hotuba ya waziri wa afya, maendeleo ya jamii...

206
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _______ HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, MHE. UMMY ALLY MWALIMU (MB), KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2020/21 APRILI, 2020 DODOMA ___________________________________________________________________________ KIMEPIGWA CHAPA NA MPIGACHAPA MKUU WA SERIKALI, DODOMA - TANZANIA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Madaktari na Wataalam wengine wa Afya nchini wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Madaktari Kitaifa tarehe 20 Februari, 2020 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam ambapo alitoa nafasi za ajira kwa watumishi wa afya 1,000 katika mwendelezo wa jitihada za kuboresha huduma za afya nchini. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongozana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan tarehe 07 Machi, 2020 wakati wakikagua Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu ambapo ni utekelezaji wa ahadi za Serikali katika kuboresha huduma za Afya nchini. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akimuelekeza kitu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu tarehe 14 Aprili, 2019 wakati walipotembelea moja ya mabanda ya maonyesho wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Taifa wa magonjwa yasiyo ya kuambukizwa katika viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma.

Upload: others

Post on 01-Feb-2021

11 views

Category:

Documents


0 download