seyyid sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/books/ghawth.pdf · seyyid sheikh abdul qadir...

38
Seyyid Sheikh

Upload: nguyenngoc

Post on 14-Jun-2018

266 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Seyyid Sheikh

Page 2: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Mtungaji:-

Swahib Sujjada:

Sheikh Salim Bin Mbarak (Dar-wesh – Mti mkavu)

P. O. Box 8105,

Zawia kuu – Arusha,

Tanzania. (E.A).

i.

Page 3: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Swahib Sujjada,

Al habib Sheikh Salim Bin Mbarak.

(Dar-wesh Mti Mkavu). ii.

Page 4: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan

(Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz).

First Addition Toleo la kwanza

iii.

Page 5: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

iv.

Swahib Sujjada:

Al Habib Sheikh Salim Mbarak

(Mti - Mkavu).

Page 6: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Yaliyomo: No. Ukurasa.

1. Dibaji……………………………………….. vi.

2. Utangulizi…………………………………... vii.

3. Jina lake la kuzaliwa……………………….. 1.

4. Nasabu yake..………………………………. 2.

5. Makuzi yake na kusoma Qur an.………........ 2.

6. Kutafuta Ilmu ……………………………… 3.

7. Masheikh zake…………………………….. 4.

8. Umaarufu wake kwa kusoma……………… 5.

9 Kusomesha kwake Ilmu……………..…….. 7.

10. Namna ya Twariqa ilvyoenea….………….. 8.

11. Siri ya Ilmu ya Tasawfu ..………………..... 10.

12. Sifa za Seyyid Abdul Qadir…..…………… 11.

13. Wake zake na watoto wake……………….. 12.

14. Wasia wake kwa mwanawe A`bdul Razaq.. 13.

15. Karama zake……………............................ 13.

16. Kifo cha Seyyid Abdul Qadir Jaylani (Qsa).. 27.

v.

Page 7: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

DIBAJI:

Sifa zote njema zinamstahiki ALLAH ambaye

amefundisha kwa wasta wa kalamu. Na akamfundisha Mwana

Adam lile asilolijua. Na Rehma na Amani Zimwendee Bwana

Mtume Saw na Ahly zake watukufu na Maswahaba wake watiifu.

Kwa ridhaa ya mtunzi wa kitabu hiki ambae ni kiongozi

mkuu na Mlezi wa Twariqatul-Qadiriya– Rrazziqiya–Jaylaniya Al

habib Sheikh Salim ibn Mbarak –(Dar-weish Mti mkavu) –

(Radhia ALLAH Anhu). Naandika Dibaji ya kitabu hiki kwa

munassaba wa kuya yakinisha yaliyomo kwenye kitabu hiki.

Kwa hakika kitabu hiki kimeelezea historia na sifa kadhaa

za Bwana wa Mawalii Seyyid Sheikh Abdul-Qadiri- Jaylani (Qada-sa-Llahu-Siral-Aziz)

Basi ukiwa utajaaliwa kusoma kitabu hiki utamjua vilivyo

alivyo Walii wa Mwenyezi Mungu na Uasili wa Twariqa kwa

ujumla.

Insha-Allah tunamuomba Allah amjaalie kila la kheri mtunzi

wa kitabu hiki Sheikh Salim amjaalie Mahaba zaidi ya kudarisisha

hususan kwa kutunga vitabu vingi zaidi vitavyotoa Ilmu na

muongozo wa ibada za Kitwariqa kwa misingi ya Kitassawfu. Aamiin Aamiin Aamiin wal-hamdulillahi Rabbil-A`alamiin

Khalifa Mohamed Omar.

Mwenyekiti wa Twariqatul-Qadiriya-Rrazziqiya-Al-Jaylaniya

Makao Makuu Ya Twariqa – Zawiya Kuu

S.L.P. 8105

Arusha.

Tanzania (E.A)

vi.

Page 8: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

UTANGULIZI:

“Assalamu alay–kum warah–matullahi –Taala wabarakatuh”.

Namshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kunijaalia fikra

na utashi wa kuandika kitabu hiki nilichokitambulisha kwa jina la

Ghawth–l–A`adham, Seyyid Sheikh – Abdul – Qadir-Jaylani.

(Qad-sa-Llahu-Siral-A`ziz)

Makusudio yangu makubwa katika kuandika kitabu hiki ni

kuelezea sifa na mwenendo wa maisha ya Bwana wa Mawalii na

kipenzi cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume (Saw).

Ni Matarajio yetu Historia hii tuliyoiandika ndani ya kitabu

hiki itahifadhika na kujenga kumbukumbu juu ya maisha ya watu

wema kwa ujumla. Kuwakumbuka watu wema na kufuatisha

matendo mema ni ufunguo wa kheri hapa duniani na Akhera.

Insha Allah Mwenyezi Mungu amjaalie kila la kheri msomaji

wa kitabu hiki na amjaalie kuwa na matendo mema.

“Eee Mwenyezi Mungu tujaalie sote

mwishilio mwema na utujaalie kuwa

watu wa peponi”

(Aamiin).

Sheikh Salim Ibn Mbarak – (Dar-weish – Mti Mkavu).

S.L.P 8105

Zawiya Kuu – Arusha.

Tanzania (E.A).

vii.

Page 9: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

viii.

Page 10: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

i. Maisha ya Seyyid Abdul Qadir (Qsa).

Seyyid Abdul Qadir ni Muajemi. Naye ni mashuhuri si

katika Ardhi tu, bali hata Mbinguni pia. Yeye ni Sheikh wa

Waislam na ni kiigizo kwa Mawalii na watu wema. Seyyid Abdul

Qadir alikuwa Imamu wa Siddikin na A`arifiyn.

Sharafu yake kwa Mawalii wenzake ni kama Sharafu ya

Nabii Muhammad kwa Mitume wenzake.

ii. Kuzaliwa kwake:

Seyyid Abdul Qadir alizaliwa katika kijiji cha Jeilan huko

Iraq. Alizaliwa usiku wa kuamkia Mwezi mosi wa Ramadhani

mwaka 470. A.H.

Bi Fatma alichukua mimba ya mtoto huyo na hali ya kuwa

umri wake ni miaka 60. Wakati ambao hapana tamaa ya kupata

mtoto yeyote.

Siku hiyo aliyomzaa Seyyid Abdul Qadir ilizagaa Nuru

ambayo ilitapakaa kijiji kizima. Mambo hayakuwa hayo tu, lakini

hapakuwa na mtu yeyote aliyethubutu kuuangalia uso wake kwa

mng‟aro na haiba yake.

Tabia zake zafanana na zile za Seyydina Muhammad

(Saw). Uzuri wake ni ule kama wa Nabii Yusuf (A.s). Ukweli wake

unalingana na Seyyidna Abu-Bakar. (R.a) Haki yake ni kama ile ya

Seyyidna Omar (R.a), na upole wake wa Seyyidna Othman. (Ra).

iii. (a) Nasabu yake kwa kuumeni

Yeye ni Seyyid Abdul Qadir bin Mussa bin Abdillah

1.

