sheria ndogo - masasidc.go.tz€¦ · ushuru kwa mujibu wa sheria ndogo hizi. wajibu wa wakala 9....
TRANSCRIPT
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
1
TANGAZO LA SERIKALI NA. 391 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA FEDHA YA SERIKALI ZA MITAA
(SURA YA 290)
________
SHERIA NDOGO ________
Zimetungwa chini ya kifungu cha 7(1) na 16(1)
________
SHERIA NDOGO (ADA NA USHURU) ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI ZA
MWAKA 2017
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI
Jina na
tarehe ya
kuanza
kutumika
1. Sheria Ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo za (Ada
na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za Mwaka 2017 na
zitaanza kutumika baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Matumizi 2. Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo lote lililo chini ya
mamlaka ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.
Tafsiri 3. Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa pale itakapoelezwa
vinginevyo:-
“Ada na Ushuru” maana yake ni malipo yanayolipwa kwa
Halmashauri au wakala wake kwa ajili ya huduma, vibali,
au leseni mbalimbali zitolewazo na Halmashauri;
“Afisa Mwidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote wa Halmashauri
aliyeteuliwa kusimamia utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi;
“Chombo cha Usafiri” maana yake ni chombo chochote
kinachotumika kusafirisha mtu, watu au mizigo kutoka
sehemu moja kwenda nyingine isipokuwa mkokoteni, au
wanyama wanaotumika kama kusafirisha watu au mizigo;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
2
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Wilaya ya Masasi;
“Kibali” maana yake ni idhini au ruhusa ya maandishi inayotolewa
na Halmashauri;
““Machinjio” maana yake ni sehemu iliyotengwa na Halmashauri
kwa ajili ya kuchinjia wanyama na kuanika ngozi;
“Masoko” maana yake ni sehemu yoyote iliyotengwa na
Halmashauri kwa ajili ya kuuza na kununua bidhaa;
“Mnada” maana yake ni sehemu iliyotengwa na Halmashauri kwa
ajili ya kuendesha shughuli za kuuza na kununua bidhaa;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi pamoja na Afisa yeyote
wa umma atakayeteuliwa kutekeleza majukumu ya
Mkurugenzi;
“Usajili wa vyombo vya usafiri” maana yake ni utaratibu
utakaowekwa na Halmashauri wa kuorodhesha idadi ya
vyombo vya usafiri vinavyofanya biashara ndani ya
mamlaka ya Halmashauri;
vibao vya matangazo maana yake ni ubao, ukuta au mahali popote
au chombo chochote ambacho kimewekewa tangazo la
biashara;
“Wakala” maana yake ni Mtu, Taasisi, Kampuni, au asasi yeyote
iliyoteuliwa kisheria na Halmashauri kukusanya mapato
kwa niaba ya Halmashauri.
SEHEMU YA PILI
NAMNA YA KUKUSANYA ADA NA USHURU
Ada na
Ushuru 4. (1) Halmashauri itatoza Ada na Ushuru mbalimbali kwa ajili
ya vibali, leseni na huduma zitolewazo na Halmashauri kama
inavyoonyeshwa katika Jedwali la Kwanza la Sheria Ndogo hizi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
3
(2) Ada na Ushuru utozwayo chini ya Sheria Ndogo hizi
utalipwa kabla ya huduma kutolewa.
(5) Huduma zitakazotozwa Ada na ushuru katika Sheria Ndogo
hizi ni;-
(a) Ushuru wa Mazao;
(b) Ushuru wa mifugo na machinjio;
(c) Ushuru wa soko;
(d) Ada ya kibali cha kufanya biashara zisizohitaji leseni;
(e) Ada ya kibali cha ujenzi;
(f) Ada ya Ukaguzi wa ramani;
(g) Ada ya kuchangia gharama za upimaji na usafishaji wa
viwanja;
(h) Ada ya Leseni mbalimbali;
(i) Ada ya Zabuni;
(j) Ada ya Uthamini wa ardhi;
(k) Ada ya kibali cha kusafirisha ngozi;
(l) Ada ya kukodi mali za Halmashauri;
(m) Faini ya adhabu kwa makosa mbalimbali;
(n) Ushuru wa Vibao vya Matangazo;
(o) Ushuru wa Kuchinja, kuwamba na kununua ngozi;
(p) Ushuru wa Mabango.
Taratibu za
kulipa Ada
na Ushuru
5. (1)Itakuwa ni Wajibu wa kila mtu anayetakiwa kulipa Ada
na Ushuru kuhakikisha kwamba analipa Ada na Ushuru kwa
viwango vilivyoainishwa kwenye jedwali la Sheria Ndogo hizi.
(2) Muda wa kukusanya Ada na Ushuru utakuwa ni kuanzia
Saa Kumi na mbili kamili (12:00) asubuhi mpaka saa kumi na mbili
(12:00) jioni.
(3) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo (2), Afisa
Mwidhiniwa au Wakala anaweza kukusanya ushuru baada ya muda
uliotajwa hapo juu endapo atakuwa na kibali maalum kutoka kwa
Mkurugenzi.
(4) Malipo ya Ada na Ushuru yatafanyika kila siku au kwa
mwezi au kwa namna yoyote itakayokubalika kulingana na
makubaliano yatakayowekwa kati ya Halmashauri/ Wakala na
mlipa ada na ushuru.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
4
(5) Malipo ya Ada na Ushuru yanayotozwa kwa Mujibu wa
Sheria Ndogo hizi yatalipwa kwa Halmashauri au Wakala wake na
kutolewa stakabadhi ya Halmashauri kama kielelezo cha malipo
yaliyofanyika.
Bidhaa za
nyumbani 6. Bila kuathiri masharti ya Sheria Ndogo hizi bidhaa zozote zenye
uzani usiozidi kilo 50 zitakazoingizwa sokoni na mtu yeyote
kwa ajili ya matumzi ya nyumbani hazitatozwa Ushuru au Ada.
Ukusanyaji
wa madeni 7. Ikiwa mtu yeyote anayetakiwa kulipa Ada au Ushuru atakataa
au kushindwa kulipa Ada au Ushuru ndani ya muda
unaotakiwa, Halmashauri inaweza kukusanya Ushuru au Ada
unodaiwa kwa njia ya Mahakama.
Uteuzi wa
Wakala 8. Halmashauri itakuwa na mamlaka ya kuteua Kampuni au
Taasisi iliyosajiliwa kwa mujibu wa Sheria kukusanya Ada au
Ushuru kwa mujibu wa Sheria Ndogo hizi.
Wajibu wa
Wakala 9. Wakala aliyeteuliwa chini ya Sheria Ndogo hizi atakuwa na
wajibu wa-
(a) kukusanya na kupokea Ada na Ushuru au madeni katika
eneo alilopangiwa kwa kiwango kilichoainishwa chini ya
Sheria Ndogo hizi;
(b) kuwasilisha makusanyo yote kwa kuzingatia masharti ya
Mkataba wa Uwakala.
SEHEMU YA III
MAKOSA NA ADHABU
Makosa 10. (1) Itakuwa ni kosa kwa:-
A. Kwa Wakala;
(a) Atakusanya Ada na Ushuru au madeni bila kibali cha
maandishi au mkataba toka kwa Halmashauri;
(b) Atajaribu au atakusanya ada na ushuru au madeni kwa
kiwango tofauti na kilichotajwa na Sheria Ndogo hizi;
(c) Atashindwa kuwasilisha au atawasilisha pungufu ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
5
kiwango cha Ada na Ushuru alichokubaliwa katika
mkataba;
(d) Atakusanya Ada na Ushuru au madeni kwa mbinu
tofauti na alizoelekezwa na Halmashauri.
B. Kwa yeyote:-
(a) Atashindwa, atadharau, au atakaidi/ Atakataa kulipa Ada
na Ushuru au kutekeleza agizo lolote alilopewa na
Halmashauri kuhusiana na ulipaji wa Ada na Ushuru
chini ya Sheria Ndogo hizi;
(b) Atamshawishi mtu au kundi la watu kukataa au kukwepa
kulipa Ada na Ushuru;
(c) Atatengeneza, atatayarisha, ataidhinisha utengenezaji, au
atatunza nyaraka za uongo kwa nia ya kujipatia
manufaa yatokanayo na ukusanyaji wa Ada na Ushuru
mbalimbali ndani ya Halmashauri;
(d) Kwa makusudi huku akijua ni kosa atatoa taarifa za
uongo kwa Halmashauri, au Atashindwa au kutoa
taarifa zitakazohitajika na Halmashauri;
(e) atashindwa kuweka Kumbukumbu, Vitabu, Hesabu, au
maelezo yoyote yatakayohitajika Halmashauri; Na
(f) Atamzuia Afisa Mwidhiniwa au Wakala kutekeleza
majukumu yake.
Adhabu 11. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na masharti ya Sheria
Ndogo hizi atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia
atatozwa faini isiyopungua shilingi laki mbili (200,000/=) na
isiyozidi shilingi milioni moja (Tshs. 1,00,000/=) au kifungo
kisichopungua miezi kumi na mbili (12) na kisichozidi miezi
ishirini na nne (24) au adhabu zote mbili kwa pamoja yaani
faini na kifungo.
Kufifilisha kosa 12. Mkurugenzi atakuwa na uwezo wa kufifilisha kosa kwa
kumtoza faini mtu yeyote aliyetenda kosa kwa mujibu wa
Sheria hizi, kiasi kisichopungua shilingi laki mbili
(200,000/=) na kisichozidi shilingi laki tano (Tsh.500, 000/=)
iwapo mkosaji atakiri kosa kwa hiari na kuwa tayari kujaza
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
6
fomu maalum iliyoambatishwa kwenye jedwali la pili la
Sheria Ndogo hizi, na atatakiwa kulipa Ada na Ushuru
anaodaiwa kwa mujibu wa Sheria Ndogo hizi.
________
JEDWALI LA KWANZA
________
(Chini ya kifungu cha 4(1))
1. Ushuru wa mazao ya kilimo.
❖ Ushuru wa mazao ya kilimo utatozwa asilimia
mbili (2%) ya bei ya kununulia.
2. Ushuru wa Madini ya Ujenzi
Madini ya Ujenzi
A. KOKOTO
Uzito wa gari Kiasi cha Ushuru
1. Madini ya ujenzi tani 1 hadi 6 5,000/= kwa kila safari
2. Madini ya ujenzi tani 7 hadi 10 10,000/= kwa kila safari
1,000/= kila tani
itakayoongezeka
B. MCHANGA
1. Madini ya ujenzi 1 hadi 6 3,000/= kwa kila safari
2. Madini ya ujenzi tani 7 hadi 10 5,000 kwa kila safari
1,000/= kwa kila tani
inayozidi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
7
3. Garama za leseni kwa Mazao ya Misitu kwa kila mita moja ya ujazo (m3)(Forest
Produce Farm gate price)
Na. AINA YA MTI DARAJA LA
MTI
KIASI KWA MWAKA
1. Mti wa Mpingo Daraja la I A 264,960/=
2. Mninga, mkongo, mbambakofi,
mpangapanga
Daraja la I B 235,520/=
3. Mbalamwezi,Mtondoo, Daraja la II 176,640/=
4. Msufi Daraja la III 132,480/=
5. Mjale Daraja la IV 88,320/=
6. Aina nyingine ya miti 150,000/=
6. Miti yenye ukubwa wa cm5-cm10 1,500/= kwa nguzo moja
7. Mti wenye ukubwa wa cm10-cm20 2,200/=
8. Matami yenye ukubwa wa cm5-
cm30
3,680/= kwa tawi moja
9. Mkaa kwa kila kilo 10 240 kwa kila kilo moja
3. Ushuru wa Mifugo na machinjio ya Mifugo.
A. Ushuru wa Mifugo (Mnadani)
Na. Aina ya Mifugo Kiasi cha Ushuru kwa kila Mfugo (Tshs)
1. Ng’ombe…………………………………………………. 3,000/=
2. Mbuzi…………………………………………....................1,000/=
3. Kondoo…………………………………………………….1,000/=
4. Nguruwe………………………………………………...….1,500/=
B. Ushuru/ ada ya Machinjio na Ukaguzi wa Nyama.
(i) Ushuru Wa Huduma Za Ukaguzi Wa Nyama
(ii) Ng’ombe ………………………………………………………..………2,000/=
(iii) Mbuzi ………………………………………………………..………….1,500/=
(iv) Kondoo…………………………………………………..……………...1,500/=
(v) Nguruwe…………………………………………………….…………..2,000/=
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
8
(ii) Ada Ya Machinjio
(i) Ngombe ………………………………………………..….1,500/=
(ii) Mbuzi na Kondoo …………………………………………1,000/=
(iii) Wanyama wengine ………………………………………..1,000/=
5. Ushuru wa Soko:
A. Ushuru wa Kushusha Mizigo katika Eneo au Soko lolote lililotengwa na Halmashauri
Na. Aina ya Mizigo na uzani Kiwango cha
Ushuru (Tshs)
1. Lori lililobeba Ndizi lenye uzani wa tani 1 5,000/=
2. Lori lililobeba Miwa, Machungwa, Parachichi nyanya au Nanasi
lenye uzani wa tani 1
6,000/=
3. Mkaa kwa gunia 1,000/=
4. Tenga au gunia la dagaa, Samaki 1,000/=
5. Gunia la Mahindi, Maharage, Kunde 2,000/=
6. Karanga za maganda na mpunga, 2,500/=
7. Mchele na karanga zilizomenywa 5,000 kwa gunia
8. Tenga la Machungwa, Parachichi, Nanasi, Papai au Nyanya 500/= kwa tenga
B. Ushuru wa bidhaa mbalimbali katika masoko, minada, magulio na maeneo mbalimbali
yaliyotengwa na Halmashauri :
Na Aina ya Biashara Ushuru/Kodi ya Pango Muda
1. Vibanda Tshs. 15,000/= kwa kibanda kwa mwezi
2. Meza Tshs. 300/= kwa meza Kwa siku
3. Wauza mitumba Tshs 1000/= Kwa siku
4. Nguo za madukani kutandaza Tshs.1,000/ Kwa siku
5. Ndizi kupika mkungu Tshs. 7,500/= Kwa mkungu
7. Ndizi mbivu mkungu Tshs. 750/= Kwa mkungu
8. Nanasi tenga Tshs. 1,500/= Kwa siku
9. Maparachici tenga Tshs. 1,000/= Kwa siku
10. Mboga-mboga tenga Tshs. 200/= Kwa siku
11. Nyanya/ nyanya mshumaa tenga Tshs. 300/= Kwa siku
12. Machungwa tenga Tshs. 1,500/= Kwa siku
13. Viatu vya mitumba Tshs.1,000/= Kwa siku
14. Mama au Baba lishe Tshs.500/= Kwa siku
15. Vyombo vya ndani Tshs.500/= Kwa siku
16. Nyama au nyama choma Tshs. 1,000/= Kwa siku
17. Urembo Tshs.500/= Kwa siku
18. Bidhaa mchanganyiko Tshs.500/= Kwa siku
19. Samani (furniture Tshs. 5,000/= Kwa mwezi
20. Wauza vyungu Tsh 500/= Kwa siku
21. Wauza miwa Tsh 500/= Kwa siku
22. Wauza bia na soda Tsh 1,000/= Kwa siku
23. Wauza Pombe za kienyeji Tsh 500/= Kwa siku
24. Wauza madawa ya asili Tsh 500/= Kwa siku
25. Bidhaa nyingine zozote ambazo
hazikutajwa
Tshs.500/= Kwa siku
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
9
6. Ada ya Kibali cha Biashara mbalimbali zisizohitaji leseni.
Aina ya kibali Kiwango cha Ada ya maombi ya
kibali (Tshs)
1. Biashara ya mitumba nje ya maeneo
ya magulio, soko na minada
Tshs. 1000/= kwa mwezi
2. Fundi cherehani, baiskeli dobi, radio,
TV, Fundi simu
Tshs. 1000/= kwa mwezi
3. Fundi viatu, Tshs 500 kwa mwezi
4.
kinyozi, saluni za wanawake/
wanaume
Tshs. 5,000/= kwa mwezi
5. Mikokoteni, matoroli yenye magurudumu Tshs. 200/= kwa siku
6. Kibali cha biashara nyinginezo zisizohitaji leseni Tshs. 2, 000/=kwa mwaka
7. Gereji za pikipiki Tsh 2000 kwa siku
8. Fundi kuchomelea kwa siku Tsh 3000 kwa siku
7. Ada ya Kibali cha Ujenzi.
N
a
Aina ya kibali Kiwango cha Ada ya kibali
(Tshs)
1 Ujenzi wa Nyumba ya makazi 30, 000/=
2 Ujenzi wa Ghala, Karakana, gereji au
karakana za magari
50,000/=
3 Ujenzi wa Viwanda vidogo vidogo,
mashine za kukoboa au kusaga nafaka
(mchele, mahindi
30,000/=
4 Ujenzi wa Nyumba ya ghorofa moja 40,000/=
5 Ujenzi wa Kibanda chochote cha biashara 6,000/=
Ujenzi wa uzio wakati wa kujenga jengo lolote 50, 000/=
8. Ada ya ukaguzi wa Ramani, Kubadili matumizi ya Majengo na Ukaguzi wa
Majengo.
Aina ya kibali Kiwango cha Ada ya kibali
1 Kukagua ramani ya jengo la Nyumba ya
makazi
Tshs. 10, 000/=
2 Kukagua ramani ya Ujenzi wa Gorofa
kwa kila hatua ya ujenzi.
Tshs. 15,000/=
3 Kuendelea na hatua ya ujenzi
inayoendelea baada ya kibali cha awali
Tshs.5,000/=
4 Ramani za maghala Tshs, 15, 000/=
5 Ramani za Makanisa na misikiti Tshs. 15, 000/=
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
10
1. Kibali cha idhini ya kubadilisha matumizi ya Ardhi/ viwanja kutoka:-
i. Makazi kwenda biashara………….....................Tshs 50,000/=
ii. Makazi kwenda kwenda viwanda…………….Tshs. 100,000/=
iii. Biashara Kwenda Makazi………………………Tshs. 40,000/=
iv. Biashara/ makazi/ viwanda Kwenda matumizi Mengine…Tshs
100,000/=
2. Kibali cha idhini ya kuhamisha miliki ya Ardhi …………..…Tsh 40,000/=
9. Ada ya Kuchangiaji gharama za Upimaji na Usafishaji wa Viwanja
Na. Aina ya Kiwanja Kiwango cha Ada
1. Kiwanja chenye Ujazo wa Msongamano Mkubwa (HD)…..Tshs. 40, 000/=
2. Kiwanja chenye Ujazo wa Msongamano wa Kati (MD)……Tshs. 50, 000/=
3. Kiwanja chenye Ujazo wa Msongamano Mdogo (LD)……..Tshs. 60, 000/=
4. Viwanja vya Taasisi za watu Binafsi/dini……………………Tshs100,000/=
5. Mashamba………………………Tshs. 100, 000/= kwa kila ekari moja.
6. Kurudia upimaji upya baada ya mipaka kufutika 50% ya ada ya upimaji wa
kiwanja au eneo husika.
7. Kurudia kuonyeshwa kiwanja baada ya ugao wa awali kufanyika…Tshs.10, 000/=
8. USHURU WA MAGARI YANAYOINGIA KATIKA MAGULIO, MASOKO NA
MINADA
(i) Garidogo la abiria………………………….……………… Shilingi 500/=
kwasiku
(ii) Garikubwa la abiria……………………...………………. Shilingi 2,000/=
kwasiku
(iii) Garidogo la mizigo……………………..………………. Shilingi 2,000/=
kwasiku
(iv) Garikubwa la mizigo……………….…….……………...Shilingi 2,500/=
kwasiku
9. Ada ya Leseni mbalimbali
Na. Aina ya Leseni au Kibali Kiwango cha Ada (Tshs)
1. Leseni ya pombe za kigeni Tshs 40,000 kwa miezi Sita
2. Leseni ya Pombe za Kienyeji Tshs 20,000.kwa miezi sita
3. Leseni ya Mazao ya Misitu 20% ya gharama/ ushuru wa leseni
10. Ada ya zabuni
Na. Aina ya Zabuni Kiwango cha Ada (Tshs)
1. Zabuni ya ujenzi wa majengo, barabara na miundo
mbinu mingine
100, 000/=
2. Zabuni za uwakala mbalimbali 50, 000/=
3. Zabuni za ugavi wa huduma mbalimbali 50, 000/=
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
11
11. Ada ya Uthamini wa Ardhi na Viwanja vya taasisi binafsi na watu binafsi
Na. Aina ya Thamani Kiwango cha Ada (Tshs)
1. Kiwanja cha Ukubwa wowote 10 % ya kiwango cha thamani ya kiwanja
2. Shamba lenye ukubwa wowote 10% ya kiwango cha thamani ya shamba
12. Ada ya kibali cha kusafirisha ngozi
Na Aina ya Ngozi Kiwango cha Ada (Tshs)
1. Ngozi za ng’ombe Tshs. 1,000/=
2. Ngozi za mbuzi Tshs. 500/=
3. Ngozi za Kondoo Tshs. 500/=
13. Ada ya kukodi ukumbi wa Halmashauri.
(i) Matumizi ya ukumbi kwa semina za mashirika na miradi....... 200,000/=
kwasiku
(ii) Matumizi ya shughuli zinazofanywa na asasi za kiraia ……... 200,000/=
kwasiku
(iii) Matumizi binafsi …………………………………………….. 300,000/=
kwasiku
(iv) Kukodi viti (kila kiti) ………………………..……..………….. 300/= kwasiku
(v) Kukodi viti vinginevyo ……………………………………...….500/= kwa siku
14. Ada ya usajili wa vikundi.
Ada ya usajili wa vikundi itakuwa ni Tsh ……………………………………………….. 20,000/=
15. USHURU WA MABANGO YA BIASHARA
(i) Mabango ya biasharayasiyon’gara (kwa kila SqFT) …………..………… 15,000/=
(ii) Mabango ya biasharayanayong’ara (kwa kila SqFT) …………...…………13,000/=
(iii) Mabango ya biashara ya muda (yanayodumu kwa hadi siku 7) ….…….….10,000/=
(iv) Mabango ya biashara ya muda (yanayodumu kwa hadi siku 14) ……..…...25,000/=
(v) Mabango ya biashara ya muda (yanayodumu kwa hadi siku 30) …..….…..35,000/=
(vi) Matangazo ya biashara kwa kutumia vipaza sauti kwa siku…………….….15,000/=
(vii) Mabango ya matangazo yaliyobandikwa kwenye magari (kwa kila SqFT…13,000/=
16. USHURU WA KUCHINJA, KUWAMBA NA KUNUNUA NGOZI
Na. AINA YA
MNYAMA
USHURU WA
KUCHINJA
USHURU WA
KUWAMBA
USHURU WA
KUNUNUA NGOZI
1. Ng’ombe 3,000/= 1000/= 1,500/=
2. Mbuzi 1,000/= 500/= 1,000/=
3. Kondoo 1,000/= 500/= 1,000/=
4. Nguruwe 1,500/= 500/= 1,000/=
5. Mnyama mwingine 1,000/= 500/= 1,000/=
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
12
17. USHURU WA STENDI
i. Ushuru wa gari ndogo ya abiria (Taxi)…….................….Shiringi 500/= kwa siku.
ii. Ushuru wa gari binafsi kwa ……………............….......... shilingi 500/= kwa siku
iii. Ushuru wa basi dogo la abiria (Hiace)...............…....... Shilingi 1,000/= kwa siku
iv. Ushuru wa basi kubwa la abiria (Cousta).....................Shilingi 1,500/= kwa siku
v. Ushuru wa basi kubwa la abiria……….....................…Shilingi 2,000/=kwa siku.
vi. Ushuru wa bajaji na Pikipiki…………..............…....….Shilingi 300/= kwa siku
vii. Ushuru wa vifaa vingine ambavyo havijatajwa…….......Shilingi 1,000/= kwa siku
18. ADA YA KUONDOA NYUKI KATIKA MAENEO MBALIMBALI;
(i) Majumbani ………………………………………………..….…………. 20,000/=
(ii) Mashirika naTaasisi ………………………………….………………..… 50,000/=
________
JEDWALI LA PILI
________
HATI YA KUKIRI NA KUFIFILISHA KOSA
(Chini ya kifungu cha 12)
Mimi …………………… nakiri mbele ya ………….ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashuri ya Wilaya ya Masasi, kwamba mnamo tarehe …… ya Mwezi ……. Mwaka ……
nilitenda kosa la kukiuka masharti ya kifungu cha …… cha Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru)
za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za Mwaka 2017.
Kwa Mamlaka aliyopewa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Niko tayari kulipa kiasi cha Ada/
Ushuru ninaodaiwa pamoja na faini.
NATHIBITISHA KWAMBA MAELEZO HAPO JUU NI YA KWELI NA NIMEYATOA KWA
HIARI YANGU KADRI YA UFAHAMU WANGU
Leo tarehe…………………..…. ya Mwezi…………….. Mwaka ………………….
Jina……………………………….. Saini…………………………………….
Mbele ya :
Jina: ……………………………………………
Cheo: ………………………………………….
Saini: …………………………………………..
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
13
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANGAZO LA SERIKALI NA. 392 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA MIJI)
(SURA YA 287)
_________
SHERIA NDOGO
_________
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
14
Zimetungwa chini ya kifungu cha 153
_________
SHERIA NDOGO ZA (AFYA NA USAFI WA MAZINGIRA) ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI,
2017
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI
Jina na mwanzo
wa kutumika 1. Sheria Ndogo hizi zitaitwa Sheria Ndogo za (Afya
na Usafi wa Mazingira) za Halmashauri ya Wilaya
ya Masasi za Mwaka 2017 na zitaanza kutumika
baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Matumizi 2. Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo lote lililo
chini ya mamlaka ya Halmashauri ya Wilaya ya
Masasi.
Tafsiri 3. Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa itakapoelezwa
vinginevyo:-
“Afisa Mwidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote wa
umma aliyeteuliwa na Halmashauri kusimamia
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
15
utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi;
“Afya” maana yake ni hali timilifu ya kimwili, kiakili
na kijamii;
“Chakula” maana yake ni kitu chochote
kinacholiwa na kunywewa na binadamu isipokuwa
madawa, hii ni pamoja na:-
(a) kitu chochote kinachotumika katika matengenezo ya chakula;
(b) kitu chochote kinachoongeza ladha ya chakula;
(c) kitu chochote kinachobadili rangi ya chakula (binzari n.k);
“Choo cha kuvuta” maana yake ni choo ambacho
kimejengwa na kuunganishwa na maji na kuwa na
tanki ya kusukuma maji kwa ajili ya kuondoa
uchafu hadi mahali palipoandaliwa;
“Choo bora” maana yake ni choo chochote cha
maji chenye sakafu, banda imara la kudumu,
limeezekwa, lina mlango imara, bomba la kutolea
hewa chafu na lenye mfuniko kwenye tundu la
choo na shimo salama na safi kwa ajili ya kutupa
kinyesi na mkojo wa binadamu, lililojengwa kwa
vifaa vya kudumu, lenye vipimo vya futi 4 x 3 na
kimo cha futi 12 na zaidi; au
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
16
“Choo cha Umma” maana yake ni choo
kilichojengwa na Halmashauri au wakala wake kwa
matumizi ya umma;
“Eneo la wazi “maana yake ni eneo lililo chini ya
Halmashauri ambalo limekatazwa kufanyia
shughuli ambayo haihusiani na matumizi
yaliyokusudiwa;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya
Wilaya ya Masasi;
“Hati ya usafi” maana yake ni hati itakayotolewa
na Afisa Muidhiniwa inayothibitisha kukaguliwa
kwa maeneo yote yaliyotajwa katika Sheria Ndogo
hizi kulingana na Kanuni za Afya;
“Jengo la biashara” maana yake ni jengo lolote
lililojengwa na kuidhinishwa na Halmashauri
kufanya biashara iliyokusudiwa;
“Kaya” maana yake ni familia ya watu akiwemo
baba, mama, mtoto au watoto na mtu mwingine
yeyote anayeishi na familia hiyo, au watu
wanaokaa katika nyumba moja na kuishi kama
familia au mtu yeyote anayeishi peke yake katika
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
17
chumba au nyumba;
“Kero au chukizo” maana yake ni kitu chochote
ambacho kipo katika hali yoyote iwe kinatumika,
kimewekwa, kimejengwa, au ni kichafu kiasi cha
kusababisha:-
(a) hatari kwa viumbe na maisha ya binadamu;
(b) harufu mbaya na kuudhi; (c) kuzaliana kwa wadudu na wanyama hatari
kama vile nzi, mende, sisimizi, panya, nyoka, nyuki, kunguni au viumbe wengine hatari;
(d) magonjwa kwa binadamu,kuhifadhi mbu, nzi, panya na viumbe wenye madhara;
“Kituo cha taka” maana yake ni kizimba cha taka
kilichowekwa na Halmashauri kwa madhumuni ya
kuweka taka ngumu kabla ya kusafirishwa hadi
kwenye dampo la taka ngumu la Halmashauri;
“Maji taka” kama ilivyo katika Sheria ya Mazingira
Na. 20 ya mwaka 2004 ni pamoja na taka
zinazotokana na kinyesi, mkojo na jasho, uchafu
wa majimaji kutoka majumbani, taasisi, majengo
ya biashara na viwandani;
“Mazao au mimea marefu” maana yake ni mazao
au mimea inayozidi sentimita 15 kwenda juu kama
vile Mtama, Mihogo, Mahindi, Mbaazi, Uwele na
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
18
mengine yote yale yanayofanana na hayo;
“Mkazi” maana yake ni mtu yeyote anayeishi
katika eneo la Halmashauri na ambaye ana kaya au
anaishi katika kaya au taasisi iliyopo katika eneo la
Halmashauri;
“Mmiliki” maana yake ni mtu yeyote ambaye ana
miliki ardhi, sehemu za starehe, nyumba za kulala
wageni, nyumba za kuuzia vyakula, kumbi za
starehe, mpangaji, wakala wa mpangishaji wa
nyumba au jengo na makazi yoyote katika mtaa,
endapo mazingira husika ni mtaa au barabara za
mtaa;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa
Halmashauri pamoja na Afisa yeyote
atakayeteuliwa kutekeleza majukumu ya
Mkurugenzi;
“Mzalishaji wa taka ngumu” maana yake ni mtu
yeyote, kaya, taasisi, biashara, kiwanda ambaye
katika kutekeleza shughuli zake huzalisha taka;
“Pavement” maana yake ni sakafu imara ya mawe
au matofali ya saruji au udongo yaliyochomwa na
kujengewa kutoka katika nyumba hadi katika
mfereji au barabara, kwa waendao kwa miguu au
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
19
watazamaji wa vitu madukani;
“Pipa la taka”maana yake ni chombo chochote
chenye mfuniko kinachoweza kuhifadhi taka
ngumu zinazozalishwa majumbani, sehemu za
biashara, maofisini ili zisisambae na kuchafua
mazingira kwa namna yoyote;
“Taka” kama ilivyo katika Sheria ya Usimamizi wa
Mazingira, 2004 maana yake ni kitu chochote
kimiminika, kigumu, gesi na mionzi, kinachotoa
harufu mbaya, au kilichohifadhiwa katika
mazingira ya hali ya ujazo, uozo au hali nyingine
yoyote inayosababisha uharibifu wa mazingira,
ambayo inajumuisha taka;
“Taka Ngumu” kama ilivyo katika Sheria ya
Usimamizi wa mazingira, 2004 ni taka ambazo
haziko katika umajimaji kutoka majumbani, katika
majengo ya biashara, viwandani na kutoka katika
shughuli za kilimo, pamoja na taka za vyakula,
karatasi, plastiki au taka laini zinazotokana na
ujenzi au ubomoaji majengo, utengenezaji bustani
na shughuli za uchimbaji madini, mizoga ya
wanyama na mabaki ya magari mabovu (scraps);
“Taka za Majumbani”maana yake itajumuisha
mabaki ya chakula, maganda ya matunda, majivu,
kinyesi cha mifugo, taka za bustani, marapurapu ya
nguo, karatasi za aina mbalimbali na vitu vingine
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
20
ambavyo baada ya kuvitumia hutupwa;
“Taka za Viwandani” kama ilivyotafsiriwa katika
Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004,
maana yake ni uchafu unaotokana na uzalishaji
viwandani au uchafu usiotokana na uzalishaji
viwandani ambao ni chanzo cha nishati, maji,
mimea iliyotiwa dawa, au mawasiliano, pamoja na
taka nyinginezo ngumu kama zilivyotafsiriwa katika
Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, 2004 sehemu
ya IX;
“Uchafu Hatari” maana yake ni kama
ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Mazingira Na 20 ya
mwaka 2004, maana yake ni kitu chochote kigumu,
chenye majimaji, gesi au taka zitokazo viwandani,
au mafuta machafu, ambayo yanaleta athari za
kikemia, kwa binadamu au mazingira;
“Uchunguzi wa Afya” maana yake ni hali ya mtu
kupima afya yake kwa kuchukuliwa vipimo vya
ndani na nje ya mwili ili kubaini kuwepo kwa
vijidudu vya magonjwa vinavyoweza kuleta
maambukizi;
“Ufugaji wa ndani” maana yake ni ufugaji wa
mifugo ndani ya eneo lililoruhusiwa tu;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
21
“Vyakula vya kupikwa au kukaangwa” maana yake
ni inajumuisha maandazi, vitumbua, 21chapati,
mikate, samaki, nyama, chipsi, kuku na vinginevyo;
“Wakala” maana yake ni mtu binafsi au kikundi cha
watu, kampuni, taasisi au shirika aliyeteuliwa
kusimamia utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi.
SEHEMU YA PILI
USAFI WA MAZINGIRA
Wajibu wa
kufanya usafi wa
mazingira
4. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mkazi au mfanyabiashara
anayemiliki eneo la nyumba kuhakikisha kwamba
anafanya usafi wa mazingira yanayozunguka
makazi au eneo lake kwa kuhakikisha kwamba:-
(a) majani yanayozunguka nyumba yake yanakatwa au kupaliliwa katika eneo lote hadi mwanzo wa mipaka ya barabara ya mbele ya nyumba yake au eneo lake;
(b) taka taka zitakusanywa, kuhifadhiwa na kupelekwa katika eneo lililoruhusiwa na Halmashauri.
kushiriki
shughuli za usafi
wa mazingira
5. (1) Halmashauri imetenga kila siku ya Ijumaa ya wiki
ya mwisho ya kila mwezi kuwa ni siku za wananchi
kushiriki katika shughuli za usafi wa mazingira
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
22
katika maeneo ya Halmashauri.
(2) Itakuwa ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha
kwamba anashiriki katika shughuli za usafi wa
mazingira katika siku maalum zilizopangwa na
Halmashauri na mwananchi atakayekataa kushiriki
katika shughuli za kufanya usafi atakuwa
ametenda kosa.
(3) Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba au
kiwanja au eneo lolote ambalo halijaendelezwa
kufanya usafi katika eneo hilo mara kwa mara.
Mimea mirefu 6. Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kupanda au
kuotesha mazao au mimea marefu katika maeneo
ambayo Halmashauri itatangaza kuwa mimea
mirefu hairuhusiwi.
Usafi wa mifereji
ya maji ya mvua. 7. Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba
kuondoa uchafu kama vile mchanga, majani, nyasi
au vitu vingine vinavyofanana na hivyo kwenye
mfereji wa maji ya mvua unaozunguka au kupita
kando ya nyumba yake au eneo la biashara yake,
kiwanja chake na kuhakikisha mfereji huo
unakuwa msafi, na imara siku zote.
Kujenga sehemu
ya watembea 8. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba
kuweka sehemu ya waenda kwa miguu
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
23
kwa miguu “pavement” mbele ya nyumba au biashara yake
kwa kadri atakavyoelekezwa na Halmashauri.
