lishe na ulaji bora kwa wagonjwa wa kifua kikuucounsenuth-tz.org/sites/default/files/lishe na ulaji...

28
Lishe na Ulaji Bora kwa Wagonjwa wa Kifua Kikuu COUNSENUTH Information Series No.15 December, 2008 GLOBAL FUND ROUND 4 PROGRAM

Upload: phungminh

Post on 09-Mar-2018

358 views

Category:

Documents


13 download

TRANSCRIPT

Lishe na Ulaji Bora kwa Wagonjwa wa Kifua Kikuu

COUNSENUTHInformation Series No.15December, 2008

GLOBAL FUNDROUND 4 PROGRAM

Kitabu hiki kimetayarishwa na:Kituo cha Ushauri Nasaha, Lishe na Afya (COUNSENUTH)

S.L.P. 8218, Dar es SalaamSimu/ Nukushi: +255 222 152 705

Barua pepe: [email protected]

Sehemu yoyote ya kitabu hiki inaweza kunakiliwa kwa ajili ya matumizi yasiyo ya kibiashara ili mradi ionyeshwe kwamba maelezo hayo yametolewa toka kwenye kitabu hiki.

ISBN 978-9987-9017-8-4

© COUNSENUTH, 2008

Lishe na Ulaji Bora kwa Wagonjwa wa Kifua Kikuu

Wahariri:Dr. Lunna KyunguRestituta Shirima

Tuzie Edwin

Kimefadhiliwa na:Global Fund Round 4 Program

ii

YALIYOMO

VIFUPISHO ............................................................................................ .. iv

SHUKRANI ............................................................................................ .. vi

FARAHASA ............................................................................................ .. vii

1.0 UTANGULIZI ............................................................................................... 1

2.0 KIFUA KIKUU NI NINI? ....................................................................... ..... 2

2.1 Utangulizi ................................................................................................. ..... 2

2.2 Jinsi maambukizi ya kifua kikuu yanavyotokea

2.3 Dalili za kifua kikuu ................................................................................ ...... 2

2.4 Mambo yanayoongeza uwezekano wa kupata kifua kikuu ..................... ...... 3

3.0 UHUSIANO KATI YA KIFUA KIKUU NA UKIMWI .......................... .... 4

4. 0 UHUSIANO KATI YA LISHE NA KIFUA KIKUU ................................... 4

4.1 Utangulizi ................................................................................................. ..... 4

4.2 Athari za kifua kikuu kwenye lishe .......................................................... ..... 4

4.3 Athari za lishe kwenye kifua kikuu .......................................................... ..... 4

5.0 LISHE NA ULAJI UNAOTAKIWA KWA MGONJWA WA

KIFUA KIKUU ....................................................................................... ...... 5

5.1 Utangulizi ..................................................................................... ..... 5

5.2 Ulaji unaoshauriwa kwa mgonjwa wa kifua kikuu ....................... ..... 5

5.3 Jinsi ya kukabiliana na matatizo ya kiafya yanayompata ..................

mgonjwa wa kifua kikuu ............................................................... ................ 7

5.3.1 Kukosa hamu ya kula ......................................................... . 8

5.3.2 Kichefuchefu na kutapika .................................................. .. 9

5.3.3 Kupungua uzito ............................................................................ ...... 9

5.3.4 Upungufu wa wekundu wa damu ................................................. ..... 10

5.3.5 Homa ............................................................................................. ..... 10

5.3.6 Kuharisha ...................................................................................... ..... 11

5.3.7 Matatizo ya ngozi .......................................................................... .... 12

6.0 MATUMIZI YA DAWA NA CHAKULA................................................. ... 13

6.1 Utangulizi ...................................................................................... .... 13

6.2 Ushauri wa matumizi sahihi ya chakula na dawa ......................... ..... 14

7.0 MAMBO YA KUZINGATIA KWA MGONJWA WA

KIFUA KIKUU......................................................................................... ..... 14

8.0 BIBLIOGRAFIA ...................................................................................... ..... 15

9.0 KIAMBATANISHO: Baadhi ya virutubishi, umuhimu na vyanzo vyake .. 16

iii

VIFUPISHO

COUNSENUTH - Centre for Counselling, Nutrition and Health Care

MoHSW - Ministry of Health and Social Welfare

VVU - Virusi Vya UKIMWI

UKIMWI - Upungufu wa Kinga Mwilini

ORS - Oral Rehydration Solution

NACP - National AIDS Control Program

TB - Tuberculosis

TFNC - Tanzania Food and Nutrition Centre

SUA - Sokoine University of Agriculture

GFR4 - Global Fund Round Four

iv

SHUKRANI

Kituo cha Ushauri Nasaha, Lishe na Afya (COUNSENUTH) kinatoa shukrani

za dhati kwa Programu ya Global Fund Round Four (GFR4) kwa ufadhili wake

ambao umewezesha kitabu hiki kutayarishwa na kutolewa.

COUNSENUTH inapenda kuwatambua wafuatao ambao walishiriki kutoa

msaada wa kitaalam wakati wa kutayarisha kitabu hiki: Dr. Grace Magembe

(Manispaa ya Ilala), Dr. Saul Nkya (TFNC), Toligwe Kaisi (SUA), Justine

Kiondo (St. Augustine University), Restituta Shirima (COUNSENUTH), Dr.

Lunna Kyungu (COUNSENUTH), Mary Materu (COUNSENUTH) na Tuzie

Edwin (COUNSENUTH). Shukrani pia kwa mashirika mbalimbali na watu

wote walioshiriki kutoa maoni yao katika kutayarisha na kukamilisha kitabu

hiki. Shukrani za dhati kwa Donald Navetta kwa kuhariri kitabu hiki.

v

FARAHASA

Asusa: Kiasi kidogo cha chakula ambacho sio mlo kamili, kinachoweza kuliwa bila matayarisho makubwa. Mara nyingi huliwa kati ya mlo mmoja na mwingine.

