mlezi wa kuihiliki miji kwa dhulma tu na hali watu
wake ni watenda mema} [Hud 447].
Na pia kuirithi ardhi, kwani kuirithi kwake kumeshartishwa kwanza kuweko
namarekebisho, Mwenyezi Mungu anasema {Na hakika tulikwisha andika katika
Zaburi baada ya Kumbukumbu, ya kwamba nchi watairithi waja wangu walio wema} [al
anbiya 413].
Vile vile kuwepo uongozi wa Mwenyezi Mungu na hifadhi yake kwa yule
aliyeshikamana na misingi sahihi ya marekebisho, Mwenyezi Mungu
amesema {Hakika Mlinzi wangu ni Mwenyezi Mungu aliye teremsha Kitabu.
Naye ndiye awalindae walio wema} [Al aaraf 454].
Pia kuna kuhifadhi kizazi, Mwenyezi Mungu {Na ama ukuta, huo ulikuwa ni
wa vijana wawili mayatima kule mjini. Na chini yake ilikuwako khazina yao;
na baba yao alikuwa ni mtu mwema. Basi Mola wako Mlezi alitaka wafikie utu
uzima na wajitolee khazina yao wenyewe, kuwa ni rehema itokayo kwa Mola
wako Mlezi. Wala mimi sikutenda hayo kwa amri yangu. Hiyo ndiyo tafsiri ya
hayo ambayo wewe hukuweza kuyasubiria}[Kahf; 43], kisa cha kujengwa
ukuta wa watoto waili mayatima kwenye kisa cha nabii Mussa (rehma na
amani zimshukie juu yake) kisa hiki kinajulikana, na kazi ya kujenga
haikuya ya bure lakini ilikuwa na athari ya wema ya mzazi wao. Imepokewa
kutoka kwa Abbas (Mwenyezi Mungu amwie radhi) ilikuwa ni kwa sababu
ya wema wa mzazi wao lakini haukutajwa wema wa watoto hao.
Pia suluhisho huleta usalama wa kutoogopa dunia na akhera, Mwenyezi
Mungu anasema { Na hatuwatumi Mitume ila huwa ni wabashiri na waonyaji. Na
wenye kuamini na wakatenda mema haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.}
[Al anaam; 24] pia huleta msamaha na upendo, Mwenyezi Mungu anasema
{. Na mkisikizana na mkamchamngu basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghfira na
Mwenye kurehemu} [Anisaa; 435]
Marekebisho yakifanyika juu ya kitu basi huwa kimepambika na ni tabia
ipendwayo na Mwenyezi Mungu na mtume wake (rehma na amani
zimshukie juu yake) kwani kupitia hayo maisha huenda itakiwavyo, na
umma unakuwa umeshikamana, myonge huwa na nguvu, waisilamu huwa
wamoja na neno lao huwa moja na huondosha mgawanyiko, na kueneza
upendo nayo ni dalili ya imani, mwenyezi mungu anasema {Hakika Waumini
ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu, na mcheni Mwenyezi Mungu
ili mrehemewe. }[Alhujraat; 41].
Na tukosapo thamani ya suluhisho basi umma utaharibika, familia
zitaporomoka, fujo zitaenea, ufisadi nao utashika nafasi na haki za
Mwenyezi Mungu zitavyunywa, maovu yatatendwa hapo ndipo jamii, taifa
na ustaarabu utakaposambaratika, kuacha kusuluhisha hupelekea kuenea
kwa adhabu hapa duniani na maangamizo ya kinafsi kama ufakiri, udhalili
na fedheha.
Sifa za waumini ndani ya kurani
17 jamad uwla 1437 H. 26022116
Imefasiriwa na
Profesa\ Ayman Ibrahim Alaasar
Kwanza: vipengele
Kumjua Mweneyzi Mungu ni njia ya imani
Imani na matendo mema ni mambo yenye mshikamano
Sifa za waumini
Kumuogopa Mwenyezi Mungu.
Kumtegemea Mwenyezi Mungu ipasavyo.
Kuhifadhi sala na kunyeyekea ndani yake.
Kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.
Ukweli, uaminifu, kutimiza ahadi, haya na tabia njema.
Neema alizoziandaa Mwenyezi Mungu kwa waumini.
Pili: Dalili:
Dadili ndani ya Kurani tukufu
Mweneyzi Mungu Mtukufu anasema {1. Hakika wamefanikiwa Waumini,2.
Ambaoni wanyenyekevu katika Sala zao, 3. Na ambao hujiepusha na mambo
ya upuuzi, 4. Na ambao wanatoa Zaka. 5. Na ambao wanazilinda tupu zao, 6.
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamilikimikono yao ya kulia. Kwani
hao si wenye kulaumiwa. 7. Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao
ndiowarukao mipaka. 8. Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao, 9.
Na ambao Sala zao wanazihifadhi 11. Hao ndio warithi,} Almuuminun 1-11.
Mwenyezi Mungu anasema: {Hakika Waumini ni wale ambao anapo tajwa
MwenyeziMungu nyoyo zao hujaa khofu, na wanapo somewa Aya
zakehuwazidisha Imani, na wakamtegemea Mola wao Mlezi. 3. Hao ambao
wanashika Sala na wanatoa katika yale tunayo waruzuku 4. Hao kweli ndio
Waumini. Wao wana vyeo, na maghfira,na riziki bora, kwa Mola wao Mlezi.
}Al anfal, 2-4.
Mwenyezi Mungu anasema: {Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola
wao Mleziwananyenyekea, 58. Na wale ambao Ishara za Mola wao
Mleziwanaziamini, 59. Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,61.
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa
kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi, 61. Basi wote hao ndio wanao kimbilia
katika mambo yakheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.} Almuuminun 57-
61.
Mwenyezi Mungu anasema {Na ukisha kata shauri basi mtegemee Mwenyezi
Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanao mtegemea.161.
Akikunusuruni Mwenyezi Mungu hapana wakukushindeni, na akikutupeni ni
nani, basi, baada yakeYeye ataye kunusuruni? Na Waumini wamtegemee
Mwenyezi Mungu tu} Al imran. 159-161.
Mwenyezi Mungu anasema: {Na waja wa Arrahman Mwingi wa Rehema ni
wale wanaotembea ulimwenguni kwa staha, na wajinga
wakiwasemezahujibu: Salama! 64. Na wale wanao kesha kwa ajili ya Mola
wao Mlezi kwa kusujudu na kusimama. 65. Na wale wanao sema: Mola wetu
Mlezi! Tuondolee adhabu ya Jahannamu. Hakika adhabu yake ikimpata
tuhaimwachi. 66. Hakika hiyo ni kituo na makao mabaya. 67. Na wale ambao
wanapo tumia hawatumii kwa fujo wala hawafanyi ubakhili, bali wanakuwa
katikati baina ya hayo.} Alfurqan 63-67.
Mwenyezi Mungu anasema: {Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na
kuweni pamoja na wakweli} Atawba,119.
Mwenyezi Mungu anasema: { Enyi mlio amini! Timizeni ahadi.
Mmehalalishiwawanyama wa mifugo, ila wale mnao tajiwa.
Lakinimsihalalishe kuwinda nanyi mmo katika Hija. HakikaMwenyezi Mungu
anahukumu apendavyo} Almaida,1.
Dalili ndani ya hadithi.
Kutoka kwa Ibn Umar (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: siku moja
tulipokuwa tumekaa pamoja na mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
akatutokezea mtu amevaa nguo myeupe sana ana nywele nyeusi
haikuonekana athari yoyote ya safari na hakuna yeyote kati yetu aliyemjua
mpaka akakaa mnele ya mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
akakutanisha magoti yake na magoti ya mtume na kuweka bega lake katika
bega la mtume kisha akasema: “ewe Muhammad nieleze kuhusu uisilamu.”
Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) akasema: “ uisilamu ni
kushuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa
Mwenyezi Mungu na hakika Muhammad (rehma na amani zimshukie juu
yake) ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na kusimamisha sala, na kutoa zaka
na kufunga ramadhani na kuhiji nyumba ukiwa na uwezo. Akasema:
“umesema kweli.” Akasema: “ nieleze kuhusu imani.” Akasema: “kumuamini
Mwenyezi Mungu na malaika wake na vitabu vyake na siku ya mwisho na
kuamini kadari kheri yake na shari yake. Akasema: “ umesema kweli.”
Akasema: “ nieleze kuhusu ihsani. Akasema: “ni kumuabudu Mwenyezi kama
kama kwamba unamuona na iwapo humuoni basi yeye anakuona. Akasema:
“Umesema kweli.” Akasema: “ nieleze kuhusu kiama. Akasema: “huenda
muulizaji akawa anaelewa zaidi kuliko anaeulizwa. Akasema: “ nieleze ishara
zake” akasema: “ mtumwa kuzaa bwana wake na kuwaona wachungaji
watembeao miguu peku wanashindana katika ujenzi wa majumba makubwa.
Akasema, kisha akaondokam nikabaki hali ya kufikiria, kisha nikamuuliza ewe
Umar unamjua ni nani huyo muulizaji? Akasema: “ Mwenyezi Mungu na
mtume wake wanaju. Akasema Yule ni Jibrilu amekujieni kukufundisheni dini
yenu.” (Muslim)
Kutoka kwa Anas bin Malik (Mwenyezi mungu amwie radhi)hakika ya mtume
(rehma na amani zimshukie juu yake siku moja alitoka na akakutana na kijana
wa kianswar anaitwa Haritha bin Nuuman, akamwambia: “ umeamkaje ewe
Haritha? Akasema: nimeamka hali ya kuwa ni muumini wa kweli. Akasema
mtume wa Mweneyzi Mungu (Rehma na amani zimshukie juu yake) angalia
usemacho, kwani kila haki ina kithibitisho, basi ni upi huo uthibitisho wa
imani yako? Akasema: Najizoea nafsi yangu kujiepusha na ya dunia,
nikakesha usiku wangu na kufunga mchana wangu, nami kama kwamba
naagalia Arshi ya Mola wangu iliyo wazi na kama kwamba naagalia watu wa
peponi namna wanavyotembeleana, na kama kwamba naangalia watu wa
motoni na namna wanavyofanyiana uadui ndani yake. Mtume rehma na
amani ziwe juu yake akamwambia. Umeona (umesema kweli) basi
jilazimishe. Kasema hivi mara mbili, mja Mwenyezi Mungu amenawirisha
imani ndani ya moyo wake.” (sehemu ya imani).
Kutoka kwa Abi Hurayra (mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
amesema mjumbe wa Mweneyzi Mungu (rehma na amani zimshukie juu
yake) imani ni sehemu sabini au sitini ya mafungu na bora ya (mafungu haya)
ni kauli ya “Lailaha illa llahu” (hapana wa kuabudiwa kwa haki isipokuwa
Mwenyezi Mungu na kuondosha uchafu njiani na kuona haya ni sehemu ya
imani.” (Muslim)
Kutoka kwa Umar (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema,
nimemsikia mjumbe wa Mweneyzi Mungu (rehma na amani zimshukie juu
yake) akisema: “ lau kama mungelimtegemea Mwenyezi Mungu kama
ipasavyo basi angelikupeni riziki kama ampavyo ndege, huondoka asubuhi
ana njaa na kurudi jioni ameshiba.” (Tirmidhi).
Kutoka kwa Ibn Abbas (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao) amesema,
mtume alikwenda kwa Umar alipokuwa yupo na masahaba zake, akasema:
“je nyinyi ni waumini?” hawakujibu. –akawauliza mara tatu- kisha mwishoni
Umar akasema. “ndio, tunaamini kile ulichotuletea, na kushukuru juu ya hali
nzuri na kusubiri juu ya balaa, na tunaamini kadari. Mtume (rehma na amani
zimshukie juu yake) Akasema: “hakika mumeamini kwa jina la Mola wa
Alkaba.” (Tabari).
Tatu: maudhui
Miongoni mwa rehema za Mwenyezi Mungu ni na upendo wake kwa waja
wake ni kuwapelekea mitume ili wawaongoze katika njia ya haki, na katika
njia iliyonyooka, ili isije ikapatikana hoja kwa mja yeyote mbele ya Mwenyezi
Mungu. Mwenyezi Mungu anasema { Mitume hao ni wabashiri na waonyaji,
ili watuwasiwe na hoja juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kuletewaMitume.
Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima }Anisaa 165.
Kumuamni Mwenyezi Mungu ni katika ilaka kubwa walizokuja nazo mitume,
ikiwa na maana kuthibiti imani ya Mwenyezi Mungu –itikadi- ndani ya moyo
wa mja, na kuamini malaika wake, vita vyake, mitume wake, na siku ya
mwisho na kadari kheri zake na shari zake. Na waumini itawalazimu watimize
wajibu wa imani nao ni kutimiza yale waliyokalifishwa ambayo yana uongofu
kutoka kwa Mwenyezi Mungu yaliyoletwa kutoka kwa mtume wetu (rehma
na amani zimshukie) katika makatazo na mahimizo.
Na kumjua Mwenyezi Munguni njia ya kwanza ya imani, Mwenyezi Mungu
anasema { Basi jua ya kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, na omba
maghufira kwa dhambi zako na za Waumini wanaume na Waumini
wanawake. Na Mwenyezi Mungu anajua mahali penu pa kwenda na kurudi,
na mahali penu pakukaa.} Muhammah, 19.
Na kitu kijulikanacho ni kuwa imani ya Mwenyezi Mungu imeshikamana na
matendo mema, na wala havitengani, imekuja katika kurani tukufu ndani ya
aya nyingi, kwa mfano, { Na wale walio amini na wakatenda mema, hao
ndiowatu wa Peponi, humo watadumu }Albaqara 82. Na { Hakika walio amini
na wakatenda mema, Mola wao Mlezi atawaongoa kwa sababu ya Imani yao.
Itakuwa inapita mito kati yao katika Mabustani yenye neema }Yunus 9. Na
aliposema { Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao
yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi }kahf 117. Na aya nyeginezo zilizo tukufu.
Imani huzidi kwa kutii na hupungua kwa maasi, na kuna sehemu (makundi)
tafauti za waumini kwa mujibu wa imani zao kwa Mwenyezi Mungu. Kutoka
kwa Abi Hurayra amesema: amasema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma
na amani zimshukie juu yake) imani ni sehemu sabini au sitini ya mafungu na
bora ya (mafungu haya) ni kauli ya “Lailaha illa llahu” (hapana wa kuabudiwa
kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na kuondosha uchafu njiani na kuona
haya ni sehemu ya imani.” Na matendo mema ni sehemu ya imani.
Na imekuja katika hadithi ya Jibrilu – juu yake rehema- iliyo mashuhuri
inayoweka wazi ukweli wa imani ambayo inapaswa kuwepo ndani ya nyoyo
ya kila muumini, hadithi yenyewe, anasema umar (Mweneyzi mungu amwie
radhi) amesema: siku moja tulipokuwa tumekaa pamoja na mtume (rehma
na amani zimshukie juu yake) akatutokezea mtu amevaa nguo myeupe sana
ana nywele nyeusi haikuonekana athari yoyote ya safari na hakuna yeyote
kati yetu aliyemjua mpaka akakaa mnele ya mtume (rehma na amani
zimshukie juu yake) akakutanisha magoti yake na magoti ya mtume na
kuweka bega lake katika bega la mtume kisha akasema: “ewe Muhammad
nieleze kuhusu uisilamu.” Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
akasema: “ uisilamu ni kushuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa
kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na hakika Muhammad (rehma na
amani zimshukie juu yake) ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na kusimamisha
sala, na kutoa zaka na kufunga ramadhani na kuhiji nyumba ukiwa na uwezo.
Akasema: “umesema kweli.” Akasema: “ nieleze kuhusu imani.” Akasema:
“kumuamini Mwenyezi Mungu na malaika wake na vitabu vyake na siku ya
mwisho na kuamini kadari kheri yake na shari yake. Akasema: “ umesema
kweli.” Akasema: “ nieleze kuhusu ihsani. Akasema: “ni kumuabudu
Mwenyezi kama kama kwamba unamuona na iwapo humuoni basi yeye
anakuona. Akasema: “Umesema kweli.” Akasema: “ nieleze kuhusu kiama.
Akasema: “huenda muulizaji akawa anaelewa zaidi kuliko anaeulizwa.
Akasema: “ nieleze ishara zake” akasema: “ mtumwa kuzaa bwana wake na
kuwaona wachungaji watembeao miguu peku wanashindana katika ujenzi wa
majumba makubwa. Akasema, kisha akaondokam nikabaki hali ya kufikiria,
kisha nikamuuliza ewe Umar unamjua ni nani huyo muulizaji? Akasema: “
Mwenyezi Mungu na mtume wake wanaju. Akasema Yule ni Jibrilu
amekujieni kukufundisheni dini yenu.” (Muslim).
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ameweka wazi katika kitabu chake kitukufu
sifa nyingi za waja wake waumini,kwa mfano, unyenyekevu kwa ajili ya
Mwenyezi Mungu, kwa kuwa unyenyekevu ni vyeo vya juu kabisa, Mwenyezi
Mungu anasema { Hakika Waumini ni wale ambao anapo tajwa
MwenyeziMungu nyoyo zao hujaa khofu, na wanapo somewa Aya
zakehuwazidisha Imani, na wakamtegemea Mola wao Mlezi. 3. Hao ambao
wanashika Sala na wanatoa katika yale tunayo waruzuku 4. Hao kweli ndio
Waumini. Wao wana vyeo, na maghfira,na riziki bora, kwa Mola wao
Mlezi.}Al anfal 2-4. Na anasema { Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa
Mola wao Mleziwananyenyekea, 58. Na wale ambao Ishara za Mola wao
Mleziwanaziamini, 59. Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,61.
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa
kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi, }Al muuminuun 57-61. Na anasema pia
{ Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, naakamcha
Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basimbashirie huyo msamaha na
ujira mwema.} Yasini, 11.
Na mtume (rehma na amani zimshukie juu yake ametupigia mfano wa hali ya
juu ya unyenyekevu. Kutoka kwa Mutarif kutoka kwa baba yake amesema:
nimemuona mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) akisali na katika
kifua chake kuna mgurumo kama mgurumo wa chombo .” (Ibn Khuzayma).
Na mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) alikuwa akimuomba
Mweneyzi Mungu ampe unyenyekevu, kutoka kwa Abi Mijlaz (radhi za
Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: Umar alitusalisha sala,
akaifupisha, na akapinga (kuwa hakufupisha) akasema, kwami sijatimiza
rukuu na sujudu? Wakasema: ndio” akasema: “kwa kuwa mimi nimeomba
kwakati wa sujudu na kurukuu dua aliyokuwa akiomba mtume (rehma na
amani zimshukie juu yake) akiomba “ewe Mola kwa elimu yako ya
visivyojulikana na kudura zako kwa viumbe nihuishe iwapo uhai una kheri
nami na unifishe iwapo kifo kina kheri nami, nakuomba unyenyekevu wako
kwa nikionacho na nisichokiona na neno la kweli niwapo na hasira na
kuridhia, na lengo wakati wa umasikini na utajiri, na kadha ya kuona uso
wako na hamu ya kukutana nawe na najikinga kwako kutokana na madha
yenye kudhuru na fitina zenye kupoteza, ewe Mola zipambe nyoyo zeteu kwa
imani na utufanye katika walioongoka.” (Ahmad).
Mshairi anasema:
Muogope mola na tarajia kila zuri * usiitii nafsi kwa maasi utajuta.
Kuwa na khofu na matarajio * na jibashirie msamaha wa Mungu iwapo ni
muisilamu.
Namiongoni mwa sifa za waumini ni kumtegemea Mwenyezi Mungu, ikiwa
na maana kuufanya moyo umtegemee Mwenyezi Mungu katika kuleta
masilahi na kuondoa madhara, na kumuachia mambo yote Yeye pamoja na
kuitakidi kuwa hakuna atoaye wala azuiaye na anayedhuru na kunufaisha
isipokuwa Yeye pekee. Muumini humtegemea Mwenyezi Mungu na hutenda
sababu zenye kupelekea kutimia matendo bila ya kutegemea matendo hayo.
Kufanya sababu haina maana kuwa humtegemei Mwenyezi Mungu, kutoka
kwa Umar (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema, nimemsikia
mjumbe wa Mweneyzi Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake) akisema:
“ lau kama mungelimtegemea Mwenyezi Mungu kama ipasavyo basi
angelikupeni riziki kama ampavyo ndege, huondoka asubuhi ana njaa na
kurudi jioni ameshiba.” (Tirmidhi).
Ama kwa wale wanaodai kuwa kumtegemea Mwenyezi mungu bila ya
kufanya kazi huku hakuitwi kumtegemea Yeye bali huko ni kuzembea na
kuzembea ametukataza mtume (rehma na amani zimshukie) na pia kukataza
sababu zinazopelekea kuzembea, kutoka kwa Muadh bin jabal ( Mwenyezi
Mungu amwie radhi) amesema; nilikuwa nyuma ya punda wa mtume (rehma
na amani zimshukie) akiitwa Ukayr. Akasema (mtume) ewe Muadh hivyo
unafahamu haki ya Mwenyezi Mungu juu ya waja na haki za waja kwa
Mweneyzi Mungu? Akasema: Mwenyezi Mungu na mtume wake wanajua.
Akasema: “haki ya Mwenyezi Mungu juu ya waja ni kumuabudu Mwenyezi
Mungu na wala wasimshirikishe na chochote na haki za waja kwa Mwenyezi
Mungu ni kutomwadhibu Yule asiyemshirikisha na chochote.” Akasema: ewe
mjumbe wa Mwenyezi Munguje niwaambie watu hivyo? Akasema:
“usiwaambie ili wasije kuzembea” (muslim). Kumtegemea kunakotakiwa
kunashikamana na maisha ya muumini, manufaa hayatopatikana au madhara
isipokuwa kwa utegemezi ulio mzuri.
