taarifa ya mwaka ya mfuko wa uwekezaji wa …
TRANSCRIPT
Asset Management and Investor Services
KAMPUNI YA UWEKEZAJI YA UTT AMIS
TAARIFA YA MWAKA YAMFUKO WA UWEKEZAJI WA
WATOTO (WATOTO FUND)
KWA MIAKA ILIYOISHIA30 JUNI 2016, 2017,2018 NA 2019
Fara ja kwa Watoto
i
YALIYOMO
1. Ratiba ............................................................................................................ ii
2. Muhtasari wa Mkutano...................................................................................2
3. Yatokanayo na Mkutano Uliopita .................................................................12
4. Taarifa ya Mwenyekiti wa Bodi.....................................................................15
5. Taarifa ya Mwangalizi wa Mfuko wa Watoto ................................................18
6. Taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za Mfuko ....................................................22
7. Taarifa ya Hesabu za Mfuko ........................................................................24
8. Taarifa ya Meneja kuhusu Uwekezaji ..........................................................29
9. Jarida la Habari............................................................................................36
Fara ja kwa Watoto
ii
KAMPUNI YA UWEKEZAJI YA UTT AMIS
MKUTANO MKUU WA WAWEKEZAJI WA MFUKO WA WATOTO,JUMAPILI TAREHE 1 DISEMBA 2019 KATIKA UKUMBI WA
MIKUTANO WA MWALIMU NYERERE, KUANZIA SAA 2:30 ASUBUHI
RATIBA NA AJENDA ZA MKUTANO
S/N MUDA SHUGHULI WAHUSIKA
1. 02.30 - 03.00 Kuwasili kwa Wajumbe na Kujiorodhesha Wajumbe/Utawala
2. 03.00 - 03.10 Matangazo na Shughuli za Utawala MC/Utawala
3 03.10 - 03.15 Akidi na Kufungua Mkutano Mwenyekiti
4. 03.15 - 03.30 Utambulisho (Wakurugenzi, Uongozi na Watoa Huduma kwa Mfuko)
Mkurugenzi Mtendaji
5. 03.30 - 03.40 Kupitia Muhtasari wa Mkutano Uliopita Wote
6. 03.40 - 03.55 Yatokanayo na Mkutano Uliopita Mkurugenzi Mtendaji
7. 03.55 - 04.25 Taarifa ya Mwenyekiti Mwenyekiti wa Bodi
8. 04.25 - 04.40 Kupokelewa kwa Taarifa ya Mwaka
1. Mwangalizi wa Mfuko
2. Mkaguzi wa Hesabu
3. Taarifa ya Hesabu
CRdB, KpMg na Mkurugenzi wa Huduma za Kampuni
9. 04.40- 05.10 Kupokea Taarifa ya Meneja Kuhusu Uwekezaji Mkurugenzi wa Uwekezaji
10. 05.10 - 05.30 Kipindi cha Maswali na Majibu Wajumbe wa Bodi / Watendaji
11. 05.30 - 05.45 Kufunga Mkutano Mwenyekiti wa Bodi
1
2 Muhtasari
Fara ja kwa Watoto
2 3
MUHTASARI WA MKUTANO WA SITA (6) WA MWAKA WA WAWEKEZAJI WA MFUKO
WA WATOTO ULIOFANYIKA TAREHE 22 NOVEMBA 2015 KATIKA UKUMBI WA
MIKUTANO WA HOTELI YA BLUE PEARL UBUNGO PLAZA, DAR ES SALAAM
WALIOHUDHURIA (Kiambatisho “A”)
BODI YA WAKURUGENZI
1. Prof. J. Kuzilwa - Mwenyekiti wa Bodi
2. Bw. J. Muhimbi - Mjumbe wa Bodi
3. Bw. P. Gamara - Mjumbe wa Bodi
4. Dkt. S. Mohamed - Mjumbe wa Bodi
5. Bw. Ramadhani Hamisi - Mjumbe wa Bodi
6. Dkt. H. S. Kibola - Mkurugenzi Mtendaji
WAALIKWA
1. Bw. E. Rugaimukamu - Mwakilishi wa Msajili wa Hazina
2. Bw. T. Dokodoko - Mjumbe wa Bodi/UTT Microfinance
3. Balozi F. Mbaga - Mjumbe wa Bodi/UTT Microfinance
4. Bw.J.Washima - AfisaMtendajiMkuu/ UTTMicrofinance
5. Bw. T. Mboma - KPMG/Wakaguzi wa Mahesabu ya Mfuko
6. Bi. M. Mponda - CRDB/Waangalizi wa Mfuko
MENEJIMENTI NA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA UWEKEZAJI YA UTT AMIS
1. Bw. S. Migangala
2. Bw. R. Mchatta
3. Bi. J. Msofe
4. Bi. P. Nchimbi
5. Bw. D. Mbaga
6. Bw. I. Wahichinenda
7. Bw. S. Bujiku
8. Bi. S. Mgaya
9. Bw. M. Zellah
19. Bi. V.Maheri
20. Bw. M. Balati
21. Bw. H. Mnongane
22. Bw. B. Liwali
23. Bw. C. Chanjarika
24. Bw. J. Joseph
25. Bi. F. Milinga
26. Bi. R. Maruma
27. Bw. A. Salmin
28. Bw. J. Masoud
29. Bw. L. Chokola
30. Bw. S. Mkomwa
31. Bw. D. Chibwana
32. Bi. M. Engel
33. Bw. B.Lukinga
34. Bw. A. Mushi
35. Bi. E. Lyimo
36. Bw. L.Temela
37. Bi. A. Lashikoni
38. Bw. W. Khijja
39. Bi. S. Twakyondo
40. Bi. V. Yuda
41. Bw. E. Bakilana
WENYE VIPANDE NA TAARIFA YA AKIDI
Wajumbe wenye Vipande waliohudhuria walikuwa 94 ambao majina yao yameambatanishwa kwenye Kumbukumbu hizi kama Kiambatisho “A”. Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji alitoa Taarifa kwamba idadi ya Vipande vilivyowakilishwa ni 1,197,946.1576 kati ya jumla ya Vipande 9,895,503.4809 vya Mfuko. Kwa mujibu wa mahudhurio Vipande vilivyowakilishwa vilikuwa asilimia 12.11% ya jumla ya Vipande vyote vya Mfuko na hivyo Mkutano ungeweza kuanza kwa sababu idadi inayohitajiwa kwenye Waraka wa Makubaliano (Deed of Trust) ni asilimia 10.
DONDOO ZA MKUTANO
1. Utambulisho (Mwakilishi wa Msajili wa Hazina, Wajumbe wa Bodi za Makampuni ya UTT, Uongozi wa Kampuni na Watoa Huduma kwa Mfuko, na Wageni waalikwa)
2. Kuthibitisha Kumbukumbu za Mkutano Uliopita
3. Yatokanayo na Kumbukumbu za Mkutano Uliopita
4. Taarifa ya Mwenyekiti
5. Taarifa ya Mwaka Kuhusu Ukaguzi wa Hesabu za Mfuko
6. Taarifa ya Meneja wa Mfuko Kuhusu Uwekezaji
7. Taarifa ya Mwangalizi wa Mfuko
8. Taarifa ya Wakaguzi wa Mfuko
Fara ja kwa Watoto
10. Bw. R. Mwanga
11. Bw. M. Kimario
12. Bi. J. Swai
13. Bi. M. Mashiku
14. Bw. P. Ndunguru
15. Bi. V. Abuogo
16. Bw. F. Bwalya
17. Bw. B. John
18. Bi. J. Mlimbila
Fara ja kwa Watoto
2 3
9. Kipindi cha Maswali na Majibu
10. Kufunga Mkutano
UFUNGUZI WA MKUTANO
Mwenyekiti alifungua mkutano saa 3.30 asubuhi kwa kuwakaribisha wajumbe Wawekezaji waliohudhuria Mkutano.
1.0 UTAMBULISHO
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS aliwatambulisha Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni, Mwakilishi wa Msajili wa Hazina, Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya UTTMicrofinance, na Menejimenti ya Kampuniya uwekezaji ya UTT AMIS. Vilevile Aliwatambulisha Wawakilishi wa Benki ya CRDB ambayo ni Mwangalizi wa Mfuko pamoja na Kampuni ya KPMG ambayo inatoa Huduma za Ukaguzi wa Mahesabu ya Mfuko, pampja na wageni wengine waalikwa.
2.0 TAARIFA YA MWENYEKITI
2.1 Mwenyekiti aliwasilisha Taarifa ya Mfuko wa Watoto kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2015.
2.2 Mwenyekiti alianza kwa kuwakaribisha wajumbe wote katika Mkutano Mkuu wa Sita (6) wa Mwaka wa Wawekezaji wa Mfuko wa Watoto ambapo alielezea furaha yake kuwa katika kipindi cha mwaka kilichoisha tarehe 30 Juni, 2015 kilikuwa cha kipekee kutokana na pato la mwaka la Mfuko kuzidi kwa kiasi kikubwa kigezo linganishi (benchmark) na pia kuzidi pato la Mfuko kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2014. Pia mwenyekiti alieleza kuwa mfuko umeendelea kukua kwa maana ya thamani ya mfuko pamoja na kuongezeka kwa idadi ya wawekezaji kutokana na kuongezeka kwa Imani ya wawekezaji kwa mifuko inayoendeshwa na UTT AMIS pamoja na elimu kwa umma kuhusu faida za mifuko ya uwekezaji wa pamoja.
2.3 Taarifa ilieleza kuwa, Pamoja na wasiwasi na kutokuwepo kwa uhakika wa hali ya kiuchumi na utendaji wa masoko ambao mara nyingi huhusishwa na uwepo wa uchaguzi mkuu na changamoto zingine, mwaka ulioishia Juni 30, 2015 pato la ndani la taifa limendelea kukua kwa kiwango cha asilimia 7.2 . Mwenyekiti alieleza kwamba hali nzuri ya ukuaji uchumi ilikuwa muhimu katika kusukuma maendeleo na ubora au ufanisi ndani ya masoko ya fedha ambamo Mfuko umekuwa ukiwekeza, na kwamba kutokana na uchumi wa Tanzania kuendelea kuwa katika hali nzuri, kipindi cha mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2015 mfumuko wa bei uliendelea kudhibitiwa katika kiwango cha asilimia 6.1. Bila kujali kushuka kwa viwango vya
riba ukilinganisha na mwaka ulioishia Juni, 2014, kiwango hicho kiliendelea kuwa juu ya asilimia 13 na hivyo kuwezesha kutoa pato halisi chanya.
2.4 Kuhusu Ukuaji wa Mifuko inayoendeshwa na Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Taarifa ilieleza kuwa katika mwaka mmoja uliopita, Mifuko yote mitano (5) ilikua kwa kiwango cha asilimia 34.36 kutoka shilingi bilioni 178.7 mwaka 2014 mpaka shilingi bilioni 240.1 mwaka 2015, na kwamba idadi ya Wawekezaji nayo iliongezeka kufikia 118,811kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni, 2015. Aidha, ilielezwa kwamba kwa Mfuko wa Watoto pekee, Ukubwa wa Mfuko uliongezeka kwa kiwango cha asilimia 44 kutoka shilingi bilioni 1.85 mpaka shilingi bilioni 2.467. Ilielezwa kwamba mafanikio hayo yalitokana na utendaji mzuri wa soko la fedha na utaalamu wa uwekezaji unaofanywa na Meneja wa Mifuko, yaani Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, juhudi za Meneja kuendelea kutoa elimu kwa umma, juhudi zilizoongeza uelewa juu ya faida za uwekezaji wa pamoja, matumizi ya mitandao ya simu katika kulipia manunuzi ya Vipande ilikuwa ni kati ya vichocheo na hivyo kuongeza kasi ya ukuaji wa mauzo ya Vipande,
2.5 Tanzania Mwenyekiti alitoa taarifa kwa wawekezaji juu ya tuzo iliyotolewa kwa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMI kuwa ni Meneja bora wa usimamizi wa rasilimali na uwekezaji Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2015 kutoka kwa kampuni ya kimataifa ya Capital Finance International (CFI). Kampuni hii hutoa hutoa taarifa, uchunguzi na tathimini kuhusu masoko ulimwenguni kote
2.6 Mwenyekiti pia alielezea Changamoto ambazo zilikuwa zinaikabili Kampuni katika utendaji wake, zikiwemo mabadiliko ya teknolojia iliyosababisha Meneja wa Mifuko kuendelea na uwekezaji katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) ili kuendana na ukuaji wa soko pamoja na kufikiamatarajio ya Wawekezaji katika Mifuko, na ujenzi wa uwezo wa Menejimenti na Wafanyakazi wa Kampuni ili kuhimili ushindani katika soko la ukanda wa Afrika Mashariki.
2.7 Kuhusu Matarajio ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Mwenyekiti pia alielezea kwamba Menejimenti ya Kampuni itandelea kutekeleza Mpango Mkakati wa Miaka Mitano (2014-2019) ambao unatoa vipaumbele pamoja na mikakati ya uendeshaji wa Mifuko, na kwamba Kampuni ilikuwa na matumaini kuwa fursa mbalimbali zitakazowezesha ukuaji wa Mifuko, mapato kwa Wawekezaji kwa kutumia fursa ya ukuaji wa kimuundo wa soko la fedha la Afrika Mashariki zitajitokeza.
2.8 Mwenyekiti, kwa niaba ya Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, alitoa shukrani kwa Wawekezaji, Serikali,
Fara ja kwa Watoto
4 5
Waangalizi wa Mfuko, Watoa huduma na Wadau wote ambao wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS. Mwisho alitoa shukrani kwa Menejimenti na Wafanyakazi wote wa Kampuni kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii kubwa kwa manufaa ya Wawekezaji na Taifa kwa ujumla.
3.0 KUTHIBITISHA KUMBUKUMBU ZA MKUTANO ULIOPITA
Baada ya kuzipitia Kumbukumbu za Mkutano Mkuu uliopita kifungu kwa kifungu, Mjumbe mmoja kwa niaba ya Wajumbe wote alisimama na kuthibitisha Kumbukumbu za Mkutano, na Wajumbe wote kwa kauli moja walipitisha na kuthibitisha Kumbukumbu za Mkutano wa Tano (5) uliofanyika terehe 23 Novemba, 2014.
4.0 YATOKANAYO NA KUMBUKUMBU ZA MKUTANO ULIOPITA
4.1. Kumbu kumbu Na: 9.2.8 : Kampuni ya UTT AMIS iliahidi kuendelea kufanya maboresho katika matumizi ya teknolojia mbalimbali za kisasa ili kurahisisha kwa wananchi kujiunga na kufanya malipo ya vipande kupitia simu za mkononi.
4.2 Utekelezaji:Mwakilishialiezakuwautafitiulifanyikana kwamba mchakato wa mradi utakaoboresha jinsi ya watanzania wengi kujiunga na kufanya malipo ya vipande kwa njia ya simu ulikuwa umeshaanza na kwamba ulitegemewa kumalizika ndani ya muda mfupi kabla ya tarehe 30 Juni 2016.
5.0 TAARIFA YA MWAKA KUHUSU HESABU ZA MFUKO WA WATOTO
5.1 Mkurugenzi wa Idara ya Fedha na Utawala ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS aliwasilisha Taarifa ya Hesabu za Mfuko katika kipindi cha mwaka wa fedha 2014/2015 ulioishia tarehe 30 Juni, 2015.
5.2 Katika Taarifa hiyo muwasilishaji alieleza kuwa taarifa ilikuwa imegawanyika katika sehemu kuu nne, ambazo ni Taarifa ya Mapato na Matumizi, Taarifa ya Urari wa Hesabu za Mfuko, Taarifa ya Mabadiliko ya Thamani ya Mfuko na Taarifa ya Mtiririko wa Fedha.
