015 elimu ya dini ya kiislamu coverf - necta...kuchuja hadithi za mtume (s.a.w) hivyo watahiniwa hao...

62
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA 015 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU TAARIFA YA UCHAMBUZI WA MAJIBU YA WATAHINIWA KATIKA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2019

Upload: others

Post on 01-Feb-2021

29 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

    015 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU

    TAARIFA YA UCHAMBUZI WA MAJIBU YA WATAHINIWA KATIKA MTIHANI WA KIDATO

    CHA NNE (CSEE) 2019

  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

    TAARIFA YA UCHAMBUZI WA MAJIBU

    YA WATAHINIWA KATIKA MTIHANI

    WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2019

    015 – ELIMU YA DINI YA KIISLAMU

  • ii

    Kimechapishwa na

    Baraza la Mitihani la Tanzania,

    S.L.P. 2624,

    Dar es salaam, Tanzania.

    © Baraza la Mitihani la Tanzania, 2019

    Haki zote zimehifadhiwa.

  • iii

    YALIYOMO

    YALIYOMO ............................................................................................................ iii

    DIBAJI ..................................................................................................................... iv

    1.0 UTANGULIZI ............................................................................................... 1

    2.0 TATHMINI YA KILA SWALI KWA MADA ............................................. 2

    2.1 SEHEMU (A) ............................................................................................. 2

    2.1.1 Swali la 1: Kuchagua Majibu Sahihi. ................................................. 2

    2.1.2 Swali la 2: Kuoanisha ......................................................................... 8

    2.2 SEHEMU B: Maswali ya kujibu kwa ufupi ............................................. 10

    2.2.1 Swali la 3: Familia ya kiislamu. ....................................................... 10

    2.2.2 Swali la 4: Mfumo wa Jamii ya Kiislamu ........................................ 13

    2.2.3 Swali la 5: Nguzo za Imani ............................................................... 15

    2.2.4 Swali la 6: Nguzo za Uislamu .......................................................... 18

    2.2.5 Swali la 7: Mambo ya lazima kufanyiwa maiti wa Kiislamu. .......... 20

    2.2.6 Swali la 8: Qur`an ............................................................................. 23

    2.2.7 Swali la 9: Sunnah na Hadithi .......................................................... 26

    2.3 SEHEMU C: Maswali ya Insha ............................................................... 29

    2.3.1 Swali la 10: Dola ya Kiislamu Madinah ........................................... 30

    2.3.2 Swali la 11: Qur'an. .......................................................................... 36

    2.3.3 Swali la 12: Nguzo za Uislamu ........................................................ 42

    2.3.4 Swali la 13: Mfumo wa Jamii ya Kiislamu ...................................... 47

    3.0 UCHAMBUZI WA KUFAULU KWA KILA MADA ............................... 54

    4.0 HITIMISHO ................................................................................................ 55

    5.0 MAPENDEKEZO ....................................................................................... 55

    6.0 Kiambatisho ................................................................................................. 56

  • iv

    DIBAJI

    Taarifa hii ya Uchambuzi wa Majibu ya Watahiniwa katika Mtihani wa Kidato cha

    Nne (CSEE) 2019 katika somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu imeandaliwa ili kutoa

    mrejesho kwa wanafunzi, walimu, wazazi, watunga sera na wadau wa elimu kwa

    ujumla kuhusu kufaulu kwa watahiniwa katika mtihani wa somo hili. Majibu ya

    watahiniwa katika mtihani ni kiashiria kimojawapo kinachoonesha mambo ambayo

    watahiniwa waliweza kujifunza kwa usahihi na yale ambayo hawakuweza

    kujifunza katika kipindi cha miaka minne ya Elimu ya Sekondari.

    Katika taarifa hii, uchambuzi wa kila swali umefanyika ambapo dosari mbalimbali

    zilizojitokeza katika majibu ya maswali zimeainishwa kwa kuonesha watahiniwa

    walioshindwa kujibu kwa usahihi. Pia uchambuzi huu umeonesha watahiniwa

    waliopata alama za juu, wastani na chini katika kila swali na sampuli za majibu ya

    watahiniwa waliofanya vizuri au vibaya zimeoneshwa. Aidha, sababu mbalimbali

    ambazo zilichangia wanafunzi kuweza au kushindwa kujibu maswali kwa usahihi

    zimeelezwa. Sababu zilizowafanya baadhi ya wanafunzi kuweza kujibu maswali

    kwa usahihi ni kama vile uelewa wa matakwa ya maswali na kuwa na maarifa ya

    kutosha juu ya mada mbalimbali za somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu. Aidha,

    uchambuzi umeonesha kuwa baadhi ya wanafunzi walishindwa kujibu maswali

    kwa usahihi kutokana na kutotambua matakwa ya maswali na kuwa na maarifa

    finyu katika mada mbalimbali na hasa katika Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya

    Kiislamu na Nguzo za Imani. Uchambuzi umebaini kuwepo kwa udhaifu katika

    kujibu maswali ya kujibu kwa ufupi na yale ya kujieleza kwa insha.

    Baraza la Mitihani la Tanzania lina imani kuwa mrejesho uliotolewa

    utawawezesha wadau wa elimu kuchukua hatua madhubuti za kuboresha mchakato

    wa ufundishaji na ujifunzaji ili hatimaye kuondoa changamoto zilizoainishwa

    katika taarifa hii. Endapo mapendekezo yaliyotolewa mwishoni mwa uchambuzi

    huu yatafanyiwa kazi, ujuzi na maarifa watakaopewa wanafunzi wa kidato cha nne

    katika somo hili utaongezeka na kiwango cha kufaulu katika somo hili

    kitaongezeka.

    Dkt. Charles E. Msonde

    KATIBU MTENDAJI

  • 1

    1.0 UTANGULIZI

    Taarifa hii inachambua kiwango cha kufaulu katika mtihani wa kidato cha

    nne (CSEE) wa mwaka 2019, somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu. Mtihani

    huo uliofanyika mwezi novemba 2019 uliandaliwa kwa kuzingatia

    muhtasari wa somo hili kwa kidato cha I hadi IV wa mwaka 2012.

    Mtihani huu ulikuwa na karatasi moja iliyokuwa na sehemu tatu: A, B na C

    zenye jumla ya maswali kumi na tatu. Sehemu A ilikuwa na maswali

    mawili. Swali la kwanza lilikuwa na vipengele kumi na tano (i-xv) ambapo

    mtahiniwa alitakiwa kuchagua majibu sahihi, swali hili lilikuwa na jumla

    ya alama 15. Swali la pili lilikuwa la kuoanisha lenye vipengele vitano (i-v)

    nalo lilikuwa na jumla ya alama 5. Sehemu B ilikuwa na maswali saba (7)

    ya kujibu kwa ufupi. Kila swali lilibeba alama 5 kwa hiyo sehemu hii

    ilikuwa na jumla ya alama 35. Sehemu C ilikuwa na maswali manne (4) ya

    insha ambapo mtahiniwa alitakiwa kujibu maswali matatu tu, kila swali

    lilikuwa na alama 15 na kuifanya sehemu hii kuwa na jumla ya alama 45.

    Jumla ya alama zote katika karatasi hii zilikuwa 100.

    Idadi ya watahiniwa walioandikishwa kufanya mtihani wa Elimu ya Dini

    ya Kiislamu mwaka 2019 ni 69,433 na waliofanya mtihani walikuwa

    67,230. Hii ni sawa na ongezeko la watahiniwa 20,361 ikilinganishwa na

    watahiniwa 46,869 waliofanya mtihani wa Elimu ya Dini ya Kiislamu

    mwaka 2018. Aidha, watahiniwa 67,035 walipata matokeo ambapo

    watahiniwa 36,565 sawa na 54.55% walifaulu. Kati ya hawa, watahiniwa

    20 (0.05%) walipata gredi A, 407 (1.11%) walipata gredi B, 11,123

    (30.42%) walipata gredi C na 25,015 (68.41%) walipata gredi D.

    Watahiniwa 30,470 sawa na asilimia 45.45 walipata gredi F. Kwa ujumla

    kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa kwa mwaka 2019 kilikuwa asilimia

    54.55.

    Taarifa hii inaonesha uchambuzi wa maswali ya mtihani na majibu

    yaliyotolewa na watahiniwa. Sampuli za majibu ya watahiniwa zimewekwa

    ili kuonesha kile kilichofanywa na watahiniwa. Kufaulu kwa watahiniwa

    kuligawanyika katika mafungu matatu ambayo ni: vizuri, wastani na

    dhaifu. Kufaulu kwa mada kulikuwa dhaifu kama kulikuwa kati ya asilimia

    0 hadi 29. kufaulu kulikuwa wastani kama kulikuwa kati ya asilimia 30

    hadi 64 na kufaulu kulikuwa vizuri kati ya asilimia 65 hadi 100.

  • 2

    2.0 TATHMINI YA KILA SWALI KWA MADA

    2.1 SEHEMU (A)

    Sehemu hii ilikuwa na maswali mawili na ilikuwa na jumla ya alama 20.

    Swali la kwanza lilikuwa la kuchagua jibu sahihi ambapo mtahiniwa

    alipewa sentensi yenye majibu matano ya kuchagua (A, B, C, D na E) na

    kutakiwa kuchagua herufi moja ya jibu sahihi na kujaza katika karatasi

    yake ya kujibia. Swali la pili lilikuwa la kuoanisha ambapo mtahiniwa

    alitakiwa aoanishe matendo matano yaliyopo katika orodha A (i - v) na

    majina ya matendo hayo katika orodha B (A hadi G) na kujaza katika

    kitabu chake cha kujibia.

    2.1.1 Swali la 1: Kuchagua Majibu Sahihi

    Swali la kwanza lilikuwa na vipengele kumi na tano (i-xv). Miongoni mwa

    mada zilizopimwa katika swali hili zilikuwa ni: (i) Dola ya Kiislamu

    Madinah, (ii) Historia ya Uislamu Baada ya Kutawafu Mtume (s.a.w), (iii-

    v) Sunnah na Hadithi, (vi-ix) Qur’an, (x) Mtazamo wa Uislamu juu ya

    Dini, (xi - xii) Familia ya Kiislamu, (xiii) Sheria katika Uislamu na (xiv -

    xv) Nguzo za Imani. Katika kila kipengele mtahiniwa alitakiwa kuchagua

    jibu sahihi kati ya majibu matano (A-E) aliyopewa na kuandika herufi ya

    jibu hilo katika kitabu chake cha kujibia. Kila kipengele kilikuwa na alama

    1, hivyo swali lote lilikuwa na jumla ya alama 15.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 67,199 (99.84%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa

    64,122 (95.46%) walifaulu. Watahiniwa 38,304 (57.00%) walipata alama

    za wastani (5 hadi 9), na watahiniwa 25,818 (38.42%) walipata alama za

    juu (10 hadi 15), ambapo kati yao watahiniwa 181 walipata alama zote 15

    za swali hili. Watahiniwa 3,077 (4.58%) walipata alama za chini (0 hadi 4)

    ambapo miongoni mwao watahiniwa 47 walipata alama 0. Chati namba 1

    inaonesha kufaulu kwa watahiniwa hawa kwa asilimia.