(2) Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuweka
biashara ya aina yoyote aidha kwa kuuza au kwa
maonyesho katika mfereji au katika pavement.
Uwekaji taa za
nje ya nyumba 9. Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba,
mpangaji au mfanyabiashara kuweka taa yenye
mwanga nje ya jengo analoishi au analolitumia
kwa shughuli yoyote na atatakiwa kuiwasha wakati
wa usiku.
Kupaka rangi
majengo 10. Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba au
mpangaji au mfanyabiashara kuhakikisha kwamba
anapaka rangi nyumba yake au duka lake ndani na
nje kila itakapochakaa kadri Halmashauri
itakavyokuwa ikielekeza.
Wajibu wa
kuondoa na
kudhibiti mazalia
ya mbu na
wadudu wengine
11. Itakuwa ni wajibu wa mmiliki wa nyumba
kuhakikisha kuwa hakuna mkusanyiko wa maji,
maji machafu, takataka au kitu chochote cha
majimaji au kigumu ambacho kinaweza kuruhusu
kuwepo kwa mazalia ya mbu au wadudu wengine
wenye madhara kwa afya ya binadamu.
Biashara ya
miwa na
matunda
12. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mfanyabiashara ya
matunda au miwa kuhakikisha kuwa ana chombo
maalum cha kuhifadhia maganda au mabaki ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
24
matunda.
(2)
Ni marufuku mtu yeyote kufanya biashara ya
matunda au miwa pembeni mwa barabara au
katika maeneo yasiyoruhusiwa, na kula na kutupa
ovyo maganda ya miwa, ndizi au matunda
mengine.
Upulizaji dawa 13. Ni marufuku kwa mtu yeyote kuendesha biashara
ya upuliziaji dawa “Fumigation” au biashara ya
kuuwa wadudu au wanyama waharibifu katika
nyumba yoyote au mahali popote bila kuwa na
cheti cha taaluma kinachotambuliwa na Serikali na
awe na leseni hai kutoka Halmashauri.
Matengenezo ya
magari,pikipiki
na mitambo
14. (1) Matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo
yatatakiwa kufanyika kwenye karakana, gereji au
maeneo yaliyoruhusiwa baada ya kupata kibali
rasmi kutoka Halmashauri.
(3) Ni marufuku kwa mtu yeyote kutengeneza gari,
pikipiki au mtambo wowote katika eneo la makazi,
eneo la wazi au eneo ambalo halikutengwa kwa
shughuli hiyo.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
25
SEHEMU YA III
UIMARISHAJI WA AFYA
Usalama wa maji
ya kunywa. 15. Itakuwa ni wajibu wa kila mkazi kuhakikisha
kwamba maji yote yanayotumika kwa kunywa ni
safi na salama kwa kuyachemsha bila kujali
yametoka kwenye chanzo gani cha maji.
Utengenezaji, na
uuzaji vyakula. 16. (1) Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote
kutengeneza, kuchoma, kupima, kuchemsha au
kuuza chakula cha aina yoyote mahali popote,
uchochoroni, magengeni au kwenye nyumba
yoyote mpaka awe ametimiza masharti na kanuni
za afya na amepata kibali kutoka kwa Bwana Afya
wa Halmashauri.
Uuzaji vyakula
vilivyopikwa. (2) Itakuwa ni wajibu wa kila mtu anayeendesha
biashara ya vyakula vya kupikwa au kukaangwa
kuhakikisha kwamba vyakula hivyo vinahifadhiwa
kwenye sanduku lililotengenezwa kwa mbao safi
na kuwekwa kioo kuzuia nzi, vumbi na wadudu
waletao madhara kwa afya kwa binadamu.
Usalama wa
vyakula. (3)
Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuuza
vyakula vikiwa vimewekwa chini, vyakula vyote
vitatakiwa kuwekwa juu ya meza.
Ni marufuku kwa mtu yeyote anayejishughulisha
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
26
(4)
(5)
na huduma ya chakula; kupembua, kupika,
kupakua na kugawa chakula na kuosha vyombo
vilivyotumika kufanyia shughuli hiyo bila kuvaa
nguo rasmi/sare zinazotambuliwa na ofisi ya afya.
mhudumu wa chakula au vinywaji atapimwa afya
yake angalau kila baada ya miezi sita, muda huo
unaweza kupungua endapo Afisa Muidhiniwa
ataona kuna sababu ya maalumu.
Uzuiaji wa
shughuli
mbalimbali
wakati wa
Magonjwa ya
mlipuko
17. (1) Afisa Muidhiniwa anaweza kutoa amri ya kuzuia
shughuli yoyote isifanyike kama vile utengenezaji
wa vyakula, pombe, mijumuiko, sherehe na
mikusanyiko yoyote kwa kutangaza kwa njia ya
kipaza sauti, maandishi, au kupitia vyombo vya
habari endapo atakuwa na sababu ya kuamini
kwamba shughuli hiyo inaweza kusababisha
kuenea kwa magonjwa ya mlipuko na kuleta athari
kwa maisha ya binadamu.
Ukamataji wa
vyombo
vilivyotumika
kuhifadhia
chakula.
(2) Vyakula, vyombo na vifaa vingine vyovyote
vitakavyokamatwa baada ya kutolewa amri ya
kuzuia kufanyika kwa shughuli hiyo ambavyo
vitakuwa vimetumika kutunzia, kubebea,
kuhifadhia na kusafirishia vitaharibiwa na
Halmashauri haitahusika na gharama zozote
zitakazotokea wakati wa utekelezaji wa amri hiyo.
(3) Mtu yeyote atakayekataa kutii amri iliyotolewa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
27
atakuwa ametenda kosa.
Machinjio na
maduka ya
nyama
18. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa duka la
kuuzia nyama (Butcher) kuhakikisha kwamba duka
lake:-
(a) jengo la kudumu lililosakafiwa kwa marumaru nyeupe hadi urefu wa futi 6 kutoka usawa wa sakafu;
(b) lina maji safi, magogo na misumeno ya kukatia nyama;
(c) lina kabati ya vioo na jokofu la kuhifadhia nyama; sehemu za mizani;
(d) kuna pipa la kuhifadhia taka taka;. (e) muuzaji ana vazi jeupe pamoja na Apron
nyeupe; (f) muuzaji anapima afya kila baada ya miezi
sita.
Kuchinja na
kuuza nyama
mahali
pasiporuhusiwa.
(2) Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuchinja, au
kuuza nyama ya aina yoyote katika maeneo
yasiyokuwa machinjio au maduka ya nyama au
katika maeneo yasiyoruhusiwa na Halmashauri.
Ufugaji 19. (1) Mfugaji yeyote wa mbwa atatakiwa kuhakikisha
kuwa mbwa wake amepata chanjo na amesajiliwa
kwa mujibu wa maelekezo ya Halmashauri.
(2) Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuacha
mifugo au kusababisha mifugo kuachwa kuzurura
ovyo, barabarani au kuchungwa kwenye eneo
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
28
lolote lisiloruhusiwa.
Usafi wa zizi (3) Itakuwa ni wajibu wa kila mfugaji kuhakikisha
kwamba sehemu anayotumia kufugia:-
(a) inakuwa katika hali ya usafi wakati wote;
(b) anakusanya uchafu wowote utokanao na wanyama kama vile kinyesi, manyoya na nyasi au mabaki ya vyakula na kwenda kutupwa kwenye dampo au kupelekwa shambani kama mbolea.
(4) Mtu yeyote atakayetenda kosa kwa chini ya
kifungu hiki atatakiwa kulipa faini isiyozidi laki tatu
(300,000/=) au kifungo kisichozidi miezi kumi na
mbili jela au vyote viwili yaani kifungo na faini.
Uendeshaji wa
biashara ya
Hoteli na Hosteli.
20. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba za
kulala wageni na hosteli au nyumba za biashara
kuhakisha anapata kibali kutoka Halmashauri kabla
hajaanza biashara.
(2) Endapo mmiliki hajakidhi masharti ya kiafya
Halmashauri inaweza kuzuia kibali cha kuendesha
biashara ya hoteli au hosteli mpaka hapo mmiliki
atakapokuwa amekidhi masharti ya kiafya
yaliyotolewa na Halmashauri.
Mahitaji ya
nyumba ya (3) Kibali cha kuendesha biashara ya nyumba ya kulala
wageni, mgahawa, Hoteli na Hosteli kitatolewa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
29
wageni na
Hosteli baada ya Halmashauri kujiridhisha kuwa mahitaji
yafuatayo yamezingatiwa:-
(a) mwanga na hewa ya kutosha; (b) nafasi na vifaa (samani ) za kutosha; (c) uimara wa jengo; (d) mfumo wa uondoshaji wa maji taka,
miminika na taka ngumu; (e) usafi wa jumla wa jengo na vifaa vyake; (f) utoshelezaji wa vyoo na mabafu kwa jinsi
zote; (g) vifaa vya zima moto; (h) tanki la kuhifadhia maji safi; na (i) vyoo na bafu vimesakafiwa kwa vigae au
marumaru na kuta zake zimewekwa vigae kiasi cha futi sita toka usawa wa sakafu;
(j) Mashuka pea nne, taulo nyeupe na blanketi kila kitanda.
Upimaji wa afya 21. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mhudumu wa hoteli,
mgahawa, baa, bucha sehemu za kuokea mikate,
nyumba za kulala wageni, grosari au mtu yeyote
anayetengeneza chakula kwa ajili ya kuuza kupima
afya zao kila baada ya miezi mitatu (03) na
watalipa ada ya upimaji wa afya kiasi cha shilingi
elfu tatu (Tsh.3, 000/=).
(2) Mmiliki yeyote atakayeruhusu mhudumu yeyote
kufanya kazi bila kupimwa afya yake atawajibika
kulipa faini isiyozidi shilingi elfu hamsini.
Uwezo wa
kukagua. 22. (1) Afisa Muidhiniwa atakuwa na uwezo wa kuingia
katika jengo lolote wakati wowote wakati wa saa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
30
za kazi kukagua utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi.
Kufungwa kwa
jengo la biashara
lisilokidhi
masharti ya afya.
(2) Afisa Muidhiniwa atakuwa na uwezo wa kuagiza
kufungwa kwa biashara yoyote au jengo ambalo
halijakaguliwa au lililokaguliwa na kukutwa
limekiuka kanuni na masharti ya afya.
Ada ya ukaguzi
wa afya. 23. (1) Halmashauri itatoza ada ya ukaguzi wa afya
ambayo italipwa kwa mwaka kabla ya mwombaji
kupewa leseni ya biashara.
Viwango vya
ada. (2) Viwango vya ada ya ukaguzi wa afya vitakuwa
kama vilivyoainishwa katika jedwali la pili la Sheria
Ndogo hizi.
Muda wa kulipa
ada. (3)
(4)
Ada ya ukaguzi wa afya italipwa kila mwanzo wa
mwaka wa fedha wa Halmashauri, yaani mwezi
Julai.
Mtu yeyote atakayeshindwa kulipa ada katika
kipindi cha miezi miwili baada ya mwaka wa fedha
kuanza atawajibika kulipa kiwango hicho pamoja
na adhabu ya asilimia hamsini ya kiwango
anachodaiwa.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
31
SEHEMU YA III
UTUPAJI TAKA
Wajibu wa
Halmashauri 24. (1) Halmashauri itatenga eneo maalum kwa ajili ya
kutupia taka (dampo) na kutoa huduma ya uzoaji
taka kwa malipo kutoka kwa wazalishaji hadi
kwenye dampo.
(2) Halmashauri itakuwa na jukumu la kuhamasisha
uundaji wa Vikundi Jamii (CBOs) na kuvitambua ili
kuviwezesha kufanya shughuli za udhibiti wa taka
ngumu pamoja na usafi wa mazingira katika mitaa
baada ya kuingia mkataba na Halmashauri.
Wajibu wa kuwa
na pipa la taka. 25. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba au
mpangaji au mfanyabiashara kuhakikisha kuwa
ana chombo imara chenye mfuniko kwa ajili
kuhifadhia taka ngumu kabla hazijachukuliwa na
Halmashauri kwa ajili ya kwenda kutupwa.
Kutupa taka
katika sehemu
maalum
(2) Itakuwa ni wajibu wa kila mkazi kuhakikisha
kwamba anatupa uchafu, taka, maganda ya
matunda, mabaki ya vocha za simu katika vyombo
maalum vilivyowekwa kwa ajili ya kutunzia taka
katika maeneo maalum yaliyotengwa.
Marufuku (3) Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kutupa taka
au uchafu wowote au kuacha kuwepo takataka au
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
32
kutupa taka ovyo uchafu kwenye nyumba, uchochoroni, kiwanja,
mfereji wa maji ya mvua, barabara na maeneo ya
nyumba au mahali popote pasipotengwa kwa
shughuli hiyo.
Uhifadhi maji
taka 26. (1) Kila mmiliki wa nyumba anatakiwa kuhakikisha
kuwa ana karo la kuhifadhi maji taka na
atawajibika kunyonya maji taka pale karo linapojaa
na itakapohitajika kunyonya.
Kutiririsha maji
taka (2) Ni marufuku kutitirisha au kuelekeza maji, kutoka
vyooni, bafuni, karoni, baada ya kufua au kuosha
vyombo kwenda barabarani, uchochoroni, mtoni,
kwenye vyanzo vya maji, meneo ya wazi, mfereji
wa maji ya mvua au sehemu yoyote isiyotengwa
kuhifadhi maji taka.
Taka za viwanda 27. (1) Itakuwa ni marufuku kwa kiwanda chochote kutoa
au kusababisha kutoa uchafu wa aina yoyote, maji
machafu au harufu mbaya na kusababisha kero
kwa wakazi wa eneo la Halmashauri.
(2) Ni wajibu wa kila mwenye kiwanda kuhakikisha
kuwa taka kama vile vumbi, maganda, moshi na
takataka nyingine zinazoweza kuleta kero au adha
kwa ujumla haziwafikii wala hazileti madhara kwa
binadamu na viumbe hai wengine .
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
33
Uendeshaji wa
viwanda (3) Ni marufuku kuendesha shughuli za karakana,
mashine ya kusaga, kuranda mbao, kukamua maji
ya matunda, kuchomelea vyuma au kuendesha
shughuli yoyote inayozalisha uchafu ambao
unaleta athari kwa binadamu na viumbe wengine
katika maeneo ya makazi ya watu bila kuzingatia
taratibu za ujenzi.
Ada ya uzoaji
taka 28. Halmashauri itatoza ada ya uzoaji taka kutoka kwa
kila kaya au mwenye jengo la biashara kwa
viwango vilivyoainishwa katika jedwali la kwanza la
Sheria Ndogo hizi.
Uteuzi wa
wakala 29. Halmashauri inaweza kuteua kampuni, kikundi,
kikundi cha jamii au Mtu binafsi kutekeleza
majukumu yake chini ya Sheria Ndogo hizi.
SEHEMU YA IV
UJENZI NA MATUMIZI YA VYOO
Wajibu wa kuwa
na choo na
kukitumia
30. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa nyumba au
mpangaji kuhakikisha kwamba nyumba yake ina
choo safi, imara na madhubuti kwa matumizi ya
wakazi wa nyumba hiyo na kuhakikisha kinatumika
wakati wote.
Umbali wa (2) Choo kinatakiwa kijengwe umbali wa mita sitini
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
34
kujenga choo (60) kutoka kisima au chanzo chochote cha maji
kinachotumika kwa matumizi ya Nyumbani.
Vyoo vya umma 31 (1) Halmashauri inaweza kumruhusu mtu binafsi,
vikundi vya watu au Taasisi kujenga vyoo vya
Umma (Public toilet) katika maeneo ambayo
Halmashauri itaona kuwa kuna haja ya kufanya
hivyo.
(2) Vyoo hivyo vitamilikiwa na Halmashauri au kwa
ubia na wajenzi na vitakuwa ni vya kulipia kama
itakavyokuwa imeelekezwa na Halmashauri katika
mkataba wake na mawakala watakaopewa
kusimamia vyoo hivyo.
Vyoo vya muda
katika
mikusanyiko
(3) Itakuwa ni wajibu wa mtu, kikundi, Taasisi yenye
lengo la kukutanisha watu kwa madhumuni ya
ujenzi, sherehe au sehemu yoyote ambayo
itakutanisha watu kwa muda maalum endapo
eneo hilo hakuna choo cha kudumu kujenga vyoo
kwa matumizi ya wakati huo kwa idhini na
usimamizi wa Halmashauri.
Vyoo katika
majengo ya
biashara
(4) Kila mmiliki wa jengo la biashara atatakiwa
kujenga vyoo viwili vyenye viwango
vinavyokubalika chini ya Sheria Ndogo hizi kwa ajili
ya matumizi ya jinsi za kike na kiume.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
35
Ilani ya kujenga
choo 32. (1) Endapo katika ukaguzi wa afya itagundulika kuwa
nyumba yoyote haina choo, choo kilichopo
kimejaa au hakifai kwa matumizi ya binadamu,
Afisa Mwidhiniwa atatoa ilani ya siku thelathini
(30) kwa mmiliki wa nyumba au mpangaji
akiainisha masharti ya kurekebisha hali hiyo.
Kufungwa kwa
jengo (2) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1)
Halmashauri inaweza kuamuru nyumba au jengo
hilo lisitumike kwa shughuli za makazi au biashara
hadi hapo hali hiyo itakapokuwa imerekebishwa.
Ilani ya kuondoa
kero 33. (1) Endapo Afisa Mwidhiniwa atagundua kuwa eneo
alilokagua lina kero yoyote atatoa ilani ya siku saba
(7) kwa mmiliki wa nyumba, mpangaji, mtumiaji,
na, au mtu yeyote anayehusika akimtaka kuondoa
kero hiyo.
(2) Mtu yeyote atakayeshindwa kutekeleza masharti
ya ilani aliyopewa ndani ya muda ulioainishwa
kwenye ilani atakuwa ametenda kosa.
Mkurugenzi
kuteua mkaguzi 34. (1) Halmashauri inaweza kumteua mtu yeyote kuwa
mkaguzi kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa usafi
katika eneo la Halmashauri.
Uwezo wa kutoa
adhabu ya papo (2) Mkaguzi atakuwa na uwezo wa kutoa adhabu ya
papo kwa papo kwa mtu yeyote atakayekutwa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
36
kwa papo amechafua mazingira kwa kutupa takataka mahali
popote pasiporuhusiwa.
(3) Faini itakayotozwa na mkaguzi haitazidi shilingi
elfu hamsini.
Makosa 35. Mtu yeyote atakuwa ametenda kosa endapo:-
(a) atamzuia au kujaribu kumzuia Afisa Muidhiniwa asitekeleze wajibu wake chini ya Sheria Ndogo hizi; au
(b) atamshawishi mtu au kundi la watu kumzuia Afisa Muidhiniwa asitekeleze wajibu wake chini ya Sheria Ndogo hizi;
(c) atamwaga takataka katika mtaa, mtaro wa maji ya mvua, uchochoroni, au mahali popote hadharani au katika eneo lolote la wazi bila idhini ya Halmashauri;
(d) ataendesha biashara ya pombe ndani ya nyumba ya makazi;
(e) atatiririsha maji machafu barabarani au katika eneo la nyumba ya jirani;
(f) ataosha magari, kufua,kunywesha mifugo na kukoroga dawa za mimea ndani ya mito, mabwawa,lambo au ndani ya chanzo au kisima kinachotumika kwa matumizi ya binadamu;
(g) atauza vyakula vilivyopikwa barabarani au nje ya majengo mengine;
(h) atafanya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo, kuendesha shughuli za viwanda katika maeneo ya wazi, makazi, barabarani, uchochoroni, au katika maeneo yasiyotengwa kwa shughuli hizo
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
37
bila kuzingatia taratibu; (i) ataanzisha au kufungua karakana katika
majengo au majumba au maeneo ya makazi;
(j) ataenda haja ndogo au kubwa hovyo barabarani, uchochoroni, upenuni au mahali popote ambapo siyo chooni;
(k) Atachinja mfugo au kuuza chakula bila kufuata taratibu;
(l) atashindwa kuhifadhi chakula kwenye kabati safi lililofunikwa na lenye kioo.
Adhabu 36. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na masharti
ya Sheria Ndogo hizi atakuwa ametenda kosa na
akipatikana na hatia atatozwa faini isiyozidi shilingi
laki tatu (300,000) au kifungo kisichozidi miezi
kumi na miwili (12) au adhabu zote mbili kwa
pamoja yaani faini na kifungo.
_______
JEDWALI LA KWANZA
________
Chini ya kifungu cha 28
ADA YA UZOAJI TAKA
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
38
Na. Eneo. Kiwango cha ada
kwa mwezi.
1. Nyumba za kuishi au makazi kwa kaya 1,000/=
2. Nyumba za kulala Wageni 2,000/=
3. Maduka 1,500/=
4. Mgahawa, Mama, baba Lishe 1,000/=
5. Hoteli, Baa, Grosari 2,000/=
6. Vibanda au meza za biashara 1,000/=
7. Wachoma chips, kuku, nyama 1,500/=
8. Saluni 1,000/=
9. Mafundi Seremala, samani na gereji 5,000/=
10. Wauza mbao au karakana za kuranda mbao 5,000/=
11. Ofisi au Taasisi 3,000/=
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
39
_______
JEDWALI LA PILI
_______
Chini ya kifungu cha 23 (2)
ADA YA UKAGUZI WA AFYA
Na. Aina ya biashara Ada kwa mwaka
1. Baa na maduka ya vinywaji (Groceries) 5,000/=
2. Migahawa na Mama Lishe 2,500/=
3. Nyumba za wageni (Guest House) na Hoteli 10,000/=
4. Kumbi za starehe au mikutano 10,000/=
5. Majengo mengine ya biashara 5,000/=
_________
JEDWALI LA TATU
_________
Chini ya kifungu cha 32
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
40
HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI
ILANI YA KUJENGA CHOO
Ilani hii imetolewa kwa mujibu wa kifungu cha 32 cha Sheria Ndogo za (Afya na Usafi wa
Mazingira) za Halmashauri ya Wilaya ya masasi, 2017.
SEHEMU ‘A’
Ndugu…………………...............wa Mtaa……………Kata ya…………………………...
Unaarifiwa kwamba katika ukaguzi uliofanyika Tarehe……mwezi………..mwaka…….
Katika nyumba yako ya Biashara/kuishi/kutolea Huduma*/ Namba………… iliyopo eneo
la ………………katika Kitongoji/Mtaa*……….……………Kata ya……………....
Imekuwa haina choo/ choo kimejaa/kimeharibika* hivyo unaamriwa kutekeleza mambo
yafuatayo;
(1) ………………………………………………………………………………… (2) ………………………………………………………………………………… (3) ………………………………………………………………………………… (4) …………………………………………………………………………………
SEHEMU ‘B’
Unapewa muda wa siku thelathini (30) tu tangu siku ya kupokea ilani hii kutekeleza
maelekezo yote yaliyoelezwa katika sehemu ‘A’ ya Ilani hii.
SEHEMU ‘C’
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
41
Ukaguzi wa kuthibitisha utekelezaji wa maelekezo uliyopewa utafanyika
tarehe……………….endepo utashindwa kutekeleza maelekezo ndani ya muda uliopewa
Halmashauri itakuchukulia hatua kali za kisheria bila kukupa taarifa nyingine.
………………………………..
AFISA MUIDHINIWA
IMETOLEWA NA; IMEPOKELEWA NA;
Jina;………………………. Jina;………………………………….
Saini……………………… saini………………………………....
Wadhifa…………………... wadhifa……………………………..
Tarehe…………………….. Tarehe……………………………...
______
JEDWALI LA NNE
______
(Chini ya kifungu cha 33 )
HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
42
ILANI YA KUONDOA KERO
Ilani hii imetolewa kwa mujibu wa Sheria Ndogo za Afya na Usafi wa Mazingira za
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, 2017.
SEHEMU ‘A’
Ndugu…………………...............wa Mtaa……………Kata ya…………………
Unaarifiwa kwamba katika ukaguzi uliofanyika Tarehe……mwezi………..mwaka….
Katika nyumba yako ya Biashara/kuishi/kutolea Huduma/kiwanja* iliyopo eneo
la………………………………………………………………………………kumekutwa
machukizo/kero/uchafu*; kama ifuatavyo:-
1) ………………………………………………………………………………….. 2) ………………………………………………………………………………….. 3) ………………………………………………………………………………….. 4) …………………………………………………………………………………..
SEHEMU ‘B’
Kwa ilani hii unaamriwa kurekebisha/kuondoa/kusafisha* kwa:-
1. ………………………………………………………………………………….. 2. …………………………………………………………………………………. 3. ………………………………………………………………………………….. 4. …………………………………………………………………………………..
SEHEMU ‘C’
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
43
Unapewa muda wa siku saba (7) tangu siku ya kupokea ilani hii, unatakiwa kutekeleza
yote yaliyoelezwa katika sehemu ‘B’ ya Ilani hii, kushindwa kwako kutekeleza ndani ya
muda uliopewa Halmashauri italazimika kukuchukulia hatua kali za kisheria bila
kulazimika kukupa taarifa nyingine.
…………………………………..
AFISA MUIDHINIWA
IMETOLEWA NA; IMEPOKELEWA NA;
Jina;………………………. Jina;………………………………….
Saini……………………… saini………………………………....
Wadhifa…………………... wadhifa……………………………..
Tarehe…………………….. Tarehe……………………………...
*Futa lisilohusika
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
44
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
Tangazo la Serikali Na. 252 la tarehe 28/07/2017
SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA
ZA WILAYA)
(SURA YA 287)
_______
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
45
KANUNI ZA KUDUMU
_______
Zimetungwa chini ya kifungu cha 70(1)
_______
KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI
ZA MWAKA 2017
YALIYOMO
SEHEMU YA I
MASHARTI YA MWANZO
1. Jina na tarehe ya kuanza kutumika 2. Tafsiri ya maneno yaliyotumika
SEHEMU YA II
MIKUTANO YA HALMASHAURI
3. Mikutano ya Kawaida ya Halmashauri 4. Mkutano Maalum wa Halmashauri 5. Mkutano wa Bajeti 6. Mkutano wa mwaka 7. Taarifa za mikutano 8. Akidi katika mikutano ya Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
46
SEHEMU YA III
TARATIBU ZA MIKUTANO
9. Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
10. Uongozi wa Mikutano ya Halmashauri 11. Kumbukumbu ya mahudhurio 12. Kuruhusu watu na Vyombo vya Habari
kwenye Mikutano ya Halmashauri
13. Utaratibu wa shughuli za Mikutano 14. Kuthibitisha muhtasari 15. Hoja za Mwenyekiti 16. Taratibu za Majadiliano 17. Fujo zinazosababishwa na Wajumbe. 18. Fujo zinazosababishwa na Umma 19. Hoja za Marekebisho ya Hoja 20. Hoja zinazoweza kutolewa bila taarifa. 21. Haki ya kujibu 22. Maswali 23. Maswali ya papo kwa papo 24. Taarifa za Kamati 25. Taarifa kutoka kwenye Kata 26. Uhuru wa Kutoa mawazo wakati wa
majadiliano 27. Kauli zenye kashfa 28. Maamuzi ya Mikutano ya Halmashauri 29. Mwaliko kwa wasiokuwa Wajumbe
kushiriki na kuzungumza kwenye vikao vya Halmashauri
30. Mihtasari ya Kata na Vijiji 31. Mihtasari kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya
na Mkuu wa Mkoa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
47
32. Hoja kuhusu matumizi 33. Kupokelewa kwa taarifa ya Kamati 34. Kuidhinishwa kwa taarifa ya Kamati 35. Uhalali wa majadiliano ya Halmashauri 36. Uwezo wa Halmashauri kujigeuza kuwa
Kamati ya Halmashauri nzima.
37. Hoja zinazohusu watumishi wa Halmashauri
38. Kushiriki kwa Umma 39. Uahirishaji wa Vikao
SEHEMU YA IV
KAMATI
40. Kamati za Kudumu 41. Mwenyekiti kuwa Mjumbe wa Kamati zote 42. Uwezo wa Kamati 43. Kamati za Pamoja 44. Kukasimu madaraka kwenye Kamati 45. Kamati Ndogo 46. Mikutano ya Kamati 47. Mwenyekiti wa Kamati 48. Mkutano Maalum wa Kamati 49. Ajenda za Kamati 50. Mahudhurio katika mikutano ya Kamati 51. Mtoa hoja kualikwa kwenye Mkutano wa
Kamati 52. Waalikwa wasiokuwa Wajumbe
kuhudhuria na kushiriki katika mikutano ya Kamati
53. Mahudhurio ya Umma na Vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya Kamati na Kamati Ndogo
54. Athari za nafasi wazi kwenye Kamati
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
48
55. Akidi kwenye Mikutano ya Kamati 56. Kanuni za Kudumu kutumika katika
mikutano ya Kamati 57. Upigaji kura kwenye mikutano ya Kamati 58. Muhtasari wa Kamati 59. Kufikiriwa upya maamuzi 60. Kutunza siri za majadiliano ya Kamati na
Kamati Ndogo 61. Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa
Kamati 62. Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwa
kwa nafasi iliyoachwa wazi.
SEHEMU YA V
UNUNUZI WA VIFAA, UPATIKANAJI WA
HUDUMU NA UJENZI
63. Taratibu za uagizaji 64. Kumbukumbu za majadiliano yanayohusu
uagizaji 65. Uzuiaji wa rushwa 66. Usimamizi wa Mikataba 67. Uvunjaji wa Mikataba 68. Rejesta ya Mikataba 69. Diwani au Afisa kutokuwa na maslahi
kwenye Mikataba
SEHEMU YA VI
MASUALA MENGINE
70. Kiapo cha kukubali wadhifa 71. Majukumu ya Diwani
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
49
72. Nafasi wazi 73. Kutokuwepo kwa Wajumbe 74. Taratibu za kutunga Sheria Ndogo 75. Ukaguzi wa nyaraka 76. Uanzishaji wa Bodi ya Huduma 77. Diwani kutembelea maeneo, shughuli
mbalimbali za ujenzi 78. Uhifadhi wa lakiri ya Halmashauri 79. Utiaji muhuri kwenye nyaraka 80. Uandikishaji wa anwani 81. Uteuzi wa Wajumbe kwenye Taasisi za nje 82. Kumwondoa Mwenyekiti madarakani
SEHEMU YA VII
POSHO KWA WAJUMBE
83. Aina za posho 84. Posho iwapo Mkutano umeahirishwa
SEHEMU YA VIII
MABADILIKO KWENYE KANUNI ZA KUDUMU
85. Kusitisha utumiaji wa Kanuni za Kudumu 86. Marekebisho na mabadiliko ya Kanuni za
Kudumu 87. Kanuni za Kudumu kutolewa kwa
Wajumbe 88. Kutafsiri Kanuni za Kudumu 89. Ziara za Wajumbe 90. Dua/sala ya kuiombea Halmashauri
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
50
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
51
SEHEMU YA 1
MASHARTI YA MWANZO
KWA KUWA Kauli-mbiu ya Halmashauri ni kuendesha shughuli kwa
namna inayozingatia demokrasia, ufanisi, tija, ushirikishwaji, uwazi
na uwajibikaji:
NA KWA KUWA jukumu la Halmashauri ni kuimarisha demokrasia
katika ngazi zote na kutoa huduma kwa wananchi kwa kuzingatia
ufanisi, usawa, haki na kwa namna inayochochea maendeleo ya
maeneo yaliyo chini ya mamlaka ya Halmashauri kwa kuwashirikisha
wananchi:
NA KWA KUWA madhumuni ya Kanuni za Kudumu ni kuweka
utaratibu wa namna Halmashauri itakavyoendesha mikutano na
shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya utawala bora:
SASA BASI, Kanuni za Kudumu hizi zinaelekeza ifuatavyo:
Jina na
tarehe ya
Kuanza
kutumika
1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za mwaka 2017 na zitaanza kutumika mara baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Tafsiri 2. Katika Kanuni hizi isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo:
“Afisa wa Serikali za Mitaa” maana yake ni mtu ambaye ameajiriwa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
52
au ambaye yumo katika utumishi wa Mamlaka ya Serikali za
Mitaa na ambaye anashika au anakaimu katika nafasi ya
menejimenti;
“Diwani” maana yake ni Mjumbe wa Halmashauri aliyetajwa kwa
mujibu wa kifungu 35 cha Sheria ya Serikali za Mitaa
(Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287;
“Fujo” maana yake ni kitendo chochote kinachoweza kufanywa na
Mjumbe au Mshiriki wa Kikao cha Halmashauri au Kamati ya
Kudumu ambacho ni kinyume na taratibu za uendeshaji wa
vikao, kinachoweza kuvuruga kikao. Mfano kuongea bila
ruhusa ya Mwenyekiti, kutoa lugha isiyofaa, kutoa kauli yenye
maudhi, kuingia kwenye kikao akiwa umelewa, kuingia na
silaha au kutoa lugha ya kashfa, matusi, kejeli au kukaidi amri
ya Mwenyekiti, kukaidi kutoka nje pale anapoamriwa kutoka
kutokana na fujo alizosababisha;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Wilaya ya Masasi;
“Kamati”
(a) Inapotumika kuhusiana na Halmashauri ina maana ya Kamati iliyoanzishwa au iliyoteuliwa na Halmashauri chini ya Sheria;
(b) Inapotumika kuhusiana na Kamati ya Maendeleo ya Kata ina maana ya Kamati hiyo;
(c) Inapotumika kuhusiana na Kamati Ndogo maana yake ni Kamati Ndogo hiyo iliyoteuliwa na Kamati;
(d) Inapotumika kuhusiana na Kamati nyingine ina maana ya Kamati hiyo;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
53
“Mamlaka ya Mji mdogo” maana yake ni Mamlaka ya Mji Mdogo
ulioanzishwa chini ya kifungu 13 cha Sheria;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Wilaya ya Masasi au Afisa yeyote aliyeteuliwa kutekeleza
majukumu ya Mkurugenzi;
“Mjumbe” maana yake ni Mjumbe wa Halmashauri kama
ilivyoainishwa na kifungu cha 35 cha Sheria;
“Mwenyekiti”
(a) Kwa madhumuni ya Halmashauri maana yake ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, na inajumuisha Makamu Mwenyekiti wakati anapotekeleza majukumu ya Mwenyekiti kwa mujibu wa Kanuni hizi;
(b) Kwa madhumuni ya Kamati, Bodi au Kamati Ndogo maana yake ni Mwenyekiti wa Kamati, Bodi au Kamati Ndogo;
(c) Kwa maana ya Bodi ya Zabuni ni Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni;
“Sheria” maana yake ni Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za
Wilaya) Sura ya 287;
“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya Serikali za
Mitaa.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
54
SEHEMU YA II
MIKUTANO YA HALMASHAURI
Mikutano
ya
Kawaida
ya Halma-
shauri
3.-(1) (a) Mikutano ya Kawaida ya Halmashauri itafanyika mara
moja kila baada ya miezi mitatu, na itafanyika mahali, tarehe na
katika muda kama utakavyokuwa umepangwa katika kalenda ya
mikutano ya Halmashauri;
(b) Mikutano ya kawaida ya Halmashauri itatanguliwa na vikao
vya Kamati za Kudumu za Halmashauri.
