-module - mwalimuwakiswahili.co.tz · stashahada ya elimu ya watu wazima na mafunzo endelevu kwa...

76
-MODULE Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Idara ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu – Kwa Masafa Kuchambua Sintaksia na Semantiki ya Kiswahili KIT 0610

Upload: others

Post on 04-Oct-2019

93 views

Category:

Documents


6 download

TRANSCRIPT

Page 1: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

-MODULE

Taasisi ya Elimu ya Watu WazimaIdara ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo EndelevuStashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu – Kwa Masafa

Kuchambua Sintaksia na Semantiki ya Kiswahili

KIT 0610

Page 2: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

MODULI

Kuchambua Sintaksia na Semantiki ya Kiswahili

KIT 0610

Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa

Page 3: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +
Page 4: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuzalisha, kunakili, wala kusambaza sehemu yoyote

ya kazi hii kwa namna yoyote isipokuwa kwa kunukuu matini fupifupi zinazoweza kutumika

kwa ajili ya utafiti na mapitio ya maandiko, bila kibali cha maandishi kutoka Taasisi ya

Elimu ya Watu Wazima.

© Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, 2014

Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa

S. L. B. 20679 Dar es Salaam,

Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania

Nukushi: +255 22 2150836 Barua-pepe: [email protected]

Tovuti: www. iae.ac.tz

Page 5: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +
Page 6: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Shukrani

Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Dkt. Fidelis M. S. Mafumiko anapenda

kutoa shukurani za dhati kwa watu mbalimbali ambao wamechangia kwa namna moja au

nyingine katika kukamilisha kazi hii. Wafuatao ambao ni wafanyakazi wa TEWW wanastahili

kutajwa kipekee kwa kuongoza mchakato huu hadi kukamilika kwake.

A. Lekule: Mkuu, Idara ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzi

Endelevu

T. Mamba: Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (Mratibu)

A. Mashaka: Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (Mwandishi)

S. Kileo: Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (Mpitiaji)

E. Samba: Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (Mhariri)

Page 7: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

ii Yaliyomo

Yaliyomo

Kuhusu moduli hii 1

Muundo wa moduli hii ...................................................................................................... 1

Maelezo ya jumla kuhusu moduli 3

Karibu katika moduli hii ................................................................................................... 3 Umahiri wa Jumla ............................................................................................................. 4 Mbinu za usomaji .............................................................................................................. 4 Je, unahitaji msaada? ........................................................................................................ 5 Mazoezi ............................................................................................................................. 6

Namna ya kutumia moduli hii 7

Ishara za pambizo ............................................................................................................. 7

Somo la Kwanza 9

Kuchambua Mikabala ya Sarufi Mapokeo na Sarufi Miundo Virai ................................. 9 Utangulizi ................................................................................................................ 9 Matokeo ................................................................................................................... 9 Kufafanu Dhana ya Mkabala na Mkabala wa Kisarufi ........................................... 9 Kufafanua Misingi ya Mkabala wa Sarufi Mapokeo ............................................ 10

Mkabala wa Sarufi Mapokeo ....................................................................... 10 Misingi ya Sarufi Mapokeo ......................................................................... 10 Zoezi ............................................................................................................ 11

Kufafanua Misingi ya Mkabala wa Sarufi Miundo Virai ...................................... 12 Mkabala wa Sarufi Miundo Virai ................................................................ 12 Misingi ya Mkabala wa Sarufi Miundo Virai .............................................. 13

Muhtasari wa Somo ........................................................................................................ 14 Zoezi la Somo ................................................................................................................. 14

Somo la Pili 15

Kuchambua Kategoria za Kisintaksia ............................................................................. 15 Utangulizi .............................................................................................................. 15 Matokeo ................................................................................................................. 15 Ufafanuzi Dhana za Msingi za Kisintaksia ........................................................... 15

Sintaksia ....................................................................................................... 15 Kategoria ...................................................................................................... 16 Tungo ........................................................................................................... 16 Neno ............................................................................................................. 17 Kirai ............................................................................................................. 17 Kishazi ......................................................................................................... 17 Sentensi ........................................................................................................ 18

Kubainisha Kategoria ya Neno .............................................................................. 18 Nomino ........................................................................................................ 19

Page 8: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Aina za Nomino ................................................................................... 19 Dhima/ Kazi za Nomino ...................................................................... 20

Kiwakilishi ................................................................................................... 21 Kivumishi ..................................................................................................... 22 Kitenzi .......................................................................................................... 23 Kielezi .......................................................................................................... 24 Kihusishi ...................................................................................................... 26 Viunganishi .................................................................................................. 27

Dhima za Kiunganishi ......................................................................... 28 Zoezi .................................................................................................... 28

Kubainisha Kategoria ya Virai .............................................................................. 29 Aina za Virai ................................................................................................ 29

Kirai Nomino ....................................................................................... 30 Kirai Kitenzi ........................................................................................ 31 Kirai Kivumishi ................................................................................... 32 Kirai Kielezi ........................................................................................ 33 Kirai Kihusishi ..................................................................................... 34 Zoezi .................................................................................................... 34

Kubainisha Vishazi vya Kiswahili ........................................................................ 35 Aina za Vishazi ............................................................................................ 35

Kishazi Huru ........................................................................................ 35 Kishazi Tegemezi ................................................................................ 35 Zoezi .................................................................................................... 37

Kubainisha Sentensi za Kiswahili ......................................................................... 38 Aina za Sentensi kwa Kigezo cha Maana/ amilifu (kisemantiki) ................ 38 Aina za Sentensi kwa Kigezo cha Kimuundo (kisintaksia) ......................... 39

Zoezi .................................................................................................... 41 Uchanganuzi wa Tungo ......................................................................................... 41

Uchanganuzi wa Tungo kwa Mkabala wa Kimapokeo ............................... 42 Uchanganuzi wa Tungo kwa Mkabala wa Kimuundo ................................. 45

Zoezi .................................................... Error! Bookmark not defined. Muhtasari wa Somo ........................................................................................................ 48 Zoezi la Somo ................................................................................................................. 48

Somo la Tatu 50

Kufafanua Semantiki ya Kiswahili ................................................................................. 50 Utangulizi .............................................................................................................. 50 Matokeo ................................................................................................................. 50 Kufafanua Dhana ya Semantiki na Maana ............................................................ 50 Kuchambua Mikabala ya Semantiki ...................................................................... 51

Viwango vya Maana .................................................................................... 53 Dhana ya Maana .......................................................................................... 54

Kufafanua Aina za Maana ..................................................................................... 56 Aina za Maana ............................................................................................. 56 Uhusiano wa Kifahiwa katika Semantiki ..................................................... 58

Sinonimia ............................................................................................. 59 Hiponimia ............................................................................................ 59 Homonimia .......................................................................................... 60 Polisemia ............................................................................................. 60

Page 9: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

iv Yaliyomo

Antonimia ............................................................................................ 61 Kufafanua Nadharia ya Maana Kimuktadha ya Ludwig Wittgenstain ................. 61

Kufafanua dhana ya nadharia....................................................................... 62 Nadharia ya Maana Kimukutadha ............................................................... 62

Kufafanua Ubora na Udhaifu wa Nadharia ya Maana Kimuktadha ..................... 63 Zoezi .................................................... Error! Bookmark not defined.

Muhtasari wa Somo ........................................................................................................ 64 Zoezi la Somo ................................................................................................................. 65

Marejeleo 66

Page 10: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

1

Kuhusu moduli hii Moduli hii imetayarishwa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima.

Moduli zote zilizotayarishwa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima

zina muundo sawa, kama ilivyoelezwa hapa chini.

Muundo wa moduli hii

Maelezo ya jumla kuhusu moduli

Maelezo ya jumla kuhusu moduli hutoa utangulizi wa jumla wa moduli. Habari zinazopatikana katika maelezo ya jumla kuhusu moduli zitakusaidia kuamua:

Kama moduli hii inakufaa.

Kitu gani unatarajia kujifunza?

Muda utakaohitaji ili kukamilisha moduli.

Maelezo haya ya jumla pia hutoa mwongozo juu ya:

Mbinu za usomaji.

Mahali pa kupata msaada.

Mazoezi ya nyumbani na tathmini.

Ishara za vitendo mbalimbali.

Masomo.

Tunatilia mkazo ushauri kwamba usome maelezo ya jumla kuhusu moduli kwa makini kabla ya kuanza masomo yako.

Yaliyomo kwenye moduli

Moduli hii imegawanywa katika masomo. Kila somo lina:

Utangulizi wa yaliyomo kwenye moduli.

Matokeo ya somo.

Istilahi mpya.

Maudhui ya kimsingi ya somo pamoja na mazoezi mbalimbali ya kusoma.

Mazoezi ya nyumbani na/au tathmini, kama inavyohitajika.

Page 11: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Kuhusu moduli hii Error! No text of specified style in document.

2

Marejeleo

Kwa wale wanaopenda kujifunza mengi juu ya mada hii, tunawapa

orodha ya marejeleo ya ziada mwishoni mwa Moduli hii; haya

yanaweza kuwa vitabu, makala au tovuti.

Maoni yako

Baada ya kukamilisha Moduli ya Kiswahili Ufahamu na Utumizi

wa Lugha tutashukuru ikiwa utatenga muda mfupi kutupa maoni

yako kuhusu kipengele cho chote cha moduli hii. Maoni yako

yanaweza kuhusu:

Yaliyomo kwenye moduli na muundo wake.

Makala za kusoma kwa moduli na marejeleo mengine.

Mazoezi ya nyumbani ya moduli.

Tathmini za moduli.

Muda wa moduli.

Usaidizi katika moduli (wahadhiri waliosimamia moduli, usaidizi wa kiufundi, n.k.)

Ukitoa maoni mwafaka utatusaidia kuboresha moduli hii.

Page 12: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

3

Maelezo ya jumla kuhusu moduli

Karibu katika moduli hii

Lengo kuu la Moduli hii kumwezesha mwanafunzi kutumia stadi

za sintaksia na semantiki ya Kiswahili sanifu katika mawasiliano.

Moduli hii inalenga kuwapatia wanafunzi maarifa ya awali ya

msingi katika uchambuzi wa taaluma ya sintaksia (miundo) na

Semantiki (maana). Kwa upande wa sintaksia kumekuwa na

mkanganyo mkubwa juuu ya suala nzima la vipashio vinavyounda

taaluma hii ikiwemo neno, kirai, kishazi, na sentensi. Hivyo,

moduli hii inatanzua uvuliuvuli (mkanganyo) huo kwa kufafanua

kwa ufasaha juu ya vipashio hivyo ambapo ndio uti wa mgongo

katika uchanganuzi wa tungo mbalimbali. Halikadhalika kwa

upande wa uchanganuzi wa tungo kumekuwa na uholela wa hali

ya juu kiasi ambacho kimewachanganya sana wanafunzi katika

suala hilo. Uholela huo umetokana na baadhi ya wanaisimu

kuchanganya istlahi za sarufi mapokeo na sarufi miundo katika

uchanganuzi. Hata hivyo, moduli hii imeondoa utata huo kwa

kuchambua misingi ya mikabala yote miwili kisha moduli

imechanganua tungo mbalimbali kwa kutumia kila mkabala yaani

pasipo kuchanganya istilahi za mikabala hiyo (kimapokeo na

kimuundo). Aidha, moduli hii inakupa maarifa yahusuyo semantiki

ambapo yatakujengea msingi katika taaluma hii. Tunakutakia

masomo mema!

Moduli hii imeandaliwa kwa ajili ya wanafunzi wa Stashahada kwa

Njia ya Masafa katika Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima. Moduli

hii inahusu Uchambuzi wa Sintaksia na Semantiki ya Kiswahili.

Page 13: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Maelezo ya jumla kuhusu moduli Error! No text of specified style in document.

4

Umahiri wa Jumla

Baada ya kukamilisha moduli hii tunakusudia kila mwanafunzi aweze:

Kutofautisha baina ya mkabala wa sarufi mapokeo na sarufi miundo virai;

Kufafanua kwa ufasaha kategoria ya neno, kirai, kishazi na sentensi;

Kubainisha kategoria za neno, kirai, kishazi na sentensi katika tungo mbalimbali;

Kuchanganua tungo mbalimbali kwa kutumia mikabala ya sarufi mapokeo na sarufi miundo virai;

Kufafanua aina mbalimbali za maana; and

Kueleza kwa ufasaha nadharia ya maana kimuktadha

Mbinu za usomaji

Kwa kuwa wewe ni mwanafunzi wa Elimu Masafa na Ana kwa

Ana, utaratibu wako wa kusoma utakuwa tofauti na ule ulioutumia

ulipokuwa bado shuleni: utachagua unachotaka kusoma, utakuwa

na motisha ya kitaalamu na/au ya kibinafsi inayokusukuma, na bila

shaka utakuwa ukiratibu shughuli zako za kiusomaji huku

ukizingatia majukumu yako mengine ya kitaalamu au kinyumbani.

Kimsingi, utakuwa unayadhibiti mazingira yako ya masomo. Kwa

hivyo, utahitajika kufikiria juu ya maswala ya utendaji

yanayohusiana na udhibiti wa wakati, kuweka malengo, udhibiti wa

shinikizo, n.k. Pengine utahitaji kujizoesha tena katika maeneo

kama upangaji wa insha, namna ya kuimudu mitihani, na kutumia

mtandao kama marejeleo ya ujifunzaji.

Mambo utakayozingatia sana ni muda na nafasi, yaani muda

unaotenga kwa masomo yako na mazingira unamosomea.

Tunapendekeza kwamba uchukue nafasi hii – kabla ya kuanza

kujisomea kibinafsi – kujifahamisha mambo haya. Kuna marejeleo

mengi mazuri kwenye mtandao. Viungo vichache

vinavyopendekezwa ni:

Page 14: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

5

http://www.how-to-study.com/

Tovuti ya “How to study” yaani “Jinsi ya kusoma” imetengwa mahsusi kwa ajili ya marejeleo ya mbinu za usomaji. Utapata viungo kuhusu kujitayarisha kusoma (orodha ya mambo tisa muhimu kuhusu mahali pazuri pa kusomea), kuandika kumbukumbu, mikakati ya kusoma vitabu vya kiada, kutumia vyanzo vya kumbukumbu, dukuduku la mitihani.

http://www.ucc.vt.edu/stdysk/stdyhlp.html

Hii ni tovuti ya Kitengo cha Maswala ya Wanafunzi, Virginia Tech. Utapata viungo vya namna ya kupanga muda wako (ikiwa ni pamoja na kiungo cha “wakati huenda wapi?”), orodha-kaguzi ya mbinu za usomaji, mbinu za kimsingi za kumakinikia jambo, udhibiti wa mazingira ya kusomea, kuandika kumbukumbu, namna ya kusoma insha kwa kusudi la kuchanganua, mbinu za kukumbuka.

http://www.howtostudy.org/resources.php

Hii ni tovuti nyingine ya “jinsi ya kusoma” iliyo na viungo muhimu kuhusu udhibiti wa wakati, kusoma kwa ufanisi, mbinu za kusaili/kusikiliza/kuchunguza, kufaidi kutokana na kutenda (ujifunzaji wa kiutendaji), kukuza kukumbuka, vidokezo vya namna ya kudumisha motisha, kukuza mpango wa ujifunzaji.

