madawa ya asili katika nchi za tropiki: iv - kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu...

54
Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV Ukimwi na Madawa ya Asili anamed Team Kitabu cha msaada kwa wanaotunza wagonjwa wa ukimwi. Toleo la 124 la anamed Kiswahili

Upload: others

Post on 07-Dec-2020

38 views

Category:

Documents


7 download

TRANSCRIPT

Page 1: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV

Ukimwi na Madawa ya Asili

anamed Team

Kitabu cha msaada kwa wanaotunza wagonjwa wa

ukimwi.

Toleo la 124 la anamed

Kiswahili

Page 2: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

UKIMWI na Madawa ya Asili.

UTANGULIZI 1

Sura 1: UKIMWI – Tumaini katika kukata tamaa ……… 3

Sura 2: Ukimwi ni nini?…………………… 7

Sura 3: Uambukizaji na uzuiaji wa Virusi vya Ukimwi (VVU)… 11

Sura 4: Njia ya anamed ………………………......... 14

Sura 5: Kuishi na Ukimwi/VVU kwa matumaini …………. 17

Sura 6: Chochea mfumo wa kinga mwilini kwa madawa ya asili…. 20

Sura 7: Jinsi ya kutibu magonjwa yanayoambatana na ukimwi kwa

mimea ya madawa 23

Sura 8: Mwitikio kutoka kwa watumiaji 39

Sura 9: Mapendekezo kumi kwa serikali za nchi za kusini 42

Nyongeza 1: Mistari ya Biblia inayosaidia 44

Nyongeza 2: Mashirika yaliyochaguliwa, matoleo mbalimbali na web – site 45

Nyongeza 3: Fomu ya kumbukumbu: Dalili, tiba na maendeleo ya

wagonjwa wa Ukimwi/ wenye VVU 46

Nyongeza 4: Fomu ya taarifa - kwa kutoa taarifa kwa anamed 47

Nyongeza 5: anamed: Matoleo na vifaa 48

Toleo la pili Julai 2007.

© 2007 na anamed

Ni matumaini ya anamed kwamba taarifa zilizo katika kijitabu hiki zitasambazwa kwa umbali

iwezekanavyo. Tungependa kuwatia moyo watumiaji wa kitabu hiki kukitafsiri katika lugha zao.

Kwa kuwa mambo yaliyomo yanaendelezwa wakati wote, ni lazima kwanza kuwasiliana na anamed.

Haki zote za tafsiri zinabaki na anamed. Hairuhusiwi kuzalisha sehemu yo yote kwa kuuza.

Bango (anamed order No. 403) linaonyesha mimea iliyoelezwa katika kitabu hiki.

Vitabu vya anamed na bidhaa zake vinauzwa kutoka:

anamed, Schwafweide 77, D-71364 Winnenden, Germany.

Email: [email protected]

Internet: www.anamed-edition.com

Shukrani kwa Bindanda Tsobi wa Kinshasa kwa uchoraji wa picha za mifano. Kwa toleo hili la ki-

swahili tunamshukuru Emmanuel Biligeya kwa kazi yake ya utafsiri, Mchungaji Hezron Shimba na

Maike Ettling kwa kuhariri na kundi la Wanaoishi na VVU (Kaza Roho) lililopo Musoma kwa

ushirikiano wao wa kufanya majaribio ya kutumia madawa yaliyotajwa katika kijitabu hiki na

kushuhudia ufanisi wake.

Pia tunaishukuru HUYAMU (Idara ya Afya ya AICT - Dayosisi ya Mara & Ukerewe) kwa

ushirikiano wao wa karibu. Jalada la mbele: Wanasemina wa anamed huko D.R Congo wakijivunia madawa waliyotengeza

wenyewe.

Page 3: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 1

UTANGULIZI

“Wapiganapo tembo, ziumiazo ni Nyasi“.

Huu ni msemo wa kiafrika na unaelezea hali ya wagonjwa wa Ukimwi kwa sasa katika

nchi zinazoendelea.

Shirika la biashara dunia linapigania haki ya mali ya akili.

Serikali za nchi tajiri zinaziburuza nchi maskini kufuata sheria ya haki miliki za

kimataifa, wakati huo huo wao wenyewe wakizama na kupiga mbizi katika

maswala yao muhimu. Pia wanatumia fedha zaidi katika kupambana na

binadamu magaidi kuliko vimelea “magaidi” kama vile VIRUSI vya UKIMWI

na vile vya malaria “Plasmodia” viuavyo mamilioni kila mwaka.

Makampuni ya madawa yana faida kama kipaumbele chao cha kwanza na

wanalinda haki miliki zao kuvuka sheria zilizokubaliwa kimataifa.

Baadhi ya serikali za nchi masikini zinawekeza zaidi katika silaha ili

kupambana na maadui binadamu kuliko katika mahitaji ya ki-afya na madawa

yanayoshambulia vimelea kama vile VIRUSI vya UKIMWI.

Shirika la afya duniani linapigania haki lakini halina nguvu.

Wizara za afya katika nchi maskini zinashutumu makampuni ya madawa kwa

kutoza gharama zisizowezekana.

Ni tatizo gani hili! Dunia pamoja na ujuzi wake wote imeshindwa kuwasaidia

mamilioni ya watu kusini mwa jangwa la sahara walio na Ukimwi. Afya ya wagonjwa

ambao pia ni maskini ina umuhimu mdogo sana hapa duniani ukilinganisha na biashara,

na haki zilizowazi zinazolinda swala la kutengeneza faidi.

Matokeo yake ni kwamba Ukimwi unaendelea kusambaa zaidi katika Afrika na

mamilioni ya watu wanateseka. Mamilioni ya watoto wamekuwa yatima, kiuchumi

watu watenda kazi wamekufa na wanazidi kufa, na baadhi ya nchi maskini kabisa

duniani zimenaswa katika kile kinachoonekana kuwa kuanguka kusikoweza kuzuilika.

Wapiganapo tembo ziumiazo ni nyasi. Labda uwezekano pekee ni kwamba nyasi ziwe

ngumu kiasi kwamba tembo waende mahali pengine kupigana.

anamed inawatia moyo watu kujiondoa katika kuwa tegemezi wa kile ambacho

kimeelezwa kama uchumi unaonyonga dunia na kutafuta kuimarisha “uchumi hai

wenye asili ya mahali walipo” katika nyanja za afya. anamed inazitia moyo jumuiya

kutumia ujuzi ambao tayari wamekuwa nao, au hata waliokuwa nao, wa jinsi ya kula

chakula cha afya na kujitengenezea madawa, ili kujitegemea zaidi katika kukidhi

mahitaji yao ya kiafya.

anamed pia inazitia moyo jumuiya kujenga hali ya kujiamini katika kudai haki ya

huduma bora kwa ajili yao na kwa ajili ya kila mtu katika dunia hii.

Kijitabu hiki kinaelezea jinsi madawa ya asili yaani matumizi halisi ya mimea

inayostawi au inayoweza kustawishwa katika nchi za tropiki inayoweza kusaidia katika

kuhudumia mgonjwa wa Ukimwi, na kuwezesha wengi kuishi maisha mazuri zaidi.

Page 4: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 2

Madawa ya asili ni zaidi ya madawa

kutokana na mimea. Msingi wake ni

katika Biblia waaguzi na waganga na

madawa ya kisasa wakishirikiana na

matumizi ya mapendekezo ya shirika la

afya duniani.

HATUDAI KWAMBA DAWA ZA ASILI ZINAWEZA KUTIBU UKIMWI!

Wagonjwa wengi wa UKIMWI tayari wameinua hali za Afya zao kwa kutumia mimea

waliyonayo katika mazingira yao, na kwa kutengeneza madawa yenye gharama ndogo.

Kwa njia hii hawategemei huruma za bodi au mashirika ya nje. Silaha bora zaidi dhidi

ya Ukimwi ni kuzuia. Lazima wakati wote hilo liwe kipaumbele, na vitabu vingi

vimeongelea jambo hilo. Katika kijitabu hiki tumeleta pamoja uzoefu wa watu wengi,

na kutoa mawazo mengi ya jinsi ya kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili na jinsi

magonjwa yanayohusiana na ukimwi yanavyoweza kutibiwa kwa njia za asili.

Toleo la kwanza la kitabu hiki

lilikubalika zaidi ya jinsi tulivyotegemea,

kama chanzo cha msaada kwa hospitali,

zahanati, mashirika yasiyo ya kiserikali,

vikundi vya kijamii, na watu binafsi.

Tunashukuru ukweli kwamba wizara ya

afya ya baadhi ya serikali zimeanza

kutoa miongozo kwa matibabu ya miti

shamba kwa huduma ya wagonjwa wa

ukimwi nyumbani, mfano Malawi

mwaka 1998 “Home – based care herbal

treatment guideline” National AIDS

Control Programme, Ministry of Health,

Lilongwe, Malawi, May, 1998. Kwa

bahati mbaya, matoleo hayo

yanasahihishwa na kuchapwa tena mara

chache sana mara akiba yake na fedha

inapokwisha. Kwa hiyo tunafurahia na

kushukuru msaada wa watu kutoka dunia

nzima kwa mchango wao wa msaada wa

uzoefu kutusaidia kutoa hili toleo la pili.

Tunaamini kwamba kijitabu hiki bado ni

cha kipekee katika kutoa maelekezo na

taarifa juu ya michanganyiko ya madawa

na vipimo vya madawa ya asili.

Tutathamini sana utoaji wako wa taarifa

juu ya mambo yaliyomo.

anamed ipo kwa ajili ya kuendesha

semina za dawa za asili kwa jamii zinazohitaji kupunguza kutegemea wale “tembo”

waliosemwa hapo juu.

Page 5: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 3

SURA I: UKIMWI: TUMAINI KATIKA KUKATA TAMAA

Upana wa tatizo.

Kutokana na Muungano wa Mpango wa Umoja wa Mataifa katika UKIMWI

(UNAIDS), mwishoni mwa 2003 takwimu za ulimwengu za UKIMWI zilikuwa kama

ifuatavyo (Kwa sehemu kubwa imechukuliwa kutoka HIV/AIDS Policy Fact sheet ya

Henry J.Kaiser Family Foundation, inayochukua takwimu zake kutoka UNAIDS, taarifa

ya ukimwi ya dunia ya 2004, July 2004.Angalia www.kff.org.).

Dunia nzima inakadiriwa watu 37.8 milioni wanaishi na Virusi vya Ukimwi au

wana UKIMWI - ni idadi kubwa isiyowahi kutokea kabla.

Kati ya hao 37.8 milioni, milioni 25 wanaishi kusini mwa jangwa la sahara,

Afrika, ambapo kulikuwa na watu milioni 3 wapya walioambukizwa mwaka

2003. 57% ya walioambukizwa ni wanawake.

Mwaka 2003, inakadiriwa watu 4.8 dunia nzima waliambukizwa virusi, ikiwa ni

pamoja na karibu watoto 630,000 (chini ya miaka 15). Hili ni ongezeko kubwa

kuliko yote tangu janga la Ukimwi lianze.

Watu milioni 2.9 walikufa kwa Ukimwi mwaka 2003. Kati ya hawa karibu nusu

ya milioni walikuwa watoto. Kati ya 15% na 40% walikufa wakiwa na

maambukizi ya ziada ya TB (kifua kikuu)

Dunia nzima watu wengi zaidi wanaoishi na VVU hawajui kwamba

wanaambukizwa.

Mategemeo ya kuishi katika nchi nyingi za Afrika chini ya Jangwa la Sahara

yanaendelea kushuka kwa kasi – inategemewa kwamba mategemeo ya maisha ya

watoto wanaozaliwa katika nchi 11 hivi karibuni itakuwa zaidi kidogo tu ya miaka 30.

Kutoka: UNAIDS/WHO AIDS Epidemic Update: December 2006

Total: 39.5 (34.1-47.1) million

Watu wazima na watoto wenye Virusi vya Ukimwi mwaka 2006

Page 6: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 4

Kabla ya pigo la UKIMWI, kwa mfano, Botswana ilikuwa ikishamili, na wastani wa

umri wa watu wake ulikuwa karibu miaka 75. Kwa sasa ndiyo nchi yenye kiwango

kikubwa kabisa cha maambukizi duniani, na inatabiriwa kuwa mtoto atakayezaliwa

mwaka 2010 atafariki kabla hajafikia umri wa miaka 27.

Ingawa kusini mwa jangwa la Sahara ndilo eneo lililoathiriwa sana, hali ni mbaya sana

pia Ulaya Mashariki na Asia nzima, ambako kiwango cha maambukizi kiko juu.

Hizi ni takwimu za kiofisi, zinazotokana na makisio yaliyobuniwa kutokana na

uchunguzi, ambao, mara nyingine, umefanyika katika nchi ambapo vipimo vichache

sana ya VVU vilivyo sahihi vimefanyika. Katika Afrika pia, ni mara chache sana

uchunguzi wa maiti unafanyika. Kwa hiyo ni mara chache sana pia kujua sababu ya kifo

na kwa hiyo inawezekana ni waathirika wa umaskini, au wa magonjwa mengine kama

ukosefu wa lishe au kifua kikuu. Kutokana na upungufu wa lishe wanapungua uzito na

kwa jinsi hiyo kupungua kwa nguvu ya mfumo wa kinga ya mwili wanaoneka na dalili

zile zile za wagonjwa wa UKIMWI.

Matukio haya ni ya hatari pia, na madawa yote ya asili yaliyopendekezwa katika kitabu

hiki ni bora kwa matatizo hayo.

Athari kwa familia na jamii

Athari za UKIMWI zote zinaeleweka vizuri sana katika jamii zilizoathirika.

- Watendakazi katika familia na watunza familia wanakufa; yaani watu ambao kwa

kawaida wanaleta chakula kwenye familia na kutunza watoto. Kisha wanawake

ambao hufanya majukumu ya wanaume wanapata mzigo mzito zaidi.

- Familia nyingi zinabeba mayatima – desturi ya utayari wa familia za ki-afrika

kuwatunza mayatima na ndugu wengine wenye shida katika familia zao ni desturi

nzuri sana lakini inahitaji nguvu na hata fedha

- Kama matokeo ya kuwa na watu wachache wenye uwezo wa kufanya kazi, na

watu wengi wa kulisha, hatari ya upungufu wa lishe, hasa kwa watoto

inaongezeka sana.

- Wakati malipo kwa ajili ya huduma ya matibabu na madawa inapohitajika, mfugo

mara nyingi utatakiwa kuuzwa, na hivyo kuzidi kupunguza mali ya familia.

- Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi

na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi kingine na

vinapotea.

- Kuongezeka kwa umaskini, na hitaji la watoto yatima kufanya kazi badala ya

kwenda shule, maana yake ni kwamba kizazi kinachofuata hakitakuwa na elimu.

Kwa hiyo kuna mzunguko wa maangamizi. UKIMWI unasababisha umaskini,

upungufu wa chakula utapiamlo, upungufu wa nguvu kazi na upotevu wa elimu. Haya

yote yanawafanya wale wanaobaki kuwa rahisi kwa kuambukizwa VVU/UKIMWI.

Athari katika nchi

Uchumi wa vijiji na miji, kwa jinsi hiyo mikoa mizima na nchi zote kwa jumla,

zinaathirika vibaya sana mara wafanyakazi wanapodhoofishwa na UKIMWI. Kilimo,

viwanda na shughuli zote zinaathirika kwa kuwa haviwezi kufanya kazi kwa juhudi na

nguvu na watumishi wanakuwa na muda wa kuwa nje ya kazi kwa sababu ya

maambukizi mbalimbali, kuhudumia wagonjwa au kuzika waliokufa.

Pamoja na hayo bajeti za Taifa na huduma za Afya zinalazimika kufanya kazi ya ziada

Page 7: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 5

ili kupambana na janga hili kwa njia za kukinga na kutibu.

Mwitikio kwa UKIMWI

a) Vikundi vya wanakijiji, vikundi vya msingi na mashirika ya wananchi yasiyo ya

kiserikali. Mengi huunda mwitikio mzuri sana kwa rasilimali ndogo sana. Mifano

imeonyeshwa katika sura ya 8.

b) Makanisa. Kwa muda mrefu mengi yamepuuzia tatizo hili. Wahubiri wengi

walihubiri kwamba UKIMWI ulikuwa ndiyo malipo ya dhambi, vivyo hivyo

makuhani wa jadi walichukulia UKIMWI kuwa ni matokeo ya kuvunja mwiko

fulani. Kukataa kwa Kanisa Katoliki kutumia njia za uzazi wa mpango na hasa

matumizi ya kondomu, imelifanya swala hili kuwa gumu zaidi.

Leo makanisa hutambua kwamba upendo wa Mungu ni kwa wote na kwamba

huduma ya Yesu ililenga hasa watu waliotengwa na jamii, na yanashughulikia swala

hili kwa nguvu kwa niaba ya wagonjwa wa UKIMWI. Semina nyingi zaidi za

anamed zinazohusu UKIMWI. Zimeandaliwa na makanisa na misheni.

c) Mashirika ya misaada ya kimataifa. Shirika la wakala wa Maendeleo Uingereza,

Action Aid, kazi yake inaonekana kwa jamii zilizo maskini katika nchi nyingi.

Inatoa misaada ya kuwasaidia watu kujitatulia matatizo wao wenyewe. Kwa mfano,

mwaka 1987 “The AIDS support Organization” (TASO) ilianzishwa Uganda ili

kusaidia watu wenye VIRUSI/UKIMWI na familia zao, na hadi kufikia miaka ya

1990 mwishoni ilikuwa imeanzisha na kuimarisha nchi nzima vituo vinavyotoa

huduma ya ushauri nasaha, elimu ya VVU/UKIMWI, misaada ya tiba na vifaa.

d) Serikali. Taarifa ya kupambana na UKIMWI Uganda ni moja kati taarifa bora zaidi.

Hata katika siku za kwanza za UKIMWI, serikali ya Uganda ilitambua kiwango cha

tatizo kilichokuwa kinawakabiri, iliomba misaada ya kimataifa na ikaweka mikakati

yenye kueleweka. Hii ni pamoja na elimu ya afya kutahadharisha jamii kwa kutumia

radio na televisheni, ushauri kwa walioathirika, na misaada ya tiba. Walikaribisha

mashirika ya kimataifa kama Action Aid na kufanya kazi kwa kushirikiana nayo.

Jambo la kuhuzunisha, serikali nyingine nyingi zimelipuuzia au hata kutojali kabisa

tatizo hili.

e) Uchunguzi wa kisayansi – madawa. Julai 2004, Medecins Sans Frontieres (MSF)

ilitoa taarifa kwamba mchanganyiko wa dawa wenye generic antiretroviral tatu

katika kidonge kimoja imehakikishwa kwa mara ya kwanza katika uchunguzi wazi

kwenye kliniki katika nchi zinazoendelea. Ufuatiliaji wa watu 60 waliotibiwa huko

Yaounde, Cameroon, imeonyesha kufaa sana.na kuwa salama. Mchanganyiko huu

(Generic fixed – dose combinations (FDCs) za antiretrovirals ndiyo msingi mzuri

katika kuelekea kutibu maambukizi ya VVU/UKIMWI katika nchi zinazoendelea.