  • 3

    Chati ya 1: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 1

    Uchambuzi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa,

    kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa kizuri kwani watahiniwa

    64,122 (95.46%) kati ya 67,199 waliojibu swali hili walipata alama 5 hadi

    15. Watahiniwa waliopata alama za wastani (5 hadi 9) waliweza kujibu

    vizuri vipengele vitano hadi tisa vya swali na wale waliopata alama za juu

    (10 hadi 15) walijibu vizuri vipengele kumi na zaidi kati ya vipengele

    kumi na tano vya swali. Miongoni mwa vipengele vilivyojibiwa vizuri na

    watahiniwa hawa ni; (iii, iv, v, vi, vii, ix, x, xi na xv) vilivyotoka katika

    mada za: Sunnah na Hadithi, Qur`an, Mtazamo wa Uislamu juu ya Dini,

    Familia ya Kiislamu na Nguzo za Imani. Hii inaonesha kuwa watahiniwa

    hawa walielewa vema vipengele hivyo na walikuwa na maarifa ya kutosha

    katika mada hizo, hivyo walifanya vizuri. Watahiniwa waliopata alama za

    chini (0 hadi 4 ) walishindwa kuchagua majibu sahihi katika vipengele

    vingi vya swali kutokana na sababu mbalimbali kama zinavyochambuliwa

    katika aya zinazofuata;

    Kipengele cha (i) kilitoka katika mada ya “Dola ya kiislamu Madinah”

    katika mada ndogo ya “Uendeshaji wa Dola ya Kiislamu Madinah”. Katika

    kipengele hiki watahiniwa walitakiwa kuchagua kundi linaloonesha vyanzo

    muhimu vya mapato katika serikali ya Kiislamu ambapo jibu sahihi

    lilikuwa ni E (Zakat, Sadaka, Jizya, Al kharaj, Al-fay, Al-ghanimah na Al-

    ushru). Watahiniwa wengi hawakuwa na ufahamu juu ya istilahi hizi, hivyo

    4.6%

    57.0%

    38.4%

    0.0 - 4.0

    5.0 - 9.0

    10.0 - 15.0

    Alama

  • 4

    hawakuweza kuchagua jibu sahihi. Wengine hawakuweza kuchagua jibu

    sahihi kutokana na kutokuwa na ufahamu juu ya mada husika kwa ujumla

    na hatimae walishindwa kufanya vizuri.

    Kipengele cha (ii) kilitoka katika mada ya Historia ya Uislamu baada ya

    kutawafu Mtume (s.a.w) kipengele hiki kiliuliza sababu ya baadhi ya watu

    kuasi Uislamu mara baada ya kutawafu kwa Mtume (s.a.w), jibu sahihi

    lilikuwa ni B (uroho wa madaraka). Watahiniwa wengi walijibu kwa

    usahihi. Watahiniwa waliokosa kipengele hiki walichagua jibu A (kukataa

    kutoa zaka) jibu linaloonesha kuwa watahiniwa hawa walichanganya

    majibu kutokana na kuwa na maarifa finyu. Kukataa kutoa Zaka ni

    matokeo ya uasi. Watahiniwa wengine walichagua jibu C (ugumu wa

    sharia za kiislamu) kwa sababu ya kutokuwa na maarifa ya kutosha.

    Kipengele cha (iii) kilitoka katika mada ya “Sunnah na Hadithi”, katika

    mada ndogo ya Uchambuzi wa Hadithi za Mtume (s.a.w). Kipengele hiki

    kiliuliza kuhusu kanuni inayotumika kuchuja Hadithi za Mtume (s.a.w) na

    jibu lake sahihi lilikuwa D (kwa kuangalia maisha ya wapokezi wa

    Hadithi). Uchambuzi unaonesha watahiniwa wengi hawakuchagua herufi

    sahihi na badala yake walichagua E (kuangalia matumizi ya hadithi hiyo

    katika maisha) kwa sababu hawakuwa na uelewa wa kanuni zinazotumika

    kuchuja Hadithi za Mtume (s.a.w) hivyo watahiniwa hao walibahatisha

    majibu kwa kuuganisha mzizi wa swali na kila jibu lililopo ikizingatiwa

    kuwa jibu E lilikuwa na muunganiko mzuri kilugha.

    Kipengele cha (iv) kilitoka katika mada ya “Sunnah na Hadithi” katika

    mada ndogo ya Tanzu za Hadithi. Kipengele hiki kilimtaka mtahiniwa

    kuchagua kundi ambalo litawekwa Hadithi iliyosimuliwa na msimulizi

    anayejulikana kuwa na uwezo mdogo wa kuhifadhi masimulizi. Jibu sahihi

    lilikuwa ni A (dhaifu). Takwimu zinaonesha wengi walijibu kwa usahihi na

    wachache waliokosa walichagua jibu C (Maudhuu). Waliokosa kipengele

    hiki hawakuwa na maarifa ya kutosha katika uchambuzi wa Hadithi, hivyo

    walishindwa kubaini vigezo vya Hadithi dhaifu.

    Kipengele cha (v) pia kilitoka katika mada ya “Sunnah na Hadithi”.

    Mtahiniwa alitakiwa kuainisha kundi la Hadithi linalotokana na Isnad

    (msururu wa wapokezi) ya watu wema na waadilifu katika maisha yao. Jibu

    sahihi lilikuwa ni E (sahihi). Watahiniwa wengi waliweza kuchagua jibu

  • 5

    hili kwa kuwa walikuwa na maarifa ya kutosha katika mada ya uchambuzi

    wa Hadithi. Watahiniwa wengi waliokosa walichagua jibu A. Watahiniwa

    hawa walionesha kuwa hawafahamu maana ya neno “Maudhuu” katika fani

    ya Hadithi.

    Kipengele cha (vi) kilitoka katika mada ya Qur`an na kilimtaka mtahiniwa

    kuainisha mafunzo ya Suratul Fatiha endapo Muislamu anataka kuanza

    kufanya jambo lolote lile. Jibu sahihi lilikuwa B (kusoma Bismillahi

    Rahmani Rahiim. Watahiniwa wengi walijibu kwa usahihi kwakuwa

    kusoma Bismillahi Rahmani Rahiim ni kitendo ambacho kimezoeleka

    kufanywa na waumini wa Kiislamu katika maisha yao ya kila siku kabla ya

    kufanya jambo lolote. Baadhi ya watahiniwa waliokosa kipengele hiki

    walichagua jibu A. Hii ni kwa sababu ya mafundisho kuwa kabla ya kuanza

    kusoma Qur’an msomaji anatakiwa kuanza kwa kumlaani shetani kwa

    kutamka Audhubillah Mina Shaytwaanir Rajiim.

    Kipengele cha (vii) kilihusiana na mada ya Qur`an katika mada ndogo ya

    “Surah zilizochaguliwa”. Swali lilimtaka mtahiniwa ataje dhambi kubwa

    inayotajwa katika suratul Humazah. Jibu sahihi lilikuwa ni B (kusengenya).

    Watahiniwa wengi walifanya vizuri katika kipengele hiki. Inaonesha kuwa

    watahiniwa hawa walikuwa na maarifa ya kutosha juu ya tafsiri ya suratul

    Humazah. Watahiniwa waliokosa kipengele hiki walikuwa hawajui

    maudhui ya Suratul Humazah, hivyo majibu yao yalikuwa ya kubahatisha.

    Kipengele cha (viii) kilitoka kwenye mada ya Qur`an, mafunzo ya Surah

    zilizoteuliwa “Suratul Bayyinah”. Mtahiniwa alitakiwa kubainisha tafsiri ya

    aya ya saba ya sura hiyo. Jibu sahihi lilikuwa B (hakika wale walio amini

    na kutenda mema basi hao ndio wema wa viumbe). Kufaulu katika

    kipengele hiki kulikuwa ni kwa wastani. Watahiniwa waliochagua jibu

    sahihi walikuwa wamehifadhi surat Bayyinah na walikuwa wanafahamu

    vizuri tafsiri yake. Watahiniwa wengi waliokosa swali hili walichagua jibu

    C (ndani yake kuna sharia madhubuti) na D (kisha kwa hakika mtaulizwa

    siku hiyo juu ya neema {mlizopewa}). Watahiniwa hawa hawakuwa

    wanafahamu “Suratul Bayyinah” katika matini na tafsiri yake.

  • 6

    Kipengele cha (ix) kilipima mada ya Qur`an katika kipengele cha adabu za

    usomaji wa Qur`an. Mtahiniwa alitakiwa kubaini katika Orodha ya adabu

    zilizoorodheshwa ni ipi haikuwa miongoni mwa adabu za usomaji wa

    Qur`an. Jibu sahihi lilikuwa ni C (kuanza kwa sauti ya chini kisha kwa

    sauti ya juu katika kusoma). Watahiniwa wengi walifanya vizuri katika

    kipengele hiki. Hii inadhihirisha kuwa walikuwa na maarifa ya kutosha

    kuhusu adabu za usomaji wa Qur`an. Waislamu wengi huzingatia adabu

    mbalimbali za usomaji wa Qur’an katika usomaji wao wa kila siku. Hivyo

    nyingi katika adabu hizi zimezoeleka na hufuatwa na wasomaji wa Qur’an.

    Hata hivyo katika kipengele hiki wapo waliochagua majibu mengine

    ambayo si sahihi. Watahiniwa hawa walionesha kutokuelewa swali na

    kutokuwa na maarifa ya kutosha kuhusu Adabu za kuisoma Qur`an.

    Kipengele cha (x) kilipima mada ya “Mtazamo wa Uislamu juu ya dini”.

    Kwenye kipengele hiki mtahiniwa alitakiwa kuchagua jibu linaloonesha

    kazi kuu ya dini kwa mtazamo wa Uislamu. Watahiniwa wengi walifanya

    vizuri katika kipengele hiki kwa kuchagua jibu sahihi ambalo lilikuwa ni A

    (kusimamia sheria na kumkomboa mwanadamu). Watahiniwa hao

    walionesha kuwa na maarifa ya kutosha juu ya kazi ya dini kwa mtazamo

    wa Uislamu. Hata hivyo majibu B, D na E hayakuchaguliwa kwa vile

    yalitaja mambo ambayo yapo kinyume na Uislamu.

    Kipengele cha (xi) kilitoka katika mada ya “Familia katika Uislamu”.

    Mtahiniwa alitakiwa kubaini jinsi ndoa inavyomuhifadhi Muislamu

    kutokana na zinaa. Jibu sahihi katika kipengele hiki lilikuwa ni C (imeweka

    utaratibu madhubuti wa kukidhi haja). Watahiniwa wengi walimudu

    kuchagua jibu sahihi katika kipengele hiki kwa sababu ndoa ni ibada

    muhimu katika jamii. Watahiniwa walionesha kuwa na maarifa ya ziada

    kuhusu mada hii. Baadhi ya watahiniwa ambao hawakulielewa swali

    walijibu kipengele hiki kwa kubahatisha.

    Kipengele cha (xii) kilitoka katika mada ya “Familia ya Kiislamu” katika

    mada ndogo ya “Talaka na Eda”. Kipengele hiki kiliuliza kuhusu hukumu

    ya mwanamke mjamzito aliyepewa talaka katika sheria ya kiislamu. Jibu

    sahihi la kipengele hiki lilikuwa ni E (eda hadi pale atakapo jifungua).

    Watahiniwa wengi walimudu kuchagua jibu sahihi katika kipengele hiki,

    kutokana na kuwa na maarifa ya kutosha kuhusu Talaka na Eda. Baadhi ya

    waliokosa kipengele hiki walichagua jibu D (eda hadi atakapo maliza

  • 7

    kunyonyesha) ambalo halikuwa jibu sahihi. Ama watahiniwa wengine

    waliochagua majibu A, B na C wote walidhihirisha kutokuwa na marifa ya

    kutosha juu ya mada ya talaka na eda.

    Kipengele cha (xiii), kilitoka katika mada ya “Sheria katika Uislamu”

    kipengele hiki kiliuliza kuhusu adhabu ya mlevi katika sharia ya Uislamu.

    Jibu la swali hili lilikuwa ni D (kuchapwa viboko arobaini). Watahiniwa

    wengi walimudu kuchagua jibu sahihi hali iliyoonesha kuwa watahiniwa

    hawa walikuwa na maarifa ya kutosha juu ya mada hii ya Sheria katika

    Uislamu. Hata hivyo wapo baadhi ya watahiniwa walichagua majibu

    mengine kama vile A, C na E kwa sababu mbalimbali: Waliochagua A

    (kuchapwa viboko mia moja) hawa walishindwa kutofautisha kati ya

    adhabu ya mlevi na mzinifu, wale waliochagua C (kuchwapwa viboko

    hamsini) na E (kuchapwa viboko ishirini na moja) walionesha kuwa

    hawana maarifa yakutosha juu ya hukumu za kisheria zilizoainishwa katika

    Uislamu kwa makosa ya ulevi hivyo walichagua majibu yao kwa

    kubahatisha.

