msirudi nyuma - mwalimu wa kiswahili · mioyo yao ya upendo juu yetu hakika hiki ni kitabu chao....
TRANSCRIPT
1
2
MSIRUDI NYUMA
Mwl. John Magoda jr.
3
Kitabu hiki kimeandaliwa na
John Magoda jr
S.L.P.30407 KIBAHA ,PWANI
+255 718821168
4
YALIYOMO
1.TABARUKU.............................
2.SHUKURANI...............................
3.UTANGULIZI.....................................
4.MAHAKAMANI .................................
5.UKWELI WANGU...............................
6.MSIRUDI NYUMA................................
5
TABARUKU
Napenda kukitabaruku kitabu hiki kwa walimu
wote wa shule za msingi ndani na nje Tanzania kwa
mioyo yao ya upendo juu yetu hakika hiki ni kitabu
chao.
Lakini pia nakitabaruku kitabu hiki kwa rafiki
yangu Salumu Mustafa kwa kunipa changamoto
chanya mpaka kukimaliza kuandika kitabu hiki
hakika hiki ni kitabu chako.
6
SHUKURANI .
Kwanza nianze kwa kumshukuru mwenyezi Mungu
muumba wa mbingu na ardhi kwa kutujalia uhai na
heri zote za dunia hii lakini pia ni kwa mapenzi yake
yeye pekee ndio yamefanikisha kukamilika kwa
kitabu hiki.
Lakini katika kukiandaa kitabu hiki wako wengi
walioshiriki kwa hali na mali hasa ushauri na
kunitimia moyo wako wengi lakini nitawataja
wachache kwa niaba ya wengine marafiki zangu
Patrick Alex Shampundu , Antony Chavala , Adeltus
Mutajwah , Jackson Msigwa ,Dickson Turuka,
7
Benjamini Mwakitalu,Costantine Peter
Masele,Brother Chriss, Jacob Joel , Yustina
Joseph ,Salum Mustapha.
Lakini pia katika eneo la ushauri wa kiuandishi
Shukurani ziende kwa Elenzian Komba ,Rasi
Mbwana, Mwanagenzi Michael the
Great ,Dk.Raymond Nusura Mgeni , kwa ushauri
wao katika kazi zangu.
Lakini shukurani zangu za dhati ziende kwa walimu
wangu na wahadhiri wangu wote kwani maarifa yao
yamekuwa na msaada mkubwa sana katika kusaidia
kuandaa kitabu hakika Mungu awabariki sana .
8
Pia shukurani zangu ziende kwa wasomaji wangu
wote wa kazi zangu hakika nawashukuru sana
maana naandika kwa ajili yenu na wamekuwa kila
wakisoma huwa wanarudisha mrejesho juu ya kazi
zangu hakika mwenyezi Mungu awabariki sana .
Pia mwisho kwa mkururo napenda kutoa shukurani
zangu za dhati kwa mpenzi wangu na rafiki yangu,
mshauri wangu Kandi kwa upendo wake kwangu
hakika amekuwa mtu ambaye akinifariji sana na
amekuwa nami katika vipindi vyote vya raha na
shida hakika nakupenda sana.
9
UTANGULIZI
MSIRUDI NYUMA ni kitabu kilicho katika muundo wa
barua ambacho kinaangalia suala la taaluma ya ualimu na
walimu kwa ujumla lakini pia lengo kubwa la kitabu hiki
ni kuwatia moyo na kuwapa hamasa na walimu ambao
ndio kiungo muhimu sana katika suala la elimu mahali
popote duniani .
Lakini pia lengo ni kutaka kukumbusha na kuelekeza
baadhi ya mambo kuhusiana na walimu na taaluma ya
ualimu na kuleta mwanga kwa ajili ya wanajamii ili
waweze kutambua masuala muhimu kuhusu taaluma ya
ualimu na maisha ya walimu kimawanda mapema .
10
Licha ya kuwa kitabu kinazungumzia masuala ya
kitaaluma na kijamii kuhusu taaluma ya ualimu na
walimu wenyewe lakini pia kimetumia lugha ya kifasihi
lengo likiwa ni kuwafanya wasomaji kuchota maarifa kwa
kutumia lugha yenye ujazo mwingi wa vionjo vya kisanii
katika suala la lugha .
Lakini kitabu kiwe taa ya kuwamulika waandishi wengine
waanze kuibuka na kuaandika kuhusu taaluma hii ya
ualimu na walimu kwa ujumla katika nyanja zote za
kielimu lakini pia kitabu hiki kimekuja wakati ambao kwa
sasa taaluma ya ualimu iko katika mtikisiko mkubwa sana
na changamoto mbalimbali mbali na zile ambazo
zimezoeleka lakini hili la sasa ni tabaka la baadhi ya
viongozi wa kiserikali kuingilia taaluma ya ualimu pasipo
11
kufuata taratibu na kuwa vikwazo na sehemu ya
kuwashusha morali walimu wengi sana nchini Tanzania .
Hivyo nikutakie usomaji mwema na wenye tafakuri ya
kina .
John Magoda jr.
©2019
12
MAHAKAMANI.
Ni majira ya asubuhi kabisa huku siku ikiwa imeanza kwa
ubaridi mororo na jua likiwa limechelewa kuchomoza ,
na sauti za kunguru na ndege ndio zilikuwa zikisikika tu
kwa wingi hii ni kutokana eneo la mahakama kulikuwa
kuna miti iliyokuwa mikubwa ambayo ndo ilikuwa ni
makazi pendwa kabisa kwa ndege kupumzika baada ya
siku ndefu ya kutafuta chochote kitu kwa ajili ya kujilisha
wao pamoja na makinda yao .
Nikitizama naona kundi kubwa la watu ambao
wamefurika kwa wingi katika eneo la mahakama ili kuja
kushuhudia hukumu ya kesi yangu ambayo imegubikwa
na utata wa hali ya juu labda niseme kuwa ni kwa mara
ya kwanza kushuhudia idadi kubwa ile ya watu katika
13
eneo la mahakama kwani ni wazee ,vijana hadi watoto
labda niseme unaweza kufananisha idadi ya watu ile
idadi ya kumpokea mgombea wa urais kwa tiketi ya
ukawa Ndugu Edward Lowasa katika uchaguzi wa
mwaka 2015 pale jijini mbeya lakini kumbe ni eneo la
mahakama wengi wakisubiria hukumu yangu .
Muda wa kuingia mahakamani ulifika watu walisimama
pale hakimu alipokuwa ameingia ndani ya mahakama ile
ambayo ilijaa watu ndani na nje ya mahakama na mpaka
ikapelekea askari wa jeshi la polisi kuongezeka eneo la
mahakama na huku wakiwa wamejidhatiti kabisa kama
vile kuna kesi ya ugaidi inaendelea katika eneo la
mahakama kumbe ni kesi ya kijana mzalendo wa
14
kitanzania mzalendo wa moyo ambaye ameponzwa na
ukaribu wake na ukarimu kwa wanafunzi wake .
