mbinu za kufundisha, ujuzi na mikabala...ya upekuzi huhimiza wanafunzi kutafuta habari ndani ya...
TRANSCRIPT
Mbinu za Kufundisha,
Ujuzi na Mikabala Kufundisha na Kujifunza Injili: Kitabu cha Maelekezo cha Waalimu na Viongozi katika Seminari na Vyuo vya
Dini.
Kufundisha ni kazi ngumu na yenye sura nyingi. Orodha ya njia au mbinu za
kufundisha zinaweza kujumuisha maoni mengi na mifano, na majadiliano kamili juu
yao inaweza kujaza kiasi. Inawezekana, hata hivyo, kuziunganisha katika baadhi ya
maeneo ya kawaida ya mafundisho, ujuzi, au mikabala ambayo ni muhimu kwa
mafundisho bora. Sehemu hii itashughulikia baadhi ya maneno haya muhimu.
Unapoamua ni mbinu gani ya kutumia katika kufundisha, ni muhimu kukumbuka
kwamba mbinu na ujuzi ni njia pekee ya mwisho, wala sio mwisho katika na
zenyewe. Waalimu wanapaswa kuchagua njia ambazo zitawasaidia wanafunzi
vyema kuelewa maudhui, mafundisho, na kanuni za umbo la maandiko na
itakayosaidia kujenga na matumizi. Kuweka akilini lengo kwa kutumia ujuzi maalum
au mbinu kutawasaidia waalimu kulitekeleza kwa njia ya maana zaidi. Ni muhimu
pia kukumbuka kwamba bila Roho, hata mbinu bora zaidi za kufundisha na
mikabala haitafaulu.
Maswali [5.1]
―Kuuliza na kujibu maswali ni kitovu cha masomo yote na mafundisho.‖
(Henry B. Eyring, ―The Lord Will Multiply the Harvest‖ [an evening with Elder Henry B.
Eyring, Feb. 6, 1998], 5–6)
Kuuliza maswali yenye ufanisi ni mojawapo wa ujuzi muhimu zaidi mwalimu anaweza
kuendeleza. Wanafunzi wanaweza kukabiliwa na maswali katika harakati ya kuelewa maandiko
na kuwasaidia kutambua na kuelewa kweli muhimu za injili. Maswali pia huwasaidia wanafunzi
kutafakari jinsi injili imebadilisha maisha yao na kufikiri jinsi wanaweza kutumia kanuni za injili
sasa na baadaye. Kuuliza maswali yenye ufanisi kunaweza kuwahimiza wanafunzi kukaribisha
Roho Mtakatifu katika uzoefu wa masomo yao kwa kutumia wakala wao na kutimiza wajibu
wao katika harakati ya masomo.
Inastahili jitihada kubwa kuweza kubuni maswali kwa makini wakati wa matayarisho ya somo
ambayo yataelekeza kwa uelewa na kushirikisha mawazo na mioyo ya wanafunzi wanapojifunza.
Wakati wa kupanga maswali, mwalimu anapaswa kwanza kutambua kusudi ambalo kwalo
wanauliza swali fulani (kwa mfano, mwalimu anaweza kutamani kuwa wanafunzi wagundue
habari ndani ya kifungu cha maandiko, kufikiri juu ya maana ya kifungu, au kushiriki ushuhuda
wa ukweli wa kanuni). Kisha mwalimu anapaswa kubuni swali kwa makini akiwa na lengo hilo
akilini. Maneno machache yaliyochaguliwa yanaweza kuleta tofauti kubwa katika kama au ikiwa
swali halileti matokeo yanayotakikana.
Waalimu wanapaswa kujitahidi kutayarisha na kuuliza maswali yanayohimiza kufikiri na hisia.
Kwa kawaida wanapaswa kuepuka maswali ambayo yanaweza kujibiwa kwa urahisi ―ndio‖ au
―la,‖ au ambapo jibu ni dhahiri kwamba wanafunzi hawahimizwi kwa kufikiri juu yake.
Waalimu wanapaswa kuepuka pia maswali yanayoweza kusababisha utata kwani hii inaweza
kukatisha tamaa wanafunzi na kuleta ubishi darasani, ambayo inahuzunisha Roho (ona 3 Nefi
11:29).
Wakati wa kuuliza maswali darasani, ni muhimu kwa waalimu kuwapatia wanafunzi muda
kufikiri juu ya majibu yao. Wakati mwingine waalimu huuliza swali, kutua kwa sekunde moja au
mbili, na kisha wakati hakuna mtu wa kujibu mara moja, wanaingiwa na hofu na kupatiana jibu
wenyewe. Maswali yafaayo, hata hivyo, mara nyingi yanahitaji mawazo na kutafakari, na
wanafunzi wanaweza kuhitaji muda ili kupata jibu katika maandiko au kubuni jibu lenye maana.
Wakati mwingine inaweza kuwa na manufaa kuwapa wanafunzi muda ili kuandika chini jibu lao
kabla ya kujibu.
Yesu Kristo, Mwalimu Mkuu, alitumia aina mbalimbali za maswali ili kuhimiza wengine
kutafakari na kutumia kanuni Alizofundisha. Maswali yake yalibadilika kulingana na kile
alichokuwa Akitafuta kuleta katika maisha ya wale alikuwa akifundisha. Maswali mengine
yaliwahimiza wasikilizaji Wake kufikiri na kurejea kwa maandiko kwa majibu, kama vile
alipoulizwa, ―Imeandikwa nini katika torati‖ wasomaje? Luka 10:26). Maswali mengine
yalikuwa na lengo la kukaribisha ahadi, kama wakati aliuliza, ―Mnapaswa kuwa watu wa aina
gani?‖ (3 Nefi 27:27).
Wakati kuna aina mbalimbali za maswali mwalimu anaweza kuuliza, kuna aina nne ya maswali
ya kawaida ambayo ni muhimu hasa katika kufundisha na kujifunza injili:
1. Maswali ambayo yanakaribisha wanafunzi kutafuta habari
2. Maswali ambayo yanaelekeza wanafunzi kuchambua kwa ajili ya kuelewa
3. Maswali ambayo yanakaribisha hisia na ushuhuda
4. Maswali ambayo yanahimiza matumizi
Maswali Ambayo Yanakaribisha Wanafunzi Kutafuta habari [5.1.1]
Maswali ya upekuzi husaidia wanafunzi kujenga uelewa wa msingi wa maandiko kwa kuwaalika
kutafuta habari muhimu zinazohusiana na maudhui ya umbo la maandiko. Kwa sababu maswali
ya upekuzi huhimiza wanafunzi kutafuta habari ndani ya maandishi ya maandiko, inafaa kuuliza
maswali kama hayo kabla ya kusoma aya ambapo majibu yanapatikana. Hii inaweka mtazamo
wa mwanafunzi na kuwaruhusu kugundua majibu ndani ya taarifa ya maandiko.
Maswali ya upekuzi kila mara hujumuisha maneno kama vile nani, nini, lini, vipi, wapi, na kwa
nini. Baadhi ya mifano ya maswali ambayo hukaribisha wanafunzi kutafuta habari ni pamoja na:
Kulingana na Mathayo 19:22, kwa nini kijana tajiri aliondoka akiwa na huzuni?
Katika 1 Samueli 17:24, jinsi gani wana wa Israeli walitenda walipoona Goliathi? Jinsi gani
Daudi alitenda katika mstari 26?
Ni shauri gani ambalo Alma alimpa mwanawe Shiblon katika Alma mlango wa 38, mstari wa
5–15?
Majibu kwa maswali ya upekuzi yanapaswa kubuni msingi wa ufahamu muhimu ambao kwao
aina nyingine za maswali yanaweza kujengwa ili kuhimiza uelewa mkubwa na matumizi. Swali
la Mwokozi, ―Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?‖ (Mathayo 16:13) ilitoa usuli wa
habari. Majibu yaliotolewa na wanafunzi Wake yaliwaandaa kwa swali la kindani na lenye hisia
kali, ―Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?‖ Mathayo 16:15
Maswali Ambayo Yanayoelekeza Wanafunzi Kuchambua kwa
Ufahamu [5.1.2]
Maswali ya kuchambua huulizwa kila mara baada ya wanafunzi kujifahamishana na mistari
wanayosoma. Yanaweza kualika wanafunzi kutafuta uelewa mpana na wa kina wa maandiko.
Yanaweza kuwasaidia wanafunzi kuchunguza uhusiano na mwelekeo au kugundua tofauti ndani
ya maandiko. Maswali ya kuchambua karibu kila mara yana zaidi ya jibu moja sahihi.
Maswali ya kuchambua kwa kawaida hutumikia angalau kwa mojawapo wa madhumuni matatu.
Yanaweza kuwasaidia wanafunzi:
Kuelewa vyema muktadha na maudhui ya maandiko.
Kutambua kanuni za injili na mafundisho.
Kuendeleza ufahamu wa kina wa kanuni na mafundisho hayo.
