uhakiki wa mtindo katika diwani ya mashairi ya...

154
UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI YA SAUTI YA DHIKI YA ABDILATIF’ ABDALLA SAMWEL IKIARA KULU Tasnifu inayowasilishwa kwa Shule ya Mafuzu ili kutosheleza baadhi ya mahitaji ya Shahada ya Uzamili katika Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Egerton. CHUO KIKUU CHA EGERTON SEPTEMBA, 2016

Upload: others

Post on 20-Jan-2020

127 views

Category:

Documents


9 download

TRANSCRIPT

Page 1: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI YA SAUTI YA DHIKI YA

ABDILATIF’ ABDALLA

SAMWEL IKIARA KULU

Tasnifu inayowasilishwa kwa Shule ya Mafuzu ili kutosheleza baadhi ya mahitaji ya

Shahada ya Uzamili katika Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Egerton.

CHUO KIKUU CHA EGERTON

SEPTEMBA, 2016

Page 2: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

ii

UNGAMO NA IDHINI

Tasnifu hii ni kazi yangu binafsi na haijawahi kuwasilishwa na yeyote kwa mahitaji ya shahada

katika Chuo Kikuu chochote kile.

_________________________ ________________________

Sahihi Tarehe

Samwel Ikiara Kulu

(AM12/2621/10)

IDHINI

Tasnifu hii ya uzamili imewasilishwa kwa ushauri na idhini yetu kama wasimamizi

walioteuliwa rasmi na Chuo Kikuu cha Egerton.

_________________________ _______________________

Sahihi Tarehe

Prof. James Onyango, Ogola

Idara ya Mawasiliano na Mtalaa wa Fasihi, Chuo Kikuu cha Laikipia.

_________________________ ________________________

Sahihi Tarehe

Prof. Wendo, Nabea

Idara ya Mawasiliano na Mtalaa wa Fasihi, Chuo Kikuu cha Laikipia

Page 3: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

iii

HAKILINZI

©2016, Samwel Ikiara Kulu

Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupigisha chapa, kutafsiri au kuitoa

tasnifu hii kwa jinsi yoyote bila idhini ya mwandishi au Chuo Kikuu cha Egerton.

Page 4: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

iv

TABARUKU

Naitabaruku ripoti hii kwa wapendwa wafuatao: Dkt Wendo Nabea, Kelly Gakii na Abib

Ufanisi.

Page 5: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

v

SHUKURANI

Namshukuru Mwenyezi Mungu kisha Chuo Kikuu cha Egerton kwa kuniruhusu kusomea

huko hadi kuhitimu. Nachukua fursa zaidi kwa heshima na taadhima kuu kuwashukuru

wasimamizi wangu katika utafiti huu. Hawa ni Profesa James Onyango Ogola na Dkt. Wendo

Nabea ambao walirekebisha kazi yangu kuanzia mwanzo hadi mwisho kwa kuwajibika bila

kuchoka. Bila ya mchango wao kazi hii ingebaki ndoto ya mchana.

Nashukuru waalimu wawili Bw. Humphreys Omwaka na Bwana Peter Owino wote wa

Moi Forces Academy – Lanet kwa mchango wao mkuu katika kazi hii. Bwana Omwaka

akanipa vitabu tele adimu huku Bw. Owino akinifaa kwa huduma za maktaba ya kifaransa

anayoongoza shuleni.

Namshukuru pia mke wangu Bi. Kelly Gakii na wanangu Kinya, Wesley na Abib kwa

kunipa nguvu hata wakati wa changamoto kuu. Baba yangu japo marehemu Bw. Daniel M.

Ikiara aliyenizaa na kunilea na hata kunielimisha hadi nilipo anakumbukwa kikamilifu kwa

heshima. Pia Bi. Kebaso na Bw. Eric Odhiambo walinifaa kwa kupiga chapa kazi nzima. Wote

walionisaidia kwa njia moja au nyingine wanakumbukwa. Ahsanteni sana. Zaidi ya wote,

Mwenyezi Mungu apokee shukrani na sifa kwa kunipa nguvu kufanya kazi ngumu na kufaulu.

Page 6: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

vi

IKISIRI

Kwa kipindi kirefu mashairi yametambulika kama sehemu ya usomi wa Kiswahili.

Mashairi ya arudhi yamekuwepo kwa karne kadha zilizopita. Haya yalilazimisha uzingativu wa

sheria za utunzi. Wataalamu wa baadaye kama Euphrase Kezilahabi,M.M Mulokozi na C.Kahigi

nao wakazua mashairi huru ambayo hulenga zaidi ujumbe na maudhui badala ya arudhi za

utunzi. Mashairi mapokeo yakapigwa vita kwa kupuuza maudhui yakizingatia fani. Kufuatia

kukubalika kwa mashairi huru,utafiti zaidi ulihitajika ili kuendelea kudumisha nafasi yake katika

fasihi ya Kiswahili. Aidha tasnifu za uhakiki hasa wa diwani ya Sauti ya Dhiki zilizopo hadi sasa

zinalenga swala mojamoja badala ya vipengele kadha vya ushairi. Utafiti huu ulilenga kuhakiki

fani na maudhui ya mashairi teule katika diwani ya Sauti ya dhiki ya Abdilatif’ Abdalla. Haya ni

mashairi mapokeo. Uteuzi huo ni kutokana na kufanana miundo kwa mashairi mengi katika

diwani husika. Ilitafitiwa jinsi malenga alivyotumia kipengele cha uhusika, kuhakiki ufundi wa

lugha na muundo pamoja na maudhui. Mashairi yaliteuliwa kimaksudi kwa kuzingatia idadi ya

beti, aina ya wahusika, tamathali za usemi na aina ya maudhui. Nadharia za

umuundo,umuundoleo na uamilifu zilitegemewa. Mbinu ya utafiti ilihusu uchambuzi wa

yaliyomo katika matini (mashairi husika). Maktaba na tovuti mbalimbali zilitegemewa kupata

taarifa kulenga mashairi mapokeo. Mchango wa utafiti huu ni kutoa mwanga muhimu wa

kuhakiki mashairi kwa wanafunzi na wasomi wa vyuo na vyuo vikuu pamoja na wapenzi binafsi

wa ushairi wa Kiswahili na uhakiki wake.

Page 7: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

vii

ABSTRACT

For long time poetry has remained a very important part in the study of Kiswahili literature.

Prosodic poems have existed for several centuries now. These poems required the poet to follow

a specific structure while composing them. Later Kiswahili scholars like Euphrase Kezilahabi,

M.M Mulokozi and C. Kahigi came up with free verse poems which focused most on themes and

message. Prosodic poems were therefore criticized for preferring form and style to themes.

Following the widespread acceptance of free verse poems, further research in prosodic poems is

required so as to continue preserving their place in Kiswahili literature .On the other hand, up to

now available research reports about analysis of Sauti ya Dhiki poems touch on single aspects of

poems instead of several. This research aimed at analyzing style and themes in selected poems

in Abdilatif’ Abdalla’s Sauti ya Dhiki. Such selection is due to similarity of the structure of many

poems in the anthology. It was researched on how the poet has used characters, poetic devices

and structure and how these components generate certain themes. The poems were purposively

sampled based on the type of characters, poetic devices, number of stanzas and themes generated

by these aspects. The research relied on structuralism, poststructuralism and functionalism

theories. The method of research used was content analysis of the relevant selected poems. It

involved visiting various libraries and websites to get information relevant to prosodic poems.

The results of the research are expected to give important insight on poetic analysis to students

and scholars in colleges and universities as well as individuals interested in Kiswahili research

and poetry.

Page 8: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

viii

YALIYOMO

UNGAMO NA IDHINI.............................................................................................ii

HAKILINZI...............................................................................................................iii

TABARUKU………………………………………………………………………..iv

SHUKURANI……………………………………………………………………….v

IKISIRI……………………………………………………………………………..vi

ABSTRACT ..............................................................................................................vii

YALIYOMO………………………………………………………………………viii

SURA YA KWANZA: UTANGULIZI ..................................................................1

1.1 Usuli wa Mada .....................................................................................................1

1.2 Suala la Utafiti ....................................................................................................4

1.3 Madhumuni ya Utafiti ..........................................................................................5

1.4 Maswali ya Utafiti................................................................................................5

1.5 Umuhimu wa Utafiti ............................................................................................6

1.6 Upeo na Mipaka ya Utafiti ...................................................................................7

1.7 Maelezo ya Istilahi ...............................................................................................8

SURA YA PILI :MAPITIO YA MAANDISHI NA MISINGI YA NADHARIA

2.1 Utangulizi .............................................................................................................10

2.2 Wahusika wa Mashairi .........................................................................................10

2.3 Mbinu za Lugha au Tamathali za Usemi .............................................................13

2.4 Muundo wa Mashairi ...........................................................................................19

2.5 Maudhui ya Mashairi……………………………………………………………25

2.6 Tafiti zinazohusiana na Utafiti huu ......................................................................29

2.7 Misingi ya Nadharia .............................................................................................33

SURA YA TATU : MBINU ZA UTAFITI ............................................................39

3.1 Utangulizi .............................................................................................................39

3.2 Muundo wa Utafiti ...............................................................................................39

3.3 Mahali pa Utafiti ..................................................................................................40

3.4 Uteuzi wa Sampuli ...............................................................................................40

Page 9: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

ix

3.5 Ukusanyaji wa Data………………………………………………………. 41

3.6 Uchanganuzi wa Data ..........................................................................................42

SURA YA NNE: UWASLISHAJI, UCHANGANUZI NA UFASIRI WA DATA

4.1 Utangulizi ...............................................................................................................43

4.2 Jinsi mshairi alivyotumia wahusika……………………………………………43

4.2.1 Sifa mbaya za wahusika………………………………………………………..44

4.2.2 Wahusika wapekuzi na werevu ...........................................................................47

4.3 Tamathali za usemi au mbinu za lugha .................................................................54

4.4 Muundo katika mashairi ......................................................................................74

4.5 Maudhui katika mashairi yaliyoteuliwa ..................................................................84

SURA YA TANO ........................................................................................................95

MUKHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ..........................................95

5.1 Utangulizi.…………………………………………………..…………………….95

5.2 Jinsi mshairi alivyotumia wahusika .....................................................................…95

5.2.2 Tamathali za usemi au mbinu za lugha ............................................................…97

5.2.3 Muundo .............................................................................................................…99

5.2.4 Maudhui ............................................................................................................…101

5.3 Hitimisho…………………………………………………………………………..102

5.4 Mapendekezo ...................................................................................................….107

Page 10: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

1

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI

1.1 Usuli wa Mada

Dhana ya ushairi katika jamii ya Waswahili imekuwepo katika fasihi simulizi kwa muda mrefu.

Mashairi ya tenzi yakawa kazi za kwanza wakati mashairi yalianza kuandikwa ikiwemo Utenzi

wa Mwalemba kuandikwa katika karne ya kumi na sita. Mwaka 1728 Mwego bin Athumani

akatunga Utenzi wa Tambuka naye Muhamadi Kijumwa akaandika Utendi wa Fumo Liyongo

mwaka 1913. Baada ya tenzi, Muyaka bin Hajji (1876) akatunga mashairi ya arudhi kama

tathlitha na tarbia kisha washairi wa baadaye kama Shaaban Robert (1933), Mathias Mnyampala

(1965) na pia Abdilatif’ Abdalla (1969) wakamuiga Muyaka kwa kiwango kikubwa katika utunzi

wao. Mashairi ya kabla ya uhuru nchini Kenya kwa mfano yaani miaka ya 1963 na kurudi

nyuma yalilenga maswala ya kidini na kijamii na pia kuanzia mwaka 1968 yakakumbwa na

upinzani kutokana na kuzuka kwa mashairi huru. Aina hizi mbili za mashairi kila wakati huwa

na fani na maudhui. Katika mantiki hii, swala la mashairi mapokeo kutungwa na hata

kuhakikiwa laonekana kuwa la lazima. Pia kuhifadhi nafasi yake katika usomi wa fasihi andishi

ya Kiswahili kusingewezekana kikamilifu bila tasnifu inayolenga vipengele kadha vya mashairi

ikiwa si vyote.

Utafiti huu ulichagua na kuhakiki mashairi teule katika diwani ya Sauti ya Dhiki ya Abdilatif’

Abdalla. Lengo lilikuwa kuweka wazi fani na maudhui ya mashairi haya. Diwani ya Sauti ya

Dhiki ni mojawapo ya diwani za mashairi yaliyojipambanua kwa kutoa mchango unaoaminika na

wasomi wengi kuwa mfano bora wa ufundi wa mashairi ya arudhi. Diwani hii ni muhimu sana

katika ushairi wa Kiswahili kwani takribani muundo wa tarbiya ambao aghalabu hutumika katika

ushairi wa Kiswahili wabainika katika diwani hii.

Abdilatif’ Abdalla ni mmojawapo wa washairi wa kusifika sana katika ulimwengu wa Kiswahili.

Alitunga diwani hii akiwa jela Shimo la Tewa na Kamiti (1969 – 1972), nchini Kenya. Yeye ni

mmojawapo wa washairi wa Kiswahili wasifika sana walio hai. Kazi yake imetafitiwa kama njia

mojawapo ya kuendeleza ushairi asilia wa Kiswahili wenye dhima nzito hata kwa ushairi wa leo

hii. Kuchanganya ushairi na siasa imekuwa sifa ya jamii ya Waswahili kwa muda na hata

Page 11: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

2

kihistoria Uswahilini, washairi kama Liyongo Fumo na Muyaka bin Haji walishiriki siasa za

maeneo yao pamoja na kutunga mashairi. Kama wakwasi hawa wa kabla yake, Abdalla ameishi

miongoni mwa Waswahili wenzake na hata kuwahi kutengwa nao akitumikia miaka mingi ya

kifungo na uhamisho. Alitumikia zaidi ya miaka mitano ya uhamisho kule Tanzania (Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam) na zaidi ya mingine kumi na tano kule London. Alishirikiana na

watetezi wengine wa kisiasa kama Ngugi wa Thiong’o kupinga utawala dhalimu wakati wa Rais

wa pili wa Kenya.

Baada ya kusoma mashairi ya mjombake wakati Abdilatif’ akiwa na umri wa miaka kumi na

miwili, pia alipata fursa ya kuzuru maeneo mengi ya Uswahilini ambapo Kiswahili

huzungumzwa. Mifano ni Mombasa,Iringa kule Tanganyika,Faza katika kisiwa cha Pate, kule

Lamu na Archipelago na Takaungu.Yeye hutumia lahaja ya Kimvita katika mashairi yake na pia

anaelewa lahaja nyinginezo nyingi. Mchango wake kustahili kutafitiwa una mashiko zaidi kwa

kuwa amechipuka kwa familia thabiti ya Waswahili katika makabila kumi na mawili ya

Mombasa jamaa zake wakiwa wasomi wa Kiislamu,washairi na matabibu wa kimila. Ndugu

zake ni kama Sheikh Adilahi Nassir, msomi maarufu wa Kiislamu na mchapishaji wa awali na

mwanasiasa wa Uswahilini pamoja na Ustadh Ahmad Nassir Juma Bhalo ambaye pia ni mshairi

maarufu na tabibu. Washairi kama hawa Uswahilini huthaminiwa sana kama wenye maarifa na

jukumu la kuzungumza kwa niaba ya wanajamii wenzao.

Abdilatif’ anatambulika zaidi kwa kazi zake nyinginezo kama ‘Kenya Twendapi.’Akapata tuzo

yake ya kwanza katika uandishi wa fasihi katika shairi lake toka kwa Kurani la Utenzi wa Adamu

na Hawaa. Kazi zake zaidi pia ni mihadhara kuhusu nafasi ya mashairi katika jamii na uhariri wa

mashairi. Zaidi ya hayo, Abdilatif’ ameandika tafsiri za Kiswahili ikiwemo riwaya ya Ayi Kwei

Arma ya Wema Hawajazaliwa pamoja na ile ya Mahmood Mamdam ya Waislamu wazuri,

Waislamu wabaya. Haya yote yanamuonyesha kama msomi maarufu wa kutoka Uswahilini na

pia aliyesifika nje ya Uswahilini. Ushairi wake ni kiwakilishi cha muoano wa ufundi wa

kizamani na wa kisasa kitaifa na kimataifa. Ushairi wake unawapa nafasi wasomi wengi wa

Afrika mashariki na kwingineko duniani kupata mguso wa ushairi wa Kiswahili uliotungwa na

Mswahili asilia.

Page 12: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

3

Kumekuwako na imani ya kimapokeo kuwa mashairi yoyote yale ni lazima yajifunge katika

kanuni za utunzi (arudhi maalum) kama inavyodhaniwa amefanya mtunzi huyu. Mifano ya

arudhi au sheria za utunzi ni uwiano wa mizani, vina, vipande na mishororo, muwala (mpangilio

mzuri wa mawazo) kwenye maneno, vipande, mishororo na beti na matumizi ya lugha Kteule

inayovutia. Mtunzi angekiuka kanuni hizi, mashairi yake yangeonekana chapwa na

yasiyokubalika kamwe. Kitula King’ei, mmoja wa watetezi wa mashairi mapokeo kwa mfano

katika utangulizi wa mashairi yake ya Miale ya Uzalendo anapinga mavue kwa kusema kuwa

dhana ya mashairi vue ni geni kabisa na isiyoambatana kamwe na kaida za ushairi wa Kiswahili.

Anasema mavue yaliletwa kwa pupa kwa kupapia ugeni toka utamaduni wa Kiingereza wala

hayana mashiko katika utamaduni wa ushairi wa kiafrika.

Lengo la utafiti huu ni kuangaza maswala kuhusu mashairi ya arudhi. Katika mashairi mapokeo

kama haya na mengineyo, ufundi wa utunzi wa mashairi ndio hutumika kukadiria kiwango cha

ubingwa wa mshairi. Kuna tafiti kadha zilizofanywa kuhusu mada tofautitofauti kulenga

mashairi ya Abdilatif’ Abdalla na Sauti ya Dhiki. Hata hivyo, vipengele vya fani na maudhui

nilivyohakiki havikulengwa katika tafiti hizo. Hili lathibitisha kuwa hakuna uhakiki kamili wa

kitaalamu uliofanywa hapo awali kulenga fani na maudhui ya mashairi haya yaliyohakikiwa.

Kipengele cha uhusika hasa kimetajwa tu katika tasnifu nyingi. Ikagundulika kuwa chahitaji

kuangaziwa zaidi. Ni kutokana na msukumo huu ulipopatikana mshawasha wa kuhakiki

vipengele hivi. Mifano ni muundo, lugha, wahusika na maudhui. Kwa kifupi, hili ndilo pengo

lililolengwa kuzibwa kuhusiana na uhakiki wa mashairi haya.

1.2 Suala la Utafiti

Malenga Addilatif’ Abdalla ni maarufu sana katika ulimwengu wa ushairi wa Kiswahili. Kuna

wataalamu kadha waliowahi kutilia guu kutafitia utunzi wake katika mashairi tofautitofauti.

Tafiti kama hizo zililenga mada fulani maalumu au kutoa mashairi yake kama mifano ya

kufafanua mada za wataalamu hao. Katika tafiti hizo, ni bayana kuwa hakuna utafiti hata mmoja

uliojitokeza kuhakiki vipengele vyote vya fani na maudhui katika tasnifu moja. Isitoshe, fani na

maudhui anayotumia ni za kipekee ingawa hazijaeleweka kikamilifu kwa wasomi wengi. Hii ni

kwa sababu mojawapo ya vipengele vya fani anavyotumia ni uhusika katika ushairi wake jambo

ambalo halijadhihirika kwa wengi. Ufundi wake wa lugha pia pamoja na muundo ni vipengele

Page 13: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

4

vinavyofaa kuchunguzwa kwa jicho la ndani zaidi kuliko vilivyobainishwa na wataalamu wa

hapo mbele. Wengi wametafitia ushairi wa Abdilatif’ lakini kwa fani na maudhui bado kuna

pengo. Kipengele cha uhusika na vile vingine vya fani na maudhui vimetafitiwa na wataalamu

wengine lakini havibainiki kutiliwa uzito unaostahili huku baadhi ya watafiti kama Marani(2014)

wakisisitiza shairi halina wahusika isipokuwa kwa tenzi na ngonjera. Kauli hii ni upotoshi kwa

wanafunzi wa ushairi. Hili lahalalisha utafiti wa kina kuhusu kipengele hiki na maudhui

yanayozuliwa nacho.

1.3 Madhumuni ya Utafiti

(i) Kutathmini jinsi mtunzi/malenga anavyotumia kipengele cha uhusika katika mashairi

yake.

(ii) Kuchambua ufundi wa lugha au tamathali za usemi katika mashairi teule ya Sauti ya

Dhiki.

(iii) Kuhakiki muundo wa mashairi teule katika diwani.

(iv) Kufafanua maudhui yanayozuliwa na fani katika mashairi yaliyoteuliwa.

1.4 Maswali ya Utafiti

(i) Kipengele cha uhusika kimetumika vipi katika mashairi teule ya Sauti ya Dhiki?

(ii) Mtunzi ametumia mbinu zipi za lugha au tamathali za usemi katika mashairi yake?

(iii) Ni vipengele vipi vya muundo alivyozingatia mtunzi katika mashairi yaliyoteuliwa?

(iv) Vipengele vya fani vinazua maudhui ya aina gani katika mashairi husika?

1.5 Umuhimu wa Utafiti

Uhakiki wa ushairi ni mada muhimu sana katika fasihi yoyote ile iwe simulizi au andishi. Usomi

wa fasihi nao ni kipengele kisichoweza kupuuzwa katika somo la Kiswahili.Utafiti huu

ulichagua sampuli za mashairi kumi na mawili katika diwani ya Sauti ya Dhiki kisha kuhakiki

fani na maudhui yaliyotumiwa na malenga. Wahusika, muundo, mbinu za lugha na tamathali za

usemi na namna vipengele hivi vinavyozua maudhui maalumu ni mambo yaliyotathminiwa.

Inaelekea kwamba wanafunzi wa viwango mbalimbali vya usomi ikiwemo wa vyuo vya juu

hupata changamoto kadha kuhusiana na uchambuzi wa mashairi. Wengi wao hata hawana

Page 14: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

5

fununu kuhusu fani ya ushairi. Marani(2006) anapotafitia hali ya Kiswahili katika vyuo vikuu

kwa mfano anaeleza kwamba vyuo vingi vya umma na vya kibinafsi vina idara za Kiswahili.

Katika idara hizo, lugha ya Kiswahili hutegemewa kufunza kozi za Kiswahili. Pia anasema

vitabu vya fasihi ya Kiswahili vyuoni ni vichache mno. Tasnifu hii inalengwa kuwa nyenzo ya

ziada kwa vitabu kama hivyo. Zaidi ni kuwa mada ya ushairi hutajwa kwa ufinyu katika vyuo

vingi vikuu kwani msisitizo huwekwa kwa semantiki, mofolojia na kazi nyinginezo za fasihi

lakini ushairi ukitajwa kwa kiwango fulani tu.

Inatarajiwa matokeo ya utafiti huu ni nyenzo ya kuimarisha usomi wa ushairi wa Kiswahili

pamoja na waratibu wa mitaala ya fasihi kupata mwanga mpya katika juhudi zao. Pamoja na

hayo, maarifa yaliyopo kwa sasa kuhusiana na pia yanayokaribiana na ya Abdilatif’

yataongezwa. Wanaojifunza ushairi wa Kiswahili kwa mara ya kwanza watafaidika zaidi. Lugha

ya Kiswahili ikiimarika sasa hivi ni afueni kubwa kwa taifa la Kenya hasa kwani tangu mwaka

wa 2010 lugha hii ni ya taifa na pia rasmi kulingana na sehemu ya 7(1), (2) na (3) sheria za

Kenya. Mwisho, uchambuzi wa ushairi ni njia mojawapo wa kueleza msamiati wa utunzi kwa

kuweka maana yake wazi hivyo basi kuimarisha mawasiliano. Pia msamiati huu ni njia

mojawapo ya kukejeli hali fulani mbaya katika jamii na hivyo kuimarisha maadili ya jamii yetu.

1.6 Upeo na Mipaka ya Utafiti

Mashairi yote yaliyohakikiwa yalitoka kwa diwani ya Sauti ya Dhiki. Kwa kuzingatia vipengele

vinne vya mada vilivyohakikiwa fani na maudhui zilihakikiwa. Sampuli kumi na mbili za

mashairi ziliteuliwa na kuchunguzwa baada ya kupangwa ifuatavyo:-

a) Mashairi yenye wahusika binadamu:- Katika kikundi hiki nilihakiki mashairi kama vile:

‘Kutendana’, ‘Ukamilifu wa mja’ na ‘Mja si mwema’.

b) Mashairi yaliyo na lugha teule na ya kitamathali. Hapa kulikuwa na mashairi kama vile

‘N’shishielo ni lilo’, ‘Wasiwasi enda zako’ na ‘Telezi’.

c) Kwa mashairi yenye muundo wa tarbia na yaliyobuniwa kwa chini ya beti kumi kulikuwa

na mashairi kama ‘Siwati’, ‘Leo nisingekuwako’ na ‘N’sharudi’.

d) Mashairi yaliyolenga maudhui ya kisiasa, kijamii na kiuchumi yalikuwa na ‘Wasafiri

Tuamkeni’, ‘Kichu Hakiwi na uchu’ na ‘Mamaetu Afrika’.

Page 15: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

6

Jumla ya mashairi katika diwani ni arubaini ila haya kumi na mawili yakateuliwa kimakusudi

kwani hayakulengwa na watafiti waliotangulia hasa wakilenga mada au nadharia ya utafiti huu.

Kuzingatia kigezo hiki kuteua sampuli hizi ndicho faafu zaidi kwa kuwa kililenga vipengele

vyote vya fani na maudhui vilivyohakikiwa. Baadaye mada lengwa ilihakikiwa kwa undani

katika kila kikundi cha mashairi kulingana na madhumuni ya utafiti. Kwa kila kikundi cha

sampuli fani zilielezwa kama zilivyobainika hivyo kuchukuliwa kama kiwakilishi mwafaka cha

ufundi wa mtunzi katika mashairi husika.

1.7 Maelezo ya Istilahi

Dhamira:- Lengo, kusudi au nia ya mshairi

Diwani :- Kitabu cha mashairi

Falsafa ya mwandishi :-Huu ni msimamo wa malenga kuhusu suala linalorejelewa katika shairi.

Maoni yake kuhusu jambo fulani ni yapi ?

Fani :- Ni jinsi au ufundi wa kuwasilisha maudhui ya shairi.

Kunga za kishairi :- Hizi ni mbinu za kishairi kama vile urefusho, ukopaji wa maneno ya

kigeni, matumizi ya maneno ya kizamani, uborongaji, lugha fiche na kadhalika.

Maudhui:- Ni mukhtasari wa mambo muhimu au hoja muhimu anazojishughulisha nazo mtunzi

wa kazi ya fasihi.

Mbinu za lugha :- Ni tamathali za usemi pamoja na fani mbalimbali zilizotumika na mshairi

kutosheleza maudhui yake. Mifano ni methali, takriri, istiara na kadhalika.

Mtindo:- ni namna ya kupanga fani au maudhui ili kujenga shairi kwa njia ambayo hubainisha

upekee wa shairi. Hujumuisha vipengele vyote vya ushairi kama vile muundo,

matumizi ya lugha, wahusika na maudhui.

Muktadha :- Sifa zinazijitokeza katika shairi kisiasa, kiuchumi, kijamii, kikazi na kadhalika.

Muktadha hutuelekeza kwenye maudhui na dhamira.

Muundo :- Ni mpango na mtiririko wa kazi ya fasihi. Katika ushairi hurejelea namna shairi

lilivyoumbwa.

Tamathali za usemi :- Ni maneno, nahau au sentensi ambazo hutumiwa na msanii wa fasihi ili

kutia nguvu katika maana, mtindo na hata sauti katika maandishi ama kusema.

Toni :- Huu ni ule mtiririko au msuko wa lugha unaodhihirisha au unaoashiria hisia ya furaha,

msiba, huzuni na kadhalika katika shairi.

Page 16: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

7

Uguni :- Ni dosari au kasoro fulani katika shairi.

Uhakiki :- Haya ni maelezo yanayoeleza undani wa kazi fulani ya fasihi (kama vile shairi] kwa

kumulika uzuri na udhaifu wake. Uhakiki wa mashairi hulenga dhamira na maudhui,

umbo, kunga za kishairi na matumizi ya lugha.

Uhuru wa kishairi :- Ni uhuru mshairi wa Kiswahili anao wa kutunga pasi na kuzingatia kanuni

za sarufi.

Umbo :- Ni sura ya nje ya shairi inayotokana na bahari, mpangilio wa mizani, vina, vipande,

mistari, vituo na idadi ya beti.

Utoshelezi :- Shairi kuwa na wazo linaloendelezwa na kukamilishwa kimantiki.

Nafsineni - ni mhusika anayesema ujumbe fulani katika shairi. Ni jina jingine la mshairi katika

shairi husika.

Page 17: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

8

SURA YA PILI

MAPITIO YA MAANDISHI NA MISINGI YA NADHARIA

2.1 Utangulizi

Sura hii ililenga kuangazia maandishi ya wataalamu mbalimbali kuhusu ushairi wa Kiswahili.

Kwa kuongozwa na madhumuni ya utafiti huu, sura hii ililenga wahusika katika mashairi,

kuchambua ufundi wa lugha au tamathali za usemi, kuhakiki muundo wa mashairi hayo kisha

maudhui. Tafiti zilizofanywa kuhusiana na diwani ya Sauti ya Dhiki na namna zilifaidi au

kutofautiana na utafiti huu ziliangaziwa. Hatimaye mtafiti akaelezea nadharia zilizokuwa msingi

wa utafiti.

2.2 Wahusika wa Mashairi

Kuhakiki shairi kwahitaji kuelewa kuhusu wahusika. Kisia na Mwarandani (2007) wanasema

kuwa katika ushairi wapo wahusika. Mhusika wa kwanza ni mtunzi mwenyewe. Yeye huwa ana

kisababisho cha utunzi huo kilichompata yeye au kukisikia kuhusu mtu ambaye ataka aseme

katika utungo wake. Pia kuna wale ambao anawasiliana nao, wale anaowakusudia ujumbe; kuna

msomaji na msikilizaji.

Kwa vile mhusika ni mtendaji, hata mtunzi hukifanya kitu kisicho na uhai ambacho huwa

amekifanya huyo mhusika wake. Ama mtunzi huweza kutumia mbinu ya litifati – mbinu ambayo

ni kama ile ya msemo halisi, ambapo mtunzi anasemewa maneno yake na mhusika mwingine

lakini maneno yenyewe yakawa kama kwamba yanasemwa na mhusika wa kwanza.

Ansani (2011) anasisitiza kwamba wahusika katika ushairi si muhimu kama walivyo kwa

nathari. Anasisitiza kuwa twaweza pata mashairi mengi yasiyo na wahusika. Mara nyingine

hakuna kiumbe yeyote hai katika ushairi. Hata hivyo, ni vigumu kupata tamthilia au riwaya bila

wahusika. Anasema pia kuna mashairi yenye wahusika ingawa wamebanwa kutokana na ufupi

wa kazi yenyewe ya sanaa. Wahusika katika shairi hutumika tu kudokeza jambo. Kulingana na

Makala yake kuhusu ‘Kujenga wahusika katika shairi’ Mei 4, 2011, shairi hutaja tu jambo

kuhusu maisha ya mhusika halafu msomaji akaachwa kulitafakari.

Page 18: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

9

Uhakiki wa mashairi ya Robert Frost uliofanywa na Sparknote (2012) nao unaonyesha kuwa

mashairi mengine huandikwa katika nafsi ya kwanza yakiwa na mhusika maalumu. Ingawa

mshairi aweza kuwa si yuleyule, kuna mambo yanayohusu sauti ya Frost mwenyewe. Haya

yanaonyesha uhusika wa Frost mwenyewe k.m anavyopambana na hali za maisha kama vile

upweke, msongo wa mawazo na mengine anapofuata njia ambayo haifuatwi na watu wengine

katika jamii. Mara nyingine mshairi mwenyewe (Frost) anajitenga na uhusika ili kuzua kinaya

kuhusu maana nzima ya shairi. Utafiti huu ulifaidi wangu kwa kuwa nilihakiki nafsineni kama

alivyosawiriwa. Pia nilihakiki sifa za wahusika waliotumiwa na mshairi huyu aidha kama

binadamu au wa aina tofauti kuwakilisha binadamu. Msisitizo wa wataalamu waliotangulia ni

kwa mashairi tofauti wangu ukiwa kwa diwani ya Sauti ya dhiki.

Kulingana na Njogu na Nganje (2006), mashairi mengi hayana wahusika lakini mashairi ya

masimulizi huwa nao. Tungo kama hizo huwa ni za kimajibizano na wahusika huongea kishairi.

Tungo nyingi hutumia wahusika katika ujengaji na upelekaji mbele wa maudhui.Wanasisitiza

kuwa katika kuhakiki wahusika twafaa kuangalia wahusika hao wana sifa za aina gani, yaani

tabia zao, wanaingiliana vipi na ni taswira gani tunayopata tukizingatia matendo yao au maneno

yao.

Waititu na Ipara (2005) wakizungumzia fani katika mashairi ya arudhi wanasema kuwa uhusika

ni kipengele mojawapo cha fani.Wanasema kuwa mengi ya mashairi ya jadi hayana wahusika

bayana. Hatahivyo, yapo machache yenye wahusika wa dhati. Watafiti hao wanatoa mfano wa

shairi la ‘N’sharudi’ wakisisitiza kuwa mhusika wa shairi hilo ni mshairi mwenyewe. Mchango

wa watafiti hao umekuwa kichocheo kwa huu hadi kuishia kuhakiki uhusika hata katika mashairi

mengine ya diwani hiyohiyo. Msisitizo ni kuwa hata katika shairi hilohilo la ‘N’sharudi’ kuna

wahusika zaidi ya nafsineni tu. Mifano ni wale wapinzani wake, jamaa na marafiki. Hata

hivyo,katika kuhakiki wahusika shairi hilo halikulengwa. Pamoja na hayo, katika madhumuni ya

kuhakiki muundo, shairi hilo limelengwa na hata wahusika zaidi ya waliotajwa na watafiti hao

kubainishwa.

Utafiti huu, unakubaliana na watafiti hawa japo shingo upande. Kwa mtazamo wa utafiti huu,

maoni yao haya ni ya kijumla na kijuujuu kwa kiwango fulani. Isipokuwa katika uhakiki wa

Page 19: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

10

mashairi ya Frost, hakuna mashairi yoyote maalumu yaliyolengwa na wataalumu hawa.

Ninaweza pia kuchukua kauli kuwa hata hayo mashairi ya Frost ni ya Kiingereza wala si ya

Kiswahili ikieleweka utafiti wangu huu ni wa ushairi wa Kiswahili hasa wa Abdilatif’ Abdalla.

Zaidi ya hayo, katika utafiti huu Ansani alipingwa kikamilifu kwa kusema kuwa haiwezekani

ushairi kutokuwa na wahusika. Katika diwani ya Sauti ya Dhiki, hakuna shairi hata moja

lisilopata wahusika wake kubainika na kuhakikiwa. Sidhani ningepotoka au kuenda nje ya mada

nikisema kuwa wataalamu hawa hawajalenga kazi yoyote ya Abdilatif’ Abdalla au hata ushairi

wa Uswahilini.

2.3 Mbinu za Lugha au Tamathali za Usemi

Uhakiki wa shairi kila wakati unalazimu mhakiki kufahamu mbinu za lugha zilivyotumika.

Ngure (2014) anapozungumzia fasihi bora anasema kuwa fasihi ni sanaa inayotumia lugha ili

kueleza maisha na tajriba ya binadamu hasa kwa namna anavyotangamana na binadamu wenzake

pamoja na mazingira yake. Anasema kuwa fasihi ni sanaa inayotuchorea taswira ya uhalisia wa

maisha ya binadamu. Hivyo inawasilisha hali, maingiliano, mivutano na mikinzano miongoni

mwa binadamu na mazingira yake.

Msomaji au msikilizaji wa kazi ya fasihi hupata na tajriba za hali inayowasilishwa na wahusika

wa kazi hiyo kama walivyosawiriwa. Kutosheka tunakopata katika kazi ya fasihi hakutokani tu

na habari tunazozipokea katika kazi hiyo bali pia kutokana na ufinyanzi wa lugha teule yaani

umbuji. Kwa maoni ya Ngure (2014) njia mojawapo ya kuelimisha, kufaulisha, kufundisha na

kuzindua kupitia fasihi ni kuteua maudhui yenye mguso kwa jamii na kuyasimulia kwa kiwango

cha juu cha umbuji.

Senkoro (1982) kwa upande wake ana maoni kuwa lugha ndiyo mzizi wa kazi ya fasihi na bila

hiyo, hakuwezi kuwa na fasihi. Ndiyo hutumiwa na msanii kuyaibusha mawazo yake katika kazi

hiyo. Kulingana naye kuna matumizi ya lugha ya aina aina. Humu tunagundua tamathali za

usemi, misemo, nahau, methali, lugha za wahusika hasa lahaja zao, uchaguzi wa msamiati,

miundo ya sentensi, ufundi wa kutoa maelezo hasa ya wahusika na utamu wa lugha yenyewe

itumiwayo. Mtaalamu huyu anachukulia tamathali za usemi kuwa maneno, nahau au sentensi

ambazo hutumiwa na wasanii wa fasihi ili kutia nguvu katika maana, mtindo na hata sauti katika

Page 20: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

11

maandishi ama kusema. Hizi wakati mwingine hutumiwa kwa njia ya lugha kuipamba kazi ya

fasihi na kuongeza utamu wa lugha. Diwani ya Sauti ya Dhiki ina matumizi ya lugha

niliyohakiki.

Ingawa maoni haya ya Ngure yanalandana na utafiti huu kwa upande mmoja, mtaalamu huyu

ameegemea upande wa kazi ya riwaya hasa ile ya Kidagaa kimemwozea ya Ken Walibora.

Hajagusia chochote kuhusu uhakiki wa ushairi ikiwa si kuhakiki mashairi ya Sauti ya Dhiki.

Senkoro pia amehakiki mseto wa kazi mbalimbali za fasihi ikiwemo riwaya, hadithi, mashairi na

hata tamthilia. Naweza kuchukua mwelekeo na hata msimamo kuwa hata yeye japo ametoa

mchango tambulika katika uhakiki, bado hajalenga au kuhakiki haya mashairi niliyohakiki.

Mmoja wa wataalamu waliohakiki diwani ya Sauti ya Dhiki ni Chacha (1992). Anasisitiza

utamthlia wa baadhi ya mashairi ambao wasomi waliotangulia pia walikuwa wameutaja.

Mashairi anayoyataja ni ‘Vuta N’kuvute’ na ‘Kutendana’. Japo mashairi anayohakiki ni kutoka

diwani ya Sauti ya Dhiki, tofauti na utafiti wangu ni kuwa anazingatia mashairi manne tu na pia

mada anayotafitia ni utamthlia wa mashairi hayo tu wala si vipengele vyote vya fani na maudhui

kama nilivyohakiki.

Matteru (1975) vilevile ni mmoja wa wasomi waliohakiki diwani ya Sauti ya Dhiki. Anadokeza

juu ya fani na mada mbalimbali ambazo mwandishi anaziibua. Katika Matteru (1975:28)

anaonyesha jinsi Sauti ya Dhiki ilivyo utetezi, maombolezo, ujumbe, kiu ya heri, sauti ya shime,

mjadala wa nafsi na kitulizo. Ieleweke kwamba Matteru anaashiria ujumbe huku nikilenga fani

na maudhui kwa ujumla. Faida yake kwa utafiti huu ni kuwa kazi yake ilitokea kuwa chanzo cha

kuhakiki diwani tena.

Ingawa Chacha anajishughulisha na swala la fani au mtindo, mwegemeo wa utafiti wake si fani

na maudhui ya mashairi haya bali tu utamthilia wake. Hata hivyo, utafiti huo unafaidi wangu

kwani kwa kiwango fulani umezingatia mawili ya mashairi niliyochunguza katika diwani hii ya

Sauti ya Dhiki. Hapa kwa hivyo nikapata upenyo muhimu wa kuhakiki kilichobaki kwa kulenga

fani na maudhui.

