serikali ya mapinduzi ya zanzibarkwa mujibu wa katiba ya zanzibar ya mwaka 1984 kifungu 112 mdhibiti...
TRANSCRIPT
SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
OFISI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU
WA HESABU ZA SERIKALI ZANZIBAR
RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU
WA HESABU ZA SERIKALI
KWA MAWIZARA YA SERIKALI YA
MAPINDUZI YA ZANZIBAR
KWA MWAKA WA FEDHA
2016/2017
ii
YALIYOMO
SURA YA KWANZA……………………………………………………………………………………………1
1.0 UTANGULIZI ......................................................................................................................... 1
1.1 MAJUKUMU YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI .............................. 1
1.2 UPEO NA MADHUMUNI YA RIPOTI YA UKAGUZI .................................................................. 2
1.3 NJIA ZILIZOTUMIKA KATIKA UKAGUZI ............................................................................... 3
1.4 UMUHIMU WA UKAGUZI KATIKA KUIMARISHA UTAWALA BORA ........................................... 4
1.5 MAFANIKIO YALIYOPATIKANA ........................................................................................... 5
1.6 CHANGAMOTO .................................................................................................................. 6
1.7 KAMATI ZA BARAZA LA WAWAKILISHI ................................................................................ 7
1.8 SHUKURANI ...................................................................................................................... 7
SURA YA PILI…….……………………………………………………………………………………………9
2.0 TAARIFA ZA FEDHA ZA MFUKO MKUU WA HAZINA YA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017 .............................................................................................. 9
2.1 MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI .............................................................................. 9
2.1.1 MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017............... 9
2.1.2 MAPATO NA MATUMIZI KWA KAZI ZA KAWAIDA NA MAENDELEO KWA MWAKA WA
FEDHA 2016/2017................................................................................................................. 9
2.1.3 MAPATO YA KODI YALIYOKUSANYWA NA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA) ...... 9
2.1.4 UKUSANYAJI WA MAPATO YA NDANI ZANZIBAR....................................................... 10
2.1.5 TAARIFA YA MATUMIZI YA KAZI ZA KAWAIDA ......................................................... 11
2.1.6 TAARIFA YA MATUMIZI YA KAZI ZA MAENDELEO ..................................................... 11
2.1.7 TAARIFA YA JUMLA YA MATUMIZI YA SERIKALI ....................................................... 11
2.1.8 TAARIFA YA DENI LA SERIKALI ............................................................................... 12
SURA YA TATU…..…………………………………………………………………………………………..13
3.0 MAMBO YALIYOBAINIKA KATIKA UKAGUZI KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017 .................... 13
3.1 UTEKELEZAJI WA HOJA ZA UKAGUZI ULIOPITA WA MWAKA WA FEDHA 2015/2016 ............. 13
3.2 UWASILISHAJI WA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA WA FEDHA 2016/2017 KWA AJILI YA
UKAGUZI ................................................................................................................................ 13
3.3 UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA 2016/2017 ............................................................ 18
3.4 AINA YA HATI ZA UKAGUZI .............................................................................................. 25
SURA YA NNE………………………………………………………………………………………………...31
4.0 MATOKEO YA UKAGUZI KWA MWAKA 2016/2017 ................................................................. 31
4.1 WIZARA YA NCHI OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI ................... 31
4.1.1 FUNGU A 01 - OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI .............. 31
iii
4.1.2 FUNGU A 02 – OFISI YA RAIS BARAZA LA MAPINDUZI – BLM .................................... 32
4.2 WIZARA YA NCHI (OR) TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ........... 33
4.2.1 FUNGU D 01 - WIZARA YA NCHI (OR) TAWALA ZA MIKOA NA IDARA MAALUM .......... 33
4.2.2 FUNGU D 02 - JESHI LA KUJENGA UCHUMI (JKU) ................................................... 34
4.2.3 FUNGU D 03 – CHUO CHA MAFUNZO ...................................................................... 34
4.2.4 FUNGU D 04 - KIKOSI MAALUM CHA KUZUIA MAGENDO (KMKM) .............................. 35
4.2.5 FUNGU D 05 – KIKOSI CHA ZIMAMOTO NA UOKOZI ................................................. 36
4.2.6 FUNGU D 06 - KIKOSI CHA VALANTIA ...................................................................... 37
4.2.7 OFISI YA USAJILI NA KADI ZA UTAMBULISHO .......................................................... 37
4.2.8 FUNGU D 07 – MKOA WA MJINI MAGHARIBI ............................................................ 38
4.2.9 FUNGU D 08 – MKOA WA KUSINI UNGUJA ............................................................... 39
4.2.10 FUNGU D 09 – MKOA WA KASKAZINI UNGUJA ..................................................... 39
4.2.11 FUNGU D 10 – MKOA WA KUSINI PEMBA ............................................................. 40
4.2.12 FUNGU D 11 - MKOA WA KASKAZINI PEMBA ........................................................ 40
4.2.13 BARAZA LA MANISPAA MJINI ............................................................................. 41
4.2.14 BARAZA LA MANISPAA MAGHARIBI - A ............................................................... 42
4.2.15 BARAZA LA MANISPAA MAGHARIBI - B ............................................................... 42
4.2.16 HALMASHAURI YA WILAYA YA KASKAZINI ‘A’ UNGUJA. ......................................... 43
4.2.17 HALMASHAURI YA WILAYA YA KASKAZINI “B” UNGUJA ........................................ 44
4.2.18 HALMASHAURI YA WILAYA YA KATI .................................................................... 45
4.2.19 BARAZA LA MJI CHAKE-CHAKE ............................................................................ 46
4.2.20 BARAZA LA MJI MKOANI ..................................................................................... 48
4.2.21 BARAZA LA MJI WETE ......................................................................................... 49
4.2.22 HALMASHAURI YA WILAYA YA MICHEWENI ......................................................... 51
4.3 WIZARA YA NCHI (OR) KATIBA, SHERIA, UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA ............ 52
4.3.1 FUNGU G 01 - WIZARA YA NCHI (OR) KATIBA, SHERIA, UTUMISHI WA UMMA NA
UTAWALA BORA ................................................................................................................. 52
4.3.2 FUNGU G 02 - MAHKAMA KUU ................................................................................. 53
4.3.3 FUNGU G 03 – OFISI YA MWANASHERIA MKUU ........................................................ 54
4.3.4 FUNGU G 04 – OFISI YA MKURUGENZI WA MASHTAKA ............................................. 54
4.3.5 FUNGU G 05 – TUME YA KUREKEBISHA SHERIA ....................................................... 55
4.3.6 FUNGU G 08 - KAMISHENI YA UTUMISHI WA UMMA ................................................ 55
4.3.7 FUNGU G 09 - TUME YA UTUMISHI SERIKALINI ...................................................... 56
4.3.8 FUNGU G 07- MAMLAKA YA KUZUIA RUSHWA NA UHUJUMU WA UCHUMI ZANZIBAR 57
4.4 WIZARA YA NCHI OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS ..................................................... 58
4.4.1 FUNGU C 01 - OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS ................................................. 58
4.4.2 FUNGU C 02 - BARAZA LA WAWAKILISHI ................................................................ 58
4.4.3 FUNGU C 03 - TUME YA UCHAGUZI ......................................................................... 59
iv
4.4.4 FUNGU C 05 – TUME YA UKIMWI ........................................................................... 59
4.4.5 FUNGU C 04 - TUME YA KITAIFA YA KURATIBU NA UDHIBITI WA DAWA ZA KULEVYA 60
4.5 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO .................................................................................... 61
4.5.1 FUNGU F 01 - WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO ...................................................... 61
4.5.2 FUNGU F 02 - HESABU ZA HUDUMA ZA MFUKO MKUU WA SERIKALI ........................ 64
4.5.3 FUNGU F 03 - TUME YA MIPANGO ......................................................................... 65
4.5.4 OFISI YA MTAKWIMU MKUU WA SERIKALI ............................................................... 65
4.6 WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI .......................................................... 66
4.6.1 FUNGU L 01 - WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI ........................... 66
4.7 WIZARA YA BIASHARA, VIWANDA NA MASOKO ................................................................. 67
4.7.1 FUNGU R 01 - WIZARA YA BIASHARA, VIWANDA NA MASOKO .................................. 67
4.7.2 TAASISI YA VIWANGO ZANZIBAR (ZBS) ................................................................... 68
4.8 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ...................................................................... 71
4.8.1 FUNGU K 01 – WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ....................................... 71
4.8.2 MRADI WA ELIMU MBADALA ................................................................................... 73
4.8.3 BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU ........................................................................ 77
4.8.4 MAMLAKA YA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR .......................................................... 78
4.8.5 SHIRIKA LA HUDUMA ZA MAKTABA ......................................................................... 78
4.8.6 TAASISI YA KARUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA .................................................. 79
4.8.7 BARAZA LA MITIHANI ............................................................................................. 80
4.9 WIZARA YA AFYA ............................................................................................................ 81
4.9.1 FUNGU H 01 - WIZARA YA AFYA .............................................................................. 81
4.9.2 FUNGU H 02 - HOSPITALI YA MNAZI MMOJA ........................................................... 81
4.9.3 WAKALA WA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI .......................................... 82
4.10 WIZARA YA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI ........................................................... 83
4.10.1 FUNGU N 01 - WIZARA YA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI ............................ 83
4.10.2 BODI YA USAJILI WA WAKANDARASI .................................................................. 84
4.10.3 BODI YA UHAULISHAJI ARDHI ............................................................................. 85
4.11 WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI .................................................. 86
4.11.1 FUNGU P 01 - WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI ................. 86
4.11.2 MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI ........................................................................ 92
4.12 WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI, WAZEE , VIJANA, WANAWAKE NA WATOTO .................. 93
4.12.1 FUNGU NAMBA Q 01 - WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI, WAZEE, VIJANA, WANAWAKE
NA WATOTO ....................................................................................................................... 93
4.13 WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, UTALII NA MICHEZO ................................................ 95
4.13.1 FUNGU NAMBA J 01 - WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, UTALII NA MICHEZO ...... 95
4.13.2 FUNGU J 02 - KAMISHENI YA UTALII ................................................................... 96
1
RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
KWA MAWIZARA YA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017
SURA YA KWANZA
1.0 UTANGULIZI
Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu 112 Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu anawajibika kukagua hesabu zote za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, pamoja na Miradi mbali mbali ya maendeleo na baadae kutoa taarifa ya
ukaguzi wa hesabu hizo kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya Zanzibar.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anawajibu wa kuhakikisha kwamba
fedha zote zinazokusudiwa kutolewa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar matumizi yake yameidhinishwa kisheria.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anawajibu wa kikatiba kuidhinisha
matumizi hayo kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
na kufanya Ukaguzi wa hesabu angalau mara moja kila mwaka na kutoa taarifa juu
ya hesabu hizo.
1.1 MAJUKUMU YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA
SERIKALI
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anawajibika kikatiba kukagua
hesabu za Taasisi za Serikali na baadae kutoa taarifa zake za ukaguzi huo kila
mwaka. Taarifa hizo zitaelezea hali halisi za mapato na matumizi ya fedha kutoka
Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na utekelezaji
wa sheria mbali mbali zikiwemo Sheria za fedha, Sheria za manunuzi na sheria
nyenginezo.
Kwa mujibu wa kifungu 112 (3) cha Katiba ya Zanzibar 1984, Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu anawajibika kufanya yafuatayo:-
“a) Kuhakikisha kwamba fedha zote zinazokusudiwa kutolewa kutoka Mfuko Mkuu
wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, matumizi yake yameidhinishwa
2
kisheria na iwapo atatosheka kwamba masharti hayo yatatekelezwa ipasavyo basi
ataidhinisha fedha hizo zitolewe.
b) Kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo matumizi yake yameidhinishwa
yanatokana na fedha zilizomo katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar au fedha ambazo matumizi yake yameidhinishwa na sheria iliyotungwa
na Baraza la Wawakilishi, na ambazo zimetumika kwa ajili ya shughuli zilizohusika na
matumizi ya fedha hizo na kwamba matumzi hayo yamefanywa kwa kufuata idhini
iliyotolewa kuhusu matumizi hayo; na
c) Angalau mara moja kwa kila mwaka kufanya ukaguzi na kutoa taarifa juu ya
ukaguzi wa hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hesabu zinazosimamiwa na
watumishi wote wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hesabu za Mahkama zote za
Zanzibar, hesabu za Tume au vyombo vyengine vilivyoanzishwa na Katiba hii na
hesabu zozote zinazohusika na Baraza la Wawakilishi. ”
Ukaguzi wa hesabu umefanywa kwa kuzingatia miongozo na vigezo mbali mbali vya
ukaguzi ili kukidhi matarajio ya wadau wetu na wananchi kwa ujumla. Ofisi ya
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaendelea kufanya uchambuzi wa
njia bora zaidi kwa kufanya ukaguzi utakaoleta tija na kuongeza wigo na maeneo
yanayokaguliwa kwa lengo la kuimarisha utendaji na uwajibikaji katika sekta za
umma.
1.2 UPEO NA MADHUMUNI YA RIPOTI YA UKAGUZI
Ripoti hii imekusanya taarifa za ukaguzi wa hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar yakiwemo Mawizara na Taasisi mbali mbali za Serikali kwa kuzingatia
taarifa za mapato na matumizi ya kawaida, matumizi ya maendeleo pamoja na
michango mbali mbali kutoka kwa Washirika wa Maendeleo, kwa kipindi cha mwaka
ulioishia 30 Juni, 2017.
Ukaguzi ulifanyika kwa mujibu wa viwango vya kitaifa na kimataifa vya Ukaguzi na
kujiridhisha kwamba taarifa zitakazotolewa zitaonyesha sura halisi ili kutoa uhakika
kwamba taarifa za mapato na matumizi zimefuata Sheria, Kanuni na taratibu
zilizopo. Taarifa za hesabu zilizokaguliwa zilijumuisha hesabu za mwisho wa mwaka
pamoja na taarifa mbalimbali zinazohusiana na hesabu hizo.
3
Miongoni mwa taarifa hizo ni kama zifuatazo:-
I. Mizania ya Hesabu
II. Taarifa ya Mapato na Matumizi
III. Taarifa kuhusu mabadiliko ya mtaji
IV. Taarifa ya mtiririko wa fedha
V. Taarifa ya uwiano na bajeti na kiasi halisi cha matumizi
VI. Sera za uhasibu na maelezo ya taarifa za fedha
Mabadiliko ya mifumo ya ukaguzi na uhasibu yanayotokea kwa mujibu wa viwango
vya kitaifa na kimataifa kumepelekea kuwepo na mafanikio makubwa katika
utendaji na uwajibikaji kwenye sekta za umma katika ukusanyaji wa mapato na
matumizi ya rasilimali za umma. Mafanikio hayo yametokana na kuimarika kwa
mfumo wa fedha pamoja na utekelezaji wa Sheria mbalimbali zikiwemo sheria za
fedha, Sheria ya Manunuzi na Ugavi, pamoja na Sheria nyenginezo na kupelekea
kuimarika kwa uwazi na uwajibikaji katika taasisi za Umma pamoja na utekelezaji wa
miradi mbali mbali ya maendeleo na kuleta tija kwa wananchi na kufanikisha lengo
la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha dhana nzima ya utawala bora.
1.3 NJIA ZILIZOTUMIKA KATIKA UKAGUZI
Njia mbali mbali za ukaguzi zilitumika katika Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar ambapo taratibu zifuatazo zilitumika: -
Kutoa barua za awali za maandalizi ya ukaguzi (Engagement Letter) kwa Taasisi
inayokaguliwa.
Kuangalia viashiria vya maeneo hatarishi katika taasisi zinazokaguliwa kwa lengo la
kupata uelewa wa mazingira ya taasisi hiyo ikiwemo mfumo wa udhibiti wa ndani na
kubaini viashiria vitakavyoathiri udhibiti wa ndani pamoja na utendaji wa taasisi.