Mkutano
wa
kwanza
wa
Halma-
shauri
(2).-(a)Mkutano wa kwanza wa kawaida wa Halmashauri
utafanyika baada ya Tume ya Uchaguzi kutangaza matokeo ya
uchaguzi wa Madiwani wa Kata na uteuzi wa Madiwani wa Viti
Maalumu na utafanyika mahali, siku na katika muda utakaopangwa
na Mkurugenzi, ilimradi Mkurugenzi atapaswa kuitisha Mkutano
huo ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya matokeo ya uchaguzi
wa Madiwani wa Kata na Uteuzi wa madiwani Viti Maalum
yanapotangazwa na Tume ya Uchaguzi ambapo moja ya ajenda za
Mkutano huo ni kumchagua Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na
Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Halmashauri;
(b) Katika Mkutano huo Mkurugenzi wa Halmashauri
atawasilisha Taarifa ya kumbukumbu ya maamuzi ya utekelezaji
wa shughuli za Halmashauri zilizofanyika katika kipindi ambacho
Baraza la madiwani lilivunjwa. Wajumbe wa Baraza watapokea
na kujadili bila kubatilisha maamuzi yaliyokwisha amuliwa ili
kudhihirisha uhalali wake.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
55
Utaratibu
wa
uchaguzi
(3) Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti utafanyika
kwa kupiga kura za siri na upigaji wa kura utafanyikia sehemu ya
faragha umbali usiopungua mita (5) kutoka kwa Msimamizi wa
Uchaguzi na mpigaji kura atachukua karatasi ya kupiga kura kutoka
kwa Msimamizi wa Uchaguzi.
Mkutano
Maalum
wa
Halma-
shauri
4.-(1) Mkutano Maalum wa Halmashauri unaweza kuitishwa na
Mwenyekiti ndani ya siku ishirini na moja baada ya kupokea
maombi ya maandishi yaliyosainiwa na si pungufu ya theluthi moja
ya Wajumbe wote kutaka Mkutano huo ufanyike na maombi hayo
yaeleze wazi madhumuni ya kuitishwa kwa Mkutano Maalum huo.
(2) Iwapo Mwenyekiti anakataa kuitisha Mkutano Maalum wa
Halmashauri baada ya kupokea maombi ya kutakiwa kufanya
hivyo,maombi yaliyosainiwa na Wajumbe wa Halmashauri
wasiopungua theluthi moja ya Wajumbe wote wakionyesha sababu
ya kuitisha Mkutano huo Maalum na kuwasilishwa kwake, au iwapo
bila kukataa, Mwenyekiti, ndani ya kipindi cha siku saba ataendelea
kutoitisha Mkutano huo Maalum baada ya kupokea ombi la kuitisha
Mkutano huo Maalum, basi theluthi mbili ya Wajumbe waliotia saini
na kuwasilisha kwa Mkurugenzi wanaweza kuitisha Mkutano huo
Maalum mara moja.
(3) Endapo ajenda ya Mkutano huo itahusu kumuondoa
madarakani Mwenyekiti, Mkutano huo utaitishwa na Mkurugenzi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
56
baada ya kupokea maombi yaliyosainiwa na Wajumbe wa
Halmashauri wasiopungua theluthi mbili ya Wajumbe wote.
(4) Baada ya Mkurugenzi kupata taarifa ya kutaka kufanyika kwa
Mkutano wa kujadili ajenda ya kumuondoa madarakani Mwenyekiti,
Mkurugenzi atamtaarifu Mwenyekiti tuhuma na sababu za kutaka
kuondolewa uenyekiti na kumtaka aandae majibu ya tuhuma ndani
ya siku Tano (5) baada ya kupokea tuhuma hizo.
(5) Mkurugenzi katika muda wa siku Tatu (3) baada ya kupokea
maelezo ya utetezi kutoka kwa Mwenyekiti, atawasilisha kwa Mkuu
wa Mkoa tuhuma pamoja na maelezo ya utetezi.
(6) Mkuu wa Mkoa katika muda wa siku tano (5) baada ya
kupokea taarifa ataunda Timu ya Uchunguzi ambayo itakua na
wajumbe wasiopungua watatu (3) na wasiozidi watano (5).
(7) Timu ya Uchunguzi itatakiwa kukamilisha Uchunguzi katika
muda wa siku kumi na nne (14) na kuwasilisha taarifa hiyo kwa
Mkuu wa Mkoa.
(8) Baada ya Mkuu wa Mkoa kupata taarifa ya Timu ya
Uchunguzi atairudisha Taarifa hiyo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri
ambaye naye katika muda wa siku kumi na Nne (14) ataiwasilisha
kwenye Kikao cha Baraza kwa uamuzi wa tuhuma hizo.
Kifungu
cha 36(5)
Sura 287
(9) Endapo Mwenyekiti hataridhika na uamuzi wa Baraza, atakata
rufaa kwa Waziri kuhusu utaratibu uliotumika kumuondoa
madarakani na siyo vinginevyo.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
57
Utaratibu
wa
kuwasili-
sha rufaa
(10) Utaratibu utakaotumika kuwasilisha na kushughulikia rufaa
iliyowasilishwa na Mwenyekiti ni ule ulioelezwa kwenye Taratibu za
kumuondoa Madarakani Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya.
(11) Taarifa ya Mkutano Maalum itatolewa angalau saa ishirini
na nne kabla ya Mkutano.
(12) Hakuna shughuli nyingine yoyote itakayojadiliwa katika
Mkutano Maalum wa Halmashauri isipokuwa ile tu iliyoelezwa
kwenye taarifa ya kuitishwa kwa Mkutano huo.
Mkutano
wa Bajeti 5. Kutakuwepo na Mkutano wa Bajeti wa Halmashauri
utakaofanyika kwa muda wa siku mbili mfululizo na utafanyika
miezi miwili kabla ya mwaka wa fedha kumalizika na utajadili
mambo yafuatayo:-
(a) Utekelezaji wa Mipango na Bajeti ya mwaka uliopita;
(b) Mipango na Bajeti ya mwaka unaofuata.
Mkutano
wa
Mwaka
6.-(1) (a) Mkutano wa Mwaka wa Halmashauri utafanyika
tarehe, mahali na muda utakaopangwa na Halmashauri katika
kalenda ya Mikutano na utaitishwa na Mkurugenzi baada ya
kuwasiliana na Mwenyekiti wa Halmashauri.
(b) Mikutano yote ya Baraza itapangwa na Baraza la Madiwani
kwa kuzingatia ratiba ya Vikao vya Bunge ili kuwezesha Wabunge
kuhudhuria Mikutano ya Baraza la Madiwani;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
58
(c) Endapo italazimika kuitishwa kwa Mkutano wa Baraza
wakati wa Vikao vya Bunge, Mkurugenzi atamjulisha au atawajulisha
Wabunge husika kuhusu kikao hicho ili wahudhurie.
(2) Mkutano wa Kwanza wa Uchaguzi wa Mwenyekiti, Makamu
Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati utaongozwa na Katibu Tawala
wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri atakuwa Katibu.
(3) Katika Mkutano wa kawaida wa mwaka, Halmashauri itajadili
mambo yafuatayo:-
(a) kumchagua Makamu wa Mwenyekiti;
(b) kuteua Wajumbe wa Kamati za Kudumu;
(c) kujadili taarifa ya utendaji na uwajibikaji wa Halmashauri kwa mwaka uliopita;
(d) kupitisha ratiba ya vikao vya Halmashauri na Kamati za Halmashauri.
Taarifa za
Mkutano 7.-(1) Mkurugenzi atatoa taarifa ya Mkutano kwa maandishi
kwa kila Mjumbe katika muda usiopungua siku saba akieleza mahali,
siku na saa ya Mkutano unaokusudiwa na mambo yatakayojadiliwa
katika Mkutano huo.
(2) Taarifa ya Mkutano itaambatana na nyaraka au
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
59
kumbukumbu muhimu zitakazotumika katika Mkutano huo.
(3) Isipokuwa kwa idhini ya Mwenyekiti na/au ya idadi ya
Wajumbe isiyopungua robo tatu ya Wajumbe waliohudhuria
Mkutano, hakuna shughuli yoyote itakayofanywa katika Mkutano
wa Halmashauri mbali na shughuli zilizotajwa katika mwaliko wa
Mkutano huo.
Akidi
katika
mikutano
ya Halma-
shauri
8.-(1) Hakuna Mkutano wa kawaida wa Halmashauri
utakaofanyika isipokuwa kama kutakuwepo idadi ya Wajumbe
isiyopungua nusu ya Wajumbe wote waliohudhuria na kujiandikisha
kwenye daftari la mahudhurio.
(2) Akidi katika mikutano Maalum ya Halmashauri itakuwa ni
theluthi mbili ya Wajumbe wote wa Halmashauri na itahesabiwa
wakati wa ufunguzi wa Mkutano.
(3) Akidi katika Mkutano wa kawaida wa mwaka na Mkutano wa
kwanza wa Halmashauri itakuwa theluthi mbili ya Wajumbe wote
wa Halmashauri.
(4) Endapo Wajumbe waliohudhuria Mkutano hawatafikia akidi
ya Mkutano, Mkurugenzi atauahirisha Mkutano huo na kuuitisha
tena ndani ya siku saba (7) na endapo akidi haitatimia tena, idadi
yoyote ya Wajumbe waliohudhuria itatengeneza akidi ya Mkutano
na Mkurugenzi atamjulisha Waziri kuwepo kwa hali hiyo.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
60
SEHEMU YA III
TARATIBU ZA MIKUTANO
Uchaguzi
wa
Mwenye-
kiti na
Makamu
Mwenye-
kiti wa
Halma-
shauri
9.-(1) Mwenyekiti na Makamu wa Mwenyekiti watachaguliwa na
Wajumbe, kutokana na Wajumbe wa Halmashauri kwa kura ya siri
itakayopigwa na Mjumbe mmoja mmoja kwenye eneo la faragha
litakalotengwa umbali usiopungua mita 5 kutoka mahali alipoketi
Msimamizi wa Uchaguzi.
(2) Mjumbe kabla ya kwenda sehemu ya faragha kwa ajili ya
kupiga Kura, atapatiwa na Msimamizi wa Uchaguzi karatasi ya
kupigia Kura kutoka kwenye chombo Maalum kitakachowekwa
mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi, na atakwenda moja kwa moja
kupiga kura yake kwenye sehemu ya faragha.
(3) Mtu atatangazwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti au Makamu
wa Mwenyekiti iwapo atapata zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa.
(4) Iwapo wakati wa kumchagua Mwenyekiti au Makamu wa
Mwenyekiti jina moja tu limependekezwa, Wajumbe watapiga kura
za siri za “ndiyo” au “hapana” na endapo kura za “ndiyo” zitazidi
asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwa basi mgombea
atatangazwa kuwa Mwenyekiti au Makamu wa Mwenyekiti.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
61
(5) Iwapo kura za “Hapana” zitazidi asilimia hamsini ya kura zote
zilizopigwa, jina la mgombea mwingine litapendekezwa kwa njia na
utaratibu uliotumika hapo awali.
(6) Iwapo kura zitafanana, uchaguzi utarudiwa kwa mara ya pili
na endapo hata baada ya kurudia uchaguzi, kura zitafanana, Baraza
litaamua kugawa muda wa kuwa madarakani kwa wagombea hao
ambao kura zao zimefanana.
(7) Kama itatokea nafasi wazi ya Mwenyekiti au Makamu wa
Mwenyekiti, Halmashauri itamchagua Mwenyekiti au Makamu
Mwenyekiti katika muda wa siku zisizozidi sitini tangu nafasi hiyo
ilipotokea kuwa wazi.
Uongozaji
wa
Mikutano
ya Halma-
shauri
10.-(1) Mkutano wa Halmashauri utaongozwa na:-
(a) Mwenyekiti; au
(b) kama Mwenyekiti hayupo, Makamu wa Mwenyekiti; au
(c) Kama Mwenyekiti na Makamu wa Mwenyekiti wote hawapo, au kama Mwenyekiti na Makamu wa Mwenyekiti wote hawawezi kuongoza Mkutano, Mjumbe yeyote atachaguliwa kutoka miongoni mwa Wajumbe waliohudhuria kwa ajili ya kuongoza Mkutano huo;
(d) Wajumbe walikuwa ndani ya ukumbi wa mikutano wa Halmashauri watavaa mavazi Maalum yaliyochaguliwa na kushonwa Maalum kwa ajili hiyo;
(e) Endapo vazi Maalum lililochaguliwa na Halmashauri ni joho
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
62
basi litavaliwa juu ya vazi la Mjumbe, na endapo Halmashauri haina joho basi Mjumbe atavaa vazi la heshima;
(f) Sare za Chama, nguo za jeans, kofia zisizohusiana na Dini hazitaruhusiwa kuvaliwa wakati wa Mikutano ya Halmashauri na vikao vya Kamati za Kudumu za Halmashauri;
(g) Vazi rasmi la Mwenyekiti na Mkurugenzi na Makamu Mwenyekiti litakuwa lenye kuonyesha rangi za Bendera ya Taifa na mazao yanayolimwa kwa wingi katika eneo la Halmashauri kadri Halmashauri itakavyoona inafaa. Hata hivyo, Kanuni hii haitaathiri majoho ambayo yanatumika kabla ya Kanuni hii;
(h) Endapo katika Mkutano huo Halmashauri itajigeuza kuwa Kamati, Wajumbe watavua majoho;
(i) Endapo Baraza litajigeuza kuwa Kamati taratibu za kuendesha Vikao vya Kamati zitatumika na Kikao hicho kitakuwa cha siri.
(2) Madaraka au jukumu lolote la Mwenyekiti kuhusiana na
uendeshaji wa mikutano yanaweza kutekelezwa na mtu
anayeongoza Mkutano huo.
(3) Halmashauri itatenga siku mbili kila wiki kwa ajili ya
Mwenyekiti kufika ofisini na kutekeleza majukumu yafuatayo:-
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
63
Kumbu-
kumbu ya
Mahu-
dhurio
(a) kusikiliza matatizo ya Wananchi;
(b) kupata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi kuhusu uendeshaji wa shughuli za Halmashauri ikiwa ni pamoja na masuala ya manunuzi;
(c) kusaini mikataba mbalimbali ya Halmashauri;
(d) kushughulikia jambo ambalo Mkurugenzi ataona linahitaji kushughulikiwa au kutekelezwa na Mwenyekiti.
11.-(1) Kila Mjumbe anayehudhuria Mkutano wa Halmashauri au
Kamati yoyote ya Halmashauri ambamo yeye ni Mjumbe
hatahudhuria Mkutano huo mpaka awe ameweka saini yake kwenye
Rejesta ya mahudhurio inayotunzwa na Mkurugenzi kwa ajili hiyo.
(2) Isipokuwa siku ya kufanyika kwa Mikutano ya Baraza au
Kamati ambayo Diwani ni Mjumbe au pale atakapoitwa kutekeleza
majukumu ya Serikali, si ruhusa kwa Diwani kuwa katika ofisi za
Halmashauri na kufanya shughuli ambazo hazihusiani na
Halmashauri au Serikali.
Kuruhusu
Watu na
Vyombo
vya
Habari
Kwenye
Mikutano
ya Halma-
shauri
12.-(1) Mikutano ya Halmashauri itakuwa wazi kwa watu wote
pamoja na vyombo vya habari.
(2) Halmashauri itapaswa kuutangazia umma kuhusu muda,
wakati na mahali pa Mkutano na italiweka tangazo hilo mahali
panapo onekana kwa urahisi katika eneo la Halmashauri siku
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
64
zisizopungua tatu (3) kabla ya siku ya Mkutano.
(3) Endapo Mkutano utakaoitishwa ni wa dharura au
umeitishwa chini ya siku tatu (3) zilizotajwa katika Kanuni ya 12(2);
Halmashauri itatangazia umma kupitia matangazo katika mbao za
matangazo na kutumia vipasa sauti.
Utaratibu
wa
Shughuli
za
Mikutano
13.-(1) Isipokuwa kama Halmashauri, kutokana na sababu za
dharura, itaamua kubadili utaratibu wa shughuli za mikutano,
utaratibu wa shughuli katika kila Mkutano wa kawaida wa
Halmashauri utakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Mwenyekiti akiongozwa na Katibu ataingia ukumbini baada
ya mratibu wa vikao kutoa ishara Maalum kuashiria
Mwenyekiti kuingia ukumbini na Wajumbe watasimama na
kukaa kimya mpaka pale Mwenyekiti atakaporuhusu
Wajumbe kukaa;
(b) mkutano utaanza kwa Sala au Dua itakayosomwa na
Mwenyekiti;
(c) baada ya Sala/Dua kusomwa Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Halmashauri watajibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa Wajumbe wa Baraza la madiwani kwa utaratibu na mpangilio kama ilivyooneshwa kwenye Kanuni hizi;
(d) kupokea na kujadili taarifa za kwenye Kata kutoka kwa Madiwani wa Kata husika;
(e) kujadili jambo lolote linalotakiwa kwa mujibu wa Sheria kushughulikiwa kabla ya shughuli nyingine yoyote;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
65
(f) Kupokea taarifa yoyote inayopaswa kupokelewa kisheria kabla ya shughuli nyingine yoyote;
(g) kusoma au kuthibitisha muhtasari wa Mkutano wa kawaida wa Halmashauri uliopita na mikutano yoyote Maalum ya Halmashauri iliyofanyika baada ya Mkutano huo wa kawaida. Hata hivyo iwapo nakala za mihtasari zimesambazwa kwa kila Mjumbe kabla au wakati wa kupeleka taarifa ya kuhudhuria Mkutano, mihtasari hiyo itachukuliwa kuwa imesomwa;
(h) kupokea taarifa yoyote ambayo Mwenyekiti atapenda itolewe kwa Halmashauri;
(i) kujibu maswali kufuatana na Kanuni ya 21 ya Kanuni hizi;
(j) kumalizia shughuli yoyote iliyobaki katika Mkutano wa kawaida uliopita;
(k) kupokea na kufikiria taarifa za Kamati za Halmashauri, kutoka kwa Wenyeviti wa Kamati ambao watahusika kujibu maswali ya Wajumbe kuhusiana na kazi za Kamati husika;
(l) kupokea na kujadili taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri;
(m) kuidhinisha utiaji Lakiri katika Hati;
(n) kufikiria hoja binafsi kufuatana na jinsi zilivyopokelewa; na
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
66
(o) kushughulikia mambo mengine yaliyoonyeshwa katika taarifa ya Mkutano.
(2) Halmashauri inaweza katika Mkutano wowote wa kawaida,
kubadili utaratibu wa hoja za mazungumzo ili kutoa kipaumbele kwa
shughuli yoyote ambayo kwa maoni ya Mwenyekiti ina uharaka wa
pekee, lakini mabadiliko hayo hayatabadilisha mpangilio wa
shughuli zilizotajwa katika aya (a) na (b) za Kanuni ya 13(1) ya
Kanuni hii.
Kuthibiti-
sha
Muhtasari
14.-(1) Katibu ataandika muhtasari wa mazungumzo ya kikao
unaozingatia majina ya Wajumbe waliohudhuria na wasiohudhuria,
jina la mtoa hoja, aliyeunga mkono hoja, mabadiliko ya hoja kwa
ufupi, ushauri uliotolewa na azimio lililofikiwa. Muhtasari huo
utasomwa, kurekebishwa, kuthibitishwa na kusainiwa na
Mwenyekiti wa Mkutano na kutunzwa katika Rejesta Maalum ya
mihtasari.
(2) Mara baada ya kusoma Muhtasari, au kama itachukuliwa
kama umesomwa Mwenyekiti atauliza swali “Je Muhtasari wa
Mkutano wa Halmashauri wa tarehe…………… ya mwezi………….
Mwaka……..utiwe saini kama kumbukumbu sahihi?”
(3) Hakuna hoja au majadiliano yatakayofanywa kuhusiana na
muhtasari isipokuwa kuhusiana na usahihi wa muhtasari, kama
hakuna swali lililoulizwa, basi mara baada ya kuthibitishwa
Mwenyekiti atatia saini katika muhtasari huo.
(4) Muhtasari ambao utakuwa umesainiwa vilivyo na kama
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
67
hakuna ushahidi wa kuwepo kwa makosa utakuwa kumbukumbu
sahihi na Mkutano utahesabika kuwa umeitishwa na kufanyika
vilivyo na Wajumbe waliohudhuria watahesabika kuwa halali.
(5) Mihtasari ya Halmashauri itakuwa wazi kwa Ukaguzi na
Wajumbe na kwa Umma kwa wakati unaofaa na kwa utaratibu
utakaokubaliwa na Halmashauri na kwamba mtu yeyote anaweza
kupewa sehemu ya muhtasari huo kama akiomba na baada ya
kulipa ada kama itakavyoidhinishwa na Halmashauri.
Hoja za
Mwenye-
kiti
15. Hoja zinazowasilishwa na Mwenyekiti hazitazidi hoja tatu,
bila kuathiri haki yake, kama Mjumbe ya kuwasilisha hoja katika
taratibu za kawaida.
Taratibu
za
Majadili-
ano
16.-(1) Isipokuwa kwa idhini ya Halmashauri mtoa hoja
atahutubia Mkutano wa Halmashauri kwa dakika zisizozidi kumi.
Wajumbe wengine ikiwa ni pamoja na mtoa hoja watazungumza
kwa muda usiozidi dakika tano kila mmoja.
(2) Mjumbe anaruhusiwa kuzungumza mara moja katika hoja
yoyote ile isipokuwa hoja inayowasilishwa bila mjadala.
(3) Mtoa hoja atakuwa na haki ya kuzungumza kwa muda usiozidi
dakika tano katika kujibu majadiliano na muda huo utaanza
kuhesabika mara atakapoanza kuchangia au kujibu. Mratibu wa
vikao atatoa ishara Maalum kumjulisha mtoa hoja kuwa muda wake
umeisha na mjadala juu ya hoja hiyo utafungwa. Utaratibu huu wa
kuhesabu muda utatumika pia kwa Mjumbe yeyote atakayepewa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
68
muda wa kuchangia hoja na mara tu baada ya kujibu mjadala juu ya
hoja utafungwa.
(4) Mjumbe yeyote aliyekwishachangia kwenye hoja hawezi
kutoa au kuunga mkono marekebisho, ila marekebisho yakitolewa
na kuungwa mkono, Mjumbe aliyekwishazungumza katika hoja ya
awali anaweza kuzungumza kwenye hoja iliyorekebishwa kwa muda
usiozidi dakika tatu.
(5) Iwapo Wajumbe wawili au zaidi watasimama kwa wakati
mmoja kuzungumza, Mjumbe atakayetamkwa na Mwenyekiti ndiye
atakayepewa nafasi kwanza.
(6) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (5) ya Kanuni hii,
Mwenyekiti atahakikisha kuwa, nafasi ya kuchangia inatolewa kwa
uwiano unaofaa miongoni mwa aina zote za uwakilishi wa Madiwani
walioomba kuchangia hoja hiyo.
(7) Mjumbe anapozungumza ataelekeza mazungumzo yake kwa
Mwenyekiti tu na atapaswa kusimama.
(8) Mjumbe anapozungumza hatakatizwa, isipokuwa kwa suala la
utaratibu, lakini anaweza kutoa nafasi kwa Mjumbe anayetaka
kujieleza.
(9) Mjumbe anaposimama kutoa taarifa kuhusu utaratibu,
Mjumbe anayezungumza ataketi na atabaki ameketi hadi hoja ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
69
utaratibu itakapokuwa imeamuliwa na Mwenyekiti, isipokuwa kama
anasimama kumweleza Mwenyekiti kuhusu suala la utaratibu.
(10) Mwenyekiti ndiye pekee mwenye uamuzi kuhusu utaratibu
katika mikutano ya Halmashauri, na anayo madaraka ya kuzuia fujo
na kuhakikisha kuwa maamuzi yake katika kusimamia usalama
yanatekelezwa mara moja. Wakati wa majadiliano Mwenyekiti
akisimama, Mjumbe anayezungumza au aliyesimama ataketi na
hakuna Mjumbe atakayesimama hadi Mwenyekiti atakapokuwa
ameketi.
(11) Hakuna Mjumbe atakayebaki amesimama wakati Mjumbe
mwingine anaelekeza mazungumzo yake kwa Mwenyekiti.
(12) Mkurugenzi wa Halmashauri atajibu swali lolote
atakaloulizwa na Mwenyekiti kutokana na shughuli zinazoendelea
kwenye Mkutano isipokuwa kama atadai haki ya kukataa kujibu
swali kwa msingi wa kwamba jibu linaweza kumweka hatiani au
kuvunja uaminifu wake au linamhusisha yeye kama mtetezi
mahakamani.
(13) Hakuna mtu kwa niaba yake mwenyewe, au kwa niaba ya
watu wengine walio kwenye ujumbe wa watu, atakayeruhusiwa
kuzungumza katika Mkutano wa Halmashauri isipokuwa kwa idhini
ya Halmashauri iliyotolewa kwa njia ya azimio. Idhini ya namna hiyo
haitatolewa isipokuwa kama mtu huyo au watu hao wanaotaka
kuihutubia Halmashauri watakuwa wamempatia Mkurugenzi au
Afisa aliyeruhusiwa naye, taarifa ya muda usiopungua siku tisa kabla
ya Mkutano wa Halmashauri ambamo wangetaka maombi yao
yafikiriwe kupewa idhini, maombi ya kimaandishi ikieleza jambo
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
70
linalotarajiwa kujadiliwa, na mpaka taarifa ya kupokelewa kwa
maombi hayo itakapokuwa imebandikwa kwenye mbao za
matangazo za Halmashauri.
(14) Hakuna zaidi ya watu wawili watakaokuwa na haki ya
kuhutubia Halmashauri kwa niaba ya uwakilishi; na wala hakuna
ujumbe utakaozidi idadi ya watu watano watakaoruhusiwa.
(15) Kiwango cha juu cha muda wa kuzungumza na Halmashauri
ikiwa ni pomoja na muda wa kusoma risala hakitazidi dakika kumi.
Fujo
zinazosa-
babishwa
na
Wajumbe
17.-(1) Katika Mkutano wowote wa Halmashauri kama Mjumbe
wa Halmashauri ataonyesha kukosa heshima kwa madaraka
aliyonayo Mwenyekiti au kudharau Kanuni za Kudumu za
Halmashauri kwa kuzuia kwa makusudi shughuli za Halmashauri
zisiendelee au vinginevyo, Mwenyekiti ataelekeza Mkutano kuhusu
tukio hilo kwa kumtaja jina mtu anayehusika.
(2) Endapo baada ya kutajwa jina mjumbe ataendelea kudharau
madaraka ya Mwenyekiti basi Mwenyekiti ataliomba Baraza
kuahirisha shughuli za Mkutano na Mwenyekiti atatafakari jambo
hilo na anaweza kuagiza yafuatayo:-
(a) Mjumbe atolewe nje ya Mkutano; au
(b) Mjumbe kuzuiwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo pamoja na
haki za vikao husika.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
71
(c) Bila kuathiri masharti ya kanuni ya 17 (2) (a) na (b), Mjumbe
huyo ataendelea kupokea posho ya mwezi ya Udiwani.
(3) Iwapo kutatokea fujo kubwa katika Mkutano wowote wa
Halmashauri, Mwenyekiti anaweza kama ataona ni muhimu kufanya
hivyo, kuahirisha Mkutano bila majadiliano au swali au kusimamisha
Mkutano kwa muda atakaoona unafaa.
Fujo
zinazosa-
babishwa
na Umma
18.-(1) Iwapo mtu yeyote kati ya umma unaohudhuria Mkutano
wa Halmashauri atavuruga Mkutano wa Halmashauri, Mwenyekiti
atamuonya mtu huyo aache kufanya hivyo na endapo mtu huyo
ataendelea kuvuruga Mkutano, Mwenyekiti ataamuru mtu huyo
atolewe nje ya chumba cha Mkutano.
(2) Endapo kutakuwa na vurugu katika sehemu yoyote ya chumba
cha Mkutano kinachotumika na umma, Mwenyekiti ataamuru
kuondolewa kwa watu wote walio katika eneo hilo.
Hoja na
Marekebi-
sho ya
Hoja
19.-(1) Taarifa ya kila hoja, isipokuwa hoja iliyowasilishwa chini
ya Kanuni za Kudumu ya. 15, itawasilishwa kwa maandishi
yaliyowekwa saini na Diwani au Madiwani waliotoa taarifa, na
itapelekwa kwa Mkurugenzi angalau siku nne kabla ya Mkutano wa
Halmashauri unaofuata na akishaipokea Mkurugenzi atagonga
tarehe na kuipa namba na kuiingiza kwenye daftari kadri hoja
zilivyowasilishwa, na daftari hilo litakuwa wazi kukaguliwa na
Mjumbe yeyote wa Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
72
(2) Mkurugenzi ataonyesha katika taarifa ya kila Mkutano wa
Halmashauri hoja zilizowasilishwa na kwa kadri zilivyopokelewa
isipokuwa kama Diwani aliyetoa hoja hiyo ameeleza kwa maandishi
wakati alipoleta hoja hiyo, kwamba anataka kuitoa katika Mkutano
utakaofanyika baadaye, au baada ya kuwasilisha ameifuta hoja hiyo
kwa maandishi.
(3) Iwapo hoja ambayo imeonyeshwa katika taarifa ya Mkutano
haiwezi kutolewa na Mjumbe aliyewasilisha taarifa; au na Mjumbe
mwingine yeyote kwa niaba yake, basi hoja hiyo isipokuwa kama
imeahirishwa kwa idhini ya Halmashauri, itachukuliwa kama
imeondolewa na haitawasilishwa tena bila ya kutoa taarifa upya.
(4) Iwapo hoja itahusu jambo linalohusu Kamati au Kamati
mbalimbali baada ya kupendekezwa na kuungwa mkono, hoja hiyo
itapelekwa bila majadiliano kwenye Kamati ambayo Halmashauri
itaelekeza ili iweze kufikiriwa na kutayarishiwa taarifa.
(5) Ni lazima kila hoja ihusu jambo ambalo Halmashauri ina
uwezo na wajibu nalo, au iwe inahusu Halmashauri ya Wilaya
husika.
(6) Marekebisho ya hoja yaliyopendekezwa na kuungwa mkono
yanaweza kuondolewa tu kwa ridhaa ya Wajumbe wa Halmashauri
walio wengi waliopo katika Mkutano.
(7) Marekebisho ya hoja yanapokuwa yamethibitishwa, hoja ya
msingi kama ilivyorekebishwa itatolewa na Mwenyekiti kama ndiyo
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
73
hoja ya msingi ambayo nayo inaweza kufanyiwa marekebisho na
kama marekebisho ya hoja hayakukubaliwa, marekebisho mengine
yanaweza kupendekezwa.
(8) Kwa idhini ya Mwenyekiti, zaidi ya rekebisho moja linaweza
kutolewa kwa wakati mmoja mbele ya Mkutano wa Halmashauri,
lakini kila rekebisho la namna hii litatolewa moja baada ya jingine
kufuatana na jinsi mapendekezo hayo yalivyotolewa.
(9) Rekebisho halitachukuliwa kuwa sahihi kama litakuwa sawa
na kuikataa hoja moja kwa moja au kama si rekebisho la hoja ya
msingi linalokusudiwa kurekebishwa.
(10) Rekebisho ambalo halikutolewa taarifa, halitapendekezwa
baada ya mjadala wa hoja inayozungumzwa kuendelea kwa nusu
saa, ila kwa mujibu wa sharti hili, taarifa ya idadi yoyote ya
marekebisho inaweza kutolewa.
(11) Hoja ya kufuta azimio itapitishwa na Wajumbe wasiopungua
theluthi mbili ya Wajumbe wote.
(12) Hoja ya kuzingatia taarifa ya Kamati au kuidhinisha
majadiliano au mapendekezo ya Kamati inaweza kutolewa na
Mwenyekiti wa Kamati husika, au na Mjumbe yeyote wa Kamati
husika kwa niaba yake.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
74
(13) Mjumbe yeyote ambaye hajachangia katika mjadala wa hoja,
au hajaitolea marekebisho, anaweza kupendekeza “kwamba
Halmashauri iendelee na shughuli inayofuata” na hoja ya aina hiyo
inaweza tu kuzingatiwa baada ya hoja kupendekezwa na kuungwa
mkono na endapo hoja inapotolewa itaamuliwa bila marekebisho au
mjadala na kama ikikubaliwa, shughuli iliyokatizwa na azimio hilo
haitaendelea kujadiliwa katika kikao hicho, hoja ya kupendekeza
kuendelea na shughuli inayofuata haitatolewa zaidi ya mara moja
katika mjadala wa jambo lolote.
(14) Baada ya mjadala kuhusu hoja kuendelea kwa muda
usiopungua nusu saa, Mjumbe ambaye hajachangia katika
majadiliano anaweza kuomba idhini ya kutoa hoja “kwamba suala
lililo mbele yetu sasa liamuliwe” na kama idhini hiyo itatolewa kwa
kukubaliwa na si chini ya Wajumbe watano, hoja “kwamba suala
lililo mbele yetu sasa liamuliwe” itawasilishwa mara moja, na kama
ikiafikiwa, mtoa hoja ya msingi anaweza kuzungumza kwa dakika
zisizozidi tano, na baada ya hapo swali au maswali yaliyo mbele ya
Halmashauri yatafanyiwa uamuzi.
(15) Hoja “kwamba suala lililo mbele yetu sasa liamuliwe”
haitatolewa zaidi ya mara moja katika mjadala unaoendelea kuhusu
jambo lolote mpaka hapo mjadala utakapokuwa umeendelea kwa
angalau nusu saa tangu kuwekwa mbele ya Mkutano hoja ya aina
hiyo ilipopendekezwa awali.
Hoja
zinazo-
weza
kutolewa
20. Hoja zifuatazo zinaweza kutolewa bila taarifa:-
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
75
bila
Taarifa (a) kumchagua Mwenyekiti wa Mkutano ambamo hoja
imetolewa;
(b) hoja kuhusu usahihi wa muhtasari, kufunga Mkutano, kuahirisha Mkutano, utaratibu wa Mkutano au suala linalofuata;
(c) kuteua Kamati au Wajumbe wa Kamati, au Wawakilishi katika taasisi za nje, unaotokana na jambo lililotaarifiwa katika wito wa Mkutano;
(d) kukubali taarifa na mapendekezo ya Kamati na maazimio yote yanayotokana na taarifa au mapendekezo hayo;
(e) kwamba idhini itatolewa kuiondoa hoja; (f) kusahihisha hoja; (g) kuongeza muda wa hotuba; (h) kuwa, jambo lililotajwa katika taarifa ya kuitisha Mkutano
litangulie; (i) kusimamisha Kanuni za Kudumu; (j) kwamba Mjumbe asisikilizwe tena au aondoke katika
Mkutano; (k) kumwomba Mjumbe abakie Mkutanoni; na (l) kutoa idhini ya Halmashauri pale ambapo idhini inatakiwa
kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu hizi.
Haki ya
kujibu 21.-(1) Mtoa hoja atakuwa na haki ya kujibu maswali wakati wa
kufunga mjadala juu ya hoja; kabla ya hoja kupigiwa kura au kabla
ya hoja kutolewa “kwamba kikao kiahirishwe.
(2) Mjumbe anayetumia haki yake ya kujibu hataanzisha hoja
nyingine mpya.
(3) Baada ya kutolewa kwa jibu ambalo linahusiana na Kanuni
hizi, uamuzi utafikiwa bila majadiliano zaidi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
76
Maswali 22.-(1) Mjumbe anaweza kumuuliza Mwenyekiti wa Kamati
swali lolote kuhusu muhtasari wa Kamati uliofikishwa mbele ya
Halmashauri.
(2) Kila swali litaulizwa na kujibiwa bila majadiliano.
(3) Swali au maswali yatajibiwa na Mwenyekiti wa Kamati mara
moja na Mjumbe anayeuliza maswali hayo hatanyimwa haki yake ya
kujadili hoja ambayo maswali hayo yanarejewa au kutoa hoja ya
marekebisho.
(4) Pale ambapo swali la maandishi limeelekezwa kwa
Mwenyekiti wa Kamati, na taarifa inayotakiwa imo katika mojawapo
ya mihtasari ya Halmashauri, kuonyesha sehemu ya muhtasari
ambapo habari hiyo imeonyeshwa, kutachukuliwa ni jibu la kutosha.
Maswali
ya papo
kwa papo
23.-(1) Halmashauri itatenga muda wa angalau dakika thelathini
katika kila Mkutano wa Halmashauri wa kawaida ambapo
Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmashauri watajibu maswali ya
papo kwa papo kutoka kwa Wajumbe kabla ya kuanza kwa shughuli
ya kawaida za Mkutano wa Halmashauri.
