sura ya pili - web viewdata ilikusanywa katika jamii ya wagogo wanaoishi kata za kikuyu,...

25
SURA YA PILI MAPITIO YA VITABU NA MACHAPISHO 2.1 Utangulizi Sura hii itajadili marejeo ya vitabu na machapisho yanayohusiana na mada ya utafiti huu. Itaonesha mtazamo wa watalaam mbalimbali ulimwenguni kuhusu visasili. Kwa kufanya hivyo maana na fasili mbalimbali za visasili zitatolewa kama zilivyotolewa na watalaam hao. Sehemu ya kwanza ya sura hii ni utangulizi, inafuatiwa na sehemu ya pili, ambayo ni mapitio ya vitabu na machapisho na sehemu ya mwisho ni hitimisho. 2.2 Mapitio ya Vitabu na Machapisho Jamii zinazopatikana Afrika, kama jamii nyingine duniani, zina mila na amali zake. Mojawapo ya amali hizo ni fasihi. Fasihi ya Kiswahili, au tuseme ya Kiafrika, kwa ujumla imegawanyika katika makundi makubwa mawili, ambayo ni fasihi simulizi na fasihi andishi. Makundi haya yote mawili ya fasihi yamekuwa na athari kubwa katika maisha ya Watanzania na Waafrika kwa ujumla wake. Hivyo basi, fasihi ni chombo muhimu sana kwa jamii yoyote ile. Ni chombo kinachowezesha jamii kujua ilipotoka, ilipo na inakokwenda. Jamii isiyokuwa na fasihi ni jamii ambayo haijakamilika. Fasihi ya Kigogo kama ile ya Kiswahili imegawanyika katika sehemu mbili vile vile, ambazo ni fasihi simulizi na fasihi andishi. Makundi haya mawili ya fasihi kila kundi limegawanyika tena katika vipengele vingine vidogo vidogo vinavyoitwa tanzu. Fasihi simulizi ya Kigogo ni pana, imepevuka na ina idadi kubwa ya tanzu.

Upload: trinhdieu

Post on 30-Jan-2018

328 views

Category:

Documents


11 download

TRANSCRIPT

Page 1: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

SURA YA PILI

MAPITIO YA VITABU NA MACHAPISHO

2.1 Utangulizi

Sura hii itajadili marejeo ya vitabu na machapisho yanayohusiana na mada ya utafiti huu. Itaonesha

mtazamo wa watalaam mbalimbali ulimwenguni kuhusu visasili. Kwa kufanya hivyo maana na

fasili mbalimbali za visasili zitatolewa kama zilivyotolewa na watalaam hao. Sehemu ya kwanza

ya sura hii ni utangulizi, inafuatiwa na sehemu ya pili, ambayo ni mapitio ya vitabu na machapisho

na sehemu ya mwisho ni hitimisho.

2.2 Mapitio ya Vitabu na Machapisho

Jamii zinazopatikana Afrika, kama jamii nyingine duniani, zina mila na amali zake. Mojawapo ya

amali hizo ni fasihi. Fasihi ya Kiswahili, au tuseme ya Kiafrika, kwa ujumla imegawanyika katika

makundi makubwa mawili, ambayo ni fasihi simulizi na fasihi andishi. Makundi haya yote mawili

ya fasihi yamekuwa na athari kubwa katika maisha ya Watanzania na Waafrika kwa ujumla wake.

Hivyo basi, fasihi ni chombo muhimu sana kwa jamii yoyote ile. Ni chombo kinachowezesha

jamii kujua ilipotoka, ilipo na inakokwenda. Jamii isiyokuwa na fasihi ni jamii ambayo

haijakamilika. Fasihi ya Kigogo kama ile ya Kiswahili imegawanyika katika sehemu mbili vile

vile, ambazo ni fasihi simulizi na fasihi andishi. Makundi haya mawili ya fasihi kila kundi

limegawanyika tena katika vipengele vingine vidogo vidogo vinavyoitwa tanzu. Fasihi simulizi ya

Kigogo ni pana, imepevuka na ina idadi kubwa ya tanzu. Hata hivyo hakuna uchunguzi mwingi na

wa kina kuhusu fasihi simulizi. Mulokozi (1983) katika makala yake ya “Utafiti wa Fasihi

Simulizi” anaonesha umuhimu wa kufanya utafiti wa fasihi simulizi anasema:

Page 2: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Tukizingatia maelezo yetu yaliyotangulia kuhusu uhusiano wa fasihi simulizi na maendeleo na migogoro ya kijamii na jinsi utafiti wowote ule ulivyo chombo muhimu cha kiitikadi cha tabaka linalotawala au linalotawaliwa ni wazi kuwa haja ya kufanya utafiti wa fasihi simulizi bado ipo (Mulokozi 1983):

Visasili ni moja ya tanzu kongwe za fasihi simulizi, imekuwapo toka awali kabla ya fasihi andishi.

Utafiti katika visasili umetupa baadhi ya majibu ya maswali mengi yaliyopo kuhusu visasili na

fasihi simulizi kwa ujumla. Licha ya nadharia mbalimbali za watu mbalimbali zilizopo hata sasa,

bado historia ya visasili haijaandikwa vya kutosha. Kutokuwa na utafiti wa kutosha wa visasili

kumesababisha upungufu wa data kuhusu visasili na hivyo kuwa na mapengo mengi kuhusu

visasili na fasihi simulizi kwa ujumla.

Hatuwezi kuukataa ukweli kwamba tanzu nyingi za fasihi andishi zimetokana na visasili na tanzu

nyingine za fasihi simulizi. Hivyo kuna uwiano mkubwa kati ya fasihi andishi na visasili na tanzu

nyingine za fasihi simulizi, kwa ujumla. Wataalamu na wanazuoni mbalimbali kutoka sehemu

mbalimbali ulimwenguni wamezungumzia kwa undani utanzu wa visasili ambao ni utanzu

mojawapo kati ya tanzu nyingi za fasihi simulizi ya Kiswahili. Mitazamo yao inatofautiana kutoka

mtaalamu mmoja hadi mwingine. Tuone maoni ya wataalamu na wanazuoni mbalimbali kuhusu

visasili. Finnegan (1970:361) anafafanua visasili kuwa ni:

Masimulizi ambayo yanaposimuliwa katika jamii yanaaminiwa kuwa ni mambo ya kweli yaliyotokea zamani. Ni masimulizi ambayo yanakubalika kama imani ya dini na yanafundishwa ili yaaminike katika jamii, na ni masimulizi ambayo yana nguvu za ziada zisizo za kawaida hivyo hutumika kama jawabu kwa maswali magumu na mashaka katika jamii.(Tafsiri yangu)

Anaeleza kuwa visasili vinafungamana na imani katika dini na miviga. Wahusika wake wakuu ni

pamoja na wanyama, miungu na mashujaa wa kiutamaduni ambao matendo yao ya kishujaa

yalijulikana kwenye ulimwengu wa zamani ambao ulikuwa tofauti sana na ulimwengu wa sasa, au

Page 3: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

katika ulimwengu mwingine kama angani au chini ya ardhi. Hata hivyo, Finnegan anaeleza kuwa

visasili ni hadithi zinazohusu zaidi wanyama. Ametoa mifano ya hadithi kama hadithi ya “Mwewe

na Kuku”, “Fisi na Sungura” Pia anatoa mifano ya hadithi chache zinazohusu watu kama “Huwezi

Kumsaidia Mtu Asiye na Bahati”.

