muongozo wa elimu ya masoko tanzania...umuhimu zoezi hili linatoa fursa ya kuonyesha faida na hasara...
Post on 08-Feb-2020
33 Views
Preview:
TRANSCRIPT
1
Muongozo wa Elimu ya Masoko
Tanzania
2
Mradi: Wekeza kwa wanawake wa kimaasai
DCI-HUM/2014/341-127
Utangulizi
Karibu kwenye programu ya elimu ya masoko. Kuanzia sasa naamini tutakuwa pamoja
kuelimishana muongozo huu wenye ujuzi wa biashara na wateja,
Muongozo huu utakusaidia katika kufundisha elimu ya masoko. Muongozo huu utakuongoza
kwa vipindi 5, vitakavyochukua siku tano. Kila Kipindi kitakuwa na shughuli mbalimbali
yanayoendana. Utakaposoma programu hii utaona kuwa ina muswada na mambo elekezi kwako
wewe mwezeshaji kama ilivyoelezewa kwa maandishi meusi.
Utakapoanza kufundisha hii program tunakushauri utumie mswada huu wakati wote na uusome
mpaka utakapojiridhisha kuwa maelezo yote ni sahihi. Ukishajirizisha tunakushauri ukubaliane
na programu hii na kutumia maelezo, shughuli na mahojiano pale unapoona inafaa.
Asante kwa ushiriki wenu nawatakia kila la kheri katika ufundishaji.
3
Sehemu ya 1
Zoezi:
Utangulizi/kuweka vipaombele sehemu za biashara
Muongozo:
Anza kwa kuwasalimia watu wote na kuwaomba wajitambulishe, ujitambulishe na
kuutambulisha muongozo.
Karibu kwenye kipindi chako cha kwanza cha elimu ya biashara na masoko. Mimi ni
mwezeshaji wa vipindi vijavyo. Wengi wenu imewabidi kuacha shughuli zenu muhimu ili
kuhudhuria kwenye darasa hili, Inawezekana una shughuli nyingi nyumbani. Wengine mme
tembea umbali mrefu kuwa hapa. Hata hivyo, kila mmoja wenu yupo hapa kwasababu ana nia ya
kuboresha maisha yake, na familia yake.
Inaweza ukawa unaogopa kuwa hauna elimu ya kutosha, au unaweza kuogopa kuwa huna vifaa
au ujuzi wa kutosha kuweza kuendesha biashara kwa mafanikio. Pamoja na kwamba wote tupo
makini katika kutunza nyumba na kuangalia familia zetu. Tunakabiliana na matatizo kama vile
kutokuwa na fedha za kununua vitu tunavyo hitaji au hatuna namna ya kupata bidhaa hizo. Hata
tukiwa na fedha bidhaa tunazohitaji hazipo. Wakati mwingine tunakabiliana na matatizo ya
kutokuwa na kazi kwa muda mfupi au muda mrefu, na hata tukipata ajira,mishahara ni midogo
sana na haitoshi.
Hapa darasani, hatutajibu tu maswali yenu bali kuwafundisha mambo unayotakiwa kuyajua ili
usipoteze fedha kama mteja na pia kuwafundisha maswala ya msingi anayotakiwa kuyajua mtu
mwenye mtazamo wa kibiashara. Kwa mtazamo wetu kuhifadhi fedha ni sawa na kutengeneza
pesa, na ndio sababu mafunzo haya ni ya muhimu. Dhumuni la mafunzo haya ni kukuwezesha
wewe kama mteja namna ya kufikiri kama mfanyabiashara.
Mafunzo haya yanaitwa Elimu ya Biashara na masoko. Mafunzo haya yametumika
kuwawezesha na kuwasaidia wanawake 1,000 wa India na sehemu nyingine za dunia.
Tumekuwa sasa tukifundisha mafunzo haya Tanzania kwa mwaka mmoja, na tumeona
yalivyoboresha maisha ya watu tuliowafundisha. Sio kila mmoja atayepata mafunzo haya
atakuwa mfanyabiashara, lakini kila mmoja atajifunza kuwa mteja mzuri ambaye itapelekea
kuwa na hela zaidi kutokana na kuhifadhi.
Unaweza kuuliza ina maana gani kuwa mteja. Sisi wote ni wateja kwa namna moja au
nyingine. Nimegundua kuwa mteja mzuri ni jambo la muhimu sana, kwa sababu ni hatua ya
kwanza inayopelekea kuwa mfanyabiashara na kupanua mawazo.
4
Masomo haya yameandaliwa baada ya kuwasoma wateja kwenye mazingira yenu na
mazingira mengine yanayofanana na haya ya kwenu. Na matokeo yake ni kwamba tuna
programu ambayo inawahudumia maelfu ya watu duniani. Kuwasaidia kuwa wateja na
wafanyabiashara wazuri.
Wakati wote wa mafunzo haya tutashiriki kwenye mazungumzo kwenye makundi ambapo
utahamasishwa kuongea. Pale utakapochangia zaidi ndipo wote waliopo hapa kwenye mafunzo
haya mtaweza kunufaika na mafunzo haya. Kumbuka kuwa utajijengea ujasiri wa kuongea
mbele ya kundi dogo, utaweza pia kuzungumza na mteja ambaye haumfahamu sokoni. Kama
mtapenda, wale wenye ujasiri wa juu waje huku mbele na kuonyesha njia kwenye hili darasa la
kwanza; na kwenye madarasa ya mbeleni utawashawishi wengine kwenye kikundi chako
kwenda mbele na kuongea!
Mafunzo haya yatakuwa pia na mazoezi marahisi ya kupeleka nyumbani ambayo
yatakuandaa kwa wiki inayofuata. Tunakushauri uchukulie uzito mazoezi haya ya kupeleka
nyumbani na uyafikirie na kuyaongelea utakapoenda nyumbani. Hii itapelekea wewe kuelewa
zaidi mazungumgunzo haya na kusababisha uzoefu ulioupata uwe wa manufaa zaidi kwako na
wote waliokuzunguka.