(2) Wajumbe ambao watataka kumwuliza Mkurugenzi na
Mwenyekiti maswali ya papo kwa papo watatakiwa kujiorodhesha
kwanza kwa Mwenyekiti angalau masaa ishirini na nne (24) kabla ya
Mkutano wa Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
77
(3) Mjumbe yeyote ambaye hatajiorodhesha kwa Mwenyekiti
ndani ya masaa ishirini na nne atahesabika kuwa amechelewa na
hataruhusiwa kumuuliza Mkurugenzi au Mwenyekiti swali la papo
kwa papo.
(4) Kabla ya kuanza kwa kipindi cha maswali ya papo kwa papo
Mwenyekiti atataja majina ya Wajumbe waliojiorodhesha kuuliza
maswali ya papo kwa papo na idadi ya maswali.
(5) Mwenyekiti ataweka utaratibu ambao ataona unafaa na
kuridhiwa na Wajumbe wa namna bora ya kuendesha kipindi cha
maswali ya papo kwa papo.
(6) Mjumbe hataruhusiwa kuuliza zaidi ya swali moja la papo
kwa papo.
(7) Maeneo ya umuhimu ambayo Wajumbe watatakiwa kuuliza
maswali ya papo kwa papo ni:-
(a) uendeshaji wa jumla wa Halmashauri;
(b) utekelezaji wa miradi ya Maendeleo;
(c) mipango ya kimkakati ya Halmashauri kuwaondolea
wananchi umaskini;
(d) mipango ya baadaye ya maendeleo ya Halmashauri;
(e) usimamizi na utekelezaji wa Mipango na Bajeti kwa mwaka
husika;
(f) mtoaji wa huduma za jamii kama vile elimu, afya, maji,
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
78
barabara na madaraja;
(g) hifadhi ya mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji;
(h) usalama wa chakula, raia na mali zao;
(i) utawala bora na utatuzi wa kero za wananchi.
(8) Baada ya kujibiwa kwa swali, muuliza swali atapewa fursa ya
kuuliza swali moja tu la ufafanuzi na maswali yatajibiwa bila
mjadala.
(9) Mwenyekiti atakuwa na uwezo wa kuruhusu au kukataa swali
lolote la papo kwa papo ambalo litaonekana linahitaji takwimu au
utafiti zaidi au swali ambalo linalenga kumdhalilisha Mwenyekiti au
Mjumbe yeyote wa Baraza na uamuzi wake utakuwa wa mwisho.
(10) Mwenyekiti atakuwa na uwezo wa kutojibu swali la papo
kwa papo iwapo swali hilo litaonekana linahitaji takwimu au tafiti
zaidi au litaonekana ni swali la kumdhalilisha Mwenyekiti au
Mjumbe wa Baraza.
(11) Mara baada ya muda wa nusu saa kumalizika, kipindi cha
maswali ya papo kwa papo kitamalizika na kuruhusu shughuli
zingine za kikao kuendelea.
Taarifa za
Kamati 24.-(1) Kila Kamati au Kamati ya pamoja iliyoteuliwa chini ya
Kanuni hizi itatoa, taarifa katika vikao vya Halmashauri, au Kamati
iliyoteua Kamati Ndogo au Kamati ya pamoja taarifa ya majadiliano
yanayohusiana na utekelezaji majukumu iliyokasimiwa, kwa ujulisho
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
79
wa Halmashauri.
(2) Muhtasari wa Kamati unaohitaji idhini ya Halmashauri, na
taarifa zozote zinazohusiana na muhtasari huo, na ambazo
zinaonekana kwa Kamati kuwa zinastahili, zitapelekwa kwa kila
Mjumbe wa Halmashauri angalau siku saba kabla ya Mkutano wa
Halmashauri ambao utafikiriwa.
(3) Mwenyekiti wa Kamati, au Mjumbe mwingine wa Kamati
kwa niaba yake, wakati wa kupendekeza kuidhinishwa kwa
muhtasari wa Kamati, anaweza kusema kuwa hakusudii kuwasilisha
kipengele au vipengele fulani vya muhtasari huo kwa lengo la
kupata idhini ya Halmashauri; katika hali hiyo Mjumbe yeyote
hataweza kukizungumzia kipengele au vipengele hivyo na muhtasari
utawasilishwa bila vipengele hivyo na kuondolewa kwa kipengele
cha aina hiyo kutatolewa taarifa kwenye Mkutano unaofuata.
(4) Taarifa ya Kamati inapokuwa imepokelewa na Halmashauri
itamaanisha kuwa hatua zilizochukuliwa na Kamati husika
zimekubaliwa na mapendekezo yaliyo kwenye taarifa hiyo
yatatekelezwa na kwamba Mkurugenzi atakuwa ameelekezwa
ipasavyo.
Taarifa za
kutoka
kwenye
Kata
25.-(1) Kila Kata itatakiwa kuwasilisha taarifa za utekelezaji
katika Mkutano wa Halmashauri ulioitishwa chini ya Kanuni ya 3(1)
ya Kanuni hizi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
80
(2) Taarifa za utekelezaji kutoka katika Kata zitawasilishwa na
Diwani wa Kata husika, au kama Diwani hayupo taarifa hiyo
itawasilishwa na Diwani wa Viti Maalum anayeishi katika Kata hiyo
na kama Diwani Viti Maalum hayupo, Mwenyekiti atamtaarifu
mapema Diwani yeyote ili ajiandae kuwasilisha taarifa hiyo.
(3) Kutakuwa na aina tatu za taarifa zitakazowasilishwa:-
(a) Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Kata
ambayo itajumuisha ujenzi wa Madarasa, Nyumba za
Walimu, Matundu ya Vyoo, Maabara, Viwanja vya
Michezo, Vituo vya Afya, Zahanati, Madaraja, Barabara,
Mashamba darasa, Ofisi za Vijiji, Mitaa, Kata na Tarafa;
Idadi ya watu na vizazi.
(b) Taarifa zinazohusu hali ya Kata ambazo zitajumuisha:-
(i) Maendeleo ya Elimu katika Kata kuhusiana na
uandikishaji wa watoto wenye umri wa kwenda shule,
ufundishaji, utoro, hali ya mahudhurio, mimba
mashuleni, ukaguzi na uratibu wa shule;
(ii) Hali ya majanga ya kibinadamu kama vile mlipuko wa
magonjwa, mafuriko, njaa na hali ya uhalifu na vifo;
(iii) Maendeleo ya Kilimo, mifugo na uvuvi ambayo
itajumuisha upatikanaji wa wataalmu, zana za kisasa na
pembejeo za kilimo, mifugo na uvuvi;
(iv) Uimarishaji wa dhana ya uzalendo na utaifa kwa
kuhamasisha vijana kuanzisha na kujiunga katika
vikundi vya Vijana Wagani kazi na mafunzo ya Jeshi la
Mgambo, ulinzi shirikishi na Polisi jamii;
(c) Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo na taarifa ya
hali ya Kata sharti ijumuishe pia taarifa za shughuli za
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
81
kiuchumi, taarifa ya mavuno ya mazao ya chakula na biashara
pamoja na taarifa ya utunzaji wa mazingira na vyanzo vya
maji.
(4) Mkurugenzi wa Halmashauri atahakikisha taarifa kutoka
kwenye Kata, zinaandaliwa na kuwasilishwa na Diwani wa Kata hiyo
kwenye Baraza la Madiwani ili ipitiwe na kuchambuliwa kwa nia ya
kupata hoja zitakazowasilishwa katika vikao vya Kamati husika na
kutoa mrejesho.
(5) Mwasilishaji wa taarifa atatakiwa kuelezea mafanikio
yaliyopatikana, changamoto zilizo jitokeza na mbinu za kukabiliana
na changamoto hizo ambazo zitaonesha malengo na muda Maalum
wa kuzitatua.
(6) Taarifa za mapokeo ya fedha na matumizi yake zitakazokuwa
zimeandaliwa na Afisa Mtendaji wa Kata, zitawasilishwa sanjari na
miradi iliyotekelezwa na gharama zake.
(7) Baada ya taarifa kutoka kwenye Kata kupokelewa na
Halmashauri, itamaanisha kuwa taarifa hizo zimeidhinishwa na
mapendekezo yaliyomo kwenye taarifa yatatekelezwa na
Halmashauri na Kata kupewa taarifa ya utekelezaji wa majukumu
hayo.
Uhuru wa
kutoa
Mawazo
wakati
wa
Majadi-
26. Kutakuwepo na uhuru wa kutoa mawazo wakati wa
majadiliano katika Mikutano ya Halmashauri na uhuru huo
hautaweza kuhojiwa katika mahakama yoyote au mahali popote nje
ya Mkutano wa Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
82
liano
Kauli
zenye
Kashfa
27.-(1) Inapotokea, kulingana na maoni ya Mwenyekiti au mtu
yeyote anayeongoza Mkutano, kuwa kauli iliyotolewa na Mjumbe
inakashifu Mtu yeyote, Mwenyekiti atamtaka Mjumbe aliyetoa kauli
hiyo kufuta kauli yake na kumwomba msamaha mtu aliyekashifiwa
kwa maandishi ndani ya muda wa siku saba tangu kauli hiyo ya
kashfa ilipotamkwa.
(2) Endapo Mjumbe aliyetoa kauli za kashfa atakataa kufuta
kauli yake na kuomba msamaha kwa maandishi kama
inavyoelekezwa katika Kanuni Ndogo (1) ya Kanuni hii, Mwenyekiti
au mtu anayeongoza Mkutano, atamsimamisha Mjumbe huyo
kuhudhuria vikao vitatu mfululizo vya Halmashauri.
(3) Mjumbe aliyesimamishwa kwa mujibu wa Kanuni ndogo (2)
ya Kanuni hii atapoteza haki zake zote ikiwa ni pamoja na posho,
nauli, upendeleo na kinga kwa muda wote wa kusimamishwa
kwake.
Maamuzi
ya
Mikutano
ya Halma-
shauri
28.-(1) Masuala yote yaliyojadiliwa na kupendekeza katika
Mkutano wowote wa Halmashauri yataamuliwa kulingana na wingi
wa kura za Wajumbe waliohudhuria Mkutano huo na ikitokea kura
za Wajumbe zikalingana, basi Mwenyekiti au Mjumbe yeyote
mwingine anayeongoza Mkutano atapiga kura ya turufu mbali ya
kura ya kawaida.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
83
(2) Iwapo suala linalopigiwa kura linahusu kutokuwa na imani au
kumwondoa Mwenyekiti madarakani au jambo lolote lingine kama
itakavyoamuliwa na Halmashauri kura zitapigwa kwa siri.
Mwaliko
kwa
wasio-
kuwa
Wajumbe
kushiriki
na
kuzungu-
mza
kwenye
Vikao vya
Halma-
shauri
29.-(1) Mwenyekiti baada ya kushauriana na Wajumbe,
anaweza kumwalika mtu yeyote kuhudhuria na kuzungumzia jambo
lolote au kushiriki kwa njia yoyote katika Mkutano wowote wa
Halmashauri lakini mwalikwa huyo hatakuwa na haki ya kupiga kura
katika Mkutano huo.
(2) Wakuu wa Idara za Halmashauri wanapaswa kuhudhuria
mikutano yote ya Halmashauri lakini hawatakuwa na haki ya kupiga
kura katika Mikutano hiyo.
Mihtasari
ya kata na
vijiji
30. Mkurugenzi wa Halmashauri atahakikisha mihtasari yote ya
Kamati za Maendeleo za Kata, Halmashauri za Vijiji na Mikutano
Mikuu ya Vijiji inapitiwa na kuchambuliwa kwa nia ya kupata hoja
zitakazowasilishwa katika vikao vya Kamati husika na kutoa
mrejesho inavyopaswa.
Mihtasari
ya Halma-
shauri
kupele-
kwa kwa
Mkuu wa
Wilaya na
Mkuu wa
Mkoa
31.-(1) Mihtasari ya Halmashauri itatolewa na kupelekwa kwa
Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa ndani ya muda wa siku 7 baada
ya kuthibitishwa kwa mihutasari hiyo.
(2) Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa wanaweza kupewa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
84
wakiomba nakala ya mihtasari au sehemu ya mihtasari ya Kamati za
Kudumu na Kamati nyingine.
(3) Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa hawatabadilisha au
kubatilisha au kuagiza kubadilisha au kubatilisha uamuzi wa
Halmashauri.
Hoja
kuhusu
Matumizi
32. Hoja yoyote isiyotokana na mapendekezo au taarifa ya
Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango na ambayo, kama ikikubaliwa
itaongeza matumizi au kupunguza mapato yaliyo chini ya usimamizi
wa Kamati yoyote, au itasababisha matumizi ya Kamati ya Kudumu,
baada ya kupendekezwa au kuungwa mkono, itaahirishwa bila
majadiliano mpaka Mkutano wa kawaida wa Halmashauri unaofuata
na Kamati yoyote inayohusika na hoja hiyo itafikiria iwapo
ingependa kutoa taarifa kuhusu athari za kifedha za hoja hiyo.
Kupoke-
lewa kwa
taarifa za
Kamati
33.-(1) Taarifa ya Kamati inapowasilishwa kwenye Halmashauri,
hoja itakuwa “kwamba taarifa ipokelewe”na baada ya kukubaliwa
na Wajumbe taarifa itaanza kujadiliwa kipengele kimoja baada ya
kingine.
(2) Mapendekezo yoyote yaliyomo katika taarifa hiyo yatapigiwa
kura baada ya nyingine iwapo Mjumbe yeyote atapenda iwe hivyo
na baada ya hapo taarifa nzima itawasilishwa mbele ya Mkutano
kwa kupokelewa ikiwa na au bila marekebisho.
Kuidhini-
shwa kwa
taarifa ya
34. Taarifa ya Kamati inapokuwa imepokelewa na Halmashauri
itamaanisha kuwa hatua zilizochukuliwa na Kamati iliyowasilisha
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
85
Kamati taarifa hiyo zimeidhinishwa na mapendekezo yaliyo kwenye taarifa
yatatekelezwa na kwamba Mkurugenzi wa Halmashauri atakuwa
ameelekezwa kama inavyotakiwa.
Uhalali wa
majadiliano
ya Halma-
shauri
35. Uhalali wa majadiliano kwenye Halmashauri hautaathiriwa
na nafasi yoyote wazi ya Mjumbe, dosari zozote zilizo katika
uchaguzi au uteuzi wa Wajumbe wa Kamati au zile za Maafisa wake.
Uwezo wa
Halma-
shauri
kujigeuza
kuwa
Kamati ya
Halma-
shauri
nzima
36. Halmashauri inaweza kujigeuza kuwa Kamati ya Halmashauri
na mara baada ya kujigeuza taratibu za kuendesha vikao vya Kamati
za Kudumu zitatumika.
Hoja
zinazo-
husu
watumi-
shi wa
Halma-
shauri
37. Kama litajitokeza jambo lolote katika Mkutano wa
Halmashauri linalohusu uteuzi, kupandishwa cheo, kufukuzwa kazi,
mishahara au mazingira ya kazi au utendaji kazi kwa jumla wa
Mtumishi yeyote wa Halmashauri jambo hilo litajadiliwa katika
Kamati ya Halmashauri nzima.
Kushiriki
kwa
Umma
38.-(1) Mtu yeyote ambaye ni mkazi katika eneo la Halmashauri
anaweza kuhudhuria Mkutano wa Halmashauri kwa nia ya
kuwasilisha hoja mbele ya Halmashauri baada ya kutoa taarifa kwa
maandishi kwa Mkurugenzi na akakubaliwa kufanya hivyo.
(2) Mtu yeyote ambaye ni mkazi katika eneo la Halmashauri
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
86
anaweza kualikwa kuhudhuria kikao cha Kamati au Kamati Ndogo
kabla uamuzi haujafanyika kuhusu masuala ambayo ana maoni
mahsusi.
Uahiri-
shaji wa
Vikao
39.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Kanuni Ndogo ya (2) ya
Kanuni 17 na Kanuni Ndogo ya 2 ya Kanuni hii, Halmashauri
haitaahirisha Mkutano wake hadi dondoo zote za agenda ya
Mkutano huo zitakapojadiliwa na kutolewa uamuzi.
(2) Pale ambapo katika Mkutano wowote wa Halmashauri akidi
haikutimia, Wajumbe waliopo wataahirisha Mkutano na utaratibu
wa kuitisha Mkutano mwingine utafanyika kwa kuzingatia
maelekezo ya Kanuni hizi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
87
SEHEMU YA IV
KAMATI
Kamati za
Kudumu 40.-(1) Uteuzi wa wajumbe wa Kamati za Kudumu za
Halmashauri utakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Halmashauri katika Mkutano wake wa mwaka itateua
Wajumbe wa Kamati za Kudumu zifuatazo ambazo zitakuwa na idadi
ya Wajumbe kama inavyooneshwa hapo chini na
itakavyorekebishwa na Halmashauri mara kwa mara;
Kamati Idadi ya
Wajumbe
Akidi
(a) Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
13 7
(b) Kamati ya Elimu,Afya na Maji 11 6
(c) Kamati ya Masuala ya Uchumi,
Ujenzi na Mazingira
10 6
(c) Kamati ya Maadili ya Madiwani 5 3
(d) Kamati ya Kudhibiti Ukimwi 5 -
(b) Halmashauri inaweza kuunda Kamati ya Kudumu mpya zaidi
ya Kamati zilizotajwa kwenye Kanuni ya 40(1)(a) hapo juu, baada ya
kupata idhini ya maandishi kutoka kwa Waziri;
(c) Maombi ya Halmashauri ya kuanzisha Kamati mpya ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
88
Kudumu lazima yakidhi na yawe na maelezo yafuatayo:-
(i) upekee wa majukumu yanayoombewa kuundwa kwa Kamati
ya Kudumu mpya na majukumu hayo yawe hayawezi
kutekelezwa na Kamati za Kudumu zilizopo na zilizotajwa
kwenye Kanuni ya 40(1) hapo juu;
(ii) gharama za uendeshaji wa Kamati hiyo kwa mwaka;
(iii) kuundwa kwa Kamati ya Kudumu hiyo mpya ni hitajio la
lazima na ni kipaumbele cha Halmashauri na jamii kwa
ujumla.
(2) Kila Mjumbe wa Halmashauri atakuwa mjumbe wa angalau
Kamati moja ya Kudumu. Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
itakuwa na Wajumbe wafuatao:-
(a) mwenyekiti wa Halmashauri ambaye atakuwa Mwenyekiti;
(b) makamu Mwenyekiti;
(c) mbunge au Wabunge wanaowakilisha jimbo au majimbo ya
Uchaguzi katika eneo la Halmashauri;
(d) wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Halmashauri;
(e) wajumbe wengine wasiozidi wawili (2) watakaopendekezwa
na Mwenyekiti na kupigiwa kura na Baraza la Halmashauri
mmoja kati yao awe Mwanamke.
(3) Halmashauri yenye Madiwani wasiozidi ishirini (20), Idadi ya
wajumbe wa Kamati wa Fedha itakuwa kama ilivyoonyeshwa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
89
kwenye Kanuni ya 40(2).
(4) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (2) ya Kanuni hii,
Halmashauri yenye idadi ya Madiwani wanaozidi ishirini (20) na
wasiozidi thelathini na tano (35) Wajumbe wa Kamati ya Fedha
watakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya 40(2) pamoja na
wajumbe wengine wawili (2) watakaotokana na orodha
itakayopendekezwa na Mwenyekiti na kupigiwa kura na Baraza la
Halmashauri mmoja kati yao awe mwanamke.
(5) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (2)(3) na (4) ya
Kanuni hii, Halmashauri yenye idadi ya Madiwani wanaozidi
thelathini na tano(35) na zaidi Wajumbe wa Kamati ya Fedha
watakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya 40(2) pamoja na
wajumbe wengine wanne(4) watakaotokana na orodha
itakayopendekezwa na Mwenyekiti na kupigiwa kura na Baraza la
Halmashauri wawili kati yao wawe wanawake.
(6) Wajumbe wa Kamati za Kudumu watashika nyadhifa zao kwa
muda wa mwaka mmoja na wataendelea kushika nyadhifa hizo
mpaka mkutano wa mwaka wa Halmashauri unaofuata, isipokuwa
wajumbe waliochaguliwa kwenye mkutano wa kwanza baada ya
Uchaguzi Mkuu watashika nyadhifa zao kwa muda uliobaki kumaliza
Mwaka wa Fedha ambapo Uchaguzi utafanyika tena.
(7) Halmashauri inaweza wakati wowote kuvunja na kuunda
upya Kamati ya Kudumu iliyoteuliwa kwa mujibu wa Kanuni hii ya
Kudumu, endapo kufanya hivyo kutakuwa ni kwa manufaa ya
Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
90
Mwenye-
kiti wa
Halma-
shauri
kuwa
Mjumbe
wa
Kamati
zote
41. Mwenyekiti wa Halmashauri atakuwa Mjumbe wa Kamati
zote za Kudumu za Halmashauri.
Uwezo wa
Kamati
42. Kamati zote za Halmashauri zitawasilisha taarifa zao kwa
Halmashauri na hakuna hatua itakayochukuliwa kutekeleza uamuzi
wowote wa Kamati yoyote mpaka hapo taarifa ya Kamati husika
itakapokuwa imewasilishwa na kukubaliwa na Halmashauri,
isipokuwa pale ambapo idhini ya kuchukua hatua imekasimiwa kwa
Kamati.
Kamati za
Pamoja 43.-(1) Halmashauri inaweza kukubaliana na Halmashauri
nyingine kuteua Kamati ya pamoja kutokana na Wajumbe wao kwa
madhumuni yoyote yale ambayo wana maslahi ya pamoja na
Halmashauri hizo zinaweza kukasimu kwa Kamati hiyo ya pamoja,
kutegemea na masharti na mipaka zitakazoweka kama
watakavyoona inafaa, madaraka au kazi ya Halmashauri
zinazohusiana na madhumuni yaliyozifanya ziunde Kamati hiyo,
isipokuwa shughuli zile ambazo Halmashauri haziruhusiwi kukasimu.
(2) Muundo, muda wa kufanya kazi wa Wajumbe na mipaka ya
eneo ambamo Kamati hiyo ya pamoja itafanya kazi itapangwa na
Halmashauri zinazoiteua.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
91
(3) Kamati ya pamoja haitaingia katika gharama zozote zaidi ya
zile ambazo zimeidhishwa na mamlaka iliyoteua Kamati hiyo.
Kukasimu
Madaraka
kwenye
Kamati
44.-(1) Kufuatana na Kanuni Ndogo ya (2) ya Kanuni hii pamoja
na masharti mengine ambayo Halmashauri itaona inafaa,
Halmashauri inaweza kukasimu kwa Kamati uwezo wa kutekeleza
kazi yoyote kwa niaba yake.
(2) Halmashauri haitakasimu kwa Kamati yoyote uwezo wa:-
(a) kutunga Sheria Ndogo;
(b) kuweka na kutoza kodi;
(c) kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Halmashauri;
(d) kutoza ada na ushuru;
(e) kuidhinisha mpango na bajeti ya Halmashauri;
(f) kuingia mikataba mbalimbali ikiwa ni pamoja na mikataba ya kukopa;
(g) kupitisha mpango wa utoaji huduma.
(3) Kazi za kila Kamati ya Kudumu ya Halmashauri ni kama
zilivyoonyeshwa katika jedwali la Kanuni za Kudumu hizi.
(4) Halmashauri inaweza kusitisha au kurekebisha uamuzi wa
kukasimu madaraka yoyote kwa Kamati, lakini usitishaji au
urekebishaji huo hautaathiri jambo lolote lililofanywa kutokana na
uamuzi wowote uliochukuliwa kihalali na Kamati.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
92
(5) Shughuli yoyote iliyotekelezwa na Kamati kutokana na
kukasimiwa kwa mujibu wa Kanuni hii itatambuliwa kuwa
imefanywa au kutekelezwa na Halmashauri.
Kamati
Ndogo 45.-(1) Kamati yoyote au Kamati ya pamoja inaweza kuteua
Kamati Ndogo kutokana na Wajumbe wake kadri itakavyoona inafaa
kwa ajili ya kuchunguza na kutoa taarifa kuhusu jambo lolote, lakini
Kamati haitakasimu madaraka yake ya kiutendaji kwa Kamati Ndogo
yoyote.
(2) Idadi ya Wajumbe wa Kamati Ndogo pamoja na muda
watakaotumikia vitaamuliwa na Kamati iliyoteua Kamati Ndogo
hiyo.
(3) Mwenyekiti wa Kamati atakuwa Mjumbe wa Kamati Ndogo
yoyote kwa mujibu wa wadhifa wake isipokuwa kama
atamfahamisha Mkurugenzi kwa maandishi kuwa hatakuwa
Mjumbe wa Kamati hiyo.
(4) Kila Kamati Ndogo inaweza kumteua mmoja wa Wajumbe
wake kuwa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo husika.
Mikutano
ya Kamati 46.-(1) Mkutano wa kwanza wa Kamati utaitishwa na
Mkurugenzi ndani ya mwezi mmoja baada ya Kamati kuteuliwa na
baada ya hapo kulingana na ratiba ya mikutano kama
itakavyoidhinishwa na Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
93
(2) Taarifa ya angalau saa ishirini na nne yenye ajenda za kikao
itabidi kutolewa kwa Wajumbe kabla ya Mkutano wa Kamati.
(3) Idadi ya Kamati haitazidi idadi ambayo itawekwa na Waziri
kutokana na uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 75(3) cha Sheria.
Mwenye-
kiti wa
Kamati
47.-(1) Katika kikao chake cha kwanza baada ya Mkutano wa
mwaka wa Halmashauri na kabla ya kuendelea na shughuli yoyote
nyingine, kila Kamati itamchagua Mwenyekiti wa Kamati kwa
mwaka unaohusika.
(2) Mwenyekiti wa Kamati, isipokuwa Kamati ya Fedha Utawala
na Mipango, atachaguliwa kwa kura ya siri ya Wajumbe walio wengi
kwa kupiga kura ya siri kwenye eneo la faragha litakalotengwa na
Mkurugenzi kwa ajili hiyo.
(3) Mwenyekiti wa Halmashauri atakuwa pia Mwenyekiti wa
Kamati ya Fedha na Utawala.
(4) Endapo nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati itakuwa wazi katika
kipindi cha mwaka husika, Mkurugenzi atatoa taarifa kwa Wajumbe
wote wa Kamati kuwa katika kikao kijacho cha kawaida cha Kamati
husika dondoo ya kumchagua Mwenyekiti wa Kamati kwa kipindi
cha mwaka kilichosalia itakuwa ya kwanza katika agenda.
Mkutano 48.-(1) Mkutano Maalum wa Kamati utaitishwa baada ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
94
Maalum
wa
Kamati
theluthi mbili ya Wajumbe wa Kamati kuomba kwa maandishi kuwa
Mkutano huo ufanyike na kueleza sababu.
(2) Taarifa ya Mkutano Maalum wa Kamati itaonyesha shughuli
itakayofanyika katika Mkutano Maalum huo na hakuna jambo
jingine lolote litakalojadiliwa katika Mkutano huo.
Ajenda za
Kamati 49. Mjumbe wa Kamati atakuwa na haki ya kuwasilisha hoja
zake na kuwekwa katika ajenda ya Kamati kama atatoa taarifa ya
angalau siku nne (4) kabla ya tarehe ya kikao.
Mahudhu-
rio katika
mikutano
ya Kamati
50.-(1) Mjumbe wa Kamati ya Kudumu au Kamati Ndogo,
ambaye ameshindwa kuhudhuria Mkutano wa Kamati Ndogo,
hataruhusiwa kutuma mtu mwingine kumwakilisha kwenye
Mkutano wa Kamati au Kamati Ndogo.
(2) Mjumbe wa Halmashauri hatakuwa na haki ya kuhudhuria
kikao chochote cha Kamati au Kamati Ndogo ambamo yeye si
Mjumbe, isipokuwa kama Kamati au Kamati Ndogo inayohusika
imemwalika kuhudhuria na hata hivyo hatakuwa na haki ya kupiga
kura au kudai posho kwa kuhudhuria Mkutano huo wa Kamati au
Kamati Ndogo.
Mtoa hoja
kualikwa
kwenye
51. Mjumbe wa Halmashauri anayewasilisha hoja ambayo
imepelekwa kwenye Kamati atapewa taarifa ya Mkutano wa Kamati
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
95
Mkutano
wa
Kamati
ambamo hoja yake imepagwa kuzungumzwa na kama atahudhuria
atapewa nafasi ya kuizungumzia.
Waalikwa
wasio-
kuwa
Wajumbe
kuhu-
dhuria na
kushiriki
katika
Mikutano
ya Kamati
52. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu au Kamati ya pamoja au
Kamati Ndogo baada ya kushauriana na Wajumbe wa Kamati ya
Kudumu, au Kamati ya pamoja au Kamati Ndogo, anaweza
kumwalika mtu yeyote kuhudhuria na kuzungumza kwenye
Mkutano kuhusu suala lolote au kushiriki kwa namna yoyote
kwenye kikao cha Kamati, lakini mtu huyo atakayealikwa hatakuwa
na haki ya kupiga kura kwenye Mkutano huo.
Mahu-
dhurio ya
umma na
Vyombo
vya
Habari
kwenye
Mikutano
ya Kamati
na Kamati
Ndogo
53. Majadiliano katika Kamati ya Kudumu au Kamati ya pamoja
au Kamati Ndogo hayatakuwa wazi kwa umma na vyombo vya
habari.
Athari za
nafasi
wazi
54.-(1) Kunapotokea nafasi wazi kwenye Kamati ya Kudumu au
Kamati ya pamoja au Kamati Ndogo, Kamati itaendelea kutekeleza
shughuli zake licha ya kuwepo kwa nafasi wazi hiyo au hizo au
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
96
kwenye
Kamati mpaka nafasi hiyo au hizo zitakapojazwa, kwa njia ya uchaguzi au
uteuzi na Mjumbe atakayejaza nafasi hiyo atashika nafasi hiyo kwa
kipindi kilichosalia cha Mjumbe ambaye nafasi yake imekuwa wazi.
(2) Uhalali wa tendo lolote au maamuzi ya Mkutano wowote wa
Kamati hautaathiriwa kutokana na hitilafu katika uteuzi wa Mjumbe
aliyeshika nafasi hiyo kuachwa wazi na Mjumbe au Wajumbe au
Mjumbe au Wajumbe kuamua kutoka kwenye kikao kwa lengo la
kukwamisha jambo linalotaka kutolewa maamuzi na Kamati hiyo.
Akidi
kwenye
Mikutano
ya Kamati
55. Endapo Wajumbe waliohudhuria Mkutano hawatafikia akidi
ya Mkutano, Mkurugenzi atauahirisha Mkutano huo na kuuitisha
tena ndani ya siku saba (7) na endapo akidi haitatimia tena, idadi
yoyote ya Wajumbe waliohudhuria itatengeneza akidi ya Mkutano
ambapo Mkutano huo utaendelea na utakuwa halali na Mkurugenzi
atamjulisha Waziri kuwepo kwa hali hiyo.
Kanuni za
Kudumu
katika
Mikutano
ya Kamati
56.-(1) Kanuni ya 16 ya Kanuni hizi za Kudumu itatumika, baada
ya kufanya marekebisho yanayostahili, kwenye mikutano ya Kamati
za Halmashauri.
(2) Mjumbe anapozungumza katika Mkutano wa Kamati
atakuwa ameketi na anaweza kuzungumza zaidi ya mara mbili juu ya
jambo linalojadiliwa.
Upigaji
kura
kwenye
Mikutano
57. Masuala yote yanayoletwa mbele ya Kamati yataamuliwa kwa
wingi wa kura za Wajumbe waliohudhuria na endapo kunatokea
kura mlingano mtu anayeongoza kikao hicho atakuwa na kura ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
97
ya Kamati turufu.
Mihtasari
ya Kamati 58.-(1) Muhtasari wa kila Kamati ya Kudumu au Kamati ya pamoja
au Kamati Ndogo, utajumuisha majina ya Wajumbe waliohudhuria
na wasiohudhuria, na utasainiwa kwenye Mkutano unaofuata na
mtu aliyeongoza Mkutano na muhtasari uliosainiwa utapokelewa
kama ushahidi bila uthibitisho zaidi endapo hautakuwa na makosa.
(2) Hakuna hoja au mjadala utakaoendeshwa kuhusiana na
muhtasari wa Kamati isipokuwa kuhusu usahihi wa suala lolote
linalohusu usahihi litatolewa kwa hoja.
Kufikir-
iwa Upya
Maamuzi
59. Pale ambapo suala lililowasilishwa limeamuliwa kwa mujibu
wa Kanuni ya 55, suala hilo halitaanza kujadiliwa upya katika
Mkutano huo wa Kamati isipokuwa kama hoja hiyo inaungwa
mkono na theluthi mbili ya Wajumbe waliohudhuria na kupiga kura.
Kutunza
siri za
majadili-
ano ya
Kamati na
Kamati
Ndogo
60. Mjumbe wa Kamati ya Kudumu au Kamati Ndogo hatatoa
nje jambo lolote lililoletwa au kuzungumzwa kwenye Kamati bila
ruhusa ya Kamati hiyo, au kuzungumza kwenye Kamati Ndogo
mpaka hapo Kamati hiyo au Kamati Ndogo hiyo itakapokuwa imetoa
taarifa kwenye Halmashauri au itakapokuwa imekamilisha
utekelezaji wa jambo hilo.
Kujiuzulu
wadhifa
wa
Mwenye-
kiti wa
61. Mwenyekiti wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifa wake kwa
kutoa taarifa ya maandishi aliyoisaini na kutuma kwa Mkurugenzi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
98
Kamati
Kujiuzulu
ujumbe
wa
Kamati na
kujazwa
kwa nafasi
iliyowazi
62.-(1) Mjumbe yeyote wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifa
wake kwa kutoa taarifa ya maandishi aliyoisaini na kuituma kwa
Mkurugenzi.
(2) Nafasi inayotokana na kujiuzulu kwa Mjumbe itajazwa na
Halmashauri katika kikao chake cha kawaida baada ya tarehe ya
kujiuzulu kwa Mjumbe.
SEHEMU YA V
UNUNUZI WA VIFAA, UPATIKANAJI WA HUDUMA NA UJENZI
Taratibu
za uagizaji
Sura ya
290
63.-(1) Uagizaji wa mali, huduma na ujenzi katika Halmashauri
utazingatia Kanuni za Manunuzi zilizotungwa chini ya kifungu cha 68
cha Sheria za Fedha za Serikali za Mitaa, Sura ya 290 na Sheria ya
Manunuzi ya mwaka 2011 au kwa kadri ya Sheria hizo
zitakavyorekebishwa.
(2) Kutakuwepo na Bodi ya Zabuni ambayo imeanzishwa kwa
mujibu wa Kanuni za Bodi ya Zabuni (Uanzishwaji na Mwenendo) za
Serikali za Mitaa na ambayo itasimamia shughuli zote za uagizaji
katika Halmashauri.
(3) Muhtasari wa Bodi ya Zabuni utapaswa kuwasilishwa
kwenye kikao kifuatacho cha Halmashauri baada ya muhtasari huo
kujadiliwa na kupitishwa kwanza na Kamati ya Fedha, Utawala na
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
99
Mipango.
