madawa ya asili...madawa ya asili katika nchi za tropiki dr. hans martin hirt bindanda m’pia 1....

159
MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi. anamed Nr. 123

Upload: others

Post on 03-Nov-2020

19 views

Category:

Documents


2 download

TRANSCRIPT

Page 1: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

MADAWA YA ASILI

KATIKA NCHI ZA TROPIKI

Dr. Hans Martin Hirt

Bindanda M’pia

1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya.

Uzalishaji wa madawa na vipodozi.

anamed

Nr. 123

Page 2: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

Anamed inalenga kuwasaidia watu

kufikia kiwango kikubwa cha kujitegemea

- kwa kulenga zaidi afya zao. Kwa

kutimiza lengo hili anamed inaendesha

semina na kufanya uchunguzi wa mimea

yenye dawa na utayarishaji wa madawa.

Anamed inalenga kufanya kazi kwa

msingi wa kutunza na kujali mazingira.

Hirt na M’pia, Madawa ya asili katika

nchi za Tropiki.

Toleo la kwanza limechapwa 2005

Haki zote zimehifadhiwa.

© Haki miliki na waandishi

Ni matumaini ya waandishi kuwa taarifa zilizomo katika kitabu hiki ienee kiasi

kiwezekanacho. Sehemu ndogondogo za kitabu hiki zinaweza kunakiliwa kwa lengo

la kuelimishana, ili mradi zitajwe zilikotoka na waandishi wataarifiwe. Hairuhusiwi

sehemu yo yote ya kitabu hiki kunakiliwa kwa ajili ya kuuzwa. Kama unataka

kutengeneza kwa wingi madawa yaliyoandikwa katika kitabu hiki, tafadhali

wasiliana nasi kwanza, kwa sababu tunaendelea kuuboresha mchanganyiko huu wa

madawa kwa njia ya uchunguzi na majaribio.

Kimechapwa na:

Toleo la pili limerudiwa kwa msaada wa Innocent Balagizo (D. R. Congo), Prof

Dr.C. Schäfer na Dr. Keith Lindsey (wote kutoka Ujerumani).

Kitabu hiki kinapatikana pia kwa Kifaransa, Kijerumaji, Kiingereza na Kihispania.

Kwa maelezo ya matoleo zaidi ya anamed, tafadhali angalia ukurasa wa mwisho.

Kwa orodha ya gharama au kuagiza tafadhali angalia toviti (web-site) yetu, au andika

kwa:

anamed (Action for Natural Medicine),

Schafweide 77,

D-71364 Winnenden,

Germany.

Email: [email protected]

Website: www.anamed-edition.com

Tafadhali usiwaandikie anamed Ujerumani kuomba nakala za bure au fedha. Kama

unaishi Afrika, Asia, au America ya kusini, agiza kupitia shirika lako lililoko Ulaya,

ambao watakulipia gharama na kukutumia vitabu.

Page 3: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

Kitabu hiki ni kwa watu wote weusi kwa weupe

wapambanao kutafuta amani, haki na afya.

Page 4: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

YALIYOMO

DIBAJI 7

UTANGULIZI .................................................................................... 13

SURA YA 1: MADAWA ASILI: MUUNGANO WA MADAWA

YA KIENYEJI NA SAYANSI YA KISASA ............ 18

1.1. HISTORIA YA MADAWA KATIKA TROPIKI YA AFRIKA ......... 18

1.2. DAWA YA KIENYEJI NA ILE YA KISASA ................................... 19

1.3. HOFU YA KUSHIRIKIANA ............................................................. 20

1.4. TOFAUTI ZILIZOPO ........................................................................ 20

1.5. JE, SIRI ZIFICHULIWE? HATARI KWA MADAWA YA KUSINI 21

1.6. HASARA ZA MADAWA YA KUSINI ............................................. 22

1.7. HASARA ZA MADAWA YA KASKAZINI ..................................... 22

1.8. LENGO LETU: “DAWA ZA ASILI.” ............................................... 23

1.9. MADAWA YA ASILI: FURSA KWA KANISA ............................... 26

1.10. MADAWA YA ASILI MAANA YAKE NI KUJIHUSISHA NA

SIASA! ............................................................................................... 27

SURA YA 2: MADAWA YA ASILI MIRADI KATIKA NGAZI

YA KIJIJI .................................................................... 31

2.1. KUFUNDISHA NA KUJIFUNZA ..................................................... 31

2.2. MFANO WA RATIBA YA SEMINA ................................................ 32

2.3. BUSTANI ZA MADAWA ................................................................. 35

2.4. KUKUSANYA MIMEA YA DAWA................................................. 37

2.5. KUKAUSHA NA KUTUNZA MIMEA YA DAWA ......................... 37

2.6. UTUNZAJI WA MADAWA .............................................................. 39

2.7. JUA: MSAADA KWA MADAWA YAKO ....................................... 40

2.8. KIASI NA DOZI ................................................................................ 42

2.9. KUTENGENEZA MIZANI RAHISI LAKINI YA UHAKIKA ......... 43

SURA YA 3: MADAWA YA AINA MBALIMBALI ...................... 47

3.1. MADAWA KWA MATUMIZI YA NDANI ...................................... 47

3.2. DAWA KWA MATUMIZI YA NJE .................................................. 48

3.3. MADAWA KWA MATUMIZI YA NDANI NA NJE ....................... 50

SURA YA 4: OKOA FEDHA NA JITENGENEZEE

MWENYEWE!............................................................ 51

4.1. UTENGENEZAJI WA SABUNI KATIKA NGAZI YA KIJIJI ......... 51

4.2. KUMWAGIA MAJIMOTO NA KUTOKOSA (INFUSIONS &

DECOCTIONS) ................................................................................. 56

4.3. MAFUTA YENYE DAWA ................................................................ 56

Page 5: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

4.4. MAFUTA YA (KUJIPAKA) DAWA................................................. 58

4.5. PODA ................................................................................................. 59

4.6. ORS (maji-chumvi) ............................................................................ 62

4.7. JIWE JEUSI ....................................................................................... 64

4.8. DIVAI YA ASALI ............................................................................. 65

4.9. DAWA YA KIKOHOZI (Cough Elixir) ............................................. 66

4.10. MADINI NA VITAMINI ................................................................... 66

4.11. MAZAO KWA MIFUGO NA MATUMIZI YA KILIMO ................. 69

SURA YA 5: MIMEA 15 MUHIMU - KAZI NA ATHARI ZAKE . 72

5.1. Allium sativum: Kitunguu Swaumu .................................................. 73

5.2. Artemisia annua anamed (A3) ............................................................ 75

5.3. Azadirachta indica: Mwarobaini ........................................................ 79

5.4. Capsicum frutescens: Pili-pili ............................................................ 84

5.5. Carica papaya: Papai ......................................................................... 86

5.6. Cassia alata (syn. Senna alata): Ringworm bush ............................... 90

5.7. Cassia occidentalis (syn. Senna occidentalis): Mwingajini ................ 91

5.8. Citrus limon: Limau ........................................................................... 93

5.9. Cymbopogon citratus: Michaichai ...................................................... 94

5.10. Eucalyptus globulus: Mkaratusi (kalafulu) ......................................... 96

5.11. Euphorbia hirta: Mziwaziwa (mwache) ............................................. 97

5.12. Mangifera indica: Mwembe ............................................................. 100

5.13. Moringa oleifera: Mlongelonge ........................................................ 101

5.14. Psidium guajava: Mpera ................................................................... 104

5.15. Zingiber officinalis: Tangawizi ......................................................... 106

SURA YA 6: MIMEA 50 ZAIDI NA MAZAO YA ASILI ............ 107

SURA YA 7: DOKEZO KWA FAMILIA, WAFANYAKAZI

WA AFYA NA HOSPITALI .................................... 141

7.1. KATIKA FAMILIA ......................................................................... 141

7.2. WATUMISHI WA AFYA KIJIJINI ................................................. 145

7.3. KITUO CHA AFYA ........................................................................ 145

7.4. GHALA LA DAWA LA HOSPITALI ............................................. 147

SURA YA 8: CHAGUO LA KWANZA KATIKA TUKIO LA

UGONJWA ............................................................... 149

ORODHA YA MANENEO YA KISAYANSI NA MAELEZO

YAKE ........................................................................ 153

Page 6: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

Tunapenda kuwashukuru wote waliochangia katika uandishi wa kitabu hiki:

Waganga wa jadi wa kiafrika, makanisa ya kiprotestanti na katoliki yanayoshirikiana

nasi hadi leo; mchoraji wa Kikongo Mr. Sugha na marafiki zake Gregor Müller,

Bindanda Nkoshi na Dorothea Layer–Stahl kwa mifano yao; Mr. M. D. Tauli wa

Organization Chestcore, Ufilipino kwa picha za mimea, vyuo vikuu katika Kinshasa,

Montpellier, Basel, Tübingen, Antwerp, Gent and Brussels vilivyoturuhusu kutumia

masalia ya vitu vya kale, maktaba na kumbukumbu mbalimbali.

Shukrani maalum kwa P. Winrich Scheffbuch, Mrs. M. Munziger, Mr. Ernst

Kranich, Mrs. U. Kohler kutoka Evangelical Assistance Programme na Mr. E. Vatter

kutoka Oberkirchenrat.

Toleo la pili limefaidi uzoefu wa washiriki wetu kutoka nchi mbalimbali pasipo

kifani: anamed Angola Annecy Ibanda, Margarete Roth

anamed Congo-Bandundu: Bindanda M'pia, Emmanuel Mufundu

anamed Congo-Kinshasha: Konda Ku Mbuta

anamed Congo Sul Kivu: Innocent Balagizi

anamed Congo-Haut Congo: Dieudonné, Umo Bombibambe

anamed Eritrea Nighisti Alazar, Micele Paliaro

anamed Ethiopia Ralph Wiegand, Alemayehu Abebe

anamed Kenya Esther Odhiambo, Walter Opiyo

anamed Mozambique Helene Meyer, Pascoal Cumbane, Dr Murray Louw

anamed Nigéria: Hannelore Bachmann, YMCA - Jos

anamed South Africa Aaron Motlhasedi, Sr. Beatrix Knubela

anamed Sudan South-west: Daniel Gumwel, James Tor, Joseph Chok, Dr Elijah

anamed Sudan South-east: Mary Yangi

anamed Tanzânia: Gideon Kibambai, Peter Mabula

anamed Uganda Kasese Thembo Patrick, Simon Challand

anamed Uganda Katakwi Oduc Naboth, Olokojo Fabiano, Ephraim Osilimo

anamed Uganda Masaka: Henry Seswannyana, Gertrude Najjemba

anamed Uganda Vurra: Samual Mundua, Buzu Venensko

anamed Uganda Kampala: Henry Seswannyana

anamed Ucrânia: Andrij Kyrtchiv

Kwa toleo hili la ki-suahili tunamshukuru Emmanuel Biligeya kwa kazi yake ya

utafsiri na Mchungaji Hezron Shimba na Maike Ettling kuhariri.

Pia tunaishukuru HUYAMU (Idara ya Afya ya kanisa la AICT - Dayosisi ya

Mara & Ukerewe) kwa ushirikiano wa karibu.

Tutafurahi kupokea mawazo yenu, lakini yanayohusu uchanganyaji wa madawa

katika kitabu hiki tu.

Tafadhali yatume kwa: Dr. Hans–Martin Hirt, anamed, Schafweide 77,

D-71364 Winnenden, Germany. Email: [email protected]

Tafadhali usiandike kuomba msaada wa fedha zako binafsi au kwa ajili ya miradi

mbalimbali. Tunapokea barua nyingi za aina hiyo, kiasi kwamba hatuwezi kuzijibu.

SHUKRANI

Page 7: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

7

Na Hans – Martin Hirt

Katika miaka yangu sita ya mafunzo kazini katika chaka la Afrika huko Zaire, Afrika

magharibi, nilikuwa na watu ambao hawajawahi hata kukusanya ndoo ndogo ya

takataka. Chochote kiwawezeshacho kuishi ndicho ambacho wangekufa nacho,

mfano kikombe cha bati. Vijana wenye miaka 12 wanatengeneza nyumba zao kwa

kutumia malighafi ya asili pamoja na panga tu. Vyumba ambavyo hudumu kwa

miaka pasipo kuvuja. Katika 1950 wanawake walikuwa bado wanabeba magunia ya

chumvi kwa vichwa vyao njia yote kutoka baharini hadi kijijini kwetu Matamba –

Solo, umbali wa kilometa 600! Nani kati yetu angeweza kuunda mitego ya nyati,

kupanda mnazi? Nani kati yetu hana magonjwa ya meno pasipo kutumia hata siku

moja mswaki au dawa ya meno?

“Dunia ya tatu” ina kila sababu ya kujivunia. Ndiyo pekee inayoonyesha dunia

misingi ya kiasili kabisa ya jinsi ya kulima ardhi hii na kuilinda dhidi ya uharibifu

inaonyesha namna ambayo dunia yetu ingedumu kwa urahisi miaka mingi mamilioni

kadhaa.

Mwanzilishi wa msemo huu, “Dunia ya tatu“, Rais Nehru, hasa alitaka kuelezea

njia ya tatu, njia bora zaidi!

Kwa kweli “Dunia“ ya kibepari “ya kwanza” imeunda ushirikiano na “dunia ya

pili” ya kikommunist zamani ushirika wenye kuitumia dunia yetu bila huruma kama

vile hakuna kesho. Muungano huu, uliokuwa sehemu kubwa kaskazini mwa dunia

yetu, bado unaiendesha “dunia ya tatu”, ambayo kwa sehemu kubwa iko kusini, kwa

ukoloni wa kiuchumi. Kaskazini inaamuru bei ya bidhaa, inaongoza biashara,

masharti ya mikopo, na jinsi ya kulipa mikopo . Kaskazini inaamsha tamaa kwa

wateja kupitia TV za satellite na mtandao wa internet. Zaidi kaskazini inafanya

mabadiliko makubwa sana kwa mazingira ya kusini kwa kusababisha mvua ya

tindikali, kwa kukata miti na kuchimba madini katika misitu ya tropiki, na kwa

kutupia huko mazao ya sumu na takataka za sumu. Utamaduni wote unakuja na

kupita, lakini utamaduni wa kokakola ulioenea ulimwengu mzima ukitoweka, upi

utakaobaki?

Watu wa asili wakati fulani walikuwa wa ufahari wa utamaduni wao na uwezo

wao. Je, bado wanajivunia mambo hayo leo? Mara kwa mara watu kutoka Latin

America, Asia na Afrika wanaililia kaskazini kwa misaada. Nchi za dunia ya tatu

zimekaa katika mtego wa mikopo. Badala ya kutumia na kufaidika kutokana na mali

asili yao, na kutumia pesa kuinua hali yao ya maisha, nyingi kati ya nchi hizi

zinapendelea kununua silaha. Kwa hiyo zinazidi kuwa maskini.

Hakuna kitengo ambacho kinaona matokeo ya wehu huu kama kitengo cha afya.

Hospitali nyingi katika nchi za Afrika zisingeweza kuendelea na kazi bila kupata

madawa ya misaada kutoka nje. Ukichunguza mara moja katika maghala ya madawa

ya hospitali za Afrika utagundua kuwa Waafrika wanatibiwa kwa mtindo wa Ulaya

pekee. Hakuna ugunduzi unaofanywa juu ya utajiri mpana wa ufahamu wa mambo

ya afya upatikanao kwa wingi katika Afrika yenyewe.

DIBAJI

Page 8: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

8

Ili kuwatuliza dhamira zao, watu wa kaskazini wanatumia dola milioni chache

kusaidia Afrika. Inaweza kuwa zawadi za makasha ya dawa za kikohozi, ambayo pia

hutokea kulinda ajira huko kaskazini. Njia yenye msaada zaidi ingekuwa kuwasaidia

Waafrika kwa:

Kuthamini walichonacho, na kujifunza upya kile walichokijua tangu mwanzo!

Hii ina maana kusambaza elimu halisi ya asili, badala ya kuingiza bidhaa kutoka

Amerika au Ulaya. Lakini kama watu wote katika maeneo ya tropiki wangetambua

hili, faida na kazi nzuri za bidhaa za viwanda vya kaskazini vingetiwa hatarini.

Ninazumgumzia makampuni yaliyochukua hati miliki kwa jambo ambalo lilijulikana

kuwa ujuzi wa kawaida katika nchi za kusini.

Tunapowauliza watu katika vijiji vya Afrika jinsi wanavyoelezea uzoefu wao wa

umaskini wanasema “sisi ni maskini kwa sababu nyinyi weupe hamtuambii siri zenu,

lakini mnachukua siri zetu na hamtulipi chochote”.

Je huu ni msemo wa kijiji hiki pekee? Hakika hapana! Balozi mshauri wa Zaire

(sasa Democratic Republic of Congo) katika Ujerumani Mr. Ziangba Begu, alikuwa

akipiga ngoma ile ile aliposema, “Nchi za magharibi haziko tayari kusikiliza

matatizo ya washirika wao. Ili kulinda ukuu wa kiufundi na kifedha, zinatunza siri za

mafanikio yake …. Kwa nini wafanyakazi wa maendeleo wanamalizia ujenzi wa

madaraja usiku wakati Waafrika wamelala?”

Sidhani kama shutuma hizi ni za kweli, lakini hisia hizi zinabaki kwa namna

fulani: Misaada mingi ya maendeleo imewafanya Waafrika kujisikia ni wa hali ya

chini.

Hapa siongelei hasira zangu na hasira za wengine dhidi ya shehena tatu zilizojaa

madawa ambayo muda wake wa kutumika umekwisha, yaliyotumwa na shirika la

misaada, wala sio juu ya dawa za kupaka miguu zilizofunguliwa tayari, wala juu ya

chakula cha kupunguza uzito kwa watoto wenye njaa, wala juu ya meno ya bandia

kutokana na watu waliokufa au mito ya silkoni ya kukuzia matiti, au chochote

ambacho kaskazini tajiri imetuma kwa hisani wakati wa miaka yangu sita katika

Zaire.

Hapana, ninaongelea juu ya kupungua kwa staha kunakowaathiri kila mmoja,

mwaka hadi mwaka, wakati ambapo 100% ya madawa yanayohitajika yanapoagizwa

kutoka nje, wakati ambapo ndege zilizojazwa na hayo zinashuka kutoka mbinguni,

mbinguni ambapo Mungu anaishi ambapo inaonekana wazi kuwa “anawapenda

weupe kuliko weusi.”

Kwa bahati nzuri, mashirika mengi yamebadilisha mtazamo. Mengine hata

yanasema na ninadhani yako sawa: “Kutoa misaada katika maendeleo maana yake ni

kufanya kila linalowezekana kuzuia watu kusini wasiwe kama sisi huku Kaskazini!”

Kuna mifano mingi, wengi wamegundua kuwa ibada zetu za Jumapili ambazo mara

nyingi hazina raha na zilizopoa hazifai kupelekwa nchi za nje, na wameomba

washirika katika Latini Amerika kuunda “Thiolojia inayoendana na utamaduni wao.”

Wengine wanajua hatari ya udongo wa Afrika kupata sumu kutokana na madawa ya

kuua wadudu kama ilivyo katika Ulaya na Marekani. Kwa jinsi hiyo baadhi ya

Page 9: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

9

misheni zinatuma washauri wa mambo ya kilimo ambao husaidia kiikolojia

kuendeleza kilimo.

Lakini ni nani sasa anaongelea mambo ya madawa kiikolojia? Katika Afrika ni

kama sijaona kabisa mitaala juu ya jambo hili! Ujuzi wetu wa madawa una hatari ya

kukaa milele pasipoonekana. Umefichwa katika kitabu kilichoandikwa kwa Kilatini

kwa manufaa ya kiwanda hicho tu. Zamani lugha ya Kilatini ilitumika kama ngao ya

kulinda walio madarakani. Martin Luther alikishambulia Kilatini cha wanatheolojia

na akawatishia katika kujistawisha. Paracelsus alikumbana na jambo kama hili pia

kwenye Kilatini cha waganga. Alikuwa na hamasa, ya kuwafundisha wanafunzi

wake katika lugha yao!

Kinyume na malengo ya kupata fedha ya maadui zake, Paracelsus aliendeleza

kutegemeana katika madawa, dini na sera za kisiasa. Alikuwa ni mwakilishi

aliyejituma katika sayansi ya uponyaji wa asili, na alifundisha jambo lililomletea

kashfa: nguvu ya mwili kujiponya wenyewe. Ilibidi atoroke kuepuka kufungwa.

Hakimu wa Basel hakufuta hukumu yake ya kukamatwa mpaka June 11, 1993 –

miaka 500 baada ya siku ya kuzaliwa kwake.

Kujificha katika “kilatini cha madawa” kunarahisisha kutengeneza fedha nyingi,

iwe katika makampuni ya nchi mbalimbali au kama mtumishi wa afya katika

hospitali kijijini. Tukirudi tena kwa Paracelsus katika safari zangu huko India ,

Nepal, Zaire, Peru, Romania na Ukraine, sijaona bango lolote lenye kutangaza juu

ya nguvu za mwili kujiponya wenyewe. Kama kiwanda hakiko tayari kutoa siri zake,

inakuwa hata muhimu zaidi kwa pamoja na wananchi wa maeneo ya tropiki,

tugundue na kushiriki siri za asili.

Dini haiwezi kutenganishwa na afya.

Katika hotuba zangu katika vyuo vikuu huko Ujerumani, wanafunzi walitoa hoja,

“Mradi huu wa madawa ya asili ni mzuri sana, lakini kwa nini uunganishwe na

kanisa?” Kwa upande wangu jibu ni rahisi. Katika nchi za tropiki mara nyingi kanisa

ni kitengo pekee ambacho bado kinaruhusiwa kuelezea mawazo mengine, kupinga,

kama Yeremia alivyothubutu kusema, “………pandeni Gileadi enyi watu wa Misri,

mkachukue dawa ya marhamu, mmetumia dawa nyingi bure, hakuna

kitakachowaponya nyinyi,” (Yeremia 46:11). Kama ungekuwa mwakilishi wa

kampuni ya kutengeneza madawa, ukadiriki kutamka mara moja tu kwa sauti mbele

ya wamiliki wa kampuni hilo au wateja wake, unafukuzwa kazi, huenda ungegundua

mara moja jinsi kusini na kaskazini zinavyofanana, katika namna za mamlaka na

uendeshaji.

Ukweli ni kwamba serikali nyingi zimeuachia mfumo wa afya kwa makanisa na

misheni. Lakini hata katika hali mbaya ya makanisa na misheni kujiondoa kwenye

tiba, watu hawaasi. Angalau hilo ndilo jambo nililoliona Zaire: Wagonjwa wanakufa

kimya kimya kwa magonjwa yaliyo rahisi kutibiwa. Tuliangalie swala hili,

magonjwa hayawafanyi watu kuwa na mwamko wa kisiasa bali huwahuzunisha,

huwachosha na kuwakatisha tamaa.

Page 10: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

10

Biblia, watu, afya na vitu vya

asili kuwa kitu kimoja

Katika mataifa mengi, kuna mashindano

baina ya mahospitali HOSPITALI YA TAIFA

ina upungufu wa fedha, ni chafu, haipokei

misaada kutoka nje, lakini ina gharama nafuu

sana. HOSPITALI YA KANISA, ni safi, hupata

madawa kutoka nje, lakini kwa sababu ya

gharama za matibabu, haipati watu.

Lengo letu ni kwamba WAKRISTO wawe

katika mfumo wa serikali au kanisa

watengeneze HOSPITALI ZA MADAWA YA

ASILI yaliyo rahisi kwa maskini na ghali kwa

matajiri, iliyo safi, yenye wingi wa madawa ya

asili, mahali ambapo pesa ndogo inayopatikana,

inatumika kuagiza dawa ambazo nafasi yake

haiwezi kuchukuliwa na miti ya madawa,

mahali ambapo pia huduma ya kiroho inatolewa.

Hii ndiyo sababu kitabu hiki kimetolewa bila

kutoa udhuru, katika mazingira ya imani ya

kikristo. Tunajaribu kuyachukua mambo haya

kwa ujumla, kuhudumia akili, mwili na roho,

kuhudumia ardhi, kuheshimu watu kwa jinsi

walivyo, na wao ni kina nani, ikiwa ni pamoja na miti yao ya madawa, uzoefu na

ujuzi wao kwa miti hiyo.

Wakati nilipokutana na mwakilishi mkuu wa madawa ya kienyeji ya kihindi

(ayurveda) huko New Delhi mchana mmoja, alianza kwanza kunifundisha dini,

ungeamini hilo? Masaa mawili! Alisema huu ndio ulikuwa msingi wa ayurveda,

vinginevyo nisingeweza kuelewa nguvu ya uponyaji wa miti.

Matumizi ya vitu vinavyopatikana katika mazingira yetu siyo tu yana msingi wake

katika Biblia, bali pia yako kwenye kiini cha malengo ya Shirika la Afya Duniani

(W.H.O.). Tangu 1977, maazimio mbalimbali ya (W.H.O.) yamekuwa yakihitaji

madawa ya asili yachunguzwe na kutumika. Kutendewa kazi kwa maazimio haya

ndiyo jambo lililobakia. Kwa jinsi hiyo hata nyakati zilizopita kidogo, askofu wa

kiafrika ameomba msaada wa lita 1,000 za dawa ya kikohozi pasipo kujua kuwa mti

wa homa ulio karibu na kanisa lake una kila kitu ambacho viwanda vya madawa

vimechukua na kutumia katika uzalishaji wa bidhaa zake.

Aidha Amerika kusini inaagiza vidonge na vichupa vya dawa na drip kutoka

Ulaya au Marekani pasipo kujua kuwa vitu vingi vinapatikana kutoka katika

“magugu” yanayoota kando ya nyumba.

Hali hii haivumiliki

Ufahamu wa muhimu utaenezwa namna gani? Katika D.R. Kongo, vyuo vikuu vingi

vya serikali vimefungwa kwa miaka mingi sasa. Vitabu vya madawa ya asili

Page 11: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

11

vitapatikanaje? Hata vingepatikana wanavijiji wasingevielewa, watumishi wa afya

wasingepata nafasi ya kuvisoma na madaktari wasingeviweza.

Katika nchi za tropiki kwa sababu ya vita, umaskini, bei za bidhaa kuongezeka,

kuongezeka kwa ukiukaji sheria, karibu 80% ya watu wote hawawezi tena kupata

madawa yanayoitwa ya “kisasa”. Lakini pia ujuzi wao juu ya miti yao ya madawa

umepotea. Wazungu wamekuwa wakishutumu kwa miongo mingi, mambo yote ya

kichawi na kishirikina, wakati huo huo wameshutumu pia madawa mazuri kabisa ya

kienyeji ya miti shamba.

Kilichobaki ni balaa ya utupu wa ujuzi wa Afya

Leo kuna matangazo mengi juu ya miti ipi itumike kwa magonjwa yapi na katika

nchi gani – Lakini hata hivyo ni taarifa kwa ufupi au kwa uhitaji wa kisayansi.

Yanakosa maelekezo ya muhimu kabisa kwa wale wanaohitaji kutumia habari hizo.

Mwenzangu ndugu Bindanda M’Pia, na mimi tumeamua, kwa jinsi hiyo, kuandika

kitabu hiki kwa namna tofauti. Hiki ni kitabu kinachotakiwa daima kukaa karibu na

wewe, siyo kitabu rahisi tu kielezacho mambo ya mchanganyiko wa madawa au

kitabu cha gharama kilichofungwa kwa dhahahu. Kwa tahadhari zote tunakuomba

ujali kwamba kitaweza kuelezea tiba mbalimbali zinazotokana na uzoefu. Uzoefu

huu ni wa watu maskini kabisa wasioweza kununua hata asprini, (asprini ni alama ya

“kuwa tajiri” katika nchi nyingi), na pia wale “matajiri,” watu wa kisasa

wanaochagua kwa vyovyote iwezekanavyo kuishi bila kutumia vidonge na sindano,

kwa sababu wanaamini swala hili liko katika kujiamria juu ya usalama wa afya zao.

Kitabu hiki kimesomwa sana na wasomi ambao wana mtazamo wa ukosoaji wa

viwanda vya madawa, na wanaotaka kuwasaidia watu katika kujitegemea, badala ya

kutegemea bidhaa zinazoingizwa kutoka kaskazini. Ambao wanataka watu walio

katika nchi za tropiki,”kuinua vichwa vyao juu sana”.

Ni vizuri kwamba taarifa nyingi zimetunzwa katika vituo vya Kumbukumbu za

kimataifa na katika Internet, na kitabu hiki kimefaidika kutokana na taarifa hizo,

lakini kwa sasa ujuzi wa mambo hayo unatakiwa kusambaa hadi kufika mahali

ambako utafanyiwa kazi. Kwa hiyo katika kitabu hiki, tumepanga kuelezea:

Baadhi ya miti fulani muhimu ya madawa.

Magonjwa na dalili ambazo inaweza kutibu.

Baadhi ya michango kwa ajili ya kutengeneza madawa na maelezo juu ya

matumizi yake

Tahadhari na madhara ya madawa hayo.

Hili toleo la pili limerudiwa kutokana na jinsi ambavyo tumekuwa tukijifunza kwa

kuwa tumekuwa tukiendesha semina zetu katika nchi nyingi za Afrika. Toleo hili

limefaidika kutokana na uzoefu na mlisho nyuma toka kwa watumia madawa,

waganga wa miti shamba, madaktari na wanasayansi, ambao mara nyingi

wanajishughulisha na makundi yao ya anamed (Action for Natural Medicine) katika

maeneo yao.

Tunakilenga kitabu hiki kwa watu walioko nchi za tropiki, wanaopenda kujitolea

kufanya kazi, na kutumia ufuzi na mazoezi kwa faida za marafiki zao, majirani,

hospitali na jumuiya mbalimbali.

Page 12: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

12

Watu wanaharibu ghala la asili la madawa kwa:

A. Kutumia magome katika madawa ya kienyeji.

B. Kuchoma mkaa.

C. Kuwasha moto pori.

B

A

C

Page 13: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

13

Na Bindanda M`Pia

Kama ungekuwa mwalimu wa shule ya msingi katika nchi za tropiki na

unasumbuliwa na maumivu ya viungo ungetakiwa kutumia pato lote la mwezi (US $

11) kununua dawa ya kupaka kwenye maumivu hayo (50g) katika duka la madawa

mjini! Hii ilinitokea Kinshasa (D.R. Kongo). Kwenye kasha utasoma kwamba kitu

kinachotibu ndani yake ni capsicum frutescens. Kwa bahati mbaya hujui kama

ambavyo mimi sikujua – kwamba hii ni pilipili, mmea ambao katika eneo la tropiki

hustawi karibu kila mbele ya mlango wa nyumba ya mtu. Kwa kutumia pesa hiyo

sasa tunaweza kuzalisha kilo 3 za dawa hiyo katika kijiji chetu.

Leo nchi za “dunia ya tatu” zinajitegemea; watu waliotawaliwa zamani sasa

wanafanya maamuzi yao na wanatatua matatizo yao wenyewe. Hiyo ni nadharia -

vitendo ni tofauti! Atakayetembelea miji na majiji ya nchi hizi ataona hali ifuatayo:

Matangazo mbele ya maduka yakisema “Bidhaa kutoka nje” yaani vitu vya gharama,

vitu vya anasa kwa wateja wa daraja la juu. Vitu vingine vyote vinaitwa “vitu vya

kienyeji”, yaani vya bei rahisi, na thamani ndogo, kiasi kwamba katika kijiji chetu

bidhaa hizi zinaitwa, “ndombe” – nyeusi!

Sababu ya kuvibeza vitu tunavyotengeneza kwa ufundi wetu (na kwa wakati huo

kuwadharau pia wenzetu wenye ujuzi huo) ina mzizi wake huko kaskazini na kusini

pia. Kutoka kaskazini vinakuja vivutio mbalimbali na zawadi za watalii, na

mawakala wa maendeleo wa serikali ambao hutumia sehemu iliyo kubwa ya misaada

“wanayotoa” kwa bidhaa waliyozalisha katika nchi zao. Kusini, ni mwanakijiji wa

kawaida, ambaye ufahamu wake juu ya maendeleo ni kuuza bidhaa wanazozalisha

kijijini hapo katika mji ulio jirani na kununua bidhaa za viwanda kutoka huko mjini,

au vizuri zaidi, kutoka nje.

Mifano ifuatavyo imechukuliwa kutoka kijijini kwetu:

Mifugo bora na yenye afya huchukuliwa na kuuzwa mjini. Kisha wanakijiji

wananunua nyama za kwenye mikopo ambayo ina nyama ya hali ya chini.

Mama hulazimika kuuza unga wa mihogo wenye lishe kwa sababu binti yake

aliye sekondari anapenda kununua biskuti zilizotengenezwa kibiashara,

ambazo hudhuru meno yake.

Ili kununua unga wa maziwa baba anakata miti adimu iliyohifadhiwa kwa

miaka maelfu na anaichoma ili kutengeneza mkaa. Lakini kuwanywesha

watoto wao maziwa ya unga toka Ulaya inahatarisha maisha yao wakati maji

yasiyochemshwa yakitumika kuchanganyia au wakati chupa zinatumika pasipo

kufanyiwa usafi kuua vimelea hatari.

Nta nzuri kabisa ya nyuki hutupwa baada ya asali kuvunjwa. Kisha dawa ya

viatu yenye nta bandia yenye ubora mdogo inaingizwa nchini na kuuzwa kwa

bei ya juu.

Wanakijiji wanalipwa pesa kidogo kwa mafuta yao ya mawese yenye thamani.

Huko mjini yanauzwa tena kwa bei ya juu zaidi na kisha yanauzwa huko

Ulaya ambako mafuta ya gharama kama vile Palmolive na mengine

UTANGULIZI

Page 14: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

14

yanatengenezwa kutokana na hayo mawese. Kisha yanasafirishwa hadi Afrika

tena na kuuzwa kwa bei ambayo mtu hawezi kwa sababu yana “mafuta ya

tropiki”.

Karanga zinauzwa nchi za nje ili kutengeneza karanga zilizokaangwa, mafuta

ya karanga, siagi ya karanga, na vipodozi, ambavyo baadaye huingizwa tena

nchini na kuuzwa.

Mtoto mwenye ukosefu wa lishe anategemea kula mayai matatu

yaliyopatikana kwenye kiota cha kuku lakini baba aliyauza ili kununua

kokakola.

Wakati watoto wanacheza mpira wa chungwa bichi, mama yao anachezea

fedha ya familia kununua dawa ya kuongeza afya ya kitoto chake, dawa

iliyotengenezwa kutokana na maji, sukari , rangi ya vyakula isiyo asili na

ladha ya machungwa ya kuunda.

Na kwa jinsi hiyo familia, vijiji, mikoa na taifa vinaendelea kuzama ndani kabisa ya

umaskini.

Jambo la kusikitisha kabisa katika Afrika ni upotezaji wake wa mali asili

Moja ya mali asili hizi ni ujuzi. Ulaya kama

maktaba ikifungwa jamii hupiga yowe. Pamoja

na hayo katika Afrika na sehemu zote za

kusini, maktaba yote imezikwa kwa pamoja na

kila mzee anayefariki.

Kwa miaka sita Dr. Hans-Martin Hirt na

mimi tulifanya kazi kwa ushirikiano wa

shughuli za kitabibu za kanisa katika Zaire,

Afrika Magharibi, katika kijiji cha Natamba-

Solo katika wilaya ya Kwango. Katika mkoa

kuna daktari moja tu kwa watu 100,000, hata

leo mwaka 2001. Watoto wanakufa kwa njaa,

kuharisha na minyoo. Kama matokeo ya

barabara mbaya mfanyabiashara mmoja tu

hufanikiwa kufika kijijini kwetu kununua

mazao ya kilimo; kwa jinsi hiyo watu watawezaje kupata fedha ya kutosha kununua

madawa?

Tumeongelea hali yetu katika semina na mamia ya waganga wa kienyeji, manesi,

wachungaji na wengine. Walitutia moyo kufanya utafiti wa ujuzi wa Afrika huko

Ulaya, ujuzi ambao tumefanikiwa kuugundua tena katika vitabu na majumba ya

kumbukumbu katika vyuo vikuu vya Ulaya huko Gent, Antwerp, Brussels, Basel,

Tübingen, Heidelberg na Montpellier. Taarifa nyingi juu ya mimea ya madawa ya

Waafrika wa eneo la tropiki, zinapatikana Ulaya – kwa kutumia kitabu hiki tunazileta

Afrika.

Page 15: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

15

Kitabu hiki hakifichui siri za ndani. Ni uonyeshaji wa Elimu ya zamani.

Michanganyiko mingi ya madawa imehakikishwa kwa majaribio maelfu mengi ya

kisayansi na mipango ya utafiti ya siku hizi ambayo haifahamiki kwa wananchi wa

kawaida.

Ni tiba gani ambayo ungechagua: “ya asili” au “ya kikemia”? Kuna baadhi ya

magonjwa ambayo ni vizuri zaidi kutumia madawa ya kikemia. Kwa swala hili

linajitokeza swali lenye kuhoji kama mgonjwa wa maeneo ya tropiki ataiweza bei

yake. Kuna magonjwa ambayo hata hivyo mimea yenye dawa inafaa zaidi kutolea

tiba. Baadhi ya mimea hii ni adimu sana, kama mbafu (Canarium schweinfurthii) au

ni magumu kuyatengeneza kwa wingi, kama mziwaziwa (Euphorbia hirta), au

inaweza kuvunwa miaka 100 baada ya kupandwa katika maeneo yaliyo magumu

kufika, kama vile miti adimu sana ya tropiki, kiasi kwamba viwanda vya madawa

haviifurahii ingawa matibabu yake ni bora zaidi.

Kwa bahati mbaya baadhi ya mimea ya madawa haifanyiwi uchunguzi kabisa.

Magonjwa ambayo ingeweza kutibu, mfano river blindness, wakati wote

yanawaathiri wale walio maskini sana kiasi cha kutoweza kuhimili bei ya dawa zake.

Kwa mara ya kwanza tuliandika kitabu hiki kwa Kifaransa kwa ajili ya maeneo ya

Afrika yanayoongea Kifaransa. Baadaye tukapokea maombi ya kitabu kuandikwa

kwa Kiingereza na lugha nyingine kutoka Amerika Kusini, Kenya, Uganda na

Kameroon. Kama matokeo ya utafiti na uzoefu wetu, na ujuzi na taarifa za wasomaji

wetu na washiriki katika semina zetu, katika toleo hili tumebadili baadhi ya

michanganyo ya madawa kadhaa na kuweka mimea mipya.

Katika kitabu hiki tunajadili mimea ya madawa ambayo inastawi karibu maeneo

yote ya tropiki. Kimetolewa siyo kwa watu wawezao kuona jua, mchanga na mateso

tu katika nchi hizi bali kwa wale waliojitoa kikamilifu kwa uelewa wa namna

nyingine wa maisha, kifo, utajiri, muda, afya n.k.

“Yule anayeithamini mimea ya tropiki anaonyesha kuwathamini kuwathamini

wakazi wa eneo la tropiki pia!” Dr. J. Courtjoie, mwandishi maarufu wa vitabu vya madawa katika Kongo.

Tumekiandika kitabu hiki kwa lugha rahisi kiasi inavyowezekana. Lengo kuu la

kitabu hiki ni kufundisha wananchi wa kawaida - hapana, kufundishana! Maswali

yanayoweza kujadiliwa, kwa mfano, ni haya: Je, tunaujua mmea huu? Unaitwaje?

Tutauita jina gani baadaye? Je, tunautumia katika namna na kwa magonjwa

yaliyoelezwa katika kitabu hiki? Tunategemea madhara gani? Tunawezaje kuulima,

kuutayarisha na kuutunza?

Uelewa wetu wa “madawa ya asili” ni tofauti na ule wa “madawa ya kienyeji ya

magharibi na kusini.” Kwa mfano unavyoeleza: Mama wa kiafrika anataka kumtibu

mtoto wake ugonjwa wa kuhara. Katika hospitali ndogo aina ya Loperamide

inatumika ili kupunguza kasi ya kuharisha. Mganga wa jadi anaweza kuchomeka

kizibo katika njia ya haja kubwa ya mtoto. “Njia“ zote hizo siyo sahihi. Njia sahihi

ingekuwa kuchanganya vifaa vya asili, maji, chumvi na sukari, kutengeneza maji –

chumvi.

Page 16: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

16

Kama hospitali yako inahitaji sukari na chumvi kwa ajili ya majichumvi, usiagize

vitu hivyo toka nchi za nje ambavyo vina takataka nyingi. Bali tengeneza

mchanganyiko huu kwa kutumia kwa wingi uwezavyo kile kinachopatikana katika

mazingira yako, pamoja na msaada wa kifedha toka nchi za nje kama ikihitajika.

Madawa ya asili yanawasaidia watu kuwa na mwamko kwa sababu wao ndio

wanawajibika zaidi kwa maisha yao.

Uzoefu wa kutumia taarifa zilizo katika kijiji chetu huko Zaire ulitufundisha

kwamba madawa ya asili yanawapelekea watu kuishi maisha yenye afya zaidi, yenye

kujithamini na yenye mafanikio zaidi bila hayo maisha kuwalazimisha kuhitaji fedha

zaidi kuliko zamani.

Ukiwa mzungu unatembelea nchi fulani katika tropiki, kitabu hiki kinaweza

kukusaidia kwa magonjwa yako. Au, unafanya kazi katika maeneo ya tropiki? Kama

ni hivyo tunaomba msaada wako katika eneo lako ili kwamba madawa ya asili

yaingizwe mashuleni na vyuo vikuu. Kwa njia hii “madawa ya asili” yatakuwa

“madawa ya darasani”.

Au wewe ni nesi mzungu, mganga au mtengeneza madawa? Ujifanye mtaalamu,

au zaidi yake, wape wenyeji wa eneo hilo nafasi, muda na hata msaada wa kifedha ili

wajifunze juu ya madawa hayo ya kienyeji, jinsi yanavyotumika, na kisha fanya

semina mbalimbali.

Kazi inayotakiwa kufanywa ni kubwa. Kwa kufanya kazi na madawa ya asili kwa

miaka 20, bado tunaendelea kupata mimea ya madawa muhimu na inayotumika

ambayo hakuna taarifa hata moja ya uchunguzi iliyoandikwa katika benki za taarifa

350 dunia nzima.

Tunatia kipau umbele madawa ya asili

na njia za maisha za asili.

Mtu anaweza kujiuliza kama “madawa ya

asili” yanaweza kuchanganywa katika

mfumo wetu wa madawa ya kisasa ya

viwandani. “Tusingependa hivi, badala

yake tunasisitiza kwamba, kinyume chake

ndiyo iwe njia bora. Tunatia kipaumbele

“madawa ya asili” na njia za maisha za

asili - swala ambalo limekuwa la “kisasa”

katika baadhi ya sehemu za Ulaya, na sasa

ni swala linalopamba moto katika nchi za

tropiki vile vile. Kisha tunaangalia dawa

zinazotoka nje, dawa za kibiashara, kutusaidia kwa yale matukio ambayo madawa ya

asili peke yake hayatoshi.

Page 17: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

17

Juu: Kamati ya kijiji ikijadili jinsi ya

kuanza kutumia madawa ya asili.

Kati kushoto: Mganga wa “kisasa”

anajadili na mkunga wa jadi juu ya mimea

ya madawa.

Kati kulia: Mtawa akijaribu sigara ya

mpapai (Carica papaya); angalia sura 5.5.

Kushoto: Ni bora zaidi kuzika madawa

ambayo wakati wake wa kutumia ulipita.

Page 18: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

18

SURA 1:

1.1. Historia ya madawa katika tropiki ya Afrika

Katika Afrika madawa ya kienyeji yamekuwepo na yamekuwa yakitumika kuliko

vile tunavyoweza kufikiri. Waafrika walijua kujitibu na kujilinda kwa kutumia

mimea hata kabla wakoloni weupe hawajaja na kutambulisha dawa zao za “kisasa”.:

Hata mbinu za upasuaji kama kushona mishipa ya damu zilifanyika. Kujikinga kwa

madawa pia kulikuwepo. Waafrika waliishi kwa miaka milioni 4 hivi katika hali ya

hewa ya hatari sana. Ni lazima tukubali kuwa madawa yaliyokuwepo kabla ya

madawa haya ya “kisasa” yalikuwa maridadi sana.

Ebu fikiri, leo China ina madaktari wapatao 20,000 katika hospitali 597 ambao

wanaganga kwa madawa ya kienyeji. Maswala ya uuguzi huko Asia hayakuteteleka

kwa sababu wamepokezana taarifa toka kizazi hata kizazi kwa njia ya maandishi.

Lakini katika Afrika na sehemu za Amerika kusini elimu ya utamaduni imekuwa

ikisafiri kwa njia ya maneno ya mdomo pekee. Kwa sababu ya maisha ya kuhama

hama, vita baina ya nchi na watu kuhamia mijiji, elimu yote inaendelea kupotea

polepole, na mambo waliyofanya wazee hayathaminiwi tena.

Tiba ya kienyeji inajumuisha kutibu kwa mimea kunakofanywa na waganga wa

miti shamba (katika D. R. Kongo wanaitwa “Kimbuki”), tiba ya kiakili, inayofanywa

na makasisi wa madawa na wenye maarifa (kiganga), na matatizo ya mzimu

yanayotibiwa na waonaji, watabiri (kingunza) wanaotegemea zaidi maono na ndoto.

Elimu hii iliendeleaje? Baadhi ya matabibu wa kienyeji ikiwa ni pamoja na wale

watumiao mimea, wanasisitiza kwamba wanapata “nguvu ya ufahamu” kupitia

mawasiliano na mababu waliokufa, kwa njia ya kuvuviwa na kwa ndoto. Wengine

wanajifunza kutoka kwa kizazi kilichowatangulia, na kwa kuangalia tabia za

wanyama. Kwa mfano punda milia mgonjwa anaweza kutembea mamia ya kilometa

ili kutafuta mmea fulani! Na nyani aliyejeruhiwa anaweza kuishi kwa kula majani

fulani.

Dunia nzima mababu zetu waligundua ukweli kuhusu madawa kwa kutumia

“nadharia ya kufananisha,” kwa kudai kuwa, “KITU KINACHOFANANA

KINATIBU KITU KINACHOFANANA NACHO.” Mababu zetu wa Ulaya

waliamini kuwa kama jinsi jani la mchicha lifananavyo na mshale kwa hiyo ni lazima

litakuwa na chuma ndani yake na litafanya kazi ya kutibu upungufu wa damu.

Mababu zetu wa Kiafrika waliamini kuwa mzizi mwekundu unatibu tatizo la

damu, na kwamba kwa kuwa harage lina sura ya figo basi linatibu matatizo ya figo.

Karibu athari zote za mmea ziligunduliwa kwa njia za majaribio (kujaribu na

kukosea). Kwa mfano watu wengi huko Amerika kusini walipoteza maisha yao kabla

haijajulikana kuwa mranaa (Datura stramonium) ina sumu kali.

MADAWA ASILI

MUUNGANO WA MADAWA YA KIENYEJI NA

SAYANSI YA KISASA

Page 19: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

19

Lakini ni Waafrika wangapi watakufa kabla pia hawajajifunza jinsi mmea huu

ulivyo wa hatari? Profesa Kabangu wa Kinshasa amesema: “Hakuna mtu leo

anayetegemewa kuhatarisha maisha yake wakati akifanya majaribio ya athari ya

mmea fulani!”

Kwa dhati tunaamini kwamba kitabu hiki kitakusaidia kuepukana na vifo

vifananavyo na hivyo.

1.2. DAWA YA KIENYEJI NA ILE YA KISASA

Wakoloni wa kwanza waliita dawa ya kiafrika kuwa ni ya “kienyeji,” na hata sasa

Waafrika bado wanaziita dawa za kutoka nje kuwa ni za “kisasa.” Lakini kila watu

wanaoishi, wanatengeneza vitu, wanatenda kufuatana na utamaduni wao! Hii ina

maana, kwa mfano, Aspirin na Penicillin zimekuwa dawa za kienyeji kwa Wazungu.

Hali ya hewa ya Ujerumani ni ya baridi kiasi cha kutoweza kustawisha mpapai,

lakini katika Ujerumani nzima kila duka la madawa lina vidonge vya minyoo au

kutoyeyushwa kwa chakula tumboni, ambavyo vimetengenezwa kwa kuchanganya

unga wa majani ya mpapai pamoja na vitu muhimu kwa ajili ya vidonge. Lakini kama

daktari wa kiafrika akiagiza matumizi ya mmea huu wa Afrika moja kwa moja kwa

Mwafrika, mgonjwa huyu atadhani mganga huyu amechanganyikiwa. Waafrika

wachache wanajua jinsi madawa ya Ulaya yaliyo na mimea ya tropiki!

Dawa ya kienyeji ni nini?

Katika toleo fulani mwaka 1978 Shirika la Afya duniani (WHO) lilielezea madawa

ya kienyeji kama ifuatavyo: “Madawa ya kienyeji ni ujuzi wote, wa njia

zinazoelezeka na zisizoelezeka za uchunguzi, uzuiaji na uondoaji wa hali isiyo

sawa kimwili, kiakili na kijamii, ikitokana hasa na ujuzi wa mtu binafsi na

matokeo yaliyorithishwa toka kizazi hata kizazi.” Hiyo maana inaonyesha kutokueleweka vizuri kulikopo: Kutokana na uzoefu,

Waafrika wamejifunza kutumia maji ya nanasi mbichi kuamsha hamu ya chakula.

Kwa kutumia hiyo maana, kwa hiyo, hii ni ya “kienyeji.” Huko Ulaya hata hivyo,

kwa kufuatia majaribio ya kisayansi, njia hii, ambayo ndiyo ile ile, inatumika, kwa

hiyo inaitwa “ya kisasa.”

Mamilioni ya Waafrika wamefanikiwa kuwa hai hadi leo kwa sababu ya Quinine,

ambayo inapatikana kwa hali zote: kama vidonge, sindano, katika maji ya sukari

(syrup) n.k. Lakini kwa urahisi Quinine inapatikana katika gome la mti wa cinchona.

Miti ya cinchona inastawi katika nchi za tropiki. Kwa jinsi hiyo Quinine ni dawa ya

“kienyeji.” Mmisionari wa Kihispania alijifunza siri ya kazi yake (cinchona) kutoka

kwa mganga wa kienyeji wa India.

Mfano mwingine ni dawa ya belladonna: Imetengenezwa Ulaya na inauzwa katika

mahospitali yote ya Afrika. Ina mchanganyiko wa ua la hatari linalochanua usiku,

(nightshade) ambalo kama jina lilivyo, lilitumiwa na vizazi vingi vilivyopita huko

Ulaya kwa uchawi.

Kwa hiyo, ni lazima tuelezee kila zao la mmea kwa kutumia uwezo wake wa

kutibu uliohakikishwa kama “wa kisasa.” Lakini madawa yote yaliyotengenezwa kwa

Page 20: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

20

vitu vya asili kwa wakati huo huo ni ya kienyeji, ya asili ya nchi yaliyomo na

yalikotoka!

Dawa za kienyeji, ni vizuri zikimaanisha:

“Jumla ya shughuli zote, njia, huduma, vitu vya ziada, na jitihada za namna

yoyote (kwa vitu halisi, kiroho au vinginevyo) ambavyo kwa vizazi vingi

vimesaidia watu kujilinda na magonjwa, kuondoa maumivu na kuleta

uponyaji.”

1.3. HOFU YA KUSHIRIKIANA

Maneno yanayotumika kuelezea dawa kama ya “kienyeji au ya “jadi” na ya “kutoka

nje” au ya “kisasa” haina maana ya kila moja kuwa kinyume cha jingine. Hofu isiyo

ya msingi ya baadhi ya watu kuhusu dawa za kienyeji inajenga jambo fulani ambalo

mtu anaweza kuliita “hofu ya ushirikiano.”

Kisa kimoja kinasimulia juu ya askari wa cheo cha juu ambaye aliugua. Kwa vile

hakuamini dawa za kienyeji alikwenda kwenye hospitali ya misheni kuhakikisha

anapata huduma ya “kisasa”. Mganga akasema, “Ndugu inabidi tukupe ganzi ya

kienyeji”. “Oh! Mungu wangu! Na nyinyi pia”! Mgonjwa alisema - kisha akatoroka

hospitalini.

Habari kama hizi zikielezea hofu na kutoelewana kwa watu wenye mitazamo

mbalimbali ya kimatibabu, ingeweza kujaza kitabu. Kufuatia mafundisho yake ya

“kisasa,” juu ya madawa nurse mmoja wa Congo, alijua mimea mingi ya kizungu

inayofaa kwa madawa, lakini hakujua hata mmoja uliostawi katika kijiji chake! Na

daktari wa kizungu atawezaje kupinga madawa ya kienyeji wakati ambapo

anawezeshwa kuishi na kufanya kazi katika nchi za tropiki kwa kutegemea mkwinini

wa jadi na kemikali zitokanazo nao?

Yawezekana sababu kubwa kwa nini waganga na wauguzi hukataa madawa ya

kienyeji ni kweli kuwa kuyakubali kutawabadili kuwa wanafunzi tena, na hata

kujifunza kutoka kwa wagonjwa wao tena, watu wale wale ambao wamekuja

kuwaonyesha umahiri wao wa “kisasa”!

Tutaongelea juu ya “madawa ya kusini” tukianza kuelezea mfumo wa kienyeji

katika nchi za tropiki. Katika kizio chote cha kusini cha dunia, njia za matibabu na

mimea inayotumika inafanana kiasi cha kushangaza! Baadhi ya matabibu katika

Kongo D. R. ambao hawajawahi hata kusoma kitabu walitueleza njia za kutibu

ambazo zinatumika vilevile katika Brazili na Ufilipino. Vivyo hivyo tutauita mfumo

wa uzalishaji madawa ulioendelezwa katika Ulaya na Amerika kaskazini kama

“madawa ya Kaskazini.”

1.4. TOFAUTI ZILIZOPO

Kuna tofauti kubwa kati ya madawa ya Kaskazini na madawa ya kusini kwa namna

mgonjwa anavyotibiwa. Madawa ya kaskazini humchukulia mgonjwa kiupekee.

