jarida la maadhimisho ya miaka 23 ya kituo cha … 23.pdf · 2017-11-23 · makala za jarida la...

36
JARIDA LA MAADHIMISHO YA MIAKA 23 YA KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR {ZLSC} YALIYOMO (i) Historia ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar. (ii) Utangulizi (iii) Malengo Makuu ya Kituo cha Huduma za sheria. (iv) Maadili ya Kituo. v) Kazi za Kituo. Kutoa Msaada wa Sheria. Kuwafundisha Wasaidizi wa Sheria. Kufundisha Sheria na Haki za Binadamu. Kusimamia Haki. Kukitangaza kituo na kazi zinazofanywa na kituo. Kutoa Majarida ya kituo. Kutoa Elimu ya Sheria kupitia Vipindi vya Tv na Redio. Huduma za Maktaba. Wanafunzi wanaokuja kituoni Zlsc kwa ajili ya Mafunzo kwa Vitendo. Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa Makundi mbali mbali. Uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya mwaka 2014. Mafunzo ya wafanyakazi wa ZLSC juu ya ufuatiliaji na Tathmini. Mafunzo ya Haki za Binadamu na Vyama vya wafanyakazi. Mikutano ya Elimu ya Katiba inayopendekezwa. Kituo na Jamii. Makala za Jarida la Mwaka wa 23 wa ZLSC juu ya safari yako na Kituo cha Huduma za Sheria.

Upload: vocong

Post on 30-Mar-2019

290 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

JARIDA LA MAADHIMISHO YA MIAKA 23 YA

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR

{ZLSC}

YALIYOMO

(i) Historia ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar.

(ii) Utangulizi

(iii) Malengo Makuu ya Kituo cha Huduma za sheria.

(iv) Maadili ya Kituo.

v) Kazi za Kituo.

Kutoa Msaada wa Sheria.

Kuwafundisha Wasaidizi wa Sheria.

Kufundisha Sheria na Haki za Binadamu.

Kusimamia Haki.

Kukitangaza kituo na kazi zinazofanywa na kituo.

Kutoa Majarida ya kituo.

Kutoa Elimu ya Sheria kupitia Vipindi vya Tv na Redio.

Huduma za Maktaba.

Wanafunzi wanaokuja kituoni Zlsc kwa ajili ya Mafunzo kwa Vitendo.

Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa Makundi mbali mbali.

Uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya mwaka 2014.

Mafunzo ya wafanyakazi wa ZLSC juu ya ufuatiliaji na Tathmini.

Mafunzo ya Haki za Binadamu na Vyama vya wafanyakazi.

Mikutano ya Elimu ya Katiba inayopendekezwa.

Kituo na Jamii.

Makala za Jarida la Mwaka wa 23 wa ZLSC juu ya safari yako na

Kituo cha Huduma za Sheria.

Bodi ya Wadhamini ndicho chombo cha juu cha maamuzi katika

utendaji wa kila siku wa Kituo cha Huduma za Sheria

Zanzibar.Kazi hiyo husaidiwa na Mkurugenzi wa Zlsc ambae ni

Katibu katika Vikao vya Bodi.Bodi ya wadhamini.Bodi ndicho

chombo cha juu chenye Mamlaka ya kuhakikisha

ufanisi,usimamizi pamoja na kuhakikisha mikakati ya kisera na

kiutendaji yote ya kituo imesimamiwa ipaswavyo ili kuhakikisha

malengo ya ofisi yanasimamiwa na kufikiwa kwa mafanikio

makubwa.

Bodi ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kabala ya hii

iliyopo sasa ilimjumuisha Profesa Haroub Othman,Mr.Hassan

Said Mzee na Bi.Fatma Maghimbi ambao walikiongoza kituo hadi

walipokamilisha mda wao.

Bodi kwa sasa inaongozwa na Profesa Chris Maina Peter,ambae

ni Profesa wa sheria,katika skuli ya sheria ya Chuo kikuu cha

Dar es Salaam,wakili wa Mahkama kuu ya Tanzania ambae ndie

Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ZLSC.

Yupo pia Bi.Josefrieda G.Pereira,Ambae ni Muhadhiri kutoka

Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Chukwani.

Bi.Salma Haji Saadat,ambae ametokea Jumuia ya Wanawake

wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA)

Nd.Daud Othman Kondo,ambae ametokea Wizara ya

Miundombinu na Mawasiliano.na

Bi.Harusi Miraji Mpatani ,Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za

Sheria Zanzibar na Wakili wa Mahkama kuu ya Zanzibar ambae

pia ni Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya ZLSC.

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar hadi kufikia mda huu

kinajumla ya wafanyakazi 28,ambapo kwa Upande wa Unguja ni

wafanyakazi 20 na Pemba 8 ambapo miongoni mwao ni Maafisa

Mipango 11madereva 2,wahasibu 3,Afisa ufuatiliaji na tathmini 1

,Afisa Habari 1,Masekretari 2,Afisa Tawala 1na Msaidizi wake

1,Mkutubi 1,Afisa Sheria 1, Wakili 1,Sekretari 2 na Afisa

Teknologia na Mawasiliano 1.

Ni jambo la kujivunia kwa Wanawake, Watoto , Walemavu na watu

wasiojiwerza pamoja na Wananchi wa Zanzibar wamekua wakipata

masaada wa sheria na utetezi wa haki za binadamu bila ya malipo kwa

muda wa miaka 23 kuanzia 1992-2015 kupitia Kituo cha Huduma za Sheria

Zanzibar.

