kenyatta university institute of open learning€¦ · kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya...

119
1 DRAFT KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING ECT 313: MBINU ZA LUGHA NA FASIHI (KISWAHILI METHODS) VINCENT. F. KAWOYA CHARLOTTE. W. RYANGA.

Upload: others

Post on 30-Aug-2019

191 views

Category:

Documents


1 download

TRANSCRIPT

Page 1: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

1

DRAFT

KENYATTA UNIVERSITY

INSTITUTE OF OPEN LEARNING

ECT 313: MBINU ZA LUGHA NA FASIHI

(KISWAHILI METHODS)

VINCENT. F. KAWOYA

CHARLOTTE. W. RYANGA.

Page 2: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

2

UTANGULIZI.

Kiswahili ni miongoni mwa masomo ya lazima katika kiwango cha elimu ya msingi

na sekondari humu nchini. Ukweli huu unadhirihisha uzito unaopewa lugha hii katika

mfumo wa maisha humu nchini.

Mwongozo huu unalenga kutoa mapendekezo ya kuelekeza wanafunzi na wasomi

wengine katika misingi ya kufundisha Kiswahili kwa njia inayofaa katika mazingira

ambamo watapaswa kufundishia.

Mwalimu akifundisha akitumia mbinu zinazostahili, matokeo yake ni kwamba

wanafunzi watakuwa na hamu ya kujifunza na kujivunia Kiswahili, ambayo ni lugha ya

taifa na kimataifa.

Ikiwa baada ya kuusoma mwongozo huu msomaji atahisi kwamba umepungukiwa

katika sehemu fulani, anashauriwa asikate tamaa. Lazima hii iwe changamoto kwake

kufidia upungufu aliougundua.

Ni matumaini yetu kwamba mwongozo huu utachangia kuchochea watu

wanaojishughulisha na usambazaji wa Kiswahili ili waweze kubuni mbinu za kufundishia

ambazo zinajikita katika misingi madhubuti ya ufahamu wa mfumo wa lugha pamoja na

hali halisi ya Kiswahili.

Page 3: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

3

YALIYOMO.

SOMO La 1 Hadhi ya Kiswahili

1.1 Lugha ni Kitambulisho cha Ubinadamu…………………………………………5

1.2 Sera za Lugha…………………………………………………………………….6

1.3 Kiswahili Ulimwenguni………………………………………………………….7

1.4 Mikakati ya Usambazaji na Upanuzi wa Kiswahili……………………………...8

SOMO La 2. Maana na Sifa za Lugha.

2.1 Sifa za Lugha…………………………………………………………………...10

2.2 Kanuni za Kufundishia…………………………………………………………16

SOMO LA 3 Ufundishaji wa Lugha ya Pili

3.1 Mbinu ya Kimapokeo…………………………………………………………...19

3.2 Mbinu ya Moja kwa Moja………………………………………………………20

3.3 Mbinu ya Uzungumzi……………………………………………………………21

3.4 Mbinu ya Kimawasiliano………………………………………………………...21

3.5 Msingi wa Mbinu ya Kimawasiliano…………………………………………….23

SOMO LA 4 Maandalizi ya Mwalimu

4.1 Silabasi…………………………………………………………………………….25

4.2 Maazimio ya Kazi…………………………………………………………………27

4.3 Mpango wa Kipindi……………………………………………………………….33

SOMO LA 5. Kusikiliza na Kuongea.

5.1 Umuhimu wa Kusikiliza……………………………………………………………42

5.2 Kusikiliza kwa Ufahamu……………………………………………………………43

5.3 Vizuizi vya Ufahamu sikizi……………………………………………………… 44

5.4 Kufanikisha Ufahamu sikizi………………………………………………………..49

5.5 Umuhimu wa Kuongea……………………………………………………………. 52

5.6 Matatizo ya Kimatamshi……………………………………………………………53

5.7 Kufundisha Matamshi………………………………………………………………58

5.8 Kufundisha Kuongea……………………………………………………………….63

5.9 Njia za Kufundishia Mazungumzo………………………………………………...65

SOMO La 6 Kusoma na Kuandika.

6.1 Kusoma kwa Sauti…………………………………………………………………68

6.2 Matatizo ya Kusoma kwa Sauti……………………………………………………69

6.3 Kusoma Kimoyomoyo…………………………………………………………….71

6.4 Maswali ya Ufahamu………………………………………………………………72

6.5 Kuandika Ufupisho…………………………………………………………………74

6.6 Kuandika Imla……………………………………………………………………...76

6.7 Uandishi wa Insha………………………………………………………………….77

SOMO La 7. Sarufi na Matumizi ya Lugha

7.1 Matatizo ya Kimsamiati na Kisarufi……………………………………………….85

7.2 Uhusiano Kati ya Maneno…………………………………………………………89

Page 4: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

4

7.3 Kufundisha Msamiati………………………………………………………...90

7.4 Ujuzi wa Sarufi……………………………………………………………….97

7.5 Kufundisha Sarufi…………………………………………………………….98

SOMO La 8. Fasihi.

8.1 Dhana ya Fasihi…………………………………………………………….106

8.2 Dhima ya Fasihi…………………………………………………………….106

8.3 Mitazamo Tofauti ya Maana ya Fasihi……………………………………..107

8.4 Tanzu za Fasihi……………………………………………………………..109

8.5 Uchambuzi wa Fasihi……………………………………………………….115

MAREJEREO………………………………………………………………… 119

Page 5: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

5

SOMO 1

HADHI YA KISWAHILI NA SERA ZA ELIMU

1.0 Utangulizi

Mara nyingi mwalimu wa lugha anapofunza lugha huingilia moja kwa moja

visehemu vinavyoorodheshwa katika mtaala. Ni nadra mwalimu kuanza kwa kuwaelezea

wanafunzi umuhimu wa lugha hususa lugha ya Kiswahili, kando na kuwa somo la lazima

kwenye ratiba ya shule. Mwelekeo huu hausaidii mwanafunzi kuwa na motisha ama

msukumo wa kumpa matamanio ya kujifunza Kiswahili kwa bidii. Hali hii huendelezwa

na fikra za watu wengi kwamba Kiswahili hakisaidii mtu anayetafuta kazi kuajiriwa, kwa

ambavyo Kiingereza hutumika kwa mahojiano na mawasiliano ya kikazi maofisini. Hii ni

kwa mujibu wa kuwa hadi sasa Kiingereza ndiyo lugha inayotambulikana kuwa rasmi

nchini Kenya.

Ili mwalimu aweze kutayarisha wanafunzi waweze kupata ari ya kupata matokeo mazuri,

ni bora tangu awali kuwaeleza umuhimu wa lugha hii, kuifahamu na kuiongea vyema.

Kiswahili kina nafasi yake nchini Kenya kama lugha ya taifa na hivyo kurahisisha

mawasiliano katika hali ya wingi wa lugha; na vile vile kama lugha inayounganisha, na

kuyatambulisha mataifa ya Afrika Mashariki, na hivi sasa, lugha mojawapo mashuhuri ya

Umoja wa Mataifa ya bara la Afrika.

MADHUMUNI YA SOMO

Kufikia Mwisho wa somo hili, inatarajiwa kwamba utaweza:

Kutambua umuhimu wa Kiswahili

Kueleza maana na sera ya lugha

Kutambua umataifa wa Kiswahili

1.1 Lugha ni kitambulisho cha ubinadamu

Lugha imesemekana kuwa sifa ya kuwabainisha viumbe vingine na binadamu.

Hivyo lugha ni muhimu kwa mawasiliano baina ya makundi ya watu na miongoni mwa

binadamu. Lugha yoyote ile hutambulisha jamii inayoitumia, na kudhihirisha utamaduni

wake. Utamaduni hudhihirika kutokana na uwasilishaji wa itikadi mbalimbali, mila za

kijamii, matamanio ya jamii na kadhalika. Pia matumizi ya lugha katika jamii huleta

ukuruba wao na kuchochea umoja, katika matumizi yake kwenye midahalo ya kijamii.

Hivyo tunaposema lugha hufungamana na utamaduni wa jamii ni kusema kwamba lugha

inapata mantiki yake kutokana na hadhi za maisha ya jamii ile. Jambo hili ni muhimu

Page 6: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

6

kwa mwanafunzi kujua tangu mwanzo ili aweze kuelewa utata unaozingira Kiswahili

kama lugha ya taifa miongoni mwa makabila yenye lugha nyingi.

Tujuavyo, taifa moja linaweza kuwa na lugha nyingi. Nchini Kenya tuna takriban

lugha 45 , kulingana pengine na makabila yaliyomo. Kawaida kila lugha hujaribu

kujipendekeza ama kila kabila huwa na matamanio ya lugha yake kuwa lugha ya taifa.

Hizi ni hisia za kawaida na penye lugha nyingi, uchaguzi wa lugha zitakazotumika rasmi

lazima ufanywe kwa kituo na umakinifu, ili kuondoa hamaki na shinikizo za ukabila.

Aidha wanafunzi wafahamishwe kuwa ujuzi wa lugha hutambulika kwa uwezo wa

kuongea, kuiandika na kuisoma lugha hiyo.

1.2 Sera za lugha

Sera ni mfumo ama utaratibu fulani unaofuatwa katika kuchagua jambo fulani.

Kwa hivyo tunapozungumzia sera ya lugha tunamaanisha utaratibu unaoongoza uteuzi

wa lugha zitakazotumiwa kirasmi nchini. Sera ya lugha nchini Kenya ina historia ndefu

tangu enzi za ukoloni hadi leo. Sera zimeendelea kubadilika kulingana na mahitaji ya

nchi wakati baada ya wakati, kwa mfano, kufikia Tume ya Mackay 1981 alipokikweza

hadhi Kiswahili kufunzwa kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu. Jambo hili

lilisababishwa na ufahamu kuwa Kiswahili ni lugha muhimu. Kwa mujibu wa Ferguson

(1968), lugha muhimu ni ile iliyo na sifa zifuatazo:

1. Kwamba inaongewa na zaidi ya watu asilimia 25 wenyeji, ama na zaidi ya watu

milioni moja;

2. Kwamba ni lugha rasmi ya nchi

3. Kwamba ni lugha ya elimu ya zaidi ya asilimia 50 ya waliofuzu vyuo vya upili

nchini.

Kuna ithibati nyingi kuonyesha kuwa Kiswahili kimefikia sifa hizi. Fergurson

anaendelea kusema kwamba lugha huwa na hadhi maalumu nchini inapotumika katika

mojawapo ya njia hizi:

1. Kutumika kwa minajili ya mahubiri ya kidini

2. Kutumika kwa minajili ya kisomo

3. Kufunzwa kama somo mojawapo katika shule za upili

4. Kutumika kama lugha ya mawasiliano na watu wengi nchini

5. Kutumika katika utendakazi wa kundi moja la watu nchini

Kulingana na vidokezo hivi vya Fergurson, umashuhuri wa Kiswahili hautiliwi

tashwishi kamwe. Kiswahili kimechangia ujenzi wa taifa pakubwa. Pamoja na kufunzwa

shule, kimechangia maarifa ya kuchambua na kuelewa nyenzo za kudumisha jamii

kuyatawala mazingira yake. Tena, kimewakweza watu na kuwaingiza katika utamaduni

wa kisasa kwa ukubalifu wake katika matumizi ya kiteknolojia hivi majuzi.

Sera hizi za lugha zimeongozwa na mabadiliko mengi ya mifumo ya kisiasa.

Pamoja na mifumo ya kisiasa pengine tungesema kwamba sera hizi zingejumuisha

matamanio ya jamii ya kutaka kuhusishwa katika ujenzi, utawala wa nchi na maendeleo

ya kiuchumi. Kwa mfano hadi sasa kufanywa kwa Kiswahili lugha ya taifa kumewasaidia

wengi wasio na kisomo rasmi kujihusisha na maendeleo nchini kwa kuweza kuchangia

katika mijadala iliyopo kwa lugha wanayoifahamu – Kiswahili. Wanafunzi waelezwe

Page 7: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

7

wazi kwamba kufunzwa kwa Kiswahili katika viwango vyote vya shule, huleta

utangamano miongoni mwa makabila tofauti kwa kujumuisha utamaduni wa Mwafrika.

1.3 Kiswahili ulimwenguni

Ni muhimu kuwafahamisha wanafunzi jinsi Kiswahili kilivyoenea ulimwenguni

katika nyanja zote za maisha. Sasa kinafunzwa katika vyuo vikuu mbalimbali huko

ulaya, kwa mfano, nchini Uingereza, SOAS (School of Oriental and African Studies),

Chuo cha Gent Ubelgiji, nchini Ujerumani, huko Marekani

Hadhi ya Kiswahili imeendelea kuimarika kuambatana na historia ya Kiswahili.

Kiswahili kimeendelea kupanuka katika msamiati na hali ya matumizi yake kiasi cha

kuweza kutumika katika ufunzaji wa mitaala tofauti na katika utafiti pia. Ukuaji wa hadhi

umesaidiwa na sera mbalimbali za elimu na lugha nchini Afrika Mashariki, hasa

Tanzania na Kenya.

Kufikia karne hii ya ishirini na moja, lugha ya Kiswahili imefahamika

ulimwenguni kote. Inasemekana kwamba Kiswahili sasa ni miongoni mwa lugha saba

ulimwenguni, zinazotambulikana na Umoja wa Mataifa (UN). Lugha maarufu nyinginezo

ni pamoja na Kifransa, Kirusi, Kihispanyola, Kichina, Kiarabu na Kiingereza.

Kuambatana na matumizi ya kimataifa, Kiingereza hutumiwa na mataifa 92, kama lugha

ya pekee iliyotumika katika mikutano ya kimataifa kwa muda mrefu. Matumizi haya

yanalingana na nyakati za historia, Uingereza ilipotawala koloni nyingi ulimwenguni.

Kifransa kilifuatia kikiongewa katika mataifa 31. Nyenzo zake za kikoloni zafahamika

kihistoria.

Lugha ya tatu kwa upana wa matumizi ni Kihispanyola, kikitumika kwenye

mataifa 21; Kihispanyola kilifuatwa na Kiarabu, kilichowahi kutumika miongoni mwa

mataifa 18. Upana huu wa matumizi ni kwa ajili ya Bara Arabu na mkondo wote wa nchi

za kasikazini mwa Afrika , ambako Kiarabu kimechukua nafasi ya lugha nyinginezo

asilia za nchi hizo kama Kimisri. Lugha ya Wamisri wa jadi ilipotea kabisa na Kiarabu

kuchukua nafasi yake. Pengine haya yalitokea wakati wa vita vya Jihadi, vya

kuwasilimisha ‘makafiri” kama walivyojulikana wasiokuwa Waislamu. Baada ya

Kiarabu, lugha nyingine ni Kichina kinachotumika katika mataifa 2, na Kirusi katika taifa

1 tu. Takwimu hizi ni kulingana na The World Almanac and Book of Facts (1983). Ni

jambo la kujivunia kwamba Kiswahili kimejiunga na mataifa haya, ijapo matumizi yake

yamesambaa miongoni mwa mataifa mengi Barani Afrika na hata Ulaya na Marekani.

Ambapo nyingi za lugha zilizotajwa zilikuwa za mababe wa ukoloni, lugha ngeni,

hivyo kusambazwa kwa msukumo wa utawala huu barani Afrika, Kiswahili kinyume cha

hayo, kilijipendekeza chenyewe kwa watumizi wake. Ni kweli kwamba enzi za ukoloni

Kiswahili kilitumiwa kwa utawala, lakini ni lugha iliyopatikana Afrika Mashariki na

kukubalika moja kwa moja kama mojawapo ya lugha nyinginezo za Kiafrika.

Ni muhimu tufahamu kwamba kutambulikana kwa lugha yo yote ulimwenguni si

jambo dogo. Kuchaguliwa kwa Kiswahili kama lugha mojawapo ya ulimwengu

hakukutokea tu hivi ghafla bin vu. Mataifa ya Kiafrika barani humu tayari walikuwa

wamekitambua kuwa lugha mashuhuri inayoweza kutumika kwa manufaa ya mataifa

yote, wala tu si Afrika Mashariki kulikochimbuka lugha hii. Viongozi wa Umoja wa

Mataifa Barani Afrika walitambua yafuatayo:

(1) Jinsi kilivyowasaidia wakoloni kuleta umoja miongoni mwa wale waliowatawala,

hivyo wakayaona manufaa yake katika kuwaunganisha watu;

Page 8: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

8

(2) Kwamba lugha hii haikujikita katika uhasama wa kikabila, kwa ambavyo matumizi

yake yameenea kote, na kuwa lugha ya taifa nchini Kenya na Tanzania, ukubalifu

huu ukapanua mipaka yake zaidi ya ile ya kikabila;

(3) Kwamba kunawiri kwa biashara miongoni mwa mataifa ya Afrika Mashariki na

Kati kumebainika kwa sababu ya matumizi ya Kiswahili, katika maingiliano ya

Wanyarwanda, Warundi, Waganda, Watanzania, Wakenya na Wakongo.

Hivi karibuni Kiswahili kimechaguliwa na mataifa ya Kiafrika, katika vikao vya

Umoja wa Mataifa (AU) kuwa lugha rasmi mojawapo zitakazotumiwa katika

mawasiliano Barani Afrika. Tayari Kiswahili nchini Kongo ni mojawapo ya lugha nne

zilizochaguliwa kuwa za taifa miongoni mwa zaidi ya lugha takriban mia mbili

zinazozungumzwa nchini humo. Sababu tatu zajitokeza kuhusu kukubalika kwa

Kiswahili:

1) Urahisi wake wa maongezi,

2) Kusambaa kwake na,

3) Ukwasi pamoja na utamaduni wake wa kifasihi miongoni mwa sifa

nyinginezo za lugha hii zilizotangulia kutajwa.

Hivi sasa Kiswahili si tu lugha tambulishi ya eneo la Afrika Mashariki bali

imejumuisha bara lote la Afrika.

ZOEZI 1.1

Utafiti wa maktabani:

1. Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma

vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo nchini

Kenya tangu tupate uhuru, mwaka 1963.

2. Kwa kutumia maelezo uliyopewa kwenye matini, fafanua jinsi matumizi

ya lugha yo yote ile yanavyowatambulisha watu mjini Nairobi.

1.3.1 Mikakati ya usambazaji na upanuzi wa Kiswahili

Wanafunzi wanahitaji kufahamishwa kwamba usambaaji wa Kiswahili

ulimwenguni umekifanya kitambulike kama lugha ya kimataifa. Tangu jadi Kiswahili

kimwekuwa lugha teule ya mawasiliano, na usambazaji wake ulisababishwa na mambo

mbalimbali. Awali enzi za ukoloni, Kiswahili kilisambazwa na wakoloni, wamishenari

katika jitihada zao za kufunza dini; na Waarabu vile vile pamoja na wakoloni katika

biashara zao za watumwa na pembe za ndovu. Biashara hizi ziliwapeleka wageni hao

bara ya Afrika Mashariki hadi kufikia maeneo ya Afrika ya Kati, kama Zaire, Rwanda na

Burundi.

Baadaye usambazaji uliendelezwa na wamishenari waliojitahidi kuwafunza

Waafrika dini yao ya Kikristo, na kufanya juhudi za kuwaelimisha kwa kufunza kusoma

Page 9: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

9

na kuandika. Masomo haya yalifunzwa kwa lugha ya Kiswahili, kwa kuchelea

kuwafunza Waafrika lugha ya mabwana zao Waingereza. La ziada ni kwamba Kiswahili

pia kilieleweka miongoni mwa makabila mengi nchini Kenya na kwingineko, na hivyo

kuwa lugha rahisi kuchaguliwa kwa shughuli hii.

Ipo mikakati mingi ya kuendeleza matumizi ya Kiswahili tangu uhuru

ulipopatikana mwaka wa 1964 hadi sasa. Kwa mfano, Mzee Jomo Kenyatta alikitangaza

Kiswahili kuwa lugha ya taifa nchini Kenya. Baadaye akatangaza kwamba kingeweza

kutumiwa kwa mijadala bungeni. Nyakati hizo pia magazeti ya Kiswahili yalianzishwa,

kama “Sauti ya Pwani,” “Taifa Leo” kwa mfano. Vyombo vya habari pia vilifungua

idhaa nyingi za Kiswahili. Tayari juhudi za kuandika makamusi zilikuwa zinaendelea.

Baadhi ya vipindi vya redio vilianzishwa kujadili fasihi na msamiati na matumizi ya

Kiswahili kwa jumla.

Hadi sasa Kiswahili kimetamalaki nyanja nyingi za matumizi ya kawaida na ya

kitaaluma. Makamusi mengi yameandikwa, na hivi sasa, huko Marekani juhudi

zimekithiri kutayarisha kamusi ambayo itatumiwa kwenye taraklishi ili kuwasaidia

waandishi kwa lugha ya Kiswahili, kuweza kusahihisha lugha yao. Matayarisho haya

yanafanywa kwa mujibu wa MICROSOFT kampuni kubwa ya taraklishi. Ambapo tayari

Kiswahili kilikuwa kikifunzwa baadhi ya nchi za Magharibi na chache za Mashariki,

kuweko kwa kamusi ya Kiswahili kwenye taraklishi kutasambaza lugha hii zaidi kote

ulimwenguni, wengi wakiweza kuifanyia utafiti na kuitumia kuandika ripoti zao.

Teknolojia hii imesaidia sana katika kuendeleza hadhi na matumizi ya Kiswahili

ulimwenguni.

Aidha yapo makamusi yaliyoandikwa kuchangia ujuzi kulingana na istilahi za

kitaaluma, kama zile za fasihi, sayansi, mazingira, utabibu, isimu na kadhalika. Sera ya

serikali kufuatia Tume ya Mackay ndiyo hasa iliyokiingiza Kiswahili katika ratiba za

shule zote nchini Kenya, kuanzia shule za msingi hadi za upili. Kwa hivyo si lugha ya

kiholela tena ama ile ya watu wasio kisomo kama ilivyotambulika zamani. Itambulike

kuwa Kiswahili kimekuwa somo muhimu hata katika vyuo vikuu vya kitaifa nchini

TAFAKARI

Zingatia sehemu unayoishi iwapo ni mjini ama kijijini. Kuna ushahidi gani

kwamba matumizi ya Kiswahili yanasambaa miongoni mwa waongezi wa

lugha nyinginezo? Ungetoa mapendekezo gani kuwasaidia watu hao

kujifunza lugha hiyo kwa njia bora zaidi?

ZOEZI 1.2

1. Eleza mielekeo iliyopo miongoni mwa jamii yako kuhusu matumizi ya

Kiswahili. Je kuna upinzani wo wote?

2. Kwa kutumia maelezo uliyopewa mwanzo, eleza jinsi matumizi ya lugha

yanavyotambulisha watu jijini Nairobi.

3. Zingatia matumizi ya Kiswahili mahali unapoishi. Je ni mbinu gani

unazoweza kutumia ili kuendeleza matumizi ya kiswahili sanifu?

Page 10: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

10

SOMO 2

MAANA NA SIFA ZA LUGHA

2.0 Utangulizi

Ikiwa mwalimu wa lugha anataka kuukabili vizuri ufundishaji wa lugha, hana

budi kufahamu vilivyo maana ya lugha pamoja na sifa za kimsingi ambazo

zinaitambulisha lugha kama chombo maalum. Kanuni na mbinu za kufundishia Kiswahili

pia ni lazima zihusishwe na ufahamu kamili wa maana na sifa za lugha. Kwa kufanya

hivyo, mwalimu anaweza kufundisha Kiswahili kwa njia inayofaa akitilia maanani

ukweli halisi wa lugha.

MADHUMUNI YA SOMO

Kufikia mwisho wa somo hili, inatarajiwa kwamba utaweza:

Kutaja na kufafanua sifa mbali mbali za lugha.

Kupendekeza kanuni za kufundisha Kiswahili unazoweza kupata kutokana na sifa

ulizotaja

Kufafanua maana ya lugha.

2.1. Sifa za lugha.

Je, lugha ni kitu gani na ina sifa gani maalum? Wataalamu wa lugha wanaeleza

maana ya lugha kwa namna mbalimbali, lakini hata hivyo huwa wanakubaliana juu ya

mambo ya kimsingi ambayo yanaiainisha lugha na kuitambulisha kwa njia maalum. Kwa

ufupi mambo hayo ni kama yafuatayo:

(a). Lugha ni mfumo kamili.

(b). Lugha ni mfumo wa sauti nasibu.

(c ) Sauti za lugha ni za kutamkwa.

(d) Lugha ni chombo cha mawasiliano.

(e) Lugha hufungamana na utamaduni wa jamii.

(f) Mfumo wa lugha ni wenye ubunifu.

2.1a. Mfumo kamili

Katika mkutadha huu, tunaposema kwamba lugha ni mfumo kamili huwa

tunataka kutilia mkazo ukweli kwamba lugha haitumiwi segemnege. Huwa inatumiwa

kwa kufuata kanuni fulani katika utaratibu maalum unaokubaliwa na wanajamii wa lugha

husika. Kwa mfano, vitamkwa vya lugha vinaunganishwa pamoja kwa utaratibu maalum

Page 11: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

11

ili kuunda maneno. Vilevile maneno nayo huwa yaunganishwa kwa mpangilio maalum ili kuunda sentensi.

Kwa mfano, lugha ya Kiswahili ina baadhi ya konsonanti na vokali zifuatazo: /i/, /a/, /b/, /m/, /s/. Kutokana na vitamkwa hivi vichache inawezekana kuunda maneno kama

yafuatayo: bima, sima, simba, siasa, sisi, bibi, mimi, mimba, miiba, iba, imba, imbia,

msiba n.k….Haya ni maneno ambayo yanaundwa kwa kuzingatia utaratibu maalum

unaokubalika katika Kiswahili. Kwa upande mwingine, maneno yafuatayo, hata ingawa

yameundwa kutokana na vitamkwa vinavyopatikana katika Kiswahili, yanakiuka

utaratibu wa Kiswahili. Hayakubaliki kama maneno ya Kiswahili:*sbaini, *bsimai *bmia

*smia.

Vitamkwa katika mifano hii vimelundikwa ovyo ovyo bila kuzingatia kanuni

zinazotawala mfuatano wa vitamkwa katika Kiswahili, na kuishia na maneno ambayo

hayana maana.

Pia maneno yakitamkwa yanatamkwa kwa kuzingatia kanuni maalum. Kwa

mfano, katika Kiswahili watu huwa wanatumia shadda. Shadda yenyewe huwa haitumiwi

bila utaratibu. Kwa kawaida shadda inawekwa kwenye silabi inayotangulia ile ya

mwisho. Kutokana na utimizaji wa kanuni hii, neno linapopanuka shadda huhamishwa.

Mifano ifuatayo inabainisha ukweli huu:

kanisa, kanisani.

karibu, karibuni.

tumeona, tumeonana.

Zaidi ya hayo, maneno nayo yanapaswa kupangwa kwa utaratibu maalum ili yalete maana. Kwa mfano, katika Kiingereza inakubalika kusema: Where is my new

book?, Where are my new tables? Kwa upande mwingine, lugha ya Kiswahili na baadhi

ya lugha zingine haziruhusu mpangilio wa namna hii. Ni kosa , kwa mfano, katika

Kiswahili kusema:

* Wapi kiko changu kipya kitabu?

* Wapi ziko zangu mpya meza?

Bila kuzingatia utaratibu unaokubalika lugha inakosa ufasaha wake. Kwa mfano

mtu akisema “Manyumba hizi ni za City Council”, hapana shaka kwamba mtu huhyu

ametumia maneno ya lugha ya Kiswahili, lakini ovyo ovyo bila kufuata utaratibu

unaokubalika. Hakuzingatia utaratibu wa ngeli za Kiswahili. Neno nyumba katika

Kiswahili halibadiliki umbo katika wingi. Limo katika ngeli ambayo majina yake

hayatumii kiambisho awali ma-. Pia msemaji huyu huwa amevunja kanuni za sarufi ya

Kiswahili anaposema nyumba hizi ni ya city council. Kwa mujibu wa utaratibu wa

Kiswahili anatakiwa kusema: nyumba hizi ni za…. Mifano ifuatayo inaonyesha zaidi

ukweli kwamba lugha ni mfumo:

Page 12: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

12

Ukichunguza kwa makini jinsi majina haya yanavyobadilika kutoka umoja na

kuwekwa katika hali ya wingi utaona kwamba kuna utaratibu unaofuatwa. Utagundua,

kwa mfano kwamba majina yenye silabi mbili huwa yanatanguliza na kiambisho ny- k.m.

uzi- nyuzi, wembe- nyembe. Yale yenye zaidi ya silabi mbili hudondosha kiambisho u-.

Kwa upande mwingine baadhi ya majina ambayo silabi yake inayofuata kiambisho awali

u- ni /b/ huwa yanadondosha kiambisho awali u- na kutumia /m/ badala yake.

Ifuatayo ni mifano mingine inayodhihirisha kwamba lugha ina utaratibu wake

maalum.

Ukichunguza maneno yanayofupishwa katika mifano hii utaona kwamba

mabadiliko yanatokana kwanza katika kimilishi. Irabu ya mwisho katika kimilishi

inahamishwa na kutumiwa badala ya irabu ya silabi ya kwanza. Kisha baada ya kuwekwa

kwa irabu hiyo silabi mpya inaunganishwa na jina; na matokeo yake ni jina na kimilishi

kama neno moja.

Majina Majina

Umoja. Wingi

ufa

uzi

uso

wembe

wayo

ukuta

utepe

ubawa

ubao

wavu

upande

unyoya

nyufa

nyuzi

nyuso

nyembe

nyayo

kuta

tepe

mbawa

mbao

nyavu

pande

nyoya

Fungu la maneno Ufupisho

Kundu lake

Mwana wake

Baba yake

Ndugu yake

Mbacha wako

Kundule

Mwanawe

Babaye

Nduguye

mbachawo

Page 13: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

13

Maana nyingine ya kauli hii ni kwamba lugha iwayo yo yote inajitosheleza kama

chombo kinachoweza kutegemewa na jamii ili kutekeleza mahitaji yao ya kimawasiliano

katika mfumo wa maisha yao. Hakuna lugha ambayo ni duni.

2.1 b. Mfumo wa sauti nasibu

Je, nini maana ya kusema kwamba lugha ni mfumo wa sauti nasibu? Maana

mojawapo ya kauli hii ni kwamba hakuna uhusiano wa moja kwa moja wala wa kudumu

kati ya maneno yanayotumiwa kuashiria vitu au dhana fulani na vitu hivyo

vinavyoashiriwa au dhana inayoashiriwa. Hakuna sababu yo yote ya kimsingi kwa nini

sauti maalum zinatumiwa kuashiria kitu au jambo fulani na wala siyo sauti zingine. Kwa

mfano, mtu ambaye hafahamu lugha ya Kifransa akisikia neno “lait”, hakuna kielelezo

cho chote katika neno hilo ambacho kinaweza kumsaidia kuelewa kile

kinachozungumziwa. Vilevile Mfransa ambaye hafahamu Kiswahili, akisikia neno

“maziwa” hawezi kukisia kwamba neno hilo lina maana ya lait ya Kifransa. Hakuna cho

chote ndani ya neno kinachoweza kusaidia mtu kutambua maana yake. Jambo hili

linawezekana tu katika maneno machache yanayofuata mwigo wa sauti, na ambayo kwa

Kingereza huitwa “Onomatopoeic”. Sauti ambazo hutumiwa kurejelea mambo na hali

tofauti zilizuka kisadfa bila kikao maalum cha watu kuamua kuhusu jinsi vitu fulani

vinastahili kuitwa. Vitu huitwa kama vinavyoitwa kwa sababu watu wa jamii ya lugha

fulani ndivyo walivyozoea kulingana na mfumo wa maisha yao.

Unasibu wa lugha unachangia katika kutumia maneno ya lugha kwa namna kama

zifuatazo:

(i). Kutumia neno moja kuashiria vitu/ maana tofauti.

(ii). Kutumia maneno tofauti kuashiria kitu kimoja /dhana moja. Kwa mfano, kila

mojawapo katika maneno yafuatayo linaweza kuambatanishwa na zaidi ya maana moja:

panda, kata, meza, mbuzi, kaa….. .Katika lugha ya Kiswahili na Kiitaliano kuna neno

vita ambalo hufanana kimatamshi katika lugha zote mbili lakini linatumiwa kwa maana

tofauti kabisa. Maana ya vita ya Kiitaliano ni uhai katika Kiswahili! Mfano mwingine ni

neno mzigo la Kiswahili ambalo linafanana na neno muzigo katika Luganda. Kimatumizi

maneno haya hayana uhusiano wo wote. Muzigo katika Luganda humaanisha mafuta ya

kupikia au kujikapa. Hali kama hii inabainisha unasibu wa lugha.Vilevile maneno shida

na taabu yanaweza kutumiwa kurejelea dhana moja.

Zaidi ya haya, kauli isemayo kwamba lugha ni mfumo uliyo nasibu inaweza

kufasiriwa kumaanisha kuwa wakati fulani matumizi yake yanaelekea kukosa mantiki.

Kwa mfano, mfumo wa Kiswahili unaruhusu sentensi kama zifuatazo ambazo zinaenda

kinyume na matarajio ya ukweli wa mambo katika maisha ya kila siku:

Nasikia njaa.

Nasikia usingizi.

Tusikate tamaa.

Sijakata shauri bado.

Tupige magoti tuombe.

Je, mtu anawezaje kusikia njia au usingizi? Kwani usingizi na njaa vinatoa sauti?

Pia inawezekanaje kwa mtu kukata tamaa au shauri wakati ambapo tunajua kwamba

tamaa na shauri haviwezi kuonekana na kushikwa kwa mkono? Na je, kupiga magoti

kuna maana ya kuchukua fimbo au kifa cho chote kile na kisha kuyatwanga?

Page 14: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

14

Jibu ni kwamba miundo kama hii inawezekana kutokana na hali kwamba lugha

kimsingi, ni mfumo ulio nasibu. Ni kutokana na hali hii ndipo mara kadhaa matumiza ya

lugha yanaelekea kukosa msimamo ulio thabiti na wazi. Hali hii inaonyeshwa katika

jedwali lifuatalo linaloonyesha baadhi ya maneno ya Kiswahili katika umoja na wingi.

Maneno ya kundi (a) yamo katika ukoo wa majina ya watu. Isipokuwa neno

mtume katika wingi maneno mengine katika kundi hili huanza na kiambisho awali wa-.

Kutofanana na maneno mengine katika kundi hili, neno mtume linatumia kiambisho mi-

kama vile yanavyofanya maneno ya kundi la (b). Je kwa nini tuseme mitume na wala si

watume?.

Tukichunguza maneno katika kundi (c) ni wazi kwamba hata ingawa yote katika

hali ya umoja yanaanza na ji-, katika hali ya wingi baadhi yake yanadondosha kiambisho

hiki na kutumia ma- badala yake, wakati ambapo mengine yanahifadhi kiambisho hiki na

kukitanguliza na kiambisho ma- cha wingi. Ikiwa mwanafunzi atauliza kwa nini tusiseme

majicho badala ya macho au mapu badala ya majipu haitawezekana kumweleza kwa nini

inakuwa hivyo, isipokuwa kusema tu haya ndiyo mazoea ya lugha ya Kiswahili!

Kutokana na mifano hii ni wazi kuwa mwalimu wa Kiswahili hapaswi

kujishughulisha na maswali ya kimantiki anapofundisha Kiswahili. La maana na manufaa

zaidi ni kuwaelekeza wanafunzi ili waweze kutumia Kiswahili kuwasiliana kwa urahisi

na ufahamu wakizingatia utaratibu wa matumizi yake. Lengo kuu la kufundisha lugha

siyo kuihakiki kimantiki, bali ni kufanikisha uwezo wa kuwasiliana ipasavyo.

2.1 c Sauti za Kutamkwa

Kwa kawaida binadamu hufanya sauti nyingi katika hali ya maisha yake ya kila

siku. Kwa mfano, anaweza kutoa sauti kwa kugonganisha vyombo na kutokana na

kukanyaga ardhi anapotembea. Anaweza pia kukohoa au kupiga chafya na wakati

Umoja Wingi

(a) mzazi

mvuvi

mtume

(a) wazazi

wavuvi

mitume

(b) mkeka

mtego

mkate

(b) mikeka

mitego

mikate

(c) jiwe

jicho

jambo

jibu

jipu

(c) mawe

macho

mambo

majibu

majipu

Page 15: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

15

mwingine kucheka. Umuhimu wa sauti zitokanazo na vitendo kama hivi ni kwamba

kutokana na sauti hizo wanaoshuhudia wanaweza kupata fununu kuhusu hali ya yule mtu

anayetoa sauti hizo. Hakuna, kwa mfano, jinsi unavyoweza kuchambua kicheko na

kuonyesha vitamkwa mbali mbali vinavyounganishwa kukiunda. Vile vile hakuna jinsi

unavyoweza kubainisha vitamkwa mahsusi vinavyounda kikohozi au chafya. Lakini kwa

upande mwingine unaweza kubainisha wazi vitamkwa vinavyounda maneno tofauti. Kwa

mujibu wa wataalamu wa lugha sauti hizo hazina hadhi ya kiisimu. Kimsingi , sauti za

lugha ni zile tu ambazo hujitokeza katika utaratibu kamili kupitia mdomo wa binadamu

kutokana na kushiriki kwa viungo kadhaa vinavyohusika katika utamkaji.

2.1 d Chombo cha Mawasiliano.

Kazi kuu ya lugha ni kufanikisha uhusiano kati ya binadamu au kuwawezesha

kuendeleza maisha yao ya kila siku. Lugha ya pamoja husaidia kufanikisha mawasiliano

katika vipengele mbali mbali vya maisha ya binadamu. Ili watu waweze kupashana

habari na kubadilishana mawazo wanahitaji kuwa na chombo cha mawasiliano. Na

chombo hiki ni lugha.

Kwa misingi ya kiisimu mawasiliano ya lugha yanashirikisha stadi zifuatazo

ambazo zinaingiliana na kutiliana nguvu: kusikiliza, kuongea, kusoma na kuandika kwa

ufahamu lugha anayojifunza.

2.1 e Lugha Hufungamana na Utamaduni.

Lugha haichimbuki katika ombwe tupu, bali ni zao la utamaduni fulani. Kwa

hivyo lugha iwayo yo yote, kwa kiasi fulani inabeba utamaduni wa jamii ulioichipuza,

pamoja na kuathiriwa na utamaduni huo. Kwa mfano, watu ambao huishi katika

mazingira yaliyo karibu na bahari wana maneno mengi yanayoambatana na shughuli

mbalimbali zinazoendelea baharini.

Sifa mojawapo ya utamaduni ni kwamba aghalabu unabadilika kufuatana na

mabadiliko ya wakati. Na jambo hili linapotokea lugha nayo pia haina budi kubadilika ili iweze kuwiana na mabadiliko. Ni kutokana na hali hii ndipo lugha inaweza kujitosheleza

kama chombo cha mawasiliano ya jamii inayohusika. Mifano ya mabadiliko hayo ni

kama vile maneno mapya kubuniwa au kukopwa na kuingizwa katika lugha. Zaidi ya

hayo baadhi ya maneno yanaweza kupanuliwa na kuzingatia upeo mpana wa maana.

Mifano ya maneno yaliyoingia katika Kiswahili hivi karibuni ni kama vile: ukimwi,

tarakirishi, barua pepe, utandawazi, n.k…. Mifano kama hii inaonyesha kuwa lugha ni

mfumo ulio wazi.

Ni muhimu kwa mwalimu wa lugha kutambua kuwa kuna uhusiano mkubwa

baina ya lugha na utamaduni. Wakati wa kufundisha anaweza kukumbana na misemo

ambayo ni vigumu kueleza maana yake bila kuelewa utamaduni uliochipuza misemo

hiyo. Misemo mingi kama vile methali imejikita katika utamaduni. Mwalimu

anapofundisha misemo hiyo hana budi kuelewa utamaduni wake. Hali kadhalika,

wanafunzi wanapojifunza lugha nyingine wanaweza kuathiriwa na utamaduni wa jamii

zao hadi kiasi cha kuhamisha misemo ya jamii zao na kuitumia katika lugha

wanayojifunza. Matokeo ya jambo hili ni kwamba huenda misemo hiyo isieleweke katika

mkutadha wa utamaduni wa lugha ya pili, au pengine inaweza kueleweka kwa namna

Page 16: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

16

isiyotarajiwa. Ni muhimu sana kwa mtu ye yote anayejifunza lugha kujitahidi kutofasiri

misemo ya lugha anayojifunza kwa misingi ya utamaduni wa jamii ya lugha yake ya

kwanza. Unaweza kuelewa maneno yote yanayotumiwa lakini ukashindwa kuelewa

ujumbe unaowasilishwa kwa kutozingatia utamaduni wa wazawa wa lugha husika. Kwa

mfano, Mtanzania anapotaka kununua anaweza kutumia neno omba. Akitaka, kwa

mfano, kununua nyama anaweza kusema, “Naomba kilo mbili za nyama”. Katika

mazingira ya Kenya, wasikilizaji huenda wakafikiria kuwa msemaji huyu anataka

kupewa nyama ya bure. Kusema kweli jambo hili lilitokea hapo Githurai. Mama mmoja

mtanzania alimwambia mwuzaji kuwa anaomba kilo mbili za nyama. Jama alifyoka na

kumwambia kuwa akitaka nyama ni lazima alipe!