Katika hospitali hutibiwa na madaktari mabingwa waliofundishwa vizuri. Mafanikio

katika mfumo wa afya yanapimwa kwa viwango maalum, mfano kuna waganga

Page 21: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

21

wangapi, fedha kiasi gani, kuna vitanda vingapi hospitalini n.k. vinavyohudumia

wakazi 100,000.

Magonjwa katika kaskazini yanaonekana kusababishwa na mambo kama kemikali

zilizovutwa katika hewa chafu au zilizoliwa kama nyongeza katika vyakula au

kuhifadhi vyakula, ulaji wa sukari nyingi, msongo wa mawazo, matumizi mabaya au

madhara ya madawa.

Kinyume chake, madawa ya kusini yanatia msisitizo katika kumchukulia mgonjwa

kama mwanajamii. Mgonjwa hukaa katika uangalizi wa familia na kijiji. Waganga

mbalimbali wa kienyeji wanaweza kuonwa kwa ajili ya mgonjwa. Wale wenye ujuzi

wa kutibu mara nyingi wana elimu kidogo, lakini wana ufahamu mkubwa wa

mahusiano. Maendeleo mazuri katika afya ya mtu yanapimwa kwa kuongezeka kwa

uhusiano mzuri kati yake na jamii. Hasa sababu za magonjwa zinaonekana kuwa

ukosefu wa chakula, ukosefu wa usafi, pasipo kujali mila, hofu ya roho mbalimbali

(pepo) na mambo kama hayo.

1.5. JE, SIRI ZIFICHULIWE? HATARI KWA MADAWA YA KUSINI

Katika semina nyingi, swali moja limekuwa likiulizwa na waganga wa kienyeji

mwanzoni mwa semina: “Mnategemea sisi tufichue siri zetu? Mtalipa kiasi gani kwa

siri moja?” Wana sababu nzuri ya kuuliza. Katika Ulaya na Marekani zaidi ya bidhaa

za madawa 7,000 zinazotokana na mimea ya dawa ziko katika soko na zinauzwa kwa

zaidi ya dola 3,000,0000,000 za kimarekani kwa mwaka!

Kwa miaka mingi tumekuwa tukikutana katika semina bila fedha yoyote kutumika

kununua siri hizo. Katika madawa ya asili tunaamini kuwa ujuzi wa sayansi

unatakiwa kujulikana kwa kila mtu - kama jinsi upendo kwa mgonjwa ulivyo - na

usilipiwe fedha yoyote. Katika kizazi hiki hati miliki ya ugunduzi ni swala lililo

katika kongamano kali. Mabadilishano ya taarifa juu ya dawa za Mungu hayana

gharama zozote, na inatusaidia wote, wenye hali na viwango vyote, kuwa na ujuzi

zaidi, na hivyo kujitegemea na kutegemeana. Kipaumbele cha viwanda vya madawa

ni kupata faida zaidi kuliko kuokoa maisha.

Tuna haki ya kuweka hoja hii ya upinzani kama kipaumbele chetu ni kinyume cha

lengo hilo. Kwa jinsi hiyo malipo yetu siyo faida, bali kufurahi kuona watu, jumuiya

mbalimbali na mazingira kwa ujumla yakiponywa na kufanywa kuwa kitu kimoja.

Hata hivyo kuna hatari tatu hivi kwenye madawa ya kusini:

1. Waganga wa kienyeji wanazidi kufa na ujuzi wao. Viwanda vinanufaika kwa

zilizotokana na ujuzi wa kienyeji ambao hawakuulipia chochote.

2. Serikali za nchi za tropiki zinaruhusu wengine kunufaika kutokana nazo kwa

kujiunga na shirikisho la biashara la dunia. Kisha mashirika ya huduma ya

kimataifa yanaruhusiwa kumiliki uzalishaji wa madawa kutokana na mimea yao

ya asili, na kuwa na haki pekee ya kuzalisha madawa na kuwauzia tena wale wale

– nchi za tropiki.

3. Hatari ya tatu inasababishwa na wakazi wa nchi hizo wenyewe. Wakati wa kipindi

cha jua sehemu kubwa ya Afrika inachomwa moto. Watu wanachoma moto

mapori kwa makusudi. Baada ya miaka mingi ardhi inapungua thamani, kwa

Page 22: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

22

sababu virutubisho vingi vinapotea katika moshi milele! Kwa jinsi hiyo muda wa

mmea kuishi unapungua.

1.6. HASARA ZA MADAWA YA KUSINI

Katika kiwango cha kijiji, vifaa vya muhimu vya utengenezaji wa madawa mara

nyingi vinapatikana. Hata hivyo matatizo yafuatayo hujitokeza mara kwa mara:

Hakuna maji na sabuni ya kuoshea vyombo na kunawia mikono vizuri.

Hakuna vipimo vya vitu vitumikavyo kutengeneza dawa wala njia maalum ya

kuzitengeneza – kwa sehemu kubwa wivu na ugomvi baina ya hao waganga ndiyo

sababu.

Ni mara chache sana kumekuwa na kanuni maalum ya vipimo vya madawa. Kwa

mimea yenye sumu, ina maana ni tishio la maisha, hasa kwa watoto.

Mara nyingi mgonjwa hajui mmea uliotumika wala madhara yake.

Baadhi ya majina ya kienyeji yanatofautiana toka kijiji kimoja hadi kingine, mimea

mingi hujulikana tu kama “maua.”

Mchanganyiko wa bidhaa za biashara na madawa ya kienyeji vinaweza kuua watu.

Mara nyingine madawa kutoka nje ya nchi yanaweza kutumika bila kuangalia kwa

makini mwisho wa muda wake wa kutumika.

Waganga wengi hata huchanganya njia za madawa ya kisasa (kama sindano) na

uchawi.

1.7. HASARA ZA MADAWA YA KASKAZINI

Septemba 1991, Wazungu 25,000 waliikimbia nchi iliyoitwa Zaire wakati ule.

Uhamaji wa ghafla namna hiyo ulipunguza kwa ghafla kiwango cha upatikanaji wa

madawa ya “kisasa.” Matokeo yake ikawa ni vifo vya maelfu ya wagonjwa

waliotegemea madawa hayo kutoka nje. Katika hali kama hiyo wale ambao wana

madawa ya kutibu hata kiasi fulani cha wagonjwa wana bahati sana, wako katika

nafasi ya kuokoa maisha ya wengi.

Kama unajua madawa yaliyo katika mimea inayostawi kuzunguka nyumba yako,

hutatembea tena km. 10, 50, 100 kufikia kituo cha afya au hospitali wakati ukiwa

mgonjwa! Hata wakati wa misukosuko ya kisiasa, kuna hatari kwamba mahospitali

yasipate madawa. Kwa upande mwingine uoto wa asili ni ghala la madawa

tulilopewa na Mungu, ambalo kama tutalitunza, daima litakuwepo kwa ajili yetu

kutumia.

Madawa ya mitishamba hayana gharama yo yote ukilinganisha na madawa ya

kuagiza toka nje! Hutegemei tena fedha, na wagawaji wa dawa wa mbali. Kama

mkitengeneza madawa ya kunywa na kupaka n.k. nyinyi wenyewe kijijini, watu

wataponyeshwa , wenyeji watapata ajira, pesa itazunguka katika uchumi wa eneo

lenu. Badala ya kuvuja na kwenda kwa matajiri nchini mwenu au walio nchi za nje.

Kwa ufupi kila mmoja ananufaika.

Kama wewe ni daktari au mhudumu wa afya katika hospitali na umejifunza

kutengeneza madawa kutokana na maelekezo ya kitabu hiki, unaweza kuokoa fedha

Page 23: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

23

ya kigeni ya kutosha ambayo ingetumika kununua, kusafirisha na kutunza madawa,

kwa nyongeza unaepuka usumbufu na gharama za ushuru wa forodha na kanuni zake

mbalimbali.

Chukua kwa mfano D. R. Kongo: Mgonjwa akija kununua dawa hushangaa jinsi

gharama yake ilivyopanda. (Mnamo mwaka 1993 thamani ya fedha ilishuka kwa

100% kwa juma na ilisababisha magonjwa yasitibike). Mgonjwa siyo tu kwamba

analipia dawa, bali analipia pia madeni ya nchi, madeni ya fedha ambayo hajawahi

kuiona, mara nyingine kwa fedha iliyotumika kununua silaha, na madeni ya benki ya

Dunia inamtaka ayalipe. Hata hivyo madawa ya Kusini mara nyingi hufanya kazi

kwa kubadilishana: Tohara moja kwa mfano, ni kuku mmoja!

Mganga wa kienyeji hutibu mgonjwa kikamilifu na matatizo mengine

yanayomzunguka. Hatibu dalili au ugonjwa kwa pekee (mfano surua, minyoo, kifua

kikuu) bali pamoja na mgonjwa mwenyewe, pia huangalia matatizo mengine kama

kukosa ajira, mazao kutostawi, ugonjwa wa mapenzi, kukosa watoto.

1.8. LENGO LETU: “DAWA ZA ASILI.”

Waafrika wameshangazwa na “wimbi la kijani.” linalofurika katika maduka ya

madawa huko Ulaya . Katika kila duka la madawa huko Ujerumani hukuta mimea

400 na chai (dawa za maji) nyingi za mimea mbalimbali zisizohesabika.

Mungu ametupa bure mimea ya maua 500,000. Karibu mimea 50,000 inatumika

kwa madawa ya kienyeji. Kutokana na WHO karibu mimea 10,000 imefanyiwa

uchunguzi kisayansi na kutolewa maelezo. Hivyo hubakiza idadi ya mimea 40,000

kufanyiwa uchunguzi ! Bado tuna kazi kubwa!

Baada ya majaribio marefu ya jinsi ya kuelezea mitazamo yetu kwa madawa,

tunachagua neno “dawa za asili” ambalo kwa sasa tunalielezea kama ifuatavyo:

“Dawa za asili” ni mchanganyiko wa faida za madawa ya kusini na zile za

madawa ya kaskazini.

Dawa za asili ni za asili kwa sababu, kwanza zimetokana na asili, na pili ni kitu

kilicho wazi na cha asili kufanya jambo kwa kutumia zana zinazopatikana. Hii ina

maana kwamba ili kutumia dawa za asili, waganga wa jadi kutoka eneo la kusini,

wahudumu wa afya, madaktari na watumishi wa maendeleo, wenye ujuzi katika

madawa ya kaskazini, wanatakiwa kujitoa kujifunza kutoka katika namna ya kutibu

na uzoefu wa kila mmoja. Kwa jinsi hii huduma muhimu ya afya, inayoweza kuhimili

kulegalega kwa siasa na uchumi vinaweza kuimarishwa.

Kitabu hiki kimeandikwa kwa lengo hilo. Kupitia matumizi yake, tumeona kuwa

tayari watu binafsi na jamii kwa ujumla wamejitegemea zaidi katika kuzuia na kutibu

maradhi. Mamia wamepata ajira kwa kulima hii mimea ya madawa na kisha

kutengeneza haya madawa. Maelfu ya watu wameweza kutibu malaria, kuhara na

magonjwa mengine. Jambo hili na liendelee - katika ngazi mbalimbali ! Kwa sababu

katika kila nchi huduma ya afya inafanyika katika ngazi zifuatazo:

1. Dawa za nyumbani: Madawa yaliyo katika mfumo wa familia, huko kaskazini,

kwa mfano, matumizi ya chai ya mranaa, kusini matumizi ya mbegu za mpapai.

Page 24: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

24

2. Dawa za “ngazi ya wilaya” au za hospitali: Madaktari na wauguzi mbalimbali

huko kaskazini, na madaktari na waganga wa jadi kusini, pamoja na ujuzi wao

maalum.

3. Madawa ya chuo kikuu: Uchunguzi na ufundishaji kuhusu madawa na jinsi ya

kuyatumia.

“Dawa za asili” zinapaswa kutumika katika ngazi zote tatu zilizotajwa hapo juu.

Dawa za nyumbani ndicho kipaumbele, kwa sababu kituo cha afya cha muhimu na

chenye manufaa zaidi ni nyumbani. Wakati wa vita vya wao kwa wao na njaa katika

nchi za tropiki mchango nyeti katika kudumisha afya nzuri katika jamii hufanywa

kwa kuongeza ujuzi na utaalamu zaidi katika ngazi ya familia.

Maendeleo yanayoendelea ya uendelezaji madawa ya hospitali ni hatua ya pili

muhimu, kwa sababu huko pia wagonjwa watanufaika na uwezo wa kuponya wa

madawa ya mimea.

Dawa za asili lazima pia zifike ngazi ya tatu, chuo kikuu, ili kupata jinsi ya kutoka

huko na kuwarudia wananchi. Nchi kama Tanzania, Uganda na Cameroon

zitanufaikaje na kufundisha waganga katika madawa ya magharibi pekee? Matokeo

yake ni kwamba waganga wengi wanahamia nchi zilizoendelea ambazo zina vifaa

vya kisasa mahospitalini na zinalipa mishahara mikubwa. “Pori ni kwa ajili ya

wamissionari, siyo kwa ajili yetu wataalam” niliambiwa na mganga kijana katika

nchi ya Peruvia akiwa katika mji mkuu wa nchi hiyo.

Kwa jinsi neno “dawa za asili” litakavyokuwa lenye kuaminika katika tiba, kwa

vyovyote kazi ya tiba vijijini itakuwa na nafasi ya kuvutia, kwa sababu maduka

mengi ya madawa yatakuwa na madawa mengi bora zaidi kuliko mjini!

WEWE NI MWANASAYANSI!

WEWE NI MWANAMAENDELEO!

Kwa makusudi kabisa hatukuweka dawa za kichawi katika kitabu hiki. Baadhi ya

mimea inatumiwa na wale wanaoitwa waganga ili kumtafuta mwenye hatia wakati

kosa limetendwa. Waganga wababaishaji au wachawi humpa dawa mtu mmoja,

kutoka mmea wenye sumu ili anywe, na mtu mwingine dawa kutoka kwenye mmea

unaofanana na huo lakini usio na sumu. Mtu wa kwanza akifa inatangazwa kuwa

mababu wamepitisha hukumu juu ya mtu huyo kwa hiyo atakuwa ni mwizi. Mambo

kama hayo yanaamsha hofu na kuchukuliwa na vijana kama mambo yaliyopitwa na

wakati na yasiyo ya kisasa, na hii ni sababu moja wapo ya vijana kuhamia mijini.

Madawa ya asili yanaunganisha sayansi, madawa ya mimea na upendo, lakini siyo

uchawi wala viini macho.

Katika Ujerumani, matangazo ya biashara za madawa katika Television wakati

wote yanafuatiwa na sentensi, iliyozoeleka lakini ya muhimu: “Kwa hatari na

madhara ya dawa soma maelezo zilizoko ndani na tafuta ushauri toka kwa mganga au

mtengeneza madawa.” Hata hivyo hizo hatari na madhara hayo hayawezi kuepukwa

hata kwa madawa ya mimea pia. Kila dawa za mimea na zile za kemikali zote zina

madhara mengi. Madhara makuu yanaweza kuonekana kwa mgonjwa mmoja,

yasionekane kwa mgonjwa mwingine, na hata kuwa ya hatari kwa mgonjwa

mwingine. Kwa mfano mmea utumikao kutibu mapigo ya moyo yaliyo chini

Page 25: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

25

(hypotension) unaweza kumuua mtu kwa mapigo ya moyo yaliyo juu (hypertension).

Kwa sababu hii hatuwezi kuwajibika na matokeo ya hatari ya kutumia miti shamba.

Kwa maneno mengine: unahusika na wewe mwenyewe ni mwana sayansi. Hii

inahusisha kujifunza daima kutokana na uzoefu wako, na kuwa na mahusiano ya

karibu na waganga wengine, ili kwamba ujifunze kutokana na uzoefu na ujuzi wao.

Waganga wa miti shamba huko Amerika ya kusini wanaitwa “Curiosa” –

wadadisi.

Hii ndiyo maana ya “maendeleo”: Kuwa mdadisi, kuwa tayari kubadilika!

Kwa jinsi hiyo swali la msingi ni: Ni kwa njia gani waganga na wauguzi, ambao

mara nyingi wamefunzwa 100% katika madawa ya kaskazini, watafanya kazi na

waganga wa jadi na wakunga kwa faida ya maskini na watu fukara? Watawezaje

kuwa “wadadisi,” kuwa tayari kiakili kujifunza pamoja?

Tangu mwaka 1985 tumekuwa tukiendesha semina ambazo zimeshirikisha

waganga kutoka sehemu zote mbili . Matokeo ni:

Watu wengi wananufaika: kamati za afya za msingi zinachagua wawakilishi

kuhudhuria semina ambao hutoa taarifa tena kwa wananchi waliowatuma ili

kwamba wote wajifunze mambo mapya.

Waganga wa mahospitalini wanafaidika: Wanapata kujua umuhimu na athari za

madawa ya mimea, na wanaanza kujifunza namna mpya za uuguzi.

Waganga wa jadi wananufaika nayo: wanajifunza jinsi ya kutoa kozi zinazofaa,

jinsi ya kutunza dawa vizuri zaidi, na wanajua hasa elimu ya afya ni nini.

Mabadilishano huwasaidia waganga kutibu magonjwa mengi zaidi kuliko awali.

Wakunga wa jadi wanafaidika: Hawalazimiki tena kufanya kazi yao kinyume cha

sheria, lakini wanaruhusiwa kufanya huduma kwa wajawazito, kuzalisha na kutoa

huduma ya watoto wachanga kwa ubora zaidi. Zaidi ya hayo wanasaidiwa jinsi ya

kufundisha wanafamilia, jinsi ya kusaidia kinamama wajawazito. Siyo hivi tu –

mwanzo mkuu wa maambukizi ya UKIMWI katika Kongo D. R. inatokana na

waganga wa jadi 40,000 wanaozunguka zunguka (wasio na mafunzo)

wamchomao sindano kila ahitajiye kwa kutumia sindano zisizo salama au zenye

usalama kiasi kidogo. Waganga na wakunga wa jadi waliofunzwa wanaweza

kutoa huduma bora zaidi bila kusambaza UKIMWI.

Tamaduni za kitropiki zinafaidika kutokana na kuboreshwa kwa huduma za afya

za jadi.

Watu binafsi wanafaidika: Mtu kujitengenezea dawa siyo tu kwamba inampa ajira

bali pia humjengea fahari.

Hata jamii za vitu vyote vya asili vinafaidika: Kupanda miti yenye madawa siyo tu

kwamba inatuletea dawa bali pia kivuli na mvua, ardhi inapata rutuba, na chakula

na makazi ya wadudu, ndege na wanyama vinapatikana.

Makanisa yanafaidika kwa uzoefu wetu: Siyo tu wakati wa semina bali hata

baadaye, baadhi ya makanisa yamekuwa na mahudhurio mazuri zaidi kwa sababu

afya njema ni wazi kuwa ni faida kwa mwili, akili na roho. Baadhi ya wachungaji

sasa wanashirikisha manufaa ya mimea ya madawa katika mahubiri yao kama

“habari njema.”

Page 26: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

26

1.9. MADAWA YA ASILI: FURSA KWA KANISA

Madawa ya asili huyapatia makanisa nafasi nzuri za mambo na kazi. Lakini kuna

matatizo. Kwanza, katika Afrika hospitali nyingi zinaendeshwa na makanisa, chini ya

uongozi wa Askofu aliyeathiriwa na Ulaya, na hata kufundishana na wakati

mwingine kutekwa na mambo ya huko. Yasikitisha kusema, baadhi ya viongozi wa

kanisa - siyo wote - wamekuwa maadui wa utamaduni wao, hata kuwa na hofu juu ya

matibabu yao ya jadi!

Pili, kwa sababu ya kukosekana kwa mimea ya madawa, waganga wengi wa jadi

katika miji mikubwa ya Afrika mfano Kinshasa, wanabadilika na kuanza shughuli

kama vile mambo ya nyota, ulozi, au “uchawi wa maneno.” Kwa sababu ya jambo

hili, dawa za jadi zinaanza kupata sifa mbaya. Dawa za asili hata hivyo, hazina

uhusiano na kuibuka tena kwa ulozi, ambao unaanza kuenea zaidi Ulaya na Amerika

ya Kaskazini.

Katika 1993 kule Kalemia, mashariki mwa Kongo D. R., wanawake 40 walikuwa

karibu kuchomwa moto kama wachawi, wakihusishwa na janga la kipindupindu.

Mauaji haya yalizuiliwa kwa jitihada ya makanisa ya kikristo, kwa kufundisha watu

jinsi huduma za afya ziwezavyo kuzuia kipindupindu. Taarifa kutoka Kenya

zilielezea jinsi watu walivyouwawa kwa mitambiko na sehemu za viungo vya

kutumika kutengenezea madawa. Hii ni changamoto kwa makanisa! Majaribio ya ki-

matibabu yaliyofanywa kwa askari wa Marekani na Urusi wakati wa majaribio ya

silaha za atomiki yalikuwa ya kikatili kwa vyovyote! Changamoto, kwa hiyo, siyo

kwamba ni kuondoa utamaduni wa Kaskazini na kuleta ule wetu wa asili, bali jinsi ya

kuendeleza utamaduni ambao unafurahisha watu, jamii mbalimbali na viumbe vyote.

Tunatakiwa kushinda - lakini namna gani? Sisi ni weusi na weupe, madaktari na

waganga wa jadi, wakristo na wasio wakristo. Uzoefu wetu kutokana na mamia ya

semina ni kama wote tukiusogelea MSALABA ghafla tutakuwa tumekaribiana.

Kama wote tukisimama kuzunguka mpapai kujifunza jinsi ya kutibu vidonda, wote

tunatumia mikono yetu na kusahau hata rangi ya ngozi yetu. Na mbegu za mpapai

zinafukuza minyoo ya tumbo kwa daktari kama zinavyofukuza kwa tumbo la mganga

wa jadi, pasipo kujali kwamba tumbo ni la mkatoliki, la mprotestanti au la mpagani!

Matokeo yake semina juu ya “Utendaji katika madawa ya asili” (Action for

Natural Medicine, anamed), juu ya mimea inayotibu, inayoratibiwa na makanisa,

itaondoa vikwazo vingi! Makanisa mengi katika Afrika wameiomba anamed

kuendesha mikutano na waganga wa jadi na madaktari, pasipo kujali imani yao. Na

wachawi wengi watumiao mitishamba walishangaa sana juu ya uwezo wa kutuliza

maumivu wa ua la Mmarakuja (passionfruit) na mafanikio ya ajabu kabisa ya

mziwaziwa katika kutibu amiba. Angalau magonjwa haya hayahitaji uchawi -hakika

hii ni habari njema kwa kanisa.

Imani ya kikristo na uponyaji vyote viwili ni watoto wa mama mmoja, aitwaye

upendo. Yesu alisema: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.” Paracelsus, baba wa

Sayansi ya tiba, alisema, “Msingi mkuu wa matibabu ni upendo.”

Katika kutibu wagonjwa tumegundua kwamba mara nyingi uhusiano wa mganga

na mgonjwa ni wa muhimu kuliko dawa. Ununuzi wa dawa yo yote siyo lazima

upelekee katika nafuu ya mgonjwa. Kuna mambo mengine ya muhimu ambayo yana

Page 27: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

27

mguso katika swala la maisha mema ya mwanadamu, mfano – haki (2. Petro 1:1) na

upendo (1. Kor 13).

Kama ukimwuliza mwafrika kukupa maana ya utamaduni wake unaweza kusikia:

“Sisi ni wale ambao hatujagundua TV wala gari. Hatuna komputa, hatuna

sementi…………..”. Kwa nini badala yake Waafrika wasimshukuru Mungu na

kusema: “Utamaduni wetu umedumu kwa miaka maelfu pamoja na vitisho vingi

mbalimbali. Watu wanaweza kuishi bila kuathiriwa na aina nyingine ya magonjwa.

Hewa yetu, udongo wetu na maji yetu bado viko safi. Hatuwaachi wagonjwa

miongoni mwetu bali tunawahudumia kwa ushirikiano na furaha kama Biblia

inavyosema. Moyo wa furaha ndiyo dawa bora zaidi”.Tusisahau kuwa maelfu ya

wazungu wanakuja katika “dunia ya tatu.” kila mwaka kutafuta mapumziko na faraja,

na makampuni mengi ya biashara huja kutafuta faida nyingi iwezekanavyo kutokana

na utajiri wa asili wa misitu, madini na mimea.

Kanisa lina kazi ya kuhubiri na kuonyesha upendo, hiyo inajumuisha siyo tu

upendo kwa jirani, bali pia kujipenda mwenyewe, utamaduni wako, na mazingira

yako. Kanisa lina nafasi ya kuwasaidia watu kuona fahari ya maisha yao. Mtazamo

huo unaunda msingi wa muhimu ambao mtu anaweza kutumia kujenga stadi na

mambo mbalimbali ambayo yamejazwa na upendo na haki.

Mfumo wa afya wa nchi za viwanda za kaskazini uliojengwa katika kutengeneza

faida kwa wenye hisa, umeathirika. Upendo haupatikani - badala yake kuwa uchoyo

usio na huruma! Hiyo ndiyo sababu ya karibu watu 500,000 waharibu afya zao kwa

madawa ya kuua wadudu kama D.D.T. yatengenezwayo na viwanda vya madawa ya

kutibu mimea? Na hiyo ndiyo sababu ya madawa kwa ajili ya UKIMWI na

magonjwa mengine yanauzwa kwa bei ambayo wagonjwa wengine wa kiafrika

hawawezi kuimudu?

Kama wakristo tunatakiwa kuyalaani mambo haya, lakini pia tufahamu kwamba

mganga wa jadi anaweza kuwakatili vilevile kama mgonjwa atakuwa maskini kiasi

cha kutoweza kulipia matibabu kwa mbuzi.

Mifumo yote miwili hata hivyo ina faida zake. Tuchukue hizi faida za kila upande

na tuanze kufanya kazi kwa pamoja. Tuiite “DAWA ZA ASILI” na tuanze

kushughulika kupiga vita ubaguzi na kutokutenda haki kwa pamoja na jamii za kidini

na za kienyeji.

1.10. MADAWA YA ASILI MAANA YAKE NI KUJIHUSISHA NA SIASA!

Pigo la sabuni lenye madini ya zebaki (mercury) Waafrika wengi na Wamarekani wa kusini pamoja na watu wengine wengi

wamebadilisha miili yao kuwa ghala la madawa, kuwa kama ghala la kuwekea

kemikali. Watu wanakusanya miilini mwao madawa mbalimbali yanayotumika

kuhifadhi vyakula, kuua wadudu, na kubadilisha rangi n.k. ambayo yana madhara

kwa afya zao kiasi kwamba leo wakazi wa maeneo ya miji ya tropiki wana D.D.T.

zaidi katika damu zao kuliko watu wa Ulaya.

Wakati fulani jambo hili litasababisha wazaliwe watoto katika nchi za tropiki

wenye kuathiriwa na madawa kama vile watoto wa Ulaya. Leo watoto 4 kati ya 10

Page 28: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

28

wazaliwao Ulaya wameathiriwa na tatizo hili. Kwa hiyo dawa za asili zinahusisha

kujiingiza katika siasa. Mfano mzuri kabisa ni dawa na sabuni za kuchubua ngozi.

Soko la madawa katika tropiki limejawa na vitu vitumikavyo kuchubua ngozi.

Mafuta yenye hydroquinone au beta methason, ambayo tena ni hatari zaidi. Hatari

mbaya zaidi ni katika sabuni yenye kiasi hadi 3% ya chumvi za zebaki. Vitu vyote

hivi vinazuia utengenezaji wa Melanin. Melanin ni chembe za hudhurungi au nyeusi

zinazosababisha ngozi kuwa na rangi hii ya kiafrika (nyeusi) na hivyo kufanya kazi

ya kuchuja miale ya jua. Kama matokeo ya uchafuzi wa hali ya hewa, wote tunapata

shida inayotokana na upungufu wa utando wa hewa ya ozone. Kwa sasa miale ya jua

inazidi kuwa mikali zaidi na zaidi – katika kizio cha kusini cha dunia ni zaidi ya kizio

cha kaskazini. Zamani watu wenye ngozi nyeusi waliweza kufanya kazi karibu uchi

siku nzima kwenye jua kali bila tatizo. Wajukuu wao leo wanapata shida ya

kuunguzwa na jua.

Kwa msaada wa mabaraza ya makanisa katika D.R. Kongo tunawashauri

wanawake wa kiafrika wasiendelee kuchukulia ngozi yao nyeusi kama ishara ya

umaskini, kama ugonjwa unaohitaji tiba. Ni kitendawili gani hiki: Wanawake

wanazitia hatarini afya zao kwa kuondoa rangi nyeusi ya ngozi zao, wakati wazungu

wanafanya kila jitihada kupata chembe hizo nyeusi? Kwa nini tusichukulie hiyo rangi

ya ngozi zetu kama zawadi ya uumbaji? Siyo kwamba kitita cha maua kinapendeza

sababu ya mchanganyiko wa rangi zake? Kwa nini hili liwe tofauti kwa watu?

Tunatakiwa kudai sabuni na manukato yote yanayotokea Ulaya yenye madini ya

zebaki yapigwe marufuku. Huko Ulaya vitu hivi vimepigwa marufuku karibu kuanzia

mwaka 1975. Hata Uingereza haiwezekani kuzinunua (angalau kisheria) lakini

makampuni ya kutengeneza marashi ya Uingereza na Hispania yanatengeneza sabuni

zenye zebaki maalum kwa ajili ya Afrika, au wanauza leseni za kuyatengeneza huku

Afrika. Tangu 1977 WHO imezisihi serikali zote za ulimwengu kutoruhusu matumizi

ya sabuni zenye zebaki. Lakini ni nini hasa kazi ya shirika hilo kama halina nguvu za

kuyapeleka Mahakamani hayo makampuni?

Sabuni hizi hazileti weupe uliosawa kwenye ngozi. Matokeo yake ni kuwa na

madoadoa, na wakati mwingine hata maeneo yaliyo meusi zaidi na mabaka inatokea,

ambayo waganga huita “confetti syndrome”. Hii ni kwa sababu zebaki huingia katika

ngozi kwa kiwango tofauti. Pamoja na hayo mwili mzima unapata sumu ya kudumu.

Mwanamke ambaye wakati wote anatumia sabuni hizi (jambo ambalo kwa bahati

mbaya linatokea zaidi katika D.R. Kongo, Tanzania, Uganda, Madagascar n.k.) ana

kiwango cha zebaki mara 400 zaidi ya yule asiyetumia, vibaya zaidi zebaki

hupenyeza ubongo na kuathiri akili. Zebaki hupenyeza mfuko wa uzazi vilevile;

huchanganyika na oksijeni na kuwekwa katika ubongo wa kitoto kilichoko tumboni.

Mkojo wa kitoto kichanga cha miezi mitatu ilipimwa na kuonekana una mara 140

zaidi ya madini ya zebaki yaliyo katika mwili wa binadamu. Mtoto alikuwa hajawahi

kuoshwa kwa sabuni hiyo, ni mama pekee aliyekuwa ameitumia!

Madhara zaidi ya zebaki ni ya kiakili (kuweweseka, kupotewa akili, tabia ya

kujinyonga), kutetemeka viungo, magonjwa ya figo, ama magonjwa ya ngozi ya

kuambukiza.

Page 29: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

29

Uchunguzi wa siku hizi unatufanya tufikirie uhusiano wa vifo kati ya matumizi ya

sabuni hizi na UKIMWI (Ugonjwa ambao katika Afrika unaathiri asilimia kubwa ya

wanawake kuliko ya wanaume).

a) Zebaki huwa ni sumu katika kinga ya mwanadamu kwenye T-lymphocytes.

Inapunguza nguvu za asili za mwanadamu kujikinga na magonjwa kama

UKIMWI.

b) Kama matokeo ya kuwa na ngozi nyepesi zaidi, miale mingi zaidi ya ultra-violet –

B inaingia mwilini, pia inadhoofisha nguvu za mwili kujikinga na maradhi.

Sehemu muhimu ya madawa ya asili ni kuwafundisha wananchi kuiheshimu na

kuitunza ngozi yao nyeusi. Mwanamke mweusi atafanyaje ili ngozi yake ionekane

nzuri zaidi? Dr. Yetunde Mercy kutoka Chuo kikuu Lagos, Nigeria anashauri

matumizi ya sabuni rahisi inayotengenezwa kwa mafuta ya mawese ambayo

inatumika katika kila familia ya kiafrika (angalia sura 4:1:6). Aina hii ya sabuni pia

ina uwezo wa kuua bacteria na haina madhara ya ngozi mengi kama zilivyo sabuni

nyingine zilizotengenezwa viwandani zilizo na triethanolamine! Mwanamke yeyote

wa kiafrika anaweza kujitengenezea sabuni isiyo na madhara, ya kujipaka kwa

kuyeyusha sabuni ya kiwandani na kuiongezea mafuta ya mbegu (sura 4:1:9).

Ujumbe ulio ndani ya bidhaa nyingi katika Afrika ni “weupe ni urembo na ni mali.”

Tunawasihi wachungaji na maaskofu watoe tahadhari juu ya tafsiri hii ya

“maendeleo” na “kwenda na wakati.” Waganga, wauguzi na wanamaendeleo,

tafadhali tuitangaze kauli hii “weusi ni uzuri” katika kuelimisha juu ya afya.

1.11 AWA ZA ASILI : HITAJI LENYE MGUSO

Asili, pamoja na miti na vichaka vyake ni ghala la madawa la aina yake. Lakini

kuzidi kuwepo kwake kunategemea ufahamu wetu juu ya mambo yaliyo mazuri kwa

ajili yake na yanayoweza kuidhuru hiyo asili. Mmoja kati ya miti mitano inayostawi

hapa duniani itatoweka katika kipindi cha miaka kumi. Kwa nini? Kwa sababu kila

mwaka msitu wenye eneo kama la nchi ya Switzerland unaharibiwa na shughuli za

kibiashara: mvua yenye tindikali kutoka kaskazini, takataka zinazoingizwa kutoka

nchi za viwanda, na kutokea moto wa porini unaowashwa kwa malengo ya kuwinda

na kilimo.

Kama mganga wa jadi atadai kugundua mmea unaotibu UKIMWI ataonekana ni

mpuuzi. Kwa upande mwingine hata wanasayansi katika Amerika ya kaskazini

hawajakata tamaa. Kila mwaka Idara ya tiba ya saratani huko Amerika huchagua

mimea 1,500 - mingi ikitoka eneo la tropiki - ili kupima nguvu zake dhidi ya

UKIMWI.

Ebu fikiri kwamba kama mababu zetu wangeua fungus aina ya penicillin! Ndugu

Fleming asingekuwa na bahati ya kugundua penicillin katika mwaka 1928. Sasa ebu

fikiri: Wanasayansi wagundue dawa ya UKIMWI katika miti ya eneo la tropiki,

lakini kwa bahati mbaya mti wa mwisho wa jamii hii umetengenezewa kabati au

umechomwa ili kutengeneza shamba la mihogo. Kupotezwa kwa mmea mmoja kama

huu kungemaanisha kibali cha kifo cha mamilioni ya watu ……………….

Kwa pamoja, mimea ya tropiki inafanya kiwanda kilicho bora zaidi cha kemikali

duniani. Kwa mfano Vinca rosea, mmea wenye maua meupe na mekundu, ambao

Page 30: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

30

unastawi mahali popote katika nchi za tropiki kama mapambo, una angalau alkaloids

65, ambazo ni muhimu katika tiba.

Mti mmoja wa Mchikichi ambao tutaupanda leo utawapa watoto wetu miti ya

kujengea nyumba, na nyua. Watapata malighafi ya vikapu, viatu, kamba, mifagio, na

brashi. Mti huu utawapatia mafuta, funza, pombe, sukari na vitamin. Na utaboresha

hali ya hewa duniani kote kwa kuzalisha hewa ya oksijeni kupitia majani yake.

Bila miti hakuna mvua

Bila mvua hakuna mimea ya dawa.

Bila mimea ya dawa maisha yetu yatategemea viwanda ambavyo vinauza mazao yake

kwetu kwa bei ya juu zaidi kadiri inavyowezekana. Viwanda havina jinsi nyingine ya

kufanya kazi: Lengo lake ni kuongeza faida, hata kama jambo hili litamaanisha

kuharibu msingi wake, yaani mazingira. Lakini sisi tuna namna nyingine ya kufanya!

Tunaweza kuchagua kama tunataka kuendelea kuharibu misitu, au kushirikiana kwa

pamoja katika mradi wa ushirikiano:

ANAMED – utendaji katika madawa ya asili!

A) Kutumia sabuni za zebaki

zinakufanya uwe “fanta juu na

chini kokakola.”

B) Vitu vya kuvutia lakini vya

hatari katika duka.

C) Wanaume huko Sudan

wanatayarisha vitu vya

kujipaka kama njia mbadala.

A B

C

Page 31: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

31

SURA 2

Katika sura zinazofuata tutatoa ushauri jinsi kuyafanyia kazi madawa ya asili na jinsi

ya kuendesha semina na miradi katika ngazi ya kijiji na jinsi ya kutengeneza

madawa.

Mradi wa “Madawa asili” unaweza kuwa na mafanikio, ikiwa tu:

Kama watu wengi watauhitaji.

Kama utakuwa ni sehemu ya mpango mzima wa maendeleo.

Kamati ya afya ya wakazi wa mahali fulani inatakiwa kutengeneza mpango wake

maalum wa maendeleo.

Swali la msingi kuuliza ni: Ni nini tuwezacho kufanya wenyewe pasipo kuhitaji

misaada?

Kisha kamati iorodheshe mambo 10 ya muhimu. Katika uzoefu wetu mambo kumi

ya msingi ambayo yamekuwa yakitajwa ni haya yafuatayo:

1. Tunahitaji nia ya kikristo.

2. Ni lazima tuepukane na kuzagaa kwa mifugo.

3. Tuanze kupanda miti na tukate tu ile iliyotupanda sisi wenyewe.

4. Tulime vichakani – siyo misituni.

5. Tupange uzazi ili tuwe na watoto wenye Afya na elimu bora.

6. Kazi ile ile kwa wanawake na wanaume. Tusibaguane katika kazi – haya ndiyo

maendeleo.

7. Tujivunie dawa zetu za asili.

8. Usafi unazuia magonjwa – tutumie vyoo na vichanja.

9. Tuwe waaminifu kwa wenzi wetu na waangalifu, ili tuepukane na Ukimwi..

10. Tufanye kazi kwa pamoja – tujitoe kwa ajili ya miradi ya kijiji.

2.1 KUFUNDISHA NA KUJIFUNZA

Mikutano: Lengo la mkutano liwekwe wazi, mfano: kufundishana kuhusu madawa

ya asili. Mmoja achaguliwe kuwa mwenyekiti, ili kuzuia uongeaji wa holela na

kuchagua mmoja mmoja achangie juu ya ufahamu wake, mshiriki mwingine aandike

miniti, kutunza kumbukumbu za taarifa muhimu ambazo zimechangiwa na

majadiliano yoyote yaliyofanyika katika lugha yao. Ni vizuri kuwepo na wakati wa

kujieleza juu ya mada fulani wanayopendelea, ambayo imetangazwa katika kundi

kabla. Haiepukiki kwamba watu watasema matatizo yote yanayohusu afya na

maendeleo. Mambo yaliyo muhimu au yanayogusa wengi yahifadhiwe kwa ajili ya

kujadiliwa katika mikutano mingine, na yaweza yakaletwa kama mada kuu kwenye

mkutano mwingine.

MADAWA YA ASILI

MIRADI KATIKA NGAZI YA KIJIJI

Page 32: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

32

KUTAMBULISHA MIMEA: Ni muhimu sana kwamba kila mtu aweze kuitambua

kwa usahihi mimea ya madawa ambayo wanataka kuitumia. Tembeleeni sehemu

inakostawi mimea hiyo. Angalieni kwa makini jinsi inavyofanana, umbo na rangi za

maua yake, majani na mbegu, nusa harufu yake, na hata ladha yake. Usionje kabisa

sehemu ya mmea usiojulikana. Wala, usimeze kabisa utomvu wa mmea usiojua;

unaweza kuwa na sumu.

KUTUNZA MAJANI YA MMEA: Katika kila mmea unaoujua kusanya majani,

maua na mbegu, kandamiza sehemu hizi za mmea kwa juma moja katika daftari, na

uzigundishe kwenye karatasi. Upe jina mmea. Uchore, elezea jinsi ya kuutumia na

kuutayarisha, onyesha hatari zake.

PICHA MBALIMBALI: Kama inawezekana chukua picha ya kila mmea, slides ni

bora zaidi, onyesha picha hizi vijiji vingine. Weka nguvu ya umeme kwenye betri

yenye volt 12, wakati wa mchana kwa kutumia panel ya solar. Wakati wa jioni

onyesha picha za slide kwa kutumia projector ndogo ya kubeba. Solar panel

inatakiwa iwe na volt 12 na karibia watt 6, na betri inatakiwa iwe na volt 12 na kati ya

Ah 3 – 6. Projector zinapatikana kutoka:

Radmar, 1263 – B Rand Road, Des plains, IL 60016, USA.

2.2 Mfano wa ratiba ya semina

Semina za kwanza zilizoendeshwa na Anamed zilikuwa Zaire, ambapo tulifanya

semina 2 hadi 4 ya siku moja moja kwa mwaka katika kanda mbalimbali tulipokuwa

na shughuli za afya. Leo walimu wa Anamed wanazunguka kwenye nchi za tropiki

kufanya semina kwa juma moja hadi mawili. Tunafanya semina katika eneo moja kila

mwaka kwa miaka 3. Baada ya semina ya kwanza washiriki wanategemewa

kuendesha semina wao wenyewe katika maeneo yao, na kufanya kwa vitendo sehemu

kubwa ya yale waliyojifunza. Semina katika mwaka wa pili na wa tatu zina lengo la

kuruhusu wahusika kuleta taarifa juu ya mafanikio na kushindwa kwao, na kuongeza

zaidi ujuzi wao kwa dawa za asili.

Katika muundo wo wote wa semina yako, ni bora wakaribishwe washiriki wenye

kuwakilisha aina mbalimbali za watu wanaoshughulika na madawa au katika ngazi

mbalimbali za uongozi yaani waganga wa jadi, wauguzi, madaktari, wafamasia na

wengine kutoka makanisa na serikalini n.k. Haisaidii kuwa na watu wengi hapo hasa

ikiwa hawana msukumo wa kuyatumia waliyojifunza.

Ni sera nzuri kuwaita waganga wakuu wa mikoa ili kufungua semina. Hii ni njia

bora zaidi ya kupata msaada wa ushirikiano na wale walio katika nafasi za ushawishi.

Kama wewe ni kiongozi wa semina ujue kuwa jinsi wewe unavyotibu magonjwa

yako kwa madawa ya mimea ndivyo watu watakavyotumia madawa ya asili kwa

wingi.

Katika kupanga semina, kumbuka kwamba kujifunza na kufundisha kuzuri

kunahitaji kuwepo kwa mambo mbalimbali. Na katika madawa ya asili kuna nafasi

ya kutosha kufanya hivyo. Hapo chini kuna mifano ya mambo ya kufanya:

Kuimba nyimbo na kutunga nyimbo zako mwenyewe kuhusu madawa ya asili.

Page 33: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

33

Michango mbalimbali kutoka kwa walimu na wanasemina juu ya magonjwa na

madawa ya asili yanayojulikana

Kazi za vikundi juu ya Maswala ya kimaendeleo.

Kuzunguka kutafuta mimea na kuitambua kwa jina na kuikusanya.

Kutayarisha na kupanda bustani ya madawa.

Kutayarisha dawa.

Kutengeneza fremu ya “A”, jiko la jua, au mizani.

Kuonyesha picha za slide.

Mchango wa washiriki. Tunapata wapi rejea za madawa ya asili katika Biblia, na

wapi tena katika misemo ya kiafrika.

Huu hapa mfano wa ratiba ya mikutano ya siku tatu:

MKUTANO WA KWANZA

Siku ya kwanza

Saa 2 asubuhi: Maombi; Mithali 17:22 (Mtumishi wa Mungu wa eneo hilo).

Saa 3 asubuhi: Majadiliano: Ni magonjwa gani ya kawaida katika eneo letu.

Mfano minyoo, malaria, maumivu ya viungo? (washiriki wote).

Saa 4 asubuhi: Jinsi ya kuzuia magonjwa – njia za jadi na zile za kisasa

(Muuguzi).

Saa 5 asubuhi: Madawa ya asili ni nini? Sehemu I (angalia sura 1:1 na 1:2)

(mganga au muuguzi).

Saa 8 mchana: Papai – mmea muhimu wa dawa (sura 5:5) (mganga au muuguzi).

Saa 9 mchana: Majadiliano : Tunatumiaje mpapai katika eneo letu? (Mganga wa

jadi).

Saa 10: Utengenezaji wa dawa moja ya kuzuia minyoo na nyingine ya kuua

minyoo na “sabuni ya majani” (kutokana na maelezo ya sura 5:5).

Saa 1 Jioni: Mhadhara juu ya mpango wa uzazi kwa picha za slide.

SIKU YA PILI

Saa 2 asubuhi: Maombi: I Nyakati 16:33, Zaburi 96:12 na Isaya 10: 18 – 19.

Saa 3 asubuhi: Rudia papai; nendeni kuzunguka kwa pamoja na kuhesabu miti ya

mipapai kijijini.

Saa 4 asubuhi: Angalieni mimea ya Artemisia annua.

Saa 5 asubuhi: Mimea inayotumika kutibu malaria (angalia sura 8).

Saa 8 mchana: Utengenezaji wa dawa za mafuta (sura 4:3) (washiriki wote).

Saa 10 mchana: Majadiliano: Tutumie miti aina gani kwa kustawisha misitu?

Saa 1 jioni: Picha za slides za mimea ya madawa - bila maelezo kutoka kwa

walimu, washiriki watoe maoni yao juu ya kila picha.

SIKU YA TATU

Saa 2 asubuhi: Maombi: Matendo 3:16

Saa 3 asubuhi: Wimbo juu ya afya (uliotunga mwenyewe)

Saa 3:30: Nini maana ya madawa ya asili? Sehemu II (angalia sura I).

Saa 4:30

asubuhi

Majadiliano (wanaume): Tufanye nini ili kuzuia watu kukimbia

mjini kwa kukosa kazi vijijii? Majadiliano (wanawake):

Page 34: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

34

Tutawezaje kuwalisha watoto chakula bora zaidi kwa kutumia kile

tulichonacho? Tumepata taarifa gani katika somo hili?

Saa 5 asubuhi: Uchaguzi wa watu watakaohusika kuandaa semina nyingine.

Saa 5:30: Maombi ya kuagana.

MKUTANO WA PILI

SIKU YA KWANZA

Saa 2 asubuhi: Wimbo uhusuo afya.

Saa 3 asubuhi: Maombi ; Kutoka 15:26 Ayubu 13:4.

Saa 4 asubuhi: Rudia: Madawa ya tiba na kinga. (washiriki wote wachangie

uzoefu wao).

Saa 5 asubuhi: Ameba - Tumia darubini kuzifanya zionekane na kuzitambua

(Muuguzi).

Saa 8 mchana: Mziwaziwa (sura 5:11) - mmea ulio mzuri kupambana na ameba.

Kutengeneza chai (dawa) kutokana na mmea huu.

Saa 9:30

mchana:

Kutengeneza sabuni (sura 4) (kwa vitendo)

Saa 1 jioni: Kuonyesha picha za slide zihusuzo UKIMWI.

SIKU YA PILI

Saa 2 asubuhi: Maombi – Uaminifu , mila na desturi, na UKIMWI (Zaburi

40:11, Kor 13, Rumi 13:10).

Saa 2:30

asubuhi:

Wimbo uhusiano Ukimwi (uliotungwa na washiriki).

Saa 3:00: Marudio - amoeba, mziwaziwa

Saa 4:00: Malaria - Kinga, huduma /tiba za kisasa (Muuguzi), tiba za jadi

(mganga wa jadi). Kubadilishana uzoefu.

Saa 9:30: Jinsi ya kufanya kama mtu ana homa (sura 7:3). Majadiliano

kati ya wauguzi na waganga wa jadi.

Saa 8 mchana: Tembelea bustani ya mimea ya dawa ya kijiji au anzisha bustani

ya mimea ya dawa.

Saa 9 mchana: Wanawake: Jukumu la mkunga wa jadi Wanaume:

Jinsi ya kupanda na kutumia mkaratusi (sura 4:1)

Saa 10 jioni: Kutengeneza sabuni za urembo na sabuni ngumu (sura 4:1).

Saa 1 jioni: Magonjwa ya ngono - kuzuia kwa njia za kisasa na za jadi.:

Majadiliano katika makundi -Wanaume peke yao na wanawake

peke yao, na baadaye kwa pamoja.

Saa 3 usiku: Kuonyesha picha za slide zilizochukuliwa katika semina ya

kwanza.

SIKU YA TATU

Saa 2:00

asubuhi:

Maombi – jinsi ya kutunza mazingira yetu ya asili (Mwanzo

2:15, Kumb. 20:19, Zaburi 96:12)

Saa 3:00

asubuhi:

Kuharisha – jinsi ya kutengeneza aina mbalimbali za maji

chumvi (angalia sura 4:6).

Page 35: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

35

MKUTANO WA TATU

Mkutano wa tatu upangwe na washiriki wa kila kundi wao wenyewe. Hata hivyo

wanaweza kukualika wewe na watu wengine ili waweze kupata msaada zaidi au

mchango. Waumini wa kanisa kwa mfano wanaweza kukutanika ili kujadili somo

hili: “Kanisa na dawa za asili” na wakunga wa jadi, waganga wa jadi, au wauguzi na

madaktari wanaweza kukutana kujadili maswala muhimu ambayo ni mahsusi katika

kundi lao.

Semina pia zinaweza kutolewa kwa makundi maalum, mfano watumishi wa afya

“wa kisasa” kutoka maeneo makubwa, au watumishi wa idara ya madawa katika

mahospitali ya kanisa.

2.3 BUSTANI ZA MADAWA

Tunatengeneza bustani mbili tofauti kwa kazi tofauti tofauti. Moja kwa ajili ya

maonyesho nyingine kwa ajili ya uzalishaji.

1. Bustani ya maonyesho

Bustani hii ni ndogo na inafanya kazi ya kuwasaidia watu kujifunza juu ya mimea

mbalimbali. Bustani hii ni kwa watu wote! Katika hospitali kwa mfano, iwekwe

karibu na lango kufuata uzio wa hospitali ili kwamba kila apitaye aweze kuiona.

Panda jamii moja hadi mbili za kila mmea ambao unajulikana kutumika katika

madawa ya jadi. Weka alama ndogo kwa kila mmea kwa kutumia kwa mfano

vipande vya plastiki visivyotumia au mabati. Katika hizo alama andika majina mawili

ya mimea, la kibotania na la kienyeji, na matumizi yake – tumia wino usioharibiwa

na maji. Panga ratiba ya watazamaji, kila upatapo nafasi. Waonyeshe wageni wako,

karibisha wanafunzi wa shule zilizo karibu na uwaelezee juu ya bustani, na

wakaribishwe watu siku za jumapili baada ya ibada ya asubuhi.

2. Bustani ya uzalishaji Hii bustani ya pili ni kwa ajili ya uzalishaji. Hapa utastawisha ile mimea pekee

unayohitaji kwa ajili ya mpango wako wa madawa ya asili. Bustani kama hiyo hata

hivyo itakuwa ya matunda na mboga. Bustani hii inaweza kuwekewa uzio. Na watu

wanaweza kuingia tu kwa makaribisho.

Anza kwa mimea ya ua wa kuzuia mmonyoko au mimea ya ua yenye kurutubisha

ardhi. Panda hii mimea ya ua katika mistari kwa umbali wa meta tatu kwenye

mteremko na meta tano kwenye tambarare, lakini wakati wote kwa kufuata mistari ya

kontua. Tengeneza ua angalau kwa jamii tatu tofauti za mimea; unaweza

kuchanganya mchaichai, mlongelonge, lesena, calliandara, Cassia spectabilis,

Tephrosia vogelii (kibaazi), mbaazi, n.k. Siha mbegu za miti kwa umbali wa

sentimeta 10 tu (mfano calliandra na lesena) au panda matawi (mfano ya Cassia

spectabilis) kwa ukaribu zaidi, tuseme sentimita 50 hivi.

Mara tu hizi nyua zinapostawi, panda mimea yako ya madawa katikati yake.

Epuka vitalu vya mimea pekee, ni vizuri kupanda katika mchanganyiko, au hata

kuichanganya kama ambavyo inaota porini. Kwa jinsi hii mimea inajitengenezea

kivuli, na hapa inawezekana kupata mavuno wakati wa ukame pia.

Page 36: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

36

Chunguza kwa kujaribu na kukosea, kupata hali zinazofaa kwa kila mmea; jua la

moja kwa moja la savanna; nusu ya kivuli kama kwenye vichaka, kivuli kabisa kama

porini udongo kichanga ama tifutifu, maji mengi au kidogo.

Kata hiyo mimea ya ua kwa urefu wa mita 1 wakati wa mwanzo wa kipindi cha

mvua, na changanya katika udongo hayo majani uliyokata ili udongo uwe na rutuba

kila mwaka na kulisha mimea ya dawa.

KUTUNZA MBEGU: Baadhi ya mbegu (mfano: embe, chungwa, limao, papai)

zinahitaji kupandwa mara moja. Nyingine kama za mbogamboga, maua na nafaka

zinahitaji kukaushwa kwa majuma mawili hadi matatu.