Kuwasaidia wanafunzi kuelewa vyema muktadha na maudhui ya maandiko. Maswali ya
kuchambua yanaweza kuwasaidia wanafunzi kupanua uelewa wao wa maandishi wa kimaandiko
na matukio kwa kuwasaidia kuchunguza vifungu katika muktadha wa kihistoria na usuli wa
kitamaduni, au kwa kuzingatia mafungu mengine ya maandiko. Maswali kama hayo yanaweza
pia kuwasaidia wanafunzi kufafanua maana ya maneno au mafungu na kuwasaidia kuchambua
maelezo ya muhtasari wa hadithi kwa maana kubwa. Mpango huu huandaa wanafunzi kuweza
kutambua kanuni na mafundisho.
Mifano ya aina hii ya maswali ni pamoja na:
Jinsi gani maelezo ya Yesu katika Mathayo 13:18–23 yanatusaidia kuelewa mafundisho Yake
katika mstari wa 3 hadi wa 8?
Ni tofauti gani tunaona kati ya majibu ya Lamani na Lemueli kwa maelekezo ya malaika na
majibu ya Nefi? (ona 1 Nefi 3:31; 4:1–7).
Ni nini kilichosababisha kupotea kwa kurasa 116 na kusababisha Bwana kumshauri Joseph
Smith kwamba ―hapangepaswa kumwogopa mwanadamu zaidi kuliko Mungu‖? (M&M 3:7).
Kuwasaidia wanafunzi kutambua kanuni na mafundisho ya injili. Wanafunzi
wanapoendeleza uelewa wao wa muktadha na maudhui ya maandiko, wanaweza kutambua
vyema kanuni na mafundisho yaliyomo. Kuchambua maswali kunaweza kuwasaidia wanafunzi
kuweka hitimisho na kueleza wazi kanuni au mafundisho yanayopatikana katika umbo la
maandiko (ona sehemu ya 2.5.1, ―Identify Doctrines and Principles‖ on page 26).
Baadhi ya mifano ya maswali haya ni pamoja na:
Ni kanuni gani inayooelezwa na mafanikio ya Nefi katika kupata mabamba za shaba licha ya
shida kubwa? (ona 1 Nefi 3–4).
Ni mafundisho gani kuhusu asili ya Mungu tunayoweza kujifunza kutoka kwa Ono la
Kwanza? (ona JS—H 1:15–20).
Ni somo gani tunaloweza kujifunza kutokana na juhudi zilizofanywa na mwanamke wa
kutokwa na damu kwa kufikia Mwokozi, na majibu Yake kama matokeo? (ona Marko 5:24–
34).
Kuwasaidia wanafunzi kukuza ufahamu mpana zaidi wa kanuni na mafundisho. Kama
ziada ya kutambua kanuni na mafundisho, wanafunzi wanahitaji kuyaelewa kabla ya kutumika
kikamilifu. Maswali yanayoelekeza kwa uelewa mzuri wa maana ya kanuni fulani au
mafundisho, yanayowahimiza wanafunzi kufikiria kuhusu kanuni katika mazingira ya kisasa, au
ambayo yanaalika wanafunzi kueleza uelewa wao wa kanuni ni muhimu hasa. Ifuatayo ni baadhi
ya mifano:
Ni nini itakuwa ushahidi kwamba sisi tulimpenda Mungu na ―mioyo, akili na nguvu zetu
zote?‖ (Moroni 10:32).
Kwa nini kuomba kila mara kutakusaidia kupata nguvu za kiroho ambazo ni muhimu kwa
kushinda majaribu kama vile kusema maneno mabaya kwa wengine au kushiriki katika
burudani ambayo inamchukiza Roho? (ona M&M 10:5).
Ni tabia na sifa zipi unaweza kuona katika maisha ya mtu ambaye alikuwa akijenga juu ya
msingi wa Kristo? (ona Helamani 5:1–14).
Kutumia kile ambacho tumesoma katika Alma 40, jinsi gani unaweza kueleza mafundisho ya
ufufuo kwa rafiki ambaye si wa imani yetu?
Maswali Ambayo Yanaalika Hisia na Ushuhuda[5.1.3]
Maswali fulani huwasaidia wanafunzi kufikiria juu ya na kuelewa kanuni na mafundisho ya injili,
hali mengine yanaweza kuwafanya kutafakari juu ya uzoefu wa kiroho na kusababisha
wanafunzi kuhisi kwa undani ukweli na umuhimu wa kanuni ya injili au mafundisho katika
maisha yao. Mara nyingi hisia hizo huleta hamu ya nguvu katika mioyo ya wanafunzi ili kuishi
kanuni ya injili kwa uaminifu zaidi. Katika hotuba kwa waalimu wa kidini wa MEK, Mzee
Henry B. Eyring alirejea maswali aina hii aliposema:
―Maswali fulani hukaribisha uongozi. Waalimu wa ajabu huuliza hayo. … Hapa kuna swali
lisiloweza kualika uongozi: ‗Nabii wa kweli hutambulika kivipi?‘ Swali hilo linaleta jibu ambalo
ni orodha, kutoka kwa kumbukumbu ya maandiko na maneno ya manabii wanaoishi. Wanafunzi
wengi wanaweza kushiriki katika kujibu. Wengi wanaweza kutoa angalau maoni wastani. Na
akili zote zitachangamshwa.
―Lakini pia tunaweza kuuliza swali kwa njia hii, kwa tofauti kidogo: ‗Wakati gani uliwahi kuhisi
kwamba ulikuwa katika uwepo wa nabii?‘ Hiyo itaalika watu kupekua kumbukumbu zao kwa
hisia. Baada ya kuuliza, tunaweza kusubiri kwa busara kwa muda kabla ya kuita mtu kujibu.
Hata wale wasioongea watafikiria juu ya uzoefu wa kiroho. Hiyo itaalika Roho Mtakatifu‖ (―The
Lord Will Multiply the Harvest,‖ 6).
Maswali hayo hualika wanafunzi kutafakari juu ya siku za nyuma, ―kupekua kumbukumbu zao
kwa hisia,‖ na kufikiria juu ya uzoefu wao wa kiroho unaohusiana na mafundisho ya injili au
kanuni inayojadiliwa. Mara nyingi, maswali haya husababisha wanafunzi kushiriki hisia hizo na
uzoefu au kutoa ushuhuda wa mafundisho au kanuni. Maswali haya husaidia kuleta injili kutoka
katika akili za wanafunzi mpaka ndani katika mioyo yao. Na wakati wanapohisi katika mioyo
yao ukweli na umuhimu wa mafundisho ya injili au kanuni, ni rahisi kwao kuitumia katika
maisha yao.
Hapa kuna mifano fulani ya maswali ambayo yanaweza kuhamasisha hisia na kuleta ushuhuda:
Ni wakati gani ambapo umewahi kuhisi amani na furaha inayotokana kwa kusamehe mtu?
Fikiria juu ya wakati ambapo Bwana aliongoza maamuzi yako kwa sababu ulimwamini
kuliko kutegemea akili zako mwenyewe. (ona Methali 3:5–6) Ulibarikiwa vipi kwa kufanya
hivyo?
Kama unaweza kibinafsi kudhihirisha shukrani zako kwa Mwokozi kwa ajili ya kujitolea
Kwake kwa ajili yenu, ungemwambia nini?
Jinsi gani maisha yako ni tofauti kwa sababu ya kile kilichofanyika katika Kichaka
Kitakatifu?
Ni wakati gani umeona wengine wakikabili majaribu kwa uaminifu? Hayo yamekuvutia
kivipi?
Neno la tahadhari: Majibu ya maswali ya aina hii yanaweza kuwa hasa kibinafsi na nyeti.
Waalimu lazima wahakikishe kwamba wanafunzi kamwe hawahisi kulazimishwa kujibu swali,
kushiriki hisia zao au uzoefu, au kutoa ushuhuda. Kwa ziada, waalimu wanapaswa kuwasaidia
wanafunzi kuelewa asili takatifu ya uzoefu wa kibinafsi wa kiroho na kuwapa moyo ili kushiriki
uzoefu huo vipasavyo. (ona M&M 63:64).
Maswali AmbayoYanahimiza Matumizi [5.1.4]
Hatimaye, lengo la kufundisha injili ni kuwasaidia wanafunzi kutumia kanuni na mafundisho
yanayopatikana katika maandiko na kustahili kupokea baraka zilizoahidiwa wale ambao ni
waaminifu na watiifu. Wanafunzi wanaoweza kuona jinsi walivyobarikiwa kwa kuishi kanuni za
injili katika siku za nyuma watakuwa makini sana na kujiandaa vilivyo kuzitumia kwa mafanikio
katika siku zijazo. Maswali yanaweza kutimiza wajibu muhimu katika kuwasaidia wanafunzi
kuona jinsi wanaweza kutumia kanuni katika hali yao ya sasa na kufikiria jinsi wanaweza
kuzitumia katika siku zijazo.