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar (ZLSC) ni asasi isiyo ya Kiserikali,

iliyo huru, ya kujitolea isiyofungamana na upande wowote wa kisiasa, na

isiyozalisha faida iliyoanzishwa rasmi mnamo mwaka 1992 na kufanikiwa

kupata Cheti cha Kukubalika chini ya Sheria ya Kijamii ya mwaka 1995

(yaani ‘Act' No. 6 of 1995).

Kazi kuu ya Kituo ni kutoa msaada wa Kisheria bila ya malipo kwa wanyonge, wanawake, watoto, wanaoishi na ulemavu, na watu wengine

wasiokuwa na fursa katika jamii; kueneza elimu ya Sheria; na kutayarisha machapisho katika nyanja zote za Kisheria kwa ajili ya watu wa Zanzibar.

Kituo kinaongozwa na Dira ambayo inasisitiza Haki na upatikanaji wake kwa wote.

Katika kufikia malengo yake Kituo pia kimejiwekea Dhamira ya kutofungamana na Chama chochote cha siasa, isiyozalisha faida, na

inayojitolea kwa dhati katika kukuza uelewa wa watu katika masuala ya Kisheria, kuhamasisha Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Malengo makuu ya Kituo ni:- 1. Kutoa msaada wa Kisheria, usaidizi wa Kisheria, na huduma nyengine za Kisheria kwa jamii, hasahasa kwa wahitaji, na watu wasiokuwa na fursa

katika jamii.

2. Kuhamasisha, kutetea, kuheshimiwa, kuangaliwa Haki za Binadamu, Utawala wa Sheria, misingi ya Kidemokrasia, utamaduni wa amani na kuvumuliana.

3. Kutoa elimu ya Sheria na ya Haki za Binadamu kwa jamii kwa ajili ya kukuza uelewa wa watu kuhusiana na haki zao za msingi pamoja na wajibu

wao.

4. Kuandaa, kuratibu au kufanya tafiti kuhusiana na mambo ya sheria,

na kufanya ushauri ndani ya mambo yanayolingana na kazi za Kituo.

5. Kuandaa miradi ya kisayansi ya kuelimisha kwa ajili ya kufundisha watu,

mmojammoja au makundi, ambao wameorodheshwa kuwa ni miongoni mwa watu watakaopata faida kutokana na mawasiliano yaliyo thabiti ya matokeo ya tafiti. Na

6. Kusaidia taasisi nyenginezo na mtu mmojammoja ambao malengo yao ni ya kujitolea kwa maana halisi ya ‘kujitolea’ kama ilivyoelezwa katika Sheria

za Zanzibar

Maadili ya Kituo

Kutokana na Katiba ya Kituo, kila mtu atakayeshiriki katika harakati za Kituo atatakiwa kuyalinda maadili yafuatayo:

a. Kuonesha imani nzuri na ya hali ya juu, na uvumilivu kwa wengine katika mambo yote yanayohusiana na Kituo.

b. Kuonesha utendaji wa kuridhisha, uaminifu, uwazi, na uwajibikaji wa dhati kwa harakati za Kituo.

c. Mtu yoyote, hatoruhusiwa kutumia mali za Kituo, jina au ushawishi kujipatia faida ama za kibinafsi, au za kiurafiki, kidini, kikabila, au faida

zinazolingana ambazo zinakwenda kinyume na malengo ya Kituo. d. Mtu asiwe na tabia ya kufanya kazi kwa upendeleo.

Kazi za Kituo ni pamoja na:-

1. Kutoa Msaada wa Sheria

Huduma hii inakusudiwa kusaidia watu wasiojiweza katika jamii ambao hawana uwezo wa kulipia gharama za Mawakili binafsi. Huduma zinazotolewa zinahusiana na uvunjifu wa Haki za Binadamu, urithi wa mali

kwa jamaa wa marehemu, vurugu dhidi ya wanawake, unyanyasaji wa watoto, watu kufungwa kimakosa, ujabari wa Polisi, mashauri ya ajira na mengine mengi.

(Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bi.Harusi Miraji Mpatani Akiwasikiliza

wateja ikiwa ni miongoni mwa shughuli yake anayoipenda kuifanya pale anapopata fursa baada ya kupunguza Majukumu mengine ya Kiutawala)

(Bango hilo hapo juu ni miongoni mwa Bango lililovutia sana katika kuzipamba sherehe za

kuadhimisha mwaka wa 23 wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Mei 29,2015)

(Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bi.Harusi M.Mpatani wa mwanzo kushoto

akizungumza na wadau wa kituo katika kongamano la wadau wa kituo moja ya shughuli zilizopangwa katika kuadhimisha mwaka wa 23 tokea kuanzishwa kwa ZLSC katikati ni Mjumbe wa Bodi ZLSC Bi.Salma Saadat na mwisho ni Mratibu wa Kongamano la wadau wa Kituo Bi.Jina

Mwinyi waziri)

(Wanafunzi wakiwa wanapatiwa Mafunzo ya namna ya kuishi pamoja na kwa Upendo kupitia alama ya kopa lilikiashira Upendo ni miongoni mwa Mafunzo yatolewayo na ZLSC katika Mafunzo

ya Ulinzi kwa Mtoto picha kwa msaada wa Gabriel Mkama Afisa Mipango ZLSC)

2. Kuwafundisha Wasaidizi wa Sheria

Mpango huu unakusudiwa kundi maalum ambalo litatumika kueneza, kusambaza na kukuza uelewa wa sheria kwa wanajamii. Kwa kawaida, kundi hili hupewa mafunzo ya Sheria mara moja kwa kila mwezi ili

waweze kueneza elimu ya Sheria katika maeneo mbali mbali ambayo watu wanaishi.

(Mratibu wa Mafunzo ya wasaidizi wa Sheria ZLSC Bi.Jina Mwinyi Waziri akiwafundisha wasaidizi

wa Sheria juu ya Sheria ya watu wenye ulemavu katika Ukumbi wa ZLSC Migombani.)