Weka kila aina kwenye bahasha ya pekee. Andika jina la mmea na siku ya kuvuna

juu ya bahasha. Tunza bahasha hizi kwenye chombo kilichofungwa kabisa ili kuzuia

wadudu na wanyama wasizishambulie. Ili kuzitunza zikiwa kavu kabisa weka mkaa

mpya uliotayarishwa kwa kupikia, baada tu ya kupoa, katika chombo hicho. Au jaza

10% ya chombo kwa mchele uliokaushwa sana, au 0.5% kwa “silica gel”

(inapatikana kwa wakemia). Silica gel huwa ina chumvi ya cobalt iliyoongezwa,

husababisha iwe ya bluu iwapo kavu, lakini huwa pink ikiwa na unyevu. Silica gel na

mchele vinaweza kukaushwa tena na tena kwa jiko la jua au kwa taratibu kwenye

moto kidogo. Ikiwezekana, tunza hicho chombo ulichotunzia mbegu kavu katika

jokovu. Tunza mbegu zenye sumu mahali wasikofika watoto!

KITALU CHA MITI: Kwa miti mingi mbegu zake huhitaji kupandwa katika

udongo mzuri au mboji katika chombo kidogo (mfano: mifuko ya plastiki, au majani

ya migomba yaliyokunjwa kama kikombe kidogo. Hiki kitalu cha miti kinaweza

kulindwa dhidi ya jua kali, mvua na wadudu. Mimea michanga ikipata nguvu ipande

nje. Kumbuka umbali wa mmea hadi mmea kwa mimea iliyokomaa.

Mimea mingine inaweza kuzalishwa kwa wingi kwa kutumia matawi yake.

Mfano, Cassia spectabilis, (angalia sura 6:12) pia miti yote ambayo imepandwa na

kuchipua kwenye ua wa jirani yako!

KUTAYARISHA MASHIMO YA KUPANDA MITI:

Udongo wenye rutuba sana (wa porini): geuza udongo kwa koleo kisha panda

miche au matawi.

Karibu na nyumbani: Usichimbe shimo refu sana kwa choo chako. Kisha lifunike,

na baada ya miezi mitatu au zaidi, chini yake chimba shimo karibu meta tano. Juu ya

hiyo choo ya zamani, jaza takataka za mimea, kama magamba ya ndizi, majani na

matawi, na udongo kiasi: panda mti wa tunda juu yake mara moja.

Katika Savana yenye rutuba ndogo:

a) Kwa upandaji wa miti: Panda meta moja toka mti hadi mti, chimba kina cha

koleo 1 – 2 chini. Chagua mti ambao hauna umuhimu sana kwa watu, kama

vile Cassia spectabilis (sura 6:12) au Mwarobaini (Azadirachta indica, sura

5:3). Kwa mwingajini, chomeka kijiti cha nusu meta chini kisha kimwagilie

vizuri. Kwa kutumia njia hii, mti mmoja wa mwingajini unaweza kuwa baba

wa msitu wote! Mwarobaini unastawi zaidi kwa kupanda mbegu. Kata nyasi

mara kwa mara kuzunguka miti hiyo, hadi meta tatu kutoka kwenye shina.

Page 37: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

37

Wakati wa mwanzo wa kipindi cha ukame, choma moto kuzunguka miti hiyo

kuepusha miti michanga kuteketewa na moto wa porini.

b) Kwa miti ya matunda au madawa: Chimba shimo kama 70×70×70 sm. Jaza

kwa mboji matawi, majani machanga, takataka za mimea za jikoni, majivu n.k.

Funika kwa udongo asilia. Kwa uzoefu wetu miche na matawi ya kupanda

vinaweza kupandwa moja kwa moja juu yake. Mwagilia maji na zuia jua kali

na wanyama wazagaao.

2.4 KUKUSANYA MIMEA YA DAWA

SEHEMU: Pata mimea hiyo toka sehemu iliyo safi, kamwe siyo pembeni mwa

barabara.

WAKATI: Maua na majani yanaweza kuvunwa mara mmea unapoanza kuchanua, ni

wakati ambao mmea una kiasi kikubwa cha dawa. Kama itawezekana, kwa

kuchemsha au kuloweka sehemu ya mmea, tumia majani mabichi au maua mabichi.

Kama hii haiwezekani unatakiwa kuyakausha na kuyatunza. Baadhi ya utayarishaji

wa madawa unahitaji majani mabichi au maua. Mfano, dawa za mafuta na za kupaka.

Mizizi na mboga zinazostawi udongoni (mfano karoti) ni nzuri kuvunwa mwisho wa

kipindi cha mvua. Matunda yana vitamini nyingi zaidi yanapoiva. Kwa sababu za

kitabibu, baadhi ya matunda yanatumika kabla ya kuiva. Mfano: papai kwa vidonda

vyenye kutoa usaha. (angalia sura 5:5).

MATAYARISHO: Mizizi inatakiwa kuoshwa na kusuguliwa vizuri. Ni mara chache

majani yanahitaji kuoshwa, (isipokuwa mijini tu). Tupa majani yote yaliyokufa,

yaliyoshambuliwa na wadudu, mba au ugonjwa wowote.

KULINDA MIMEA: Unapohitaji mmea mzima, chukua uliozeeka, uiache iliyo

michanga. Ukihitaji mizizi, chukua mizizi ya ziada, na uache mingine na mzizi mkuu

bila kuujeruhi! Kama huhitaji mizizi ya mimea, iache mizizi chini ili ichipue mmea

tena. Ukihitaji gamba, chukua sehemu kutoka katika matawi! Usikate gamba kutoka

katika shina. Hii ndiyo tabia mbaya katika madawa ya jadi, na mti utakufa kama

utafanya hivyo. Ukihitaji majani chukua machache tu kutoka tawi lolote. Chukua

majani kutoka matawi yanayoelekea katikati ya mti, kwa sababu ni mara chache

yanatoa matunda. Stawisha na uendelee kulima mimea mingine – wewe na watoto

wako mtayahitaji.

2.5 KUKAUSHA NA KUTUNZA MIMEA YA DAWA

Mara nyingi mimea mibichi ni bora kwa tiba kuliko iliyokaushwa. Kwa hiyo

hakikisha wakati wote una mimea yenye nguvu na afya katika bustani yako ya dawa!

Mara nyingine ni muhimu kukausha mimea yako. Mfano, ukitaka kutengeneza

mafuta, dawa ya kujipaka au sigara ya dawa kutokana na mimea ya dawa.

Wakati mwingine unatakiwa kutunza mimea ya dawa. Mziwaziwa kwa mfano,

haupatikani wakati wa ukame. Kwa hiyo uvunwe na kuhifadhiwa wakati wa kipindi

cha mvua.

Page 38: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

38

Kwa kulinda salama na kutumia mimea ya dawa na

miti ya dawa anzisha bustani ya dawa.

Page 39: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

39

KUKAUSHA: Kwa vile kitabu hiki kinatumika katika mazingira mbalimbali palipo

na joto na ubaridi, palipo na unyevu na ukame, ni vigumu kutoa maelekezo

yanayoweza kufaa mahali pote. Hata hivyo, kama “sheria ya msingi”, hakikisha

umekausha mmea wako katika namna ambayo utakuwa umekauka kabisa baada ya

siku tatu.

1. Tayarisha mimea yako: Mizizi lazima ioshwe vizuri. Osha mbegu na majani kama

tu machafu, mfano mijini. Maua hayawezi kuoshwa.

2. Kama tu majani yatahitajika, toa vikonyo vyote, kama ni muhimu, pia nyuzi za

majani (mfano: majani ya mpapai). Kata kata majani kama unavyokata mboga kwa

kawaida. Vipande visiwe vikubwa zaidi ya sm 1.

3. Wakati wote kausha maua kivulini. Kausha matunda na mizizi kwenye mwanga

wa jua. Kausha majani kwenye jiko la solar, kama lipo au masaa machache

kwenye jua kali. Majani yakiwa yamepoteza unyevu karibu wote, endelea

kuyakausha kivulini. Sehemu nzuri ya kukaushia ni dalini, chini ya paa ili mradi

sehemu hiyo ni safi.

Wakati wa majira ya mvua, majani yanaweza kuwa bado yana unyevu hata baada

ya siku hizo tatu za ukaushaji. Katika hali hii yaweke katika jiko la jua, lakini acha

mfuniko wazi ili joto lisizidi 50˚.

KUTUNZA: Kama unataka kutunza mimea yako ya dawa, huna budi kusimamia

ukavu wake. Jambo hili linaweza kufanywa kwa kutumia kipima unyevu

(hygrometer). Chenyewe pamoja na kiganja kizima cha mimea mikavu ya dawa

viwekwe katika chombo kisichopitisha hewa kwa dakika 15. Jedwali lifuatalo

linaonyesha muda ambao mimea yako itakaa katika chombo hicho wakati wa joto.

Unyevu hewani

unaopimwa kwa

hygrometer

Unyevu wa mmea Mmea utadumu kwa

60% 6% Miezi 4

50% 5% Miezi 6

40% 4% Mwaka 1

Kwa kutumia mbinu hii unaweza pia kujua ni kwa muda gani vyakula vyako

vikavu, kama unga wa muhogo, mahindi na maharage vinaweza kutunzwa na kwa

muda gani mbegu zako zinaweza kutunzwa kabla hazijapoteza uwezo wa kuota.

KUHIFADHI: Huwezi kuhifadhi mimea katika mifuko ya karatasi kwa sababu

wadudu wanaweza kuishambulia na inaweza kupata unyevu. Kama imekaushwa

sana, na imefungwa vyema katika chombo cha glass, plastic au metali inaweza

kutunzwa kwa muda mrefu.

2.6 UTUNZAJI WA MADAWA

Vijidudu vinasubiri kila mahali kushambulia na kuharibu madawa yako.

Vinapatikana katika mikono, vyombo, chupa, katika hewa, katika maji (kama

Page 40: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

40

hayakuchemshwa vya kutosha) … kwa ufupi, kila mahali! Tunawezaje sasa kutunza

dawa zetu zenye thamani ya uhakika tuliyojitengenezea majumbani?

Ili kutunza uhalisi na umaridadi wa dawa vifaa vilivyo safi wakati wa kutengeneza

dawa; vifanye kuwa safi kwa kuvichemsha.

Bidhaa inaweza kudumu kwa ubora kama:

Itakuwa kavu sana (mfano: unga (poda)).

Itakuwa na sukari nyingi (mfano: syrup)

Itakuwa na chumvi nyingi (mfano: samaki aliyepakwa chumvi).

Itakuwa na kileo kingi (mfano: tincture)

Haichachi (mfano: mafuta)

Amua mwenyewe unavyotaka kuhifadhi dawa yako. Kwa mafuta tunashauri

mawese ya kujitengenezea, mafuta ya shea (mandingo) au mafuta ya biashara

(madukani). Baadhi ya mafuta yanayotengenezwa nyumbani hayadumu muda mrefu

(kama mafuta ya karanga).

Umande ni tishio kwa aina za unga na mimea iliyokaushwa. Viwanda vinatumia

kemikali kuhifadhi bidhaa, lakini kemikali hizi zinaweza kutuathiri, kwa hiyo

tunapendelea vifaa raslimali tuliyo nayo katika kukausha dawa zetu; kwa nini

usitumie jua!

2.7 JUA: MSAADA KWA MADAWA YAKO

Jua ni la muhimu kwa uhai wote kutoa mwanga na nishati. Tuonyeshe njia mbadala

na njia ile potovu ya kuchoma miti na mafuta . Tutumie nguvu ya jua kama teknolojia

inayotufaa. Na kwa kufanya hiyo tutachangia kulinda mali asili iliyo muhimu sana

kwetu kwa siku zijazo! Tunaweza kunufaika na hii dhana ya ajabu, ya bure, kwa

kutengeneza JIKO LA JUA (angalia picha).

Kwa kupikia na kuokea.

Kwa kukaushia chakula ili kukitunza, mfano, mahindi, karanga, udaga, na

katika mikoa mingine panzi kama senene n.k.

Kwa kuyeyusha masega ili kutenganisha na asali.

Kukausha nguo.

Kuondoa chawa kwenye nguo.

Kuwaua wadudu waliovamia chakula.

Kutengeneza dawa ya kujipaka, wakati wa kuyeyusha vitu (kwa kuweka

chombo ndani ya maji ya moto kwenye jiko la jua).

Katika hospitali, kuua na kuzuia kuzaliana kwa wadudu kwenye vifaa

mbalimbali (sterilization).

Ni rahisi kutengeneza jiko la jua kuliko ambavyo ungedhani. Sehemu yake kuu ni

kasha/sanduku. Linaweza kutengenezwa kwa kutumia vitu mbalimbali: Mbao, bati,

plastiki, udongo wa mfinyanzi au kapu. Ndani ya kasha kunawekwa vitu mbalimbali

vya kutunza joto, kama nyasi, karatasi, pamba, maranda au matambara ya nguo.

Sehemu ya ndani ya kasha inatengenezwa kwa bati lililonyoshwa kuondoa matuta na

Page 41: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

41

KAUSHIO LA JUA

a = kioo

b= aluminium foil

c= ubao

d= kopo cheusi

A) Kaushio la Jua: hewa inagia

chini, kupata joto na kukausha

majani au matunda kama

maembe yaliyowekwa kwenye

nyavu.

B) Jiko la jua (solar oven):

Sanduku linalofungwa na vioo.

Mfuniko (ulio na aluminium

foil) unawekwa kufuatana na

jua.

C) Kaushio la jua, Ilitengenezwa na Chuo Kikuu Hohenheim,

Ujerumani. Urefu wake ni mita 18, upana wake ni mita 2, eneo la

kukaushia ni 20 m². Inafaa sana kwa kukausha majani na matunda ki-

biashara.

Page 42: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

42

kisha kupakwa rangi nyeusi. Kasha linafunikwa kwa kioo, ni bora vikibebana viwili.

Mwanga wa jua unafyonzwa na uso mweusi ulio ndani ya jiko hilo na vyombo vyeusi

vya kupikia. Miale ya mwanga wa jua inabadilishwa na kuwa joto. Joto linaweza

kufikia 100˚ - 180˚C, kutegemea na ukali wa jua na jinsi jiko lilivyozibwa na kujazwa

vizuia joto kutoka. Kiakisio cha mwanga (maana yake ni kifuniko cha kasha

kilichofunikwa kwa karatasi ya aluminium) kinasaidia kuakisi mwanga wa ziada

katika kasha. Unaweza kutengeneza kasha (jiko) lenye ukubwa wowote kufuatana na

mahitaji yako binafsi. Kama vioo havipatikani unaweza kutumia karatasi za plastiki.

Kwa maelezo zaidi ya utengenezaji angalia katika kitabu cha anamed “Use Water

Hyacinth!” rejea ukurasa 160.

Kama huna chombo cha kukaushia, tumia mfuko wa plastiki usio na rangi, na

kasha linalotosha ndani yake. Weka mimea yako ya dawa ndani ya kasha, na kisha

ndani ya mfuko wa plastiki, weka kwa pamoja kwenye jua. Kwa jinsi hii joto ndani

ya mfuko litafika haraka 80˚C, juu zaidi ya joto linalohitajika kukausha madawa ya

mmea, ambayo yanatakiwa kukaushwa kwa joto lisilozidi 50˚ C. Kwa jinsi hiyo

hakikisha kasha umeliweka wazi kwa kiasi fulani.

KAUSHIO LA JUA: Rejea picha (SOLAR DRIER) Hii ndiyo njia bora na ya haraka ya kukausha mimea ya madawa bila kuharibu viini

maalum vya mimea ambavyo vingeharibiwa na miale ya ultraviolet au joto kali zaidi.

Hewa hupita katika nafasi kati ya ubao unaoteremka uliopakwa rangi nyeusi na kioo

kinachoufunika. Hewa inachemshwa, inakwenda juu na kupitia katika bomba. Mimea

ya dawa inayotakiwa kukaushwa inawekwa kwenye nyavu zilizofungiwa kwenye

hilo bomba.

JINSI YA KUTENGENEZA RANGI NYEUSI YA KUPAKA CHOMBO CHA

JUA

Kama unataka kuhakikisha kuwa rangi nyeusi haina madini yoyote yenye sumu,

unaweza kujitengenezea rangi mwenyewe. Nunua black ferric oxide (inapatikana

kwenye duka la mkemia na gram 5 zinatosha kwa kutengenezea jiko moja.

Ichanganye na varnish ya mbao au chuma isiyo na rangi. Unaweza kujitengenezea

varnish mwenyewe kwa kutumia mafuta ya kawaida au utomvu mzito. (Rejea sura

6:10, elemi). Au, kufanya kipande cha metali kiwe cheusi, weka mbegu za mafuta

(karanga, au mbegu za mbono) katika sufuria. Funika sufuria kwa kifuniko cha metali

kisha chemsha hadi mbegu ziwe mkaa, ni wakati ambapo kifuniko kitakuwa cheusi

pia.

2.8 KIASI NA DOZI

a) Kiasi katika kutengeneza dawa Professa Kabangu anasema, “Dozi ni jambo ambalo hujadiliwa sana na watu ambao

wanadharua madawa ya jadi. Kwa uzoefu wetu siyo tu watu wenye tabia ya kuonea

mashaka bali “watu wa kawaida.” Pia wana mashaka ya kunyweshwa sumu kwa

kunywa kozi zisizo za uhakika zinazotolewa na mganga wa jadi.

Wakati wa kutayarisha madawa, inawezekana hata vijijini kuwa na vipimo halisi.

Page 43: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

43

Vijiji vichache vina mizani, lakini kwa dawa nyingi za maji ujazo unaweza

kupimwa kwa uhakika zaidi.

Chupa 1 (bia) ml 700 au 0.7 lita

Kikombe 1 ml 500

Matone 20 ya maji ml 1 au gram 1

Kusema kijiko cha mezani (ml 10- 20) au kijiko cha chai (ml 3 – 10) siyo kipimo

halisi, kwa sababu tu ukubwa wa vijiko unatofautiana kwa hiyo kwa kutengeneza

dawa ni bora zaidi kutumia “kipimo fulani”. Mfano: vijiko 3 vilivyojaa (kama

kipimo) cha kitu fulani (A) kujumlisha vijiko vitatu (kijiko kiwe kipimo) ya (B)

vitafanya uwiano wa moja kwa moja kama kijiko kile kile kimetumika wa A na B.

b) Dozi katika kuelezea madawa.

Majani: Kama tukipendekeza kiganja kilichojaa majani kwa siku kwa mtu mzima,

mtoto tutampa kiasi gani? JIBU: Kwa kiganja kilichojaa tunajua kiasi ambacho

mgonjwa anaweza kukunja katika kiganja chake. Kwa jinsi hiyo kwa mtoto tumia

kiasi ambacho mtoto anaweza kukunjia katika kiganja chake.

Vimiminika: Kama tukipendekeza lita moja kwa siku kwa dawa fulani

tutapendekeza kiasi gani kwa mtoto? Jibu: Fuata mwongozo huu:

DOZI KWA WATOTO, KAMA DOSE YA WAKUBWA NI ML 1,000

UMRI WA MTOTO DOZI

Miezi 6 Ml 100

Mwaka 1 Ml 150

Miaka 2 - 3 Ml 200

Miaka 4 - 5 Ml 250

Miaka 6 – 10 Ml 350

Miaka 11 - 14 Ml 600

Miaka 15 - 16 Ml 800

Miaka 17 na zaidi Ml 1000

Hata hivyo uwe mwangalifu, siyo kila dawa iliyo nzuri kwa watu wazima ni nzuri pia

kwa watoto!

2.9 KUTENGENEZA MIZANI RAHISI LAKINI YA UHAKIKA

Kozi halisi zinaweza tu kutayarishwa na kutumika kwa msaada wa mizani. Siyo tu

waganga wa jadi bali hata zahanati nyingi hawana njia halisi za kupima kati ya gram

1 na 50.

Tuchukulie kwamba katika semina kila mmoja kati ya washiriki 30

anajitengenezea mzani wake.

Vifaa vya kutumia: Unahitaji vitu vyenye uzito halisi kati ya gram 1 na gram 20,

kisu, bisibisi ndogo, kalamu za kuwekea alama zisizofutika (marker pen), gundi

imara, tupa ya chuma na kifaa cha kuanzishia tundu kwa ajili ya parafujo (inaweza

kuwa nyundo na msumari).

Page 44: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

44

Zana zinazohitajika kwa mzani (kumbuka vipimo

vyote ni vya makadirio).

a. Kipande 1 cha ubao, chenye sm 3 za mraba na

urefu sm 30, kama inavyoonyeshwa.

b. Parafujo 1, urefu sm 5.

c. Kipande 1 cha ubao, 40×14×3 sm, kama

inavyoonyeshwa.

d. Egemeo 1, upana sm 3, na mikono karibu urefu

sm 10 na 7.5.

e. Parafujo 3, mm 3.5 × 16.

f. Mche wa kuungia metali, au mche wowote wa

metali, sm 33 urefu na kipenyo mm 3.

g. Ubao wa miraba 6 iliyo sawa, sm 2 za mraba, na tundu la mm 3 kupitia katikati

yake (ili kupitisha ule mche wa metali F)

h. Parafujo duara 1, urefu sm 2.

i. Mche wa metali 1, sm 25 urefu na mm 1.6 kipenyo.

j. Parafujo za umeme 2 (kasha ya chocolate) za kuunganishia, kipenyo cha ndan mm

3.

k. Vikombe 3 vya plastic visivyo na vishikio vyenye ujazo wa ml 500, vyenye

vitako vya mviringo ikiwezekana.

l. Kamba ya nailoni mita 2.5, kipenyo mm 1

m. Vikopo 5 vya mikanda ya picha iliyo tupu, hasa yenye rangi nyeupe.

n. Mshumaa wa nyumbani 1.

o. Mfuko wa plastiki uwezao kuzibwa, ukubwa wa 45.

Kutengeneza 1. Chukua vipande A kwa C kama inavyoonyeshwa na parafujo B.

2. Chukua mkono mrefu zaidi wa egemeo D kwenye mhimili A.

3. Tafuta sehemu ya kati hasa ya mche F kwa kukunja kipande cha kamba chenye

urefu wa mche – vipande viwili. Weka alama katikati kwa kutumia kalamu ya

wino usiofutika (markerpen) na kisha weka alama kwa sentimeta moja kila

upande.

4. Kandamiza kibao cha

miraba 6, G kwenye

ule mche, kiunganishe

kwa gundi kwenye ule

mche katikati ya zile

alama mbili

zilizotengenezwa kwa

sm 1 kila upande.

5. Laza mche kwenye

meza, ingiza parafujo

ya duara H ndani ya

kibao cha miraba sita, katikati kabisa na kwa pembe mraba na ule mche wa

metali.

Page 45: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

45

6. Tengeneza tundu dogo lenye ukubwa sawa wa kuchukua mche I likiwa kinyume

na parafujo duara uunganishe kwa gundi huu mche katika hiyo nafasi yake kiasi

kwamba iwe pembe mraba na mche F.

7. Pitisha kamba fupi kwenye mduara wa parafujo duara, ifunge kwenye tundu la

mwisho la egemeo.

8. Ingiza viunganishi J kila upande wa mche F kiasi kwamba uzito wa mche

ulingane kila upande.

9. Tayarisha vyombo viwili vya plastiki vya kupima K. Kama unatumia vikombe

ondoa vishikio. Tengeneza matunda katika umbali sawa karibu na sehemu ya juu

kabisa ya vyombo hivi. Kata vipande viwili kutoka kamba L, kata urefu wa sm 60

hivi na ufunge kwenye kila tundu lililo kinyume na jingine. Ninginiza kila

chombo kwenye viunganishi J.

10. Mizani ni lazima kila upande ulingane na mwingine. Kama sivyo, rekebisha kwa

uangalifu nafasi za viunganishi.

11. Katikati kabisa ya kibao cha msingi C, weka wastani unaoonekana, ulionyooka,

kuanzia nyuma hadi mbele. Wakati vipimo vya uzito vikilingana (vyombo)

kionyesho I kitaonyesha kwenye mstari huu.

Kutengeneza mizani rahisi zaidi.

Chukua mbao kwa ajili ya mhimili wa ulalo, ambao utaning’inizwa kwenye chango

kwenye ukuta katikati yake kabisa. Vyombo vya kuwekea vipimo vitawekwa kila

upande wa mhimili. Mche wa kuonyeshea (kipande cha chuma kama vile I)

kinafungwa kwa nyuzi 90˚ katikati kabisa ya ule ubao kiasi kwamba kinaelekea chini.

Nyuma ya hii mizani rahisi, mstari wa wima unachorwa kwenye ukuta kiasi kwamba

upimaji unapokuwa sawa, mstari unafichuka kabisa.

Kutengeneza uzani Kama tuna uzani uliohakikishwa, basi tunaweza kutengeneza uzani mwingine

mwingi. Tunahitaji kutumia vifaa visivyonyonya maji, kiasi kwamba tutakuwa na

uzito ule ule wakati wa ukavu na majira ya unyevunyevu. Ni bora kutumia plastiki na

mishumaa ya kuwasha.

Ni vizuri kutengeneza uzani ufuatao 1×1g, 2×2g, 1×5g, 2×10g, 1×20g. Kwa

kutumia uzani ufuatao tunaweza kupima madawa, mfano majani, hadi kufikia gram

50. Kwa kutumia vikopo vya plastiki vya mikanda ya picha kata kwa vipimo vya

gramu 1, 2 na 5 kwa kufuata uzani halisi. Andika uzito kwenye hivyo vikopo kwa

kutumia rangi isiyofutika (markerpen). Tengeneza uzani kwa gramu 10 na gram 20

kwa kujaza vipande vya mishumaa hadi vifikie uzani halisi pamoja na kile kikopo.

Kisha tena andika kiasi cha uzito juu yake, na uvitunze vyote katika mfuko wa

plastiki O ili visichafuke.

Kutumia vipimio Kipimo ni lazima kitumike katika chumba kisichopitiwa na upepo. Kabla ya kupima

kila siku hakikisha vipimo vyako viko sawa, uvirekebishe kama inabidi. Hii inaweza

kufanyika kwa kuweka vipande vya karatasi kwenye upande wa chombo kilichoinuka

hadi vyote viwe usawa. Weka uzito kwenye chombo kilekile. Weka dawa kwenye

chombo kile kingine, hadi vipimo vilingane tena.

Page 46: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

46

VIFAA VYA KUJITENGENEZEA kwa ajili ya madawa ya asili.

Fukizo – maji

(water bath)

Jiko la jua

Mizani

Page 47: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

47

SURA 3

Mimea ya madawa mara nyingi ina ladha tofauti (chungu, tamu, ukakasi) kutokana

na viasili vilivyo katika mmea.

Ili kupata dawa viasili hivi vinasindikwa katika kimiminika kwa hiyo njia ya

msingi na iliyozoeleka ya kutengeneza dawa ni:

Mmea + KIMIMINIKA + JOTO = DAWA

Madawa yanayotengenezwa kwa njia hii ni ya aina tatu:

Kwa matumizi ya ndani tu (kunywewa)

Matumizi ya nje tu (kuwekwa kwenye ngozi)

Kwa matumizi ya ndani na nje (zinaweza kunywewa au kupakwa kwenye ngozi)

3.1. MADAWA KWA MATUMIZI YA NDANI

Kumbuka: Mapendekezo yote ya Utunzaji wa dawa yanahusu zaidi hali za maisha ya

kijiji katika maeneo ya Tropiki, kwa kuchukulia kuwa hakuna jokovu.

KUTENGENEZA KWA MAJI YA BARIDI

Ni njia inayotumika kutengeneza viasili vinavyoharibiwa na joto; mfano mbaazi

(Tephrosia): ili kupata dawa bora.

1) Majani: Yakatekate vipande vidogo.

2) Mizizi: Itwange kwa kinu.

3) Tumbukiza vitu hivi katika maji kwa usiku mzima.

Kisha chuja: Hii dawa rahisi inatakiwa kutengenezwa (upya) kila siku.

KUMWAGIA MAJI MOTO (INFUSION): Chemsha maji lita moja na umwagie

kwenye dawa kiasi cha kiganja kimoja. Baada ya dakika 15 – 20 chuja kwa kitambaa

kisafi. Itumie dawa hiyo kwa siku moja.

KUTOKOSA (DECOCTION): Ukitaka kupata dawa kutokea kwenye majani

manene, mizizi au magamba, wakati wote tumia njia hii. Chemsha kiganja kimoja

cha hiyo sehemu ya mmea katika lita moja ya maji kwa karibu dakika 20. Dakika

zihesabiwe kuanzia maji yanapoanza kuchemka. Ni vizuri kutumia chungu cha

udongo au kauli kuliko kikaango chochote cha metali. Tengeneza dawa ya

kuchemsha upya kila siku. Kuongeza sukari hakuongezi thamani ya dawa.

SODA (Maji ya limau): Soda (maji ya limau) ni kinywaji kinachoburudisha na

chenye tiba. Mfano: Kamua limau 2. Ongeza lita moja ya maji ya moto kwenye maji

ya limau na uiongezee sukari kuifanya tamu. Tumia kwa siku moja.

SYRUP (DAWA TAMU): Baadhi ya madawa ya mmea hayana ladha nzuri. Ili

kufanya dawa idumu kwa muda zaidi au iwe na ladha nzuri, unaweza kuifanya tamu.

Kwanza tayarisha dawa ya maji, chuja, kisha ongeza kikombe kimoja cha sukari kwa

kikombe kimoja cha dawa ya maji. Ili kuyeyusha mchanganyiko huu weka kwenye

moto na kisha koroga wakati wote. Dawa hiyo tamu (Syrup) imiminwe kwenye chupa

wakati bado inatokota. Kama una mizani chukua gramu 1.650 za sukari kwa gramu

MADAWA YA AINA MBALIMBALI

Page 48: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

48

1.000 za dawa ya maji. Utapata lita mbili za dawa tamu (syrup), iwezayo kutunzwa

kwa siku tatu.

Dawa iliyoanza kuvunda itupwe. Tafadhali kumbuka kuwa sukari haina dawa

ndani yake, isipokuwa kwa shida ya utapiamlo. Kwa kweli kinyume chake ndiyo

kweli: sukari ni hatari kwa meno yako. Sukari inaongezwa kwenye dawa ili tu

kutunza dawa na kuongezea ladha.

TINCTURE (Dawa yenye kileo): Kwa nyongeza kwenye dawa ya mimea, dawa ya

maji ina viwango tofauti vya maji na kileo. Kwa matumizi ya kunywa usitumie kile

kilichogeuzwa asili, lakini bora utumie vinywaji (konyagi na mvinyo) vyenye

asilimia kubwa ya kileo, angalau 20%.

Dawa ya maji (tincture) yenye kemikali: Kemikali zinayeyushwa katika

mchanganyiko wa kileo na maji (mfano: Iodine tincture).

Dawa ya maji (Tincture) ya mimea ya dawa: Kwa kawaida, gram 100 za sehemu

ya mmea inachanganywa na lita moja ya kileo na maji (zaidi hasa 45% au 70%

kileo). Usichemshe, bali mimina katika chupa na utunze kwa utulivu kwenye sehemu

ya uvuguvugu kwa juma moja. Tikisa kila mara, kisha chuja. Kiwango kikubwa cha

kileo ndicho kinaongeza muda wa dawa kudumu zaidi. Katika hali ya hewa ya

kitropiki kama chupa imefungwa kabisa tunapendekeza:

20% kileo: Mwaka 1

30% kileo: Miaka 3.

40% na zaidi Miaka 5.

Kuongeza sukari kunasababisha dawa idumu zaidi.

DAWA YENYE DIVAI: Ni nzuri pia kwa kufuata ukweli kuwa viasili vingi vya

madawa vinayeyuka vizuri katika kileo. Divai nzuri ina kileo (kama 12%), sukari na

vitu vinavyoweka rangi. Weka mimea iliyokaushwa (mfano: kola zilizosagwa) katika

divai ya asali au iliyotengenezwa kwa mzabibu, kisha funga chupa. Itunze kwa juma

moja. Itumie baada ya kuchuja. Kufuatana na kiwango cha kileo (kinachofanya kazi

la kulinda dawa) unaweza kuitumia kwa

mwezi 1 – 6.

ENEMA: Enema huingizwa katika matumbo kupitia mkunduni kwa njia ya mpira

mdogo. Kuna enema kwa ajili ya shida ya kufunga choo na strida ya kuharisha. Kama

mtoto hawezi kunywa maji chumvi (rejea sura 4:6) anaweza kupewa kupitia

mkunduni.

Kwa ujumla, haturuhusu matumizi ya enema za jadi, hasa kwa kuharisha kwa

watoto. Tumekuwa tukiona enema ikifanywa kwa mimea yenye sumu. Kwa jinsi

sumu inanyonywa kwa kupitia ngozi laini za utumbo katika Afrika watoto wengi

wanakufa baada ya kuhudumiwa kwa enema za namna hii.

3.2 . DAWA KWA MATUMIZI YA NJE

MWOGO MAALUM (LOCAL BATH): Huduma itolewayo kwenye sehemu moja

tu ya mwili, ambayo inashirikisha viasili vya dawa za mimea (zaidi sana

Page 49: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

49

iliyochemshwa), inaitwa mwogo maalum (local bath). Mfano: mwogo-miguu,

mwogo-paja, mwogo-jicho, mwogo-sikio).

KUBANA (KUHUDUMIA KIDONDA) – Compress: Kati ya madawa yote

yatumikayo nje, kubana ndiyo njia rahisi zaidi. Kwa jipu au uvimbe mmea unawekwa

moja kwa moja kwenye ngozi, na kufungwa kwa kitambaa, kamba au uzi. Kinyume

na ushauri mwingi unaotolewa kaitka vitabu kuhusu madawa ya jadi, tunashauri

kwamba usiweke jani moja kwa moja kutoka mtini au lisilochemshwa kwenye

kidonda au uvimbe wa kuungua. Juu ya majani hayo huwa mamilioni ya vijidudu

(staphylococci, pepopunda, virusi, fungus n.k.) vinavyoweza kudhuru kidonda. Kwa

hiyo wakati wote chemsha jani kabla ya kulitumia kwa nje. Badilisha jani mara tatu

kwa siku.

KUSUKUTUA: Dawa za kusukutua hutumika kusafisha na kutibu mdomo na makoo

(siyo za kumeza). Dawa hizi zikitengenezwa nyumbani zihifadhiwe kwa siku moja

tu.

DAWA YA KUPAKA: Dawa ya kupaka zimetengenezwa zikiwa laini kwa kupaka

kwenye ngozi. Zinatumika kama kufunika ngozi (kama vipodozi) kuhudumia ngozi,

mfano wakati wa matatizo ya fungus, au kusaidia dawa kupenya kwenye sehemu za

misuli kwa ndani. Mfano: Kutibu maumivu ya viungo. Ili kutayarisha dawa ya

kupaka, chemsha mimea ya dawa kwa mafuta ya kula katika fukizo-maji (water

bath), chuja, ongeza nta iliyo yeyushwa (mfano: nta ya nyuki au mshumaa) na uiache

ipoe. Kwa taarifa zaidi angalia sura 4.4 .

Dawa ya namna hii iliyo na maji inaitwa cream; kama ina unga inaitwa paste.

SABUNI: Sabuni ni matokeo ya urejeo wa kikemia kati ya nyongo (mfano: Sodium

hydroxide, NaOH) na mafuta , aidha mafuta ya mbogamboga au ya wanyama. Kama

sabuni ina NaOH kuliko mafuta, inasafisha vizuri lakini inachoma ngozi. Kama ina

mafuta mengi zaidi ya NaOH, sabuni itakuwa na uwezo mdogo wa kusafisha lakini

itakuwa nzuri kwa ngozi (rejea sura 4:1).

Kama, baada ya kuoga, unataka kulinda ngozi yako, tumia mafuta (rejea chini) ili

kulinda viasili vinavyolinda ngozi. Baada ya kuoga watu wengine hujipaka sabuni,

usifanye hivyo.

SABUNI ZENYE DAWA: Sabuni hizi zina dawa aina fulani kwa matumizi ya

hospitali. Yeyusha sabuni iliyosagwa pamoja na maji kidogo katika chombo, ongeza

dawa (mfano: sulphur, mafuta ya mwarobaini, au dawa ya kuua vidudu vya

maambukizo), na uuache mchanganyiko upoe.

Usitumie zile zinazoitwa “sabuni za kuzuia wadudu wasizaliane” (antiseptic soap)

ambazo zina madini ya zebaki, kwa kufanya ngozi kuwa nyeupe. Ni za hatari kwa

ngozi na kwa afya yako.

DAWA YA MAJI (TINCTURE): Divai itengenezwayo kijijini kwa kawaida ni bei

nafuu kuliko vileo vya kiwandani. Katika jadi, divai iliyotengenezwa kutokana na

ndizi, mchele au mahindi huchemshwa na mvuke wake hupoa kwa kupitia mrija

wenye urefu wa meta 10 wa mwanzi. Pima kiasi cha kileo chake kutumia kipima

kileo. Nunua kileo pale tu unapohitaji chenye zaidi ya 70%; kwa kileo chenye nguvu

ya chini ya 70% anaweza kutumia vile vinavyopatikana vijijini.

Page 50: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

50

Kwa sababu za usalama, tumia vile vifuatavyo tu:

1) Kama kuzuia vidudu vya maambukizi, kuzuia matumizi mabaya, ongeza tone

moja la shampoo au dawa ya maji ya kuoshea katika lita moja ya kileo. Hii

hutengeneza spirit iliyoharibiwa asili.

2) Kwa kutengeneza dawa ya maji ya mimea kwa matumizi ya nje tu (mfano:

Dawa ya maji ya Cassia alata) Rejea sura 5.

3.3. MADAWA KWA MATUMIZI YA NDANI NA NJE

UNGAUNGA: Ungaunga unaweza kutumika kwa ndani au kwa nje. Gamba, mzizi,

majani, mbegu, mara nyingine mmea mzima hukatwa na kuachwa kukauka,

ikiwezekana kivulini. Ni vizuri kama mmea ukiwa mkavu sana kabla hujautwanga

katika kinu. Funga kipande cha nguo ya nailoni juu ya chujio la kawaida kwa

vishikizo. Chekecha unga kupitia katika nailoni kwa kuusugua kwa kipande cha ubao

au plasitiki chenye kingo zilizonyoka.

Mfano: Unga wa mkaa kwa kuharisha.

DAWA ZA MAFUTA (Medicinal Oil): Tengeneza mafuta kwa kutumia karanga,

ufuta, kokoa, nazi, mchikichi, mwarobaini, shea na mengine kama hayo. Aina hizi za

mafuta ya mimea siyo tu kwamba vina lishe bali pia vina viasili vya dawa hata bila

matengenezo mengine.

a) Matumizi ya ndani: Ni nzuri kwa sababu ina kiwango kikubwa cha vitamini A,

D, na E (rejea sura 4:10). Pia inatumika kwa mafuta ya mbono katika hali ya

kufunga tumbo – kukosa choo.

b) Matumizi ya nje: kama vile matunzo ya ngozi, kuzuia maambukizi au kwa

bawasiri. Pia inatumika kwa vipodozi na kama mafuta ya kuchua.

Mafuta ya wanyama yanatumika mara chache sana vijijini kwa sababu ni adimu

na ghali (tunashauri kutotumia mafuta ya chatu ili kulinda jamii za chatu zisitoweke).

Katika utengenezaji dawa mara nyingi tunatumia mafuta ya mawese, ambayo

yanapatikana wakati wote katika vijiji vingi vya Afrika; kama sivyo, panda

michikichi! Badala ya mawese mekundu (yanayotengenezwa kutokana na matunda

yake) unaweza pia kutumia mafuta yasiyo na rangi yanayotokana na kokwa la

mchikichi.

Kama ukitaka kutumia mawese ya kujitengenzea, ni vizuri yatengenezwe siku ile

ile matunda yanapovunwa, ili kwamba matunda ya mchikichi yasitunzwe mpaka

yavunde (jambo ambalo kwa bahati mbaya hutokea mara nyingi).

Tunapotayarisha mafuta kwa ajili ya matumizi ya nje kutokana na kanuni ya

kutengenezea dawa, jaribu kutumia mafuta ambayo yanapatikana hapa kijijini, kwa

bei rahisi zaidi.

Ili kutengeneza dawa ya mafuta, changanya kipimo kimoja cha majani makavu au

maua, na vipimo kumi vya mafuta. Chemsha mchanganyiko huo kwa saa 1 katika

fukizo maji, ichuje na uiache ipoe.

Mafuta yaliyotengenezwa kwa njia hii yanatumika kutibu upele, maumivu ya

viungo na magonjwa ya ngozi. Kwa vipodozi, mafuta kama hayo ni bora zaidi ya

vipodozi vya madukani, kwa sababu rangi mbalimbali na kemikali za kuhifadhi.

Page 51: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

51

SURA YA 4

4.1 UTENGENEZAJI WA SABUNI KATIKA NGAZI YA KIJIJI

1. Kwa mujibu wa hadithi ya kirumi, sabuni ilivumbuliwa katika mlima Sapo. Katika

mlima huu watu walitoa kafara kwa miungu. Baada ya mvua kubwa kunyesha, maji

yalijichanganya na majivu pamoja na mafuta ya wanyama waliotolewa kafara na

kuunda kitu cha kushangaza kilichotiririka kutoka mlimani kuelekea bondeni. Watu

waliokuwa wakifua katika mto Tiber waligundua kwamba kitu hicho kipya

kilirahisisha kazi ya ufuaji. Mchanganyiko wa maji, majivu na mafuta umebadilika na

kuwa sabuni!

2. Usafi na elimu nzuri ya afya ni muhimu na nafuu kuliko (aina nyingi za) madawa.

Kwa hiyo mtu anahitaji sabuni. Lakini itakuwaje kama hata sabuni iliyotengenezwa

kwa gharama nafuu utainunua kwa bei kubwa?

UFUMBUZI A: Kukusanya fedha barani Ulaya, kununua sabuni na kuzituma

Afrika. Katika suala hili, bidhaa itakuwa imeagizwa kutoka ng’ambo, wakati ambapo

zaidi ya 90% ya vitu vinavyochanganywa katika utengenezaji wa sabuni vinapatikana

kwa wingi barani Afrika. Mawese na maji!

UFUMBUZI B: Kuendesha semina ili watu waweze kujitengenezea sabuni katika

Vijiji vyao, bila vifaa vyovyote maalum, kama vile mizani. Nimewahi kufungwa kwa

sababu, eti, kutengeneza sabuni kutasababusha serikali kupoteza mapato ya kodi.

3. Tumeandaa maelezo rahisi kwa ajili ya aina mbali mbali za sabuni. Sabuni hizi

hazina tofauti na sabuni za biashara, iwe kwa muonekano au ubora. Na badala yake,

zina muwasho kdiogo kwa sababu hazihitaji rangi na madawa.

Sabuni yetu ni zao la kikemikali lenye vitu vitatu: maji, mawese na sodium

hydroxide (NaOH), ambayo inapatikana katika mji wowote mkuu wa nchi za tropiki.

Inapatikana katika pakiti za kilo 1, inauzwa ikiwa katika vibonge vidogovidogo kwa

kusafishia (mfano choo). Unaweza ukaipata kwa bei nafuu katika mifuko ya kilo 50

kutoka kwenye viwanda vya kemikali. Unaweza ukapata anwani zao kwenye

kiwanda cha pombe kilicho karibu (viwanda vya pombe hutumia NaOH kwa

kusafisha chupa).

Ili kutengeneza sabuni unahitaji vyombo na vifaa vifuatavyo:

- Sufuria au chungu kimoja (cha mfinyanzi au udongo mwingine).

- Chombo kimoja cha plastiki (lita 5)

- Bakuli kubwa moja (plastiki au mfinyanzi)

- Ubao mdogo mmoja

- Kikombe 1 cha maji (plastiki, kauri au mfinyanzi)

- Kisu kimoja

- Mikopo tupu (tazama chini)

- Maji

OKOA FEDHA NA JITENGENEZEE MWENYEWE!A

Page 52: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

52

- Mafuta, pamoja na kwamba maelezo haya yanahusu “mawese” vilevile

unaweza ukatumia: mawese mekundu (red palm oil), mafuta ya kokwa la

mawese, mafuta meupe ya mawese, mawese meupe ya kiwandani (Tazama

sura 6:22) au mafuta ya shea.

Vyombo zaidi vinavyoweza kusaidia ni:

- Kitambaa cha nailon au karatasi la plastiki

- Kasha moja la mbao lililo mraba.

4. Vipimo vya kipima (mara zote vikae wima)

Kama vipimo vya kupimia chukua chombo cho chote cha plastic (kwa mfano

kikombe, kopo n.k.)

Vipimo vyote ni vya ujazo.

5. Tahadhari: Sodium hydroxide ni hatari. Katika semina za vijijini ni lazima

mjadili namna ya kuiweka mbali na mahali wanakofika watoto. Kama mtoto atameza

sodium hydroxide, lazima apewe maziwa mengi au kikombe 1 cha mchanganyiko wa

juisi ya limau/siki na vikombe 20 vya maji; kwa tukio lolote lile lazima apewe maji

mengi.

Sodium hydroxide hushambulia ngozi, kila mara nawa mikono vizuri! Kwa kuwa

hali ya unyevu katika hewa huibadili sodium hgydroxide kuwa kimiminika, ni lazima

ihifadhiwe kwenye vyombo visivyopitisha hewa.

Sodium hydroxide hushambulia aina zote za metali. Kwa hiyo ni bora zaidi

kutumia vyombo vya mfinyanzi vilivyotengenezwa kijijini (na hii itasaidia wakati

huohuo kutoa ajira kwa wenyeji!). Na kama vyombo vya mfinyanzi havipatikani

tumia aina nyingine za vyombo vya kufinyanga au plastiki.

6. Uzalishaji wa sabuni ya kugandisha

a) Chemsha vipimo 7 vya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya

kimiminika, na chujia kwenye chungu cha mfinyanzi au bakuli la plastiki.

b) Mimina vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki. Ongeza kipimo

1 cha sodium hydroxide kwa UANGALIFU MKUBWA. Mchanganyiko

utakuwa wa moto sana - usiweke mfuniko kwenye chombo. Subiri hadi sodium

hydroxide yote imeyeyuka.

c) AMA: Subiri mpaka mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta vikaribie

kupoa. Kisha, taratibu, ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye

mawese, huku ukikoroga harakaharaka bila kusita kwa kutumia ubao. Hii ni

njia nzuri zaidi.

d) AU: Chemsha mafuta kwenye joto la kadri ya 55˚C. Subiri hadi sodium

hydroxide nayo imefikia joto hilo. Kisha changanya vimiminika hivyo viwili,

huku ukikoroga kwa nguvu.

e) Wakati sodium hydroxide yote itakapokuwa imewekwa, koroga sana kadri

uwezavyo. Taratibu sabuni itageuka kuwa laini.

f) Kabla ile namna ya sabuni haijawa ngumu kwa kumwagia, mwaga sabuni

ndani ya boksi la mbao lililotanguliziwa karatasi nyembamba za plastiki.

Baada ya saa 3, sawazisha kwa rula au kitu kingine kilichonyoka, kisha huku

ukigandamiza, ipanguse iwe laini kwa kutumia kitambaa kilicholainishwa.

Page 53: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

53

g) Katakata sabuni vipande (saizi ya kuuza). Iweke ikauke katika sehemu yenye

kivuli kwa muda wa miezi 2. (Mfano, katika boksi la karatasi nene kwa ndani

chini ya sehemu iliyoezekwa).

MUHIMU: Ni muhimu kukoroga sana mchanganyiko huu kadri uwezavyo! Ni sawa

na ni bora kuiacha sabuni ikauke kwa muda usiopungua miezi 2, kwa sababu tendo la

kikemikali linalozalisha sabuni bado huendelea kwa kipindi kirefu. Epuka majaribu

ya kuitumia mapema, kwa sababu itakuwa bado na uwezo wa kushambulia ngozi.

7. Sabuni nyekundu – nyeupe – njano:

Mawese huwa na rangi ya njano – nyekundu kutokana na carotene iliyomo. Kwa

sababu hii, na kwa maelezo ya hapo ju, unapata sabuni ya njano. Hii ni rangi halisi na

ya asili ambayo haina madhara yoyote. Ila kama unataka kutumia sabuni hii kufua

nguo nyeupe inahitaji kuharibu carotene.

Fanya hivi kwa kuchemsha mawese kwa uangalifu kwa dakika 30 kwenye moto, hadi

kipande cha karatasi utakachokichovya katika mafuta kitoke bila rangi. Mchakato

huu hutoa moshi mbaya na mafuta yanaweza yakashika moto kwa urahisi, kwa hiyo

vaa miwani na hakikisha kwamba hakuna watoto karibu!

Unaweza ukatengeneza sabuni nyekundu kwa kuongeza kipimo 1 cha mbegu za

bixa orellana (tazama SURA 6.7.) kwenye mawese. Chemsha katika fukizo maji kwa

dakika 30, chuja na endelea na utaratibu kama unavyofanya kwa mafuta

yasiyosafishwa hapo. Rangi ya bixa orellan ina carotene na haina madhara.

8. Jaribio la kwanza (mfano, katika semina) Wakati unajaribu kutengeneza sabuni mara ya kwanza tumia kipimo kidogo tu,

mfano kijiko (cha mti au plastiki)

Mawese - vijiko vya chai 7

Maji vijiko vya chai 5

Sodium hydroxide - kijiko cha chai 1

9. Sabuni za urembo Sabuni hizi haziegemei upande wowote. Zina mafuta yaliyosafi, na ni nzuri kwa

mwili kwa sababu ya tabia yake ya kuufanya kama unapakwa mafuta kila wakati.

Kabla sabuni haijawa ngumu kwa kukoroga, unaweza ukakata kwa maumbo

unayotaka (chemsha cha kukatia au kichovye kwenye mafuta ya taa) au kitu

kinaweza kugandamiziwa juu ya sabuni ili kuweka urembo.

a) Chukua na endelea kama ilivyoelezwa katika (6) juu;

- Mawese vipimo 8

- Maji vipimo 5

- Sodium hydroxide - kipimo 1

b) Au badala yake, tumia:

- Sabuni ya kugandisha (ya biashara au iliyotengenezwa nyumbani) vipimo 4

- Mafuta ya mbogamboga (mawese, mafuta ya karanga) kipimo 1

- Maji kipimo 1

Twanga sabuni, na changanya katika mafuta na maji. Chemsha taratibu hadi sabuni

iyeyuke. Koroga mchanganyiko mpaka upoe, kisha mimina kwenye kifyatulio.

Page 54: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

54

10. Sabuni ya asali au cream Tumia maelezo ya (a) kwenye sabuni ya urembo juu, lakini punde vitu hivi vitatu

vinapochanganywa ongeza kipimo 1 cha asali.

11. Sabuni ya manukato

Tengeneza sabuni ya urembo kama ilivyoelezwa hapo juu. Baada ya majuma 8 ni

lazima itengenezwe upya kama ifuatavyo: Twanga sabuni, na kwa vipimo 8 vya unga

wa sabuni, ongeza kipimo 1 au 2 vya maji na yeyusha kwenye joto kidogo. Mara

baada ya sabuni kuyeyuka koroga mchanganyiko huo, na mchanganyiko

utakapokuwa mgumu kukoroga ongeza matone kadhaa ya marashi au kipimo 1 cha

michaichai mikavu na iliyosagwa hadi kuwa unga. Mimina katika vifyatulio.

Usiwe na haraka wala pupa unapotengeneza sabuni za manukato! Kama hutasubiri

kwa majuma 8 kabla ya kuzitoa, sodium hydroxide itaharibu manukato.

12. Cream ya kunyolea

- Majani mabichi yanayonukia

(k.k. mkaratusi, limau, michaichai, lavender) kipimo 1

- Maji kipimo 1

Ongeza maji ya moto, chuja na ongeza:

- asali vipimo 3

- Sabuni ya kugandisha

(yenye muda usiopungua miezi 2) iliyotwangwa vipimo 5

Taratibu chemsha mchanganyiko huu hadi uwe kitu kimoja. Na hii ni nzuri kama

itafanyika kwenye jiko la jua ili kupunguza kiwango cha mvuke. Utakaotoweka,

vinginevyo lazima maji yaongezwe ili kurudisha katika ujazo wa awali. Koroga

hivyo hivyo wakati inaendelea kupoa, hadi ipoe kabisa. Hifadhi katika chombo

kisichopitisha hewa ili kuzuia isikauke. Chombo kinaweza kikawa cha kioo, plastiki

au kauri.

13. Sabuni ngumu (inatumika kuondoa uchafu mgumu)

- Mawese vipimo 6

- Maji vipimo 5

- Sodium hydroxide kipimo 1

Kabla sabuni haijawa ngumu sana, ongeza vipimo 2 vya kaolin iliyochekechwa

vizuri (kaolini ni udongo mweupe wa mfinyanzi, unaopatikana mitoni, katika Afrika

hutumika kupamba kuta). Kama kaolin haupatikani, unaweza vilevile ukatumia

majivu ya kuni yaliyochekechwa vizuri. Iache sabuni miezi mitatu kabla ya kutumia.

14. Sabuni ya unga Ukilinganisha na sabuni ya kugandisha, sabuni ya unga huwa ina mawese kidogo:

- Mawese vipimo 5

- Maji vipimo 4

- Sodium hydroxide kipimo 1

Weka ikauke kwa miezi 2 – 3, kisha itwange na tumia chekecheo lenye matunda

ya wastani ili kupata chenga zenye ukubwa sawa.

Page 55: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

55

15. Na kama utapata matatizo….. Iwapo sabuni haikutoka kama ilivyotarajiwa (mfano, kama inaonyesha rangi tofauti

au kama ina muundo wa semolina, ikatekate vipande vidogovidogo siku moja baada

ya kuiandaa, na chemsha vipimo 9 vya sabuni pamoja na kipimo 1 cha maji katika

sufuria mpaka mchanganyiko uyeyuke. Iache ikauke bila kukoroga.

16. Sabuni isiyo na gharama - au nini cha kufanya kama sodium hydroxide

haipatikani. Njia hii, hata hivyo, inahitaji juhudi na kazi kubwa. Tumia: Maganda ya ndizi za

kupikia, magogo ya mapapai au aganda ya mbegu za kakao.

Kausha vitu hivi juani, au kwenye jiko la jua, na vichome. Nadhani si usumbufu sana

kukusanya majivu mikavu kutoka mahali unapopikia mara moja kwa wiki, lakini

majivu ni lazima yatokane na kuni au karatasi ambazo hazikuandikwa, sio jivu la

plastiki au vitu visivyo vya asili. Jaza ndoo ya lita 20 ya plastik kwa lita 10 za majivu

na ongeza lita 15 za maji ya moto. Koroga vizuri. Baada ya dakika 10, chuja kwa

kutumia kitambaa kwenda kwenye ndoo ya plastiki (kazi hii inaweza ikachukua saa

12).