Ifuatayo ni mifano fulani ya maswali ambayo yanaweza kuwasaidia wanafunzi kufikiria hasa juu
ya njia wanayoweza kutumia kanuni na mafundisho katika maisha yao wenyewe:
Ni mabadiliko gani ambayo ungependa kufanya ili kuweka siku ya Sabato kuwa takatifu ili
uweze kuwa mkamilifu zaidi bila madoa kutokana na ulimwengu? (ona M&M 59:9–13).
Je, ni kitu gani nabii ameshauri ambacho unaweza kufuata kwa usahihi zaidi? (ona Alma
57:1–27).
Ni kwa jinsi gani kanuni hiyo kwamba kama tutatafuta ufalme wa Mungu kwanza,
tutabarikiwa katika maeneo mengine ya maisha yetu itakusaidia kuyapa kipaumbele malengo
yako na shughuli kwa miaka miwili au mitatu ijayo? (ona Mathayo 6:33).
Majadiliano ya Darasa [5.2] Mijadala yenye maana hutimiza wajibu muhimu katika kufundisha na kujifunza injili.
Majadiliano ya darasa hutokea wakati waalimu wanaposhiriki kwa mazungumzo na wanafunzi
na wanafunzi wanaposhiriki kwa mazungumzo mmoja na mwengine kwa njia inayokuza
kujifunza. Mjadala mzuri unaweza kuwasaidia wanafunzi kujifunza umuhimu wa kutafuta
majibu kwa maswali muhimu na thamani ya kusikiliza na kujifunza kutoka kwa maoni, mawazo,
na uzoefu wa wengine. Inaweza pia kuwasaidia wanafunzi kukuza kiwango cha umakinikaji na
ushiriki katika darasa ambalo mara nyingi husababisha ufahamu mpana zaidi wa mafundisho na
kanuni za injili zinazojadiliwa, pamoja na hamu halisi zaidi katika mioyo yao ili kuishi mambo
ambayo wanajifunza na kuhisi.
Yafuatayo ni mawazo fulani ya kuwasaidia waalimu kuelekeza mijadala ya darasa yenye kuvutia
na maongozi.
Panga majadiliano. Kama vile njia zingine za kufundisha, majadiliano huhitaji kutayarishwa
kwa makini na kisha kufanywa chini ya ushawishi wa Roho. Mwalimu anapaswa kuwa
amefikiria jinsi majadiliano yatasaidia wanafunzi kuelewa wanachohitaji kujifunza, ni mfululizo
gani wa maswali utaelekeza kwa dhamira hiyo, jinsi ya kuuliza maswali hayo kwa njia ya ufanisi
zaidi, na jinsi ya kujibu kama jibu la mwanafunzi linaongoza majadiliano katika mwelekeo
usiotarajiwa.
Epuka ufafanuzi mwingi wa mwalimu. Waalimu ambao wanatoa maoni kupita kiasi juu ya
mada ya mjadala wanaweza kuwavunja moyo wanafunzi kutokana na kufanya jitihada za
kushiriki kwa sababu wamejifunza kwamba mwalimu wao mara nyingi ana wahaka wa kutoa
jibu. Ufafanuzi mwingi wa mwalimu unaweza kuwafanya wanafunzi kuhisi kuwa michango yao
haina thamani na kuwasababisha kupoteza hamu.
Alika wanafunzi wote kushiriki. Waalimu wanapaswa kijitahidi kutafuta njia za kualika
wanafunzi vipasavyo kushiriki katika mijadala muhimu, hata wale wanaosita kushiriki kwa
sababu mbalimbali. Waalimu lazima wawe makini wasije wakaaibisha wanafunzi kwa kuwaita
wakati wanajua mwanafunzi hajajiandaa kutoa majibu.
Wakati mwingine mwanafunzi au idadi ndogo ya wanafunzi huelekea kutawala majadiliano ya
darasa. Waalimu wanaweza kuhitajika kuzungumza kwa faragha na watu kama hao,
kuwashukuru kwa upendeleo wao wa kushiriki, kuelezea jinsi ilivyo muhimu kuwahamasisha
washiriki wote wa darasa kushiriki, na kueleza kwa nini hawawezi kuitwa kila wakati
wanapojitolea kujibu.
Ita wanafunzi kwa majina. Kuita wanafunzi kwa majina ili kujibu swali au kutoa wazo
husaidia kukuza mazingira ya kujifunza ya upendo na heshima.
Usiogope ukimya. Wakati mwingine wakiulizwa swali muhimu, wanafunzi pengine hawatajibu
mara moja. Ukimya huu haupaswi kumtia mwalimu wasiwasi kama haujaendelea kwa muda
mrefu. Mara kwa mara, wanafunzi wanahitaji nafasi ya kutafakari juu ya kile wameulizwa na
jinsi wanavyoweza kujibu swali. Mtazamo kama huo unaweza kuwezesha mafundisho kwa Roho
Mtakatifu.
Badilisha swali. Mara kwa mara wanafunzi wanaweza kujikakamua kujibu swali kwa sababu
swali sio wazi. Mwalimu anaweza kuhitajika kubadilisha swali au kuuliza wanafunzi kama
wameelewa kilichoulizwa. Waalimu wanapaswa kujizuia kuuliza maswali kwa mfululizo bila
kuwaruhusu wanafunzi muda wa kutosha kufikiri vya kutosha kwa undani ili kuandaa majibu
sahihi.
Sikiza kwa makini kisha uliza maswali ya kufuatilia. Waalimu wakati mwingine wanakuwa
na wasiwasi juu ya kitu ya kusema au kufanya baadaye kiasi kwamba hawawi makini na kile
wanafunzi wanasema. Kwa kuangalia na kusikiliza wanafunzi kwa makini, waalimu wanaweza
kutambua mahitaji yao na kuongoza majadiliano chini ya uongozi wa Roho Mtakatfu. Waalimu
wanaweza kuhakikisha wanaelewa majibu ya wanafunzi kwa kuuliza maswali kama ―Je,
unaweza kunisaidia kuelewa unachomaanisha kwa hiyo?‖ au ―Unaweza kunipatia mfano wa kile
unachomaanisha?‖ Kuuliza maswali ya kufuatilia mara nyingi kutakaribisha mwanfunzi
kushiriki zaidi ya kile wanachowaza na kuhisi na mara nyingi hualika roho wa ushuhuda katika
majibu. Waalimu wanapaswa kuwakumbusha wanafunzi kusikiliza kila mmoja vile vile na si
kuzungumza wakati mtu mwingine anaongea.
―Chagueni mwalimu miongoni mwenu, na wote wasiwe wazungumzaji kwa wakati mmoja; bali
azungumze mmoja na wengine wote wasikilize maneno yake, ili wote watakapokuwa
wamezungumza wote wapate kujengana.‖
(Mafundisho na Maagano 88:122)
Elekeza upya maoni au maswali ya mwanafunzi. Mara nyingi majadiliano ya darasa hufuata
mfano ambapo mwalimu anauliza swali, mwanafunzi anajibu, na kisha mwalimu anaongeza
ufahamu wake kwa jibu la mwanafunzi kabla ya kuuliza swali linalofuata. Mijadala inaweza
kuwa yenye maana sana, ya kusisimua, na ufanisi wakati mwalimu anaelekeza upya jibu au
maoni kutoka kwa mwanafunzi mmoja kwa wanafunzi wengine. Maswali rahisi kama ―Ni nini
unaweza kuongezea kwa hiyo?‖ au ―Ni nini mawazo yako juu ya maoni hiyo?‖ yanaweza
kujenga mfano ambapo wanafunzi wanajibu wanafunzi. Hii mara nyingi huongeza sana uzoefu
wa kujifunza. Kawaida, isipokuwa wakati uwe mdogo, wanafunzi wote wanaotaka kutoa maoni
wanapaswa kuwa na nafasi ya kuzungumza.
Kubali majibu kwa njia changamfu. Wakati mwanafunzi anatoa majibu, mwalimu anahitaji
kuyatambua kwa namna fulani. Hii inaweza kuwa ―asante‖ ya kawaida au maoni kuhusu majibu.
Wakati majibu yasiyo sahihi yamepeanwa, mwalimu anapaswa kuwa makini asije akaibisha
mwanafunzi. Mwalimu mweledi anaweza kujenga juu ya sehemu ya maoni ya mwanafunzi
ambayo ni sahihi au kuuliza swali la kufuatilia ambalo linaruhusu mwanafunzi kufikiria upya
majibu yake.
Someni Maandiko Pamoja Darasani [5.3] Kusoma maandiko darasani kunaweza kuwasaidia wanafunzi kuzoea na kuelewa vyema aya
wanazosoma. Inaweza pia kuwasaidia kuwa na ujasiri zaidi katika uwezo wao wa kusoma
maandiko wenyewe. Waalimu wanapaswa kuwa waangalifu wasije wakaaibisha wale wasiosoma
vyema au walio na haya sana. Wanafunzi ambao hawapendi kusoma kwa sauti hawapaswi
kulazimishwa kufanya hivyo, lakini waalimu wanaweza kuwatia moyo kushiriki katika njia
ambayo wanajisikia vizuri kwayo. Kwa mfano, kutoa kifungu kifupi cha maandiko kwa
mwanafunzi kabla ili aweze kufanya mazoezi ya kukisoma kunaweza kuwa njia sahihi kwa
mwanafunzi huyo kushiriki katika darasa.