Finnegan (ameshatajwa), anaona kuwa kuelezea visasili ni vigumu maana vinachukua karibu aina

zote za hadithi zinazohusu wanyama na binadamu. Na hii ndiyo maana baadhi ya wanafasihi

simulizi hawatofautishi kati ya visasili kama utanzu wa fasihi simulizi na tanzu nyingine hasa

ngano na visasuli. Wataalamu hawa wameathiriwa na mtazamo wa Finnegan.

Wanafasihi wengine wana maoni na mtazamo tofauti na ule wa Finnegan. Hawakubaliani na

mawazo kwamba aina zote za hadithi zinazohusu wanyama na binadamu ni visasili. Wao wanaona

kuwa kuna tofauti kubwa kati ya visasili na hadithi nyingine kama ngano. Knappert (1977:11)

anatoa maana ya visasili, anasema:

Visasili vinajumuisha masimulizi ya vitendo vya miungu na mizimu ambayo katika hadithi huaminika kuwa ni kweli. (Tafsiri yangu).

Knappert akiwasilisha mawazo tofauti, anahusisha visasili na matendo ya miungu na mizimu wa

kale. Miungu na mizimu wanapewa nafasi ya pekee katika visasili kwa mujibu wa Knappert.

Tofauti na hadithi za fisi na sungura au kuku na mwewe, masimulizi hayo ya matendo ya miungu

na mizimu yanaaminika kuwa ni mambo ya kweli yaliyotokea zamani. Fasili nyingine ya visasili

tunaipata toka kwenye The Longman Encyclopedia (1989) ambayo inaeleza kuwa,

Visasili ni mambo ya kidini yanayoaminika kuwa ni kweli, yanayohusu namna ulimwengu unavyotokea na kuwa kama ulivyo, ulimwengu na nguvu za asili.

Page 4: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Inaendelea kueleza kuwa, visasili ni hadithi za asili zilizotokea na kusimuliwa zamani na hadithi

hizo zinaelezea zaidi kuwapo kwa nguvu za asili. Visasili vinaelezea kuumbwa kwa ulimwengu na

watu waliomo na mabadiliko ya jamii kwa ujumla.

Rettova (2007:126) ameeleza maana ya visasili, anasema:

Visasili vya asili ni maelezo kuhusu asili ya kifo, asili ya mwanadamu, hasa mtu mweusi, kutokana na mchanganyiko wa utaifa (rangi) kusini mwa Afrika.

Rettova hahusishi kabisa visasili na wanyama au vitu isipokuwa mwanadamu. Isitoshe

anatofautisha kabisa kati ya visasili na ngano, kwamba, visasili ni historia ya taifa fulani wakati

ngano ni hadithi zinazosimuliwa watoto wakati wa mapumziko. Ngano mara nyingi zinasimuliwa

na nyanya au babu na kwamba mbali na kuburudisha watoto, pia zinatoa maarifa kuhusu vyanzo

vya magonjwa, zinaelezea kuhusu maumbile ya wanyama mbalimbali na mahusiano yao, na pia

hufunza maadili kwa watoto. Visasili vinaeleza huhusu asili ya kifo au mwanzo wa binadamu.

Naye Gould (1964:450) anatoa fasili ya visasili inayokaribiana na ile aliyotoa Materu (1989) na

Soyinka (1979) lakini yeye ameongeza wazo la maisha na maana ya ulimwengu na watu,

anasema:-

Visasili ni masimulizi yanayohusu miungu, maisha na maana ya ulimwengu na watu. Katika upande wa siasa na mazingira ya jamii inamaanisha kwamba ni jumla ya mambo yote ya dunia yanayochukuliwa, na watu wanavyothaminiwa.

Hapa tunaona Gould anahusisha visasili na suala zima la siasa tofauti na wanafasihi wengine

ambao hawajagusia kabisa suala la siasa. Isitoshe, anaongelea kuhusu suala zima la mazingira,

yaani jumla ya mambo yote yanayomzunguka mwanadamu. Fasili hii

Page 5: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

ni pana zaidi ukilinganisha na nyingine, hata hivyo suala la miungu na mizimu bado limepewa

nafasi ya pekee katika fasili hii.

Balisidya (Materu), (1989) anaona kuwa miungu na binadamu ni wahusika kati ya wahusika

wengi wa aina mbalimbali katika visasili. Yeye anaongeza kitu ambacho Knappert

(ameshatajwa) hakukisema, kwamba visasili husimuliwa juu ya matokeo ya kiada na hueleza

miviga na imani za dini.

Naye Mulokozi (1996:56), mbali na kutoa fasili ya visasili ametoa aina tatu za visasili. Anasema,

Visasili ni hadithi za kale zenye kuwakilisha imani na mtazamo wa jamii inayohusika kuhusu asili ya ulimwengu na mwenendo wake, kuhusu asili yao wenyewe, na maana na shabaha ya maisha yao. Mara nyingi hadithi hizi huaminika kuwa ni kweli tupu, na hutumika kuelezea au kuhalalisha baadhi ya mila na madhehebu ya jamii inayohusika.

Mulokozi naye pia anaona kuwa, huwezi kutenganisha visasili na suala zima la imani za dini, na

kwamba visasili vinaweza kuwa mwanzo au asili ya madhehebu mbalimbali ya dini. Tofauti na

watalaam wengine, Mulokozi hakuishia tu kutoa maana ya visasili bali amekwenda hatua moja

zaidi na kutoa aina mbalimbali za visasili na kueleza tofauti ya aina moja na nyingine kwa kutoa

maana na mifano ya kila aina ya visasili hivyo. Kwa mujibu wa Mulokozi kuna aina tatu za visasili

kama ifuatavyo, aina ya kwanza ya visasili anasema ni visasili vya usuli.