FDCs zina faida mbili ambazo ni urahisi wa kutumia na kuwa na bei nafuu

ukilinganisha na dawa nyingine zenye majina makubwa (MSF Press release, 2 July

2004), uchunguzi katika Maendeleo kutibu VIRUSI/UKIMWI katika nchi

zinazoendelea. Mchanganyiko wa dozi za dawa za generic antiretroviral

imehakikishwa kwenye majaribio ya kliniki) Lakini hata hivyo, hadi sasa ni 7% tu

ya watu katika nchi zinazoendelea wanaopata huduma ya antiretroviral (chanzo:

UNAIDS)

f. Shirika la Afya duniani (WHO). Mpango wa “tatu kwa tano” unalenga kuhudumia

watu milioni tatu kwa madawa ya UKIMWI hadi kufikia mwaka 2005. Ni wachache

Page 8: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 6

wanaoamini juu ya uwezekano huu.

g. Mpango wa “tumia kondomu”. Ni wazo zuri kabisa, kama tu kondomu za kutosha

zingepatikana katika ukubwa mbalimbali, katika bei nzuri, kutunzwa mbali na

mwanga wa jua, na kama tu wanaume wangekubali kuzitumia!

h. Ulinzi kwa wanawake. Katika nchi nyingi zinazoendelea ambapo kiwango cha

maambukizi ni kikubwa zaidi kwa wanawake, wanawake hawaruhusiwi kukataa

tendo la ngono. Uchunguzi unaendelea kufanyika juu ya dawa ya kuua vimelea

ambayo watakuwa wanajipaka kabla na baada ya tendo la ndoa ili kuua virusi, lakini

hii haielekei kupatikana baada ya miaka michache ijayo. Nyingine ambazo

zinasaidia na zinapatikana kwa sasa ni kondomu za kike na viwambo (diaphrams)

ambavyo vinazuia virusi kugusa cervix (mlango wa mfuko wa uzazi)

i. Ufadhili. Matumizi ya dunia nzima kwa UKIMWI yameongezeka toka Dola 1.2

bilioni za kimarekani mwaka 2003 hadi kisio la dola bilioni 6 mwaka 2004. Fedha

ya dunia ya kupambana na UKIMWI, kifua kikuu na malaria katika bajeti yake

inapungukiwa na dola za kimarekani bilioni 1.6 ili kukidhi hitaji lililotegemewa

katika mzunguko wa tatu na ruzuku katika Oktoba 2004. Mfuko wa dunia umelipa

dola bilioni 1.5 za kimarekeni kwa ruzuku kwenye mipango 160 katika nchi 85

katika mzunguko wake wa kwanza na wa pili wa ruzuku. Marekani inatoa fedha

nyingi zaidi kwa UKIMWI kuliko nchi nyingine yoyote, lakini inapendelea

kuzitumia yenyewe bila kushirikiana na nchi nyingine kwa hiyo inakosolewa

kwamba inasaidia makampuni yake ya madawa.

j. Mpango wa kimataifa. Mpango wa kimataifa wa kutengeneza dawa inayozuia

virusi viharibifu inayotengenezwa na nchi zinazotengeneza madawa yawezayo

kununuliwa na watu katika Afrika na Asia una mafanikio kiasi fulani, hasa Afrika

kusini. Lakini, jambo la kusikitisha, ukweli unabaki kwamba hata kama bei

ingepunguzwa kwa 90% bado zisingewafikia watu walio wengi zaidi katika maeneo

ya vijijini.

Baada ya kutaja mambo yote haya, uwezekano kwamba wagonjwa wengi wa UKIMWI

wana uwezekano mkubwa wa kuwa waathirika wa umaskini na magonjwa mengine

yanayohusiana na umaskini, anamed inaamini kwamba dawa za asili ndiyo raslimali

muhimu. Madawa ya asili yanawasaidia watu wa hali ya chini kujiamini kwa sababu

wanakuwa na uwezo mkubwa wa kujitegemea kwa kutumia malighafi inayopatikana

katika mazingira yao na kwa gharama ya chini kabisa. Hatuko peke yetu katika kuamini

kwamba mimea ya madawa ni ya muhimu sana. Vyuo vikuu vingi sana duniani kote

vinafanya uchunguzi na majaribio ya jinsi ya kutumia mimea yenye dawa katika tiba ya

VVU/UKIMWI.

(Awour et al (1993), “Traditional Medicine and herbs for treatment of HIV related ailments in Kenya”

Int. Conf. AIDS June 6-11;

Burford et all (2000) “Traditional Medicine and HIV/AIDS in Africa” Journal of Alternative and

Complementary Medicine vol. 6 (5) pp 457 – 471;

Martin and Edzard (2003) “Antiviral agents from plants and herbs: a systematic review” Antirivival

therapy, vol 8 (2) pp 77 – 90)

Chuo cha “Cornell Medical College, New York, kinasema “katika yote, mimea inatoa matumaini

mazuri katika uchunguzi wa tiba ya HIV. (Chang and Kong (1996) “Meta – survey of plants and herb

material as a treatment for HIV” Int. Conf. on AIDS Canada, July 7-12, vol 11 (1) p 22) .

Page 9: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 7

Wanaoishi wa Virusi vya Ukiwi mara nyingi

wanaajisikia kuchoka sana

SURA 2: UKIMWI NI NINI?

Kwa ufupi UKIMWI inasimama badala ya ukosefu wa kinga mwilini. Unasababishwa

na virusi vinavyoitwa HIV au Human Immunodeficiency Virus. Kwa kuua au

kudhoofisha chembe nyeupe za mwili, zinazoitwa Lymphocytes, HIV inadhoofisha

mfumo wa kinga mwilini. Kwa jinsi hiyo mwili unapungukiwa uwezo wa kupambana

na maambukizi na baadhi ya aina za kansa.

Kwa jumla watu husemwa kwamba ana Ukimwi kama:

a) Mfumo wake wa kinga unakuwa dhaifu sana kwa sababu ya virusi wa HIV, au

b) Upungufu wa kinga yao unaohusiana na virusi vya Ukimwi unakuwa wa hatari kiasi

kwamba maambukizi yenye kutishia maisha (magonjwa tegemezi) na/au saratani

kutokea.

Mara mtu anapoambukizwa virusi vya ukimwi inamchukua wastani wa miaka 5-8

kupata Ukimwi. Watu wanaweza kuambukizwa virusi vya ukimwi lakini wakajisikia na

kuonekana wazima kwa miaka mingi, kwa jinsi mfumo wao wa kinga unavyoendelea

kupigana na virusi. Ni mpaka baadaye ambapo mfumo wa kinga hauwezi tena

kuukinga mwili, ndipo dalili za ndani na za nje zinaanza kujionyesha.

Watu walio na magonjwa sugu kama TB (kifua kikuu) au wale wanaoteseka kwa

udhaifu wa afya au wanaopata lishe ndogo, wataingia katika hatua ya kuugua ukimwi

haraka zaidi kwa sababu mfumo wao wa kinga tayari ni dhaifu.

Jinsi ya kuutambua UKIMWI

Dalili za UKIMWI ni tofauti kwa

watu tofauti. Kwa muda mrefu

inaweza isiwe wazi kama mtu

ana Ukimwi au la. Dalili ni zile

za magonjwa ya kawaida lakini,

kwa kawaida, yanakuja kwa

nguvu sana na yanadumu muda

mrefu.

Dalili nyingine za kawaida ni:

Kupungua uzito

kunakoendelea.

Kuhara kwa muda mrefu.

Homa ya muda mrefu,

ambayo inaweza kuja na kuondoka

Kikohozi kibaya cha muda mrefu, na maambukizi mengine ya mapafu.

Ukurutu.

Maambukizi ya macho.

Kujisikia uchovu mara kwa mara.

Ugunduzi wa UKIMWI bila vyombo vya maabara

Madaktari wengi wana njia zao za kugundua UKIMWI. Zote zinajumuisha uwepo wa

maambukizi nyemelezi. Panapokosekana zana halisi za kupimia UKIMWI, Shirika la

Page 10: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 8

Afya duniani (WHO) limependekeza mwongozo ufuatao:

Maana ya UKIMWI ya shirika la Afya duniani kwa watu wazima.

Mahali pasipo na vipimo vya virusi vya UKIMWI, mtu ataonekana kuwa ana

virusi vya UKIMWI kama akipatikana angalau na mbili kati ya dalili hizi kuu

hapa chini zikiwa pamoja na angalau dalili moja ndogo. Mgonjwa asiwe na

sababu nyingine yoyote inayosababisha kupungua kwa kinga ya mwili kama vile

saratani au upungufu mkubwa wa lishe.

Kuwepo kwa kaposis sarcoma au cryptococcal meningitis pekee kunatosha

kuonyesha uwepo wa ukimwi.

Dalili kuu:

Kupungua uzito kwa 10%

Kuharisha kunakoendelea zaidi ya mwezi mmoja.

Homa inayoendelea zaidi ya mwezi mmoja.

Dalili ndogondogo

Kikohozi kinachozidi mwezi mmoja

Kuwashwa ngozi mwili mzima

Jamii ya mkanda wa jeshi inayojirudirudia

Mtando mweupe mdomoni (Oropharyngeal candidiasis)

Maambukizi ya ngozi yanayoendelea na kusambaa mwilini

yanayosababishwa na jamii za virusi

Kuvimba matezi na mitoki (Generalised Lymphadenopathy)

Kupima UKIMWI kwa vifaa vya maabara

Ni kipimo cha maabara pekee kinachoweza kuhakikisha kama kweli mtu ana UKIMWI

au la. Kipimo ni idadi ya 200 CD4+ T-cells au pungufu kwa microlitre kukiwepo na

maambukizi ya virusi vya ukimwi. Watu wenye umri wa miaka 5 na zaidi ambao kinga

yao ya mwili inafanya kazi vizuri kwa kawaida wana CD4+T- cell kati ya cell 800—

1300 kwa microlitre.

CD4+ cell ni nini?

Virusi vya ukimwi hushambulia lympocytes, aina ya chembe nyeupe za damu zilizo na

receptor protein, zinazoitwa CD4, katika ngozi yake ya nje. Cells zenye CD4 receptor

zinaitwa CD4+cells au helper T lymphocytes.

T lymphocytes ni za muhimu sana katika mfumo wa kinga mwilini, kwa sababu

zinasaidia kuulinda mwili dhidi ya aina za virusi, na zinaweza kutambua na kuharibu

baadhi ya chembe za saratani.

Virusi vya UKIMWI vikiingia mwilini, huingia katika T-lymhocytes, na genetic

material za virusi huungana na zile za lymphocyte. Hapo virusi vinazaliana katika ile

chembe na hatimaye vinaiharibu. Pia inatoa virusi vingine vipya ambavyo hushambulia

lymphocytes nyingine.

Retrovirusi ni nini?

Virusi vya UKIMWI ni Retrovirusi. Retrovirusi ni aina ya virusi inayotunza taarifa za

genetic kama ribonucleic acid (RNA) zaidi kuliko inavyofanya deoxyribonucleic acid

(DNA). Virusi vikiingia katika chembe vinatoa RNA yake pamoja na kimeng’enyo

Page 11: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 9

(enzyme), kisha vinatengeneza DNA kwa kutumia RNA na virusi kama kielezo

(pattern). Kisha DNA ya virusi inaingizwa katika DNA ya ile chembe.

Kila mara ile chembe ikigawanyika hutengeneza nakala mpya ya DNA ya virusi iliyo

kamili pamoja na gene zake. Kwa wakati huohuo DNA ya virusi inaweza kuingilia na

kuifanya ile chembe itengeneze virusi vingine. Virusi hivi vipya humwaga nje ya

chembe iliyoathiriwa na kuvamia chembe nyingine.

Mfuatano wa magonjwa yanayohusiana na UKIMWI

Hatua ya 1: Mwili unaingiliwa na virusi vya ukimwi, na virusi vinazaliana kwa haraka

sana hadi antibodies hutengenezwa mwilini - mchakato unaoitwa “seroconversion“.

Wakati wa seroconversion , watu wengi huugua kwa kuonyesha dalili kama homa,

mwili kutokuwa katika hali yake ya kawaida, kichefuchefu, ukurutu, na vidonda

kuzunguka mdomo, mkundu na sehemu za siri.

Wakati wa kipindi chote hiki mtu ana uwezo wa kumwambukiza mtu mwingine ye yote,

ingawa kipimo cha virusi vya ukimwi huonyesha uwezo wa virusi baada ya

seroconversion kufanyika.

Hatua ya 2: Watu wengi huendelea kuwa na hali nzuri kwa miaka kadhaa wakiwa na

kiwango kidogo cha hivi virusi katika damu yao.

Hatua ya 3: Baada ya miaka 5 hivi, watu wengi huanza kupata matatizo mengi kama

matokeo ya kudhoofishwa kwa kinga ya mwili, kulikosababishwa na idadi ya chembe

za CD4 kuwa chini ya 500 kwa microlitre. Kupungua uzito kwa zaidi ya 10%

kunatokea, mtu anajisikia kutokuwa katika hali ya kawaida, na maambukizi ya nguvu

kama vile kuhara kwa kipindi kirefu kisichoelezeka hutokea.

Hatua ya 4 - UKIMWI: Mara chembe za CD4 zinapokuwa chini ya 200, mgonjwa

anapata maambukizi makuu. Wasipopata matibabu kwa kinga yao ya mwili na

maambukizi hayo, kwa kawaida hufariki katika kipindi cha mwaka mmoja.

Mfuatano wa magonjwa yanayohusiana na ukimwi

Upungufu wa kinga: Mwanzoni katikati mwishoni

CD4>500 500<CD4>200 CD4<200

1000

Idadi ya

CD4

Cells

kwa 500 micro-

litre

200

0 0 Kama wiki 10 kama miaka 5 kama miaka 10

Sero-

Conversion

Illness

Kipindi kisicho

na dalili

Maambukizi yasiyo na

nguvu sana

Homa, jacho wakati

wa usiku, udhaifu wa

mwili

Magonjwa

nyemelezi

yenye

nguvu

Page 12: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 10

Ni tiba gani ya hospital iliyokubalika ?

Dawa zinazotumika zinaitwa anti-retroviral (ARV) drugs. Lengo lake ni kupunguza

nguvu za virusi vya ukimwi na kuvizuia kuzaliana, na jinsi hiyo kupunguza kasi ya

ugonjwa.

Kuna makundi matatu ya ARV.

a) Nucleoside reverse transcriptase inhibitors (NRTI) kama vile AZT, ddl, ddc, d4t,

3TC na abacavir.

b) Non –nucleoside reverse transcriptase inhibitors (NNRTI) kama vile nevirapine,

delavirdine na efavirenz.

c) Protease inhibitors (PI) kama vile saquinavir, ritonavir, indinavir na nelfinavir.

“Highly active antiretroviral therapy” (HAART), ni jina la matibabu lililokubaliwa na

mabingwa wa VVU (virusi vya Ukimwi) kwa kudumaza kwa nguvu kuzaliana kwa

virusi na kuendelea kwa ugonjwa

wa VVU. Mfumo wa kawaida wa

HAART unajumuisha dawa tatu

au zaidi, kama vile nucleoside

reverse transcriptose inhibitors

mbili na protease inhibitor moja,

nucleoside reverse transcriptase

inhibitors na non – nucleoside

reverse transeriptase inhibitor

moja, au michanganyiko mingine.

Mifumo hii ya matibabu

imeonekana kupunguza kiwango

cha virusi kiasi kwamba haviwezi

kuonekana katika damu ya

mgonjwa. Hasara yake ni

kwamba sehemu kubwa ya dawa

hizi husababisha madhara, hasa

kichefuchefu, kutapika, kuharisha

na maumivu ya kichwa.

Kama ukibahatika kupata dawa za

ARV, zitumie kwa kufuata

maelekezo. Kutofanya hivyo

kunatoa nafasi kwa virusi

kubadilika kimaumbile (mutate), na

dawa haitaweza kufanya kazi.

Usikose hata dozi moja, na

hakikisha kwamba unaelewa

maelekezo. Kama dawa ikikufanya

usijisikie kawaida au madhara mengine usiache kuvitumia. Mwite kwanza daktari.

Kunaweza kupatikana madawa mbadala.

Watu wengi wana hofu ya kukaa na wagonjwa

wa UKIMWI Hakuna kabisa madhara/hatari ya

kuambukizwa ukimwi kwa kuchangia choo na

mgonjwa wa Ukimwi. Lakini weka choo katika

hali ya usafi na wakati wote nawa mikono yako

baada ya hapo, kuepuka kupata maambukizi ya

aina nyingine.

Page 13: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 11

Ukimwi hausababishwi na wadudu.

Unaweza kulala kwa usalama karibu

na mgonjwa wa UKIMWI kwa amani

kabisa.

Sura 3: Kuambukiza na kuzuia VVU (Virusi vya Ukimwi)

Sababu za janga la VVU/UKIMWI ni nyingi na za namna nyingi . Mambo

yanayochangia ni pamoja na umaskini, ujinga, uhamiaji na kuhamahama. Kuwa na

wapenzi wengi, jambo lingine la muhimu, pia imepelekea kupata magonjwa mengine

yaambukizwayo kwa njia ya kujamiiana. Kusini mwa jangwa la sahara kujamiiana

kunawajibika katika 90% ya maambukizo ya VVU, kukifuatiwa na maambukizi kutoka

kwa mama hadi kwa mtoto.

Ninaambukizwa kwa namna gani?

VVU vinaweza tu kuishi katika damu, maji ya ukeni, shahawa, na maziwa ya kina

mama walioambukizwa, na vinaweza tu kupelekwa au kuambukizwa kwa njia ya

kubadilishana haya majimaji ya mwili.

Unaweza kupata VVU kutoka kwa yeyote aliyeambukizwa kwa kuwa mara nyingine

inachukua miezi au hata miaka kwa dalili za kwanza za ugonjwa kuonekana. Mtu

mwenye virusi anayeambukiza ugonjwa huu anaweza kuonekana mwenye afya nzuri.

VVU vinaambukizwa kwa njia zifuatazo:

A. Kujamiiana.

Kwa kufanya mapenzi na mtu aliye na VVU. Katika Afrika sehemu kubwa ya

maambukizi ni matokeo ya kufanya ngono bila kinga.

Kufanya ngono ya mdomoni na mtu

mwenye maambukizi, hasa ukiwa na

vidonda mdomoni mwako au fizi zivujazo

damu. Maeneo mengine vijana hufanya

ngono kwa mdomo ili kulinda ubikira wao.

B. Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto

Wakati wa mimba.

Wakati wa kujifungua na

Wakati wa kunyonyesha kwa matiti.

C. Damu.

Kwa kutumia sindano au bomba ambalo

halikuchemshwa ili kuua vijidudu tangu

lilipotumika mara ya mwisho.

Kuongeza damu yenye maambukizi.

Kwa kutumia vifaa vya kukatia au kutobolea ambavyo havikuhudumiwa ili kuua

vijidudu. Mfano: Kutoboa masikio, kupiga chale, au kutahiri.

UKIMWI hausambazwi kwa kugusana kwa kawaida na mtu aliyeambukizwa. Tofauti na

malaria hauambukizwi kwa njia ya mdudu wa aina yeyote. Na tofauti na magonjwa ya

njia ya hewa hauambukizwi kwa kuvuta hewa yenye maambukizi.

Kwa hiyo ni salama kabisa

kuishi katika chumba au nyumba moja na mtu mwenye UKIMWI.

kuonyesha heshima au upendo kwa kushikana mikono, kukumbatiana na kubusu

kwenye shavu.

kuchangia choo kisafi na mgonjwa.

kula pamoja.

Page 14: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 12

Una uwezekano mkubwa sana wa kuambukizwa UKIMWI, kama:

ukifanya mapenzi na mpenzi zaidi ya mmoja.

ukianza kufanya mapenzi katika umri mdogo.

ukifanya ngono bila kinga.

ukikataa kujifunza ukweli juu ya UKIMWI.

usipotibu kwa haraka magonjwa ya zinaa.

ukishiriki katika mambo ya kitamaduni kama vile tohara katika kikundi kwa kutumia

kisu kimoja.

ukirithi mke.

ukihangaishwa na umaskini na matokeo yake:

- ukila chakula kisichotosha na kisicho bora.

- usipopata uchunguzi wa afya na matibabu.

- ukikosa hata fedha ya kununulia kondomu wakati inapohitajika.

- ukihamia sehemu nyingine kutafuta kazi, na kisha kuwa na mahusiano mengine

a kimapenzi au kufanya mapenzi na wanaofanya biashara ya ngono.

Bila chakula, mfumo wa kinga unadhoofika na maambukizi yatokanayo na upungufu

wa chakula yanapata nafasi. Chakula bora ni bora kuliko dawa ya anti-retroviral ya aina

yoyote. Kuna uhusiano kati ya VVU na njaa: VVU kusababisha njaa, na njaa kuchangia

nguvu za VVU. Msumbiji kwa mfano ilipoteza 2.3% ya wakulima wake mwaka 2000

na inategemea kupoteza 20% kufikia 2020 (The Food and Agricultrue Organisation quoted

by Rory Carroll in The Guardian “Africa’s ugly sisters leave trail of death”, 30 October 2002).

