chuo cha serikali za mitaamuki.lgti.ac.tz/documents/lgti_mwezeshaji_mwongozo_swahili.pdf · za...

39
CHUO CHA SERIKALI ZA MITAA MWONGOZO WA MWEZESHAJI Mwongozo huu wa Mwezeshaji umetayarishwa kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (ORTAMISEMI), Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), uliopo Dar es Salaam, Tanzania © Chuo cha Serikali za Mitaa, 2018 Toleo la kwanza ,(Elimu masafa), 2018 Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili au kukitoa kitabu hiki kwa njia yoyote ile bila idhini ya maandishi ya Chuo cha Serikali za Mitaa.

Upload: others

Post on 26-Jan-2021

32 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

  • CHUO CHA SERIKALI ZA MITAA

    MWONGOZO WA MWEZESHAJI

    Mwongozo huu wa Mwezeshaji umetayarishwa kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali

    za Mitaa (ORTAMISEMI), Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Mradi wa

    Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani

    (USAID), uliopo Dar es Salaam, Tanzania

    © Chuo cha Serikali za Mitaa, 2018 Toleo la kwanza ,(Elimu masafa), 2018

    Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili au kukitoa kitabu hiki kwa njia yoyote ile bila

    idhini ya maandishi ya Chuo cha Serikali za Mitaa.

  • Yaliyomo 1.0 Fahamu namna ya kutumia Moodle(MUKI) .................................................................................... 3

    2.0 Sajili kozi mpya ................................................................................................................................ 3

    2.1 Anza .............................................................................................................................................. 4

    3.0 Uhariri wa Vipengee vya Kozi Yako ................................................................................................ 6

    4.0 Maelekezo ya ujumla ya upakiaji wa kozi. ....................................................................................... 6

    5.0 Mahitaji Katika Utengenezaji wa Kozi ............................................................................................. 8

    6.0 Uongezaji wa bloku kwenye kozi yako .......................................................................................... 10

    7.0 Usimamizi wa kozi yako................................................................................................................. 12

    8.0 Kuongeza Rasilimali ....................................................................................................................... 12

    9.0 Kuweka Kazi .................................................................................................................................. 14

    10.0 Kazi ............................................................................................................................................... 15

    10.1 Hatua kwa ajili ya kupangilia kazi ............................................................................................ 15

    10.2 Matini ya Mtandaoni ................................................................................................................. 17

    10.3 Upakiaji wa faili wa juu ............................................................................................................ 17

    10.4 Kupakia faili moja .................................................................................................................... 18

    11.0 Kusahihisha Kazi .......................................................................................................................... 19

    12.0 Zoezi la Papo kwa Papo ................................................................................................................ 20

    12.1 Kutengeneza Maswali ............................................................................................................... 20

    12.2 Mipangilio ya kawaida kwa aina zote za maswali .................................................................... 21

    13.0 Aina ya Maswali ........................................................................................................................... 22

    13.1 Swali la insha ............................................................................................................................ 23

    13.2 Majibu yaliyounganishwa na (Vaana) Maswali ....................................................................... 23

    13.3 Maswali ya kuchagua ................................................................................................................ 24

    13.4 Swali la Nambari ...................................................................................................................... 24

    13.5 Maswali ya Kweli/Si kweli ...................................................................................................... 25

    14.0 Jukwaa .......................................................................................................................................... 25

    15.0 Soga .............................................................................................................................................. 29

    16.0 Faharasa ........................................................................................................................................ 30

    17.0 Kitabu cha alama .......................................................................................................................... 33

    17.1 Kuingiza na kuweka alama ........................................................................................................ 33

    18.0 Tathmini ........................................................................................................................................ 34

    19.0 Hariri wasifu wako........................................................................................................................ 36

    20.0 Kutuma ujumbe wa faragha ......................................................................................................... 38

  • 3

    1.0 Fahamu namna ya kutumia Moodle(MUKI)

    Nenda kwenye wavuti ya Moodle (elms.lgti.ac.tz). Hii itakupeleka kwenye ukurasa wa kuingia ndani ya mfumo:

    Ingiza "jina la mtumiaji" na “Nywila,” bofya kwenye kitufe “Ingia.” Itakupeleka kwenye ukurasa wa mwanzo wa mfumo.

    2.0 Sajili kozi mpya

    Jukumu la mwalimu linaweza kuhariri au kuongeza maudhui kwenye kozi ambayo

    imeshasajiliwa. Kama unahitaji kua na kozi mpya ni lazima umuombe msimamizi

    wa mifumo asajili kozi mpya kwa ajili yako ama vinginevyo akupe haki ya msajili

    kozi.

    Ukishaingia ndani ya mfumo unaweza kufungua kozi yako kwa kubofya “Kozi za

    Madiwani” kwenye kategoria ya kozi kisha bofya kwenye kozi yako.