Kuna njia nyingi za kusoma maandiko pamoja katika darasa:
Wawezeshe wanafunzi kusoma kwa sauti, aidha moja kwa moja au kwa pamoja.
Wawezeshe wanafunzi kusoma kwa kila mmoja.
Wawezeshe wanafunzi kusoma kifungu kimya kimya.
Wape wanafunzi tofauti kusoma maneno yaliyosemwa na watu mbali mbali katika hadithi.
Soma kwa sauti kwa wanafunzi wakifuata katika maandiko yao.
Mawasilisho ya Mwalimu [5.4] Wakati umuhimu wa wanafunzi wa kushiriki nafasi hai katika harakati ya masomo ni muhimu
kwa uelewa wao na matumizi ya maandiko, hakubadilishi haja ya mwalimu kuwasilisha habari
ipasavyo nyakati tofauti wakati wanafunzi wanasikiliza. Kwa madhumuni ya kitabu cha
maelekezo hiki, wakati ule mwalimu anapozungumza na wanafunzi wanasikia utaitwa
―mawasilisho ya mwalimu.‖ Yakitumiwa ipasavyo, mawasilisho ya mwalimu yanaweza
kuboresha mbinu zingine za kufundisha. Kama yanatumika kupita kiasi, hata hivyo, shughuli hii
inaozingatia-mwalimu inaweza kupunguza ufanisi wa kufundisha na kupunguza nafasi ya
mwanafunzi ya kujifunza kwa utafiti na imani.
Mawasilisho ya mwalimu yanaweza kuwa mazuri sana wakati wa kufupisha kiasi kikubwa cha
kifaa, kuwasilisha habari mpya kwa wanafunzi, kufanya mabadiliko kati ya maeneo mbalimbali
ya somo, kufanya uamuzi. Mwalimu anaweza kuhitaji kueleza, kufafanua, na kuonyesha ili
kwamba wanafunzi waweze kuelewa wazi muktadha wa umbo la maandiko. Mwalimu anaweza
pia kufafanua mafundisho na kanuni na kuwahimiza wanafunzi kuzitumia. Labda muhimu zaidi,
waalimu wanaweza kushuhudia juu ya kweli za injili na kuonyesha upendo wao kwa Baba wa
Mbinguni na Mwanawe.
Unapotumia mawasilisho ya mwalimu, kama wakati wa kutumia njia yoyote ile, waalimu
wanatakiwa daima kutathmini umakini wa wanafunzi kwa kuwauliza maswali kama: ―Je,
wanafunzi wangu wamevutiwa na ni makini?‖ na ―Je, wanaelewa kinachowasilishwa?‖
Mwishowe, ufanisi wa hii au njia nyingine ya kufundisha inatambulika na kama au la wanafunzi
wanajifunza kwa Roho, kuelewa maandiko, na kutamani kutumia kile wanachojifunza.
Maoni yafuatayo yanaweza kumsaidia mwalimu kutumia mbinu hii kwa ufanisi.
Panga sehemu ya mawasilisho ya mwalimu ya somo. Mara kwa mara, waalimu huandaa kwa
makini sehemu nyingine ya somo lakini hawazingatii kwa usawa sehemu hizo za somo
watakapokuwa wakifanya wingi wa maongezi. Moja ya wasi wasi kuhusu mawasilisho ya
mwalimu ni kwamba wanafunzi wanaweza kuwa kwa urahisi washiriki baridi katika uzoefu wa
kujifunza. Kwa hiyo, mawasilisho ya mwalimu pia yanahitaji maandalizi makini na matayarisho,
ambayo yanajumuisha kuamua jinsi ya kuanza na jinsi ya kukuza mafundisho katika mtindo wa
mantiki.
Wanapopanga matumizi ya mawasilisho ya mwalimu, waalimu wanatakiwa kuzingatia kwa
makini mahali ambapo ni muhimu sana hasa kwa wanafunzi kuchukua nafasi hai. Kwa ujumla,
somo linapoendelea kutokana na kuelewa muktadha na maudhui ya umbo la maandiko kwa
ugunduzi, majadiliano, na utekelezaji wa kanuni na mafundisho, umuhimu wa wanafunzi
kushiriki kuchukua nafasi hai huongezeka.
Changanya mawasilisho ya mwalimu na mbinu zingine.Matumizi bora ya mawasilisho ya
mwalimu darasani ni kuyatumia kama sehemu ya mpango wa jumla wa somo ambalo
linashirikisha mbinu zingine na njia ndani ya mafundisho. Mawasilisho yanapaswa kuwa rahisi
ya kutosha ili kuruhusu mabadiliko kama ni wazi kuwa wanafunzi wamechoka au
wamechanganyikiwa. Kwa njia hii, hata kama waalimu wanazungumza, lengo hubakia juu ya
wanafunzi na katika mafundisho, na mwalimu anaweza kufanya marekebisho inavyohitajika.
Mtu aliwahi kufananisha mawasilisho ya mwalimu na kamba katika mkufu wa lulu. Lulu ni
mbinu mbalimbali ambazo mwalimu hutumia (maswali, majadiliano, kazi ya kikundi,
maonyesho ya kuona na kusikia, nk), lakini zimeshikanishwa na kuunganishwa pamoja kwa
maelekezo na maelezo ya mwalimu. Kamba pekee haiwezi kufanya mkufu kuvutia.
Tumia aina sahihi. Kuna njia ya kutanguliza tofauti katika mawasilisho ya mwalimu. Waalimu
wanaweza kuzuia mfanano kwa kubadilisha kupinda kwa sauti, toni, na ujazo wa sauti na kwa
kuhamia ndani ya chumba wakati mawasilisho yakiendelea. Pia kunaweza kuwa na aina
mbalimbali katika kila aina ya nyenzo inayowasilishwa. Kwa mfano, waalimu wanaweza
kuhusisha hadithi, kutumia ucheshi sahihi, kurejelea picha au maonyesho mengine ya darasa,
kusoma dondoo, kutumia ubao au mawasilisho ya sauti na picha, na kutoa ushuhuda. Aina sahihi
katika mawasilisho ya mwalimu lazima kila wakati yazidishe uwezo wa wanafunzi wa kuelewa
na kutumia kanuni za maandiko.
Hadithi [5.5] Hadithi zinaweza kusaidia kujenga imani ya wanafunzi katika injili ya Yesu Krsito. Zinaweza
kuleta hamu na kuwasaidia wanafunzi kuelewa injili kupitia uzoefu wakilishi. Hadithi zinaweza
kuwa hasa muhimu katika kuwasaidia wanafunzi kuelewa kanuni za injili ambazo
zimetambuliwa ndani umbo la maandiko. Kwa kufafanua kanuni ya injili katika muktadha wa
kisasa, pamoja na muktadha wa maandiko, hadithi zinaweza kuwasaidia kuelewa jinsi kanuni ya
injili inahusiana na maisha yao, pamoja na kuwasaidia kuhisi hamu ya kuishi.
Mzee Bruce R. McConkie alifunza: ―Hakuna kwa hakika, makosa kwa kusimulia hadithi ya
kukuza imani-ya kisasa, ambayo imetokea katika kipindi chetu. Hakika, hii inapaswa kuhimizwa
kwa ukamilifu. Tunapaswa kufanya kila juhudi kuonyesha kwamba mambo hayo hayo
yanafanyika katika maisha ya Watakatifu leo kama ilivyofanyika miongoni mwa waumini wa
kale. …
―Pengine mfano kamili katika kuwasilisha hadithi za kukuza- imani ni kuwafundisha kile
kinachopatikana katika maandiko na kisha kuweka muhuri wa ukweli hai juu yake kwa
kuwaambia jambo kama hilo na sawa na yale yaliyotokea katika kipindi chetu na kwa watu wetu
na —ifaavyo sana—kwetu kama watu binafsi.‖ (―The How and Why of Faith-Promoting
Stories,‖ New Era, July 1978, 4–5).
Waalimu wanaweza kushiriki hadithi kutoka kwa maisha ya manabii na kutokana na historia ya
Kanisa, vile vile hadithi zinazopatikana katika mahubiri ya mkutano mkuu na magazeti ya
Kanisa. Wanaweza pia kushiriki hadithi za kweli kutoka kwa uzoefu wao wenyewe. Baadhi ya
uzoefu wa maana zaidi na wenye matokeo ya kujifunza hutokea wakati waalimu wanapoalika
wanafunzi kushiriki hadithi kutoka kwa maisha yao wenyewe yanayoonyesha jinsi
walivyobarikiwa kwa kuishi kanuni ya injili.
Baadhi ya tahadhari na ushauri unapaswa kukumbukwa kuhusu matumizi ya hadithi.