Kabla ya shughuli yetu ya kwanza, ningependa kuuliza kama kuna mtu ana swali na pia
niwaulize maswali.
Unafikiri mafunzo haya yanahusu nini?
Utapenda kupata nini kwenye mafunzo haya?
Kwakuwa kila mtu anaonekana yupo tayari, nitawaomba sasa mkae kwenye makundi ya watu
wane au watano kwa ajili ya shughuli yetu ya kwanza.
Makundi yamzunguke mwalimu kwa mduara. Ikienda vizuri, labda uwaruhusu watu wakutane
kwa makundi halafu warudi tena kuongea kuwawezesha watu kusogea na kuwa na nguvu zaidi..
Hapa unaweza kuona picha zinazoendana zinazoonyesha vipengele mbalimbali vya
biashara. Kwa shughuli hii mahususi tunatumia picha za biashara za shanga ili itusaidie kuelezea
dhana hii kwa uwazi zaidi. Sehemu tofauti za biashara kama tulivyoonyesha ni: Pesa, Usafiri,
Mali ghafi (shanga), duka, mteja na bidhaa iliyokamilika.
Tunakuomba usome na kuelewa vipengele hivi sita vya biashara na kutueleza kuwa ni
kipengele gani kilicho cha muhimu sana kati ya hivi sita, kinachohitajika katika kuanza biashara,
tutakaporudi kipindi cha pili na cha tatu. Na utueleze ni kwa nini umechagua kila kipengele na ni
sababu ipi imepelekea kuchagua umuhimu wake. Kwa mfano, naweza kuamua na kikundi
changu kuwa kipengele muhimu kwenye biashara ni uzalishaji halafu nielezee ni kwa nini
nafikiri hivyo.
Sasa tutakupa dakika 15 kuzungumza na kikundi chako na kuamua kutoa majibu. Baada
ya muda huu kisha mtu mmoja wa kikundi chako ataombwa kuja na kujadili jibu lenu. Kwa hiyo
kwa mara nyingine tena, unafikiri ni sababu zipi za muhimu zinazopelekea kuanzisha biashara?
5
Kabla hatujaanza kuzungumza kwenye vikundi, kuna mtu yeyote mwenye maswali kuhusiana na
zoezi hili.
Zunguka na kuonyesha picha za vipengele sita muhimu kwenye kila kikundi, kusaidia kila kundi
kuelewa. Waeleze wote waanze kwanza kuzungumza halafu utembelee kila kikundi na picha.
Kila kundi litakuja na kuonyesha
Baada ya kila kikundi kuonyesha, washukuru na kuwauliza kama kuna mtu yeyote mwenye
jambo la kuongeza au kujadili kuhusu yale yote yalioyoelezewa na kila kikundi.
Jibu kwa haya yafuatayo
Napendekeza kwenu kuwa sehemu ya muhimu zaidi kwenye biashara ni mteja. Bila mteja,
hakuna chochote kitakachosababisha uwe na biashara. Kati ya mambo yote tulioyazungumza,
mteja ndo sehemu pekee ambayo haitaweza kuondolewa na bado tukaweza kuwa na biashara.
Kwa mfano, tuna mteja aliyekuja kutembelea duka na kuulizia mchele. Kama muuza
duka akisema hana mchele dukani na mteja akaondoka, jambo gani litatokea? Biashara
itaendeleaje kama haitaweza kuwahudumia wateja.
Wengi wenu mmesema pesa, lakini naamini hicho sio cha muhimu kwenye kuanzisha
biashara. Labda unaweza kunipa kitu kama chakula au mbuzi kwa mabadilishano ya kitu kwa
kitu kwahiyo pesa haitahisika hapa. Labda hata biashara yangu haihusiani na bidhaa
inayoonekana au kushikika. Mwalimu kwa mfano anatumia ujuzi alionao kufanya biashara.
Thamani inaweza kuchukua sura mbalimbali na inaweza kuruhusu kupata ubunifu wa aina
mbalimbali wa kuanzisha biashara. Tutazungumzia zaidi kuhusu umuhimu wa thamani kwenye
vipindi vijavyo.
Sasa mchukulie mtu mwenye wazo la kuanzisha biashara ya chakula, na ana banda la
kuuza chakula kijijini lakini hakuna mauzo. Unafikiri ni kwa nini hakuna mauzo? Ni mambo
gani yanasababisha?
Nitawapa wote dakika 5 za kuzungumza mawazo yenu na wanakikundi. Mara mtakapomaliza
kuzungumza, nitaalika kila kikundi kije mbele na kueleza darasa wamejifunza nini na jambo gani
ndio la muhimu kwenye biashara ili iweze kufanikiwa.
Vikundi vinaonyesha tena.
Kwa mara nyingine tena nasisitiza kuwa mteja ndio jambo la muhimu sana kwenye biashara.
Nawashawishi wote mzungumze na kuchangia.
Zoezi la nyumbani
Majibu mazuri kutoka kwenu wote? Sasa katika maandalizi ya kipindi chetu kinachofuata, tuna
zoezi dogo la kufanyia nyumbani. Nawaomba mfikirie uzoefu wenu katika manunuzi. Fikiria
unachonunua ukienda dukani. Unafanyaje manunuzi? Umewahi kudanganywa? Kw nini unanua
6
vitu pale unaponunua? Kwa nini unanua kile unachonunua? Tabia zipi kati ya hizi ni nzuri na
zipi ni mbaya? Uje ukiwa tayari kutueleza kwenye kipindi kinachofuata. Rudia zoezi hili mara
mbili. Mteja
Pesa/Mtaji
7
Uzalishaji
Mali ghafi
8
Usafiri
Duka/Sehemu
9
Sehemu ya 2
Zoezi
Igizo la duka la rejareja
Dhumuni
Kujifunza changamoto za kuwa mteja
Umuhimu
Zoezi hili linatoa fursa ya kuonyesha faida na hasara ya mazoea ya wateja wakati wa wanunuzi
na kuwaelimisha kuhusu haki na majukumu ya mteja.