Page 21: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

12

Mohammed (1977) anaiona fani ya Sauti ya Dhiki kama zao la kariha, ghamidha na ghadhabu za

mtunzi. Anapoijadili fani anataja mtindo wa utunzi, lahaja anayotumia kiutunzi na uteuzi wa

maneno kama njia yenye mguso hasa katika kuelezea maudhui. Ingawa anadokeza fani na

maudhui, yeye haingilii vipengele hivi kwa kina. Nililenga kuhakiki vipengele vyote vya fani na

maudhui vinavyotambulika katika mashairi haya teule.

Zaidi ya watafiti hao, Mwamzandi (1996) amehakiki matumizi ya mbinu za kimaigizo katika

tungo za Abdilatif Abdalla. Tungo zilizoshughulikiwa ni pamoja na Utenzi wa maisha ya Adamu

Hawaa (1991), ‘Mnazi, Vuta N’kuvute’, ‘Kutendana’ na ‘Usiniuwe’. Yeye hazingatii mashairi

mengi bali haya manne tu kutoka kwa diwani ya Sauti ya Dhiki. Pia halengi sehemu kadha za

fani na maudhui kama nifanyavyo ila mbinu za kimaigizo peke yake. Hii ndiyo tofauti kati ya

tafiti zetu.

Mekacha (1996) anauona ushairi kama mojawapo ya tanzu za sanaa itumiayo lugha ili kusawiri

na kuakisi uyakini wa maisha. Pia ni utanzu wa fasihi ambao kama tanzu nyingine za fasihi

huwa na maudhui. Lyndon Harries na marehemu W. Hichens (1962) wana maoni kuwa mshairi

huweza kuwa na ufundi wa kutumia maneno ya kigeni kwa mfano lugha ya Kiarabu au Kituruki

katika shairi la Kiswahili. Hii huonyesha athari kutokana na mazingira au dini ya mshairi. Pia

kuna ufundi wa kupangua maneno katika mshororo. Lengo hapa huwa kuzua mubalagha au

kusisitiza jambo. Utafiti huu ulilenga kupinga hali kama hiyo kwa kusisitiza kuwa hufanyika

katika utunzi maalumu au hata kipindi maalumu cha wakati pamoja na mazingira ya utunzi

wenyewe. Katika hali ambayo mshairi hakuathiriwa au hataki athari yoyote ya kigeni, ushairi

wake utakuwa katika lugha ya Kiswahili pekee.

Kuhusiana na dhana ya uradidi katika Kiswahili, Ashton (1944:316) ameonyesha matumizi ya

aina nne za dhana hii: Kutilia mkazo jambo, kuonyesha uendelezo wa jambo na kuonyesha

mueneo wa jambo. Polome (1967:82, 84, 94, 104-105) pamoja na Kapinga (1983:180)

wamegusia uradidi kwa kusema kuwa huhusu kutaja kitu kilekile mara mbili. Maelezo ya

wataalamu hawa yameonyesha kwa mifano kuwa tendo la kukariri au urudiaji wa sauti ndio

msingi wa dhana hii ya uradidi kama aelezavyo Winter (1970:190) kuwa “uradidi unaweza

Page 22: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

13

kusemwa kuwa ni urudiaji wa sauti nzima au sehemu yake au mfuatano wa sauti katika neno.

Ufundi huu ukatajwa hapa na ukaenea hadi kutafitiwa katika tasnifu hii. Hii ni faida si haba.

Ingawa Ilihakikiwa takriri kama mojawapo ya matumizi ya lugha, imeonyeshwa aina zaidi ya

takriri kuliko zinazotajwa na wataalumu hawa. Mifano ni takriri ya vina vya kati na vya mwisho,

ya kibwagizo na hata ya umbo la shairi kama vile la tarbia katika shairi moja au hata mashairi

kadha. Hata hivyo, sababu ya kutumika hivyo ilibainika kuwa ileile ya kusisitisa ujumbe au

kudumisha ufundi wa mashairi.

Mtaalamu zaidi aliyeshughulikia fani ya mashairi ni Alembi (1999). Anasema fani ya ushairi

hutathmini mkondo ambao kupitia kwake ujumbe wa shairi hupitishwa kwetu. Hurahisisha

uelewa wetu wa shairi. Kulingana na Alembi, fani huhusisha shada, mkazo/ msisitizo, mizani/

mapigo, takriri, vina, tashihisi, taswira, ishara (kuwakilisha dhana), uteuzi na matumizi ya

maneno, onomatopia / tanakali sauti, takriri ya silabi za mwanzo, mshabaha wa irabu za shada

katika maneno mawili au zaidi na mubalagha/ kutia chumvi.

Utafiti wa mtaalamu huyu unahusiana na huu kwani ililazimu kuhakikiwe vipengele hivi vya

fani kama vinavyotumika katika diwani ya Sauti ya Dhiki. Pia yafaa kueleweka kwamba Alembi

pamoja na wataalamu waliotangulia hawakujishughulisha na diwani hii. Hii ndiyo tofauti ya

utafiti huu na wao. Kwa upande mwingine, Ramadhani (Mulika na.3) anazieleza sifa za msingi

zinazohusu ushairi wa Kiswahili. Anasema hizi huwasilishwa kwa msomaji kwa njia ya lugha

teule ya kitamathali. Pia shairi ni muungano wa yaliyomo (maudhui) na fani.

Ilihakikiwa ni kwa nini Abdilatif alilenga kuwasilisha hisi zake kwa lugha teule na ikiwa hii ni

ya kitamathali. Pia ikahakikiwa namna aina ya maudhui aliyozungumzia mshairi

yanavyosababisha au kuchangia lugha ya kitamathali. Euphrase Kezilahabi naye anasema ushairi

ni hali, tukio au wazo ambalo limeonyeshwa kwetu kutokana na upangaji mzuri wa maneno

fasaha yenye mizani kwa ufupi ili kuonyesha ukweli fulani wa maisha. Kulingana na J.

Ramadhani, katika ushairi vitu hupewa nafsi na utu; picha ni sifa muhimu za ushairi na huweza

kuwa na mpangilio wa maneno usio wa kawaida. Pia una ridhimu[mizani],mlingano wa sauti na

mapigo na shairi ni lazima lionyeshe sifa ya kiuimbaji lisiwe nakala ya shairi jingine. Kuhusiana

Page 23: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

14

na diwani hii nililenga kuhakiki iwapo Abdilatif alizingatia kigezo hiki au la kwani Ramadhani

hakumrejelea kamwe.

Kwa upande wa lugha katika Utenzi wa Mwanakupona, Mulokozi (2000) anahakiki ni lahaja ipi

imetumiwa na ikiwa mshairi anaimudu vizuri, ikiwa ni lugha nyepesi au inayolenga kuonyesha

ubingwa wa mshairi kwa kutumia maneno mazito na msamiati mgumu. Pia anaangalia lugha ya

picha hususan tashbiha, istiara na taswira. Nilipofanya uhakiki wa Sauti ya Dhiki nilizingatia

kilahaja (Kimvita) wala si Kiamu kama katika Utenzi wa mwanakupona na pia uzito au wepesi

wa lugha na msamiati, yote haya yakizingatiwa na washairi husika kwa azma tofauti.

David na Wamuhu (1989) nao wanasema kuwa ni muhimu kupata hisia na maoni ya mshairi

kwani hueleza tajriba yake. Ufundi waweza kuhusu lugha rahisi kueleweweka kama lugha ya

Wimbo wa Lawino. Ni muhimu kuelewa maana ya ushairi kwanza. Taswira ndiyo tamathali

muhimu zaidi kwa shairi. La sivyo, ushairi utakuwa sawa na nathari. Taswira hupatikana kwa

mshairi kuzingatia mifano ya maisha halisi. Wanasisitiza kuwa kuna aina mbili za taswira. Ya

kwanza ni istiara au jazanda. Mfano ni kusema mtu fulani ni ‘simba’ ikiwa na maana ya ndani.

Pia kuna taswira kwa tashbihi. Baada ya hapa ni muhimu kuelewa hali au toni ya shairi. Hii

yamaanisha hisia au mwelekeo wa sauti katika shairi. Mshairi aweza kutoa hasira, upendo,

furaha, huruma, msongo, kuchanganyikiwa au kejeli. Washairi hushirikiana nasi kero au silika

kuu waliyonayo. Hii ni sawa na hatibu ambaye huzungumza hotuba wala si kuipa hadhira nakala

ya hotuba iliyoandikwa . Kuna ridhimu ya sauti pamoja na takriri. Baadhi ya mashairi hutegemea

sauti za maneno kuliko mashairi mengine. Pia kuna kuanza mshororo kwa konsonanti moja.

2.4 Muundo wa Mashairi

Katika kuhakiki mashairi, muundo hutiliwa maanani. Kuhusu muundo wa kazi ya fasihi Senkoro

(1982) anasema muundo ni mpango na mtiririko wa kazi hiyo kwa upande wa visa na matukio.

Hapa basi tunachunguza vile ambavyo msanii au mtunzi alivyofuma, alivyounda na

alivyounganisha tukio moja na lingine, kitendo kimoja na kingine, wazo na wazo, sura moja na

nyingine, ubeti na ubeti na hata mstari wa ubeti na mwingine. Licha ya maelezo kuhusu muundo,

Senkoro hakulenga chochote kuhusu muundo wa mashairi haya ya Sauti ya Dhiki niliyohakiki.

Page 24: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

15

Topan (1971) akizungumzia muundo wa mashairi anasema ingawa tenzi zimetukuka sana toka

mwaka 1728 mpaka miaka hii ya leo, watunzi wengi wamependa kutumia zaidi mashairi kuliko

tenzi. Mashairi ya tathlitha, yenye mistari mitatu kila ubeti na ya takhmisa, yenye mistari mitano

kila ubeti yametumiwa na washairi wachache sana lakini mashairi ya tarbia yenye mistari minne

kila ubeti na hasa ya uzani wa mizani kumi na sita iliyogawanyika kwa mizani nane nane

yamestawishwa vikubwa. Imekuwa kama mtu akiamua kuandika mashairi kwa kawaida

ataandika shairi la muundo huo. Litakuwa na mizani kumi na sita zilizogawanyika katikati, vina

vya ndani na vya mwisho na pia kituo.

Kulingana na Mekacha (1996), uwezo wa kuathiri linaokuwa nao shairi unatokana na lile umbo

lake maalumu. Baadhi ya vipengele vinavyolipa umbo la shairi upekee ni mpangilio wa sauti

wenye mapigo ya kimuziki na wizani, maelezo mafupi na yenye kunata, matumizi bora ya picha,

ishara na tamathali za semi na ukiukaji wa mfuatano wa kawaida wa maneno katika tungo

(Kahigi 1975, Mulokozi 1975 na Finnegan 1970 na 1977).

Mekacha anasema washairi huweza kuwianisha sauti za lugha na ujumbe unaodhamiriwa.

Muafaka huu wa sauti na maana husababisha baadhi ya sauti kubebeshwa maana za zaidi licha

ya maana za msingi. Jambo hili laweza kufanywa kwa mfano kwa kurudiarudia. Shairi vilevile

laweza kuwa na wizani fulani utokanao na mapangilio wa sauti fulani katika lugha, kwa mfano:

‘Titi la mama li tamu hata likiwa la mbwa’. Mashairi mengine ya kimapokeo huwa na urari wa

vina na mizani. Urari huu hutokea kuwa na mguso wa kipekee unaotekenya ngoma za masikio.

Mpangilio wa sauti za lugha huleta mguso wa kiusikivu na wa kisanaa.

Abdulaziz (1979) anadai kuwa kuhusiana na mashairi mapokeo kuna marefu ya beti nyingi na

hata mafupi ya ubeti mmoja tu. Pia anasema kubadilika kwa idadi ya silabi (mizani) katika

kipande husababisha shairi la mapokeo kuwa guni. Utafiti wangu ulifaidika sana na maoni haya

ya Kahigi (1975), Mulokozi (1975), Finnegan (1977) na Abdulaziz (1979). Hii ni kwa sababu

nilihakiki mashairi marefu na pia ya beti nyingi. Kuhusiana na muundo, beti, mishororo, vina na

mizani zilikuwa baadhi ya arudhi za utunzi nilizohakiki.

Page 25: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

16

Quinn (1992) anapozungumzia namna ambavyo fasihi hufanya kazi anasema kuwa shairi fupi ni

muundo changamano; muundo wa maneno na sintaksia. Kuelewa linavyofanya kazi huhusisha

kuchunguza namna lilivyounganishwa, yaani ule ujenzi au muundo wake. Shairi pia laweza

ashiria jinsi ulimwengu unavyofanya kazi. Anasema tusome riwaya au shairi kwa kutegemea

kazi hiyo ilivyo na kwa kuridhika tunakopata kutokana na maneno ya shairi hilo yalivyopangwa

na yanavyofanya kazi. Anasema mashairi huwasilisha uhalisia au ukweli ambao ni lazima

tuuelewe na hatuwezi kuupuuza. Twafaa kuelewa mtunzi anamaanisha nini au anajaribu

kumaanisha nini. Kulingana na Quinn (1992:211), ili kazi ya sanaa ifanye kazi kama riwaya au

shairi kwa vyovyote vile, ni lazima iwe na dhima ya kimaadili kwa jamii. Anasisitiza kuwa wazo

fulani laweza ingizwa na mtunzi kwa kazi ya sanaa likihitaji kuchunguzwa kwa undani. Zaidi ya

hayo, anasema kuwa mhakiki akitenga muundo na maudhui kwa azima ya uhakiki, riwaya au

shairi hilo hutawanyika kwa mawazo yetu mpaka tutakapoliunganisha tena upya. Anamalizia

kwa kusema shairi ambalo huadilisha kwa njia ya moja kwa moja kama mahubiri ni shairi bovu.

Kazi ya sanaa kwa hivyo haifai kutuelekeza kwa njia ya moja kwa moja kwa ambacho twafaa au

tusichofaa kufanya.

Quinn (1992) anaelezea pia kuwa muundo huhusu mipangilio ambayo hutawala kazi ya sanaa.

Anasema umbo huweza kuchunguzwa katika matini fulani maalumu. Umbo ndilo kazi fulani ya

sanaa huweza au inaweza kuzishirikisha kazi zingine kiutoshelevu bila kuonekana kama familia

au tamaduni. Muundo huo ndio huleta upekee wa kazi fulani ya sanaa.

Massamba (1983:5) anarejelea Shaaban Robert, mmoja wa wanamapokeo kuhusiana na maana

ya ushairi. Shaaban anasema, “Ushairi ni sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno

machache au muhtasari”. Kuhusu wimbo, ushairi na tenzi anasema kuwa wimbo ni shairi dogo,

ushairi ni wimbo mkubwa na utenzi ni upeo wa ushairi. Kina nacho ni mlingano wa sauti za

herufi. Kwa maneno mengine huitwa mizani ya sauti na ufasaha ni uzuri wa lugha. Mawazo,

maoni na fikra za ndani zinapoelezwa kwa muhtasari ujumbe wa shairi huvuta moyo kwa namna

ya ajabu.

Maelezo ya Mulokozi (1999) kuhusu Utenzi wa Mwanakupona yanasisitiza kuwa fani ya ushairi

huzingatia mambo yafuatayo: Mpangilio wa mawazo, ikiwa kuna kujirudiarudia, mpangilio wa

Page 26: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

17

beti (zipi zafaa kuwa mwanzoni au mwishoni), na ni sehemu ipi inatawala, kama vile dua. Pia

tunaangalia mpangilio wa mizani na vina.

Zaidi ya hao,Williams anahakiki Diwani ya Mnyampala. Kuhusu muundo anatambua kuwa

mengi yana wa aina moja tu – yaani mistari minne kila ubeti (mstari wa nne ukiwa ndio kituo na

silabi zikiwa kumi na sita, nane nane kila kipande na vina vyenye utaratibu wa :

a b

a b

a b

b a

Mshairi mwenyewe asema kuwa afuata muundo huu kwa sababu ndio muundo ambao umezoewa

na wasomaji na wasikilizaji mashairi toka jadi. Mshairi anapojaribu kubadili muundo huu

anamletea taabu mwimbaji aliyezoea muundo wa tarbia na wasomaji wengi wanaonekana kuwa

hawapendi mabadiliko. Hivyo, Mnyampala kajaribu kuyaunda mashairi yake katika muundo

mpya anaouita ‘msisitizo’. Muundo hapa ni wa mishororo sita kila mshororo mmoja ukiwa

mfupi kuliko mingine ili kutoa msisitizo. Shaaban Robert pia alitumia muundo kama huu kwa

kuandika ukwapi kwa Kiswahili na utao kwa Kiingereza. Kinyume na washairi wengi,

Mnyampala alitunga mashairi yenye ubeti mmoja tu kwa mfano shairi aliloandika juu ya taifa.

Indende (2008:73 – 94), anapozungumzia taswira ya umbo awali na umbo la kisasa anasema

kuwa wanakipindi cha urasmi mkongwe na urasmi mpya walienzi sana umbo la shairi

lililoasisiwa na Muyaka bin Hajji, Shaaban Robert, Mathias Mnyampala, na mwalimu Hassan

Mbega na kadhalika. Walidumisha na kuendeleza umbo hili kiasi cha kwamba yeyote ambaye

angeulizwa juu ya ufafanuzi wa ushairi wa Kiswahili angeeleza kuwa ushairi wa Kiswahili ni

tarbia na huwa na umbo lifuatalo;

___________ 8a ________8b

____________8a __________8b

____________8a __________8b

____________8b__________8a

Page 27: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

18

yaani mishororo minne kila ubeti, mizani nane kila kipande na urari wa kina cha kati na cha

mwisho. Kina cha mshororo wa nne hubadilishana nafasi ambapo kile cha mwisho huja kati na

cha kati huja mwisho au mshairi aamue kuzua kina kingine ilivyoonyeshwa katika muundo huo.

Utawala na uzoefu wa umbo hili uliwafanya wahakiki, watafiti, wanafalsafa wa kifasihi na

wasomi wengineo kufikiria kwamba ushairi wa Kiswahili haubadiliki.

Kulingana na utafiti wa Massamba (1983:57), Abdilatif Abdalla naye akasema kwamba utungo

ufaao kupewa jina la shairi si utungo wowote bali ni utungo ambao katika kila ubeti wake kuna

ulinganifu wa vina vitukufu vilivyopangwa kimoja baada ya chenziye; wenye vipande vilivyo na

ulinganifu wa mizani zisizo zaidi. Vipande hivyo viwe vimetandwa na maneno ya mkato

maalum na yenye lugha nyoofu, tamu na laini, lugha ambayo ina uzito wa fikra tamu kwa

mdomo wa kusema, tumbuizi kwa masikio ya kusikia na yenye kuathiri moyo uliokusudiwa na

kama ilivyokusudiwa.

Wataalamu wa uhakiki wa ushairi wakiwemo King’ei na Kemoli (2001:19) na Mwai (1988:44),

wameelezea kwamba utungo wa unne au tarbia ulizuka karne ya 18 hasa katika utunzi wa

mashairi ya Muyaka. Njogu na Chimerah (1999:100) nao wameeleza kuwa utungo ukiwa na

mishororo minne huitwa tarbia na ukiwa na mishororo mitano huitwa takhmisa. Pia King’ei na

Kemoli (2001:18) wanafasili tarbia kuwa shairi lililo na mishororo minne katika beti zake

(unne).

Mayoka (1984:3) ana maoni kuwa ushairi ni mtungo wa kisanaa ulio na mpangilio maalumu na

lugha ya mkato ambayo ndani yake ina vina, urari wa mizani na muwala maalumu ambavyo kwa

pamoja huwa na fani na maudhui yahusuyo hisi fulani au tukio juu ya maisha ya mtu au watu wa

mazingira na wakati maalum. Kufafanua haya Indende anatoa mfano wa shairi la ‘Mcheza kwao

hutuzwa’ la Wallah (1988:154).

Kitula na Kemoli(2001) nao wanatambua kuna tathlitha yenye vipande viwili vya mizani 6a – 6b

na pia ya vitatu vyenye 8 – 8 – 8. King’ei (2008) anatumia vichwa vya mashairi, umbo na

mtindo, msamiati na maudhui kuonyesha mashairi ya Muyaka Bin Hajji yalivyowaathiri

washairi wa karne ya ishirini kama Ahmad Nassir. Katika utafiti huu King’ei anadokeza kuwa

Page 28: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

19

washairi wa hivi karibuni walibuni upya kimaudhui shairi la Abdalla liitwalo “Usiniuwe” likawa

“Nimekuua”, “Nishakuua” na kadhalika. King’ei anataja shairi hili tu wala hajahakiki fani na

maudhui yake kamwe. Utafiti wangu unaingilia hapa ili kuliziba pengo hili. Kuhusiana na umbo

na mtindo, King’ei anazungumzia mtindo wa “Nudhuma” yaani mshairi kutumia neno lilelile

kuanzia kila mshororo katika shairi zima. Anaonyesha namna Nassir alivyoiga mtindo huo kwa

Muyaka kama inavyobainika katika shairi la Nassir linaloitwa ‘Owa’. Pia anazungumzia utarbia

wa Mashairi ya Nassir, mizani nane nane na pia kina cha mwisho. Nassir pia anatia mkarara

katika mshororo wa mwisho kila ubeti kama alivyofanya Muyaka.

2.5 Maudhui ya Mashairi

Kuelewa maudhui ya shairi ni kulielewa shairi. Ongang’o (2002) anachambua mambo ambayo

mshairi anazingatia katika shairi lake. Haya ndiyo anaita maudhui. Anasema kila ubeti unaweza

kuwa na maudhui yake maalum. Jina lingine la maudhui ni ujumbe. Maudhui yanaweza

yakagawanywa mara mbili :-

(a) Maudhui kuu, yaani wazo kuu linalojitokeza (linalotawala) katika beti zote au shairi lote.

(b) Maudhui madogo, yaani mawazo madogo yanayosaidia kukuza au kujenga maudhui kuu.

Kulingana naye, umuhimu wa maudhui ni kuwa hutuambia mshairi anazungumzia juu ya nini.

Pia hutuambia mshairi anatungia mtu au watu gani, anasifu au anatetea mtu au watu gani, na pia

anaponda au kukosoa mtu au watu gani na kwa nini anafanya hivyo. Msimamo wa mshairi juu

ya hatua zinazostahili kuchukuliwa ili kuyatatua maswala anayoshughulikia katika shairi lake pia

ni umuhimu wa maudhui. Mshairi huyu anahakiki mashairi yake mwenyewe bali hataji chochote

kuhusu kazi za Abdilatif Abdalla.

Mtaalamu mwingine aliyehakiki ushairi wa Kiswahili ni Msokile (1993 :55). Anayaona maudhui

kama jumla ya mambo yanayoeleza kazi ya kifasihi. Maudhui hujumuisha dhamira, mtazamo

ama msimamo, ujumbe, maadili na falsafa. Mtaalamu huyu anahakiki shairi la ‘Ua la Moyoni

Ua’ na kuonyesha kuwa linazungumzia mapenzi. Pia anahakiki shairi la ‘Siafu wamekazana’

akidokeza kuwa shairi hili linahusu swala la kisiasa ambapo umma unafanya mambo mengi kwa

kujitoa mhanga ili kupata ukombozi. Huu ni mgogoro wa juhudi za ukombozi dhidi ya

Wajerumani kule Tanzania. Hata kama Msokile amehakiki mashairi kadha ya Kiswahili, ni

Page 29: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

20

muhimu kuelewa kuwa pia naye hajahakiki kazi yoyoyote ya Abdilatif Abdalla ambayo uhakiki

huu ulilenga.

Wamitila (2003 :225) kwa upande wake anaona huwa maudhui ya shairi kuwa neno

linalotumiwa kujumlisha yaliyomo katika kazi ya kifasihi. Msomaji anapaswa kuangalia

dhamira, ujumbe na falsafa ya mshairi. Anasema dhamira ya mtunzi ni lengo lake katika utungo

huo. Dhamira hutokeza kwa wazo kuu ambalo hukuzwa katika utungo unaohusika kuanzia

mwanzo mpaka mwisho. Katika kuliendeleza wazo hili kuu masuala mengine huibuka.

Mtaalamu huyu anaambatanisha maelezo haya na kuhakiki shairi la ‘Mamba’ katika diwani ya

Sauti ya Dhiki. Anaeleza kuwa shairi hilo lina dhamira ya kumtahadharisha kiongozi wa

kimabavu kuwa dhuluma ina mwisho. Mshairi ametumia fumbo akimlinganisha kiongozi huyo

na mamba majini. Maji hapa ni sitiari nyingine inayosimamia nchi, taifa au hata nguzo ya watu.

Mamba huyo amedanganywa na hadaa za ulimwengu ; ametawaliwa na kileo cha cheo na

kudhani ataishi milele. Mshairi anamtanabahisha mamba (kiongozi) huyu kuwa siku yake ya

‘kufa’ au kuondoka madarakani itafika. Katika ubeti wa mwisho tunatambua kuwa

anayezungumziwa ni binadamu. Kwa upande mmoja shairi hili ni onyo kwa viongozi wa kiimla

ilhali kwa upande mwingine linawatia moyo wanaoteswa wajue hakuna refu lisilokuwa na

mwisho.

Kuhusu ujumbe wa shairi kama sehemu ya maudhui, Wamitila anasema ni neno ambalo

humaanisha taarifa aipatayo msomaji asomapo shairi au kazi ya kifasihi. Anasema ujumbe

unaweza kuwa mbaya au mzuri. Mfano ni katika shairi hilo ambapo tunaelezwa kuwa dhuluma

ina mwisho na kuwa hakuna refu lisilokuwa na mwisho. Huu ni ujumbe wa kuwashajiisha na

kuwatia moyo wanaodhulumiwa kisiasa.

Mwisho, Wamitila anasema falsafa ya mwandishi ni fikra kuu za mtunzi au mwandishi wa kazi

ya kisanaa. Fikra hizo hutokana na imani na misimamo ya mwandishi anayehusika na huathiri

kwa kiasi kikubwa jinsi anavyoyatazama mazingira yake. Mazingira hayo yanaweza kuwa ya

kisiasa, kitamaduni, kiuchumi au kijamii. Shairi hili linaonyesha falsafa ya mwandishi ya

kupinga udhalimu, mateso na uongozi wa ki-imla.

Page 30: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

21

Ingawa Wamitila amelihakiki shairi la ‘Mamba’ kutoka diwani ya Sauti ya Dhiki, alichozamia ni

maudhui pekee wala hajagusia chochote kuhusu vipengele vingine vya fani ya shairi lenyewe

wala mashairi mengine ya diwani husika. Vipengele hivi vilipohakikiwa katika utafiti huu, bila

shaka ni mkondo tofauti wa uhakiki.

Kwa upande wake, mtaalamu Indende (2001) alizingatia diwani ya Sauti ya Dhiki alipochunguza

uchanganuzi wa kipragmatiki wa kazi za sanaa za Kiswahili zinazohusu maswala ya kisiasa.

Inabainika mifano aliyozingatia ni Sauti ya Dhiki ya Abdilatif Abdalla (1973), Cheche cha Moyo

ya Alamin Mazrui (1988) na Ficho la Ndani ya S. A. Mohammed (2002). Shairi analorejelea

Indende katika Sauti ya Dhiki ni ‘Wasiwasi enda zako’ (uk. 32). Hili linahusu wakati mgumu

aliopitia mshairi katika maisha ya jela. Hapa anapinga matakwa ya moyo wake kwa kuzungumza

nao kana kwamba ni binadamu. Hii ni mbinu ya tashihisi. Hii inazua upweke wake kuhusiana na

maisha ya jela.

Indende vilevile anadokeza shairi ‘Nshishielo ni Lilo’ (uk. 21) anapotaja kuwa mshairi alifungwa

jela kwa kusema ukweli na kuapa kuwa hataacha kamwe. Pia anarejelea shairi la ‘Mamba’ (uk.

10) kuzua ileile tashihisi ya kijamii na kisiasa. Mtaalamu yuyu huyu katika Swahili Forum 15

(2008 :73-94) anaandika mada kuhusu, ‘Mabadiliko katika umbo la ushairi na athari zake katika

ushairi wa Kiswahili’. Hapa anataja mashairi mawili katika diwani ya Sauti ya Dhiki. Anasema

kuwa shairi la ‘Mnazi vuta N’kuvute’ la Abdilatif Abdalla (1973 : 17-22) ni ngonjera

inayoonyesha taswira ya watu wawili ambapo Badi amekwea mnazi na kuukatalia na Ali

amenyimwa nafasi ya kuukwea huo mnazi. Hata hivyo, Indende hataji kingine chochote kuhusu

shairi hili.

Shairi lingine analotaja katika diwani hii ni lile la ‘Sikate tamaa’. Anasema kuwa Abdilatif

anajitokeza katika kundi la wanamapokeo lakini anapomwandikia Said Ahmed Mohammed

utangulizi wa ‘Sikate tamaa’ anampongeza kwa ujasiri aliofanya katika kubadilisha miundo ya

ushairi zoelevu. Inaelekea Indende analitaja shairi hili tu na kinachozungumziwa wala sio fani

yake kamwe. Baada ya utafiti wa wataalamu hawa nami nikapate mwanya wa kutoa mchango

Page 31: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

22

wangu kuhakiki fani na maudhui katika baadhi ya mashairi hata waliyohakiki kwani walilenga

mada na hata nadharia tofauti.

2.6 Tafiti zinazohusiana na Utafiti huu.

Senkoro (1982 :28) anapotafitia fani ya kazi ya fasihi anabainisha kwamba kuhusiana na aina

mabalimbali za fani, aina hizi huweza kutolewa kauli tu pale ambapo mhakiki au hadhira huwa

amekwisha zipitia kazi mabalimbali za msanii ahusikaye ili kuweza kuzitolea kauli moja.

Senkoro anachunguza mtindo wa kishairi ujitokezao katika kazi zisizo za kishairi kama vile

riwaya, hadithi fupi, tamthilia na uandishi wa habari. Anachunguza fani ya kazi ya kiimbila ya

Ubeberu utashindwa na pia kazi za Kezilahabi kama riwaya ya Rosa mistika pamoja na Diwani

ya Kichomi. Zaidi ya kazi hizo anachunguza riwaya na mashairi ya Shaaban Robert na pia ya

Mnyampala.

Hali kadhalika anatoa mifano ya mashairi kama ‘Al-Inkishafi’ na ‘Utenzi wa Mwanakupona’

katika diwani ya Tenzi tatu za kale. Pia anazungumzia taswira ya maisha ya jela aliyopitia

Abdilatif’ Abdalla kwa kutoa mifano ya mashairi ya ‘Usiniuwe’ na ‘Mnazi’ toka diwani ya Sauti

ya Dhiki. Ingawa mtaalamu huyu ametoa mifano ya mashairi ya Abdilatif’ hajahakiki fani na

maudhui yake na hapo ndipo utafiti huu ulipata pengo. Abdilatif’ ni miongoni mwa washairi

wachache wa kijadi ambao wamejitahidi katika uandishi wao wa mashairi. Ustadi anaodhihirisha

katika utunzi wake unastahili kutafitiwa kwa undani. Kulingana na Chacha (1992), kufikia sasa

ni kazi chache sana zilizojishughulisha na ushairi wa mtunzi huyu. Kutokana na sababu hiyo,

utafiti huu ulilenga kuhakiki fani na maudhui aliyotumia mshairi.

Knappert (1967) alichunguza mtindo wa drama katika kazi za Abdilatif’ Abdalla. Alilenga

Utenzi wa maisha ya Adamu na Hawaa katika utafiti wake. Utafiti wake unahusiana na huu kwa

sababu sote twalenga kuhakiki tungo za Abdilatif’ Abdalla japo ni tungo tofauti. Tofauti ni kuwa

twalenga vipengele tofauti vya sanaa, yeye akilenga drama, nami fani na maudhui kwa ujumla.

Pia twalenga kazi tofauti.

Zaidi ya hayo, Topan naye (1971 :67-79) anahakiki kazi kadha za tamthilia kama vile

‘Nakupenda lakini’ ya Henry Kuria pamoja na ule mchezo wa Gerishon Ngugi wa ‘Nimelogwa!

Nisiwe na Mpenzi ?’ Lengo la Topan ni kuonyesha umbo la mchezo wa kuigiza katika kazi hizo.

Page 32: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

23

Katika uhakiki wake Topan anarejelea tenzi kama vile Utenzi wa maisha ya Adamu na Hawaa

uliotungwa na Abdilatif’ Abdalla Muhammad wa Mombasa. Anaeleza kuwa utenzi huu (wenye

beti, 630) unahadithia kisa cha Adamu na mke wake jinsi walivyoonja tunda marufuku wakaja

wakatolewa peponi wakaletwa duniani. Kuhusiana na tenzi hizi pia analenga kuonyesha sifa za

mchezo wa kuigiza. Anatafakari drama inayotendeka. Ieleweke kwamba utenzi huu pamoja na

diwani ya Sauti ya Dhiki ni kazi za mwandishi mmoja ; Abdilatif’ Abdalla. Tofauti ya kazi

yangu na ya Topan ni kuwa nalenga fani na maudhui katika Sauti ya Dhiki. Tunafanana tu kwa

kuhakiki kazi za Abdilatif’ ingawa mbili tofauti.

Chacha (1992) anasisitiza utamthilia wa baadhi ya mashairi ya Abdilatif’ ambao wasomi

waliotangulia pia walikuwa wameutaja. Mashairi anayotaja ni ‘Vuta N’Kuvute’ na ‘Kutendana’

katika diwani ya Sauti yaDhiki. Japo anayoyalenga ni kutoka diwani ya Sauti ya Dhiki, tofauti na

utafiti huu ni kuwa anazingatia mashairi manne tu wala si fani na maudhui kwa ujumla.

Mshairi huyu anaanza kwa kueleza historia fupi ya maisha ya mwandishi katika tasnifu yake

ukurasa wa tatu hadi tisa. Msingi wa nadharia anaozingatia ni ule wa umaksi (uk. 9 – 11) katika

utenzi aliohakiki na pia mashairi ya Sauti ya Dhiki. Pia anazungumzia ujuzi wa Abdalla kama

mshairi. Mwelekeo wake ni kueleza ujumbe wa mashairi haya kwa kuzingatia muktadha

yalimotungwa na pia maadili kuhusu maisha ya binadamu na pia uozo wake. Zaidi ya hayo,

anaeleza jinsi Muyaka na Abdalla walivyoathiriwa na usuli sawa.

Utafiti mwingine wa hivi karibuni zaidi kulenga diwani hii ya Sauti ya Dhiki ulifanywa na

Maitaria (2008). Mtafiti huyu alitathmini matumizi ya methali kama fomula katika utunzi na

uwasilishaji wa ushairi wa Kiswahili akisisitiza kuwa utanzu huu una historia ndefu na kuwa

matumizi ya methali bado yanaendelea kutegemewa hata wakati wa sasa. Alizungumzia ushairi

unaotumia methali nyingi na unaotumia chache. Alizingatia mashairi yaliyotumia methali mbili

au zaidi. Mifano ni ‘Mnazi vuta N’kuvute’, ‘Kutendana’ na ‘Zindukana’.Mtafiti huyu ana maoni

kuwa methali huweza kutumiwa katika shairi kama mbinu ya kuibua taharuki kwa hadhira.

Mtafiti huyo aliufaa utafiti huu kwa kutafitia fani ya methali katika Sauti ya Dhiki. Utafiti huo

unatofautiana na huu kwa kuhakiki mada tofauti kwani hata katika shairi la ‘Kutendana’

haikuhakikiwa methali kwani Maitaria ashafanya hivyo tayari.

Page 33: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

24

Walibora(2009) pia ni mmoja wa watafiti waliotafitia mashairi ya Sauti ya Dhiki. Mada yake ni

kuhusiana na mashairi yalitotungwa katika mazingira ya jela. Walibora anaelezea kuwa

Abdilatif’ alitumikia kifungo jela kwa uhaini wakati wa utawala wa Jomo Kenyatta baada ya

uhuru. Mtafiti huyu anaelezea kuwa kuandikia jela kulikuwa na athari kuu kwa umbo na

maudhui ya ushairi wa Abdalla.

Walibora aendelea kusema kuwa kwa kiwango kikubwa mazingira mabaya ya jela aliyokumbwa

nayo mshairi yalisababisha na kuimarisha athari ya kisaikolojia na kifalsafa hivyo kusababisha

toni ya aina mbalimbali katika mashairi husika. Lengo la Walibora hasa lilikuwa kusoma diwani

ya Sauti ya Dhiki huku akitathmini hisia za Abdalla kwa mateso aliyopata jela.

Utafiti wake uliufaa huu katika kuhakiki maudhui tu ilipoonyeshwa mateso aliyopata Abdalla

lakini katika mada tofauti na ya Walibora ikilengwa fani na maudhui jambo ambalo hasa

halikulengwa naye. Utafiti huu umeonyesha wahusika na sifa zao, ufundi wa lugha na maudhui

kwa kila shairi lililohakikiwa jambo ambalo Walibora hakufanya.

Utafiti wa hivi majuzi zaidi unaohusiana na huu ni uliofanywa na Karanja (2014). Alichunguza

matumizi ya taashira,istiari na tashbihi katika diwani ya Sauti ya Dhiki. Mojawapo ya

madhumuni yake ilikuwa ni kuwapa watafiti wengine shauku za kuchunguza mbinu nyingine za

tamathali alizotumia mshairi. Mtafiti huyu alilenga tamathali hizi tatu pekee katika mashairi

ishirini kati ya arubaini. Alitumia nadharia ya mtindo. Utafiti wake uliufaa huu kwani ametoa

mifano michache kwa mashairi yaliyohakikiwa hapa. Tofauti yake kuu ni pale kazi yake

inaonyesha mfano wa kiuchanganuzi wa mishororo ya mashairi husika tu na kutawaliwa na

mbinu hizo tatu pekee anazolenga. Kwa mantiki kama hiyo ikalazimu kufanywa uhakiki

kamilifu wa tamathali kadhaa pamoja na wahusika,muundo wa mashairi na hata maudhui

,mambo ambayo mtafiti huyo hakulenga hata kidogo. Bila shaka hata anapozingatia nadharia ya

mtindo na utafiti huu ukihusisha umuundo, umuundoleo na uamilifu ni tofauti tosha.

Mgeni(2014) anapozungumzia fani na maudhui, anasema kuwa ni vipengele vinavyojenga shairi.

Anasema kuna uhusiano mkubwa kati ya fani na maudhui kwa mtunzi yeyote wa kazi ya sanaa.

Page 34: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

25

Kuhusiana na wahusika, mtafiti huyu anasema kuwa mashairi ya kawaida hayategemei sana

wahusika ili kuwasilisha ujumbe. Hata hivyo, kuna baadhi ya bahari za ushairi ambazo hutumia

sana wahusika ambao aghalabu hutumiwa kama kinywa cha kuwasilishia hadhira jumla ya fikra

za mtunzi. Anasema pamoja na bahari hizo, ni ngonjera au tenzi ambazo mara nyingi hubainisha

kuwepo kwa nafsineni na nafsinenewa, sifa ambayo aghalabu huandamwa na mashairi ya

Kiingereza.

Utafiti huo uliufaa huu kwa kuwa kitangulizi cha kipengele cha uhusika katika ushairi. Hata

hivyo, hakuna lolote lililotajwa kuhusu ushairi wa Abdilatif’ Abdalla. Utafiti ulikita mizizi

katika uhusika kama maudhumuni mojawapo. Imebainishwa kuwa mashairi yana wahusika

tofauti na alivyosema Mgeni kuwa hawako.

2.7 Misingi ya Nadharia

Utafiti ulitegemea nadharia za umuundo na umuundoleo kuonyesha jinsi vipengele vya fani

vinashiririkiana kujenga mashairi yaliyohakikiwa pamoja na uamilifu kuonyesha jukumu

linalotekelezwa na kila kipashio.Nadharia zilichangishana kwa kila shairi lililohakikiwa.