Na miongoni mwa sifa za waumini ni kuhifadhi sala na kunyeyekea ndani
yake. Mwenyezi Mungu anasema { Hakika wamefanikiwa Waumini,2. Ambao
ni wanyenyekevu katika Sala zao,}. Sala ni alama ya uisilamu na imeamrishwa
kupitia aya nyingi Mwenyezi Mungu anasema{Na shikeni Sala, na toeni Zaka,
na inameni pamoja na wanao inama}Albaqara 43. Na mtume (rehma na
amani zimshukie) akaifanya ni moja ya nguzo tano za kiisilamu, kutoka kwa
Ibn Umar (Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema; amesema mjumbe wa
Mwenyezi Mungu (reahma na amani zimshukie) “ uisilamu umejemngea juu
ya nguzo tano: kushuhudia kuwa hapana Mola wa haki isipokuwa Mwenyezi
Mungu, na Muhammad ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu nakusimamisha
sala, na kutoa zaka, na kuhiji nyumba na kufunga Ramadhani.” (Bukharin a
Muslim).
Na watu wametafautiana kidaraja za unyenyekevu ndani ya sala, wapo
wapatao malipo kamili, na wengine hawana wapatacho zaidi ya
kujihangaisha na tabu, kutoka kwa Abi Hurayra (Rehma na amani ziwe juu
yake) amemsikia mjumbe wa Mwenyezi Mungu akisema: “ huenda
anaesimama usiku kusali fungu lake likawa ni kukesha tu usiku, na huenda
anaefunga fungu lake likawa ni kukaa na njaa na kiu.” (Albaihaqi). Sala ni
sababu za kuifunza nafsi tabia na nyendo na kujiweka mbali na yenye
kuchukiza, mwenye kusali huwa yuko mbali sana na sababu za kuingia katika
maasi na maovu. Mwenyezi Mungu anasema { na ushike Sala.Hakika Sala
inazuilia mambo machafu na maovu.}Al ankabuut 45. Na katika yenye
kuthibitisha kuwa ni lazima sala iwe na unyenyekevu ni hadithi iliyopokelewa
na Anas bina Malik (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake)amesema;
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu
yake) inakuwaje watu hunyanyua macho yao juu (mbinguni) ndani ya sala
zao, akasisitizaneno lake hili mpaka akasema: waache hivyo au Mwenyezi
Mungu atapofua macho yao.” (Bukhari).
Na miongoni mwa sifa za waumini ni kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kwa
maana ya utoaji wa zaka iliyolazimishwa na sadaka za kujitolea, kutoka kwa
Ibn Umar (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: “mkono wa juu (utoao)
ni bora kuliko wa chini (usiotoa), na anza kwa unaowalisha, na sadaka iliyo
bora ni ile itolewayo kwa kificho na anayeacha kuomba Mungu atamsaidia na
anayejitosheleza basi Mungu atamtoshelezea.” (Bukhari). Kutoka kwa Ibn
Masuud (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amepokea kutoka kwa mtume
(rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ mtu akitoa kwa ajili ya
watu wake huhesabiwa ni katika sadaka.” (muslim). Muumini huamini kuwa
mali aliyonayo ni kama dhamana kwake, na fadhila zipo mikononi mwa
Mwenyezi Mungu. Kutoka wa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi)
kwamba mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: “ kijana
mmoja alipokuwa akitembea jangwani akasikia sauti utoka mawinguni,
nyoshelezea bustani ya Fulani, mawingu yale yakasogea kachota maji yake
katika chombo, tahamaki kile chombo kikajaa maji chote, mara kuna mtu
mwengine amemsimama kwenye bustani yake akijaribu kunyoshelezea maji,
akamwambia: ewe mja wa Mweneyzi Mungu, unaitwa nani? Akasema, ni
Fulani lile jina alililisokia kutoka katika mawingu, akamwambia, kwa nini
unaniulia jina langu, akamwambia: “ nimesikia sauti kutoka mawinguni
ambayo yamenipa maji yake, yakisema “ nyosheleza bustani ya Fulani kwa
kutaja jina lako, wewe kwani unafanya nini ndani ya bustani hiyo? Akajibu:
“kwa kuwa umeuliza basi mimi huwa matunda yakiwa tayari basi hutoa
sadaka thuluthi na mimi mwenyewe na wanangu hula thuluthi najirudisha
thuluthi yake.
Na kurani imeashiria sifa za waumini kama ifuatavyo kwa mfano,
wanajiepusha nay a upuuzi, na huchunga amana, Mwenyezi Mungu anasema
{1. Hakika wamefanikiwa Waumini,2. Ambaoni wanyenyekevu katika Sala
zao, 3. Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi, 4. Na ambao wanatoa
Zaka. 5. Na ambao wanazilinda tupu zao, 6. Isipo kuwa kwa wake zao au kwa
iliyo wamilikimikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa. 7. Lakini
anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndiowarukao mipaka. 8. Na ambao
wanazitimiza amana zao na ahadi zao, 9. Na ambao Sala zao wanazihifadhi
11. Hao ndio warithi, 11. Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo}
Almuuninuun 1-11. Aya zikaweka wazi kuwa mafanikio na kufuzu ni kwa
atakayesifika kwa sifa hizi za unyenyekevu ndani ya sala, kujiepusha na
upuuzi, kutoa zaka, kuhifadhi tupu, kuhifadhi amana na kuzifikisha kwa
wenyewe, kutimiza ahadi na yote hayo yametajwa ndani ya kurani kama ni
sifa kwa waumini na tabia zao.
Kwa waumini ni lazima wawe na tabia ya kutimiza ahadi kama ilivyokuja
ndani ya kurani ili ajidhaminie mafanikio duniani na akhera, ikipatikana imani
ndani ya moyo wa mja kama itakiwavyo basi itamuhifadhi na chuki na itikadi
kali na kutenda yaliyokatazwa na itamfanya ampendelee mwengine zaidi
kuliko hata nafsi yake na atajiepusha na kauli za uongo na kukaa vikao vya
kipuuzi, na atakuwa na pupa ya kufanya mema kwa ajili ya manufaa ya jamii
na taifa lake. Ama kwa wanaojidai kuwa ni wauminina tabia zake zikawa ni
mbaya na mwenendo wake ukawa si mzuri basi imani yake huwa ni pungufu.
Kwani imani ahihi hujulikana, Kutoka kwa Anas bin Malik (Mwenyezi mungu
amwie radhi)hakika ya mtume (rehma na amani zimshukie juu yake siku moja
alitoka na akakutana na kijana wa kianswar anaitwa Haritha bin Nuuman,
akamwambia: “ umeamkaje ewe Haritha? Akasema: nimeamka hali ya kuwa
ni muumini wa kweli. Akasema mtume wa Mweneyzi Mungu (Rehma na
amani zimshukie juu yake) angalia usemacho, kwani kila haki ina kithibitisho,
basi ni upi huo uthibitisho wa imani yako? Akasema: Najizoea nafsi yangu
kujiepusha na ya dunia, nikakesha usiku wangu na kufunga mchana wangu,
nami kama kwamba naagalia Arshi ya Mola wangu iliyo wazi na kama
kwamba naagalia watu wa peponi namna wanavyotembeleana, na kama
kwamba naangalia watu wa motoni na namna wanavyofanyiana uadui ndani
yake. Mtume rehma na amani ziwe juu yake akamwambia. Umeona
(umesema kweli) basi jilazimishe. Kasema hivi mara mbili, mja Mwenyezi
Mungu amenawirisha imani ndani ya moyo wake.” (sehemu ya imani).
Inatakiwa muumini asifike kwa sifa njema za ukweli, uaminifu, kutekeleza
ahadi, ukarimu, haya, msimamo, upole, msamaha, unyeyekevu, uadilifu,
hisani, kuathiri na tabia nyengine njema ambazo kurani imehimiza, Mwenyezi
Mungu anasema {Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na kuweni
pamoja na wakweli}At tawbah 119. Na akasema { Na ambao wanazichunga
amana zao na ahadi zao } Al maarij 32. Na akasema kuhusu alama za wakweli
wacha Mungu. { na wanao timiza ahadi yao wanapo ahidi, na wanaovumilia
katika shida na dhara na wakati wa vita; haondio walio sadikisha, na hao ndio
wajilindao } Al baqara 177.
Na Mwenyezi Mungu amewandalia waumini wenye kusifika kwa tabia njema
kwa malipo mazuri na thawabu njema, akasema { Hakika wale walio amini na
wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi118.
Watadumu humo; hawatataka kuondoka.} Kahf 117-118.
Uhusiano wa kifamilia ulio bora
23 Jamad Akhir 1437 H. sawa na 1 Aprili 2116 AD
Vipengele
Nafasi ya familia katika uisilamu.
Njia za uongofu katika kuwepo kwa utulivu wa kifamilia.
Uchaguzi bora
Kuchunga ya haki na yaliyo lazima
Kuwepo kwa upendo na huruma
Kuishi kwa salama
Uadilifu kati ya watoto.
Athari za kuwepo kwa utulivu wa familia katika jamii.
Pili: dalili
Ndani ya Qurani Tukufu.
Mwenyezi Mungu anasema {Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni
wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao.Naye amejaalia
mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara
kwa watu wanaofikiri} (Aruum. 21).
Mwenyezi Mungu anasema { Na Mwenyezi Mungu amekuumbieni mwake
katika jinsi yenu, na akakujaalieni kutoka kwa wake zenu wana na wajukuu,
na akakuruzukuni vitu vizuri vizuri. Basi je, wanaamini upotovu na
wanazikataa neema za Mwenyezi Mungu?}(An hahl. 72)
Mwenyezi Mungu anasema { Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema
katika watumwa wenu na wajakazi wenu. Wakiwa mafakiri Mwenyezi Mungu
atawatajirisha kwa fadhila yake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa
Mwenye kujua.}(An nuur 32)
Mwenyezi Mungu anasema { Nao wanawake wanayo haki kwa Sharia kama
ile haki iliyo juu yao. }(Al baqara 228)
Mwenyezi Mungu anasema { Na kaeni nao kwa wema, na ikiwa
mmewachukia, basi huenda mkakichukia kitu, na Mwenyezi Mungu ametia
kheri nyingi ndani yake.}(Anisaa 19.)
Mwenyezi Mungu anasema {Na mkichelea kutakuwapo mfarakano baina ya
mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume,na
muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Mwenyezi Mungu
atawawezesha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye khabari}(Anisaa
35)
Mwenyezi Mungu anasema { Mwenye wasaa atoe kadiri ya wasaa wake, na
mwenye dhiki atoe katika alicho mpa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu
hamkalifishi mtu ila kwa kadiri ya alicho mpa. }(Atalaak.7)
Dalili katika hadithi
Kutoka kwa Abdallah bin Masuud (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie)
amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie) “ enyi vijana mweneye kuweza miongoni mwenu kuoa basi na
aowe, kwani hivyo ni kuinamisha macho na kuhifadhi tupi. Na asiyeweza basi
afunge kwani hiyo ni kinga.” (Bukhari na Muslim).
Na kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema:
Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie) :
“mwanamke huolewa kwa mambo manne; kwa mali yake na nasaba (ukoo)
yake na uzuri wake na dini yake, chagua aliye na dini ili ubarikiwe mikono
yako.” (Bukhari).
Kutoka kwa Anas (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema: Wageni
watatu walikuja katika nyumba za wake wa Mtume (rehma na amani
zimshukie) kuja kuuliza kuhusu ibada ya Mtume (rehma na amani zimshukie)
na walipoelezwa wakawa kama kwamba wamejiona ni wadogo wakasema:
“tuko wapi sisi na Mtume? Amekwishasamehewa madhambi yaliyotangulia
na yaliyochelewa. Na mmoja wao akasema: “ ama mimi nitasali sala za usiku
milele. Mwengine akasema: “ mimi nitafunga na wala sitofuturu. Na wa
mwisho akasema: “ama mimi nitajiepusha na wanawake na sitaoa milele.
Mtume (rehma na amani zimshukie) akawaendea akasema: “ni nyinyi
muliosema hivi na hivi, ama mimi naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu
ninamuogopa Mweneyzi Mungu kuliko nyinyi nyote lakini ninafunga na
kufuturu, ninasali na kulala na ninaoa wanawake, na mwenye kujiweka mbali
na mwenendo wangu basi hayuko nami.” (Bukhari.)
Kutoka kwa Abi hatim Almuzaniy amesema: amesema Mjumbe wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukie): atakapokujieni Yule munayemridhia dini
yake na tabia zake basi muozesheni, na musipofanya hivyo itakuwa ni fitina
duniani na ufisadi. Wakasema: “ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na akiwa
naye? “ akasema: “atakapokujieni Yule munayemridhia dini yake na tabia
zake basi muozesheni, mara tatu. (Tirmidhi) na katika kitabu cha Bayhaqi
(atakapokuja yule munayemridhia dini yake na tabia zake basi muozesheni,
na musipofanya hivyo itakuwa ni fitina katika dunia na ufisadi mkubwa mno.)
Kutoka kwa Umar (Mwenyezi Mungu amwie radhi) hakika Mtume (rehma na
amani zimshukie juu yake) amesema: nyote ni wachungaji, na nyote
mutaulizwa juu ya mulivyovichunga. Imamu ni mchungaji naye ataulizwa juu
ya aliowachunga, mume ni mchungaji juu ya watu wake naye ataulizwa juu
ya aliowachunga, mke ni mchungaji katika nyumba ya mumewe naye
ataulizwa juu ya aliowachunga, mtumishi ni mchungaji juu ya mali ya bwana
wake naye ataulizwa juu ya alichokichunga.” Mpokezi akasema nadhani
alisema: “kijana ni mchungaji wa mali ya baba yake naye ataulizwa juu ya
alichokichunga, nyote ni wachungaji na mutaulizwa juu ya mulichokichunga.”
(Bukhari)
Kutoka kwa Abdallah bin Amru bin Al`as (Radhi za mwenyezi Mungu ziwe juu
yao) amesema: nimemsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu akisema:
“inatosha mtu kuwa na madhambi kwa kukizembea kile
anachokilisha.”(Ahmad). Na katika mapokezi ya Hakim (inatosha mtu kuwa
na madhambi kwa kukizembea kile anachokilea.)
Maudhui
Uisilamu umejali sana familia kwani ni nguzo ya kwanza ya kujenga, jamii
familia ikitengemea na jamii nayo hutengemea na ikiharibika na jamii pia
huharibika. Kwa ajili hiyo uisilamu ukaweka shuruti na vipimo
vitakavyosimamia jambo hili, kwa ajili ya kuwepo na utulivu na usalama kwa
lengo la kuhifadhi watu na jamii nzima, kwani utulivu wa familia ni utulivu wa
jamii.
***********************
Uisilamu umefuatilia uhumimu wa familia hata kabla ya makutano (ndoa)
katika wa wanajamii kwa kutaka kuwepo upendo, huruma na ushirikiano na
kupunguza kila kinachopelekea uharibifu wa jengo hilo. Na ukawataka
wafuasi wake kutengeneza familia kwa njia zinazokubalika zenye kuhifadhi
utu na heshima ya mwanadamu yenye kwenda sambamba na maumbile yake
na njia hiyo ni ya kuozana ambayo ni mojawapo ya mwenendo wa Mwenyezi
Mungu kwa viumbe vyake vyote. {na kila kitu tumekiumba viwiliviwili ili
mupate kukumbuka} (Adhariyat. 49). Na anasema pia {utukufu ni wake
aliyeumba kike na kiume katika vile viotavyo katika ardhi na katika nafsi zenu
na katika vile musivyovijua} Yaasin. 36). Ndoa ni mwenendo wa kimaumbile.
Na mwenyezi Mungu akaifanya kuwa ni mojawapo ya ishara za utukufu wake
na nguvu zake na miujiza yake mikubwa yenye kushangaza, akasema { Na
katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu
ili mpate utulivu kwao.Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu.
Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaofikiri.}(Ruum.
21).
Na kama uisilamu ulivyopendekezesha kutengeneza familia na utulivu wake
kuwa ni kuijenga ardhi na kuleta masilahi kwa jamii na ujenzi wa taifa na
kuwa ni njia ya kufikia katika lengo lililokusudiwa: nalo ni kueneza heshima
na utu na kuilinda jamii kutokana na aina zote za uchafu na maovu, na
kuunganisha familia kwa njia ya kuozana, pamoja na hekima nyengine na
malengo yaliyo mazuri. Mwenyezi Mungu anasema { Na waozeni wajane
miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu na wajakazi wenu.
Wakiwa mafakiri, Mwenyezi Mungu atawatajirisha kwa fadhila yake. Na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa Mwenye kujua. 33. Na wajizuilie na
machafu wale wasio pata chakuolea, mpaka Mwenyezi Mungu awatajirishe
kwa fadhila yake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao
mikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikieni kama mkiona wema
kwao. Na wapeni katika mali ya Mwenyezi Mungu aliyo kupeni. Wala
msiwashurutishe vijakazi vyenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta pato la
maisha ya dunia, ilhali wao wanataka kujihishimu.Na atakaye walazimisha
basi Mwenyezi Mungu baada ya kulazimishwa kwao huko, atawasamehe,
kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.} (Anuur
32.33). bali pia Mtume (rehma na amani zimshukie) amewahimiza vijana
wafikie lengo la kuona kwa kuweka wazi manufaa yake na faida zake
akasema: ““ enyi vijana mwenye kuweza miongoni mwenu kuoa basi na
aowe, kwani hivyo ni kuinamisha macho na kuhifadhi tupi. Na asiyeweza basi
afunge kwani hiyo ni kinga.” (Bukhari na Muslim).
Kinyume na hivyo, uisilamu umekataza mambo yenye kupingana na
uimarishaji wa ulimwengu, mfano kukaa bila ya kuoa na kujiweka mbali na
wanawake (kukataa kuoa), mtme (rehma na amani zimshukie) amekataza
kukaa bila ya kuoa, Saad bin abi Waqas (radhi za Mwenyezi Mungu
zimshukie) amesema, hali ya mtume (rehma na amani zimshukie) kumjibu
Othman bin Mad ghun kuhusu kuacha kuoa, na lau kama angeruhusiwa basi
nasisi tungelihusika pia.” (Muslim). Na kutoka kwa Anas (radhi za Mwenyezi
Mungu zimshukie) amesema wageni watatu walikuja katika nyumba za wake
wa Mtume (rehma na amani zimshukie) kuja kuuliza kuhusu ibada ya Mtume
(rehma na amani zimshukie) na walipoelezwa wakawa kama kwamba
wamejiona ni wadogo wakasema: “tuko wapi sisi na Mtume?
Amekwishasamehewa madhambi yaliyotangulia na yaliyochelewa. Na mmoja
wao akasema: “ ama mimi nitasali sala za usiku milele. Mwengine akasema: “
mimi nitafunga na wala sitofuturu. Na wa mwisho akasema: “ama mimi
nitajiepusha na wanawake na sitooa milele. Mtume (rehma na amani
zimshukie) akawaendea akasema: “Ni nyinyi muliosema hivi na hivi, ama
mimi naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu ninamuogopa Mweneyzi Mungu
kuliko nyinyi nyote lakini ninafunga na kufuturu, ninasali na kulala na ninaoa
wanawake, na mwenye kujiweka mbali na mwenendo wangu basi hayuko
nami.” (Bukhari.)
Na ilivyokuwa utulivu wa familia ni kitu kitakiwacho kisheria na hata kidunia
basi usilamu ukaweka nguzo madhubuti na misingi imara ili ukoo na familia
idumu kati ya wanandoa na upatikane utulivu unaotakiwa, na miongoni mwa
misingi hiyo ni:-
Uchaguzi mwema kwa kila mwanandoa kwa mwengine, Mtume (rehma na
amani zimshukie) aliusia wakati wa kuchagua mke kuwa uchaguzi uwe
mwema kwani una masilahi na unahifadhi mali na heshima na ni starehe
nzuri duniani. Kutoka kwa Abdalla bin Amruu (radhi za Mwenyezi Mungu
ziwashukie) amesema: amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na
amani zimshukie): “ dunia ni starehe na starehe iliyo bora zaidi ni mke
mwema.” Na familia inapojengwa kwa uchaguzi uliobora basi ndipo utulivu,
mapenzi ya kudumu, kuoneana huruma kunapatikana, na hapo tena ndoa
inakuwa ni yenye Baraka na kuwa na athari.
Na katika uchaguzi hakuna budi iwe ni kwa misingi ya dini na tabia,
imepokewa na Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) Amesema
Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie) : “mwanamke
huolewa kwa mambo manne; kwa mali yake na nasaba (ukoo) yake na uzuri
wake na dini yake, chagua aliye na dini ili ubarikiwe mikono yako.” (Bukhari).
Na katika mapokezi ya Imam Ahmad kutoka kwa Abi Saad Alkhudriy (radhi za
Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema: amasema Mjumbe wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukie) “mwanamke huolewa kwa moja ya
mambo matatu; huolew mwanamke kwa mali zake, huolewa mwanamke
kwa uzuri wake, na huolewa mwanamke kwa dini yake, chukua mwenye dini
na tabia ubarikiwe mkono wako. (Ahmad)
Mke ana nafasi kubwa katika kulea familia, akiwa mwema basi nayo huwa
njema na jamii itakuwa na utulivu na kama si mwema basi familia
huporomoka.
Mshairi anasema:
Mama ni shule pindi ikiandaa * itaandaa watu weney asili njema.
Pia Mtume (rehma na amani zimshukie) ameusia wakati wa kuchagua mke
kuwa uchaguzi uambatane na dini na tabia. Kutoka kwa Abi Hatim Almuzaniy
(radhi za mwenyezi Mungu zimshukie) amesema Mjumbe wa Mwenyezi
Mungu (rehma na amani zimshukie): atakapokujieni Yule munayemridhia dini
yake na tabia zake basi muozesheni, na musipofanya hivyo itakuwa ni fitina
duniani na ufisadi. Wakasema: “ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na akiwa
naye“ akasema: “atakapokujieni Yule munayemridhia dini yake na tabia zake
basi muozesheni, mara tatu. (Tirmidhi). Mtume akafanya kuwa dini na tabia
kuwa ndivyo sifa muhimu za ndoa njema, kwa ajili hiyo, uchaguzi sahihi ni
misingi ya dini ambayo utulivu wa familia utapatikana ambao utakuwa ni
sababu ya kuendelea kwa jamii.