Aidha askari Mtanzania anaweza kumwambia mshukiwa “Naomba

twandamane….”. Kwa mtu ambaye amelelewa katika mazingira ambamo askari hawana

sifa ya kutumia lugha kwa upole, anaweza akafikiria kuwa ana hiari ya kutoandamana na

askari huyu. Amri ya askari huenda asiielewe kama amri kwa sababu ya mazoea ya

utamaduni wa jamii yake. Mifano hii inakufundisha wewe kama mwalimu kwamba

ukitaka wanafunzi wako waimudu vizuri lugha unayofundisha huna budi kuwadokezea

kuhusu utamaduni wa jamii ya lugha hiyo.

Lugha ni kama kioo cha utamaduni wa jamii. Kwa hivyo mwalimu anaweza

kufundisha utamaduni wa jamii fulani kupitia lugha anapofundisha methali. Methali

zifuatazo, kwa mfano zimebobea utamaduni wa watu wa pwani ambao unaweza kutatiza

wanafunzi kutoka sehemu zisizo za pwani:

Mgema akisiwa tembo hutilia maji.

Usiache mbachao kwa msala upitao.

Aliyekupa kiti ndiye kanipa kuti.

Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.

Mwenda tezi na omo marejeo ni ngamani.

2.1. f Ubunifu wa lugha.

Lugha ni chombo chenye ubunifu. Hali hii inawezesha binadamu, kwa mfano,

kuunda maneno chungu nzima kutokana na idadi ndogo ya vitamkwa vinavyopatikana

katika lugha. Vilivile kutokana na maneno machache watu wanaweza kuunda sentensi

zisizo na idadi kamili. Pamoja na haya, mtu anapoimudu lugha fulani anaweza kuibuka

na miundo mipya ya sentensi ambayo haijawahi kutamkwa hapo awali na watu wengine.

Sifa hii ya lugha huchangia kuipa lugha uhai ambao huifanya kuwa chombo ambacho

kinajitosheleza kwa mawasiliano ya jamii. Ubunifu husaidia lugha kuendelea kupanuka

kila uchao kwa kupokea na kuingiza maneno mapya.

2.2 Kanuni za kufundishia.

Je mwalimu anaweza kupata maarifa gani ya kanuni za kufundisha lugha

kutokana na sifa zilizotajwa hapo mbeleni?

Miongoni mwa mambo yaliyotajwa kuhusu sifa za lugha ni kwamba ni mfumo

kamili wa sauti za kutamkwa. Kauli hii inabainisha kwamba lugha imejikita katika

utaratibu wa sauti. Kwa hivyo, ufundishaji wa lugha zungumzi unapaswa kupewa uzito

unaostahili katika mpango wa kufundisha lugha. Pamoja na hayo mwalimu wa lugha

Page 17: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

17

anatakiwa kuwa na fununu kuhusu viungo vinavyohusika katika utoaji wa sauti na jinsi

viungo hivyo vinavyohusika katika utoaji wa sauti. Jambo hili litamsaidia mwalimu

katika juhudi za kushughulikia matatizo ya kimatamshi ambayo huenda yakawakumba

wanafunzi wake.

Na mashauri unayoweza kupata kutokana na kauli isemayo kuwa lugha ni mfumo

kamili ni kwamba somo la lugha linapaswa kuendeshwa kwa utaratibu maalum na

kuzingatia uhalisia wa lugha inayohusika. Kila lugha inapaswa kufundishwa kama

chombo ambacho kinajitosheleza. Haipaswi kufundishwa kupitia lugha nyingine. Pia

haifai kwa mwalimu kufundisha wanafunzi matamshi ya maneno na maana tu bila

kuwaonyesha namna ya kupanga maneno hayo katika utaratibu kamili unaokubalika na

jamii husika. Kwa vile lugha ni mpangilio kamili wa maneno, mwalimu anashauriwa

asifundishe tu maneno bila kuyatumia katika vielelezo vya sentensi. Sentensi hutoa

mkutadha bora wa kubainishia matumizi ya maneno.

Kutokana na unasibu wa lugha, mashauri yanayoweza kupatikana ni kwamba

mwalimu anapofundisha hapaswi kujishughulisha na maswali ya kimantiki. La maana na

manufaa zaidi ni kufundisha lugha kama vile ilivyo ili wanafunzi waweze kuitumia

kuwasiliana kwa urahisi bila kutatizika wala kuwatatiza wengine. Na ikiwa lugha ni

chombo cha mawasiliano, mwalimu anashauriwa kuhakikisha kuwa anafundisha akiwa

anatilia mkazo juu ya uwezo wa kuwasiliana. Lazima afundishe kwa kutumia mbinu

ambazo zitachochea mawasiliano miongoni mwa wanafunzi.

Ni jukumu lako kama mwalimu kuona kwamba wanafunzi wako wanashirikishwa

vya kutosha katika shughuli kamili za matumizi ya Kiswahili. Washirikishwe kama

wahusika wawasilishaji wa ujumbe. Washirikishwe pia kama wahusika wapokezi wa

ujumbe. Unapaswa kuhakikisha kwamba wanafunzi wanapata fursa ya kuendeleza stadi

zote za lguha: kusikiliza, kuongea, kusoma na kuandika.

Kwa ufupi ufanikishaji wa mawasiliano upewe kipaumbele katika mpango wa

kufundisha lugha. Ni lazima wanafunzi wakuze uwezo wa kuwasilisha na kupokea

ujumbe bila shida.

Kauli nyingine ni ile isemayo kuwa lugha hufungamana na utamaduni. Neno

utamaduni aghalabu huashiria mambo kama vile mila, desturi, itikadi, na mfumo wa

maisha kwa jumla. Lugha ni kama kioo cha utamaduni wa jamii ya watu wanaohusika.

Hii ina maana kuwa, kwa kiasi fulani, lugha inamulika hali ya maisha ya watu

wanaoitumia, matarajio yao, mtazamo wao wa maisha, pamoja na mazingira yao kwa

ujumla. Kwa hivyo, mwalimu anashauriwa kutilia maanani uwezekano wa mwingiliano

wa utamaduni kati ya lugha ya wanafunzi na Kiswahili wakati anapofundisha. Mtu

anaweza kufahamu maneno yanayotumiwa katika msemo fulani, lakini hata hivyo

huenda akashindwa kuelewa ujumbe uliyomo ndani kutokana na hali ya utamaduni

wenye kuchipuza msemo huo. Hali kadhalika, lugha hubadilika kufuatana na mabadiliko

ya utamaduni. Kwa hivyo, mwalimu naye ni lazima awe tayari kufundisha akizingatia

matokeo ya mabadiliko ya wakati.

Kauli ya mwisho ni ile isemayo kuwa lugha ni mfumo wenye ubunifu. Ukweli

huu unamdokezea mwalimu kwamba anapofundisha wanafunzi lugha, ni lazima awape

nafasi tele kujifunza namna mbalimbali za matumizi ya lugha. Wapewe nafasi ya

kushuhudia na kushiriki katika mitindo tofauti ya lugha ndipo nao waweze kuitumia

kivyao.

Page 18: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

18

2.3 HITIMISHO

Somo hili limejishughulisha hasa na sifa za kimsingi zinazoiainisha lugha.

Kutokana na sifa hizi mwalimu wa Kiswahili anaweza kupata maarifa kadhaa ambayo

yanaweza kumsaidia katika kufundisha. Kwa kurejelea sifa hizo zilizotajwa tunaweza

kufasiri lugha kwa njia kama ifuatayo:

Lugha ni mfumo kamili ulio nasibu wa sauti za kutamkwa ambao jamii ya watu

wa utamaduni fulani hutumia kwa madhumuni ya kuwasiliana.

Kutokana na ufafanuzi huu ni wazi kwamba lugha asilia ni lugha ya kusema.

Lugha ya kuandika ni kiwakilishi tu cha lugha ya kusema. Ni kutokana na ukweli huu

ndipo tunaona kuwa kuna watu wengi ambao wanaweza kuzungumza lugha yao bila

kujua jinsi ya kuandika lugha hiyo.

ZOEZI 2

1. Ukitoa mifano mwafaka ya kutilia maki jibu lako, fafanua zaidi sifa za

lugha

2. Taja sifa za lugha zozote tatu, na kwa kila mojawapo ya sifa hizo eleza

kanuni za kufundisha Kiswahili unazoweza kupata kutoka kwake

3. Toa fasiri yako ya neno lugha ukizingatia sifa za kimsingi

zinazoitambulisha lugha.

Page 19: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

19

SOMO 3

UFUNDISHAJI WA LUGHA YA PILI.

3.0 Utangulizi

Kuna mikabala/ mikondo mbalimbali katika historia ya ufundishaji wa lugha ya

pili ambayo imewahi kutumiwa. Baadhi ya mikabala hiyo, mpaka sasa imeendelea

kuathiri ufundishaji wa lugha ya pili. Ujuzi wa mikabala hiyo ni jambo muhimu kwa

mwalimu wa Kiswahili kwa sababu unaweza kumsaidia kupata fununu kuhusu asili ya

mbinu tofauti tofauti zinazotumiwa kufundisha lugha ya pili. Hapo awali mbinu hizi

zililenga hasa ufundishaji wa lugha ya Kingereza kama lugha ya pili. Hata hivyo, baadhi

ya mambo ambayo hupendekezwa katika mbinu hizo yanaweza kumsaidia mwalimu

ambaye anajishughulisha na ufundishaji wa Kiswahili kama lugha ya pili.

Madhumuni Ya Somo

Kufikia mwisho wa somo hili utaweza kutoa mifano ya mbinu za

kufundishia lugha na kueleza jinsi kila mojawapo ya mbinu hizo

inaweza kutumiwa katika ufundishaji wa Kiswahili.

3.1 Mbinu Ya Kimapokeo

Hii ni mbinu ambayo hapo awali ilitumika kama njia ya kufundishia lugha za

kijadi kama vile Kiyonani na Kilatini. Ilitawala ufundishaji wa lugha za kizungu na

kigeni kati ya miaka 1840 na 1940. Lengo kuu la mbinu hii ni kufanikisha ufahamu wa

sarufi pamoja na uwezo wa kuandikia kwa usahihi katika lugha inayolengwa. Pia

inalenga kuwezesha mwanafunzi kuwa na upeo mpana wa msamiati unaotumika sana

katika lugha ya uandishi katika lugha husika, ili hatimaye aweze kuthamini umuhimu

pamoja na thamani ya nakala zinazohusika.

Katika mazingira ya darasani, mwalimu anatazamiwa kutekeleza malengo haya

kwa kushirikisha wanafunzi katika kazi ya kutafsiri mara kwa mara kutoka lugha zao

hadi katika lugha inayofunzwa. Kabla ya kutafsiri, wanafunzi wanapaswa kwanza

kijifunza maneno ya lugha inayolengwa ili waweze kutafsiri katika lugha mpya. Pamoja

na hayo, wanafunzi wanapewa maelezo marefu kuhusu sheria za kisarufi. Kisha

wanapewa zoezi la kutunga sentensi ili kubainisha ufahamu wao wa sheria hizo. Uwezo

wa mwanafunzi katika kutafsiri huwa ndicho kigezo muhimu kinachotumiwa kama

chombo cha kupima ustadi wake katika kipengele cha sarufi na msamiati.

Udhaifu hasa wa mbinu hii ni kwamba haitilii mkazo juu ya matamshi sahihi

pamoja na stadi za kimawasiliano. Inasisitiza sana ujuzi wa sheria za kisarufi bila kupatia

wanafunzi nafasi ya kutosha kujieleza kutokana na nafsi zao. Matokeo ya kujishughulisha

sana na ufundishaji wa kanuni na vighairi ni kwamba waalimu huishia kwa kufundisha

Page 20: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

20

wanafunzi lugha ya ulimwengu wa vitabu, lugha isiyokuwa na uhai, na ambayo mara

nyingi haina manufaa katika ufanikishaji wa mawasiliano ya kawaida.

Utumiaji wa mbinu hii unalifanya somo la lugha kukosa ubunifu unaotakikana.

Wanafunzi hawapati nafasi ya kutumia lugha kama chombo wanachoweza kukitegemea

kutekeleza mahitaji yao ya kimawasiliano. Shughuli ya kujifunza lugha inageuka kuwa

zoezi la kukariri maneno chungu nzima na kanuni kemkem za kisarufi. Hakuna hakikisho

kwamba baada ya kukariri maneno na kanuni wanafunzi watakuwa na uwezo wa kutumia

kanuni na maneno vilivyokaririwa katika mawasiliano ya nje ya darasa. Shughuli ya

kufundisha na kujifunza lugha inakuwa kama zoezi la kuchemsha bongo tu.

3.2. Mbinu Ya Moja Kwa Moja

Hali ya kutoridhika na mbinu ya kimapokeo ni miongoni mwa mambo ambayo

yalichangia kuibuka kwa mbinu ya moja kwa moja. Iliibuka katika karne ya 19 kuchukua

mahali pa mbinu ya kimapokeo. Wanaopendelea mbinu hii hushikilia kwamba njia

mwafaka ya kujifunza lugha ya pili ni kukabiliana nayo moja kwa moja na kuitumia

kama vile mtoto mdogo anavyofanya anapojifunza lugha ya mama. Kulingana na mbinu

hii ni marufuku kutumia lugha ya wanafunzi au lugha nyingine yo yote ile.

Mbinu hii husisitiza umilisi wa lugha bila tafsiri wala maelezo rasmi juu ya sheria

za kisarufi. Wanafunzi wanatakiwa kijifunza lugha kwa kushirikishwa kikamilifu kama

wahusika watendaji katika matumizi tofauti tofauti ya lugha. Inasisitizwa kwamba ikiwa

maana inaweza kuwasilishwa moja kwa moja kwa kushirikisha maono au vitendo hakuna

haja ya kutafsiri.

Kwa upande wa sarufi, mbinu hii inashikilia kwamba njia bora ya kuendeleza

ufahamu wake ni kutokana na uzoefu wa kutumia mara kwa mara lugha inayohusika.

Mwanafunzi akipewa fursa ya kutosha kukumbana na matumizi ya lugha, itakuwa rahisi

kwake kutambua na kujifunza sheria zinazotawala sarufi ya lugha hiyo.

Mbinu hii inasisitiza haja ya kutoa nafasi kwa mwanafunzi ya kujifunza lugha

kama vile mtoto anavyojifunza lugha yake ya kwanza. Mtoto anajifunza na kuimudu

lugha kwa kukumbana nayo moja kwa moja katika mkutadha maalum wa mawasiliano.

Hakuna mtu anayemfafanulia kanuni za kisarufi za lugha yake. Hata hivyo anazing’amua

kanuni hizo yeye mwenyewe baada ya kushuhudia matumizi yake katika vielelezo vya

sentensi. Huwa anajifunza lugha ya jamii yake katika mazingira yanayoshirikisha vitendo

na maono. Ushirikishaji wa maono na vitendo unachangia kujenga hali ambayo husaidia

mtoto kukisia maana ya kile kinachosemwa. Anajifunza lugha ya jamii yake kwa

kusikiliza kwanza na baadaye kuigiza yale anayosikiza.

Kwa mujibu wa mbinu hii mwalimu anapofundisha lugha ya pili anashauriwa

kutotegemea tafsiri. Anashauriwa vile vile kutofundisha moja kwa moja sheria za

kisarufi. Ana wajibu wa kuambatanisha ufundishaji wake na vitendo, uigizaji na

mazungumzo. Lakini ikiwa mwalimu hana budi kufundisha sarufi, inafaa ufundishaji wa

sarufi uzingatie kiwango cha matumizi ya lugha huko mkazo ukitiliwa juu ya madondoo

ya kisarufi yanayotumika sana sana hasa katika mazungumzo.

Kwa mujibu wa mbinu hii, dhima ya mwalimu ni kupanga na kufanikisha utumizi

wa lugha badala ya kujishughulisha na ufafanuzi pamoja na uchambuzi wa kanuni za

kisarufi. Ili mwalimu aweze kufaulu kutumia mbinu hii anapaswa kuwa na ujuzi wa

kiwango cha hali ya juu katika lugha anayofundisha. Ni lazima pia awe na ubunifu wa

Page 21: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

21

kumwezesha kuwasilisha maana bila kutumia lugha nyingine yo yote zaidi ya ile ambayo

anafundisha. Anatarajiwa pia kujitahidi kujenga mazingira ya kufundishia ambayo

yanakaribia kufanana yale ya lugha ya kwanza. Mazingira hayo yanatarajiwa kufanikisha

ufahamu wa lugha kupitia mazoezi ya kusikiliza pamoja na mazungumzo. Lazima yawe

mazingira ambayo yanaweza kuchangia katika kuhamasisha mwanafunzi kutaka

kujifunza lugha inayohusika.

Kwa kawaida mtoto anapojifunza lugha yake ya kwanza anakuwa na hamu ya

kujifunza lugha hiyo ili aweze kutangamana na jamii ya watu wanaomzunguka. Jamii

hiyo pia humsaidia kuendelea kwa kumtia shime. Pamoja na hayo mtoto huwa na muda

mwingi wa kusikia na kutumia lugha hiyo. Lugha inakuwa sehemu ya maisha yake ya

kila siku.

3.3 Mbinu Ya Uzungumzi.

Mbinu hii ilizuka na kukita mizizi katika miaka ya 1950 kutokana na mwamko

mpya nchini Amerika wa kujishughulisha na ufunzaji wa lugha za kigeni. Tukio muhimu

ambalo lilichangia pakubwa kuamsha ari ya Wamerika katika lugha za kigeni ilitokea

mnamo mwaka wa 1957. Mwaka huo Warusi walifaulu kupeleka chombo chao (sputnik)

angani. Jambo hili lilikuwa changamoto kubwa kwa taifa la Amerika. Kufuatia tukio hilo,

serikali ya Amerika iliamua kujishughulisha kikamilifu katika ufundishaji wa lugha za

kigeni ili isiachwe nyuma katika maendeleo ya kisayansi.

Jambo ambalo linapewa kipaumbele katika mbinu hii ni ufasaha wa kuzungumza.

Ufasaha unaotarajiwa unahusu matamshi bora, sarufi, pamoja na uwezo wa kuitikia upesi

na kwa urahisi katika hali tofauti zinazohusisha utumizi wa lugha katika mazungumzo.

Ufahamu sikizi, matamshi, sarufi na msamiati vinapofundishwa huwa kama njia

mojawapo ya kufanikisha ufasaha wa kuzungumza. Vilevile wanafunzi

wanaposhirikishwa katika kuandika na kusoma mambo haya yanaambatanishwa na ustadi

wa kutumia lugha ya mazungumzo.

Kulingana na mbinu hii, stadi za lugha zinastahili kufundishwa kwa kuzingatia

mfuatano huu: Kusikiliza, Kuongea, Kusoma na Kuandika.

Katika hatua za mwanzo mwanzo, kusoma na kuandika vinachukuliwa tu kama

mambo ambayo yanaweza kuchangia kuimarisha ustadi wa kusikiliza na kuongea.

Vinatiliwa mkazo zaidi katika viwango vya juu wakati ambapo wanafunzi wana uzoefu

unaofaa ili kuweza kukabiliana na mitindo zaidi ya lugha ya kimaandishi.

Madondoo ya lugha yanapofundishwa kwa kutumia mbinu hii huwa

yanawasilishwa kupitia mjadala ambao ni chombo muhimu cha kutoa mkutadha wa

kufundishia kile kinacholengwa. Zaidi ya kushiriki katika mjadala, wanafunzi huwa

wanatakiwa, mara kwa mara, kukariri vielelezo vya sentensi.

3.4 Mbinu Ya Mawasiliano.

Msingi wa mbinu hii ni imani kwamba kazi kuu ya lugha ni kufanikisha

maingiliano pamoja na mawasiliano katika jamii. Lugha ni chombo ambacho

kinamwezesha binadamu kushirikiana na watu wengine na pia kutekeleza mahitaji ya

maisha yake. Kwa hivyo, kulingana na waasisi wa mbinu hii, lengo kuu la kufundisha

Page 22: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

22

lugha ni kuwezesha mwanafunzi kuwa na uwezo wa kuwasiliana akitumia lugha

inayohusika.

Njia moja ya kuhakikisha kuwa mwanafunzi anakuwa na uwezo wa kuwasiliana

ni, kwanza, kumpa fursa ya kushiriki kama mhusika mpokezi. Mwanafunzi anapata fursa

ya kupanua upeo wake wa lugha kupitia kusikiliza na kusoma. Baada ya kushiriki katika

matumizi ya lugha akiwa mhusika mpokezi mwanafunzi anashirikishwa kama mhusika

mwanzilishi wa mawasiliano. Kulingana na waasisi wa mbinu ya mawasiliano, lugha

ambayo ni ya maana / manufaa kwa wanafunzi inatilia nguvu juhudi za kujifunza. Kwa

hivyo ni muhimu kwa walimu kuhakikisha kwamba wanapochagua kazi ya wanafunzi

wanatilia maanani uwezo wa kazi hiyo wa kuwashirikisha katika matumizi ya lugha

yenye maana na uhalisi.

Kwa kawaida, mawasiliano hufanyika katika mazingira ya watu wakiwa katika

vikundi. Pia, aghalabu, mawasiliano huchukua mkondo wa mazungumzo (conversation)

na majidiliano (discussion). Wakizingatia ukweli huu, wanaounga mkono mbinu ya

kimawasiliano wanapendekeza kugawanya wanafunzi katika vikundi vidogo vidogo. Hii

ni njia bora ya kuendeleza uwezo wa wanafunzi wa kuwasiliana kwa kutumia lugha

inayofundishwa. Wakiwa katika vikundi vya watu wachache, wanafunzi wanakuwa na

fursa bora ya kutumia lugha halisi. Pia wanapata nafasi ya kujieleza kwa ufasaha bila

wasiwasi. Ustadi katika kusoma na kuandika unaweza kukuzwa kutokana na msingi

imara wa kutumia lugha kwa uhalisi.

Je jukumu hasa la mwalimu ni nini? Kwa mujibu wa waasisi wa mbinu hii,

jukumu la mwalimu ni kuhamasisha wanafunzi na kutoa kwao nafasi ya kujieleza katika

lugha inayohusika. Ana wajibu wa kuhamasisha wanafunzi kutumia lugha kwa njia

mbalimbali. Anapaswa pia kuhakikisha kuwa kila mwanafunzi anapata fursa ya kujieleza.

Pamoja na hayo, mwalimu ana wajibu kuhakikisha kwamba wanafunzi wanaelewa vizuri

kwa nini wanafundishwa kile wanachofundishwa. Hivi ndivyo watakavyoweza kushiriki

kwa njia ya maana na manufaa kwao. Vilevile ni lazima mwalimu ahakikishe kuwa

wanafunzi wake wanahusika zaidi kuliko vile anavyohusika mwenyewe.

Aidha, mwalimu anashauriwa kushirikisha wanafunzi katika vitendo ambavyo

vinaweza kuwalazimisha kuwasiliana kwa kutumia lugha inayofaa kulingana na

mkutadha. Kwa maneno mengine, mwalimu anapaswa kubuni hali na mazingira ambamo

wanafunzi hawawezi kukidhi mahitaji na matarajio yao bila kuwasiliana. Wakijikuta

katika mazingira ya namna hii hawatakuwa na budi kutafuta ufumbuzi kwa kutumia

lugha. Kwa ufupi, mwalimu anaweza kusaidia kuendeleza uwezo wa wanafunzi wa

kuwasiliana wakitumia lugha kwa kuzingatia mfuatano wa hatua zifuatazo:

1. Mapokezi ya lugha.

2. Ufafanuzi / Maelezo

3. Majaribio ya matumizi ya lugha

4. Mawasiliano huru

Katika hatua ya mapokezi wanafunzi wanashiriki kama wahusika wapokezi. Kazi

yao katika hatua hii ni kupokea ujumbe unaowasilishwa na watu wengine na kupata

maana ya ujunbe unaowasilishwa. Wanaweza kutekeleza jambo hili kupitia zoezi la

kusikiliza au kusoma. Zoezi la kusikiliza husaidia wanafunzi kupata nafasi ya kupanua

upeo wa lugha. Kupitia zoezi hili wanaweza kujifunza msamiati mpya na miundo

Page 23: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

23

mbalimbali ya kisarufi. Vilevile wanafunzi wanaimarisha ujuzi wao wa yale ambayo

wamejifunza tayari.

Kwa upande mwingine, katika hatua ya ufafanuzi (maelezo) mwalimu anaweza

kudondoa madondoo fulani ya lugha ambayo wanafunzi wamewahi kukumbana nayo,

katika zoezi la kusikia na kusoma. Kisha anatoa maelezo kuhusu madondoo hayo ili wanafunzi wayatilie maanani zaidi kuliko mengine kwa wakati huo. Baada ya

kuhakikisha kwamba wanafunzi wanafahamu kiini cha somo mwalimu anawapa

wanafunzi nafasi ya kujaribu kutumia madondoo hayo katika vielelezo vya sentensi

wakizingatia maagizo yaliyotolewa.

Katika hatua ya mawasiliano huru wanafunzi wanapata fursa zaidi ya kujieleza

bila kufuata maagizo ya mwalimu. Wanaweza kujieleza kwa njia halisi kulingana na

mahitaji ya mawasiliano katika mkutadha unaohusika. Wanafunzi watateua lugha

kulingana na hali halisi inayowakabili wakati huo. Mawasiliano huru huwapa wanafunzi

fursa ya kutambua kuwa lugha siyo somo ambalo linajikita katika mipaka ya mazingira

ya darasani tu., lakini pia ni chombo cha mawasiliano nje ya mipaka ya darasa.

Mawasiliano huria huwapa wanafunzi nafasi ya kutumia lugha kwa njia ya ubunifu katika

miktadha tofauti tofauti ya kijamii. Wanatumia lugha bila usimamizi wa mwalimu, lakini

kulingana na hali halisi katika mazingira ya mawasiliano. Huwa wajitegemea wao

wenyewe. Kadiri wanavyoshiriki katika mikutadha tofauti ya mawasiliano na kushuhudia

jinsi lugha inavyotumiwa, ndivyo wanavyoendelea kukuza na kuimarisha uwezo wao wa

kimawasiliano (communicative competence). Uwezo huu ni muhimu kwa mwanafunzi

kwa sababu akiwa nao anaweza kufasiri lugha kwa njia iliyo sahihi akizingatia mkutadha

unaohusika. Na akifanya hivyo anaweza kuitikia kama inavyotarajiwa. Kwa mfano

mwalimu akiingia darasani ambamo mna joto jingi na agundue kuwa madirisha

yamefungwa, anaweza akasema: Mbona joto limezidi sana humu ndani. Mwanafunzi

mwenye uwezo wa kimawasiliano atatambua kuwa mwalimu angetaka madirisha

yafunguliwe, na ataitikia kwa kuyafungua. Yule asiyekuwa na uwezo huo atachukulia

usemi wa mwalimu kama kauli ya kawaida tu.

3.5 Msingi wa Mbinu ya Kimawasiliano

Asili ya mbinu ya kimawasiliano ni imani inayoshikilia kwamba:

(a) Lugha ni mfumo wa kueleza maana.

(b) Jukumu kuu la lugha ni kufanikisha maingiliano na mawasiliano baina ya

watu.

(c) Shughuli ambazo zinachangia kufanikisha ufahamu wa lugha ni zile

ambazo zinatoa kwa wanafunzi nafasi ya kushiriki katika mawasiliano

halisi (real communication).

(d) Vitendo vinavyohusisha matumizi ya lugha ili kutekeleza shughuli za

maana (meaningful tasks) husaidia kufanikisha ujuzi wa lugha.

(e) Lugha yenye maana kwa wanafunzi inaimarisha hali ya kujifunza.

(f) Mawasiliano hufanyika ikiwa wale wanaohusika wana hamu (motisha) ya

kuwasiliana.

Page 24: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

24

3.6 HITIMISHO.

Somo hili limezungumzia baadhi ya mikabala (mbinu) tofauti inayotambulikana

katika historia ya ufundishaji wa lugha ya pili. Ni jukumu la mwalimu kuteua na kutumia

mbinu inayofaa kulingana na matarajio yake. Lakini, kwa vyo vyote vile mwalimu

anapaswa kutilia maanani kiwango cha wanafunzi, jambo linalotiliwa mkazo, uwezo

wake, idadi ya wanafunzi na kupatikana kwa vifaa vya kufundishia.

ZOEZI 3.

Eleza jinsi unavyoweza kufundisha mambo yafuatayo ukitumia

mbinu ya mawasiliano:

(a). Kauli ya kutendea.

(b) Matumizi ya –ki- na kwa.

Page 25: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

25

SOMO LA 4

MAANDALIZI YA MWALIMU.

4.0 Utangulizi:

Matayarisho ni jambo la lazima katika utekelezaji wa kazi ya aina yo yote. Haifai

kwa mtu kutegemea kupata matokeo mazuri katika kazi anayofanya ikiwa ataikabili ovyo

ovyo bila kujitayarisha kwa kazi hiyo. Kila mfanya kazi anahitaji kujitayarisha na

kujihami kulingana na kazi yake. Njia mojawapo ya kujihami ni kuhahakikisha kwamba

ana vifaa vya utekelzaji wa kazi inayohusika.

Je unaweza kujihami namna gani kuikabili kazi ya kufundisha? Ni hatua gani

ambazo utachukua kuhakikisha kwamba kazi yako inafanyika kwa utaratibu mzuri?

Katika somo hili tutajadili vyombo muhimu unavyohitaji katika maandalizi yako

kwa kazi ya kufundisha. Na vyombo hivi ni: Silabasi, Maazimio ya kazi, na Mpango wa

kipindi cha somo.

MADHUMINI YA SOMO

Kufikia mwisho wa somo hili, inatarajiwa kwamba utaweza:

(i) Kueleza umuhimu wa silabasi, maazimio ya kazi na

mpango wa kipindi cha somo, katika taaluma ya uwalimu

(ii) Kutayarisha maazimio ya kazi na mpango wa kipindi cha

somo.

(iii) Kutoa sababu kueleza kwa nini mambo fulani yanapaswa

kuonyeshwa katika vyombo vya kufundishia

vinavyohusika.

4.1 Silabasi.

Miongoni mwa hatua ambazo unapaswa kuchukua ili uweze kujihami ipasavyo

kwa kazi ya kufundisha ni kuhakikisha kwamba unafahamu yaliyomo katika Silabasi ya

Kiswahili. Silabasi ni chombo muhimu kinachotayarishwa na wakuza mtaala nchini ili kuwaongoza waalimu kuhusu madhumuni ya ujumla ya somo, madhumuni mahsusi ya

Page 26: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

26

vitengo vya somo, pamoja na yale yanayotarajiwa kufundishwa katika viwango tofauti

vya elimu shuleni.

Je, unaweza kufikiria jinsi mambo yangekuwa nchini kama kusingekuweko

silabasi ya pamoja? Matokeo yangekuwa kwamba kila mwalimu angefundisha mambo

tofauti kulingana na matakwa yake, jambo ambalo lingesababisha viwango tofauti vya

elimu nchini. Pia ingekuwa vigumu kwa baraza la mitihani nchini kuwa na kielelezo bora

cha kutumia kama kigezo wakati wa kutahini wanafunzi mwishoni mwa masomo yao.

Kuwepo kwa silabasi kunahakikisha kwamba waalimu wote wanafuata mwongozo sawa

pamoja na kuwa na mwelekeo sawa katika ufundishaji wa somo linalohusika. Kupitia

silabasi wizara ya elimu inaweza, kwa kiasi fulani, kudhibiti mfumo wa elimu nchini na

kuhakikisha kwamba waalimu wanatekeleza wajibu wao sambamba na sera za elimu

nchini.

Je, unayakumbuka mambo ya kimsingi ambayo yanatiliwa mkazo na sera za

elimu nchini Kenya? Ni lazima uyakumbuke mambo hayo kwa sababu ufundishaji wa

Kiswahili, kama vile ulivyo ufundishaji wa masomo mengine, ni lazima uchangie katika

utekelezaji wa madhumuni ya kitaifa. Kwa muhtasari, shabaha za elimu za kitaifa nchini

Kenya zinalenga kutoa elimu ya kuelekeza vijana katika mambo yafuatayo:

(a) Umoja wa taifa.

(b) Maendeleo ya taifa kiunchumi na kijamii.

(c) Maendeleo ya mtu binafsi.

(d) Usawa wa kijamii.

(e) Uthamini na ukuzaji wa utamaduni.

(f) Mwamko wa kimataifa.

Mambo haya, bila shaka , yalitiliwa maanani na wakuza mtaala wakati wa

kutayarisha silabasi. Nawe pia, ukiwa mtekelezaji mkuu wa sera za elimu, huna budi

kuyatilia maanani unapotekeleza wajibu wako wa kufundisha.

Kimuundo mpangilio wa silabasi ya Kiswahili ni hivi kwamba ina sehemu ya

madhumuni ya ujumla ya somo na mgawanyiko wa somo zima katika vitengo vinne

vifuatavyo:

(i) Kusikiliza na kuzungumza.

(ii) Sarufi na matumizi ya lugha.

(iii) Kusoma.

(iv) Kuandika.

Somo zima limegawanyika katika vitengo hivi kuanzia kidato cha kwanza mpaka

kidato cha nne. Pia kila kitengo kinachohusika kinaambatanishwa na shabaha mahsusi

zinazotarajiwa kutekelezwa. Na mambo yanayotarajiwa kufundishwa katika kila kidato

yameorodheshwa chini ya kitengo cha somo kinachohusika.

Kutokana na silabasi hii unaweza kujiandaa kukabili ufundishaji wa somo kwa

kutayarisha maazimio ya kazi, ambayo ni chombo kingine muhimu katika taaluma ya

uwalimu. Kwa hivyo, kabla ya kutayarisha maazimio ya kazi huna budi kuichunguza kwa

undani silabasi ya somo lako ili ufahamu vizuri yaliyomo ndani yake. Ni kufuatia

ufahamu wa mambo haya ndipo utakapokuwa tayari kuukabili vyema ufundishaji wa

somo lako. Itakuwia rahisi, kwa mfano, kuamua kuhusu vitabu vinavyostahili kutumiwa

Page 27: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

27

na wanafunzi ukitumia silabasi kama kielelezo cha kimsingi cha kupimia utoshelevu wa

vitabu hivyo.

ZOEZI 4.1

(a) Chagua shabaha yo yote ya elimu ya kitaifa, na kisha ueleze

jinsi ufundishaji wa Kiswahili shuleni unavyoweza kuchangia

katika ufanikishaji wa shabaha hiyo.

(b) Eleza umuhimu wa silabasi katika utaratibu wa kufundisha.

4.2 Maazimio Ya Kazi.

Katika sehemu iliyotangulia hapo mbeleni tulizungumza juu ya silabasi kama

kimojawapo cha vyombo muhimu katika utekelezaji wa kazi ya kufundisha. Pamoja na

kuwa na silabasi ni lazima mwalimu awe na chombo kingine; na chombo hiki ni

maazimio ya kazi.

Je, maazimio ya kazi ni nini? Na nini umuhimu wake katika taaluma ya uwalimu?

Maazimio ya kazi hutayarishwa kutokana na silabasi. Kwa hivyo ili uweze

kufaulu kutayarisha maazimio ya kazi yanayofaa ni lazima kwanza uwe na ufahamu

mzuri wa silabasi ya somo linalohusika. Maazimio ya kazi ni mpangilio wa mada ambazo

wewe kama mwalimu unaazimia kufundisha katika mfululizo wa vipindi maalum wakati

wa msimu fulani wa masomo. Msimu wa masomo huchukua mwaka mzima ambao

hugawanyika katika mihula mitatu. Na muhula wa masomo huwa na karibu wiki kumi na

tatu hivi. Maazimio ya kazi hutayarishwa kwa kuzingatia mpangilio wa mambo haya.

Wakati wa kutayarisha maazimio ya kazi unadondoa kutoka silabasi mada mbalimbali

ambazo unatarajia kufundisha katika muda fulani. Baada ya kuzidondoa mada hizo

unazivunjavunja katika sehemu ndogondogo kurahisisha ufunzaji wake kwa ufahamu

rahisi. Kisha inakubidi kuzipanga kwa mfuatano wa kimantiki, ukitanguliza kwa mfano

mada zisizo ngumu na kuziweka zile ngumu baadaye.

Kwa ufupi, utayarishaji wa maazimio ya kazi unajishughulisha na uteuzi wa

mada, vipengele vya mada, ufafanuzi wa malengo, uteuzi wa kazi ya wanafunzi pamoja

na vifaa vya kufundishia. Vile vile unajishughulisha na makadirio ya muda ambao

utahitajika kukamilisha ufundishaji wa mada mbalimbali. Muda unaohitajika lazima

ukadiriwe kulingana na kiwango cha ugumu wa mada inayohusika pamoja na upana

wake.

Licha ya kuwa na silabasi, unahitaji kuwa na vitabu vya somo la Kiswahili wakati

wa kutayarisha maazimio ya kazi. Hivi vitakusaidia katika utaratibu wa kuteua kazi na

mazoezi ya kushirikisha wanafunzi ili kufanikisha malengo yaliyowekwa. Silabasi inataja

tu yale yanayohitajika kufundishwa. Ni wajibu wako kama mwalimu kuamua jinsi ya

kufundisha mambo hayo na kuwashirikisha wanafunzi wako. Hapo ndipo vitabu vya

somo la Kiswahili vinapoweza kukusaidia.

Page 28: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

28

ZOEZI 4.2

Je, maazimio ya kazi yana umuhimu gani, na yana faida gani

kwako kama mwalimu? Hebu fikiria kwa makini swali hili na ujaribu

kulijibu mwenyewe kabla ya kuendelea na maelezo yafuatayo.

4.3 Umuhimu Wa Maazimio ya Kazi.

Kwa upande wako kama mwalimu maazimio ya kazi yanakusaidia kutambua

kiasi cha kazi ambayo utakabiliana nayo wakati ujao. Kupitia mpangilio wa kazi unajua

mpangilio wa vipindi utakavyofundisha wakati fulani wa muhula pamoja na mambo

ambayo utayatilia mkazo katika vipindi tofauti. Kwa kurejelea mpangilio huo

unaoonyeshwa katika maazimio ya kazi unaweza kupanga mapema kwa wakati unaofaa

mikakati ya kutumia kukabiliana na uendeshaji wa vipindi vyako. Unaweza kuamua juu

ya vifaa vya kufundishia vinavyohitajika, kuvitafuta na kuvipanga kwa wakati unaofaa

kabla muda wa kufundisha haujawadia. Ikiwa una mada fulani ambazo unahitaji kujua

zaidi juu yake unaweza kuzifanyia utafiti mapema ili usihangaike sana wakati wa

kufundisha unapofika. Vile vile maazimio ya kazi ni chombo muhimu ambacho kinaweza

kukusaidia kuhakikisha kwamba mada za somo lako zinapangwa kwa mtiririko bora

kulingana na jinsi zinavyohusiana na kuingiliana. Hali kadhalika yanakuwezesha

kujitathimini na kuhakikisha kwamba ufundishaji wako unaenda sambamba na masharti

ya silabasi na kuzingatia yanayotarajiwa kuzingatiwa katika kiwango kinachohusika na

kwa muda unaofaa.

Kwa upande mwingine, maazimio ya kazi yanaweza kutumiwa kama

kumbukumbu ya kazi kwako binafsi, pamoja na kwa mwalimu mwingine ambaye

pengine huenda akalazimika kuchukua mahali pako. Katika hali kama hii mwalimu mpya

atakuwa na kielelezo cha kumsaidia kuendelea na kazi iliyoanzwa na mwalimu

mwenzake. Hali kadhalika, maazimio ya kazi ni kifaa bora cha marejeleo wakati wa

kutayarisha kazi ya kutathimini maendeleo ya wanafunzi mwishoni mwa msimu wa

masomo.

Zaidi ya haya, ni chombo mwafaka kinachoweza kutumiwa na wakaguzi pamoja

na wasimamizi wa elimu wakati wanapotaka kufuatilia na kutathimini utendaji kazi wa

mwalimu. Vile vile maazimio ya kazi yanahitajika wakati wa kutayarisha mpango wa

kipindi. Baadhi ya mambo yanayowekwa katika mpango wa kipindi hudondolewa kutoka

maazimio ya kazi.

4.4 Muundo wa Maazimio Ya Kazi

Siyo lazima muundo wa maazimio unaotumiwa na waalimu uwe unafanana.

Unaweza kubadilika kutoka shule moja hadi nyingine. Hata hivyo yapo mambo ya

Page 29: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

29

kimsingi ambayo ni lazima yashirikishwe katika maazimio yo yote ya kazi. Mambo hayo

yanaweza kupangwa katika vipengele vifuatavyo:

(i) Madhumuni ya muhula

(ii) Mwezi

(iii) Juma / Wiki

(iv) Kipindi

(v) Mada / Yaliyomo

(vi) Madhumuni / Malengo ya kipindi

(vii) Mazoezi / Kazi ya wanafunzi

(viii) Vifaa / Marejeleo

(ix) Maoni

Kwa kawaida msimu wa masomo unagawanyika katika mihula mitatu: muhula wa

kwanza, wa pili, na wa tatu. Maazimio ya kazi inafaa yatayarishwe kwa kuzingatia

mfuatano wa mihula, kila muhula ukiwa na maazimio yake. Kwa hivyo unapotayarisha

kazi ya muhula ni lazima uonyeshe maazimio yanayohusika ni ya muhula gani.