Kama kuwaambia hadithi kutakuwa mbinu kuu au njia za kufundisha, hadithi zenyewe
zinaweza kuwa kiini cha somo, kupunguza muda halisi unaotumika katika maandiko na
kupunguza maana ya mafundisho na kanuni wanazofundisha.
Matumizi ya hadithi nyingi sana kutoka kwa maisha ya mwalimu mwenyewe inaweza
kusababisha kujitweza kibinafsi na waalimu ―[wanajiinua] wawe nuru ya ulimwengu‖ (2 Nefi
26:29).
Wakati hadithi zinapoweza kuangaza na kuchangamsha kufundisha injili na kuwasaidia
wanafunzi kuhisi uwezo wa Roho, hazipaswi kamwe kutumika kuchezea hisia.
Waalimu lazima wawe makini wasije wakapamba kweli za hadithi ya kweli ili kuifanya kuwa
kubwa zaidi au yenye matokeo.
Ikiwa hadithi si kweli, hadithi kama hiyo yenye vichekesho vinavyoelezea wazo, ni lazima
ielezwe wazi katika mwanzo wa hadithi kwamba si ya kweli.
Mijadala ya Kikundi Kidogo na Kufanya
kazi [5.6] Wakati mwingine kuna manufaa kugawa darasa katika jozi au katika vikundi vidogo vidogo ili
wanafunzi waweze kushiriki katika shughuli za kujifunza au majadiliano ya pamoja. Shughuli za
kikundi kidogo mara nyingi zinaweza kuruhusu idadi kubwa ya wanafunzi kushiriki na zinaweza
kuleta mazingira salama ambapo wanafunzi wanaweza kushiriki hisia, mawazo, na ushuhuda na
kila mmoja. Shughuli hizi zinaweza pia kutoa fursa kwa wanafunzi za kufundisha injili kwa watu
wengine na kusaidia kuwaandaa kufundisha injili katika siku zijazo. Majadiliano katika vikundi
vidogo yanaweza kuhusisha vyema wale ambao wanaonekana kupoteza hamu na usikivu,
pamoja na kuwawezesha wanafunzi kukuza ujuzi wa mawasiliano na kuimarisha uhusiano sahihi
wa kijamii na kiroho. Wanaweza pia kutia matumaini kwa wanafunzi wa akiba, kupata kutoka
kwao ushiriki wenye maana zaidi.
Wakati unaweka wanafunzi kufanya kazi katika majozi au makundi madogo madogo, inaweza
kuwa na manufaa kukumbuka yafuatayo:
Kabla ya kutenganisha wanafunzi katika makundi madogo madogo, waalimu wanatakiwa
kutoa maelekezo dhahiri ya kile wanafunzi watatakiwa kufanya wakati wa shughuli. Mara
nyingi ni muhimu kuandika haya maelekezo kwenye ubao au kuchapishwa kwenye kitini,
kuruhusu wanafunzi kuyarejelea wakati wa shughuli.
Shughuli za kujifunza za kikundi kidogo ambazo ni muhimu kwa maisha ya wanafunzi na
mazingira kwa jumla zinakuza maslahi muhimu na ushiriki.
Kuweka kiongozi wa wanafunzi kwa kila kikundi vile vile wakati maalum husaidia kikundi
kudhibiti kazi. Shughuli ndefu za kikundi mara nyingi husababisha makundi kumaliza kwa
nyakati tofauti na zinaweza kuleta utata katika darasa.
Mara nyingi wanafunzi hushiriki katika shughuli kwa hamasa kubwa ikiwa mwalimu
anawaalika kabla ili kujiandaa na kushiriki na au kufundisha darasa kitu wamejifunza kutoka
kwa shughuli. Hii pia inatoa fursa kwa wanafunzi kufanya mazoezi ya kufundisha injili kwa
wengine.
Wanafunzi kila mara hufanya vyema katika vikundi wanapopekua maandiko, kusoma
dondoo, au kutimiza wajibu mwingine binafsi kabla ya kukusanyika pamoja.
Kwa makundi ya wanafunzi watano au zaidi, inaweza kuwa vigumu kwa kila mtu kushiriki
vifaavyo. Kuongezea, makundi makubwa kawaida yana ugumu mwingi sana wa kufanya
kazi.
Kufanya kazi katika vikundi vidogo pengine sio njia bora kwa kujibu maswali rahisi kwa
sababu ya muda unaohitajika wa kupanga wanafunzi kwa vikundi vidogo vidogo.
Wakati shughuli za kikundi za kujifunza zimetumika visivyo, zinaweza kukosa mwelekeo.
Wakati wa majadiliano au kazi za kikundi kidogo, wanafunzi wanaweza kupoteza maono katika
shughuli, matembezi kwa ajili ya mambo binafsi, au kulegea kwa juhudi zao za kujifunza.
Mwalimu anayebakia hai kwa kutenda kwake kwa kusonga kutoka kundi hadi kundi na kufuatia
shughuli za masomo anaweza kuwasaidia wanafunzi kukaa katika wajibu na kunufaika sana
kutokana kazi.
Mazoezi ya Kuandika [5.7] Waalimu wanapaswa kualika wanafunzi kushiriki katika mazoezi ya kuandika kama vile kuchua
maoni, kazi za jarida, karatasi za kuandika, mtazamo wa kibafsi, na insha. Wakati mwingine,
kualika wanafunzi kujibu swali la kuwaza kwa kuandika husaidia kupanua na kubainisha fikira
zao. Kualika wanafunzi kujibu swali kwa kuandika kabla ya kushiriki mawazo yao pamoja na
darasa kunawapatia muda wa kujenga maoni yao na kupokea maongozi kutoka kwa Roho
Mtakatifu. Wanafunzi wanaweza kuvutiwa kushiriki mawazo yao wakisha yaandika kwanza, na
yale wanayoshiriki kila mara yatakuwa wa umuhimu zaidi. Miongoni mwa vitu vingine, kazi za
kuandika huwapatia wanafunzi fursa ya kushiriki kibinafsi, kupokea maongozi, kujitayarisha
kufundisha na kushiriki hisia zao pamoja na wengine, kutambua mkono wa Bwana katika maisha
yao, na kuonyesha ushuhuda. Waalimu wanapoamua ni mazoezi yapi yafaayo kwa uzoefu wa
masomo, wanapaswa kufikiria kanuni hii iliyoshirikishwa na Mzee David A. Bednar: ―Kuandika
chini kile tulichokisoma, kufikiria, na kuhisi tunaposoma maandiko ni njia nyingine ya
kutafakari na mwaliko wenye nguvu kwa Roho Mtakatifu kwa mafunzo daima‖ (―Because We
Have Them before Our Eyes, New Era,Apr. 2006, 6–7).
Mazoezi ya kuandika kwa wanafunzi walio wadogo au ambao uwezo wao ni mdogo sana
yanapaswa kubadilishwa ili kuwasaidia kufaulu. Kwa mfano, mwalimu anapaswa kutayarisha
zoezi ya kujaza pengo ambapo maelezo zaidi yamepeanwa kwa wanafunzi na kuulizwa maswali
machache. Waalimu wanaweza kuwasaidia wanafunzi hawa kwa kulenga kazi ya kuandika
kwenye vifungu vifupi vya maandiko au maswali mahuhusi na kwa kuwapa muda wa kutosha ili
kukamilisha zoezi hilo.
Kwa kawaida wanafunzi hunufaika zaidi kutokana na shughuli za kuandika wakati:
Waalimu wanapotoa maelezo yaliyo dhahiri, ambayo yameandikwa kwamba wanafunzi
kurejelea kwayo wakati wote wa zoezi.
Shughuli inalenga kwenye mawazo yao ya kweli za injili ambazo ni muhimu kwa hali zao
binafsi.
Shughuli hiyo inawasaidia katika kutumia kweli hizo kibinafsi.
Wanafunzi wanaungwa mkono na kusaidiwa na mwalimu wao kwote katika shughuli ya
kuandika.
Viwango maalum vya muda vinabuniwa mara kwa mara kulingana na ugumu wa zoezi.
Wanafunzi wanaalikwa kuelezea, kushiriki, au kushuhudia juu ya kitu walichojifunza kutoka
kwa shughuli.
Wanafunzi wanahakikishwa kwamba shughuli za kuandika zinazolenga kwenye hisia za mtu
binafsi au masharti hazitashirikishwa na wengine, ikiwemo mwalimu, bila ruhusa ya
mwanafunzi.
Shughuli hii ni sehemu muhimu ya mpango wa somo na haipatianwi kama ―kazi yenye
shughuli‖ au kama adhabu kwa tabia mbaya.
Mbinu mbadala ya kunakili fikira na mawazo zimepeanwa kwa wale walio na ugumu wa
kuandika. Haya yanaweza kujumuisha kuweka mwanafunzi mwengine kutumika kama
mwandishi, kunasa sauti, na kadhalika
Shughuli za kuandika hazijatumika sana visivyo.