Viungo vilivyo hapo juu ni mapendekezo yetu ya kukuwezesha kuanza. Wakati tulipoandika, viungo vya tovuti hizi vilikuwa vinatumika. Ikiwa unataka kupata tovuti zaidi, nenda kwa www.google.com kisha upige taipu na kutafuata “self-study basics” (misingi ya usomi wa kibinafsi), “self-study tips” (vidokezo vya usomi wa kibinafsi), “self-study skills” (mbinu za usomi wa kibinafsi) au tovuti nyingine zenye mada kama hizo.

Je, unahitaji msaada?

Ndugu mwanafunzi, katika mchakato wako wa kujifunza, unaweza

kuhitaji msaada kuhusu mambo mbalimbali, kwa mfano, mahali

unapoweza kupata msaada na namna ya kupata msaada huo.

Pamoja na hayo, unaweza kuhitaji ufafanuzi kuhusu moduli

unazosoma. Hivyo basi, unashauriwa kuomba ufafanuzi wa yote

hayo kwa mratibu wa kituo chako au mwezeshaji wako. Pia,

unaweza kufungua tovuti ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima

yenye anwani hii: www.iae.ac.tz au piga simu hii +255 22

2150836.

Page 15: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Maelezo ya jumla kuhusu moduli Error! No text of specified style in document.

6

Mazoezi

Baada ya kila somo, unahitajika kujibu maswali ya zoezi la somo.

Majibu ya zoezi hili la kila somo hautayawasilisha kwa mwezeshaji

wako, ni kwa ajili ya kufanya tafakuri ya ulichojifunza. Pia,

utapewa majaribio na mazoezi ambayo utayafanya na

kuyawasilisha kama utakavyoongozwa na mwezeshaji wako.

Pamoja na hayo, utatakiwa kufanya mitihani ya dhihaki/utamirifu

kwa ajili ya upimaji wa maendeleo yako ya kitaaluma.

Page 16: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

7

Namna ya kutumia moduli hii

Ishara za pambizo Wakati ukijifunza moduli hii utagundua kwamba kuna matumizi

mengi ya ishara za pambizo. Ishara hizi zina jukumu la kushiria

aina fulani ya matini, kazi mpya au kubadilika kwa zoezi.

Zimetumiwa ili kukuongoza ujue namna ya kuitumia moduli hii.

Seti nzima ya ishara imetolewa hapa chini. Tunapendekeza kuwa

ujizoeze ishara hizi na maana yaka kabla ya kuanza masomo yako.

Zoezi Tathmini Zoezi la Mada Kisa Mafunzo

Mjadala Zoezi la Kikundi Usaidizi Kumbuka!

Matokeo Kusoma Tafakari Mbinu za

Usomaji

Muhtasari Istilahi Muda Kidokezi

Page 17: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +
Page 18: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

9

Somo la Kwanza

Kuchambua Mikabala ya Sarufi Mapokeo na Sarufi Miundo Virai

Utangulizi

Katika sura hii tunakusudia kuchambua mikabala ya sarufi

mapokeo na sarufi miundo virai ambapo mambo yafuatayo

yatashughulikiwa. Mosi, sura inalenga kufafanua dhana ya mkabala

na chimbuko lake. Pili, tutafafanua misingi ya sarufi mapokeo

ambapo usuli wa sarufi mapokeo utafafanuliwa, kisha tutachambua

misingi ya sarufi mapokeo. Vilevile, katika sura hii tutafafanua

dhana ya sarufi miundo virai sambamba na misingi yake. Mwisho

sura imefumbata maswali/ mazoezi kwa ajili ya kujima.

Matokeo

Baada ya kukamilisha somo hili utaweza:

Kufafanua na Kufasili dhana ya mkabala wa kisarufi;

Kueleza chanzo cha kuibuka kwa mikabala ya kisarufi;

Kufafanua dhana na misingi ya sarufi mapokeo;

Kufafanua dhana na misingi ya sarufi miundo virai;

Kutofautisha baina ya sarufi mapokeo na sarufi miundo;

Kueleza maana ya dhana za misingi zifuatazo (kategoria, tungo, kirai, kishazi na sentensi);

Kubainisha virai vya lugha ya Kiswahili;

Kubainisha vishazi vya lugha ya Kiswahili;

Kubainisha sentensi za lugha ya Kiswahili; na

Kuchanganua sentensi kwa njia mbalimbali.

Kufafanu Dhana ya Mkabala na Mkabala wa Kisarufi

Kwa mujibu wa TUKI (2004) Mkabala ni utaratibu unaofuatwa ili

kukabili jambo. Kwa hiyo mkabala ni mtazamo wa namna ya

kufanya jambo fulani. Mkabala wa kisarufi unaweza kufafauliwa

kuwa ni mtazamo au utaratibu maalumu unaofuatwa katika

Page 19: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Kwanza Error! No text of specified style in document.

10

kuchanganua vipashio na kanuni mbalimbali zinazotawala lugha

fulani. Asili ya neno sarufi ni ugiriki ambapo kwa kigiriki inamana

ya “gramamantike”. Taaluma ya sarufi iliasisiwa na wanafalsafa

wa Ugiriki wakiwemo Plato na Aristotle. Katika harakati za

kuchimbua taaluma ya sarufi ndiko kulikozua mikabala mbalimbali

ya kisarufi.

Ndugu mwanafunzi, sasa tupitie aina za mikabala mbalimbali

ya sarufi na ufafanuzi wake kama ilivyojadiliwa hapa chini:

Taaluma ya sarufi imefafanuliwa katika mikabala mbalimbali ila

katika kiwango chetu tutatazama mikabala miwili ambayo ni:

a) Mkabala wa sarufi Mapokeo; na

b) Mkabala wa sarufi Miundo Virai

Kufafanua Misingi ya Mkabala wa Sarufi Mapokeo

Ndugu wanafunzi kipindi kilichopita tulijifunza kuhusu dhana ya

mkabala ambapo tulipitia kuhusu maana, chimbuko na aina ya

mikabala. Katika kipindi hicho tulitaja kuwa kuna aina mbili za

mkabala yaani: sarufi mapokeo na mkabala wasarufi miundo. Kwa

hiyo katika kipindi hiki tutajadili kwa undani aina hizo za mikabala

kwa kuangalia maana, chimbuko, misingi yake. Tuanze na mkabala

wa sarufi mapokeo:

Mkabala wa Sarufi Mapokeo

Huu ni mkabala wa awali/ kale ulioshughulikia sarufi ya lugha.

Mkabala huu ulizuka kuanzia karne ya 5 K.K (kabla ya Kuzaliwa

Kristo). Waasisi wake ni Plato, Aristotle, Protagoras, Thrax na

wengineo. Mkabala huu ulishughulikia sarufi kwa mtazamo wa

falsafa, dini, fasihi n.k. Katika sarufi mapokeo vipashio vya

uchanganuzi wa sarufi vilikuwa ni neno na sentesi.

Misingi ya Sarufi Mapokeo

Saufi mapokeo imejengwa na misingi mbalimbali kama ifuatavyo:

a) Mkabala wa sarufi mapokeo ulitumia lugha ya kilatini kama

msingi wa uchambuzi wa sarufi za lugha zote. Kwa wakati huo

lugha ya kilatini ilikuwa ipo katika maandishi. Kwa hiyo

Page 20: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

11

kanuni na sheria za sarufi ya kilatini ndizo zilizotumika katika

kuchambua sarufi za lugha nyingine.

b) Wanasarufi mapokeo walichukulia kuwa lugha ya maandishi

ni bora zaidi kuliko lugha ya maadishi. Hii ndiyo sababu ya

kutumia kilatini kwani lugha ambazo hazikuwa katika

maandishi zilichukuliwa kuwa hazina sarufi.

c) Wanasarufi mapokeo walipendekeza kanuni za matumizi ya

lugha. Hivyo lugha ilipaswa iandikwe na kutamkwa kama

kanuni zinavyoelekeza kinyume chake lugha hiyo ilionekana

ni batili. Baadhi ya kanuni hizo ni kama vile:

Sentensi hapaswi kuanza na kiunganishi wala kuishia na

kihusishi, na

Vikanushi viwili au zaidi havipaswi kuambatana.

d) Mkabala wa sarufi mapokeo ulibainisha muundo wa sentensi

kuwa sentensi inaundwa na sehemu kuu mbili yaani kiima na

kiarifu. Plato ndiye aliyebaini kuwa sentensi imekitwa katika

kiima na kiarifu. Kiima huashiria mtenda na kiarifu huashiria

mtendwa.

e) Wanasarufi mapokeo pia waliainisha aina za maneno.

Dionysious thrax aliyebaini kuwa lugha ina aina nane za

maneno kama vile: Nomimo, Kitenzi, Kibainishi, Kihusishi,

Kibadala, Kielezi, Kiungo, Faridi pekee –mofimu huru.

f) Wanamkabala wa sarufi mapokeo walihusisha lugha na

taaluma ya sanaa, mantiki na falsafa. Hivyo lugha ilitumika

katika kazi hizo na lugha iliyotumika katika uchunguzi wa

sarufi ni ile iyotumiwa na wasomi, wanasiasa wakubwa na

watu maarufu tu, wale watu tabaka la chini walichukuliwa

hawajui lugha.

g) Aidha, wanamkabala wa kimapokeo waliainisha kategoria za

kisarufi kuwa ni nafsi, njeo kauli, dhamira uhusika na hali.

Ndugu mwanafunzi, baada ya kupitia kwa undani dhana ya

sarufi mapokeo, chimbuko na misingi yake sasa hebu chukua

kalamu na daftari tufanye zoezi lifuatalo:

Zoezi

1. Mkabala wa sarufi mapokeo ulizuka mnamo ...........................

Page 21: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Kwanza Error! No text of specified style in document.

12

2. Taja waasisi wawili wa mkabala wa sarufi mapokeo:

a) ...........................................................................................

b) ............................................................................................

3. Katika mkabala wa sarufi mapokeo sentesi iligawanywa

katika sehemu mbili ambazo ni:

a) ...........................................................................................

b) ...........................................................................................

4. .................... ni mwanamapokeo aliyeainisha aina za maneno.

5. Taja aina nane za maneno zilizoainishwa na wanasarufi

mapokeo.

6. Kila taaluma huwa na misingi yake. Jadili misingi ya

mkabala wa sarufi mapokeo.

Kufafanua Misingi ya Mkabala wa Sarufi Miundo Virai

Mkabala wa Sarufi Miundo Virai

TUKI (2004) wanafasili dhana ya muundo kuwa ni mpangilio wa

vipashio mbalimbali katika lugha.

Sarufi miundo virai ni utanzu unaojishughulisha na uchanganuzi

wa mpangilio wa maneno katika sentensi na uhusiano wa vipashio

vyake (Massamba na wenzake, 2001).

Naye, Besha (2007) ameiita sarufi miundo virai kama “kanuni

vikundi” ambapo anafasiri kuwa ni sarufi inayoonyesha uhusiano

wa maneno na vipashio vingine vinavyojenga sentensi za lugha.

Hivyo, kutokana na fasili za wanaisimu hapo juu tunaweza kusema

kuwa mkabala wa sarufi miundo virai ni mkabala wa kisarufi

unaochunguza namna vipashio vidogo vinavyoungana ili kuunda

vipashio vikubwa zaidi. Hii ina maana kuwa namna neno na neno

linavyoungana ili kuunda kirai na kirai na kirai vinavyungana

kuuda kishazi na kishazi na kishazi vinavyoungana kuunda

sentensi. Mkabala huu unasisitiza kuwa vipashio katika tungo ni

sharti vichanganuliwe katika makundi (virai). Mkabala huu ulizuka

baada ya mkabala wa kimapokeo kushindwa kuchanganua miundo

Page 22: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

13

ya lugha mbalimbali. Mkabala huu ni wa kisasa kwani huchunguza

lugha kisayansi. Mwasisi wa mkabala huu ni Noam Chomsky

(1957) katika kitabu chake cha “Syntactic Structure”.

Baada ya kufafanua dhana na chimbuko la mkabala wa sarufi

miundo virai sasa tutazame misingi ya mkabala huu.

Misingi ya Mkabala wa Sarufi Miundo Virai

Misingi ya sarufi miundo virai inafafanuliwa kama ifuatavyo:

a) Mkabala huu unatilia mkazo upekee wa lugha kuwa kila

lugha inaupekee wake. Hivyo lazima ichunguzwe kwa

misingi ya muundo wake wa vipashio kama vile maneno,

virai, vishazi na sentensi.

b) Mkabala wa sarufi miundo virai unasisitiza umuhimu wa

kuwa na kanuni zinazozalisha tungo au sentensi kutoka

darajia ya juu kabisa hadi ya chini

c) Mtazamo wa sarufi miundo virai unagawa sentensi katika

sehemu kuu mbili yaani Kirai Nomimo (KN) na Kirai Kitenzi

(KT).

d) Mtazamo huu unasisitiza kuwa kila kipashio katika sentensi

kipo katika kategoria fulani. Mfano kategoria ya neno, kirai,

kishazi ua sentensi.

e) Miundo Virai inaona kuwa kanuni za vipashio ni sharti

zifafanuliwe kwa kutumia msimbo mfano: N, KV nk.

f) Mkabala wa sarufi miundo virai unachanganua vipashio

mbalimbali katika tungo kwa kuonyesha uhusiano wake.

Page 23: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Kwanza Error! No text of specified style in document.

14

Muhtasari wa Somo

Katika somo hili tumejifunza sehemu kuu mbili katika muundo wa

sentensi ambazo ni Kirai Nomino (KN) na Kirai Kitenzi (KT).

Katika somo hili mwanafunzi amepitia mada ndogo zifuatazo:

Misingi ya Mkabala wa Sarufi Mapokeo, Misingi ya Mkabala wa

Sarufi Mapokeo na Misingi ya Mkabala wa Sarufi Miundo Virai,

Misingi ya Mkabala wa Sarufi Miundo Virai. Katika mada hizi

vipengele vifutavyo vilipitiwa: kategoria ya neno au virai

vinavyounda kirai nomino (KN), au virai vinavyounda kirai kitenzi

(KT) na maneno yanayounda virai vilivyoainishwa na kufafanua

dhana za kisintaksia lugha na sarufi na kuonyesha uhusiano uliopo

katika tanzu za sarufi.

Pia tumejifunza sifa mbalimbali za lugha pamoja na uhusiano

uliopo kati ya tanzu mbalimbali za fasihi. Sasa basi hebu chukua

kalamu yako na daftari ufanye zoezi fupi ili kupima uelewa wako

katika yale yaliyojadiliwaa hapo juu mambo muhimu ya

uchanganuzi wa tungo kwa mkabala wa sarufi miundo virai.

Zoezi la Somo

1. Mkabala wa sarufi miundo virai uliasisiwa na mwanaisimu

.....................mwaka...............

2. Eleza kwa kifupi chanzo cha kuibuka kwa mkabala wa sarufi

miundo virai.

3. Mkabala wa sarufi miundo virai unagawa sentensi katika

sehemu mbili ambazo ni ................................................. na

...........................................

4. Fafanua 4 hatua mbalimbali utakazofuata katika uchanganuzi

wa sentensi kwa mkabala wa sarufi miundo virai.