Na miongoni mwa utulivu ni; kila mmoja katika wanafamilia achunge wajibu
na haki. Kwani Uisilamu umetoa haki na wajibu ulio sawa kwa wanandoa
wote, Mwenyezi Mungu akasema { Nao wanawake wanayo haki kwa Sharia
kama ile haki iliyo juu yao.}(Al baqara 128). Mwanafamilia hatotakiwa
kutekeleza haki ya mwengine kabla ya kutekeleza haki aliyonayo yeye
kwanza ili upendo na utulivu upatikane vitu ambavyo vinaituliza familia.
Uisilamu ukaweka wazi wajibu na haki hizi, na ukazigawa kwa wanandoa na
kutaka kila mmoja kujilazimisha na kuzihifadhi, kwani kuna haki za kimali na
za kiroho na kimalezi, pia kuna haki za kushirikiana katika ujenzi wa
kutekeleza majukumu. Na umuhimu wa kusaidiana kati ya wanafamilia
kutokana na mahitajio ya maisha. imepokewa katika hadithi ya Abdallah bin
Amru (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) kwamba yeye amemsikia
Mjumbe wa Mweneyzi Mungu akisema nyote ni wachungaji, na nyote
mutaulizwa juu ya mulivyovichunga. Imamu ni mchungaji naye ataulizwa juu
ya aliowachunga, mume ni mchungaji juu ya watu wake naye ataulizwa juu
ya aliowachunga, mke ni mchungaji katika nyumba ya mumewe naye
ataulizwa juu ya aliowachunga, mtumishi ni mchungaji juu ya mali ya bwana
wake naye ataulizwa juu ya alichokichunga.” Mpokezi akasema nadhani
alisema: “kijana ni mchungaji wa mali ya baba yake naye ataulizwa juu ya
alichokichunga, nyote ni wachungaji na mutaulizwa juu ya mulichokichunga.”
(Bukhari). Na kutoka kwa Abdallah bin Amru bin Al`as (Radhi za mwenyezi
Mungu ziwe juu yao) amesema: nimemsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu
akisema: “inatosha mtu kuwa na madhambi kwa kukizembea kile
anachokilisha.”(Ahmad).
Mmoja wa masahaba alimuuliza Mtume (rehma na amani zimshukie)
akasema: “ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni ipi haki ya mke wa mmoja
wetu kwake?” akasema: “kumlisha unapokula, kumvisha unapovaa au
unapopata, usimpige usoni, wala usimnange (usimwambie kama ni mbaya)
na wala usimkimbie isipokuwa ndani ya nyumba.” (Abi Daudi).
Mfano huu wa Asmaa bint Yazid Al ansareyyah anamuuliza Mtume (rehma na
amani zimshukie) anasema: “ Kwa hakika sisi wanawake kuna wengi wetu
wamefungwa na kuwekwa ndani katika misingi ya nyumba zenu na kumaliza
matamanio yenu na kubeba mimba za watoto wenu. Nyinyi wanaume
mumefadhilishwa sana kuliko sisi kwa kusali sala ya Ijumaa na sala za
pamoja, kuwatembelea magonjwa, kushindikiza jeneza, kuhiji tena na tena,
na bora kuliko yote ni kuwa munapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi
Mungu, na mtu yeyote miongoni mwenu akitoka na kwenda kuhiji au
kufanya umra tunakuhifadhieni mali zenu na kukutengeeni nguo na kuwalea
watoto wenu, hivyo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu hatushirikiani nanyi
katika malipo? Akasema: “Mtume (rehma na amani zimshukie) akawageukia
sawa sawa (kwa uso wake) masahaba zake kisha akasema: “ mmesikia
masuala ya mwanamke hakuna mazuri kama hayo katika masuala ya dini
yaliyoulizwa, ni nani muulizaji?wakasema: “ewe Mjumbe wa Mwenyezi
Mungu hatukuwa tukidhani kwamba mwanamke angeweza kuuliza kama
hivi. Mtume (rehma na amani zimshukie) akamgeukia mwanamke na kisha
akasema: “ ondoka ewe mwanamke, na waeleze wanawake walio nyuma
yako kuwa, mwanamke akiwa mwema kwa mumewe na kutaka radhi zake na
kumtii basi hupata malipo sana na hayo yote.” Akasema: “mwnamke
akaondoka hapo hali ya kusema “Lailahailla llah na Allahu Akbar, hali ya
kujibashiria mema. (Mlango wa sehemu ya imani).
Kwa ajili hiyo kufanikiwa kwa familia ya kiisilamu ipo katika kuhifadhi haki na
wajibu kati ya wanandoa na kujiepusha na uzembe na kukiuka mipaka.
Na miongoni mwa mambo yenye kusaidia kuleta utulivu ndani ya familia; ni
kuenea kwa upendo kati ya wanafamilia, kwani upendo ni nguzo muhimu
ndani ya nyumba na ni chanzo cha mafanikio yote ndani ya familia yenye
njema. Nao ni muhimili mkubwa ambao unapaswa kwa kila mwanafamilia
kuwa nao ili familia ineemeke kwa utulivu, upendo na msimamo, Mwenyezi
Mungu anasema { Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu
kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao.Naye amejaalia mapenzi na
huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu
wanaofikiri} (Ruum.21). Upendo kwa wanajamii wote umewekewa rehani
kwa kuwepo katika familia. Na tuna kigezo kizuri kwa Mtume (rehma na
amani zimshukie) kwani alikuwa ni mfano wa upendo kwa watu wa familia
yake wote bila kubaguwa, wake zake, watoto wake na hata wajukuu wake na
mtumishi wake kwani yeye (rehma na amani zimshukie) alikuwa ni mbora
kwa watu wake.
Na iwapo nyumba haina upendo basi maisha ya familia huwa ni mabaya na
magumu, hivo, ni wajibu wa kila mwanafamilia awe makini katika kuhakikisha
kuna upendo.
Na miongoni mwa utulivu wa familia: ni kuishi kwa wema, na hili nalo
ametuamrisha Mola wetu na Mtume wetu nae ametuusia. Mwenyezi Mungu
anasema Na kaeni nao kwa wema, na ikiwa mmewachukia, basi huenda
mkakichukia kitu, na Mwenyezi Mungu ametia kheri nyingi ndani
yake.}(Anisaa 19.) kila mwanandoa anahitajika kuwa na mawasiliano na
mwengine ili upendo uenee na ushirikiano uzidi hapo ndipo lengo la ilaka-
uhusiano- litapatikana. Mwenyezi Mungu anasema { Wao ni vazi kwenu, na
nyinyi ni vazi kwao.}(Al baqara 187) na akasema pia { Na katika Ishara zake ni
kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu
kwao.Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila
ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaofikiri.}(Ruum. 21). Na akasema { na
katika hiyo hiyo akamfanya mwenzi wake, ili akae naye kwa utulivu. } (al
araaf. 189).
Na katika yaletayo uhusiano mwema ni pamoja na maneno mazuri vitendo
vyema, kusameheana, kusaidiana, kuheshimiana, kushauriana, kulinda siri,
kujiepusha na mzozo na matatizo na mambo mengineyo yaliyo mazuri.
Na Mtume (rehma na amani zimshukie) pamoja na masahaba zake
wametuwekea mifano mizuri kuhusu uhusiano wa kuishi na familia zao.
Imepokewa kutoka kwa Aswad, amesema,: nimemuuliza Aisha (rehma na
amani zimshukie) Mtume alikuwa akifanya nini nyumbani kwake? Akasema:
“alikuwa akifanya kazi za watu wake- yaani alikuwa akiwasaidia wakeze -
muda wa sala ukifika alikuwa akitoka na kwenda kusali. (Muslim). Na kutoka
kwa ibn Abbas (radhi za Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema: Mimi
ninapenda kujipamba kwa mwanamke (mke wangu) kama nipendavyo yeye
ajipambe kwa ajili yangu, kwani Mwenyezi Mungu anasema { Nao wanawake
wanayo haki kwa Sharia kama ile haki iliyo juu }(Al baqara 228). Na nipendalo
ni usafi kwa haki zangu zote, kwani Mwenyezi Mungu anasema { Na
wanaume wana daraja zaidi kuliko wao.} (Albaqara 228) (kitabu cha Ibn Abi
Shayba).
Na miongoni mwa uhusiano mwema kati ya wanandoa; ni kumuachilia
mmoja wapo matatizo yote ya ndani ya ndoa, uhusiano mwema unakusanya
maana zote zinazoshikamana na uhai wa wanandoa. Hakina ya uisilamu
unahimiza sana kuwepo kwa uhusiano wa mapenzi, kufahamiana na kuwa
pamoja na hii ni hatua nzuri ya kujenga jamii.
Na miongoni mwa mambo ambayo yatasaidia kuendeleza familia: ni
kushauriana kati ya wanandoa, kwani katika kushauriana kunaleta upendo
kati yao. Hata katika mambo ambayo yataonekana kwa baadhi ya watu kuwa
ni madogo mfano suala la kumnyonyesha mtoto miaka miwili, Mwenyezi
Mungu anasema {Na kama wote wawili wakitaka kumwachisha ziwa kwa
kuridhiana na kushauriana, basi si vibaya kwao.} (Al baqara. 233).
Mashauriano kati ya wanandoa na hata wanafamilia hujenga muongozo wa
maisha ya dini yetu tukufu ya kiisilamu. Na amri iliyokuja katika aya hii ni kwa
ujumla aliposema { Na wanao mwitikia Mola wao Mlezi, na wakashika Sala,
na mambo yao yakawa ni kwa kushauriana baina yao, na kutokana na tulicho
waruzuku wakawa wanatoa }(Ashuraa.38). na jambo hili ndilo alilolofanya
Mtume (rehma na amani zimshukie) kimatendo. Na katika mienendo
mengine ya kushauriana kwake na wakeze, mfano; kama ilivyotokea kati
yake (rehma na amani zimshukie) na mkewe bibi Umu Salama (radhi za
Mwenyezi Mungu zimshukie) siku ya Hudaibiya. Baada ya Mtume kumaliza
kuweka ahadi za suluhu kati yake na watu wa Makka, akawaambia masahaba
zake: “ simameni na chinjiyeni kisha nyoeni”. Mpokezi wa hadithi akasema:
naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu hajasimama mtu yeyote mpaka akarudia
kusema tena hivyo mara tatu. Na ilivyokuwa hajasimama yeyote Mtume
(rehma na amani zimshukie) akaingia hemani kwa Ummu salama akamueleza
yaliyotokea kati yake na watu wake. Ummu salama akamwambia: “Ewe
Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unataka wakusikilize kuhusu hilo? Toka kisha
usizungumze na yeyote mpaka utakapochinja mnyama wako na kumuita
kinyozi wako na kukutaka nywele. Mtume akatoka na hakumsemesha yeyote
mpaka akachinja mnyama akamwita kinyozi na kumnyoa, na watu
walipomuona wakasimama na kunyoa na wengine wakanyoana mpaka
wakakaribia kusongamana.) (Muslim) Hassan Basriy (radhi za Mwenyezi
Mungu zimshukie) amesema; “ijapokuwa Mtume hakuwa na ulazima wa
kufuata ushauri wa Ummu Salama isipokuwa amefanya hivyo ili watu wapate
kumfuata na wala mwanamme asihisi kuwa kuna kasoro katika kufuata
ushauri wa mwanamke.
Pia miongoni mwa misingi ya utulivu wa familia: ni kutoa mahitajio kwa
wanafamilia wote, kwani ni haki ambayo sheria ya kiisilamu imewajibisha.
Mwenyezi Mungu anasema { Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa
kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao
wanayo yatoa. }(Anisaa 34). Na kusema { Na juu ya baba yake chakula cha
kina mama, na nguo zao kwa mujibu wa ada. Wala halazimishwi mtu ila kwa
kadiri ya uwezo wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mwanawe, wala
baba kwa ajili ya mwanawe. Na juu ya mrithi mfano wa hivyo. }(Albaqara
233). Na akasema pia {7 Mwenye wasaa atoe kadiri ya wasaa wake, na
mwenyedhiki atoe katika alicho mpa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu
hamkalifishi mtu ila kwa kadiri ya alicho mpa.} (Atalaq. 7).
Na miongoni mwa mambo yenye kusaidia kuwepo kwa utulivu ndani ya
familia: kuwepo kwa uadilifu kwa wanafamilia, malezi mema ya kidini kwa
watoto na kuwafundisha mambo ya dini. Uadilifu ni nguzo muhimu sana
katika kuendelea kwa familia, Mtume (rehma na amani zimshukie)
ametuhadharisha kuwatafautisha watoto katika kuwa nao kwa ajili ya
kuhifadhi ushirikiano na kuwa pamoja kwa wnafamilia. Imepokewa na
Nuuman bin Bashiir (radhi za Mwenyezi Mungu ziwashukie) amesema: baba
yangu alinitolea sadaka kwa baadhi ya mali zake. Ummu Umra bint Rawaha
akasema: “ sikubali mpaka tumuweka Mtume kuwa ni shahidi, baba yangu
akaondoka mpaka kwa Mtume (rehma na amani zimshukie) ili awe ni shahidi
wa sadaka yangu. Mtume (rehma na amani zimshukie) akamuuliza, je,
umefanya hivyo kwa wototo wako wengine? Akasema: “hapana” akasema: “
Muogopeni Mwenyezi Mungu na wafanyieni uadilifu watoto wenu.” Baba
yangu akarudi na kuirudisha ile sadaka. (Muslim).
Uisilamu umeiangalia familia kwa mtazamo wa heshima na kuitukuza, kwani
ni mfungamano uliosafi na ni malengo yaliyo matakatifu, na ukataka familia
ibakie kuwa ni madhubuti yenye kushikamana. Ifikie malengo yake na
isimame imara penye matatizo. Kwa ajili hii, uisilamu ukaiangalia kwa
umakini zaidi na kuweka adabu ambazo zitakuwa ni msingi wa kujenga
familia iliyoshikamana na yenye nguvu. Na yenye kuhifadhi utulivu wa jamii
na kuweko mbali na aina zote za kiugaidi na utumiaji wa nguvu.
Jamii itakapokuwa na utulivu wa watu wote watahisi usalama katika nyanja
zote, kinafsi, kimwili kijamii na kiuchumi, kitu ambacho kitaakisi jamii ya
kiisilamu na uwepo wake wa amani na utulivu. Uisilamu umezingatia utulivu
wa familia ni njia mojawapo ya kuhakikisha usalama wa kijamii kwa
kuepukana na ufisadi na mizozo, mwanzo wa usalama wa jamii unatokana na
familia, kisha shuleni na baadae katika jamii nzima.
Familia ni shule ya kwanza ambayo mtoto huelimishwa zuri na baya, kheri na
shari, na kujifunza kutimiza majukumu na uhuru wa maoni. Familia ndio
imjengayo mtoto na kujulikana nini akitakacho na iwapo atakuwa ni raia
mwema ndani ya jamii yake.
Usalama hauletwi kwa nguvu, hutetwa na wanajamii weneywe, kupitia
dhamiri zao na kwa nafasi kuu ya familia katika kutengeneza dhamiri na
kuikuza katika nafasi za watu wake.
Fadhila za masahaba (radhi za Mwenyezi Mungu
ziwashukie)
na mifano ya historia yao njema 44 Jamad Akhar 4257H. sawa na 33/5/3144
Kwanza: vipengele
7. Nafasi za masahaba na kupanda vyeo vyao.
1. Fadhila za masahaba ndani ya Qurani Tukufu.
3. Kuwapenda masahaba ni katika imani.
3. Mahimizo ya kuwaiga masahaba watukufu.
2. Makatazo ya kuwatusi au kuwasema vibaya.
2. Mifano katika historia yao.
Pili: dalili
Ndani ya Qurani Tukufu
7. Mwenyezi Mungu anasema { Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.
Na walio pamoja naye wana nguvu mbele ya makafiri, na wana hurumiana
wao kwa wao. Utawaona wakiinama na kusujudu wakitafuta fadhila na
radhi za Mwenyezi Mungu. Alama zao katika nyuso zao, kwa athari ya
kusujudu. Huu ndio mfano wao katikaTaurati. Na mfano wao katika Injili ni
kama mmea uliotoa chipukizi lake, kisha ukalitia nguvu, ukawa mnene,
ukasimama sawa juu ya ubuwa wake, ukawafurahisha wakulima, ili
kuwakasirisha kwa ajili yao makafiri. Mwenyezi Mungu amewaahidi walio
amini na wakatenda mema katika wao msamaha na ujira mkubwa.}(Alfathi.
13)
1. Mwenyezi Mungu anasema { Na wale walio tangulia, wa kwanza,
katikaWahajiri na Ansari, na walio wafuata kwa wema,Mwenyezi Mungu
ameridhika nao, na wao wameridhika naye; na amewaandalia Bustani
zipitazo mito kati yake,wadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu
kukubwa.}(Atawba. 711).
3. Mwenyezi Mungu anasema {Na wa mbele watakuwa mbele. 77. Hao ndio
watakao karibishwa 71. Katika Bustani zenye neema. 73. Na wachache
katika wa mwisho. 73. Fungu kubwa katika wa mwanzo, }(alwaqia. 71-73)
3. Mwenyezi Mungu anasema { Basi wale walio muamini yeye, na
wakamhishimu, na wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyo teremshwa
pamoja naye - hao ndio wenye kufanikiwa.}(Alaaraf. 721).
2. Mwenyezi Mungu anasema {Mwenyezi Mungu amekwisha pokea toba ya
Nabii na Wahajiri na Ansari waliomfuata katika saa ya dhiki, pale baada ya
kukaribia nyoyo za baadhi yao kugeuka. Basi akapokea toba yao, kwani
hakika Yeye kwao wao ni Mpole na ni Mwenye
kuwarehemu}(Atawaba.771)
2. Mwenyezi Mungu anasema {Lakini Mtume na wale walio amini pamoja
naye waliwania Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Hao ndio watakao pata
kheri nyingi, na hao ndio wenye kufanikiwa.23. Mwenyezi Mungu
amewatengenezea Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Huko
ndiko kufuzu kukubwa.}(Atawaba.22-23)
1. Mwenyezi Mungu anasema { Kwa hakika Mwenyezi Mungu amewapa radhi
Waumini walipo fungamana nawe chini ya mti, na alijua yaliyomo nyoyoni
mwao. Basi akateremsha utulivu juu yao, na akawalipa kwa ushindi wa
karibu.}(Alfathi.72)
2. Mwenyezi Mungu anasema {Wapewe mafakiri Wahajiri walio tolewa
majumbani mwao na mali yao kwa ajili ya kutafuta fadhila kutoka kwa
Mwenyezi Mungu na radhi zake, na wanamsaidia Mwenyezi Mungu na
Mtume wake. Hao ndio wa kweli. 3. Na walio na maskani zao na Imani yao
kabla yao,wanawapenda walio hamia kwao, wala hawaoni choyo katika
vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi
zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa
nafsi yake,basi hao ndio wenye kufanikiwa.} (Alhashri.2-3)
Ndani ya hadithi
7. Kutoka kwa Abdala bin Masud (radhi za Mwenyezi Mungu
zimshukie) kutoka kwa Mtume (rehma na amani zimshukie)
amesema: “bora ya watu ni waliopo katika wakati wangu, kisha
wanaowafuatia, kisha wanaowafuatia, kisha watakuja watu shahada
ya mmoja wao itatanguliwa na kiapo na kiapo chake kwa shahada
yake.” (Muslim na Bukhari).
1. Kutoka kwa Abi hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie)
amesema: amaesma Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie): “ Msiwatusi masahaba zangu, msiwatusi masahaba
zangu, naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake lau
kama mmoja wenu angelitoa dhahabu mfano wa jabali la Uhud basi
asingelifikia kwa utoaji huo wala nusu yake.” (Bukhari na Muslim).
3. Mtume (rehma na amani zimshukie) anasema: “Tahadharini,
tahadharini kuhusu masahaba wangu. Tahadharini, tahadharini kuhusu
masahaba wangu. Msiwavunjie heshima baada yangu, mwenye
kuwapenda basi kwa mapenzi yangu nitampenda, na mwenye
kuwachukia basi kwa chuki yangu nitamchukia, na mwenye kuwakera
basi kwa hakika amenikera mimi, na anikeraye hakika huwa
amemkera Mwenyezi Mungu, na amkeraye Mwenyezi Mungu pana
wasiwasi wa kuchukuliwa.” (Ahmad).
3. Kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie)
amesema: amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie) nani kaamka hali ya kuwa amefunga? Abu Bakar
akasema: “Mimi”. Akasema: “Ni nani kati yenu aliyeshindikiza
jeneza?” Abu Bakar akasema: “Mimi” akasema: “Ni nani kati yenu
aliyelisha masikini?” Abu Bakar akasema: “Mimi” akasema: “Ni nani
kati yenu aliyetembelea mgonjwa?” Abu Bakar akasema: “ Mimi”
Mtume (rehma na amani zimshukie) akasema mambo haya
yakikusanyika kwa mtu basi ataingia peponi.” (Muslim).
Tatu: maudhui
Mwenyezi Mungu Mtukufu amemchagulia Mtume wake (rehma na amani
zimshukie) watu wasafi, masahaba walio wema, waliomuamni na kumuunga
mkono na kumnusuru, waliosoma na kupasi kutoka katika chuo cha Nabii
Muhammad (rehma na amani zimshukie), waliolelewa katika mikono yake,
waliokunywa kinywaji cha chemuchemu safi ambayo inatoa maji ya imani,
wakawa watu wenye imani ya kweli, na wenye elimu kubwa, na ufahamu wa kina,
na matendo mema zaidi. Waliibeba bendera ya dini katika ulimwengu wote,
hawakuwa wakiogopa lawama kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kwa ajili hiyo,
wakafanikiwa kupata radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu. Naye akawasifu ndani
ya Qurani Tukufu kwa kusema { Na wale walio tangulia, wa kwanza, katika
Wahajiri na Ansari, na walio wafuata kwa wema,Mwenyezi Mungu ameridhika
nao, na wao wameridhikanaye; na amewaandalia Bustani zipitazo mito kati
yake,wadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa.}(Atawbah. 711). Hao
ndio masahaba wa Mtume (rehma na amani zimshukie) ambao Mwenyezi Mungu
amewateua kwa Mtume wake wa mwisho.
