kauli za ma´ulamaa kuhusu maulidi

29
1 Mfasiri: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

Upload: wanachuoni

Post on 28-Apr-2015

267 views

Category:

Documents


19 download

DESCRIPTION

Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

TRANSCRIPT

Page 1: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

1

Mfasiri:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

Page 2: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

2

Yaliomo:

1. Maulidi Hayana Kheri Yoyote

2. al-Faakihaaniy Kuhusu Sherehe Ya Maulidi

3. Mgawanyiko Wa Imaam ash-Shaafi'iy Wa Bid´ah Hauyasapoti Maadhimisho

Ya Maulidi

4. Maadhimisho Ya Maulidi Yanapingana Na Qur-aan, Sunnah Na Matendo Ya

Salaf

5. Ibn Hajar Kuhusu Bid´ah Nzuri Ya Maadhimisho Ya Maulidi

6. Maadhimisho Ya Maulidi Ni Kujifananisha Na Manaswara

7. as-Suyuutwiy Asemae Maadhimisho Ya Maulidi Ni Bid´ah Nzuri

8. Shaytwaan Anapenda Sherehe Ya Maulidi

9. Imaam al-Albaaniy Kuhusu Maadhimisho Ya Maulidi

10. Je, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) Anahudhuria Katika Sherehe

Ya Maulidi?

11. Hukumu Ya Kusherehekea Maulidi Msikitini

12. Shaykh Ibn ´Uthaymiyn Akiwaombea Du´aa Waliopotea Katika Bid´ah Ya

Maulidi

13. Inajuzu Kusherehekea Maulidi Kama Ada Tu Na Si ´Ibaadah?

14. Maulidi Hayakufanywa Na Mtume Wala Maswahabah

15. Tofauti Kati Ya Sherehe Ya Maulidi Na Siku Ya Taifa

16. Maulidi Yana Bid´ah Na Shirki

17. Kupeana Hongera Siku Ya Maulidi

18. Kufanya Maulidi Ni Bid´ah

19. ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Madu´aat Wanaohudhuria Katika Maulidi

20. Kufunga Siku Ya Maulidi Ya Mtume (´alayhis-Salaam)

21. Je, Kusherehekea Maulidi Ni Katika Kumpenda Mtume (´alayhis-Salaam)?

Page 3: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

3

22. Sikukuu Za Makafiri Kama Krismasi Na Za Waislamu Kama Maulidi

23. Wajinga Wanaodanganywa Kwamba Kusherehekea Maulidi Ni Kumpenda

Mtume

Ma´ulamaa waliomo:

1. Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah

2. Imaam Abu Hafs Taadj-ud-Diyn al-Faakihaaniy

3. Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy

4. Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

5. Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

6. 'Allaamah Hamuud bin 'Abdillaah at-Tuwayjiriy

7. ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

8. ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aal ash-Shaykh

9. ´Allaamah Swaalih bin Muhammad al-Luhaydaan

10. ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy

11. Shaykh Swaalih bin Sa´iyd as-Suhaymiy

Page 4: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

4

Dibaji Ya Mfasiri:

Alhamdulillaah. Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad.

Amma ba´ad:

Nimekusanya baadhi ya kauli za ma´ulamaa waliotangulia (Rahimahumu

Allaah) na wa sasa (Hafidhwahumu Allaah) kuhusiana na Bid´ah sugu hii ya

Maulidi ambayo Shaytwaan amewapambia baadhi ya Waislamu. Natumai hoja

zilizotajwa humu zitawaondolea shubuha kwa wale waliokuwa wakifuata

kichwa mchunga na kibubusa walinganiaji wapotofu ambao wamekuwa kwa

siku nyingi wakiwadanganya ndugu zetu Waislamu wasiokuwa na elimu ya

kwamba kusherehekea Maulidi ni kumpenda Mtume. Allaah Atukinge.

Ama kuhusiana maimamu wakubwa wa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah

waliotangulia ambao wameonelea ya kwamba yanajuzu, hoja zao zimerudishwa

na kuradiwa (kupigwa Radd) na ma´ulamaa wakubwa wa Ahl-us-Sunnah wal-

Jamaa´ah. Kama alivyosema Imaam Maalik “Sote kauli zetu zinachukuliwa – yaani

pale ambapo zimeafiki Kitabu na Sunnah, na kurudishwa – pale ambapo zimekhalifu

Kitabu na Sunnah.” Na huu ndio msimamo sahihi wa Salaf na waliowafuata kwa

wema.

Kauli za ma´aulamaa tumezigawa sehemu mbili; wanachuoni wa Salaf – yaani

tukimaanisha wale wambao wameshatangulia makaburini (Allaah Awarehemu)

na wanachuoni wa Khalaf – wale ambao bado wako hai kwa sasa (Allaah

Awahifadhi).

Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Atuoneshe haki na Atuwafikishe

tuwe ni wenye kuifuata, na Atuoneshe batili na Atuwafikishe tuwe ni wenye

kuifuata. Aamiyn.

Page 5: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

5

Wanachuoni Wa Salaf

1. Maulidi Hayana Kheri Yoyote

Hali kadhalika na kwa yale waliozua baadhi ya watu ima ili kuiga manaswara

au kwa ajili ya mapenzi na kumuadhimisha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam). Huenda Allaah Akawalipa kwa mapenzi na shughuli hii, lakini si kwa

Bid´ah hii ya kusherehekea Maulidi ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam). Isitoshe, kuna tofauti kuhusiana na tarehe sahihi [za kuzaliwa kwake].

Jambo hili halikufanywa na Salaf, ingawa walikuwa na uwezo juu ya hilo

wakati vikwazo vyake kulikuwa hakuna. Lau jambo hili lingekuwa na kheri

ndani yake, au lau lingekuwa na faida nyingi kuliko khasara, basi Salaf

(Radhiya Allaahu ´anhum) walikuwa na haki zaidi juu yake kuliko sisi.

Walikuwa wakimpenda Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) zaidi kuliko

sisi vile vile kama ambavyo walikuwa wakimuadhimisha (Swalla Allaahu 'alayhi

wa sallam) zaidi kuliko sisi. Walikuwa na hima ya kufanya matendo mema

kuliko sisi.

Lakini mapenzi kamilifu na uadhimisho unapatikana katika kumfuata na kumtii,

kufuata amri zake, kuhuisha Sunnah zake sawa za ndani na za dhahiri, kueneza

mafunzo yake na kupigana kwa hilo kwa moyo, mkono na ulimi. Hii ndio njia

ya wale Makhalifah wa kwanza katika Muhaajiruun na Answaar, na wale

waliowafuata kwa wema.