Kwenye majivu yaliyobaki, ongeza tena lita 5 za maji ya moto, koroga kwa dakika

10 halafu chuja. Weka pamoja vile ulivyochuja kwenye chombo cha mfinyanzi.

(Kama utatumia chombo cha metali kitaharibika). Chemsha hadi kibaki kikombe

kimoja tu (200 ml). Ongeza kikombe kimoja cha mawese, halafu chemsha tena kwa

muda mfupi. (Kuwa makini mchanganyiko huu hutoa povu jingi). Mimina kwenye

kifyatulio na acha ikauke.

17. Sabuni iliyotengenezwa kwa mafuta mengine. Faida ya mawese na mafuta ya shea ni kwamba hata katika joto la ndani ya nyumba,

huwa zinakuwa ngumu. Hii hufanya uzalishaji wa sabuni kuwa rahisi; glycerine

ambayo inatokana na utengenezaji wa sabuni haitenganishwi na sabuni bali hubakia

humohumo kwenye sabuni.

Kama utataka kutumia mafuta aina nyingine au shahamu (mfano, mafuta ya

karanga), hapa utengenezaji utakuwa ni mgumu zaidi: Yeyusha gramu 36 za sodium

hydroxide kwenye ml 200 za maji (Uwe mwangalifu), ongeza gramu 200 za shahamu

(shahamu ni mafuta ya wanyama kama nguruwe/mifugo) au mafuta yatokanayo na

mbogamboga; koroga. Ongeza ml 600 za maji ya moto halafu mchanganyiko

uhifadhiwe kwenye joto la 70˚- 80˚C angalau kwa saa 6 (k.k. katika jiko la jua),

koroga kila baada ya dakika 15. Kisha ongeza mchanganyiko wa chumvi ya kawaida

gramu 120 na maji ml 200.

Acha ipoe: Sabuni itatuama juu ya maji.

Mwaga maji, kisha mimina sabuni ndani ya

vifyatulio na ikae kwa mwezi moja hadi tatu

ili ikauke.

Sabuni iliyotengenezwa

nyumbani ni nzuri zaidi kuliko

za kiwandani.

Page 56: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

56

4.2 KUMWAGIA MAJIMOTO NA KUTOKOSA

(INFUSIONS & DECOCTIONS)

Kwa maelekezo ya namna ya kutengeneza infusions na decoctions angalia sura ya 3.

Chai kwa ajili ya Mimea na Sura:

Amoeba dysentery Mpera 5.14; mwembe 5:12; mpaipai 5.5; mziwaziwa 5.11

Ugonjwa wa pumu Mkaratusi 5.10; mziwaziwa (mwache) 5.11

Bronchitis Limau 5.8; mkaratusi 5.10.

Kufunga choo Mwingajini 5.7; ringworm bush 5.6.

Kikohozi Mkaratusi 5.10; limau 5.8; mchungwa 6.14, Parachichi 6.38.

Maumivu ya kunyonga (cramps) Mziwaziwa 5.11; mana ya passionfruit 6.37

Kisukari Maharage 6.39; mahindi 6.50; vitunguu maji 6.2

Kuharisha Mziwaziwa na ORS 5.11; mpera na ORS 5.14,

mwembe na ORS 5.12.

Tumbo kujaa hewa Mkaratusi 5.10.

Homa Mchaichai 5.9; kurimbasi 6.35

Bawasiri Mwingajini 5.7; mwembe 5.12; artemisa 5.2.

Hepatitis Mpapai 5.5

Shinikizo la damu Mahindi 6.50; vitunguu maji 6.2; vinka rosea 6.49

Indigestion Kechu 6.40; dawam mchuzi 6.19

Maambukizo ya figo (kidney infection) Mziwaziwa 5.11; mahindi 6.50

Mapigo ya moyo kuwa chini (Low blood pressure) Kahawa 6.16

Malaria Artemisia 5.12, cinchoma 6.13; mtukutu 6.48; mpapai

5.5; mchaichai 5.9.

Kuvimbewa (Oedema) Mahindi 6.50; mwembe 5.12.

Vidonda mdomoni Mwembe 5.12

Upungufu wa vitamin C Limau 5.8; mpera 5.14

Kukosa usingizi Matunda passion 6.37; njugu 6.6.

Maumivu ya koo (sore throat) Mwembe 5.12

Maumivu ya Tumbo Mpera 5.14

4.3 MAFUTA YENYE DAWA

Maelezo: MMEA + MAFUTA + JOTO = MAFUTA YENYE DAWA.

Kwanza tayarisha maji robo au nusu ujazo wa fukizo. Chungu kingine kidogo

kiweke ndani ya hicho kilicho kwenye stovu. Mchanganyiko unachemshiwa kwenye

hiki chungu kidogo. Funika vyungu vyote viwili. Mtindo huu unahakikisha kwamba

joto halipandi na kuvuka 100˚C. Hakikisha kwamba hakuna maji yanayoweza

kuingia katika chungu kidogo hata yatakapoanza kutokota - kama mafuta yaliyo

kwenye chungu cha ndani yataingiliwa na maji, mafuta yatachacha haraka sana.

Majani lazima yawe makavu kabisa, ili kwamba pasiwepo maji yatakayoingia

kwenye mafuta toka kwenye majani.

Tumia mafuta yanayopatikana katika maeneo yenu: mawese, mafuta ya kokwa.ya

mawese, mafuta ya shea, mafuta ya alizeti, mafuta ya karanga, mafuta mengine ya

aina yanayofaa kwa ngozi. Weka mchanganyiko katika fukizo maji na acha maji

Page 57: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

57

yatokote kwa dakika 60 hivi. Koroga kila baada ya dakika 15. Chuja na acha ipoe bila

kukoroga. Dawa hii yenye mafuta inahitaji kuhifadhiwa pasipo na jua, joto na hewa.

Kwa hiyo tunza mafuta haya ndani ya vyombo vilivyofungwa vizuri. Vijaze tele ili

kupunguza kiasi cha hewa. Kamwe usichanganye bidhaa ya kale na mpya! Mafuta

yanayotoa harufu ya kuchacha yamwagwe mara moja.

Usijiendekeze kwa bidhaa za kibiashara kwa sabuni ya rangi au manukato yake.

Rangi hizo na madawa yaliyomo vinaweza kukusababishia mzio (allergy). Mafuta na

dawa za kujitengenezea nyumbani kwako bila shaka ni bora kwa afya yako!

Vitu kwa ajili ya maelezo haya vimetokwa katika vipimo vya ujazo (k.m kikombe

cha maji ya kunywa, kopo, kikombe cha chai).

Kiasi kwa upande wa mimea ni kwa ile iliyokauka vizuri na kusagwa na isiwe na

vijidudu.

A) Mafuta ya mtoto (baby oil):

- Michaichai (sura 5.9) kipimo 1

- Mafuta ya mbogamboga vipimo 9

B) Mafuta ya urembo

- Michaichai au majani ya

mlimau au mchungwa vipimo 2

- Mafuta ya mbogamboga vipimo 8

C) Mafuta kwa ajili ya kuchua:

- Majani ya mkaratusi vipimo 2

- Michaichai (sura 5.9) vipimo 2

- Mafuta ya mbogamboga vipimo 8

D) Mafuta kwa ajili ya maumivu ya viungo

- Pilipili kavu iliyotwangwa kipimo 1

- (kama inapatikana) elemi resin (sura 6.10) kipimo 1

- Mafuta ya mbogamboga vipimo 4

Angalia yasiingie machoni! Na usiitumie kutibu watoto wadogowadogo.

Unapochua sehemu ambayo ngozi ni nene sana, ongeza kaolin kidogo ili kuleta

hali ya ujoto zaidi. (Tazama jalada la nyuma).

E) Mafuta kwa aliyevimba mishipa ya sehemu ya haja kubwa (Bawasiri) Tumia mimea ifuatayo – kutegemea na upatikanaji tumia baadhi au yote. Majani

yakatwekatwe na kukaushwa. Tumia baadhi au vyote vifuatavyo:

- Majani ya michaichai (sura 5.9),

majani ya msubili (lazima yakaushwe vizuri 6.3), majani ya mpera (5.14),

majani ya chamomile (6.29), majani ya mkurimbasi (6.35) ,

majani ya artemisia (5.2) jumla vipimo 2

- Mafuta mazuri ya mbogamboga , k.m. mafuta ya shea,

mafuta ya kokwa la mawese, au mafuta ya mzeituni vipimo 10

F) Mafuta kwa ajili ya upele Hapa hatuchemshi, bali tunachanganya tu:

- Mafuta ya taa (yatumikayo kwenye taa) kipimo 1

Page 58: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

58

- Mafuta ya mbogamboga kipimo 1

Paka mara tatu kwa siku kwa muda wa siku 2.

Kama hospitali itajua juu ya maelezo haya haihitaji tena kununua benzyl benzoate

ambazo ni ghali au mchanganyiko wa Lindan!

Kwa chawa kichwani, paka kijiko kimoja cha chai cha haya mafuta kwenye

nywele mara mbili kwa siku, lakini isiwe zaidi ya siku 2 hadi 3. Mafuta haya

vilevile yanaangaliwa kama yenye uwezo wa kumsaidia mgonwja

anayesumbuliwa na filaria. Paka kwenye ngozi palipovimba.

4.4 MAFUTA YA (KUJIPAKA) DAWA

Maelezo: MMEA + MAFUTA + JOTO + NTA = MAFUTA YA DAWA

Ili kupata haya mafuta ya dawa, chemsha vitu vilivyotokana na mmea pamoja na

mafuta kwa dakika 60, katika fukizo – maji kama ilivyoelezwa katika sura 4.3.

Usipotumia njia hii mafuta yanaweza kuharibika kutokana na kupata joto kupita

kiasi. Chuja mafuta yakiwa bado na joto. Weka mabaki kwenye rundo moja. Yeyusha

nta na uichuje, changanya mafuta yaliyochujwa (yakiwa bado na joto) na nta

iliyochujwa (ikiwa bado na joto) na kisha koroga taratibu kwa dakika moja.

Mmea ni lazima uwe mkavu kabisa na utwangwe hadi kuwa kama unga.Tumia

mafuta yaliyo bora zaidi kadri inavyowezekana (k.m. mafuta ya mzeituni, mafuta ya

kokwa la mawese ) kwa kuvimba kwa mishipa ya sehemu ya haja kubwa (bawasiri)

na vipodozi. Tumia mafuta ya gharama nafuu kama vile mawese, au mafuta ya

karanga kwa ajili ya mafuta ya kuchua au ya maumivu ya viungo.

Faida ya mawese ni kwamba mafuta ya dawa yaliyotengenezwa kwa mawese

hayawezi kuvunda hata baada ya miaka mitano. Hata hivyo kama mafuta haya

yatatunzwa katika sehemu yenye joto kubwa, yanaweza kuwa yanakwaruza.

Kuyapasha joto kidogo huyafanya kurudia hali yake ya kawaida.

NTA: Kwa kutengeneza vipodozi au mafuta ya dawa kwa ajili ya ngozi laini

tumia nta ya nyuki tu. Kwa ajili ya mafuta ya kuchulia au maumivu ya viungo,

unaweza ukatumia nta za madukani; kwa kiasi kidogo cha dawa, mishumaa isiyo na

ranghi inafaa kabisa. Mchanganyiko wa mafuta /nta ni bora zaidi ukilinganisha na

Vaseline, kwa sababu Vaseline haipenyi kwenye ngozi. Kinyume na imani ya wengi,

vaseline ambayo pia huitwa “petroleum jelly’ sio nzuri kwa ngozi yako! Na hii

(Vaseline) ni kama mfuko wa plastiki juu ya ngozi yako; kwa maana hiyo, ni nzuri

kuitumia kabla ya kufanya kazi kama vile kutengeneza baiskeli au magari. Kamwe

usiitumie kama kipodozi kwa ajili ya uso wako!

Tunza mafuta ya dawa sehemu yenye ubaridi iwezekanavyo!

A) Mafuta ya dawa kwa ajili ya watoto (ointment for babies): - Mafuta ya mtoto (baby oil) (Taz. Sura 4.3) vipimo 9

- Nta ya nyuki kipimo 1

Chemsha mafuta na nta - tumia water bath kwa kuchemsha mafuta - halafu

changanya

B) Mafuta ya dawa kwa maumivu ya viungo: - Mafuta ya maumivu ya viungo (Taz. Sura 4.3) vipimo 9

Page 59: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

59

- Nta ya nyuki kipimo 1

(Kama nta ya nyuki ni ghali, tumia kipimo 1 cha nta ya mshumaa)

Chemsha mafuta na nta - tumia water bath kwa kuchemsha mafuta - halafu

changanya.

C) Mafuta ya dawa kwa kuvimba mishipa ya sehemu ya haja kubwa (bawasiri). - Mafuta kwa kuvimba mishipa ya sehemu ya

haja kubwa (Taz. Sura 4.3) vipimo 9

- Nta ya nyuki kipimo 1

Chemsha mafuta na nta - tumia water bath kwa kuchemsha mafuta - halafu

changanya.

D) Mafuta ya dawa kwa ajili ya majeraha na kuungua - Vitunguu maji vilivyokatwa katwa,

na kukaushwa kwa siku moja kivulini kipimo 1

- Mafuta mazuri ya mbogamboga vipimo 10

- Asali safi vipimo 10

Chemsha mafuta na vitunguu kwa dakika 30 katika fukizo-maji na chuja. Ili

kuboresha uthabiti, unaweza kuongeza kipimo 1 cha nta ya nyuki iliyoyeyushwa.

Usiongeze zaidi, ya kipimo 1, kwa vile inaweza kupunguza kasi ya jeraha kupona,

kutokana na kupungua kwa kiwango cha oksijen kinachoingia kwenye jeraha.

Halafu ongeza asali na koroga taratibu.

E) Mafuta ya dawa kwa upele Changanya sehemu 1 ya sulphur kwenye sehemu 20 za Vaseline au mafuta ya

nguruwe ili kupata mafuta yenye 5% ya sulphur.

F) Uzuri wa ngozi ya uso

- Nyama ya parachichi lililoiva sana vipimo 6

- Juisi ya limau kipimo 1

Kipimo kimoja kinaweza kuwa kijiko 1 cha chai. Changanya muda wa jioni,

halafu paka usoni au ngozi iliyodhurika, na uioshe asubuhi bila kutumia sabuni.

G) Dawa ya kung’arisha viatu au protective grease - Mafuta ya mbogamboga ya bei rahisi vipimo 7

- Nta ya mshumaa usio na rangi vipimo 3

Chemsha pamoja, na acha ipoe. Hii

inaweza kutumika badala ya Vaseline.

Kwa viatu vyeusi, ongeza kipimo 1

cha mkaa uliotwangwa hadi kuwa kama

poda.

4.5 PODA

A. Poda ya watoto

Tumia mihogo tu, iliyokauka vizuri na iwe

nyeupe kabisa. Ikaushe tena kwa siku moja

kwenye jiko la jua. Itwange na uchekeshe

Page 60: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

60

kwa kitambaa cha nailon. Kama huna jiko la jua, kausha kikombe 1 cha unga wa

mhogo taratibu sana kwenye sufuria lako hadi ukauke kabisa na kuwa kahawia

(brown) kidogo. Chekecha moja kwa moja baada ya kuchemsha , kwa kutumia

kitambaa cha nailoni. Kama ukipenda unaweza kuongeza tone moja la marashi kwa

kikombe kimoja cha unga uliochekecha. Tunza kwenye chombo kisichopitisha hewa.

B. Poda ya mkaa

Kuni kutoka kwenye mti, ambao hauna sumu wala utomvu unaojivuta (unaonata)

huchomwa hadi kuwa mkaa, kwa njia zilezile zinazotumika katika nchi za tropiki.

Kwa kuwa kuni mara nyingi ni rasilimali adimu, unaweza ukakata matawi ya katikati

ya mti wa mwembe kwa sababu matawi haya huwa hayatoi matunda. Au badala yake

chemsha maganda ya karanga ndani ya sufuria iliyofunikwa hadi yawe mkaa. Uwe

mwangalifu, kwa sababu unga huu unaweza ukaungua kuwa majivu muda wowote

sababu ya joto. Watoto wakae mbali kabisa. Ukipoa, utwange mkaa huo na

uchekeche kwa kutumia kitambaa cha nailoni. Ili kuua vijidudu kwenye unga wako

uliotengeza kutokana na mti wa mwembe au maganda ya karanga , chemsha unga

wako tena katika sufuria hadi uone chembe nyekundu: sasa vijidudu vyote vitakuwa

vimekufa. Hifadhi kwenye vyombo visivyopitisha hewa.

Unga huu hufyonza sumu na hewa. Kwa hewa tumboni, harufu mbaya mdomoni,

na kuharisha, watu wazima watumie kijiko 1 cha chakula mara 3 kwa siku.

Hata hivyo, kama watoto wanaharisha, kitu muhimu zaidi ni kurudisha maji

yaliyopotea kwa kumpa mtoto ORS, (Taz. Sura 4.6)

Kwa vidonda vinavyonuka na kutoa usaha, unaweza ukaweka katika jeraha, lakini

vidonda ni lazima viwe vya juu tu.

Kama mtu amekula mmea wenye sumu na hospitali /kituo cha afya kiko mbali,

jaribu kumtapisha (kwa kumwekea kidole kooni sehemu ya chini). Na kwa

kuongezea umpe vijiko vingi, ina maana gram 50 -100 za poda ya mkaa pamoja na

chai inayosababisha apate choo) (Taz. Mwingajini sura 5.7). Kama mtu amekunywa

mafuta ya taa, petroli au dizeli, usimtapishe kwa sababu ya uwezekano mkubwa wa

kupatwa na kichomi cha pafu, bali mpeleke mgonjwa kwenye kituo cha afya kilicho

karibu haraka iwezekanavyo. (Taz. pia mbono, sura 6.42).

C. Poda (unga ) yenye madini (Bolus rubra) Katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, udongo mwekundu, ambao huitwa

“Itsama” na wenyeji wa huko hupatikana karibu na mito. Kidesturi wanawake

wajawazito hula udongo huu ili kukamilisha mahitaji yao ya madini.

Uchambuzi wa udongo huo ulikuwa kama ifuatavyo:

Calcium mg 2450/kg

Magnesium mg 1400/kg

Chuma mg 1400/kg

Manganese mg 152/kg

Copper mg 16/kg

Zinc mg 18/kg

Cobalt mg 3/kg

Madini mengi sana ajabu!! Sehemu kubwa ya jamii isingeweza kujipatia vidonge

vyenye madini haya vinavyopatikana kwenye maduka ya dawa.

Tunapendekeza kwamba unakausha udongo, unauchekecha na kisha unauchemsha

katika sufuria ili kuua vijidudu vinavyoweza kuwa kwenye udongo.

Page 61: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

61

Jinsi ya kutumia:

Watoto wenye upungufu wa damu kijiko kimoja cha chai kwa siku.

Wakinamama wajawazito kijiko kimoja cha chakula kwa siku

Kama ikiwezekana, ili kusaidia utaratibu wa madini kufyonzwa kwenda mwilini,

kunywa pamoja na juisi ya limau saa moja kabla ya mlo.

D. Chumvi yenye madini ya joto.

Kausha kabisa kilo 1 ya chumvi na uisage kuwa unga. Ichanganywe taratibu na mg.

30 za potassium Iodine (Ili kuzuia goitre).

E. Chakula cha mtoto, cha unga Kuanzia umri wa miezi 6 mtoto wako anahitaji chakula ili kuongezea katika maziwa

ya mama. Epukana na matangazo yenye ushawishi na usinunue chakula chochote cha

mtoto dukani!! Chakula cha kutoka shambani daima ni bora! Na kama hakipatikani

(k.m. safarini) hapa kuna pendekezo kwa chakula cha mtoto cha kutengenezea

nyumbani ambacho ni cha kupendeza na chenye lishe bora:

- Vyakula aina ya mbegu (uwele, mchele, mahindi, ngano au mtama na ulezi)

viwe vikavu kabisa (Tumia sun box, vinginevyo oka kwa dakika 20,)

halafu saga gramu 650 au vikombe 3.

- Mikundekunde (maharage ya soya, maharage, njegere, dengu) chemsha kadri

ya dakika 20, kisha kausha kabisa na utwange gramu 350 au vikombe 2.

- Mbegu zenye mafuta (Njugu zisizo na magamba, ufuta gramu 100 au

kikombe 1.

- Majani ya kijani ya mlongelonge yaliyokaushwa (kama yapo) gramu 25 au ¼

kikombe.

- KWA UTAPIAMLO TU

- inaweza kuharibu meno yako! – sukari gramu 50 au ½ kikombe.

Changanya kwa mpangilio uliopo na uhifadhi kwenye chombo kisichopitisha

hewa, kutegemea na kiwango cha ukavu, (Taz. SURA 2.7). Mchanganyiko huu

hudumu kati ya juma 1 na mwaka 1. Kama unga sio mkavu sana vya kutosha, fungi

(mba) hatari huota na huhatarisha afya ya mtoto wako.

Kwa mlo mmoja, chemsha vijiko 2 vya chakula (unga) vilivyojaa kabisa vya

mchanganyiko huu kwa ml 350 za maji (nusu ya chupa ya lita yenye ujazo wa 0.7

lita) au changanya unga na maji ambayo yamechemshwa na yakapoa.

F. Poda (unga) kwa ajili ya meno

1. Kwa matumizi ya kila siku:

- Majani yaliyokaushwa ya mkaratusi kipimo 1

- Chumvi kavu (ya mezani) kipimo 1

Tafuta mti wa mkaratusi ulio katika mazingira safi (k.m. kwenye msitu) na vuna

majani mazuri zaidi ya mita mbili kutoka ardhini; yaoshe, yakaushe na yatwange

vizuri. Chemsha chumvi ndani ya sufuria. Ikiwa bado ya moto, imwage kwenye kinu

kilicho kisafi kabisa, wakati huohuo ukiongeza majani ya mkaratusi yaliyotwangwa.

Twanga pamoja, na chekecha kwa kitambaa cha nailoni. Tunza kwenye chombo

kisichopitisha hewa. Weka kiasi kidogo kwenye mswaki wako.

Page 62: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

62

2. Poda kwa meno yanayooza. Changanya kipimo 1 cha chumvi na kipimo 1 cha jivu la kuni lililosafi. Weka kitawi

cha mwarobaini (au kitawi cha mkaratusi) ndani ya huu mchanganyiko na kisha

sugua kwa uangalifu kwenye madoa ya kahawia (brown) yaliyo kwenye meno. Sugua

mara 3 kwa siku. Hii inasaidia tu iwapo madoa ya uozo bado yako juujuu.

4.6 ORS (maji-chumvi)

Kwa matatizo yote ya kuharisha (hata kama yanaambatana na malaria, homa ya

matumbo, bacillary infection etc.) daima mpe mgonjwa ORS! Endelea kumpa

vyakula kama kawaida, ili kuzuia upungufu wa vitamin. Unaweza ukatengeneza

mwenyewe ORS, hakuna haja ya kununua vifurushi ambavyo ni ghali; hata vifurushi

vya bure vya ORS huwafanya watu kuwa tegemezi.

A. Vitu vilivyomo

Kwa mtu anayeharisha, kitu muhimu zaidi ni kurudisha maji yaliyopotea. Kwa

watoto au watu wazima, daima mpe mgonjwa maji haya yenye chumvi (ORS) ya

kutosha.

MAJI (ORS) haya yana vitu vitatu: Maji, sukari,

chumvi.

MAJI: Tumia maji mazuri, kama hakuna maji safi ya chemchemi karibu, tumia

maji yaliyochemshwa . Au pika chai ya majani ya mapera.

SUKARI: Ni vizuri zaidi ukitumia asali. Vinginevyo tumia sukari ya nyumbani

(katika hospitali tumia glucose). Kama huna sukari, au mgonjwa ana kisukari,

unaweza kutumia vitu vifuatavyo badala yake:

a) Kutwanga kiasi cha gramu 10 za ndizi sukari (usichemshe).

b) Viazi vitamu gramu 100 - chemsha dakika 5.

c) Gramu 30 (vijiko vya chai 3 vilivyojaa kabisa vya unga wa ngano, mchele

uliotwangwa au uwele. Chemsha vyote katika maji kwa muda wa kawaida.

CHUMVI: Ikiwezekana tumia chumvi ya kienyeji (iliyotengenezwa kienyeji

kutokana na majivu yaliyopatikana kutoka kwenye kuni zilizochomwa). Hii kwa

namna moja ni nzuri, kwa sababu jivu huwa lina potassium. Vinginevyo tumia

chumvi ya nyumbani (sodium chloride).

POTASSIUM: Ni kitu ambacho hakina budi kuongezwa kama mgonjwa

ataendelea kuharisha kwa siku kadhaa. Hata hivyo, potassium huongezwa kama

mgonjwa ana uwezo wa kukojoa. Potassium husaidia misuli ya utumbo na

matumbo kufanya kazi kwa hali yake ya kawaida. Potassium inapatikana katika

parachichi, ndizi, maboga, maji ya nazi, karoti, soya iliyopikwa, njugu, mchicha

na mboga zenye rangi ya kijani – nyeusi zilizopikwa kwa mvuke.Na kwa watoto

wadogo wanaohitaji potassium, a) wape sehemu ya chakula hicho, au b) wape

chumvi iliyotengenezwa kienyeji, au c) ongeza kijiko1 cha jivu safi (kutokana na

miti au nyasi zisizo na sumu, au majani ya magugu maji Eichhornia crassipes

yaliyokaushwa, ambayo ina potassium kwa wingi) kwenye lita moja ya maji

uliyotumia kutengeneza ORS (Taz. chini). Baada ya dakika chache, chuja maji.

Page 63: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

63

Kama kitu kimojawapo ulichotumia (sukari, chumvi, maji) hakikuwa safi

kabisa, chemsha mchanganyiko kwa muda mfupi ili kuua bacteria.

B. Utengenezaji wa ORS nyumbani:

a) Katika lita 1 ya maji, ongeza vijiko vya chakula 4 vya asali au vijiko 2 vya sukari

(gramu 30), na chumvi kijiko 1 cha chai, au

b) Kwenye kikombe 1 (ml 500) cha maji, ongeza asali vijiko vya chakula 2 au kijiko

1 cha sukari, na chumvi kidogo (kiasi cha chumvi unachoweza kushika kati ya

kidole gumba na shahada).

C. Jinsi ya kutumia ORS: Mpe mgonjwa kwa siku: Ml 200 (glasi moja) kwa kila kilogramu ya uzito wa mtoto.

Kama hujui uzito wa mwanao na huwezi kupima mililita, lakini una chupa tupu, na

safi ya vinywaji baridi, jedwali lifuatalo litakusaidia:

Jedwali 4.1. : MATUMIZI YA ORS

UMRI Ukubwa wa chupa

Ml. kwa

siku

Lita 0.33 Lita 0.5 Lita 0.7 Lita 1

Chini ya miezi 6 700 Chupa 2 Chupa 1½ Chupa 1 Chupa ¾

Miezi 6 hadi

miaka 2

1,400 Chupa 4 Chupa 3 Chupa 2 Chupa 1½

Miaka 2 – 5 2,100 Chupa 6 Chupa 4 Chupa 3 Chupa 2

Zaidi ya miaka 7 2,800 Chupa 8 Chupa 6 Chupa 4 Chupa 3

Watu wazima 3,500 Chupa 10 Chupa 7 Chupa 5 Chupa 3½

D. Utengenezaji wa ORS mahospitalini:

Si busara kuagiza kutoka nje vifurushi vya ORS ambavyo vina dozi moja; hospitali

yo yote inaweza kujitengenezea.

Vitu vinavyohitajika kwa lita moja ya maji:

- Sodium chloride (chumvi ya kula) NaCl gramu 3.50

- Potassium chloride KCl gramu 1.50

- Glucose (dextrose) anhydrous gramu 20.00

- Sodium bicarbonate NaHCO3 gramu 2.50

Badala ya gramu 2.5 za sodium bicarbonate unaweza kutumia gramu 3.0 za

trisodium citrate dehydrate.

Kausha kabisa chumvi ya mezani na potassium chloride (k.m. katika jiko la jua),

twanga na halafu chekecha. Changanya chumvi, potassium chloride na bicarbonate,

kisha ongeza glucose (vyote viwe karibu kiasi sawa). Weka kwenye maboksi

yasiyopitisha hewa na kila boksi liwe na dozi 30. Vama hakuna glucose, tumia gramu

30 za sukari (sukari ya miwa) badala ya gramu 20 za glucose. Hii haitapunguza

nguvu ya ORS.

Page 64: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

64

E. Tatizo la kuhifadhi Kwa kuwa vyombo visivyopitisha hewa ni vichache katika nchi za tropiki, na mara

chumvi inakuwa na vibonge au unyevunyevu; tumeandaa maelezo yafuatayo katika

pharmacy yetu:

- Potassium chloride gram 33

- Chumvi ya kula gram 100

- Sukari ya miwa (ya dukani) gram 600

- Maji ml 400

Yeyusha potassium chloride, kisha chumvi, halafu sukari (Tilia maanani

mpangilio ulioonyeshwa!) kwenye maji ya mtoto. Chemsha na chuja. Hii ina hata

manufaa ya kiafya kwa kuwa sukari na chumvi, ambavyo wakati mwingine huingiwa

na uchafu au vijidudu wakati wa kutayarisha au wakati wa usafirishaji kwenye

malori, wadudu hao huuwawa unapotumia maji ya moto.

Dozi: Weka vijiko 4 vya chai kwenye 0.7 lita ya maji.

4.7 JIWE JEUSI

Jiwe jeusi hutumiwa baada ya mtu kuumwa na nyoka au wadudu wenye sumu kali,

mfano nge. Nguvu zake ziko katika tabia ya jiwe hili ya kufyonza kiwango kikubwa

cha majimaji. Lina vifereji vingi sana na vifereji hivi vinafyonza kwa njia ya hewa

inayopenya katika vifereji hivyo na kwa njia hiyo kunata kwenye sehemu

ilipowekwa hadi kujazwa hadi mwisho.

Kwa kufanya majaribio, weka jiwe hilo jeusi kwenye ulimi wako; hunyonya majimaji

na kung’ang’ania kwenye ulimi. Lisipoondolewa haraka, huenda hata likasababisha

ulimi kuvuja damu wakati utakapoliondoa baadaye.

Muundo wa jiwe jeusi bado ni siri, kitu ambacho huwafanya baadhi ya wakristo

kutuhumu kuwa ni uchawi. Uwezo wake wa kufyonza sumu nyingi na vitu vingine

vya hatari ambavyo hutokana na kuumwa, umeelezwa katika vitabu vya tiba. Ni

lazima lipachikwe haraka mara baada ya kumwa. (ila

snake serum ina nguvu zaidi, lakini katika vituo vingi

vya afya ama haipatikani au ni ghali mno).

Namna ya kutengeneza jiwe jeusi Chukua sehemu ya katikati ya mfupa wa paja la

ng’ombe; kata kwa msumeno vipande vipande, (ukubwa unaokaribia sm 4 × sm 1.5).

Vichemshe mara mbili kwenye maji safi. Kisha chemsha tena kwenye maji yenye

sabuni au sodium hydroxide ili kuondoa mafuta yote yaliyobakibaki . Chemsha tena

katika maji safi ili kuondoa sabuni. Weka juani ukauke kwa muda wa siku 5 au katika

jiko la jua kwa siku moja. “Jiwe jeusi” ni lazima lishikwe au kubebwa kwa uangalifu

mkubwa: usiliweke katika maji ya moto wala kuliweka mahali joto linapobadilika

kwa haraka, kwa sababu kwa hali hizo vifereji vilivyomo ndani ya jiwe, ambavyo

huleta uwezo wa kufyonza, huharibika mara moja. Liache likauke ama kwa siku 3

juani na kisha ndani ya sufuria kavu juu ya moto au kwa siku moja ndani ya jiko la

jua. “Mawe” haya sasa huonekana kama pembe za ndovu.

Fungasha kila kipande ndani ya karatasi 2 nyembamba za aluminia (aluminium

foil). Weka vipande hivyo kwenye sehemu ile nyekundu sana ya moto wa mkaa

Page 65: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

65

katikati , na funika kwa mkaa kidogo uliotwangwa. Kagua kipande kimoja baada ya

dakika 40; linatakiwa kubadilika kuwa jeusi na gumu, kuwa kama makaa ya mawe,

lakini bila kuungua. Kama limetengenezwa kwa njia sahihi, jiwe jeusi hunata kwenye

ulimi. Na kama haling’ang’anii ulimi, linahitaji kurudishwa kwenye moto. Kama jiwe

linavunjika kwa urahisi au hata limekuwa kama majivu meupe, basi jiwe hilo

litakuwa limeungua.

Lakini likiwa jeusi, gumu na linanata kwenye ulimi, litakuwa limekamilika na

tayari kwa kutumika.

Namna ya kutumia jiwe jeusi:

Kuumwa na nyoka: Gandamiza kwenye jeraha hadi jiwe ligusane na majimaji.

Mara jiwe linapogusana na damu, hung’ang’ania kwenye jeraha na haliondoki

hadi sumu yote na uchafu vimefyonzwa . Na hii inaweza ikachukua siku nzima.

Majipu na vijeraha vyenye usaha: Vunja jiwe jeusi kulingana na ukubwa wa jipu/

jeraha. Ligandamizie kwenye jipu/ jeraha hadi ligusane na majimaji ya kwenye

jipu/ jeraha. Jiwe jeusi huondoa kila uchafu, kwenye jipu/ jeraha, hivyo kufanya

sehemu kubwa ya vijidudu kufyonzwa na kuondolewa.

KULIPA NGUVU TENA JIWE JEUSI Baada ya kutumika jiwe jeusi huchemshwa kwenye maji kwa dakika 10, kwanza

kwenye maji ya sabuni, kisha kwa dakika 10 zingine kwenye maji safi. Hii inafanyika

ili kuliondolea uchafu katika vifereji vyake na kulisafisha kabisa jiwe ili kuzuia

maambukizi yoyote kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

4.8 DIVAI YA ASALI

Mvinyo ya asali inatumika kama kitu cha msingi kwa mvinyo zenye dawa na syrups.

Ikitengenezwa vizuri ina kileo 12 – 14%

Asali lita 2.5 sawa na chupa 2 ½ ya lita 1

Maji lita 2.25 sawa na chupa 2 ¼ ya lita 1

Juisi ya matunda lita 0.25 sawa na robo chupa au kikombe 1 cha chai.

Kama asali haipatikani:

Sukari kilo 2

Maji lita 2.75

Juisi ya matunda lita 0.25

Unaweza kutumia juisi kutoka kwenye tunda lolote

k.m. embe, chungwa, limau. Juisi ni muhimu kwa

kuwa hutoa hamira na madini yanayohitajika.

Chemsha mchanganyiko kwa dakika 15, chuja na

mimina kwenye chombo chenye ujazo wa lita 5

(inapendekezwa chombo kiwe cha glasi au plastiki).

Acha mchanganyiko upoe. Ongeza hamira nusu

kijiko cha chai (kuna hamira maalum kwa kazi hii, lakini hamira ya kawaida ya

kuokea inafanya kazi pia).

Page 66: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

66

Toboa tundu dogo kwenye mfuniko wa chombo na ingiza mpira mwembamba

wenye uwazi katika (k.m. mipira inayotumika kuongeza maji wagonjwa mahospitali

ni).

Ncha nyingine ya mpira huo inaingizwa kwenye kikombe cha maji kilichojaa. Hii

inasaidia carbon dioxide isiyohitajika kuweza kutoka nje - bila oksijen kuingia ndani

ya chombo na kuharibu mvinyo.

Tunza chombo chenye kinywaji hiki sehemu yenye uvuguvugu na uitikise taratibu

kila siku. Baada ya majuma 2 – 3 utaratibu wa kutengeneza chachu unakamilika.

Chuja mvinyo kutumia kitambaa safi. Tunza mvinyo kwenye chupa isiyoingiza hewa,

kwenye sehemu baridi na isiyo na mwanga.

4.9 DAWA YA KIKOHOZI (Cough Elixir)

Divai ya asali lita 5

Majani ya mkaratusi makavu yaliyotwangwa gramu 250

Changanya na tunza sehemu yenye uvuguvugu, ikiwa imefunikwa bila kukaza sana,

kwa siku 5. Chuja na hifadhi ndani ya chupa isiyoingiza hewa, sehemu yenye ubaridi

na isiyofikiwa mwanga.

Jinsi ya kutumia:

Watu wazima Kijiko 1 cha chai, mara 3 kwa siku.

Watoto (mwaka 1 na kuendelea) Matone 20 – 40 , mara 3 kwa siku.

4.10 MADINI NA VITAMINI

Ni kitu kinachosikitisha sana, kwa sababu tu ya ukosefu wa pesa, watu wengi katika

nchi za tropiki wanaugua au hata kufa kwa njaa. Lakini inakuwa ni vibaya zaidi

wakati ambapo matatizo haya yanatokana na matangazo ya kibiashara

yanayokushawishi kununua bidhaa zinazoelezwa kuwa ni za “kuleta hamu ya

chakula”, juisi za vitamini n.k.

Bidhaa hizi siyo za lazima wala hazistahili. Nyama ni gharama nafuu na

inakuongezea nguvu kuliko dawa ya “sana – vita – liver – extract.”; “Vitamin E”

inapatikana kwa wingi katika majani ya mihogo kuliko katika vidonge vya “paradiso

– impotex.”

Kuna mwanamke mmoja katika kijiji chetu nchini D.R. Kongo ambaye alitumia

ujira wake wa wiki nzima kwa kununua chupa moja ya maji mekundu ya madukani

akiamini yataimarisha damu ya mwanae. Je mama huyu alikuwa ni mwanakijiji wa

kawaida? Ngoja tuangalie pia kidogo katika baadhi ya hospitali za serikali na

makanisa, hata katika miji mikuu. Bajeti zinapangwa kwa ajili ya vitu kama “vidonge

vya vitamini B,” “vitamin E forte,” “haemo-vit-orange” na dawa zingine zenye

majina ya kutamanisha sana.

Watu wanaohusika nadhani wangefanya vizuri zaidi kama wangeweka

machungwa na karanga kwenye makabati ya maduka yao ya dawa!!

1. Vitamin A: Ni muhimu kwa kusaidia macho kuona vizuri . Inapatikana kwenye

matunda na mbogamboga zote zenye rangi nyekundu na rangi ya machungwa:

papai, karoti, nyanya, embe, kwenye mayai na matunda jamii ya nazi. Pia

Page 67: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

67

mawese yana vitamin A kwa wingi sana. Katika nchi za Afrika ambapo mawese

hupatikana kwa wingi, ni watu wachache wanaopata upofu. Kwa nchi za

mashariki na kusini mwa Afrika, ambako michikichi ni michache, tunapendekeza

kupanda na kula viazi vitamu vyenye rangi ya njano (chungwa), ili kuepuka

kutumia vidonge vya vitamini A.

2. Vitamin ‘B’ Complex: Ni muhimu kwa watu wanaojihisi kuwa dhaifu na kwa

matatizo ya mishipa ya fahamu. Vitamin hizi ni za muhimu kwa kusaidia

uyeyushaji na ufyonzaji wa carbohydrates (wanga), k.m. sukari na unga. Chakula

kinachopatikana katika maeneo ya vijijini kama vile njugu, soya, maharage,

karanga, nyama, samaki, mboga zenye majani ya kijani, hamira, makapi ya

mpunga na maziwa ya mama ambayo yana kiwango kikubwa cha vitamini hizo.

Kwa hiyo, ni kosa kubwa, kuuza njugu ili kununua biskuti za vitamin ‘B’.

3. Vitamin C: Mfumo wa asili wa ulinzi wa miili yetu ambako huulinda na

maambukizi, hupatikana katika vitamin C. Watoto wenye umri hadi miezi 6

hupata kiasi cha kutosha cha vitamin C kutoka maziwa ya mama zao. Zaidi ya

umri huu ni lazima mtoto ale aina zote za matunda (hasa machungwa, ndimu, na

matunda ya passion), mbogamboga (majani ya kijani, vitunguu maji, viazi vitamu

n.k.). Matunda na mbogamboga ni bora zaidi vikiliwa bila kupikwa, kadri

unapozidi kuvipika vitamini C hupungua zaidi. Tofauti na vitamin A, vitamin C

huwa haihifadhiwi mwilini, kwa hiyo matunda na mbogamboga ni lazima viliwe

kila siku.

4. Vitamin D: Husaidia ukuaji wa mifupa. Vilevile mwili una uwezo wa

kujitengenezea vitamini D kutokana na jua. Mayai na mafuta ya wanyama pia

vina vitamin D.

5. Vitamin E: Inapatikana kwenye majani ya kijani na mafuta ya mbogamboga.

Manufaa yake kwa afya ya binadamu bado hayajafahamika wazi. Katika

matangazo vitamin hii huitwa “vitamin ya rutuba”; lakini, pamoja na hayo,

hakuna mtu hata mmoja ambaye amepata mtoto kwa ajili ya dawa ya Vitamin E.

6. Vitamin K: Husaidia damu kuganda unapopatwa na ajali (k.m. kujikata).

Inapatikana kwenye majani ya kijani na huzalishwa vilevile na baadhi ya vijidudu

vya kwenye utumbo. Kuna desturi moja ambayo haina manufaa na hufanywa na

baadhi ya wodi za wazazi, ya kumpa vitamin K kila mama baada ya kujifungua.

Hii vitamin inastahili tu kwa mjamzit mwenye upungufu wa Vitamin K.

7. Folic acid: Ni ya lazima kwa watu wenye matatizo ya kupungukiwa damu.

Inapatikana kwa kiwango kikubwa katika maini na mboga za majani za kijani.

8. Calcium : Calcium ina jukumu muhimu katika ufanyaji kazi wa seli za mwili,

hasahasa katika misuli na mifupa . Kidonge cha calcium kilichonunuliwa dukani,

kina kiwango kilekile cha calcium (gram 200) kama samaki mkavu gram 10,

unga wa maziwa gram 30, mboga mboga za kijani gram 100, au maharage gram

200.

9. Chuma: Madini ya chuma huiwezesha miili yetu kuzalisha haemoglobin,

ambayo huleta rangi nyekundu katika damu. Kujaribu kutibu upungufu wa damu

Page 68: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

68

Vitamins – chaguo ni letu!

A. Kwanza umepewa mifano ya vitamin.

B. Halafu ikupase kuzinunua kwa bunda la noti kutoka duka la madawa.

C. Pale ambapo asili inakupa vitamini hizo bure.

B

A

C

Page 69: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

69

kwa kutumia juisi au soda nyekundu, hakuna manufaa yoyote! Ni bora zaidi kula

aina zo zote za mboga za majani. Jaribu kufanya lolote linalowezekana ili kuzuia

magonjwa yanayosababisha upungufu wa damu, k.m. malaria, kuharisha kwa

muda mrefu na safura!

Matumizi ya vikaango na masufuria yaliyotengenezwa kwa chuma halisi ni njia

vilevile inayopendekezwa, lakini sio yaliyotengenezwa kienyeji kutokana na bodi

za magari au mapipa, kwa sababu haya huwa yamechanganywa na baadhi ya

metali zenye sumu.

Ili kukifanya chakula kiwe na madini mengi ya chuma, unaweza ukaweka

misumari yenye kutu (lakini iwe misafi) kwenye sufuria wakati wa kupika. Kwa

njia hii kiasi kidogo sana cha chuma huingia kwenye chakula na hivyo mwilini

(miili yetu inafyonza madini kidogo sana kwa siku moja). Au unaweza kuchoma

msumari mrefu wenye kutu ndani ya chungwa au limau (msumari uwe msafi) na

baada ya siku tatu uchomoe na kula hilo tunda; au kamua juisi na kunywa, juisi

itakuwa na madini ya chuma. (Tindikali iliyomo kwenye tunda hubadili chuma na

kuwa madini yaliyoyeyukia ndani ya tunda).

10. Madini ya joto: Katika maeneo yaliyo mbali na bahari, watu wengi hupatwa na

goitre sababu ya upungufu wa madini ya joto, ambayo sanasana hupatikana kwa

viumbe (samaki) wa baharini. Kwa hali hiyo tunapendekeza kununua ml. 30 za

“lugol 0.1%” kutoka duka la madawa, na halafu weka matone 1 – 10 kwa siku

kwa kila mtu katika chakula ulichokiandaa.

Maelezo kwa duka la madawa: Changanya mg. 100 za madini ya joto na mg

200 za Potassium Iodide, na yeyusha mchanganyiko huu kwenye ml. 100 za maji,

yaliyochemshwa na kuchujwa. Gawanya na tunza kwenye vyombo vya kioo, sio

uya plastiki au metali.

4.11 MAZAO KWA MIFUGO NA MATUMIZI YA KILIMO

A. Matofali ya kulamba kwa mifugo:

Sementi Mifuko (2 kilo 50

kila mfuko)

Udongo mwekundu Toroli 2

Chumvi ya kula kilo 35

Iron Sulphate kilo 2

Copper sulphate kilo 1

Magnesium sulphate gramu 100

Manganese sulphate gramu 100

Matofali ya kulamba hutengenezwa kwa kifyatulio. Kama aina hizo tofauti za

sulphate hazipatikani chukua sementi, udongo mwekundu, na chumvi tu. Kama

hakuna sementi wala kifyatulio, tengeneza mchanyanyiko wa udongo mwekundu,

jivu la kuni na chumvi. Lakini kama hivi navyo havipatikani wape mifugo majivu ya

kuni.

B. Upele na kupe: Kwa chawa au kupe waliong’ang’ania kabisa kwenye ngozi, ama tumia mafuta ya

upele (Taz. Sura 4.3.f). au twanga majani makuukuu ya Tephrosia na (ukiwa umevaa

mipira) paka kwenye ngozi pamoja na maji kidogo au mafuta.

C. Maumivu ya viungo: Taz. Sura 4.3.D.

Page 70: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

70

D. Mkaa kwa wanyama wanaoharisha: Taz. Sura 4.5.B.

Mpe gramu 0.1. – 0.5. kwa kila kilo ya uzito wake kila siku. Mkaa wa biashara

hufanya kazi vizuri.

E. Dawa ya viroboto kwa kuku (ndege wafugwao)

Katika nchi za tropiki, hasa wakati msimu wa mvua, kufuga vifaranga ni vigumu

sana. Mara tu vifaranga wanapototolewa, melfu ya viroboto kutoka kwa kuku huanza

kuvishambulia. Viroboto hung’ata na kung’ang’ania eneo linalozunguka macho ya

vifaranga na kuku.

Matokeo yake kuku hutaga mayai kidogo na upande wa vifaranga hupoteza damu,

hudhoofika na baadaye kufa. Viuatilifu vyenye kemikali kama DDT na Lindane ni

vya hatari sana na vinatufanya hatimaye kula sumu pindi tulapo mayai yenye dawa.

Ili kuzuia hali hii,

kuku wapewe majivu ya kuchakurachakura.

viota vyao vitandaziwe majani ya mikaratusi, majani ya tumbaku au

michaichai na pia majivu.

vifaranga wapate nafasi ya kuzungukazunguka kwenye maeneo yenye nyasi.

paka mawese kwenye vichwa vya vifaranga mara 1 – 3 kwa wiki, kwa wiki 3

za kwanza za maisha yao.

Kwa vifaranga vikubwa na kuku, tumia mchanyanyiko wa kipimo 1 cha mawese na

kipimo 1 cha mafuta ya taa. Kwa kukushukuru kuku wako watataga mayai mengi

zaidi.

F. Dawa ya minyoo kwa wanyama

Taz. Sura 5.5; mpapai: Mpe juisi ya papai bichi, (ml. 3 kwa kila kilo 10 za uzito wa

mwili). Halafu endelea kuwapa mbegu za mapapai mara kwa mara. Mbwa wetu

(mwenye kilo 10) aliwahi kula papai zima mara kwa mara. Mbwa vilevile hupendelea

kula michaichai ili kupigana na minyoo. Nguruwe anatakiwa ale papai moja bichi

kila siku.

G. Tiba ya majeraha (kwa wanyama tu)

1. Tiba ya Antiseptic

Mafuta ya mbogamboga yasiyo ghali gramu 140 (kopo 1 dogo)

Nta gram 20 (½ mishumaa)

Commercial creosote gram 5 (kijiko cha chai)

Chemsha mawese na nta, acha vipoe kidogo, ongeza kijiko cha chai cha creosote

na koroga hadi mchanganyiko ubadilike kuwa dawa ya mafuta. Au badala yake,

twanga majani mabichi ya tumbaku au mkaritusi na funga kwenye jeraha.

2. Tiba ya antiseptic kwa wanyama wadogowadogo .

Tumia sukari au kipande cha papai bichi kama ilivyoelezwa kwa binadamu.

Mchanganyiko wa mafuta ya mbogamboga na majani ya mkaratusi (Taz. Sura

5.10) husaidia kuzuia nzi kutua kwenye jeraha.

3. Tiba ya antiseptic kwa mifugo

Kusafisha vidonda, tumia mkaa uliotwangwa na kuchekecha kutokana na majani

ya mkaratusi na majani ya tumbaku, chumvi kidogo au mchanganyiko wa vyote

hivi. Kiasi kidogo sana cha oil ya magari vilevile kinaweza kutumika.

Page 71: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

71

H. Upungufu wa madini na vitamin kwa kuku (ndege)

Katika maeneo mengi “kuku wa kisasa” wanapatikana, na hiyo ni nzuri. Lakini mara

nyingine watu watakushawishi kununua chakula “cha kisasa” kwa kuku wako kwa

vile kina madini na protein nyingi zinazohitajika kwa kuku hawa. Usidanganyike kwa

hadithi hizo za ki-biashara – virutubisho vyote vinapatikana katika kijiji chako!

PROTINI:

Kuku na vifaranga wako wanahitaji “nyama” (lakini sio unga wa maziwa, ingawaje

unaweza kuwa umeandikwa katika vitabu). Wakati wa mchana waruhusu kuku

kuzurura ili kujitafutia vijidudu vya kula. Wape majani ya kijani wanayopendelea.

Weka rundo la mchanganyiko wa vitu vinavyooza ndani ya zizi la kuku. Rundo hili

litawavutia nzi na minyoo wengi; vyote hivi ni protini nzuri tu ambayo italiwa na

kuku na vifaranga wako!

VITAMIN:

Mara kwa mara wape aina zote za matunda na mbogamboga; mapapai, maembe, nazi,

vitunguu maji, pilipili kichaa n.k. Matunda yaliyodondoka na yakaanza kuoza

yatupwe kwenye ngome ya kuku.

Unapowalisha mahindi, usiyasage bali uyaloweke (yale tu utakayowapa kwa siku)

usiku kucha kwenye maji. Kisha mwaga maji asubuhi, na uyaache mahindi kwenye

unyevunyevu na kivulini kwa siku zingine 2 – 3 (yaoshe mara mbili kwa siku) hadi

kimea kifikie sm 3. Halafu wape vifaranga mahindi hayo yaliyoota – yana vitami

nyingi mno!

MADINI:

Wawekee kuku majivu kutoka jikoni na vilevile uwachanganyie na uwape

mchanganyiko wa kilo moja ya udongo mwekundu, chumvi gram 100 na gram 100

za chokaa iliyotiwa maji (slaked lime), ambavyo watavifikia muda wowote wakitaka.

Vilevile wape makaka ya mayai, lakini yawe yamechemshwa sana na kutwangwa, au

kuchemshwa katika jiko la jua, ili kuzuia kusambaza magonjwa.

I. Viuatilifu (insecticides) kwa matumizi ya kilimo:

Epuka vuatilifu vyenye kemikali inapowezekana. Hatari ni kwamba, kama wadudu

watakuwa na sumu, hata ndege wanaowala wanakula sumu. Na sio ndege tu

wanaokufa, ambao hudhibiti ongezeko la wadudu na mbu, lakini kemikali hizi

zinaweza pia kuua watu. Mfano E. 605, au kubaki katika mazingira kwa miaka mingi

mfano DDT.

Viuatilifu vinaweza kuzalishwa kutokana na mwarubaini (Azadirachta indica,

Taz. Sura 5.3), tumbaku (Nicotiana tabacum, sura 6.34) na tephroson (Tephrosia

vogelii, sura 6.46). Madhara ya tumbaku na tephrosia ni kwamba wadudu wote

wanauwawa hapo hapo, na mimea iliyonyunyiziwa dawa haiwezi kuliwa hadi wiki

mbili zipite.

Mwarubaini una sumu kidogo na mtu anaweza kula mboga ambayo

imenyunyiziwa dawa ya mwarubaini moja kwa moja, na wadudu wenye manufaa

kama vile nyuki watakaotua kwenye mimea hawafi.

Page 72: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

72

SURA YA 5

UTANGULIZI Sura hii ina maelezo ambayo tunayapendekeza sana. Tunawatia moyo kupanda na

kutumia mimea hii 15 ya dawa; ni mimea yenye manufaa na ina matumizi mengi.

Karibu mimea yote hii hutumiwa na viwanda vya madawa barani Ulaya kutengeneza

mazao ya biashara, ambayo wakati mwingine huuzwa barani Afrika kwa bei kubwa.

Ili kuchagua tiba iliyo bora kwa ugonjwa fulani, tafadhali rejea sura ya 8. Katika

sura hiyo mimea na michanganyiko yake vimeelezwa, kwa mjibu wa uzoefu wetu, na

kwa kufuata nguvu za madawa yenyewe.

Kwa kutumia mimea hii, hata familia masikini zinaweza kutengeneza dawa na

kutibu magonjwa fulani wao wenyewe kwa gharama ndogo sana.

Kwa hiyo tunapendekeza uanzishe bustani ya dawa, ambayo ni yako mwenyewe,

ukianza na mimea hii 15. Na utaweza kutumia mimea hiyo chini ya mwaka1 tangu

kusiha au kupanda.