2.7.1 Umuundo

Utafiti ulijikita katika nadharia ya umuundo,umuundoleo na ile ya uamilifu. Nadharia ya

umuundo iliasisiwa na wataalamu wawili:- Ferdinard de Saussure na Claude Levi Strauss. De

Saussure alikuwa mwanaisimu wa Kiswisi aliyegawa lugha katika matapo mawili:- Langue na

Parole. Langue ni zile sheria zilizo kwenye ubongo wa mtumiaji lugha. Parole ni utendaji kwa

kutumia sheria hizo katika muktadha mahsusi. Hali hizi mbili zikaendelezwa na Noam Chomsky

kama umahiri na utendaji. Mambo hayohayo yakaendelezwa na William Labov. Alipendekeza

kwamba lugha imegawanywa katika umahiri wa kiisimu na umahiri wa kimawasiliano.Claude

Levi Strauss alisema kwamba jamii imeundwa na vipengele kama uchumi, siasa na kadhalika.

Nadharia imeshikilia kuwa kila kitu ni zao la ushirikiano wa vipande mbalimbali. Ushairi kwa

mfano umeundwa na maudhui, dhamira, ujumbe, wahusika, lugha na kadhalika. Lengo la

kuchunguza lugha au ushairi ni kutambua au kupata miundo na ruwaza zake. Kulingana na

Page 35: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

26

umuundo, kuna madaraja tofautitofauti ya vipashio tofauti, kategoria, ruwaza na mahusiano.

Vipashio tofauti huhusiana kati yao katika kufanya kazi.

Kulingana na Grimes (1975) na Stubbs (1983), umaumbo hutafuta vipashio vidogo au vijenzi

ambavyo vina uhusiano kati yao na ambavyo hutokea katika mpangilio mahsusi unaotawaliwa na

sheria au mikabala.Wanamiundo huchunguza muundo ulio zaidi ya Sentensi au Kishazi (Stubbs,

1983) na Van Djik (1985:4). Huchunguza viwango au madaraja tofauti kwa misingi ya vipashio

tofauti, kategoria, ruwaza na mahusiano. Msingi wa umaumbo ni jinsi vipashio tofauti huhusiana

kati yao katika kufanya kazi. Kila neno ni lazima kuonyeshwa maana yake kimatumizi.

Umuundo wa baadaye ulitokea miaka ya 1950-1960. Mwelekeo huu ulianzishwa na wahakiki wa

fasihi kama Roland Barthes ambao hawatafuti kueleza matini maalumu. Badala yake wanalenga

mtindo wa ujenzi wa matini fulani. Umuundo unahusu kuhakiki matini bila kushughulika na

athari za nje ya matini husika. Hupuuza maswala ya kitamaduni au ya kijamii na kulenga namna

ujumbe husika umejengwa.

Umuundo wa miaka ya sabini na themanini ulihusika na uhuru wa parole au utendaji. Unaitwa

umuundoleo. Kulingana na Katoto (2015), hatuwezi kuzungumzia nadharia ya umuundoleo bila

ya kuhusisha umuundo. Kwa maana hiyo, nadharia hizi huzungumziwa kwa pamoja. Matokeo ya

umuundoleo yaliingia katika fasihi ya Kiingereza na Kimarekani miaka ya themanini. Mwanzo

wa karne ya ishirini, umuundo huu pamoja na uhakiki mpya wa fasihi ulikita mizizi. Nadharia hii

huchukulia fasihi kuwa huru na hivyo kutofautisha kazi iliyo ya kisanaa na isiyo ya kisanaa.

Husisitiza kuwa kila kitu ni ubunifu na kupinga uwezekano wa kuwa na ukweli wa kilimwengu

unaowakilishwa na ubunifu husika.

Msingi wa kijamii, watu au kihistoria ulioathiri kazi husika hupuuzwa. Hulenga beti na ufundi

mzima wa ushairi. Sababu ya kuchagua nadharia hii ni kuwa mshairi wa Sauti ya Dhiki

anazungumzia vipengele tofautitofauti vya kijamii, kisiasa na kiuchumi. Kuhusiana na fani na

maudhui kuna vipengele ambavyo huijenga. Hivi ni maudhui, muundo, lugha na wahusika.

Nguzo za Umuundo

1. Ujumbe wa matini sio wala hauwezi kuwa nyenzo kamili inayowakilisha uhalisia wa

kilimwengu.

Page 36: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

27

2. Hatuwezi kutoka nje ya ujumbe wa matini na kufaulu kupata chochote zaidi ya hapo.

3. Nadharia inakisia kwamba uzungumzi au ujumbe wa matini ndio wa pekee tunaoweza

kujua au kujadili.

4. Kufafanua au kuhakiki vijenzi vya kazi fulani ya sanaa,yaani kilichomo kwa matini

husika ni toshelevu kuelezea mada inayohusika.

Umuundo umetegemewa sana katika uhakiki wa riwaya lakini kila uchao nadharia hii inazidi

kutegemewa kwa wingi katika uhakiki wa mashairi. Ingawa kimsingi ilikuwa nadharia ya

Kiingereza na hasa Kifaransa iliyonawiri miaka ya sitini, wakati huo ilipendelewa sana na

wahakiki wa Kimarekani. Hulenga kuhakiki matini kwa mbinu fulani ingawa nadharia yenyewe

imelaumiwa kuwa inakinzana na historia ya fasihi. Hii ni kwa sababu mwanamiundo huamini

kuwa kazi husika ni muhimu kuliko mtunzi, hadhira na ulimwengu ilimochotwa. Pia

wanamiundo hawashughuliki na hisia za mshairi, majibu ya hadhira kwa shairi au ukweli na

uhalisia wa kilimwengu unaowakilishwa na kazi hiyo.

2.7.2 Uamilifu/ Ujukumu

Nadharia hii ilipendekezwa na wataalamu Branslaw Malinowski, Radicliffe Brown, Emile

Durkheim, Isadore OKpeihwo, Edward Leech na Raymond Firth. Mwanzo wa nadharia hii ni

kazi za Emile Durkhein ambaye alihusika hasa na namna jamii yaweza kuwa imara au thabiti.

Nadharia hutafsiri kila kipengele cha jamii kwa misingi ya namna kila kimoja huchangia uthabiti

wa jamii nzima. Aliamini kuwa jamii ni muhimu kuliko kipengele kimoja kwa hivyo kila kimoja

chafaa kutenda kazi ili kuleta uthabiti wa jamii hiyo nzima. Durkheim alisisitiza kuwa vipengele

tofauti kimsingi ni taasisi za jamii na kila kimoja pia huwa na matokeo kwa jamii nzima.

Vipengele hivyo tofauti hutegemeana. Nadharia hii imejikita katika misingi ya nadharia mfumo.

Inashikilia yafuatayo:-

Kila kitu kinajengwa na vipengele ambavyo kila kimoja hushirikiana na wenziwe katika

kudumisha kuendelea kuwepo kwa kitu hicho. Kila mojawapo ya vitu hivyo kina kazi mahsusi

katika mfumo wa kitu kizima. Mhakiki akitumia nadharia hii anafaa:

a) Kueleza kitu hicho na jinsi kinavyofanya kazi kwa pamoja

b) Unatenganisha vipande na kuchukua kipande kimoja na kukitafutia utendakazi wake.

Page 37: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

28

c) Unachunguza kile kipande ulichoamua katika mazingira yake ya kutenda kazi.

Nadharia ya uamilifu huchukulia lugha kama chombo cha kuwasilisha maana ya kiutenda kazi.

Hutilia mkazo mwelekeo wa kisemantiki na ule wa mawasiliano badala ya sifa za kisarufi pekee.

Uamilifu hujihusisha na majukumu ya kijamii yanayotekelezwa na matumizi fulani ya lugha.

Swala muhimu pia ni kuchunguza muktadha ambao hulazimu aina fulani ya matumizi ya lugha

kama vile wa kitamaduni. Lugha hutekeleza majukumu tofautitofauti na kuonyesha utofauti wa

wanajamii. Kulingana na Leech (1983), lugha ni kioja cha kijamii.

Uamilifu au ujukumu huhusisha vipengele vya lugha vinavyohusu maana na utendakazi badala

ya vipashio vya muundo na sarufi. Lugha ina majukumu ambayo yako nje ya mfumo wenyewe

wa lugha. Majukumu haya huathiri mpangilio wa ndani wa mfumo wa lugha. Sababu ya

kuchagua nadharia hizi ni kuwa mshairi wa Sauti ya dhiki anazungumzia vipengele tofautitofauti

vya kijamii, kisiasa na kiuchumi. Kuhusiana na fani na maudhui, kuna vipengele ambavyo

huijenga. Hivi ni maudhui, muundo, lugha na wahusika. Pia ni majukumu fulani

yanayotekelezwa na aina fulani ya fani na maudhui.

Namna nadharia ziliongoza Utafiti

Nadharia ya umuundo iliongoza utafiti kwa kufafanua au kuhakiki vijenzi vya mashairi yote

yaliyolengwa kutegemea madhumuni yaani wahusika, mbinu za lugha, muundo na vipengele

vyake pamoja na maudhui. Ushirikiano wa vijenzi hivi vya fani na maudhui uliwekwa bayana

kupitia nadharia hii. Umuundo nao ukatumika kwa kuwa kila kipengele cha muundo

kinaathiriwa na mazingira ya kutumiwa kwa mfano muktadha wa wakati.

Kwa upande mwingine ikalazimu kutegemea nadharia ya pili, yaani ile ya uamilifu. Sababu ni

kuwa kufafanua maudhui ya kisiasa ni swala halisi la kihistoria katika muktadha maalumu wa

wakati nchini Kenya. Maudhui kama vile tamaa, dini, migongano ya kitabaka na mapinduzi ya

kijamii ni mambo yanayolandana na uhalisia wa kilimwengu ulioathiri utunzi wa mashairi

husika. Mambo kama haya hayawezi kulengwa na nadharia ya umuundo na umuundoleo pekee.

Pia, kuonyesha namna vijenzi vya sanaa kama wahusika, lugha na muundo vinavyozua maudhui

maalumu ni swala la kiuamilifu. Kwa mantiki hii, kutegemea nadharia za umuundo na

umuundoleo pamoja na uamilifu zikifidiana likawa jambo lisiloepukika.

Page 38: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

29

SURA YA TATU

MBINU ZA UTAFITI

3.1 Utangulizi

Katika sura hii kuna muundo wa utafiti, mahali pa utafiti huo, uteuzi wa sampuli na ukusanyaji

wa data. Mwishowe kumeonyeshwa namna uchanganuzi wa data nzima ulivyofanywa. Sura hii

inaangazia jinsi utafiti wenyewe ulivyofanywa. Inaangazia mahali halisi data ya utafiti

ilikusanywa, uteuzi wa sampuli, mbinu za kukusanya data hiyo na jinsi data

ilivyochanganuliwa.

3.2 Muundo wa Utafiti

Utafiti huu uliongozwa na muundo wa kimaelezo. Huu ni muundo wa kisayansi unaohusu

utazamaji na uelezaji wa hali ya kitu pasipo kukishughulisha au kukirekebisha kwa vyovyote vile

(Mugenda, O. na Mugenda, A. (1999). Utafiti huu ulilenga kuchunguza kwa uhakiki mashairi

halisi katika diwani ya Sauti ya Dhiki. Muundo wa utafiti huu ulikuwa wa kimaelezo. Lengo la

muundo wa aina hii ni kueleza data na sifa ya vipengele vya fani na maudhui vilivyochunguzwa,

yaani wahusika, lugha, muundo na maudhui. Muundo huu ulihusu umaratokezi, ujumla na sifa za

kihesabu. Ingawa muundo huu ni sahihi kwa kiwango cha juu hauelezi visababisho vya hali

fulani. Muundo huu wa utafiti ulitegemewa zaidi kwa kuwa utafiti ulilenga kupata kuelewa zaidi

kuhusu ufundi wa mashairi husika. Muundo wenyewe hutegemewa kuchunguza kazi

zilizoandikwa kwa mfano vitabu mtafiti akilenga kilichoandikwa tayari. Hali ilielezwa ilivyo

katika mashairi hayo bila kuyaathiri au kuyarekebisha kwa vyovyote vile. Lengo lilikuwa kupata

taswria ya jumla ya utunzi husika.

Muundo wenyewe ulitegemewa pia kwa kuwa haiwezekani kupima sampuli nyingi

zinazohusika. Matokeo yalitegemewa kukadiria ubora au udhaifu wa mashairi au diwani husika.

Muundo huu wa utafiti huweza kuelekeza ni wapi kwa kuchunguzwa kiuwingi idadi. Udhaifu wa

muundo huu ni kuwa vibadiliki vinavyochunguzwa haviwezi kuhesabika hivyo kuchunguzwa

kisayansi.

3.3 Mahali pa Utafiti

Huu ni utafiti wa fasihi andishi ya kiswahili. Kazi iliyohakikiwa ni ya kishairi. Mashairi yote

yalitolewa kutoka kwa diwani ya Sauti ya Dhiki ya Abdilatif’ Abdalla wa Mombasa. Kazi

Page 39: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

30

tofautitofauti za kishairi na zinginezo kuhusu maudhui, muundo, lugha na wahusika zilipekuliwa

kwa uangalifu kulenga mada ya utafiti huu. Pia tasnifu za tafiti za wataalamu waliolenga mada

hii na ushairi kwa ujumla zilichunguzwa kwa uangalifu. Kwa njia hii, kisicholengwa na watafiti

husika kuhusu fani na maudhui katika mashairi hayo kilitambulika. Hilo likawa pengo

lililozibwa na utafiti huu. Kwa kifupi, huu ni utafiti wa maktabani.

3.4 Uteuzi wa Sampuli

Sampuli za mashairi ziliteuliwa toka diwani ya Sauti ya Dhiki ya Abdilatif’ Abdalla. Madhumuni

ya utafiti wenyewe yalitiliwa maanani zaidi katika kuteua sampuli hizo ili zijumuishe

madhumuni yote. Kulikuwa na mashairi matatu kwa kila sampuli na ambayo hayakuwa

yamehakikiwa na wataalamu waliotangulia wakilenga mada hii. Mashairi yaliyo na wahusika

bainifu yaliteuliwa yakifuatwa na yenye lugha teule (isiyo ya kawaida) na tamathali za usemi

pamoja na muundo maalumu na maudhui ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Kisha baadaye, upekee

wa mshairi kwa kila kikundi cha sampuli ulihakikiwa na kuripotiwa ifaavyo.

3.5 Ukusanyaji wa Data

Data ya utafiti huu ilikusanywa kwa uchambuzi wa yaliyomo katika sampuli za mashairi

yaliyoteuliwa kuegemea maudhui, muundo, lugha na wahusika katika mashairi hayo. Mbinu hii

huhusu uchambuzi wa matini zenye ujumbe. Mifano ni vitabu, majarida, magazeti au matini

zungumzwa au andishi. Kabla ya 1940, mbinu hii ilihusu kazi zenye data ambayo yaweza kuwa

na sifa za kuchanganuliwa kiuwingi idadi. Hizi ni sifa zilizoweza kutambuliwa. Baada ya 1950,

mbinu hii ilijihusisha na uchambuzi wa ujumbe husika kiuthamano. Mbinu hii ya utafiti

inahusiana na Bernard Berelson. Ililenga kuchambua kilichomo katika kazi husika au kazi

lengwa. Uchambuzi wa kilichomo katika matini husika ulizingatia kuangalia na kupima vipimo

vya kila kipengele husika.

Uchambuzi wa kilichomo katika matini huwa muhimu sana mtafiti anapotafitia matini

zilizozungumzwa. Utafiti huu unahusu kuhakiki matini iliyochapishwa. Uchanganuzi waweza

kuwa katika kiwango sahili au changamano. Huwa changamano mtafiti anapochunguza mielekeo

ya mchapishaji kuhusiana na kazi fulani. Utafiti huu ulikuwa kwa uchanganuzi sahili. Hii ni kwa

sababu vipengele vyote vya maudhui, muundo, lugha na wahusika viliweza kutambulika

Page 40: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

31

waziwazi kwa diwani hii na hata kuhesabika. Kwa kifupi diwani yenye mashairi husika

ilipekuliwapekuliwa kwa uangalifu kwa kuzingatia madhumuni husika ili kupata data

iliyotarajiwa. Data husika ilipatikana kwa kuyasoma mashairi husika kwa kina. Utafiti wa

Maktabani ulitegemewa ili kupata yale ambayo yamekwisha fanywa kuhusu mashairi mapokeo

na hata yale ya Sauti ya Dhiki. Kudurusu katika mitandao na tovuti mbalimbali pia kulitegemewa

sana.

3.6 Uchanganuzi wa Data

Mwanzo ilikuwa ni kusoma mashairi kwa uangalifu, wahusika, muundo lugha na maudhui

vikitiliwa maanani. Data iliyokusanywa ilichanganuliwa kwa kuhakiki na kufafanua vipengele

vyote vya fani na maudhui katika sampuli za mashairi yaliyolengwa. Kuhusu wahusika nilihakiki

sifa za nafsineni zinazobainika katika mashairi yote lengwa na vitu vinavyowakilisha watu au

wanyama. Pia ni nani au vitu gani anazungumza navyo na kilichomsababisha kuzungumza

hivyo. Nililenga jinsi mtunzi mwenyewe anavyoonekana kwa kila shairi husika yaani zile sifa

zake chanya au hasi. Pia nilihakiki wanyama na sifa zao kisha hatimaye kueleza sifa za wahusika

wa aina hiyo.

Kwa upande wa tamathali za usemi au matumizi ya lugha ililengwa misemo na nahau, sitiari na

tashbihi, lahaja, toni, taswira, tashihisi na aina zote za takriri zinazobainika. Pia ni lugha ya

kigeni na ufundi kwa jumla na namna haya yanaafiki muktadha husika. Kuhusu muundo,

yaliyolengwa ni mishororo, vipande, beti, vina na mpangilio mzima wa mashairi pamoja na

bahari zinazobainika. Pia mandhari ya mashairi yalilengwa.

Mwisho ilikuwa maudhui ambapo mambo kama tamaa, dini, utabaka na migongano ya hadhira

yalilengwa. Maelezo sahihi ya maudhui, muundo, lugha na wahusika katika sampuli hizo za

mashairi yalitolewa. Maelezo haya yalitumiwa kama ithibati ya fani bora au duni aliyotumia

mshairi huyu.Utafiti huu ulifanywa kwa kipindi cha miezi saba kati ya Machi 2014 na

Septemba 2014. Umuhimu wake unatarajiwa kuboresha uhakiki na hatimaye ubora wa usomi wa

mashairi kwa wanafunzi na wasomi wengineo wanaopendelea ushairi.

Page 41: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

32

SURA YA NNE

UWASILISHAJI,UCHANGANUZI NA UFASIRI WA DATA

4.1 Utangulizi

Sura hii inalenga kuonyesha matokeo ya data iliyobainika katika mashairi yote yaliyohakikiwa

kwa kila kikundi. Maelezo yametolewa kwa kufungamana na madhumuni ya kwanza hadi ya

nne. Hali kamili kama ilivyo kwa kila shairi imetolewa maelezo bila kubadilisha chochote.

Mifano ya mashairi yenye sifa husika kwa kila madhumuni imeonyeshwa. Mihimili ya nadharia

nayo imeonyeshwa ilivyobainika kwa kila madhumuni. Nadharia hizi zinabainika katika

matokeo ya kila madhumuni.

4.2 Jinsi mshairi alivyotumia Wahusika

Katika mashairi yaliyohakiwa hapa, wahusika ni binadamu wa jinsia ya kike na kiume na walio

na sifa tofautitofauti. Pia, sifa za Mwenyezi Mungu zimeangaziwa hapa na pale. Sifa za

binadamu zimeelezwa kwanza. Shairi la ‘Ukamilifu wa mja’ kwa mfano linazungumzia

binadamu kwa kutaja sifa zake za ndani kwa kulinganisha na sehemu zake za mwili. Lile la ‘Mja

si mwema’ nalo linaonyesha mshairi akitumia ufundi wa tashihisi kuzungumza na mkono wake

kana kwamba ni binadamu. Anautaka uandike shairi kwa hati nzuri ili wenye kusoma

waifahamu. Huyu ndiye mhusika wa kwanza wa shairi hili. Wahusika wengine ni wale wasomaji

wa shairi ambao watakiwa kuwa na sifa ya kufahamu na kuyapima yaliyomo. Katika ubeti wa

pili mkono watakiwa usikawie. Kuna walimwengu nao ambao watakiwa kujitunza. Zaidi ya hao

kuna mhusika ambaye ni mja.

Shairi la ‘Kutendana’ kwa upande wake limezungumzia sifa za mwanaume na pia zile za

mwanamke. Ikiwa tutajiuliza ni kwa nini mshairi akatumia wahusika kama hawa, twafaa

kuelewa kuwa maisha ya binadamu yana pande mbili; kuukeni na kuumeni. Katika shairi hili pia

kumetajwa sifa za kimada wa mume ambaye ataangaziwa sifa zake baadaye.

4.2.1 Sifa mbaya za Wahusika

Katika mashairi matatu yaliyohakikiwa hapa, kunaonekana sifa ya wahusika kuwa wabaya au

waovu. Mshairi katika ubeti wa saba wa shairi la ‘Ukamilifu wa mja’ anasema kuwa kuna watu

wema na waovu, wenye heshima na wengine adabu mbovu. Anasema pia kuwa kuna wahalifu

sugu ingawa pia kuna watiifu wa vitendo na misemo. Ubeti huo ni ufuatao:

Page 42: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

33

Ubeti wa 7

Kuna waja walo wema, kadhalika na waovu,

Wako wenye na hishima, na wenye adabu mbovu

Na wako wenye huruma, piya na watenzi nguvu

Mtu kuwa na kidevu, si kwamba mekamilika

Katika ubeti wa kumi wa shairi lili hili, mshairi anaendelea kuzungumzia waja wakorofi na

wachochezi wa kutia mambo chuku. Kuna wenye moyo mweupe na wengine mbaya. Anataja

kuwa sifa ya kuwa na ulimi haimkamilishi mja yeyote. Zaidi ya sifa hizi zote, kuna waja

wengine wakarimu na wengine bahili. Kuna pia madhalimu na wadhulumiwa. Mshairi akasema

mtu aweza kuwa na pua na asikamilike.

Ubeti wa 10

Kuna watu wakorofi, abadani hawatumi

Na wako wataswarufi, moja huzalisha kumi

Kuna wenye roho swafi, Wingine zao sisemi

Mtu kuwa na ulimi, si kwamba mekamilika (uk. 13)

Zaidi ya hayo katika shairi la ‘Ukamilifu wa mja’ mshairi anazungumzia sifa mbaya za mhusika

anayeitwa Mwafulani. Mshairi alimwamini naye mja huyo asiaminike ingawa ni baada ya

mshairi kufikwa na jambo baya tayari. Huyo mwafulani haaminiki, amemtenda mshairi vibaya

na ni katili asiye na imani, watu humwambaa ili asiwahasiri na pia hana haya usoni mwake.

Aidha ni mbaya kwani huchimba shimo ili wenzake waanguke mle. Pia hufurahia maumivu ya

wenzake hivyo basi mshairi anaifahamisha hadhira kuwa ni mja mmoja tu kwa mia ambaye

huwa mzuri. Beti mbili zifuatazo, yaani ule wa tano na wa sita zafafanua sifa hizo.

5

Meniuwa mja, mja ni nduli, tahadharini

Mjaye daraja, nda kikatili, hana imani

Muonapo mja, kaani mbali, mujitengeni

Asije akaja, kwa habari, kuhasirini

6

Page 43: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

34

Mja hana haya, haya hazimo, mwake usoni

Mja ni mbaya, hutimba shimo, ungiye ndani

Na ukishangiya, azome zomo, furaha gani!

Mmoja kwa miya, ndiye hayumo, baya kundini

(Sauti ya Dhiki, uk. 34)

Shairi la ‘kutendana’ pia lina sifa mbaya za wahusika. Shairi linachora mume kuwa na sifa

mbaya kwani akipata pesa nyingi, yeye hugura nyumbani asijulikane aliko. Yeye ni mbadhirifu

na akimaliza na kubaki bila peni hurudi hadi kwa mke mlangoni akijiliza ili aonewe imani. Sifa

nyingine mbaya ya mume huyu ni kuwa hana shukrani. Alimpa mke mashaka pamoja na taabu

zisizoelezeka. Pia hakumbuki alivyopewa pesa kwa furaha. Mke ajidhikisha kwa kumpa mume

pesa na pia furaha. Ufidhuli wa mume huyu umetiwa kikomo. Beti zifuatazo zina sifa mbaya ya

mume.

MWANAMKE

Kila mambo naelewa, yaliyo ndiyo na siyo

Si mwana wa kuhadawa, Khaswa kwa unambiyayo

Japo wasema ni dawa, sikupi ngakuwa nayo

Na kama yatakuwa, kuja kwa maradhi hayo

N’lishakupeleleza, hata n’kakubaini

Muda pesa ukijaza, humo mwako mfukoni

Huanza kujikimbiza, na kunigura nyumbani

Ngapita kukuuliza, uliko hujulikani

Ukisha kuzimaliza, kutolibakisha peni

Ndipo ndiyo huongoza, hadi kwangu mlangoni

Na kuanza kujiliza, n’kuonee imani

Leo sitakusikiza, hata unganambiyani

(Sauti ya Dhiki, uk. 90)

Mume yuyu huyu anamdharau mkewe licha ya kuwa mke alimtunza hapo awali wakati mume

hakuwa na kazi. Mume anatafuta kimada. Tunaona mume akimwonyesha mkewe uhuni. Aidha

Page 44: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

35

twaweza sema hana jamala kwa mazuri aliyotendewa na mkewe. Kimada naye ana sifa mbaya

ya kuwa mzinzi kwani anakubali mahusiano ya kuwa mpenzi wa mume ambaye ana mke na

familia. Aidha ni nduma kuwili kwani hatimaye anamfukuza mume kutoka kwake. Anamkataa

ghafla na kukataa fadhila zote alizokuwa akimtendea hapo awali. Hii ni licha ya kula vya mume

huyo.

4.2.2 Wahusika wapekuzi na werevu

Sifa zaidi ya wahusika katika mashairi yaliyohakikiwa ni kuwa ni wapekuzi na werevu

wanaofahamu barabara kinachoendelea katika jamii zao au miongoni mwa wanajamii wenzao.

Katika shairi la ukamilifu wa mja kwa mfano ubeti wa tatu, mshairi anasisitiza kuwa kuna watu

werevu na kuna pia wapumbavu wasiojua hata jambo moja. Pia kuna wenye nguvu na wengine

dhaifu ambao huonewa. Kwa hivyo mtu kuwa na kifua hakumkamilishi. Mshairi anazidi

kusisitiza kuwa kukamilika kwa mja ni kuielewa dunia kwa marefu na mapana, kupitia njia

zenye miiba michungu na kuvuka bahari zenye vina virefu.

Mshairi au nafsineni katika shairi la ‘Ukamilifu wa mja’ naye anabainika kuwa mshauri

anayeiasa hadhira / wasomaji wa shairi kuhusu matarajio kulenga mja aliyekamilika. Mshairi

huyu ni mdadisi anayeelewa wanajamii anaoishi nao. Hii inathibitishwa na kule kufahamu sifa

zao. Yeye ni mfumbaji kwani anaitaka hadhira kujipelelezea hulka za mja aliyekamilika.

Anasema hivi:

Ubeti wa 3

Kuna waliyo werevu, ambao ni waelewa

Na kuna na wapumbavu, Moja jambo wasojuwa

Piya kuna wenye nguvu, na dhaifu huonewa

Mtu kuwa na kifuwa, si kwamba mekamililka.

(Sauti ya Dhiki, uk. 12)

Ubeti wa 18

Aiyelewe duniya, kwa marefu na mapana

Azipite zile ndiya, za miba mitungu sana

Avuke bahari piya, zilo na virefu vina

Page 45: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

36

Hiyo ni yangu maana, ya mja kukamilika.

(Sauti ya Dhiki, uk. 14)

Tukiendelea na sifa ya mshairi katika shairi la ‘Mja si mwema’ mshairi / nafsineni anaonekana

kuwa tayari amefunzwa na ulimwengu kuchuja watu wa kuamini na wasio wa kuamini. Sasa

amebaki kuamini mtu mmoja tu kwa mia. Nafsineni anawataka wanajamii wenzake wajue

alichotendewa na mja mwenzake ili wabaki salama bila kuhasirika kama yeye. Hata hivyo hapo

mbeleni aliamini watu bila kuwadadisi hulka zao kamili hadi hatimaye akahasirika. Baya

likamfika kwa kukosa uangalifu. Amebaki kujutia makosa yake na kujilaumu kwa kumuamini

mja mwenzake. Anasema hakupasa kumthamini hata sehemu. Msisitizo hapa ni kuwa mshairi

mwenyewe sasa amezinduka na kuwa mpekuzi na mwerevu baada ya kuteswa na wanajamii

wenzake.

Kwa upande mwingine, katika shairi la ‘Kutendana’ mwanamke ameerevuka hasa kwa kurejelea

ubeti wa nne. Mume anapofika nyumbani akiwa na mwako unaomsababisha hata kunyiwa na

mvua akitaka kusaidiwa na mkewe, mke anakataa kwani mume huyo hamsaidii kwa chochote

wakati wote. Mwanamke anashangazwa na hata kutamaushwa na huo ukosefu wa kila wakati.

Mke huyu amezinduka kwani anamtaka mume arudi atokako na kutafutia mwako wake njia ya

kuutolea. Hataki kusikia lolote kwani yeye sio jaa la kutupiwa takataka za mume. Ubeti

wenyewe ni huu ufuatao.

MWANAMKE

Rudi kuko utokako, siniletee udhiya

Tafutia mwako wako, ndiya ya kuutoleya

Mimi ndiye jaa lako, takazo kunitupiya?

Mwanamume nenda zako, sina n’takalosikia

(Sauti ya Dhiki, uk. 89)

Katika beti zinazofuata mwanamke anasawiriwa kuwa mwenye kuelewa mambo yaliyo na

yasiyo. Hapa hawezi kuhadawa na maneno ya mume. Yeye ni mwenye msimamo thabiti. Mke

anasisitiza kuwa penzi lake kwa mume limekwisha. Anasema amefumbuka macho hivyo

kumtaka mume aache kujisumbua kwani tayari wametengana.

Page 46: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

37

4.2.3 Wahusika Maskini

Kuna baadhi ya wahusika wenye sifa ya umaskini. Nafsineni katika shairi la ‘Ukamilifu wa mja’

anasema pale ubeti wa nne kuwa kuna watu matajiri kupindukia ingawa wengine ni maskini

zaidi.

Ubeti wa 4

Kuna wasemao kweli, na wasemaji urongo

Kuna waliyo na mali, zilizopita kiwango

Na wingine zao hali, nda kuinamisha shingo

Mtu kuwa na maungo, si kwamba mekamilika(Sauti ya Dhiki, uk. 89).

Lile shairi la ‘Kutendana’ nalo linaonyesha mwanaume akiwa na sifa hii ya umaskini katika

ubeti wa kwanza. Anaomba kupewa kitu na mwanamke na asipompa atakopa kisha alipe

baadaye. Hata hivyo, yeye hana cha kumpa huyo mwanamke.

MWANAUME

Kama bure utanipa, nipa sinisimbuliye

Kama hutaki ‘takopa, nikulipe baadaye

Hivi sasa cha kukupa sina; kweli nikwambiye

Mtu huwa hakutupa, amfaapo mwenziye.

(Sauti ya Dhiki, uk.89).

Sifa ya umaskini inaandamana na ya utajiri kwa mke. Mke anasisitiza ameamuacha mume

kikamilifu. Anasema, “Kama waweza kuumba, umba mimi mwinginewe’’ (uk.101). Pia, yeye ni

tajiri kwani anakataa hata pesa za mume. Mke huyu ameweza kujinunulia mafuta aliyofukiza

vyema. Pia ana nyudi za Arabuni, ambari na kujivika leso mbili mpya kutoka dukani siku hiyo

hiyo. Kichwani napo ana nywele nzuri, pini na shada la asumini. Utajiri huo wa mke

unamwezesha kujipamba kwa kidani shingoni. Pia amejipamba kwa liwa (pambo la Kiswahili)

usoni ungadhani si mja bali malaika (uk.103).

Mke amepaka wanja wa manga machoni na kupaka mdaa midomoni. Ana vyombo vya dhahabu

viungoni, kipini puani, vipuli masikioni, pete vidoleni na bangili mikononi. Pamoja na urembo

wake asilia, mapambo hayo yanamzidisha urembo kiwango mpita njia angemwona moyo

Page 47: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

38

ungemwenda mbio na bila shaka ashiki zikazidi kumpanda. Mke huyu hamtegemei mume tena

kwa kuwa amejitegemea kiuchumi.

4.2.4 Wahusika Waaminifu

Zaidi ya sifa hizo, wahusika katika mashairi haya ni wenye imani kwa Mungu. Mshairi katika

shairi la ‘Ukamilifu wa mja’ ni mfano. Anasema kuwa hakuna mja kamilifu ila Mola tu.

Anasisitiza kuwa kukamilika kwa mtu ni tofauti na kwa Mola. Mtu hukamilika tu akifika daraja

aliloumbiwa. Kuna binadamu wenye sifa nzuri na wengine mbaya. Mhusika mwingine

anayebainika ni Mwenyezi Mungu. Sifa zake naye ni kuwa yeye ni kamilifu na tofauti na

binadamu. Ukamilifu wake ni tofauti na ule wa mja na pia ndiye Muumba. Imani kwa Mungu

inasababisha mja kuwa mwadilifu. Mja kuwa kamilifu ni kufikia daraja aliloumbiwa na Mungu,

kuielewa dunia kwa marefu na mapana na pia kuwa na ujasiri wa kuvumilia miiba michungu na

kuvuka bahari zenye vina virefu. Pia ni kwa kusubiri yote yatakayomfika hata kwa maisha ya

baadaye. Mshairi naye ni mwadilifu kwa kuwa kuna maadili aliyothamini na ambayo anashikilia

kama falsafa yake. Mifano ni huruma, Subira, utiifu, wema na kadhalika. Ithibati ni beti mbili

zifuatazo:

Ubeti wa 16

Hakuna mja kamili, ndivyo twalivyoambiwa,

Kadhalika mimi hili, nasema li sawasawa

Mkamilifu wa kweli, nakubali ni Moliwa

Maana yangu’ tatowa, ya mja kukamilika.

Ubei wa 17

Kukamilika kwa mja, ni mbali na kwa Moliwa

Kwa mja nitakutaja, ili upate kwelewa

Ni kufikiya daraja, ile aliyoumbiwa

Hapo ndipo huambiwa, mja amekamilika

(Sauti ya Dhiki, uk.14)

Kwa upande wa shairi la ‘Kutendana’ mke amechorwa kuwa mcha Mungu/ mwenye imani kwa

Mungu. Anasema Mungu amzidishie mume uhodari wa kumsaidia kwa maisha ya mbeleni

Page 48: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

39

ingawa kwa mke huyu mume hathaminiwi. Licha ya imani hiyo kwa Mungu, mke huyu vilevile

ni mshirikina. Katika beti za kumi na mbili hadi kumi na tano, mke anamtaka mume akatolewe

pepo kilingeni. Pia amejua mume ana macho ya nje kwa kuwa mume huyo ana pesa zake.

Madhumuni haya ya kwanza yanapohusishwa na nadharia ya umuundo, ni bayana kuwa kila

shairi hapa limeundwa na wahusika mbalimbali. Wahusika hawa ni kama vile mshairi,

wanajamii wenzake (wazuri na wabaya) pamoja na mwenyezi Mungu katika shairi la ‘Ukamilifu

wa mja’. Bila hawa, mshairi asingefaulu kupitisha ujumbe wake kulenga sifa zao kikamilifu.

Ametumia wahusika hawa kwa kutaja sehemu zao za mwili kama vile miguu, macho, meno,

mikono na zinginezo akisisitiza kuwa si muhimu sana maishani ikiwa mja hana hulka nzuri

ndani yake. Vipashio hivi vya muundo vimetajwa na mshairi katika kila ubeti. Kila hulka

imetajwa pamoja na kuonyesha upungufu unatokea mja anapokosa hulka fulani ingawa ana

sehemu husika ya mwili. Sehemu hizi za mwili pamoja na hulka hizo japo zina uhalis kijamii.

Kwa muktadha wa nadharia ya umuundo, ni sahihi kusema kuwa huu ni ubunifu wa kisanaa tu

lakini unaopitisha ujumbe kwa njia isiyokanganya. Kazi hii inabaki kuwa muhimu sana kuikosoa

na hata kuwaelimisha wanajamii kwa mujibu wa nadharia ya ‘uamilifu’.

Katika shairi la ‘mja si mwema’ pia nadharia ya umuundo na hata ya uamilifu zinabainika.

Umuundo unashikilia kuwa kila kitu ni zao la ushirikiano wa vipande mbalimbali. Shairi hili

kwa upande wa wahusika limeundwa na mshairi / nafsineni, mkono wake (tashihisi),

walimwengu wanaotakiwa kujitunza na hata mja (Mwafulani). Kila kipashio kulingana na

nadharia ya uamilifu kinatarajiwa kutekeleza jukumu lake katika ule ushirikiano. Mkono katika

ubeti wa kwanza `watakikana kuandika shairi kwa hati njema inayosomeka ili isomwe na

watakaosoma na hata kuifahamu. Pale ubeti wa pili hadi wa sita pametajwa mja ambaye

anatenda mabaya kwa mshairi baada ya kumuamini, kumuua mshairi kikatili, kuhasiri wenzake

na kufurahia mshairi na wanajamii wenzake wakiingia kwa matatizo au shimoni. Sifa kama hizi

za kutajwa mja au binadamu wa aina hii bila kutaja jina la mwanajamii maalumu ni kwamba

kuna uwezekano kuwa na watu wengi wa aina hii katika utangamano wetu.

Kwa nadharia ya ujukumu / uamilifu, ujumbe kutokana na sifa za mhusika huyu unaimarisha

maisha ya mtu anapoendelea kutangamana na wenzake katika maisha ya kila siku. Kuna maadili

Page 49: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

40

wanayofunzwa watu katika shairi hili. Mifano yake ni kuelewa pande mbili za hulka na

kuchagua wema kila wakati hasa kwa kumuiga mwenyezi Mungu. Kila sifa ya wahusika

iliyotajwa kwa kila ubeti wa shairi ingawa kwa daraja tofauti inahusiana na sifa katika hizo beti

zingine ili kujenga ujumbe mzima anaolenga kupitisha mshairi kwa mshikamano wenye mnato.

Masuala au muktadha katika mashairi ya ‘ukamilifu wa mja’, ‘mja si mwema ‘ na hata

‘kutendana’ ni wa kijamii.

Nadharia hizi vilevile zimefungamana na uhakiki wa shairi la ‘kutendana’. Shairi hili lina

wahusika watatu. Hawa ni mume, mke na kimanda wa mume. Wote wanashirikiana kulijenga

shairi hili. Umoja wa wahusika hawa Ukitengwa, shairi halitapitisha ujumbe kwa njia ifaayo.

Ujumbe katika shairi hili ni ubunifu wa kisanaa na umewekwa wazi katika shairi. Baada ya

kuhakiki sifa za wahusika hawa, dhamira ya mshairi ya kuwazindua wanawake wanaoteswa na

waume inapitishwa kwa njia ya waziwazi. Haya ni kwa kutegemea nadharia ya umuundo.

Kuhusiana na uamilifu mume ametumika kuwakilisha hulka mbaya na hata adhabu kwa

wahusika wa aina yake hasa kutokana na kimanda aliyemwacha baada ya kupata pesa za mume.

Mke wa mume anatumika kuonyesha wanawake wanaonyanyaswa, kuchukua hatua na hatimaye

kukatalia mbali urafiki na waume waliowatesa. Muktadha hapa ni wa maisha ya ndoa na

changamoto zake, yaani wa kijamii.