Pamoja na hayo, kila muhula inafaa ufafanue madhumuni ya ujumla ambayo

unatarajia kutimiza katika muhula unaohusika. Ni kutokana na madhumuni hayo ndipo

baadaye unapoweza kupata madhumuni maalum ya vipindi.

Kuhusu mwezi, unachohitaji kutaja ni mwezi wa kufundishia. Kwa mfano, kama

ni muhula wa kwanza, mwezi unaweza kuwa wa kwanza (Januari), wa pili (Februari), au

wa tatu (Machi). Kwa sababu mwezi wenyewe hugawanyika katika majuma/ wiki, inafaa

pia kuonyesha ni wiki gani katika mwezi ambapo unapanga kufundisha jambo fulani. Ni

vizuri pia uonyeshe ni kipindi cha ngapi wiki hiyo. Kwa hivyo kabla ya kutayarisha

maazimio ya kazi ni lazima uchunguze katika ratiba ya masomo ya shule ili ujue idadi ya

vipindi ambavyo unatarajiwa kufundisha kila wiki katika somo lako. Kwa kawaida

vipindi vya Kiswahili huwa ni vitano kila wiki lakini vinaweza vikawa vingi au vichache

zaidi kulingana na mpango wa shule.

Mada ni kiini cha somo au funzo muhimu katika kipindi fulani. Kwa mfano, mada

inaweza kuwa: Insha ya methali. Kama hiyo ndiyo mada ya kipindi chako inakubidi pia

ujiulize kile ambacho unatarajia wanafunzi wafanye kuhusu mada inayohusika. Tuseme,

kwa mfano, kwamba unataka wanafunzi wako waandike insha inayobainisha ukweli wa

methali fulani. Ni lazima ueleze jambo hili kwa kauli maalum; na unapofanya hivyo

utakuwa unatoa lengo la kipindi.

Page 30: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

30

ZOEZI 4. 3 B

Je, unaweza kuandika lengo mwafaka la kipindi kutokana na

mada hii?

Pamoja na kufafanua malengo / madhumuni maalum ya kipindi ni lazima

upendekeze kazi ya kushirikisha wanafunzi wakati kipindi cha somo kinapoendelea. Kazi

ya kushirikisha wanafunzi ni lazima ihusiane na mada inayohusika pamoja na malengo

yaliyowekwa. Kazi yenyewe inalenga kuchangia katika utekelezaji wa malengo

yaliyofafanuliwa. Wakati mwingine kazi hii hujulikana kama enabling objectives kwa

Kingereza. Ni kupitia mazoezi haya / kazi hii ndipo malengo yanayotarajiwa kufikiwa

yanapoweza kutimizwa.

Hali kadhalika, unapotayarisha maazimio ya kazi unahitaji vifaa ambavyo huenda

ukavitumia wakati wa kufundisha. Hivi navyo vimetengewa nafasi yake katika muundo

wa maazimio ya kazi.

Sehemu nyingine muhimu ni ile ya maoni. Katika sehemu ya maoni unapaswa

kutoa maelezo kuhusu jinsi mada fulani ilivyofundishwa. Unaeleza jambo lo lote ambalo

huenda lilitokea na kuathiri utekelezaji wa mpango wako. Kila unapoandika maoni

kuhusu kipindi cha somo huwa unajitathimini utendaji kazi wako. Maoni unayoandika

yanalenga kukusaidia unapojiandaa kwa vipindi vitakavyofuata baadaye. Ikiwa kwa

mfano, kipindi chako kilikuwa cha kufana, inafaa ueleze mambo ambayo yalichangia

kukifanikisha. Hali kadhalika, ikiwa kipindi hakikufaulu kama ilivyotarajiwa inafaa

uonyeshe hatua unazopanga kuchukua ili kurekebisha hali. Kwa hivyo, ni lazima utilie

maanani sana mambo unayoandika kama maoni

Page 31: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

31

MFANO WA MAAZIMIO YA KAZI

MUHULA: 1 KIDATO I

Madhumuni/ Malengo: Kufikia mwisho wa muhula wanafunzi wataweza : (1) Kukuza kipawa cha kusikiliza kwa makini na kusoma kwa ufahamu.

(2) Kusikiliza na kuongea kwa matamshi bora.

(3) Kuzingatia sarufi bora na matumizi ya maneno ya aina mbali mbali.

(4) Kuandika insha fupi zenye ukamilifu wa mawazo

MWEZI JUMA KIPINDI YALIYOMO MUDHUMUNI/ MAZOEZI / KAZI YA VI

MALENGO WANAFUNZI VI

February 1 1 Ufahamu Wanafunzi wasikilize Kusikiliza hadithi. Na

2004 Sikizi/ Fasihi kwa makini na kujibu Kutaja hoja muhimu had

Simulizi maswali ya ufahamu katika hadithi hiyo. nya

Kusoma hadithi. ma

Kueleza msamiati

mgumu.

Kujibu maswali ya

ufahamu.

Kutumia maneno

mapya katika sentensi

2 Matamshi/ Wanafunzi watambue na Kusikiliza. Na

maneno kuzingatia matamshi bora Kunakili makosa ya Ta

yanayotatani Wapambanue sauti kimatamshi (Ta

sha zinazokaribiana yanayofanywa na 18/

kimatamshi kimatamshi wenzao.

Kusoma kwa sauti

Kujadiliana katika

vikundi.

Kutamka maneno.

Kutunga sentensi.

Kujibu maswali ya

ufahamu n.k…

MWEZI JUMA KIPINDI YALIYOMO/

MADHUMUNI/

MAZOEZI/ KAZI

VITA

MADA MALENGO YA WANAFUNZI VIFA

3 Kuandika Insha Wanafunzi waandike Kuangalia picha Picha

insha fupi zinazoonyeshwa na zinazo

isiyopungua kurasa mwalimu. matum

nne kuhusu matumizi Kutunga sentensi mbali

ya maji nyumbani. juu ya picha hizo. ya ma

Kuigiza vitendo maish

kadhaa vinavyohusu

matumizi ya maji.

Kueleza mambo

yanayoigizwa n.k…

4 Msamiati/ Maneno Wanafunzi watunge Kutaja maneno

siku.

Page 32: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

32

yenye maana zaidi sentensi kubainisha

yenye maana zaidi Picha

ya moja (Panda) maana tofauti za neno ya moja. ya had

panda.

Wataje maneno

mengine yenye

maana zaidi ya moja

na kuyatunia katika

sentensi tofauti.

Kuangalia picha.

Kutunga sentensi

juu ya picha hizo.

Kusoma nakala.

Kutaja maana za

neno panda

zinazojitokeza

katika kifungu cha

taarifa

kinachohusika.

Kutunga sentensi

Kujibu maswali ya

ufahamu.

MWEZI JUMA KIPINDI YALIYOMO/

MADHUMUNI/

MAZOEZI/

VITA

MADA MALENGO KAZI YA VIFA

WANAFUNZI

February 5 Sarufi/ Ngeli ya 5/6 Wanafunzi waweze Kuangalia picha. Kadi y

2004 ( li-, ya- ) kutumia majina ya Kuulizana na Nakal

ngeli ya 5/6 katika kujibu maswali hadith

sentensi wakitumia juu ya picha. “Kijan

viambisho mwafaka Kutumia majina Mapen

vya sifa na viarifa. ya 5/6. ( li-, ya- ) Mafun

Kusoma hadithi. Kiswa

Kugeuza katika

umoja na wingi

majina ya 5/6.

Kutunga sentensi.

Kujibu maswali

ya ufahamu.

u.k 8

Page 33: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

33

Katika mfano wetu tumeonyesha mpangilio wa vipindi vya muda wa wiki moja tu

ya kwanza. Kwa kufuata mfano huu unaweza kuendelea kuonyesha mpangilio wa vipindi

katika wiki ya pili, tatu na nne. Unapounganisha mpangilio wa vipindi katika wiki moja

hadi nyingine kwa miezi kama mitatu hivi, utaishia kwa kupata maazimio ua muhula

mmoja. Kwa sababu tumezingatia wiki moja tu, kuna mambo mengi ambayo

hayakuonyeshwa katika mpangilio wetu wa kazi. Mara kwa mara, kwa mfano, unahitaji

kuwapatia wanafunzi kazi ya kutathimini maendeleo yao. Na mwishoni mwa muhula,

wanafunzi watahitajika kufanya mtihani wa muhula. Mambo hayo yote unashauriwa

kuyaonyesha katika maazimio ya kazi.

ZOEZI 4.3 C

Chagua kidato cho chote unachotarajia kufundisha katika muhula

fulani. Ukirejelea silabasi ya Kiswahili pamoja na vitabu vya

Kiswahili vinavyopendekezwa kwa kidato kinachohusika, andaa

maazimio ya kazi ya wiki moja. Kisha mwonyoshe mwalimu

mwenzako kazi hiyo na umwombe aikosoe kazi yako.

4.5 Mpango wa Kipindi.

Mpango wa kipindi ni nini? Na una umuhimu gani kwako kama

mwalimu?

Mpango wa kipindi unatayarishwa kutokana na maazimio ya kazi.

Unapotayarisha mpango wa kipindi huwa unaonyesha kile unachotarajia kufundisha

katika muda wa kipindi fulani cha somo au vipindi (kama viwili hivi) na jinsi

unavyotarajia kuukabili ufundishaji wake. Kuwa na mpango wa kipindi ni kwa maana

sana kwa sababu unakupa uwezo wa kuendesha somo ukiwa na mwelekeo maalum

pasipo kubabaika. Mpango wa kipindi ni kama ramani ya barabara inayokuonyesha njia

tofauti unazopaswa kufuata ili kufika vizuri mwisho wa safari yako. Kwa kuzingatia

utaratibu wa mpango wa kipindi mwalimu anakuwa na uhakika kwamba wanafunzi

wanashirikishwa na kushughulikiwa kwa njia inayofaa kwanzia mwanzo wa kipindi hadi

mwisho wake.

Page 34: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

34

Kama vile kuhusu maazimio ya kazi, utayarishajui wa mpango wa kipindi nao pia

una masharti yake ambayo unawajibika kutimiza. Kwa ufupi masharti hayo yanahusu

vipengele vifuatavyo unavyoshauriwa kuonyesha katika kila mpango wako wa kipindi

cha somo:

(i) Mada

(ii) Madhumini / Malengo

(iii) Yaliyomo

(iv) Mazoezi / Kazi ya wanafunzi

(v) Marejeleo / Vifaa

(vi) Muda

Page 35: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

35

Mpangilio wa vipengele hivi unaonyeshwa katika mfano wa mpango wa kipindi

ufuatao

MFANO WA MPANGO WA KIPINDI

SCHOOL: BIAFRA Kidato 1A

Mada: Kuandika / Insha Wakati 11.00-12.00

MADHUMUNI (MALENGO): Kufikia mwisho wa kipindi wanafunzi

. wataandika hadithi ya maneno 200 hivi iliyo na:

(a) matukio yanayoenekana kama yametokea kweli

(b) mifano maridhawa.

(c) msamiati wa kuvutia na kumalizika hivi: kuona

vile tulimpigia makofi mwenzetu kumshangilia

kwa uhodari wake.

MUDA YALIYOMO MAZOEZI/ KAZI YA

KUSHIRIKISHA WANAFUNZI

MAREJEREO

VIFAA

dak 5 Utangulizi:

maelezo ya maneno

rinda,

tiara,

kujiuzulu,

pengo

Wanafunzi wangalie mwalimu

akichora picha ya mama mnene na

tiara ubaoni. Wasikilize maelezo ya

mwalimu.

(i). Picha ya

mama

akifukuzwa na

mlinzi

(ii) Mchoro

wa tiara

dak 15 Mwili:

Hadithi ya ‘Rinda

lapeperuka kama

tiara’

Wanfunzi wataisoma hii hadithi kila

mmoja kimya kimya. Kisha

wataandika katika vikundi sababu

zote zilizofanya hii hadithi ipendeze.

Nakala ya

hadithi “Rinda

lapeperuka

kama tiara’ dak 10 Yanayopendeza

- matukio kama

ya kweli

- mifano

- msamiati wa

kuvutia

Wanafunzi wamwongoze mwalimu

akiandika ubaoni yote yale

yanayopendeza:

Kama kweli Mifano Msamiati

Makadara mbio za umati

Nairobi hatua kuinua mkwaju

ratili mia chache aliamuru

mbili kortini kukanyaga

hatua kama one, two akaamua

kumi hivi n.k. mama watu wa hivi

mlinzi hivi

mama, mama hakuwa

na wasi wasi

pengo

lilipanuka.

dak 10 Tamati

Kazi ya kuandika

hadithi

Wanafunzi waaandike hadithi zao

kufuatana na mfano uliotolewa.

Jaribio la hadithi zao liwe taayari

juma lifuatalo.

Daftari zao za

kazi

Page 36: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

36

4.6 Vipengele vya Mpango wa Kipindi

Kila mojawapo ya vipengele vilivyo katika mpangilio wa kipindi kina umuhimu

wake maalum. Tutajaribu kueleza umuhimu huo kwa ufupi.

Mada

Kila kipindi lazima kiwe na jambo maalum ambalo kinalenga kulishughulikia na

kulitilia mkazo. Jambo hilo ambalo hujitokeza kama kiini cha kipindi ndilo hujulikana

kama mada. Kwa hivyo, kwa kila kipindi cha somo ambacho unafundisha ni lazima

uamue juu ya jambo muhimu ambalo litatawala mkondo wa mafunzo yako. Mambo yote

ambayo utayashughulikia darasani wakati wa kipindi yalenge kufanikisha ufafanuzi wa

mada yako kuu. Katika mpango wa kipindi uliotolewa kama mfano mada ni Insha; na

yale mambo yote ambayo yanapendekezwa kuonyeshwa na mwalimu pamoja na yale ya

kuwashughulisha wanafunzi yana lengo la kuandaa wanafunzi kwa zoezi la kuandika

insha.

Mada za kushughulikia katika vipindi vyako vya somo unazipata kutoka

maazimio yako ya kazi. Umuhimu wa kutaja mada katika mpango wa kipindi ni kwamba

mada inatoa, kwa kiasi fulani, mkutadha wa mafunzo yako na kukuongoza kuhusu

maenezi yake.

Madhumuni / Malengo.

Kwa kawaida, wakati unapofunga safari, huwa huamki kwa ghafla na kwenda

binvu bila mwelekeo maalum. Ikiwa utafanya hivyo, safari inaweza ikaishia kwa

kuhatarisha maisha yako au kwa kutokuwa na faida yo yote.

Taaluma ya kufundisha inaweza kufananishwa na ufungaji wa safari. Kama vile

msafiri anavyopaswa kujua kule anakoelekea kabla hajaanza safari yake, ndivyo pia nawe

kama mwalimu unavyopaswa kujua mwelekeo wa somo lako kabla hujaanza kufundisha.

Na njia mojawapo ya kujua mwelekeo huo ni kuwa na madhumuni / malengo ya kipindi.

Lengo au madhumuni ya kipindi ni kauli maalum inayofafanua kile ambacho

mwanafunzi anatarajiwa kufanya kufikia mwisho wa kipindi fulani cha somo. Matarajio

hayo ndiyo yatakuwa kama dira ya kukuongoza wakati wa kuendesha somo lako, na

kuhakikisha kwamba unafuata utaratibu unaofaa. Mara nyingi vipindi vya lugha

vinaendeshwa ovyo ovyo na kukosa kuwa na manufaa kwa wanafunzi kutokana na

ukweli kwamba waalimu huwa wanafundisha bila kuwa na lengo wazi

wanalolishughulikia. Katika hali kama hiyo zoezi la kufundisha linakuwa kama mchezo

wa bahati nasibu.

Kwa upande mwingine, lengo ni kielelezo bora ambacho kinaweza kutumiwa

kama kigezo cha kupimia kufaulu au kutofaulu kwa somo. Baadaya kipindi fulani, kwa

mfano, utarejelea lengo lako uliloweka wakati unapotunga maswali ya kutahini

wanafunzi juu ya kiini cha somo kinachohusika.

Page 37: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

37

ZOEZI 4.4 A

Kwa maoni yako ni masharti gani ambayo yanapaswa

kuzingatiwa wakati wa kufafanua lengo la kipindi? Jibu

swali hili kabla ya kuendelea na maelezo yafuatayo.

Miongoni mwa masharti ambayo unapaswa kuzingatia wakati unapofafanua lengo

la kipindi ni pamoja na yafuatayo:

Kuhakikisha kwamba lengo lina uwiano na mada inayohusika.

Lifafanuliwe hivi kwamba linaweza kutimizika katika muda uliopo wa kipindi

cha somo.

Lazima lifafanuliwe kinaganaga kwa viarifa vinavyorejelea vitendo vilivyo

wazi.

Liegemee upande wa mwanafunzi na wala siyo upande wa mwalimu.

Litaje wazi wazi kile kinachotarajiwa kufanywa na mwanafunzi kufikia

mwisho wa kipindi.

Ni lazima lijikite katika maenezi ya stadi maalum pamoja na kuwa na kipimo / kikomo fulani cha utekelezaji.

Je, ina maana gni kusema kwamba lengo ni lazima liwe na uwiano na mada?

Kauli hii inamaanisha kwamba lengo linapaswa kuwa na uhusiano wa kimantiki na kiini

au wazo kuu la kipindi. Lijishughulishe na mambo ambayo hayana uhusiano wo wote na

wazo kuu linalotarajiwa kuzungumziwa katika kipindi. Kwa mfano wakati wa kipindi cha

somo la fasihi kama unazungumzia wahusika na sifa zao katika kitabu fulani, utakosea

kutayarisha lengo ambalo badala ya kushughulikia kutaja na kueleza sifa za wahusika

fulani, litawataka wanafunzi kufafanua na kutoa mifano ya tamathali mbali mbali za

usemi.

Kwa upande wa muda wa kipindi, unapofafanua lengo ni lazima utilie maanani

muda utakaohitajika kutekeleza lengo hilo. Lisiwe lengo ambalo haliwezi kutimizika

katika muda uliyowekwa au ambalo linahitaji muda kidogo zaidi kuliko ule uliyowekwa.

Kwa hivyo, unaweza kuwa na lengo moja au zaidi ya moja kulingana na kiasi cha muda

ulio nao.

Viarifa vinavyorejelea vitendo wazi ni viarifa vya namna gani? Ni vipi kwa

mfano, kati ya viarifa vifuatavyo vinaweza kuelezwa kuwa vinarejelea vitendo wazi?

Kutaja, kujua, kutoa mifano, kufahamu, kueleza maana, kufurahia, kuthamini…..? Na

vipi kati ya viarifa hivi vinafaa kutumika katika ufafanuzi wa lengo la kipindi cha somo?

Ni vipi havistahili kutumika, na kwa nini?

Hivi vifuatavyo ndivyo havistahili kutumiwa: kujua, kufahamu, kufurahia,

kuthamini. Havistahili kwa sababu vinaashiria vitendo ambavyo utimilifu wake hauwezi

kutambulika moja kwa moja kwa njia iliyo wazi. Havina kielelezo cho chote ambacho

kinaweza kusaidia kutambua kama mambo vinayoashiria yametimilika. Kwa mfano,

ukitaka kutambua ikiwa mwanafunzi anafurahia au anathamini jambo fulani utahitaji

kuchunguza mwenendo wake na vitendo vyake vya nje. Kwa upande mwingine, viarifa

Page 38: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

38

vifuatavyo vinafaa kutumika: kutaja, kutoa mifano, kueleza maana. Utimilifu wake

unaweza kutambulika moja kwa moja bila shida. Ukipanga, kwa mfano, kwamba

wanafunzi wataeleza maana ya dhana fulani na kutoa mifano ya kuonyesha dhana hiyo,

unaweza kutambua moja kwa moja ikiwa wametekeleza matarajio yako au la.

Shule ni mahali pa kumsaidia mwanafinzi kujiendeleza kimasomo, na mambo

yanayotendeka darasani yanakusudia kuchangia ufanisi wa jambo hili. Kwa hivyo wakati

unapotayarisha mpango wa kipindi ni lazima uyape kipaumbele mahitaji ya mwanafunzi.

Ili hukakikisha kwamba mahitaji ya mwanafunzi yanazingatiwa kikamilifu wakati wa

kipindi cha somo unashauriwa kufafanua lengo la kipindi kwa kumshirikisha

mwanafunzi kama mhusika mtendaji mkuu. Sababu mojawapo ya kufanya hivi ni

kuhakikisha kwamba wanafunzi wanapewa fursa ya kushughulika kikamilifu katika

kipindi. Kwa mujibu wa sharti hili, kwa mfano, utakuwa umekosea kuandika lengo kama

lifuatalo: Kufikia mwisho wa kipindi mwalimu ataeleza maana ya “ubwege” na kutoa

mifano ya kutilia maki maelezo yake kutoka tamthilia ya Amezidi.

Kosa la lengo hili ni pale ambapo mwalimu ametumiwa badala ya mwanafunzi.

Lengo limeegemea upande wa mwalimu badala ya mwanafunzi, jambo ambalo linaenda

kinyume na maelezo yaliyotolewa kuhusu ufafanuzi wa lengo la kipindi.

Unapojiandaa kufundisha huwa unatarajia kwamba malengo unayojiwekea

yatafikiwa katika muda mahsusi. Unapoandika lengo la kipindi ni bora urejelee muda huo

unaotarajiwa kutumiwa ili kutimiza lengo lililowekwa. Kauli isemayo kwamba lengo

litaje kile kinachotarajiwa kufanywa na wanafunzi kufikia mwisho wa kipindi

inazungumzia jambo hili. Kwa kawaida, somo la Kiswahili linachukua muda wa kipindi

kimoja; na ukiwa zaidi huwa hauzidi vipindi viwili mfululizo. Katika mfano wa lengo

ambao ulitolewa hapo awali, unaweza kuona kwamba sharti hili limezingatiwa kulingana

na maneno yanayotumiwa katika sehemu ya utangulizi. Maneno hayo yanataja wakati

ambapo lengo linalohusika linatarajiwa kutekelezwa. Ni muhimu kwako kama mwalimu

kuzingatia jambo hili kwa sababu litakuwa kumbusho kwako kuhusu kiasi cha muda ulio

nao usije ukapanga kazi ambayo hailingani na muda wa kufundishia.

Je, tunamaanisha nini kusema kwamba lengo ni lazima lijikite katika maenezi ya

stadi maalum ya lugha? Kama tujuavyo, lugha ni somo ambalo limejikita sana sana

katika umilisi na uimarishaji wa stadi mbali mbali za mawasiliano. Kutokana na ukweli

huu, unashauriwa kuona kwamba unapotayarisha lengo la kipindi unatilia maanani stadi

fulani ya lugha. Na wakati wa kufundisha huna budi kushirikisha wanafunzi wako katika

mazoezi yanayoambatanisha stadi hiyo.

Jambo jingine ambalo ni muhimu katika lengo la kipindi ni kipimo / kikomo cha

utekelezaji. Hiki ni kama kiwango cha ufanisi ambacho unatarajia mwanafunzi ataweza

kufikia. Ni kigezo ambacho unaweza kutumia kutathimini mafanikio ya wanafunzi

pamoja na uwezo wao kuhusu mada iliyoshughulikiwa. Tukirejelea mada ya ubwege,

kwa mfano, tunaweza kuandika lengo kama lifuatalo: Kufikia mwisho wa kipindi

mwanafunzi ataeleza kwa kuandika maana ya ubwege na kutoa, angalau, mifano minne

ya kutilia maki maelezo yake kutoka tathimilia ya AMEZIDI.

Kulingana na matarajio ya lengo hili, kuna idadi ya mifano ambayo mwanafunzi

anatakiwa kutoa. Idadi hii inatoa kielelezo cha utendaji kinachotarajiwa kwa upande wa

mwanafunzi kama ushahidi kwamba amefikia kiwango kinachotarajiwa. Kila

mwanafunzi ambaye angetimiza idadi ya mifano iliyowekwa ingesemekana kuwa

amefikia kile kiwango kinachohitajika. Lengo hili pia limetimiza masharti mengine

Page 39: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

39

yaliyotajwa katika maelezo kuhusu utayarishaji wa lengo la kipindi kwa jumla. Kwa

mfano, limeeleza wazi wazi jinsi mwanafunzi anavyotarajiwa kueleza maana ya ubwege.

Limejikita katika maenezi ya stadi ya uandishi. Hata ingawa wakati wa kipindi wanafunzi

wanaweza kushiriki katika mazungumzo, ni wazi kulingana na lengo kwamba

kipaumbele katika kipindi kitapewa stadi ya uandishi.

ZOEZI 4.6 B

Onyesha ikiwa, kwa maoni yako malengo

yafuatayo yemefafanuliwa kwa utaratibu unaofaa kwa

kuweka alama ( X) katika nafasi iliyoachwa pembeni

mwa lengo husika.

Kufikia mwisho wa kipindi SAWA SI SAWA

1. Wanafunzi watafahamu sifa za shairi.

2. Wanafunzi watatoa, angalau mifano mitatu ya

tasfida kutoka kifungu cha habari

watakachosoma.

3. Wanfunzi watajua maana ya majina ya majazi.

4. Nitafundisha maneno yenye maana zaidi ya moja

5. Wanafunzi watafafanua maana ya moja kati ya

methali zifuatazo na kuandika insha ya maneno

kama 500 hivi ambayo inabainisha ukweli wa

methali hiyo.

Nyani haoni kundule.

Fimbo ya mbali haiui nyoka

Nazi haishindani na jiwe.

6. Wanafunzi watandika insha juu ya

mmomonyoko wa udongo

Page 40: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

40

ZOEZI 4.6 C

Chagua mada zo zote nne kutoka silabasi ya Kiswahili

zinazopendekezwa kufundishwa katika kidato fulani. Kwa

kuzingatia masharti ya ufafanuzi wa malengo ya kipindi,

andika lengo mwafaka linaloambatana na mada inayohusika.

Yaliyomo

Kila unapochagua mada ya kufundisha katika kipindi fulani cha somo huna budi

kuamua ni mambo gani ambayo unapanga kuzungumzia au kugusia juu ya mada hiyo.

Maelezo ya vitengo vya ndani vya mada ndiyo hujenga yale yaliyomo katika kipindi

fulani. Kwa maneno mengine, yaliyomo ni mgawanyiko wa vijisehemu vidogo vidogo

vya mada inayohusika. Ni muhimu kwako kama mwalimu kuonyesha mgawanyiko huo

kwa sababu unapofanya hivyo unapata mwongozo kuhusu mambo mbali mbali ambayo

utagusia katika hatua tofauti za kipindi chako cha somo. Unapata nafasi ya kufikiria juu

ya mambo hayo mapema kabla ya somo; na wakati wa somo unapata nafasi ya kuendesha

somo lako kwa mtiririko unaofaa bila kuchanganyikiwa kimawazo wala kuwakanganya

wanafunzi wako.

Tuchukue mfano wa mada kama Ushairi katika kipindi cha somo la fasihi. Baada

ya kufafanua lengo kuambatana na mada hii ni wajibu wako kuvunjavunja na

kuigawanya mada yako katika vipengele tofauti ambavyo unatarajia kugusia katika hatua

tofauti za kufundisha somo. Inakubidi uonyehse ni jambo gani litashughulikiwa katika

hatua ya utangulizi, ya mwili/ upanuzi, na tamati/ hitimisho. Katika utangulizi, kwa

mfano, unaweza kuwa na yaliyomo kama vile:

(i) Marejeleo ya kipindi kilichotangulia.

(ii) Tanzu za fasihi andishi.

Na katika sehemu ya mwili wa kipindi unaweza kuwa na yaliyomo kama vile:

(i) Tofauti za ushairi na fani nyingine za fasihi.

(ii) Aina za mashairi

(iii) Sifa za kimsingi za shairi n.k……

Katika sehemu ya tamati (utamamatisho) miongoni mwa mambo ambayo

unaweza kupendekeza ni kama vile:

(i) Muhtasari wa somo.

(ii) Kazi ya zoezi n.k…….

Mazoezi ya /Kazi ya Wanafunzi

Mazoezi ya wanafunzi yanaonyesha mambo ambayo wanafunzi

watajishughulisha nayo katika kila hatua ya kipindi cha somo. Ni lazima uhakikishe

kwamba mazoezi ambayo yanapendekezwa yana uhusiano na yaliyomo yanayohusika.

Pia unapaswa kutoa mazoezi ya aina tofauti. Mazoezi ya wanafunzi yanatofautiana kabisa

na yaliyomo pamoja na shughuli zako kama mwalimu. Kwa hivyo, usieleze shughuli za

mwalimu katika sehemu ya mpango wa kipindi ambayo inatengwa kwa mazoezi.

Page 41: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

41

Kutofanana na yaliyomo, mazoezi ya wanafunzi hufafanuliwa katika vielelezo vya

sentensi, wakati ambapo yaliyomo yanaonyeshwa tu kwa vifungu vya maneno ambayo

hayatowi taarifa kamili. Yaliyomo ni vichwa tu vya yale yanayoshughulikiwa lakini

mazoezi hutaja kikamilifu vitendo vya wanafunzi.

Marejeleo / Vifaa:

Hivi ni vyombo vyote ambavyo utavitegemea katika utekelezaji wa kazi yako ya

kufundisha. Mfano ni kama vile vitabu, vitu halisi, picha, michoro n.k….

Muda:

Unapoandaa mpango wa kipindi ni jambo la busara kuonyesha wakati unaotarajia

kutumia ili kukamilisha hatua tofauti za kipindi chako. Makadirio ya muda ni muhimu

kwa sababu husaidia kuhakikisha kwamba kipindi kinafululiza kwa mwendo unofaa.

HITIMISHO

Somo hili limegusia mambo muhimu ambayo unawajibika kufanya ili kujiandaa

kwa kazi ya kufundisha. Unashauriwa kwamba ni lazima usikose kujihami kwa kuwa na

silabasi, maazimio ya kazi, pamoja na mpango wa kipindi. Vyombo hivi vitatu

vinahusiana na kuathiriana. Silabasi ni chombo ambacho mwalimu hutegemea

anapotayarisha maazimio ya kazi; na ni kutokana na maazimio ya kazi ndipo anatayarisha

mpango wa kipindi. Ni wajibu wako kama mwalimu kuhakikisha kwamba unapata

silabasi ya somo lako mapema ili uichunguze kwa undani na kufahamu vilivyo kile

unachotarajiwa kufanya kulingana na silabasi hiyo. Kisha unaweza kuandaa maazimio ya

kazi ambayo yatakufaa wakati wa kuandaa mipango yako ya vipindi vya somo.

ZOEZI 4.6 D

Ukirejelea mada zo zote tatu kati ya mada nne ulizochagua

katika zoezi 4.6 C, tayarisha mpango kabambe wa kipindi

unaolenga kushughulikia kila mojawapo ya mada hizo.

( ie. mipango mitatu)

Page 42: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

42

SOMO LA 5

KUSIKILIZA NA KUONGEA

5.0 Utangulizi.

Kusikiliza na kuongea ni stadi muhimu sana katika utaratibu wa kujifunza na

kufundisha lugha. Pia stadi hizi mbili hutegemewa zaidi katika shughuli za mawasiliano

ya kila siku kuliko Kusoma na Kuandika. Kulingana na wataalamu, kusikiliza na kuongea

vinachukua karibu asilimia 75%, ya shughuli za mawasiliano ya kila siku. Kwa upande

mwingine, kusoma na kuandika vinachukua karibu asilimia 25%. Kwa mujibu wa

wataalamu hao, kusikiliza kwenyewe kunachukua karibu asilimia 45%, hali ambapo

kuongea kunachukua asilimia 30%.

Katika somo hili, tutatoa mapendekezo ya mambo ambayo unaweza kufanya ili kusaidia wanafunzi wako kuendeleza na kuimarisha uwezo wao wa kusikiliza na kuongea

Kiswahili kwa ufahamu.

MADHUMUNI YA SOMO.

Kufikia mwisho wa somo hili utaweza:

Kueleza umuhimu wa kusikiliza na kuongea katika

utaratibu wa kufundisha Kiswahili.

Kupendekeza mbinu mwafaka unazoweza kutumia

kusaidia wanafunzi wenye shida za kusikiliza kwa

ufahamu.

Kupendekeza mbinu tofauti unazoweza kutumia kukuza

uwezo wa wanafunzi wa kujieleza kwa ufasaha wa lugha

na matamshi bora.

5.1 Umuhimu Wa Kusikiliza.

Kulingana na ukweli wa mambo katika shule, kusikiliza na kuongea havitiliwi

sana mkazo katika mfumo wa elimu. Hata mwishoni mwa masomo mitihani inajikita

katika lugha andishi. Kutokana na hali hii, hata ufundishaji wa lugha unaelekea

kuegemea zaidi katika lugha ya uandishi kuliko lugha ya uzungumzi. Ukiwa mwalimu

wa Kiswahili unashauriwa kutofuata mtindo huu wa kufundisha ambao unawanyima

wanafunzi nafasi ya kuidhibiti lugha kikamilifu na kuzimudu mbinu zake zote za

mawasiliano.

Uwezo wa kusikiliza ni muhimu sana katika kipengele cha mawasiliano na

uhusiano wa kibinadamu. Kwa kawaida ni rahisi zaidi kuwasiliana na kuelewana na mtu

mwenye umakinifu wa kusikiliza kuliko yule ambaye anakosa umakinifu. Pia, katika

Page 43: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

43

mkutadha wa mazingira ya darasani kusikiliza ni muhimu sana kutokana na ukweli

kwamba mafunzo ya darasani hutegemea sana lugha ya mazungumzo. Ili aweze kufaidika

kutokana na mafunzo hayo, ni lazima mwanafunzi awe na uwezo wa kusikiliza na

kufahamu ipasavyo. Hali kadhalika, kupitia mazoezi ya kusikiliza mwanafunzi anapata

fursa ya kupanua upeo wa msamiati wake pamoja na ujuzi wa sarufi. Kadiri

anavyosikiliza ndivyo anavyozidi kuimarisha ujuzi wake wa msamiati pamoja na sarufi.

Ikiwa unataka wanafunzi wako waimarishe ujuzi wao wa Kiswahili una wajibu wa

kuwashirikisha katika vipindi vya kusikiliza mazungumzo tofauti ya Kiswahili.

Vilevile kusikiliza kunasaidia katika juhudi za kufundisha matamshi. Ili mwanafunzi aweze kutamka vizuri, ni lazima kwanza awe na uwezo wa kupambanua

sauti zinazohusika katika usikizi wake. Bila uwezo huu ataishia kwa kutamka maneno na

kuzungumza kwa namna ambayo inakanganya.

ZOEZI 5.1

Eleza kwa nini watu hujishughulisha na kusikiliza

yale wanayoyasikiliza.

5.2 Kusikiliza Kwa Ufahamu (Ufahamu Sikizi).

Je, ufahamu sikizi unahusu nini? Na ni mambo gani ambayo huenda yakamzuia

mwanafunzi kusikiliza kwa ufahamu?

Ufahamu sikizi ni fani ya lugha ya uzungumzi ambayo kwayo msikilizaji hupokea

ujumbe wa mzungumzaji na kuuambatanisha na maana inayotakikana. Ni fani ambayo

inahusisha utoaji wa ujumbe na upokeaji wake kupitia sauti. Madhumuni hasa ya

kushirikisha wanafunzi katika zoezi la kusikiliza kwa ufahamu ni kuwaelekeza katika

misingi ya kuwawezesha:

Kuwa na umakinifu katika kusikiliza

Kupokea ipasavyo ujumbe unaowalishwa katika mazungumzo

Kuambatanisha ujumbe unaopokelewa na maana sahihi na kuitikia ipasavyo.

Kudhibiti ujumbe unaopokelewa katika kumbukumbu.

Kutambua mambo muhimu na kuyatenganisha na yasiyo muhimu.

Kila moja kati ya mambo ambayo yametajwa lina umuhimu katika ufanisi wa

ufahamu. Mwanafunzi kwa mfano, akiwa mmakinifu atasikiliza kwa uangalifu akitilia

maanani kila jambo linalosemwa. Hatapoteza kwa urahisi mwelekeo wake katika

kusikiliza. Huwa na uwezo wa kujikinga dhidi ya mambo yanayoweza kukatiza usikizi

wake na kutatiza ufahamu wake. Anaweza kutambua uhusiano na mwingiliano kati ya

yanayosemwa pamoja na kufuata vizuri mtiririko wa mawazo katika mazungumzo. Vile

vile anaweza kujihusisha vilivyo na mkondo wa mazungumzo na kuitikia kama

inavyostahili kulingana na hali ya mazungumzo hayo. Kwa kufuatilia mwitiko wa

wanafunzi wewe kama mwalimu unaweza kutambua jinsi mazungumzo yako

yanavyopokelewa. Unaweza kutambua ikiwa mazungumzo hayo yanaibua hisia

zinazostahili au la.

Page 44: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

44

Umakinifu ni jambo la kimsingi na ambalo pia husaidia kufanikisha utekelezaji

wa madhumuni mengine yaliyotajwa. Mwanafunzi asipokuwa na umakinifu, kwa mfano,

hawezi kutambua kwa urahisi mambo muhimu na yale yasiyo muhimu. Hawezi pia

kuupokea ipasavyo ujumbe unaowasilishwa na kuuambatanisha na maana inayotarajiwa.

Hali kadhalika hatakawia kusahau yale anayosikiliza. Na ikiwa kufikia mwisho wa zoezi

la kusikiliza atakuwa amesahau yaliyozungumzwa hali hii itaathiri vibaya kiwango cha

ufahamu wake.

ZOEZI 5.2

Jaribu kufananua kwa undani zaidi madhumuni ya zoezi

la ufahamu yaliyotajwa.

5.3 Vizuizi Vya Ufahamu Sikizi.

Je, unaweza kukumbuka wakati wo wote ambapo wewe ukiwa mhusika

msikilizaji umewahi kushindwa kusikiliza kwa ufahamu? Unaweza kukumbuka ni kwa

sababu gani hukuweza kusikiliza kwa ufahamu? Je, unaweza pia kukumbuka wakati

mwingine, ambapo wewe ukiwa mhusika mzungumzaji, wale waliokusikiliza

walishindwa kukusikiliza kwa ufahamu? Chanzo hasa cha hali hiyo kilikuwa nini?

Hali kama hiyo inaweza kutokea na kutatiza kiwango cha ufahamu wa wanafunzi.

Wewe kama mwalimu una wajibu kuelewa matatizo yanayohusika ili uweze

kuhakikisha kwamba wanafunzi wako wanaepukana nayo wakati wanaposikiliza. Kwa

ufupi matatizo haya yanaweza kuainishwa katika makundi yafuatayo:

Chanzo cha habari ( Mzungumzaji)

Msikilizaji

Mazingira

Ujumbe husika

.

Chanzo Cha Habari.

Aghalabu kusikiliza kunaambatana na kuzungumza. Unaposikiliza, ule ujumbe

unaopokea huwa haujitokezi katika ombwe tupu. Unawasilishwa na mtu fulani moja kwa

moja au kupitia chombo fulani cha mawasiliano. Upokezi wa ujumbe unaohusika

unaweza kufanikishwa au kutatizwa na yule anayeutoa au chombo kinachotumiwa

kuwasilisha ujumbe huo. Chanzo cha habari kinaweza kutatiza ufahamu sikizi kwa

sababu kama zifuatazo:

Matamshi mabaya

Uteuzi mbaya wa maneno.

Mpangilio mbaya wa mawazo.

Page 45: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

45

Upazaji wa sauti.

Hulka ya mzungumzaji

Wakati unaposikiliza huwa unapokea ujumbe unaowasilishwa na mzungumzaji

kupitia maneno anayotamka. Ikiwa mzungumzaji ana shida ya kimatamshi huenda

akatamka vibaya na kuishia kwa kupotosha maana. Kwa mfano, maneno yafuatayo

yanatakiwa kutamkwa kwa njia tofauti: fua, vua; pua, bua. Ikiwa mzungumzaji ana

shida ya kutofautisha kati ya /f/ na /v/, /p/ na /v/ atachanganya matamshi ya maneno

yenye vitamkwa hivi na kuishia kwa kupotosha maana, jambo ambalo litamfanya

msikilizaji atafsiri ujumbe kwa njia isiyokusudiwa. Tuchukue mfano wa mzazi ambaye

anatoa agizo kama hili kwa mtoto mchanga: “Usisahau kuvua soksi zako kabla ya

kulala”. Kwa sababu ya utiifu wake, mtoto anaweza kuitikia kulingana jinsi anavyoelewa.

Lakini baadaye mtoto huyu atagundua kwamba kitendo alichofanya siyo kile ambacho

kilikusudiwa na mzazi wake wakati alipotoa agizo! Mtoto anashindwa kusikiliza kwa

ufahamu kwa sababu ya matamshi ya mzazi wake. Mfano mwingine wa tatizo la

kimatamshi unahusu ile hali ya kugeuza mfuatano wa vitamkwa katika maneno. Tamthili

ya hii ni maneno haya: karibuni, kaburini, sitini, tisini, kusihi, kuhisi.

Ukichunguza maneno haya utatambua kwamba yana vitamkwa sawa ila tu

mfuatano wa vitamkwa hivyo ndio unatofautiana. Mzungumzaji asipokuwa mwangalifu

huenda akatamka neno lingine badala ya lile alilokusudia na kumfanya msikilizaji

asielewe ujumbe kama inavyostahili.