5.3 Kwa upande wa Mapato na Matumizi, ilielezwa kuwa katika kipindi cha mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2015 jumla ya Mapato ya Mfuko kabla ya kodi yalikuwa shilingi 605,514,000/= ikilinganishwa na mapato ya shilingi 401,812,000/= kwa mwaka uliopita. Pia ilelezwa kuwa jumla Mfuko ulilipa Kodi ya shilingi 17,339,000/= ikilinganishwa na shilingi 14,227,000/= kwa mwaka uliopita,
na hivyo Faida ya Mfuko baada ya Kodi ilikua shilingi 588,175,000/= ikilinganishwa na shilingi 387,585,000/= kwa mwaka uliopita.
5.4 Kwa upande wa Urari wa Hesabu za Mfuko, ilielezwa kuwa Rasilimali za Mfuko zilikuwa shilingi 2,716,125,000/= ikilinganishwa na shilingi 1,886,567,000/= mwaka uliopita. Pia Dhima za Mfukozilipunguakufikiashilingi32,353,000/=tokashilingi 37,980,000/= mwaka ulioishia 30 Juni, 2014. Kutokana na Taarifa hiyo, Thamani Halisi ya Mfuko kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2015 ilikuwa shilingi 2,683,772,000/= ikilinganishwa na shilingi 1,848,587,000/= mwaka uliopita.
5.5 Katika Taarifa ya Mabadiliko ya Thamani ya Mfuko ilielezwa kuwa, Mauzo ya Vipande (Sales) yalikuwa shilingi 356,969,000=/ ikilinganishwa na shilingi 200,357,000/= kwa mwaka uliopita. Pia Ununuzi wa Vipande (Repurchases) ilikuwa ni shilingi 109,959,000/= ukilinganisha na shilingi 50,363,000/= mwaka uliopita. Hivyo Thamani Halisi ya Mfuko kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2015 ilikuwa shilingi 2,683,772,000/= ikilinganishwa na shilingi 1,848,587,000/= mwaka uliopita.
5.6 Kwa upande wa Taarifa ya Mtiririko wa Fedha, ilielezwa kuwa Mapato Halisi kabla ya marekebisho ya mtaji wa uendeshaji yalikuwa Shilingi 169,951,000/= ikilinganishwa na Shilingi 128,517,000/= mwaka uliopita. Fedha iliyopatikana kutoka kwenye shughuli za uendeshaji baada ya marekebisho ya mtaji ilikuwa shilingi 183,300,000/= ikilinganishwa na shilingi 80,898,000/= mwaka uliopita. Fedha Halisi itokanayo na shughuli za Uendeshaji ilikuwa shilingi 602,772,000/= ikilinganishwa na shilingi 339,863,000/= mwaka uliopita. Fedha Halisi iliyotumika katika shughuli za uwekezaji ilikuwa shilingi 723,202,000/= ikilinganishwa na shilingi 509,943,000/= ambapo amana ya mfuko iliongezeka mpaka shilingi 247,010,000 ukilinganisha na milioni 149,994,000 za mwaka 2014. Hivyo basi baki la fedha halisi lilikuwa shilingi 126,578,000 ikilinganishwa na shilingi (20,086,000) kwa mwaka 2014
6.0 TAARIFA YA MENEJA WA MFUKO KUHUSU UWEKEZAJI
6.1 Mkurugenzi wa Idara ya Uwekezaji wa Kampuni wa Uwekezaji ya UTT AMIS aliwasilisha Taarifa ya Meneja kuhusu uwekezaji katika kipindi cha mwaka wa fedha 2014/2015 ulioishia tarehe 30 Juni, 2015.
6.2 Taarifa ilieleza kuwa, Mfuko wa Watoto uliendelea kupata mafanikio makubwa katika mwaka wa fedha wa 2014/2015 katika ukuaji wa Thamani ya Kipande na ukubwa wa Mfuko. Thamani ya Kipande ilikua kutoka shilingi 210.54/= mwezi
Fara ja kwa Watoto
4 5
July, 2014 hadi shilingi 275.92/= Juni, 2015 wakati Rasilimali za Mfuko zilipanda kutoka Shilingi 1.85 bilioni hadi 2.68 bilioni mwishoni mwa mwezi Juni, 2015 ambalo niongezeko la asilimia 44.86
6.3 Taarifa hiyo iliainisha kwamba mgawanyo wa Uwekezaji wa Mfuko uliendelea kufanyika kwa kuzingatiaserayauwekezaji ilikufikiamgawanyoanuwai wa Hisa, Dhamana za Serikali na mabenki. Taarifa ilieleza kuwa mgawanyo wa Mali za Mfuko ulikuwa asilimia 44 zilizowekezwa kwenye Hisa zilizoorodheshwa katika soko la hisa la dar es salaam, asilimia 41 zilizowekezwa katika Akaunti za Muda Maalum katika mabenki, asilimia 2 zilizowekezwa katika Hati fungani za makampuni binafsi, wakati asilimia 12 ziliwekezwa katika Dhamana za Serikali, na kiasi kilichobaki cha asilimia 1 ziliwekezwa katika Akaunti za Muda Mfupi katika mabenki.
6.4 Taarifa ilieleza kwamba Mfuko wa Watoto tangu uanzishwe umekuwa na mafanikio makubwa kwani Faida ya Mfuko toka uanzishwe ilifikia asilimia16.90, wakati Faida kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita ilikuwa ni asilimia 31.47 wakati ambapo asilimia 31.24 ilipatikana kwa miaka miwili iliyopita. Taarifa ilieleza kuwa ufanisi huo unaridhisha ikilinganishwa na faida zinazotolewa na Dhamana za Serikali za siku 182 ambazo mpaka mwezi Juni, 2015 zilikuwa zikitoa faida ya asilimia 11.47 pamoja na viwango vingine vyote vya Riba katika soko la fedha.
6.5 Taarifa ilisema kuwa Uchumi wa Tanzania uliendelea kukua katika kiwango cha kuridhisha ukilinganisha na makadirio yaliyokuwa yametolewa hapo awali, na kwamba Pato halisi la Taifa lilikua kwa asilimia 7 katika mwaka 2015 ambao ni mdogo zaidi ukilinganisha na pato la asilimia 7.3 kwa mwaka uliopitia. Ilielezwa kuwa, ukuaji wa uchumi kwa kipindi cha mwaka 2015 ulichangiwa na hali ya hewa kuwa nzuri, ongezeko la ujenzi wa miundo mbinu, biashara imara ya jumla pamoja na rejareja, kuimarikakwausafirishaji,usindikajinashughulizaviwanda ambapo shughuli za ujenzi zimechangia asilimia14.1,shughulizausafirishajinausindikajizimechangia asilimia 12.5 , shughuli za kifedha na bima zimechangia asilimia 10.8 huku shughuli za biashara za jumla na rejareja zimechangia asilimia 10
6.6 Taarifa ya Meneja pia ilibainisha kwamba sekta ya fedha iliendelea kufanya vizuri, hususani mabenki, ambapo taasisi hizo zilikuwa na Mitaji mikubwa na Ukwasi wa kutosha. Pia katika kipindi cha mwaka chakufikiaMachi,2015,jumlayaMaliKatikaSektayamabenkiilikuakwaasilimia11.4mpakakufikiakiasi cha shilingi bilioni 23,479.1, na wakati huo huo Amana za wateja zilikua kwa asilimia 13.9 mpakakufikiakiasichashilingibilioni17,904.7.
6.7 Taarifa ilielezea kwamba hali ya Mfumuko wa bei iliendelea kubakia katika viwango vya tarakimu moja katika kipindi chote cha mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2015. Kwa ujumla kasi ya mfumuko wa bei ilipungua hadi asilimia 6.1 Juni, 2015, kutoka asilimia 6.4 mwezi Juni, 2014. Ilielezwa kwamba kuimarika kwa kiwango cha mfumuko wa bei kulichangiwa na sera madhubuti ya fedha, kuimarika kwa hali ya chakula, kushuka kwa gharama za umeme pamoja na kushuka kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia.
6.8 Taarifa ya Meneja ilieleza ya kwamba viwango vya Riba katika Dhamana za Serikali kutoka Benki Kuu ya Tanzania viliendelea kuwa mwongozo wa viwango vya Riba katika soko. Wastani wa Riba hizo ulipungua kwa wastani wa asilimia 16.43 Juni, 2014 hadi asilimia 16.07 mwezi Juni, 2015. Kwa kipindi cha mwaka mzima ulioishia Juni 2014, viwango hivyo vya Riba katika mabenki ya biashara vilishuka, ambapo Riba katika Amana za mabenki zilipanda mpaka wastani wa asilimia 8.89 Juni, 2015 ukilinganisha na wastani wa asilimia 8.12 mwezi Juni, 2014.
6.9 Kwa upande wa Thamani ya shilingi ya Tanzania ikilinganishwa na fedha za kigeni, Taarifa ilibainisha ya kwamba shilingi ya Tanzania kwa dola moja ya Kimarekani imeshuka thamanikufikiawastaniwashilingi 1,647.70 kwa dola moja kama ilivyokuwa tarehe28Juni,2014hadikufikiakiasichashilingi1,951.7 kwa dola moja mnamo tarehe 30 Juni, 2015.
6.10 Kwa upande wa Soko la Hisa la Dar es Salaam, katika mwaka wa fedha ulioishia mwezi Juni 30, 2015 bei za Hisa zilifanya vizuri, ambapo kulingana na takwimu za soko, mauzo yameongezeka na kufikia kiasi cha Shilingi bilion 878 ukilinganishana shilingi bilioni 274 mauzo yaliyo ripotiwa mwaka uliopita. Pia taarifa ilieleza kwamba ukubwa wa soko la hisa kwa ujumla uliongezeka kwa thamani ya shilingi Trilioni 4.8 na shilingi Trilioni 2.4 kwa ukubwa wa soko ndani ya nchi.
6.11 Taarifa ya Meneja ilimalizia kwa kuwahakikishia Wawekezaji kuwa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS itataendelea kubuni na kuvumbua mianya stahili ya uwekezaji kadri inavyojitokeza katika soko ili kuongeza mapato na faida kwa Wawekezaji na taifa kwa ujumla.
Fara ja kwa Watoto
6 7
7.0 TAARIFA YA MWANGALIZI WA MFUKO
7.1 Mwakilishi wa Benki ya CRDB ambayo ni Mwangalizi wa Mfuko wa Watoto, aliwasilisha Taarifa iliyoeleza kwamba jukumu lao ni kusimamia na kuhakikisha kuwa utendaji wa Meneja wa Mfuko unazingatia Waraka wa Makubaliano ili kuhakikisha maslahi bora ya wenye Vipande.
7.2 Mwakilishi huyo wa Benki ya CRDB alieleza kuwa katika utekelezaji wa kazi yao kama Mwangalizi wa Mfuko wana majukumu mbalimbali yakiwemo uangalizi wa mali za Mfuko, kuhakikisha Meneja wa Mfuko anatumia njia au mbinu sahihi kukokotoa mahesabu ya thamani ya Mfuko sambamba na Mkataba wa Makubaliano, na pia kuhakikisha viwango vya uwekezaji vinazingatiwa.
7.3 Mwakilishi wa Benki ya CRDB alisema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha kilichoanzia tarehe 01/07/2014 mpaka 30/06/2015, Benki ya CRDB kama Mwangalizi wa Mfuko wa Watoto wameendeleza uangalizi wa mwenendo wa shughuli za Meneja wa Mfuko, utekelezaji wake na kuangalia changamoto kwenye uwekezaji.
7.4 Mwakilishi wa benki ya CRDB alihitimisha kwa kuwathibitishia Wawekezaji wa Mfuko kwamba shughuli za uwekezaji kwenye Mfuko wa Watoto na wajibu wa Meneja wa Mfuko vimeendeshwa/vimetekelezwa kufuatana na vipengele vya Waraka wa Makubaliano na kwamba maslahi ya wenye Vipande ndani ya Mfuko wa Watoto yanalindwa na kuzingatiwa ipasavyo.
8.0 TAARIFA YA MWAKA KUHUSU UKAGUZI WA HESABU ZA MFUKO WA WATOTO
8.1 Mwakilishi kutoka Shirika la Wahasibu la KPMG ambao ni Wakaguzi wa Mfuko aliwasilisha Taarifa kuhusu ukaguzi wa Hesabu za Mfuko kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2015. Alieleza kuwa Taarifa ya Hesabu za Mfuko zilizowasilishwa yaani Taarifa ya Mapato na Matumizi, Urari wa Hesabu za Mfuko, Taarifa ya Mabadiliko ya Thamani ya Mfuko na Taarifa ya Mtiririko wa Fedha ni sehemu ya Taarifa kamili ya Hesabu za Mfuko iliyokaguliwa na kupitishwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya UTT AMIS ambayo ni Meneja wa Mfuko tarehe 30 Oktoba, 2015 na kutiwa saini na Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya Wakurugenzi pamoja na Mjumbe mwingine wa Bodi.
8.2 Taarifa ilieleza kuwa ili kupata taswira kamili ya ufanisi wa Mfuko na Hesabu zake kwa mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2015, ni muhimu kuchambua Taarifa kamili ya Hesabu za Mfuko inayopatikanakatikaofisizaKampuniyaUwekezajiya UTT AMIS.
8.3 Mwakilishi huyo alihitimisha Taarifa yake kwa kueleza kuwa Taarifa kamili ya Hesabu za Mfuko zimekaguliwa na Shirika la Wahasibu la KPMG na ripoti yake isiyo na kasoro juu ya hali ya Hesabu za Mfuko kwa kipindi hicho imetolewa.
9.0 KIPINDI CHA MASWALI NA MAJIBU
9.1 Wawekezaji wa Mfuko waliuliza maswali pamoja na kutoa hoja zifuatazo:-
9.1.1 Shukrani zilitolewa kwa Bodi ya wakurugenzi na wafanyakazi wa UTT AMIS kwa mafanikio yaliyopatikana mpaka sasa.
9.1.2 Ushauri ulitolewa kwa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS ambayo ni Meneja wa Mfuko wa Watoto kwamba katika mfumo wake wa ungozi wa ngazi ya juu hususani katika Bodi ya Wakurugenzi kuwepo na wawakilishi kutoka pande zote mbili za nchi (Bara na Visiwani) ili watanzania waliopo visiwani wapate wawakilishi katika bodi hiyo ya wakurugenzi.;
9.1.3 Ushauri ulitolewa kwa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS kwamba elimu zaidi juu ya Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja inayosimamiwa na Kampuni itolewe katika mikoa yote ya Tanzania hususani Tanzania visiwani (Pemba na Unguja) kwani ni haki ya kila Mtanzania kuelimishwa juu ya fursa zitokanazo na Mifuko hiyo na kwamba bado idadi kubwa ya Wananchi kwa upande wa Tanzania visiwani hawajapata ufahamu juu ya Mifuko ya UTT AMIS na hivyo kutonufaika nayo;
9.1.4 Ufafanuzi ulihitajika kuhusiana na utaratibu wa kodi inayotozwa katika mfuko wa watoto kwa nini pesa ambayo anawekewa mtoto chini ya miaka 18 inatozwa kodi?