Muongozo
Leo tutaanza kwa kuwaita baadhi ya watu ili waweze kutueleza kuhusu lile zoezi la kupeleka
nyumbani. Kama sehemu ya kujikumbushia kwenye kipindi kilichopita kufikiria kuhusu
unachonunua ukienda kufanya manunuzi. Unafanyaje manunuzi? Umewahi kudanganywa?
Kwanini unanua vitu pale unaponunua? Kwa nini unanunua unachonunua? Tabia zipi kati ya hizi
ni nzuri na zipi ni mbaya? Kama hukutumia muda wowote kufikiria kuhusu zoezi hili la
nyumbani. Nakushauri sana ufanye hivyo baada ya kipindi hiki, kuna thamani ya kuendelea
kufikiri shughuli/mazoezi haya.
Wachukue watu watano watakaojitolea kutoa mawazo yao, jaribu kuchagua watu ambao bado
hawajasimama mbele ya darasa kuzungumza, mruhusu yeyote anayetaka kushiriki ashiriki.
Vizuri, sasa tumetambua kidogo kuhusu namna ya kufanya manunuzi na kuangalia kidogo
tunachofanaya kwa sasa, tunaenda kufanya zoezi kidogo. Katika hili zoezi nitaenda kuandaa
duka na mtakuja kununua bidhaa kutoka kwangu, ni rahisi sana. Nitahitaji watu watatu watakao
kuwa wanunuzi na watatu watako kuwa watazamaji wakati wanunuzi wanakuja huku mbele.
kutakuwepo na duka ambalo litatengeneza na kusisimua uzoefu wa manunuzi kwa mtoa
huduma. Viwepo vitu mbalimbali vichache kama sabuni ya kuoga, na ya kufulia kuwakilisha
bidhaa zingine.
Orodhesha bidhaa tulizonazo na bei
Chapa kubwa (chapa x) ya dawa ya meno (inakuwa na mswaki wa bure mswaki
umeondolewa na kuuzwa tofauti) = ugx2500
Dawa ya meno = ugx1000
Sabuni kubwa
Chapa Y dawa ya meno (100g) – MRP = Tsh. 1600
Chapa kuu (chapa Z) sabuni ya kuoga (100g) – MRP = Tsh. 1200
Chapa Z sabuni za kuoga (100g; 3 nos. ndani ya pakiti)- MRP= Tsh. 3600 + (zawadi ya
bure ya kuweza kwenda kununua kifaa).
10
Hii ni mifano inayoonyesha, na bidhaa zilizochaguliwa, hasa ambazo zinaonyesha uhalisia wa
mazingira ya hapa. Walimu au msaidizi anapaswa kuwa na jukumu la kawaida ya duka la
rejareja/ mtunza fedha na mtoa huduma wawepo katika duka la rejareja. Wanapaswa kuuza na
bidhaa na kuangalia huduma ya biashara kwa ujumla ikiwepo madeni, kukusanya malipo, na
kusambaza bidhaa. Wauzaji wanapaswa kutumia zote mbili kukusudia na inaonekana katika
makosa ya kawaida katika masoko ya ndani, kama vile suala zisizo za muswada wa bidhaa
kununuliwa, makosa ya jumla, utoaji wa bidhaa vibaya, au uuzaji wa bidhaa feki, na usambazaji
wa bidhaa zilizoisha muda wake. Washiriki kumi wanaweza kuambiwa waonyeshe jukumu la
wanunuzi na wanaobaki waangalie zoezi linavyofanyika.
Washiriki ambao walijitolea kwa jukumu la wanunuzi waelimishwe kwamba wanapaswa kuwa
na mahitaji ya familia zao katika akili, wachague bidhaa zao wanazopendelea, na kununua
bidhaa kama wangekuwa katika shughuli zao za kila siku.
Muuzaji lazima kufanya baadhi ya makosa ya kukusudia na kutumia mazoea ya udanganyifu,
kama vile utofauti katika bili na jumla na katika bidhaa zinazotolewa, na katika utoaji huwa
inatoa na zawadi pia inaweza kufanyika makosa katika bidhaa zinazotolewa. Baadhi ya
wanunuzi wanaweza kulipa kiasi baada ya kupokea bili, au wanaweza kudai muswada huo.
Baadhi ya wanunuzi wanaweza kuthibitisha muswada huo na jumla, ambapo wengine wanaweza
kuangalia muswada huo, na wangeweza kufanya hivyo ili kuweza kulipa bidhaa na kulipa kiasi
kwa kuulizwa na muuza duka. Baadhi ya wanunuzi wanaweza kuthibitisha MRP, tarehe ya
kumalizika, na kutoa maelezo ya bidhaa hiyo. Baadhi ya wanunuzi wapate kurejea tena dukani
na kumjulisha muuza duka makosa yake kupewa haki yao na kuelewana vizuri na muuzaji japo
wengine wanaweza kupuuza makosa yao. Baadhi ya wateja wanaweza ugomvi na wenye
maduka.
Baada ya washiriki kukamilisha ununuzi wa masharti (groceries), mwalimu lazima kukaribisha
watu wawili au watatu na kueleza kuwa wataenda kuagizwa dawa chache, ambayo wanapaswa
kununua dukani kama wanavyofanya katika maisha ya kawaida. Mwalimu lazima kuandika
majina ya dawa moja au mbili ambazo hazipatikani katika duka. Muuzaji lazima kutenda makosa
katika bei, hesabu na kusambaza madawa sahihi.
Matokeo
Baada ya kukamilisha zoezi, mwalimu lazima awaulize washiriki kushiriki uchunguzi wao.
Mwalimu lazima kuwezesha majadiliano kwa kutambua uwezo na udhaifu wa mazoea ya wateja
kwamba kuna vitu hawakuzingatia katika zoezi na ziorodheshwe majibu. Haya majibu yanaweza
kufafanuliwa na iwekwe kama haki na wajibu wa wanunuzi, na lazima ieleweke kwenye chati
kwa majadiliano zaidi.
