hoja ya muungano wa tanzania na muundo wa serikali mbili (kiswalili)

52
  1 HOJA YA MUUNGANO WA TANZANIA NA MUUNDO WAKE WA SERIKALI MBILI (Omar R. Mapuri) UTANGULIZI Hoja ya Muungano wa Tanzania inasimama juu ya msingi wa sera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Sera ya CCM kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuwa Tanzania ina ncha mbili; yaani kuulinda na kuudumisha Muungano wenyewe kwa upande mmoja na muundo wa Muungano huo kuwa wa Serikali mbili kwa upande wa pili. CCM inaushabikia Muungano na kupania kuulinda na kuudumisha kwa sababu kwanza inaamini kuwa Muungano huu ni wa watu wenyewe na pili, uliasisiwa na vyama wazazi wake, yaani TANU na ASP. Zaidi ya hivy o, CCM yenyewe ni matokeo ya Muungano huo na chachu ya kuziimarisha kwani tendo la kuviunganisha vyama vya TANU na ASP kuunda CCM lilitokana na utashi wa kukamilisha hatua za kuunda Muungano. CCM inaunga mkono muundo wa Muungano wa Serikali mbili kwa sababu kwanza ndio ulioamuliwa na waasisi wa Muungano, Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume, na pili

Upload: shafii-muhudi

Post on 06-Oct-2015

454 views

Category:

Documents


0 download

DESCRIPTION

HOJA YA MUUNGANO WA TANZANIA NA MUUNDO WA SERIKALI MBILI (Kiswalili)

TRANSCRIPT

  • 1

    HOJA YA MUUNGANO WA TANZANIA NA MUUNDO

    WAKE WA SERIKALI MBILI

    (Omar R. Mapuri)

    UTANGULIZI

    Hoja ya Muungano wa Tanzania inasimama juu ya msingi wa sera ya

    Chama Cha Mapinduzi (CCM). Sera ya CCM kuhusu Muungano wa

    Tanganyika na Zanzibar kuwa Tanzania ina ncha mbili; yaani kuulinda na

    kuudumisha Muungano wenyewe kwa upande mmoja na muundo wa

    Muungano huo kuwa wa Serikali mbili kwa upande wa pili.

    CCM inaushabikia Muungano na kupania kuulinda na kuudumisha kwa

    sababu kwanza inaamini kuwa Muungano huu ni wa watu wenyewe na pili,

    uliasisiwa na vyama wazazi wake, yaani TANU na ASP. Zaidi ya hivyo,

    CCM yenyewe ni matokeo ya Muungano huo na chachu ya kuziimarisha

    kwani tendo la kuviunganisha vyama vya TANU na ASP kuunda CCM

    lilitokana na utashi wa kukamilisha hatua za kuunda Muungano.

    CCM inaunga mkono muundo wa Muungano wa Serikali mbili kwa sababu

    kwanza ndio ulioamuliwa na waasisi wa Muungano, Marehemu Baba wa

    Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume, na pili

  • 2

    umezingatia vya kutosha uhalisi wa mambo wa nchi kubwa na ndogo

    kuungana. Muundo huo ndio unaohakikisha umadhubuti wa Muungano

    wenyewe bila ya nchi ndogo (Zanzibar kwa muktadha huu) kumezwa na

    nchi kubwa (Tanganyika).

    CCM inajivunia Muungano huu na muundo wake wa Serikali mbili kwani

    hata baada ya miaka 40 ya kuundwa kwake bado ndio mfano pekee wa

    Muungano uliofanikiwa wa nchi huru zilizoungana katika Bara la Afrika.

    Zaidi ya yote, Muungano huu umeweza kuhimili misukosuko yote ya ndani

    uliyokumbana nayo ambayo ingeweza kuudhofisha au hata kuuvunja.

    Pamoja na makelele mengi ya kisiasa yenye kuulalamikia, Muungano huu na

    muundo wake wa Serikali mbili unaungwa mkono na Watanzania walio

    wengi. Ushahidi wa kitakwimu utatolewa katika makala haya kwamba

    muundo wa Serikali mbili ndio unaotakiwa na Watanzania walio wengi, na

    muundo wa Serikali tatu unaopigiwa debe sana na vyama vya upinzani na

    baadhi ya wasomi ndio unaokataliwa na Watanzania wengi kuliko muundo

    mwingine wowote.

    Kabla ya kuendelea na hoja, inafaa katika hatua hii kutazama maandiko

    rasmi ya kisera ya CCM kuhusu Muungano na muundo wake, kama yalivyo

    katika Ilani za Uchaguzi za CCM za 1995 na 2000.

    Ibara ya 47 ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 1995 inasomeka ifuatavyo:

    47. Sera ya Kuimarisha Muungano

  • 3

    Muundo wa Muungano, ambao unakubaliwa na CCM, ni

    Muungano wenye Serikali mbili: Serikali ya Jamhuri ya

    Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

    Sera hii imethibitishwa mwaka 1994 wakati wanachama wetu

    walio wengi walioshiriki katika kura za maoni kote nchini

    walitaka sera hii iendelee. Katika kipindi cha miaka mitano

    ijayo, CCM itaendelea kudumisha Muungano wa Tanzania

    katika muundo wa Serikali mbili.

    Kwa upande wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2000, ibara

    zinazozungumzia kuimarisha Muungano ni za 116 na 117 ambazo

    zinasomeka ifuatavyo:-

    116. Umoja wa kitaifa wa Watanzania ambao umedumu kwa kipindi

    kisichopungua miaka 36 unatokana na Muungano wa

    Tanganyika na Zanzibar ambao ulizaa Tanzania. Katika

    kipindi chote hicho muundo wa muungano ambao umeendelea

    kukubaliwa na Chama Cha Mapinduzi ni muungano wenye

    Serikali mbili: Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Sera hii imeendelea

    kuthibitishwa na wanachama wa CCM na wananchi kwa jumla.

    117. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo (2000 2005) Chama

    Cha Mapinduzi kitaendelea kuhakikisha kuwa mafanikio

    yaliyorithiwa kutoka kwa Waasisi wa taifa letu Baba wa Taifa,

    Mwalimu J.K. Nyerere na Makamu wake wa Kwanza Sheikh

    Abeid Aman Karume yanaendelezwa na kulindwa kwa

  • 4

    kuhakikisha kuwa Tanzania inaendelea kuwa huru, Taifa lenye

    Umoja, Udugu na Mshikamano na nchi yenye amani na utulivu.

    Aidha, muundo wa Muungano utaendelea kuwa wa Serikali

    mbili: yaani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali

    ya Mapinduzi Zanzibar.

    Hivyo ndivyo inavyosema Sera ya CCM kuhusu Muungano na muundo

    wake. Ni muhimu hili kuwekwa sawa kwani wapinzani wa CCM, hasa kule

    Zanzibar, hupenda kujichukulia uhuru wasiopewa wa kuisemea CCM

    wapendavyo wao. Hupenda sana kuipotosha sera hii kwa kuinukuu kilaghai

    kwamba eti ni ya Serikali mbili kuelekea moja. Kauli hiyo imewahi

    kutoka katika vikao vya CCM kama kauli nyingi nyenginezo zilivyowahi

    kutoka. Kwa mfano, Bunge, likiwa na Wabunge wa CCM watupu liliwahi

    kupitisha azimio la kutaka kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika ndani ya

    Muungano. Lakini baada ya yote hayo na kauli zote zilizosemwa na/au

    kuandikwa, ulipofika wakati wa kutunga sera rasmi, Chama kiliamua bila ya

    kigugumizi kuendelea na sera ya Muungano wa Serikali mbili na kuiweka

    kwa uwazi na bila ubabaishaji katika Ilani za Uchaguzi.

    NGUZO ZA MUUNGANO

    Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulijengwa juu ya msingi wa

    kijiografia na kihistoria uliowafanya watu wa maeneo haya kuwa wamoja,

    ndugu, wenye tamaduni zilizoingiliana na hata wenye utashi wa kisiasa

    uliofanana.

  • 5

    Juu ya msingi huo, zimesimama nguzo nne zinazouhimili Muungano huo.

    Nguzo ya kwanza ambayo imejengeka kwa muda mrefu katika historia ni

    kwamba Muungano huu ni wa watu wenyewe. Nguzo hii inaupa Muungano

    uhalali wa kijamii na hata wa kisiasa. Nguzo ya pili ni msukumo wa

    kujenga umoja wa Afrika. Nguzo hii inaupa Muungano uhalali wa kisiasa

    za kimataifa. Nguzo ya tatu ni Hati ya Muungano ambayo iliujengea

    Muungano uhalali wa kisheria ambao unaendelezwa na Katiba ya Jamhuri

    ya Muungano wa Tanzania ya 1977 na Katiba ya Zanzibar ya 1984. Nguzo

    ya nne inayouhimili Muungano na ambayo inaendelea kujengeka ni ya

    uendelevu wa Muungano wenyewe. Muungano wa Tanzania umeshatimiza

    miaka 40 ukiendelea kuimarika. Umeweza na unaendelea kuhimili

    misukosuko mingi, ambapo kila unapoingia kwenye tanuri la misukosuko,

    unaibuka ukiwa imara zaidi. Nguzo hii inaupa Muungano uhalali wa kisiasa

    za ndani.

    Sasa tuzitazame nguzo hizi moja moja.

    Nguzo Ya Umoja wa Watu Wenyewe

    Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umejengeka kutokana na mahusiano

    ya dahari na karne baina ya watu wa visiwa vya Zanzibar na mwambao wa

    Afrika ya Mashariki, hasa Mrima ambayo ni sehemu kubwa ya Tanzania

    Bara ya sasa.

  • 6

    Kabla ya Kuja Kwa Wageni Toka Nje ya Afrika

    Wanahistoria (mfano Ingrams) wakijenga hoja kutokana na maandiko ya

    kale ya Periplus (karne ya kwanza AD) na ngano za watu wa kale,

    wanakubaliana kwamba watu wa kwanza kabisa kufika katika visiwa vya

    Zanzibar ni Waafrika kutoka Mrima katika harakati za uvuvi. Ushahidi wa

    kiakiolojia wa hivi karibuni umethibitisha usahihi wa imani hiyo.

    Wakati wa Himaya ya Zenj

    Lakini hata baada ya kuja kwa wageni kutoka nje ya Afrika, mahusiano ya

    watu wa pande hizi mbili siyo tu yaliendelea, bali yalizidi kuimarika hasa

    kutokana na kuongezeka kwa ubora wa teknolojia ya usafiri wa baharini.

    Himaya ya Waajemi (Washirazi) katika eneo hili ambayo baadhi ya

    wanahistoria wanaiita Himaya ya Zenj (Zenj Empire) ilipojengeka kutokana

    na ujio wa wale Ndugu saba wa El-Hasa mnamo karne ya 13 ambao

    walianzisha tawala katika vituo mbali mbali vya mwambao wa Afrika

    Mashariki (mfano Kilwa, Barawa, Lamu, Unguja, Pemba, n.k.), maingiliano

    ya watu wa maeneo haya yaliendelea bila ya vikwazo.

    Wakati wa Himaya ya Biashara ya Zanzibar

    Mnamo karne za 16 hadi katikati ya 19, ilijengeka Himaya ya Kibiashara

    ambayo kitovu chake kilikuwa Zanzibar. Himaya hiyo iliyojumuisha

    biashara ya watumwa, vipusa na viungo, ilienea hadi maeneo ya Maziwa

    Makuu kwa upande wa Kaskazini Magharibi na maeneo ya Ziwa Nyasa na

    Mto Ruvuma kwa upande wa Kusini mwa Tanzania ya leo. Katika kitabu

  • 7

    chake cha Slaves, Spices & Ivory in Zanzibar Profesa Abdul Sheriff

    anazungumzia dhana ya Bara ya Zanzibar (The Hinterland of Zanzibar)

    akiwa na maana ya eneo la Bara lililokuwa chini ya ushawishi wa Zanzibar

    (bila shaka na Sultani wake), ambalo kwa kiasi kikubwa ni hili hili eneo la

    Tanzania Bara ya leo. Dhana hiyo ilipewa methali maarufu ya: Inapopigwa

    ngoma Zanzibar, wanacheza katika Maziwa Makuu.