9.1.5 Ufafanuzi ulihitajika kuhusiana na mgawanyo wa uwekezaji katika mfuko wa watoto hususani uwekezaji katika mabenki, je mfuko umewekeza kiasi gani cha pesa katika Amana za mabenki za muda maalumu na muda mfupi, katika hisa na pia katika dhamana za serikali za muda mrefu.;
9.1.6 Pongezi zilitolewa kwa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS kwa kuboresha utoaji Taarifa za Mikutano kwa Wawekezaji katika Mifuko, na kwamba juhudi katika kufikisha taarifa hizo kupitia ujumbemfupiwa simu ziongezwe kwani utoaji taarifa kupitia magazetihufikiaWawekezajiwachachezaidi;
9.1.7 Ufafanuzi ulihitajika kuhusiana na faida ambayo mfuko imepata, wawekezaji walitaka kujua kipande cha mfuko wa watoto kimepanda kwa kiasi gani ukitoa gharama za uendeshaji?;
9.1.8 Ufafanuzi ulihitajika kuhusiana na umri wa mtoto unaoruhisiwa kwa mzazi au mlezi kumwandikisha mtoto katika Mfuko na pia njia rahisi ya kununua vipande kwa wakaazi wa Tanzania visiwani;
Fara ja kwa Watoto
6 7
9.1.9 Ushauri ulitolewa kwa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS kwamba makabrasha kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Mfuko yatolewe wiki moja (1) kabla ya Mkutano ili Wawekezaji wapate fursa ya kuweza kuyapitia kwa makini na kujiandaa kwa ajili ya Mkutano;
9.1.10 Wawekezaji walitoa malalamiko kwa huduma mbovu na zisizoridhisha katika baadhi ya matawi ya Benki ya CRDB kwa mfano kutokufahamu namba ya Akaunti ya Watoto na pia kutokufahamu mifuko ya UTT AMIS
9.1.11 Pendekezo lilitolewa kwamba badala ya wateja wa UTTAMIS kuhudumiwa na Benki ya CRDB pekee ingekuwa vema kama wangeitumia pia Benki ya NMB ambayo imeenea nchi nzima
9.1.12 Ufafanuzi ulihitajika kwa mwekezaji aliyenunua vipande mwanzoni na anayenunua sasa endapo thamani yao inalingana. Kwa mfano mwekezaji aliyetoa Sh.100,000/- kununua vipande wakati mauzo ya awali na aliyetoa thamani hiyo hiyo kwa kununua vipande sasa;
9.2 Wawakilishi wa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS walitoa ufafanuzi ufuatao:-
9.2.1 Shukrani zilipokelewa na Wawakilishi wa Kampuni kutokana na pongezi mbalimbali ambazo Wawekezaji walizitoa. Wawakilishi hao wa Kampuni waliahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili waweze kutoa huduma bora zaidi kwa Wawekezaji. Aidha Ushauri mbalimbali uliotolewa ulipokelewa na Wawakilishi hao waliahidi pia kufanyia kazi mapendekezo ya Wawekezaji ili kuboresha ufanisi wa huduma katika Mifuko na ustawi na ukuaji wa Mifuko kwa ujumla;
9.2.2 Kuhusu ushirikishwaji wa Wawekezaji na wananchi wa Tanzania visiwani katika ngazi za juu za uongozi wa kampuni ya uwekezaji wa UTT AMIS Mwenyekiti alisema kwamba Tanzania Visiwani ina mwakilishi katika bodi ya wakurugenzi ambaye ni Dkt Mohammed Suleiman kutoka Chake chake- Pemba hivyo wawekezaji kutoka Tanzania visiwani waondoe shaka kwani wanae mwakilishi imara katika bodi ya wakurugenzi ya kampuni hii.
9.2.3 Ushauri ulipokelewa kuhusiana na utoaji zaidi wa elimu juu ya Mifuko ya Uwekezaji ya Pamoja inayosimamiwa na Kampuni kwa Watanzania wengi zaidi nchi nzima hususani Tanzania Visiwani (Pemba na Unguja) ili nao wanufaike na faida zinazopatikana na uwekezaji huo. Ilielezwa pia Meneja wa Mifuko ameendelea na juhudi za kutoa elimu kwa umma katika mikoa yote nchini Bara na Visiwani,ambapo ilibainishwa kwamba Kampuni imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kutoa elimu juu ya Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja na faida zake kupitia redio, televisheni, magazeti, mitandao na blogu za kijamii, mikutano na Wananchi, pamoja
na ziara mbalimbali katika mikoa takriban yote ya Tanzania na kwamba juhudi hizo zimechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa mauzo ya Vipande vya Mifuko inayosimamiwa na Kampuni;
9.2.4 Ufafanuzi ulitolewa kuhusiana na Kodi katika mfuko wa watoto kwamba anayelipa kodi si mtoto anayewekewa pesa katika mfuko wa watoto bali utaratibu uliotumika kuanzisha mifuko unatupasa kulipa kodi ya mifuko pia mifuko imesamehewa kodi kubwa kama vile kodi ya mapato na kodi zote kubwa, kodi inayolipwa ni ile kodi ya zuio tu, ambayo haina madhara makubwa kwa uendeshaji na ukuaji wa mfuko.;
9.2.5 Ufafanuzi ulitolewa na kuhusiana na mgawanyo wa uwekezaji kwenye Mfuko wa Watoto kwamba kampuni ya UTTAMIS kama meneja wa mfuko wamepewa ilo jukumu la usimamizi wa mifuko kisheria na kuna taratibu zinazoongoza jinsi ya kuwekeza pia kampuni imekua ikifanya utafitikabla ya kuwekeza eneo husika, vilevile kabla ya maamuzi ya mwisho ya uwekezaji Menejimenti ya kampuni inaripoti kwa kamati husika na Bodi ya wakurugenzi ili kupata kibali kabla ya uwekezaji kuanza:
9.2.6 Ushauri ulipokelewa na Wawakilishi wa Kampuni juu ya utoaji wa Taarifa za Mikutano ya Mwaka kwa Wawekezaji kupitia njia mbalimbali za mawasiliano ya umma zikiwemo Televisheni, ambapo ilielezwa kwamba Kampuni itaendelea kutumia njia mbalimbalizitakazorahisishaufikishwajiwaTaarifajuu ya Mikutano ya Mwaka kwa Wawekezaji wengi zaidi ili ushiriki wao katika Mikutano hiyo nao uwe mkubwa zaidi;
9.2.7 Ufafanuzi ulitolewa kuhusiana na faida ambayo mfuko imepata ni kwamba, Mfuko wa Watoto uliendelea kupata mafanikio makubwa katika mwaka wa fedha wa 2014/2015 katika ukuaji wa Thamani ya Kipande na ukubwa wa Mfuko. Thamani ya Kipande ilikua kutoka shilingi 210.54/= mwezi Juni, 2014 hadi shilingi 275.92/= Juni, 2015 wakati Rasilimali za Mfuko zilipanda kutoka Shilingi 1.85 bilioni hadi 2.68 bilioni mwishoni mwa mwezi Juni, 2015.
9.2.8 Ufafanuzi kuhusu umri wa mtoto kujiunga na Mfuko wa Watoto ulitolewa kwamba mtoto yeyote kuanzia umri wa siku moja (0) mpaka miaka kumi na nane (18) anaweza kujiunga na Mfuko. Aidha, ilielezwa kwamba mtoto ambaye tayari ni mwanachama ndani ya Mfuko atakoma kuwa mwanachama iwapoatafikishaumriwamiakaishirininanne(24),kuhusu njia rahisi ya kununua vipande kwa wakaazi wa Tanzania Visiwani Menejimenti ya UTT AMIS ilieleza kuwa kwa sasa Mtanzania yeyote anaweza kununua vipande vya mfuko wa watotona Mifuko mingine kwa kupitia katika tawi lolote la Benki ya CRDB na pia kupitia mitandao ya simu za mkononi
Fara ja kwa Watoto
8 9
kama Tigo (Tigo pesa) na Vodacom (M-pesa) wakati wowote na mahala popote, vile vile kwa UngujaunawezapatahudumahiyokatikaoffisiyaUTTMicrofinanceiliyopoPostaKijangwani;
9.2.9 Ushauri ulipokelewa kuhusiana na utoaji mapema wa makabrasha kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Mfuko ili kutoa fursa kwa Wawekezaji kujiandaa mapema, ambapo ilielezwa kuwa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS itaendelea kuwatumia Wawekezaji wote waliowasilisha anuani zao za barua pepe makabrasha ya Mikutano ya Mwaka ya Mifuko kama ambavyo ilikuwa imefanya kwa mwaka huo na kwamba Taarifa na makabrasha hayo pia yatawekwa mapema katika tovuti ya Kampuni ili kurahisisha upatikanaji wake kwa Wawekezaji;
9.2.10 Kuhusu lawama kwa huduma mbovu katika baadhi ya matawi ya Benki ya CRDB kwa mfano kutokufahamu namba ya Akaunti ya Watoto n.k. Malalamiko yana ukweli, tunaendelea kulifanyia kazi jambo hili. Hata hivyo tatizo hili linatokana na baadhi Matawi kubadili wafanyakazi wake mara kwa mara na wafanyakazi wapya wanakuwa hawajui huduma za wateja wa UTT AMIS zinatolewaje hapo CRDB lakini pia menejiment ya UTT AMIS imekua ikiendelea kutoa elimu kwa wafanyakazi wa CRDB juu ya mifuko ya uwekezaji ya UTT AMIS, vile vile UTT AMIS ingependa kuwakumbusha wateja wake kupiga simu katika kituo chetu cha huduma kwa wateja ili kupata suluhisho la haraka pale wanapokwama kupata huduma kutoka kwa mawakala wetu:.
9.2.11 Kuhusu pendekezo lilitolewa kwa wateja wa UTT AMIS kuhudumiwa na Benki mbili yaani CRDB na Benki ya NMB. UTT AMIS iliona umuhimu wa kupanua huduma kwa wateja wake, ndio maana imeanzisha utaratibu wa wakezaji wake kununua vipande vya mfuko wa watoto na mifuko mingine kwa mitandao ya simu za mkononi kama Tigo (Tigo pesa) na Vodacom (M-pesa) wakati wowote na mahala popote vile vile kwa Unguja unaweza pata huduma hiyo katika offisi ya UTTMicrofinance iliyopo Posta Kijangwani na katikamikoa ya Arusha, Mwanza, Mbeya na Dodoma . Tunatoa ushauri pia kwa wafanyakazi ambao ni wawekezaji ili kupunguza usumbufu wa kwenda Benki wanaweza kumwomba mwajiri wao kukatwa kutoka mishahara yao na mwajiri kutumia Cheque UTT AMIS
9.2.12 Ufafanuzi ulitolewa kwamba mwekezaji aliyenunua vipande mwanzoni na anayenunua sasa thamani hazilingani. Kwa mwekezaji aliyetoa Sh.100,000/- katika mauzo ya awali alinunua kipande kimoja kwa Sh.100/- na sasa vipande hivyo thamani yake itakua imeongezeka. Kwa kuwa thamani ya kipande hupanda kila siku,
mwekezaji anayetoa Sh.100,000/- sasa atanunua kipande kimoja kwa bei ya sasa, hivyo hatapata idadi ya vipande sawa na yule aliye awali;
10.0 KUFUNGA MKUTANO
Kwa kuwa hakukuwa na masuala zaidi ya kujadili, Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS aliwashukuru Wawekezaji wote kwa kuhudhuria katika Mkutano huo. Pia aliwahakikishia ya kuwa mawazo na mapendekezo ya Wawekezaji yaliyotolewa katika Mkutano yatazingatiwa na yale yanayowezekana yatatekelezwa. Mwisho aliwatakia heri ya sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya 2015. Mkutano ulifungwa saa 6.30 Mchana.
.
................................... ...................................
MWENYEKITI KATIBU
....................................
TAREHE
Fara ja kwa Watoto
8 9
KIAMBATISHO “A”
ORODHA YA WAWEKEZAJI WA MFUKO WA WATOTO WALIOHUDHURIA KWENYE MKUTANO MKUU ULIOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA
HOTELI YA BLUE PEARL UBUNGO PLAZA, DAR ES SALAAM TAREHE 22 NOVEMBA 2015 KUANZIA SAA 3.30 ASUBUHI
S/No. JINA LA MWEKEZAJI CHEO1. AMINA HAMADI Mjumbe
2. IBRAHIM HAMADI ‘’
3. GRACE ACHIULA ‘’
4. GLORY ACHIULA ‘’
5. DANO BABILE ‘’
6. MARY BABILE ‘’
7. DAVIS KIDUNDA ‘’
8. HAPPYNESS JOHN ‘’
9. GETRUDA JOHN ‘’
10. GEORGE JOHN ‘’
11. JAMEEL ADAM ‘’
12. ERNAS ADAM ‘’
13. HASHIM NYANGE ‘’
14. MARYGORETH MUNISH ‘’
15. TAITAS LELO ‘’
16. MWANAMVUA ALMASY ‘’
17. MOHAMED SAOKO ‘’
18. LAURIAN CHOKOLA ‘’
19. DAUD VALENTINE ‘’
20. MARY GOMES ‘’
21. SOCIAL ACTION TRUST FUND ‘’
22. ELLY MWAMBENE ‘’
23. ACBARY MUSHI ‘’
24. JESSICA SWAI ‘’
25. FAITH MILLINGA ‘’
26. DAUDI ELISHA ‘’
27 REHEMA R. SINGOYI ‘’
28. ANTHONY M. IZEGELE ‘’
29. JUMA B. MUSSA ‘’
30 BONEFACE LINGWANDA ‘’
31. MARY MKWANGA ‘’
S/No. JINA LA MWEKEZAJI CHEO32. JULIETA BAGUMA ‘’
33. DAVIS M. MABEBA ‘’
34 JACKLINE HENRY ‘’
35 RADHIA MUMBA ‘’
36 EPHRAIM DICKSON ‘’
37 AISHA RASHID ‘’
38 SYSLVESTER SONGALIN ‘’
39 ZAHARA SIMBA ‘’
40 KISICHOFAA KILENGA ‘’
41 ROBINSON SHAYO ‘’
42 ERASTO CHIWANGA ‘’
43 MICHAEL H. ZELLAH ‘’
44 JUMA B. MUSSA ‘’
45 ROSE M. KAWISHE ‘’
46 ANESTUS RUTAKENGWA ‘’
47 EVODIA P. MSAFI ‘’
48 ATHANAS G. CHIWALO ‘’
49 DORIN J. MWANRY ‘’
50 ALCARD MARCO ‘’
51 AMWAA MDOE ‘’
52 FATUMA S. SALUM ‘’
53 FATUMA R. LOWASA ‘’
54 ASHA SEIF MOHAMED ‘’
55 MARY G. LYIMO ‘’
56 FRANK T. MALANGO ‘’
57 TAMASHA J. MTAITA ‘’
58 GUHEN MTAITA ‘’
59 RUKIA ALIABBAS ‘’
60 MWARAMI M. NGASINDA ‘’
61 GODSON MAKANYA ‘’
62 MECKLENE ENGEL ‘’
Fara ja kwa Watoto
10
S/No. JINA LA MWEKEZAJI CHEO63 RODRICK MAFTAH ‘’
64 OKOLEWA MWAKAGENDA ‘’
65 NEEMA L. MAANGA ‘’
66 ELIFURAHA G. MTALO ‘’
67 FLORA K. RUTTA ‘’
68 SOPHIA MGAYA ‘’
69 RAJABU JUMAPILI ‘’
70 ABDULMALIK JUMAPILI ‘’
71 UMULKHERI A. ‘’
72 PETER C. MBILAANGA ‘’
73 PETER WANO ‘’
74 DORCAS MWENDA ‘’
75 DORYIN MWENDA ‘’
76 SUSAN TITO ‘’
77 YASON N TITO ‘’
78 EVA PETER ‘’
S/No. JINA LA MWEKEZAJI CHEO79 LUCY LUCAS ‘’
80 MELVIN PETER ‘’
81 MELVIN PETER ‘’
82 MERY KILUSWA ‘’
83 FREDRICK SANGA ‘’
84 EVETHA MREMA ‘’
85 SALAMA MARIJANI ‘’
86 MKUNDE H. MSHANGA ‘’
87 JAMES A. AMO ‘’
88 ANDREW NAMINGA ‘’
89 BARAACKA PETER ‘’
90 PETER PETER ‘’
91 LIGHTNESS NYAMUNGU ‘’
92 WAIALES EZEKIEL ‘’
93 PASCHAL H. ‘’
94 BERTHA S. SOMI ‘’
11
3 Yatokanayo na Mkutano Uliopita
Fara ja kwa Watoto
12 PB
YATOKANAYO NA MUHTASARI WA MKUTANO WA SITA (6) WA MWAKA WA MFUKO WA WATOTO ULIOFANYIKA
TAREHE 22 NOVEMBA 2015
Katika Mkutano wa sita (6) wa Mfuko wa Watoto uliofanyika tarehe 22 Novemba 2015 katika Ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Blue Pearl iliyopo katika Jengo La Ubungo Plaza Dar es Salaam. Mkutano uliazimia na kuelekeza mambo kadhaa. Ifuatayo ni taarifa ya utekelezaji wa maamuzi hayo:
UAMUZI/MAELEKEZO UTEKELEZAJI
4.0 Yatokanayo na kumbukumbu za mkuta
4.2 Utekelezaji: Mwakilishi alieza kuwa utafiti ulifanyika na kwamba mchakato wa mradi utakaoboresha jinsi ya watanzania wengi kujiunga na kufanya malipo ya vipande kwa njia ya simu ulikuwa umeshaanza na kwamba ulitegemewa kumalizika ndani ya muda mfupi kabla ya tarehe 30 Juni 2016.