Watu wengi katika watu hawa ambao wako na bidii ya kujishughulisha na

Bid´ah hii - angalau kwa nia njema na shughuli ambayo tunatarajia watapewa

ujira kwa ajili yake - ni madhaifu katika kufuata amri za Mtume (Swalla Allaahu

'alayhi wa sallam). Utawapata wao ni kama yule mwenye kuipamba Qur-aan

bila ya kuisoma au anaisoma lakini bila ya kuifuata. Mtu kama huyo ni kama

yule anaeupamba Msikiti bila ya kuswali au anafanya hivyo mara chache.

Mwandishi: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah

Page 6: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

6

Iqtidhwaa´ as-Swiraat al-Mustaqiym (2/123-124)

Daar-ul-'Asimah, 1419

2. al-Faakihaaniy Kuhusu Sherehe Ya Maulidi

Watu wema wameuliza mara nyingi swali kuhusu ukusanyanyikaji unaofanyika

na baadhi ya watu katika Rabiy´ al-Awwal, ambayo wanaiita "Maulidi". Je, yana

msingi katika Dini? Wanataka jibu la ufafanuuzi. Nikajibu na kwa Allaah ndio

kwenye mafanikio:

Sijui kuwa Maulidi haya yana msingi katika Qur-aan au Sunnah. Na haijathibiti

kutoka kwa mwanachuoni yeyote wa Ummah ambaye ni ruwaza njema katika

Dini na ambaye anashikamana na wa kale. Ukweli ni kwamba jambo hili ni

Bid´ah. Yalizushwa na wavivu na watu waroho. Dalili ya hilo ni kwamba, ikiwa

tutayakutanisha na zile hukumu tano, tungelisema kuwa jambo hili ima ni

wajibu, limependekezwa, linaruhusiwa, linachukiza au haramu pia.

Ni jambo waislamu wamekubaliana ya kwamba si wajibu au kupendekezwa.

Jambo lililopendekezwa ni jambo ambalo Shari´ah imeliamrisha bila ya

kumhukumu yule ambaye hakulifanya. Jambo hili Shari'ah haikuliruhusu.

Maswahabah na waliokuja baada yao hawakulifanya. Na wala sijui ya kwamba

wanachuoni wa Dini walilifanya. Hili ndio jibu langu mbele ya Allaah (Ta´ala)

ikiwa nitaulizwa kuhusu hilo.

Hayawezi pia kuwa yanaruhusiwa kwa sababu jamhuri imekubaliana ya

kwamba ni haramu kuzusha katika Dini.

Hivyo, jambo hili linaweza kuwa ima lenye kuchukiza au haramu pia. Katika

hali hii mtu anaweza kuyaongelea katika njia mbili tofauti:

Jambo la kwanza: Mtu kufanya hilo na mke wake, rafiki zake na familia yake,

kuyasimamia kwa pesa zake mwenyewe na kula tu wakati wa mkusanyiko bila

ya kushiriki dhambi yoyote. Ni mkusanyiko huu ndio tunauelezea kuwa ni

Bid´ah yenye kuchukiza na kitendo cha machukizo. Kwa maana hakuna mtu

yeyote katika karne za kale, ambaye ni mwanachuoni wa Uislamu na watu

aliyeyafanya.

Page 7: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

7

Jambo la pili: Kwamba dhambi imeshiriki [katika Maulidi hayo] na mtu

anaomba wengine pesa kwa ajili yake. Roho imejisalimisha kwa hilo wakati

moyo unateseka kwa mateso ya dhuluma. Baadhi ya wanachuoni wamesema:

"Kuchukua pesa kwa kustahi ni kama kuzichukua kwa upanga."

Na hili ni hususan pale ambapo mkusanyiko unafuatana na nyimbo na vyombo

kama matari na vijana wanawake na wanaume ambao wanakaa pamoja na

vijana wasiokuwa na ndevu na waimbaji. Hili linaweza kufanyika kwa

mchanganyiko wa moja kwa moja au kwamba wanawake kuwahudumia

wanaume na kucheza kwa kuamsha hisia. Aidha, mkusanyiko unakuwa na

burudani zisizohitajika ambapo husahau Siku ya Qiyaamah.

Hali kadhalika wanawake wanapokusanyika wao wenyewe, kupandisha sauti

zao, kuimba na kushindwa kusoma na kumkumbuka Allaah kwa njia ya kidini

na ya kawaida. Wanapuuza Maneno ya Allaah (Ta´ala):

إن ربك لبالمرصاد

“Hakika Mola wako bila shaka Yuko katika Kuchunga (na kuwavizia).” (89:14)

Hakuna yeyote anayeonelea hili linajuzu. Si mwenye heshima, busara na

wanaume shujaa kuona hili ni zuri. Watu ambao wanaruhusu jambo hili ni wale

wenye mioyo ya maradhi ambao hawaachi dhambi. Na hawakutosheka na hilo.

Wanafikia mpaka kusema hata ya kwamba jambo hili ni aina ya ´Ibaadah na

halikukatazwa. Inna liLlaahi wa inna Ilayhi raaji´uun. Uislamu ulianza kitu

kigeni na utarudi kuwa kama ulivyoanza.

Imaam Abu 'Amr bin al-' Alaa' kapatia aliposema:

"Watu watakuwa katika hali nzuri maadamu wanastaajabu katika ajabu."

Isitoshe mwezi huu - Rabiy' al-Awwal – ambao Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi

wa sallam) alizaliwa katika mwezi huo, ni mwezi huo huo alifariki. Hakuna haki

zaidi ya kufurahia katika mwezi huo kuliko kusikitika.

Hili ndio limelazimika kwangu kulisema. Ninamuomba Allaah Ataqabali ´amali

hii.

Mwandishi: Imaam Abu Hafs Taadj-ud-Diyn al-Faakihaaniy (d. 734)

al-Mawrid fiy 'Amal-il-Mawlid, uk. 20-27

Page 8: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

8

3. Mgawanyiko Wa Imaam ash-Shaafi'iy Wa Bid´ah

Hauyasapoti Maadhimisho Ya Maulidi

ar-Rifaa'iy kasema:

"Kinachothibitisha ya kwamba tendo hili ni Bid´ah nzuri, ni maneno ya ash-

Shaafi'iy yaliyopokelewa na al-Bayhaqiy: "Kuna aina mbili ya Bid´ah. Ya kwanza

ni ile inayopingana na Qur-aan, Sunnah, mapokezi au Ijmaa´1. Bid´ah hii ni

upotofu. Bid´ah ya pili si ni ile inayopingana na moja katika hayo tuliyotaja.

Bid´ah hii sio yenye kulaumiwa. 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhu) kasema kuhusu

Swalah ya usiku katika Ramadhaan: "Bid´ah nzuri ilioje hii!"