    Maelezo haya yanajaribu kujenga hoja kwamba eneo ambalo leo linaitwa

    Tanzania, kwa kiasi kikubwa ndilo lililokuwa Himaya ya Kibiashara ya

    Zanzibar ya enzi hizo. Kwa maneno mengine nchi hii ilikuwa moja toka

    enzi hizo ingawa yenye mipaka hafifu. Watu wa eneo lote hili

    waliunganishwa na harakati za biashara. Biashara ya utumwa iliwafanya wa

    huku waende kule na wa kule waje huku, ingawa katika mazingira ya

    uchungu. Watumwa walichukuliwa Bara na kupelekwa visiwani Zanzibar

    ambako vizazi vyao vimeendelea hadi leo na kufanya sehemu kubwa ya

    Wazanzibari. Kwa upande mwengine, wako wafanyabiashara ya watumwa

    walioanzia Zanzibar na kuhamia Bara na kufanya maskani yao huko. Vizazi

    vyao vinaendelea hadi leo na wamekuwa sehemu ya jamii ya Watanzania

    Bara. Hivi sasa, katika mazingira ya uhuru, watu wa kila upande kati ya

    pande mbili hizi wanaendelea kuhamia na kuweka maskani katika upande

    wa pili bila ya vikwazo.

    Utenganishi wa Wakoloni wa Kizungu

    Kitendo kilichowatenganisha watu wa pande hizi ni kile cha wakoloni

    kutoka Ulaya (Wazungu) kugawana makoloni katika Bara la Afrika, katika

    nusu ya pili ya karne ya 19. Baada ya kinyanganyiro baina yao, wakoloni

  • 8

    hao walikutana katika Mkutano wa Berlin wa 1887 ambapo waligawana

    Afrika. Katika mgao huo, sehemu ya Bara (ukiondoa ukanda wa mwambao

    wa pwani ulioitwa Mrima) walipewa Wajerumani. Koloni hilo ambalo

    lilijumuisha Burundi na Rwanda ya sasa liliitwa Deutsche Ost Afrika (yaani

    Afrika Mashariki ya Wajerumani). Sultani wa Zanzibar aliachiwa visiwa

    vya Unguja, Pemba na Mafia na ukanda wa Mrima. Miaka mitatu baadae,

    chini ya Mkataba wa Heligoland wa 1890, Sultani alilazimishwa kuuza kwa

    Wajerumani ukanda wa Mrima na kisiwa cha Mafia, na hivyo kubakiwa na

    visiwa vya Unguja na Pemba tu, na yeye mwenyewe kuwekwa chini ya

    Himaya ya Mwingereza. Watu wa Bara na Visiwani wakawa

    wametenganishwa.

    Kuanza Kurejeana

    Baada ya Vita Vikuu vya Kwanza vya Dunia (1915 1919), majaaliwa

    yalianza kuwakurubisha tena watu wa pande hizi mbili. Kufuatia kushindwa

    kwa Wajerumani katika vita hivyo, Rwanda na Burundi walipewa Wabelgiji

    na sehemu iliyobaki ya Deutsch Ost Afrika iliitwa Tanganyika Territory na

    kupewa Waingereza. Kwa hivyo watu wa Zanzibar na Tanganyika ingawa

    waliendelea kuwa na nchi mbili tofauti, lakini angalau wakawa chini ya

    mkoloni mmoja.

    Hali hiyo ilijenga mazingira ya kuweza kurejea kwa mawasiliano baina ya

    watu wa Bara na wa Visiwani ambayo yalikuwa yameathirika vibaya kwa

    kipindi cha kiasi cha miaka 30. Mwamko wa kudai uhuru wa kijamii na

    baadae wa kisiasa ulipoanza kujengeka, watu wa pande hizi mbili, hususan

  • 9

    wenyeji wa asli (yaani Waafrika) hawakusita kuitumia fursa hiyo

    kushirikiana na kusaidiana katika azma hiyo.

    Mwaka 1927, Waafrika wa Dar es Salaam walianzisha jumuiya yao

    iliyoitwa African Association kwa ajili ya kupigania maslahi yao ya

    kijamii. Mwaka 1934, Waafrika wa Zanzibar nao walianzisha African

    Association yao, pengine kutokana na ushawishi wa ndugu zao wa Dar es

    Salaam. Nao Waafrika wa Zanzibar wakawashawishi wale wa Dodoma na

    kupelekea kuundwa kwa African Association ya Dodoma. Jumuiya tatu

    hizi zilijenga umoja wa kufanya mikutano mikuu ya pamoja ya mwaka kwa

    zamu baina ya miji hiyo, na zilikuwa chachu ya kufunguliwa kwa matawi ya

    African Association katika miji mbali mbali Tanganyika na Zanzibar.

    Ziara za Michezo

    Sambamba na ushirikiano huo wa kijamii, wananchi wa Tanganyika na

    Zanzibar walianzisha utamaduni wa kubadilishana ziara za kimichezo. Ziara

    hizo zilikuwa zikifanyika wakati wa mapumziko ya Pasaka, kwa utaratibu

    wa zamu ambapo kama mwaka huu wanamichezo wa Zanzibar wanakwenda

    Tanganyika, mwaka ujao wa Tanganyika watakwenda Zanzibar. Utamaduni

    huo unaendelea hadi leo na umezidi kupanuka kwa kujumuisha wasanii na

    hata wananchi tu wa kawaida.

    Ushirikiano wa Kisiasa

    Upepo wa harakati za kudai uhuru kutoka kwa wakoloni ulipofika maeneo

    haya, watu wa Tanganyika na Zanzibar walihamasishana, kushirikiana na

  • 10

    kusaidiana katika jukumu hilo la kudai na kupigania uhuru wa nchi zao.

    Mwaka 1954, chama cha Tanganyika African National Union (TANU)

    kilianzishwa Tanganyika kutokana na Tanganyika African Association, kwa

    ajili ya kudai uhuru wa Tanganyika. Zanzibar nako mwaka 1957

    ilianzishwa Afro-Shirazi Party (ASP) kutokana na kuungana kwa African

    Association na Shirazi Association (iliyokuwa imeundwa 1938). Kuundwa

    kwa ASP kulishuhudiwa na Rais wa TANU, Mwalimu Julius K. Nyerere.

    Ushirikiano wa TANU na ASP katika mapambano ya kudai uhuru hadi

    ulipopatikana Uhuru wa Tanganyika Disemba 9, 1961 na kufanikiwa kwa

    Mapinduzi ya Zanzibar Januari 12, 1964 unajulikana na hauna haja ya

    kuufafanua hapa. Dhamira angalau ya ASP (wakati wa kupigania uhuru) ya

    kuiunganisha Zanzibar na Tanganyika baada ya uhuru haikuwa siri. Hiyo

    inadhihirishwa na maelezo yafuatayo ya Marehemu Sheikh Thabit Kombo

    kama yalivyonukuliwa na Rais Benjamin Mkapa katika hotuba yake ya

    kihistoria aliyoitoa Zanzibar kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 40 ya

    Muungano tarehe 26 Aprili, 2004:-

    Mafisadi wanalalamika, kwa nini muungano umefanyika haraka

    haraka; Mapinduzi Januari na Muungano Aprili, miezi mitatu tu!

    Wako wanaodhani kuwa Mwalimu Nyerere ndiye aliyelazimisha

    Muungano.

    Wazo la Muungano ni wazo la Afro-Shirazi tokea mwanzo.

    Utakumbuka katika Manifesto yetu tulisema kuwa tukipata Uhuru

    azma ya ASP ni kuona kuwa Afrika yote inakuwa moja yenye nguvu.

    Lakini kwa Tanganyika na Zanzibar ahadi ya muungano ni ahadi ya

  • 11

    wanachama wenyewe waliyokuwa wanaitoa katika mikutano yao

    yote Watu wa Tanganyika na watu wa Zanzibar ni wale wale,

    tofauti ni sisi wa Zanzibar kutawaliwa na Sultani. Mazungumzo

    yalikuwa mafupi sana, yalichukua siku moja tu; maana hakukuwa na

    swali kama tuungane au tusiungane. Hoja ilikuwa tu muungano wetu

    uwe na sura gani..

    Muungano Kama Tukio la Kimantiki

    Kutokana na ukweli huo wa kihistoria wa umoja, udugu na ushirikiano wa

    muda mrefu baina ya watu wa pande hizi, na kufuatia TANU na ASP

    kushika madaraka baada ya Uhuru na Mapinduzi, Muungano wa Tanganyika

    na Zanzibar kuwa Tanzania uliokamilishwa rasmi tarehe 26 Aprili, 1964

    lilikuwa ni tukio la kimantiki na halipaswi kuwa la kushangaza.

    Ni ukweli wa kihistoria kwamba pamoja na kwamba watu wa Tanganyika na

    Zanzibar wamekuwa wamoja katika zama zote za kihistoria, lakini

    Tanganyika na Zanzibar hazikuwa nchi tulizoziunda. Ziliundwa na

    wakoloni na mipaka yake ilikuwa ikipangwa na kupanguliwa na wakoloni

    kwa maslahi yao. Tanganyika na Zanzibar pamoja na mipaka yake tuliirithi

    tu kutoka kwa wakoloni baada ya uhuru. Lakini Tanzania tumeiunda

    wenyewe.. Katika kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya

    Tanzania, Mwalimu Julius K. Nyerere anasisitiza kwa fahari: Tanzania ni

    lulu ya pekee kabisa katika historia ya Afrika huru. Nchi nyingine zote ni za

    kurithi kutoka katika Ukoloni. Tanzania ni ya kuundwa na sisi wenyewe,

    kwa hiari yetu wenyewe, baada ya kukomboa sehemu zake mbili kutoka

    katika Ukoloni. (uk.57).

  • 12

    Pamoja na hayo, kama itakavyofafanuliwa baadae, wapo watu

    wanaoshangaa na kuhoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

    kwa hoja kwamba eti hayakutafutwa maoni ya wananchi kwanza. Katika

    kuwabeza watu hao, Mwalimu Nyerere katika kitabu chake hicho hicho cha

    Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania anasema ifuatavyo kwa kejeli:-

    Pwani ya Tanganyika na Zanzibar ya sasa zilikuwa pamoja kwa muda

    mrefu sana kabla ya kutengwa na Wakoloni Waingereza na

    Wajerumani. Kama zingebaki zimetengana, kwa wazalendo hao

    hiyo ingekuwa ni halali, maana zilitengwa kwa hila na mitutu ya

    bunduki za Mabwana. Lakini uamuzi wa Tanganyika huru na Zanzibr

    huru kuungana, na hivyo kuwaunganisha tena ndugu waliokuwa

    wametengwa na Mabeberu, tendo hilo kuna wanaosema kuwa

    halikuwa halali. Hatukutafuta maoni ya watu kwa njia ya demokrasia

    wanayoijua wao. Wajerumani na Waingereza walitafuta maoni ya

    wazee wetu kwa mtutu wa bunduki! Hiyo ilikuwa halali. Nchi

    walizounda kwa njia hizo zilikuwa halali. Tunatakiwa tujivunie

    Utanganyika na Uzanzibari uliopatikana kwa njia hizo; lakini tuuonee

    haya Utanzania, tunda la uhuru wetu wenyewe. Sikuamini kuwa

    Wakoloni walifaulu kiasi hiki katika kuzinywesha kasumba na

    kuzitawala akili za baadhi yetu!. (uk.58).

    Tarehe 5 Februari, 1977 vyama vya TANU na ASP viliungana na kufanya

    Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika tukio ambalo lilikuwa na maana ya

    kuzidi kuuimarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Tena kuundwa

    kwa CCM kulitanguliwa na mashauriano ya kutosha. Aidha, ilifanywa kura

  • 13

    ya maoni ya wanachama ambayo matokeo yake yalikuwa kama

    yanavyoonekana katika Jedwali Na. 1 na 2 hapa chini:-

    JEDWALI Na. 1: MATOKEO YA MAONI YA WANACHAMA WA

    TANU KUHUSU KUUNGANISHWA TANU NA ASP

    Matawi Idadi Asilimia

    Idadi ya Matawi Yote ya TANU 6,639 100.00

    Yaliyokutana 6,427 96.81

    Yasiyokutana 212 3.19

    Yaliyokubali 5,424 99.95

    Yaliyokataa 3 0.05

    Idadi ya Matawi Madogo ya TANU 38 100,00

    Yaliyokutana 38 100.00

    Yaliyokubali 38 100.00

    Yaliyokataa 0 0.00

    Chanzo: Tathmini ya Miaka 20 ya CCM, 1977 1997

    JEDWALI Na. 2: MATOKEO YA VIKAO NA WANACHAMA WA

    ASP KUHUSU MAONI YA KUUNGANISHWA TANU NA ASP

    Matawi Idadi Asilimia

    Idadi ya Matawi ya ASP 257 100.00

    Yaliyokubali 257 100.00

    Yaliyokataa 0 0.00

    Idadi ya Wanachama Wote Walioshiriki 103,983 100.00

    Waliokubali 103,574 99.06

    Waliokataa 409 0.04

    Chanzo: Tathmini ya Miaka 20 ya CCM, 1977 1997.