Kuandaa mikakati ya ukaguzi kuanzia mpango wa awali hadi mpango mkuu wa
ukaguzi (Pre Planning, Strategic Planing and detailed Planning) itakayozingatia
muelekeo na upeo wa ukaguzi ambapo utaonyesha dira na dhamira nzima ya
ukaguzi huo.
Kufanya kikao cha kuanza kazi za ukaguzi (Entrance Meeting) pamoja na uongozi wa
Taasisi zinazokaguliwa.
4
Kupitia na kuhakiki nyaraka mbalimbali pamoja na kupata taarifa kutoka kwa
wahusika ili kupata uelewa wa kazi za Taasisi zinazokaguliwa.
Kutumia njia na mbinu mbalimbali za ukaguzi kama ilivyoainishwa kwenye muongozo
wa ukaguzi (Regularity Audit Manual).
Kufanya kikao cha kumaliza ukaguzi (Exit Meeting) na uongozi wa Taasisi
inayokaguliwa baada ya kumaliza ukaguzi ambapo katika kikao hicho hupitia kwa
pamoja hoja zilizojitokeza wakati wa ukaguzi.
Kutoa ripoti ya ukaguzi ya awali (Management letter) kwa uongozi wa taasisi
inayokaguliwa itakayoainisha hoja za ukaguzi pamoja na mambo mbalimbali
yaliyobainika wakati wa ukaguzi na kutoa nafasi kwa uongozi kutoa majibu na
vielelezo kuhusiana na ripoti hiyo kwa muda unaotakiwa kwa mujibu wa sheria.
Kufuatilia majibu ya hoja za ukaguzi yaliyotolewa katika ripoti ya ukaguzi ya awali ili
kuweza kujiridhisha na majibu ya hoja hizo.
Kutoa ripoti ya ukaguzi ya mwisho kwa taasisi zinazokaguliwa inayoonesha hoja za
ukaguzi zilizotolewa katika ripoti ya ukaguzi ya awali ambazo hazikupata majibu
yenye kuridhisha kutokana na hoja zilizotolewa.
Kutoa ripoti kuu ya mwaka kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mujibu wa
Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
1.4 UMUHIMU WA UKAGUZI KATIKA KUIMARISHA UTAWALA BORA
Katika kuimarisha dhana nzima ya Utawala Bora suala la ukaguzi wa hesabu lina
umuhimu wa kipekee katika kuimarisha uwajibikaji katika utumiaji wa rasilimali za
umma. Lengo kuu la kufanya ukaguzi ni kuhakikisha kwamba fedha inayoidhinishwa
kwa mujibu wa sheria inatumika ipasavyo na kwa malengo yaliyokusudiwa kwa
maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.
Kuimarika kwa utendaji wa kazi za ukaguzi kutapelekea kuongezeka na kuimarika
kwa uwazi na uwajibikaji katika mapato na matumizi ya fedha na rasilimali za umma
ili kuleta tija na ufanisi katika utekelezaji wa malengo yaliyopangwa na Serikali kwa
wakati uliopangwa na kwa kuzingatia hali ya uchumi wa nchi kwa ajili ya maendeleo
ya wananchi na taifa kwa ujumla.
Katika kufanikisha malengo ya Serikali ya kuimarisha utawala bora nchini, Ofisi ya
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali imejipanga kutekeleza majukumu
5
yake ya kikatiba kwa kuongeza ufanisi wa kazi pamoja na kuendelea na jitihada zake
za kuwajengea uwezo wafanyakazi kwa kuwapatia mafunzo na mbinu mbali mbali
za ukaguzi ili kwenda sambamba na mabadiliko ya mifumo ya uhasibu na ukaguzi
pamoja na mabadiliko ya kasi ya teknolojia duniani katika masuala ya udhibiti na
ukaguzi wa hesabu za Serikali.
1.5 MAFANIKIO YALIYOPATIKANA
Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali katika kutekeleza
majukumu yake imebaini kwamba kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017
kumekuwa na mafanikio makubwa katika usimamizi wa ukusanyaji mapato pamoja
na uwajibikaji katika matumizi ya rasilimali za umma. Hata hivyo bado msukumo
unahitajika kwa baadhi ya Taasisi kurekebisha dosari zilizobainika katika ukaguzi
uliofanyika.
Baadhi ya mafanikio hayo ni uwasilishaji wa Taarifa za hesabu za mwisho wa mwaka
ambapo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 imebainika kwamba
uwasilishaji wa taarifa za hesabu za Serikali umeimarika ambapo hesabu hizo
zimewasilishwa kwa wakati na kupelekea kuanza kwa kazi za ukaguzi kwa mujibu wa
utaratibu tuliojipangia.
Ukaguzi umebaini kwamba ufungaji wa hesabu za mwisho wa mwaka umeimarika
kwa kiasi kikubwa kutokana na mfumo wa udhibiti wa fedha uliopo, hata hivyo kwa
baadhi ya Taasisi imebainika kujitokeza kwa dosari katika ufungaji wa hesabu hizo.
Mafanikio haya yanatokana na uwajibikaji mzuri wa watendaji na kuendelea kufuata
ushauri na mapendekezo yanayotolewa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali juu ya udhibiti mzuri wa mapato na matumizi ya fedha na
rasilimali za Umma.
Aidha jitihada zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika
utekelezaji na ufuatiliaji wa ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa uwajibikaji katika utendaji wa
shughuli za Serikali na kupelekea kuimarika kwa Utendaji katika taasisi za Serikali.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inachukuwa hatua mbali mbali katika kuimarisha
utawala bora kwa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya
6
mwaka 1984 na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kutekeleza maoni na ushauri
unaotolewa na kamati za kudumu za Baraza la Wawakilishi ikiwemo Kamati ya
Kudhibiti na Kuchunguza Hesabu za Serikali (PAC).
Jitihada hizi zimeleta mafanikio makubwa katika kuimarika kwa uwajibikaji na uwazi
katika utendaji na nidhamu katika matumizi ya rasilimali za umma na kupelekea
kuongezeka kwa kasi ya maendeleo nchini kutokana na kuimarika kwa hali ya
uchumi na kuleta tija kwa wananchi wa Zanzibar.
1.6 CHANGAMOTO
Katika mwaka 2016/2017 Ofisi imekabiliwa na changamoto mbali mbali zinazotokana
na mabadiliko ya mifumo ya uhasibu na ukaguzi kitaifa na kimataifa. Mabadiliko
hayo yamesababishwa na kukuwa kwa teknolojia duniani na kupelekea kuathiri kwa
baadhi ya miongozo ya ukaguzi inayotumiwa na Taasisi mbali mbali za ukaguzi
duniani ikiwemo Ofisi yetu.
Mabadiliko ya mara kwa mara katika mfumo wa malipo wa kielektroniki unaathiri
utendaji wa kazi za ukaguzi na kupelekea kuchelewa kukamilisha Ripoti kuu ya
Ukaguzi kwa wakati muafaka.
Katika kukabiliana na changamoto hiyo Ofisi inaendelea kuchukua hatua mbali mbali
za kimaendeleo na kuongeza wigo wa ukaguzi utakaoleta tija kwa maendeleo ya
wananchi wa Zanzibar na taifa kwa ujumla pamoja na kuendelea kuunga mkono
jitihada mbali mbali zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika
kuimarisha dhana nzima ya Utawala Bora na Uwajibikaji katika matumizi ya rasilimali
za Umma kwa maendeleo endelevu.
Ofisi imejipanga kuongeza idadi ya wafanyakazi wenye taaluma katika kada
mbalimbali zitakazosaidia kazi za ukaguzi na kuongeza viwango vya taaluma ili
waweze kwenda sambamba na mabadiliko ya sayansi na teknolojia katika kada
mbali mbali ikiwemo uhasibu, ukaguzi na nyenginezo.
Aidha Ofisi itaendelea kutafuta njia na mbinu mbali mbali zitakazosaidia kufanya kazi
za ukaguzi kwa ufanisi zaidi pamoja na kuongeza vifaa vya teknolojia ya kisasa
vinavyokwenda sambamba na mabadiliko hayo.
7
1.7 KAMATI ZA BARAZA LA WAWAKILISHI
Kamati za Baraza la Wawakilishi ni muhimu sana katika kuimarisha uwajibikaji na
kuleta ufanisi katika kufikia malengo ya Serikali iliyojipangia. Kamati hizi zinatoa
mchango mkubwa katika kujenga na kusimamia misingi ya Utawala Bora na
uwajibikaji wa matumizi ya rasilimali za umma.
Kutokana na umuhimu mkubwa wa Kamati za Baraza la Wawakilishi, Ofisi imekuwa
ikishirikiana na Kamati hizo katika kufuatilia utekelezaji wa bajeti ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na kuhakikisha kwamba taasisi za Serikali
zinatekeleza malengo waliyojipangia kama yalivyoanishwa katika Bajeti
zilizoidhinishwa na Baraza la Wawakilishi.
Aidha Kamati ya Kudhibiti na Kuchunguza Hesabu za Serikali (PAC) inatoa mchango
mkubwa katika kusimamia uwajibikaji katika matumizi ya rasilimali za umma na
Kamati hii imekuwa ikishirikiana na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu katika
kufuatilia ripoti zake na kutoa ushauri na mapendekezo mbali mbali kwa Serikali kwa
lengo la kuimarisha ufanisi, uwazi na uwajibikaji kwa matumizi ya rasilimali hizo kwa
maendeleo ya wananchi wa Zanzibar.
Tunatoa shukurani za dhati kwa wenyeviti na wajumbe wa kamati zote za Baraza la
Wawakilishi kwa jitihada zao wanazochukuwa kusimamia uwajibikaji katika
kutekeleza majukumu yao kwa sekta mbali mbali.
Shukurani za pekee ziwaendee wenyeviti na wajumbe wa Kamati ya Kudhibiti na
kuchunguza Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Kamati ya Sheria,Utawala Bora na
Idara Maalum kwa jitihada mbali mbali wanazochukuwa katika kutoa maoni yao na
ushauri kwa Ofisi pamoja na Serikali ambapo ushauri, maoni na michango yao
imesaidia kuimarika kwa uwajibikaji na nidhamu ya matumizi ya rasilimali za umma.
1.8 SHUKURANI
Napenda kutoa shukurani kwa wote waliochangia kwa namna moja au nyengine
kuanzia kazi za ukaguzi, ufuatiliaji wa maeneo mbali mbali yaliyokaguliwa hadi
kukamilika kwa ripoti hii ya ukaguzi ya mwaka 2016/2017.
Nichukue fursa hii kumshukuru na kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein kwa jitihada zake
8
anazozichukuwa katika kufuatilia Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali kwa lengo la kusimamia uwajibikaji wa matumizi ya rasilimali za umma na
kupelekea kuimarisha utawala bora nchini.
Aidha, natoa shukurani zangu za dhati kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa
jitihada mbali mbali zinazochukuliwa katika kuimarisha Ofisi hii kiutendaji na
watendaji kwa ujumla. Vile vile napenda kuwapongeza na kuwashukuru
wafanyakazi wote wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa
juhudi zao wanazochukuwa hadi kufanikisha kukamilika kwa ripoti hii kwa wakati.
Hali kadhalika, ninawashukuru viongozi na watendaji wakuu wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar na watendaji wa taasisi mbali mbali za Serikali kwa mashirikiano mazuri
wanayotupa wakati wa kutekeleza kazi zetu za ukaguzi.
Kwa mara nyengine tena napenda kuzishukuru Kamati ya Kudhibiti na Kuchunguza
Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Sheria,Utawala Bora na Idara Maalum za
Baraza la Wawakilishi pamoja na wale wote waliochangia kwa njia moja au nyengine
katika kuleta maendeleo katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali.
………………………………...
FATMA MOHAMED SAID
MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
ZANZIBAR
9
SURA YA PILI
2.0 TAARIFA ZA FEDHA ZA MFUKO MKUU WA HAZINA YA SERIKALI YA
MAPINDUZI YA ZANZIBAR KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017
2.1 MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI
2.1.1 Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2016/2017
Taarifa ya Mapato
Kwa kipindi cha mwaka 2016/2017 mapato yaliyokadiriwa kukusanywa ni jumla
ya shilingi 814.237 bilioni. Makadirio hayo yalitarajiwa kutoka katika vianzio mbali
mbali ikiwemo mikopo, misaada ya kibajeti na washirika wa maendeleo ambapo
jumla ya shilingi 455.137 bilioni zilitarajiwa kutoka ndani na jumla ya shilingi 326.1
bilioni zilitarajiwa kutokana na misaada ya kimaendeleo kutoka kwa washirika mbali
mbali wa maendeleo pamoja na mikopo ya ndani yenye jumla ya shilingi 33 bilioni.
Taarifa ya Matumizi
Kwa upande wa matumizi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilitarajia kutumia jumla
ya shilingi 841.48 bilioni ambazo shilingi 565.66 bilioni ni kwa kazi za kawaida na
shilingi 275.477 bilioni ni kwa kazi za maendeleo.
2.1.2 Mapato na Matumizi kwa kazi za Kawaida na Maendeleo kwa
mwaka wa fedha 2016/2017
2.1.3 Mapato ya kodi yaliyokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA)
Kwa mwaka 2016/2017 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilikadiriwa kukusanya
jumla ya shilingi 135,052,783,000. Hadi kufikia 30 Juni 2017 makusanyo halisi
yalikua ni shilingi 257,925,155,000 ambapo ni sawa na asilimia 190.98 ya makadirio
ikiwa na ongezeko la shilingi 122,872,372,000 sawa na asilimia 90.98 ya ongezeko.
Ukaguzi umebaini kwamba makusanyo yameongezeka kwa mwaka 2016/2017 kwa
kukusanya jumla ya shilingi 257,925,155,000 ukilinganisha na mwaka wa fedha
2015/2016 ambapo makusanyo halisi yalikuwa shilingi 170,870,794,000 ikiwa na
ongezeko la shilingi 87,054,361,000 ambalo ni sawa na asilimia 51 ya ongezeko.
10
2.1.4 Ukusanyaji wa mapato ya ndani Zanzibar
2.1.4.1 Mapato ya kodi yaliyokusanywa na Bodi ya Mapato Zanzibar
(ZRB)
Bodi ya Mapato Zanzibar ni taasisi iliyopewa mamlaka na jukumu la kukusanya
mapato ya ndani kisheria na inawajibika kukusanya mapato mbali mbali kupitia kodi
zilizowekwa na sheria zilizotungwa na Baraza la Wawakilishi.
Kwa mwaka 2016/2017 Bodi ya mapato Zanzibar ilikadiriwa kukusanya jumla ya
shilingi 259,676,299,000. Hadi kufikia 30 Juni 2017 mapato halisi yaliyokusanywa na
kuingizwa katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
yalikuwa ni shilingi 296,468,088,000 sawa na asilimia 114.2 ya makadirio ikiwa ni
ongezeko la shilingi 36,791,789,000 sawa na asilimia 14.2 ya ongezeko.
Ukaguzi umebaini kwamba makusanyo yameongezeka kwa mwaka 2016/2017 kwa
kukusanya jumla ya shilingi 296,468,088,000 ukilinganisha na mwaka wa fedha
2015/2016 ambapo makusanyo halisi yalikuwa shilingi 207,661,610,608 ikiwa na
ongezeko la shilingi 88,806,477,392 sawa na asilimia 30 ya ongezeko.
2.1.4.2 Ukusanyaji wa mapato katika Wizara na Taasisi za Serikali
Kwa kipindi cha mwaka 2016/2017 Wizara na Taasisi mbali mbali za Serikali
zilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 34,493,875,000 .Hadi kufikia 30 Juni 2017
makusanyo halisi yalikua ni shilingi 28,027,930,000 ambapo ni sawa na asilimia 81
ya makadirio hivyo kuonyesha upungufu wa makusanyo ya shilingi 6,465,945,000
sawa na asilimia 19 ya upungufu.