Chakula: Kitu chochote kinacholiwa na kuupatia mwili virutubishi.

Kafeini: Kiini kilichoko kwenye vinywaji kama vile chai, kahawa na soda ambavyo huchangamsha mwili; lakini huweza kuathiri ufanisi wa baadhi ya virutubishi mwilini.

Lishe: Sayansi ya jinsi mwili unavyokitumia chakula. Lishe inahusisha jinsi mwili unavyosaga, unavyoyeyusha chakula na hatimaye virutubishi kufyonzwa na kutumika mwilini.

Mlo kamili: Mlo unaotokana na mchanganyiko wa angalau chakula kimoja kutoka katika makundi mbalimbali ya vyakula.

Nishati-lishe: Nguvu inayouwezesha mwili kufanya kazi mbalimbali.

Nyuzi-nyuzi: Aina ya kabohaidreti ambayo mwili hauwezi kuyeyusha. Hupatikana kwenye matunda, mboga-mboga na nafaka

zisizokobolewa. Nyuzi-nyuzi pia hujulikana kama makapi-mlo.

Ulaji bora: Hutokana na kula chakula mchanganyiko na cha kutosha. Ikiwa ni pamoja na kutumia mafuta, chumvi na sukari kwa

kiasi.

Utapiamlo: Hali ya kupungua au kuzidi kwa virutubisho mwilini.

Vimelea: Vijidudu au viumbe vidogo sana ambavyo havionekani kwa macho.

Virutubishi: Viini vilivyoko kwenye vyakula ambavyo mwili hutumia kufanya kazi mbalimbali.

1

1.0 UTANGULIZI

Katika Afrika ugonjwa wa kifua kikuu ndio chanzo cha vifo vingi zaidi vinavyotokea kutokana na maambukizi yanayoweza kutibika. Inakadiriwa kuwa karibu theluthi moja ya watu duniani wameambukizwa vimelea vinavyosababisha ugonjwa wa kifua kikuu. Katika Tanzania inakadiriwa kuwa zaidi ya watu 50,000 wanaugua kifua kikuu kila mwaka; kati ya hao, zaidi ya asilimia 25 wapo mkoa wa Dar es Salaam.

Utapiamlo ni tatizo kubwa kwa wagonjwa wa kifua kikuu. Pamoja na ukubwa wa tatizo hilo, hakuna taarifa za kutosha kuhusu jinsi ya kumhudumia na kukabiliana na matatizo yanayompata mgonjwa wa kifua kikuu kilishe. Hali nzuri ya lishe husaidia dawa kufanya kazi kwa ufanisi na kuboresha kinga ya mwili.

Madhumuni ya kitabu hiki ni kutoa maelezo muhimu kuhusu lishe na ulaji bora kwa mgonjwa wa kifua kikuu.

Kitabu hiki kinajumuisha taarifa kuhusu uhusiano kati ya ugonjwa wa kifua kikuu na lishe, lishe na ulaji unaoshauriwa kwa mgonjwa wa kifua kikuu na jinsi ya kukabiliana na matatizo mbalimbali yanayompata mgonjwa wa kifua kikuu.

Walengwa wa kitabu hiki ni watoa huduma za afya, watoa huduma katika ngazi ya jamii ikijumuisha watoa huduma majumbani; wagonjwa wa kifua kikuu na jamii kwa ujumla.

Ni matumaini yetu kuwa taarifa zilizomo katika kitabu hiki zitakuwa ni msaada mkubwa katika kuboresha matunzo na huduma kwa wagonjwa wa kifua kikuu.

2

2.0 KIFUA KIKUU NI NINI?

2.1 UtanguliziKifua kikuu ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na vimelea vya bakteria ajulikanae kama Mycobacterium tuberculosis. Kifua kikuu kwa kawaida kinaathiri mapafu, lakini huweza kuathiri pia sehemu nyingine za mwili kama uti wa mgongo, mifupa, moyo, ubongo na figo.

2.2 Kifua kikuu kinavyoambukizaKifua kikuu huambukizwa kwa njia ya hewa. Mtu mwenye uambukizo wa kifua kikuu ambaye bado hajaanza matibabu akikohoa, kupiga chafya, kuongea, kuimba au hata kucheka, vimelea vya kifua kikuu husambaa hewani na huweza kumuathiri mtu aliye karibu naye anapovuta hewa yenye vimelea hivyo. Baada ya vimelea vya kifua kikuu kuingia mwilini, mambo matatu huweza kutokea ambayo ni:

i. Uambukizo ambao hauonyeshi daliliMara nyingi vimelea vya kifua kikuu vikiingia katika mwili wa mtu aliye na hali nzuri ya lishe na afya, kinga ya mwili huweza kuviangamiza au kuvizuia vimelea hivyo kuzaliana. Hali hii ya uambukizo huweza kuonyesha dalili kidogo za muda mfupi au kutoonyesha dalili zozote kwani uambukizo unakuwa umezuiwa. Hali hii ya uambukizo ndio hutokea kwa watu wengi.

ii. Uambukizo unaoendelea na kusababisha kifua kikuuUambukizo wa aina hii hutokea pale ambapo kinga ya mwili hushindwa kupambana na vimelea vya kifua kikuu vilivyoingia mwilini. Vimelea hivyo huzaliana na kuenea sehemu mbalimbali za mwili. Dalili huanza kujionyesha katika kipindi cha wiki sita hadi nane baada ya uambukizo.

Mara nyingi uambukizo wa aina hii hutokea kwa watu ambao hali zao za lishe na afya ni duni; kwa mfano watoto wachanga, watoto au watu wazima wenye utapiamlo na watu ambao kinga yao ya mwili imepungua.

iii. Uambukizo unaojitokeza baadaye Uambukizo wa aina hii hutokea baada ya miezi au miaka michache baada ya kupata uambukizo ambao haukuonyesha dalili. Vimelea vya kifua kikuu huweza kuendelea kuishi bila ya kuzaliana na bila athari yoyote mwilini kwa muda mrefu. Kinga ya mwili inapodhoofika kwa sababu mbalimbali, vimelea huanza kuzaliana na kusababisha ugonjwa wa kifua kikuu.