Visasili vya usuli ni visasili vinavyojaribu kuelezea asili au chimbuko la Taifa au jamii fulani au

wanadamu kwa ujumla. Anatoa mfano wa hadithi ya Wayahudi ya kuumbwa kwa ulimwengu na

kutokea kwa wanadamu (Adam na Hawa) kuwa ni mfano mzuri wa kisasili cha usuli. Anasema

kuwa, hadithi hii hivi sasa imeenea dunia nzima kupitia katika dini za Ukristo na Uislamu.

Page 6: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Mulokozi anaendelea kufafanua kuwa, hapa Afrika Mashariki, karibu kila kabila linacho kisasili

chake cha usuli. Anatoa mfano wa kisasili cha “Gikuyu na Mumbi”cha Wagikuyu (kinasimulia

chimbuko la koo tisa za Wagikuyu), hadithi ya “Kintu ya Waganda”(inahusu asili ya wanadamu),

hadithi ya “Mrile” ya Wachagga (inahusu asili ya moto), na hadithi zihusuzo chimbuko la

Wamijikenda wa Pwani ya Kenya. Hivi vyote ni mifano ya visasili vya usuli. Anasema kuwa

baadhi ya visasili vya usuli huelezea asili ya mila au madhehebu fulani ya jamii.

Aina ya pili ya visasili, kwa mujibu wa Mulokozi, ni visasili vya ibada na dini. Hivi huhusu

matendo ya ibada na imani mbalimbali za dini na mara nyingine hutendwa kisanaa yaani huigizwa

katika ibada. Kwa mfano, katika dini ya Kikristo, ekaristi (kula pamoja chakula cha Bwana) ni

maigizo ya chakula cha mwisho ambacho Yesu Kristo anasemekana alikula na wanafunzi wake

kabla ya kusulubiwa, na kusimuliwa katika kisasili kihusucho tukio hilo.

Aina ya mwisho ni visasili vya Miungu na Mizimu. Visasili hivi hupatikana zaidi katika mataifa

yenye miungu wengi, kwa mfano Asia na Ulaya ya Kale. Pia Misri ya kale ilikuwa navyo vingi.

Visasili vya aina hii husimulia matendo na visa vya miungu ya jamii inayohusika. Hapa Afrika

visasili hivi hupatikana kwa wingi katika jamii ya Wayoruba huko Nigeria, na katika falme

zinazozunguka Viktoria Nyanza.

Naye Soyinka (1979) anatoa maana ya visasili inayofananafanana sana na ile aliyotoa Materu.

Mwanafasihi mwingine aliyefasili neno visasili ni Kipury (1983). Hata hivyo fasili aliyotoa

inakaribiana sana na fasili zilizotolewa na wataalamu wengine kama tulivyoona hapo awali.

Page 7: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Hakuna wazo jipya analoibua. Visasili ni aina ya ndoto zilizokusanywa ambazo ni rahisi

kutafsiriwa ili kuleta maana iliyofichika. Visasili kama matokeo ya vitu vya kufikirika juu ya

ukweli wa vitu vilivyotokea vinahusu zaidi hisia na siyo sababu ya kitu fulani. Pia ni kuhusu zaidi

jinsi Miungu wanayofanya mambo makubwa, ukuu wao na uhusiano na vitu au viumbe vya asili.

Chimera na Njogu (1999:151) pia wametoa maana ya visasili, nao wanasema:

Visasili ni aina ya hadithi zilizojikita katika asili ya vitu au mambo kama visa vinavyohadithia asili ya kwa mfano maisha ya binadamu, viumbe, dunia, mwezi na jua, magonjwa, kifo na kadhalika.

Hata hivyo wanafasihi hawa, wanaonekana kuwa na mtazamo tofauti na ule wa Mulokozi

(ameshatajwa) kwani wanachanganya dhana ya visasili na miviga. Wakati vile ambavyo Mulokozi

anaona kuwa ni aina za visasili wao wanaona kuwa ni utanzu mwingine wa fasihi simulizi yaani

miviga. Wanasema:

Miviga ni hadithi ambazo ukiweka katika mizani ya kisayansi, kihistoria, au hata ya kimaumbile, hazioneshi ukweli wowote , lakini wenyewe waliozitunga, kuzisimulia na kuzirithisha vizazi vyao vichanga, huziamini kwamba ni kweli tupu. Matukio katika hadithi hizo basi huaminika yalitendeka kweli na ni ya kihistoria.

Wanaendelea kueleza kuwa hadithi hizi zinahusu, kwa mfano, chimbuko la makabila. Kila kabila

duniani, au kundi lolote la watu ambalo linajichukulia kuwa mlango mmoja, huamini kuwa kuna

mwanzilishi wa kabila hilo ambaye ajulikana vizuri sana. Aghalabu, jina la mwanzilishi huyo

huwa ndilo jina la kabila lenyewe. Wanatoa baadhi ya mifano ya miviga kuwa ni pamoja na kisa

cha Adamu na Hawaa. Wanasema;

Siku hizi za Uislamu na Ukiristo kutawala dunia nzima, watu wengi ulimwenguni wamekuja kuamini kwamba mvyele wao wa awali ni Adamu na mama yao ni Hawaa, mkewe Adamu. Hata hivyo, zamani imani haikuwa hiyo kwa watu wote, hata kidogo. Zamani hizo zitajwazo hapa, Adamu aliaminiwa tu

Page 8: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

kwamba ni baba wa Wayahudi na Waarabu, na Hawa ndiye mama yao wa kwanza.

Wakati Njogu na Chimerah wanaona kuwa huu ni mfano wa aina ya kwanza ya miviga, mfano huu

huu Mulokozi anauweka kwenye kundi la aina mojawapo ya visasili yaani visasili vya usuli. Hii

inajidhihirika pia hata kwenye mifano mingine iliyotolewa na watalaamu hawa. Hata hivyo hoja ya

msingi hapa inabaki kuwa miviga ni sehemu ya visasili, kwa mujibu wa watalaamu mbalimbali.

Kwa mfano kisa cha Gikuyu na Mumbi ambacho kimetolewa mfano na Mulokozi (ameshatajwa),

kimeelezwa pia na Njogu na Chimerah japo wao wamekielezea kisa hiki kama mfano wa aina za

miviga na si visasili. Wanaeleza kuwa;

Wakikuyu wanaamini kwamba baba yao wa kwanza kabisa ni Gikuyu, mama yao ni Mumbi.