5. Tofautisha baina ya mkabala wa sarufi mapokeo na sarufi

miundo virai.

Page 24: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

15

Somo la Pili

Kuchambua Kategoria za Kisintaksia

Utangulizi

Lengo la sura hii ni kuchambua kategoria za kisintaksia kwa

kuamisha kategoria mbalimbali za kisintaksia. Kwanza kabisa

tutafasili dhana za msingi kama sintaksia. Pili, kuchambua

kategoria za kisintaksia kama vile neno, kirai, kishazi na sentensi.

Katika uchambuzi huo wa kategoria tutajikita kwenye aina na

miundo yake. Tatu, tutachambua tungo na sentensi kwa njia ya

maelezo, mshale, matawi na jedwali. Aidha katika uchanganuzi wa

tungo na sentensi tutatumia mikabala yote miwili yaani mkabala

wa kimapokeo na ule mkabala wa kimuudo (sarufi miundo virai).

Matokeo

Baada ya kukamilisha somo hili utaweza:

Kufafanua dhana za msingi za Kisintaskia

Kubainisha kategoria ya neno

Kubainisha kategoria ya Virai

Ufafanuzi Dhana za Msingi za Kisintaksia

Sintaksia

Kwa mujibu wa Harper (2001-2010) Online Etymology Dictionary,

neno sintaksia liliibuka takribani miaka ya 1600 na linatokana na

neno la Kifaransa syntaxé au la Kilatini au Kigiriki syntaxis ambalo

maana yake ni kupanga au kuweka vitu pamoja katika mpango.

Hata hivyo, wataalamu wengi wa masuala ya sintaksia

wanakubaliana kuwa neno hili lina asili ya Kigiriki kwa kuwa

Wagiriki ndio wakongwe katika taaluma mbalimbali hapa duniani,

ikiwa ni pamoja na taaluma ya lugha. Hata hivyo historia ya isimu

inaonesha kuwa, uchunguzi wa kwanza wa lugha ulianza na

Wamisri mnamo karne ya 5 Kabla ya Kuzaliwa Kristo (KK),

Page 25: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

16

Wagiriki ndio walioweka msingi wa taaluma ya lugha tuijuavyo

hivi leo (Khamis & Kiango, 2002: 1).

Kwa hiyo, sintaksia ni nini katika taaluma ya isimu?

Besha (1994: 84) anafasili sintaksia kama taaluma inayojihusisha

na uchambuzi na ufafanuzi wa muundo wa sentensi za lugha Kwa

mujibu wa O’Grady (1996: 181), sintaksia ni taaluma

inayochunguza jinsi maneno yanavyounganishwa ili kuunda

sentensi. Sintaksia kwa mujibu wa Massamba na wenzake (2009:

34) wanafasili sintaksia kama ni utanzu wa sarufi

unaojishughulisha na uchanganuzi wa mpangilio wa maneno katika

sentensi na uhusiano wa vipashio vyake.” Wanaendelea kusema

kuwa katika utanzu huu kinachochunguzwa ni zile sheria au kanuni

ambazo hazina budi kufuatwa katika kuyapanga maneno ya lugha

katika mfuatano (neno moja baada ya jingine) kwa namna ambayo

itayafanya maneno hayo yalete maana inayokubalika na kueleweka

katika lugha husika.

Kwa hiyo, sintaksia inaweza kufasiliwa kuwa ni taaluma

inayochunguza miundo ya tungo na kanuni mbalimbali za lugha

zinazotawala miundo hiyo. Katika uchunguzi huo, sintaksia

huhusika na mpangilio wa maneno katika miundo mitatu

iliyopangwa kidarajia, yaani jinsi maneno yanavyopangwa ili

kuunda virai, vishazi na sentensi.

Kategoria

Hamisi na Kiango (2009) wanafasili dhana ya kategoria kama

jamii, seti, kundi au makundi ya maneno yanayofanya kazi ya

kufanana. Kwa mantiki hiyo tunaweza kusema kuwa kategoria ni

darajia yoyote ya vipashio inayotumika katika uchambuzi wa lugha

fulani.

Tungo

Massamba na wenzake (2001) wanafasili dhana ya tungo kama

neno au maneno yanayotoa taarifa fulani ambayo inaweza kuwa

kamili au isiwe kamili. Anaendelea kufafanua zaidi kwa kutaja aina

za tungo kuwa ni neno, kirai, kishazi na sentensi. Hivyo, tungo

inaweza ikadokeza maana kamili na isiyo kamili.

Page 26: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

17

Neno

Dhana ya neno inautata katika kuifasili hii ni kutokana na

mitazamo mbalimbali inayotumiwa katika somo letu tutatizama

dhana ya neno kisarufii ambapo inaelezwa kama ifuatavyo: Tungo

Mdee (1988) anafasili dhana ya neno kisarufi kuwa ni kipashio cha

kiisimu ambacho kipo kati ya mofimu na kifungu cha maneno.

Kirai

Dhana ya kirai imefafanuliwa na wataalamu kama ifuatavyo:

Matei (2008) anafasili kirai kama fungu la maneno ambalo hufanya

kazi kama neno moja. Kirai hudokeza maana lakini maana hiyo si

kamili...na hakina muundo wa kiima-kiarifu.

Massamba na wenzake (2009) wanafasili dhana ya kirai kama

kipashio cha kimuundo chenye neno moja au zaidi lakini ambacho

hakina uhusiano wa kiima kiarifu

Kutokana na fasili za wataalamu hao tunabaini kuwa kirai

kinaweza kuwa sehemu ya kiima au kiarifu. Hivyo, tunaweza

kuhitimisha kwa kufasili dhana ya kirai kuwa ni kipashio cha

kimuundo kinachoanzia neno moja na kuendelea ambacho hakina

muudo kamili wa kiima na kiarifu.

Kishazi

Kishazi ni tungo ndogo yenye uoanifu ambayo nikubwa kuliko

neno au kirai lakini iliyo sehemu ya sentensi kubwa (Massamba na

wenzake, 2001).

Matei (2008) anafasili dhana ya Kishazi kama kundi la maneno

ambalo lina kiima kimoja na kiarifu kimoja.

Naye, Matinde (2012) anafasili dhana ya kishazi kuwa ni neno au

kifungu cha maneno chenye kiima na kiarifu au kiarifu pekee

ambacho ni sehemu ya sentensi kuu.

Hivyo, kwa ujumla tunaweza kuwa kishazi ni tungo ambayo ina

kiima na kiarifu na inaweza kusimama pekee na kukamilisha

maana au inaweza isisimame pekee na kukamilisha maana.

Page 27: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

18

Sentensi

Sentensi ni tungo iliyokamili kisarufi ambayo inajitegemea

kimaana (Wahiga, 1999)

Besha (2007) anadai kuwa sentensi ni tungo iliyo kamilifu kisarufi

isiyotegemea mazingira ya mwasiliano ili kueleweka.

Kwa hiyo, kutokana na fasili za wataalamu hao tunaweza kufasili

dhana ya sentensi kuwa ni tungo yenye kifungu cha maneno chenye

muundo wa kiima na kiarifu inayojitosheleza kiimaana.

Ndugu mwanafunzi, baada ya kufafanua dhana tangulizi za

msingi katika sura hii, sasa tunajikita katika kubainisha tungo/

kategoria mbalimbali za kisintaksia ambapo tutaangalia

maana, aina, muundo na uamilifu wa tungo hiyo katika lugha

ya Kiswahili kama ifuatavyo:

Kubainisha Kategoria ya Neno

Lugha imeundwa na maneno mbalimbali, na maneno hayo

hugawanywa katika makundi kulingana na kazi zake. Hata hivyo

kategoria za maneno hazijafungika bali ziko wazi ili kupokea

maneno mapya kwa kadri yanavyozaliwa/ kujitokeza. Kila

kategoria ya maneno ina maneno mengi yenye mpangilio wake

wenye kanuni fulanifulani. Aidha, watalaamu mbalimbali

wanatofautiana katika kuainisha idadi ya maneno na istlahi

wanazotumia. Wapo wanaotaja kategoria saba (tazama Nkwera,

1978; Kapinga, 1983, Massamba na wenzake 2009). Kwa uapnde

wa wataalamu walioanisha kategoria nane (tazama Kihore, 1996).

Katika mjadala wetu wa leo tutajadili kategoria/ aina saba za

maneno kama zinavyoainishwa hapa chini:

i) Nomino,

ii) Kitenzi,

iii) Kivumishi,

iv) Kielezi,

v) Kihusishi,

vi) Kiwakilishi, na

Page 28: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

19

vii) Kiunganishi.

ANGALIZO: Ndugu mwanafunzi, mbali na kwamba

wanasarufi wanakubaliana kuhusiana na aina hizo saba za maneno

zilizoanishwa hapo juu, bado kuna haja ya kuifahamu aina ya nane

ya neo kmama ilivyoanishwa na (Kihore, 1996) anaongezea aina ya

nane katika kategoria za maneno yaani “Vihisishi”. Haya ni

maneno ambayo yanaonyesha hisia, kwa mfano, Aaah! Mungu

wangu! Jamani!

Ndugu mwanafunzi, hebu sasa tuanze kufafanua na kudadavua

kategoria za maneno katika upekee wake ili kuzielewa

kategoria hizi kwa undani zaidi. Hebu sasa tupitie kategoria

hizo kama ifatavyo:

Nomino

Khamisi (2002) anafasili dhana ya nomino kuwa ni maneno

ambayo huwakilisha majina ya watu, vitu na mahali nk.

Nomino ni neno linalotaja mtu, kitu, hali au mahali (Wahiga,

1999). Mwanasarufi huyu anafafanua zaidi kwa kusema kuwa

nomino ni muhimu sana katika lugha kwa sababu kila sentensi ni

lazima iwe na nomino au kiwakilishi chake. Hivyo, nomino ni

maneno yanayodokeza/ kutaja majina ya watu, mahali, vitu, hali

n.k. Wataalamu mbalimbali wameainisha aina za nomino kama

ifuatavyo:

Ndugu mwanafunzi zipo aina mbalimbali za nomino kutokana

na mitazamo mbalimbali ya wanasarufi lakini kuu ambazo

zinajulikana na kutumiwa na wataalamu mbalimbali ni kama

ifauatavyo:

Aina za Nomino

1) Nomino za pekee: Hizi ni nomino ambazo hutaja vitu

mahususi / vya asilia mf: mahali, mito, bahari, viungo vya

mwili n.k mfano: mlima, Dodoma, Pasfiki nk

2) Nomino za kawaida: Ni aina ya nomino ambazo hutaja majina

ya watu mfano: Eliya, Hasssani, Amina nk.

Page 29: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

20

3) Nomino za dhahania: Hizi ni nomino ambazo huwakilisha/

hutaja vitu vya kufikirika au hisi mf: Mungu, wema upendo,

malaika, uzuri, uchoyo n.k

4) Nomino za familia/ kikundi: hizi huwakilisha/ hutaja majina

yenye vitu vingi ndani yake mf: kikosi, kamati, bunge , baraza,

kundi n.k

5) Nomino za kitenzi jina: hizi hueleza vitu vinavyotokana na

matendo mbalimbali aghalabu nomino hizi hufungamana na -

ku mwanzoni mf: kuimba, kucheza, kufurahi n.k.

Dhima/ Kazi za Nomino

Nomino huweza kutofautishwa na maneno ya kategoria nyingine

kutokana na kazi zake ndani ya miundo ya tungo. Haya

yanadhihirishwa kama ifuatavyo:

i) Nomino hufanya kazi kama kiima mf:

Mtoto/ anacheza

K

Ndugu wanafunzi kabla ya kuendelea zaidi ni vema tuangalie

dhana ya kiima. Kiima ni sehemu ya mwanzo katika tungo ambayo

hueleza/ hubeba mtenda wa jambo. Kiima chaweza kuundwa na

neno moja au zaidi.

ii) Nomino hufanya kazi kazi kama yambwa. Mf:

Mwalimu/ amenunua / kitabu

K y

Ndugu mwanafunzi, hebu sasa tuone maana ya dhana hii ya

yambwa.

Yambwa ni neno au kikundi cha maneno ambacho hueleza

mtendwa wa jambo au kitu au mtu ambaye huathiriwa moja kwa

moja na kitendo kutoka kuwa mtenda. Kwa mfano, katika tungo

hiyo hapo juu neno kitabu ndiyo linaathiriwa na tendo.

iii) Vilevile nomino hufanya kazi kama yambiwa. Mf:

Mwalimu amemnunulia mwanafunzi kitabu

Yambiwa

Page 30: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

21

Ndugu mwanafunzi, kutokana na mfano huo hapo juusasa kuna

umuhimu pia ya kujua maana ya dhana ya yambiwa ili tuweze

kuelewa zaidi dhana ya hii.

Yambiwa ni neno ambalo linadokeza mtendewa wa jambo na pia ni

mtendwa ambaye haathiriwi moja kwa moja na tendo kutoka kwa

mtenda. Hivyo katika sentensi hiyo hapo juu neno mwanafunzi

linatendewa kitendo husika lakini kitendo hakimuathiriri moja kwa

moja bali huonyesha hali ya kutendewa.

Angalizo: Ndugu mwanafunzi, sentensi inaweza kuwa na

yambwa tu. Wakati mwingine inaweza kuwa na vyote, yaani

yambwa na yambiwa. Katika hali hii kuna kitu kimoja wapo

ambacho kinapokea tendo moja kwa moja na kingine hupokea

tendo lile sio moja kwa moja. Hali hii ndiyo huleta yambwa na

yambiwa

iv) Nomino huweza kuwa kijalizo yaani katika kukamilisha tu

maana ya sentensi na mara nyingi nomino ya namna hii hutokea

mwishoni mwa sentensi. Kwa mfano:

Mwalimu amenunua kitabu (Neno kitabu hapa limetumika kama

kijalizo)

Kiwakilishi

Ni maneno ambayo husimama badala ya nomino katika tungo/

sentensi kwa maana ya kuwakilisha nomino au kikundi nomino.

Aina za Viwakilishi

i) Viwakilishi vya nafsi: mimi,wewe, yeye, sisi, ninyi, wao

—Mimi ni mwalimu

—Yeye ni mwalimu

ii) Viwakilishi Vionyeshi: huyu/Yule, hiki/kile, hili/lile, hii/ ile

huu/ule hapa/pale

— Huyu ni mwalimu

— Kile ni kitabu

iii) Viwakilishi Viulizi: gani, lini, nini nk

Page 31: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

22

— Nani ni mwalimu

— Yapi yameiva

iv) Viwakilishi vimilikishi: wangu/wetu, wako/wenu,

wake/wao, yangu/yetu, lake/lao, n.k

— Kwake sikujui

— Lao limepotea

v) Viwakilishi vya sifa. Hivi ni viwakilishi ambavyo

huwakilisha nomino kwa kutaja sifa zake. Kwa mfano:

warefu, wadogo, wafupi n.k.

_ Wakubwa kwa wadogo wanasoma

_Wafupi wasimame

vi) Viwakilishi vya idadi: wote, kimoja, michache, mengi,

kumi nk.