11
Washiriki wanaweza kuorodhesha yafuatayo
Wanunuzi wanapaswa kuwa na maarifa kuhusu bidhaa za kununuliwa, kwa mfano,
viungo na matumizi
Wanunuzi wanapaswa kuuliza katika maduka mbalimbali kabla ya kuamua juu ya duka
gani la kununulia
Wanunuzi wanapaswa kutathmini thamani kwa kulinganisha bei na ubora na sifa ya
bidhaa mbalimbali
Wanunuzi wanapaswa kulinganisha bei na kiasi au ukubwa wa furushi ili kuamua
ukubwa wa bidhaa za kununua
Wanunuzi wanapaswa kuamua kama kununua, au kufanya bidhaa fulani kutoka viungo,
kwa mfano, pilipili tayari mchanganyiko unga dhidi viungo kama vile pilipili,
kachumbari dhidi limao na vitunguu, na nguo iliyoshonwa tayari dhidi ya nguo ambayo
bado haijashonwa.
Wanunuzi unapaswa kuona haja halisi kwa bidhaa na kwa kiasi fulani cha bidhaa kabla
ya kununua (kwa mfano, kama wanapaswa kununua mashine ya maji au kutumia huduma
ya viwanda vya kusaga, kama wanapaswa kununua bidhaa zaidi kabla ya kuharibika
kuliko wangeweza kutumia kabla kuharibika, na kama wanapaswa kununua kiasi
kikubwa zaidi ya matumizi yao ya kawaida kwa sababu ya bei nafuu)
Wanunuzi wanapaswa kuangalia uzito na udogo na kuwa macho kuhusu mbinu ya uzito.
Wanunuzi wanapaswa kupanga mapema kwa ajili ya ununuzi na kuepuka kupoteza
muda.
Wanunuzi wanapaswa kuzuia matumizi ya fedha zao na wakati usiofaa kusafiri maeneo
ya mbali ili kufanya manunuzi
Wanunuzi wanapaswa kuomba, kama ni lazima, mahitaji, gharama kutoka kwa muuzaji
kwa bidhaa za kununuliwa
Wanunuzi wanapaswa kuthibitisha kiasi cha gharama kwa jumla, na bidhaa hutolewa,
kabla ya kuondoka dukani
Wanunuzi wanapaswa kuthibitisha tarehe ya kutengenezwa, uzito, na tarehe ya
kumalizika matumizi ya bidhaa
Wanunuzi wanapaswa kuwa macho kuhusu bidhaa bandia
Wanunuzi wanaweza kutafuta taarifa kuhusu bidhaa kutoka kwa muuzaji au msambazaji
Mnunuzi anaweza kutafuta msaada wa wengine ili kupata ushauri wa kiufundi au
ufafanuzi au maelezo kabla au baada ya kununua (kwa mfano, wanunuzi wanaweza
kutafuta msaada wa daktari wao kuhusu kipimo na majina ya madawa, na kutafuta
msaada wa wauzaji au huduma wanayotoa kuhusu kazi na bidhaa za elektroniki)
Wanunuzi wanapaswa kuangalia dhamira ya kampuni ya juu ya dhamana, vipindi
udhamini wa bidhaa, na baada ya mauzo ya huduma nyingine
12
Ufupisho
mwalimu anaweza kurejea masomo muhimu waliojifunza kutokana na vikao vya mwanzo na
kukusanya masomo yao kama inavyoonyeshwa hapo chini na kuelekeza washiriki kwenye haki
na wajibu wa walaji:
Wateja wanapaswa kupanga manunuzi kwa makini
Wateja wanapaswa kutafuta, na kujifunza kuhusu, bidhaa, bei, na maduka, pia wateja
waombe gharama hizo, risiti kwa malipo, na kadi ya udhamini
Wateja wanapaswa kuangalia bidhaa kabla ya kupokea, ikiwa ni pamoja na tarehe ya
kumalizika muda
Wateja wanapaswa kutumia haki zao wakati wa kujadiliana au mazungumzo na wenye
maduka
Wateja lazima wakatishe tamaa tabia ambazo sio nzuri
Wateja wanapaswa kuwa na uwezo na tayari kulipia gharama za bidhaa na huduma
wanazopokea kutoka kwa muuzaji au mtoa huduma. Mwalimu anaweza kuuliza maswali
yafuatayo katika muhtasari wa majadiliano:
Nani mtazamo wake umefanikiwa leo?
Mwalimu lazima kuwezesha mjadala na kuhimiza washiriki kushiriki matatizo yao, kama vile
usalama, huduma kwa wakati, maeneo inapopatikana, au bei nafuu, na kuwakumbusha kuwa
mteja lazima kutathmini faida anayopata kwa bidhaa pamoja na kutangaza na kuangalia uwiano
wa fedha anazolipa, gharama anazotumia na hata kwa wateja. Ni lazima kuwepo na dhana ya
majumuisho na majadiliano na thamani, umakini wa kutathmini thamani ya fedha; mwalimu
anaweza kutumia Kielelezo 1 kuelezea dhana ya thamani, k.v., biashara ili kujua anachopata
mteja kama ina thamani na alichopewa.
Kazi ya nyumbani/zoezi la nyumbani
Wiki hii nina baadhi ya kazi rahisi ya ninyi kufanya nyumbani. Mimi nataka wewe uende na
kufikiri maeneo matatu ambayo mabadilishano ya thamani yanatokea na kwanini. Kwa mfano
unaweza kusema wewe kusafishwa nyumba yako na kwamba wewe kubadilishana muda na
nishati uliyotumia kusafisha mazingira vizuri zaidi kwamba ni bora kwa afya yako.
Unaweza kusema umesafisha nyumba yako na umebadilishana muda na nguvu uliotumia
kusafisha nyumba kuwa katika mazingira mazuri zaidi kwa afya yako.
13
Sehemu ya 3
Kuwashukuru washiriki wote kwa kuja, jambo la kwanza tunalotaka kufanya kwa leo ni kurejea
masomo tuliyojifunza katika kipindi kilichopita ambayo ni tabia za kufanya manunuzi.kwa
hakika na kwa haraka nataka nirudie maeneo muhimu.
