kimazingira na kijamii na mpango wa...

25
!. viromen-alSc:a MRADI WA UMEME WA GESI YA .. Environmental & Social * Assessment & Management SONGO SONGO . 5: Plan Sum m ary - Sw ahili -- --- ------------ -- - ---- - ---- - ------- -- --- -------------- -- -- ------------------------------ ::Plan Summary - Swahili *: - - ------ O TATHMINI ZA KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI 0 14 ~~~~Muhtasari wa Tafirti za Athari za Kimazingira na Mpango wa Kina wa Udhibiti Oktoba 2001 E65 v.2 October 2001 9. 9. .-. 0- ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ *. .. , _ ;d.-- - v-~ = -- l . . ,= D i (_ -t * . .,.,. .( * 0 . . ,:;5! . i½. ' . ,' ' 'o P y .. ~~ :. .... -i, .. :.E, ......... .. : .q :.;,-.. . . S.. " ':y,, .D ,,,,s, 0 N;~~~('~~igu 0* Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized

Upload: others

Post on 10-Feb-2020

14 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

!. viromen-alSc:a MRADI WA UMEME WA GESI YA.. Environmental & Social

* Assessment & Management SONGO SONGO. 5: Plan Sum m ary - Sw ahili -- --- ------------ -- - ---- - ---- - ------- - - --- -------------- - - - - ------------------------------::Plan Summary - Swahili

*: - - ------ O TATHMINI ZAKIMAZINGIRA NA

KIJAMII NA MPANGOWA UDHIBITI

0 14 ~~~~Muhtasari wa Tafirti za Athari za Kimazingira na Mpangowa Kina wa Udhibiti

Oktoba 2001

E65 v.2October 2001

9.

9. .-.

0- ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~

*. .. , _ ;d.-- - v-~ = --l . . ,= D i (_ -t

* . .,.,. . ( * 0 .

. ,:;5! .i½. ' . ,' ' 'o P y

.. ~~ :. .... -i, ..:.E, ......... . .: .q :.;,-..

. .

S..

" ':y,, .D ,,,,s, 0 N;~~~('~~igu

0*

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

Pub

lic D

iscl

osur

e A

utho

rized

TATHMINI ZA KIMAZINGIRA NA KIIAMI NA MPANGOWA UDHIBITI

Oongas

Mradi wa Umeme wa Gesi ya Songo Songo

TA-HMINI Z KIMAZINGIR NA KIJAMII NA HMANGO WA UDuIBITI

Congas

Mradi wa Umeme wa Gesi ya Songo Songo

Tathmini za Kimazingira na Kijamii na Mpango wa Udhibiti

Muhtasari waTafiti zaAthari za Kimazingira na Mpango wa Kina wa Udhibiti

Oktoba 2001

Kampuni ya Songas

Nyumba ya Maarifa

Mtaa wa Ohio

Dar es Salaam

Simu: +255-22-21 1-7313

Faksi: +255-22-21 1-3614

www.songas.com

[email protected]

TATHmINI ZA KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

Mombasa- ,

Tanga,.Pernba

-~i1. -ZANZI BAR

I_____ 1'

__ I - ~~~~~Unguia

F____ Kh ha $Ka arLi -SMtambowaurjmc rvU DAR ES SALAAM

Mkuranga O'0

Mazomorao

_ ~~~~BunguO , ,-- ~NgulakulaVSW0

I. ! --4 -! - _ i,- ,0 ,AVYAMAFIA zMbvera _

Sormanga Visima vya GesinaMtarbowa a:

Kitwa Kivinieo Kusafisha Gsi <

Kitwa hlasokoLindi

Mitwara '

(Gesi iliyogunduliwa Mnazi Bay)

Ramani 1: Eneo la Mradi wa Gesi ya Songosongo

2

TATHMINI ZA KIMAZING,RA NA KIJAmII NA MPANGO WA UDHIBITI

SURAYA

UfupishoGesi asilia iligunduliwa mwaka 1974 katika kisiwa cha Songo Songo kilicho nje kidogo ya pwani ya

mashariki mwa Tanzania. Mradi wa gesi ya Songo Songo kuzalisha umeme umepangwa kuendeleza

na kuuza raslimali ya gesi asilia nchini Tanzania.

Wadhamini wa sekta binafsi wa mradi wa Songo Songo ni Shirika laAES na Kampuni ya Nishati

ya PanAfrica. Kampuni ya utekelezaji inaitwa Songas Limited (Songas), ambayo ni kampuni binafsi

kwa asilimia kubwa na imesajiliwa kwa mujibu wa sheria yaTanzania.Washiriki wa Mitaji wa CDC

pamoja na Shirika la Maendeleo ya Fedha laTanzania (TDFL) ni wawekezaji wa hisa pia.

Wakopeshaji wa mradi huu ni Benki ya Dunia na Benki yaWawekezaii ya Ulaya.