4.3 Tamathali za Usemi au Mbinu za Lugha katika Mashairi teule

4.3.1 Kisengerenyuma na Kiona mbele

Katika kuhakiki ufundi huu, kila mbinu ya lugha au tamathali imeangaziwa pamoja na mifano

yake katika mashairi yote yaliyohakikiwa. Mashairi yaliyohakikiwa ni ‘N’shishiyelo ni lilo’,

‘Wasiwasi enda zako’ na ‘Telezi’. Katika shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’ kuna mbinu ya

kisengerenyuma hasa katika ubeti wa pili ikionyesha urejeshi wa uneni wa walimwengu wa

zama zilizopita kwamba kweli ni chungu kwa aambiwaye. Ubeti huo ni huu:

2

Walinena walimwengu, wa zama zilopisiye

Kwamba kweli i utungu, kwa yule aambiwaye.

Nami haya ndugu yangu, sasa niyaaminiye

Asojuwa nasikiye, apeleleze ajuwe. (uk.1)

Page 50: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

41

Katika shairi la ‘wasiwasi enda zako; kuna mbinu ya utabiri au kiona mbele. Hapa ni pale

mhusika ambaye ni ‘wasiwasi’ anamwambia mshairi kuhusu yatakayotokea baadaye. Wasiwasi

unamwambia nafsineni kuwa atakapotoka mle gerezani, kule nje angojewa na maisha magumu.

Hili ni jambo ambalo bado halijatokea lakini langojewa siku za usoni. Mbinu ya urejeshi

inatumika ili nafsineni kuonyesha kuwa jambo analozungumzia kuhusu ‘kweli’ ni la tangu jadi

kwa hivyo si geni. Utabiri huu nao ni kiwakilishi cha hisia inayopita kwa maisha ya mshairi

kuhusiana na kusekwa jela.

Shairi la ‘Telezi’ pia lina mbinu inayokaribiana na kisengerenyuma. Hii ni ile ya usimulizi. Hii

yahusiana na matukio ya shairi kusimuliwa katika wakati uliopita. ‘Mvua’ inaelezwa kuwa

ilinyesha, mimea ilitekuka, wakulima wakafikwa na hasara, walioogopa mvua wakakimbia

majumbani, mvua ilibwaga shindo kubwa, tope zilitapakaa kote na telezi zikambwaga nafsineni.

Haya yote ni masimulizi katika wakati uliopita. Hata shairi hili lina mbinu ya kionambele au

utabiri. Mbinu hii inabainika katika ubeti wa sita mshairi anapotaja mambo ya siku za usoni.

Kuanzia ubeti wa kwanza hadi wa tano, ujumbe umetajwa katika wakati uliopita lakini unapofika

hapa unatajwa katika wakati ujao. Mfano wa ubeti ni ufuatao:

6

Japo hivyo zilikuwa, ndiya hazipitiki

Bali mimi haamuwa, kwenenda japo kwa dhiki

Kumbe vile nitakuwa, ni mfano wa samaki

Ni mfano wa samaki, kuiendeya ndowana.

(Sauti ya Dhiki, uk. 24)

Mbinu hii imerudiwa katika ubeti wa nane hadi wa kumi na moja. Nafsineni anangojea siku

ambayo idhilali itaisha na jibu kumwondokea. Pia anangoja kwa matarajio makuu siku ambayo

jasho jembamba litamtoka njia mbili kisha atetemeke kwa uchungu utakaozidi sana kisha moyo

wake ufurahie. Mwishowe anatarajia kuliuguza jeraha kwa kulitia dawa hadi lipoe na afya yake

irudi halafu aruke na kucheza kwa kuingiwa na furaha tele.

Page 51: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

42

4.3.2 Tashihisi

Kando na mbinu hizo zinazokaribiana, kuna mbinu ya tashihisi inayoonekana kutanda katika

madhumuni haya ya pili. Katika shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’ tunaelezwa kuwa kweli

imemfunga nafsineni ndani ya chumba asitoke nje. Kweli hiyohiyo inasemekana kumlaza

nafsineni chini kwenye baridi kali. Katika ubeti wa 12 nao kweli inamnyima haki zilizo ngomeni

kama vile jamaa kuja kumtazama, kuandika wala kuletewa barua. Hapa chini kuna ubeti wa

kumi na mbili.

12

Kweli pia meninyima, haki zilizo ngomeni

Wangu kuja nitizama, hilo haliwezekani

Haya nnayoyasema, ndivyo yalivyo yakini

Baruwa sitakikani, Kwandika wala kwetewa

(Sauti ya Dhiki , uk.2)

Mshairi anatumia mbinu hii ili kuepuka shutuma kutoka kwa aliopinga kisiasa. Hapa anailaumu

kweli aliyosema badala ya kulaumu watawala aliokosoa kisha kuishia kufungwa jela. Pia

kutumia ufundi huu ni njia mwafaka ya kuzua mguso katika shairi na hadhira iishie kutekwa na

ujumbe zaidi.

Shairi la ‘Wasiwasi enda zako’ laonekana kutawaliwa hata zaidi na ufundi huu wa tashihisi.

Nafsineni anazungumza na hisia ya wasiwasi kana kwamba ni kiumbe hai kama vile binadamu.

Kuanzia ubeti wa kwanza anauambia wasiwasi huo umwondokee uende zake, uondoke uandame

njia na kumwondoshea uso wake. Pia anauuliza ikiwa unasikia na kuutaka uwache jeuri zake na

kujishughulisha na mambo yake badala ya yale ya mshairi.

Katika ubeti wa pili anaujuza wasiwasi huo kwamba haitaki suhuba yake kwani si nzuri na

haistahimiliki kwani uovu umekithiri. Suhuba ya wasiwasi hata ikinyoshwa hainyoki hivyo

mshairi hataki shari. Anautaka wasiwasi huo uende zake. Ubeti wa tatu unasisitiza ileile tashihisi

kwa kusisitiza kuwa hauna kazi uifanyayo ila kuwafitinisha na kuwagonganisha viumbe. Hii

ndiyo kazi yenye kufurahisha, isiyochosha na ambayo wasiwasi umeizoea.

Page 52: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

43

Kwa upande mwingine, wasiwasi huo wamvunja mshairi moyo kwa sababu wakaapo

humwambia hayawi ayatakayo na kuwa hata akitia tamaa asumbua moyo wake tu. Pia ni

kwamba hata akingojea hayo ayangojeayo hatayapata bali ni kujisumbua bure. Zaidi ya hayo, ni

tashihisi kuwa wasiwasi unamletea habari kuhusu mambo yalivyo nyumbani kuwa si mazuri na

yote ni mabaya. Wamtaka afikiri kuwa yasemwayo ni kweli lakini wasiwasi huo ukitaka apate

kusononeka tu.

Wasiwasi utapata kufurahika kwa kurejelea ubeti wa sita. Tashihisi inazidi kuonekana wakati

wasiwasi unamwambia kuhusu afya za wenzake walio nyumbani. Kila mara unamwambia kuwa

hali zao zi taabani. Unazidi kumkata moyo kwani hata atakapotoka gerezani maisha magumu

yamngojea nje. Mshairi anashangaa ikiwa ulilokusudia ni kumtia wazimu. Naye anauambia

kuwa ikiwa hiyo ndiyo hamu ya wasiwasi wenyewe utaaibika. Hatimaye, nafsineni anakataa

urafiki na wasiwasi na kuutaka utokomee.

Sababu za nafsineni kutumia ufundi kama huu ni kuwa anazungumza na hisia ya wasiwasi iliyo

ndani yake kwa sababu hana mwingine wa kuzungumza naye. Katika mandhari ya jela,

Abdilatif’ hakuruhusiwa kutangamana na jamaa au rafiki. Ni kawaida kwa kila binadamu akiwa

katika hali kama hii kujaribu au kujitahidi kujituliza mwenyewe kwa vyovyote vile. Inatarajiwa

pia kuna sababu ya kutosha kumsababisha mfungwa kama huyu kuwa na mawazo ya kujali

jamaa na marafiki aliowaacha nyumbani na hivyo kuwa na mawazo mengi kuwahusu kwani

hawaonani. Mifano ni kule kuhangaika kuhusu afya ya jamaa zake hao kule nyumbani. Pia,

maisha magumu anayotarajia nafsineni baada ya jela / kifungo ni lazima kumtisha mfungwa

kama huyu. Hii ndiyo sababu tunamuona akihangaishwa na maisha hayo ya baadaye.

4.3.3 Sitiari/ Jazanda

Uhakiki wa mashairi haya umegundua yametumia ufundi wa sitiari au jazanda. Katika shairi la

‘N’shishiyelo ni lilo’ pale ubeti wa tatu kuna istiara ya kutaja kweli kuwa kama sumu. Mfano

mwingine ni mshairi kuwa ‘firauni’ kwa kusema kweli. Pia mshairi analindwa chumbani bila

kuruhusiwa kutoka. Analindwa kama simba marara. Ubeti wa tatu ni ufuatao:

Kweli nnaifahamu, haipendwi aswilani

Kwa mja hiyo ni sumu, mbaya iso kifani

Mwenye kuitakalamu, hapendezi katwaani

Page 53: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

44

Sasa nshayaamini, ni kweli haya ni kweli

(uk.1)

Sitiari katika shairi la ‘wasiwasi enda zako’ inapatikana kwa mshororo mmoja tu. Mfano huo ni

ubeti wa pili nafsineni anaposema kuwa hataki suhuba ya wasiwasi kwani si nzuri. Hii ina maana

ya ndani kuwa hataki wasiwasi huo umwingie kwa vyovyote sawa na suhuba iingiavyo mtu

moyoni.

Kuna jazanda zaidi katika shairi la ‘telezi’. Ufundi huu unahusu kutaja vitu vilivyozoeleka katika

mazingira yetu ingawa katika shairi maana yake ni ya ndani. Baadhi ya jazanda hapa zina utata

yaani kufasirika kwa maana zaidi ya moja. Mfano wa kwanza ni mvuwa (mvua). Nafsineni

anasema kuwa mvua kubwa ya maradi na ngurumo ilinyesha bila kipimo kutwa kucha. Hata

hivyo haikuwanufaisha wakulima bali iliwaletea hasara. Hii ni kwa sababu mvua hiyo ilitekua

mimea yao na kazi yao ngumu ikaharibika hadi wakakosa kuvuna matunda waliyokuwa

wakitaka. Iliwalazimu walioiogopa mvua hiyo kukimbilia upenuni na wengine majumbani mwao

na kuikomea milango. Maji hayo yakajaa barabarani na matope kutapakaa kote hadi

kukakosekana njia ya kupitia.

Ingawa njia hazikupitika, nafsineni aliamua kwenda lakini ikawa kama samaki kuiendea ndoana.

Alishindwa kutembea kwa telezi hadi zikambwaga chini. Licha ya hayo, anaahidi kutowacha

lakini kubadili mwendo. Mbali na maana ya kijuujuu kuhusu faida ya mvua na hasara yake kwa

mimea na wakulima, neno mvua laweza kuwa na maana tofauti. Yamaanisha jumuiya ya shairi

hili la ‘telezi’ haikunufaika kikamilifu kwa juhudi za kumtimua mkoloni na hatimaye kujitwalia

utawala wa kisiasa. Wanajamii kujikomboa na kupata uhuru kuliingia kwa kishindo ikitarajiwa

faida kuu kwa kila mwanajamii jambo ambalo lilitokea kuwa kinyume cha matarajio hayo.

Katika shairi, inasemekana mvua ilinyesha kwa radi na ngurumo kutwa kucha lakini wakulima

wakafikwa na hasara. Mbinu hii ya jazanda imetumiwa na nafsineni kama njia ya kukosoa

utawala wa jumuiya kwa njia fiche isiyoonekana na watawala kama dharau kwao kwa kuwa

mshairi hakuusema kwa njia ya moja kwa moja.

4.3.4 Ufundi wa Kinaya

Mbinu mojawapo iliyobainika katika uhakiki huu ni ile ya kinaya. Katika ubeti wa tano wa shairi

la ‘N’shishiyelo ni lilo’ kuna mbinu hiyo. Baada ya kusema kweli mshairi analipwa kwa

Page 54: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

45

kuwekwa taabuni. Hii ni kinyume cha matarajio ya hali halisi ya maisha. Kwa kupinga utawala

wa serikali anashikwa himahima na kuadhibiwa ndani ya ngome ili ajute. Kuna kinaya pia kwa

sababu nafsineni anapewa adhabu kali za kila aina ili aache kunena lakini anasema bado atainena

kweli na mateso hayatakuwa dawa ya kumzuia kusema. Pia ni kinaya kusema kuwa ukijaliwa

mateso ya duniani umshukuru mwenyezi Mungu na kujikaza kuyachukua (ubeti wa 17). Kuna

wanaharakati wengi ambao tayari wanasumbuliwa na kuuliwa kwa kusema ukweli na hata hivyo

kutobadili nyoyo. Mshairi anasisitiza kuwa naye vilevile ataandama njia hiyohiyo na kufuata

nyayo zao. Hii ni kinaya.

Ubeti wa 17

Ama hakika mwendani, kwa mwenye moyo wa sawa

Mateso ya duniani, wakati kijaaliwa

Hushukuru Rahamani, Kajikaza kutukuwa

Nami yangawa yakuwa, Hikaza moyo si ila.

(Sauti ya Dhiki uk. 3)

Mbinu hii imetumika kama njia ya kusisitiza bidii aliyo nayo mshairi katika kuendeleza maadili

hayo ya kusema kweli kwa jumuiya yake ambayo haiko tayari kuipokea kweli yenyewe.

Hata shairi la ‘Telezi’ limetungwa kwa ufundi huu wa kinaya. Ni kinaya kuwa mvua tele

ilinyesha nabadala ya kuwaletea wakulima faida kwa mimea kunawiri ikaiharibu mimea

yenyewe. Ufuatao ni ubeti wa pili ambao una ujumbe huo:

Mimeya waliopanda, ilitekukatekuka

Kazi ngumu walotenda, yote ikaharibika

Hawakuvuna matunda, waliyo wakiyataka

Waliyo wakiyataka, yakawa ya mbali nao

(Sauti ya Dhiki, uk.24)

Mfano mwingine ni kuwa nafsineni mwenyewe baada ya wanajamii wenzake kuiogopa mvua

kisha kujificha majumbani mwao, yeye aliamua kwenenda japo kwa dhiki. Inashangaza yeye

kuchagua dhiki wenzake wakichagua usalama. Kinaya ni kuwa hali hiyo ilibadilika kuwa mfano

wa samaki kuiendea ndoana. Hatimaye, telezi zilimbwaga kwa kutojua kuziendea. Licha ya

matatizo hayo anaahidi kutoacha kutembea ila kubadili mwendo.

Page 55: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

46

4.3.5 Tamathali ya Takriri

Mashairi yote matatu yametumia mbinu ya takriri ya mishororo minne katika kila ubeti. Shairi la

‘Wasiwasi enda zako’ nalo limetumia aina nyingine ya takriri. Katika ubeti mmojammoja kuna

mbinu hii katika vina vya kati na vile vya mwisho. Vina vya kati vinafanana katika mishororo ya

kwanza mitatu. Mfano ni ubeti wa kwanza hapa ulio na ya, wa pili ki, wa tatu yo, ule wa nne ya,

wa tano ri, wa sita ya, ule wa saba ni ya, na wa nane ko. Vina vya mwisho navyo kuanzia ubeti

wa kwanza ni ko, ri, sha, yo, ni, mu na sha.

Katika shairi la ‘Telezi’ mbinu hii ya takriri pia imetumika katika vina vya kati kufanana katika

ubeti mmojammoja yaani katika ubeti ingawa tofauti toka ubeti hadi ubeti. Vile vya mwisho

navyo pia vyafanana katika ubeti. Mfano ni ubeti wa kwanza ambapo vina ni sha, mo katika

mishororo ya kwanza mitatu. Ubeti wa pili ni nda, ka na wa tatu ni wa, ni. Ule wa nne nao ni

ndo, ni na wa tano ya, pe. Ubeti wa sita ni wa, ki na wa saba ya, pe. Ubeti ni tofauti kikamilifu.

Mapigo haya ya vina vinavyofanana katika ubeti hulipa shairi mdundo unaopendeza hadhira na

pia kusababisha shairi liimbike.

4.3.6 Chuku

Halikadhalika, kuna mbinu ambazo zimetumika katika mashairi fulani tu lakini hazikutumika

kwa mashairi yote. Katika shairi la ‘N’ shishiyelo ni lilo’ kwa mfano kumetumika mbinu ya

chuku katika ubeti wa tisa. Mlinzi kuwa mlangoni pasi na kuondoka wakati wowote ni chuku.

Hii yatumika kusisitiza namna nafsineni alivyozuiliwa gerezani kwa lengo la kumzuia

kuendeleza harakati zake za kusema kweli.

Katika shairi la ‘Telezi’ nalo, ni chuku kuwa mvua iliponyesha mimea yote ilitekuka, wakulima

kukimbilia majumbani mwao lakini nafsineni akaamua kuenenda japo kwa dhiki. Kiwango

chake cha ujasiri kimepigiwa chuku kama vile ‘Kumbe nitakuwa mfano wa samaki kuiendea

ndoana.’ (uk. 24).

4.3.7 Utohozi,Taswira na Taharuki

Mbinu myingine iliyotumika katika shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’ ni ile ya utohozi. Mshairi

kulala ‘simitini’ ni mfano wake. Katika ubeti wa kumi na moja nao kuna taswira ya mandhari ya

jela. Mshairi yumo ngomeni mwenye kuta ndefu bila kutangamana na mahabusu wengine lengo

Page 56: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

47

likiwa asinene alilo nalo akawaambukiza wenzake. Shairi la ‘Telezi’ pia limejaa tamathali hii ya

taswira takribani katika beti zote. Tunapata picha ya mawazoni kuhusu hali ilivyokuwa wakati

mambo fulani fulani yanapotajwa. Mifano ni mvua kutajwa ikiwa na radi na ngurumo usiku na

mchana, mimea iliyopandwa kutekuka, wenye kuicha mvua isiwatose mwilini kukimbilia penuni

na kuikomea milango, mikondo ya maji kujaa barabarani, kutapakaa tope kote na njia kutopitika.

Aidha, kuna taharuki katika ubeti wa mwisho nafsineni anaposema kuwa hatawacha kutembea

ila kubadili mwendo. Baada ya kushindwa kuziendea telezi kisha kubwagwa chini, hatujui

kilichojiri baadaye au hata matokeo ya kubadili mwendo kwake. Mbinu hii ya taswira

imetumiwa ili kuisababisha hadhira kupata ujumbe wa shairi kikamilifu kwa kutumia mifano

halisi iliyozoeleka katika mazingira ya jamii hasa msimu wa mvua.

4.3.8 Balagha na Uzungumzi nafsia

Mbinu ya balagha imetumika katika shairi la ‘Wasiwasi enda zako’ peke yake. Mifano ni katika

ubeti wa kwanza, wa sita na saba. Ubeti wa kwanza kwa mfano ndio huu hapa chini:

Wasiwasi n’ondokeya, ondoka enenda zako

Ondoka andama ndiya, n’ondosheya uso wako

Ondoka! Wanisikiya? Ziwate jeuri zako

Jishughulishe na yako, yangu wayatakiyani?

(Sauti ya Dhiki, uk. 32).

Mbinu hii inatumika kuonyesha msimamo wa nafsineni wa kupinga au kukataa matakwa ya

mwenzake (wasiwasi). Haikosi hata huku kuzungumza na wasiwasi ni tamathali ya uzungumzi

nafsia kwani wasiwasi wenyewe umo ndani ya mshairi huyu ingawa ufundi wa shairi

wauonyesha kana kwamba ni mhusika mwingine kando. Ni bayana kuwa kitovu cha ushairi

mzima huu ni uzungumzinafsia. Swali ni je, ingawa tashihisi inabainika, inawezekanaje mshairi

huyu akazungumza na wasiwasi wenyewe kana kwamba ni binadamu mwenzake? Ieleweke

kwamba ana mdahalo na nafsi yake mwenyewe. Lile swala zima la kusekwa jela akiwa pweke

linazua hali kama hii katika hisia zake. Sababu ni mradi kujituliza kwa namna yoyote awezayo.

Wasiwasi wenyewe unamkaba hadi kuzungumza kwa upweke. Nafsineni amekumbwa na

Page 57: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

48

matatizo kama vile kusumbua moyo, kutengwa na jamaa (ubeti wa tano) kuteseka kwa afya za

jamaa hao, uwezekano wa maisha magumu baada ya jela, masikitiko na mateso.

4.3.9 Tamathali ya Mvutano

Katika shairi la ‘wasiwasi enda zako’ peke yake kuna ufundi wa lugha unaojulikana kama

mvutano. Hapa ni pale ambapo wahusika wawili au taswira mbili huvutana katika kazi ya fasihi

hasa ushairi. Katika shairi hili tunaona nafsineni akiendelea kuvutana na kuzungumza na

wasiwasi hadi hatimaye akaushinda kwa kukatalia matakwa yake yote. Twaweza kukubali kuwa

hili ni funzo maalumu kwa hadhira ya shairi kama hili kuwa yafaa kuyashinda mawazo au silika

zote hasi kama vile wasiwasi. Kuushinda wasiwasi ni mfano bora pia wa tamathali ya uadilifu

wa kifasihi. Kwa kuwa wasiwasi ni mfano wa mhusika mkuu kuanzia mwanzo wa shairi hili hadi

mwisho, yeye ni mhusika mkinzani.

4.3.10 Uhuru wa Kishairi: Kilahaja na Inkisari

Kibali cha kishairi katika mashairi haya kwa upande mwingine ni jambo lililotumika na

nafsineni kuimarisha ufundi wake. Maneno ya kikale ni mfano kama huo. Hii ni lugha ya

Kiswahili cha kizamani; maneno ambayo leo hii hutumika kwa mashairi mapokeo pekee bali si

kwa lugha sahihi.

Mifano ni nipulikiza (uk.1) ikimaanisha nisikilize na idhilali ikimaanisha dhaifu. Mtima nao ina

maana ya moyo na katiti ni kidogo. Haya ni katika shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’. Uhakiki

umebainisha kuwa mifano yenyewe imetumika kuhifadhi historia ya maendeleo ya lugha ya

Kiswahili. Ni bayana kuwa maneno kama haya huenda yakasahaulika na kubaki kutumika kwa

uchache.

Katika shairi lili hili kumetumika uhuru wa inkisari. Hii inahusu kufupisha maneno katika

mshororo ili kupata idadi ifaayo ya mizani katika kila mshororo wa ubeti. Mifano ni kadha katika

shairi hili. Ndu yangu imetumika badala ya ndugu yangu, nasikiye ikimaanisha na asikie na pia

iso kwa maana ya isiyo. Tabuni yafaa kuwa taabuni na menibaidisha ni imenibaidisha. Zaidi ya

Page 58: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

49

hayo kuna menitenganisha ikifaa kuwa imenitenganisha na walo kwa walio. Mifano mingine ni

mesema badala ya nimesema, ilo na baridi ikifaa kuwa iliyo na baridi na ‘tasonga’ kwa maana ya

nitasonga.

Shairi la ‘Telezi’ pia limebuniwa kwa uhuru huu wa inkisari. Mfano ni kazi ngumu walotenda

badala ya waliyotenda, waliyo kwa waliyotaka na haamua ilkifaa kuwa nikaamua. Zaidi pia kuna

kuzendeya telezi badala ya kuziendea talezi. Mshairi ametumia uhuru huu katika mashairi husika

ili kupata mizani zinazotosha katika kila mshororo yaani nane katika ukwapi na nane katika utao.

4.3.11 Tabdila

Uhuru wa tabdila nao unahusu kubadilisha umbo la neno bila kuongeza au kupunguza idadi ya

mizani. Lengo lake huwa kuzua mapigo ya aina moja hasa kwa vina vya ndani au nje katika

ubeti wa shairi. Mapigo kama haya hupelekea shairi husika kuimbika. Mifano katika shairi la

‘N’shishiyelo ni lilo’ ni siwati kwa maana ya siiwachi, lilo ikiwa hilo na ajuwe badala ya ajue.

Mifano zaidi ni ingawaje ikiwa ingawaye na wamenitiya ikifaa kuwa wamenitia. Halikadhalika

kuna wangi badala ya wengi na dasturi ikiwa desturi. Mahabusu wingine iwe mahabusu wengine

na mambo mingine iwe mambo mengine. Hoja ya kimsingi kuhusiana na uhuru huu wa tabdila ni

kuwa idadi ya mizani katika neno haifai kuongezeka wala kupunguka. Usahihi wa neno tu ndio

uliovurugika. Hali kama hii huchangiwa na lafudhi au eneo la kijiografia atokalo mshairi husika.

Yeye huthamini kuhifadhi matamshi ya kikwao na anapofanya hivi hatarajii kukosolewa na

wanaisimu au wataalamu wa sarufi.

Shairi la ‘wasiwasi enda zako pia lina tabdila. Baadhi ya maneno yamevurugwa kiumbo kwa

hivyo yakawa sio sahihi. Mifano ni uwovu badala ya uovu. Pia kuna ela kuwafitinisha badala ya

ila kuwafitisha. Zaidi ya hayo kuna najisumbuwa badala ya najisumbua na ningojeyayo badala

ya niyangojeayo. Kuna pia hunijiya kwa nafasi ya hunijia. Mifano zaidi ni kukhusu badala ya

kuhusu, waliyo iwe walio, yaningojeya kwa yaningojea na kutiya wazimu ikifaa kuwa kutia

wazimu.

Zaidi ya mifano iliyotolewa katika mashairi hapo juu, lile la ‘telezi’ nalo lina tabdila. Mifano

anayotumia nafsineni ni kama vile mvuwa, mimeya, wakakimbiliya, hawakutuwa, kukomeya

Page 59: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

50

milango, isibakiye udhiya, kuiendeya ndowana sikujua na pia kutembeya. Kisahihi maneno haya

yanafaa kuwa mvua, mimea, wakakimbilia, hawakutua kukomea milango, isibakie udhia,

kuiendea ndoana, sikujua na kutembea. Tunasema ni tabdila kwa sababu idadi ya mizani

haipungui wala kuongezeka katika neno husika. Mshairi ametumia uhuru huu ili shairi liwe na

mdundo unaoweza kukaririka au kuimbika vizuri.

4.3.12 Kuboronga Sarufi

Katika mashairi yaliyohakikiwa kulibainika uhuru wa kuboronga sarufi. Hii inahusu kupangua

maneno katika baadhi ya mishororo ya shairi. Mifano katika shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’ ni

‘ninenayo usikiye badala ya usikie ninenayo. Zaidi kuna ‘yaliyo moyoni mwangu ningependa

nikwambiye’ badala ya ‘,ningependa nikwambie yaliyo moyoni mwangu’. Pia kuna ‘ndani

waniweke badala ya waniweke ndani’. Nyingi mno adhabu nayo yafaa kuwa adhabu nyingi mno

na juwa kuota ni dhiki’ nayo ‘iwe ‘kuota jua ni dhiki.’ Daima ni yangu hali yafaa kuwa hali

yangu daima.’

Katika ubeti wa kumi na mbili kuna sitakikani kuandika wala kuetewa barua ambayo yafaa kuwa

sitakikani kuandika wala kuletewa barua. Kainama wangu mdomo nayo iwe mdomo wangu

kainama. Mno wanganiadhibu, kweli siati kusema katika uhai wangu yafaa kuwa ‘Siachi kusema

kweli katika uhai wangu. Tunaweza kukubali kuwa uhuru huu wa kishairi ni mpangilio wa

wamaneno usiokuwa katika lugha ya kawaida kama vile ya nathari.

Hata katika shairi la ‘wasiwasi enda zako’ mshairi ameboronga sarufi. Kuna kwa mfano ‘sitaki

yako shari, enda zako wasiwasi badala ya siitaki shari yako, wasiwasi enda zako. Kuna pia vitwa

kuwagotanisha badala ya kuwagotanisha vichwa pamoja na mno umeizowea badala ya umeizoea

mno. Kwa upande mwingine kuna ‘Kwamba tamaa ngatiya nasumbua wangu moyo ambayo

yafaa kuwa ‘ningatia tamaa, nasumbua moyo wangu. Bure najisumbua, na kingine kisahani,

kuhusu zao afiya na kama hiyo ndiyo hamu nayo yawe najisumbua bure, na kisahani kingine,

kuhusu afya zao na kama hiyo ndiyo hamu yako.

Mwisho, shairi la ‘telezi’ pia limeborongwa sarufi. Mifano ni ‘ilibwaga kubwa shindo’ badala

ya ‘ilibwaga shindo kubwa. Pia kuna kunyesha iliposiya badala ya iliposiya kunyesha. Mfano

Page 60: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

51

mwingine ni ukawa mwingi udhiya badala ya udhiya ukawa mwingi. Mifano zaidi ni: Pa kupita

zisitupe, japo hivyo zilikuwa, zikanibwaga telezi na lakini tena siwezi. Yafaa kuwa zisitupe pa

kupita, japo zilikuwa hivyo telezi zikanibwaga na lakini siwezi tena. Sababu ya mshairi

kuboronga sarufi / kubananga sarufi katika mishororo hii ni ili kufaulu kujenga urari wa vina vya

kati au vile vya mwisho, yaani kumalizia na neno lenye silabi itakayofanana na za mishororo

iliyotangulia. Hapa kwa mfano ni ubeti wa tano katika shairi hili la ‘telezi’.:

Kunyesha iliposiya, kukatapakaa tope

Zilijaa kila ndiya, isibakie nyeupe

Ukawa mwingi udhiya, pa kupita zisitupe

Pa kupita zisitupe, kwa ndiya kukosekana

(Sauti ya Dhiki, uk.24).

Katika ubeti huu mshairi ameweza kupangua maneno katika mishororo fulani ili kuhakikisha

vina vya kati ni ya na vya mwisho pe.

4.3.13 Kilahaja

Mbinu ya kilahaja nayo inaonekana kutamalaki katika mashairi yaliyohakikiwa. Katika shairi la

‘N’shishiyelo ni lilo,’ lahaja iliyotumika na mshairi ni ile ya Kimvita. Kulingana na Chiragdin na

Mnyampala (1977:40), Kimvita ni lahaja ambayo asili yake ni kisiwa cha Mombasa. Hapo

zamani kuliitwa Mvita kutokana neno vita. Wenyeji wa kisiwa hiki walikuwa mara kwa mara

wakipigana vita na watawala wa kigeni; Wareno, Waarabu na hata Waingereza. Pia walipigana

na miji mbalimbali ya mwambao iliyokuwa ikishirikiana na wageni hao. Wataalamu hawa wa

historia ya Kiswahili wanafafanua kwamba katika Kimvita sauti /h/ huwa /ch/ katika lugha

sahihi, /nd/ huwa /nj/ na /v/ huwa /z/. Wanasisitiza kuwa Kimvita ni mojawapo ya lugha za

Kiswahili zenye historia ndefu ya fasihi. Mmoja wa washairi wa Kiswahili cha Kimvita ni

Muyaka wa Muhaji wa Mombasa.

Mtunzi wa mashairi haya Addilatif’ Abdalla naye pia ni mzawa wa mji huohuo. Ni bayana kuna

athari kuu ya Muyaka kwa washairi wa baadaye kama Abdilatif Abdalla. Mulokozi (2002: 16)

anadokeza kwamba kipengele kimoja cha uhakiki wa fani ya mashairi ni lahaja iliyotumika na

mshairi na hufaa kuchunguzwa ikiwa anaimudu vizuri, ikiwa ni lugha nyepesi au inayolenga

Page 61: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

52

kuonyesha ubingwa wa mshairi kwa kutumia maneno mazito na msamiati mgumu. Musa na

Hijazy (1977:1) nao wanaeleza kwamba mtunzi wa mashairi huathiriwa sana na lahaja ya mahali

alipozaliwa na hii hudhihirika kwa mashairi yake. Kuna ushahidi wa lahaja ya Kimvita katika

shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’. Mifano ni maneno kama ‘siwati’ badala ya Siiwachi imani, ndu

kuwakilisha ndugu, utungu kuwakilisha uchungu, nti hini badala ya nchi hii, moya ikifaa kuwa

moja ilipowatoma kumaanisha ilipowachoma, nde kumaanisha nje, wanati badala ya wananchi,

mtana kusema mchana, kutukuwa ikiwa kuchukua na awate kumaanisha awache, Pia kuna sil’ati

kumaanisha siliachi. (Sauti ya dhiki, uk. 1-3)

Katika shairi hili, mshairi anaonekana kutumia lugha ya Kiswahili kwani ujumbe wake

unaeleweka kwa kiwango fulani. Twaweza kusema kuwa lugha hii ni rahisi. Hata hivyo, yale

matumizi ya tamathali au ufundi wa lugha pamoja na vipengele kadhaa vya idhini ya kishairi

yamesababisha utata japo kwa upeo mdogo. Kuna maneno yasiyokuwa Kiswahili sahihi

kutokana na ukweli kuwa yamefupishwa, kurefushwa au umbo lake kuvurugwa. Mifano ni

usikiye, ndu, zilopisiye, ujuwe, niishishiye, ilipowatoma na mengineyo. Baadhi ya maneno pia

yameegemea kwa lahaja ya Kimvita na pia lugha ya kikale. Nafsineni ametumia kilahaja kwa

lengo la kujinasibisha na lugha na jamii yake anayothamini sana na pia kwa lengo la kutia shairi

mguso wa kisanaa.

Ingawa shairi la ‘Wasiwasi enda zako’ halijatumia uhuru wa kilahaja, lile la ‘telezi’

limeuzingatia uhuru huu hapa na pale. Lahaja yenyewe ni ileile ya Kimvita iliyotumika katika

‘N’shishiyelo’ ni lilo’. Mifano yake ni ndiya ikifaa kuwa njia. Pia kuna haamua kwa maana ya

nikaamua na henezi ikiwa polepole au taratibu. Mwisho kuna sitawata kwa maana ya sitawacha.

Mifano hii ni michache kwa kuwa shairi hili linalenga jumuiya nzima ya Wakenya baada ya

uhuru. Kamwe swala hili si la pwani au Mvita peke yake. Pia kutumia kilahaja yaonekana kuwa

ufundi mwafaka wa kupitisha ujumbe kwa hadhira kwa jinsi yenye mguso na mnato na pia

kuepuka lugha kavu isiyovutia au isiyo na ladha kisanaa. Katika shairi hili, licha ya mshairi

kutumia uhuru wa kishairi wenye miundo, msamiati au mpangilio wa lugha usiokuwa sanifu

hapa na pale, bado hajatoka nje ya misingi ya lugha inayohusika. Shairi hili linaendelea

kueleweka na mtu anayefahamu lugha ya Kiswahili.

4.3.14 Idhini ya Mazida

Page 62: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

53

Zaidi ya idhini hiyo, kuna uhuru wa mazida, yaani kurefusha maneno. Lengo lake huwa kupata

idadi ya mizani zinazolingana kwa kila mshororo. Katika shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’ kuna

niishishiyo badala ya niishiyo na kuniadhibisha ngomeni badala ya kuniadhibu ngomeni.

Inabainisha kwamba baada ya mshairi kutumia tabdila na inkisari, hakupata matatizo mengi ya

kumhitaji kutumia mazida ili kusawazisha mizani ndipo akatumia mifano hii miwili tu.

Katika shairi ‘Wasiwasi enda zako’ pia kuna mazida. Mifano ni ‘ondoka enenda zako’ ikifaa

kuwa ‘ondoka enda zako’. Hapa mizani zimeongezwa zikawa tatu badala ya mbili. Pia kuna

‘hiino ndiyo kaziyo’ kwa maana ya ‘hii ndiyo kazi yako’. Neno hiino limerefushwa na kupata

mizani tatu badala ya mbili. Katika ‘telezi’ kuna mifano kama maradi badala ya radi (ubeti wa

kwanza), ilitekukatekuka ambayo silabi zimerudiwa katika ubeti wa pili na pia mijaji badala ya

maji katika ubeti wa nne. Hata mazida imetumika na mshairi kusawazisha idadi ya mizani katika

mishororo. Njia hii imetumika hasa pale mshairi amegundua asipolirefusha neno moja katika

mshororo kwa njia yoyote ile, mizani hapo zitapungua.

4.3.15 Maneno ya Kigeni/ Kukopwa

Uhakiki wa shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’ ulibainisha kwamba mshairi ametumia maneno ya

kigeni kama njia ya kuonyesha kibali chake cha kishairi. Maneno kama haya hukopwa kutoka

kwa lugha ngeni na kutumika yakiwa vilevile bila kubadilishwa na mshairi kwa vyovyote vile.

Mfano ni neno Rasuli katika ubeti wa ishirini ambalo chanzo chake ni lugha ya Kiarabu na

hutumika katika dini ya Kiislamu yenye asili Arabuni. Zaidi ya hilo, kuna neno Rahamani katika

ubeti wa kumi na saba. Msamiati kama huu una chimbuko lake katika dini ya mshairi. Ingawa

ameteswa ngomeni (jela), anaendelea kuamini Mungu aliyempa maadili ya kusema kweli.

Katika shairi lili hili kumetumika maneno yaliyokopwa na kutoholewa (kuswahilishwa) na neno

‘Firauni’ ni mfano wake. Latokana na jina la cheo cha wafalme wa zamani wa Misri. Pia

lamaanisha mtu yeyote mwenye vitendo vichafu. Mshairi amelitumia katika ubeti wa nne,

mshororo wa tatu anaposema, ‘Wameniona mbaya kumshinda Firauni?’ Kuna pia maneno

‘burangetini’ kutokana na neno la Kiingereza ‘blanket’. Pia kuna neno ‘simitini’ kutokana na

cement’. Matumizi ya utohozi yanachangiwa na ukweli kuwa nomino hizi zimeingia Uswahilini

kutoka maeneo au mataifa ya nje ya Afrika au Afrika mashariki. Toni katika shairi hili nayo ni

ile ya msongo na hasira. Ingawa hii si uhuru wa kishairi, mshairi anaeleza kuhusu jinsi kujitoa

Page 63: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

54

mhanga kusema kweli kulivyomletea uchungu na adhabu ya kufungwa gerezani (ngomeni).

Baada ya kuwaambia wakuu (viongozi) pamoja na wananchi kuhusu kweli hiyo, mshairi

anateseka sana. Kweli yenyewe iliwachoma kwelikweli. Licha ya machungu anayopata

nafsineni, msisitizo wake ni kuwa haachi kusema kweli ile hata kama itaishia kwa kifo.

Umuhimu wa kutumia ufundi kama huu katika shairi husika ni kuwasilisha ujumbe kwa jamii,

watu waielewe hali halisi ilivyo katika uongozi wa jumuiya kwa kurejelea usuli wa wakati huo.

Ufundi aliotumia ni wa wastani isipokuwa maneno ya kilahaja ya Kimvita ambayo huweza

kutatiza mtu wa kawaida kuelewa ujumbe wa shairi.

Ieleweke kwamba nadharia zilizoongoza utafiti huu zimebainika katika mashairi yaliyohakikiwa

hapa. Kwa msingi wa nadharia ya umuundo, mshairi ameonyesha umahiri wa kimawasiliano

kama alivyotaja Noam Chomsky. Umahiri huo umedhihirika kwa kutumia ufundi wa lugha

aliotumia mshairi. Ujumbe wa mshairi umefika kwa hadhira ya mashairi kwa kutumia mbinu

kama chuku, kinaya, tashihisi, takriri, mvutano, balagha na hata jazanda na taswira pamoja na

mbinu zinginezo.

Nafsineni vilevile ametegemea uhuru kemkem wa kishairi ikiwemo inkisari, mazida, kilahaja,

kubananga sarufi na uhuru mwingineo kama ulivyotajwa kwa maelezo yaliyotangulia.

Tunalazimika kukubali kuwa mashairi yote matatu, yaani ‘N’shishiyelo ni lilo’, ‘wasiwasi enda

zako’ pamoja na ‘telezi’ ni zao la ushirikiano wa mbinu hizi mbalimbali za lugha pamoja na ule

uhuru wa kishairi. Vyote vyafanya kazi kwa pamoja ili kupitisha dhamira na ujumbe wa kila

shairi kwa njia yenye mguso na ya kutamanika. Ni bayana kuwa mbinu zote zilizotumika

zingaliondolewa kwa mashairi husika, lengo la mshairi lisingetimia ifaavyo.