Wateja ni lazima waweke mipango ya kufanya manunuzi kwsa uwangalifu
Wateja ni lazima watafute, wajifunze kuhusu, bidhaa, bei na uhifadhi.
Wateja ni lazima waulize wanachodaiwa (bili zao), risiti za manunuzi,kadi ya
kudhibitisha ubora kwa muda maalum.
Wateja ni lazima wakague bidhaa bidhaa kabla ya kuinunua, na ni pamoja na muda wa
kutumika kuisha.
Wateja ni lazima kuonyesha na kusimamia haki zao wakati wa kuanza mazunguzo na
wauzaji wa madukani.
Wateja ni lazima wakatae tabia na mazoea mabaya ya wafanyibiashara.
Wateja ni lazima wawe na uwezo na utashi wa kulipa bidhaa na huduma kutoka kwa
muuzaji au mtoa huduma
Kwa hiyo tumalizie zoezi la kufanya nyumbani tuliyopeana wiki iliyopita. Ngoja niwakumbushe
kama mtakuwa mmesahau, Niwaeleza kwenda kuangalia sehemu tatu na kuona kama thamani
ya mabadilishano yanatokea. Nitawapa dakika tano mzungumze katika vikundi vyenu na
mjadiliane na mtu mmoja aje kuwasilisha mawazo yenu hapo mbele. Kama itawezekana, nahitaji
mtu ambaye hajaongea mbele ya kikundi kuja mbele na kuwasilisha.
Mawasilisho ya watu binafsi. Baada ya hapo ruhusu kujadili majibu yaliyotolewa na kuwasaidia
kuwe na mjadala mkali..
Nawashukuruni, namshukuru kila mmoja kwa mawazo au maoni yake aliyotoa.Kama
mnavyoona katika maoni yaliyotolewa, yapo maeneo katika maisha yenu ambapo thamani ya
mabadilishano.Ongezeko la thamani katika mabadilishano yanatokea kote kunakotuzunguka.
Kama tukienda kuokota kuni kwa mfano, tunafanya mabadilishano na muda ili kuokota kuni.
Hapa muda ndiyo kitu ambacho tunachofanya mabadilishano kwa kuni ambayo ndiyo ya
thamnai kwetu.
Ngoja tuchukue mfano mwingine.sema katika hali hii tunaenda kwenye stoo na kununua sabuni.
Katika mabadilishano ya ongezeko la thamani tunabadilishana na pesa ambayo ina thamani kwa
muuza duka, na badala yake kupata sabuni ambayo ina thamani kwetu. Kama tunahitaji kwenda
ndani zaidi, tunaweza kujiuliza kwanini sabuni ina thamani kwetu.
Uliza kama kila mmoja ataweza kujibu swali hili, anza majadiliano katika mada iliopo.
14
kama hakuna maoni: tunathamini sabuni kwa sababu inatufanya kuwa wasafi na kutuzuia kuwa
wagonjwa. Tunatumia thamani ya pesa kusimamia thamini ya bidhaa ambayo itafanyakazi ya
kutuletea faida ya afya. Mfano mwingine wa mabadilishano ya thamani inaweza kuwa ni
uchaguzi wa mteja kwa masoko mawili, moja linaweza kuwa ni soko lililoko mbali na inauza
kwa bei ndogo na nyingine lipo karibu linauza vitu kwa bei ya juu. Mtu anapaswa kulinganisha
kati ya muda, nguvu na pesa zitakazotumika kukamilisha shughuli na achague ni njia ipi inaweza
kuwa nzuri kwao.
Kwa sasa naenda kuwaonyesha picha mbili za watu wanaofanyakazi ya mabadilishano ya
thamani na nahitaji wewe unieleze kuwa ni ni ipi thamani na zipi ambazo ni mabadilishano.
Onyesha picha za mwanamke anyefanya maamuzi kati ya stovu nyingi.
Mjadala.
Moja linuzwa kwa bei ya juu lakini haisababishi kukohoa na adha zingine na nyepesi kutumia.
Moja ni rahisi lakini inaumiza mapafu
Onyesha picha za mtu akifikiri
Mjadala.
Kwa ipande mmoja anaona muda atakayotumia kujifunza na hatua atakazochukua.
Kwa upande mwingine anjiona mwenyewe kama anapanda kiwango katika kufikia hatima.
Onyesha picha ya mtu anavyofikiri kuhusu umbali na vitu hapo kwenye duka.
Mjadala.
Kwa mbali, atapata vitu anavyotaka kwa gharama nafuu kwa gharama yake ya muda.
Je, atanunua ndogo au kubwa, ndogo itagharimu bei kidogo,lakini inaweza isiwe nzuri na kufaa.
Lile kubwa litakuwa na changamoto ya kuisafirisha nk.
Jitahidi kuelezea kila mabadilishano ya thamani ya kila mmoja wakati ukifundisha, lakini weka
mkazo zaidi katika kuwafanya waweze kufikiri zaidi na kuja na majibu wao wenyewe.
Zoezi la mnyororo wa thamani.
Sasa tunaenda kuvumbua seti nyingine ya mabadilishano, ambayo ina wajibu mkubwa katika
biashara.zoezi hili linalenga kwenye mnyororo wa thamani na kuelewa thamani iliongezwa
katika kila hatua za kutengeneza bidhaa na kwanini.katika mfano wa mwanzo naenda kuwaeleza
kwenda katika hatua zote za ujasiriamali katika kutengeneza wa jewe la thamani. Tumeweka
misingi ya mnyororo wa thamani kwa ajili yako katika picha ili kukuwezesha kuona kwa usahihi
njia mbalimbali ambao ni nzuri kidogo.
15
Onyesha picha ya jiwe la thamani na mnyororo wa thamani, elezea kila hatua katika picha.
Anza na mpangilio wa mchoro wa jiwe la thamani
Halafu nenda kwenye uzalishaji unaofanywa na watu wa kawaida
Uza jiwe la thamani kwa mtu binafsi
Halafu rudisha katika mazingira yake.