Maelezo kuhusu MradiMradi utatoa gesi asilia kutoka kwenye visima vya gesi huko Songo Songo na kuipeleka kwenye

mtambo wa kuzalisha umeme wa Ubungo unaoendeshwa na Shirika la Umeme Tanzania

(TANESCO).Vilevile gesi itapelekwa kwenye kiwanda cha Saruji chaWazo, jijini Dar-es-Salaam.

Eneo lote la mradi limeonyeshwa kwenye ramani namba 1.

Sehemu kuu za mradi ni pamoja na:(i) visima vya gesi katika kisiwa cha Songo Songo (tazama picha ukurasa 3);

(ii) mfumo wa kukusanya gesi na kiwanda cha kuisafisha katika kisiwa cha Songo Songo;

(iii)kilomita 25 za bomba litakalolazwa chini ya maji kutoka kisiwa cha Songo Songo hadi

Somanga Funga na kilomita 207 za bomba litakalozikwa ardhini kutoka Somanga Funga hadi

Dar-es-Salaam;

(iv)kilomita 16 za bomba kuelekea kiwanda cha Saruji chaWazo;

(v) mitambo ya kuzalisha umeme (tabaini) iliyoko kwenye kituo cha umeme cha Ubungo yenye

uwezo wa kuzalisha megawati 112 za umeme na yenye uwezo wa kutumia gesi asilia;

(vi)udhibiti wa mfumo, kituo cha uendeshaji na miundombinu mingineyo pale Ubungo, na

(vii)utawala na mafunzo kwa mradi.

Ahadi za Songas za masuala ya mazingira na kijamiiSongas, kwa kupitia wafadhili wake pamoia na Serikali yaTanzania, inakusudia kwa dhati kuendeleza

mradi wa Songo Songo kwa utaratibu ambao utaweka mizania (wakati wote na kwa kuwajibika)

kati ya uhifadhi wa mazingira na sura ya kijamii ya Tanzania na uondoaji wa umaskini na faida za

kiuendeshaji za mradi. Kwa kutumia filosofia hii na mwelekeo huu, Songas itadumisha fursa bora

na za muda mrefu za kibiashara kwa ajili ya wadhamini wa mradi huu na maslahi yanayoambatana

nayo ya washikadau wa nchi, kanda, na mahali ambapo mradi unatekelezwa.

AES, kampuni inayoongoza kwa hisa, ina sera ya kuchangia hadi asilima 5 (5%) ya mapato halisi

kwa ajili ya maendeleo ya jamii. Maamuzi yanayohusiana na kiwango na mahali ambapo msaada uta-

tolewa umeachiwa mameneja wa zaidi ya mitambo ya umeme 125 inayoendeshwa na kampuni ya

AES duniani kote. Kwa makubaliano na wanahisa wengine wa Songas, kampuni ya Songas itaanzisha

TATHMINI ZA KIMAZINGIRA NA KI.AMII NA MPANGOWA UDHIBITI

Kisima cha Gesi cha Nchi Kavu

i- - A - ;_____- - I__C

__

_ __ S _ |~~S

|~~~~~~ ~ _

-

Kisima cha Gesi cha Baharini

3

TATHiM NI ZA KImAZINGIRA NA KrJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

sera kama hiyo nchini Tanzania. Mwezi Juni mwaka 2000, sheria ya kodi ya Tanzania ilibadilishwa,

hivyo kuipa moyo zaidi Songas kuchangia maendeleo ya kijamii nchini Tanzania.

Sera na Masharti ya Kiurekebishaji na ya KisheriaMradi wa Songo Songo umeandaliwa na utaendeshwa kwa kulingana na matakwa ya kanuni na she-

ria, ikiwa ni pamoja na zile za Serikali yaTanzania na Benki ya Dunia.

Mashauriano na Uarifu wa UmmaSehemu muhimu tatu za mradi wa Songo Songo, tayari zimekamilika. Mafanikio ya sehemu hizi

ndogo tatu za mradi yanaonyesha mawasiliano mazuri ya Songas na mashauriano yenye mafanikio

kati yake na watu waliothirika na mradi. Mradi wa Songo Songo unafahamika sana na umma wa

Tanzania na umeelezewa vizuri sana katika magazeti, redio na televisheni. Songas imepanga kuen-

delea kuwasiliana vizuri na washikadau wote na watu walioathirika na mradi ili kuwe na taarifa

sahihi zinazotolewa kwa washirika wote kuhusiana na mradi.

Zaidi ya kuwepo kwa majadiliano mengi na umma pamoja na tathmini, Songas imekubaliana na

masharti rasmi ya uarifu ya Benki ya Dunia kwa ajili ya tathmini za mazingira kwa kutoa taarifa zake

kwa Kitengo chaTaarifa cha Benki ya Dunia na hapa nchini. Kwa kuzingatia hilo, ripoti yaThathmini

za Mazingira na Kijamii na Mpango wa Udhibiti, ilisambazwa kwa washikadau wote ndani na nje

ya Tanzania.

