makubaliano mapya ya ulaya kuhusu maendeleo · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja...

54
SN 3109/17 YML/ik 1 DG C 1 USAMBAZAJI KWA UMMA UMEDHIBITIWA SW MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO ‘ULIMWENGU WETU, HESHIMA YETU, MUSTAKABALI WETU’ 1. Ajenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu 1 (Ajenda ya 2030), iliyokubaliwa na Umoja wa Mataifa mnamo Septemba 2015, ni suluhisho la jamii ya kimataifa la changamoto na mitindo ya ulimwengu mzima kuhusiana na maendeleo endelevu. Huku Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG) yakiwa ni kiini chake, Ajenda ya 2030 ni utaratibu wa kisiasa wenye kuleta mabadiliko na wenye nia ya kumaliza umaskini na kutimiza maendeleo endelevu ulimwenguni kote. Inasawazisha vipengele vya kiuchumi, kijamii, na kimazingira vya maendeleo endelevu, ikiwa ni pamoja na masuala makuu ya utawala na jamii zenye amani na ujumuishwaji, na kutambua uhusiano muhimu uliopo baina ya maazimio na malengo yake. Ni lazima itekelezwe kikamilifu na sio kwa kuchagua vipengele fulani tu. Ajenda ya 2030 inaazimia kutomuacha yeyote nyuma na inalenga kuwafikia kwanza walio nyuma sana kimaendeleo. 2. Mabadiliko kutoka kwa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDG) hadi Malengo ya Maendeleo Endelevu yanaonyesha badiliko la mtazamo wa maendeleo ya ulimwengu mzima. Mtazamo huu, ambao unazingatia maendeleo endelevu na haki za binadamu, unaambatana kikamilifu na maadili na kanuni za Umoja wa Ulaya. Ajenda ya 2030 na Malengo yake 17 ya Maendeleo Endelevu yanawahusu wote na yanatumika kwa nchi zote katika viwango vyote vya maendeleo, kulingana na umiliki wa kitaifa na majukumu ya pamoja. Ushirikiano wa wadau mbalimbali ni muhimu katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu. 3. Ajenda ya Utendaji ya Addis Ababa 2 (AAAA), kama sehemu muhimu ya Ajenda ya 2030, inatoa mtazamo mpya wa utekelezaji kupitia matumizi yanayofaa ya mbinu za kifedha na zisizo za kifedha, kwa kuziweka hatua za ndani ya nchi na sera bora katika mstari wa mbele. Aidha, Ajenda ya 2030 inasaidiwa na Utaratibu wa Sendai kuhusu Upunguzaji wa Hatari za Janga 3 , na Mkataba wa Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa 4 , ambao unatoa utaratibu wa kisheria na kuleta mwelekeo mpya katika juhudi za ulimwengu mzima za kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa. Utekelezaji wa ahadi hizi lazima uzingatie utaratibu wa 1 A/RES/70/1 2 A/RES/69/313 3 A/RES/69/283 4 FCCC/CP/2015/L.9/REV.1

Upload: buicong

Post on 02-Mar-2019

256 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 1

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO

‘ULIMWENGU WETU, HESHIMA YETU, MUSTAKABALI WETU’

1. Ajenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu1 (Ajenda ya 2030), iliyokubaliwa na Umoja wa

Mataifa mnamo Septemba 2015, ni suluhisho la jamii ya kimataifa la changamoto na mitindo

ya ulimwengu mzima kuhusiana na maendeleo endelevu. Huku Malengo ya Maendeleo

Endelevu (SDG) yakiwa ni kiini chake, Ajenda ya 2030 ni utaratibu wa kisiasa wenye kuleta

mabadiliko na wenye nia ya kumaliza umaskini na kutimiza maendeleo endelevu

ulimwenguni kote. Inasawazisha vipengele vya kiuchumi, kijamii, na kimazingira vya

maendeleo endelevu, ikiwa ni pamoja na masuala makuu ya utawala na jamii zenye amani na

ujumuishwaji, na kutambua uhusiano muhimu uliopo baina ya maazimio na malengo yake. Ni

lazima itekelezwe kikamilifu na sio kwa kuchagua vipengele fulani tu. Ajenda ya 2030

inaazimia kutomuacha yeyote nyuma na inalenga kuwafikia kwanza walio nyuma sana

kimaendeleo.

2. Mabadiliko kutoka kwa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDG) hadi Malengo ya

Maendeleo Endelevu yanaonyesha badiliko la mtazamo wa maendeleo ya ulimwengu mzima.

Mtazamo huu, ambao unazingatia maendeleo endelevu na haki za binadamu, unaambatana

kikamilifu na maadili na kanuni za Umoja wa Ulaya. Ajenda ya 2030 na Malengo yake 17 ya

Maendeleo Endelevu yanawahusu wote na yanatumika kwa nchi zote katika viwango vyote

vya maendeleo, kulingana na umiliki wa kitaifa na majukumu ya pamoja. Ushirikiano wa

wadau mbalimbali ni muhimu katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu.

3. Ajenda ya Utendaji ya Addis Ababa2 (AAAA), kama sehemu muhimu ya Ajenda ya 2030,

inatoa mtazamo mpya wa utekelezaji kupitia matumizi yanayofaa ya mbinu za kifedha na

zisizo za kifedha, kwa kuziweka hatua za ndani ya nchi na sera bora katika mstari wa mbele.

Aidha, Ajenda ya 2030 inasaidiwa na Utaratibu wa Sendai kuhusu Upunguzaji wa Hatari za

Janga3, na Mkataba wa Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa

4, ambao unatoa utaratibu

wa kisheria na kuleta mwelekeo mpya katika juhudi za ulimwengu mzima za kupambana na

mabadiliko ya hali ya hewa. Utekelezaji wa ahadi hizi lazima uzingatie utaratibu wa

1 A/RES/70/1

2 A/RES/69/313

3 A/RES/69/283

4 FCCC/CP/2015/L.9/REV.1

Page 2: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 2

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

ulimwengu mzima unaotilia maanani sheria, huku ushirikiano baina nchi ya mbalimbali

ukiwa ndio kanuni yake kuu na msingi wake ukiwa ni Umoja wa Mataifa.

4. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wamejituma ili kuhakikisha kuwa watu wote

wanaishi maisha yenye heshima yanayopatanisha maendeleo na ufanisi wa kiuchumi, jamii

zenye amani, ujumuishi wa kijamii na uwajibikaji kwa mazingira. Kwa kufanya hivyo, juhudi

zitaelekezwa katika kumaliza umaskini, kupunguza udhaifu na kushughulikia ukosefu wa

usawa ili kuhakikisha hakuna mtu yeyote anayeachwa nyuma. Kwa kuchangia katika

kutimiza Ajenda ya 2030, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watakuza pia Ulaya

thabiti, endelevu, jumuishi, salama, na yenye ustawi zaidi.

5. Makubaliano haya ya Ulaya kuhusu Maendeleo yanatoa utekelezaji wa Ajenda ya 2030 kwa

ushirikiano na nchi zote zinazoendelea, huku yakizingatia utaratibu uliotolewa na Mkataba wa

Lisbon. Aidha, Mkakati wa Ulimwengu wote wa Sera ya Umoja wa Ulaya ya Masuala ya

Kigeni na ya Usalama (Mkakati wa Ulimwengu wote) unatoa dira ya jumla ya ushirikiano

unaojumuisha watu wote, wenye kuaminika, na wenye mwitikio duniani.

6. Madhumuni ya Makubaliano haya ni kutoa utaratibu wa mtazamo wa pamoja wa sera ya

maendeleo ambao utatumika na taasisi za Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake huku

wakiheshimu majukumu na uwezo tofauti wa kila mmoja wao. Yataelekeza hatua ya taasisi za

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama katika ushirikiano wao na mataifa yanayoendelea.

Hatua za Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake zitakuwa zenye kuhimizwa na wote na

zilizoratibiwa ili kuhakikisha wanakamilishana na zinaleta matokeo mazuri.

Page 3: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 3

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

1. SULUHU LA UMOJA WA MATAIFA KWA AJENDA YA 2030

1.1. Utendaji thabiti na unaofaa zaidi wa Umoja wa Ulaya katika ulimwengu

unaobadilika

7. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake lazima watoe suluhu kwa changamoto na fursa

zinazokumba ulimwengu mzima kwa kuambatana na Ajenda ya 2030. Watatekeleza Ajenda

ya 2030 katika sera zote za ndani na za nje kwa njia ya utendeti na kimkakati, wakijumuisha

vipengele tatuvya maen deleo endelevu kwa namna yenye usawa na ushikamano, na

wakishughulikia uhusiano baina ya Malengo ya Maendeleo Endelevu na vile vile matokeo

mapana ya vitendo vyao vya ndani ya nchi katika kiwango cha kimataifa na cha ulimwengu

wote. Utekelezaji (wa Ajenda ya 2030) utaratibiwa kwa karibu na utekelezaji wa Mkataba wa

Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa na mikataba mingine ya kimataifa, ikiwa ni pamoja

na Ajenda ya Jiji Lipya5.

8. Ndani ya utaratibu huu jumuishi, mtazamo wenye ushikamano na uratibu wa vitendo vya nje

ya nchi vya Umoja wa Ulaya utakuwa muhimu katika utekelezaji wenye ufanisi wa agenda ya

2030 ulimwenguni kote. Ukiwa na muundo wake wa kitaasisi na nyenzo za kisiasa

zinazopeanwa chini ya Mkataba wa Lisbon, Umoja wa Ulaya umejitayarisha vilivyo ili

kupambana na changamoto na fursa za ulimwengu wote pahali zinapotokea.

9. Mkakati wa Ulimwengu wote wa Umoja wa Ulaya unatoa dira ya ushirikiano wa Umoja wa

Ulaya duniani, kupitia sera kadhaa. Unaangazia jukumu muhimu ya Ajenda ya 2030, ambayo

ina uwezo wa kuchochea mabadiliko yanayohitajika ili kuunga mkono kanuni za Umoja wa

Ulaya na malengo ya vitendo vya nje ya nchi vya Umoja wa Ulaya. Malengo ya Maendeleo

Endelevu yatakuwa ni kipengele jumuishi cha kazi yote ya kutekeleza Mkakati wa

Ulimwengu wote wa Umoja wa Ulaya. Makubaliano haya yatachangia katika maafanikio ya

vipaumbele vya vitendo vya nje ya nchi vya Umoja wa Ulaya, ikiwa ni pamoja na kupitia

kuunga mkono uthabiti katika viwango vyote. Kwa kufanya hivyo, Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake watakuza mtazamo wa uthabiti wenye vipengele tofauti na wenye nguvu,

ili kukabiliana na udhaifu unaoweza kusababisha hatari mbali mbali zinazohusiana.

5 A/RES/71/256

Page 4: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 4

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

1.2. Suluhu ya maendeleo

1 0 . Makubaliano haya ndiyo msingi wa sera ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa, ambayo ni

sehemu ya jumla ya suluhu ya Umoja wa Ulaya kwa ajenda ya 2030. Lengo kuu la sera ya

maendeleo ya Umoja wa Ulaya, kama lilivyoainishwa katika Kifungu cha 208 cha Mkataba

wa Utendakazi wa Umoja wa Ulaya, ni kupunguza, na mwishowe, kumaliza umaskini. Umoja

wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watatumia kanuni ya ushikamano wa sera kwa ajili ya

maendeleo (PCD), na watazingatia malengo ya ushirikiano wa maendeleo katika sera zake

zote za ndani na nje ya nchi watakazozitekeleza na ambazo zinaweza kuathiri nchi

zinazoendelea. Ushikamano wa sera kwa ajili ya maendeleo (PCD) ni sehemu kuu ya

mchango wa Umoja wa Ulaya katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu.

1 1 . Sera ya maendeleo ya Umoja wa Ulaya pia inafuatilia malengo ya vitendo vya nje ya Umoja

wa Ulaya, hasa yale yaliyoainishwa katika Kifungu cha 21(2)(d) cha Mkataba kuhusu Umoja

wa Ulaya (TEU) wa kukuza maendeleo endelevu ya kiuchumi, kijamii na kimazingira ya nchi

zinazoendelea, lengo kuu likiwa ni kumaliza umaskini. Kuambatana na malengo yaliyoko

kwenye Kifungu cha 21(2) cha Mkataba kuhusu Umoja wa Ulaya, sera ya maendeleo pia

huchangia katika, miongoni mwa mengine, kuunga mkono demokrasia, utawala wa sheria na

haki za binadamu, kudumisha amani na kuzuia migogoro, kuboresha hali ya mazingira na

usimamizi endelevu wa rasilimali asilia za ulimwengu wote, kusaidia watu, nchi na maeneo

kukabiliana na majanga asilia na yale yanayosababishwa na vitendo vya binadamu, na

kuendeleza mfumo wa kimataifa unaotegemea ushirikiano thabiti zaidi baina ya nchi

mbalimbali na utawala mzuri wa ulimwengu wote. Kwa hivyo, Mkataba huu utachangia pia

katika hitaji la kuhakikisha uthabiti baina ya nyanja tofauti za vitendo vya nje ya Umoja wa

Ulaya, na baina ya nyanja hizi na sera zake zingine.

1 2 . Jambo kuu katika utimizaji wa malengo haya ya pamoja ni Umoja wa Ulaya kufanya kazi

kwa pamoja. Kwa hivyo, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanajitolea kufanya

kazi vyema zaidi kwa moja. Ushikamano mkubwa zaidi unahitajika baina ya Nchi

Wanachama na taasisi za Umoja wa Ulaya. Ushirikiano wenye ushikamano na uthabiti

utapelekea kuwepo na uaminifu, uhalali, uwajibikaji, thamani iliyoongezwa, ushawishi na

athari zuri zaidi katika ulimwengu. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake lazima

waungane katika utofauti wao, kwa kutumia mitazamo na uzoefu mbalimbali, wakitilia

maanani faida za ulinganifu wa kila mmoja.

Page 5: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 5

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

1.3. Kanuni na maadili yanayoongoza hatua ya maendeleo

13. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake hutenda kazi kulingana na kanuni za vitendo vya

nje ya Umoja wa Ulaya zilizoainishwa katika Kifungu cha 21(1) cha Mkataba kuhusu Umoja

wa Ulaya: demokrasia, utawala wa sheria, hali ya haki za binadamu kuwa za watu wote na

kutogawanyika kwa haki hizo na aina tofauti za uhuru ambazo ni msingi, udumishaji wa

heshima ya binadamu, kanuni za usawa na umoja, na udumishaji wa kanuni za Mkataba wa

Umoja wa Mataifa na sheria ya kimataifa. Maadili haya ya watu wote na utawala mzuri ni

kiini cha Ajenda ya 2030.

14. Majadiliano ya kisiasa ni njia muhimu ya kuendeleza kanuni za maendeleo na pia yana

kipengele cha uzuiaji kinacholenga kuhakikisha kuwa maadili ya Umoja wa Ulaya

yanadumishwa. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watajumuisha udumishaji wa

haki za binadamu, demokrasia, utawala wa sheria na usawa wa kijinsia katika majadiliano ya

kisiasa. Mazungumzo haya yatafanyika ndani na nje ya serikali washirika na yatakuwa

jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo

yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa kutambuliwa.

15. Usawa wa kijinsia ni msingi wa maadili ya Umoja wa Ulaya na umejumuishwa katika

utaratibu wake wa kisiasa na kisheria. Una umuhimu katika kutimiza Malengo ya Maendeleo

Endelevu na yanahusika katika Ajenda yote ya 2030. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama

wake wataendeleza haki za wanawake na wasichana, usawa wa kijinsia, uwezeshaji wa

wanawake na wasichana na ulinzi wao kama jambo la kupewa kipaumbele katika nyanja zote

za utendaji.

16. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watatekeleza mtazamo wa ushirikiano wa

maendeleo unaozingatia haki, na wenye kujumuisha haki zote za binadamu. Wataendeleza

ujumuishwaji na ushirikishwaji, kutobagua, usawa na usawa, uwazi na uwajibikaji. Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendelea kuwa na jukumu kubwa katika kuhakikisha

kuwa hakuna yeyote anayeachwa nyuma, mahali popote wanapoishi watu, na bila kuzingatia

kabila, jinsia, umri, ulemavu, dini au imani, mvuto wa kijinsia na utambulisho wa kijinsia,

hali ya uhamiaji na mambo mengine. Mtazamo huu unajumuisha kushughulikia aina

mbalimbali za ubaguzi unaoukumbana na watu walio katika hali ya udhaifu na vikundi

vilivyotengwa.

Page 6: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 6

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

17. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanathamini kushiriki kwa mashirika ya asasi za

jamii (CSO) katika maendeleo na wanahimiza sehemu zote za jamii kushiriki kiamilifu.

Wanatambua majukumu mbalimbali ya mashirika ya asasi za jamii kama waendelezaji wa

demokrasia, walinzi wa wenye haki na utawala wa sheria, haki ya kijamii na haki za

binadamu. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza nafasi ya asasi za jamii

na kuboresha uungaji mkono wao wa kujenga uwezo wa mashirika ya asasi za kijamii, ili

kuimarisha mchango wao katika mchakato wa maendeleo na kuendeleza mazungumzo ya

kisiasa, kijamii na kiuchumi.

18. Ufanisi wa maendeleo ni muhimu katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu na ni lazima

yajumuishwe katika miundo yote ya ushirikiano wa maendeleo. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake watatumia kanuni za ufanisi wa maendeleo zilizokubaliwa katika

Muungano wa Ulimwengu mzima wa Ushirikiano Fanifu wa Mendeleo (GPEDC) wakati wa

Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Busan kuhusu Usanifu wa Msaada mnamo mwaka wa 2011 na

uliosasishwa wakati wa Mkutano wa Ngazi ya Juu uliofanyika Nairobi mnamo mwaka wa

2016: ambazo ni, umiliki wa vipaumbele vya maendeleo kwa mataifa yanayoendelea,

uangaziaji wa matokeo, miungano jumuishi ya maendeleo, uwazi na uwajibikaji wa pande

zote husika.

2. UTARATIBU WA UTENDAJI

19. Utekelezaji wa Ajenda ya 2030 unahitaji mikakati mipana ya kitaifa ya maendeleo endelevu

inayozingatia Malengo ya Maendeleo Endelevu na uhusiano wao. Wakati wa kupanga na

kutekeleza ushirikiano wa kimaendeleo, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watazingatia hasa uhusiano wa aina hiyo na vitendo jumuishi ambavyo vinaweza kuleta

manufaa ya pamoja na kufikia malengo mengi kwa njia yenye ushikamano. Katika muktadha

huu, hatua zinazochukuliwa na Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake zitaonyesha

dhamira kuu za Ajenda ya 2030: Watu, Sayari, Maendeleo, Amani na Ushirikiano.