Page 11: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

bin Yahya bin Muhammad bin Daudi bin Mussa bin Abdillah Bin

Mussa bin Abdillahi bin Hassan bin Seyyid Hassan bin Ally bin

Abi Talib. Yaani nduguye Mtume (Saw).

(b). Nasabu yake kwa kukeni.

Yeye ni mtoto wa Bi Fatma Bint Seyyid Abdillah Sawmaiy

Bin Seyyid Mahmoud bin Issa Bin Muhammad Bin Ali Bin Mussa

Bin Jaafari Swadiq Bin Muhammad Bin Seyyidna Hussein Bin

Ally Bin Abi Talib.

Unapoangalia nasabu zake zote yaani kukeni na kuumeni, utaona

kama zimekutana kwa Seyyidna Ali bin Abi Talib; yaani nduguye

Mtume (Saw).

iv. Kukua kwake na kusoma Qur ani

Seyyid Abdul Qadir alikuwa akikua na akiishi katika hali

nzuri. Mji wake uliingia neema kubwa kabisa baada ya kuzaliwa

kwake. Seyyid Abdul Qadir alipewa Uwalii na hali ya kuwa ni

mtoto kama Nabii Isa alivyopata Utume katika hali hiyo hiyo.

Ishara zilizoonyesha kama yeye ni Walii ni nyingi na katika

hizo ni:-

(i) Kutamka „Hatifu‟ maneno siku ya mwanzo

alipopelekwa chuoni kusoma Qur an. Maneno

yenyewe ni haya “Mfanyieni nafasi ya kukaaWalii wa

Mwenyezi Mungu”.

(ii) Kusifiwa kwake na „Abdal‟ kwa kusema: “Mtoto

2.

Page 12: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

huyu atakuwa na mambo matukufu

atakayosifiwa mwishoni kwake”.

(iii). Bishara ya Mtume aliyompa Baba yake

usingizini - “kwamba atamzaa mtoto ambaye

atakuwa na mambo matukufu atakayosifiwa

mwishoni kwake”.

v. Kutafuta Ilmu:

Seyyid Abdul Qadir alipotimia miaka 18, alimwomba

ruhusa mama yake kusafiri kwa kutafuta Ilmu ambayo ni wajibu

kwa kila Mwislamu mwanamke na mwanaume. Aliondoka kwenda

Baghdad pamoja na Nabii Khidhri. Lakini kabla ya kuingia ndani

ya Mji wa Baghdad; Nabii Khidhri alimpa Seyyid Abdul Qadir

sharti ambalo atakapolitekeleza ndipo atapompeleka kwa Masheikh

kusoma. Sharti yenyewe ni kukaa pale nje ya mji na kufanya ibada

kwa muda wa miaka mitatu kamili. Seyyid Abdul Qadir alikubali.

Tangu siku ile Nabii Khidhri hakupapita tena mpaka mwaka

ukamalizika.

Baada ya kutimia mwaka mmoja, Nabii Khidhri alikwenda

kumzuru Seyyid Abdul Qadir. Seyyid Abdul Qadir alipomwona

Nabii Khidhri alimsimamia. Lakini Nabii Khidhri alikataa

kunyanyukiwa na kumwambia akae kitako.

Siri ya kuwekwa Seyyid Abdul Qadir peke yake kwa

muda wote ule, apate kuitakasa roho yake na ile sehemu

inayoharibiwa na Shetani. Vitisho alivyokuwa akivipata mahala

pale havikuwa na mfano. Lakini Mwenyezi Mungu alimlinda Walii

wake na akamhifadhi na kila baya na vitisho. Ulipotimia mwaka

wa tatu. Nabii Khidhri alikwenda mahala pale kwa ajili ya

kumchukua Seyyid Abdul Qadir.

3.

Page 13: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Juu ya kuwa wamo ndani ya safari pamoja, Seyyid Abdul

Qadir kabisa alikuwa hamjui mtu anayefuatana naye. Lakini alikuja

kumjua baadaye hapo alipokwenda Baghdad kumkagua.

Seyyid Abdul Qadir alisoma kwa juhudi na ari kubwa na

aliwashinda wenzake wote kwa Ilmu na ufasaha wa lugha. Na

alikuwa jogoo mkubwa wa Madhehebu ya Shafi na Hambali. Na

alikuwa akijibu na akifutu masuali kwa Madhehebu hayo mawili.

Lakini yeye mwenyewe alikuwa akifuata madhehebu ya Hambal.

vi. Katika baadhi ya Ilmu alizosoma.

(i) Qur an (Tafsiri)

(ii) Fiqh

(iii) Hadith

(iv) Usuli-fiq

(v) Tarikh (historia)

(vi) Tasawuf

(vii) Lugha. n.k.

vii. Masheikh zake:

Seyyid Abdul Qadir amesoma Ilmu kwa Masheikh wengi

na kila mmoja katabahari katika fanni mbalimbali. Masheikh

wenyewe ni:-

1 Sheikh Abdil-Wafa Ali Bin Ukayl.

2. Sheikh Abi Said-al-Mubaraq.

3. Sheikh Abdil Khatib Mahfudh

Kaludhany.

4.

Page 14: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

4. Sheikh Abi – Hassan Muhammad.

5. Sheikh Kadhi Abi Said.

6. Sheikh Yahya Bin Ali.

7. Sheikh Abi Ghalib Muhhamad bin Abdul

Karim.

8 Sheikh Abu Said Muhammad bin Abdul

Karim.

9. Sheikh Muhammed bin Muhammed

10 Sheikh Abubakar Ahmed bin Ahmed

11. Sheikh Abu Jafar bin Ahmed

12. Sheikh Abu Kassim Ali bin Ahmed

13. Sheikh Abu Talibu Abdul Kadir bin

Muhammad

14. Sheikh Abdul Rahman bin Yusuf.

15. Sheikh Abdul Rahaman bin Ahmed

16. Sheikh Abu - Barakat Hibatullah

17. Sheikh Abdul-Izzi Muhammed bi

Mukhtar.

18 Sheikh Abu – Nasri Muhammed

19. Sheikh Abu – Ghalib Ahmad

20. Sheikh Abu – Abdalla Yahya

21. Sheikh Abu – Hassan Mubarak

22. Sheikh Mansur Abdul Rahman

23. Sheikh Abu Barakat Taibat Akuly.

viii. Umaarufu wake kwa kusoma

Sifa za Seyyid Abdul Qadir zilizagaa kwa Ilmu yake.

Ingawa wengi walifurahi kwa mambo hayo, lakini mahasidi wake

walikuwa wakikereka - Nao ni katika nafsi ya wanachuoni

wenzake.