3

Walio katika uwezekano mkubwa wa kupata aina hii ya uambukizo ni watu:

• walioambukizwavirusivyaUKIMWI(VVU);• wenyeutapiamlo;• wazee;• dhaifu;• wenyeugonjwawakisukari;• wenyematatizoyafigo;• wenyesaratanikamavilesarataniyadamu;• wanaotumia dawa za kuongeza nguvu (steroid) au dawa zinazo

punguza kinga ya mwili;• wanaovutasigara;na• walevi.

2.3 Dalili za kifua kikuuDalili za kifua kikuu hutegemea vimelea hivyo vimeathiri sehemu gani za mwili. Dalili kuu za kifua kikuu ni pamoja na:

• Kukohoamfululizozaidiyawikimbili;• Kukohoamakohoziyenyemchanganyikonadamu;• Kupunguauzito/kukonda;• Maumivuyakifuanakupumuakwashida;• Homazajionizaidiyawikimbilizinazoambatananakutokwana

jasho jingi usiku;• Kujisikiauchovumarakwamara;• Kukosahamuyakula;na• Uvimbe au maumivu katika kiungo kilichoathirika iwapo kifua

kikuu si cha mapafu.

2.4 Mambo yanayoongeza uwezekano wa kupata kifua kikuu• Utapiamlo;• UpungufuwavitaminiD;• MaambukiziyaVVU;• Kuishinamgonjwawakifuakikuuambayehajaanzamatibabu;

KUMBUKA:Mtu mwenye kifua kikuu anaweza kuwa na dalili kama za maradhi mengine.

4

• Kuwanakisukariambachohakidhibitiwisawasawa;• Kupunguakwakingayamwili;• Kuvutahewayamoshiausigara;na• Baadhiyasarataninamatibabuyake.

3.0 UHUSIANO KATI YA KIFUA KIKUU NA VVU

Kifua kikuu ndio ugonjwa nyemelezi unaojitokeza zaidi kwa watu walioambukizwa VVU. Maambukizi ya VVU hupunguza kinga ya mwili na hivyo kufanya mwili uwe katika hatari zaidi ya kushambuliwa na maradhi mbalimbali ikiwemo kifua kikuu.

Kuwepo kwa maambukizi ya VVU kumechangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa wagonjwa wa kifua kikuu kwani idadi ya watu waliopata maambukizi ya VVU pia wameambukizwa kifua kikuu.

Ugonjwa wa kifua kikuu na UKIMWI vinapojitokeza kwa pamoja, huathiri afya kwa kiasi kikubwa. Iwapo maradhi hayo hayatakabiliwa kikamilifu, mgonjwa huweza kupoteza maisha.

4. 0 UHUSIANO KATI YA LISHE NA KIFUA KIKUU

4.1 UtanguliziHali ya lishe ya mtu huchangia kwa kiasi kikubwa uwezo wa mwili kupambana na maambukizi mbalimbali. Hali duni ya lishe huweza kusababisha kupungua kwa kinga ya mwili na hivyo kuongeza uwezekano wa mtu kupata maradhi ikiwemo kifua kikuu.

KUMBUKA:• Dalili za kifua kikuu na zile za maambukizi ya VVU huweza

kufanana, hivyo ni muhimu kuchunguza afya katika kituo cha tiba.

• KumbukasiokilamgonjwawakifuakikuuanamaambukiziyaVVU

5

4.2 Athari za ugonjwa wa kifua kikuu kwenye lisheVimelea vya kifua kikuu vinapoanza kuzaliana mwilini, mahitaji ya virutubishi huongezeka na hivyo huweza kusababisha uzito wa mwili kupungua hata kabla ya mtu kugundua kama ana ugonjwa wa kifua kikuu. Wakati huo huo, dalili zinazojitokeza kwa mgonjwa wa kifua kikuu kama vile kukosa hamu ya kula, kutapika, homa na kukohoa huchangia mtu huyu kushindwa kukidhi ongezeko la mahitaji ya virutubishi mwilini. Vilevile, kutokana na mabadiliko yanayotokea mwilini, ufanisi wa matumizi ya virutubishi kama vile protini huweza kupungua. Ulaji duni, ongezeko la mahitaji ya virutubishi na kupungua kwa ufanisi wa utumikaji wa virutubishi huweza kusababisha utapiamlo.

4.3 Athari za lishe duni kwenye kifua kikuuMtu mwenye utapiamlo yupo katika hatari zaidi ya kupata uambukizo wa kifua kikuu kwani kinga yake ya mwili ni dhaifu. Endapo mtu alipata uambukizo ule ambao haonyeshi dalili, wakati hali yake ya lishe na afya ni thabiti, akipata utapiamlo vimelea hivyo huanza kuzaliana na hivyo huweza kusababisha kuugua kifua kikuu.

Utapiamlo kwa mgonjwa wa kifua kikuu husababisha kurefusha kipindi cha kuugua, mwili hudhoofika zaidi, kushindwa kukabiliana na matatizo ya kiafya yanayoambatana na ugonjwa wa kifua kikuu na pia ufanisi wa matibabu huweza kupungua.

5.0 LISHE NA ULAJI UNAOSHAURIWA KWA MGONJWA WA KIFUA KIKUU

5.1 UtanguliziMatibabu ya ugonjwa wa kifua kikuu yazingatie ulaji bora ambao unaojumuisha kula vyakula mbalimbali. Mgonjwa wa kifua kikuu anahitaji msaada wa jinsi ya kukabiliana na matatizo ya kiafya yanayojitokeza ambayo yanachangia kuwa na ulaji duni. Matatizo yanayoweza kujitokeza ni kama vile kukosa hamu ya kula, kichefuchefu, kutapika, kupungua uzito, homa, kuharisha, upungufu wa wekundu wa damu na matatizo ya ngozi. Matatizo

6

hayo huweza kuingilia ulaji na uyeyushwaji wa chakula na pia ufyonzwaji wa virutubishi.