Jambo la kwanza, sio maoni ya wanachuoni ndio yenye kuamua

yanayoruhusiwa na yasiyoruhusiwa, kizuri, haramu na kibaya. Dalili ni Qur-

aan, Sunnah, Ijmaa´ au kauli ya Swahabah rafiki maadumu haijulikani ya

kwamba kuna Swahabah mwingine ana maoni tofauti. Alichosema ash-Shaafi'iy

(Rahimahu Allaah) hakitolei dalili uzushi wa Maulidi, au Bid´ah nyingine kwa

jambo hilo, kuwa ni nzuri. Kutokana na maneno yake, mtu anapata kuelewa ya

kwamba maadhimisho ya Maulidi yamekatazwa kwa vile yanakwenda kinyume

na Qur-aan, Sunnah, mapokezi na matendo ya Salaf taarifa na maimamu.

Aidha, maneno ya ash-Shaafi'iy yamepokelewa kwa taarifa nyingine. Abu

Nu'aym kapokea katika "al-Hilyah" yake kutoka kwa Ibraahiym bin al-Junayd

ambaye kasema: Harmalah bin Yahyaa katueleza ambaye kasema kwamba

alimsikia Muhammad bin Idriys ash-Shaafi'iy akisema:

"Kuna aina mbili ya Bid´ah. Bid´ah inayosifiwa na Bid´ah ya kulaumiwa.

Inayokwenda sambamba na Sunnah inasifiwa na inayokwenda kinyume na

Sunnah inalaumiwa. "

Kisha akatumia hoja kwa maneno ya 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhu) kuhusu

Swalah ya usiku katika Ramadhan:

"Bid´ah nzuri ilioje hii!"

1 Makubaliano ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum)

Page 9: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

9

Ibn Rajab kasema katika 'Jaami'-ul-'Uluum wal-Hikam":

"ash-Shaafi'iy anamaanisha ya kwamba msingi wa Bid´ah ya kulaumiwa ni

kuwa ni ile inayokosa msingi katika Shari'ah ambao mtu anaweza kuurejea.

Ndio maana ya Bid´ah kwa mujibu wa Shari'ah. Ama kuhusiana na Bid´ah

yakusifiwa, hiyo inayokwenda sambamba na Sunnah. Inamaana ina msingi

ambao mtu anaweza kuurejea. Kwa njia hii, hii ni Bid´ah tu ya kilugha2, na sio ya

Dini, hivyo inakwenda sambamba na Sunnah."

Jambo la pili, uzushi wa Maulidi hauna msingi katika Shari'ah. Jambo hili

linapingana na uongofu wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam) na Sunnah. Hivyo ni kitendo cha Bid´ah ya kulaumiwa.

Jambo la tatu uzushi wa Maulidi unapingana na Qur-aan, Sunnah, mapokezi na

matendo ya Salaf na maimamu.

Mwandishi: 'Allaamah Hamuud bin 'Abdillaah at-Tuwayjiriy

ar-Radd al-Qawiy, uk. 44-45

4. Maadhimisho Ya Maulidi Yanapingana Na Qur-aan,

Sunnah Na Matendo Ya Salaf

ar-Rifaa'iy kasema kuwa maadhimisho ya Maulidi hayapingani na Qur-aan,

Sunnah na Ijmaa´ ya Waislamu, hata kama yamekuja baada ya Mtume (Swalla

Allaahu 'alayhi wa sallam) na kufa kwa Maswahabah wake. Kwa hiyo, mtu

hawezi kusema ya kwamba tendo hili ni la kulaumiwa kwa seuze tusiseme ya

kuwa ni dhambi na kuwa ni Bid´ah ovu.

2 Anasema Shaykh ´Allaamah al-Fawzaan: ”Bid´ah ya kilugha ni kwa mfano wa hii gari yako. Gari yako hii ni Bid´ah lakini ni Bid´ah ya kilugha. Kwa kuwa ni kitu kipya ambacho hakikuwepo, mwanzoni watu walikuwa wakipanda punda na mipando mingine. Kukaja badala yavyo gari n.k. Hii ndio Bid´ah ya kilugha.” (Sharh Sunnah lil-Barbahaariy).

Page 10: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

10

Maadhimisho ya Maulidi ni Bid´ah katika Uislamu na maadhimisho yake

yanapingana na Qur-aan, Sunnah na matendo ya Waislamu tangu wakati wa

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wakati wa sallam) hadi karne ya 600.

Yanapingana na Qur-aan pale ambapo Allaah Anamuamrisha mja Wake kufuata

yale Aliyoteremsha na hapana mwingine badala Yake. Allaah (Ta´ala) Anasema:

ن ربكم ول ت تبعوا من دونه أولياء رون اتبعوا ما أنزل إليكم م ا تذك قليلا م

”Fuateni yale mliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wenu (Qur-aan na Sunnah) na wala msifuate badala Yake (Allaah), awliyaa (marafiki wapenzi, walinzi wanaokuamrisheni kufru, shirki). Ni machache mnayoyakumbuka.” (07:03)

Maadhimisho ya Maulidi yanaingia katika makatazo haya ya jumla yaliyotajwa

katika Aayah hii tukufu. Si Allaah wala Mtume Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam) hakuamrisha kitendo hichi. Yule ambaye kaamrisha hili, ni yule ambaye

kalizusha, yaani ni mfalme wa Arbil3. Wale ambao wanasherehekea Maulidi

wanamfuata mfalme wa Arbil na wanafanya yale Aliyokataza Allaah pale

wanapofuata wengine badala Yake.

ين ما ل يأذن به الل ه ن الد أم لم شركاء شرعوا لم م

“Je, wanao washirika waliowaamuru (Shari’ah ya) Dini ambayo Allaah

Hakuitolea idhini?” (42:21)

Sherehe ya Maulidi inaingia katika makatazo haya ya jumla yaliyokatazwa

katika Aayah hii tukufu. Allaah (Ta´ala) Hakuweka kitendo hichi katika

Shari´ah. Ni mfalme Arbil ndio kaiweka. Wale wenye kusherehekea Maulidi

wanafuata sheria ambayo Allaah Hakuitolea idhini. Isitoshe, maadhimisho ya

Maulidi yanapingana pia na Sunnah. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi

wa sallam) kasema:

“Shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifah wangu waongofu

baada yangu. Ziumeni kwa magego yenu. Na tahadharini na mambo mepya ya

kuzusha, kwa hakika kila jambo lenye kuzushwa ni Bid´ah na kila Bid´ah ni

upotofu.”

Maadhimisho ya Maulidi sio katika Sunnah ya Mtume wa Allaah (Swalla

Allaahu 'alayhi wa sallam) na Makhalifah wake. Kitendo hichi ni katika mambo

3 http://en.wikipedia.org/wiki/Erbil

Page 11: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

11

yaliyozushwa na hivyo yanaingia katika yale ambayo Mtume wa Allaah (Swalla

Allaahu 'alayhi wa sallam) aliyokataza.