    Kipengele cha (xiv), kilitoka katika mada ya “Nguzo za Imani” katika

    kipengele cha “kuamini siku ya mwisho”. Kipengele hiki kiliuliza kuhusu

    maana sahihi ya kuamini siku ya mwisho ambapo jibu lake sahihi lilikuwa

    ni B (kuna maisha ya milele baada ya kufufuliwa). Kufaulu kwa

    watahiniwa katika kipengele hiki kulikuwa kuzuri kwani watahiniwa wengi

    waliweza kuchagua jibu hilo kwa sababu walikuwa na maarifa ya kutosha

    kuhusiana na mada ya Imani ya siku ya mwisho. Watahiniwa wachache

    walichagua majibu ambayo hayakuwa sahihi kama vile C (unapokufa nchi

    moja utafufuliwa nyingine) na wengine D (haiwezekani kufufuliwa tena

    baada ya kufa). Watahiniwa hawa walionesha kuwa wameathiriwa na

    imani kuwa mtu akifa sehemu moja ya dunia hufufuliwa kwa kuzaliwa tena

    upya sehemu nyingine. Watahiniwa wengine walijibu kwa mtazamo wa

    makafiri kuwa hakuna maisha baada ya kufa.

    Kipengele cha (xv) kilitoka katika mada ya Nguzo za Imani katika

    kipengele cha Kuamini Mitume wa Mwenyezi Mungu. Katika kipengele

    hiki watahiniwa walitakiwa kubaini sababu ya kuhitajika Mtume mwingine

    baada ya Mtume wa kwanza kurejea kwa mola wake. Jibu sahihi lilikuwa

    ni D (Mtume aliyetangulia alipelekwa kwa taifa maalum). Kufaulu kwa

    watahiniwa katika kipengele hiki kulikuwa kwa wastani.

  • 8

    Baadhi ya watahiniwa walichagua jibu B (Mtume aliyefuata alikuwa na

    mafundisho tofauti na aliyetangulia), watahiniwa hawa walishindwa

    kuelewa kuwa misingi ya mafundisho ya mitume haitofautiana.

    Watahiniwa wachache walichagua majibu A, C na E ambayo hayakuwa

    majibu sahihi. Majibu haya yanaashiria kuwa watahiniwa hawa hawakuwa

    na ufahamu kuhusu mada husika hivyo walikuwa wanabahatisha.

    2.1.2 Swali la 2: Kuoanisha Swali hili lilitoka katika mada ya Nguzo za Uislamu, mada ndogo ya Hija

    na Umrah. Mtahiniwa alitakiwa kuoanisha matendo ya Hija yaliyokuwa

    katika orodha A (i-v) na majina ya matendo hayo kutoka orodha B (A-G)

    na kisha kuandika herufi ya jibu sahihi kwa kila kipengele katika kitabu cha

    kujibia.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 67,124 (99.70%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa

    30,672 (45.70%) walipata alama 0 hadi 1 katika swali hili. Watahiniwa

    27,242 (40.58%) walipata alama 2 hadi 3 na watahiniwa 9,210 (13.72%)

    walipata alama 4 hadi 5. Chati namba 2 inaonesha kufaulu kwa watahiniwa

    hao kwa asilimia.

    Chati ya 2: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 2

    45.7 40.6

    13.7

    0

    10

    20

    30

    40

    50

    60

    70

    80

    90

    100

    0.0 - 1.0 2 - 3.0 4.0 - 5.0

    Asi

    lim

    ia y

    a w

    ata

    hin

    iwa

    Alama

  • 9

    Uchambuzi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    kiwango cha kufaulu katika swali hili ni cha wastani kwani watahiniwa

    36,452 (54.31%) waliojibu swali hili walipata alama 2 hadi 5. Watahiniwa

    hawa walionesha kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu ibada ya Hija na

    Umra jambo ambalo liliwawezesha kuoanisha kwa usahihi vipengele vingi

    na wengine vyote vya swali hili. Vipengele ambavyo kwa kiasi kikubwa

    watahiniwa hawa walimudu kuvioanisha kwa usahihi ni: (i), (iii) na (v). Hii

    ni kwa sababu Mahujaji huvirejea vitendo hivi kwa kuvitaja kwa majina

    kila wanapoeleza namna walivyotekeleza ibada ya Hija.

    Kipengele cha (i) chenye sentensi inayosema "mahujaji husimama, kuleta

    dhikri na kuomba dua mchana kutwa " ni miongoni mwa vipengele

    ambavyo watahiniwa walifanya vizuri. Jibu la kipengele hiki lilikuwa ni

    herufi D (Arafa). Tukio la mahujaji kusimama Arafa linakumbukwa sana

    na waumini ambao hawakwenda Makka kufanya ibada ya Hija ili waweze

    kutekeleza Sunnah ya kufunga inayoambatana na siku hiyo. Watahiniwa

    ambao hawakuoanisha kipengele hiki kwa usahihi, wengi walioanisha na

    herufi G (miqaat) ambalo halikuwa jibu sahihi. Watahiniwa hawa

    walihusisha neno miqaati na ''mahujaji kusimama" kwasababu miqaat ni

    sehemu au vituo ambavyo mahujaji husimama kwa ajili ya kutia nia ya Hija

    na kuvaa ihram ili kuendelea na hatua nyingine.

    Katika kipengele cha (iii) chenye sentensi inayosema "mahujaji hutembea

    mara saba baina ya safwa na marwa" pia ni miongoni mwa vipengele

    ambavyo watahiniwa walifanya vizuri. Jibu la kipengele hiki lilikuwa ni F

    (sa`i). Watahiniwa walioshindwa kuonanisha kipengele hiki kwa usahihi

    waliweka majibu ya kubahatisha. Baadhi yao walioanisha na herufi C

    (Tawafu) kwa sababu kitendo cha Tawafu hufanyika mara saba kama ilivyo

    kitendo cha (sa`i), hivyo majibu yaliwachanganya.

    Kipengele cha (v) chenye sentensi isemayo "mahujaji huzunguka al-kaaba

    mara saba kuanzia jiwe jeusi" ni miongoni mwa vipengele ambavyo

    watahiniwa wengi walimudu kuonanisha kwa usahihi. Jibu la kipengele

    hiki lilikuwa ni C (Tawafu). Watahiniwa ambao hawakuonanisha kipengele

    hiki kwa usahihi walichagua herufi E (Qiraan) na wengine A (ifraad) kwa

    sababu hawakuwa na maarifa ya kutosha kufahamu kuwa hizo zilikuwa ni

    aina za Hija.

  • 10

    Uchambuzi zaidi katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa vipengele

    ambavyo watahiniwa wengi hawakufanya vizuri ni (ii na iv). Katika

    kipengele cha (ii) kinachosema mahujaji hutia nia ya hija na kuvaa ihram,

    jibu lake lilikuwa G (Miqaat). Watahiniwa wachache waliweza kuoanisha

    kipengele hiki kwa usahihi. Watahiniwa wengine walioanisha kipengele

    hiki na herufi A (Ifraad) kwa sababu kitendo hiki cha kutia nia na kuvaa

    Ihram katika Miqaat hakipewi uzito mkubwa katika mafundisho ya ibada

    ya Hija pia watahiniwa kutojua maana ya neno “infraad” hivyo

    wakabahatisha ili kuona kama yanaendana.

    Kipengele cha (iv) kiliwataka watahiniwa kubaini Hija iliyo nafuu kwa

    mahujaji wanaotoka mbali na Makka. Jibu sahihi katika kipengele hiki

    lilikuwa B (Tamattu). Watahiniwa wengi walishindwa kuonisha kwa

    usahihi kwa sababu ya kutokuwa na maarifa ya kutosha kuhusu aina za

    Hija na kukosa uzoefu kutoka kwa watu waliowahi kuhudhuria ibada hii.

    2.2 SEHEMU B: Maswali ya kujibu kwa ufupi

    Sehemu hii ilikuwa na maswali saba ya majibu mafupi ambayo mtahiniwa

    alitakiwa kujibu maswali yote. Kila swali lilikuwa na alama tano (5) hivyo

    jumla ya alama zote katika sehemu hii ilikuwa 35. Maswali katika sehemu

    hii yalitoka katika mada zifuatazo: Familia ya kiislamu, Mfumo wa jamii

    ya Kiislamu, Nguzo za Imani, Nguzo za Uislamu, Mambo ya lazima ya

    kufanyiwa maiti Muislamu, Qur`an na Sunnah na Hadithi.

    2.2.1 Swali la 3: Familia ya Kiislamu.

    Swali hili lilitoka katika mada ya Familia katika Uislamu ambapo

    mtahiniwa alitakiwa kufafanua kwa ufupi kwa nini mwanamke wa kiislamu

    haruhusiwi kuolewa na mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Swali

    lilijibiwa na watahiniwa 64,952 (96.50%) kati ya watahiniwa 67,309

    waliofanya mtihani huu. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa 42,737

    (65.80%) walipata alama 0 hadi 1 za swali hili. Watahiniwa 20,206

    (31.11%) walipata alama 1.5 hadi 2.5 na watahiniwa 2,009 (3.09%)

    walipata alama 3.5 hadi 5. Chati namba 2 inaonesha kufaulu kwa

    watahiniwa hawa katika asilimia.

  • 11

    Chati ya: 3: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 3

    Uchambuzi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    kufaulu kwa watahiniwa katika swali hili kulikuwa ni wastani, kwa kuwa

    watahiniwa 22,215 (34.20%) kati ya 64,952 waliojibu swali hili walipata

    alama 1.5 hadi 5. Watahiniwa 20,206 (31.11%) walipata alama za wastani

    (1.5 hadi 3) na watahiniwa 2,009 (3.09%) walipata alama za juu (3.5 hadi

    5). Watahiniwa 20,206 (31.11%) waliopata alama za wastani hawakuweza

    kutoa ufafanuzi wa kutosha kwenye hoja walizozitoa kuelezea sababu za

    Uislamu kukataza mwanamke kuolewa na mume zaidi ya mmoja kwa

    wakati mmoja ingawa hoja zao zilikuwa sahihi.

    Watahiniwa waliopata alama za juu (3.5 hadi 5) walionesha kuwa na

    maarifa ya kutosha juu ya mada hii ya Familia ya Kiislamu. Vile vile

    walielewa vema matakwa ya swali na waliweza kutoa hoja madhubuti na

    kufafanua kwa usahihi kwanini mwanamke wa kiislamu haruhusiwi

    kuolewa na mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Ufafanuzi waotoa

    ulijumuisha hoja kama vile: mwanamke atakapopata mimba mtoto

    hatafahamika baba yake wa halali, Kwa hali hii mtoto atakoseshwa haki

    zake za msingi ikiwemo nasaba, malezi ya baba na mirathi. Mtoto huyu

    anaweza kuchukua mirathi isiyo haki yake. Itakuwa ni ngumu mwnamke

    huyu kutekeleza majukumu ya mke kwa mume ikizingatiwa kuwa mume ni

    kiongozi katika familia. Matokeo ya hali hii itakuwa ni migogoro katika

    65.8%

    31.1%

    3.1%

    0.0 - 1.0

    1.5 - 3.0

    4.0 - 5.0

    Alama

  • 12

    jamii. Kielelezo namba 3.1 kinaonesha sampuli ya majibu ya mtahiniwa

    aliyejibu kwa kuzingatia matakwa ya swali.