5.2 Ulaji unaoshauriwa kwa mgonjwa wa kifua kikuuUshauri wa lishe hutolewa ili kukabiliana na matatizo mbalimbali yanayojitokeza wakati wa ugonjwa wa kifua kikuu. Mgonjwa yeyote wa kifua kikuu anashauriwa kufanya yafuatayo:

• Kula mlo kamili angalau mara tatu kwa siku. Mlo kamilihutayarishwa kutokana na mchanganyiko wa angalau chakula kimoja kutoka katika makundi ya chakula yafuatayo:• Nafaka,mizizinandizi;• Jamiiyakundenaasiliyawanyama;• Mboga-mboga;• Matunda;na• Mafutanasukari.

• Kulavyakulavinavyoupatiamwilinguvu(nishati-lishe)kwawingiili kuzuia kupungua uzito, kuongeza nguvu na kusaidia kupona haraka. Vyakula vyenye nishati-lishe kwa wingi ni pamoja na mahindi, mtama, uwele, mchele, ngano, viazi aina zote, mihogo, magimbi na ndizi za kupikwa. Vyakula vingine ni mafuta ya alizeti, mawese, mbegu zitoazo mafuta, siagi, majarini, maziwa, jibini, asali na sukari.

• Kula vyakula vyenye protini kwa wingi ili kusaidia kujenga

misuli, kukarabati mwili na kuimarisha mfumo wa kinga. Vyakula vyenye protini kwa wingi ni kama maharagwe, choroko, njegere, kunde, dengu, njugu mawe, karanga, korosho, aina zote za nyama, samaki, mayai na maziwa.

• Kulamatundanamboga-mbogakwawingiilikupatavitamininamadini kwa ajili ya kuwezesha kupona haraka na kuboresha kinga ya mwili.

KUMBUKA:Ni muhimu kujenga tabia ya kula mlo kamili ikiwa ni pamoja na kula matunda na mbogamboga kiasi cha kutosha katika kila mlo.

7

• Kula vyakula vyenye Vitamini B6 kwa wingi kama vile viazivitamu, maharagwe, mahindi yasiyokobolewa, parachichi, nyama na samaki kwani baadhi ya dawa za kutibu kifua kikuu huingilia matumizi ya vitamini hiyo mwilini.

• Kulavyakulavyenyemadinichumakwawingiilikuzuiaupungufuwa wekundu wa damu. Vyakula vyenye madini chuma kwa wingi ni kama maini, dagaa, figo, nyama, samaki, mbaazi, maharagwe, korosho, choya (rozela), kisamvu, majani ya kunde, matembele na mchicha.

• KulavyakulavyenyeVitaminiAkwawingi ili kuboresha mfumo wa kinga na kuzuia matatizo ya ngozi. Vyakula vyenye Vitamini A kwa wingi ni kama vile maini, mawese, samaki wenye mafuta, kisamvu, matembele, majani ya kunde, maboga, karoti, papai, embe na viazi vitamu vyenye rangi ya manjano.

• KulavyakulavyenyeVitaminiDkwawingikamavilenyama,samaki, mafuta ya samaki na maziwa. Vilevile, Vitamini D hupatikana kwenye jua. Upungufu wa vitamini hii huweza kufanya hali ya mgonjwa kuwa mbaya zaidi.

5.3 Jinsi ya kukabiliana na matatizo mbalimbali ya kiafya yanayompata mgonjwa wa kifua kikuu

Matatizo mbalimbali ya kiafya yanayompata mgonjwa wa kifua kikuu huweza kukabiliwa kilishe. Kufuata ulaji unaoshauriwa kutaimarisha kinga ya mwili na kuepusha mwili kudhoofika. Matatizo ya kiafya yanayoweza kumpata mgonjwa wa kifua kikuu ni pamoja na kukosa hamu ya kula, kupungua uzito, homa, kuharisha, upungufu wa wekundu wa damu na matatizo ya ngozi.

8

5.3.1 Kichefuchefu na kutapikaKichefuchefu hupunguza hamu ya kula na huweza kusababisha kutapika. Ili kupunguza kichefuchefu na kutapika, mgonjwa wa kifua kikuu anashauriwa kufanya yafuatayo:

- Kuepuka kula vyakula vyenye viungo vingi, mafuta mengi au sukari nyingi kwani vyakula hivyo huongeza kichefuchefu.

- Kula vyakula vikavu na vyenye chumvi kidogo kama mkate, muhogo, ndizi au kiazi cha kuchoma au kuchemsha.

- Kunywa maji mengi na vinywaji vingine kama vile maziwa, togwa, juisi ya matunda halisi, madafu na supu ili kuongeza kiasi cha maji mwilini.

- Kunywa juisi ya limau au ndimu iliyochanganywa na maji ya moto.

- Kula vyakula vilivyochachushwa kama mtindi na togwa.

- Kula milo midogo midogo mara kwa mara yaani si chini ya mara tano kwa siku.

- Kula taratibu.- Kula akiwa amekaa wima au amejiegemeza

kidogo kwenye mto. Aepuke kujilaza mara tu baada ya kula.

- Kuepuka kukaa muda mrefu bila kula au kunywa chochote.

5.3.2 Kukosa hamu ya kulaMgonjwa wa kifua kikuu anapokosa hamu ya kula anashauriwa kufanya yafuatayo:

- Kuongeza viungo kidogo, kama kitunguu saumu, tangawizi, limau, ndimu, mdalasini, kotimiri au iliki kwenye vinywaji au vyakula mbalimbali. Mara nyingi viungo husaidia kuongeza ladha ya chakula na hivyo kuongeza hamu ya kula.