Kizazi kilichoweza kubadilisha mwenendo wa maisha, waliibeba nuru aliyokuja
nayo bwana wetu, Mtume Muhammad (rehma na amani zimshukie) kwa
ulimwengu wote. Na kadiri tutakavyojaribu kuwafukuzia basi hatutaweza, na
inatosha kuelewa kuwa lau kama tutatoa sadaka ya dhahabu kila siku mfano wa
jabali la Uhudi hatofikia mmoja wenu thamani ya kile walichokitoa masahaba wala
nusu yake. Hivi ni kama alivyoashiria Mtume (rehma na amani zimshukie)
aliposema… “Naapa kwa Yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake lau
kama mmoja wenu angelitoa dhahabu mfano wa jabali la Uhud basi asingelifikia
kwa utoaji huo wala nusu yake.” (bukhari na Muslim). Na hii ni kwa sababu
walihimili matatizo ya kueneza hii dini na kufikwa yaliyowafika, wakajitolea
kinafsi zao, roho zao na mali zao katika njia ya kuinusuru dini ya Mwenyezi
Mungu na kumnusuru Mtume wake (rehma na amani zimshukie), akasema
Mwenyezi Mungu { Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao
na mali zao kwa kuwa wao watapata Pepo. Wanapigana katika Njia ya Mwenyezi
Mungu - wanauwa na wanauwawa. Hii ni ahadi aliyo jilazimisha kwa Haki katika
Taurati na Injili na Qur'ani. Na nani atimizae ahadi kuliko Mwenyezi Mungu? Basi
furahini kwa biashara yenu mliyo fanya naye. Na huko ndiko kufuzu
kukubwa,}(Atawbah.777).
Na iwapo ni katika haki zetu kwa Mtume (rehma na amani zimshukie) kuisoma
historia yake na mwenendo wake na kufuata uongofu wake na kutenda kwa mujibu
wa sheria yake, basi pia katika haki zetu kwa upande wa masahaba ni kuelewa
ubora wao na nafasi zao na kusoma historia zao ili tuweze kufanana nao katika
kuwa na maadili mazuri, katika kumtii na kumuabudu Mwenyezi Mungu Mola wa
ulimwengu wote, na tuchukue mazingatio na mawaidha katika maish yao. Kwani
wao wamechaguliwa na Mwenyezi Mungu ili wawe pamoja nae (rehma na amani
zimshukie) na kueneza ujumbe baada ya kuondoka kwake, kwani wao ni watu bora
katika umma huu kwa kuwa Mwenyezi Mungu amewasifu kwa sifa za ukamilifu
na kuwasafisha, hakuna katika watu aliyeweza kuelewa mfano wa uchaji Mungu
kama walivyokuwa hawa wakimcha Mungu . Mwenyezi Mungu amewasifu na
akaweka wazi ni kipi alichowaandalia katika malipo makubwa, akasema { Na wa
mbele watakuwa mbele. 77. Hao ndio watakao karibishwa 71. Katika Bustani
zenye neema. 73. Na wachache katika wa mwisho. 73. Fungu kubwa katika wa
mwanzo,}(Alwaqiah. 71-73).
Na kwa kuweka wazi nafasi zao na kupanda kwa cheo chao Mwenyezi Mungu
akawapa sifa miongoni mwa sifa zake ndani ya Qurani Tukufu, si hivyo tu, bali pia
wamesifiwa katika Taurati na Injili akasema { Muhammad ni Mtume wa
Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye wana nguvu mbele ya makafiri, na wana
hurumiana wao kwa wao. Utawaona wakiinama na kusujudu wakitafuta fadhila na
radhi za Mwenyezi Mungu. Alama zao katika nyuso zao, kwa athari ya kusujudu.
Huu ndio mfano wao katikaTaurati. Na mfano wao katika Injili ni kama mmea
uliotoa chipukizi lake, kisha ukalitia nguvu, ukawa mnene, ukasimama sawa juu ya
ubuwa wake, ukawafurahisha wakulima, ili kuwakasirisha kwa ajili yao makafiri.
Mwenyezi Mungu amewaahidi walio amini na wakatenda mema katika wao
msamaha na ujira mkubwa} (Alfathi.13). Mwenyezi Mungu akawasifu kuwa wao
ni wenye nguvu mbele ya makafiri pasi na kudhulumu na weney kuoneana hurumu
kati yao, wakimuabudu Mwenyezi Mungu mmoja bila ya kumshirikisha na
chochote, wakirukuu na kusujudu, hawatafuti fadhila na radhi isipokuwa zitokazo
kwa Mwenyezi Mungu, na ibada imewaathiri mpaka ikadhihiri alama zake katika
viungo vyao, ukimuona mmoja wapo basi utaelewa tu ni katika wale wamuogopao
Mwenyezi Mungu na kumcha. Hivyo, masahaba (radhi ziwe juu yao) ni neema
kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa waja wake, akasema { Kwa hakika Mwenyezi
Mungu amewapa radhi Waumini walipo fungamana nawe chini ya mti, na alijua
yaliyomo nyoyoni mwao. Basi akateremsha utulivu juu yao, na akawalipa kwa
Ushindi wa karibu.}(Alfathi 72) .
Na tukiusoma mwenendo wa Mtume (rehma na amani zimshukie) tutaona kuwa
umejaa masimulizi yenye kuonyesha ubora wao na kukuwa kwa nafasi zao, kwa
mfano, kukiri kwake Mtume (rehma na amani zimshukie) kuwa wao ni katika watu
wa karne (wakati) bora na bora ya umma. Kutoka kwa Abdala bin Masud (radhi
za Mwenyezi Mungu zimshukie) kutoka kwa Mtume (rehma na amani zimshukie)
amesema: “bora ya watu ni waliopo katika wakati wangu, kisha wanaowafuatia,
kisha wanaowafuatia, kisha watakuja watu shahada ya mmoja wao itatanguliwa na
kiapo na kiapo chake kwa shahada yake.” (Muslim na Bukhari). Na wamekuwa
watu bora kwa kuwa walimuamini Mtume (rehma na amani zimshukie) wakati
watu wengine walipomkanusha, na kumsadiki wakati wengine walipomuona
muongo, na kumnusuru kwa mali zao na nafsi zao kwa ajili ya Mwenyezi Mungu .
imepokewa katika kitabu cha imam Ahmad, kutoka kwa Abdalla bin Masud (radhi
za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema: “Mwenyezi Mungu ameangalia katika
nyoyo za waja akaona moyo wa Muhammad (rehma na amani zimshukie) ni bora
kati ya nyoyo za waja, akamchagua yeye, na akampa ujumbe wake, kisha
akaangalia nyoyo za waja baada ya moyo wa Muhammad akaona nyoyo za
masahaba ni nyoyo bora kati ya nyoyo za waja, akawafanya kuwa ni mawaziri wa
Mtume wake (rehma na amani zimshukie) wenye kuipigania dini yake, na kile
waonacho waisilamu ni jema basi na kwa Mwenyezi Mungu pia ni jema, na
walionalo kuwa si jema basi kwa Mwenyezi Mungu pia si jema.”
Pia katika ubora wa masahaba ni kama alivyosema Mtume (rehma na amani
zimshukie) kuwa wao ni amana ya umma, Mtume (rehma na amani zimshukie)
anasema: “nyota ni amana kwa mbingu, na nyota ziondokokapo basi mbigu huleta
kile kilichoahidiwa, na mimi ni amana kwa masahaba zangu nikiondoka basi
masahaba zangu wanaleta kile walichoahidiwa, na masahaba zangu ni amana kwa
umma wangu wakiondoka basi umma wangu wataleta kile walichoahidiwa.”
(Muslim) . Ikawa kuwepo kwa masahaba (radhi za Mwenyezi Mungu ziwashukie)
ni amana kwa umma ya kutokuwepo kwa uzushi, lakini pia kutokana na Baraka
zao zimeenea na kufika hadi katika kizazi cha pili baada yao. Kutoka kwa Saad
Alkhudriy (rehma na amani zimshukie) kwamba Mtume (rehma na amani
zimshukie) amesema: “watakuja watu watawapigana vita na kundi jengine,
watasema: “yupo katika nyie aliyekuwa na Mtume (rehma na amani zimshukie)?”
watasema: “ ndio” basi watafunguliwa. Kisha watakuja watu watapigana vita na
kundi jengine, itasemwa ““yupo katika nyie aliyekuwa na waliokuwa na Mtume
(rehma na amani zimshukie)? Watasema: “ndio” watafunguliwa. Kisha watakuja
watu watapigana vita na kundi jengine, itasemwa, “yupo katika nyie aliyekuwa na
waliokuwa pamoja na waliokuwa na Mtume (rehma na amani zimshukie)?
Watasema “ndio” watafunguliwa. (Bukhari naMuslim).
Pia Mwenyezi Mungu amewashuhudia kuwa ni watu waliokuwa na moyo wa
kujitolea, ukarimu na juhudi za kutafuta radhi na mafanikio kwa Mwenyezi
Mungu. Naye akawaandalia kutokana na hili pepo ya milele yenye neema.
Akasema {Lakini Mtume na wale walio amini pamoja naye waliwania Jihadi kwa
mali zao na nafsi zao. Hao ndio watakao pata kheri nyingi, na hao ndio wenye
kufanikiwa 23. Mwenyezi Mungu amewatengenezea Bustani zipitazo mito kati
yake, wadumu humo. Huko ndiko kufuzu kukubwa. }(Atawbah22-23). Umar
(radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) anasema: “siku moja Mtume (rehma na
amani zimshukie) alituamrisha tutoe sadaka, ikawa ninazo mali, nikasema: “ leo
nitamshinda Abu Bakar nikishindana naye, nikaja na nusu ya mali yangu. Mtume
(rehma na amani zimshukie) akasema: “ watu wako umewabakishia kitu gani?
Nikasema: “mfano wake. Akasema: “akaja Abu Bakar (radhi za Mwenyezi Mungu
zimshukie) na kila alichonacho, Mtume akamwambia. “watu wako umewabakishia
kitu gani? Akasema: “nimeaachilia Mwenyezi Mungu na Mtume wake, nikasema
(Umar) siwezi kushindana na wewe kwa kitu chochote milele..” (Tirmidhi).
Na iwapo hii ndio nafasi ya masahaba wa Mtume (rehma na amani zimshukie) basi
kuwapenda kwao (radhi za Mwenyezi Mungu ziwashukie ) na kukiri ubora wao
kuliko wengine ni katika imani ya lazima juu ya kila muisilamu. Kwani ni ishara
ya kumpenda Mtume (rehma na amani zimshukie) ambaye aliwapenda na
kuwachagua kuwa ni masahaba wake. Muumini hupenda kila apendacho Mtume
(rehma na amani zimshukie) wakiwemo masahaba zake. Imepokewa na Abdalla
bin Mugh-qal (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema: amesema Mjumbe
wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie) “tahadharini, tahadharini
kuhusu masahaba wangu. tahadharini, tahadharini kuhusu masahaba wangu.
Msiwavunjie heshima baada yangu, mwenye kuwapenda basi kwa mapenzi yangu
nitampenda, na mwenye kuwachukia basi kwa chuki yangu nitamchukia, na
mwenye kuwakera basi kwa hakika amenikera mimi, na anikeraye hakika huwa
amemkera Mwenyezi Mungu, na amkeraye Mwenyezi Mungu pana wasiwasi wa
kuchukuliwa.” (Ahmad). Na katika kitabu cha imam bukhari na muslim kutoka
kwa Bara`a ibn A`zib, kutoka kwa Mtume (rehma na amani zimshukie) amesema
kuhusu Maanswar; hawapendi hao (Maanswar) isipokuwa ni muumini, na wala
hawachukii isipokuwa ni mnafiki, atakaewapenda basi atapendwa na Mwenyezi
Mungu, na mwenye kuwachukia atachukiwa na Mwenyezi Mungu. Kuwapenda ni
dalili ya imani na ni kumtii Mwenyezi Mungu, na kuwachukia ni unafiki na uasi.
Imepokewa na Anas bin malik (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) kutoka kwa
Mtume (rehma na amani zimshukie) amesema: “dalili ya imani ni kuwapenda
Maanswari, na dalili ya unafiki ni kuwachukia Maanswari.” (Bukhari).
Uisilamu umeharamisha kuwasema vibaya masahaba (radhi za Mwenyezi Mungu
ziwashukie) kwani aliowachagua ili wawe na Mtume –naye ni Mwenyezi Mungu –
amewasifu na kuwaridhia. Na kama alivyotukataza Mtume (rehma na amani
zimshukie) juu ya kuwatusi. Kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu
zimshukie), hakika ya Mtume (rehma na amani zimshukie) amesema: Musiwatusi
masahaba wangu, musiwatusi masahaba wangu naapa kwa Yule ambaye nafsi
yangu imo mikononi mwake lau kama mmoja wenu angelitoa dhahabu mfano wa
jabali la Uhud basi asingelifikia kwa utoaji huo wala nusu yake.” (Muslim). Na
kutoka kwa Abdalla bin Umar (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema.
Musiwatukane masahaba wa Mtume Muhammad (rehma na amani zimshukie),
kwani kisimamo cha ibada ya mmoja wao cha saa moja ni bora kuliko ibada ya
miaka arobaini ya mmoja wenu.” (ubora wa masahaba, Imam Ahmad). Kwa ajili
hiyo ni wajibu wetu kuwapa heshima na kuelewa vyeo vyao.
Na mwenye kuangalia maisha ya masahaba (radhi za Mwenyezi Mungu
ziwashukie) ataona kiwango kikubwa sana cha imani waliyokuwa nayo, na kufuata
amri za Mwenyezi Mungu na Mtume wake (rehma na amani zimshukie), atakutia
kuwa kuna ufasiri wa kiuhakika wa utendaji matendo mazuri, walikuwa ni
viongozi wema walioonyesha mfano wa utoaji, elimu, utendaji, kujitolea muhanga
kwa ajili ya kuinusuru dini ya Mwenyezi Mungu, mpaka wakateremshiwa aya {
Wapewe mafakiri Wahajiri walio tolewa majumbani mwao na mali yao kwa ajili
ya kutafuta fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu na radhi zake, na wanamsaidia
Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hao ndio wa kweli.}(Alhashri.2) .
Na mfano wa wazi kabisa ni, sahaba Ali bin Abi Twalib (radhi za Mwenyezi
Mungu zimshukie) alipojitolea kulala katika kitanda cha Mtume (rehma na amani
zimshukie) usiku wa kuhama kwa Mtume ili ajitoe muhanga kwa nafsi yake na
roho yake hali ya kuelewa kuwa washirikina wanamsaka kwa mapanga kwa ajili
ya kumuua.
Pia sahaba Suhayb Ruumi alijitolea muhanga wa mali zake kwa ajili ya kuinusuru
dini ya Mwenyezi Mungu, na kumnusuru Mtume (rehma na amani zimshukie)
wakati alipotaka kuhamia Madina. Makafiri wa kikuraish wakamwambia: “ulikuja
kwetu huna kitu, ukaupata utajiri kutoka kwetu, na kufikia ulipofikia kisha unataka
kutoka wewe na nafsi yako, hiyo haiwezekani. Akawaambia: “Mnaonaje iwapo
nitakupeni mali zangu mutaniachia? Wakasema: “ ndio” akasema: “ninakuwekeni
mashahidi kuwa mali yangu nimewaachilia nyinyi.” Ikamfika hilo Mtume (rehma
na amani zimshukie) akasema: Suhayb amepata faida, suhayb amepata faida.” (Ibn
Haban).
Mfano mwengine ni Abu bakar (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) anatupa
mfano mzuri wa maadili mema, na sifa nzuri mpaka akawa ni kigezo cha kila
jema. Na Mtume akamshuhudia kwa hili kuwa ni katika watu wa peponi. Kutoka
kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema: amesema
Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie) nani kaamka hali ya
kuwa amefunga? Abu Bakar akasema: “mimi”. Akasema: “ni nani kati yenu
aliyeshindikiza jeneza?” Abu Bakar akasema: “mimi” akasema: “ni nani kati yenu
aliyelisha masikini?” Abu Bakar akasema: “mimi” akasema: “ni nani kati yenu
aliyetembelea mgonjwa?” Abu Bakar akasema: “ mimi” Mtume (rehma na amani
zimshukie) akasema mambo haya yakikusanyika kwa mtu basi ataingia peponi.”
(Muslim).
Nae sahaba Umar (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) siku moja alikuwa
akitembea usiku, tahamaki kuna mwanamke ana watoto na chungu kipo motoni na
watoto wamejikunyata. Umar akasema: Amani juu yenu enyi watu wa mwangani,
alichukia kusema enyi watu wa motoni, mwanamke akasema: “nawe amani iwe
juu yako”. Akasema (Umar) je nikaribie? Akasema (mwanamke) ikiwa kwa heri
karibia na kama kwa shri usikaribie, akakaribia, akasema: “ muna nini? Akajibu:
“usiku umekuwamfupi kwetu pamoja na baridi. Akasema: “na hawa watoto wana
nini mbona wamejikunyata? Akasema: „ni njaa. Akasema: “ndani ya chungu hiki
muna kitu gani?” Akasema: “cha kuwadanganyia mpaka walale, na Mwenyezi
Mungu yupo pamoja nasi juu ya Umar. Akasema “Mungu akurehemu, munamjuaje
Umar?” akasema: “Umar unatuongoza kisha anatusahau.” Zaid – mpokezi wa
hadithi- anasema: “ akanikabili kisha akaniambia tuondoke, tukaondoka huku
tunakazana mpaka tukafika nyumba ya unga (nyumba ya hazina), akatoa kiwango
cha unga na kopo la mafuta, akasema: “ nibebeshe: “ nikamwambia: “ mimi
nitakubebea: “je nawe utanibebe mzigo wa madhambi yangu siku ya kiyama?
Nikambebesha, akaondoka nami nikaondoka nae hali yakukazana. Tulipofika kwa
Yule mwanamke tukautua akampa unga, akawa anamwambia tupa juu yangu na
ninakutetemeka mimi mwenywe, akawa anapuliza chungu. Akasema: “ nipe kitu
chochote (cha kupakulia) akapewa na kupakuwa ndani yake huku akisema:
“walishe na mimi nitawashikia, akawa katika hali hiyo mpaka wakashiba, na
baadae wakamuacha akaondoka nami (Zaid) nikaondoka nae. Naye Yule
mwanamke akawa nasema Mungu akulipe kila la kheri, jambo hili ulilolifanya ni
jema kuliko afanyavyo kiongozi wa waumini: „nikamwambia “ sema mema pindi
kiongozi wa waumini atakapokujia, na nisimulie kuhusu yeye akipenda Mungu,
kisha akajiweka upande na baadae akamsogelea na kukaa kitako ,na kumpokea
tukamwambia: “ tuna jambo jengine lisilo hili na akawa hatuzungumzishi mpaka
nilipowaona watoto wamelala na kutulizana, akasema : amani, hakika njaa
imewafanya wasilale na kuwafanya walie na nilipendelea kuwa nisiondoke mpaka
nione niliyoyaona. (ubora wa masahaba, imamu Ahmad).
Na hata masahaba wa kike (radhi za Mwenyezi Mungu ziwashukie) nao wana
fadhila na misimamo ya kujitolea muhanga kwa ajili ya dini ya Mwenyezi Mungu,
kwa mfano: -
Msimamo wa Mama wa waumini Khadija (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie)
alivyokuwa na msimamo wa kueneza dini ya Mwenyezi Mungu pale aliposimama
wima na mumewe na kujitolea muhanga kwa mali zake na nafsi yake, na
kumtuliza kutokana na hofu aliyokuwa nayo (rehma na amani zimshukie) wakati
alipoteremshiwa wahyi katika jabali la Hiraa,na kumwambia kwa kujiamini, na
wala kutetereka: “ hakika Mwenyezi Mungu hakuhuzunishi katu, wewe utaunga
ukoo, na kubeba yote na kumpata asiyekuwepo, na kumtuliza mgeni na kusaidia
kwenye haki. (Bukhari) akawa ni katika wake wema sana mwenye kujua wajibu
wake na haki. Vilevile Mtume (rehma na amani zimshukie) alikuwa akimtaja sana
na kumsifia, kutoka kwa Aisha (radhi za Mwenyezi Mungu) amesema: Mtume
(rehma na amani zimshukie) alikuwa akitajwa Khadija huwa anamsifia,, akasema:
“ nikawa na wivu siku moja, nikasma: “mbona unamtaja sana huyu mwenye uso
mwekundu yaani khadija ,na Mwenyezi Mungu amekubadilishia mbora kuliko
yeye. Mtume akasema (rehma na amani zimshukie) Mwenyezi Mungu
hajanibadilishia mbora zaidi yake, kwani yeye aliniamni wakati watu wakinipinga,
na kuniona ni mkweli wakati watu wakiniona ni mwongo, na kuniliwaza kwa mali
zake wakati watu walinitenga, na Mwenyezi Mungu amenipatia kutoka kwake
watoto wakati sikupata watoto kutoka kwa wanawake wengine.” (Ahmad)
Na mfano mwengine mwema na wa kuigwa wa masahaba wa kike (radhi za
Mwenyezi Mungu ziwashukie) ni Mama Umarah nasiybah bint Ka`ab Al answari
ambaye Mtume (rehma na amani zimshukie ) alisema kuhusu yeye: “ mimi katika
vita ya Uhud sikuwa nikigeuka upande wa kulia wala wa kushoto isipokuwa
nilikuwa nikimuona Umu Umarah akipigana pamoja nami.” Mpaka mtu akitaka
kumuua Mtume (rehma na amani zimshukie) anamuona Umu Umrah yupo mbele
yake, na hupigana naye kwa panga mpaka bega lake likajawa na damu kutokana na
mapigo ya mapanga. Mtume akamwambia: “ ni adhabu gani uipatayo ewe umu
umarah, akajibu”: “lakini ninaweza kuivumilia, ninaweza, ninaweza ewe Mjumbe
wa Mwenyezi Mungu. Mtume (rehma na amani zimshukie) niombe ewe Umu
Umarah” akasema: “naomba niwe nawe peponi ewe Mjumbe wa Mwenyezi
Mungu. Mtume (rehma na amani zimshukie) akasema sio wewe peke yako bali na
watu wa nyumba yako pia. Akasema (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie) sijali
kwa yanipatayo duniani.” Kitabu cha Siyra A`alam Anubalaa)
Na iwapo tunataka kuendelea na kuokoa na matatizo na kufanikiwa kwa kupata
radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu hapa duniani na kesho akhera, basi hatuna
budi tufuate mwangaza tuliomurikiwa kwa nuru ya masahaba wa Mtume (rehma
na amani zimshukie) na kufuata mwenendo waona tabia zao, wao ni kigezo cha
waumini na waislamu wote. Mtume (rehma na amani zimshukie ) katuhimiza
kuwafuata na kushikamana na mwenendo wao pia, kutoka kwa Urbaadh bin
Sariyah kuwa Mtume (rehma na amani zimshukie) amesema: “ jilazimisheni
kufuata mwenendo wangu na mwenendo wa makhalifa walioongoka, na chukueni
kwa kukaza magego, na tahadharini na yenye kuzuka, kwani kila la uzushi ni
upotofu.” (Ibn Majah).