Ubao wa chokaa au Ubao mweupe [5.8] Ubao wa chokaa au ubao mweupe ulioandaliwa vilivyo unaweza kuwa thibitisho la matayarisho
ya mwalimu na kuleta hisia ya lengo moja ndani ya darasa. Matumizi mema ya ubao wakati wa
somo yanaweza kuwasaidia wanafunzi kujifunza na kuleta kushiriki kunakofaa, haswa kwa wale
wanaotaka kujifunza kwa maono. Wanapotumia ubao, waalimu wanapaswa kukumbuka
kuandika dhahiri na ukubwa vya kutosha kwa kila mtu kuona, kuhakikisha kwamba kifaa
kimepewa nafasi ifaayo, vizuri, na rahisi kusoma. Ambapo ubao wa chokaa au ubao mweupe
haupatikani, karatasi kubwa ama ubao wa bango unaweza kutumika kwa dhamira hiyo hiyo.
Kwenye ubao, mwalimu anaweza kuelezea wazo kuu kwa muhtasari au kanuni ya somo, kuchora
fundisho au tukio, kuchora ramani, kubuni mchoro wa mfuatano, kuonyesha au kuchora picha za
mambo yanayopatikana katika maandiko, kutengeneza chati inayoonyesha matukio ya kihistoria,
kuorodhesha mambo kutoka kwa maandiko kadri wanafunzi wanapoyopata, au kufanya wingi
wa kazi hizo zingine zitakazoongeza kujifunza.
Vitu na picha [5.9] Ni vigumu kila mara kufundisha mawazo yasiyoshikika ya injili. Kutumia vitu na picha
kunaweza kuwa njia bora kwa waalimu kuwasaidia wanafunzi kuelewa kanuni za kiroho. Kwa
mfano, kitu cha kufahamika kama vile sabuni kinaweza kuwasaidia wanafunzi kuelewa kanuni
ya kudhahania kama toba. Mara kwa mara Mwokozi alirejelea vitu vya dunia (kama mkate, maji,
mishuma, na vipima) ili kuwasaidia wasikilizaji wake kuelewa kanuni za kiroho.
Vitu na picha vinaweza kutumika kwa kuwasaidia wanafunzi kupiga taswira vile watu, mahali,
matukio, vitu, na ishara katika maandiko yalivyofanana. Badala ya kuongea kuhusu nira pekee
(ona Mathayo 11:28–30), mwalimu anaweza kuleta nira darasani, kuonyesha picha ya nira moja,
au kuieleza kwenye ubao wa chokaa. Wanafunzi wanaweza kunusa au kugusa maua
wanapofundisha kuhusu ―maua ya mashamba‖ (Mathayo 6:28–29). Wanaweza kuonja mkate
usiotiwa chachu.
Vitu na picha, vikiwemo ramani na chati, vinaweza kuwa muhimu katika kuwasaidia wanafunzi
kupiga taswira, kuchanganua, na kuelewa maandiko, haswa zinapotumika kuchangamsha
majadiliano. Kuwa na kitu au picha kwa maonyesho wakati wanafunzi wanapoingia darasani
kunaweza kuzidisha mazingira ya masomo na kuhimiza moyo wa maulizo miongoni mwa
wanafunzi.
Kuna mashauri mawili ya kufikiria unapotumia vitu na picha: Kwanza, yanapaswa kuimarisha
dhamira ya somo badala ya kuondoka kutoka kwayo. Pili, hadithi ya kimaandiko inapaswa kuwa
ndio chanzo cha majadiliano ya darasa ya mipangilio na utondoti wa tukio, badala ya ufafanuzi
wa msaani wa tukio au hadithi.
Mawasilisho ya Sauti/Picha na Kompyuta [5.10] Maandiko yamejawa na hadithi za Bwana akiwasaidia watoto Wake kuelewa mafundisho Yake
kupitia kwa kuona na kusikia (ona 1 Nefi 11–14; M&M 76; Musa 1:7–8, 27–29). Nyenzo za
sauti na picha na teknologia, zinapotumika vilivyo na vyema, zinaweza kuwasaidia wanafunzi
kuelewa vyema maandiko na kujifunza na kutumia kweli za injili.
Nyenzo za sauti na picha zinaweza kuelezea matukio muhimu kutoka kwa maandiko na
zinaweza kusaidia wanafunzi kupiga taswira na kuona matukio haya. Nyenzo hizi zinaweza
kuonyesha jinsi watu wanatumia kanuni za injili ili kushinda changamoto na matatizo yao na
zinaweza kupeana fursa kwa Roho kutoa ushuhuda wa kweli.
Teknologia ya kompyuta inaruhusu waalimu kuonyesha vipande vya video; ili kuonyesha
maswali muhimu, picha, au dondoo kutoka kwa Viongozi Wakuu wenye Mamlaka; au kusisitiza
kanuni na mafundisho yaliyoelezwa wakati wa somo. Mawasilisho ya kompyuta yanaweza
kutumika sana kama vile ubao wa chaki au ubao mweupe unavyoweza kutumika—ili kufafanua
wazo muhimu la somo, kuonyesha marejeleo ya maandiko, na kutoa maelezo ya picha kwa
shughuli za kujifunza za jozi, kundi, au mtu binafsi. Kutumia teknologia katika njia hizi
kunaweza kuwasaidia wanafunzi wanaojifunza kwa vielelezo na kunaweza kuwasaidia
wanafunzi kupanga na kuelewa vyema wanachojifunza.
Matumizi ya nyenzo za sauti na picha, kompyuta, au za teknologia zingine zinapaswa kusaidia
kufanya masomo kueleweka, kupendeza, na ya kuvutia na hazipaswi kuvuruga wanafunzi
kukosa kuhisi uvutio wa Roho.
Mawasilisho ya sauti na picha yanaweza kuwasaidia wanafunzi kujifunza na kutumia vyema
kanuni za injili zinapotumika kuchechemua mawazo na hisia na kuweka wanafunzi katika
maneno ya maandishi. Inaweza kusaidia kuandika kwenye ubao mambo mahususi ambayo
wanafunzi wanaweza kuangalia au maswali wanayoweza kufikiria wanapotazama au kusikiliza
mawasilisho. Kunaweza kuwa pia na thamani katika kutuliza wakati wa mawasilisho ili kuuliza
maswali au kuonyesha habari zitakazosaidia wanafunzi. Mara nyingi sehemu ya nyenzo za sauti
na picha pekee ni muhimu kwa kukamilisha lengo la mwalimu. Waalimu wanaotumia mbinu
zingine, kama vile majadiliano na mazoezi ya kuandika, pamoja na matumizi ya vyombo vya
habari na teknologia huzidisha uwezekano kwamba kanuni za injili zitaeleweka na kutumika.
Panapopatikana, kutumia tafsiri za habari kwenye mawasilisho ya sauti na picha kunaweza
kuongeza ufahamu na utendaji wa wanafunzi, haswa kwa wale ambao wana ugumu wa kusikia.
Unapotumia nyenzo za sauti na picha au teknologia ya kompyuta katika somo, waalimu
wanapaswa kuandaa chombo kabla darasa kuanza na kuhakikisha kwamba kinafanya kazi
ipasavyo. Pia wanapaswa kuhakikisha kwamba wanafunzi wote wataweza kusikia mawasilisho
na kuisikia kutoka kwa viti vyao. Kabla ya darasa, waalimu wanapaswa kuandaa nyenzo za sauti
na picha au kompyuta ili kuanzia pahali panapofaa katika somo. Pia inaweza kuwa wazo nzuri
kwa waalimu kujaribu kutumia teknologia kwa mawasilisho kabla ya kuitumia katika somo.
Mwongozo [5.10.1]
Pengine zaidi ya mbinu zingine za kufundisha, matumizi ya nyenzo za sauti na picha na
teknologia huja na changamoto asili na matatizo yake. Waalimu wanapaswa kutumia hekima
wanapoamua kama mawasilisho ya sauti na picha au kompyuta yanaweza kuwa sahihi na ya
usaidizi kwa uzoefu wa masomo. Kutegemea kwingi kwa teknologia kunaweza kuelekeza kwa
masomo yanayoongozwa na vyombo vya mawasiliano badala ya masomo yanayolingana na
maandiko na yenye kulenga msomaji. Maswali yafuatayo yanaweza kusaidia waalimu katika
kufanya maamuzi yenye hekima katika utumizi wa nyenzo za sauti na picha na kompyuta:
1. Je, nyenzo inasaidia wanafunzi kujifunza kitu muhimu? Mawasilisho ya sauti na picha
yanaweza kuwa ya kufurahisha au kuvutia kwa wanafunzi, lakini yanachangia moja kwa moja
kwa dhamira ya somo na kwa kile wanafunzi wanahitaji kujifunza? Kutumia nyenzo hizi kwa
burudani au kama majazo ya muda sio sababu tosha kwa matumizi yao. Waalimu wanapaswa
kuona ama kusikiza mawasilisho kabla ya kuyatumia darasani na kuhakikisha kwamba
yanaimarisha au yanaunga mkono maandiko na mafundisho na kanuni zinazofundishwa
katika somo.