Hata kwa kuoanisha mashairi haya na umuundo wa baadaye, mshairi huyu amefaulu kuzingatia

mtindo wa matini kwa njia ifaayo na hata uhakiki wake si lazima kushughulishwa na athari za

nje ya shairi husika. Japo maswala ya kitamaduni na kijamii yaliyolengwa na mshairi ni swala

halisi la kihistoria nchini Kenya, kamwe haijawa lazima kuyahakiki mashairi haya kwa misingi

hiyo. Uhakiki kama huu kwa hivyo haujajikita kwa athari za nje ya mashairi husika. Haimhitaji

mtu kujishughulisha na athari hizo ili kuyaelewa mashairi haya. Katika ufafanunuzi wa mbinu

Page 64: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

55

zilizotumika, imebainika kuwa mashairi yanaeleweka kwa kutegemea yaliyomo katika mashairi

husika kama mifano toshelevu ya mbinu hizo za sanaa. Kwa hivyo mada husika hapa inaeleweka

barabara bila kutegemea mashairi zaidi.

Kuhusiana na nadharia ya uamilifu, kila mbinu ya lugha iliyotumiwa na mshairi ina nafasi yake

katika kudumisha kuwepo kwa kila shairi husika. Umuhimu au nafasi hiyo imeelezwa kwa

maelezo yaliyotolewa kuhusu kila mbinu husika ya lugha. Ni bayana kuwa kila mbinu

haijatumika na mshairi hivihivi tu kwani inatekeleza jukumu lake katika kila shairi. Jukumu hilo

ni kuzua taswira mwafaka kwa hadhira, kuhifadhi siri ya kishairi na hata kuleta mvuto.

4.4 Kuhakiki Muundo katika Mashairi

4.4.1 Beti, Mishororo na Vipande

Katika madhumuni haya, mashairi yaliyolengwa ni ‘siwati’, ‘Leo N’singekuwako’ na

‘N’sharudi’. Uhakiki wa mashairi haya ulithibitisha kuwa yote yana muundo unaokaribia

kufanana. Hata hivyo kulibainika tofauti za hapa na pale. Shairi la ‘Siwati’ kwa upande wake

lina umbo la beti nne, mishororo minne kila ubeti na kiishio. Kiishio hapa ni ule mshororo wa

mwisho katika kila ubeti ambao unatofautiana kutoka ubeti hadi ubeti. Kila mshororo hapa

umegawanywa katika ukwapi na utao isipokuwa ubeti wa kwanza mshororo wa kwanza na ubeti

wa nne mshororo wa tatu. Mishororo hii miwili imegawanywa katika ukwapi, utao na

mwandamizi, yaani sehemu tatu. Katika ubeti wa kwanza sababu ya kipande cha pili ni kutoa

msisitizo kuwa nafsineni hawachi aliloshikilia kwani hana sababu maalumu ya kufanya hivyo.

Mshororo wenyewe ni: ‘Siwati n’shishiyelo, siwati, Kwani niwate? (Sauti ya Dhiki uk.9).

Katika ule ubeti wa mwisho mshororo wa tatu, nafsineni ametumia sehemu ya pili kulinganisha

kuacha aliloshika na nzi hasa kwa kuwa nzi hawi na maono ya mbali. Mshororo huo nao ni:

‘Siwati kisha nikawa, kama nzi; hivyo siwi. (uk.9).

Kuhusiana na shairi la ‘Leo N’singekuwako,’ hili vilevile ni shairi la arudhi ambalo lakaribiana

kimuundo na lile la ‘Siwati.’ Hata hivyo, kuna tofauti za kimuundo hapa na pale. Katika shairi

hili, kuna jumla ya beti tano katika shairi zima. Ingawa beti hizi zahusu kukumbuka madhila,

machungu na mateso aliyopitia mshairi akiwa jela, kila ubeti una wazo lake au ujumbe wake kwa

hivyo tunaweza kukubali kuwa hapa napo pana utoshelezi wa beti. Ubeti wa kwanza kwa mfano

Page 65: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

56

unaeleza kwamba taabu ingekuwa mauti mshairi asingekuwako kwani angekuwa maiti

aliyebakiza sikitiko tu. Angekuwa mfu na kufunikwa kwa mchanga.

Katika ubeti wa pili, nafsineni anasema kuwa leo hii angekuwa amesahaulika na ikaachwa

kusemekana tu kwamba aliwahi kuishi. Ule ubeti wa tatu unaeleza kuwa angekuwa marehemu

aliyekwishaoza na kusahau masumbufu, taabu na masumbuko yake. Anauliza ikiwa taabu hizo

zingeweza kufika aliko. Ule ubeti wa nne nao unarejelea mshairi kuombolezwa na jamaa

kuomba dua ili aende salama baada ya kifo. Baadaye ingekuwa kusahauliwa kwa moyo na

matamko. Ubeti wa tano unadokeza kuwa licha ya mateso aliyopata, bado leo hii yu hai kwa

kuwa moyo wake wahimili masumbuko na kwa hivyo angetamaushwa na yaliyompata, hakika

asingekuwa hai sasa hadi kuandika shairi hili. Msisitizo hapa ni kuwa katika beti zote hizi, kila

ubeti umejitosheleza kutoa ujumbe wake bila kutegemea ubeti mwingine. Umuhimu wa hali

kama hii ni kuwa mshairi ameonyesha umahiri wake katika kumudu stadi hii muhimu katika

utunzi wa mashairi mapokeo stadi ambayo inawezesha beti chache tu kama hizi tano kupitisha

ujumbe wenye maadili kemkem.

Sawa na shairi la ‘siwati’, la ‘leo N’singekuwako’ pia lina mishororo minne katika ubeti likiwa

pia ni tarbia. Kila mshororo nao una ukwapi na utao ikiwa bahari ya mathnawi. Katika shairi hili

kumetumika kibwagizo /kipokeo au mkarara ambao ni ‘leo N’singekuwako kama tabu ni mauti.’

Mkarara huo umerudiwa katika kila ubeti kwa lengo la kusisitiza ujumbe mkuu wa nafsineni.

Anasisitiza kuwa asingekuwa hai ingekuwa kupata taabu ni sawa na mauti. Kipokeo hicho pia

kinasababisha taswira ya kudumu kwa hadhira na pia hakikisho kuwa mshairi sasa yu hai licha

ya dhuluma zote alizopitia.

Halikadhalika, shairi la ‘N’sharudi nalo limezingatia muundo wa beti tano. Kila ubeti una

mishororo minne na hata hilo likiwa muundo wa tarbia. Kila mshororo nao una ukwapi na utao

hiyo ikiwa bahari ya mathnawi. Zaidi ya arudhi hizo, sawia na mashairi yaliyotangulia, katika

madhumuni haya, mawazo yanaonyesha muumano ufaao kuanzia pale ubeti wa kwanza hadi wa

tano. Katika ule wa kwanza kwa mfano, mshairi anatoa utangulizi wa kuwa anayezungumza sio

mwingine bali ni yule yule kijana wa kutoka Mvita, mtaaa wa Kuze. Anaeleza hapo ndipo shina

lake na kusisitiza kuwa amerudi kwao nyumbani tena hivyo aliye na la kusema aseme. Katika

Page 66: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

57

ubeti wa pili anasisitiza kuwa amekuja na ingawa amenyamaza kwa muda mrefu, leo ndio

anazungumza tena. Ubeti wa tatu unaeleza kuwa hajachoka wala kuogopa kuzungumza kuhusu

jambo liendalo kombo atakaloliona katika jumuiya yake. Anasema katika ubeti wa nne kuwa

macho yake bado yanaona na masikio vilevile yanasikia ili yamwingie hata yaliyompita siku

zilizotangulia. Anamalizia kwa kusisitiza kuwa hata hivyo ahitaji kwanza kupata muda wa kuona

mambo ya kutosha ili ayazungumzie na hivyo hataki kuzungumza moja kwa moja ingawa

amerudi kwao.

Inabainika kuwa ujumbe mkuu katika shairi ni mmoja unaojengwa kwa jinsi inayokaribiana sana

katika beti hizi tano. Yabainika hakuna tofauti kubwa sana ya ujumbe toka ubeti mmoja hadi

mwingine. Kauli ya jumla yaweza tolewa kuwa shairi hili tofauti na yaliyohakikiwa hapa halina

utoshelezi kamilifu wa beti kwani kila ubeti haujitegemei kikamilifu kupitisha wazo lake. Hii ni

kwa sababu ujumbe wa ubeti umejengwa sana kwa kutegemea ubeti uliotangulia.

4.4.2 Mizani

Kipengele zaidi cha muundo kilichotambulika katika uhakiki wa mashairi haya ni kile cha

mizani. Katika shairi la ‘Siwati’, kuna mizani kumi na sita yaani nane nane kwa kila mshororo

isipokuwa mishororo miwili iliyo na sehemu tatu. Vina vya kati navyo vinafanana katika

mishororo ya kwanza mitatu katika ubeti mmojammoja. Vile vya mwisho navyo vinafanana

katika mishororo hiyohiyo mitatu. Kina cha mwisho katika mshororo wa tatu kila ubeti nacho

chatokea kuwa cha kati katika mshororo wa nne kwa kila ubeti. Mfano bora ni ubeti wa kwanza

hapa;

Siwati nshishiyelo, siwati; kwani niwate?

Siwati ni lilo hilo ‘talishika kwa vyovyote.

Siwati ni mimi nalo, hapano au popote

Hadi kaburini sote, mimi nalo tufukiwe.

(Sauti ya Dhiki, uk. 9)

Inaweza kukubalika mshairi akitumia mpangilio kama huu wa vina vya kati na vya nje ili shairi

lake liweze kuzua mahadhi ya mapigo ya kimuziki yanayoweza kuimbika. Mbali na kuonyesha

ufundi wake wa kutumia takriri, mpangilio kama huu pia unasaidia kusisitiza msimamo wake

katika shairi zima. Umbo zima la shairi hasa kule kutunga ushairi mfupi wa beti nne tu

Page 67: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

58

kunaelekea kutufahamisha kuwa tayari hadhira yake imepokea ujumbe wake kuhusu

anachoshikilia kama falsafa na maadili yake. Hapa haina haja kutunga utungo mrefu tena ila

kusisitiza kuwa hawachi aliloshikilia na kuamini. Katika muktadha huu basi, shairi lenyewe ni

fupi.

Shairi la ‘Leo N’singekuwako’ nalo sawia na lile la ‘Siwati’ limebuniwa kwa mizani kumi na

sita kwa kila mshororo isipokuwa ubeti wa tatu mshororo wa tatu na ule wa nne mshororo wa

kwanza. Kila mshororo kati ya hii miwili ni mizani kumi na tano. Mlingano wa mizani kila

mshororo ni muhimu sana ili kusababisha mapigo ya kimuziki na ufundi unaopelekea shairi

kukaririka au kuimbika kwa mahadhi ya kuvutia. Hata mahali pasipofaa mizani kumi na sita,

mshairi amedumisha uhuru wa mazida na hata inkisari ili aidha kupunguza au kuzidisha mizani

hadi zitoshe. Hata hivyo, nafsineni amedumisha mizani hizo kumi na tano kwa kuwa mishororo

hiyo yazungumzia matokeo ya kifo chake kama vile kuondokewa na taabu na kuliliwa na jamaa

jambo ambalo halikutendeka kwani bado yu hai. Upungufu kama huo hapa wafaa. Kibwagizo

cha shairi kina mizani kumi na sita hata katika beti zenye mshororo mmoja wenye mizani kumi

na tano.

Ufafanuzi wa mizani unapoendelea ni bayana kuwa shairi la ‘N’sharudi’ lina mizani nane katika

ukwapi na nane katika utao kwa kila mshororo. Katika shairi hivyo basi, kumezingatiwa takriri

kwa kiwango cha juu. Umbo la tarbia limerudiwa katika beti zote tano. Mkarara kila ubeti ni

‘basi’ n’sharudi aliye na lake nanene.’ Katika ukwapi na utao, kuna mizani kumi na sita na vina

vinavyotiririka. Maelezo haya yanaonyesha muoano katika ufundi na umbo au muundo. Ni

bayana kuwa shairi hili, kutokana na mpangilio unaovutia wa mizani na vina linaweza kuimbika

na hata kukaririka kwa urahisi.

4.4.3 Bahari za Mashairi

Zaidi ya vipengele vilivyotajwa kuhusiana na muundo, mshairi amezingatia bahari za mashairi

kama vile mathnawi, ukaraguni, kikwamba na sakarani. Mathnawi ni bahari yenye sehemu ya

ukwapi na utao kwa mishororo kama ilivyo katika shairi la ‘siwati.’ Mishororo kama ile ya

kwanza mitatu kuanza kwa neno moja kama ilivyo hapa nayo ni bahari ya kikwamba yaani neno

‘siwati’ kutumiwa mwanzo wa kila mshororo. Ufuatao ni ubeti wa pili katika shairi hilo:

Page 68: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

59

Siwati ngaadhibiwa, adhabu kila mfano

Siwati ningaambiwa, tapawa kila kinono

Siwati lililo sawa, silibanduwi mkono

Hata ningaumwa meno, mkono siubanduwi

(Sauti ya Dhiki, uk.9)

Vina vya kati vinatofautiana na pia vya mwisho ni tofauti kila ubeti. Bahari kama hii nayo ni

ukaraguni. Kuchanganya bahari hizi mbalimbali katika shairi moja nako kunazua bahari ya

sakarani. Kwa maoni hayo, haikosi ushairi huu ni tarbiya, mathnawi, kikwamba, ukaraguni na

pia sakarani.

Katika shairi la ‘leo N’singekuwako’ vina vyote vya mwisho vinafanana. Vyote ni ko. Vile vya

kati navyo vinafanana katika beti zote isipokuwa ubeti wa kwanza. Vina hivi ni ti katika ubeti

huo wa kwanza lakini wa katika beti hizo zingine. Vya kibwagizo ni ko, ti. Ni ubeti wa kwanza

tu au utangulizi wa shairi ulio tofauti na beti zingine kuhusiana na mpangilio mzima wa vina.

Mpangilio wa vina ambapo vyote vya mwisho vinafanana na vya kati kutofautiana ni bahari ya

ukara. Shairi hili ni bahari ya mathnawi pia kwa sababu kuna ukwapi na utao katika kila

mshororo. Kwa muktadha wa ujumbe anaopitisha mshairi, ujumbe kuhusu maisha yake unatajwa

katika sehemu ya utao. Huu ndio anaosisitizwa kwa kutumia neno lenye silabi ya mwisho ko ili

kusababisha mapigo yanayotekenya ngoma za masikio ya hadhira kisha ujumbe kunata zaidi.

Maneno yote yenye ko kama vile kuweko, sikitiko, funiko, alikuwako na mengine yametumiwa

mwishoni mwa kila mshororo ili kusisitiza ujumbe wa mshairi. Katika shairi la ‘N’sharudi’ nalo,

vina vyote vya kati ni le na vya mwisho na. Kule kufanana kwa vina vyote vya kati na pia vyote

vya mwisho kunasababisha bahari ya mtiririko. Vina vya kibwagizo ni na, ne navyo pia

vikifanana kila ubeti. Aidha, kina cha mwisho mshororo wa tatu kinatokea kuwa cha kati katika

mshororo wa mwisho kila ubeti. Kina hicho ni na. Kuna urari wa vina vya mwisho na hata vya

kati. Kupanga vina kwa njia hii kunamwezesha mshairi kudumisha mwendo wa ujumbe

aliodhamiria kufikia hadhira kiustadi na hata ukanata kwao. Inabainika swala kama hili la

mvutano baina ya nafsineni na waliomfunga jela ni swala nyeti linalohitaji wapinzani wa mshairi

kupata na kuelewa msimamo wake kwa njia barabara. Jambo hilihili limesisitizwa kwa kutumia

bahari ya pindu pale ambapo kina cha mwisho wa mshororo wa tatu kinatumika kama kina cha

Page 69: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

60

kati katika ukwapi wa kabwagizo. Hapa chini kumetolewa ithibati toka ubeti wa kwanza na wa

pili katika shairi hili.

Si mwingine ni yuyule, wa Ki-mvita kijana

Mzawa mji wa kale, mtaa Kuze kwa jina

Huwo ndiwo mzi mle, tipuzi ya langu shina

Basi n’sharundi tena, alo na lake nanene

Nijile tena nijile, mneni nijile tena

Zangu tomi zinyemele, Zinyemele kwa maana

Tangu siku n’toshile, hi’leo ndiyo nanena

Basi n’sharudi tena, alo na lake nanene

(Sauti ya Dhiki, uk, 111).

4.4.4 Utoshelezi wa Arudhi za Utunzi

Katika shairi la N’sharudi, mshairi anaonyesha kujifunga katika arudhi zote zinazotarajiwa

kuzingatiwa katika mashairi mapokeo. Isipokuwa kwa lugha iliyosukwa kwa njia maalumu kama

kilahaja, idhini ya kishairi na tamathali za usemi, kusingekuwa na changamoto kwa hadhira

kuhusiana na muundo. Kuna utoshelezi wa arudhi katika kila ubeti.

Katika shairi la ‘Siwati’, kutumia neno ‘siwati’ kila ubeti kunasababisha utoshelezi wa beti.

Inaibuka kwamba kila ubeti unawasilisha ujumbe wake kikamilifu bila kutegemea ubeti

mwingine. Pia kila ubeti umezingatia arudhi za utunzi kama vile ubeti, mshororo, vipande na

mizani kama ilivyo katika beti zote. Kuna mfano wa bahari ya mandhuma pale ambapo ukwapi

unatoa wazo na utao kutoa jibu la wazo hili. Inaonekana mawazo kwa kila mshororo na pia beti

yamefululiza kuanzia mwanzo hadi mwisho kwa muungano unaofaa ili mshairi afaulu

kupatanisha mawazo ya ujumbe wake mzima. Muundo mzima wa shairi hili pamoja na mapigo

ya kimuziki katika vina vya kati na vya nje yanaathiri hadhira barabara kwa kufikisha ujumbe

mzima kwa njia yenye mnato ufao.

Shairi hilo japo fupi la beti nne tu linawasilisha ujumbe wa mshairi kwa ukamilifu hasa kutokana

na kurudiarudia neno kuu la ujumbe wake mzima. Kwa muktadha huohuo kunaonekana muundo

Page 70: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

61

wa kinyumbizi au mnyambuliko katika ubeti wa tatu mshororo wa kwanza. Hii yamaanisha

urudiaji ambapo neno fulani linanyambuliwa na kuunda maneno mengine yanayofanana nalo.

Kimsingi, hii ni sifa inayoingiliana sana na muundo wenyewe wa lugha ya Kiswahili na lugha

zetu mbalimbali. Huwa muhimu sana katika ukuzaji na uimarishaji wa wizani au ridhimu.

Mshororo wenyewe ni ufuatao:

‘Siwati si ushindani, mukasema nashindana?

(Sauti ya dhiki, uk.9)

Hapa, neno ‘nashindana ni mnyambuliko kutoka kwa ‘ushindani’. Mshairi amezingatia ukamilifu

wa arudhi zote za utunzi wa mashairi mapokeo hasa yale ya tarbia. Arudhi hizi zinasababisha

ujumbe wake kueleweka barabara licha ya kutumia uhuru wa kishairi kwa njia kadha. Licha ya

kuwa beti ni nne tu, adili lililolengwa limegonga ndipo na hata ameepuka kutumia mkarara ili

asipoteze nafasi yote ya kutoa msimamo zaidi. Kwa hivyo hataki marekebisho ya mwanajamii

yeyote katika msimamo wake au imani maishani. Hata akisema kwa kifupi namna hii au hata

kwa kirefu, hilo halibadili msimamo wake huo. Maelezo haya yanalandana na nadharia ya

uamilifu kwa kuonyesha utendakazi wa muundo wa aina hii. Kuunganisha vipengele vyote vya

muundo kama ailivyofanya mshairi ni njia bora ya vijenzi hivi kuunda shairi kwa pamoja nayo

ikioana na nadharia ya umuundo.

Kuhusiana na shairi la ‘Leo n’singekuwako’ inaonekana usambamba mwingine pamoja na

kinyumbizi au mnyambuliko. Katika ubeti wa kwanza maneno ‘ningekuwa yameendelea

kurudiwa katika kila ukwapi nayo maneno ‘kungebaki’ katika ubeti wa pili. Maneno

yananyambulika na kuishia kutofautiana hapa na pale kwa mfano ‘n’singekuwako, ningekuwa,

ningekuwako na ‘n’ngekuwa. Vilevile kuna mabadiliko katika maneno haya kwa kuangalia

mizani kwa kuwa zinazidi kutofautiana idadi kutoka neno hadi neno licha ya kuwa maneno hayo

yametokana na neno moja. Huku kubadilika kunafanya swala hili hili kuchukuliwa kuwa la

muundo badala ya la ufundi wa lugha. Ubeti wa kwanza na wa pili ndizo hizi:-

Kama tabu ni mauti, Leo n’singekuwako

Ningekuwa ni maiti, Mebakiza sikitiko

Ningekuwako tiyati, mtanga ndilo funiko

Leo n’singekuwako, kama tabu ni mauti

Page 71: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

62

Hivi leo n’ngekuwa, kana kwamba sikuwako

Kitambo n’shafukiwa, nimo kaburini huko

Kungebaki kuambiwa; Atifu alikuwako;

Leo n’singekuwako, kama tabu ni mauti.

(Sauti ya Dhiki, uk. 63)

Katika mashairi haya inakubalika mshairi amefaulu kuunganisha arudhi zote za utunzi wa

mashairi mapokeo hadi kuzua shairi la beti nne katika shairi la ‘siwati’, tano katka ‘Leo

N’singekuweko’ na tano katika ‘N’sharudi’ Mawazo ya kila ubeti pia yameunganishwa kwa njia

bora kuanzia mwanzo hadi mwisho. Haya ni kwa kulinganisha na nadharia ya umuundo ambapo,

mishororo, vina, vipande na vipengele vyote vya muundo vinaonekana kushirikiana kwa

mshikamano murua ili kujenga kila shairi kiwango kwamba kila mojawapo imetawala nafasi

yake kisahihi. Kwa maneno machache, mshairi huyu ameweza kupitisha maadili ya kutowacha

mambo yafaayo hadi kaburini, kuvumilia mateso na taabu pamoja na msimamo wake wa

kuikosoa jumuiya iliyopotoka. Vipengele vyote vya kimuundo vemeshirikiana kikamilifu

kupitisha maadili yote haya na hivyo utunzi wenyewe unatimiza majukumu fulani maalumu

kulingana na nadharia ya uamilifu. Kila kipashio kina jukumu lake.

4.5 Maudhui katika Mashairi yaliyoteuliwa.

4.5.1 Pingamizi na Unyanyasaji

Mashairi yaliyohakikiwa katika madhumuni haya ni ‘Wasafiri tuamkeni; ‘kichu hakiwi ni uchu’

na ‘Mamaetu Afrika’. Katika mashairi haya kulionekana maudhui ya pingamizi na unyanyasaji.

Katika shairi la ‘wasafiri tuamkeni’ mshairi anawahimiza wanajamii wenzake ambao ni wasafiri

wasichoke wala kuwa dhaifu ingawa safari yao ni ndefu. Juhudi nzima inayozungumziwa katika

shairi, kama kawaida ya shughuli yoyote ya kisiasa ina wapinzani. Katika ubeti wa kumi na

mbili mshairi anazungumzia adui ambaye hataki safari ifanyike. Huyo anasemekana kuwa adui

wa wasafiri hawa na hata kwake mwenyewe. Mshairi anamkumbusha kuwa asifikiri atafaulu

kwa lengo hilo la kuwapinga. Juhudi nzima yahitaji mshikaji bendera kuishika vizuri na daima

kuwa imara bila kulegea. Pia afaa kuiongoza barabar hadi wafike huko waendako.

Shairi la ‘Kichu hakiwi ni uchui’ nalo lina maudhui sawa au yaliyokaribiana na haya. Kuna

maudhui ya ubinafsi na unyanyasaji. Mshairi anazungumzia mtu aliye na vitu kwa milima (tajiri)

Page 72: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

63

mkubwa lakini wa kujifaa yeye binafsi bali sio binadamu wenzake. Yeye huvikusanya

(kujilimbikia mali) na kuendelea kuitazama tu. Mtu huyo analinganishwa na ndovu. Hapa kuna

pia maudhui ya kupuuza na kunyanyasa maskini. Katika ubeti wa thelathini mshairi anataja mtu

aliye na mali iliyokiuka mipaka lakini anatupilia mbali wenye shida na mashaka. Ubeti wa

thelathini na moja unataja mhusika anayezungumziwa katika shairi kuwa na nguvu za kimabavu

na kutumia magumi na mateke hadi kuwanyima wenzake utulivu. Akitokea hao hutetemeka kwa

kumuogopa. Mtu huyo huishia kuzitumia nguvu hizo mitaani akidhulumu wenzake ambao ni

wanyonge mfano wa ‘mnyonge msonge’ bila wa kumzuia. Mshairi hapa anarejelea matumizi

mabaya ya cheo /madaraka. Anazumgumzia mhusika huyo kuwa na cheo juu ya wenzake wote

lakini wawapo na shida, yeye kamwe hawasaidii kwa chochote au hata kutaka kuwasikia. Kuna

mfano wa ubeti wa thelathini na moja hapa chini:

Au awe yuna nguvu, Kikubwa kifuwa chake

Ziwe nguvu za mabavu, na magumi na mateke

Iwe sasa utulivu, hawaupati wenzake

Iwe ni watetemeke, muda’ye akitokeya

(Sauti ya Dhiki, uk. 86)

Badala ya kuchukua fursa hiyo na kuitumia vizuri, yeye huanzisha takaburi, kuwatesa

anaowaongoza na hata kuwatendea jeuri. Mshairi anasisitiza kuwa mtu kama huyo hafai kuitwa

mtu bali mnyama wa porini.

Katika lile shairi la ‘Mamaetu Afrika’ mshairi ameonyesha nyanyaso kwa bara la Afrika.

Anarejelea Afrika kama ‘mama yetu.’ Mbinu ya tashihisi kwa hivyo imetegemewa sana.

Anaangazia swala la utengano wa Waafrika pale mwanzo wa shairi. Waafrika wamekumbwa na

msiba kwani ndugu hawasikizani. Kila mmoja wao ataka kuwa kiongozi wa wenzake. Kwa

jambo hili ambalo nafsineni anasema haliwezekani, anaitaka Afrika iwaamue. Anazungumzia pia

fitina inayochochewa na wale maadui (wakoloni) ambao hawataki kuiona Afrika ikipata amani.

Unyanyasaji zaidi ni kuwa kuna dhuluma ya wakoloni toka Ulaya ambao walitawala maeneo

mengi ya Afrika kabla ya uhuru. Mshairi anataja kuwa bado wamo duniani wakiwa na fikra

zilezile za kikoloni. Wanatamani kuidhulumu Afrika tena. Waliishikia Afrika shokoa na kupora

mali yake yote. Wakaijaza mali hiyo vyomboni kama shehena wakaipeleka mataifa yao. Kwa

Page 73: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

64

hivyo ni wezi. Hawakuona huruma yoyote kwani waliiacha Afrika maskini bila kujali vizazi

vijavyo vingetegemea nini. Utumwa nao unatajwa ambapo watu weusi ambao ni ndugu za

nafsineni walitiwa utumwani bila utu. Kutokana na rangi yao nyeusi walionekana kama nyani .

Hao watumwa walitegemewa kufanya kazi kule Ulaya bila malipo yoyote. Mshairi anasisitiza

kuwa mali toka Afrika ilitajirisha Ulaya na kuipa sifa kemkem. Sifa hizo zisingalikuwapo leo hii

isingalikuwa kutokana na mali na kazi ya watumwa toka Afrika. Mali hiyo iliwalisha wakoloni,

kujenga miji yao na hata kuwatajirisha sana. Mshairi anaeleza kuwa kabla ya ukoloni hata hiyo

Ulaya ilikuwa maskini. Hapa kunanakiliwa mifano ya ubeti wa tisa na kumi kufafanua maudhui

hayo.

9

Mama lau si wanayo, kupelekwa ugenini

Lau kwamba si maliyo, kubwakurwa mikononi

Hivi leo bara hiyo, iitwayo Ulayani

Ingekuwa haifani, na kupawa sifa mama

Ndiyo yaliyowalisha, na kutengenezeya huko

Miji wakasimamisha, kwa nguvu za mali yako

Lililowatajirisha, ni jasho la mwili wako

Na damu ya wana wako, ndiyo kuwa hayo mama

(Sauti ya Dhiki, uk. 37)

4.5.2 Kiburi na Utawala Mbaya

Kuna maudhui ya kiburi pamoja na utawala mbaya katika mashairi haya. Japo hivyo, swala hili

labainika zaidi katika shairi la ‘Kichu hakiwi ni uchu’ na lile la ‘Mamaetu Afrika. Katika shairi

la ‘Kichu hakiwi ni uchu’ mshairi anauliza ni nani aliyeambiwa yu mtu kwa kuwa na kitu.

Mshairi huyu anataja huo kuwa uongo kwani utu wa mtu kwa wenzake ndio kitambulisho cha

umuhimu wake. Hata kama kuna watu wengi walio na pato la juu, utu wao haupimwi kwa

kiwango chao cha pato bali kwa utu kwa wanajamii wenzao. Mshairi anatumia jazanda ya ndovu

akigawanywa vipande vitatu ili kuweza kufahamishana kuhusu utu. Mwili wa ndovu ni mkuu na

mwituni hana mfano wake. Kwa sehemu zote za mwili, umbo lake ni nono na la kipekee. Hata

Page 74: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

65

kuna wanajamii ambao kwa ukuu wao huwaona wenzao kama ndovu aonavyo wenzake mwituni.

Yule ndovu huwahangaisha viumbe wengine pamoja na miti kutokana na uwezo wake mkubwa.

Huwahangaisha hadi kuwatia mbioni wakihofia kuumizwa.

Kuhusu kiburi, nafsineni anazungumzia watu ambao hujisifia nguvu zao kwamba wao huweza

kuvutana hata na watu mia. Hujidai kuwa hata watu hao wakiungana kumvuto kwa pamoja

hawamwezi kutokana na uwezo wake mkubwa. Ndovu (mtu) kama huyo hung’oa miti na pia

kuangamiza wenzake kwa teke na pia kwa pumzi zake. Mtu kama huyo vilevile hujivunia

thamani au sifa zake zinazojulikana pembe zote za dunia mjini na vijijini na kumfanya

kutambulika. Yule ndovu pia ana pembe ambazo huuzwa mnadani kwa bei ghali hivyo uwezo

wake huwa ni si haba.

Mshairi anazidi kusisitiza ule mfano aliotoa wa ndovu ambaye ana uwezo kama vile ukubwa na

thamani kuu. Kila mtu kwa hivyo hutafuta uwezo kama huo na akiupata huringa na hata

kufurahi hadi magego kuonekana. Mshairi anatamaushwa na kuwa hata mtu ambaye

anamrejelea kama ‘mnyama mwitu’ akipata uwezo kama huo unaosifiwa huchukuliwa kuwa mtu

mzuri. Hata hivyo, anasema kuwa hata mtu mjinga seuze mwenye akili hafai kukubali kuwa

uwezo wa mtu mbaya waweza mfanya mzuri. Rafiki mwenyewe akiambiwa mambo kama hayo

atayapuuzilia mbali na kuyaona yasiyo na mashiko.

Mshairi ameonyesha maudhui ya utawala mbaya katika shairi la ‘kichu hakiwi ni uchu’ na pia

‘Mamaetu Afrika.’ Mtu mwenye nguvu anatawala kwa makonde na mabavu (ubeti wa 40).

Wanaoongozwa hulazimika kwenda mbio kwa kumuogopa kiongozi kama huyo. Kuna pia

matumizi mabaya ya nafasi au uwezo. ‘Ndovu’ huyo apandwapo na ghadhabu huviharibu hadi

kuviangamiza vitu vyote. Huviharibu hadi kuviangamiza vitu vyote vilivyo karibu naye kama

vile kulaza mwitu, manyasi na miti yake. Jazanda hizi ni mifano ya watawala wenye nguvu

kuwaangamiza na kuwanyanyasa walio wengi katika jamii na ambao wako kwa madaraja tofauti

ingawa huangamizwa na ndovu mmoja tu. Hapa napo pameonyeshwa ubeti huo wa arobaini:

Na kwa wa nguvu upande, ‘tawaleza pasi shaka

Iwapo ni wa makonde, na mabavu kutumika

Watu iwe mbiyo wende, kwa kucha kuzidirika

Page 75: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

66

Vifenene kadhalika, viumbe viwili hivi

(Sauti ya Dhiki, uk. 87)

Utawala mbaya katika shairi la ‘Mamaeta Afrika’ unahusiana na ukoloni mamboleo. Wakoloni,

licha ya mapambano dhidi yao yaliyofanywa na Waafrika hadi kufaulu hawakukata tamaa ya

kupata walichotamani Afrika. Walianza kuwatawanya Waafrika ili waendelee kuwatumikia.

Wakawatumia baadhi yao kama vibaraka waliorudi Afrika kuiba kilichobaki na kukipeleka

ulaya. Hao vibaraka ndio huleta michafuko ya kisiasa kwani adui amewanunua. Hata hivyo,

mshairi anasema kuwa watapata masumbuko kwa haya wayatendeayo bara lao. Nafsineni na

Waafrika wenzake wanaendelea kuungana walinde bara lao ingawa vibaraka hawana nia moja na

wao. Hao wanachukua rasilimali za kiafrika na kuziuza kirahisi hadi kuivunjia Afrika hadhi. Huu

ni ubinafsi unaoishia kuporomosha chumi zetu.

4.5.3 Maudhui ya Ukombozi

Maudhui ya ukombozi vilevile yanabainika katika mashairi haya. Haya yanachochewa zaidi na

ukoloni pamoja na utawala mbaya ambao tayari umetolewa maelezo. Katika shairi la ‘Wasafiri

tuamkeni’ nafsineni anawahimiza wanajamii wenzake ambao anawataja kuwa wasafiri

wasichoke wala kuwa dhaifu ingawa safari yao ni ndefu. Anawataka pia waondoe hofu kwa

kuwa huu ni mwanzo tu wa safari yenyewe. Kinachosababisha maudhui ya ukombozi kuonekana

ni taashira ya bendera katika ubeti wa pili. Kwa kawaida bendera huashiria uhuru. Wanajamii

hawa wanausaka uhuru wao. Nafsineni kwa hivyo anawataka wasonge mbele na wasianguke

hadi wafikie mlima mbele yao na pale kileleni waitundike bendera.

Mshairi anazungumzia ugumu wa safari hivyo kuwataka kuwa na stahamala. Anataja jazanda ya

miiba yenye sumu akiwataka wenzake watahadhari wasianguke. Kuna pia misitu yenye miti

mirefu njiani iliyojaa wanyama mwitu. Kila mmoja kwa nafasi yake wakikiona kitu ni lazima

wakishike. Changamoto nyingine inayokumba mapambano yao ni bahari pana yenye kina kirefu

na mawimbi makubwa yenye nguvu ila anawahimiza wenzake wapambane hadi waivuke. Safari

pia ni ngumu na hatari lakini anawataka wasitishike kwani ni lazima waimalize licha ya urefu

wake.

Page 76: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

67

Zaidi ya hayo, anawasisitizia ileile haja yao ya kuitundika bendera na hivyo hawafai kukata

tama, nia kutetereka au nyoyo kuvunjika. Zaidi kuna maudhui ya ushirikiano wa wanajamii wote

katika juhudi hizi za kupata uhuru au kujitawala. Waume kwa wake watakiwa kujifunga

vibwebwe kikamilifu na kuingia safarini bila kubabaika. Kujikomboa hakuhitaji kujilegeza wala

kutetemeka kwa kuwa haja ni kuimaliza safari yenyewe kikamilifu. Wanajamii wahimizwa

kutegemea mbinu fulani maalumu kama vile mwenye chake kujitwika, kupanga mistari na safu

na kushirikiana wana na wazee kwa mchanganyiko. Aidha kwahitajika wakitaka wasitake, walio

na afya wanyoshe miguu na vilema wabebwe na wanajamii wenzao.

Dhamira ya mshairi katika shairi hili kuanzia kwa kichwa cha shairi ni kuwazindua na

kuwahamasisha wanajamii wenzake kujitayarisha kwa safari yao ambayo ndio tu mwanzo wake.

Pia analenga kuwatanabahisha kuwa safari yenyewe ina changamoto tele kabla wafikie lengo lao

la kujikomboa. Mifano ya changamoto ni ugumu wa safari, njia yenye miiba, misitu na

wanyama mwitu na bahari pana yenye mawimbi makali. Pia analenga kuwakumbusha kuwa

wanafaa kutia bidii na makundi yote kuungana ili kumshinda adui yao anayepinga kufaulu kwa

juhudi zao.

Ujumbe tunaopata katika shairi ni chanya. Ni kuwa juhudi za kujikomboa hasa kisiasa (kwa

kutaja bendera) sio rahisi kwani ni safari ngumu na ndefu yenye changamoto tele na hata

upinzani mkali. Juhudi hizo huhitaji watu kujitoa, kuwa na lengo maalumu la kujua wanakoenda

(mlima ule) na hata kutia bidii. Aidha kwahitajika ushirikiano wa makundi yote ya wanajamii

kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Falsafa ya mshairi hapa ni kuwahimiza wanajamii kuwa kupata ukombozi au uhuru sio mchezo.

Ni safari ndefu yenye changamoto, matatizo na upinzani mkali. Kwa sababu hiyo, swala zima

haliwezi kufaulu bila bidii, ushirikiano na hata azma yenyewe ya kufaulu hatimaye. Kwa mantiki

ya nadharia ya uamilifu, Abdilatif anasifika sana kama mshairi mwenye maono yaliyokuwa

mwafaka kwa taifa la Kenya katika muktadha wake wa kiwakati kwani ilikuwa miaka michache

sana baada ya uhuru. Kwa maoni yake, aliona uhuru wa pili ambao ulikumbwa na dhuluma na

upinzani anaozungumzia katika shairi lake. Kwa sababu hiyo kulihitajika juhudi kabambe za

wanajamii wote ili kufaulu. Twaweza kukubali kuwa changamoto zilizokumba nchi ya Kenya

Page 77: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

68

baada ya uhuru kama vile kisiasa, kiuchumi na hata kijamii hazikuwa rahisi kutatua na hata

hazingetandarukiwa na watu wachache kwani mkono mmoja haulei mwana.

Maudhui ya ukombozi yanazidi kuzungumziwa katika shairi la ‘Mamaeta Afrika’. Nafsineni

anasema kuwa baada ya bara Afrika kunyang’anywa mali na kukosa mtu wa kulitetea, Waafrika

walijitokeza kulilia bara lao. Wakati huo, ingawa walikuwa dhaifu na kuanguka chini

waliposukumwa, walisimama na kuwatia wakoloni mbaroni hadi kuwashinda. Ubeti wa kumi na

tatu unathibitisha hayo kama ilivyoonyeshwa hapa chini:

Kwani siku hizo mama, twali dhaifu yakini

Mtu akitusukuma, twali kianguka tini

Sisi nao kusimama, na kuwatiya mbaroni

Ikawa haimkini, sisi kuwashinda mama

(Sauti ya Dhiki, uk. 37)

Wakoloni walipogundua mambo yaliwaendea vibaya walianza kutumia mbinu mpya ya kuvunja

juhudi za mapambano. Wakaanza kuwatenganisha Waafrika ili umoja wao ukiondoka waendelee

kuwanyanyasa. Hapo ndipo kuliwekwa mipaka ya maeneo na hata kutenganisha koo.

Kulitokea vita vya kumfukuza mkoloni. Taabu ilipozidi, Waafrika waliamua kuwaondoa kwa

njia ya silaha. Ingawa walikuwa mbalimbali na kila ukoo kivyake, wote kutoka pembe zote

walikaribiana, watoto kwa wazee wakaingia vitani. Kufa kupona walipambana hadi kukata

minyororo ya utumwa na Afrika ikawa huru. Hata hivyo damu nyingi ya Waafrika ilimwagika na

wengi kuaga dunia. Rasilimali nyingi pia zilitumika. Uhuru ulipatikana hatimaye. Walimshinda

adui hadi akalazimika kutoka. Kwa kuwa na tamaa ya kuendelea kuidhuru Afrika mkoloni

nusura adinde kuondoka. Licha ya uhuru kupatikana, mshairi anadokeza kuwa kuna maeneo au

mataifa ambayo wakati huo yalibaki utumwani. Mifano ni maeneo ya Afrika Kusini. Msumbiji,

Zimbabwe, Angola na Guinea- Bisau. Nafsineni anasema kuna matumaini yao pia kuwa huru

kutokana na mapigano kuendelea na kuungana kujitoa mhanga kwa lengo moja la kuwashinda

wakoloni hao.