Gikuyu ndiye mtu wa kwanza aliyeumbwa na Mungu na kisha akaumbiwa mke, Mumbi. Mungu

wao aliitwa Murungu au Mugai (Ngai). Huyu Murungu alizoea kukalia kiti chake kinachong’ara

daima hapo kileleni, mlima wa Kerinyaga (Kenya).

Maelezo haya ya watalaamu hawa japo yanatofautiana kidogo hapa na pale, lakini yote

yanashadidia kuwa suala la miviga, imani katika miungu na mizimu na imani ya dini kwa ujumla

ni jambo la msingi na la muhimu tunapozungumzia suala zima la visasili. Tunaweza kusema kuwa

hii ni sifa muhimu sana ya visasili inayoweza kupambanua na kutofautisha kati ya utanzu huu wa

visasili na tanzu nyingine za fasihi simulizi kama ngano na nyingine.

Hivyo, visasili ni hadithi za “kwa nini” na “kwa vipi” kwa sababu zinaelezea asili na tabia ya

wanyama mbalimbali, mimea desturi na mila za jamii na hata kuhusu sura ya nchi yaani milima,

Page 9: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

mito, na mabonde. Visasili vina sifa kubwa ya umajumui kwani vinaeleweka duniani kote;

vinaeleza kuhusu jua, mwezi na tabia za binadamu. Kwa mfano, kuna visasili vinavyoeleza “kwa

nini wanaume wengi hupiga wake zao”, na vingine vingi. Visasili ni matukio ya kibunifu na ya

kizamani yanayooanishwa na sababu au asili ya jambo, kitu au hali fulani. Tuna, kwa mfano,

visasili vinavyozungumzia kwa nini ikawa vinyama kama paka na panya au tumbili na mbwa

havipatani, au kwa nini kuna vinyama vyenye maumbile haya au khulka zile, kama vile sungura

kuwa na masikio marefu, ndovu kuwa mpole, na au mbuzi kuwa na papara.

Wanaendelea kusema kuwa, kitu cha kukifahamu ni kuwa visasili si mikasa inayosimuliwa kwa

kufurahisha tu watu, bali kusudio lake hasa ni kupeleka ujumbe au kutoa funzo fulani kwa

mlengwa. Kwamba hao kina mbwa na tumbili, paka na panya, au sungura na fisi watajwao humu,

huwa hawakusudiwi wao hasa, bali ni wanadamu wenye sifa kama za hao wanyama. Maana

kwenye maisha halisi wako wanadamu wenye papara kama za mbuzi, uroho kama wa fisi au

mahasimu kama mbwa na tumbili! Katika tafsiri hii tunaona kuwa mfasili anahusisha wanyama

katika visasili. Mtazamo kama huu tumeuona pia kwa Finnegan (ameshatajwa), jambo ambalo

linapingwa na wataalamu wengine kama tulivyoona kwenye mjadala hapo juu. Jambo la pekee

linaloelezwa hapa , tofauti na anavyoeleza Finnegan, ni kwamba pamoja na kwamba hadithi hizo

zinahusu wanyama ndani yake zina mafunzo yanayolenga kumfundisha mwanadamu mambo

kadha wa kadha kuhusiana na maisha ya kila siku.

2.3 Hitimisho

Sura hii imeshughulikia maoni ya watalaamu mbalimbali ulimwenguni kuhusu visasili. Imeangalia

kwa undani maana ya utanzu huu wa visasili kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali. Imebainika

Page 10: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

kuwa watalaam mbalimbali wa fasihi simulizi pamoja na kueleza kwa namna mbalimbali kuhusu

visasili, wana mtazamo sawa kuhusu dhana hii. Mtafiti ana mtazamo sawa na watalaamu wa fasihi

waliotoa fasili ya neno visasili. Mbali na kujikita kuangalia maana ya visasili, sura hii pia

imejishughulisha na kubainisha sifa bainifu za visasili. Tumeona kuwa watalaamu wa fasihi

wametoa sifa ambazo zinawezesha kutofautisha baina ya utanzu wa visasili na tanzu nyingine za

fasihi simulizi. Kwa ujumla sura hii imepitia marejeo mbalimbali yanayohusu mada husika.

a teacher has to do some administrative works that sometimes stand as a hazard for him. A teacher spends more time by filling the OMR sheet or signing on different places than the time he spends for checking the answer scripts. No doubt, both the works need time and both of them are important but unfortunately the examiner gives importance to the administrative work rather than checking the answer scripts. On an average, a teacher gets maximumo4262008

Assessment may be defined as a method, which is used for better understanding the current knowledge that a student possesses. (Elison, 1999). It means that with the assessment a teacher can easily justify students ‘ability. Hence, the importance of assessment is not ignorable. According to “Pittsburg State University 2005”. Assessment helps departments to focus on those things in their curricula and courses that are going well. Assessment also helps to identify what is not going well, and often points to the specific changes that might be needed. Thus, assessment is an ongoing and continuous effort to improve the quality of instruction, student learning, and overall effectiveness of a department or unit. It is the systematic collection and analysis of information to improve students’ learning

Page 11: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

SURA YA TATU

MBINU ZA UTAFITI

3.1 Utangulizi

Sura hii ya tatu inajadili mbinu mbalimbali zilizotumika katika utafiti huu. Mbinu hizo za utafiti ni

kama kubainisha na kuelezea eneo la utafiti, sampuli ya utafiti, taratibu za usampulishaji, mbinu za

ukusanyaji wa data na taratibu zilizotumika katika kuchambua data. Kadhalika, mkabala

uliotumika pamoja na kiunzi cha nadharia kilichotumika katika utafiti huu vimeelezwa. Pia usanifu

wa utafiti huu umeelezwa katika sura hii.

3.2 Usanifu wa Utafiti

Utafiti huu, kwa sehemu kubwa, ni wa uwandani na sehemu ndogo ilifanyika maktabani. Kwa

mujibu wa Kombo na Tromp (2006) usanifu wa utafiti ni ule muundo wa utafiti. Hivyo usanifu wa

utafiti ni mpangilio wa taratibu zinazotumika kukusanya na kuchambua data kwa namna

inayounganisha data zinazopatikana na malengo ya utafiti. Mbinu za ukusanyaji wa data

zilizotumika ni mahojiano, usaili na dodoso. Mbinu hizi inawezesha upatikanaji wa data za

kutosha kwa urahisi na kwa haraka. Mbinu ya uchambuzi matini pia ilitumika kupata data za

msingi ambazo zilipatikana maktabani kwa kusoma matini mbalimbali zinazohusiana na mada ya

utafiti huu. Data zilizopatikana zilichambuliwa kulingana na malengo ya utafiti huu.