Katika sura hii, tunaorodhesha mimea kwa kufuata alfabeti, na kwa mjibu wa

majina yake ya kilatin, (majina ya kisayansi).

Kwa kila mmea tumetoa:

Maelezo ya kibotania

Baadhi ya vidokezo namna ya kulima

Sehemu za mimea zinazotumika.

Baadhi ya matumizi kutoka nchi zingine, hata hivyo sababu ya upungufu wa

uzoefu na ufahamu, hatuwezi tukayapendekeza.

Maelezo ya kina ya magonjwa ambayo tunajua yanaweza kutibika, na maelezo

ya kina ya utengenezaji na usimamizi wa madawa ambayo tuna uzoefu nayo.

Maelezo ya madhara yanayoweza kutokea.

Wafanyakazi wa afya na wahudumu wanaombwa kutoa maonyo ya wazi na yasiyo

ya mzaha, kwamba michanganyiko hii ya madawa haina maana kuwa ni badala ya

darubini au baadhi ya vifaa vya kitaalamu vinavyotumika kwenye vituo vya afya

kupima magonjwa. Pia michanganyiko hii haina uwezo kamwe wa kutumiwa kama

chanjo.

Michanganyiko hii imekusudiwa kuboresha uhusiano mzuri kati ya wagonjwa na

madaktari na wahudumu wengine wa afya. Maelezo haya yanaongeza kwa kiwango

kikubwa tiba zilizopo mahospitalini, vituo vya afya na majumbani. Lakini

TAFADHALI UWE MWANGALIFU. Baadhi ya mimea iliyoelezewa katika kitabu

hiki pia ni sumu, na inaweza kusababisha matatizo makubwa kama utabadili maelezo,

au kutumia isivyotakiwa.

MIMEA 15 MUHIMU - KAZI NA ATHARI ZAKE

Page 73: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

73

5.1 Allium sativum Kitunguu, Swaumu

Maelezo ya kibotania: Familia: Liliaceae Kitunguu swaumu ni zao linalovumilia hali ngumu ya hewa. Huweza kufika urefu wa

sm 30 hadi 90 na kitumba chake huzaa vikonyo kati ya 5 na 15. Asili yake ni sehemu

ya Kaskazini ya dunia na Afrika ya Kusini na sasa vinalimwa pia katika nchi za joto.

UKULIMA

Kitungu swaumu hupendelea udongo wenye rutuba na

laini. Tenganisha vikonyo kwa uangalifu kutoka

kwenye kitunguu, na panda sehemu yenye kivuli kadri

ya sm 5 kwenda ardhini, sm 15 kutoka mstari na sm 30

kutoka mche. Katika hatua za kwanza za ukuaji,

kitunguu swaumu huhitaji maji mengi. Mara mmea

unapoanza kutoa maua, likate ua ili nguvu ya mmea

ielekee kwenye kitunguu (kitumba). Muda wa kuvuna

ni pale majani yanapobadilika kuwa kahawia na

kuanza kunyauka. Viweke vitunguu swaumu vikauke,

kwenye kivuli ambapo kuna mkondo mzuri wa hewa,

na kisha kwa uangalifu pangusa udongo na majani ya

nje (hii ikifanyika katika hali ya unyevu, vikonyo vitaharibika). Tunza kwenye

chombo cha udongo (ili kukinga unyevunyevu).

SEHEMU INAYOTUMIKA: Vikonyo

MATUMIZI KATIKA NCHI MBALIMBALI Kitunguu swaumu ni kiungo muhimu katika chakula kwa sehemu nyingi duniani. Na

katika Misri ya zamani, kililimwa kwa ajili ya miungu!

UTENGENEZAJI WA DAWA ZA KITUNGUU SWAUMU

Asali ya kitunguu swaumu. Jaza jagi la kioo kwa vikonyo vya vitunguu

vilivyomenywa na kukatwakatwa. Halafu mimina asali taratibu ambayo itaingia na

kujaa kwenye mianya iliyo kwenye vikonyo. Weka jagi (gudulia) kwenye sehemu ya

uvuguvugu wa kadri ya 20° C. Kwa muda wa wiki 2 hadi 4, asali itafyonza juisi ya

kitunguu swaumu, na kitunguu kitakuwa tepetepe na kizito. Usichuje, na uitumie

katika muda wa miezi.

Mchanganyiko wa dawa ya kikohozi ya kitunguu swaumu. Twanga kijiko cha

chai kimoja cha vikonyo vya kitunguu swaumu na kiasi kile kile cha sukari au asali.

Tumia hapo hapo, mfano kwa kikohozi.

Mafuta ya kitunguu swaumu. Weka gram 200 za vitunguu swaumu

vilivyomenywa na kupondwapondwa ndani ya gudulia lenye mdomo mpana na

ongeza mafuta ya kutosha ya mzeituni (au mafuta mazuri ya mbogamboga) ili

kufunika. Funga vizuri kabisa gudulia, na likae sehemu yenye ujoto wa kadri ya 20º

kwa siku tatu. Litikise mara chache kila siku. Kisha hifadhi sehemu yenye ubaridi,

bila kuchujwa. Tumia katika muda usiozidi mwezi mmoja.

Dawa ya maji ya kitunguu swaumu. Loweka gram 200 za vitunguu swaumu

vilivyomenywa na kukatwakatwa katika lita moja ya mvinyo kali ya zabibu au

Page 74: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

74

alcohol nzuri 40 – 50% kwa siku 14 katika joto la 20º ndani ya chupa yenye mfuniko

uliobana kabisa. Tikisa chupa mara kadhaa kwa siku. Kamua vipande vya kitunguu

swaumu. Dawa hii hudumu hadi mwaka mmoja.

MAPENDEKEZO YA NAMNA YA KUTUMIA

Kula kitunguu swaumu kisichopikwa – hii ni bora zaidi!

Tumia katika mapishi.

Kula Vitunguu swaumu kwa wingi kwa ajili ya kuzuia magonjwa. Kitunguu

swaumu ni mfano mzuri ambao ni halisi, kwamba chakula chako kiwe ndio dawa

yako, na dawa yako kuwa chakula chako. Hata hivyo, hii ni kweli pale tu ambapo

vitaliwa vibichi, kwa kuwa virutubisho vingi huharibika vinapopikwa. Vitunguu

swaumu vibichi huimarisha mfumo wa kinga. Ulaji wa vitunguu swaumu kwa

utaratibu maalum umeonyesha kupunguza matukio ya matatizo ya moyo, saratani,

shinikizo la damu, mafua na kiharusi.

Tunapendekeza sana kwa Waathirika wa UKIMWI kula vitunguu swaumu vibichi

na kuvitumia katika milo ya kila siku, ili kupunguza matukio ya magonjwa mengine.

Kwa sababu kinatumika nje na ndani kama kisafisha mwili, kitunguu ni muhimu

katika tiba ya magonjwa yote ya kuambukiza: Homa ya matumbo, minyoo, kichocho,

malaria, kusafisha damu n.k. Zaidi, vitunguu swaumu vibichi huimarisha uwezo wa

kukumbuka, kupunguza shinikizo la damu na homa, na kina nguvu dhidi ya kuvimba

kwa arteri na kuwa ngumu (Arteriosclerosis).

Vilevile kitunguu swaumu kina anti-viral na anti-fungal properties.

1. Majipu au majipu yasiyo na midomo na warts

Ponda ponda vitunguu swaumu vibichi, halafu weka mseto ulioponda kwenye jipu,

jipu lisilo na mdomo au mara mbili kwa siku kwa kutandaza kwenye jipu. Anza tiba

hii mapema iwezekanavyo.

2. Ameba

Katakata vitunguu swaumu katika vipande vidogovidogo kisha chukua kijiko 1

kikubwa pamoja na chai mara 3 kwa siku (Usitafune, ili kuzuia harufu mbaya).

Endelea na tiba hii kwa siku tano.

3. Malaria

Katakata kitunguu swaumu vipande vidogovidogo sana. Kisha tumia kijiko1 cha

chakula cha vitunguu viulivyokatwakatwa mara 3 kwa siku, na kunywa lita 2 za chai

ya michaichai kwa siku. Endelea na tiba hii kwa siku tano. Tazama pia chini ya

malaria sura 8.

4. Kisukari, shinikizo la damu, kuzuia arteri kuvimba na kuwa ngumu

(Arteriosclerosis).

Kula vitunguu swaumu kwa wingi – vitunguu swaumu na vitunguu maji hupunguza

kiwango cha sukari katika damu, kiwango cha lehemu katika damu na shinikizo la

damu. Au tumia matone 20 ya dawa ya maji ya kitunguu swaumu mara tatu kwa siku,

lakini hii haina manufaa makubwa.

5. Kikohozi, mafua, madonda ya koo na sinusitis a) Kula kikonyo kimoja cha kitunguu swaumu mara tatu kwa siku.

Page 75: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

75

b) Tumia kijiko kimoja cha chai cha asali ya kitunguu swaumu kila baada ya saa

chache.

c) Watoto wanaweza kutumia kijiko kimoja cha chai cha mchanganyiko wa dawa ya

kikohozi ya kitunguu swaumu kila baada ya saa chache.

d) Tumia kijiko cha chai kimoja cha mafuta ya kitunguu swaumu mara 6 kwa siku.

6. Mtando mweupe mdomoni (fungus)

Tumia kijiko cha chai kimoja cha kitunguu swaumu au asali ya kitunguu swaumu kila

baada ya saa chache. Kaa nayo mdomoni muda mrefu iwezekanavyo.

7. Maambukizi ya mba ikiwemo athlete’s foot. Funika eneo lililoathirika kwa kutumia ama juisi ya kitunguu swaumu kibichi au

mafuta ya kitunguu swaumu

8. Homa ya matumbo na maambukizi mengine

Kwa matatizo ya homa ya matumbo, kifua kikuu, kipindupindu, malale (sleeping

sickness) na bacillary dysentery, daima ongeza vitunguu swaumu katika tiba yako ya

kawaida.

9. Kuzuia damu kugandaganda (thrombosis)

Vitunguu swaumu huifanya damu kuwa laini na huzuia muundo wa damu kuganda

ambako husababisha thrombosis. Na hii ni muhimu zaidi kwa wagonjwa ambao

wamekuwa vitandani kwa muda mrefu.

10. Kwa watoto wanaoota meno

Sugua fizi kwa kikonyo cha kitunguu swaumu.

ATHARI (SIDE EFFECTS)

Vitunguu swaumu vinaweza kuleta mwasho kwa ngozi, hususani baada ya kutumiwa

kwa muda mrefu. Angalia sana kisiingie machoni.

5.2 Artemisia annua anamed (A3)

Maelezo ya kibotania: Familia: Compositae Jamii za porini za Artemisia annua hustawi katika hali ya hewa ya joto dunia nzima.

Artemisia annua anamed ya mbegu mbili tofauti imetokana na mimea ya asili ya

China na Vietnam. Ina ubora kwa kuwa inastawi katika maeneo ya tropiki, hutoa

majani kwa wingi, na majani haya yana artemisinin kwa wingi, kitu ambacho kina

nguvu sana ya kutibu malaria. Mmea huu wa mbegu mbili tofauti hukua hadi kufikia

urefu wa meta 3, lakini haustahimili theluji na unahitaji ukulima wa uangalifu na

makini sana.

UZURI WA ARTEMISIA ANNUA Kwa sababu vimelea vya malaria vimeanza kuonyesha usugu kwa dawa za madukani,

ambazo zimekuwa zikitumiwa kutibu malaria kwa miaka mingi, madawa haya

yanaonekana kupungua nguvu, na mara kwa mara zimeonekana kushindwa kutibu

malaria. Mmea wa Artemisia annua umekuwa ukitumiwa kwa miaka zaidi ya 2000

na Wachina kwa kutibu homa, na hivi karibuni kabisa kutibu malaria. Tumegundua

mmea huu kuwa na mafanikio katika kutibu malaria kama madawa yale tuliyoyazoea,

Page 76: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

76

na bila kuwa na madhara ambayo siyo ya kupendeza. Artemisia annua anamed (A3)

kinaweza kuifanya hospitali, au jamii kupata tiba ya malaria kabisa bila gharama

kinachohitajika tu kufanya kazi kwa bidii na juhudi!

UKULIMA

Mbegu na miche ni midogo midogo sana na miepesi kushituliwa na hali ya hewa.

Inahitaji uangalizi wa hali ya juu. Lazima uandae muda wa kutosha kila siku ikiwemo

Jumamosi na Jumapili.

Kuandaa udongo, changanya sehemu 10 kwa ujazo za udongo uliooza au udongo

mweusi kwa sehemu 10 za ujazo za mchanga. Ongeza sehemu 20 za maji na chemsha

mchanganyiko kwa dakika kama 5 au zaidi kidogo ili kuua mbegu zote za magugu.

Baadaye, kama inapatikana, ongeza sehemu moja ya ujazo ya polystyrene

iliyotwangwatwangwa na plastiki nyeupe inayopatikana kwenye vifurushi vya vifaa

vya umeme, hii hufanya udongo kuwa laini.

Inasaidia sana kutengeneza kitalu kinachobebeka. Hii inaweza ikawa nusu jerry-

can au sahani ya mbao lenye ukingo wa sm 10. Mbegu 1000 zinahitaji meta moja ya

mraba. Jaza sahani udongo wa sm 5 kwa kina. Mwagilia, weka mashimo sehemu ya

chini ya sahani ili kuyawezesha maji ya ziada kutoka. Tawanya mbegu juu ya

udongo. Usizifunike kwa udongo, mbegu zimeshachanganywa na kaolin ambayo

huzifunika kiasi cha kutosha. Artemisia huota ikiwa sehemu yenye mwanga kwahiyo,

weka sahani yako sehemu ya jua la moja kwa moja, Baada ya kati ya siku 4 na 7

majani laini huonekana. Kwa wiki 6 zitakazofuata mwagilia kwa uangalifu mkubwa,

kwa kuyaruhusu maji kuingia kupitia matundu ya pembeni, au kwa kuweka sahani

kwa dakika chache ndani ya sahani kubwa lenye maji ili maji yaingie kwa kupitia

chini. Pandikiza miche inayokuwa pamoja kwa karibukaribu sehemu iliyosafi

kwenye sahani ya mbegu kwa kutumia kikoleo au kibano. Wakati miche inapokuwa

na urefu wa sm 3, hii itakuwa kama wiki sita baada ya kusiha, pandikiza kwenye

vyungu na kisha itakapofikia urefu wa sm 15, kadri ya wiki 10 baada ya kusiha,

pandikiza sehemu za wazi kwenye udongo.

Udongo huo lazima uwe na rutuba na laini

jinsi ulivyo. Kwa hiyo kwanza changanya

udongo na matawi, majani, vijiti n.k.

Weka meta moja ya mraba kwa mmea

moja hadi mitatu. Kama msimu wa kiangazi

umekaribia chini ya miezi minne au mitano,

unaweza kupanda karibu karibu. Msimu wa

kiangazi ni mkali kwa mimea, mimea huanza

kutoa maua, na lazima ivunwe haraka hapo

hapo. Changamoto ni namna ya kuitunza

mimea bila kutoa maua kwa muda mrefu

iwezekanavyo! Mara tu maua ya kwanza

yanapoonekana, vuna majani kutoka kwenye

shina (matawi) ya mmea wote na uyakaushe.

Matawi na mashina yaliyobaki yanafanywa

kuwa mbolea.

Page 77: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

77

Kutoka kwenye mimea iliyo hai, unaweza ukachukua vipande kwa kukata,

ukapanda mimea zaidi na hata wagonjwa zaidi kutibiwa, na mimea hii inaweza

kusambazwa kutoka mwaka mmoja hadi unaofuata. Tunapendekeza kwamba

uchukue vipande vya kukata kila mwezi, na kuvipanda katika sehemu tofauti tofauti.

Kwa njia hii kuna uwezekano mdogo wa mimea yako kutoa maua kwa wakati moja.

Na vilevile, utajifunza ni wapi mimea inastawi vizuri zaidi.

Kwa kichukua vijiti kuna njia tatu:

Njia ya kwanza: Kata matawi katika vipande vifupivifupi kwa kutumia wembe. Mmea „mama“ lazima

uwe wenye afya na wenye umri wa miezi 2 – 4. Usiwe unakaribia kutoa maua (vijito

vyote vitakuwa vinatoa maua moja kwa moja).

Kila kijito kiwe na vikonyo viwili.Ondoa majani yote ya sehemu ya chini.

Kwenye katawi ka pembeni usiondoe majani yake.

Chukua chombo cha aina yo yote na ukijaze na maji. Funga gunia an wavu juu

yake. Ingiza vipande vifupivifupi kwenye gunia au wavu – sehemu ya chini iwe

majini.

Unaweza kuongeza virutubisho vya aina yo yote kwenye maji. Maji yakianza

kunuka vibaya, yabadilishwe. Weka chombo juani. Baada ya wiki 2-4 vijito huanza

kupata mizizi.

Njia ya pili:

Andaa kitalu kama ilivyoelezwa juu. Weka vipande vifupivifupi ardhini (vilazwe

kidogo ili kurahisisha uotaji wa mizizi). Weka kitalu mahali penye mwanga na jua.

Njia ya tatu: Mmea ukifikia urefu wa sm 50 vitawi vyote vya chini vikatwe nusu kwa kutumia

wembe. Kunja vitawi palipokatwa na uviweke ardhini. Weka jiwe juu yake ile vitawi

vibaki vilivyowekwa. Baada ya wiki nne mizizi itkuwa imeota. Ondoa vijiti kwenye

mmea „mama“ na uvihamishie mahali pengine.

Kutoka mmea mmoja tu, kadri ya miezi miwili kabla ya kuanza kwa msimu wa

mvua unaweza ukapata vipande vya kupanda hadi 1000! Kama kila mmea wa vijiti

hivi utazaa mmea wenye urefu wa meta moja, kila mmea utatoa angalau 200g za maji

yaliyokaushwa. Kutoka kwenye mimea 1000 tunaweza tukapata kilo 200. Wakati kila

tiba ya malaria inahitaji kama gram 35, hii itatosha kwa wagonjwa 5,714 ambao ni

watu wazima – na hii ni kutoka kwa mmea “mama” mmoja tu!

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Majani, kwa majani mabichi, uzito unaotakiwa ni

mara tano zaidi.

MAPENDEKEZO YA JINSI YA KUTUMIA

1. Malaria Kufuatana na dozi zilizotolewa ndani ya jedwali chini, tengeneza infusion kwa

kumimina maji ya moto kwenye majani makavu ya A3, acha yapoe kwa dakika 15

halafu chuja. Gawanya chai itakayopatikana kwa sehemu 4 zilizosawa, na kunywa

kila baada ya saa 6 (maana yake utakunywa mara 4 kwa siku) (Unahitaji kipimo

kizuri! – au gram 5 ni kiasi ambacho kinatosha kabisa, kikibanwa vizuri, katika mm

35 za kikaratasi chembamba cha plastiki). Unaweza kutumia gram 25 za majani

mabichi badala ya gram 5 za majani makavu.

Page 78: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

78

Dozi ya Artemisia annua (chai) kwa kutibu malaria

Umri Ujazo wa chai Majani makavu uzito

Watu wazima Lita 1 gram 5

Watoto zaidi ya mika 13 ml 500 gram 4

Watoto zaidi ya miaka 11 ml 500 gram 3

Watoto zaidi ya miaka 7 ml 500 gram 2

Mpe dozi hii kwa siku 7. Kama katika eneo lenu, homa karibia hurudi katika muda

wa wiki 3, kuna mambo mawili katika tiba. La kwanza ni kutumia chai ya Artemisia

kwa jumla ya siku 12. Na la pili ni kutumia chai ya Artemisia kwa siku 7, na katika

siku ya tatu ya tiba kunywa vidonge 3 vya Fansidar (SP) au dawa nyingine ya malaria

inayotumika. Chai ya Artemisia inaweza kufanywa tamu kwa kuweka sukari au asali.

Wajawazito wasitumie chai ya Artemisia, hasa hasa miezi ya kwanza ya ujauzito.

Watoto wadogo wapewe chai ya Artemisia chini ya usimamizi na ushauri wa daktari.

DOKEZO: Unaweza kuifanya chai hii kuwa na nguvu zaidi kwa kusaga majani makavu kabla ya

kumimina maji ya moto juu yake. Uache mchanganyiko utulie kwa dakika 15.

Usichuje, ila tikisa na kunywa mchanganyiko wote.

2. Bawasiri (Haemorrhoids) Tokosa kwa kuchemsha kijiko 1 cha chai (kiasi cha gram1.5) cha majani kwa lita

moja ya maji kwa muda wa dakika 10. (Tazama tofauti kutoka maelezo namba moja

juu). Acha utulie kwa dakika zingine 10, chuja na kunywa kwa vipindi kwa siku

moja.

3. Kuvimba kwa utumbo mkubwa (Colitis)

Fuata mchanganyiko No. 2, lakini tumia gram 5 za majani makavu. Tiba itolewe kwa

muda wa wiki tatu na sio zaidi.

4. UKIMWI Wagonjwa wa Ukimwi wana upungufu wa kinga ya cellular na kinga ya humoral

iliyo juu. Artemisinin huongeza kinga ya cellular na kupunguza kinga ya humoral na

tayari ni dhahiri kwa matumizi kwa wagonjwa wa UKIMWI. Kwa hiyo,

tunapendekeza kwamba wagonjwa wa UKIMWI wanywe chai ya mchanganyiko

namba moja, kwa kutumia gram 5 kwa siku kwa kipindi cha mwezi mmoja, au gram

moja kwa siku kwa kipindi cha miaka kadhaa

5. Kichocho

Maelezo ni kama yale ya malaria.

6. Magonjwa ya macho na conjunctivitis macho mekundu)

Tengeneza chai kama ilivyoelezwa kwa bawasri juu. Chuja kwa karatasi, na loweka

vitambaa viwili visafi kwenye chai uliyochuja. Badala ya kupoa, weka kitambaa

kimoja kwa dakika 10 kwa kila jicho na kitambaa chake.

7. Mtando mweupe mdomoni (Candida) Daima tafuna majani safi ya Artemisia kabla ya mlo. Unapokwenda kulala, weka

majani kadhaa mdomoni kwenye mashavu.

Page 79: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

79

8. Kikohozi, mafua na sinusitis Vuta mvuke kutoka kwa chai ya moto ya Artemisia kwa dakika kumi mara tatu kwa

siku. Kama ikiwezekana, chai isiwe na joto kali wakati wa kuvuta mvuke.

9. Majipu

Kwa jipu lililo wazi, osha majani kidogo na yachemshe katika maji kidogo kwa

dakika 20. Twanga na weka kwenye jipu. Kwa majipu yaliyoziba: Weka majani

mabichi yaliyotwangwa, mara mbili kila siku.

Kama dawa ya kuzuia magugu

Jaribu kusambaza majani ya Artemisia kwenye ardhi – yanaweza kuzuia kuota kwa

magugu.

10. Kutengeneza kinywaji cha afya cha kuburudisha! Chukua ml 50 za chai ya Artemisia iliyotengenezwa kama ilivyoelezwa kwenye

mchanganyiko No.2 juu, ongeza ml 950 za maji baridi, juisi ya limau mbili na gramu

50 sukari. Koroga vizuri. Kinywaji hiki na mbadala mzuri wa soda ya dukani.

ATHARI Kwa matumizi ya kunywa, kwa kufuata dozi sahihi, hakuna madhara yanayoeleweka.

Kwa matumizi ya nje inaweza kusababisha kuwashwa.

5.3 Azadirachta indica Mwarobaini

Maelezo ya kibotania: Familia: Meliaceae Mti wa mwarobaini ni wa kijani na hukua hadi kufikia urefu wa meta 25 hadi 30. Na

kwa kawaida huanza kutoa matunda

baada ya miaka 3 hadi 5, na hufikia

kiwango cha juu cha uzaaji baada ya

miaka 10. Katika hali ya hewa iliyo

nzuri, mti mmoja utatoa kiasi cha kilo 50

za matunda kwa mwaka na kilo 350 za

majani ya kijani. Kilo 50 za matunda

hutoa kilo 30 za mbegu ambazo zina

uwezo wa kutoa mafuta kilo 6 na

mashudu kilo 24. Mti wa mwarobaini

huishi kati ya miaka 100 na 200 na

huweza kufikia urefu wa meta 30 na

upana wa meta 20.

Mwarobaini mara nyingi hutumiwa

kwa kuimarisha misitu na ni mzuri kwa

mbao za kujengea, sababu

haushambuliwi na mchwa. Mti huu

ambao hukua haraka hupatikana barani Afrika, Asia na Amerika kusini.

Mbegu kavu za kutokana na matunda husagwa na kukamuliwa ili kupata mafuta.

Katika majaribio kwa wanyama mafuta ya mwarobaini na mashudu yalionyesha

Page 80: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

80

kuwa na nguvu ya antidiabetic, antibiotic (mfano dhidi ya kifua kikuu), antiviral,

diuretic, spermicidal effects. Vilevile yana nguvu dhidi ya protozoans (malaria,

malale). Yanapunguza homa na huzuia mzio (anti-allergic).

Kwa matumizi ya kilimo, vinatilifu hutengenezwa mbegu au majani (Tazama

chini). Wadudu wanaotua katika mafuta au mashudu ya mwarobaini hawafi hapo

hapo, tofauti, kwa mfano, baada ya kutumia kinatilifu cha tephrosia au tumbaku

(Tazama sura 4.11) lakini huharibiwa tu ule utaratibu wao wa maisha na kufa katika

muda wa siku chache. Na kwa wadudu wengine, vinatilifu vya mwarobaini hutumika

kama kifukuza wadudu, hivyo wadudu hukaa mbali. Mimea iliyopuliziwa dawa ya

mwarobaini ni mara chache hutokea ikashambuliwa na wadudu. (Hata litokeapo

balaa la nzige miti ya mwarobaini hubaki salama).

UKULIMA

Mwarobaini ni bora zaidi ukapandwa kutokana na mbegu zake. Chagua mbegu nzuri

– mbegu zitaota iwapo tu hazizidi umri wa miezi mitatu. Weka mbegu juu ya gazeti

lililolazwa juu ya plastiki kivulini, na uzinyunyizie maji kila siku ili zikae na

unyevunyevu. Badilisha gazeti kila baada ya siku mbili. Baada ya siku 4 – 7 mbegu

hupasuka na kuanza kutoa. Panda kwenye mchanganyiko wa udongo 50% na samadi

ya ng’ombe iliyooza vizuri ndani ya mifuko ya plastiki. Upande miche kwenye

sehemu ulizozitarajia baada ya miezi mitatu.

Kupanda miti kutokana na matawi: Chukua kitawi kidogo na majani yake (cha

mwishoni) na kichomeke kwenye udongo wenye unyevunyevu.

Miti hii inaweza kupandwa kwenye miteremko ya milima, ardhi isiyo na rutuba,

pembeni ya barabara au sehemu yenye mawe yasiyoenda chini sana.

Mwarobaini unastawi katika nyanda za chini na vilevile katika nyanda za juu,

kwenye mchanga, mawe mawe au hata udongo tifutifu. Inastawi vizuri katika hali ya

hewa ya unyevu wa muda mrefu, lakini miti hii inaweza kuhimili vipindi virefu vya

ukame.

Mwarobaini una uwezo wa kustawi katika ardhi yenye tindikali (acid) ambapo pia

utasaidia kupunguza acid kwa majani yale yanayoanguka na kuoza.

SEHEMU ZINAZOTUMIKA

Majani, mbegu, vitawi, mafuta ya mbegu.

Ili kupata mafuta ya mwarobaini, twanga mbegu kavu, kisha ongeza maji kidogo

ili kupata kama ujiuji mzito. Baada ya kufinyanga kwa muda mfupi, mafuta huanza

kuvuja.

MATUMIZI KATIKA NCHI NYINGINE. India: Mafuta yanatumika kwa wenye minyoo (kwa ndani) na pombe ya majani kwa

malaria na maumivu ya viungo. Nchini India pia watu huoga kwenye maji ya moto

ambamo majani ya mwarobaini yalikuwa yamelowekwa, ili kutibu aina zote za

maambukizi ya ngozi. Kazi ya mwarobaini kama dawa ya malaria imerekodiwa

katika vitabu vya Ayurveda kuwa imekuwa ikitumika tangu mwaka 2000 BC (miaka

2000 kabla ya Kristo). Jina lake katika Ki-suahili lina maana arobaini, sababu ya

madai kwamba unaweza kutibu magonjwa mengi sana . Nchini Uingereza dawa ya

meno ya mwarobaini iko madukani.

Page 81: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

81

Nchini Congo (Kinshasa) na Angola, mmea ufananao na mwarobaini Melia

azedarach (Tazama 6.31) mara kwa mara huitwa mwarobaini ki-makosa. Mmea huu

ni mzuri, huweka matunda baada ya mwaka mmoja tu; na kwa ishara namba 5-10

chini, ama ni mzuri au ni bora kabisa. Hata hivyo, kwa viashirio

1- 4, Melia azedarach ni vizuri uepukwe kwa sababu una sumu zaidi. Baadhi ya

tofauti kati ya miti hii miwili ni:

Mwarobaini

(Azadirachta indica) Melia

(Melia azedarach)

Mbegu Ndefu Duara

Maua Meupe Pinki hadi violet

Majani Pinnate Bipinnate (branched)

MAPENDEKEZO YA JINSI YA KUTUMIA

MUHIMU: Katika maelezo yote haya, tunapoongelea jani, tuna maana ya jani moja

dogo tu. Hivyo, picha katika ukurasa wa inaonyesha majani 10 kwa mujibu wa

maelezo yetu.

1. Malaria

Mimina lita moja ya maji ya moto kwenye majani 40 mabichi, au gram 5 za majani

makavu na kunywa chai yake kwa siku moja. Isitumiwe na wamama wajawazito.

2. Kuzuia meno kuoza. Sugua meno yako kwa kitawi kidogo cha mwarobaini mara mbili kwa siku. Njia hii

sio tu kwamba inasafisha meno, lakini pia ina – kufuatana na baadhi ya vitu

vilivyomo kwenye gamba la mwarobaini – nguvu ya kushambulia bacteria

wanaoozesha meno.

3. Sleeping sickness (Trypanosomiasis) (Malale)

Toa tiba ya kawaida kwa kunywa chai ya majani ya mwarobaini kila siku (Tazama

maelezo No. 1 juu)

4. Chawa wa kichwani Osha nywele zako kila siku. Tumia kimoja kati ya vifuatavyo:

i) Weka gram 10 za majani makavu ya mwarobaini ndani ya ml 100 za kileo

(pombe) (45%, mfano gin au vodka) kwa siku 7. Chuja, na tumia kama lotion ya

nywele mara tatu kwa siku muda wa siku tano.

ii) Paka matone kidogo ya mafuta ya mwarobaini kwenye nywele, mara tatu kwa

siku, muda wa siku tano.

iii) Twanga mbegu kidogo za mwarobaini ili kutengeneza kitu kama uji mzito. Kila

jioni, baada ya kuosha nywele paka kama kijiko kimoja cha chai kwenye nywele

na uziache na dawa hivyo hivyo hadi kesho yake jioni.

5. Matatizo ya ngozi Mwarobaini ina nguvu ya kutibu magonjwa yaliyo mengi ya ngozi kama vile acne,

magonjwa yaletwayo na mba (fungus), psoriasis, upele (scabies) na eczema.

Mwarobaini unaweza kutumika pia kutibu matatizo ya mzio (allergy).

Unaweza:

Page 82: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

82

Kuoga: Kijadi watu wa India walioga kwenye maji ya moto yakiwemo majani

ya mwarobaini.

Dawa ya mafuta ya kutengeneza: Chukua gram 100 za mafuta ya

kujitengenezea (ya dawa) na ongeza gram 10 za mafuta ya mwarobaini.

Tengeneza dawa ya maji: Loweka gram 20 za majani makavu kwenye ml 100

za kileo 70% (kilicho au ambacho hakikuharibiwa tabia uasili). Baada ya wiki

moja, chuja huo mchanganyiko. Punde kabla ya kutumia, changanya kijiko 1

cha chai cha dawa hii ya maji kwa kijiko kimoja cha chai cha mafuta ya

mbogamboga na paka kwenye sehemu iliyoathirika.

a) Athlete’s foot: Ama sugua kwa majani eneo lililoathirika au kwa dawa ya

maji/mchanganyiko wa mafuta.

b) Tiba ya ngozi kwa ndui au tetekuwanga: Mafuta ya mwarobaini au dawa ya

maji ya mwarobaini inaweza ikatoa tiba ya anti-viral kwa ndui na tetekuwanga.

Hii ni kwa sababu ina uwezo wa kuzuia virus kuendelea kusambaa.

c) Warts: Paka mafuta moja kwa moja kwenye ngozi.

d) Scabies (aina fulani ya upele): Kuna njia nyingi za kufanya

i) Twanga majani na maji kidogo hadi yalainike, na kisha paka kwenye sehemu

iliyoathirika.

ii) Paka mafuta ya mwarobaini sehemu iliyoathirika.

iii) Saga hadi kuwa ujiuji mchanganyiko wa majani mabichi ya mwarobaini na

dawam mchuzi kwa uwiano wa 4-1 kwa uzito (au kiganja kimoja cha majani

ya mwarobaini kwa kipande cha dawam mchuzi ½ ya urefu wa kidole cha

shahada). Paka mwili mzima na uache ikauke.

e) Scrofula, indolent ulcers, ringworm, psoriasis.

Tumia mafuta ya mwarobaini. Kama yana nguvu sana changanya na mafuta ya

mbogamboga. Badala yake: Chemsha majani kidogo katika maji ya kutosha kwa

dakika 15, na kisha laza majani yakiwa bado na joto juu ya kidonda kwa dakika

15 asubuhi na jioni. Baadhi wanapendekeza pia tiba hii kwa vidonda vya wakoma,

lakini fuata ushauri wa daktari.

f) Majeraha ya kuungua yenye maambukizi

Chemsha kiganja kimoja cha majani mabichi kwenye lita moja ya maji kwa

dakika 20, chuja ikiwa bado ya moto (kuzuia maambukizi), poza, na itumie

papohapo kusafisha kidonda. Tengeneza na tumia chai hii kwa njia hii mara tatu

kwa siku. Mgonjwa akae ndani ya chandarua ili kuepuka maambukizi mapya.

g) Majipu: Kama majipu hayajatoa midomo, dawa ya kubandikiza ya majani inaweza

ikatumika. Kwa majipu yaliyo wazi, ulcers na eczema majani lazima yachemshwe

vizuri katika maji kidogo kabla ya kutumiwa kama dawa ya kubandika.

h) Fungus za mdomoni (candida)

Changanya sehemu moja ya mafuta ya mwarobaini kwa sehemu tisa za vitu

vifuatavyo:

Kwa candida ya mdomoni: asali

Kwa candida ya ukeni: mafuta ya mbogamboga au yoghurt.

Kwa candida ya ngozi: mafuta ya mbono au mafuta yoyote ya mbogamboga.

Page 83: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

83

Tumia mchanganyiko huu kupaka eneo lililoathirika.

6. Kuhara na kuhara damu: Kwa siku tayarisha chai ya majani ya mwarobaini kwa kuchemsha majani 40

mabichi na yaliyo safi kwenye kikombe kikubwa cha maji kwa dakika tano. Watu

wazima wanywe chai hii kwa siku moja, huku wakinywa maji ya aina nyingine

kwa wingi. Endelea na tiba hii kwa siku tatu. Daima ongeza ORS (Tazama sura

4.6).

7. Kilimo: Vinatilifu kutokana na matunda Vuna matunda yaliyoiva, ondoa mnofu, osha mbegu na uzikaushe kabisa juani.

Tunza kwenye gunia linalopitisha hewa. Kwa kudhibiti maradhi, twanga kikombe

kimoja cha mbegu na uziweke ndani ya lita moja ya maji kwa saa sita. Chuja na

pulizia, au nyunyizia mchanganyiko huo kwenye mimea ya shambani siku hiyo

hiyo, kwa sababu haidumu muda mrefu. Rudia tena kuweka dawa baada ya siku

sita. Ili kuzuia maradhi kwa mazao yako, tumia mchanganyiko ufuatao (chukua

nusu kikombe cha mbegu kwa lita moja ya maji) kwa mimea yako kila wiki.

8. Kinatilifu kutokana na majani Kama hakuna matunda, chukua kilo moja ya majani mabichi na chemsha kwa

dakika 10 ndani ya lita 5 ya maji, acha ipoe kwa saa 3, chuja na tumia.

9. Dawa ya kupulizia wadudu

Maelezo kwa mchanganyiko wa kupulizia ndani ya nyumba: Saga gram 100 za

mbegu kavu za mwarobaini, hadi kuwa unga, mimina ml. 500 za kileo –kikali (au,

kama hakipo, mafuta ya taa) juu yake, hifadhi ndani ya chombo kilichofungwa

vizuri kabisa kwa siku 10. Kisha chuja mara mbili kwa kutumia karatasi (paper

strainer) na jaza kwenye bomba la kupulizia.

10. Kama dawa ya kuhifadhi chakula

Kwa vyakula kama vile mpunga, maharage au mahindi changanya vitawi

vidogovidogo pamoja na majani gram 250 za majani makavu, changanya na kilo

moja ya majivu makavu na weka mchanganyiko huu katika kilo 50 za chakula

ulichokihifadhi. Osha chakula kabla ya kutumia.

11. Dawa ya kufukiza (au insectifuge) Ili kufukuza wadudu kutoka ndani ya nyumba, weka majani ya mwarobaini

kwenye mkaa wa moto (unaowaka).

12. Kwa kupiga vita nematodes (minyoo wenye madhara wasioonekana waishio

ardhini) Weka majani kidogo ya mwarobaini pamoja na miche au mbegu kwenye mashimo

uliyoandaa kwa kupanda.

ATHARI: Baada ya matumizi ya ndani (kunywa) ya muda mrefu, hali ya kusikia moto

(irritation) kwenye maini au mafigo inaweza kutokea. Kwa sababu ya uzoefu mdogo

kwa mmea huu, matumizi ya kunywa hayapendekezwi kwa wajawazito.

Page 84: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

84

5.4 Capsicum frutescens Pili-pili

Maelezo ya kibotania: Familia: Solanaceae Mmea huu hufikia urefu wa meta 2. Matunda yake ni madogomadogo, sm 1-2 urefu

na sm 0.5 upana. Huanza kwa kuwa kijani,

na huwa nyekundu kabisa zinapoiva.

Dawa iliyopo inaitwa capsaicine.

UKULIMA

Hupendelea ardhi yenye rutuba na tifutifu

na iwe juani. Huhitaji joto la chini

lisilopungua 18-21º C. Bora ikapandwa

kutokana na mbegu (kusiha), kwa

kusambaza gram moja kwa meta moja ya

mraba. Panda kwa nafasi sm 40 katika

mistari sm 60 mbali kutoka mche. Vuna

baada ya miezi minne.

SEHEMU ZINAZOTUMIWA: Matunda, majani.

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE Sehemu mbalimbali duniani pilipili

hutumika kutibu maumivu ya viungo.

Katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo

inatumika zaidi kwa maumivu ya meno na

tumbo. Visiwa vya Hawaii inajulikana

sana kwa tabia ya kushambuliwa bacteria (bactericidal properties). Nchini

Cameroon na Kusini mwa bahari ya Pacific, pilipili inatumika kienyeji kwa

magonjwa ya ngozi.

MAPENDEKEZO JINSI YA KUTUMIA

Pilipili, pamoja na mapapai, ni mojawapo ya vitu vyenye nguvu na kwa hiyo kufanya

ni dawa zinazouzwa sana za mimea. Nchini Uswisi unakuta kuna aina kama sita

tofauti za mafuta ya dawa kwa maumivu ya kuvimba kwa viungo (rheumatic

arthritis) zikiwa na dawa itokanayo na Capsicum frutescens. Mafuta yatokanayo na

majani na matunda yanaonyesha uwezo wa kusafisha tumbo, mfano, dhidi ya

schistosoma mansoni, kimelea kisababishacho kichocho.

Na inadhaniwa kwamba Wathailand, ambao chakula chao huwa na kiasi kikubwa

cha pilipili, mara chache sana hushambuliwa na matatizo ya moyo sababu ya

fibrinolytic action (huyeyusha damu inayoganda ) ya kimeng’enya (enzyme)

capasaicien.

1. Maumivu ya viungo (baridi yabisi/ rheumatism); kuteguka, maumivu ya

misuli, kuvimba kwa viungo (arthritis), maumivu ya kiuno, na kuuma kwa

mshipa wa nyuma wa paja.

Nyumbani: Twanga kijiko kimoja kikubwa cha pilipili mbichi au kavu na kijiko

kimoja kikubwa cha mafuta ya mbogamboga. Mchue mgonjwa kwa mchanganyiko

Page 85: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

85

huu kwa nguvu sana hadi asikie maumivu. Na uendelee kuviweka viungo katika hali

ya joto.

Mahospitalini: Tazama sura 4.3 “Mafuta kwa maumivu ya viungo” na sura 4.4.

“Mafuta ya dawa kwa maumivu ya viungo,” Tazama vilevile picha ya jalada.

2. Aina ya kisukari cha miguu (diabetic feet) Tumia maelezo namba 1 juu, lakini tibu miguu kwa uangalifu mkubwa. Usichubue

ngozi.

3. Maumivu ya miguu

Changanya vitu vifuatavyo:

Pilipili (iliyosagwa) kijiko 1 cha mezani.

Unga (mfano, wa muhogo) kijiko 1 cha mezani.

Mafuta ya mbogamboga vijiko 3 vya mezani.

Koroga ili kupata ujiuji. Halafu sambazia kwenye kipande cha nguo na kisha fungia

kwenye sehemu ya miguu iliyoathirika. Ili kuepuka kuwashwa ondoa kitambaa baada

ya saa 12 – 24.

4. Tumbo kujaa hewa (flatulence) na bawasiri (haemorrhoids)

Ongeza pilipili katika chakula chako. Ndiyo, hata kwa matatizo ya bawasiri! Sababu

ni kwamba bawasiri mara kwa mara huzidi sana kwa sababu ya fungus katika

matumbo, na hawa fungus huuawa na pilipili.

5. Magonjwa ya ngozi, mkanda wa jeshi (herpes zoster)

Tumia mafuta ya pilipili au dawa ya mafuta ya pilipili kwa kiasi ambacho mgonjwa

atakuwa bado ana uwezo wa kuvumilia maumivu.

6. Kupunguza uchungu wakati wa kujifungua Mama hupewa tunda moja la pilipili, la kuweka katikati ya meno wakati wa

kujifungua. Mawazo yake yatahama kabisa kutoka eneo la tumbo na kuhamia

mdomo.

7. Nywele kutoka (hair loss) Tumia madini (udongo unaoponya, sura 4.5)! Ili kuboresha mzunguko wa damu

kwenye ngozi ya kichwani, kaa kwenye kiti na lazia kichwa nyuma; msaidizi achue

ngozi ya kichwa kwa uangalifu kwa kutumia mafuta ya maumivu ya viungo (sura

4.3) na yaoshwe na kuondolewa baada ya dakika 30. Angalia sana mafuta haya

yasiingie machoni, yafunike!

8. Uhifadhi (preservation) Kwa dawa za mafuta pilipili hufanya kazi kama natural preservative.

ATHARI: Tahadhari! Capsaicine ni kitu chenye uwezo mkubwa wa kushambulia ngozi kati ya

mimea mingi. Daima nawa mikono yako mara baada ya kutengeneza au kutumia

dawa yenye Capsicum frutescens. Epuka kugusa macho, pua, sehemu za siri au

vidonda na majeraha. Capsaicine inaweza ikasababisha upofu kama itaingia

machoni. Unapotoa dawa, hakikisha kwamba unamtarifu kila mtu aliye karibu.

Page 86: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

86

5.5 Carica papaya Papai

Maelezo ya kibotania: Familia: Caricaceae

Papai ni tunda la jadi na

mmea wa dawa. Hurefuka

hadi kufikia meta 7 kwenda

juu. Mpapai umetokea nchi za

tropiki za Amerika na sasa

unapatikana katika maeneo ya

joto duniani kote, ambapo

ardhi ina rutuba ya kutosha.

UKULIMA Kuna mapapai ya kiume

(hayazai matunda) na ya kike.

Weka mbegu 3 kwa pamoja

katika shimo na baadaye

ondoa miche ya kiume. Papai

moja la kiume linatosha kwa

mapapai 10 – 20 ya kike.

Panda pamoja na vitu vinavyooza au mbolea iliyooza. Panda mapapai mengine kila

miaka 4 -5 kabla hayajarefuka sana kiasi cha kushindwa kuyafikia matunda kwa

urahisi.

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Matunda mabichi na yaliyoiva, mbegu, maua,

majani, mizizi.

MATUMIZI KATIKA NCHI NYINGINE Mpapai wenyewe tu ni duka la madawa. Maelezo juu ya matumizi yake katika

maeneo mbalimbali yanaweza yakajaza kwa urahisi kitabu. Hapa kuna mifano

machache: Barani Ulaya na Asia papai linatumika kutibu minyoo na kuhara damu.

Barani Afrika, kikohozi, kuhara damu, malaria, kisonono, kifua na matatizo ya ini.

America, maw worm, amoeba na pumu. Juisi ya papai bichi imesajiliwa ndani ya

United States Pharmacopoeia 1985 kwa matumizi ya majeraha yaliyoingia hadi

kwenye mfupa.

NAMNA YA KUTUMIA Sehemu zote za mmea zina vitu vyenye thamani ya dawa, kama vile flavonoids,

antibiotics, fungicides, vitamini, na vimeng’enya. Kimeng’enya papaine kinajulikana

kimsingi kama kiua – minyoo; kinapatikana katika sehemu zote za mmea, hususani

katika mbegu za tunda lililoiva au kwenye mnofu wa tunda bichi.

1. Kusafisha majeraha machafu

Safisha vidonda vichafu kwa “maji yaliyodondoshewa juisi ya papai bichi”: Maji

yaliyochemshwa yakapoa pamoja na matone kidogo ya papai bichi ambalo bado liko

mtini. Ili kupata utomvu (juisi) kwanza osha tunda vizuri kabisa, kisha chana chale

kuelekea chini kwa papai hilo bichi. Kinga matone ya utomvu mweupe kwa kijiko au

Page 87: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

87

kikombe kisafi. Kisu na kijiko vitakavyotumika visiwe na kutu, kwa sababu kutu

huharibu papaine.

2. Minyoo Papaine hufanya kazi kwa ujumla, lakini kwa viwango tofauti, kwa kuondoa aina

mbalimbali za minyoo ya tumboni, na hata tegu. Utomvu (latex) hugemwa kwa

kukata chale kwenye tunda bichi ambalo bado liko mtini.

DOZI YA UTOMVU WA PAPAI BICHI KATIKA KUTIBU MINYOO

UMRI (MIAKA) IDADI YA VIJIKO VYA CHAI

Miezi 6 – hadi mwaka 1

Mwaka 1 – 3

Miaka 4 – 6

Miaka 7 – 13

Miaka 14 na kuendelea

½

1

2

3

4

Dawa hii hutolewa mara moja, nyakati za asubuhi kabla ya kula chochote, pamoja na

dawa ya kuharisha (kulainisha choo) (mfano, tazama 5.6). Tiba ya minyoo inaweza

kutolewa hata kama mgonjwa anaharisha. Papaine haiondoi minyoo yote, kwa hiyo

tunapendekeza kurudiwa kwa tiba hiyo baada ya wiki moja kama hatua ya tahadhari.

3. Kama dawa ya kuzuia minyoo na ameba Tafuna kipande cha jani la papai (ukubwa: sm 5 × sm 5) kila siku, au kula kijiko cha

mezani kimoja cha mbegu. Minyoo huonekana kuchukia zaidi ladha hiyo hata kuliko

binadamu na minyoo watatoka! (Mfanyakazi mmoja wa kike huko mashariki ya

Congo – Kinshasa, ambaye mara kwa mara alikuwa akisumbuliwa na ameba, aliweza

tu kuendelea na shughuli zake kwa sababu ya tiba hii!).

4. Upungufu wa Vitamini A, B, na C. Kula kwa wingi mapapai yaliyoiva ili kuimarisha kiwango cha vitamin; vitamin A

kwa kusaidia macho kuona, vitamin B kwa mishipa ya fahamu, vitamin C kusaidia

mfumo wa kinga dhidi ya maambukizi.

5. Matatizo madogo ya kuhara kunatolewa na ameba (amoebic dysentery)

a) Mizizi na majani inajitosheleza yenyewe bila kuongeza chochote: Osha vizuri

na katakata kiganja kimoja cha majani ya mpapai. Ongeza lita moja ya maji,

chemsha kwa dakika 5 na acha ipoe kwa robo saa. Chuja na kunywa kwa siku

moja, Au

b) Tafuna kijiko kimoja cha chai cha mbegu za papai mara 3 kwa siku kwa siku 7.

6. Kuhara damu kwa ameba (severe amoeba dysentery)

a) Tazama sura 5.11 Euphorbia hirta, matumizi namba 2 yaliyopendekezwa .

Tumekwisha tumia tiba hii kwa mafanikio kwa maelfu ya wagonjwa. Au

b) Madaktari wanaofanya kazi na Anamed wamepata matokeo mazuri, kwa

kuwapa wagonjwa kijiko cha mezani cha mbegu za mapapai zilizosagwa mara

3 kwa siku, kwa siku 7.

Page 88: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

88

7. Malaria (matatizo madogo madogo) Mimina lita moja ya maji ya moto kwenye majani mabichi ya mpapai yatoshayo

kiganja kimoja. Chuja baada ya dakika 15. Watu wazima wanywe kwa siku moja,

watoto wadogo, kwa mjibu wa umri wao. Isitumiwe na wajawazito.

8. Kuvimbewa Papaine ni kimeng’enya ambacho husaidia kuyeyusha chakula. Pamoja na chakula,

ama tumia matone machache ya utomvu wa papai, au kipande kidogo cha jani la

mpapai, au tafuna mbegu tatu za mpapai.

9. Kikohozi Chimba kiganja kimoja cha mizizi ya mpapai (sio mzizi mkuu), osha vizuri na

chemsha kwa dakika 15 pamoja na lita moja ya maji. Chuja. Namna ya kutumia:

Watu wazima: kikombe 1 mara tatu kwa siku, watoto wadogo, itategemea na uzito

wao.

10. Matatizo ya ini, homa ya manjano, manjano ya ngozi na macho

kunakosababishwa na nyongo katika damu. Kileo chochote kile ni marufuku! Kula matunda mengi! Kisha pia, ama

a) kula kwa mpangilio, mapapai mabichi yaliyopikwa kama mboga au

b) chemsha kiganja kimoja cha mizizi ndani ya lita moja ya maji kwa dakika 10,

acha hivyo kwa dakika 15 na kunywa kwa siku moja, au

c) kila siku kunywa kinywaji kilichotengenezwa kwa kumimina lita moja ya maji ya

moto kwenye kiganja kimoja cha maua ya mpapai wa kiume au gamba la mpapai.

11. Maambukizi kwenye njia ya mkojo:

Tafuna kijiko kimoja cha mezani cha mbegu safi za papai lilioiva, mara tatu kwa

siku, kwa siku 7- 14. Hata hivyo, tiba hii haitoshelezi kutibu magonjwa ya ngono.

12. Kusumbuliwa na pumu Ili kuleta unafuu kwa matatizo ya pumu, vuta majani makavu ya mpapai kwenye kiko

au yaliyofungwa katika karatasi kama sigara, au choma majani karibu na kitanda

chako na vuta moshi.

13. Vidonda vyenye vijidudu Maji yenye kileo yaliyotokana na majani yana nguvu ya kuua bacteria, hasa hasa

staphylococci – wadudu hawa mara kwa mara hupatikana kwenye ngozi ambayo

yameingiliwa na bacteria. Changanya:

Majani ya mpapai makavu na yaliyosagwa na safi gram 10

Kileo kilichoondolewa uasili 70% ml 100

Baada ya wiki moja, kamua na chuja. Dondoshea kwenye kidonda mara kwa mara

kwa siku nzima. Pia tafuna kijiko 1 cha mezani cha mbegu za papai mara 3 kwa siku,

kwa siku 3.

14. Majipu yaliyo wazi, vidonda vyenye vijidudu, au majeraha madogo madogo

yanayotoa usaha

Osha papai bichi lililo bado mtini kwa kitambaa na maji ya moto. Safisha kisu,

kiweke kwenye maji ya moto, halafu kata kipande kidogo cha papai unene wa kidole

Page 89: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

89

kidogo cha mtoto. Laza kipande hicho kwenye kidonda na funga kitambaa kisafi.

Kiache kwa saa 4. Kama kinaleta maumivu makali, kitoe mapema.

Endelea na tiba hii mara 4 kwa siku, kwa siku kadhaa hadi usaha umeacha

kuonekana. Badilisha na tiba hii kwa asali/sukari kama tiba iliyoelezwa sura ya 6.33.

Baada ya kila tiba ya asali/sukari, weka kipande cha papai bichi; kwa maana hiyo

unaacha tunda kwenye mti wake.

15. Majeraha makubwa yanayotoa usaha Osha kidonda mara kadhaa kila siku kwa “maji yaliyowekewa utomvu wa mapapai.”

Tazama maelezo namba moja juu. Pia tafuna kijiko kimoja cha mezani cha mbegu za

papai mara 3 kwa siku, kwa siku 3. Mgonjwa lazima aende kwenye kituo cha afya

kilicho karibu! Usikifunge kidonda, na mgonjwa alale katika chandarua.