UTT AMIS imeendelea kuboresha huduma kwa kutumia Tehama kama ifuatavyo:-
1. Huduma ya kununua vipande kupitia mitandao ya simu. Hadi sasa wawekezaji wanaweza kununua vipande vya mifuko yote ya inayosimamiwa na UTT AMIS kupitia Tigopesa (*150*01#), MPesa (*150*00#), Airtel Money (*150*60#) na TPesa (*150*71#). Tuko mbioni kujiunga na Halotel na Zantel.
2. Pia tumeanza kutoa huduma zetu kupitia njia fupi (short code) *150*82# inayoitwa SimInvest kwa wateja wa Tigo, Vodacom na Airtel. Kwa Halotel na Zantel tunakamilisha uunganishaji. Huduma hii inapatikana kwa simu zote za viganjani (simu Janja na simu za kawaida). Huduma zinazopatikana kupitia short code hii ni: Kufungua akaunti ya uwekezaji, kupata taarifa fupi ya uwekezaji wako, kujua kiasi kilichopo katika akaunti zako, kuangalia thamani ya kipande na kujua kiasi kinachotakiwa katika awamu za uwekezaji kwenye mfuko wa Wekeza Maisha.
3. Katika kuendelea kuboresha huduma, Taasisi imetengeneza program (App) kwa ajili ya wawekezaji wanaotumia Simu Janja. Programu hii iitwayo UTT AMIS inapatikana kwenye Apple Store au Play Store. Mwekezaji anaipata kwa kupakua UTT AMIS kwenye simu yake. Huduma zote zinazopatikana kwenye njia fupi fupi (short code) *150*82# pia zinapatikana katika programu ya UTT AMIS.
4. UTT AMIS pia imeunganisha mfumo wake wa operesheni na mfumo wa Benki ya CRDB. Hivyo, wateja wote wa CRDB wanaotumia Fahari Huduma, Sim Banking, Mfumo wa kibenki katika matawi yote ya Benki ya CRDB wanaweza kununua vipande moja kwa moja na kuweza kupokea ujumbe wa simu kuthibitisha kupokelewa kwa pesa zao na UTT AMIS.
Haya yote tunaamini ni faraja kwa wawekezaji. Mipango ya kujiunga na taasisi nyingine za fedha inaendelea.
Fara ja kwa Watoto
PB 13
TAARIFA FUPI YA MWAKA YA MFUKO WA WATOTO
Fara ja kwa Watoto
14 1514
4 Taarifa ya Mwenyekiti wa Bodi
Fara ja kwa Watoto
14 1515
TAARIFA YA MWENYEKITI
Utangulizi
Ndugu Wawekezaji,
Napenda kuwakaribisha katika Mkutano Mkuu wa Saba (7) wa Mfuko wa Watoto. Nikiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, naomba kutoa shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuniteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTT AMIS. Vilevile, namshukuru Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango, kwa kuwateua Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi. Napenda kuwashukuru Wawekezaji wote wa Mfuko wa Watoto kwa kuendelea kuwa na imani na UTT AMIS hata katika kipindi cha miaka 2016, 2017 na 2018 ambacho Mikutano ya Wawekezaji haikufanyika kutokana na kutokuwepo kwa Bodi ya Wakurugenzi. Ni matarajio yangu kuwa Bodi ya Wakurugenzi mtaendeleza ushirikiano na UTT katika siku zijazo.
Nichukue fursa hii kuipongeza Bodi ya Wakurugenzi iliyomaliza muda wake, chini ya Mwenyekiti Prof. Joseph Kuzilwa, kwa kazi nzuri waliyoifanya kuhakikisha kuwa rasilimali za wawekezaji ziko salama na zinaendelea kukua. Sisi kama Bodi mpya tutaendeleza pale walipoishia ili kuongeza ufanisi wa utendaji wa mifuko na kuhakikisha kuwa mifuko ya uwekezaji wa pamoja inakuwa ni sehemu muhimu ya uchumi wa Nchi.
Ndugu Wawekezaji,
Kwa upande wa menejimenti ya UTT AMIS, napenda kuwajulisha kuwa Dk. Hamis Kibola, ambaye alikuwa Mkurugenzi Mtendaji alistaafu mwezi Juni 2017 na hivyo Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango alimteua Ndugu Simon Migangala kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa UTT AMIS. Kabla ya uteuzi huo, Simon alikuwa Ofisa Uendeshaji Mkuu toka mwaka 2013.
Taarifa ya mfuko
Ndugu Wawekezaji,
Ni matumaini yangu kuwa mmepokea na kuichambua taarifa ya Mfuko kwa kipindi kilichoishia tarehe 30 Juni, 2019 ambayo pia inajumuisha taarifa ya mwaka 2018, 2017 na 2016. Pamoja na changamoto katika soko, ninayo furaha kuwajulisha kuwa utendaji wa Mfuko kwa kipindi cha miaka yote minne umekuwa mzuri. Faida katika Mfuko imekuwa juu ya kigezo linganishi (Performance Benchmark) ikiwa na wastani wa faida ya asilimia Kumi (10%) kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Katika kipindi hiki chote thamani ya Mfuko imeendelea kukua pamoja na idadi ya wawekezaji kuongezeka kutokana na kuongezeka kwa imani na uelewa kuhusu mifuko ya uwekezaji wa pamoja.
Maendeleo ya Uchumi na Masoko ya Fedha
Ndugu Wawekezaji,
Kwa kuzingatia kuwa Mfuko wa Watoto ni sehemu ya mifumo muhimu katika soko, imekuwa ni kawaida kuchambua kwa ujumla maendeleo ya kiuchumi ili kuweza kutathmini utendaji wa Mfuko, kutambua fursa mpya zinazojitokeza na kufanya maamuzi kwa faida ya Mfuko. Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Fedha na Mipango ya mwaka wa fedha 2019/2020, inaonesha kuwa uchumi ulikua kwa asilimia saba nukta moja (7.1%) kwa mwaka 2018/2019 na hivyo kufanya Tanzania kuwa ni kati ya nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi barani Afrika.
Katika kipindi kilichoishia tarehe 30 Juni, 2019, kiwango cha mfumuko wa bei kilikuwa asilimia tatu nukta saba (3.7%) na wakati huo huo kiwango cha riba cha muda mfupi kimeendelea kuwa tarakimu moja kwa kipindi chote cha miaka mitatu iliyopita. Kwa upande wa soko la hisa, kumekuwa na changamoto kubwa kama inavyoonekana katika mabadiliko ya Faharisi ya Hisa ya Tanzania (Tanzania Share Index). Matokeo ya uchambuzi wa faharisi ya hisa kuanzia mwisho wa mwezi Juni 2015, inaonyesha kuwa kwa kipindi chote cha miaka minne, faharisi imeshuka kwa wastani wa asilimia ishirini na tisa nukta tano mbili (29.52%) kutoka elfu nne mia sita themanini na nne nukta sifuri tisa (4,684.09) mpaka elfu tatu mia tatu na moja nukta mbili mbili (3,301.22). Kubadilika kwa Faharisi katika kipindi hiki inamaanisha kuwa, pamoja na kwamba soko la hisa limekuwa likipanda na kushuka, bei hazijaongezeka kufikia kiwango cha bei za hisa kilichofikiwa mwaka 2015. Hali hii na maendeleo ya soko la hisa kwa ujumla wake yamekuwa na athari katika utendaji wa soko kwa ujumla na Mfuko wa Watoto.
Fara ja kwa Watoto
1616
Utendaji wa Mifuko na Maendeleo Mengineyo
Ndugu Wawekezaji,
Ukubwa wa rasilimali za mifuko ni kigezo mojawapo katika kupima utendaji wa kampuni za uwekezaji. Kampuni ya UTT AMIS imekuwa ikizingatia ukubwa wa rasilimali za mifuko inayoisimamia katika kutathmini utendaji wa kampuni pamoja na maendeleo ya biashara yake. Pamoja na changamoto katika soko la hisa thamani ya mifuko chini ya usimamizi wa UTT AMIS imeendelea kukua kuendana na maendeleo ya soko kwa ujumla.
Ili kuwahudumia wawekezaji kwa njia rahisi zaidi, UTT AMIS imeendelea kuwekeza katika mifumo mipya ya tehama ili kuwezesha uwekezaji kwa njia ya simu. Mifumo hii inafanya kazi na mwekezaji anaweza kuitumia kwa kupiga *150*82# na kisha kufuata maelekezo. Maboresho zaidi yanaendelea kufanyika ili kuwawezesha watumiaji wa simu za kisasa (Smart phone) kupata huduma kwa urahisi zaidi. Kwa kuanzia, mifumo ya UTT AMIS imeunganishwa na mifumo ya benki ya CRDB ambayo pia ni msimamizi wa mifuko. Hivyo basi, mwekezaji anaweza kununua vipande moja kwa moja kwa kutumia mfumo wa benki ya CRDB.
Ndugu Wawekezaji,
Kwa kuzingatia maendeleo ya soko, wawekezaji wameendelea kupata faida nzuri ikilinganishwa na kigezo linganishi. Kigezo linganishi ni wastani wa kipato cha faharisi ya hisa Tanzania kwa asilimia 37.5 na kipato cha dhamana ya serikali ya siku 182 kwa asilimia 62.5. Kwa kuzingatia hali ya soko kwa sasa, Mfuko wa Watoto ni chaguo zuri la uwekezaji.
Ndugu Wawekezaji,
Naomba nitumie fursa hii kuwajulisha kuwa katika kipindi cha mwaka ulioishia tarehe 30 Juni 2019, Serikali ilifanya uamuzi wa kuzihamisha shughuli za taasisi ya UTT PID (Kampuni ya UTT iliyokuwa inashughulikia Maendeleo ya Miradi na Miundombinu) kwenda UTT AMIS. Uamuzi huu ulianza kutekelezwa tarehe 1 Mei, 2019. Kwa vile mifuko inaendeshwa kama taasisi zinazojitegemea, uamuzi wa kuzihamishia shughuli za UTT PID kwenda UTT AMIS hauna athari yoyote katika utendaji wa Mfuko wa Watoto na mifuko mingine.
Matarajio kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
Ndugu Wawekezaji,
Baada ya uteuzi wa Bodi ya Wakurugenzi, UTT AMIS imekamilisha utayarishaji wa Mpango Mkakati wa Miaka Mitano kuanzia 2019/2020 hadi 2023/2024. Mpango huu umeainisha vipaumbele vitakavyotekelezwa ndani ya kipindi hicho cha miaka mitano. Kati ya vipaumbele vilivyoainishwa ni pamoja kuweka mifumo ya kisasa ili kuboresha huduma kwa wawekezaji na kudhibiti athari katika uwekezaji. UTT AMIS itaendelea kutoa elimu juu ya faida za uwekezaji na kuwafikia wawekezaji wengi. Uboreshaji wa mifumo utapokuwa umekamilika, wawekezaji watapata huduma nyingi zaidi kupitia simu zao za mkononi.
Shukrani
Ndugu Wawekezaji,
Mwisho, napenda kutoa shukrani zangu kwa wadau wote walioshirikiana na UTT AMIS kwa namna moja ama nyingine katika kipindi chote kufikia tarehe 30 Juni 2019. Aidha, napenda kutoa shukrani za dhati na kipekee kwa Wizara ya Fedha na Mipango, Ofisi ya Msajili wa Hazina, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, Mwangalizi wa Mfuko, Soko la Hisa la Dar es Salaam, Wawekezaji, Wafanyakazi wa UTT AMIS pamoja na wadau wote ambao wameendelea kuiwezesha UTT AMIS kutekeleza majukumu yake kwa kipindi chote. Ni matumaini yangu kuwa ushirikiano huu utaendelea kwa manufaa ya wawekezaji wetu na maendeleo ya soko la mitaji na sekta ya fedha nchini.
Casmir Sumba KyukiMwenyekiti wa Bodi
1717
5 Taarifa ya Mwangalizi wa Mfuko wa Watoto
Fara ja kwa Watoto
18
TAARIFA YA MWANGALIZI WA MFUKO KWA WAWEKEZAJI WA MFUKO WA WATOTO
Tukiwa ni waangalizi wa Mfuko wa Watoto, Jukumu letu ni kusimamia kwamba utendaji wa meneja wa mfuko unaendana/unazingatia waraka wa makubaliano ili kuhakikisha maslahi bora ya wenye vipande. Katika utekelezaji wa jukumu hili, mwangalizi wa mfuko ana majukumu yafuatayo; Uangalizi wa mali za mfuko, kuhakikisha meneja wa mfuko anatumia njia/mbinu sahihi katika kukokotoa mahesabu ya thamani ya mfuko sambamba na mkataba wa makubaliano, na pia kuhakikisha viwango vya uwekezaji vinazingatiwa.
Katika kipindi cha mwaka wa fedha ulioishia 30 Juni 2016, 2017, 2018 na 2019, Benki ya CRDB kama mwangalizi wa mfuko wa Watoto, tumeendeleza uangalizi wa mwenendo wa shughuli za meneja wa mfuko, utekelezaji wake na kuangalia changamoto kwenye uwekezaji.
Kwa kuzingatia hayo, tunapenda kuwathibitishia kwamba shughuli za uwekezaji kwenye mfuko wa Watoto na wajibu wa meneja wa mfuko (UTT AMIS PLC), vimeendeshwa/ vimetekelezwa kufuatana na vipengele vya waraka wa makubaliano. Tukizingatia suala la imani/ uaminifu wa wenye vipande kwenye mfuko, tunathibitisha kwamba maslahi ya wenye vipande ndani ya mfuko wa Watoto yanalindwa na kuzingatiwa ipasavyo, na meneja ameendesha mfuko kulingana na waraka wa makubaliano.
……………………….............Abdulmajid M. Nsekela Benki ya CRDB Plc Tarehe: 20/11/2019
6 Taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za Mfuko
19
Fara ja kwa Watoto
20 21
Fara ja kwa Watoto
20
TAARIFA YA MKAGUZI KUHUSU MUHTASARI WA HESABU ZA MFUKO WA WATOTO (WATOTO FUND)
KPMGJengo la Luminary Simu: +255 22 2600330Ghorofa ya 2, Kitalu Na. 574 Barua Pepe: [email protected] ya Haile Selassie, Msasani Tovuti: www.kpmg.co.tzS. L. P 1160
Maoni
Muhtasari wa hesabu za Mfuko ambao unajumuisha Urari wa hesabu za Mfuko mnamo tarehe 30 Juni 2016, tarehe 30 Juni 2017, tarehe 30 Juni 2018 na tarehe 30 Juni 2019, muhtasari wa Mapato na Matumizi, muhtasari wa Mabadiliko ya Thamani ya Mfuko pamoja na muhtasari wa Mtiririko wa Fedha umetayarishwa kutoka katika taarifa kamili ya ukaguzi ya Mfuko wa Watoto kwa kipindi cha miaka inayoishia tarehe 30 Juni 2016, tarehe 30 Juni 2017, tarehe 30 Juni 2018 na tarehe 30 Juni 2019.