  • 14

    Yaani wanachama wa TANU katika katika 99.95 ya matawi yao yaliyotoa

    maoni na matawi yote madogo waliafiki chama chao kuunganishwa na ASP.

    Kwa upande wa Zanzibar, wanachama wa ASP katika matawi yao yote

    waliafiki chama chao kiunganishwe na TANU. Na kwa wanachama mmoja

    mmoja walioshiriki katika kura hiyo ya maoni, ni 409 tu kati ya wote

    103,983, yaani sawa na asilimia 0.04 tu ndio waliokataa.

    Huu ulikuwa ni ushahidi madhubuti usio shaka wa kitakwimu wa imani ya

    wananchi kwa Muungano. Kwa kura hiyo, watu wa Tanganyika na Zanzibar

    kupitia vyama vyao vya TANU na ASP ambavyo vilikuwa pekee wakati

    huo, waliuthibitishia Ulimwengu kwamba Muungano ni wao na haukuwa wa

    viongozi tu kama inavyodaiwa na wapinzani wachache wa Muungano.

    Kabla ya kuunganishwa kwa TANU na ASP, Katiba ya Muda ya Jamhuri ya

    Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliitaja Jamhuri hiyo kuwa ni ya

    mfumo wa chama kimoja ambapo kwa Tanganyika Chama hicho ni TANU

    na kwa Zanzibar chama hicho ni ASP. Kwa maneno mengine, Jamhuri

    ilikuwa chini ya chama kimoja kwa viwili, jambo ambalo lilileta dosari

    kubwa katika uimara wa Muungano. Baada ya TANU na ASP kuungana na

    kuwa CCM, dosari hiyo iliondolewa na hivyo kikawa ni kitendo cha

    kuimarisha Muungano. Zaidi ya yote, tukio hilo ndilo lililochochea

    kutungwa rasmi kwa Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano wa

    Tanzania ya 1977.

    Kwa hivyo, kwa majumuisho, inasisitizwa tena kwamba Muungano wa

    Tanganyika na Zanzibar ni wa watu wenyewe. Waasisi wa Muungano huo,

  • 15

    yaani Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume

    kupitia Serikali zao, waliwezesha tu kufikiwa kwa matarajio ya wananchi

    wenyewe. Mzee Karume alilielezea tukio hilo kwa maneno yafuatayo kama

    alivyonukuliwa na Rais Benjamin Mkapa katika hotuba yake ya tarehe 26

    Aprili, 2004:-

    Napenda mfahamu wananchi wote, kazi hii si kazi ya Abeid Karume.

    Jambo hili, jambo la wenyewe Waafrika wote. Mwalimu Julius

    Nyerere na Abeid Karume wao ni watumishi wa wenyewe wana wa

    nchi, na sisi tumekubali kuwatumikia wenyewe wananchi.

    Tunawatumikia wananchi kwa utumishi wao maalum, ule walioona

    wao wenyewe bora. Basi jambo hili la kufanya Union, Tanganyika na

    Zanzibar, ni jambo ambalo lililofikiriwa na wenyewe wananchi wa

    Tanganyika na Zanzibar

    Hatimaye, mwaka 1977, watu wenyewe, kupitia vyama vyao waliithibitisha

    hatua ya Waasisi ya kuunganisha Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.

    Hiki ni kielelezo cha wazi cha umadhubuti wa nguzo hii ya Muungano ya

    kwamba Muungano ni wa watu wenyewe, na jinsi nguzo hii inavyoupa

    uhalali wa kijamii na hata wa kisiasa Muungano wetu.

    Nguzo Ya Msukumo wa Kujenga Umoja wa Afrika

    Nguzo ya pili inayouhimili Muungano ni utashi wa kujenga umoja wa

    Afrika. Manifesto (Ilani za Uchaguzi) za TANU na ASP toka enzi za

    mapambano ya kudai uhuru zilikuwa na vipengele vya kutaka umoja wa

  • 16

    Afrika. Aidha, vyama vyote vilishiriki kikamilifu katika majukwaa yote

    yaliyowaunganisha Waafrika wa nchi mbali mbali katika kudai uhuru kwa

    lengo la kuja kuziunganisha nchi hizo baada ya uhuru. Kwa mfano, TANU

    na ASP zilikuwa wanachama wa PAFMECA na baadae PAFMECSA,

    vyombo ambavyo viliviweka pamoja vyama vilivyokuwa vikidai uhuru

    kutoka nchi mbali mbali za eneo la Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika.

    Katika hili, hata Chama cha Hizbu (ZNP) cha Zanzibar kilikuwa kikishiriki.

    Katika jitihada za kufikia ndoto hiyo ya umoja wa Afrika, nchi za Afrika

    Mashariki (yaani Kenya, Uganda, Tanganyika na Zanzibar) zilijaribu

    kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki baada ya uhuru wa nchi hizo. Baada

    ya kuona dalili za kukawia kufikiwa kwa lengo hilo katika upeo wa Afrika

    Mashariki, Rais Nyerere wa Jamhuri ya Tanganyika na Rais Karume wa

    Jamhuri ya Watu wa Zanzibar walikubaliana zianze Tanganyika na Zanzibar

    ili kuonyesha njia na kuendeleza shauku ya kutafuta umoja wa Afrika.

    Dhamira hiyo inajieleza katika maneno ya Mwalimu Nyerere katika hotuba

    yake katika Mkutano Maalumu wa Bunge la Tanganyika, tarehe 25 Aprili,

    1964, lililoitishwa kujadili na kuridhia Hati ya Muungano. Mwalimu

    anajinukuu katika kitabu chake cha Uhuru na Umoja kama ifuatavyo:-

    Ikiwa, basi, nchi ambazo ni marafiki na ni jirani, na hasa zile ambazo

    zilipata kuwa moja bali zikagawanywa na wakoloni wapya; ikiwa hizo

    zitashindwa kuungana, kushindwa huko kunaweza kukaleta wasi wasi

    katika bara letu la Afrika na shauku yake ya Umoja. Bali ikiwa nchi

    hizo zaweza kuungana, muungano huo waweza ukawa ni thibitisho la

    vitendo kwamba matumaini ya bara letu si ya bure. (uk.292).

  • 17

    Miaka miwili baadae, wakati wa sherehe za Muungano kutimiza miaka

    miwili zilizofanyika Dar es Salaam mwaka 1966, Mzee Karume naye

    aliithibitisha dhamira hiyo. Kama alivyonukuliwa na Rais Benjamin Mkapa

    katika hotuba yake ya kilele cha maadhimisho ya miaka 40 ya Muungano

    tarehe 26 Aprili, 2004 mjini Zanzibar, Mzee Karume alisema yafuatayo:-

    Muungano wa Tanzania unaonyesha mithali katika Afrika. Mithali

    yenyewe (ni) kuthibitisha nini viongozi wa Kiafrika kabla ya

    hawajapata independence walikuwa wakisema. Neno lililokuwa

    likisemwa ni hili hapa Tanzania (Muungano). Ya kwamba kila

    mmoja akijitapa, mara tu nikipata Serikali yangu katika nchi yangu

    lazima nilete uhusiano na Muungano wa Uafrika, tuzidi kuendelea

    kwa maendeleo yaliyo bora. Lakini si bahati mbaya (kuwa

    hawajatekeleza). Watanzania mjue kuwa si bahati mbaya. Bahati

    nzuri, Muungano ndiyo huu hapa. Watanzania tena mnataka nini?

    Muungano wa Tanzania ndiyo hatua ya mwanzo. Na msife moyo

    wananchi wa Tanzania. Wenzetu wako jirani watakuja unga.

    Muungano wa Tanzania ni kani inayoendeleza uhai wa dhamira ya

    kuwaunganisha Waafrika na hivyo umeijengea heshima kubwa nchi yetu.

    Uhai wa dhamira hiyo inayopata msukumo kutokana na Muungano wetu,

    unajidhihirisha katika kuingia hatua ya kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika

    (African Union) wenye nguvu zaidi kutoka hatua ya uliokuwa Umoja wa

    Nchi Huru za Kiafrika (OAU). Na katika eneo letu la Afrika Mashariki,

    hatua za kuanzisha Shirikisho la Afrika Mashariki zimefufuliwa kutokana na

    uhai wa dhamira hiyo.

  • 18

    Kwa hivyo, nguzo hii ya msukumo wa kujenga umoja wa Afrika imeupa pia

    Muungano wetu uhalali wa siasa za kimataifa, hasa Barani Afrika.

    Watanzania wanajivunia heshima hii na wanapenda iendelee. Heshima hiyo

    itaendelea tu kwa kuudumisha Muungano na kamwe si kwa kuudhofisha au

    kuuvunja.

    Nguzo ya Kisheria

    Nguzo ya tatu inayouhimili na kuupa uhalali Muungano wa Tanzania ni

    ukweli kwamba Muungano huo umesimama juu ya msingi wa sheria za nchi

    na za kimataifa. Ulijadiliwa, ukatungiwa mkataba wa kimataifa (Hati ya

    Muungano) ambao ulitiwa saini tarehe 22 Aprili, 1964 na Wakuu wa Nchi

    (Marais Nyerere na Karume) na hatimae kuridhiwa na Mabaraza ya kutunga

    sheria ya nchi zote mbili (yaani Bunge la Tanganyika na Baraza la

    Mapinduzi la Zanzibar) kwa niaba ya wananchi wao.

    Kama itavyoonekana baadae, wapo waliowahi kudhani kwamba kwa upande

    wa Zanzibar, hatua za kuuhalalisha Muungano kisheria hazikutimia kwa

    madai eti kwamba Hati ya Muungano haikuridhiwa na baraza la kutunga

    sheria kwa niaba ya wananchi. Lakini hoja yao ilinyauka pale

    walipozinduliwa kwamba wasilitazame Baraza la Mapinduzi kwa sura yake

    ya Baraza la Mawaziri tu, bali walione pia katika sura yake ya pili

    liliyokuwa nayo wakati huo ya Baraza la Kutunga Sheria.

  • 19

    Nguzo ya Uendelevu

    Nguzo ya nne inayouhimili na kuupa uhalali wa kisiasa Muungano wa

    Tanzania na ambayo inaendelea kuimarika kila kukicha, ni uendelevu wa

    Muungano wenyewe. Hadi sasa, miaka arobaini baada ya kuasisiwa kwake,

    Muungano huu unabaki kuwa mfano pekee Barani Afrika wa muungano wa

    nchi zilizo huru uliodumu. Kama ilivyokwishagusiwa kabla, juhudi za

    kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki mara tu baada ya uhuru, zilivia.

    Ulijaribiwa pia Muungano wa Misri, Libya na Syria (ulioitwa Jamhuri ya

    Umoja wa Kiarabu) katika miaka ya sitini, lakini haukufika mbali. Senegal

    na Gambia nazo zilijaribu Senegambia katika miaka ya themanini lakini bila

    ya mafanikio.

    Kama itavyofafanuliwa baadae, Muungano wa Tanzania umefaulu majaribu

    mengi. Badala ya kuudhofisha, majaribu hayo yamekuwa yakiuimarisha

    zaidi. Muungano ulianza na mambo 11 tu katika orodha ya mambo ya

    Muungano, lakini hivi sasa yamefikia 22. Wasioutakia mema Muungano

    wamekuwa wakidai kwamba eti mambo yaliyoongezwa yaliingizwa

    kinyemela na kwa kuiburuza Zanzibar. Lakini madai kama hayo ambayo

    hayana chembe ya ukweli, mara nyingine yamekuwa yakiambatana na

    unafiki. Kwa mfano, waliosimamia na kuhakikisha Usalama wa Taifa wa

    Zanzibar unawekwa chini ya Serikali ya Muungano mwaka 1984, ndio hao

    hao sasa wanaoongoza kampeni ya kutaka Watanzania na hasa Wazanzibari

    waamini kwamba eti mambo yanaingizwa kiholela tu na kwa kuwaburuza

    Wabunge wa Zanzibar kutokana na uchache wao Bungeni.