16. Maambukizi ya mba

a) Majimaji ya matunda mabichi (utomvu) yana nguvu ya kutibu mba (mfano,

ugonjwa wa mabaka kichwani). Changanya matone 10 ya utomvu kwa kijiko

kimoja cha mezani cha mafuta ya mboga mboga. Sugua sehemu zilizoathirika kwa

mchanganyiko huu mara 3 kwa siku. Tayarisha mchanganyiko mwingine kila

siku.

b) Ongeza majani ya Cassia alata (ringworm bush) kwenye mchanganyiko huu

(Tazama sura 5.6, mapendekezo namba 2)

17. Minyoo wa Guinea (Guinea worms)

Kwa pamoja twanga vitu vifuatavyo kwenye chombo kisafi:

Utomvu wa papai matone 10

Nyamanyama kutoka kwenye mrama mbichi

wa Thorn Apples (Datura stramonium,

tazama sura 6.20) kijiko 1 cha chai

Chumvi (iliyosalama kwa kuchemshwa) Nusu kijiko

Paka eneo lililoathiriwa mara tatu kwa siku kwa siku 2 – 3, ukiandaa mchanganyiko

mpya kila unapotaka kupaka. Uzoefu wetu nchini Sudan ni kwamba katika siku ya

tatu mnyoo anakuwa amepooza na anaondolewa kwa urahisi.

18. Kufanya nyama ngumu kuwa laini

Viwanda hutumia papaine kufanya nyama kuwa laini. Kwa matumizi ya nyumbani

nyama ngumu hufungwa kwenye jani bichi la mpapai usiku kucha.

19. Sabuni mbadala Wakati sabuni inazidi kupanda bei kila wiki, isingekuwa bora mtu “kustawisha”

sabuni yake mwenyewe? Miti ya mapapai inatupa sabuni bure: paka mikono na mwili

kwa majani yaliyotwangwa – lakini usiharibu mpapai wa jirani yako!

ATHARI Matumizi ya ndani: (kunywa) papaine inaweza sababisha tumbo kuuma.

Matumizi ya nje: mzio unaweza kutokea kwa kuitumia kwa kipindi kirefu. Epuka

majimaji ya papai (utomvu) kugusa au kuingia machoni.

Page 90: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

90

5.6 Cassia alata (syn. Senna alata) Ringworm bush

Maelezo ya kibotania: Familia: Caesalpiniaceae Mmea huu asili yake ni Amerika ya kusini na umeenea katika maeneo yote ya nchi za

joto. Hukua hadi meta 2 – 3 kwa urefu, na majani makubwa yenye manyoya

manyoya. Maua huonekana kama mshumaa. Tunda limeumbika kama mkunde

ulionyoka na unafikia sm 25 kwa urefu. Cassia alata hufunga majani yake wakati wa

giza (kama hakuna mwanga): ujaribu kwa kuweka ndoo iliyogeuzwa kwenye tawi

kwa dakika 30.

UKULIMA

Cassia alata hustawi katika

nyanda za chini, kwenye

udongo ambao una mboji kwa

wingi. Panda kwa kusiha moja

kwa moja udongoni.

SEHEMU

ZINAZOTUMIKA: Majani, mizizi

MATUMIZI KATIKA NCHI

ZINGINE:

Nchini New Guinea, Cassia

alata inatumika kama dawa ya

kuharisha na ya fungus, nchini

Philippines inatumika kwa

ugonjwa wa ngozi aina ya

impetigo na maambukizi

mengine ya ngozi. Huko Mali

ina jukumu la kutibu upele aina

ya scabies, nchini Congo

inatumika kama dawa ya

kitulizo. Nchini Senegal mmea

unatumika kwa minyoo aina ya

maw worms, maambukizi ya

mba na vilevile kama dawa ya kuharisha. Wa Ivory Coast hutumia kama dawa ya

minyoo, na watu wa Congo pia kwa ukoma.

MAPENDEKEZO YA JINSI YA KUTUMIA Katika maeneo ya nchi za joto, mmea huu unafahamika sana kwa nguvu zake za

madawa; nchini New Guinea wamefikia hatua ya kuuita “mmea duka la madawa”

miongoni mwa vitu vingine, ina tindikali ya njano ya chrisophane, ambayo

imefahamika kwa miaka 100 barani Ulaya kwa nguvu zake dhidi ya mba (fungus).

Cassia alata huwashambulia staphylococi, bacteria ambao mara nyingi hupatikana

kwenye vidonda vyenye vijidudu. Uwezo wake wa kufanya mtu aharishe vilevile

umethibitishwa kabisa.

Page 91: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

91

1. Shida ya kufunga choo (constipation) Mimina kikombe 1 cha maji ya mto kwenye kijiko 1 cha chai cha majani makavu au

gamba la mzizi, chuja baada ya dakika 10. Kunywa kabla ya kwenda kulala; itafanya

kazi baada ya saa 8. Pia kunywa lita 3 za maji kila siku.

2. Maambukizi ya mba, impetigo, mabaka ya kichwani, upele (scabies),

psoriasis:

Mchanganyiko mzuri ni kama ifuatavyo: Twanga majani katika kinu ili kupata aina

fulani ya “manyoya kijani ya pamba” Changanya na kiasi kilekile cha mafuta ya

mbono (kama hayapo, mawese au mafuta mengine yoyote ya mbogamboga), paka

eneo lililoathirika mara 2-3 kwa siku. Dawa hii hudumu kwa siku moja tu na

kuharibika.

Kwa maambukizi ya mba na impetigo, ongeza matone 10 ya majimaji ya papai

(utomvu), kama yanapatikana (tazama sura 5.5.).

3. Madonda yenye maambukizi

Changanya pamoja:

Majani makavu ya Cassia alata, yaliyotwangwa gram 10

Kileo kilichoondolewa uasili 98% ml 70

Maji ya moto ml 30

Au

Majani makavu ya Cassia alata, yaliyotwangwa kikombe 1

Spiriti (mfano, pombe, cognac, kileo kadri ya 50 % chupa 1

Acha kwa wiki moja, chuja na tumia kama dawa ya kusafisha kidonda.

Majeraha makubwa yanahitaji tiba za hospitali.

ATHARI

Epuka kunywa dawa hii kwa muda mrefu, na usinywe wakati wa ujauzito au

kunyonyesha.

5.7 Cassia occidentalis (syn. Senna occidentalis) Mwingajini

Maelezo ya kibotania: Familia: Caesalpiniaceae

Kamti kafupi meta 0.8. – 1.5 urefu. Majani yake yako pinnate na yanaota kwa

kufuatana, maua yake ni njano. Maganda yake ya mbegu yana urefu wa sm 15,

yamepinda kidogo na huwa na mbegu 10 – 20. Unapatikana sehemu za nchi za

tropiki katika maeneo ya vijijini.

UKULIMA Cassia occidentalis huhitaji ardhi yenye mboji kwa wingi. Siha moja kwa moja

udongoni na mwagilia maji.

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Majani, mizizi, mbegu

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE Nchini Sudan, Cassia occidentalis inatumika kwa magonjwa ya ngozi; Philippines

inatumika kwa watu waliofunga choo na wenye shinikizo la juu la damu; nchini

Page 92: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

92

Congo inatumika kwa

kutibu bawasiri na

kisonono. Wazulu wa

Afrika Kusini wanatumia

mti huu kama dawa ya

minyoo; katika Jamhuri

ya Afrika ya kati, Benin

na Ivory Coast inatumika

kama dawa ya malaria,

matatizo ya ini, na

kisonono. Huko Burkina

Faso mbegu zilizosagwa

zinanywewa kwa ajili ya

minyoo aina ya Guinea

worms. Katika Jamhuri ya

Kidemokrasia ya Congo

utomvu wa mizizi

husaidia kupanua njia ya

uzazi wakati wa

kujifungua (oxytocicum).

Sumu iliyo katika mbegu

hupotea zinapokaangwa.

Siku za nyuma, Cassia

occidentalis ilitumika

katika hospitali za kikoloni kutibu homa ya manjano na blackwater fever.

1. Mapendekezo ya matumizi

Chemsha kijiko 1 cha chai cha majani makavu na glasi moja ya maji, acha ikae kwa

dakika 15, kisha chuja. Kunywa kabla ya kwenda kulala. Kwa tatizo la kufunga choo

kunywa lita 3 za maji kila siku.

2. Kuvimba mwili sababu ya majimaji (oedema)

Chemsha kijiko 1 cha mezani cha majani makavu au mizizi katika lita 1 ya maji kaw

dakika 15. Chuja na kunywa kidogokidogo wakati wa siku moja.

3. Magonjwa ya ngozi

Ponda ponda kiganja kimoja cha majani mabichi, sambaza majani yaliyotwangwa

kwenye ngozi na funika kwa kitambaa kisafi. Badilisha mara mbili kwa siku.

4. Badala ya Kahawa

Oka kwa moto mbegu; usioke kwa muda mrefu sana na tayarisha “kahawa” kwa

kuchemsha gram 30 ndani ya lita moja ya maji. Chuja.

ATHARI

Dawa itokanayo na majani ya kunywa: Ukizidisha dozi inaweza sababisha tumbo

kusokota. Usitumie dawa hii zaidi ya wiki 1 – 2, wala isitumiwe na wajawazito au

wanyonyeshao.

Page 93: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

93

5.8 Citrus limon Limau

Maelezo ya kibotania: Familia: Rutaceae Ni mti mdogo kadri ya meta 6 – 9.

UKULIMA: Inahitaji udongo mwepesi, hasa tifutifu ya mchanga na mfinyanzi. Panda mbegu moja

kwa moja pale ambapo mti unataka uwe. Hutoa matunda kati ya miaka 2 – 6.

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Majani,

matunda mabichi na yaliyoiva, maganda (mafuta

ambayo ni mepesi kutoweka yanapatikana kwa

wingi katika maganda).

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE

Barani Ulaya kinywaji cha moto cha juisi ya

limau hutengenezwa kwa ajili ya homa, ili

kuongeza utoaji wa jasho. Huko Asia majimaji ya

majani machanga hutumika kwa masikio yenye

maambukizi, na chai ya maganda inatumika kwa

kichefuchefu. Nchini Ivory Coast chai kwa ajili

ya kikohozi na mafua hutengenezwa kutokana na

majani machanga.

MAPENDEKEZOYA MATUMIZI

1. Kikohozi:

Chemsha viganja 2 vya majani machanga (makavu au mabichi) na lita moja ya maji.

Chuja na kunywa kidogo kidogo kwa siku.

2. Matatizo za kifua Katakata kiganja kimoja cha maganda ya limau. Ongeza lita 1 ya maji ya moto na

acha hivyo kwa dakika 15, kisha chuja. Watu wazima: kunywa kwa siku moja.

Watoto wadogo, kwa mjibu wa uzito wa mwili.

3. Upungufu wa Vitamin C Kila siku, kula angalau limau 1, danzi 1, machungwa 2 au machenza 5.

4. Homa Kuliko kunywa aspirin ni bora zaidi kuimarisha mfumo wa kinga! Mara tatu kwa siku

kunywa juisi ya limau kikombe kimoja kikubwa kwenye maji ya moto (ml 500).

Usichemshe juisi, utaharibu vitamin C.

5. Mafua Minya kipande cha ganda la limau na vuta mafuta mafuta mepesi yatakayotoka

kwenye ganda.

6. Vidonda kwenye midomo au mdomoni (Herpes labialis) Ugonjwa huu hufanya vidonda vidogovidogo kwenye midomo au mdomoni. Mara

kadhaa kwa siku, minya ganda la limau mpya (au chungwa au chenza) ama:

a) Moja kwa moja kwenye vidonda au

b) Kwenye kipande cha plastiki chembamba, ambacho utakiweka kwenye vidonda.

Page 94: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

94

Kama kinauma sana, ongeza tone la mafuta ya mbogamboga.

ATHARI

Angalia isiguse machoni. Watoto wadogo na watu wanaoumwa matumbo wanaweza

wakaumizwa na dawa hii kwa kuumwa matumbo kama wataitumia kwa kiwango

kikubwa.

5.9 Cymbopogon citratus Michaichai

Maelezo ya kibotania: Familia: Poaceae

Majani hufikia hadi sm 50 urefu.

UKULIMA

Gawanya mmea uliostawi. Panda sehemu yenye rutuba na tifutifu na kwenye kivuli

kidogo. Yamwagilie maji vizuri katika hatua za awali.

SEHEMU ZINAZOTUMIWA: Majani

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE

Katika maeneo yote ya nchi za joto chai hupikwa kwa mchaichai kutibu homa.

Barani Asia mmea huu hutumika kuongeza harufu katika mvinyo na kama kiungo

katika vyakula. Vile vile husaidia kwa maumivu ya meno, kipindupindu na tumbo

kujaa hewa. Pia husaidia kumfanya mtu kukojoa sana. Huko Afrika Magharibi mmea

wote hutumika kwa matatizo ya homa, mafua, kisonono. Mafuta ya mchaichai

hutumika kutia manukato katika sabuni

na marashi.

MAPENDEKEZO YA MATUMIZI

Michaichai haihitaji uangalizi wa hali

ya juu na bora ikapandwa katika kila

bustani. Tunapendekeza kwamba kila

zahanati na hospitali ipande michaichai

kama sehemu ya ua ili kuzia

mmomonyoko wa udongo. Mistari ya

kontua katika bustani za dawa

inapandwa kwa kuchanganya

michaichai na miti.

Michaichai ina myrcene na citral

kwa wingi, vitu vyenye kazi ya kutibu

cramps na kuchochea uyeyushaji wa

chakula. Kunywa chai ya michaichai

kunaongeza kiwango cha mwili

kujisafisha na ukojoaji wa mara kwa

mara ambako kunasaidia kuondoa

pyrogens, ambayo ni mazao ya

microbial yanayosababisha homa kwa

ujumla, unywaji wa maji mengi,

Page 95: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

95

unapendekezwa kwa magonjwa mengi, sababu husaidia mwili wote kufanya kazi

vizuri zaidi. Hii ni bora zaidi katika hali ya hewa ya joto ambapo kupungukiwa maji

daima ndio hatari kubwa. Michaichai hutia ladha nzuri katika maji.

1. Matatizo ya kifua, mafua, sinusitis

Chemsha kiganja 1 cha michaichai kwenye lita moja ya maji na vuta mvuke wake.

2. Homa, malaria

Unapokuwa na malaria, kunywa lita 2 za chai ya michaichai. Tengeneza viganja 2

vya michaichai kwa kumwagia maji ya moto lita 2. Kama ni lazima, kwa kuongezea

kunywa chai ya kuzuia malaria, mfano, Artemisia (5.2) au mtukutu (6.48). Kunywa

ikiwa na uvuguvugu na kidogokidogo siku nzima. Watoto wanywe kidogo kufuatana

na uzito wao.

3. Bawasiri (haemorrhoids)

Majani makuukuu yana tannins zaidi kuliko mapya. Kwa hiyo, chemsha kiganja 1

cha majani makuukuu ya mwembe au mkaratusi kwenye lita 2 za maji kwa dakika

15. Kisha ongeza viganja viwili vya michaichai na endelea kuchemsha kwa dakika

zingine mbili. Acha kwa dakika 15, chuja na ongeza maji zaidi vuguvugu, na kisha

oga sehemu za mapaja na kiuno kwa dakika 20.

4. Maumivu ya meno; harufu mbaya mdomoni

Tafuna jani bichi lililosafishwa 2 – 3 kwa siku.

5. Dawa ya kufukuza wadudu

Weka majani mengi kwenye mkaa ndani ya nyumba (juu ya moto mdogo), au panda

mimea hii kwenye vyungu ndani ya nyumba.

6. Mafuta ya watoto na mafuta ya kuchulia: Tazama sura 4.3

7. Dawa ya mafuta kwa ajili ya mwili: Tazama sura 4.4.

8. Dawa ya mafuta kwa bawasiri. Tazama sura 4.4.

9. Utengenezaji wa sabuni: Tazama sura 4.1.

ATHARI: Hakuna zinazoeleweka.

5.10 Eucalyptus globulus Mkaratusi (kalafulu)

Maelezo ya kibotania: Familia: Myrtaceae Urefu meta 30, mti mwembamba, umetokea Australia. Kuna aina 150 zinazotumika

kwa namna mbalimbali (E. globulus, na E. robusta ni “officinalis” katika dawa, E.

citriodora inatumika kwa kuzalisha marashi). Majani ya E. globulus ni marefu na

membamba na hutoa harufu iliyokolea.

UKULIMA Husambazwa kwa mbegu. Panda miche kwenye udongo tifutifu na wenye rutuba

sehemu yenye jua. Unavumilia theluji. Mkaratusi hufanya udongo kuwa na tindikali

zaidi, na matokeo yake ni kwamba mazao hayawezi kustawi karibu na miti hii.

Page 96: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

96

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Majani, gamba

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE: Barani America na Ulaya chai ya

mkaratusi hutumiwa kwa wenye matatizo ya kifua, kuhara damu na magonjwa ya njia

ya mkojo. Barani Afrika muuke unawutwa kwa ajili ya mafua. Nchini Afrika kusini

inatumika kwenye majipu. Huko Asia ni dawa

ya kikohozi, makamasi, kifua kikuu, pumu na

minyoo.

MAPENDEKEZO YA MATUMIZI Mkaratusi una aina mbalimbali ya mafuta

muhimu. Hasahasa yale yanayofaa ambayo ni

eucalyptol na cireol, yana nguvu ya antiseptic

(kuua wadudu) na expectorant (kulainisha

makohozi). Majani pia yana phenol, dawa

yenye nguvu ya kusafisha vidonda, na tannins

ambayo husaidia mucous membrane katika

kuzuia mashambulizi kutoka kwa bacteria.

1. Kikohozi, magonjwa ya njia ya mkojo,

madonda ya koo.

a) Chai ya mkaratusi: twanga kiganja 1 cha

majani makavu au mabichi na chemsha

pamoja na lita moja ya maji kwa dakika 5.

Chuja na kunywa kidogokidogo kwa siku. Chai hii ni msaada kwa mgonjwa wa

kifua kikuu anapoendelea na tiba ya Hospitali.

b) Syrup ya kikohozi: Mimina ml 250 za maji ya moto kwenye gram 20 za majani

makavu, funika na acha kwa saa moja. Chuja kwenye kikombe 1 cha chai hii

ongeza kikombe kimoja cha sukari, chemsha kidogo na chuja. Watoto wa miaka 7

watumie kijiko1 cha chai mara 3 kwa siku, na wadogo zaidi kwa mjibu wa uzito

wa miili yao. Watoto wakubwa na watu wazima ni bora wanywe chai kuliko

kutumia syrup. Isipewe kwa watoto chini ya miaka miwili.

c) Matone ya kikohozi: Dawa ya maji ya mkaratusi: mimina mchanganyiko wa ml

700, kileo (95%) na ml 300 za maji yaliyochemshwa na kuchujwa kwenye gram

100 za majani makavu ya mkaratusi. Baada ya wiki moja kamua na ondoa majani.

Watu wazima watumie matone 30, (nusu kijiko cha chai) mara 3 kwa siku.

2. Madonda ya koo

Tafuna nusu jani taratibu kwa masaa kadhaa, mara 3 kwa siku.

3. Homa, tiba ya msaada kwa malaria

Chemsha kiganja 1 cha majani na lita 2 za maji kwa dakika 5. Kunywa ikiwa moto,

kidogo kidogo kwa siku moja. Matokeo ni kuongeza na kusaidia mwili kupambana

na vijidudu au sababu zingine zinazoleta homa.

4. Tiba ya msaada kwa kisukari na magonjwa za njia mkojo. Fuata maelezo namba 3 juu. Kukojoa mara kwa mara ni tokeo mojawapo. Na kwa

wagonjwa baadhi wa kisukari kiwango cha sukari katika damu hupungua. Hata

hivyo, tumia tiba hii kwa siku chache tu.

Page 97: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

97

5. Mafua, maumivu ya viungo. Mafuta ya mkaratusi: chemsha kiganja 1 cha majani makavu ya mkaratusi

yaliyosagwa kwenye ml 100 za mafuta ya mbogamboga katika fukizo maji kwa saa

moja. Chuja, sugua kifuani kwa nguvu kwa mafuta hayo.

6. Kwa kusafisha vidonda: Ili kusafisha kidonda, tumia mchanganyiko wa maelezo namba 5 (chuja kabla ya

kutumia) kwenye kidonda. Au chemsha kijiko 1 cha mezani cha majani makavu

yaliyokatwakatwa na ml 100 za maji kwa dakika 15, chuja na tumia kwa kuosha

vidonda. Tengeneza mpya kila unapotaka kusafisha kidonda.

7. Pumu, matatizo ya kifua

Twanga kiganja 1 cha majani mabichi au makavu na kisha chemsha katika lita 1 ya

maji. Vuta mvuke wake kwa dakika 15 ikiwa bado moto, huku kichwa na chungu

vikiwa vimefunikwa kwa kitambaa kizito.

8. Usafi wa meno

Tumia katawi kadogo kama mswaki

9. Nzi na mbu

Ili kufukuza wadudu

a) Tengeneza mafuta ya mbu: Changanya gram 100 ya majani makavu

yaliyotwangwa na mafuta ya mbogamboa nusu lita. Chemsha kwa saa moja

katika fukizo maji na kisha chuja. Mafuta haya hudumu hata mwaka mzima.

b) Au, rahisi zaidi, jisugulie majani mabichi mwili mzima au choma majani makavu

ndani ya nyumba.

ATHARI: Kwa sababu ya nguvu zake, matumizi ya kunywa hayapendekezwi kwa

watoto chini ya miaka 2. Watu wazima waitumie kwa siku chache.

5.11 Euphorbia hirta Mziwaziwa (mwache)

Maelezo ya kibotania: Familia: Euphorbiaceae

Mmea wa kawaida katika nchi za tropiki, mara nyingi hupatikana vijijini, urefu sm 30

– 40, wakati mwingine hutambaa ardhini, jani huota kinyume na jingine, katika

vitawi vifupi. Mmea huu una vinywele vya njano , vigumu na vidogovidogo sana.

Utomvu ni mweupe, maua yake ambayo ni madogomadogo ni ya kijani na yako

kwenye vitawi vifupi. Tunda lina mbegu 3 zenye rangi nyekundu, kahawia, iko na

kingo tatu na urefu mm 0.8.

UKULIMA Husambazwa kwa mbegu. Mmea huu hupendelea udongo mkavu wa kichanga ambao

una mchanganyiko wa mabaki ya mimea na iwe juani.

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Mimea wote. Wakati wa kuvuna, kata mmea kwa

mkasi, ili mizizi ibaki ardhini, vinginevyo utamaliza mimea yote katika eneo lako na

usibakiwe na kitu!

Page 98: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

98

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE Katika nchi za Senegal, Mali, Burundi, Benin na D.R. Congo mmea huu hutumika

kutibu sana kuhara na kuhara damu; nchi Niger kwa pumu; Nigeria kwa tatizo la

kufunga choo na kuvimba matumbo (enteritis). Huko Afrika Magharibi mmea huu

vilevile unajulikana sana kwa uwezo wake kuchochea utoaji wa maziwa kwa mama.

Barani Asia mziwaziwa unatumiwa sana kwa pumu, na magonjwa ya njia ya hewa.

Indian Pharmacopoeia inapendekeza mmea huu utumike kwa minyoo kutibu watoto

wa kuchochea utoaji wa Maziwa kwa wanawake; utomvu wake kwa tumbo

linalosokota na kuondoa uvimbe (warts). Mmea huu umesajiliwa katika Afrikan

Pharmacopoeia (OAU, 1985). Kama ingekuwa rahisi kuulima pengine ungetumika

kwa malengo ya tiba huko Ulaya pia – lakini mmea huu hauwezi ukastawishwa

katika maeneo makubwa!

Katika mji wa Kasai, huko D. R. Congo, mmea huu huitwa “Dawa ya mtoto wa

jicho.” Wakati mtoto wa jicho anapokuwa katika hatua za awali, watu huweka tone 1

la utomvu katika jicho mara tatu kwa siku, na matokeo yake ni mazuri. Hata hivyo,

hatujui athari za tiba hii. Ukitumia tiba hii, hakikisha mmea umeoshwa vizuri, ili

kuepuka kuambukiza jicho na vijidudu vingine.

Katika majaribio ya kisayansi kwa wanyama dawa kutoka katika E. hirta

ilionyesha mafanikio yafuatayo: kuondoa wasisi (anxiolytic), kupunguza maumivu

(analgesic), kuondoa uvimbe na ni kitulizo.

Vilevile ilionyesha kuwa na uwezo kwa

matatizo ya kuharisha (hata kama hii

ilisababishwa na kemikali).

MAPENDEKEZO YA MATUMIZI Mziwaziwa uko katika familia ya

Euphorbiaceae, ambayo mimea mingi ni

ya muhimu, na baadhi ya mimea ina sumu

sana na/au inasababisha kansa

(carcinogenic). Kwa sababu hii ni lazima

uwe na uhakika kabisa kwamba una mmea

sahihi. Utumie mmea ukiwa bado mbichi,

kwa sababu wakati wa ukaushaji sehemu

kubwa ya nguvu hupotea. Tofauti na

mimea mingine mingi, kwa upande wa E.

hirta unachukua kiasi kilekile cha uzito cha

mmea mkavu sawa na unapotumia mmea

mbichi.

1. Kuhara damu kunakoletwa na

Ameba (amoebic dysentery)

Chemsha gram 15 – 30 (kiganja 1

kilichojaa) cha mmea mbichi na uliooshwa

(au mmea mkavu) kwa chupa moja ya maji, dakika 15. Chuja na kunywa

kidogokidogo kwa siku nzima. Rudia tiba kwa siku 8 mfululizo. Vilevile kunywa

ORS (Tazama sura 4.6).

Page 99: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

99

2. Kuhara kukali kwa ameba (severe amoebic dysentery) bacillary dysentery. Kwa magonjwa makali, osha na changanya:

Mziwaziwa (mmea wote) kiganja 1 kilichojaa

Majani ya mpapai kiganja 1 kilichojaa

Majani ya mwembe machanga, ya kijani kiganja 1 kilichojaa

Majani ya mpera kiganja 1 kilichojaa

Chemsha kwa dakika 15 katika lita moja ya maji, kisha chuja. Kunywa

kidogokidogo kwa siku nzima. Kiwango cha kunywa kwa watoto, tazama sura 2.6.

Watu wazima na watoto wote ni lazima wanywe ORS daima (Tazama 4.6.).

Endelea kunywa chai hii kwa siku 8, hata kama dalili za ugonjwa zitapotea baada

ya siku 2, na hii kwa uzoefu wetu hutokea mara kwa mara.

Mchanganyiko huu umeisaidia anamed kuokoa maisha ya watu wengi hasa katika

matatizo ambapo watu:

wenye magonjwa ya amoeba walikuwa wakisumbuliwa sana na tumbo baada

ya kutumia dawa ya Metronidazol/Flagyl na kwa hiyo wakaacha kutumia dawa

hii ya “kisasa” ya tiba.

wenye bacillary dysentery iliyosababishwa na wadudu ambao walikuwa

hawauwawi na antibiotics karibu zote.

Mimea yote iliyotajwa hapo juu ina nguvu dhidi ya ameba kwa hiyo inaweza

kutumiwa kipekee.

Kwa wagonjwa wenye kichefuchefu, au kwa watoto, usiongeze majani ya mpapai

(yana ladha mbaya) kwa siku za kwanza.

3. Magonjwa ya njia ya mkojo, magonjwa ya figo, kuhara, matatizo ya tumbo

(intestinal cramps)

Kunywa dawa ya kumwagia maji ya moto kutoka mchanganyiko namba 1, ila haitibu

kisonono! Kama tahadhari, usitumie kwa zaidi ya siku 8. Kwa matatizo ya kuharisha

daima tumia ORS (Tazama sura 4.6).

4. Minyoo ya kwenye utumbo

Osha na changanya

Mziwaziwa, mmea wote bila mizizi kiganja 1 kilichojaa

Majani ya mpapai kiganja 1 kilichojaa

Chemsha kwa dakika 15 katika lita 1 ya maji, kisha chuja. Kunywa kidogokidogo

kwa siku nzima. Kama mtoto atakataa kutumia chai hii, tengeneza kwa kutumia

Mziwaziwa pekee kiganja kimoja. Tiba nyingine yenye mafanikio ni utomvu wa

papai (Tazama sura 5.5.)

5. Pumu

a) Vuta majani makavu yaliyosokotwa kama sigara, au

b) Weka kichwa chako juu ya kiganja 1 cha majani haya wakati wa usiku, au

c) Tumia mchanganyiko namba 1 juu

6. Hali ya wasiwasi, fadhaa, cramps

Tumia mchanganyiko namba 1 juu.

7. Uvimbe (warts)

Tumia utomvu mweupe wa baadhi ya miti kwenye warts.

Page 100: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

100

ATHARI: Hazijulikani. Kwa matatizo ya ameba au bacillary dysentery na pumu, E.

Hirta. daima ndio chaguo la kwanza kwa sababu ina nguvu sana. Lakini usizidishe

dozi iliyopendekezwa.

5.12 Mangifera indic Mwembe

Maelezo ya kibotania: Familiae: Anacardiaceae Mti unafikia urefu wa meta 25, huota maeneo yote ya tropiki.

UKULIMA Mwembe hustawi katika maeneo ya joto na nyanda za chini. Panda katika vyombo

vya plastiki mbegu, na panda mahali unapotaka katika umbali wa meta 8 kutoka mti

hadi mti. Miti hutoa matunda baada ya miaka 4 – 6.

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Majani

machanga, gamba, maua, matunda, mbegu.

Ili kuyalinda maisha ya mti, chukua

magamba kutoka kwenye matawi tu (na

iwe kutoka upande mmoja tu). Kamwe

usitoe gamba kwenye shina.

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE Nchini Australia chai iliyotengenezwa kwa

majani inanywewa kwa ajili ya kuhara kwa

ameba (amoebic dysentery). Huko Mali na

Niger gamba na majani vinatumika kutibu

vidonda vya koo, meno kuuma, upungufu

wa vitamin C na homa, nchini Senegal

utomvu katika majani inajulikana kama

dawa kwa magonjwa ya akili. Katika nchi

ya Ivory Coast majani yanatumika kwa

matatizo ya kifua, pumu na michubuko.

MAPENDEKEZO YA MATUMIZI

Majani ya mwembe yana tannins 10% - vitu ambavyo vina jukumu kubwa kwa

kuzuia kuharisha. Zaidi ni flavonoids ambazo zinaongeza ukojoaji nazo zinapatikana.

1. Kuharisha; amoebic dysentery Chukua gram 30 (kiganja 1) majani mabichi na machanga, chemsha pamoja na lita

moja ya maji kwa dakika 30, chuja na kunywa kidogokidogo kwa siku nzima.

Changanya na Mziwaziwa kwa utendaji kazi mzuri zaidi, Tazama aya 5.11.

2. Tatizo la kufunga choo

Kula maembe yaliyoiva kwa wingi sana.

3. Kikohozi, matatizo ya kifua

Chukua gram 30 (kiganja 1) za majani machanga na chemsha katika lita moja ya maji

kwa dakika 10. Chuja na kunywa kidogokidogo kwa siku nzima.

Page 101: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

101

4. Homa Tumia mchanganyiko namba 3, ila kunywa lita 2 – 3 za maji. Kunywa kwa siku

nzima kidogokidogo. Hii huongeza uwezo wa mwili kujisafisha na kukojoa mara kwa

mara na vyote viwili vinasaidia kuondoa pyrogens. i.e. ni mazao ya microbial

ambayo husababisha homa.

5. Bawasiri (haemorrhoids)

Chukua viganja 5 vya majani makuukuu na chemsha katika lita 5 za maji kwa dakika

30. Chuja na tumia mtokoso huu kwa kuoga sehemu za mapaja.

6. Donda koo Tayarisha mchanganyiko namba 2, jisukutue kwa ½ kikombe cha mchanganyiko huu

kila baada ya saa moja.

7. Kuvimba fizi, upungufu wa vitamin C

Fizi zinaweza zikavimba kwa sababu ya upungufu wa vitamin C. Ili kuzuia, kula

matunda kwa wingi! Kama hayapo, tafuna majani 3 machanga ya mwembe kila siku,

yana vitamin C kwa wingi na pia tannins.

8. Minyoo

a) Kausha kabisa kokwa moja la embe, halafu oka na twanga. Chemsha unga na

chupa moja ya maji. Gawanya mara mbili na kunywa siku hiyo hiyo, au

b) Weka kiganja kimoja cha maua yaliyotwangwa katika 0.7 ya lita ya maji na acha

hivyohivyo usiku kucha. Chuja; kunywa kwa sehemu mbili kesho yake na yote

iishe.

Hata hivyo, tunapendelea tiba ya mpapai (sura 5.5.) au Mziwaziwa (sura 5.11).

ATHARI Majani makuukuu ya mwembe yana sumu, usiyatumie kwa kunywa wala kutafuna.

5.13 Moringa oleifera Mlongelonge

Maelezo ya kibotania: Familia: Moringaceae

Moringa oleifera ni mti mdogo unaokuwa haraka na hupukutisha majani, hufikia hata

meta 12 kwa urefu unapokomaa . Una asili ya India. Ni mti laini, gamba lake ni

jepesi na mizizi yake huenda chini sana. Hukua vizuri penye joto kati ya 26º C -

40ºC, kiwango cha mvua kwa mwaka zaidi ya mm 500 na mwinuko chini ya meta

1000. Unavumilia ukame. Siyo jamii ya mikundemikunde.

UKULIMA

Mti huu hukua haraka kutokana na mbegu au vitawi, hata katika ardhi isiyo na

rutuba. Hupendelea ardhi tifutifu na ya kichanga. Kadri mti unavyokua, unavyozidi

kukatwa ndivyo utakavyotoa majani zaidi.

SEHEMU ZINAZOTUMIKA: Majani, maganda ya mbegu, mbegu, gamba, mizizi,

maua, mafuta, utomvu.

Page 102: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

102

MAPENDEKEZO YA JINSI YA KUTUMIA

1. Majani na magamba: kwa Utapiamlo

Panda mti wa mlongelonge nje ya dirisha la jikoni. Majani yana chanzo cha vitamin

A, B, C. Yana madini kwa wingi, hasa calcium, chuma na phosphorus na protein

nyingi.

Yana chuma mara 3 zaidi ya

mchicha na mara 4 zaidi vitamin A

ukilinganisha na karoti. Katika mradi

uliofanyika Senegal majani

yameonekana kusaidia sana wagonjwa

wa Utapiamlo, hasahasa miongoni mwa

watoto.

Yanaweza yakaliwa mabichi, au

yanaweza yakakusanywa

yanapokomaa, kukaushwa, kutwangwa

na kuhifadhiwa. Yanaweza pia

yakavunwa wakati wa kiangazi,

ambapo mboga za majani nyingine

huwa ni haba.

Kukausha majani: Vuna, kausha kwa

siku tatu, kama inawezekana kivulini.

Ukikaushia juani vitamin A hupotea;

yatwange na hifadhi kwenye magudulia

yasiyopitisha hewa. Ikiwezekana pima

kiwango cha unyevu kwa hygrometer,

ili ujue ni kwa muda gani unaweza kuyahifadhi.

Unga huu wa majani unaweza kuongezwa katika wali, makande na kwa kweli ni

katika chakula chochote. Kwa watoto wenye Utapiamlo na matatizo mengine ya

kiafya, kijiko 1 kiongezwe katika milo yao mara 3 kwa siku.

Maganda na mbegu pia yanaliwa. Yakatwe vipande vidogo vidogo na kupikwa na

kuliwa kama maharage machanga. Yanapokuwa yamekomaa, yachemshe na komba

mbegu na nyama ya ndani. Yanapokuwa makubwa na yamekomaa, tumia mbegu tu

ambazo huitwa njugu za mlongelonge. Zikaange katika mafuta na kula kama

Karanga.

- Mizizi ina ladha kama mlonge.

- Maua ya mlongelonge ni chanzo cha asali nzuri.

2. Mafuta: Kwa Utapiamlo na matumizi katika vipodozi Mbegu ya mlongelonge ina gamba laini, kwa hiyo mafuta yanaweza yakapatikana

kwa kutumia mikono kwa screw press (pia inajulikana kama “spindle” au “bridge”

press).

Kwanza mbegu inapondwa, yanaongezwa maji 10% kwa ujazo, inafuatwa na

uchemshaji kidogo kwenye moto kidogo kwa dakika 10 – 15, uwe mwangalifu

usiunguze mbegu.

Page 103: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

103

Jaribio moja kama hilo lilitoa lita 2.6 za mafuta, kutoka kwenye kilo 11 za

makokwa.

Mara njia nzuri za kukamua mafuta zitakapogunduliwa, huenda ufanisi ukafikia

65%.

Mafuta ya mlongelonge yanaweza yakatumiwa:

a) Kwa kupikia; yana lishe kama mafuta ya mzeituni.

Hayachachi upesi, na ni mazuri kwa salad.

b) Kwa kulainisha mitambo laini.

c) Kwa kutengenezea sabuni.

d) Ni kitu cha msingi kwa vipodozi.

e) Kwenye taa

3. Matumizi kwa magonjwa mengine

Hatuna uzoefu sisi binafsi kwa dawa ya mlongelonge. Kwa mjibu wa maelezo, hata

hivyo, sehemu nyingi za mmea huu, ikiwemo mizizi, gamba, shina, majani, maua na

maganda yakiwa na mbegu zake, vinatumika kama dawa katika nchi nyingi.

a) Majani yanatibu kuharisha, upungufu wa damu na madonda.

b) Kwa kisukari, chai iliyotokana na majani hunywewa mara kadhaa kwa siku.

c) Vilevile mafuta ya mbegu za mlongelonge yanasaidia kwa waliovimba viungo

(gout), tumbo kuvurugika (stomach disorders) na maumivu ya viungo.

d) Mizizi ni michungu na inaongeza nguvu mwilini na kwenye mapafu. Inaweza

kukufanya kuongeza kukojoa na kuboresha damu. Ni nzuri kwa kutibu uvimbe,

majeraha ya kifuani, magonjwa ya kifua, bawasiri na kukosa hamu ya chakula.

e) Magonjwa ya ngozi yanaweza yakatibiwa kwa dawa nzito kama uji kutoka

kwenye mbegu.

4. Matumizi ya kusafisha maji Mbegu ni bora zikaachwa zikomae zikiwa mtini na zivunwe zikiwa kavu. Ganda la

juu na gamba la mbegu yanaondoka kwa urahisi, na kuacha mbegu nyeupe za ndani.

Hizi zinatwangwa kwa kutumia mwichi na kinu. Kiasi cha mbegu kinachohitajika

kutibu maji ya mtoni kinategemea na uchafu uliomo katika maji hayo. Watumiaji

huzoea haraka mahitaji yanayobadilika ya maji yao kwa kuwa kiwango cha uchafu

hubadilika kufuatana na msimu.

Ili kutibu maji lita 20 (wastani wa ndoo kubwa) mbegu kama 10 zinahitajika

(mbegu moja inaweza kusafisha lita 2 za maji). Ongeza kiasi kidogo cha maji kwenye

mbegu ulizoponda ili kupata ujiuji mzito. Weka katika chupa safi - chupa ya soda

ndio inafaa zaidi. Ongeza kikombe 1 (ml 200) cha maji na tikisa kwa dakika 5. Tendo

hili huziamsha kemikali zilizo katika mbegu zilizopondwa.

Chuja mchanganyiko huu kwa kutumia kitambaa cheupe cha pamba kwenda

kwenye ndoo ya lita 20 ya maji unayotaka kuyatibu. Koroga haraka haraka kwa

dakika 2, halafu endelea kukoroga taratibu kwa dakika 10 – 15. Wakati wa kipindi

hiki cha kukoroga taratibu, mbegu za mlongelonge hushikana pamoja, vipunje

vidogovidogo na bacteria kuwa vibonge vikubwa ambavyo huzama na kutuana

kwenye kitako cha ndoo. Baada ya siku moja hadi mbili maji safi yanaweza

yakaondolewa.

Page 104: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

104

Mchakato huu utaondoa 90-90% ya bacteria ambao wamenata kwenye vibonge

vya mlongelonge, na pia kuyasafisha maji. Hata hivyo, kama maji yamechafuliwa

sana, baadhi ya vidudu vyenye madhara kwa binadamu vinaweza visiondolewe. Kwa

maji ya kunywa tiba zaidi ya maji inapendekezwa, ama kwa kuchemsha (ikiwezekana

katika jiko la sola) au kuchujwa kwa chujio rahisi ya mchanga (simple sand filter).

MUHIMU: Mbegu za mlongelonge zinaweza zikatumika kwanza kukamuliwa

mafuta. Na mashudu yaliyobaki, ambayo yanaweza kukaushwa na kuhifadhiwa, yana

nguvu ileile kama mbegu kwa kutibu maji.

UHIFADHI: Mbegu zilizokaushwa (ondoa zilizoharibika rangi) na unga vinaweza vikatunzwa.

Hata hivyo dawa ni lazima itengenezwe mpya kila unapotaka kutumia.

5. Matumizi katika kilimo

a) Kilimo cha misitu: Mlongelonge ni muhimu sana kwa kuzuia upepo na ua – hukua

tena haraka baada ya kukatwa. Kwa kweli, kuukata mti mara kwa mara

kutaongeza uzaaji wa majani. Ua labda ndio njia nzuri ya kuyaweka pamoja

manufaa ya mlongelonge mfano, uzalishaji wa majani, kuni, kivuli, kizuia upepo,

kuzuia mmomonyoko wa udongo, kugawanya mashamba.

b) Chakula cha ng’ombe na mbolea: Majani na mashudu.

5.14 Psidium guajava Mpera

Maelezo ya kibotania: Familia: Myrtaceae

Ni mti mdogo urefu meta 3 – 5. Majani yake ni magumu na hunukia vizuri.

Kutegemea na aina matunda yake ni duara au yana umbo la yai na yana nyamanyama

nyekundu au nyeupe ambayo ni tamu.

UKULIMA

Hayavumilii theluji. Huhitaji mvua zaidi ya meta moja kwa mwaka, au kumwagiliwa,

na ardhi yenye rutuba. Hutoa maua baada ya mwaka mmoja. Husambaa kwa mbegu.

SEHEMU ZINAZOTUMIWA: Majani machanga, matunda na mizizi.

MATUMIZI KATIKA NCHI ZINGINE

Barani Ulaya na Asia chai iliyotengenezwa kutokana na majani inajulikana kama

dawa ya kuharisha, nchini Misri na Hongkong kwa kikohozi, Senegal kwa kufanya

hedhi itoke kawaida, nchini Hawaii kwa maambukizi ya bacteria.

MAPENDEKEZO YA JINSI YA KUTUMIA Majani ya Mpera yana vitu vingi ambavyo kusaidia wagonjwa wanaoharisha: tannins,

ambayo ina nguvu ya kulinda mucous membranes: flavonoids ambayo ina nguvu ya

antispasmodic na antibiotic; na mafuta mepesi ambayo yanasafisha mwili.

1. Kuharisha kwa watu wazima na maumivu ya tumbo a) Rahisi zaidi, kula mapera kadhaa mabichi, au

Page 105: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

105

b) Tengeneza chai ya mpera: chukua kiganja kimoja cha majani ya mpera (kiasi

ambacho mgonjwa anaweza shikilia ndani ya kiganja chake) na ongeza lita

moja ya maji. Chemsha kwa dakika 20 katika chombo kilichofunikwa, na kisha

chuja. Ongeza maji mengine hadi yafikie lita moja tena. Kunywa kidogokidogo

kwa siku nzima.

2. Kuharisha kwa watoto, na kuharisha kukali kwa watu wazima

Katika lita moja ya chai ya mpera (Tazama maelezo namba 1) ongeza vijiko 4 vya

mezani vya asali au vijiko viwili vya mezani vilivyojaa sukari, na chumvi kijiko 1

cha chai. Kama hakuna majani ya mpera, chukua maji, chumvi na sukari tu.

Dozi: Kila siku, mpe mtoto ml 200 (glass moja) kwa kila kilo ya uzito wa mwili.

Kama hujui uzito wa mtoto, mpe, chini ya miezi 6: ml 700; miezi 6 hadi miaka 2: ml

1,400, miaka 2 – 5: ml 2,100; zaidi ya miaka 7: ml 2,800, na watu wazima: ml 3,500.

3. Kiseyeye (upungufu wa vitamin C)

Kula matunda mengi yaliyoiva sana.

4. Kuhara damu kwa amoeba Kwa kuhara kuliko nafuu, fuata maelezo 1 b juu.

Kwa kuhara kubaya sana, tengeneza chai kwa kuchanganya na mimea mingine

(Tazama sura 5.11.2)

5. Kikohozi Fuata maelezo 1b, au tafuna jani moja

changa la mpera mara 5 kwa siku.

6. Kisukari

Wakati mwingine matumizi ya chai ya

mapera au juisi yanaweza

yakapunguza kiwango cha sukari

katika damu. Fuata maelezo 1 b.

Kachunguze matokeo katika maabara.

7. Vidonda vinavyovuja damu

Chemsha viganja 2 vya majani

mabichi kwa lita moja ya maji hadi

ibaki kikombe 1 (ml 500) cha

mchanganyiko huu. Chuja na tumia kwa kuosha vidonda.

8. Majipu yaliyowazi Osha kiganja kimoja cha majani mabichi, twanga na ongeza kijiko kimoja cha chai

cha chumvi na cha sukari. Chemsha katika sufuria bila maji, mpaka mchanganyiko

uwe wa kahawia (sio mweusi).

9. Kusafisha sehemu za siri (wanawake) Tumia mtokoso (dawa ya kutokosa) wenye uvuguvugu wa majani ya mapera baada

ya kujifungua.

ATHARI: Hazifahamiki

Page 106: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

106

5.15 Zingiber officinale Tangawizi

Maelezo ya kibotania: Familia: Zingiberaceae Ina asili ya nchi za tropiki za Asia. Tangawizi inaweza ikafikia urefu wa meta moja,

huota kutokana na rhizome. Rhizome ina mafuta mepesi ambayo husisimua mishipa

ya fahamu, kuzifanya makini kwa ujoto na hivyo kuleta hisia ya joto.

UKULIMA: Tangawizi inachukuliwa kama zao la mwaka au la miaka miwili hadi

kukomaa. Hustawi vizuri katika tifutifu na wenye nitrogen kwa wingi na inahitaji jua

au kivuli kidogo. Unaweza ukasambaza tangawizi kwa kugawanya rhizome

mwanzoni mwa msimu wa mvua.

UTENGENEZAJI WA DAWA ZA TANGAWIZI Poda (unga) ya mizizi ya tangawizi: inatengenezwa

kwa kuosha, kukausha, kutwanga na kuchekecha

rhizome. Ikitwangwa vizuri, kijiko cha chai kilichojaa

wima hupimwa 1.5 g.

Tincture ya tangawizi: Osha na menya mizizi, chukua

gram 25 tangawizi safi iliyokatwakatwa, ongeza kileo

80% ili kufikisha ujazo wa ml 100, acha kwa wiki moja,

na kamua.

Mafuta ya tangawizi: Chemsha gram 10 za Tangawizi

zilizooshwa, kukaushwa na kukatwakatwa, kwenye gram

50 za mafuta ya mbogamboga kwa dakika 60 katika

fukizo maji, kamua na ondoa mabaki.

MAPENDEKEZO YA JINSI YA KUTUMIA:

1. Travel sickness. Tumia kijiko 1 cha chai cha unga wa

tangawizi dakika 30 kabla ya kuondoka.

2. Kuzuia kutapika kabla ya operesheni. Tumia kijiko 1 – 2 vya unga wa tangawizi

dakika 30 kabla ya operesheni.

3. Kuzuia kichefuchefu na kutapika wakati wa ujauzito. Tumia nusu kijiko cha

chai cha unga wa tangawizi mara 3 kwa siku.

4. Bacillary dysentery. Tumia gram 45 za tangawizi, kidogokidogo kwa siku nzima.

5. Hookworms. Tumia tangawizi mbichi gram 60 mara 2 – 3 kwa siku. Kwa watoto

wadogo, changanya na asali kidogo.

6. Kikohozi, kifua, kuvimbewa. Kunywa matone 10 – 20 ya tangawizi tincture 3 – 4

kwa siku.

7. Maumivu ya viungo (Rheumatism). Fuata mchanganyiko namba 6. Na kwa

kuongezea tumia mafuta ya tangawizi ya kienyeji.

8. Majeraha. Tumia tincture ya tangawizi kama dawa ya kuua wadudu kwa

majeraha madogomadogo.

9. Malaria isiyo kali. Kula kiganja kimoja cha tangawizi mbichi kila siku, au

chemsha kiganja kimoja kwa dakika kumi. Usichuje, bali kula kila kitu mpaka

homa itakapotoweka. Kwa homa kali, tumia mtukutu (Vernonia amygdalina, sura

6.49) au Artemisia annua (sura 5.2).

Page 107: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

107

SURA YA 6

Mimea iliyoelezwa katika sura ya 5 hutumika zaidi; na pia ni mimea ambayo ni

muhimu kwa ye yote anayependa kutumia madawa ya asili. Katika maeneo ya tropiki

kuna mimea ya dawa. Baadhi ni:

Ile iliyotajwa mar chache katika vitabu vya ki-pharmacia (mfano: Kalanchoe)

Ile inayojulikana kama viungo (mfano pilipili).

Ile inayojulikana kama sumu (mfano: mranaa - Datura Stramonium)

Ile inayotumika kwa malengo ya manukato (mfano tururu)

Ile inatumika kama chakula (mf. Machungwa, makaranga)

Ile inayotumika kutibu ardhi au kuzuia mmonyoko wa udongo (mf.

Mchongoma)

Katika sura hii, tutaelezea baadhi ya mimea hiyo. Pia tumeunganisha baadhi ya

vitu vya asili vilivyo muhimu ambavyo wakati huo huo si mimea hasa na inabaki

kuwa asili (mf. asali, sukari, chumvi)

Mwonekano katika sura hii ni tofauti na ile ya sura ya tano. Katika sura hii ya 6

tumepigia mistari matibabu ambayo hasa tuliyoshauri, ama kwa sababu tulitumia

matibabu hayo sisi wenyewe, au kwa sababu matibabu hayo yanakubalika katika

vitabu vya madawa. Lakini siku zote “ACHA UZOEFU WAKO UWE

MWONGOZO WAKO.”

6.1. Adansonia digitata Mbuyu Familia: Bombaceae

Mti huu hupandwa mara chache sana. Hustawi

katika maeneo makavu kabisa na huweza kuishi

maelfu ya miaka. Mti huu una viasili ambavyo

hufaa kwa magonjwa ya moyo, kuhara, pumu,

homa na shinikizo la damu.

MATUMIZI KATIKA TROPIKI KWA

UJUMLA: Tunda lake huliwa na hutumika

kutengeneza juisi. Hutumika kutibu homa na

kuongeza utoaji wa jasho. Toka mwaka 1884, gome

limekuwa likitumika huko Ulaya mbadala badala ya

magome ya miti itumikayo kutengenezea dawa

kama kwinini kutibu homa.

Kutibu kuharisha kwa watoto: Chukua gramu 20

za nyama ya ndani ya tunda na chemsha katika

maji. Mbegu zina mafuta ambayo hutumika kwa

kupikia na vipodozi. Majani machanga yanaweza

kupikwa na kuliwa kama mchicha, au kukaushwa,

kusagwa na kutumika katika mchuzi. Mbegu nyeusi zinaweza kukaangwa,

kuandaliwa na kuliwa kama Karanga.

MIMEA 50 ZAIDI NA MAZAO YA ASILI

Page 108: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

108

6.2. Allium cepa Kitunguu maji Familia: Amaryllidaceae

Ni mmea wa msimu mmoja na aina mbalimbali ikitofautiana katika rangi. Asili yake

Asia. Mashina yake hustawi zaidi katika hali ya joto, hii ndiyo sababu katika Afrika,

vitunguu hupandwa mwanzoni mwa kiangazi.

ASIA: Hutumika kwa kikohozi, vidonda vya koo, shinikizo la damu, dawa ya

kuongeza mkojo.

AFRIKA MASHARIKI: Hutumika kwa ajili ya homa. Jamii za Waarabu huweka

vitunguu kwenye majipu. Vitunguu swaumu hutumika kwa ugonjwa ule ule kwa dozi

ya chini.

1. Upungufu wa vitamin (Upungufu wa vitamini A,B, na C)

Changanya vitunguu katika mlo wako wa kila siku. Vitunguu vinaweza kuliwa

katika umri wowote. Ikiwezekana kula vitunguu vikiwa vipya na vibichi.

2. Kuongeza kumbukumbu: Kula vitunguu vingi vibichi mara kwa mara au zaidi

vitunguu swaumu.

3. Kikohozi na madonda ya koo: Changanya ½

kikombe cha vitunguu vilivyokatwa katwa na ½

kikombe cha maji, koroga, kunywa kwa siku

nzima.

4. Maambukizi ya utumbo: Kula vitunguu vibichi

vingi vilivyo katwa katwa.

5. Shinikizo la damu, maambukizo katika njia ya

mkojo (UTI), kisukari: wakati wote kula ½

kikombe cha vitunguu vilivyo katwa katwa kwa

siku nzima. Usisahau kwenda katika kituo cha

afya kwa uchunguzi wa afya yako.

6. Maambukizo ya mba (fungus), majipu: Twanga

½ kiganja cha kitunguu kilicho- katwa na

pangusa kidonda, au eneo lililoathirika kwa maji

ya kitunguu; au weka ½ kitunguu kwenye jipu na

funga eneo hilo kwa kitambaa. Tiba hii hufaa,

ingawa kikonyo cha kitunguu swaumu

kilichokatwa, kwa vyovyote, kina nguvu zaidi,

lakini huwasha zaidi.

7. Maumivu ya sikio au linalotoa usaha: Chukua

kiganja 1 cha vitunguu vilivyokatwa vizuri,

weka katika kipande cha kitambaa cha pamba

chepesi. Tumia kitambaa hiki kugandamiza juu na nyuma ya sikio. Tunza hali hii

kwa kufunga kitambaa kuzunguka kichwa; kutunza joto; badilisha kitunguu

asubuhi na jioni.

ATHARI: Kwa watu wenye mzio au kwa kutumia muda mrefu, mwasho wa ngozi

unaweza kutokea. Kuzuia kukutana na macho.

Page 109: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

109

6.3. Aloe vera (syn. Aloe barbadensis) Aloe ferox and Aloe arborescens Msubili

Familia: Liliaceae

Msubili hutengeneza (huotesha) matawi kutoka katika shina.

Mimea ya madawa inayostawi kwa miaka mingi, matawi machanga huwa na madoa

meupe na kuwa maua ya rangi ya njano inayongaa.