Page 12: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

3.3 Eneo la Utafiti

Utafiti huu ulifanyika mkoa wa Dodoma. Kutokana na malengo ya utafiti, data zilizotakiwa

zilipatikana kwa kuwahoji baadhi ya wakazi wa Dodoma wakiwemo wazee ambao wanafahamu

vizuri historia ya Wagogo na waliweza kutoa data za kutosha na zilizotakiwa na mtafiti. Kati ya

wilaya tano za mkoa wa Dodoma, wilaya ya Dodoma mjini ndiyo inasemekana kuwa na Wagogo

asilia, ukilinganisha na wilaya nyingine. Eneo jingine la utafiti huu ni mkoa wa Dar es Salaam.

Wahojiwa wanne toka mkoa wa Dar es Salaam walihojiwa ili kupata data zaidi. Pia data

zilipatikana maktabani na makavazini, hasa maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, makavazi

ya Taifa na makavazi ya Taasisi ya Taaluma za Kiswahili.

3.4 Sampuli ya Utafiti na Usampulishaji

Babbie (1992) anasema sampuli ni sehemu ya idadi watu ambayo mtafiti anavutiwa nayo katika

kupata taarifa na kutoa hitimisho la utafiti wake. Pia Kombo na Tromp (2006) wanasema jambo la

msingi ni kuanza na idadi kubwa na kadri utafiti unavyoendelea, mtafiti atabaki na eneo husika la

utafiti ambamo data zitakusanywa. Sampuli ya kimakusudi imetumika nyanjani kuteua wahojiwa

kwa sababu mtafiti anawafahamu baadhi yao. Aidha mtafiti alitumia sampuli elekezi ili kuwa na

utoshelevu wa wahojiwa waliochangia pakubwa utafiti huu. Wahojiwa wanawake kumi na tano

(15) na wanaume kumi (10) waliteuliwa kutoka kata za Makole, Mailimbili, Kizota, Uzunguni na

Kikuyu. Kwa hiyo, jumla ya watafitiwa katika mkoa wa Dodoma ilikuwa wahojiwa ishirini na tano

(25). Wahojiwa waligawanywa kama ifuatavyo:

a) Wazee wanawake na wanaume kumi na tano (15).

b) Vijana wa kike na wa kiume sita (6)

c) Watoto wa kike na wa kiume wanne (4)

Page 13: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Kutoka mkoa wa Dar es Salaam sampuli ilikuwa na wahojiwa wanne (4). Wahojiwa watatu (3) ni

wanaume na mmoja (1) mwanamke. Umri wao ni kati ya miaka ishirini na nane (28) na hamsini na

nane (58). Hawa walipatikana toka sehemu mbalimbali za mkoa wa Dar es Salaam, lakini wote ni

Wagogo toka sehemu mbalimbali za mkoa wa Dodoma. Hivyo jumla ya wahojiwa wote ni ishirini

na tisa (29). Idadi hii ilikidhi malengo na mahitaji ya utafiti.

Sampuli ya kimakusudi na elekezi ndiyo iliyomwongoza mtafiti kuteua wahojiwa ishirini na tisa

(29). Sampuli elekezi haihitaji idadi kubwa ya wahojiwa kwani huchukua muda mrefu kwa mtafiti

kuwapata na pia gharama za kukamilisha zoezi la ukusanyaji data zinakuwa kubwa. Wahojiwa

walioteuliwa wamekuwa ni wawakilishi wa wanajamii wote wa jamii ya Wagogo kwa kuzingatia

maoni yao.

Visasili viwili vya jamii ya Wagogo vilipatikana kwa kutumia mbinu bahatishi na kwa kuzingatia

malengo ya utafiti. Visasili viwili vimezingatiwa kwa sababu hakuna visasili vingi vilivyopatikana

katika jamii ya Wagogo. Kupata idadi kubwa ya visasili inawezekana lakini ingemlazimu mtafiti

kufanya utafiti katika eneo kubwa zaidi na pia kuongeza muda wa kufanya utafiti. Hata hivyo,

mtafiti aligundua kuwa utanzu wa visasili haujulikani sana ukilinganisha na tanzu zingine za fasihi

simulizi. Sababu zake zimeelezwa kwa kina katika sura ya nne.

3.5 Vyanzo vya Data na Taarifa

Kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya kukusanya data, mtafiti aliweza kupata data za msingi na

data za ziada.

Page 14: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

3.5.1 Data za Msingi

Data za msingi zilikusanywa uwandani ili kufidia upungufu uliandikwa kuhusu jamii ya Wagogo

na pia ndio kiini hasa cha kupata data za msingi za utafiti huu. Sababu za kwenda uwandani ni

pamoja na kutimiza lengo la utafiti kwani utafiti huu toka awali ulikusudiwa kufanyika uwandani,

ili kuchunguza na kubainisha dhima ya visasili katika kabila la Wagogo. Vilevile, hatukutegemea

sana data za maktabani kutokana na sababu mbalimbali. Sababu hizo ni pamoja na ukweli

kwamba, hakuna data za kutosha zilizohifadhiwa kuhusu visasili vya Wagogo na hii ndiyo sababu

iliyomchochea mtafiti kufanyia utafiti mada hii. Pia, data chache zilizohifadhiwa maktabani ni za

muda mrefu, tukizingatia ukweli kwamba fasihi hubadilika kuendana na mabadiliko yanayotokea

katika jamii, suala la kwenda uwandani lilikuwa ni muhimu na la lazima. Mtafiti alisikiliza

mazungumzo na kushuhudia matendo wakati wa usimuliaji, jambo ambalo alinufaika nalo kwa

kupata data za msingi. Kadhalika, mtafiti aliweza kunasa yaliyosimuliwa na watafitiwa kutokana

na kuwapo na utulivu. Zoezi la kurekodi lilikubalika kwa wahojiwa. Mtafiti alinukuu daftarini

maelezo yanayohusiana na uchunguzi husika. Mtafiti basi alikuwa ni mmoja kati ya washiriki wa

shughuli na hivyo kumrahisishia zoezi la ukusanyaji wa data. Kanda za sauti zilizorekodiwa na

watu mbalimbali zinazohusu visasili na historia ya jamii ya Wagogo kwa ujumla zilizingatiwa

wakati wa ukusanyaji wa data za msingi. Isitoshe kanda za sauti zilitumiwa na mtafiti kunasa

maelezo ya wahojiwa wakati wa mahojiano kati ya mtafiti na watafitiwa mbalimbali. Kanda hizo

zilimsaidia mtafiti wakati wa uwasilishaji, uchambuzi na mjadala kwani aliweza kujikumbusha

yale yaliyosemwa na watafitiwa kwa kusikiliza tena kanda hizo. Vilevile, watafitiwa walihojiwa

ili kupata uhalisi wa data kulingana na malengo ya utafiti.