1 - 1_ ; J

_N~L ,

4~~

_ F~~~~~71_

Mkutano wa wananchi walioathirika na Mradi

TATHMINI zA KIMAZNGIRA NA KilAmii NA MPANGO WA UDHIlM

Upembuaji waVibadala na Uteuzi wa NjiaSongas imechunguza vibadala vingi, ikiwa ni pamoja na njia mbadala za kuzalisha umeme, umbo

mbadala la mradi, na njia mbadala za bomba la majini na la nchi kavu ili kufikia mfumo unaokubali-

ka na usio na gharama kubwa.

Muhtasari waTafiti za Kimazingira na KijamiiKatika kuupa mwega mradi wa Songo Songo, Songas imegharamia utayarishaji wa ripoti maalum

zipatazo 28 zinazohusu mazingira na mada nyingine za kijamii tangu 1993. Kama ilivyodokezwa, kazi

hii ilifanywa i1i kutekeleza masharti ya tathmini ya Benki ya Dunia na Sekta mbalimbali zaTanzania

zinazohusiana na mazingira na wajibu wa kijamii. Kwa ufupi, ripoti hizo zinapendekeza kuwa mradi

hautakuwa na athari mbaya za kimazingira na kijamii kama Songas na makandarasi wake wakubwa

na wadogo watatekeleza hatua za kupunguza makali zilizopendekezwa, kusimamia na kufuatilia

hatua hizo.

Athari za Kimazingira na Kijamii na Mpango wa UdhibitiSongas inakusudia kutumia "mwenendo bora" wa kimataifa katika udhibiti wa athari za kimazingi-

ra na kijamii za mradi wa gesi ya Songo Songo wa kuzalisha umeme. Songas itasanifu, kuunda na

kuendesha mradi na kutekeleza mfumo wa usimamizi wa mazingira, afya na usalama ambao

umeegemea kanuni za Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO), ISO 14001.

Muundo wa Utawala wa SongasSongas itakuwa na wajibu kamili kwa mambo yote yanayohusu mradi wa Songo Songo kwa kutu-

mia timu ya uongozi yenye uzoefu katika kuendesha majukumu yake.Wakati wa kipindi cha ujen-

zi, majukumu ya kuchukua hatua mbalimbali za kimazingira na kijamii kwa ajili ya udhibiti na usi-

mamizi yataachiwa makandarasi. Katika mazingira kama hayo, Songas itabaki na uwezo wa kusi-

mamia i1i kuhakikisha kuwa makandarasi wanatekeleza wajibu wao.

Wajibu wa MakandarasiSongas itahakikisha kuwa mikataba na makandarasi wakuu na wadogo wa ujenzi inazingatia vipen-

gele maalum vya mfumo wa usimamizi wa mazingira, afya na usalama ambavyo vitakuwa ndani ya

wigo na wajibu wa mkandarasi.

Maelezo kuhusu Masuala Muhimu:RidhaaUkuzaii wa mpango wa udhibiti wa kimazingira na kijamii kwa aiili ya mradi wa Songo Songo

umeridhia Sera za Utekelezaji na Maagizo ya Benki ya Dunia kama inavyoonyeshwa katika jedwalilinalofuata:

TATHMINI ZA KIMAZINGIRA MA KIJAMII NA MPANGO WA UCDI-ITI

OP 4.01 :Tathmini ya Mazingira. Mradi unaridhia:Tathmini ya mazingira imetayarishwa kulingana namasharti ya mradi wa kategoria A.

OP/BP 4.04: Makazi Asilia Mradi unaridhia: Mradi umetumia mwelekeo wa kitahadhari katika usi-mamizi wa rasilimali za asili katika jitihada za kuhifadhi na kulinda makaziasilia, kuyaepuka makazi muhimu na kudumisha shughuli za kiekolojia. Kilainapokuwa budi hatua za kupunguza na kuondoa tatizo zimebainishwa ilikupunguza kasi ya upoteaji wa makazi pale ambapo hali haizuiliki.Mdhamini wa mradi atatoa pia uhakika wa fursa za maendeleo endelevuya muda mrefu katika nchi kwa kupitia mpango wake wa maendeleo yajamii, michango na ushiriki katika Bodi ya Mfuko wa Kanda ya Mashariki(The Eastern Arc Endowment Trust Fund) na Chama cha Hifadhi yaWanyamapori chaTanzania,

OP 4.09: Udhibiti wa wanyama Mradi Unaridhia: Mdhamini wa mradi hatatekeleza shughuli yoyote yaau wadudu waharibifu kudhibiti wanyama au wadudu waharibifu.

OPN 11.03: Mali ya Kijadi Mradi unaridhia: Usanifu kamambe wa njia utaepuka uharibifu mkub-wa kwenye mali za kitamaduni zinazofahamika na zisizoweza kurejeshwaupya. Zaidi ya hayc, mdhamini wa mradi atasanifu na kutekeleza programuya uandani ya kushughulikia'mali ya Kijadi itakayobahatika kuonekana'yaani 'Chance finds' wakati wa ujenzi wa mradi.