— Mmoja ni mwalimu

— Vyote ni vitabu

Dhima za viwakilishi

Kiwakilishi hufanya kazi kama kiima cha tungo

Aidha , kiwakilishi kinadhima ya kuwakilisha nomino

Kivumishi

Ni neno/ maneno ambayo hufafanua au kueleza zaidi juu ya

nomino. Hivyo kivumishi hutoa sifa juu ya nomino yaani jinsi

nomino ilivyo, inavyoonekana, inavyofikiriwa, tabia na idadi yake.

Aina za vivumishi

Vivumishi vinaweza kugawanywa kama ifuatavyo:

i) Vivumishi vya Sifa: -ema, -dogo, -chafu, nyenyekevu n.k. Kwa

mfano:

Page 32: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

23

Mtoto mwema amekuja

Nguo chafu zimefuliwa

ii) Vivumishi vya Idadi: -chache, -ingi, -kubwa n.k

Idadi kubwa ya watanzania ni wakulima

Wanafunzi wengi wamefaulu mitihani

iii) Vivumishi vya umiliki: -ake, -anu, -etu n.k

Mwalimu wetu amesafiri

Kitabu chenu kimechanika

iv) Vivumishi viulizi: -ngapi, -gani, -ipi

Nyuzi ngapi zimekatika

Tunda lipi limeoza

v) Vivumishi vya pekee: -ingine, -ote (wote) n.k

Kucheza kwingine ni hatari

Mwanafunzi yeyote asipite hapa

Dhima za Kivumishi Kisarufi

Kivumishi hukumusha nomino; yaani hutoa taarifa juu ya nomino

au kiwakilishi chake.

. Kivumishi hutumika kama kijalizo. Angalia mfano ufauatao:

Juma ni mzuri

Hivyo, katika tungo hiyo hapo juu neno mzuri linakamilisha kitenzi

ni.

Kitenzi

Ni kategoria ya maneno yanayoeleza tendo linalofanywa na

nomino. Kisarufi huwa na sehemu kuu mbili yaani: kiima na

kiarifu. Pia ifahamike kuwa kitenzi ndiyo msingi wa sentensi kwa

maana bila kitenzi kwa hakika sentensi husika haiwezi kueleweka.

Page 33: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

24

Aina za Kitenzi

Aina za vitenzi zimejadiliwa na wanaisimu mbalimbali kwa namna

tofauti tofauti. Wataalamu hawa wameanisha aina mbili (2) za

vitenzi nazo zinafafanuliwa hapa chini:

i) Vitenzi Halisi

ii) Vitenzi Vishirikishi

i) Vitenzi halisi ni aina ya vitenzi vinavyoarifu tendo

linaliofanywa na mtu, mnyama, mdudu nk. Mfano:

analima, alikuwa anacheza n.k.

Aidha vitenzi hivi vimegawanyika katika makundi mawili yaani

vitenzi vikuu na visaidizi.

Vitenzi vikuu hubeba ujumbe unaorejelewa na kiima

Kwa mfano: analima, anacheza nk.

Vitenzi visaidizi husaidia vitenzi vikuu kuleta maana

kamili katika tungo kwa mfano: alikuwa, anataka nk.

h) Vitenzi vishirikishi nia aina ya vitenzi ambavyo hueleza

hali, tabia, sifa na mazingira ya wahusika. Kwa mfano: ni,

ndiye, u, angali, yu, si nk.

— Musa ni mkulima

— John ndiye fisadi

— Wewe u mwanafunzi mzuri

Ifahamike kuwa umbo la msingi la vitenzi ni lile ambalo

halijanyambulishwa mfano: -l-a, pig-a, fung-a, f-a, som-a, nyw-a,

som- nk.

Dhima za Vitenzi

Vitenzi hufanya kazi kama kiarifu kwa maana hutoa taarifa kile

kinachofanywa na nomino husika.

Kielezi

Kielezi ni aina ya maneno yanayofafanua juu ya kitenzi, kivumishi

na kielezi chenyewe. Kielezi kinapoeleza juu ya kitenzi ni dhahiri

Page 34: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

25

kwamba hudokeza jinsi, wakati, kwanini na kwa kiwango gani

tendo hilo linatendeka. kwa mfano:

Mwizi alipigwa sana = kielezi cha kitenzi

Mtoto ni mweupe sana = kielezi cha kivumishi

Mwalimu anaongea upesi mno = kielezi cha kielezi

Aina za Vielezi

Vielezi vimegawanywa na watalaamu katika makundi mbalimbali.

Hatahivyo hapa tutagawa kielezi katika makundi makuu manne

kama ifuatavyo:

i) Vielezi vya namna: haraka, chubwi, fofofo, kifudifudi,

mno, n.k

Mtoto anatembea haraka mno

Kikongwe amelala fofofo

ii) Vielezi vya kiasi: mara nyingi, daima, mwaka huu, mara

tano n.k

Mvua hunyesha maranyingi

Asha ni mwigizaji daima

iii) Vielezi vya mahali: ndani, juu, shimoni, nyuma n.k

Panya ameingia shimoni

Mtoto anacheza nyuma ya nyumba

iv) Vielezi vya wakati: asubuhi, mapema, siku, wiki, mwaka

n.k

Mgeni anakuja jioni

Sherehe itafanyika wiki ijayo.

Dhima/ kazi ya Kielezi

Kazi kubwa ya kielezi ni kufafanua/ kutoa taarifa juu ya vitenzi,

vivumishi na vielezi vingine

Page 35: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

26

Kihusishi

Ni maneno yanayoonyesha uhusiano wa vitu, watu, matukio, hali

na muda. Mathalani maneno hayo huonyesha uhusiano baina ya

sehemu mbili au zaidi. Haya ni maneno ambayo yana kazi ya

kisarufi ya huhusianisha maneno katika tungo au sentensi. Zipo

aina mbalimbali za vihusishi kama vile vihusishi vya wakati,

mahali, jinsi, kiasi n.k.

Aina za Vihusishi

Kimuundo vihusishi huweza kugawanywa katika makundi 2

i) Vihusishi vya a- unganifu yaani a- hupachikwa katika nafasi

iliyowazi. Kwa mfano: wa,ya,cha,la, za, vya, na, pa, mwa,

kwa nk. Hata hivyo maneno hayo hutumika pamoja na

maneno mengine kama vile: mbele ya, kwa kalamu, wakati

wa, na mwlimu, mahali pa, juu ya nk. Zingatia sentensi

zifuatazo:

a) Mtoto anacheza nyuma ya mlango

b) Musa anatembea kwa miguu

c) Kuna tofauti kati ya mwalimu na mwanafunzi

NB: Ikumbukwe kwamba a-unganifu pia hutumika kuunda

vivumishi na vielezi

ii) Aina ya pili ya vihusishi ni vile vya mkopo kwa maana

kwamba maneno hayo yametokana na kategoria nyingine za

maneno ya Kiswahili ama toka lugha za Kigeni. Aina

nyingine za maneno zinazoweza kujitokeza katika vihusishi

ni Nomino, Vitenzi na Vielezi kwa mfano: hadi, katika, tena,

kuliko, hata, lakini, bila, pasipo, ama, au, tangu, kwamba,

ingawa nk. Kama inavyodhihirika katika mifano ifuatayo:

a) Juma amenipiga tena amevunja mkono

b) Anakimbia toka shuleni hadi nyumbani

Maneno tena na hadi katika sentensi hapo juu ni vielezi lakini

katika sentensi hizo yametumika kuhusisha maneno mbalimbali.

Kwa maneno mengine katika tungo hizo yanafanya kazi ya

uhusishi pasi na uelezi, kwa mfano:

Page 36: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

27

c) Raia wameuawa pasipo makosa

d) Jino linauma sana kuliko jicho

Halikadhalika maneno pasipo na kuliko kwa uhalisia ni vitenzi

lakini katika sentensi hizo yametumika kuhusianiasha maneno

husika. Hapa pia ni vema kukumbuka kwamba sintaksia haijikiti na

dhana za maneno bali huchunguza namna vipashio vinavyofanya

kazi katika tungo kwa kuangalia mpangilio na uhusiano wake.

Dhima za Kihusishi

• Kihusishi hufanya kazi ya kuhusisha na kueleza

Viunganishi

Viunganishi ni maneno yanayounganisha maneno au mafungu ya

maneno ama sentensi. Viunganishi ni lazima viunganishe maneno

au kategoria za hadhi sawa. Kwa mfano:

Baba na mama.

Kaka analima lakini dada anasuka mkeka.

Katika mifano hiyo utaona kuwa kiunganishi na kimeunganisha

neno na neno pia kiunganishi lakini kimeunganisha sentensi na

sentensi. Aidha ni vema ikumbukwe kuwa viunganishi na vihusishi

vinashabihiana kwa sababu wakati mwingine maneno yaleyale

hutumika katika kategoria zote. Cha msingi ni kuzingatia namna

yanavyojitokeza katika tungo na kazi inayobebwa na neno hilo.

Zingatia mifano ifuatayo:

1) Baba analima na mama anapika.

2) Mwizi amepigwa na askari.

Sentensi zote hapo juu zimetumia neno na. Hatahivyo neno hilo

limebeba dhima tofauti ambapo katika sentensi ya 1 na limetumika

kama kiunganishi kwa maana kwamba kinaunganisha sentensi

mbili yaani “baba analima na mama anapika”. Katika sentensi ya

2 neno na limetumika kama kihusishi kwa mantiki kwamba

linahusisha tendo la kupigwa na askari.

Page 37: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

28

Dhima za Kiunganishi

Kiunganishi kazi yake ni kuunganisha maneno, tungo hadi sentensi.

Ndugu wanafunzi baada ya kubainisha aina za maneno na

kutazama mifano kuntu sasa tufanye zoezi lifuatalo:

Zoezi

1. Bainisha nomino katika sentensi zifuatazo na ueleze ni aina gani

ya nomino:

i) Maradhi hayo yamefutiwa chanjo

ii) Kuiga mitindo ya kigeni kumemletea madhara makubwa

iii) Darasa lile linafanya vizuri katika mitihani

iv) Utandawazi umerahisisha maisha

v) Kipungu huruka juu kwa madaha.

2. Taja dhima 4 za nomino

3. Taja aina 5 za vivumishi kisha kwa kila kivumishi tunga sentensi

mbilimbili

4. Bainisha vitenzi katika sentensi zifuatazo kisha eleza ni aina gani

ya kitenzi

i) Mbiu ya mgambo ingali inalia

ii) Kikombe ki mezani

iii) Mwalimu alikuwa anataka kupumzika

iv) Sahani zimo kabatini

v) Yule ni mhariri

vi) Babu angali analima

vii) Sisi tu wachezaji hodari

5. (a) Eleza maana ya kielezi

(b) Pigia mstari vielezi katika sentensi zifuatazo

Page 38: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

29

i) Minazi imepandwa Mombasa

ii) Mgonjwa alimeza vidonge mara mbili kwa kutwa

iii) (iii) Amina anatembea kilimbwende

iv) (iv) Daudi anazungumzwa haraka sana

v) Mwalimu anawapenda wanafunzi kwa dhati

6. Tofautisha baina ya kategoria ya kiunganishi na kivumishi

7. Tunga sentensi mbilimbili ukitumia vihusishi katika

a) Kulinganisha

b) Wakati

c) Mahali

d) Sababu

e) Mtenda

Baada kujadili kina na kufanya zoezi fupi kuhusiana kategoria

ya neno sasa tuingie katika kuangalia kategoria ya virai.

Katika mada hii ndogo tutajikita katika kubainisha kategoria

ya kirai (kikundi) ambapo tutajikita zaidi katika kubainisha aina

za virai, muundo na dhima za virai kwa ujumla. Sasa tuanze moja

kwa moja na kubainisha aina za virai vya Kiswahili kama

ifuatavyo:

Kubainisha Kategoria ya Virai

Aina za Virai

Wanaisimu mbalimbali wamebainisha aina tofautitofauti za virai

lakini kimsingi tuna aina tano za virai kama zinavyoainishwa hapa

chini:

a) Kirai Nomino (KN)

b) Kirai Kivumishi (KV)

c) Kirai Kitenzi (KT)

d) Kirai Kielezi (KE)

Page 39: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

30

e) Kirai Kihusishi (KH)

Kirai Nomino

Massamba na wenzake (2001) wanafasiri dhana ya kirai nomino

kuwa ni kirai ambacho muundo wake umekitwa kwenye nomino na

mahusiano ya nomino na neno au mafungu ya maneno. Kirai

nomino hujengwa kwa nomino moja au zaidi au kiwakilishi cha

nomino (Matinde, 2012). Hivyo kwa ujumla, tunaweza kufasili

kirai nomino kama aina ya kirai ambacho neno kuu ni nomino au

kiwakilishi cha nomino.

Muundo wa Kirai Nomino

Kirai Nomino kinaweza kuundwa na maneno yafuatayo:

(i) Nomino pekee, kwa mfano:

Baba anakula

(ii) Kiwakilishi pekee, kwa mfano:

Wewe unapenda Kiswahili?

(iii) Nomino zaidi ya moja, kwa mfano:

Walimu na wazazi walihudhuria mkutano.

(iv) Nomino na kivumishi kimoja au zaidi

Mtoto mdogo analia.

Kijana mweusi mfupi mkorofi ameumia

(v) Kiwakilishi na kivumishi

Ile nyeupe inauzwa.

(vi) Nomino na kishazi tegemezi (sentensi) kwa mfano:

Kitabu kilichonunuliwa kimepotea.

(vii) Nomino, kivumishi na kishazi tegemezi kwa, mfano:

Meza kubwa niliyopewa imevunjika.

Page 40: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

31

(viii) Nomino ya kitenzi jina kwa, mfano:

Kutembea kumenichosha.

(ix) Nomino ya kitenzi jina na kivumishi

Kucheza kwake kunahatarisha.

(x) Nomino na kihusishi/ vihusishi

Mtoto wa jirani

Askari wa jeshi la anga la Kibaha

Dhima ya Kirai Nomino

Kirai Nomino kina dhima kama kiima, yambwa na yambiwa katika

sentensi.

Kwa mfano;

Walimu wakuu waliwapa wanafunzi wao wote vyeti vyao

Kiima yambiwa yambwa

Kirai Kitenzi

Massamba na wenzake (2001) wanaeleza kirai kitenzi kama kirai

ambacho kimekitwa katika kitenzi au katika mahusiano ya kitenzi

na neno au mafungu ya maneno.

Kirai kitenzi huundwa kwa kitenzi na maneno mengine

yanayohusiana kitenzi hicho (Matinde, 2012)

Hivyo, Kirai kitenzi ni aina ya kirai ambacho neno kuu lake ni

kitenzi. Kirai hiki kina miundo ifuatayo:

Muundo wa Kirai cha Kitenzi

(i) Kitenzi kikuu pekee, kwa mfano:

Amekuja.

(ii) Kitenzi kikuu na nomino moja au zaidi, kwa mfano:

Wamenunua vitabu.

Page 41: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

32

Amempa mwanafunzi zawadi.

(iii) Kitenzi kisaidizi kimoja au zaidi na kitenzi kikuu, kwa

mfano:

Alikuwa anakula

Alikuwa anataka kununua gari

(iv) Kitenzi kikuu na kielezi

Mtoto analia sana

(v) Kitenzi kishirikishi na nomino

Juma ni mgonjwa

(vi) Kitenzi kikuu na kihusishi

Anapigwa na askari

Dhima za Kirai kitenzi

Kidhima, kirai kitenzi kinafanya kazi ya kiarifu.