Page 15: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

3.5.2 Data Fuatizi

Maandishi mbalimbali yalipitiwa maktabani, ikiwa ni pamoja na vitabu, makala, majarida na

kwenye mtandao wa mawasiliano ili kupata mwelekeo muafaka kuhusu mada ya utafiti. Aidha

maandishi jumulifu ya fasihi na utamaduni yamesomwa ili kumwongoza mtafiti katika uchunguzi

wake. Tafiti tangulizi zimesomwa kupata mwangaza kuhusu nadharia, mbinu za ukusanyaji data,

uwasilishaji, na uchanganuzi wa matokeo ya utafiti. Vitabu na tasnifu juu ya visasili na fasihi

simulizi kwa ujumla vilitiliwa mkazo zaidi kwani ndicho kiini cha utafiti huu. Maandishi yahusuyo

jamii ya Wagogo pia yaliufaa utafiti huu kwa kupata historia na maelezo kuhusu utamaduni wa

jamii ya Wagogo.

3.6 Ukusanyaji wa Data

Ikumbukwe kwamba katika utafiti wowote ule, ukusanyaji wa data unahusu kukusanya taarifa

mahsusi zilizokusudiwa kutoa au kupinga uhalisia wa mambo fulani (Kombo na Tromp 2006).

Halikadhalika, katika utafiti huu taarifa mbalimbali zilikusanywa kutoka maktabani na uwandani

kwa kutumia mbinu na vifaa mbalimbali vilivyoandaliwa na mtafiti.

Data ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole,

Uzunguni na Chizota. Kata hizi zilizingatiwa kwa kuwa zina wakazi wengi ambao ni Wagogo na

pia ni kata zilizokaribiana hivyo ilimwezesha mtafiti kukusanya data kwa urahisi. Pia ukusanyaji

wa data ulifanywa katika mkoa wa Dar es Salaam kwa sehemu ndogo. Usaili wa ana kwa ana

ulihusishwa wakati wa kukusanya data za msingi. Hii ni kwa sababu baadhi ya data kama vile

utendaji haziwezi kupatikana katika kanda zilizorekodiwa. Pia data ilikusanywa kwa kuzingatia

kanda zilizorekodiwa na watu wengine zinazohusu jamii ya Wagogo, pamoja na zile kanda

alizorekodi mtafiti wakati akiwa uwandani akiwahoji watafitiwa. Kanda hizi zilifidia upungufu

Page 16: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

uliojitokeza kwani si rahisi mtafiti kunukuu kila kitu. Ili kukusanya data ya kutosha mtafiti

alinukuu daftarini yale yote muhimu yaliyomwezesha kufikia malengo ya utafiti kwa kupata data

toshelevu na ya kina.

3.6.1 Vifaa vya Kukusanyia Data

Mtafiti aliandaa vifaa vya utafiti kulingana na mada na malengo ya utafiti. Vifaa hivi

vilimwezesha mtafiti kukusanya data husika na kupata taarifa sahihi za utafiti wake. Katika utafiti

huu, data na taarifa zilikusanywa kwa kutumia vifaa mbalimbali, vifaa hivyo ni pamoja na dodoso,

tepurikoda, kamera, kompyuta, shajara na kalamu.

Hojaji ni maswali yaliyoandaliwa na mtafiti kwa lengo la kumhoji mtafitiwa, na maswali haya

yanafungamana na malengo ya utafiti husika. Mtafiti alitumia maswali hayo kama mwongozo

wake katika kupata data husika kutoka kwa mtafitiwa. Hivyo, hojaji ilimwezesha mtafiti kupata

data za msingi na fuatizi. Hojaji lililotumika katika utafiti huu limeambatishwa mwishoni pamoja

na viambatisho vingine.

Shajara na kalamu: Vifaa hivi vilimsaidia mtafiti katika kunukuu na kuhifadhi baadhi ya data za

msingi kama vile tarehe, majina ya wahojiwa na mahali pa wahojiwa na data fuatizi katika utafiti

huu.

Tepurikoda ni kifaa kinachotumika katika kunasa na kurekodi sauti wakati wowote katika

muktadha wowote ule. Katika utafiti huu, tepurikoda ilitumika uwandani ambako mtafiti alirekodi

mahojiano baina yake na watafitiwa. Taarifa zilizorekodiwa katika tepurikoda zilitumika katika

uchambuzi wa data katika utafiti huu.

Page 17: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Kamera ni kifaa kilichotumika katika kupata taarifa mbalimbali za kuona ambazo haziko katika

maandishi. Kwa mfano picha za wahojiwa na maeneo mbalimbali ambayo yanahusiana na mada

husika. Kwa mfano kuna picha inayoonesha mahali ambapo inasadikiwa kuwa ni asili ya neno

Dodoma.

Kompyuta ilitumika katika kutafutia matini kutoka katika tovuti na wavuti na pia kuhifadhi taarifa

mbalimbali. Data zilizohifadhiwa zilichambuliwa na kutolewa mahitimisho kisha kuandaa ripoti ya

utafiti. Pia kompyuta ilitumika kama sehemu ya maktaba tembezi.

3.6.2 Mbinu za Ukusanyaji wa Data

Kutokana na malengo ya utafiti huu ya kuangalia dhima ya visasili katika kabila la Wagogo, data

zilizokusanywa ni data asilia kutoka uwandani kwa wanajamii wa kabila la Wagogo. Mbinu

zilizotumika ni pamoja na mahojiano, majadiliano na kushiriki.

Mtafiti alitumia mbinu ya kushiriki katika kukusanya data, na alikuwa sehemu ya hadhira wakati

wa kusimulia visasili. Mbinu za majadiliano na mahojiano vile vile zilitumika.

3.6.2.1 Mbinu ya Mahojiano

Hii ni njia ya kupata data kwa kutumia maswali na majibu yanayofanywa kwa mazungumzo kati

ya mtafiti na mtafitiwa (Kothari 2008). Katika utafiti huu mtafiti aliongozwa na hojaji katika

kuwauliza watafitiwa wake maswali ya utafiti wake. Mojawapo ya maswali yaliyoulizwa

uwandani ni pamoja na maswali ya utafiti huu. Je, kuna visasili katika kabila la Wagogo? Swali

jingine lilikuwa, Je, visasili katika kabila la Wagogo vina dhima yoyote, unaweza kueleza?