Aidha, ukaguzi umebaini kwamba makusanyo yameongezeka kwa mwaka 2016/2017
kwa kukusanya jumla ya shilingi 28,027,930,000 ukilinganisha na mwaka wa fedha
2015/2016 ambapo makusanyo halisi yalikuwa shilingi 22,848,931,000. Ongezeko
hilo ni shilingi 5,178,999,000 ambalo ni sawa na asilimia 22.7 .
Kuongezeka kwa makusanyo kumetokana na jitihada mbali mbali zinazochukuliwa na
Serikali katika kuimarisha usimamizi wa ukusanyaji wa mapato.
11
2.1.5 Taarifa ya matumizi ya kazi za kawaida
Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali ilikadiria kutumia kiasi cha
shilingi 565.66 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kazi za kawaida kutoka Mfuko Mkuu
wa Hazina ya Serikali ambapo jumla ya shilingi 491.6 bilioni zimetumika kwa kazi
mbali mbali za kawaida sawa na asilimia 86.90 ya makadirio, ikiwa na upungufu wa
shilingi 74.06 bilioni sawa na asilimia 13.10 ya makadirio.
2.1.6 Taarifa ya matumizi ya kazi za maendeleo
Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali ilikadiria kutumia kiasi cha
shilingi 275.477 kwa ajili ya matumizi ya kazi za maendeleo kutoka Mfuko Mkuu wa
Hazina ya Serikali ambapo jumla ya shilingi 275.477 zimetumika kwa kazi mbali
mbali za maendeleo sawa na asilimia 100 ya makadirio.
2.1.7 Taarifa ya jumla ya matumizi ya Serikali
2.1.7.1 Matumizi ya Kawaida
Matumizi ya Serikali kwa ujumla kwa mwaka 2016/2017 ilikuwa kama ifuatavyo: -
Matumizi ya kawaida yameongezeka kutoka shilingi 402,446,410,000 kwa mwaka wa
fedha 2015/2016 hadi kufikia shilingi 491,600,000,000 kwa mwaka 2016/2017
kukiwa na ongezeko la shilingi 89,153,590,000 sawa na asilimia 22.15 ya ongezeko.
2.1.7.2 Matumizi ya Maendeleo
Matumizi ya maendeleo yameongezeka kutoka shilingi 37,823,042,000 kwa mwaka
wa fedha wa 2015/2016 hadi kufikia shilingi 275,477,000,000 kwa mwaka wa fedha
2016/2017 kwa kiasi cha ongezeko la shilingi 237,653,958,000 ikiwa ni sawa na
asilimia 628.33 .
Aidha, ukaguzi umebaini kwamba kwa ujumla matumizi ya Serikali yameongezeka
kutoka shilingi 440,269,452,000 kwa mwaka wa fedha 2015/2016 hadi kufikia
shilingi 767,077,000,000 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa kiasi cha ongezeko la
shilingi 326,807,548,000 sawa na asilimia 74.22 ya ongezeko.
12
Uchambuzi wa matumizi hayo ni kama ifuatavyo: -
Matumizi
ya Serikali
2015/2016
(TSH)
2016/2017
(TSH)
Ongezeko/
(Upungufu)
(TSH)
Ongezeko /
(Upungufu)
(%)
Matumizi ya
kawaida
402,446,410,000 491,600,000,000 89,153,590,000 22.15
Matumizi ya
Maendeleo
37,823,042,000 275,477,000,000 237,653,958,000 628.33
Jumla 440,269,452,000 767,077,000,000 326,807,548,000
2.1.8 Taarifa ya Deni la Serikali
Ukaguzi umebaini kwamba deni la Serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha
uliyoishia 30 Juni, 2017 limefikia shilingi 403,300,000,000 ambalo linajumuisha deni
la ndani la shilingi 129,700,000,000 na deni la nje la shilingi 273,600,000,000 kama
inavyoonekana hapo chini: -
Deni la
Serikali
2015/2016
(TSH)
2016/2017
(TSH)
Ongezeko
(TSH)
Ongezeko
(%)
Deni la
Ndani
116,952,746,000 129,700,000,000 12,747,254,000 10.90
Deni la Nje 268,636,088,000 273,600,000,000 4,963,912,000 1.85
Jumla 385,588,834,000 403,300,000,000 17,711,166,000
13
SURA YA TATU
3.0 MAMBO YALIYOBAINIKA KATIKA UKAGUZI KWA MWAKA WA FEDHA
2016/2017
3.1 Utekelezaji wa Hoja za Ukaguzi uliopita wa Mwaka wa Fedha
2015/2016
Utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti ya mwaka 2015/2016
imebainika kwamba Wizara za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimechukuwa hatua
mbali mbali katika kurekebisha dosari za kiutendaji na kupelekea kuimarika kwa
uwekaji wa kumbukumbu na ufungaji wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa wakati
muafaka.
Kutokana na tathmini ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa katika hoja za
ukaguzi za mwaka 2015/2016 zilizotolewa kwa Wizara mbali mbali tumebaini
kwamba mapendekezo na ushauri uliotolewa umefanyiwa kazi na kuonesha
kuimarika kwa nidhamu ya matumizi ya fedha na rasilimali za umma na kupelekea
kuleta ufanisi katika utekelezaji wa malengo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali itaendelea kutoa ripoti za
ukaguzi wa hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kutoa ushauri na
mapendekezo mbali mbali katika uwajibikaji na usimamizi wa mapato na matumizi
ya rasilimali za umma kwa lengo la kuimarisha dhana nzima ya utawala bora na
kuimarisha uchumi wa nchi kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar .
Tunapongeza juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika
kusimamia nidhamu ya matumizi ya fedha na rasilimali za umma na kupelekea
kuimarika kwa utendaji na uwajibikaji katika Taasisi za umma.
3.2 Uwasilishaji wa hesabu za mwisho wa mwaka wa fedha 2016/2017
kwa ajili ya ukaguzi
Kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 imebainika kwamba uwasilishaji wa
taarifa za hesabu za Serikali umeimarika ambapo hesabu hizo zimewasilishwa kwa
wakati.
14
Kwa mujibu wa kifungu namba 119(1) cha Sheria ya Usimamizi wa Fedha za Umma
Namba 12 ya mwaka 2016, Wizara na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
zinatakiwa zitayarishe na ziwasilishe kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali, hesabu za mwisho wa mwaka ndani ya miezi mitatu baada ya kumalizika
mwaka wa fedha ambapo hesabu hizo zitajumuisha taarifa za mapato na matumizi
ya Taasisi hizo.
Hesabu za mwisho wa mwaka wa fedha 2016/2017 zilizowasilishwa kwa ajili ya
ukaguzi ni kama ifuatavyo: -
Nam Fungu Wizara/Taasisi Tarehe iliyowasilishwa kwa
ukaguzi
2015/2016 2016/2017
1 A 01 Ofisi ya Rais na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi
21/09/2016 26/09/2017
2 A 02 Ofisi ya Rais Baraza la
Mapinduzi – BLM
17/08/2017 28/09/2017
3 C 01 Afisi ya Makamo wa Pili wa
Rais
9/10/2017 27/09/2017
4 C 02 Baraza la Wawakilishi 03/10/2016 29/09/2017
5 C 03 Tume ya Uchaguzi 27/09/2016 29/09/2017
6 C 04 Tume ya Kitaifa ya Kuratibu
na Udhibiti wa Dawa za
kulevya.
30/09/2016 29/09/2017
7 C 05 Tume ya Ukimwi 30/09/2016 29/09/2017
8 D 01 Wizara ya Nchi (OR) Tawala
za Mikoa,Serikali za Mitaa na
Idara Maalum
30/09/2016 28/09/2017
15
9 D 02 Jeshi la Kujenga Uchumi –
JKU
30/092016 29/09/2017
10 D 03 Chuo cha Mafunzo 30/09/2016 26/09/2017
11 D 04 Kikosi cha KMKM 27/09/2016 29/09/2017
12 D 05 Kikosi cha Zimamoto na
Uokozi
15/08/2016 28/09/2017
13 D 06 Kikosi cha Valantia 27/09/2016 28/09/2017
14 D 07 Mkoa wa Mjini Magharibi 29/09/2016 26/09/2017
15 D 08 Mkoa wa Kusini Unguja 29/09/2016 26/09/2017
16 D 09 Mkoa wa Kaskazini Unguja 23/09/2016 29/09/2017
17 D 10 Mkoa wa Kusini Pemba 28/09/2016 29/09/2017
18 D 11 Mkoa wa Kaskazini Pemba 20/09/2016 28/09/2017
19 D 12 Afisi ya Usajili na Kadi za
Utambulisho
03/10/2016 29/09/2017
20 F 01 Wizara ya Fedha na Mipango 29/09/2016 29/09/2017
21 F 02 Mfuko Mkuu wa Serikali 18/10/2016 22/01/2018
22 F 03 Tume ya Mipango 30/09/2016 26/09/2017
23 G 01 Wizara ya Katiba na Sheria 06/10/2016 29/09/2017
24 G 02 Mahkama Kuu 27/09/2016 25/09/2017
25 G 03 Afisi ya Mwanasheria Mkuu 30/09/2016 28/09/2017
26 G 04 Afisi ya Mkurugenzi wa
Mashtaka
29/09/2016 28/09/2017
27 G 05 Tume ya Kurekebisha Sheria 30/09/2016 29/09/2017
28 G 07 Mamlaka ya Kuzuia Rushwa 29/09/2016 29/09/2017
16
na Uhujumu Uchumi
29 G 08 Kamisheni ya Utumishi wa
Umma
28/09/2016 30/09/2017
30 G 09 Tume ya Utumishi Serikalini 28/09/2016 25/09/2017
31 H 01 Wizara ya Afya 30/09/2016 29/09/2017
32 H 02 Hospitali ya Mnazi Mmoja 30/09/2016 27/09/2017
33 J 01 Wizara ya Habari, Utalii,
Utamaduni na Michezo
29/09/2016 28/09/2017
34 J 02 Kamisheni ya Utalii 30/09/2016 29/09/2017
35 K 01 Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Amali
27/09/2016 28/09/2017
36 L 01 Wizara ya Kilimo, Maliasili ,
Mifugo na Uvuvi
27/09/2016 26/09/2017
37 N 01 Wizara ya Ardhi, Makaazi
,Maji na Nishati
03/10/2016 29/09/2017
38 P 01 Wizara ya Ujenzi
Miundombinu, Mawasiliano na
Usafirishaji
28/09/2016 28/09/2017
39 Q 01 Wizara ya Kazi,Uwezeshaji,
Wazee, Vijana, Wanawake na
Watoto.
11/10/2016 28/09/2017
40 R 01 Wizara ya Biashara, Viwanda
na Masoko
03/10/2016 29/09/2017
41 Ruzuku Baraza la Manispaa Magharibi
“A”
23/09/2016 28/09/2017
42 Ruzuku Baraza la Manispaa Magharibi 23/09/2016 25/09/2017
17
“B”
43 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya
Kaskazini ‘A’
6/10/2016 06/10/2017
44 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya Kati 23/09/2016 29/09/2017
45 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya
Kaskazini ‘B’
26/09/2016 21/09/2017
46 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya
Micheweni
28/09/2016 27/09/2017
47 Ruzuku Baraza la Mji Chake Chake 28/09/2016 02/10/2017
48 Ruzuku Baraza la Mji Mkoani 30/09/2016 28/09/2017
49 Ruzuku Baraza la Mji Wete 21/09/2016 29/09/2017
50 Ruzuku Baraza la Manispaa Mjini 31/10/2016 20/12/2017
51 Ruzuku Shirika la Huduma za
Maktaba
29/09/2016 29/09/2017
52 Ruzuku Mamlaka ya Usafiri Baharini 03/10/2016 29/09/2017
53 Ruzuku Bodi ya Mikopo ya Elimu ya
Juu Zanzibar
23/09/2016
11/09/2017
54 Ruzuku Bodi ya Uhaulishaji Ardhi
Zanzibar
30/09/2016 02/10/2017
55 Ruzuku Bodi ya Usajili wa
Wakandarasi
29/09/2016 28/09/2017
56 Ruzuku Wakala wa Maabara ya
Mkemia Mkuu Zanzibar
27/09/2016 12/09/2017
57 Ruzuku Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa
Serikali
3/10/2016 02/10/2017
18
3.3 Utekelezaji wa Bajeti kwa Mwaka 2016/2017
Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2016/2017 umebaini kuimarika kwa
udhibiti katika ukusanyaji wa mapato na kupelekea kuongezeka kwa mapato
yanayokusanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia vyanzo mbali mbali.
Kuongezeka kwa makusanyo kumepelekea kuimarika kwa hali ya uchumi na
kuiwezesha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutekeleza mipango iliyojipangia kwa
ufanisi mkubwa.
Hali ya matumizi kwa taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilikuwa kama
ifuatavyo:-
Matumizi ya Kawaida
NAM
FUNGU
WIZARA/
TAASISI
MAKADIRIO
(SH)
MATUMIZI
HALISI (SH)
ASILI
MIA
ONGEZEKO/
(UPUNGUFU)
1 A 01 Ofisi ya Rais
na
Mwenyekiti
wa Baraza
la
Mapinduzi
4,998,200,000 5,115,085,859 102.3 116,885,859
2 A 02 Ofisi ya Rais
Baraza la
Mapinduzi –
BLM
1,492,000,000 1,403,455,900 94 (88,544,100)
3 C 01 Afisi ya 16,641,166,000 15,561,845,376 93.5 (1,079,320,624)
58 Ruzuku Baraza la Mitihani 29/09/2016 29/09/2017
59 Ruzuku Taasisi ya Viwango Zanzibar 13/01/2017 27/12/2017
60 Ruzuku Hesabu za Huduma za Mfuko
Mkuu wa Serikali
18/10/2016 29/09/2017
19
Makamo wa
Pili wa Rais
4 C 02 Baraza la
Wawakilishi
17,138,500,000 16,969,109,649 99 (169,390,351)
5 C 03 Tume ya
Uchaguzi
1,360,200,000 1,328,959,350 97.7 (31,240,650)
6 C 04 Tume ya
Kitaifa ya
Kuratibu na
Udhibiti wa
Dawa za
kulevya.