Page 78: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

69

Baada ya hapo, ukombozi ukafuatwa na majuto. Adui alipoona chakula kitamu kishamtoka

kinywani, alichanganyikiwa akakosa la kufanya ndipo akafikiri jinsi ya kukirudisha kwake. Hata

hufikiria kurudi ingawa huogopa mapambano. Ikiwa ni kuja mwenyewe au kutuma wanawe, ajua

kuwa hilo haliwezekani kamwe. Waafrika sasa hivi wanalinda bara lao usiku na mchana lisije

tawaliwa tena na wakoloni.

Mwisho kuhusiana na maudhui ni kuwa katika shairi la ‘kichu hakiwi ni uchu’ kunaonekana

maudhui ya fahari. Nafsineni anajivunia uwezo wake wa utunzi `wa mashairi kwa lahaja ya

Kimvita. Anageuza Kiswahili cha kigunya alichobambanya alivyoweza kuanzia ubeti. Kutokana

na ubahili, matajiri huibana mali yenyewe zaidi. Ile jazanda ya ndovu inafaa sana hapa. Nadharia

nazo zimezingatiwa ifaavyo. Kuhusiana na umuundo ni kuwa ujumbe katika mashairi haya

umehakikiwa kama ulivyo na likiwa swala la kifasihi. Chochote nje ya mashairi husika

hakikutiliwa maanani. Katika utafiti, ujumbe wa matini ndio uliozingatiwa katika uhakiki

wenyewe. Kuhakiki vijenzi vya Wahusika, ufundi wa lugha, muundo na maudhui kumeonekana

kuwa toshelevu katika kueleza mada inayohusika. Hii ni kwa sababu vipengele vyote vinavyofaa

kuchunguzwa kulenga uhakiki wa mashairi vinaeleweka. Mada nzima ilizingatia mashairi hayo

zaidi kuliko mtunzi au ulimwengu yalimochotwa.

Kwa misingi ya uamilifu ni kuwa kila shairi hapa limejengwa kwa vipengele hivi vinne ambavyo

ni muhimu sana na hata kimoja kikiondolewa hakutakuwa na shairi. Kazi ya wahusika kwa

mfano ni kupitisha maudhui pamoja na dhamira ya mashairi husika. Muundo wa mashairi

unawezesha kila wazo kupitishwa katika ubeti wake na vina na vibwagizo kudumisha mapigo

yafaayo ili kuivutia hadhira. Ufundi wa lugha katika mashairi nao ni njia ya kupitisha baadhi ya

maudhui kwa njia fiche na ufundi mwingine ukionyesha uwezo wa mshairi katika utunzi. Lugha

kama hiyo pia inaleta mvuto kwa hadhira kiwango kwamba kuelewa anacholenga mshairi

kunafaulu kirahisi. Kupitia maudhui aliyobuni mshairi ndipo tunaelewa msimamo wake na hata

falsafa yake kwa maswala hayo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa.

Page 79: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

70

SURA YA TANO

MUHTASARI,HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.1 Utangulizi

Katika sura hii, mtafiti amejishughulisha na muhtasari wa matokeo ya utafiti kama yalivyoibuka

katika mashairi yaliyoteuliwa toka kwa diwani ya Sauti ya Dhiki. Vilevile, mtafiti ameangazia

manufaa ya utafiti huu na hali kadhalika matatizo yaliyokumba uhakiki pamoja na mapendekezo

ya utafiti zaidi. Kumetolewa mukhtasari wa kazi nzima kuanzia madhumuni, njia ya utafiti na

matokeo. Lengo ni kuonyesha uwiano au utofauti na maoni ya wataalamu mbalimbali

inapolazimu. Mfuatano wa vipengele vyote vilivyolengwa katika madhumuni umezingatiwa.

Mapendekezo pamoja na hitimisho ya mada husika yametolewa. Pengo la utafiti zaidi kulenga

mada husika au hata mahali pa utafiti limeonyeshwa hapa na pale inapolazimu.

5.2 Muhtasari wa Matokeo

Sehemu hii inatoa matokeo ya utafiti huu kwa kifupi kwa kuegemea madhumuni manne ya

uhakiki wa fani na maudhui katika mashairi ya diwani ya Sauti ya Dhiki. Madhumuni ya kwanza

ilihusu kutathmini jinsi malenga alivyotumia wahusika katika mashairi hayo, ya pili ikihusu

kuchambua ufundi wa lugha. Ya tatu ilihusu kuhakiki muundo na ya mwisho kufafanua

maudhui yaliyozuliwa na fani katika mashairi hayo teule.

5.2.1 Kutathmini Malenga alivyotumia Wahusika

Katika kuangazia madhumuni ya kwanza kuhusu malenga alivyotumia wahusika katika mashairi

teule ya Sauti ya Dhiki, ilibainika kuwa katika mashairi hayo kuna wahusika. Mifano ni nafsineni

na nafsinenewa. Kukabainika sifa za wahusika hao kuwa hasi na nyingine chanya. Pia

kukabainika mhusika zaidi ambaye ni Mwenyezi Mungu lakini sifa zake zikiwa chanya pekee.

Hata hivyo,hakukuonekana kitu chochote kisicho uhai ambacho kimetumiwa na malenga kama

mhusika wa shairi lolote. Pia mshairi hakuonekana kusemewa maneno aliyofaa kusema na mtu

mwingine. Ni bayana kuwa kila shairi lilionekana kuwa na wahusika. Shairi la ‘Ukamilifu wa

mja’ kwa mfano lina wahusika kama nafsineni, binadamu(waja) na Mwenyezi Mungu. Wahusika

hawa wametajwa kwa njia waziwazi katika shairi husika. Lile la ‘Mja si mwema’ pia lina

nafsineni, mja na walimwengu wanaozungumziwa. Katika mashairi haya mawili, wahusika hawa

Page 80: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

71

ni muhimu sana na ni lazima wawepo ili ujumbe wa mshairi ufikie na kunata hadhira ifaavyo.

Ikiwa tunaweza kukubali maoni ya Ansani, hali ingekuwa hata potovu zaidi katika shairi la

‘Kutendana’. Wahusika wa shairi hili ni mwanamke na mwanaume ambao wanazungumza kwa

njia ya waziwazi na ambao sifa zao ni bayana. Ikiwa wahusika kama hawa si muhimu, basi

haitakuwa tofauti na kulitupilia mbali shairi zima. Hapa pia, hakuna kitu chochote kisicho hai

ambacho kimetumika kuwakilisha wahusika. Utafiti huu kwa hivyo umefaulu kuchukua

mwelekeo unaokinzana na yale maoni ya Kisia na Mwarandani pamoja na ya Ansani.

Kwa kulinganisha na mashairi ya Robert Frost, kuna mfanano na baadhi ya mashairi ya Abdilatif

Abdalla ingawa sio katika kikundi hiki cha mashairi yanayolenga wahusika. Mfano wa shairi

linaloonyesha mshairi mwenyewe akizungumza ni lile la ‘N’sharudi’. Hata hivyo, huyu ni

mshairi mwenyewe anayezungumza katika nafsi ya kwanza bali si watu wengine waliopewa

nafasi hiyo.

Zaidi ya hoja hizi, katika shairi la ‘Mja si mwema’ nafsineni anaonekana kutumia au

kuzungumza na sehemu ya mwili, yaani mkono wake akiutaka kuandika yaliyomsababishia

majuto. Kutumia sehemu ya mwili kama mhusika kwa kunena nayo kama binadamu ni jambo

ambalo halionekani mara nyingi katika mashairi na hata wataalamu waliotafitia wahusika wa

ushairi hawakutaja aina hiyo ya uhusika. Sababu ya nafsineni kuzungumza na mkono wake ni

kuwa amebaki kujiamini yeye tu baada ya waja wenzake kumponza na hata kutoaminika. Hali

kama hii inaoana na mashairi ya Robert Frost ambaye anaonekana kupambana na hali

tofautitofauti katika hisia zake. Hata Abdilatif hapa si tofauti kwani kuzungumza na mkono wake

ni sawa na kuzungumza na hisia zake mwenyewe (uzungumzi nafsia) kwani hapati mja

mwaminifu wa kuzungumza naye wakafaana.

Katika madhumuni haya ya kutathmini jinsi mtunzi alivyotumia wahusika katika mashairi yake,

kumebainika wahusika wa aina mbalimbali ikiwemo wa kike na kiume pamoja na Mwenyezi

Mungu. Wahusika wote wamefafanuliwa sifa zao barabara hivyo basi kueleweka kukawa rahisi

kwa hadhira. Wamepitisha ujumbe unaokaribiana na hali halisi ya maisha katika jumuiya jambo

linalofanya mashairi haya kuwa faafu katika kuiadilisha jamii inavyofaa.

Page 81: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

72

5.2.2 Kuchambua Ufundi wa Lugha au Tamathali za Usemi katika Mashairi teule ya Sauti

ya Dhiki

Kuhusiana na mukhtasari kulenga tamathali za usemi na mbinu za lugha ni kuwa mashairi

yaliyohakikiwa yametumia mbinu mbalimbali za lugha ambazo zilibainika katika uhakiki huo.

Maoni ya Ngure (2014), kuwa fasihi bora yafaa kuwa sanaa inayotumia lugha ili kueleza maisha

na tajriba ya binadamu katika mazingira na utangamano na wenzake na hata kutuchorea taswira

ya uhalisia wa maisha ni jambo linalobainika baada ya kuhakiki mashairi katika sehemu hii.

Katika shairi la ‘N’shishiyelo ni lilo’ kwa mfano lugha imesukwa kwa kutumia tamathali kadha

za usemi hali inayosababisha hata hadhira kumhurumia nafsineni kwa yaliyompata. Akasema

ukweli ndipo akatiwa jela ili asirudi kusema ukweli huo tena. Nafsineni akapata yasiyoridhisha

kamwe swala zima likilenga ukweli wa maisha ya kila siku.

Mtaalamu huyo (Ngure) anaposema kuwa kutosheka tunakopata tusomapo kazi ya fasihi

kunatokana na ufinyanzi wa lugha teule au umbuji ni mawazo yanayokubalika na kudhihirika

waziwazi katika matokeo ya utafiti huu. Mtunzi wa ‘N’shishiyelo ni lilo’ amethibitisha mawazo

haya ya Ngure kwa kutumia ufundi wa urejeshi, istiara, kinaya , balagha, tashihisi na utohozi.

Mawazo haya pamoja na ya Senkoro yanapata mashiko katika uhakiki wa shairi hili. Ufundi na

tamathali hizi zote za usemi umeweza kulipamba shairi hili kikamilifu na hata kulipa nguvu ya

kufundisha na kuzindua jumuiya inayolengwa.

Swala moja ambalo ni bayana na mbalo watafiti waliotangulia kuhakiki diwani ya ‘Sauti ya

Dhiki’ hawakusisitiza ni lile la kibali cha kishairi. Hili limetiliwa maanani sana katika utafiti huu.

Uhakiki huu umebainisha waziwazi kuwa Abdilatif’ ametumia uhuru wa maneno ya kikale,

inkisari, tabdila, maneno ya kigeni, utohozi, kilahaja, mazida na hata kuboronga sarufi kwa

kiwango cha kupigiwa mfano. Matumizi ya uhuru wa kishairi ni mtindo ulio na mueneo kwa

wingi katika mashairi haya matatu. Inaonekana kana kwamba malenga ameegemea zaidi katika

uhuru kama huu au anaupenda sana. Matokeo yake ni kuwa ushairi wenyewe unaelekea kuwa na

mguso kwa mfano wa lahaja ya mshairi yaani Kimvita. Pia unasaidia kudumisha siri ya kishairi.

Mashairi yote yaliyohakikiwa katika madhumuni haya ya pili yananuia kuonyesha mgogoro wa

swala nyeti la kisiasa ambalo kama mshairi asingelitunga fumbo la jazanda na hata kutumia

uhuru kama huu wa kishairi, swala hilo lingemponza hata zaidi. Kwa njia isiyo ya moja kwa

Page 82: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

73

moja kwa hivyo, akaamua kutoa ujumbe kwa hadhira iliyojumuisha hata wale watawala

waliomhangaisha.

5.2.3 Kuhakiki Muundo wa Mashairi teule katika diwani

Kuhusu uhakiki wa muundo, mashairi yaliyohakikiwa yameonyesha ukaribiano wa muundo japo

yana tofauti za hapa na pale. Uhakiki wa shairi la ‘Siwati’ umeonyesha limebuniwa kwa beti nne

zenye mpangilio wa mishororo unaolingana. Licha ya kuwa kila ubeti una ujumbe wake,

kibwagizo kimetumiwa kila mwisho wa ubeti jambo ambalo linasababisha muumano ufaao wa

beti hizo nne. Kuna muungano wa ubeti hadi ubeti.

Abdilatif’ kwa kutunga shairi hili la tarbia amethibitisha kuwa mashairi ya tarbia na mizani kumi

na sita kila mshororo yamestawishwa sana. Hata hivyo shairi hili limethibisha kuwa mashairi

mapokeo hayawi na urari wa vina na mizani pekee lakini ule wa vina waweza kuwa katika ubeti

mmojammoja kivyake kama ilivyo kwa shairi hili la ‘Siwati; kuna mguso wa kiusikivu japo kwa

kiwango fulani tu.

Uhakiki wa muundo tu katika shairi vilevile umeweza kupinga mawazo ya Quinn (1992:11)

kuwa mhakiki akitenga muundo na maudhui kwa azma ya uhakiki, ushairi huo hutawanyika kwa

mawazo yetu mpaka tutakapouunganisha tena upya. Imegundulika kauli hii ni potovu kwa kuwa

uhakiki wa shairi lolote lile utategemea lengo la mhakiki husika. Ikiwa lengo hilo ni kuhakiki

muundo peke yake basi jambo hilo litafanyika bila tashwishi. Haya ndiyo yalifanyika katika

shairi hili. Mawazo ya William pia yamepingana na uhakiki wa shairi hili. Alisema kuwa

muundo uliozoewa na wasomaji na wasikilizaji wa mashairi toka jadi ni ule wa mistari minne

kila ubeti na silabi zikiwa kumi na sita au nane nane kila kipande na vina vyenye utaratibu wa:

a b

a b

a b

b a

Yapingwa maoni haya baada ya kuhakiki shairi hilo la ‘Siwati’ kwa kusema kuwa mashairi

mengi kama hili lilivyo huweza kuwa na ukwapi wenye mizani nane, utao mizani tatu na

mwandamizi tano, yaani 8, 3, 5. Hali hii ni bayana katika ubeti wa kwanza mshororo wa tatu.

Page 83: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

74

Zaidi ya hayo, wanamapokeo kama Muyaka Bin Hajji, shaaban Robert, Mathias Mnyampala na

Mwalimu Hassan Mbega waliposema kuwa ushairi wa Kiswahili ni tarbia yenye umbo la mizani

nane katika ukwapi na nane katika utao ni jambo ambalo utafiti huu umeonyesha kuwa si la

lazima. Massamba anashikilia msimamo huohuo kuwa utungo ufaao kuitwa shairi ni lazima uwe

na ulinganifu wa vina na mizani katika beti.

Katika uhakiki wa muundo uliofanywa hapa, Abdilatif’, licha ya kuathiriwa na washairi hao

waliotajwa ameonyesha kwamba vina vya kati vyaweza fanana katika ubeti mmoja lakini

kutofautiana na beti zinginezo za shairi lilo hilo. Hali hii ni kweli katika shairi la ‘Siwati’ kwani

ni tofauti kutoka ubeti mmoja hadi mwingine. Kuhusiana na mizaniyasisitizwa kuwa arudhi ya

mizani sawa katika ukwapi na utao (8a, 8b) nayo ni sheria isiyokuwa ya lazima hasa katika kila

ubeti. Katika muktadha wa uhakiki huu wa muundo, Abdilatif amezingatia mizani chache katika

baadhi ya mishororo hasa anapozungumzia swala nyeti katika ujumbe mzima wa shairi lake

husika. Mfano ni katika shairi la ‘Siwati’ ubeti wa mwisho mshororo wa mwisho mshairi

anapotamatisha shairi kwa dua kwa Mwenyezi Mungu. Hapa anatumia mizani kumi na saba

kutofautisha na mishororo mingine ya shairi iliyozingatia mizani kumi na nane kila mmoja.

Mifano mingine ni katika shairi la ‘Leo ‘N’singekuwako’ mshairi alipotunga kwa mizani kumi

na sita kila mshororo lakini kumi na tano katika ubeti wa tatu mshororo wa tatu anaposema, ‘Na

taabu haondokewa, ‘ngenijiya niliko?’ Licha ya kuwa mshairi bado yu hai, anataja kifo chake

ambacho ni swala nyeti hivyo kutofautisha ujumbe huo na ule wa mishororo mingine katika beti

zote. Kuna mfano pia wa ubeti wa nne mshororo wa kwanza anaporejelea namna ambavyo

angeliliwa na jamaa zake ikiwa angeaga dunia. Sababu ya kutaja haya yote ni kuwa inapingwa

maoni ya wataalamu wa kimapokeo waliotajwa katika utafiti huu kwa kusisitiza kuwa ufundi wa

muundo wa shairi utategemea jambo analorejelea mshairi fulani maalumu.

5.2.4 Kufafanua Maudhui katika Mashairi Yaliyoteuliwa

Mukhtasari wa mwisho ni kuhusiana na maudhui ya mashairi ‘Wasafiri tuamkeni’, ‘Kichu

hakiwi na uchu’ na ‘Mamaetu Afrika’, katika uhakiki wa maudhui ya kisiasa, ya kijamii na

kiuchumi katika mashairi husika. Mifano ya maudhui ni dhuluma za wakoloni kwa Waafrika,

uporaji wa mali ya umma, kiburi na mengineyo mengi.

Page 84: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

75

Katika shairi la ‘Wasafiri tuamkeni’ kwa mfano, nafsineni ana falsafa kuwa mapambano yoyote

ya kisiasa si lelemama. Anayalinganisha na safari kwa kuwa huenda yasichukue muda mfupi.

Mapambano yao yalihitaji kujitahidi na hata kuondoa hofu. Aidha, mshairi anaamini kuwa licha

ya jumuiya yake kupata uhuru wa bendera (wa kisiasa) bado wanahitaji kujikomboa kutoka kwa

madhalimu wa leo hii. Hadhira wasipotahadhari huenda wakadungwa na miiba yenye sumu au

hata kuumizwa na wanyama wa mwitu. Changamoto zote alizotaja mshairi ikiwemo kuikabili

bahari, urefu wa safari na zinginezo zingekabiliwa kwa ushirikiano wa wanajamii wote, watoto

kwa wazee. Katika ‘kichu hakiwi ni uchu’ nalo, nafsineni anasisitiza kuwa kamwe haiwezekani

utu wa mtu katika jamii ukipimwa kwa uwezo wake wa kiuchumi bali kwa utu wake wa kuwafaa

na kuwasaidia wenzake anaoishi nao. Hii ndiyo maana kamili ya utu. Katika shairi la ‘Mamaetu

Afrika,’ anaendelea kukumbusha hadhira kuwa bara lilikuwa na uwezo wa rasilimali kabla ya

kuporwa na wakoloni na hivyo kuwahimiza Waafrika wasikubali kudhulumiwa tena hata kama

uozo huo utafanywa na Waafrika wenzao walio na nia mbaya kwa bara.

Katika mashairi haya, mtunzi amefaulu kujumuisha mseto wa vipengele vya muundo kama vile

beti, mishororo minne kila ubeti, ukwapi, utao, mkarara pamoja na vina vya mwisho

vinavyotiririka kuzungumzia maudhui yenye mchomo, mnato na hata ushawishi mzito kwa

hadhira. Wanajamii wasiojua hali ilivyokuwa kwa mfano au hata nafasi yao katika juhudi nzima

za ukombozi wa kisiasa wanapata fursa nzuri kupitia mashairi haya.

5.2 Hitimisho

Hitimisho katika sehemu hii limefanywa kwa kufungamana na madhumuni ya utafiti. Kwa

kulenga wahusika, inakaziwa kuwa uhakiki kama huu una nafasi ya kutegemewa kuhakiki

uhusika katika mashairi mengine ya Abdilatif’ Abdalla na hata washairi tofauti ikiwa ni pamoja

na kupinga kikamilifu maoni ya wataalamu wanaoshikilia kuwa wahusika katika ushairi hawana

umuhimu mkubwa. Kwa maoni haya, yasisitizwa kuwa uhusika ni uti wa mgongo wa shairi

kama ilivyo kwa tamthilia, riwaya na hadithi fupi na hata kwa tungo za fasihi simulizi.

Katika muundo, mshairi amezingatia zaidi umbo la tarbia, ukwapi na utao na pia mpangilio wa

vina vya kati na nje uliokaribia kufanana katika mashairi yote yaliyohakikiwa na hata idadi ya

Page 85: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

76

mizani kumi na sita kila mshororo. Hata hivyo, katika shairi la ‘Mja si mwema’, ametumia

ukwapi, utao na mwandamizi. Ieleweke kwamba muundo huu wa tarbia kutamalaki si hoja

kwani ufundi wake wa lugha unadumisha ujumi wa kutamanika katika mashairi yote husika. Pia

maudhui anayolenga ni tofautitofauti jambo ambalo linazidisha mvuto wa hadhira kwa mashairi

yote. Mafunzo au maadili nayo ni kemkem kutoka shairi moja hadi jingine.

Mshairi huyu vilevile anaonekana kufuata nyayo za washairi wenzake wa jadi ambao kwa

kiwango kikubwa walibuni mashairi yenye umbo kama lake. Kwa tathmini ya jumla ya washairi

kama mwalimu Sikujua, Suud bin Said al-Mamiry, Muyaka bin Hajji, Shaaban Robert na

Mathias Mnyampala, washairi hawa isipokuwa Shaaban Robert wamezingatia tarbia kikamilifu

katika mashairi yao. Mfano ni yale mashairi ya Muyaka ambayo umbo lake ni lile moja tu la

tarbia katika mashairi yote. Mnyampala vilevile katika Diwani ya Mnyampala amezingatia umbo

lilo hilo katika mashairi yake yote.

Zaidi ya hayo, ufundi wa kilahaja waonekana kudumishwa sana katika mashairi yote jambo

ambalo laweka ukweli bayana kuwa mshairi huyu athamini lugha ya kwao sana. Pia anaonekana

kuzingatia na hata kuutawala uhuru wake wa kishairi kwani kwa mashairi yake yote

yaliyohakikiwa na hata yaliyobaki, ni nadra kukosa mazida, inkisari, tabdila, kubananga sarufi na

hata maneno ya kale. Mshairi ametumia kibali chake hicho barabara katika mashairi hayo

yaliyolengwa kuhakiki matumizi ya lugha. Abdilatif’ ametumia maneno ya kigeni kwa uchache

sana katika mashairi hayo. Hata yale aliyotumia ni yenye chimbuko katika dini yake ya

Kiislamu. Hata mafunzo / maadili mengi anayotoa Abdilatif yamefungamana na mafunzo ya

Kiislamu. Hata hivyo, kule kurudia neon ‘Mungu’ kila wakati katika mashairi haya

hakukuchangiwa tu na imani ya dini pekee bali pia na msongo na matatizo aliyopata jela

ikiwemo kunyimwa vitabu vyote akaruhusiwa kurani na shashi tu.

Lugha inayotumiwa katika mashairi yote yaliyohakikiwa ni Kiswahili na inaeleweka kwa

wasomi wa lugha hii katika viwango mbalimbali. Uasilia wake ni wa kupigiwa mfano hasa kwa

Abdilatif’ kutumia lahaja ya kwao nyumbani. Ujumbe huu unaifikia na hata kuinata hadhira

barabara hasa kuhusiana na ujumbe unaofaa kupokelewa kwa njia ya moja kwa moja.

Panapoonekana kuwa na utata tu ni katika shairi la ‘kutendana’ kwa sababu kuwa swala zima

pale ni mvutano wa kijamii (wa mume na mke) pamoja na tabia mbovu za mume. Kwa kawaida

Page 86: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

77

swala hili halisemwi kwa njia ya hadharani kikamilifu. Hata njia kama hii ya kutunga shairi

inadumisha adabu na heshima kwani mambo yote hayasemekani waziwazi. Ingawa kwa tathmini

ya ubora wa shairi, shairi lenyewe ladumisha siri ya kishairi, mshairi/ nafsineni kusema ‘nyege ni

kunyegezana’ inaonekana kama ukosefu wa adabu au maadili hasa kwa wanajamii wenye umri

mdogo kama vile watoto.

Yasisitizwa zaidi kuwa mashairi haya ya Abdilatif’ ni ya kiwango cha kutajika kwani amefaulu

kuepuka lugha ya Kiingereza katika mashairi yake yote au hata kuonyesha uchanganyaji wa

lugha kwa kiwango cha kukinaisha. Mchango wake kwa hivyo katika fasihi ya Kiswahili ni wa

kutajika na wa kustahili wasomi kuhamasishwa kumuiga inapowezekana. Mshairi huyu, sawa na

Muyaka, Ali koti, Seyyid Omar bin Amir Zaid, Mngumi na Mwego Athumani waliohamisha

ushairi kutoka msikitini hadi sokoni, naye amezingatia au kutungia maswala kadha ya kijamii,

kiuchumi na kisiasa badala ya kidini peke yake.

Kuhusiana na maudhui, Abdilatif kwa upande mwingine ameangazia matatizo ya bara la Afrika

hasa kuhusiana na mapambano na wabeberu wa kikoloni waliotawala maeneo mbalimbali ya

bara hili. Anazungumzia tatizo la ukoloni mamboleo pamoja na juhudi zinazolazimu kufanywa

ili kupambana na tatizo hili. Haya yamezingatiwa katika shairi la ‘Mamaetu Afrika’ huku akitaja

kinachofaa kufanywa na wazalendo wa kiafrika ili kuzuia wakoloni kurudisha dhuluma hata

baada ya wao kuondoka.

Hapa imedokezwa kuwa mshairi ametoa mchango muhimu sana katika mashairi yake haya.

Amefaulu kuwakilisha ukweli wa maisha ya watu ambao amewazungumzia katika mashairi

haya. Ujumbe katika mashairi kama vile ‘Ukamilifu wa mja’ ‘Mamaetu Afrika’ ‘Mja si mwema’

na hata ‘Kichu hakiwi ni uchu’ una nguvu na uwezo wa kuleta mapinduzi katika maisha na fikra

za watu kwa faida yao wote.

Kwa upande wa nadharia zilizoongoza utafiti huu, ni bayana kuwa kuhusiana na umuundo,

vipashio vyote vya muundo wa mashairi haya vimeunganishwa kwa njia yenye mvuto wa

kutosha na hata muwala unaokubalika katika ushairi wa kimapokeo. Utendaji kazi wa kila

Page 87: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

78

kipashio nao kwa kuhusisha na nadharia ya uamilifu ni mwafaka kwani kila mojawapo

chaonekana kutekeleza jukumu lake barabara.

Kwa upande wa pili, inasisitizwa kuwa hakuna kizuri kisicho na ila kwani si kila alichofanya

Abdilatif katika mashairi haya kinachoweza kusemekana kuwa cha kiwango tambulika. Ni

bayana kwa mfano kuwa shairi lake la ‘Kutendana’ ni refu na lenye beti nyingi zaidi kiwango

kwamba urefu huo unaathiri kueleweka kwa shairi lenyewe na hata ufaafu wake katika kupitisha

maadili kwa njia ya waziwazi.

Hata kama shairi lenyewe linaangazia kuzinduka kwa mwanamke hadi kutetea haki zake, shairi

kama hili lingeandikwa kwa beti chache kuliko hali ilivyo hapa ili ujumbe kama huo hata uifae

jamii / hadhira lengwa kwa mguso zaidi. Mshairi pia ameruhusu mhusika mmoja kutawala beti

nyingi zaidi hata kabla ya mwenzake kutoa ujumbe wake. Hali kama hii inamzuia msomaji

kufuata muwala wa kadhia nzima kutoka kwa beti zilizotangulia.

Katika shairi la ‘Mja si mwema’ nalo, mshairi ametilia chuku sifa za mja kwa kusema kuwa ni

mja mmoja tu kwa mia asiye mbaya kundini. Jambo hili linakosolewa kwa kuwa ni mshairi

mwenyewe aliyejiponza kwa kuamini ‘mja’ bila uangalifu. Afaa kujilaumu badala ya

kuwalaumu waja wote na pia asisahau kuwa baniani mbaya kiatu chake dawa. Waja wote

hawawezi kuwa wabaya kiwango anachozungumzia mshairi huyu. Hata hivyo, shairi hili ni

muhimu sana katika kutoa elimu kwa vijana au watoto ambao watarajiwa kuwachuja watu wa

kutangamana nao kwani baadhi waweza kuwachafua tabia. Hawafai kungojea hadi wahasirike

kisha wajute kama alivyofanya mshairi.

Katika shairi la ‘Ukamilifu wa mja’ nalo sifa za mja zimewekwa bayana kikamilifu yaani upande

wake mzuri na mbaya. Jambo hili nalo latuwezesha kufahamu tunachofaa kutarajia katika

uhalisia wa maisha yaani kutarajia mazuri na hata mabaya kwa mja. Kule kulinganisha sifa hizi

na za Mungu nako kunampa mja matumaini kuwa inawezekana kuiga sifa nzuri kwa Muumba.

Hata kwa muundo, mshairi ameonyesha udhaifu wa kutegemea tarbia katika mashairi yote ikiwa

kwaweza kuwa na miundo zaidi. Hata hivyo, uhakiki wa mashairi umebaini kuwa yana mseto wa

Page 88: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

79

mawaidha, maswala ya dini, siasa, historia, uvumilivu na hata utamaduni. Kwa upande wa

ufundi hasa bahari za mashairi haya ni chache sana. Imekuwa nadra kuonekana pindu, msuko na

hata mtiririko. Pia katika baadhi ya mashairi, isipokuwa kwa kutumia kilahaja, ujumbe

unaeleweka kwa njia rahisi zaidi kuliko katika mashairi ya watunzi kama Muyaka au hata

Shaaban Robert. Sehemu hii yahitimishwa kwa kusema kwamba mtafiti yeyote wa ushairi ako

huru kuzamia mada kama vile matumizi ya fasihi simulizi katika fasihi andishi hata akilenga

sampuli zizi hizi za mashairi zilizohakikiwa hapa.

5.3 Mapendekezo

Baada ya matokeo na mukhtasari wa utafiti huu, kwanza inapendekezwa watafiti kulenga

kipengele cha uhusika katika mashairi. Pengo linalobaki baada ya kuhakiki uhusika katika

tasnifu hii ni kuwa kuna mashairi yaliyobaki katika diwani ya ‘Sauti ya Dhiki’ bila kuhakikiwa

kipengele hiki. Hata yale yaliyolenga vipengele tofauti kama lugha, muundo na maudhui

yanaweza hakikiwa baadaye yakilenga kipengele hiki hiki cha uhusika.

Zaidi ya mapendekezo hayo, kuhusiana na madhumuni ya kuhakiki tamathali za usemi au mbinu

za lugha, kwatolewa mwanya wa utafiti na hata uhakiki zaidi katika mashairi yayo hayo

yaliyohakikiwa mradi utafiti kama huo unuie kuhakiki maudhui, muundo au swala jingine lolote

bora lisiwe lililohakikiwa katika tasnifu hii. Watafiti zaidi wanaweza pia kuhakiki mashairi ya

diwani husika wakilenga ufundi wa lugha na hata uhuru wa kishairi. Hayo nayo yawe ni mashairi

yaliyobaki bila kuhakikiwa katika utafiti huu.

Hata kulenga maudhui, mashairi yaliyolengwa katika sehemu hiyo au mengineyo katika diwani

husika yanaweza hakikiwa ingawa kwa sharti moja kwamba uhakiki kama huo utachukua

mkabala tofauti na umuundo au uamilifu na hata ikiwezekana mada tofauti.

Page 89: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

80

MAREJELEO

Abdalla, A. (1973). Sauti ya Dhiki. Nairobi : Oxford University Press.

Abdulaziz, M. H. (1979). Muyaka, 19th Century Swahili Popular Poetry. Nairobi: Kenya

Literature Bureau.

Ahmed, N. (1997). Mwangaza Wa Kiswahili. Nairobi-Kampala: East African Educational

Publishers.

Alembi, E. B. (1999). Understanding Poetry.Nairobi: Acacia Stantex Publishers.

Amana, B. (1971). Malenga wa Vumba. New York: Oxford University Press.

Davin ,D. and Wamuhu ,P. (1989). Enjoying Poetry. London: Macmillan Press Limited.

Emenyonu, E.N (edt). (2006). New directions in African literature. Nigeria PLC Ibadan:

Heinemann educational books.

Farouk, M. T (Mh). (1971). Uchambuzi wa Maandishi ya Kiswahili. New York: Oxford

University Press.

_____(1977). Uchambuzi wa Maandishi ya Kiswahili. London: Oxford University Press.

Freadman & Miller. (1992). Re-thinking theory. Cambridge University Press.

Glazer,M.(1996).’’Functionalism’’www.utpa.edu/faculty/mglazer/Theory/fuctionalism.htm-

06.02.2012-9.10am

Glencoe. (1976) . Literrature: The readers choice. U.S.A: MC Graw Hill.

Page 90: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

81

Gromov, M. D. (2006). “The question of Kiswahili Style Again?’’ The Poetry of Kithaka Wa

Mberia in Kiswahili: Jarida La Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Juz 69: 109 – 126.

Holman, H, Harmon, W. (5th Edition). (1986). Ahandbook to literature. U.S.A: Macmillan

Publishing Company.

HURIA, (2007). Journal of the Open University of Tanzania, Volume II, No.2, Dar es Salaam.

Indende F. (2008b), Mabadiliko Katika umbo la shairi na athari zake katika ushairi wa

Kiswahili Swahili Forum Journal, 15: 73 – 94.

Jim,R.(1965).Understanding poetry. London: Heinemann.

Kenneth, Q. (1992). How literature works. The Macmillan press ltd.

Kothari, C. R. (2011), Reseach Methodology, Methods and Techniques. New Age International

Publishers.

Kuhenga, C. (1977). Tamathali za usemi. Nairobi: East African Literature Bureau.

Lauri R, Breman, P (eds). (2008). The heritage series of black poetry,1962-1975. U.S.A: Ashgate

publishing ltd.

Lawrence, A. & Brenda ,T. (2009). The literature review.U.S.A: Corwin Press.

Leitch, Vincent, B. (ed)(2010). The Norton Anthology of Theory and criticism 2nd edition. New

York: W.W. Norton and Company.

Maina, K. (2013). ‘‘Uchanganuzi wa lugha na itikadi za mamlaka ya kijinsia katika nyimbo za

harusi kutoka jamii ya Wakikuyu wilaya ya Kirinyaga.’’ Tasnifu ya M.A ya Chuo Kikuu cha

Egerton.

Page 91: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

82

Mathooko, J. M, Mathooko, F. M, Mathooko, P. M. (2007). Academic Proposal Writing: A

guide to preparing proposals for academic research, UMU Press.

Msokile, M. (1993). Misingi ya uhakiki wa fasihi. Nairobi: East African Educational Publishers.

Mugenda, O.M. na Mugenda, A.G (1999). Research methods: Quantitative and Qualitative

Approaches. Nairobi. Act Press.

Mulokozi, M. M (Mh). (1999). Tenzi tatu za kale. TUKI: Chuo Kikuu cha Dar es Salaaam.

Musa, M. & Omari, S. H. (1977). Tujifunze Mashairi. Nairobi: Macmillan Educational

Publishers Ltd.

Mwamzandi I. Y. (1996), Mbinu za kimaigizo katika tungo za Abdilatif Abdalla, M. A thesis,

Egerton University.

Mwihaki A. N. (1998), Phonetics and the stylistic appreciation of Kiswahili verses in Kiswahili:

Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili: Juz 61:74 – 78.

Njogu K. na Nganje D. K. (2006), Kiswahili kwa vyuo vya ualimu, J. K. F.

Ong’ang’o G. O. (2002), Nyota elekezi ya ushairi, Frajopa printers mall, Nairobi.

Podis A. L & Podis M. J. (1984), Writing: Invention, form and style, Scott Foreman and

Company, Glenview, Illinois.

Richards, J. C & Rodgers T. S (1986), Approaches and methods in language teaching: A

desription and analysis, Cambridge University Press.

Senkoro, F. E. M. K. (1982). Fasihi. Dar es Salaam: Press and publicity centre.

Page 92: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

83

_ (2007). Lugha na fasihi ya Kiswahili Afrika mashariki. Dar es Salaam: CHAKAMA.

Wamitila, K. W. (2003). Kichocheo cha fasihi simulizi na andishi. Nairobi: Focus Publishers

Limited.

Wamitila, K. W. (2003), Kamusi ya Fasihi, Istilahi na nadharia. Nairobi: Focus Publication Ltd.

Wanyonyi M. M. (2010), “Style and meaning in funeral oratory : The Case of Babukusu

Khuswala Kumuse”. Unpublished M. Phil Thesis, School of Arts and Social Sciences, Moi

University.

The Journal of Pan African Studies, Vol. 2, no.8, March 2009.

Rubanza, Y. I. (1997), “Dhana ya Uradidi katika Kiswahili” in Kiswahili: Jarida la Taasisi ya

Uchunguzi wa Kiswahili. Juz 59: 53 – 56.

Wisker, G. (2005). The good supervisor : Supervising postgraduate and undergraduate research

for Doctoral Theses and Dissertations,Palgrave Macmillan.

Page 93: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

84

VIAMBATISHO

KIMBATISHO A

Kutendana

MWANAMUME

Kama bure utanipa, nipa sinisimbuliye

Kama hutaki “takopa, nikulipe baadaye

Hivi sasa cha kukupa sina; kweli nikwambiye

Mtu huwa hakutupa, amfaaapo mwenziye

MWANAMKE

‘Sina’ Kila siku ‘sina’, ‘Sina’ kwako i maisha

Huna siku utanena :ninacho ‘kanirambisha?

Hiyo ‘Sina’ yako Bwana, sasa ishanichokesha

Nyege ni kunyegezana, kwangu huba zinkwisha

MWANAMUME

Nnatoka nitokako ,mwendo kiguu na ndiya

Sikujali masumbuko, ya mvua kuninyiya

Mwenzi wako nina mwako, tafadhali niridhiya

Nipa kwa hisani yako, wata kunisimbuliya

MWANAMUME

Rudi kuko utokako,siniletee udhiya

Tafutia mwako wako,ndiya ya kutoleya

Mimi ndiye jaa lako,takazo kunitupia?

Mwanamume nenda zako,sina n’takalosikia

MWANAMKE

Page 94: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

85

Laiti kwamba wajua,uhisivyo wangu moyo

Laiti ungetambua, niumiavyo mwenziyo

Kattu hungenisumbua,na kunifanyia choyo

Ndiwe wa kuiyondoa,hii dhiki niliyo nayo

Mwenziyo n’nalemewa, si dhihaka n’semayo

Sina pa kwenda itowa, hii hamu nilonayo

Na hata wewe wajuwa, kwamba sina badaliyo

Ni mgonjwa nauguwa, na dawa yangu ni hiyo

MWANAMKE

Kila mambo naelewa, yaliyo ndiyo na siyo

Si mwana wa kuhadawa, khaswa kwa unambiyayo

Japo wasema ni dawa, sikupi ngakuwa nayo

Na kama yatakuuwa, kufa kwa maradhi hayo

N’ilishakupeleleza, hata n’kakubaini

Muda pesa ukijaza, humo mwako mfukoni

Huanza kujikikimbiza,na kunigura nyumbani

Ngapita kukuuliza,uliko hujulikani

Ukisha kuzimaliza, kutolibakisha peni

Ndipo ndiya huongoza, hadi kwangu mlangoni

Na kuanza kujiliza, n’kuonee imani

Leo sitakusikiza, hata unganambiyani

MWANAMUME

Amma um’badilika , hu tena kama zamani

Waniona nadhikika hutaki kuniauni

Mwenziyo naatabika, hunionei imani

Page 95: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

86

Hufanyi hafarijika, hatowa pepo kitwani?