  • 4

    2.1 Anza

    Ukurasa wa mwanzo wa kozi unafanana na picha ya kiwamba ifuatayo. Upande wa

    kulia chini kuna bloku ambazo zinaweza kuongezwa ama kuondolewa, na kushoto ni

    "eneo la kufanyia kazi".

  • 5

    Unaweza kuanza kufanya kazi kwa kuruhusu uhariri, kwenye kitufe kilichopo juu kulia

    kwenye menyu ibukizi chagua “Ruhusu uhariri”:

    Ukurasa wa mwanzo wa kozi baada ya kuruhusu uhariri;

  • 6

    3.0 Uhariri wa Vipengee vya Kozi Yako

    Wakati uhariri umewezeshwa, Kila kipengee kwenye ukurasa wa mwanzo wa kozi yako na

    kila sehemu/bloku kutakua na ikoni pembeni yake ambazo zote ninafanya kazi mbalimbali

    kama vile kuhariri /hamisha / durufu/ futa/ ficha.

    Alama Kazi

    Ikoni ya uhariri inakuwezesha kubadili maneno au mipangilio wa kipengee

    Ikoni ya onyesha/ficha inawezesha kipengee kionkane au kisionekane kwa wanafunzi

    Ikoni za mishale ya kushoto na kulia inatumika kujongeza vipengee vya kozi

    Ikoni za mishale ya Juu na Chini zinatumika kuhamisha vipengee na bloku kwenda juu ama chini.

    Ikoni ya kuhamisha inawezesha kuhamisha kipengee kwenda kwenye mada au bloku nyingine.

    Ikoni ya"crosshairs" inakuwezesha kuhamisha vipengee au sehemu kwa kukokota na kuachia.

    au

    Ikoni ya kufuta inaondoa kabisa vipengee ama bloku kwenye kozi yako Delete.

    Groups icon allows you to change between no groups or separate/visible groups

    Roles icon allows you to assign roles locally in the item.

    Ikoni ya msisitizo inakuwezesha kusisitiza sehemu kama eneo lililopo kwa wakati huu.

    4.0 Maelekezo ya ujumla ya upakiaji wa kozi.

    Utakapo bofya kwenye ikoni hapo juu ukurasa ufuatao utaonekana;

    Bofya hapa kuongeza taarifa za jumla

    za kozi. Jina la kozi, Maelezo na

    Madhumuni.

  • 7

    Weka Muhtasari wa kozi hapa

    Kama tayari,Bofya

    hapa kuhifadhi

    mabadiliko

    Andika jina la kipengele

  • 8

    5.0 Mahitaji Katika Utengenezaji wa Kozi

    Ona Mfano Hapo chini

  • 9

    Msimbo na Jina la Kozi

    Maelezo na

    Malengo ya

    Kozi

    Maelezo ya

    Kozi

    4. Mada ya Mafunzo na

    Maudhui Yake (Vidokezo,

    PPT, Video, Maswali,

    Marejeleo na Shughuli)

  • 10

    6.0 Uongezaji wa bloku kwenye kozi yako

    Bloku zinatokeza upande wa kushoto chini wa eneo la kufanyia kazi ambamo unaongeza

    kazi na vitendea kazi vyako.

    Kuna bloku nyingi za kawaida ambazo zinakuwezesha, kwa mfano, kuonyesha kalenda,

    shirikisha matokeo ya zoezi, onyesha RSS feeds, ongeza maudhui binafsi, o n y e s h a

    m t u m i a j i a l i e k o h e w a n i , o n y e s h a m a o n i k w e n y e k o z i y a k o nk. M w a l i m u

    a n a w e z a k u o n g e z a b l o k u m p y a w a k a t i u h a r i r i u k i w a u m e w e z e s h w a k w a

    Mada iliyogawanywa katika sehemu sita

    Faharasa

    Marejeo

    Tathmini

    http://docs.moodle.org/22/en/Remote_RSS_feeds_block

  • 11

    k u b o f y a "Ongeza Bloku" kwenye menyu chini kushoto mwa ukurasa:

    Hiyo ni mifano ya bloku, pia

    unaweza kuongeza bloku

    kutegemeana na Matukio

    unayohitaji kuyaonesha kwa

    mwanafunzi.

  • 12

    7.0 Usimamizi wa kozi yako

    Sehemu ya usimamizi wa kozi ya mipangilio ya bloku inamuwezesha mwalimu kusimamia

    nyanja mbalimbali za kozi zao. Watumiaji –wanaweza kuwaandikisha watuamiaji wapya. Vichujio - inaweza kuwezesha au kuzima vichujio vilivyoruhusiwa vya kozi yako. Alama-inawezesha kuona,kuongeza na kuhariri alama za wanafunzi wako. Cheleza/Rejesha - v iu n g a n i sh i h i v i v in a ku w e z e sh a ku d u r u f u k o z i ya k o a u

    k u re je sh a k oz i ku t ok a mah a l i p op ot e .