Kirai Kivumishi

Matinde (2012) anafafanua kirai kivumishi kuwa ni kirai ambacho

kimekitwa kwenye kivumishi.

Kwa hiyo, kirai kivumishi ni aina ya kirai ambapo neno kuu lake ni

kivumishi. Miundo ya kirai kivumishi inaweza kuchanganuliwa

kama ifuatavyo:

Miundo ya Kirai Kivumishi

(i) Kivumishi kimoja au zaidi, kwa mfano:

Mtoto mzuri

Kijana mrefu mweusi mtanashati

(ii) Kivumishi na nomino moja au zaidi, kwa mfano:

Mti wenye matunda

Page 42: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

33

(iii) Kivumishi na kihusishi, kwa mfano:

Kamusi kubwa ya Kiswahili

(iv) Kivumishi na kishazi tegemezi, kwa mfano:

Mtoto mzuri aliyepewa zawadi

(v) Kivumishi na Kielezi kimoja au zaidi, kwa mfano:

Kiti ni kizuri mno

Amenunua mpira mweusi mzuri sana

Dhima ya Kirai kivumishi

Kirai kivumishi kinadhima ya kuvumisha.

Kirai Kielezi

Kirai kielezi ni kirai ambacho neno lake kuu ni kielezi. Kirai

kielezi kimejengwa na miundo mbalimbali kam ifuatavyo:

Miundo ya Kirai kielezi

(i) Kielezi kimoja au zaidi, kwa mfano:

Anatembea polepole.

(ii) Anaongea haraka sana.

(iii) Kielezi na kivumishi, kwa mfano:

Amekwenda shuleni kwetu.

(iv) Kielezi na kihusishi kimoja au zaidi, kwa mfano:

Amekaa ofisini kwa mwalimu.

Amenunua gari zuri kwa fedha za mkopo.

Dhima ya Kirai kielezi

Kirai kielezi kinafanya kazi ya kueleza.

Page 43: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

34

Kirai Kihusishi

Kirai kihusishi ni kikundi ambacho neno lake kuu ni kihusishi.

Kirai kihusishi kimekitwa kwenye miundo ifuatayo:

Miundo ya Kirai Kihusishi

(i) Kihusishi kimoja au zaidi na nomino

Ameweka fedha juu ya kabati

Nyimbo zitaimbwa wakati wa ibada ya mchana

(ii) Kihushi na nomino cha kitenzi jina, kwa mfano:

Amehukumiwa kwa kusaini mkataba wa kilaghai

Amepewa zawadi kwa kucheza kimasai

Dhima ya Kirai kihusishi

Kirai kihusishi hufanya kazi ya huhusisha na kueleza nomino,

kivumishi, kitenzi na kielezi

Ndugu wanafunzi baada ya kubainisha kategoria za virai

Kiswahili kwa kuzingatia vigezo vya aina, muundo na dhima

yake katika lugha, kwa sasa hatunabudi kufanya zoezi lifuatalo

ili kukazia maarifa kwa yale tuliyojifunza. Hebu sasa chukua

kalamu na daftari la mazoezi ili tuweze kufanya zoezi hili.

Zoezi

1) Tunga sentensi 10 kisha bainisha :

(a) Kirai nomino (b) Kirai kivumishi

(b) Kirai kitenzi (d) Kirai kielezi

(e) Kirai kihusishi

2) Eleza kwa mifano dhima ya Kirai Nomino katika Kiswahili.

3) Pigia mstari virai katika sentensi zifuatazo:

(i) Uwajibikaji wake ulinusuru kipato cha familia yake.

(ii) Askari wa jeshi la anga Kibaha atafanya ziara yake kesho.

Page 44: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

35

(iii) Mamba wengi hukaa kwenye ukingo wa mto.

(iv) Hawa wametumia madaraka ya kiofisi kwa manufaa yao.

(v) Furushi hilo lilipatikana katikati ya taka nyingi.

4) Bainisha dhima ya kisarufi ya kihusishi.

5) Fafanua miundo mbalimbali ya virai vya Kiswahili.

Kubainisha Vishazi vya Kiswahili

Katika kubainisha vishazi vya Kiswahili tutachunguza aina na

muundo wa vishazi tegemezi na dhima za vishazi hivyo katika

tungo za lugha ya Kiswahili. Ndugu mwanafunzi, jiandaye

kupitia mada yetu hii ndogo kwa ufasaha ili uweze kuelewa

kwa undani kuhusiana na aina ya vishazi:

Aina za Vishazi

Katika lugh lugha ya Kiswahili kuna aina kuu mbili za vishazi

ambavyo ni:

i. Kishazi Huru ( K/H)

ii. Kishazi Tegemezi ( K/Tg)

Kishazi Huru

Kishazi huru ni kishazi ambacho kinaweza kusimama peke yake na

kuleta maana kamili. Kwa mfano:

(a) Baba anakula.

(b) Tunda limedondoka.

Kishazi Tegemezi

Ni kishazi ambacho hakiwezi kusimama peke yake na kukamilisha

maana kamili. Kwa mfano:

(a) Mtoto aliyekuja jana ..............................................................

Page 45: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

36

(b) Mwalimu aingiapo darasani ...................................................

Muundo wa Vishazi Tegemezi

i. Vishazi tegemezi vyenye muundo “o” rejeshi. Hivi ni vile

vishazi tegemezi ambavyo huundwa na “o” rejeshi na -

amba-. Vishazi hivi hurejelea nyuma jambo

linalozungumzwa na Kirai Nomino Kwa mfano:

Ukuta uliojengwa umebomoka

Mbuzi aliyekata kamba amekatwa tena

ii. Muundo wa Vishazi tegemezi vyenye viambishi vya

masharti. Hivi ni vile viambaishi rejeshi ambavyo

huundwa na viambishi vya masharti kama vile : ki, nge,

ngali nk) Kwa mfano:

Wananchi wakinichagua hawatajuta.

Miundo mbinu ingeimarishwa maendeleo makubwa

yangepatikana.

Maneno yalokozwa wino hapo juu ni vishazi tegemezi

ambavyo vinadokeza masharti fulani katika tungo hizo.

iii. Vishazi tegemezi vyenye muundo wa viunganishi tegemezi.

Hivi ni vishazi ambavyo hujengwa na maneno ambayo

hudokeza utegemezi. Viambishi tegemezi huweza

kujitokeza mwanzoni mwa tungo vile: kama, ikiwa, kwa

kuwa, kwamba, japo, iwapo nk. Kwa mfano:

(a) Kama utakubali tutasafiri sote

(b) Ikiwa katiba mpya itakubaliwa wananchi

watanufaika sana.

(c) Kwa sababu zisizozuilika mkutano umeahirishwa

Maneno kuwa, kama, na ikiwa ni vishazi rejeshi vyenye

viunganishi vya masharti

iv. Vishazi tegemezi vyenye muundo wa viambishi vya wakati.

Hivi ni vishazi tegemezi ambavyo hudokezwa na matumizi

ya vihusishi vya wakati. Mara nyingi vishazi rejeshi hivi

huwa kama vijalizo katika sentensi Kama vile: hadi, kwa

Page 46: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

37

sababu, baada ya, kabla ya nk. Vilevle vishazi rejeshi

nyenye muundo huu kiambishi “ko” cha mahali na “po” cha

hali. Tazama mifano ifuatayo:

(a) Nitafurahi mno kazi hii itakapomalizika.

(b) Mgeni rasmi amekwenda wanakofuga mbuzi

(c) Sipendi namna vijana wanavyovaa.

Dhima za Vishazi Tegemezi

Katika muundo wa Kiswahili kishazi tegemezi huwa na dhima

zifuatazo:

i. Vishazi tegemezi huwa na dhima ya kivumishi cha Nomino

kwa maana hutoa taarifa juu ya Nomino/ KN. Aghalabu

vishazi hivyo huwa vimeshushwa hadhi na kushika nafasi

ya KN

(a) Mchezaji aliyetia fora amepata zawadi.

(b) Wanafunzi waliokaa wasimame.

ii. Pia kishazi tegemezi hufanya kazi ya kielezi. Hivi ni vishazi

ambavyo huwa vimeshushwa hadhi na kushika nafasi ya

kiezi au KE. Kwa mfano:

(a) Mtoto amekwenda wanakovua samaki.

(b)Mwanafunzi amechaguliwa anapopapenda.

Ndugu mwanafunzi, baada ya kupitia mada ndogo in inayohusu

uanishaji na uchambuzi wa vishazi, hebu sasa chukua kalamu yako

na daftari la mazoezi ufanye zoezi lifuatalo ili kujimairisha zaidi na

kuakazia maarifa katika mada hii.

Zoezi

Jibu maswali yafuatayo:

(1) Tunga sentensi 10 zenye vishazi huru na vishazi tegemezi.

(2) Tunga Vishazi tegemezi 5 vyenye viambishi vya masharti.

(3) Tunga vishazi tegemezi 10 vyenye viunganishi tegemezi.

Page 47: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

38

(4) Kwa kutumia mifano dhahiri bainisha kazi za kisarufi za

kishazi tegemezi.

Ndugu mwanafunzi, mada yetu ndogo inayofuata inahusu

kubainisha sentensi za Kiswahili kwa kuangalia muundo wake.

Karibu ili tuweze kuipitia mada hii kwa ufasaha:

Kubainisha Sentensi za Kiswahili

Katika mada hii ndogo, tutabainisha aina za sentensi kwa kigezo

cha kimaana na kimuundo (sintaksia) ila hatutajikita sana

kuzungumzia sentensi kwa mujibu wa kimaana kwani kozi yetu

inahusika na muundo pekee.Vilevile tutashughulikia sifa na

miundo ya sentensi mbalimbali. Hivyo sentensi za Kiswahili

zinaainishwa kama ifuatavyo:

Aina za Sentensi kwa Kigezo cha Maana/ amilifu (kisemantiki)

Katika kigezo hiki sentensi huainishwa kwa kuzingatia uamilifu

wake hususani ujumbe uliobebwa na kuwasilishwa na sentensi

hiyo. Hivyo kwa kigezo hiki tunapata sentensi zifuatazo:

(i) Sentensi swali/ ulizi. Sentensi hizi uamilifu wake ni kuuliza.

Kwa kawaida sentensi hizi huwa na pengo la taarifa

linalohitaji kujazwa na taarifa fulani na hutambulishwa kwa

uwepo wa alama ya kuuliza. Rejea mifano ifuatayo:

(a) Wanafunzi wanasoma kweli?

(b) Juma amekwenda wapi?

(ii) Sentensi maelezo/ taarifa/ arifu. Ni sentensi ambazo hulenga

kutoa taarifa fulani. Sentensi hizi huishia na nukta/ kituo

kikuu. Mifano ya sentensi za aina hii ni kama ifuatavyo:

(a) Walimu wetu wanafundisha kwa bidii.

(b) Asha ameondoka.

iii) Sentensi amri/ agizi. Sentensi hizi kwa kawaida huwa

hazina kiima na huwa na lengo la kuamuru tendo fulani

Page 48: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

39

lifanywe. Huundwa na kitenzi cha kuamuru. Sentensi hizi

huishia na alama ya mshangao. Zingatia mifano ifuatayo:

(a) Njoo hapa!

(b) Kaa chini haraka!

iv) Sentensi mshangao:

Hizi ni sentensi zinazooyesha kushangazwa kwa msemaji

na tukio fulani. Ni sentensi za kitashititi ambazo huweza

kuuliza swali ambalo jibu lake linafahamika. Rejea mifano

ifuatayo:

(a) Baba kafariki kweli?

(b)Timu yetu imefungwa kweli?

(c) Hata wewe umefeli?

Aina za Sentensi kwa Kigezo cha Kimuundo (kisintaksia)

Uainishaji wa sentensi kimuundo huzingatia muundo wa sentensi

hususani muundo wa vipashio vilivyounda sentensi na mahusiano

ya vipashio hivyo. Kimuundo sentensi huweza kuainishwa katika

makundi yafuatyo:

(i) Sentensi sahili

(ii) Sentensi changamani

(iii) Sentensi ambatano.

Labda tuanze kuzichambua mojamoja ili kuelewa miundo yake.

Sentensi Sahili

Hizi ni sentensi zinazoundwa kimsingi na kishazi kikuu/huru

kimoja ambacho maana yake ni kamilifu. Mara nyingi sentensi

sahili huwa na muundo wa kiima na kiarifu. Vile vile sentensi

sahili huwa na wazo moja.

Muundo wa Sentensi Sahili

Sentensi sahili huweza kuundwa na vijenzi vifuatavyo:

i. Kitenzi kikuu au kishazi huru kimoja, kwa mfano:

Page 49: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

40

- Mkulima analima.

- Rais anahutubia taifa

ii. Kitenzi kikuu na kitenzi kisaidizi kimoja au zaidi, kwa

mfano:

- Mama alikuwa anapika chakula.

- Mama alikuwa anataka kupika chakula.

iii. Kitenzi kishirikishiki, kwa mfano:

- Ndizi zi mbovu.

- Mimi ni kiongozi.

- Kapu halina kitu.

Sentensi Changamani

Hizi ni sentensi zinazoundwa na kishazi kikuu/ huru kimoja na

kishazi tegemezi kimoja au zaidi. Hivyo, sentensi changamani

inatokana na kuwapo kwa vipashio yenye hadhi tofauti katika

tungo moja yaani kishazi tegemezi na kishazi huru. Sasa tutazame

miundo mbalimbali ya sentensi changamani kama ifuatavyo:

i. Muundo wa vishazi tegemezi vyenye urejeshi na kishazi huru

kwa mfano:

- Chuo kilichofungwa kimefunguliwa

- Mtoto alipozawadiwa zawadi alikimbia

ii. Muundo wa vishazi tegemezi vyenye viunganishi tegemezi na

kishazi huru kwa mfano:

- Wakati mvua inanyesha wageni walikuja.

- Ikiwa katiba mpya itakubaliwa wananchi watanufaika

sana

iii. Muundo wa vishazi tegemezi vyenye viambishi vya masharti na

kishazi huru, kwa mfano:

- Wananchi wakinichagua hawatajuta

- Angekuja kuniomba ningemsaidia

Page 50: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

41

Sentensi Ambatani/Ambatano

Hizi ni sentensi ambazo huundwa na vishazi huru viwi au zaidi.

Vishazi huru hivi huweza kunganishwa na viunganishi ambatani

kama: na, lakini, tena, wala nk. Tutazame miundo ya sentensi hii:

i.Vishazi huru viwili au zaidi, kwa mfano:

- Siogopi wala kutishika.

- Mama analima na kupanda lakini watoto wanacheza.

ii. Vishazi tegemezi na vishazi huru, kwa mfano:

- Mtoto uliyemuona jana ameondoka na mama yake

amesafiri.

