uhifadhi wa kazi za fasihi simulizi · sifa bainifu za fasihi simulizi •huwasilishwa kwa njia ya...

Post on 11-Sep-2020

226 Views

Category:

Documents

7 Downloads

Preview:

Click to see full reader

TRANSCRIPT

UHIFADHI WA KAZI ZA FASIHI

SIMULIZI(KIDATO CHA PILI)

Mussa Shekinyashi+255 743 98 98

MALENGO YA SOMO

• Kufikia mwisho wa somo:

• Tujikumbushe maana ya Fasihi Simulizi

• Tufahamu sifa bainifu za Fasihi Simulizi

• Tufahamu Njia za uhifadhi wa Fasihi Simulizi

tukizingatia: Ubora na athari (udhaifu) zake kwa

fasihi simulizi.

MAANA YA FASIHI SIMULIZI

• Fasihi simulizi ni aina ya fasihi inayowasilishwa

kwa njia ya mazungumzo ya mdomo.

• Aina hii ya fasihi imekuwepo tangu enzi na

enzi.

• Imekuwa ikirithishwa kutoka kizazi kimoja

hadi kingine kwa njia ya mazungumzo ya

mdomo.

• Mfano wa fasihi simulizi ni hadithi

tunazosimuliwa na wazazi wetu, nyimbo

tunazoimba, maigizo yanayoigizwa.

SIFA BAINIFU ZA FASIHISIMULIZI

• Huwasilishwa kwa njia ya mzungumzo ya mdomo.

• Huifadhiwa kichwani

• Humpa uhuru msanii wa kufanya mabadiliko kwa

kuzingatia mazingira na uhitaji.

• Huwa ni mali ya jamii nzima.

• Huwa na wakati maalum na pahala maalum pa

kuiwasilisha.

• Huwa inaruhusu fanani na hadhira kukutana ana

kwa ana.

• Huruhusu viungo vingine vya mwili kutumika

katika uwasilishaji.

• Huwa inaruhusu hadhira kushiriki katika

UHIFADHI

• Fasihi inaweza kukusanywa na kuhifadhiwa

kwa njia zifuatazo :

• Kichwa

• Maandishi

• Kanda za kunasia sauti

• Kanda za video, televisheni na filamu za

sinema (CD,DVD na kompyuta)

KICHWA

• Kwa asili uhifadhi wa fasihisimulizi hufanywa kwa vichwavya watu kutoka kizazi hadikizazi.

• Njia hii imetumika kwa kipindikirefu sana.

• Kutokana na njia hii fasihiimeweza kuwepo kutokavizazi vya kale hadi hiki cha sasa.

UHIFADHI WA KICHWA

UDHAIFU/ ATHARI ZA UHIFADHIWA KICHWA

• Kupungua kwa kumbukumbu za mhifadhi/fanani

• Kufa kwa fanani

• Fanani anaweza kubadilisha mambo muhimu katikasimulizi na hivyo kubadili kiini cha masimulizi hayo.

• Ukosekananji wa wahifadhi wa fasihi kwa kichwa. Ni vigumu kupata watu wanaopenda na wanaoweza kuhifadhifasihi simulizi

MAANDISHI

• Njia hii imeimeza fasihi simulizi kwa manufaa ya

baadae.

• Ugunduzi wa alama za uandishi ndio uliopelekea

fasihi simulizi kuhifadhiwa katika maandishi.

• Leo hii ni vigumu kuifahamu kazi ya fasihi simulizi

iliyowekwa kwenye maandishi.

• Njia pekee ya kuipambanua ni kuangalia tabia za

fasihi simulizi ambazo ni: “paukwa…pakawa”au

“hadithi….hadithi njoo”

MAANDISHI

UDHAIFU/ATHARI YA UHIFADHIWA MAANDISHI

• Uhifadhi kwa maandishi huwa na matatizo yafuatayo:

• Kukosekana kwa utendaji,sauti,kuimba vitabia.

• Kukosekana kwa uhusiano wa moja kwa moja kati ya

hadhira na fanani

• Kukosekana kwa mabadiliko ya mara kwa mara.

• Ufinyu wa hadhira, itakuwa na watu wachache tu, wale

wanaojua kusoma na kuandika.

• Inakuwa ni nyenzo ya kibiashara ambapo inahitaji

kugharamiwa.

KANDA ZA KUNASIA SAUTI

• Njia hii pia hutumika kuhifadhi fasihi simulizi.

• Hii ni teknolojia iliyochipukia baada ya maandishi.

• Ilikuwa na uwezo zaidi wa kuhifadhi uhalisia wafasihi simulizi ukilinganisha na njia ya uhifadhi kwamaandishi.

• Katika njia hii kanda hutumika, kanda hizo hushikasauti pamoja na vichombezo vyake.

KANDA ZA KUNASIA SAUTI NAREDIO

UDHAIFU/ATHARI ZA KANDA ZAKUNASIA SAUTI

• Sauti husikika, lakini…

• Ni vigumu kuona matendo ya fanani .

• Hadhira haishirikishwi

• Ni gharama kuipata

• Uhifadhi unahitajika uwe wa hali ya juu

• Kudumaa kwa kazi ilihifadhiwa, haitapata

mabadiliko kamwe.

KANDA ZAVIDEO,TELEVISHENI,FILAMU ZASINEMA, KOMPYUTA, MTANDAO, SIMU ZA MIKONONI, CD NA DVD• Uhifadhi wa namna hii hujumuisha sura na sauti

zinazoonekana kwenye skirini ya video.

• Vifaa maalumu hutumika kutengeneza picha za

namna hiyo.

• Fasihi simulizi imeweza kuhifadhiwa katika vifaa

hivi.

• Hapa uhalisia wa fasihi simulizi hujitokeza zaidi

ukilinganisha na njia zile za mwanzo.

• Hapa matendo na sauti vinaonekana wazi.

CD/DVDHutumika kuhifadhi fasihi simulizi

KANDA ZA VIDEOHizi hutumika pia kurekodi matukio

ya fasihi simulizi.

MTANDAOKwa njia hii fasihi simulizi

huifadhiwa kisha kusambazwa

katika jamii zote duniani .

KOMPYUTAKifaa hiki hutumika kuhifadhi na

kuonesha kazi za fasihi simulizi.

SIMU YA MKONONIHii ni njia rahisi ya kurekodi na

kusambaza kazi za fasihi simulizi

kupitia mitandao ya kijamii kama

facebook, whatsApp na mingineyo

UDHAIFU/ ATHARI YA NJIA HIIYA UHIFADHI

• Upungufu wa ushirikishwaji wa hadhira

• Njia hii ni ya gharama sana

• Haitabadilika kulingana na mahitaji ya hadhira

• Uhifadhi wa vifaa hivi ni wa gharama sana.

UMUHIMU WA KUHIFADHI KAZIZA FASIHI SIMULIZI

• Hukuza na kuendeleza utamaduni wa jamii.

• Zinasaidia katika kuvutia watalii

• Ni sehemu ya ajira.

• Kazi ya fasihi inapohifadhiwa huwa ni chachu

ya umoja wa kitaifa.

ASANTENI SANA!

top related