Page 7: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 7

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

20. Huku wakitambua kwamba lazima Ajenda ya 2030 itekelezwe kwa ukamilifu, na sio kwa

kuchagua vipengele fulani, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watashughulikia

vipengele tofauti jumuishi ili kufikia maendeleo endelevu na kuongeza kasi ya mabadiliko,

kama vile: vijana; usawa wa kijinsia; uhamiaji na uhamaji; nishati endelevu na mabadiliko ya

hali ya hewa; uwekezaji na biashara; utawala mzuri, demokrasia, utawala wa sheria na haki za

binadamu; ushirikiano bunifu na nchi zinazoendelea zilizosonga mbele zaidi; na kukusanya na

kutumia rasilimali za ndani ya nchi.

2.1. Watu – Maendeleo na heshima ya kibinadamu

21. Ukuaji na mabadiliko ya kidemografia duniani, pamoja na mabadiliko ya kiuchumi, kijamii

na kimazingira, unatoa fursa kwa, na wakati huo huo, kuibua changamoto kwa maendeleo

endelevu. Idadi ya watu ulimwenguni inatarajiwa kuongezeka kwa kiasi cha bilioni 2.4

ifikiapo mwaka wa 2050, ambapo watu bilioni 1.3 watakuwa wanaishi Afrika. Kushughulikia

mahitaji ya kielimu ya watoto na vijana ni muhimu sana katika kuendeleza uraia uliowajibika,

kuendeleza jamii endelevu na zenye maendeleo na kutia nguvu ajira ya vijana.

22. Kumaliza umaskini, kupambana na ubaguzi na ukosefu wa usawa na kutomuacha yeyote

nyuma vyote viko katika kiini cha sera ya ushirikiano wa kimaendeleo ya Umoja wa Ulaya.

Umaskini una sifa mbalimbali na unahusiana na vipengele vya kiuchumi, kijamii,

kimazingira, kitamaduni na kisiasa. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watajituma

kumaliza njaa na aina zote za utapiamlo na vile vile kuendeleza ufikivu wa huduma za afya

kwa watu wote, ufikivu wa elimu na mafunzo bora kwa wote, ulinzi unaotosha na endelevu

wa jamii na ajira zuri kwa wote katika mazingira safi. Maendeleo katika nyanja hizi yatatoa

msingi thabiti zaidi wa maendeleo endelevu. Umoja wa Ulaya unasisitiza tena ahadi yake ya

kugawa asilimia 20 ya Usaidizi wake Rasmi wa Maendeleo (ODA) ili kugharamia

ujumuishwaji wa kijamii na maendeleo ya binadamu.

23. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono nchi washirika katika kutimiza

majukumu yao ya kuimarisha sera za kitaifa na utawala ili kuziwezesha kutoa huduma

muhimu na kutimiza haki za kibinadamu kwa njia endelevu.

Page 8: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 8

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

24. Ukosefu wa chakula chenye virutubishi vinavyotosha na utapiamlo ni vikwazo vikuu vya

maendeleo na mzingo wa maisha, kwa sababu unasababisha upungufu wa kuelewa, unashusha

uwezo wa watoto shuleni na kusababisha afya mbaya na upungufu wa uzalishaji wa

kiuchumi. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watajizatiti ili kuhakikisha watu wote

wanaweza kupata chakula salama, kinachotosha, na chenye virutubishi vinavyofaa. Watu

walio katika hali zenye hatari zaidi watazingatiwa kwa karibu sana, wakiwemo watoto wa

chini ya miaka tano, wasichana wa makamo na wanawake hasa walio na mimba na

wanaonyonyesha. Watafanya juhudi zilizoratibiwa, kwa haraka, na zinazojumuisha sekta

mbalimbali ili kumaliza njaa, kuongeza uwezo wa uzalishaji wa chakula ndani ya nchi na

kwenye eneo, kuhakikisha kuna chakula cha kutosha na chenye virutubishi na kuboresha

uthabiti wa walio hatarini zaidi, hasa katika nchi zenye majanga yaliyoendelea kwa muda

mrefu au yanayotokea mara kwa mara. Wataendelea kuwekeza katika maendeleo ya watoto

wachanga kwa kushughulikia aina zote za utapiamlo, ikiwa ni pamoja na kutokua kwa urefu

na uzito kwa watoto kupitia usaidizi wa huduma za kimsingi katika afya, virutubishi, usafi wa

maji na wa mwili, na ulinzi wa kijamii.

25. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watasaidia jamii zilizo maskini zaidi kuboresha

ufikiaji wa ardhi, chakula, maji, na nishati safi, ya bei nafuu na endelevu, huku wakiepuka

madhara yoyote mabaya kwa mazingira. Wataendeleza miradi ya sera na kuunga mkono nchi

washirika katika kupanga na kutekeleza mtazamo jumuishi ili kushughulikia kikamilifu

uhusiano unaofaa zaidi kati ya ardhi, chakula, maji na kawi.

26. Ongezeko kubwa la mahitaji ya maji na uhaba wa maji katika miongo inayofuata, litapelekea

changamoto kuu hasa katika ujirekebishaji kufuatia mabadiliko ya hali ya hewa. Ufikiaji wa

maji safi ya kunywa kwa watu wote, usafi wa mazingira na wa mwili vinahitajika ili kuwepo

na afya na uzima, ukuaji na uzalishaji. Rasilimali za maji zinaweza kuathiriwa hasa na

uharibifu wa mazingira, ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa, yanayotishia kilimo

na uwepo wa chakula cha kutosha. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga

mkono usimamizi wa maji endelevu na jumuishi na pia matumizi bora ya maji na utumiaji wa

majichafu kwa mara ya pili baada ya kuisafisha ikiwa ni pamoja na kupitia mtazamo wa

kimkakati zaidi wa maendeleo na ujumuishi wa kanda.

Page 9: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 9

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

27. Afya ni muhimu kwa maisha ya watu na ni kipengele kikuu cha ukuaji na maendeleo

endelevu na wenye usawa, ikiwa ni pamoja na umalizaji wa umaskini. Umoja wa Ulaya na

Nchi Wanachama wake wanasisitiza tena ahadi yao ya kulinda na kuendeleza haki ya kila

mmoja ya kufurahia afya ya mwili na ya akili ya hali ya juu zaidi iwezekenavyo ili

kuendeleza heshima ya binadamu, uzima na maendeleo. Wataendelea kuunga mkono nchi

washirika katika juhudi zao za kujenga mifumo ya afya ambayo ni imara, bora, na thabiti,

kwa kutoa ufikiaji sawa wa huduma za afya na kuhakikisha wote wanapata huduma za afya.

Kwa madhumuni haya, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watasaidia nchi

zinazoendelea katika kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa sekta ya afya, kuwaajiri,

kuwasambaza nyanjani na kuwapa mafunzo zaidi katika taaluma zao. Wataendeleza

uwekezaji katika na uwezeshaji wa wafanyakazi wa kijamii walio katika mstari wa mbele

ambao huwa na jukumu muhimu sana la kuhakikisha sehemu zilizo mbali sana mashambani,

zisizo na huduma za kutosha, zenye umaskini na zinazokubwa na migogoro zinapata huduma

za afya. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendelea kuwekeza katika kuzuia na

kupambana na magonjwa ya kuambukiza, kama vile VVU/Ukimwi, kifua kikuu, malaria na

homa ya manjano na watasaidia kuhakikisha kuwa watu wote wanaweza kupata dawa na

chanjo muhimu kwa bei nafuu. Wataendeleza utafiti na uwekezaji katika, na uundaji wa

teknolojia mpya za afya. Watachukua hatua ili kupambana na hatari za afya za ulimwengu

mzima, kama vile majanga na viini sugu, kupitia mtazamo wa afya ya umma. Watafanya kazi

ili kupunguza vifo vya watoto wachanga na kina mama wajawazito/wanaonyonyesha,

kuendeleza afya ya akili na kushughulikia ongezeko la magonjwa yasiyo ya kuambukiza

katika nchi washirika pamoja na kutatua uchafuzi wa mazingira wa kemikali na hewa chafu.

Kwa sababu ya uhusiano mbalimbali uliopo, wataunga mkono nchi washirika katika

kuendeleza mtazamo wa “afya katika sera zote”.

28. Kuhakikisha watu wote wanapata elimu bora kunahitajika ili vijana wawe wanaweza

kuajiriwa na kuwepo na maendeleo yanayodumu. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

wataunga mkono mafunzo jumuishi na ya kujitolea ili kujiendeleza kibinafsi au kitaaluma na

elimu bora yenye usawa, hasa katika masomo ya watoto wadogo na wale walio katika shule

ya msingi. Vile vile wataendeleza elimu katika kiwango cha sekondari na cha ngazi ya juu,

mafunzo ya kiufundi na taaluma na pia mafunzo ya kazini na ya ngumbaru, ikiwa ni pamoja

na katika hali za dharura au janga. Fursa za elimu na mafunzo kwa wasichana na wanawake

zitapewa kipaumbele. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataongeza juhudi zao za

kuhakikisha kila mmoja ana ufahamu, ustadi, uwezo na haki wanazohitaji kufurahia maisha

yenye heshima, kushiriki kikamilifu katika jamii kama watu wazima wanaowajibika na

Page 10: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 10

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

wanaoweza kufanya kazi, na kuchangia katika uzima wa jamii zao kiuchumi, kimazingira, na

kijamii.

29. Mahitaji, haki, na maazimio ya watoto yanafaa kutiliwa maanani. Hatua zenye manufaa

makubwa zaidi kiuchumi na kijamii ni pamoja na miradi mipana ya uendelezaji wa watoto

wachanga. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataongeza juhudi zao za kutoa

mazingira salama na yanayokuza watoto kama kiungo muhimu cha kuongeza idadi ya vijana

wanaoweza kufikia uwezo wao kamili. Aidha, wanatambua kwamba kila mtoto anafaa kuwa

na maisha matulivu ya utotoni na elimu bora, ikiwa ni pamoja na nyakati za dharura na hali za

majanga ili kuzuia hatari ya kuwepo na ‘kizazi kilichopotea’. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake watafanya kazi na nchi washirika ili kuboresha ulinzi wa watoto na

kushiriki kwao katika maamuzi yanayowahusu.

30. Kuambatana na kanuni ya kutomuacha yeyote nyuma, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama

wake watawapa kipaumbele maalum wale walio katika hali za udhaifu, hatari na zilizotengwa

wakiwemo watoto, wazee, watu wenye ulemavu, wasagaji, shoga, wanaovutiwa na jinsia zote

mbili, wasenge, na wenye sifa za jinsia mbili, pamoja na watu asilia. Hii itajumuisha hatua za

kuwalenga, kuwalinda na kuwasaidia vizuri zaidi ili kuwapa fursa sawa na kuhakikisha

hakuna ubaguzi.

31. Takriban watu bilioni moja ulimwenguni kote wana ulemavu, huku asilimia 80 yao wakiishi

katika nchi zinazoendelea. Watu wenye ulemavu aghalabu huwa ndio maskini zaidi katika

jamii wanazoishi, na hukumbana na viwango vya juu zaidi vya unyanyapaa na ubaguzi.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watazingatia mahitaji mahususi ya watu wenye

ulemavu katika ushirikiano wao wa maendeleo. Kuambatana na Kanuni ya Umoja wa Mataifa

ya Haki za Watu wenye Ulemavu, wataendeleza zaidi haki za watu wenye ulemavu na

kuchukua hatua thabiti za kuhakikisha wanajumuishwa kikamilifu katika jamii na wanashiriki

kwa usawa katika soko la ajira.

32. Kuanzisha ajira bora na zinazotosha kwa vijana kutaendelea kuwa changamoto kuu. Sera

zinazowalenga vijana na uwekezaji unaowafaa zinahitajika ili kuendeleza haki za vijana,

kuwawezesha kushiriki katika maisha ya kijamii, kiraia na kiuchumi, na kuhakikisha

wanachangia kikamilifu katika ukuaji na maendeleo endelevu. Vijana wanapaswa kushiriki

pia katika michakato ya kidemokrasia na kujitwika majukumu ya uongozi.

Page 11: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 11

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Vijana

Vijana ni wahusika wakuu wa kuchochea maendeleo na mabadiliko na hivyo basi wana mchango

muhimu katika Ajenda ya 2030, ikiwa ni pamoja na kupitia uwezo wao wa kubuni. Kutoshughulikia

mahitaji yao ya kielimu, ajira, kijamii na kisiasa kutarudisha nyuma ufikiaji wa Malengo ya

Maendeleo Endelevu na kuwaacha wakiwa katika hatari ya kutumbukia katika uhalifu na itikadi

kali hasa katika hali za migogoro.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataangazia hatua halisi za kutimiza mahitaji ya

vijana, hasa wanawake wachanga na wasichana, kwa kuongeza fursa bora za ajira na ujasiriamali,

zinazoungwa mkono na sera zinazofaa katika elimu, mafunzo ya taaluma, uendelezaji wa ustadi, na

ufikiaji wa teknolojia na huduma za kidijitali. Hili litalenga kutumia uwezo wa ubunifu wa kidijitali

na kuleta fursa za kunufaika na maendeleo ya kiteknolojia. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama

wake watalenga pia kuimarisha haki za vijana na uwezeshaji wao wa kujihusisha na masuala ya

umma ikiwa ni pamoja na kuendeleza kushiriki kwao katika mambo ya uchumi wa mitaa, jamii, na

kufanya maamuzi hasa kupitia mashirika ya vijana.

33. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendelea kutimiza wajibu wao chini ya

Kanuni ya Kumaliza Aina Zote za Ubaguzi dhidi ya Wanawake. Wataendeleza zaidi ulinzi na

utimizaji wa haki za wanawake na wasichana na kufanya kazi pamoja na washirika ili

kumaliza aina zote za unyanyasaji na ubaguzi kwa misingi ya jinsia, ikiwa ni pamoja tabia

zenye kulet madhara mabaya kama vile ndoa za kulazimishwa, za mapema, na zile za baina

ya watoto wenye umri mdogo, na ukeketaji. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watachukua hatua na kuimarisha mazungumzo kuhusu sera ili kuwawezesha wanawake na

wasichana, kuendeleza jukumu lao muhimu kama wahusika wakuu wa kuchochea maendeleo

na mabadiliko na kuongeza hatua zinazolenga kuleta usawa wa kijinsia. Hii itajumuisha

kuendeleza haki zao za kiuchumi na kijamii na uwezeshaji, uimarishaji wa sauti zao na

ushirikishwaji wao katika maisha ya kijamii, kiuchumi, kisiasa, na kiraia, wakihakikisha

uadilifu wao kimwili na kiakili, na kubadili mitindo ya taasisi za Umoja wa Ulaya na nchi

Wanachama wake ili kutimiza ahadi zao. Kuendeleza ufikiaji sawa wa ajira yenye faida kwa

wanawake, kazi zuri, malipo sawa na huduma za kifedha kutanufaisha watu wote katika jamii.

Page 12: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 12

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

34. Umoja wa Ulaya unazidi kujitolea kuendeleza, kulinda, na kutimiza haki zote za binadamu na

kutekeleza Mpango wa Utendaji wa Beijing na Programu ya Utendaji ya Kongamano la

Kimataifa kuhusu Idadi ya Watu na Maendeleo (ICPD) kwa ukamilifu na kwa njia inayofaa

na matokeo ya kongamano zao za kutathmini na unazidi kujitolea kuendeleza haki na afya ya

uzazi na ya jinsia (SRHR), katika muktadha huu. Ikitilia hayo maanani, Umoja wa Ulaya

unasisitiza tena kujitolea kwake katika kuendeleza, kulinda, na kutimiza haki ya kila mtu ya

kudhibiti kikamilifu, na kuamua kwa hiari na kwa kuwajibika katika masuala yanayohusiana

na ujinsia wao na afya ya jinsia na uzazi, bila ubaguzi, matumizi ya nguvu na unyanyasaji.

Zaidi, Umoja wa Ulaya unasisitiza haja ya watu wote kufikia taarifa na elimu kamili ya afya

ya ngono na uzazi zilizo bora na za bei nafuu, ikiwa ni pamoja na elimu kamili ya masuala ya

kijinsia, na huduma za afya.

Page 13: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 13

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Usawa wa Kijinsia

Usawa baina ya wanawake na wanaume wa umri wote ni muhimu sana kwa maendeleo endelevu.

Una athari zinazoongeza uwezo wa kutimiza umalizaji wa umaskini na ni muhimu katika

kuchochea maendeleo ya jamii za kidemokrasia kwa misingi ya haki za binadamu, haki ya kijamii

na uendelevu. Aidha, usawa wa kijinsia unachangia katika ongezeko la ustawi, uthabiti na matokeo

mazuri katika nyanja za afya na elimu. Umoja wa Ulaya na nchi Wanachama wake wanatambua

wanawake na wasichana kuwa wahusika wakuu wa kuchochea maendeleo na mabadiliko, ikiwa ni

pamoja na mchango wao katika kudumisha amani na kusuluhisha migogoro na utoaji wa usaidizi

wa kibinadamu.

Hata hivyo, bado kuna wanawake na wasichana wengi wanaozidi kunyimwa haki, rasilimali na

nafasi ya kusikika. Ukosefu wa usawa wa kijinsia una uhusiano na aina zingine za kutojumuishwa.

Kuendeleza ukuzaji wa hadhi ya wanawake na wasichana na usawa wa kijinsia kunahitaji kufanya

kazi na wavulana, wanaume, wasichana na wanawake ili kuelewa haki, usawa, na majukumu katika

jamii. Hii inajumumisha pia kufanya kazi na wadau wakuu katika jamii kama vile waalimu,

viongozi wa dini na wale wa jamii ili kumaliza ubaguzi dhidi ya wasichana na wanawake.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watahakikisha kuwa mtazamo wa jinsia

umejumuishwa kwa utaratibu katika sera zote kama mchango mkuu wa utimizaji wa Malengo ya

Maendeleo Enedelevu. Watazidisha juhudi zao za kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa

wanawake kwa kukuza zaidi ushirikiano wa wadau mbalimbali, kuimarisha uwezo wa uundaji wa

bajeti inayozingatia masuala ya jinsia, upangaji, na kuhakikisha ushirikishwaji amilifu wa

wanawake na mashirika ya wanawake katika kufanya maamuzi.