Maadhimisho ya Maulidi yanapingana hata na matendo ya Waislamu kwa

miaka 600. Ni jambo linalojulikana ya kwamba ilikuwa ni mfalme wa Arbil ndio

mtu wa kwanza kuyasherehekea Maulidi. Aliyafanya Maulidi kuwa sherehe ya

kuadhimishwa kila mwaka. Yalizushwa mwisho wa karne ya sita au mwanzo

wa karne ya saba. Kabla ya hili ilikuwa ni kitendo kisichojulikana kwa

Waislamu. Lau kama kungekuwepo mazuri yoyote katika kitendo hichi basi

Maswahabah wangeliyafanya. Hakuna watu waliokuwa na hima katika

matendo mazuri kama Maswahabah. Hakuna mtu yeyote katika Ummah huu

ampendae Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kama Maswahabah.

Hakuna mtu yeyote ashikamanae na kufuata Sunnah zake kama Maswahabah.

Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kasema kuwa kundi

lililookoka ni lile linalofuata yale ambayo yeye na Maswahabah wake

wanayofuata.

Mwandishi: 'Allaamah Hamuud bin 'Abdillaah at-Tuwayjiriy

ar-Radd al-Qawiy, uk. 122-123

5. Ibn Hajar Kuhusu Bid´ah Nzuri Ya Maadhimisho Ya

Maulidi

Vilevile kama alivyonukuu as-Suyuutwiy, anasema Ibn Hajar kwanza kuwa

sherehe ya Maulidi ni Bid´ah ambayo haikuthibiti kutoka kwa Salaf yoyote.

Sentensi hii ya Ibn Hajar inatosha kuyahukumu Maulidi. Yangelikuwa mazuri,

Maswahabah, waliokuja baada yao, na maimamu baada yao

wangeliyasherehekea. Kisha Ibn Hajar akasema:

"Lakini ikiwa jambo hili lina mazuri na mabaya, hivyo ni Bid´ah nzuri ikiwa mtu

atafanya hayo mambo mazuri na kuepuka hayo mabaya na vinginevyo hapana."

Kasema pia:

Page 12: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

12

"Naamini ya kwamba jambo hili lina msingi imara. al-Bukhaariy na Muslim

wamepokea ya kwamba wakati Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)

alipoenda al-Madiynah, alikuta Mayahudi wanafunga siku ya Aashuura´.

Akawauliza kuhusu hilo na wao wakasema wanafunga siku hiyo kumshukuru

Allaah kwa kumuokoa Muusa na kumuangamiza Fir´awn siku hiyo. Kutokana

na hili, tunapata kujua ya kwamba ni sahihi kumshukuru Allaah kwa siku fulani

Kaneemesha au Kuondosha mabaya na kwamba inaweza kufanywa siku hiyo

hiyo mwaka baada ya mwaka. "

Ambayo anasema Ibn Hajar yanaradiwa na maneno yake ya kwanza, nayo ni

kwamba sherehe ya Maulidi ni Bid´ah ambayo haikuthibiti kutoka kwa Salaf

yoyote. Nimekwishataja Aayah na Hadiyth zinazokataza na kutahadharisha

Bid´ah na kubainisha kwamba hayakubaliwi. Kuna Radd ya kutosha kwa

maneno ya mwisho ya Ibn Hajar.

Mwandishi: 'Allaamah Hamuud bin 'Abdillaah at-Tuwayjiriy

ar-Radd al-Qawiy, uk. 30-31

6. Maadhimisho Ya Maulidi Ni Kujifananisha Na

Manaswara

Kuhusu nukuu ya ar-Rifaa'iy ya as-Sakhaawiy ambaye amesema:

"Ikiwa wakristo wamefanya Krismasi kuwa sikukuu, Waislamu wana haki zaidi

juu yake kwa Mtume wao."

hakuna shaka kwamba maadhimisho ya Maulidi yamejengeka juu ya

kujifananisha na manaswara ambao wamechukua kuzaliwa kwa Masiyh kuwa

ni sikukuu. Hili linathibitisha maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam):

"Mtafuata desturi (mwenendo) za waliokuwa kabla yenu shibri kwa shibri na

pima kwa pima hata wakiingia katika shimo la mburukenge (yaani ndani ya

shimo lenye mnyama anayeweza kukudhuru) mutaingia nao.” Tukasema: “Je,

Page 13: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

13

unakusudia mayahudi na manasara?” Akasema: “Ni nani wengine ikiwa si

wao?"

Imepokelewa na Imaam Ahmad, al-Bukhaariy na Muslim kutoka kwa Abu

Sa'iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu 'anhu).

Wakati mtu anajua kuwa maadhimisho ya Maulidi ya wajinga msingi wake

umejengeka juu ya kujifananisha na manaswara, basi mtu anapaswa pia kujua

kwamba imekatazwa vikali kujifananisha na manaswara na washirikina. Mtume

(Salla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema:

“Yule anayejifananisha na watu basi [mtu huyo] ni katika wao.”

Imepokelewa na Imaam Ahmad na Abu Daawuud kutoka kwa 'Abdullaah bin

'Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa).

Mwandishi: 'Allaamah Hamuud bin 'Abdillaah at-Tuwayjiriy

ar-Radd al-Qawiy, uk. 25-26

7. as-Suyuutwiy Asemae Maadhimisho Ya Maulidi

Ni Bid´ah Nzuri

Kuhusiana na nukuu ya ar-Rifaa'iy ya as-Suyuutwiy ambaye kasema:

"Maulidi ni katika Bid´ah nzuri ambayo mtu hupewa thawabu juu yake."

maneno ya as-Suyuutwiy yanaradiwa na maneno ya Mtume (Swalla Allaahu

'alayhi wa sallam):

"Na shari ya mambo ni [mambo] ya kuzua."

na:

"Kila Bid´ah ni upotofu, na kila upotofu ni Motoni."

na:

Page 14: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

14

"Yule ambaye atafanya ´amali isiyokuwa humo na mri yetu atarudishiwa

mwenyewe."

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kaeleza Bid´ah kuwa ovu na upotofu.

Sifa hizi ni mbaya na zimekatazwa. Yeye (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)

kaeleza pia kwamba matendo yao yanatupiliwa mbali na kwamba yanaingia

Motoni. Hii ni dalili ioneshayo ya kwamba mtu wa Bid´ah hapewi ujira kwa

Bid´ah yake. Badala yake, kuna khatari ya kupata mtihani na adhabu chungu.

Allaah (Ta´ala) Kasema:

نة أو يصيب هم عذاب أليم ف ليحذر الذين يالفون عن أمره أن تصيب هم فت

“Basi watahadhari wale wanaokhalifu amri yake, isije kuwasibu fitnah au

ikawasibu adhabu iumizayo.” (24:63)

Aidha, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kasema:

"Kila Bid´ah ni upotofu, na kila upotofu ni Motoni."