439,900,000 393,608,467 89.5 (46,291,533)
7 C 05 Tume ya
Ukimwi
1,230,728,838 721,560,550 58.6 (509,168,288)
8 D 01 Wizara ya
Nchi (OR)
Tawala za
Mikoa,Serik
ali za Mitaa
na Idara
Maalum
6,103,370,423 5,835,877,704 95.62 (267,492,719)
9 D 02 Jeshi la
Kujenga
Uchumi –
JKU
14,737,814,104 14,594,755,630 99 (143,058,474)
10 D 03 Chuo cha
Mafunzo
9,280,578,000 10,639,961,511 114.65 1,413,383,511
11 D 04 Kikosi cha
KMKM
16,771,028,863 16,768,147,664 99.9 (2,881,199)
12 D 05 Kikosi cha
Zimamoto
na Uokozi
5,068,080,000 5,853,106,302 115.49 785,026,302
13 D 06 Kikosi cha
Valantia
7,776,307,440 7,692,296,415 98.9 (84,011,025)
14 D 07 Mkoa wa
Mjini
1,760,247,600 1,696,799,440 96.39 (63,448,160)
20
Magharibi
15 D 08 Mkoa wa
Kusini
Unguja
1,336,872,350 1,324,252,633 99.05 (12,619,717)
16 D 09 Mkoa wa
Kaskazini
Unguja
1,341,070,350 1,339,022,100 99.85 (2,048,250)
17 D 10 Mkoa wa
Kusini
Pemba
2,057,578,950 1,972,988,950 95.88 (84,590,000)
18 D 11 Mkoa wa
Kaskazini
Pemba
1,574,300,000 1,573,381,100 99.94 (918,900)
19 D 12 Afisi ya
Usajili na
Kadi za
Utambulisho
2,144,900,000 2,067,297,280 96.4 (77,602,719)
20 F 01 Wizara ya
Fedha na
Mipango
901,338,151,028 547,086,484,884 60.69 (354,251,666,144)
21 F 02 Huduma za
Mfuko Mkuu
wa Serikali
101,129,000,000 101,261,000,000 99.8 (168,000,000)
22 F 03 Tume ya
Mipango
2,157,905,540 2,023,631,312 93.78 (134,274,228)
23 G 01 Wizara ya
Katiba na
Sheria
6,374,731,096 5,239,880,863 82.19 (1,134,850,233)
24 G 02 Mahkama
Kuu
5,399,878,300 5,136,900,000 95.13 (262,978,300)
25 G 03 Afisi ya
Mwanasheri
a Mkuu
1,082,073,727 1,073,511,950 99.2 (8,561,777)
26 G 04 Afisi ya
Mkurugenzi
1,732,698,506 1,701,884,940 98.22 (30,813,566)
21
wa
Mashtaka
27 G 05 Tume ya
Kurekebisha
Sheria
491,520,504 475,887,580 96.81 (15,632,924)
28 G 07 Mamlaka ya
Kuzuia
Rushwa na
Uhujumu
Uchumi
925,050,000 1,010,923,449 109.3 85,873,449
29 G 08 Kamisheni
ya Utumishi
wa Umma
739,950,000 735,104,050 99.35 (4,845,950)
30 G 09 Tume ya
Utumishi
Serikalini
412,500,000 410,924,050 99.62 (1,575,950)
31 H 01 Wizara ya
Afya
35,747,204,731 36,637,709,265 102.5 890,504,534
32 H 02 Hospitali ya
Mnazi
Mmoja
9,035,992,950 8,951,922,195 99.1 (84,070,755)
33 J 01 Wizara ya
Habari,
Utalii,
Utamaduni
na Michezo
5,907,995,250 5,402,585,264 91.44 (505,409,986)
34 J 02 Kamisheni
ya Utalii
1,112,900,000 1,091,556,976 98.08 (21,343,024)
35 K 01 Wizara ya
Elimu na
Mafunzo ya
Amali
101,895,896,988 98,894,150,775 97.05 (3,001,746,213)
36 L 01 Wizara ya
Kilimo,
Maliasili ,
Mifugo na
18,031,601,555 17,493,023,289 97.01 (538,578,266)
22
Uvuvi
37 N 01 Wizara ya
Ardhi,
Makaazi
,Maji na
Nishati
9,555,400,000 6,276,825,948 65.68 (3,278,574,052)
38 P 01 Wizara ya
Ujenzi
Miundombin
u,
Mawasiliano
na
Usafirishaji
6,932,012,488
6,704,441,494
96.72
(227,570,994)
39 Q 01 Wizara ya
Kazi,Uwezes
haji, Wazee,
Vijana,
Wanawake
na Watoto
12,804,605,250
11,815,304,233
92.27
(989,301,017)
40 R 01 Wizara ya
Biashara,
Viwanda na
Masoko
3,884,401,000 3,712,962,621 95.59 (171,438,379)
23
Matumizi ya Maendeleo
NAM FUNGU WIZARA/
TAASISI
MAKADIRIO
(SH)
MATUMIZI
HALISI (SH)
ASILI
MIA
ONGEZEKO/
(UPUNGUFU)
1 A 01 Ofisi ya Rais
na
Mwenyekiti
wa Baraza la
Mapinduzi
500,000,000 500,000,000 100 -
2 D 01 Wizara ya
Nchi (OR)
Tawala za
Mikoa,Serikal
i za Mitaa na
Idara
Maalum
20,272,299,657
20,210,913,847
99.7
(61,385,810)
3 D 04 Kikosi cha
KMKM
1,242,000,000 1,118,561,809 90.06 (123,438,191)
4 F 01 Wizara ya
Fedha na
Mipango
5,855,898,696 5,366,252,356 91.64 (489,646,340)
5 F 03 Tume ya
Mipango
1,255,211,545 1,255,211,545 100 -
6 G 01 Wizara ya
Katiba,
Sheria,
Utumishi wa
Umma na
Utawala
Bora
557,349,000 412,452,543 74 (144,896,457)
7 G 02 Mahkama
Kuu
38,900,000 37,582,000 96.61 (1,318,000)
8 G 03 Afisi ya
Mwanasheria
Mkuu
113,928,226 111,928,225 98.24 (2,000,001)
9 G 04 Afisi ya
Mkurugenzi
49,500,000 49,002,150 98.99 (497,850)
24
wa Mashtaka
10 G 05 Tume ya
Kurekebisha
Sheria
35,000,000 21,371,420 61.06 (13,628,580)
11 G 07 Mamlaka ya
Kuzuia
Rushwa na
Uhujumu
Uchumi
11,250,000
8,692,201 77.26 (2,557,799)
12 G 08 Kamisheni ya
Utumishi wa
Umma
69,250,000 69,250,000 100 -
13 G 09 Tume ya
Utumishi
Serikalini
13,000,000 13,000,000 100 -
14 H 01 Wizara ya
Afya
18,448,166,270 7,336,411,625 39.76 (11,111,754,645)
15 J 01 Wizara ya
Habari,
Utalii,
Utamaduni
na Michezo
6,149,679,000
2,949,622,929
47.96
(3,200,056,071)
16 K 01 Wizara ya
Elimu na
Mafunzo ya
Amali
1,628,209,600 1,007,086,835 61.85 (621,122,765)
17 L 01 Wizara ya
Kilimo,
Maliasili ,
Mifugo na
Uvuvi
30,946,159,445 7,221,828,728 23.33 (23,724,330,717)
18 N 01 Wizara ya
Ardhi,
Makaazi
,Maji na
Nishati
47,900,786,000 35,349,867,225 73.8 (12,550,918,775)
25
19 P 01 Wizara ya
Ujenzi
Miundombin
u,
Mawasiliano
na
Usafirishaji
145,294,472,364
7,474,121,864 5.14
(137,820,350,500)
20 Q 01 Wizara ya
Kazi,Uwezes
haji, Wazee,
Vijana,
Wanawake
na Watoto.
275,650,000
38,731,929
14.05
(236,918,071)
21 R 01 Wizara ya
Biashara,
Viwanda na
Masoko
3,000,000,000 2,345,987,028 78.19 (654,012,972)
3.4 Aina ya Hati za Ukaguzi
Hati za ukaguzi zinatolewa kutokana na matokeo ya ukaguzi ambapo hati hizo
huonesha aina ya hati inayotolewa kulingana na taarifa za hesabu zilizokaguliwa
zenye kuonyesha hali halisi ya hesabu hizo.
Aina tofauti ya hati za ukaguzi zinatolewa kwa mazingira tofauti kulingana na usahihi
wa hesabu zilizokaguliwa. Hati zenyewe ni kama zifuatazo:-
Hati inayoridhisha, Hati isiyoridhisha, Hati yenye mashaka na Hati mbaya.
Hati inayoridhisha
Hati ya aina hii inatolewa pale ambapo ukaguzi umejiridhisha kutokana na kukidhi
viwango vilivyotumika katika uandaaji wa hesabu, usahihi wa taarifa pamoja na
ushahidi uliopatikana wakati wa ukaguzi, na kupelekea kutoa sura sahihi na halisi ya
hesabu hizo.
26
Hati isiyoridhisha
Hati ya aina hii inatolewa pale ambapo ukaguzi umejiridhisha kwamba taarifa za
hesabu zilizoandaliwa imebainika kuwa zina dosari kubwa na za umuhimu, dosari
ambazo zinaweza kusababisha taarifa za hesabu kupoteza uhalisia wake na hivyo
kutoaminiwa na kupelekea kutokuonyesha sura sahihi na halisi ya hesabu hizo.
Hati yenye shaka
Hati ya aina hii hutolewa baada ya Ukaguzi kujiridhisha kuwa, kulingana na ushahidi
wa kiukaguzi mambo yafuatayo yamejitokeza.
Taarifa za fedha zilizoandaliwa zina dosari kubwa ambazo zinaweza kuathiri hesabu
endapo zikichukuliwa aidha moja baada ya moja au kwa ujumla wake kwenye taarifa
hizo haitoweza kuleta sura sahihi na halisi za hesabu hizo.
Pale ambapo ukaguzi umeshindwa kupata taarifa, nyaraka na vielelezo vya kutosha
vitakavyosaidia kufanya ukaguzi na kuweza kutoa maoni ya ukaguzi kwa hesabu
hizo.
Kuwepo kwa kiasi kikubwa cha mapato na matumizi yasiyokua na nyaraka muhimu
na kufanya matumizi bila ya kuwa na kibali halali au matumizi ya mapato ambayo
hayakuidhinishwa kutumika.
Kutozingatiwa kwa sheria na kanuni mbali mbali ambapo kunapelekea madhara
makubwa ambayo yanaweza kusababisha kutokutoa sura sahihi na halisi ya hesabu
hizo kwa mfano, kuwa na vitu ambavyo vilitakiwa kuripotiwa kwenye taarifa za
hesabu lakini havikuripotiwa na manunuzi ya vifaa hayakufuata sheria na kanuni za
manunuzi.
Kufanya matumizi ambayo hayakuleta tija kwa taasisi husika.
Kutofanyika kwa usuluhisho wa benki hali inayopelekea kushindwa kupata usahihi
wa salio la fedha mwishoni mwa mwaka wa fedha.
Hati mbaya
Hati hii hutolewa pale ambapo ukaguzi umeshindwa kupata nyaraka na vielelezo vya
kutosha wakati wa ukaguzi ili kuweza kutoa maoni ya ukaguzi kutokana na
27
mapungufu yaliyojitokeza na kushindwa kugundua mambo ambayo yanaweza
kusababisha madhara makubwa katika Taasisi.
Hati zilizotolewa ni kama ifuatavyo: -
Nam Fungu Wizara/Taasisi Aina ya Hati iliyotolewa
1 A 01 Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi
Hati inayoridhisha
2 A 02 Ofisi ya Rais Baraza la
Mapinduzi – BLM
Hati inayoridhisha
3 C 01 Afisi ya Makamo wa Pili wa Rais Hati inayoridhisha
4 C 02 Baraza la Wawakilishi Hati inayoridhisha
5 C 03 Tume ya Uchaguzi Hati inayoridhisha
6 C 04 Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na
Udhibiti wa Dawa za kulevya.
Hati inayoridhisha
7 C 05 Tume ya Ukimwi Hati inayoridhisha
8 D 01 Wizara ya Nchi (OR) Tawala za
Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara
Maalum
Hati inayoridhisha
9 D 02 Jeshi la Kujenga Uchumi – JKU Hati inayoridhisha
10 D 03 Chuo cha Mafunzo Hati inayoridhisha
11 D 04 Kikosi cha KMKM Hati inayoridhisha
12 D 05 Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Hati inayoridhisha
13 D 06 Kikosi cha Valantia Hati inayoridhisha
14 D 07 Mkoa wa Mjini Magharibi Hati inayoridhisha
15 D 08 Mkoa wa Kusini Unguja Hati inayoridhisha
28
16 D 09 Mkoa wa Kaskazini Unguja Hati inayoridhisha
17 D 10 Mkoa wa Kusini Pemba Hati inayoridhisha
18 D 11 Mkoa wa Kaskazini Pemba Hati inayoridhisha
19 D 12 Afisi ya Usajili na Kadi za
Utambulisho
Hati inayoridhisha
20 F 01 Wizara ya Fedha na Mipango Hati inayoridhisha
21 F 02 Mfuko Mkuu wa Serikali Hati inayoridhisha
22 F 03 Tume ya Mipango Hati inayoridhisha
23 G 01 Wizara ya Katiba na Sheria Hati inayoridhisha
24 G 02 Mahkama Kuu Hati inayoridhisha
25 G 03 Afisi ya Mwanasheria Mkuu Hati inayoridhisha
26 G 04 Afisi ya Mkurugenzi wa
Mashtaka
Hati inayoridhisha
27 G 05 Tume ya Kurekebisha Sheria Hati inayoridhisha
28 G 07 Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na
Uhujumu Uchumi
Hati inayoridhisha
29 G 08 Kamisheni ya Utumishi wa
Umma
Hati inayoridhisha
30 G 09 Tume ya Utumishi Serikalini Hati inayoridhisha
31 H 01 Wizara ya Afya Hati inayoridhisha
32 H 02 Hospitali ya Mnazi Mmoja Hati inayoridhisha
33 J 01 Wizara ya Habari, Utalii,
Utamaduni na Michezo
Hati inayoridhisha
34 J 02 Kamisheni ya Utalii Hati inayoridhisha
29
35 K 01 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Amali
Hati inayoridhisha
36 L 01 Wizara ya Kilimo, Maliasili ,
Mifugo na Uvuvi
Hati inayoridhisha
37 N 01 Wizara ya Ardhi, Makaazi ,Maji
na Nishati
Hati inayoridhisha
38 P 01 Wizara ya Ujenzi Miundombinu,
Mawasiliano na Usafirishaji
Hati inayoridhisha
39 Q 01 Wizara ya Kazi,Uwezeshaji,
Wazee, Vijana, Wanawake na
Watoto.
Hati inayoridhisha
40 R 01 Wizara ya Biashara, Viwanda na
Masoko
Hati inayoridhisha
41 Ruzuku Baraza la Manispaa Magharibi
“A”
Hati inayoridhisha
42 Ruzuku Baraza la Manispaa Magharibi
“B”
Hati inayoridhisha
43 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya
Kaskazini ‘A’
Hati inayoridhisha
44 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya Kati Hati inayoridhisha
45 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya
Kaskazini ‘B’
Hati inayoridhisha
46 Ruzuku Halmashauri ya Wilaya ya
Micheweni
Hati inayoridhisha
47 Ruzuku Baraza la Mji Chake Chake Hati inayoridhisha
48 Ruzuku Baraza la Mji Mkoani Hati inayoridhisha
30
49 Ruzuku Baraza la Mji Wete Hati inayoridhisha
50 Ruzuku Baraza la Manispaa Mjini Hati inayoridhisha
51 Ruzuku Shirika la Huduma za Maktaba Hati inayoridhisha
52 Ruzuku Mamlaka ya Usafiri Baharini Hati inayoridhisha
53 Ruzuku Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
Zanzibar
Hati inayoridhisha
54 Ruzuku Bodi ya Uhaulishaji Ardhi
Zanzibar
Hati inayoridhisha
55 Ruzuku Bodi ya Usajili wa Wakandarasi Hati inayoridhisha
56 Ruzuku Wakala wa Maabara ya Mkemia
Mkuu Zanzibar
Hati inayoridhisha
57 Ruzuku Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa
Serikali
Hati inayoridhisha
58 Ruzuku Baraza la Mitihani Hati inayoridhisha
59 Ruzuku Taasisi ya Viwango Zanzibar Hati inayoridhisha
60 Ruzuku Hesabu za Huduma za Mfuko
Mkuu wa Serikali
Hati inayoridhisha
31
SURA YA NNE
4.0 MATOKEO YA UKAGUZI KWA MWAKA 2016/2017
Katika ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 imebainika kwamba uwekaji wa
kumbukumbu na taarifa mbali mbali za hesabu ikiwemo fedha na rasilimali za umma
pamoja na udhibiti wa ndani .