    Ingiza ndani - unaweza kuingiza shughuli kwenye kozi yako hapa. Anzisha upya–inawezesha kuondoa taarifa za watumiaji wa zamani mwishoni mwa mwaka

    wa masomo au kipindi ili kuanza upya

    8.0 Kuongeza Rasilimali

    Pamoja na kuongeza zoezi shirikishi kwa wanafunzi wako, unaweza kuwapa rasilimali

    tuli.

    Kuongeza rasilimali, wezesha uhariri, chagua sehemu kwenye ukurasa wako wa kozi

    ambapo ungelipenda ionekane na bofya kwenye menyu kunjufu "Ongeza rasilimali au

    shughuli".

    Kitabu - inamuwezesha mwalimu kuweka rasilimali yenye kurasa nyingi kama kitabu chenye

    sura.

    Faili - Kama unataka kupakia nyaraka za kozi katika mtindo mwingine, unaweza

    kuzihifadhi katika Moodle na ukarahisisha wanafunzi kuzifikia.

    Folda - Kama ukipakia maudhui mengi , ungeweza kuyakusanya kwenye

    makabrasha. Unaweza kuyaonyesha maudhui ya folda lote badala ya fail i

    moja baada j ingine.

    Maudhui ya IMS - Maudhui ya IMS inaruhusu maudhui yaliyowekwa kulingana

    na maudhui ya IMS y a o n e k a n e k w e n y e k o z i . IMS n i c h o m b o

    k i n a c h o s a i d i a k u a i n i s h a k a n u n i z a k i t a a l a m z a v i t u

    m b a l i m b a l i , maudhui ya kimtandao ya kujifunzia.

    Lebo - L e b o i n a w e z e s h a m a t i n i n a t a s w i r a z i c h o m e k w e m i o n g o n i m w a v i u n g a n i s h i v y a s h u g u l i .

    Urasa- Ukurasa unawezesha ukurasa wa tovuti uonekane na kuhaririwa ndani ya kozi.

    URL - Unaweza kutengeneza kiurahisi viunganishi vya tovoti nyingine nje ya kozi ya Moodle.

  • 13

    Orodha ya Rasilimali na kazi

    Chagua Rasilimali au Kazi

    kisha Bofya hapa kuweka

  • 14

    9.0 Kuweka Kazi

    Moodle inatoa idadi kubwa ya shuguli za kujifunzia kwa wanafunzi. Kuweka kazi wezesha

    uhariri, chagua sehemu kwenye ukurasa wa kozi yako ambapo ungependa ionekane kisha

    bofya kwenye menyu kunjufu "Weka kazi"

    K a z i : Kuwaambia wanafunzi watume kazi

    S o g a : Pangilia chumba cha kusogoa kwa wanafunzi

    Chaguo: Pangilia kura kwa wanafunzi

    K a n z i d a t a : Pangilia kanzi data ya wanafunzi ya kuchangia

    J u k w a a : Pangilia majukwa ya wanafunzi washiriki kwenye majadiliano

    F a h a r a s a : Pangilia faharasa ambamo wanafunzi wanaweza kuchangia.

    S o m o : Pangilia somo la kujisahihisha.

    Z o e z i : Pangilia jaribio la kujisahihisha mwenyewe kwa kutumia maswali ambayo

    umetunga kwa kutumia akiba ya maswali ya moodle.

  • 15

    10.0 Kazi

    Kazi inatumika wakati unataka wanafunzi wako watume kazi kupitia Moodle (isipokua kazi za

    nje ya mtandao). Kazi ikishatumwa unaweza kutoa alama na kutoa mrejesho kupitia Moodle.

    Alama zinatunwa kwenye kitabu cha alama cha kozi. Kuna aina nne za kazi. Chaguo lako la

    aina ya kazi inategemea unataka wanafunzi wako wafanye nini.

    M a t i n i y a M t a n d a o n i

    Mwanafunzi anachapa ndani ya kiboksi kwenye Moodle – wanakua na kihariri cha

    Moodle WYSIWYG hivyo wanatumia vitendea kazi vilivyomo; kujiunganisha kwenye

    tovuti, kuonesha picha, nk.

    P a k i a f a i l i m o j a

    Wanafunzi watapaswa kupakia faili. Mwalimu ataamua ukubwa wa mwisho wa faili la

    kupakia wakati akipanga kazi.

    Pakia faili zaidi ya moja

    Mwalimu anaweza kuruhusu upakiaji wa faili zaidi ya moja. Kwa aina hii ya kazi,

    mwanafunzi anaweza kufuta kazi ambayo tayari ilikua imepakiwa na kutuma

    upya.

    Kwahiyo aina hii ya zoezi ni muhimu hasa kama unataka wanafunzi wako watume

    nakala ya rasimu ambayo unaweza kutoa mrejesho kabla hijaboreshwa na

    mwanafunzi kisha atume upya. Mara toleo la mwisho litakapokua limepakiwa,

    wanafunzi wanaweza kubofya ‘tuma kwa ajili ya usahihishaji’.