Lakini ninachokiamini ni mimi na Mungu pekee ndiyo
tunaojua ukweli wa tukio hilo kwani kwa walimwengu
licha ya kujieleza kadri ya uwezo wangu kuwaambia
kuwa kamwe sikuhusika na tukio hilo na sitambui lolote
lile kwao ilikuwa ni ngumu sana maana mshikwa na
ngozi ndio mla nyama na kweli ngozi ilishikwa kwangu
lakini kamwe kwa dhati ya moyo hiyo nyama sikuila
lakini kwa vile hali imeshatokea hakuna nmna zaidi ya
kusubiria kile ambacho Mheshimiwa hakimu atakiamuru
lakini ndani ya akili yangu nilijua kuwa tayari
nimeshapoteza dira na uelekeo wa maisha yangu mapema
kabisa .
15
Ndani ya mahakama ile nilipokua nikitazama watu
machoni mwao hasa walimu wenzangu wengi macho
yalikuwa ni mekundu sana wengi wakijizuia kulia
kutokana na uchungu lakini kwa vile ni eneo la
mahakama ilibidi wajikaze kisawasawa hili kusubiria
hukumu ya muheshimiwa hakimu kuitoa juu yangu dhidi
ya tukio la mauaji ambalo lilitokea ambalo liligubikwa na
utata mkubwa sana .
Na ikumbukwe kuwa zilikuwa zimepita wiki kama mbili
nyuma kuna mwalimu alihukumiwa kwa kunyongwa
mpaka kufa kwa kosa la kumuadhibu mwanafunzi hali
iliyoacha simanzi kubwa sana katika taaluma ya ualimu
lakini pia kuna walimu ambao waliandamana kwa ajili ya
madai ya malipo yao na kutopandishwa madaraja kwa
16
muda mrefu lakini waliishia mikononi kwa polisi ambapo
walipigwa na kupelekea wengine kupata ulemavu wa
viungo hiyo yote ni kwajili ya kudai haki yao stahiki
yao ,lakini pia ni katika mfuatano huo wa matukio ndo
ambapo kuna mwalimu alifuatwa na kiongozi wa kata
ofisni na kutolewa lugha ya matusi na kebehi ya hali ya
juu kabisa kwa hakika taaluma ya ualimu ilikuwa katika
miezi migumu sana lakini hapo sijaelezea wale walimu
ambao walikuwa wanasumbuliwa na imani za kishirikina
kutoka kwa wanajamii yani usiku wanalala ndani na
asubuhi wanajikuta wamelala mchangani na wengine
wakijikuta wako juu ya miembe .
17
Kwa muda huo mahakama ilikuwa imetulia watu
wote wakiwa wametulia ili kujua nini hatima ya kesi
yangu huku wakimsubiria hakimu Patrick
Shampundu kutoa hukumu hiyo na baada ya taratibu
za kimahakama kumalizika sasa ilifika kipindi cha
kusikiliza hukumu juu ya kesi yangu iliyokuwa
inanikabiri hakika nafsi na moyo vilisimama kwa
muda mpaka nikahisi labda nimepooza mara baada
ya hakimu Patrick Shampundu alipoanza kuisoma
hukumu yangu ndipo alipotamka hukumu ambayo
kwangu ilikuwa kama mkuki wa moto uliopenya
ndani ya moyo wangu .
18
Hakika nilibubujikwa na machozi ambayo sijawahi
kububujikwa na machozi kiasi kile hasa niliposikia
kuwa nahukumiwa kunyongwa mpaka kufa hakika
sio ndani ya mahakama tu bali hadi nje ya
mahakama vilisikika vilio kama vile kuna msiba
mkubwa sana kama ule wa mwaka 1999 wa hayati
baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
hakika watu hawakuamini kuwa naweza kusitisha
maisha yangu ndani ya muda mfupi kabisa hakika
hili lilikuwa pigo kubwa sana sio kwa familia yangu
tu bali kwa taifa kwa ujumla kusubiria hukumu
yangu hiyo hakika ilikuwa ni siku mbaya zaidi
kwangu .
19
Basi ikawa hivyo hukumu ikatoka natakiwa
kunyongwa na sio kunyongwa tu mpaka nife hakika
niliumia sana na watu wote waliumia sana hasa
walimu wenzangu wote waliumia zaidi sana maana
ni muda mfupi tu tangu nihamie katika shule hiyo
ambayo ilikuwa nyuma kielimu lakini mabadiliko
makubwa sana yalianza kuonekana lakini hakuna
nmna lazima nitumikie hukumu yangu hiyo hakika
niliondoka eneo la mahakama huku nyuma vilio
vikiongezeka sana nikawa sina budi kuwapungia
mikono na kuwaambia kamwe wasirudi nyuma .
Mbaya zaidi hukumu yangu ilivyopita ilikuwa katika
orodha na majina ya hukumu yangu yalisainiwa na
20
rais wa nchi tukiwa na wengine hivyo ikawa
inabakia siku ya kunyongwa kwangu
Hakika majonzi na huzuni viliendelea kutawala
mtaani na maeneo ya Tanzania kwa ujumla
walihuzunika sana tena sana huku mimi moyoni
nikiwa nalia sio tu kwa ajili ya kunyongwa bali
ndoto zangu na mipango yangu mikubwa katika
elimu ya nchi yangu ya Tanzania na ambavyo
sijaitumia kabisa maarifa yangu na ujuzi wangu
kikamilifu hicho ndo kinachoniuma zaidi.
Siku ya kunyongwa ilikuwa ni tarehe 30/4/1990 na
nilikuwa na siku mbili tu za kuendelea kuwa hai
21
lakini nilikuwa na nafasi moja tu ya kuwaelezea
umma wa Tanzania kuhusu yale yaliyonisibu na
kuhusu taaluma ya ualimu na elimu kwa ujumla
licha ya kuwa na changamoto mbalimbali kamwe
msirudi nyuma . Ndipo nilipewa peni na karatasi ili
niweze kuaga kabla tamati ya maisha yangu kufika .
22
UKWELI WANGU.
Kwenu Wanajamii .
Nashika kalamu ndogo kabisa lakini naiona nzito
mithili ya chuma chenye uzito wa kilo mia tano
sabini na huku moyo wangu ukivuja damu kutokana
na uchungu mkubwa wa maisha yangu kuishia
njiani kwa namna hii lakini natambua kuwa kila
nafsi itaonja umauti ila katika njia ambayo
mwenyezi Mungu pekee ndio anafahamu hivyo
nikiendelea kuhuzunika kwa hakika nitakuwa na
mkufuru mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na
ardhi inanibidi nimuachie yeye pekee kwa yote
23
yaliyotokea mimi mwenzenu lakini kamwe msirudi
nyuma .
Kutoka ndani ya moyo wangu licha ya kuwa na
kinyongo kizito lakini haina budi nikiri kupitia
waraka huu kuja kwenu walimu wenzangu
nimewasamehe wale wote katika kipindi cha maisha
yangu walinikiwaza na kuniudhi lakini pia hata
katika kesi iliyokuwa ikinikabiri pia nawasamehe
sitaki kuondoka katika dunia hii pana kabisa nikiwa
na kinyongo cha namna yoyoye ile hivyo moyo
wangu kwa sasa ni mweupe mithili ya theluji ya
mlima Kilimanjaro unaoangaza Afrika nzima
24
kutokea kaskazini mwa nchi yangu ninayoipenda
tokea utoto wangu hadi hatua hii .