Katika ukaguzi huo kulijitokeza dosari za kiutendaji kwa baadhi ya Wizara na Taasisi
za Serikali ambapo baadhi ya dosari ziliweza kurekebishwa na kupatiwa ufafanuzi
lakini kuna baadhi ya hoja za ukaguzi hazikuweza kupatiwa ufafanuzi hadi ukaguzi
unakamilika. Matokeo ya ukaguzi ni kama ifuatavyo:-
4.1 WIZARA YA NCHI OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA
MAPINDUZI
4.1.1 FUNGU A 01 - OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA
MAPINDUZI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi umefanywa kwa kuzingatia Sheria,kanuni,
taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na
kimataifa.
Taarifa ya matumizi
Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa mwaka wa
fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 4,998,200,000 kwa kazi za
kawaida na jumla ya shilingi 500,000,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, Wizara imeingiziwa jumla ya shilingi 5,115,085,859 kwa
kazi za kawaida sawa na asilimia 102.3 ya makadirio na shilingi 500,000,000 kwa
kazi za maendeleo sawa na asilimia 100 ya makadirio.
32
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017
zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na
kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.1.2 FUNGU A 02 – OFISI YA RAIS BARAZA LA MAPINDUZI – BLM
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 1,492,000,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 1,403,455,900 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 94 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
33
4.2 WIZARA YA NCHI (OR) TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA NA
IDARA MAALUM
4.2.1 FUNGU D 01 - WIZARA YA NCHI (OR) TAWALA ZA MIKOA NA IDARA
MAALUM
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Wizara ya Nchi (OR) Tawala za
Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni,
taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na
kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Nchi (OR) Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara maalum kwa
mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia shilingi 6,103,370,423 kwa kazi za
kawaida na shilingi 20,272,299,657 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2017 Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,
Serikali za Mitaa na Idara Maalum iliingiziwa na kutumia jumla ya shilingi
5,835,877,704 kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 95.62 ya makadirio na shilingi
20,210,913,847 kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 99.7 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Nchi (OR) Tawala za
Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni,
2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na
kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Nchi (OR) Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara
Maalum imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
34
4.2.2 FUNGU D 02 - JESHI LA KUJENGA UCHUMI (JKU)
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Jeshi la Kujenga Uchumi umefanywa
kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika
kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Jeshi la kujenga Uchumi lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 44,400,000 katika
kipindi cha mwaka 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi
45,300,000 zilikusanywa sawa na asilimia 101 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Jeshi la kujenga Uchumi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 lilikadiriwa kutumia jumla
ya shilingi 14,737,814,104 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 14,594,755,630 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na asilimia 99 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Jeshi la Kujenga Uchumi kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Jeshi la Kujenga Uchumi limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.3 FUNGU D 03 – CHUO CHA MAFUNZO
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Chuo cha Mafunzo
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Chuo cha Mafunzo kilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 60,578,000 katika kipindi
cha mwaka 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 30,500,000
zilikusanywa sawa na asilimia 50 ya makadirio.
35
Taarifa ya Matumizi
Chuo cha Mafunzo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 9,280,578,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 10,639,961,511 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na asilimia 114.65 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.2.3.1 Hati ya malipo iliyokosekana kwa ukaguzi shilingi
208,280,945.75
Ukaguzi umebaini kwamba jumla ya shilingi 208,280,945.75zimelipwa kutoka Mfumo
wa malipo wa Wizara ya Fedha kutoka Fungu la Chuo cha Mafunzo kwa
kumbukumbu ya malipo namba 17CR1004 katika mwezi wa Juni 2017.
Ukaguzi umeshindwa kupata hati ya malipo hayo ya shilingi 208,280,945.75ili
kuweza kuthibitisha uhalali wa malipo hayo.
Aidha maelezo pamoja na vielelezo vya malipo hayo havikupatikana kwa ukaguzi,
kufanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria ya Usimamizi wa Fedha za Umma
Nambari 12 ya mwaka 2016.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Chuo cha Mafunzo kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Chuo cha Mafunzo kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.4 FUNGU D 04 - KIKOSI MAALUM CHA KUZUIA MAGENDO (KMKM)
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Kikosi cha KMKM umefanywa kwa
kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana
na viwango vya kitaifa na kimataifa.
36
Taarifa ya Matumizi
Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 16,771,028,863 kwa matumizi ya kazi za kawaida na
shilingi 1,242,000,000 kwa matumizi ya kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 16,768,147,664 ziliingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ikiwa ni sawa na asilimia 99.9 ya makadirio na shilingi
1,118,561,809 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 90
ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Kikosi cha Kuzuia Magendo kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Kikosi cha Kuzuia Magendo kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.5 FUNGU D 05 – KIKOSI CHA ZIMAMOTO NA UOKOZI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Kikosi cha Zimamoto na Uokozi kilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 21,084,000
kwa kipindi cha mwaka 2016/2017, hadi kufikia Juni 2017 jumla ya shilingi
21,250,000 zilikusanywa na kuingizwa katika Mfuko Mkuu ambapo sawa na asilimia
100.1 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Kikosi cha Zimamoto na Uokozi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 5,068,080,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 5,853,106,302 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na asilimia 115 ya makadirio.
37
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Kikosi cha Zimamoto na Uokozi kimepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.6 FUNGU D 06 - KIKOSI CHA VALANTIA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Kikosi cha Valantia umefanywa kwa
kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana
na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Kikosi cha Valantia kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kilikadiriwa kukusanya jumla ya
shilingi 18,000,000.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 18,000,000 zimekusanywa sawa na
asilimia 100 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Kikosi cha Valantia kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 7,776,307,440 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 7,692,296,415 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 99 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Kikosi cha Valantia kwa mwaka
wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Kikosi cha Valantia kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.7 OFISI YA USAJILI NA KADI ZA UTAMBULISHO
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Ofisi ya Usajili na Kadi za Utambulisho
umefanywa kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
38
Taarifa ya Matumizi
Ofisi ya Usajili na Kadi za Utambulisho kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 2,144,900,000 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni
2017 jumla ya shilingi 2,068,297,281 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za kawaida
ambayo ni sawa na asilimia 96.4 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Ofisi ya Usajili na Kadi za
Utambulisho kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi
na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Ofisi ya Usajili na Kadi za Utambulisho imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.8 FUNGU D 07 – MKOA WA MJINI MAGHARIBI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Mkoa wa Mjini Magharibi
umefanywa kwa kuzingatia sheria,kanuni,taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Mkoa wa Mjini Magharibi ulikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 35,989,000 katika
kipindi cha mwaka 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Mkoa wa Mjini Magharibi
ulikusanya jumla ya shilingi 20,332,000 sawa na asilimia 56 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Mkoa wa Mjini Magharibi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ulikadiriwa kutumia jumla
ya shilingi 1,760,247,600 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 1,696,799,440 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 96 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mkoa wa Mjini Magharibi kwa
39
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mkoa wa Mjini Magharibi umepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.9 FUNGU D 08 – MKOA WA KUSINI UNGUJA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Mkoa wa Kusini Unguja umefanywa
kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika
kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Mkoa wa Kusini Unguja kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ulikadiriwa kutumia jumla
ya shilingi 1,336,872,350 kwa matumizi ya kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni
2017, kiasi cha shilingi 1,324,252,633 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za kawaida
sawa na asilimia 99 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mkoa wa Kusini Unguja kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mkoa wa Kusini Unguja umepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.10 FUNGU D 09 – MKOA WA KASKAZINI UNGUJA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Mkoa wa Kaskazini Unguja
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Mkoa wa Kaskazini Unguja kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ulikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 1,341,070,350 kwa ajili ya matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 1,339,022,100 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 99.85 ya makadirio.
40
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mkoa wa Kaskazini Unguja kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mkoa wa Kaskazini Unguja umepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.11 FUNGU D 10 – MKOA WA KUSINI PEMBA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Mkoa wa Kusini Pemba umefanywa
kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika
kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Mkoa wa Kusini Pemba kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ulikadiriwa kutumia jumla
ya shilingi 2,057,578,950 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 1,972,988,950 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 95.88 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mkoa wa Kusini Pemba kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mkoa wa Kusini Pemba umepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.12 FUNGU D 11 - MKOA WA KASKAZINI PEMBA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Mkoa wa Kaskazini Pemba
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
41
Taarifa ya Matumizi
Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ulikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 1,574,300,000 kwa ajili ya matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 1,573,381,100 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 99.94 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mkoa wa Kaskazini Pemba umepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni 2017.
4.2.13 BARAZA LA MANISPAA MJINI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Baraza la Manispaa Mjini umefanywa
kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika
kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Baraza la Manispaa Mjini lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 4,532,474,000
kutoka katika vianzio vyake mbali mbali kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 5,218,869,414 zilikusanywa na Baraza
sawa na asilimia 113 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Manispaa Mjini lilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 4,532,474,000 kwa
kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 5,333,234,047
zimetumika kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 118 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Manispaa Mjini kwa
42
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Manispaa Mjini limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.14 BARAZA LA MANISPAA MAGHARIBI - A
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Baraza la Manispaa Magharibi - A
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Baraza la Manispaa Magharibi - A lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
500,000,000 kutoka katika vianzio vyake mbali mbali kwa mwaka wa fedha
2016/2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 557,402,000 zilikusanywa na Baraza sawa
na asilimia 111 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Manispaa Magharibi - A lilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 499,006,000
kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 490,584,671
zimetumika kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 98 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Manispaa Magharibi - A
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Manispaa Magharibi - A limepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.15 BARAZA LA MANISPAA MAGHARIBI - B
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Baraza la Manispaa Magharibi - B
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
43
Taarifa ya Mapato
Baraza la Manispaa Magharibi - B lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
1,402,703,098 kutoka katika vianzio vyake mbali mbali kwa mwaka wa fedha
2016/2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 1,373,449,767 zilikusanywa na Baraza
sawa na asilimia 98 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Manispaa Magharibi - B lilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 1,402,703,098
kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 1,391,504,233
zimetumika kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 99 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Manispaa Magharibi - B
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Manispaa Magharibi - B limepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.16 HALMASHAURI YA WILAYA YA KASKAZINI ‘A’ UNGUJA.
Ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini
‘A’ Unguja umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja ilikadiriwa kukusanya jumla ya
shilingi 505,500,000 kutoka katika vianzio vyake mbali mbali kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni 2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 329,323,463 zilikusanywa sawa na
asilimia 65 ya makadirio.
44
Taarifa ya Matumizi
Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 545,500,750 kwa kazi za kawaida .Hadi kufikia
30 Juni 2017 jumla ya shilingi 528,372,031 zimetumika kwa kazi za kawaida ambazo
sawa na asilimia 97 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya
Kaskazini ‘A’ Unguja kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura
sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja imepata hati
inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.17 HALMASHAURI YA WILAYA YA KASKAZINI “B” UNGUJA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Halmashauri ya Wilaya ya
Kaskazini ‘B’ Unguja umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo
vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja ilikadiriwa kukusanya jumla ya
shilingi 560,500,000 kutoka katika vianzio vyake mbalimbali kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni 2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 672,779,781 zilikusanywa sawa na
asilimia 120 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “B” kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 341,932,180 kwa kazi za kawaida na jumla ya shilingi
256,592,820 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 322,293,085 zimetumika kwa kazi za
kawaida sawa na asilimia 94 ya makadirio na shilingi 321,074,632 kwa kazi za
maendeleo sawa na asilimia 125 ya makadirio.
45
Maoni ya ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya
Kaskazini ‘B’ Unguja kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura
sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja imepata hati
inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.18 HALMASHAURI YA WILAYA YA KATI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Halmashauri ya Wilaya ya
Kati umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Halmashauri ya Wilaya ya Kati Unguja ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
420,000,000 kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni 2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017
jumla ya shilingi 426,654,636 zilikusanywa sawa na asilimia 102 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Halmashauri ya Wilaya ya Kati kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 273,717,292 kwa kazi za kawaida na shilingi 146,282,708 kwa kazi
za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 397,929,568 zimetumika kwa kazi za
kawaida ambazo sawa na asilimia 145 ya makadirio na shilingi 76,579,331 kwa kazi
za maendeleo sawa na asilimia 52 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Kati
Unguja kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Kati imepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
46
4.2.19 BARAZA LA MJI CHAKE-CHAKE
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Baraza la Mji la Chake-
Chake umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Baraza la Mji Chake Chake lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 305,000,000
kutoka katika vianzio vyake mbali mbali kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 320,524,600 zilikusanywa sawa na
asilimia 105 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Mji Chake Chake kwa mwaka wa fedha 2016/2017 lilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 196,070,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida na jumla ya shilingi
108,930,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 211,438,710 ziliingizwa na kutumika kwa
kazi za kawaida ikiwa ni sawa na asilimia 107.84 ya makadirio na shilingi
103,154,994 kwa kazi za maendeleo ikiwa ni sawa na asilimia 94.7 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.2.19.1 Malipo yasiokuwa na vielelezo shilingi 10,230,720
Ukaguzi umebaini jumla ya shilingi 10,230,720 zimetumika kwa matumizi mbali
mbali lakini vielelezo husika havikuambatanishwa na hati za malipo ili kuweza
kuthibitisha uhalali wa malipo hayo.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria Nambari 12 ya Usimamizi wa Fedha na
mali za Umma ya mwaka 2016 ya Zanzibar.
47
Malipo yenyewe ni kama ifuatavyo:-
Nam Hati Nam Hundi Nam Thamani Aliyelipwa Maelezo
6/8 001850 3,234,000 Abatter Auto
Parts
Ununuzi wa vifaa
kwa ajili ya magari
yanayopeleka fusi
Michakaini.
54/8 001887 354,000 Pemba
General
Supply &
Insurance
Agency.
Ikiwa ni malipo kwa
ajili ya kulipia Bima.
17/10 001929 529,200 Adult Training
Centre.
Malipo ya mwanzo
ya fedha kwa ajili
ya ununuzi wa vifaa
mbalimbali vya
kuandikia kwa
matumizi ya
B/M/Chake na
malipo ya
vitambulisho vya
madiwani.
12/12 002003 1,000,000 Zanzibar
Petroleum
Station.
Ununuzi wa mafuta
kwa matumizi ya
ofisi.
6/4
002195 665,420 Suleiman Seif
Rashid.
Ununuzi wa vifaa
mbalimbali kwa ajili
ya matumizi ya ofisi
ya B/M/Chake.
48
18/2
002109 937500 Bakar Petrol
Station.
Ununuzi wa mafuta
kwa ajili ya kazi za
Baraza.
20/3
002156 950,600 Khamis
Yussuf
Hamad.
Ununuzi wa mabero
kwa ajili ya usafi
wa maeneo mbali
mbali.
34/3
002166 2,560,000 Hafidh Salum
Rashid.
Malipo kwa ajili ya
kutengeneza alama
za barabarani.
Jumla 10,230,720
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Mji Chake Chake kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Mji Chake Chake limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.20 BARAZA LA MJI MKOANI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Baraza la Mji Mkoani
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
49
Taarifa ya Mapato
Baraza la Mji Mkoani lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 213,000,000 kutoka
katika vianzio vyake mbalimbali kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 201,357,614 zilikusanywa sawa na
asilimia 95 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Mji Mkoani kwa mwaka wa fedha 2016/2017 lilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 148,000,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida na shilingi 65,000,000 kwa
matumizi ya kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 135,146,100 zimetumika kwa kazi za
kawaida sawa na asilimia 91.32 ya makadirio na shilingi 66,105,263 zimetumika kwa
kazi za maendeleo sawa na asilimia 101.7 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Mji Mkoani kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Mji Mkoani limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.21 BARAZA LA MJI WETE
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Baraza la Mji Wete
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Baraza la Mji Wete lilikadiriwa kukusanya shilingi 250,000,000 kwa mwaka wa fedha
2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Baraza limekusanya jumla ya shilingi
138,528,048 sawa na asilimia 55.41 ya makadirio.