Watauza au kuwapa madini hayo kwa watu wengine
.Mahitaji ya wateja itaendesha mzunguko kuanza tena.
Majadilianno yawe katika makundi kwanza na wawezeshe kuweza kuieleza ongezeko la thamani
katika kila hatua kadri iwezekanavyo. Kilakikundi kiwe na mwakilishi na afike mbele na
kuiwakilisha.
Baada ya sasa kupitia huu mnyororo wa thamani, tumeelewa kwanini mtu anapaswa kushiriki
katika sehemu za kila biashara kwa kuchukua sehemu ya kila hatua kwa kuongeza thamani
katika bidhaa zetukila iwezekanavyo,lakini kama mabadilishano katika thamani itafanyakazi
kwa manufaa yetu kwa muda mrefu. Hebu tuangalie mfano mwingine wa mnyororo wa thamani
wakati huu tutaangalia ni wakati gapi thamani inaongezwa katika uzalishaji wa ndizi.
Onyesha na jadili picha ya ndizi.
Mgomba unachukua fursa ya uwekezaji wa
Muda
Rasilimali
Nguvu
Ardhi
Mmea hukua na kuuzwa kwa wasafirishaji.
Wasafirishaji wanapata bidhaa
Wakulima wanpata pesa
Urahisi wa kuweka mahesabu (usiwe na chombo cha usafiri binafsi au tafuta
masoko mengine)
Mkulima anaweza kupata faida kubwa ya pesa kama wangesafirisha vitu/bidhaa
hivyo wao wenyewe?
Wasafirishaji wataleta kwa muuza duka.
Watapunguza muda wa muuza duka na rasilimali katika kustawisha mimea yako
mwenyewe.
Awapatia pesa wasafirishaji
Utapata ndizinzuri za kuuza
Muuza duka atauza bidhaa
Atapata faida kwa mauzo
Mauzo yanaweza kuongeza bei ya kununulia na kuleta kwa wateja
Muuzaji atapata pesa
Wateja watapata kwa urahisi chakula, hawahitaji kuzalisha chakula chao au
kusafiri kwenda shamba.
Wateja watapata chakula kwa mabadilishano kwa pesa.
Thamani ya kuonja
Thamani ya ubora wa bidhaa
16
Kwa sasa tumeenda kuonyesha hatua mbili za mnyororo wa thamani tunaweza kuwa katika
uwelewa mzuri wa mabadilishano ya thamani na mchakato mwingine unaongeza thamani ya
bidhaa zetu, huduma nk. Wakati tunapangilia uzalishaji wa bidhaa tulitazama maamuzi Fulani,
kila kitu katika bidhaa lazima inalenga katika kuongeza thamini au sio ya muhimu kuongeza
katika bidhaa yetu. Hebu tuchambue picha hii inayoonyesha hatua mbalimbali katika
utengenezaji wa mkate kama bidhaa. Nahitaji uongee na vikundi vyako kwamba ni kwanini kila
bidhaa katika picha hapa chini zimeongezwa na ni thamani gani inaongeza katika mkate.
Majadiliano haalafu mawasilisho.
Mayai na ngano inakupa nguvu
Sukari, chumvi, na maziwa inaongeza ladha
Hamira na ikichangwa na hivyo hapo juu inaipa bidhaa muundo na ulani wake.
Nawashukuru kila mmoja. Hebu tutafakari umuhimu wa thamani na mabadilishano katika vitu
tunavyovifanya . Tumeona kila siku ya maisha yetu na mabadilishano haya ni ya lazima na ni ya
wajibu mkubwa katika kutubadilisha maisha yetu ya baadaye. Kwa kuzingatia faida na
mabaddilishano katika thamani ya bidhaa tumeweza kuwa wateja wazuri, wajasiriamali, na watu.
Zaidi.
Kazi za nyumbani.
Kwa kazi za nyumbani kwa wiki hii. Nahitaji kila mmoja wenu kufikiri zaidi kuhusu mnyororo
wa thamani.nahitaji kila mtu afikiri kuhusu biashara laakini siyo ya kutengeneza mkate.ni namna
gani watu wanapata bidhaa, usambazaji,usafiri wake nk. Tafadhali njoo na mnyororo wa thamani
katika bidhaa hiyo na ni namna gani thamani ilivyoongezwa katika matunda kama ilivyoelezwa
mapema katika vipindi. Je, kuna mtu mwenye swali/ maswali kuhusu kazi za nyumbai.
17
Picha kwa ajili ya kipindi cha tatu (3)
Mifano ya mbadilishano wa thamani
18
19
20
21
Sehemu ya 4
Habari za leo kila mtu. Ninafurahi kwa kuwa kila mtu ameweza kufika katika kipindi chetu hiki
cha nne, lakini nahitaji kuanza kipindi hiki kwa kupita kazi niliyowapa ya nyumbani wiki
iliyopita. Kama mtakumbuka vema, niliwauliza mfikiri /kufikiri juu ya biashara ambayo siyo ya
kutengeneza shanga. Nilipotoka niliwataka mnieleze watu wanapataje bidhaa, usambazaji,
usafirishaji wake n.k.? nikataka tena mje na mnyororo wa thamani kwa bidhaaa hiyo au huduma
na mnieleze ni namna gani thamani ya kitu inaongezwa kwa kial hatua kama ilivyo katika hatua
ya kuongeza mnyororo wa thamani wa tunda uliofanyakatika kipindi cha awali. Kwa mfano
naweza kuja na wazo labiashara ya simu ya samasa katika biashara hii nauza samosa na kikapu
ili kuweza kuleta bidhaa yangu kwa wateeja.In this business hii inaongeza thamani kwa samosa
ya awali kwa kurahisisha upatikanaji wake kwa wateja.Nitawapa dakika kumi kujadili katika
vikundi vyenu ili kuona mlichofikiri kaatika kiipindi kilichopita na nitawahitaji watu watatu wa
kujitolea waje watueleze ni walichofikiria. Kama hakuna wakaojittolea nitawauliza watu watatu
kwa kuwachagua sehemu mbalimbali..