3. Kufundisha Sheria na Haki za Binadamu

Malengo ya mafunzo haya ni kupata watu wengi itakavyowezekana, kuweza kufahamu alama za Kitaifa na Kimataifa kuhusu uvunjwaji wa Haki za Binadamu, viwango na utendaji wa kimataifa kuhusiana na

uangalizi wa kanuni za Haki za Binadamu. Nafasi maalum inatolewa kwa Polisi, Maafisa wa Vyuo vya Mafunzo, na asasi zisizo za Kiserikali za

Zanzibar,ambazo moja kwa moja zinafanya kazi pamoja na jamii ya watu na viongozi wao.

(Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdan Kh.Makame wa Pili kushoto akiwa katika Picha ya Pamoja na Maafisa wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi mara baada ya kufungua Rasmi Mafunzo

juu ya Umuhimu wa Jeshi la Polisi kulinda Haki za Binadamu wakati wa Operesheni zao mbali mbali za kikazi Anaefata kushotoni kwake ni Mkurugenzi Mtendaji ZLSC Bi.Harusi Miraji Mpatani kushoto kwa Mkurugenzi ni Mratibu wa Mafunzo hayo Bi.Jina Mwinyi na kulia kwa Kamishna ni

Mrakib wa Polisi Madema Ndugu Kitole)

(Mafunzo ya kulinda haki za Binadamu kwa Maofisa Polisi yalifanyika pia kwa Mikoa yote ya

Kipolisi kwa Upande wa Pemba Anaetoa hotuba ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba Sheihan Mohammed Sheihan kushoto kwa kamanda ni Mwanasheria kutoka Wilaya ya Chake

Chake Omar Mcha Hamza na anaefata kulia ni Mratibu wa ZLSC Pemba Bi.Fatma Kh.Hemed kulia mwa Bi.Fatma ni Afisa Mipango wa ZLSC Pemba Bi.Safia Saleh Sultan)

4. Kusimamia Haki

Kazi hii inawajumuisha watu mbalimbali wanaohusika na usimamizi wa

Haki katika nchi.

Kuna sheria nyingi katika nchi zinazowapa watu na taasisi

nguvu/mamlaka ambayo kwa njia moja au nyingine zinaathiri haki za raia, ni muhimu kuhakikisha kuwa nguvu au mamlaka haya hayatumiwi vibaya. Majaji na Mahakimu hawatakiwi kujuwa sheria za nchini tu, bali

hata vyombo vya kimataifa ambavyo Tanzania ni mwanachama.

Jaji Mkuu wa Zanzibar Mh.Omar Othman Makungu akiteta jambo na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Jaji Mshibe Ali Bakari na Pembeni ni Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Nd.Ibrahim Mzee Ibrahim katika Uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu ZLSC Migombani.

(Mafunzo ya Haki za Binadamu na Uchaguzi katika kuelekea Uchaguzi wa Katiba Inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu October 2015 katika Ukumbi wa ZLSC Migombani.Mbele ya Picha hii ni Maofisa kutoka Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC wakiwasilisha Muongozo uliotolewa

na ZEC katika kusimamia Elimu ya Uraia na Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa)

Picha ya pamoja ya wadau wa kituo mara baada ya Mkurugenzi Mtendaji na Mjumbe wa Bodi ya

Wadhamini kuwataka wadau hao waeleze Mapungufu ya kituo pamoja na mafanikio ya kituo katika kuadhimsha miaka 23 ya ZLSC.

5. Jarida la ‘Sheria na Haki’

Malengo makuu ya jarida hili ni kuwapasha habari watu waliokaribu na Kituo na jamii kwa ujumla kuhusiana na harakati za Kituo pamoja na

taarifa za Haki za Binadamu na matatizo ya Kisheria Zanzibar.

(Majarida mbali mbali ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar yanayotolewa kila baada ya miezi

3 kwa lengo la kutoa taaluma ya sheria mbali mbali kupitia Majarida hayo)

Vipindi vya Redio na Televisheni

Kituo kinatayarisha na kurusha vipindi vya dakika 30 kwa kushirikana na

Redio ya Sauti ya Tanzania Zanzibar na Televisheni. Vipindi vya redio

vinaitwa ‘Haki na Sheria’ wakati vile vya Televisheni vinaitwa ‘Ijuwe Sheria’. Vipindi hivi vinazungumzia sheria mbalimbali za nchi, muundo wa sheria,

utawala wa sheria, elimu ya uraia na Haki za Binadamu.

Moja ya vipindi vya Televisheni vilivyorushwa na ZBC TV katika kipindi cha Ijue Sheria ambapo Tulipata nafasi ya kuelimisha jamii juu ya Sheria Mpya ya Shirika la Taifa la Biashara Zanzibar

ZSTC Sheria nambari 2 ya 2014.Vipindi hivyo ni muendelezo wa elimu ya sheria mbali mbali zinazotolewa na ZLSC.Anaesalimiana na muendesha kipindi ni Mkurugenzi Fedha ZSTC Nd.Ismail Bai, katikati ni Mwanasheria wa ZSTC Nd.Ali Bilal na Mwendesha Kipindi ni Nd.Suleiman A.Salim

kutoka ZLSC.

7. Huduma za Maktaba

Kituo pia kinatoa huduma za maktaba ndani za ofisi zake mbili zilizopo Unguja na Pemba. Maktaba hizi zimesheheni sio tu vitabu vya sheria na

Haki za Binadamu, bali hata vitabu vyengine katika fani zisizokuwa za sheria. Machapisho haya huwasaidia wale wanaofanya kazi katika fani za sheria, wanaharakati wa Haki za Binadamu, na raia wa kawaida katika

kupata taarifa kuhusu sheria na Haki za Binadamu.