Aloe ferox: Kinyume na Aloe vera, ni kijiti chenye shina moja, hukuwa na kufikia

kimo cha mita 2 – 3, maua yake ni njano, rangi ya machungwa, au nyekundu.

Aloe arborescens: Ina shina refu ambalo matawi yake huota kufuata urefu wake.

KIULIMWENGU: Utomvu wa njano upatikanao kwa

kuchanja tawi hutumika kama dawa ya kulainisha choo

(aloin).

Gel isiyo na rangi iliyo ndani sehemu ya ndani ya

jani ina tabia ya anti-allergic na anti-inflammatory.

Inatumika kwa sehemu zilizoungua, fizi zilizougua ,

ukurutu, na kwa kufunga vidonda na diabetic ulcers

(vidonda ndugu).

Nchini Uganda chai iliyotengenezwa kutokana na

majani inatumika kwa maumivu ya tumbo (gastritis):

Kiganja kimoja cha majani, yaliyokatwa vizuri, katika

lita moja ya maji ya moto.

1. Kutengeneza dawa ya kuharisha: Osha jani kwa maji

ya moto likiwa bado kwenye shina, kausha na likate.

Weka kwenye kikombe, likiwa limekatwa katikati hadi chini. Baada ya dakika 15

pima utomvu uliopatikana na changanya na sukari kipimo mara tatu zaidi. Kausha

mchanganyiko wa “Aloe sugar” juani, ndani ya chandarua.

Watu wazima watumie gram 3 wakati wa jioni kama dawa ya kuharisha, lakini sio

wakati wa ujauzito, na wala sio kwa matumizi ya muda mrefu.

2. Kuungua: Kata na osha vizuri jani la mmea. Safisha kisu kikali na kukiweka

kwenye maji ya moto. Kata sehemu za pembeni na za mwisho za jani, na kisha

kata sehemu ya katikati ili kupata sehemu kubwa ya ndani ya jani. Paka sehemu

yenye utomvu ya jani (“aloe gel”) kwenye sehemu yote iliyoungua. Fanya hivyo

mara nne kwa siku. Mgonjwa akae ndani ya chandarua ili kuzuia inzi. Tiba hii

kwa majeraha ya kuungua hutoa matokeo bora kuliko hata Vaseline gauze ya

kawaida.

3. Vidonda, ulcers na diabetic ulcers: Fuata mchanganyiko namba 2. Kila baada ya

tiba, tumia kipande kidogo cha papai bichi, asali au sukari kama ilivyoelezwa

katika sura 5.5. na 6.30.

4. Conjunctivitis: Kwa macho mekundu, fuata mchanganyiko namba 2. Weka jani

juu ya jicho kwa dakika 5, mara 4 kwa siku.

5. Nywele kutoka: Chukua aloe gel kutoka kwenye jani. Changanya kijiko kimoja

cha mezani kwa kiini cha yai bichi na chua nywele kila jioni kwa kutumia

mchanganyiko huu. Au tumia aloe gel peke yake.

6. Vidonda vya magonjwa ya zinaa: Tibu mara 3 kwa siku kwa kufuata

mchanganyiko namba 2. Halafu kunywa antibiotics.

Page 110: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

110

6.4. Amaranthus gracilis Mchicha

Familia: Amarantaceae

Kuna aina nyingi mbalimbali za mchicha, lakini zote

zinafanana kitabia.. Ni zao la mwaka, na ni mmea wenye

lishe, na hustawi vizuri kwenye ardhi yenye naitrojen

kwa wingi. Majani yake yana vitamin C kwa wingi,

chuma na protini na ni mboga nzuri sana. Mbegu vilevile

zina lishe ya hali ya juu na protini kwa wingi.

KATIKA TROPIKI

Majani yanatumika kama mboga na kutibu upungufu wa

Vitamin C na upungufu wa damu.

Mchicha usichukuliwe tu kama magugu, lakini

uthaminiwe na kulimwa zaidi; panapokuwa na nafasi

tupu shambani (mfano: kati ya mhogo na mhogo) siha

mchicha.

6.5. Ananas comosus Nanasi Familiae: Bromeliaceae

Nanasi lina kimengenya kiitwacho “bromiline,” ambacho hupunguza inflammation.

Nanasi lililoiva lina vitamini C kwa wingi.

1. Oedema na inflammation kwa nje: Funga kipande cha nanasi bichi kwenye

oedema au sehemu iliyovimba (mfano, kwa kitambaa chembamba.)

2. Amenorrhea (kutokuingia hedhini), magonjwa ya njia ya mkojo, dawa ya

kuongeza mkojo na kwa minyoo; changanya kiasi cha gram 500 cha nanasi

mbichi kwa 0.7 ya lita ya maji, chemsha pamoja, na kunywa kidogokidogo kwa

siku nzima. Kama ni lazima rudia kwa siku kadhaa.

3. Upungufu wa Vitamin C na homa: Kunywa juisi nyingi ya nanasi zilizoiva ili

kusaidia mfumo wa kinga wa mwili wako. Juisi za matunda yafuatayo nazo zina

vitamin C kwa wingi pia: limau,

machungwa, papai, machenza,

matunda damu.

4. Kuvimbewa: Juisi ya nanasi

mbichi ni ya kufaa sana na

inasaidia.

5. Kama papaine ya papai, bromeline

nayo hufanya nyama ngumu kuwa

laini. Funga nyama ngumu ndani

ya ganda la nanasi mbichi usiku

kucha. Angalia juisi ya nanasi

isiguse macho. Juisi ya nanasi

mbichi haipendekezwi kutumiwa na wajawazito au wagonjwa wenye vidonda vya

tumbo.

Page 111: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

111

6.6. Arachis hypogaea Karanga Familia: Papilionnaceae

Mmea una urefu wa sm 20 – 30, matunda hukomalia

ardhini.

KATIKA TROPIKI

Karanga zina protini na vitamin kwa wingi. Protini

iliyomo katika maziwa ya unga ni sawa na karanga

zilizokaushwa, lakini, katika maeneo ya tropiki,

protini huwa ni mara kumi zaidi. Mafuta yana lishe

pia, na yanaweza yakakamuliwa katika maeneo ya

vijijini kwa kutumia mashine rahisi. Ingawaje

hayadumu kwa muda mrefu.

Kukosa usingizi: Kunywa dawa ya kumwagia maji ya

moto kikombe kimoja cha maji ya moto kwenye

kiganja kimoja cha majani ya Karanga.

6.7. Bixa orellana (lipstick tree) Annatto

Familiae: Bixaceae

Bixa ni kimti kinachokua haraka katika maeneo ya

tropiki; mbegu zake ni nyekundu zilizokoka. Rangi

hii (annatto, terra indica) ina carotinoids, haina

madhara yoyote na inatumika duniani kote kwa

kuweka rangi kwenye jibini, mtindi, mandazi, nyanya

zilizopikwa kiwandani, lipstick, nywele, pamba na

hariri.

AMERIKA YA KUSINI

Rangi inatumika kwa kulinda ngozi dhidi ya jua

wakati wa safari ndefu.

1. Kusafisha vidonda (PHILIPPINES): Chemsha

vijiko 10 vya mbegu za Bixa (nzuri ni zile

utakazochukua kwenye maganda yanayokaribia

kupasuka) katika vijiko 10 vya maji, chuja, na

ongeza kijiko 1 cha juisi ya kitunguu swaumu kipya.

2. Kuungua: Chemsha vipimo 10 vya mafuta ya mbogamboga kwa kipimo 1 cha

mbegu safi za bixa; chemsha kwa dakika 10 katika joto la 100º na chuja.

3. Tunatumia Bixa kuweka rangi katika sabuni (Tazama sura 4.1.7.) na dawa ya

mafuta, kwa kuongeza mbegu mpya katika mafuta yanayochemka.

Michanganyiko ya maji inaweza kuwekewa rangi nyekundu kama ifuatavyo:

Acha gram 100 mbegu na gram 0.5. NaOH (Sodium hydroxide) katika ml 200 za

maji kwa saa 6, chuja na ongeza maji kadri unavyotaka. Au: kutengeneza wino

mwekundu, ongeza gram 20 kwenye mchanganyiko huu (kama dawa ya

kuhifadhi). Hii inafaa pia kwa kunyesha wino kalamu za highlighter!

Page 112: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

112

6.8. Brassica oleracea Kabeji Familia: Brassicaceae

Mboga yenye chuma kwa wingi;

inaweza kuliwa mbichi au

imepikwa. Utomvu wa kabeji

mbichi una kitu chenye uwezo

wa kuzuia vidonda (anti-

ulcerous) ambacho hutunza

sehemu laini ya (mucous

membrane) tumbo – DR.

KONGO – KIVU, ULAYA:

Mboga huliwa kwa kutibu

upungufu wa vitamin C na

huliwa mbichi kwa vidonda vya

tumboni. Majani mapya

hutumiwa kutibu magonjwa ya ngozi, hasa eczema ambayo haijulikani chanzo.

6.9. Cajanus cajan Mbaazi Familia: Fabaceae

Ni mmea wenye jamii ya mikunde

mikunde, urefu wake ni meta 2, maua

yake ni njano na yana urefu wa kadri

ya sm 1.5. Ganda lake lina nywele

nywele sm 4 – 7 urefu na lina mbegu

2 – 7. Majani yake ni mbolea nzuri.

Hukua katika maeneo ya tropiki

kuanzia usawa wa bahari hadi

mwinuko wa meta 2,400. Ni mmea

unaofaa sana.

Kwa kuzuia mmonyoko wa udongo:

Kwa sababu hii panda mbaazi kwa

kukingama Mteremko, kufuata mistari

ya kontua . Panda sm 20 kutoka mmea

hadi mmea, katika mistari meta 3 – 5

mbalimbali. Kati ya mistari hii lima

mazao ya chakula na mimea ya dawa.

ASIA: Hutumika katika majipu

yanapokuwa katika hatua za awali,

mseto wa ndizi mbichi na mbegu za

mbaazi unawekwa katika sehemu

iliyoathirika na kufungwa kwa kitambaa kisafi.

AFRIKA: Mmea wa kufunika ardhi: Mbegu zina protini kwa wingi, na zinaweza

kuliwa. Ziloweke kwa saa kadhaa, zitwange na kisha ama kanga au pika kwa mvuke.

Mbaazi ambazo hazijakomaa zinaweza kuchemshwa na kuliwa kama mboga.

Page 113: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

113

6.10. Canarium Schweinfurthii Mbafu Familiae: Burseraceae

Mti mkubwa wa porini wenye gome

lenye nyufa. Tunda lake kama mzeituni,

likipikwa na kuwekewa chumvi ni laini.

Mara baada ya kukata katika gamba,

utomvu unaonata na laini (“elemi),

hujitokeza, wenye harufu kali kama

terpenes.

AFRIKA: Elemi inatumika katika tochi,

au inawashwa moja kwa moja kama

mbadala kwa mshumaa. Katika

makanisa ya Catholic hutumika kama

ubani. Kwa dawa hutumika katika dawa

ya mafuta na mafuta ya maumivu ya

viungo na kuvimba viungo. (Tazama

sura 4.3) na upele (scabies). Nchini

Congo dawa ya kutokosa ya gamba la

mti hutumika kwa maumivu ya tumbo,

maumivu ya baada ya kujifungua na

kondo la nyuma kuchelewa kutoka.

ULAYA: Utengenezaji wa “elemi

depuratum” chemsha utomvu taratibu, chuja kwa nguo na tunza kwenye chombo

kisichopitisha hewa. Hutumiwa katika plasta ili kuchochea ngozi kuweza kufanya

kazi. Hutumika katika useremala kutengeneza varnish. Varnish ya kawaida ni mafuta

ya mbono, mbegu za kitani, au ufuta kama hii ni ghali sana. Changanya (ujazo)

kipimo kimoja cha elemi na vipimo 2 vya nta

(mshumaa) kwenye vipimo 7 vya dizeli, chemsha

katika oven ya sola (kamwe usichemshie kwenye

moto!) na chuja ikiwa moto. Kwa matumizi ya

nje, oil ya injini inatumika badala ya dizeli.

6.11. Cannabis sativa Bangi Familia:

Cannabaceae

Mmea wa porini unaopatikana duniani kote. Ncha

za mmea wa kike huvunwa na kutumiwa. Joto la

kukaushia lisizidi 50ºC.

AFRIKA: Bangi mara nyingi huvutwa na watu

wenye magonjwa ya akili au masikini sana.

Inatumika kama dawa kuondoa – maumivu na

“kuwa mtu wa juu.” Kwa kawaida ukulima wa

Page 114: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

114

bangi na biashara vinapigwa marufuku.

KATIKA TROPIKI: Kama morphine, bangi iko katika opioid analgesics. Kama

hakuna opiods za biashara, au kama ni ghali sana kwa wagonjwa wenye kansa au

UKIMWI bangi inaweza ikawapunguzia maumivu – lakini hakikisha unazitaarifu

mamlaka zinazohusika kwanza. Kabila la Wagenia nchini D. R. Kongo hutumia chai

iliyotengenezwa kwa majani. Kuosha na kusuuza ukeni kama mtoto njiti anatarajiwa

kuzaliwa.

Kutapika kwa wagonjwa wa kansa na UKIMWI, maumivu makali, psychotic crying:

Mpe sigara ya bangi. Hufanya kazi, karibia hapo hapo, hukolea zaidi baada ya dakika

30 na hutoka baada ya saa 3. Au badala yake chai ya bangi au tincure inaweza

kutumika. Hizi huchukua karibu saa moja kufanya kazi, lakini nguvu yake hukaa

kadri ya saa 8.

ATHARI: Athari ni pamoja na kichefuchefu, kupoteza kumbukumbu kidogo,

wasiwasi, kufunga choo na schizophrenia.

6.12. Cassia spectabilis Familia: Caesalpiniaceae

Ingawaje huu mti hautumiki sana kwa

shughuli za tiba, tumeuingiza hapa kwa

sababu ya thamani kubwa kama “Ua

unaoishi,” kwa kustawisha misitu na

kuzuia mmomonyoko katika bustani za

dawa. Hujiotesha katika misitu ya nchi

za tropiki, una maua makubwa ya

njano sana, umbo lake linafanana na

maua ya mti horse chestnut tree wa

Ulaya.

Kwa kukata vitawi vyenye urefu

kama wa meta moja unaweza

kuanzisha pori jipya.

Chini ya matawi ya mti huu kilimo

kinaweza kufanyika. Ili kuzuia

mmomonyoko, weka vitawi hivyo sm

50 kwa kina ardhini, ukiacha kati ya

mti na mti sm 20. Mwanzo wa msimu

wa mvua, kata ua hadi urefu wa meta 1,

na fukia matawi udongoni kama

mbolea.

Maambukizi ya mba (fungal infections)

kama Cassia alata (ringworm bush, Tazama sura 5.6) haipatikani, tumia Cassia

sptectabilis badala yake.

Page 115: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

115

6.13. Cinchona officinalis

Familia: Rubiaceae

Aina mbalimbali ziko katika Cinchona

officinalis, mfano, Cinchona succiruba,

mti ambao hufikia urefu wa meta 24

kwenda juu. Miti ya Cinchona, ambayo

ina asili ya Andes, huota mahali popote

katika maeneo ya tropiki, na hustawi vizuri

kwenye mwinuko kati ya meta 1,000 na 2,

400. Gamba la Cinchona huvunwa ama

kwa kukata miti yenye umri wa miaka 8 na

kuondoa gamba, au kwa kukata vipande

vyembamba vya gamba wakati mti ukikua.

Majeraha ya mti yanafunikwa kwa

mfinyanzi au moss. Gamba lililovunwa

linakaushwa juani.

Miti ya Cinchona iliyo porini imekuwa

ikiteketezwa kwa ukataji usiodhibitiwa.

Kama una bahati ya kuishi katika maeneo

yenye mwinuko sahihi kwa upandaji wa Cinchona, panda miti hata 3 katika bustani

yako. Gamba la Cinchona limekuwa likitumiwa kwa zaidi ya miaka mia tatu kutibu

homa na malaria.

Kutegemea na aina, gamba lina asilimia kati ya 1 na 3 quinine, na kadri ya

asilimia 4 quinine na alkaloids zingine. Kwa uzalishaji wa kiwandani, quinine

ambayo ina nguvu ya kutibu malaria, inatengenezwa kuwa vidonge (dozi ya kila siku

kwa watu wazima: gram 1 – 2) . Quinidine inatumika kwa wagonjwa ambao

magonjwa yao yanaambatana na moyo (mapigo ya moyo yanakwenda haraka sana).

1. Malaria: Kama chaguo la kwanza, tumia Artemisia annua (Tazama sura 5.2), kwa

kuwa ina madhara kidogo. Tumia cinchona iwapo tu Artemisia annua haifanyi

kazi. Chemsha gram 10 au vijiko vya chai vitatu vilivyojaa kabisa vya gamba la

cinchona lililosagwa vizuri katika lita 1 ya maji kwa dakika 10, chuja na kunywa

kidogokidogo kwa zaidi ya saa 24. Hii ni sawa na kama mg 350 za quinine.

Watoto wapewe kidogo kutegemea uzito wa miili yao.

2. Kama ungependa kuwapa wageni wako “soda” chemsha gram 1 au ¼ kijiko cha

chai cha gamba la cinchona kwenye kikombe 1 cha maji kwa dakika 10. Ongeza

juisi na ganda lililokunwa la limau 3, chemsha tena kidogo na chuja. Sasa ongeza

gram 300 au vikombe 2 vya sukari na lita 3 na maji baridi. Tumia ikiwa imepoa.

3. Lotion ya nywele: Chua nywele kwa kutumia mchanganyiko namba 1 juu.

ATHARI

Ikitumiwa kwa ndani: kuumwa kichwa, kutapika au kuharisha. Huchochea mtu

kujifungua, kwa hiyo usitumie mchanganyiko namba 1 kama kuna hatari ya mimba

kutoka. Kama ikitumiwa kwa kipindi kirefu, kuharibika kwa kiini tete, macho

kuharibika na hata kutokusikia kunaweza kujitokeza.

Page 116: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

116

6.14. Citrus sinensis Chungwa Familia: Rutaceae

Mti hukua hadi meta 5 urefu, na

maua meupe yenye harufu nzuri.

Matunda hubadilika kuwa njano au

orenji yanapoiva. Ganda lina

mafuta yaliyo muhimu sana. Juisi

ina tindikali, sukari na vitamin C.

KIULIMWENGU: Ganda linaleta

hamu ya chakula na kusaidia

kuyeyusha chakula. Kata kata

ganda. Chemsha vijiko 10 vya

mezani katika lita moja ya maji

kwa dakika 2, kamua na kunywa

kwa siku nzima.

AFRIKA: Kwa pumu, kikohozi,

kuumwa kichwa (migraine):

Chemsha kiganja 1 cha majani katika lita 1 ya maji kwa dakika 2 na kunywa siku

moja. Kwa madonda ya midomo au mdomoni, fuata mchanganyiko uleule kama wa

limau; sura 5.8.

6.15. Cocos nucifera Nazi

Familia: Palmae

Nazi ni mmea wenye chakula

chenye lishe. Wakati wa vita ya II ya

dunia, Askari wa kiingereza barani

Afrika walitumia juisi ya nazi badala

ya glucose (ina 5% glucose safi –

lakini hili siyo pendekezo!)

AFRIKA: Juisi humwagwa mbali

mara nyingi . Baada ya kuongeza

chumvi kidogo inaweza ikatumika

kama kinywaji cha kuongeza maji

kwa watoto wanaoharisha (kama

Oral Rehydration solution). D. R.

Congo inatumika kama lotion ya

nywele na ngozi pia.

Page 117: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

117

6.16. Coffea sp Kahawa Familia: Rubiaceae

Katika nyanda za chini aina ya “robusta”

hulimwa, katika nyanda za juu “Arabica.”

Aina mpya “arabusta” hustawi vizuri

katika safu za miinuko.

KIULIMWENGU: Kahawa hunywewa:

a) Kwa aina fulani ya maumivu makali ya

kichwa (migraine)

b) Kichefuchefu

c) Kwa kuamsha, kuchochea na

d) Katika kiasi kikubwa, lakini ikiwa na

maji mengi, kama dawa ya kuongeza mkojo.

Isitumiwe na watu wenye vidonda tumboni. Kahawa huongeza kiwango cha mapigo

ya moyo.

6.17. Cola acuminate, cola nitida Ugongolia Familia: Sterculiaceae

Miti hii inapatikana Afrika Magharibi. Karanga zake zina kadri ya 2% catechine –

caffeine (colanine). Mapigo ya moyo yanazidi na mkojo unaongezeka kwa kiwango

cha chini ukilinganisha na kahawa (Baadhi ya Waafrika hawawezi kunywa kahawa,

lakini kiasi kilekile cha caffeine kilicho katika ugongolia hakiwaletei matatizo

yoyote!).

Karanga mbichi lazima

zitunzwe kwenye ardhi yenye

unyevu au mchanga. Karanga

hukaushwa kwa kukatwa

katwa vipande vyembamba na

kuzikausha kwa saa 24 katika

joto la 80ºC. Kuzioka

zikatwekatwe vipande na

kuokwa kama kahawa.

ULAYA: Kichocheo chenye

nguvu

Kwa kuumwa kichwa (migraine), kuharisha, neuralgia na kutumiwa kama kichocheo

au cardiotonic.Tumia gram 1 – 4 karanga kavu, zilizotwangwa kila siku.

Kwa huzuni, kukosa hamu ya chakula, na kwa kuondoa majonzi: Tumia Karanga 1

kila siku.

Page 118: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

118

6.18. Cucurbita maxima Boga Familia: Cucurbitaceae

Mmea unaotambaa, ni wa mara moja kwa

mwaka.

KIULIMWENGU: Boga, mbegu na majani

ni chakula bora. Mbegu zina nguvu ya

kutibu minyoo na prostatitis (Kuvimba kwa

tezi za kiume, ambacho husababisha ugumu

wa kukojoa hasa kwa wanaume wazee).

1. Kwa tegu: Tumia gram 100 (au vijiko 20

vya mezani) mbegu mbichi zilizosagwa

pamoja na dawa ya kuharisha kabla ya

kula. Dawa ya kuharisha ni muhimu

sana, kwa sababu minyoo hafi, ila

hupooza. Kama dawa ya asili ya kusaba

bisha kuharisha, kula mapapai au

maembe mengi yaliyoiva sana.

2. Kuchochea Maziwa kutoka baada ya

kujifungua: Tumia vijiko 2 vya mezani

vya mbegu mbichi zilizosagwa na maji kwa wingi kwa siku 7 mara mbili kwa siku

(asubuhi na jioni).

3. Prostatitis: Mchanganyiko uleule kama namba 2 juu, tumia kwa mwezi 1 – 2.

6.19. Curcuma longa Dawam mchuzi Familia: Zingiberaceae

Ni mmea, majani 15 kwa sm 40, hutokea kwenye shina (rhizome) lenye umbo la

kiganja. Maua huota kwa kujitegema kutoka

kwenye majani moja kwa moja kutoka

kwenye shina (rhizome), ambalo ni la njano

na lina ladha kama ya tangawizi.

Ili kuhifadhi, kata vipande vyembamba,

acha vikauke, na hifadhi sehemu yenye

ubaridi na kavu.

MATUMIZI DUNIANI KOTE

1. Kwa maumivu na kuvimba kwa viungo

(Baridi Yabisi)

Kula mara 3 kila siku gram 0.5 za unga

wa dawam mchuzi. Hii imethibitishwa

katika kliniki.

2. Kwa tumbo kujaa hewa, kuvimbewa,

hedhi isiyo na utaratibu maalum, na

kuchochea utoaji wa nyongo:

a) Kula gram 1 dawam mchuzi (unga)

mara 3 kwa siku, au

Page 119: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

119

b) Twanga gram 3 za dawam mchuzi kavu, au gram 10 za shina (rhizome) bichi,

chemsha katika 0,7 lita ya maji kwa dakika 5, na kunywa kwa siku nzima.

Rudia kwa siku kadhaa au

c) Changanya gram 50 za mizizi mikavu iliyotwangwa ya dawam mchuzi kwa

ml 100 za kileo kizuri 50%, chuja baada ya wiki moja. Dozi kwa watu

wazima: matone 20 mara 3 kila siku.

3. Kwa kikohozi: Tumia gram 6 kavu, au gram 20 za rhizome mbichi; twanga,

chemsha katika 0.7 lita ya maji kwa dakika 5, kunywa wakati wa mchana, na kwa

siku kadhaa. Dawam mchuzi vilevile inatumika kama kitu muhimu katika binzali.

Curcumin ambao inaweza ikapatikana katika dawam mchuzi, inatumika kuweka

rangi katika pamba, hariri, nta , jibini, poda na krimu.

6.20. Datura stramonium Mranaa Familia: Solanaceae

Mmea wenye sumu sana, hufikia urefu wa meta 1, unapatikana katika nchi za Tropiki

kuanzia mwinuko wa meta 0 – 2,000 hupendelea

kuota kwenye kifusi au madampo. Maua yana

urefu kadri ya sm 8, muundo wa tarumbeta meupe

au blue. Mranaa una atropine na anti-spasmodic

alkaloids zingine. Kwa sababu hii hutumika kama

dawa ya kupunguza cramps.

AFRIKA: Majani yalichemshwa na

kutwangwa huwekwa kwenye majeraha ya

kuungua ili kupunguza maumivu. Na hii ifanyike

tu kama jeraha la kuungua ni dogo, kwa sababu ya

hatari ya sumu. Majani lazima yachemshwe ili

kuzuia maambukizo ya bacteria kwenye jeraha.

1. Kuumwa na wadudu: Pangusa sehemu

iliyoathirika ya ngozi kwa utomvu kutoka

kwenye majani (Baadaye nawa mikono).

2. Pumu: Majani huvutwa kama sigara kutibu

pumu. Sigara za pumu zenye nguvu hutengenezwa kama ifuatavyo:

- Majani makavu ya mranaa mg 150

- Majani makavu ya mkaratusi mg 150

- Majani makavu ya mpapai mg 700

Tengeneza sigara kwa karatasi, au tumia kiko.

3. Magonjwa mbalimbali; Tincture ya mranaa (kwa matumizi ya hospitalini tu)

- Mbegu za mranaa, zilizokaushwa (sio zaidi ya joto la 50º C)

- na kupandwa vizuri gram 8

- Plain alcohol 95% ml 45

- Maji yaliyochujwa ml 55

Changanya, baada ya wiki moja kamua na ondoa mbegu. Dawa hii ni sawa na

belladonna iliyoagizwa nje yenye atropine (0.03%) na ni sawa kwa matumizi na dozi

Page 120: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

120

(watu wazima, isizidi matone 30 mara 3 kila siku, watoto: Isizidi tone 1/kilo ya uzito

wa mwili mara 3 kila siku).

Matumizi yake:

A. Intestinal spasms, figo au bile colics, kushambuliwa na pumu

Matone 30 kila saa zipitazo 2, sio zaidi ya matone 90 kwa siku.

B. Pumu sugu, madonda ya tumbo: Matone 5 – 10 mara 3 kila siku.

C. Dawa ya awali kabla ya operesheni: Dozi kwa mjibu wa daktari katika hali mbaya

pamoja na chai ya bangi.

D. Parkinson’s disease: Anza na matone 5 mara 3 kwa siku, na ongeza dozi hadi

athari ziwe kubwa kuliko manufaa.

E. Poisoning with organophosphates: Tumia matone 30 (au zaidi, kama ilivyoelezwa

na daktari) kila dakika 30 mpaka kupiga kwa moyo au mishipa kumekuwa

kawaida.

F. Katika kipindi cha msukosuko, kwa mfano vita, unaweza kutafuna mbegu moja

kwa moja badala ya kutumia tincture. Matone 2 ni sawa na mbegu 1, kwa hiyo:

watu wazima: Tumia mbegu zisizozidi 15, mara 3 kwa siku. Hii ina maana, siyo

zaidi ya mbegu 45 kwa siku. Watoto: Mara 3 kwa siku, kiasi cha mbegu 1 kwa

kila kilo 2 za uzito wa mwili.

ATHARI: Datura stramonium ni mmea wenye sumu kali. Dozi inayotumika kwa

matibabu na dozi inayokuwa sumu inakaribiana sana. (K.m. mbegu 10 zinaweza

kuwa dawa, mbegu chache zikiongezwa, tayari zinaweza kuwa sumu)

Alkaloids iliyo katika majani hubadilika wakati wa mchana, lakini mbegu

tulizokusanya zilikuwa na 0.4% alkaloids zisizobadilika, zilikuwa ni

atropine/hyoxyamine. Kwa sababu hii tunatumia mbegu na

sio majani.

6.21. Daucus carota Karoti Familia: Apiaceae

Katika nchi za tropiki, karoti hustawi sana katika nyanda za

juu. Mizizi yake ni chakula (na ni bora zaidi, zikiliwa

mbichi kuliko kupikwa) kwa kuwa zina carotene,

provitamin A (ambayo hugeuzwa mwilini kuwa vitamin A).

KIULIMWENGU: Karoti mbichi zinatumika kuimarisha

tumbo, utumbo na matumbo. Kwa maana hiyo zinafaa kwa

yote: kwa kutibu kuharisha na kwa kutibu shida ya

kutokupata choo (obstipation) - hasa kwa watoto, kwa

tumbo lililojaa hewa na tumbo lililosumbuliwa na Kemikali

kali iliyomo tumboni (gastric acid). Karoti zina nguvu

kidogo kwa minyoo ya safura, hedhi isiyo na utaratibu

maalum, na prostatitis. Kula karoti mbichi kila siku

hupunguza kiwango cha lehemu na kwa hiyo ni hatua ya

kuzuia mishipa kuvimba na kuwa migumu

(arteriosclerosis).

Page 121: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

121

6.22. Elaeis guineensis Mchikichi Familia: Palmaceae

Mchikichi una asili ya Afrika, na sasa unapatikana katika nchi zote za tropiki.

Mawese yanapatikana kwa wingi madukani, na yamekuwa sehemu ya milo barani

Afrika kwa karne nyingi sasa. Yanaweza pia yakatengenezwa kutokana na miti yenye

matunda iliyoota porini, lakini upatikanaji wa mawese kwa wingi unatoka kwenye

miti iliyopandwa na kutunzwa . Hustawi vizuri mahala ambapo kuna joto mwaka

mzima, kati ya 25º na 28° C, mvua nyingi na udongo wa ki-mchanga. Kwa hiyo

unaweza ukahitaji kurutubishwa. Katika hali hizi, mchikichi utaanza kuzaa matunda

miaka 3 – 4 baada ya kupanda.

Kutoka kwenye mchikichi, mtu anaweza akazalisha mawese au palm kernel oil.

1. Mawese:

Ili kutengeneza mawese bora, tengeneza siku

ileile mbegu zilipovunwa. Tumia mawese

wekundu kwa kupika, au bora zaidi tumia

matunda mabichi ya chikichi, unapopika kwa

mafuta. Rangi ya nyekundu iliyokolea ni kwa

sababu ya carotene nyingi iliyomo, ambayo pia

huitwa “provitamin A”. Kama utatumia kijiko

kimoja cha chai kwa siku cha mawese,

unaweza ukatupa vidonge vyote vya vitamin A!

Miongoni mwa vitu vingine, vitamin A hulinda

macho. Katika nchi ambazo chikichiki hustawi,

watu wachache hupata upofu!

Usafirishaji wa mawese duniani ni wa pili

tu kwa mafuta ya soya. Kiwango kikubwa

husafirishwa kutoka Afrika kwenda

kutengenezwa upya na kurudishwa tena Afrika

kama “mafuta safi” mawese yasiyo rangi. Kwa

kweli, vitamin zimeondolewa, kwa hiyo mafuta haya ni halisi kwamba “hayana

vitamin” au “hayana lolote.” Yaache kabisa mafuta haya, kama inawezekana

zalisha ya kwako mwenyewe.

Mawese ni muhimu katika utengenezaji wa sabuni, dawa za mafuta, na

vipodozi. Hapa tunapata jina Palmolive!

Kama unataka kweli mawese yasiwe na rangi, labda kutengeneza sabuni

nyeupe, chemsha mawese katika chungu; chemsha sana hadi carotene iharibike

(itolewe) (inakuwa tayari pale ambapo karatasi nyeupe iliyochovywa kwenye

chungu haibadiliki kuwa njano); Lakini kwa makini. Huruka sana, na kuna hatari

kubwa kwa mafuta kushika moto. Vaa miwani, na watoto wakae mbali.

2. Palm kernel oil:

Huzalishwa kwa kuondoa gamba la juu la mbegu, kuzioka ndani ya sufuria,

kuponda ponda mbegu hadi kuwa kama uji mzito, kuongeza maji, kuchemsha na

hatimaye kuengua mafuta ya juu. Mafuta haya lazima yachemshwe tena ili

kuondoa dalili zote za maji. Mafuta haya hayana rangi, na kipodozi kizuri.

Yanatumika kutengeneza chochote, na kama kitu cha msingi kwa kutengeneza

Page 122: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

122

suppositories; yeyusha vipimo 6 palm kernel oil na vipimo 4 kama unaishi

maeneo ya baridi, au vipimo 5 (maeneo ya joto) vya nta ya nyuki.

Baada ya kuzalisha palm kernel oil, mabaki, mashudu ya palm kernel oil yana

protini kwa wingi na yanaweza yakapewa mifugo.

6.23. Harungana madagascariensis Mdura

Familia: Hypericaceae

Utomvu wa mmea unaweza kutumiwa kwa

magonjwa ya ngozi, kwa upele (scabies) na kama

haemeostatic (hii ina maana – kuzuia damu kuvuja),

kwa mfano baada ya tohara. Kwa mjibu wa

majaribio ya maabara, mtokoso (dawa ya kutokosa)

kutoka kwenye gamba una nguvu ya kushambulia

tegu, magonjwa ya njia ya mkojo “Trichonomas-

vaginalis” na malaria. Utomvu mwekundu wa mmea

huu unatumika kupaka rangi nguo.

D. R. CONGO: Mbegu hutumika kuharakisha

kujifungua, au kwa kutoa mimba.

AFRIKA MASHARIKI: Mtokoso kutoka kwenye mizizi au gamba, ukitumiwa mara

mbili kwa siku, husimamisha hedhi.

UJERUMANI: Tincture iliyozalishwa kutoka kwenye majani na gamba la mmea

huboresha utoaji wa juisi zinazoyeyusha chakula kutoka kwenye nyongo na

kongosho. Watu wazima watibiwe kwa tincture iliyotengenezwa kwa mg 35 majani

na gamba la mdura kwenye kijiko 1 cha mezani cha kile (45%) mara moja kwa siku.

ATHARI:

Kuhisi mwanga wa jua kwa urahisi sana. Kwa hiyo epuka kukaa juani moja kwa

moja wakati wa tiba.

6.24. Helianthus annuus Alizeti Familia:

Asteraceae

Alizeti sanasana hupandwa kwa madhumuni ya

mapambo. Hustawi vizuri kila mahali katika

maeneo ya tropiki. Mafuta ya hali ya juu

yanaweza yakakamuliwa kutoka kwenye mbegu.

Pamoja na vitu vingine, yanatumika katika

margarine na vipodozi. Mmea ni chakula kizuri

kwa mifugo, na ni mzuri kama mbolea ya asili.

PHILIPPINES: Dawa ya kutokosa (mtokoso)

kutoka kwenye mbegu inaotumika kwa kuumwa

kichwa. KIULIMWENGU: Mbegu zinatumika

kama chakula (zina protini na mafuta, hasahasa

safarini.

Page 123: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

123

6.25. Hibiscus sabdariffa Ufuta Familia: Hibisceae

Kimti kinachopatikana Sudan, sasa

kinapatikana katika maeneo yote ya tropiki.

MAENEO YA TROPIKI: Chai kutoka kwenye

maua ya ufuta ina ladha nzuri na chachu

kidogo. Inatumika kama chai ya kuburudisha

na chai ya kifungua kinywa. Ukitumia kiasi

kikubwa cha chai yake, ina nguvu ya kuongeza

mkojo na huleta kuongezeka kwa utoaji wa

nyongo na jasho. Katika majaribio ya kliniki

ufuta ulionyesha tendo la kuchelewesha ukuaji

wa bacteria na kifua kikuu, kwa hiyo, kunywa

chai hii mara kwa mara kwa tiba yoyote

uliyopewa ya kifua kikuu.

ULAYA: Inatumika kuweka rangi nyekundu

ya kuvutia kwenye chai ya dawa ya mmea.

6.26. Ipomoea batatas Viazi vitamu Familia: Convolvulaceae

Mmea wa mwaka wenye maua meupe na bluu. Ni mmea mzuri kwa kufunika udongo

(udongo unaopigwa jua hupungua rutuba – kama ilivyo katika mashamba ya

mihogo). Zao ambalo ni mzizi lina protini kwa wingi sana kuliko mhogo na hivyo

lipewe kipaumbele. Viazi vya njano husaidia kuzuia upofu, hasa kwa watoto, vina

vitamin A kwa wingi sana na majani yake. Majani yake huliwa yamepikwa, yana

vitamini C kwa wingi na chuma, ambayo huyafanya yawe na uwezo wa kupambana

na upungufu wa damu.

MAENEO YA TROPIKI: Viazi vitamu

huliwa lakini, cha kusikitisha majani huliwa

kwa nadra sana kama mboga.

PHILIPPINES: Majani yanatumika kama

dawa ya kuzuia kuharisha.

AMERIKA KUSINI: Dawa inayofahamika

kwa wengi, majani yanatumika kwa uvimbe

(tumours) hasahasa wa kikoromeo.

ASIA: Kwa gastritis, viazi vitamu

vilivyopikwa hukatwakatwa, kukaushwa na

kutwangwatwangwa kuwa unga. Kijiko 1

cha chai kinachukuliwa kwa maji kidogo.

Kwa mjibu wa mchanganyiko mwingine wa

kuzuia kuharisha, viazi vibichi

hukatwakatwa, kukaushwa na kisha

kuchemshwa hadi kuwa mkaa, kusagwa na

unga kutumiwa kwa kumeza.

Page 124: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

124

6.27. Kalanchoe pinnata Kineterete Familia: Crassulaceae

Mmea wa mapambo ambao hukua hadi

urefu wa meta 1. Mimea mipya inaweza

kuzalishwa kwa kukata majani na

kuyapanda.

INDIA: Huitwa “Mmea wa ugonjwa wa

kichwa”; dawa nzito kama uji

iliyotengenezwa kwa majani unawekwa

sehemu ya mbele ya kichwa.

MAENEO YA TROPIKI: Kwa

kuungua: Majani yaliyotwangwa

yanachemshwa kwa dakika 20 ndani ya

maji kidogo na kutumiwa kwenye ngozi

iliyoungua kama dawa ya kubandika.

Kwa majeraha: Ponda kiganja kimoja

cha majani yaliyooshwa, ongeza sukari

au asali kijiko 1 cha chai, na chemsha

mchanganyiko hadi ubadilike kuwa

kahawia (caramel – like). Inatumika

kama dawa ya kuweka kwenye kidonda

na iwekwe mpya mara mbili kwa siku.

SENEGAL: Hutengenezwa dawa nzito ya majani kwa ajili ya maumivu ya viungo.

NCHI NYINGI ZA TROPIKI: Kwa magonjwa ya masikio (otitis) kwa kukamua jani

lililochemshwa weka matone kidogo ndani ya sikio linalougua mara 3 kila siku.

6.28. Leucaena glauca Lesena

Familia: Mimosaceae

Mti mdogo, meta 2 – 6 urefu, wenye

majani kama manyoya. Mti ni mzuri kwa

kustawisha msitu, kuni na kutunza majani

ya msitu tofauti na ardhi iliyolimwa.

Kama mbaazi (6.9) tunapendekeza

kupanda lesena ili kuzuia mmomonyoko

wa udongo. Kama miti ya lesena

itapandwa kuzunguka bustani na

mashamba, na matawi yanakatwa na

kuchimbwa udongoni, hapa rutuba ya

ardhi inaimarishwa. Majani yanafanya

kazi kama mbolea ya asili, yanachangia

madini ambayo inaletwa na mti kutoka

mbali udongoni, na kwa sababu mti huu

Page 125: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

125

ni mkundekunde, mizizi inatunza nitrogen ndani ya udongo.

PHILLIPPINES: Kwa minyoo ya safura (hookworms) na roundworms. Kausha

mbegu 30 zilizoiva, zisage vizuri na tumia unga kwa kunywa na kikombe kimoja cha

maji ya moto masaa 2 baada ya kifungua kinywa. Watoto watumie kidogo kutegemea

na uzito wao. Sio nzuri kwa watoto chini ya miaka 7.

ATHARI: Matatizo ya tumbo, kuharisha.

6.29. Matricaria chamomilla (syn. M. recutila) Familiae: Asteraceae

Mmea wa mwaka, una harufu kali, na maua madogomadogo yenye vichwa vilivyo

wazi ndani. German chamomile vilevile hustawi katika subtropics na katika nyanda

za juu sana katika maeneo ya tropiki.

Dawa ya kumwagia maji ya moto

(infusion) ya maua ya chamomile

inatumika ndani na nje; na nguvu kwa

tumbo lililojaa hewa; hulainisha tumbo,

huondoa cramps, ni antiseptic na anti –

inflammatory.

1. Inatumika kama chai kwa wagonjwa

wa gastritis au kama dawa ya kuoshea

macho kwa conjunctivitis (macho

mekundu): mimina lita moja ya maji

ya moto kwenye kiganja 1 cha maua.

Kwa kunawa macho, kwanza chuja

chai kwa kutumia karatasi.

2. Kutumika kama dawa ya mafuta kwa

majeraha, kuvimba kwa ngozi (skin-

infection), kuwashwa kwa ngozi kwa

watoto, vidonda vya magonjwa ya

ngono, eczema na bawasiri: Chemsha

gram 100 za maua ya chamomile

katika ml 500 za mafuta ya

mbogamboga katika fukizo – maji

(water-bath) kwa dakika 60, kisha

chuja. Ongeza gram 60 za nta ya nyuki, chemsha kidogo tena, na acha ipoe.

Tumia aina nzuri ya mafuta ya mboga uliyonayo, mfano, mafuta ya mzeituni, shea

butter, palm kernel oil.

3. Ili kuzalisha suppositories kwa ajili ya bawasiri, fuata mchanganyiko namba 2,

lakini badala ya gram 60 za nta ya nyuki, tumia gram 200 za nta ya nyuki, na kwa

mafuta, tumia mafuta magumu kidogo au grisi. Mwaga katika vifyatulio.

Page 126: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

126

6.30. Mel: asali

Asali ni mchanganyiko wa aina mbalimbali za sukari, (70 – 80% glucose na

fructose; saccharose chini ya 5%) maji (hayazidi 22%) vitu vyenye harufu nzuri,

rangi na antiobiotics.

Uzalishaji: Licha ya ukweli kwamba asali ina ubora wa hali ya juu sana, katika

maeneo ya tropiki huuzwa kwa bei nafuu sana. Ili kuhakikisha kwamba una asali

yenye ubora sahihi, nunua masega (yaliyokomaa tu, na kufunikwa na nta, na bila

larvae) na jitengenezee asali mwenyewe.

Kama huna vifaa maalum, fanya mseto wa masega, kwa kutumia meat-mincer,

bila kutumia grinding disk. Tengeneza usiku, vinginevyo utajiletea hatari ya

kushambuliwa na nyuki! Sambaza mchanganyiko huu juu ya kipande cha nguo

kilichofungwa juu ya ndoo ya aluminum. Weka ndoo ndani ya sun-box. Kadri joto

litakavyotokea juu, asali na nta vitatiririka kupitia kwenye nguo. Baada ya saa 24,

ondoa asali na pia utando wa nta, ambayo unaweza ukatumia kwa kutengeneza dawa

za mafuta (Tazama sura 4.4.). Mseto unaobaki katika kitambaa cha pamba unaweza

kuchanganywa na maji kwa uwiano wa 1 kwa 1, kuchemshwa na baadaye

kutengenezwa kuwa mvinyo ya asali (Tazama sura 4.7). Mvinyo ya asali inatumika

katika utengenezaji wa syrup za kikohozi na mvinyo zingine za dawa. Kinachobaki

huwekwa katika vikapu vyenye kina kirefu, na kuning’inizwa mtini, hulindwa

kutokana na mvua kwa kufunika na kipande cha bati, na sasa huwa tayari kwa

kufanywa kuwa mzinga mpya wa nyuki.

Tunapendekeza kwamba, inapowezekana, tumia asali badala ya sukari, mfano,

kwenye syrup za dawa, Oral Rehydration Solution (ORS) na katika tiba ya

Utapiamlo.

Katika baadhi ya nchi infusions zilikuwa zikitengenezwa kwa asali safi

iliyopunguzwa nguvu kwa kuchangwya na vitu vingine. Asali inatumika katika kuleta

ladha kwenye tumbaku, na kwa matumizi ya nje katika sabuni, dawa za mafuta,

cream za kunyolea nywele na creams za kulainisha ngozi.

Tunapendekeza kwamba asali itumike kwa njia ya chakula kwa magonjwa ya

moyo, kuharibika kwa ini na kikohozi.(Tazama sura 4.8).

Kwa nje, kwa sababu ya tabia yake ya osmotic and antibiotic properties, asali ni

tiba nzuri kwa majeraha kama ilivyoelezwa na Dr. Efrem kutoka Nigeria katika

“Jenne Afrique” 2/89,”Asali ina bacterial substance inayoitwa inhibine. Kitu hiki

huondoa vimelea kutoka kwenye jeraha. Asali hufyonza maji na hukausha kabisa

jeraha. Katika muda wa wiki chache huwezesha madonda kuanza kupona ambayo

yamekataa kila aina ya tiba kwa kipindi kirefu.”

Kutibu jeraha; kwanza safisha, halafu weka mchanganyiko ulio sawa wa sukari

na asali. Sukari huzuia asali kutiririka. Kwa kuwa ni anti-bacterial, asali huacha

kidonda ikiwa safi. Kidonda ni lazima kitibiwe kwa mchanganyiko wa asali/sukari

mara kadhaa kwa siku, bila kukiosha tena.

Kama utajitengenezea asali mwenyewe, hakikisha kuwa kila kitu ulichotumia ni

safi kabisa. Hapo unaweza ukatumia asali moja kwa moja; vinginevyo ichemshe asali

kwa dakika 10 ili kuua vijidudu – lakini hii husababisha kupotea kwa nguvu zingine

za antiobiotic.

Page 127: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

127

6.31. Melia azedarach

Familia: Meliaceae

Melia una uhusiano wa karibu sana na

mwarobaini, Tazama sura 5.3. Ni mti

unaokua haraka, mzuri kwa kutengeneza

pori, hasa katika maeneo ambayo huvamiwa

sana na nzige (mti huu haushambuliwi), au

katika maeneo ambayo mbao

zisizoshambuliwa na mchwa zinahitajika kwa

ujenzi. Maua yake ni bright violet kwa rangi,

majani yake yamegawanyika (branched)

zaidi kuliko mwarobaini, mbegu na matunda,

kinyume na mwarobaini, ni mviringo kabisa.

KATIKA TROPIKI: Chai iliyotengenezwa

kwa majani inatumika kidesturi kwa minyoo

na malaria.

MAREKANI: Gamba lililotwangwa lilitumika kutibu minyoo ya kwenye utumbo

(intestinal worms).

Melia azedarach haujafanyiwa utafiti kama uliofanywa kwa mwarobaini, na hivyo

kwa sababu ya sumu yake, utumike tu kwa shughuli za kilimo kama za mwarobaini,

Tazama sura 5.3.

Insecticidal products: Mazao ya dawa yaliyotengenezwa kutokana na Melia

azedarach yana nguvu kuliko yale yaliyotengenezwa kutokana na mwarobaini.

6.32. Morus nigra Mforsadi Familia: Moraceae

Kimti meta 2 – 3 urefu, majani yake pembeni kama meno ya msumeno. Matunda

yanayoliwa ni kama yai kwa umbo, sm 1.5 –

3 urefu, rangi nyekundu hubadilika kuwa

zambarau yanapoiva. Yana nyamanyama na

ladha tamu yenye uchachu kidogo (kama ile

ya European blackberry).

KATIKA MAENEO YA TROPIKI:

Hulimwa kwa ajili ya matunda, yana vitamin

C kwa wingi. Mforsadi vilevile hulimwa ili

kulisha silkworms (wadudu wa hariri) katika

sericulture (kilimo cha hawa wadudu) .

Katika dawa gamba la mzizi hutumika kama

dawa ya kuharisha na kwa tegu. Yakiliwa

kwa wingi, matunda yana nguvu ya

kukufanya uharishe na yanasaidia kwa

kikohozi. Yanatumika kuweka rangi katika

mvinyo.

Page 128: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

128

6.33. Natrium Chloratum Chumvi ya mezani chemical formula: NaCl

Katika tropiki chumvi ni muhimu sana. Kama haipatikani, watu wanaoishi katika

maeneo ya ndani ya Afrika huzalisha chumvi mbadala; huchukua majivu ya kuni,

kuchemsha pamoja na maji, kuchujwa, na kisha kuchemsha maji yaliyochujwa

taratibu hadi vitu vyeupe vituane au kujiunda kwenye chombo.

1. Kama nutrient, mtu mzima huhitaji gram 4 za chumvi kwa siku.

2. Kama dawa hutumika:

a) Katika michanganyiko ya chumvi hutumika kama drip mahospitalini.

b) Chumvi ya madini ya joto (jinsi ya kutengeneza: tazama sura 4.5.D)

c) Kufunga majeraha na vidonda vya kuungua: Chumvi ina tabia ya kuponya:

A. Osha jeraha, ama kwa maji ya mpera yaliyopikwa au kwa mchanganyiko

wa maji ya chumvi (chumvi vijiko 2 vya chai au gram 9 kwa lita 1 ya maji

yaliyochemshwa).Kama jeraha au kuungua ni kidogo na hakuna usaha, asali

inaweza ikatumika kwa tiba (Tazama sura 6.30). Kama jeraha ni ndogo

lakini lina wadudu, fuata ushauri katika sura 5.5 mpapai. Kama jeraha ni

kubwa, mgonjwa anahitaji kusafirishwa kwenye kituo cha afya kilicho

karibu haraka iwezekanavyo.

B. Yeyusha chumvi vijiko 2 vya chai katika lita moja ya maji. Chemsha

kipande cha nguo, kitakachotumika kama bendeji, kwa dakika 20 katika

mchanganyiko huu wa maji na chumvi. Kikipoa, weka kitambaa kwenye

jeraha. Tunza jeraha likiwa na unyevu wakati wote kwa kutumia

mchanganyiko wa maji na chumvi. Rudia utengenezaji wa maji yenye

chumvi kila siku (Tazama pia sura za 6.30 asali na 5.5 mpapai).

Kwa majeraha ya kuungua, epuka dawa za mafuta (ointments). Ni bora

kumimina huu mchanganyiko wa maji na chumvi juu ya jeraha mara

kadhaa kwa siku. Kwa njia hii unaruhusu oksijeni kusafisha kidonda au

jeraha. Tumia chandarua kuzuia maambukizi ya jeraha kutoka kwa nzi.

Tazama pia sura 6.3 Aloe vera.

3. Kwa dawa za mifugo: Mpe gram 50 – 100 kama dawa ya kuongeza mkojo kwa

mifugo.

4. Kama dawa ya kuhifadhia: Kata vipande vidogovidogo vya nyama isiyo na mafuta

mengi au samaki ndogondogo iwezekanavyo, funika na kiwango kilekile cha

chumvi kwa saa 24. Kisha kausha ndani ya sun-box kwa siku 1-2 pamoja na maji

ya chumvi yaliyojitokeza. Tunza nyama iliyokaushwa au samaki kwenye chombo

kisichopitisha hewa. Chumvi inayoganda kutokana na maji ya chumvi ndani ya

sun-box inaweza ikatumika tena; mfano, kutengeneza matofali ya kulamba kwa

wanyama.

Page 129: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

129

6.34. Nicotiana tabacum Tumbaku Familia: Solonaceae

Tumbaku ni mojawapo ya mmea

unaofahamika sana kwa kuwa na sumu kwa

wingi duniani. Hakuna mji mkuu wa nchi

hapa duniani, katika tropiki ambao hauna

kiwanda chake cha sigara. Lakini, tafadhali

jizuie kwa gharama yoyote ile majaribu ya

kuvuta sigara. Nicotine ina nguvu ya uraibu

(strongly addictive) na huongeza sana

uwezekano wa kuugua kansa ya mapafu na

matatizo ya njia ya hewa. Dawa

inayofahamika kwa wengi nchini VIETNAM;

majani huliwa kama dawa ya kusababisha

kuharisha na huko PHILIPPINES kama

kitulizo, ambapo dawa ya kutokosa

(mtokoso) kutokana na majani hutumika pia

kwa minyoo. Hata hivyo tunatoa onyo kali dhidi ya michanganyiko hii: Mtokoso

(decoction) wa sigara moja una nguvu ya kutosha kuua mtoto!

Hata hivyo, tunaweza tukanufaika kutokana na nguvu kubwa ya tumbaku kama

kiuatilifu (insecticide) (ingawaje majani ya mwarobaini ni bora kwa sababu yana

sumu kidogo, sura 5.3). Weka kama gram 10 za majani makavu ya tumbaku katika

lita moja ya maji kwa saa 12, chuja na nyunyizia

mboga zako kwa mchanganyiko huu (subira wiki 2

kabla ya kuvuna au mpaka mvua inyeshe). Wanyama

walioshambuliwa na wadudu wanatibiwa kwa kupaka

mchanganyiko huu huu kwenye sehemu iliyoathirika

ya ngozi, au rahisi zaidi sugua sehemu hiyo kwa

majani ya tumbaku. Weka majani kidogo kwenye

viota vya kuku, hasa pale wanaposhambuliwa sana na

viroboto; au badala yake tumia majani ya mwarobaini

au mkaratusi.

6.35. Ocimum basilicum Kurimbasi

Familia: Lamiaceae

Kimti kidogo, cha msimu, hukua karibu na nyumba,

una majani kama msumeno ncha zake, na yenye

harufu nzuri. KATIKA TROPIKI NA ULAYA.