  • 20

    Ukweli ni kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayalinda vya kutosha

    maslahi ya Zanzibar kwani inatamka wazi kwamba hakuna jambo

    litaloongezwa au kupunguzwa katika orodha ya mambo ya Zanzibar ila kwa

    thuluthi mbili ya kura za Wabunge wanaotoka Zanzibar na thuluthi mbili za

    Wabunge kutoka Bara. Kwa hivyo, wingi wa Wabunge wa Bara hauna

    nafasi ya kuwaburuza wenzao wa Zanzibar.

    Itoshe tu kusisitiza kwamba uendelevu wa Muungano ni nguzo madhubuti

    ya kuuhimili Muungano huu ambayo pia inaupa uhalali wa kisiasa za ndani.

    Katika sehemu hii, zimezungumziwa nguzo nne zinazouhimili

    Muungano wa Tanzania na hata kuupa sura mbali mbali za uhalali. Ni

    kutokana na umadhubuti wa nguzo hizo ndiyo maana umehimili na

    unaendelea kuhimili misukosuko mbali mbali kama itavyofafanuliwa

    baadae. Katika hotuba yake ya kuliaga Bunge tarehe 28 Julai, 1995,

    Rais Ali Hassan Mwinyi ambae alikuwa anastaafu wakati huo alisema

    kwa fahari kubwa:-

    Katika kipindi hiki Muungano wetu umepita katika tanuri la moto

    na kutokea upande wa pili ukiwa bado imara na wenye nguvu.

    Matatizo yaliyojitokeza yalishughulikiwa kwa ukamilifu na katika

    hali ya maelewano baina ya pande zote mbili. Tumefanya pia

    marekebisho katika Katiba ambayo nina imani yatazidi kuimarisha

    Muungano wetu katika kipindi hiki cha mageuzi ya kisiasa na

    kiuchumi.

  • 21

    SABABU ZA MUUNGANO

    Kwa kadiri CCM inavyohusika, sababu kubwa na za msingi zilizowaongoza

    Waasisi wa Muungano katika kuuanzisha ni hizi tatu zifuatazo:-

    1. Kuurejesha na kuuthitibisha umoja wa watu waliokuwa

    wametenganishwa.

    2. Kutekeleza azma ya kujenga umoja wa Afrika.

    3. Kulinda Uhuru wa Tanganyika na Mapinduzi ya Zanzibar.

    Sababu mbili za kwanza zimekwishajadiliwa kwa kina hapo kabla na hivyo

    hapana haja ya kuurejea mjadala huo. Kwa sababu ya tatu, ufafanuzi

    unapatikana kutokana na maelezo ya Sheikh Thabit Kombo kama

    alivyonukuliwa na Rais Mkapa katika hotuba yake ya maadhimisho ya

    miaka 40 ya Muungano. Maelezo hayo yaliyotolewa kama faida ya

    Muungano ni kama yafuatavyo:-

    Matumaini ya kudumu kwa amani na usalama yamekuwa

    makubwa kwa nchi zote mbili; wasiwasi mwingi wa usalama

    umeondoka. Fikiri mwenyewe kusingekuwako muungano, na maadui

    wa Zanzibar wakazidisha vitimbi vyao, kusingekuwako usalama wala

    amani; si Bara wala si hapa Zanzibar. Lakini kwa nguvu za

    muungano wakorofi wanasita kidogo

    Lakini usingekuwako muungano tungekuwa na hasara kubwa, kwa

    Tanganyika na kwa Zanzibar pia. Zanzibar pamoja na mapinduzi

    yake, ingedumu katika wasiwasi kwamba mbinu zingeweza kutumika

    kumrudisha Sultani. Na Tanganyika nayo pamoja na ukubwa wake,

    isingekuwa salama kabisa kama kungekuwako vurugu visiwani hapa.

  • 22

    Maadui wangeweza kuitumia Zanzibar kuihujumu Tanganyika kwa

    urahisi sana

    Pamoja na kwamba kauli hiyo ya hadharani ilitoka muda mrefu baada ya

    Mapinduzi, ipo kila sababu ya kuamini kwamba suala la usalama wa

    Mapinduzi ya Zanzibar na hata Uhuru wa Tanganyika ni miongoni mwa

    mambo yaliyozingatiwa wakati wa mazungumzo ya Muungano. Na pengine

    ndilo lililochangia katika kuharakisha Muungano hasa ikizingatiwa ukweli

    kwamba watawala waliopinduliwa Zanzibar walikuwa wamekimbilia nje

    ambako wangeweza kupanga mbinu za kujaribu kurudisha utawala wao.

    Hao ni maadui wa Mapindizi ambao wasingeweza kupuuzwa. Na hofu hiyo

    ilithibitishwa na majaribio 17 ya mapinduzi yaliyofanywa bila ya mafanikio

    na maadui wa Mapinduzi ya 1964. Muungano bila shaka una mchango

    wake katika kuyaviza majaribio hayo.

    Kumekuwa pia na hoja kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

    ulipata msukumo kutokana na vita baridi vya wakati huo kati ya Marekani

    na Urusi na kambi zao. Hoja ni kwamba eti Marekani ndiyo iliyoshawishi

    ufanyike Muungano kwa lengo la kuidhibiti Zanzibar eti isiwe Cuba ya

    Afrika. Wana-CCM hawaafikiani na hoja hiyo. Mtazamo wao ni kwamba

    kama kweli Wamarekani walikuwa na mawazo hayo, hawakwenda zaidi ya

    kuomba Mungu tu tukio hilo litokee. Lakini wenyewe Watanganyika na

    Wazanzibari waliungana kwa utashi wao na kwa maslahi yao. Hawakuwa

    na habari na ndoto za Marekani na maslahi yake.

    Katika hili, Rais Mkapa alitoa msisitizo ufuatao katika hotuba yake ya

    maadhimisho ya miaka 40 ya Muungano:-

  • 23

    wapo wanaodhani Muungano wetu ulikuwa lazima wakati ule kwa

    sababu tu ya vita baridi duniani, na mapambano ya mataifa makubwa

    kutafuta himaya barani Afrika. Swali linabaki. Vita baridi

    vilikwisha, na harakati za wakubwa kujenga himaya Afrika nazo

    zimekwisha. Lakini Muungano unaendelea, kwa nini? Kwa sababu

    msingi wa Muungano haukuwa vita baridi, bali shauku kubwa

    iliyozuiliwa na wakoloni kwa miaka mingi ya watu wa Tanganyika

    na Zanzibar kuungana kama walivyokuwa zamani.

    KWA NINI SERIKALI MBILI?

    Muundo wa Muungano wa Tanzania ni wa Serikali mbili; yaani Serikali ya

    Jamhuri ya Muungano ambayo inashughulikia mambo ya Muungano na

    mambo yote ya Tanzania Bara (baada ya Serikali ya Tanganyika kufa) na

    Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoshughulikia mambo yasiyokuwa ya

    Muungano kwa upande wa Zanzibar.

    Muundo huu umekuwa jambo la mjadala mkubwa na wenye kuendelea

    miongoni mwa Watanzania. Wapo wanaouona muundo huu kuwa haufai

    kwa kuwa ni tofauti na miungano mingine inayojulikana duniani. Wapo

    wanaoamini kuwa unasababisha kero nyingi na hivyo haukidhi matarajio ya

    Watanzania. Wapo wanaoamini kuwa haupendwi na Watanzania. Wapo pia

    waliojaribu kujenga hoja kwamba eti Waasisi wa Muungano walipokuwa

    wanaunganisha nchi hizi mbili, lengo lao la baadae lilikuwa ni muungano

    wa Serikali moja na kwamba huu wa Serikali mbili ulikusudiwa uwe wa

    muda tu. Wapo wengine waliojaribu kujenga hoja kwamba eti Waasisi hao

  • 24

    walichounda ni Shirikisho la Serikali tatu ambapo Serikali ya Tanganyika

    imefichwa ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

    CCM inatofautiana na mawazo yote hayo. Kufaa au kutokufaa na

    kukubalika au kutokubalika kwa muundo huu kwa Watanzania kutajadiliwa

    baadae chini ya Misukosuko Iliyohimiliwa Na Muungano.

    Katika sehemu hii, inatazamwa dhamira halisi ya Waasisi katika kufikia

    uamuzi wa Muundo huu. CCM inaamini kwamba Waasisi walikusudia

    muundo wa Serikali mbili na walikuwa wanakijua walichokuwa wanafanya.

    Wao wenyewe ndio walioijua zaidi dhamira yao kuliko wale wanaojaribu

    kuitafsiri.

    Kwa mnasaba huo, tunaanza na kuwanukuu kauli zao kama walivyosema

    wenyewe.

    Katika Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, Mwalimu Nyerere

    anaifichua dhamira yao na sababu za kuamua muundo wa Serikali mbili

    kama ifuatavyo:-

    Nchi mbili zinapoungana na kuwa Nchi Moja mifumo ya kawaida ya

    miundo ya Katiba ni miwili: Muungano wa Serikali Moja, au

    Shirikisho la Serikali Tatu. Kwa mfumo wa kwanza kila nchi itafuta

    Serikali yake, na Nchi mpya inayozaliwa itakuwa ni Nchi Moja yenye

    Serikali Moja. Katika mfumo wa pili kila Nchi itajivua madaraka

    fulani ambayo yatashikwa na Serikali ya Shirikisho, na itakuwa

    Serikali ambayo itakuwa na mamlaka juu ya mambo yaliyobaki.

  • 25

    Tanganyika na Zanzibar zilipoamua kuungana na kuwa Nchi Moja,

    tungeweza kufuata mmojawapo wa mifumo hiyo ya kawaida. Lakini

    tulishindwa kufanya hivyo kwa sababu ya udogo wa Zanzibar na

    ukubwa wa Tanganyika. Zanzibar ilikuwa na watu laki tatu (300,000)

    na Tanganyika watu milioni kumi na mbili (12,000,000). Muungano

    wa Serikali Moja ungefanya ionekane kama Tanganyika imeimeza

    Zanzibar. Tulikuwa tunapigania Uhuru na Umoja wa Afrika;

    hatukutaka tudhaniwe, hata kwa makosa, kwamba tunaanzisha

    ubeberu mpya. Kwa hiyo mimi nilipinga mfumo wa Serikali Moja.

    Shirikisho la Serikali Tatu lingekuwa ni gharama kubwa mno kwa

    Tanganyika. Zanzibar ingeendesha Serikali yake na kuchangia

    gharama za kuendesha serikali ya Shirikisho; na Tanganyika

    ingefanya vivyo hivyo. Lakini ni dhahiri kwamba mchango wa

    Tanganyika ndio hasa ungeendesha Serikali yake ya watu 12,000,000

    na pia ndiyo ingetoa sehemu kubwa ya kuendesha Serikali ya

    Shirikisho la watu 12,300,000. Ni watu wanaofikiri kwa ndimi zao

    wanaodhani kuwa gharama ya Serikali yo yote kati ya hizo ingekuwa

    ndogo. Gharama ya Serikali ya Tanganyika isingekuwa ndogo,

    (waulizeni Wazanzibari) na wala Serikali ya Shirikisho isingekuwa

    ndogo, hata bila gharama za mambo yasiyo ya Shirikisho. Na

    gharama zote hizo kwa kweli zingebebwa na Tanganyika.

    Kwa hiyo ilitupasa tujiulize kwa nini tunataka kuibebesha Tanganyika

    gharama zote hizo; na hasa kwa nini tunataka Serikali ya

    Tanganyika? Hivi tuna hofu ya kwamba Tanganyika, bila kuwa na

    Serikali yake, itaonekana kuwa imemezwa na Zanzibar? Hofu yetu ni

  • 26

    kwamba tukiwa na Serikali Moja Tanganyika itaonekana kuwa

    imeimeza Zanzibar. Basi na tutafute muundo ambao utaiondolea

    Zanzibar hofu hii ya kumezwa, bila kuibebesha Tanganyika mzigo wa

    kuendesha Serikali mbili zenye uzito unaolingana.