OD 4.20: Wenyeji Haihusiki: Hakuna mwenyeji, kama ilivyofafanuliwa na OP 4.20, ambayeataathinika na mradi.

OD 4.30: Kulazimika kuhamia Mradi unaridhia: Mdhamini wa mradi ametayarisha Programu ya tath-Makazi Mapya mini ya Kiuchumi-jamii ili kuhakikisha kuwa wale waathirika wa mradi

wanasaidiwa ipasavyo kwa ajili ya mali walizopoteza na kwamba mapatoyanarejeshwa au kuboreshwa kulingana na sera.Tafiti nyingine zinapen-dekezwa za kukagua uridhiaji wa sera na kuongezea kanzi ya data zakiuchumi-jamii kwa ajil. ya jambo hili.

OP 4.36: Misitu Mradi unaridhia Mradi haujihusishi na biashara ya magogo au ununuziwa vifaa vya magogo. Kwa kuwa uoto fulani utafyekwa katika maeneoyaliyopangwa, mfadhili wa mradi atatekeleza hatua za kupunguza uharibi-fu ili kupunguza kwa kiasi kikubwa madhara katika uoto pamoja na hatuanyingine yoyote ziiakazopendeke7wa na Idara ya Misitu yaTanzania.Mfadhili wa mradi atafanyakazi pia na wenyeji, na MashirikaYasiyo yaKiserikali (NGO's) kila inapobidi, ili kuendeleza hatua za uimarishaji naurejeshaji uoto juu ya ardhi.

OP/BP 4.37: Usalama wa Haihusiki: Mradi haujishughulishi na ujenzi wa mabwawa.Mabwawa

OP/BP/GP 7.50: Miradi iliyoko Haihusiki: Mradi utaendeshwa katika eneo la maji yaTanzania pekee.katika Njia za Maji za Kimataifa

OP/BP/GP 7.60: Miradi katika Haihusiki: Mradi hauko wala hautaingia hadi kwenye maeneo yenyeMaeneo yenye mgogoro mgogoro.

Sera ya Utoaji wa Habari Mradi unaridhia:Taarifa kuhusiana na mradi zimekuwa zikitolewa nazitaendelea kutolewa nchini Tanzania na katika Kitengo cha habari chaBenki ya Dunia.

Viwango vya Kazi Mradi unaridhia: Mdhamini wa mradi hatatumia ajira ya watoto au yanguvu.

6

TAT-MINI ZA KiMAZINGIRA NA KIJAMIl NA MPANGO A UDHIRcI

Masuala muhimu ya Kimazingira na KijamiiSura ya 7 ya ripoti ya mazingira ambayo huu ni muhtasari wake inajumuisha muhtasari na masuala

ya mazingira ya asili na pia tafiti za kijamii, matumizi ya ardhi na kiuchumi-jamii, ikiwa ni pamoja na

masuala ya afya, makazi na fidia. Sehemu hizi zinajumuisha haii za msingi za mazingira kufuatana na

aina na unyeti wa mazingira katika ukanda unaopita bomba.

Sura ya 8 inaeleza kwa kina athari zinazoweza kutokea za kijamii (ikiwa ni pamoja na za kiuchu-

mi-jamii) na athari za kimazingira pamoja na hatua zitakazochukuliwa na Songas ili kupunguza athari

hizo na kuongeza faida zinazotokana na mradi kwa wenyeji na taifa zima.

Masuala muhimu ya kimazingira na kijamii, yaliyo chanya na hasi, yaliyobainishwa wakati wa

uchanganuzi wa tathmini ya athari za mradi huu na namna Songas itakavyoyadhibiti yameorod-

heshwa hapa chini.

1. Bioanuwai - Spishi za kimamalia zinazohitajika kuhifadhiwa zinapatikana katika eneo la

mradi. Shughuli za mradi zitafanywa kwa namna ambayo haitaziathiri spishi hizi wakati wa

ujenzi na uendeshaji wa mradi.

2. Misitu - Haki ya njia inapitia katika maeneo yenye uoto wa asili. Songas itatumia njia zote

zinazowezekana kupunguza ukataji wa miti na itasaidia shughuli za usimamizi mzuri wa misitu

katika ukanda unaopita bomba.

3. Maji - Songas itawapatia wakazi wa kisiwa cha Songo Songo maji safi ya kunywa (pamoja na

umeme) kutoka kwenye kiwanda cha gesi.

4. Mmomonyoko wa Udongo - Mkandarasi atahakikisha kwamba maeneo yanay-

omomonyoka kirahisi yanaimarishwa baada ya kutibuliwa.

5. Taka - Songas itatekeleza mkakati wa kudhibiti taka ngumu kwa mradi wote ili kuhakikisha

kwamba taka zinaondoshwa kwa namna isiyohatarisha mazingira.