Ni wazi kutakuwa na upungufu wa uzalishaji wa chakula, hata katika miaka yenye hali

nzuri ya hewa.

Jinsi ya kuzuia UKIMWI

A. Mambo ya ngono

a) Kutofanya mapenzi kabisa.

b) Kuwa mwaminifu kwa kufanya

mapenzi na mpenzi mmoja

mwaminifu.

c) Kondomu kama wewe au

mpenzi wako akifanya

mapenzi na mpenzi mwingine,

wakati wote atumie kondomu,

na aitumie ipasavyo.

d) Kwa kutofanya mapenzi na

mtu aliye na wapenzi wengi,

hasa kama mmoja kati ya

wapenzi wao ni kahaba.

Kamwe usifanye mapenzi na

mtu afanyaye biashara ya

kuuza mwili wake.

Page 15: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 13

Virusi vya Ukimwi vinaambukizwa kupitia

damu. Kwa hiyo uwe mwangalifu

unapowahudumia watu waliopata ajali.

B. Damu

a) Kwa kuhakikisha kwamba vifaa vya kutahiria, kutobea masikio vinachemshwa

kila wakati kabla havijatumika.

b) Kwa vyovyote ikiwezekana jaribu kuzuia upungufu wa damu na hivyo kuepuka

kuongezwa damu. Kama ni lazima uongezwe damu uliza kama imepimwa kuona

kama ina virusi vya UKIMWI.

c) Kwa kupata Ushauri Nasaha kutoka kwa mganga wako au kliniki kwa ajili ya

huduma baada ya kugusa damu kwa bahati mbaya au majimaji ya wakati wa

ngono, kubakwa au kuchomwa kwa sindano iliyotumika au wembe.

d) Kwa kuvaa mipira wakati wa kushika damu, mfano wakati wa ajali au wa kutoa

huduma ya kwanza. Damu inaweza kuwa na VVU na vinaweza kuingia mwilini

kwa njia ya jeraha au vidonda katika mikono yako.

C. Kutibu maambukizi.

a) Kwa kutibu maambukizi yote

haraka iwezekanavyo na kwa

uhakika.

b) Kwa kuchunguza magonjwa

ya ngono (STD) vidonda vya

sehemu za siri na majimaji

yatokayo katika uume au uke,

na kuyatibu haraka

iwezekanavyo. Magonjwa ya

ngono yanaongeza uwezekano

wa maambukizi ya VVU,

lakini yanaweza kutibiwa

haraka na kwa uthabiti.

D. Kutoka kwa mama kwenda

kwa mtoto

Kama mama ameambukizwa VVU

uwezekano wa kumwambukiza

mtoto wake umekadiriwa kuwa kati

ya 15% na 45%. Hii imegawanyika

kama ifuatavyo: (TALC, ” HIV

Infection – virology and transmission

(Africa)”

5-10 % wakati wa mimba.

10-20 % wakati wa kujifungua

2-10 % miezi miwili ya kwanza ya kunyonyesha kwa matiti.

5-10 % wakati wa kuendelea kunyonyesha.

Katika baadhi ya nchi dawa ya kuzuia uwezekano wa maambukizi ya VVU toka kwa

mama kwenda kwa mtoto inapatikana. Ni muhimu pia kutoongeza uwezekano kwa

kutofanya mapenzi bila kinga. Uwezekano kwa njia ya kunyonyesha unaweza

kupunguzwa kwa kunyonyesha kwa njia ya chupa, lakini hiyo inaweza kusababisha

madhara mengine, yawezekana makubwa zaidi.

Page 16: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 14

Sura 4: Njia ya anamed

Kwa nini “Madawa ya Asili?”

Kwa karne nyingi waganga wa kienyeji wamekuwa ndiyo watoaji wakuu wa huduma ya

afya ya msingi kwa waafrika wengi zaidi. Hata leo, inakadiriwa na shirika la Afya

duniani (WHO) kwamba 80% ya watu walio kusini bado wanatumia huduma ya afya ya

jadi kwanza. Kwa upande wa viwanda, shirika la afya duniani linakadiria kwamba 25%

ya madawa yanayopatikana kibiashara yametokana na mimea ambapo kwanza

yalitumika kwa kienyeji.

Kwa hiyo mimea imekuwa ikichangia sehemu muhimu katika suala la afya, na kwa

watu wengi zaidi katika sehemu za vijijini Afrika, bado wanaendelea kuitumia.

Kazi ya mimea ya madawa Ulaya na Amerika kaskazini ni ya muhimu vilevile,

inaendelea wakati wote kuchunguzwa ili kugundua dawa mpya.

Kwa kawaida dunia nzima kumekuwa na tabia yenye nguvu ya watu kupendelea

kutegemea huduma za afya za kizamani maana yake ni kwamba waganga na wauguzi

kwa upande mmoja na madawa ya kujitengenezea kwa upande wa pili. Watu wameanza

hata kugundua kuwa huduma za afya za kisasa ndizo zimekuwa chanzo cha matatizo ya

afya zao kuliko hata wao wenyewe.

Huko Ulaya na Amerika ya Kaskazini leo, hesabu ya watu wanaotumia tiba za asili

inazidi kuongezeka. Kwa mara nyingine wamekatishwa tamaa na kwamba madawa

mengi ya kibiashara yana madhara mabaya sana, na wanatamani kwa mara nyingine

kuchunga maisha yao kuliko wakati wote kuwategemea waganga maalum.

Mtu kuwajibika kwa afya yake maana yake ni kujali

a) kile anachokula na kunywa – yaani kupenda vyakula vya asili (vilivyolimwa

nyumbani), maji ya matunda na maji safi ya kunywa.

b) mtindo wa maisha - mfano kwa kutumia choo ambacho kinakuwa safi wakati

wote, kwa kufanya mazoezi, kwa kunawa mikono baada ya kutoka chooni na

kabla ya kula, kwa kutokuvuta sigara n.k.

c) hitaji la watu katika jamii kufanya kazi kwa pamoja, kwa mfano kufanya

maamuzi ya pamoja katika jamii, kuanzisha miradi ya kijamii n.k

d) kutafuta huduma bora mtu akiugua

Kwa sababu ya kuwa tegemezi katika madawa ya viwandani, wengi wetu tumepoteza

ujuzi na stadi za kutumia malighafi za asili kujitibu.

Tunajuaje kuwa madawa tuliyopendekeza ni salama na yanafaa?

Wengi wameuliza jinsi anamed ilivyounda mchanganyiko wa madawa katika vitabu

vyetu. Kwa miaka 20 iliyopita tumetumia mbinu hii:

1. Tunakusanya taarifa kuhusu mmea fulani au ugonjwa kutoka katika maktaba

mbalimbali, Internet, na kwa watumiaji wa mimea au madawa ya asili.

2. Tunaamua ubora na kufaa kwa kile tunachokipokea. Kuna michanganyiko mingi

ya madawa ambayo watu wameiendeleza toka kizazi hata kizazi. Kama

tukigundua kwamba mmea ule ule umekuwa ukitumika kwa njia ileile kutibu

ugonjwa ule ule katika dawa za jadi kwa zaidi ya nchi moja, basi hii inakuwa ni

njia ya kisanyansi, isiyo ya majaribio, na tuna uhakika zaidi katika mchanganyiko

Page 17: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 15

huu.

3. Tunatathimini dawa kwa kuangalia jinsi inavyofanya kazi na madhara yake –

tunalinganisha faida na hasara zake.

4. Ndipo tunawashirikisha washirika wetu waliotapakaa duniani pote katika hali ya

“kushirikishana ujuzi wa jadi” ambao lazima utumiwe kwa tahadhari.

5. Tunaupandishwa “ujuzi wa jadi” hadi kuwa “mapendekezo katika dawa ya asili”

kama

a) mchanganyiko huu tayari ni sehemu ya dawa za kisasa, (mfano eucalyptus

tincture),

b) masomo ya utabibu sasa yamehakikisha uwezo wake (mf. chai ya Artemisia)

au

c) washirika wetu katika nchi za tropiki wanatupa habari za matumaini makubwa

(mfano chai a mchaichai kwa wagonjwa wa UKIMWI).

Msingi wa Kikristo kwa anamed.

Mungu Baba aliumba dunia, na uzuri wake wa aina mbalimbali za viumbe hai, mimea

na wanyama. Alituweka katika dunia iliyojaa maliasili, ili kwamba kila jamii ya

viumbe vipate kukidhiwa mahitaji yake, kuvisaidia kuishi maisha bora. Aliumba

mwanadamu awe wakili katika mali hizi kuvilinda na kuvidumisha, na kugundua

matumizi yake. Mungu Mwana alikuja kama kristo masihi kutufundisha jinsi

tunavyoweza kuokolewa katika uchoyo wetu na katika hisia za hatia kwa makosa yetu.

Alionyesha kuwajali maskini na waliotengwa na jamii na akaendelea kuponya

wagonjwa.

Mungu Roho Mtakatifu anatupa nguvu na hamasa kupita katika hatua za Yesu katika

kuwafikia watu katika hitaji lao la ndani. Hii inajumuisha huduma ya uponyaji,

msisitizo ukiwa kwa wale wasioweza kulipia matibabu ya kawaida.

Kwa njia ya “dawa za asili” kwa hiyo, anamed inalenga kusaidia watu

a) kugundua tena mimea inayoweza kuponya. Maana yake ni kujifunza kugundua na

kustawisha mazao ya madawa, kutengeneza madawa na kutibu maumivu na

magonjwa.

b) kulinda rutuba ya ardhi, usalama wa maji ya kunywa, thamani ya mazingira na

jamii zote za mimea na mazingira.

c) kushirikiana kuinua afya zao na afya za kimwili na za kiuchumi za jamii kupitia

uzalishaji wa kawaida wa vyakula, madawa na huduma mbalimbali.

d) kukuza stadi na kujiamini kunakotakiwa kujenga ushawishi wa kisiasa, ili

kwamba miundo inayoruhusu malengo haya kufikiwa iendelezwe.

e) katika yote haya kumfurahia Mungu na uumbaji wake.

anamed leo ni ushirika wa watu na makundi yaliyosambaa dunia nzima, na hasa Afrika,

ambao wanatenda kazi katika hatua za mwanzo kabisa kuwasaidia watu kujitegemea

zaidi kwa upande wa afya zao na kuboresha hali zao kijamii, kiroho, na kiuchumi.

Vikundi vya anamed vinakutania DR. Kongo, Eritrea, Ethiopia, Ujerumani, Kenya,

Malawi, Msumbiji, Myanmar, Nigeria, Afrika ya Kusini, Sudani, Switzerland, Tanzania,

Uganda na Ukraine.

Page 18: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 16

Maana ya dawa za Asili

Faida za dawa za kimagharibi (za kisasa) Faida za dawa za asili, za mimea.

1. Zinajali usafi 1. Inatumia mimea inayopatikana katika

mazingira ya watu.

2. Zimekubalika kisayansi na kimataifa

2. Matumizi ya mimea matokeo yake ni

kiwango kidogo sana cha takataka zenye

madhara yanayoonekana kwa sasa na

yatakayoonekana baadaye.

3. Mganga ana mafunzo mengi, hivyo

anaelewa vyema mwili na ugonjwa.

3. Hakuna tatizo la fedha za kigeni kwa

madawa ghali, wala kuchelewesha

forodhani.

4. Wagonjwa wanafanyiwa uchunguzi

kamili kwa vipimo vya maabala

4. Kuna gharama chache kwa mganga,

hivyo ni nafuu kwa mgonjwa.

5. Dozi ni sahihi kabisa 5. Huleta ajira binafsi kwa bustani za

madawa na utengenezaji wa madawa.

6. Dawa zinatunzwa vizuri

6. Fedha zinazolipwa kwa huduma zinakaa

kijijini kwa hiyo zinachochea shughuli za

kijijini.

7. Mimea inatambulishwa kwa majina yake

ya kisayansi.

7. Mganga anaangalia pia matatizo ya

familia na jamii.

8. Serikali inasimamia viwango vya

huduma za tiba. 8. Inahamasisha kujitegemea.

9. Idadi kubwa ya wagonjwa inaweza

kutibiwa (mfano katika mlipuko wa

Ugonjwa)

9. Mganga anatumia lugha ileile ya watu.

10. Kuna ujuzi katika usimamizi na uongozi.

10. Waganga wa jadi wameenea nchi nzima,

hata vijijini zaidi na maeneo yasiyofikika

kwa urahisi.

11. Inafanya kazi bila ulozi. 11. Mara nyingine ndiyo huduma pekee ya

tiba inayopatikana.

anamed inaeleza maana ya “dawa za asili” kama

mchanganyiko wa faida za dawa za jadi za mitishamba na faida za dawa za kisasa.

Kwa hiyo, dawa za asili zina faida zote zilizotajwa hapo juu.

Kwa nyongeza waganga wa dawa za asili wanahamasishwa

a) kuelewa afya kwa undani wake, na kujali ubora wa maji ya kunywa, vyoo, nyumba

nzuri (mfano dohani), elimu, utunzaji wa ardhi na utupaji wa takataka

b) kutunza mazingira, kupanda miti na kulinda miti ya dawa porini.

c) kutengeneza bustani za madawa ili kupata kiwango cha dawa kinachofaa, matunda na

mbogamboga.

Kwa njia hii, huduma ya afya inayoeleweka zaidi hata katika kiwango kidogo cha bajeti

ya afya, inaweza kutolewa.

Page 19: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 17

Ukiishi na VVU na

kupata mimba, lishe bora

ni muhimu sana.

Ujamiiane na mme wako

tu na hata kwa hiyo

utumie kondom.

SURA 5: KUISHI NA UKIMWI/ VVU KWA MATUMAINI

Wagonjwa wa UKIMWI wanahitaji huduma maalumu kwa hiyo wahudumie kwa

upendo, huruma na kuwatia moyo!

Paracelsus, mwanafizikia mswizi wa karne ya 16, alisema juu ya tabibu “Msingi wa

muhimu kuliko yote katika dawa ni upendo“. Kwenye Biblia, Mithali 17:22 inasema juu

ya mgonjwa “Moyo uliochangamka ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka huikausha

mifupa”.

Kwa vitendo kumtibu mtu kwa upendo, huruma na kumtia moyo maana yake ni:

a) Kumweka mgonjwa katikati ya familia. Mkumbatie na mmfanyie mambo mengi

yanayohusisha kumgusa kimwili mwongee naye sana. Kama hawezi kuamka,

mweke katika chumba chenye shughuli nyingi nyumbani na kwenye mambo

mbalimbali na ya kumvutia kama inavyowezekana. Mpe matumaini, watu wengi

wamedumu hai wakiwa na magonjwa ya hatari sana, hata UKIMWI.

b) Wasaidie wagonjwa kujisikia wana thamani na umuhimu. Wagonjwa wanaweza

kusaidia katika bustani, kuwatunza wagonjwa wengine walio wagonjwa zaidi yao,

kutoa maelezo ya ugonjwa katika mashule na kutoa msaada na kutia moyo

wagonjwa wengine wa UKIMWI. Wakati wote kuna mambo mengi ya kufanya!

Hospitali liwe kimbilio la mwisho.

c) Tayarisha chakula bora. Wagonjwa wa UKIMWI,

kama watu wote kwa kweli, lazima wale lishe bora

ambayo ina proteini, vitamini, na madini. Matunda

na mboga za majani vina umuhimu wake katika

kumfanya mtu azidi kuwa na afya. Juice ya matunda

ya asili na chai ya mimea ya madawa (angalia sura

inayofuata) lazima vinywewe. Vinywaji vya

kibiashara vyenye sukari lazima viepukwe kabisa.

Maji salama kutoka kwenye kisima kilichotunzwa

ndiyo bora zaidi.

Fuata maelekezo yaliyotolewa katika sura I ya

“Madawa asili katika eneo la Tropiki: Tiba” Kama

una miti ya Moringa, tengeneza na utumie unga wa

majani ya moringa. Ni kirutubisho bora kabisa katika

vitamini, madini na proteini zilizomo.

Watu walio na virusi vya ukimwi wanahitaji vitamini

na madini zaidi kila siku kuliko wale wasio na virusi.

Madini muhimu ya zinki, magnesium, na chuma

yanapatikana kwenye mboga za kijani, jamii za

karanga, moringa, vitunguu saumu, uyoga na mayai n.k.

Ni bora kwa wagonjwa kula kidogo kidogo kila wakati, kuliko kutegemea kiasi

kikubwa cha chakula kinachopatikana mara chache kwa siku. Walio wagonjwa sana

wanatakiwa kupewa chakula ambacho kinayeyuka kwa urahisi kama vile supu

kuliko vyakula vigumu.

Kwa njia hizi kupoteza uzito kunaepukwa na mwili unakuwa na nguvu zaidi – na

hivyo kujikinga na maambukizi.

Page 20: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 18

Fanya kazi na wenzako!

Shirikishana matatizo na wengine

Someni kitabu hiki kwa pamoja

Anzisheni na msimamie bustani za mimea ya

madawa, mboga mboga na miti ya matunda.

Tengenezeni dawa za asili kwa pamoja.

d) Punguza uwezekano wa maambukizi. Tayarisha maji salama, tunza vyoo kwa

usafi, epuka hewa yenye moshi wa sigara, na epuka maambukizi toka kwa watu

wengine.

e) Fanya mazingira yawe ya kuvutia kadri iwezekanavyo. Fanya chumba kiwe cha

kupendeza, mwanga wa jua uwake ndani, na picha kwenye ukuta. Weka kitanda

kizuri. Tunza godoro kwa plastiki au shuka zilizorahisi kufua. Weka chandarua na

weka maua na majani yanayofukuza mbu chumbani. (mfano: tagetes, michaichai,

artemisia, mkaratusi).

f) Fanya massages: Tengeneza mafuta ya kuchua kwa kutumia mchanganyiko wa

majani ya mkaratusi na majani ya mlimau (angalia “maumivu ya misuli”, Sura 7)

g) Tibu magonjwa nyemelezi mara moja. Watu wachache wenye UKIMWI hufa kwa

athari za moja kwa moja za maambukizi ya VVU. Kwa kawaida kifo husababishwa

na mkusanyiko wa athari mbalimbali za maambukizi ya fursa au vimbe mbalimbali.

Viumbe au magonjwa ambayo kwa kawaida huleta tishio dogo kwa watu wenye afya

vinaweza kupelekea kifo kwa haraka kwa wale wenye UKIMWI hasa idadi ya CD4

+ lymphocyte inapopungua chembe 50 kwa microlitre ya damu.

Kwa hiyo ni muhimu kutibu maambukizi yote ya wagonjwa wa UKIMWI haraka na

kwa uhakika – angalia sura 7.

Kama una UKIMWI:

Kaa juani angalau nusu saa kila siku, ili kunufaika na miale ya nguvu za jua

inayoleta vitamini D

kwa ajili ya ngozi.

Fanya mazoezi kila

siku. Ni muhimu

kudumu na siha njema

kwa kadri uwezavyo.

Kwa hiyo kufanya kazi

kiasi fulani - kama kazi

ya bustani ndogo -

kunasaidia sana.

Uwe na matumaini. Mshukuru Mungu kwa

kila kitu katika maisha

yako ambacho ni cha

matumaini. Uone

UKIMWI kama

changamoto, ambayo

haiwezi kukushinda.

Wakati wote tumia kondomu wakati wa

kujamiiana ili

kutojiongezea

maambukizi au mwenzi wake.

Page 21: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 19

Mchukulie mgonjwa wa ukimwi

kama mwenzenu katika familia!

Mnaweza kula pamoja na

kuchangia vyombo mkiwa salama

kabisa. Tumieni muda wenu pamoja

naye kama ilivyokuwa kawaida

Endelea kufanya kazi! Kama ni kulima

shambani, kufanya kazi kama

seremala, au kufanya kazi ofisini - po

pote pale: endelea kufanya kazi! Fuata

maelekezo yaliyopo kwenye sura

inayofuata ili kuongeza kinga yako

kwa kutumia madawa ya asili.