Waniwata nateseka, hali ni wako mwendani

Huwati hafarijika, haondosha tabu hini?

Jambo la chache dakika, bure nyonda wanikhini

Nipa nipate ondoka,nikuondokee matoni

MWANAMKE

E mtu mume ondoka, sin’etee kisirani

Hilo ambalo wataka, kwangu halipatikani

Ni bure utasumbuka, sikupi ungasemani

Usidhani ni dhihaka, nisemayo ni yakini

Usemayo ni hakika,si urongo aswilani

Ni kwa kuwa nnachoka,kukufanya mhisani

Ndipo n’kabadilika, hakutowa maanani

Mjinga ‘meerevuka,mwerevu u mashakani

Pepo aliyekushika,mimi anikhusiyani?

Kumtowa ukitaka, nenda naye kilingeni

Mimi sitashughulika, kumpunga pepo duni

Tafuta pa kumpeka, pepo wako masikini

Kwa huyo unakopeka, pesa zako mwafulani

Na leo kuko geuka, nenda akakuauni

Apate kukutunuka, akuondowe tabuni

Sikubali kusumbuka, na faida siioni

MWANAMUME

Zako sijaziafiki, jawabu za ukaidi

Page 96: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

87

Ungazijibu sichoki, na wala nyuma sirudi

Kwa sababu n’na dhiki, nami kwako sina budi

Ni kweli kwamba hutaki, au ni yako inadi?

MWANAMKE

Hata usipoafiki, huo si wangu muradi

Lako halitimiziki, leo bwana hufanidi

Mzito hutukuliki, mno n’najitahidi

Kikwelikweli sitaki, ni heri kuko urudi

MWANAMUME

Tushakaa wewe nami,kwa siku tumbi nzima

Sijainuwa ulimi,kukueneza lawama

Baya kwako silisemi, la kukuudhi mtima

Leo unani na mimi, haja yangu kuninyima?

Mwenzangu huyatizami,twalotoka nayo nyuma?

Nyuma ungeangalia, toka twalipoanzana

‘Ngekumbuka mazoweya , na wema tulotendana

Ungejua ni vibaya, kunifanyia khiyana

Mwenzako nihururumiya,si vizuri kutesana

Siku zote twalokuwa, pamoja tukiwekana

Nili sijakutunguwa, kukwelewa ewe nana

Leo n’nafunukiwa,mahaba na mimi huna

Tamaa itakuuwa, iwa na hadhari sana.

MWANAWAKE

Wajuwa yake maani,ya la wama kutendana

Page 97: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

88

Naapa n’na yakini,huyajuwi, hungenena

Lau ungeyabaini ,vilivyo haya maaana

Wallahi hungetamani, uso wako kwonekana

Fadhila ungekumbuka,hayano usingenena

Kwako mno’mesumbukoa, hayano, tena

kwa kila namna

Nikawa nakueleka, kana kwakwamba

mbwangu mwana

Hayo usingetamka, lau wajua maana

Hii kaa ukijua, kwako huba sina tena

Mizizi n’shaingowa ,hayawezi shikamana

Uwate kujisumbua, mi nawe tushatokana

Nilikuwa sina niya, nawe kukashifiyana

Kwani si yangu tabiya, maneno kutupiyana

Ni jambo nalitukiya, sipendi kuliona

Hishima kumuwekeya, kiumbe napenda

sana

Lau hungenianziya, singesubutu kunena

Kwakuwa ‘metanguliya, kunipaka baya jina

N’nakuwa sina ndiya, ela ni kujibizana

Siwezi kuvumiliya, kutukanwa nikiona

Na ambayo ‘takwambiya, sidhani waweza

kana

Kwani ni mambo sawiya, urongo ndani

hamuna

Urongo sitatumiya, kweli tupu tainena

Mwanamume huna haya, hunayo; kabisa

huna

MWANAMUME

Sikuja kukuandamiya, kwamba tuje

kuzozana

Na wala sikukujiya, tuje kuhutubiyana

Nililolifuwatiya, kitambo n’shalinena

Au unkusudiya, mwenzangu kunitukana?

MWANAMKE

Ungapandwa na hamaki, sitakuwata kuesma

Lile ambalo ni haki, kulisema ni lazima

Endaye tokoza nyuki, pana budi kumuuma?

Mwenzangu huswarifiki, si leo n’nakupima

Urongo sita tumiya,kweli tupu ‘tainena

Sikutaka kujinaki,kulipiga langu goma

Na wala sifurahiki, kukusimbuliya njema

Na kunyamaa ni dhiki, bure ’tajipa nakama

Unamtokoza nyuki, ndipo sasa akuuma

Unnitafuta baa, pasi kukuanza shari

Kwakuwa n’nakataa, haja yako kuikiri

Wasema n’natamaa, na kwamba nitahadhari

Wajuwa wajihadaa, hiliwajuwa vizuri

Page 98: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

89

Hakika linniwasha, tamshi ulotamka

Sitaweza kuipisha, ila ulonibandika

Ndipo name najibisha, japo hili sikutaka

Na unnilazimisha, ya zamani kukumbuka

Naanza kukukumbusha, kama ushaghafilika

Ni habari ’takupasha, ambazo zintendeka

Nawe ’kiweza jibisha, unalo lajibika

Au iwa kukanusha, ambalo lakanushika

Nali hijikalifisha, kwamba nipate kuweka

Hifunguwa langu kasha, kila likihitajika

Nikawa nikikulisha, pamoja na kukuvika

Vipi wanambiya kasha, tama inishika?

Nikikusitarehesha, kwa kila unachotaka

Hikupa mema maisha, upate kufurahika

Hikupa cha kukutosha, chakula na cha

kukuweka

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika?

Ulikuja unkwisha, muwili untukuja

Ulikuwa untusha, uso unsawidika

Umbo likawa latisha, kwa

kukombokakomboka

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika?

Mno ukisikitisha, kwangu miye hakuweka

Hawa hikutononesha, nawe ukatononeka

Ndipo hakunenepesha, ukawa wanang’anika

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishik

Hawa ‘kijibidiisha, dakika kila dakika

Kila la kutangamsha, na furaha kukuweka

N’kawa hakusemesha, usipate ungulika

Vipi wanambiya kisha, tamaa innishika?

Mtu wewe hutanisha, zingapita nyingi nyaka

Un’jisahaulisha,ulivyonipa mashaka?

Mno unnikutisha, tabu zisoelezeka

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika?

Pesa ‘kinitumilisha,idadi isosemeka

Matumizi yasokwisha, ungiyapo na kutoka

Nazo kila zikikwisha, hikupa huku nateka

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika?

Raha ‘kikuonesha, kikupa unachotaka

Japo kwa kujidhikisha, upate kusitirika

N’lilo ‘kiliepusha, upate azirika

Vipi wanambiya kasha, tamaa innisha?

Hilo halikunichosha, siku moja sikuchoka

Wala sikukimwa; hasha! Na wala

kununu’unika

Bali ‘ kinifurisha,hiona wafurahika

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika?

Page 99: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

90

MWANAMUME

Ewe wangu mliwaza, yote hayo yajihani?

Badili ya kunutuza, na kunitowa tabuni

Wazidi kuniumia, na kunitoma moyoni

Yaliyokwwisha jilaza, wayaamshiya nini?

MWANAMKE

Ndiwe uloyaamsha, mimi Siye niletaka

Siku tumbi zinkwisha, ‘mepata kuyatamka?

Kidonda‘menitonesha, ndipo name n’karuka

Kwamba menikokomosha,panabudi

kutapika?

Ilipoanza kunisha, akiba nilokiweka

Haanza kuviswafisha, vyangu vya

kudhamika

Mpaka mwisho langu kasha, likawa

linkauka

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika

Vyombo vya dhamani tosha, rahani

nikaviweka

Kimoja sikubakisha, dhahabu na kadhalika

Vyote n’kavisozesha, upate kusitirika

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika?

Rahani ikiviwekesha, bila kuwa na hakika

Itakayoniwezesha, kuvikomboa hitaka

Piya nikajasirika, haidhuru hitamka

Vipi wanambiya kasha, tamaa innishika?

Na hiyo vilipokwisha, vikawa vishasozeka

Hayo hayakunitosha, vingine nkajitweka

Hangiliya kukopesha, kwa n’naoaminika

Vipi wanambiya kisha, tamaa innishika?

Hapo hajirafikisha, kwa walio na maduka

Kwao hajiaminisha, wasinitilie shaka

Wakawa wanikopesha, kwa n’naoaminika

Vipi wanambiya kisha, tamaa innishika?

Kwa kucha kuwajulisha, deni hazitolipika

Nikawa nabadilisha, duka baada ya duka

Kote n’kajizungusha, hadi yakaamalizika

Vipi wanambiya kisha, tamaa innishika?

Deni zikanikondesha, kwa zilivyonizunguka

Afiya yangu ikesha, na muwili kunyauka

Zikawa zinikosesha, usingizi ngautaka

Vipi wanambiya kisha, tamaa innishika?

Wakawa wakinitisha, pesa zao wazitaka

Sizidi kuchelewesha, wazitaka kwa haraka

Au watanigikisha, mbele kwenye mashitaka

Vipi wanambiya kasha, tmaa innishika?

Kwa kutaka kuy’ondosha, japo nusu ya

mashaka

Nguo zangu hafungasha, niuze za kuuzika

Nipate kujiepusha, na deni zilonifika

Vipi wanambiya kisha, tamaa innishika?

Page 100: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

91

Nguo sikuzibakisha, ela zisotamanika

N’kawa n’kijivisha, nguo zilizotatuka

Haya zikinionyesha, nde hishindwa kutoka

Kisha baada ya kwisha, tamaa in’kushika!’

Amma yanitekesha, hayo uloyatamka

Kwisha kunikorofisha, n’kawa ndaa nanuka

Leo wajisimamisha, na kuanza kupayuka

Ati wanihadharisha, tama innishika

Maelezo

Tangu hapo mwanamke, akisema kwa ukali

Na rangi ya uso wake, ikawa imbadili

Mwili umtetemeke, mkali ja pilipili

Kwa sababu ya mwenzake, alivyo

kumfidhuli

Ukali ulimzidi, palipotajwa tama

Na khaswa nyuma ‘kirudi, kwa maisha

walokaa

Hapo akaona hadi, mwanamume hajifaa

Ndipo akakosa budi, maudhiko kumjaa

Na kwa hakika laudhi, tamko la huyo bwana

Lavundiya mtu hadhi, kwa ajuwaye maana

Ni yupi mwenye kuridhi, mtu aje mtukana

Kisha hayo ayaridhi, bila yakujibizana

Mwanamume alituli, bibi alichokinena

Ameitunza akili, asikiza vyema sana

Huku nyuso zao mbili, zali zinlekeyana

Bwana asikiza kweli, ambayo asema nana

Mwamume alidhani, ni maneno ya dhihaka

Mwanzo hakuyaamini, bibi alokitamka

Hakujuwa mwa fulani, kamba mambo

‘megeuka

‘kionekana zamani, ‘tapata anachotaka

Hakuiona sababu, ya bibiye kumnyima

Itakwendaje muhibu, leo awe atagoma?

Hajapata kujaribu, maisha yetu mazima

Akawa taratibu, na kwenye moyo kusema

Hakuweza kukumbuka, japo kuwa siku moja

Ambayo ‘mehangaika, kuipata yake haja

Muda alipokipata, hakuwa ‘kipawa hoja

‘kitimiziwa haraka, bila ya kwambiwa ngoja

Alipokufunukiwa, dafule halifuniki

Katakata ‘mekatwa, hataki bibi hataki

‘kazidi mnyonge kuwa, maguu hayamshiki

Yu mgojwaauguwa, na mwenye twiba

hataki

Akija akiyapima, aloambiwa na mwana

Vyema akayatizama, kwa marefu na mapana

Bibi kweli maisema, urongo ndani hamuna

Page 101: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

92

Toka mwanzo hadi tamma, kweli

inaandamana

Mate yakamkauka, akakosa la kunena

Angaa la kujibika, akatafuta hakuna

Hasira zikamushika, akakasirika sana

Moyoni akatamka : leo n’napatikana

Kwenenda pasi kujibu, maneno aloambiwa

Akaona kuba tabu, japo yote ni ya sawa

Kuondoka ni aibu, bila jawabu kutowa

Kwamba limpe jawabu, bongo akalisumbua

Bongo likamfunziya, maneno ya kujibisha

Ukavu akajitiya, na mato kuyakausha

Akajikosesha haya, tembe hakuzibakisha

Bibi akamlekeya, hayano akampasha

MWANAMUME

Vyema n’nayasikiya, yote uliyoyanena

Orodha ‘menipangiya, ya mambo kila

namna

Yote ‘menihisabiya, ulobakisha hakuna

Ni kweli ‘menifanyiya, moja siwezi likana

Basi kwa kutenda wema, ndiyo sasa

wauimba?

Hayo usingeyasema, ela kwamba wajigamba

Sikuja n’kasimama, mlango ya wako

nyumba

Kama ‘masikini mama’, na kuanza

kukuomba

Bure silete utesi, kwa hayo uyanenayo

Sikukushika kikosi, unitimiziye hayo

Ni yako mwenye nafusi, na pendo la wako

moyo

Mayowe nda nini basi, hayo unipigiayo?

MWANAMKE

Katika uhai wangu, sijapata kumuona

Mwinginewe mlimwengu,ambaye fadhila

hana

Wewe ndiye mosi kwangu, wala sitaona

tena

Naapa haki ya Mn’ngu ! kamawe sitamuona

Nikweli hukunijiya, ukaomba n’kufaye

Ni kweli hikufanyiya, kwa hiyari yangu mie

Na wewe ukipoyeka, kusudi tumbo lijae

Nilipo hikwegesheya, kwanini usikatae?

Maelezo

Dume hiyo kusikiya, bibiye aloyatamka

Kuona sasa vibaya, kooni yalimfika

Uso ukangiya haya, tunu akauinika

Akatamani kiliya, kwa aibu kumfika

Akangiwa na kidaka, mdomo kutofunguwa

Moyo ukampasuka, vipandepande ukawa

Akadangana hakika, kwa jawabu alopawa

Page 102: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

93

Amma aliaibika, mpenda kuegeshewa

Vyema mpate elewa, dume lilivyohizika

Ni kama alovuliwa, nguo zikamuanguka

Yu tuputupu akawa, na hali anainuka

Huotama twaambiwa, bali ye aliinuka

Ikamjia akili, ya kubadili msemo

Akaona afadhali, ni kuipiga horomo

Kwani wake ufidhuli, anshatiwa kikomo

Ili kusudi anali, akatengeza mdomo

Kumrai akaanza, na huku akumsifu

Mno akamtukuza, kwa kila la utukufu

Ulingoni kamkweza, juu palipo parefu

Kusudi apate weza, kupawa kwa ukundufu

Si kwamba ‘kumdanganya, la! Sivyo! Hata

nusu

Maradhi yalimpenya, akawa yu mahabusu

Alobakisha kufanya, ni maguu kumbusu

Moyo asingeukanya, ‘ngejitiya hata kisu

Halafu akaingilia, mno kujisikitisha

Lau ungemsikiya, alivyo kujisemesha

Ungemsikitiya, sikitiko lisokwisha

Naye akiyatiliya, mahanjamu ya kutosha

Hakubakisha kusema, kila la kumtamkika

Na hapo akalalama, mwisho wa kulalamika

Kumweleza mwana-mama,tabu iliyomfika

Amuonee huruma, ampe analotaka

Akasema ‘mejaribu, kutafuta usingizi

Kusudi hii adhabu,ngaa inipe pumzi

Bali ikawa ni tabu, kufumbika langu ozi

Nipoza wangu tabibu, ni mgojwa sijiwezi

MWANAMUME

‘Mejaribu kila ndiya, halikutaka fumbika

Kila nikiliambiya, yangu halikuyataka

Mwenzangu nisaidiya, siniwate hateseka

Tabu yangu yakweleya, sivyo n’livyoshikika

N’nangaangaa mno, kitanda changu shahidi

Lau chasema maneno, ningefanya jitihadi

N’kakileta hapano, kikueleze zaidi

N’ondosheya tabu hino, nana usinikaidi

N’nahisabu boriti, moja baada ya moja

Kwamba nivute wakati, usingizi kuungoja

Sikuona tafauti, wala ishara ya kuja

Yomi n’siye bahati, n’saidiya mbeja

La kutenda n’kakosa, ‘ngetendani? Nambiya

Aseme kwa kugigisa, na sauti ya kuliya

Na mato kuyapepesa, yakawa kutotuliya

Shingo utadhani sasa, tini itaangukiya

Ela akazidi sema, wewe kukufikiriya

Hainuka hasimama, na kuiandama ndiya

N’liona ni lazima, mwenzangu

kukuandamiya

Page 103: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

94

Basi huoni huruma, langu ukakubaliya

Itizame inyeshavyo, hebu itizame mvuwa

Hisi kitetemeshavyo, kibaridi cha kuuwa

Piya haja vivyo hivyo, kwa kuwa

nimelemewa

Basi nana hivi ndivyo, nenende bila

kupawa?

Maelezo

Una mambo ukosefu, ukitokusubiriwa

Hupa mtu kuwa pofu, kadhalika zuzu kuwa

Akajiona yu dufu, hafai kudhaminiwa

Akawa mtu dhaifu, hajiwezi ‘ngaonewa

Na hapa mtu kusema, yasiyofaa kusemwa

Za upuuzi kalmia, zake na za kuazimwa

Akaziona ni njema, kwanza zafaa ungamwa

Na kutojali hishima, yu radhi awe mtumwa

Bibi kusikiya haya, akalianguwa teko

Teko akamtekeya, lile lile la kimeko

Lililojaa kinaya, na sitihizai fuko

Ni mfano kumwambiya: kwangu mimi huna

lako

Page 104: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

95

MWANAMKE

Mn’ngu akuzidishiye, uhodari wa uneni

Ili kusaidiye, kwa maisha ya mbeleni

Elakini kwangu miye, hauna tena dhamani

Hata lipi unambiye, kweli yeke siioni

Licha maneno matamu, ambayo waniambiya

Hata matozi ya damu, lau hayo utaliya

Hayawezi n’lazima, wewe kukuhurumiya

Uombe wako ugumu, upate kusaidiya

N’nani aliyeanza, kufanya mwende mjinga

Si wewe? Hebu nambiza, au urongo natunga?

‘ Mepata ulichoweza, nacho ushakibananga

Basi sikae ‘ kiwaza, kwamba kwangu utaunga

Maelezo

Ni kama jiwe moyowe, mgumu kulainika

Hata lipi uambiwe, hauwi kubadilika

Afadhali hilo jiwe, lipondwa hupondeka

Mwanamume ki mwenyewe, moyoni akatamka

Tamaa hakuikata, akazidi bembeleze

Akasema yalopita, ni bora kuyanyamaza

Kuliok kuyafuwata, na kisasi kulipiza

Yalopita yashapita, si vyema kuyaregeza

MWANAUME

Nayakubali makosa, niswamehe wangu nyonda

Nayatubu hivi sasa, uaminifu kuvunda

Page 105: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

96

Nadhani hutaniwasa, mswamaha kuuonda

Mwenziyo radhi niwiya, nipa nafasi nyingine

Nitakudhihirisha, wewe mwenyewe uwone

Kwamba sitaendeleya, kutenda baya jingine

Kamwe sitakutendeya, tuketi tusikizane

Ni radha kukufanyayi, lolote ilisemalo

Piya kukutimiziya, kila lile utukalo

Haya na mfano haya, sitakataa liwalo

Na wewe niangaliya, sendi kinyume na hilo

Kumbuka tulivyokuwa, tukipendana zamani

Piya sasa kwangu iwa, ulivyokuwa mwanzoni

Natusiyatiye dowa, mahaba yetu mwendani

Ni mgonjwa niaguwa, nioneleya imani

MWANAMKE

Moyoni mwako nitowa, unifute n”siwemo

Mahaba n”shayatuwa,moyoni mwangu hayamo

Siwi wala sitakuwa, kama zamani; horomo:

Niwapo hivyo ‘takuwa, najitiya kwenye shimo

Sasa nihisabu kwamba, n’shakufa kwako wewe

Na kaburi ukatimba, nimo ndani nifukiwe

Siwe na haja kuomba, kurudiyana mi nawe

Kama waweza kuumba, umba mimi mwinginewe

Mimi nawe tuagane, wenende huko wendako

Wende kwa huyo mwingine, abebe mahaba yako

Asaa musikizane, ukapata farijiko

Sitakubeba vyengine, n’shafunguwa mbeleko

Page 106: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

97

Labda si mimi tena, hili fahamu ujuwe

Sinite kwa langu jina, hirudiyana mi nawe

Na lau utaniona,mauti yanitukuwe

Kurudi huna namna, bure usijizuzuwe

Maelezo

Kila ye akiambiwa, wimbo huo siuwimbe

Yeye hujibu ya kuwa, n’taubakiza tembe

Hana la kumtopowa, ela huba za mpambe

Ndwee hii kuuguwa, binadamu ‘siombe

Juu ya jawabu hizo, si kwamba kuyarudiya

Hakutoshelezwa nazo, hakuona ‘mejibika

Ile ile yakwe nguzo, akazidi kuishika

Mfano wa hamnazo, akarudi kuropoka

Maneno yayo kwa yayo, akawa kuyarudiya

Tokeya maneno hayo, mtu ‘kiona nda ndiya

Hata mwisho masikiyo, yakachoswa kusikiya

Mwanamume ana payo, hawezi kujizuwiya

Akamtajiya pesa, mwanamume kazitaja

Kwamba ati toka sasa, na siku ambaazo zaja

Hatakuwa akikosa, kumtimiziya haja

Tena kilala anasa, atampa bila hoja

MWANAMUME

Zozote uzitakazo, ‘takuwa radhi kutowa

Zote ‘tazokuwanazo, kibindoni’ tafunguwa

Kila muda hipatazo, peni sitalinyotowa

Page 107: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

98

Kwako nitakuja nazo, sitangoja kuambiwa

MWANAMKE

Ituze yako akili, ituze kama unayo

Si mali Bwana si mali, niliyo na haja nayo

Mahaba yangu ni ghali, na bei yake si hiyo

Kwangu tena huyanali, hata kwa bei iwayo

Hata lau yangekuwa, kwa pesa yanunulika

Na kwamba wewe ukawa, kuyanunuwa wataka

Yasingelinunuliwa, na mtu wewe hakika

Kwani’ngeliradhiwa, kaburini kuyazika

Maelezo

Zilikuwa zishapita, saa tano za usiku

Ni hapo alipokata, shauri la kuja huku

Dirisha akaligota, Ku! Ku! Ku! Ku! Ku! Ku!

Ili Bibiye kumwita, kwa kubwa mno shauku

Bibi ali mejinyosha, kitanda cha ukumbini

Taa aliirudisha, utambi ukawa tini

Kusudi kuliepusha, joto lisizidi ndani

Na piya halikutosha, kipepeo mkononi

Manukato muwilini, leso mbili ‘mejivika

Mpya ambazo dukani, leo zintoka

Nazo piya chetezoni, alikuwa ‘meziweka

Zafurahisha puani, harafu njema zanuka

‘Kimtizama kitwani, nyele zilivyotanika

Uzitizame na pini, jinsi alivyotomeka

Page 108: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

99

Na shada la asumini, alivyo kulipatika

Lazima utatamani, ngaa upate zishika

Basi uje na shingoni, shingo mfano ya ninga

Ni mjuzi kwa yakini, huyo aliyeitonga

Ukitizame kidani, shingoni alojifunga

Sijuwi ni fundi gani, ambaye alikitunga

Liwa jembamba usoni, alikuwa ampaka

Akatinda na sikini, vizuri ikatindika

Nacho kijembe nyushini, hakikusahaulika

Umwonapo utadhani, si mja ni malaika

Na humo mwake matoni, ni wanda ameupaka

Ule wamda wa Mangani, mno unaosifika

Namo mwake midomoni, wekundu unzunguka

Si wa rangi Ulayani, ni mdaa kutumika

Vya dhahabu viungoni, vyombo amvipambiza

Kipini kimo puwani, kilipo kimpendeza

Vipuli masikiyoni, vyandani pete ongeza

Na bangili mikononi, kiyasi hakuzijaza

Kwa ufupi hakubaki, kwa mapambo kujiunda

Mpita hiyo twariki, angataka kujipinda

Moyo utataharaki, uwe ni mbiyo kumwenda

Na bila shaka ashiki, zitzzidi kumpanda

Ndipo hapo kusikiya, dirishale la chumbani

Hakuwa yakimeleya, aligotaye ni nani

Papale akabakiye, hakutukutika sini

Wala kusema ngojeya, au hivyo mathalani

Page 109: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

100

Alipoona kwazidi, kugogotwa dirishani

Ikawa itambidi, kumuuliza n’nani

Agotaye kwa juhudi, huyuno ni mtu gani?

Jawabu haikurudi, ya kusema ni furahi

Basi alipoinuka, kwenenda kujioneya

Jito likamdirika, aliyemfahamiya

Baada ya shaka shaka, na vyema kutunguliya

Akaipata hakika, ndiye alemdhaniya

Kabla kumuuliza, asema aliojiya

Naye kabla kuweza, kunena alofwatiya

Kila mtu akaganza, mwenziwe kumngojeya

Na kila mato kuanza, yenze kuyakodoleya

Lilompa kungojeya, Bibi ‘kawa kutonena

Alistaajabuya, Bwana kujizusha tena

Nyezi nyingi zimesiya, tangu walipokutana

Aligura hata ndiya, hakuwa ‘kionekana

Akatafuta ni lipi, leo lilomrundisha?

Au yuwatoka wapi, hapo akajipitisha?

Na siku zote yu kupi, mbona alijihamisha?

Leo yankwenda vipi, kuja kwake akabisha

Bibi alivyo ‘mepanga, ndani mwa akili yake

Alitaka kulifunga, hilino dirisha lake

Kusudi mwenye kugonga, hapo pake aondoke

Ende pasi na kuzingza, atokomee na zake

Page 110: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

101

Naye mume saa hiyo, akaona ni lazima

Haja yake alonayo, asifite kuisema

Aukaze wake moyo, amweleze mwana-mama

Na tumbi visingiziyo, vilivyompa kuhama

Ndipo hapo mvutano, ulipoanza mwanzowe

Utadhani mashindano, ya malenga mfanowe

Kila atowaye neno,’kijibiwa na mwenziwe

Ukawa ule mfano, wa ‘twaa’ na ‘twaa wewe’

Hebu msomaji wangu, ulipofika simama

Kaa tupige mafungu, haya mambo kuyapima

Tujuwe tama an tungu, la kumiza na kutema

Ukiyakubali yangu, kidogo turudi nyuma

Pili twangaliye saa, yalipotukiya hayo

Giza lali mesambaa, kwa mvuwa kuu inyayo

Hata zile nyingi taa, mbingu ziing’arishayo

Hata mojapo angaa, haikujitokezayo

Katika huu ubeti, nataka kukwelezeya

Giza ndiye afiriti, wa kukuza maasiya

Lingiyapo huzatiti, nyoyo zikayaendeya

Lenyewe halijifiti, kila mtu yamweleya

Ongeza na kibadiri, kilicho cha kuviviya

Hicho kinaposhitadi, na mfupani kungiya

Rafiki hukosi budi, pa joto kukimbiliya

Basi hapo si zaidi, kwa mwenye huu udhiya

Tatu hebu kumbukiya, manukato nilotaja

Bibi aliyojitiya, kuikusudiya haja

Page 111: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

102

Naku yanavyonukiya, nuka tena mara moja

Halafuye niambiya, baadaye sasa ngoja

Nne timiza mapambo, bibi alojipambiwa

Fikiri vipi mrembo, ambavyonalitokeya

Lau angekuwa chombo, samaki angeshikiya

Yaswawiri haya mambo, n’nayodondoleya

Fikiri wewe mwenyewe, zi vipi ashiki zake

Sasa hayoyatukuwe, kwa la kwanza uyapeke

Yawake pamoja yawe, pamoja yakutanike

Ili kwamba uijuwe, mwanamume hali yake

Bila shaka taabani, haliye ilivyokuwa

Mbaya isiyo kifani, vigumu kuhadithiwa

Pima mwako akilini, huna haja kuambiwa

Kwani sitaweza sini, ‘ngataka fafanuwa

Sasa naturudi nyuma, pale twalipowatiya

Mke alipo kinena, ya pesa kuyajibuya

Tumsikize na Bwana, vipi aliendelea

Msikize vyema sana, ‘endeleyavyo kuliya

MWANAMUME

Un’tendavyo si vyema wala si haki mwendani

Na kweli n’kiisema, haya sikutumaini

‘Mejikosesha huruma, chache hunayo moyoni

Toba Yaa Rabbi salama, kiumbe n’nakoshani?

Natoseka kwa mvuma, ni chapachapa mwilini

Aua hivi ni muruwa, kusema kwa dirishani?

Page 112: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

103

Mlango hebu funguwa, uwate ningine ndani

Ngaa nipate pumuwa, japo hutaniauni

MWANAMKE

Bwana jishikiya ndiya, rudi kuko utokako

Siwezi kufunguliya, siijali tabu yako

Wakatiwo ushasiya, kwangu hupati mashiko

Sina ‘talokutendeya, rudi ulikokuwako

Na hili n’kueleza, lipate kukueleya

Hapa sijicheleweze, hivi sasa n’ondokeya

Nina mtu n’kwambize, na miyadi ‘metimiya

Bwana usinivundize, usoweza nijengeya

Maelezo

N’na mtu ni tamko, Bibi alilotumiya

Lali kama mripuko, wa kombora nakwambiya

Tena kuripuka huko, liliporikiya

Liliripuka ambako, kwa asolitarajiya

Sivyo ambavyo aruke! Kwa kombora kuripuka

Mwaname moyo wake,jinsi ulivyo gutuka

Lau si bahati, kwenye kiguzo kiguzo kushika

Angeona kazi yake, lazima angeanguka

Mke kwisha kuyasema ,hayano maneno yake

Zaidi hakusimama,kutupa wakati wake

Ela alilisukuma, ‘kafunga dirisha lake

Akakomelea hima, na tumbuu yake

Kitendo hicho baada, kilipokwisha tukiya

Akasimama kwa muda, akizidi kungojea

Page 113: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

104

Akifikiri labuda, Mwana ‘tabadili niya

Hakuiona shahada,ya alotumainiya

Kisha ‘kakata kauli, hapo kujiondokea

Mchofu kama hamali, mbebaji magunia

Enda huku kwenye mwili, mvuwa yamnyeshea

Guu mosi guu pili, huyo akasshika ndiya

Ndiya aliyoshika, nikueleza mwendani

Nindiya ya kumpeka, hadi kwa mishi nyumbani

Kwa huyo ndiyo kumbuka Bwana kipeka mapeni

Ndipo sasa akataka, enda akalipwa ndani

Akambwa nasitikika, nafasi sinayo Bwana

Na ambalo nakutaka, ni kutenda kiungwana

Anza sasa kugeuka, ndiya I swafi na pana

Mi nawe tulipofika, mbele hatwendi tena

Bwana hata hakuiweza, kusema neon liwalo

Akabaki kunyamaza, kama hakusikiyalo

Jambo alilofanyiza, ni kulitimiza hilo

Uso’we akageuza, lipa tena jinginelo?

Fulifuli mijitozi, enda huku yamtoka

Ndiya mbili mitilizi, ‘kawa yamminika

Sababu vyake vipenzi, vyote visha mgeuka

Yawaliya kwa simanzi, aliya adsikitika

Akazurura na ndiya, badala kwenda nyumbani

Ovyo akajilanginya, kote mabalabalani

Ni kama alopoteya, bado yu kuzururani

Page 114: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

105

Mnong’ono kwa msomaji

Ndoo n’kunongo’neze, au tunoong’onezane

Nilonayo n’kweleze, ya maana tupanane

Ndoo kwangu jijongeze, sitaki kusilikane

Jifite sijitokeze, kwamba tusionekane

Hebu kweli niambiya, mi nawe tusifitane

Hivi ukiy’angaliya, haya waja watendene

Yupi alotenda baya, kumtendea mwingine?

Ni yupi mwenye hatiya? Usinifite mnene

Ni mwanamke wa kwanza, alejitweka ulezi?

Mwanamume ‘kamtunza, wakati hanayo kazi

Hilino alilofanya, lali ni la upuuzi?

Sidhani litakutanza, lenyewe li waziwazi

Ingawa sote twajuwa, mambo haya hutokeya

Lakini tukiyunguwa, kwaza kiutu tabiya

Alifanya sawasawa, dume kuliangaliya

Na hali huyo hakuwa, mwenzi wake wa shariya?

Na hilino neon zima , pia nalo n’julisha

Tushamwona mwana-mama, a’vyomsarhesha

Je alifanya vyema, mwendo kudadirisha

Mwenziwe kuja mnyima, alipomzoesha?

Kisha tizama na hili, mwanamke alotenda

Ni sawa huyu fahali, kwa bibi huyo kwenenda?

Akapewa maakul, nguo pamwe na kitanda?

Na yeye akakubali, moja basi kulikinda?

Page 115: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

106

Je hivi ndivyo kiume, bwana alivyofanyiza?

Ni sawa kwa mwanaume, hivino kukilegeza?

Badalaye ajitume, japo kunazi kuuza

Kwa maguuye akwime, asipate kulombeza

Na hili liangaliye, unipe hukumu yake

Kati yao afaaye, kumweka mwenzi wake

Ni mke awekwe yeye, aula yeye awekw?

Angaliaunambiye, lifunuwe lifunuke

Lifuwatalo lipime, tena vizuri kabisa

Waone ni wanaume, amaye ana makosa

Kwa kurudi amuume, aliye akijiasa

Ajili amtizame, tabu ‘siwe kumgusa?

Wakati alipokuwa, hana mbele hana nyuma

Sote piya tushajua, alionewa huruma

Vyema akapokelewa, na huyuno mwana-mama

Kwa kila kitu kupewa, na vyema kumtazama

Aliponafasikiwa, kuanza kuwa na chake

Alivyafanya ni sawa, kumpiga mwende teke?

Na kusahau ya kuwa, ndiye mfadhili wake?

Afaa kuhukumiwa, kumuhuni mwanamke?

Na mwisho ni huyu mishi, alotenda tushaona

Kwa kumuiza bilashi, alipomwendeya Bwana

Uweke kando ubishi, alitenda kiungwana?

Usiwe mlalamishi, sitaki lalamishi

Alitenda kiungwana, kumkataa ghafla?

Page 116: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

107

Na hali vya huyu bwana, ni yaye alo ‘kivila?

Halafu vili tena, kuzisahau fadhila?

Tafuta yakwe maana, uyajibu masuala

Mwisho wa hayano yote, nitowe yangu maoni

Singetaka n’kufite, yaliyo mwangu moyoni

Kwa hivyo sasa niwate, n’kupe wangu undani

Kwangu mimi hao wote, nawatiya makosani

Si huyu Mishi baini, mkukutaji mwenzake

Wala si la samahani, hilo jenginewe jike

Na wala dume, ‘sidhani, tamuwata aondoke

Wote wamo makosani, kila mtu kosa lake

Na ambavyo nawaona, watendaji hivi visa

Wantafauiyana, kwa kadiri ya makosa

Yuko aliyekazana, kidogo akayagusa

Wako walozidiyana, na alozidi kabisa

Sasa palipobakiya, ni pako si pangu tena

Kazi n’takuwatiya, tuwe kusaidiyana

Hili ukiliridhiya, anza bongo kulikuna

Upate kunifanyiya, hii kazi ‘tayonena

Hawano watu watatu, walopatwa na hatiya

Muhukumu kila mtu, kulingana na shariya

Siwe kuogopa kitu, na wala kupendeleya

Wala ‘sidhulumu mtu, wala kumhurumiya

Sisemi kadiri gani, ya makosa walonayo

Sitakwambiya Fulani, afaa hukumu hiyo

Sikwambii aswilani, haya ya makadiriyo

Page 117: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

108

Tafuta yako mizani, ya kuyapimiya hayo

Patoosha n’lipofika, hapa ndipo ‘tapokoma

Kalamu tini naweka, kusema kwingi si kwema

Kitu n’nachokutaka, shairi wishapo soma

Jaribu kuyaepuka, haya ulosoma nyuma

KIAMBATISHO B

N’sharudi

Si mwingine ni yuyule, wa ki-Mvita kijana

Mzawa mji wa kale, mtaa Kuze kwa jina

Huwo ndiwo mzi mle, tipuzi ya langu shina

Basi n’sharudi tena, alo na lake nanene

Nijile tena nijile, mneni nijile tena

Zangu tomi zinyemele, zinyemele kwa maana

Tangu siku n’toshile, hi’ leyo ndiyo nanena

Basi n’sharudi tena, alo na lake nanene

Maozi yangu mbonile, yatizama na kuona

Na masikizi vivile, nayasikiziya sana

Ili kwamba yaningile, yaliyonipita jana

Basi n’sharudi tena, alo na lake nanene

Sitatongowa tongole, leo niya hiyo sina

Leo sikukusudile, kungali mapema sana

Mwanzo n’atani niole, mambo nipate yaona

Basi n’sharudi tena, alo na lake nanene

Page 118: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

109

KIAMBATISHO C

Ukamilifu wa Mja

1

Twaa nakupa pokeya, pokeya usidharau

Yaliyomo ni ya ndiya, katika waadhi huu

Twaa kwa kuzingatiya, mazingatiyo makuu

Mtu kuwa na maguu, si kwamba mekamilika

2

Ameumbwa mwanadamu, kwa lililo zuri umbo

Basi si wote fahamu, waliyo na sawa mambo

Wako waliyo timamu, na wingineyo wa kombo

Na mtu kuwa na kifuwa, si kwamba mekamilika

3

Kuna waliyo werevu, ambao ni waelewa

Na kuna na wapumbavu, moja jambo wasojuwa

Piya kuna wenye nguvu, na dhaifu huonewa

Mtu kuwa na kifuwa, si kwamba mekamilika

4

Kuna wasemao kweli, na wasemaji urongo

Kuna waliyo na mali, zilizopita kiwango

Na wingine zao hali, nda kuinamisha shingo

Mtu kuwa na maungo, si kwamba mekamilika

5

Kuna waliwo wembamba, na walo wanene mno

Na wako ambao kwamba, wako kati ya hawano

Mwenyezi ametuumba, kwa mbali mbali mifano

Mtu kuwa na mikono, si kwamba mekamilika

Page 119: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

110

6

Kuna walo mafidhuli, lugha yao ni matango

Na kuna wenye kauli, zisokuwa na ushingo

Kuna wake kwa wavuli, vipofu na wenye tongo

Na mtu kuwa na shingo, si kwamba mekamilika

7

Kuna waja walo wema, kadhalika na waovu

Wako wenye na hishima, na wenye adabu mbovu

Na wako wenye huruma, piya na watenzi nguvu

Mtu kuwa na kidevu, si kwamba mekamilika

8

Kuna walio warefu, na wenye vifupi vimo

Wako walo wahalifu, wa kupitisha kipimo

Piya kuna watiifu, kwa vitendo na misemo

Mtu kuwa na mdomo, si kwamba mekamilika

9

Kuna walo kimya sana, na wenye mingi maneno

Kuna watu wa maana, wahishimiwao mno

Wingine hilo hawana, wapuuzi hawano

Na mtu kuwa na meno, si kwamba mekamilika

10

Kuna watu wakorofi, abadani hawatumi

Na wako wataswarufi, moja huzalisha kumi

Kuna wenye roho swafi, wingine zao sisemi

Mtu kuwa na ulimi, si kwamba mekamilika

11

Page 120: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

111

Kuna walo makarimu,na mabakhili elewa

Na wakubwa kwa hirimu,wazazi kwa wazaliwa

Kadhalika madhalimu,na wanaodhulumiwa

Na mtu kuwa na puwa,si kwamba mekamilika

12

Kuna walo makhawafu, ‘kitishwa hwenenda mbiyo

Na kuna wasiyokhofu, ni shujaa zao nyoyo

Kuna walo wapotofu, na waongofu waliyo

Na kuwa na masikiyo, huko si kukamilika

13

Kuna walio na haya, zilowajaa na mato

Kuna watenda mabaya, wazi pasi na ufito

Kuna wenye swafi niya, na kuna wenye vijito

Na mtu kuwa na mato, si kwamba mekamilika

14

Kuna walo na fikira, na wenye vibovu vitwa

Kuna walo na subira, husubiri; kucha kutwa

Wengine tabiya bora,hino hawanayo katwa

Na mtu kuwa na kitwa, si kwamba mekamilika

15

Nilivyotaja si vyote, viungo vya muilini

Vinginevyo tuviwate, tuifupishe lisani

Ili kwamba tutafute, haya ‘mesema kwa nini

Nikupe yangu maani, ya mja kukamilika

Page 121: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

112

16

Hakuna mja kamili, ndivyo twalivyoambiwa

Kadhalika mimi hili, nasema li sawa sawa

Mkamilifu wa kweli, nakubali ni Moliwa

Maana yangu ‘tatowa ya mja kukamilika

17

Kukamilika kwa mja, ni mbali na kwa Moliwa

Kwa mja nitakutaja, ili upate kwelewa

Ni kufikiya daraja, ile aliyoumbiwa

Hapo ndipo huambiwa, mja amekamilika

18

Aiyelewe duniya, kwa marefu na mapana

Azipite zile ndiya,za miba mitungu sana

Avuke bahari piya, zilo na virefu vina

Hiyo ni yangu maana, ya mja kukamilika

19

Akishafika na hayo, si kwamba ndiyo akhiri

Lazima awe na moyo, wa kuweza kusubiri

Kuyasubiri ambayo, yote yatayomjiri

Kama huyo ‘tamkiri, ni mja mekamilika

13 Mei 1970

KIAMBATISHO D

Wasiwasi Enda Zako

1

Wasiwasi n’ondokeya, ondoka enenda zako

Ondoka andama ndiya,n’ondosheya uso wako

Page 122: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

113

Ondoka! Wanisikiya? Ziwate jeuri zako

Jishughulishe na yako, yangu wayatakiyani

2

Wasiwasi siitaki, suhuba yako si nzuri

Haisitahamiliki, uwovu umekithiri

Inganyoshwa hainyoki, ikukutene kikiri

Siitaki yako shari, enda zako wasiwasi

3

Huna kazi ufanyayo, ela kuwafitinisha

Viumbe na zao nyoyo, vitwa kuwagotanisha

Hiino ndiyo kaziyo, yenye kukufurahisha

Ni kazi isokuchosha, mno umeizoweya

4

Tukaapo wanambiya, hayawi niyatakayo

Kwamba tama ngatiya, nasumbuwa wangu moyo

Kwamba hata hingojeya, hayo niyangojeyayo

Ng’o Siyapati hayo, ni bure najisumbuwa

5

Mara waja na habari, mambo yalivyo nyumbani

Ati mambo si mazuri, mambo yote tafashani

Wanitaka nifikiri, usemayo ni yakini

Nisononeke moyoni, upate kufurahika

6

Au mara hunijiya, na kingine kisahani

Kukhusu zao afiya, hao waliyo nyumbani

Huwa hwishi kunambiya, hali zao taabani

Zingawa; watakiyani? Ni zako au ni zao

Page 123: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

114

7

Na mara huja nambiya, nitakapotoka humu

Ya kwamba yaningojeya, nde maisha magumu

Ulilonikusudiya,ni kunitiya wazimu

Kama ndiyo yako hamu,basi unshatahayari

8

Huo urafiki wako, wa kuja niungulisha

Kunipa masikitiko, na mateso yasokwisha

Kutoka leo ni mwiko, sitautaka maisha

Kamwe hutanikondesha,tokomeya mwana kwenda

KIAMBATISHO E

Mja si Mwema

1

Mkono inuka inuka hima twaa kalamu

Upate ya’ndika kwa khati njema hino nudhumu

Ipate someka wenye kusoma waifahamu

Wapate yashika na kuyapima yaliyo humu

2

Kuandika anza anza ‘sikawe mkono wangu

Na mimi naanza kisa chenyewe cha mlimwengu

Alivyonifanza nao wajuwe waja wenzangu

Wapate jitunza salama wawe hawa ndu zangu

3

Mja sikudhani sikudhania tanizunguka

Nikamuamini hafikiria hatageuka

Kumbe mwafulani hakuzoweya kuaminika

Page 124: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

115

N’shambani ingawa baya lishanifika

4

Menitenda kisa kisa adhimu mja mcheni

‘Mezinduka sasa n’shafahamu najuwa kwani

Ni yangu makosa najilaumu kumuamini

Sikuwa napasa hata sehemu kumthamini

5

Meniuwa mja mja ni nduli tahadharini

Mjaye daraja nda kikatili hana imani

Muonapo mja kaani mbali mujitengeni

Asije akaja (kwani habali) kuhasirini

6

Mja hana haya haya hazimo mwake usoni

Mja ni mbaya hutimba shimo ungiye ndani

Na ukishangiya azome zomo furaha gani!