Kwa Maoni yetu, Muhtasari wa Hesabu za Mfuko wa Watoto unaendana na taarifa kamili za hesabu za Mfuko zilizokaguliwa kulingana na vigezo vilivyoelezwa kwenye dokezo namba 1.
Muhtasari wa Taarifa ya Hesabu za Fedha
Muhtasari wa taarifa ya hesabu za fedha haioneshi taarifa zote kwa mujibu wa viwango vya kimataifa vya utoaji wa taarifa za kifedha (International Financial Reporting Standards (FRS)). Muhtasari huu wa hesabu pamoja na hii taarifa yetu siyo mbadala wa taarifa kamili ya hesabu za kifedha iliyokaguliwa. Muhtasari wa hesabu za kifedha pamoja na taarifa kamili ya hesabu zilizokaguliwa haijumuishi matukio au miamala baada ya tarehe za taarifa ya hesabu za fedha zilizokaguliwa.
Taarifa ya Ukaguzi na Hesabu za Fedha zilizokaguliwa
Maoni ya ukaguzi (audit opinion) yasiyokuwa na kasoro juu ya taarifa kamili ya ukaguzi wa hesabu za fedha za Mfuko yalitolewa kwenye taarifa ya tarehe 22 Oktoba 2019 kwa miaka ya fedha iliyoishia tarehe 30 Juni 2016, tarehe 30 Juni 2017, tarehe 30 Juni 2018 na taarifa ya tarehe 25 Novemba 2019 kwa mwaka unaoishia tarehe 30 Juni 2019.
Taarifa kwa miaka ya fedha inayoishia tarehe 30 Juni 2016, tarehe 30 Juni 2017 na tarehe 30 Juni 2018 inajumuisha mambo mengine Muhimu juu ya ukaguzi wa hesabu za mfuko.
Majukumu ya Meneja Kuhusu Muhtasari wa Hesabu za Fedha za Mfuko
Meneja wa Mfuko anahusika na utayarishwaji wa muhtasari wa hesabu za fedha za Mfuko kwa mujibu wa vigezo kama ilivyoainishwa kwenye dokezo namba 1.
Majukumu ya Mkaguzi wa Hesabu za Mfuko
Majukumu yetu kama wakaguzi wa hesabu za Mfuko ni kutoa maoni kama muhtasari wa hesabu za Mfuko unaendana na taarifa kamili ya ukaguzi wa hesabu za fedha na kwa mujibu wa taratibu zetu za ukaguzi, ukaguzi ambao ulifanywa kwa mujibu wa viwango vya kimataifa vya ukaguzi (International Standars on Auditing-ISA) 810 (kama ilivyorekebishwa), “Kazi za kuripoti juu ya Muhtasari wa taarifa za kifedha”
Hili ni toleo lililotafsiriwa la ripoti ya Mkaguzi liyosainiwa katika toleo la Kiingereza.
Fara ja kwa Watoto
20 21
Fara ja kwa Watoto
21
Dokezo Namba I
Dokezo juu ya vigezo vya kutayarisha Muhtasari wa Hesabu
Muhtasari wa taarifa ya hesabu za fedha umetayarishwa kutoka kwenye taarifa kamili ya ukaguzi, iliyotayarishwa kwa mujibu wa viwango vya kimataifa vya utoaji wa taarifa za kifedha (IFRS) mnamo tarehe 30 Juni 2016, 30 Juni 2017, 30 Juni 2018 na 30 Juni 2019.
Taratibu za kutayarisha muhtasari wa hesabu za fedha unaitaka menejimenti kuamua kiwango cha taarifa zitakazojumuishwa katika muhtasari ili kuendana kwa kiwango kikubwa na taarifa kamili ya ukaguzi au kutoa taswira ya muhtasari iliyosawa na taarifa ya hesabu za fedha zilizo kaguliwa
Menejiment imetayarisha hesabu hizi kwa kuzingatia vigezo vifuatavyo:
(a) Muhtasari wa Hesabu unajumuisha hesabu zote za mfuko zilizoko katika taarifa ya hesabu zilizokaguliwa;
(b) Taarifa zilizopo kwenye muhtasari wa hesabu zinashabihiana na taarifa ya hesabu za mfuko zilizokaguliwa na
(c) Jumla kuu, jumla ndogo pamoja na taarifa linganifu zilizopo kwenye hesabu zilizokaguliwa zimeonyeshwa pia katika muhtasari wa hesabu ulioandaliwa
Taarifa ya hesabu za mfuko wa Watoto zilizokaguliwa zinapatikana katika ofisi ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT (UTT AMIS).
22
7 Taarifa ya Hesabu za Mfuko
Fara ja kwa Watoto
23
TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI (Income statement) KWA MIAKA ILIYOISHIA 30 JUNI 2016, 2017, 2018 NA 2019
2019 2018 2017 2016 2015
TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000
Mapato yatokanayo na riba 341,988 415,902 382,578 322,372 236,619
Mapato mengineyo (227,370) 171,742 (9,578) (199,127) 435,563
Jumla ya Mapato 114,618 587,644 373,000 123,245 672,182
Gharama za uendeshaji (76,010) (82,028) (84,912) (80,022) (66,668)
Mapato halisi kabla ya Kodi 38,608 505,616 288,088 43,223 605,514
Kodi (3,820) (24,792) (27,341) (23,897) (17,339)
Mapato halisi baada ya Kodi 34,788 480,824 260,747 19,326 588,175
Ongezeko halisi la thamani ya Mfuko 34,788 480,824 260,747 19,326 588,175
Fara ja kwa Watoto
24 25
URARI WA HESABU ZA MFUKO (BALANCE SHEET) MNAMO TAREHE 30 JUNI 2016, 2017, 2018 NA 2019
2019 2018 2017 2016 2015
TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000
Rasilimali za Mfuko
Fedha Taslim 54,388 409,056 866,519 812,008 613,320
Akaunti za muda katika mabenki 5,981 475,979 625,353 677,618 516,608
Dhamana za Serikali na Hati Fungani za Makampuni 2,167,189 1,414,278 928,253 480,667 373,760
Hisa 937,998 1,181,902 1,112,841 998,438 1,181,887
Rasilimali nyinginezo (other receivable) 57,916 23,671 24,126 17,994 30,550
Jumla ya Rasilimali 3,223,472 3,504,886 3,557,092 2,986,725 2,716,125
Dhima ya Mfuko
Kodi ambayo haijalipwa (1,876 ) (6,076) (6,076 ) (5,712) (6,072)
Dhima (41,254 ) (38,354) (41,131) (35,822 ) (26,281)
Jumla ya Dhima ya Mfuko (43,130) (44,430) (47,207) (41,534) (32,353)
Thamani Halisi ya Mfuko 3,180,342 3,460,456 3,509,885 2,945,191 2,683,772
Inawakilishwa na:
Thamani Halisi ya Mfuko 3,180,342 3,460,456 3,509,885 2,945,191 2,683,772
Idadi ya Vipande 9,500,774 9,932,443 11,661,143 10,585,941 9,726,799
Thamani ya Kipande 334.75 348.40 300.98 278.22 275.92
Thamani ya kipande iliyotangazwa 337.71 332.77 293.84 278.55 279.71
Fara ja kwa Watoto
24 25
TAARIFA YA MABADILIKO YA THAMANI YA MFUKO (STATEMENT OF CHANGES IN NET ASSETS ATTRIBUTABLE TO UNIT HOLDERS) KWA MIAKA ILIYOSHIA 30 JUNI
2016, 2017, 2018 NA 20192019 2018 2017 2016 2015
TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000
Thamani ya mfuko mwanzoni mwa mwaka(Julai 1) 3,460,456 3,509,885 2,945,191 2,683,772 1,848,587
Matokeo ya mabadiliko sheria ya ripoti ya fedha (IFRS 9)
(172 364) - - - -
Mabadiliko/Ongezeko ya thamani ya mfuko 34,788 480,824 260,747 19,326 588,175
3,322,880 3,990,709 3,205,938 2,703,098 2,436,762
Miamala (Transactions) ya wenye vipande kwa mwaka
Mauzo ya vipande (Sales) 287,472 261,348 598,036 351,980 356,969
Ununuzi ya vipande (Repurchase) (430,010) (791,601) (294,089) (109,887) (109,959)
Mabadiliko ya thamani ya mfuko (142,538) (530,253) 303,947 242,093 247,010
Thamani halisi ya Mfuko 3,180,342 3,460,456 3,509,885 2,945,191 2,683,772
Fara ja kwa Watoto
26 27
TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA (CASH FLOW STATEMENT) KWA MIAKA ILIYOISHIA 30 JUNI 2016, 2017, 2018 NA 2019
2019 2018 2017 2016 2015
TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000
FEDHA ITOKANAYO NA SHUGHULI ZA UENDESHAJI
Mapato kabla ya Kodi 38,608 505,616 288,088 43,223 605,514
Imerekebishwa na:
Gawio kwenye hisa (33,825) (63,227) (25,409) (58,045) (50,696)
Faida/(Hasara) itokanayo na mabadiliko ya thamani ya dhamana isiyostahili kugawana
253,861 (142,689) 9,578 199,127 (435,563)
Marekebisho ya gharama ya Kodi (Tax written off) (4,200) - - - -
Faida ya Mauzo ya Hisa (14,734) (22,388) - - -
Faida kabla ya mabadiliko ya Mtaji wa uendeshaji: 239,710 277,312 272,257 184,305 119,255
Mabadiliko ya Mtaji wa uendeshaji
Ongezeko /(Kupungua) kwa dhima ambazo mfuko haujalipwa
(32,040) (3,518) 1,266 (6,784) 4,705
Ongezeko /(Kupungua) kwa Dhima 2,900 (2,777) 5,309 14,570 (6,874)
Fedha iliyopatikana kutoka kwenye shughuli za uendeshaji
210,570 271,017 278,832 192,092 117,086
Kodi iliyolipwa hadi sasa (3,820) (24,792) (26,977) (24,257) (16,090)
Fedha halisi itokanayo na shughuli za uendeshaji 206,750 246,225 251,855 167,835 100,996
FEDHA KATIKA SHUGHULI ZA UWEKEZAJI ULIOFANYWA NA MFUKO
Mabadiliko yatokanayo na:
Uwekezaji katika Akaunti za muda kwenye mabenki 469,998 149,374 52,265 (161,010) (260,835)
Uwekezaji katika Dhamana za serikali (910,541) (390,010) (457,164) (306,034) 409,728
Malipo ya gawio 31,620 67,201 18,011 72,355 66,214
Mauzo/Ununuzi wa Hisa (9,957) - (114,403) 183,449 (436,535)
Fedha halisi iliyotumika katika shughuli za Uwekezaji (418,880) (173,435) (501,291) (211,240) (221,428)
AMANA YA MFUKO (FINANCING ACTIVITIES)
Mauzo ya Vipande (Sales of Units) 287,472 261,348 598,036 351,980 356,969
Ununuzi (Repurchase) wa Vipande (430,010) (791,601) (294,089) (109,887) (109,959)
Fedha/Amana halisi toka kwa wenye vipande (142,538) (530,253) 303,947 242,093 247,010
Fara ja kwa Watoto
26 27
TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA (CASH FLOW STATEMENT) KWA MIAKA ILIYOISHIA 30 JUNI 2016, 2017, 2018 NA 2019
2019 2018 2017 2016 2015
TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000 TZS’000
Ongezeko halisi la Fedha (354,668) (457,463) 54,511 198,688 126,578
Salio la fedha mwanzoni mwa Mwaka 409,056 866,519 812,008 613,320 486,742
Salio la fedha mwishoni mwa Mwaka 54,388 409,056 866,519 812,008 613,320
.....................................Mkurugenzi
Tarehe: Novemba, 2019
.....................................Mkurugenzi
Tarehe: Novemba, 2019
28
8 Taarifa ya Meneja kuhusu Uwekezaji
Fara ja kwa Watoto
29
Taarifa ya Meneja Kuhusu Uwekezaji
KUANZISHWAOKTOBA 2008
30 JUNI 2019
THAMANI YA KIPANDENAV SH 337.7066
UKUBWA WA MFUKO
SH 3.2 BILIONI
FAIDA YA MWAKA
4.94%
Fara ja kwa Watoto
UTT AMIS tunatambua umuhimu wa mtoto kwa maendeleo ya taifa katika siku zijazo. Kwa sababu hii, Mfuko wa Watoto (Watoto Fund) ulizinduliwa. Mfuko wa watoto ni suluhisho la kifedha ambalo linalenga katika kukuza mtaji na faida ya muda mrefu kwa ajili ya maendeleo ya watoto wetu wapendwa. Mfuko huu ni wa wazi wenye lengo la kukuza mtaji.
Watoto wote wenye umri wa miaka 0 hadi 18 wanaweza kujiunga na mpango huu. Kiasi cha awali kinachohitajika kwa uwekezaji ni shilingi 10,000/=. Uwekezaji wa ziada ni kuanzia shilingi 5,000/= na kuendelea ambao unaweza kufanywa kadiri ya mwekezaji awezavyo.
Ukubwa wa mfuko na thamani ya kipande
Ukubwa wa Mfuko umeongezeka kwa shilingi bilioni 0.53, kutoka shilingi bilioni 2.67 mnamo 30 Juni, 2015 hadi shililingi bilioni 3.2 mnamo 30 Juni, 2019. Ukuaji huu ni sawa na ongezeko la asilimia 19.85 la ukubwa wa mfuko. Thamani ya kipande (NAV) iliongezeka hadi kufikia shilingi 337.70 ikionyesha ukuaji wa asilimia 20.73 kwa kipindi cha miaka minne iliyopita 2015/16 hadi 2018/19..
Chati namba I hapo chini inaonyesha ukuaji wa mfuko kutoka Mwanzo hadi Juni, 2019.
Chati I: Ukuaji wa mfuko na thamani ya kipande kwa mfuko wa Watoto hadi 30 Juni, 2019
Taarifa ya Meneja Kuhusu Uwekezaji
UTT AMIS tunatambua umuhimu wa mtoto kwa maendeleo ya taifa katika siku zijazo. Kwa sababu hii, Mfuko wa Watoto (Watoto Fund) ulizinduliwa. Mfuko wa watoto ni suluhisho la kifedha ambalo linalenga katika kukuza mtaji na faida ya muda mrefu kwa ajili ya maendeleo ya watoto wetu wapendwa. Mfuko huu ni wa wazi wenye lengo la kukuza mtaji.
Watoto wote wenye umri wa miaka 0 hadi 18 wanaweza kujiunga na mpango huu. Kiasi cha awali kinachohitajika kwa uwekezaji ni shilingi 10,000/=. Uwekezaji wa ziada ni kuanzia shilingi 5,000/= na kuendelea ambao unaweza kufanywa kadiri ya mwekezaji awezavyo. Ukubwa wa mfuko na thamani ya kipande Ukubwa wa Mfuko umeongezeka kwa shilingi bilioni 0.53, kutoka shilingi bilioni 2.67 mnamo 30 Juni, 2015 hadi shililingi bilioni 3.2 mnamo 30 Juni, 2019. Ukuaji huu ni sawa na ongezeko la asilimia 19.85 la ukubwa wa mfuko. Thamani ya kipande (NAV) iliongezeka hadi kufikia shilingi 337.70 ikionyesha ukuaji wa asilimia 20.73 kwa kipindi cha miaka minne iliyopita 2015/16 hadi 2018/19.. Chati namba I hapo chini inaonyesha ukuaji wa mfuko kutoka Mwanzo hadi Juni, 2019. Chati I: Ukuaji wa mfuko na thamani ya kipande kwa mfuko wa Watoto hadi 30 Juni, 2019
KUANZISHWA OKTOBA
2008
30 JUNI 2019
THAMANI YA KIPANDENAV
SH 337.7066
UKUBWA WA MFUKO
SH 3.2 BILIONI
FAIDA YA MWAKA
4.94%
Mgawanyo wa Uwekezaji:
Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2018/19, UTT-AMIS PLC kama meneja wa Mfuko alitumia uzoefu na weledi katika kufikia mgawanyo anuai wa rasilimali zilizowekezwa kwenye mfuko wenye kuleta tija huku ikizingatia sera na miongozo mbalimbali ya uwekezaji katika mfuko wa Watoto.