Mtu anapewa ujira tu wakati anamfuata Mjumbe (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam) na kuipa kipaumbele uongofu wake kabla ya kila kitu kingine. Allaah

(Ta´ala) Kasema:

بون الل ه فاتبعون يببكم الل ه وي غفر لكم ذنوبكم والل ه غفور رحيم قل إن كنتم ت

”Sema (ee Muhammad صلى هللا عليه وآله وسلم): “Mkiwa mnampenda Allaah, basi

nifuateni, Atakupendeni Allaah na Atakughufurieni dhambi zenu. Na

Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufiria - Mwenye kurehemu).”

(03:31)

ي الذي ي ؤمن بالل ه وكلماته واتبعوه لعلكم ت هتدو ن فآمنوا بالل ه ورسوله النب الم

”Basi mwaminini Allaah na Mtume Wake, an-Nabiyyi al-Ummiyy (Mtume

Muhammad صلى اهلل عليه وآله وسلم asiyejua kusoma wala kuandika) ambaye

anamwamini Allaah na Maneno Yake, na mfuateni ili mpate kuongoka.” (07:158)

Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala) Kafanya watu kupata sehemu ya mapenzi Yake,

uongofu wake na msamaha wake ikiwa tu watamchukua Mtume (Swalla

Allaahu 'alayhi wa sallam) kama mfano mzuri wa kuigwa. Maadhimisho ya

Maulidi sio katika uongofu wala Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam). Ni katika uongofu na Sunnah ya mtawala Irbil na aliishi takriban miaka

600 baada ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam).

Page 15: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

15

Mwandishi: 'Allaamah Hamuud bin 'Abdillaah at-Tuwayjiriy

ar-Radd al-Qawiy, uk. 29

8. Shaytwaan Anapenda Sherehe Ya Maulidi

Shaytwaan hufurahia maadhimisho ya Maulidi wakati Bid´ah zote ni katika

matendo na upambiaji wa Shaytwaan. Hakuna shaka ya kwamba Shaytwaan

hufurahia Waislamu kufanya Bid´ah anazowachochea. Ibn-ul-Jawziy kapokea ya

kwamba Sufyaan ath-Thawriy kasema:

"Ibliys anapenda Bid´ah zaidi kuliko dhambi. Mtu hutubia kwa dhambi tofauti

na Bid´ah."

Dalili ya kuwa Bid´ah zote katika Dini ni katika matendo ya Shaytwaan ni

kwamba Allaah (Ta´ala) Katueleza ya kuwa Shaytwaan kasema:

هم ولضلن

”Na hakika nitawapoteza.” (04:119)

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kasema:

"Na shari ya mambo ni [mambo] ya kuzua, na kila Bid´ah ni upotofu."

Aayah na Hadiyth Swahiyh zinatoa dalili kwamba Bid´ah za Dini ni katika

upotofu wa Shaytwaan.

Mwandishi: 'Allaamah Hamuud bin 'Abdillaah at-Tuwayjiriy

ar-Radd al-Qawiy, uk. 24-25

Page 16: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

16

9. Imaam al-Albaaniy Kuhusu Maadhimisho Ya Maulidi

Imaam al-Albaaniy:

Maulidi yanayofanywa Iraaq, Oman au Syria, kwa hakika ni katika mambo

yaliyozuliwa. Kule kutenga siku maalum, na kuiita “Sherehe ya Maulidi ya

Mtume”, hili bila ya shaka ni katika mambo yaliyozuliwa.

Isitoshe, kuna mukhaalafah4 mwingi katika yanayofanywa katika sherehe hii. Kwa

mfano kunatokea mukhaalafah wa Kishari´ah mwingine, mukhaalafah unazidi.

Ama kwa mfano kunafanywa mihadhara, katika mihadhara hii

wakakumbushana kitu katika Siyrah na Sunnah ya Mtume, hili bila ya shaka

ingekuwa ni kheri kubwa kuliko kutenga siku ya Maulidi [kuzaliwa kwake].

Lakini pamoja na hivyo, haijuzu kutenga mwezi maalum au siku maalum

kusherehekea Maulidi hata kama itakuwa sherehe hii haina ndani yake

mukhaalafah unaokwenda kinyume na Shari´ah.

Muulizaji:

Katika sherehe hii huletwa vyakula Shaykh.

Imaam al-Albaaniy:

Kila kinachofanywa katika mwezi huu, ni katika mambo yaliyozuliwa.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=7wdda0LQDRo

10. Je Mtume (´alayhis-Salaam) Anahudhuria Katika

Sherehe Ya Maulidi?

4 Mambo yanayofanywa yanayokwenda kinyume na Qur-aan na Sunnah.

Page 17: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

17

Baadhi ya watu wanaamini ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa

sallam) anahudhuria wakati wa sherehe ya Maulidi. Hii ndio sababu ya wao

kumkaribisha huko. Jambo hili ni katika uongo mkubwa sana na ujinga wa

kuchukiza. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) hatotoka nje ya kaburi

lake mpaka Siku ya Qiyaamah. Hana mawasiliano na mtu yoyote. Hahudhurii

katika mkusanyiko wowote. Bado yuko katika kaburi lake mpaka Siku ya

Qiyaamah. Nafsi yake iko kwa Mola katika jamii ya juu, katika makazi ya

maisha ya kupendeza. Allaah (Ta´ala) Kasema katika Suurat "al-Mu'minuun":

ثم إنكم بعد ذلك لميتون ثم إنكم يوم القيامة تبعثون

“Kisha nyinyi baada ya hayo, ni wenye kufa. Kisha hakika nyinyi Siku ya

Qiyaamah mtafufuliwa.”(23:15-16)

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kasema:

"Mimi ndo mtu wa kwanza atakayetoka ndani ya kaburi siku ya Qiyaamah.

Mimi ndo muombezi wa kwanza. Mimi ndo wa kwanza ambaye shafaa´ah

uombezi wake utakubaliwa. "

Ninaomba baraka na salaam za Mola Wake ziwe pamoja naye.

Aayah na Hadiyth hii tukufu - na Aayah na Hadiyth zingine – zinatoa dalili ya

kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) na wengine wote wamekufa

au watakufa. Watatoka katika makaburi yao siku ya Qiyaamah. Suala hili

wamekubaliana juu yake wanachuoni wa Waislamu. Kwa hivyo, Waislamu wote

wanatakiwa kuzingatia masuala haya. Aidha, ni lazima watahadhari na Bid´ah

na ukhurafi wa watu wajinga na mfano wao waliozusha. Allaah Hakuteremsha

dalili yoyote kuhusiana na masuala haya.