Page 14: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 14

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

35. Utamaduni ni chombo kinachowezesha maendeleo na ni kiungo muhimu cha maendeleo na

unaweza kuwezesha ujumuishwaji wa kijamii, uhuru wa kujieleza, kujenga utambulisho,

uwezeshaji wa raia na uzuiaji wa migogoro huku ukiimarisha ukuaji wa uchumi. Wakisisitiza

kuwa Umoja wa Ulaya unaongozwa na ufikiaji kwa wote, kutogawanyika, uwepo wa

uhusiano na hali ya utegemeano wa haki zote za binadamu, Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake wataendeleza mazungumzo ya ushirikiano baina ya tamaduni mbalimbali,

utofauti wa tamaduni na watalinda urithi wa kitamaduni, kutia nguvu viwanda vya bidhaa na

huduma za kitamaduni na ubunifu na wataunga mkono sera za kitamaduni ambapo hizi

zitasaidia kutimiza maendeleo endelevu huku zikizingatia hali za mahali pale.

36. Umoja wa Ulaya na nchi Wanachama wake watachukua hatua ili kupunguza ukosefu wa

usawa wa matokeo na kuendeleza fursa sawa kwa watu wote. Kwa kufanya hivyo, watasaidia

moja kwa mojawatu walio maskini na dhaifu zaidi katika jamii na watasaidia pia kuendeleza

ukuaji ulio jumuishi na endelevu zaidi na ambao hauathiri uwezo wa vizazi vijavyo wa

kukidhi mahitaji yao. Ukuaji wa uchumi hudumu na hunufaisha zaidi walio maskini sana

ikiwa utakuwa jumuishi. Ili kukabiliana na ongezeko la ukosefu wa usawa wa kiuchumi na

kijamii, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono mipango ya maendeleo

ya kitaifa inayoleta matokeo na athari zuri zaidi za kijamii. Watafanya kazi pamoja na nchi

washirika ili kuendeleza sera za umma zinazonuia kuongeza kodi inayotozwa kuambatana na

ongezeko la kiasi kinachotozwa na ugavi wa kodi hiyo kwa miradi ya jamii, na zinazozingatia

ugavi wa faida za ukuaji, utengenezaji wa mali na utoaji wa kazi zuri na uboreshaji wa ufikiaji

wa vipengele vya uzalishaji, kama vile ardhi, fedha, na rasilimali watu.

37. Ili kukabiliana na ukosefu wa usawa, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga

mkono pia mifumo ya ulinzi wa jamii iliyo bora na endelevu ili kuhakikisha mapato ya

msingi, kuzuia kurudi tena kwenye umaskini uliokidhiri na kujenga ustahimilivu.

Watatathmini mambo yanayoamua uwepo wa, na mitindo ya, ukosefu wa usawa wa kiuchumi

na kijamii na wataimarisha nyenzo na mitazamo yao ili kuifanya bora zaidi katika

kushughulikia ukosefu wa usawa. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watajumuisha

upunguzaji wa ukosefu wa usawa katika ushirikiano wao wa maendeleo na kuunga mkono

mitindo bunifu ya kijamii.

Page 15: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 15

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

38. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataimarisha uthabiti, hasa kwa watu walio

hatarini, wakati wanapokumbwa na hali za hatari za kimazingira na kiuchumi, majanga asilia

na yale yanayosababishwa na vitendo vya binadamu, migogoro na hatari za ulimwengu wote

kwa afya. Watajumuisha kwa utaratibu ustahilivu katika hatua zao, wakihakikisha kuwa watu

binafsi, jamii, taasisi na nchi zinaweza kujitayarishia vyema, kustahimili, kujirekebisha, na

kupata afueni haraka kufuatia mikazo na mishtuko bila kuathiri uwezekano wa maendeleo ya

kudumu. Hii itafanyika pia katika kipindi cha kuleta afueni baada ya janga kutokea,

urekebishaji na urudishaji wa hali ya kabla ya janga. Ni lazima kudumisha ushirikiano wa

karibu na vitendo vya kukamilishana baina ya wadau wa maendeleo na watoaji msaada kwa

binadamu, unaotegemea uchanganuzi wa pamoja wa hatari na udhaifu.

39. Uhamaji ni swali tata, linalodumu na kuathiri ulimwengu mzima, na hivyo linahitaji

ushughulikiaji kupitia sera iliyoundwa kwa uangalivu, usawa, na inayozingatia ushahidi

ambao utatilia maanani ustadi wa kila taifa, na hasa ambao hautaathiri haki ya Nchi

Wanachama chini ya Kifungu cha 79(5) cha Mkataba wa Utendakazi wa Umoja wa Ulaya

(TFEU) ya kuamua kiasi cha raia wanaokubalika kuhamia Umoja wa Ulaya kutoka katika

mataifa yanayoendelea wakitafutta ajira. Kusimamia vyema uhamaji na utembeaji wa watu

kunaweza kuchangia katika ukuaji jumuishi na maendeleo endelevu. Uhamaji na utembeaji

wa kiwango cha kawaida unaweza kuleta faida kupitia uhamisho wa maarifa, ustadi na uwezo

wa uzalishaji kwa wahamiaji wao wenyewe, familia zao na kwa nchi wanazotoka na zile

wanazoelekea. Wakati huo huo, uhamaji wa kiwango kisicho cha kawaida unaweza kuibua

changamoto na kuleta madhara mabaya kwa nchi wanazotoka wahamiaji, wanazopitia, na

wanazoelekea. Uhamaji umekuwa suala lenye msukumo zaidi kwa nchi zinazoendelea na hata

zile zilizoendelea. Katika hali zingine, watu ambao ni wahamiaji wananyimwa haki zao za

kibinadamu na ufikiaji wa afya na elimu, na wana hatari ya kuwa waathiriwa wa utumwa na

usafirishaji wa binadamu usio halali. Ushirikiano imara utasaidia kuwezesha uhamaji na

utembeaji wa watu ulio salama, wenye mpangilio, na wa kiwango cha kawaida, ikiwa ni

pamoja utekelezaji wa sera za uhamaji zilizopangwa na kusimamiwa vizuri.

Page 16: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 16

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

40. Kushughulikia uhamaji kuna uhusiano na nyanja zote za sera, ikiwa ni pamoja na maendeleo,

utawala mzuri, usalama, haki za binadamu, ajira, afya, elimu, kilimo, chakula cha kutosha,

ulinzi wa kijamii na mazingira, na vile vile mabadiliko ya hali ya hewa. Kupitia mtazamo wa

Utaratibu wa Ushirikiano, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watashughulikia kwa

utendeti hali mbalimbali za uhamaji na uhamishwaji wa kushurutishwa, ikiwa ni pamoja na

upitishaji na usafirishaji haramu wa binadamu, usimamizi wa mipaka, utumaji pesa kutoka

nchi za nje, utatuzi wa vyanzo vikuu, ulinzi wa kimataifa na urudishwaji wa watu wasiohitaji

ulinzi, kukubali wahamiaji na kuwajumuisha tena katika jamii, kwa msingi wa uwajibikaji wa

pande zote husika na uzingatiaji kamili wa majukumu ya haki na msaada kwa kibinadamu.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watazingatia mtazamo ulioratibiwa, unaozingatia

masuala yote husika, na wenye muundo zaidi, wakifaidi kutokana na umoja wa nguvu zao na

wakitumia faida inayohitajika kwa kutumia sera, nyenzo na mbinu zote husika za Umoja wa

Ulaya, ikiwa ni pamoja na maendeleo na biashara. Kupitia juhudi hizi zilizoimarishwa, Umoja

wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono kwa uamilifu utekelezaji zaidi wa

Mpango pamoja wa Utendaji wa Valleta wa mwaka wa 2015 na ufafanuzi wa Makubaliano ya

Ulimwengu kuhusu Uhamaji na Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa, kama ulivyoitishwa na

Maazimio ya New York ya mwaka wa 2016 ya Wakimbizi na Wahamiaji.

41. Kupitia sera ya maendeleo, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watashughulikia

vyanzo vikuu vya uhamaji wa kiwango kisicho cha kawaida na, pamoja na mengine,

watachangia katika ujumuishwaji endelevu wa wahamiaji katika nchi zinazowapokea na

kusaidia kuhakikisha wahamiaji wanaorudi katika nchi zao za asili au walizopitia

wanafanikiwa kuingiliana na jamii na uchumi wa nchi hizi. Hii itajumuisha kuendeleza

uwekezaji, biashara na ubunifu katika nchi washirika ili kuongeza ukuaji na fursa za

ajiraikiwa ni pamoja na kupitia ushirikiano na watu walio katika mataifa ya kigeni, kusaidia

mifumo ya jamii na uchumi, na vile vile kufanya kazi pamoja na washirika wa sekta ya

kibinafsi na wengineo ili kupunguza gharama ya kutuma pesa kutoka nchi za nje na

kuendeleza utumaji wa pesa kwa haraka, kwa bei nafuu na salama zaidi katika nchi

zinapotoka na zinapopokelewa, na hivyo kufaidi na uwezo wake wa kuleta maendeleo.

Page 17: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 17

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Utembeaji na uhamaji

Ajenda ya 2030 inatambua kwa uwazi mchango mzuri wa uhamiaji na utembeaji kwa ukuaji

jumuishi na maendeleo endelevu. Wahamiaji ni viungo wakuu wakuendeleza uchumi wa

ulimwengu, hasa kupitia pesa wanazotuma nchi walizotoka. Kushughulikia uhamiaji katika miundo

yake yote, uwe ni wa kiwango cha kawaida au kisicho cha kawaida, kunahitaji suluhu, sera na

taratibu za kisheria za muda mfupi na za kudumu zinazojumisha sekta mbalimbali, ili kukidhi

mahitaji ya wahamiaji na watu wa nchi walipopokelewa na kuhakikisha usalama wao. Inakubalika

kuwa kuna changamoto nyingi katika nchi zinazoendelea. Kuhusiana na suala hilo, hatua muhimu

ziliafikiwa katika Mkutano wa Valleta uliofanyika Novemba 2015, ambapo mpango wa utendaji

wenye matumaini makubwa ulikubaliwa.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataongeza juhudi za kushughulikia vyanzo vikuu vya

uhamiaji usio wa kiwango cha kawaida na uhamishwaji wa kulazimishwa, na kuendeleza usimamizi

bora wa uhamaji katika nchi washirika katika miundo yake yote. Wataendelea kujumuisha uhamaji

kama sehemu muhimu ya mazungumzo ya sera ya masuala ya kigeni ya Umoja wa Ulaya, ikiwa ni

pamoja na kupitia ufafanuzi wa ushughulikiaji unaoambatana na hali na ushirikiano ulioimarisha

kwa njia ya uwazi na ya kidemokrasia.

42. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza heshima na ustahimilivu wa watu

walioondolewa makwao kwa muda mrefu na ujumuishwaji wao katika masuala ya kiuchumi

na maisha ya kijamii ya nchi na jamii walipopokelewa, wakitambua kuwa uwezo wa watu

waliohamishwa makwao ni rasilimali yenye muhimu inayoweza kuhamishwa, yenye thamani

kwa ustahimilivu wao na katika kujenga maisha yao tena, na vile vile kama mchango kwa

jamii zilizowapokelea. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watatumia mtazamo

unaozingatia haki, wakitilia maanani kwa karibu wanawake, wato ambao wanaambatana na

wasioambatana na watu wazi, na watu walio hatarini. Watalinda mifumo ya kijamii ya

kudumu, wakijumuisha watu waliohamishwa makwao kwa muda mrefu katika mipango

mipana ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na kupitia ufikiaji wa elimu na kazi zuri.

Page 18: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 18

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

2.2. Sayari - Kulinda mazingira, kusimamia rasilimali asilia na kukabiliana na

mabadiliko ya hali ya hewa

43. Uzima wa binadamu na jamii zenye ustahimilivu hutegemea mazingira bora na mifumo ya

mazingira inayofanya kazi vizuri. Uharibifu wa mazingira, mabadiliko ya hali ya hewa, hali

mbaya zaidi za hewa, na majanga asilia au yanayosababishwa na vitendo vya biandamu

yanaweza kurudisha nyuma faida zinazoletwa na maendeleo na ustawi wa uchumi, hasa kwa

watu maskini. Hii inaweza kuongeza hali za udhaifu na mahitaji, na kuhatarisha amani na

uthabiti na kusababisha uhamaji wa kiasi kikubwa. Kando na vitendo vya kujitolea,

uzingatiaji wa mazingira unahitaji kujumuishwa katika sekta zote za ushirikiano wa

maendeleo, ikiwa ni pamoja na kupitia hatua za uzuiaji. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake wataendeleza matumizi mazuri na utumiaji na uzalishaji endelevu,

ikiwemo usimamizi endelevu wa kemikali na uchafu, wakiwa na nia ya kutenganisha ukuaji

wa kiuchumi kutoka kwa uharibifu wa mazingira na kuwezesha kugeuka kuelekea uchumi wa

mzunguko. Sekta ya kibinafsi inayowajibika na kufanyisha kazi kwa utaratibu kwa kanuni ya

“mchafuzi atalipa” pia kutachangia pakubwa kwa ufanisi. Watasaidia kujenga uwezo wa

udumishaji uendelevu wa mazingira, malengo ya mabadiliko ya hali ya hewa na uendelezaji

wa ukuaji unaohifadhi mazingira katika mikakati ya maendeleo ya kitaifa na ya mitaa.

Isitoshe, watatumia vizuri zaidi sayansi, teknolojia na ubunifu ili kuendeleza uendelevu wa

kimazingira, na kuunga mkono washirika wao watumie data na habari za kina zinazopatikana

kupitia mipango ya uangalizi ya Ulaya na ya Dunia ya kimataifa ili kuunga mkono matumizi

yaliyo na msingi wa uthibitisho na yanayotilia maanani hali ya mazingira.

Page 19: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 19

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

44. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono udumishaji na usimamizi

endelevu wa rasilimali zote asili, na udumishaji na matumizi endelevu ya bayoanuwai na

mazingira, ikiwemo misitu, sehemu za pwani, mabonde ya maji ya mto, na mifumo mingine

ya mazingira, ili kutoa huduma za mifumo ya mazingira. Kuambatana na ahadi za kimataifa,

watapambana na ukataji miti haramu na biashara inayohusiana nayo, uharibifu wa ardhi na

vichaka, ueneaji wa jangwa, ukame, na kupotea kwa aina mbalimbali za viumbe.

Wataendeleza faida za pamoja zinazotokana na usimamizi endelevu, ikiwemo kuwezesha

ustahimilivu na uzoeaji wa hali ya hewa. Wataboresha ujumuishwaji wa uendelevu katika

sekta zote za ushirikiano na kuinua hadhi ya masuala ya mazingira katika mazungumzo na

washirika wao. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza matumizi ya

uhasibu wa mali rasilimali asilia. Wataunga mkono utawala bora na ukuzaji wa uwezeshaji

wa usimamizi endelevu wa rasilimali asilia, ikiwemo uzuiaji wa matumizi haramu ya misitu.

Wataendeleza pia ushirikishwaji wa wadau wa eneo husika na uzingatiaji wa haki za wote,

wakiwemo watu wenyeji na jamii za eneo hilo. Watatua uwindaji haramu wa wanyama pori,

biashara haramu ya wanyama pori na mbao, na utumiaji usio halali wa rasilimali zingine

asilia. Ili kuwa na bahari zuri na zenye uzalishaji, wataendeleza ulinzi na urejeshaji wa

mifumo ya mazingira ya baharini kwa hali ya kawaida, usimamizi endelevu wa rasilimali za

baharini na kilimo endelevu cha samaki, ikiwemo kupitia usimamiza bora wa bahari na

uendelezaji wa uchumi wa bidhaa zitokazo kwa maji.

Page 20: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 20

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

45. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watajumuisha mazingira na mabadiliko ya hali

ya hewa katika mikakati yao yote ya ushirikiano wa maendeleo, ikiwemo kwa kuendeleza

usawa unaofaa baina ya kupunguza athari na uwezo wa kubadilika kulingana na hali.

Watatekeleza Ajenda ya 2030 na Makubaliano ya Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa

kupitia matendo yaliyoratibiwa na yenye ushikamano, na watatumia vyema zaidi umoja wa

nguvu zao. Wataunga mkono mikakati ya kitaifa, ikiwemo upangaji na mipangilio ya

serikali yote, inayoendeleza ustahimilivu, kupunguza hatari ya hali ya hewa na kuchangia

katika kupunguza uchafuzi wa hewa, kuambatana na utekelezaji wa Michango

Inayoamuliwa na Taifa (NDC), wakizingatia changamoto zinazozikumba nchi

zinazoendelea, hasa Nchi Zenye Maendeleo Kidogo Zaidi (LDC) na Nchi Zinazoendelea

ambazo ni Visiwa Vidogo (SIDS). Watachangia katika kuibua watetezi wa hali ya hewa wa

sehemu zile na kusambaza na kuboresha kiukamilifu miradi inayofuata mitindo bora zaidi,

ikiwemo kwa kuunga mkono mipangilio inayowahusisha wadau mbalimbali. Hali ya

Mkataba wa Paris unaobana kisheria na hitaji la kutayarisha Michango Inayoamuliwa na

Taifa (NDC) kunaweza pia kuchochea upangaji wa maendeleo wa kitaifa katika muktadha

wa Ajenda ya 2030.

Page 21: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 21

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Nishati endelevu na mabadiliko ya hali ya hewa

Nishati ni kiungo muhimu sana kinachowezesha maendeleo na ni msingi kwa suluhu za sayari

endelevu. Nchi zinazoendelea zinahitaji nishati ili kuendeleza ukuaji jumuishi na na kuboresha

zaidi hali za maisha. Uwekezaji katika nishati endelevu unaweza kuhakikisha na kuongeza

ufikiaji wa maji safi, upishi usiochafua mazingira, elimu na huduma za afya, na unaweza pia

kuleta ajira na kusaidia biashara za eneo lile kwa njia isiyodhuru mazingira.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza malengo matatu yanayoingiliana:

kutatua ukosefu wa ufikiaji wa nishati; kuongeza matumizi bora ya nishati na uzalishaji wa

nishati inayodumu ili kufikia usawa endelevu baina ya uzalishaji na matumizi ya nishati; na

kuchangia katika juhudi za ulimwengu za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa

kuambatana na Mkataba wa Paris na Michango husika Inayoamuliwa na Taifa (NDC)

iliyowasilishwa na Wanachama. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watapambana na

ukosefu wa nishati kwa kuchangia katika ufikiaji kwa wote wa huduma za nishati ambazo ni za

bei nafuu, za kisasa, zinazoweza kutegemewa na endelevu, wakiangazia zaidi katika nishati

inayodumu na matumizi bora ya nishati. Nishati inayodumu na isiyochafua mazingira inaweza

kutolewa kupitia suluhu zinazoongozwa na jamii, zilizo kando na mifumo ya kawaida ya

usambazaji wa nishati au kutoka kwa mifumo midogo ya usambazaji wa nishati, na hivyo

kuwezesha ufikiaji wa nishati katika sehemu za vijijini.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza umalizaji wa ruzuku za mafuta

yatokanayo na kaboni na ambayo yana athari mbaya kwa mazingira, masoko ua nishati ambayo

ni thabiti na wazi na utekelezaji wa mifumo ya usambazaji wa nishati ambayo inatumia

teknolojia za kisasa na za kidijitaji ili kusimamia nishati endelevu. Mkakati huu ulioboreshwa

utakuwa sambamba na hatua ya Umoja wa Ulaya inayoambatana na uongozi wake ulimwenguni

wa kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa na kusaidia mataifa yanayoendelea kukabiliana

na mabadiliko ya hali ya hewa na mchakato wa kuanzisha uchumi ulio na uchafuzi mdogo wa

hewa na wenye ustahimilivu wa hali ya hewa.