Kwa ufupi: Kwa kutoa aina hii ya upendo na kujali, maambukizi makuu

yanayoambatana na UKIMWI yanaweza kupunguzwa sana. Familia nzima na jamii

vikifanya kazi kwa ushirikiano, maisha ya kiroho ya wote yananufaika.

Mwanakanisa wa kujitolea anayefanya kazi na Family AIDS Caring Trust (FACT)

Zimbabwe (HIV/ AIDS Study Pack for Community Development Workers, Tearfund, 1999)

aliandika yafuatayo:

“Walimjengea kijumba kidogo ambapo alilala mchana na usiku, akisubiri kufa. Hakuna aliyemtembelea kuongea naye, hata kuweka chakula chini tu na kuondoka. Nilienda kumtembelea lakini hakuna aliyeniruhusu kuingia katika chumba chake. Niliwasihi waniruhusu. Nilipofungua mlango ili kuingia, kulikuwa na harufu kali usiyoweza kuamini! Nilitoka nje nikatafute maji na kuyachemsha, nilimwosha nikisaidiwa na vijana wawili katika familia hiyo. Tulimweka juani - jambo ambalo alikuwa hajapata kwa miezi. Tulisafisha chumba chake na kufua nguo zake na blanketi ambazo zilikuwa zimegandamana kwa uchafu. Wakati tukisafisha chumba, uji ulikuwa ukitokota jikoni. Baada ya usafi, nilikaa pale nikimnywesha uji na kuongea naye. Kila siku nilikwenda kumwona, kumwosha na kumlisha. Ndugu na jamaa zake wakaanza kufanya hivyo hivyo. Alifariki baada ya majuma matatu, siyo tena kama aliye najisi na kutengwa bali kama aliyependwa aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu. Nilipomwambia Mungu anampenda na kwamba Yesu alikufa kwa ajili yake, alishikilia mkono wangu kwa nguvu. Ni kwa jinsi gani habari hii ni ya hatari ! Unafahamu matukio mengine yaliyo kama hayo? Kama tu familia hii wangechukulia sura hii ya kitabu kwa umuhimu, na wangekuwa wanajua juu ya madawa ya asili! Huyu mtu labda angeishi maisha mazuri kwa miaka kadhaa zaidi”.

Page 22: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 20

SURA YA 6: Chochea mfumo wa kinga mwilini kwa madawa ya asili

Kwa ujumla, dawa za ukimwi, ziwe za viwandani au za asili, zinafanya kazi ya:

1. kuzuia kuzaliana kwa VVU na |au.

2. kuua virusi vya UKIMWI na | au.

3. kuimarisha mfumo wa kinga mwilini (kwa kuongeza idadi ya chembe za T-

helper) na | au.

4. kuponya dalili za UKIMWI (kwa mfano kuharisha kunakoma, uzito

unaongezeka, siku za hedhi zinandelea tena, matatizo ya ngozi yanatoweka, na

matatizo ya kiakili (kisaikolojia) yanapungua.

Kuimarisha mfumo wa kinga, njia zote zilizotajwa katika sura iliyopita lazima zifuatwe.

Hasa hakikisha kwamba chakula chako ni bora na ni mlo kamili na ukae na hali nzuri ya

mwili kadri uwezavyo, tembea, endesha baiskeli au fanya kazi yoyote ya viungo katika

shamba kila siku. Kwa nyongeza, tumia angalau moja kati ya madawa ya asili

yafuatayo:

1. Allium sativum (vitunguu saumu) Weka vitunguu saumu vingi iwezekanavyo katika chakula cha kila siku, ili kuimarisha

mfumo wa kinga.

Subhuti Dharmananda (Subhuti Dharmananda (1996) “Garlic as the central Herb therapy for

AIDS” Institue for Traditional Medicine, Portland, Oregon, USA. Habari nzima inaweza kusomwa

kwenye web-site ya Gaia Research Institute, South Africa: www.gaiaresearch.co.za/garlic.html)

anapendekeza yafuatayo;

“Mara kiwango cha CD+T-cells kinapopungua kama 200 kwa mm³, matumizi ya dawa za

anti-retroviral hamna maana tena. Kushindwa kwa namna hiyo katika mfumo wa kinga

mwilini kunaendelea kwa kasi zaidi mara ukimwi unapostawi. Kwa hiyo, kila

liwezekanalo lifanyike ili kuzuia UKIMWI usistawi zaidi, na kutibu mara moja

maambukizi yoyote yanayojitokeza, ili kutoupa mzigo mfumo wa kinga mwilini.

Idara ya dawa za jadi inapendekeza dozi ya gramu 50 za vitunguu saumu kila siku (kama

kitunguu kimoja kizima) kwa matibabu ya maambukizi ya magonjwa mbalimbali kwa

wagonjwa wa UKIMWI. Kwa lengo la kuzuia maambukizi mengine mbalimbali dozi ya

chini kidogo inashauriwa ambayo ni vikonyo vitatu kwa siku.

Vitunguu saumu vinafanya kazi kama antiseptic, antibiotic, antiviral, anti-fungal, na anti-

diabetic. Umuhimu wake kwa UKIMWI ni kweli kwamba vitunguu saumu vimeonyesha

kuwa na uwezo kuzuia herpes simplex 1, ambayo ni aina ya virusi vinavyochochea

kuzaliana kwa VVU.

Watu wanaopata maumivu ya tumbo kama matokeo ya kula kiasi kikubwa cha vitunguu

saumu, wanashauriwa kunywa kiasi kidogo cha mafuta ya maji kama vile Alizeti au siagi

ambayo hufunika ngozi za tumbo na husambaza viasili vinavyosababisha maumivu. Huko

China vitunguu saumu vinatumika kutibu madonda ya tumbo.”

Kuna mabishano juu ya matumizi ya vitunguu saumu wakati mtu anatumia dawa za

ARV. Wachunguzi wengine wanasema vitunguu saumu vinapunguza nguvu ya dawa za

ARV, wakati wengine hawakubaliani (Dr. J.M. Louw (2004) “Garlic for HIV” - unpublished

paper, MEDUNSA (Medical University of South Africa) .

2. Artemisia annua

Kutokana na vitabu mbalimbali, wagonjwa wengi zaidi wa UKIMWI wana kinga ndogo

Page 23: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 21

katika chembe za mwili (cellular immunity) na kinga kubwa katika majimaji ya mwilini

(humoral immunity). Maana yake ni kwamba wana kiwango kidogo cha T-helper cells,

na kiwango kikubwa cha antibodies zinazoweza kuyeyuka. Kutokana na Dharmananda

(http:/www.gpo.or.th/rdi/NetZine./V3N42/pcp.htm) pamoja na haki miliki fulani (Luo,

Xuande (1998) “Qinghaosu Derivates against AIDS” European Patent Office, EP

713877), artemisinin inaongeza kinga ya chembe na kupunguza kinga katika majimaji

ya mwili na kwa hiyo kurudisha ulinganifu katika hali hii ya mwili.

“Mganga wa madwa ya kichina katika jiji la New York (Susan Paul) amekuwa akitumia

mmea huu katika kutibu wagonjwa wa UKIMWI kwa miaka mitatu iliyopita na amedai

kuwa ni salama na yenye manufaa dhahiri” (Dharmananda).

Haki miliki iliyotajwa hapo juu inasema “Lengo la ugunduzi wa sasa ni kupata kuzuia

UKIMWI chenye kiasi kidogo cha sumu, bei ndogo …” na pia linadai kwamba, kwa

kulinganisha na dawa za retroviral za kawaida, vitu vinavyopatikana katika Artemisia

annua“vina uwezo mkubwa wa kuua VVU , wakati uleule madhara ni machache!”

Sisi katika anamed hatujui ni kwa kiasi gani hii ni kweli, lakini watu wengi wenye VVU

wamefaidika kwa kiasi kikubwa sana, kama inavyodokezwa na habari ifuatavyo:

Sister Beatrice, muuguzi katika hospitali fulani huko Afrika ya Kusini, amelima shamba la Artemisia annua. Anatumia majani yake mabichi kila wakati kwa kutibu wagonjwa wa UKIMWI, wagonjwa wa njia ya hewa, kikohozi na mafua. Alitusimulia habari ifuatavyo:

Mfanyakazi wa hospitali aliyekuwa na VVU alikuwa anaharisha na kukohoa kwa majuma matatu. Alipewa maji chumvi (ORS), lakini alizidi kuwa dhaifu. Beatrix alitengeneza chai kwa kutumia viganja viwili vya majani ya artemisia. Siku moja baadaye mgonjwa alikuwa bado dhaifu, lakini aliweza kutembea na alipata njaa. Mgonjwa aliendelea kunywa chai ya artemisia na akaaanza kujisaidia haja kubwa ya kawaida, kikohozi chake kikakoma, alikula na kuongezeka uzito na ngozi yake ikawa na hali nzuri. Alipokuwa amekonda hakuna aliyemtembelea – lakini sasa wanamtembelea.

Kwa kupata historia hii tunaendelea kupendekeza yafuatayo: Kwa siku kumi za kwanza

weka lita moja ya maji yanayotokota kwenye vijiko vitatu vya chai vya majani makavu

ya artemisia. Iache kwa angalau dakika 15, ichuje na uinywe katika siku moja tu.

Baada ya hapo, kila siku, changanya kikombe kimoja (ml 250) za maji yanayotokota

katika kijiko kimoja cha majani makavu ya A-3. Acha itulie kwa angalau dakika 15,

chuja na kunywa chai hii asubuhi.

Kijiko kimoja cha chai cha majani makavu ya artmesia ni kama gramu 1.5. Badala ya

haya unaweza kutumia pia gramu 7.5 za majani mabichi. Kwa hiyo, kama una miti ya

artmesia shambani kwako, unaweza kuvuna majani kila siku. Idara ya Mazao ya Asili

huko Punjab, India, imeorodhesha Artmesia annua kama majani ya mimea 52 ambayo

“ina nguvu sana kuhusiana na UKIMWI na inayochunguzwa juu ya UKIMWI na

madhara yake, na imeonyesha kuwa na uwezekano wa kupambana na VVU”

(Bharate sandip B(2003) “Medicinal Plants with anti HIV potential” Journal of Med.

And Aromatric Plant Sci June, vol 25 (2) pp 427-440).

3. Azadirachta indica (mwarobaini)

Uwezekano wa maambukizo ya ngozi unaweza kupunguzwa kwa kutumia wakati wote

sabuni ya mwarobaini au maji ya kuogea ya moto ambamo kumewekwa majani ya

Page 24: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 22

mwarobaini. The Kibisom Project (Kenya), inayoshughulika na wagonjwa wengi wa

UKIMWI, inashauri kwamba wale makapi ya mwarobaini kila siku (yanayotokana na

mabaki ya mafuta ya mwarobaini). The Permaculture Project (Malawi) na Kuluva

Hospital (Uganda) wanatengeneza unga wa majani makavu ya mwarobaini na

wanawapa wagonjwa wa UKIMWI kijiko kimoja hadi viwili vya chai mara moja kwa

wiki.

4. Cymbopogon citratus (mchaichai)

Chai ya mchaichai: Chemsha kiganja kimoja cha majani mabichi ya mchaichai kwa

dakika mbili katika lita moja ya maji, acha kwa dakika 15 kisha chuja kwa chujio la

chai. Kunywa lita 2 kwa sehemu sehemu katika siku moja. Katika Moretele Sunrise

Hospice kule Afrika ya kusini Mpho Motlhasedi na wenzake wamegundua kwamba

wagonjwa wa UKIMWI wanaokunywa dawa hii kwa kufuata kanuni hii wanapata hamu

ya chakula, wanaongeza uzito na wanakuwa na nguvu.

5. Mangifera indica (mwembe)

Chai ya majani ya mwembe: Chukua kiganja kimoja cha majani machanga ya kijani ya

mwembe, chemsha taratibu katika lita moja ya maji kwa dakika 15, chuja na unywe

kwa sehemu sehemu katika siku moja.

6. Aloe vera

The Insitute of Herbal Medicine (Nairobi, Kenya) inafanya

uchunguzi wa Aloe katika kuimarisha kinga ya mwili. Aloe ina

acemannon, kiasili kinachoharibu VVU kwa kubadili ngozi yake

ya proteini kiasi kwamba haiwezi ikajishikiza kwenye T-

lymphocites. anamed inashauri kwamba wagonjwa wa UKIMWI

watumie kijiko kimoja hadi viwili vya nyama laini ya ndani ya

aloe kila siku.

7. Mazao ya asili ya Nyuki

Idara ileile inashauri matumizi ya Propolis kwa wagonjwa wa UKIMWI. Inapatikana

katika mizinga ya nyuki na imeonyeshwa kufanya kazi kama antibiotic, antifungal,

antiseptic na antiviral. anamed Bukavu (D.R Kongo) inatoa chai ya artemisia na

mchanganyiko wa asali na aloe kwa siku 20 kila mwezi na kitunguu saumu kila siku.

Chai ya Artemisia inatumika kama kwa malaria. Nyama laini za ndani za majani matatu

ya aloe zinachanyanywa na lita moja ya asali, na dozi yake ni vijiko vitatu vya

mchanganyiko huu mara tatu kwa siku, kabla ya kula. Vikonyo 10 vya vitunguu saumu

vinakatwa vipande vidogovidogo na kunywewa kwa maji mara tatu kwa siku.

8. Dawa ya maji (tincture) ya UKIMWI.

Daktari wa Hospitali ya ki-katoliki ya Neisu, D.R.Kongo, ametengeneza mchanganyiko

ufuatao wa madawa ambao wamekuwa wakiutumia kwa miaka kumi:

Kausha na usage kiasi kilicho sawa cha majani ya baadhi au yote kati ya mimea

ifuatayo: Azadirachta indica, Artemisia annua, Ocimum basilicum na Aloe vera.

Changanya gramu 100 za unga huu na ml 700 za kileo 95 % (kinachonywewa) na ml

300 za maji yaliyochemshwa. Chuja baada ya juma moja. Kunywa matone 30 mara tatu

kwa siku.

Page 25: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 23

SURA 7: Jinsi ya kutibu magonjwa yanayohusiana na UKIMWI kwa

mimea ya madawa

Kumbuka 1: Katika michanganyiko hii, mkono mmoja maana yake ni kiasi ambacho

mgonjwa anaweza kubeba, au kuficha, katika kiganja chake.

Kumbuka 2: Rejea zinafanywa mahali pote katika sura hii kwa matoleo mengine ya

anamed, kama ifuatavyo:

NM I “Madawa Ya Asili Katika Nchi Za Joto I; na Hirt na Mpia,

NM II “Madawa Ya Asili Katika Nchi Za Joto II: Uzoefu”

NM III “Natural Medicine in the Tropics III: Teachers´ Resource Kit“

Kumbuka 3: Siyo michanganyiko yote ya madawa inaweza kutengenezwa nyumbani

kwa urahisi. Tunapendekeza kwamba muungane au mtengeneze kikundi chenu cha

kusaidiana. Tafuteni msaada wa muuguzi au mfamasia katika kundi lenu ili kutengeneza

dawa nzuri zaidi za asili, au dawa za “kemikali” zinazotolewa katika NM III kwa

matatizo ya ngozi.

Kumbuka 4: Katika sura hii tunaorodhesha dalili au magonjwa mengi ambayo mara

nyingine, lakini siyo wakati wote, yanahusiana na maambukizi ya VVU.

Onyo: Baadhi ya magonjwa haya yanaweza kuwa ya hatari na yanatakiwa

yachunguzwe na kutibiwa katika Kituo cha Afya, hasa kama mapendekezo yetu hayaleti

ahueni haraka.

Maumivu ya tumbo.

Sababu zinazoweza kuwa zimesababisha zimeelezewa hapa chini kama vile gastritis

au maambukizi ya minyoo, malaria au homa ya matumbo (angalia kuharisha).

Sababu zingine ni kutoyeyushwa kwa chakula tumboni, matatizo ya utumbo,

maumivu wakati wa hedhi, shida za viungo vya uzazi na appendicitis.

Tibu minyoo. Kama maumivu yakiendelea na sababu haijulikani, jaribu yafuatayo:

Zingerber officinale (tangawizi): Saga kiganja kimoja cha tangawizi kwa dakika 10

katika lita moja ya maji. Kunywa katika siku moja.

Psidium guajava (mpera): Kama maumivu ya tumbo yalifuatiwa na kuharisha,

chemsha kiganja kimoja cha majani katika lita moja ya maji kwa dakika 20. Chuja na

unywe katika siku moja

Aloe vera (shubiri): Kila siku asubuhi kula nyama laini ya shubiri pamoja na maji

kidogo na asali.

Anaemia - Upungufu wa damu.

Upungufu wa damu hutokea wakati kuna chembe kidogo sana nyekundu za damu, au

chembe hizo hazina haemoglobin ya kutosha. Inaweza kusababishwa na kutopata

lishe bora, na madawa, na chemical (kama madawa ya kulevya) ambazo

zinasababisha chembe nyekundu kufa, au inaweza kuwa imesababishwa na safura.

Upungufu wa damu unaweza kusababisha uchovu, kupoteza hamu ya chakula, ngozi

kuwa nyeupe na hata kuwa na hamu ya kula majivu au udongo mfinyanzi, ambayo

ndiyo njia ya mwili kujaribu kupata madini – chumvi zaidi.

Kula vyakula vyenye wingi wa chuma. Hivi ni pamoja na nyama (hasa ini) na

samaki, mboga za majani yenye kijani sana (kama moringa, mchicha, majani ya viazi

Page 26: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 24

vitamu), maharage. Kula mboga na matunda ambazo zina vitamini C kunasaidia

mwili kufyonza chuma. Kupikia katika vyungu vya chuma kunasaidia (epuka vyungu

vya aluminium kama inawezeana). Kama hakuna njia nyingine ya kupata madini ya

chuma, chomeka misumari safi ya chuma katika tunda la limau, na kunywa maji yake

baada ya siku kadhaa.

Wakati huo huo, mtibu mgonjwa kwa tiba ya minyoo kama ilivyoelezwa hapa chini.

PUMU (Asthma)

Pumu husababisha upumuaji kuwa mgumu sana, kwa sababu mirija midogo midogo

ya hewa katika mapafu inazibwa na makohozi. Mara nyingi kuna sauti kama filimbi

wakati mgonjwa anapumua. Mara nyingine hali inakuwa mbaya zaidi usiku. Mara

kwa mara pumu inarithiwa, inaweza kuwa reaction kwa kitu kilicholiwa au

kilchovutwa katika pumzi, na inaweza kuchochewa na mafua ya kawaida.

Lazima wakati wote pumu ishughulikiwe kikamilifu, kwa sababu wakati wowote

inaweza kuwa mbaya zaidi.

1. Mziwaziwa (Euphorbia hirta) (numba ANM-001)

a) Vuta kama sigara majani makavu yaliyosokotwa kama sigara, au

b) weka kichwa chako juu ya kiganja kimoja cha majani haya usiku au

c) chemsha gramu 15-30 (kiganja kimoja) za majani mabichi yaliyooshwa (au

yaliyokaushwa kama itahitajika) katika kikombe kimoja cha maji (ml 500) kwa

dakika 10. Iache itulie kwa dakika 15, kisha chuja, kunywa kwa

sehemusehemu katika siku moja. Rudia tiba hiyo kwa siku 8 mfululizo.

2. Mkaratusi (Eucalyputus globulus): Twanga kiganja kimoja cha majani mabichi

au yaliyokaushwa kisha yaweke katika ml 250 za maji yanayochemka. Vuta kwa

dakika 15 wakati bado yanaendelea kutoa mvuke wa moto, wakati kichwa na

sufuria vikiwa vimefunikwa kwa taulo (ANM – 002)

3. Papai (Carica papaya): Vuta moshi wa majani machanga mabichi yaliyokaushwa

katika kiko au yakiwa yamekunjwa kwenye karatasi kama sigara, au choma

majani hayo pembeni mwa kitanda, au katika chumba ulichokaa, na uvute moshi

wake. (ANM-003).