Kumbu-
kumbu za
majadiliano
yanayo-
husu
uagizaji
64. Bodi ya zabuni ya Halmashauri itaweka kumbukumbu ya
majadiliano yanayohusu taratibu za ununuzi zikiwa na angalau
taarifa zifuatazo:-
(a) maelezo mafupi kuhusu vitu, ujenzi au huduma zinazotarajiwa kutolewa na haja iliyosababisha Bodi kuitisha zabuni;
(b) majina na anuani za Wazabuni waliowasilisha zabuni, maelezo kuhusu sifa au ukosefu wa sifa za Wazabuni waliowasilisha zabuni zao;
(c) bei au msingi wa upangaji wa bei na muhtasari wa masharti mengine muhimu ya kila zabuni na ya kila mkataba wa uagizaji wa mali, huduma na ujenzi;
(d) muhtasari wa tathmini na mlinganisho wa zabuni pamoja na upendeleo uliokuwepo katika tathmini hiyo;
(e) kama zabuni zilikataliwa tamko kuhusu uamuzi huo na sababu za uamuzi huo;
(f) kama utaratibu mwingine wa kupata vitu au huduma mbalimbali ya utaratibu wa zabuni ndio uliotumika, basi tamko kuhusu sababu zilizoifanya Bodi iamue kutumia utaratibu huo mwingine;
(g) kama zabuni ilikataliwa kwa kuwa mzabuni alitoa, alikubali kutoa moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja, kwa Mtumishi wa sasa au wa zamani wa Halmashauri, bakshishi ya aina yoyote, ahadi ya kumwajiri au kitu chochote kinachohusiana na ajira au chenye thamani, kama hamasisho kwa utendaji au uamuzi au utaratibu wa kutumia, tamko kuhusu jambo hilo;
(h) katika upataji wa huduma, sababu na hali iliyoifanya Bodi kuchagua utaratibu wa kutumia katika upataji huo wa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
100
huduma;
(i) katika upataji wa vitu au huduma ambao Bodi imeamua kudhibiti ushiriki kwa misingi ya Taifa, Mkoa au Wilaya, tamko kuhusu sababu na hali iliyofanya Bodi kudhibiti ushiriki huo;
(j) katika upataji wa vifaa na huduma kwa kuwaomba watoaji kutoa mapendekezo yao moja kwa moja tamko la sababu na hali iliyofanya Bodi kuamua kutumia utaratibu huo; na
(k) muhtasari wa maombi yoyote ya ufafanuzi kuhusu mchujo wa zabuni au nyaraka za zabuni na majibu yaliyotolewa pamoja na muhtasari wa marekebisho yoyote yaliyofanywa katika nyaraka hizo.
(2) Sehemu ya kumbukumbu zilizotajwa kwenye Kanuni Ndogo
ya (1) (a) na (b) ya Kanuni hii zitatolewa, kama zikiombwa, kwa mtu
yeyote baada ya zabuni kutangazwa, kufunguliwa na kukubaliwa au
baada ya kusimamishwa kwa taratibu za uagizaji bila ya kuingia
katika mkataba wa uagizaji.
(3) Sehemu ya kumbukumbu zilizoelekezwa katika Kanuni
Ndogo ya (1) (c) hadi (g) ya Kanuni hii kama itaombwa, itatolewa
kwa Wazabuni waliowasilisha zabuni baada ya zabuni kukubaliwa au
baada ya kusitishwa bila ya kuingia kwenye mkataba wa utoaji wa
vitu au huduma.
(4) Isipokuwa kama itaelekezwa hivyo na mahakama yenye
mamlaka na kutegemeana na masharti ya maelekezo hayo, Bodi
haitatoa habari:-
(a) ikiwa utoaji huo wa habari utakuwa kinyume cha Sheria, utazuia utekelezaji wa Sheria, hautakuwa na maslahi kwa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
101
umma, utahatarisha maslahi halali ya kibiashara ya wahusika au utazuia ushindani halali; na
(b) habari zinazohusu uchambuzi, tathmini na ulinganisho wa zabuni pamoja na bei mbali ya muhtasari ulioelezwa kwenye Kanuni Ndogo ya (1) (e) ya Kanuni hii.
(5) Mara baada ya zabuni kujadiliwa na Bodi, Katibu atamjulisha
Mzabuni aliyefanikiwa ili makubaliano ya nyaraka za mkataba
yaweze kufikiwa.
(6) Nakala za muhtasari zitapelekwa kwa siri kwa kila Mjumbe
wa Bodi, Mkurugenzi, Mweka Hazina, Mkaguzi wa Ndani na Mkuu
wa Idara husika kwa taarifa na kumbukumbu.
(7) Kila Mzabuni ambaye hakufanikiwa atajulishwa na akiomba
sababu za kutokubaliwa kwa zabuni yake atapaswa kupewa sababu.
(8) Bodi ya Zabuni kwa kuzingatia masharti ya Kanuni za uagizaji
itaandaa taarifa ya mwenendo na maamuzi ya zabuni zilizoitishwa
na kuwasilishwa kwenye Mkutano wa kawaida wa Halmashauri
kupitia Kamati ya Kudumu husika.
Uzuiaji wa
Rushwa 65. Katika mkataba wowote wa kimaandishi, yatawekwa
maneno ambayo yataonyesha kuwa Halmashauri itakuwa na haki
kusitisha mkataba na kumdai Mkandarasi malipo ya fidia kutokana
na kusimamishwa kwa mkataba huo endapo Mkandarasi atabainika
kuwa ameahidi kutoa au ametoa, au amekubali kutoa kwa mtu
yeyote zawadi yoyote au upendeleo wa aina yoyote kama
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
102
kishawishi au zawadi kwa kufanya au kumpendelea au kutomkubali
mtu yeyote kuhusiana na mkataba na Halmashauri au kama vitendo
hivyo vitakuwa vimefanywa na Mtumishi yeyote aliyeajiriwa naye au
kwa niaba yake iwe Mkandarasi anafahamu au hafahamu atakuwa
ametenda kosa chini ya Sheria ya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa ya
mwaka 2007.
Usima-
mizi wa
Mikataba
66.-(1) Mkurugenzi wa Halmashauri atawajibika katika
usimamiaji na ufuatiliaji mzuri wa Mikataba.
(2) Mkataba wa upataji vitu hautabadilishwa kwa namna yoyote
ile baada ya kutiwa saini na pande zinazohusika isipokuwa kama
mabadiliko hayo ni:-
(a) kwa faida ya Halmashauri na hayailetei hasara Halmashauri;
(b) yamethibitishwa na Bodi ya zabuni ya Halmashauri; na
(c) upande mwingine unaafiki.
(3) Malipo ya mwisho hayatafanywa mpaka mkataba mzima
utakapokuwa umekamilika kutokana na kuridhika kwa Halmashauri
na kulingana na vipengele vya mkataba unaohusika.
(4) Malipo ya fedha za salio hayatalipwa mpaka upite muda wa
miezi sita na kazi iwe haina kasoro.
Uvunjaji
wa 67. Pale ambapo mkataba uliotiwa lakiri/muhuri na Halmashauri
haukufuatwa na Mkandarasi, ikiwa ni pamoja na ucheleweshaji
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
103
Mkataba usiokuwa wa kimsingi, Mkurugenzi atashauriana mapema
iwezekanavyo na Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango kwa
kuzingatia taratibu zilizowekwa kwenye mkataba, itaamua hatua
muafaka za kuchukua na kumfahamisha Mkandarasi juu ya uamuzi.
Rejesta ya
Mikataba 68.-(1) Mkurugenzi atatunza maelezo yote ya mikataba kwenye
rejesta ya mikataba na atafanya ulinganifu wa malipo halisi na yale
yaliyoidhinishwa.
(2) Taarifa ya matumizi yote ya ziada lazima yapelekwe kwenye
Bodi ya Zabuni yakiambatana na maelezo kutoka kwa Mkurugenzi.
Diwani/
au Afisa
kutokuwa
na
maslahi
katika
Mikataba
69.-(1) Endapo Diwani au Afisa wa Halmashauri ana maslahi ya
kifedha ya moja kwa moja au vinginevyo katika mkataba wowote,
mkataba unaopendekezwa au jambo lolote na yupo kwenye
Mkutano wa Halmashauri au Kamati ambapo mkataba huo au
mkataba unaopendekezwa au jambo lingine lolote linajadiliwa,
atatangaza jambo hilo mara Mkutano utakapokuwa umeanza na
hatashiriki wala kuwepo katika majadiliano au kupiga kura kuhusu
jambo linalohusu mkataba au mkataba unaopendekezwa au jambo
lingine lolote ambalo ana maslahi nalo.
(2) Kanuni hii haitatumika kuhusiana na maslahi katika mkataba
au suala lingine ambalo Mjumbe au Afisa wa Halmashauri ana
maslahi nalo kama mlipa kodi au mkazi katika eneo lililo katika
himaya ya Halmashauri.
(3) Diwani atahesabika kuwa na maslahi ya moja kwa moja katika
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
104
mkataba au jambo jingine endapo:-
(a) yeye au Mtu aliyemchagua ni Mjumbe wa Kampuni au chombo kingine au anayo hati ya hisa katika Kampuni ambayo itaingia au imependekezwa iingie katika mkataba au anao uhusiano wa kifedha katika jambo linalojadiliwa; au
(b) yeye ni mbia au ameajiriwa na Mtu ambaye mkataba unafanywa naye au utakuwa chini yake au anao uhusiano wa kifedha wa moja kwa moja katika suala linalojadiliwa au kuzungumzwa.
(4) Katika Kanuni hii maslahi ya moja kwa moja na yasiyo ya
moja kwa moja ya mwanandoa au ndugu wa familia kama
inafahamika kwa Mjumbe wa Halmashauri itachukuliwa kuwa ni
maslahi ya moja kwa moja au yasiyo ya moja kwa moja.
(5) Taarifa ya jumla itakayotolewa kwa Mkurugenzi na Diwani au
Afisa wa Halmashauri kuhusiana na yeye, mkewe, mumewe au
ndugu yake kwamba ana maslahi ya moja kwa moja au yasiyo ya
moja kwa moja katika mkataba unaokusudiwa au jambo lingine na
akieleza aina ya maslahi itachukuliwa, isipokuwa pale atakapoondoa
taarifa hiyo, kuwa ametoa taarifa ya kutosha ya maslahi yake
kuhusiana na suala ambalo limo katika mjadala.
(6) Mkurugezi ataandika taarifa za watu wenye maslahi waliotoa
taarifa chini ya Kanuni Ndogo ya (1) na taarifa yoyote iliyomo katika
Kanuni Ndogo ya (5) itakuwa wazi kwa ukaguzi wakati wa saa za
kazi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
105
(7) Halmashauri inaweza baada ya kupata kibali cha Waziri,
kuondoa kizuizi chini ya Kanuni hii kinachoifanya ishindwe wakati
wowote kufanya Mkutano pale ambapo idadi ya Wajumbe wenye
maslahi ni kubwa mno kiasi cha kukwamisha shughuli za
Halmashauri au itakuwa ni kwa maslahi ya wakazi wa Halmashauri
kuondoa kikwazo hicho.
(8) Katika Kanuni za Kudumu hizi, ndugu wa familia itachukuliwa
kuwa ni pamoja na baba, mama, mtoto, kaka, au dada na wanandoa
wao.
SEHEMU YA VI
MASUALA MENGINE
Kiapo na
kukubali
Wadhifa
70. Kila Diwani kabla ya kushika wadhifa wake kama Diwani na
kabla ya Mkutano wa kwanza wa Halmashauri:-
(a) atakula kiapo kama kilivyoonyeshwa kwenye nyongeza ya kwanza ya Kanuni hizi za Kudumu kitakachosimamiwa na Hakimu Mkazi, Hakimu wa Wilaya au Kamishna wa Viapo; na
(b) atatoa tamko la kimaandishi lililoandikwa kwa Mkurugenzi akiahidi kutekeleza jambo linalohusiana na tamko la maslahi katika shughuli za kibiashara, mali na kadhalika na kuzifuata Kanuni za Maadili ya Madiwani.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
106
Majukumu
ya Diwani 71.-(1) Diwani atakuwa na majukumu yafuatayo:-
(a) kuwa karibu na wapiga kura na kupata ushauri wa Wananchi katika mambo yanayotarajiwa kujadiliwa kwenye Halmashauri;
(b) kutoa maoni na mapendekezo ya wananchi kwa Halmashauri;
(c) kuhudhuria mikutano ya Halmashauri na ya Kamati au Kamati Ndogo ambamo yeye ni Mjumbe;
(d) kutenga angalau siku moja kila mwezi kukutana na wananchi katika eneo lake la uchaguzi;
(e) kutoa taarifa kwa wapiga kura kuhusu maamuzi ya jumla ya Halmashauri na hatua zilizochukuliwa na Halmashauri kuondoa matatizo yaliyowahi kuelezwa na wakazi wa eneo lake la uchaguzi;
(f) kuchangia ujuzi na uzoefu wake katika majadiliano yanayofanyika katika mikutano ya Halmashauri na Kamati za Halmashauri; na
(g) kushiriki katika shughuli za pamoja za maendeleo katika eneo lake la uchaguzi na katika eneo zima la Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
107
(2) Katika kutekeleza wajibu wake Diwani atazingatia:-
(a) Maslahi ya Taifa na maslahi ya Wananchi katika eneo la Halmashauri;
(b) Katiba, Sheria na Kanuni;
(c) Kanuni za Maadili ya Madiwani, Mwongozo juu ya mahusiano ya Madiwani na Watumishi na miiko mingine.
Nafasi
Wazi 72.-(1) Kiti cha Mjumbe wa Halmashauri kitakuwa wazi endapo
Mjumbe:-
(a) amefariki;
(b) anakubali ajira kama Mtumishi wa Halmashauri;
(c) kwa mujibu wa Sheria yoyote anatangazwa kuwa hana
akili timamu;
(d) yuko chini ya hukumu ya kifo au kifungo kinachozidi miezi
sita kilichotolewa kwake na mahakama;
(e) kwa mujibu wa Sheria yoyote anatamkwa kuwa anapoteza
sifa za kuendelea kuwa Mjumbe;
(f) atakoma kuwa mwanachama wa chama cha siasa
kilichompendekeza kuwa mgombea wa kiti cha udiwani;
(g) anapokuwa amepatikana na kosa kutokana na Kanuni za
Maadili ya Madiwani na adhabu ya kosa alilotenda ni
pamoja na kumwondoa Mjumbe madarakani; na
(h) anapoteza ujumbe kwa mujibu wa Kanuni ya 71 (2) ya
Kanuni hizi za Kudumu;
(i) anahukumiwa kwa kosa la kutotaja maslahi yake;
(j) amejiuzulu kutoka kiti chake;
(k) Halmashauri imevunjwa na kuathiri mipaka ya majimbo ya
uchaguzi;
(l) uchaguzi wa Mjumbe umetangazwa kuwa batili;au
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
108
(m) bila sababu ya kuridhisha au bila idhini au kibali cha
maandishi cha Mwenyekiti, Mjumbe anakosa kuhudhuria
mikutano mitatu ya kawaida inayofuatana ya Halmashauri
au Kamati ambamo yeye ni Mjumbe.
(2) Waziri atatangaza kiti kuwa wazi pale atakapojulishwa na
Mwenyekiti wa Halmashauri kwa maandishi kwamba kiti kiko wazi
kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 42(1) cha Sheria ya Serikali
za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287.
Kutoku-
wepo kwa
Wajumbe
73.-(1) Halmashauri yaweza kutoa idhini ya kutokuwepo katika
mikutano yake kwa muda usiozidi miezi kumi kwa Mjumbe yeyote
anayetaka kwenda nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(2) Pale ambapo Mjumbe kwa sababu yoyote ile amekuwa nje ya
nchi kwa muda unaozidi miezi kumi kiti chake cha udiwani
kitachukuliwa kuwa kipo wazi.
Taratibu
za
kutunga
Sheria
Ndogo
74.-(1) Pale ambapo Halmashauri inakusudia kutunga Sheria
Ndogo itatoa tangazo kwa wakazi wa eneo husika kuhusu kusudio
hilo katika namna ambayo itahakikisha kuwa watakaoathirika na
Sheria Ndogo inayokusudiwa kutungwa wanafahamu vilivyo na
kuwaomba wanaopenda kutoa pingamizi lolote au mapendekezo
yao kwa maandishi katika muda uliowekwa.
(2) Pale ambapo baada ya muda wa taarifa kumalizika hakuna
pingamizi au malalamiko yaliyowasilishwa, au hakuna mtu yeyote
aliyetoa pingamizi linalokubalika mbele ya Halmashauri,
Halmashauri itaendelea kutunga Sheria Ndogo ikizingatia
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
109
malalamiko na pingamizi zilizotolewa.
(3) Sheria Ndogo zikishatungwa na Halmashauri zitapelekwa
kwa Mkuu wa Mkoa ambamo Halmashauri husika imo ili aweze
kuzitolea maoni yake na kisha kuziwasilisha kwa Waziri.
(4) Waziri anaweza kuidhinisha, kukubali au kukataa kuidhinisha
Sheria Ndogo au kutoa au kusimamisha kibali chake kwa kutoa
masharti atakayoyaeleza na anaweza baada ya kutoa idhini yake,
kupanga tarehe ya kuanza kutumika kwa Sheria Ndogo hizo.
(5) Waziri anaweza kabla ya kuidhinisha Sheria Ndogo zenye
athari kwenye maeneo yaliyotengwa au maeneo Maalum au kwa
Sheria nyingine yoyote, kushauriana na Waziri anayehusika na
Sheria husika au na jambo lililotungiwa Sheria Ndogo kadri
itakavyokuwa.
(6) Sheria Ndogo yoyote iliyotungwa na Halmashauri lazima
itangazwe katika Gazeti la Serikali kabla ya kuanza kutumika.
Ukaguzi
wa
Nyaraka
75.-(1) Mjumbe ataweza kwa madhumuni ya kutekeleza wajibu
wake kama Mjumbe na si vinginevyo, kukagua waraka wowote
ambao umejadiliwa na Kamati ya Halmashauri na kama nakala
zinapatikana, anaweza kupewa akiomba nakala kwa madhumuni
hayo hayo.
(2) Mjumbe hatakagua kwa makusudi au kutaka apewe nakala
ya waraka wowote unaohusu jambo ambalo yeye ana maslahi nalo
kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya),
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
110
Sura ya 287. Hata hivyo Kanuni hii haitamzuia Mkurugenzi kuzuia
kukaguliwa kwa waraka wowote ambao umezuiliwa kutolewa kwa
mujibu wa Sheria yoyote au Kanuni zilizotungwa chini ya Sheria
hizo.
Uanzishaji
wa Bodi
za
Huduma
76.-(1) Halmashauri inaweza kwa mujibu wa kifungu 88 cha
Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura ya 287 kwa
madhumuni ya kutekeleza kazi zake katika eneo lililo chini ya
mamlaka yake kuunda Bodi za Huduma kwa hati rasmi
iliyotangazwa kwenye Gazeti la Serikali kama itakavyoona inafaa
kufanya hivyo.
(2) Bodi ya Huduma iliyotajwa katika Kanuni Ndogo ya (1) ya
Kanuni hizi itawajibika moja kwa moja kwenye Halmashauri kupitia
Kamati ya Kudumu husika na itatekeleza kazi zake kama
ilivyofafanuliwa katika hati inayoianzisha.
Diwani
kutembelea
maeneo,
shughuli
mbalimbali
za ujenzi
n.k
77.-(1) Mjumbe wa Halmashauri anaweza kutembelea eneo,
jengo au shughuli za ujenzi zinazotekelezwa na au kwa niaba ya
Halmashauri na anaweza kutuma taarifa kwa Mkurugenzi akieleza
sababu za matembezi yake ili aweze kupangiwa Wataalam wa mradi
au shughuli husika kwa ajili ya kupata maelekezo ya kitaalam.
(2) Mjumbe wa Halmashauri anapotembelea shughuli au miradi
ya maendeleo inayotekelezwa na/au kwa niaba ya Halmashauri
hataruhusiwa kutoa maelekezo au maagizo ya kitaalam awapo
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
111
kwenye eneo la mradi.
(3) Baada ya Diwani kutembelea maeneo au majengo kama
ilivyoainishwa kwenye Kanuni Ndogo ya (1) ya Kanuni hii anaona
kuna umuhimu wa kutoa maoni au mang’amuzi yake juu ya
matembezi hayo atafanya hivyo kwa kuwasilisha maoni au
mang’amuzi yake kwa Mkurugenzi ambaye atafanyia kazi au
kuyapeleka kwa Afisa anayesimamia kazi husika kwa utekelezaji.
(4) Endapo maoni au mang’amuzi ya Diwani hayawezi kufanyiwa
kazi na Mkurugenzi au Afisa mhusika, basi atamshauri Diwani
kupeleka maoni au mang’amuzi yake kwa Kamati inayohusika ili
yachunguzwe zaidi na kuamuliwa.
(5) Kamati za Kudumu za Halmashauri zinaweza kutembelea
miradi ya maendeleo au shughuli yoyote inayotekelezwa na/au kwa
niaba ya Halmashauri na ambayo inaihusu Kamati husika, na katika
kutembelea miradi hiyo Kamati itaongozana na Wataalam wa mradi
au shughuli husika ili kupata maelekezo ya kitaalam.
(6) Kamati ya Kudumu itatembelea miradi au shughuli za
maendeleo kabla ya kikao cha Kamati ambacho kitajadili mradi au
shughuli hiyo.
Uhifadhi
wa lakiri
ya Halma-
shauri
78. Lakiri ya Halmashauri itatunzwa kwa usalama na kufungiwa
katika kasiki kwenye Ofisi ya Mkurugenzi mwenyewe.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
112
Utiaji
muhuri
kwenye
Nyaraka
79.-(1) Lakiri ya Halmashauri haitabandikwa katika hati yoyote
mpaka ubandikaji huo umeidhinishwa na azimio la Halmashauri
likiidhinisha kukubaliwa kwa zabuni, ununuzi, uuzaji au upangishaji
au kuchukua mali yoyote, utoaji wa hati yoyote ya ukopeshaji fedha,
uwasilishaji wa madai yoyote, uwekaji wa viwango vya kodi, uingiaji
kwenye mkataba, kutunga Sheria Ndogo au hati yoyote iliyo rasmi
ambayo kwa mujibu wa Sheria au Kanuni yoyote inahitaji kuwekwa
Lakiri ya Halmashauri.
(2) Lakiri itashuhudiwa au kuthibitishwa na Mwenyekiti au
Makamu Mwenyekiti na Mkurugenzi na hati zilizowekwa lakiri
zitasainiwa na Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti kama hali
itakavyokuwa.
Uandiki-
shaji wa
anuani
80.-(1) Itakuwa wajibu wa kila Mjumbe katika kikao cha kwanza
cha Halmashauri baada ya uchaguzi kutoa taarifa ya maandishi kwa
Mkurugenzi juu ya anuani yake ya Kudumu ya kupokelea taarifa,
hivyo taarifa zilizopelekwa kwa kutumia anuani iliyoandikishwa
itachukuliwa kama ndiyo sahihi na inatosheleza kwa matumizi yote.
(2) Iwapo Mjumbe atatoa taarifa ya maandishi kwa Mkurugenzi
kuwa angependa taarifa ya mikutano ya Halmashauri iwe inatumwa
kwake kwa kutumia anuani atakayoitaja kwenye taarifa hiyo
ambayo ni tofauti na ile katika Kanuni Ndogo ya (1), taarifa yoyote
itakayoachwa au itakayotumwa kwa njia ya posta kwa kutumia
anwani hiyo itachukuliwa kuwa inatosha kwa ajili ya kutoa taarifa
inayotakiwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu hizi.
Uteuzi wa
Wajumbe
kwenye
81.-(1) Katika Mkutano wake wa kwanza Halmashauri itateua
wawakilishi wake kwenye Bodi na Taasisi za nje ambazo
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
113
Taasisi za
nje Halmashauri inastahili kuwakilishwa.
(2) Mjumbe au Wajumbe wanaoiwakilisha Halmashauri kwenye
Bodi na Taasisi za nje, watatakiwa kuwasilisha kwa Mkurugenzi
taarifa kuhusu shughuli za Bodi au Taasisi zinazogusa sera na
maslahi ya Halmashauri na wakazi wake kijumla na Mkurugenzi
atachukua hatua zifaazo.
Kumwo-
ndoa
Mwenye-
kiti
madara-
kani
82.-(1) Halmashauri inaweza kumwondoa Mwenyekiti
madarakani kwa azimio linaloungwa mkono na theluthi mbili ya
Wajumbe kutokana na sababu yoyote kati ya sababu zifuatazo:-
(a) kutumia nafasi yake vibaya; (b) kushiriki katika vitendo vya rushwa; (c) kushindwa kutekeleza majukumu yake; (d) mwenendo mbaya au ukosefu wa adabu; au (e) ulemavu wa kimwili au kiakili kwa kiasi cha kumfanya
kushindwa kutekeleza majukumu yake kama Mwenyekiti.
(2) Hoja au sababu zitakazotolewa lazima iwe imetimiza
masharti yafuatayo:-
(i) iwe na tuhuma mahsusi yenye ushahidi wa kutosha;
(ii) iwe imetolewa maelezo kamili na yenye kueleweka kuhusu
tuhuma zinazohusika.
(3) Kwa madhumuni ya kumwondoa Mwenyekiti madarakani,
kwa sababu zozote zilizotamkwa chini ya Kanuni Ndogo ya (1) ya
Kanuni hii, Halmashauri itatumia taratibu zilizotolewa katika
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
114
Taratibu za Kumwondoa Mwenyekiti zilizotangazwa na Waziri
kwenye Gazeti la Serikali kwa mujibu wa Sheria.
SEHEMU YA VII
POSHO KWA WAJUMBE
Aina za
Posho 83.-(1) Wajumbe wa Halmashauri watalipwa posho mbalimbali
kama itakavyopendekezwa na Halmashauri na kuidhinishwa na
Waziri.
(2) Posho zitakazolipwa kwa Wajumbe wa Halmashauri zitakuwa
za aina zifuatazo:-
(a) posho ya usafiri;
(b) posho ya kuhudhuria kikao;
(c) posho ya madaraka;
(d) posho ya kujikimu;
(e) posho ya mwezi; na
(f) kiinua mgongo.
(3) Endapo Mjumbe wa Halmashauri ataugua au ataumia wakati
akifanya kazi aliyotumwa na Halmashauri, gharama za matibabu
yake zitalipwa na Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
115
Posho
endapo
Mkutano
umehairi-
shwa
84. Endapo Mkutano wa Halmashauri au Kamati utaahirishwa
kwa sababu ya kukosekana kwa akidi, Mjumbe au Wajumbe
waliofika kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano huo ulioahirishwa
watastahili malipo yaliyotajwa katika Kanuni ya 83(2) (a) na (d)
iwapo wamelazimika bila kukusudia, kulala njiani au kwenye makao
makuu ya Halmashauri, hakuna malipo ya posho ya kuhudhuria
kikao yatakayofanywa katika hali ya namna hiyo.
SEHEMU YA VIII
MABADILIKO KWENYE KANUNI ZA KUDUMU
Kusitisha
utumiaji
wa
Kanuni za
Kudumu
85.-(1) Kanuni yoyote inaweza kusitishwa kwa azimio lililoungwa
mkono na theluthi mbili za Wajumbe waliohudhuria Mkutano wa
Halmashauri kwa hoja iliyopendekezwa bila taarifa kwa madhumuni
ya kuwezesha shughuli yoyote iliyofafanuliwa ili ishughulikiwe na
Halmashauri kama jambo la dharura au lenye manufaa.
(2) Halmashauri haitasitisha matumizi ya Kanuni yoyote kama
kusitisha huko kutasababisha kufanya jambo ambalo limezuiliwa na
Sheria au kutofanya jambo linalotakiwa kufanywa kwa mujibu wa
Sheria yoyote.
Marekebi-
sho na
mabadi-
liko ya
Kanuni za
Kudumu
86. Halmashauri inaweza kubadilisha, kuongeza, kurekebisha au
kutengua Kanuni hizi za Kudumu kwa azimio lililoungwa mkono kwa
wingi usiopungua theluthi mbili ya kura na baada ya kupata idhini ya
Waziri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
116
Kanuni za
Kudumu
kutolewa
kwa
Wajumbe
87. Mkurugenzi atatoa nakala iliyochapishwa ya Kanuni za
Kudumu hizi kwa kila Mjumbe.
Kutafsiri
Kanuni za
Kudumu
88. Uamuzi wa Mwenyekiti kuhusu maana ya matumizi ya
Kanuni hizi au mwenendo wa Mkutano wa Halmashauri
hautapingwa wakati wa Mkutano wowote wa Halmashauri.
SEHEMU YA IX
ZIARA ZA WAJUMBE
Ziara za
Wajumbe 89.-(1) Wajumbe wa Halmashauri wanaweza kwenda ziara
mbalimbali za mafunzo ili mradi ziara hizo ziwe zimeainishwa
kwenye mpango na bajeti ya Halmashauri, isipokuwa kwa ziara
ambazo gharama zake hazihusiani na bajeti ya Halmashauri,
Wajumbe watafanya ziara hizo kwa mujibu wa ratiba ya mpango
huo.
(2) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (1) ya Kanuni hizi
Halmashauri kabla ya kuruhusu kufanyika kwa ziara itahaikikisha
kwamba:-
(a) shughuli ya ziara hiyo inafanana na shughuli zinazofanywa
na Halmashauri;
(b) ziara hiyo itafanyika baada ya kupata kibali cha Mkuu wa
Mkoa;
(c) wajumbe wanakitu cha kwenda kuonyesha kule
wanakokwenda kujifunza;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
117
(d) ziara zinazofanyika nje ya Mkoa zihusishe wadau
mbalimbali wa Halmashauri kutegemeana na maudhui ya
ziara husika;
(e) ziara inatarajiwa kuwa na matokeo yanayoonekana;
(f) Wajumbe walioshiriki kwenye ziara warejeapo wanatakiwa
kuandaa na kuwasilisha taarifa ya maandishi kwa
Halmashauri kuhusu mambo mapya na ya msingi
waliyojifunza na kuweka utaratibu mzuri wa kuyatekeleza
kwenye Kata zao na kwenye Halmashauri;
(g) ziara zitafanywa kwa kuzingatia walengwa na mahitaji kama
itakavyokubalika na Halmashauri.
Wimbo/
Dua na
sala ya
kuiombea
Halma-
shauri
90. Kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Halmashauri utaimbwa
wimbo wa Taifa na kufuatiwa na Dua au Sala ya kuiombea
Halmashauri ifuatayo;
“Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba wa Mbingu
na Dunia umeweka katika Dunia Serikali za Wanadamu ili haki
yako itendeke. Twakuomba, uibariki Halmashauri yetu ya
Wilaya ya Masasi idumishe uhuru, umoja, haki na amani.
Uwajalie viongozi wetu wa Halmashauri hekima, afya njema na
maisha marefu ili pamoja na wanaowashauri wadumishe
utawala bora. Utuongezee hekima na busara sisi Madiwani wa
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na utupe uwezo wa kujadili
kwa dhati, mambo yatakayoletwa mbele yetu leo, ili tufanye
maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi wa
Halmashauri yetu. Mungu Ibariki Tanzania AMINA”
Tangazo
la Serikali
Namba .....
.............
91. Kanuni hizi zinafuta Kanuni za kudumu za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za mwaka 2004.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
118
JEDWALI
Chini ya Kanuni ya 42(3)
HADIDU ZA REJEA ZA KAMATI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI ZA
WILAYA
Madhumuni ya jumla:
1. Kuishauri Halmashauri kutengeneza malengo yanayozingatia matakwa ya Wilaya na kuchukua hatua ambazo zitaonekana zinafaa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
2. Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya sera muhimu. 3. Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya utoaji wa
huduma kulingana na rasilimali walizo nazo. 4. Kuiwezesha Halmashauri kutengeneza taratibu
zitakazoongoza utendaji wa Kamati, Kamati Ndogo, na ule wa watumishi ili watimize wajibu wao.
5. Kufanya mapitio yatakayowezesha Halmashauri kuamua juu ya kuongeza, kupunguza, kubinafsisha au kuwashirikisha wadau katika utoaji wa huduma.
6. Kuhakikisha kuwa miundo na taratibu za utendaji wa Halmashauri zinazingatia ufanisi, uthabiti na tija katika kufikia malengo ya Halmashauri.
7. Kuiwezesha Halmashauri kujenga mahusiano imara kati yake na Serikali kuu, Serikali zingine za Mitaa na Umma kwa ujumla.
A. Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango:
Majukumu ya jumla:
Kamati hii inawashirikisha wenyeviti wa Kamati zote za Kudumu
na inapaswa kukutana kila mwezi mara moja. Aidha, madaraka
ya Kamati hii ni kama ya Kamati zingine za Kudumu na hivyo
hairuhusiwi kisheria kufanya kazi/majukumu ya Kamati zingine za
Kudumu.
Kwa ujumla, majukumu yake ni pamoja na kusimamia na
kudhibiti ukusanyaji wa mapato na matumizi ya mali ya
Halmashauri kwa kupitia vikao vyake.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
119
Majukumu Maalum ya Kamati:
1. kuweka mikakati na kupendekeza uongezaji wa mapato.
2. kuwasilisha mapendekezo ya Bajeti na mpango wa
Maendeleo kwenye Halmashauri ili kuidhinishwa na
Halmashauri.
3. kusimamia utunzaji wa hesabu za fedha ikiwa ni pamoja na
uhakiki wa mali za Halmashauri, ukusanyaji wa mapato,
kufuta madeni, na kuomba vibali Maalum kwa matumizi
yanayohitaji kibali cha Waziri mwenye dhamana ya Serikali
za Mitaa.
4. kufikiria na, pale inapowezekana, kupendekeza kwenye
Halmashauri masuala yanayohusu Sheria Ndogo na
utendaji katika ngazi za chini za Halmashauri.
5. kupokea na kuzingatia mapendekezo ya kubadili matumizi
ya mafungu ya fedha (re-allocation) yaliyopo katika
makisio yaliyoidhinishwa na kuyapeleka kwa Halmashauri.
6. kuratibu mapendekezo kutoka kwenye Kamati zingine
kuhusu matumizi ya kawaida na miradi na kuyawasilisha
kwenye Halmashauri.
7. kufikiria na kupendekeza kwenye Halmashauri mikopo
yote ya Halmashauri.
8. kutoa mapendekezo ya vitega uchumi kwa madhumuni ya
kuongeza mapato kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za
Serikali za Mitaa, Sura ya 290.
9. kupokea na kujadili taarifa za wakaguzi wa fedha na mali
ya Halmashauri na kupendekeza hatua za kuchukuliwa
kutokana na maelekezo na maoni ya wakaguzi kwa mujibu
wa Sheria za Serikali za Mitaa, Sura ya 290.
10. kusimamia na kudhibiti matumizi ya fedha za Halmashauri,
kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na Waziri na taratibu
nyingine zitakazowekwa na Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
120
11. kupitia marekebisho yote yaliyopendekezwa hususan
kuhusu taratibu za fedha, ikiwa ni pamoja na mapitio ya
mara kwa mara yanayohusu thamani ya fedha ambapo
Kanuni mbalimbali za manunuzi ya mali na vifaa hutumika.
12. kufikiria na kupendekeza mabadiliko ya viwango vya kodi,
ada na ushuru mbalimbali, vinavyotolewa na Halmashauri.
13. kufikiria mapendekezo ya Bajeti na Mipango ya
Maendeleo ya kila Kamati ya Kudumu na kuiwasilisha
kwenye Halmashauri ili kupata idhini.
14. kushughulikia tofauti ya mapato na matumizi katika bajeti
yote na kupendekeza hatua stahiki ya kuchukua kuondoa
mapungufu katika mapato au ziada matumizi.
15. kufikiria mapendekezo yote yanayohusu matumizi
makubwa ya fedha kabla hayajawasilishwa kwenye
Halmashauri ili kupata idhini.
16. kupokea mahesabu ya mwaka ya Halmashauri na
kuhakikisha taarifa ya mahesabu ya mwaka inawasilishwa
kwa wakati kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali.
17. kupitia na kuidhinisha mpango wa manunuzi wa
Halmashauri kwa kuzingatia mpango wa Bajeti
uliopitishwa na Halmashauri.