9

- Kuepuka kutayarisha vyakula mwenyewe au kukaa jikoni au karibu na jiko, kwani harufu ya vyakula huweza kupunguza hamu ya kula.

- Kuepuka kunywa maji au vinywaji vingine wakati wa kula kwani hii itasababisha tumbo kujaa haraka.

- Kuongeza vyakula kama vile karanga, maziwa au mafuta kwenye vyakula mbalimbali ili kuviboresha na kuvifanya viwe rahisi kumeza. Vyakula hivi viongezwe kwa kiasi kidogo, kwani vikitumika kwa kiasi kikubwa huweza kusababisha kuharisha.

- Kubadili ladha na aina ya vyakula, kwani mtu anapokula vyakula vya aina mbalimbali na vyenye ladha tofauti hamu ya kula huongezeka. Mbinu mbalimbali za kupika kama kuchemsha, kupika kwa mvuke kutokosa, kuchoma na kubanika zikitumika huweza pia kusaidia.

- Kunywa vinywaji vilivyo bora na kula vyakula anavyovipenda. Pale inapowezekana mgonjwa asile peke yake, ale pamoja na familia au marafiki.

- Kufanya mazoezi mbalimbali kwani husaidia kuongeza hamu ya kula na uyeyushwaji wa chakula tumboni. Hata hivyo aina ya mazoezi hutegemea hali ya mgonjwa.

- Kula milo midogo midogo mara nyingi kwa siku.- Iwapo njia zote zilizoshauriwa hazitasaidia, inabidi mgonjwa

ajilazimishe kula kwani chakula ni muhimu sana.

5.3.3 Kupungua uzito Ili kukabiliana na tatizo la kupungua uzito inashauriwa ifuatavyo:

- Kuongeza kiasi cha chakula, idadi ya milo kwa siku pamoja na kula vyakula vya aina mbalimbali.

- Kuboresha chakula kwa kuongeza vyakula kama karanga, mafuta, siagi, maziwa, sukari au asali, kwani vyakula hivi vina nishati-lishe kwa wingi.

- Kutumia asusa mara kwa mara kati ya mlo na mlo. Asusa zinazoweza kutumika ni kama karanga, matunda, mtindi, uji ulioboreshwa, andazi, sambusa, chapati, kitumbua, muhogo, kiazi au ndizi.

- Kuongeza kiasi kidogo cha viungo katika chakula ili kuongeza hamu ya kula na kusaidia uyeyushwaji wa chakula.

10

- Kutumia vyakula vilivyochachushwa kama maziwa ya mgando na togwa kwani vyakula hivyo huyeyushwa kwa urahisi na husaidia uyeyushwaji wa vyakula vingine na ufyonzwaji wa virutubishi mwilini.

- Kuepuka kunywa maji mengi kabla tu au wakati wa kula kwani huweza kujaza tumbo na hivyo kumfanya mgonjwa kushindwa kula chakula cha kutosha.

- Kufanya mazoezi kwani husaidia kuongeza hamu ya kula na kujenga misuli. Aina ya mazoezi hutegemea hali ya mgonjwa.

5.3.4 Upungufu wa wekundu wa damuUpungufu wa wekundu wa damu huweza kukabiliwa kwa kufanya yafuatayo:

- Kula vyakula vyenye madini chuma kwa wingi, kama vile maini, samaki, dagaa, figo, nyama, kisamvu, matembele, majani ya kunde, mchicha, choya, maharagwe, choroko, njegere, kunde, dengu, njugu mawe, na korosho.

- Kula matunda kwa wingi pamoja na mlo, hasa yale yenye Vitamini C kwa wingi kama vile mapera, machungwa, machenza, mapesheni, mananasi, mabungo, ubuyu na ukwaju. Vitamini C husaidia ufyonzwaji na utumikaji wa madini chuma yaliyoko kwenye vyakula vyenye asili ya mimea.

- Kuepuka vinywaji kama chai, kahawa au soda wakati wa mlo, kwani vina kemikali iitwayo kafeini ambayo huzuia upatikanaji wa madini chuma yaliyoko kwenye vyakula vyenye asili ya mimea. Iwapo italazimu kutumia vinywaji hivyo ni vema kuvitumia saa moja kabla au saa moja baada ya kula chakula na si wakati wa kula.

- Kutibu maradhi kama vile malaria na minyoo mapema

KUMBUKA:Mtu mwenye kifua kikuu anashauriwa kupima uzito mara kwa mara ili kufuatilia maendeleo yake na kuchukua hatua inayofaa.

11

kwani huchangia kuleta upungufu wa wekundu wa damu.- Kumuona daktari kwa ushauri zaidi ikiwa ni pamoja na kupewa

vidonge vya madini chuma na foliki asidi ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa wekundu wa damu.

5.3.5 HomaMtu anapokuwa na homa anashauriwa yafuatayo:

- Kunywa maji safi na salama na vinywaji vilivyo bora kwa wingi mara kwa mara ili kusaidia kupunguza joto la mwili na kurudishia maji yanayopotea.

- Kula milo midogo midogo mara nyingi ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya virutubishi mwilini linalosababishwa na homa.

- Kuoga maji ya uvuguvugu na kupunguza nguo nzito mwilini.- Kumuona daktari kwani homa huashiria kuwepo kwa tatizo fulani

mwilini.

5.3.6 KuharishaIli kukabiliana na tatizo la kuharisha, mgonjwa anashauriwa kufanya yafuatayo:

- Kunywa maji safi na salama kwa wingi (zaidi ya lita moja na nusu) ili kuzuia upungufu wa maji mwilini.

- Kunywa vinywaji kama, madafu, togwa, supu, maji ya matunda na supu ya mchele.

- Kutumia mchanganyiko maalum wa maji, sukari na chumvi yaani “Oral Rehydration Solution” (ORS).

- Kuongeza vitunguu saumu kiasi kwenye vinywaji vya moto kama vile supu na vinginevyo.