Lakini pia kwa wale ambao nilishawahi kuwakwaza
au kuwa kero katika kipindi chote cha maisha yangu
nichukue nafasi hii kuwaomba radhi najua kabisa
ombi langu litawafikia huko popote mlipo wale wote
kuanzia chekechea hadi elimu yangu ya juu hadi
kule finland msamaha wangu ufike huko hadi kusini
mwa nchi yangu msamaha ufike na uvuke mipaka
yote ya nchi kutoka ndani ya moyo wangu nasema
kuwa nahitaji msamaha wenu ndugu zangu
nafahamu fika sina nafasi nyingine ya kuwaomba
msamaha isipokuwa katika waraka wangu huu kwa
25
hakika naomba Mungu uwajalie roho nyepesi ya
kuweza kunipatia msamaha ndugu yenu .
Nikifikiri siku yangu ya kuwekwa ndani ya kitanzi
na kunyongwa hakika moyo wangu unakuwa mzito
na mwili unashikwa na ganzi kabisa lakini sina tena
nafasi ya kuwa nanyi kimwili isipokuwa kimawazo
naweza ishi nanyi milele na milele hasa nikiangalia
kwa jicho la kumbukizi safari ya maisha yangu ya
kitaaluma tokea elimu ya awali hadi kufikia katika
shahada ya pili na huku nikiwa katika kumalizia
kuandika tasnifu yangu ya shahada ya tatu kuhusu
ubora wa darasa la awali na mafanikio ya kitaaluma
ambapo naamini ingeenda kuwa msaada mkubwa
26
sana kwa elimu ya awali ambayo ndo msingi
mkubwa sana katika maendeleo ya kielimu katika
taifa lolote lile ulimwengu .
Nafahamu fika imetolewa hukumu ndani ya muda
mfupi tu na pia nikahukumiwa adhabu ya
kunyongwa mpaka kufa hakika mpaka sasa sifahamu
ni nani aliyeamua hayo yote kunifika mimi kabisa
hakika ndo nashikwa na uchungu kutoka ndani ya
moyo wangu lakini lakini kamwe siwezi mlaumu
mtu yeyote yule kuhusu suala la hukumu yangu
sababu kwa hali halisi ilivyokuwa hakika sio hakimu
wala polisi na hata wapelelezi wa kesi yangu lakini
kwa uchungu kabisa naingalia safari yangu ya
27
kitaaluma na malengo yangu na mipango yangu yote
inaelekea kupotea hewani hakika nafsi inaniuma
sana lakini hakuna namna naamini kupitia waraka
huu kuna vitu mfajifunza na tutakwenda kupiga
hatua lakini mwili na nafsi vyote vinauma na masaa
nayo yanakimbia kwa mithili ya moto wa nyika
uliowekewa mafuta ya petroli ukisindikizwa na
upepo mkali kama wa kanda ya kati Dodoma hasa
katika maeneo ya kongwa ndo nilivyoyaona masaa
hayo yalivyokuwa yakikimbia.
Hakika naomba waraka huu ufike pande zote za nchi
kuanzia kusini kule kwa ndugu zangu na upande
hadi kanda ya kati kote lakini pia ufike hadi kule
28
nyanda za juu kusini mikoa yenye uzalishaji
mkubwa kabisa wa chakula katika taifa langu lakini
waraka usikomee huko bali upande hadi kaskazini
mwa nchi yangu ikibidi ufike hadi katika kilele cha
mlima Kilimanjaro lakini ushuke na kufika
magharibi mwa taifa langu hadi mashariki huko na
pia uvuke mipaka ya nchi kwa majirani zetu wote
wenye mapenzi ya dhati na sisi .
Hakika uwafikie wanafunzi wote ,wakulima na hata
wale waajiriwa wa serikali na hata wafanyakazi
waliojiajiri wenyewe lakini pia uwafikie wakina
mama wote walioko mahospitalini wanaojiandaa
kutuletea watoto wapya katika uso huu wa dunia hii
29
iliyojaa walimwengu wa kila aina lakini waraka
uwafikie hata kule katika vijiji vya ndani kabisa ya
taifa hili kwa watu wa jinsia zote ,rangi zote hakika
naamini kuwa siku zangu za kuendelea kuishi ni
chache kabisa kuendelea kuishi nilikuwa na malengo
na maono makubwa sana ya kuja kutumia taaluma
yangu ya ualimu na utaalamu katika elimu kuja
kuinua suala la elimu ya awali na kwa wanafunzi
wenye mahitaji maalum hasa matatizo mahususi ya
ujifunzaji kwa lugha ya kiingereza wanaita specific
learning difficulties .
Natambua kuwa hukumu yangu ilitoka na wengi
walikuwa na maswali mengi na asilimia kubwa
30
walipata habari juu kuwa nimeua mwanafunzi wa
kike na kumuweka ndani ya kabati baada ya
kumuingilia kimwili mbaya zaidi hadi kinyume cha
maumbile ili niweze kupata utajiri na kupata vyeo
katika taaluma ya ualimu na kupata nafasi ya
kualikwa zaidi na zaidi katika makongamano
makubwa duniani kama muelimishaji ndo maana
nikaamua kufanya mauaji hayo ya kinyama tena kwa
mwanafunzi ambaye nilikuwa naye bega kwa bega
tena wa jinsia tofauti na mimi jina lake Asha hakika
nafsi yangu inaumia sana nilivyokuwa nikisikia
shutuma zangu dhidi ya suala hilo lakini kwa vile
nilijitahidi kadri ya uwezo wangu kuelezea lakini
31
sikueleweka zaidi niliambulia kupigwa zaidi na
kupelekea mwili wangu kuwa na vidonda na mambo
mengi niliyofanyiwa hakika siwezi sema nitakufa
nayo .