- Mahindi yaliyokobolewa ni ya Juma lakini yale

ambayo hayajasagwa ni ya Asha.

iii.Vishazi huru visivyounganishwa na viunganishi ambatani, kwa

mfano:

- Mwambie aondoke

- Ametibiwa hajapona

Ndugu mwanafunzi, baada ya kupitia mada yetu ndogo ya

kubainisha sentensi za Kiswahili, hebu sasa tufanye zoezi fupi

lifuatalo ili kupima uelewa wetu na kukazia maarifa:

Zoezi

Jibu maswali yote kwa ukamilifu:

1. Tunga sentensi tano kwa kila aina ya sentensi zifuatazo yaani;

sahili, ambatani, amri, ulizi, changamani, arifu.

2. Jadili miundo ya sentensi mbalimbali (sahili, changamani,

ambatani).

Uchanganuzi wa Tungo

Ni mchakato wa kubainisha vipashio mbalimbali vinavyounda

tungo. Vipashio hivyo hubainishwa kwa kuanzia vipashio vikubwa

hadi vidogo. Vipashio hivyo huainishwa kwa njia mbalimbali

kama vile:

Page 51: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

42

i) Maelezo,

ii) Mshale

iii) Jedwali/ visanduku

iv) Matawi/ ngoe/ mchoroti

Aidha, uchanganuzi wa tungo hujiegemeza katika mkabala fulani

yaani hutumia mtazamo/ mkondo fulani wa mawazo. Hivyo, katika

uchanganuzi wetu tutatumia mikabala yote miwili yaani; mkabala

wa sarufi mapokeo na mkabala wa sarufi muundo virai.

Uchanganuzi wa Tungo kwa Mkabala wa Kimapokeo

Kutokana na mjadala uliopita, tukumbuke ya kwamba, sarufi

mapokeo ilijikita katika kuchanganua sentensi sahili pekee.

Vilevile katika sarufi hiyo sentensi zilichanganuliwa kwa

kuzingatia uamilifu yaani kazi za vipashio hivyo katika tungo. Hata

hivyo, uchanganuzi wa tungo katika mkabala ulipitia awamu

mbalimbali, kilichojitokeza katika awamu hizo ni mabadiliko ya

istlahi za kiuchambuzi. Mkabala wa kimapokeo ulitumia vigezo

vifuatavyo:

(i) Kubainisha sehemu kuu mbili za sentensi yaani kiima na kiarifu

(ii) Kubainisha aina za maneno

Ndugu mwanafunzi baada ya kupitia vigezo vitumikavyo

katika uchanganuzi wa tungo kimapokeo sasa tutachanganua

tungo kwa kutumia vigezo hivyo:

a) Njia ya maelezo, kwa mfano,

Mtoto anakula chakula kizuri.

Sentensi imeundwa na kiima na Kiarifu. Kiima kimeundwa na

nomino, nomino ni mtoto. Kiarifu kimeundwa na kitenzi,

shamirisho na chagizo. Kitenzi ni anakula, shamirisho ni nomino

na chagizo ni kielezi. Nomino ni chakula na kielezi ni kizuri.

Page 52: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

43

b) Njia ya matawi

Mwanafunzi ameleta machungwa mengi.

S

K A

T SH CH

N T N E

Mwanafunzi ameleta machungwa mengi

c) Njia ya jedwali

Walimu wanne wamekuja leo

S

K A

N V T CH

E

Walimu Wane Wamekuja Leo

d) Njia ya mshale

Kijana mtanashati amenunua gari zuri.

S K + A

K N + V

N Kijana

V mtanashati

A T + SH + CH

T amenunua

Page 53: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

44

SH N

N gari

CH E

E zuri

Ndugu wanafunzi katika uchanganuzi wa tungo kimapokeo

tumeona kuwa kuna istlahi mbili zimejitokeza yaani kiarifu

shamirisho na chagizo. Ni vema tukazieleza kwa kifupi kabla ya

kuendelea zaidi

Kiarifu

Kiarifu ni kategoria maalum katika sentensi inayotaja kiambajengo

kikubwa kimojawapo katika muundo wa sentensi ambacho ni kirai

kitezi. Kiarifu hubeba viambajengo vingine muhimu vya sentensi

vikitanguliwa na kitenzi abavyo hujadiliwa pamoja. Ni kategoria

ambayo kwa ujumbe wake hutupa habari kuhusu kiima cha

sentensi. Mfano:

(i) Mtoto amekula chakula

ii) Mama amenunua kikombe kizuri sana

Shamirisho (yambwa, yambiwa)

Ni kipashio cha kikazi (kiuamilifu) ambacho hutokea katika

sehemu ya kiarifu hudokeza mtendewa au kitendewa na mtendwa

au kitendewa na jambo. Kwa maneno mengine shamirisho ni

nomino inayojitokeza upande wa kiarifu. Rejea mifano ifuatayo:

(i) Mama anapika ugali

ii) Mwalimu amempa mwanafunzi zawadi

Chagizo

Ni kipashio cha kikazi ambacho hutokea upande wa kiarifu hutoa

taarifa juu ya tendo namna, wapi saa ngapi limefanyika. Hivyo,

chagizo ni sehemu ya tungo inayokaliwa na kielezi. Zingatia

mifano hapa chini:

(i) Ondoka upesi

(ii) Mwanafunzi anatembea harakaharaka

Page 54: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

45

Uchanganuzi wa Tungo kwa Mkabala wa Kimuundo

Katika uchanganuzi wa tungo kwa mkabala wa sarufi miundo virai

vigezo vifuatavyo huzingatiwa. Rejea hapa chini:

i. Kubainisha aina ya tungo

ii. Kubainisha sehemu kuu mbili ya kikundi nomino na

kikundi kitenzi (KN na KT)

iii. Kubainisha virai vinavyounda sehemu kuu za sentensi

iv. Kubainisha aina za maneno katika virai vilivyobainisha

v. Andika sentensi tena mwishoni

Ndugu mwanafunzi, baada ya kutizama vigezo vya kuzingatia

katika kuchambua tungo kimuundo sasa tuingie katika uchanganuzi

wa tungo kwa njia mbalimbali kama ifuatavyo:

a) Njia ya Mshale

Mwanafunzi hodari amefaulu mitihani yake

S Sahili

S KN + KT

KN1 N1 +KV1

N1 Mwanafunzi

KV1 V1

V1 Hodari

KT T +KN2

T Amefaulu

KN2 N2 +KV2

N2 Mitihani

KV2 V2

V2 Yake

Page 55: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

46

b) Njia ya Matawi

Kuku mgeni atakaa na kamba mguuni

S. Sahili

KN KT

N1 KV T KH KE

V H KN2 E

N2

Kuku mgeni atakaa na kamba mguuni

c) Njia ya Maelezo

Mwanafunzi aliyeleta vitabu ameondoka leo.

Sentensi mwanafunzi aliyeleta vitabu ameondoka leo ni sentensi

changamano ambayo imeundwa na Kirai Nomino na Kirai Kitenzi.

Kirai nomino kimeundwa Nomino na Kirai Kivumishi, Nomino ni

mwanafunzi na Kirai kivumishi kimeundwa na kivumishi na

Nomino. Kivumishi ni aliyeleta na nomino ni vitabu. Kirai kitenzi

kimeundwa na kitenzi na Kirai kielezi, kitenzi ni ameondoka na

Kirai kielezi kimeundwa na kielezi. Kielezi ni leo.

Angalizo: Katika uchanganuzi wa sentensi changamano kishazi

tegemezi huweza kuchanganuliwa kama kirai kivumishi, kirai

kielezi na sentensi. Rejea zaidi kwenye kipengele cha dhima za

kishazi tegemezi hapo juu (2.5)

d) Njia ya Visanduku

Baba mkubwa analima shambani na watoto wa jirani wanacheza

mpira.

Page 56: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

47

S. Ambatani

S1 U S2

KN KT KN KT

N1 KV T KE N2 KH T KN

V E H N N

Baba Mkubwa analima shambani na Watoto wa jirani wanacheza mpira

Page 57: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Pili Error! No text of specified style in document.

48

Muhtasari wa Somo

Katika somo hili ya pili, tumejifunza sehemu uchambuzi wa

sintaksia ya Kiswahili. Somo hili imejikita kuchambua kategoria za

kisintaksia ambapo imeanza kwa kufafanua dhana za msingi kama

vile: kategoria, tungo, neno, kirai, kishazi na sentensi. Vilevile,

somo hili limemakinikia kwa kubainisha kategoria za maneno,

virai, vishazi na sentensi ambapo katika ubainishaji huo aina,

miundo na dhima za kategoria hizo vimeelezwa kwa kina ili

kujenga msingi thabiti katika uchanganuzi wa tungo mbalimbali.

Mwisho, katika somo hili la pili sentensi zimechanganuliwa kwa

njia mbalimbali na kwa kutumia mikabala ya sarufi mapokeo na

miundo virai. Katika somo hili pia, tumejifunza sehemu kuu mbili

za sentensi katika muundo wa Kirai Nomino (KN) na Kirai Kitenzi

(KT). Pia tumejifunza sifa mbalimbali za lugha pamoja na uhusiano

uliopo kati ya tanzu mbalimbali za fasihi.

Ndugu mwanafunzi, baada ya kupitia vipengele hivyo hapo

juu, hebu tufanye zoezi fupi la kujipima uelewa wako

kuhusiana na mada yetu tuliyojifunza. Hebu chukua kalamu

yako na daftari la mazoezi ufanye zoezi hili.

Zoezi la Somo

Jibu maswali yafuatayo:

1. Changanua tungo zifuatazo kwa kutumia mkabala wa sarufi

miundo virai:

(i) Kitabu kilichopotea jana kimeokotwa shimoni (matawi)

(ii) Mwalimu hodari anafundisha kwa bidii na wanafunzi

makini wanasikiliza kwa makini lakini wanafunzi watundu

wanacheza bila woga (mshale)

(iii) Baba analima na mama anachota maji bombani kwa John

(Jedwali)

(iv) Askari kanzu wa Mwanalumango aliyeongoza magari

amepewa zawadi (maelezo)

2. Tunga sentensi tano kisha changanua kwa kutumia mkabala

wa sarufi mapokeo (tumia njia zote)

Page 58: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

49

3. Kwa kutumia mifano dhahiri fafanua vipengele vifuatavyo:

(i) Kiima

(ii) Kiarifu

(iii) Shamirisho

(iv) Chagizo

4. Tofautisha uchanganuzi kwa kutumia mkabala wa sarufi

mapokeo na ule wa sarufi miundo virai.

Page 59: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

50

Somo la Tatu

Kufafanua Semantiki ya Kiswahili

Utangulizi

Katika sura hii ya tatu tutashughulikia semantiki ya Kiswahili

katika muktadha wa maana kwa kuzingatia misingi ya kinadharia

ya kiisimu. Semantiki ya Kiswahili itafafanuliwa kwa kuzingatia

mambo yafuatayo: Kwanza, sura hii itafafanua dhana ya maana na

utata wake katika kufasiliwa.Vilevile katika sura hii

tutashughulikia mikabakla ya semantiki, aina mbalimbali za maana

na uhusiano wa kifahiwa. Sura hii pia itafafanua nadharia ya maana

kimuktadha ambapo misingi ya nadharia hii itaelezwa. Mwisho

sura itafafanua ubora na udhaifu wa nadharia kimuktadha.

Matokeo

Baada ya kukamilisha somo hili utaweza:

Kufanunua dhana ya semantiki na maana

Kuchambua mikabala ya semantki

Kufafanua aina za maana

Kufafanua Nadharia y

Kufafanua Dhana ya Semantiki na Maana

Dhana ya semantiki imejadiliwa na wataalamu wengi kwa

mitazamo tofautitofauti kama inavofafanuliwa hapa chini:

Richards et al (1985) wanaeleza kuwa, semantiki ni stadi ya maana.

Awali neno semantiki lilitumika kumaanisha sayansi ya “maana”

kwa ujumla na ambayo ilishughulikiwa na wanasaikolojia,

wanamantiki, wanaanthropolojia na wengine. Baadaye stadi hii

ilijishughulisha zaidi na maana katika muktadha wa lugha ya

mwanadamu.

Semantiki ni utanzu wa isimu unaochunguza maana za maneno

katika lugha ya mwanadamu (Habwe na Karanja, 2004).

Page 60: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

51

Matinde (2012) anafasiri dhana ya semantiki kama utanzu wa isimu

unaochunguza maana katika lugha.

Ndugu mwanafunzi, kwa kuzingatia mitazamo ya wataalam

mbalimbali kuhusiana na dhana ya semantiki tuaweza kusema

kuwa, semantiki ni tawi la isimu linaloshughulikia maana za

maneno katika tungo za lugha ya Kiswahili katika viwango

mbalimbali. Vilevile, tunaweza kusema kuwa, semantiki ni utanzu

wa isimu unaochunguza maana katika lugha ya mwanadamu kwani

hutafiti maana za fonimu, mofimu, maneno na tungo. Maana

hushughulikiwa katika viwango vyote vya lugha kama vile sauti,

maneno na sentensi.

Kuchambua Mikabala ya Semantiki

Maana ndicho kiepengele muhimu zaidi katika uchunguzi wa lugha

ya mwanadamu. Hii ni kwa sababu kazi kuu ya lugha ni

mawasiliano na mawasiliano huhusisha upashaji wa ujumbe ambao

hueleweka katika maana ya tamko. Pasipo kupasha ujumbe

hapatakuwa na mawasiliano na kwa hivyo lugha haitakuwa

imetekeleza wajibu wake. Ujumbe hudhihiriki katika maana na

ufafanuzi wa maana zilizobebwa na vipashio vya lugha

vinavyohusika kama vile fonimu, neno na sentensi. Lengo la

kisheria za kifonolojia na kisintaksia ni kuunda tungo zenye maana

katika muktadha wa sentensi.

Kwa sababu hii ni sawa kusema kuwa maana hushughulikiwa

katika tanzu za isimu kama fonolojia, mofolojia na sintaksia.

Semantiki inakuwa ndio makutanio ya taaluma hizi kama

ilivyowakilishwa katika mchoro ufuatao:

Fonolojia Mofolojia

SEMANTIKI

Sintaksia

Aidha semantiki huonyesha uhusiano baina ya vipashio na dhana

au vitu ambavyo vipashio hivi huwakilisha katika mazingira.

Page 61: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

52

Ndugu mwanafunzi, kwa ujumla semantiki hujishughulisha na

masuala sita (6) ya msingi. Sasa hebu zingatia madondoo

yafauatayo ili uweze kuelewa kwa undani dhana hii ya

semantiki na maeneo ambayo taaluma hii imejikita:

1. Maana na uanishaji wa maana za maneno

2. Maana za tungo

3. Taratibu za kuchambua maana

4. Etimolojia za maana ya maneno

5. Uhusiano wa kimaana katika sentensi

6. Nadharia za uchambuzi wa maana

Ndugu mwanafunzi, zipo sababu mbalimbali ambazo zilifanya

tawi hili la semantiki kutokuendelea kama matawi mengine ya

isimu. Hii inaonekana kwamba, katika uchunguzi wa kiisimu,

inaonyesha kuwa semantiki ndilo tawi ambalo

halikushughulikiwa kwa undani na upana kama matawi yale

mengine. Hebu sasa tupitie mjadala huu mfupi ili tuweze

kuelewa sababu hasa zilizofanya tawi hiili kuwa nyuma.