    Kielelezo 3.1: Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 3

    Uchambuzi zaidi unaonesha kuwa watahiniwa 42,737 (65.80%) walipata

    alama za chini (0 hadi 1), miongoni mwao watahiniwa 32,235 (47.90%)

    walipa alama 0. Watahiniwa hawa walijibu tofauti na matakwa ya swali

    kwa sababu ya kutokuwa na maarifa ya kutosha juu ya kipengele

    kilichoulizwa hivyo wakapata alama 0. Baadhi yao walikuwa wakirejea

    msingi wa swali kuwa: Mwanamke wa kiislamu haruhusiwi kuolewa na

    mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja kwa sababu dini ya kiislamu

    hairuhusu, na majibu mengine yanayofanana na hayo kama vile: Dini yetu

    ya kiislamu haijaeleza kuwa mwanamke wa kiislamu aolewe na mume zaidi

    ya mmoja kwa wakati mmoja, mwanamke haruhusiwi kuolewa akiwa ndani

    ya ndoa, dini ya Kiislamu hairuhusu, Qur'ani hairuhusu, kwa sababu hiyo

    ni sheria ya Uislamu, kwa sababu Allah (s.w) amejaalia aolewe na mume

    mmoja. Wengine walitoa hoja moja kuwa: Mwanamke hawezi kuwahimili

    wala kuwatosheleza wanaume wawili kwa wakati mmoja wala kutekeleza

    majukumu, mwanamke ameumbwa dhaifu hivyo hana uwezo wa kumudu

    mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Kielelezo namba 3.2 kinaonesha

    sampuli ya majibu ya mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali kama

    ilivyotakiwa.

  • 13

    Kielelezo 3.2: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 3

    2.2.2 Swali la 4: Mfumo wa Jamii ya Kiislamu Swali hili lilitoka katika mada ya “Uchumi katika Uislamu” na

    liligawanyika katika sehemu mbili; (a) na (b) ambapo katika sehemu (a)

    mtahiniwa alitakiwa kuainisha madhara matatu ya riba na katika sehemu

    (b) alitakiwa kutoa hoja mbili zinazoonesha jinsi gani atalitatua tatizo la

    riba.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 65,330 (97.10%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa

    35,567 (54.40%) walipata alama 1 hadi 2, na miongoni mwao watahiniwa

    17,345 (25.80%) walipata alama 0. Watahiniwa 25,151 (38.50%) walipata

    alama 1.5 hadi 3, na watahiniwa 4,612 (7.06%) walipata alama 3.5 hadi 5

    ambapo miongoni mwao watahiniwa 450 (0.70% ) walipata alama zote 5.

    Chati namba 4 inaonesha kufaulu kwa wanafunzi hao kwa asilimia.

    Chati no: 4: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 4

    54.4% 38.5%

    7.1%

    0.0 - 1.0

    1.5 - 3.0

    3.5 - 5.0

    Alama

  • 14

    Kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa katika swali hili kilikuwa cha

    wastani, kwani watahiniwa 29,763 (45.56%) kati ya 65,330 waliojibu swali

    hili walipata alama kati ya 1.5 hadi 5. Watahiniwa 25,151 (38.50%)

    walipata alama za wastani (1.5 hadi 3) kwa sababu walitoa hoja pungufu

    katika sehemu zote mbili na wengine walijibu sehemu moja na kuacha

    nyingine. Baadhi yao walijibu sehemu zote mbili lakini maelezo yao

    hayakutosheleza kupata alama za juu.

    Watahiniwa 4,612 (7.06%) waliopata alama za juu (3.5 hadi 5) waliweza

    kuainisha madhara ya riba kwa usahihi. Waliweza pia kutoa hoja

    madhubuti kuonesha namna ya kuondokana na tatizo la riba. Watahiniwa

    hawa walielezea madhara ya riba kuwa ni: Riba huchafua moyo wa tajiri,

    riba inamkandamiza mnyonge na mwenye dhiki, riba inaharibu uchumi wa

    jamii na maendeleo yake, riba ni mali ya dhuluma. Pia walielezea utatuzi

    wa tatizo la riba kwa njia mbalimbali kama vile; Kukopesha bila riba,

    kushirikiana katika mtaji na kugawana gharama za uendeshaji faida na

    hasara na kuanzisha benki za Kiislam. Watahiniwa hawa vilevile

    walielezea suala la kuielimisha jamii juu ya riba na madhara yake. Kwa

    ujumla watahiniwa hawa walikuwa na maarifa ya kutosha kuhusu

    kipengele cha Uchumi katika Uislamu hivyo waliweza kupata majibu

    sahihi ya swali hili kwa kuzingatia matakwa ya swali na walipata alama za

    juu. Kielelezo namba 4.1 kinaonesha sampuli ya majibu ya mtahiniwa

    aliyejibu vizuri.

    Kielelezo 4.1 Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 4

  • 15

    Uchambuzi zaidi uliofanywa katika majibu ya wanafunzi unaonesha kuwa

    watahiniwa 35,567 (54.40%) walipata alama za chini (0 hadi 1) ambapo

    miongoni mwao watahiniwa 17,345 (25.80%) walipata alama 0.

    Watahiniwa hawa walishindwa kuainisha madhara ya riba na kuonesha

    ufumbuzi wa tatizo la riba. Baadhi yao walibainisha adhabu za Allah (s.w)

    dhidi ya mtoaji na mpokeaji riba kama vile; Kuingia motoni, milango ya

    pepo itafungwa, hataingia peponi, hupata madhambi na kupatiwa adhabu

    na Mola. Baadhi ya watahiniwa hawakujibu kabisa swali hili kwakuwa

    hawakuwa na ufahamu wowote kuhusu majibu ya swali hili. Kwa ujumla

    watahiniwa hawa walipata alama hafifu na wengine alama 0 kwa sababu ya

    kutokuwa na uelewa wa kutosha kuhusu mada iliyoulizwa na

    kutokufahamu matakwa ya swali. Kielelezo 4.2 kinaonesha sampuli ya

    majibu ya mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali la 4 kama linavyotakiwa.

    Kielelezo 4.2 Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 4.

    2.2.3 Swali la 5: Nguzo za Imani Swali hili lilitoka katika kipengele cha kuamini Qadar ya Mwenyezi

    Mungu, ambapo mtahiniwa alitakiwa kutoa tofauti kati ya Qudra na Qadar

    ya Mwenyezi Mungu. Watahiniwa 58,913 (87.50%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu walijibu swali hili. Takwimu zinaonesha

    kuwa watahiniwa 41,608 (70.60%) walipata alama 0 hadi 1. Watahiniwa

    15,592 (26.47%) walipata alama 1.5 hadi 3 na watahiniwa 1,713 (2.91%)

    walipata alama 3.5 hadi 5. Chati namba 5 inaonesha kufaulu kwa

    watahiniwa hawa kwa asilimia.

  • 16

    Chati ya: 5: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 5

    Uchambuzi unaonesha kuwa kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa katika

    swali hili ni dhaifu kwani watahiniwa 41,608 (70.60%) kati ya 58,913

    waliojibu swali hili walipata alama 0 hadi 1 ambapo miongoni mwao

    watahiniwa 37,122 (55.20%) walipata alama 0. Watahiniwa hawa

    walishindwa kutofautisha kwa usahihi kati ya Qudra na Qadar ya

    Mwenyezi Mungu. Hii ilisababishwa na watahiniwa hao kutokuwa na

    maarifa ya kutosha juu ya nguzo hii ya sita ya Imani. Baadhi ya watahiniwa

    waliielezea Qudra kuwa ni: Bahati aliyomjalia mja na Qadar ni makadirio

    ya mwanadamu aliyokadiriwa, Qudra ni neema anazotoa Allah (s.w)

    kwenda kwa mja wake na Qadar ni nguzo ya tano ya Uislamu. Watahiniwa

    wengine walibuni majibu yao na kuonesha kuwa Qudra ni kinyume cha

    Qadar. Miongoni mwa majibu hayo ni: Qudra ni kuamini tofauti na

    maamrisho ya Allah (s.w) na Qadar ni kuamini kuwa hapana apasae

    kuabudiwa kwa haki ila Allah (s.w), Qudra ni maneno yanayosemwa na

    watu bila kuyatekeleza maamrisho yake na Qadar ni hali ya kutekeleza

    maamrisho ya Allah (s.w).Watahiniwa hawa hawakuwa na maarifa ya

    kutosha katika kipengele hiki cha nguzo za imani hivyo walipata alama

    hafifu na wengine walipata alama 0. Kielelezo 5.1 kinaonesha sampuli ya

    majibu ya mtahiniwa aliyeshindwa kutoa majibu sahihi ya swali.

    70.6%

    26.5%

    2.9%

    0.0 - 1.0

    1.5 - 3.0

    3.5 - 5.0

    Alama

  • 17

    Kielelezo 5.1: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 5

    Watahiniwa 15,592 (26.47%) walipata alama za wastani kutokana na

    kushindwa kutoa maelezo ya kutosha juu ya tofauti iliyopo kati ya Qudra

    na Qadar ya Mwenyezi Mungu. Baadhi ya watahiniwa waliweza kueleza

    maana ya neno moja tu kati ya Qadar na Qudra kwa usahihi hivyo walipata

    alama za wastani.

    Uchambuzi zaidi unaonesha kuwa watahiniwa 1,713 (2.91%) walipata

    alama za juu (3.5 hadi 5) miongoni mwao watahiniwa 213 (0.30%)

    walipata alama zote 5. Watahiniwa hawa waliweza kuelezea kwa usahihi

    tofauti iliyopo kati ya Qadar na Qudra ya Mwenyezi Mungu, kama vile:

    Qudra ya Mwenyezi Mungu ni uwezo wake juu ya kila kitu usio na mipaka

    na Qadar ya Mwenyezi Mungu ni mpango/mpangilio wa kuendesha mambo

    yote. Watahiniwa hawa walionesha kuwa na maarifa ya kutosha kuhusu

    mada ya Nguzo za Imani na walitumia maarifa yao vema kueleza dhana

    hizo hivyo waliweza kupata alama za juu. Kielelezo namba 5.2 kinaonesha

    sampuli ya majibu ya mtahiniwa aliyejibu vizuri.

    Kielelezo 5.2 Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 5

  • 18

    2.2.4 Swali la 6: Nguzo za Uislamu Swali lilitoka katika mada ya Nguzo za Uislamu kipengele cha Swaumu ya

    Ramadhani, na lilimtaka mtahiniwa aorodheshe mambo matano ambayo

    yanaweza kubatilisha swaumu ya mume na mke katika mchana wa

    Ramadhani. Watahiniwa 66,422 (98.70%) kati ya watahiniwa 67,309

    waliofanya mtihani huu walijibu swali hili. Takwimu zinaonesha kuwa

    watahiniwa 35,823 (53.93%) walipata alama 1.5 hadi 3. Watahiniwa

    16,683 (25.10%) walipata alama 0 hadi 1 na watahiniwa 13,916 (20.95%)

    walipata alama 3.5 hadi 5. Chati namba 6 inaonesha kufaulu kwa

    wanafunzi hawa kwa asilimia.

    Chati namba 6 Kufaulu kwa watahiniwa kwa asilimia katika swali la 6

    Uchambuzi uliofanywa kwenye majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa kizuri kwani watahiniwa

    49,739 (74.88%) waliojibu swali hili walipata alama kuanzia 1.5 hadi 5

    ambazo ni alama za kufaulu kwenye swali hili. Watahiniwa 1,112 (1.70%)

    walipata alama zote 5. Watahiniwa hawa walionesha kuwa na maarifa ya

    kutosha kuhusiana na mada ya Funga ya Ramadhani na walielewa matakwa

    ya swali. Watahiniwa hawa waliweza kubainisha mambo ambayo

    yanaweza kubatilisha Funga ya mume na mke kwa pamoja katika mchana

    wa mwezi wa Ramadhani kama vile: kula na kunywa mchana wa

    Ramadhani kwa makusudi, kufanya tendo la ndoa, kujitapisha kwa

    makusudi kujitoa manii na kunuia kuvunja swaumu.