- Kula matunda kama ndizi mbivu, tikiti maji na mboga-mboga zilizopikwa ambazo hazina nyuzi-nyuzi nyingi kama karoti na maboga ili kurudisha madini na vitamini zinazopotea kutokana na kuharisha.

- Kula milo midogo midogo mara nyingi kwa siku ili kurudisha virutubishi vinavyopotea na kumwezesha kukidhi mahitaji ya mwili kilishe.

- Kutafuna chakula mpaka kilainike au kula vyakula laini ili kurahisisha uyeyushwaji na hivyo upatikanaji wa virutubishi.

12

- Kutumia maziwa ya mgando au togwa kwani huyeyushwa kwa urahisi na huweza kupunguza kuharisha.

- Kuzingatia kanuni bora za afya ikiwa ni pamoja na usafi na usalama wa chakula na maji.

Vyakula ambavyo mtu anapaswa kuviepuka wakati wa tatizo la kuharisha ni:

- Vyakula vyenye mafuta mengi, viungo vingi au pilipili nyingi kwani vimeonekana kuzidisha tatizo la kuharisha

- Matunda yasiyoiva vizuri au yenye uchachu mkali kama embe, nyanya, chungwa, chenza, au limau kwani wakati mwingine huweza kuongeza kuharisha.

- Chai, kahawa na soda, kwani vina kafeini ambayo husababisha upotevu zaidi wa maji.

- Pombe kwani huzuia uyeyushwaji na ufyonzwaji wa baadhi ya virutubishi na huongeza upotevu wa maji mwilini.

- Vyakula vyenye nyuzi-nyuzi kwa wingi, kama nafaka zisizokobolewa, vyakula vya jamii ya kunde, matunda kama vile papai, embe, parachichi; na mboga-mboga kama vile kabichi, mchicha na matembele. Vyakula hivi huweza kuzidisha tatizo la kuharisha.

5.3.7 Matatizo ya ngoziBaadhi ya matatizo ya ngozi huweza kusababishwa na upungufu wa baadhi ya vitamini hasa Vitamini A na Vitamini B6. Ulaji wa vyakula vyenye Vitamini A au Vitamini B6 kwa wingi huweza kupunguza au kuzuia maradhi hayo, hata hivyo matibabu huweza kuhitajika.

KUMBUKA:Tatizo la kuharisha linapoisha mgonjwa anashauriwa kuendelea kula kama kawaida.

13

Mgonjwa mwenye matatizo ya ngozi anashauriwa kufanya yafuatayo:• KulavyakulavyenyeVitaminiAkwawingikamavilemawese,

maini, kisamvu, matembele, mayai, maziwa, papai, embe na karoti.

Kumbuka kuongeza mafuta wakati wa utayarishaji wa vyakula ili kusaidia ufyonzwaji na upatikanaji wa Vitamini A mwilini.

• Kula vyakula vyenye Vitamini B6 kwa wingi kama vilemaharagwe, mboga za kijani, karanga, mahindi yasiyokobolewa, nyama, samaki, viazi vitamu na parachichi.

5.3.8 Kupumua kwa shidaMgonjwa anashauriwa kufanya yafuatayo:

• Kuongezatangawizinavitunguusaumukatikachakulanavinywajimbalimbali vya moto.

• Kutumiavitunguusaumuvilivyopondwatembetanohadisitakwasiku.

• Kujikanda kifuani kwa kutumia maji yaliyochemshwa natangawizi. Usimkande mtu ambaye ni dhaifu sana au mwenye homa kali.

6.0 MATUMIZI YA DAWA NA CHAKULA

6.1 UtanguliziChakula na dawa huweza kuwa na mwingiliano ambao huwa na faida au hasara. Chakula huweza kuingilia usharabu wa dawa tumboni, usambazwaji wake na pia utoaji wa mabaki ya dawa mwilini. Baadhi ya vyakula huweza kuboresha usharabu na namna dawa inavyofanya kazi na vingine huweza kupunguza.

Kwa upande mwingine, baadhi ya dawa huweza kuingilia usharabu wa virutubishi, matumizi ya virutubishi mwilini na utoaji mabaki mwilini. Tatizo hili linaweza kukabiliwa kwa kuepuka au kupunguza aina ya chakula kinachoingiliana na dawa

14

hiyo mwilini, kuongeza kiasi cha chakula au kutumia virutubishi vya nyongeza ili kuongeza kiwango cha aina ya virutubishi vinavyoathiriwa na dawa hiyo.

Baadhi ya athari zitokanazo na dawa huweza kumfanya mgonjwa ashindwe kula chakula cha kutosha, pia kudhoofisha usharabu wa virutubishi mwilini. Kwa mfano, baadhi ya dawa husababisha kichefuchefu, mabadiliko ya ladha, kukosa hamu ya kula, kutapika n.k.

6.2 Ushauri wa matumizi sahihi ya chakula na dawaMgonjwa anapaswa kuzingatia yafuatayo:

• Kupanga utaratibu wa kumeza dawa na kula chakula kwakuzingatia maelekezo yaliyotolewa na mtaalamu wa afya kuhusu matumizi ya dawa na chakula ili kuepuka kuathiri matibabu na hali ya lishe ya mgonjwa.

• Kuendeleakumezadawakamaalivyoelekezwanamtaalamuwaafya, hata kama amepata nafuu.

• Kutumiamajikumezeadawanasikutumiavinywajikamajuisi,soda, chai au kahawa.

• Kuepukakutumiachaiaukahawamudamfupibaadayakumezadawa.

• Kunywamajisafinasalamakwawingiangalauglasi8kwasikuili kuondoa mabaki yatokanayo na dawa mwilini.

• Kukabiliananaatharizinazowezakusababishwanamatumiziyadawa kama vile kichefuchefu, kutapika, kuharisha, n.k. Rejea kipengele cha Tano ya kitabu hiki kuhusu jinsi ya kukabiliana na athari hizo.