Mwandishi: Imaam 'Abdul-' Aziyz bin 'Abdillaah bin Baaz

Fataawaa Arkan-ul-Islam, uk. 109-110

Daar-ud-Daa'iy, 1420

11. Hukumu Ya Kusherehekea Maulidi Msikitini

Page 18: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

18

Swali:

Inajuzu kwa Waislamu kusherehekea sikukuu katika Misikiti kumbukumbu ya

usiku wa Maulidi [kuzaliwa] kwa Mtume katika tarehe ya kumi na mbili Rabiy'

al-Awwal bila ya kuzembea katika siku hii kama mtu alivyo siku ya 'Iyd?

Tulipata maoni tofauti katika suala hili na baadhi ya wengine wakasema kuwa ni

Bid'ah nzuri wakati baadhi wakasema sio Bid'ah nzuri.

´Allaamah Ibn Baaz:

Haijuzu kwa Waislamu kusherehekea siku ya Maulidi ya Mtume (Swalla

Allaahu 'alayhi wa sallam), sawa ikiwa yatafanyika tarehe kumi na mbili Rabiy'

al-Awwal au siku nyingine yoyote, kama jinsi haijuzu kusherehekea kuzaliwa

kwa mtu mwengine yeyote. Kusherehekea kuzaliwa ni Bid'ah katika Dini.

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) hakusherehekea kuzaliwa kwake

katika maisha yake na yeye ni mjuzi zaidi wa Mola katika Dini na Shari´ah.

Hakuamrisha hilo na wala halikufanywa hilo na Makhalifah wake waongofu,

Maswahabah wengine au mtu mwingine katika wao ambaye kawafuata kwa

wema miongoni mwa karne tatu bora. Kutokana na hili mtu anapata kujua ya

kwamba jambo hili ni Bid'ah. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kasema:

"Yule mwenye kuzusha kitu kisichokuwa humo na amri yetu kitarudishwa." (al-

Bukhaariy (2697) na Muslim (1718).)

Katika mapokezi mengine ya Swahiyh Muslim kumesemwa:

"Yule ambaye atafanya ´amali isiyokuwa humo na amri yetu atarudishiwa

mwenyewe."

Imaam 'Abdul-'Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

Fataawaaa al-´Ulamaa´ Balad al-Haraam, uk. 467

Page 19: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

19

12. Shaykh Ibn ´Uthaymiyn Akiwaombea Du´aa Waliopotea

Katika Bid´ah Ya Maulidi

Swali:

Wanadai watu hawa ya kwamba wanampenda Mtume, wakaleta sherehe ya

Maulidi. Ipi hukumu ya kusherehekea Maulidi kwa vile wao wanadai ya

kwamba ni kumpenda Mtume?

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Hili swali limeshaulizwa sana nikalijibu. Mwenye kumpenda Mtume, basi afuate

Sunnah zake. Mwenye kumpenda Mtume, basi asizue katika Dini ya

Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Na wala haifai juu yetu wala

kwa mwengine [... sauti haiko wazi... ] kwa Mtume na ubainisho.

Tunachowaombea kwa Allaah (Ta´ala) Awaongoze ndugu zetu katika Njia

iliyonyooka.

Yaa Subhaana Allaah! Yuko wapi Abu Bakr, ´Umar, ´Uthmaan, ´Aliy,

Maswahabah katika jambo hili au hawakuyajua au waliyapuuza? Ni moja katika

mambo haya; ima hawakujua haki ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

kwa kutofanya kwao Maulidi au walipuuza. Karne tatu [bora] zote zinapita

hawakufanya Bid´ah hii halafu tunasema kuwa yanajuzu na kwamba

yanapendwa na Allaah na Mtume Wake na wanayoyafanya? Haiwezekani.

Isitoshe, Maulidini kunatokea maovu makubwa na kuchupa mipaka kwa Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kuna mambo mengi.

Tunamuomba Allaah (Ta´ala) Aturuzuku sote kumfuata Mtume, Imani

isiyokuwa ndani yake na mapungufu, yakini isiyokuwa ndani yake na shaka,

Ikhlaasw isiyokuwa ndani yake Shirki, kufuata kusiokuwa ndani yake na kuzua.

Chanzo: http://youtu.be/EBbhs_vJOdE

Page 20: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

20

Wanachuoni Wa Khalaf

13. Inajuzu Kusherehekea Maulidi Kama Ada Tu Na

Si ´Ibaadah?

Swali:

Sisi tunasherehekea siku ya Maulidi kama ada na hapana ´Ibaadah?

Shaykh as-Suhaymiy:

Bali kwa watu wengine ni ´Ibaadah; wanasoma, wanamdhukuru, wanasoma

mashairi na Anashiyd. Yote haya wanayafanya... Hata ikiwa mnayafanya kama

ada, je Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walifanya kuwa ada?

ابقون سان والس بعوهم بإحأ نصار والذين ات مهاجرين والأ لون من الأ و الأ

"Na wale waliotangulia awali (katika Uislamu) miongoni mwa Muhaajiriyn

(waliohajiri kutoka Makkah), na Answaar (waliowasaida na kuwanusuru

Muhaajiriyn katika wakaazi wa Madiynah), na wale waliowafuata kwa ihsaan."

(09:100)

Kuwa katika wale waliowafuata kwa wema.

Chanzo: http://youtu.be/r2ZckS6aH6c

14. Maulidi Hayakufanywa Na Mtume Wala Maswahabah

Swali:

Page 21: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

21

Ipi hukumu ya kusherehekea Maulidi ya Mtume?

´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh:

Sisi tunasema, kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni msingi

katika mambo ya msingi ya Dini na ni katika mambo yanakamilisha Dini.

“Hatoamini mmoja wenu mpaka mimi niwe napendwa kwake zaidi kuliko

watoto wake, wazazi wake na watu wote.”

Waislamu wanajua hilo. Sherehe ya Maulidi tukiangalia asli yake haikupatikana

isipokuwa baada ya karne tatu bora. Imekuja kupatikana katika karne ya tano au

baada yake. Na wala hayakuwa hata yakitajwa katika karne ya kwanza, ya pili

wala ya tatu. Na wala Maswahabah na waliokuwa baada yao hawakuwa

wakiyajali: Abu Bakr, ´Umar, ´Uthmaan na ´Aliy walikuwa wakijua usiku wa

Maulidi [kuzaliwa] na kufa kwa Mtume lakini hawakuyajali. Na wala hakufanya

siku ya kumi na mbili [Rabiy´ al-Awwal] Khutbah, kusoma, ukumbusho na

Qaswiydah. Hawakufanya haya. Haina maana walipunguza katika haki za

Mtume, lakini hawakuwa na msingi wanaoutegemea.

Msiba ni kwamba, kuna baadhi ya Suufiyyah wanafanya makosa makubwa. Na

kama mlisikia mkanda kuhusu Maulidi, ni mambo maovu sana kukiwemo

taarabu na nyimbo yanayofanywa ambayo Mtume yuko mbali nayo.