18. kupitia taarifa ya kila robo mwaka kuhusu Manunuzi
iliyowasilishwa na Afisa Masuuli.
19. kusimamia utekelezaji wa mikataba ya Halmashauri kwa
kukagua miradi inayotekelezwa na vifaa vilivyopokelewa.
20. kumwelekeza Mkurugenzi kufanya manunuzi au ukaguzi
wa huduma au vifaa vilivyonunuliwa ili kupata thamani
halisi, itafanyika hivyo endapo itadhihirika kwamba,
maelezo yaliyotolewa kuhusu manunuzi ya vifaa au
huduma hayaridhishi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
121
21. kuidhinisha majina ya wajumbe wa Bodi ya zabuni na wa
Bodi zingine kwa mujibu wa Sheria husika.
22. kushughulikia orodha ya wadaiwa wote
itakayokayowasilishwa kwenye Kamati na kutoa
mapendekezo ya hatua za kuchukua.
23. kupendekeza njia na taratibu za kuondosha vifaa chakavu.
Uondoshaji wa vifaa unaweza kufanyika kwa njia ya kuuza
au kuviharibu.
24. kujadili na kupitia taarifa za fedha za kila mwezi na kila
robo mwaka.
25. kupendekeza kwa Halmashauri hatua za kuchukua kuhusu
kufuta madeni ya Halmashauri.
26. kushughulikia Sera kuhusu kukopa na uwekezaji.
27. kujadili na kupendekeza mabadiliko ya viwango vya kodi,
ada na ushuru mbalimbali vinavyotozwa na Halmashauri.
28. kubuni na kupendekeza mpango wa kuanzisha na
kuendeleza uhusiano na Halmashauri nyingine.
29. kurekebisha na kusimamia makusanyo na matumizi ya
mapato ya vijiji na miji midogo kwa mujibu wa Sheria, Sura
ya 287.
30. kuteua wakaguzi wa fedha/mali za Serikali za Vijiji kwa
mujibu wa Sheria, Sura ya 290.
31. kujadili na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa
kuhusu mambo yote ya yanayohusu masuala ya ajira na
kinidhamu ya wafanyakazi na watumishi.
32. kujadili na kutoa mapendekezo kuhusu masuala
yanayohusu nyumba za Halmashauri.
33. kupokea na kutoa uamuzi juu ya mapendekezo ya
watumishi wanaokwenda masomoni.
34. kujadili na kupendekeza masuala yote yanayohusu maslahi
ya jumla ya watumishi, ikiwa ni pamoja na mikopo,
nyumba, usafiri, matibabu, rambirambi na motisha
nyinginezo.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
122
35. kupitisha mapendekezo ya kuthibitisha watumishi kazini
baada ya kumaliza kipindi cha majaribio kulingana na
miundo husika ya utumishi.
36. kupendekeza Sheria Ndogo zinazohusu Kamati hii.
B: Kamati ya Elimu, Afya na Maji:
Majukumu ya Jumla.
Kushughulikia mambo yote yanayohusu afya ya jamii, elimu
na huduma za maji. Kamati hii pia itashughulikia mambo
yanayohusiana na jitihada za wanannchi vijijini kujiletea
maendeleo yao kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwa ni
pamoja na kushauri, kushawishi, kuzindua, kuelimisha na
kushirikisha wananchi hao hasa katika kutayarisha,
kutekeleza, kusimamia na kutathmini mipango yao ya
maendeleo.
Majukumu Maalum ya Kamati:
1. kuandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya upanuzi na
ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati.
2. kuandaa mipago ya maendeleo ya upanuzi na ujenzi wa
shule za awali na msingi na elimu ya watu wazima kwa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
123
mujibu wa Sheria ya Elimu ya 1978 kama ilivyorekebishwa
mwaka 1995.
3. kupendekeza mipango ya ujenzi au upanuzi wa
vituo,viwanja, majengo na mazingira ya burudani,
starehe, mapumziko na michezo.
4. kuamua juu ya mambo yanayohusu uhifadhi wa mambo ya
kale na mandhari mbalimbali zenye sura nzuri.
5. kuandaa na kuratibu njia bora juu ya uhifadhi wa nyaraka
muhimu kwa ajili ya kumbukumbu hizo zitahifadhiwa kwa
mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa Sura ya 287.
6. kupendekeza njia bora juu ya uhifadhi wa sanaa
mbalimbali za ufundi na za maonyesho kwa mujibu wa
Sheria ya Serikali za Mitaa Sura ya 287.
7. kupendekeza matumizi mazuri ya lugha ya taifa.
8. kupendekeza namna ya malezi ya vijana ili waweze kuwa
wazalishaji katika Taifa.
9. kupendekeza namna ya malezi ya vijana ili waweze kuwa
wazalishaji katika Taifa.
10. kusimamia uanzishaji wa uendelezaji wa vikundi vya jamii
na vya hiari vya wananchi katika Halmashauri kwa mujibu
wa sera wa maendelo ya jamii.
11. kusimamia na kuhakiki maeneo ya misitu, mapori, na
mbuga zilizotengwa kama hifadhi ya mamlaka ya Serikali
za Mitaa.
12. kupendekeza na kufanya tathmini ya uendelezaji wa
mabonde, mito na mabwawa.
13. kubuni na kupendekeza namna ya kidhibiti moto.
14. kubuni na kupendekeza mikakati ya utumiaji wa nishati
mbadala, kuzuia ukataji miti ovyo, na kuhimiza upandaji
miti kwa wingi.
15. kuhakikisha kwamba ukaguzi wa majengo unafanyika mara
kwa mara.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
124
16. kupendekeza mipango madhubuti ya ujenzi wa barabara
vijijini na wilayani kwa ujumla.
17. kupendekeza Sheria Ndogo zinazohusu Kamati hizi.
C: Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira:
Majukumu ya jumla
Kamati hii itashughulikia masuala ya uzalishaji mali ikiwemo
kilimo, mifugo, viwanda, madini, Biashara n.k. Aidha
itashughulikia pia miundombinu na suala zima la mendeleo ya
Ardhi na hifadhi ya mazingira.
Majukumu Maalum ya Kamati;
1. kupendekeza kwa Halmashauri mipango ya kupanua
biashara na jinsi ya kukusanya mapato yatokanayo na
upanuzi huo.
2. kupendekeza mipango ya matumizi ya ardhi katika eneo la
Halmashauri.
3. kusimamia matumizi ya Sheria ya nguvu kazi.
4. kuandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya upanuzi wa
kilimo katika Halmashauri
5. kusimamia na kuhakiki miradi ya ujenzi wa masoko,
minada,majosho na vituo vya mifugo.
6. kushughulikia uanzishaji na uendelezaji wa vyama vya
ushirika kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika,
D: Kamati ya Kudumu ya Kudhibiti Ukimwi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
125
Majukumu ya Kamati:
1. kushirikisha wadau tofauti katika maeneo husika ili
kuongeza uchangiaji wa mawazo na/au nyenzo,
usimamizi, uratibu na utekelezaji wa kazi za Tume za
kudhibiti UKIMWI;
2. kusimamia uundaji wa Kamati zote za kudhibiti UKIMWI;
3. kupendekeza na kuchambua hali ya UKIMWI/Mipango na
utekelezaji wake na kufikisha katika ngazi husuka kwa
hatua zaidi;
4. kutathmini hali ya UKIMWI katika eneo lake kuhusu;
(a) idadi ya waathirika: wagonjwa, yatima, wajane,
(b) kasi ya maambukizo
(c) mazingira Maalum yanayochangia maambukizo;
(d) uelewa wa wananchi juu ya janga hili.
5. Serikali haitatoa fedha kwa Halmashauri isiyokuwa na
mipango madhubuti ya kudhibiti UKIMWI.
6. kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kila mtoto
aliyefikia umri wa kwenda shule anafanya hivyo,
7. kuweka mikakati ya makusudi juu ya njia bora za
kuchangia baadhi ya huduma za Elimu na Afya.
8. kubuni na kupendekeza njia bora za kuzuia na kudhibiti
magonjwa ya milipuko.
9. kupendekeza Sheria Ndogo za Kamati hii.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
126
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
127
FAHARASA – HALMASHAURI YA WILAYA
Kanuni Na. Kifungu cha Sheria
A
Ajenda za Kamati
Akidi katika mikutano ya Halmashauri
Akidi kwenye mikutano ya Kamati
Athari za nafasi wazi kwenye Kamati
B
C
D
Diwani au Afisa kutokuwa na maslahi
katika mikataba
Diwani kutembelea maeneo, shughuli
mbalimbali za ujenzi.
Dua ya kuiombea Halmashauri
E.
F
Fujo zinazosababishwa na umma
49
8
55
54
69
77
90
Sura ya 287 kif.64
Sura ya 287 kif.84(2) na (3)
Sura ya 287 kif.84(1);84(3)
Sura ya 287 kif.71
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
128
Fujo zinazosababishwa na Wajumbe
18
17
G
H
Haki ya kujibu
Hoja kuhusu matumizi
Hoja na marekebisho ya hoja
Hoja za Mwenyekiti
Hoja zinazohusu watumishi wa
Halmashauri
Hoja zinazoweza kutolewa bila taarifa
I
J
K
Kamati Ndogo
Kamati za Kudumu
Kamati za pamoja
Kanuni za Kudumu kutumika katika
21
32
19
15
37
20
45
40
43
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
129
mikutano ya Kamati
Kanuni za Kudumu kutolewa kwa
Wajumbe
Kauli zenye kashfa
Kiapo na kukubali wadhifa
Kuidhinishwa kwa Taarifa ya Kamati
Kufikiriwa upya maamuzi
Kufutwa kwa Kanuni zilizopo
Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwa
kwa nafasi iliyoachwa wazi.
Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa
Kamati
Kukasimu madaraka kwenye Kamati
Kumbukumbu ya mahudhurio.
Kumwondoa Mwenyekiti madarakani
Kupokelewa kwa taarifa za Kamati
Kuruhusu watu na vyombo vya Habari
kwenye mikutano ya Halmashauri
56
87
27
70
34
59
91
62
61
44
11
82
33
Sura ya 287 kif.79
Sura ya
287 kif.36(5); GN 263/95
Sura ya 287 kif.67(1)
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
130
12
Kushiriki kwa Umma
Kusitisha utumiaji wa Kanuni za Kudumu.
Kutafsiri Kanuni za Kudumu
Kuthibitisha muhtasari
Kutokuwepo kwa Wajumbe
Kutunza siri za Majadiliano ya Kamati na
Kamati Ndogo.
L
M
Maamuzi ya mikutano ya Halmashauri
Mahudhurio katika mikutano ya Kamati
Mahudhurio ya Umma na vyombo vya
habari kwenye mikutano ya Kamati/Kamati
Ndogo
Majukumu ya Diwani
Marekebisho na mabadiliko ya Kanuni za
Kudumu
Maswali
Maswali ya papo kwa papo
38
85
88
14
73
60
28
50
53
Sura ya 287 kif.114(1)(b)
Sura ya 287 kif.41(2)na (3)
Sura ya 287 kif.86 na 67(2)
Sura ya 287 kif.66
Sura ya 287 vif.86; 67 (2)
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
131
Mihtasari ya za Kata na vijiji.
Mihtasari ya Halmashauri kupelekwa kwa
Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa.
Muhtasari wa Kamati
Mikutano ya kawaida ya Halmashauri
Mikutano ya Kamati
Mtoa hoja kualikwa kwenye Mkutano wa
Kamati.
Mkutano wa Bajeti
Mkutano wa Mwaka
Mkutano Maalum wa Halmashauri
Mkutano Maalum wa Kamati
Mwaliko wa wasiokuwa Wajumbe
Mwenyekiti kuwa Mjumbe wa Kamati zote
N
Nafasi wazi
71
86
22
23
30
31
58
3
46
51
5
6
4
48
29
41
Sura ya 287 kif. 70(1)
Taz.pia Sura ya 290 kif.47
Sura ya 287 kif.83(2)
Sura ya 287 kif.63(1)
Sura ya 287 kif.63(3)
Sura ya 287 kif.74(1)
Sura ya 287 kif.42(1) (a) 172
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
132
72 (1);41 (4);Tangazo la Serikali
Na.139/82 aya ya 23 na40 na
Sheria Na.4/79 kif.40(1)(b);40 (1)
(b) na SheriaNa 4/79kif.40(i) (b)
(i); na Sheria Na.4/79
kif.40;tangazo la Serikali Na.
280/2000 kif.35;41(3)41(3) na
kif.71(8).
P
Aina za Posho
Posho iwapo Mkutano umeahirishwa
Q
83
84
R
Rejesta ya mikataba
S
T
Taarifa za Kamati
Taarifa kutoka kwenye kata
Taarifa za mikutano
Tafsiri
Taratibu za kutunga Sheria Ndogo
Taratibu za Majadiliano
Taratibu za Uagizaji
68
24
25
7
2
74
16
63
Sura ya 287 kif.85
Sura ya 287 kif.155
Na.21/2004
Sura ya 290 kif.68
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
133
U
Uahirishaji wa vikao
Uandikishaji wa Anwani
Uanzishaji wa Bodi za Huduma
Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu wa
Mwenyekiti wa Halmashauri
Uhalali wa majadiliano ya Halmashauri
Uhifadhi wa lakiri ya Halmashauri
Uhuru wa kutoa mawazo wakati wa
majadiliano
Ukaguzi wa nyaraka
Uongozi wa mikutano ya Halmashauri
Upigaji kura kwenye mikutano ya Kamati
Usimamiaji wa mikataba
Utaratibu wa shughuli za mikutano
Uteuzi wa Wajumbe kwenye Taasisi za nje
Utiaji mhuri kwenye Nyaraka
Uvunjaji wa mkataba
Uwezo wa Halmashauri kujigeuza kuwa
Kamati ya Halmashauri nzima.
Uwezo wa Kamati
Uzuiaji wa Rushwa
39
80
76
9
35
78
26
75
10
57
66
13
81
79
67
Sura ya 287 kif.88
Sura ya 287 kif.36(2)
Sura ya 287 kif.72
Sura ya 287 kif.65
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
134
36
42
65
V
W
Waalikwa wasiokuwa Wajumbe
kuhudhuria na kushiriki katika mikutano ya
Kamati.
X
Y
Z
Ziara za Wajumbe
52
89
Sura ya 287 kif.75(4)
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
135
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KIAPO CHA DIWANI
Mimi …………………………............................................……
naapa/natamka kwa dhati kwamba
nitaitumikia Halmashauri ya………………….. kwa wadhifa wangu wa
Udiwani na kwamba nitahifadhi, nitalinda na kutetea, Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria za Tanzania, Maadili ya
Madiwani na Kanuni za Kudumu za Halmashauri kama zilivyowekwa
kwa mujibu wa Sheria na kwamba nitaitumikia Halmashauri ya
Wilaya ya Masasi kwa uaminifu kwa uwezo na moyo wangu wote.
(Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie)
Kiapo/Tamko hili limetolewa hapa:……………………....…………………
Na……………………………………………………………………………..
Leo tarehe…………………… Mwezi wa………………….........20..……….
Mbele ya:………………………………………..
Jina:………………………………………………
Cheo:………………………………………..…….
Saini:……………………………………….………
Anuani…………………………………..………….
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
136
……………………………………….……………..
HAKIMU
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
137
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU
RASILIMALI NA MADENI
(Kwa mujibu wa kifungu cha 9 na cha 11 cha Sheria ya Maadili ya
Viongozi wa Umma)
Mimi……………………………………………………………………………….…………………
Anuani:……………………baada ya kuchaguliwa/kuteuliwa na kuapishwa
katika wadhifa wa…….……...tarehe……………………….mwaka
20….Ninatamka rasmi na kwa moyo mnyofu kwamba hadi sasa nina
rasilimali na madeni
yafuatayo:-
(1) Fedha taslimu, Amana katika benki au taasisi ya fedha; taja
namba ya akaunti, benki au taasisi ya fedha na kiasi:
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………...................................................................
.....………………
2) Hawala za Hazina (Treasury Bills) na dhamana nyingine Maalum:-
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………...................................................................
....………………
3) Faida ya akiba, mafungu ya mgawanyo wa faida zinazotokana na
hisa n.k.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
138
…………………………………………………………………………………………………………
……………………………………….....................................................................
...…………………
4) Nyumba au majengo ya kupangisha, taja mahali yalipo na ukubwa
au eneo:
…………………………………………………………………………………………………………
……………………………………........................................................................
.…………………
* Rasilimali zinazotakiwa ni pamoja na zifuatazo, ambazo ni zako
binafsi, za mume/mke au watoto wadogo wasiooa au kuolewa wa
kiongozi wa umma.
(a) fedha taslimu na amana katika benki au taasisi nyingine ya fedha.
(b) hawala za Hazina Treasury Bills) na nyinginezo za dhamana
Maalum zinazotolewa au kudhaminiwa na Serikali au vyombo vya
Serikali.
(c) faida itolanayo na fedha iliyowekwa akiba benki, chana cha Ujenzi
au taasisi nyingine ya fedha.
(d) mgao wa fedha kutokana na fungu la rasilimali ya kampuni
(stocks) au hisa za kiongozi wa umma katika kampuni au shirika
lolote.
(e) maslahi katika chombo cha biashara kisichokuwa na mkataba na
Serikali, na kisichokuwa na au kisichotawala amana zinazouzwa
bayana na vyombo vya umma.
(f) mashamba ya kibiashara.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
139
(g) mali halisi zisizohamishika ambazo si rasilimali zisizotakiwa
kutajwa; na
(h) rasilimali zinazoleta faida, ambazo si rasilimali zisizotakiwa
kutajwa na ambazo zinamilikiwa kwa mbali.
(5) Mashamba ya kibiashara, mifugo, madini n.k.
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
……………………………................................................................................
....................…………
(6) Magari na aina nyingine za usafiri wa kibiashara;
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………...................................................................................................
..............................………
(7) Mashine za kusaga nafaka, viwanda na shughuli nyingine za
kibiashara au
mitambo:…………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
………………..............................................................................................
..................................…………
(8) Rasilimali nyinginezo au maslahi ambayo kiongozi wa umma
anapenda
kutaja:………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………..........................................
......................
(9)Madeni:………………………..………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
140
……………………………………………………………................................................
............................
Tamko hili linatolewa na kusainiwa mbele yangu
………………………………..............................................................................
.................................
na (mtoa
tamko) ..................................................................................................
..……………………
ninayemfahamu binafsi, au aliyetambulishwa kwangu na
…………………………………………………........................................................…
………………ambaye ninamfahamu leo tarehe …………………………......….
Mtoa tamko
Mwezi wa …………………………………………………..…….
saini………………………………………………………..……...
Wadhifa:…………………………………………………....……..
Anuani:……………………………………………….....………...
……………………………………………………….....………….
(Tamko hili lazima litolewe mbele ya Kamishna wa Viapo)
KWA: KAMISHINA WA MAADILI, SEKRETARIETI YA MAADILI,
S.L.P 13341,
DAR ES SALAAM.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
141
Muhuru wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
umewekwa katika Lakiri ya Sheria Ndogo hizi kufuati
Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri
leo tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya
wafuatao:-
……………………………………………..
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya Masasi
……………………………………………….
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya Masasi
NAKUBALI,
……………………………
……………………….
Dodoma GEORGE B.
SIMBACHAWENE (MB.),
23 Mei, 2017 Waziri wa
Nchi – OR TAMISEMI
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
142
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
143
TANGAZO LA SERIKALI NA. 396 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA)
(SURA YA 287)
________
SHERIA NDOGO ________
Zimetungwa chini ya kifungu cha 153(1)
________
SHERIA NDOGO ZA (UHIFADHI WA MALIASILI NA VYANZO VYA MAJI) ZA HALMASHAURI YA
WILAYA YA MASASI, 2017
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
144
Jina na mwanzo wa
kuanza kutumika 1. Sheria ndogo hizi zitaitwa Sheria Ndogo za
(Uhifadhi wa Maliasili na Vyanzo vya Maji) za
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za mwaka 2017,
na zitaanza kutumika baada ya kutangazwa kwenye
Gazeti la Serikali.
matumizi 2. Sheria Ndogo hizi zitatumika kwenye eneo lote
lililopo chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.
Tafsiri 3. Katika Sheria hizi isipokuwa pale itakapoelekezwa
vinginevyo:-
“Afisa Muidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote
atakayeteuliwa na Halmashauri kusimamia
utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya
Wilaya ya Masasi;
“Mkazi” maana yake ni mtu yeyote anayeishi na
kupata huduma za kijamii katika Wilaya ya
Masasi;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi au Afisa
yeyote wa umma atakayeteuliwa kutekeleza
majukumu ya Mkurugenzi;
“Msitu” maana yake ni eneo la ardhi lilotengwa na
kuwekwa mipaka lenye uoto wa asili au
lilopandwa miti kwa ajili ya matumizi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
145
maalum;
“Miti” maana yake ni pamoja na vichaka, mianzi,
miche na uoto wa aina yoyote wa asili au wa
kupandwa;
“Viumbe hai” maana yake ni pamoja na wadudu,
ndege na wanyama wanaohifadhiwa na
mazingira ya asili;
“Mifugo” maana yake ni wanyama wowote
wanaomilikiwa na binadamu kwa matumizi
maalum wakiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo
na nguruwe;
“Kibali” maana yake ni idhini ya maandishi
inayotolewa na Halmashauri kwa ajili ya
kuruhusu shughuli yoyote inayohusu Sheria
Ndogo hizi;
“Miti ya kupandwa” maana yake ni miti yote
iliyopandwa au kuoteshwa katika sehemu
yoyote ya Halmashauri kwa ajili ya manufaa
ya mauzo au kuboresha mandhari na
mazingira;
“Madini” maana yake ni rasilimali inayochimbwa na
kuhamishwa kutoka sehemu moja kwenda
sehemu nyingine kwa matumizi
yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na udongo,
mchanga, kokoto, mawe na vito mbalimbali;
“Chanzo cha maji” maana yake ni kijito, chemchem,
mto, mifereji ya asili, eneo tepetepe, lenye
uwezo wa kuzalisha maji kwa matumizi ya
mimea na viumbe wengine na maeneo
yanayozunguka yaliyotajwa kisheria kama
chanzo cha maji;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
146
“Eneo la wazi” maana yake ni eneo lililotengwa kwa
ajili ya matumizi ya jamii na lisiloruhusiwa
kujengwa vikiwemo viwanja vya michezo,
bustani na maeneo mengine yaliyotengwa
kwa matumizi ya aina hiyo;
“Msitu wa hifadhi” maana yake ni eneo lililotengwa
lenye uoto wa asili au miti ya kupandwa kwa
ajili ya manufaa au matumizi maalum kwa
mujibu wa Sheria Ndogo hizi;
“Makazi” ni sehemu iliyopimwa au isiyopimwa
ambayo imejengwa nyumba kwa ajili ya kuishi
au kwa ajili ya upatikanaji wa huduma za
jamii.
0754589056Wajibu
wa mkazi 4. (1) Kila mkazi wa eneo la Halmashauri ambaye
anamiliki ardhi au kiwanja Kisheria au kimila
atawajibika kupanda miti isiyopungua mitano katika
ardhi hiyo.
(2) Mti au Miti iliyopandwa karibu na nguzo za
mtandao wa umeme uwe ni mita tano (5).
(3) Mtu yeyote atakayemiliki ardhi katika eneo la
Halmashauri ambalo limeota, kupandwa miti au
uzio wa miti atawajibika kutunza, kupunguza na
kuweka uzio katika hali ya usafi nyakati zote.
Kukata miti ovyo 5. (1) Haitaruhusiwa kwa mtu yeyote kukata au
kung’oa mti wowote uliopandwa au ulioota sehemu
yoyote bila kuwa na idhini ya maandishi kutoka
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
147
Halmashauri.
(2) Idhini ya kukata au kung’oa mti au miti
itaambatana na ulipaji wa ada ya Shilingi elfu kumi
(10,000/=) kwa Halmashauri kwa kila mti
utakaokatwa au kung’olewa.
(3) Halmashauri itakuwa na mamlaka ya kutoa amri
halali kwa Mkazi au jamii katika sehemu yoyote
ndani ya Halmashauri ili kuongeza kiwango cha
kupanda miti kadiri itakavyoona inafaa.
(4) Afisa Mwidhiniwa atakuwa na mamlaka wakati
wowote kuingia katika eneo la makazi akiwa na
kitambulisho na kukagua sehemu yoyote ndani ya
eneo la Halmashauri ili kuhakikisha kuwa Sheria
Ndogo hizi zinazingatiwa.
Shughuli
zilizokatazwa kwenye
eneo lililopandwa
miti
6. (1) Haitaruhusiwa kwa mtu yeyote kufanya
shughuli za kibinadamu katika msitu, shamba la miti
au eneo lililopandwa miti bila kuwa na idhini ya
maandishi kutoka Halmashauri.
(2) Bila kuathiri masharti yaliyowekwa katika
kifungu kidogo cha (1) hapo juu, mtu yeyote
hataruhusiwa:-
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
148
(a) kukata miti kwa ajili ya kuchoma mkaa, kuni,
mijengo au fito;
(b) kupasua mbao;
(c) kuchoma moto misitu au miti;
(d) kuwinda wanyama, ndege au wadudu;
(e) kujenga nyumba, kulima au kulisha mifugo;
(f) kuvuna asali;
(g) kuchimba madini, mchanga, kokoto, mawe
na udongo;
(h) kuosha magari, kunawa, kuoga au kufua
nguo;
(i) kufanya matambiko au utafiti wa aina
yoyote ile;
(j) kutupa au kumwaga taka.
Wajibu wa kuhifadhi
vyanzo vya maji 7. (1) Kila mkazi wa Halmashauri atakuwa na
wajibu wa kutambua, kuainisha na kutunza vyanzo
vyote vya maji vilivyopo kwenye maeneo ya makazi
ili kuepusha uchafuzi na kuwa endelevu.
(2) Kila mkazi anatakiwa kuzingatia maelekezo
ya kitaalam kuhusu usimamizi na uendeshaji wa
miradi ya maji iliyopo katika vyanzo hivyo kwa
mujibu wa miongozo ya Halmashauri na Sera ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
149
maji ya Taifa.
Ukataji miti ovyo
kwenye vyanzo vya
maji
8. (1) Mtu yeyote hataruhusiwa kukata, kung’oa
au kuharibu mti au miti iliyoota au kupandwa ndani
ya ukanda wa mita 30 wa kingo mbili za mto au
nusu kipenyo cha mita 20 kutoka katikati ya kisima,
chemchem au bwawa bila kuwa na kibali kutoka
Halmashauri.
(2) Bila kuathiri kifungu kidogo cha (1) hapo
juu, mtu yeyote haruhusiwi kufanya shughuli za
ujenzi, kilimo kulisha mifugo, kuosha gari, kufua
nguo, kunawa, kuoga au kuchimba madini au dawa
kwenye vyanzo vya maji.
Shughuli
zilizokatazwa kwenye
vyanzo vya maji
9. (1) Mtu yeyote hataruhusiwa kufanya
shughuli za kibinadamu katika maeneo ya vyanzo
vya maji bila kuwa na idhini ya maandishi kutoka
Halmashauri.
(2) Bila kuathiri masharti yaliyowekwa katika
kifungu kidogo cha (1) hapo juu, Mtu yeyote
hataruhusiwa:-
(a) kukata miti kwa ajili ya kuchoma mkaa,
kuni, mijengo au miti ya dawa na fito;
(b) kupasua mbao;
(c) kuchoma moto miti au misitu;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
150
(d) kujenga nyumba, kulima ua kulisha mifugo;
(e) kuchimba madini, mchanga kokoto, mawe
au udongo;
(f) kuosha gari, kunawa, kuoga au kufua nguo.
Wajibu wa kutunza
bustani 10. (1) Kila mkazi wa Halmashauri atakuwa na
wajibu wa kushiriki katika utunzaji wa Bustani na
maeneo ya wazi ili kuyaboresha na kuyaendeleza.
(2) Mtu yeyote hataruhusiwa kufanya
shughuli yoyote kwenye maeneo ya wazi au bustani
bila kuwa na idhini ya maandishi kutoka
Halmashauri.
(3) Usimamizi na utunzaji wa maeneo ya wazi
au bustani utazingatia ushauri wa wataalam wa
Halmashauri na wadau mbalimbali watakaojitokeza
kushirikiana na Halmashauri katika kuendeleza
maeneo hayo.
Shughuli
zilizokatazwa kwenye
maeneo ya wazi na
bustani
11.
(1) Mtu yeyote hataruhusiwa kufanya
shughuli za kibinadamu kwenye bustani au maeneo
ya wazi bila kuwa na idhini kutoka Halmashauri.
(2) Bila kuathiri masharti yaliyowekwa katika
kifungu kidogo cha (1) hapo juu, mtu yeyote
hataruhusiwa:-
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
151
(a) kutengeneza gari, pikipiki au baiskeli;
(b) kufanya biashara ya aina yoyote;
(c) kwenda haja kubwa au ndogo;
(d) kuharibu uzio au mipaka iliyowekwa;
(e) kuharibu au kuhamisha mimea au mali
yoyote iliyopo kwenye eneo;
(f) kufanya mikutano, mihadhara, mafunzo au
semina;
(g) kupiga picha za kamera au video.
Wajibu wa
kuwaendeleza nyuki 12. (1) Kila mkazi wa Halmashauri atakuwa na
wajibu wa kuwatunza nyuki kwa manufaa ya jamii
kwa kuzingatia Kanuni za kitaalam.
(2) Kila mkazi wa Halmashauri anawajibika
kuzingatia ushauri wa kitaalam katika ufugaji,
uvunaji wa asali na utunzaji wa asali katika vyombo
vyenye ubora unaostahili.
(3) Nyuki wasumbufu wanaovamia maeneo
yasiyostahili wataondolewa na wataalamu wa
Halmashauri kwa kulipia gharama kwa viwango
vilivyoainishwa na Halmashauri.
Uuzaji wa asali 13. Mfanyabiashara yeyote wa asali anatakiwa
kutumia vyombo rasmi kwa ajili ya kutunzia na
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
152
kuuzia asali. Ni marufuku kutumia chupa za kioo
zilizokwishatumika kuhifadhi bidhaa nyingine kwa
ajili ya kuhifadhi au kuuzia asali.
Biashara ya Nyara za
Serikali 14. (1) Kila mfanyabiashara hatatakiwa kufanya
biashara ya Nyara za Serikali bila kuwa na leseni.
(2) Wafanyabiashara wote watakaoomba
leseni za biashara ya Nyara za Serikali watalipa ada
ya maombi kwa kiwango cha Tsh. 5,000/= kwa kila
fomu.
(3) Wafanyabiashara wote wanaosafirisha
Nyara nje ya nchi watawajibika kuilipa Halmashauri
asilimia (20%) ya malipo ya Serikali Kuu kwa ajili ya
biashara hiyo.
Makosa na Adhabu 15. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na
masharti ya Sheria Ndogo hizi atakuwa ametenda
kosa na akipatikana na hatia atatozwa faini isiyozidi
Shilingi Laki Tatu (300,000/=) au kifungo cha miezi
kumi na miwili jela au adhabu zote mbili kwa
pamoja yaani faini na kifungo.
Uwezo wa kufifirisha
kosa 16.
Mkurugenzi anaweza kumtoza faini isiyozidi
Shilingi Laki Mbili (200,000/=) mtu yeyote endapo
mkosaji kwa hiari yake mwenyewe atakiri kosa kwa
maandishi na kukubali kulipa faini anayodaiwa.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
153
_______
JEDWALI
______
(Limetungwa chini ya kifungu cha 16)
Mimi …………………… nakiri mbele ya ………….ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashuri ya Wilaya ya Masasi, kwamba mnamo tarehe …… ya Mwezi ……. Mwaka ……
nilitenda kosa la kukiuka masharti ya kifungu cha …… cha Sheria Ndogo za (Uhifadhi wa
maliasili na Vyanzo vya Maji) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za Mwaka 2017.
Kwa Mamlaka aliyopewa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Niko tayari kulipa kiasi
cha Ada/ Ushuru ninaodaiwa pamoja na faini.
NATHIBITISHA KWAMBA MAELEZO HAPO JUU NI YA KWELI NA NIMEYATOA KWA
HIARI YANGU KADRI YA UFAHAMU WANGU
Leo tarehe…………. ya Mwezi………… Mwaka ………………….
Jina……………………………….. Saini…………………………………….
Mbele ya :
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
154
Jina: ……………………………………………
Cheo: ………………………………………….
Saini: …………………………………………..
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
155
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANGAZO LA SERIKALI NA. 395 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA)
(SURA YA 287)
________
SHERIA NDOGO
________
Zimetungwa chini ya kifungu cha 153(1)
________
SHERIA NDOGO YA (UANZISHAJI WA MFUKO WA AFYA YA JAMII) ZA
HALMASHAURI YA WILAYA ZA MASASI 2017
Jina na Tarehe ya
kuanza kutumika 1. Sheria Ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo za
(Uanzishaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii) za
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za Mwaka 2017, na
zitaanza kutumika baada ya kutangazwa kwenye Gazeti
la Serikali.
Matumizi 2. Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo lote la
mamlaka ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.
Tafsiri 3. Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa kama itaelezwa
vinginevyo:-
“Ada ya mtumiaji” maana yake ni ada anayolipa
mtumiaji wa huduma kwa Hospitali, Kituo cha afya
au Zahanati, kwa ajili ya Huduma ya Afya
iliyotolewa kwa mtumiaji;
Sura ya 287 ”Bodi” maana yake ni chombo kinachosimamia Huduma
za Afya ya Halmashauri iliyoundwa kwa mujibu
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
156
wa kifungu Na. 88 cha Sheria ya Serikali za Mitaa
(Mamlaka za Wilaya) Sura Na. 287;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Wilaya ya
Masasi;
“Huduma za Afya” maana yake ni huduma zote za Afya
zinazotolewa na Hospitali, Vituo cha Afya,
Zahanati na Kliniki maalum zinazomilikiwa na
Serikali, Mashirika ya Dini, Mashirika yasiyo ya
Serikali au Watu binafsi;
“Kadi” maana yake ni kadi itakayotolewa kwa
Mwanachama wa Mfuko wa Afya ya Jamii;
“Kaya” maana yake ni:-
(a) Baba, Mama na Watoto wenye umri chini
ya miaka kumi na nane; na
(b) Mwanachama yeyote aliyefikia umri wa
miaka kumi na nane au zaidi na awe na
Mtoto au bila Mtoto mwenye umri chini ya
miaka kumi na nane; au
(c) Taasisi yoyote;
“Kituo cha Huduma kilichoteuliwa” maana yake ni kituo
kinachotoa Huduma za Afya na ni pamoja na kituo
chochote kilichoanzishwa au kinachoendeshwa
kwa malengo ya kutoa Huduma za Afya
kinachomilikiwa na Halmashauri, Serikali, Asasi
za Kidini, Mtu au Watu binafsi ambacho
kinahusika na Mfuko wa Afya ya Jamii;
“Malipo ya huduma” maana yake ni malipo ya papo kwa
papo yanayolipwa katika Kituo cha kutolea
Huduma za Afya na Mtu au Watu ambao si
Wanachama wa Mfuko wa Afya ya Jamii;
“Mchango” maana yake ni mchango wa fedha wa hiari,
utakaotolewa na Wanachama wa Mfuko wa Afya
ya Jamii;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
157
“Mganga Mkuu wa Wilaya” maana yake ni Daktari
ambaye ni Msimamizi Mkuu wa shughuli zote za
Huduma za Afya katika Wilaya;
“Mwanachama” ni Mtu yeyote ambaye anachangia
mfuko wa Afya ya Jamii;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi au Afisa yeyote
atakayeteuliwa kutekeleza majukumu ya
Mkurugenzi;
“Taasisi” maana yake ni pamoja na Shule au Chuo
kilichosajiliwa kwa mujibu wa Sheria au Taasisi
yoyote itakayokuwa imekubaliwa na kuidhinishwa
na bodi kuwa Mwanachama;
“Wizara” maana yake ni Wizara yenye dhamana ya
masuala ya Afya.