50
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Mji Wete kwa mwaka wa fedha 2016/2017 lilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 150,000,000 kwa kazi za kawaida na shilingi 100,000,000 kwa kazi za
maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 121,578,048.73 zimetumika kwa kazi za
kawaida sawa na asilimia 81.1ya makadirio na shilingi 16,950,000 kwa kazi za
maendeleo sawa na asilimia 17 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.2.21.1 Malipo yasiokuwa na vielelezo shilingi 11,728,956
Ukaguzi umebaini kwamba jumla ya shilingi 11,728,956 zimetumika kwa matumizi
mbali mbali lakini vielelezo husika havikuambatanishwa na hati za malipo ili kuweza
kuthibitisha uhalali wa malipo hayo.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria Nambari 12 ya Usimamizi wa Fedha na
Mali za Umma ya mwaka 2016 ya Zanzibar.
Malipo yenyewe ni kama ifuatavyo:-
Nam. Nam. ya
Hati
Nam. ya
Hundi
Thamani Alielipwa Maelezo
57/9 668579 3,960,180 Moh’d Khalfan
Adeyoum
Ununuzi wa vifaa
vya usafi kwa kazi
za baraza.
20/3 668762 2,188,776 Chasasa S.
Station.
Ununuzi wa mafuta
kwa matumizi ya
ofisi ya Baraza.
16/4 668795 5,580,000 B/M/Wete Ununuzi wa vifaa
vya ujenzi kwa ajili
ya uezekaji wa skuli
ya Chasasa
sekondari.
Jumla 11,728,956
51
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Mji Wete kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Mji Wete limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.2.22 HALMASHAURI YA WILAYA YA MICHEWENI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Halmashauri ya Wilaya ya
Micheweni umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kukusanya jumla ya shilingi 150,000,000 kutoka katika vianzio vyake mbali mbali.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 141,111,662.97 zilikusanywa sawa na
asilimia 94 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni kwa mwaka wa fedha 2016/2017 lilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 92,500,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida na shilingi
54,500,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 90,664,465 zimetumika kwa kazi za
kawaida sawa na asilimia 98.02 ya makadirio na shilingi 25,036,310 kwa kazi za
maendeleo sawa na asilimia 45.94 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya
Micheweni kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
52
Kwa hali hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.3 WIZARA YA NCHI (OR) KATIBA, SHERIA, UTUMISHI WA UMMA NA
UTAWALA BORA
4.3.1 FUNGU G 01 - WIZARA YA NCHI (OR) KATIBA, SHERIA, UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Nchi (OR) Katiba,
Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora umefanywa kwa kuzingatia
Sheria,kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango
vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Nchi(OR) Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora ilikadiriwa
kukusanya jumla ya shilingi 85,604,004 katika kipindi cha mwaka wa fedha
2016/2017.Hadi kufikia 30 Juni 2017 Wizara imekusanya jumla ya shilingi
62,293,578 sawa na asilimia 73 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Nchi(OR) Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka
wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 6,374,731,096 kwa kazi za
kawaida na jumla ya shilingi 557,349,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 5,239,880,863 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambayo ni sawa na asilimia 82.19 ya makadirio na shilingi
412,452,543 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 74
ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Nchi(OR) Katiba,
Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha unaoishia 30
Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa
na kimataifa.
53
Kwa hali hiyo Wizara ya Nchi (OR) Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala
Bora imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.3.2 FUNGU G 02 - MAHKAMA KUU
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Mahkama Kuu umefanywa
kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika
kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Mahkama Kuu ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 301,776,000 katika kipindi cha
mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Mahkama Kuu ilikusanya
jumla ya shilingi 392,453,470 sawa na asilimia 130 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Mahkama Kuu kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi
5,399,878,300 kwa matumizi ya kazi za kawaida na jumla ya shilingi 38,900,000 kwa
matumizi ya kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 5,136,900,000 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 95 ya makadirio na jumla ya shilingi
37,582,000 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 97 ya
makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mahkama Kuu kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo
vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mahkama Kuu imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
54
4.3.3 FUNGU G 03 – OFISI YA MWANASHERIA MKUU
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 1,082,073,727 kwa kazi za kawaida na shilingi 113,928,226 kwa
kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 1,073,511,950 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na asilimia 99 ya makadirio na shilingi
111,928,225 zimetumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 98 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Ofisi ya Mwanasheria Mkuu imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.3.4 FUNGU G 04 – OFISI YA MKURUGENZI WA MASHTAKA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Ofisi ya Mkurugenzi wa
Mashtaka umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 1,782,198,506 . Kati ya hizo shilingi 1,732,698,206 kwa
kazi za kawaida na shilingi 49,500,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 1,071,884,940 ziliingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 98.2 ya makadirio na shilingi 49,002,150
zimetumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 99 ya makadirio.
55
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.3.5 FUNGU G 05 – TUME YA KUREKEBISHA SHERIA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Tume ya Kurekebisha
Sheria umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Tume ya Kurekebisha Sheria kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 491,520,504 kwa matumizi ya kazi za kawaida na shilingi
35,000,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 475,887,580 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ikiwa ni sawa na asilimia 97 ya makadirio na shilingi 21,371,420
zimetumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 61 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Tume ya Kurekebisha Sheria kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Tume ya Kurekebisha Sheria imepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.3.6 FUNGU G 08 - KAMISHENI YA UTUMISHI WA UMMA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Kamisheni ya Utumishi wa
Umma umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
56
Taarifa ya Matumizi
Kamisheni ya Utumishi wa Umma kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 739,950,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida na shilingi
69,250,000 kwa matumizi ya kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 Kamisheni ya Utumishi ya Umma iliingiziwa na kutumia
jumla ya shilingi 735,104,050 kwa matumizi ya kazi za kawaida sawa na asilimia 99
ya makadirio na shilingi 69,250,000 kwa matumizi ya kazi za maendeleo sawa na
asilimia 100 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Kamisheni ya Utumishi wa Umma
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Kamisheni ya Utumishi wa Umma imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.3.7 FUNGU G 09 - TUME YA UTUMISHI SERIKALINI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Tume ya Utumishi Serikalini
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Katika kipindi cha fedha 2016/2017 Tume ya Utumishi Serikalini ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 412,500,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida na shilingi
13,000,000 kwa matumizi za kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 Tume ya Utumishi Serikalini iliingiziwa jumla ya shilingi
410,924,050 kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 99.6 ya makadirio na shilingi
13,000,000 kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 100 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Tume ya Utumishi Serikalini kwa
57
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Tume ya Utumishi Serikalini imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.3.8 FUNGU G 07- MAMLAKA YA KUZUIA RUSHWA NA UHUJUMU WA
UCHUMI ZANZIBAR
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Mamlaka ya kuzuia Rushwa
na Uhujumu wa Uchumi umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na
vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi kwa mwaka wa fedha
2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 925,050,000 kwa matumizi ya kazi za
kawaida na shilingi 11,250,000 kwa matumizi za kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi
imeingiziwa jumla ya shilingi 1,010,923,449 kwa kazi za kawaida sawa na asilimia ya
109 ya makadirio na shilingi 8,692,201 kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 77
ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na
Uhujumu Uchumi kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura
sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi imepata hati
inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
58
4.4 WIZARA YA NCHI OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS
4.4.1 FUNGU C 01 - OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Ofisi ya Makamo wa Pili wa
Rais umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 793,766,000
katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017.Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya
shilingi 856,098,797 zilikusanywa sawa na asilimia 107.85 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais kwa mwaka wa fedha 2016/2017 lilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 16,641,166,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 15,561,445,376 zimeingizwa na
kutumika kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na asilimia 93.51 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.4.2 FUNGU C 02 - BARAZA LA WAWAKILISHI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Baraza la Wawakilishi
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Wawakilishi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 lilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 17,138,500,000 kwa matumizi ya kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017,
59
jumla ya shilingi 16,969,109,649 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za kawaida
ambazo ni sawa na asilimia 99 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Wawakilishi kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Wawakilishi limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.4.3 FUNGU C 03 - TUME YA UCHAGUZI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Tume ya Uchaguzi
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Katika mwaka wa fedha 2016/2017, Tume ya Uchaguzi ilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 1,360,200,000 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya
shilingi 1,328,959,350 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za kawaida sawa na
asilimia 97.7 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Tume ya Uchaguzi kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Tume ya Uchaguzi imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.4.4 FUNGU C 05 – TUME YA UKIMWI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2015/2016 kwa Tume ya Ukimwi
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
60
Taarifa ya Matumizi
Katika mwaka wa fedha 2016/2017, Tume ya Ukimwi ilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 1,230,728,838 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya
shilingi 721,560,550 zilitumika kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 58.6 ya
makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Tume ya Ukimwi kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo
vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Tume ya Ukimwi imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.4.5 FUNGU C 04 - TUME YA KITAIFA YA KURATIBU NA UDHIBITI WA
DAWA ZA KULEVYA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu
na Udhibiti wa Dawa za Kulevya umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu
na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya kwa mwaka wa fedha
2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 439,900,000 kwa matumizi ya
kawaida. Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shilingi 393,608,467 zimeingizwa na
kutumika kwa kazi matumizi ya kazi za kawaida sawa na asilimia 89.5 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na
Udhibiti wa Dawa za Kulevya kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017
zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na
kimataifa.
61
Kwa hali hiyo Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya imepata
hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.5 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
4.5.1 FUNGU F 01 - WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Fedha na
Mipango umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Fedha na Mipango ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 842,378,200,000
kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kutoka vyanzo vyake vya kodi na visivokuwa vya
kodi. Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 491,213,563,612 zilikusanywa
ambazo ni sawa na asilimia 58 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 901,338,151,028 kwa kazi za kawaida na jumla ya shilingi
5,855,898,696 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 547,086,484,884 zimeingizwa na
kutumika kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 61 ya makadirio, na shilingi
5,366,252,356 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 92
ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.5.1.1 DOSARI KATIKA UJENZI WA JENGO LA WIZARA TATU
GOMBANI PEMBA SHILINGI 7,424,606,610
Ukaguzi umebaini dosari za ukiukwaji wa taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata
mjenzi wa jengo la wizara tatu liliopo Gombani Pemba ambapo wajenzi tofauti
walishindanishwa kwa vigezo mbali mbali vilivyowekwa katika Zabuni za ujenzi huo.
Kwa mujibu wa taarifa ya kamati ya tathmini ya Zabuni pamoja na Bodi ya Zabuni
juu ya mzabuni aliyeshinda alikuwa ni Kampuni ya M/S Rans Company Ltd ambae
62
alikidhi vigezo vilivyowekwa kulingana na matakwa ya Zabuni ya ujenzi huo.
Ukaguzi umebaini kwamba kulikuwa na dosari ya kutokufuata maamuzi na ushauri
uliotolewa na kamati ya tathmini ya Zabuni. Dosari zenyewe ni kama zifuatazo:-
(a)Kutokufanyiwa kazi mapendekezo ya Kamati ya Tathmini ya Zabuni
pamoja na Bodi ya Zabuni juu ya Mzabuni alieshinda ujenzi wa Jengo la
Wizara tatu Gombani Pemba.
Ukaguzi uliofanyika ulipitia tathmini ya Zabuni iliyofanywa na kamati ya Zabuni ya
ujenzi wa jengo la Wizara tatu Gombani Pemba kwa wazabuni waliowasilisha taarifa
zao kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa na Wizara. Ukaguzi umebaini kwamba
kamati ya tathmini ilitoa mapendekezo ya kuwa Mshindi wa Zabuni ni Kampuni ya
M/S Rans Company Ltd kwa kukidhi vigezo vyote vitano vya awali na vigezo sita vya
mwisho ukilinganisha na wazabuni wengine.
Kwa mujibu wa vigezo vyote vilivyowekwa na Wizara Kati ya Wazabuni walioingia
katika mchakato wa tathmini ya Zabuni kwa gharama ya shilingi 6,372,856,090
ikijumuisha kodi ya ongezeko la thamani (VAT) na badala yake Zabuni hiyo
ikazawadiwa kwa Kampuni ya Quality Building Contractor Ltd aliyeshika nafasi ya
pili kwa gharama ya ujenzi ya shilingi 7,424,606,610 ikijumuisha kodi ya ongezeko la
thamani (VAT) kukiwa na tofauti ya shilingi 1,051,750,520.
Ukaguzi umebaini kwamba ujenzi huo utatumia jumla ya shilingi 7,424,606,610
badala ya shilingi 6,372,856,090 zilizokubaliwa na Bodi ya Zabuni kwa kampuni
iliyoshinda.Dosari hii imepelekea kuongezeka kwa gharama za ujenzi wa shilingi
1,051,750,520.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na kifungu 28 (1)(j) cha Sheria ya manunuzi na
uondoshaji wa mali za Umma nambari 12 ya mwaka 2016.
(b) Ongezeko la gharama ya Mshauri Elekezi wa Ujenzi wa jengo la Wizara
tatu Pemba( Cost Overrun)
Wizara ya Fedha imeingia mkataba na mshauri elekezi wa ujenzi wa jengo la Wizara
tatu Gombani Pemba kwa gharama za shilingi 69,000,000.
63
Ukaguzi umebani kwamba gharama za mshauri elekezi imekuwa ikiongezeka hadi
kufikia shilingi 474,124,000 na kufanya ongezeko la shilingi 405,124,000 ambazo ni
zaidi ya gharama za awali.
Aidha imebainika kuwepo kwa ongezeko la mikataba na kupelekea kuengezeka kwa
gharama za mshauri elekezi bila ya kuwepo vielelezo vilivyoidhinishwa na Bodi ya
Zabuni ya Wizara ikiwemo mchanganuo wa gharama za usimamizi pamoja na taarifa
nyenginezo kuhusiana na mikataba hiyo.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria ya manunuzi na uondoshaji wa Mali za
Umma nambari 12 ya mwaka 2016.
Malipo yaliyolipwa kwa mshauri elekezi ni kama ifuatavyo:-
Nam Mkataba Gharama za
mshauri elekezi
Jumla ya gharama
1 Mkataba wa awali 69,000,000 69,000,000
2 Mkataba wa ziada
namba 1
307,243,000 376,243,000
3 Mkataba wa ziada
namba 2
97,881,000 474,124,000
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Fedha na Mipango
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Fedha na Mipango imepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
64
4.5.2 FUNGU F 02 - HESABU ZA HUDUMA ZA MFUKO MKUU WA SERIKALI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa hesabu za Huduma za
Mfuko Mkuu wa Serikali umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na
vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Hesabu za Huduma za Mfuko Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ulikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 101,429,000,000. Hadi kufikia 30 Juni 2017
hesabu za Huduma za Mfuko Mkuu wa Serikali imeingiziwa na kutumia jumla ya
shilingi 101,261,000,000 sawa na asilimia 99.8 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.5.2.1 Malipo ya kiinua mgongo kwa ajili ya mirathi ambayo
hayakuthibitika kupokelewa Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana,
shilingi 38,110,347
Jumla ya shilingi 38,110,347 zimetolewa kutoka Hesabu ya Huduma za Mfuko Mkuu
wa Serikali kwa ajili ya malipo ya viinua mgongo kwa warithi wa marehemu mbali
mbali ambazo zimehaulishwa kwenda Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana kwa
ajili ya malipo kwa warithi mbali mbali.
Ukaguzi umeshindwa kuthibitisha kupokelewa kwa malipo hayo ya shilingi
38,110,347 kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana.