2. Je, ni nyenzo kwa somo au kwa dhamira yake kuu? Mzee Boyd K. Packer alishauri:
―Vielelezo vya sauti na picha katika darasa vinaweza kuwa baraka au laana, kulingana na jinsi
vinavyotumika. Vinaweza kulinganishwa na viungo na vikolezo vinavyotumika na chakula.
Vinapaswa kutumika mara chache kusisitiza au kufanya somo kufurahisha‖ (Teach Ye
Diligently, rev. ed. [1991], 265).
3. Je, inafaa na katika kuweka viwango vya Kanisa? Je, inajenga? Bidhaa nyingi
zinazotengenezwa duniani zinaweza kuwa na ujumbe mzuri lakini huja mara nyingi na ujazo
usiopendeza unaoweza kuudhi Roho au kupuuza mawazo yasiyowiana na mafundisho ya
injili. Kipande cha video au cha sauti, hata kama kinafaa, hakipaswi kutumiwa ikiwa kinatoka
katika rejeo ambalo lina ujazo usiofaa. Bidhaa zenye ubishani au za kushtua mara nyingi
hazijengi imani na ushuhuda.
4. Je, zitakiuka sheria za hati miliki au sheria zingine husika? Video nyingi, nyimbo, na vifaa
vingine vya sauti na picha vimetumia vizuio kwa ajili ya sheria za hati miliki au maelewano
ya mtumizi. Ni muhimu kwamba waalimu wote wa seminari na vyuo na viongozi wafuate
sheria za hati miliki za nchi ambako wanafundisha na kwamba wanatii sheria zinazotumika na
majukumu ili kwamba sio wao wala Kanisa wanastahili hatua ya kisheria.
Mwongozo ufuatao unatumika na waalimu na viongozi wa seminari na chuo katika mataifa yote.
Matumizi ya Kifaa Kitolewacho na Kanisa [5.10.2]
Isipokuwa pengine ionyeshe kwenye kifaa kitolewacho na Kanisa, waalimu na viongozi
wanaweza kunakili na kuonyesha filamu, video, picha, na miziki iliyotolewa na Kanisa kwa
matumizi yasiyokuwa ya kibiashara ya Kanisa na seminari na chuo. Muziki
kutoka Nyimbo, Kitabu cha Nyimbo cha Watoto, na magazeti ya Kanisa yanaweza kutumika kwa
matumizi yasiyokuwa ya kibiashara ya Kanisa na seminari na chuo, isipokuwa sehemu ambayo
kizuio kimewekwa kwenye wimbo au muziki. Waalimu wa seminari na viongozi wanaweza
kufungua na kuonyesha vifaa vitolewavyo na Kanisa darasani, isipokuwa vifaa kama hivyo vina
kizuio kinachoeleza vinginevyo.
Matumizi Kifaa Kisichotolewa na Kanisa [5.10.3]
Kama sheria kwa kawaida, vipindi, programu ya kompyuta, na vifaa vya sauti na picha
havipaswi kutolewa kutoka kwenye intaneti au kuonyeshwa darasani kutoka kwa Intaneti
isipokuwa leseni zifaazo zimenunuliwa. Isipokuwa video, wimbo, au kifaa cha sauti na picha
kinamilikiwa na Kanisa, kuna hatari kuu, katika nchi yoyote, kwamba kuonyesha kitu kama
hicho darasani kunaweza kukiuka sheria za hati miliki. Kwa hivyo, kama sheria kwa kawaida,
waalimu na viongozi wa seminari na chuo ulimwenguni kote hawapaswi kuonyesha madarasa
yao vitu ambavyo havijatolewa na Kanisa.
Unakili wa maonyesho yaliyo na muziki wenye hati miliki (kama vile muziki kwa wingi au
vinaso vya muziki) ni ukiukaji wazi washeria za haki ya kunakili isipokuwa idhini ilioandikwa
imepeanwa na mmiliki wa hati miliki. Unakili wa shairi zenye hisia zilizo na hati miliki kwenye
wimbo pia ni kinyume bila ruhusa.
Mwongozo ufuatao hasa unaeleza kwa muhtasari baadhi ya maondoleo kwa sheria za hati miliki
za Marekani ambazo zitawasaidia waalimu na viongozi wa seminari na chuo katika Marekani
kuonyesha kanda ya video katika darasa bila kupata leseni kwanza kutoka kwa mmilikaji wa hati
miliki ya video. Wakati maondoleo kama hayo yapo katika nchi nyingine, waalimu wa seminari
na chuo wanapaswa kuwasiliana na Afisi ya Intellectual Property ili kuamua sheria maalum na
maondoleo yanayotumika hasa kwa nchi yao kabla ya kuonyesha kanda ya video kutoka kwa
video za kibiashara au vipindi vilivyorekodiwa kutoka hewani au kutoka kwa Intaneti.
Matumizi ya video za kibiashara. Sheria ya Marekani inajumuisha ondoleo linaloruhusu
waalimu na wanafunzi kutumia video za kibishara darasani bila kununua leseni kuweza kufanya
hivyo. Katika suala hili, hata hivyo, video za kibiashara zinaweza kutumika tu chini ya ondoleo
hili ikiwa masharti yote yafuatayo yametimizwa. Kanda ya video inayoonyeshwa lazima:
(a) itoke kwa nakala halali; (b) itumike kwa mafundisho ya uso kwa uso, kumaanisha kwamba
mwalimu au kiongozi wa seminari na chuo au lazima ahudhurie wakati kanda inapoonyeshwa;
(c) kuonyeshwa darasani au sehemu sawa iliotengewa mafundisho; (d) kuonyeshwa na shirika la
elimu lisilokuwa la faida, kama vile darasa la seminari au chuo; na (e) kuonyeshwa kwa lengo la
kufundisha ambalo linahusiana moja kwa moja na mtaala wa kozi na wala sio kwa burudani.
Kuonyesha vyombo vya habari vya kukodiwa au kununuliwa kabla, wakati wa, au baada ya
darasa tu kama burudani ni kinyume na ni udanganyifu. Hii inaweza kuwa ndio hali wakati
sinema kamili imeonyeshwa.
Matumizi ya vipindi vilivyonaswa kutoka hewani. Katika Marekani kipindi cha televisheni
kinachotolewa bila malipo kwa umma na kunaswa kutoka hewani, au kupitia kwa simu,
kinaweza kutumiwa darasani ikiwa tu masharti yafuatayo yametimizwa: (a) Nakala inabakizwa
pasipozidi siku 45, kisha ni lazima ifutwe mara moja. (b) Nakala inatumika darasani kwa siku
10 za kwanza kufuatia tarehe nakala ilipotolewa (kufuatia siku 10 (b) za kwanza, lakini bado
ndani ya siku 45 za kwanza, nakala inaweza kutumika tu kwa utathmini wa mwalimu au
kubainisha kama vipindi vinapaswa kutumika kwa masomo yajazo). (c) Nakala inaonyeshwa tu
mara moja (mara mbili ikiwa tu usisitizaji wa mafunzo unahitajika). (d) Nakala inaonyeshwa tu
darasani au pahali kama vile palipotengewa kwa mafunzo. (e) Ujumbe mkuu au maudhui wa
kipindi haujabadilishwa. (f) Nakala haiwezi kunakiliwa tena ili kushiriki pamoja na wengine.
(g) Nakala yoyote lazima ijumuishe tangazo la hati miliki kwa kipindi kama kilivyorekodiwa.
(h) Kipindi hakijaunganishwa kwa vipande (kwa kawaida au kielektroniki) vya vipindi tofauti ili
kujenga mtungo wa kufundisha au bidhaa nyingine.
Kuongezea kwa masharti za utangulizi, mikato kutoka kwa video za kibiashara na vipindi
vilivyonaswa kutoka hewani au Intaneti vinapaswa: (a) kuonyesha tu pande za video au kipindi;
(b) kutumika bila marekebisho yoyote au kuhariri vipindi vyenyewe; (c) visitumike kwa njia
inayoashiria kuwa watengenezaji wa vipindi au wamiliki wanaidhinisha Kanisa, seminari na
vyuo au mafundisho yao, au kwa njia inayoonyesha kuwa Kanisa au seminari na vyuo
vinaidhinisha vipindi hivyo au watengenezaji wake au wamiliki; (d) visitumike kwa njia ambayo
inakweza Kanisa au seminari na vyuo; na (e) kutumika kulingana na amri zijulikanazo za unasaji
na sera ya Kanisa.