6. Hewa - Utoaji wa hewa kutoka kwenye mradi utazingatia miongozo ya Benki ya Dunia. Gesi

zitakazotolewa zitachangia kwenye utoaji wa gesi zenye kuongeza kiwango cha joto katika

angahewa duniani, lakini kwa kiasi kidogo zaidi kuliko kama mitambo ya kuzalisha umeme

(tabaini) zingeendelea kutumia fueli mafuta.

7. Bomba - (Majini na Nchi Kavu) - Ili kushughulikia uvujaji wa gesi utakaotokea kwa bahati

mbaya, Songas itaunda na kutekeleza mpango wa dharura wa kudhibiti hali itakayotokana na

uvujaji wa gesi.

7

TATHmI-NI ZA KIMAZ NGIRA NA KjAmII NA MPANGO WA UDHIBITI

.

j ' -fI;'., I . , _

Kikundi cha wahasibu wakilipa fidia kwa walioathirika na mradi

8. Masuala ya Kiuchumi-jamii - Ujenzi na uendeshaji wa bomba utatoa ajira za kutosha

nchini Tanzania na katika eneo la mradi. Songas itamhitaji mkandarasi kutumia nguvukazi ya

wenyeji na kununua bidhaa na huduma za wenyeji wa eneo la mradi. Songas itaziunganisha

jumuiya zilizoathirika na mpango wa mikopo midogomidogo.Jumuia zitafaidika pia na ukuzaji

wa biashara ndogondogo.

9. Masuala yanayohusiana na Afya - Kwenye kisiwa cha Songo Songo, Songas itainua viwan-

go vya watumishi wa afya na kituo kinachotoa huduma ya afya ili kuhudumia vizuri zaidi

wananchi na watumishi wa mradi. Songas itaandaa mkakati wa kuthibiti ueneaji wa

VIRUSI/UKIMWI katika maeneo yote ya mradi.

Makazi MapyaShughuli za kuwapatia wananchi makazi mapya zilifanyika chini ya Mipango ya Utekelezaji ya Makazi

Mapya iliyopangwa kutekeleza masharti ya Benki ya Dunia na yale ya Serikali ya Tanzania, hii ni

pamoja naAgizo la Kiutendaji nambari 4.30 la Benki ya Dunia:Mpango wa Kulazimika kuhamia

Makazi Mapya. Songas imekwishafanya uchunguzi unaohitaiika, ikaandaa mipango inayotakiwa, na

katika baadhi ya maeneo ikaanza utekelezaji na ufuatiliaji wa programu zinazohitajika ili kuhakik-

isha kuridhia kwa sera za Benki ya Dunia za usalama wa kijamii, ikiwa ni pamoja na Mpango wa

Kulazimika KuwapatiaWananchi Makazi Mapya.

Programu za fidia za Songas ziliandaliwa mahsusi kuwarejeshea mapato watu walioathirika na

mradi. Mradi umelipa fidia kwa viwango vya soko, ambavyo ni vikubwa kuliko viwango vilivyowek-

wa na serikali yaTanzania.Viwango vya fidia ni vikubwa mara tatu zaidi ili kurejesha mapato ya watu

8

TATHMINI ZA KIMAZINGIRA NA KIUAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

waliofidiwa na huku yakiwepo makusudio ya kuboresha, au kukaribia hali ya maisha yao kabla ya

kuathirika na mradi.

Kwa ujumla, jambo lililozingatiwa sana katika kupanga njia litakamopita bomba lilikuwa ni

kupunguza usumbufu na kuwapatia wananchi makazi mapya. Kutokea mahali bomba linapoibukakutoka majini na kuingia nchi kavu hadi viungani mwa Dar es Salaam (umbali na takribani kilomita

200), ni kaya 33 tu ndizo zilizohitajika kupatiwa makazi mapya. Zaidi ya hayo, ingawa bomba linapi-tia katika eneo kubwa la jiji la Dar es Salaam, ni kaya 155 tu zilihitaji kuhamishwa kutoka kwenye

eneo la njia ya bomba katika maeneo ya mji.

Maeneo mawili yalichaguliwa kwa ajili ya makazi mapya ya familia katika eneo la Dar es Salaam

- Kinyerezi, kusini mwa Dar es Salaam, na Salasala, huko kaskazini (tazama ramani namba 2). Kaya

nyingine 155 zilizoathiriwa na mradi, ni kaya ambazo zilikuwa katika maeneo yaliyotengwa kwa

matumizi ya umma, zimefidiwa pia na kuhamishiwa humo humo ndani ya maeneo ya makazi mapya.

Makazi haya mawili yaliyopangwa vizuri ni rasilimali kubwa kwa jiji la Dar es Salaam.

Mpango wa Ufuatiliaji wa Mazingira na JamiiSongas inatekeleza Mpango wa Ufuatiliaji wa Mazingira naJamii ili kufuatilia athari za mradi. Mpango

huu unajumuisha maeneo yanayohusika na bomba la Songas, mitambo ya kuzalisha gesi na uende-

shaji wa mtambo wa kuzalisha umeme.