    10.1 Hatua kwa ajili ya kupangilia kazi

    Kupangilia zoezi kunafanana kwa aina zote za mazoezi isikuwa kuna sehemu maalumu yenye

    mipangilio mahsusi kwa ajili ya aina ya kazi iliyochaguliwa.

    Mipangilio ya Ujumla (Inafanana kwa aina zote za kazi)

    • Wakati uhariri umewezeshwa kwenye kozi yako, nenda kwenye sehemu

    ambapo ungependa kuweka kazi bofya ‘ongeza kazi...’

    • Chagua aina ya kazi.

    • Weka jina la kazi (jina litakua kiunganishi ambacho wanafunzi wako watabofya)

    • Kwen ye k isanduku cha maelezo wap e wanafunz i wako maelekezo wan ayoh ita j i kukamil i sha kaz i .

  • 16

    Bainisha ni namna gani utasahihisha kazi kwa kutumia ‘alama’ kwenye menyu kunjufu.

    • Amua kama unataka kudhibiti ni wakati gani wanafunzi wako wanaweza kuanza

    kutuma kazi kwako. Unaweza pia kupangilia ni lini iwe mwisho wa kutuma kazi au

    ukazima hali tumizi hii kwa pamoja (kwa kutumia vijisanduku vya chaguzi).

    • A m u a k a m a u t a w a r u h u s u w a n a f u n z i w a t u m e k a z i k w a k u c h e l e w a a u i s i t u m i w e

    mipangilio ‘zuia utumaji uliocheleweshwa’ (kama umechagua kutumia tarehe ya mwisho hapo kwanza). The next section of settings is specific to the assignment type you chose.

    Andika Maelezo ya kazi yako hapa

    Unaweza kuweka tarehe ya

    kukamilisha kazi hapa

  • 17

    10.2 Matini ya Mtandaoni

    10.3 Upakiaji wa faili wa juu

    Endelea kufanya Machaguo mbali

    mbali na ukamilishe kazi yako.

  • 18

    Ukubwa unaoruhusiwa wa faili : Chagua ukubwa wa juu wa faili ambao

    wanafunzi wanaweza kupakia kwa kila faili moja.

    R u h u s u u f u t a j i : Mwanafunzi anaweza kufuta faili lilitomwa au la?

    I d a d i y a j u u y a m a f a i l i y a t a k a y o p a k i w a : Amua ni mafaili

    mangapi yatumwe kwaajili ya kazi.

    Ruhusu notsi: Je unataka kuwapa wanafunzi wako mahali pakuandika notsi notes,mf. maelezo ya kuainisha faili.

    F i c h a m a e l e z o k a b l a t a r e h e k u f i k a : Kama utachagua hili,

    maelekezo ya kazi yatafichwa na kubadilishwa na: ‘Samahani, kazi hii haipatikani

    bado. Maelekezo ya kazi yataoneshwa hapa kwenye tarehe ilioonesha chini.

    T a a r i f a z a b a r u a p e p e k w a w a l i m u : K a m a Moodle i n a f a h a m u

    anuani yako ya barua pepe na umechagua ndio utapokea barua pepe kila wakati

    mwanafunzi akituma kazi kwako.

    W e z e s h a u t u m a j i k w a a j i l i y a k u s a h i h i s h a : K a m a u k i c h a g u a n d i o mwan af u n z i a t ab of ya k i t u f e k i l i ch oan d i kw a

    ‘Tuma kwaajili ya kusahihisha’ wakati watakapopakia mafaila yaliyotayari. Kama

    hapana, kazi itaonekana kama imeshatumwa mara tu mwanafunzi anapopakia

    faili

    10.4 Kupakia faili moja

    Ruhusu kutuma upya: Kama ‘Ndio’ wanafunzi wanaweza kutuma upya kazi

    zao. Kama ‘Hapana’ na mwanafunzi ametuma kazi kimakosa hakuna

    namna ya kuanza upya.

    T a a r i f a z a b a r u a p e p e k w a w a a l i m u : Hii inafanana na aina

    zingine za kazi juu. Kama Moodle inafahamu anuani yako ya barua pepe

    na uchague ndio utapokea barua pepe kila wakati ambapo mwanafunzi

    atatuma kazi kwako.

    Ukubwa wa juu wa faili: Inafana na pakia faili zaidi ya moja. Chagua ukubwa

    wa juu wa faili ambao mwanafunzi anaweza kupakia.

  • 19

    11.0 Kusahihisha Kazi

    Wanafunzi wanapowasilisha kazi unaweza kuipata kwa kubonyeza kazi na kufuata

    kiungo chini ya "Muhtasari wa alama" ambayo inasema 'Angalia maoni yote au'

    Hakuna majaribio yamefanywa juu ya kazi hii '. Kiungo hiki kinakuwekea kuwa

    orodha ya wanafunzi waliojiandikisha kwenye kozi.

    Unapoanza kuweka alama kuna machaguo ya aina mbili.Utaratibu ni ule ule kwa

    machaguo mawili.