    Hivyo ndivyo tulivyofanya, na hiyo ndiyo asili ya muundo wa

    Muungano wa Serikali Mbili. Badala ya kutungua mfumo uliopo

    kama wapumbavu, tulitazama hali halisi yetu ilivyokuwa na tukabuni

    mfumo utakaotufaa zaidi. ( uk.15 16).

    Mzee Abeid Amani Karume kwa upande wake aliielezea kwa ushupavu

    zaidi dhamira ya kuunda Muungano kwa kutumia neno la Kiingereza la

    Union ili kuziba mwanya wa kubabaisha na shirikisho. Katika hotuba yake

    ya maadhimisho ya miaka 40 ya Muungano, Rais Mkapa alimnukuu Mzee

    Karume kutokana na hotuba yake maarufu aliyoitoa siku za mwanzoni za

    Muungano ambayo husikika sana katika redio. Katika nukuu hiyo Mzee

    Karume alitamka yafuatayo:-

    Leo tumekuja kuonana na nyinyi wananchi wote. Na ikiwezekana

    kuusia mambo. Sababu baadhi ya watu wengi, wanataka kufahamu

    (kuhakikishiwa kwamba) Serikali ya Unguja (kwa maana ya

    Zanzibar) na Serikali ya Tanganyika zimechanganyika, zimekuwa

    Union moja tu.

    Kwa hivyo, ni dhahiri kabisa kwamba walipoamua muundo huo wa

    Muungano walikuwa wanajua walichokuwa wanakifanya na walichokuwa

    wanakitaka. Na wala haina maana kwamba labda walipoamua muundo huo

  • 27

    walidhani hautokuwa na matatizo. Matatizo walijua yatakuwepo lakini

    waliamua kwa makusudi wakabiliane nayo ndani ya Muungano badala ya

    kusubiri yamalizike kwanza ndio waunganishe nchi. Ukweli huo

    unadhihirishwa katika kitabu cha ASP cha Maendeleo ya Mapinduzi ya

    Afro-Shirazi Party 1964 1974 kama ifuatavyo:-

    Nchi mbili huru, kama zilivyokuwa Zanzibar na Tanganyika,

    zinapoungana, kuna njia mbili za kuunganisha. Njia ya kwanza ni

    kuungana kwa yale wanayokubaliana, hata yakiwa ni machache,

    madamu tu nia ipo, ni kuitekeleza ile nia na halafu zikaendelea

    kutanzua matatizo yao na kujenga juu ya ile nia iliyokwisha

    kutekelezwa. Njia ya pili ni kukaa na kutanzua matatizo kwa

    makubaliano mpaka kifikilie kima cha makubaliano kiwezacho kuleta

    muungano. Zote hizi njia mbili si rahisi na kila moja ina matatizo

    yake yanayoweza kuchukua muda mrefu kutanzuliwa. Tanganyika na

    Zanzibar zilichukua njia ya kwanza, siyo kwamba ndiyo iliyokuwa

    rahisi, bali kwa sababu nchi mbili hizi zilikubaliana na kutekeleza nia

    yao ya kuungana na kutanzua matatizo yaliyosalia ya muungano huku

    zimo katika Muungano. (uk.33).

    Kwa hivyo, matatizo ambayo yamekuwa yakiukabili Muungano ambayo

    mengine yamefikia kuutia katika misukosuko mikubwa hayawezi yakawa ni

    kioja, kwani yalitabiriwa. Hata hivyo, kuendelea kuimarika kwa Muungano

    ndani ya mazingira ya matatizo hayo, ni kielelezo cha udhati wa nia ya

    kuungana na usahihi wa uamuzi wa kuteua muundo wa Serikali mbili.

  • 28

    Katika hotuba yake ya kihistoria iliyoimarisha hoja ya Muungano tarehe 26

    Aprili, 2004 kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 40 ya Muungano,

    Rais Mkapa alitoa majumuisho mazuri ya suala hili kama ifuatavyo:-

    Muungano wetu umefikisha miaka 40, na upo imara. Nguvu yake ni

    Watanzania wenyewe, wengi wao asilimia 84.8 wakiwa hawajui

    uraia mwingine isipokuwa Utanzania. Watanzania hawa waliozaliwa

    mwaka 1964 na kuendelea, ambao leo wana umri wa miaka 40 au

    chini zaidi, hawana uzoefu wa kuwa kitu kingine isipokuwa kuwa

    Watanzania.

    Na hawajui mfumo mwingine wa Muungano isipokuwa mfumo wa

    Serikali mbili, wenye manufaa mawili makubwa ambayo ni sehemu ya

    msingi wa Muungano wetu. Kwanza, mfumo huu unadhihirisha

    kuwa kweli sisi tumeungana, serikali yetu ni muungano, si

    shirikisho. Na, muungano ni imara kuliko shirikisho.

    Msingi wa pili ni madaraka kamili ya Zanzibar kwa mambo ambayo

    si ya muungano. Madaraka hayo yanasaidia kuhakikisha kuwa

    Zanzibar inahifadhi utambulisho wake na haimezwi na Tanzania

    Bara. Wapo wanaoamini kuwa mfumo huu hauna haiba nzuri; ati

    haupendezi. Kwao napenda kusema kuwa jambo muhimu kuliko yote

    katika msingi wa nyumba si sura yake, muhimu zaidi ni uimara wake.

    Na mimi nakuhakikishieni, Ndugu Wananchi, kuwa mfumo wa Serikali

    mbili ndicho chombo imara kilichotuvusha salama katika bahari ya

    miaka 40 iliyopita, na Inshallah, ndicho kitatuvusha salama katika

    miaka ijayo.

  • 29

    MISUKOSUKO ILIYOHIMILIWA NA MUUNGANO

    Kama ilivyokwishaelezewa, Muungano umeweza na unaendelea kuhimili

    misukosuko mingi. Misukosuko hiyo imekuwa ni changamoto

    inayouwezesha kujidhatiti zaidi, kwani kila unapoishinda changamoto moja,

    unaibuka imara zaidi. Hii ni kwa sababu changamoto hizo huwafanya

    wahusika, hasa Serikali zote mbili, kutoa ufafanuzi kusafisha upotoshaji

    unaotolewa au kuyafanyia kazi na kuyapatia ufumbuzi matatizo

    yanayojitokeza ambayo hutumiwa kuutia misukosuko Muungano.

    Awali, misukosuko ilijikita zaidi katika kuhoji uhalali wa Muungano

    wenyewe. Baadae, baada ya shaka kuondolewa kuhusu uhalali wake,

    misukosuko imeelekea zaidi katika kuhoji muundo wa Serikali mbili.

    Kuhoji Muungano Wenyewe

    Hoja ya kwamba Muungano haukuwa halali kwa sababu eti haukupata

    ridhaa ya wananchi na haukukamilisha taratibu za kisheria zilianza kusikika

    hadharani Zanzibar mwanzoni mwa miaka ya themanini. Seif Sharif Hamad

    na wenzake ambao baadae walikiri kuwa walikuwa wapinzani ndani ya

    CCM na Serikali, waliitumia fursa iliyotolewa kwa nia njema na CCM ya

    kuanzisha mjadala wa kitaifa wa marekebisho ya Katiba kutaka kuudhofisha

    au hata kuuvunja Muungano. Watu hao hao ni wale wale ambao baada ya

    kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi waliunda chama chao cha CUF

    katika miaka ya tisini.

  • 30

    Kipindi hicho cha msukosuko wa kwanza mkubwa kuutikisa Muungano

    kilikuwa baina ya 1983 na 1984 na kinajulikana kwa umaarufu wa

    kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar. Madai yaliyokuwa

    yameshika nguvu wakati huo ni ya kudai kura ya maoni ya wananchi ili eti

    kuupa uhalali Muungano huo na kukamilisha hatua za kisheria.

    Imekwishaelezewa kwa kina katika sehemu ya Nguzo za Muungano jinsi

    Muungano ulivyo na uhalali unaotokana na watu wenyewe, na kwamba

    umekidhi matakwa ya sheria.

    Mtazamo wa CCM kuhusu kura za maoni ni kwamba si jambo la lazima na

    wala si njia pekee ya kupima utashi wa wananchi. Hadi wakati Tanganyika

    na Zanzibar zinaungana hakukuwa na nchi duniani zilizokuwa zimeungana

    baada ya kuitishwa kura za maoni. Miungano mikubwa mikubwa iliyodumu

    na iliyo madhubuti kabisa kama ile ya Marekani (USA) na Uingereza (UK)

    haikuanzishwa kwa kura za maoni. Na wala hadi leo haikupigiwa kura za

    maoni za kuithibitisha. Kinyume chake,Marekani iliwahi kuingia katika vita

    vya wenyewe kwa wenyewe kuulinda Muungano baada ya majimbo ya

    Kusini kutaka kujitoa. Wanaolalamikia Muungano hupenda kutaja mifano

    ya nje kuzipa nguvu hoja zao, lakini mifano hii ya Marekani na Uingereza

    hawaitaji katika muktadha huu. Kwa mazingira ya wakati ule na hasa

    kuzingatia usalama wa Mapinduzi ya Zanzibar, isingeweza kutumika njia

    nyengine zaidi ya iliyotumika. Hata hivyo, suala hili la kura ya maoni

    lilikuwa agenda kuu ya uchaguzi katika Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa

    1990 ambapo Dr. Salmin Amour alichaguliwa kuwa Rais wa tano wa

    Zanzibar. Uchaguzi huo uliambatana na kampeni kubwa ya chini kwa chini

    iliyowataka watu waususie hadi kwanza itapoitishwa kura ya maoni.

  • 31

    Inasadikiwa katika CCM kwamba kampeni hiyo iliongozwa na kundi la

    wanasiasa chini ya uongozi wa Seif Sharif Hamad waliokuwa wamefukuzwa

    kutoka CCM kwa sababu za usaliti. Ni watu hao hao ndio wanasadikiwa pia

    kuongoza kampeni ya chini kwa chini ya kutaka Sheikh Idris Abdul-Wakil

    apigiwe kura za HAPANA wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 1985.

    Kampeni zote hizo hazikufanikiwa. Kushindwa kwa kampeni ya 1990

    iliyotaka kura za maoni kuliidhoofisha kwa kiasi kikubwa hoja ya kwamba

    Muungano eti Wazanzibari hawakuwa wameuridhia. Kujitokeza kwa wingi

    kwa wananchi kupiga kura na kumchagua Dr. Salmin Amour ambae

    kampeni yake na ya CCM ilikuwa ya kupinga kura za maoni ulikuwa

    ushahidi wa kutosha kwamba Wazanzibari hawakuwa na tatizo na

    Muungano.

    Kwa upande wa uhalali wa kisheria, kitendawili kiliteguliwa na Tume ya

    Chama Kimoja au Vyama Vingi (maarufu Tume ya Nyalali) katika miaka ya

    tisini. Tume hiyo ilijiridhisha kwamba Baraza la Mapinduzi la Zanzibar

    likikaa kama Baraza la Kutunga Sheria, liliiridhia Hati ya Muungano kama

    lilivyofanya Bunge la Tanganyika, na hivyo kukamilisha taratibu za

    kisheria.Profesa Haroub Othman katika makala yake ya Forty Years of the

    Union: Is It Withering Away? naye kwa njia zake amejiridhisha hivyo.

    Ugunduzi huu ukawa umeimaliza kabisa hoja dhidi ya uhalali wa

    Muungano. Kilichoendelea kutokea baada ya wakati huo katika mjadala wa

    Muungano yakawa ni masuala ya muundo na kero za Muungano tu.

  • 32

    Kuhoji Muundo wa Serikali Mbili

    Baada ya uhalali wa Muungano kuthibitika bila ya chembe ya shaka, sasa

    hoja zimehamia kwenye muundo, labda na kero za Muungano.