Na juu yetu kujifunza na watoto wetu na wake zetu juu ya mwenendo wa
masahaba watukufu, ni namna gani walikuwa wakimfuata Mtume (rehma na amani
zimshukie) na kujitolea kwao muhanga kwa ajili ya kuinusuru dini na kumnusuru
Mtume (rehma na amani zimshukie) kwani waliziuza nafsi zao kwa ukweli na kwa
uyakini hii yote ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mtukufu.
Haki ya mtoto katika ukuaji mzuri na maisha bora na
maandalizi mazuri kwa ajili ya mustakbali
Prof. Muhammad Mukhttar Juma
Waziri wa wakfu
Kimefasiriwa na
Prof. Ayman Ibrahim Al-Asar
11 jamad Uwla 1437 H. Sawa na 19-2-2116 A.D.
Kwanza : Vipengele
Watoto ni neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu inapaswa kuishukuru.
Huduma ya uisilamu kwa watoto
Nguzo muhimu za ukuzaji mzuri wa watoto.
Kumchagulia jina zuri.
Kumnyonyesha kidesturi.
Kuwafanyia wema na kuacha kutumia nguvu na ukali
Uadilifu na usawa kwa watoto wote.
Ulazima wa kuwahakikishia watoto maisha bora.
Umuhimu wa kuwa na tama maishani mwetu.
Dalili: ndani ya Kurani tukufu na hadithi
Mwenyezi Mungu anasema: { Ufalme wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi
Mungu anaumba apendavyo, anamtunukia amtakaye watoto wa kike, na
anamtunukia amtakaye watoto wa kiume. 51 Au huwachanganya wanaume
na wanawake, na akamfanya amtakaye tasa. Hakika Yeye ni Mjuzi Mwenye
uweza.}Ashura, 49-51.
Mwenyezi Mungu anasema: { Na Mwenyezi Mungu amekuumbieni wake
katika jinsiyenu, na akakujaalieni kutoka kwa wake zenu wana nawajukuu, na
akakuruzukuni vitu vizuri vizuri. Basi je, wanaamini upotovu na wanazikataa
neema za MwenyeziMungu?} Anahl, 72.
Mwenyezi Mungu anasema: { Na wazazi wanawake wawanyonyeshe watoto
wao miaka miwili kamili kwa anaye taka kutimiza kunyonyesha. Na juu ya
baba yake chakula cha kina mama, na nguo zao kwa mujibu wa ada. Wala
halazimishwi mtu ila kwa kadiri ya uwezo wake. Mama asitiwe taabuni kwa
ajili ya mwanawe, wala baba kwa ajili ya mwanawe. Na juu ya mrithi mfano
wa hivyo. Na kama wote wawili wakitaka kumwachisha ziwa kwa kuridhiana
na kushauriana, basi si vibaya kwao. Na mkitaka kuwapatia watoto wenu
mama wa kuwanyonyesha basi hapana ubaya kwenu mkitoa mlicho ahidi
kwa mujibu wa ada. Na mcheni Mwenyezi Mungu, na jueni kwamba
Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayo yatenda.}Albaqara, 233.
Mwenyezi Mungu anasema: { Na wale wanao sema: Mola wetu Mlezi! Tupe
katikawake zetu na wenetu yaburudishayo macho, na utujaalietuwe
waongozi kwa wachamngu }Alfurqan, 74.
Mwenyezi Mungu anasema: { Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata
kwaImani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na walahatutawapunja hata
kidogo katika vitendo vyao. Kilamtu lazima atapata alicho kichuma.}At tuur,
21.
Mwenyezi Mungu anasema: {Na Luqman alipo mwambia mwanawe kwa
kumpa mawaidha: Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu. Kwani
hakika ushirikina bila ya shaka ni dhulma iliyo kubwa. 14 Na tumemuusia mtu
kwa wazazi wake wawili. Mamayake ameichukua mimba yake kwa udhaifu
juu ya udhaifu, na kumwachisha ziwa baada ya miaka miwili. (Tumemuusia):
Nishukuru Mimi na wazazi wako. Ni kwangu Mimi ndiyo marudio. 15 Na pindi
wakikushikilia kunishirikisha na ambayo huna ilimu nayo, basi usiwat'ii. Lakini
kaa nao kwa wema duniani, nawe ishike njia ya anaye elekea kwangu. Kisha
marejeo yenu ni kwangu Mimi, na Mimi nitakuambieni mliyo kuwa
mkiyatenda. 16 Ewe mwanangu! Kikiwapo kitu cha uzito wa chembe
yakhardali kikawa ndani ya jabali au ndani ya mbingu au ndani ya ardhi, basi
Mwenyezi Mungu atakileta. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa
yaliyofichika, Mwenye khabari za yote. 17 Ewe mwanangu! Shika Sala, na
amrisha mema, na kataza maovu, na subiri kwa yanayo kupata. Hayo ni
katika mambo ya kuazimiwa. 18 Wala usiwabeuwe watu, wala usitembee
katika nchi kwa maringo. Hakika Mwenyezi Mungu hampendi kila
anayejivuna na kujifakhirisha. 19 Na ushike mwendo wa katikati, na
teremsha sauti yako. Hakika katika sauti mbaya zote bila ya shaka iliyo zidi ni
sauti ya punda.}Luqman 13-19.
Mwenyezi Mungu anasema: {Enyi mlio amini! Jilindeni nafsi zenu na ahali
zenuna Moto ambao kuni zake ni watu na mawe. WanausimamiaMalaika
wakali, wenye nguvu, hawamuasi Mwenyezi Mungu kwa anayo waamrisha,
na wanatenda wanayoamrishwa} At tahriim, 6.
Dalili za hadithi
Kutoka kwa Umar (Mwenyezi Mungu amwie radhi) hakika Mtume (rhma na
amani zimshukie juu yake) amesema: nyote ni wachungaji, na nyote
mutaulizwa juu ya mulivyovichunga. Imamu ni mchungaji naye ataulizwa juu
ya aliowachunga, mume ni mchungaji juu ya watu wake naye ataulizwa juu
ya aliowachunga, mke ni mchungaji katika nyumba ya mumewe naye
ataulizwa juu ya aliowachunga, mtumishi ni mchungaji juu ya mali ya bwana
wake naye ataulizwa juu ya alichokichunga.” Mpokezi akasema nadhani
alisema: “kijana ni mchungaji wa mali ya baba yake naye ataulizwa juu ya
alichokichunga, nyote ni wachungaji na mutaulizwa juu ya mulichokichunga.”
(Bukhari)
Kutoka kwa Maaqil bin Yasaar (Mwenyezi Mungu amwie radhi) kutoka kwa
mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake)
amesema: “hakuna mja ambaye Mwenyezi Mungu humpa wa kumchunga,
akafariki mchungaji hali ya kuwa amefanya hadaa basi Mwenyezi Mungu
atamuharamishia pepo.” (Bukharin a Muslim).
Kutoka kwa Ibn Abbas (Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema: “siku
moja nilikuwa nyuma ya mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
akasema: “ ewe kijana mimi nitakufundisha maneno, muhifadhi Mwenyezi
Mungu naye atakuhifadhi, muhifadhi Mwenyezi Mungu utamkuta mbele
yako, na pale uombapo basi muombe Mwenyezi Mungu, na pale utakapo
msaada basi taka msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu, tambua kuwa lau
umma utakusanyika juu ya kutaka kukunufaisha kwa kitu basi hawataweza
kukunufaisha isipokuwa kile alichokuandikia Mwenyezi Mungu. Na lau
wakikusanyika juu ya kutaka kukudhuru kwa kitu basi hawataweza
kukudhuru kwa kitu isipokuwa kile alichokuandikia Mwenyezi Mungu,
kalamu zishanyanyuliwa na kurasa zishakauka.” (Tirmidhi).
Kutoka kwa Abdalla Bin Amru bin A`s (Mwenyezi Mungu awawie radhi)
amesema: nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie juu yake) akisema: “mtu inatosha kuwa na madhambi kwa kule
kutomjali anaye mlea.” (Kitabu cha Hakim).
Kutoka kwa Saad Bin Abi Waqas (Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema:
“mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) alikuwa akinitembelea mwaka
wa hija ya kuagana, kutokana na maumivu yaliyonizidi, nikasema: “
nimefikwa na maumivu, nami nina mali, na hakuna atakayeirithi isipokuwa
mwanangu wa kike, je nitoe sadaka thuluthi mbili za mali yangu? Akasema :
“hapana,” nikasema: “nusu? Akasema: “Hapana”, kisha akasema: “ thuluthi,
na thuluthi ni nyingi, kwani wewe ukiacha kizazi chako matajiri ni bora kuliko
kuwaacha ni watu waombao wengine, kwani (pia) hutumii matumizi yoyote
aikawa uanataka radhi za Mwenyezi Mungu isipokuwa utalipwa kwayo.”
(Bukhari).
Kutoka kwa Thauban (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema, amesema
mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake) “Dinari
bora aitoayo mtu ni ile dinari anayoitoa kwa ajili ya familia yake, na dinari
aitoayo kwa ajili ya kipando chake katika njia ya Mweneyzi Mungu na dinari
aitoayo kwa wenzake katika njia ya Mweneyzi Mungu.” Abu Qalabah
akasema “ akaanza kwa watoto, kisha akasema Abu Qilabah: na hakuna mtu
mwenye kupata malipo mazuri kama Yule anayetoa kwa ajili ya watoto ili
kuwazuilia wasiombe au kuwanufaisha kwa ajili ya Mweneyzi Mungu na
kuwatosheleza.” (Muslim).
Kutoka kwa Athman Hatabiy amesema: nimemsikia Ibn Umar (Mwenyezi
Mungu amwie radhi) akimwambia kijana: “ mfunze heshima (adabu)
mwanao, kwani wewe utaulizwa juu ya mwanao, ni kitu gani umemfunza? Na
yeye ataulizwa juu ya wema wako na kukutii kwako.” (Imam Albayhaqiy –
Sunan Kubra).
Kutoka kwa Abi Dardai (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: amesema
mjumbe wa Mweneyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu yake) “hakika
nyinyi mtaitwa siku ya kiama kwa majina yenu na majina ya baba zeni, basi
majina yenu yafanyeni kuwa mazuri.” (imepokewa na Daud).
Kutoka kwa Aamir, amesema: nimemsikia Nuumaan bin Bashiir (Mweneyzi
Mungu awawie radhi) naye yuko juu ya membari akisema: “Baba yangu
amenipa zawadi, Umrah bint Rawaha akasema: sikubali mpaka mtume
(rehma na amani zimshukie juu yake) aishuhudie. Mtume (rehma na amani
zimshukie juu yake) akaja, akasema: “mimi nimempa mwanagu kutoka kwa
Umrah bint Rawaha zawadi, akaniamrisha kuwa nikufanye wewe kuwa ndiye
shahidi ewe mjumbe wa Mwenyezi mungu, akasema: “je wanao wengine
umewapa kama hiki?” akasema: “ hapana.” Akasema “ muogopeni Mwenyezi
Mungu na fanyeni uadilifu juu ya watoto wenu.” Akasema, akaichukua
zawadi yake. (Bukhari).
Kutoka kwa Umara Bin Salama (Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema:
nilikuwa katika chumba cha mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) na
mkono wangu ulikuwa ukitangatanga ndani ya sahani akaniambia “ewe
kijana taja jina la Mwenyezi Mungu ( sema Bismillahi) na kula kwa mkono
wako wa kulia na kula kilicho mbele yako.”
Tatu: Maudhui
Miongoni mwa neema kubwa sana ambazo Mweneyezi Mungu
amemneemesha mwanadamu baada ya imani ya Mweneyezi Mungu
Mtukufu ni neema ya mtoto ambayo huhifadhi kizazi na hutuliza moyo.
Watoto ni neema ya Mwenyezi Mungu, ni zawadi kutoka kwake humpa
amtakae katika waja wake, Mwenyezi Mungu anasema: { Ufalme wa mbingu
na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu anaumba apendavyo, anamtunukia
amtakaye watoto wa kike, na anamtunukia amtakaye watoto wa kiume. 51
Au huwachanganya wanaume na wanawake, na akamfanya amtakaye tasa.
Hakika Yeye ni Mjuzi Mwenye uweza }Ashuura, 49-51. Watoto huyafanya
maisha kuwa ni ya furaha na ucheshi, huondoa kiza ndani ya nyumba na
huingiza mwanga, wao ni taa za nyumba, utulivu wa macho na ni vipenzi vya
nyoyo, wao ni pambo la maisha ya dunia, kama alivyosema Mola wetu ndani
ya Kuran Tukufu {Mali na wana ni pambo la maisha ya dunia. Na
memayanayo bakia ni bora mbele ya Mola wako Mlezi kwamalipo, na bora
kwa matumaini.} Kahf 46.
Hivyo basi, neema hii – ya watoto – inapasa kushukuriwa Mwenyezi Mungu
Mtukufu, kipenzi cha Mwenyezi Mungu mtume Ibrahim (rehma na amani
zimshukie juu yake) baaya ya kupewa mwana na Mwenyezi Mungu alisema:
{Alhamdulillahi! Himdi zote ni za Mwenyezi Mungu aliye nipa juu ya uzee
wangu Ismail na Is-haq. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kusikia
maombi. 41. Mola wangu Mlezi! Nijaalie niwe mwenye kushika Sala, na
katika dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu.}
Ibrahim 39-41. Kuishukuru neema ni kuihifadhi, Mwenyezi Mungu Mtukufu
anasema { Na alipo tangaza Mola wenu Mlezi: Mkishukuru nitakuzidishieni;
na mkikufuru, basi adhabu yangu ni kali } Ibrahim, 7. Na inapasa
kuwahudumia ili akue katika kizazi kitakachomtambua Mwenyezi Mungu,
kujua haki za wazazi wake, haki za jamii na taifa.
Uisilamu umetoa huduma kubwa sana kwa watoto na kwa kuwalea vyema
basi hupatikana furaha duniani na akhera kwa watoto na wazazi. Uisilamu
ukamjali mtoto kabla hata ya kuja duniani ukamtaka mwenye kutaka kuoa
achague mke mwema, kwani nyumba itakapokuwa imezingirwa na mazingira
ya imani athari zake njema huenea kwa waliomo, na hivi ni kama alivyosema
Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) aliposema: “ ..mchague aliye na
dini mikono yako ipate kubarikiwa” (Muslim).. na uisilamu umejali mtoto
kabla ya hata kuanzishwa kwa taasisi za kimataifa zeneye kujali haki za
watoto, kwa kuwa kipindi hiki ni hatari na chenye misukosuko katika maisha
ya mwanadamu. Utoto ni kipindi kigumu na uhimu ambacho kila mtu ni
lazima apitie kisha apitea ujana. Hivyo, uisilamu ukajali sana utoto ili wawe
ongezeko zuri na chanzo chenye kuwa na faida katika jamii. Ukawapa
hukumu (sheria) nyingi kuhusu wao ambazo zinarudi kwa mtoto, familia,
kisha jamii kwa manufaa na faida njema.
Uisilamu umechunga kuhusu watoto tokea yupo tumboni mwa mama yake,
ukaweka hukumu na sheria zenye kumkinga na kumlinda uanadamu wake
katika kumchunga na kumpa malezi yote anayostahiki., hiki ni kipindi cha
mwanzo ambacho pia anastahiki kutunzwa na kuchungwa. Kwa maana hiyo,
uisilamu umedhamini haki ya maisha yake hali ya kuwa bado yu tumboni
mwa mama yake. Ukaharamisha utoaji wa mimba kwa makusudi, na
kuwajibisha kutunzwa kwa mama mja mzito, na ukaruhusu kwa mama mja
mzito kutofunga katika mwezi wa Ramadhani pindi akihofia mtoto wake
tumboni, mpaka akue kama kawaida. Kutoka kwa Anas (Mwenyezi Mungu
amwie radhi) kwamba mtume (rehma na amani zimshukie juu yake
amesema: “ hakika ya Mweneyzi Mungu ameondosha kwa msafiri nusu sala
na funga na kwa mja mzito na mwenye kunyonyesha.” (Nisai).
Vilevile katika yanayohusu kutunzwa kwa watoto: kumchagulia jina zuri,
wazazi waliotangulia walikuwa wakijilazimisha kuwachagulia wana wao
majina mazuri watakayoitwa, kwani jina zuri huleta furaha nyoyoni na utulivu
tafauti na jina baya. Kutoka kwa Abi Dardai (Mwenyezi Mungu amwie radhi)
amesema: amesema mjumbe wa Mweneyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie juu yake) “hakika nyinyi mtaitwa siku ya kiama kwa majina yenu na
majina ya baba zenu, basi majina yenu yafanyeni kuwa mazuri.” (imepokewa
na Daud). Wazazi wawili wanaporuzukiwa mwana basi wameamrishwa
wamchagulie jina zuri, mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
amesema “mtoto anakuwa katika rehani kwa akika yake, atachinyiwa siku ya
saba, atapewa jina, na kunyolewa kichwa chake.” (Tirmidhi).
Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) amependelea kwa umma wake
wachague majina ayapendayo Mwenyezi Mungu, kutoka kwa Naafi`, kutoka
kwa Ibn Umar (Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema: “ majina
yapendwayo na Mwenyezi Mungu ni Abdullah na Abdulrahman.” (Abu
Daudi). Nakatika mapokezi ya imamu Muslim, kutoka kwa Umar, amesema:
amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani zimshukie juu
yake): “ hakika majina yenu yapendwayo sana na Mwenyezi Mungu ni
Abdullah na Abdulrahman.” Na mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
alikuwa akikataza kuwaita wana majina mabaya, akasema “ usimwite mtoto
wako jina la Rabaha wala Yasara wala Aflaha wala Naafia` (Muslim).
Na sababu ya kukatazwa kuitwa majina mabaya ni kwa upande wa nafsi ya
mtoto, ili isije kumsababishia aina Fulani ya makero ya nafsi. Mzee mmoja
alikuja kwa Umar bin Khatwab (Mwenyezi Mungu amwie radhi) akimshtakia
kuhusu mwanawe, Umar akawita mzazi na mwanawe na kumlaumu mwana
juu ya haki ya mzazi wake na kwa kusahau kwake haki hizo, mtoto akasema,
ewe kiongozi wa waumini, kwani mtoto hana haki kwa wazazi wake?
Akasema: “anazo.” Akamuuliza: “ ni zipi haki zenyewe? Akasema Umar: “ ni
kuwa mwema mama yake, kumchagulia jina zuri, kumfundisha kitabu
(kurani). Mtoto akasema: “ewe kiongozi wa waumini hakika baba yangu
hakufanya hata moja katika hayo, mama yangu alikuwa mtu mweusi
aliyekuwa akimilikiwa na mwenye kuabudu moto na ameniita kombamwiko
(mbawakawa) na wala hakunifundisha hata herufi moja ndani ya kitabu.
Umar akamgeukia mzee akamwambia, “wewe umekuja kwangu kumshtakia
mwanao juu ya haki yako, lakini wewe umekeuka haki zake kabla ya yeye
kukeuka haki zako na umemtendea sivyo kabla ya yeye kukutendea sivyo.”
(Malezi ya watoto katika uisilamu).
Sufyan Thauri amesema: “ haki ya mtoto kwa wazazi wake ni kuitwa jina zuri,
kumuoza pindi akibaleghe, na kumfunza heshima (adabu) njema.” Kwani
kumchagulia jina zuri humsaidia katika kuishi maisha mazuri atakayoweza
kuepukana na kutaniwa na kufanyiwa kujeli, pia atapata raha na utulivu wa
nafsi pale atakapoitwa kwa jina lake, jina ni kitambulisho cha mtu.