    Ni juuu yako kuchagua uchaguzi upi wa uwekaji wa alamaKutegemea na unachosahihisha

    unaweza kupendelea mmoja

    Uwekaji wa alama wa msingi:

    1. Bofya ‘alama’ katika safu ya hali ya mwanafunzi wa kwanza, hii inaleta dirisha jipya

    2. T o a a l a m a n a j a z a k a t i k a m r e j e s h o

    3. Bofya ‘hifadhi na onyesha kinachofuata t’ kuona mwanafnzi anayefuata

  • 20

    Utoaji wa haraka wa alama:

    1. Ingiza daraja na maoni moja kwa moja kwenye ukurasa ambapo unaweza kuona

    orodha ya wanafunzi wote.

    2. Kutoa alama kwa haraka hakutakuwezesha kutoa maoni ndani ya maandishi ya

    kazi ya maandishi ya mtandaoni. Hata hivyo, kupiga haraka mara kwa mara

    kunafaa wakati wa kuingiza alama na maoni kwa faili zilizopakiwa au shughuli za

    nje ya mtandao

    3. . Kubadili uwekaji wa alama wa haraka 'Chagua kweye kisanduku' (chini ya kulia)

    na kisha bonyeza 'Hifadhi mabadiliko yote ya haraka'.

    12.0 Zoezi la Papo kwa Papo

    Tumia mazoezi kama unataka kutunga mtihani wa kujitegemea kwa wanafunzi wako,

    ukitumia mchanganyiko wa aina za maswali (maswali ya kuchagua, kweli na uongo,

    majibu mafupi ... nk). Kwa moduli ya mazoezi unahitaji kuunda benki ya maswali kabla

    ya kufanya mazoezi

    12.1 Kutengeneza Maswali

    Katika sehemu yako ya uendeshaji wa kozi bofya kwenye benki ya maswali.

  • 21

    12.2 Mipangilio ya kawaida kwa aina zote za maswali

    1. Katika benki ya mswali bofya kichupo

    2. Amua ni aina gani / folda unayotaka kuuliza maswali

    3. Choose the type of question you wish to make using the ‘create new question’ drop

    down menu , Chagua aina ya swali unalotaka kutumia ‘tengeneza swali jipya ’

    4. . Lipe swali jina linalojieleza

    5. Andika swali kwenye boksi la ‘Swali la maandishi’ . Unachokiandika hapa kitatofautiana na aina ya swali lilichogaliwa (kweli/si kweli, mlinganisho….n.k

    6. ‘Muundo wa msingi wa uwekaji wa alama “ ni alama ya tuzo itakayopewa kwa jibu sahihi .

    7. ‘Adhabu’ Ni alama itakayokatwa kwa sababu swali limejibiwa kimakosa na likajaribu kujibiwa tena

  • 22

    8. Unapotunga swali una nafasi ya kuiweka 'mode adaptive' ifanye kazi au isifanye kazi

    Maana yake mwanafunzi anakua na kitufe kinachomuwezesha kutuma jibu moja moja anapomaliza kufanya swali (badala ya kujibu maswali na kuyatuma mwishoni wa zoezi)

    13.0 Aina ya Maswali

    Kuna aina 10 tofauti za aina ya maswali ambazo zinawea kutumika katika maswali ya moduli.

    Aina Matumizi

    Maswali ya kimahesabu To create lots of versions of a mathematical

    question with different value

    Maelezo Kutoa maelezo ambayo yanaweza

    yakasaidia swali linalofuata ambalo

    mwanafunzi anaweza akalijaribu.

    Insha Kuuliza maswali ambayo yanakua na aya

    kadhaa, Aina hii ya maswali yanakutaka

    usahihishe bila kufuata mtiririko Fulani

    yaani kwakusoma wazo na kuliona kama

    lipo sahihi.

    Mlinganisho Orodha ya sentensi ambayo inaweza

    ikalinganishwa na orodha nyingine ya

    sentensi.

    Majibu yaliyounganishwa (vaana) Kujaza nafasi zilizo wazi katika aya ya maandishi

    Maswali ya kuchagua To answer questions where there is a list of

    answers to choose from,Kujibu maswali ambapo kuna orodha ya majibu

    Majibu mafupi Kutunga swali la kimahesabu ambapo

    wanafunzi watajaza majibu kwenye boksi

    la maandishi

    Nambari Kutunga swali ambalo jibu lake ni neno au misemo

    Majibu yanayolingana Unapokua na majibu mafupi kwenye

    benki ya Moodle na unataka

    kuyabadilisha kwemye maswali

    yanayolingana

  • 23

    Kweli/Si kweli Kuamua kwamba sentensi ni kweli au sio

    kweli

    Maelezo (Hili sio swali) Hii inatumika wakati unapotaka kutoa maelezo ambayo yatakua na umuhimu kwenye

    maswali.

    Hili sio swali –Ni kama alama katika benki ya maswali.