    Kabla ya kuendelea na uchambuzi, kwanza tuwatazame hao wanaouandama

    Muungano, hasa upande wa Zanzibar. Vitimbi vya wasaliti wa Chama

    wakati wa Chaguzi Kuu za 1985 na 1990 vimekwishaelezwa. Lakini ni

    kundi hilo hilo ndilo lililokuwa mapema zaidi (mwaka 1984) limemfitini

    katika Chama (CCM) Rais wa pili wa Zanzibar, Sheikh Aboud Jumbe

    kwamba alikuwa anataka kuvunja Muungano kwa azma yake ya kutaka

    kupendekeza muundo wa Serikali tatu. Ni kutokana na fitina hizo ndio

    akalazimika kujiuzulu. Wakati huo walijifanya wapenzi wakubwa wa

    Muungano na wenye uchungu mkubwa nao. Lakini kufikia 1990, wakautilia

    shaka kiasi cha kutaka kuuitishia kura za maoni. Kufikia 1992, waliunda

    chama chao cha CUF na sera yao ya Muungano ikawa ya Serikali tatu. La

    kujiuliza ni jee, inakuwaje sera ya Serikali tatu ya Jumbe iwe ya

    kuvunja Muungano lakini sera ya Serikali tatu ya CUF isiwe ya

    kuvunja Muungano? Pamojawapo lazima pana unafiki. Ili kupabaini,

    tutazame historia kidogo.

    Kwamba muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilikuwa sera ya ASP toka

    wakati wa kudai uhuru, hapana ubishi. Sheikh Thabit Kombo amethibitisha

    hivyo kwa uwazi. Lakini kwa upande wa pili, inajulikana pia kwamba

    chama cha Hizbu kilikuwa kinaipinga vikali sera hiyo. Kauli mbiu ya

    chama hicho ilikuwa ASP itaiuza Zanzibar kwa Nyerere. Aidha, Hizbu

    ilijenga chuki dhidi ya watu wenye asili ya Bara na kuna wakati kwa

  • 33

    ushawishi wake, Sultani alitoa meli ya kuwarejesha kwao Wabara. Hata

    hivyo wito huo haukuitikiwa vyema kwani hao Wabara walijua kwamba

    Zanzibar walikuwa kwao.

    CCM inaamini kwamba waliokuja unda CUF wana mnasaba na Hizbu, na

    zaidi, CUF iliundwa kutokana na ushawishi wa waliokuwa viongozi wa

    Hizbu. Kama Hizbu haikutaka Muungano, hapawezi kuwa na taabu sana

    kuamini kwamba na CUF iliyochipua kutoka kisiki chake haijaukinai

    kikweli Muungano. Ikumbukwe kwamba Ilani ya Kwanza ya Uchaguzi ya

    CUF ilizungumzia kuirejesha Zanzibar ya zamani. Kwa hivyo, madai ya

    kura ya maoni na sera ya Serikali tatu ni visingizio tu vya kilaghai

    vinavyoficha nia ya CUF ya kuvunja Muungano. Halikadhalika, Wana-

    CCM wengi hawaamini kwamba ile fitina dhidi ya Jumbe waliyoifanya

    viongozi wa sasa wa CUF walipokuwa ndani ya CCM na Serikali ilikuwa

    kielelezo sahihi na cha kweli cha imani yao kwa Muungano.

    Ni kutokana na mtazamo huo ndio maana CCM inaamini kwamba CUF

    hawautaki Muungano, lakini maadam hawawezi kusema hivyo bayana

    kutokana na kuujua ukweli kwamba Muungano umekwishajikita ndani ya

    nyoyo za Wazanzibari na Watanzania kwa jumla walio wengi, jitihada

    wanazofanya ni kutafuta fursa za kuutia misukosuko kwa lengo la

    kuudhoofisha au hata kuuvunja. Ndio hizo kelele za kura ya maoni na sera

    ya Serikali tatu.

    Vyama vingine vya upinzani ambavyo nguvu zake ziko zaidi Bara navyo

    vina sera ya Serikali tatu. Lakini kwao wao Sera hii inaelekea kuchochewa

    zaidi na hasira tu ya Zanzibar kujiunga na OIC; hasira waliyoidaka kutokana

  • 34

    na kundi la Wabunge wa CCM (maarufu G 55) waliopeleka hoja Bungeni

    mwaka 1993 kutaka Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano. Hili

    litazungumziwa zaidi baadae. Sababu nyengine ya sera ya Serikali tatu kwa

    vyama hivyo pengine tu ni kuwa na kitu tofauti na CCM.

    CCM inaamini kwamba kuanzisha Shirikisho la Serikali Tatu kutoka

    Muungano wa Serikali Mbili ni kurejea nyuma na kuudhofisha Muungano.

    Tendo hilo litajenga mazingira ya hata kuuvunja kabisa Muungano. Maneno

    yafuatayo ya Mwalimu Nyerere yaliyomo katika Uongozi Wetu na Hatima

    ya Tanzania yanatoa kwa majumuisho ujumbe huo:-

    mimi nasema, ukifufua Tanganyika,utaua Tanzania. Fahali wawili

    hawakai zizi moja. Yeltsin wa Tanganyika ataua Tanzania. (uk. 6)

    Alipozungumzia Yeltsin, Mwalimu alikuwa akimaanisha jinsi Muungano

    wa Kisovieti ulivyosambaratika. Yeltsin alipoingia katika madaraka ya

    kuwa Rais wa Russia, Jamhuri iliyokuwa kubwa kuliko zote zilizokuwa

    ndani ya Muungano wa Kisovieti na akaamua kujitenga, Muungano huo

    ulisambaratika kwa urahisi tu. Hilo linaweza kutokea kwa urahisi pengine

    zaidi ya huo kama Tanganyika inafufuliwa na kuwa na Serikali yake na

    Serikali hiyo ikapata viongozi wasiotaka Muungano.

    Muungano wa Serikali Mbili Ulivyoweza Kuhimili Misukosuko

    Kama ilivyokwishaelezwa, Muungano, katika muundo wake huu wa Serikali

    mbili umeweza kuhimili misukosuko mingi na mikubwa, na kufaulu

  • 35

    majaribu kadha. Katika sehemu hii tutajaribu kubainisha misukosuko na

    majaribu hayo na jinsi Muungano ulivyoyashinda.

    Kuchafuka Kwa Hali ya Hewa ya Kisiasa Zanzibar (1982 1984)

    Mtikisiko uliopata Muungano katika kipindi hicho umekwishaelezewa.

    Itoshe tu kueleza kwamba baada ya malumbano makali na hoja za nguvu na

    jazba za kuhoji uhalali wa Muungano, Katiba za Zanzibar na Jamhuri ya

    Muungano zilifanyiwa marekebisho makubwa. Katiba ya Zanzibar ni kama

    iliandikwa upya (kutokana na ile ya 1979) ndiyo maana inaitwa Katiba ya

    1984. Katiba hiyo ilipanua upeo wa demokrasia Zanzibar na iliwiyanishwa

    vizuri zaidi na ile ya Jamhuri ili kupunguza migongano. Katiba ya Jamhuri

    nayo iliongezewa mambo katika orodha wa mambo ya Muungano ikiwa ni

    mwelekeo wa kuimarisha Muungano.

    Uchaguzi Mkuu wa 1990

    Kampeni ya chini kwa chini ya kuwataka Wazanzibari wasusie Uchaguzi

    Mkuu wa 1990 hadi iitishwe kura ya maoni kwanza, imekwishaelezewa.

    Itoshe tu kusisitiza kwamba Wazanzibari waliipuuza kampeni hiyo na

    wakajitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo na hivyo kuthibitisha imani

    yao kwa Muungano.

    Mjadala wa Mfumo wa Chama Kimoja Au Vingi (1991 1992)

    Kufuatia upepo wa mageuzi ya kisiasa uliokuwa unavuma Duniani wakati

    huo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliunda Tume ya

  • 36

    kuratibu maoni ya wananchi na hatimae kupendekeza kama Tanzania

    iendelee na Mfumo wa Chama Kimoja au iingie katika Mfumo wa Vyama

    Vingi. Tume hiyo imepata umaarufu wa Tume ya Nyalali kutokana na jina

    la Mwenyekiti wake.

    Katika kufanya kazi yake, Tume hiyo pia ilitaka na kupokea maoni ya

    wananchi kuhusu muundo wautakao wa Muungano.

    Kama inavyoeleweka, Tume ilipendekeza kwamba Tanzania iingie katika

    Mfumo wa Vyama Vingi pamoja na ukweli kwamba asilimia 80 ya

    wananchi waliotoa maoni yao walitaka Mfumo wa Chama Kimoja uendelee.

    Pendekezo hilo la Tume lilikubaliwa.

    Kuhusu suala la muundo wa Muungano, Tume ilipendekeza muundo wa

    Shirikisho la Serikali Tatu. Pendekezo hilo lilikataliwa na CCM na baadaye

    Bunge kwa sababu za kisera kama zilivyokwishaelezwa lakini pia kwa

    sababu haukupatikana kabisa ushahidi kwamba watu wenyewe waliutaka

    muundo huo.

    Kwa mujibu wa takwimu za Tume, ni Watanzania 49 (sawa na asilimia

    0.13) tu kati ya wote 36,279 waliotoa maoni yao ndio waliotaka muundo huo

    wa Serikali Tatu. Uchambuzi unaonekana katika Jedwali na. 3 hapo chini:

  • 37

    JEDWALI Na. 3: WATANZANIA WALIOTAKA MUUNDO WA

    SERIKALI TATU

    Washiriki Wote Waliotaka Asilimia

    Tanzania Bara 32,279 45 0.13

    Zanzibar 3,000 4 0.13

    Tanzania 36,299 49 0.13

    Chanzo: Kiambatanisho cha Tume ya Nyalali (Uk.i) (pamoja na makosa ya

    hesabu)

    Hakukuwa na maafikiano ndani ya Tume yenyewe kuhusu pendekezo hili

    kwani Wajumbe tisa walipinga na wakaandika maoni yao (dissenting

    opinion). Miongoni mwa hoja nyingi zenye uzito mkubwa za kukataa

    pendekezo hili walizotoa wajumbe hao, ilikuwamo ifuatayo:-

    Pamoja na kuelewa kuwa kwa baadhi ya mambo mengine ya kisiasa

    sio lazima uamuzi wake kutegemea wingi wa watoa maoni, lakini pia

    tunaona kuwa sio busara kupendekeza mabadiliko makubwa kama

    haya ya mfumo wa Muungano wetu kwa kutegemea maoni ya

    Watanzania 49 kati ya Watanzania 36,299 walioshiriki katika mjadala

    wote ulioendeshwa na Tume ya Rais. Idadi hii ni ndogo isio na uzito

    wa kitakwimu (statistically insignificant).

    Hoja hiyo pamoja na nyengine za wajumbe hao waliotofautiana na wenzao

    ziliwavutia Wabunge ambao kwa hivyo, walilikataa pendekezo la Serikali

    Tatu mwezi wa Aprili, 1992.

    Hoja ya G 55 (1993)

  • 38

    Baada ya uamuzi wa kuingia katika mfumo wa Vyama Vingi, ilibidi baadhi

    ya vifungu vya Katiba vihitaji marekebisho. Rais Ali Hassan Mwinyi,

    mwishoni mwa 1992, aliunda Kamati ya kupendekeza marekebisho hayo

    ikiwa chini ya Mwenyekiti wake Jaji Mark Bomani. Miongoni mwa mambo

    iliyotakiwa iyatazame ni namna ya kupata Makamu wa Rais katika mfumo

    wa vyama vingi ambao utafungua milango ya uwezekano wa Rais wa

    Jamhuri na yule wa Zanzibar kutoka vyama tofauti. Wakati huo wa mfumo

    wa Chama Kimoja, Rais wa Zanzibar alikuwa moja kwa moja Makamu wa

    Rais wa Jamhuri ya Muungano. Lakini ujio wa vyama vingi ulileta hofu ya

    uwezekano wa kuigawa Taasisi ya Rais (inayojumuisha Makamu wa Rais)

    katika itikadi zinazopingana ikitokezea Rais na Makamu wake kutoka

    vyama tofauti.

    Kamati hiyo ilipendekeza kwamba Makamu wa Rais apatikane kwa

    utaratibu wa Mgombea Mwenza ili kuhakikisha kuwa wote wanatoka chama

    kimoja. Pamoja na pendekezo jengine kwamba kama Rais anatoka upande

    mmoja wa Muungano, Makamu wa Rais atoke wa upande wa pili, utaratibu

    huu ulikuwa unamwondoa Rais wa Zanzibar katika Umakamu wa Rais wa

    Jamhuri.