Mfuko wa Afya ya
Jamii 4. - (1) Kutakuwa na mfuko wa Afya ya Jamii ambao ni
mpango wa hiari wenye lengo la kutoa msaada kifedha
katika kugharamia matibabu, ambapo kaya zitakuwa
zikilipia Huduma za Afya, na Serikali itatoa mchango
wake wa fedha kama jazilio kwa mchango kutoka
kwenye Kaya Mwanachama.
(2) Matumizi ya fedha yatafanywa na kusimamiwa na
Bodi kwa Mujibu wa Sheria Ndogo hizi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
158
Madhumuni ya
Mfuko 5. Madhumuni ya Mfuko yatakuwa ni-
(a) Kuboresha huduma za afya katika Jamii kwa
kugawanya madaraka na kuzipa nguvu Jamii
katika kufanya maamuzi na kuchangia katika
masuala yanayohusu afya zao;
(b) Kutoa huduma bora za afya zinazopatikana na kwa
kutumia mipango endelevu; na
(c) Kutafuta vyanzo vya mapato kutoka katika Jamii
kwa ajili ya kutoa huduma bora za afya kwa
Wanachama.
Usimamizi wa
Mfuko wa Afya ya
Jamii.
6. (1) Usimamizi na uendeshaji wa Mfuko utakuwa chini
ya:-
(a) Halmashauri ya Wilaya kupitia Bodi ya
Huduma za Afya ya Halmashauri ya
Wilaya; na
(b) Kamati ya Maendeleo ya Kata kupitia
Kamati ya Afya ya Kata, katika ngazi ya
Kata.
(2) Mfuko kwa ujumla utakuwa chini ya usimamizi wa
Bodi ambayo itakuwa na majukumu ya:-
(a) kuratibu shughuli zinazohusu mfuko;
(b) kusimamia, kudhibiti na kuelekeza
usimamizi katika vyanzo vya mfuko;
(c) kuhakikisha kuwa mfuko unatumika na
kusimamiwa kikamilifu na kwa ufanisi; na
(d) Serikali ya kijiji kupitia Kamati za Huduma
za Jamii katika ngazi ya kijiji.
(2) Majukumu ya Mratibu wa Mfuko wa Afya ya
Jamii yatakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Kufuatilia, kusimamia na kuratibu uendeshaji
wa Mfuko wa Afya ya Jamii kwenye vituo vya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
159
kutolea Huduma za Afya;
(b) Kuwa kiungo kati ya Halmashauri, Jamii na
Wadau mbalimbali kwa ushirikiano na
Mhasibu wa Mfuko; na
(c) Kuandaa taarifa za Mfuko wa Afya ya Jamii za
robo na za Mwaka pamoja na majukumu
mengine atakayopangiwa na Mkurugenzi;
(d) Kuhudhuria vikao vyote vya Bodi na kutoa
taarifa za utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa
Afya ya Jamii;
Bodi 7. Kutakuwa na Bodi ya Mfuko wa Afya ya Jamii
itakayoundwa kwa mujibu wa Sheria Ndogo hizi ambayo
itakuwa ni chombo kinachosimamia huduma za afya
katika Halmashauri.
Muundo wa Bodi 8. (1) Bodi itakuwa na wajumbe wafuatao:-
(a) Wawakilishi wanne wa Watumiaji wa
Huduma za Afya, kati yao wawili lazima wawe
ni Wanawake;
(b) Mwakilishi mmoja kutoka kwa Watoa huduma
za afya binafsi bila faida;
(c) Mwakilishi mmoja kutoka kwa Watoa
Huduma za Afya binafsi waliochaguliwa na
Halmashauri kutoka katika Vituo ambavyo
vina mkataba na Bodi wa kutoa Huduma za
Afya ;
(d) Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Afya,
Elimu na Maji;
(e) Wajumbe Wataalamu ambao ni:-
(i) Afisa Mipango wa Halmashauri;
(ii) Mganga Mkuu wa Halmashauri ambaye
atakuwa Katibu wa Bodi;
(iii) Mwakilishi mmoja kutoka Hospitali ya
Halmashauri;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
160
(iv) Mwakilishi mmoja kutoka Timu ya
uendeshaji wa Huduma za Afya ya Mkoa.
(2) Wajumbe wa Bodi waliotajwa katika kifungu
cha 8(1) (e) (i) – (v) hawataruhusiwa kupiga kura.
(3) Mwenyekiti wa Bodi atachaguliwa kutoka
miongoni mwa Wajumbe waliotajwa katika kifungu (1)
(a) – (c) hapo juu.
Sifa za Wajumbe wa
Bodi 9. Mjumbe wa Bodi atakuwa na sifa zifuatazo:-
(a) Awe raia wa Tanzania, isipokuwa kwa
Wajumbe kutoka Mashirika yasiyo ya
Kiserikali;
(b) Awe na umri usiopungua miaka ishirini na
tano (25);
(c) Awe amehitimu Elimu ya Sekondari na
kuendelea;
(d) Awe na uzoefu na amewahi kuonyesha uwezo
wake wa kuongoza katika shughuli za huduma
ya jamii;
(e) Awe na akili timamu;
(f) Asiwe amewahi kutiwa hatiani kwa kosa lolote
la jinai;
(g) Asiwe na wadhifa wowote katika chama
chochote cha siasa;
(h) Awe Mwanachama hai wa Mfuko wa Afya ya
Jamii; na
(i) Mjumbe wa kuchaguliwa awe ni mkazi wa
Halmashauri.
Kazi za Bodi 10. (1) Bodi itakuwa na kazi zifuatazo:-
(a) Itasimamia masuala na shughuli zote
zinazohusu Mfuko wa Afya ya Jamii ;
(b) Kusimamia Huduma za Afya katika
Halmashauri;
(c) Kushauriana na Timu ya uendeshaji ya
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
161
Huduma za Afya ya Halmashauri na
kuhakikisha kuwa Huduma za Afya
zinazotolewa ni bora na za Kitaalamu;
(d) Kukusanya na kusimamia mapato ya Mfuko
wa Afya ya Jamii;
(e) kupendekeza kwa Halmashauri Watu
wanaostahili kusamehewa kutoa mchango
kwenye Mfuko;
(f) kubuni malengo ya Mfuko;
(g) kupitia taarifa kutoka Kamati ya Afya ya Kata
au chanzo kingine chochote;
(h) kuratibu ukusanyaji wa michango na kudhibiti
matumizi; na
(i) Kupanga mipango ya afya ya Mwaka kwa ajili
ya kuthibitishwa na Halmashauri.
(2) Bodi katika kutekeleza majukumu yake, itapokea na
kutekeleza maagizo ya Halmashauri kwa mujibu wa
Sheria, Kanuni, na Taratibu.
Muda wa kukaa
Madarakani 11. (1) Mjumbe wa Bodi atakuwa madarakani kwa kipindi
cha miaka mitatu kuanzia tarehe ya uzinduzi wa Bodi na
anaweza kuchaguliwa tena kwa kipindi kingine cha
miaka mitatu (3) tu.
(2) Endapo nafasi yoyote ya Mjumbe wa Bodi itaachwa
wazi kwa sababu ya kifo, kujiuzulu au kwa sababu
nyingine yoyote ile, Mjumbe mwingine atachaguliwa
kujaza nafasi hiyo iliyoachwa wazi kwa kipindi
kilichobaki.
(3) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (2)
hapo juu, haitaruhusiwa kuchagua mjumbe mwingine
iwapo kipindi kilichobaki ni chini ya miezi sita.
Akaunti ya Mfuko 12. (1) Kutakuwapo na Akaunti Maalum itakayotumika na
Halmashauri ambayo fedha zote zitakazokusanywa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
162
kwa ajili ya Mfuko zitahifadhiwa na kutolewa.
(2) Wawekaji saini wa Akaunti ya Mfuko
watachaguliwa na Bodi na watakuwa ni wa kutoka
Kundi “A” na Kundi “B”, kama ifuatavyo:-
Kundi A Kundi B
1. Mwenyekiti wa
Bodi
2. Mjumbe Mmoja
wa Bodi
1. Katibu wa Bodi
2. Mweka Hazina wa
Halmashauri
(3) Fedha hazitatolewa kwenye akaunti ya mfuko bila
saini ya mmojawapo kutoka kila Kundi.
(4) Akaunti ya Mfuko itakaguliwa kwa mujibu wa
Kanuni za Fedha za Serikali.
Taarifa ya Fedha 13. Bodi itaandaa na kuwasilisha kwa Halmashauri, taarifa
ya mapato na matumizi ya fedha ya kila baada ya miezi
mitatu (3).
Matumizi ya Fedha
za Mfuko 14. Fedha zitakazokusanywa na mfuko zitatumika kwa
madhumuni yafuatayo:-
(a) Masuala yanayohusiana na afya yaliyotajwa katika
mpango kabambe wa afya wa Halmashauri na
kuidhinishwa na Halmashauri; na
(b) Suala au shughuli yoyote muhimu ya afya
itakayoonekana inafaa na kama itaidhinishwa na
Bodi.
Vyanzo vya mapato 15. Vyanzo vya mapato ya mfuko vitatokana na:-
(a) Fedha zote zitakazopokelewa kutokana na
michango ya Wanachama;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
163
(b) Ruzuku kutoka Halmashauri, na Serikali Kuu,
Wahisani mbalimbali toka ndani na nje ya
Halmashauri;
(c) Michango ya watu binafsi wanaoishi ndani na nje
ya Halmashauri;
(d) Ushuru utakaotozwa na Halmashauri kutoka
vyanzo mbalimbali na kutengwa kwa ajili ya
mfuko;
(e) Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya; na
(f) Fedha zozote halali ambazo Mfuko unaweza
kupata toka mahali pengine popote.
Mipango 16. (1) Bodi itaandaa mipango ya Bajeti ya Mwaka kwa
kuzingatia ratiba za vikao vya Bajeti vya
Halmashauri.
(2) Bodi itapokea, itajadili, itachambua na kuidhinisha
mpango wa afya na kuwasilisha kwa Halmashauri
kwa ajili ya kuidhinishwa kwa kupitia Kamati za
Halmashauri.
(3) Bodi itatoa maoni ya bajeti ya nyongeza kama
kutakuwa na haja ya kufanya hivyo na kama
mazingira yataruhusu.
(4) Mipango ya bajeti ya Mfuko itaandaliwa kulingana
na utaratibu kama ulivyoainishwa katika kifungu
kidogo cha (1) hapo juu, ambayo ni lazima
iwasilishwe Halmashauri kwa ajili ya kuidhi-
nishwa.
Kamati ya Afya na
Kata (SURA 409) 17. Kutakuwa na kamati ya Afya ya Kata kama ilivyotajwa
kwenye Sheria ya Mfuko wa Afya ya Jamii.
Wajumbe wa kamati
ya Afya ya Kata
(SURA 409)
18. (1) Kamati ya Afya ya Kata itakuwa na Wajumbe
wafuatao:-
(a) Diwani anayewakilisha Kata husika;
(b) Afisa Mtendaji wa Kata;
(c) Mwalimu Mkuu mmoja kutoka kwenye
Shule ya msingi ambayo ipo kwenye Kata
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
164
husika;
(d) Wajumbe wawili watakaowakilisha jamii
husika ambapo mmoja wao ni lazima awe
Mwanamke;
(e) Tabibu Mfawidhi au Tabibu Mfawidhi
Msaidizi; wa kituo cha Afya au Zahanati,
ambaye atakuwa katibu wa Kamati;
(f) Mjumbe mmoja atakayeteuliwa na kamati ya
maendeleo ya kata kutokana na watu
waliopendekezwa na Kamati za Kata
zilichomo ndani ya eneo la Kata; na
(g) Mjumbe mmoja atakayeteuliwa na Kamati
ya maendeleo ya Kata kutoka kwenye vyama
vya kijamii kutoka kwenye Kata.
(2) Mwenyekiti wa Kamati ya Afya ya Kata
atachaguliwa kutoka miongoni mwa wajumbe
lakini asiwe Diwani, Mtendaji wa Kata au
Mtendaji wa Mtaa.
(3) Endapo Kamati ya Afya ya Kata itashindwa
kutekeleza kazi zake, Bodi itatoa onyo au
kuivunja na Halmashauri itafanya utaratibu wa
uchaguzi wa wajumbe wengine katika muda
usiozidi miezi mitatu (3) tangu tarehe ya
kuvunjwa kwa Kamati hiyo.
Kazi na majukumu
ya Kamati ya Afya
ya Kata.
19. (1) Kamati ya Afya ya Kata itakuwa na majukumu
yafuatayo:-
(a) Kuhamasisha na kuandaa Jamii kujiunga na
Mfuko wa Afya ya Jamii;
(b) Kuandaa na kuthibitisha orodha na kuratibu
idadi ya Wanachama wa Mfuko wa Afya wa
Jamii;
(c) Kusimamia ukusanyaji wa michango ya
Mfuko;
(d) Kuratibu viwango vya uchangiaji kwenye
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
165
Huduma za Afya;
(e) Kupitia utendaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii
na kutoa mapendekezo na ufumbuzi kwa
Halmashauri kupitia Bodi ya Afya;
(f) Kuanzisha na kuratibu Mipango ya Afya na
Jamii na;
(g) Kuendesha mikutano ya Wanachama wa
Mfuko wa Afya ya Jamii ndani ya Kata.
(2) Kamati ya Afya ya Kata, itakaa kila baada ya miezi
mitatu (3) na Katibu atatoa taarifa ya maandishi
siku saba (7) kabla ya siku ya kikao.
Utoaji wa Huduma
za Afya. 20. Kila Mwanachama:-
(a) Atakuwa na haki ya kisheria kupata Huduma ya
Afya aliyolipia kabla ya kuugua ndani ya eneo la
Halmashauri au eneo lingine lolote kadri itakavyo-
kubaliwa;
(b) Atakuwa na haki ya kutoa mapendekezo kuhusu
Huduma za Afya kupitia kamati husika ambayo
yatafanyiwa kazi na Bodi; na
(c) Atashirikishwa kikamilifu katika uandaaji na
utekelezaji wa mpango wa upatikanaji wa Huduma
za Afya katika eneo la Halmashauri.
Mchango wa
Mwanachama 21. (a) Mtu yeyote atakayetaka kuwa Mwanachama wa
Mfuko wa Afya ya Jamii atapaswa kulipa kila
mwaka mchango kiasi cha Shilingi elfu kumi tu
(10,000/=);
(b) Viwango hivi vinaweza kufanyiwa marekebisho na
Halmashauri wakati wowote iwapo itaonekana
kuna umuhimu wa kufanya marekebisho hayo.
Muda wa
Uanachama 22. (a) Mtu yeyote atabaki kuwa Mwanachama wa Mfuko
wa Afya ya Jamii kila atakapolipa mchango wake
wa Uanachama; na
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
166
(b) Kila Mwaka utakapoisha Uanachama wa mtu
utafikia mwisho hadi pale atakapotimiza masharti
ya kifungu (a) hapo juu.
Malipo ya Papo kwa
papo 23. (1) Mtu yeyote ambaye hatakuwa Mwanachama wa
mfuko huu atalipa malipo ya papo kwa papo kila
atakapoenda kupata matibabu katika kituo cha
kutolea Huduma za Afya.
(2) Malipo ya papo kwa papo yatalipwa kwa ajili ya
kusajiliwa, kumwona Daktari, na kupewa dawa kwa
mujibu wa viwango vifuatavyo;-
(a) Hospitali shilingi elfu kumi (10,000/=);
(b) Vituo ya Afya shilingi elfu tano ( 5,000/=);
(c) Zahanati elfu tatu (3,000/=).
Utaratibu wa
Misamaha 24. Misamaha kwa wasioweza kulipia gharama za matibabu
utatolewa na kulipiwa na Halmashauri baada ya
kuzingatia utaratibu ufuatao:-
(a) Serikali ya Mtaa katika vikao vyake itawatambua,
kuwajadili na kuwasilisha mapendekezo ya Orodha
ya majina ya watu wanaostahili kupewa Msamaha
kwenye Kamati ya Maendeleo ya Kata;
(b) Kamati ya Maendeleo ya Kata itawajadili wale
wasioweza kulipia gharama na kuthibitisha orodha
yao na kuiwasilisha kwenye Bodi; na
(c) Bodi ya Afya itapokea na kujadili mapendekezo
husika na kuyawasilisha pamoja na gharama zake
kwa Halmashauri kwa ajili ya kulipiwa.
Utoaji wa Kadi kwa
Mwanachama 25. (1) Kila Kaya Mwanachama wa Mfuko atapewa kadi
baada ya kulipa mchango wake wa Mwaka wa
Shilingi elfu kumi (10,000/=) au kiwango kitaka-
chopendekezwa na Bodi na kuidhinishwa na
Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
167
(2) Kila mtu atakaye samehewa kulipa mchango
atapewa kadi ya Uanachama na Halmashauri
italipa gharama ya kadi hiyo.
(3) Viwango vya kulipia uanachama vitapendekezwa
na Kamati ya Maendeleo ya Kata na kujadiliwa na
Bodi kisha kuidhinishwa na Halmashauri.
Makosa na Adhabu 26. Mtu yeyote ambaye:-
(a) Atakwenda kinyume na masharti yoyote ya Sheria
Ndogo hizi;
(b) Atafanya kitendo chochote ambacho kitazuia Bodi
kufanya kazi zake kwa ufanisi;
(c) Atatumia vibaya mali na rasilimali za Mfuko;
(d) Atafanya udanganyifu ili aweze kunufaika na
Huduma za Afya zitolewazo kwa utaratibu wa
Mfuko wa Afya ya Jamii; au
(e) Atazuia utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi.
Atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia
atatozwa faini isiyozidi Shilingi Laki Tatu (300,000/=),
au kifungo kisichozidi miezi kumi na miwili (12) au
adhabu zote mbili kwa pamoja yaani faini na kifungo.
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
NAKUBALI
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
168
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANGAZO LA SERIKALI NA. 394 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA)
(SURA YA 287)
________
SHERIA NDOGO ________
Zimetungwa chini ya kifungu cha 153(1)
________
SHERIA NDOGO ZA (ULINZI WA UMMA) ZA HALMASHAURI YA
WILAYA YA MASASI ZA MWAKA 2017
Jina na mwanzo wa
kuanza kutumika 1. Sheria Ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo za
(Ulinzi wa Umma) za Halmashauri ya wilaya ya
Masasi za mwaka 2017, na zitaanza kutumika baada
ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Matumizi 2. Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo lote lililipo
chini ya mamlaka ya Halmashauri ya Wilaya ya
Masasi.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
169
Tafsiri 3. Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa pale
itakapoelekezwa vinginevyo:-
“Afisa Muidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote
atakayeteuliwa na Halmashauri kusimamia
utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Wilaya
ya Masasi;
“Mkazi” maana yake ni mtu yeyote ambaye anaishi
ndani ya Halmashauri;
“Kaya” maana yake ni mtu yeyote anayeishi kwa
kujitegemea kundi la watu/jamii wanaoishi
kwa kumtegema mmoja wao kama Mkuu wa
Kaya;
“Eneo” maana yake ni eneo lote la kijiji, Kata na
Tarafa;
“Ulinzi wa Umma” maana yake ni ulinzi na uangalizi
wa mali zote za wananchi katika kijiji, Kata na
Tarafa;
“Kiongozi wa kikundi cha Ulinzi” maana yake ni mtu
ambaye anasifa ya Uongozi wa ulinzi ambaye
amechaguliwa na wakazi wa kijiji, Kata na
Tarafa.
Wajibu wa kila mkazi 4. (1) Kila Mkazi anawajibika kushiriki katika ulinzi wa
Umma kama utakavyoratibiwa na Uongozi wa
Serikali ya Kijiji, Kata na Tarafa.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
170
(2) Mkazi atahesabika kuwa ametekeleza Kifungu
kidogo cha (1) hapo juu iwapo atafanya
yafuatayo:-
(a) atashiriki ulinzi yeye mwenyewe kwa muda
usiopungua saa nane katika muda wa saa
ishirini na nne mfululizo;
(b) Kaya yake:-
(i) itachangia kiasi cha fedha
kilichoidhinishwa na Serikali ya kijiji,
Kamati ya maendeleo ya Kata au
Halmashauri kutegemeana na hali
halisi ya eneo husika kwa ajili ya
kugharimia shughuli za ulinzi wa
umma;
(ii) itakodisha ama kuchangia malipo ya
kampuni ya ulinzi ya binafsi;
(iii) itanunua vifaa vya ulinzi kama tochi,
betri, mishale, pinde, filimbi, sare au
vifaa vinginevyo vyovyote muhimu kwa
ajili ya ulinzi.
Kikundi cha ulinzi
5. Kutaanzishwa Kikundi cha Ulinzi katika kila Kijiji, Kata
na Tarafa katika Halmashauri kwa lengo la
kuimarisha ulinzi katika eneo husika.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
171
Kiongozi wa kikundi
cha ulinzi
6. Kila kikundi cha ulinzi kitakuwa na Kiongozi
atakayetambuliwa kama Kamanda wa kikundi
ambaye atateuliwa kutoka miongoni mwa watu
wanaounda kikundi cha ulinzi cha kijiji, Kata na
Tarafa.
Kuandaa orodha ya
wakazi
7. Kila Kamanda wa kikundi atatakiwa kuwa na orodha
ya wakazi wote wanaostahili kushiriki ulinzi katika
eneo husika na orodha hiyo itahifadhiwa katika
daftari maalum kwa ajili hiyo na kutunzwa katika
Ofisi za Maafisa Kijiji, Kata na Tarafa.
Kuwasilisha taarifa
8. Kamanda wa kikundi cha ulinzi akisaidiwa na
Makamanda Wasaidizi watawajibika kusimamia kila
kikundi kitakachokuwa zamu kwa siku inayohusika
na watakuwa na wajibu wa kuwasilisha orodha ya
walinzi waliopo zamu na taarifa ya utekelezaji ya kila
siku katika Ofisi ambamo kikundi cha ulinzi kimo.
Taarifa ya hali ya
ulinzi na usalama
9. Kamanda wa kikundi cha ulinzi na usalama
atawasilisha katika vikao vya mikutano ya mwaka
hali ya ulinzi na usalama katika sehemu yake na
kujadiliwa na wajumbe na kutoa tamko la kikao
kuhusu hali hiyo na mtazamo wa wananchi juu ya
kazi hiyo.
Makosa 10. Mtu yeyote atakuwa ametenda kosa iwapo:-
(a) hatashiriki shughuli za ulinzi katika eneo
husika;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
172
(b) atamshawishi mtu yeyote asishiriki ama
kumsaidia mtu yeyote kukwepa kushiriki
katika ulinzi ndani ya eneo lake au eneo
jingine lolote katika Halmashauri.
Adhabu 11. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na kifungu
chochote cha Sheria Ndogo hizi atakuwa ametenda
kosa na akipatikana na hatia atatozwa faini isiyozidi
Shilingi Laki Tatu (300,000/=) au kifungo kisichozidi
miezi kumi na miwili jela au adhabu zote mbili kwa
pamoja yaani faini na kifungo.
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
173
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANGAZO LA SERIKALI NA. 397 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA FEDHA ZA SERIKALI ZA MITAA
(SURA 290)
________
SHERIA NDOGO _________
Zimetungwa chini ya Vifungu vya 7(1) na 16(1)
_________
SHERIA NDOGO ZA (USHURU WA HUDUMA) ZA HALMASHAURI YA
WILAYA YA MASASI, 2017
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
174
Jina na mwanzo wa
kuanza kutumika
1. Sheria Ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo za
(Ushuru na Huduma) za Halmashauri ya Wilaya ya
Masasi za mwaka 2017, na zitaanza kutumika baada
ya kutangazwa katika Gazeti la Serikali.
Matumizi
2. Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo la mamlaka
ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.
Tafsiri
Sura 212
Sheria Na.7 ya
mwaka 2011
3. Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa pale
itakapoelezwa vinginevyo:-
“Afisa Mwidhiniwa” maana yake ni ya Afisa yeyote
wa umma au mtu mwingine atakayeteuliwa na
Halmashauri kusimamia utekelezaji wa Sheria
Ndogo hizi;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Wilaya
ya Masasi;
“Hesabu” maana yake ni jumla ya mauzo ya bidhaa,
kazi au Huduma katika mwaka wa fedha;
“Kampuni” maana yake ni kampuni iliyosajiliwa kwa
mujibu wa Sheria ya Makampuni;
“Kazi” maana yake ni kama ilivyotafsiliwa kwenye
Sheria ya Manunuzi ya Umma;
“Kipindi Maalum cha Hesabu” maana yake ni muda
ambao mfanyabiashara anatakiwa kuwasilisha
hesabu za biashara kwa Halmashauri;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi au Afisa
yeyote atakayeteuliwa kutekeleza majukumu ya
Mkurugenzi;
“Taasisi ya biashara” maana yake ni taasisi
iliyosajiliwa inayofanya biashara, kazi au kutoa
huduma kwa lengo la kupata faida;
“Tawi la Kampuni” maana yake ni tawi la kampuni
iliyosajiriwa kwa mujibu wa Sheria ya
Makampuni;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
175
“Ushuru wa Huduma” maana yake ni ushuru
unaotozwa au kukusanywa na Halmashauri
kutoka kwa Kampuni, Tawi la kampuni, Taasisi
ya biashara, au mfanyabiashara kwa huduma
anazopata kutokana na kutumia miundombinu ya
Umma inayomuwezesha kufanya biashara katika
eneo la Halmashauri;
“Ukokotoaji” maana yake ni namna ya kuandaa kiasi
cha Ushuru wa Huduma kitakacholipwa kwa
mujibu wa kifungu cha 7 cha sheria Ndogo hizi.
Utozaji wa Ushuru
wa Huduma 4. Halmashauri itatoza na kukusanya Ushuru wa
Huduma kwa kampuni, taasisi ya biashara au tawi la
kampuni au Mfanyabiashara mkubwa mwenye
kampuni ya biashara kwa kiwango kisichozidi asilimia
sifuri nukta tatu (0.3%) kutokana na uzalishaji wa
bidhaa, kazi na huduma zinazofanyika ndani ya eneo
la Halmashauri baada ya kutoa kodi ya ongezeko la
thamani (VAT) na kodi ya mlaji.
Wajibu wa kulipa
Ushuru wa Huduma 5. (1) Itakuwa ni wajibu wa kila mfanyabiashara,
kampuni, taasisi ya biashara au tawi la kampuni kulipa
Ushuru wa Huduma utokanao na utoaji wa huduma,
kazi, mauzo ya bidhaa katika eneo la Halmashauri.
(2) Mfanyabiashara atawasilisha kwa Halmashauri
taarifa za hesabu za mauzo kwa kila mwezi husika na
atalipa Ushuru wa Huduma kwa mujibu wa viwango
vitakavyotokana na hesabu hizo au viwango
vilivyotajwa na Sheria Ndogo hizi kwa
mfanyabiashara asiye na vitabu vya biashara.
(3) Endapo mfanyabiashara, kampuni, taasisi ya
biashara au tawi la kampuni itashindwa kuwasilisha
taarifa sahihi za mauzo kwa wakati, Mkurugenzi kwa
maandishi anaweza kumtaka Mfanyabiashara yeyote
kuwasilisha taarifa hizo ndani ya siku thelathini (30)
zinazohusu kipindi maalum cha hesabu zikionyesha
kiasi na thamani ya fedha za mauzo ya bidhaa
zilizoingizwa, kusambazwa au kuuzwa na kazi au
huduma zitolewa.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
176
(4) Mkurugenzi au Afisa Mwidhiniwa anaweza
kumtaka kwa maandishi mtu yeyote mwenye taarifa
kuhusu taasisi yoyote ya mfanyabiashara yeyote
anayepaswa kulipa ushuru kwa mujibu wa Sheria
Ndogo hizi, kuwasilisha kwake taarifa na ambazo
zitatumiwa kama taarifa sahihi.
Ukokotoaji Ushuru
wa Huduma 7. Halmashauri kwa kuzingatia taarifa zilizowasilishwa
kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Sheria Ndogo hizi
itakokotoa na kutoza Ushuru wa Huduma.
Makosa 8. Itakuwa ni kosa kwa kampuni au tawi la kampuni,
taasisi ya biashara, mfanyabiashara:-
(1) kushindwa kuwasilisha taarifa sahihi ndani ya
muda ulioainishwa kwa mujibu wa Sheria Ndogo hizi.
(2) kuwasilisha taarifa zisizo sahihi.
(3) kutolipa Ushuru wa Huduma.
(4) kutolipa kwa wakati Ushuru wa Huduma ndani ya
muda uliowekwa na Sheria Ndogo hizi.
(5) atashawishi kampuni, tawi la kampuni, taasisi ya
biashara au mfanyabiashara kukataa au kukwepa
kulipa Ushuru wa Huduma.
(6) atamzuia mtumishi wa Halmashauri kutekeleza
majukumu aliyopewa kwa mujibu wa Sheria
Ndogo hizi.
Adhabu 9. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na masharti ya
Sheria Ndogo hizi atakuwa ametenda kosa, na
akipatikana na hatia atatozwa faini isiyopungua
shilingi laki mbili (200,000/=) na isiyozidi shilingi
milioni moja (1,000,000/=) au kifungo kisichopungua
miezi kumi na mbili na kisichozidi miezi ishirini na
nne au vyote kwa pamoja.
Kufifilisha kosa 10. Mkurugenzi anaweza kumtoza mtu yeyote faini
isiyopungua shilingi laki mbili (200,000/=) na
isiyozidi Shilingi laki tano (500,000/=), iwapo mkosaji
kwa hiari yake mwenyewe atakiri kosa kwa maandishi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
177
na kukubali kulipa faini anayodaiwa.
_______
JEDWALI
_______
KUFIFILISHA KOSA
Limetungwa Chini ya kifungu cha 10
Mimi ………………………………………………wa S.L.P……………….……….. nakiri
KWA HIYARI YANGU MWENYEWE mbele
ya……………………………………..ambaye ni mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kwamba mnamo tarehe……ya
Mwezi….Mwaka………nilitenda kosa la kukiuka masharti ya kifungu cha …………..cha
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za mwaka 2017.
Kwa mamlaka aliyopewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri.Niko tayari kulipa kiasi
cha Ada na Ushuru ninaodaiwa pamoja na faini.
NATHIBITISHA KWAMBA MAELEZO HAPO JUU NI YA KWELI NA NIMEYATOA
KWA HIYARI YANGU KWA KADIRI YA UFAHAMU WANGU
Leo tarehe……………..ya mwezi……………mwaka……………………
Jina……………………………..…………………………...Saini……………………........
Mbele ya:
Jina……………………………..……………….
Saini…………………………………….…........
Wadhifa………………………………………
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
178
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANGAZO LA SERIKALI NA. 390 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA FEDHA YA SERIKALI ZA MITAA
(SURA YA 290)
________
SHERIA NDOGO
_______
(Zimetungwa chini ya kifungu cha 7(1) na 16(1))
________
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
179
SHERIA NDOGO ZA (USHURU WA MASOKO) ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI ZA MWAKA
2017
Jina na tarehe ya
kuanza kutumika 1. Sheria Ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo
za (Ushuru wa Masoko) za Halmashauri ya Wilaya
ya Masasi, 2017 na zitaanza kutumika mara baada
ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Matumizi 2.
Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo lote lililo
chini ya mamlaka ya Halmashauri ya wilaya ya
Masasi..
Tafsiri
3.
Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa itakapoelezwa
vinginevyo:-
“Afisa Mwidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote
aliyeteuliwa kusimamia utekelezaji wa Sheria
Ndogo hizi;
“Dalali” maana yake ni mtu yeyote anayeuza bidhaa
za sokoni kwa njia ya mnada kwa niaba ya mwenye
bidhaa kwa mujibu wa Sheria na taratibu za soko;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya
wilaya ya Masasi;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
180
”Kibali” maana yake ni idhini ya maandishi
inayotolewa na Mkuu wa Masoko kwa mujibu wa
Sheria Ndogo hizi;
“Masoko” maana yake ni masoko yanayomilikiwa
na Halmashauri;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa
Halmashauri pamoja na Afisa yeyote
atakayeteuliwa kutekeleza majukumu ya
Mkurugenzi;
“Mfanyabiashara” maana yake ni mtu yeyote
anayeuza bidhaa sokoni kwa jumla au rejareja
kwenye eneo ambalo limeruhusiwa kwa mujibu wa
Sheria Ndogo hizi;
Mkuu wa Masoko” maana yake ni mtu yeyote
aliyeteuliwa na Halmashauri kusimamia shughuli
zote katika soko/masoko;
“Wakala” maana yake ni mtu yeyote, taasisi au
kikundi cha watu aliyeteuliwa na Halmashauri
kusimamia Sheria Ndogo hizi;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
181
“Wadau wa Soko” maana yake ni wafanyabiashara
binafsi, vikundi au vyama vya ushirika vinavyofanya
shughuli za biashara katika soko;
Usimamizi wa
Masoko
4.(1)
(2)
Masoko yote yaliyoko katika eneo la Halmashauri
yatakuwa chini ya usimamizi Halmashauri.
Halmashauri itakuwa na wajibu wa:-
(a) kuendeleza masoko; (b) kusimamia usafi na ulinzi na usalama wa
masoko; (c) kusimamia ufikishaji wa huduma za
umeme, maji na huduma nyingine za kijamii katika masoko.
Mkuu wa Masoko
5.
Kutakuwa na Mkuu wa masoko atakayeteuliwa na
Halmashauri kusimamia shughuli za uendeshaji wa
soko pamoja na:-
(a) kukusanya ada na ushuru mbalimbali kama zilivyoainishwa kwenye jedwali la pili la Sheria Ndogo hizi;
(b) kuimarisha huduma za ulinzi, maji na umeme katika soko;
(c) kusimamia na kupitia usajili wa wadau wa soko kwa kushirikiana na Kamati ya soko;
(d) kusimamia usafi na uondoshaji wa taka katika soko;
(e) kuhakikisha kuwa biashara hazifanywi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
182
kwenye eneo ambalo haliruhusiwi kwa shughuli hiyo;
(f) kutekeleza majukumu mengine yoyote atakayoagizwa na Halmashauri.
Uteuzi wa Wakala 6. (1) Halmashauri inaweza kumteua wakala ambaye
atawajibika katika uendeshaji wa soko kwa niaba ya
Halmashauri.
(2)
Wakala atakayeteuliwa kwa mujibu wa Sheria
Ndogo hizi atasimamia shughuli za uendeshaji wa
soko kwa kipindi alichopangiwa kuanzia tarehe ya
uteuzi wake.
Kamati ya Wadau
wa soko 7. (1) Kutakuwa na Kamati ya Wadau wa soko ambayo
itaundwa na Wadau kwa mujibu wa Sheria Ndogo
hizi.
(2) Wajumbe wa Kamati ya Wadau wa soko watakuwa
ni Mwenyekiti na Katibu kutoka kwenye kila kikundi
cha Ushirika ndani ya soko.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
183
Usajili wa Wadau (3) Wadau wote watasajiliwa na Mkuu wa soko
akishirikiana na kamati ya soko.
Vikao vya Kamati ya
wadau wa soko
8. (1)
(2)
Kutakuwa na kikao cha Kamati ya wadau wa soko
kitakachofanyika mara moja kila mwezi.
Mkuu wa Soko atakuwa Katibu katika vikao vyote
vya Kamati ya wadau wa Soko.
Kazi za Kamati ya
Wadau wa soko
9.
Kazi za Kamati ya Wadau wa soko zitakuwa ni;-
(a) kuhakiki biashara na utendaji wa soko; (b) kuboresha ustawi wa wanachama wa
vyama vya ushirika; (c) kuhakikisha kuwepo nidhamu katika
shughuli za soko; (d) kukuza na kuendeleza mfumo wa biashara; (e) kutekeleza kazi zingine watakazoelekezwa
na Mkuu wa soko.