    Haiwezi kufanya kazi vizuri ikiwa umechagua kuzuia maswali bila mpangilio

    1. Chagua ‘Maelezo’ kutoka ‘Tunga swali’ menyu kunjunzi

    2. Yape maelezo jina la maelezo

    3. Katika nakala ya swali jaza maelezo unayotaka kuwapa wanafunzi.

    4. Hifadhi mabadiliko

    13.1 Swali la insha

    Swali la muundo huu linahitaji jibu ambalo sio lenye aya kadhaa. Hili swali huhitaji

    usahihishaji usio na mpangilio zaidi ya kuangalia wazo lililojengwa na mwanafunzi. Alama za

    wanafunzi zitakua 0 hadi utakaposahihisha

    1. Chagua ‘swali la insha kutoka ‘Tunga swali jipya menyu kunjunzi

    2. Yape maelezo jina la maelezo

    3. . Katika nakala ya swali jaza swali lako

    4. Badilisha daraja la msingi kwa idadi ya alama swali linalofaa

    5. kama unataka kutoa malezo bila kujali jibu lilitolewa, w e k a m a j u m u i s h o y a

    p a m o j a k a t i k a s a n d u k u l a k u w e k e a . Kumbuka kwamba hii itaonekana

    utakaposahihisha swali bila mpangilio mahsusi..Chochote utakachoandika

    kitaonekana moja kwa moja wakati swali litakapowasilishwa.

    6. Unaposahihisha swali una sehemu pia ya kuandika maoni yako.

    13.2 Majibu yaliyounganishwa na (Vaana) Maswali

    Aina hii ya maswali inatumika unapotaka wanafunzi wajaze nafasi zilizo wazi katika aya ya

    maandishi.Wanafunzi wanapaswa kuandika kwenye visanduku au kwenye menyu kunjuzi

    1. Chagua ‘Majibu yaliyoungwa (vaana)’ Kutoka ‘Tunga swali jipya’ menyu kunjunzi

    2. Lipe swali maelezo ya jina

    3. Katika sehemu ya aya andika aya yako na huisha kwa kutumia msimbo wa Moodle ili

    kuzalisha aina tofauti za mapungufu Unaweza kupata maelezo ya kumbukumbu juu

    ya hili kwa kubonyeza alama ya swali juu ya ukurasa (upande wa “ Majibu

    mjumuiko’).

  • 24

    13.3 Maswali ya kuchagua

    1. Maswali ya aina hii hutumika unapotaka wanafunzi wajibu maswali panapokua na

    orodha ya majibu ya kuchagua.. Kunaweza kuwa na jibu moja sahihi au

    majibukadhaa sahihi.

    2. Chagua ‘Uchaguzi mwingi’ kutoka ‘Tunga swali jipya’ menyu kunjuzi.

    3. Lipe swali maelezo ya jina.

    4. Katika sehemu ya swali andika swali lako.

    5. Unaweza kuamua kubadilisha daraja la msingi la swali – hasa hasa kama unataka

    kuchagua zaidi ya jibu sahihi moja.

    6. Amua ni majibu sahihi mangapi yatakuwepo katika orodha ya majibu 7. Orodha ya majibu sio mara zote inaonekana katika mpangilio unaofanana. 8. Unaweza kubadilisha njia ambazo uchaguzi huchapishwa kwa kutumia 'Idadi ya chaguzi'katika menyu kunjuzi

    9. Kwa kila moja ya majibu ya kuchagua unahitajika kujaza jibu kwa daraja lililofanana

    na maoni. Inawezekana kuongeza majibu / uchaguzi zaidi kwa kubofya Vipengele 3

    Zaidi vya kuchagua'

    10..Mrejesho kitengo wa jumla ni wa muhimu kwa sababu unaweza kuweka jumbe za

    mrejesho kwa wanafunzi wakati wanpojibu swali walilopewa kwa usahihi ,sio sahihi

    sana au sio sahihi kabisa.

    11. Hifadhi mabadiliko

    13.4 Swali la Nambari

    Aina hii ya swali inatumika kutunga swali la kimahesabu ambapo mwanafunzi huweka jibu

    katika kisanduku. Hili swali linafanana na swali la majibu mafupi isipokua ni la kimahesabu.