Mmoja kwa miya ndiye hayumo baya kundini

10 Januari 1971

KIAMBATISHO F

Mamaetu Afrika

1

Mamaetu Afrika, wanayo tu msibani

Msiba ametufika, ndugu hatusikizani

Kila mmoja ataka, awe mshika sukani

Litawezekana lini? Hebu tuamuwe mama

2

Wale maadui zetu, haweshi kutufitini

Page 125: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

116

Si watu hawa si watu, ni wanyama wa mwituni

Hawapendi mamaetu, kukwona u furahani

Bali uwe simanzini, ndivyo watakavyo mama

3

Hawa ndiwo wale wale, madhalimu wa zamani

Usidhaniye wafile, wakalimo duniyani

Na fikira zile zile, zikali mwao vitwani

Wakali wakitamani, kukudhulumu wewe mama

4

Mama madhalimu hawa, walikujiya zamani

Wakakushika shokowa, nyayo hadi utosini

Vyako vikatukuliwa, hata vilivyo mwilini

Mali nyingi ya thamani, wakakupokonya mama

5

Mali ulokuwanayo, ndiyo waloyatamani

Wakajaza mali hayo, shehena mwao vyomboni

Wakenenda nayo mbiyo, hadi mwao majumbani

Ni wevi waso kifani, walokuibaya mama

6

Mno waliyapapiya, pasi kuona imani

Ilikuwa yao niya, kukuwata masikini

Hawakukufikiriya, kisha’ye utafanyani

Au utakula nini, na sisi wanayo mama

Page 126: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

117

7

Si mali tu mamaetu, hawakutosheka kwani

Vile vile ndugu zetu, wakatiwa utumwani

Hawakuthamini utu, wa walo na ngozi hini

Wakituona manyani, kwamba tu weusi mama

8

Wakenda nao makwao, huko bara Ulayani

Ndugu zetu nguvu zao, zikatiwa makazini

Pasi na kulipwa nao, ingawa malipo duni

Wanali wakoloni, kwa bwerere hiyo mama

9

Mama lau si wanayo, kupelekwa ugenini

Lau kwamba si maliyo, kubwakurwa mikononi

Hivi leo bara hiyo, iitwayo Ulayani

Ingekuwa haifani, nakupawa sifa mama

10

Ndiyo waliyowalisha, na kutengezeya huko

Miji wakasimamisha, kwa nguvu za mali yako

Lililowatajirisha, ni jasho la mwili wako

Na damu ya mwana wako, ndiyo kuwa hayo mama

11

Juu ya zao akili, zisifikazo kabisa

Walipungukiwa mali, mali ndicho walokosa

Wakaona afadhali, waje kwako kupukusa

Maliyo pasi ruhusa, wakakutwalia mama

Page 127: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

118

12

Wakakunyang’anya vyako, hivi mtana mtana

Mmoja hakukuwako, wakusubutu kunena

Mama uli peke yako, hata muombezi huna

Ila sisi wako wana, tukakuliliya mama

13

Kwani siku hizo mama, twali dhaifu yakini

Mtu akitusukuma, twali kianguka tini

Sisi nao kusimama, na kuwatiya mbaroni

Ikawa haimkini, sisi kuwashinda mama

14

Tulipopata fahamu, kuweza kukuteteya

Wakaona madhalimu, yatawendeya vibaya

Ndipo walipoazimu, kutumiya mpya ndiya

Kuzivunda zetu niya, wazidi kukula mama

15

Hapo wakakatikiwa, kwamba watutenganishe

Kwani wa moja tukiwa, tutawakanyaga weshe

Waona kubwa dawa, wano watutenganishe

Ili wakukorofishe, na kukunyonya wewe mama

16

Tukawekewa mipaka, kila ukoo na pao

Walifanya kwa kutaka umoja tusiwe nao

Walijuwa pasi shaka, u karibu mwisho wao

Wa kushungiwa makwao, wakuhame wetu mama

Page 128: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

119

17

Wakawa waendelea, kutukuwa yako mali

Na sisi wanayo pia, wakitupa idhilali

Tukawa twalingjeya, mwisho wake jambo hili

Sikuye ikiwasili, tutende kitendo mama

18

Tulipoona ya mno, yashatukoma kooni

Tukasema tabu hino, sasa natuyondosheni

Tukakunduwa mikono, tukaingiya vitani

Kuwapiga wakoloni, wakwambaye wetu mama

19

Japo twali mbali mbali, kila ukoo pekee

Tukaona afadhali, kila tapo lisongee

Kila pembe na mahali, adui tumlemee

Wana walo wazee, tukawa vitani mama

20

Mama tukaanza vita, kukupiganiya wewe

Maguu tukayakita, tukasema tufe nawe

Minyoo tukayakata, ili kwamba huru uwe

Twalolitaka mwishowe,tukawa tunalo mama

21

Nyingi mno damu yetu, ikabidi kumwaika

Baadhi ya ndugu zetu, roho zao zikatoka

Na kila kilicho chetu, kwa wingi kikatumika

Kwa kutaka kuiweka, hadhi yetu nawe mama

22

Adui tukamshinda, ikawa sasa atoke

Tukamwamba toka nenda, na kumpiga mateke

Page 129: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

120

Alikuwa yuwadinda, hakutaka kwenda zake

Kwa nyingi tama yake, ya kukudhulumu mama

23

Baadhi ya wana wako, bado wangali tabuni

Wangali na masumbuko, kwa wateswavyo wendani

Wakoloni wangaliko, kwa wanao wa kusini

Bado wangali na kani, kutesa wanayo mama

24

Msumbiji vile vile, bado hawajakondoka

Nako Zimbabwe wa tele, hawajataka kutoka

Na Angola wabakile, wangali wakikushika

Guinea-Bissau kadha’ka, wamekugandama mama

25

Watoto wako hawano, ni midume sawa sawa

Wamo kwenye mapigano, kutaka kukukombowa

Na kwa lao ungamano, na moyo wa kujitowa

Adui watamtowa, hilo litakuwa mama

26

Adui hivyo kuona, kishamtoka kanwani

Chakula kitamu sana, tena hakipatikani

Akawa amendangana, hajui afanye nini

Ili kwamba mkononi, akirudishecho mama

27

Ikawa anapokaa, huwa roho yampapa

Hurudiwa na tamaa, ya kuja tena kujepa

Bali aogopa baa, lau atarudi hapa

Ni mbwa kuona fupa, akacha kuliguguna

Page 130: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

121

28

Kurudi yeye mwenyewe, kuja kuyatwaa mali

Au kutuma mwanawe, aitimize shughuli

Haya mama utambuwe, yote kwake ni muhali

Ajuwa kwamba si kweli, hawezi faulu mama

29

Kwani wingi wa wanayo, mato yao yako wazi

Kutokeya siku hiyo, hawanao usingizi

Hata yao masikiyo, daima ni masikizi

Angaja kwa unyenyezi, watamsikiya mama

30

Tamaa hakuikata, ya kupata atakalo

Kufikiri hakusita, lipi liwezekanalo?

Litalonipa kupata, lile nihitajilo

Kwani sina buni nalo, ndivyo kiwaza’ye mama

31

Tahamaki akazua, jambo atakalofanya

Akaona kubwa dawa, ambayo itamponya

Ni wanayo hawa hawa, aanze kuwatawanya

Mapande kuwagawanya, wamtumikiye mama

32

Baadhi awatumiye, wawe vibaraka vyake

Baadaye wakujiye, watimize kazi yake

Wanayo wakuibiye, chako kipelekwe kwake

Hiyo ndiyo haja yake, aliyoitaka mama

Page 131: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

122

33

Wanayo hao ni hawa, waletao machafuko

Adui ‘mewanunuwa, wamo ndani kwa mfuko

Ndu zetu wameradhiwa, kuikosa radhi yako

Watapata masumbuko, kwa wayatendayo mama

34

Badala ya kuungana, tuwe ni kitu kimoja

Tupate shirikiyana, sisi na wao pamoja

Tukulinde sana sana, kwa kila litakalokuja

Bali wao yao haja, si sawa na yetu mama

35

Ndiyo mwanzo ndugu zetu, wenda kinyume na sisi

Wakishika kila chetu, na kukiuza rahisi

Waivunda hadhi yetu, sote tuliyo weusi

Wapenda zao nafusi, na maaduizo mama

36

Sisi hatutakubali, kurudishwa utumwani

Kurudiya idhilali, tuliyo pawa zamani

Mama wala yako mali, kupelekwa Ulayani

Hatarudi mkoloni, tuamini wetu mama

37

Tukakulinda vilivyo, pasipo kurudi nyuma

Na vyote ulivyonavyo, vitabakia salama

Vitabaki vivyo hivyo, kimoja hakitahama

Tutamtafuna nyama, atakaye kugusa mama

Page 132: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

123

38

Tu tayari damu zetu, kwa mikondo imwaike

Tu tayari roho zetu, kwa maelfu zitoke

Tukuhami Mamaetu, kila baya likuepuke

Hishimayo tuiweke, Afrika wetu mama

29 Januari 1971

KIAMBATISHO G

Wasiwasi Enda Zako

1

Wasiwasi n’ondokeya, ondoka enenda zako

Ondoka andama ndiya,n’ondosheya uso wako

Ondoka! Wanisikiya?Ziwate jeuri zako

Jishughulishe na yako, yangu wayatakiyani

2

Wasiwasi siitaki, suhuba yako si nzuri

Haisitahamiliki, uwovu umekithiri

Inganyoshwa hainyoki, ikukutene kikiri

Siitaki yako shari, enda zako wasiwasi

3

Huna kazi ufanyayo, ela kuwafitinisha

Viumbe na zao nyoyo, vitwa kuwagotanisha

Hiino ndiyo kaziyo, yenye kukufurahisha

Page 133: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

124

Ni kazi isokuchosha, mno umeizoweya

4

Tukaapo wanambiya, hayawi niyatakayo

Kwamba tama ngatiya, nasumbuwa wangu moyo

Kwamba hata hingojeya, hayo niyangojeyayo

NG’O’ Siyapati hayo, ni bure najisumbuwa

5

Mara waja na habari, mambo yalivyo nyumbani

Ati mambo si mazuri, mambo yote tafashani

Wanitaka nifikiri, usemayo ni yakini

Nisononeke moyoni, upate kufurahika

6

Au mara hunijiya, na kingine kisahani

Kukhusu zao afiya, hao waliyo nyumbani

Huwa hwishi kunambiya, hali zao taabani

Zingawa; watakiyani? Ni zako au ni zao

7

Na mara huja mambiya, nitakapotoka humu

Ya kwamba yaningojeya, nde maisha magumu

Ulilonikusudiya, nde maishani magumu

Ulilonikusudiya, ni kunitiya wazimu?

8

Huo urafiki wako, wa kuja niungulisha

Kunipa masikitiko, na mateso yasokwisha

Kutoak leo ni mwiko, sitautaka maisha

Kamwe hutanikondesha mwana kwenda

Page 134: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

125

1

KIAMBATISHO H

N’shishiyelo ni Lilo

1

Nipulikiza ndu yangu, ninenayo usikiye

Yaliyo moyoni mwangu, ningependa nikwambiye

Ujue imani yangu, ambayo niishishiye

Siiwati ingawaye, n’shishiyelo ni lilo

2

Walinena walimwengu, wa zama zilopisiye

Kwamba kweli i utungu, kwa yule aambiwaye

Nami haya ndugu yangu, sasa niyaaminiye

Asojuwa nasikiye, apeleleze ajuwe

3

Kweli nnaifahamu, haipendwi aswilani

Kwa mja hiyo ni sumu, mbaya iso kifani

Mwenye kuitakalamu, hapendezi katwaani

Sasa nshayaamini, ni kweli haya ni kweli

4

Kweli imenitongeya, kwa kuinena mwendani

Wale nalowaambiya, wamenitiya dhikini

Wameniona mbaya, kumshinda Firauni

Kweli, sasa naamini, si wangi waipendao

5

Kweli naliwambiya, wakuu wa nti hini

Haelaza moya moya, kwa wanati wa ntini

Kuhusu walofanyiya, upande wa Upinzani

Page 135: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

126

Sasa kuwamo tabuni, nalipwa kwa hiyo kweli

6

Kweli ilipowatoma, kama desturi yake

Wao wakaona vyema, afadhali wanishike

Wanishike hima hima, hima ndani waniweke

Ngomeni n’adhibike, nijute kusema kweli

7

Kweli yanipasha tabu, ndugu yangu niamini

Na ninyi mno adhabu, za moyoni na mwilini

Yote haya ni sababu, ya kunena kweli hini

Ndipo sasa hamini, kweli i utungu kweli

8

Kweli menibaidisha, na huko kwetu mjini

Pia menitenganisha, na walo wangu nyumbani

Kuja kuniadhibisha, kwa kunileta ngomeni

Yote sababu nini? Ni kwamba mesema kweli

9

Kweli menifunga ndani, ya chumba nde sitoki

Kutwa kucha ni chumbani, juwa kuota ni dhiki

Na mlinzi mlangoni, yu papo kattu ha’ndoki

Nilindwavyo bilhaki, ni kama simba marara

10

Kweli yanilaza tini,ilo baridi kali

Ningawa burangetini,natetema kweli kweli

Na maumivu mwilini,daima ni yangu hali

Shauri ya idhilali,ya kulazwa simitini

Page 136: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

127

11

Kweli japo ni ngomeni,kwenye kuta ndefu nene

Kabisa sitangamani ,na mahabusu wingine

Na lengo kubwa nadhani,ni :nilonalo ‘sinene

Hazuwa mambo mingine,kwa kuambukiza watu

12

Kweli pia meninyima ,haki zilizo ngomeni

Wangu kuja nitimizama ,hilo haliwezekani

Haya nnayoyasema,ndivyo yalivyo yakini

Baruwa sitakikani,kwandika wala kwetewa

13

Sendi mbele ‘tasimama ,sikupi kwa tafswili

Kusudi nirudi nyuma ,kwa ubeti wa awali

Ili nipate kusema,imani yangu kamili

Ujuwe kwa jambo hili,mtima wangu ulivyo

14

Nilipoenua kimo,kutaka niseme kweli

Nilidhani yaliyomo,hinena sina aili

Kanama wangu mdomo,waja fungika kauli

Nisiseme bilkuli,kuwaeleza wanati

15

Mno wanganiadhibu ,adhabu kila namna

Na mengi yanganiswibu ,ya usiku na mtana

Hayatakuwa sababu ,ya kuniasa kunena

Kweli nitakapoiyona ,tanena siinyamai

16

Page 137: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

128

Mateso yao yangawa,nda kuumiza mtima

Hayatakuwa ni dawa,ya kutonipa kusema

Ni bure wajisumbuwa , nilipo nnasimama

Si ‘mi wa kurudi nyuma ,kweli ilipo ‘tasonga.

17

Ama hakika mwendani ,kwa mwenye moyo wa sawa

Mateso ya duniani ,wakati kijaaliwa

Hushukuru Rahamani ,kajikaza kutukuwa

Nami yangawa yakuwa,hikaza moyo si ila

18

Mateso humbadili,aso na moyo thabiti

Apawapo idhilali ,Japo ingawa katiti

Huona ni afadhali ,awate yakwe ya dhati

Ela langu siliwati ,n’shishiyelo ni lilo

19

Wangi washasumbuliwa,waneni wa kweli hiyo

Na wangi washauliwa ,kwa kutobadili nyoyo

Na mimi nimeradhiwa,ku’yandama sera hiyo

‘Tafuwata zao nyayo , n’shishiyelo ni lilo

20

Atwambizile Rasuli ,kipenzi cha bwana Mn’gu

Ya kwamba tuseme kweli,japokuwa i utungu

Na mimi siibadili ,ni yiyo imani yangu

Nililoamini tangu ,ni lilo hilo sil’ati.

Page 138: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

129

21

Kweli naitiya tamma ,nikuage ndugu yangu

Kweli si mwenye kukoma,kuwambiya walimwengu

Kweli si’yati kusema,katika uhai wangu

Nami kwa upande wangu,hi’yambiwa ‘takubali

KIAMBATISHO I Septemba 1969

Telezi

Mvua iliyonyesha ,ya maradi na ngurumo

Kutwa na kucha kukesha ,kunyesha pasi kipimo

Haikunufaisha wakulima ,wenye kazi na vilimo

Wenye kazi za vilimo,walifikwa na hasara

2

Mimeya waloipanda ,ilitekukatekuka

Kazi ngumu walotenda,yote ikaharibika

Hawakuvuna matunda ,waliyo wakiyataka

Waliyo wakiyataka ,yakawa ya mbali nao

3

Wenye kuicha mvuwa,isiwatose mwilini

Baadhi yao wakawa ,wakimbiliya penuni

Wengine hawakutuwa ,hadi mwao majumbani

Hadi mwao majumbani ,na kukomeya milango

4

Wenzangu dhihaka kando,nisemayo ni yakini

Ilibwaga kubwa shindo ,mvuwa hiyo jamani

Na mijaji kwa mikondo ,yakawa barabarani

Yakawa barabrani,mvua kwisha kunyesha

Page 139: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

130

5

Kunyesha iliposiya ,kukatapakaa tope

Zilijaa kila ndiya,isibakiye nyeupe

Ukawa mwingi udhiya ,pa kupita zisitupe

Pa kupita zisitupe,kwa ndiya kukosekana.

6

Japo hivyo zilikuwa, ndiya hazipitiki

Bali mimi haamuwa ,kwenenda japo kwa dhiki

Kumbe vile nitakuwa,ni mfano wa samaki

Ni mfano wa samaki, kuiendeya ndowana.

7

Zikanibwaga telezi,sikujua kuzendeya

Ningekwenda kwa henezi,yasingenifika haya

Lakini tena siewezi,mwendo huo kutumiya

Sitawata kutembeya,ila tabadili mwendo.

3 Agosti 1973

7

Jambo nilingojeyalo ,ni kutimu yake siku

Ningojeyalo ni hilo,tena kwa kubwa shauku

Itimupo ndimi nalo,ja mwewe na mwana huku

Ni furaha hiyo siku,kwangu na wenzangu piya.

8

Siku ya kuiva kwake ,hiyo ndiyo siku kweli

Huo ndiwo mwisho wake ,na mwisho wa idhilali

Idhilali in’ondoke ,mimi nayo tuwe mbali

Siku hiyo ni wawili,kuteka au kuliya

Page 140: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

131

9

‘Taliminya litumbuke ,lisinisumbue tena

Usaha wote utoke ,utoke nikiuona

Midamu itiririke ,kama ng’ombe alonona

Jipu hili mwana lana,Mn’ngu mbwalipa hizaya.

10

Jasho jembamba litoke,ndiya mbili likitona

Na hapo nitetemeke,si kwa baridi kuona

Bali kwa utungu wake,utakaozidi sana

Hapo ndipo nitasona ,na moyo kufurahiya

11

Baada ya yote haya,jaraha niliuguze

Kwa madawa kulitiya ,ili kwamba yalipoze

Irudi yangu afiya ,na zaidi niongoze

Nirukeruke niteze,kwa furaha kiningiya

KIAMBATISHO J

Siwati

Siwati nshishiyelo ,siwati ;kwani niwate?

Siwati ni lilo hilo ,’talishika kwa vyovyote

Siwati ni mimi nalo,hapano au popote

Hadi kaburini sote,mimi nalo tufukiwe

Siwati ngaambiwa ,adhabu kila mifano

Siwati ningaambiwa,’tapawa kila kinono

Siwati lililo sawa, silibanduwi mkono

Hata ningaumwa meno,mkono siubanduwi

Page 141: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

132

Siwati si ushindani,mukasema nashindana

Siwati ifahamuni ,sababuye waungwana

Siwati ndangu imani ,niithaminiyo sana

Na kuiwata naona,itakuwa ni muhali

Siwati nimeradhiwa,kufikwa na kila mawi

Siwati ningaambiwa ,niaminiyo hayawi

Siwati kisha nikawa ,kama nzi; hivyo siwi

Thamma nakariri siwi ,na Mn’gu nisaidiya

-15 machi 1970

KIAMBATISHO K

Leo N’singekuwako

Kama tabu ni mauti, leo n’singekuwako

Ningekuwa ni maiti ,’mebakiza sikitiko

Ningekuwako tiyati, mtanga ndilo funiko

Leo n’singekuwa ,kama tabu ni mauti

Hivi leo n’ngekuwa ,kana kwamba sikuwako

Kitambo n’shafukiwa ,nimo kaburini huko

Kungebaki kuambiwa :’Atifu alikuwako

Leo n’singekuwako,kama tabu ni mauti

Marehemu ningekuwa,n’shaoza ni mnuko

Hawata kusumbuliwa ,ni tabu na masumbuko

Na tabu haondokewa ,’ngenijiya niliko?

Leo n’singekuwako , kama tabu ni mauti

Kwa siku ngeliliwa ,na jamaa waliyoko

Na maduwa kuombewa ,nende salama nendako

Kisha hasahauliwa ,kwa moyo na matamko

Leo n’singekuwako ,kama tabu ni mauti

Page 142: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

133

Na kwamba hata yakawa,hadi leo hawa niko

Ni kuwa huu moyowa, wahimili masumbuko

Ngeliya kwa yalokuwa ,hakika singekuwako

Leo n’singekuwako,kama tabu ni mauti

-14 juni 1971

KIAMBATISHO L

Wasafiri Tuamkeni

1

Bado safari ni ndefu,wasafiri tusichoke

Natusiwe madhaifu ,twendeni hadi tufike

Tusafiri bila hofu,wenye nazo ziwatoke

Huu ndiwo mwanzo wake, siwo mwisho wa safari

2

Twendeni tusonge mbele,twendeni tusianguke

Mwauona mlima ule? Pale ndipo mwisho wake

Tupande chake kilele,bendera tuitundike

Huu ndiwo mwanzo wake ,siwo mwisho wa safari

3

Twendeni tukifahamu ,kila mtu akumbuke

Safari yetu ni ngumu,si rahisi ndiya yake

Kuna miba yenye sumu, tunzani tusidungike

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

4

Page 143: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

134

Ni ndiya yenye misitu, na mirefu miti yake

Imejaa nyama mwitu ,kila mmoja na pake

Na wakionapo kitu,ni lazima wakishike

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

5

Na kuna bahari pana , na kirefu kina chake

Mawimbi makubwa sana, ni ajabu nguvu zake

Hiyo hatuna namna ,ni lazima tuivuke

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

6

Japo ni ngumu safari ,wendaji tusigutuke

Ingawa ina hatari ,twendeni tusitishike

Ingawa ndefu safari,lazima imalizike

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

7

Tamaa tusiikate,niya zisiteteleke

Ndiya natuifuate, nyoyo zisituvundike

Haja yetu tuipate,bendera yetu tutweke

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

8

Vibwebwe tujifungeni,tuvifungeni vifungike

Tuvikaze viunoni ,waume kwa wanawake

Tungiyapo safarini,twende tusibabaike

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

9

Wenzangu nawahimiza ,haya shime muinuke

Page 144: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

135

Tuwate kujilegeza ,wala tusitetemeke

Haja ni kuimaliza ,isiwatwe nusu yake

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

10

Tuenukeni twendeni,mwenye chake najitweke

Ngiyani misitarini,safu safu mupangike

Wana na wazee ndani,pamoja tutanganyike

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

11

Kusafiri ni lazima ,tukitaka tusikate

Wale waliyo wazima ,maguu nayanyosheke

Na aliye na kilema ,naabebwe na wenzake

Huu ndiwo mwanzo wake,siwo mwisho wa safari

12

Mwenye kutaka safari,ya kwamba isifanyike

Huyo aduwi dhahiri ,kwetu pamoja na kwake

Na wala asifikiri ,atafaulu kwa lake

Huu ndiwo mwanzo wake, siwo mwisho wa safari

13

Na mshikaji bendera, kwa vizuri naishike

Daima nawe imara , wala asilainike

Ayongoze barabara, huko twendako tufike

Huu ndiwo mwanzo wake, siwo mwisho wa safari

4 Septemba 1971

KIAMBATISHO M

Kichu Hakiwi ni Uchu

Page 145: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

136

1

Ni nyani ambidhiweo , yu nchu kwa chake kichu?

Ni nyani nnena hao, ntaka hadaa vachu

Nadhengee vangineo, jura hatopacha kwechu

Nchu kwambiwa yu nchu, ni uchu kwa wendiwe

2

Na kama ni chwambiwavo,kichu na uchu ni chicho

Dhiko na dhingi dhilidho,dhenye dhichu kochokocho

Chwambe dhina uchu nadho,thibabu ni lavo pacho?

Nchu si kwa lake pacho,ni uchuwe kwa wendiwe

3

Hela ndovu chunchude ,awe ni mfano wechu

Chumuawanye dhipande ,awe dhipande dhichachu

Ili kasidi chwenende ,chufahamishe uchu

Chuyive nchu ni kichu ,au uchu kwa wendiwe?

4

Kwanda ni mwili wake,uliyo nkuru nno

Kwa namna mwichu wendake ,hauna wakwe mfano

Apeche umbo la pweke ,kuru tena lilo nono

Si chanda si lakwe ino,si madodi ila mato

5

Ndhengee avoneo,mwene kuwavona vachu

Vachu ndovu wavoneo,awapo kachika mwichu

Umvudhe :vachu hao,wavonao hicho kichu

Achi huwaye wendechu,sura wataajabuvo

6

Pili nguvu alonadho,dhiyani dhalomweneya

Ni nguvu dhiwachishadho,dhiumbe na michi piya

Page 146: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

137

Dhidirikano nadho,hadhina budi kuliya

Au mbiyoni kungiya,kwa kucha kudhidirika

7

Vako ambao hunena,nguvudhe kudhisifiya

Kwamba huwedha vuchana ,na hata na vachu miya

Na hata vangaungana ,kumvucha kwa pamoja

Hawawi kuwedha piya,kwa nguvu alidhonadho

8

Ata dhiumbe vanche, kwa nguvu alidhopowa

‘kichumiya kifuwache ,awapo andoudhiwa

Mishi isiyo michache ,hungiliya kuang’owa

Nyuteni yivani kuwa ,hawi mbwa kudhivilika

9

Kando ni lakwe iteke,libikapo hwangaamidha

Pumudhidhe pweke yake,chwaambiwa huumidha

Dhivudhiyapo chendake ,mbali hukichokomedha

Humbiriya dhikapadha,na tiyati kuchangusha

10

Chachu ni yakwe thamani ,asoiyiva hakuna

Ichengee duniani ,kupi kaiyulikana

Dhiungani na miyini,nno huchambulikana

N’nyani mwene kunena,haiyisi thamaniye

11

Pacha kwenda utukuni,pembedhe dhidhanyiwapo

Au nenda nnadani,kwahali dhinadiwapo

Page 147: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

138

Uyivwonee matoni,n-da dhinunuliwapo

Ndipo utayiwa hapo,thamani ya nama thamaniye

12

Thamani yakwe si chocho,thamani ya nana huu

Chakwe iye kidhanuwacho,hoko kwene utukuu

Mwene kukinunuwacho ,hulipiya bei kuu

Beiye kwamba i yuu,ndipo kudhanywa hiyau

13

Kiswahili cha kigunya ,kwacho ‘kiwazungumza

‘Mejaribu kubambanya ,kiyasi n’livyoweza

Sasa n’takalofanya ,nataka kukigeuza

Kwamba n’pate maliza,n’lilolikusudiya

14

N’likijuwa zamani,tangu utotoni mwangu

Wakati ni magunyani,pamoja na babu yangu

Na tangu huko nihuni,si leo miyaka tungu

Kwa hivyo fahamu yangu ,kwacho ‘menipungikiya

15

Changu ni cha kimvita ,tangu mwa mama tumboni

Sikwenda kukitafuta ,n’likikuta nyumbani

Mi nacho ni kama pata,twendapo hatuwatani

Na tangu kwinukiyani,hicho ndicho hutumiya

16

Kwangu ndicho mahasumu,mno nakipendeleya

Ndicho kinishacho hamu,mashairi hitungiya

Page 148: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

139

Huwa siyaoni tamu,hiwata kuchadikiya

Huyaona ni mabaya ,ha ya tamu ha ya nyamu

17

Hicho ndicho kiswahili,ambacho chanipendeza

Kwake sioni badali,ndipo nikakitukuza

Kwangu ki kama asali,tamu isokinaiza

Ndicho hunitosheleza ,wakati wa kutungiya

18

Kwanza nataka fasiri ,maana ya neno ‘kitu’

Tueleze vizuri ,afahamu kila mtu

Maanaye idhihiri ,kwa kila mmoja wetu

Mtu kiambiwa ‘kitu’,lipate kumueleya

19

Ni mengi maana yake,nikianza yadondowa

Lau yote niandike ,iwe kuyafafanuwa

Ndugu zangu mukumbuke ,kazi kubwa itakuwa

Basi yote sitatowa ,ingawa yanieleya.

20

Katika lugha iweyo,hata iwe nda Kichina

Kuna maneno ambayo ,kwa mato ukiyaona

Utayadhaniya hayo,hayana maana pana

Yaani yao maana, moja hayakuzidiya

21

Lakini sivyo yalivyo ,si ambavyo huwa

Vilivyo ambavyo ndivyo ,ambavyo vilivyo sawa

Page 149: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

140

Hutegemeya ambavyo,neno linavyotumiwa

Ndipo utapamabanua ,maanaye mbalimbali

22

Na Kiswahili ni vivyo,vyenginewe usidhani

Neno ulitumiyavyo,liwapo li kifunguni

Nalo ndivyo likupavyo ,tafauti ya maani

Ukaweza kubaini ,maana yatakiwayo

23

Kwa maana ya jumla,ya neno ‘kitu’ wenzangu

Ni ambacho au kila ,kilo kwenye ulimwengu

Mfano nguo ,chakula ,neno,roho au rungu

Jiwe,mtu au tungu,kila kimoja ni kitu

24

Ndipo mfano hatowa,wa ndovu alivyonavyo

Ukubwa aliopawa,ni kama hivyo ulivyo

Na nguvuze twazijuwa,zistaajabishavyo

Na thamaniye ilivyo,si ndogo meelezeya

25

Vyote hivino ni vitu,tena si vitu vidogo

Ndivyo vitu kila mtu,huviwekeya mitego

Kimojapo mwenzi wetu, ‘kipata hutupa shingo

Hufurahi hadi jego,likawa laonekana

26

Iwapo ni hicho kitu,mno kinachosifiwa

Ndicho kimpacho mtu,naye yu mtu kwambiwa

Page 150: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

141

Basi huyu nyama mwitu,ambaye meelezewa

Kitu chamfanya kuwa,kwambiwa naye yu mtu?

27

Licha mtu akili ,ambayo iko razini

Hata mjinga wa kweli,mtopeya ujingani

Hataweza kukubali,kabisa hataamani

Ati nyama wa mwituni,awe yu sawa na mtu

28

Lau hayo watamka,na kumwambiya mwendani

Hakika atakuteka,akutiye uzuzuni

Maana kufikiria ,hayangii akilini

Hilo haliwezekani ,ni bure ungamwambiya

29

Basi na mtu ambaye ,yuna vitu kwa milima

Maadamu vyake yeye,hafalii binadama

Bali huvikusanyaye,na kupenda vitizama

Huwa sawa na mnyama,tuliyemuelezeya

30

Mfano awe na mali ,yalokiuka mipaka

Akatupiliya mbali ,wenye shida na mashaka

Akawa hata hajali ,tabu zinazowafika

Huyo si mtu hakika ,kwani mtu mbwake utu

31

Au awe yuna nguvu,kikubwa kifuwa chake

Ziwe nguvu za mabavu,na magumi na mateke

Page 151: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

142

Iwe sasa utulivu,hawaupati wenzake

Iwe ni watetemeke,muda’ye akitokeya

32

Nguvu hizo sasa ziwe,hatumii ajikinge

Bali ndiyo mwanzo awe ,kwenye mitaa arange

Akidhulumu wenziwe,ambao kwamba wanyonge

Yawe ‘mnyonge msonge, hana wa kumzuwiya

33

Au awe yuna cheo ,juu ya wenziwe wote

Na kisha wemziwe hao,alonao saa zote

Wawapo na shida zao,hawafai kwa chochote

Iwe ‘poteleya pote,hataki kuwasikiya

34

Badili hiyo furusa ,kuitumiya vizuri

Kwake sivyo ;bali sasa ,huanzisha takaburi

Wende awe kuwatesa,awatende jeuri

Huyo ni mnyama wa pori,hafai kuitwa mtu

35

Walio na sifa hizo,viumbe niwanenao

Mali wangakuwa nazo,ukubwa wangawa nao

Wangawa na nguvu hizo,wadhiliyazo wenzao

Siweki viumbe hao,kwenye daraja ya watu

36

Uliyo wangu muradi,wa kuyanena hayo

Viumbe hao idadi ,pamoja na ndovu huyo

Page 152: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

143

Sikioni cha zaidi ,kati ya waliyonayo

Naona wa sawa kwayo,kipi walopitaniya

37

Iwapo ni hayo mali,watu yasosaidiya

Sababu ya ubakhili,wakawa wayabaniya

Wasijali wasibali,dhiki za wapita ndiya

Na ndovu anayo piya, kama nalivyoeleza

38

Ndovu na bakhili sawa,ha wa mbali kwa masafa

Ya bakhili hurithiwa ,baada ya kwake kufa

Mara nyingi hutumiwa ,ovyo pasi maarifa

Na ya ndovu ni kufa ,ndipo yake yatwaliwe

39

Kwa hivyo hapa twaona ,viumbe hivi viwili

Ambavyo wamfanana ,kwa hayano yao mali

Hayawi kupatikana ,ela watwawe na nduli

Kuna gani afadhali,baina wawili hawa?

40

Na kwa wa nguvu upande, ‘taweleza pasi shaka

Iwapo ni wa makonde,na mabavu kutumika

Watu iwe mbiyo wende,kwa kucha kuzidirika

Vifenene kadhalika,viumbe viwili hivi

41

Apandwapo na ghadhabu ,huyu ndovu ‘mewambiya

Vilivyo naye karibu ,na alivyovilekeya

Page 153: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

144

Huanza kuviharibu ,vikawa kuangamiya

Huulaza mwitu piya,manyasi na miti yake

42

Kwani muda hifikiri ,hizo nguvu walonazo

Ni nguvu za kuhasiri,na kudhili wasonazo

Hazitumiwi kwa kheri,bali kwa maangamizo

Basi wafenene kwazo,ipi tafauti yao

43

Na iwapo ni ukuu,huyo mtu alonao

Ukuu wa kudharau,wasiwo na hicho cheo

Basi ndovu nao huu,na yeye piya anao

Ipi tafauti yao,walotafautiyana

44

Basi tusidanganyike ,tusiwe mbwa kuhadawa

Mtu si kwa kitu chake,japo kwacho asifiwa

Utu wake kwa wenzake,ndiwo wa kuhisabiwa

Vyengine sitaambiwa,nami nikaviamini

Page 154: UHAKIKI WA MTINDO KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA …ir-library.egerton.ac.ke/jspui/bitstream/123456789/1501/1/Uhakiki wa fani na maudhui...UHAKIKI WA FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI

145