Sababu za Tawi la Semantiki Kutoendelea kama Matawi

mengine ya Isimu

Tawi la semantiki ni tawi ambalo halikutiliwa mkazo na wanaisimu

wengi kinadharia na pia katika maandishi. Hii ni kwa sababu ya

utata uliokuwa umezuka miongoni mwa wanaisimu kuhusiana na

tawi hili. Utata huo umetokana na sababu zifuatazo:

1. Taswira miongoni mwa baadhi ya wanaisimu kuwa semantiki ni

taaluma ngumu. Ugumu huu unatokana na kuwa taaluma hii

haijajulikana katika kiwango cha nadharia, kama tutakavyoona

baadaye, misingi ya kinadharia ya semantiki si thabiti kama ilivyo

katika tanzu nyingine za kiisimu kama fonolojia, mofolojia na

sintaksia.

2. Baadhi ya wanaisimu hushughulika na muundo wa lugha na

kuupuuzia misingi ya kisarufi ktegemea maana kwa imani kuwa ni

rahisi kuchunguza muundo kwani una ruwaza inayotambulika ilhali

maana ni ya kinadharia. Kwa mfano, ni rahisi kuchambua muundo

wa neno “mwalimu” kama {mu + alimu} kuliko kueleza maana

yake. Hii ni kwa sababu, katika kuchambua maana, licha ya kujua

muktadha wa matumizi ni sharti ufahamu fikra za mzungumzaji

Page 62: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

53

jambo ambalo si rahisi. Hii ndiyo sababu iliyofanya maana

kushughulikiwa zaidi katika filosofia hapo awali.

3. Maana wakati mwingine hurejelea vitu ambavyo havipatikani

katika mfumo wa lugha na hivyo huhitaji ujuzi mwingi wa

mazingira yaliyo ne ya lugha. Hapana mtu aliye mjuzi wa mabo

yote yaliyo katika mazingira.

4. Hakuna misingi mahususi ya kinadharia misingi mahususi ya

kinadharia ambayo imezuliwa kuhusu semantiki. Kuna mitazamo

mingi inayotofautiana kuhusu taaluma hii ya semantiki ambayi

imeletezea kuwepo na utata na matawi mengine. Utata huu

unatokana na ukweli kuwa semantiki ni tawi la isimu lenye

usambamba na matawi mengine ya isimu. Kwa mfano, uhusiano

wa mofu na mofimu katika mofolojia na ule wa muundo wa ndani

na wan je wa sentensi katika sintaksia ni uhsiano wa kimaana. Hata

hivyo si rahisi kuonyesha wazi kwa kutumia nadharia muafaka na

kuweka mipaka kati ya mofolojia na semantiki au kati ya sintaksia

na semantiki au kati ya sintaksia na semantiki katika mifano hii.

Hivyo basi, semantiki haishughulikiwi kikamilifu kwa sababu

haijulikani ni wapi iambatishwe.

5. Hata hivyo taaluma hii imeanza kushughulikiwa na wataalamu

wengi wa isimu katika miaka ya hivi karibuni kwamba hata misingi

yake ya kinadharia imeanza kuaimarika. Ingawa bado taaluma hii

haijakua kiasi cha tanzu nyingine lakini imeaendelea kwa kiasi

fulani kuliko kipindi cha hapo awali.

Viwango vya Maana

Kama tulivyoeleza hapo awali, jukumu la kimsingi la semantiki ni

kueleza maana ya maneno na dhana katika viwango mbalimbali

kama ifuatavyo:

Kwanza, ni kiwango cha vipashio huru ambapo wanasemantiki

hushughulikia maana katika viwango vya kipashio huru na maana

ya vipashio hivi katika tungo. Hii ina maana kuwa maana

huchunguzwa katika kiwango cha maana cha maneno huru na

maana katika tungo kama vile sentensi ambacho huitwa maana ya

kileksika.

Pili, ni kiwango cha maneno ya kisarufi ambacho huitwa maana ya

maneno ya kisarufi katika sentensi.

Tatu ni kiwango cha matini ambapo baadhi ya wanaisimu

wameshughulikia maana kwa kaiwango cha matini. Uchunguzi wa

maana kwa kiwango cha matini huitwa pragmatiki. Ni vigumu sana

Page 63: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

54

kuweka mipaka katika vitengo hivi vya uchunguzi. Hata hivyo ni

muhimu kutambua kwamba ili mtaalamu yeyote wa semantiki

kufaulu, ni sharti awe na ujuzi wa kutosha wa muundo na

utamaduni wa lugha.

Ndugu mwanafunzi, baada kujadili kwa kina historia ya

semantiki na ufafanuzi wa dhana hii kwa mujibu wa wataalam

mbalimbali, hebu sasa tupate ufafanuzi wa dhana ya maana

kama ifuatavyo:

Dhana ya Maana

Dhana ya maana imeshughulikiwa na wataalamu wengi kama vile:

Habwe na Karanja (2004), Massamba (2004), Matinde (2012) na

wengineo. Hata hivyo, wataalamu hawa wanakiri kwa dhati kuwa

dhana ya maana ina utata katika kufasiliwa kwake. Kuna mogororo

mkubwa kati ya wataala wa isimu kuhusiana na dhana ya maana.

Utata huo unatokana na ukweli kwamba:

- Maana ni dhana dhahania ijengekayo kichwani mwa msemaji

na msikilizaji

- Hakuna mlandano wa moja kwa moja baina ya maana na

taswira, jambo au kitu

kinachozungumziwa/kinachowakilishwa

- Aidha utata wa kufasiri maana unatokana na ukweli kwamba

baadhi ya maana hazibainishwi na neno, au ishara yoyote bali

hujidhihirisha katika kinyume cha kitu kizungumzwacho.

Hivyo, kutokana na madai hayo ndiyo maana tunaona kuwa dhana

ya maana ni telezi yaani haiwezi kuelezwa kiuraisi na kijuujuu.

Hali hali hii ilipelekea kuzuka nadharia mbalimbali zinazotanzua

dhana ya maana.

Kwa mujibu wa Ogden na Richards (1923) kama alivynukuliwa na

Wanjala (2002), wametoa orodha ndefu sana ya maana ya dhana ya

maana kama ifuatavyo: Maana kama:

- Sifa halisi ya kitu

- Maneno yanayofafanua neno

- Athari ya kitu Fulani katika mustakabali wetu

- Unasibishaji wa neno

Page 64: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

55

- Nafasi ya kitu katika mfumo kama vile chai ni kiamsha

kinywa.

- Uwezekano wa kiuaminifu wa kitu

- Kinachorejelewa na mtumiaji ishara fulani

- Kinachoaminika kuwa kinarejelewa na mtumiaji ishara Fulani.

- Kinachoaminika kurejelewa na mpokeaji kuwa kinarejelewa na

mtumiaji ishara Fulani.

Wataalamu hawa mametoa orodha hii kuonesha mkanganyiko

utokeao kutokana na jamii kutokukubaliana juu ya maana ya

istilahi za kimsingi katika lugha. Hata hivyo, wanakubali kuwa

fikra na lugha haviwezi kutenganishwa.

Bloomfield (1933) kama alivyonukulia na Wanjala (2002),

anajaribu kutanzua mgogoro huu kwa kupendekeza kuwa mtindo

wa kisayansi utumike katika utafutaji wa maana yaani kueleza

maana ya dhana kwa kutaja viambato vyake.

Kwa mujibu wa Habwe na Karanja (2004:204) neno maana lina

fahiwa nyingi. Watu wa kawaida wamelitumia kumaanisha vitu

mbalimbali. Kwa mfano baadhi ya fahiwa zake ni kama

zinavyoelezwa katika matumizi yafuatayo ya sentensi za Kiswahili:

1. Una maana gani kwa kufika umechelewa?

2. Yale mawingu meusi yana maana mvua itanyesha sasa hivi

3. Hiyo nguo nyekundu inamaanisha hatari.

4. Neno “vilua” lina maana gani?

5. Mradi huu una maana kubwa.

Tungependa kuangalia maana inayozingatiwa wakati neno

linapotumiwa katika masuala kama vile katika sentensi ya (4) hapo

juu. Katika kujaribu kueleza maana ya maana, wanaisimu

wameieleza dhana hii katika vitengo viwili vikuu; maana ya msingi

na maana ya ziada

Maana ya ziada pia huweza kuwa na vitengo vyake kama maana

husishi, maana elekezi na maana ya umaanisho.

Dhana ya maana ni ya kidhahania kwa sababu maana haina

muundo thabiti kama vile viamabjengo vingine vya lugha vya

Page 65: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

56

kifonolojia, kimofoloji au kisintaksia. Maana hutegemea pia

dhamira ya mtoa ujumbe na fasiri ya mpokeaji. Maana kwa hiyo ni

dhana tata ambayo si rahisi kueleweka kwa uwazi.

Hata hivyo, wanaisimu wamejaribu kuieleza dhana hii ya maana

kitendaji. Kama tulivyoona hapo awali, maana inaweza

kubainishwa kiisimu katika kiwango cha neno na katika kiwango

cha tungo kama vile sentensi na zaidi ya sentensi yaani kiwango

cha matini.

Kufafanua Aina za Maana

Aina za Maana

Wanaisimu mbalimbali wameeleza dhana ya aina za maana katika

vitengo viwili vikuu; maana ya msingi na maana ya ziada. Hata

hivyo Leech (1981) amebainisha aina za maana zifuatazo:

1. Maana ya msingi (conceptual meaning)

Hii ni aina ya maana ambayo haibadiliki mfano; mwanamke,

mwanaume. Maana hii hutaja sifa zake kuu pamoja na zile sifa

bainifu ambazo hupelekea kupata maana kuhusu mtu au kitu.

Maana ya msingi huweza kuwekwa katika viwango mbalimbali

kwa mfano, katika kiwango cha neno huru huitwa maana ya

kileksika. Hii hurejelelea maana ya msamiati wa lugha ambayo ni

ile inayowakilishwa na vidahizo kama kamusi. Vidahizo hivi ni

kwa mfano maneno kama vile “gari”, “mtu”, “barabara”, na

mengine yenye kujisimamia kama maneno huru.

Maana ya kileksika pia huitwa maana ya msingi ambayo ndiyo

maana kuu ya neno. Maana hii huwa haibadiliki kutegemea athari

za kimazingira au muktadha. Fahiwati nyingine zote za maana

zinazoibuka, huibuka kutokana na msingi na maana hii. Maneno

katika muktadha wa maana kimsingi yanaweza kuwa na maana

nyingi za ziada lakini zote zikiibuka hutokana na maana hii ya

msingi.

2. Maana ya Kisarufi

Hii ni aina nyingine ambayo hurejelea maana katika muktadha wa

matumizi. Hapa maana ya neno huangaliwa kulingana na mazingira

ambamo limetumiwa. Hii ndiyo maana inayorejelwa wakati mtu

Page 66: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

57

anapoulizwa swali kuwa: una maana gani? Katika kujibu tukio

fulani la mawasiliano.

3. Maana ya Ziada

Maana hii hurejelea ile maana ya kimuktadha au kimazingira,

lakini yenye kuwa na msingi, kuzalishwa na kuhusiana na maana

ya msingi Hapa tunaweza kusema kuwa kile mtu anachokisema si

lazima kiwe ndicho anachokimanisha. Kile anachokisema ndicho

maana ya msing na kila anachokimaanisha ndicho maama ya

muktadha. Kwa mfano, tuangalie maana katika sentensi zifuatazo:

4. Maana dokezi (Connotative meaning)

Ni aina ya maana ambayo hutokana na umbo la kitu, kisaikolojia,

kimatamshi mf. Kiumbo kushika mimba, kisaikolojia umama.

5. Maana ya kijamii / kimtindo (social meaning)

Ni aina ya maana ambayo hupatikana kutokana na mazingira ya

kijamii, wakati, utamaduni, kijiografia, kiuwasilishaji, hadhi,

ubinafsi n.k

6. Maana ya kihisi (emotive meaning)

Ni maana za kihisia ambazo hutokana na upotoshaji wa aina fulani

wa maana ya msingi. Ni maana itokanayo na utumizi usio wa moja

kwa moja ili kutoa maana. Maana ya kitu huwa ni ya mzunguko,

fiche, kwa mfano maana za hisia hutegemea sana Kiimbo

kiwekwacho katika neno au Kiimbo kiwekwacho katika sentensi.

7. Maana ambatani (collocative meaning)

Maana ambatani au tangamano, ni aina ya maana itokanayo na

utangamano au uambatani wa baadhi ya maneno. Kwa maneno

mengine ukitaja neno fulani linaukilia maana fulani. kwa mfano:

- Mrembo – Msichana

- Ujamali – Mvulana

- Jitu hili ni la miraba mine – Mwanaume

Page 67: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

58

Katika lugha maneno pia hujengwa kwa mtindo huo mifano zaidi

Samaki – Kiumbe wa majini/baharini au Swala - Kiumbe wa

msituni. Ukitaja kimoja tu mfano samaki unakuwa umekiondoa

kingine swala.

8. Maana ya kidhima/kidhamira (thematic meaning)

Hizi ni aiana za maana ambazo ujumbe wake unapangwa kufuatana

na msisitizo wa kitu. Maana hutokana na dhamira ambayo msemaji

alikusudia ili imfikie msikilizaji, kwa mfano sentensi zifuatazo:

(a) Mwalimu amempiga mtoto (Mwl. Mtenda)

(b) Mtoto amepigwa na mwalimu (Mtoto Mtendwa)

(c) Msichana yupo darasani (Jibu la swali lililoulizwa) – Msichana

yuko wapi?

(d) Darasani kuna msichana (Swali)

9. Maana akisi/Kimwangwi (reflected meaning)

Ni maana ambazo ukitaja kitu fulani au maana fulani unakonyeza

maana nyingine. Maana akisi haziachani kwa mfano: Jamii –

Mkusanyiko wa watu pamoja.

Ndugu mwanafunzi, baada ya kujadili kwa kina aina

mbalimbali za maana kuna haja ya kuangalia uhusiano wa

maneno mbalimbali katika semantiki. Uhusiano huu huitwa

uhusiano wa kifahiwa. Karibu sasa katika mada yetu hii ili

tuweze kuipitia kwa undani.

Uhusiano wa Kifahiwa katika Semantiki

Uhusiano wa kifahiwa ni kipengele kimojawapo katika semantiki

leksia. Maneno katika lugha yoyote huingia katika mahusiano

mbalimbali. Licha ya mahusiano ya vikoa vya maana, maneno

huweza kuhusiana hivi kwamba maana ya neno moja inaweza

kuwa kinyume cha maana nyingine. Katika uhusiano huu maana ya

neno moja kueleweka na pengine hata kuwepo kwa neno lingine

katika mfumo mzima wa ishara za lugha ( Saussure 1916).

Mahusiano ya maneno haya husaidia kutoa maana ya maneno

mengine. Kuna aina nyingi za uhusiano wa kifahiwa katika lugha

za binadamu kama ifuatavyo:

Page 68: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

59

Sinonimia

Usinonimia ni uhusiano wa kileksia ambapo huwa kuna maumbo

kati ya lugha amabyo maana zake zake ni sawa. Maumbo haya

huitwa sinonimu ambavyo ni visawe vya dhana moja. Maneno haya

yanaingia katika uhusiano mwimo. Usinonimia huweza kuletwa na

sababu mbalimbali kama ifatavyo:

(i) Ukopaji wa msamiati: Kwa mfano, teknolojia –technology

(ii) Jinsia: Kwa mfano, hali ya kuwa na sura nzuri hurejelewa kwa

kisaawe cha urembo kwa wanawake na ujamali kwa wanaume.