Kwa dhati ya moyo kabisa sikuweza fanya tukio hilo
wengi wakihusisha tukio hilo na maendeleo yangu
ya kitaaluma na safari nyingi za nje ya nchi kwenye
mataifa makubwa na bora kielimu nilipokuwa napata
nafasi ya kwenda kushiriki katika maboresho ya
masuala yao ya kielimu na kupelekea kupata kipato
kikubwa sana na mara thelathini zaidi ya mshahara
wangu wa ualimu wa shule ya msingi tena nikiwa
nimechagua kufundisha kama mwalimu wa elimu
32
ya awali na huku nikiwa nimekataa ofa za kazi zaidi
ya arobaini kutoka katika vyuo vya ndani ya nchi na
nchi jirani kuwa mhadhiri kwenye vyuo vikuu na
vya kati lakini kutokana na tangu nikiwa mtoto
mdogo nilisema nitakuwa mwalimu wa awali
nilifanya hivyo
Labda niwaeleze jinsi jumba bovu hilo la kesi ya
mauaji liluvuonitokea mimi mwenzenu nilikuwa
mwalimu wa awali katika shule moja huko nyanda
za juu kusini ambako ndo chimbuko la asili yetu na
kweli nilipendwa sana na wanafunzi wangu
waliokuwa idadi ya wanafunzi hamsini na katika
33
shule hiyo kutokana na mfumo wa ufundishaji
ambao niliokuwa nau
tumia katika kuwafundisha wanafunzi hao yani
mwalimu nilikuwa kama sehemu ya muwezeshaji
lakini wao ndio walikuwa wagunduzi wakubwa
kutokana na kuwa mbobezi katika eneo hili na huku
nikiwa na ongozwa na kauli mbiu ya "don't teach
them everything but let them discover "ambayo
ilikuwa inaendana kabisa na elimu ya awali kwa
hakika darasa langu lilikuwa ni darasa ambalo
lilikuwa linavutia sana sio kwa wanafunzi wangu tu
bali hata kwa wanajamii husika wa eneo lenyewe na
hata wanafunzi wa madarasa mengine walikuwa
34
wanatamani waanze chekechea kwa ajili tu ya
mambo yalivyokuwa yanakwenda katika darasa
langu hilo .
Kwa hakika darasa langu hilo lilikuwa na sifa za
kimataifa kwa ajili ya darasa la awali kwani
nilitumia vyema maarifa na ujuzi wangu wote
niliopata katika vyuo vikuu mbalimbali duniani
kutoka katika nchi zenye maendeleo makubwa
katika sekta ya elimu ndio lilifanya darasa langu
kupendeza na kuvutia na kwa kuwa kazi ya ualimu
ilikuwa ni moja ya taaluma ambayo tangu nikiwa
mdogo nilitamani sana nije kuwa mwalimu maana
nilikuwa na utamaduni wa kucheza michezo ya
35
kitoto na nikiwa kama mwalimu katika kundi la
watoto wenzangu huku wengine wakitaka kuwa
makomando na wengine polisi hivyo kutokana na
sinema za kivita walizokuwa wanaziangalia.
Kwa kuwa shule ambayo niliyokuwa nafundisha
ilikuwa haina umeme lakini haikuwa mbali sana na
nguzo za shirika la umeme Tanzania (Tanesco)
hivyo kwa kutumia urafiki wangu na wanafunzi
wenzangu niliyosoma nao shahada ya pili katika
masuala ya elimu ya awali nchini Finland hakika
nilipata ufadhilii wa kuweka umeme katika darasa
hili na vile tukaweza kujenga madarasa mawili
mapya kabisa yenye viwango vya kimataifa lakini
36
pia nikiomba ruhusa kwa mkuu wa shule ili
nikabidhiwe jukumu la kuchukua wanafunzi wa
awali walionekana wameshindikana kabisa kuelewa
katika shule za jirani na nilipewa ruhusu hiyo na
darasa langu likaanza .
Mshahara wangu wa ualimu niliamua kuutumia
katika uboreshaji wa mfumo wa ujifunzaji na
ufundishaji hapo shuleni hasa katika elimu ya awali
kwani nilikuwa nafundisha kwa kuwa nilikuwa
naipenda taaluma ya ualimu lakini sio kwa ajili ya
kupata kipato kwani kwa muda huo nilikuwa
namiliki biashara mbalimbali na mashamba
makubwa sana ya mpunga huko kyela na kilimo cha
37
umwagiliaji katika bonde la mto Rufiji katika mkoa
wa Pwani mbali na hayo bado nilikuwa nimeweza
kumiliki idadi kubwa ya ng'ombe huko kaskazini
katika mkoa wa Manyara katika wilaya ya Simanjiro
hivyo nilifundisha kama kulipa fadhila kwa jamii na
vilevile ni kitu ambacho nakipenda sana.
Kwa hakika ilikuwa mtu yeyote akifika katika
darasa langu la awali lazima aulize ni darasa
linalomilikiwa na mtu binafsi au serikali maana
wengi huwa wanaamini kuwa vitu vizuri vipo katika
shule za binafsi hivyo hii ilifanya suala la utoro
kutokuwepo kwa wanafunzi wangu maana ulikuwa
ukiingia darasani lazima ukumbuke enzi za utoto
38
maana darasa lilikuwa linaongea maana picha za
herufi na wanyama mbalimbali zilikuwa ukutani
lakini pia meza pana na zenye viti vyake vya kitoto
lakini pia hapo ilikuwa ni sehemu ya darasa la
kujifunzia ambao mbele kulikuwa na ubao mweupe
ambao unatumia maka peni na sio chaki kama
ilivyozoeleka na walimu wengi hapa nchini kwetu .
Lakini pia kulikuwa kuna screen kubwa sana ya inchi
zaidi ya thelathini na sita aina ya sony ambayo
ilikuwepo ukutani huku pembeni kukiwa kuna redio
kubwa kiasi aina ya sabufa pembeni ya meza lakini
pia kulikuwa kuna projekta ndogo yenye uwezo wa
39
kuonyesha picha kwa kiwango cha HD hapo
nikimaanisha high definition hivyo wanafunzi
walikuwa na nafasi ya kuwaona wanafunzi wenzao
kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa maana
niliandika barua ya maombi ya udhamini wa kupata
intaneti ya bure na ikakubaliwa na mtandao mmoja
wa simu nchini.
Kwa hakika nikifikiria hali ya darasa langu na
wanafunzi wangu hakika napata uchungu sana
kutoka moyoni nikiwa sijui kama wanafunzi wangu
wataendelea kupata huduma ambazo mwalimu wao
nilikuwa najitahidi kadri ya uwezo wangu ili waweze
40
kuzipata maana wengi sana waliokuwa
wakinishangaa kwa nini nisianzishe shule binafsi ya
awali kwa ajili ya kujipatia fedha lakini lengo langu
lilikuwa ni kujenga msingi imara kwa elimu ya
watoto wa awali maana hicho ni kipindi cha
muhimu sana katika kujitambua vyema .
Yale yalikuwa mazingira katika darasa la kujifunzia
kwenye kile chumba cha kwanza lakini pia katika
chumba cha pili ambacho kilikuwa kipana zaidi
humo ndani kulikuwa na vifaa mbalimbali vya
kujifunzia na kuchezea kwa watoto na katika
chumba hicho cha pili nilikipa jina chumba cha
41
ubunifu (creativity room )ambapo niliamini kuwa
watoto wanahitaji kucheza zaidi na kushiriki katika
shughuli nyingi zaidi za kitoto katika kukuza hali ya
ubunifu na afya ya akili hivyo kuanzia
midoli ,magari ,mikasi na kila aina ya zana na vifaa
vya kitoto vilipatikana ndani ya darasa langu hilo .