Jaji Mkuu wa Tanzania Nd.Mohammed Chande Othman wakati alipoitembelea Maktaba ya Kituo cha Huduma za Sheria wakati alipokuja katika Mahafali ya Pili ya Wasaidizi wa Sheria kushoto ni

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa kituo Prof.Chris Mainer Peter.

8. Mafunzo ya Vitendo kwa Wanafunzi

(Kutoka kushoto ni Zuwena Saleh Zubeir,Mohammed O.Kombo,Saleh M.Thabit,Haji Sungura Makame na Yumna Ali Mwinjuma wote hawa ni Wanafunzi wa Sheria na Social Work kutoka Chuo Kikuu Tunguu waliofika Ofisi zetu za ZLSC kwa Mafunzo ya Vitendo)

Pia Kituo kina kawaida ya kupokea na kuwapa mafunzo ya vitendo

wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini wanaomaliza mafunzo

yao.

shamra shamra za maadhimisho ya miaka 23 ya ZLSC

Kwa maksudi kituo kimeamua kuutumia mwezi wa Mei,2015 kufanya

shughuli mbalimbali ili kuwa miongoni mwa maadhimisho hayo;

(Picha ya kwanza kushoto ni washiriki mbali mbali waliojitokeza

katika Uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya Mwaka

2014.Picha ya pili ni Watendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria

Zanzibar walipokua katika picha ya pamoja walipojumuika katika

Dener ya kituo.Picha kwa msaada wa Afisa Habari ZLSC)

Picha ya kwanza kushoto ni Mkurugenzi kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC akiwa pamoja na Afisa Mipango wa kituo hicho Nd.Gabriel Mkama walipokua katika kipindi cha Live Redio Hits fm Mwandishi ni Zuhra Husein.Picha ya Pili ni watoto wa skuli za Maandalizi Kaskazini Unguja

walipopatiwa Mafunzo ya kujilinda na vitendo vya udhalilishaji katika chuo cha Amali Mkokotoni.

(Picha ya kwanza ni Afisa Habari ZLSC wa mwanzo kushoto Nd.Suleiman A.Salim ,akifuatiwa na

Afisa Mipango Bi.Jina Mwinyi Waziri,kulia ni Bi.Farhat Rashid na katikati ni Mtangazaji wa Bomba fm Redio Nd.Mohd waliposhiriki katika kipindi cha Live Redio kituo hicho.Picha ya Pili ni Mratibu

wa ZLSC Pemba Bi.Fatma Kh.Hemed wa Pili kulia akiwa na timu ya watendaji wa ZLSC Pemba walipoenda kuwatembelea wagonjwa Hospitali ya Chake Chake na kuwafariji)

Mafunzo ya haki za binadamu kwa makundi mbalimbali ya jamii ya

Zanzibar ikiwemo

Mafunzo kwa watu wenye Ulemavu

Jumla ya washiriki 40 kutoka jumuia mbalimbali za watu wenye ulemavu

walipatiwa mafunzo ya haki za Binadamu . Mafunzo hayo yalikua na lengo

la kuwaelewasha wanachama mbalimbali kutoka asisi zinazoshughulikia

ulinzi na utetezi wa haki za watu wenye ulemavu. Mafunzo hayo yalifanyika

katika ukumbi wa kituo cha ZLSC Chake Chake Pemba na yalifunguliwa na

Mratibu wa Kituo kwa Pemba Bi.Fatma Kh.Hemed ambapo aliwaeleza

washiriki hao kwamba lengo kuu ni kuadhimisha miaka 23 ya Kituo cha

Huduma za Sheria tokea kuasisiwa mwaka 1992.

Mwanasheria Mohd Ali Maalim kutoka Wizara ya Sheria na Katiba Pemba akitoa mada juu ya watu wenye ulemavu katika Mafunzo ya Haki za Binadamu na kundi la watu wenye ulemavu

katika ukumbi wa ZLSC.Chake Chake Pemba.

Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa Watu wanaoishi na virusi vya

Ukimwi

Kwa mara ya kwanza Kituo kwa kushirikiana na Tume ya UKIMWI Zanzibar

(ZAC) kimefanya mafunzo ya haki za binadamu na sheria ya watu wanaoishi

na virusi vya Ukimwi Zanzibar Nambari 11/2015. Mafunzo hayo

yaliwajumisha watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI 39 wakiwemo

wanawake 26 na wanaume 13.wakiwemo wanawake 29 na wanaume 11 kwa

upande wa Pemba.

Washiriki walipata nafasi ya kukitambua Kituo na kuomba kuendeleza

mashirikiano na utetezi kwa watu hao kwani wanakumbana na matatizo

mengi ya unyanyapaa katika jamii ya Zanzibar.

Dr.Sihaba Saadat wa Tume ya Ukimwi Zanzibar (ZAC) akiwasilisha mada katika Mafunzo ya watu

wanaoishi na virusi vya Ukimwi VVU Yaliyoandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria ZLSC kwa ushirikiano na Tume ya Ukimwi Zanzibar.

Washiriki kutoka ZAPHA +PEMBA wakiwa katika picha ya Pamoja na Mratibu wa ZLSC Bi.Fatma

Kh.Hemed na Wanasheria wa Kituo cha Huduma za Sheria wakati wa Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa watu wanaoishi na VVU.

Mafunzo ya Elimu ya uraia kwa walimu wa Sekondari wa Somo la Uraia.