Page 22: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 22

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

46. Kiasi cha uwekezaji wa kifedha unaohitajika kuhakikisha watu wote wanafikia huduma za

nishati salama na isiyochafua mazingira kinahitaji ushirikiano na wadau wengi. Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake wataongeza ushirikiano wao na wadau wote husika,

ikiwemo sekta ya kibinafsi, katika usimamizi wa mahitaji ya nishati, matumizi bora ya

nishati, uzalishaji wa nishati ya kudumu na uundaji na uhamishaji wa teknolojia isiyoathiri

mazingira. Wataunga mkono uboreshaji wa taratibu za udhibiti zinazofaa kwa sekta ya nishati

yenye ushindani na iliyo endelevu na kufaidi kutokana na fedha kutoka kwa watu/mashirika

binafsi. Watakusanya fedha za ziada, ikiwemo kutoka kwa sekta ya kibinafsi na kupitia miradi

na nyenzo bunifu za ugharamiaji. Kuunga mkono Afrika na ujirani wa Umoja wa Ulaya

katika haya mabadiliko ya nishati kutakuwa sehemu ya utaratibu wenye uwezeshaji kwa

Muungano wa Nishati wa Umoja wa Ulaya.

2.3. Ustawi - Ukuaji na ajira jumuishi na endelevu

47. Kutoa nafasi za kazi, hasa kwa wanawake na vijana ni muhimu kwa ukuaji jumuishi na

endelevu. Ustawi na ukuaji unaowashirikisha wote unachangia katika maslahi na heshima ya

binadamu. Ukuaji endelevu wenye ujumuishi hujenga ustahimilivu wa kudumu katika nchi

washirika, kwa kutoa fursa za makundi ya watu walio dhaifu na wale walio hatarini zaidi,

kushiriki katika, na kunufaika na, mali na utoaji wa nafasi za ajira zuri. Umoja wa Ulaya na

Nchi Wanachama wake wataendeleza mabadiliko ya kiuchumi yanayotoa nafasi za ajira zuri,

yanayoongeza uwezo wa uzalishaji, na kuzalisha mapato yanayotosha kugharamia huduma za

umma na ulinzi wa jamii, yanayokuza mifumo ya thamani endelevu na uundaji wa bidhaa

na/au utoaji wa huduma tofauti tofauti, ikwemo ujenzi wa viwanda endelevu. Hii ni pamoja

na kuendeleza mitindo endelevu ya matumizi na uzalishaji katika uchumi wa mzunguko,

ikiwemo kuendeleza utumiaji tena wa vitu visivyo na kemikali, matumizi bora ya rasilimali,

na mabadiliko kuelekea utumiaji wa nishati yenye madhara madogo kwa mazingira na

uchumi unaostahimili athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

Page 23: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 23

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

48. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanatambua jukumu la mashirika madogo zaidi,

madogo kiasi na ya wastani (MSME) kama wawezeshaji wa maendeleo endelevu, na vile vile

kama wadau muhimu katika kukabiliana na umaskini. Mashirika madogo zaidi, madogo kiasi

na ya wastani (MSME) ni wadau wakuu wanaowezesha ukuaji, ajira, ubunifu na maendeleo

ya kijamii. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono hatua zinazohusisha

vitendo na zilizo bunifu kupitia sera ya maendeleo ili kuongeza kushiriki kwa mashirika

madogo zaidi, madogo kiasi na ya wastani (MSME) katika kutekeleza hatua halisi uwanjani

na kufungulia uwezo wao wa kuleta maendeleo. Watawezesha ufikiaji wa taarifa muhimu

kwa mashirika madogo zaidi, madogo kiasi na ya wastani (MSME), katika Umoja wa Ulaya

na nchi washirika, na watayajumuisha katika mifumo ya usambazaji na ya thamani, huku

wakishughulikia upungufu wa fedha za ugharamiaji katika mashirika madogo zaidi, madogo

kiasi na ya wastani (MSME). Watahimiza ushirikiano na mazungumzo baina ya biashara

mbalimbali kati ya mashirika madogo zaidi, madogo kiasi na ya wastani (MSME) yaliyo

kwenye Umoja wa Ulaya na katika nchi washirika au maeneo.

Uwekezaji na biashara

Uwekezaji endelevu wa umma na binafsi ni kiungo muhimu kinaoendesha maendeleo endelevu.

Unasaidia kufanya uchumi uwe wa namna mbalimbali, kukuza ukuaji na kuleta nafasi zuri za kazi,

kutengeneza bidhaa na kutoa huduma bunifu, kuunganisha uchumi za nchi na mifumo ya thamani

ya maeneo na ya ulimwengu, kuendeleza ujumuishwaji na biashara ya eneo, na kukidhi mahitaji ya

jamii. Ajenda ya 2030 na Ajenda ya Vitendo ya Addis Ababa hutoa utaratibu ambapo uwekezaji

uliowajibika unaweza kuchangia kwa maendeleo endelevu katika miundo yake yote.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watachukua hatua ili kuinua uwekezaji kwa kuleta

pamoja ufadhili wa maendeleo endelevu, usaidizi wa kiufundi ili kuendeleza miradi endelevu na

kuvutia wawekezaji, na hatua za kusaidia kuboresha usimamizi wa uchumi na mazingira ya

biashara, kukabiliana na ufisadi na kushirikisha sekta ya kibinafsi. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake watachangia pia kwa kuinua uwekezaji wa binafsi na umma katika uchumi

unaotumia nishati yenye madhara madogo kwa mazingira, na unaostahimili mabadiliko ya hali ya

hewa.

Mbinu moja ya kutimiza hatua hizo itakuwa Mpango wa wa Ulaya wa Uwekezaji katika Nchi za

Nje, ambao utajumuisha hakikisho la kupunguza hali ya hatari za kuwekeza katika nchi

zinazoendelea na hivyo kunufaika kutokana na fedha za zaida, hasa kutoka kwa sekta ya kibinafsi.

Utachangia katika kutimiza Malengo ya Maendeleo Endelevu, na hivyo kusaidia kukabiliana na

vyanzo vikuu vya uhamiaji usio wa kiwango cha kawaida.

Page 24: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 24

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Kupitia sera yake ya biashara, Umoja wa Ulaya pia utaendelea kuhakikisha kwamba nchi

zinazoendelea, hasa zile zilizo dhaifu sana, zinapata faida za ukuaji jumuishi na maendeleo

endelevu kutokana na ushirikishwaji ulioboreshwa katika ushirikiano wa eneo na katika mfumo wa

biashara baina ya nchi mbalimbali.

49. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watasaidia kukuza mazingira yanayofaa kwa

biashara katika nchi zinazoendelea, yanayozingatia viwango na kanuni za kimataifa za haki za

binadamu. Watachangia katika kuboresha hali za shughuli jumuishi za uchumi kwa

keundeleza sera na taratibu za udhibiti zilizo endelevu zaidi, haki za biandamu, vikiwemo

viwango vikuu vya kazi na mahitaji ya ukaguzi, mazingira yanayofaa zaidi kwa biashara,

mifumo mipya ya biashara na uwezo mkubwa zaidi wa serikali. Wataendeleza ufikiaji mpana

wa huduma za kifedha na za mikopo midogo, ikiwemo kwa wanawake, maskini na kwa

mashirika ya biashara yaliyo madogo sana, madogo kiasi na ya wastani (MSME).

Wataendeleza pia miradi ya sekta ya kibinafsi na mashirika ya jamii, miungano ya mashirika,

wajasiriamali wanawake na vijana, ili kuinua utoaji wa huduma kwa eneo husika na vile vile

mifumo ya biashara iliyo jumuishi na isiyodhuru mazingira. Wataendeleza ununuzi enedelevu

na wazi wa bidhaa na huduma na serikali ili kuunga mkono maendeleo endelevu na

kuwezesha ufikiaji wa mashirika ya biashara yaliyo madogo sana, madogo kiasi na ya wastani

(MSME) wa fedha za serikali za kununua bidhaa na huduma kutoka kwa sekta ya kibinafsi.

Uwekezaji wa sekta ya umma katika utafiti na ubunifu na ushirikiano katika sayansi na

teknolojia unaweza pia kuwa ufunguo wa uwekezaji wa sekta ya kibinafsi na kusaidia

kuendesha ukuaji endelevu na jumuishi katika nchi zinazoendelea.

50. Fedha chafu, ufisadi, utumaji na upokeaji haramu wa pesa, na ukwepaji na uepukaji wa kulipa

kodi yote yanazidi kurudisha nyuma maendeleo endelevu, huku yakiathiri sana hasa nchi

zinazoendelea. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya kazi pamoja na nchi

washirika ili kuendeleza utozaji ushuru unaoongezeka kulingana na kiwango cha mapato,

hatua za kupambana na ufisadi na sera za ugavi wa mapato ya nchi kwa miradi inayofaidi

umma, na kukabiliana na utumaji na upokeaji haramu wa pesa ili kuendeleza ufikiaji wa

huduma bora za msingi kwa watu wote.

51. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataleta pamoja ustadi na rasilimali za sekta ya

kibinafsi na Msaada wa Biashara, sera na nyenzo za biashara, na diplomasia ya kiuchumi

zenye kuunga mkono maendeleo. Wataendeleza Msaada wa Biashara ili kuunga mkono

utekelezaji wa Ajenda ya 2030 na kushughulikia vyema mahitaji ya biashara na uwezo wa

Page 25: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 25

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

uzalishaji wa nchi zinazoendelea. Mahitaji ya nchi zenye maendeleo madogo zaidi (LDC) na

nchi zinazoendelea zisizokuwa na bandari (LLDC), ambazo uwezeshaji wa biashara na

miundo msingi ya biashara ni mambo muhimu yanaoendesha maendeleo, na Nchi

Zinazoendelea ambazo ni Visiwa Vidogo (SIDS), zinafaa kutiliwa maanani.

52. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza na kuwezesha biashara na

uwekezaji katika nchi zinazoendelea ili kuunga mkono maendeleo endelevu. Umoja wa Ulaya

utazidi kuendeleza biashara na ushirikiano wa maeneo kama viendeshaji vikuu vya ukuaji na

upunguzaji wa umaskini katika nchi zinazoendelea. Kupitia utekelezaji wa mkakati wa

“Biashara kwa Wote”, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono

washirika wao wa biashara, ikiwemo kupitia makubaliano ya ushirikiano wa kiuchumi, ili

kujumuisha maendeleo endelevu katika viwango vyote vya sera ya biashara. Kuambatana

ahadi za makubaliano ya Ushikamano wa Sera kwa ajili ya Maendeleo (PCD), usaidizi wa

maendeleo utatumika pale unapofaa ili kuhakikisha kwamba masharti yaliyoko kwenye

mikataba ya biashara yanayohusiana na biashara na maendeleo endelevu yanatekelezwa na

kutumika ipasavyo. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watendeleza ukuaji endelevu

wa uchumi na kusaidia nchi zinazoendelea kuanza kutumia mifumo ya ukuaji inayozingatia

uhaba wa rasilimali na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa. Hii ni pamoja na

maendeleo uendelevu katika mifumo ya thamani na viwango vya mazingira na jamii.

53. Sekta ya kibinafsi inaweza kuchangia katika utekelezaji wa Ajenda ya 2030. Umoja wa Ulaya

na Nchi Wanachama wake, kwa uratibu wa karibu na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya,

wataendeleza ukusanyaji wa rasilimali binafsi kwa ajili ya maendeleo, huku wakiendeleza

uwajibikaji katika sekta ya kibinafsi, katika nyanja zenye uwezo mkubwa wa mabadiliko ya

maendeleo endelevu. Hii ni pamoja na kilimo endelevu, nishati salama na isiyo na madhara

kwa mazingira, usimamizi jumuishi wa wa rasilimali za maji, miundo msingi thabiti, afya,

utalii endelevu, uchumi usioathiri mazingira na wa mzunguko, mawasiliano na teknolojia ya

kidijitali.

Page 26: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 26

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

54. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya kazi na sekta ya kibinafsi, yakiwemo

mashirika ya waajiri na wafanyakazi, ili kuendeleza mitazamo yenye uwajibikaji, endelevu na

bora, ikiwemo kupitia mazungumzo katika kijamii. Utumiaji wa kiwango cha juu cha mifumo

na mitindo ya biashara yenye uwajibikaji na ujumuishwaji kwa kampuni tofauti za Umoja wa

Ulaya zenye mifumo ya usambazaji katika nchi zinazoendelea, kwa ushirikiano wa karibu na

wadau wa umma na binafsi, na kuendeleza biashara yenye usawa, uwazi na inayozingatia

maadili, ikiwa ni pamoja na wazalishaji wadogo katika nchi zinazoendelea, unaweza

kuchangia pakubwa katika utekelezaji wa Ajenda ya 2030. Viwango na wajibu wa haki za

binadamu unaokubalika kimataifa kuhusu maendeleo endelevu, uwazi, na uwajibikaji wa

mashirika kwa jamii vinahitaji kujumuishwa katika mifumo ya biashara, ikiwemo kwa

ushirikiano na mchanganyiko wa sekta za umma na binafsi, kupitia mbinu tofauti, kama vile

kushiriki mitindo bora zaidi. Hii ni pamoja na kuhakikisha usimamizi na matumizi endelevu

ya rasilimali asilia kama vile madini na mbao. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watazidi kuunga mkono mitindo ya biashara yenye uwajibikaji na usimamizi wa mifumo ya

usambazaji unaowajibika, kuheshimu haki za muda wa ajira na kuunganisha haki za

binadamu na za kazi, uadilifu katika masuala ya fedha na viwango vya mazingira na ufikiaji.

Watafanya kazi ili kuzuia ukiukaji wa haki za binadamu na kuendeleza Kanuni za Umoja wa

Mataifa Zinazoongoza Biashara na Haki za Binadamu. Wataendeleza viwango vya kazi

ambavyo vinahakikisha hali zuri za kufanyia kazi na mishahara bora kwa wafanyakazi, hasa

vile vinavyopeanwa na Shirika la Wafanyakazi Ulimwenguni, katika sekta rasmi na isiyo

rasmi, ikiwemo kwa kuunga mkono mabadiliko kutoka kwa uchumi usio rasmi kuelekea ulio

rasmi na kwa kukabiliana na ajira ya watoto.

Page 27: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 27

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

55. Kilimo endelevu, pamoja na uvuvi na kilimo cha samaki endelevu, kinaendelea kuwa

kiendeshaji kikuu cha umalizaji wa umaskini na maendeleo endelevu na ni muhimu kwa

kumaliza njaa na kuhakikisha uwepo wa chakula cha kutosha. Thuluthi mbili za watu walio

maskini ulimwenguni kote hutegemea kilimo ili kujikimu kimaisha na nchi kadhaa

zinazoendelea zinasalia kutegemea sana biashara ya bidhaa chache. Usaidizi kwa wakulima

wadogo wadogo, wakiwemo wakulima wa familia na wachugaji mifugo, unaendelea kuwa

wenye umuhimu mkubwa, na unachangia katika kuhakikisha kuna chakula cha kutosha na

katika kupambana na mmomonyoko wa udongo na kupotea kwa bayoanuwai, huku ukitoa

ajira. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono uboreshaji wa utawala

unaohusiana na usimamizi endelevu wa misitu, usimamizi wa sehemu za malisho ya mifugo

wenye ushirikishwaji, ufikiaji sawa wa uwezo wa kumiliki ardhi, hasa kwa wanawake,

kuzingatia haki za watu wanaoishi sehemu husika na za watu wenyeji wa sehemu hiyo,

ikiwemo matumizi ya ardhi kwa njia za kitamaduni na ufikiaji wa maji. Wataendeleza

uundaji wa mashirika na vyama vya ushirika vya wakulima ili kushughulikia, pamoja na

mambo mengine, uzalishaji bora wa mashamba ya familia, haki za matumizi ya ardhi mifumo

ya mbegu za wakulima ya zamani. Watachangia katika kuongeza ubora wa hali za usafi wa

mwili na wa mazao ya miti. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watalenga

kuendeleza masoko ya kilimo na mifumo ya thamani katika nchi washirika ambayo inafaidi

maskini na kuhimiza viwanda vya kilimo kutoa ajira na thamani inayoongezewa. Hii

itajumuisha kuunga mkono ujumuishwaji wa vijana na uwezeshaji wa wanawake, na

kuendeleza utafiti na ubunifu. Uwekezaji katika kilimo endelevu na katika sekta ya kilimo cha

chakula vinahitajika ili kuleta mifumo tofauti tofauti ya uzalishaji wa sehemu na eneo husika,

kuzuia utapiamlo, kuleta ongezeko la uzalishaji na kutoa nafasi za kazi zuri, bila kuathiri

mazingira. Kuna haja ya uwekezaji mwingi wa sekta ya umma na binafsi katika kilimo

endelevu kwa nchi nyingi zinazoendelea, hasa barani Afrika. Uwekezaji na madailiko haya

sera lazima yawe na uwajibikaji na ujumuishwaji, na yawafaidi watu wanaoishi katika

sehemu husika.