Kuundwa Kamati
ndogo
10.
Kamati ya Wadau wa soko itaunda Kamati ndogo
zenye wajumbe watatu (3) kutoka miongoni mwa
wajumbe wa Kamati ya wadau wa soko ambazo ni:-
(a) Kamati ndogo ya miundo mbinu na usafi; (b) Kamati ndogo ya biashara na utawala; (c) Kamati ndogo ya Ulinzi na Usalama.
Usajili wa
Wafanyabiashara wote wa soko watatakiwa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
184
Wafanyabiashara 11. (1) kusajiliwa na Mkuu wa soko kwa kushirikiana na
Kamati ya wadau wa soko.
(2)
Itakuwa ni marufuku kwa mfanyabiashara
asiyesajiliwa kufanyabiashara ndani ya soko bila
kuwa na idhini ya maandishi kutoka kwa Mkuu wa
Soko.
Usajili wa Wadau Kutakuwa na Usajili wa Wadau wa Soko kwa lengo
la kuwatambua na kuorodhesha Wadau kwenye
rejista maalum.
Kibali cha
watumiaji wengine.
12. (1)
Mfanyabiashara yeyote ambaye anataka kufanya
biashara ambayo awali haikuwapo au haikuwa na
eneo ndani ya soko ataomba kibali kwa Mkuu wa
soko.
(2)
Kibali hicho kitatolewa kwa mwombaji baada ya
kulipa ada na kitadumu kwa muda wa mwaka
mmoja toka siku ya kupewa. Endapo
mfanyabiashara atataka kuendelea
kufanyabiashara katika soko atatakiwa kuomba
tena kibali kingine kwa Mkuu wa soko.
Kufuta kibali 13 Mkuu wa soko kwa kuagizwa na kamati anaweza
kufuta kibali kilichotolewa chini ya Sheria Ndogo
hizi endapo mwenye kibali hicho:-
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
185
(a) atakuwa na malimbikizo ya madeni ya kodi au ushuru;
(b) atakuwa amesimamisha shughuli zake kwa muda wa zaidi ya miezi mitatu bila ya taarifa;
(c) atakuwa amekiuka masharti ya Sheria Ndogo hizi hata baada ya kuonywa;
(d) atawashawishi wafanyabiashara wengine kutofuata Sheria Ndogo hizi na kusababisha uvunjifu wa amani.
Saa za kazi 14. (1) Soko litakuwa wazi siku zote kuanzia saa kumi na
mbili kamili asubuhi hadi saa kumi na mbili kamili
jioni.
(2)
Mkuu wa soko kwa kushirikiana na Kamati ya
wadau wanaweza kufunga soko kwa ajili ya
matengenezo na sababu nyingine yoyote ya
dharura pale itakapoonekana inafaa ili mradi watoe
taarifa ya maandishi kwa Mkurugenzi na kupata
idhini.
Udhibiti wa
nidhamu sokoni
15. Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote:-
(a) kubandika Tangazo au kubandua tangazo lolote bila ya idhini ya Mkuu wa Soko;
(b) kuweka bendera za Vyama vya Siasa ndani ya eneo la soko;
(c) kufanya shughuli za kisiasa ndani ya Soko. (d) kuharibu miundombinu ya soko;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
186
(e) kutumia lugha ya matusi ndani ya soko; (f) kufanya shughuli yoyote kwenye eneo
ambalo haliruhusiwi au halijajengwa kwa shughuli hiyo;
(g) kupangisha kizimba au eneo la biashara kwa mfanyabiashara mwingine;
(h) kufanya biashara nje ya eneo la soko; (i) kutupa taka ovyo na kutiririsha maji
machafu.
Usafi wa soko
16. (1)
(2)
(3)
(4)
Kila mfanyabiashara anayefanya shughuli za
biashara katika soko atawajibika kuweka eneo lake
katika hali ya usafi wakati wote au kugharamia
shughuli hiyo kwa njia yoyote ile.
Mkuu wa Soko kwa kushirikiana na Kamati ya
Wadau wa soko watapanga siku na muda wa
kufunga soko mara moja kwa juma kwa ajili ya
kufanya usafi wa jumla katika eneo lote la soko.
Kila mfanyabiashara katika soko atatakiwa kushiriki
katika usafi wa jumla wa soko bila kukosa.
Kila mfanyabiashara sokoni atatakiwa kufuata
Kanuni za afya.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
187
Uingizaji wa bidhaa
sokoni 17. (1)
(2)
Bidhaa zote zinazoingizwa katika soko zitatakiwa
kuhifadhiwa kwenye makasha maalum ya
kusafirisha bidhaa.
Itakuwa ni marufuku kwa mkulima, mfanya-
biashara, Dalali au mtu mwingine yeyote kuingiza
bidhaa sokoni zilizofungwa na majani.
(3) Mtu yeyote atakaye ingiza bidhaa sokoni zilizo-
fungwa kwa majani atakuwa ametenda kosa.
Ukusanyaji wa Kodi,
Ada na ushuru.
18. (1)
(2)
Mkuu wa soko atakuwa ndiye msimamizi Mkuu wa
ukusanyaji wa mapato yote ya soko.
Mfanyabiashara yeyote sokoni atatakiwa kulipa
kodi, Ada na ushuru kwa Halmashauri au wakala
wake kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali la pili la
Sheria Ndogo hizi.
Ada ya kupangisha
eneo 19. (1) Halmashauri itatoza ada ya kupanga eneo la
biashara ambayo italipwa na Mfanyabiashara
yeyote aliyesajiliwa kufanya biashara katika eneo la
soko.
(2)
Ada hiyo italipwa kwa Halmashauri au wakala kama
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
188
inavyoonekana kwenye jedwali la pili la Sheria
Ndogo hizi.
Ushuru wa jokofu
20.
Mtu yeyote atakayetumia chumba cha baridi au
jokofu kwa kuhifadhia bidhaa ndani ya eneo la soko
atalipa ushuru kwa Halmashauri au wakala kwa ajili
ya kutumia sehemu hiyo kwa viwango
vitakavyoamuliwa na Halmashauri.
Malipo ya Ada/
Ushuru kwa wakati. 21. Mtu yeyote atakayeshindwa kulipa ada au ushuru
katika muda uliopangwa atalipa ada hiyo au ushuru
huo pamoja na tozo la asilimia ishirini na tano
(25%) ya kiasi anachodaiwa.
Huduma ya usafi,
ulinzi, maji na
umeme
22.
Kila mfanyabiashara katika soko atawajibika
kugharamia huduma ya ulinzi, usafi, maji na
umeme kulingana na mahitaji yake kila mwezi
kufuatana na utaratibu utakaowekwa na Kamati ya
Wadau wa Soko.
Ushuru wa kupakua
na kupakia mizigo
23.(1)
Kutakuwa na ushuru utakaotozwa kwa kila gari
litakaloingia ndani ya eneo la soko au barabara za
soko kwa ajili ya kupakuwa au kupakia bidhaa kama
ilivyoainishwa kwenye Jedwali la piIi la Sheria
Ndogo hizi.
Magari yataruhusiwa kuingia katika eneo la soko
kwa lengo la kushusha au kupakia bidhaa kuanzia
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
189
(2) saa 12.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
Adhabu 24. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na masharti
ya Sheria Ndogo hizi atakuwa ametenda kosa na
akipatikana na hatia atatozwa faini isiyopungua
shilingi laki mbili (200,000/=) na isiyozidi shillingi
milioni moja (Tsh. 1,000,000) au kifungo
kisichopungua miezi kumi na mbili na kisichozidi
miezi ishirini na nne au vyote kwa pamoja.
Uwezo wa
kufifilisha kosa 25.
Mkurugenzi anaweza kumtoza faini isiyopungua
shillingi laki mbili (Tsh. 200,000) na isiyozidi shilingi
laki tano (500,000) mtu yeyote aliyetenda kosa na
kukiri kwa maandishi na kukubali kulipa faini na
kiasi cha ada au ushuru anaodaiwa kwa kujaza
fomu iliyoambatanishwa kwenye jedwali la tatu la
Sheria Ndogo hizi.
______
JEDWALI LA KWANZA
______
KIBALI CHA KUTUMIA SOKO
1. Jina la mwombaji ...................... ……………………………………………
2. Anuani ya mwombaji......................................................................................
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
190
3. Kibali cha …………………………………………………………………….
4. Eneo ambalo kibali hicho kitatumika………………………………………….
5. Muda wa kibali ni kuanzia tarehe……………………hadi tarehe……………..
6. Masharti ya kutumia kibali hicho;
(a) …………………………………….
(b) …………………………………….
(c) ……………………………………..
(d) ……………………………………..
(e) ………………………………………
6. Tarehe ya kikao iliyoidhinisha kibali …………………………………………….
Muhtasari No. …………
7. Imesainiwa na:
Jina …………………………….. Jina ……………………………..
Saini …………………………… Saini …………………………
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
191
Mkuu wa Soko
Mwombaji
Tarehe ………………………. Tarehe …………………………..
Mhuri;
______
JEDWALI LA PILI
______
(limeundwa chini ya kifungu cha 18(2))
Na. Aina ya chanzo cha mapato Kiwango kwa
siku cha ushuru
Ada kwa mwezi
1. Mkungu wa ndizi 50.00
2.
Vibanda
100.00
5,000/=
3.
Bucha
200.00
50,000/=
4.
Vizimba
100.00
5,000/=
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
192
5. Wapanga chini 100.00
6.
Vizimba vya kuku
200.00
5,000/=
7.
Kukwangua makongoro/Vichwa
100.00
7,000/=
9.
Kizimba cha nazi
100.00
7,000/=
10.
Gunia, Tenga au Kiroba
100.00
11.
Maduka
200.00
50,000/=
12.
Nafaka
200.00
30,000/=
13.
Simu
200.00
5,000/=
12.
Jengo la lishe
5,000.00
50,000.00
13.
Eneo la matenga
10,000.00
50,000.00
14.
Banda la vichwa na miguu ya ng’ombe
10,000.00
100,000.00
15.
Machinjio ya kuku
50,000.00
150,000.00
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
193
16. Hifadhi ya mizigo 50,000.00 150,000.00
17.
Ofisi ndani ya soko
10,000.00
50,000.00
19. Kupakuwa na kupakia mizigo
1. Tani “0 hadi 3” 2. Tani “3 hadi 6” 3. Tani “6 hadi 10” 4. Tani “10 na kuendelea
______
JEDWALI LA TATU
______
(Limetungwa chini ya kifungu 25)
Mimi …………………… nakiri mbele ya ………….ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashuri ya Wilaya ya Masasi, kwamba mnamo tarehe …… ya Mwezi ……. Mwaka ……
nilitenda kosa la kukiuka masharti ya kifungu cha …… cha Sheria Ndogo za (Ushuru wa
masoko) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za Mwaka 2017.
Kwa Mamlaka aliyopewa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Niko tayari kulipa kiasi
cha Ada/ Ushuru ninaodaiwa pamoja na faini.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
194
NATHIBITISHA KWAMBA MAELEZO HAPO JUU NI YA KWELI NA NIMEYATOA KWA
HIARI YANGU KADRI YA UFAHAMU WANGU
Leo tarehe…………. ya Mwezi………… Mwaka ………………….
Jina……………………………….. Saini…………………………………….
Mbele ya :
Jina: ……………………………………………
Cheo: ………………………………………….
Saini: …………………………………………..
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
195
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANGAZO LA SERIKALI NA. 390 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA FEDHA YA SERIKALI ZA MITAA
(SURA YA 290)
________
SHERIA NDOGO
_______
(Zimetungwa chini ya kifungu cha 7(1) na 16(1))
________
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
196
SHERIA NDOGO ZA (USHURU WA MASOKO) ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI ZA MWAKA
2017
Jina na tarehe ya
kuanza kutumika 1. Sheria Ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo
za (Ushuru wa Masoko) za Halmashauri ya Wilaya
ya Masasi, 2017 na zitaanza kutumika mara baada
ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Matumizi 2.
Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo lote lililo
chini ya mamlaka ya Halmashauri ya wilaya ya
Masasi..
Tafsiri
3.
Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa itakapoelezwa
vinginevyo:-
“Afisa Mwidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote
aliyeteuliwa kusimamia utekelezaji wa Sheria
Ndogo hizi;
“Dalali” maana yake ni mtu yeyote anayeuza bidhaa
za sokoni kwa njia ya mnada kwa niaba ya mwenye
bidhaa kwa mujibu wa Sheria na taratibu za soko;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya
wilaya ya Masasi;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
197
”Kibali” maana yake ni idhini ya maandishi
inayotolewa na Mkuu wa Masoko kwa mujibu wa
Sheria Ndogo hizi;
“Masoko” maana yake ni masoko yanayomilikiwa
na Halmashauri;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa
Halmashauri pamoja na Afisa yeyote
atakayeteuliwa kutekeleza majukumu ya
Mkurugenzi;
“Mfanyabiashara” maana yake ni mtu yeyote
anayeuza bidhaa sokoni kwa jumla au rejareja
kwenye eneo ambalo limeruhusiwa kwa mujibu wa
Sheria Ndogo hizi;
Mkuu wa Masoko” maana yake ni mtu yeyote
aliyeteuliwa na Halmashauri kusimamia shughuli
zote katika soko/masoko;
“Wakala” maana yake ni mtu yeyote, taasisi au
kikundi cha watu aliyeteuliwa na Halmashauri
kusimamia Sheria Ndogo hizi;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
198
“Wadau wa Soko” maana yake ni wafanyabiashara
binafsi, vikundi au vyama vya ushirika vinavyofanya
shughuli za biashara katika soko;
Usimamizi wa
Masoko
4.(1)
(2)
Masoko yote yaliyoko katika eneo la Halmashauri
yatakuwa chini ya usimamizi Halmashauri.
Halmashauri itakuwa na wajibu wa:-
(d) kuendeleza masoko; (e) kusimamia usafi na ulinzi na usalama wa
masoko; (f) kusimamia ufikishaji wa huduma za
umeme, maji na huduma nyingine za kijamii katika masoko.
Mkuu wa Masoko
5.
Kutakuwa na Mkuu wa masoko atakayeteuliwa na
Halmashauri kusimamia shughuli za uendeshaji wa
soko pamoja na:-
(g) kukusanya ada na ushuru mbalimbali kama zilivyoainishwa kwenye jedwali la pili la Sheria Ndogo hizi;
(h) kuimarisha huduma za ulinzi, maji na umeme katika soko;
(i) kusimamia na kupitia usajili wa wadau wa soko kwa kushirikiana na Kamati ya soko;
(j) kusimamia usafi na uondoshaji wa taka katika soko;
(k) kuhakikisha kuwa biashara hazifanywi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
199
kwenye eneo ambalo haliruhusiwi kwa shughuli hiyo;
(l) kutekeleza majukumu mengine yoyote atakayoagizwa na Halmashauri.
Uteuzi wa Wakala 6. (1) Halmashauri inaweza kumteua wakala ambaye
atawajibika katika uendeshaji wa soko kwa niaba ya
Halmashauri.
(2)
Wakala atakayeteuliwa kwa mujibu wa Sheria
Ndogo hizi atasimamia shughuli za uendeshaji wa
soko kwa kipindi alichopangiwa kuanzia tarehe ya
uteuzi wake.
Kamati ya Wadau
wa soko 7. (1) Kutakuwa na Kamati ya Wadau wa soko ambayo
itaundwa na Wadau kwa mujibu wa Sheria Ndogo
hizi.
(2) Wajumbe wa Kamati ya Wadau wa soko watakuwa
ni Mwenyekiti na Katibu kutoka kwenye kila kikundi
cha Ushirika ndani ya soko.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
200
Usajili wa Wadau (3) Wadau wote watasajiliwa na Mkuu wa soko
akishirikiana na kamati ya soko.
Vikao vya Kamati ya
wadau wa soko
8. (1)
(2)
Kutakuwa na kikao cha Kamati ya wadau wa soko
kitakachofanyika mara moja kila mwezi.
Mkuu wa Soko atakuwa Katibu katika vikao vyote
vya Kamati ya wadau wa Soko.
Kazi za Kamati ya
Wadau wa soko
9.
Kazi za Kamati ya Wadau wa soko zitakuwa ni;-
(f) kuhakiki biashara na utendaji wa soko; (g) kuboresha ustawi wa wanachama wa
vyama vya ushirika; (h) kuhakikisha kuwepo nidhamu katika
shughuli za soko; (i) kukuza na kuendeleza mfumo wa biashara; (j) kutekeleza kazi zingine watakazoelekezwa
na Mkuu wa soko.
Kuundwa Kamati
ndogo
10.
Kamati ya Wadau wa soko itaunda Kamati ndogo
zenye wajumbe watatu (3) kutoka miongoni mwa
wajumbe wa Kamati ya wadau wa soko ambazo ni:-
(d) Kamati ndogo ya miundo mbinu na usafi; (e) Kamati ndogo ya biashara na utawala; (f) Kamati ndogo ya Ulinzi na Usalama.
Usajili wa
Wafanyabiashara wote wa soko watatakiwa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
201
Wafanyabiashara 11. (1) kusajiliwa na Mkuu wa soko kwa kushirikiana na
Kamati ya wadau wa soko.
(2)
Itakuwa ni marufuku kwa mfanyabiashara
asiyesajiliwa kufanyabiashara ndani ya soko bila
kuwa na idhini ya maandishi kutoka kwa Mkuu wa
Soko.
Usajili wa Wadau Kutakuwa na Usajili wa Wadau wa Soko kwa lengo
la kuwatambua na kuorodhesha Wadau kwenye
rejista maalum.
Kibali cha
watumiaji wengine.
12. (1)
Mfanyabiashara yeyote ambaye anataka kufanya
biashara ambayo awali haikuwapo au haikuwa na
eneo ndani ya soko ataomba kibali kwa Mkuu wa
soko.
(2)
Kibali hicho kitatolewa kwa mwombaji baada ya
kulipa ada na kitadumu kwa muda wa mwaka
mmoja toka siku ya kupewa. Endapo
mfanyabiashara atataka kuendelea
kufanyabiashara katika soko atatakiwa kuomba
tena kibali kingine kwa Mkuu wa soko.
Kufuta kibali 13 Mkuu wa soko kwa kuagizwa na kamati anaweza
kufuta kibali kilichotolewa chini ya Sheria Ndogo
hizi endapo mwenye kibali hicho:-
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
202
(e) atakuwa na malimbikizo ya madeni ya kodi au ushuru;
(f) atakuwa amesimamisha shughuli zake kwa muda wa zaidi ya miezi mitatu bila ya taarifa;
(g) atakuwa amekiuka masharti ya Sheria Ndogo hizi hata baada ya kuonywa;
(h) atawashawishi wafanyabiashara wengine kutofuata Sheria Ndogo hizi na kusababisha uvunjifu wa amani.
Saa za kazi 14. (1) Soko litakuwa wazi siku zote kuanzia saa kumi na
mbili kamili asubuhi hadi saa kumi na mbili kamili
jioni.
(2)
Mkuu wa soko kwa kushirikiana na Kamati ya
wadau wanaweza kufunga soko kwa ajili ya
matengenezo na sababu nyingine yoyote ya
dharura pale itakapoonekana inafaa ili mradi watoe
taarifa ya maandishi kwa Mkurugenzi na kupata
idhini.
Udhibiti wa
nidhamu sokoni
15. Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote:-
(j) kubandika Tangazo au kubandua tangazo lolote bila ya idhini ya Mkuu wa Soko;
(k) kuweka bendera za Vyama vya Siasa ndani ya eneo la soko;
(l) kufanya shughuli za kisiasa ndani ya Soko. (m) kuharibu miundombinu ya soko;
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
203
(n) kutumia lugha ya matusi ndani ya soko; (o) kufanya shughuli yoyote kwenye eneo
ambalo haliruhusiwi au halijajengwa kwa shughuli hiyo;
(p) kupangisha kizimba au eneo la biashara kwa mfanyabiashara mwingine;
(q) kufanya biashara nje ya eneo la soko; (r) kutupa taka ovyo na kutiririsha maji
machafu.
Usafi wa soko
16. (1)
(2)
(3)
(4)
Kila mfanyabiashara anayefanya shughuli za
biashara katika soko atawajibika kuweka eneo lake
katika hali ya usafi wakati wote au kugharamia
shughuli hiyo kwa njia yoyote ile.
Mkuu wa Soko kwa kushirikiana na Kamati ya
Wadau wa soko watapanga siku na muda wa
kufunga soko mara moja kwa juma kwa ajili ya
kufanya usafi wa jumla katika eneo lote la soko.
Kila mfanyabiashara katika soko atatakiwa kushiriki
katika usafi wa jumla wa soko bila kukosa.
Kila mfanyabiashara sokoni atatakiwa kufuata
Kanuni za afya.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
204
Uingizaji wa bidhaa
sokoni 17. (1)
(2)
Bidhaa zote zinazoingizwa katika soko zitatakiwa
kuhifadhiwa kwenye makasha maalum ya
kusafirisha bidhaa.
Itakuwa ni marufuku kwa mkulima, mfanya-
biashara, Dalali au mtu mwingine yeyote kuingiza
bidhaa sokoni zilizofungwa na majani.
(3) Mtu yeyote atakaye ingiza bidhaa sokoni zilizo-
fungwa kwa majani atakuwa ametenda kosa.
Ukusanyaji wa Kodi,
Ada na ushuru.
18. (1)
(2)
Mkuu wa soko atakuwa ndiye msimamizi Mkuu wa
ukusanyaji wa mapato yote ya soko.
Mfanyabiashara yeyote sokoni atatakiwa kulipa
kodi, Ada na ushuru kwa Halmashauri au wakala
wake kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali la pili la
Sheria Ndogo hizi.
Ada ya kupangisha
eneo 19. (1) Halmashauri itatoza ada ya kupanga eneo la
biashara ambayo italipwa na Mfanyabiashara
yeyote aliyesajiliwa kufanya biashara katika eneo la
soko.
(2)
Ada hiyo italipwa kwa Halmashauri au wakala kama
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
205
inavyoonekana kwenye jedwali la pili la Sheria
Ndogo hizi.
Ushuru wa jokofu
20.
Mtu yeyote atakayetumia chumba cha baridi au
jokofu kwa kuhifadhia bidhaa ndani ya eneo la soko
atalipa ushuru kwa Halmashauri au wakala kwa ajili
ya kutumia sehemu hiyo kwa viwango
vitakavyoamuliwa na Halmashauri.
Malipo ya Ada/
Ushuru kwa wakati. 21. Mtu yeyote atakayeshindwa kulipa ada au ushuru
katika muda uliopangwa atalipa ada hiyo au ushuru
huo pamoja na tozo la asilimia ishirini na tano
(25%) ya kiasi anachodaiwa.
Huduma ya usafi,
ulinzi, maji na
umeme
22.
Kila mfanyabiashara katika soko atawajibika
kugharamia huduma ya ulinzi, usafi, maji na
umeme kulingana na mahitaji yake kila mwezi
kufuatana na utaratibu utakaowekwa na Kamati ya
Wadau wa Soko.
Ushuru wa kupakua
na kupakia mizigo
23.(1)
Kutakuwa na ushuru utakaotozwa kwa kila gari
litakaloingia ndani ya eneo la soko au barabara za
soko kwa ajili ya kupakuwa au kupakia bidhaa kama
ilivyoainishwa kwenye Jedwali la piIi la Sheria
Ndogo hizi.
Magari yataruhusiwa kuingia katika eneo la soko
kwa lengo la kushusha au kupakia bidhaa kuanzia
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
206
(2) saa 12.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
Adhabu 24. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na masharti
ya Sheria Ndogo hizi atakuwa ametenda kosa na
akipatikana na hatia atatozwa faini isiyopungua
shilingi laki mbili (200,000/=) na isiyozidi shillingi
milioni moja (Tsh. 1,000,000) au kifungo
kisichopungua miezi kumi na mbili na kisichozidi
miezi ishirini na nne au vyote kwa pamoja.
Uwezo wa
kufifilisha kosa 25.
Mkurugenzi anaweza kumtoza faini isiyopungua
shillingi laki mbili (Tsh. 200,000) na isiyozidi shilingi
laki tano (500,000) mtu yeyote aliyetenda kosa na
kukiri kwa maandishi na kukubali kulipa faini na
kiasi cha ada au ushuru anaodaiwa kwa kujaza
fomu iliyoambatanishwa kwenye jedwali la tatu la
Sheria Ndogo hizi.
______
JEDWALI LA KWANZA
______
KIBALI CHA KUTUMIA SOKO
1. Jina la mwombaji ...................... ……………………………………………
2. Anuani ya mwombaji......................................................................................
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
207
3. Kibali cha …………………………………………………………………….
4. Eneo ambalo kibali hicho kitatumika………………………………………….
5. Muda wa kibali ni kuanzia tarehe……………………hadi tarehe……………..
6. Masharti ya kutumia kibali hicho;
(f) …………………………………….
(g) …………………………………….
(h) ……………………………………..
(i) ……………………………………..
(j) ………………………………………
6. Tarehe ya kikao iliyoidhinisha kibali …………………………………………….
Muhtasari No. …………
7. Imesainiwa na:
Jina …………………………….. Jina ……………………………..
Saini …………………………… Saini …………………………
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
208
Mkuu wa Soko
Mwombaji
Tarehe ………………………. Tarehe …………………………..
Mhuri;
______
JEDWALI LA PILI
______
(limeundwa chini ya kifungu cha 18(2))
Na. Aina ya chanzo cha mapato Kiwango kwa
siku cha ushuru
Ada kwa mwezi
1. Mkungu wa ndizi 50.00
2.
Vibanda
100.00
5,000/=
3.
Bucha
200.00
50,000/=
4.
Vizimba
100.00
5,000/=
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
209
5. Wapanga chini 100.00
6.
Vizimba vya kuku
200.00
5,000/=
7.
Kukwangua makongoro/Vichwa
100.00
7,000/=
9.
Kizimba cha nazi
100.00
7,000/=
10.
Gunia, Tenga au Kiroba
100.00
11.
Maduka
200.00
50,000/=
12.
Nafaka
200.00
30,000/=
13.
Simu
200.00
5,000/=
12.
Jengo la lishe
5,000.00
50,000.00
13.
Eneo la matenga
10,000.00
50,000.00
14.
Banda la vichwa na miguu ya ng’ombe
10,000.00
100,000.00
15.
Machinjio ya kuku
50,000.00
150,000.00
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
210
16. Hifadhi ya mizigo 50,000.00 150,000.00
17.
Ofisi ndani ya soko
10,000.00
50,000.00
19. Kupakuwa na kupakia mizigo
5. Tani “0 hadi 3” 6. Tani “3 hadi 6” 7. Tani “6 hadi 10” 8. Tani “10 na kuendelea
______
JEDWALI LA TATU
______
(Limetungwa chini ya kifungu 25)
Mimi …………………… nakiri mbele ya ………….ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashuri ya Wilaya ya Masasi, kwamba mnamo tarehe …… ya Mwezi ……. Mwaka ……
nilitenda kosa la kukiuka masharti ya kifungu cha …… cha Sheria Ndogo za (Ushuru wa
masoko) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za Mwaka 2017.
Kwa Mamlaka aliyopewa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Niko tayari kulipa kiasi
cha Ada/ Ushuru ninaodaiwa pamoja na faini.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
211
NATHIBITISHA KWAMBA MAELEZO HAPO JUU NI YA KWELI NA NIMEYATOA KWA
HIARI YANGU KADRI YA UFAHAMU WANGU
Leo tarehe…………. ya Mwezi………… Mwaka ………………….
Jina……………………………….. Saini…………………………………….
Mbele ya :
Jina: ……………………………………………
Cheo: ………………………………………….
Saini: …………………………………………..
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
212
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANGAZO LA SERIKALI NA. 393 la tarehe 29/09/2017
SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA)
(SURA YA 287)
________
SHERIA NDOGO ________
Zimetungwa chini ya kifungu cha 153(1)
________
SHERIA NDOGO ZA (UTUNZAJI WA BARABARA) ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI ZA
MWAKA, 2017
Jina na
mwanzo wa
kuanza
kutumika
1. Sheria Ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo za
(Utunzaji wa Barabara) za Halmashauri ya Wilaya ya
Masasi za Mwaka 2017 na zitaanza kutumika baada ya
kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
213
Matumizi 2. Sheria Ndogo hizi zitatumika katika eneo lote lililipo
chini ya mamlaka ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.
Tafsiri
3. Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa pale
itakapoelekezwa vinginevyo:-
“Afisa Muidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote
atakayeteuliwa na Halmashauri kusimamia
utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi;
“Barabara” Maana yake ni Barabara zote zinazopitika
kwa Watu na magari katika eneo lote la
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi;
“Eneo la Barabara” maana yake ni sawa na iliyotajwa
kwenye kifungu cha 6 cha Sheria Ndogo hizi;
“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Wilaya
ya Masasi;
“Kijiji” maana yake ni Kijiji kilichoanzishwa na
kusajiliwa kwa mujibu wa kifungu cha 22 cha
Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya)
Sura ya 287;
“Mifugo” maana yake itajumuisha Ng’ombe, Punda,
Kondoo, Mbuzi, mbwa na wanyama wengine
wafugwao na Binadamu;
“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi au Afisa yeyote
wa umma atakayeteuliwa kutekeleza majukumu
ya Mkurugenzi.
Wajibu wa 4. Halmashauri itakuwa na wajibu wa kuanzisha,
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
214
kuanzisha Barabara. kupandisha hadhi, au kukarabati Barabara katika
maeneo yaliyopo katika mamlaka yake ili kuwezesha
kufikika kwa urahisi kutoka eneo moja na jingine kwa
dhumuni la kurahisisha utoaji wa huduma kwa
Wananchi na kukuza uchumi.
Wajibu wa
kutunza
Barabara
5. (1) Itakuwa ni wa Halmashauri kuhakikisha kuwa
Barabara zote zilizo kwenye eneo lake zinatunzwa na
kuweza kupitika majira yote ya mwaka.
(2) Halmashauri itaweka taratibu za kufuatwa katika
utumiaji wa Barabara ikiwa ni pamoja na matakwa ya
kuzingatia alama za Barabarani, alama za uthibiti wa
uzito, kutumia maeneo maalumu ya kuvusha mifugo,
na kutekeleza maelekezo mengine yatakayotolewa na
Halmashauri.
Maeneo ya
hifadhi ya
Barabara
6. (1) Maeneo ya Hifadhi ya Barabara yatakuwa:-
(a) eneo la umbali wa mita kumi na mbili (12) kila upande kutoka katikati ya Barabara za Vijiji;
(b) eneo la umbali wa mita ishirini (20) kila upande kutoka katikati ya Barabara za Halmashauri;
(c) eneo la umbali wa mita thelathini (30) kila upande kutoka katikati ya Barabara za Mkoa.
(2) vipimo vya eneo la hifadhi ya Barabara vinaweza
kubadilika kutokana na kupanda hadhi kwa
Barabara husika au wakati wowote
itakapoelekezwa na Halmashauri.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
215
Utunzaji wa
madaraja 7. Halmashauri itaweka alama za uwepo wa daraja na
alama za uzito unaoruhusiwa kuvushwa katika daraja
kwa madhumuni ya kuepusha uwezekano wa kutokea
ajali na kutunza madaraja.
Mabango na
matangazo 8. Halmashauri itatoa idhini wa kuweka mabango au
kutangaza tangazo katika maeneo maalum ambapo
mabango au matangazo hayo hayatazuia muonekano
wa alama za barabarani, hayatawekwa kwenye
makutano ya barabara, kona, au mzunguko wa
barabara ambapo yatazuia muonekano mzuri wa
Barabara.
Uthibiti wa
Mifugo 9. Halmashauri itadhibiti matumizi ya barabara kwa
kutenga njia maalum za mifugo zitakazotumika
kwenda na kurudi kutoka malishoni au mnadani.
Makosa 10. Itakuwa ni kosa kwa mtu yeyote:-
(a) kujenga au kulima kwenye maeneo ya hifadhi ya Barabara;
(b) kupitisha kwenye barabara au daraja chombo chochote cha usafiri kilichozidi uzito unaotakiwa au ulioelekezwa kwenye vibao maalumu vya matumizi ya barabara au daraja;
(c) kupitisha mifugo ndani na kando ya Barabara; (d) kufanya biashara ndani ya eneo la Barabara; (e) kuburuza nondo au vitu vizito Barabarani;
(f) kutupa takataka Barabarani;
(g) kuendesha au kukokota chombo cha usafiri ambacho kinaweza kusababisha uharibifu wa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
216
namna yoyote wa barabara;
(h) kubeba mizigo ambayo itaning’inia, kumwagika au kuburuzwa barabarani na
(i) kufanya jambo lolote linaloweza kufanya uharibifu wa Barabara.
Notisi 11. (1) Halmashauri itampa notisi ya siku kumi na nne (14)
mtu yeyote aliyejenga, kulima au kufanya shughuli
yoyote ya kibinadamu kwenye maeneo ya hifadhi
ikimtaka Mtu huyo kubomoa jengo lake au kung’oa
mazao au kusitisha shughuli hiyo.
(2) Endapo Mhusika atashindwa kutekeleza masharti
ya kifungu kidogo cha (1) hapo juu; Halmashauri
itakuwa na uwezo wa kubomoa jengo hilo au kusitisha
shughuli au kung’oa mazao yaliyopandwa baada ya
kupata kibali cha Mahakama na kumtaka Mhusika
kulipa gharama ambazo Halmashauri imeingia.
Adhabu 12. Mtu yeyote atakakwenda kinyume na masharti ya
Sheria Ndogo hizi atakuwa ametenda kosa na
akipatikana na hatia atatozwa faini isiyozidi shilingi laki
tatu (300,000/=) au kifungo kisichozidi miezi kumi na
mbili (12) au adhabu zote mbili kwa pamoja yaani
faini na kifungo.
Kufifilisha kosa 13. Mkurugenzi anaweza kumtoza faini ya Shilingi Laki
Mbili (200,000/=) mtu yeyote endapo mkosaji kwa
hiari yake mwenyewe atakiri kosa kwa maandishi na
kukubali kulipa faini anayodaiwa.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
217
______
JEDWALI
______
HATI YA KUKIRI KOSA
(Chini ya kifungu cha 13)
Mimi………………………………………………………………………….….. kwa hiari yangu
mwenyewe nakiri mbele ya …………………………….……. Mkurugenzi wa Halmashauri
ya Wilaya ya Masasi kwamba mnamo tarehe……… ya mwezi
wa………………….mwaka……… . nilitenda kosa kwa kukiuka masharti ya kifungu
cha ……………….. cha Sheria Ndogo za (Utunzaji wa Barabara) Halmashauri ya
Wilaya ya Masasi za Mwaka 2017,
Nipo tayari kulipa kiasi cha faini ya Shilingi ……………….. ninachodaiwa ikiwa
Mkurugenzi ataamua kutekeleza mamlaka aliyopewa chini ya Sheria Ndogo hizi
kifungu cha 13.
Nathibitisha kwamba maelezo ya hapo juu ni ya kweli na nimeyatoa kwa hiari
yangu kadri ya ufahamu wangu.
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
218
Tarehe…………………………….. Sahihi…………………………
Mhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi umewekwa katika Lakiri ya Sheria
Ndogo hizi kufuatia Mkutano wa Baraza la Madiwani ulioketi Halmashauri leo
tarehe 29 mwezi 10 mwaka 2014 mbele ya Wafuatao:-
CHANGWA M. MKWAZU,
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
JUMA M. SATMAH,
Mwenyekiti
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
NAKUBALI
Dodoma, MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),
13 Julai, 2017 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
Sheria Ndogo za (Ada na Ushuru) za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi
Tangazo la Serikali Na. 391 (linaendelea…)
219