(iii) Dini: Kwa mfano neno kwaresma kwa wakristo na saumu kwa

waisilamu au neno mjahidina kwa waisilamu na muumini wa

wakristo, neno msikiti wa kwa waisilamu na kanisa kwa wakristo.

(iv) Tofauti za kimaeneo: Kwa mfano neno ugali linaweza likawa

sima Tanzania, sembe Congo, Rwanda na Burundi.

(v) Tofauti za kilahaja: Kwa mafo neno chumvi na munyu, kwa

hiyo maneno haya yana maana moja lakini hutumika katika

maeneo tofautitofauti.

(vi) Taaluma: Kwa mfano neno aya katika riwaya na neno ubeti

katika shairi, zote zina maana inayofanana.

(vii) Wakati, kwa mfano:

Kwa kuhitimisha kipengele cha usinonimia, kwa mfano kuwepo

kwa neno “mahaba” katika Kiswahili kunasaidia kueleza neno

“mapenzi”. Tunaweza kusema kuwa, maneno haya huweza kuingia

katika uhusiano wa aina hii unaitwa usinonimia. Maana ya maneno

haya hayapatikani kwa misingi wa vijenzi vya lugha lakini kwa

jinsi ambavyo yanahusiana na maneno mengine.

Hebu tuangalie aina nyingine za mahusiano ya kifahiwa kama

ifuatavyo:

Hiponimia

Ni maneno ambayo maana yake hujumuishwa katika maana ya

neno jingine, yaani uhusiano uliopo kati ya neno maalum na lile la

kijumla. Kwa maneno mengine haiponimia ni uhusiano wa lugha

ambapo maana Fulani ya neno ni sehemu ya maana kubwa ya neno.

Neno hilo lenye maana kubwa huitwa neno jumuishi ilihali maneno

yenye maana ndogo huitwa haiponimu. Katika lugha ya Kiswahili,

Page 69: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

60

neno mnyama, ambalo ni neno kuu, lina uhusiano wa kihaponimia

na maneno ng’ombe, mbuzi, duma, nguchiro, nguruwe n.k. Kwa

hiyo neno mnyama limejumuisha maneno yote yaliyotajwa hapo

juu.

Homonimia

Huu ni uhusiano mwingine wa kileksika ambapo kuna mafano wa

maneno katika maumbo yake lakini yana maana tofauti. Hata hivyo

kufanana huku ni kwa kisadfa tu kwani maeneo haya hayan usuli

mmoja wa kihistoria. Maana za maneno haya huwa ni tofauti.

Ifuatayo ni baadhi ya mifano ya homonimia katika lugha ya

Kiswahili:

(a) Panda –kuweka mbegu ardhini

Panda – kukwea mti au mlima

Panda – kugawaika kwa njia

Panda – chombo cha mgambo

(b) Ota – kuona picha usingizini

Ota – kuonyesha kwa kidole

Ota – kukaa juani ili kujipasha joto

Tunasema kuwa maneno haya ni homonimu kwa sababu

yamefafana katika maubo ya kifonetiki. Katika kamusi maneno

haya huingizwa kwa vidahizo tofauti (Taz Kamuisi ya Lugha

Sanifu, 1981). Hii ina maana kuwa kila homonimu huwa na leksia

na huwa na mnyambuliko wake tofauti. Kwa kuhitimisha tunawe

za kusema kuwa, homonimia huwa ni maneno yenye maana tofauti

na yaya historia tofauti katika lugha lakini kufanana kwake katika

maubo ni kwa kisadfa tu.

Polisemia

Hii ni hali ambapo maneno huwa na maana zaidi ya moja na

maneno hayo yanakuwa na uhusiano wa kihistoria. Tofauti na

homonimia ambapo maneno hayana uhusiano wakati katika

polisemia, maneno huwa na uhusiano. Polisemi ni uhusiano

ambapo kuna umbo moja la neno lenye maana mbalimbali. Mifano

ya polisemi ni kama ifauatavyo:

(i) Mdomo- neno mdomo hapa inaweza kumaanisha mdomo wa

binadamu au Mdomo wa chupa

Page 70: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

61

(ii) Mguu - neno hili linaweza kumaanisha – mguu wa binadamu

au mguu wa meza au kiti.

(iii) Jicho – neno hili linaweza kumaanisha jicho la mti, jicho la

sindano n.k

Aghalabu, polisemia ni uhusiano ambapo maana moja hutokana na

maana ya neno jingine. Hali hii huwepo kwa sababu kuna sifa

Fulani za kufanana katika vitajwa viwili. Kwa mfano, kuna

uhusiano baina ya “mdomo wa chupa” na “mdomo wa binadamu”.

Antonimia

Ni uhusiano wa kimuundo ambapo kuna maneno katika lugha

anbayo maana za ke ni kinyume, yaani many ya maneno

hupingana. Kwa mfano:

Cheka --- lia

Nenda --rudi

Pata – poteza

Penda --- chukia

Moto -- baridi

Mara nyingi katika lugha huwa kuna vinyume vya utoano.

Vinyume vya viwango ni kama vile moto/ baridi. Hii ina maana

kuwa ni maana ambazo ziko kwenye mkondo mmoja. Kitum

kinapokuwa baridi huwa kina moto mdogo ilhali kitu kinapokuwa

moto sana huwa na baridi kidogo. Antonimu zingine huwa ni za

kimtoano kwa maana kuwa anaposema huwa unatoa ile nyingine.

Kwa mfano, neno “mke” na “mume” ni antonimu za kiutoano.

Ndugu mwanafunzi, baada ya kujadili kwa kina uhusiano wa

maneno mbalimbali katika semantiki yaani mahusiano ya

kifahiwa. Karibu sasa katika mada yetu hii ndogo ya mwisho ili

tuweze kufikia tamati ya moduli yetu.

Kufafanua Nadharia ya Maana Kimuktadha ya Ludwig Wittgenstain

Ndugu mwanafunzi kabla ya kuzama kiundani katika kufafanua

nadharia ya Ludwig ni vema tukadurusu kwa kifupi dhana nzima

ya nadharia ili kujenga mwega wa mhadhara wetu kama ifuatavyo:

Page 71: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

62

Kufafanua dhana ya nadharia

Massamba (2004) anafasili dhana ya nadharia kuwa ni taratibu,

kanuni na misingi ambayo imejengwa katika muundo wa mawazo

kwa madhumuni ya kutumiwa kama kiolezo cha kuelezea jambo.

Kwa mantiki hiyo, nadharia inaweza kufasiliwa kuwa ni maelezo

yanayojengwa katika misingi ya kanuni na taratibu ambazo

huongoza katika kutekeleza jambo na hatimaye kupata hitimisho

fulani.

Nadharia ya Maana Kimukutadha

Nadharia hii iliasisiwa na mwanafalsafa Ludwig Wittgenstein

katika miaka ya 1930. Katika nadharia yake anadai “maana ya neno

ni matumizi yake katika lugha” (Philosophical Investigations,

1963:43). Hii ina maana kuwa ili kupata maana ya neno ni sharti

lihusishwe na muktadha wa matumizi wa neno hilo.Hivyo,

nadharia hii inachukulia kuwa muktadha ndiyo mwafaka na

muhimu katika kufasiri na kufafanua maana ya maneno mbalimbali

nadharia hii imejengwa katika misingi ifuatayo:

- Nadharia hii inasisitiza kuwa katika muktadha wa kijamii

ndipo maana hupatikana. Hii ina maana kuwa kuna maneno

ambayo huwa, na maana katika jamii fulani na yasiwe na

maana katika jamii zingine. Kwa mfano jamii ya wafugaji

huwa na majina fulani yanayorejelea mifugo yao lakini hali

itakuwa kinyume kwa jamii isiyofuga. Katika matumizi ya

neno ndipo unaweza kupata maana. Kwa manzili hiyo neno

haliwezi kupata maana bila kupelekwa katika uwanja wake wa

kimatumizi

- Vilevile nadharia inaona kuwa ili maana ipatikane ni sharti

ihusishwe na muktadha wa usemaji. Kwa manzili hiyo ni

dhahiri kuwa muktadha wa usemaji ndio huongoza uteuzi wa

maneno fulani. Kwa mfano, neno “chai mbili” litapata maana

ikiwa litatumiwa mgahawani, hotelini na sehemu yoyote

inayotoa huduma ya chakula kinyume na hapo neno hilo halina

maana.

- Aidha nadharia inasisitiza kuwa maana hupatikana kwa

kutumia muktadha wa kiisimu. Hii ina maana kuwa maana ya

neno hutegemea nafasi ya utokeaji katika sentensi. Kwa mfano

neno “kifaru” litapata maana yake kutokana na mazingira ya

kiisimu ambamo neno hilo limetumika.

Page 72: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

63

Nadharia hii haina matatizo ya nadharia zilizotangulia kwa vile

inawezekana kabisa kuzungumzia matumizi ya neno lolote lile, na

kwa hakika, ni matumizi yaukiliayo maana za maneno. Watoto

wajifunzapo lugha hujifunza maana za viyambo vya lugha

kutokana na jinsi viyambo hivyo vitumiwavyo na wanalugha, na

jinsi wao wenyewe wavitumiavyo viyambo hivyo katika

kuwasiliana na wanalugha hao.

Kufafanua Ubora na Udhaifu wa Nadharia ya Maana Kimuktadha

Ubora wa nadharia ya maana kimuktadha unaweza kuelezwa kama

ifuatavyo:

a) Ni kweli maana za maneno hupatikana pale maneno hayo

yanapotumika

b) Wajifunzaji lugha hujifunza jinsi mneno yanavyotumiwa na

wanalugha husika

Aidha nadharia hii ina mapungufu yafuatayo:

a) Si kweli kuwa maana hupatikana katika matumizi yake

kwani kuna maneno mengi katika lugha huweza kupewa

maana yake kabla ya kutumiwa. Kwa mfano ‘istilahi’ au

maneno yaelezayo dhana mpya huundwa kabla maneno

hayo hayajatumiwa kama vile: neno “tehama”.

b) Kwa kutumia nadharia hii maana za mneno zinaweza

zikapunguzwa Kwa mfano neno “moshi” tunaweza

kutambua kuwa fahiwa yake katika muktadha huo ni “kileo

kikali”, hatuwezi kusema kuwa maana ya moshi ni

matumizi yake yarejeleayo “kileo kikali”. Badala yake

tutasema kuwa mojawapo ya maana ya ‘moshi’ ni kileo

kikali.

Ndugu wanafunzi tufanye zoezi lifuatalo:

Page 73: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Somo la Tatu Error! No text of specified style in document.

64

Muhtasari wa Somo

Katika moduli hii mwanafunzi amepitia mada mbalimbali

zimepangwa katika masomo mbalimbali; Somo la kwanza imejadili

dhana ya mkabala, aina na misingi ya sarufi mapokeo na miundo

virai. Pia, sehemu hii imegawanyika katika sehemu mbili, yaani ya

sehemu ya kwanza na sehemu ya pili. Misingi ya Mkabala wa

Sarufi Mapokeo, Misingi ya Mkabala wa Sarufi Mapokeo na

Misingi ya Mkabala wa Sarufi Miundo Virai, Misingi ya Mkabala

wa Sarufi Miundo Virai. Katika mada hizi vipengele vifutavyo

vilipitiwa: kategoria ya neno au virai vinavyounda kirai nomino

(KN), au virai vinavyounda kirai kitenzi (KT) na maneno

yanayounda virai vilivyoainishwa na kufafanua dhana za

kisintaksia lugha na sarufi na kuonyesha uhusiano uliopo katika

tanzu za sarufi.

Somo hili ya tatu imeshughulikia ufafanuzi wa semantiki ya

Kiswahili. Katika ufafanuzi huo mambo yafuatayo

yameshughulikiwa. Kwanza, sura hii imefasiri dhana za semantiki

na dhana ya maana kwa undani. Pili, somo hii imefafanua mikabala

ya semantiki.

Somo hili imefafanua aina mbalimbali za maana. Mwisho somo

limefafanua nadharia ya maana kimuktadha ya Ludwig

Wittgeinstein ambapo nadharia imejadiliwa kwa ufasaha

sambamba na kufafanua ubora na upungufu wa nadharia hii. Baada

ya kupitia moduli yetu hii, mwanafunzi atakuwa amepata maarifa

ya kutosha huhusiana na moduli hii.

Page 74: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

65

Zoezi la Somo

Jibu maswali yote kwa kuandika ili kujipima uelewa wako, katika

mada hii ya utumizi wa lu

1. Fafanua aina mbalimbali za maana.

2. Elezea chanzo cha mgogoro kuhusiana na dhana ya maana.

3. Elezea mtazamo wa Bloomfield kuhusiana na dhana ya maana.

4. Kuna aina nyingi za uhusiano wa kifahiwa katika lugha za

binadamu. Jadili mahusiano ya kifahiwa katika semantiki kwa

kutoa mifano.

5. Jadili misingi mbalimbali ya nadharia ya maana kimuktadha.

6. Fafanua ubora na udhaifu wa nadharia ya maana kimuktadha.

7. Bainisha viwango vya maana kwa kutoa mifano.

Page 75: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Marejeleo Error! No text of specified style in document.

66

Marejeleo Besha, R. M. (1994). Utangulizi wa Lugha na Isimu. Dar es

Salaam: Dar es Salaam University Press.

Habwe, J. na Peter, K. (2004). Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi: Phonix.

Khamis, A. M na John. K. G. (2002). Uchanganuzi wa Sarufi ya Kiswahili. Dar es Salaam: Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Massamba, D. P. B. na wenzie (2001) Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu: Sekondari na Vyuo. (SAMIKISA), Dar es Salaam: TUKI.

Massamba, D. P. B (2004), Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha, Dar es Salaam: TUKI.

Matei, A. K. (2008). Darubini ya Sarufi ya Kiswahili: Ufafanuzi Kamili wa Sarufi. Nairobi: Phonix.

Matinde, R.S (2012). Dafina ya Lugha: Isimu na Nadharia,Kwa sekondari, Vyuo vya kati na Vikuu, Mwanza, Tanzania: Serengeti Educational Publishers (T) Ltd.

Wahiga G. (2003). Sarufi Fafanuzi. Nairobi Longhorn Publishers Ltd.

Wesana-Chomi, E. (2003). Kitangulizi cha Mofolojia ya Kiswahili. Sebha: Chuo Kikuu cha Sebha.

Ogden, C. K & Richards, I. A. (1923). The meaning of meaning. London: Routledge & Kegan Paul.

Page 76: -MODULE - mwalimuwakiswahili.co.tz · Stashahada ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu kwa Masafa S. L. B. 20679 Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed Tanzania Nukushi: +

Kimeandaliwa na:Taasisi ya Elimu ya Watu WazimaS.L.P 20679, Dar es Salaam, TanzaniaSimu:+255 22 2150836 Barua pepe: [email protected], Tovuti: www.iae.ac.tz