    25.1

    53.9

    21.0

    0

    10

    20

    30

    40

    50

    60

    70

    80

    90

    100

    0.0 - 1.0 1.5 - 3.0 3.5 - 5.0

    Asi

    lim

    ia y

    a w

    ata

    hin

    iwa

    Alama

  • 19

    Watahiniwa 35,823 (53.93%) waliopata alama za wastani waliezea majibu

    pungufu kulingana na yaliyohitajika katika kujibu swali hili. Vile vile

    watahiniwa hawa walichanganya majibu yaliyo sahihi na mengine yasiyo

    sahihi, kama vile: Kuamka na janaba, kutokusimamisha swala, matendo

    maovu, kutokwa na najisi, kusengenya, kutamani, kutooga janaba, kuvaa

    nguo zinazoonesha, kutotii sharia za Ramadhani, kubusiana mke na mume

    na kufuata nafsi matamanio. Kielelezo namba 6.1 kinaonesha sampuli ya

    majibu ya mtahiniwa aliyejibu kwa kuzingatia matakwa ya swali.

    Kielelezo namba 6.1 Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 6.

    Uchambuzi zaidi wa majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa watahiniwa

    16,683 (25.10%) walishindwa kujibu swali hili kwa usahihi hivyo walipata

    alama hafifu (0 hadi 1) na miongoni mwao watahiniwa 3,786 (5.60%)

    walipata alama 0. Hii ni kwa sababu ya kutozingatia matakwa ya swali na

    kutokuwa na maarifa ya kutosha juu ya mambo ya jumla yanayo batilisha

    Funga ya mume na mke kwa pamoja. Baadhi yao badala ya kuandika

    yanayo batilisha Funga waliandika mambo ambayo yanadhaniwa kuwa

    yanabatilisha Funga. Mambo hayo ni kama vile: kukumbatiana mke na

    mume, kupigana busu mke na mume, kutamaniana mke na mume, kuamka

    na janaba na kulia.

    Watahiniwa wengine badala ya kuandika yanayobatilisha Funga,

    waliandika mambo ambayo yanapunguza uzito au thamani ya Funga, kama

    vile: Kusengenya, kutukana, kusema uongo, kuchonganisha, kugombana,

    kudhulumu, kutosimamisha swala na kutovaa stara. Kutokana na majibu

    haya watahiniwa hawa walipata alama hafifu au alama 0. Kielelezo namba

    6.2 kinaonesha mfano wa majibu ya mtahiniwa aliyeshindwa kujibu kwa

    kuzingatia matakwa ya swali.

  • 20

    Kielelezo 6.2: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 6

    2.2.5 Swali la 7: Mambo ya lazima kufanyiwa maiti wa Kiislamu

    Swali hili lilitoka katika mada ya mambo ya lazima ya kufanyiwa maiti wa

    kiislamu. Mtahiniwa alitakiwa kueleza hatua tano za kumkafini maiti wa

    kiume. Watahiniwa 63,063 (93.70%) kati ya watahiniwa 67,309 waliofanya

    mtihani huu walijibu swali hili. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa

    57,238 (90.8%) walipata alama 0 hadi 1. Watahiniwa 5,060 (8.02%)

    walipata alama 1.5 hadi 3 na watahiniwa 765 (1.21%) walipata alama 3.5

    hadi 5. Chati namba 7 inaonesha kufaulu kwa wanafunzi hao kwa asilimia.

    Chati namba 7: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 7

    Uchambuzi uliofanywa kwenye majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa dhaifu kwani watahiniwa

    57,238 (90.8%) waliojibu swali hili walipata alama 0 hadi 1. Miongoni

    90.8%

    8.0%

    1.2%

    0.0 - 1.0

    1.5 - 3.0

    3.5 - 5.0

    Alama

  • 21

    mwao watahiniwa 41,561 (61.70%) walipata alama 0, kwa sababu ya

    kushindwa kuelewa matakwa ya swali na kutokuwa na maarifa ya kutosha

    juu ya namna ya kukafini maiti wa kiislamu. Baadhi ya watahiniwa

    hawakuelewa na kuandika mambo ya lazima ya kufanyiwa maiti Muislamu

    badala ya hatua za kukafini maiti wa kiume. Majibu waliyo andika ni:

    kuosha maiti, kuvika sanda maiti, kuswalia maiti na kuzika. Watahiniwa

    wengine waliandika hatua za kuosha maiti Muislamu kama vile: Kumfunika

    maiti kwa nguo yenye kupenyeza maji na kumwagia maji na kumsugua kwa

    kumgeuzageuza, kumbinya kutoa uchafu tumboni, kumkalisha na kumbinya

    tena, kumtilisha udhu maiti na kumvalisha sanda. Watahiniwa wengine

    walieleza hatua za kumkafini maiti mwanamke badala ya hatua za kukafini

    maiti wa kiume. Hivyo watahiniwa hawa hawakuelewa matakwa ya swali.

    Kielelezo namba 7.1 kinaonesha mfano wa majibu ya mtahiniwa

    aliyeshindwa kujibu kwa kuzingatia matakwa ya swali.

    Kielelezo 7.1: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 10

    Watahiniwa 5,060 (8.02% ) waliopata alama za wastani (1.5 hadi 2.5)

    waliweza kutaja baadhi ya hatua bila maelezo ya kutosha juu ya hatua hizo

    za kumkafini maiti wa kiume na wengine walielezea hatua pungufu ya

    tano.

  • 22

    Uchambuzi zaidi kwenye majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa katika

    watahiniwa 765 (1.21%) waliopata kuanzia alama 3.5 hadi 5 ni watahiniwa

    102 (0.20%) tu walipata alama zote 5 za swali hili. Watahiniwa hawa

    waliopata alama za juu walionesha kuwa na maarifa ya kutosha juu ya

    namna ya kumkafini maiti wa kiislamu. Vile vile walielewa matakwa ya

    swali, hivyo waliweza kueleza kwa usahihi hatua tano za kumkafini maiti

    wa kiume kwa kuandika kama vile: kuweka pande la kwanza la sanda juu

    ya jamvi, kisha la pili na la tatu, kutoa kamba katika pande zote za jamvi la

    kwanza, Kamba nyingine zitolewe kwenye jamvi la tatu kwa ajili ya

    kumfungia maiti ili sanda isije kumvuka akabakia uchi. Maiti alazwe juu ya

    mapande yote matatu na kuzibwa kwa pamba zilizofukizwa manukato

    katika matundu yote ya mwili, Maiti atatizwe (afunikwe) kwa mapande yote

    matatu moja baada ya jingine na kamba zitumike kufunga vitanzi miguuni,

    tumboni na kichwani. Kielelezo namba 7.2 kinaonesha sampuli ya majibu

    ya mtahiniwa aliyejibu kwa kuzingatia matakwa ya swali na kueleza kwa

    ufasaha hatua muhimu katika kukafini.

    Kielelezo namba 7.2: Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 7

  • 23

    2.2.6 Swali la 8: Qur`an

    Swali hili lilitoka katika mada ya Qur'an, katika mada ndogo ya kushuka na

    kuhifadhiwa kwa Qur'an. Swali lilikuwa na vipengele viwili; (a) na (b).

    Katika kipengele (a) mtahiniwa alitakiwa atoe sababu mbili kueleza

    kwanini Qur'an ilishushwa kidogokidogo na katika kipengele (b)

    mtahiniwa alitakiwa kuelezea njia kuu tatu zilizotumika katika kuihifadhi

    Qur'an.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 64,957 (96.50%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Watahiniwa 31,101 (47.88%) walipata

    alama 1.5 hadi 3. Watahiniwa 30,349 (46.70%) walipata alama 0 hadi 1 na

    watahiniwa 3,507 (5.40%) walipata alama 3.5 hadi 5. Chati namba 8

    inaonesha kufaulu kwa wanafunzi hawa kwa asilimia.

    Chati namba 8: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 8

    Uchambuzi uliofanywa kwenye majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa cha wastani kwa kuwa

    watahiniwa 34,608 (53.28%) walipata alama 1.5 hadi 5. Watahiniwa

    waliopata alama za juu walionesha kuwa na maarifa ya kutosha juu ya

    mada ya Qur'an. Watahiniwa hawa walielewa matakwa ya swali hivyo

    waliweza kuandika kwa usahihi sababu za kushuka Qur'an kidogo kidogo

    na njia kuu tatu zilizotumika katika kuihifadhi Qur'an.

    46.7%

    47.9%

    5.4%

    0.0 - 1.0

    1.5 - 3.0

    3.5 - 5.0

    Alama

  • 24

    Katika kipengele (a) waliandika sababu za kushushwa kidogo kidogo kwa

    Qur’an kuwa ni: Ili uthibitishwe moyo wa Mtume (s.a.w) kwa aya mpya, ili

    kuwa wepesi kwa Mtume (s.a.w) kufikisha ujumbe uliotangulia kwa

    ukamilifu kabla ya ujumbe uliofuata na ili iwe wepesi kwa waumini wa

    mwanzo kusoma na kuhifadhi Qur'an.

    Katika kipengele (b) waliainisha njia kuu zilizotumika kuihifadhi Qur'an

    kama vile: Kuhifadhishwa Mtume (s.a.w) na kuahidiwa kutosahau,

    waislamu kuhifadhi Qur'an vifuani mwao baada ya kusomewa na Mtume

    (s.a.w) na Qur'an kuhifadhiwa katika maandishi chini ya usimamizi wa

    Mtume (s.a.w).

    Watahiniwa 31,101 (47.88%) walipata alama za wastani kutokana na

    sababu tofauti tofauti. Baadhi yao walijibu kipengele kimoja tu kati ya (a)

    na (b) na kuacha kingine badala ya kujibu vipengele vyote viwili. Wengine

    waliandika hoja pungufu katika kipengele kimoja au vyote viwili.

    Sababu nyingine iliyosababisha watahiniwa hawa kupata alama za wastani

    ni kuchanganya majibu sahihi na yasiyo sahihi katika vingele vya swali

    kwa mfano katika kipengele (a) waliandika hoja kama vile: Hali aliyokuwa

    nayo Mtume (s.a.w) wakati anapokea wahyi, kutokujua kusoma na

    kuandika, watu waweze kusilimu, kuaminika Qur'an, kwa sababu Qur'an ni

    tukufu. Pia katika kipengele (b) Mtume aliwaomba waandishi wake

    wamsomee, kwenye juzuu, kanda, katika mapango na majabali. Kielelezo

    namba 8.1 kinaonesha sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyejibu kwa

    kuzingatia matakwa ya swali.

    Kielelezo namba 8.1: Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 8

  • 25

    Uchambuzi zaidi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    watahiniwa 30,349 (46.70%) walipata alama kuanzia 0 hadi 1, kati yao

    watahiniwa 6,171 (9.20%) walipata alama 0. Watahiniwa hawa walijibu

    kinyume na matakwa ya swali kutokana na kukosa maarifa ya kutosha juu

    ya mada ya Qur'an. Baadhi yao hawakufanya kabisa swali hili katika

    vipengele vyote viwili (a) na (b).

    Watahiniwa wengine waliandika mahali au sehemu ambayo Mtume (s.a.w)

    alishushiwa Qur'an badala ya kueleza kwa nini Qur’an ilishuka kidogo

    kidogo kama ilivyoulizwa. Katika majibu yao walielezea: Qur'an

    ilishushwa kidogo kidogo Mtume (s.a.w) alipokuwa Jabal Hiraa, Qur'an

    ilishushwa kidogo kidogo Mtume (s.a.w) alipokuwa anaelekea Makka.