Jambo lingine ambalo linaweza kumkanganya mwanafunzi na kumfanya asiweze

kusikiliza kwa ufahamu ni uteuzi mbaya wa maneno yanayotumiwa na mzungumzaji

kuwasilisha ujumbe wake. Maneno ni chombo muhimu kinachotegemewa katika

mawasiliano ya lugha. Ikiwa unataka ujumbe wako ueleweke vizuri huna budi kutumia

maneno yanayofaa. Kwa mfano, ikiwa utatumia neno mpunga badala ya mchele

utawakanganya wasikilizaji wako. Kulingana na matumizi ya Kiswahili sanifu kwa

mfano kuna tofauti kubwa kati ya neno sana na zaidi, lakini kuna watu ambao

hawang’amui tofauti kati ya maneno hayo na huwa wanatumia neno zaidi katika

mkutadha ambamo neno mwafaka lingekuwa sana. Ukisema kwa mfano, ‘Nimechoka

zaidi”, badala ya kusema “ Nimechoka sana”, msikilizaji ambaye anaimudu vizuri lugha

ya Kiswahili ataelewa kwamba unalinganisha hali yako ya kuchoka na ya mtu mwingine

au watu wengine ambao pia wamechoka. Kile ambacho ataelewa ni kwamba wewe

umechoka zaidi kuliko wao. Mfano mwingine unahusu matumizi ya –dogo na –chache.

Wapo watu ambao hutumia –dogo badala ya –chache. Usipokuwa mwangalifu unaweza

kupotoshwa na matumizi yao ya neno hilo. Chanzo cha tatizo hili pengine ni kwamba

katika lugha zao za mama dhana ya idadi na ukubwa huwasilishwa na neno moja tu

wakati ambapo katika Kiswahili kila dhana huwasilishwa kwa kutumia neno tofauti.

Kama mzungumzaji ana shida ya kung’amua maenezi ya maana za maneno huenda

akakanganya wasikilizaji wake. Wasipokuwa waangalifu na kufasiri ujumbe kwa

kuzingatia vizuri mkutadha wa matumizi wa maneno yanayohusika wanaweza kushindwa

kuelewa ujumbe ipasavyo.

Wakati mwingine, wanafunzi au wasikilizaji wanaweza kukosa kusikiliza kwa

ufahamu kutokana na hali ya kuudhiwa na mzungumzaji. Ikiwa mazungumzo

yanamwudhi msikilizaji, bila shaka atakosa hamu ya kusikiliza kwa makini, jambo

ambalo litaathiri vibaya hali yake ya ufahamu. Mzungumzaji anaweza kuwaudhi vipi

Page 46: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

46

wasikilizaji wake? Anaweza kuwaudhi , kwa mfano kama lugh ayake inachochea hisia za

chuki. Pengine anaweza kuwaudhi kwa kutotumia lugha kwa uangalifu na kuishia kwa

kuwakosea heshima wasikilizaji wake kutokana na mifano anayoitoa kutilia maki

mazungumzo yake. Mifano hiyo inaweza kuwa inawahusu baadhi ya wasikilizaji, na

wanaweza kuyachukulia mazungumzo kama kwamba yanawalenga wao makusudi! Ikiwa

ni hivyo, huenda wakaamua kuyapuza mazungumzo hayo na kutosikiliza.

Kwa hivyo, ni wajibu wako kama mwalimu kuhakikisha kwamba unatilia

maanani hisia za wanafunzi juu ya mambo yanayotumiwa kufundishia ufahamu.

Kitu kingine kuhusu chanzo cha habari ambacho kinaweza kutatiza ufahamu wa

msikilizaji ni upangaji wa mawazo mbaya katika mazungumzo. Ujumbe ambao

unaeleweka kwa urahisi ni ule ambao unawekwa katika muundo maalum wa

kimawasiliano. Wazo kuu la ujumbe huo labainika wazi na ufafanuzi wake unajitokeza

kwa mtiririko bora wa mawazo. Lakini mawazo yakilundikwa ovyo ovyo bila mfululizo

wa kimantiki, msikilizaji anaweza kukanganywa na kushindwa kusikiliza kwa ufahamu.

Itakuwa vigumu kwake kuupokea na kuzingatia vizuri ujumbe unaowasilishwa.

Mawasiliano huwa hayajakamilika kabla ujumbe haujamfikia mhusika mpokezi.

Katika mkutadha wa mazungumzo, mawasiliano hukamilika wakati ambapo msikilizaji

amesikia ujumbe huo. Mzungumzaji akiwa na shida ya kutoa sauti kwa njia ya kusikika

ufahamu nao hautawezekana. Kwa hivyo, wakati unaposhirikisha wanafunzi katika zoezi

la ufahamu sikizi ni lazima uhakikishe kwamba ujumbe unaohusika unawafikia vizuri

wanafunzi wako.

Mara nyingi pia hali na tabia ya mzungumzaji kwa jumla vinaweza kuchangia

kufanikisha au kutatiza ufahamu wa msikilizaji. Ni kweli, nyumba si mlango; lakini pia

ni kweli kwamba bila mlango nyumba huwa haifai kitu. Vile vile kama mlango wa

nyumba haupitiki nyumba yenyewe haina faida! Hulka ya mzungumzaji inaweza

kufananishwa na mlango wa nyumba. Pia ujumbe unaowasilishwa unaweza

kufananishwa na nyumba. Ikiwa mlango wa nyumba unavutia, huenda watazamaji

wakitamani kuingia ndani ya nyumba hiyo wajionee yale yaliyomo. Lakini kama uchafu

umelundikana kwenye mlango ambao nao pia umekaa segemnege watazamaji

hawatakuwa na hamu ya kutaka kuingia ndani ya nyumba hiyo. Matokeo yake ni

kwamba hawataweza kujua vitu vilivyomo ndani ya nyumba. Hali kadhalika, katika

mkutadha wa mazungumzo kama hulka ya mzungumzaji hairidhishi na kuvutia, itakuwa

vigumu kwa wasikilizaji kusikiliza kwa makini. Na matokeo ya utovu wa umakinifu ni

kukosekana kwa ufahamu unaofaa.

Msikizaji:

Kuna mambo ambayo yanaweza kumzuia mtu kusikiliza kwa ufahamu ambayo

chanzo chake ni hali ya msikilizaji mwenyewe. Baadhi ya mambo hayo ni kama vile:

Kutosikiliza kwa dhati.

Usikizi mbaya.

Ufasiri wa maana kwa njia isiyofaa.

Uhakiki wa kupindukia.

Udhaifu katika lugha.

Mtu ambaye anasikiliza kwa dhati anatia bidii katika shughuli hiyo. Hutia bidii

kwa sababu huwa na ari ya kusikiliza; lakini akikosa ari hatajishughulisha kwa bidii. Kwa

Page 47: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

47

sababu ya kutokuwa na ari huenda akasikiliza bila umakinifu, jambo ambalo linachangia

hali ya kutofahamu ipasavyo. Atashindwa kufahamu kwa sababu hatashughulikia

kikamilifu yale yanayosemwa. Kwa hivyo, wewe kama mwalimu ukitaka wanafunzi

wako wasikilize kwa dhati na makini ni lazima uwahamasishe na kuhakikisha kwamba

wanaposikiliza wanakuwa na lengo mahsusi la kusikiliza. Hivyo ndivyo wanvyoweza

kusikiliza kwa dhati na kufahamu yasemwayo. Bila kuwa na lengo mahsusi watasikiliza

ili kutimiza mradi tu. Lakini wakielewa vizuri matarajio ya zoezi la kusikiliza

watajishughulisha inavyostahili. Jambo lingine ambalo linaweza kuwafanya wanafunzi

kutosikiliza kwa dhati ni uchovu wa kimwili na kiakili. Ikiwa unataka washiriki kwa njia

inayofaa huna budi kulishughulikia tatizo hili.

Je, na usikizi mbaya ni usikizi wa namna gani? Na unatokana na nini? Mfano

mmoja wa usikizi mbaya ni ile hali ya kutosikia yale yanayosemwa kwa sababu pengine

ya matatizo ya kimaumbile. Mfano mwingine unahusu ile hali ya kushindwa kung’amua

tofauti za kimatamshi kati ya maneno yanayotofautiana kwa misingi ya kimatamshi.

Mwanafunzi akiwa na shida ya namna hii atakumbwa na shida ya kuelewa ipasavyo

wakati wa mazungumzo. Wanafunzi walio wengi wanaweza kukumbwa na tatizo hili

kutokana na tofauti baina ya mfumo wa sauti wa Kiswahili na ule wa lugha zao za mama.

Kwa mfano, kama mwanafunzi hasikii tofauti kati ya maneno yafuatayo, atakuwa na

shida ya kuelewa maana inayokusudiwa maneno haya yanapotumiwa katika

mazungumzo:

doa: ndoa

buni: mbuni

sima: zima

msasi: mzazi

kuku: gugu

mtutu: mdudu

chombo: shombo

chana: jana

fua: vua

pua: bua

Ikiwa maneno haya yangetumiwa hivi kwamba si rahisi kutambua maana

kulingana na mkutadha wa matumizi, mwanafunzi angekanganywa na kuwa na shida ya

kusikiliza kwa ufahamu. Vile vile, mwanafunzi anaweza kushindwa kusikiliza kwa

ufahamu kama hafuati mtindo unaostahili kupata maana ya maneno yaliyo mapya kwake.

Kuna uwezekano kwamba kila neno jipya linapotokea mwanafunzi anasita na kwanza

kufikiria juu ya maana ya neno jipya. Kila anapofanya hivyo huwa anakosa kufuata

kikamilifu mkondo wa mazungumzo. Matokeo ya jambo hili ni kwamba huenda asielewe

ipasavyo kiini cha ujumbe unaowasilishwa.

Kwa hivyo, ni wajibu wa mwalimu kuwahimiza wanafunzi wasijaribu kutafuta

maana ya neno moja moja. Badala yake wajaribu kutambua maana kwa kuzingatia

uhusiano wake na maneno mengine katika mkutadha wa sentensi nzima. Hata kama si

rahisi kutekeleza jambo hili ni bora zaidi kuendelea kusikiliza kuliko kushughulikia

maana ya neno moja tu. Wanafunzi washauriwe kwamba kila wanaposikia neno lo lote

jipya ni vizuri waliandike halafu watafute maana yake baadaye.

Page 48: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

48

Je, kwa nini inafaa kuhimiza wanafunzi watafute maana kwa kuzingatia uhusiano

kati ya maneno katika mkutadha wa sentensi nzima?

Kwa kawaida mawasiliano ya lugha hufanyika kwa mtindo wa kutumia maneno

katika vielelezi vya sentensi ambazo kwa msingi wake kila neno hupata maana maalumu.

Tukizungumza kuhusu sifa za lugha tulisema kuwa ni mfumo nasibu. Maana mojawapo

ya kauli hii ni kwamba vipashio mbali mbali vya lugha vimo katika mpangilio maalum.

Mfano mmoja wa vipashio vya lugha ni maneno. Aghalabu maneno hupata maana

kutokana na mwingiliano wake ma maneno mengine katika mkutadha wa sentensi.

Maana yake inageuka kutoka mkutadha mmoja hadi mwingine. Kwa mfano maneno

kama vile piga, kata hupata maana tofauti kutokana na maneno mengine yanayoambatana

nayo katika sentensi. Hata maneno ambayo kwa kawaida huwa na maana iliyo wazi

yanaweza kupata maana isio ya kawaida yakitumiwa katika mkutadha usiyo wa kawaida.

Tuchukue mfano kama vile: kigeugeu, simba, sungura, fisi. Maneno haya yakitumiwa

katika mkutadha usio wa kawaida, msikilizaji inambidi kuzingatia maana yake kwa

mtazamo wa kijamii. Asipofanya hivyo atakosa kuelewa maana inayowasilishwa katika

mazungumzo yanayohusika.

Kizuizi kingine cha ufahamu sikizi ni tabia ya kuhakiki kwa namna ya kupindukia

wakati wa kusikiliza. Kuna wanafunzi ambao hawawezi kujizuia kukosoa mzungumzaji

au ujumbe unaowasilishwa wakati wanaposikiliza. Badala ya kuzingatia ujumbe

wanaweza, kwa mfano kujishughulisha na makosa yanayofanywa na mzungumzaji.

Pengine wanajifanya kuwa wanajua vya kutosha kuhusu mada inayoshughulikiwa katika

mazungumzo. Wanafunzi wa namna hii hawana nafasi ya kusikiliza kwa dhati, na

hatimaye wanashindwa kuelewa kiini cha ujumbe.

Njia mojawapo ya kusaidia wanafunzi wa namna hii ni kuwahimiza wasikilize

kwanza kabla ya kumkosoa mzungumzaji na ujumbe wake. Baada ya kuupokea ujumbe

watakuwa na nafasi bora zaidi ya kukosoa. Hata mzungumzaji mwenye shida ya lugha

anayo maarifa ya maana ambayo hayastahili kupuzwa. Kama walivyosema wahenga

“Baniani mbaya kiatu chake dawa”. Kuna kizuizi kingine cha ufahamu sikizi ambacho ni kama kinyume cha ukosoaji.

Msikilizaji anaweza kuvutiwa na kukumbwa na msisimko wa yanayosemwa na mtindo

wa kuwasilishwa kwake hivi kwamba hazingatii maana ya ujumbe tena.

Usikilizaji wa aina hizi mbili una kasoro na haustahili. Wanafunzi wakizoea

kusikiliza kwa namna hizi hawawezi kutathimini ujumbe kwa msingi na mtazamo wa

haki. Inafaa wahimizwe kukawilisha ukosoaji na ushabiki wao hadi watakapomaliza

kusikiliza.

Mazimgira:

Mawasiliano hayafanyiki katika ombwe tupu. Watu wanapozungumza na

kusikiliza wanafanya hivyo katika mazingira maalum ya kimaumbile na kijamii. Hali ya

mambo ndani ya darasa inaweza kuchangia kufanikisha au kutatiza mawasiliano ya

darasani. Ikiwa kwa mfano wakati zoezi la kusikiliza linapoendelea hakuna utulivu ndani

ya darasa au kuna kelele nje karibu na darasa itakuwa vigumu kwa wanafunzi kusikiliza

kama inavyostahili.

Kwa upande mwingine, hali ya kimaumbile ndani ya darasa inaweza kuwafanya

wanafunzi wakose utulivu kimwili na kiakili. Uhaba wa nafasi, kwa mfano, unaweza

kusababisha mfinyano kwa kiasi ambapo wanafunzi hawawezi kukaa kwa utulivu

Page 49: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

49

kuweza kuzingatia kikamilifu ujumbe unaowasilishwa na mzungumzaji. Katika hali kama

hii inakuwa shida kusikiliza kwa ufahamu.

Habari (Ujumbe).

Ujumbe unaowasilishwa unaweza kutatiza msikilizaji na kumfanya asielewe.

Mazungumzo, kwa mfano, yakijikita katika mambo ambayo hayawavutii wanafunzi

watakosa ari ya kusikiliza kwa makini. Vile vile kama mazungumzo yanashughulikia

mambo ambayo hayana uwiano na kiwango cha uwezo wa wanafunzi si rahisi kwao

kuyafuata kwa ufahamu.

Licha ya haya, ujumbe unaohusika ukikosa kuwa na muundo unaobainika wazi

huenda wanafunzi wakakanganywa na kutoelewa vizuri.

ZOEZI 5.3

(i) Ukitoa mifano maridhawa kutilia maki jibu lako onyesha jinsi

mwanafunzi mwenyewe binafsi anavyoweza kuwa ndiye chanzo

cha kutosikiliza kwa ufahamu.

(ii) Pendekeza mambo unayoweza kufanya ili kuboresha uwezo wake

wa kusikiliza kwa ufahamu kamili.

B.

(i) Ukitoa mifano inayofaa eleza jinsi hali ya kimazingira

inavyoweza kutatiza shughuli za wanafunzi za kusikiliza kwa

ufahamu.

(ii) Ni hatua gani unazoweza kuchukua ili kuhakikisha kwamba hali

ya kimazingira darasani haitatizi juhudi za wanafunzi za

kusikiliza?

5.4 Kufanikisha Ufahamu Sikizi

Ufahamu ni mfanyiko wa ndani. Mwalimu hana uwezo wa moja kwa moja juu

yake. Hata hivyo kuna baadhi ya mambo ambayo anaweza kufanya, na kupitia mambo

hayo akachangia ufanikishaji wa mfanyiko wa ufahamu.

Kwa ufupi mambo haya yanaweza kugawanyika katika vipengele vifuatavyo:

Page 50: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

50

Uteuzi bora

Maandalizi bora

Uwasilishaji bora

Mazingira bora

Uteuzi Bora

Ni wajibu wako kama mwalimu kuona kwamba unateua mapema kabla ya kipindi

mambo ambayo unataka wanafunzi wasikilize. Usingoje dakika chache kabla ya kipindi

ndipo uamue kuhusu mambo hayo. Unapochagua matini ya usikizi ni lazima uhakikishe

kwamba maudhui yake pamoja na lugha vinawiana vizuri na kiwango cha wanafunzi.

Maudhui yake yawe ya kuvutia na kuwatia changamoto vya kutosha. Pia ni lazima

uhakikishe kwamba huchagui matini ambayo usikilizaji wake utachukua muda wote wa

kipindi. Inafaa usikilizaji uwe sehemu ndogo tu ya kipindi kizima.

Baada ya kuteua matini inayofaa kufundishia unashauriwa kuipitia kwa uangalifu

ili uweze kutambua ni wapi katika matini yako wanafunzi wanahitaji kupewa usaidizi na

usaidizi huo utakuwa wa namna gani.

Maandalizi Bora

Maandalizi yanahusu ile hali ya kujihami kwa mwalimu kabla ya kipindi pamoja

na hatua anazochukua anapofika darasani ili kutayarisha wanafunzi kushiriki katika

shughuli za kipindi.

Kwa mfano, uteuzi wa mambo yanayotarajiwa kushughulikiwa darasani ni hatua

mojawapo ya maandalizi ya mwalimu kabla ya kipindi. Pia uteuzi wa mbinu zinazofaa

kutumia kuendesha kipindi ni hatua muhimu katika maandalizi ya mwalimu kabla ya

kipindi. Hali kadhalika wakati wa maandalizi haya mwalimu anatarajiwa kuamua kuhusu

muda utakaohitajika kwa shughuli ya zoezi la kusikiliza, na muda ambao utatumiwa kwa

shughuli nyingine. Haitarajiwi kuwa zoezi la kusikiliza litachukua muda wote wa kipindi.

Linapaswa kuambatanishwa na ufundishaji wa mambo mengine. Kwa hivyo ni muhimu

kwa mwalimu kuamua mapema jinsi zoezi hili litakavyoambatanishwa na ufundishaji wa

mambo mengine.

Kisha mwalimu anapofika darasani inambidi kuona kwamba wanafunzi

wanatayarishwa kukipokea kipindi cha somo kinachohusika. Matayarisho haya ni

muhimu sana, na hayastahili kupuuzwa. Mwalimu asifyatuke moja kwa moja kama risasi

na kuwashirikisha wanafunzi katika zoezi la kusikiliza kabla ya kuhakikisha kwamba

amejenga mazingira bora ya kufanikisha zoezi hilo.

Je unaweza kuyajenga namna gani mazingira ya kufanikisha shughuli ya

kusikiliza kwa ufahamu?

Ukweli ni kwamba hakuna mbinu yoyote ambayo ni ya lazima kwa kila

mwalimu. Lakini kwa vyo vyote vile ni lazima utoe utangulizi hivi kwamba unaweza

kudhibiti mwelekeo wa mawazo ya wanafunzi na kuwatamanisha kujihusisha na yale

yanayoendelea. Mambo ambayo unayatenda inafaa yalenge maudhui muhimu ya zoezi,

Page 51: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

51

licha ya kuwiana na kiwango cha wanafunzi wako. Mifano ya baadhi ya mambo ambayo

unaweza kufanya ili kuwatayarisha wanafunzi kwa shughuli hii ni pamoja na:

Kuwatia chonjo kwa namna yo yote inayofaa.

Kuhakikisha kuwa kuna hali ya ututlivu.

Kuwatia changamoto kwa kuwauliza maswali yanayolenga mada kuu ya

kipindi n. k…

Mifano ya mambo yanayoweza kufanywa ili kuwatia chonjo wanafunzi ni kama

vile:

Maonyesho ya picha zinazowiana na matarajio ya mada kuu.

Maigizo ya mambo yenye uwiano na mada kuu.

Maelezo mafupi juu ya malengo ya kipindi.

Uwasilishaji Bora

Ili shughuli ya kusikiliza iwe ya maana na manufaa kwa wanafunzi ni wajibu

wako kama mwalimu kuzingatia masharti yafuatayo:

Matamshi ya mzungumzaji yawe ya kueleweka.

Sauti ya mzungumzaji iwe ya kusikika na yenye kiimbo sahihi kuwiana na

maana inayowasilishwa.

Mzungumzaji azingatie kikamilifu vituo, na kuzungumza kwa mwendo

unaofaa. Asizungumze kwa kasi sana wala kwa kujikokota.

Sauti ya mzungumzaji iwe ya kuvutia.

Ukiamua kufundisha ukitegemea ukanda wa sauti inafaa uchague ukanda kwa

kutilia maani masharti haya. Pia, ukiamua wewe mwenyewe kusoma kwa sauti ni lazima

uzingatie masharti haya unaposoma. Masharti haya yakitiliwa maanani ni njia moja ya

kuhakikisha kuwa wanafunzi wanashawishiwa na kushirikishwa kwa njia ya maana na

manufaa.

Mazingira Bora

Mazingira bora kwa shughuli ya kusikiliza ni yale yenye utulivu na ushirikiano

bora kati ya wanaohusika. Kwa hivyo, kabla ya kuwashirikisha wanafunzi katika

kusikiliza ni wajibu wako kuona kwamba kuna hali ya utulivu miongoni mwa wanafunzi.

Kila mwanafunzi ni lazima ajihisi kuwa amestarehe na kutokuwa na wasiwasi.

Usichangie katika kuzusha hali ya wasiwasi na utovu wa utulivu kupitia vitendo

vyako na matamshi yako. Aidha ikiwa kuna wanafunzi ambao wana shida ya kusikia

washughulikie ipasavyo na kuona kwamba wanakaa karibu na chanzo cha habari. Pia

kama kuna kitu cho chote ndani ya darasa ambacho kinaweza kuwasumbua wanafunzi na

kuwazuia kusikiliza kwa makini, ikiwezekana kitu hicho kiondolewe kwa muda au

kifunikwe.

Wanafunzi wakimaliza kusikiliza unaweza kuwaongoza kuzungumza juu ya yale

waliyoyasikia. Wapewe nafasi ya kutoa maoni yao pamoja na kujibu maswali ya

ufahamu juu yake.

Page 52: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

52

ZOEZI 5.4

A. Ni mambo gani ambayo watoto wa shule hupendelea kusikiliza? Je, kwa

maoni yako, mambo hayo yanafaa kufundishia ufahamu sikizi katika

somo la Kiswahili au la? Toa sababu za kutilia nguvu jibu lako.

B. Ukirejelea matini yo yote ya usikizi ambayo

ungependa kutumia kufundishia ufahamu sikizi katika kidato fulani eleza

mambo ambayo utayafanya katika utangulizi ukiwa na lengo la kuiteka

nadhari ya wanafunzi ili waweze kusikiliza kwa makini na ufahamu bora.

5.5 Umuhimu Wa Kuongea.

Katika sehemu za somo zilizotangulia tumegusia fani ya ufahamu sikizi mkazo

ukutiliwa hasa juu ya mambo ambayo wewe kama mwalimu unaweza kufanya ili kusadia

wanafunzi wawe na uwezo wa kusikiliza na kupokea kwa ufahamu mzuri ujumbe

unaowasilishwa katika mazungumzo. Maelezo haya yanahusu hasa wajibu wa

mwanafunzi kama mhusika mpokezi wa ujumbe unaowasilishwa.

Katika sehemu za somo zinazofuata tutajishughulisha hasa na mbinu unazoweza

kutumia kusaidia wanafunzi kuwa na uwezo wa kuongea vizuri na kuwasilisha ujumbe

walio nao kwa njia inayofahamika. Lakini kabla ya kuzungumzia mbinu hizo inatupasa

kwanza tuelewe mambo ya kimsingi kuhusu kuongea. Moja kati ya mambo haya ni

umuhimu wake. Je, kwa maoni yako kuongea kuna umuhimu gani katika utaratibu wa

kujifunza na kufundisha Kiswahili? Kuna ubaya wo wote wa kufundisha Kiswahili bila

kushughulikia rasmi uwezo wa kuongea?

Sababu moja ya kutilia mkazo uwezo wa kuongea ni kwamba wanafunzi

wanaposhiriki katika shughuli ya kuongea wanapata fursa ya kutumia msamiati wa aina

tofauti katika mkutadha maalum wa mawasiliano. Pia wanapata fursa ya kuendeleza na

kuimarisha ujuzi wa sarufi. Bila kuongea wanafunzi wasingekuwa na fursa ya kuzoea

kuwasiliana wakitumia maneno mbalimbali pamoja na miundo ya kisarufi ambavyo

wanatarajiwa kudhibiti matumizi yake. Kupitia kuongea, vile vile wanafunzi wanaweza

kupanua fikra zao pamoja na kukuza uwezo wa kujieleza kwa mtiririko wa mawazo juu

ya jambo fulani. Kwa mfano, mwanafunzi akiagizwa na mwalimu atetee au apinge kauli

fulani itambidi kutafuta hoja, kufikiria juu yake, na kuziwasilisha kwa namna ambayo

inaweza kushawishi msikilizaji akubaliane naye.

Hali kadhalika zoezi la kuongea ni muhimu kwa kuendeleza matamshi.

Mwanafunzi akiongea, huwa anatamka maneno yaliyoundwa kwa mpangilio wa

vitamkwa vinavyopatikana katika lugha husika. Kwa hivyo kupitia zoezi la kuongea

mwanafunzi anaweza kusaidiwa kutambua makosa yake ya kimatamshi na

kuyarekebisha. Ni muhimu kuona kwamba mwanafunzi anakuwa na matamshi bora kwa

sababu matamshi sahihi yanachangia katika kufanikisha mawasiliano, lakini yasipokuwa

sahihi yanaweza kutatiza hali ya mawasiliano na kuzusha hali ya kutoelewana.

Page 53: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

53

Kwa upande mwingine kuongea ni muhimu kutokana na ukweli kwamba uzoefu

ambao mwanafunzi anapata kupitia uzungumzi unakuwa msingi bora kwa ufanisi wake

katika lugha ya uandishi. Mwanafunzi akizoea kuongea kwa njia inayofaa itakuwa rahisi

kwake pia kuandika kwa njia inayofaa. Lakini mwanafunzi akiwa, kwa mfano, na

mazoea ya kutamka vibaya kuna uwezekano kwamba matamshi yake mabaya yataathiri

maandishi yake. Mara kadhaa watu wana tabia ya kuandika kama wanavyotamka. Kwa

hivyo njia mojawapo ya kuboresha uandishi wa wanafunzi ni kuhakikisha kwamba

wanaongea Kiswahili kwa matamshi bora.

Kuongea ni muhimu pia kwa mtazamo wa kijamii. Uwezo wa kuongea unasaidia

kujenga uhusiano na kudumisha utangamano wa kijamiii. Bila uwezo huu inakuwa

vigumu kwa watu kupashana habari na kuendeleza maisha yao. Ili mwanafunzi aweze

kukabiliana na hali ya maisha ya kila siku inampasa kujua jinsi ya kuongea na watu

katika miktadha mbali mbali ya mawasiliano.

Yapo mambo ya kimsingi ambayo yanawiana na uwezo huu na kuchangia

kuufanikisha. Moja kati ya mambo hayo ni matamshi. Sasa tutazungumzia jambo hili

kwa undani katika maelezo yatakayofuata.

ZOEZI 5.5

Jadili umuhimu wa kushughulikia uwezo wa

kuongea katika ufundishaji wa somo la

Kiswahili.

5.6 Matatizo Ya Kimatamshi.

Kuna makosa ya aina tofauti ambayo wanafunzi wanafanya wanapoongea

Kiswahili. Makosa hayo hutokea kwa sababu tofauti. Yale ambayo yanashuhudiwa sana

yanaweza kuainishwa katika makundi yafuatayo:

Mpishano wa vitamkwa.

Upachikaji wa vitamkwa.

Udondoshaji wa vitamkwa.

Ni muhimu kwako kama mwalimu kuelewa aina ya kosa linalofanywa na

mwanafunzi ili uweze kushughulikia urekebishaji wake kwa kutumia mbinu inayofaa.

Mpishano Wa Vitamkwa.

Kosa hili hutokea wakati ambapo badala ya kutamka kitamkwa kinachotarajiwa

mwanafunzi anatamka kingine kinachokaribiana nacho. Mifano ifuatayo inabainisha aina

ya kosa hili:

Page 54: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

54

Je, chanzo cha kosa hili ni nini? Linaweza kutokea kutokana na ukweli kwamba

kitamkwa kinachotarajiwa hakipatikani katika lugha ya mama ya mwanafunzi. Anatamka

kitamkwa ambacho amezoea katika lugha yake.

Kosa la kutamka: mbaka badala ya mpaka, kubima badala ya kupima, na mbira

badala ya mpira linaweza kuchukuliwa kama kosa la mpishano wa vitamkwa lakini

chanzo chake ni tofauti na kile cha matamshi ya maneno mengine. Asili yake siyo utovu

katika lugha ya mwanafunzi wa kitamkwa kinachotarajiwa.

Vitamkwa vyote vinavyohusika vinapatikana katika lugha ya mama ya

mwanafunzi na pia katika Kiswahili. Mwanafunzi anayehusika huwa anatamka hivyo

kufuatana na kanuni za kifonolojia za lugha ya mama. Kwa mfano, katika lugha ya

Kinandi kuna /p/ na /k/ lakini vitamkwa hivi vikitokea katikati ya vokali vinageuka na

kutamkwa kama /b/ na /g/ mtawalia. Hii ni sababu kwa nini unaweza kusikia wanafunzi

kutoka jamii hii wakitamka * kugata badala ya kukata na * kubima badala ya kupima.

Mfano mwingine wa kutamka kimakosa maneno ya Kiswahili kwa kuzingatia

kanuni za kifonolojia za lugha ya mama unahusu kitamkwa /p/. Katika Kinandi kitamkwa

hiki kinapotanguliwa na /m/ huwa kinatamkwa kama /b/ . Kwa sababu ya kuzingatia

kanuni hii ya fonolojia ya lugha yao ya mama wanafunzi kutoka jamii hii wanatamka

neno mpira kama *mbira na mpaka kama *mbaka. Kwa wanafunzi hawa matamshi ya

vitamkwa vinayohusika yanategemea mazingira ya kifonolojia. Vimo katika mpishano

wa kimazingira.

Neno linalotarajiwa Neno linalotamkwa

mdudu

mzazi

uchumi

gugu

vuta

vua

chombo

mbishi

bua

kupima

kugawa

mpaka

mpira

mtutu

msasi

ujumi

kuku

futa

fua

shombo

mpishi

pua

kubima *

kukawa

mbaka *

mbira *

Page 55: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

55

Upachikaji Wa Vitamkwa:

Kosa hili hutokea wakati ambapo mwanafunzi hutamka neno linalohusika kwa

kuweka kitamkwa cha ziada kwenye neno hilo na kuishia na neno tofauti na lile

lililokusudiwa. Mifano ifuatayo inabainisha aina ya kosa linalohusika:

Katika Kikamba, kwa mfano, vitamkwa /d/, /b/ na /g/ vinapotokea mwanzoni

mwa neno ni lazima viwe vimetanguliwa na sauti ya kipua. Kwa kuzingatia sharti hili

wanafunzi kutoka jamii hii wanapokabiliana na maneno ya Kiswahili yenye miundo

ambayo katika lugha yao inahitaji sauti ya kipua hupachika sauti hiyo ili kutimiza

masharti ya matumizi ya lugha yao.

Wakati mwingine upachikaji wa vitamkwa hutokea wanafunzi wanapokabiliana

na maneno ya Kiswahili yenye mfuatano wa konsonanti. Wanapachika vokali ili kurahisisha matamshi kufuatana na mpangilio wa vitamkwa katika lugha zao za mama

ambao, aghalabu, hauruhusu mfuatano wa namna hiyo. Ifuatayo ni mifano inayobainisha

jambo hili:

Neno linalotarajiwa Neno linalotamkwa

doa

buni

bali

basi

dawa

gari

ndoa

mbuni

mbali

mbasi *

ndawa *

ngari *

Page 56: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

56

Hali kadhalika baadhi ya wanafunzi hupachika vokali mwanzoni mwa maneno ili

kurahihisha matamshi ya mfuatano wa konsonanti. Jambo hili linatokea sana hasa katika

maneno yenye muundo wa silabi moja kama vile katika mifuano ifuatayo:

Udondoshaji Wa Vitamkwa.

Kosa hili hutokea wakati ambapo kitamkwa kimoja kinafutwa na kutotamkwa

kama katika mifano ifuatayo:

Matamshi Sahihi Matamshi Yasiyo Sahihi

alfajiri

umri

ilmradi

halmashauri

amrisha

kunradhi

jamhuri

alhamisi

alifajiri

umuri

ilimuradi

halimashauri

amurisha

kuniradhi

jamuhuri

alihamisi

Matamshi Sahihi Matamshi Yasiyo Sahihi

nje

nchi

nzi

mbu

mbwa

inje

inchi

inzi

umbu

umbwa

Page 57: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

57

Matokeo ya kutamka namna hii ni kwamba mwanafunzi huishia kwa kuwasilisha

maana iliyo tofauti na ile iliyokusudiwa. Pia, wakati mwingine, huishia kwa kutamka

maneno ambayo hayana maana yo yote katika Kiswahili. Kwa kawaida, wasikilizaji

wanaweza kupokea maana iliyokusudiwa kutokana na mkutadha wa mawasiliano. Lakini

kuna wakati ambapo matamshi yakiwa mabaya, wanaweza kushindwa kupokea ujumbe

kwa maana iliyokusudiwa. Hali kama hii hutokea wakati ambapo hakuna kielelezo katika

mkutadha wa mawasiliano kinachoweza kuwasaidia kukisia maana.

Matatizo haya ambayo yamezungumziwa ndiyo matatizo sugu. Kuna aina

nyingine za matatizo ambayo huenda yakijitokeza hata ingawa si sana. Wakati mwingine,

kwa mfno, baadhi ya wanafunzi wanakumbwa na aina za shida za kimatamshi zifuatazo:

Kuunganisha vitamkwa

Kutenganisha vitamkwa

Kuunganisha Vitamkwa

Kosa hili linatokea wakati ambapo mwanafunzi anashindwa kutenganisha

vitamkwa vinavyotakiwa kutenganishwa na badala yake kuvitamka kama kwamba ni

silabi moja. Tatizo hili linahusu maneno yenye vitamkwa /p/ na /b/ vikitanguliwa na

kitamkwa /m/. Ikiwa kitamkwa /m/ kinasimamia silabi kamili ni lazima matamshi ya

neno linalohusika yaonyeshe hivyo kwa kutokitamka kama kwamba kinaungana kisilabi

na kitamkwa /p/ na /b/ kinachofuatia. Maneno mpaka na mbaya katika sentensi zifuatazo

yanastahili kutamkwa kwa njia ambayo inabainisha kwamba /m/ katika maneno haya ni

silabi kamili:

Neno linalotarajiwa Neno linalotamkwa

ndege

ngumi

ngao

mbuni

mbali

mbawa

mbele

kidimbwi

mazingira

mazingaombwe

kindakindaki

dondosha

dege

gumi

gao

buni

bali

bawa

bele

kidibwi

mazigira

mazigaobwe

kidakidaki

dodosha

Page 58: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

58

(i) Tulikutana karibu na m.paka wa Kenya na Uganda.

(ii) Kijana huyu ni m.baya sana.

Lakini ikiwa mzungumzaji atatamka /m/ kama kwamba si silabi kamili atakuwa

amefanya kosa la kuunganisha vitamkwa.

Kutenganisha Vitamkwa.

Kosa hili ni kinyume cha lile la kuunganisha vitamkwa. Badala ya kutamka

vitamkwa vinavyofuatana kama silabi moja mwanafunzi huvitamka kama kwamba ni

silabi tofauti za neno. Kwa mfano, maneno mpaka na mbaya katika sentensi zifuatazo

yanapaswa kutamkwa kwa njia ambayo inadhihirisha kwamba /m/ katika maneno haya si

silabi kamili:

(iii) Mtoto hakulala mpaka asubuhi

(iv) Saa yangu ni mbaya.

Ni lazima /m/ itamkwe pamoja na vitamkwa viwili vinavyofuatia kama silabi

moja ya neno. Lakini, ikiwa mwanafunzi ataitamka kama kwamba ni silabi kamili

atakuwa amefanya kosa la kutenganisha vitamkwa.

Sentesni zifuatazo zinaweza kukusaidia kuelewa vizuri zaidi dhana ya

kuunganisha na kutenganisha vitamkwa katika matamshi ya maneno ya Kiswahili:

(v) Kijana mbaya ana sura mbaya.

(vi) Hatutasimama mpaka mpaka wa nchi.

ZOEZI 5.6

Ukitoa mifano inayofaa eleza sababu nyingine

zaidi ambazo kwa maoni yako huwafanya

wanafunzi waongee Kiswahili kwa makosa ya

kimatamshi.

5.7 Kufundisha Matamshi.

Ufanisi wa mwanafunzi katika matamshi unategemea, kwa kiasi fulani, uwezo

wake wa kusikia, kupambanua (kuchanganua) katika usikizi wake na pia katika

uzungumzi wake vitamkwa mbalimbali vya lugha. Kwa hivyo, wewe kama mwalimu wa

Kiswahili ni lazima uhakikishe kwamba unasitawisha uwezo huu ili wanafunzi wako

waweze kuongea Kiswahili kwa matamshi bora. Ili kutekeleza jambo hili inakubidi

uzingatie hatua za kimsingi zifuatazo:

Page 59: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

59

Kuendeleza upokezi sikizi.

Kuendeleza upambanuzi sikizi.

Kuendeleza upambanuzi zungumzi.

Hatua hizi zinalenga hasa kushirikisha wanafunzi katika matumizi ya lugha

ambayo yatawapatia mazoea mema ya kuwasaidia kuongea kwa matamshi bora.

Zinalenga pia kuwasaidia kutambua makosa ya kimatamshi na kuyarekebisha.

Upokezi Sikizi.

Upokezi sikizi unahusu ile hali ya msikilizaji ambayo kwayo masikio yake

hunakili sauti. Upokezi sikizi wa sauti unamwezesha mwanafunzi kuzoea sauti za lugha

fulani na kuzitofautisha na zile za lugha nyingine. Kinachopaswa kushughulikiwa katika

hatua hii ni kuona kwamba mwanafunzi anapata fursa ya kusikia matamshi sahihi ya

Kiswahili ambayo anaweza kuyaiga. Mkazo katika hatua hii unatiliwa juu ya kutoa fursa

kwa wanafunzi ya kupokea na kusikia matamshi ya vitamkwa mbalimbali katika

muktadha wa mfululizo wa maneno.

Baada ya kushirikisha wanafunzi katika zoezi la ukuzaji wa usikizi, unaweza

kuwashirikisha katika hatua nyingine ambayo ni ya upambanuzi sikizi.

Upambanuzi Sikizi.

Licha ya kuwa na uwezo wa kunakili sauti katika masikio yake, ni lazima

mwanafunzi awe na uwezo wa kuchanganua sauti mbalimbali anazosikia. Ni lazima

abainishe katika usikizi wake kwamba hayachanganyi maneno ambayo yanakaribiana

kimatamshi. Bila uwezo huu matamshi yake yatakuwa ya kukanganya kwa sababu

atatamka kulingana na usikizi wake wenye kukanganya, na ataishia kwa kuwakanganya

wasikilizaji. Pia, hata yeye mwenyewe atakuwa na shida ya kusikiliza kwa ufahamu.

Kile kinachoshughulikiwa katika hatua hii ni kuona kuwa mwanafunzi

anayapokea kwa usahihi maneno yanayotamkwa bila kuyageuza kutokana na

kuchanganya vitamkwa vinavyounda maneno hayo. Unapotamka, kwa mfano, mzazi

mwanafunzi inatakiwa asikie vivyo hivyo na wala siyo msazi, au msasi. Vile vile

ukitamka karibuni ni lazima asikie viyo hivyo na wala siyo kaburini. Licha ya kusikia ni

lazima mwanafunzi aonyeshe kwamba anasikia kwa usahihi. Njia mojawapo ya

kuendeleza na kutathimini uwezo wa mwanafunzi wa kuchanganua sauti katika usikizi

wake ni kumtaka afanye kitendo ambacho utekelezaji wake unategemea usikizi sahihi wa

vitamkwa vinavyounda neno. Kwa mfano, ukimwambia mwanafunzi kuvuta kiti, na

badala ya kufanya hivyo anakifuta, itakuwa wazi kwamba ana shida ya upambanuzi

sikizi wa vitamkwa /v/ na /f/. Hali kadhalika ukimwambia aandike neno mfugo na badala

ya kuandika neno hilo aandike mfuko, utajua kuwa katika usikizi wake ana shida ya

kuchanganya vitamkwa /g/ na /k/.

Mwanafunzi huyu anahitaji mazoezi ya kusikiza ambayo humpa fursa ya kusikia

matamshi ya vitamkwa vinavyomkanganya.

Page 60: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

60

Upambanuzi Zungumzi.