4. Sigara ya pumu yenye nguvu; kwa kutumia mranaa (Datura stramonium)

Sigara zenye nguvu kwa ajili ya pumu hutengenezwa kama ifuatavyo:

Majani makavu ya Datura stramonium 150mg

Majani makavu ya Eucalyptus globulus 150mg

Majani makavu ya Carica papaya 700 mg.

Yafanye kuwa sigara kwa kutumia karatasi, au yavute katika kiko. (ANM-004).

Harufu mbaya mdomoni

Safisha meno kwa kufuata kanuni, tumia kitawi cha mwarobaini au mkaratusi, au dawa

ya kusafisha meno uliyojitengenezea (angalia NM I). Kama tatizo likiendelea, tatizo

linatoka tumboni. Kwa tatizo hili tumia mkaa kidogo wa dawa. (ANM – 011)

Madonda ya kitandani

Kwa kuzuia na kutibu tumia dawa ya mafuta ya vitunguu maji (angalia NM II) (ANM –

015).

Page 27: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 25

Tumaini kwa wakati ujao!

Mama kutoka nchi ya Kongo

anamwonesha mtoto wake papai

ambalo lina uwezo wa kutibu

magonjwa mbalimbali.

Magonjwa ya njia ya hewa, kikohozi na mafua.

1. Vitunguu saumu (Allium sativum) (ANM – 021).

Matibabu yote ya vitunguu saumu yanaweza kuambatana na kunywa juisi ya

malimau mawili katika maji. Limau

huongeza vitamini, na husaidia mwili

kutumia vitunguu saumu.

a) Kula vitunguu saumu vibichi –

kikonyo kimoja kutwa mara tatu. Kwa

tatizo kubwa zaidi ongeza kiwango hiki

mara mbili hadi mara tatu.

b) Asali ya vitunguu saumu: Jaza chupa/

glasi kwa vikonyo vya vitunguu saumu

vilivyomenywa na kukatwa katwa

vipande vidogo vidogo. Taratibu

mwaga asali ndani yake ili ijaze nafasi

zote kati ya vitunguu saumu

zilizokatwa katwa. Weka chupa/ glasi

hiyo kwenye sehemu yenye joto kiasi

cha nyuzi 20° C. Katika majuma

mawili hadi manne asali itanyonya

majimaji ya vitunguu saumu na

vitakuwa laini na nyeusi nyeusi.

Usiichuje. Itumie katika miezi 3.

Kunywa kijiko cha chai kila baada ya

masaa kadhaa.

c) Mchanganyiko wa sukari na

vitunguu saumu: Tiba hiyo ni nzuri

kwa kikohozi. Saga vitunguu saumu

kiasi cha kijiko kimoja cha chai.

Changanya na kiasi kilekile cha sukari au asali. Tumia siku hiyohiyo. Tumia

kijiko kimoja cha chai kila baada ya masaa kadhaa.

2. Vitunguu maji (Allium cepa); (ANM – 022).

Ni kama vitunguu saumu lakini si vikali.

a) Mchanganyiko wa kitunguu maji na sukari: Katakata kitunguu maji

kibichi na nyunyizia sukari ya hudhurungi (brown sugar) juu yake, funika

kwa sahani na ukandamize kwa kitu kizito juu yake. Baada ya saa chache

hutoa maji maji mengi ya hudhurungi ambayo ni matamu na hutibu kikohozi

kwa umri wowote.

b) Kinywaji cha kitunguu maji: Changanya ½ kikombe cha kitunguu

kilichokatwa katwa na ½ kikombe cha maji, koroga, kunywa mchanganyiko

huo kwa sehemusehemu ndani ya siku moja.

3. Artemisia (Artemisia annua): (ANM – 023)

a) Chai ya artemisia. Kunywa kikombe cha chai ya artemisia kutwa mara tatu

iliyotengenezwa kwa kumwaga vikombe vitatu vya maji yanayotokota

Page 28: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 26

kwenye kijiko kimoja cha chai cha majani makavu ya artemisia (au mara tano

zaidi kama majani ni mabichi).

b) Kuvuta mvuke

c) Weka kijiko kizima cha majani makavu au kiganja kimoja cha majani mabichi

ndani ya maji ya moto na uvute mvuke wake.

4. Mwembe (Mangifera indica): Chukua gramu 30 (kiganja kimoja) cha majani

machanga mabichi ya kijani na uyachemshe katika lita moja ya maji kwa dakika

10. Chuja na unywe kwa sehemu sehemu katika siku moja. Usiitumie kwa

mfululizo kwa zaidi ya siku 8. (ANM – 024)

5. Mkaratusi (Eucalyptus globulus): (Siyo kwa watoto walio chini ya mwaka 1)

a) Chai ya mkaratusi: Twanga kiganja kimoja cha majani makavu au mabichi

na uyachemshe katika lita moja ya maji kwa dakika 5. Chuja na unywe kwa

sehemu sehemu katika siku moja. (ANM-025 a).

b) Mafuta ya mkaratusi: Taratibu chemsha kiganja kimoja kikavu na

kilichosagwa cha majani ya mkaratusi katika nusu kikombe cha mafuta ya

kula kwa saa moja katika fukizo – maji. Sugua kifua kwa mchanganyiko huu

mara mbili kwa siku. Usitumie kwa watoto waliochini ya mwaka 1. (ANM-

025 b)

c) Dawa ya kikohozi ya mkaratusi (Syrup): Mwaga lita moja ya maji

yanayochemka kwenye gram 65 za majani makavu, funika na weka kwenye

sehemu yenye joto kiasi kwa masaa 6. Chuja. Ongeza gramu 180 za sukari

katika kila ml 100 za chai hii, chemsha kwa muda mfupi kisha chuja. Watoto

wenye miaka 7 watumie kijiko kimoja cha chai mara tatu kwa siku, na walio

chini ya umri huo watumie kidogo zaidi kufuatana na uzito wao. Walio na

umri mkubwa zaidi pamoja na watu wazima watumie chai ya mkaratusi

kuliko hii dawa yenye sukari (syrup). (ANM-025 c)

d) Matone ya kikohozi ya mkaratusi:

Mwaga mchanganyiko wa 700 ml za kileo (chenye kileo 95% yenye ubora wa

kunywewa) na ml 300 za maji yaliyochemshwa na kuchujwa, kwenye gramu

100 ya majani makavu ya mkaratusi. Baada ya juma moja, yakamue na

kuondoa majani. Watu wazima watumie matone 30 ya hii dawa ya maji,

kutwa mara tatu (ANM-025 d).

e) Dawa ya kikohozi ya mkaratusi iliyo na kileo: Chanyanga gramu 250 za

majani makavu yaliyotwangwa ya mkaratusi katika lita tano za divai ya asali

na ukoroge vyema. Weka sehemu yenye joto kiasi, ikiwa imefunikwa lakini

bila kukoroga, kwa siku tano. Chuja na tunza katika chupa za lita moja moja

zisizoruhusu hewa kuingia. Baada ya kufungwa tunza katika sehemu isiyo na

unyevu wala mwanga. Kipimo: Watu wazima: kijiko kimoja cha chai, kutwa

mara tatu; watoto (mwaka mmoja na zaidi): matone 20-40, kutwa mara tatu

(ANM – 025 e).

f) Kuvuta mvuke wa mkaratusi: Twanga kiganjwa kimoja cha majani mabichi

au makavu, kisha chemsha katika ml 250 za maji. Vuta kwa dakika 15 wakati

bado inaendelea kutoa mvuke, kichwa chako kikiwa kimeinamishwa ndani ya

chombo hicho na vyote vikiwa vimefunikwa taulo. (ANM – 025 f)

Page 29: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 27

6. Limau (Citrus limon): (ANM-026)

a) Chai ya majani ya mlimau: Chemsha viganja 2 vya majani machanga

(makavu au mabichi) katika lita moja ya maji. Chuja na unywe kwa sehemu –

sehemu ndani ya siku moja. (ANM-026 a)

b) Chai ya ganda la limau: Katakata vipande vidogo vidogo vya maganda ya

limau. Changanya kiganja kimoja na lita 1 ya maji yanayochemka. Acha

kwenye sehemu yenye joto kiasi kwa dakika 15, kisha chuja. Watu wazima:

Kunywa kiasi hiki katika siku moja. Watoto: wanywe kiasi kidogo zaidi

kufuatana na uzito wao. Kumbuka limau hizi zisiwe zimepuliziwa madawa

ya kuua wadudu. (ANM-026 b)

7. Tangawizi (Zingiber officinale) (ANM – 027 )

a) Dawa ya tangawizi (Tincture): Chukua tangawizi iliyokatwa katwa na

changanya na kileo cha kutosha chenye 80% ya kileo, chenye ubora wa

kunywewa, kitakachofanya ujazo wa ml 100. Iache kwa juma moja, kisha

kamua. Kunywa matone 10-20 ya dawa hii mara 3-4 kila siku. (ANM – 027a)

b) Chai ya tangawizi: Tengeneza dawa ya kuchemsha ya mizizi ya tangawizi

mibichi au mikavu, na uchanganye na kijiko kimoja cha chai cha asali (ANM

– 027 b)

8. Embe mafuta (Persea americana): Tengeneza dawa ya kuchemsha kutokana na

majani machanga (kiganja kimoja katika lita moja ya maji) na uinywe kidogo

kidogo ndani ya siku moja (ANM-028)

9. Chungwa (Citrus sinensis): Chemsha kiganja kimoja cha majani katika lita 1 ya

maji kwa dakika 2; na unywe yote ndani ya siku moja. (ANM-029)

10. Michaichai (Cymbopogon citratus): Chemsha kiganja kimoja cha majani katika

maji kidogo na uvute mvuke wake. (ANM-030)

11. Chumvi ya mezani: Yeyusha vijiko viwili vya chai vya chumvi katika lita 1 ya

maji. Ipulizie kuelekea puani mwako na uvute hewa kwa nguvu. (ANM – 031)

“Miguu inayowaka moto”

Wagonjwa wengi wa UKIMWI hulalamika juu ya hali ya miguu kuchemka. Fuata

mapendekezo yetu kwa matibabu ya “matatizo ya ngozi”

Saratani

Angalia Kaposi´s Sarcoma (Saratani ya ngozi).

Candida ya mdomoni (Mtando mweupe mdomoni)

Ni maambukizi ya mba (fungus) yanayosababishwa na yeast candida albicans. Mba

ya aina hii inapatikana katika midomo ya watu wengi. Kwa kuwa mara kwa mara

husababisha uvimbe (inflammation) wakati kinga ya mwili ikipungua, basi ugonjwa

huu wa mdomoni hujitokeza kwa wagonjwa wenye tatizo la kinga ya mwili (mfano:

Ukimwi).

Candida inaweza kusababsiha uvimbe (inflammation) pia vijidudu ambavyo kwa

kawaida vinaishi juu ya ngozi vikikosekanawa. Hii inaweza kutokea kama mgonjwa

ametumia dawa ya antibiotic kwa muda mrefu.

Maambukizi hudhihirishwa na vidonda vidogo vidogo vyenye rangi ya maziwa au

mabaka mekundu. Dalili nyingine ni kupoteza hamu ya kula (inayosababishwa na

Page 30: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 28

maumivu ya mdomoni), ulimi kuwa mweupe, vidonda mdomoni na mara nyingine

kuvimba tezi. Matibabu yafuatayo husafisha mdomo na kusaidia madonda kupona.

Nyingine huchochea utoaji wa mate, ambao husaidia kufanya mdomo ukae na

unyevu.

1. Chai ya majani la mwembe (angalia juu) (ANM-040)

2. Nyonya nyanya iliyoiva sana, au kipande cha nanasi iliyoiva - mara mbili kwa

siku (ANM-041)

3. Nyonya tini pori mara mbili kwa siku (ANM-042)

4. Nyonya limau, au likamulie katika maji na chumvi (ANM-043)

5. Chai ya mchaichai (angalia huko juu) (ANM-044)

6. Kitunguu saumu na asali – tumia kijiko kimoja cha chai kila baada ya masaa

kadhaa (ANM-045)

7. Tafuna majani mabichi ya Artemisia annua masaa katikati ya milo. Watoto

wanaweza kupendelea mchanganyiko wa kijiko cha chai cha asali na kijiko cha

chai cha majani makavu yaliyosagwa ya artemisia – (ANM-046)

8. Sukutua kooni kwa chumvi na maji.( ANM-047)

9. Safisha mdomo kwa kikombe chenye maji yaliyochanganywa na kijiko kimoja

cha chai cha bicarbonate of soda. (ANM – 048)

Kama kula ni tatizo, epuka matunda jamii ya machungwa na malimau kwa muda,

kwa sababu yanasababisha maumivu. Kula chakula mara kinapopoa na ule vyakula

laini kama vile uji na viazi vilivyopondwa pondwa.

Maambukizi makali ya Candica, mfano maambukizi yanayosababsiha chakula

kutokupita kwenye mfereji wa chakula: Madaktari katika hospitali moja ya watoto

ya Afrika ya kusini, wametengeneza namna ifuatayo, ambayo imefanya kazi hata

ambapo tiba za kisasa zimeshindwa:

Menya vikonyo vya vitunguu saumu, twanga gramu 50 na uchanganye na ml 100 za

maji baridi (salama na safi). Tikisa kwa nguvu sana. (Kama kinapatikana weka

mchanganyiko huu kwenye kikorogeo cha umeme). Chuja, chukua maji na uyatunze

katika sehemu ya baridi sana uwezavyo. Kipimo: mtoto mwenye umri wa mwaka

mmoja: kunywa ml 1 kila baada ya saa 4; mtu mzima: kunywa ml 5 kila baada ya saa

4. Kama itafaa changanya na ml 50 za maji ya machungwa. (ANM-049)

Candida ukeni (maambukizi ya mba ukeni)

Dalili za maambukizi hayo ni mwasho mkali, na midomo ya uke inakuwa mikundu

sana na inauma. Inaweza kuleta maumivu wakati wa kukojoa. Osha au pulizia eneo

hilo kwa maji ya vinegar (changanya vijiko 6 vya chai vya vinegar (siki) katika lita 1

ya maji yaliyochemshwa na kupoa). Kama hakuna vinegar karibu tumia maji ya

limau yaliyochanganywa na maji. Kwa matibabu ya ndani, kunywa chai ya mchaichai

au chai ya majani ya mwembe, na utumie kitunguu saumu katika chakula chako kila

siku. Kwa nje tumia moja ya haya yafuatayo:

a) Mchanganyiko wa vitunguu saumu vilivyopondwa pondwa na mafuta, katika

uwiano wa 1:1 (ANM – 060)

b) Mchanganyiko wa vitunguu saumu viliyopondwa na Yoghurt katika uwiano wa

1:10 (ANM –061)

Page 31: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 29

c) Ointment ya Artemisia au mafuta ya Artemisia (ANM – 062)

Cytomegalovirus

Ni virusi viletavyo ugonjwa wa ngozi wa malengelenge ambao mara nyingi huathiri

wagonjwa wa UKIMWI. Kwa matibabu, angalia maambukizi ya ngozi na jamii ya

mkanda wa jeshi.

Kuharisha

Kuharisha kunaweza kusababishwa na maambukizi ya Ukimwi yenyewe, ukosefu wa

lishe bora, maambukizi ya amiba, malaria, salmonella, homa ya matumbo,

kipindupindu n.k. Angalia NM II kwa maelezo zaidi ya jinsi ya kutibu uharishaji wa

aina mbalimbali. Tayarisha maji-chumvi (ORS) kwa kuweka vijiko viwili vya chai

vilivyojaa vya sukari na nusu kijiko cha chai cha chumvi kwenye maji

yaliyochemshwa. Wakati wote tumia hii (ORS) ukiambatanisha na matibabu

yafuatayo:

1. Chai ya mziwaziwa (Euphorbia hirta): Chemsha kiganja kimoja cha majani

mabichi yaliyooshwa katika lita moja ya maji kwa dakika 5. Chuja na unywe

kidogo kidogo ndani ya siku moja. Endelea na matibabu haya kwa siku 8

mfululizo. (ANM-070)

2. Chai ya majani ya mwembe (angalia sura 6) (ANM-071)

3. Kikombe kimoja cha chai ya mchaichai na kikombe kimoja cha maziwa (angalia

sura 6) (ANM-072)

4. Karoti: Osha karoti kubwa mbili, zikatwe vipande vidogo vidogo, vichemshe

kwa taratibu kwa dakika 5 katika lita moja ya maji na ule kila kitu. Au ule karoti

bichi mbili. (ANM-073)

5. Chai ya Artemisia: Inaamanika kwamba chai hii huondoa maambukizi ya

magonjwa kwenye matumbo na huimarisha mfumo wa kinga mwilini (ANM-

074)

6. Mchele (Oryza sativa): Kunywa maji ya mchele (maji ambamo mchele ulikuwa

umepikwa), au tengeneza mkaa wa dawa kutokana na mchele au maganda ya

karanga kwa kutumia njia iliyoelezwa katika NM I (ANM – 075)

7. Mwarobaini (Azadirachta indica): Chemsha majani 40 ya mwarobaini (yaliyo

moja moja) katika kikombe kikubwa cha maji kwa dakika 5. Chuja, poza na

unywe katika siku moja (ANM-076)

8. Kula kiasi kidogo cha chakula kwa wakati mmoja. Ndizi zilizopondwa pondwa

ni nzuri. Epuka vyakula vya mafuta. (ANM-077)

Maumivu ya sikio – maambukizi ya sikio

a) Kitunguu maji (Allium cepa): Kata kata kiganja kimoja cha vitunguu maji

vipande vidogo vidogo sana. Viweke kwenye kipande cha nguo nyepesi. Tumia

hivyo kama kikandamizo kwenye na nyuma ya sikio. Vifungie kwenye kichwa

kwa kutumia kitambaa. Badilisha vitunguu asubuhi na jioni. Hata usiku mzima

sikio lililoathirika likiwa kwenye kifuko kilichojazwa vitunguu vilivyokatwa

katwa vipande vidogo vidogo. (ANM-090)

b) Mwarobaini (Azardirachta indica): Weka matone machache ya mafuta ya

mwarobaini ndani ya sikio (ANM-091)

Page 32: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 30

Uchovu/ ulegevu

1. Chai ya mimea ya dawa – hasa michaichai, majani ya mwembe au chai za

artemisia (ANM-100)

2. Hewa nzuri na mazoezi (ANM-101)

3. Kula vyakula vyenye wingi wa madini ya chuma (mfano moringa) na vitamini

(hasa matunda) (ANM – 102)

Homa

Maambukizi ya UKIMWI pekee yanaweza kusababisha homa, kama uwezavyo

mlolongo wa maambukizi yanayofuatana na UKIMWI, mfano: malaria, kichomi cha

mapafu, homa ya matumbo, uti wa mgongo, surua.

1. Cymbopogon citratus (mchaichai): Kunywa lita tatu za chai ya mchaichai kila

siku. (ANM – 110)

2. Mangifera indica (mwembe) au Tamarindus indica (ukwaju): Chemsha viganja 3

vya majani katika lita 2 za maji kwa dakika 5, acha ipoe na tumia maji haya

kumwosha mgonjwa. Au ongeza maji baridi zaidi, loweka taulo ndani yake na

uweke kwenye kichwa, kifua au miguu ya mgonjwa.

Maumivu wa tumbo/ vidonda vya tumbo (Gastritis)

Ugonjwa wa tumbo unaosemwa hapo ni mwako wa tabaka la ndani la tumbo.

Inaweza kusababishwa na athari za matumizi ya asprini, au kwa hasira inayojirudia.

Vidonda vya tumbo ni madonda katika tumbo au utumbo mdogo yanayosababishwa

na tindikali. Dalili za vidonda ni tumbo kuuma sana, kuwaka kama moto na njaa.

Maumivu huonekana kutokea wakati tumbo likiwa tupu. Mara nyingi maumivu

yanaondolewa na kunywa maziwa, kula au kwa kunywa maji mengi, lakini yanaweza

kuongezeka saa moja baadaye. Ni bora kula kidogo kidogo mara kwa mara kuliko

kula kiasi kikubwa mara moja tu. Vidonda vya tumbo huonekana kupona, na

baadaye vinaanza tena.