Siku moja walimjia wanachuoni 100 wakati alipokuwa

akisomesha ili kumhoji. Na kila mmoja katika hao alikuwa na

suala mbalimbali, na muradi wao ashindwe ili afedheheke.

5.

Page 15: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Wakati huo watapata kueneza kama hajui kitu kuliko wao. Mara tu

wale wanachuoni walipofika pale walikaa kitako kumsikiliza.

Baada ya kukaa, Seyyid Abdul Qadir alikiimanisha kichwa chake.

Na wakati huo lilimtoka pande la Nuru kifuani mwake

likanyakuwa yote waliyoyadhibiti katika vifua vyao. Mara wakawa

wanababaika na kuwayawaya, huku wanapiga makelele wakirarua

nguo zao mfano wa wenda wazimu. Wote walivua vilemba vyao na

wakamwendea Sheikh pale alipokaa. Kila mtu alikuwa akinyanyua

mguu wa Seyyid Abdul Qadir na kujiwekea kichwani kwake. Hii

ni ishara kuonyesha kama wameridhika na kukinai kuwa ni

Mwanachuoni na amewazidi. Na kila mtu alipokuwa akifanya hayo

yeye alikuwa akimkumbatia.

Waliporudi vikaoni mwao, yote waliyokuwa wameyasahau

wakayakumbuka tena. Seyyid Abdul Qadir alimwambia kila mtu

suala aliyokusudia kuuliza na akampa jawabu nzuri ambayo hata

yeye mwenyewe hakufikiria. Wote walistaajabu na walimpa heko.

ix. Muda wa kutoa waadhi

Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitoa waadhi mara tatu kila

wiki kwa muda wa miaka 40. Masheikh, Mafaqih na wanachuoni

wengi wa Baghdad walikuwa wakimiminika kumsikiliza waadhi

wake.

Naam, Katika jumla ya wasikilizaji wa waadhi; Mayahudi

na Manasara walikuwamo.

Taathira kubwa ilipatikana kila waadhi aliokuwa akiutoa

kwani Mayahudi na Manasara wengi kabisa walisilimu. Na

miongoni mwa Waislamu wengi wafanyao maasi walitubu katika

maasi yao.

6.

Page 16: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Ama masomesho yake yalizidi kupatia utukufu. Kwani Bibi

mmoja alijitolea nafsi yake aolewe na Seyyid Abdul Qadir bila

mahari yoyote, isipokuwa alimpa sharti moja, nayo ni

kuwasomosha watu Ilmu kwa muda maalum. Muda ulipotimia,

Bibi yule aliolewa kama alivyotamani.

X. Kusomesha kwake Ilmu:

Katika chuo chake, Seyyid Abdul Qadir alikuwa

akisomesha Ilmu 13 za sheria. Na katika Ilmu hizo 13, aliweka

darsa moja kusomesha Madhehebu mbalimbali na darsa nyinginezo

alikuwa akisomesha Hitilafu za Wanachuoni. Baada ya sala ya

Alfajiri, alikuwa akisomesha Tafsir ya Qur an na akisomesha

Hadithi za Mtume (Saw) Darsa hizo zilikuwa zikisomwa na kila

mtu aliyetaka. Ama Ilmu za Madhehebu mbalimbali, Khitilafu za

Wanachuoni, Adabu, Fiq na Usuli Dini zilikuwa zikismwa na

Mawalii tu.

Wakati wa Adhuhuri, ilikuwa ikisomwa Qur an kwa Kiraa

(visomo) 7. Darsa ilikuwa ikihudhuriwa na wanafunzi 650

waliokuwa mahodari sana. Wasomaji wake wakubwa wa Qur ani

walikuwa Sheikh Masoud al Hashimiy na Sheikh Abdul Wahab bin

Abdul Qadir (mwanawe).

xi. Kufutu kwake masuala

Katika fatwa zake, Sheikh alikuwa halazi suala wala

alikuwa hafikiri, Bali alikuwa hanafutu mara moja tu. Kabla ya

kufutu au kujibu suala yoyote, ilikuwa ikisomwa Qur an. Jawabu

zake zilikuwa ama za kuandika au za mdomo. Na jawabu zake

zilikuwa zikiwafurahisha watu kwa ustadi wake.

7.

Page 17: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

xii. Namna ya Twariqa ilivyoenea

Asili ya Twariqa inatokea kwa Mwenyezi Mungu. Yeye

akamfundisha Seyyidna Jibril As, na Seyyidna Jibril akamfundisha

Seyyidna Muhammad (Saw), tena Nabii Muhammad akamfundisha

Seyyidna Ali (R.a) Baadaye ikaendelea kwa Masheikh hawa hata

nao wakaifikisha hapa Tanzania na mwenginepo:-

1. Seyyidna Hassan al Busry.

2. Seyyidna Arif Samdany

3. Alhabibul Ajemy.

4. Daud Taiy

5. Maaruf al Karkhy.

6. Sharif Sakaty

7. Abi Kasim al Juneid

8. Abu Bakar Shily

9. Abu Fadhi Abdul Wahid

10. Abu Faraj Tusy

11. Seyyidna Abdul Hassan

12. Seyyidna Abu Said –al – Makhzumy.

13. Seyyid Abdul Kadir al Jeilany na kadhalika.

xiii. Siri ya Ilmu ya Twariqa

Ilmu ya twariqa imefanywa kwa Qur an na Hadithi za

Mtume (Saw) pamoja na mambo yafuatayo:-

(i) Kusafisha moyo

(ii) Ukarimu

(iii) Ustahamilivu

(iv) Kuwasamehe waliokuudhi

(v) Kuacha au kujiepusha na maasi

(vi) Kufanya Ibaada kwa jitihada.

8. .

Page 18: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Faida. i.

Hizi Twariqa ziko namna nyingi, nazo zinapata kama 17.

Katika hizo ni Qadiry, Shadhily, Nakshahabandy, Indarusy

n.k.

Ama Twariqa yoyote akiifuata mtu kama

inavyohitajia, basi itaweza kumfikisha kwa Mwenyezi

Mungu. Kwani lengo lao ni moja tu lakini kwa yote hayo

niliyoeleza inapasa kupatikana Sheikh Mwongofu wa

kukupa „Ijaza‟ na kukufundisha njia za kupita na kukupa

wasia. Huyu mtu anayepewa „Ijaza‟ na Sheikh huitwa

„Muridi‟ Kwa hivyo kila Murid ajitahidi sana kutekeleza

ahadi atakazopewa na Sheikh wake.

Faida ii. Yatakiwayo kwa Muridi

1. Kutubia kwa Mwenyezi Mungu.

2. Kufanya Ibaada kiasi ya uwezo wake.

3. Kufanya mambo yalio halali

4. Kuacha mambo yaliyo haramu.

5. Kumdhukuru Mungu

6. Kushikamamna na “Laa ila ha illa Llah” hasa baada

ya kila Sala mara 165 na wakati mwngine kiasi ya

kuweza kwake.