Kisha usiku wa mwisho, wanaamini ya kwamba roho ya Mtume inawahudhuria

na kwamba wanaona roho yake na kadhalika katika mambo ya ukhurafi na

uongo na batili. Kunaimbwa Qaswiydah za Shirki kumsifu Mtume na

kumuomba shafaa´ah uombezi kutoka kwake n.k. Mtume yuko mbali kabisa na

yote haya.

Enyi ndugu zangu! Kumpenda Mtume wa Allaah ni kufuata Sunnah zake.

Kumsifu Mtume wetu si katika siku maalum, hapana! Bali ni katika kila siku;

katika kula kwetu, kunywa kwetu, Swalah yetu, Wudhuu wetu, kutembea

kwetu na katika harakati zetu zote. Usitenge siku maalum. Bali ni jambo la

daima na milele. Swalah na salaam zimwendee.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=55y01uXEDv4

Page 22: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

22

15. Tofauti Kati Ya Sherehe Ya Maulidi Na Siku Ya Taifa

Swali:

Baadhi ya watu wanaona kujuzu kusherehekea Maulidi, licha ya kwamba

yamezushwa, wanasema ni sawa na sherehe zingine zinazoadhimishwa kama

vile Siku ya Taifa.

´Allaamah al-Fawzaan:

Sherehe ya Maulidi ni jambo la kidini na huchukuliwa ni Bid´ah. Ama kuhusiana

na Siku ya Taifa, huku ni kujifananisha na makafiri ambao wanaadhimisha siku

zao za kitaifa na sherehe. Ina maana ni kujifananisha nao. Mtume (Swalla

Allaahu 'alayhi wa sallam) kasema:

"Yule mwenye kujifananisha na watu basi [mtu huyo] ni katika wao."

'Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzan

Mhadhara: al-Fitan wa Mawqif-ul-Muslim Minhaa

Chanzo: http://alfawzan.ws/allmohadrat?page=2

16. Maulidi Yana Bid´ah Na Shirki

Swali:

Je, Bid´ah ya kusherehekea Maulidi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) ni Bid´ah khafifu inayotujuzushia kukaa na wanayoifanya au hapana?

Page 23: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

23

´Allaamah al-Fawzaan:

Kusherehekea Maulidi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Bid´ah

bila ya shaka. Kwa kuwa ni kitendo ambacho hakikufanya Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam), Makhalifah wake waongofu wala karne bora. Wala

hayakuzushwa isipokuwa baada ya karne ya nne, wakati utawala wa

Faatwimiyyuun, ambao ni Mashia wanaotoka magharibi. Wao ndio walikuja na

Bid´ah ya Maulidi. Hivyo ni Bid´ah bila ya shaka.

Isitoshe, yanaingia kitu katika Shirki, nayo ni kumuomba msaada Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuomba atatue haja na kumshtakia kwa

mambo yaliowasibu Waislamu. Wanamshtakia Mtume na wala hawamshtakii

Allaah (Jalla wa ´Alaa). Na wala hawamuombi msaada Allaah, wanamuomba

msaada Mtume katika mnasaba huu. Na wao wanajua ya kwamba hutokea kitu

katika haya. Hivyo yamejumuisha baina ya Bid´ah na baina ya Shirki.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/alldroos?tid_1=164 &

http://www.youtube.com/watch?v=zC27-UOohPY

17. Kupeana Hongera Siku Ya Maulidi

Swali:

Je, inajuzu kupeana hongera siku ya Maulidi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kila Bid´ah haijuzu kuifanya na wala haijuzu kupeana hongera kwayo, kwa

kuwa kupeana hongera ni kuiridhia na kuishaji´isha5. Na wajibu ni kinyume

chake, kukataza na si kupeana hongera.

5 Kuipa nguvu

Page 24: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

24

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/alldroos?tid_1=240 &

http://www.youtube.com/watch?v=clh2iXpO-hE

18. Kufanya Maulidi Ni Bid´ah

´Allaamah al-Luhaydaan:

Bila ya shaka, kufanya Maulidi ni Bid´ah. Kwa hakika haya Maulidi hayajulikani

kuwepo kwake katika uhai wa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam), wala katika uhai wa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum), wala

katika uhai wa Taabi´iyn6, wala katika uhai wa maimamu wanne, wala uhai wa

wanafunzi wao. Hayakujulikana katika ulimwengu wa Uislamu kitu

kinachoitwa Maulidi kabisa. Sehemu ya kwanza yalipopatikana ni Misri,

yalizusha na Faatwimiyyuun, dola iliyokuwa chafu ya maovu; al-Baatwiniyyah.

Na yalipoanza kusambaa, katika watu wa Ahl-us-Sunnah mtu wa kwanza

aliyeanza kuyasambaza ni mfalme aitwae Irbil Iraaq kutokana na ujinga wake

wa kuwaiga manaswara ambao na wao wanaadhimisha siku ya ´Iysa (´alayhis-

Salaam). Wakakataza wanachuoni hilo. Yakaendelea kukua mpaka yakaenea leo

katika ulimwengu wa Uislamu. Maulidi yanaingia katika maneno ya Mtume:

“Na tahadharini na mambo ya kuzua, kwa hakika kila kitakachozushwa ni

Bid´ah na kila Bid´ah ni upotevu."

Na yanaingia katika maneno ya Mtume:

"Atakayefanya ´amali isiyokuwa humo amri yetu, atarudishiwa."

Mtu asijikurubishe kwa kitu anachokizingatia kuwa ni utiifu na kujikurubisha

kwa Allaah isipokuwa kwa dalili. La sivyo atarudishiwa mwenyewe. Na

kuichukulia siku hii kama ´Iyd, na pengine kukafanywa makubwa zaidi ya

yanayofanywa katika ´Iyd. Mtume alipoenda Madiynah na walikuwa Answaar

na siku ambazo wanasherehekea, akawaambia:

"Allaah Amewapa badala ya sikukuu za Kijaahiliyyah, Amewapa Idi al-Fitwr na

Id-ul-Adhhaa."

6 Waliokuja baada ya Maswahabah

Page 25: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

25

Chanzo:

http://www.alharamain.gov.sa/index.cfm?do=cms.scholarsubject&schid=30981

& http://www.youtube.com/watch?v=etf2lUZSpZA

19. ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Madu´aat Wanaohudhuria

Katika Maulidi

Swali:

Baadhi ya watu wa Bid´ah Suufiyyah na khasa Tijaaniyyah katika mji wetu wana

harakati mbali mbali kwa mnasaba wa kusherehekea Maulidi. Kunakuja baadhi

ya Madu´aat na wanahudhuria nao na wanawaombea mwishoni siha na afya na

Du´aa nyinginezo katika Mashaykh wa Suufiyyah walioandaa mambo haya. Ipi

hukumu ya mambo kama haya na kuhudhuria Madu´aat hao?