Walimu wapatao 50 wakiwemo wanawake kutoka Mikoa mitatu ya Unguja

wameendelea kupata elimu na taaluma ya jinsi ya kufundisha mada

zilizomo katika mtaala wa somo ya Uraia kwa Sekondari. Mada mbalimbali

ziliwasilishwa zikiwemo Misingi ya Haki za Binadamu Kimataifa, Kikanda na

Kitaifa , Demokrasia ,Usalama Barabarani,Serikali ya Tanzania,Wajibu wa

Raia,Tabia Njema na utayari wakati wa kufanya maamuzi,Usawa kati ya

wanawake na wanaume na Elimu ya stadi za Maisha.

Walimu wa Mikoa Mitatu ya Zanzibar wanaofundisha somo la uraia walipopata nafasi ya Mafunzo juu ya Silibus ya somo la Uraia na Haki za Binadamu kama Mada hizo zilivyofafanuliwa kaika Somo

hilo wa Mtaala wa Sekondari.

Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa Waandishi wa Habari

Katika kuadhimisha miaka 23 kituo kiliandaa Mafunzo maalum kwa ajili ya

waandishi wa habari na wahariri wa vyombo ya habari vilivyopo Zanzibar

kwa lengo la kukitangaza kituo lakini pia kuwafahamisha waandishi juu ya

kutumia kalamu zao na midomo yao katika kulinda na kutetea haki za

binadamu Zanzibar. Jumla ya Waandishi 39 walipatiwa Mafunzo ambapo

Wanaume walikua ni 24 na Wanawake 15 kwa Upande wa Unguja wakati

kule Pemba jumla ya Waandishi wa Habari 36 walipigwa msasa juu ya Haki

za Binadamu ambapo Wanaume walikua14 na Wanawake 22.

(Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari kisiwani Pemba wakati walipopatiwa

Mafunzo ya Haki za Binadamu katika kuzitumia vyema kalamu zao zisijekusababisha uvunjifu wa haki za Binadamu katika Ukumbi wa ZLSC Chake Chake Pemba)

(Waandishi wa Habari wa Unguja wakipigwa msasa katika mada ya Haki za Binadamu na kazi za Uandishi wa Habari ili kuhakikisha waandishi hao wanazitumia vizuri kalamu zao na Midomo yao

wakati wakiripoti matukio mbali mbali katika vituo vyao vya Utangazaji ili wasijekusababisha uvunjifu wa haki za Binadamu)

Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa Jeshi la Polisi na Utambulisho wa

Wasaidizi wa Sheria

Kamanda wa Polisi Mkoa wa kaskazini Unguja Hassan Nassir akipokea Salut ya heshima wakati akikaribishwa katika Mafunzo ya Haki za Binadamu na Jeshi la Polisi kwa Mkoa wa kaskazini yaliyoandaliwa na ZLSC Anaeshuhudia Salut hiyo wa mwanzo kushoto ni Mkurugenzi wa ZLSC Bi.Harus Miraji Mpatani ,akifuatiwa na Mrakib wa Polisi Madema Ndugu Kitole na mwisho ni

Mratibu wa Mafunzo Bi.Jina Mwinyi Waziri )

Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja na Kaskazini Pemba ikiwa ni miongoni mwa kazi za kituo kuwaeleimisha wasimamizi hao wa sheria katika kuhakikisha

wanazilinda Haki za Binadamu katika kutekeleza Operesheni zao mbali mbali za kikazi.

(Mafunzo ya Haki za Binadamu kwa Jeshi la Polisi Zanzibar Mkoa wa Kusini Pemba na Kusini

Unguja katika Kuhakikisha kwamba Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kinawakumbusha Askari hao juu ya Umuhimu wa Kulinda Haki za Binadamu katika Majukumu yao)

Uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu 2014

Jaji Mkuu wa Zanzibar Mh.Omar Othman Makungu akizindua Ripoti ya Haki za Binadamu kwa Mwaka 2014 katika Sherehe zilizofanyika katika viwanja vya ZLSC Migombani wanaoshuhudia kwa Upande wa kushoto ni Nd.Thabit Abdulla Mwanasheria ZLSC,Bi.Salma Saadati Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ZLSC,Bi.Harusi M.Mpatani Mkurugenzi Mtendaji ZLSC na Nd.Ibrahim Mzee

Ibrahim Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar.

(Makundi mbali mbali ya wananchi,Asasi,na Wanafunzi walijitokeza katika uzinduzi wa Ripoti ya

Haki za Binadamu kwa mwaka 2014 uliofanyika katika Viwanja vya ZLSC Migombani Mnamo tarehe 21.Mei .2015)

Mafunzo ya kuwajengea uwezo Wafanyakazi wa ZLSC juu ya Ufuatiliaji

na Tathmini.

Mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa kituo kuhusu ufuatiliaji na

tathmini ambayo yaliandaliwa kwa wafanyakazi wa Kituo cha Huduma za

Sheria kwa Ofisi za Unguja na Pemba. Kwa upande wa Unguja mafunzo

hayo yalifanyika tarehe 17/05/2015, katika ukumbi wa ZLSC ambapo

Jumla ya wafanyakazi 14 akiwemo na Mjumbe mmoja wa bodi walishiriki

mafunzo. Pia kwa upande wa Pemba mafunzo kama hayo yalifanyika tarehe

27/05/2015 ambapo jumla ya wafanyakazi 7 na Mjumbe mmoja wa bodi

walishirki katika mafunzo. Lengo kuu ilikuwa ni kuwajengea uwezo

wafanyakazi katika masuala ya ufuatiliaji na tathmini ikiwemo masuala ya

uandishi wa Ripoti, ukusanyaji wa taarifa, namna ya kupima malengo kwa

kutumia viashiria na masuala yanayohusu uwasilishaji mzuri wa mada kwa

hadhira.