1. Mlongelonge (Moringa oleifera) na kabeji (Brassica oleracea). Ongeza unga wa

moringa na/au kabeji mbichi katika chakula cha kila siku (ANM-120)

2. Mpera (Psidium guajava)

a) Kula matunda mabichi ya mpera (ANM-121 a)au

b) tengeneza chai ya majani ya mpera: Chemsha kiganja kimoja cha majani ya

mpera katika lita moja ya maji kwa dakika 20. Chuja. Kunywa kidogo

kidogo katika siku moja (ANM-121b)

3. Shubiri (Aloe vera (syn. Aloe barbadensis), Aloe ferox na Aloe arborescens).

Kata na uoshe vizuri jani la mmea. Osha kisu kikali kwa kukiweka ndani ya maji

yanayochemka. Kata miisho na pande za jani na uzitupe, kisha kata kupitia

katikati ili kupata eneo kubwa la ndani ya jani. Chukua nyama hizi za ndani

zisizo na rangi kwa kutumia kijiko cha chai.

Tumia kijiko kimoja cha chai cha nyama hizi mara tatu kwa siku (ANM-122).

4. Mranaa (Datura stramonium). Tumia matone 5 hadi 10 ya dawa ya maji ya

mranaa, kutwa mara 3. (Hii lazima itayarishwe na mfamasia mzoefu pekee kwa

sababu ya sumu iliyomo) (ANM-123)

5. Viazi vitamu (Ipomoea batatas). Pika viazi vitamu, vikate vipande vidogo

Page 33: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 31

vidogo, vikaushe na uviponde hadi kuwa unga. Kunywa kijiko kimoja cha chai

kwa maji kidogo, kutwa mara tatu (ANM-124)

Maumivu ya kichwa.

Maumivu ya kichwa yanaweza kusababishwa na uchovu, mkandamizo wa mawazo

na mahangaiko, mapigo ya moyo kuwa juu (high bloodpressure), uti wa mgongo,

ugonjwa wa macho na ukosefu wa miwani kwa matatizo ya macho, na mafua.

Kunywa lita 3 za maji safi kwa siku. Tibu chanzo cha tatizo kama kinajulikana. Kwa

maumivu makali ya kichwa, jaribu kahawa, au chai iliyotengenezwa kwa majani ya

mti wa mkahawa, au chai ya artemisia, au chai ya majani ya karanga, au majani ya

passionfruit. Kwa mbadala wa kahawa, tafuna ngongolia kama inapatikana. (NM-

130)

Herpes (Vilengelenge vya ngozi)

Herpes Zoster (Jamii za mkanda wa jeshi): Watoto duniani kote kwa kawaida

wanapatwa na maambukizi kama tetekuwanga. Kwa kawaida unatambulika kwa

malengelenge yanayouma sana ambayo yanatokeza upande mmoja wa mwili.

Herpes simplex (cold sores): Vidonda hivi mara nyingi vinapatikana vikizunguka

mdomo. Vidonda katika viungo vya uzazi vinasambazwa kupitia njia ya kujamiiana.

Jamii za mkanda wa jeshi na vidonda visivyouma vyote ni maambukizi ya virusi, na

vinaweza kutibiwa kama ifuatavyo:

1. Allium sativum (vitunguu saumu): Tengeneza mafuta ya vitunguu saumu kwa

kuweka vitunguu vilivyokatwa katwa au vilivyopondwa pondwa kwenye mafuta

mazuri ya mbegu za mimea (siyo pamba) kwa siku kadhaa. Weka mafuta haya

kwenye vidonda mara mbili au tatu kwa siku (ANM-120)

2. Plumeria regio (frangipani; msanapichi). Kamulia utomvu mweupe kutoka

kwenye kitako cha ua kwenye kidonda. Inaua vijidudu na inasababisha ganzi.

(ANM – 142)

3. Azadirachta indica (mwarobaini) (ANM-143)

i. Weka mafuta ya mwarobaini kwenye sehemu iliyoathirika hadi vilengelenge

vitakapokauka. (ANM-143a)

ii. Kunywa dawa ya maji iliyotengenezwa kwa gramu 2.5 za majani makavu

katika lita moja ya maji ya moto. Tumia katika siku moja kwa siku saba.

Tengeneza dawa mpya kila siku. (Dawa hii pia inasaidia kurudisha hamu ya

chakula.) (ANM-143 b)

Mwako wa mapafu, matumbo au macho.

Kunywa chai iliyotengenezwa ama kwa maua ya Matricaria chamomilla

(chamomile) au kwa Artemisia annua. Ili kutibu macho chuja moja ya chai hizi kwa

karatasi na uoshe macho kwa chai iliyopoa, kwa kutumia kitambaa ambacho

kimechemshwa ili kuua vijidudu vyote. (ANM – 150)

Mishtuko ya matumbo.

1. Dawa ya maji ya mranaa inaweza kutengenezwa kama ifuatavyo. Changanya:

- mbegu za mranaa (Datura stramonium) zilizokaushwa na kusagwa gramu 8

- kileo halisi chenye ubora wa kunywewa 95% ml 45

Page 34: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 32

- maji salama na safi ml 55

badala ya kuchanganya maji na kileo halisi unaweza kutumia kileo chenye 45%

(kati ya 40 na 50%), mfano gin au whisky.

Acha kwa juma moja, kamua na uchuje. Dawa hii ni sawa na dawa ya maji ya

belladona kwa kuzingatia kiwango cha atropine kilichomo.

Matumizi:

Watu wazima: Kiwango cha juu ni matone 30 mara 3 kwa siku.

Watoto: Tone moja kwa kila kilo ya uzito, mara 3 kwa siku. (ANM – 160)

Onyo: Dawa itengenezwe na Mfamasia tu !!

2. Mbegu za mranaa. Kama dawa ya maji ya mranaa haipatikani, ama tumia dawa

inayouzwa katika maduka ya madawa, au tafuna na kumeza kati ya mbegu 10

hadi 15 za Datura stramonium, kiwango cha juu kiwe mara tatu kwa siku hadi

mishtuko itakapokoma. Kwa kuwa mmea huu una atropine, tiba hii ina madhara

ya kukausha kinywa, mapigo ya moyo kuwa juu (high bloodpressure) na matatizo

ya usagaji wa chakula tumboni. Tumia kwa uangalifu – mmea una sumu kali

sana!

Kaposi´s Sarcoma. (Saratani ya ngozi)

Ni namna ya saratani ambayo mara nyingi inatokea kwa wagonjwa wa UKIMWI.

Kwa kawaida mara ya kwanza inatokeza kama baka lenye rangi ya pink, nyekundu,

au zambarau ambalo linaweza kuwa na umbo la duara au la yai. Mabaka haya

yaweza kutokeza sehemu yoyote katika mwili, mara nyingi usoni. Katika kipindi cha

miezi kadhaa yanaweza kutokeza katika sehemu mbalimbali mwilini, ikiwa ni

pamoja na mdomoni, katika viungo vya ndani na kwenye lymphnodes za mwilini

ambapo husababisha damu kuvujia mwilini.

Vitabu vya kisayansi vya siku hizi vinataarifu kuwa Artemisia annua inaweza

kutumika kutibu baadhi ya aina za kansa na hasa kansa ya damu na kansa ya matiti.

Kama hakuna aina nyingine za dawa ya kansa zinazopatikana, jaribu mchanganyiko

ufuatao: Mpe mgonjwa vidonge vyenye madini ya chuma (vya kuongeza damu;

Ferrous) asubuhi, na mchana mpe lita 1 ya chai ya artemisia kwa kutumia gramu 5 za

majani makavu. Endeleza matibabu haya kwa juma moja, na urudie kwa juma moja

kila mwezi. (ANM-170)

Kupoteza uzito wa mwili

Kula aina mbalimbali za vyakula vinavyopatikana katika mazingira yako. Usitumie

sukari, maziwa ya unga au vitu vilivyoingizwa kutoka nchi za nje – vyakula

tunavyozalisha ni vizuri kama siyo bora zaidi ya vile tunavyoagiza. Angalia jedwali

katika sura 1 ya NM I (ANM – 180)

Malaria

Angalia NM II kwa maelezo zaidi ya jinsi ya kutibu malaria.

Yafuatao ni madawa ya asili unayoweza kutumiwa kwa kutibu malaria, kwa kuanzia

na zile za malaria isiyo kali na kumalizia na zile za malaria kali.

Cymbopogon citratus (mchaichai) (ANM –190)

Allium sativum (vikonyo vya kitunguu saumu) (ANM – 191)

Zingiber officinale (mizizi ya tangawizi) (ANM-192)

Page 35: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 33

Psidium guajava (chai ya majani ya mpera) (ANM-193)

Carica papaya (chai ya jani la mpapai) (ANM-194)

Cassia occidentalis (sanamaki) (ANM-199)

Azadirachta indica (chai ya mwarobaini) (ANM-195)

Vernonia amygdalina (chai ya majani au mizizi ya majani machungu) (ANM-196)

Cinchona officinalis (chai ya gamba la mwinini) (ANM-197)

Artemisia annua (chai ya majani ya artemisia) (ANM-198)

Maumivu ya misuli

Kama mgonjwa ana maumivu ya misuli, na/au anaonekana kuzidi kukonda, mchue

kila siku. Tengeneza mafuta ya kuchulia kama ifuatavyo:

Kwanza twanga majani, ambayo lazima yawe yamekaushwa vizuri. Tumia moja au

yote kati ya mimea mitatu ifuatavyo: Mkaratusi, mlimau na mchungwa. Kisha chukua

kikombe kidogo (kama ml 100) cha unga wa kila mmea na uchanganye na lita moja

ya mafuta ya kula. Chemsha mchanganyiko huu katika fukizo – maji kwa saa moja.

Chuja huo mchanganyiko, na uache mafuta ya kuchua yapoe bila kuyakoroga. Tunza

hayo mafuta katika chombo kisichopitisha hewa kwenye sehemu yenye giza. (ANM-

200)

Kichefuchefu na kutapika

Angalia pia matibabu kwa magonjwa ya tumbo.

1. Tumia unga wa tangawizi kijiko kimoja cha chai (kisichojaa) kutwa mara tatu.

(ANM-210).

2. Kunywa chai ya tangawizi kabla au wakati wa chakula. Kwa kila kikombe cha

maji chukua vipande 2 vya tangawizi vibichi vilivyooshwa, vichemshe polepole

kwenye maji ya moto kwa dakika 10 (ANM-211).

3. Kula hasa vyakula kama vile wali au mkate, na vyakula vilivyochemshwa kama

viazi, magimbi, uji. Punguza kiwango cha mafuta kinachotumika kwenye upishi,

na ule matunda jamii ya machungwa na limau kwa sababu yanasaidia mwili

kuyeyusha mafuta. (ANM – 212)

4. Kwa utapikaji wa hali ya juu, tumia Cannabis sativum (angalia chini ya

“maumivu’) (ANM-213)

Harufu ya mwili

Hii inaweza kutokea kwa sababu ya vidonda vyenye uchafu na usaha.

Tibu tatizo! Angalia matibabu chini ya vidonda. Inaweza pia kutokea kama matokeo

ya kuharisha na kukojoa kitandani. Uwe makini kwa usafi, osha mwili wakati wote

na kwa makini, fanya chumba kipate hewa vizuri, na ingiza maua yanayonukia vizuri

chumbani.

Maumivu

Kunywa chai iliyotengenezwa kwa kuchemsha majani ya Hibiscus sabdariffa

(rosella). Maua ya Hibiscus yana Vitamin B ambayo inasaidia kwa maumivu ya

mishipa ya fahamu. Inazuia pia kukua kwa bakteria za kifua kikuu. (ANM-220)

Maumivu ya kichwa mara nyingine yanaweza kuondolewa kwa kunywa kahawa.

Kwa maumivu ya matumbo, angalia kwenye vidonda yya tumbo na mishtuko ya

Page 36: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 34

matumbo.

Kama mgonjwa anakaribia kufa na anasikia maumivu, avute majani machanga

makavu ya Cannabis sativum (mbangi) ili kupunguza maumivu. Kwa mbadala, bangi

inaweza kutumika kama dawa ya maji (kwa kunywa) au kama tincture. Omba ruhusa

kwenye mamlaka inayohusika na madawa – katika nchi nyingi matumizi ya mbangi

hayaruhusiwi kisheria. (ANM-221)

Kichomi cha mapafu (pneumonia)

Haya ni maambukizi makali ya mapafu, na kinaweza kuanza kutokana na magonjwa

yoyote ya njia ya hewa kama vile kikohozi au magonjwa ya mirija ya hewa. Dalili

zake ni pamoja na baridi ya ghafla na kisha homa kali, kupumua kwa juu juu na kwa

haraka haraka, kukohoa, mara nyingine kikiambatana na makohozi na mara nyingi

vidonda (herpes) usoni au kwenye midomo.

Inabidi mgonjwa atafute huduma ya matibabu. Ikikosekana, tiba zilizoorodheshwa

chini ya “magonjwa ya njia ya hewa, kikohozi na mafua” ndizo zifuatwe, hasa uvutaji

wa mvuke wa mkaratusi au artemisia. (ANM-230)

Kutunza ngozi na usafi

Kwa kumwoshea mgonjwa tumia sabuni ya maji uliyojitengenezea. Inatengenezwa

kama ifuatavyo;

Vipimo vinne vya sabuni (ya viwandani au uliyojitengenezea) isiyo na rangi, kipimo

kimoja cha mafuta ya kula na kipimo kimoja cha maji. Pondaponda hiyo sabuni na

uichanganye na hayo maji na mafuta. Chemsha mchanganyiko huo taratibu hadi

sabuni iyeyuke na kuungana na maji na mafuta. Koroga mchanganyiko huo hadi

utakapopoa, na uumwage kwenye vyombo vyenye umbo unalotaka. Acha kwa

majuma mawili kabla ya kutumia. (ANM-240)

Sabuni hii inaweza “kuwekewa dawa” kwa kuiongezea matone kadhaa ya mafuta ya

mwarobaini, au majani makavu ya mwarobaini yaliyotwangwa/sagwa au

mlongelonge kabla ya kumwagwa kwenye vyombo vyenye maumbo.

Saratani ya ngozi.

Panapokuwa hakuna dawa nyingine, tumia mafuta ya mwarobaini au nyama za ndani

za jani la shubiri (Aloe vera) kupaka kwenye eneo lililoathirika mara mbili kwa siku.

Kwa nyongeza kunywa chai ya artemisia, angalia pia Kaposi´s Sarcoma. (ANM-250)

Matatizo ya ngozi.

Wagonjwa wa UKIMWI mara nyingi wanalalamika juu ya “mwako wa miguu” na

matatizo ya ngozi yasiyo na chanzo kinachojulikana, kama vile upele aina ya

“eczema”. Tunapendekeza kwamba uanze kwa kuishughulikia ngozi kwa kutumia

vitu vinavyoipa afya, na kwa makini ukiendelea kwa tiba za kuua vijidudu ambazo

pia zinaongeza ukali wa matibabu kwa jinsi athari zinavyozidi kujitokeza.

Tukianza na ile yenye nguvu za chini, tunapendekeza yafuatayo:

Persea americana (embe mafuta): Changanya nyama za embe mafuta lililoiva na

matone kiasi ya maji ya limau na upake kwenye sehemu iliyoathirika kwa masaa

12 kwa siku - mfano kwa usiku mzima (ANM-264)

Mafuta ya kula, kama vile mafuta ya mawese, mafuta ya alizeti, mafuta ya

karanga: Changanya kijiko kimoja cha chai cha mafuta haya na kimoja cha maji

Page 37: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 35

Washiriki wakichuana taratibu kwa

mafuta ya yabisi baridi wakati wa

Semina ya anamed huko Koritok,

Uganda.

katika kiganja cha mkono, na usugue kwenye sehemu iliyoathirika. (ANM-265)

Nyama za jani la shubiri (Aloe vera) (ANM-266)

Brassica oleracea (kabeji): Tumia jani kama kifungio (ANM-262)

Mafuta yaliyotengenezwa kutokana na mafuta ya mboga mboga na mimea kama

vile mpera, chamomile na artemisia. Kwa maelezo ya jinsi ya kuchanganya,

angalia mchanganyiko wa mafuta ya bawasiri katika NM-I (ANM-267)

Dawa ya mafuta iliyotengenezwa kutokana na mafuta haya ukiongeza 10% ya nta

ya nyuki (ANM-268)

Mafuta ya mbono (kutokana na

Ricinus communis), ama ikiwa

imetengenezwa kiwandani au kwa

kienyeji kijijini au kwa kufuata

maelezo ya jinsi ya kuchanganya

katika NM I. (ANM-269 a)

Cassia alata: Tengeneza

mchanganyiko (kama uji mzito) kwa

kutumia majani yaliyosagwa na

mafuta. (ANM-263)

Azadirachta indica (mwarobaini):

Osha sehemu iliyoathirika kwa chai

ya mwarobaini, au ifunge kwa

kitambaa ambacho wakati wote

utakilowanisha kwa chai ya

mwarobaini au sehemu iliyoathirika

ikae katika maji vuguvugu ambamo

chai ya mwarobaini imechanganywa.

Matibabu yenye nguvu zaidi ni uji-uji

wa majani yake uliochanganywa na

mafuta au maji au dawa ya mafuta

kutokana na majani, au mafuta ya

mwarobaini (ANM-261)

Allium cepa (kitunguu maji): Kama

mafuta au dawa ya mafuta (ointment).

Angalia NM I (ANM-269 b)

Capsicum frutescens (pilipili): Paka mafuta ya pilipili au dawa ya mafuta ya

pilipili kwenye sehemu iliyoathirika. Pilipili ina dawa ya kuua vijidudu na mara

nyingine huondoa mwasho. Angalia dawa ya mafuta ya yabisi baridi katika NM I

(ANM-269 c).

Allium sativum (vitunguu saumu): Mafuta ya vitunguu saumu yanatengenezwa

kama ifuatavyo: Weka vitunguu saumu vilivyomenywa na kukatwa vipande

vidogo kwenye chombo na ufunike kwa kutumia mafuta ya mzeituni (au mafuta

mazuri ya mbogamboga). Funga chombo hicho na ukiache kwenye sehemu yenye

uvuguvugu wa kama 20°C kwa siku tatu. Itikise mara kadhaa kila siku. Kisha

itunze kwenye sehemu baridi, bila kuichuja. Uitumie ndani ya kipindi cha siku

Page 38: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 36

tatu. (ANM-260)

Mafuta ya upele: Mchanganyiko ya nusu kwa nusu na mafuta ya taa na ya mafuta

ya kula hautumiki tu kwa kutibu upele, bali pia kwa matatizo mengine, mfano

kuwashwa kunakosababishwa na filaria. (ANM-269 d)

Allium sativum (kitunguu saumu): Menya na ukate vitunguu saumu na uvisugue

kwenye eneo lililoathirika. Kwa ajili ya tiba bora zaidi, funga kipande cha

kitunguuu saumu au vitunguu saumu vilivyopondwa pondwa kwenye sehemu

iliyoathirika wakati wa usiku. (ANM-269 e)

Maelezo zaidi juu ya matatizo ya ngozi yanaweza kupatikana katika NM I na II.

Kama kwa mfano michanganyiko yote hii haifanyi kazi, unaweza kujaribu madawa

yenye gharama zaidi ambayo yana mchanganyiko kwa mfano wa cortisone, iodine au

sulphur. Lakini pamoja na hayo huhitajiki kutumia fedha nyingi. Muulize muuguzi au

mfamasia aliye karibu nawe ili kupata mchanganyiko wa kemikali uliotajwa katika

NM III.

Uchovu

Pata mapumziko ya kutosha, kula matunda mengi, kunywa chai ya mimea ya dawa,

hasa chai ya mchaichai, majani ya mwembe na chai ya artemisia na kula chakula

chenye virutubisho vyote (angalia NM I).

Kifua kikuu (TB)

Kifua kikuu ni ugonjwa wa kuambukizwa na unaoweza kuua. Unasababishwa na

bakteria walio katika hewa (Mycobacterium tuberculosis, M. bovis au M. africanum).