Lakini kwa nje pia kulikuwa na uwepo wa bembea
mbali mbali na kuburudika na hata za kuzungusha
ambazo zilikuwa zinawatamanisha na hata watu wa
wazima wa eneo husika maana watoto walikuwa
wanajifunza kwa raha zao hakika walikuwa
wanajifunza kwa furaha na nilikuwa naamini kuwa
kujifunza kwa burudani ni bora zaidi kuliko kwa
42
vitisho na hasira na hiyo inanikumbusha
nilipohudhuria semina ya wiki tatu ya mafunzo ya
elimu ya awali nchini Finaland mkurugenzi wa Bodi
ya elimu nchini Finaland alisema kua (an educated
country can not created by force "akiwa na maana
kuwa taifa lililoelimika haliwezi kuandaliwa kwa
kutumia nguvu akiwa na maana mfumo wa elimu
uwe wa kushirikiana na sio kushindana .
Kwa hakika wanafunzi wangu walikuwa na utofauti
kabisa na wanafunzi wengine na nilikuwa na
ushirikiano wa kutosha wazazi wa wanafunzi hao
huku nilikuwa nawapa darasa elekezi kwa ajili ya
malezi ya watoto wao kwani niliwahi kuhudhuria
43
mafunzo ya Family and school Partnership nchini
Singapore hivyo nilikuwa na ujuzi wa kutosha
kabisa ambao leo hii unaambulia adhabu ya
kunyongwa mpaka kufa .
Inaniuma sana zaidi ya sana pale nilipoambiwa
kuwa nimehusika kumuua na kumuingilia kinyume
na maumbile mwanafunzi wangu wa kike na tukio
hilo lilihisishwa na imani za kishirikina ili niweze
kuendelea kupata mafanikio zaidi na kukubalika kwa
wanajamii maana walisema haiwezekani mtu
kutumia mali zake kwa ajili ya watoto wasio wake
hakika walijua tu kuwa nilikuwa natumia imani za
kishirikina na kutokana na imani hiyo ilipelekea
44
kumuua mwanafunzi wangu kitu ambacho sio cha
kweli na ndo kinanipa uchungu kabisa kutoka ndani
ya moyo wangu huku nikijiuliza kuwa iweje leo hii
mimi ambaye nilikuwa natumia muda mwingi kwa
ajili ya wanafunzi wangu na niliyekuwa natumia
taaluma yangu yote kwa ajili ya wanafunzi na
kuinua eneo la elimu ya awali leo nifanye mauaji
kwa binti mdogo kabisa asiyekuwa na hatia yeyote
ile kabisa tena wengi wanamini kuwa inawezekana
kuwa nilikuwa nafanya mapenzi na katoto hako
maana nilikuwa nakapa sana zawadi na nilikuwa
nako karibu sana tena kwa michezo mbalimbali
hivyo katika hilo hapakuwa na shaka na muda
45
mwingine walikuwa wananiita mwalimu rafiki
wakiwa hivyo kutokana na kushindwa hivyo
wakawa wananiita rafiki hakika jamii ilifikiria
tofauti kabisa na hali halisi na ikapelekea kukosa wa
kunitetea hakika siwalaumu hata kidogo sababu
kutokana na mwili wa binti huyo mdogo ulivuokuwa
umeharibiwa vibaya kweli halafu wanapata taarifa ni
mimi ndiyo nilikuwa nahusika kwa kuwa walifika
katika hatua ya juu kabisa ya hasira hivyo adhabu ya
kunyongwa waliona ilikuwa halali yangu kabisa .
Nakumbuka Asha ni mwanafunzi ambaye alikuwa
chini ya uangalizi wangu wa kitaaluma na
kisaikolojia na kifizikia licha ya kutokuwa katika
46
elimu ya awali lakini nilipewa jukumu la kujua
tatizo lake ni nini hasa na alikuwa ni kabinti kadogo
kazuri na kacheshi lakini mwenye tabia ya udadisi
sana muda mwingi alikuwa ni mtu wa maswali na
aina ya uulizaji wake ulikuwa ni kwa nini na vipi ,
kiumri Asha alikuwa na miaka sita kama sio saba
lakini anayepata tabu katika kusoma na kuandika
kwa kiwango kikubwa sana lakini alikuwa ni
muongeaji sana na mwimbaji mzuri wa nyimbo
hicho ni kiliwafanya wengi waamini kuwa Asha
alikuwa na kiburi na hakupenda kusoma kabisa
sababu vitu vingine alikuwa anafanya kwa nini suala
la kusoma na kuandika limshinde .
47
Walimu waliamua kuwa wanamchapa sana na
wengine wakimuona ni mjinga na kisirani sana
mpaka wakamkatia tamaa jambo lilifanya familia
yake wamsuse baada ya kupata taarifa hizo
nikiomba awe katika uangalizi wangu wa kitaaluma
na kisaikolojia sababu suala alilokuwa akisumbuliwa
nalo Asha ni gumu kwa walimu wengi
hawakufundishwa namna ya kuwasaidia wanafunzi
wa nmna ile lakini kwa vile nilikuwa nimebobea
katika eneo ambalo kitaalamu linaitwa specific
learning difficulties yaani matatizo mahususi ya
ujifunzaji nilitambua fika neema alikuwa na shida .
48
Nakumbuka baada ya kukaa kwa karibu na kwa
muda wa miezi miwili na kumpa majaribio ambayo
niliyopata nilipokuwa nachukua shahada yangu ya
pili nchini Finland katika chuo kikuu cha Henlisiki
kwenye ubobezi wa matatizo mahususi ya ujifunzaji
ambapo Asha alikuwa anasumbuliwa na matatizo
mawili moja ni dyslexia ambalo ni matatizo katika
suala la usomaji na dysgraphia ambalo ni matatizo
katika suala la uandishi ambao mtoto anakuwa na
uwezo wa kufanya mambo mengine vizuri lakini
linapokuja katika maeneo hayo mawili anakuwa
anapata ugumu sana hivyo ilibidi niwe naye karibu
49
sana na kumuanzishia programu maalum kwa ajili
yake.
Kwanza kwenye suala la ujifunzaji ilikuwa lazima
nitumie mbinu mbadala ambazo ikiwa na mazoezi
ya awali yani pre reading exercise lakini pia katika
suala la kuandika ilibidi nimpe mazoezi ya mikono
na shughuli mbalimbali za kuongeza nguvu katika
vidole vyake ikiwa pamoja na kutumia sana mikasi
katika ukataji wa maboksi kwa muda wa wiki zaidi
ya tatu mabadiliko makubwa sana nakumbuka
yalianza kutokea kwa Asha mpaka walimu na watu
wa karibu na Asha hawakuweza kuamini kama Asha
sasa alianza kusoma na kuanza kuumba herufi
50
hakika kwangu lilikuwa ni jambo la furaha sana
kwani niliweza kumsaidia Asha mpaka
akawa anaweza kusoma na kuandika vizuri kabisa
baada ya matumizi ya mbinu mbalimbali hakika
ukaribu wangu na Asha alikuwa mkubwa sana
sababu kisaikolojia wanafunzi wenye matatizo ya
namna hiyo inashauriwa tuwe nao karibu sana
ilifikia kipindi Asha alikuwa akigoma kufanya kitu
hasikilizi mpaka niende mimi.
lakini nakumbuka nilipata kazi ya kuandaa programu
ya kufundishia walimu wa shule za msingi katika
wilaya fulani hivyo nilihitajika kuindaa hivyo
51
nilikuwa nashinda shule kwa muda mfupi sana lakini
wanafunzi wangu walikuwa tayari nilishawapa
mapumziko ya kitaaluma hivyo walikuwa wanakuja
kucheza tu kumbe nilikuwa sijapata taarifa kuwa
Asha naye hakuwepo nyumbani kwao walimtafuta
sana hawakumpata mpaka inafika usiku
hawakumuona mpaka inafika saa tatu usiku
nakumbuka hawakumuona lakini usiku ambao
kwangu ulikuwa ni mchungu sana maana nilikuwa
katika chumba changu ambacho kilikuwa kama ofisi
yangu ndogo maana kazi zangu nyingi nilikuwa
nafanya humo na siku hiyo nilichelewa sana kulala
na mlango sikuwa nimefunga.