Page 28: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 28

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

56. Itabidi mifumo endelevu ya kilimo na chakula, ikiwemo uvuvi endelevu, itatue mahitaji ya

idadi inayoongezeka ya watu ulimwenguni huku ikilinda mazingira. Umoja wa Ulaya na nchi

Wanachama wake wataunga mkono mitindo na vitendo vya ukulima unaotilia maanani

michakato ya mazingira na viumbe ili kupunguza hasara ya kupoteza chakula baada ya

kuvuna na uharibifu wa chakula, na vile vile kulinda udongo, kuhifadhi rasilimali za maji,

kusimamisha na kuzuia ukataji miti, kupanda miti tena ili kukuza misitu, na kudumisha

bayoanuwai na mazingira bora. Uwezo wa kilimo endelevu na udongo wa kupunguza utoaji

wa gesi zinazosababisha ongezeko la kiwango cha joto duniani ni lazima utumiwe, na

ustahimilivu wa athari za mabadiliko ya hali ya hewa unapaswa kuboreshwa. Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake watendeleza uvuvi endelevu na mitindo ya kilimo cha

samaki, na kuunga mkono hatua za kukabiliana na uvuvi haramu, uchafuzi wa bahari na athari

za mabadiliko ya hali ya hewa.

57. Umoja wa Ulaya na nchi Wanachama wake watazidi kuunga mkono teknolojia za habari na

mawasiliano katika nchi zinazoendelea kama viungo vikuu vya kuwezesha ukuaji jumuishi na

maendeleo endelevu. Teknolojia za kidijitali zinatumika katika nchi zinazoendelea kwa

kiwango cha juu mno. Hata hivyo, ukosefu wa uunganisho unaendelea kuwa kikwazo kikuu

cha maendeleo katika nyingi ya nchi zinazoendelea, hasa kwenye sehemu za vijijini na zile

zilizo mbali sana, hususan barani Afrika. Aidha, ukosefu wa ushindani mara nyingi unaweza

kufanya teknolojia za kidijitali kuwa ghali na vigumu kupatikana kwa watu wengi. Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya kazi ili kujumuisha suluhu za kidijitali katika

maendeleo na kuendeleza matumizi ya teknolojia za kidijitali katika nyanja tofauti muhimu

(kama vile utawala kwa mifumo kielektroniki, kilimo, elimu, usimamizi wa maji, afya, na

kawi). Wataunga mkono mazingira yanayowezesha uchumi wa kidijitali kwa kuboresha

uunganisho wa bure, wazi, na salama, na kuondoa vikwazo ili kudhihirisha uwezo wake

kamili wa kuleta maendeleo endelevu. Wataunga mkono ujasiriamali wa kidijitali, yakiwemo

mashirika madogo sana, madogo kiasi na ya wastani ya biashara (MSME), ili kuendeleza

maudhui yanayofaa kwa sehemu husika na kuendeleza ubunifu na utoaji wa nafasi za kazi

zuri. Wataunga mkono ufahamu na ustadi wa teknolojia ya dijitali ili kuwezesha watu, hasa

wanawake na watu walio kwenye sehemu za hatari na zilizotengwa, kuendeleza ujumuishwaji

kwa jamii na kuwezesha kushiriki katika utawala wa kidemokrasia na uchumi wa kidijitali.

Page 29: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 29

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

58. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono usanifu, ujenzi na uendeshaji

wa miundo msingi na mijengo bora ambayo inatumia vizuri rasilimali na nishati. Wataunga

mkono uundaji wa mitandao ya usafirishaji na uchukuzi, iliyo endelevu, yenye uchafuzi

mdogo kwa mazingira, na yenye uunganishi na miundo misingi ingine thabiti na isiyodhuru

mazingira, kama vile mitandao ya kawi, mifumo ya maji na mifumo ya kusimamia takataka,

ili kuendeleza ufikiaji sawa na wa bei nafuu kwa watu wote, ukuaji, biashara na uwekezaji.

Watajumuisha kwa utaratibu malengo ya kupunguza utoaji wa gesi zinazoongeza kiwango

cha joto katika miradi ya miundo msingi.

59. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wanasisitiza haja ya uzingatiaji kamili wa viwango

vya kimataifa vya mazingira na usalama wa nyuklia katika nchi washirika.

60. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya juhudi za kuinua uwezo wa miji kama

vitovu vya ukuaji na ubunifu endelevu na jumuishi, wakizingatia jamii zao pana zilizo vijijini

na maendeleo ya eneo yenye usawa. Wataendeleza maendeleo ya miji jumuishi na endelevu

ili kukabilifu na ukosefu wa usawa, wakiangazia wale wenye mahitaji zaidi, wakiwemo watu

wanaoishi kwenye mitaa ya mabanda na vitongoji duni. Wataunga mkono washirika ili

kuboresha utoaji wa huduma msingi na ufikiaji sawa wa chakula cha kutosha na makazi

mazuri, ya bei nafuu, na yanayopatikana, na kuboresha hali ya maisha ya idadi ya watu

inayoongezeka na ambayo inaishi kwenye miji. Kuambatana na Ajenda ya Miji Mpya ya

Umoja wa Mataifa, wataendeleza upangaji wa matumizi endelevu ya ardhi, usimamizi sawa

wa masoko ya ardhi, usafirishaji endelevu kwenye miji na miji salama, ya kisasa inayotumia

fursa za teknolojia za kidijitali. Watendeleza sera za maeneo na miji zilizo jumuishi, zenye

usawa, na ujumuishwaji, na uratibu wa viwango mbalimbali vya serikali, wakikuza uhusiano

imara baina ya sehemu za vijijini na mijini. Watajenga ustahimilivu wa miji kwa misukosuko

na kutumia fursa za uchumi wenye madhara madogo kwa mazingira na unaostahimili

mabadiliko ya hali ya hewa.

Page 30: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 30

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

2.4. Amani – jamii zenye amani na jumuishi, demokrasia, taasisi bora na zenye

uwajibikaji, utawala wa sheria na haki za kibinadamu kwa wote

61. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza maadili ya demokrasia ya watu

wote, utawala bora, utawala wa sheria na haki za kibinadamu kwa wote, kwa sababu ni

masharti yanayopaswa kutimizwa ili kuwepo na maendeleo endelevu na uthabiti, katika

viwango mbalimbali vya ushirikiano na vya nyenzo katika hali na nchi zote, ikiwemo kupitia

hatua ya maendeleo. Wataunga mkono juhudi za ndani ya nchi, zinazoafikiana na mahitaji na

muktadha wa kila jamii ili kujenga nchi za kidemkorasia, zinazoweza kustahimili athari za

misukosuko ya nje na ya ndani ya nchi na kushughulikia sababu zinazoendesha udhaifu wa

jamii, ikiwemo ukosefu wa usawa.

Utawala mzuri, demokrasia, utawala wa sheria na haki za biandamu

Utawala mzuri, demokrasia, utawala wa sheria ni muhimu kwa maendeleo endelevu. Utawala wa

sheria unahitajika ili kulinda haki zote za kimsingi. Taasisi na mifumo bora ya utawala na ambayo

inashughulikia mahitaji ya umma hutoa huduma muhimu na huendeleza ukuaji jumuishi, huku

michakato ya kisiasa ikihakikisha kuwa raia wanaweza kuwataka maofisa wa umma wawajibike

katika viwango vyote.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza taasisi zinazowajibika na wazi,

zikiwemo bunge za taifa, na kukuza ushirikishwaji katika kufanya maamuzi na ufikiaji wa taarifa

kwa umma. Wataendeleza mahakama huru na zisizoegemea upande wowote, na kuunga mkono

utoaji wa haki yenye usawa, ikiwemo ufikiaji wa usaidizi wa kisheria. Wataunga mkono uwezeshaji

wa taasisi thabiti na utawala wa viwango mbalimbali, kwa kushirikisha watu walio kwenye hali za

udhaifu na wale wa makundi madogo katika jamii kupitia ushirikiano baina ya serikali za kitaifa,

serikali ndogo za kitaifa, na zile za mitaa na kwa kutumia uwezo wa suluhu za kidijitali. Wataunga

mkono miradi ya kukabiliana na ufisadi na kuleta uwazi na uwajibikaji zaidi katika ufadhili

unaotokana na fedha za umma na katika utoaji wa huduma za umma.

Page 31: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 31

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

62. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga mkono nafasi wazi na yenye

uwezeshaji kwa asasi za kijamii, mitazamo jumuishi na uwazi katika kufanya maamuzi katika

viwango vyote. Watazidi kuunga mkono chaguzi jumuishi, wazi, na za kuaminika kwa kutoa

usaidizi kwa muda unaofaa katika wakati wote wa mzunguko wa uchaguzi, na vile vile

kuendeleza vyama vya kisiasa vya kidemokrasia na vinavyowajibika na ushirikishwaji amilifu

wa raia katika mchakato wote wa uchaguzi. Ujumbe Huru wa Uangalizi wa Uchaguzi wa

Umoja wa Ulaya ni mbinu muhimu ya kuafikia lengo hili. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake wataunga mkono na kuendeleza utawala wa kidemokrasia unaohakikisha

uhuru wa mambo muhimu unadumishwa, kama vile uhuru wa kuwa na dhana, wa dini au

imani, uhuru wa kukusanyika na kushirikiana, ikiwemo kwa watu wa makundi yaliyotengwa,

na ambao unazingatia haki za binadamu za watu wote, haijalishi kama ni za kiraia, kisiasa,

kiuchumi, kijamii au kiutamaduni. Watatetea uhuru wa kujieleza na wa kuwa na maoni na

kutoa usaidizi kwa vyombo vya habari vilivyo huru na vyenye kuheshimu maoni ya watu

tofauti na vinavyotoa habari bora kulingana na ukweli na data.

63. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watakuza mifumo ya mahakama iliyo bora, wazi,

huru, na inayaowajibika na kuendeleza ufikiaji wa haki kwa wote - hasa maskini na watu

walio hatarini. Hii inajumuisha juhudi za kukabiliana na uhalifu, ukiwemo uhalifu na vurugu

mijini, na juhudi za kupambana na makundi ya uhalifu yanayotoka mataifa mbalimbali

yanayohusiana na uuzaji na usafirishaji haramu wa silaha, madawa ya kulevya na binadamu.

64. Umaskini, migogoro, udhaifu na uhamishwaji wa lazima zina uhusiano mkubwa na ni lazima

pia zishughulikiwe kwa utendeti na kwa ushikamano kama sehemu ya uunganisho baina ya

msaada wa kibinadamu na maendeleo. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watashughulikia vyanzo vyao vikuu katika viwango vyote, ikwemo kutengwa, ukosefu wa

usawa, ukosefu wa chakula cha kutosha, ukiukaji wa haki za binadamu na dhuluma, uepukaji

wa adhabu na ukosefu wa utawala wa sheria, ukiwemo pia uharibifu wa mazingira na

mabadiliko ya hali ya hewa.

Page 32: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 32

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

65. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watatumia ushirikiano wa maendeleo kama

sehemu ya sera na nyenzo mbalimbali za kuzuia, kusimamia na kusaidia kutatua migogoro na

hali za hatari, kuepukana na mahitaji ya kibinadamu na kuleta amani ya kudumu na utawala

bora. Ushirikiano wa maendeleo unaangazia sana umalizaji wa aina zote za umaskini, na

juhudi zote zitaelekezwa katikakutimiza lengo hilo. Wataendeleza mfumo pana wa kutatua

migogoro na hali za hatari kupitia matumizi bora ya mikakati ya mpwito na ya mfumo wa

kutoa tahadhari ya mapema wa Umoja wa Ulaya, wakiangazia udhaifu, usalama wa binadamu

na kutambua uunganisho uliopo baina ya maendeleo endelevu, hatua ya msaada wa

kibinadamu, amani na usalama.

66. Udumishaji wa amani na ujenzi wa nchi ni muhimu kwa maendeleo endelevu na vinafaa

kufanyika katika viwango vyote, kuanzia ulimwengu mzima hadi kwa eneo husika, na katika

hatua zote za mchakato wa mgogoro, kuanzia tahadhari ya mapema na uzuiaji hadi kwa

kushughulikia hatari na kuleta hali ya utulivu. Katika muktadha wa ushirkiano wa maendeleo,

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanaweza pia kushirikiana na sekta ya kibinafsi

ili kuzipa uwezo wa kuhakikisha uafikiaji wa malengo ya maendeleo endelevu, hasa utimizaji

wa jamii jumuishi na zenye amani. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza

suluhu za wote kwa changamoto za usalama na maendeleo, ikiwemo kupitia kuunga mkono

utawala wa kidemokrasia wa sekta ya kibinafsi, ufanisi wake katika kutoa usalama kwa

binadamu, na kukuza uwezeshaji. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanatambua

haja ya kuzuia na kupambana na uenezaji wa itikadi kali za kidini unaosababisha vitendo

vibaya vya dhuluma, ikiwemo kupitia kukuza maelewano na majadiliano baina ya dini

mbalimbali. Wataendelea kuunga mkono kanuni ya wajibu wa kulinda na uzuiaji wa vitendo

vya ukatili. Katika muktadha huu, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watendelea

kukuza ushirikiano wao na Umoja wa Mataifa na washirika wa kitaifa na wa kanda.

67. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watachangia kwa Mabadiliko ya Sekta ya Ulinzi,

ambayo yanaweza kuchangia kuleta udhibiti bora wa kidemokrasia na uwajibikaji, uboreshaji

wa usalama wa binadamu, maendeleo endelevu na umalizaji wa umaskini. Mabadiliko ya

sekta ya ulinzi ni lazima yaambatane na mahitaji ya nchi washirika na izingatie umiliki wa

kitaifa ulio wazi na unaodumu.

Page 33: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 33

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

68. Nchi zilizo kwenye hali za udhaifu au zinazoathiriwa na migogoro zinahitaji kushughulikiwa

kwa makini na kuendeleza ushirikiano wa kimataifa ili kufikia maendeleo endelevu. Malengo

ya kudumisha amani na kujenga nchi ni muhimu ili kukuza uwezo wa nchi wa kuunganisha

kikamilifu masuala ya kiuchumi, kijamii na kimazingira na yale ya usalama ma maendeleo.

Katika usaidizi wao wa kimaendeleo, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watazingatia hasa nchi zilizo dhaifu na zinazoathiriwa na migogoro na watasaidia wale walio

wadhaifu zaidi. Kwa kuendeleza na kulinda haki za binadamu, demokrasia, utawala wa

kisheria na utawala bora, watajituma ili kuchangia katika uthabiti na usalama na vile vile

katika ustahimilivu. Watajumuisha ufahamu wa masuala ya migogoro katika kazi zao zote, ili

kuwe na matokeo mengi na mazuri katika juhudi za kuleta amani. Wataendeleza uwazi,

uwajibikai na ufikiaji wa haki, kwa kuwashirikisha wadau wote katika michakato ya uzuiaji

wa migogoro, udumishaji na upatikanaji wa amani. Wataunga mkono haki ya mpwito kupitia

hatua zinazohusiana na muktadha husika na ambazo zinaendeleza ukweli, haki, fidia na

uhakikisho wa kutotokea tena. Uimarishaji unahitaji kuziba pengo lililopo kati ya usuluhishaji

wa mgogoro na michakato ya kudumu ya mabadiliko, na kukuza uaminifu baina ya serikali na

raia, ikiwemo kupitia kuboresha utoaji wa huduma. Katika muktadha huu, Umoja wa Ulaya

na Nchi Wanachama wake wataimarisha ushirikiano na washirika wa kanda wanaostahili.

Ufanisi wa juhudi za uingiliaji kati zinazohusiana na amani na ulinzi hutegemea hasa

ushirikiano na wadau wa eneo husika na umiliki wao wa mchakato huo. Kujifunza kutokana

na nchi zingine zenye udhaifu na zinazokumbwa na migogoro pia kunaweza kusaidia. Umoja

wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watashughulikia mambo yote yanayohusiana na uzuiaji

na utatuaji wa dhuluma ya kimapenzi na yenye msingi wa kijinsia wakati wa migogoro na

baada ya migogoro kutokea, usuluhishaji wa migogoro, kuleta afueni na utulivu, na kukuza

amani inayodumu.

Page 34: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 34

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

69. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watatekeleza hatua ya usaidizi wa kibinadamu na

ushirikiano katika maendeleo kwa njia yenye ushikamano na kukamilishana zaidi,

wakichangia kwa uamilifu katika kujenga ustahimilivu wa watu binafsi, jumuiya, jamii na

nchi, wakishughulikia umaskini uliokidhiri, kuzuia na kukabiliana na hali za hatari,

wakipunguza udhaifu wa kila wakati na kujenga uwezo wa kujitegemea. Suluhu za kudumu

zinahitaji mitazamo inayowashirikisha wadau mbalimbali, uingiliaji kati katika viwango

tofauti na dira ya muda mrefu. Hii inamaanisha kuimarisha uhusiano baina ya utoaji wa

msaada wa kutuliza, na wa kurekebisha na maendeleo, ikiwemo kupitia ubadilishanaji mpana

wa taarifa, uratibu wa wafadhili na uchanganuzi wa pamoja wa mapengo, hatari na udhaifu,

na dira ya pamoja ya mikakati ya kupewa kipaumbele, mapema iwezekanavyo. Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake watahakikisha uhusishwaji wa mapema na ushirikiano wa

karibu baina ya wadau wa kisiasa na wa maendeleo kuanzia mwanzo hadi tamati na kufuata

juhudi za uingiliaji kati za wadau wanaotoa msaada wa kibinadamu wakati wa dharura na

wanaoleta afueni ya mapema majanga yanapotokea. Hii itafanyika kwa njia ambayo

inadumisha kanuni za msaada kwa binadamu kulingana na sheria ya kimataifa ya msaada kwa

binadamu.

70. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataongeza juhudi zao za kukuza ustahimilivu

na uwezo wa kujirekebisha kulingana na mabadilika, kuambatana na, pamoja na mengine,

Utaratibu wa Sendai wa Upunguzaji wa Hatari za Janga wa 2015-2030 na Mkataba wa Paris

kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa. Kusaidia watu na jamii ili wawe wamejitarisha vilivyo,

kupunguza uwezekano wao wa kukumbwa na hatari na udhaifu, na kuimarisha uthabiti wa

kustahimili na kurudia hali ya kawaida baada ya mishtuko na majanga ni muhimu katika

kupunguza madhara zaidi na kuepuka kupoteza maisha na riziki. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama watajumuisha utathmini wa hatari na uchanganuzi wa pengo katika programu

zao za ushirikiano wa mendeleo. Wataendelea pia kukuza uwezo wa kujitayarisha kwa hatari

kwa afya zinazoweza kutokea kati ya mipaka mbalimbali, kulingana na Kanuni za Kimataifa

za Afya, hasa kupitia kutoa uwezeshaji wa mifumo ya afya ya kitaifa na ya kanda na

uboreshaji wa kushiriki taarifa. Wakijifunza kutokana na hali za hatari za afya ya ulimwengu,

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watazidi kuendeleza miradi inayoshirikisha sekta

mablimbali katika viwango vya kimataifa, kanda, na vya eneo husika na watafanya

uimarishaji wa mifumo ya afya ya kiwango kimoja kuwa msingi wa mipangilio ya maendeleo

ya sekta ya afya.