Kwa kawaida hawa bakteria wakivutwa katika hewa, kwa haraka mfumo wa kinga

mwilini unawazuia kufanya kazi. Wakati mwingine vidudu hutulia ndani ya mwili

bila kufanya kazi, kisha wakati fulani mfumo wa kinga mwilini ukiwa dhaifu, kwa

mfano kwa sababu ya UKIMWI, hao bakteria wanaanza kazi. Kifua kifuu

kinaenezwa wakati mgonjwa wa kifua kikuu akiwakohoa bakteria, ambao wanaweza

kukaa hai katika hewa kwa masaa kadhaa. Kifua kikuu kwa kawaida huanzia kazi

kwenye mapafu, lakini kinaweza kuathiri sehemu nyingine za mwili.

Dalili za kifua kikuu ni kikohozi kisichopona, hasa baada tu ya kuamka, homa kidogo

wakati wa mchana, kutoka jacho (mara nyingine kwa wingi) wakati wa usiku,

maumivu kifuani, kupungua uzito na kwa watu wenye ngozi nyeusi, ngozi kupauka.

Jinsi ugonjwa unavyoendelea unaweza kusababisha kukohoa damu.

Ugonjwa huu unazuiwa kwa kuimarisha kinga ya mwili katika njia zilizoelezwa hapo

juu. Mgonjwa wa kifua kikuu anahitaji madawa ya antibiotic na misaada mingine ya

kiuguzi. Kwa nyongeza fuata maelekezo yaliyotajwa chini ya magonjwa ya njia ya

hewa hapo juu.

Minyoo

Kuna aina mbalimbali za minyoo na viumbe wengine wadogo wadogo sana.(vimelea)

ambao wanaweza kuishi kwenye matumbo ya watu na kusababisha magonjwa.

Minyoo wakubwa zaidi, kama roundworms, threadworms na tegu inaweza kuonekana

katika haja kubwa. Hookworms (safura) na whipworms ni mara chache zinaweza

kuonekana kwenye haja kubwa, ingawa inaweza kuwa imekwishaingia katika tumbo.

Page 39: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 37

Kuzuia:

1. Wakati wote tumia vyoo.

2. Wakati wote vaa viatu wakati wa kulima.

3. Kula kipande cha jani la mpapai (Carica papaya) (ukubwa wa 5 x 5cm) kila siku

au baada ya siku kadhaa kula kijiko cha mezani kimoja cha mbegu za mpapai.

Minyoo inaonekana kuchukia ladha hii hata zaidi ya binadamu na itaondoka na

kukuacha. (ANM-270)

Tiba:

1. Papai (Carica papaya)

Matunda mabichi ya mpapai yana kimeng’enyo kiitwacho papaine ambacho

huondoa karibu aina zote za minyoo ya tumbo, hata tegu. Utomvu wake

unavunwa kwa kuchana tunda bichi likiwa bado mtini.

Utomvu unatumiwa mara moja, wakati wa asubuhi wakati tumbo likiwa tupu,

kwa pamoja na maji mengi na dawa ya kusababisha kuharisha. Dawa moja nzuri

ya kusababisha kuharisha ni ringworm bush (Cassia alata): Mwaga kikombe cha

maji ya moto kwenye kijiko kimoja cha chai cha majani makavu au gamba la

mzizi, chuja baada ya dakika kumi na unywe kabla ya kwenda kulala. Pia

kunywa maji mengi.

Kipimo cha utomvu wa papai kutibu minyoo:

Umri (miaka) Idadi ya vijiko vya chai.

miezi 6 - mwaka 1

mwaka 1- miaka 3

Miaka 4 - 6

miaka 7 - 13 miaka

miaka 14 na zaidi

½

1

2

3

4

Haya matibabu ya minyoo yanaweza pia kutolewa kwa mgonjwa ambaye

anaharisha. Papaine inaweza isiondoe minyoo yote kwa mara moja, kwa sababu

hiyo tunapendekeza kurudiwa kwa matibabu baada ya juma moja kama hatua ya

tahadhari. (ANM-271)

Kwa mbadala kula kijiko cha mezani kilichojaa cha mbegu za papai lililoiva kwa

siku tatu, mara tatu kwa siku. Kwa watoto iwe pungufu, kutokana na uzito wa

watoto. Kwa kuondoa minyoo iliyokufa, kunywa maji mengi. (ANM-275)

2. Mziwaziwa (Euphorbia hirta)

Osha na uchanganye:

mziwaziwa (mmea mzima bila mizizi) kiganja kimoja

majani ya mpapai kiganja kimoja

Chemsha kwa dakika 5 katika lita moja ya maji, kisha chuja. Kunywa kwa

taratibu na iishe ndani ya siku moja. Kama mtoto akikataa kunywa chai hii,

itayarishe kwa kutumia kiganja kimoja cha mziwaziwa pekee (ANM-272)

3. Lesena (Leucaena glauca) – kwa ajili ya hookworms (safura) na roundworms

Page 40: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 38

Kausha mbegu 30 zilizoiva, zisage na unywe unga wake kwa kikombe cha maji

ya kunywa ya moto masaa 2 baada ya kifungua kinywa. Watoto watumie kidogo

kufuatana na umri na uzito wao. Siyo nzuri kwa watoto wenye umri chini ya

miaka 7. Madhara yake: Matatizo ya tumbo, kuharisha. (ANM – 273)

4. Boga (Cucurbita maxima) – kwa tegu.

Changanya gram 100 (au vijiko vya mezani 20) za mbegu mbichi zilizosagwa

pamoja na maji na uvile pamoja na dawa ya kusababisha kuharisha kabla ya kula

chochote (asubuhi). Dawa ya kuharisha ni muhimu sana, kwa sababu minyoo

haiuawi, bali hupooza tu. Kwa dawa ya kuharisha ya asili kula mapapai yaliyoiva

mengi sana au maembe. (ANM-274)

Madonda, majipu, vidonda vyenye maambukizi

Vitibu kama ilivyopendekezwa katika NM II. Vitibu haraka mara tu vinapoonekana,

kwa sababu uponaji huenda polepole sana kwa mwili wenye kinga dhaifu.

Kwanza osha kidonda: Weka kijiko kimoja cha mezani kilichojaa chumvi katika lita

moja ya maji yaliyochemshwa au hata vyema zaidi weka katika chai ya majani ya

mpera. Kwa kuosha kidonda chenye maambukizi weka matone matatu ya utomvu wa

papai lisiloiva katika mchanganyiko huu.

Mimea na vifaa ambavyo mara nyingi vinatumika kutibu vidonda ni:

- Mchanganyiko wa asali na sukari (ANM-280)

- Kwa vidonda vinavyotoa usaha, changanya gramu moja ya sukari na tone moja la

utomvu mweupe wa papai bichi. Jaza na ufunike kidonda kwa mchanganyiko huu.

Funika kwa kitambaa na urudie tendo hilo mara moja kwa siku (ANM-286)

- Kipande cha papai (Carica papaya) kwa kuondoa usaha (ANM-282)

- Vipande vya vitunguu saumu (Allium sativum) kuondoa usaha chini ya ngozi.

Kwa hiyo vitumiwe kwa majibu yasiyo na mdomo. (ANM-283)

- Dawa ya mafuta ya vitunguu maji (Allium cepa) kwa kubandika juu ya vidonda.

(ANM-284)

- Dawa ya mkaa inaweza kuwekwa juu ya kidonda kilicho juu juu kinachotoa

usaha. (ANM-285).

Page 41: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 39

SURA 8: Mwitikio kutoka kwa wanaotumia

HUYAMU - (Idara ya Afya, AICT, Mara & Ukerewe Dayosisi, Tanzania)

HUYAMU ina vikundi viwili vya Wanaoishi na VVU vinavyojulikana kwa jina la

"Kaza Roho" . Pamoja na kutiana moyo, kutembeleana na kufundishana,

wanatengeneza madawa ya asili.

Madawa mengi ya ANAMED yanaonesha mafanikio ya ajabu - hasa Artemisia,

inayolimwa katika shamba kubwa nje ya Musoma. Artemisia huwa inatumiwa kwa wiki

nne mfululizo ile mara ya kwanza mtu anapokuja kwenye kundi. Baadaye inatumika

mara moja kila mwezi kwa siku 7.

Wagonjwa wengi waliokuja wakiwa wamedhoofika sana au hata wale waliotembelewa

nyumbani kwa kushindwa kutembea, walipata nafuu sana kutokana an Artemisia.

Lakini pia majani ya Mlonge yanaonesha mafanikio makubwa. Wanakikundi wote

wanatumia Mlonge katika milo yao.

Mlonge pia inaonesha mafanikio makubwa kwa watoto wanaoishi na VVU. Kwa watoto

watatu waliokuwa wadhaifu na wenye uzito pungufu, Mlonge ilileta nguvu na

wameongeza uzito sana.

Mafuta ya Artemisia pia inaonesha mafanikio makubwa kwa kila aina ya shida ya ngozi

na wengi walishuhudia msaada mkubwa kwa matatizo ya ngozi kutokana na mafuta ya

Artemisia.

Mwanakikundi mmoja alikuwa na CD4 count ya 28 alipoanza kuja kwenye kikundi.

Kutokana na Artemisia na Mlonge CD4 ilipanda kuwa 207 na pia aliongeza kilo 15 za

uzito na kuwa mwenye Afya njema.

Mifano mingi zaidi zingeweza kutajwa!

Kwa wanaotumia ARVs Artemisia na Moringa zinasaidia sana pia. Wanakikundi

wanasema zinapunguza matatizo yanayoweza kujitokeza kwa upande wa matumizi ya

ARVs lakini pia inasaidia kupata lishe bora hata kama hela hazipo.

The Moretele Sunrise Hospice, Temba, South Afrika

Mpho Sebanyoni – Motlhasedi aliacha kazi yake kama muuguzi Januari 1997 ili

kuanzisha Moretele Sunrise Hospice.

Maono ya Mpho na wasaidizi wake ni kupata jamii inayojali, iliyo na ujuzi wa mambo,

inayoendesheka, na yenye huruma. Mambo yanayoendeshwa na kituo hicho ni pamoja

na:

1. Kuwatembelea wagonjwa wa UKIMWI pamoja na familia zao majumbani mwao.

2. Kutoa elimu kuhusu utunzaji wa wagonjwa majumbani.

3. Mambo ya watoto.

4. Kusaidia vikundi vya watu wa rika mbalimbali.

5. Ushauri: Huu ni pamoja na ushauri kabla ya kupimwa, ushauri baada ya

kupimwa, ushauri wakati wa tatizo kujitokeza, na ushauri wakati wa kufiwa.

6. Kuanzisha na kuendeleza miradi ya uzalishaji.

7. Bustani ya mboga na mimea ya madawa.

8. Mpango wa kuwasaidia wanaowatunza waathirika

Page 42: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 40

9. Upimaji wa VVU.

10. Kuchua kwa kutumia mafuta yaliyotengenezwa nyumbani kutokana na madawa

ya mimea ya kwenye bustani ya madawa.

Watu wengi hununua mafuta, chai za dawa, na dawa za mafuta ambazo kituo

hutengeneza kutokana na mimea yake, na wengi wanakuja kwa ajili ya mafunzo.

Mpho anasema kwamba, katika kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI

chai ya mchaichai hufanya maajabu – inawapa wagonjwa nguvu na hamu ya

chakula.

chai ya majani ya mwembe ni bora sana kwa matibabu ya magonjwa ya njia ya

hewa, kukohoa, na madonda ya koo.

chai ya chamomile husaidia kutibu maambukizi ya makoo, yaani maambukizi ya

njia ya hewa kama vile ugonjwa wa kuumia kikoromeo (sehemu ya koo inayotoa

sauti) - (laryngitis)

Kibisom Women´s Group Project, Kisiwa cha Rusinga Kenya

Esther Odhiambo ameanzisha na anaendesha mradi mzuri sana unaojitegemea huko

katika kisiwa cha Rusinga. Ni mahali pazuri na pasipo na mawasiliano ambapo watu

wanateseka na umasikini mbaya mno. UKIMWI umeenea. Esther na kikundi chake cha

watu wanaojitolea wanafanya shughuli mbalimbali. Kundi hili la watu wanaojitolea,

linajumuisha vijana wenye uelewa, waliosoma vizuri lakini hawana ajira pamoja na

wajane wengi ambao wanawalea wajukuu zao.

- Wanatoa mwongozo na ushauri katika namna ambayo inaruhusu watu kueleza

hofu zao na matatizo kwa siri.

- Katika makundi wanajadili matatizo ya UKIMWI, na uhusiano wake na tabia ya

ngono, kwa wazi kabisa na bila hofu.

- Wamejenga shule ya watoto, ili kwamba watoto yatima, hata wale wa familia

maskini kabisa, waweze kupata elimu ya msingi.

- Wanatumia madawa ya asili na wanawafundisha wengine. Sabuni

walizojitengenezea zina mafuta ya mwarobaini ambayo yanasaidia kwa matatizo

mengi ya ngozi.

- Wameanzisha miradi ya uzalishaji ambayo hutoa siyo tu kipato bali pia nafasi

kwa watu kujisikia wana umuhimu na kuthaminiwa tena.

Miitikio mingine ya anamed

Sister Beatrix kutoka Afrika ya Kusini anayejishughulisha zaidi na wazee anasema

kwamba chai ya artemisia hurudisha hamu ya kula na anaitumia mara nyingi kwa

magonjwa ya njia ya hewa na kwa kuharisha. Alipewa mbegu za Artemisia annua

mapema 2001 na bado hadi leo anazalisha artemisia!

Kiongozi wa tiba wa Grace Church huko Bukavu, DR Kongo, Patrick Milabyo, aliandika: Mwaka 2003 tulizalisha kilo 17 za dawa ya mafuta ya yabisi baridi, na pia

chai ya artemisia na dawa ya mafuta ya maambukizi ya mba, yote ni kutokana na

mimea. Kwa kila dollar tuliyotumia tulirudisha dollar 3, yaani kiwango cha faida 200%

kwa ajili ya hospitali yetu.

Teresa Alajo wa CHIPS peace-making team ya kaskazini – mashariki ya Uganda

Page 43: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 41

anaripoti baadhi ya mambo ya kushangaza. Baada ya kuwa amefundishwa katika

semina ya anamed jinsi ya kutengeneza “dawa ya mafuta ya yabisi baridi” kutokana na

pilipili, ameweza kufanikiwa kuitumia kutibu aina mbalimbali za matatizo ya ngozi! Pia

anatumia “mafuta ya upele ya anamed” kwa upele na Carica papaya kwa minyoo.

Kwenye kambi za wakimbizi, mahali ambapo hali ya afya na usafi hayakuwa nzuri,

chai ya Euphorbia hirta (mziwaziwa) ilikuwa ndiyo iliyotumwa na Mungu kwa ajili ya

kuharisha.

anamed AIDS Care, Kinshasa, inayoongozwa na Maledi Ibanda, inaendesha semina

za kuzuia UKIMWI, na tiba yake kwa madawa ya asili, katika majimbo mengi

mbalimbali huko Kongo ya magharibi. Maledi anasema kwamba mama mmoja

mwenye miaka 25 aliyekuwa na UKIMWI alikunywa chai ya artemisia kila siku na

kuongeza unga wa majani ya mlongelonge kwenye chakula chake. Baada ya miezi

mitatu alikuwa ameongeza kg 5 kwenye uzito wake. Kwa sasa anaendesha kikundi cha

kujitegemea kwa wagonjwa wengine.

Innocent Balagizi wa Bukavu, DR Kongo aliwatibu wanakikundi wa kikundi cha

kujitegemea (“kujitegemea kwa mazao ya asili”) – kwa kutumia chai ya artemisia,

shubiri (Aloe vera), asali na vitunguu saumu. Wanane kati yao walionyesha kuongezeka

kwa uzito, ongezeko la idadi ya chembe nyeupe za damu, na kuongezeka kwa kiwango

cha kuganda kwa damu. Uchunguzi huu ulifanyika katika maabara ya hospitali huko

Goma. Tutafurahi kusikia uchunguzi zaidi kama huo kutoka kwa wasomaji wetu.

Innocent pia anasema kwamba chai ya artemisia, chai ya Vernonia amygdalina na

shubiri (aloe)/asali kwa sasa viko katika matumizi ya kawaida kwa wagonjwa wa

UKIMWI huko Kongo ya Mashariki. Mama mmoja ambaye kila siku alikula nyama za

shubiri (aloe), asali na vitunguu saumu, aliongeza uzito wake kutoka kilo 40 hadi 65

katika mwaka mmoja, na sasa ndiye mhamasishaji mkuu wa kikundi cha UKIMWI

Goma.

Page 44: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 42

SURA 9: Mapendekezo kumi kwa serikali za nchi za kusini

Kutokana na taarifa zote zilizo katika kijitabu hiki, anamed inaamini kwamba, kama

serikali zingechukua hatua zifuatazo, hali yao ya utoaji wa huduma ya afya

ingeboreshwa sana:

1. Zisaidie matumizi ya madawa ya asili, na kwa mahusiano ya karibu ya utendaji kazi

kati ya waganga wa jadi na madaktari. Shirika la Afya Duniani (WHO) tayari

limeendeleza mahusiano hayo tangu Azimio la Alma Ata la 1978, na limeendeleza

“Mkakati wa madawa ya jadi 2002-2005” (Angalia WHO Policy Perspectives on

Medicines, No 2, May 2002, “Traditional Medicine – Growing Needs and Potential”.)

2. Zisaidie vyama vya waganga wa jadi, siyo kutokana na madai yao bali kutokana na

jinsi wanavyofuata “Sheria ya mwongozo kwa waganga wa asili”. (Angalia Hirt and

Lindsey (2002), “Dawa za asili katika nchi za tropiki II: Tiba“, toleo la pili, anamed.

3. Zisaidie hasa zile hospitali zitumiazo malighafi inayopatikana katika mazingira ya

watumiaji, hasa mimea inayotibu. Zizitie moyo hospitali kuanzisha bustani ya

mimea ya madawa.

4. Kwa sababu ya hitaji la muhimu, fungua shule au vyuo vya madawa ya kienyeji ili

kwamba kila muuguzi, daktari na mganga wa jadi aweze kupata ujuzi mkubwa zaidi

wa mimea ya asili. Zitambue na zisaidie vile vituo vinavyojishughulisha na madawa

ya asili ambavyo tayari vipo.

5. Ziliombe Shirika la Afya duniani (WHO) liwasaidie kwa kutoa msaada wa kisayansi

kwa uchunguzi wa mimea ya kienyeji yenye dawa.

6. Zisisitize kwamba misaada ya kiganga kutoka nchi za nje zina nafasi ya kusaidia

njia za namna ya kuzuia magonjwa na uzalishaji wa madawa ya asili kuliko kuagiza

madawa kutoka nchi za nje.

7. Pinga kwa kila namna inayowezekana ule utengenezaji wa haki miliki ya ujuzi wa

jadi wa watu wako, na nchi yako juu ya mmea wowote, maumbile ya wanyama au

watu.

8. Kujiondoa katika uanachama wa World Trade Organisation (WTO) yaani Shirika la

biashara duniani sasa na kwa muda wote Shirika la biashara duniani likiendelea

a) hung’ang’ania maamuzi yake ya kuendeleza kutetea kuongeza muda wa haki

miliki kwa madawa ya viwandani kutoka kwa miaka 5 kuwa 20, ambayo itaanza

tarehe 1 January 2005. Sisitiza juu ya haki ya kupata madawa ya bei rahisi

kabisa ya kuokoa maisha bila kukabiliana na vitisho vya changamoto za kisheria

au vikwazo vya biashara. (The World Trade Organisation´s Trade Related Aspects

of Intellectual Property Rights (TRIPS) imetengeneza utaratibu wa dunia nzima wa

kanuni za kulinda haki miliki. Mfano: Sheria ya ulinzi wa haki miliki kwa miaka 20

wa aina zote za uzalishaji na utengenezaji).

b) huzuia nchi zinazoendelea katika kuendeleza viwanda vyao vya madawa.