    Zanzibar ilisita kulikubali pendekezo hilo kwa madai kwamba haliendani na

    dhamira ya makubaliano yaliyomo katika Hati ya Muungano ingawa baadae

    iliridhia lifikishwe Bungeni ambako lilipitishwa. Wakati mashauriano

    kuhusu suala hilo yakiendelea, Zanzibar ilijiunga na Umoja wa nchi za

    Kiislamu (OIC).

  • 39

    Ilikuwa katika mazingira hayo lilipoibuka kundi la Wabunge walioanzia 44

    hadi kufikia 55 waliowasilisha Bungeni hoja ya kutaka ianzishwe Serikali ya

    Tanganyika ndani ya Muungano, Agosti, 1993. Wabunge wote hao

    walikuwa wa CCM na wa kutoka Bara.

    Kabla ya hapo, mjadala kuhusu Muungano na muundo wake ulikuwa zaidi

    mkali Zanzibar. Makelele mengi dhidi ya Muungano yalisikika zaidi

    Zanzibar kuliko Tanzania Bara. Inaelekea dhahiri kwamba msimamo wa

    Zanzibar kuhusu Makamu wa Rais na OIC ndio uliochangia kwa kiasi

    kikubwa kuamsha hisia na hata hasira miongoni mwa Wabunge hao wa Bara

    na waliowaunga mkono. Uamuzi wa Zanzibar kujiunga na OIC ulihusishwa

    na kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa vile hoja

    yao ilipitishwa na Bunge, ni dhahiri kwamba Wabunge hao walipata

    uungwaji mkono mkubwa. Tukio hilo ndilo lililoupa Muungano mtikisiko

    wa kweli na mkubwa pengine kuliko yote ya kabla na baadae. Taifa

    lilikuwa katika hatari ya kweli ya kugawanyika na Muungano kuvunjika.

    Kipindi chote cha 1993-1994 kilikuwa kigumu sana kikihanikizwa na

    mijadala mikali mikali ndani ya Chama na Serikali na katika jamii. Azimio

    la Bunge ambalo dhahiri lilikuwa kinyume na sera ya CCM lilileta

    mtafaruku mkubwa ndani ya Chama.

    Baada ya mashauriano ya muda mrefu, Zanzibar ilijitoa katika OIC.

    Hatimae Chama kiliamua kufanya uhakiki wa mtazamo wa wanachama

    kuhusu muundo wa Muungano ili kujiridhisha kama kweli Wabunge

    walizisoma kwa usahihi hisia za wanachama au la. Tarehe 12 14

    Novemba, 1993, ulifanyika Mkutano Maalumu wa Pamoja kati ya

  • 40

    Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Wajumbe wa Kamati ya Wabunge wa

    CCM, Wajumbe wa Kamati ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa

    CCM, na Mawaziri wa Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya

    Zanzibar. Mkutano huo ulifanyika Dodoma.

    Mkutano huo uliamua kwamba kwa kuwa suala la kutazama upya Muundo

    wa Muungano linahusu Sera ya CCM, wana-CCM waulizwe juu ya suala

    hili na watoe maoni yao.

    Kura za maoni za siri za wana CCM zilipigwa nchi nzima mwezi Aprili,

    1994 na matokeo yalikuwa kama inavyoonekana katika Jedwali na. 4,5 na 6

    hapa chini:

    JEDWALI Na. 4: MATOKEO YA KURA ZA SIRI ZA WANA-CCM

    WA TANZANIA NZIMA

    Mtazamo Idadi Asilimia

    Waliotaka Serikali moja 394,157 29.21

    Waliotaka Serikali mbili 833,285 61.75

    Waliotaka Serikali tatu 112,934 8.37

    Kura zilizoharibika 9,115 0.67

    Jumla ya Wote walioshiriki 1,349,501 100.00

    Chanzo: CCM Makao Makuu

  • 41

    JEDWALI Na. 5: MATOKEO YA KURA ZA SIRI ZA WANA-CCM

    WA ZANZIBAR

    Mtazamo Idadi Asilimia

    Waliotaka Serikali moja 452 0.52

    Waliotaka Serikali mbili 85,175 98,78

    Waliotaka Serikali tatu 386 0.45

    Kura zilizoharibika 214 0.25

    Jumla ya Wote walioshiriki 86,227 100.00

    Chanzo: CCM Makao Makuu

    Jedwali Na. 6: MATOKEO YA KURA ZA SIRI ZA WANA-CCM WA

    TANZANIA BARA

    Mtazamo Idadi Asilimia

    Waliotaka Serikali moja 393,715 31.17

    Waliotaka Serikali mbili 748,110 59.22

    Waliotaka Serikali tatu 112,548 8.91

    Kura zilizoharibika 8,901 0.70

    Jumla ya Wote Walioshiriki 1,263,274 100.00

    Chanzo: CCM Makao Makuu

    Matokeo hayo yalionyesha kwamba asilimia 61.75 ya wanachama wote wa

    CCM walioshiriki katika kura hiyo ya maoni bado walikuwa na imani na

    sera ya Chama chao ya Serikali mbili, na hivyo kuithibitisha tena. Imani

    hiyo kwa upande wa Zanzibar ilikuwa kubwa zaidi (asilimia 98.78).

    Muundo wa Serikali Tatu waliotaka kuulazimisha Wabunge uliungwa

    mkono na asilimia 8.37 tu ya wanachama na ndio uliothibitika kukataliwa

  • 42

    kabisa na wanachama ambapo ulishindwa hata na ule wa Serikali Moja kwa

    pande zote mbili za Muungano.

    Baada ya kura hiyo ya maoni iliyothibitisha kwamba Wabunge walienda

    mchomo, Wabunge walilazimika kurudi kwenye mstari kwa kuifuta hoja

    yao Bungeni. Aidha, toka wakati huo, CCM ilianza kuhakikisha kwamba

    sera ya Muundo wa Serikali Mbili inaingizwa bayana katika Ilani zake za

    Uchaguzi. Kabla ya hapo, ilikuwa ikilichukulia tu kuwa ni jambo

    linaloeleweka.

    Kabla ya CCM kuamua kuendesha kura kwa wanachama wake tu

    zilikuwapo hoja kwamba kura ya maoni ilipaswa iwe ya wananchi wote.

    Mwalimu Nyerere aliijibu hoja hiyo kama ifuatavyo kama alivyojinukuu

    katika Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania:-

    Muundo wa Muungano, pamoja na kwamba hatutaki uwe ukitibuliwa

    tibuliwa mara kwa mara, ni suala la sera, si amri ya Mungu. Vyama

    vya siasa mbali mbali vinaweza vikawa na maoni mbali mbali kuhusu

    muundo unaofaa kwa katiba ya Nchi yetu. Muundo utakaokubaliwa

    na Wananchi walio wengi ndio utakaokuwa sehemu ya Katiba ya

    Nchi. Muundo wa Serikali mbili unakubaliwa na Wananchi, lakini

    unatokana na sera ya TANU na ASP na kwa sasa CCM. Maoni ya

    Wananchi yanaweza kukifanya Chama kibadili sera zake; lakini si

    lazima. Chama chochote kinaweza kubadili sera zake bila kutafuta

    kwanza maoni ya Wananchi. Siku ya Uchaguzi Mkuu maoni ya

    Wananchi yatajulikana. (uk. 29)

  • 43

    Uchaguzi Mkuu wa 1995

    Uchaguzi Mkuu wa 1995 ndio uliokuwa wa kwanza kufanyika ndani ya

    mfumo wa vyama vingi baada ya Uhuru na Mapinduzi. Vyama vyote vya

    upinzani viliendesha kampeni ya bidii kubwa ya kupinga muundo wa

    Serikali Mbili na viliwaahidi wananchi kwamba kama vitachaguliwa

    vitaanzisha muundo wa Serikali Tatu. Matokeo yake ni kwamba

    vilishindwa vibaya na huo ni ujumbe wa dhahiri kwamba sera ya Muundo

    wa Serikali Tatu ilikataliwa na wananchi. Badala yake, kwa ushindi

    mkubwa wa CCM, Muungano wa muundo wa Serikali Mbili ulithibitishwa

    tena na Watanzania.

    Kamati Ya Kuratibu Maoni Kuhusu Katiba (1999)

    Mwaka 1999, Serikali ya Jamhuri ya Muungano ilitoa waraka wa

    mapendekezo (white paper) kuhusu mambo mbali mbali iliyokuwa inafikiria

    kuyazingatia wakati wa marekebisho ya Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu wa

    2000. Rais aliunda Kamati ya Kuratibu maoni ya wananchi kuhusu

    mapendekezo ya Serikali yaliyokuwamo katika waraka huo. Kama kawaida,

    Kamati hiyo imepewa umaarufu wa Mwenyekiti wake, Jaji Kisanga.

    Suala la muundo wa Muungano kwa mara nyingine tena, lilikuwa miongoni

    mwa mambo yaliyotakiwa maoni ya wananchi. Lakini kwa mara nyingine

    tena, Watanzania walioshiriki kutoa maoni yao walithibitisha imani yao kwa

    muundo wa Serikali Mbili kwa kiwango cha asilimia 88.87, ambapo

    Zanzibar ilikuwa asilimia 96.25 na Bara asilimia 84.97. Muundo wa

    Serikali tatu ulipata asilimia 4.32 tu ambapo Zanzibar ilikuwa asilimia 3.48

  • 44

    na Bara asilimia 4.76. Jedwali Na. 7, 8 na 9 hapo chini zinatoa uchambuzi

    wa takwimu za matokeo hayo.

    JEDWALI Na. 7: MAONI YA WANANCHI WA TANZANIA

    KUHUSU MUUNDO WA MUUNGANO UNAOFAA

    Mtazamo Idadi Asilimia

    Waliotaka Serikali moja 4,326 6.54

    Waliotaka Serikali mbili 58,750 88.87

    Waliotaka Serikali tatu 2,855 4.32

    Waliotaka Miundo Mingineyo 174 0.26

    Wote walioshiriki 66,105 100.00

    Chanzo: Ripoti ya Kamati Ya Kisanga

    JEDWALI Na. 8: MAONI YA WANANCHI WA ZANZIBAR

    KUHUSU MUUNDO WA MUUNGANO UNAOFAA

    Mtazamo Idadi Asilimia

    Waliotaka Serikali moja 41 0.18

    Waliotaka Serikali mbili 22,017 96.25

    Waliotaka Serikali tatu 797 3.48

    Waliotaka Miundo Mingineyo 19 0.08

    Wote Walioshiriki 22,874 100.00

    Chanzo: Ripoti ya Kamati ya Kisanga

  • 45

    JEDWALI Na. 9: MAONI YA WANANCHI WA TANZANIA BARA

    KUHUSU MUUNDO WA MUUNGANO UNAOFAA

    Mtazamo Idadi Asilimia

    Waliotaka Serikali moja 44,285 9.91

    Waliotaka Serikali mbili 36,733 84.97

    Waliotaka Serikali tatu 2,058 4.76

    Waliotaka Miundo Mingine 155 0.36

    Wote Walioshiriki 43,231 100.00

    Chanzo: Ripoti ya Kamati ya Kisanga

    Kama ilivyofanya Tume ya Nyalali, Kamati hii nayo iliyaacha maoni ya

    wananchi na badala yake ikapendekeza Muundo wa Serikali Tatu kwa

    kutumia hoja za jazba na maneno mengi. Haishangazi kwamba na Kamati

    hii nayo ilikuwa na kikundi cha wajumbe wake walioandika maoni tofauti

    (dissenting opinion) kwa suala hili kama ilivyokuwa kwa Tume ya Nyalali.

    Pendekezo hilo la muundo wa Serikali Tatu lilikataliwa na Serikali.

    Uchaguzi Mkuu wa 2000

    Wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2000, Muungano wenye Muundo wa Serikali

    Mbili ulitiwa tena kwenye mtihani. Wapinzani waliuza tena sera ya Serikali

    Tatu na CCM iliendelea kuuza sera yake ya Serikali Mbili. CCM ilishinda

    kwa ushindi mkubwa zaidi kuliko hata ule wa 1995. Muungano ukapasi

    tena mtihani huu.