7. Kusoma sana Qur an kwa kila hali.

8. Kuwasamehe wenye kukuudhi.

9. Kuwa mstahamilivu.

10. Kuwa karimu

11. Kuacha husda, kijicho, choyo, uwongo wa

kuwasengenya watu.

12. Kudumu na udhu.

13. Kumsalia Mtume (S.a.w) kwa wingi.

9.

Page 19: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

xiv. Siri ya Ilmu ya tasawuf:

Ilmu ya Tasawfu imefanywa kwa mambo yafuatayo:-

(i) Ukarimu.

(ii) Kuridhia hukumu ya Mungu.

(iii) Subira

(iv) Ishara

(v) Upweke

(vi) Kuvaa nguo za sufi

(vii) Kwenda sana

(viii) Umaskini.

Faida:-

Katika hizo sifa nane zilizotajwa hapo juu, zimechukuliwa

kutokana na Mitume wanane mbalimbali:-

1. Ukarimu: Ilikuwa sifa kubwa sana ya Nabii Ibrahim

(Asw).

2. Ridhaa: (kuridhia), ni sifa ya Nabii Is-haq. (As).

3. Subra: Ni sifa ya Nabii Ayub, (A.s)

4. Ishara: Ni sifa ya Nabii Zakaria (A.s)

5. Sufi: Ni kivazi cha Nabii Yahya (A.s)

6. Upweke: Ni sifa ya Nabii Yusufu (A.s)

7. Kwenda : Ni sifa ya Nabii Issa, (As) na ndio maana

akaitwa „Masihi‟

8. Umaskini: Ni sifa ya Nabii Muhammad (Saw). 10.

Page 20: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

xv. Sifa za Seyyid Abdul Qadir (Qsa).

Seyyid Abdul Qadir alikuwa karim sana na mwenye sifa na

tabia nzuri za kupigiwa mfano. Alikuwa na kimo cha wastani, si

mrefu sana wa kuchusha wala hakuwa mfupi. Alikuwa mwekundu

wa weupe. Alikuwa na nyusi nzuri sana. Mwili wake ulikuwa

mwembamba, macho yake yalikuwa yenye haiba kubwa. Kifua

chake kilikuwa kipana chenye Ilmu nyingi. Alikuwa mkali kama

babu yake Sayyidna Ali bin Abi Talib. Ama ndevu zake zilikua

ndefu namna zile za Nabii Harun (As).

Seyyid Abdul Qadir alikua na cheo au makamo matukufu

mbelel ya Mwenyezi Mungu. Katika Ulimwengu alikuwa ni mtu

mwenye kusikilizwa sana sauti. Sauti yake iliokuwa nzuri na

nyororo kama lulu. Anaposema husema upesi upesi. Hakupata

kupenga makamasi wala kutema makohozi. Mwisho inzi hakupata

kumtua juu ya mwili wake.

Seyyid Abdul Qadir alikuwa mnyenyekvu na mkweli.

Alikuwa na kawaida ya kumtolea mtu salamu mwanzo kila

wanapokutana naye.

Aidha alikuwa akikaa na maskini kama alivyokuwa

akifanya Nabii Muhammad (Saw). Pamoja na utukufu aliokuwa

nao, alikuwa akiwasimamia watoto wadogo na alikuwa

akiwatukuza watu wazima kama ilivyokuwa ada yake Mtume

(Saw). Ingawa alikuwa akiwasimamia watoto lakini hakupata

kumsimamia mtu yeyote katika watu watukufu.

Seyyid Abdul Qadir hakupata kugonga mlango wa

Mfalme au waziri yeyote kwa kumtaka haja ya kilimwengu.

Kazi yake ilikuwa ni kuamrisha mema na kukataza maovu.

Alikuwa akila na wageni na marafiki zake.

Kadhalika alikuwa akiwapa nguo na chakula maskini.

Vile vile alikuwa akiwapa zawadi nzuri nzuri wanapomwendea

kwake. Kwa ukarimu wake hakupata kumrejesha mtu yeyote

aliyemwomba wakati wa shida, seuze wakati wa raha.

11.

Page 21: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Mavazi yake yalikuwa ya fahari, kama mavazi ya kifalme. Mavazi

hayo aliyavaa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.

Siku moja alipita mtu mwenye haja na akavua nguo hizo

akampa yeye. Alitoa Joho ambalo thamani yake yadi moja ni

Dinari 20; yaani Sh. 240/-Alitoa na kilemba ambacho thamanai

yake ni Dinari 70,000 yaani sh. 840,000/- .

xvi. Wake zake

Seyyid Abdul Qadir hapo mwanzoni mwake alikaaa muda

mrefu sana bila ya kuoa. Alikaa muda mrefu kwa Ibaada na

alichelea kuvaana na mambo ya ndoa asije akashughulika na

akapunguza Ibaada zake kwa mshughuliko wa wakeze. Siku moja

aliendewa na Mtume(Saw) akamwambia aoe. Kwa kupata nasaha

hiyo ndipo alipooa, na alioa wake wanne.

xvii Watoto wake:

Watoto aliozaa Seyyid Abdul Qadir ni 49. Katika hao 27

walikuwa watoto wanaume na 22 walikuwa wanawake.

Hawa wafuatao ni miongoni mwa hao watoto wa kiume wa

Seyyid Abdul Qadir aliowaacha baada ya kufa:-

1. Sheikh Abdul Wahab

2. Sheikh Abdul Razak

3. Sheikh Abdul Aziz

4. Sheikh Abdul Jabbar

5. Sheikh Abdul Ghafur

6. Sheikh Abdul Ghina

12.

Page 22: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Faida:- Sayyid Abdul Qadir alipokuwa akiumwa siki moja aliwahi

kuzimia. Wakawa wanawe na wakeze wanalia, Mara tu baada ya

kupata fahamu, alisema, “Msilie nitapona, kwani mgongoni

mwangu bado yuko mtoto mmoja Yahya” wale watu walidhania ati

maneno ya kigonjwa. Kumbe ni ya kizima. Kwani alipona katika

ule ugonjwa, na alimzaa huyo Yahya kama alivyosema. Mtoto

huyo alimpata kwa Suria wake Halima. Mtoto huyo ndiye

aliyekuwa kitinda-Mimba.

xviii Wasia wake juu ya mwanawe, Abdul-Razak.

1. Kumcha Mungu.

2. Kumtii Mungu.

3. Kufuata sharia

4. Kuhifadhi mipaka ya Mungu

5. Kuwatunza na kuwarehemu mafukara

6. Kuwatukuza Masheikh

7. Kuishi na ndugu kwa wema.

8. Kuacha kugombana ila kwa mambo ya Dini ikiwa

inavunjwa.

9. Kutomtegemea mtu kwa kumfanyia kazi zake.

xvii. Karama za Seyyid Abdul Qadir.

(maana ya karama). Karama ni mambo ya ajabu yenye kudhibiti kwa Mawalii.