    Kundi lingine la watahiniwa waliofanya vibaya katika swali hili walieleza

    awamu ama hatua za kushuka kwa Qur’an (kutoka Lauhim mahfudh mpaka

    wingu wa dunia na kuletwa duniani) badala ya kutoa sababu za Qur'an

    kushuka kidogo kidogo kutoka wingu wa dunia kuja kwa Mtume (s.a.w).

    Kundi lingine liliandika kuwa Qur'an kushushwa kidogo kidogo ni Qur'an

    kushushwa Makka na Madinah.

    Katika kipengele (b) kadhalika, baadhi ya watahiniwa badala ya kueleza

    njia kuu zilizotumika kuhifadhi Qur'an walitoa maelezo kuwa: Qur'an

    iliandikwa na kuhifadhiwa kwenye: Magome ya miti, mawe, mapangoni

    katika mifupa na katika milima mirefu.

    Aidha kuna watahiniwa wengine walijbu kipengele hiki cha (b) kwa

    kuandika njia anazotumia Allah (s.w) kuwasiliana na waja wake, kama

    vile: kutumia malaika, ndoto za kweli na kutumia vibao. Kielelezo namba

    8.2 kinaonesha mfano wa majibu ya mtahiniwa aliyeshindwa kujibu kwa

    kuzingatia matakwa ya swali.

  • 26

    Kielelezo 8.2: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 10

    2.2.7 Swali la 9: Sunnah na Hadithi

    Swali hili lilitoka katika mada ya Sunnah na Hadithi, katika mada ndogo ya

    uchambuzi wa hadithi za Mtume (s.a.w). Swali lilikuwa na vipengele viwili

    (a) na (b). Katika kipengele (a) mtahiniwa alitakiwa aeleze tofauti kati ya

    Hadithi Qudusy na Hadithi Nabawiyyah na katika kipengele (b) mtahiniwa

    alitakiwa atofautishe Aljar-hi na Ata-adil.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 47,917 (71.20%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa

    32,412 (67.7%) walipata alama 0 hadi 1. Watahiniwa 14,772 (30.83%)

    walipata alama 1.5 hadi 3 na watahiniwa 733 (1.53%) pekee ndio walipata

    alama 3.5 hadi 5. Chati namba 8 inaonesha kufaulu kwa wanafunzi hao

    kwa asilimia.

  • 27

    Chati no: 9: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 9.

    Uchambuzi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa cha wastani ambapo

    watahiniwa 15,505 (32.36%) kati ya 47,914 waliojibu swali hili walipata

    alama 1.5 hadi 5. Watahiniwa hawa walionesha kuwa na maarifa ya

    kutosha juu ya mada ya uchambuzi wa Hadithi za Mtume (s.a.w) hivyo

    waliweza kutofautisha kwa usahihi baina ya Hadithi Qudusy na Hadithi

    Nabawiyyah, vilevile Aljar’hi na Ata’adili kwa namna ambayo

    iliwawezesha kupata alama za juu.

    Miongoni mwa tofauti walizozitoa ni kuwa: (a) Hadithi Qudusyi ni habari

    aliyoitoa Mtume (s.a.w) kama alivyoipokea kutoka kwa Allah (s.w) ilihali

    Hadithi Nabawiyyah ni usemi au habari aliyoitoa Mtume (s.a.w) kwa watu

    kwa maneno yake. Hadithi za aina hii zinaanza kwa maneno amesema

    Mtume (s.a.w).

    Kipengele (b) Aljar-hi ni kumtia dosari msimulizi kwa kukataa hadithi yake

    kutokana na udhaifu aliokuwa nao ilihali Ata-adili ni kumkubali msimulizi

    wa hadithi kutokana na sifa nzuri alizokuwa nazo. Kutokana na maelezo

    haya waliyoyatoa, watahiniwa hawa waliweza kupata alama nzuri.

    Watahiniwa 14,772 (30.83% ) walipata alama za wastani (1.5 hadi 3) kwa

    sababu walijibu kipengele kimoja na kuacha kingine. Vile vile waliandika

    67.7%

    30.8%

    1.5%

    0.0 - 1.0

    1.5 - 3.0

    3.5 - 5.0

    Alama

  • 28

    maelezo yasiyotosheleza kuhusu istilahi zilizoulizwa. Watahiniwa hawa

    walipata alama za wastani. Kielelezo namba 9.1 kinaonesha mfano wa

    majibu ya mtahiniwa aliyeweza kutofautisha vipengele hivyo vya Hadithi.

    Kielelezo 9.1: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 9

    Uchambuzi zaidi uliofanywa kwenye majibu ya watahiniwa unaonesha

    kuwa watahiniwa 32,412 (67.60%) waliopata alama hafifu (0 hadi 1)

    walijibu kinyume na matakwa ya swali kutokana na kutokuwa na maarifa

    ya kutosha juu ya mada ya uchambuzi wa Hadithi za Mtume Muhammad

    (s.a.w). Watahiniwa hawa walishindwa kutofautisha istilahi walizopewa

    kama ilivyotakiwa na wengine waliacha kabisa kujibu swali hili.

    Baadhi ya watahiniwa hawa walitafsiri neno Aljar-hi na Ata-adil kama aina

    au tanzu za Hadithi kama vile: Aljar-hi ni hadithi fupi fupi kutoka kwa

    Mtume wetu (s.a.w) na Ata-adili ni hadithi ndefu ndefu zenye aya ndefu,

    Aljar-hi ni hadithi ambayo imesimuliwa na nabii mussa wakati ata-adil ni

  • 29

    hadithi ambayo imesimuliwa na nabii Ibrahim na aljar-hi ni hadithi zenye

    wapokezi wengi wakati at-adil ni hadithi zenye wapokezi kidogo.

    Baadhi ya watahiniwa ambao hawakuwa na maarifa ya kutosha kuhusu

    kipengele (a) walitoa majibu yafuatayo: Hadithi qudusy ni hadithi ambayo

    imepokelewa Makka na mahujaji na nabawiyya ni hadithi ambayo

    ilipokelewa Madina kwa lengo la kuendeleza uislamu, Qudusy ni hadithi

    iliyoandikwa enzi za Mtume (s.a.w) na Nabawiyyi ni Hadithi

    zilizopokelewa na Imamu muslim na Bukhar, Nabawiyya ni hadithi dhaifu

    na Qudusy ni Hadidhi sahihi na Qudusy ni hadithi za kuhifadhiwa

    vichwani na hadithi Nabawiyya ni hadithi za kuhifadhiwa kwenye misahafu

    na juzuu.

    Wengine katika kujibu kipengele (a) walifananisha Hadithi Qudusy na

    Nabawiyah kama vile Hadithi Mutawatir na Ahad na kuzieleza kama;

    hadithi qudusy ni hadithi ambayo imesimuliwa na watu wachache wakati

    Nabawiyyah ni hadithi ambayo imesimuliana watu wengi. Kutokana na

    majibu haya na mengine yanayofanana na hayo watahiniwa hawa walipata

    alama hafifu au alama 0. Kielelezo namba 9.2 kinaonesha mfano wa majibu

    ya mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali kwa usahihi.

    Kielelezo 9.2: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 10

    2.3 SEHEMU C: Maswali ya Insha Sehemu hii ilikuwa na jumla ya maswali manne ya insha ambapo

    mtahiniwa alitakiwa kujibu maswali matatu. Kila swali lilikuwa na alama

    15. Jumla ya alama katika sehemu hii ilikuwa 45. Maswali katika sehemu

    hii yalitoka katika mada za: Dola ya Kiislamu Madina, Qur an, Nguzo za

    Uislamu na Mfumo wa jamii ya Kiislamu.

  • 30

    2.3.1 Swali la 10: Dola ya Kiislamu Madinah Swali hili lilitoka katika mada kuu ya Dola ya kiislamu Madinah katika

    kipengele Kutawafu kwa Mtume (s.a.w). Watahiniwa walitakiwa kueleza

    mafunzo manne wanayopata Waislamu kuanzia kuumwa hadi kutawafu

    kwa Mtume Muhammad (s.a.w).

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 45,147 (67.10%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa

    27,210 (60.30%) walipata alama 0 hadi 4.5. Watahiniwa 16,501 (36.55%)

    walipata alama 5 hadi 9.5 na watahiniwa 1,436 (3.18%) walipata alama 10

    hadi 15 za swali hili. Chati namba 10 inaonesha kufaulu kwa wanafunzi

    hao katika asilimia.

    Chati 10: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 10

    Kwa ujumla kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa katika swali hili

    kilikuwa cha wastani kwani watahiniwa 17,937 (39.73%) kati ya

    watahiniwa 45,147 waliojibu swali hili walipata alama 5 hadi 15.

    Watahiniwa waliopata alama za juu waliweza kubainisha mafunzo sahihi

    kutokana na kuugua hadi kutawafu kwa Mtume (s.a.w). mafunzo hayo ni

    kama vile: Ugonjwa sio sababu ya mtu kuacha kufanya ibada na majukumu

    mengine, kiongozi anapopata dharura sio sababu ya mambo kusimama bali

    akabidhi mtu mwingine majukumu yake, tunafundishwa kuwa ni bora maiti

    60.3%

    36.5%

    3.2%

    0.0 - 4.5

    5.0 - 9.5

    10.0 - 15.0

    Alama

  • 31

    ashughulikiwe na ndugu zake wa karibu kinasaba na uchungu wa umauti

    utampata kila mtu akiwa mwema au muovu. Kielelezo namba 10.1

    kinaonesha sampuli ya majibu ya mtahiniwa aliyeweza kueleza kwa

    usahihi mafunzo yatokanayo na kuugua hadi kutawafu kwa Mtume (s.a.w).

  • 32

    Kielelezo namba 10.1 Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 10

    Watahiniwa 16,501 (%) walipata alama za wastani (5 hadi 9.5) kutokana na

    kushindwa kutoa maelezo ya kutosha katika hoja walizozianisha ingawa

    hoja zao zilikuwa sahihi. Wengine walitoa hoja pungufu ya nne ambazo

    zilihitajika katika swali hili. Watahiniwa wengine walichanganya majibu

  • 33

    sahihi na yasiyo sahihi kama vile: Imani ya kweli, malipo mazuri ni kutoka

    kwa Allah (S.W), kuamini qadar, tunajifunza kuwa Allah (S.W) ni Muweza

    wa kila jambo na Allah (S.W) ndiye aliyemtuma Mtume (s.a.w).

    Watahiniwa 27,210 (60.30%) walishindwa kujibu swali hili kwa usahihi

    hivyo walipata alama hafifu (0 hadi 4.5) ambapo miongoni mwao

    watahiniwa 3,246 (4.8%) walipata alama 0. Hii ni kwa sababu ya

    kushindwa kujua matakwa ya swali na wengine kutokuwa na maarifa ya

    kutosha juu ya historia ya kutawafu kwa Mtume (s.a.w).

    Baadhi ya watahiniwa walionesha kuwa hawakuelewa kabisa matakwa ya

    swali kwani waliorodhesha vitendo vya waja wema kama mafunzo

    kutokana na tukio hili, mfano wa majibu hayo ni kama vile: uvumilivu,

    uchamungu, subra, kufanya mambo mema kuutangaza Uislamu, kumuamini

    Mwenyezi Mungu, kusoma Qur'an kiufasaha, kujua jinsi ya kuishi na jirani

    na kujipamba na tabia njema.

    Watahiniwa wengine walielezea sifa na uwezo wa Mwenyezi Mungu kama

    mafunzo, mfano: Allah (s.w) ni Mola wa viumbe vyote humchukua

    amtakaye, Allah (s.w) humnusuru amtakaye, Allah (s.w) ndiye mwenye

    mamlaka ya kufanya chochote na Allah (s.w) humpa amtakaye na

    kumnyima amtakaye.