Katika hatua ya upokezi na upambanuzi sikizi mwanafunzi anashirikishwa katika

somo kama mhusika msikilizaji. Kazi yake ni kutega masikio na kupokea matamshi ya

mwalimu au mzungumzaji mwingine ambaye matamshi yake yanatumiwa kama mfano.

Kwa upande mwingine katika hatua ya upambanuzi zungumzi mwanafunzi

anashirikishwa kama mhusika mzungumzaji. Kazi yake ni kubainisha uwezo wake wa

kupambanua vitamkwa kupitia matamshi yake mwenyewe kama mhusika mzungumzaji.

Kinachoshughulikiwa katika hatua hii ni kuona kwamba mwanafunzi anatamka

maneno kwa kuzingatia matamshi sahihi ya vitamkwa vinavyounda maneno

yanayohusika. Lakini ni lazima tukumbuke kwamba uwezo huu unaambatana na uwezo

wa mwanafunzi wa kusikia na kung’amua matamshi hayo katika usikizi wake. Bila

kufanya hivyo itakuwa vigumu kwake kutamka kama inavyostahili na ataongea kwa njia

ambayo haifahamiki kwa urahisi. Kutokana na uwezo wa kupambanua vitamkwa katika

uzungumzaji mwanafunzi hatachanganya matamshi ya jozi za maneno zifuatazo:

dhamini

nadhiri

karamu

mdudu

mbishi

mchango

upupu

thamini

nathiri

kalamu

mtutu

mpishi

mjango

ububu

Kwa ufupi, unapofundisha matamshi unaweza kutumia kinasa sauti, au

kuwasomea kwa sauti wanafunzi wasikilize jinsi maneno mbali mbali yanavyotamkwa,

na kisha wajaribu kuiga matamshi hayo. Unaweza , kwa mfano kuzipitia hatua hizi tatu

zilizozungumziwa kwa kutumia jozi finyu za maneno. Maneno ya jozi finyu huwa

yameundwa na vitamkwa vinavyofanana isipokuwa kimoja tu. Pia mpangilio wa

vitamkwa hivyo katika maneno hayo unafanana. Ufuatao ni mfano wa jozi finyu za

maneno na maelezo kuhusu jinsi unavyoweza kuzitumia ukirejelea mfuatano wa hatua

hizi tatu za kimsingi: Upokezi sikizi, Upambanuzi sikizi, Upambanuzi zungumzi.

Page 61: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

61

A

_____________________

1. mpishi

2. papa

3. chombo

4. msasi

5. mtutu

6. fahari

7 dhana

8 nathiri

9 sima

10. kuku

B

__________________

mbishi

baba

shombo

mzazi

mdudu

fahali

zana

nadhiri

zima

gugu

Upokezi Sikizi / Hatua ya kwanza.

Unasoma kwa sauti maneno katika sehemu ya A ukianza na neno la kwanza

mpaka la kumi huku wanafunzi wakisikiliza matamshi yako. Kisha unasoma maneno

katika sehemu ya B ukianza na neno la kwanza mpaka la kumi.

Upambanuzi Sikizi / Hatua ya Pili.

Unatamka maneno jozi kwa jozi huku wanafunzi wakisikiliza matamshi ya

maneno hayo. K. m:

mpishi – mbishi

nathiri – nadhiri

kuku - gugu.

fahari - fahali.

Katika hatua hii unaweza kutamka neno fulani na kuwaambia wanafunzi

waonyeshe neno ulilotamka. Kwa mfano, ukitamka neno nadhiri mwanafunzi anaweza

kujibu kwa kusema kwamba ni 8 B. Ukitamka shombo jibu linaweza kuwa 3A. Lengo

katika hatua hii ni kuendeleza uwezo wa mwanafunzi wa kung’amua maneno

yanayotamkwa. Kwa hivyo ni lazima uhakikishe kwamba zoezi lo lote katika hatua hii

linachangia kufanikisha uwezo huu.

Upambanuzi Zungumzi / Hatua ya tatu

Kama ilivyoelezwa hapo awali lengo katika hatua hii ni kumshirikisha kama

mhusika mzungumzaji. Kwa hivyo, ukirejelea jozi finyu za maneno unaweza kuonyesha

Page 62: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

62

baadhi ya maneno na kumtaka mwanafunzi ayatamke. Akifanya makosa unamsaidia kwa

kutamka maneno hayo tena.

Katika maelezo haya tumependekeza utumiaji wa maneno ili kufundisha

matamshi. Siyo lazima ufundishe kwa kutumia maneno tu; unaweza kufundisha kwa

kutumia maneno yenye vitamkwa unavyotaka kushughulikia katika vielelezo vya

sentensi. Mbinu hii hutoa fursa kwa mwanafunzi ya kujifunza mambo mengine

yanayoambatana na matamshi, kwa mfano shadda na kiimbo. Sentensi hutoa mkutadha

bora wa kufundishia mambo haya. Sentensi kama zifuatazo ni mfano bora wa

kufundishia matamshi:

(a) Mpishi huyu ni mbishi sana.

(b) Mzazi wake ni msasi hodari.

(c) Chombo hiki chanunka shombo

(d) Zima moto huo baada ya kupika sima.

Wanafunzi wanaweza kukusikiliza ukisoma sentensi hizi kwa sauti na kisha

wanajaribu kuzisoma wao wenyewe.

Njia nyingine unazoweza kutumia kuendeleza upambanuzi sikizi ni kama vile:

Kutamka neno linaloashiria kitu fulani na kumtaka mwanafunzi aonyeshe kitu

kinachoashiriwa. Kwa mfano: basi, pasi; kamba, gamba; pua, bua.

Kumwambia mwanafunzi kutimiza kitendo fulani. Kwa mfano: pika – piga;

futa – vuta; soma – zoma.

Kutamka maneno yanayotofautiana kimatamshi na kumtaka mwanafunzi

aeleze kama umetamka neno moja mara mbili au maneno mawili yaliyo

tofauti. Kwa mfano:

(a) Mama huyu ni mbishi kweli kweli

(b) Mama huyu ni mpishi kweli kweli

Kutamka neno fulani zaidi ya mara moja na kumtaka mwanafunzi aeleze

kama umetamka maneno tofauti au neno moja zaidi ya mara moja.

Kutoa zoezi la imla.

Kwa upande mwingine, upambanuzi zungumzi unaweza kuendelezwa kwa

kushirikisha wanafunzi katika mazoezi kama yafuatayo:

Kujibu maswali yanayoshirikisha vitamkwa unavyotaka kushughulikia. Kwa

mfano, kuonyesha kitu fulani au kuigiza kitendo fulani na kumtaka

mwanafunzi aeleze anachoona…..

Kukamilisha msemo kwa kutamka neno linalofaa

Kusoma kwa sauti.

Page 63: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

63

ZOEZI 5.7

A. Eleza kikamilifu hatua ambazo utachukua kusaidia wanafunzi

ambao wana shida ya kutofautisha katika matamshi yao kati ya

maneno yenye vitamkwa vinavyowakilishwa na mfuatano wa

herufi zifuatazo:

(i) ch -sh

(ii) dh - th

B. Mwanafunzi wako ametamka sentensi ifuatayo: Nimeshidwa

kuufuga mlago wa nyuba yagu kwa ufuguo huu

(i) Ainisha kosa ambalo amefanya..

(ii) Utachukua hatua gani kumsaidia mwanafunzi huyu ili aweze

kutambua na kurekebisha kosa lake?

5.8 Kufundisha Kuongea / Mazungumzo.

Lengo kubwa la kushirikisha mwanafunzi katika zoezi la kuongea ni kumwezesha

kujieleza bila shida, kwa matamshi mazuri, kiimbo kinachotakikana na kwa mfululizo

bora wa mawazo.

Ili kufanikisha lengo hili kuna mambo muhimu ambayo, kama mwalimu

unashauriwa kutilia maanani. Baadhi ya mambo hayo ni kama yafuatayo:

Uteuzi wa mada.

Maandalizi ya wanafunzi.

Kutia shime.

Kushirikisha kila mwanafunzi.

Uteuzi Wa Mada

Unapochagua mada za kuzungumzia unapaswa kuwa mwangalifu kuona kuwa

unachagua mambo yanayoambatana na kiwango pamoja na uzoefu wa wanafunzi wako.

Page 64: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

64

Mada unazochagua inafaa ziambatane na mambo wayajuayo wanafunzi na ambayo

yanawahusu katika maisha yao ya kila siku. Ziwe mada za kuvutia na kugusia hisia zao.

Pia, ni wajibu wako kuhakikisha kwamba unachagua mada ambazo zina

vipengele vya kutosha vya kuzungumzia. Kama sivyo wanafunzi hawatachangia vya

kutosha na huenda wakaishia kwa kuzungumzia mambo ambayo hayana uhusiano na

mada inayohusika. Lakini mada ikiwa na vipengele vya kutosha inakuwa rahisi

kushirikisha wanafunzi waliyo wengi.

Maandalizi Ya Wanafunzi.

Mazungumzo hayafanyiki katika ombwe tupu. Yanafanyika katika mazingira

maalum ya kijamii. Kwa hivyo kabla hujashirikisha wanafunzi katika shughuli ya

kuongea ni wajibu wako kuhakikisha kwamba hakuna cho chote ambacho kinaweza

kuwazuia kushiriki na kujieleza darasani.

Wakati mwingine baadhi ya wanafunzi husita kushiriki katika mazungumzo kwa

sababu ya hofu na haya. Huwa wanahofia kuwa wenzao huenda wakawacheka. Wengine

wanaogopa kukaripiwa na mwalimu hali ambapo kuna wale ambao wanaogopa kufanya

makosa. Ni wajibu wako kuwatuliza na kuwaondolea hofu wanafunzi. Kuhusu ufanyaji

wa makosa inafaa uwafahamishe kuwa hakuna asiyefanya makosa. Pia wajulishe

kwamba wakiogopa kufanya makosa hawatajifunza lugha kwa sababu makosa ni jambo

la kawaida katika matumizi ya lugha.

Ni muhimu pia kuhakikisha kwamba wanafunzi wanafahamu vizuri lengo la

mazungumzo.

Kutia Shime

Jiepushe na tabia ya kukosoa wanafunzi wakati wanapochangia katika

mazungumzo. Unapofanya hivyo unawavunja moyo. Mwanafunzi akifanya kosa, liandike

kisha ulishughulikie baadaye. Pia jitahidi kuwatia shime wanafunzi wakati wanapoongea.

Unaweza kutekeleza jambo hili kwa kufanya mambo kama yafuatayo:

Kusikiliza kwa makini na kuonyesha kwa mwitiko wa mwili wako kuwa

unasikiliza.

Kuwapongeza wanafunzi.

Kuuliza maswali ya udadisi ambayo yanalenga kusaidia wanafunzi kujieleza

bora zaidi.

Kushirikisha Kila Mwanafunzi.

Ni wajibu wako kuona kuwa kila mwanafunzi anapata fursa ya kushiriki katika

mazungumzo. Usiache wanafunzi wachache ambao huwa wanataka sana kuongea wawe

ndio wanatawala. Wanafunzi wanaoogopa kuongea unaweza kuwatia moyo kwa

kuwauliza maswali rahisi nao waweze kuchangia.

Page 65: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

65

ZOEZI 5.8

A. Kwa maoni yako ni mambo gani ambayo

huwafanya wanafunzi kushindwa kushiriki

kikamilifu katika mazungumzo?

B. Unaweza kuchukua hatua gani kushughulikia

matatizo hayo uliyotaja?

5.9. Njia Za Kufundishia Mazungumzo.

Ziko njia mbali mbali ambazo unaweza kutumia ili kutoa nafasi kwa wanafunzi

ya kujieleza katika mazungumzo. Miongoni mwa njia hizo ni hizi zifuatazo:

Majadiliano ya vikundi.

Maigizo.

Masimulizi.

Majibizano.

Majadiliano Ya Vikundi

Katika ufafanuzi wa lugha tulisema kuwa ni chombo cha mawasiliano. Na njia

moja ya kufanikisha mawasiliano miongoni mwa wanafunzi ni kuwaweka katika vikundi

vidogo vidogo ili wajadiliane juu ya mada fulani. Wakiwa katika vikundi vya watu

wachache wanafunzi wanapata fursa nzuri ya kutumia lugha halisi. Kila mwanafunzi

hupata nafasi ya kujieleza kwa uwezo wake bila wasi wasi. Hata wanafunzi ambao kwa

kawaida huogopa kuongea hadharani hujitolea kuongea wakiwa katika kikundi cha watu

wachache.

Jukumu lako kama mwalimu ni kuona kwamba wanafunzi katika kila kikundi

wanafanya kazi waliyopewa kulingana na maagizo uliyotoa. Ni lazima uhakikishe

kwamba wanaelewa vizuri kile wanachotarajiwa kufanya.

Maigizo:

Maigizo yanaweza kutokana na vitabu vinavyotumiwa darasani. Yanaweza pia

kutokana na tukio lo lote ambalo wanafunzi wameshuhudia. Wanafunzi wachache

waigize mbele ya darasa huko wengine wakitazama na kusikiliza.

Uzuri wa kuigiza ni kwamba kunawapa wanfunzi fursa ya kukuza kipawa chao

cha kubuni. Vile vile mwanafunzi anapoigiza anapata nafasi ya kujihusisha na kuhisi

uhalisi wa ukweli wa mambo ambayo kwa kawaida asingeyatilia maanani. Pia anapata

nafasi ya kutumia lugha kulingana na mkutadha maalum wa mawasiliano.

Page 66: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

66

Jukumu lako kama mwalimu ni kuwashauri wanafunzi watilie maanani

ushirikishaji wa mwili na kiimbo kulingana na ujumbe unaowasilishwa. Ikiwa ni huzuni,

kwa mfano, sura na sauti ya mwanafunzi vionyeshe huzuni.

Masimulizi:

Mwanafunzi mmoja baada ya mwingine anaweza kupewa nafasi kusimulia juu ya

tukio au kisa fulani. Anapofanya hivyo huwa anakuza uwezo wa kupanua na kupanga

mawazo yake kwa mtiririko. Vile vile wanafunzi wengine wanaposikiliza huwa

wanaendeleza stadi ya kusikiliza kwa ufahamu.

Mwanafunzi anapomaliza kuzungumza wenzake wanaweza kupewa fursa ya

kuuliza maswali juu ya yale yaliyosemwa. Wajibu wako kama mwalimu ni kuona

kwamba zoezi haligeuki kuwa kitu kingine. Masimulizi yanaweza kuchukuliwa kama

insha ya mdomo. Kwa hivyo, ukitaka unaweza kutoa vichwa vya habari tofauti na

kuwambia wanafunzi watoe masimulizi juu yake. Kwa mfano, unaweza kuwambia

wanafunzi tofauti watoe kisa kinachobainisha ukweli wa moja kati ya methali zifuatazo:

(a) Kichwa cha nyoka hakibandiki mtungi.

(b) Kamba ya mbali haifungi kuni.

(c) Kitanda usicholalia huwajui kunguni wake.

(d) Dalili ya mvua ni mawingu.

Majibizano.

Majibizano yanaweza kuwa: kati ya mwalimu na mwanafunzi au, kati ya

mwanafunzi na mwanafunzi. Unaweza kuonyesha wanafunzi kifaa fulani cha maono.

Kisha wanafunzi wanaweza kuulizana na kujibiana maswali juu ya kifaa hicho. Nawe

vile vile unaweza kuwauliza na kuwadadisi wanafunzi kadhaa juu ya kifaa

kinachohusika. Unapouliza maswali unapaswa kuhakikisha kuwa wanafunzi hawatoi

majibu ya pamoja. Mifano ya vifaa vya maono unavyoweza kutumia ni kama vile: picha,

vibonzo na michoro ya aina mbali mbali. Vifaa hivi vinaweza kuwavutia wanafunzi na

kuwapa motisha ya kuongea. Ukijitahidi huwezi kukosa kupata vifaa katika vitabu na

magazeti.

Mfano mwingine wa majibizano ni zoezi la kutegeana na kutegua mafumbo.

Kupitia zoezi hili mwanafunzi hupata nafasi ya kupanua fikra zake, kupanga mawazo na

kujieleza kwa nafsi yake. Zoezi hili pia husaidia kukuza ubunifu katika kutumia lugha.

Kwa upande mwingine, mwanafunzi msikilizaji anaendeleza ustadi wa kusikiliza kwa

makini na uwezo wa kutatua matatizo.

Kuna njia nyingine ambazo unaweza kutumia ili kuchangia uwezo wa wanafunzi

wa kuongea. Matokeo mazuri yatatokea ikiwa utateua kwa uangalifu njia zinazofaa,

kuwahamasisha wanafunzi wako na kuwashirikisha kwa utaratibu.

Page 67: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

67

ZOEZI 5.9

A. Chagua au tayarisha kifaa cho chote cha maono

unachotaka kutumia kama chombo cha kufundisha

mazungumzo kwa wanafunzi wa kidato cho chote

unachotarajia kufundisha. Kisha eleza jinsi

utakavyotumia kifaa hicho ili kutekeleza lengo

lako.

B. Eleza hatua unazoweza kuchukua ili kushughulikia

wanafunzi wenye shida zifuatazo:

(i) Kutotaka kuongea.

(ii) Kuongea kwa kupindukia.

(iii) Kutozingatia mada inayohusika

wanapoongea.

HITIMISHO

Mkazo katika somo hili umetiliwa juu ya kusikiliza na kuongea na umuhimu

wake katika utaratibu wa kujifunza lugha. Mawasiliano kila siku hufanyika zaidi kupitia

kusikiliza na kuongea kuliko kusoma na kuandika. Kwa hivyo wewe kama mwalimu

unapaswa kuhakikisha kwamba mambo haya unayapa uzito unaostahili katika mpango

wako wa kufundisha Kiswahili.

Ni wajibu kuona kwamba unatumia mbinu zo zote zile ambazo kwa maoni yako

zinaweza kuchangia kukuza uwezo wa wanafunzi wako wa kusikiliza na kuongea vizuri

Kiswahili.

Page 68: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

68

SOMO LA 6

KUSOMA NA KUANDIKA

6.0 Utangulizi

Kusoma na kuandika ni stadi za lugha andishi ambazo zinatiliwa sana mkazo

katika mfumo wa elimu. Mwanafunzi akimudu vizuri stadi hizi mbili anaweza kujitimizia

mahitaji yake ya kimawasiliano.bila kutegemea msaada wa nje.

Katika somo hili tutatoa mapendekezo ambayo, wewe kama mwalimu, unaweza

kufanya ili kuendeleza na kuimarisha uwezo wa wanafunzi wako wa kusoma na kuandika

Kiswahili kama inavyostahili.

MADHUMUNI YA SOMO

Kufikia mwisho wa somo hili, inatarajiwa kuwa utaweza:

(i) Kueleza tanzu tofauti za kusoma na kuandika, na kueleza

umuhimu wake katika utaratibu wa kufundisha Kiswahili.

(ii) Kupendekeza na kueleza mbinu tofauti zinazofaa

kutumiwa ili kuboresha usomaji na uandikaji Kiswahili wa

wanafunzi wako

6.1 Kusoma Kwa Sauti.

Kwa kawaida mtu akisoma anaweza kufanya hivyo kimya au kwa sauti kulingana

na mkutadha wa kimawasiliano unaohusika. Kama kuna haja ya watu wengine kusikia

ujumbe wa mwandishi, msomaji atasoma kwa sauti, lakini ikiwa hakuna haja atasoma

kimoyomoyo ili ujumbe huo uwe siri yake.

Katika ufundishaji wa lugha, zoezi la kusoma kwa sauti ni muhimu kutokana na

ukweli kwamba kupitia zoezi hili mwanafunzi anapata fursa ya kuimarisha hali ya

matamshi yake. Kila anaposoma kwa sauti huwa anafanya mazoezi ya kutamka maneno

ya Kiswahili na kiimbo cha Kiswahili kwa jumla. Ikiwa, kwa mfano, kuna vitamkwa

tatanishi ambavyo unataka wanafunzi wajifunze matamshi yake unaweza kupanga

maneno yenye vitamkwa hivyo, kuyaweka katika sentensi na kisha kuwasomea

wanafunzi sentensi hizo kwa sauti. Pia wanafunzi nao wanapewa fursa ya kusoma

sentensi hizo kwa sauti. Kwa mfano ukitaka kushughulikia matamshi ya /z/ na /s/

unaweza kusomea wanafunzi wako sentensi kama zifuatazo:

(a) Wakereketwa wa haki za kibinadamu wanapinga sana utengenezaji wa zana

za vita.

(b) Alimzomea baada ya kumsomea barua yake.

Wakati mwingine kusoma kwa sauti kunaweza kuambatanishwa na zoezi la

kusoma kimya kama njia ya kutilia maki ujumbe uliyojikita katika maandishi. Maneno

yakisomwa kwa sauti yanaweza kuzua na kuibua hisia fulani ambazo si rahisi kuibuka

Page 69: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

69

yanaposomwa kimya. Maana ambayo haiwezi kubainishwa kwa urahisi kupitia

maandishi inaweza kubainika wazi zaidi kupitia sauti. Kwa mfano, hisia kama vile

mshangao, huzuni, na furaha zinaweza kuwasilishwa mtu anaposoma kwa sauti. Kusoma

kwa sauti kunampa mwanafunzi nafasi bora ya kujihusisha na hisia za mwandishi au

mhusika fulani. Wakati wa kufundisha somo la fasihi, kwa mfano, unaweza kuamua

kuchagua sehemu fulani katika riwaya, hasa zile za majibizano kati ya wahusika na

kuzisoma kwa sauti ili wanafunzi wajihusishe na kile kinachoendelea.

Aidha kusoma kwa sauti, kunasaidia mwanafunzi kuwa mwangalifu. Ni lazima

kwanza atambue maneno yaliyoandikwa kisha ayaambatanishe na matamshi yake sahihi

ndipo aweze kuwasilisha ujumbe unaohusika. Ikiwa anaweza kusoma ujumbe

uliyoandikwa kwa njia ambayo inaleta maana hiyo ni ishara kwamba ana uwezo wa

kusoma vizuri kwa sauti. Mazoea haya yanakuwa msingi mzuri kwa zoezi la kusoma

kimoyomoyo.

Wakati mwingine kusoma kwa sauti ni njia mwafaka ya kuandaa na kuhamasisha

wanafunzi katika somo la fasihi ili wawe tayari kwanza kusoma kitabu kinachohusika

kwa hamu. Unaweza kutanguliza ufundishaji wako kwa kuwasomea kwa sauti sehemu

fulani kutoka kitabu ambacho wanatarajiwa kuanza kusoma. Lengo hasa la kufanya hivyo

ni kuwatia wanafunzi wako hamu ya kusoma kitabu hicho wakiwa na shabaha maalum.

ZOEZI 6.1

A. Eleza jinsi kusoma kwa sauti kunavyohusiana

na kutofautiana na kusoma kimya.

B. Jadili umuhimu wa kusoma kwa sauti katika

utaratibu wa kufundisha Kiswahili.

6.2 Matatizo Ya Kusoma Kwa Sauti.

Msomaji kwa sauti anaweza kukumbwa na aina mbali mbali za matatizo, ambayo

yanaweza kumfanya msikilizaji ashindwe kuzingatia vizuri yale yanayosomwa. Matatizo

hayo yanaweza kusababishwa na sababu kama zifuatazo:

Matamshi mabaya

Kuruka na kupachika maneno.

Kusoma kwa mwendo usiyofaa.

Kutosikika.

Matamshi Mabaya.

Matamshi mabaya yanatokea pale ambapo msomaji anaposhindwa kutamka

maneno kama inavyostahili na kuishia kwa kuupotosha ujumbe unaowasilishwa. Wakati

mwingine anaweza kushindwa kuzingatia vituo na kutumia kiimbo sahihi kulingana na

maana ya ujumbe unaohusika. Shida nyingine ya kimatamshi inahusu ile tabia ya

kuvunjavunja maneno na kumfanya msikilizaji afuate kwa shida. Usomaji wa namna hii

Page 70: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

70

husumbua wasikilizaji, na wasipokuwa wavumilivu wanaweza kukata tamaa na

kumpuuza msomaji.

Urukaji na Upachikaji wa Maneno.

Kuna wasomaji ambao kwa sababu ya kutokuwa waangalifu, hawasomi maneno

yaliyomo kwenye taarifa wanayosoma na badala yake wanasoma maneno mengine

ambayo pengine hayana uhusiano wo wote na ujumbe. Msomaji asiposoma neno fulani

katika sentensi anasababisha pengo katika mfululizo wa mawazo; na matokeo yake

yanaweza kuwa upotoshaji wa ujumbe unaokusudiwa. Tuchukue mfano wa sentensi

ifuatayo:

(a) Watoto walifika nyumbani karibu saa mbili usiku.

Ikiwa msomaji ataruka neno karibu sentensi itakuwa : (b.) Watoto walifika nyumbani saa mbili asubuhi

Katika hali kama hii, msikilizaji atapokea ujumbe ambao ni tofauti

kabisa na ule anaowasilishwa na mwandishi. Hali kadhalika, msomaji akitamka neno

jingine badala ya lile lililoandikwa atapotosha ujumbe asilia. Hivyo ndivyo ilivyo pia

akiongeza neno jingine katika sentensi. Sentensi zifuatazo zinaonyesha matokeo ya hali

hii:

(c) (i) Tutakutana karibuni

(ii) Tutakutana kaburini

(d) (i) Watoto walikuwa wamechoka

(ii) Watoto walikuwa wamechoka sana.

Kusoma Kwa Mwendo Usiyofaa:

Mwendo usiyofaa unaweza kuwa ama wa kasi sana au wa kujikokota. Msomaji akisoma kwa mwendo wa kasi inakuwa vigumu kwa wasikilizaji kuzingatia ujumbe

vizuri. Kwa upande mwingine, akisoma kwa kujikokota anaweza kuwatamausha

wasikilizaji. Mwendo unaofaa ni ule wa wastani.

Kutosikika:

Kuna wasomaji ambao wanasoma kama kwamba hakuna watu wanaowasikiliza.

Kusoma kwa namna hii hakuridhishi hata kidogo. Mawasiliano hayakamiliki ikiwa

ujumbe unaowasilishwa hauwezi kumfikia mpokeaji. Kwa hivyo, wewe kama mwalimu

unapaswa kuwahimiza wanafunzi wanaposoma wahakikishe kwamba wanasikika

ipasavyo.

Kwa ufupi unaposhirikisha wanafunzi katika zoezi la kusoma kwa sauti ni lazima

uzingatie na kutilia maanani mambo yafuatayo:

Wanafunzi wahimizwe kusoma kwa mwendo wa wastani.

Wasome kwa mkumbo wa maneno kulingana na maana.

Wazingatie vituo.

Watumie kiimbo sahihi kulingana na maana.

Wasome kwa matamshi sahihi ya maneno.

Wasome kwa njia ya kusikika.

Wasifiche nyuso zao katika matini inayosomwa.

Page 71: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

71

ZOEZI 6.2

Jadili matatizo ambayo kwa maoni yako

huwakumba wanafunzi wanaposoma Kiswahili

kwa sauti. Je unaweza kuchukua hatua gani

kushughulikia matatizo hayo?

6.3 Kusoma Kimoyomoyo

Mwanafunzi anaposoma kimoyomoyo huwa anajisomea yeye mwenyewe bila

kutamka yale asomayo. Kama ilivyo katika zoezi la kusikiliza, kupitia zoezi la kusoma

kimoyomoyo mwanafunzi anaweza kujiongezea maarifa., kupanua msamiati wake na

kuimarisha ujuzi wake wa lugha. Vile vile kupitia zoezi la kusoma kimya kimya

mwanafunzi anaweza kujiburudisha na kukuza uwezo wa kuchunguza na kudadisi

(kuhakiki) mambo.

Katika sehemu hii tutazungumzia kusoma kimoyomoyo tukitilia mkazo fani ya

kusoma kwa ufahamu (Ufahamu andishi). Kinyume na ufahamu sikizi, ufahamu andishi

ni fani ya lugha andishi ambayo kwayo msomaji anapokea ujumbe wa mwandishi na

kuuambatanisha na maana inayostahili. Madhumuni hasa ya kushirikisha wanafunzi

katika zoezi la ufahamu andishi ni nini? Zoezi hili linalenga hasa kusaidia wanafunzi

wakuze uwezo wao wa kusoma upesi bila shida na kufahamu ipasavyo. Linalenga pia

kukuza uwezo wa mwanafunzi wa kusoma kwa makini na kung’amua yaliyo muhimu na

yasiyo muhimu.

Ili wanafunzi wako waweze kusoma kwa ufahamu unapaswa kushughulikia

matatizo ambayo yanaweza kuwazuia kusoma kwa ufahamu. Baadhi ya matatizo hayo ni

kama yale yaliyotajwa katika somo lililotangulia (Rej 5.3). Zaidi ya matatizo hayo

tunaweza kuongeza yafuatayo:

Upachikaji wa maneno.

Kufuta maneno.

Kutozingatia vituo.

Upachikaji Wa Maneno.

Asili ya jambo hili ni utovu wa umakinifu kwa msomaji. Na matokeo yake, kama

ilivyoonyeshwa katika sehemu 6.2 ya somo hili, ni kupotosha ujumbe asilia kama katika

mfano ufuatao:

(a) Tutaonana kesho.

(b) Tutaonana kesho kutwa.

Mwanafunzi akisoma (b) badala ya (a) atapotosha ujumbe asilia. Hali kadhalika,

akifuta maneno yaliyomo kwenye taarifa anayosoma ataishia kwa kutoelewa kama

ilivyotarajiwa. Tuchukue mfano ufuatao:

(c) Tukutane kabla ya saa nne.

(d) Tukutane saa nne.

Page 72: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

72

Akisoma sentensi (d) badala ya (c) atakuwa ameshindwa kuelewa ipasavyo

ujumbe asilia.

Kutozingatia Vituo:

Mwanafunzi asipozingatia vituo kwa mfano viulizi anaweza kuchukulia swali

kama kauli ya kawaida. Matokeo yake ni ufahamu mbaya.

Jambo jingine unaloshauriwa kutilia maanani ukitaka kuwezesha wanafunzi

kusoma kwa ufahamu ni maandalizi bora. Mambo unayoweza kufanya kutekeleza jambo

hili ni kama yale yaliyotajwa katika somo lililotangulia (Rej 5.4).

ZOEZI 6.3

Ukitoa mifano ya kutilia maki jibu lako eleza

mambo ambayo yanaweza kumfanya mwanafunzi

asisome kwa ufahamu. Unaweza kuchukua hatua

gani kumsaidia mwanafunzi anayekabiliwa na

shida ulizotaja?

6.4 Maswali Ya Ufahamu

Maswali ni chombo muhimu ambacho unaweza kutumia kuelekeza wanafunzi

wako kusoma kwa ufahamu wa ndani. Pia ni kigezo muhimu cha kupimia kiwango cha

ufahamu wa wanafunzi. Kwa hivyo ukitaka wanafunzi wako wasome kwa ufahamu

kamili ni lazima utayarishe na kutunga maswali ya ufahamu kwa uangalifu.

Wanaposoma, kwa mfano, kifungu fulani kutoka katika kitabu kinachotumiwa darasani si

lazima utegemee maswali ya mwandishi. Unaweza kutunga na kuuliza maswali yako

mwenyewe. Kwa ufupi maswali unayouliza ni lazima yazingatie masharti kama

yafuatayo:

Kuwa wazi.

Matini inayohusika.

Kuzingatia kikamilifu ufahamu.

Kumpa mwanafunzi nafasi ya kujieleza.

Uwazi.

Ni lazima uhakikishe kwamba maswali unayouliza hayana utatanishi wa aina yo

yote. Yawe na mwelekeo maalum. Kumbuka kwamba lengo la maswali siyo

kuwatatanisha wanafunzi na kuwatumbukiza katika makosa. Ukiuliza maswali

yasiyoeleweka vizuri hata majibu yao yatakuwa ya kutatanisha.

Matini Inayohusika

Maswali unayouliza yahusiane kimantiki na matini inayohusika. Ni lazima

yatokane na matini hiyo na wala siyo nje yake. Sharti yawe maswali ambayo yanaweza

kujibiwa kwa kuzingatia mambo yaliyomo katika matini inayohusika. Lengo lake ni

Page 73: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

73

kutathimini uwezo wa mwanafunzi wa kusoma kifungu fulani na kuelewa ujumbe wake.

Kwa hivyo ni lazima maswali yanayoulizwa yajikite katika kifungu hicho hicho.

Kuzingatia Kikamilifu Ufahamu.

Mtu anaposoma kifungu fulani cha habari anaweza kukichunguza na kufahamu

kifungu hicho kwa viwango mbali mbali. Kwa hivyo unapotunga maswali ya ufahamu

juu ya kifungu kilichosomwa na wanafunzi ni wajibu wako kuona kuwa maswali

unayatunga kwa kuzingatia maenezi yote ya stadi za ufahamu. Usiulize maswali ya aina

moja; lakini uliza maswali ambayo yanashirikisha viwango mbali mbali vya ufahamu.

Mfano wa viwango hivi ni kama:

Ukweli halisi wa mambo.

Ufahamu kwa kuhusisha mambo kimantiki (Ufahamu fasirizi)

Uhakiki/ Utathimini.

Matumizi ya lugha.

Kiini cha taarifa n.k…..

Ukweli halisi unahusu habari halisi kama ilivyo. Kama mwandishi anasema kuwa

mtu fulani alitenda jambo fulani wakati fulani, msomaji anapaswa kuelewa vivyo hivyo

na wala siyo vingine.

Ufahamu kwa kuhusisha mambo kimantiki unahusu uwezo wa mwanafunzi wa

kudadisi na kufikia ukweli uliojikita ndani ya ujumbe wa mwandishi. Unamwezesha

mwanafunzi kuchimbua na kubaini mambo yasiyoelezwa wazi wazi. Mwandishi kwa

mfano, si lazima aseme kinagaubaga kwamba jambo analozungumzia ni la kuaibisha,

kufurahisha au kuhuzunisha. Inampasa mwanafunzi ang’amue mwenyewe kwa

kuzingatia maneno yaliyotumiwa pamoja na mkondo wa hadithi kwa jumla.

Unapotunga maswali inafaa uulize maswali ambayo yanatoa kwa mwanafunzi

fursa ya kujieleza kwa mfululizo wa maneno. Usiulize maswali yanayoweza kujibiwa

kwa neno moja tu: siyo, ndiyo, hapana! Ikiwa swali linahitaji jibu la aina hiyo inafaa

mwanafunzi aagizwe kutoa hoja za kutilia nguvu jibu lake. Inafaa aeleze kwa nini

anasema ndiyo au hapana.

Kuhusu maswali yanayolenga kutathimini ufahamu wa lugha inafaa yaulizwe kwa

kurejelea kipengele kinachotahiniwa katika mkutadha wa sentensi kinamotumiwa.

Maneno au mafungu ya maneno yasiulizwe maana yake bila kuhusishwa na mkutadha wa

matumizi yake katika kifungu kilichosomwa. Sababu mojawapo ya kufanya hivi ni

kusaidia wanafunzi kujizoeza kutafuta maana kwa kuzingatia mkutadha. Maana ya neno

inaweza kubadilika kulingana na mkutadha ambamo limetumiwa. Tuseme kwa mfano

maneno yafuatayo yametumiwa katika kifungu kilichosomwa: donge, chai. Utakuwa

umeuliza vibaya ukimwambia mwanafunzi:

Eleza maana ya maneno yafuatayo:

(a) donge

(b) chai

Njia bora zaidi ni kunukuu sentensi ambamo maneno hayo yametumiwa na

kumtaka mwanafunzi aeleze maana ya maneno hayo kulingana na matumizi yake katika

sentensi.

Page 74: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

74

ZOEZI 6.4

Ukirejelea kifungu mahsusi cha kusoma eleza hatua

ambazo utachukua kuwasaidia wanafunzi wako

kukisoma kifungu hicho na kufahamu ipasavyo yale

wasomayo.

6.5 Kuandika Ufupisho

Ufupisho ni aina ya mawasiliano ambayo kwayo ujumbe fulani unaopokelewa na

msomaji au msikilizaji unawasilishwa upya kwa njia ya mkato inayozingatia tu hoja

muhimu. Zoezi la kuandika ufupisho ni muhimu kwa mwanafunzi kwa sababu linasaidia

kukuza stadi ya kusoma kwa ufahamu. Ni aina fulani ya kufahamu kwa sababu uwezo wa

mwanafunzi wa kufupisha unategemea kiwango chake cha kufahamu yale asomayo.

Asipofahamu vizuri asomayo itamwia vigumu kufupisha kwa usahihi. Pia zoezi hili latoa

nafasi kwa mwanafunzi ya kuendeleza na kupanua ujuzi wake wa lugha. Kwa ufupi zoezi

hili linachangia kuelekeza mwanafunzi katika mambo yafuatayo:

Kusoma kwa makini na dhati.

Kung’amua hoja muhimu.

Kutambua uhusiano kati ya hoja tofauti.

Kujieleza kwa ufupi bila kurudiarudia wala kupotosha ujumbe.

Kujieleza kwa lugha yenye mtiririko na mpangilio mzuri wa mawazo.

Je, unaweza kuwaongoza vipi wanafunzi wako ili waibuke na ufupisho wa

kuridisha? Unaweza kuwaongoza kwa kupitia mfuatano wa hatua zifuatazo:

Usomaji wa kifungu chote cha taarifa.

Udondozi wa hoja aya kwa aya.

Mchujo wa hoja zilizodondolewa.

Kuandika kwa kuunganisha hoja zilizoteuliwa.

Kutathimini ufupisho kwa kuulinganisha na kifungu asilia.

Kwa ufupi, kabla wanafunzi hawajajishughulisha na kazi ya kufupisha ni wajibu

wako kuona kwamba wanakipitia kifungu kinachohusika ili kutambua maudhui yake

muhimu. Kisha majadiliano yanaweza kuibuka juu ya maudhui hayo. Wakati huo huo

matatizo ya lugha yanaweza kushughulikiwa. Baada ya majadiliano hayo sasa unaweza

kuwauliza wanafunzi maswali yanayolenga kuwaongoza kutaja hoja ndogo ndogo

ambazo mwandishi anatoa katika juhudi za kujenga na kutilia maki hoja yake kuu.

Kifungu kizima kichambuliwe aya kwa aya na kisha baadaye hoja hizo zipangwe kwa

mtiririko mzuri wa mawazo. Hoja ziteuliwe kulingana na uzito wake katika kuendeleza

maudhui yanayohusika. Swali la kuuliza hapa ni: Je, hoja hii inachangia kutilia maki

maudhui au la? Ni marudio kwa namna nyingine ya hoja iliyotajwa tayari? Ni hoja

ambayo inaweza kujisimamia yenyewe au la? Kama inaweza kujitegemea inafaa

kuhifadhiwa, lakini kama haiwezi itupiliwe mbali.

Page 75: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

75

Baada ya kuzichagua hoja zote, zipangwe kulingana na uzito wake. Kisha

unaweza kuwaagiza wanafunzi waanze kuandika ufupisho wao bila kurejelea kifungu cha

taarifa kinachohusika wala kukikariri neno kwa neno. Wanafunzi wakimaliza kuandika

ufupisho wao kila mwanafunzi ahimizwe kusoma ufupisho wake na kuulinganisha na

kifungu asilia kuhakikisha kwamba maudhui yake yamezingatiwa vilivyo. Vile vile

lugha, mtiririko na uhusiano wa mawazo vichunguzwe na kutiliwa maanani.

Maelezo haya yamejishughulisha zaidi na mapendekezo kuhusu jinsi unavyoweza

kuongoza wanafunzi waweze kufupisha kifungu chenye ukubwa wa zaidi ya aya moja.

Lakini kabla mwanafunzi hajafikia kiwango cha uwezo wa kufupisha vifungu nya aina

hii anapaswa kuwa na uzoefu wa kueleza ujumbe kwa ufupi kupitia mazoezi kama

yafuatayo:

Kusoma na kupendekeza vichwa vinavyofaa kwa vifungu vya taarifa

visomwavyo.

Kupanga kwa mtiririko mzuri baadhi ya sentensi zilizopangwa kwa mfuatano

usiyofaa.

Kuandika kwa ufupi sentensi zinazowasilisha ujumbe kwa mtindo wa

kujirudiarudia

Mwanafunzi anapofanya zoezi hili la mwisho anaweza akaambiwa ataje maneno

katika sentensi hiyo ambayo yana maana sawa kabla hajaiandika upya. Ikiwa kuna

vifungu vya maneno ambayo maana yake inaweza kuwasilishwa kwa maneno machache

zaidi au kwa neno moja moja mwanafunzi anaweza kuagizwa ataje vifungu hivyo na

kupendekeza njia ya mkato inayoweza kutumiwa kuwasilisha ujumbe unaowasilishwa na

vifungu hivyo vya maneno. Ifuatayo ni mifano ya kubainisha jambo hili:

(a) Akina mama na baba, wasichana na wavulana ambao wanaishi katika mtaa

wa Sokomjinga, na ambao siku mbili zilizopita hawakuweza kuhudhuria

mkutano wa harambe uliyofanyika wakati huo na kutoa mchango wao

wanaarifiwa sasa kuwa mkutano mwingine kama huo utafanywa tena katika

muda wa siku tatu zijazo. Kila mtu anahimizwa kutoa mchango wa aina yo

yote kulingana na uwezo wake, iwe pesa, kuku, mbuzi, kondoo, bata au

machungwa, maembe, mapapai na kadhalika.