    1. Chagua ‘namnari’ kutoka ‘Tunga swali jipya’ menyu kunjuzi.

    2. Lipe swali maelezo ya jina

    3. Katika sehemu ya swali andika swali lako

    4. In the answers section put the correct answer, its corresponding grade (100%),

    accepted error and feedback (optional).Katika sehemu ya majibu weka majibu sahihi

    5. Hifadhi mabadiliko

  • 25

    13.5 Maswali ya Kweli/Si kweli

    Maswali ya aina hii yanatumika unapotaka kujua kama sentensi ni kweli ama sio kweli

    1. Chagua ‘Jibu fupi’ kutoka ‘Tunga swali jpya’ menyu kunjuzi.

    2. Lipe swali maelezo ya jina.

    3. Katika sehemuya maandishi tengeneza sentensi iliyo sahihi au isiyo sahihi

    4. Chagua kama sentensi uliyoandika ni sahihi au siyo sahihi kwa kutumia ‘jibu sahihi’ menyu kunjuzi

    5. Toa mrejesho sambamba wakati wanafunzi wanapochagua Kweli au Sio kweli

    6. Hifadhi mabadiliko

    14.0 Jukwaa

    Unapoongeza jukwaa la majadiliano kwenye kozi ya Moodle.unatengeneza ujumbe wa

    taarifa za mtandaoni kw ajili ya wanafunzi wako kuongea wao kwa wao au kuongea na

    wewe.Jukwaa la majadiliano ni rahisi sana kutengeneza na zipo aina tano tofauti. Jukwaa lipi

    linalochaguliwa inategemea ni kwa namna gani majadiliano yatafanyika.

    Aina tofauti za majadiliano ni :

    Mjadala moja rahisi - Mada moja ya majadiliano ambayo kila mtu anaweza kujibu

    Kila mtu anaandika mjadala mmoja - Kila mwanafunzi anaweza kuchapisha mada

    moja katika majadiliano mapya, ambayo kila mtu anaweza kujibu

    Q na A jukwaa la mjadala - Wanafunzi wanapaswa kwanza kuweka maoni yao kabla ya kuangalia maoni ya wanafunzi wengine

    Mijadala ya kawaida inaonyeshwa kwenye muundo wa blogu wa wazi ambapo

    mtu yeyote anaweza kuanza majadiliano mapya wakati wowote, na ambapo mada

    ya mjadala inaonyeshwa kwenye ukurasa mmoja na kiungio "Jadili mada hii".

    Mjadala wa kawaida kwa matumizi ya jumla - Jukwaa wazi ambapo mtu yeyote anaweza kuanza majadiliano mapya muda wowote

    H a t u a za kutengeneza mjadala wa majadiliano

    1. Kwenye sehemu ya kuhariri kwenye kozi yako nenda kwenye mada / sehemu ambapo ungependa

    Jukwaa la kuonyesha na bonyeza 'Ongeza shughuli ...' kisha 'Mjadala'

    2. Lipe jina jukwaa la majadilano (Hii inakua ni kiungio ambacho wanafunzi wako wata

    bofya kuingia kwenye jukwaa la mjadala )

    3. Chagua aina ya mjadala unayopendelea kutumi kutoka kwenye menyu kunjunzi.

    4. Lipe Jukwaa la mjadala Utanguliz

  • 26

    5. Utakapokua umejaza utangulizi unapaswa kuchagua kutoka kwenye mipangilio ifuatayo.

    Unaweza kuacha mpangilio uliokua umewekwa mwanzoni

  • 27

    Hapo utakuwa tayari umeshaweka mjadala, sasa Fungua kwa kubofya Jukwaa hapo chini

    Andika Jina la jukwaa

    la majadiliano hapa

    Andika maelezo ya Jukwaa hapa

    Hifadhi kumbukumbu

  • 28

    Kwa mara ya kwanza hakutakuwa na Mada iliyowekwa mezani, hivyo unapaswa kuweka mada kwa ajili ya majadiliano.

    Dirisha lifuatalo litafunguka

    Bofya hapa kuweka mada

    Andika kichwa cha habari cha

    mjadala

    Andika ujumbe hapa

    Pia unaweza kuambatanisha

    mafaili ya mjadala hapa

    Baada ya kumaliza, Bofya hapa

    kuingia kwenye mjadala

  • 29

    15.0 Soga

    Moduli ya sogoa inakuwezesha kutengeneza sogoa yamtanadaoni ambapo wanafuzni wako

    watafanya mijadala kwa kutuma na kupokea mazungumzo ya papo kwa papo..Wale

    wanafunzi waliosajiliwa tukwenye kozi yako ndio wataweza kushiriki. Kama mwalimu

    unaweza kushauriana nao nakala za mazungumzo ya zamani, unaweza hata kuanzisha

    chumba cha mazungumzo ili wanafunzi waweze kuona mazungumzo yaliyopita.

    T e n g e n e a z a c h u m b a c h a m a z u n g u m z o : Katika Moodle kozi yako weka kihariri kifanye kazi na nenda katika sehemu unayotaka

    kuongeza chumba cha mazungumzo.

    Chagua ‘Soga’ Kutoka ‘Ongeza shughuli...’ menyu kunjuzi.

  • 30

    Kipe chumba cha mazungumzo jina. Kama kawaida , hii itakua kiunga kwa wanafunzi

    watakayobofya kila mara.

    16.0 Faharasa

    Kwa kutengeneza faharasa katika kozi yako unatoa maana ya maneno yaliyotumiwa katika

    kozi.