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu anaafikiana nao na kuwasifu. Halijuzu hili, halijuzu hili. Isipokuwa tu

wakati tu pale unapohudhuria unawakataza na kuwabainishia kuwa hili

halijuzu na wasifanye mambo haya na si sawa. Walinganie kwa Allaah kabla na

la sivyo jendee zako waache. Usikae nao, unaafikiana, ukala nao chakula

ukapiga nao vijicheko. Ukadai ni kuwalingania [Da´wah]! Hapana katu hii si

Da´wah.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/alldroos?tid_1=252 &

http://www.youtube.com/watch?v=VK1EA5bDcio

20. Kufunga Siku Ya Maulidi Ya Mtume (´alayhis-Salaam)

Page 26: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

26

Swali:

Inajuzu kufunga siku ya kuzaliwa kwa Mtume?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, ni Swawm ambayo Haikuweka Allaah wala Mtume Wake na wala

haikuwekwa kwetu kufunga. Naam, siku ya Juma tatu unafunga, hapana ya

tarehe 12 Rabiy´ al-Awwal - unafunga Juma tatu kwa kila wiki, hii ni Sunnah.

Ama tarehe 12 ya Rabiy´ al-Awwal ikikutana na siku ya Juma tatu

unasherehekea [na kufunga] kwa kuwa imeangukia siku ya Maulidi, hapana

haijuzu hili.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=AZNuq_-Nm7w

21. Je, Kusherehekea Maulidi Ni Katika Kumpenda Mtume

(´alayhis-Salaam)?

Swali:

Je, kusherehekea Maulidi ni katika kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Hili ni katika Bid´ah. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

hapendi Bid´ah.

Kasema:

Page 27: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

27

”Na tahadharini na mambo ya kuzuliwa...”

Mtume hapendi Bid´ah na anaikataza. Vipi utadai ya kwamba unampenda na

hali ya kuwa unamuasi? Unapenda maadui wa mpenzi [Mtume] kisha unadai

unampeda? Mapenzi yako yako wapi?

Na wakasema wengine [washairi]:

”Lau mapenzi yako yangekuwa ya kweli basi ungelimtii, hakika mwenye kupenda kwa

yule ampendae humtii.”

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa

22. Sikukuu Za Makafiri Kama Krismasi Na Za Waislamu

Kama Maulidi

Swali:

Ipi hukumu ya kusherehekea sikukuu, iitwayo "Sikukuu ya manaswara", au

"Krismasi". Ipi nasaza yako kwa Waislamu ambao wanashiriki katika hili na

wanapeana zawadi na kuwapa pongezi n.k.?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu kwa Muislamu kushiriki sikukuu za manaswara - hata sikukuu za

Waislamu ambazo zimezushwa. Kama Maulidi na kadhalika, sherehe ya Maulidi

- haijuzu kwa kuwa ni sherehe za Bid´ah.

Na sikukuu za manaswara ni sikukuu za Bid´ah na Shirki, kwa kuwa wao

hufanya kwa kuitakidi kama ´Ibaadah kwa ´Iysa (´alayhis-Salaam).

Haijuzu kuwashaji´isha kwa hili wala kuwapongeza. Kule kuwapa tu pongezi ni

jambo lisilojuzu. Vipi kwa yule ambaye anahudhuria kwao? Hata kuwauzia,

asiwauzie mtu vifaa ambavyo vitawasaidia kufanya hayo Maulidi. Wala mtu

asiwape pongezi kwayo, wala asiwauzie kwa haya Maulidi na wala asile katika

kichinjo chao. Muislamu anatakiwa awasuse kabisa kwa haya Maulidi.

Page 28: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

28

Kama alivyosema hilo al-´Allaamah Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah na

mwanafunzi wake Ibn-ul-Qayyim katika kitabu "Ahkaam Ahl-idh-Dhimmah."

Ni wajibu kujiweka mbali kuwashiriki katika mambo haya, kwa kuwa haya ni

katika Dini yao. Na sisi tumekatazwa kuwashaji´isha au kuwasaidia katika

Kufuru zao na Shirki zao.

Chanzo: http://youtu.be/-wHD0HfeV18

23. Wajinga Wanaodanganywa Kwamba Kusherehekea

Maulidi Ni Kumpenda Mtume

Swali:

Ipi hukumu ya kusherehekea Maulidi ya Mtume katika Shari´ah ya Kiislamu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hukumu ya kusherehekea Maulidi ya Mtume ni katika Bid´ah kwa Ahl-us-

Sunnah wal-Jamaa´ah na hayakufanywa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) na ni kuzaliwa kwake, maisha yake yote. Na hayakufanywa na

Makhalifah wanne waongofu ambao ni wenye ufahamu zaidi wa Ummah na

wenye kumpenda zaidi Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Na hayakufanywa na Swahabah yoyote katika Maswahabah kamwe, na wala

waliokuja baada yao katika wanachuoni mpaka siku ya Qiyaamah.

Hivyo ni katika Bid´ah ambayo inakuwa na shari ambayo watu hawawezi kuwa

wajinga kwayo, kama mchanganyiko, mashari – burdaa ya al-Buswiyriy7

7 ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu at-Tijaaniyyun Na Burda Swali: Katika mji wetu Tijaniyyuun [kipote cha Mashia na Masufi] wanamrehemu Buswiyriy [Gogo la Suufiy aliyetunga Qaswiydah ya Burdaa, kaburi lake liko ndani ya Msikiti Misri] na wanamtakasa.

Page 29: Kauli Za Ma´ulamaa Kuhusu Maulidi

29

ambayo iko na Shirki na uongo. Wanasema Mtume anadhudhuria pamoja na

wao katika usiku ambao kutakuwa sherehe ya Maulidi wanadai ya kwamba

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anahudhuria usiku ule pamoja nao.

Na huu ni katika uongo kwa Allaah na Mtume Wake (´alayhis-Swalaat was-

Salaam).

Hawa watu wajinga katika Suufiyyah wapotofu na katika watu wajinga ambao

hawana elimu na ambao huwadanganya na kusema ”nyinyi mnampenda

Mtume wa Allaah” kwa kusherehekea kuzaliwa kwake.

Watu watahadhari kutokana na Bid´ah hii ambayo imebainishwa upotofu wake

na wanachuoni wa zamani na wa sasa.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=4e3oXfa-vjk

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na

Maswahabah ajmaa´iyn.

´Allaamah al-Fawzaan: Si katika mji wenu tu, ni kila mahala. Baadhi yao wanasema Burdaa ni bora kuliko hata Qur-aan. Hivyo ndo maana hawaipi umuhimu Qur-aan. Wanaipa umuhimu Burdaa, wanaihifadhi, wanaiimba kila wakati. Huu ni upotevu - A´udhubi Allaah. Huu ni mtihani khasa ukizingatia Burdaa ina baadhi ya maneno maalumu, ya kupambia, kuimbika vizuri. Hii ni fitina - Allaah Atukinge. Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/alldroos?tid_1=252