Page 18: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Maswali mengine yalikuwa, Je jamii ya Wagogo inaamini nini kuhusu mizimu na miungu? Je,

kuna matambiko yanayofanyika katika kabila la Wagogo? Je, nini asili ya kabila la Wagogo? Je,

Wagogo wanaamini kuhusu kuumbwa kwa dunia na ulimwengu? Na mengine mengi. Majibu

yaliyopatikana kuhusiana na maswali haya yalitofautiana kutoka mhojiwa mmoja na mwingine.

Kuna wahojiwa waliosema kuwa kuna visasili katika jamii yao, na walifanikiwa kutoa mifano ya

visasili. Idadi kubwa ya wahojiwa japo walikubali kuwa kuna visasili, mifano waliyotoa haikuwa

visasili. Walichanganya visasili na tanzu nyingine za fasihi simulizi kama visasuli, visakale na

ngano. Changamoto kubwa katika utafiti huu ilikuwa ni suala la neno visasili kuwa msamiati

mgumu kwa baadhi ya wahojiwa. Ilimlazimu mtafiti kufafanua maana ya visasili kwa undani ili

kuhakikisha kuwa data zinazopatikana ni sahihi. Wakati mwingine ilimlazimu mtafiti kutumia

lugha ya Kigogo kufafanua dhana ya visasili ili kuhakikisha kwamba watafitiwa wanaelewa vizuri.

Changamoto nyingine iliyojitokeza ni kwamba baadhi ya wahojiwa hawakuwa tayari kuzungumza

kuhusu vitu kama matambiko na miviga kwa sababu waliamini kuwa mizimu na miungu

watakasirika. Jambo hili lilisababisha ugumu wa kupata data zilizotakiwa.

3.7 Mkabala wa Uchambuzi wa Data

Data zilizokusanywa zilitolewa maelezo, zilichambuliwa na kufupishwa kwa kutumia mkabala wa

kimaelezo yaani mkabala usio wa kiidadi. Kothari (1990) anasema mkabala usio wa kiidadi ni njia

ya kuchambua data katika muundo wa maelezo pasipo kufuata taratibu za kitakwimu. Katika

utafiti huu mkabala huu ulimwezesha mtafiti kupata data zilizo katika maelezo kupitia njia ya

mahojiano kwa kutumia hojaji lililoandaliwa na mtafiti. Data hizo zilifupishwa kwa namna

ambayo ni rahisi kuchambuliwa na kueleweka kwa kuzingatia malengo ya utafiti huu. Katika

Page 19: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

utafiti huu, visasili viwili vya jamii ya Wagogo vilivyopatikana vilichambuliwa ili kubainisha

dhima ya visasili katika jamii husika kama malengo ya utafiti huu yanavyoonesha

3.8 Uchambuzi wa Data

Data zilikusanywa kutoka vyanzo kwa kuzingatia malengo ya utafiti. Mtafiti kwa kutumia mkabala

wa kimaelezo amechambua visasili viwili vya jamii ya Wagogo vilivyopatikana. Uchambuzi pia

umehusisha visasuli, visakale pamoja na ngano zilizotolewa mifano na wahojiwa waliokuwa

wanachanganya tanzu za fasihi simulizi. Dhima ya visasili viwili vya kabila la Wagogo

vilivyopatikana zilibainishwa. Hali kadhalika ubainishaji wa dhima ulihusisha visasuli, visakale na

ngano zilizotolewa mifano na wahojiwa.

3.9 Kiunzi cha Nadharia

Zipo nadharia nyingi ambazo zinaweza kutumika katika utafiti wa fasihi simulizi. Finnegan (1970)

ametoa muhtasari mzuri wa shughuli za utafiti wa fasihi simulizi ya Afrika katika karne ya kumi

na tisa na nadharia zilizoongoza utafiti huo. Kwa mujibu wa Finnegan utafiti kuhusu fasihi simulizi

ya Afrika ulianza katikati ya karne kumi na tisa. Nadharia ambazo amezijadili Finnegan na

zinaweza kutumika katika utafiti wa fasihi simulizi ni pamoja na nadharia ya mageuko (evolution

theory), nadharia ya mweneo au msambao (diffusion theory), nyingine ni nadharia ya Umuundo-

uamilifu (structural functional) na nadharia ya kimuziki (musicological approach). Tutajadili kwa

undani kidogo baadhi ya nadharia hizo zilizotajwa na Finnegan.

Page 20: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Nadharia ya mageuko kuhusiana na jamii kwa ujumla ilianza karne ya kumi na tisa (19) na

mwanzoni mwa karne ya ishirini (20). Ilikuwa ni nadharia changamani sana na ilichukua sura au

umbo au mtindo tofauti tofauti. Nadharia hii iliamini kwamba jamii yoyote lazima ipitie kwenye

hatua za mabadiliko ya kijamii na ya kiutamaduni ambayo hayafuati mstari mnyoofu. Inaweka

msisitizo kwenye asili au mwanzo wa kitu chochote kuwa ni muhimu sana. Pia inaamini kuwa

mwelekeo wa hayo mabadiliko ni kukua au kubadilika kuelekea juu yaani kutoka kwenye ujinga

kwenda kwenye uelewa.

Nadharia hii pia iliweza kutumika katika utafiti wa fasihi simulizi hasa kwenye karne ya ishirini

(20). Ilitumiwa zaidi na wanazuoni wa Uingereza. Msisitizo uliwekwa kwenye asili na mabadiliko

ya fasihi. Swali liliulizwa; aina gani ya fasihi ilianza kuwepo katika historia ya mwanadamu? Je, ni

ngano yaani hadithi (folk literature) au ni sanaa ya jadi (folk-lore). Walilinganisha fasihi ya wakati

huo na hatua ya jamii ya mabadiliko ya wakati huo yaani ujima. Waliona kuwa fasihi simulizi

ilikuwa sawa kwa jamii zote na watu wote waliokuwa wanapita katika hatua moja ya mageuko.

Fasihi katika jamii zilizokuwa katika hatua ya ujima ilikuwa tofauti kabisa na ile ya jamii

zilizokuwa “zimestarabika” au zimeendelea.