Ikiwa waalimu wa seminari na vyuo au viongozi wana maswali yasiyojibiwa kupitia mwongozo
huu, rejelea sehemu ya 21.1.12, ―Copyrighted Materials‖ katika kitabu cha maelekezo cha
Kanisa. (Handbook 2: Administering the Church[2010], 21.1.12). Kisha, kama ikihitajika,
wasiliana na:
Intellectual Property Office
50 E. North Temple Street, Room 1888
Salt Lake City UT 84150-0018
Simu: 1-801-240-3959 or 1-800-453-3860, upanuzi 2-3959
Faksi: 1-801-240-1187
Barua pepe: [email protected]
Muziki [5.11] Muziki, haswa nyimbo za Kanisa, zinaweza kuhusika kwa wajibu muhimu katika kuwasaidia
wanafunzi kuhisi mwongozo wa Roho Mtakatifu katika uzoefu wao wa kujifunza injili. Katika
dibaji ya kitabu cha nyimbo cha Kanisa, Urais wa Kwanza ulisema: ―Muziki wa kuvutia ni
sehemu muhimu ya mikutano yetu ya kanisa. Nyimbo zinaalika Roho wa Bwana, kuleta hisia za
uchaji, kuunganisha kama washiriki, na kutoa njia kwetu ya kutoa sifa kwa Bwana.
―Mengine ya mahubiri ya ajabu yanahubiriwa kwa kuimba kwa nyimbo. Nyimbo hutuelekeza
kwa toba na matendo mema, kujenga ushuhuda na imani, kufariji wachovu, kufariji wenye
huzuni, na kutuongoza kuvumilia hadi mwisho‖ (Hymns, ix). Mzee Dallin H. Oaks alifundisha:
―Nashangaa ikiwa tunatumia vyema nyenzo hii ya kimbinguni katika mikutano yetu, katika
madarasa yetu, na katika nyumba zetu. …
―Muziki wetu mtakatifu ni maandalizi ya nguvu kwa ajili ya maombi na kufundisha injili‖
(―Worship through Music,‖ Ensign,Nov. 1994, 10, 12). Waalimu wanapaswa kuwasaidia
wanafunzi kuelewa umuhimu wa muziki katika ibada na jinsi unavyoweza kusaidia kujenga
mazingira ambako Roho anaweza kutenda ipasavyo.
Ifuatayo ni baadhi ya njia waalimu wanaweza kutumia muziki ili kuzidisha uzoefu wa wanafunzi
wa kujifundisha injili:
Cheza muziki wa maongozi wanafunzi wanapoingia darasani au wakati wa darasa
wanapofanya kazi ya kuandika.
Alika na kuhimiza wanafunzi kushiriki ipasavyo wanapoimba nyimbo pamoja kama darasa.
Hakiki kanuni za injili na kutoa umaizi wa ziada wakati wa somo kwa kuimba wimbo au
ubeti wa wimbo unaohusiana moja kwa moja na kile kinachofundishwa kwa siku hiyo. Kuna
vielelezo viwili vya maandiko na mada upande wa nyuma wa kitabu cha nyimbo
vinavyoweza kusaidia katika hali hii.
Toa fursa ambako kusoma maneno ya maandiko kunaweza kuwasaidia wanafunzi kujenga na
kudhihirisha ushuhuda wa mafundisho na kanuni za injili.
Alika wanafunzi kuimba nyimbo sahihi za muziki darasani.
Unapofanya uamuzi kuhusu matumizi ya muziki darasani kwa lengo lolote (kama vile muziki wa
usuli, umahiri wa maandiko, au kukariri), ni muhimu kukumbuka tahadhari ifuatayo kutoka kwa
Mzee Boyd K. Packer: ―Kumekuwa na majaribio kadhaa ya kuchukua dhamira takatifu ya injili
na kushikanisha na miziki za kisasa kwa matumaini ya kuvutia vijana wetu kwenye ujumbe. …
Sijui jinsi hayo yanaweza kufanywa na kusababisha ongezeko la kiroho. Nafikiria haiwezi
kufanyika‖ (That All May Be Edified [1982], 279). Hatimaye, ni wajibu wa waalimu kuhakikisha
kwamba muziki wowote unaotumika katika uzoefu wa kujifunza una upatanifu na viwango vya
Kanisa na kwamba hauudhi kwa njia yoyote Roho wa Bwana.
Ushauri Mkuu na Tahadhari [5.12] Hali hamu ya kujenga uhusiano mwema na wanafunzi ni sahihi, hamu ya kutaka kusifiwa, kama
haijatambulika au haijatazamwa, inaweza kusababisha waalimu kujali zaidi kuhusu kile
wanafunzi wanafikiria juu yao kuliko wanavyofanya kuwasaidia wanafunzi kujifunza na
kuendelea. Hii mara nyingi huongoza waalimu kubadilisha mbinu zilizokusudiwa kuboresha sura
yao machoni pa wanafunzi kwa mbinu zilizobuniwa kualika Roho Mtakatifu. Waalimu
wanaoanguka katika mtego huu wana hatia ya ukuhani wa uongo kwa ajili ―wanajiinua wawe
nuru ya ulimwengu, ili wafaidike na wapate sifa za ulimwengu‖ (2 Nefi 2:26). Waalimu
wanapaswa kuwa waangalifu kwamba matumizi yao ya ucheshi, hadithi za kibinafsi, au njia
nyingine ya mafundisho hayafanyiki kwa nia ya burudani, ushawishi, au kupata sifa za
wanafunzi. Badala yake, lengo la waalimu wa kidini lazima liwe ni kumtukuza Baba wa
Mbinguni na kuongoza wanafunzi wao kwa Yesu Kristo.
Rais Howard W. Hunter alifundisha: ―Nina hakika mmetambua uwezekano wa hatari ya kuwa
mashuhuri sana na wa kuvutia sana kiasi kwamba wanafunzi wenu wanajenga utii kwenu badala
ya injili. Sasa hilo ni tatizo la ajabu kuweza kushindana nalo, na tungetumaini kwamba nyinyi
nyote ni waalimu wenye haiba kubwa. Lakini kuna hatari halisi hapa. Hiyo ndio sababu
unapaswa kualika wanafunzi wako katika maandiko wenyewe, sio tu kuwapatia ufafanuzi wako
na mawasilisho yake. Hii ndio sababu unapaswa kualika wanafunzi wako kuhisi Roho wa
Bwana, sio tu kuwapa umaizi wako wa kibinafsi wa hayo. Hio ndio sababu, hatimaye, unapaswa
kualika wanafunzi wako moja kwa moja kwa Kristo, sio tu kwa yule anayefundisha mafundisho
yake, hata kama kwa ustadi. Hautakuwepo kila mara kwa wanafunzi hawa. Huwezi kushikilia
mikono yao baada ya wao kuondoka shule ya sekondari au chuo. Na hauna haja ya wafuasi wa
kibinafsi‖ (―Eternal Investments‖ [an evening with President Howard W. Hunter, Feb. 10,
1989], 2).
Zaidi ya hayo, ushauri ufuatao na tahadhari inahusu mbinu tofauti za kufundisha na hali:
Matumizi ya mashindano. Waalimu wanapaswa kuwa waangalifu katika matumizi ya
mashindano darasani, haswa wanafunzi wanaposhindana kibinafsi dhidi ya mmoja na
mwengine. Mashindano yanaweza kusababisha ubishi, kuvunjika moyo, kejeli, au aibu na
kusababisha Roho kuondoka.
Kuimarisha hasi. Waalimu wanapaswa kutumia hekima katika kuonyesha masikitiko kwa
darasa au kwa mwanafunzi binafsi. Wanafunzi wengi huhisi wapungufu kwa kiasi fulani na
huhitaji kujengwa na kuhimizwa badala ya kuimarisha udhaifu wao.
Kejeli. Kama ikisemwa na mwalimu kwa mwanafunzi au kutoka kwa mwanafunzi mmoja na
mwingine, kejeli karibu kila mara ni hasi na ya kuumiza na inaweza kusababisha dharau na
kutoweka kwa Roho.
Mawasiliano yasiofaa na lugha. Waalimu wanapaswa kuepukana na kupiga kelele kwa au
kubishana na wanafunzi. Matusi na upunjufu hayana nafasi katika mazingira ya elimu ya dini.
Matumizi ya nguvu ya kimwili. Waalimu kamwe hawapaswi kutumia ukubwa wao wa kimwili
na nguvu kutisha au kushinikiza mwanafunzi kuwa na tabia nzuri. Hata michezo ya kimwili
inaweza kueleweka vibaya au kugeuka kuwa kitu kibaya zaidi. Waalimu wanapaswa kutumia
nguvu kwa mwanafunzi ikiwa tu usalama wa mwanafunzi mwengine unahitajika.
Jinsia-lugha mahususi. Waalimu wanapaswa kujua kuhusu na kuwa makini kwa lugha
mahususi ya jinsia katika maandiko. Maandiko mengine yameandikwa kwa lugha ya kijinsia
ya kiume kulingana na asili ya lugha zilizotokana kwazo. Waalimu wanapaswa
kuwakumbusha wanafunzi kwamba majina mengine ya jinsia ya kiume yanahusu wanaume
na wanawake wote. Wakati Adamu alipoambiwa kwamba ―watu wote, kila mahali, lazima
watubu‖ (Musa 6:57), hakika Bwana alikuwa akiongea kuhusu wanaume na wanawake. Kuna
nyakati ambapo maelezo ya umbo ni bayana na sahihi. Kwa mfano, washiriki wa Uungu ni
wanaume, na marejeo kwa majukumu ya ukuhani inahusu kina ndugu.