(Wafanyakazi wa Kituo cha Huduma za Sheria wakifatilia kwa karibu Mafunzo ya kuwajengea

uwezo yaliyoandaliwa na Afisa Ufuatiliaji na Tathmini wa ZLSC Nd.Mohammed Khatib Mohammed.)

Sheria za Kazi na Haki za Binadamu kwa Viongozi na Wanachama wa

Vyama vya Wafanyakazi

Kituo kinaamini kuwa ''Kazi Pekee ndio huzaa utajiri wa mali katuka jamii''

Kifungu cha 22(1) cha Katiba ya Zanzibar ya 1984.

Katika kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanazijua sheria za Kazi na wajibu

wao kwa mujibu wa sheria za Zanzibar Kituo wamefanya mafunzo ya sheria

za kazi kwa wanachama wa chama cha wafanyakazi ZUPHE( Chama cha

watoa Huduma na Afya) kwa tawi la Pemba. Jumla ya Wanachama 82

walipatiwa mafunzo hayo ambapo Wanaume ni 39 na Wanawake 42 .

(Mgeni Rasmi katika Ufunguzi wa Mafunzo ya wafanyakazi wa ZUPHE kisiwani Pemba Nd.

Bw. ZAHRAN MOH'D NAASOR akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo hayo kulia ni Mratib wa zlsc Pemba Bi.Fatma Kh.Hemed)

Elimu ya Katiba Inayooendekezwa

Katika moja ya mkakati wa kituo ni kuhakikisha jamii inakua na uwelewa

mpana juu ya elimu ya katiba pamoja na sheria mbali mbali za nchi.Katika

kulisimamia hilo kituo kimeweza kufanya Mikutano ya wazi katika Mikoa

yote Mitano ya Zanzibar juu ya Elimu ya Katiba inayopendekezwa Unguja na

Pemba.

(Mwanasheria Gabriel Mkama wa ZLSC na Mustafa Shariff wakiwafafanulia wananchi Jinzi Haki za Binadamu zilivyozingatiwa katika Katiba Inayopendekezwa wakati walipofika Bumbwini na Jimbo

la Mji Mkongwe kutoa Elimu ya Katiba Inayopendekezwa)

Kinamama wa kikiji cha Dunga Mkoa wa kusini Unguja waliojitokeza katika elimu ya katiba

inayopendekezwa iliyotolewa na Kituo cha Huduma za Sheria tarehe 15.05.2015

( Picha za hapo juu zinaonesha ushiriki wa Wananchi kutoka mikoa yote mitano ya Zanzibar Unguja na Pemba waliopatanafasi ya kuelemishwa juu ya Katiba Inayopendekezwa kupitia

Masheha wa Shehia husika kwa Mikoa hiyo Elimu iliyosimamiwa na Kituo cha Huduma za Sheria )

Vipindi vya kuelimisha Jamii na kutambulisha miaka 23 ya Kituo

Katika kujitangaza na kuielimisha jamii juu ya haki za binadamu na sheria

mbalimbali za Zanzibar kituo katika mwezi wa Mei mwaka 2013 pekee,

kiliweza kutembelea na kurikodi jumla ya vipindi 23 vya LIVE na vile vya

kurikodi .Aidha kituo kiliweza kujitangaza katika magazeti ya

Mwananchi,Zanzibar leo,Nipashe na Mtanzania ambapo waandishi wa vituo

vyote hivyo wamekua ni wadau wakubwa katika kukitangaza kituo.

(Picha zikionesha namna tunavyoshiriki katika vipindi vya tv na habari za Magazeti katika

kuwafikia Wananchi kihabari popote walipo katika visiwa hivi vya Unguja na Pemba)

Kituo na Jamii

(Katika kuadhimisha miaka 23 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kilikwenda kuwatembelea

wagonjwa katika wodi ya watoto Hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja na kwa Upande wa Pemba walikwenda kuwatembelea wagonjwa katika Hospitali ya Chake Chake na kituo cha Kulelea

watoto yatima Mabaoni Mkoa wa Kusini Pemba)

Safari yangu na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar

Bi.Harusi Miraji Mpatani.

Niliweza kukifahamu Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar nikiwa

mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar

University). Kilichonipeleka huko kutumia maktaba ya sheria baada ya

kupewa kazi na mwalimu. Ilikua mwaka 2014. Bahati nzuri nilifanikiwa

kupata vitabu lakini pia ilikua ni bahati ya kuonana na Profesa Haroub

Othman baada ya kutambulishwa na Mkutubi bi. ..................ili aweze

kunisaidia suala langu.

Professa Haroub alinisaidia sio tu kujibu suala langu bali pia alinipa

maneno ya kunitia moyo na kuengeza juhudi katika masomo yangu ya chuo

kikuu . Nakumbuka aliniazima Kitabu chake ili kinisaidie kwa masharti ya

kukirejesha wiki inayofuata. Baada ya kukirejesha sikurudi tena Kituoni ,

wakati huo kilikua wireless Kisiwandui.

Mwaka 2005 kwa kupitia Zanzibar Youth Forum nilichaguliwa kutoa elimu

ya Uraia na Upigaji kura katika Jimbo la Mjimkongwe chini ya usimamizi wa

Kituo.

Baada ya kumaliza Shahada yangu ya Sheria niliajiriwa na Kituo kama Afisa

mipango katika sehemu ya Maktaba. Nilifanya kazi hiyo huku nikisimamia

Dawati la Watoto Kituoni hapo chini ya ufandhili wa Shirika Save the

Children .

Mwaka 2011 nilifanikiwa kuwa Kaimu mkurugenzi na mwaka 2013

nilithibitishwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji.

Licha ya Changamoto katika sehemu ya kazi nimejifunza mengi katika

maisha ya Kituo cha Huduma za Sheria.