KUMBUKA:• Dawailiyoelekezwakumezwakablayakulachakulaimezwesaa

moja kabla ya kula au saa mbili baada ya kula.• Mudawakumezadawaugawanywekatikasikunzimaambayoni

saa 24. Kwa mfano, dawa iliyoelekezwa kumezwa mara tatu kwa siku, imezwe kila baada ya saa 8; na ile iliyoelekezwa kumezwa mara mbili kwa siku, imezwe -kila baada ya saa 12. Hali kadhalika, dawa iliyoelekezwa kumezwa mara nne kwa siku, imezwe kila baada ya saa 6.

15

• Kuepukamatumiziyapombe,tumbakunabidhaazakenamadawaya kulevya.

• Kumuonamtaalamuwaafyaiwapoatharizitokanazonamatumiziya dawa zitazidi.

7.0 MAMBO YA KUZINGATIA KWA MGONJWA WA KIFUA KIKUU

• Kupatamatibabusahihikutokakatikakituochatibanakutimizamasharti yote aliyopewa na mtaalam wa afya;

• Kulamlokamili;• Kufuata ulaji unaoshauriwa wakati wa matatizo mbalimbali ya

kiafya;• Kupatamudawakupumzika;• Kujenga tabia ya kutafuta taarifa kuhusu afya kwa kusoma

vijarida, kusikiliza redio na kuhudhuria vipindi vya elimu ya afya katika kituo cha huduma au katika jamii; na

• Kuepukamatumiziyapombenasigara.

8.0 BIBLIOGRAFIA

COUNSENUTH; Lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI; Kitabu cha Mafunzo na Rejea, 2004

COUNSENUTH and APHFTA; Ulaji na Mtindo Bora wa Maisha: Kitabu cha Wanafunzi wa Shule za Msingi , 2008

Ministry of Health and Social Welfare; Manual of the National Tuberculosis and Leprosy Programme in Tanzania, 2006

NACP; Kifua Kikuu na UKIMWI: Ujumbe Muhimu kwa Jamii, Dar –es-Salaam 2008

PATH TB/HIV Project; Kifua Kikuu/UKIMWI Mahali Po Pote Pale ni Kifua Kikuu/UKIMWI Kila Mahali

Ramakrishna Mission Tuberculosis Sanatorium; The Role of Nutrition in Tuberculosis, 2007

USAID –Africa’s Health in 2010; Nutrition and Tuberculosis: A Review of the Literature and Considerations for TB Control Programs, USAID, Washington 2008

Wizara ya Afya; Mwongozo wa Matibabu ya Wagonjwa wa Kifua Kikuu Majumbani, 2005

Wizara ya Afya; Kifua Kikuu (TB) ni Ugonjwa Hatari: Fahamu Ukweli Kuhusu Kifua Kikuu

16

Ain

aU

muh

imu

BA

AD

HI

YA

VIR

UT

UB

ISH

I, U

MU

HIM

U N

A V

YA

NZ

O V

YA

KE

9.0

VIA

MB

AT

AN

ISH

O

Hup

atik

ana

kwa

win

gi k

wen

ye:

Kab

ohai

dret

i

Vita

min

i B2

Vita

min

i B1

Prot

ini

Maf

uta

Vita

min

i A

Mah

indi

, mch

ele,

nga

no, u

wel

e, m

tam

a,

ulez

i, ai

na z

ote

za v

iazi

, mih

ogo,

mag

imbi

, nd

izi,

asal

i, su

kari

Maz

iwa,

nya

ma,

mbo

ga z

a ki

jani

, naf

aka

zi-

sizo

kobo

lew

a, s

amak

i, m

ahar

agw

e, k

aran

ga,

koro

sho

Naf

aka,

mah

arag

we,

nya

ma,

sam

aki,

kuku

, m

ayai

, kar

anga

, kor

osho

Ain

a zo

te z

a ny

ama,

ain

a zo

te z

a m

ikun

de,

sam

aki,

daga

a, w

adud

u, m

aziw

a, ji

bini

, may

ai

Siag

i, m

afut

a ya

sam

aki,

sam

li, m

afut

a ya

ny

ama,

mbe

gu z

itoaz

o m

afut

a ka

ma

kara

nga,

al

izet

i, m

awes

e, u

futa

, kw

eme,

kor

osho

, m

begu

za

mab

oga

Mai

ni, m

boga

za

kija

ni, f

igo,

may

ai, s

amak

i, jib

ini,

siag

i, vi

azi v

itam

u (h

asa

vya

man

jano

),

mab

oga,

kar

oti,

maw

ese

na m

atun

da h

asa

yeny

e ra

ngi y

a m

anja

no a

u ny

ekun

du k

ama

papa

i na

embe

Huu

pa m

wili

ngu

vu z

a ku

fany

a ka

zi n

a jo

to

linal

otak

iwa

Hus

aidi

aum

etab

oli w

a ni

shat

i-lis

he, h

usai

dia

mac

ho k

uona

viz

uri n

a hu

bore

sha

ngoz

i

Hus

aidi

a um

etab

oli w

a ni

shat

i-lis

he m

wili

ni, h

uong

eza

ham

u ya

kul

a na

hus

aidi

a m

fum

o w

a fa

ham

u

Uku

aji w

a m

wili

na

kute

ngen

eza

vim

eng’