(b) Mwanaume mmoja mwenye asili ya Kihindi alijikuta mashakani wakati

ambapo alipelekwa mahakamani. Baada ya kushitakiwa na kusikilizwa kwa

kesi yake makama ilimhukumu kwenda jela na kukaa ndani yake pamoja na

wafungwa wengine kwa muda usiyozidi wala kupungua miezi kumi na miwili

hivi baada ya mahakama kumpata na hatia ya kuingia na kuanza kufanya

kazi nchini bila kuwa na kibali rasmi kinyume na masharti ya sheria za nchi

yetu

Sentensi kama hizi ni kielelezo cha matumizi ya lugha kwa njia ya mzunguko.

Unaweza kutumia mifano kama hii kutayarisha wanafunzi kwa zoezi la kuandika

ufupisho. Kabla wanafunzi hawajafanya ufupisho inakubidi mwenyewe ufanye ufupisho

wako. Pia kabla wanafunzi hawajajaribu kuzifupisha unaweza kujadiliana nao juu yake ili watoe maoni yao juu yake. Wanapomaliza kuzifupisha, ufupisho wa wanafunzi

ulinganishwe na wanafunzi wengine watoe maoni yao juu yake.

Page 76: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

76

ZOEZI 6.5

A. Eleza maana ya ufupisho na umuhimu wa kuufundisha

katika mpango wa kufundisha lugha.

B. Utajua namna gani kuwa mwanafunzi ameandika

ufupisho wa kuridhisha?

C. (i) Andika vifungu vitatu kila kifungu kikiwa na

sentensi zisizozidi tatu zinazoeleza juu ya maudhui

fulani kwa njia ya mzunguko.

(ii) Eleza jinsi utakavyofundisha kila mojawapo ya

vifungu hivyo.

6.6 Kuandika Imla.

Umuhimu wa zoezi la imla kwa mwanafunzi ni kwamba linamfanya ajitahidi

kusikiliza kwa makini. Pia kupitia zoezi hili, mwanafunzi anajifunza jinsi ya kuendeleza

maneno pamoja na kuzingatia masharti ya kuwakifisha. Pamoja na hayo, mwanafunzi

anaposhiriki katika zoezi la imla anapata fursa ya kukuza uwezo wake wa kukumbuka

yale anayoyasikia.

Je, ni mbinu gani ambazo unaweza kutumia kufundisha imla?

Unapaswa kwanza kutambua kwamba zoezi la imla linahusisha uwezo wa namna

mbili kwa wakati mmoja. Mwanafunzi anaposhirikishwa katika zoezi hili anapaswa

kwanza kukumbuka maneno ambayo anasikia, na kisha baadaye anatakiwa kuandika

maneno hayo kwa njia iliyo sahihi. Kwa hivyo, wewe kama mwalimu ni sharti uelewe

vizuri ni lipi kati ya mambo haya mawili unataka kushughulikia. Hata hivyo, kwa vyo

vyote vile ni lazima uhakikishe kuwa kazi ambayo unapatia wanafunzi haihusishi mambo

mengi magumu. Lengo la kazi ya imla siyo kuwakanganya wanafunzi na kuwatumbukiza

katika ufanyaji wa makosa, bali ni kuendeleza uwezo wao wa kusikia maneno

yanapotamkwa na kisha kuyaandika kama inavyotakikana kulingana na masharti ya

uwakifishaji.

Unapotoa zoezi la imla uanshauriwa kutilia maanani mambo haya yafuatayo:

Kusoma na kutamka maneno kwa njia sahihi bila kupotosha maana.

Kusoma kwa kuzingatia mafungu mazima ya maneno yaletayo maana.

Maneno au sentensi vinavyotakwa kuandikwa visomwe mara ya kwanza mara

moja. Kisha vikishomwa kwa mara ya pili wanafunzi waandike.

Kuhimiza wanafunzi kusema kimoyomoyo, bila kufungua midomo, yale

wanayosikia. Pia wafanye vivyo hivyo wakati wanapoandika.

Wanafunzi wakimaliza kuandika, wasomee tena kazi inayohusika ili waweze

kusikiliza tena na kurekebisha kazi yao ikiwa kuna haja ya kufanya hivyo.

Page 77: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

77

N. B. Ikiwa lengo lako hasa ni kutilia mkazo uandikaji wa maneno maalum inafaa

maneno hayo uyatumie katika sentensi halafu uwambie wanafunzi waandike maneno

hayo tu badala ya kuandika sentensi nzima. Mfano:

(a). Andika neno dhamini katika sentensi ifuatayo:

Masumbuko anatafuta bado mdhamini wa kumlipia mtoto wake karo

(c) Andika neno chombo katika sentensi ifuatayo:

Chombo cha kupikia samaki chanuka shombo.

ZOEZI 6.6

A. “Imla haifai kama njia ya kufundishia Kiswahili”.

Jadili.

B. Kwa maoni yako, kusema kimoyomoyo kuna faida

gani kwa mwanafunzi wakati anapofanya zoezi la

kuandika imla?

6.7 Umuhimu Wa Uandishi Wa Insha

Insha ni mtungo wa kinathari ulioandikwa juu ya mada fulani na kupangwa kwa

mfululizo wa aya. Mwanafunzi anapoandika insha huwa anajieleza juu ya jambo fulani

kwa mtiririko wa mawazo ambayo yamepangwa katika aya tofauti zinazofuatana kwa

utaratibu maalum. Ili mwanafunzi aweze kujieleza ni sharti atumie lugha, ambayo ni

chombo muhimu cha kumfanikishia malengo yake ya kimawasiliano. Kutokana na

ukweli huu ni wazi kwamba zoezi la uandishi wa insha linatoa nafasi kwa mwanafunzi ya

kufanya mazoezi ya lugha. Kupitia zoezi hili, kwa mfano, mwanafunzi hupata nafasi ya

kutumia msamiati wa aina tofauti pamoja na madondoo mbalimbali ya kisarufi.

Anapoandika insha za aina tofauti huwa anajifunza kutumia Kiswahili kwa adabu

kulingana na mikutadha tofauti ya mawasiliano.

Jambo jingine ni kwamba uandishi wa insha hutoa changamoto kwa mwanafunzi

kufikiria juu ya mada ambazo anatarajiwa kuandika juu yake. Hali kama hii humsaidia

kuwa na nidhamu, kujenga na kupanua fikra zake. Zaidi ya haya mwanafunzi

anapoandika huwa anafanya mazoezi ambayo yanamsaidia kuimarisha ujuzi wa kanuni

zinazotawala uandishi wa Kiswahili.

Wewe kama mwalimu unapaswa kuutambua umuhimu wa zoezi hili. Jambo hili

litakusaidia kupata fununu juu ya mambo ambayo unastahili kutilia mkazo

unaposhirikisha wanafunzi katika kazi ya kuandika insha.

Licha ya kutambua umuhimu wa zoezi ni sharti pia ufahamikiwe vizuri malengo

ya zoezi hili. Je, kwa maoni yako ufundishaji wa kuandika insha unapaswa kuwa na

malengo gani? Kwa njia ya ufupi tunaweza kusema kwamba lengo lake ni : kumsaidia

mwanafunzi aweze kujieleza juu ya mada fulani akiandika kwa utoshelevu wa mawazo,

mtiririko bora wa mawazo na kwa usahihi wa lugha.

Kwa kurejelea kauli hii inabainika kwamba unapofundisha uandishi wa insha

unapashwa kutilia maanani mambo yafuatayo:

Page 78: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

78

Utoshelevu wa mawazo.

Mtiririko wa mawazo.

Matumizi ya lugha na

Maandishi .

Ni sharti kuona kwamba unasaidia wanafunzi wako kuzingatia mambo hayo

katika insha zao kwa sababu, kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya waalimu, wanafunzi

wengi wanaandika insha ambazo haziridhishi kutokana na kushindwa kuzingatia

utimizaji bora wa mambo hayo yaliyotajwa. Usipowasaidia kuhusu mambo hayo

watakosa kuwa na msingi bora wa uandishi wa insha. Pia huenda wakazoea kufanya

makosa ambayo yasipokomeshwa mapema yatakuwia magumu kuyarekebisha. Baadhi

yao wanashindwa kuzingatia kikamilifu anwani ya insha na kufafanua mawazo juu yake.

Wanakumbwa pia na shida ya kupanga mawazo yao kwa njia nzuri. Kutokana na hali ya

kupungukiwa mawazo wanafunzi wanashindwa kujikita katika anwani ya insha na

kuandika mambo ambayo hayana uhusiano wo wote nayo.

Njia moja ya kukabiliana na matatizo ya namna hii ni kuhakikisha kwamba wewe

kama mwalimu huwashirikishi wanafunzi wako moja kwa moja katika uandishi bila

mwongozo unaofaa. Wanafunzi, hasa wa vidato vya chini inafaa washirikishwe kwanza

katika kuandika insha za mwongozo. Unapowashirikisha katika uandishi wa insha za aina

hii unaweza kuwaongoza kuibuka na insha nzuri kwa kutilia maanani mambo kama vile:

anwani, mawazo na lugha.

Anwani ni kichwa cha mambo ambayo unataka wanafunzi wayaandike.

Unapaswa kuchagua anwani hiyo kwa uangalifu sana ukitilia maanani uwezo wa

wanafunzi. Usiwe na mazoea ya kuchagua anwani ya aina yo yote na kuwapatia

wanafunzi waandike juu yake. Anwani hiyo ikiwa ngumu au kama haina maagizo

yanayoeleweka vizuri, wanafunzi watashindwa kujieleza vizuri juu yake. Kwa hivyo ni

lazima uchague anwani ambayo itampa mwanafunzi fursa ya kueleza mawazo yake

kadiri ya uwezo wake. Akipewa anwani ngumu atashindwa kupata mawazo na matokeo

yake yatakuwa kwamba mwanafunzi ataandika mambo mengine ambayo hayana

uhusiano na anwani hiyo. Ili kuziuia matokeo kama haya unashauriwa uwape wanafunzi

anwani ambazo zinaambatana na hali ya mambo katika maisha yao. Pia baada ya kuwapa

anwani ambayo unatarajia waandike juu yake ni sharti uhakikishe kwamba wanaelewa

vizuri kile ambacho wanatarajiwa kuandika juu ya anwani hiyo. Ni lazima utoe maagizo

ambayo yanaeleweka wazi. Maagizo kama yafuatayo kwa mfano hayafai:

(a) Andika insha kuhusu mmomonyoko wa udongo.

(b) Andika kuhusu ajali.

Je, maagizo haya yana kasoro gani?

Page 79: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

79

ZOEZI 6.7

A. Jadili umuhimu wa kushirikisha wafunzi katika uandishi

wa insha.

B. (i) Kuna tofauti gani kati ya insha ya mwongozo na

insha isiyo ya mwongozo?

(ii) Ukitoa mifano ya kutetea jibu lako eleza kwa nini

wanafunzi wa vidato vya chini hawastahili kuandika

insha zisizo za mwongozo.

Kuongoza Wanafunzi

Lengo la kuongoza wanafunzi ni kuzuia ufanyaji wa makosa ya aina mbali mbali.

Unatoa mwongozo ili wanafunzi wako waweze kuandika insha zenye utoshelevu wa

mawazo, mtiririko bora wa mawazo, usahihi wa lugha na mtindo unaofaa. Unaweza

kuwaongoza wanafunzi kwa kutumia mbinu tofauti kulingana na kiwango cha ujuzi wao

pamoja na aina ya vifaa vya kufundishia vinavyopatikana. Miongoni mwa mbinu hizo ni

pamoja na:

Majadiliano

Vifaa vya maono

Vidokezi vya maneno

Mfano kamili wa insha

Majibu ya maswali

Upangaji wa sentensi.

Majadiliano

Baada ya kuteua anwani ya insha usiwapatie wanafunzi na kuwaagiza waandike

juu yake moja kwa moja. Ni jukumu lako kuona kwamba wanapewa maandalizi mazuri

ya kuwasaidia kushughulikia anwani inayohusika kikamilifu. Majadiliano hayo

yanalenga kufafanua anwani ya insha na kuelekeza wanafunzi kuhusu matarajio ya insha

inayohusika. Ni muhimu kwa sababu, licha ya kutoa nafasi kwa wanafunzi ya kujieleza

katika mazungumzo, yanawasaidia kukusanya mawazo kuhusu anwani ya insha.

Majadiliano juu ya anwani yanasaidia kupanua fikra za wanafunzi juu ya anwani na

kuipa insha yao mwelekeo unaofaa. Jambo hili linapunguza ile hali ya kupungukiwa

haraka mawazo na kuanza kuandika nje ya anwani.

Page 80: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

80

Wakati wa majadiliano, kila mwanafunzi ahimizwe kutoa mchango wake. Hoja

zinazotolewa ziandikwe kwa ufupi kwenye ubao. Kisha wanafunzi, wakiongozwa nawe,

watoe mapendekezo kuhusu jinsi hoja hizo zinavyofaa kufuatanishwa katika aya tofauti

za insha. Wapendekeze mgawanyiko wa hoja katika aya tofauti.

Vifaa vya maono.

Kama ilivyoelezwa hapo awali, wanafunzi mara nyingi wanakumbwa na tatizo la

upungufu wa mawazo. Njia moja ya kusaidia wanafunzi kukusanya mawazo ya

kuwasaidia katika insha zao ni kutumia vifaa vya maono kama vile vitu halisi, michoro,

picha, vibonzo n k…. Ukiamua kutumia kifaa cha maono unapaswa kuchagua kifaa

kinachobainisha mambo tofauti tofauti ambayo mwanafunzi anaweza kuyazungumzia

katika insha yake. Unaweza kuwaongoza wanafunzi kwa kuwauliza maswali kadhaa juu

ya kifaa kinachohusika. Kila mwanafunzi ajaribu kueleza kile anachokiona. Uzuri wa

kifaa hiki ni kwamba kinatoa mkutadha mzuri wa kuendeleza mazoezi ya kutumia

msamiati na sarufi. Ukirejelea kifaa hicho unaweza kuwapa wanafunzi vidokezo vya

maneno ambayo wanaweza kuyatumia katika insha yao.

Uteuzi wako wa kifaa utategemea lengo la insha ambayo wanafunzi wanatarajiwa

kuandika. Vifaa fulani, kwa mfano vinafaa kwa insha za maelezo wakati ambapo vingine

vinaweza kuibua mawazo yanayofaa kwa insha za masimulizi. Ikiwa huwezi kupata kwa

urahisi vifaa vinavyoweza kuyakidhi mahitaji yako usisite kujitayarishia vifaa vyako

mwenyewe, au kutafuta msaada wa watu wengine wenye ujuzi wa kutayarisha vifaa

hivyo. Kwa mfano baada ya kusoma kisa fulani cha kusisimua unaweza kufikiria jinsi

unavyoweza kuwasilisha matukio katika kisa hicho kwa njia ya maono. Kama wewe

huna kipawa cha uchoraji unaweza kumtafuta mtu mwenye kipawa na kumwomba

akuchoree (picha) mchoro unaoonyesha matukio muhimu katika hadithi uliyosoma.

Kisha unaweza kutumia mchoro huo kama chombo cha kufundishia insha ya masimulizi.

Unapofika darasani unaonyesha mchoro wako wanafunzi watoe maelezo yao kuhusu kile

kinachoendelea. Mbali na kueleza kile ambacho wanafikiri kinaendelea, wanafunzi

wanaweza kujaribu kupendekeza anwani ambazo kwa maoni yao zinafaa kueleza

matukio katika mchoro unaohusika. Ukitaka unaweza kuchagua moja kati ya anwani

zilizopendekezwa na kuwataka wanafunzi wako waandike insha yenye anwani hiyo.

Ukifanya hivyo utawahamasisha wanafunzi kwa kuwa watahisi kwamba hata wenyewe

walishirikishwa katika uteuzi wa kazi ya uandishi.

Utumiaji wa vifaa vya maono ni njia bora ya kulipa somo uhai na kulipunguzia

ukavu. Hulifanya somo kuwa la kuvutia kwa wanafunzi.

Videkezo Vya Maneno.

Ukitaka wanafunzi waandike kuhusu anwani fulani unaweza kuwapa vidokezi

vya maneno ili kuwasaidia wakati wanapoandika. Unachagua maneno hayo kwa kutilia

maanani lengo la insha. Haimanishi kwamba ni lazima kwa wanafunzi kutumia maneno

ambayo umependekeza. Si lazima pia kwao kuyatumia yote.

Tuseme kwamba unataka wanafunzi wako waandike insha ya kubuni kuhusu ajali

ya gari ambayo walishuhudia. Unaweza kuwapatia vidokezo kama vifuatavyo:

Jumamosi jioni, kijana na wenzake, gari la kifahari, kulewa chakari, mvua nyingi,

barabara kuteleza, mtelemko, gari ya mbele kusimama ghafla, piga breki, kosa

Page 81: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

81

mwelekeo, gari kupinduka, mayoe, damu kutiririka, wasamaria wema, majeruhi

kupelekwa hospitalini n k…. Matokeo ya kuwapatia wanafunzi vidokezo vya maneno ni kuwa wanapata

mazoezi ya kujieleza wakitumia maneno fulani bila usumbufu mwingi.

Mfano Kamili Wa Insha.

Kuna waalimu ambo wana mazoea ya kufundisha uandishi wa insha kwa kutoa

maelezo tu kuhusu muundo wa insha na mitindo ya kuandika aina tofauti za insha.

Ufundishaji wa namna hii hauna faida yo yote. Wanafunzi hawawezi kujifunza kuandika

kwa kusikiliza tu maelezo yako. Inafaa uwatolee mifano kamili ya insha zilizoandikwa na

watu wengine. Kisha zungumzia vipengele vya insha unavyotaka kueleza kwa kurejelea

mfano mahsusi wa insha. Ukitaka kwa mfano kuzungumzia sehemu tofauti za insha

inafaa uwapatie nakala ya insha uzungumzie sehemu hizo hatua kwa hatua ukirejelea

nakala uliyowapatia wanafunzi. Sehemu hizo ambazo inafaa utilie mkazo ni: utangulizi,

katikati na mwisho. Pamoja na sehemu hizi inafaa uzungumzie aya kama kiungo muhimu

cha insha. Wasaidie wanafunzi kuelewa kila mojawapo ya sehemu hizo kwa kuwauliza

maswali yaliyojikita katika mfano wa insha uliotolewa. Ukiwaeleza umuhimu wa sehemu

hizo kwa kuambatanisha maelezo yako na mfano mahsusi wataelewa vizuri zaidi kuliko

vile wangeelewa bila kuwa na mfano wa kurejelea.

Baada ya kuwaonyesha mifano kamili ya insha unaweza sasa kuwashirikisha kwa

kuwapa kazi ya kuandika wakijishughulisha na sehemu moja tu ya insha. Baada ya

kuwapa, kwa mfano, anwani ya insha unaweza kumwambia kila mwanafunzi aandike

sentensi moja inayoweza kuwa utangulizi wa insha wanayotarajiwa kuandika.

Wakimaliza kuandika wapewe fursa ya kusoma sentensi zao. Kisha wape mawaidha

kuhusu lengo la sentensi ya utangulizi.

Njia nyingine ya kuwaongoza wanafunzi ni kutoa mfano wa utangulizi wa insha

na kuwataka wakamilishe kwa kuandika sehemu nyingine. Unaweza pia kuawatolea

hitimisho na kuwataka waandike utangulizi na sehemu ya katikati vinavyofaa

kukamilisha insha.

Majibu Ya Maswali.

Njia nyingine ya kusaidia wanafunzi kupata na kupanga mawazo wanayohitaji

katika insha ni kuwauliza kwa utaratibu maswali ambayo yakijibiwa, majibu yake

yanaweza kuleta habari kamili. Mbinu hii inafaa sana, kwa mfano, unapowataka

wanafunzi kuandika insha ya maelezo. Lengo hasa la kuuliza maswali ni kutoa fursa kwa

wanafunzi ya kufikiria kwa mapana juu ya mada wanayotarajiwa kuandika juu yake.

Huwasaidia kutilia maanani vipengele vya mada ambavyo, pengine, wasingefikiria juu

yake. Ni wajibu wako kama mwalimu kuona kwamba, kupitia maswali unayomwuliza

unamsaidia mwanafunzi kuzingatia mada inayohusika kikamilifu. Tuseme, kwa mfano,

unataka wanafunzi waandike insha wakieleza matokeo mbali mbali ambayo

yameonekana tangu utekelezaji wa masharti mapya katika magari ya abiria. Unaweza

kutoa maagizo kama yafuatayo: Andika insha isiyokosa kujaza angalau kurasa tano za

daftari ukieleza jinsi utekelezaji wa masharti mapya kwa magari ya usafiri wa umma

ulivyoathiri na kuendelea kuathiri watu katika eneo lako.

Mfano wa maswali unayoweza kuuliza ni kama vile:

Page 82: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

82

Eneo lako ni la mjini au shambani?

Masharti mapya yanuhusu nini? Yalianza kutekelezwa lini?

Kwa nini waziri wa uchukuzi aliwajibika kuweka masharti haya mapya?

Masharti haya yalipokelewa vipi na watu wa tabaka mbali mbali.

Je, utekelezaji wa masharti haya umekuwa na matokeo gani kwa wananchi

ambao hutetgemea magari ya umma?

N.B: Sambamba na maswali haya unaweza kuwaonyesha wanafunzi picha za

magazetini. Unaweza pia kuwahimiza wasome magazeti yanayozungumzia tukio hili.

Upangaji Wa Sentensi;

Ili kuendeleza uwezo wa wanafunzi wa kupanga vizuri sentensi katika aya

unaweza kuwapatia sentensi kadhaa ambazo zimefuatanishwa vibaya na kuwaagiza

wazipange upya kwa mtiririko bora. Zoezi la kupanga sentensi katika mtiririko unaofaa

hutoa nafasi kwa wanafunzi ya kujizoesha kuandika wakizingatia mtiririko wa kimantinki

na kiwakati. Ni wajibu wako kuona kwamba unapotoa mazoezi ya kupanga sentensi

unazingatia aina zote mbili za mtiririko. Wapewe mazoezi ya kupanga sentensi kwa

msingi wa kimantiki pamoja na mfuatano wa matukio kiwakati. Ufuatao ni mfano wa

zoezi la sentensi ambazo zimefuatanishwa vibaya.:

(a) Kisha lilianza kumporomoshea makombora ya ngumi kama kwamba lilikuwa

limerukwa na akili. Ghafla jambazi moja lilitokea likauchovya mfuko wa

kijana huyo. Ulikuwa wakati wa asubuhi. Kufumba na kufumbua, utingo

aliligeukia na kulikaba kooni, lakini liliweza kujisalimisha kwa kumrushia

teke tumboni.

Juzi juzi wakazi wa mtaa wa Somali mjini Kakamega walijionea sinema ya bure

na kutumbuizwa kwa mchezo wa ndondi.

Kisha alichomeka pesa yake katika mfuko wa nyuma wa suruali yake na

kujitayarisha kuingia ndani ya gari. Utingo mmoja alikuwa tayari kumwarifu dreva

aondoe gari kwa sababu lilikuwa limejaa tayari. Aliondoa kibao cha kutangazia wasafiri

mwisho wa safari:

(b) Mtiririko unaofaa:

Juzi juzi wakazi wa mtaa wa Somali mjini Kakamega walijionea sinema ya bure

na kutumbuizwa kwa mchezo wa ndondi.

Ulikuwa wakati wa asubuhi. Utingo mmoja alikuwa tayari kumwarifu dreva

aondoe gari kwa sababu lilikuwa limejaa. Aliondoa kibao cha kutangazia wasafiri

mwisho wa safari. Kisha alichomeka pesa yake katika mfuko wa nyuma wa suruali yake

na kujitayarisha kuingia ndani ya gari.

Ghafla, jambazi moja lilitokea likauchovya mfuko wa kijana huyo. Kufumba na

kufumbua, utingo aliligeukia na kulikaba kooni, lakini liliweza kujisalimisha kwa

kumrushia teke tumboni. Kisha lilianza kumporomoshea makombora ya ngumi kama

kwamba lilikuwa limerukwa na akili.

Page 83: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

83

ZOEZI 6.8

A (i) Toa hoja za kutetea na kupinga mazoea ya waalimu ya

kuwapatia wanafunzi insha za mwongozo.

(iii) Je, kulingana na maoni yako wanafunzi wanastahili

kuongozwa kwa kiasi gani?

C. Andika anwani yo yote ya insha ambayo ungetaka wanafunzi

wa kidato fulani (kitaje) waandike insha juu yake. Kisha eleza

kinagaubaga jinsi utakavyoelekeza na kuwasaidia wanafunzi

kuandika juu ya anwani hiyo insha yenye utoshelevu wa

mawazo na mtiririko bora.

Usahihishaji.

Je ni mambo gani ambayo unapaswa kuchunguza na kuzingatia unaposahisha

insha za wanafunzi na kuwapatia alama?

Miongoni mwa mambo muhimu ambayo unashauriwa kutilia maanani wakati wa

kusahihisha insha ni pamoja na:

Sarufi

Msamiati

Maudhui

Mtindo

Kuhusu sarufi unapaswa kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyozingatia kanuni za

utungaji wa sentensi. Kwa mfano, unachunguza jinsi mwanafunzi anavyotumia

viambisho vya ngeli kulingana na ngeli tofauti za majina na mambo mengine

yanayohusiana na sarufi ya lugha.

Kwa upande wa msamiati, unachunguza uteuzi wa maneno. Je, mwanafunzi

ameteua maneno yanayofaa kulingana na maudhui ya insha? Je maneno hayo

ameyatumia kwa usahihi au la?

Swali muhimu la kuuliza kuhusu maudhui ni ikiwa mwanafunzi amezingatia

kikamilifu mada inayohusika au amekiuka maagizo aliyopewa. Ametoa hoja za kutosha

kuendeleza maudhui ya insha kwa kadiri ya kiwango cha ujuzi wake?

Mtindo kwa upande mwingine unahusu mambo kama vile mtiririko wa sentensi

katika aya na mtiririko wa aya katika insha nzima. Unahusu vile vile unadhifu wa kazi,

kusomeka kwa mwandiko, utumizi wa herufi kubwa na ndogo kwa usahihi, maendelezo

ya maneno na utumiaji wa vituo.

Ni lazima uwe na mwongozo ambao unaonyesha alama ambazo utatoa kwa kila

mojawapo ya mambo hayo. Jumla ya alama ambazo mwanafunzi atapewa inafaa iwe

kielelezo bora cha uwezo wa mwanafunzi katika vipengele tofauti vya uandishi wake.

Page 84: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

84

Hali kadhalika, unashauriwa kuwa na mtindo wa kusahihisha ambao unatoa fursa

kwa wanafunzi ya kutambua makosa yao na kuyasahihisha wao wenyewe. Unaweza kwa

mfano kupiga mstari chini ya kosa na kuonyesha aina ya kosa kwa kutumia alama

mahsusi. Ni lazima uhakikishe kwamba wanafunzi wanafahamu vizuri maana ya alama

unazotumia. Mfano wa alama hizo ni kama vile:

Sf: sarufi

Ms: msamiati

Mt: mtindo

Mz: maendelezo

Mfano wa mwongozo wa kusahihisha:

Hitimisho

Somo hili na lile la tano ni masomo ambayo yamejishughulisha na stadi za

kiisimu ambazo ni kama uti wa mgongo wa lugha. Stadi hizi ni: Kusikiliza, Kuongea,

Kusoma na Kuandika. Hizi ni stadi ambazo zinaingiliana na kutiliana nguvu. Kusikiliza

na kuongea ni stadi ambazo zinajikita katika lugha andishi.

Kwa upande mwingine, Kusikiliza na Kusoma ni stadi ambazo zinahusu upokezi

wa habari wakati ambapo Kusema na Kuandika ni stadi zinazohusu upashaji wa habari.

Kwa mujibu wa wataalamu, stadi hizi zinachukua asilimia ifuatayo ya shughuli za

mawasiliano ya kila siku:

Je unaweza kujifunza nini kuhusu mkabala wa kufundisha Kiswahili kutokana na

tarakwimu hizi?

Stadi Asilimia

Kusikiliza

Kuongea

Kusoma

Kuandika

45%

30%

16%

09%

Sarufi

Msamiati

Maudhui

Mtindo

6

5

5

4

Jumla 20

Page 85: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

85

SOMO LA 7

SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (MSAMIATI NA SARUFI)

7.0 Utangulizi:

Mtu anapojifunza lugha ni lazima aumudu msamiati pamoja na sarufi yake.

Msamiati ni jumla ya maneno yanayopatikana katika lugha, na sarufi ni mfumo wa

kanuni zinazotawala utaratibu wa kutumia maneno katika vielelezo vya sentensi. Neno

pekee halina maana kamili, ila tu liwe limetumika katika mpangilio wa maneno mengine.

Haina faida kwa mtu kujifunza maneno chungu nzima kama hana uwezo wa kutumia

maneno hayo katika vielelezo sahihi vya sentensi.

Kwa hivyo ufundishaji wa msamiati ni lazima uambatanishwe na ufundishaji wa

sarufi.

Madhumuni.

Kufikia mwisho wa somo hili inatarajiwa kuwa utaweza:

(i) Kueleza matatizo ya kimsamiati na kisarufi yanayowakumba

wanafunzi kutokana na athari za lugha zao za mama.

(ii) Kupendekeza na kueleza mbinu ambazo unaweza kutumia

kusaidia wanafunzi kupanua upeo wa msamiati na kuutumia

ipasavyo.

(iii) Kupendekeza na kueleza mbinu mbali mbali unazoweza

kutumia kukuza uwezo wa kisarufi wa mwanafunzi

7.1 Matatizo Ya Kimsamiati Na Kisarufi.

(a) Msamiati

Mtu anapojifunza lugha yake ya mama anazoea namna fulani ya kutumia maneno

kuashiria vitu na kuzungumzia dhana tofauti kufuatana na mfumo wa kanuni za lugha ya

jamii fulani. Kisha mtu huyu anapojaribu kujifunza lugha nyingine analazimika

kuzungumzia ukweli ambao anaujua tayari kwa kutumia maneno yaliyo tofauti na yale ya

lugha yake ya mama. Kwa mfano, kuna lugha zinazotumia neno moja tu kuzungumzia

kile kitendo cha kusafisha vyombo na nguo kwa kutumia maji. Kinyume na lugha hizi,

lugha ya Kiswahili inatumia vitenzi tofauti kulingana na kile kinachosafishwa. Kwa

hivyo wanafunzi kutoka jamii ambazo lugha zao hutumia neno moja tu itawalazimu

kujifunza kuzungumzia mambo ambayo tayari wana uzoefu nayo, kwa msingi wa

mtazamo wa lugha ya Kiswahili.

Matokeo ya hali kama hii ni kwamba wakati mwingine wanafunzi hushindwa

kufuata mfumo wa lugha ya Kiswahili na kuishia kwa kufanya makosa ya kimsamiati.

Wanafanya makosa kwa sababu inakuwa vigumu kwao kuacha kufikiria kwa njia

Page 86: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

86

ambayo wamezoea na kuanza kufikiria kwa njia mpya. Kwa ufupi mwanafunzi anaweza

kufanya makosa katika kiwango cha msamiati kutokana na sababu kama zifuatazo:

Maneno yenye umbo sawa / karibu sawa kuwa na maana tofauti.

Maneno yenye umbo sawa / karibu sawa kuwa na maenezi tofauti ya maana.

Kuwasilisha kwa neno moja dhana zinazowasilishwa kwa maneno tofauti.

Ukweli ni kwamba kuna baadhi ya maneno katika Kiswahili na lugha za

wanafunzi ambayo yanafanana au yanakaribiana kimaumbo lakini yana maana tofauti

katika lugha zote mbili. Asipokuwa mwangalifu au asipoelezwa, mwanafunzi anaweza

kufikiri kwamba neno la Kiswahili lina maana ile ile ya lugha ya jamii yake. Na

akilitumia kwa maana hiyo hiyo ataeleweka visivyo, na watu wengine wakitumia neno

hilo hilo kwa maana ya Kiswahili huenda asielewe kama ilivyotarajiwa. Kwa mfano

katika Kiluhya kuna neno indama ambalo linakaribiana na neno ndama la Kiswahili.

Wakati mmoja neno ndama lilitumiwa katika kifungu cha habari ambacho wanafunzi

walitakiwa kusoma wakati wa kipindi cha Kiswahili. Kwa bahati mbaya mwalimu

mwenyewe hakuelewa maana ya neno hili kama ilivyotarajiwa! Kwa hivyo, wanafunzi

walipomaliza kusoma alitoa agizo na kuwambia: Shikeni ndama.

Mfano mwingine wa maneno yanayofanana au yanayokaribiana sana ni mzigo na

kifo ambayo katika Luganda huandikwa: muzigo, kifo. Maana ya muzigo katika Luganda

ni aina fulani ya mafuta ya kupikia, na maana ya kifo ni nafasi au mahali. Siku moja

mtawa mmoja kutoka Uganda alishituka kwenye kizuizi cha barabarani nchini Kenya

alipomwona askari akigusa mzigo wake huko akiuliza: “Mzigo huu ni wa nani?” Kwa

mshangao mkubwa, mtawa huyu alijiuliza katika lugha yake ya mama kama mtu huyu

alifikiri kuwa yeye angeweza kuweka muzigo kwenye nguo!

Kwa upande mwingine kuna uwezekano kwamba baadhi ya maneno katika lugha

za wanafunzi na Kiswahili ambayo yana umbo sawa au yanakaribiana yana maana ya

pamoja. Lakini licha ya kuwa na maana ya pamoja yanaweza kutofautiana kuhusu

maenezi yake. Kwa mfano maneno kunywa na mchele yanapatikana katika lugha za

wanafunzi. Lakini kinyume na lugha nyingine lugha ya Kiswahili inatumia maneno hayo

kwa maenezi finyu ya maana. Kutofanana na Kiswahili, maneno haya yana maenezi pana

katika lugha nyingine. Kutokana na ukweli kwamba maneno haya yana maenezi pana

katika lugha za wanafunzi si ajabu kwa mwanafunzi kutunga sentensi kama zifuatazo:

(i) Watoto wa shule walifumaniwa wakinywa sigara*

(ii) Nimechoka kula mchele kila siku*

Shida hasa ni kwamba katika mfumo wa lugha ya mwanafunzi anayehusika dhana

ya kunywa na kuvuta hazipambanuliwi. Hali kadhalika, dhana ya mchele na wali

hazipambanuliwi. Lugha yake hutumia neno moja kutaja mambo ambayo kwa mtazamo

wa utamaduni wa Waswahili yanapaswa kutajwa kwa kutumia maneno tofauti.

Mwanafunzi anapowasiliana katika Kiswahili ni lazima atambue kwamba kinyume na

hali ilivyo katika lugha ya jamii yake mfumo wa lugha ya Kiswahili unapambanua kati

ya: mpunga, mchele na wali. Ni lazima ajue pia kwamba mfumo wa Kiswahili

unapambanua kati ya kunywa na kuvuta. Hauruhusu kitenzi kunywa kuambatanishwa na

nomino sigara kama kitendwa.

Tatizo lingine kuhusu matumizi ya maneno linabainika wakati ambapo lugha ya

mwanafunzi hutumia neno moja kuwasilisha dhana ambazo katika Kiswahili

Page 87: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

87

zinapambanuliwa na kuwasilishwa kwa maneno yaliyo tofauti. Tofauti iliyopo na mfano

uliotangulia ni kwamba maneno yanayohusiana katika mfano huu hayafanani kabisa

katika lugha zote mbili. Mfano unaobainisha vizuri tatizo hili unahusu dhana ya idadi na

ukubwa. Katika baadhi ya lugha za wanafunzi dhana hizi mbili huwa hazipambanuliwi

kileksia kwa kutumia maneno yaliyo tofauti. Lakini katika Kiswahili dhana hizi huwa

zinapambanuliwa kileksia kwa kutumia maneno –chache na dogo. Ni kutokana na hali

kama hii, kwa mfano, ndipo unaweza kuona mwanafunzi akitumia sentensi kama

ifuatayo akiwa na maana ya uchache wa watu:

(iii) Mkutano uliahirishwa kwa sababu watu waliokuja walikuwa wadogo

sana.

Kutokana na mifano hii ni wazi kwamba unapofundisha msamiati wajibu wako

siyo kufundisha wanafunzi maneno mapya tu, bali pia ni kuona kwamba wana uwezo wa

kuzingatia matumizi yake sahihi katika vielelezo vya sentensi.

(b) Sarufi:

Lugha ni mfumo wa maneno. Hii inamaanisha kwamba maneno ya lugha huwa

yanapangwa kwa kuzingatia kanuni maalum za lugha inayohusika. Mfumo wa sarufi ya

Kiswahili una sifa zake ambazo wakati mwingine zinatofautiana na zile za lugha za

wanafunzi. Hali kama hii inaweza kuwa chanzo cha baadhi ya makosa ambayo

wanafunzi wanafanya katika Kiswahili. Kwa mfano, lugha ya Kiluo haiweki majina

katika makundi ya ngeli na kupambanua majina hayo katika umoja na wingi kwa kutumia

viambisho kama ifanywavyo katika Kiswahili. Mifano ifuatayo inabainisha ukweli huu:

Mara nyingi watu kutoka jamii ya Waluo wanakuwa na shida ya kutumia

viambisho vya ngeli kwa usahihi. Sababu mojawapo ya shida yao inatokana na mfumo

wa lugha ya jamii yao. Hata wale ambao wana mfumo wa ngeli katika lugha zao

wanafanya makosa ya kutumia viambisho vya ngeli visivyofaa. Asili hasa ya kukosea ni

kwamba majina yanayohusika huwa yanawekwa katika ngeli tofauti katika lugha ya

Kiswahili na zile za wale wanaohusika. Kwa kawaida, baadhi ya lugha za kibantu

huweka majina ya wadudu na wanyama katika ngeli ya 9/10. Hali ni tofauti katika

Kiswahili ambapo majina hayo huwekwa katika ngeli ya 1 / 2.

Kutokana na ukweli huu, unaweza kushuhudia sentensi kama zifuatazo kutoka

kwa wanafunzi:

Kiswahili Luo

Chakula kizuri.

Msichana mzuri.

Samaki wazuri.

Kiti kimevunjika.

Mti umevunjika.

Miti imevunjika.

Chemor maber.

Nyako maber.

Rech maber.

Kom otur.

Yath otur.

Yiem otur.

Page 88: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

88

(iv) Kuna mbu nyingi hapa.*

(v) Kuku yangu imekufa.*

Aina nyingine ya kosa inahusu majina ya ukoo yanapohusishwa na kimilishi. Kwa

mujibu wa sarufi ya Kiswahili ni lazima kimilishi kiambatanishwe na kiambisho cha

ngeli ya 9/10. Kwa upande mwingine, lugha nyingine za kibantu zinatumia kiambisho

cha ngeli ya 1 /2. Kwa sababu hii unaweza kuwasikia wanafunzi wakisema:

(vi) =Alienda kwa nyanya wake.*

Kosa lingine la kisarufi ambalo hutokea mara kwa mara linatokana na tabia ya

wanafunzi ya kuhamisha moja kwa moja madondoo ya kisarufi kutoka lugha zao za

mama na kuyaingiza katika matumizi ya Kiswahili. Ifuatayo ni mifano inayobainisha

tabia kama hii:

(vii) Ninataka kumwonako padre.*

(viii) Tulipitianga hapo zamani.*

Hali kadhalika wanafunzi wanaweza kukanganywa na wakati mwingine kufanya

makosa kutokana na ukweli kwamba dondoo fulani la kisarufi linatumiwa kwa njia

tofauti na ile waliyozea katika lugha yao. Ni kawaida, kwa mfano, kusikia mwuzaji

ambaye anataka mteja anunue kitu fulani kutoka kwake akisema,

(ix) Customer, njo uninunulie……

Msemaji huyu huwa anazungumza hivi kwa sababu katika lugha ya jamii yake

huwa wanatumia kauli ya kutendea katika mkutadha kama huo. Mwanafunzi kutoka jamii

hii anapojifunza sarufi ya Kiswahili itambidi kutambua kwamba katika Kiswahili kauli

ya kutendea haiwezi kutumiwa katika mkutadha kama huo.

Ni wajibu wako kama mwalimu kuwa chonjo ili uweze kutambua aina mbali

mbali za matatizo ya kimsamiati na kisarufi yanayoweza kuwakumba wanafunzi wako

kutokana na tofauti kati ya Kiswahili na mfumo wa lugha mama za wanafunzi wako. Ni

baada ya kutambua matatizo hayo ndipo utakapoweza kuchukua hatua zinazofaa

kuyashughulikia.

ZOEZI 7.1

(a) Ukitoa mifano inayofaa eleza jinsi utumiaji wa maneno katika

lugha za jamii za wanafunzi na Kiswahili unavyoweza

kutofautiana na kutatiza mawasiliano ya wanafunzi katika

Kiswahili.

(b) Onyesha jinsi wanafunzi wanavyoweza kuhamisha kanuni za

kisarufi za lugha za jamii zao katika Kiswahili na kuishia kwa

kufanya makosa ya kisarufi.

Page 89: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

89

7.2. Uhusiano Kati ya maneno.

Maneno ya lugha yanaweza kugawanywa katika makundi kulingana na jinsi

yanavyohusiana na kuingiliana kwa msingi wa maana (kisemantiki). Kwa mfano,

tukirejelea maneno katika kundi la kwanza tunaona kwamba kila moja kati ya maneno

hayo linaweza kuambatanishwa na zaidi ya maana moja. Kwa hivyo maneno yenye sifa

hizi yanaweza kuainishwa pamoja. Vile vile maneno yaliyopangwa jozi kwa jozi katika

kundi la pili nayo yanahusiana kwa namna maalum. Manenao katika jozi hizi yana karibu

maana sawa. Kwa upande mwingine yale katika kundi la tatu ni maneno yenye maana

kinyume.