SULEIMAN A.SALIM

Ilikua ni mwaka 2010 mwezi wa saba nikiwa muajiriwa wa Kituo cha TV cha

Zanzibar wakati huo kikijuilikana Televisheni Zanzibar (TVZ ) ambapo Mkuu wa

Vipindi wa TVZ Hiji Shajak aliponiomba niwe muendeshaji wa kipindi cha Ijue

Sheria.

Kwa vile sikuwamwanagenzi na uendeshaji wa vipindi mbali mbali katika kituo

hicho cha matangazo ya TV nilikubali na kuanza kufanya vipindi hivyo.Niwe

Mkweli kabla ya kuendesha vipindi hivyo sikuwa na uwelewa wa kutosha

kuhusu huduma zitolewazo na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar.

Safari ya kutokea mwaka 2010 mpaka mwaka 2015 ni miaka 5 sasa wakati ule

nikiwa muajiriwa wa Televisheni Zanzibar na sasa mwaka 2015 nimekuwa

muajiriwa wa Kituo cha Huduma za Sheria katika nafasi ya Afisa Habari .

Awali nilikifahamu kituo kama taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na utoaji

wa msaada wa kisheria pekee ( legal Aid) lakini baada ya kushiriki vipindi mbali

mbali na shughuli mbali mbali zinazofanywa na kituo nimekuja kutambua

kwamba kumbe ile kazi ya kutoa msaada wa kisheria ni sehemu moja tu ya kazi

za kituo.

Kumbe kuna utitiri wa kazi zifanywazo na kituo hichi ikiwa ni pamoja na utoaji

wa machapisho mbali mbali ya kisheria kama vile Jarida la Kituo,Zanzibar

Yearbook of law,Ripoti ya Haki za Binadamu na Vijarida vyengine vidogo vidogo

vinavyochapishwa kwa shughuli mahsus.

Kuna sehemu kubwa ya utoaji wa taaluma ya sheria kwa ngazi ya cheti na hii

imekipa Kituo cha Huduma za Sheria sifa kubwa katika kuwasaidia wananchi wa

Zanzibar nafasi ya kuwa wasaidizi wa sheria katika maeneo yao waliyotoka pasi

na kuwa ni wenye Shahada za Sheria lakini wanafahamu kesi zote za Jinai na

Madai na wanauwezo wa kuzipokea na kuzifikisha panapostahili kwa ajili ya

hatua za upatikanakaji wa haki.

Hili si jambo dogo hata kidogo kwani kadiri kituo kinavyoendelea na utoaji wa

wasaidizi wa sheria hawa ndivyo idadi kubwa ya wananchi wasiojua sheria

inavyopungua na hatimae watu wataweza kudai haki na watatekeleza wajibu

baada ya kupata elimu ya sheria.

Kuna hili la utetezi wa haki mbali mbali za watoto ni eneo moja wapo ambalo

muda mrefu tunashuhudia kupitia vyombo mbali mbali vya habari kwamba

watoto wananyanyaswa, wanabakwa na kutumikishwa kupitia mradi wa

pamoja kati ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar (ZLSC) na Save the Chilren

kumekua na ufuatiliaji na tathmini katika maeneo kadhaa ya Zanzibar yenye

lengo la kupunguza na hatimae kulimaliza kabisa suala la udhalilishaji na

unyanyasaji wa mtoto.

Mwisho katika makala hii nizungumzie suala la ushiriki wa Kituo cha Huduma za

Sheria katika utoaji wa Elimu ya uraia na uangalizi wa chaguzi mbali mbali za

kitaifa na Kimataifa.Mfano mzuri ni Pale Kituo kilipotuma Mwangali wa

uchaguzi katika uchaguzi uliofanyika nchini Kenya mwaka 2013 lakini pia

chaguzi za hapa kwetu tumekua tukishiriki katika timu ya waangali wa ndani na

kutoa ripoti zetu juu ya chaguzi hizo.

Haya na mengine mengi ni miongoni mwa mafanikio makubwa ambayo Kituo

cha Huduma za Sheria Zanzibar kimeweza kuyafikia na kipokatika harakati za

kuyaendeleza kwa sasa na siku za baadae ni vyema kila Mtumishi miongoni

mwa waajiriwa wa kituo hichi akawa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba

kunapatikana mafaniko zaidi katika utendaji wa kila siku wa kituo hichi.

MAFANIKIO YA MIAKA 23 KWA MAKUNDI YANAYOANGALIWA NA KITUO

CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR

JINA MWINYI WAZIRI

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kiliazishwa mnamo mwaka 1992 na

watu watatu ambao ni Profesa Haroub Othman Miraji , Bi Ftma Magimbi na

Bwana Hassan Mzee. Ni moja ya Asasi isiyokuwa ya kiserikali ambayo ni ya

kujitolea, inayojitegemea na ni asasi ambayo si ya kibiashara. Lengo kuu la

Kituo ni kutoa huduma za sheria kwa watu wote wa Zanzibar wasiojiweza

wakiwemo;

1. Maskini 2. Wanawake 3. Watoto 4. Watu wenye ulemavu 5. Wazee.

Mafanikio na ufafanuzi kwa makundi haya ni kama

ifuatavyo:-

a. Maskini. Ndani ya miaka 23 Kituo kimeweza

kuwasiadia kisheria wananchi wengi walio masikini

kwa Unguja na Pemba, katika kazi hii wanacnhi walio

maskini wanashauriwa kisheria juu ya tatizo lolote la

kisheria ambalo linamkabidi, kama vile matatizo ya

Ardhi, ndoa, udhalilishaji na migogoro ya kazi .