Na katika matunzo ya uislamu kwa mtoto: inatakiwa kumyonyesha iwe ni
haki yake inayotambulika, Mwenyezi Mungu anasema: { Na wazazi
wanawake wawanyonyeshe watoto wao miaka miwili kamili kwa anaye taka
kutimiza kunyonyesha. Na juu ya baba yake chakula cha kina mama, na nguo
zao kwa mujibu wa ada. Wala halazimishwi mtu ila kwa kadiri ya uwezo
wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mwanawe, wala baba kwa ajili ya
mwanawe. Na juu ya mrithi mfano wa hivyo. Na kama wote wawili wakitaka
kumwachisha ziwa kwa kuridhiana na kushauriana, basi si vibaya kwao. Na
mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha basi hapana
ubaya kwenu mkitoa mlicho ahidi kwa mujibu wa ada. Na mcheni Mwenyezi
Mungu, na jueni kwamba Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayo
yatenda.}Albaqara, 233. Katika aya hizi tukufu wazazi wa kike
wameamrishwa kama kwamba wameambiwa. “enyi wazazi wanyonyesheni
watoto wenu kwa miaka miwili kamili, kani mtoto kipindi hiki huwa anahitaji
maangalizi muhimu ya chakula ambayo yatamsaidia katika kukuza mwili
wake na hakuna chakula kilicho bora kama maziwa ya mama yake ambayo
Mwenyezi Mungu ameyaandaa kwa ajili hiyo. Na amesema kweli Mwenyezi
Mungu: { Asijue aliye umba, naye ndiye Mjua siri, Mwenyekhabari?} Almulk
14. Ama iwapo mama ana matatizo ambayo kisheria ameruhusika
kutonyonyesha au mtoto kajizuilia kunyonya au mzazi kufariki basi hapa
sheria ya kiisilamu imelazimisha kwa mzazi wa kiume kumtafuta myonyeshaji
wa huyu mwana kwa malipo ili mwana apate usalama wake.
Na elimu za kiafya na nafsi zimethibitisha kuwa kipindi cha kunyonyesha
mtoto kilichotajwa kisheria cha miaka miwili ni lazima kwa ajili ya ukuaji wa
mtoto ukuaji unaohitajika nayo ni kwa pande mbili:- kisiha na kinafsi. Na
kumkuza mtoto katika mazingira ya upendo, utulivu na amani nayo haya yote
hayapatikani isipokuwa kwa mama ambaye atamsaidia mwana kukua katika
ukuaji bora na kumfanya aishi maisha mazuri.
Na miongoni mwa misingi ya ukuzaji wa mtoto: kumtendea wema na kuacha
kutumia nguvu na ukali. Kwani hujulikana kisheria kuwa upendo hauleti
isipokuwa jema. Kutoka kwa mama wa waumini Aisha (Mwenyezi Mungu
amwie radhi) hakika mjumbe wa Mwenyezi Mungu (rehma na amani
zimshukie juu yake) amesema: “ewe Aisha Mwenyezi Mungu ni mpole naye
hupenda upole, humpa mwenye mpole kile ambacho hampi (humnyima)
asiyekuwa na upole (mwenye kutumia mabavu) na kile ambacho hawapi
wengineo.” (Muslim). Nguvu na ukakamavu katika malezi na kutumia
mabavu katika malezi hupelekea kumfanya mtoto mara nyingi kuharibika
kitabia na kumfanya amchukie mzazi wake (mlezi) na kutosikia maneno yake.
Imepokewa katika hadithi tukufu kwa mba mtume (rehma na amani
zimshukie juu yake) alikuwa akimbeba Hassan na Hussein (Mwenyezi Mungu
awawie radhi) juu ya mabega yake na akicheza nao. Na katika misingi
aliyotumia mtume mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) ilikuwa ni
upole na ulaini. Kutoka kwa Burayda kapokea kutoka kwa baba yake
amesema: “mtume alipokuwa juu ya mimbari akihutubia, mara Hassan na
Hussein wakaingia hali ya kusota na walikuwa wamevaa nguo nyekundu,
mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) akashuka akawabeba kisha
akasema: “Mwenyezi Mungu amesema kweli { Hakika mali yenu na watoto
wenu ni jaribio} Ataghaabun,15. Nami nimewona hawa wakitembea na
kusota sikuweza kusubirio bali nikashuka na kuwabeba (Nisai).
Mlezi mwema- sawa ni mzazi au mwalimu – yeye ndie achungae misingi hii
mikubwa ya malezi nayo ni matendo ya upole na laini. Na kujiepusha na
maguvu na ukakamavu, hutibu tatizo kwa hekima na upole, maguvu
husababisha hofu ndani ya nyoyo ya mtoto na woga ukiachana na wasiwasi
wa kinafsi na kuona haya na kutojiamini. Ahnaf bin Qiys amesema katika
moja ya nasaha zake: “ usiwe kwao kufuli ili wasije wakatamani kifo chako na
wakachukia kukuona upo karibu nao na kuyachukia maisha yako.”
Kuwatendea upole haina maana kuwa usitumie adhabu wakati inapobidi,
lakini ni lazima tukumbushe kuwa adhabu ni lazima iwe kwa hekima na wala
isiwe kwa kila kosa alikosalo (alitendalo).
Na vilevile miongoni mwa malezi bora kwa watoto: ni uadilifu na usawa kati
yao. Uadilifu kwa viumbe vyote ni haki ya lazima katika sheria ya kiisilamu,
Mwenyezi Mungu anasema {Enyi mlio amini! Kuweni wasimamizi madhubuti
kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mkitoa ushahidi kwa haki. Wala kuchukiana na
watu kusikupelekeeni kutofanya uadilifu. Fanyeni uadilifu. Hivyo ndio kuwa
karibu mnona uchamngu. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika
MwenyeziMungu anazo khabari za mnayo yatenda}Almaida, 8. Na jambo hili
linapasa kwanza lianze kwa mzazi na watoto wake.
Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) ameelekeza wazazi wa kike na
wa kiume misingi ya lazima ambayo ni lazima waifuate, si hivyo tum bali pia
ameambatanisha na uchaji wa Mungu Mtukufu, kutoka kwa Amir, Kutoka
kwa Aamir, amesema: nimemsikia Nuumaan bin Bashiir (Mweneyzi Mungu
awawie radhi) naye yuko juu ya membari akisema: “Baba yangu amenipa
zawadi, Umrah bint Rawaha akasema: sikubali mpaka mtume (rehma na
amani zimshukie juu yake) aishuhudie. Mtume (rehma na amani zimshukie
juu yake) akaja, akasema: “mimi nimempa mwanagu kutoka kwa Umrah bint
Rawaha zawadi, akaniamrisha kuwa nikufanye wewe kuwa ndiye shahidi ewe
mjumbe wa Mwenyezi mungu, akasema: “je wanao wengine umewapa kama
hiki?” akasema: “ hapana.” Akasema “ muogopeni Mwenyezi Mungu na
fanyeni uadilifu juu ya watoto wenu.” Akasema, akaichukua zawadi yake.
(Bukhari). Na imepokewa na Abdulrazaak katika kitabu chake kwamba
mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) alimuita kijana mmoja wa
kianswar, akaja (mbele ya mtume) kisha mtoto wake wa kiume akaja na
akambusu na kumbeba na kumkumbatia na kukaa nae, kisha (baadae) akaja
mtoto wake wa kike akamshika mkono akammkalisha chini, mtume rehma na
amani zimshukie juu yake) “lau ungeliwafanyia uadilifu ingelikuwa ni bora
kwako, jikurubisheni kwa watoto wenu hata pale munapowabusu.”
Na katika kufanya uadilifu kwa wote kuna faida kubwa mno na huwasaidia
ndugu kusaidiana katika mema na pia huwasaidia katika kutengeneza kizazi
chema ndani ya jamii kama inavyosaidia kujenga undugu wa ukweli kati ya
jamaa.
Kinyume na haya tunaona mtafaruku kati ya wanandugu ambayo ni sababu
kubwa sana ya kuasi wazazi, kuwakimbia na kuwachukia na pia ni sababu ya
kupandikiza chuki kati ya wanandugu.
Baadhi ya matukio ya wanaelimu ya nafsi yamethibitisha kuwa mtoto mara
nyingi humili kuhisi kufanya mabaya kwa sababu ya dhuluma na
kutotendewa usawa ndani ya familia. Na mfano mzuri sana ni kisa cha nabii
Yussuf (rehma na amani ziwe juu yake) kwa kuboreshwa kwake zaidi yao,
Mwenyezi mungu anasema {Kwa yakini katika Yusuf na nduguze ziko ishara
kwawanao uliza 8.Pale walipo sema: Hakika Yusuf na nduguyewanapendwa
zaidi na baba yetu kuliko sisi, hali sisini kikundi chenye nguvu. Hakika baba
yetu yumo katika upotofu wa dhaahiri. 9. Muuweni Yusuf, au mtupeni nchi
mbali ili uso wababa yenu ukuelekeeni nyinyi. Na baada ya haya
mtakuwawatu wema.} Yusuf 7-9.
Vilevile katika misingi ambayo uisilamu umeiweka kwa ajili ya kudhibiti ukuaji
bora wa mtoto: ni malezi na mafundisho ya sheria. Mwenyezi Mungu
mtukufu amewamrisha wazazi wa kike na wa kiume ndani ya kurani tukufu
umuhimu wa kuikinga nafsi na jamaa ili wasiingia katika maangamizi,
akasema {Enyi mlio amini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenuna Moto ambao
kuni zake ni watu na mawe. WanausimamiaMalaika wakali, wenye nguvu,
hawamuasi Mwenyezi Mungu kwa anayo waamrisha, na wanatenda
wanayoamrishwa}At tahrim, 6. Na kumlea mtoto na kumfundisha adabu ni
misingi itakiwayo na sheria nazo pia ni haki miongoni mwa haki za mtoto kwa
wazazi wake. Kutoka kwa Ibn Abass (mwenyezi Mungu awawie radhi)
wamesema: ewe mjumbe wa Mweneyzi Mungu, tumekwisha elewa haki ya
mzazi kwa mwanawe, lakini ni zipi haki za mwana kwa mzazi? Akasema;
“kumfundisha adabu njema na kumlea vizuri.” (Sehemu ya imani. Kitabu cha
Bayhaqiy) na amepokea Tirmidhi katika kitabu chake kwamba mtume (rehma
na amani zimshukie juu yake amesema: “hakuna wema autendao mzazi kwa
mwana kuliko wema wa kumlea malezi mema.”
Na miongoni mwa misingi muhimu ya ukuzaji watoto ni kuwaelekeza na
kuwalea malezi bora, malezi na maelekezo yanatakikana yawe kwa utaratibu
na si mbele ya wengine, na hivi ndivyo alivyokuwa akifanya mtume (rehma
na amani zimshukie juu yake) Kutoka kwa Ibn Abbas (Mwenyezi Mungu
awawie radhi) amesema: “siku moja nilikuwa nyuma ya mtume (rehma na
amani zimshukie juu yake) akasema: “ ewe kijana mimi nitakufundisha
maneno, muhifadhi Mwenyezi Mungu naye atakuhifadhi, muhifadhi
Mwenyezi Mungu utamkuta mbele yako, na pale uombapo basi muombe
Mwenyezi Mungu, na pale utakapo msaada basi taka msaada kutoka kwa
Mwenyezi Mungu, tambua kuwa lau umma utakusanyika juu ya kutaka
kukunufaisha kwa kitu basi hawataweza kukunufaisha isipokuwa kile
alichokuandikia Mwenyezi Mungu. Na lau wakikusanyika juu ya kutaka
kukudhuru kwa kitu basi hawataweza kukudhuru kwa kitu isipokuwa kile
alichokuandikia Mwenyezi Mungu, kalamu zishanyanyuliwa na kurasa
zishakauka.” (Tirmidhi).
Kisha tena mtume (rehma na amani zimshukie juu yake analea na kufunza na
kuelekeza adabu njema kwa kupigia mifano mizuri juu ya mtoto, imepokewa
Kutoka kwa Umara Bin Salama (Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema:
nilikuwa katika chumba cha mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) na
mkono wangu ulikuwa ukitangatanga ndani ya sahani akaniambia “ewe
kijana taja jina la Mwenyezi Mungu ( sema Bismillahi) na kula kwa mkono
wako wa kulia na kula kilicho mbele yako.”(Muslim). Imam ghazali (Mweyezi
Mungu amrehemu) “mtoto ni amana mbele ya wazazi wake, moyo wake uko
safi suio na dosari, pindi ukizoweshwa mazuri na kufundishwa mema basi
atafurahia duniani na akhera.”
Juu ya mlezi awe kiongozi kwa watoto wake, ajiweke katika tabia njema kabla
ya kuwaamrisha, kwani watoto huiga.
Ana haki aliyesema:
Watoto wetu hukuwa kutoka kwetu * kama vile wazazi wake
walivyomzowesha
Na la msingi kulitaja ni kuwa, malezi hayawi kwa wazazi peke yaolakini pia
kwa mwalimu. Mwalimu ni sehemu katika jamii na ana umuhimu na ulazima
wa kukuza kizazi kwa kuzingatia tamaduni za jamii anayoishi. Watoto
niamana inayobebwa na jamii kwa ujumla na ni jukumu lililo katika shingo
zao, na inapasa kuwalea ipasavyo.wote pamoja wafahamu jukumukubwa
walilolibeba kuhusu watoto, na hakuna mfano wa wazi zaidi ya kauli ya
mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) Kutoka kwa Umar (Mwenyezi
Mungu amwie radhi) hakika Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake)
amesema: “nyote ni wachungaji, na nyote mutaulizwa juu ya
mulivyovichunga. Imamu ni mchungaji naye ataulizwa juu ya aliowachunga,
mume ni mchungaji juu ya watu wake naye ataulizwa juu ya aliowachunga,
mke ni mchungaji katika nyumba ya mumewe naye ataulizwa juu ya
aliowachunga, mtumishi ni mchungaji juu ya mali ya bwana wake naye
ataulizwa juu ya alichokichunga.” Mpokezi akasema nadhani alisema: “kijana
ni mchungaji wa mali ya baba yake naye ataulizwa juu ya alichokichunga,
nyote ni wachungaji na mutaulizwa juu ya mulichokichunga.” (Bukhari)
Dini ya kiisilamu inambebesha mzigo wazazi wa kuhifadhi watoto kwani
imepokewa Kutoka kwa Umar (Mwenyezi Mungu amwie radhi) hakika
Mtume (rehma na amani zimshukie juu yake) amesema: hakika yaMweneyzi
Mungu atamuuliza kila mchungaji kwa kile alichokichunga je amekihifadhi au
amezembea, mpaka atamuuliza pia mume juu ya watu wa nyumba yake.”
(imepokewa na Ibn Haban.) na tumuangaliapo mtoto basi tumuangalia kama
mtu aliyekamilika na kuwa na haki zote za kimwili, kinafsi, kimali, kielimu, na
malezi na ni wajibu kuzihifadhi ili awe na maisha mema na bora na ili jamii
iwe na ustaarabu na kuenea upendo, mapenzi na huruma.
Na tunasisitiza umuhimu wa kuwa na tama juu ya watoto wetu kwa kuwa
mwanadamu hawezi kuishi bila ya tama. Hakuna maisha iwapo tamaa haipo,
na ikikosekana tamaa maisha hupotea. Wasomi wameeleza ya kuwa “kukata
tamaa ni kuchanganyikiwa na kujichanganya huwa ni katika makosa
makubwa.” Abdallah Bin Abass (Mweneyzi Mungu awawie radhi) anasema:
“kuna kijana kasema: “ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni yepi madhambi
makubwa: akasema: “kumshirikisha Mwenyezi Mungu, kupoteza matumaini
kwa Mweneyzi Mungu. kukata tamaa katika rehema za Mwenyezi Mungu, na
atakaeepushwa na Mwenyezi Mungu na hayo basi amedhaminiwa kuingia
peponi.”
nyote ni wachungaji, na nyote mutaulizwa juu ya mulivyovichunga. Imamu ni
mchungaji naye ataulizwa juu ya aliowachunga, mume ni mchungaji juu ya
watu wake naye ataulizwa juu ya aliowachunga, mke ni mchungaji katika
nyumba ya mumewe naye ataulizwa juu ya aliowachunga, mtumishi ni
mchungaji juu ya mali ya bwana wake naye ataulizwa juu ya alichokichunga.”
Mpokezi akasema nadhani alisema: “kijana ni mchungaji wa mali ya baba
yake naye ataulizwa juu ya alichokichunga, nyote ni wachungaji na
mutaulizwa juu ya mulichokichunga.” (Bukhari)
Hatari za ulinganio potofu na umuhimu wa kuuzuia
kwa ajili ya upatikanaji wa amani na utulivu
29 Safar 1437 H.
Sawa na 11 Disemba 2115 A.D
Kwanza: Mambo muhimu
Neema ya amani na utulivu.
Utulivu wa nchi ni katika mambo ya lazima kisheria na kitaifa.
Vitendea kazi vya utulivu katika taifa.
Raia kuipenda nchi yake.
Kueneza upendo na msaada kati ya watu.
Kuwasikiliza na kuwatii viongozi wa nchi kwa lile atakalo Mwenyezi Mungu,
na kulitumikia taifa.
Kujiepusha na fitina.
Hatari ya ulinganio potofu kwa mtu mmoja mmoja na kwa jamii.
Ulazima wa kuzuia ulinganio huu.
Pili: Dalili
Ndani ya Kurani Tukufu
Mwenyezi Mungu anasema : { Na alipo sema Ibrahim: Ee Mola wangu Mlezi!
Ufanye huu uwe mji wa amani, na uwaruzuku watu wake matunda.. }
Albaqara aya ya 126.
Mwenyezi Mungu anasema : { Na Ibrahim alipo sema: Ewe Mola wangu
Mlezi! Ujaalie mji huu uwe wa amani, na uniepushe mimi na wanangu na
kuabudu masanamu.} Ibrahim aya ya 35.
Mwenyezi Mungu anasema : {Wale ambao wameamini, na
hawakuchanganya imani yao na dhulma - hao ndio watakao pata amani na
wao ndio walio ongoka. } Al an aam aya ya 82.
Mwenyezi Mungu anasema : {1. Kwa walivyo zoea Maqureshi. 2. Kuzoea
kwao safari za siku za baridi na siku za joto. 3 Basi nawamuabudu Mola Mlezi
wa Nyumba hii, 4. Ambaye anawalisha wasipate njaa, na anawalinda na
khofu.} Quraish aya ya 1-4.
Mwenyezi Mungu anasema : { Je! Kwani Sisi hatukuwaweka imara katika
pahala patakatifu, penye amani, ambapo huletewa matunda ya kila aina
kuwa ni riziki itokayo kwetu? Lakini wengi wao hawajui.} Al qaswas aya ya 57.
Mwenyezi Mungu anasema : { Je! Hawaoni ya kwamba tumeifanya nchi
takatifu ina amani, na hali watu wengine wananyakuliwa kote kwa majirani
zao? Je! Wanaamini upotovu, na neema za Mwenyezi Mungu wanazikataa? }
Al ankabuut aya ya 67.
Mwenyezi Mungu anasema : { Na baina yao na miji mingine tuliyo ibariki
tuliweka miji iliyo dhaahiri, na tukaweka humo vituo vya safari.
Tukawaambia: Nendeni humo usiku na mchana kwa amani } Sabaa aya 18.
Mwenyezi Mungu anasema : { Walio ambiwa na watu: Kuna watu
wamekukusanyikieni, waogopeni! Hayo yakawazidishia Imani, wakasema:
Mwenyezi Mungu anatutosha, naye ni mbora wa kutegemewa } Al imraan
173.
Mwenyezi Mungu anasema : { Na jikingeni na Fitna ambayo haitowasibu
walio dhulumu peke yao kati yenu. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mkali
wa kuadhibu. } Al anfaa aya 25.
Mwenyezi Mungu anasema : { Kwa hakika wale wanao penda uenee uchafu
kwa walio amini, watapata adhabu chungu katika dunia na Akhera. Na
Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.} Al nuur aya 19.
Mwenyezi Mungu anasema : { Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na
mt'iini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo
basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini
Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye
mwisho mwema.} Al nisaa 59.
Mwenyezi Mungu anasema : {Na linapo wafikia jambo lolote lilio khusu
amani au la kitisho wao hulitangaza. Na lau kuwa wangeli lipeleka kwa
Mtume na kwa wenye mamlaka kati yao, wale wanao chunguza wangeli lijua.
Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenu na rehema yake mngeli
mfuata Shet'ani ila wachache wenu tu.} Al nisaa 83.
Hadithi za Mtume (Saw)
Kutoka kwa Ibnu Ubayd llah bin Mehsan Al-hatmiy, kutoka kwa baba yake,
amesema, amesema Mtume (Saw): “ atakaeamka hali ya kuwa yupo salama
katika nafsi yake, ana siha katika mwili wake, na ana chakula cha siku yake
basi kama kamba amemilikishwa dunia”. (Imepokewa na Tirmidhy).
Kutoka kwa Ibn Abbas (Mwenyezi Mungu amwie radhi), amesema,
amemsikia Mtume (Saw) anasema: “ macho mawili hayataguswa na moto;
jicho lililolia kwa ajili ya kumuogopa Mwenyezi Mungu na jicho lililokesha
kulinda kwenye njia ya Mwenyezi Mungu”.
Kutoka kwa Abdullah bin Ady bin Hamraa, amesema: nimemuona Mtume
(Saw) amesimama katika eneo la Haz-wara akasema: “ hakika eneo hili ni
eneo bora katika maeneo ya ardhi ya Mwenyezi Mungu, na eneo lipendwalo
na Mwenyezi Mungu, na lau kama nisingelikuwa nimefukuzwa hapa, basi
nisingelitoka”. (Kitabu cha Ahmed na Tirmidhy). Haz-wara hili ni eneo lililopo
nchini Makka.
Kutoka kwa ibn Abbas (Mwenyezi Mungu awawie radhi) amesema: amesema
Mtume (Saw) kuhusu Makka: “Mji bora ulioje na niupendao na lau kama
watu wangu hawakunifukuza basi nisingelikaa katika mji mwengine”
(Imepokewa na Tirmidhy).
Kutoka kwa Aisha (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: Mtume (Saw)
amesema: “Ewe (Mwenyezi Mungu tupendezeshe kuupenda mji wa Madina
kama ulivyotupendezesha kuupenda mji wa Makka. (Imepokewa na Bukhari).
Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
amemsikia Mtume (Saw) akisema: “atakaenitii mimi basi hakika amemtii
Mwenyezi Mungu, na atakaeniasi basi hakika amemuasi Mwenyezi Mungu,
na atakaemtii kiongozi basi amenitii mimi, na atakaemuasi kiongozi basi
ameniasi mimi, kwani kiongozi ni kizuizi hupambana kwa ajili yao na
humuogopa Mwenyezi Mungu kwa ajili yao, na pindi akiamrisha kumtii
Mwenyezi Mungu na kufanya uadilifu atapata malipo mema kwa hilo, na
iwapo atakuwa kinyume na hivyo basi mzigo huwa ni wake. (Imepokewa na
Bukhari).
Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi), kutoka kwa
Mtume (Saw) amesema: “atakaejitoa katika utiifu na kuachana na kundi
(umoja) kisha akafariki, basi huwa kafariki katika kifo cha kijahilia, na yeyote
atakaepigana chini ya bendera ya upofu, hukasirika kwa ajili ya koo yake au
huendeleza chuki au kutaka ushindi kwa koo yake kisha akafariki, basi huwa
kafariki katika kifo cha kijahilia. Na yeyote katika umma wangu akatoka
akawa anawapiga wema na waovu na wala hakuna anaesalimika nae na wala
hatimizi ahadi kwa wenye ahadi ya ulinzi, basi huyo si katika mimi na mimi si
katika yeye. (Imepokewa na Muslim).
8. Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
“amesema Mtume (Saw): “ Itakujakuwa fitina kiasi ambacho fitina ya aliyekaa
ni bora kuliko fitina ya aliyesimama. na fitina ya aliyesimama ni bora kuliko ya
anaetembea. na fitina ya anaetembea ni bora kuliko fitina ya anaeieneza.
Yoyote mwenye kutafuta utukufu kutokana na fitina hiyo basi ataupata. Na
mwenye kupata kimbilio basi ajilinde kwa kimbilio hilo. (Imepokewa na
Bukhari na Muslim).
Tatu: Maudhui
Hakika miongoni mwa neema kubwa za Mwenyezi Mungu kwa mwanadamu
ni neema ya usalama na utulivu, bila ya hizo akili na nafsi ya mwanadamu
hautulizani, na katu hatopata furaha ulimwenguni hata kama atakuwa
anamiliki dunia na vilivyomo, kwani bila shaka furaha na neema ya
ulimwengu ni kuwepo kwa amani na utulivu, kwani katika hadithi ya Mtume
(Saw) : “ atakaeamka hali ya kuwa yupo salama katika nafsi yake, ana siha
katika mwili wake, na ana chakula cha siku yake basi kama kwamba
amemilikishwa dunia”. (Imepokewa na Tirmidhy).
Neema ya amani na utulivu ni matakwa ya kila kiumbe ulimwenguni, hata
nabii ibrahim (amani iwe juu yake) aliwaombea watu wake aliposema. {Na
alipo sema Ibrahim: Ee Mola wangu Mlezi! Ufanye huu uwe mji wa amani, na
uwaruzuku watu wake matunda, wale wanao muamini Mwenyezi Mungu na
Siku ya Mwisho.} Albaqara aya 126.
Hapa nabii Ibrahim (amani iwe juu yake) anamuomba Mwenyezi Mungu
aibariki Makka kwa amani na pato (rizki), na katanguliza kuomba amani kabla
ya rizki kwa sababu rizki haitokuwa na utamu wake pindi ikikosekana amani,
kupitia amani mwanadamu hupata utulivu na anahisi umuhimu wa maisha.
Naye Mwenyezi Mungu akamuitikia mtume wake na kipenzi chake kwa
kuifanya Makka kuwa ni sehemu tulivu kwa uwezo wake na utashi wake, na
kuifanya nchi ya uisilamu, na hii yote ni kwa baraka za maombi ya nabii
Ibrahim (amani iwe juu yake). Si hivyo tu bali nabii Ibrahim (amani iwe juu
yake) ametanguliza neema ya usalama –amani – kabla ya tauhidi, akasema
{Na Ibrahim alipo sema: Ewe Mola wangu Mlezi! Ujaalie mji huu uwe wa
amani, na uniepushe mimi na wanangu na kuabudu masanamu.} Ibrahim aya
35.
Na kama Mwenyezi Mungu mtukufu alivyowaneemesha makuraish kwa
neema hii kubwa, akawapa maisha mazuri na utulivu katika nchi, Mwenyezi
Mungu amesema :{3.Basi nawamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii. 4.
Ambaye anawalisha wasipate njaa, na anawalinda na khofu.} Quraesh aya 3-
4.
Na kama alivyowaneemesha kwa kuifanya Al kaaba kuwa ni mahala pa
utulivu, Mwenyezi Mungu anasema {Je! Hawaoni ya kwamba tumeifanya
nchi takatifu ina amani, na hali watu wengine wananyakuliwa kote kwa
majirani zao? Je! Wanaamini upotovu, na neema za Mwenyezi Mungu
wanazikataa?} Al ankabuut 67.
Kupitia amani na utulivu taifa hukua na watu hupata utulivu wa maisha yao
na utafutaji wa riziki zao, taifa nalo huendelea pamoja na jamii, uchumi pia
hukua, na haya tayari Mwenyezi Mungu ameshayaeleza katika Kurani tukufu
wakati alipowaneemeha watu wa Saba-a kwa neema ya amani na utulivu,
akasema {Na baina yao na miji mingine tuliyo ibariki tuliweka miji iliyo
dhaahiri, na tukaweka humo vituo vya safari. Tukawaambia: Nendeni humo
usiku na mchana kwa amani.} Saba-a aya 18.
Hakuna taifa lililotangulia miongoni mwa mataifa, na wala jamii miongoni
mwa jamii isipokuwa amani na utulivu upo kwa raia zake.
Kuyumba kwa amani na utulivu huathiri pakubwa taifa na raia hata katika
ibada – ambayo ni lengo kuu la kuumbwa wanadamu – kwa ajili hiyo, hata
sala isaliwayo wakati wa wasiwasi (sala ya hofu) ipo tafauti na sala isaliwayo
wakati wa amani kimuundo na kimatendo. Na hata ibada ya kuhiji pia
inashurutishwa kuwepo na amani njiani, na kama njia itakuwa haina amani
basi ibada ya hijja huwa si lazima kuitimiza, hapa tunafahamu kuwa, hata
ibada haitokamilika kama itakiwavyo pindi tu pakiwa na ukosefu wa amani na
utulivu.
Amani na utulivu ukiwepo katika taifa na ikawa kila mmoja yupo salama yeye
mwenyewe, mali zake, heshima yake, bila shaka jamii hii wataishi katika
utulivu wa hali ya juu kabisa, pasi na hofu wala wasiwasi, na jamii itanufaika
kwa maendeleo na ukuaji, na maendeleo ni vitu vya lazima kisheria na ni
matakwa ya taifa pia ni lengo kuu na muhimu miongoni mwa malengo ya dini
tukufu.
Vitendea kazi vya kuleta utulivu: raia inamlazimu aipende nchi yake ambayo
anaishi kwa uhuru unaokubalika, na ahisi umuhimu wa taifa ambalo amekulia
katika mchanga wake, na hivi ndivyo alivyopiga mfano Mtume (Saw)
kivitendo, wakati anahama Makka Tukufu na kuhamia Madina Munawara,
kwani Mtume (Saw) ametufundisha mapenzi ya taifa na ubora wa
kujifaharisha nalo, na mapenzi yake (Saw) juu ya nchi yake ya Makka na hisia
zake juu ya taifa hilo ilikuwa ni jambo kubwa, pamoja na ubaya wa watu
wake, akasema ingawa ameathirika kuliacha: {Hakika hii ni ardhi bora ya
Mwenyezi Mungu na ni ardhi ya Mwenyezi Mungu niipendayo na lau kama
watu wangu hawakunifukuza basi nisingelitoka.” (Kitabu cha Ahmad na
Tirmidhy).
Na katika mapokezi ya Ibni Abbas (Mwenyezi Mungu awawie radhi)
amesema: amesema Mtume (Saw) kuhusu Makka” (“ Mji bora ulioje na
niupendao na lau kama watu wangu hawakunifukuza basi nisingelikaa katika
mji mwengine” (Imepokewa na Tirmidhy).
Na alipohamia Mtume (Saw) katika mji wa Madina akaanza kujenga taifa la
kisasa kwa lengo la kuwafundisha masahaba zake na ulimwengu kwa ujumla
ya kuwa taifa halijengwi isipokuwa kwa wale wenye kulipenda, na dua yake
kubwa ilikuwa kama ilivyokuja kutoka kwa mama wa waumini Aisha
(Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema: amesema Mtume (Saw) “ Ewe
Mwenyezi Mungu tupendezeshee mji wa Madina kama ulivyotupendezeshea
mji wa Makka au zaidi”. (Imepokewa na Bukhari)
Na Mtume (Saw) hakuwa akitaka kuonesha upendo wa taifa isipokuwa
kutaka kuwepo kwa amani na utulivu ili kila mmoja awe na usalama.
Kwa ajili hiyo ni lazima kwa kila raia ahifadhi taifa lake na alipende na alilinde
pia alitetee, na asimamie wajibu wake na majukumu yake kwa ajili ya taifa.
Taifa kwa mtazamo wa kiisilamu ni kitu kikubwa sana na kuzembea kuhusu
haki ya taifa ni hatari sana, kwa ajili hiyo, Mtume (Saw) amempa cheo kila
ambae atahifadhi utulivu wa taifa lake na kujitolea muhanga kwa ajili yake,
kwani Mwenyezi Mungu hatomuadhibu na wala moto hautogusa macho
yake, kwani malipo huwa sana na matendo.
Imepokewa na Ibn Abbas (Mwenyezi Mungu awawie radhi amesema:
nimemsikia Mtume (Saw) akisema; “ macho mawili hayataguswa na moto;
jicho lililolia kwa ajili ya kumuogopa Mwenyezi Mungu na jicho lililokesha
kulinda kwenye njia ya Mwenyezi Mungu”. (Imepokewa na Tirmidhy).
Kulipenda taifa ni katika mambo muhimu sana yaletayo utulivu nchini kwa
jamii yoyote, kwani mtu akilipenda taifa lake na akihisi jukumu lake la
kuhifadhi amani na utulivu na wala hayuko pamoja na wanaoliharibu katika
wenye kuhubiri, kwani mwanadamu akipata utulivu ndani ya nchi yake basi
pia utulivu wa nafsi yake utakuwepo na ataleta mafanikio katika kazi zake na
chumo lake.
Na katika vitendea kazi vya utulivu: ni kueneza upendo, ushirikiano kati ya
watu, Mtume (Saw) anasema “ Muumini kwa muumini mwenziwe ni sawa na
jengo hushikana wenyewe kwa wenyewe na kisha akagandisha vidole vyake”
(imepokewa na Bukhari na Muslim).
Na kujiepusha na tofauti na migongano, kwani hiyo ni shari inayowapelekea
kwenye mgawanyiko na upotevu, Mwenyezi Mungu anasema (Na mt'iini
Mwenyezi Mungu na Mtume wake, wala msizozane mkaingiwa woga, na
zikapotea nguvu zenu. Na subirini. Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja na
wanao subiri) Al anfaal 46.
Tujiepushe sana na ushabiki au vikundi vikundi kwani hivyo ni shari
ipelekeayo kusambaratika kwa jamii, na inapasa kuunga jamii na kuwepo
ushirikiano ili amani na utulivu uwepo na hivi ndivyo alivyoamrisha Mwenyezi
Mungu {Na saidianeni katika wema na uchamungu. Wala msisaidiane katika
dhambi na uadui. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni
Mkali wa kuadhibu. } Almaaidah aya 2.
Na katika mambo muhimu ambayo husaidia kuleta utulivu nchini: ni kuwatii
wenye madaraka bila ya kuasi Mwenyezi Mungu, kwani Mwenyezi Mungu
anasema {Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume na
wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni
kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na
Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema}
Alnisaa 59.
Kwani wenye madaraka ni kama kivuli cha Mwenyezi Mungu katika ardhi,
kama alivyosema Mtume (Saw) “viongozi ni kivuli cha Mwenyezi Mungu
katika ardhi, yeyote atakaewakarimu naye atakirimiwa na Mwenyezi Mungu
na atakaewadhalilisha, nae atadhalilishwa na Mwenyezi Mungu”. Imepokewa
na Tabariy na Bayhaqiy.
Na pia Mtume (Saw) amesema, “yeyote atakaemkirimu kiongozi atendae kwa
ajili ya Mwenyezi Mungu duniani, basi naye Mwenyezi Mungu atamkirimu
siku ya kiyama, na yeyote atakaemdhalilisha kiongozi atendae kwa ajili ya
Mwenyezi Mungu basi naye atadhalilishwa siku ya kiyama”. (Imepokewa na
Ahmad)
Hakika kumtii kiongozi ni kwa kumtii Mwenyezi Mungu na kwa masilahi ya
taifa na kwa imani ya waisilamu, na kiongozi akimrisha au kukataza itapasa
kumtii pindi tu si katika maasi ya Mwenyezi Mungu. Imepokewa na Abi
Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema, amemsikia Mtume
(Saw): “ yeyote atakaenitii mimi basi amemtii Mwenyezi Mungu, na yeyote
atakaeniasi basi amemuasi Mwenyezi Mungu, na yeyote atakaemtii kiongozi
basi amenitii mimi, na yeyote atakae muasi kiongozi basi ameniasi mimi,
kwani kiongozi ni kizuizi hupambana kwa ajili yao na humuogopa Mwenyezi
Mungu kwa ajili yao, na pindi akiamrisha kumtii Mwenyezi Mungu na kufanya
uadilifu atapata malipo mema kwa hilo, na iwapo atakuwa kinyume na hivyo
basi mzigo huwa ni wake.” (Imepokewa na Bukhari). Kinachokusudiwa ni
kumtii kiongozi bila ya kumuasi Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kutengeneza
dini na dunia.
Kwa ajili hiyo ni wajibu wa raia kusikia na kutii viongozi, na wala asitengane
na kundi la waisilamu, imepokewa kutoka kwa Abi Hurayra, kutoka kwa
Mtume (Saw) kwamba yeye amesema: “atakaejitoa katika utiifu na kuachana
na kundi (umoja) kisha akafariki, basi huwa kafariki katika kifo cha kijahilia,
na yeyote atakaepigana chini ya bendera ya upofu, hukasirika kwa ajili ya koo
yake au huendeleza chuki au kutaka ushindi kwa koo yake kisha akafariki,
basi huwa kafariki katika kifo cha kijahilia. Na yeyote katika umma wangu
akatoka akawa anawapiga wema na waovu na wala hakuna anaesalimika nae
na wala hatimizi ahadi kwa wenye ahadi ya ulinzi, basi huyo si katika mimi na
mimi si katika yeye. (Imepokewa na Muslim).
Na huenda sababu ya kulazimika kuwatii na kuwasikiliza viongozi ni kwa vile
iwapo wataacha mema basi hapo ndipo italazimu kutowatii kwani kufanya hivyo
kutapelekea kuzidi uasi, na kitakiwacho ni kunasihiana ambako kuko kwa njia
tofauti zilizo salama na za kidemokrasia, na hii ni kwa ajili ya kufanya neno la
umma liwe ni moja, na kuzuia mipasuko na makundi, ambayo huenda
yakasababisha mauaji, umwagaji wa damu, kuvunjiana heshima, kufanya
yaliyoharamishwa, kuangamiza taifa, kupoteza mali, kudhoofisha ushirikiano na
haya yote yapo wazi kwa kila mtu kwa sababu ya matatizo yaliyosababishwa kwa
kutowasikiliza viongozi.
Na katika mambo makubwa yanayoondosha utulivu wa taifa: ni kueneza
fitina ambazo zinapelekea kuondoka kwa neema na kuleta maafa, na kukata
ushirikiano kati ya mataifa na mengine, na kueneza machafu na kuondosha
mazuri, na kutangaza roho ya uadui na chuki na kuacha kueneza roho ya
upendo na undugu.
Fitina ni moto wenye kuangamiza kikavu na kibichi, yenye kutenganisha kati
ya mtu na mwengine, mama na mwanawe, mtu na mkewe, na inampelekea
mja kuacha kumtii Mola wake. Na yeyote anaechochea fitina ni amelaanika,
na muenezaji wake ni mtu fitina mwenye kuharibu hali njema na kuzifanya
kuwa mbaya, ama muuaji na aliyeuliwa wote watafikia motoni na ni makazi
mabaya yaliyoje.
Kwa ajili hiyo, uisilamu umefanya pupa kubwa zaidi ili kuepukana na fitina, na
Mtume (Saw) ametuelekeza maelekezo ya kuweza kuepukana na fitina, na
kumfundisha muisilamu ni namna gani ataweza kutaamali na fitina. Kwani
imepokewa kutoka kwa Abdallah Bin Amru bin Al-as (Mwenyezi Mungu
awawie radhi), hakika ya Mtume (Saw) amesema: “ itakuwaje pindi
mukifikwa na wakati, ambao watu watapetwa na wakabaki wabaya kati yao
wametimizi ahadi zao na amana zao, kisha wakahitilafiana hata wakawa
kama hivi” akakutanisha vidole vyake, masahaba wakasema, unatuamrisha
nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “ Kichukueni mukijuacho
kuwa ni haki, na kiacheni mukichukiacho, na mukubali jambo mulionalo ndilo
na kuacha mambo (mabaya) yatendwayo na wengi.
Shime tena shime kuhifadhi umoja wa taifa. Na tahadhari kisha tahadhari na
fitina zilizo wazi na zilizo jificha, kwani hata Mwenyezi Mungu
ametuhadharisha nazo katika sehemu nyingi ndani ya Kurani, na katika hizo
ni kama alivyosema kuwa fitina ikifika mahala huwa haibagui katia ya aiungae
mkono na aipingae, akasema { Na jikingeni na Fitina ambayo haitowasibu
walio dhulumu peke yao kati yenu. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mkali
wa kuadhibu.} Al anfaal 25.
Pia naye Mtume (Saw) ametuhadharisha sana, imepokewa kutoka kwa
hudhaifa (Mwenyezi Mungu amwie radhi, amesema, amemsikia Mtume
(Saw) akisema: “ fitina hupita nyoyoni kama nyoyo za mkeka wenye nyuzi
nyuzi wazi, nyoyo yoyote itakayoikubali, basi huwekewa kidoto cheusi na
nyoyo yoyote itakayoikataa huwekewa kidoto cheupe hata huwa cheupe
mfano wa almasi, mtu huyo hatodhuriwa na fitina kwa muda wote wa
kuwepo mbingu na ardhi. (Imepokewa na Muslim)
Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
“amesema Mtume (Saw): “ Itakujakuwa fitina kiasi ambacho fitina ya aliyekaa
ni bora kuliko fitina ya aliyesimama. na fitina ya aliyesimama ni bora kuliko ya
anaetembea. na fitina ya anaetembea ni bora kuliko fitina ya anaeieneza.
Yoyote mwenye kutafuta utukufu kutokana na fitina hiyo basi ataupata. Na
mwenye kupata kimbilio basi ajilinde kwa kimbilio hilo. (Imepokewa na
Bukhari na Muslim).
Hakika ni wajibu kwa mwisilamu mwenye akili ajiepushe na fitina na kiali
lenye kupelekea fitina, na ataamali na fitina kwa hadhari sana, kwani
imepokewa na Anas (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema; amesema
Mtume (Saw) kuwambia Maanswari: “ Mutakuja kuona baada yangu athari,
basi kuweni na subira mpaka mutakapokutana nami, na ahadi yenu ni
kunywa katika hodhi. Hapa Mtume (Saw) anakusudia kuwa wataona athari za
mambo ya kuliwaza ya kidunia, na wasio wema watafadhilishwa zaidi wa
walio wema,na hawatokuwa na nafasi.
Kufunga njia zinazopelekea katika fitina na kujikinga nazo ni kitu kitakiwacho
kwa muisilamu ambae anataka kufanikiwa duniani na akhera, na hivyo
ndivyo Mtume (Saw) anamsifia anaechukua hadhari na kujiepusha kuzama
katika fitina kadiri ya uwezo wake.
Kutoka kwa Abi Hurayra (Mwenyezi Mungu amwie radhi) amesema:
“amesema Mtume (Saw): “ Itakujakuwa fitina kiasi ambacho fitina ya aliyekaa
ni bora kuliko fitina ya aliyesimama, na fitina ya aliyesimama ni bora kuliko ya
anaetembea, na fitina ya anaetembea ni bora kuliko fitina ya anaeieneza,
yoyote mwenye kutafuta utukufu kutokana na fitina hiyo basi ataupata, Na
mwenye kupata kimbilio basi ajilinde kwa kimbilio hilo. (Imepokewa na
Bukhari na Muslim).
Na kujikinga na fitina kutatokana na kufuata maamrisho ya Mwenyezi Mungu
na maamrisho ya Mtume wake (Saw), na kuwa pamoja na jamaa na kuwatii
viongozi kwa wema. Na kwa ajili ya masilahi ya taifa, hivyo basi, Mwenyezi
Mungu amemtahadharisha mwenye kuacha jamaa na kuzama katika fitina
duniani ya kuwa atakumbana na adhabu iliyo kali. Mwenyezi Mungu
anasema {Basi nawatahadhari wanao khalifu amri yake, usije ukawapata
msiba au ikawapata adhabu chungu} Alnuur 63.
Ni wajibu wa kila mmoja wetu kusaidiana kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu
lilobarikiwa, kujitahidi kulitukuza kwa kufaya juhudi na kuhifadhi mali zake na
kuzingatia tabia na maadili yake, kanuni na sheria zake ili tupate kujiinua kwa
kuhifadhi usalama wetu na utulivu wetu. Raia mwema ni yule mwenye
kujenga nchi yake na kuleta utulivu na kuuhifadhi na wala hawi pamoja na
watu wenye nyoyo za msilahi yao ya kibinafsi, na wenye ulinganio potofu
wenye kubomoa na ambao wanafanya kazi ya kuliharibu taifa na kueneza
fujo.