TATHMINI ZA KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

_A1TONGA A~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~At:,,, ; Nt -:~~~~~~~~~~~~A . _ .

-V

BAHARI HINDI

1, ~ ~ s S. lani

0~~~~~~~~~~~~

>111~ 'h 'Ii

/; I I' E, n e,

Xi-.z; D1ar-es Salaam- :

7 _ >_;F_ 1 ,-^ s~~~~~~Kituo .

60~~~~~~~~~~~~

~~~~~~~~~~~~~~

,.--,S'-~ ~ ~~>-~. I;; ,I - . ....

TA -- --- -- ---- , .

Maka, mapya Mkaz, Bambamin kgog Njla ya ges ya Songosongo

~~~~~~~~~~~~~~~~~~ -- Maneoy i'm a Yaal e. --u M starl ya kontuaRamMani k2: .Maeneo-kMto yMkzap

Ramani 2: Maeneo ya Makazi Mapya~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

TATHMINI ZA KiMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBIT

SURAYA

2

Shughuli za Programu yaMaendeleo ya Jamii hadi

Januari 2001

Fursa za kuboresha mapatoMapato ya watu walioathirika na mradi inawezekana hayakuwa hasi, hasa katika maeneo ya vijijini

ambako watu waliofidiwa na mradi bado wanaendelea kutumia mashamba ambayo tayari wame-

fidiwa. Hili lilifanyika i1i kujenga uhusiano mzuri kati ya mradi na jamii za wenyeji.

MajiKwenye kisiwa cha Songo Songo, mradi umejenga tangi la maii lenye mabomba kwa ajili ya kuwa-

patia wananchi maji yaliyowekewa dawa (maji safi na salama) kutoka mapangoni wakati wakisubiri

kupatiwa maii (yatakayofikishwa hadi kwenye mpaka wa mtambo wa gesi na mradi) kutoka kwenye

mtambo wa gesi. Kuwepo kwa mfumo wa kuwekea maji dawa kumeongeza sana ubora wa maji.

UsafiUtoaji wa maji kisiwani umeboresha afya na usalama, kwani ugumu wa kuchota maji toka kwenye

mapango yenye kina kirefu umepungua. Upatikanaji wa maji umesababisha kuwepo na mazingira

mazuri zaidi kwa wanakijiji.

Nyumba BoraKumekuwepo mabadiliko toka nyumba za kuezeka kwa makuti hadi nyumba za bati, hasa katika

maeneo yaliyofidiwa na mradi, kwa mfano: Rungungu, Bungu na Jaribu Mpakani.Wananchi wame-

boresha sana ubora wa nyumba zao na sasa wanapanga kuvuta umeme hadi vijijini mwao.

Mipango JijiMakazi mapya ya mradi huko Kinyerezi na Salasala yalikuwa maeneo yenye sifa za kijiji na ambayo

hayakupimwa. mradi umeyabadilisha na kuwa makazi yaliyopangwa yenye idhini kamili ya

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, kama yanavyoonekana katika ramani namba 3 na 4.

ElimuMradi wa Songo Songo umesaidia katika ukarabati wa Shule ya Msingi ya Songo Songo, ambapo

mradi umechangia vifaa vya ujenzi kama vile mifuko ya saruji, mabati ya kuezekea na mbao za

kuandikia madarasani. Zaidi ya hayo, mradi uliwahamasisha watoto kwenda shule kwa kutoa ufad-

hili kidogo kwa wanafunzi wanaoendelea na masomo ya sekondari na vyuo. Kalamu na madaftari

vimetolewa kama msaada kwa shule kadhaa katika maeneo litakamopita bomba na katika kisiwa

cha Songo Songo.

TATHM[NI ZA KIMAZINGIAm NA KIIAMl NA MPANGO WA UDHIRM

I., ~ ~ ~ *

_ _ _ _ _ _ , _ _ _ _ _ _ _ _ _

ak_ Mk2i Nj. Y g. Y. S---- -w,,):

*1.~~~~~~~~~~~~~1

q~~~~~~~~~~~ - -;{

- N N P-,

,. ~ ~ ~ ~ ~ ~ 6,, OAOg MAt'M

Msnoaionmkz -- MN we

Ramani 3: Eneo la Makazi Mapya Kinyerezi

12

Ramani 4: Eneo la Makazi Mapya Salasala

Machirnba ' MTONGANI

a i

' m~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~ ya Mawe -~ '

Makazi m-pya 4 Makatl mapya Banabana n go _ __, Mlitatya bomba la gesl ya SongoM.sya Ma go

i.4

p~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

3 .4 ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~-~~~~~~~~~~~~~I~~~~0

MaEEE, mapyE Makazi m~~~~~~~~~ya Barabara WI NilE ~~~~~~~E bombs Ia YEsI ya Songosongo~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~BambOo 09090 ~ ~~~~~~~~ 040001150 komua~ ~~~'P0 1