Page 35: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 35

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

71. Uhamaji, maendeleo endelevu na uthabiti yana uhusiano mkubwa. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake wamejitolea kuratibu hatua za kushughulikia vyanzo vikuu vya uhamiaji

usio wa kawaida na uhamishwaji wa kulazimishwa, kama vile migogoro, udhaifu wa nchi,

ukosefu wa usalama na kutengwa, umaskini, ukosefu wa chakula cha kutosha, ukosefu wa

usawa na ubaguzi, uharibifu wa mazingira, ikiwemo mabadiliko ya hali ya hewa.

Wataendeleza haki za binadamu na heshima ya watu, ujenzi wa demokrasia, utawala bora na

utawala wa sheria, ujumuishwaji kwa jamii na utangamano, fursa za kiuchumi zenye kazi zuri

na kupitia biashara zinazozingatia watu, na nafasi ya sera za asasi za jamii. Watakabiliana na

usafirishaji usio halali wa wahamiaji na biashara haramu ya kusafirisha watu, ambavyo

ndivyo vyanzo vya ukosefu wa uthabiti. Ni muhimu kukukuza ushirikiano imara na nchi

ambazo wahamiaji hutoka, kupitia, na kuelekea, kwa kutumia sera za kudumu na za muda

mrefu zinazoshughulikia hali mbalimbali za changamoto hii.

3 USHIRIKIANO – UMOJA WA ULAYA KAMA NGUZO YA UTEKELEZAJI

WA AJENDA YA 2030

72. Huku ikitambua kwamba kila nchi ina wajibu mkuu wa maendeleo yake ya kiuchumi na

kijamii, Ajenda ya 2030 ni lazima itekelezwe na nchi zote na wadau wote kwa ushirikiano.

Tasnia ya maendeleo inazidi kupanuka, na kuwajumuisha wadau wengi zaidi na wapya.

Bunge, vyama vya kisiasa, mamlaka za maeneo na mitaa, taasisi za uchunguzi, mashirika ya

kutoa msaada, vyama vya ushirika, sekta ya kibinafsi na asasi za jamii waote wamekuwa

washirika wakuu katika kuwafikia watu walio dhaifu na waliotengwa zaidi. Uendelezaji na

ulinzi wa nafasi ambapo wadau hawa wanaweza kufanya kazi kwa usalama ni muhimu ili

kufikia maendeleo endelevu.

Page 36: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 36

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

3.1. Kufanya kazi vyema zaidi kwa kushirikiana

73. Ili kushughulikia changamoto za ulimwengu, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

wataboresha zaidi jinsi wanavyoshirikiana, ikiwemo kwa kufanya kazi vyema zaidi kwa

pamoja, wakizingatia faida zinazotokana na uwezo wa kila mwanachama. Hii ni pamoja na

kuboresha ufanisi na matokeo mazuri kupitia uratibu na utangamano zaidi, kwa kutumia

kanuni za ufanisi wa maendeleo na kwa kufanikisha ushirikiano katika maendeleo kama

sehemu moja ya hatua ya jumla ya ndani na nje ya nchi ya kuendeleza utekelezaji wa Ajenda

ya 2030. Ili kufanikiwa zaidi katika kuendeleza malengo haya, na kuambatana na azimio kuu

la kumaliza umaskini, sera ya maendeleo ya Umoja wa Ulaya inapaswa kuwa na uwezo wa

kubadilika na iwe inayoweza kushughulikia mahitaji, hali za hatari na masuala muhimu

yanayobadilika kila siku.

74. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataratibu na kuendeleza misimamo ya pamoja

kuhusu masuala yanayohusiana na sera ya maendeleo katika viwango vya kimataifa. Hii

itaboresha jumla ya ushawishi wa Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake na itachangia

katika majadiliano yenye ufanisi baina ya nchi mbalimbali.

75. Katika kiwango cha nchi, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wataboresha Mipangilio ya

Pamoja katika ushirikiano katika maendeleo ili kuongeza matokeo yao ya jumla kwa kuleta

pamoja rasilimali na uwezo wao. Mipangilio ya Pamoja inapaswa kuendelezwa na

kuimarishwa, na kuwa ya kujitolea kwa hiari, iwe inayoweza kubadilika kwa urahisi, yenye

jumuishi, na inayozingatia muktadha wa nchi, na vile vile inayotoa nafasi ya kubadilisha hati

za mipangilio za Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama na mahali pake kuchukuliwa na hati

za Mipangilio ya Pamoja za Umoja wa Ulaya. Ushirikiano wa nchi washirika,ugavi na umiliki

ni muhimu kwa mchakato huu. Mipangilio ya Pamoja ni lazima iongozwe na mkakati wa

maendeleo wa nchi mshirika na iambatane na vipaumbele vya maendeleo vya nchi mshirika.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama watafanya kazi pamoja ili kuunda hatua za kimkakati

za ushughulikiaji zinazotegemea maarifa ya pamoja, thamani iliyoongezwa, mafunzo na

uchanganuzi wapamoja wa muktadha wa nchi, ikiwemo umaskini na uendelevu, na uhusiano

wa jumla wa nchi na Umoja wa Ulaya. Kwa kufanya hivyo, watazingatia nyenzo

zinazopatikana za ufadhili wa maendeleo, kulingana na Ajenda ya Utendaji ya Addis Ababa.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wataendeleza uratibu ulioboreshwa na nguvu za

pamoja katika nchi zenye udhaifu na zinazoathiriwa na migogoro, ikiwemo kupitia michakato

Page 37: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 37

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

ya Mipangilio ya Pamoja na uchanganuzi wa pamoja wa migogoro. Watachangia pia katika

Makubaliano Mapya ya Ushirikiano katika Nchi zenye Udhaifu.

76. Kuongezeka kwa matumizi ya masuluhisho ya pamoja ya Umoja wa Ulaya unaotokana na

Mipangilio ya Pamoja ya Umoja wa Ulaya kunaweza kuhakikisha kuna matokeo mazuri zaidi

kwa Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake kunaonekana zaidi katika maeneo husika.

Mtazamo huu utasaidia kukusanya rasilimali, kupunguza mgawanyiko na kuzidisha wa

maafanikio. Uangalizi wa pamoja na taratibu za matokeo zitakuwa viungo vikuu vya

ushughulikiaji wa pamoja wa kudumisha kasi, vya kutoa taarifa muhimu katika majadiliano

na kuimarisha uwajibikaji wa pande zote husika. Mipangilio ya Pamoja ni lazima iwe wazi

kwa wafadhili na wadau wengine wa kimataifa wanaohusika jambo iwapo hili

limetathminiwa na Umoja wa Ulaya na wawakilishi wa Nchi Wanachama na kuonekana

linafaa.

77. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya juhudi za kusaidia nchi washirika

kupitia utekelezaji wa pamoja wakati panafaa. Utekelezaji wa pamoja ni njia ya keundeleza

usaidizi wa Umoja wa Ulaya wenye ushikamano, ufanisi na ulioratibiwa kulingana na

malengo ya pamoja katika sekta teule au katika mada maalum kwenye sekta mbalimbali na

yanayolingana na hali za nchi tofauti. Utekelezaji wa pamoja utafuata uchanganuzi wa

pamoja, utazingatia rasilimali zinazopatikana na utaangaliwa na kutathminiwa kwa pamoja.

Utekelezaji wa pamoja unaweza kufanyika katika kiwango cha kitaifa, eneo, au ulimwengu na

unaweza kuunganishwa na nyanja zingine za hatua za nje ya nje kama inavyofaa.

78. Utekelezaji wa pamoja utakuwa jumuishi na wazi kwa washirika wote wa Umoja wa Ulaya

wanaokubali na kuchangia kwa dira ya pamoja, wakiwemo mawakala wa Nchi Wanachama

na taasisi zao zinazofadhili maendeleo, sekta ya kibinafsi, asasi za jamii na wanazuoni. Iwapo

utathmini utaonyesha kuwa ni muhimu, serikali zingine zenye mtazamo sawa zinaweza

kujumuishwa, na vile vile Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa na ya kanda

na taasisi za kifedha. Utekelezaji wa pamoja unaweza kuhusisha mbinu tofauti za ufadhili,

kama vile ufadhili wa pamoja, ushirikiano kupitia wajumbe, na vile vile mbinu za utekelezaji

zisizo za kifedha, na unapaswa kufuata faida zinazoletwa na uwezo wa wadau mbalimbali na

kushiriki kwa mitindo bora zaidi. Katika muktadha huu, Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wakewatendelea kujifunza kutokana na na kushiriki katika matukio ya Nchi

Wanachama wote, ikiwemo matukio ya mpito.

Page 38: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 38

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

79. Kuunda mipango ya maendeleo kulingana na eneo au mada kutafuatilia utaratibu wa miaka

mingi. Katika ushirikiano wao katika maendeleo, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watatumia mbinu tofauti na zinazokamilishana (kama vile usaidizi katika miradi, usaidizi wa

programu ya sekta, usaidizi wa sekta na wa bajeti ya jumla) na njia za utoaji wa msaada

(ushirikiano baina ya miji, usaidizi wa kiufundi na ukuzaji wa uwezeshaji), kulingana na

mbinu itayofaa zaidi kwa kila nchi kwa kuzingatia uwezo, mahitaji, na utendakazi wa nchi, na

vile vile kulingana na hali maalum.

80. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake, inapofaa, watatafuta fursa za kukusanya

rasilimali na kufanya maamuzi ya haraka na yanayoweza kubadilishwa na utekelezaji ili

kuleta matokeo, ufanisi, na kuonekana zaidi kwa ushirikiano wa maendeleo wa Umoja wa

Ulaya wa kutimiza malengo ya maendeleo endelevu (SDG), kupitia miradi, hasa Hazina za

Amana za Umoja wa Ulaya zinazotumika wakati wa dharura, baada ya dharura au matendo

yenye azimio moja, ambayo yanaweza kutoa fursa za utendaji wa pamoja wenye ufanisi wa

Umoja wa Ulaya, Nchi Wanachama na washirika wengine wa maendeleo. Wanafaa kuleta

ufanisi wa usimamizi na thamani nyongeza na wanapaswa kuwa na ujumuishi kwa

kuwashirikisha wafadhili wote, wakiwemo wafadhili wadogo. Tume itahakikisha uwazi kwa

kutoa, kati ya mengine, taarifa za mara kwa mara kwa Bunge na Baraza la Ulaya, na kupitia

kuhusika kwao kunaofaa katika miundo muhimu ya utawala, kulingana na sheria husika ya

Umoja wa Ulaya. Hazina za Amana zitatumia kanuni mbalimbali za ufanisi wa maendeleo na

zitaambatana na vipaumbele vya kudumu vya maendeleo, mikakati ya kitaifa na ya nchi ya

Umoja wa Ulaya na nyenzo na programu zingine muhimu.

Page 39: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 39

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

81. Kazi iliyoratibiwa na Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake kuhusu usaidizi wa bajeti

itasaidia kuendeleza juhudi za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu katika nchi

washirika, kuboresha usimamizi wa uchumi mkubwa na wa fedha za umma, na kuboresha

mazingira ya biashara. Usaidizi wa bajeti, unapoweza kutumika na pamoja na wale walio

tayari kushiriki, utasaidia kuimarisha ushirikiano, mazungumzo ya kisiasa, umiliki wa nchi na

uwajibikaji wa pande zote husika na nchi zinazoendelea, kulingana na kanuni, malengo na

maslahi ya pamoja na kufuatia hali za kisiasa, kiuchumi na kijamii katika nchi washirika.

Usaidizi wa bajeti utatumiwa kuambatana na kanuni za ufanisi wa maendeleo na ambapo hali

ni sawa na mifumo ya udhibiti wa utawala imetekelezwa, na utakuwa pamoja na ukuzaji wa

uwezo, uhamisho wa ujuzi na utaalamu. Hivyo utakuwa nyongeza kwa juhudi za nchi

zinazoendelea za kukusanya mapato mengi zaidi na kutumia vyema kwa kuunga mkono

maendeleo endelevu, na kuendeleza ukuaji jumuishi na utoaji wa nafasi za ajira, umalizaji wa

umaskini, upunguzaji wa ukosefu wa usawa na jamii zenye amani. Usaidizi wa bajeti

unaweza pia kuchangia katika kutatua vyanzo vya udhaifu na katika kuendeleza udhaifu na

ujenzi wa nchi katika mataifa yenye hali za udhaifu au yenye serikali za mpwito.

82. Mchanganyiko wa hiba na mikopo, kama njia ya kufaidi kutokana na fedha za ziada

zinazotoka kwa sekta ya kibinafsi, ni mbinu nyingine muhimu ya kutekeleza Ajenda ya 2030.

Mchanganyiko unajumuisha maeneo yote ya ushirikiano wa Umoja wa Ulaya na nchi za nje

katika sekta zikiwemo kawi, miundo msingi ya uchukuzi na maji, usaidizi kwa mashirika ya

madogo na ya kadiri ya biashara, sekta za kijamii na mazingira. Ushirikiano imara zaidi na

sekta ya kibinafsi utahitajika, kwa kutumia nyenzo za kifedha ili kuvutia ufadhili kutoka kwa

sekta ya kibinafsi kwa ajili ya maendeleo endelevu, ikiwemo kwa lengo la kukabiliana na

mabadiliko ya hali ya hewa. Huku ukihakikisha nyongeza ya usaidizi kwa mapato, na

kuangazia umuhimu wa maendeleo, mchanganyiko utatumiwa kuboresha ufanisi na

kushughulikia kutofauli kwa masoko huku ukipunguza kudhoofika kwa masoko. Shughuli za

mchanganyiko wa ufadhili zitaendeleza uwajibikaji wa mashirika ya kibiashara kwa jamii,

ikiwemo kupitia utekelezaji wa miongozo, kanuni na nyenzo muhimu zinazokubalika

kimataifa. Mchanganyiko wa ufadhili ni sehemu kuu ya Mpango wa Ulaya wa Uwekezaji wa

Nje ya Nchi. Ushirikiano wa karibu na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) na taasisi zingine

za kifedha za Nchi Wanachama kutakuwa sifa kuu ya shughuli za kuchanganya ufadhili za

Umoja wa Ulaya. Taasisi zingine za kifedha za kimataifa zitashirikishwa pia.

Page 40: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 40

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

3.2. Kukuza miungano ya wadau mbalimbali iliyo imara, na jumuishi zaidi

83. Miungano imara ndio msingi wa mtazamo wa Umoja wa Ulaya kwa utekelezaji wa malengo

ya mendeleo endelevu. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya kazi kwa

ushirikiano wa karibu zaidi na wadau wengine wote wanaohusika ili kuendeleza utekelezaji

wa Ajenda ya 2030 na kuimarisha uwezo wao wa umiliki wa demokrasia. Bunge na vyama

vya kisiasa na vile vile mamlaka za eneo na za mitaa ni lazima zitimize wajibu wao

kikamilifu, ikiwemo wajibu wa kuchunguza, pamoja na serikali za kitaifa, na ni lazima

zishiriki kwa uamilifu katika michakato ya kufanya maamuzi. Hii ni pamoja na jukumu

muhimu la bunge za kitaifa na za kanda katika uundaji wa sheria, uidhinishaji bajeti na kwa

kuhakikisha serikali zinawajibika.

84. Serikali za kitaifa zina wajibu mkuu wa utekelezaji wa Ajenda ya 2030. Kwa kushirikiana na

nchi washirika, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watasisitiza upya umiliki wa

nchi, ushirikiano na majadilano, ili kuchangia katika ufanisi zaidi. Watatoa msaada kwa

upangaji mpana na jumuishi katika nchi zinazoendelea na unaofuata mikakati ya maendeleo

ya kitaifa na ya taifa dogo, programu na bajeti. Wataendeleza mazungumzo wazi ya serikali

na wadau wote katika awamu za kufanya maamuzi, kupanga, kutekeleza na kutathmini.

Michakato ya aina hiyo itasaidia serikali za kitaifa kukadiria mbinu za utekelezaji

zinazopatikana, kutambua mapengo na kuchagua nyanja zinazofaa kwa maendeleo na

ushirikiano mwingine katika ngazi ya kimataifa.

85. Baadhi ya malengo ya msingi yatakuwa ni kukuza uwezo wa nchi zinazoendelea wa

kutekeleza Ajenda ya 2030 katika ngazi za eneo, kanda, na kitaifa, ili kuendeleza mazingira

ya sera yanayofaa, hasa kwa jamii zilizotengwa zaidi, na kuunga mkono kujifunza na

kushiriki ujuzi. Hii itajumuisha pia kuunga mkono ukusanyaji na matumizi bora ya fedha za

umma za nchi, ambao ndio chanzo kikubwa na imara zaidi cha ugharamiaji wa maendeleo

endelevu. Itajumuisha pia kuenldeza mifumo ya Serikali ya kieletroniki ili kusaidia katika

ukusanyaji bora wa kodi na uwazi katika matumizi ya fedha za umma. Umoja wa Ulaya na

Nchi Wanachama wake wataunga mkono ukuzaji wa uwezo katika taratibu za uangalizi

zinazomilikiwa na taifa, ukusanyaji, ugawanyaji na uchanganuzi bora wa data kupitia nyenzo

za uangalizi za kidijitali na ushikamano wa sera kwa ajili ya maendeleo endelevu.

Page 41: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 41

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

86. Utimizaji wa mengi ya malengo ya maendeleo endelevu unategemea sana uhusishwaji amilifu

wa mamlaka za mitaa na za eneo. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataunga

mkono mabadiliko yenye nia ya kuleta uwazi, uwajibikaji na ugatuzi, inapofaa, ili

kuziwezesha mamlaka za eneo na za mitaa kuwa na utawala bora na matokea mema ya

maendeleo, na kushughulikia vyema ukosefu wa usawa ndani ya nchi. Wataunga mkono

michakato ya kusaidia watu kushirikiana vyema na serikali katika ngazi zote za kupanga na

kutekeleza sera, na wataimarisha ushirikiano wao na mamlaka za mitaa na zingine za kiwango

kidogo cha taifa, ikiwemo kupitia ushirikiano uliogatuliwa.