enyo

, vi

choc

heo

na s

eli z

a m

wili

Huu

pa m

wili

ngu

vu, j

oto

na k

usai

dia

uyey

ushw

aji n

a us

hara

bu w

a ba

adhi

ya

viru

tubi

shi

Uku

aji w

a ak

ili n

a m

wili

, hui

mar

isha

che

mbe

ch

embe

za

king

a ya

mw

ili n

a hu

said

ia m

acho

ku

ona

vizu

ri

17

Vita

min

i B3

Vita

min

i D

Vita

min

i E

Mad

ini C

hum

a

Vita

min

i B6

Vita

min

i B12

Vita

min

i C

Maz

iwa,

may

ai, n

yam

a, k

uku,

kar

anga

, sa

mak

i, m

ahar

agw

e, n

afak

a zi

sizo

kobo

lew

a

Kiin

i cha

yai

, sam

aki h

asa

wen

ye m

afut

a,

maz

iwa,

sia

gi n

a m

ionz

i ya

jua

Mbo

ga z

a ki

jani

, maf

uta

yato

kana

yo n

a m

imea

, mai

ni, k

iini c

ha y

ai n

a ai

na n

ying

ine

za m

boga

-mbo

ga

Nya

ma

nyek

undu

, sam

aki,

may

ai, a

ina

za

mik

unde

kam

a ka

rang

a, m

ahar

agw

e, b

aadh

i ya

mat

unda

yal

iyok

aush

wa,

mbo

ga z

a m

ajan

i za

kija

ni n

a ba

adhi

ya

nafa

ka

Via

zi v

itam

u, m

ahar

agw

e, m

ahin

di,

para

chic

hi, n

yam

a, s

amak

i, ka

bich

i

Nya

ma,

sam

aki,

kuku

, jib

ini,

may

ai, m

aziw

a,

vyak

ula

viliv

yoch

achu

shw

a (f

erm

ente

d)

kam

a m

tindi

na

togw

a

Map

era,

mac

hung

wa,

nya

nya,

ukw

aju,

m

alim

au, n

dim

u, m

ache

nza,

mad

alan

si,

ubuy

u, k

arak

ara

(pes

heni

), m

abun

go, n

a ai

na

nyin

gine

za

mat

unda

Hub

ores

ha n

gozi

, hus

aidi

a ka

tika

umet

abol

i wa

nish

ati-

lishe

, mfu

mo

wa

chak

ula

na f

aham

u

Huw

ezes

ha u

fyon

zwaj

i wa

mad

ini y

a ch

okaa

na

fosf

oras

i. H

utum

ika

katik

a ku

teng

enez

a m

ifup

a na

men

o. H

uim

aris

ha m

fum

o w

a fa

ham

u na

hu

wez

esha

moy

o ku

fany

a ka

zi v

izur

i.M

uhim

u ka

tika

king

a ya

mw

ili n

a ka

tika

kute

ngen

eza

na u

kuaj

i wa

seli

za m

wili

Huz

uia

chem

bech

embe

za

dam

u zi

siha

ribi

we,

hu

zuia

mw

ili u

sipa

twe

na m

agon

jwa

Hus

afir

isha

hew

a ya

oks

ijeni

kw

enye

dam

u,

huon

doa

chem

bech

embe

nye

kund

u za

dam

u zi

lizoc

haka

a au

kuh

arib

ika

na k

uten

gene

za

nyin

gine

Hus

aidi

a us

hara

bu n

a ut

umik

aji w

a m

afut

a na

pr

otin

i, hu

said

ia k

uten

gene

za c

hem

bech

embe

ny

ekun

du z

a da

mu

Hut

enge

neza

che

mbe

chem

be z

a da

mu

na s

eli z

a ne

va

Muh

imu

kwa

king

a ya

mw

ili n

a hu

said

ia u

sh-

arab

u w

a m

adin

i ya

chum

a

18

Mad

ini y

a C

hoka

a

Mag

nesi

a

Sele

niam

Zin

ki

Mad

ini J

oto

Maz

iwa,

may

ai, n

yam

a, k

uku,

kar

anga

, sa

mak

i, m

ahar

agw

e, n

afak

a zi

sizo

kobo

lew

a

Naf

aka,

mbo

ga z

a ki

jani

, vya

kula

vya

ba

hari

ni, j

amii

ya m

ikun

de, k

aran

ga

Cha

nzo:

Im

ebor

eshw

a na

kut

afsi

riw

a ku

toka

Net

wor

k of

Afr

ican

Peo

ple

Liv

ing

wit

h H

IV/A

IDS,

200

9

Nya

ma,

sam

aki,

kuku

, jib

ini,

may

ai, m

aziw

a,

vyak

ula

viliv

yoch

achu

shw

a (f

erm

ente

d)

kam

a m

tindi

na

togw

a

Nya

ma,

kuk

u, s

amak

i, na

faka

na

mbo

ga-

mbo

ga

Sam

aki,

vyak

ula

ving

ine

vya

baha

rini

, ch

umvi

iliy

owek

wa

mad

ini y

a jo

to

Hub

ores

ha n

gozi

, hus

aidi

a ka

tika

umet

abol

i wa

nish

ati-

lishe

, mfu

mo

wa

chak

ula

na f

aham

u

Hui

mar

isha

mis

uli,

muh

imu

katik

a m

fum

o w

a fa

ham

u, u

kuaj

i na

huim

aris

ha m

ifup

a na

men

o

Huz

uia

kuha

ribi

ka k

wa

mis

uli y

a m

oyo

Hus

aidi

a ki

nga

ya m

wili

, hus

aidi

a uy

eyus

hwaj

i w

a ch

akul

a na

usa

firi

shw

aji w

a V

itam

ini A

Uku

aji,

husa

idia

ubo

ngo

na m

fum

o w

a fa

ham

u ku

fany

a ka

zi v

izur

i

Kijarida hiki kimetayarishwa na:

The Centre for Counselling, Nutrition and Health Care (COUNSENUTH)

United Nations Rd./Kilombero Str.Plot No. 432, Flat No. 3

P.O Box 8218, Dar es Salaam, Tanzania.Tel/Fax: +255 22 2152705, Cell: +255 755 165112

Email: [email protected]

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:Mkurugenzi Mtendaji

The Centre for Counselling, Nutrition and Health Care (COUNSENUTH)

ISBN 978-9987-9017-8-4

© COUNSENUTH, 2008

Kimefadhiliwa na:

GLOBAL FUND ROUND 4 PROGRAM

Designed &Printed by:DeskTop Productions Limited

P.O Box 20936, Dar es Salaam, Tanzania.