Ruhusu dakika kumi za mjadala na fafanua kama tena itahijika..
Twatu watatu au zaidi wa kuwakilisha: gawanya ongezeko la thamani na poteza katika hatua
mbalimbali za mnyororo wa thamani kama itahitajika waulize maswali mara nyingi ya kwanini
na jaribu watoe ufafanuzi kila inapowezekana.
Sasa tusonge mbele katika somo letu la leo. Kwa leo tutaenda kupanua uelewa wetu kuhusu
biashara ni nini. Hii itatuwezesha kuwa na uwanja mpana wa kufahamu na kuelewa biashara
zinazotufaa na kuangalia biashara na uwekaji binafsi wa kumbukumbu za hesabu kwa uwanja
mpana. Tutazungumzia pia kuhusu mahitaji ya mteja na kuona namna mahitaji ya mteja
inavyobadilisha mtizamo wa dunia inayotuzunguka na kuleta mabadiliko. Hadi mwisho wa wa
majadiliano haya ya leoo, natumaini mtakuwa na misingi wa namna ya kufikiri namna mahitaji
yanavyobadilisha maisha yako na namna ambavyo tutatumia mahitaji mbalimbali ya wateja
kubadili biashara yako.kufahamu mahitaji mbalimbali ya wateja itasaidia kukubadilisha tabia
yako ya kusimamia vema manunuzi yako na thamnai ya mabadilishano katika maisha yako. .
Wakati tukijadili katika kipindi cha kwanza, kuwa na mteja ni jambo la msingi na la muhimu
sana wakati kuanza biashara. Ili kuwapata wateja hawa, tunahitajika na muda wa kufanya utafiti
na kujifunza juu ya wateja na upatikanai wa soko.
Kwa kufahamu mahitaji ya mteja, tutaenda kuandaa vitu ambavyo biashara yetu itaviuza au
biashara ipi ya kufanya. Kama tutakuwa tutakuwa na biashara zetu tayari , na kufahamu mahitaji
ya wateja kama walengwa wetu na wapi wateja hawa wataturuhusu kufanya marekesbisho ya
wapi pazuri pa kuweka masoko ili kukidhi mahitaji yetu
Lakini biashara zetu zitafanya nini? Ili kupanua ufafanuzi wetu ya kuwa biashara ni nini
inatupasa tutofautishe aina mbalimbali za biashara. Ni muhimu kutofautisha baina ya bidhaa
katika huduma. Bidhaa ni kitu kinachoshikika wakati huduma ni kitu ambacho hakishikiki lakini
22
inatoa huduma na inatosheleza mahitaji ya mteja. Kwa mfano, nyanya ni mfano wa bidhaa na
itakupeleka mahali ambapo utaona kama inakupa huduma. Kwa sasa nawaonyesha seti za picha
ambazo mtazijadili katika vikundi na kuona kama picha zipi zitakuwa zinaonyesha bidhaa na
zipi zinaonyesha huduma na mnieleze kwa nini. Weka akili mwako kuwa vitu vinaweza kuwa ni
huduma na pia bidhaa.
Jadili picha, hakikisha unajiuliza maswali ya kwanini mara kwa mara.
23
24
Nampongeza kila mtu kwa ushiriki, kwa kurudia jambo ambalo tulikwisha lijifunza, kuwa kuna
aina mbalimbali za biashara na shughuli zenye tija. Tunaweza kuweka katika makundi biashara
hizo, huduma, au kuchanganya pamoja kuwa ni bidhaa na huduma. Kutoka hapa tuanweza
kupanua mawazo yetu ni namna gani biashara yetu biashara yetu itakuwaje.
Tukiangalia kwa undani kuhusu bidhaa hizi na huduma zinatukumbusha tena kuwa zinakuja
kutoka kwa wateja na mahitaji yao. Tukizungumza kuhusu mahitaji ya mteja ni vema tukazigawa
mahitaji haya katika makundi kwasababu hii, tuzigawe mahitaji haya katika makundi ya asilia au
kuzaliwa nacho na mahitaji ya kimwili. Vitu ambavyo vinakidhi mahit mahitaji au mahitaji asilia
ni vitu ambavyo tunahitaji ili tuishi. Chakula na maji kwa mfano vinatupa mfano wa vitu vya
kukidhi mahitaji ya asilia. Mahitaji ya kimwili inajumuisha vitu tunavyovitaji kuimarisha akili
zetu. Kusikiliza muziki kwa mfano inatosheleza mahitaji ya kimwili na roho zetu ili
kuburudisha.
Kwa kuanza mjadala katika hili nawataka kwenda katika vikundi vyenu na kushiriki katika
zoezi.
Sambaza mawazo haya katika vikundi.
Kikundi cha kwanza kijadili mahitaji unayohitaji kutosheleza wakati wa kununua viatu.
25
Kundi linalofuata litajadili mahitaji unayotegemea katika dawa ya mswaki
Kundi linalofuata, litazungumzia mahitaji yanayotimizwa katika mwili kwa kutengeneza chakula
na kukila.
26
Nitarudia swali langu.Tafadhali jadili mahitaji inayohusiana na ununuzi wa viatu. Kikundi
kingine kijadili mahitaji yanyopatikana katika dawa ya meno.kikundi kingine kijadili mahitaji
assilia na mahitaji ya mwili na roho inayotoshelezwa kwa kwa kula katika mgahawa.
Rudia kile ambacho watu wamekisema na tafakari juu ya majibu yaliyotolewa ambazo ni mazuri.
Kama tulivyosikia katika majdiliano, kuwa kuna nambari za fursa kwa ajili ya biashara na
huduma ambayo inafanyakazi ya kutosheleza mahitaji ya mteja katika njia mbalimbali yawe ya
mahitaji ya kimwili na kiroho au za kiasili. Kwa mfano mgahawa ni mfano wa huduma kwa
kuwa mtu mmoja ataweza kupikia na kutoa huduma ya chakula, lakini inaweza pia kutupa
bidhaa kwa chakula tunachopewa. Chakula kinatulisha na kutoshelza mahitaji yetu ya kimwili
wakati ladha nzuri ya chakula inatosheleza mahitaji yetu kisaikolojia.