Ama mambo kama hayo yanapotokana na Mitume huitwa

„Miujiza‟. 13.

Page 23: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Kwa hakika Seyyid Abdul Qadir alikuwa na karama nyingi mno.

Karama zilikuwa ni dalili za kuonyesha kama alikuwa ni Walii. Na

kila zikizidi ni ishara au ni dalili ya kuonyesha utukufu wa daraja

yake kwa Mwenyezi Mungu.

Kila Muridi wa Seyyid Abdul Qadir, ajue kama

amebahatika mno. Kwani Muridi wake hafi ila awe ametubia, kwa

Mungu, Na huko Ahera hatoingia Motoni.

Mwenyezi Mungu atudumishie mapenzi yetu kwa Seyyid

Abdul Qadir hasa, na Mawalii wengine kwa jumla.Tena Mwenyezi

Mungu atuepushe na madhambi makubwa na madogo pia.

Amin! Amin! Amin!

Hizi ni baadhi ya katika karama zake:

Kwenda mbinguni 1. Hekaya:-

Seyyid Abdul Qadir alikwenda Mbinguni, si kwa kiwili

wili na roho, bali ni kwa roho tu. Huko ni kusema alikwenda

Miiraji. Naye alisimama mahala pale pale „Kaaba kawsayn‟

ambapo alisimama Mtume wakati alipokwenda Miiraji, Huko

alimwona Seyyidna Israil, aliiona Lawhil-Mahfudh na Kursy, Si

tu; bali aliiona mpaka Nuru ya Mwenyezi Mungu (Jalla -Jalaluhu).

Wakati alipofika hapo “Kaaba Kawsayni” alipewa amri ya

kusimama na akaambiwa “Njoo, usiogope. Tumeyakunja mapazia

yetu. Hebu inama unywe upate kuniona.

“Neema iliyoje, mtu kuiona Nuru ya Mwenyezi Mungu”.

14.

Page 24: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Kuwasalisha Mawalii hewani:

2. Hekaya:-

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alikuwa akitafutwa na

Masheikh wa Baghdad wa Twariqa ya Fawqany. Waliambiwa

kama amekwenda upande wa Mto Tigris. Huko walimwona

anakwenda juu ya maji na huku samaki wa mle mtoni

wanamwendea makundi makundi wakimtolea salam na wakimbusu

mkono wake kwa mboni za macho yao.

Mara tu waliponyanyua macho yao juu waliliona zulia

kubwa rangi ya kijani lililopambwa kwa dhahabu na fedha yenye

kung‟aa. Mtu yeyote akiliangalia atadhania kama labda ni lile zulia

la Nabii Suleiman. Na pale juu ya zulia palikuwa na kitabu

kielezacho utukufu wa Sayyid Abdul Qadir. (Q.s.a).

Ulipoingia wakati wa Adhuhuri kiasi cha saa 6.30; wale

Masheikh wa Baghdad waliwaona Mawalii wengi sana

wamefuatana na wakubwa wao wanakwenda kwenye zulia. Na

pale penye zulia walikuwa wamekaa “Rijalul – ghayb” (Mawalii)

na mkubwa wao yuko mbele. Ulipofika wakati wa kusali, yule mtu

aliyekaa mbele; alikimu Sala na walisimama Mawalii wote huku

wakitazamana nani atakayesalisha. Mara alipita mbele Seyyid

Abdul Qadir kusalisha. Aliwasalisha wale Mawalii pamoja na

mkubwa wao, pamoja na Masheikh wa Baghdad na mkubwa wao.

Baada ya kusali Seyyid Abdul Qadir alinyanyua mikono yake juu

kuomba. Aliomba hivi:- “Ewe Mola Mtukufu, ninakuomba

asife Murid wangu mwanamume au mwanamke mwenye

kunipenda ila awe ametubia kwa Mola wake”. Baada ya

kuomba, walisikia Malaika wakiitikia “Amiin”. Na walisikia sauti

isemayo:

“Furahi, hakika nimeikubali dua yako”.

Hakika Mungu ndiye Mtukufu, na humpa utukufu yeyote

amtakaye. Heri iliyoje ya kumwomba Mungu na akakujibu papo

kwa papo.

15.

Page 25: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Kumbusu mtume mkono wake. 3. Hekaya:

Seyyid Abdul Qadir alipokwenda Madina kumzuru Mtume

(Saw) muda wa siku 40 alisimama mbele ya kaburi. Ilipotimia siku

ya 40 alimwomba autoe mkono wake nje (kutoka kaburini) ili

aubusu. Pale pale Mtume (Saw) aliutoa mkono wake na Seyyid

Abdul Qadir aliushika na kuubusu. Tena alijiwekea juu ya kichwa

chake. Alhamdulillah, utukufu ulioje wa karama.

Kukutana na Mtume kwenye membari. 4. Hekaya:- Siku moja Seyyid Abdul Qadir alisimama kwenye

membari kutoa waadhi. Mara akashuka na akasimama kimya

kitambo hivi kwa adabu na heshima. Baadaye akasimama na

akatoa waadhi.

Mara alipokwisha kutoa waadhi, watu walimwuliza

yaliyomtokea. Alijibu ya kuwa wakati ule Mtume alikuja pale na

akampisha pale alipokaa. Na alipokuwa anaondoka alimwambia

asimame na atoe waadhi alioukusudia.

Kufuturu nyumba 70. 5. Hekaya:-

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alipewa taarifa na watu 70

mablimbali, akafuturu kwao. Ulipofika wakati wa kufuturu, kila

mtu alifurahi kumwona Seyyid Abdul Qadir kuhudhuria kwake.

Habari hiyo ilitapakaa Baghdad nzima. Lakini mmoja katika

watumishi wake alikua akikanya kama

16.

Page 26: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

si kweli, kwa sababu yeye alimwona kakaa juu ya takia lake wala

hakutoka. Mwisho mwenyewe SEyyid Abdul Qadir

aliyathibitisha maneno wayasemayo watu kuwa ni kweli.

Alimwambia yule mtumishi wake, “Ni kweli nimekwenda kufuturu

kwa watu 70. mmoja mmoja”.

Kumfufua maiti aliyekwisha kuoza

6. Hekaya:-

Siku moja Seyyid Abdul Qadir alipita katika kijiji, na

aliwakuta watu wawili wanashindana. Mmoja kati ya hao alikuwa

Mwislam na wa Pili alikuwa Mkristo. Seyyid Abdul Qadir

aliwauliza sababu ya kushindana kwao. Yule Mwislam alijibu

“Huyu Mkristo eti anasema kuwa Mtume wao ni bora kuliko

Mtume wetu. Na mimi nasema kuwa Mtume wetu ndiye bora

zaidi”. Seyyid Abdul Qadir alimwuliza yule Mkristo. “Dalili gani

uliyonayo inaonyesha kuwa Nabii Isa ni bora kuliko Nabii

Muhammad (Saw)?” Yule Mkristo alijibu, “ Mtume wetu alikuwa

akifufua maiti.” Tena Seyyid Abdul Qadir alimwambia Mkristo.