Mel Nia YE mig~~~~~~~~~~~~~~~~~~~a ~ ~ ~ ~ Mto ~ ~ ~ ~

TATHMINI ZA KIMAZINGtRA NA KIJAMil NA MPANGO WA UDHIBITI

UshauriWatumishi wa mradi waliwatembelea MaafisaWatendaji wa Kata na kuzungumza nao juu ya mata-

tizo kadhaa ya kijamii na kimazingira vijijini mwao. Maofisa wa mradi waliwapatia MaafisaWatendaii

Kata, viongozi na wazee wa kijiji changamoto mbalimbali. Matokeo yake ni kwamba watoto wengi

zaidi wameandikishwa shule na watu wengi zaidi wamehudhuria vituo vya afya.

Wakati wa Programu ya Kufidia Haki ya Kupita Njia, watumishi wa mradi walishauriana mara

kwa mara na wanavijiji katika jamii zilizoathirika juu ya masuala yanayohusu maisha yao na masu-

ala mengine yanayohusiana na mradi kama vile elimu na afya. Hili lilifanyika katika mikutano kadhaa

wakati wa kuzitembelea ofisi mbalimbali vijijini.

MiundombinuWakazi wa kisiwa cha Songo Songo hurusiwa kutumia viti vilivyo wazi kwenye ndege za kukodish-

wa kutoka kisiwani hadi mikoa ya Dar es Salaam na Lindi. Zaidi ya hayo, wanatumia gati la saruji

(ambalo linahitaji kukarabatiwa) kufunga vyombo vyao wakati wa kupakia na kupakua mizigo na

abiria, kwani gati lao la zamani la mbao halitumiki tena.

Mabadiliko ya Hali ya MaishaKumekuwepo na mabadiliko ya hali ya maisha katika maeneo kadhaa kama vile Kinyerezi na kati-

ka kisiwa cha Songo Songo kwani watu sasa wanaishi katika nyumba nzuri zaidi baada ya kulipwa

fidia na baada ya programu ya uhamasishaii iliyofanyika kisiwani. Programu ya uhamasishaji ilifanyi-

ka ili kuwaandaa wakazi wa kisiwa kwenda sambamba na mabadiliko yanayohusiana na mradi kati-

ka vipengele vingi kwa mfano: kutayarisha nyumba zao kwa ajili ya kuingiza umeme.

14

TA:HMINI ZA KIMAZINGIPA NA KIrAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

SURAYA

3

Mpango wa Shughuli zaBaadaye za Programu ya

Maendeleo ya Jamii

ElimuKwenye kisiwa cha SongoSongo, Songas hutoa ada kwa wanafunzi watatu wa kwanza wanaochag-

uliwa kuendelea na elimu ya sekondari baada ya kufaulu mtihani wa taifa wa darasa la saba.

Programu hii ilianzishwa mwaka 2000 na itaendelea wakati wa utekelezaji wa mradi. Hadi sasa

wanafunzi watatu (3) wanafaidika na programu hii.

Programu nyingine za kielimu na misaada zitatolewa kwa kisiwa cha Songo Songo na jamii zilizomo

katika maeneo linakamopita bomba la gesi. Hii itakuwa huduma moja miongoni mwa huduma nyin-

gi zitakazotolewa kwa jamii zilizoko kwenye maeneo linakamopita bomba la gesi, kulingana na

wajibu wa kimazingira na kijamii ambao Songas imeahidi kutekeleza.

Maji na UmemeSongas itawapatia wakazi wa kisiwa cha Songo Songo maji na umeme bure hadi kwenye mpaka

wa mtambo wa gesi. Usambazaji wa maji na umeme katika maeneo muhimu ya jamii utafanywa na

Programu ya Usambazaji UmemeVijijini.

MiundombinuSongas itapanua na kuboresha miundombinu, ikiwa ni pamoja na barabara na upatikanaji wa maji

na umeme kwa jamii za makazi mapya ya Kinyerezi na Salasala jijini Dar es Salaam.

Juhudi za kurejesha mapatoSongas itaziunganisha jumuiya zilizoathirika kwenye mipango ya mikopo midogomidogo. Jumuiya

zitafaidika pia na uendelezaji wa biashara ndogondogo. Mipango hii itaendelezwa kupitia mashauri-

ano kati ya wanavijiji na watumishi wa mradi.

UshauriSongas ina mpango wa kuendelea kuwa na mashauriano na wanavijiji katika jamii zilizoathirika juu

ya masuala ya Programu ya Maendeleo yajamii hasa yanayohusu mipango ya mikopo midogo mido-

go, uendelezaji wa biashara ndogo ndogo na masuala mengine yanayohusiana na mradi.