  • 46

    MAFANIKIO YA MUUNGANO

    Kama alivyosema Rais Mkapa kwenye kilele cha sherehe za kuadhimisha

    miaka 40 ya Muungano, kule kudumu hadi kufikia miaka 40, pakee ni

    mafanikio ya Muungano hata kama hakuna mafanikio mengine, hasa

    ikizingatiwa kwamba umeruka vihunzi vingi. Lakini yapo mafanikio

    mengine mengi ya msingi. Kwanza kurejesha na kudumisha umoja na

    udugu wa watu waliokuwa wametenganishwa na wakoloni ni mafanikio

    yasiyo kifani. Muungano umefanikiwa kuyalinda Mapinduzi ya Zanzibar na

    uhuru wa Tanganyika, na kuhakikisha amani na utulivu wa nchi. Hali hiyo

    imewezesha kushughulikia maendeleo ya kijamii na kiuchumi tunayoyafaidi

    hivi sasa. Muungano umesaidia kuharakisha kurejeshwa kwa demokrasia

    Zanzibar na umekuwa muhimili wa utulivu (stabilizing factor) kwa siasa za

    ndani za Zanzibar. Muungano umefungua milango ya fursa kwa wananchi

    kujiendeleza kiuchumi bila ya kujali upande gani wa Muungano mtu

    anatoka.

    Muungano umekuwa muhimili madhubuti wa umoja siyo wa Tanzania

    nzima tu, bali pia wa kila upande wa Muungano huo, yaani Tanzania Bara

    (Tanganyika) na Zanzibar. Katika Hotuba yake ya kihistoria ya tarehe 13

    Machi, 1995 kwenye mkutano wa waandishi wa habari Hoteli ya

    Kilimanjaro, Dar es Salaam wakati vumbi la hoja ya Tanganyika (ya G55)

    halijatulia vyema; hotuba ambayo imeandikwa katika kitabu cha Nyufa,

    Mwalimu Nyerere aliifafanua dhana hiyo kama ifuatavyo:-

    Watu wazima wamezungumza Muungano, kwamba tuuvunje au

    uendelee. Ilikuwa ipo hatari ya kuvunjika na wala haijaisha. Watu

  • 47

    wamezungumza Uzanzibari, baadhi ya viongozi wetu! Nadhani

    wengine wanafikiria hata kujitenga. Wapo, si wengi; lakini wapo.

    Kujitenga maana yake ni kuvunja nchi ivunjike tusiwe na nchi moja,

    tuwe na nchi mbili. Ni jambo linalozungumzwa. Tunataka kiongozi

    na viongozi watakaoelewa hivyo. Huku kuzungumza Uzanzibari si

    fahari. Si jambo la fahari. Hatima yake itavunjika Zanzibar. Mtu

    mwenye akili hawezi kufikiri anayeona Uzanzibari ni fahari ana akili.

    Hawezi akautukuza Uzanzibari kwa kujiita sisi Wazanzibar na wao

    Watanganyika.

    Sidhani kwamba Uzanzibari ule una usalama ndani yake. Hatima

    yake Zanzibar itajitenga; na Zanzibar ikijitenga kutokana na ule tu

    kuwa (sisi) Wazanzibari na wao Watanganyika, haibaki. Wakumbuke

    kwamba Muungano ndio unaowafanya wanasema sisi Wazanzibari

    wao Watanganyika. Nje ya Muungano, hawawezi kusema hivyo:

    kuna wao Wapemba na sisi Waunguja

    Watanganyika (nao) wakiwakataa Wazanzibari kwa tendo la dhambi

    ile ile ya sisi Watanganyika, wao Wazanzibari, wakautukuza usisi

    Tanganyika na, kwa ajili hiyo, wakawafukuza Wazanzibari,

    hawatabaki salama. Hapatakuwa na Tanganyika. Wakishajitenga tu,

    Wazanzibari wako kando hivi, mmewafukuza mnajidai wakubwa

    nyinyi: hawa nani hawa, wao wana Rais sisi hatuna kwa nini

    tusiwatimue?. Mkiwatimua mkabakia kwenu hapa, hambaki kweni

    mtasemaji? Mtakuwa mmeshatoa sababu ya kusema wale ni wao na

    nyinyi ni nyinyi, wao vipi Wazanzibari; halafu mbaki nyinyi?.

  • 48

    Maana kama leo wapo kabila la Wazanzibari, mmewabagua, mtaanza

    vijumba vya Wapemba, vipo vijumba vya Wapemba humu. Basi

    watakimbia Wapemba. Baadhi yao wamo waliokimbia wakati ulee

    wa zamani. Vijumba vya kwanza mtasema Wapemba Wapemba

    kama kwa sauti ya nyinyi mliokuwa mnajiita sisi Watanganyika

    mtakapoanza kuchoma nyumba za Wapemba. Mnazichoma moto zile,

    mtakuta eh! sisi wote si wamoja. Mbona za Wapemba tulizichoma

    moto za Wachaga hatuchomi kwa nini? Maana Wachaga si wazawa

    bwana! Hapa kuna wazawa, sasa mnachoma za Wapemba tu za

    Wachaga mnaacha? Mtakuta hakuna watu wanaitwa Watanganyika.

    Mtakuta mnajidanganya tu. Mnadhani kuna watu wanaitwa

    Watanganyika. Hakuna! Kuna Wagogo, Wanyamwezi, Wasukuma,

    Wazanaki, Wakuria, Wamwera eh, wengi sana siwezi kuwataja wote.

    Matakuta hakuna hiki kitu kizima kinaitwa sisi Watanganyika. (uk.

    9-12)

    Zaidi ya kuimarisha umoja wa ndani ya nchi, Muungano pia umelijengea

    heshima kubwa Taifa letu na unaendelea kudumisha shauku ya kujenga

    umoja wa Afrika.

    MATATIZO

    Wapinzani wa Muungano na hata wanaoutakia mema wanaweza

    kuorodhesha matatizo au kero nyingi kwa idadi, lakini nyingi yake zilikuwa

    zisizokuwa za msingi. Kero zimekuwapo, zipo na zitaendelea kuwapo.

    Zipo zinazopatiwa ufumbuzi, zipo zinazoshughulikiwa na zipo

    zitazoshughulikiwa kadiri zitavyojitokeza. Kero ni sehemu ya maisha.

  • 49

    Ukiiondoa hii inazuka nyingine. Kero ziko katika nchi zisizoungana, seuze

    zilizoungana kama yetu. Na kama ilivyokwishaelezewa, wakati Muungano

    unaundwa, matatizo yalitarajiwa kuwa yatakuwapo na yataendelea kwa

    muda mrefu. Na hata tungekuwa na muundo wa Serikali Tau au Moja,

    matatizo yangekuwapo tu ingawa ya sura tofauti.

    Kazi ya kuimarisha Muungano ni ya kudumu kama ilivyo kazi ya kujenga

    demokrasia. Haina mwisho. Waingereza walioungana toka karne ya 18

    bado hadi leo wamo katika kuimarisha. Seuze sisi wa miaka 40 tu.

    Kwa bahati nzuri, malumbano mengi yanayotokea hapa Tanzania juu ya

    Muungano na muundo wake aghlabu huwa zaidi baina ya viongozi wa

    Serikali na wa kisiasa, kuliko baina ya wananchi wenyewe.

    Hivi sasa kuna Muafaka wa Serikali zote mbili uliofikiwa kufuatia

    mapendekezo ya Kamati ya Wataalamu ya Kushughulikia matatizo ya

    Muungano (Kamati ya Shellukindo) ya 1992. Muafaka huo ambao

    unaendelea kutekelezwa hatua kwa hatua unatoa dira ya kuondoa kero za

    Muungano. Miongoni mwa hatua zilizokwisha chukuliwa hadi sasa kufuatia

    Muafaka huo ni Serikali ya Muungano kuipatia Serikali ya Mapinduzi ya

    Zanzibar asilimia 4.5 ya faida ya Benki Kuu na misaada ya nje; kuondoa

    paspoti kwa Watanzania kuingia Zanzibar; kutungwa kwa sheria moja ya

    Uraia; kuundwa kwa Tume ya Pamoja ya Fedha ambayo itashughulikia

    malalamiko yote yanayohusu uchumi na fedha, n.k.

    Pamoja na wingi wa kero zinazozungumzwa aghlabu kwa kutiwa chumvi na

    kwa jazba, ni heri kuzungumzia kero hizo kuliko kuzungumzia historia ya

  • 50

    muungano uliovunjika kama ambavyo pengine tungekuwa tunafanya hivi

    sasa kama tungekuwa na Muungano wa Serikali Tatu. Ni rahisi zaidi

    kuondoa kero kuliko kufufua muungano uliovunjika.

    HITIMISHO

    Imedhihirika katika hoja hii kwamba uhalali wa Muungano wa Tanzania

    hivi sasa si suala tena la mjadala. Mjadala uliohamishiwa kwenye kuhoji

    muundo wa Serikali Mbili nao unapungukiwa nguvu kutokana na wananchi

    walivyothibitisha imani yao kwa muundo huo kila walipoulizwa. Baada ya

    kukosa nguvu ya hoja, wapinzani wa muundo huo sasa wanategemea tu

    mbinu ya hoja ya nguvu; maneno mengi, makelele na jazba.

    Muungano wenye muundo wa Serikali mbili umefaulu mtihani wa nyakati

    (has stood the test of time) kwa kuhimili misukosuko mikubwa na kudumu

    kwa miaka 40 sasa, ukiwa mfano wa pekee Barani Afrika.

    Matatizo ya Muungano yanaweza kuwa kwa idadi kwenye orodha, lakini

    hayauzidi uzani wa mafanikio yake. Na mwelekeo uliopo ni kwamba

    mafanikio na uimara wa Muungano vinazidi kuongezeka wakati kero

    zinapungua.

    Chini ya mfumo wa vyama vingi, kila chama cha siasa kina haki ya kuwa na

    sera yake ya muundo wa Muungano na kuiwasilisha kwa wananchi. Kwa

    upande wa CCM, sera ya muundo wa Serikali Mbili inaendelea.

    MUNGU IBARIKI TANZANIA

  • 51

    REJEA

    A.S.P. (1974); Maendeleo ya Mapinduzi Ya Afro-Shirazi Party; Printpak

    Tanzania Ltd.; Dar es Salaam.

    CCM (1994); Taarifa ya Kura za Maoni Ya Wana-CCM Kuhusu Muundo

    Muafaka wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Taarifa

    isiyochapishwa.

    CCM (1998); Tathmini ya Miaka 20 ya CCM, 1977 1997; KIUTA;

    Dar es Salaam.

    Mapuri, O.R. (1996); The 1964 Revolution: Achievements and

    Prospects;TEMA Publishers; Dar es Salaam.

    Mkapa, B.W, (2004); Hotuba Ya Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa

    Tanzania, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, Kwenye

    Sherehe za Kuadhimisha Miaka 40 ya Muungano; Mpiga

    Chapa Mkuu wa Serikali; Dar es Salaam.

    Mdundo, Minael Hosanna O. (1999); Masimulizi ya Sheikh Thabit

    Kombo Jecha; DUP (1996) Ltd.; Dar es Salaam.

    Mwinyi, A.H. (1995); Hotuba ya Rais Ali Hassan Mwinyi Akiagana na

    Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mpiga Chapa

    Mkuu wa Serikali; Dar es Salaam.

  • 52

    Nyerere, J.K. (1968); Uhuru na Umoja; OUP; Dar es Salaam.

    Nyerere, J.K. (1994); Uongozi Wetu na Hatima Ya Tanzania; Zimbabwe.

    Publishing House; Harare

    Nyerere, J.K. (1995); Nyufa; Taasisi ya Mwalimu Nyerere; Dar es

    Salaam.

    Othman, Haroub (2004); Forty Years of The Union: Is It Withering

    Away?; Unpublished

    Serikali ya Tanzania (1991); Ripoti ya Tume Ya Nyalali Kuhusu Mfumo wa

    Vyama Vingi au Chama Kimoja; Mpiga Chapa Mkuu wa

    Serikali; Dar es Salaam.

    Serikali ya Tanzania (1999); Ripoti ya Kamati Ya Kuratibu Maoni Kuhusu

    Katiba (Kamati ya Kisanga); Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali;

    Dar es Salaam.

    Sherif, Abdul (1987); Slaves, Spices & ivory In Zanzibar; Tanzania.

    Publishing House, Dar es Salaam

    Shivji I.G. (1990); Tanzania The Legal Foundations of the Union;

    Dar es Salaam University Press; Dar es Salaam.