    Kawaida faharasa inaruhusu wanafunzi wako kuchangia ufafanuzi wao wenyewe (unaweza

    kuacha hii kama unataka) hivyo walimu wanaweza kuuliza wanafunzi kufafanua maneno

    mapya ambayo yanaweza letwa na wanafunzi. Kwa upande mwingine, ufafanuzi huu unaweza

    kuwa bora na kupelekwa kwenye ghala kuu ambayo wanafunzi hawawezi kuhariri

    Jaza sehemu za wazi kisha bofya

    chini kuweka soga

  • 31

    Machapisho yana uwezo wa 'kuunganisha moja kwa moja '. Hii inamaanisha kuwa ikiwa

    neno, lililopo kwenye faharasa, linawekwa mahali fulani katika kozi, neno hilo litahusishwa

    moja kwa moja na ufafanuzi wake katika faharasa. Hivi ndivyo faharasa inavyoonekana:

    Namna ya kutengeneza faharasa

  • 32

    Andika jina hapa

    Weka Maelezo ya Faharasa

    Bofya Kuchagua Aina

    ya Faharasa

    Bofya Kuhifadhi Bofya Kuhifadhi

    Kama Umemaliza ,Bofya

    hapa Kuhifadhi

  • 33

    17.0 Kitabu cha alama

    Alama kwa kila mwanafunzi kwenye kozi zinaweza kupatikana kwenye'Taarifa ya alama' chini

    Alama’ Chaguo katika Utawala wa Kozi

    17.1 Kuingiza na kuweka alama

    1. Nenda kwenye kozi unayotaka kuongeza alama

    2. Bofya ‘Alama’ na halafu ‘Taarifa ya alama’ katika Utawala wa kozi.

    3. Kulia kwako juu kwenye kona utaona kitufe cha "Washa kiharirio"

    button. Bofya hiki kitufe kuwezesha kuingiza ingozo za alama.

    4. Nenda sehemu ya mazoezi ambayo ungependa kuingiza alama na andika alama za

    wanafunzi katika boksi husika la maandishi

    5. Kwa alama ambazo tayari zimeingizwa moja kwa moja kwa mazoezi yaliyopewa alama

    , bofya kitufe cha kuhariri mbele ya boksi la maandishi

    6. Katika ukurasa unaofuata , angalia screen, check the "overridden" check box and na

    ingiza alama katika alama za mwisho katika sanduku la maandishi

  • 34

    18.0 Tathmini

    Moduli ya shughuli ya tathmini inatoa nyenzo kadhaa za ukusanyaji taarifa ambazo

    zimethibitishwa kuwa zinafaa kupima na kuchochea usomaji kwa njia ya mtandao.

    Mwalimu anaweza kutumia nyenzo hizi kukusanya taarifa kutoka kwa wanafunzi ambazo

    zitawasaidia kujifunza kuhusu kozi yao na kujitahmini ufundishaji wao..

    Kuweka Tathmini fanya yafuatayo,

    Baada ya kubofya weka Tathmini, Dirisha lifuatalo litafunguka.

  • 35

    Weka Jina la Tathmini

    Andika Maelezo ya Tathmini hapa

    Jaza taarifa nyingine za

    Tathmini

    Kama umeshamaliza kujaza ,Bofya

    hapa Kuweka Tathmini

    Weka Tathmini Weka

    Tathmini

  • 36

    19.0 Hariri wasifu wako

    Watumiaji mmoja mmoja wanaweza kuhariri nyasifuzao kwa kubofyakiungo cha Hariri

    wasifu wako inayopatkana katika ukurasa wa katika menyu ya mtumiaji ( juu kulia )

    Bofya jina la mtumiaji;

    Hariri Maelezo Mafupi

    Bofya kuhariri taarifa

    zako

    Hariri taarifa zako

    Badili nywila

  • 37

    Unaweza

    kuhariri

    taarifa zako

    hapa

    Pia Unaweza kuweka Picha yako kwa

    kubofya mshale huu hapa Ukimaliza kuweka taarifa

    zako sawa ,Bofya hapa

    kuhuisha taarifa

  • 38

    20.0 Kutuma ujumbe wa faragha

    Moodle inaruhusu watumiaji kutuma ujumbe wa faraghakwa wanafunzi , walimu , wahadhiri na

    kwa mtumiaji yoyote Yule .Kutuma ujumbe wa faraghafuata hatua zifuatazo chini hapa mara

    unapokua kwenye kozi yako , bofya washiriki wa kozi

    1. Bofya jina la mtu unayetaka kumtumia ujumbe.

    Bofya hapa

    kuona

    washiriki

  • 39

    Bofya kitufe au kiungio cha Tuma ujumbe

    Baada ya kutuma ujumbe wako, unaweza kuangalia ujumbe ulotuma au kama kuna ujumbe uliotumiwa, kufanya hivo angalia picha chini.

    Bofya Kutuma ujumbe

    Sehemu ya kuandika ujumbe Sehemu ya kutuma ujumbe

    Tazama ujumbe uliotuma au

    kutumiwa hapa