“Mimi vilevile nafufua maiti wala si mtume, bali ni mfuasi wake

tu. “Tena Seyyid Abdul Qadir. alimuliza Mkirsto, “Je nikimfufua

maiti utamwamini Nabii Muhammad?” “ Ndiyo, alisema Mkristo.

Tena alisema Seyyid Abdul Qadir alimwambia yule Mkristo,

“Nionyeshe kaburi la mtu aliyekufa zamani.”

Yule Mkristo alifuatana na Seyyid Abdul Qadir na yule

kijana kwenda kwenye kaburi ambalo mwenyewe keshaoza

zamani. Walipofika pale Seyyid Abdul Qadir alimuliza yule

Mkristo “Mtume wenu alikuwa akiwafufua maiti wenu kwa

maneneo gani?” Yule Mkristo alisema, “Alikuwa akimsemeza

maiti kwa kumwambia asimame kwa idhini ya Mungu. Seyyid

Abdul Qadir alimwambia Mkristo

“Mimi nitamfufua kwa idhini yangu” Mara baada ya kusema

17.

Page 27: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Vile, Seyyid Abdul Qadir alimwambia maiti “Simama kwa idhini

yangu”. Saa ile ile alitoka hali ya kuwa yu hai. Yule Mkirsto

kuona vile basi hakusita ila alitoa shabaha mbiombio, na

kumwamini Nabii Muhammad (Saw) mbele ya Seyyid Abdul

Qadir (k.s.a).

Haramia kumgeuza kuwa kutbu:

7. Hekaya:-

Seyyid Abdul Qadir alipokuwa anarudi Madina kwenda

Baghdad, alikumbana na haramia njiani akimngojea mtu ye yote

apitae amnyang‟anye vitu alivyokuwa navyo. Seyyid Abdul Qadir

alipofika pale alimwuliza yule mtu, “Nani wewe?” Yule mtu

alisema kuwa yeye ni haramia. Pale pale Seyyid Abdul Qadir

alikashfiwa na aliona jina lake ni miongoni mwa watu waovu.

Lakini yule mwizi ilimpitia katika roho yake na akawaza kuwa

asiwe huyu ndiye Seyyid Abdul Qadir. Mara tu alivyofikiri vile na

Seyyid Abdul Qadir alimwambia, “Mimi ndiye Abdul Qadir.” Yule

mtu aliposikia vile mara alianguka chini ya miguu ya Seyyid Abdul

Qadir na akasema, “Ewe Bwana wangu, Abdul Qadir kipenzi cha

Mungu.” Muda ule ule Seyyid Abdul Qadir alisikia akiambiwa,

“Ewe Ghawth Mtukufu, mfundishe huyo mwizi njia ya haki”. Tena

Seyyid Abdul Qadir alimfundisha njia ya haki yule mwizi na

mwishoni alikuwa ni mmoja katika Makutbu (Mawalii).

Kusilimu kafiri kwa kuona karama za seyyid

Abdul Qadir. 18.

Page 28: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

8. Hekaya:- Mtu mmoja alitamani kwenda kumzuru Seyyid Abdul

Qadir, kwa wingi wa sifa zake anazozisikia. Pindi alipofika

Baghdad, alipita mahali ambapo, walikuwapo farasi 40 wakila

majani pasina kuchungwa. Farasi hao walikua wake Seyyid Abdul

Qadir. Alipozidi kuwaangalia aliwaona wanayo minyororo ya

dhahabu na fedha na matandiko yao ni ya hariri. Basi ikamjia fikra,

“Ala! Vipi Walii mkubwa kama huyu ashughulikie mambo kama

haya ya kilimwengu? Haya niliyoyaona kwake hata wafalme

hawana.”

Yule mgeni alipata maradhi makubwa sana kabla ya kufika

alikokusudia. Kwa hiyo ilimbidi afikie nyumba nyingine badala ya

nyumba ya Seyyid Abdul Qadir. Madaktari wengi walikwenda

kumwangalia kwa kutaka kumtibu.

Mwisho alikwenda Daktari mmoja wa Kinasara ambaye

alisema kama mgonjwa yule dawa yake ni maini ya Farasi wenye

sifa kadha. Watu walishughulika sana kuwatafuta. Lakini

aliyekuwa na Farasi hao ni Seyyid Abdul Qadir tu. Siku ya pli watu

walimwendea Seyyid Abdul Qadir kumwomba. Naye aliwapa bure

farasi mmoja na kunywa dawa nyingine, Yule mgonjwa alipata

nafuu kidogo. Kuona vile, watu walizidi kumwendea na

kumwomba tena na waliendelea mpaka farasi wote 40 wakesha.

Baada ya kupoa, yule mgeni alimuaga mwenyeji wake na

akaenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir na kumshukuru kwa wema

aliomfanyia hata akapata nafuu. Seyyid Abdul Qadir alimwambia

yule mgeni “Ewe kijana, hao farasi mimi niliwanunua kwa sababu

yako wewe; kwa kuona unayo mapenzi makubwa juu yangu. Na

ulipotia azma ya kuja kunizuru mimi nilijua kama utaumwa na

dawa yako ni maini ya farasi. Lakini wewe pale ulipopita karibu

yao na ukawaona, roho yako iliharibika na ukaleta fikra mbaya juu

yangu.” Tena yule kijana alimwomba msamaha na kumtaka radhi

kwa tukio hilo.

19.

Page 29: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Seyyid Abdbul Qadir alimwita yule Daktari Mnasara akampa ile

minyororo ya dhahabu pamoja na yale matandiko ya hariri. Pale

yule Mnasara alisilimu mbele ya Sheikh Seyyid Abdul Qadir kwa

kuona mambo ya siri na karama zake.

Kufuturu chakula cha peponi:

9. Hekaya:-

Seyyid Abdul Qadir alikaa Riadha siku 40 kwa kufanya

Ibada. Siku zote hizo alikuwa ndani ya Siami (funga). Ilimpitia

rohoni mwake kutokufuturu kitu chochote isipokuwa maji mpaka

Mwenyezi Mungu amteremshie chakula cha peponi.

Ilipofika siku ya 38, aliona sakafu ya nyumba inapasuka na

alimwona mtu mwenye birika ya dhahabu katika mkono mmoja na

katika mkono wa pili alikuwa amechukua sahani ya fedha yenye

matunda. Tena hivyo vitu aliviweka mbele ya Seyyid Abdul Qadir.