87. Utekelezaji fanifu wa Ajenda ya 2030 unahitaji pia kuendeleza miungano imara zaidi kando

na ile ya serikali. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watapanua miungano na sekta

ya kibinafsi, asasi za jamii, ikiwemo miungano ya wafanyakazi na mashirika ya waajiri,

mashirika ya kimataifa na ya kanda, wanazuoni, watu wanaoishi/kufanya kazi katika nchi za

nje na wadau wengine husika. Wataendelea kuunga mkono ukuzaji wa uwezo wa wadau

hawa, ili kuwapa nafasi ya kutimiza wajibu wao wa kuunda, kutekeleza, kuangalia na

kutathmini mikakati ya maendeleo endelevu.

88. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watazidisha ushirikiano wao na mashirika ya

kiraia katika kuunga mkono maendeleo endelevu. Wataendeleza nafasi na mazingirira ya

mashirika ya kiraia yanayowawezesha kuendeleza shughuli zao, kwa ushirikishwaji kamili wa

umma, ili kuwapa nafasi ya kutimiza wajibu wao kama watetezi huru, watekelezaji na

waendeshaji wa maendeleo, katika kutoa elimu ya maendeleo na uhamasishaji na katika

kuangalia na kuhakikisha mamlaka zinawajabika ipasavyo. Wataunga mkono kujitolea kwa

mashirika ya kiraia kwa ushirikiano katika maendeleo wenye ufanisi, uwazi, uwajibikaji na

unaonuia kuleta matokeo mazuri.

89. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watatambua jukumu kuu la sekta ya kibinafsi

kama injini ya maendeleo endelevu ya kudumu na haja ya kushirikiana nayo kupitia

mazungumzo yenye utaratibu na malengo ya pamoja ya maendeleo. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake wataendeleza mipangilio halisi ya ushirikiano ambayo inashirikisha

wengine, ina uwazi, na inayotoa nafasi kwa biashara, raia na wadau wengine kushiriki.

Wataunga mkono shughuli za biashara zilizo endelevu na zenye maadili mema na kuunda

vichochezi vya uwekezaji wa sekta ya kibinafsi katika maendeleo endelevu ya ulimwengu.

Page 42: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 42

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

90. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataimarisha ushirikiano wao na mashirika ya

kimataifa, ukiwemo mfumo wa Umoja wa Mataifa, Hazina ya Fedha ya Kimataifa, Kundi la

Benki ya Ulimwengu, benki za maendeleo za kanda, G7, G20, Shirika la Ushirikiano wa

Kiuchumi na Maendeleo (OECD) na taasisi zingine za kanda na za kimataifa. Watawahimiza

kuambatanisha upangaji wao wa kimkakati na shughuli za uendeshaji na Ajenda ya 2030 na

kukuza usaidizi ulioratibiwa na unaofaidi pande zote katika utekelezaji wake, kulingana

kikamilifu na mikakati ya kitaifa ya maendeleo endelevu. Ili kuboresha ufanisi wa Umoja wa

Mataifa na mfumo wake wa maendeleo, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

wataendeleza mabadiliko na nguvu za pamoja ndani ya Umoja wa Mataifa, katika ngazi ya

Ofisi kuu na pia katika kiwango cha nchi, wakiwa na nia ya kuufanya mfumo wa Umoja wa

Mataifa kuwa wa ‘kufanya kazi kwa pamoja’. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

wataendeleza kushiriki kwa nchi zinazoendelea katika usimamizi wa mashirika ya kimataifa.

3.3 Kuambatanisha ushirikiano katika maendeleo na uwezo na mahitaji

91. Ushirikiano katika maendeleo utaendelea kufuata muktadha wa nchi au eneo, kulingana na

mahitaji, mikakati, vipaumbele na rasilimali za washirika wenyewe. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake watashirikiana na nchi zinazoendelea kwa njia tofauti zaidi na kwa jinsi

inayozingatia muktadha husika. Miungano inapaswa kujumuisha ushirikiano katika

maendeleo na usaidizi wa kifedha, lakini pia ujumuishe ndani mikakati, sera na nyenzo

mbalimbali, ili ushughulikie ongezeko la hali tofauti za nchi zinazoendelea.

Page 43: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 43

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

92. Huku ukiheshimu vipaumbele vya kila Nchi Mwanachama, ushirikiano katika maendeleo wa

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake utalenga pale ambapo kuna haja kubwa zaidi na

ambapo unaweza kuleta matokeo mazuri zaidi, hasa katika Nchi Zilizo na Maendeleo

Machache zaidi na katika hali za udhaifu na migogoro. Nchi hizi, ambazo nyingi hupatika

barani Afrika, zina idadi kubwa na inayozidi kuongezeka ya watu maskini zaidi ulimwenguni

na zina uwezo wa chini mno wa mapato na udhaifu mkubwa katika mbinu za kutimiza

malengo ya maendeleo endelevu. Watazidi kutegemea pakubwa fedha za jamii ya kimataifa

za kufadhili huduma za umma katika siku zijazo. Misaada ya kimataifa ya fedha za umma

ambayo ina masharti nafuu, hasa hiba, ni lazima ielekezwe kwa nchi ambazo zina mahitaji

sana, zikiwemo zile zilizo katika hali ya udhaifu. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watazingatia changamoto mahususi za nchi ambazo zinapanda ngazi kutoka kiwango cha

mapato ya chini hadi kile cha mapato ya kadiri.

93. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watajihusisha na ushirikiano wa maendeleo,

mazungumzo kuhusu sera na kuungana na Nchi zenye Mapato ya Kadiri (MIC) katika

maendeleo endelevu, umalizaji wa umaskini, hatari za wahamiaji zinazoendelea kwa muda

mrefu na maslahi mengine ya pamoja. Wataleta pamoja ushirikiano wa kisiasa, kiulinzi,

kiuchumi, kisayansi, kiufundi, kiteknolojia na kifedha, kama inavyofaa. Mazungumzo kuhusu

sera na mabadiliko kwa umma yatatilia maanani sifa tofauti za Nchi zenye Mapato ya Kadiri,

yaendeleze maslahi ya pande zote husika na kutambua vipaumbele vya pamoja, miungano na

kanuni za ushirikiano. Wataunga mkono utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu,

ambayo yanatoa utaratibu wa pamoja na jumuishi wa ushirikiano, na kushughulikia pia mali

na changamoto za umma wa ulimwengu.

Page 44: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 44

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

94. Nchi nyingi zenye Mapato ya Kadiri zina idadi kubwa ya watu wanaoishi katika umaskini

ndani ya mipaka yao na mara nyingi huwa na viwango vya juu vya ukosefu wa usawa na

kutengwa katika jamii. Suala kuu la kuangazia katika ushirikiano na Nchi zenye Mapato ya

Kadiri litakuwa ni kuhakikisha kwamba hakuna yeyote anayeachwa nyuma, kwa kukabiliana

na umaskini na vile vile vizuizi rasmi na visivyo rasmi vya ujumuishwaji katika jamii kupitia

utengenezaji na ugavi sawa wa mali. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watashughulikia pia haja ya kuongeza kasi na kuunga mkono uendelezaji wa mifumo

endelevu ya matumizi na uzalishaji, upunguzaji wa takataka, usimamizi wa kemikali wenye

uwajibikaji na matumizi bora ya rasilimali. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watafanya kazi ili kushiriki utaalamu na kuwezesha uhamisho wa teknolojia na ubadilishanaji

wa mitindo bora, ikiwemo kupitia kuanzisha ulingo wa biashara kwa Mashirika Madogo

zaidi, Madogo Kiasi, na ya Kadiri, kuhimiza uwekezaji wenye uwajibikaji na mabadiliko

katika masuala ya fedha, na badala yake kutumia nishati mbadala, usimamizi endelevu wa

rasilimali asilia na uendelezaji wa utawala bora, utawala wa sheria na haki za binadamu.

95. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataanzisha pia ushirikiano bunifu na nchi

zinazoendelea zilizo juu zaidi kimaendeleo, ikiwemo na zaidi ya ushirikiano wa kifedha, kwa

sababu nchi hizi zinahitaji mbinu chache za usaidizi zenye masharti nafuu au hata hazina haja

ya mbinu hizo. Nchi hizi ni muhimu katika utekelezaji wa Ajenda ya 2030 na kwa maana

uchumi wao ni muhimu, athari zake kwa mali na changamoto za umma wa ulimwengu,

yakiwemo mabadiliko ya hali ya hewa, zinazidi kuongezeka pakubwa.

Page 45: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 45

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Ushirikiano bunifu na nchi zinazoendelea na zilizo juu zaidi kimaendeleo

Nchi zinazoendelea na zilizo juu zaidi kimaendeleo zina athari na ushawishi muhimu ndani ya

maeneo yao, zikiwemo kama vyanzo vya uthabiti wa eneo. Ushirikiano wao na nchi zingine

zinazoendelea unazidi kuongezeka kwa kasi sana na ni sehemu kubwa ya mgao wa ushirikiano wa

kimataifa.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataanzisha miungano mipya na nchi zinazoendelea na

zilizo juu zaidi kimaendeleo ili kuendeleza utekelezaji wa Ajenda ya 2030 kupitia ushirikiano wa

aina mbalimbali. Msingi wa miungano hii ni mazungumzo kuhusu sera na mabadiliko kwa umma.

Mazungumzo kuhusu sera yataendeleza maslahi ya pande zote husika na kutambua vipaumbele vya

pamoja, miungano na kanuni za ushirikiano katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu,

ambayo yanatoa utaratibu wa pamoja na jumuishi wa ushirikiano. Miungano hii mipya itaendeleza

ubadilishanaji wa mitindo bora zaidi, usaidizi wa kiufundi na kushiriki ujuzi. Aidha, Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya kazi na nchi hizi ili kuendeleza ushirikiano baina ya

nchi zinazoendelea, na baina ya nchi zinazoendelea zikisaidiwa na nchi iliyoendelea/zilizoendelea

kulingana na kanuni za ufanisi wa maendeleo.

96. Mikataba, taratibu, mikakati, miungano na sera za kanda zinazohusiana na nchi zote

zinazoendelea zitaongozwa na Makubaliano haya na zatafuata malengo, kanuni na maadili ya

pamoja. Wataendeleza utekelezaji wa Ajenda ya 2030 katika ngazi ya kanda na nchi

washirika, zikiwemo zile zilizo Afrika, Karibia na Pasifiki, na vile vile zilizoko Amerika ya

Kusini na Asia.

97. Makubaliano haya yataongoza hatua za Umoja wa Ulaya katika nchi zinazoendelea za

maeneo jirani kwa ushikamano na kuambatana na Sera ya Ujirani ya Ulaya. Umoja wa Ulaya

na Nchi Wanachama wake watatumia nyenzo mbalimbali katika ujirani wao, kuambatana na

hatua zingine za Umoja wa Ulaya chini ya Ajenda ya 2030.

Page 46: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 46

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

4. KUIMARISHA MBINU ZA KUBORESHA MATOKEO YA HATUA

ZINAZOCHUKULIWA NA UMOJA WA ULAYA

4.1. Kuleta pamoja na kutumia ipasavyo mbinu zote za utekelezaji

98. Ili kuonyesha utaratibu uliowekwa katika Ajenda ya Utendaji ya Addis Ababa (AAAA) na

Ajenda ya 2030, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake ni lazima wabadilishe mtazamo

wao ili kuleta pamoja na kutumia vizuri mbinu zote za utekelezaji, ikiwemo kupitia mifumo

bunifu ya ufadhili. Hii inahitaji kuangazia upya kuanzisha mazingira ya sera yanayowezesha

na kufaa katika ngazi zote. Hii ni pamoja na kukusanya na kutumia ipasavyo fedha za umma

za ndani ya nchi na za kimataifa, kuleta pamoja sekta ya kibinafsi ya ndani ya nchi na ya

kimataifa, kuimarisha uwezo wa nchi washirika wa kuleta mabadiliko, kuchochea biashara na

uwekezaji, kukuza sayansi, teknolojia na ubunifu, na hata kushughulikia changamoto na

kufaidi kutokana na matokeo mazuri ya uhamaji.

99. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watafanya kazi na nchi washirika ili kuendeleza

mazingira mazuri ya sera kwa ajili ya utekelezaji wa Ajenda ya 2030. Wataunga mkono

uwezo wa nchi wa kuunda na kutekeleza sera jumuishi za kitaifa za maendeleo endelevu na

taratibu za matokeo na vile vile kuongeza uwajibikaji na ushughulikiaji wa maslahi ya raia.

Wataendeleza sera zinazounganisha hatua za umma na za sekta ya kibinafsi zinaounga mkono

maendeleo na mazingira yanayowezesha ukuaji jumuishi na endelevu na ugavi wake kwa njia

ya usawa kupitia bajeti za kitaifa. Watapanga ushirikiano wao katika maendeleo wakizingatia

uimarishaji wa uwezo wa kila nchi wa kutekeleza Ajenda ya 2030 na kutimiza mahitaji na

maazimio ya raia wake.

100. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataangazia zaidi kuzalisha rasilimali za ziada

kwa ajili ya maendeleo endelevu katika nchi washirika. Hii itajumuisha kuendeleza

ukusanyaji wa rasilimali za ndani ya nchi, kuendeleza mazingira ya kuongeza ufadhili kutoka

kwa sekta ya kibinafsi ya ndani ya nchi, kuimarisha biashara ya kimataifa kama injini ya

maendeleo na kukabiliana na vyanzo na matumizi haramu wa fedha zisizotozwa ushuru.

Page 47: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 47

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Kukusanya na kutumia rasilimali za nchi

Kuboresha ukusanyaji wa rasilimali za ndani ya nchi ni muhimu kwa juhudi zote za serikali za

kufikia ukuaji jumuishi, umalizaji wa umaskini na maendeleo endelevu. Unaongeza uhakika na

uthabiti wa ugharamiaji wa maendeleo endelevu na kupunguza utegemeaji wa msaada. Pamoja na

usimamizi bora wa matumizi ya umma, ukusanyaji wa rasilimali za nchi unatoa mali na huduma za

umma mahali zinapohitajika, nahivyo kuimarisha kandarasi ya kijamii baina ya serikali na raia.

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza ukusanyaji na matumizi fanifu na bora

ya rasilimali, ikiwemo kupitia mipango kama vile mtazamo wa ‘Kusanya Zaidi, Tumia Vyema

Zaidi’. Watakabilianana wanaokwepa na kuhepa kulipa ushuru, vyanzo na utumiaji haramu wa

pesa, na ubora, ufanisi na usawa wa mifumo ya ukusanyaji ushuru na wa ufadhili wa ulinzi wa

kijamii. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake pia wataunga mkono Mpango wa Ushuru wa

Addis (Addis Tax Initiative) na kazi ya Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo

(OECD)/G20 ya kushughulikia tatizo la kampuni zinazohamisha faida zao kwa nchi zisizotoza

ushuru wa juu/zenye shughuli chahce za biashara, ikiwemo utoaji ripoti wa kila nchi na

ubadilishanaji wa taarifa za ushuru, ili kuhakikisha kwamba kampuni zinalipa ushuru unaolingana

na faida na shughuli zao za kibiashara. Wataunga mkono kushiriki kwa nchi zinazoendelea katika

usimamizi wa ushuru wa ulimwengu na majadiliano muhimu ya kimataifa na michakato ya kuweka

viwango, ikiwemo katika Jukwaa la Ulimwengu kuhusu Uwazi na Ubadilishanaji wa Taarifa kwa

Madhumuni ya Ushuru na majadiliano ya G20/Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo

(OECD). Wanajitolea kuendeleza ushikamano baina ya sera zao za ushuru na athari zake kwa nchi

zinazoendelea.

Page 48: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 48

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

101. Mapato ya nchi yanayotokana na ulipaji ushuru ni muhimu katika kutekeleza Ajenda ya 2030

katika nchi zote. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watongeza usaidizi kwa nchi

zinazoendelea katika juhudi zao za kuimarisha ukusanyaji wa mapato, usimamizi wa ulipaji

wa madeni na gharama za umma, za kuanzisha mifumo ya ushuru, kuongeza ubora na ufanifu

wa matumizi ya umma na kumaliza ruzuku za mafuta ya petroli yenye madhara kwa

mazingira. Usaidizi Rasmi wa Maendeleo una jukumu muhimu katika kupiga jeki juhudi za

nchi – hasa zile ambazo ni maskini na dhaifu zaidi – za kukusanya rasilimali zilizoko ndani ya

nchi. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanaweza kuchangia katika kuboresha

ufanisi wa uwekezaji wa umma katika nchi washirika kwa kuunga mkono mifumo ya uthabiti

wa uchumi mkubwa na wa kifedha, sera na mabadiliko bora ya sekta, taratibu pana za bajeti

za baada ya kila mwaka na nusu muhula na mifumo ya usimamizi unaofaa wa fedha za umma,

ikiwemo ununuzi wazi na endelevu.

102. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake ni wakarimu katika kutoa msaada wa ushirikiano

kwenye maendeleo, na wametoa zaidi ya nusu ya Usaidizi Rasmi wa Maendeleo kote

ulimwenguni katika miaka ya hivi majuzi. Ingawa Usaidizi Rasmi wa Maendeleo ni wa

kiwango kidogo kwa ujumla kwa nchi zinazoendelea, ni chanzo kikuu cha fedha kwa nchi

zilizo maskini zaidi na Nchi zenye Maendeleo Machache Zaidi, ambazo hazina uwezo wa

kupata fedha kutoka vyanzo vingine. Usaidizi Rasmi wa Maendeleo unaweza kunufaika pia

na mbinu zingine za utekelezaji, hasa ufadhili wa umma wa ndani ya nchi na uwekezaji wa

sekta ya kibinafsi, na hata pia sayansi, teknolojia na ubunifu.

103. Umoja wa Ulaya kwa pamoja umejitolea kutoa asilimia 0.7 ya Jumla ya Mapato ya ya Taifa

(GNI) kama Usaidizi Rasmi wa Maendeleo kuambatana na ratiba ya Ajenda ya 2030. Ili

kuelekeza rasilimali pale ambapo zinahitajika zaidi, hasa Nchi zenye Maendeleo Machache

Zaidi na zile zilizo kwenye hali za udhaifu na migogoro, Umoja wa Ulaya umehapa kutimiza

kwa pamoja lengo la asilimia 0.15-0.20 ya Usaidizi Rasmi wa Maendeleo/Jumla ya Mapato

ya Taifa kwa Nchi zenye Maendeleo Machache Zaidi katika kipindi kifupi, na kufikisha

asilimia 0.20 ya Usaidizi Rasmi wa Maendeleo/Jumla ya Mapato ya Taifa kwa Nchi zenye

Maendeleo Machache Zaidi kuambatana na ratiba ya Ajenda ya 2030. Umoja wa Ulaya na

Nchi Wanachama wake pia wanatambua changamoto mahususi zinazozikumba nchi za

Afrika. Kwa hili, Umoja wa Ulaya unasisitiza umuhimu wa kuelekeza Usaidizi Rasmi wa

Maendeleo kwa bara hilo huku ukiheshimu vipaumbele vya kila Nchi Mwanachama katika

usaidizi wa maendeleo. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanatilia mkazo ahadi

zao za Usaidizi Rasmi wa Maendeleo za kila mmoja na za pamoja na watachukua hatua halisi

Page 49: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 49

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

na zinazoweza kuthibitishwa kutimiza ahadi hizi. Wataendelea kuangalia maendeleo na kutoa

ripoti kila mwaka ili kutoa nafasi ya uwazi na uwajibikaji kwa umma.

104. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake pia wataendelea kuimarisha ukusanyaji wa fedha

za kugharamia miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kama sehemu ya juhudi

za ulimwengu, hasa kwa kutoa uungaji mkono imara kwa juhudi za kupunguza visababishi na

athari za mabadiliko ya hali ya hewa katika nchi zinazoendelea, kulingana na masharti chini

ya Utaratibu wa Kanuni kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa wa Umoja wa Mataifa na

Mkataba wa Paris. Wanatambua haja ya kuongeza juhudi na ufadhili wa kukabiliana na athari

za mabadiliko ya hali ya hewa na upunguzaji wa ongezeko la hali joto duniani, ikiwemo

kupitia sera zao za ushirikiano na nchi za nje ya Umoja wa Ulaya na ushirikiano katika

maendeleo. Watajizatiti kuimarisha na kuongeza faida za pamoja za hali ya hewa katika

programu za ushirikiano wa maendeleo. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

wamejitolea kukusanya mgao wao wa lengo la nchi zilizoendelea la kukusanya kwa pamoja

Dolaza Marekani bilioni 100 kila mwaka ifikapo mwaka wa 2020 na hadi mwaka wa 2025 za

kukabiliana na visababishi na athari za mabadiliko ya hali ya hewa, kutoka kwa vyanzo,

nyenzo na mbinu tofauti. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza

mazungumzo ya masuala ya siasa ili kuboresha ahadi kutoka kwa wafadhili wengine.

105. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watazidi kuhakikisha kuwa Usaidizi Rasmi wa

Maendeleo una lengo linalofaa na unatumika kimkakati na kwa ushikamano kulingana na

mbinu zingine za utekelezaji kutoka kwa vyanzo vyote. Kwa muktadha huu, Umoja wa Ulaya

utashirikisha mipangilio ya kupima vyema aina zote za ufadhili wa maendeleo, kama vile

hatua inayopendekezwa ya Jumla ya Usaidizi Rasmi kwa Maendeleo Endelevu ya Shirika la

Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo.

106. Ushirikiano wa maendeleo utasaidia nchi washirika kuleta ukuaji jumuishi kupitia kushiriki

katika biashara ya kimataifa, na vile vile kuimarisha mchango wa sera ya biashara ya Umoja

wa Ulaya kwa maendeleo endelevu. Ushirikiano wa maendeleo utasaidia kuimarisha

ujumuishwaji na utekelezaji wa sura zinazohusu biashara na maendeleo endelevu katika

mikataba ya biashara, upendeleo zaidi wa ufikiaji wa soko la Umoja wa Ulaya kwa nchi zilizo

dhaifu na uungaji mkono wa biashara ya haki na inayoongozwa na maadili mema, na

kuanzisha zaidi sera za kuhakikisha usimamizi wenye uwajibikaji wa mifumo ya usambazaji.

Hii inajumuisha pia kuunga mkono utekelezaji wa Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi na

Mikataba ya Biashara Huru na nchi zinazoendelea, na pia upendeleo wa ufikiaji wa soko la

Page 50: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 50

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

Umoja wa Ulaya bila kutozwa kodi au kuwekewa vikazo unaopewa Nchi zenye Maendeleo

Machache Zaidi kupitia utaratibu wa Kila Kitu isipokuwa Silaha. Kuratibu programu za

msaada na ushirikiano katika sehemu hizi utatoa nafasi ya Umoja wa Ulaya kutumia fursa na

kunufaika na uhusiano wa karibu wa kibiashara ili kuendeleza agenda yake inayofuata kanuni

kwa washirika wake wa biashara.

107. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza matumizi ya mbinu zingine za

utekelezaji, ikiwemo sayansi, teknolojia na ubunifu. Watanuia kutumia vyema zaidi fursa

zitokanazo na sayansi, teknolojia na ubunifu ili kutafuta suluhu mpya kwa changamoto za

ulimwengu, wakizingatia kazi ya Mfumo wa Uwezeshaji wa Teknolojia, Benki ya Teknolojia

ya Nchi zenye Maendeleo Machache Zaidi na mashirika mengine muhimu. Watazidi

kuwekeza katika utafiti na maendeleo katika na kwa nchi zinazoendelea, ikiwemo kwa

uboreshaji wa mifumo ya ubunifu ya kitaifa. Watalenga kuimarisha matokeo yanayopimika

kuhusu hatua za kueleke kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu kupitia mfumo wa Utafiti

na Ubunifu Unaowajibika, ikiwemo ufikiaji wazi wa matokeo na data ya utafiti wa miradi

inayofadhiliwa na umma na elimu kwa ajili ya sayansi.

4.2. Ushikamano wa sera ili kutimiza malengo ya maendeleo endelevu (SDG)

108. Maendeleo endelevu ni msingi wa mradi wa Umoja wa Ulaya na umejikita katika Mikataba,

ikiwemo ya ushirikiano wake na mataifa ya nje ya Umoja wa Ulaya. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake wamejitolea kuleta maendeleo yanayotimiza mahitaji ya sasa bila

kuhatarisha uwezo wa vizazi vijavyo wa kukidhi mahitaji yao. Kuhakikisha ushikamano wa

sera kwa maendeleo endelevu kama ilivyo katika Ajenda ya 2030 kunahitaji kuzingatia athari

ya sera zote kuhusu maendeleo endelevu katika ngazi zote – kitaifa, ndani ya Umoja wa

Ulaya, katika nchi zingine na katika kiwango cha ulimwengu mzima.

109. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wanasisitiza tena kujitolea kwao kwa

Mshikamano wa Sera kwa ajili ya Maendeleo (PCD), ambao unahitaji kuzingatia malengo ya

ushirikiano wa maendeleo katika sera zinazoweza kuathiri nchi zinazoendelea. Hiki ni

kipengele muhimu cha mkakati wa kutimiza Malengo ya Maendeleo Endelevu na mchango

muhimu katika lengo pana la Mshikamano wa Sera kwa ajili ya Maendeleo Endelevu

(PCSD). Ajenda ya 2030 inatoa msukumo kwa Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

kuunda na kutekeleza sera zinazohusisha na kuathiri pande zote.

Page 51: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 51

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

110. Makubaliano haya yataongoza juhudi za kutekeleza Mshikamano wa Sera kwa ajili ya

Maendeleo katika sera na nyanja zote zinazojumuishwa katika Ajenda ya 2030, yakitafuta

nguvu za pamoja, hasa kwa biashara, fedha, mazingira na mabadiliko ya hali ya hewa, uwepo

wa chakula cha kutosha, uhamaji na ulinzi. Masuala ya kukabiliana na fedha zenye chanzo

haramu na zisitozwa ushuru, ukwepaji wa kulipa ushuru, na uendelezaji wa biashara na

uwekezaji unaowajibika yataangaziwa kwa karibu.

111. Kupata matokeo kwa mfumo wa wote wa maendeleo endelevu katika tasnia ya ushirikiano wa

maendeleo ni jukumu la pamoja la wadau wote. Maendeleo endelevu yanahitaji mtazamo wa

sera wa jumla na unaoshirikisha sekta mbalimbali, na bila shaka ni suala la utawala

linalohitaji kuendeleza kwa ushirikiano na wadau wote na katika ngazi zote. Hivyo basi,

Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza mitazamo ya serikali zima na

kuhakikisha juhudi za uangalizi na uratibu wa kisiasa katika viwango vyote kwa ajili ya

utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu. Ili kuunga mkono vizuri uundaji wa sera na

uamuzi, watahakikisha msingi wa uthibitisho wa sera unaleta matokeo kwa nchi

zinazoendelea kupitia mashauriano, ushirikiano na wadau, utathmini wa utabiri wa matokeo

na ukadiriaji wa matokeo ya miradi mikuu ya sera. Hatua za Umoja wa Ulaya zinazoendelea

zenye nia ya kuleta uendelevu katika mifumo ya ulimwengu ya usamabazaji, kama vile katika

sekta za mbao na nguo, zinazonyesha faida ya ziada ya kuendeleza mfumo wa ushikamano.

Miradi ya utekelezaji wa sera, inapofaa, inapaswa kuonyesha jinsi inavyochangia kwa

maendeleo endelevu katika nchi zinazoendelea. Hii ni muhimu pia kwa Umoja wa Ulaya na

Nchi Wanachama wake ili kuboresha utoaji ripoti na uangalizi wao wa Mshikamano wa Sera

kwa ajili ya Maendeleo

112. Kwa kuwa Ajenda ya 2030 inawahusisha watu wote, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama

wake watahimiza pia nchi zingine zitathmini athari za sera zao wenyewe katika kutimiza

Malengo ya Maendeleo Endelevu, ikiwemo katika nchi zinazoendelea. Aidha, Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake wataimarisha mazungumzo na nchi washirika kuhusu

mshikamano wa sera na kusaidia nchi washirika katika juhudi zao za kutekeleza taratibu za

kuwezesha mshikamano wa sera kwa ajili ya maendeleo endelevu. Wataongoza katika

kuendeleza mshikamano wa sera katika ngazi za kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa na

G20, kama sehemu ya uungaji mkono wa jumla kwa Ajenda ya 2030 katika ushirikiano wao

na nchi zingine zisizo za Ulaya.

Page 52: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 52

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

4.3 Ufanisi wa maendeleo

113. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watasisitiza kujitolea kwao katika kutumia

kanuni kuu za ufanisi wa maendeleo kama zilivyokubaliwa huko Busan mnamo mwaka wa

2011 na kusasishwa katika Kongamano la Ngazi ya Juu la Nairobi mnamo mwaka wa 2016.

Wanajitolea kuimarisha uangaziaji wa matokea, kuboresha uwazi na uwajibikaji wa pande

zote husika, kuboresha umiliki wa nchi na kuendeleza miungano jumuishi ya maendeleo.

Wanatambua haja ya rasilimali zote za maendeleo na washirika wote kufanya kazi pamoja

kwa ufanisi ili kuleta matokeo endelevu na kuhakikisha hakuna yeyote anayeachwa nyuma

kimaendeleo. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza kazi hii kwa

wahusika wote, ikiwemo katika muktadha wa Muungano wa Ulimwengu mzima kwa ajili ya

Ufanisi wa Ushirikiano wa Maendeleo (GPEDC). Ushirikiano wao wa maendeleo

utaendelezwa kwa kushirikiana kwa karibu na washirika wengine na kwa kuwa wazi

kikamilifu kwa raia walio Ulaya na wale wa nchi zinazoendelea.

114. Kanuni za ufanisi wa maendeleo zinatumika kwa aina zote za ushirikiano wa maendeleo. Hii

inajumuisha fedha za umma za kimataifa, kama vile Usaidizi Rasmi wa Maendeleo na

ushirikiano baina ya nchi zinazoendelea na baina ya nchi zinazoendelea wakihusisha ufadhili

kutoka kwa nchi zilizoendelea, mikopo yenye masharti nafuu na isiyokuwa na masharti nafuu,

na shughuli za wadau wa asasi za jamii, sekta ya kibinafsi na wakfu wa wahisani. Umoja wa

Ulaya na Nchi Wanachama wake wanatarajia washirika wote wa maendeleo wajumuishe

kanuni hizi katika shughuli zao wenyewe, kuambatana na hali husika.

115. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watazidi kutetea uwazi, ambao unapaswa

kuendelea kutekelezwa katika rasilimali mbalimbali za maendeleo. Wataanzisha nyenzo za

kuwasilisha na kutumia ipasavyo data ya ya ushirikiano katika maendeleo. Watasaidia nchi

washirika kuunganisha rasilimali za maendele na matokeo, kwa kuunganisha vyema zaidi

michakato ya uandalizi na uundaji bajeti ili kuboresha michakato na viwango vya uwajibikaji.

Page 53: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 53

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

116. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendeleza na kuangalia zaidi matumizi ya

mifumo ya nchi katika mbinu za usaidizi, ambapo ubora unaruhusu, ikiwemo katika kiwango

cha chini kabisa, ili kusaidia kuboresha umiliki wa demokrasia na ufanisi wa taasisi katika

ngazi ya kitaifa na ngazi dogo ya taifa. Watatathmini kwa pamoja ufanisi wa mifumo ya nchi

washirika, ili kuhakikisha ina utaratibu wenye ujuzi na ulioratibiwa. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake watajibidiisha kutoa usaidizi usio na masharti ya mahali pa kununua bidhaa

au huduma na kuhimiza wote wanaoshirikiana katika maendeleo, zikiwemo nchi za uchumi

unaoibuka, kufanya vivyo hivyo. Wanalenga kuweka wazi zaidi maana ya usaidizi usio na

masharti ya mahali pa kununua bidhaa au huduma ili kuhakikisha kwamba watoaji wa

kimataifa usaidizi wa kifedha, wakiwemo washirika wa maendeleo wanaoibukia, wanatoa

masharti ya msaada wao vilevile.

5. KUFUATILIA AHADI ZETU

117. Kuhusiana na ushirikiano wa maendeleo, Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

wamejitolea kikamilifu kufuata mfumo pana, wazi, na wenye uwajibikaji wa kuangalia na

kutathmini kusudi la utekelezaji wa Ajenda ya 2030. Hii inajumuisha uwajibikaji kwa raia wa

Umoja wa Ulaya, ikiwemo kupitia bunge za Ulaya na za kitaifa.

118. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake wataendelea kubadili mifumo yao ya utoaji ripoti

katika tasnia ya ushirikiano wa maendeleo ili iambatane na michakato na viashiria vya

ufuatiliaji vya Ajenda ya 2030. Wataimarisha ubora na upatikanaji wa data kuhusu shughuli

za ushirikiano wa maendeleo, katika Ajenda yote ya 2030. Watafanya kazi kuhakikisha utoaji

ripoti una ulinganifu na kuambatana zaidi na ule wa mikataba mingine ya kimataifa.

119. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watajumuisha Ajenda ya 2030 na kuunga mkono

matumizi ya viashiria vya Malengo ya Maendeleo Endelevu ili kupima matokeo ya

maendeleo katika kiwango cha nchi. Hasa, viashiria vya Malengo ya Maendeleo Endelevu

vinaweza kukuza na kuwezesha mfumo wa pamoja wa Umoja wa Ulaya unaonuia kuleta

matokeo na unapoendelea utoaji ripoti ya matokeo yaliyosawazishwa katika kiwango cha nchi

mshirika, zikiwemo taratibu za matokeo katika kiwango cha nchi mshirika, iwapo zipo.

Page 54: MAKUBALIANO MAPYA YA ULAYA KUHUSU MAENDELEO · jukwaa kuu la utendaji, ambapo maelewano ya pamoja yataendelezwa, maendeleo yatarekebishwa mara kwa mara na hatua za usaidizi zinazofaa

SN 3109/17 YML/ik 54

DG C 1 USAMBAZAJI

KWA UMMA

UMEDHIBITIWA

SW

120. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watatoa ripoti ya pamoja ya mukhtasari wa

Makubaliano kuhusu Maendeleo ikiwemo matokeo ya hatua zao za kuunga mkono Ajenda ya

2030 katika nchi zinazoendelea, kama mchango wa Umoja wa Ulaya ukiripoti kwa Jukwaa la

Kisiasa la Ngazi ya Juu la Umoja wa Mataifa (HLPF), unapokutana katika ngazi ya Viongozi

wa Nchi kila baada ya miaka minne. Ripoti hii itatumia na kufuata ripoti zingine muhimu za

Umoja wa Ulaya, ikiwemo kutoa ripoti kuhusu matokeo, Usaidizi Rasmi wa Maendeleo,

uwajibikaji katika ufadhili wa maendeleo, Ushikamano wa Sera kwa ajili ya Maendeleo, na

uangalizi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu katika muktadha wa Umoja wa Ulaya.

121. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake watainua uwezo wa kitakwimu wa nchi

zinazoendelea, ikiwemo kupitia kuimarisha uwezo wa uzalishaji na uchanganuzi wa data, ili

kuongoza sera na katika kufanya maamuzi. Data hii inapaswa kugawanywa inapowezekana

kulingana na mapato, jinsia, umri na mambo mengine, na kutoa taarifa kuhusu makundi

yaliyotengwa, dhaifu na ambayo ni vigumu kuafikia, utawala jumuishi na masuala mengine,

kuambatana na mtazamo unaozingatia haki wa Umoja wa Ulaya. Itajumuisha pia uwekezaji

katika taasisi imara zaidi za takwimu katika kiwango kidogo cha kitaifa, kiwango cha kitaifa

na cha eneo, na matumizi ya teknolojia na vyanzo vipya vya data. Umoja wa Ulaya na Nchi

Wanachama wake watahimiza nchi zao washirika kujumuisha michango ya jamii

zilizotengwa katika kuangalia malengo ya maendeleo endelevu na kuendeleza mbinu hali za

kufikia lengo hili.

122. Aidha, elimu na uhamasishwaji kuhusu maendeleo inaweza kuchangia pakubwa katika kuinua

viwango vya ushirikiano miongoni mwa umma na katika kushughulikia Malengo ya

Maendeleo Endelevu katika ngazi ya kitaifa na ulimwengu, na hivyo kuchangia katika uraia

wa ulimwengu mzima.

123. Utathmini wa katikati ya muhula wa utekelezaji wa Makubaliano haya utafanyika ifikapo

mwaka wa 2024. Itaainisha jinsi Makubaliano haya yametumika na yapi yametimiza katika

kuunga mkono utekelezaji wa Ajenda ya 2030. Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake

watapima maendeleo kwa utaratibu na kubadili vitendo vyao ili kuhakikisha ushirikiano wao

katika maendeleo, ikiwemo kupitia uhusiano wake na nyanja za sera husika, unaendelea

kuunga mkono utekelezaji wa Ajenda ya 2030 katika nchi zinazoendelea.