Aidha kituo kiko mstari wa mbele kuwaandikia wananchi

hati mbalimbali za kisheria kama vile hati za Madai, majibu

ya Madai, hati za Viapo na Maombi ya Mahkama.

Ili kuifanikisha vyema kazi hii Kituo kimeajiri wasaidizi wa

sheria kuanzia mwaka 2007 hadi sasa katika majimbo yote

ya uchaguzi pamoja na vikosi vya serikali ya mapinduzi ya

Zanzibar. Kazi zao kubwa ni kuwasidia maskini wasio na

uwezo wa kutia mawakili mahakamani wanapopata matatizo

ya kisheria.

Ili kwenda sambamba na hili Kituo kila mwaka ifikapo

tarehe 13 Disemba kinaadhimisha siku ya Msaada wa

Kisheria kwa kuwafikia wanachi wa vijijini kuwapatia elimu

hii ya kisheria na ushauri wa kisheria.

b. Wanawake. Kituo kiko mstari wa mbele kuhakikisha

kuwa wanawake wanapata haki zao, katika kipindi cha

miaka 23 kimeweza kuwatetea wanawake mbalimbali

wanaovunjiwa haki zao.

Wazo la kituo kwa kuwapa kipaumbele wanawake ni kwa

sababu ya mila za kizanzibari kuwa wanawake wengi wana

aibu na kushindwa kutetea haki zao.

Kituo kinatekeleza vyema mkataba wa kimataifa wa kupinga

ubaguzi kwa wanawake na kinaadhimisha maadhimisho ya

kimataifa ya siku ya wanawake duniani kila ifikapo tarehe 8

Machi kwa makongamano na warsha pamoja na vipindi vya

redio na Televisheni.

c. Watoto. Watoto ni hazina muhimu sana katika jamii,

kituo kimeweka nafasi maalum kwa watoto ili kulinda

haki zao. Katika miaka 23 ya Kituo, Kituo kilishirikiana

na Shirika la Kimataifa la Save the Children pamoja na

Wizara ya Ustawi wa Jamii Wanawake na Watoto

kupatikana kwa sheria ya Mtoto nam. 6 ya 2011.

Aidha kituo kilikuwa mstari wa mbele kupatikana kwa

mahakama ya watoto Zanzibar ili kuwasimamia watoto

wote wenye mikinzano na sheria.

Ili kwenda sambamba na mkataba wa kimataifa wa watoto

kituo kinaadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika kila ifikapo

tarehe 16 Juni ya kila mwaka, na kuanzisha miradi

maalum inayohusu haki na wajibu wa mtoto kisheria.

d. Watu wenye Ulemavu. Hili ni kundi linalopata tabu

sana katika kuvunjiwa haki zao na jamii pamoja na

Serikali ikiwa moja kwamoja au si moja kwa moja.

Kituo katika miaka 23 kimefanya mafunzo mbalimbali ya

kwa watu wenye Ulemavu kuhusu sheria, mikataba ya

kimataifa na masuala ya haki za binadamu.

Aidha kituo kinashirikiana na taasisi mbali mbali

zinazohudumia watu wenye ulemavu ili kuweza kutetea

haki zao wenyewe.

e. Wazee. Kundi la mwisho linaloangaliwa na Kituo ni

wazee ambao hawawezi kufuatilia na kusimamia haki

zao. Katika kufanikisha hili Kituo kinawasaidia wazee

katika kupata haki zao za kisheria kwa kuwapa

mafunzo ya haki za binadamu na sheria.

Kwa miaka 23 tokea Kituo kuanzishwa kimefikia malengo

yake kwa wazanzibari walio wengi ingawa kuna

changamoto ndogondogo zinazozikabili Kituo.

SHAIRI LA KUTIMIZA MIAKA 23 YA MSAADA WA SHERIA

akika twakipongeza Kituo chetu muruwa

Kimedumu na kuweza Huduma nyingi kutowa

Kwingi kishajitangaza Watu wengi wakijuwa

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

rodha ya kazi zake Baadhi nawatajia

Kufanya itambulike Taaluma ya Sheria

Raia waelimike Haki zao kuzijua

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo

chetu.

akala za majarida Hutolewa kwa awamu

Mambo mengi ya faida Unayakutia humu

Kusoma hayana shida hupambwa na lugha

tamu

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

harama hapa haipo hulipi hata thumni

Msaada upewapo Lako kubwa shukrani

Lakini kwenye malipo Hudaiwi abadani

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo

chetu.

ndapo mtu kakwama hajui pa kuanzia

Kituo kinasimama Msaada kumpatia

Na endepo ni lazima Mahakamani kungia

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

atiba ya kufundisha Wasaidizi wa Sheria

Ili kwenda elimisha majimbo wanotokea

Hili limeshajiisha Umma kuwasaidia

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

H O

N

G

E R

idha kinashiriki Kwenye yake majukumu

Kuzielimisha haki Zote za kibinadamu

Watu wengi kwa malaki Wameshapata elimu

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

ao la Kituo hiki Ni Profesa Haroubu

Kwake aliona dhiki Jamii kupata tabu

Kwa watu kunyimwa haki Hakutaka awe bubu

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

eo tunashereheka Kukua Kituo chetu

Kimeshapata miaka Ni ishirini na tatu

Kote kinatambulika Hii ni fakhari yetu

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

ifa nyingi tuwapeni Viongozi wa Kituo

Ukweli wapo makini Kusaka mafanikio

Sote tunawaamini Kuleta maendeleo

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

hris Maina Peter Mwenyekiti madhubuti

Bi Harusi anafata Mkurugenzi thabiti

Mambo mengi mmeleta Hongera kazeni buti

Miaka ishirini na tatu Hongera Kituo chetu.

A

Z

L

S

C