Mwenyezi Mungu anasema, {Na shikamaneni kwa Kamba ya Mwenyezi
Mungu nyote pamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi
Mungu iliyo juu yenu: vile mlivyo kuwa nyinyi kwa nyinyi maadui naye
akaziunganisha nyoyo zenu; kwa neema yake mkawa ndugu. Na mlikuwa
ukingoni mwa shimo la Moto, naye akakuokoeni nalo. Namna hivi Mwenyezi
Mungu anakubainishieni Ishara zake ili mpate kuongoka.} Al imran aya ya
113.
Na miongoni mwa fitina kubwa zenye kupoteza amani na utulivu ndani ya
jamii: ni ulinganio potofu ambao unaotolewa na wenye imani dhaifu, ambao
hawana upendo na taifa lao na wenye misimamo mikali ambao kazi yao ni
kuhakikisha kuisambaratisha jamii na kuleta hali ya misukosuko ndani yake,
na kubomoa nguzo zake na kuharibu vyanzo vyake. Na pia hawatosheki na
mipango yao miovu ya kuangamiza ambayo lengo kuu ni kuliangusha taifa na
kupoteza utulivu wake.
Na hatari kubwa iliyoje ndani ya taifa ambayo hupelekea kuwepo mtafaruku
ni kule kuitumia dini vibaya, na kuzidisha yasiyokuwemo na matumizi mabaya
ya ulinganio usio na malengo au kwa hutuba za midomoni tu au kwa
majadiliano mengi yasiyo na matokeo yoyote muhimu. Na hivi karibuni sauti
nyingi potofu na zenye kuharibu zimesikika ambazo zinaita bila ya hata haya
kuharibu taifa, kumwaga damu, na kuwahofisha walio katika usalama na
kueneza machafu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema katika kitabu chake
kitukufu {Kwa hakika wale wanao penda uenee uchafu kwa walio amini,
watapata adhabu chungu katika dunia na Akhera. Na Mwenyezi Mungu
anajua na nyinyi hamjui.} Al nuur 19.
Ulinganio huu potofu ambao wenye wana malengo ya kuiharibu jamii na
kueneza fujo na kupoteza umuhimu wa kuwepo kwa sheria ni moja wapo ya
hatari kubwa tena sana za kupoteza usalama ndani ya taifa, na ni moja wapo
wa umuhimu wa kuamsha moto za kuwepo vitndo vya kigaidi, na huifanya
jamii isifike kwa sifa zisizostahiki. Hakika ulinganio huo ambao wanaoueneza
unapelekea kuwepo fitina kubwa ambayo itayumbisha taifa na waja pia kwa
kuwepo mauaji, uharibifu, kuyumbisha hali ya usalama kati ya mtu mmoja
mmoja na kwa jamii nzima, na kuna mifano ya kuanguka na kuporomoka
mataifa mbali mbali kutokana na hali ya kukosa usalama. Dini yetu tukufu ya
kiisilamu inalingani yote yaletayo usalama na utulivu na kupinga vikali aina
zote za uadui na ugaidi.
Amana ya neno na majukumu yake
1 Rajab 1437H. sawa na Aprili 2116 A.D
Kwanza: vipengele:
1. Nafasi ya neno katika uisilamu. 2. Kuhifadhi ulimi ni katika dalili za kuwa na imani. 3. Amana ya neno na majukumu yake ni jambo la lazima kisheria na kimaadili. 4. Hatari ya neno na athari zake kwa mtu na kwa jamii.
Pili:Dalili
Ndani ya Kurani Tukufu
7. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : { Enyi mlio amini! Mcheni
Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya sawasawa 17. Apate
kukutengenezeeni vitendo vyenu na akusameheni madhambi yenu. Na anaye
mt'ii MwenyeziMungu na Mtume wake, bila ya shaka amefanikiwa
mafanikio makubwa.} (Al ahzab. 11-17)
1. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : {.. na semeni na watu kwa wema, }
(Albaqara. 23)
3. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : { Waambie waja wangu waseme
maneno mazuri, maana Shet'ani huchochea ugomvi baina yao. Hakika
Shet'an ini adui aliye dhaahiri kwa mwanaadamu } (Israa. 23)
3. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : { Mema na maovu hayalingani. Pinga
uovu kwa liliojema zaidi. Hapo yule ambaye baina yako naye pana uadui
atakuwa kama rafiki jamaa wa kukuonea uchungu.} (Fussilat. 33)
5. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : {Arrah'man, Mwingi wa Rehema 2. Amefundisha Qur'ani. 4. Akamfundisha kubaini. 3. Amemuumba mwanaadamu,} (Arahman.1-4)
6. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : {Hebu hukuona vipi Mwenyezi Mungu alivyo piga mfano wa neno zuri? Ni kama mti mzuri, mizizi yake ni imara,na matawi yake yako mbinguni. 25. Hutoa matunda yake kila wakati kwa idhini ya Mola wake Mlezi. Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifano ili wapate kukumbuka. 26. Na mfano wa neno ovu ni kama mti muovu, uliong'olewa juu ya ardhi. Hauna imara.} (Ibrahim.24-26)
7. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : { Kauli njema na usamehevu ni bora kuliko sadaka inayo fuatiliwa na maudhi. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujitosha na Mpole } (Albaqara. 263)
8. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : { Wala msiseme uwongo, kwa kuropokwa na ndimi zenu:Hichi halali, na hichi haramu - mkimzulia uwongo Mwenyezi Mungu. Hakika wanao mzulia uwongo Mwenyezi Mungu hawatafanikiwa.} (Anahl.116)
9. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema : {. Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka. 44. Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa.} (Taha.43-44)
Dalili ndani ya hadithi
1. Kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) kutoka kwa Mtume (rehma na amani zimshukie) amesema: “hakika ya mja hunena neno la kumridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na akawa hajalizingatia isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu humnaynyua kupitia neno hilo daraja. Na hakika ya mja hunena neno la kumkasirisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na akawa hajalizingatia basi huingia kupitia neno hilo katika moto wa jahannamu.” (Bukhari na Muslim).
2. kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: amasema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu (rehema na amani zimshukie) “ kila salamu ni sadaka, kila siku ichomezewayo jua akawa anafanya uadilifu kati ya watu wawili ni sadaka, na kumsaidia mtu katika kipando au kumsaidia kupandisha mzigo juu ya kipando ni sadaka. Neno zuri ni sadaka. Na hatua aipigayo kuelekea msikinitini ni sadaka. Na uchafu auondoshao njiani ni sadaka.” (Bukhari na Muslim)
3. Kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) hakika ya Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu (rehema na amani zimshukie) amesema: “ dalili za mtu mnafiki ni tatu, asemapo huongopo. Akiahidi hatimizi ahadi. Na akiaminiwa hufanya khiyana.”
4. Kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu (rehema na amani zimshukie ):“ anaeamini Mwenyezi Mungu Mtukufu na siku ya mwisho basi asimuudhi jirani yake. Na anaeamini Mwenyezi Mungu Mtukufu na siku ya mwisho basi amkirimu mgeni wake. anaeamini Mwenyezi Mungu Mtukufu na siku ya mwisho basi aseme neno zuri au anyamaze.” (Bukhari na Muslim)
5. Kutoka kwa Ibn Abass ((radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao) kuna mtu nguo (shuka) yake ilipeperushwa kwa upepo katika zama za Mtume (rehema na amani zimshukie ) akaulaani upepo. Mtume (rehema na amani zimshukie ) akamwambia: “ usiulaani kwani umetumwa, kwani yeyote mwenye kukilaani kitu pasi na haki basi laana ile humrudia mwenyewe.” (Abu Daudi)
6. Kutoka kwa Muadh bin Jabal (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: nilikuwa safarini na Mtume (rehema na amani zimshukie )nikawa karibu naye … kasha akasema: “je, nikueleze juu ya umiliki wa hayo yote? Akasema: “ nikasema: “ndio ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu: akaashiria katika ulimi wake na kusema: “jizuie na huu”. Nikasema: “ kwani sisi tunahesabiwa kwa tukisemacho? Akasema: “ ewe Muadhi,mama yako akupotea hivyo unadhani watu wataingia motoni kwa sababu ya nyuso zao –au amesema- kwa pua zao – huoni kuwa wataingia motoni kwa sababu ya ndimi zao..” (Tirmidhiy)
Tatu: Maudhui
Mwenyezi Mungu Mtukufu amemneemesha mwanadamu kwa neema nyingi
zisizohesabika akasema: { Na mkizihisabu neema za Mwenyezi Mungu,
hamwezi kuzidhibiti. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira,Mwenye
kurehemu.} (Anahl.18) Na miongoni mwa neema kubwa sana ni ulimi akasema
{Kwani hatukumpa macho mawili? 9. Na ulimi, na midomo miwili?} (albalad.8-
9) na kasha akaupa ulimi neema nyengine nayo ni kuweza kutamka ambayo
humtenganisha mwanadamu na viumbe wengine, akasema Mwenyezi Mungu
Mtukufu anasema : {Arrah'man, Mwingi wa Rehema 2. Amefundisha Qur'ani.
4. Akamfundisha kubaini. 3. Amemuumba mwanaadamu,} (Arahman.1-4).
Neno ni anuani ya ulimi na ni njia ya kuwasiliana na mwengine na kupitia
maneno maisha huendelea, na hakuna sheria yoyote iliyojali neno kama sheria
ya kiisilamu, imejali kwa hali zote sawa iwe kweli au matani. Kuna maneno
hufutahisha watu na mengine hukasirisha, na kwa neno heshima na umwagaji
wa damu huhifadhika.
Na kutokana na hatari ya neno Mwenyezi Mungu Mtukufu ameleta amri ya
kutaka ulimi uhifadhiwe, na kuacha kutamka lenye kuondoa heshima za watu,
na kuzungumzia yasiyohusu wala yasiyo na faida, akasema { Hatamki neno ila
karibu yake yupo mwangalizi tayari } (Qaf.18). viungo vyote vya mwanadamu
vimeshikamana na ulimi, ulimi ukiwa mwema navyo huwa vilevile na ukiwa
mbaya navyo huwa vibaya. Kutoka kwa Abi Said Alkhudriy (radhi za Mwenyezi
Mungu ziwe juu yake) amesema: mwanadamu afikapo asubuhi viungo vyote
husemeza ulimi na kuuambia: muogope Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa ajili
yetu kwani ukiwa sawa nasi tutakuwa sawa na kama utapinda nasi tutapinda.”
(Tirmidhi).
Na Mtume (rehema na amani zimshukie ) ameweka wazi kwa kumwambia
Muadh kuwa ulimi ni sababu ya kumfanya mtu aingie peponi au motoni.
Akasema : nilikuwa safarini na Mtume (rehema na amani zimshukie )nikawa
karibu naye … kasha akasema: “je, nikueleze juu ya umiliki wa hayo yote?
Akasema: “ nikasema: “Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu:
akaashiria katika ulimi wake na kusema: “jizuie na huu”. Nikasema: “ kwani sisi
tunahesabiwa kwa tukisemacho? Akasema: “ Mama yako akupotea ewe
Muadhi, hivyo unadhani watu wataingia motoni kwa sababu ya nyuso zao –au
amesema- kwa pua zao – huoni kuwa wataingia motoni kwa sababu ya ndimi
zao..” (Tirmidhiy)
Neno ni amana na inabidi kwa atamkaye amuogope Mwenyezi Mungu
Mtukufu kwalo, kwani lina madhara na hatari kubwa pia lina faida na
mafanikio mengi. Imepokewa kutoka kwa Abi Hurayra (radhi za Mwenyezi
Mungu ziwe juu yake) kutoka kwa Mtume (rehma na amani zimshukie)
amesema: “ hakika ya mja hunena neno la kumridhisha Mwenyezi Mungu
Mtukufu na akawa hajalizingatia isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu
humnaynyua kupitia neno hilo daraja. Na hakika ya mja hunena neno la
kumkasirisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na akawa hajalizingatia basi huingia
kupitia neno hilo katika moto wa jahannamu.” (Bukhari na Muslim).
Na ilivyokuwa neno zuri ni dalili ya imani ya mtamkaji kama alivyotueleza
Mtume (rehema na amani zimshukie) pale aliposema: “anaeamini Mwenyezi
Mungu Mtukufu na siku ya mwisho basi aseme neno zuri au anyamaze.” Na
Mwenyezi Mungu Mtukufu ametuamrisha kusema neno la kweli kwa yeyote
bila ya kutafautisha na wala tusitamke isipokuwa tamshi jema ambalo hujenga
na wala halibomoi, huimarisha na si kuporomosha, akasema (na semeni na
watu kwa wema, } (Albaqara. 83). Pia akasema {Waambie waja wangu waseme
maneno mazuri, maana Shet'ani huchochea ugomvi baina yao. Hakika Shet'ani
ni adui aliye dhaahiri kwa mwanaadamu } (Israa. 53)na akasema pia {Enyi mlio
amini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya sawasawa 71. Apate
kukutengenezeeni vitendo vyenu na akusameheni madhambi yenu. Na anaye
mt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, bila ya shaka amefanikiwa mafanikio
makubwa.} (Al ahzab. 71-71). Kutengemea kwa matendo na kupata msamaha
wa madhambi upo kupitia matamshi mema na kwa maneno mazuri. Kwa ajili
hiyo maelekezo ya uisilamu ni kuchunguza na kuwa na uhakika wa
ukisemacho, Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {. Enyi mlio amini! Akikujieni
mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua,
na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyo yatenda.}(Alhujuraat.6).
Kwa ajili hiyo itafahamika kuwa kuhifadhi ilimi ni dalili ya imani, na ni katika
uisilamu mzuri na ni njia ya kufikia pepo ya Firdausi ya juu, Mwenyezi Mungu
Mtukufu anasmea { Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,}
Almuuminuun.3) mpaka aliposema {Hao ndio warithi,11. Ambao watairithi Pepo
ya Firdausi, wadumu humo.} (Almuuminuun11.11). na kutoka kwa Saad bin
Muadh (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) kutoka kwa Mtume (rehema na
amani zimshukie) amesema: “yeyote atakayenipa dhamana ya kuhifadhi kilichopo
kati ya ulimi wake na kilichopo kati ya miguu yake miwili basi nami ninampa
dhamana ya kuingia peponi.” (Bukhari).
Na amana ya neno na majukumu yake ni jambo la lazima kwa upande wa sheria
na kimaadili, kwani huufanya umma uwe pamoja na kuwa na nguvu na kuweza
kumbadilisha adui kuwa rafiki na chuki kuifanya kuwa ni upendo na kuondoa
matendo na vitimbi vya shetani, Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema {34 Mema
na maovu hayalingani. Pinga uovu kwa liliojema zaidi. Hapo yule ambaye baina
yako naye pana uadui atakuwa kama rafiki jamaa wa kukuonea uchungu.}
(fussilat.34). na kama ilivyokuwa neno zuri hukutanisha nyoyo na kurekebisha
nafsi na kuondosha huzuni na hasira na kufanya kuhisi kuridhia na furaha hasa
hasa linapoambatanishwa na tabasamu. Imepokewa kutoka kwa Abi Dhari (radhi
za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake)amesema: amesema Mjumbe wa Mwenyezi
Mungu Mtukufu (rehma na amani zimshukie) “kutabasamu katika uso wa ndugu
yako ni sadaka.” (Bukhari).
Na kama ilivyokuwa amana ya neno linahitaji kwa msemaji kuwa asiseme
isipokuwa kwa kheri na ukweli, asiseme uongo wala kwa hadaa au kwa kutoa
ushahidi wa uongo na kugeuza ukweli na wala asizungumze bila ya kujua.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema Wala msiseme uwongo, kwa kuropokwa na
ndimi zenu: Hichi halali, na hichi haramu - mkimzulia uwongo Mwenyezi Mungu.
Hakika wanao mzulia uwongo Mwenyezi Mungu hawatafanikiwa.} (Anahl.116).
Pia katika amana za neno ni kutoa nasaha na ushauri mwema, kwani dini ni
kushauriana kama alivyotueleza Mkweli Muaminifu (rehema na amani zimshukie)
kutoka kwa Tamim Aldaramiy (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) kuwa
Mutume wa Mwenyezi Mungu Mtukufu (rehema na amani zimshukie ) amesema:
“ dini ni nasaha”. Tukasema: “ ni kwa nani.? Akasema: “ ni kwa (ajili) ya Mwenyezi
Mungu Mtukufu na Mtume wake na kwa viongozi wa waumini na wengineo.”
(Muslim). Na kutoka kwa Abi hurayra (radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake)
amesema: amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu (rehema na amani
zimshukie ) “mweney kutaka ushauri basi amesalimika.” (Daudi). Hivyo basi,
nasaha na ushauri wa ukweli mambo mengi hutengemea ikiwemo amani na ,
upendo katika taifa.
Neno ni silaha ya hatari sana yenye pande mbili, linaweza kuwa ni sababu ya
kuimarika kwa taifa pindi ni zuri na la ukweli na linaweza pia kuwa ni sababu ya
kuporomoka, ufisadi na uharibifu pindi liwapo si la ukweli. neno si kitu kidogo lina
umuhimu mkubwa sana katika maisha ya watu, na kwa yale wafanyiayo mfano wa
kuuziana, ahadi na makubaliano na mifano mwngine yenye kuhitaji ukweli katika
mazungumzo.
Haifichikani kuwa neno zuri lina athari nzuri kati ya watu, wema kwa jirani kupitia
neno zuri huenda ikawa ndio sababu ya kuingia peponi, na ubaya wake kwao
ikawa ndio sababu ya kuingia motoni. Imepokewa kutoka kwa Abi Hurayra
amesema: Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu (rehema na amani zimshukie )
aliambiwa: “ ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu kuna mwanamke Fulani
anasali usiku na kufunga mchana, na hufanya (mema) na hutoa sadaka na
huwakera majirani zake kwa ulimi. Mtume (rehema na amani zimshukie )
akasema: hana jema huyo yeye ni katika watu wa motoni.” Akaambiwa:“na kuna
mwanamke fulani husali sala za lazima tu na hutoa sadak ، lakini hamkeri mtu.
Mtume (rehema na amani zimshukie ) akasema yeye nikatika watu wa peponi.”
(Bukhari).
Vilevile neno lina athari kubwa katika mahusiano kati ya muisilamu na asiyekuwa
muisilamu, hata pamoja na maadui zetu Mwenyezi Mungu Mtukufu
ametuamrisha tuseme nao kwa maneno mazuri, Mwenyezi Mungu Mtukufu
anasema { Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka. 44.
Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa.} (Taha. 43-44)
Na katika jambo la msingi kulitaja hapa ni kuwa neno lililoandikwa linaweza kuwa
na maafa na madhara makubwa ya kuangamiza taifa na halina tafauti na neno
litamkwalo, aina zote hizi ni amana, na ni wajibu wa kila ashikae kalamu aipe haki
yake kama itakiwavyo na awe na pupa na kujiepusha na makosa kwani ni kalamu
ndio itakayomuweka wazi juu ya misimamo yake na inahitajika aitumie kwa
kunusuri haki na kuilingania pia. Imam Jahidh anasema “kalamu ni ndimi mbili
nayo ni yenye kubakisha athari.” Si hivyo tu bali ni upanga mkali sana na weney
nguvu na unafika mbali kuliko hata upanga wenyewe.
Kwa ajili hiyo kila mwandishi amuogope Mwenyezi Mungu Mtukufu aache
kueneza habari za uongo na kuupotosha ukweli pia kuzungumzia heshima za watu
na kuacha kabisa kila lenye kuleta madhara kwa jamii kwani jambo hili huwa ni
khiyana ya neno.
Mshairi anasema:
Mwandishi yeyote atatoweka * na alichokiabdika kitabakia
Basi mkono wako usiandike kitu isipokuwa * siku ya kiama ukikiona utafurahi
Kila mtu aelewe jukumu la neno na kuwa atasimamishwa mbele ya Mwenyezi
Mungu Mtukufu na mbele ya dhamira yake kwa kila alichokizungumza, ili isije
ikawa ndio sababu ya kutengana na kukimbiana kati ya wanajamii na mtu na
mwengine na kutengana kati ya mwanfamilia na kuharibu mahusiano kati ya
watu.
Tunahitajia sana maneno mazuri ya kweli kati ya watu na jamii ili kueneza
mapenzi na ukaribu na kuondosha mtengamano na mfarakano. Neno zuri lina
athari nzuri na yenye kuleta masilahi mazuri na pia huleta msamaha wa makosa.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu
na semeni maneno ya sawa sawa 71. Apate kukutengenezeeni vitendo vyenu na
akusameheni madhambi yenu. Na anaye mt'ii MwenyeziMungu na Mtume wake,
bila ya shaka amefanikiwa mafanikio makubwa.} (Al ahzab. 71-71).
Index
2 Utangulizi 3
3 Uisilamu ni dini ya ujenzi na ya uimarishaji 5
4 Ubora wa maadili katika ujumbe wa Muhammad 29
5 Miongoni mwa aliyokirimiwa Mtume Muhammad (Saw) 42
6 Wajibu wetu kwa upande wa Kurani tukufu 57
7 Wito wa Manabii na Mitume katika urekebishaji kwa mtazamo
wa kurani tukufu 72
8 Sifa za waumini ndani ya kurani 83
9 Uhusiano wa kifamilia ulio bora 95
: Fadhila za masahaba (radhi za Mwenyezi Mungu
ziwashukie)
:8
21 Haki ya mtoto katika ukuaji mzuri na maisha bora na maandalizi mazuri kwa ajili ya mustakbali
219
22 Hatari za ulinganio potofu na umuhimu wa kuuzuia kwa ajili ya upatikanaji wa amani na utulivu
234
23 Amana ya neno na majukumu yake
248
top related