Ujerumani ilikuwa na miaka 85 ya kuendeleza viwanda vyake vya madawa bila

sheria zozote za mikataba ya kimataifa.(yaani kutoka 1883 hadi 1968). (1883,

Mkutano wa Paris kwa ajili ya kulinda haki miliki binafsi. Hadi 1968 sheria hii

ilikuwa bado haijatumika kwa madawa huko ujerumani! Kwa hiyo kwa miaka 85

Ujerumani iliweza kuendeleza viwanda vyake vya madawa). Matokeo yake,

ujerumani ndiyo imekuwa nchi inayoongoza duniani kwa kuuza madawa nchi za

Page 45: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 43

nje. Kwa hiyo sisitiza katika kupata nafasi kama hiyo ili kuendeleza viwanda

vyenu vya madawa!

c) hukataa kuadhibu nchi na mashirika ambayo katika jina la biashara huria,

hutengeneza au huruhusu utengenezaji wa bidhaa za hatari huko kaskazini

wakati ambapo matumizi yake au mauzo yake yamepigwa marufuku; mfano:

baadhi ya viuatilifu, sabuni ambazo zina zebaki.

9. Fanya kazi kwa ushirikiano na idara za kisayansi na makanisa ili kuunda dawa za

kibaiolojia na kikemia, na kuunda na kuendeleza benki za mbegu za mimea ya

madawa. Kuna ulazima wa kimaadili kwamba taarifa zote zinazopatikana juu ya

uzalishaji wa madawa ni lazima zipatikane kwa faida ya watu maskini kabisa.

10. Uyaunge mkono mashirika yanayozalisha mazao ya afya palepale walipo. Mzalishe

na kuuza mazao yenye ubora wa hali ya juu katika nchi yenu wenyewe, mfano dawa

za asili, sabuni na vipodozi visivyo na madhara, vyakula vilivyozalishwa kiasili bila

vinatilifu, nyama zinazofaa kwa binadamu n.k.

Kataa kuagiza bidhaa zenye thamani ya chini au ubora wa hali ya chini, na hasa

vilivyo na madhara, mfano nyama zenye vichocheo vya kukua, sabuni na vipodozi

vyenye zebaki, viuatilifu na kemikali za kilimo zilizopigwa marufuku huko

kaskazini.

Ni salama kabisa kusalimu wagonwa wa UKIMWI kwa kushikana mikono.

Vilevile, inatoa picha nzuri kwa watu wote na makundi yote kijijini, katika

wilaya, au hata katika nchi, kushikana mikono na kukaa pamoja ili kuongea.

Kwa kujadiliana, uwezekano mpya hutokea ambapo tatizo la UKIMWI linaweza

kushughulikiwa kwa pamoja.

Page 46: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 44

Kanisa mara nyingi iligombana na

mtazamo wa ki-mila juu ya suala

la ndoa, hasa kwa vile kanisa

lilisisitiza msimamo wa "mme

mmoja, mke mmoja"

Siku hizi, kwa sababu ya Ukimwi,

mila na desturi zingine zinabadilika,

k.mf. ndoa za wake wengi na desturi

ya kutakasa kwa wanawake

waliofiwa.

NYONGEZA 1: Mistari ya Biblia inayosaidia

(Shukrani kwa Mchungaji Sam Mugote, The AIDS Intervention Programme (TAIP), Uganda

kwenye “HIV/AIDS Study Pack for Community Development Workers” Tearfund; 1999).

2 Wakorintho 1:3-4 unatutia moyo

kuwafariji wengine kwa faraja tuliyopata

kutoka kwa Bwana.

Mathayo 22:39 inatoa taarifa ya jibu la

Yesu akituambia kuwapenda jirani

alipoulizwa ni amri ipi iliyokuwa kubwa

kati ya zote.

Mathayo 25:31-46 inaeleza mfano wa

kondoo na mbuzi ambamo hukumu ya

milele imehusishwa na jinsi tulivyo

onyesha imani yetu kwa njia ya matendo

kwa wahitaji.

Marko 1:40-45 inatuonyesha Yesu

anavyomhurumia mwenye ukoma,

ugonjwa ambao wakati wa Agano jipya

uliambatana na fedheha na kutengwa.

Yohana 8:2-11 inamwonyesha Yesu akikataa

kumhukumu mwanamke aliyekamatwa

katika uzinzi na kumruhusu “yeyote asiye

na dhambi” kwenye ule umati kuwa wa

kwanza kumrushia jiwe.

Luka 10:25-37 inatutia moyo kusaidia kwa

vitendo na kwa kujitoa, kupitia habari ya

msamaria mwema, ambaye alimhudumia

mtu fulani pamoja na kuwepo kwa chuki

ya kikabila kati ya wayahudi na

wasamaria. Alitumia chakula (divai) alichokuwa nacho kutibu vidonda - mfano

mzuri wa kutumia chakula kama dawa.

Mithali 3:5-8 inatutia moyo kutofuata njia zetu bali njia za Mungu. Kwa hiyo

tunaweza kujiuliza “Ni ipi njia ya Mungu kuhusiana na mahusiano yetu ya mambo

ya kujamiiana“?

Page 47: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 45

NYONGEZA 2: Mashirika, matoleo, na web-sites

Kwa kuelewa hali ya dunia na jitihada za kimataifa kupambana UKIMWI.

UNAIDS ni ungano la Programu ya Umoja wa Mataifa juu ya UKIMWI, United Nations Programme

on AIDS, na inaleta pamoja mfumo wa mashirika 8 ya Umoja wa Mataifa, yaani UNICEF, UNDP,

UNFPA, UNDCP, ILO, UNESCO na WHO na World Bank (Benki ya dunia).

Anuani: UNAIDS, 20 avenue Appia, 1211 Geneva 27, Switzerland, e-mail: [email protected]

Internet: www.unaids.org. Taarifa nyingi zinaweza kuchukuliwa kutoka katika web-site yao.

Kwa taarifa kuhusu mambo ya tiba ya VVU/ UKIWMI:

TALC - Teaching AIDS At Low Cost, P.O. Box 49, St. Albans, Herts, AL1 15TX, UK. e-mail:

[email protected]. Web.-site: www.talcuk.org. TALC inatoa vitabu vizuri, seti za slide na CD-ROMS

kuhusu tiba juu ya UKIMWI.

US Department of Health and Human Services. Taarifa juu ya uchunguzi wa kihospitali,

kutibu na kuzuia VVU, na miongozo ya huduma za kiganga kwa watumiaji na watoaji wa huduma ya

afya: www.aidsinfo.nih.gov/guidelines.

The South African National AIDS Treatment Advocacy Project: http:/www.natap.org/

Kwa ajili ya taarifa ya huduma ya madawa ya asili kwa wagonjwa wa UKIMWI: “Home – based care herbal treatment guideline”, National AIDS Control Programme, Ministry of

Health, Lilongwe, Malawi, May 1998.

Kwa taarifa kuhusu mpango wa kueneza dawa za VVU/ UKIMWI kwa gharama nafuu n.k.:

Medecines sans Frontieres: www.accessmed-msf.org/ “Campaign for access to essential

medicines” MSF International Office: Rue de la Tourelle 39, Brussels, Belgium.

Third world network briefing paper, June 2001, “TRIPS, patents and access to medicines: Proposals

for clarification and reform. Frederick M. Abbott, Commission on Intellectual Property Rights, Study Paper 2a, “WTO TRIPS

Agreement and ist implications for Access to Medicines in Developing Countries”.

The Buko Pharma-Kampagne, yenye makao yake Ujerumani, kwa miaka 20 iliyopita imekuwa

ikishughulikia shughuli za masoko ya dawa za viwandani katika nchi zinazoendelea na Ulaya

www.bukopharma.de.

“Stop AIDS Campaign“ (Mpango wa kuzuia UKIMWI) ni mpango ulioanzishwa na UK NGO AIDS Consortium, ukiletwa kwa pamoja baadhi ya vikundi vya maendeleo na VVU/ UKIMWI

www.stopaidscampaign.org.uk.

Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanayojishughulisha na VVU/ UKIMWI katika nchi

zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara:

Action Aid inashauri kwamba shughuli ya kupambana na VVU/ UKIMWI lazima pia ishughulike na

umaskini. Wanatoa msaada kwa watu wenye VVU/ UKIMWI na familia zao katika nchi zaidi ya 30

katika Afrika, Asia, Latin America, na Caribbean www.actionaid.org.uk/index.asp?page id = 1195.

Afro AIDS info: Habari za VVU/UKIMWI kwa nchi za kusini mwa Afrika: www.afroaidsinfo.org

Mashirika ya msaada kwa VVU/ UKIMWI

The international AIDS/ HIV Alliance ni shirikisho la msaada, linalotoa msaada wa kiufundi na

kifedha kwa makundi ya watu yanayoshughulika na uzuiaji wa VVU, miradi ya kuwajali wenye

UKIMWI na watoto yatima katika nchi zinazoendelea. Anuani: 2 Pentonville Road, London N1 9HF,

UK. Web: www.aidsalliance.org.

Nchi nyingi zina mashirika yake ya kuratibu UKIMWI. Katika Kenya, kwa mfano, ni Kenya

AIDS NGOs Consortium (KANCO). Na nchi karibu zote zimekuwa na mashirika

mbalimbali ambayo yameanzishwa ili kuhudumia wagonjwa wa UKIMWI. Tafadhali tafuta

mashirika yanayojishughulisha na wagonjwa wa UKIMWI katika wilaya yako, na

uyaelekeze kutumia “madawa ya asili”.

Page 48: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi
Page 49: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

anamed Nyongeza 3.

Form ya kumbukumbu: Dalili, matibabu na maendeleo ya mwenye VVU/ mgonjwa wa UKIMWI

Jina _______________________________ Jina la ukoo ____________________________________ Umri ________

Me/ke anuani ________________________________________Tarehe ya kuanza matibabu: ___________________________

Na Dalili Mwezi tangu kuanzisha matibabu

Mwezi tangu kusimamisha

matibabu

1 2 3 4 5 6 1 2 3

1 Kuharisha (idadi kwa siku)

2 Homa isiyoisha (kiwango cha joto)

3 Uzito (kg)

4 Kikohozi kisichopona (kifua kikuu/ Pneumonia) *

5 Candida alibicans (mtando mweupe mdomoni) *

6 Kansa ya ngozi (Kaposi´s sarcoma) *

7 Mkanda wa jeshi *

8 Matatizo ya ngozi *

* Tafadhali jaza kama ifuatavyo: - hakuna dalili; + tatizo la kawaida; ++ tatizo kubwa kiasi; +++ tatizo kubwa sana.

Maelezo ya matibabu yaliyotolewa

Mwezi 1

Mwezi 2

Mwezi 3

Mwezi 4

Mwezi 5

Mwezi 6

Page 50: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi
Page 51: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 47

Nyongeza 4: Fomu ya taarifa – Utoaji wa taarifa kwa anamed.

Tafadhali rudisha (kwa posta pekee) kwa

anamed

Schafweide 77

71364 Winnenden

Germany

Tarehe ______________________

Umegundua mchanganyiko gani wa madawa unaosaidia (tafadhali tuandikie namba

zake).

Ni dawa gani ambayo haikusaidia? (tafadhali tuandikie namba zake)

Mapendekezo mengine yoyote?

Jina _____________________________________

Anuani ________________________________________________________________

______________________________________________________________________

Email/fax _______________________________________

Maswali juu ya UKIMWI au mimea ya madawa (tafadhali andika jina la kisayansi

(scientific name) yapelekwe kwa Dr. Keith Lindsey, email: [email protected]. Tafadhali

usitutumie mimea au madawa. Maombi yoyote ya msaada wa fedha hayatajibiwa kwa

sababu sisi wenyewe hatuna fedha.

Page 52: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Ukimwi na Madawa ya Asili 48

Nyongeza 5: anamed: Matoleo na vifaa (hadi September 2006)

Schwafweide 77,71364 Winnenden, Germany, Tel. +497195910225. Email: [email protected]

Angalia web-site kwa ajili ya matoleo mapya na bei: www.anamed-edition.com

KIINGEREZA:

Namba kwa kuagiza/orodha ya vitu.

105 Hirt/M’Pia, ”Natural Medicine in the Tropics I”,

106 This book together with colour posters (403)

109 Hirt/Lindsey, “Natural Medicine: II Treatments” Seminar handbook

113 “Natural Medicine: III Seminar Leader's Resource Kit”

114 Lindsey, "Making peace: Biblical principles"

115 Natural Medicine IV "AIDS and Natural Medicine"

116 Document: “Four ULOG solar ovens and one drier: Construction plans and uses”

117 Document: “Neem in medicine and agriculture”

403 Colour poster of 60 tropical med. plants (folded or as roll?)

107 Lindsey/Hirt ”Use Water Hyacinth!” (inc. instructions for solar oven constr.)

201 Report ”Mercury Soaps: A Modern Day Scandal”

204 Document ”Malaria: Artemisia annua” with an illustrated cultivation guide

GERMAN

101 Hirt/M’pia ”Natürliche Medizin in den Tropen I”

102 This book together with colour poster (401)

401 Colour Poster, 70x100cm, ”Heilpflanzen in den Tropen" (folded or as roll?)

303 Information re seeds of healing plants: purchase, preservation

202 Document "Malaria: Artemisia annua" with an illustrated cultivation guide

FRENCH

103 Hirt/M’Pia ”La Medecine Naturelle Tropicale I”

104 This book with colour poster (402)

112 “La Medecine Naturelle Tropicale: II Traitements" Seminar handbook, 40pp

118 “La Medecine Naturelle Tropicale: III Guide du Formateur”

122 “La Medecine Naturelle Tropicale: IV Le SIDA et la Médecine Naturelle"

402 Colour poster, 70x100cm, ”Plantes médicinales tropicales"(folded or as roll?)

206 Report ”Mercury Soaps: A Modern Day Scandal” (French)

203 Document ”Malaria: Artemisia annua” with an illustrated cultivation guide

PORTUGUESE (KIRENO)

120 Hirt/M’Pia “Remédios Naturais nos Trópicos I”

111 ”Remédios Naturais nos Trópicos: II Tratamentos” Seminar handbook

205 Information ”Malaria: Artemisia annua” with an illustrated cultivation guide

405 Colour poster of 60 tropical med. plants (folded or as roll?)

SPANISH (KIHISPANIA.)

110 Hirt/M’Pia ”Medicina Natural I” 160pp

121 “Medicina Natural” – Part B includes extracts from NMII, III & IV. 40 pp A4

207 Information: "Malaria: Artemisia annua" with an illustrated cultivation guide

KISWAHILI

123 Hirt/M’Pia, “Madawa za asili: I”

119 Hirt/Lindsey, “Dawa za asili katika nchi za joto: II Uzoefu” Seminar handbook

124 Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV Ukimwi na Madawa ya Asili

ZANA NYINGINE

400 Karatasi nyeupe, 70 x 100 cm, kwa ajili ya kufundishia/kuandikia kwa kalamu kubwa (Markers)

404 Karatasi kubwa ya rangi ya mimea 60 ya madawa, bila maelezo, kwa kutumia kalamu kubwa (Markers)

419 Mbegu za Moringa oleifera zikiwa na muhtasari wa maelezo kwa kiingereza pamoja na maelezo zaidi

kwa kifaransa.

408 Mbegu za mimea 10 tofauti ya eneo la tropiki (tayari kwa kuota).

409 Vikorokoro vya kuanzia vya mpango wa malaria wa anamed vyenye mbegu 5000.

Vikorokoro hivi vinauzwa kwa ajili ya msaada wa kibinadamu tu. Vinajumuisha mbegu na zana zote na

taarifa zote zinazohitajika kwa ulimaji na matumizi.

412 Mbegu za artemisia, kifurushi cha kujaza tena, kinapatikana kwa watu walionunua 409.

411 Majani ya artemisia makavu kwa matumizi ya kisayansi. gramu 50.

Page 53: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

anamed pia inapendekeza matumizi ya

“Where there is no doctor: A Village Health Care Handbook for Africa

na David Werner.

Kinapatikana katika maduka mengi na kutoka TALC, P.O. BOX 49 St Albans,

Herts AL I 4AX, England.

Matoleo mengine ya anamed

“Natural Medicine in the Tropics I: Tropical plants as a source of health care.

Production of Medicine and cosmetics” (englisch second Edition 2001)

By Hans-Martin Hirt and Binanda M´Pia

Kitabu kinapatikana pia kwa kijerumani: “Natürliche Medizin in den Tropen”; kifaransa: “La Medecine

Naturelle Tropicale”, kihispania: “Medicina Natural”, kireno: “Remedios Naturais nos Naturelle

Tropicos” na urainian

Kitabu hiki kinaelezea umuhimu wa kijamii na kiuchumi wa madawa ya kienyeji, mimea 15 kwa

ufafanuzi wa kina, mimea 50 zaidi na mazao yake ya asili na jinsi ya kutengengeza chai zake, mafuta

yake, dawa za mafuta na madawa mengine.

Bango la rangi “Mimea inayotibu katika eneo la tropiki”

Picha za mimea 60 ya madawa, zinapatikana kwa kiingereza, kifaransa, kijerumani au kireno.

“Natural Medicine in the Tropics: II Treatments” Kijitabu cha semina cha anamed. Kinapatikana pia kwa kifaransa, kireno na kiswahili.

“Natural Medicine in the tropics: III Seminar Leader´s Resource Kit”

Vikorokoro kwa viongozi wa semina; mkusanyiko wa zana kwa ajili ya kazi kwa vikundi,

tafakari za biblia, na wingi wa taarifa za mshindo nyuma juu ya mada kadhaa. Pia kwa kifaransa.

Vikorokoro vya kuanzia – Malaria - artemisia. Vikorokoro hivi vinajumuisha mbegu na zana zote zinazohitajika kwa ulimaji na matumizi kwa

miaka kadhaa. Taarifa za kisayansi na maandishi, “mpango wa ulimaji”, fomu za kumbukumbu,

barua za taarifa kwa miaka miwili.

Kila box limetayarishwa na taarifa katika lugha husika.

Malaria: Artemisia annua anamed Ulimaji wa Artemisia annua na matumizi yake katika kutibu Malaria.

Kwa kiingereza, kifaransa, kijerumani, kihispania na kireno.

Mercury Soap: A Modern Day Scandal Taarifa zinaelezea tatizo la kutumia sabuni na vipodozi vyenye zebaki kwa lengo la kung’arisha

ngozi. Inajumuisha mkusanyiko wa habari kutoka kwenye magazeti, majarida ya kisayansi na

taarifa nyingine za muhimu. Anamed inatafuta kuweka sheria ya kutouza mazao hayo ya sumu

duniani.

Kwa kiingereza na kifaransa.

Making Peace: Biblical Principles Chanzo chake ni kundi la CHIPS, ambalo imeanzishwa na wakristo nchini Uganda. Kitabu hiki

kinaeleza jinsi tabibu wa dawa za asili wawezavyo kuchangia katika kutengeneza amani

anamed, Schafweide 77, 71364 Winnenden, Germany Email: [email protected]

Page 54: Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: IV - Kwa sababu ya kufa kabla ya wakati kwa wasomi na watu wazima, elimu ya jadi na ujuzi wa kilimo, ufundi na madawa haririthishwi kwa kizazi

Huu mchoro wa zamani sana kutoka Ukraine unaonyesha mtoto wa kiafrika akikimbia

kumwokoa mtoto wa kizungu aliyeanguka katika jamii ya mpungate, akiwa ameshikilia

dawa husika kwa kuua sumu.

Bado ni kweli kwamba hata leo Waafrika wana mengi ya kufundisha juu ya mimea

inayoponya. Pamoja na pigo la UKIMWI, ujuzi mwingi zaidi unazidi kupotea jinsi

wazee wanavyokufa kabla hawajarithisha elimu yao ya jadi kwa kizazi kinachofuata.

Kwa hiyo, kila siku, kazi ya kushirikishana ujuzi kuhusu UKIMWI na madawa ya asili

inaendelea kuhitajika zaidi

anamed aktion natürliche medizin

action nature et medecine

action for natural medicine