    Baadhi ya watahiniwa badala ya kuandika mafunzo ya tukio hili, walieleza

    sifa za Mtume (s.a.w) kama ilivyozoeleka kwa jamii kumsifia kiongozi

    anapofariki, kama vile: alikuwa na mapenzi makubwa na watu, alikuwa

    mwaminifu, alikuwa mkarimu, alikuwa mchamungu na alikuwa akitoa

    zakat sadaka. Kwa ujumla watahiniwa hawa hawakuwa na maarifa juu ya

    mada hii na wengine hawakuelewa kabisa matakwa ya swali, hivyo baadhi

    yao walipata chini ya alama tano (5) huku wengine wakipata alama 0.

    Kielelezo namba 10.2 kinaonesha sampuli ya majibu ya mtahiniwa

    aliyeshindwa kujibu swali hili kama inavyostahili.

  • 34

  • 35

    Kielelezo namba: 10.2 Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 10

  • 36

    2.3.2 Swali la 11: Qur'an. Swali hili lilitoka katika mada ya Qur'an, katika mada ndogo ya kushuka na

    kuhifadhiwa kwa Qur'an. Swali lilimtaka mtahiniwa aeleze namna Mtume

    (s.a.w) alivyoteremshiwa Qur'an kwa mara ya kwanza na kueleza mafunzo

    manne yanayopaswa kufanyiwa kazi katika maisha ya kila siku kutokana

    na tukio hilo.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 48,693 (72.30%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Watahiniwa 28,239 (58.00%) walipata

    alama 0 hadi 4.5. Watahiniwa 18,973 (39.0%) walipata alama 5 hadi 9.5 na

    watahiniwa 1,481 (3.04%) walipata alama 10 hadi 14.5. Chati namba 11

    inaonesha kufaulu kwa watahiniwa hawa kwa asilimia.

    Chati namba 11: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 11

    Kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa katika swali hili kilikuwa cha

    wastani kwani watahiniwa 20,454 (42.01%) kati ya 48,693 waliojibu swali

    hili walipata alama 5 hadi 14.5. Watahiniwa waliopata alama za juu (10

    hadi 14.5) waliweza kueleza kwa umahiri namna Mtume (s.a.w)

    alivyoteremshiwa Qur'an kwa mara ya kwanza na kubainisha mafunzo

    manne yanayopaswa kufanyiwa kazi katika maisha ya kila siku kutokana

    na tukio hilo. Watahiniwa hawa walieleza kuwa: Mtume (s.a.w) alianza

    kushushiwa Qur'an mwaka 610 A.D akiwa na umri wa mika 40 katika

    pango la Jabal Hira katika usiku wa mwezi wa Ramadhani. Malaika Jibril

    58.0%

    39.0%

    3.0%

    0.0 - 4.5

    5.0 - 9.5

    10.0 - 14.5

    Alama

  • 37

    alimuendea mtume pangoni hapo na kumuamuru asome. Mtume (s.a.w)

    alijibu kuwa hajui kusoma. Jibril alimbana kwa nguvu na alipomuachia

    alimsomea aya tano za mwanzo za suratul Alaq. Mtume alirejea nyumbani

    na aya hizi huku akitetemeka kwa hofu na alimuhadithia mkewe Bi Khadija

    yote yaliyompata. Mafunzo waliyoyatoa kutokana na tukio hili ni pamoja

    na: Elimu ni amri ya kwanza aliyopewa mtume (s.a.w), kutafuta elimu sio

    jambo jepesi bali tutakumbana na magumu mengi, utukufu wa Mwezi wa

    Ramdhani unatokana na Qur'an kuanza kushuka mwezi huo hivyo tuzidishe

    kusoma Qur'an katika mwezi huo na Qur'an ni kitabu cha Allah (s.w).

    Watahiniwa 18,973 (38.96% ) walipata alama za wastani (5 hadi 9.5)

    kwakuwa hawakutoa maelezo ya kutosha juu ya historia ya kushushwa kwa

    Qur'an kwa mara ya kwanza na mafunzo tunayoyapata. Baadhi ya

    watahiniwa waliandika hoja pungufu ya nne na walichanganya majibu

    sahihi na yasiyo sahihi kama vile: Kutekeleza maamrisho na kuacha

    makatazo, tunapaswa kufuata sharia na kanuni, tunapaswa kumuamini

    Allah (s.w) na Mtume wake, Jibril ndiye aliyekuwa akishusha wahyi na

    kutii amri Allah (S.w) ni sababu ya kupata radhi zake. Kielelezo namba

    11.1 kinaonesha sampuli ya majibu ya mtahiniwa aliyejibu kwa kuzingatia

    matakwa ya swali.

  • 38

  • 39

    Kielelezo namba 11.1: Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 11

    Uchambuzi zaidi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    watahiniwa 28,239 (58.00%) walipata alama hafifu (0 hadi 4.5) ambapo

    miongoni mwao watahiniwa 2,455 (3.60%) walipata alama 0. Watahiniwa

    hawa walijibu kinyume na matakwa ya swali kutokana na kutokuwa na

    maarifa ya kutosha juu ya historia ya kushushwa na kuhifadhiwa kwa

    Qur'an.

    Baadhi ya watahiniwa hawa badala ya kueleza namna Mtume (s.a.w)

    alivyoshushiwa Qur'an kwa mara ya kwanza na mafunzo tunayoyapata

    kutokana na tukio hilo waliandika majibu ya jumla yaliyokuwa kinyume na

    matakwa ya swali kama vile, hali aliyokuwa nayo Mtume (s.a.w) baada

    kupokea wahyi, kwamba: Alikuwa mwoga sana baada ya kumuona Jibril,

    baada kushushiwa Qur'an alikuwa anatetemeka, Mtume (s.a.w) alibadilika

    haiba, Mtume (s.a.w) alipewa jukumu la kufundisha Qur'an na alikuwa

    hajui kusoma wala kuandika.

  • 40

    Watahiniwa wengine waliandika faida za kuisoma Qur'an na kuifuata kama

    vile: Qur'an ni kinga kwa mwanadamu, Qur'an inamfanya Mtu kuwa

    mchamungu, Qur'an humrahisishia mtu kufanya jambo, Qur'an inamfanya

    mtu kuwa muadilifu, Qur'an inafanya waislamu kushirikiana, Qur'an

    inapelekea watu kuwa na hofu juu ya Allah (S.W) na Qur'an imepelekea

    kuvumbuliwa kwa Sunnah.

    Kwa ujmla watahiniwa hawa hawakuwa na maarifa juu ya historia ya

    kushushwa kwa Qur’an, hivyo baadhi yao walipata alama hafifu na

    wengine walipata alama 0. Kielelezo 11.2 kinaonesha sampuli ya majibu ya

    mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali hili kwa kuzingatia matakwa ya

    swali.

  • 41

    Kielelezo namba 11.2: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 11

  • 42

    2.3.3 Swali la 12: Nguzo za Uislamu

    Swali hili lilitoka katika mada ya Nguzo za Uislamu katika mada ndogo ya

    kusimamisha Swala za jamaa. Mtahiniwa alitakiwa kueleza mambo matano

    ya kuzingatia wakati wa kuandaa Khutba ya Ijumaa.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 32,967 (49.00%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Watahiniwa 25,356 (76.90%) walipata

    alama 0 hadi 4.5 za swali hili. Watahiniwa 4,988 (15.13%) walipata alama

    5 hadi 9.5 na watahiniwa 2,623 (7.96%) walipata alama 10 hadi 15. Chati

    namba 11 inaonesha kufaulu kwa watahiniwa hao katika asilimia.

    Chati namba: 12: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 12

    Uchambuzi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa

    kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa dhaifu, kwakuwa

    watahiniwa 25,356 (76.90%) kati ya 32,967 waliofanya swali hili walipata

    alama 0 hadi 4.5 ambapo miongoni mwao watahiniwa 9,369 (13.90%)

    walipata alama 0. Watahiniwa hawa walijibu kinyume na matakwa ya swali

    kwa sababu ya kutokuwa na maarifa ya kutosha juu ya khutuba ya Swala

    ya ijumaa, hususani nguzo zake, badala ya kueleza mambo ya kuzingatia

    wakati wa kuandaa khutuba ya Ijumaa watahiniwa wakaelezea hatua za

    76.9%

    15.1%

    8.0%

    0.0 - 4.5

    5.0 - 9.5

    10.0 - 15.0

    Alama

  • 43

    kufuata katika kufikisha khutuba ya Ijumaa, kama vile: salamu na

    utangulizi, mwanzo wa hutuba, kiini au katikati ya khutuba na mwisho wa

    khutuba au hitimisho. Watahiniwa wengine walifahamu kuwa mambo ya

    kuzingatia kabla ya kuandaa khutuba ni namna khatibu anavyotakiwa kuwa

    au sifa za khatibu na khutuba yenyewe, hivyo wakatoa sifa kama vile:

    Khatibu awe na udhu, awe nadhifu, awe mnyenyekevu, awe amehifadhi

    Qur'an na kuielewa, awe amehifadhi Hadithi na kuzielewa, awe anajua

    tafsiri ya sura zote na awe amehifadhi tafsiri ya Hadithi zote.

    Na katika sifa za khutuba wakaeleza kuwa: Khutuba iwe fupi nzuri na

    yenye kueleweka, khutuba itumie lugha ya walengwa, khutuba ilenge jamii

    husika, khutuba ilenge matatizo ya jamii, isiwe ya kusengenya mtu, isiwe

    na utata na izingatie muda. Pamoja na kuwa baadhi ya mambo

    waliyoyaeleza ni ya kweli lakini sio majibu sahihi kwa sababu sio nguzo za

    khutuba ya Ijumaa, hivyo watahiniwa hawa walipata alama hafifu na

    wengine alama 0. Kielelezo namba 12.1 kinaonesha sampuli ya majibu ya

    mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali hili kwa kuzingatia matakwa ya

    swali.

  • 44

  • 45

    Kielelezo namba 12.1: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 12

    Watahiniwa 4,988 (15.13%) waliopata alama za wastani (5 hadi 9.5)

    walikuwa na mapungufu mbalimbali kama vile: Baadhi walitaja majibu

    sahihi lakini hawakutoa maelezo kamili juu ya mambo hayo. Wengine

    walieleza pungufu ya mambo matano yaliyohitajika na baadhi yao

    waliochanganya majibu sahihi na yasiyo sahihi, kama vile: kutoa salamu

    kwa waislamu, kuwaruhusu waislamu kuomba dua, kuweka kituo baina ya

    khutuba mbili, kuwa na mfano wa aya na hadithi, lugha ya khutba ifanane

    na wale wanaohutubiwa, mada iendane na jamii na khutuba iwe ni yenye

    kuelimisha. Baadhi ya mambo haya ni kweli hufanyika wakati wa khutuba

    ya Ijumaa lakini sio katika misingi ya kuandaa khutuba ya Ijumaa.

    Uchambuzi zaidi uliofanywa kwenye majibu ya watahiniwa unaonesha

    kuwa watahiniwa 2,623 (7.96%) walipata alama za juu ambapo miongoni

    mwao watahiniwa 7 walipata alama zote 15 za swali hili, watahiniwa hawa

    walionesha kuelewa matakwa ya swali na walikuwa na maarifa ya kutosha

    juu ya uandaaji wa khutba ya Swala ya Ijumaa.

    Watahiniwa hawa waliweza kueleza kwa usahihi mambo matano ya

    kuzingatia wakati wa kuandaa khutuba ya Ijumaa kuwa ni: Kuanza khutuba

    ya Ijumaa kwa kumhimid au kumshukuru Allah (s.w,), kisha kumswalia au

    kumtakia rehema na Amani Mtume (s.a.w), kuwausia waislamu juu ya

    kumcha Allah (S.w), kusoma aya au sura yeyote katika Qur'an na

    kuwaombea waislamu/waumini wote dua. Kielelezo namba 12.2

  • 46

    kinaonesha sampuli ya majibu ya mtahiniwa aliyejibu kwa kuzingatia

    matakwa ya swali.