Nadharia nyingine ni ile ya mweneo au msambao. Hii ni nadharia inayojikita katika kuangalia

ueneaji wa vitu katika eneo la kijiografia. Katika karne ya kumi na tisa (19) na ya ishirini (20),

msukumo mkubwa wa wanazuoni ulikuwa ni kujua eneo la kigeografia na historia nzima ya

hadithi za aina mbalimbali katika ulimwengu. Hivyo, ilikuwa inalenga zaidi katika kutafuta

mweneo wa fasihi simulizi kihistoria na kijiografia.

Page 21: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

Nadharia hii ilianzishwa na Boas na wenzake kwenye karne ya ishirini (20) huko Marekani. Jambo

la msingi la kukumbuka hapa ni kwamba nadharia hii haikujihusisha na uchunguzi wa kina wa

kujua umuhimu wa tanzu za fasihi simulizi katika jamii. Wala haikujihusisha sana na ukusanyaji

wa tanzu hizo za fasihi simulizi ili kupata rekodi ya kutosha japokuwa hayo yote yalikuwa

yanatakiwa sana. Msisitizo mkubwa uliwekwa kwenye masimulizi ambayo motifu zake zingeweza

kupatikana kwa urahisi. Hata hivyo msisitizo mkubwa zaidi ulikuwa kwenye ushairi kuliko tanzu

nyingine.

Nadharia hii ilianzia huko Amerika ikaenea kwingineko. Kwa kuwa lengo lake kubwa ni

kuangalia asili na chanzo cha kijiografia cha hadithi na mweneo wake toka sehemu moja hadi

nyingine, wakati mwingine inatambua hadithi moja ambayo inapatikana katika jamii mbalimbali

ili kurahisisha upatikanaji wa eneo halisi ambapo hadithi hiyo ilianzia na baadaye kuenea sehemu

nyingine. Mifano mingi ya uchanganuzi wa namna hii imetolewa, mfano mmojawapo ukiwa ni ule

wa Stith Thompson’s unaoitwa Motif- Index of Folk-literature ambamo motifu mbalimbali za

hadithi zimeorodheshwa kwa ajili ya rejea na ufananishaji wa asili yake.

Zipo nadharia nyingi ambazo zimependekezwa na Finnegan kutumika katika utafiti wa fasihi

simulizi, hata hivyo hatuwezi kuzijadili zote. Nadharia hizo zinaweza kutumika katika utafiti wa

tanzu mbalimbali za fasihi simulizi.

Kutokana na malengo, maswali na tatizo la utafiti huu, nadharia iliyotumika ni ile ya kiuamilifu.

Nadharia zilizojadiliwa hapo juu haziwezi kutumika katika utafiti huu kwa kuwa haziendani na

malengo na maswali ya utafiti husika. Nadharia ya Mweneo au Msambao kwa mfano, inajikita

katika kuchunguza eneo la kijiografia ilipoanzia fani fulani ya fasihi simulizi na jinsi ilivyosambaa

Page 22: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

au kuenea katika maeneo mengine. Hili si lengo la utafiti huu. Wala nadharia hii haitasaidia kujibu

maswali ya utafiti huu.

Nadharia ya kiuamilifu hutumika katika uchunguzi wa fasihi simulizi ambapo huwawezesha

watafiti kuchunguza dhima za tanzu mbalimbali za fasihi simulizi mathalani, methali, ngano

vitendawili na visasili. Japokuwa nadharia hii haijihusishi moja kwa moja na uchunguzi wa utanzu

wa visasili peke yake, bado ni nadharia inayofaa kutumika kwa kuwa visasili ni mojawapo ya

tanzu za fasihi simulizi ambazo zinaweza kuchunguzwa kwa kutumia nadharia hii.

Nadharia hii ilianzishwa na Herper Spencer ilianzia kwenye stadi ya biolojia. Nadharia hii

inalinganishwa na mwili wa binadamu jinsi unavyofanya kazi. Viungo vya mwili vinafanya kazi

kwa kushirikiana na hivyo vinahusiana kimoja na kingine na vinategemeana. Viungo vyote kwa

pamoja ndivyo vinavyosababisha kuwepo kwa maisha ya kiumbe. Hivyo basi, nadharia hii ina

mtazamo huohuo kuhusu jamii, kwamba asasi mbalimbali katika jamii zinafanya kazi kwa

kushirikiana na nyingine ili kuelimisha jamii. Kwa hiyo nadharia hii inaweza kutumika kuchunguza

na kuchambua tanzu za fasihi simulizi, visasili vikiwemo. Katika visasili mtafiti anaangalia

maudhui kwa kuzingatia vipengele vinavyojenga maudhui, dhima zake na mchango wa kila

kipengele katika kujenga visasili. Nadharia hii ilisaidia sana katika utafiti huu uliolenga kuelezea

visasili vya jamii ya Wagogo na kubainisha dhima za visasili vya kabila hilo.

3.10 Mipaka na Mawanda ya Utafiti

Jamii ya Wagogo ina aina na tanzu nyingi za fasihi simulizi zilizofanyiwa utafiti na nyingine

nyingi bado hazijafanyiwa utafiti wowote. Tanzu hizo ni kama vile hadithi, vitendawili, ngano,

Page 23: SURA YA PILI -    Web viewData ilikusanywa katika jamii ya Wagogo wanaoishi kata za Kikuyu, Mailimbili, Makole, Uzunguni na Chizota

methali, nyimbo na nyinginezo. Hata hivyo utafiti huu umejikita katika kuchunguza visasili vya

jamii ya Wagogo na kubainisha dhima yake katika jamii hiyo. Uchunguzi umejikita katika

manispaa ya Dodoma kata za Makole, Mailimbili, Kizota, Uzunguni na Kikuyu. Pia data nyingine

ilipatikana kutoka mkoa wa Dar es Salaam kwa baadhi ya Wagogo wanaoishi sehemu mbalimbali

za mkoa wa Dar es Salaam.

3.11 Muhtasari wa Sura ya Tatu

Kwa ujumla sura hii imeelezea mbinu mbalimbali zilizotumika katika ukusanyaji wa data ili

kujibu maswali ya utafiti huu. Mbinu hizo ni pamoja na eneo la utafiti, sampuli ya utafiti,

michakato ya usampulishaji, njia na mbinu za ukusanyaji wa data, michakato ya uchambuzi wa

data, mipaka na mawanda ya utafiti. Aidha kiunzi cha utafiti, mafanikio na matatizo ya mbinu za

ukusanyaji data na vikwazo vilivyojitokeza wakati wa ukusanyaji wa data pia vimeelezwa.

Uchambuzi na mjadala wa data zilizokusanywa pamoja na uwasilishaji wa data zilizochambuliwa

utafanyika katika sura inayofuata.