Mpango wa Usambazaji UmemeVijijiniMpango wa kusambaza umeme unaotokana na miale ya jua (umeme wa sola) unachunguzwa kwa

ajili ya familia zilizo karibu na njia ya bomba. Uchunguzi huu umeonyesha pia kwamba watu waishia

15

TATH-MINI ZA KIMPZINGIrIA NA KIJAMI, NA MPANCO WA UDHIBITI

4:S

L~~~~',

#_'_ s

p~~~~~~~~~~~ -- t.^

2 B . j. :1 m .2' .- . -

i r ______ &iX

Ene Ia Mrd Kiiw cha Songosong-

;' pes' 11ri,,;9S,.,^,,q,...16

TATHMINI ZA KIMAZINGIRA NA KIJAM I NA MPANGC WA UDHIBITI

~~- r ~~ S S v : e M5 Lr- ,r --- i:''

W.~~~~~~~~~N

_i~~~ ~ J- -- _

4:- _ ---#> ' -- 3i '. 4 S

,-11 _ A . . . .Ai_

Mitambo wa Umeme - Ubungo

17

TATHMIN ZA KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGOWA UDHIBrTI

karibu na njia ya bomba wanatoa kipaumbele cha juu kwa maji na elimu. Hivyo kuna uwezekano

kwamba baadhi ya fedha zilizotengwa kupitia mradi huu zitatumika kwa aiili ya shughuli nyingine

za jamii zilizopewa kipaumbele, licha ya umeme. Songas itashiriki na kusaidia dhana yoyote itakay-

oonekana inafaa kwa aiili ya utoaii wa gesi na/au umeme na huduma nyinginezo.

Ahadi ya Songas ya Kutimiza Majukumu ya KijamiiSongas itachangia kwenye miradi ya maendeleo ya kijamii na ya kitaifa, ikitilia mkazo maalum kati-

ka miradi iliyomo kwenye maeneo ya mradi,yaani kisiwa cha Songo Songo,eneo linamopita bomba

na Ubungo. Mahitaji ya haraka sana kwenye kisiwa cha Songo Songo na katika maeneo linamopita

bomba yanahusu afya na elimu.Aidha Songas itachangia kulinda na kuboresha mazingira na pia

kuwa kichocheo cha kuleta mawasiliano miongoni mwa serikali za mitaa, serikali kuu na mashirika

yasiyo ya kiserikali (NGOs).

Wakati ambapo miradi yote ya maendeleo ya namna hii huzua mambo na masuala mbalimbali,

mradi wa Songo Songo utafuata:-

* Sheria, Sera naViwango vya Tanzania;

* Sera za Usalama za Benki ya Dunia;

* Miongozo ya Benki ya Dunia ya Kupunguza Uchafu wa mazingira, na

* Miongozo ya Afya na Usalama ya Shirika la Fedha la Kimataifa.

Kwa ujumla, masuala yamkini hasi ya kimazingira na kijamii yanayoweza kuibuliwa na mradi wa gesiya Songo Songo yanaweza kudhibitiwa ili kwamba athari zake zipungue. Songas inaamini kuwa

athari zozote hasi zitafidiwa kwa kiwango kikubwa na mazuri mengi yatakayotokana moja kwa

moja na mradi katika maeneo ya mradi na faida kubwa kwa nchi kutokana na kuendeleza rasilimali

hii muhimu.

18

TATHMINI ZA KIMAZINGIRA NA KJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

USAMBAZAJIWA RIPOTIYA UHAKIKIWA MAZINGIRA

Uhakiki wa athari za mazingira, kijamii- uchumi na namna ya kuzirekebisha umekwishafanyika kama

ilivyoelezwa hapo awali. Uhakiki wa kwanza ulikamilika mwaka 1994 na tangu hapo ripoti 28

za utafiti wa mazingira na kijamii - uchumi zimekwishatengenezwa. Ripoti zote hizo zimeungan-

ishwa pamoja na kupata ripoti moia kuu ambayo niTathmini za Kimazingira na Kijamii na Mpango

wa Udhibiti.

Ripoti hiyo ambayo huu ni muhtasari wake imesambazwa kwa washikadau wote. Baadhi ya sehe-

mu ambazo inaweza kupatikana ni kwa wakuu wa mikoa ya Lindi, Pwani na Dar es Salaam; wakuu

wa wilaya za Kilwa, Rufiji, Mkuranga,Temeke, llala na Kinondoni.Vile vile inapatikana katika sehemu

zifuatazo:-

Katibu Mkuu Mkurugenzi Mkuu

Wizara ya Nishati na Madini TANESCO

Barabara ya Sokoine na Mkwepu Mtaa wa Samora

Dar es Salaam Dar es Salaam

Mkurugenzi Mkuu Mratibu wa Mazingira,Afya na Usalama

Baraza la Usimamizi wa Mazingira Songas

Barabara ya Sokoine Nyumba ya Maarifa

Dar es Salaam Mtaa wa Ohio

Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania Ofisi ya Benki ya Dunia

Barabara ya Ali H. Mwinyi Kitalu namba 50

Dar es Salaam Mtaa wa Mirambo

Dar es Salaam

19