  • 47

    Kielelezo namba 12.2: Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 12

    2.3.4 Swali la 13: Mfumo wa Jamii ya Kiislamu Swali hili lilitoka katika mada ya Mfumo wa jamii ya Kiislamu katika

    mada ndogo ya Sheria katika Uislamu. Mtahiniwa alitakiwa afafanue kazi

    tano za sheria ya Kiislamu katika jamii.

    Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 56,876 (84.50%) kati ya watahiniwa

    67,309 waliofanya mtihani huu. Takwimu zinaonesha kuwa watahiniwa

    34,211 (60.20%) walipata alama 0 hadi 4.5 za swali hili. Watahiniwa

    19,454 (34.20%) walipata alama 5 hadi 9.5 na watahiniwa 3,211 (5.65%)

    walipata alama 10 hadi 15. Chati namba 13 inaonesha kufaulu kwa

    watahiniwa hawa katika asilimia.

  • 48

    Chati namba 13: Alama za watahiniwa kwa asilimia katika swali la 13

    Uchambuzi uliofanywa katika majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa,

    kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa cha wastani kwani

    watahiniwa 22,665 (39.85%) kati ya 56,876 waliofanya swali hili walipata

    kuanzia alama 5 hadi 15.

    Watahiniwa waliopata alama za juu (10 hadi 15) walielewa vema matakwa

    ya swali na walionesha kuwa na maarifa ya kutosha juu ya mada ya sheria

    katika Uislamu. Watahiniwa hawa waliweza kubainisha kazi za sheria ya

    kiislamu katika jamii kama vile: Kumlinda mwanadamu dhidi ya madhara

    yanayoweza kusababishwa na mwenendo wake mbaya, kulinda watu na

    mali zao, kuhifadhi maadili ya jamii, kuhifadhi amani na usalama, kupanga

    utaratibu namna ya kuendesha shughuli mbalimbali zenye maingiliano ya

    kijamii na kulinda na kuhifadhi dini.

    Watahiniwa 19,454 (34.20%) waliopata alama za wastani (5 hadi 9.5)

    hawakutoa ufafanuzi wa kutosha kuhusu kazi tano za sheria ya kiislamu

    ingawa walizitaja kazi hizo kwa usahihi. Baadhi ya walitaja walitaja kazi

    pungufu ya zile zilizohitajika katika swali na wengine waliandika kazi tano

    za sheria za Kiislamu huku wakizirejea hoja zao kwa maneno mbadala na

    kuziandika kama hoja mpya.

    60.2%

    34.2%

    5.6%

    0.0 - 4.5

    5.0 - 9.5

    10.0 - 15.0

    Alama

  • 49

    Watahiniwa wengine waliachanganya majibu sahihi na yasiyo sahihi ndani

    ya insha moja, kama vile: kujenga jamii mpya, kutoa hukumu ya mambo

    mbalimbali, kutatua juu ya migogoro na kuwaongoza waumini katika lengo

    la kuumbwa. Kutokana na sababu hizi, watahiniwa hawa walipata alama za

    wastani. Kielelezo namba 13.1 kinaonesha sampuli ya majibu ya mtahiniwa

    aliyejibu kwa kuzingatia matakwa ya swali.

  • 50

    Kielelezo 13.1: Sampuli ya majibu sahihi ya mtahiniwa katika swali la 13

  • 51

    Uchambuzi zaidi uliofanywa kwenye majibu ya watahiniwa unaonesha

    kuwa watahiniwa 34,211 (60.20%) walipata alama hafifu (0 hadi 4.5) kati

    yao watahiniwa 6,860 (10.20%) walipata alama 0. Watahiniwa hawa

    walijibu kinyume na matakwa ya swali, kutokana na kutokuwa na maarifa

    ya kutosha juu ya mada ya sheria katika Uislamu na kazi zake katika jamii.

    Watahiniwa hawa badala ya kuandika kazi ya sheria ya Kiislamu katika

    jamii waliandika makatazo mbalimbali ya sheria ya Kiislamu kama vile:

    sheria inakataza kuiiba, sheria inakataza kuzini, sheria inakataza kuuwa,

    sheria inakataza riba, sheria inakataza kufanya maovu. Kwa ujumla

    watahiniwa hawa walishindwa kuelewa kazi za msingi za sheria ya

    Kiislamu katika jamii. Watahiniwa wengine walieleza maamrisho ya sheria

    ya Kiislamu kama vile: kusoma Qur'an, kufunga ramadhani, kusimamisha

    swala, kutenda mema na kuwa mtiifu kwa kazi yeyote.

    Baadhi ya watahiniwa walibadilisha maudhui ya swali kutoka kazi tano za

    sheria ya Kiislamu na kuelezea kama nguzo tano za Uislamu, kwa hiyo

    walifafanua nguzo tano za Uislamu badala ya kazi za sheria ya Kiislamu

    katika jamii. Watahiniwa wengine katika kundi hili walijitunga majibu

    yasiyohusiana na mada ya sheria katika Uislamu kama vile masharti ya

    utoaji Zakat na Sadakat wakichanganya ndani yake nguzo za Uislamu, kwa

    mfano: kuwapa wanaostahiki, kutoa vilivyo halali, kwenda kuhiji makka,

    kutoa zakat na kufunga ramadhani. Kielelezo namba 13.2 kinaonesha

    sampuli ya majibu ya mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali hili kama

    ilivyotakiwa.

  • 52

  • 53

    Kielelezo 13.2: Sampuli ya majibu yasiyo sahihi ya mtahiniwa katika swali la 13

  • 54

    3.0 UCHAMBUZI WA KUFAULU KWA KILA MADA

    Mtihani wa somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa mwaka 2019 ulikuwa

    na jumla ya maswali 13 ambayo yalitungwa kutoka katika mada kumi na

    moja (11) ambazo ni: Dola ya kiislamu Madinah, Historia ya Uislamu

    Baada ya Kutawafu Mtume (s.a.w), Sunnah na Hadithi, Qur’an, Mtazamo

    wa Uislamu juu ya Dini, Familia ya Kiislamu, Mfumo wa Jamii ya

    Kiislamu, Nguzo za Uislamu, Mambo ya lazima kufanyiwa maiti wa

    Kiislamu, Sheria katika Uislamu na Nguzo za Imani.

    Mada zilizotahiniwa katika swali la kwanza ni: Dola ya Kiislamu Madinah,

    Historia ya Uislamu baada ya Kutawafu Mtume (s.a.w), Sunnah na

    Hadithi, Qur’an, Mtazamo wa Uislamu juu ya Dini, Familia ya Kiislamu,

    Sheria katika Uislamu na Nguzo za Imani ambazo kwa ujumla watahiniwa

    walifanya vizuri na kufaulu kwa asilimia 95.42.

    Uchambuzi wa takwimu wa matokeo ya watahiniwa katika mada

    mbalimbali unaonesha kuwa na kiwango cha wastani cha kufaulu katika

    mada zifuatazo: Nguzo za Uislamu (50.76%), Qur’an (47.64%), Mfumo wa

    Jamii ya Kiislamu (42.71%), Dola ya Kiislamu Madinah (36.55%), Familia

    katika Uislamu (34.20%) na Sunna na Hadithi (32.36%). Kiwango hiki cha

    kufaulu kilitokana na: Watahiniwa kujibu maswali kwa maelezo

    yasiyojitosheleza, kutotimiza idadi ya vipengele vilivyotakiwa kujibiwa

    kwenye maswali na kuchanganya majibu sahihi na yasiyo sahihi katika

    majibu yao.

    Aidha mada zilizokuwa na kiwango cha chini cha kufaulu ni: Nguzo za

    Imani (29.37%) na Mambo ya lazima kufanyiwa maiti wa Kiislamu

    (9.24%). Uchambuzi uliofanywa umebaini kuwa sababu kubwa za mada

    hizi kuwa na kiwango cha chini cha kufaulu ni watahiniwa kutokuwa na

    maarifa ya kutosha na kushindwa kuelewa matakwa ya maswali.

    Muhtasari wa uchambuzi wa kufaulu kwa watahiniwa kwa mada

    umeoneshwa kwenye kiambatisho ambapo rangi nyekundu inaonesha

    kiwango hafifu cha kufaulu, rangi ya njano inaonesha kufaulu kwa wastani

    na rangi kijani inaonesha kiwango kizuri cha kufaulu katika swali husika.

  • 55

    4.0 HITIMISHO

    Kwa ujumla kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa wa Elimu ya Dini ya

    Kiislaamu kidato cha nne mwaka 2019 ni cha wastani (43.29%).

    Uchambuzi huu umeonesha changamoto mbalimbali ambazo hazina budi

    kutatuliwa ili kuboresha kiwango cha kufaulu. Aidha changamoto

    zilizobainika ni kama vile: Watahiniwa kutofuata maelekezo ya swali hivyo

    kushindwa kutoa majibu yanayojitosheleza; Kuchanganya majibu sahihi na

    yasiyo sahihi; Kutoa maelezo yasiyojitosheleza kwa hoja sahihi walizozitoa

    na uelewa mdogo wa mada mbalimbali.

    Ili kuinua zaidi kiwango cha kufaulu kwenye mada zote katika mitihani

    ijayo jitihada zinahitajika katika ufundishaji na ujifunzaji ili kuwajengea

    watahiniwa uwezo wa kuelewa matakwa ya maswali, namna ya kuyajibu

    kwa usahihi, na kuboresha namna ya kuwasilisha hoja kwa maandishi

    katika muundo wa insha au majibu mafupi.

    5.0 MAPENDEKEZO

    Ili kuinua kiwango cha kufaulu katika somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu,

    mambo yafuatayo yanapendekezwa:

    (a) Walimu waboreshe ufundishaji wa mada kwa kuwaongoza wanafunzi

    katika vikundi kueleza namna ya kutekeleza haki za maiti Muislamu.

    (b) Walimu waboreshe ufundishaji wa mada kwa kuwaongoza wanafunzi

    kivitendo au kwa kutumia igizo kuonesha namna ya kutekeleza haki za

    maiti Muislamu.

    (c) Walimu waboreshe ufundishaji kwa kuwaongoza wanafunzi kwa

    kutumia mbinu ya maswali na majibu kueleza dhana (istilahi)

    mbalimbali za kiitikadi na kubainisha umuhimu wake.

  • 56

    6.0 Kiambatisho

    UCHAMBUZI WA KUFAULU KWA WATAHINIWA KWA MADA

    Na. Mada

    Kufaulu wa Kila

    Swali Asilimia ya wanafunzi

    waliopata wastani wa

    alama 30 au zaidi

    Maoni Nambari

    ya

    Swali

    Asilimia

    ya

    Kufaulu

    1

    Dola ya Kiislamu

    Madinah, Historia ya

    Uislamu baada ya

    Kutawafu Mtume

    (s.a.w), Sunnah na

    Hadithi, Qur’an,

    Mtazamo wa Uislamu

    juu ya Dini, Familia

    ya Kiislamu, Sheria

    katika Uislamu,

    Nguzo za Imani.

    1 95.42

    95.42

    Vizuri

    2 Nguzo za Uislamu

    2

    6

    12

    50.76 58.46 Wastani

    3 Qur’an 8

    11 47.64 48.12 Wastani

    4 Mfumo wa Jamii ya

    Kiislamu.

    4

    13 42.71 42.71 Wastani

    5 Dola ya Kiislamu

    Madinah 10 39.73 39.73 Wastani

    6 Familia katika

    Uislamu 3 34.20 34.20 Wastani

    7 Sunnah na Hadithi 9 32.36 32.36 Wastani

    8 Nguzo za Imani 5 29.37 29.37 Dhaifu

    9

    Mambo ya lazima

    kufanyiwa maiti

    Muislamu.

    7 9.24 9.24 Dhaif

    Wastani wa Jumla wa Kufaulu 43.29 Wastani