Seyyid Abdul Qadir aliuliza, “Vitu gani hivi?” Yule

mtumishi alijibu, “Hivyo ni vyakula nimepewa nikuletee.” Seyyid

Abdul Qadir alisema: “Mtume amekataza kulia vyombo vya

dhahabu na fedha. Viondoe hivyo vitu“. Yule Rohani alitoka mbio

na vyombo vyake. Lakini ulipofika wakati wa kufuturu, alishuka

Malaika na sahani iliyojaaa chakula. Yule Malaika alisema: “Ewe

Ghawthil-A`adham, hii ni dhifa yako inayotoka kwa Mwenyezi

Mungu. Seyyid Abdbul Qadir alipokea kile chakula akala yeye

pamoja na wengi wa marafiki zake. Na Mwenyezi Mungu

humruzuku amtakae pasina kudhani kama ataipata riziki hiyo kwa

muda huo.

20.

Page 30: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Mtoto wa kike kugeuka mwanaume.

10.Hekaya:-

Mtu mmoja alimwendea Seyyid Abdul Qadir kumtaka

amuombee dua ili apate mtoto mwanamme. Ghawth alijibu,

“Nimeshakuombea kwa Mungu na atakupa huyo umtakaye”. Yule

Bwana alimpata mtoto, lakini alikuwa mwanamke. Kwa hivyo

alimchukua mpaka kwa Sheikh na kumwambia, “Mimi nilimtaka

mtoto wa kiume, si wa kike”. Seyyid Abdul Qadir alisema: “Basi

mfunike nguo na umrudishe nyumbani, utaona yatakayotokea“.

Mara tu alipofika nyumbani alimwona yule mtoto wa kike

amegeuka kuwa mtoto wa kiume. Kama alivyotaka hasa.

Tajiri kuwaona ngamia wake waliopotea:

11. Hekaya:-

Siku moja Tajiri mmoja alikuwa akisubiri msafara ili

afuatane nao kwenda kufamya biashara. Alikuwa na ngamia 6

ambao amewatwisha magunia ya sukari.

Walipofika katikati ya njia. Ngamia wake walipotea pamoja

na mizigo yao. Aliwatafuta sana, lakini hakuwaona. Basi akapiga

ukelele, “Ewe Seyyid Abdul Qadir, ngamia wangu wamepotea

pamoja na mizigo yao”. Kutazama mbele yake alimwona mtu

amevaa nguo nyeupe anampungia mkono, Alipokwenda kule

hakumwona yule mtu bali aliwaona wale ngamia wake pamoja na

mizigo yao.

Ndege kusikiliza maneno: 21.

Page 31: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

12. Hekaya:-

Siku moja alikaa Seyyid Abdul Qadir, anazungumza. Basi

akasema: “Lau kama Mwenyezi Mungu angetaka kumleta Ndege

rangi ya kijani kusikilza maneno yangu, basi angekuja”. Baada ya

kumaliza kusema hivi, mara alitokea ndege mzuri wa rangi ile ile

ya kijani. Aliingia ndani ya mkono wa kanzu yake kusikiliza

maneno wala hakonekana tena mahala alikokwenda.

Kukatika ndege vipande vipande:

13. Hekaya:-

Siku moja Seyyid Andul Qadir alikuwa akizungumza, Mara

akaja ndege mzuri wa rangi ya kijani akatua mbele yake ili

kusikiliza maneno yake. Seyyid Abdul Qadir akasma, “Lau

ningemwambia huyu ndege kufa na kukatika vipande vipande basi

angalikufa.” Basi pale pale alianguka na akakatika vipande.

Kuhujumiwa simba mbele ya banda la farasi

14. Hekaya:-

Alikuwapo Walii mmoja jina lake Sheikh Ahmad

Zamdah. Sheikh Ahmad alikuwa akipanda simba na kutembea

naye anapokwenda kwa Mawalii wengine. Pale anapofika humtaka

mwenyeji wake ampe Ng‟ombe mmoja, yaani chakula cha simba

wake. Siku moja yule Sheikh Ahmad alifika Baghdad na akaenda

kwa Seyyid Abdul Qadir.

22.

Page 32: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Basi akamwambia: “Mimi ninayo desturi, pahala ninapofika

hupewa ng‟ombe na kumpa Simba wangu ale, Sasa unasemaje?”

“Nitampa ng‟ombe anayevuta maji”. Alisema Seyyid Abdul Qadir.

Alipokuwa anakwenda kwenye ng‟ombe alipitia pale penye

banda la Farasi wa Ghawth. Pale alikaa mbwa mmoja na

mwanawe. Alipopita Sheikh Ahmad walimfuata. Yule mbwa

alimweka pale alipokaa simba. Mara simba alitaka kumshambulia

mbwa wa Seyyid Abdul Qadir, lakini bahati mbaya mbwa

alimhujumu vikali simba yule na alimwua. Tena Sheikh Ahmad

alirudi kwa Seyyid Addul Qadir na kumtaka radhi kwa

yaliyotokea. Vile vile alitubia kwa Mwenyezi Mungu.

Kifo cha ndege mia:

15. Hekaya:- Ilitokea siku moja Seyyid Abdul Qadir alikaa pahala

akifanya Ibada zake. Juu kikapita kikundi kikubwa cha Ndege mia.

Walipomwona Seyyid Abdul Qadir wote walishuka wakatua na

wakamzunguka. Pale walipokaa wakawa wanafanya kelele. Seyyid

Abdul Qadir akatazama juu akasema, “Ewe Mola hawa ndege

wananishughulisha hapa”. Ndege wote walikufa saa ile ile.

Alipowaona wote ni maiti alisema “Ewe Mola unajua sababu ya

kifo chao”. Kusema vile mara wote walifufuka na kwenda zao.

Kujitenga kwenye magofu ya baghdad:

16. Hekaya:-

Seyyid Abdul Qadir alijitenga kwenye magofu kwa muda

23.

Page 33: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

usiopungua miaka 25 akifanya Ibada. Siku moja alisikia sauti

iliyomwambia, “Rudi Mjini watu wanakuhitaji kwa manufaa ya

Akhera“. Alisema Seyyid Abdul Qadir:- "Mimi nimekuja huku

kufanya Ibaada kwa kutafuta salama ya Dini yangu, na kuepuka na

fitina za Baghdad“. Kusikia vile tena akaambiwa.“Rudi na

utasalimika Mungu akipenda“. Kusikia vile Seyyid Abdul Qadir

alirudi huku moyo wake umejaa siri za Mungu.

Maneno kujitokeza:

17. Hekaya:-

Kila alipokuwa akikaa Ghawth-A`adham walikuwa

hawaondoki Mawalii – Iwapo amekaa kimya basi maneno hutaka

kujitokeza na kufika mpaka kwenye koo. Basi yakifika hapo hua

hawezi tena kunyamaza bali huwapa siri katika elimu ya “Hakika”.

Unyayo wangu uko shingoni mwa kila walii:

17. Hekaya:-

Maneno haya alipewa idhini na Mtume kuyasema. Na siku

alipoyatamka Baghdad, Mawalii wote wa Ulimwengu mzima

waliyasikia na kila mmoja aliinamisha shingo yake kwa kuridhia

maneno yaliyotamkwa.