52
Ghafla nikasikia mlango ukifunguliwa kwa ghafla na
mtu akaingia huku nikiwa nashangaa kumba alikuwa
Asha muda huo alikuwa akivuja damu na
zikuchuruzika katika mapaja yake huku nikiwa
katika hali ya mshangao ghafla Asha alidondoka
chini kabisa kama gunia lilikuwa limesimamishwa
ukutani huku akiwa anakoroma kwa kweli
nilishikwa na butwaa kubwa huku nikiwa
nimeduwaa na kushikwa na mshangao kama dakika
tano nikiwa sitambui nini cha kufanya yani nilikuwa
kama sanamu ambalo limechongwa na
kusimamishwa ama kweli kumbe siku ya kufa nyani
miti huteleza mara nilisikia sauti za hodi kutoka nje
53
hivyo kwa hali hiyo niliamua kumsukumia Asha
katika kabati lililokuwa tupu pembeni ya chumba
kile .
Kumbe walikuwa ni mapolisi na wazazi wa Asha na
walimu wengine ambao waliamua kuja kwangu
kunipa taarifa na kunilizia mimi sababu mimi ndo
nilikuwa moja kati ya walimu ambao tulikuwa
karibu sana na Asha waliingia mapolisi watatu na
wazazi na walimu wengine kuniulizia hata kabla
hawajaongea chochote ghafla mlango wa kabati
ambapo nilimuweka Asha kwa muda ili kutathimini
hatua za kuchukua katika tukio lile mlango wa
kabati ukafunguka na mwili wa Asha ukaanguka
54
chini hakika watu wote walibaki na mshangao
mkubwa sana ghafla bila kutarajia nilipokea kofi
zito kutoka kwa afande aliyekuwa upande wa
kushoto kwangu na ilipigwa simu ya ghafla wakaja
askari wengine na taarifa zilisambaa kwa kasi ya
ajabu sana juu ya tukio hilo na ikaenea kuwa mimi
nimemuua Asha na kufanya naye mapenzi kwa
nguvu yaani nilimbaka.
Hakika nilikuwa nimebaki na butwaa sikuamini kile
kilichotokea nikiendelea kulia kwa uchungu sana
kutokana na hali ile sababu moja ya wanafunzi
wangu ambao nilijitolea kumfundisha kwa hali na
mali kabisa leo anakufa lakini nashutumiwa mimi
55
mbaya zaidi nahusishwa na imani za kichawi
kutokana na mafanikio yangu makubwa katika eneo
la elimu kwa kweli taarifa zilisambaa Tanzania
nzima hadi nje ya mipaka ya Tanzania lakini ilikuwa
ni vigumu sana watu wasiamini kuwa mimi sihusiki
lakini kwa hali halisi watu wengi waliamini kuwa
nahusika kwa kiwango kikubwa sana kwa kweli
lilikuwa ni pigo kubwa sana.
Taratibu zote nakumbuka zilifuatwa za kipelelezi na
kisheria mpaka naingia kwenye hukumu juu ya
kunyongwa hadi kufa kwa kweli hadi leo sifahamu
ni nani aliyemtendea unyama ule mwanafunzi
wangu mpendwa hivyo hawakuumiza sana vichwa
56
bali nilihusishwa moja kwa moja na kutokana na
hilo nikahukumiwa kunyongwa .
Lakini kutoka ndani ya moyo wangu sikuhusika na
tukio hilo kabisa mpaka sasa zimebakia siku mbili tu
niweze kunyongwa lakini naumia sana zaidi ya sana
moyo wangu unamaumivu kama kidonda kibichi
kilichomwagiwa maji ya betri nikililia nafsi lakini
mbaya zaidi taifa langu kwenye masuala kielimu
kwa kweli nilikonda ndani ya siku mbili tu lakini pia
niliumia kuwa mipango yangu katika suala la elimu
yatakuwa yamepotea hivyo lakini pia taaluma ya
ualimu itakuwa kama imeingiliwa jini baya sana la
mikosi maana matukio mengi sana yalitokea na hili
57
la kuhukumiwa kunyongwa likiwa pigo jingine
kubwa sana katika taaluma ambayo naimani
itasababisha walimu wengi kuamua kuacha taaluma
ya ualimu lakini kamwe msirudi nyuma hivyo
niwaombe sana walimu wenzangu msirudi nyuma
taifa linatutegemea sana.
Mpaka hapa nilipo naumia sana zaidi ya sana lakini
namuomba mungu licha ya kuwa nitanyongwa na
kufa lakini naamini siku moja ukweli utakuja
kubainika ni nani aliyesababisha mauaji ya
mwanafunzi Asha angali mdogo kiasi kile lakini
alikuwa na ndoto ya kuja kuwa mwanasheria
mbobezi ili aje kuwatetea wanyonge wote
58
wanaonewa na wenye fedha lakini ndoto zake
zimekatizwa pasipo kutimia barua hii naimani
itakuwa imetoa dukuduku langu la kuzungumza hali
halisi ya tukio husika kuhusu utata wa kifo cha Asha
huko mliko msichoke kumwombea Mungu
amuweke mahali pepa peponi amina.
Ni mimi
Mwalimu J.M
59
MSIRUDI NYUMA.
Habari za huko mliko walimu tarajiwa natuma
salamu zangu za dhati kabisa kutokea huku niliko
mbali na uso wa dunia ambayo nyie mpo ,salamu
zangu zifike kwenye vitivo vyote vya elimu katika
vyuo vikuu kuanzia kule chuo kikuu cha Dar es
salaam hadi kule katika kitivo cha elimu pale chuo
kikuu cha Dodoma lakini salamu zangu ziwafikie
hadi wale wa DUCE lakini zipande hadi kaskazini
mwa nchi yangu kule Makumira na zipandishe hadi
kanda ya ziwa zifike SAUT pale maeneo ya
malimbe lakini upepo uvumishe salamu zangu
mpaka nyanda za juu kusini kule Muce na Rucu
60
lakini zisogee juu kidogo kule Teku na kipindi
zinarudi ziwafikie pale Mzumbe na pale Jordani
Hakika kwa dhati ya moyo pia natuma salamu zifike
kwa walimu wa ngazi za vyeti hadi diploma
vilivyopo pande zote za taifa langu la Tanzania
lakini salamu zivuke mawimbi ya bahari mpaka
Zanzibar nako huko zifike lakini ikiwezekana zivuke
na mipaka ya nchi zifike hadi kwa majirani zetu
tunaopakana nao ni salamu ambazo nazituma huku
ikiwa ni nafasi ya pekee ya kutuma salamu zangu na
kuwasalimu na hatua kuwakumbusha yale machache
lakini ya umuhimu naandika haya huku nikiwa na
maumivu makali lakini napata faraja kubwa nikiona
61
kundi kubwa la vijana makini ambao wameamua
kuingia katika taaluma hii nzito kabisa hapa chini ya
jua baada ya kuandika waraka huu kwenu naimani
kabisa kuwa moyo wangu utakuwa mweupe kama
theluji ya Mlima Kilimanjaro sababu kuchanika kwa
jamvi sio mwisho wa maongezi hakika naamini .