Mnamo 30 Juni 2019 mgawanyo anuai wa rasilimali za mfuko ilikuwa kama inavyoonekana kwenye chati namba II hapo chini:-
Fara ja kwa Watoto
30 31
Mgawanyo wa Uwekezaji: Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2018/19, UTT-AMIS PLC kama meneja wa Mfuko alitumia uzoefu na weledi katika kufikia mgawanyo anuai wa rasilimali zilizowekezwa kwenye mfuko wenye kuleta tija huku ikizingatia sera na miongozo mbalimbali ya uwekezaji katika mfuko wa Watoto. Mnamo 30 Juni 2019 mgawanyo anuai wa rasilimali za mfuko ilikuwa kama inavyoonekana kwenye chati namba II hapo chini:- Chati II: Mgawanyo wa uwekezaji katika mfuko wa Watoto tarehe 30 Juni, 2019
HISA30.45%
HATI FUNGANI ZA SERIKARI
67.99%
AMANA ZA MABENKI ZA MUDA MFUPI
1.56%
HISA
HATI FUNGANI ZA SERIKARI
AMANA ZA MABENKI ZA MUDA MFUPI
Chati namba II hapo juu inaonyesha mgawanyo wa uwekezaji katika mfuko wa watoto. dhamana za serikali za muda mrefu ilichukua sehemu kubwa ya asilimia 67.99 ikifuatiwa na hisa, asilimia 30.45 na amana za mabenki za muda mfupi ilikuwa asilimia 1.56. Amana za muda mfupi zimewekezwa kwa lengo la kukidhi gharama za mfuko ikiwemo kulipa wawekezaji pindi wanapouza vipande vyao. Faida Wastani wa faida kwa miaka minne iliyopita kutoka Julai, 2015 hadi Juni, 2019 ilikuwa 4.94% .Kwa mwaka ulioishia 30 Juni 2019, mwenendo katika soko la hisa haufanya mzuri hivyo kusababisha faida ya mfuko wa Watoto kushuka mpaka asilimia 1.48 tofauti na asilimia 13.22 iliyorekodiwa mnamo 30 Juni, 2018. Maelezo juu ya faida kwa muda wa miaka nne ni kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini;
Chati II: Mgawanyo wa uwekezaji katika mfuko wa Watoto tarehe 30 Juni, 2019
Chati namba II hapo juu inaonyesha mgawanyo wa uwekezaji katika mfuko wa watoto. dhamana za serikali za muda mrefu ilichukua sehemu kubwa ya asilimia 67.99 ikifuatiwa na hisa, asilimia 30.45 na amana za mabenki za muda mfupi ilikuwa asilimia 1.56.
Amana za muda mfupi zimewekezwa kwa lengo la kukidhi gharama za mfuko ikiwemo kulipa wawekezaji pindi wanapouza vipande vyao.
Faida
Wastani wa faida kwa miaka minne iliyopita kutoka Julai, 2015 hadi Juni, 2019 ilikuwa 4.94% .Kwa mwaka ulioishia 30 Juni 2019, mwenendo katika soko la hisa haufanya mzuri hivyo kusababisha faida ya mfuko wa Watoto kushuka mpaka asilimia 1.48 tofauti na asilimia 13.22 iliyorekodiwa mnamo 30 Juni, 2018. Maelezo juu ya faida kwa muda wa miaka nne ni kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini;
Jedwali I: Faida ya mfuko wa Watoto kwa miaka minne hadi 30 Juni, 2019
Na. Mwaka wa Fedha Ukubwa wa mfuko Shilingi Bilioni Utendaji katika Asilimia
Faida Kigezo cha ufanisi
1 2018/19 3.20 1.48 -3.2
2 2017/18 3.31 13.22 4.5
3 2016/17 3.43 5.47 4.6
4 2015/16 2.95 -0.41 6.41
Kumb: Kigezo cha ufanisi-Mjumuiko wa utendaji wa hisa na hati fungani za muda mfupi
Ili kupima mafanikio ya mfuko inabidi kulinganisha faida ya mfuko wa Watoto na viwango linganifu vya riba vinavyotolewa na soko kwenye amana za mabenki kama zilivyoainishwa kwenye jedwali na II hapo chini:
Jedwali II: Viwango vya riba katika amana za mabenki kwa kipindi cha robo mwaka
Kipindi kinachoishia robo mwaka Juni-18 Sept-18 Des-18 Mar-19 Juni-19
Riba za amana za mabenki [%] 2.09 2.66 2.64 2.59 2.09
Jedwali III: Viwango vya riba katika amana za mabenki kwa kipindi cha mwaka
Kipindi kinachoishia mwaka Juni-15 Juni-16 Juni-17 Juni-18 Juni-19
Riba katika amana za mabenki [%] 3.52 3.37 3.17 2.09 2.44
** Chanzo; Benki Kuu ya Tanzania
Fara ja kwa Watoto
30 31
Mambo mengine muhimu ya kuzingatia wakati wa kulinganisha faida za uwekezaji katika Mfuko wa Watoto na amana katika mabenki;
• Viwango vya riba vilivyoonyeshwa hapo juu ni kabla ya kutoa kodi ya zuio (withholding tax) ya asilimia 10 wakati mapato ya mfuko wa Watoto ni baada ya kutoa kodi ya zuio ya asilimia 10.
• Jambo lingine la muhimu la kuzingatia ni kwamba mfuko wa Watoto unaruhusu wanachama wake kuuza vipande vyao wakati wowote hivyo kumpa fursa mwekezaji kupata fedha pindi anapozihitaji na kwamba hakuna kiwango cha chini cha uwekezaji kinachoruhusu kupata faida.
• Viwango vya faida ya mfuko vinatolewa sawa kwa wawekezaji wote (wawekezaji wa kipato kidogo, wa kipato cha kati na wale wenye kipato kikubwa).
Kuwekeza kwenye mfuko wa Watoto kuna faida zaidi ya kuwa na akaunti ya amana kwa sababu inakuongezea kipato kikubwa kutokana na viwango bora vinavyotolewa na mfuko zaidi ya viwango vya amana vilivyopo kwenyo soko la fedha.
Mwenendo wa Uchumi wa Tanzania:
Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika ambazo uchumi wake unakua kwa kasi na ni stahimilivu. Kwa mujibu wa ofisi ya Taifa ya takwimu nchini, mwaka 2016 uchumi ulikua kwa asilimia 6.9, mwaka 2017 kwa asilimia 6.8 na mwaka 2018 kwa asilimia 7.0.
Hata hivyo, hali ya ukuaji wa uchumi kwa mwaka 2019 kwa mujibu wa hotuba ya bajeti ya mheshimiwa waziri wa fedha na mipango kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ni asilimia 7.1 huku vichagizo vikubwa vikiwa ni ujenzi kwa asilimia 13.1, usafirishaji asilimia 11.1 na shughuli za madini kwa asilimia 10.0.
Aidha, ukuaji katika shughuli za ujenzi unachangiwa na ujenzi wa miradi ya reli ya kisasa (SGR), barabara pamoja na madaraja. Kwa upande mwingine kukua kwa shughuli za uchimbaji ikilinganishwa na robo ya kwanza ya mwaka 2018 kwa kiasi kikubwa imechangiwa na ongezeko la uzalishaji wa madini ya almasi na makaa ya mawe.
Jedwali IV: Mwenendo wa ukuaji Uchumi wa Tanzania.
Mwaka 2015 2016 2017 2018 2019
Pato halisi la Taifa [%] 6.20 6.90 6.80 7.0 7.10
Chanzo: Benki kuu ya Tanzania
Mfumuko wa Bei
Hali ya mfumuko wa bei nchini mpaka tarehe 30 Juni 2019 ilifikia asilimia 3.70 kutoka asilimia 3.40 kwa kipindi cha mwezi Juni 2018.
Jedwali V: Hali ya Mfumuko wa Bei.
Mwaka Juni 15 Juni 16 Juni 17 Juni 18 Juni 19 2017Mfumuko wa Bei [%] 6.10 5.50 5.40 3.40 3.70
Chanzo: Ofisi ya Taifa ya Takwimu
Fara ja kwa Watoto
32 33
Sekta ya Mabenki:
Kwa kipindi cha mwaka kilichoishia Juni 2019 hali na mwenendo wa ukwasi katika mabenki nchini iliendelea kuwa stahimilivu kutokana na sera madhubuti za kifedha za benki kuu.
Rasilimali za mabenki ziliongezeka kwa shilingi trilioni 0.25 hadi kufikia shillingi 28.83 trilioni kutoka shilingi trilioni 28.58 mwezi Juni 2018. Ongezeko la rasilimali katika mabenki limechangiwa zaidi na ongezeko la mikopo kwa sekta binafsi na uwekezaji katika dhamana za serikari za muda mrefu.
Ubora wa rasilimali ambao unapimwa kwa uwiano wa mikopo chechefu na rasilimali kwa ujumla umeimarika kutoka asilimia 11.60 hadi asilimia 11.10 mwaka uliopita.
Katika kipindi hichohicho hali ya hatari kwa rasilimali za mabenki imezidi kupungua kutokana na benki kuu kuendelea kuimarisha viwango vya usimamizi wa mikopo. Hivyo basi kutokana na kuimarishwa kwa viwango na usimamizi wa mikopo nchini kulipelekea mabenki ya biashara kubaki na ziada ya rasilimali ambazo ziliongeza uwekezaji katika dhamana za serikali.
Matumizi ya teknolojia kwenye shughuli za kibenki zimerahisisha na kuboresha zaidi mifumo ya utendaji kazi nchini na kumeongeza imani kwa umma. Huduma na mifumo ya kibenki imeendelea kurahisishwa na uwepo wa mawakala pamoja na muunganiko wa simu za viganjani na mifumo ya kibenki.
Dhamana za Serikali:
Kwa kipindi cha mwaka mmoja ulioishia 30 Juni 2019, Benki Kuu ya Tanzania kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano ilipunguza kiasi cha dhamana za serikali za muda mfupi mnadani ikilinganishwa na mwaka ulioishia 30 Juni 2018 kwa shilingi bilioni 681.53 kutoka shilingi bilioni 4,348.30 hadi shilingi bilioni 3,666.77 Juni 2019. Uhitaji wa dhamana za serikali za muda mfupi ulipungua kutoka shilingi bilioni 6,621.19 mwaka 2018 hadi kufikia shilingi bilioni 4,427.05 mwaka 2019. Riba katika dhamana za serikali za muda mfupi iliongezeka kwa asilimia 1.90 kutoka faida ya asilimia 6.69 Juni 2018 hadi asilimia 8.59 Juni 2019.
Kiasi cha dhamana za serikali za muda mrefu kwenye soko la awali mwezi Juni 2019 ni shilingi bilioni 2,341.73 ikilinganishwa na shilingi bilioni 2,527.70 iliyoorodheshwa Juni 2018. Kiwango cha ushiriki kwenye minada hiyo kilipungua hadi shilingi bilioni 1,507.84 ikilinganishwa na shilingi bilioni 3,244.18 Juni 2018. Aidha kiwango kilichokubaliwa na Benki Kuu ya Tanzania kilipungua kwa shilingi bilioni 1,652.72 kutoka shilingi bilioni 2,585.43 mwaka 2018 hadi shilingi bilioni 932.71 mwaka 2019.
Mnamo Septemba 2018 kwa mara ya kwanza Serikali ya Tanzania ilizindua dhamana ya serikali ya miaka 20 ambayo ilifanikiwa kuvuka lengo la kiasi kilichohitajika kwa shilingi bilioni 4.90 iliyouzwa kwa wastani wa riba ya asilimia 17.69.
Viwango vya Riba:
Riba katika dhamana za serikali za muda mfupi ziliongezeka kutoka wastani wa asilimia 6.69 mwezi Juni 2018 hadi asilimia 8.59 Juni 2019. Wastani wa riba za Amana za Mabenki ilifika asilimia 7.43 ikilinganishwa na asilimia 8.13 Juni 2018.
Riba ya siku moja baina ya mabenki (interbank money market) kwenye soko la fedha zilifika kiasi cha shilingi bilioni 8.00 mwezi Juni 2019 kwa wastani wa riba ya asilimia 5.75 ikilinganishwa na shilingi bilioni 59 kwa riba ya wastani wa asilimia 1.88 mwaka 2018.
Viwango vya riba jumuishi za mikopo katika mabenki ya biashara zilishuka kwa wastani wa asilimia 1.18 hadi kufikia asilimia 16.43 mnamo Juni 2019. Punguzo la riba za mikopo lilitokana na kuboreshwa kwa viwango vya rasilimali za benki pamoja na taratibu za upatikanaji wa mikopo.
Fara ja kwa Watoto
32 33
Hifadhi ya akiba ya kisheria ya benki kuu kwa benki za biashara pamoja na kiwango cha punguzo la riba imepunguzwa kwa lengo la kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi nchini. Aidha, hifadhi ya akiba ya kisheria ilipungua hadi asilimia 8.00 kutoka asilimia 10.00 Juni 2018. Mnamo Agosti 2018 punguzo la riba ya mabenki kukopa Benki kuu ilipungua hadi kufikia asilimia 7.00 kutoka asilimia 9.00.
Mabadiliko ya riba katika soko la fedha na mitaji huathiri moja kwa moja thamani ya mifuko ya uwekezaji wa pamoja na uchumi kiujumla. Vivyo hivyo kuongezeka kwa riba sokoni hupelekea kuongezeka kwa thamani ya mifuko pindi uwekezaji mpya unapofanyika.
Viwango vya Kubadilisha Fedha za Kigeni:
Katika kipindi cha Juni 2018 hadi Juni 2019, viwango vya kubadilisha fedha kati ya Shilingi ya kitanzania na fedha za kigeni vimeendelea kuwa stahimilivu. Thamani ya Shilingi kwa Dola moja ya kimarekani ilikuwa imara na ya kuridhisha, ingawa ilipungua kwa takribani shilingi 23.16 na kufikia Shilingi za kitanzania 2,300.90 mwezi Juni 2019.
Thamani ya shilingi iliimarika dhidi ya paundi ya Uingereza kwa shilingi 72.14 na sarafu ya Ulaya (Euro) kwa shilingi 26.97. Pia kwa kipindi hichohicho, thamani ya shilingi kwa fedha ya Japani ilidorora kwa senti 67.
Ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, shilingi ya Tanzania iliongezeka thamani dhidi ya shilingi ya Kenya kwa senti 5 na faranga ya Burundi kwa senti 41. Vilevile mdololo dhidi ya shilingi ya Uganda na faranga ya Rwanda kwa shilingi ya Tanzania ni asilimia 5.95 na asilimia 16.04 mtawalia.
Kuanzishwa kwa sheria mpya katika soko la fedha za kigeni ya 2018/19 kulipelekea kufutwa kwa sheria ya zamani ya mwaka 2015. Mabadiliko hayo yamefanyika ili kuondoa ubadilishaji fedha holela na kuboresha soko la fedha za kigeni nchini.