Malipo yenyewe ni kama ifuatavyo:-
Nam. Hati Nam. Tarehe Aliyelipwa Jumla ya Fedha
1. PD/181/8 30-Aug-16 K/Mtendaji
Kamisheni Ya
Wakfu Unguja
37,476,747
2. PD/185/8 30-Aug-16 K/Mtendaji
Kamisheni Ya
Wakfu Unguja
633,600
Jumla 38,110,347
65
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Huduma za Mfuko Mkuu wa
Serikali kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo hesabu za Huduma za Mfuko Mkuu wa Serikali zimepata hati
inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.5.3 FUNGU F 03 - TUME YA MIPANGO
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Tume ya Mipango
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Matumizi
Tume ya Mipango kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 2,157,905,540 kwa matumizi ya kazi za kawaida na jumla ya shilingi
1,255,211,545 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 Tume ya Mipango imeingiziwa 2,023,631,312 na kutumika
kwa matumizi ya kazi za kawaida sawa na asilimia 93.7 ya makadirio na shilingi
1,255,211,545 kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 100 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu Tume ya Mipango kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo
vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Tume ya Mipango imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.5.4 OFISI YA MTAKWIMU MKUU WA SERIKALI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa
Serikali umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
66
Taarifa ya Matumizi
Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 1,312,000,000 kwa kazi za kawaida na jumla ya shilingi
10,845,710,522 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali imeingiziwa jumla ya
shilingi 1,303,249,072 kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 99.3 ya makadirio na
shilingi 4,502,435,515 kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 41.5 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa
Serikali kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.6 WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI
4.6.1 FUNGU L 01 - WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Kilimo, Maliasili,
Mifugo na Uvuvi umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya
ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
2,817,599,000 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni
2017 Wizara ilikusanya jumla ya shilingi 3,995,027,986 sawa na asilimia 142 ya
makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 18,031,601,555 kwa kazi za kawaida na shilingi
30,946,159,445 kwa kazi za maendeleo.
67
Hadi kufikia 30 Juni 2017, kiasi cha shilingi 17,493,023,289 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 97 ya makadirio na jumla ya shilingi
7,221,828,728 kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 23.3 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo
na Uvuvi kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi imepata hati inayoridhisha
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.7 WIZARA YA BIASHARA, VIWANDA NA MASOKO
4.7.1 FUNGU R 01 - WIZARA YA BIASHARA, VIWANDA NA MASOKO
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2015/2016 kwa Wizara ya Biashara,
Viwanda na Masoko umefanywa kwa kuzingatia Sheria,kanuni, taratibu na vigezo
vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
371,230,000 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni
2017 Wizara ilikusanya jumla ya shilingi 298,770,089 sawa na asilimia 80 ya
makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 3,884,401,000 kwa kazi za kawaida na jumla ya shilingi
3,000,000,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla shilingi 3,712,962,621 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida ambapo ni sawa na asilimia 95.6 ya makadirio na shilingi
2,345,987,028 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia
78 ya makadirio.
68
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Biashara Viwanda na
Masoko kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko imepata hati inayoridhisha
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.7.2 TAASISI YA VIWANGO ZANZIBAR (ZBS)
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Taasisi ya Viwango Zanzibar
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Taasisi ya Viwango Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kukusanya
jumla ya shilingi 1,979,000,000. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Taasisi imekusanya jumla
ya shilingi 2,887,683,308 sawa na asilimia 146 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Taasisi ya Viwango Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 1,086,425,337 kwa kazi za kawaida, na shilingi 1,183,880,000 kwa
kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shilingi 863,361,585 ziliingizwa na kutumika kwa
kazi za kawaida sawa na asilimia 79.5 ya makadirio na shilingi 1,174,108,552
ziliingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 99.2 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
HESABU YA FEDHA ZA MAPATO NAMBA 051108000122
4.7.2.1 Risiti za mapato ambazo hazikurikodiwa katika daftari la
kuhifadhia Fedha Taslimu shilingi 75,748,950 na USD 11,220
Ukaguzi umebaini kwamba jumla ya shilingi 75,748,950 na USD 11,220
zimekusanywa kwa kupitia risiti mbali mbali za mapato lakini risiti za makusanyo
69
hayo hazikurikodiwa katika daftari la kuhifadhia fedha taslimu (Cash Book). Kufanya
hivyo ni kwenda kinyume na Sheria ya Usimamizi wa Fedha namba 12 ya mwaka
2016.
Risiti zenyewe ni kama zifuatazo:-
Nam. Stakabadhi Nam.
Fedha zilizokusanywa
(Tsh)
Fedha zilizokusanywa
(USD)
1. 411 305,000 -
2. 412 303,750 -
3. 428 302,500 -
4. 429 271,000 -
5. 430 271,000 -
6. 431 302,500 -
7. 432 273,750 -
8. 433 273,750 -
9. 434 303,750 -
10. 435 303,750 -
11. 436 303,750 -
12. 437 547,000 -
13. 438 30,000 250
14. 439 851,250 -
15. 440 140,000 450
16. 441 577,000 -
17. 442 303,750 -
18. 443 30,000 125
19. 444 851,000 -
20. 445 303,750 -
21. 446 303,000 -
22. 447 303,000 -
23. 448 303,000 -
70
24. 449 1,392,500 -
25. 450 576,250 -
26. 453 580,000 -
27. 01400 200,000 -
28. 01410 800,000 -
29. 01411 200,000 -
30. 01484 200,000 -
31. 01523 200,000 -
32. 058 303,700 -
33. 059 2,463,750 -
34. 067 1,198,500 -
35. 076 - 75
36. 082 120,000 -
37. 106 - 125
38. 107 30,000 195
39. 118 - 250
40. 126 20,000 500
41. 127 - 800
42. 128 1,125,000 -
43. 130 300,000 -
44. 131 - 500
45. 132 200,000 -
46. 352 – 400 17,155,000 -
47. 01051 – 01100 10,808,000 7,950
48. 01251- 01300 30,119,000 -
Jumla Tsh 75,748,950 USD 11,220
71
4.7.2.2 Vitabu vya risiti ambavyo havikupatikana kwa ukaguzi
Ukaguzi umebaini kwamba Taasisi inatumia vitabu mbali mbali vya kukusanyia
mapato lakini baadhi ya vitabu hivyo havikupatikana kwa ukaguzi. Kufanya hivyo ni
kwenda kinyume na Sheria ya Usimamizi wa Fedha namba 12 ya mwaka 2016.
Vitabu vyenyewe ni kama vifuatavyo:-
Namba Kitabu Namba Maelezo
1. 151 - 200 Hakikupatikana
2. 701 - 750 Hakikupatikana
3 01301 - 013050 Hakikupatikana
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Taasisi ya Viwango Zanzibar kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Taasisi ya Viwango Zanzibar imepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.8 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
4.8.1 FUNGU K 01 – WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Amali umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
38,320,000 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017
Wizara ilikusanya jumla ya shilingi 79,590,000 sawa na asilimia 207 ya makadirio.
72
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla shilingi 101,895,896,988 kwa kazi za kawaida na jumla ya shilingi kwa
1,628,209,600 kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shilingi 98,894,150,775 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 97 ya makadirio, na shilingi 1,007,086,835
zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 62 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.8.1.1 Dosari katika zabuni ya ununuzi wa madaftari
Ukaguzi umebaini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imetoa zabuni ya ununuzi
wa madaftari kwa ajili ya wanafunzi wa Unguja na Pemba kwa kampuni ya Sabah
Store kwa fedha zenye thamani ya shilingi 2,166,501,948.
Dosari zilizobainika katika utolewaji wa zabuni hiyo ni kama zifuatazo:-
Kutotangazwa kwa zabuni ya wazi ya kimataifa ili kuwepo na ushindani wa wazi kwa
wazabuni wa ndani na nje ya nchi kama inavyoelezwa katika kifungu 2 (4) cha
jadweli ya nne inayotajwa na kifungu namba 73(1) cha Sheria ya Manunuzi na
Uondoshaji wa Mali za Umma nambari 11 ya mwaka 2016.
Thamani ya zabuni husika inatakiwa itangazwe zabuni ya kimataifa kwa mujibu wa
maelezo ya jadweli la tano la sheria ya manunuzi na uondoshaji wa mali za umma
nambari 11 ya mwaka 2016.
Ukaguzi haukupata muhtasari wa kikao cha Bodi ya zabuni hivyo umeshindwa
kujiridhisha kuwa aina ya manunuzi yaliyofanywa kama iliidhinishwa na Bodi ya
Zabuni ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na kifungu namba 28 (1) (j) cha sheria ya
manunuzi na uondoshaji wa mali za umma nambari 11 ya mwaka 2016.
73
Maelezo ya malipo hayo ni kama yanavyoonekana katika jadweli:-
Hati
namba
Hundi
namba
Jumla ya
fedha
iliyolipwa
Alielipwa Maelezo
OC/E/08
/06 -
05/06/20
17
TT 1,117,662,139 SABAH STORE Ikiwa ni malipo ya awamu ya
kwanza kwa ajili ya ununuzi wa
madaftari kwa ajili ya wanafunzi
wa skuli za Unguja na Pemba
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Amali kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.8.2 MRADI WA ELIMU MBADALA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Mradi Wa Elimu Mbadala
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Mradi huu unasimamiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali na kufadhiliwa na
mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB), Benki ya Maendeleo ya nchi za
Kiarabu (Badea) kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mradi huu
umeanzishwa kwa ajili ya kutekeleza malengo yafuatayo:-
Kutoa elimu mbadala kwa vijana wenye mahitaji maalum ambao hawakumaliza
elimu ya Lazima
74
Kujenga uwezo kwa Taasisi zitakazotoa elimu stadi kwa vijana kwa ajili ya kuweza
kujiajiri, Taasisi hizo ni Mamlaka ya Mafunzo ya Amali,Chuo cha Maendeleo ya Utalii
Zanzibar, Taasisi ya Sayansi ya Karume,na Kamisheni ya Kazi ya Zanzibar
Taarifa ya matumizi
Mradi Wa Elimu Mbadala kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ulikadiriwa kutumia jumla
shilingi 26,308,217,285. Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shilingi
4,186,778,666.53 zimeingizwa na kutumika sawa na asilimia 15.91 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.8.2.1 Udhaifu katika mfumo wa udhibiti wa ndani
Ukaguzi ulifanya tathmini juu ya uimara wa mfumo wa udhibiti wa ndani katika
mradi wa uimarishaji wa elimu mbadala na kubaini dosari ambazo hazikuwa
zimebainika na kitengo cha ukaguzi wa ndani wa Wizara.
Dosari hiyo ni kutolewa kwa hundi zenye thamani ya USD 24,771 na Tsh. 2,000,000
katika hesabu ya mradi bila ya kuingizwa katika daftari la kutunzia hesabu za mradi
(Cash Book) pamoja na maelezo na vielelezo kuhusiana na matumizi hayo.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sheria ya Usimamizi wa fedha za Umma
nambari 12 ya mwaka 2016 na kunaweza kupelekea kufanyika matumizi kinyume na
malengo yaliokusudiwa na mradi husika.
Hundi zilizobainika kutolewa ni kama zifuatazo:-
Nam Nambari ya
Hundi
Jumla ya fedha
(USD)
Alielipwa
1 000230 3,320 Hakuna maelezo
yaliopatikana
2 000231 5,890 Hakuna maelezo
yaliopatikana
3 000235 5,890 Hakuna maelezo
yaliopatikana
75
4 000241 3,781 Hakuna maelezo
yaliopatikana
5 000234 5,890 Hakuna maelezo
yaliopatikana
Jumla USD 24,771
6 000601 TZS 2,000,000 Hakuna maelezo
yaliopatikana
Jumla TZS 2,000,000
4.8.2.2 Hati za malipo zilizokosekana kwa ukaguzi shilingi 102,671,186
Ukaguzi umebaini kufanyika kwa malipo ya shilingi 102,671,186 kwa ajili ya
kugharamia shughuli za mradi dosari iliyobainika na ukaguzi ni kukosekana kwa hati
za malipo hayo hivyo ukaguzi umeshindwa kuthibitisha asili na uhalali wa malipo
hayo.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sheria ya usimamizi wa fedha za umma
nambari 12 ya mwaka 2016. Maelezo ya malipo hayo yanaonekana katika jadweli:-
Tarehe ya malipo Alielipwa Nambari
ya hundi
Jumla ya fedha
iliyolipwa
14-07-16
Vocational Training 000545 12,561,700
29-07-16 Karume Institute of
Science 000453 6,030,000
01-08-16 Vocational Training 000455 12,690,000
14-09-16 Vocational Training 000470 14,060,000
19-9-2016 ALSD II 000467 2,500,000
23-09-16 Project Staff 000475 240,000
04-10-16 Income Tax
000487 533,086.30
76
Department
31-10-16 Vocational Training 000497 5,474,000
04-11-16 ALSD II PROJECT 000603 1,190,000
03-12-16 ALSD II PROJECT 000611 6,200,000
14-12-16 ALSD II PROJECT 000614 3,970,000
10-01-17 ALSD II PROJECT 000625 662,400
19-01-17 ALSD II PROJECT 000632 2,480,000
19-01-17 ALSD II PROJECT 000632 1,520,000
24-01-17 ZANZIBAR PETROL 000635 5,865,000
01-02-17 Vocational Training 000638 10,715,000
10-02-17
Karume Institute of
Science 000639 9,180,000
10-02-17 Vocational Training 000641 4,510,000
10-02-17
Karume Institute of
Science 000641 2,290,000
Jumla 102,671,186
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mradi wa uimarishaji wa Elimu
Mbadala unaoishia Juni 30 2017 zinaonesha sura halisi na sahihi na kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa
Kwa hali hiyo Mradi wa Uimarishaji wa Elimu Mbadala umepata hati inayoridhisha
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
77
Mambo ya Kuzingatiwa
Bila ya kuathiri maoni ya Ukaguzi yaliotolewa hapo juu mambo yafuatayo ni ya
kuzingatiwa:-
Hati za Malipo zilizokosekana kwa Ukaguzi shilingi 100,171,186.
Hundi zilizotolewa bila ya kurekodiwa katika daftari la kutunzia hesabu za mradi
USD 24,771.
Kuchelewa kumalizwa kwa kazi ya ujenzi wa vituo vya Elimu Mbadala
Makunduchi na Daya Mtambwe.
4.8.3 BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya
Juu umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
1,073,725,000 katika kipindi cha mwaka 2016/2017. Hadi kufikia Juni 2017 Bodi ya
Mikopo ya Elimu ya Juu ilikusanya jumla ya shilingi 1,117,662,476 sawa na asilimia
104 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 6,119,080,000
kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shilingi 7,034,351,390
ziliingizwa na kutumika sawa na asilimia 115 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
78
4.8.4 MAMLAKA YA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Mamlaka ya Mafunzo ya
Amali Zanzibar umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya
ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Mamlaka ya Mafunzo ya Amali ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 1,288,010,000
kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 1,441,569,297.87
zimekusanywa sawa na asilimia 112 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Mamlaka ya Mafunzo ya Amali ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 1,288,010,000
kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 1,393,618,498
ziliingizwa na kutumika sawa na asilimia 113 ya makadirio na shilingi 37,658,063
zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mamlaka ya Mafunzo ya Amali
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mamlaka ya Mafunzo ya Amali imepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.8.5 SHIRIKA LA HUDUMA ZA MAKTABA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Shirika la Huduma za
Maktaba umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Shirika la Huduma za Maktaba lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 365,570,000
katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Shirika la
Huduma za Maktaba lilikusanya jumla ya shilingi 382,620,750 sawa na asilimia 105
ya makadirio.