Labda niseme kwa dhati ya moyo wangu popote pale
mlipo hakika nyie ni majemedari makini kabisa
ambao mmeamua kumuunga mkono hayati
Mwalimu J.K.Nyerere kupigana vita kati ya moja ya
maadui wale wa tatu yaani adui ujinga kwa hakika
hilo ni jambo la kupendeza sana na kutia moyo
maana adui huyu akishambuliwa na akiwa katika
62
hali mbaya hakika inakuwa rahisi sana
kuwashambulia kwa urahisi kabisa hao maadui
wengine yani maradhi na umaskini sababu nia ya
kuwapiga tunayo na nguvu ya kuwapiga tunayo
hakika niwapongeze sana kutoka ndani ya moyo
wangu natamani mngeweza kuona ndani ya moyo
wangu licha ya kuwa na maumivu lakini naliona
tumaini jipya na lenye matumaini mazuri kabisa
hakika hata siku ya hukumu yangu ikitekelezwa
nafahamu kuwa kuna watu imara wako na nia ya
dhati kabisa katika taifa letu.
Walimu tarajiwa natambua fika kuwa wengi wenu
mmeacha taaluma mbalimbali na kuamua kuja
63
katika taaluma hii ya ualimu iwe kwa kupenda au
mfumo umekufanya kuchagua kuja huku hiyo
haitakufanya usihesabike kama mwalimu napenda
utambue kuwa mbali na changamoto mbalimbali
lakini umechagua fungu lililo jema kabisa maana sisi
ndo ambao bila sisi maana halisi ya elimu rasmi
haiwezi kutokea lakini pia tambua kuwa walimu
tunamsaidia Mungu katika uumbaji na ni watumishi
ambao Mungu anatuamini kwa kiwango kikubwa
sana .
Napenda nikwambie yale baadhi ya mambo ambayo
yanapatikana katika taaluma hii ya ualimu yapo ya
kufurahisha na hata kuzunisha na kukatisha tamaa
64
kabisa lakini kamwe msirudi nyuma maana hatma ya
taifa hili limo mikononi mwenu walimu tarajiwa
kwanza ni vijana lakini pia mmetokea katika zama
za sayansi na teknolojia hivyo mna nafasi kubwa
sana ya kuleta mabadiliko katika mfumo wa elimu
hasa ya awali maana huko ndiko mahali ambako
wamepasahu lakini naamini kuwa mtakuja na mbinu
na njia mbalimbali za kusaidia katika eneo hilo
hakika nyie ni watu muhimu sana na Mungu
analitambua hilo fika licha kuwa kwa sasa thamani
yetu imeshuka kwa kasi kubwa .
Naongea haya kuhusu nyie walimu tarajiwa ambao
ndio mmeamua kuingia katika mfumo huu wa
65
taaluma maana kuna kipindi mnaweza kata tamaa
lakini kamwe msirudi nyuma sababu watoto wa taifa
hili wapo mikononi mwenu na nyie ndo wenye
uwezo wa kujenga taifa imara au taifa lisilo imara
maana wanafunzi wanawasakiliza kwa umakini sana.
Naandika haya nikiwa naingalia jamii yangu kuhusu
mitazamo yao kuhusu taaluma ya ualimu na asilimia
kubwa wengi wanaichukulia taaluma yetu kama
sehemu ambayo watu ambao wamefeli au wamepata
alama ambazo zinawafanya wakose sifa ya
kuchaguliwa katika taaluma nyingine na ndo maana
mkaamua kuja katika taaluma hii huenda ikawa
kweli lakini sio kwa wote kuna waalimu wenye
66
ufaulu mkubwa kabisa lakini wamekuja katika
taaluma hivyo licha ya maneno hayo kamwe msirudi
nyuma maana endapo mkiamua kurudi hakika
mtakuwa imerirudisha nyuma sana taifa lenu tena
kwa kiwango kikubwa kabisa hivyo kamwe msirudi
nyuma .
Lakini pia natambua kabisa kuna kipindi kitafika
viongozi wengi watakuja kwenu na kutoa matamko
ya kudhalilisha na kejeli sana dhidi yenu tena baadhi
ya viongozi hao wengi wenu mmewazidi elimu
lakini mbali na kuwazidi elimu na wengine hata
umri lakini watawasema sana kuhusu kufeli kwa
wanafunzi kama vile kuna mwalimu anayependa
67
kuona mwanafunzi wake anafeli bila kusahau kuwa
katika suala la ufundishaji na ufaulu sio suala la
mwalimu tu bali inabidi kuwe na timu shirikishi
ambayo itajumuisha serikali ,shule na ambayo
inajumuisha walimu na wafanyakazi wengine wa
shuleni lakini pia inajumuisha na wanajamii pia
lakini hao wote hawataonekana utaonekana wewe
pekee ndio mhusika mkuu kamwe usije ukarudi
nyuma katika hilo maana litakuwa kosa kubwa sana
cha msingi ni kupiga moyo konde na kusonga mbele
kwa niaba ya taifa lako.
Natambua fika kutokana na makato kutoka bodi ya
mikopo ya elimu ya juu mshahara wako utabaki
68
kidogo licha ya ahadi kubwa ambazo mtaendelea
kupokea kutoka kwa viongozi na siku zitakwenda
bila kupatiwa lakini kamwe usirudi nyuma tambua
fika furaha na baraka ya mwalimu ni kuona
wanafunzi wake wanafaulu vizuri sana najua
maumivu yatazidi sana pale ambapo wenzenu
walioenda katika sekta nyingine watakavyokuwa
wakiongezewa mishahara yao kimya kimya na
posho juu lakini hali kwako itakuwa tofauti kabisa
usirudi nyuma bali ongeza juhudi katika kufundisha
wanafunzi wako huenda siku moja watakuja
kukusaidieni katika maboresho ya sera nzuri kuhusu
walimu hivyo kipato kuwa kidogo najua itakuwa
69
changamoto lakini unaweza jiongeza kuwa kuanza
kufanya shughuli nyingine za kuongeza kipato
kutokana na mshahara wako unaweza ukalima na
hata ukafuga au ukaingia kwenye shughuli za
ununuzi wa hisa au suala la usafirishaji lengo kuu
likiwa kuongeza kipato chako lakini usijisahau sana
mpaka ikapelekea kusahau majukumu yako ya
kiutumishi hakika utakuwa ujautendea haki ualimu
wako kamwe mbali na hayo usirudi nyuma .