Yasemekana walii mmoja wa Damask, Sheikh Rasalam

alisema: “Ewe Mwenyezi Mungu, ninakushuhudiza wewe na

Malaika wako kuwa nimeyasikia maneno ya Bwana

24.

Page 34: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

wa Mawalii na nimeyakaribisha. Tena akanyoosha shingo yake

kuonyesha kuwa ameridhia.

Nuru katika kidole chake.

18.Hekaya:-

Siku moja Seyyid Abdbul Qadir aliondoka usiku pamoja

na Masheikh watatu kwenda kuzuru kaburi la Imam Aba Hanifa,

Usiku huo ulikuwa na giza kubwa sana. Hapa na hapo huwezi

kupaona. Lakini Seyyid Abdul Qadir alipofika penye jiwe au mti

aliashiria kwa kidole chake. Na wakati huo lile jiwe au mti

hung‟ara sana mfano wa mbalamwezi kali. Waliendelea na hali

hiyo mpaka wakafika walikotaka na wakafanya waliyokusudia.

Wakati wa kurudi Seyyid Abdul Qadir alikuwa akiashiria

kwa kidole vile vile kwenye hatari na kutoka mwanga mkali

kwenye kile kitu. Tena walipofika

nyumbani kwa Seyyid Abdul Qadir, wale Masheikh waliaga na

wakaenda zao.

Mifupa kuigeuza kuku aliye hai:

19. Hekaya:-

Bibi mmoja alimpeleka mwanawe kwa Seyyid Abdul

Qadir kusomeshwa elimu. Mtoto huyo aliwekwa mahala maalum

kazi yake ni kufanya ibada tu kabla ya kusomeshwa Ilmu.

Siku moja mama yake yule mtoto kuja kumkagua. Lakini

hali alivyomwona nayo mwanawe kidogo haikumpendeza.

Alikuwa amedhoofu sana. Alipita ndani ili

25.

Page 35: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

aonane na Seyyid Abduil Qadir. Kwa uchungu wa mwanawe

ilimtoka subra na akawa anamwandama Seyyid Abdul Qadir kwa

maneno. Alisema: “Ewe Ghawthil Aadham, unakula kuku na

unamwacha mwanangu anakula vipande vya mikate ya shairi hata

amekuwa mwembamba kama uzi?“ Seyyid Abdul Qadir hakujibu

chochote isipokuwa aliikusanya ile mifupa na akasema mbele ya

yule mwanamke: “Ewe kuku simama kwa idhini ya Mungu

mwenye kuhusisha mifupa iliyochakaa,” Mara tu baada ya kusema

vile mifupa iligeuka kuku ambaye alisimama mbele ya yule

mwanamke.

Naam hapo Seyyid Abdul Qadir ndipo alipomneneza yule

mwanamke kwa kusema: “Ninapenda mwanao aweze kama haya,

kwa kupata daraja kama hili, anaweza kula chakula chochote

akitakacho mwenyewe”. Mwisho yule bibi alimtaka radhi Seyyid

Abdulm Qadir na akamwambia, “Ewe Seyyid Abdul Qadir,

yaliyonipelekea kusema hayo ni uchungu wa mwanangu tu. Na

tangu sasa hivi nakupa uhuru ufanye utakavyo juu ya mtoto huyo.”

Kushiba kwa kufyonza kidole:

20. Hekaya:-

Sheikh Muhammad Shawry Sabty aliondoka Misri

kwenda kumzuru Seyyid Abdul Qadir. Alikaa huko kwa siku

nyingi. Sheikh Muhammad alipofunga safari ya kwenda nyumbani,

alipewa wosia na Seyyid Abdul Qadir. Wosia wenyewe ni huu:

"Usitake haja kwa mtu yeyote.“ Baada ya kuusiwa alipewa zawadi

na vyakula vya kula anapokuwa safarini. Lakini kabla ya kuondoka Seyyid Abdul Qadir alikitia

kidole chake ndani ya kinywa cha Sheikh Muhammad na

akamwambia akifyonze. Baada ya kufanya hivyo tena

26.

Page 36: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

akashika njia akaenda zake. Jambo la kustaajabisha ni kuona kuwa

Sheikh Muhammad hakushikwa na njaa wala kiu mpaka akafika

kwake Misri. Na alipokitizama kile chakula alikiona kimeongezeka

wala hakikuharika. Baada ya kupumzika alikula chakula hicho

pamoja na watoto wake na Watu waliokuja kuonana naye.

Kifo cha seyyid Abdul Qadir (Qsa):

Seyyid Abdul Qadir alikufa siku ya Ijumaa, Mfungo saba,

mwaka 561 (A.H). Alizikwa kwenye chuo chake

“ Babuluzji”. Kafa na umri wa miaka 91. Watu wengi walimimminika mazikoni kwake, utasema

labda wanakwenda Arafa kwa vile watu walivyokuwa wengi

ilionekana ni bora zaidi awekwe ili azikwe usiku. Pamoja na hayo

hakubakia mtu yeyote katika Baghdad ila alihudhuria Maziko

yake. Katika majia, masoko na majumba yote yalijaa watu.

Seyyid Abdul Qadir alisalishwa na mwanawe Sheikh

Abdul Wahab na alisaliwa na watu wengi mno; Miongoni mwao

ni wanawe, wanfunzi wake na marafiki zake. Kifo chake Seyyid

Abdul Qadir kilitokea katika zama za Imam Yusufu bin

Muktafa. Wale watu waliokosa kumsalia Sheikh, walipewa nafasi

ya kumsalia wakati wa mchana ulipofunguliwa mlango.

27.

Page 37: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

Jihad:

Kwa yeyote anayetaka kutabaruk katika Jihad hii ya

kuchangia katika kuchapisha vitabu vya Dhikri, Tawwasul n.k.

Kwa kuwa hiki ni toleo la kwanza, tunategemea kutoa matoleo

zaidi. Awasiliane na mtunzi wa kitabu hiki moja kwa moja kupitia

simu namba: 0755 547 771 au aitie michango yake kwenye

Account ya Benk:

NMB – CLOCK TOWER A/C. 4082300209. ARUSHA.

TWARIQATUL QADIRIA ARRAZZIKIA JAILANIA.

MAKAO MAKUU

ZAWIA KUU.

P. O. BOX 8105

ARUSHA.

Wabillahit Tawfiq.

28.

Page 38: Seyyid Sheikh - al-faqeer.comal-faqeer.com/library/Books/ghawth.pdf · Seyyid Sheikh Abdul Qadir Jaylan (Qad-dasa-Llahu Siral A`ziz). First Addition Toleo la kwanza iii

KIMETOLEWA NA:-

Mtungaji:-

Swahib Sujjada:

Al Habib Sheikh Salim Bin Mbarak.

(Dar-wesh – Mti mkavu)

P.O. Box 8105,

Zawia kuu.

Arusha - Tanzania.

(E.A)