Uimara wa viwango vya kubadilisha fedha ni muhimu kwa mifuko ya uwekezaji wa pamoja na serikali kwa ujumla inasaidia kutunza thamani ya rasilimali ambazo thamani yake ipo katika shilingi za kitanzania na kuvutia wawekezaji kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Soko la Hisa na Mitaji:
Hali ya soko la hisa la Dar es Salaam kupitia viashiria vyake kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2019 imeshuka ikilinganishwa na kipindi kilichoishia Juni 2018.
Kwa mwaka ulioishia 30 Juni 2019, ukubwa wa mtaji wa soko la hisa la Dar es Salaam ulifikia thamani ya shilingi trilioni 18.64 kutoka shilingi trilioni 22.25 mwaka ulioisha 30 Juni 2018 sawa na anguko la shilingi trilioni 3.61 ambayo ni asilimia 16.22..
Viashiria vingine vilivyoshuka katika kipindi kilichoishia Juni 2019 ni pamoja na mauzo ya hisa kwa asilimia 22.62. Aidha, kiashiria cha bei za hisa za kampuni za ndani na nje ya nchi (DSEI) imeshuka kwa asilimia 17.05 na kwa kampuni za ndani (TSI) ilishuka kwa asilimia 21.10.
Mtaji wa soko ulishuka kwa shilingi trilioni 4.55 jambo ambalo lilisababishwa na kushuka kwa bei za hisa katika soko la hisa la Dar Salaam moja kwa moja hali hiyo imeakisi mdororo wa shughuli za mauzo ya hisa sokoni.
Faida katika uwekezaji kwenye mapato ya yasiyobadilika imeendelea kuwavutia wawekezaji wengi nchini ikilinganishwa na soko la hisa nchini. Mauzo ya Hati fungani za serikari kupitia soko la pili mnamo tarehe 30 Juni 2019 ni shilingi bilioni 0.11 ikilinganishwa na shilingi bilioni 16.64 mnamo tarehe 30 Juni 2018.
Kwa mwaka ulioishia Juni 2019 hapakuwa na kampuni iliyoorodheshwa katika soko la hisa la Dar es Salaam ikilinganishwa na kipindi kilichopita ambapo kampuni mbili za TCCIA Investment Plc na National Investment Company Ltd zilizoorodheshwa.
Fara ja kwa Watoto
34 PB
Jumla ya shilingi bilioni 9 na shilingi bilioni 83 ni fedha zilizopatikana kupitia mauzo ya Hati fungani kwa kampuni binafsi ya Tanzania Mortgage Refinance Company (TMRC) na benki ya NMB mtawalia.
Mauzo ya Hati fungani ya benki ya NMB yalizidi lengo kwa asilimia 333 na asilimia 16 kwa kampuni ya TMRC.
UTT AMIS inapenda kuwahakikishia wawekezaji wake kuwa itaendelea kubuni na kuvumbua fursa stahiki za uwekezaji kadiri inavyojitokeza katika soko ili kuongeza mapato na faida. Lengo letu ni kuvuka matarajio ya wawekezaji kwa ajili ya maendeleo yao na taifa kwa ujumla.
Mwisho ninawatakia nyote msimu wa sikukuu uliojaa furaha tele na heri ya mwaka mpya wa 2020
Wekeza Uwezeshwe!
9 Jarida la Habari
35
36
Jarida la Habari la UTT AMIS [Hadi tarehe 30 Septemba, 2019]
36
37
1.0 Maelezo Mafupi juu ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS • Hadikufikiatarehe30Septemba2019,kampuniyauwekezajiyaUTTAMISinajumlayamifukoyauwekezaji
wapamojasita(6)ijulikanayokama;MfukowaUmoja,MfukowaWekezaMaisha,MfukowaWatoto,MfukowaKujikimu,MfukowaUkwasinaMfukowaHatiFungani.
• Mwaka2017KampuniyaUTTAMISilianzishahudumayausimamiziwamalikwamakampuninawatubinafsiinayoitwaUTTWEALTHMANAGEMENTyenyejumlayawateja55wenyeuwekezajiwenyethamaniyazaidiyashilingibilioni13.
• UTTAMISInasimamiarasilimalizenyejumlayathamaniyazaidiyashilingiBilioni307.• Wawekezajizaidiya146,589.• Mifukohutoafaidashindanikatikasoko.
2.0 Taarifa za ujumla za Mifuko iliyoanzishwa na kusimamiwa na kampuni ya UTT AMIS
NA JINA LA MFUKO MAELEZO2.1 Mfuko wa Umoja Mfukohuuulianzishwatarehe16Mei,2005.Mfukoumelengakatikakutimizamahitaji
tofautiwaliyonayowawekezaji.Baadhiyasifazamfukohuunikamazifuatavyo;
• Vipandevinauzwakwathamanihalisi[hakunagharamazakujiunga]• Kiwangochachinichakujiunganivipande10tu• Gharamayakujiondoainatozwaasilimiamoja(1)yathamanihalisiyakipande.• Urahisiwakujiunganakutoka–manunuzinamauzohufanyikakilasikuyakazi• Mauzoyasehemuyavipandeyanaruhusiwa
Chati 0I; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
2
Jedwali 01; Faida kwa kipindi hadi tarehe 30 Septemba 2019
Faida [%] Hadi Septemba 2019
Tangu Kuanzishwa [Mei,2005] Miaka 5 Miaka 4 Miaka 3 Miaka 2 Mwaka 1
13.38% 5.71% 6.12% 7.17% 6.86% 3.04%
Chati 0I; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
108
62 58 62 74 84 86 97115
208 218 218 207224 217
- 100 200 300 400 500 600 700
0
50
100
150
200
250
Nov-
05
Sep-
06
Sep-
07
Sep-
08
Sep-
09
Sep-
10
Sep-
11
Sep-
12
Sep-
13
Sep-
14
Sep-
15
Sep-
16
Sep-
17
Sep-
18
Sep-
19
Tham
ani y
a Ki
pand
e
Ukub
wa w
a M
fuko,
Shil
ingi B
n
Muda
Ukubwa wa Mfuko, Shilingi Bilion i Thamani ya Kipande
2.2
Mfuko wa
Wekeza
Maisha
Mfuko huu ulianzishwa tarehe 16 Mei, 2007. Mfuko unamwezesha mwekezaji kupata faida pacha, yaani
mapato mazuri pamoja na mafao ya bima.
Sifa za mfuko;
• Taasisi na watu binafsi wenye umri kati ya miaka 18 na 55 ndio wanaoruhusiwa kujiunga
• Mfuko unatoa fursa za aina mbili za mpango wa kuchangia\kuwekeza: (a) Kuchangia kwa awamu
na (b) Kuchangia kwa mkupuo mmoja
• Vipande vinauzwa kwa thamani halisi ya wakati huo [hakuna gharama za kujiunga]
• Kujiunga ni shilingi 8,340/-‐ tu kwa mwezi [inatumika kama mpango wa kuchangia ni shilingi
Milioni Moja]
• Mafao ya bima yanayopatikana ni:-‐ Bima ya maisha,Bima ya ulemavu wa kudumu na Bima ya ajali
• Mfuko unampa fursa mwekezaji kuwekeza kwa mpangilio maalum, mathalani anaweza kuchagua
kuchangia kwa mwezi, mara mbili kwa mwaka au mara moja kwa mwaka
37
38
NA JINA LA MFUKO MAELEZO2.2 Mfuko wa Wekeza Maisha Mfukohuuulianzishwatarehe16Mei,2007.Mfukounamwezeshamwekezajikupata
faidapacha,yaanimapatomazuripamojanamafaoyabima.
Sifa za mfuko;
• Taasisinawatubinafsiwenyeumri katiyamiaka18na55ndiowanaoruhusiwakujiunga
• Mfukounatoafursazaainambilizampangowakuchangia\kuwekeza:(a)Kuchangiakwaawamuna(b)Kuchangiakwamkupuommoja
• Vipandevinauzwakwathamanihalisiyawakatihuo[hakunagharamazakujiunga]• Kujiunganishilingi8,340/-tukwamwezi[inatumikakamampangowakuchangiani
shilingiMilioniMoja]• Mafaoyabimayanayopatikanani:-Bimayamaisha,Bimayaulemavuwakudumu
naBimayaajali• Mfuko unampa fursa mwekezaji kuwekeza kwa mpangilio maalum, mathalani
anawezakuchaguakuchangiakwamwezi,marambilikwamwakaaumaramojakwamwaka
Chati 02 ; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
3
Jedwali 02; Faida kwa kipindi hadi tarehe 30 Septemba 2019
Faida [%] Hadi Septemba 2019
Tangu Kuanzishwa [Mei,2007] Miaka 5 Miaka 4 Miaka 3 Miaka 2 Mwaka 1
12.40% 7.88% 8.14% 13.77% 11.91% 12.93%
Chati 02 ; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
0.550.91
1.28 1.481.98 2.08 2.37
3.37 3.44 3.67
1.751.22 1.16
0
100200300
400
500
0.0
1.0
2.0
3.0
4.0
Dis
07
Sep-
08
Sep-
09
Sep-
10
Sep-
11
Sep-
12
Sep-
13
Sep-
14
Sep-
15
Sep-
16
Sep-
17
Sep-
18
Sep-
19
Tham
ani y
a Ki
pand
e
Ukub
wa w
a M
fuko,
Shil
ingi B
n
Muda
Ukubwa wa Mfuko, Shil ingi Bilioni Thamani ya Kipande
2.3
Mfuko wa
Watoto
Mfuko huu ulianzishwa tarehe 1 Oktoba 2008. Mfuko unalenga kuwasaidia watoto katika maendeleo
yao hapa nchini.
Sifa za Mfuko;
• Uwekezaji ni kwa ajili ya mtoto mwenye umri chini ya miaka 18.
• Kiwango cha chini cha uwekezaji kisichopungua shilingi 10,000/= na unaruhusiwa kuendelea
kuwekeza kidogo kidogo kwa kiwango kisichopungua shilingi 5,000/=
• Vipande vinauzwa kwa thamani halisi ya wakati huo. [ hakuna gharama za kujiunga ]
• Mfuko unatoa Mpango wa kukuza mtaji.
• Mwekezaji anaruhusiwa kuuzaa vipande vyake pindi mtoto anapofikisha umri wa miaka 12.
38
39
NA JINA LA MFUKO MAELEZO
2.3 Mfuko wa Watoto Mfukohuuulianzishwa tarehe1Oktoba2008.Mfukounalenga kuwasaidiawatotokatikamaendeleoyaohapanchini.
Sifa za Mfuko;• Uwekezajinikwaajiliyamtotomwenyeumrichiniyamiaka18.• Kiwangochachinichauwekezajikisichopunguashilingi10,000/=naunaruhusiwa
kuendeleakuwekezakidogokidogokwakiwangokisichopunguashilingi5,000/=• Vipandevinauzwakwathamanihalisiyawakatihuo.[hakunagharamazakujiunga]• MfukounatoaMpangowakukuzamtaji.• Mwekezajianaruhusiwakuuzaavipandevyakepindimtotoanapofikishaumriwa
miaka12.
Chati 03; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
4
Jedwali 03; Faida kwa kipindi hadi tarehe 30 Septemba 2019
Faida [%] Hadi Septemba 2019
Tangu Kuanzishwa [Okt,2008] Miaka 5 Miaka 4 Miaka 3 Miaka 2 Mwaka 1
12.18% 5.51% 5.21% 3.20% 8.13% 5.49%
Chati 03; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
0.72 0.79 0.710.97 1.10 1.39
2.392.73
2.993.48 3.29 3.22
-
100
200
300
400
0.0
1.0
2.0
3.0
4.0
Nov-
08
Sep-
09
Sep-
10
Sep-
11
Sep-
12
Sep-
13
Sep-
14
Sep-
15
Sep-
16
Sep-
17
Sep-
18
Sep-
19
Tham
ani y
a Kipa
nde
Ukub
wa w
a M
fuko,
Shil
ingi B
n
Muda
Ukubwa wa Mfuko, Shil ingi Bilioni Thamani ya Kipande
2.4
Mfuko wa
Jikimu
Mfuko huu ulianzishwa tarehe 3 Novemba 2008. Lengo la mfuko ni kukidhi mahitaji ya wawekezaji
wanaohitaji uhakika wa mapato ya mara kwa mara kama vile wastaafu.
Sifa za Mfuko:
• Mipango ya uwekezaji : (a) Mpango wa gawio wa robo mwaka [Kiwango cha chini cha uwekezaji
ni Shilingi 2 Milioni], (b) Mpango wa gawio wa mwaka [Kiwango cha chini cha uwekezaji ni
Shilingi 1 Milioni] na (c) Mpango wa mwaka wa kukua [Shilingi. 5,000/-‐]
• Vipande vinauzwa kwa thamani halisi ya wakati huo [ hakuna gharama za kujiunga ]
• Gharama za kujitoa: Mfuko unatoza (a) asilimia 2.00 kwa uwekezaji uliodumu ndani ya mfuko
kwa kipindi kisichozidi mwaka mmoja (b) asilimia 1.5 kwa uwekezaji uliodumu ndani ya mfuko
kwa kipindi cha zaidi ya mwaka 1 na chini ya miaka 2(c) asilimia 1 kwa uwekezaji uliodumu
ndani ya mfuko kwa kipindi cha zaidi ya miaka 2 na chini ya miaka 3 na (d) uwekezaji uliodumu
ndani ya mfuko kwa kipindi cha zaidi ya miaka 3 hakuna gharama za kujitoa.
39
40
NA JINA LA MFUKO MAELEZO2.4 Mfuko wa Jikimu Mfukohuuulianzishwatarehe3Novemba2008.Lengolamfukonikukidhimahitaji
yawawekezajiwanaohitajiuhakikawamapatoyamarakwamarakamavilewastaafu.
Sifa za Mfuko:• Mipangoyauwekezaji:(a)Mpangowagawiowarobomwaka[Kiwangochachini
cha uwekezaji ni Shilingi 2Milioni], (b)Mpangowa gawiowamwaka [KiwangochachinichauwekezajiniShilingi1Milioni]na(c)Mpangowamwakawakukua[Shilingi.5,000/-]
• Vipandevinauzwakwathamanihalisiyawakatihuo[hakunagharamazakujiunga]• Gharamazakujitoa:Mfukounatoza(a)asilimia2.00kwauwekezajiuliodumundani
yamfuko kwa kipindi kisichozidi mwakammoja (b) asilimia 1.5 kwa uwekezajiuliodumundaniyamfukokwakipindichazaidiyamwaka1nachiniyamiaka2(c)asilimia1kwauwekezajiuliodumundaniyamfukokwakipindichazaidiyamiaka2nachiniyamiaka3na(d)uwekezajiuliodumundaniyamfukokwakipindichazaidiyamiaka3hakunagharamazakujitoa.
Chati 04; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
5
Jedwali 04; Faida kwa kipindi hadi tarehe 30 Septemba 2019
Faida [%] Hadi Septemba 2019
Tangu Kuanzishwa [Nov, 2008] Miaka 5 Miaka 4 Miaka 3 Miaka 2 Mwaka 1
8.88% 7.48% 9.11% 10.32% 11.19% 11.55%
Chati 04; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
0.73 1.05 3.336.55 6.27 8.50
14.77
22.9927.32
21.91 20.56 20.27
- 20 40 60 80 100 120 140 160
0
7
14
21
28
35
Dis
08
Sep-
09
Sep-
10
Sep-
11
Sep-
12
Sep-
13
Sep-
14
Sep-
15
Sep-
16
Sep-
17
Sep-
18
Sep-
19
Tham
ani y
a Kipa
nde
Ukub
wa w
a M
fuko,
Shil
ingi B
n
Muda
Ukubwa wa Mfuko, Shil ingi Bilioni Thamani ya Kipande
2.5
Mfuko Wa
Ukwasi
(Liquid Fund)
Mfuko huu ulianzishwa tarehe 30 Aprili, 2013. Ni Mfuko wa uwekezaji wa pamoja ambao unatoa fursa ya
uwekezaji mmbadala kwa wawekezaji wakubwa na/au taasisi ambazo wangependa kuwekeza fedha zao
za ziada kwa kipindi kifupi ama cha kati huku wakikuza mtaji wao.