Pumzika hapa uone kama kuna mtu mwenye maswali au anayehitaji ufafanuzi.
Kama katika vitu vingi vilivyo, mahitaji ya mteja inayobadilika kila wakati na hivyo hivyo kwa
biashara kwa ajili ya kufikia mahitaji hayo. Kwa ajili ya kufikia hali ya mabadiliko ya mahitaji
ya wateja, biashara inaweza kubakia yenye faida na inayojiendeleza yenyewe kila wakati. Kwa
mfano, kuhitajika kwa ufanisi na mawasiliano ya haraka kulingana na umbali imepelekea
kugundulika kwa simu ambazo kulingana na muda itafanya kuwepo kwa hatua za miundo
mbalimbali ili kufikia mahitaji ya mteja kwa ufanisi zaidi katika uzalishaji wa bidhaa. Kwa
wakati huu tunazo simu zilizoboreshwa kwa aina tofauti tofauti kwa kuzifanya kuwa ndogo,
inayochukulika, na inayofanya shughuli nyingi.
*kujadiliana katika vikundi na kuziwasilisha, na kuendelea kuhamasisha*.
Kazi za nyumbani:
Jaribu nenda kila kipndi ambazo kulizimaliza wiki iliyopita na jikumbushe umejifunza nini.
Wote ninyi mtaulizwa wiki ijayo kitu ulichojifunza na kila mmoja atakiwa kusema kitu fulani
ambacho ni tofauti na kile kilichosemwa na mwenzake na kuendela hadi kumalizika kwa
kukisema kitu halisi ulichokijifunza.
27
Sehemu ya 5
Napenda kuwashukuru wote mliohudhuria kwenye kipindi hiki cha mwisho cha mafunzo ya
biashara na masoko. Kipindi cha leo kitalenga zaidi kurejea tulichojifunza na baadae
kuzungumzia mazoea endelevu. Tutaanza na mazoezi ya kufanyia nyumbani ya wiki iliyopita.
Wiki iliyopita niliwaambia mpitie mambo yote mliojifunza kwenye hivi vipindi, na niliwaambia
kuwa kila mmoja atapaswa kueleza alichojifunza. Kwa hiyo nitakupa dakika ya kufikiria hili
tena na nitaanza kuzunguka nikimuuliza kila mmoja alieleze jambo.
Zunguka ukimuuliza kila mmoja akueleze jambo. Jadili na kufafanua mada inapowezekana. Hii
sehemu itachukua muda.
Mmefanya kazi nzuri, inaonekana kuwa kila mmoja wetu amejifunza sana kwenye vipindi hivi.
Sasa naomba mnivumilie na kuniruhusu nirudie baadhi ya mambo tuliojifunza wiki zilizopita.
Kwenye kipindi cha kwanza tumejifunza kuhusu vipengele tofauti vya biasharana zoezi ambalo
tulifanya kupanga vipengele muhimu katika kuanzisha biashara. Kwenye majadiliano haya
tulikubaliana kuwa kipengele cha muhimu sana kwenye biashara ni mteja. Hivyo basi tulitambua
umuhimu wa kutafuta mteja wako na tulifafanua baadae na kujadiliana namna ya kutafiti
mahitaji ya mteja inavyoweza kusaidia katika kuanzisha biashara.
Tulia kidogo nakuuliza kama kuna mtu ana swali au jambo la kuongeza kuhusiana na siku ya
kwanza au kujadiliana zaidi kuhusu walichojifunza.
Baada ya hapo tutaenda kwenye kipindi cha mwisho ambapo tulilenga kwenye ujuzi tulionao
kwa kuwa wateja wazuri. Tulipanga duka na mkanunua kutoka kwangu. Niliwadanganya baadhi
yenu na kwa ujumla nilikuwa muuza duka mbaya. Kwa hiyo hili lilikufundisha kuwa makini
tunapoenda dukani/sokoni na kuwa makini na kuangalia kila kitu. Kwenye majadiliano tulitaja
mambo kadhaa kama vile
Wateja wanapaswa kupanga manunuzi yao kwa uangalifu
Wateja wanapaswa kutafuta na kujifunza kuhusu bidhaa, bei na maduka?
Wateja wanapaswa kuulizia risiti ya malipo na kadi ya uthibitisho.
Wateja wanapaswa kuangalia bidhaa na tarehe ya mwisho wa matumizi kabla ya kupokea,
Wateja wanapaswa kutumia haki yao kudai punguzo au katika mazungumzo na mwenye
duka
Wateja wasiendekeze mazoea yasiofaa
Wateja wawe tayari na kukubali kulipa gharama ya bidhaa na huduma kutoka kwa muuzaji
au mtoa huduma.
Kuna mtu yeyote mwenye jambo lingine ambalo tumejifunza analotaka kuongezea. Waombe
watu wawili waongezee kama kuna mtu atapenda kujitolea.
28
Mwisho wa kipindi chetu cha pili, tutajiimarisha katika sehemu yetu kama wateja na
kujiunganisha kuwa wateja wazuri kama sehemu ya kuwa wafanyabiashara wenye mafanikio.
Kwa kuwa wateja wenye uelewa, kwa upande mwingine tunajifunza zaidi na kuelewa maswala
ya biashara na masoko.
Uendelevu
Swali hili la uendelevu ni la nini?
Lenga uendelevu kwenye….
Biashara
Kuheshimu wateja
Kujenga mahusiano
Kutengeneza mikataba
Jiboreshe na tafuta maoni
Dunia
Heshimu mali
Epuka mafuta yalioganda ukiweza
Panda mbogamboga
Ufugaji usio endelevu kwenye eneo moja
Kilimo cha kuhama hama
Madhara yanayosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi
Kama tupo makini, tutaboresha mambo. Kama tutachukua hatua kwenda mbele pamoja,
tutafanya jambo. Dunia ina changamoto lakini tunaweza kupata yalio mazuri.
top related