Aina nyingine ya uhusiano ni ile inayobainika katika jozi za maneno ambayo

yanaashiria hali ya mshikamano au ya mambo ambayo huwa yanapatikana kwa wakati

MFANO WA MANENO AINA YA UHUSIANO

1 Panda Kaa

Ua meza Vitate

2 (i) panda kwea

(ii) iva komaa.

(iii) zunguka zurura

(iv) shida taabu

Visawe

3 (i) panda shuka

(ii) chini juu

(iii) mbele nyuma

Vinyume

4 (i) giza usiku

(ii) nuru mchana

(iii) jua joto

Viandamizi

5 (i) mchana giza

(ii) usiku nuru Vikingamizi

6 kupiga magoti

kupiga simu

kukata shauri

kukata tamaa

kula kiapo

kupiga kidoko

Nahau

Page 90: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

90

mmoja. Kwa kawaida usiku huandamana na giza; na mchana huwa unaandamana na

nuru. Kwa upande mwingine yale katika kundi la tano huashiria hali ya mambo

yanayotengana. Uhusiano wa maneno katika jozi hizi ni wa utenganifu. Kwa kawaida,

kwa mfano, giza haipatikani mchana; na wala nuru haipatikani usiku. Kwa Kingereza

uhusiano katika kundi la nne hujulikana kama collocation na ule katika la tano hujulikana

kama exclusion.

Kundi la sita lina semi ambazo hujulikana kama nahau. Nahau ni usemi ambao

maana yake haiwezi kutabiriwa kwa kuzingatia maana ya neno moja moja katika usemi

huo. Unaweza kuwa unafahamu kila neno ambalo limetumiwa katika usemi fulani lakini

ukashindwa kuelewa maana ya usemi huo. Kupiga magoti, kwa mfano, hakuna maana ya

kushika fimbo au kifaa cho chote kile na kuyatwanga magoti.

Ni muhimu kwako kama mwalimu kuwa na fununu kuhusu vile ambavyo maneno

ya lugha yanaingiliana na kuhusiana. Jambo hili litakusaidia kupanga ufundishaji wako

wa msamiati kwa utaratibu ukitilia maanani uhusiano huo. Badala ya kuchanganya

maneno ya aina tofauti na kuyafundisha kwa pamoja unaweza kutumia uhusiano kama

kigezo kinachoweza kukuongoza kuteua maneno utakayofundisha.

ZOEZI 7.2.

Licha ya kueleza aina tofauti za makundi ya maneno, kila kundi

linapewa jina maalum. Pendekeza istilahi ambazo, kwa maoni

yako zinafaa zaidi, na kisha utoe hoja za kutetea pendekezo lako.

7.3 Kufundisha Msamiati

Maneno ni chombo muhimu cha ufanikishaji wa mawasiliano. Mtu asipokuwa na

maneno ya kutosha anakuwa na shida ya kuwasilisha ujumbe. Vile vile, anakuwa na

shida ya kufahamu kwa urahisi ujumbe unaowasilishwa na wengine. Kwa hivyo

ufundishaji wa msamiati unalenga kuwezesha mwanafunzi kuwa na maneno ya kutosha

ili aweze kuwasilisha na kupokea bila shida ujumbe katika miktadha tofauti ya

mawasiliano. Unalenga kumwezesha kusoma, kusikiliza, kuzungumza na kuandika kwa

ufahamu bora.

Ujuzi wa msamiati siyo jambo ambalo linaweza kufanyika kwa ghafla au katika

muda mfupi wa mafundisho. Unatokana na mazoea ya kushiriki katika matumizi ya lugha

kwa muda mrefu. Kwa hivyo wewe kama mwalimu usichukulie ufundishaji wa msamiati

kama wakati wa kushindilia maneno chungu nzima kwenye vichwa vya wanafunzi. Pia

ujuzi wa msamiati hautegemei idadi ya maneno magumu ambayo mwanafunzi anaweza

kuwakanganya nayo watu wengine. Ni kazi bure kwa mtu kujua maneno mengi au

maneno magumu kama hana uwezo wa kutumia maneno hayo kuwasiliana kwa ufahamu

na watu wengine. Kwa hivyo unapofundisha msamiati usiwe na mazoea ya kufundisha

maneno mengi katika muda wa kipindi kimoja cha somo. Usiwe pia na mazoea ya

Page 91: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

91

kufundisha tu maneno magumu. Inafaa ufundishe maneno machache, na uambatanishe

ufundishaji wake na mambo mengine. Kile unachopaswa kukazania ni kuona kwamba

unashirikisha wanafunzi wako katika shughuli mbali mbali za mawasiliano ambayo

yanaweza kutoa nafasi kwao ya kujiongezea msamiati na kuimarisha uwezo wa kutumia

msamiati huo kama inavyopaswa.

Je ni mbinu gani ambazo unaweza kutumia kufundishia msamiati, na unaweza

kuzitumia namna gani? Miongoni mwa mbinu hizi ni pamoja na zifuatazo:

Mkutadha Wa Maneno

Maono

Maigizo

Visawe

Vinyume

Asili ya neno

Tafsiri

Mkutadha Wa Maneno

Aghalabu neno likitumiwa pekee yake bila kuambatanishwa na maneno mengine

katika muundo wa senstensi inakuwa vigumu kutambua maana yake mahsusi. Maana ya

maneno mengi inategemea mtagusano wake na maneno mengine. Kwa mfano, neno piga

linakuwa na maana tofauti kulingana na maneno mengine yanayotumiwa pamoja nalo

kama katika mifano ifuatayo:

magoti

yowe

mbizi

Kupiga kalamu

ngumi

kofi

kidoko

pasi

Uzuri wa kutolea neno mkutadha ni kwamba unasaidia mwanafunzi kutambua

maana kwa urahisi. Ni rahisi pia kwa mwanafunzi kukumbuka maneno yanayohusika

pamoja na matumizi yake. Mbinu ya mkutadha inafaa sana kwa sababu inatilia maanani

ukweli kwamba lugha ni chombo cha mawasiliano. Kwa hivyo unapotaka kufundisha

neno lo lote inafaa ulitolee mkutadha maalum utakaowasaidia wanafunzi kung’amua

maana yake. Kwa ufupi unaweza kufuata hatua kama zifuatazo:

(a) Bainisha matumizi ya maneno yanayohusika katika mkutadha wa

mawasiliano.

Page 92: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

92

(b) Fahamisha wanafunzi maneno yaliyolengwa, na kuwasaidia kufafanua

maana kwa kurejelea mkutadha wa matumizi yake.

(c) Shirikisha wanafunzi katika mazoezi yanayolenga kutoa kwao nafasi ya

kutumia maneno yanayohusika ili waweze kubainisha na kuendeleza ujuzi

wao wa maneno.

Tuseme kwa mfano mada ya somo lako ni “maneno yenye maana zaidi ya moja”.

Umeamua kufundisha mada hii na miongoni mwa maneno ambayo umeamua kutoa kama

mfano ni neno panda. Je, utafundisha vipi ukitumia mbinu ya mkutadha?

Kwanza utalitolea mkutadha neno hili kama katika mfano ufuatao:

PANDA.

(a)

Miaka ishirini iliyopita Mzee Omari alipanda koko la embe. Mwembe

ulupokomaa alitwambia tupande hadi katika panda la mti ili tukate matawi kiasi ya

kutengeneza panda za kuwindia ndege na panda za nguzo kwani alisikia fununu kwamba

vifaa hivi vimepanda bei huko mjini.

Baada ya kutayarisha vifaa vyake, Mzee Omari alipanda matatu kuelekea mjini.

Matatu ilichomoka mbio na kupanda milima kwa kasi sana bila kusimama mpaka

ilipofika kwenye njia panda. Kutoka hapo, ilielekea kulia, njia inayopitia msituni ambako

Mzee Omari alimwona panda akiwa malishoni. Walipofika mjini walisikia sauti ya

parapanda ikilia kwa mbali.

(b)

Hapo kale palikuwa na watoto wawili Karisa na Kitsao. Karisa alikuwa binamu

ya Kitsao. Alfajiri moja walitoka kwa mbalamwezi wakaenda shambani kulima. Baadaye

kidogo walichukua mbegu za mtama na kuanza kuzipanda humo shambani.

Walipomaliza kupanda mbegu, Kitsao alimshauri binamu yake waende kuwinda ndege,

na Karisa akajibu ya kwamba hakuwa amebeba panda yake na kwa hivyo asingeweza

kwenda kuwinda. Kitsao alimwarifu kwamba yeye aliwahi kubeba panda mbili.

Basi waliandamana kwenda mawindoni. Muda kidogo hivi Karisa aliona ndege

juu ya matawi ya mwembe, akalenga shabaha na ile panda na kumpiga kwa sokota moja.

Lakini badala ya kuanguka chini, yule ninga alisaki juu ya kitagaa cha mwembe. Kuona

hivyo, Karisa alipanda juu ya mwembe na kumtoa yule ndege.

Vijana hawa wawili waliendelea kuwinda ndege huko mwituni kwa muda mrefu.

Walichelewa kurudi nyumbani; na katika ile hali ya kurejea nyumbani walifika njia

panda. Walitatizika sana kwa kutojua njia ipi kati ya zile mbili ndiyo inayokwenda kwao.

Karisa alimwambia mwenzake wabahatishe kwa kufuata moja kati ya njia hizi mbili.

Waliifuata na punde si punde wakajikuta wamewasili kwao nyumbani. Walieleza mkasa

uliowapata wakapewa pole.

Ilipofika liamba siku ya pili, Kitsao alitumwa dukani kununua mkate, maziwa na

majani chai. Kufika dukani akatoa senti alizopewa na mama yake lakini mwenye duka

Page 93: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

93

akamwambia bei za vitu zilikuwa zimepanda siku iliyopita. Kitsao alipanda baiskeli yake

akarudi nyumbani kumwambia mama yake. Aliongezewa pesa akarudi huko dukani

kununua vitu alivyotumwa.

Baada ya chai ya asubuhi, Kitsao na Karisa walitumwa kwenda sokoni kununua

vifaa mbali mbali vilivyohitajiwa siku hiyo. Walipomaliza shughuli zilizowapeleka huko

walipanda gari wakarudi nyumbani. Kufika nyumbani walistaajabu kuona umati wa

watu. Walipouliza, waliambiwa kwamba walikuwa wamekusanyika kwa vile mjomba

wao alikuwa amepandishwa cheo kazini.

Ufundishaji.

Ukifika darasani unaweza kufuata hatua zifuatazo:

Kuwasomea wanafunzi kwa sauti nakala. Wewe au mwanafunzi mmoja.

Kuwapatia wanafunzi nakala ili wasome kimya.

Kuwataka wataje neno ambalo limerudiwa mara kwa mara.

Ukirejelea sentensi tofauti ambamo neno panda limetumiwa wambie

wanafunzi wajaribu kueleza maana ya neno hilo.

Wanafunzi watunge sentensi zaidi zinazobainisha maana tofauti za neno

panda.

Waulize wanafunzi jinsi maneno ya namna hii huitwa.

Watoe mifano mingine ya maneno ya namna hii na kuyatumia katika sentensi

tofauti kubainisha maana mbali mbali.

Mfano mwingine wa kutumia mkutadha:

(c)

Bwana Kizenga aliishi katika mtaa wa Makogoro. Hapo alikaa katika maisha ya

taabu. Aliyamudu maisha yake kwa kufanya kazi ya kuchoma makaa. Kwa kuuza makaa

hayo aliweza kujipatia pesa akaanza starehe. Alijijengea nyumba ya mawe inayoweza

kukaa kwa miaka mingi sana. Nyumba yake ilijengwa kwa ustadi hivi kwamba mtu

angeweza kukaa ndani mchana kutwa bila kuchukizwa.

Mimi mwenyewe niliyashuhudia haya nilipomtembelea hivi majuzi. Yeye na

familia yake walikuwa wamevalia nguo zilizowakaa vizuri. Tulikaa kwenye viti kabambe

vilivyopambwa kwa vitambaa maridadi tulipokuwa tukikaribishwa kwenye mlo wa

mwaka.

Nje ya nyumba na au la miti, na pembeni mlikuwa na bwawa dogo ambamo

Bwana Kizenga liwafuga wanyama wadogowadogo wa majini kama vile kaa, vyura na

hata samaki kwa minajili ya kupendeza wageni.

Vifaa Vya Maono.

Hii ni mbinu ambayo inahusisha utumiaji wa vifaa kama vile vitu halisi, picha au

michoro ya aina tofauti. Unapotumia mbinu hii mwanafunzi anapata fursa ya kung’amua

maana ya neno kwa kuliambatanisha moja kwa moja na kitu, kielelezo cha kitu

kinachohusika, au kitendo kinachoashiriwa. Pamoja na hayo utumiaji wa vifaa vya

maono hulipa somo uhai licha ya kuzoesha wanafunzi kukumbuka kwa urahisi. Hali

kadhalika ni mbinu kabambe ya kuhamasisha wanafunzi kujieleza kwa nafsi zao.

Page 94: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

94

Wakati unapotumia mbinu hii unaweza kutunga maswali na kuwataka wanafunzi

wajibu maswali hayo. Wakati wa kujibu maswali juu ya picha au mchoro wanafunzi

watakuwa wakifanya mazoezi ya kutumia lugha. Tukirejelea mfano wa neno panda

unaweza kuonyensha vitu na michoro kama vile:

Manati.

picha ya mtu anayekwea juu ya mti.

watu wakiingia ndani ya matatu.

watu wakiweka mbegu ardhini.

kifaa cha kushikilia nguo zinapoanikwa n.k..

Kufundisha kwa njia hii ni bora zaidi kuliko kufundisha kwa kuwaagiza

wanafunzi wataje maana tofauti za neno. Kufanya hivyo hakuwasaidii kuzingatia

ipasavyo matumizi ya neno linalohusika.

Maigizo.

Maigizo ni namna ya maonyesho kwa vitendo. Humpa mwanafunzi nafasi ya

kukisia maana ya neno kwa kuliambatanisha moja kwa moja na kitendo kinachoigizwa au

kinachofanywa. Uigizaji huo unaweza kufanywa na wanafunzi au na wewe mwenyewe.

Uzuri wa mbinu hii ni kwamba inaambatanisha maono na vitendo, mambo ambayo

yanachangia kufanikisha hali ya kukumbuka na kufahamu. Aghalabu, ukiona

unakumbuka rahisi zaidi, na ukitenda jambo unafahamu zaidi kuliko unaposikia tu.

Maneno kama yafuatayo yanaweza kufundishwa kwa maigizo: chungulia, nyemelea,

mshangao, huzuni, chomoa, dundadunda, kujipinda, myayo, nong’ona.

Visawe:

Maana ya maneno inaweza kuelezwa kwa kutaja neno lingine lenye maana karibu

sawa. Lakini lazima ikumbukwe kuwa si rahisi kupata maneno mawili ambayo maana

yake ni sawa kabisa. Hata maneno yanayotambuliwa kuwa ni visawe yanatofautiana.

Kwa mfano, maneno iva na komaa yanafikiriwa kama visawe. Kila mojawapo ya maneno

haya linaweza kutumiwa badala ya lingine kama inavyobainika katika sentensi zifuatazo:

(a) Tunda hili halijakomaa vizuri.

(b) Tunda hili halijaiva vizuri.

Lakini neno komaa haliwezi kutumiwa badala ya iva katika sentensi ifuatayo:

(c) Chakula kimeiva vizuri.

Hali kadhalika neno iva haliwezi kutumiwa mahali pa komaa katika sentensi

ifuatayo:

(d) Kijana huyu amekomaa kiakili.

Mifano hii inaonyesha wazi kwamba hata maneno ambayo yanafikiriwa kuwa

sawa hayamo katika mpishano huria katika mikutadha yote ya mawasiliano. Ni lazima

uhakikishe kwamba wanafunzi wanatambua ukweli huu kuhusu maneno hayo.

Unapotumia kisawe pia kama njia ya kufundishia neno unapaswa kuhakikisha kwamba

neno ambalo unataja kama kisawe ni neno ambalo tayari wanafunzi wanalijua. Ukitumia

neno ambalo ni geni kwao utawakanganya zaidi badala ya kurahisisha ufahamu wao.

Ni wajibu wako kuona kwamba wanafunzi wanatambua vizuri ukweli kwamba

visawe havimo katika mpishano huria katika kila mkutadha wa mawasiliano. Kutambua

ukweli huu kutawasaidia sana hasa wanapotumia kamusi kutafuta maana za maneno. Ni

Page 95: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

95

kawaida katika kamusi kukuta maneno kadhaa yakiwa yameorodheshwa kama visawe

vya neno ambalo maana yake inafafanuliwa. Wanafunzi wasipotambua ukweli huu,

huenda wakatumia kimakosa maneno yaliyotajwa katika mkutadha ambamo hayastahili

kutumiwa. Ujuzi wao wa msamiati hautakuwa kamili kama hawana uwezo wa kutumia

kwa usahihi kisawe kinachohusika katika vielelezo vya sentensi.

Kwa hivyo unapotumia mbinu hii usiishie kwa kutaja visawe peke yake.

Unapaswa pia kushirikisha wanafunzi katika mazoezi yanayolenga kuendeleza uwezo

wao wa kutambua mikutadha ambamo maneno yanayohusika yanaweza kutumiwa moja

badala ya lingine na ile ambamo haiwezekani kufanya hivyo. Kwa mfano, unaweza

kuwapatia zoezi la kukamilisha sentensi kwa kujaza katika pengo neno linalofaa kutoka

orodha ya visawe ulivyoorodhesha. Ikiwa inawezekana kutumia maneno yote

yanayochukuliwa kuwa visawe wajaze yote mawili, neno moja likiwekwa katika mabano.

Unaweza pia kuwapa maneno yanayofikiriwa kuwa visawe na kuwambia:

(i) Watunge sentensi ambamo kila mojawapo ya maneno hayo linaweza

kutumiwa badala ya lingine.

(ii) Watunge sentensi ambamo moja kati ya maneno hayo haliwezi kutumiwa

badala ya lingine.

Vinyume.

Unapotumia kinyume unajaribu kueleza maana ya neno fulani kwa kutoa mfano

wa neno lenye maana inayopingana na ya neno hilo. Kwa mfano:

Ili uweze kufaulu vizuri ni lazima uhakikishe kwamba neno unalotaja kama

kinyume si geni kwa wanafunzi. Kama sivyo utawatatiza zaidi. Lazima ukumbuke pia

kwamba siyo kila neno linaweza kuwa na kinyume. Kwa hivyo usiwambie wanafunzi

kutaja kinyume cha neno lo lote bila kutilia maanani ukweli huu. Lazima pia

uambatanishe utajaji wa kinyume na zoezi la kutumia katika sentensi maneno

yanayohusika ili maana inayopingana iweze kubainika wazi.

Neno linalohusika Kinyume

nyuma

zima

chungu

kuasi

furaha

chali

juu

mbele

washa

tamu

kutii

huzuni

kifudifudi

chini.

Page 96: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

96

Asili Ya Neno

Wakati mwingine unaweza kuongoza wanafunzi kukisia maana ya neno kwa

kuwaonyesha chanzo cha neno hilo ikiwa inawezekana. Unaweza, kwa mfano, kusaidia

wanafunzi kukisia maana ya maneno yafuatayo kwa kurejelea mwanzo wake:

Tafsiri:

Ikiwa huna njia yo yote ya kueleza maana ya neno unaweza kueleza maana yake

kwa kutumia lugha nyingine ambayo wanafunzi wanaielewa. Lakini unapotumia mbinu

hii inafaa ukumbuke kuwa siyo kila neno linaweza kutafsiriwa moja kwa moja kutoka

lugha moja hadi nyingine. Vile vile, mbinu hii haistahili kutegemewa sana kwa sababu

wanafunzi wakiizoea sana huenda wasitilie maanani lugha ya Kiswahili kama lugha

kamili ambayo inaweza kujitosheleza kama chombo cha kufanikisha mawasiliano.

Uteuzi Wa Msamiati:

Msamiati ambao utafundisha wanafunzi wako unategemea sana vitabu

vinavyotumiwa katika viwango unavyofundisha. Lakini, hata hivyo, unashauriwa mara

kwa mara kuteua msamiati ambo unafaa wanafunzi wako na kuufundisha. Ni wajibu

wako pia kuwaongoza wanafunzi kusoma vitabu mbali mbali na makala tofauti ili waweze kupanua msamiati wao.

ZOEZI 7.3.

A. Pendekeza mbinu nyingine zaidi unazoweza kutumia

kufundishia msamiati. Kwa kila mbinu

unayopendekeza toa mifano kuonyesha jinsi

unavyoweza kuitumia .

B. Jadili uzuri na udhaifu wa mbinu zifuatazo kama njia

za kufundishia msamiati:

(i) Kutumia vitu halisi.

(ii) Kutumia visawe.

(iii) Kutafsiri.

Neno Asili yake

Kutafakari

Kutarazaki

Tarathimini

Fikiri

Riziki, ruzuku

Taarifa, tathimini.

Page 97: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

97

7.4 Ujuzi wa Sarufi:

Ufundishaji wa sarufi unalenga kuwezesha mwanafunzi kutumia maneno ya lugha

inayohusika katika utaratibu unofaa. Kwa hivyo unapofundisha sarufi ya Kiswahili

unapaswa kushirikisha wanafunzi katika mazoezi ya matumizi ya lugha ambayo yanatoa

kwao fursa ya kung’amua na kutumia kanuni zinazotawala matumizi ya maneno katika

utaratibu unaotakikana kulingana na mkutadha wa mawasiliano. Wanafunzi wakiwa na

uwezo huu watakuwa wanafahamu sarufi.

Mwanafunzi akiimudu sarufi ya Kiswahili atakuwa na uwezo wa kufanya mambo

kama yafuatayo:

Kutumia maneno ya Kiswahili katika vielelezo sahihi vya sentensi.

Kutambua miundo ya sentensi inayokiuka utaratibu wa Kiswahili.

Kutambua maana ndani ya sentensi kwa kuzingatia mfuatano wa maneno

yaundayo sentensi kama:

(i) Ali alimzomea Amina

(iii) Amina alimzomea Ali.

Kutambua uhusiano wa maana katika sentensi tofauti k.m.

(i) Baba alipiga mtoto

(ii) Mtoto alipigwa na baba

Kutambua maana ya sentensi kwa kuzingatia mageuzi yanayotokea katika

maumbo ya maneno k.m.

a.

(i) Tunda hili haliliwi.

(ii) Tunda hili haliliki.

b..

(i) Mama alipika chakula.

(ii) Mama alipikisha chakula.

(iii) Maama alipikiwa chakula

Kung’amua utata ndani ya sentensi k.m.

(i) Watoto walipanda miti.

(ii) Musa aligombana na Ali akampiga teke akaangukia mbuzi

Kutumia Kiswahili kwa njia ya ubunifu.

Kutokana na mambo haya ni wazi kwamba wewe kama mwalimu una jukumu la

kujitahidi kusaidia wanafunzi wawe na uwezo wa kutekeleza mambo haya yaliyotajwa.

ZOEZI 7.4

A. Toa mifano ya sentensi zenye utata ndani yake. Kwa kila

mfano eleza chanzo cha utata huo, na kisha pendekeza

jinsi ya kuondoa utata huo.

B. Ukitoa mifano ya kutilia maki jibu lako eleza maana ya

kutumia Kiswahili kwa njia ya ubunifu.

Page 98: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

98

7.5 Kufundisha Sarufi:

Somo la sarufi ni mojawapo ya masomo ambayo hayapendwi na wanafunzi.

Sababu mojawapo ya kutopendwa ni kwamba baadhi ya walimu wana mazoea ya

kufundisha sarufi kama kwamba ni lugha ya aina ya pekee ambayo inatumika katika

mazingira ya darasa. Walimu wa namna hii wanafundisha sarufi kama kwamba haina

uhusiano na lugha ya nje ya darasa. Wengine wanachukulia wakati wa kufundisha sarufi

kama wakati wa kufundisha kanuni za matumizi ya lugha na uchambuzi wake kwa

misingi ya kiisimu. Matokeo ya mtindo huu ni kuwafanya wanafunzi wachukie vipindi

vya sarufi. Ni wajibu wako kama mwalimu kuhakikisha kwamba unafundisha sarufi kwa

kutumia mbinu ambazo zinawezesha wanafunzi wako kujifunza sarufi ya Kiswahili bila

kupoteza hamu.

Kwanza kabisa kabla ya kufundisha sarufi, ni lazima uwe na lengo maalum

unalotarajia kutimiza. Ukifika darasani ni bora zaidi kuwasilisha dondoo la kisarufi

unalolenga kufundisha kupitia mkutadha wa mawasiliano kuliko kutoa maelezo ya moja

kwa moja juu ya dondoo hilo. Inafaa uonyeshe matumizi ya dondoo la sarufi

linaloshughulikiwa katika mkutadha mahsusi wa mawasiliano. Wanafunzi wanapaswa

kupewa fursa ya kung’amua kanuni zinazotawala matumizi ya dondoo linalohusika

kutokana na mkutadha maalum wa mawasiliano. Ni baada ya kushuhudia matumizi yake

ndipo unapoweza kutoa maelezo kuhusu kanuni za kisarufi. Kwa mfano, ikiwa unapanga

kufundisha wakati uliopita unaweza kutafuta kisa cho chote kinachofaa kinachosimulia

matukio ya wakati uliopita. Baada ya wao kusoma kisa hicho au wewe kuwasomea

unaweza kudondoa sentensi za wakati uliopita na kuzungumzia jambo hilo kwa kurejelea

mifano mahsusi. Ikiwa unataka unaweza,kabla ya kuzungumzia jambo hilo, kuuliza

wanafunzi maswali ya ufahamu juu ya kisa hicho. Wakati wanapojibu maswali hayo

watalazimika kutunga sentensi zilizomo katika wakati uliopita. Kisha, baada ya majibu

hayo unaweza kutoa maelezo kuhusu wakati uliopita.

Tuseme umepanga kufundisha jinsi ya kutendea katika kidato cha kwanza.

Unaweza kutayarisha lengo kama lifuatalo na kufundisha ukifuata hatua

zinazopendekezwa hapo chini.

Kidato : 1

Mada : Jinsi ya kutendea.

Lengo : Kufikia mwisho wa kipindi wanafunzi watatunga angalau sentensi nne

kuonyesha matumizi tofauti ya jinsi ya kutendea.

Utangulizi:

Ukionyesha kifaa fulani, wambie wanafunzi wataje kifaa hicho k.m. ufunguo,

wembe, kijiko, panda.

Waulize wanafunzi kifaa hicho kinatumiwa kufanya nini. Kisha andika

sentensi hiyo ubaoni na upige mstari chini ya kitenzi cha jinsi ya kutendea.

Kwa mfano: Mpishi hutumia kisu kukatia nyama.

Page 99: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

99

Mpatie mwanafunzi mmoja kifaa fulani halafu umwagize mwingine atunge

sentensi inayoeleza kitendo ambacho umefanya. Mwanafunzi anaweza

kutunga sentensi kama ifuatayo:

Umempatia wembe wa kukatia uzi.

Endelea kuuliza maswali tofauti ambayo yatalazimisha wanafunzi kutoa

majibu ambayo yanahusisha vitenzi katika jinsi ya kutendea.

k.m Ulizaliwa wapi?

Ulikulia wapi?

Ulisomea wapi masomo ya msingi?

Maelezo Rasmi.

Waeleze wanafunzi kwamba katika Kiswahili maana ya kitenzi inaweza

kubadilika kufuatana na matumizi ya viambisho tofauti kama katika mifano ya

vitenzi vilivyopigwa mstari chini yake katika sentensi zilizo ubaoni.

Mabadiliko ya namna hii huitwa jinsi /kauli katika Kiswahili. Waeleze pia

kwamba kuna jinsi / kauli tofauti. Vitenzi katika mifano iliyo kwenye ubao

vimo katika jinsi ya kutendea. Eleza pia kwamba jinsi ya kutendea inatumiwa

kuwasilisha maana tofauti kama katika mifano iliyotolewa.

Toa mifano zaidi ya vitenzi ili kubainisha sheria zinazotawala uundaji wa jinsi

ya kutendea kufuatana na utangamano wa irabu kama katika mifano ifuatayo:

Kitenzi Jinsi ya kutendea

pata

panga

pita

zima

funga

nunua

soma

zoma

tenda

jenga

patia

pangia

pitia

zimia

fungia

nunulia

somea

zomea

tendea

jengea

Page 100: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

100

Mazoezi ya Kuendeleza Matumizi ya Jinsi ya Kutendea.

Wape wanafunzi mazoezi yanayolenga kuendeleza ufahamu wa jinsi ya

kutendea. Wanaweza kwa mfano, kutoa mifano zaidi ya vitenzi na kuvitumia

katika sentensi vikiwa katika jinsi ya kutendea.

Washirikishe wanafunzi katika zoezi la kusoma au kusikiliza kifungu fulani

cha habari kilicho na vitenzi katika jinsi ya kutendea. Kisha waulize maswali

juu ya kifungu hicho ambayo majibu yake yatahusisha vitenzi vilivyo katika

jinsi ya kutendea.

Kwa ufupi unapofundisha sarufi usifundishe ukiwa na lengo la kufafanulia

wanafunzi kanuni za kisarufi na istilahi zake. Inafaa lengo lako kuu liwe kuwezesha

wanafunzi wako kutambua na kuzingatia kanuni hizo kutokana na mifano kamili ya

vielelezo vya sentensi. Unapofundisha ngeli, kwa mfano, haifai kuwaeleza tu jinsi

kiambisho fulani hubadilika katika wingi na kisha kuwapatia orodha ya majina na

kuwaagiza wataje majina hayo katika hali ya wingi. Njia bora zaidi ni kuonyesha

mabadiliko hayo kupitia kifungu fulani kinachohusisha mifano ya majina ya ngeli tofauti

unazotaka kuzungumzia. Wanafunzi wasome au wasikilize kwanza kifungu hicho ili waweze kushuhudia moja kwa moja jinsi majina ya ngeli kadhaa hubadilika na kuathiri

maneno mengine yanayoambatanishwa nayo katika sentensi. Ukizungumzia mabadiliko

hayo baadaye maelezo yako yatakuwa na maana zaidi. Lazima ukumbuke kwamba

inawezekana kwa mtu kujifunza na kuimudu lugha bila kuelezwa moja kwa moja kanuni

zinazotawala miundo ya lugha inayohusika. Mtoto mdogo, kwa mfano, anajifunza na

kuelewa miundo mbali mbali ya lugha ya jamii yake kwa kuiambatanisha na mikutadha

maalum ya mawasiliano ambamo inatumiwa. Kwa mfano, akiona baba yake akiondoka

nyumbani na kusikia mama akisema Baba anaenda kazini, au wakati ndugu na dada zake

wakienda shuleni huenda akisikia mama akisema Fulani anakwenda shuleni. Kadiri

muda unavyoendelea mtoto huyo ataanza kufasiri kiambishi –na- na kukiambatanisha na

kitendo kinachoendelea kufanyika. Kwa upande mwingine mtoto huyu akisikia mama

akisema ‘Baba ameenda kazini’, wakati baba yake akiwa ameshaondoka, ataanza

kutambua kwamba kiambishi –me- huashiria wakati uliopita hali timilifu.

Kutokana na mifano hii ni wazi kwamba unapofundisha sarufi si lazima

utangulize ufundishaji wako kwa maelezo ya kanuni za kisarufi. Unaweza kutaja kanuni

hizo baada ya ubainishaji wake katika mikutadha maalum ya vielelezo vya sentensi.

Page 101: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

101

ZOEZI 7.4

A. Eleza uhusiano uliopo kati ya sarufi na msamiati. Je, mafunzo

ya sarufi ya Kiswahili yana manufaa gani kwa mwanafunzi?

B. Ukitoa mifano ya kutilia maki jibu lako eleza jinsi

unavyoweza kufundisha mambo yafuatayo kwa wanafunzi

wako:

(i) matumizi ya –enye, -enyewe

(ii) matumizi ya –ji-, kwa

(iii) ukanusho katika wakati uliopita

Aina Za Mazoezi

Mazoezi unayopatia wanafunzi yanachangia pakubwa katika kuimarisha na

kuendeleza udhibiti wao wa sarufi. Unaweza kutayarisha mazoezi tofauti kulingana na

mahitaji ya wanafunzi pamoja na kiwango cha uwezo wako. Miongoni mwa aina za

mazoezi unayoweza kupatia wanafunzi ni pamoja na:

Mpishano wa maneno.

Ugeuzi wa umbo.

Ukamilishaji.

Mpishano Wa Maneno.

Mazoezi ya mpishano wa maneno humpa mwanafunzi fursa ya kutunga sentensi

mbali mbali za muundo fulani kwa kubadilisha maneno yenye ukoo mmoja. Kupitia

mazoezi ya namna hii mwanafunzi hujizoesha muundo fulani wa sentensi kwa kuurudia

mara kadhaa. Mazoezi ya mpishano wa maneno yanafaa sana hasa unapotaka wanafunzi

wajizoeshe kutumia viambisho vinavyofaa kulingana na ngeli ya jina. Baada ya kumpatia

mwanafunzi kielelezo fulani cha sentensi, kwa mfano, unamtaka aandike sentensi hiyo

upya akitumia maneno unayopendekeza badala ya neno fulani katika sentensi hiyo. Kila

anapotumia neno jipya itamlazimu kufanya mabadiliko yanayotakiwa kwa kuzingatia

ngeli ya jina.

Mfano:

Kitabu ambacho kilikuwa hapa sikioni tena.

Agizo: Andika sentensi hii upya ukitumia maneno yafuatayo badala ya kitabu:

tunda, vitabu, mfuko, matunda, wembe, nyuzi, mifuko.

Mfano wa sentensi mpya

Tunda ambalo lilikuwa hapa silioni.

Page 102: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

102

Vitabu ambavyo vilikuwa hapa sivioni.

Mfuko ambao ulikuwa hapa siuoni.

Zoezi la namna hii ni zuri kwa wanafunzi ambao wana shida ya kutumia

viambishi sahihi vya ngeli.

Njia nyingine ya kushirikisha wanafunzi katika zoezi la mpishano wa maneno ni

kutumia jedwali la mpishano wa maneno kama katika mfano ufuatao:

Wakirejelea jedwali hili, wanafunzi wanaweza kutunga sentensi mbali mbali.

Ukitaka kuwapa mazoezi zaidi ya kutunga sentensi wakitumia majina ya ngeli tofauti

unaweza kuwambia watumie majina ya ngeli tofauti zaidi ya yale yaliyopendekezwa.

Kwa mfano mwanafunzi akitumia shoka, matunda, mfuko n.k., anaweza kutunga sentensi

kama zifuatazo:

Shoka hili ni la Bakari.

Matunda yale yalikuwa ya watoto.

Mfuko huu si wa Atieno.

Ugeuzi wa Umbo:

Umbo asilia la sentensi linabadilika mwanafunzi anapoziandika upya kulingana

na maagizo ambayo unampatia. Kwa hivyo mwanafunzi anaweza kuandika sentensi za

aina mbali mbali kulingana na maagizo anayopewa.

Mfano:

(1) Andika upya sentensi zifuatazo ukigeuza majina katika hali ya wingi:

Kitabu hiki ni kizuri.

Mtoto yule alilia sana.

Ukuta huo ulijengwa vibaya.

Ufa huo unastahili kuzibwa.

Tunda hili haliliwi.

(2) Kanusha sentensi hizi:

Simama hapa.

Mtoto amelala.

Walifika jana.

Jina Kionyeshi Kitenzi Kiunganishi

Kimilishi

Jina

Kitabu

Kikombe

hiki

kile

hicho

ni

si

kilikuwa

kitakuwa

cha

Makhoha

Atieno

Bakari

nk

Page 103: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

103

Tutaonana kesho.

Watoto wanakula ugali.

Wapatieni watoto chakula.

Ukifika mapema tutasafiri pamoja.

(3) Ziandike upya sentensi zifuatazo ukianza na neno la mwisho.

Mbwa alifukuza mtoto.

Mtoto amepika chakula.

Mama amejengesha nyumba.

Umeona mtoto?

Ukamilishaji:

Zoezi la aina hii hutoa nafasi kwa wanafunzi ya kukamilisha sentensi kwa

kutumia neno linalofaa. Wakati mwingine huenda mwanafunzi akapewa arodha ya

maneno na kuambiwa achague neno linalofaa kutoka maneno aliyopewa.

Mfano.

Kamilisha sentensi hizi kwa kutumia maneno yanayofaa:

Fahali wawili……………..zizi moja.

Mama …………………chakula bado. (pika)

Watoto………………shuleni kesho. (enda)

Kama ningalimwona mwizi……………….

Nikifika nyumbani………………………

Kama tusingekuwa hapa………………..

Kama wangalikuja nasi…………………….

Mwenye pupa……………………kula utamu.

Usichukulie aina hizi za mazoezi kama ndizo tu unazoweza kutumia. Ni jukumu

lako kama mwalimu kujitahidi kuibuka na aina nyingine zinazoweza kukuwezesha

kusaidia wanafunzi wako kuimudu sarufi ya Kiswahili.

Page 104: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

104

ZOEZI 7.5

Ukirejelea kila moja kati ya sentensi zifuatazo:

Andika sentensi hiyo kwa usahihi.

Eleza mbinu utakazotumia kusaidia mwanafunzi ambaye

ametunga sentensi inayohusika ili aweze kutambua na

kuyarekebisha makosa yake.

Sentensi.

(a) Matunda na viazi zenye zilikuwa kwa mfuko yangu

zimeharibika zaidi.

(b) Nataka kisu ya kukatisha nyama kabla niende kwa

nyumba.

(c) Tukule kwanza; utaongea na simu baada ya kukula.

HITIMISHO.

Katika somo hili la saba tumezungumzia juu ya ufundishaji wa sarufi na

msamiati. Mambo haya ni kama pande mbili tofauti za sarafu moja. Kila upande una sifa

zake lakini pande zote mbili huwa zinaingiliana na kutegemeana. Haina maana

kufundisha msamiati bila kuonyesha utaratibu ambamo msamiati unaohusika unapaswa

kutumiwa. Kwa hivyo, msamiati na sarufi vinapashwa kufundishwa kwa pamoja katika

mkutadha fulani wa mawasiliano. Vile vile ufundishaji wake unapaswa kuambatanishwa

na ufundishaji wa mambo mengine. Ni wajibu wako kama mwalimu kuhakikisha

kwamba unatumia mbinu zinazoweza kuwashirikisha kikamilifu wanafunzi na

kuwawezesha kuumudu msamiati pamoja na sarufi kwa njia yenye maana na manufaa

kwao. Na unapofundisha maneno ni lazima uhakikishe kwamba wanafunzi

wanayamuudu maneno yanayohusika katika viwango vifuatavyo: matamshi, maendelezo

na maana.

Pia ni jukumu lako kuona kwamba mambo haya yanafundishwa kwa kipimo

kinachofaa.

Page 105: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

105

SOMO LA 8

FASIHI

8.0 Utangulizi

Waalimu wengi hufikiria kwamba kila mwanafunzi anafahamu dhana na dhima

ya fasihi katika jamii. Hivyo waalimu wengi hawazingatii kueleza kwa ufasaha dhana za

kimsingi kuhusu maana ya fasihi na nafasi yake miongoni mwa jamii. Pia kama

inavyoonekana kwamba tamthilia, riwaya na shairi vina maumbo tofauti, basi hufikiriwa

watu hufahamu jinsi unavyoweza kuzibainisha nyanja hizi tatu za fasihi andishi kwa

urahisi na hawazitangulizi sura bainishi. Si ajabu kwamba hata vyuoni, licha ya shule za

upili, swali la kuzibainisha huleta utata kwa wengi. Mwalimu haachilii hoja yoyote kwa

matumaini kwamba mwanafunzi anafahamu tayari ama kuwa ni rahisi kufahamika, hivyo

si lazima kufunzwa darasani. Unapoanza kufunza, kulingana na daraja unalofunza na

utaratibu wa mafunzo, ni vyema kuwapa wanafunzi utangulizi utakaowatayarisha na

kuwasaidia kuzielewa hoja nyeti za somo hilo kadri linavyoendelea. Katika sehemu hii

msimamo huu ndio uliofuatwa katika kufunza hata ingawa kila jambo haliwezi

kuzungumziwa kwa ajili ya wakati.

MADHUMUNI YA SOMO

Kufikia mwisho wa somo hili, inatarajiwa kwamba utaweza:

Kufafanua dhana ya fasihi kwa upana wake

Kubainisha kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi

Kueleza umihimu wa fasihi miongoni mwa jamii

8.1 Dhana ya fasihi

Ni muhimu kabla ya kuzungumzia juu ya nyanja mbalimbali za fasihi mwalimu

amweleze mwanafunzi mambo mawili mahususi:

1. Dhana ya fasihi.

2. Dhima ya fasihi

Katika kutekeleza haya, jambo la kwanza ni kueleza fasihi ni nini.