Sifa za mfuko:
• Ni rahisi kwa mwekezaji kupata fedha zake za mauzo ya vipande, (ndani ya siku 3 za kazi baada
ya maombi ya kuuza vipande kupokelewa katika ofisi za UTT-‐AMIS makao makuu)
• Mfuko wa Ukwasi hautozi ada ya kujitoa wala kujiunga
• Mfuko unatoa unafuu wa gharama za uwekezaji
• Unafaa kwa wawekezaji mmoja mmoja, vikundi na taasisi
• Kiwago cha chini cha uwekezaji ni shilingi 100,000 na uwekezaji wa nyongeza usiopungua ni
shilingi 10,000.
• Mfuko unaruhusu uhamishaji wa vipande kutoka mwekezaji mmoja kwenda mwekezaji
mwingine.
• Mfuko hauruhusu kuhamisha vipande kwenda kwenye mifuko mingine.
• Vipande vinauzwa kwa thamani halisi ya wakati huo[ hakuna gharama za kujiunga ]
40
41
NA JINA LA MFUKO MAELEZO
2.5 Mfuko Wa Ukwasi (Liquid Fund)
Mfuko huu ulianzishwa tarehe 30 Aprili, 2013. Ni Mfuko wa uwekezaji wapamojaambaounatoafursayauwekezajimmbadalakwawawekezajiwakubwana/autaasisiambazowangependakuwekeza fedhazaozaziadakwakipindikifupiamachakatihukuwakikuzamtajiwao.
Sifa za mfuko:• Nirahisikwamwekezajikupatafedhazakezamauzoyavipande,(ndaniya
siku3zakazibaadayamaombiyakuuzavipandekupokelewakatikaofisizaUTT-AMISmakaomakuu)
• MfukowaUkwasihautoziadayakujitoawalakujiunga• Mfukounatoaunafuuwagharamazauwekezaji• Unafaakwawawekezajimmojammoja,vikundinataasisi• Kiwago cha chini cha uwekezaji ni shilingi 100,000 na uwekezaji wa
nyongezausiopunguanishilingi10,000.• Mfuko unaruhusu uhamishaji wa vipande kutoka mwekezaji mmoja
kwendamwekezajimwingine.• Mfukohauruhusukuhamishavipandekwendakwenyemifukomingine.• Vipandevinauzwakwathamanihalisiyawakatihuo[hakunagharamaza
kujiunga]
Chati 05; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
UKWASIUhuru kwa mwekezaji
6
Jedwali 05; Faida kwa kipindi hadi tarehe 30 Septemba 2019
Faida [%] Hadi Septemba 2019
Tangu Kuanzishwa [Mar, 2013] Miaka 5 Miaka 4 Miaka 3 Miaka 2 Mwaka 1
12.88% 13.29% 13.56% 13.35% 12.69% 12.48%
Chati 05; Ukubwa wa Mfuko na Thamani ya Kipande tangu kuanzishwa hadi 30 Septemba 2019
41
42
SN DESCRIPTION DETAILS
2.6 Mfuko wa Hati Fungani (Bond Fund)
Mfukohuuulianzishwatarehe16Septemba,2019.NimfukowawaziambaoambaokiasikikubwaunawekezakatikaHatiFunganizaSerikalinamakampuni.Mfukounalengolakutoagawio,kulingananafaidaitakayopatikananakukuzamtajikwawawekezajiwamudamrefu.
Sifa za mfuko: KunaainatatuzampangowauwekezajikatikaMfukohuu:• Mpangowakukuzamtaji;• Mpangowagawiokilamwezi;na• Mpangowagawiokilabaadayamiezisita.
Kiwangochachinichakuanzakuwekeza.(a)Shilingi50,000kwampangowakukuzamtaji;(b)Shilingimilioni10kwampangowagawiokilamwezi;na(c)Shilingimilioni5kwampangowagawiokilabaadayamiezisita.
2.7 FAIDA TAARIFA: Faida katika Mifuko hadi tarehe 30 Septemba 2019
Mfuko Annualized Return
Tangu Kuanzishwa hadi 30 Sept 2019
Kwa Kipindi cha Robo Mwaka kilichoishia 30 Sept 2019
UmojaFund 13.38% 11.56%
WekezaMaisha 12.40% 19.05%
WatotoFund 12.18% 12.25%
JikimuFund 8.88% 12.07%
LiquidFund 12.88% 15.13%
42
43
3.0 Elimu kwa Wawekezaji
NA JINA LA MFUKO MAELEZO
3.1 Unawezaje kujiunga na Mifuko ya UTT AMIS?
MwekezajianatakiwakujazanakukamilishaFomuyaMaombiyaKujiunganaMfukona kuweka fedhakatikaakauntiyaMfukokupitiamatawi yabenki yaCRDBnamadalaliwotewalioidhinishwanaSokolaHisalaDaresSalaam.
Baada ya kukamilisha kufungua akaunti na taratibu zote za utambuzi (KYC),mwekezajianawezakuwekezakwakutumiasimuyamkononikwakupigamsimbowa*150*82#auprogramu tumizi yaUTTAMISambayo inawezakupakuliwakutokakwenye“AppStore”au“Playstore”.Taratibuzakinazimetolewakwenyefomuyamaombi.
• Tembeleaofisi za Kampuni yaUwekezaji yaUTT (UTTAMIS) zilizopoDaresSalaamnaDodoma,madalaliwasokolahisalaDaresSalaamautawilolotelabenkiyaCRDBnchini.Piapigasimuzaburekwanambazifuatazo:0754800455 au 0754800544 [Kwa watumiaji wa voda] au 0715800455au 0715800544 [kwa watumiaji wa tigo] na kwa watumiaji wa airtel0782800455iliuwezekupata‘AkauntiNamba’yauwekezaji.
• Baadayahapo,nendatawilolotelabenkiyaCRDBkuwekakiasichapesaunachopenda kuwekeza. [tafadhali hakikisha unaandika nambari yako yauwekezaji katika fomu ya kuweka pesa ya CRDB ]. Pia unaweza kutumiaKuwekezakwaKutumiamtandaowasimuwaTigoPesa,M-pesanaAirtelmoney.
3.2 Nini maana ya Mfumuko wa bei? Na jinsi gani inamuathiri mtu wa kawaida?
Kwatafsirirahisi,mfumukowabeiniongezekolabeikatikabidhaanahudumakatikauchumikwakipindifulani.Wakatibeizabidhaanahudumazinapopanda,matokeoyakeni kushukakwa thamani ya fedha.Hivyo,uwezowa fedhawakununuabidhaanahudumahupungua.
Kunasababunyingizakiuchumizinazopelekeakutokeakwahalihii,hususaniongezekolafedhakatikamzungukokusikoendananakasiyaukuajiwaUchuminahivyomatokeoyakekupelekeamfumukowabei.
Kiujumla, vigezo vilivyokubalika kupima viwango vya mfumuko wa bei nipamojanaBeizabidhaazaJumla(WholesalePriceIndex)],Beizamahitajiyakawaidayawalaji(ConsumerPriceIndex),Mabadilikoyapatolandanilanchi(GDP)n.k.Vilevile,Beizamahitajiyakawaidayawalaji(ConsumerPriceIndex)inapima gharama za bidhaambalimbali zamsingi zinazotumiwa na kundi lawatu ikiwakilishamakundiyoteya jamiikamakigezochaupimajiwauchumikatikanchi.
Nimuhimukutambuakuwa,kaziyakuangaliahaliyamfumukowabeikatikanchihufanywanaBenkiKuu.Kaziyaufuatiliajinakuchukuahatuastahikikatikakudhibitikasiyamfumukowabeiinachukuamuda.
Jambo lamsingi lakujifunzani kuwa,Katikauchumiwenyemfumukowabei,unashauriwakuwekezamarakwamarahatakamakiasichakuwekezanikidogo.Kwakujenganidhamuyauwekezaji,unawezausionemadharaauatharihasizakuongezekakwamfumukowabeikatikauwekezaji.
43
44
NA JINA LA MFUKO MAELEZO
3.3 Nini maana ya Kompaundi?
Kwa ufupi, ni faida inayopatikana kutoka katika uwekezaji ambao hugeuzwamtajinahivyokutoafaidakubwazaidihapobaadaetofautinauwekezajiwamudamaalumambaofaidainayopatikanainatokanatunamudauliokaandaniyauwekezaji.
Je, utajali ikiwa utapata riba ya asilimia 10 au 12 katika uwekezaji?
Ukweli ni kuwa, ukizingatia hilo utaweza kutengeneza tofauti kubwa katikaukuaji wa faida na mtaji kadiri muda unavyoenda/unavyoongezeka. Faidaitokanayonakompaundiinatokananafaidakuendeleakuongezamtajiambaohuletamapatomakubwa kilamwaka.Mapatomakubwa au faida kubwa auuwekezajiwamudamrefuinaongezakiasichamtajikwauwianowakijiometri.
Matokeo ya KompaundiKwa kutumia jedwali hapo chini, unaweza kuona matokeo ya nguvu yakompaundina faidazakekutokananauwekezajiuliofanywa maramojakwakiasi cha shilingi 50,000/= na 5,000,000/= katika vipindi mbalimbali na kwakutumiaviwangotofautivyariba.
Jedwali 07;
Jedwali namba 8, linaoneshamatokeo ya nguvu ya kompaundi kutokana nafaidazakekwauwekezajiuliofanywamaramojakwakiasichashilingimilionihamsini(50)nashilingimilionimiamoja(100)katikavipindimbalimbalinakwakutumiaviwangotofautivyariba.
Jedwali 08;
Riba 12% 14%
Mwaka/Kiasi 50,000/= 5,000,000/= 50,000/= 5,000,000/=
1 56,000.00 5,600,000.00 57,000.00 5,700,000.00
3 70,246.40 7,024,640.00 74,077.20 7,407,720.00
5 88,117.08 8,811,708.42 96,270.73 9,627,072.91
10 155,292.41 15,529,241.04 185,361.07 18,536,106.57
20 482,314.65 48,231,465.47 687,174.49 68,717,449.36
Riba 12% 14%
Mwaka/Kiasi
50,000,000/= 100,000,000/= 50,000,000/= 100,000,000/=
1 56,000,000.00 112,000,000.00 57,000,000.00 114,000,000.00
3 70,246,400.00 140,492,800.00 74,077,200.00 148,154,400.00
5 88,117,084.16 176,234,168.32 96,270,729.12 192,541,458.24
10 155,292,410.42 310,584,820.83 185,361,065.71 370,722,131.41
20 482,314,654.66 964,629,309.33 687,174,493.59 1,374,348,987.19
44
45
Nguvuyakompaundinafaidayakeinaoneshwakwenyemajedwaliyafuatayokwamwekezajianaewekezakiasichashilingi50,000/=,100,000/=,500,000/=,nashilingimilioni1kwakilamwezikwakutumiaviwangotofautivyariba.
Jedwali 09; Uwekezajiwashilingi50,000/=kilamwezikwakutumiaviwangotofautivyariba.
Jedwali 10;Uwekezajiwashilingi100,000/=kilamwezikwakutumiaviwangotofautivyariba.
Jedwali 11;Uwekezajiwashilingi500,000/=kilamwezikwakutumiaviwangotofautivyariba.
Awamu za kuweka pesa
Riba/ Mwaka
10% 12% 14%
12 1 1,256,556.81 1,268,250.30 1,280,074.54
36 3 4,178,182.11 4,307,687.84 4,442,279.95
60 5 7,743,707.22 8,166,966.99 8,619,512.51
120 10 20,484,497.89 23,003,868.95 25,906,891.21
240 20 75,936,883.60 98,925,536.54 130,116,600.51
Awamu za kuweka pesa
Riba/ Mwaka
10% 12% 14%
12 1 6,282,784.05 6,341,251.51 6,400,372.68
36 3 20,890,910.55 21,538,439.18 22,211,399.75
60 5 38,718,536.09 40,834,834.93 43,097,562.55
120 10 102,422,489.45 115,019,344.73 129,534,456.05
240 20 379,684,417.99 494,627,682.69 650,583,002.53
Awamu za kuweka pesa
Riba/ Mwaka
10% 12% 14%
12 1 628,278.40 634,125.15 640,037.27
36 3 2,089,091.05 2,153,843.92 2,221,139.98
60 5 3,871,853.61 4,083,483.49 4,309,756.26
120 10 10,242,248.95 11,501,934.47 12,953,445.60
240 20 37,968,441.80 49,462,768.27 65,058,300.25
45
46
Jedwali 12; Uwekezajiwashilingi1,000,000/=kilamwezikwakutumiaviwangotofautivyariba.
BKutokananajedwalihapojuu,utagunduakuwasiobusarakupotezamudanapesakwakuwekafedhazakokwenyeuwekezajiusionafaidazakuridhishakwakipindichamudamrefu.Inabidiutambuekuwa,MUDAnikigezomuhimukatikakufanyamaajabuyakompaundi.
Jambo la msingi la kujifunza:
(1)Wakatiwote,tumiafursazilizopokatikauwekezajizenyekutoafaidakubwaukilinganishanauwekezajimwingine
(2)Endeleakuwekezakwamudamrefuiliunufaikenamaajabuyakompaundi.
4.0 Mawasiliano ForanyadditionalinformationonUTTlaunchedschemes,pleasecontactusatthefollowingaddress:
Awamu za kuweka pesa
Riba/ Mwaka
10% 12% 14%
12 1 12,565,568.09 12,682,503.01 12,800,745.36
36 3 41,781,821.09 43,076,878.36 44,422,799.50
60 5 77,437,072.17 81,669,669.86 86,195,125.10
120 10 204,844,978.90 230,038,689.46 259,068,912.10
240 20 759,368,835.99 989,255,365.39 1,301,166,005.06
Ofisi za Dar es SalaamMkurugenziMtendaji,UTTAMISPlc,JengolaSukari,GhorofayaPili,MtaawaSokoineDrivenaOhio,SandukulaPosta14825,DaresSalaamSimuNa:+255222128460NambazaBure:0754/0715/0782800455&544Nukushi:+255222137593BaruaPepe:[email protected]:www.uttamis.co.tz
Ofisi za UTT AMIS, DodomaJengolaPSSSFHouse,GhorofayaSita,MtaawaMakole,S.L.P1310,Dodoma-Tanzania,Simu:+255(0)262329062+255262323861Nukushi:+255(0)262329063+255262323862Email:[email protected]
47
48
Mfuko Wa WatotoFaraja kwa Watoto!
Mifuko Mingine ya Kampuniya Uwekezaji ya UTT AMIS
UKWASIUhuru kwa mwekezaji
UKWASIUhuru kwa mwekezaji
Fara ja kwa Watoto
OFISI YA DAR ES SALAAMMkurugenziMtendajiJengolaSukari,GhorofayaPili,MakutanoyaBarabarayaSokoinenaOhio,S.L.P14825,DaresSalaamSimu:+255222128460SimuyaBure:0754/715800455&800544Nukushi:+255222137593Baruapepe:[email protected]|Tovuti:www.uttamis.co.tz
OFISI YA DODOMAJengolaPSSSFHouse,GhorofayaSita,MtaawaMakole,S.L.P1310,Dodoma-Tanzania,Simu:+255(0)262329062/+255262323861Nukushi:+255(0)262329063/+255262323862Email:[email protected]
Kwamawasilianozaidi,tafadhaliwasiliananasi:
UTT AMIS PLC