Mwalimu tarajiwa najua unasikia mengi sana lakini
pia unajua kuwa kuna chama cha walimu ndio
chama kipo na tena ndio wawakilishi wetu lakini
tambua kuna mengi ambayo yapo nyuma yao hasa
70
kuhusu katika taaluma yetu ya ualimu wengi wao
kabla ya kupata nafasi za kuiongoza chama hicho
harakati zao zote za utetezi wa walimu huwa
unapotea maana labda kwa vile madaraka yanalevya
na wengine wanasema kuwa viongozi wengi ni
wanachama hai wa wenye dola yetu hivyo ni ngumu
sana kwenda kuwapigania walimu sababu
watakuwa wanakwenda kinyume na chama tawala
lakini bado mwalimu una nafasi ya kuchagua
viongozi wenye uzalendo na taaluma lakini wenye
uzalendo wa kutosha na taaluma lakini pia wana
elimu na uelewa wa kutosha juu ya taaluma husika
na masuala ya wafanyakazi hiyo itawasaidia sana
71
katika kutetea maslahi yenu kupitia chama chenu
cha taaluma najua kabisa mambo yatakuwa mengi
kabisa na mtawalalamikia sana na huenda ikapelekea
kupunguza morali ya kazi kwenu kamwe hasira
dhidi yao usiirudishe katika darasa lako na
kupelekea kuathiri suala zima la ujifunzaji na
ufundishaji nakuomba sana kamwe usirudi nyuma .
Wewe ni mwalimu na sifa ya mwalimu sio tu
kufundisha lazima utambue hili kuwa mwalimu
huwa anakuwa zaidi ya mwalimu anatekeleza
majukumu zaidi na ufundishaji kwa mwanafunzi
wake kuna muda utakuwa kama
daktari ,mshauri ,mlezi ,kocha ,na mengine mengi
72
lazima ujitahidi kadri ya uwezo wako kumjenga
mwanafunzi katika maeneo yote muhimu
kimwili ,kiakili na kiroho pia hii itamfanya
mwanafunzi awe na uwezo mkubwa sana wa
kutumia akili yake ipasavyo nafahamu kuwa kuna
wanafunzi ambao huwa wanatabia ambazo kwa
kweli huwa hazipendenzi kabisa lakini kwa kuwa
wewe ni mwalimu kero hizo za mwanafunzi huyo
zisikutishe tamaa na ikapelekea kumsusa kabisa
kamwe usifanye kosa hilo tambua taifa
linakutegemea sana .
Nilipenda niandike mengi sana kuwahusu walimu
tarajiwa na taaluma husika lakini muda wangu ni
73
mdogo sana na hata karatasi niliyopewa kwa ajili ya
kuandikia barua yangu hii imeshajaa naamini kuwa
mtakwenda kufanya mabadiliko makubwa sana
katika mfumo wa elimu katika nchi ya Tanzania na
mabadiliko makubwa sana yatakwenda kutokea
katika mfumo wetu wa elimu .
Natuma salamu hizi ziwafikie huko mliko kuwa
nawapenda sana ndugu walimu wenzangu hakika
Mungu atakuwa nanyi siku zote kwa maisha yenu na
yatakuwa na baraka kubwa sana .
Lakini walimu tarajiwa tambueni kuwa wanajamii
ambao wanawazunguka wanauelewa mdogo sana
74
kuhusu masuala ya elimu na wengi wanatambua na
kuamini kuwa mwalimu na shule pekee ndio
wanajukumu la kufuatilia suala la elimu kitu
ambacho siyo cha kweli basi msichoke kuwapa
semina elekezi kuhusu umuhimu wa ushiriki wao
katika kuinua elimu hapo lazima kuwepo umoja
baina ya jamii ,wanafunzi na walimu mkilifanikisha
hili mtakuwa mmelisaidia sana taifa katika eneo la
elimu .
Natambua kuwa wengi wenu baada ya kuhitimu
masomo yenu ya ualimu mtaingia shuleni na kuanza
kufundisha na kuna kipindi mtakuwa mnapata
semina elekezi kuhusiana na taaluma husika
75
kitaalamu ni induction program lakini kwa kiwango
kikubwa wanaochaguliwa kujiunga na programu
hizo ni wachache na tena ni kwa upendeleo hivyo
isikukatishe tamaa ya kutafuta maarifa sehemu
nyingine kuhusu taaluma yako ili uendane na
mabadiliko ya ulimwengu wa elimu huu itakusaidia
kuwa mwalimu makini kabisa .
.
Lakini walimu tarajiwa lazima tufahamu kuwa
mwalimu sio Mungu mtu bali ni daraja bora la
ujifunzaji na ufundishaji shuleni hivyo pale ambapo
wanafunzi watakuwa wanaleta mawazo na maoni
76
yao kamwe usiyakatae na ushirikiane nao na uwe
tayari kujifunza kutoka kwao maana na wewe ni
binadamu huwezi kuwa unatambua kila kitu hii
itaongezea wigo mpana wa kuyatambua mengi zaidi
sana mwalimu tarajiwa .
Ubunifu katika ufundishaji na ujifunzaji ni suala
muhimu sana kulitambua walimu tarajiwa lazima
ukae na ufikirie jinsi ya kuja na mbinu na njia
ambazo ni rafiki katika ujifunzaji na ufundishaji
kuliko kutumia mbinu zilizozoeleka miaka yote
lazima mbinu za ufundishaji ziwe na ubunifu mzuri
kabisa yaendane sambamba na matumizi ya zana na
ufundishaji mwalimu hata kama serikali haitaleta
77
lakini lazima utambue kutumia mbinu mbalimbali za
kiualimu katika kuandaa zana zako za ufundishaji
wako yaani improvisation in education media and
technology Sababu tunaishi katika jamii ambazo
kuna malighafi ambazo tunaweza kuzitumia katika
ujifunzaji na ufundishaji.
Mwisho kabisa naandika haya nikiwa natambua
kuwa walimu tarajiwa mtakuja kuleta mabadiliko
makubwa na tambueni kuwa heshima na thamani ya
taaluma ya ualimu iko mikononi mwenu kamwe
msikubali wachache waishushe heshima ya taaluma
hii adhimu kabisa hivyo ilindeni kwa jasho na damu
ilindeni taaluma yenu kamwe narudia tena
78
msiruhusu kikundi cha watu wachache washushe
heshima ya taaluma ya ualimu maana hapo ndio
chemchem ya maarifa ya taifa ilipo hivyo inabidi
patunzwe kwa hali ya juu na hekima na busara
kubwa sana.
"The best teacher teach from the heart not from the
book"
Our main focus is children not the subject matter"
Teaching is mother of all other Profession
79
Hakika Mungu awajalie hekima na busara nyingi
sana kwenu ili muweze kushirikisha maarifa bora
kwa manufaa ya taifa .
Ni mimi mwalimu mwenzenu.
J.M.
80
ASANTENI SANA.
S