1. Dhana ya fasihi

Fasihi ni maandishi ya kisanaa yanayoweza kuwa ya kihalisia ama ya kifantasia,

yaani kidhahania. Maudhui ya fasihi huchukuliwa miongoni mwa jamii na huwahusu

jamii anamoishi mwandishi. Tofauti ya maandishi ya kifasihi na maandishi mengine ni

ile hali ya fasihi kutumia kitengo cha ubunifu, kwamba mwandishi anaelezea maudhui

yake kwa njia ya kipekee. Fasihi hata ikiwa juu ya mambo halisia, haiwezi kuwa historia

Page 106: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

106

ya jambo linaloelezwa. Hoja za kihistoria katika fasihi hunakshiwa kwa usanii hivyo japo

jambo ni la kweli, maelezo yake hayakubaliki kama historia. Msanii anaweza kutia katika

habari hizo za ukweli mambo ya kidhahania ili kuondoa kazi yake isifananishwe moja

kwa moja na hali zinazoonekana katika jamii hiyo.

Fasihi andishi hugawanyika katika nyanja tatu muhimu:

1. Riwaya

2. Tamthlia

3. Shairi

Tofauti ya nyanja hizi za fasihi ni katika umbo la uandishi wake.

8.2. Dhima ya fasihi

Wakati mwingi waalimu hawaoni haja ya kueleza dhima ya fasihi. Hili ni kosa na

upungufu wa ujuzi kwa upande wa mwalimu. Kujua fasihi ni nini pekee bila kutambua

nafasi na kazi yake miongoni mwa jamii hakutoshelezi. Kufahamu fasihi ni nini pekee

hakuifanyi fasihi kuwa mashuhuri na kufunzwa shuleni na vyuoni. Ujuzi huu hukamilika

unapoongezwa na ule wa umuhimu, na nafasi yake katika jamii.

Dhima ya moja kwa moja ni kuelemisha na pia kuwa kama kiliwazo katika

burudani ya jamii. Huelimisha kwa sababu msanii wa fasihi hujaribu kutatua matatizo ya

jamii, kuhusu maswala yanayowakumba. Mwandishi huwa tayari amechunguza

yanayoendelea miongoni mwa jamii yake, kuchambua na kudhihirisha masuala

yanayokumba jamii na kujaribu kuyatatua katika uandishi wake.

Kazi ya fasihi huhamasisha jamii hali kadhalika kuhusu fikra mpya ambazo huwa

chochezi kwenye mawazo ya jamii kuhusu hali zao za maisha katika mazingira yao.

Mwandishi huhamasisha kwa makusudi ya kuzingatia jinsi jamii inavyoweza

kujiendeleza, kubadilisha hali zao kuwa bora zaidi, kama watu binafsi ama jamii nzima.

Dhima nyingine yahusu kuliwaza jamii kwa ambavyo lugha ya fasihi huandikwa

kwa fani ya kupendeza, maudhui yake huazimiwa kuwafurahisha watu na wasomaji

wengi husoma fasihi ili wafurahike moyoni kwa sanaa hiyo. Mwanafunzi anatakikana

kutoa mifano kudhihirisha kuwa usomi wa fasihi hutumika kama kiburudisho kwa wengi.

Mfano watu wengi husoma vitabu vya hadithi jioni baada ya kazi za mchana koma. Nia

yake ni kujiburudisha kutokana na mawazo mazito ya shughuli za mchana kutwa. Pia

wengi hutazama maonyesho ya michezo ama filamu kwa kuburudika, haya yote yakiwa

katika kundi la fasihi na sanaa, isipokuwa kwa njia tofauti.

Katika kueleza maana ya fasihi watu wengi husahau kuifasiri fasihi kwa dhana

yake pana. Wengi wanapofikiria fasihi huzingatia tu kazi za sanaa zilizoandikwa.

Wengine pia hufikiria fasihi kuwa maandishi ya jamii fulani iliyoishi wakati fulani.

Wengine huona fasihi andishi kuwa zile kazi zilizopata umaarufu wa kisanaa. Kama

mwalimu ni muhimu ufahamu upotofu wa baadhi ya tafsili hizi. Aidha ukwepe kutoa

fasili finyu ya fasihi kwa wanafunzi wako.

Katika kupanua uwezo wa fikra wa mwanafunzi, utahitaji kuitazama fasihi kwa

hali ya kipragmatiki kulingana na maendeleo na mabadiliko ya kijamii. Kwa mfano,

tunaweza kutazama fafanuzi zifuatazo kuhusu fasihi.

Page 107: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

107

TAFAKARI

Bainisha kati ya dhima ya fasihi na dhana ya fasihi. Toa mifano

inayodhihirisha dhima na dhana kama ulivyoelezea .

8.3 Mitazamo tofauti ya maana ya fasihi

Fasihi kama sanaa yo yote nyingine

Maelezo yanayotokana na mtazamo huu hudai kuwa fasihi ni kama kazi ya sanaa

yoyote nyingine kama vile michoro, michongo, ufundi na ustadi wa tungo tofauti. Sanaa

hutumia nakshi ya aina fulani, kusawiri ujumbe fulani ambao msanii anatarajia kuelezea

jamii kupitia kwa chombo alichochagua. Chombo hiki chaweza kuwa matumizi ya lugha,

ama uhunzi, au kuchora tu picha.

Katika usanii msanii huchanganya ubunifu na mambo halisia anayoyaona

yakiendelea mazingarani anamoishi. Fasihi hivyo huwasilishwa kwa maneno yenye

usanii ndani yake. Maneno haya yanaweza kuandikwa ama kusimuliwa . Basi maandishi

ama masimulizi ni nyenzo tu za kuwasilisha mawazo yanayohitajika kuelezwa jamii na

msanii ama mtungaji. Wanafunzi wafahamu wazi kuwa mbinu ya usimulizi kama ile ya

uandishi ni vyombo tu vya kuwasilisha na kuendeleza fasihi kwa aina na madhumuni ya

uwasilishaji kwa wakati wake.

Tunapolinganisha na sanaa nyingine, mbinu za usimulizi ama uandishi ni kama

uchoraji ambapo msanii hupaka rangi karatasi na brashi. Basi mtu hutumia usimulizi kwa

maneno, ama uandishi kwa kalamu na karatasi kueleza hisia ama ujumbe uliopo. Vile

vile ni kama mfumi anavyochukua kitambaa, sindano (fumo) na uzi kufuma nakshi katika

kitambaa hicho.

Ipo dhana ya fasihi kuwa mtungo wa maneno katika kueleza jambo fulani.Vile

vile, kama mtungo tunaweza kufananisha na msanii wa shanga za kuvaliwa shingoni,

ama zinazotungwa kwa kunakshi mavazi ya Wamasai kwa mfano. Kazi hizi zote

zinaonyesha usanii wa aina yake, na kama tungo zote huwasilisha maana fulani kwa jamii

inayohusika.

Ni muhimu kwa mwanafunzi kutambua kwamba sanaa hutokana na ubunifu wa

msanii kulingana na mambo halisi maishani anayoyaona na pia udhahania anaofikiria

yeye mwenyewe, bora uwe unawasilisha ujumbe fulani. Kama sanaa nyingine kwa hivyo

fasihi ina sifa hii pia. La muhimu ni kufahamu kuwa iwe sanaa ama fasihi inatokana na

hali halisi katika mazingira ama yatokana na fikra za msanii mwenyewe, lazima, ubunifu

wa msanii binafsi ndio utakaoifanya sanaa ama fasihi hiyo kufanikiwa na kuonewa

fahari. Pia ubunifu huu ndio utakaotoa ujumbe kwa hali ya wazi ili ufahamike bila

tashwishi.

Ambapo sanaa nyingine hutumia vitu kama vyuma, karatasi, rangi nguo na

kadhalika, sanaa ya fasihi hutumia lugha katika utunzi wake. Matumizi haya ya lugha

katika utunzi wake ndiyo hufanya watu wengine kuwa na maoni kuwa fasihi ni sanaa ya

lugha. Hii itaelezwa katika sehemu ifuatayo.

Page 108: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

108

Fasihi kama sanaa ya lugha.

Mtazamo huu wa pili wazingatia fasihi kuwa chombo kinachodhihirisha ufanisi

wa lugha katika matumizi mbalimbali yanayotokea kwenye uandishi wa fasihi. Kama

tulivyosema fasihi hujumuisha umbuji na ubunifu wa msanii. Jinsi lugha inavyotumiwa

kwa madhumuni ya kupendekeza kazi hiyo kwa wasomi huweza kufananishwa na nakshi

juu ya sanaa ya mchongo kwa mfano ama urembo wa rangi zilizojitokeza katika mchoro

fulani.

Kwa mtazamo huu aidha ni vyema kumfahamisha mwanafunzi jinsi mtu binafsi

anavyotumia lugha kisanii huweza kumbainisha kutokana na msanii mwingine. Hii ni

kusema, baada ya msomaji kusoma vitabu vya fasihi vya mwandishi mmoja, anaweza

kujua kitabu kingine cha mwandishi huyo hata kama hajaangalia jina, kwa sababu ya ule

mtindo wa uandishi wa kitabu. Kwa mfano, jinsi Katama Mkangi anavyoandika ni tofauti

na Shaaban Robert, ijapokuwa wote wawili waliandika riwaya. Kando na maudhui kitu

nyeti kinachowatenganisha ni mtindo. Mtindo huu hudhihirika katika matumizi ya lugha

sahali, lugha ya mafumbo, matumizi ya masimulizi katika hadithi, nyimbo na kadhalika.

Kwa upande wa lugha kuna matumizi ya tanakali za lugha kwa mfano : sitiari, tashbihi,

majazi, kinaya, kupiga chuku,taashira, tashtiti, lakabu, taniaba, na tashhisi miongoni mwa

nyinginezo.

Aina nyingine za mitindo hutumia aina za misamiati tofauti ambayo mwandishi

hupendelea kuliko mingine. Uchaguzi huu wa msamiati hutegemea aina ya maudhui, na

madhumuni ya fasihi ile na pengine hadhira lengwa pia. Hapa inadhihirika kwamba si

jambo la bahati nasibu kwamba mwandishi ametumia lugha kwa namna fulani.

Mwandishi mpevu hudhamiria kutumia lugha jinsi anavyotumia anapoanza kuandika,

mara anapofikiria maudhui yake, hadhira yake na madhumuni ya kazi yake miongoni

mwa jamii.

Katika ufafanuzi uliotangulia hapo juu, tunapata fikra ya kuifafanua fasihi kuwa ni

mtindo wa mtu. Mwalimu aweza kueleza dhana hii kwa kutumia vitabu vinavyojulikana

na wanafunzi kutofautisha jinsi kwa mfano waandishi wawili wanavyotumia lugha.

Mfano wa rahisi kubainisha waweza kuchunguza urefu na ufupi wa sentensi. Waandishi

wengine hupenda kutumia sentensi ndefu ndefu ambapo wengine hutumia sentensi fupi

fupi. Bado wengine hutumia istilahi nzito na ngumu na wengine hutumia lugha sahali. Ni

kweli mwanadishi anaweza kugeuza mtindo wake, bali kazi zake nyingi hufuata kawaida

yake katika tabia yake ya matumizi ya lugha. Mlinganisho huu waweza kufanywa hata

kwenye uteuzi wa maudhui. Mfano Mkangi kazi zake za fasihi zimejikita katika maudhui

ya utetezi wa wanaonyanyaswa, watu wasiojiweza kiuchumi na kijamii.

Fasihi ni kioo cha jamii

Kumbuka kwamba tumetangulia kusema kwamba fasihi ama sanaa inaweza kuwa

ya jambo halisi hivyo ikaitwa fasihi ya kihalisia, ama kuwa ya kidhahania kwa ambavyo

imechimbuka kutokana na fikra za msanii. Mwanafunzi anapaswa kuelezwa tofauti hii

aifahamu tangu awali.

Tunnapozungumzia fasihi kuwa kioo cha jamii/lugha, tunasema kwamba fasihi

humwirika, ama huangaza maisha ya jamii fulani ambayo mwandishi anaishughulikia.

Mara nyingi jamii hii ni ya pale mahali mwandishi mwenyewe anapoishi. Kazi ya kiyoo

Page 109: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

109

ni kuonyesha sura ya mtu ama kitu, jinsi kilivyo moja kwa moja. Mtu ama kitu hicho

huwa kimesimama mbele ya kiyoo ili sura hiyo itokee. Kiyoo hakionyeshi kufanana bali

mtu ama kitu halisia.

Mwalimu atumie maelezo haya kuwafanya wanafunzi wafahamu maana ya fasihi

kama kiyoo cha jamii, kwamba mwandishi hujaribu kueleza shughuli zinazoendelea

maishani miongoni mwa jamii waziwazi ili jamii ile ijione kupitia kwa kazi za fasihi ile.

Jambo hili hutekelezwa kupitia kwa maudhui teule ya kitabu, wahusika jinsi

wanavyosawiriwa na mazingira mathalan, muktadha na mandhari.

TAFAKARI:

Zingatia jinsi unavyoweza kuchambua fasihi ukajua madhumuni ya

mwandishi na somo alilotaka kuwafunza hadhira yake. Je ni nini

unachopata kama ujumbe unapochanganua mchoro wa picha kwa mfano ya

Dedan Kimathi kizimbani na minyororo?

ZOEZI 8.1

1. Eleza kwa ufasaha kwa nini unadhani fasihi yalinganishwa na sanaa

nyingine kama michoro, michongo na kadhalika.

2. Ukitoa mfano wa kitabu cha fasihi ulichosoma, eleza dhihirisho la

fasihi kuwa sanaa ya lugha.

3. Zingatia kitabu cha Mazrui, KILIO CHA HAKI ujadili hoja ya kuwa

fasihi ni kiyoo cha jamii.

8.4 Tanzu za fasihi

Baada ya kuzungumzia yaliyotangulia, ni bora sasa wanafunzi kuelezwa kwamba

fasihi ni pana na inajidhihirisha kwa tanzu zake. Tanzu za fasihi ni mbili kwa jumla:

1) Fasihi Simulizi

2) Fasihi Andishi

Tanzu hizi mbili za fasihi hujitambulisha kwa mbinu zake za mawasilisho, jinsi

zinavyohifadhiwa na kupendekezwa kwa watu. Utanzu mmoja wa fasihi huwasilishwa

kwa njia ya masimulizi. Hii huitwa Fasihi Simulizi. Utanzu wa pili huwasilishwa kwa

matumizi ya maandishi, na huitwa Fasihi Andishi. Kati ya aina hizi mbili, Fasihi

Simulizi ilianzia awali zaidi ya Fasihi Andishi. Ambapo fasihi Andishi ilitokea wakati

ambapo hati na maandishi yalibuniwa, Fasihi Simulizi ilitokea mara tu mawasiliano baina

ya binadamu yalipotukia.

Kwa upande wa dhima ya fasihi, aina zote mbili zina nafasi yake miongoni mwa

jamii. Aidha nafasi hizo zinapolinganishwa, nyingine ni bainishi na nyingine ni

unganishi. Pengine kwanza tuichunguze kila aina pekee yake kwa undani ili tufahamu

sifa unganishi na bainishi tunazozizungumzia.

Page 110: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

110

Fasihi Simulizi

Fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia ya maongezi. Aidha huhifadhiwa kutoka

kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya masimulizi na kukumbukwa katika fikra za jamii

mwaka baada ya mwaka. Si ajabu kwamba hadithi moja inaweza kuwa tofauti

inapotambwa na watu mbalimbali kwa sababu ya kutegemea kiasi cha kila mtu

atakavyokumbuka masimulizi ya awali. Kila msimulizi wa tungo hupewa sifa za kuwa

msanii na ana uhuru wa kueleza tungo hizo kwa umbuji wake mwenyewe. Hivyo

anaweza kuongeza fani mpya na kuendeleza maudhui anavyopenda. Ndiposa, tungo

katika fasihi simulizi hazina mtu maalumu anayesemekana kuwa msanii wake. Wingi wa

tungo hizo huwa mali ya jamii zinamoshughulikiwa.

Sifa za fasihi simulizi

Yapasa mwalimu amuongoze mwanafunzi kuzibainisha sura mbalimbali za aina

hizi za fasihi kando na kufahamu mbinu za mawasilisho yake.

1. Masimulizi hufanyika kwa njia ya maongezi, hivyo, chombo maalum cha fasihi

simulizi ni lugha ya maongezi. Tena kama ambavyo maongezi huhusisha hadhira,

hali kadhalika fasihi simulizi huhusisha hadhira katika kuiwasilisha, wakati

hadhira inaposikiza yanayosimuliwa. Masimulizi yanapoendelea, hadhira

huruhusiwa kuchangia na kumpa motisha msimulizi kwa kuitikia, kuimba naye,

ama kuuliza maswali na kushangilia hapo kwa hapo. Msanii ama mtunzi katika

fasihi simulizi hupata fursa ya kuingiliana na hadhira yake ana kwa ana na hata

katika majibizano.

2. Ni muhimu kwa wanafunzi kujua kwamba mtunzi ama msimulizi wa fasihi hii

huwa miongoni mwa wasimulizi wake. Wakati anaposimulia hutumia ishara za

miondoko ya mwili na anaweza kujua wakati huo huo kwamba anayosimulia

yapendeza hadhira ama la. Aidha msanii anaweza kujua ikiwa ujumbe katika

masimulizi yake wafahamika ama la.

3. Sifa nyingine bainifu ni kwamba fasihi hii haihifadhiki kwa njia nyingine

isipokuwa akilini mwa wale wasikizi waliopo. Kwa ajili hii hupitishwa chini kwa

vizazi vya baadaye kupitia masimulizi vile vile. Hivyo kadri ya vizazi

vinapoadimika ndivyo fasihi nyingi simulizi za jamii zinavyoadimika katika fikira

na myoyo yao.

4. Fasihi simulizi hubadilikabadilika kulingana na mapisi ya wakati, msimulizi na

madhumuni ya masimulizi yale. Kwa mfano, ngano iliyosimuliwa miaka ya

hamsini, sasa hata kama inajulikana bado kwa kupitishwa vizazi kwa vizazi,

itakuwa na tofauti katika maelezo yake, kwa ajili ya mengine kusahaulika, ama

mengine kuongezwa ama jinsi ilivyopokelewa na kufahamika tofauti na watu wa

eneo jingine.

Page 111: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

111

5. Kwa ambavyo chombo kikuu cha Fasihi Simulizi ni mazungumzo, basi sifa

yake kubwa ni kwamba hubuniwa na kuwasilishwa wakati huo huo na yule

mtungaji kwa hadhira iliyipo na mara moja kuhifadhiwa katika akili za watu.

6. Baada ya miaka kadha kupita Fasihi Simulizi huwa miliki ya jamii. Watunzi

asilia huweza kusahaulika na nyimbo, ngano za mtunzi fulani zikawa urithi wa

jamii yake. Huu ni mfano mzuri wa sifa ya nne hapo juu.

7. Fasihi simulizi huwaunganisha watu wa vizazi vilivyopita na vya kisasa katika

kusikiliza mapisi ya wazee wao katika masimulizi yaliyojenga jamii hiyo, kwa

upande wa burudani, ufundishaji na maonyo.

8. Fasihi simulizi pia zimedhihirisha ushupavu wa matumizi ya lugha. Katika

umbuji wa ngano, vitendawili nyimbo na hata sarakasi, walioshiriki walihitaji

kuifahamu lugha kwa undani ili kuweza kuibua utungo wa sanaa miongoni

pengine mwa wasanii wengine. Hoja hii ni muhimu tunapofikiria nyimbo za

majigambo, mashairi ya ngonjera na kadhalika.

Aina za fasihi simulizi.

Aina za fasihi simulizi ni nyingi kuambatana na tajriba za wana-jamii. Hivyo, aina

zake zinaweza kuainishwa ifuatavyo:

Ngano

Hadithi

Mafumbo:

Vitendawili

Methali,

Semi

Ushairi:

Nyimbo

Majibizano

Ngonjera

Sarakasi

Tumeainisha aina hizo kwa makundi manne kwa jinsi ya utekelezaji na utenda kazi wake

na matazamio ya hadhira. Pengine ni vyema kusema kwamba aina za fasihi simulizi

hutegemea jamii mbalimbali na vitengo vya kijamii katika mazingira na utamaduni

fulani.

Page 112: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

112

TAFAKARI:

1. Unapotafakari aina za fasihi simulizi katika jamii yako, unaweza

kuainisha makundi mangapi? Andika aina hizo kwa makundi uliyoainisha.

2. Fikiria ngano/hadithi ama wimbo unaosifika zaidi miongoni mwa jamii

yako ( si wa redioni, wala kanda zozote) na uchunguze wasanii asilia hasa

walikuwa akina nani. Ikiwa wasanii hao hawajulikani wafikiri ni kwa

sababu gani? Eleza na utoe ithibati.

ZOEZI 8.2

1. Linganisha na ulinganue sifa za fasihi andishi na fasihi simulizi

2. Kwa nini wafikiria vitendawili, methali na semi vimeainishwa katika

kundi moja?

3. Wasaidie wanafunzi wakupatie sifa za sarakasi katika jamii zao.

Bainisha sifa hizo na sifa za tamthlia.

4. Chunguza na ueleze jinsi fasihi simulizi inavyoendelezwa katika jamii

yako.

Sifa za Wasanii wa Fasihi Andishi na Fasihi Simulizi

1. Sifa muhimu yahusu wasanii wenyewe. Msanii wa fasihi andishi huwa pekee na vifaa

vyake vya uandishi anapokuwa akitunga kazi yake. Bali msanii wa fasihi simulizi tangu

awali huhusisha jamii ambao huwa hadhira yake anaposimulia na kueleza ujumbe wake

katika tungo anayowasilisha.

2. Ambapo mwandishi wa Fasihi Andishi ana nafasi ya kusahihisha kazi yake, kabla ya

kuitoa kwa wasomaji, msanii wa Fasihi Simulizi hana wakati huo, hivyo lazima

atahadhari kutoa utungo unaopendeza anapoanza kutunga. Msanii wa Fasihi Andishi

hukumbukwa hata baada ya karne kadha kupita kwa sababu kazi zake za kisanii

huhifadhiwa na jina lake kuendelea kuishi milele. Kinyume na haya msanii wa Fasihi

Simulizi kama tulivyotangulia awali kusema jina lake husahaulikwa kadri wakati

unavyopita na kazi kumilikiwa na jamii, kwa sababu ya kutojua mtunzi asilia.

Kumbuka kuwa wewe mwalimu, una jukumu la kuwasaidia wanafunzi wafikirie jamii

zao na tajriba wanazopitia katika jamii hizo kuhusu fasihi simulizi. Wahimize wanafunzi

kutoa mifano ya fasihi zinazopatikana katika jamii zao, na wachambue tofauti

zinazodhihirika.

Page 113: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

113

ZOEZI 8.4

1. Chunguza jamii yako na jirani jinsi fasihi simulizi inayoendelezwa humo.

2. Linganisha aina za fasihi simuliza kama iliyoelezwa hapa na ile

inayopatikana katika jamii yako.

3. Chunguza jinsi fasihi simulizi inavyoendelezwa katika jamii yako.

4. Toa fafanuzi ya fasihi kama ilivyoelezwa hapa. Je, unakubaliana na dhana

hiyo?

8.4 Tanzu za Fasihi Andishi

Sehemu tuliyotoka tulishughulika na fasihi simulizi na tanzu zake mbalimbali. Sehemu

inayofuata tutashughulikia fasihi andishi.

MADHUMUNI YA SOMO

Kufikia mwishi wa sehemu hii, inatarajiwa kwamba utaweza:

Kubainisha kati ya tanzu tatu za fasihi andishi

Kufafanua jinsi kila utanzu unavyoendelezwa

Kubainisha aina mbalimbali za kila utanzu

Kuonyesha mahali pa tanzu hizi katika jamii.

RIWAYA

Kwa ufupi riwaya ni hadithi ndefu ambayo msanii ametumia maandishi kuisimulia. Ni

muhimu kumueleza mwanafunzi tofauti hii kati ya hadithi ndefu na dhana ya riwaya. Je,

hadithi yatakikana kuwa na urefu gani ili ikiandikwa iwe riwaya? Je, ni urefu na uandishi

vinavyounda na kufafanua riwaya? Ni sura gani zinazobainisha riwaya? Je, ni umbo

maalumu, matumizi ya fani na lugha? Fikra hizi zote zaonyesha jinsi ambavyo fafanuzi

ya riwaya ina utata unaohitaji kutatuliwa. Aidha yaonyesha matatizo yaliyopo ya

kubainisha aina za hadithi zinazowezekana kuwa riwaya.

Ni vyema kuwaeleza wanafunzi maoni mbalimbali kuhusu riwaya. Baadhi ya wataalamu

wanasema kuwa riwaya ni hadithi ndefu ambayo ina visa na vitushi na migogoro

inayoashiria shughuli zinazoendelea miongoni mwa jamii. Wengine husema kwa jumla

kuwa riwaya ni hadithi au kisa kirefu kilichoandikwa katika umbo la mtiririko wa

masimulizi. Ijapokuwa masimulizi haya yanahusiana na shughuli za jamii huu huwa ni

Page 114: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

114

msingi tu. Ujengaji wa matini hujumuisha ubunifu wa msanii, jinsi ambavyo anauona

ulimwengu katika mazingira yake. Ubunifu huu hujumuisha uhalisia wa mambo na hali

ya kidhahania katika umbuji wa msanii. Mtindo wa aina hii huifanya riwaya kufahamika

kama sanaa ya kubuni. Ubunifu kwa hivyo, umejikita katika hali halisia za maisha ya

kijamii na viumbe vingine katika mazingira anamoishi mtungaji wa riwaya hiyo.

Kutokana na yaliyoelezwa basi yamkinika kwamba riwaya ni hadithi ndefu iliyoandikwa

kwa mtiririko fulani kuambatana na ubunifu wa mwandishi mwenyewe.

Yamkinika riwaya ama hadithi andishi barani Afrika ilijitokeza mnamo karne ya 19

na 20. Twasema hivi kwa sababu hati za uandishi zilijitokeza wakati huo kwa majilio ya

kisomo cha kiarabu cha dini na kuruhani, na vile vile, kisomo cha dini ya kikristo. Fasihi

andishi nyingi nchini Kenya zilichipuka wakati huu, kutokana na waandishi wa kiafrika,

ambapo zamani riwaya za Kiswahili na vitabu vya tafsiri kutokana na vitabu

vilivyoandikwa kwa Kiingereza kama vile:

Boi, “wema hawajazaliwa,”

“Juliasi Kaizari,”

“Kisima chenye hazina” n.k.

Siku hizi vitabu vilivyoandikwa asilia kwa Kiswahili ni vingi madukani na

vinaendelea kuchapishwa. Baadhi yavyo vimetia fora katika kutambaa kwenye maudhui

mbalimbali yanayoweza kuwavuta wasomaji wa Kiafrika. Aidha kwenye nchi

zilizotaarabika zamani, riwaya zimekuwa zikiandikwa kwa muda mrefu zaidi, kwa

sababu utamaduni wa kisomo ulianza zama hizo

Awali tumeuliza swali kutaka kutafakari kile kigezo cha urefu wa riwaya, ikiwa

urefu huu waweza kupimwa kuhusu ukamilifu wa riwaya

Yasemekana urefu wa riwaya watambulika katika matumizi yake au kuwa na

tukio zaidi ya moja, kujumuisha visa vingi, ujenzi wa wahusika wa aina mbalimbali

wanaoendelezwa katika hali za maendeleo na upevu wao maishani, na katika mazingira

wanamoishi. Baadhi ya wataalamu hueleza urefu wa riwaya kutokuwa chini ya maneno

35000. Katika urefu wake lazima mwandishi awe anafululiza maudhui kwa kuoanisha

vipengele hivyo vyote, na kuonyesha mwanzo unaendelea kupevuka hadi hatima ya

riwaya hiyo. Mtiririko huu uwe wa kuaminika na unaoweza kumshawishi msomaji

usahihi na uhalisi wa maudhui hayo. Kama hadithi inavyohusisha hadhira yake wakati wa

masimulizi, riwaya yatakika kuwaathiri na kuteka bakunja wasomaji wake na kuwatia ari

ya kusoma tangu awali hadi mwisho wa kitabu.

La ziada, pamoja na urefu, kuna upana wa mazingira na miktadha tofauti

inayopatikana katika riwaya. Mfano riwaya haiwezi kuanzia,” Sebuleni” na ikaendelea na

kuishia hapo tu bila kwingineko. Riwaya hujumuisha wahusika wengi na kila mmoja

huwa na nafasi maalum katika mfululizo wa maudhui ya riwaya.

Katika uandishi wa riwaya kutokana na yale yaliotangulia kuzungumzwa

unahusu: vipengele kadha kama vijenzi vya riwaya maudhui, ploti (kiini cha hadithi),

wahusika, migogoro, mandhari (mazingira), muundo na mtindo wa lugha. Uwiano wa

hayo yote unadhihirika kutegemea kiwango cha umbuji wa mwandishi. Kabla ya

kuchambua nafasi ya vipengele hivi vilivyotajwa kama vijenzi vya riwaya pengine

tungeeleza kuwa riwaya zipo aina tofauti. Kwa mfano, kuna riwaya ya uhalisia,

kijazanda, upelelezi, wasifu, kidhahairia n.k.

Page 115: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

115

Jambo la kimsingi hapa mradi wanafunzi wafahamu msingi, muhimu na bainishi

ya riwaya kama ilivyozungumziwa hapo juu. Vigezo vya jumla vya riwaya hupatikana

katika aina hizi zote, ndiposa zikaitwa riwaya. Lakini, kila aina ina sifa, bainifu

zinazoleta ubinafsi wa kila aina, kulingana na jina lake.

AINA ZA RIWAYA

Zipo aina kadha za riwaya kama zilivyoainishwa na waandishi tofauti. Kwa mujibu

wa Wamitilla (2003), kuna aina nne dhahiri:

1. Riwaya sira

2. Riwaya kitawasifu

3. Riwaya kiambo

4. Riwaya ya kisaikolojia

Waandishi wengineo huzungumzia aina nyingine zinazoambatana na maudhui

yanayoendelezwa kwenye kitabu. Aina hizi ni kama :

Riwaya za upelelezi

Riwaya za Wasifu

Riwaya za uhalisia wa kijamii

Riwaya za Kifalsafa

Katika majina haya yote itabainika kwamba uzingativu wa ujumbe unaoshikilia

hadithi yote na mtindo wa hadithi huweza kumsaidia mwanafunzi kutambua aina ya

riwaya asomayo.

ZOEZI1.8.3

Kutokana na riwaya zilizoainishwa hapo juu jaribu kutafuta kitabu kimoja

kwa kila aina yazo kama ithibati yake.

Page 116: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

116

HADITHI FUPI

Tumesema kwamba riwaya ni hadithi ndefu. Hii yamaanisha kuwa zipo hadithi

fupi, tena zilizoandikwa. Hivyo si kila hadithi iliyoandikwa ni riwaya ingawa tulitangulia

kusema kuwa riwaya ni hadithi iliyoandikwa. Pengine maneno, “hadithi fupi au ndefu”

ndiyo muhimu katika ubainishaji wa riwaya na hadithi fupi. Zote zimeandikwa bali

hadithi moja ni fupi na nyingine ni ndefiu. Ufupi wa hadithi hapa wategemea zaidi

upande wa mtindo na vipengele vinavyohusushiwa wakati wa utungaji na vilevile umbuji

wa msanii.

Jambo la kukumbukwa ni kwamba aina zote mbili za kuhadithia, kama ni riwaya

ama ni hadithi fupi – zote hutumia vipengele kadha vinavyolingana. Hivi ni kama

maudhui, mtindo, muundo, mazingira, wahusika, muktadha, migongano na pia dhamira

ya mwandishi au mtunzi.Vipengele hivi vyote huzingatiwa wakati wa uchambuzi wa

riwaya yoyote ile. Ili mwandishi afanikiwe katika riwaya yake, mambo hayo yote yabidi

kuafikiana na kuwa na mtiririko mzuri katika mwumano wake. Hivi ni kusema kwamba

vipengele hivyo vyote vitiririshi, maudhui kwa hali ya kupevusha na kurutubisha ploti ya

kisa/hadithi inayotungwa na kuandikwa.

8.5 Uchambuzi wa fasihi

Sehemu hii itachunguza vipengele vya uchambuzi wa fasihi andishi. Kwa jumla

ni muhimu kujua kwamba uchambuzi wa kazi yoyote ya fasihi iwe fasihi andishi ama

simulizi huwa mfano wa mfanyiko. Ili uweze kuchambua nyanja moja lazima kwanza,

uweze kuibainisha na zile zingine. Pia lazima sura/fani bainishi kuziainisha. Tatu,

vipengele vya jumla vya uchambuzi wa fasihi vitumike kama inavyohitajika. Wanafunzi

hapa yabidi wafahamu kwamba mtu hawezi tu kujitosa kwenye uchambuzi wa kitabu

kiholela ama pasi kuwa na utaratibu wenye mwelekeo. Kila moja wapo ya nyanja hizi

zina misingi yake muhimu ya kuweza kuichambua. Mwalimu atambue kuwa wanafunzi

wengi wakiona vitabu hivyo vitatu huweza kusema hiki ni kitabu cha shairi, hiki ni cha

tamthilia na kile: cha riwaya – bila kutambua sifa bayana. Mwalimu achukue jambo hili

kama jukumu la kimsingi.

SIFA BAINISHI ZA RIWAYA

Kwanza tumesema riwaya ni hadithi ndefu inayojumuisha visa vingi

vilivyoendelezwa kwa hali ya muumano na maafikiano kufanikisha maudhui ya

riwaya yenyewe.

Huwa kuna ploti inayoendelezwa na visa vingi vinavyojitikeza kwenye

riwaya na huwa vinaendeleza ploti hii moja. Ploti ni kama shina linalochomoza

miche inayonawirisha mti.

Riwaya ina mgawanyiko wa sura. Nambari ya sura katika riwaya inategemea

urefu wa sura, visa vinavyoendeleza ploti na utofauti wa mandhari, wakati,

muktadha na wahusika, dhamira ya sura hiyo katika riwaya na migongano

Page 117: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

117

inayotukia miongoni mwa jamii husika. Sura hizi huifanya riwaya isichoshe

msomaji kwa urefu wake.

Maudhui wakati mwingi huwa ni ile kubwa/msingi na maudhui ndogondogo

kulingana na visa vinavyoandikwa. Ifahamike kuwa maudhui ndogo zote

zitakikana kuchangia maudhui kubwa/msingi ya riwaya. Haiwezekani mwandishi

mweledi kuiruhusu maudhui yoyote ndogo kujisimamia, kwani ingepnekana kuwa

hadithi ya pekee. ……

Maudhui ya riwaya hujikita katika jamii ya mwandishi kwa kawaida. Tajriba

ya mwandishi maishani huathiri sana maudhui ya riwaya.

Wahusika huwa wengi kulingana na urefu wa riwaya. Hawa hugawanyika

katika wahusika wakuu na wahusika wadogo kuambatana na nafasi wanayochukua

katika mtiririko wa maudhui.

Lazima kila riwaya iwe na kilele chake. Kilele ni upeo wa riwaya katika

uandishi na hata usomaji ambapo visa vilivyosimuliwa hupamba moto na

mgongano kutokea ama suluhu kupatikana. Hiki ni kilele kinachojengwa tangu

mwanzo wa uandishi wa riwaya hadi mwisho

Dhamira ya mwandishi hujitokeza kadri maudhui na mtiririko wake na aina

ya wahusika na jamii wanavyoendelezwa.

Sura hizi zote husaidia kuifanya riwaya ipendeze kwa msomaji na humpa mwelekeo

mwandishi katika kufanikisha riwaya yake kwa wanii unaofanya kazi hiyo ya fasihi

ijipendekeze kwa wasomaji.

ZOEZI 8.5

1. Sifa zilizoorodheshwa hapo juu ni za riwaya. Zingatia hizo na uorodheshe

sifa za hadithi kulingana na jinsi inavyosimuliwa katika jamii yako.

3. Je kuna tofauti zozote? Hebu zieleze.

Pengine tungeeleza kwa jumla uchambuzi wa fasihi andishi , yaani vipengele vya kijumla

vinavyohitajika kufahamika na mwanafunzi.

Maelezo ya kumwelekeza mwanafunzi kuhusu uchambuzi wa fasihi kwa jumla ni kama

uzingatifu kuhusu:

1. Ploti,

2. Maudhui,

3. Wahusika walivyosawiriwa,

4. Mgogoro

5. Taharuki

6. Mtindo wa mwandishi,

7. Matumizi ya lugha,

8. Mandhari.

Page 118: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

118

1. Maudhui

Hapa mwanafunzi aongozwe zaidi ya kuona tu ujumbe wa hadithi unaojitokeza. Ni

muhimu mwalimu kumsaidia mwanafunzi kuiona dhamira ya mwandishi katika kutunga

riwaya ile pia. Jambo analodhamiria mtunzi ndilo linaloendelezwa kwenye maudhui ya

riwaya. Kwa kutofautisha bayana, dhamira hasa yahusu fikra ya mwandishi

inayokaririwa katika visa na maswala yote yatakayoshughulikiwa katika riwaya hiyo,

kama kazi ya sanaa.

Ploti

Katika kuchambua maudhui mradi mwanafunzi azingatie ploti ya mwandishi. Ploti ni

wazo kuu ambalo ni kama uti wa hadithi inayoandikwa. Ni kutokana na ploti ambapo

maudhui huendelezwa na kuwekewa mipaka ya mapana na marefu yake; ujengaji wa

wahusika na vitushi vitakavyosimuliwa. Ploti hushikilia vipengele mbalimbali

vinavyohitimisha hadithi kama muktadha, mazingara na nafasi za wahusika katika

riwaya.

Wahusika

Mchambuzi wa Fasihi yapasa atambue viwango vya wahusika waliomo kwenye

riwaya ama tamthlia, na nafasi zao katika usimulizi wa hadithi yote. Huwako muhusika

mkuu anayeanza hadithi na kuendelea hadi tamati. Tena wako wahusika saidizi . Hawa

husaidia kumjenga muhusika mkuu katika tabia na hulka yake kwa jumla. Hawa ndio

wanaoendeleza maudhui kadri yanavyotiririka hadi kufikia kikomo.

Yapasa mwanafunzi aelezwe kuwa msanii wa kazi ya fasihi huchagua lugha

anayoitumia katika utunzi wake kwa makini zaidi. Wakati wa kuchambua itabidi

kuchunguza kama lugha inaeleweka vyema na kufaa maudhui yaliyopo au la. Je, ni lugha

ngumu ama rahisi kwa wasomaji wa kazi hiyo.

Mwalimu atalazimika kuelezea jinsi kila kipengele kinavyochangia ufanisi wa

matini inayochambuliwa.

La kutaja hapa ni kwamba uchambuzi wa shairi utakuwa tofauti kiasi kwa ajili ya

mtindo wake tofauti. Ingawaje, tofauti kubwa ni kule kutokuwa na wahusika

waliosawiriwa kama katika tamthlia na riwaya. Ni juhudi ya mwalimu aweze kumfanya

mwanafunzi wake apende mashairi pasi kuogopa. Wengi huyaona mashairi kuwa

magumu kueleweka, pengine ni kwa sababu, hata waalimu wenyewe hawachukui wakati

wa kuyasoma na kuyaeleza vilivyo.

VIFAA VYA KUFUNZA FASIHI

Mwalimu anaweza kutumia vifaa tofauti kulingana na umbuji wake na kiwango

cha wanafunzi wake. Ikiwa wakati upo, ni vyema kwa mfano kuiga onyesho moja la

tamthlia unayoifunza darasani. Hivyo watapata tajriba ya wahusika, kuupa uhai mchezo

na kuzua hisia zinazotakikana kudhihirishwa na uteuzi wa lugha iliyotumika.

Wakati mwingine kama ni tamthlia, riwaya ama shairi, hata kusoma kwa sauti

darasani husaidia kuwafanya wanafunzi wakumbuke hoja muhimu. Na, ikiwa yapo

makundi ya watu wanaoweza kukariri mashairi, ama kuiga michezo jukwani, ni vyema

kujaribu kuwapeleka wanafunzi wako wakajionee. Yote haya yategemea mwalimu

mwenyewe na mbinu atakazofuata za ufundishaji.

Page 119: KENYATTA UNIVERSITY INSTITUTE OF OPEN LEARNING€¦ · Kutokana na maelezo ya jumla ya sera ya lugha kwenye matini, soma vitabu maktabani na uandike kwa ufupi sera za lugha zilizokuwepo

119

MAREJELEO.

1. Rocha Chimerah & Njogu Kimani (1999): Ufundishaji wa Fasihi: Nadharia Na

Mbinu. Jomo Kenyatta Foundation. Nairobi.

2. Vincent Kawoya (1988), Mbinu za Kufundisha Kiswahili. Nairobi University

Press

3. Goeffrey K. King’ei & Paul M. Musau (2002), Utata wa Kiswahili Sanifu,

Didaxis, Nairobi, Kenya

4. Musau P.M. & Chacha L.M. (2001): Mbinu sa Kisasa za Kufundisha Kiswahili,

Kenya Literature Bureau.

5. Gerald Njagi Matti (2002), Introduction to The Study of Literature, Institute of

Open Learning, Kenyatta University.

6. K. W. Wamitilia (2002), Uhakiki wa Fasihi Msingi na Vipengele Vyake. Phoenix

Publishers Ltd

7. Wilkins, D. D. (1972) Linguistics in Language Teaching, Edward Arnold,

London..

8. Kiswahili Syllabus for Kenya Certificate of Secondary Education, K.I.E.

.