79
Taarifa ya Matumizi
Shirika la Huduma za Maktaba ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 355,230,000 kwa
kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shillingi 377,694,467 ziliingizwa
na kutumika sawa na asilimia 106 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Shirika la Huduma za Maktaba
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Shirika la Huduma za Maktaba limepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.8.6 TAASISI YA KARUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Taasisi ya Karume ya
Sayansi na Teknolojia umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo
vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
1,304,730 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017
Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia ilikusanya jumla ya shilingi
1,300,210,854 sawa na asilimia 99.9 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi
1,304,730 kwa kazi za kawaida.Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shillingi
1,302,175,290 ziliingizwa na kutumika sawa na asilimia 99.9 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Taasisi ya Karume ya Sayansi na
Teknolojia kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
80
Kwa hali hiyo Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia imepata hati inayoridhisha
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.8.7 BARAZA LA MITIHANI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Baraza la Mitihani
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Baraza la Mitihani lilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 1,989,553,925 katika
kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Baraza la Mitihani
lilikusanya jumla ya shilingi 2,036,114,025 sawa na asilimia 102 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Baraza la Mitihani lilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 1,590,000,004 kwa kazi za
kawaida.Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shilingi 1,973,133,053 ziliingizwa na
kutumika sawa na asilimia 124 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Baraza la Mitihani kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Baraza la Mitihani limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
81
4.9 WIZARA YA AFYA
4.9.1 FUNGU H 01 - WIZARA YA AFYA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Afya umefanywa
kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika
kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Afya ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 188,011,000 katika kipindi cha
mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Wizara ilikusanya jumla ya
shilingi 147,307,173 sawa na asilimia 78 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi
35,747,204,731 kwa kazi za kawaida, na shilingi 18,448,166,270 kwa kazi za
maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 36,637,709,265 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 102.5 ya makadirio na shilingi 7,336,411,625
zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 39.8 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Afya kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo
vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Afya imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
4.9.2 FUNGU H 02 - HOSPITALI YA MNAZI MMOJA
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Hospitali ya Mnazi Mmoja
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
82
Taarifa ya Mapato
Hospitali ya Mnazi mmoja ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 1,014,300,000
katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Hospitali
ya Mnazi Mmoja ilikusanya jumla ya shilingi 449,803,544 sawa na asilimia 44 ya
makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Hospitali ya Mnazi Mmoja kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla
ya shilingi 9,035,992,950 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya
shilingi 8,951,922,195 zimeingizwa na kutumika kwa kazi za kawaida sawa na
asilimia 99 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Hospitali ya Mnazi Mmoja kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Hospitali ya Mnazi Mmoja imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.9.3 WAKALA WA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wakala wa Maabara ya
Mkemia Mkuu wa Serikali umefanywa kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na
vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilikadiriwa kukusanya jumla ya
shilingi 48,000,000 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30
Juni 2017 Wakala ilikusanya jumla ya shilingi 77,206,919 sawa na asilimia 161 ya
makadirio.
83
Taarifa ya Matumizi
Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi kwa kazi za kawaida 574,500,000 na shilingi
500,000,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 562,721,705 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 97.95 na shilingi 828,172,020 zimeingizwa na
kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 166 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wakala wa Maabara ya Mkemia
Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura
sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imepata hati
inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.10 WIZARA YA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI
4.10.1 FUNGU N 01 - WIZARA YA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA
NISHATI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Ardhi, Makaazi,
Maji na Nishati umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya
ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
6,100,000,000 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni
2017 Wizara ilikusanya jumla ya shilingi 4,514,632,801 sawa na asilimia 74 ya
makadirio.
84
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 9,555,400,000 kwa kazi za kawaida na jumla ya
shilingi 47,900,786,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni 2017, jumla ya shilingi 6,276,825,948 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 66 ya makadirio, na shilingi 35,349,867,225
zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 74 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na
Nishati kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati imepata hati inayoridhisha
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.10.2 BODI YA USAJILI WA WAKANDARASI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Bodi ya Usajili wa
Wakandarasi umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya
ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Bodi ya Usajili wa Wakandarasi ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 510,144,000
katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 kupitia vyanzo vyake vya mapato.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 438,448,000 sawa na asilimia 85.94 ya
makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Bodi ya Usajili wa Wakandarasi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 466,235,768 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni 2017 kiasi
cha shilingi 471,050,238.5 zimetumika kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 101.03
ya makadirio.
85
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Bodi ya Usajili wa Wakandarasi
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Bodi ya Usajili wa Wakandarasi imepata hati inayoridhisha kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.10.3 BODI YA UHAULISHAJI ARDHI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Bodi ya Uhaulishaji Ardhi
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Bodi ya Uhaulishaji wa Ardhi Zanzibar ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
1,243,300,000 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 kupitia vianzio tofauti
vya mapato. Hadi kufikia 30 Juni 2017 mapato halisi yaliyokusanywa ni shilingi
1,228,160,690 sawa na asilimia 99 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Bodi ya Uhaulishaji Ardhi Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa
kutumia jumla ya shilingi 1,243,300,000 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia tarehe 30
Juni 2017 jumla ya shilingi 1,191,328,840 zimetumika kwa kazi za kawaida sawa na
asilimia 96 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Bodi ya Uhaulishaji Ardhi Zanzibar
kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi
kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Bodi ya Uhaulishaji ardhi Zanzibar imepata hati inayoridhisha kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
86
4.11 WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI
4.11.1 FUNGU P 01 - WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA
USAFIRISHAJI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Ujenzi,
Mawasiliano na Usafirishaji umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na
vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi
1,762,800,000 kwa mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2017
Wizara ilikusanya jumla ya shilingi 1,561,113,400 sawa na asilimia 88.6 ya
makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 6,932,012,488 kwa kazi za kawaida na shilingi
145,294,472,364 kwa kazi za maendeleo. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2017 jumla ya
shilingi 6,704,441,494 zimetumika kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 96.7 ya
makadirio na shilingi 7,474,121,864 zimetumika kwa kazi za maendeleo sawa na
asilimia 5 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
4.11.1.1 Mapato ambayo hayakupelekwa benki shilingi 29,929,000
Ukaguzi umebaini kwamba Idara ya Leseni imekusanya jumla ya shilingi 30,135,000
na kutumika kinyume na utaratibu.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria ya Usimamizi wa Fedha namba 12 ya
mwaka 2016.
87
Mapato yenyewe ni kama ifuatavyo:-
MAKUSANYO YATOKANAYO NA NJIA ZA GARI
Tarehe ya makusanyo
Stakabadhi ya makusanyo
Kiasi kilichokusanywa
8/7/16 276397-276399 30,000
21/7 312407-429 70,000
28/7 323219-224 90,000
29/7 323225-227 30,000
12/8 339849-850 20,000
16/8 336613-616 40,000
24-26/8 445657-683 299,500
31/8 445699-720 20,000
31/8 449101-105 62,000
2/9 449113-118 70,000
23/9 449650-422651 40,000
12-17/10 505483-500 152,000
18/10 578501-523 230,000
22/10 549106-132 310,000
31/10 5491247-549142 80,000
30/10 07015-020 60,000
22/12 407028-037 100,000
27/12 407046-050 52,000
21/2 185440-446 72,000
4-5/1 406323-340 182,000
28/2 185772-750 90,000
15/3 460092-028 360,000
19/4 479884-887 40,000
88
9/5 470075-050 62,000
5/6 196001-043 448,500
7/6 198101-139 591,000
8/6 198140-150 110,000
8/6 198401-425 250,000
Jumla 3,951,000
MAKUSANYO YATOKANAYO NA MAUZO YA VIBALI
Tarehe ya makusanyo Stakabadhi ya makusanyo
kiasi kilichokusanywa
4-5/7 291765-791 435,000
8/7 291794-520 105,000
8/12 291006-0026 315,000
12-14 291027-047 30,000
8-13/7 291006-0022 255,000
21-22/7 322554-578 375,000
27/7 322599-600 30,000
27-29/7 323051-074 36,000
4/8 337555-559 75,000
25-26/8 449201-221 105,000
22/9 439746-153 120,000
30/9 505774-785 50,000
12-19/10 518101-143 645,000
31/10 549989-997 119,000
20-21/11 406510-550 567,000
22/2 405001-026 405,000
1-6/1 233903-930 370,000
9/1 233931-950 271,000
89
9/1 238901-918 254,000
11/1 238919-933 225,000
13/1 232352-360 122,000
19-20 231516-548 539,000
8/2 232796-800 165,000
16-21/2 186251-300 752,000
21-22/2 186451-467 255,000
24/2 186478-496 295,000
27-2/3 187901-932 482,000
13/4 461734-737 60,000
Jumla 7,457,000
MAKUSANYO YATOKANAYO NA MAUZO YA BEJI
Tarehe ya makusanyo
Stakabadhi ya makusanyo
Kiasi kilichokusanywa
4/8 337782-729 528,000
16/8 442301-336 432,000
25/8 449574-600 324,000
26/8 449159-188 384,000
31/8 446724-750 324,000
31/8 444901-907 84,000
30/9 505351-365 180,000
18/18 518251-275 384,000
20/10 550101-150 600,000
24/10 549851-894 528,000
27/10 080600-092 396,000
90
28/10 05601-629 348,000
21/11 09796-379 396,000
25/11 06171-7190 240,000
28/11 06191-131 480,000
30/11 07230-659 360,000
7/12 408851-876 408,000
22/12 406693-177 420,000
4/1 405864-900 444,000
5/1 238601-633 372,000
27/1 233524-540 204,000
2/2 234887-900 168,000
20/1 186901-934 408,000
23/2 187551-580 360,000
28/2 188551-569 228,000
4/5 471179-185 84,000
8/5 471105-117 156,000
Jumla 9,240,000
MAKUSANYO YATOKANAYO NA MAUZO YA LESENI ZA UDEREVA
Tarehe ya makusanyo Stakabadhi ya makusanyo
Kiasi kilichokusanywa
4/10/16 71091 22,000
12/10 71099 22,000
18/10 71100 102,000
18/10 518451 102,000
18/10 518452 22,000
26/10 518453 22,000
27/10 518454 22,000
91
23/11 518464 22,000
28/11 518465 22,000
2/3 518492 22,000
Jumla 470,000
MAKUSANYO YATOKANAYO NA MAUZO YA MAFUNZO YA UDEREVA
Tarehe ya makusanyo Stakabadhi ya makusanyo
Kiasi kilicho kusanywa
21-22/7 323751-800 418,000
28/7 339030-639 312,000
29/7 339627-708 292,000
10/8 440851-887 376,000
16/8 442201-238 308,000
17/8 442240-450 104,000
25/8 449323-350 234,000
5/9 448183-810 226,000
6/9 448811-850 294,000
16/9 422851-856 58,000
19/9 448578-900 374,000
27/9 505563-600 426,000
12/10 518155-200 468,000
20/10 549372-400 274,000
28/10 08451-500 482,000
31/10 09301-317 150,000
21/11 05266-300 330,000
28/11 409901-950 431,000
5/1 233951-950 338,000
13/2 185251-300 418,000
21/2 188001-050 218,000
92
23/2 188201-243 368,000
27/2 188805-850 412,000
28/2 187951-976 154,000
11/3 462521-550 280,000
21/3 465001-027 270,000
13/6 194008-4050 490,000
23/6 355357-383 306,000
Jumla 8,811,000
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na
Usafirishaji kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na
halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji imepata hati
inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.11.2 MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Mamlaka ya Usafiri Baharini
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Mamlaka ya Usafiri Baharini ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 3,642,689,600
kwa mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni 2017 Mamlaka imekusanya
jumla ya shilingi 3,565,177,186 sawa na asilimia 97 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Mamlaka ya Usafiri Baharini kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia
jumla ya shilingi 3,169,414,001 kwa kazi za kawaida.
93
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 3,169,414,001 zimetumika kwa kazi za
kawaida sawa na asilimia 100 ya makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mamlaka ya Usafiri Baharini kwa
mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana
na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Mamlaka ya Usafiri Baharini imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa
fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
4.12 WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI, WAZEE , VIJANA, WANAWAKE NA
WATOTO
4.12.1 FUNGU NAMBA Q 01 - WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI,
WAZEE, VIJANA, WANAWAKE NA WATOTO
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji,
Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni,
taratibu na vigezo vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na
kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto ilikadiriwa
kukusanya jumla ya shilingi 487,400,000 kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Hadi kufikia 30 Juni 2017 jumla ya shilingi 583,466,000 zimekusanywa, sawa na
asilimia 120 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017, Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee,
Vijana, Wanawake na Watoto ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 12,804,605,250
kwa matumizi ya kazi za kawaida na jumla ya shilingi 275,650,000 kwa kazi za
maendeleo.
94
Hadi kufikia 30 Juni 2017 kiasi cha shilingi 11,815,304,233 ziliingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 92.3 ya makadirio, na shilingi 38,731,929 kwa
kazi za maendeleo sawa na asilimia 14 ya makadirio.
MATOKEO YA UKAGUZI
HESABU YA MAENDELEO NAMBA 9928190604
4.12.1.1 Uhaulishaji wa fedha shilingi 233,407,255
Ukaguzi umebaini kwamba jumla ya shilingi 233,407,255 zimehaulishwa kutoka
Hesabu ya Maendeleo Namba 9928190604 kwenda Hesabu ya Amana Namba
9928161804 kwa mujibu wa barua yenye kumbukumbu namba
WUUJVWW/0019/15/VOL.16/10 ya tarehe 24/6/2016 kwa ajili ya awamu ya pili ya
ujenzi wa kituo cha umeme wa jua – Kibokwa. Fedha hizo zilitengwa kwa ajili ya kazi
hiyo zilitengwa katika bajeti ya mwaka 2015/2016 ambapo Wizara ilizitenga fedha
hizo zitumike katika mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho.
Hadi ukaguzi wa hesabu za mwaka 2016/2017 unakamilika hakuna hatua yoyote
iliyochukuliwa kwa ajili ya ujenzi huo. Aidha hakuna ufafanuzi kuhusiana na
matumizi ya fedha hizo.
Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria ya Usimamizi wa Fedha namba 12 ya
mwaka 2016 ya Zanzibar.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Kazi, Uwezeshaji,
Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017
zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na
kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto
imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
95
4.13 WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, UTALII NA MICHEZO
4.13.1 FUNGU NAMBA J 01 - WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,
UTALII NA MICHEZO
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Utalii na Michezo umefanywa kwa kuzingatia misingi, taratibu na vigezo
vya ukaguzi vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo ilikadiriwa kukusanya jumla ya
shilingi 547,268,000 kwa mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni, 2017
jumla ya shilingi 313,880,045 zimekusanywa sawa na asilimia 57 ya makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ilikadiriwa kutumia jumla ya shilingi 5,907,995,250 kwa kazi za kawaida na shilingi
6,149,679,000 kwa kazi za maendeleo.
Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya shilingi 5,402,585,264 zimeingizwa na kutumika
kwa kazi za kawaida sawa na asilimia 91.4 ya makadirio na shilingi 2,949,622,929
zimeingizwa na kutumika kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia 47.96 ya
makadirio.
Maoni ya Ukaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Wizara ya Habari, Utamaduni,
Utalii na Michezo kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura
sahihi na halisi kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo imepata hati
inayoridhisha kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017.
96
4.13.2 FUNGU J 02 - KAMISHENI YA UTALII
Ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2016/2017 kwa Kamisheni ya Utalii
umefanywa kwa kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na vigezo vya ukaguzi
vilivyokubalika kulingana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Taarifa ya Mapato
Kamisheni ya Utalii ilikadiriwa kukusanya jumla ya shilingi 2,000,000,000 katika
kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017. Hadi kufikia 30 Juni, 2017 Kamisheni ya
Utalii imekusanya jumla ya shilingi 2,198,802,648.25 sawa na asilimia 110 ya
makadirio.
Taarifa ya Matumizi
Kamisheni ya Utalii kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikadiriwa kutumia jumla ya
shilingi 1,112,900,000 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia 30 Juni, 2017 jumla ya
shilingi 1,091,556,976 ziliingizwa na kutumika kwa kazi za kawaida sawa na asilimia
98 ya makadirio.
Maoni ya Mkaguzi
Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za hesabu kwa
mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Kamisheni ya Utalii kwa mwaka
wa fedha unaoishia 30 Juni, 2017 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na
vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.
Kwa hali hiyo Kamisheni ya Utalii imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha
unaoishia 30 Juni, 2017.
97