Kurimbasi hutumika kama kiungo katika upishi.

DR. CONGO: Kwa homa na tumbo kujaa hewa

tayarisha dawa ya kumiminia maji (infusion) ya moto:

Mimina lita 1 ya maji ya moto kwenye gram 20 za

mmea mbichi, acha kwa dakika 5, kamua na kunywa

kidogo kidogo wakati wa siku.

Page 130: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

130

6.36. Oryza sativa Mpunga Familia: Poaceae

Mmea huu unaweza kukua na kufikia meta

2.”Mpunga mkavu” unalimwa kwenye ardhi ya

kawaida, mfano, Cameroon na Uganda; “Mpunga

maji” hulimwa kwenye mashamba yaliyomwagiliwa

maji na kufunika (hasa Asia). Katika nchi za

mashariki ya Asia mpunga huchukuliwa kama dawa.

ASIA: Kutibu kuharisha kwa watu wazima: Punje za

mchele huokwa vizuri na kusagwa.

Kuharisha kwa watoto: Supu ya unga wa mchele

hufanya kazi vizuri kama hakuna sukari na chumvi ya

kutengenezea ORS.

KATIKA TROPIKI: Makapi ya Mchele ni dawa nzuri

ya kutibu upungufu wa vitamin B1 (beriberi).

Daima tumia mchele “brown” wa kienyeji kuliko

mchele mweupe.

6.37. Passiflora incarnata Matunda damu Familia: Passifloraceae

Passiflora coerulea hutumika pia. Aina zote hizi mbili zina matunda ya njano, saizi

ya mayai. Ni mmea unaotambaa na hufikia hadi urefu wa meta 10. Matunda yana

ladha ya kuvutia. Kwanza mmea huu ulilimwa na wakazi asilia wa America kusini

(wa Aztec), na kisha kusambazwa na wamisionari wa Kihispania. Pale

inapowezekana matunda damu yapandwe kwenye ua, ili ua wako uwe ni chanzo

kizuri cha vitamin! Yana kitulizo kinachoitwa maracugine. Katika maeneo ya

TROPIKI, mizizi inatumika kama dawa ya kuongeza mkojo, kiganja 1 cha mizizi

huchemshwa katika lita 1 ya maji kwa dakika 10, ambayo baadaye hunywa

kidogokidogo kwa siku nzima. Kwa pumu, majani makavu huvutwa kwa kutumia

kiko.

1. Kwa kukosa usingizi, hali ya wasiwasi

na spasms (cramps): Tengeneza tincture

kwa gram 10 za majani makavu ndani ya

ml 100 za kileo (70%). Matumizi yake

matone 30 mara 1 hadi kila siku.

2. Kwa cramps, hali ya wasiwasi, pumu na

kama kitulizo: chemsha kiganja 1 cha

majani machanga kwenye 0.7 ya lita ya

maji kwa dakika 10, kunywa kwa siku.

3. Kwa kukosa usingizi: Chemsha kiganja 1

cha majani, makavu au mabichi, kwenye

kikombe 1 cha maji kwa dakika 10,

chuja na kunywa wakati wa jioni.

Page 131: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

131

4. Kwa upungufu wa Vitamin C, kula matunda kwa wingi kwa sababu yana vitamin

C kwa wingi.

6.38. Persea americana Avakado Familia: Lauraceae

Ni mti wenye urefu hadi meta 20. Matunda

yake yana mafuta ambayo ni muhimu kwa

matumizi ya binadamu kutumia kwa mkate;

nyamanyama yake ni bora zaidi kuliko

margarine ya kawaida, ambayo katika

maeneo ya tropiki huwa na madawa mengi ya

kuihifadhi. Ni tunda zuri kwa watu

wanaougua utapiamlo.

D.R. CONGO: Kwa kikohozi: Dawa ya

kutokosa huandaliwa kutokana na majani

machanga (kiganja 1 katika lita moja ya maji).

ASIA: Kwa kuharisha: Majani makavu yenye

kijani – nyeusi huchemshwa katika lita 1 ya

maji kwa dakika 15. Namna ya kutumia: kwa

watu wazima tumia majani gram 20, watoto

wakubwa gram10, na watoto wadogo gram 5. Dawa hii ya kutokosa itumiwe kidogo

kidogo kwa siku nzima (Ushauri: Tumia kwa pamoja na ORS, Tazama sura 4.5).

6.39. Phaseolus vulgaris Maharage Familia: Fabaceae

Mmea huu unapatikana karibu kila sehemu

duniani; kuna aina tofauti 500. Katika nchi

nyingine mbegu tu zinazoliwa, lakini Maharage

mabichi na maganda yake pia ni chakula chenye

thamani.

Matumizi: Kama dawa ya kuongeza mkojo, kwa

gout, maumivu ya kuvimba kwa viungo (baridi

yabisi), magonjwa ya figo na kama hatua ya

kusaidia kwa kisonono: Maharage yaliyo kwenye

maganda yaliyokaushwa (gram 10) hulowekwa

katika lita 1 ya maji usiku kucha, halafu

yanachemshwa baadaye yanachujwa. Kunywa

wakati wa mchana. Kwa wagonjwa wenye

kisukari tiba hii hupunguza kidogo kiwango cha

sukari katika damu. Maharage makavu,

yaliyosagwa yanatumika kama dawa kwenye

weeping eczema, na kama poda kwa mwili.

Page 132: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

132

6.40. Piper guineense Kechu Familia: Piperaceae

Mmea unaotambaa katika

maeneo ya misitu ya

mvua ya tropiki. Matunda

makavu yaliyoiva

yanatumika kama kiungo

na kuongeza ladha ya

chakula. Kuna aina kama

700 za pilipili katika

tropiki.

D.R.CONGO: Kama

kiungo na kwa tumbo

linalouma . Kwa

kuvimbewa kinywaji

hutayarishwa, pamoja na Curcuma longa. Kwa maumivu ya mgongo na maumivu ya

kuvimba kwa viungo: Changanya kijiko kikubwa kimoja cha unga wa pilipili (kechu)

kwa kijiko kikubwa kimoja cha mafuta ya mbogamboga, na kisha, kwa dawa hii;

mchue mgonjwa kwa nguvu hapohapo.

AFRIKA: Kwa maumivu ya kuvimba kwa viungo na magonjwa ya zinaa dawa ya

kupika kutokana na mizizi hunywewa; kwa kikohozi dawa kutokosa (decoction)

hutengenezwa kutokana na majani.

6.41. Rauwolfia vomitora Kimusukulu – (Kikongo) Familia: Apocynaceae

Mti mdogo (meta 3 – 4) huota kandokando

ya vijiji na katika ardhi iliyolimwa na

haikupandwa. Matunda yake ni kama red

berries muundo wake. Wakati wa ukoloni

gamba la mzizi lilikuwa malighafi

iliyofahamika sana. Rauwolfia ina alkaloids

nyingi, na baadhi yake ni sumu. Kiwanda

cha madawa hutumia mmea huu kuzalisha

dawa za kitulizo na madawa kwa shinikizo

la damu la kupanda.

1. Poda (unga) ya Rauwolfia: Kupunguza

shinikizo la damu na kama kitulizo kwa

msukosuko, kupotewa akili na psychotic

crying.

Gamba kavu la mzizi lililotwangwa la

Rauwolfia vomitor (katika Asia

Rauwolfia serpentina).

Page 133: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

133

Namna ya kutumia: Meza mg100 – 150 mara mbili kila siku. Kwa kuwa ni

vigumu kupima viwango hivi vidogovidogo sana, hospitali zinaweza zikafuata

mchanganyiko huu: Changanya gram 100 za unga wa Rauwolfia kwa gram 900 za

unga mwingine-huu unaweza kuwa maziwa ya unga, sukari, unga wa ngano wa

madukani, au unga wa mahindi mkavu uliochemshwa kidogo na kuanza

kubadilika kuwa brown na kisha kusagwa vizuri. Ni muhimu unga wa

kuchanganya ukawa na saizi ileile ya punje au unga uliyosagwa sawa na poda ya

Rauwolfia. Halafu jaza capsule yenye gram 1, au mifuko ya karatasi

uliyotengenezea nyumbani, kwa gram 1ya mchanganyiko huu. Watu wazima

watumie gram 1 ya mchanganyiko huu mara tatu kwa siku.

2. Upele (scabies) kwenye maeneo madogomadogo tu, mfano, katika mikono tu:

Sugua kwa majani mabichi sehemu iliyoathirika mara 3 kwa siku, kama ni lazima

pamoja na matone kidogo ya mafuta ya mbogamboga.

ATHARI: Ukizidisha dozi inaweza ikasababisha udhaifu wa misuli, wasiwasi na

huzuni (fadhaa). Kwa hiyo, dozi sahihi ni muhimu sana, na huhitaji uzoefu wa hali

ya juu katika matumizi yake. Hata kwa matumizi ya nje ni lazima itumike kwa

kiasi kidogo.

6.42. Ricinus communis Mbono Familia: Euphorbiaceae

Mbono ni mti wenye nguvu

ambao mara nyingi hupatikana

kwenye kifusi au ardhi

iliyolimwa bila kupandwa.

Baada ya kusiha, mti unaweza

kukua hadi kufikia meta 3 – 4,

kwa mwaka mmoja. Sehemu

zote za mmea zina sumu, na

mbegu zina ricin, protini ambayo

ni sumu kabisa. Mbegu

zilizosagwa, mizizi iliyosagwa

au majani mabichi vinatumika

kutibu magonjwa ya ngozi; Kwa

hiyo unaweza ukasugua majani

mabichi kwenye eneo

lililoathirika mara 3 kwa siku.

Mbegu zilizopandwa hadi kuwa

ujiuji kienyeji hutumika katika

majeraha kama dawa ya kuzuia

damu kuvuja na kusafisha jeraha.

Mbegu zisiliwe wala kutumiwa

kwa njia yoyote ile ya mdomo

kwa sababu ni sumu.

Page 134: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

134

1. Mafuta ya mbono kwa matumizi ya ndani: Mafuta lazima yakamuliwe kutokana

na mbegu mbichi (cold seeds). Hii inaweza tu kufanyika kwa kutumia vifaa

vyenye pressure ya hali ya juu, kwa hiyo, mafuta lazima yanunuliwe kutoka

maduka ya dawa. Inatumika kimadawa;

a) Kama dawa ya kuharisha. Ina nguvu wakati kufungwa kwa choo kunapofikia

hali mbaya. Namna ya kutumia: Watu wazima; kijiko cha chai 1 hadi 2 mara

mbili kila siku. Watoto ½ hadi kijiko1 cha chai mara mbili kwa siku. Tumia

hadi uanze kuharisha.

b) Kwa matatizo ya kunywa mafuta ya taa, petrol au dizeli. Kwa hali kama hiyo,

kamwe usimtapishe kabisa mgonjwa; ni hatari sana. Namna ya kutumia ni

kama kwa aliyefunga choo, Tazama (a) juu.

2. Mafuta ya mbono kwa matumizi ya nje: Kwa matumizi ya nje, mafuta ya mbono

yanaweza yakatengenezwa nyumbani. Twanga vikombe viwili vya mbegu mbichi

kutokana na mbono lakini usitumie chungu kilekile unachotumia kutwanga

chakula! Hii huzalisha kikombe kimoja cha ujiuji kama peanut butter. Ongeza

kikombe kimoja cha maji na kikombe kimoja cha mafuta ya mbogamboga.

Koroga vyote pamoja katika sufuria, na chemsha kwa muda mrefu utakaofanya

maji yote kutoweka (hii huharibu kile kitu kinacholeta kuganda). Sasa kwa

uangalifu ongeza vikombe 10 vya maji, weka mfuniko kwenye sufuria na

chemsha kwa dakika 10 (hii huharibu sehemu kubwa ya ricin). Mimina kila kitu

ndani ya chupa yenye shingo nyembamba, na ongeza maji moto ya kutosha ili

kujaza chupa. Baada ya siku moja ondoa utando wa mafuta kwa kutumia sindano

(syringe). Mafuta haya yana 30% mafuta ya mbono, na yanaweza kutumiwa:

a) kwa ngozi na kwa usafi na ulinzi wa nywele

b) kwa ugonjwa wa ngozi wa aina ya Neuro-dermatitis.

c) pekee au pamoja na utomvu wa mapapai (sura 5.5) au Cassia alata majani

yake (sura 5.6) unatumika kutibu mba kwenye ngozi na ringworm.

3. INDIA: Mafuta ya mbono yanatengenezwa kama ifuatavyo:chemsha kg 2 za

mbegu katika lita 10 za maji kwa saa moja. Kamua mbegu kutumia 3KW (au

mashine ya kukamua mafuta ya mkono). Acha itulie kwa wiki 1, na kisha mimina

vizuri mafuta na tupa mabaki yaliyo magumu. Mafuta hutumika kwa ulinzi wa

ngozi na nywele na kwa viwango vidogo sana, kuhifadhi mbegu.

4. Kuhifadhi mbegu za mahindi au maharage (hii ina maana kwa mbegu za kupanda

tu), twanga kiganja 1 cha mbegu za mbono, na changanya na kg. 20 za mbegu za

mahindi au maharage.

5. Kwa sababu mbegu za mbono zina sumu kali, unaweza kuzitumia kama sumu ya

panya. Changanya kipimo1 cha karanga kwa kipimo1 cha mbegu za mbono,

twanga pamoja, na weka mchanganyiko huu pale ambako panya hutembelea au

hukaa. TAHADHARI: Weka mbali sana na watoto, na wanyama wengine wote

kama vile kuku au ndege, watakufa wote kama watakula mchanganyiko huu.

Page 135: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

135

6.43. Sesamum indicum Ntungo Familia:

Pedaliaceae

Mmea mrefu sm 50 hadi 80, majani marefu

yenye meno meno, kama msumeno, maua

meupe, au yakiwa na madoa ya njano na

zambarau. Tunda ni kama sm 2.5 urefu. Mbegu

zake maarufu kama chakula.

D. R. CONGO: Kinywaji kutokana na majani

kinatumika kwa wagumba wa kiume na wa

kike.

ASIA: Kwa waliofunga choo: Meza vijiko 3

vya chai vya mafuta yake. Kwa maumivu ya

kuvimba kwa viungo, gram 20 za majani

makavu huchemshwa katika 0.7 ya lita ya maji,

kuchujwa na kunywewa kwa siku moja.

6.44. Tagetes erecta Tururu Familia: Asteraceae

Mmea wa mapambo, una asili ya Mexico,

umeenea maeneo yote ya tropiki na Ulaya.

Maua na majani yana harufu ya kipekee.

KIULIMWENGU: Mafuta yake muhimu

hupunguza shinikizo la damu (B.P) na kupanua

bronchia; vile vile yana anti-spasmodic, anti-

inflammatory na sedative effects. Majani

hufanya kazi kama dawa ya kuongeza mkojo

na kuongeza transpiration. Siku hizi

yanatumiwa katika uzalishaji wa manukato ya

biashara. Mbegu zake zina uwezo wa kuua

minyoo na pia kama dawa ya kuharisha. Mmea

wote una nguvu ya kuua nematodes (minyoo

wenye madhara waishio udongoni, ugonjwa wa

kawaida katika nchi za tropiki). Inashauriwa

kusiha tururu bustanini mwisho wa msimu wa

mvua!

ASIA:

1. Kwa kikohozi, bronchitis, kuumwa jino, hedhi isiyo na utaratibu: Mimina

vikombe 2 vya maji ya moto kwenye gram 10 za majani makavu, acha itulie kwa

dakika 20, kamua , kunywa kikombe 1 asubuhi na jioni.

2. Kwa magonjwa ya macho: compress iliyolowanishwa na mchanganyiko huu

hutumika.

Page 136: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

136

3. Kwa Kifaduro: Mimea 0.7 lita ya maji ya moto kwenye maua 15, mabichi au

makavu, na kunywa kidogokidogo wakati wa siku moja.

4. Suppurating mammary gland, majipu: Chukua kiganja 1 cha maua kwa kijiko

kimoja cha chai cha chumvi na chemsha kwenye ½ kikombe cha maji. Weka

compress iliyolowanishwa na mchanganyiko huu.

6.45. Tamarindus indica Ukwaju Familia: Caesalpiniaceae

Ni mti mzuri unaovumilia ukame

wenye matawi ya kusambaa, gamba

lake ni grey-black na lina vilima na

vibonde, majani ni kijani isiyokolea

(yenye jozi

9 hadi 12 za vijani). Wakati wa mvua,

maua ni kijivu – njano na yanakuwa

red-veined na hufuatwa na matunda ya

kahawia, yenye mbegu za umbo la figo

ndani ya nyamanyama ya kahawia.

Matunda yana vitamin C kwa wingi, na

huliwa bila kupikwa au kutengeneza

kinywaji. ASIA na AFRIKA: Matunda

mabichi au yaliyokaushwa hutumika

kuongeza uchachu kama limau, juisi au

siki, katika samaki.

Baada ya kuondoa gamba la juu, mbegu

zinaweza zikaliwa hivyo au kuokwa.

Zinaweza zikatumika kutengeneza aina

fulani ya unga, na kama chakula cha

wanyama. Mafuta ya mbegu yanaweza

yakatumika kwenye sabuni.

Mti huu una mfumo wa mizizi uliosambaa na mpana na hivyo ni mzuri kwa kuzuia

mmomonyoko wa udongo. Japokuwa mti una naitrogen, hudondosha majani yenye

tindikali (acid), kwa hiyo siyo mzuri kwa mchanganyiko wa mazao (inter-cropping).

Mbao hutumika kutengeneza mitumbwi, samani, michi na vinu, nguzo za uzio, na

mkaa.

Kimadawa, matunda huliwa kwa waliofunga choo, na hutumika kupunguza homa,

kuponya magonjwa ya kwenye utumbo, kutibu pumu, kuondoa kichefuchefu kwa

wajawazito, na kama kitu kinachowekwa katika dawa kutibu matatizo ya moyo na

kupunguza sukari katika damu. Hutumika kwa nje kama dawa ya kukausha kwa

magonjwa ya ngozi.

Page 137: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

137

6.46 Tephrosia vogelii Mbaazi Familia: Papilionaceae

Ki-mti urefu meta 1 – 2, hupatikana vijijini

katika nchi za tropiki. Una rotenone (kitu

ambacho ni chepesi kuhisi joto), kwa hiyo

majani ni lazima yakaushwe kivulini.

Hutumika katika ua kuzuia mmonyoko wa

ardhi. Ng’ombe na Mbuzi huwa hawali miti hii.

D. R. CONGO: Gamba la mzizi husagwa,

huchanganywa na pilipili kichaa na kutumiwa

kwa meno yanayouma.

NCHI ZA TROPIKI: Hutumika kinyume cha

sheria kuwapoozesha samaki ili kurahisisha

uvuaji wake. Mbaazi ina nguvu ya kutibu upele

(scabies): Sugua ngozi kwa majani. Mbaazi

vilevile hutumika kutengeneza kiuatilifu

(insecticide): tayarisha kwa kuloweka kg. 1 ya

majani mabichi yaliyopondwapondwa kwenye

lita 10 za maji kwa saa 8. Acha wiki mbili

zipite kabla ya kuvuna mazao uliyonyunyizia

dawa.

Kutengeneza kiuatilifu cha unga (insecticidal powder) kausha majani yaliyokomaa,

yatwange na yachekeche. Ama peke yake au pamoja na pilipili kichaa ya unga

inaweza ikatumika ndani ya nyumba kufukuza wadudu, lakini tunza vizuri

wasikofika watoto! Gram 100 za majani yaliyokaushwa ya mbaazi huchanganywa na

kg. 50 za mahindi kuyalinda dhidi ya wadudu kwa kipindi cha miezi mitatu. Osha

mahindi kabla ya kuyatumia.

6.47 Tithonia diversifolia Familia:

Asteraceae

Mmea huu huboresha udongo

ulioharibika, na ni wa manufaa zaidi

ambako mmomonyoko wa ardhi

umetokea. Ni mbolea nzuri (green

manure) kwa ardhi yenye upungufu

wa naitrojeni. Hutumika kujenga ua ili

kuzuia mmomonyoko wa ardhi! Hata

hivyo mmea huu ukipandwa ni

vigumu tena kuondoa, hivyo panda

kuzunguka shamba sio shambani .

Kisha fukia matawi yaliyokatwa

kwenye ardhi utakayopanda mazao

yako, ukihakikisha kwamba matawi

Page 138: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

138

hayana mbegu, na panda mazao yako haraka iwezekanavyo.

AFRIKA MASHARIKI: Chai iliyotengenezwa kwa majani inatumika kutibu

maumivu ya tumbo na ini, na maumivu ya tumbo wakati wa ujauzito: “Decotion” ya

kutumia nusu au jani moja hutumika kwa siku. D. R. CONGO: Chai iliyotengenezwa

kutokana na majani inatumika kutibu “bacillary dysentery.” Majani yaliyotwangwa

yanatumika kwa dermatitis na ngozi inayowasha.

6.48 Vernonia amygdalina Mtukutu Familiae: Asteraceae

Mti unaokua haraka, meta 3 – 8 urefu, rangi ya majani nyeupe kuelekea bluu kidogo.

Unaweza mti huu ukasambazwa kwa urahisi kwa kutumia vipande vya miti.

UGANDA: Wenyeji huchemsha majani mara 3 kwenye maji na kisha kuyala kama

mchicha. Mmea huu wa muhimu ingawaje mchungu sana hutumika nchini Uganda

kutibu malaria. Baadhi ya wauguzi walituambia kwamba wanapendelea sana kutumia

mtukutu ukilinganisha na quinine au chloroquine kwa sababu wagonjwa wanapata

madhara kidogo (tunaweza tukathibitisha hili).

Tunapendekeza mchanganyiko

ufuatao kwa malaria: chemsha kiganja

1 cha majani au, kwa chai yenye

nguvu, kiganja 1 (gram 15) za gamba

kavu la mzizi, katika lita moja ya maji

kwa dakika 20; chuja na kunywa kwa

siku nzima.

Kwa mjibu wa tiba, mmea huu pia

una nguvu ya kutibu surua, kisukari,

pumu, kuharisha, kifua kikuu, malale,

aina fulani za kansa, minyoo, na

kufunga choo. Wanyama nao hutumia

mtukutu kwa kichocho

(schistosomiasis), matatizo ya

tumboni na parasites.

Kama kwa Mwarobaini (sura 5.3) na

melai (sura 6.31), Vernonia

amygdalina inaweza ikatumika katika

kilimo kuua “nematodes” na majani

kwa kuhifadhi chakula.

NIGERIA : Kutafuna matawi machanga ya mtukutu huzuia meno kuoza. Majimaji ya

majani ya mtukutu yana nguvu ya anti-oxidizing; kwa hiyo unaweza kuwa dawa ya

kuhifadhi ya ki-asili (Natural preservative) ambayo inaweza kuzuia dawa kuchacha.

ATHARI: Mmea una cytotoxic mbili, vernodalin na vernomygdin. Mmea huu wa

kufaa sana huenda ukawa na athari, lakini bado, kumekuwa na utafiti mdogo juu ya

somo hili.

Page 139: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

139

6.49 Vinca rosea (syn. Catharanthus roseus) Vinka Familiae: Apocynaceae

Mmea mfupi kadri ya sm 60 urefu. Maua ni meupe na pinki na yana petali 5, kila jani

linaelekea upande wake. Una sumu! Kwa hiyo utumiwe wakati wa hali mbaya tu.

Hupandwa hasa kama mmea wa mapambo, husitawi vizuri kwenye mchanga.

Unaweza ukasambazwa kwa mbegu au vitawi ambavyo havijatoa maua. Majani

yavunwe kabla au wakati mmea unapotoa maua.

Nchini SENEGAL, MALI NA TOGO mmea wote

unatumika kwa kuzuia kuharisha; visiwa vya

COMORO kwa kisonono, NIGER kwa hepatitis,

nchini PHILLIPINES kwa bacterial dysentery.

Katika British pharmacopoeia chai

iliyotengenezwa kwa majani imesajiliwa kama

dawa ya kisukari. Zaidi ya kipindi cha miaka 15,

Vinca rosea imekuwa ikifanyiwa utafiti kuliko

mmea mwingine wa dawa wowote kwa sababu una

aina tofauti 65 za alkaloids. Maisha ya maelfu ya

watoto wanaougua kansa ya damu yamekwisha

okolewa kwa sababu alkaloids 2 ( vincristine na

vinbalastine) zimethibitisha kuwa na uwezo wa

kushambulia aina hii ya kansa kwa watoto.

MATUMIZI ULIMWENGUNI KOTE:

1. Kisukari: Weka gram 5 za majani makavu au

kiganja 1 (kiasi ambacho mgonjwa anaweza

kukuficha kiganjani) cha majani mabichi katika lita 1 ya maji ya moto, chemsha

kidogo kwa dakika 15. Chuja na kunywa kidogokidogo kwa siku moja. Mkojo na

damu ni lazima vipimwe katika kituo cha afya mara kwa mara.

2. Shinikizo la damu: Kausha mizizi ya mti, menya gambalake na twanga gamba

hilo. Chukua kijiko 1 cha chai na chemsha pamoja na vikombe 2 vya maji kwa

dakika 10, chuja na kunywa wakati wa asubuhi au kabla ya kula.

3. Bacillary dysentery

a) Tayarisha mchanganyiko namba 1 kila siku. Mmissionari kutoka Hant – D. R.

Congo alitutaarifu kwamba, wakati wa mlipuko wa bacillary dysentery

ambayo iligoma kupona (ilikuwa sugu) kwa antibiotic, kwa kutumia

mchanganyiko huu, aliweza kuokoa kadri ya asilimia 50% ya watoto

waliougua, ilikuwa na maana maisha ya mamia ya watoto katika eneo hilo

pekee.

b) Tumia mchanganiko wa chai hiyo na chai ya ameba (mziwaziwa na majani ya

mpera – taz. Sura 5.11) kutibu ameba.

4. Kansa: Kama hakuna dawa nyingine (tu!) inayoweza patikana, jaribu

mchanganyiko namba 1. Unaweza kuongeza msubili na mapapai mabichi katika

chai. Kwa nje, tumia kinachoonyesha kuwa na manufaa; kufunga vidonda kwa

msubili, au papai bichi; au kukamulia majani ya vinka yaliyochemshwa kidogo na

ikapondwa pondwa.

Page 140: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

140

ATHARI:

Inapotumiwa kwa kipindi kirefu, shinikizo la damu (blood pressure) linaweza kuwa

la chini na maumivu ya tumbo yanaweza kutokea. Vinka isitumiwe kabisa na

wanawake wajawazito, na matumizi yake kamwe yasiwe ya muda mrefu. Kama

madawa mengine yote ya kansa, Vinca rosea yenyewe inaweza ikakuletea kansa.

6.50 Zea mays Mahindi Familia: Poaceae

Mahindi kiasili yalitoka Amerika ya kusini. Sehemu muhimu zaidi ya mmea ni

nywele za mhindi. Nywelenywele hukusanywa kabla ya mbelewele wakati mmea una

maua. Yaweke kivulini na uyaache yakauke

upesi. Yana alkaloid allantoin, na anodyne

(pain-soothing = kutuliza maumivu) ambayo

nguvu yake kwa magonjwa ya kibofu cha

nyongo imethibitishwa.

UFARANSA.: Nywele za mahindi zinatumika

kwa kuongeza mkojo.

GUINEA, ULAYA NA MAREKENI:

Inatumika kwa magonjwa ya njia ya mkojo.

ANGOLA: Kama dawa ya kuongeza mkojo;

ASIA: Kama tiba ya kisukari, oedema na

shinikizo la juu la damu.

1. Kisukari: Chukua gram 15 nywele nywele

kavu za mahindi na chemsha katika lita 1

ya maji kwa dakika 5. Kunywa

kidogokidogo kwa siku nzima.

DOKEZO: Fuata masharti ya milo kwa

kisukari: Punguza matumizi ya chumvi na

usitumie kabisa sukari katika milo ya kila

siku. Changanya na mmea mingine ambayo husaidia kupunguza kiwango cha

sukari katika damu, k.m. kitunguu maji (6.2) au green bean (6.39) (aina ya

maharaghe ambayo inaliwa na maganda yake).

2. Magonjwa ya figo, oedema, shinikizo la damu, na mawe ya figo: Fuata

mchanganyiko kwa ajili ya kisukari. Unaweza ukanywa chai hii kwa zaidi ya

miezi 6 bila kutokea madhara yoyote.

DOKEZO: Kwa vile nywelenywele za mahindi mara nyingine hazipatikana unaweza

kutumia gunzi yake badala yake. Kwa vile nguvu yake ni chini kuliko nywelenywele,

tumia gunzi gr 100 badala ya gr 15 za nywelenywele.

Hakuna madhara yanayofahamika, lakini yakitumiwa kwa muda mrefu lazima

kuchunguzwa katika kituo cha Afya mara kwa mara. Ni muhimu zaidi hasa kwa

wenye kisukari na shinikizo la juu la damu.

Page 141: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

141

SURA YA 7

7.1. KATIKA FAMILIA

“Tusiibadili miili yetu kuwa ghala la madawa”

1. Kula vizuri!

Chakula chetu kiwe dawa yetu! Vyakula bora vinajenga nguvu na mfumo wa kinga

ya mwili; ina maana kwamba uwezo wa kupambana na kuzuia maambukizi na

magonjwa unaongezeka. Vyakula visivyo bora hupelekea kupungukiwa lishe, na

kusababisha urahisi wa kuambukizwa magonjwa.

AINA MUHIMU ZA VYAKULA

Kwa kupata nishati

(energy) kirahisi

Mizizi yenye wanga: Mihogo, viazi, taro

Matunda yenye wanga: ndizi, ndizi kuu, mfenesi.

Kwa nishati na protini

bora

Nafaka na mbegu: Ngano, mahindi, mchele,

mawele, mtama

Mkate: Ngano isiyokobolewa ni bora zaidi ukitumia

kuliko mkate wa ngano iliyokobolewa! Viazi

mviringo na viazi vitamu vyote vina protein.

Vyakula vya kushibisha Mbegu za mafuta: boga, tikiti maji, ufuta, alizeti.

Jamii ya kunde: Maharage, karanga, soya, dengu.

Vyenye gamba: Njugu mawe, korosho, kungu

Wanyama: Maziwa, mayai, jibini, samaki, kuku,

nyama yoyote.

Vyakula vyenye wingi

wa virutubisho

Mbogamboga: majani ya mihogo, viazi vitamu na

majani yake, nyanya, karots, mboga, majani

ya Mlonge n.k.

Matunda: Maembe, machungwa, malimau, mapapi,

mapera, passion fruits n.k.

Juisi ya matunda

Kwa ajili ya kinga ya

mwili iliyo imara

Kula vitunguu swaumu vilivyo vibichi

Lima mwenyewe matunda na mbogamboga! Panda miti ya matunda na miti mingine

– maembe, papai, nanasi, migomba, n.k. Panda mlongelonge na kula majani yake.

Watoto wanatakiwa kulishwa mara kadhaa kwa siku kwa chakula cha aina

mbalimbali. Wanahitaji kiasi kidogo kwa mara nyingi. Kama, kwa mfano, wakila

mtama au mihogo tu, watadhurika kwa sababu haitakidhi haja yao ya protini, nguvu,

vitamin na madini. Kunywa maji ya matunda asili – Afrika ina aina nyingi na nzuri

za matunda! Soda na vinywaji vingine vya biashara vina kila aina ya mchanganyiko

DOKEZO KWA FAMILIA, WAFANYAKAZI WA

AFYA NA HOSPITALI

Page 142: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

142

na vikolezo vya utamu usio wa asili ambao hauna faida kwa afya yako. Vyakula vya

viwandani vina aina za mafuta na madawa ya kuvitunza vyenye kuleta magonjwa.

Kama kwa vyovyote inawezekana wanyonyesheni watoto wenu kwa maziwa ya

titi la mama – usijaribiwe na matangazo ya ki-biashara ya maziwa ya chupa. Watoto

wanakunywa uchafu na maambukizi kupitia chupa hizo – ambayo husababisha

kuharisha na magonjwa mengine. Jitahidi kujiepusha na vyakula vya watoto vya ki-

biashara vinaharibu tu hali ya uchumi ya kifamilia.

2. Uchumi mzuri wa nyumbani

Kama wewe na familia yako mnazidi kukonda huenda ukawa unasumbuliwa na

magonjwa kama minyoo na kifua kikuu. Lakini mnaweza pia kuwa mnasumbuliwa

na “ugonjwa” mwingine unaoitwa “hali mbaya ya uchumi nyumbani”.

Kwa mfano, kijijini unatakiwa kuuza kilo 20 za karanga zenye maganda ili

kununua kilo 1 ya maziwa ya unga kiwango cha protini katika vitu hivyo viwili viko

sawa, kwa kufuata uzito, iko sawasawa kabisa (270g protein katika kilo 1). Mtu

mzima anaweza kuishi siku 46 kwa kilo 20 za karanga lakini akaishi siku 2 tu kwa

kilo moja ya maziwa ya unga!

Mifano mingine zaidi:

- Unauza machungwa yenye vitamin C nyingi ili kununua chupa ya soda,

ambayo imetengenezwa kwa maji, sukari, na rangi tu.

- Unauza ndizi, ambazo kwa kweli zina vikombe 3 vya sukari ya asili (ilifichika)

ili kununua kikombe kimoja cha sukari dukani.

- Huwezi kupata asali ya kutengenezea, maji chumvi kwa sababu baba

ameitumia yote kutengenezea pombe.

- Kijana anayesoma sekondari hudhani kuwa ana elimu kubwa kiasi kwamba

hawezi kumsaidia mama yake kulima, hata wakati wa likizo. Mwili wa mama

uliofanya kazi zaidi ya uwezo wake hauwezi kutoa maziwa ya kumtosha mtoto

wake; mtoto ataugua itambidi baba auze gunia la karanga lililo salia ili kulipia

gharama za matibabu. Njaa inaanza kuingia kijijini.

Je, umeelewa sasa, kuwa “vitu vyenye kuvutia” havitasaidia familia yako?

3. Chunga maji yako!

Hakikisha maji unayokunywa ni safi. Kutokana na ubora wa maji yako, unaweza

kujenga chujio la mchanga, au unaweza kutumia mbegu za Moringa zilizosagwa

kama ilivyoelezwa katika sura 5:13. Kuchemsha maji, hata katika jiko la jua ndiyo

njia bora zaidi.

Kama watu wakiosha nguo zao, au hata baiskeli na magari, katika maji ambayo

wengine wanayatumia kunywa, basi wanasababisha matatizo!

4. Hifadhi ardhi yako katika ubora na rutuba ya asili.

a) Panda mimea jamii ya mikunde (ambayo kwa asili huweka naitrojeni ardhini).

Mimea jamii ya mikunde ni pamoja na mboga kama maharage na jamii za

Karanga, na miti kama Leucena. Leucena inaweza kupandwa katika kontua ili

kuzuia mmomonyoko wa udongo na kukatwa wakati wote ili kutengeneza ua.

Matawi yanayokatwa yanasaidia kurutubisha ardhi.

Page 143: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

143

b) Tengeneza mboji kwa kutumia vitu vyote vyenye asili ya wanyama na mimea.

Maganda ya matunda, majani ya mboga, masalio ya shambani – (lakini epuka

mbegu za magugu). Vinyesi vya kuku na wanyama vitunzwe (siyo karibu sana na

nyumba). Kama vikihifadhiwa katika hali ya uvuguvugu na unyevu, ardhi nyeusi

itapatikana baada ya miezi mitatu, ambayo ikichanganywa katika shamba lako,

kwa taratibu itaingiza virutubisho (naitrojeni na madini) ardhini.

c) Epuka utumiaji wa kemikali za kilimo. Usitumie kabisa, au tumia kiasi kidogo

sana cha mbolea za viwandani au madawa ya kuua wadudu. Vinaharibu maji,

vinaua maisha ya mimea na wanyama visivyo na madhara (mara nyingine vyenye

faida), na kudhuru rutuba ya asili ya ardhi.

5. Vyoo vya kienyeji ni visafi na vinafanya kazi . Vinyesi na mkojo vinabeba maambukizi mengi; chimba shimo, jenga nyumba juu

yake. Shimo lifunikwe muda wote. Weka bomba la hewa chafu; yaani bomba

lisimamishwe (lizibwe juu kwa waya wa mbu) ambalo huchukua hewa chafu kutoka

kwenye shimo, kupitia kwenye sakafu na paa hadi kwenye hewa safi ya nje. Hapo

haitanuka. Shimo likijaa fukia kwa udongo na panda mwembe! Kisha tengeneza tena

choo cha kienyeji kwenye eneo jingine. Kwa kweli vyoo vya kienyeji ni bora kuliko

vyoo vya maji; vinatunza virutubisho kwa upandaji wa baadaye, wakati ambapo vyoo

vya maji vinasababisha uchafuzi wa mito na vijito. Pia vinatumia maji ambayo katika

sehemu nyingi ni mali adimu. Choo kisafi cha kienyeji ni bora mara 1,000 ya vile

vinavyoitwa vyoo vya maji vya kisasa ambavyo ni vichafu kwa ukosefu wa maji!!

6. Utupaji makini wa takataka!

“Mioto ya milele” ambayo mara chache huzima na ambamo taka zote hutupwa, ni

hatari kwa afya. Na haipendezi. Kama vitu fulani, mfano PVC na aluminium

vikichomwa kwa pamoja kwa moto kidogo hewa yenye sumu kali sana iitwayo

dioxins inatokea. Pia, taka zisiachwe kuzagaa ovyo. Vinatoa picha mbaya, vitu

vyenye ncha kali vinaweza kutukata; beteri na vifaa vingine vya umeme vina sumu

na maji ya mvua hujikusanya katika vitu, matairi yaliyozeeka na kutengeneza sehemu

za kuzaliana kwa mbu wa malaria.

a) Matairi, vioo, plastiki, betari kama kuna namna yoyote ya kuvitumia tena au

kuvitengeneza upya vitu hivi fanya hivyo. Kama sivyo, vikusanye pamoja na kila

mwezi uvizike chini sana ardhini; betri zina sumu zaidi. Usipande mboga juu ya

mahali ulipovizika!

b) Karatasi: vikusanye kwa pamoja kwa juma moja kisha kila Jumamosi uzichome

mchana kwa muda mfupi kama dakika 5 hivi. Zika majivu pamoja na plastiki

n.k.

c) Mbao: Zichomwe na upeleke majivu shambani; yana madini.

d) Taka za mimea na wanyama: Ziozeshe utengeneze mboji.

7. Usafi:

Mila ya kiafrika ya kuosha mikono kwa maji na sabuni wakati wote kabla ya kula au

kutayarisha chakula, na baada ya kutoka chooni ni ya muhimu na bora zaidi. Kama

huna sabuni jitengenezee kwa kutumia majani ya mipapai.

Page 144: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

144

Kuoga mwili mzima kuanzia kichwani hadi kwenye vidole vya miguu kila jioni

hufanya mwili na kitanda vikae safi.

8. Usafi wa mdomo na meno Kuoza kwa meno siyo tena ugonjwa wa Wazungu. Bali katika nchi za tropiki pia hasa

katika miji mikubwa, watu wengi zaidi wanahangaika na kuoza meno. Soda nyingi

wanazopewa kila mgeni bure ndizo za kulaumu kwa sehemu kubwa. Matunda mazuri

zaidi ya asili na maji ya matunda halisi hayasababishi matatizo kama hayo!

Kuongezeka kwa kiwango cha ulaji wa mikate mieupe pia huchangia kuongezeka

kwa tatizo la kuoza kwa meno. Wakati ambapo mihogo ni rahisi kwa meno, kwa

sababu wanga wa mihogo haubadilishwi na mate kuwa sukari kwa urahisi.

Kama una bahati ya kuishi vijijini, unaweza kuendelea kutumia baadhi ya matawi

(kama mwarobaini, angalia sura 5.3) kwa usafi wa meno. Kama unaishi mjini, tumia

mswaki wako kila baada ya kila mlo, hasa jioni; kama hakuna dawa ya meno usihofu,

kwa sababu jambo kubwa ni usafishaji wa meno, kupiga mswaki.

Badala ya dawa ya meno, unaweza kutumia kiasi kidogo cha chumvi au unaweka

kipande kidogo sana cha sabuni ya jibini (uliyojitengenezea) au sabuni yoyote nzuri

(angalia sura 4) kwenye mswaki wako. Itenge hiyo sabuni kwa kazi hiyo tu. Unaweza

pia kutumia poda ya meno, angalia sura 4.5.

9. Kwa upishi wa ndani, weka dohani! Kama mara nyingi uko katika chumba kilichojaa moshi, uko kwenye hatari kubwa ya

kupata matatizo makubwa ya macho na mapafu. Suluhisho bora kabisa la tatizo ni

kujenga jiko lenye kubana matumizi ya nishati (yaani kutumia kuni chache zaidi)

pamoja na dohani ili kwamba moshi wote utoke nje.

10. Mazoezi na uimara wa mwili.

Watu wengine wana shughuli nyingi zaidi, mfano mwanamke atakiwaye kutembea

kilomita nyingi kwa siku ili kutafuta kuni na maji; wengine wana shughuli ndogo

zaidi. Fanya maamuzi yako mwenyewe kutazama kama familia yako “imeendelea”

au “haijaendelea”! Katika familia “zilizoendelea” mwanamke na mwanamme

wanashirikiana shughuli, kwa hiyo wana mazoezi ya aina moja. Kwa jinsi hii

mwanamke hawi mwembamba na dhaifu zaidi, wala mwanamme hanenepi sana.!

Tunapokuwa imara tunakuwa na kinga ya mwili dhidi ya maradhi.

11. Epuka magonjwa yaambukizwayo kwa ngono na UKIMWI.

Hakuna uhakika kuwa kuna mmea wowote usio na sumu unaoweza kutibu kaswende

au maradhi mengine ya ngono, lakini mimea fulani inaweza kutumika kutuliza dalili

fulani (kama vile kuwashwa). Antibayotiki lazima zitumike, kama hali ya uchumi

inaruhusu. Tumetembelea mbilikimo ambao wamefanikiwa kutibu magonjwa ya

ngono (hata yaliyo sugu kwa antibayotiki) kwa kutumia mimea ya madawa, lakini

kwa uwezekano wa kumdhuru kwa sumu mgonjwa. Kwa dhati kabisa tunawashauri

mtumie njia yoyote ya tiba isiyo na madhara (ya kisasa au ya jadi) iliyochunguzwa

katika maabara.

UKIMWI: Hakuna njia ya kisasa au ya jadi iwezayo kuponya UKIMWI. Ni juu

yako kujiepusha na UKIMWI au maambukizi mengine mabaya.

1. Uwe mwaminifu kwa mwenzako.

Page 145: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

145

2. Usitibiwe na “manesi wanaosafiri” (wazururao na kuchoma sindano na kuathiri

watu).

3. Hakikisha nesi hamchanji mtoto wako kwa sindano ile ile au bomba lililokwisha

tumiwa kwa mtoto mwingine (kuna hatari ya maambukizo kama sindano haiku

chemshwa).

4. Zuia upungufu wa damu mwilini ili kuepuka kuongezwa damu wakati wa kuugua,

baada ya ajali au wakati wa kuzaa.

7.2. WATUMISHI WA AFYA KIJIJINI

Kwa kawaida kituo kimoja cha afya au zahanati kinahudumia vijiji 20 – 30 kwenye

haya maeneo ya jirani. Kwa kufikiria bila uhakika, katika kila moja ya vijiji hivi,

kuna mwanamme mmoja (Mhudumu wa afya) na mwanamke mmoja (mkunga wa

jadi) wanaofanya kazi kwa kujitolea (!) ili kuboresha hali ya afya kijijini kwao.

Vifaa vya Mhudumu wa Afya kama huyo ni: Vitambaa vya kufungia, aspirin,

chloroquine (kwa malaria), mebendazole (kwa minyoo), iodine au dawa nyingine za

kusafishia. Wahudumu wa afya wanatakiwa kuwa na ufahamu mkubwa wa madawa

ya kienyeji, na pia wawe na ruhusa ya kuyatumia kwa namna ya kuwajibika. Ifuatayo

ni mifano ya jinsi Mhudumu wa afya wa kijiji anavyoweza kutumia madawa ya asili:

a) Kusafisha vidonda na uvimbe kwa kutumia papai, asali, sukari, au Aloe Vera.

b) Kutumia chai za dawa, angalia sura 4.2.

c) Kuzuia na kutibu kuharisha kwa watoto kwa kuwaonyesha wazazi jinsi ya

kutayarisha maji yenye mchanganyiko wa sukari na chumvi kwa kutumia chombo

cha chumvi, chombo cha sukari na kikombe.

d) Kuwafundisha watoto juu ya njia ya maisha yenye afya , kwa kushirikiana

kutundika matangazo mfano juu ya “Afya” au “Kamwe usitumie sabuni za kuzuia

vijidudu!” (Kwa sababu, katika eneo la tropiki sabuni hizi zina 1 – 3% ya zebaki).

e) Kwa kuwa na bustani ya madawa na kuitumia kwa juhudi zote! Hii inaweza

kutumika kama sehemu ya kufundishia na kama sehemu ya kuzalishia wakati

wote malighafi ya madawa.

7.3. KITUO CHA AFYA

Tafsiri potofu ya dispensary (zahanati): Neno dispensary mara nyingi limeeleweka

vibaya. Linatokana na neno la kilatini “dispensere” likimaanisha kugawanya,

kugawia watu, kutoa msaada, kunywesha. Kwa hiyo hii mara moja inatoa tafsiri isiyo

yenyewe. Yaani ya nyumba ambayo madawa (mara nyingi kutoka nchi za nje)

hugawiwa au kutolewa kwa msaada. Nimeona zahanati nyingi ambapo wagonjwa

wanashughulikiwa kama ofisini: – Mafile yanashughulikiwa zaidi kuliko waki

wenyewe. Nesi mmoja alinionyesha dispensary (zahanati yake) iliyojengwa kwa

namna hiyo: “….hapa katika chumba cha kwanza wagonjwa wanachunguzwa, cha

pili analipia, cha tatu wanadungwa sindano kisha wanatoka kwa mlango wa

nyuma….”.

Wazo potofu juu ya sindano. Sisi Wazungu tumefanya nini katika nchi za tropiki?

Sindano imekuwa na maana sawa na madawa bora ya kimagharibi, tiba bora (ya kiasi

Page 146: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

146

chochote) kama hakikisho la kupona haraka. Sasa ni juu ya manesi kupambana na

imani isiyo ya kweli juu ya nguvu ya sindano. Sindano zitolewe tu kama mgonjwa

hajitambui, au kama dawa haipatikani katika hali ya vidonge, au kama suppositories

(mfano chanjo).

Wazo potofu kwamba homa ni ugonjwa: Utoaji wa aspirin ni wa kawaida kabisa

katika vituo vya afya vya kawaida hapa Afrika. Madawa kama aspirin, metamizol au

Paracetamol yanaweza kutuliza dalili za magonjwa (maumivu ya kichwa, homa)

lakini kamwe hayawezi kutibu ugonjwa (aspirin hata siku moja haiwezi kuua vimelea

au vijidudu).

Homa siyo ugonjwa lakini kinyume chake, ni zawadi toka kwa Mungu! Homa

hutuelekeza kujali kuhusu kudhurika kwa mfumo fulani katika uhai wetu, kisha

kutulazimisha kupumzika. Unaweza kulinganisha homa na mwanga mdogo

mwekundu kwenye gari unaoashiria kwa kumaanisha “simama,” kuna tatizo katika

gari!”. Unadhani dereva anaye haribu taa hii ndogo nyekundu kwa nyundo atafurahia

gari lake kwa muda mrefu? Hakika siyo kweli. Lakini mfano huu ni kioo

kinachotuonyesha tabia yetu ya kunywa aspirin kila mara na dawa nyingine kisha

tunaendelea na maisha kama kawaida.

Leo tunajua kuwa homa siyo ishara pekee iliyo nzuri, ishara ya hali ya afya zetu

lakini pia ni silaha muhimu kwa kuchoma vijidudu na kusafirisha masalio yake nje ya

mwili. Lakini utawezaje kuchoma takataka kama mwingine anajitahidi kuuzima

moto? Kwa kweli unadhuru mwili wako (hasa tumbo lako) kama utakunywa vidonge

mara tu utakaposhambuliwa na malaria au baridi ya bisi.

Imeonekana kuwa manesi wenye elimu ya chini ndio walio wepesi kutoa aspirin

kwa wagonjwa.

Joto chini ya 38.5ºC kwa watoto na 39°C kwa watu wazima halihitajiki

kuteremshwa kwa kutumia madawa ya kemikali, kinyume chake kama joto liko chini

tunashauri lipandishwe kwa kutumia chai moto ya mimea ifuatayo (mapera,

mkaratusi, au michaichai).

Kuongezeka kwa kiwango cha kutoa jasho kunaongeza kiwango cha utoaji uchafu

mwilini. Uchafu mwingi hutolewa kwa njia ya jasho kuliko kwa njia ya mkojo!

Kama joto likipanda sana, taulo iliyoloweshwa inaweza kulishusha kama ikiwekwa

juu ya mwili wa mgonjwa. Mpe vidonge kama tu njia hii haisaidii.

Dawa za asili: Inategemea naminifu na ujuzi wa watumishi waliopo kama

wanaruhusiwa kutengeneza madawa wao wenyewe. Jinsi kituo cha afya kilivyo mbali

na bohari la madawa, ndivyo ilivyo bora zaidi kwa manesi kujitengenezea madawa

yao wenyewe, mfano: yale ya maji, ya mafuta ya baridi ya bisi, dawa za mafuta kwa

ajili ya upele. Ni muhimu pia kwamba mikutano ifanywe baina ya waganga wa

kienyeji ikiandaliwa na watumishi wa afya kwa msingi wa utaratibu na kawaida ili

kuondokana na imani juu ya bidhaa zilizoagizwa toka nje, ikiwa ni pamoja na

madawa.

Alama bora ya kuonyesha kituo bora zaidi cha afya siyo idadi kubwa ya wagonjwa

wanaotibiwa kwa mwaka, bali idadi kubwa ya wale wasiotibiwa kwa mwaka ambayo

ni ishara ya afya bora inayotokana na mafundisho mazuri katika semina mbalimbali.

Page 147: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

147

7.4. GHALA LA DAWA LA HOSPITALI

A. Nini kizalishwe:

1. Tunza na tengeneza madawa yanayotumika tu: Katika mahospitali mengi nimeona

madawa ya vivutio tu! Tonics (dawa za kutia afya na nguvu – kama zinavyoitwa),

vitamin za maji (vitamin syrup) n.k. Ni upotezaji wa jinsi gani huu wa muda na

fedha! Chunguza pia dawa zako zilizoingizwa toka nje; angalia kiasi cha sukari,

chumvi, maji, na mafuta yaliyomo, vyote kutoka Ulaya? Ninadhani kama 80%!

Kwa kutumia utengengezaji wa dawa ulio katika kitabu hiki mnaweza kupunguza

kwa 50% idadi ya dawa zinazoagizwa kutoka nje, okoa karibu 30% ya fedha yako,

tunzeni mishipa yenu ya fahamu na nguvu muridhike na uzalishaji wa bidhaa za

hali ya juu nyinyi wenyewe!

2. Tengeneza dawa za maji pale tu zinapohitajika. Dawa nyingi za maji zinazidi

kutajirisha watengeneza madawa tu! Watu wazima hawahitaji hizo dawa. Kwa

watoto kidonge kinaweza kugawanywa kabla ya kunyweshwa na kuchanganywa

na maji (au asali) kabla ya kumnywesha, jambo ambalo huokoa karibu 95% ya

gharama. Kwa watu wazima dawa za asili za maji na matone vinatosha, mfano

matone ya dawa ya kikohozi (sura 5:10). Kwa kikohozi kwa watoto, kunywa chai

nyingi au maji inasaidia zaidi kuliko dawa yoyote ya maji ya kikohozi!

Katika hali ya hewa ya tropiki hata dawa hizo zilizochanganywa na maji na sukari

hazitunziki bali zinahitaji vikolezo vya kuzitunza. Uingiaji mwilini wa hivyo

vikolezo unapelekea kuongezeka kwa madhara yake.

3. Tengeneza nzito – ambazo ni gharama kuzisafirisha au kuziagiza kutoka nje. Pia

usitegemee misaada kutoka nje, kwa sababu siku moja hii misaada itakoma au

unaweza kuwa umesahau kutengeneza dawa wewe mwenyewe!

4. Tengeneza inayookoa fedha – bidhaa nyingine ni rahisi kuzalisha, lakini ni

gharama kubwa kununua; mfano: ni bora kutumia chai ya Artemisia, badala ya

vidonge vyenye gharama kubwa vya kutibu malaria, au dawa ya mafuta ya kutibu

bawasiri. Mara nyingine nimeona, kinyume chake, watengeneza madawa ambao

wanazalisha vidonge kwa gharama kubwa lakini vinanunuliwa kwa bei rahisi.

5. Tengeneza iliyo muhimu: Lakini siyo iliyo katika orodha ya “madawa muhimu”

na kwa jinsi hiyo itakuwa ghari. Mahospitali mengi yamekubaliana na ubora na

madawa ya asili baada ya kuona vidonda vilivyooza vikitibiwa kwa kipande

chembamba cha papai bichi. Kisha kuharisha damu kwa (ameba) amiba

kukitibiwa kwa chai iliyotengenezwa kutokana na Euphorbia hirta, malaria kwa

kutumia chai ya Artemisia annua na kuvimba kwa viungo vya mifupa kwa

kutumia dawa ya mafuta ya kutibu baridi ya bisi (iliyotengenezwa kwa pilipili).

B. Madawa yaliyotengenezwa kutokana na mimea hatari Tengeneza kile wengine wasichoweza kutengeneza . Michanganyo mingine ya

madawa lazima itengenezwe katika mahospitali tu; mfano dawa ya maji ya Datura,

unga wa kimusukulu, dawa ya maji ya mbangi. Hizi zinatakiwa kutengenezwa na

wafanyakazi waliofuzu utengenezaji wa madawa katika mahospitali.

Page 148: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

148

C. Jinsi ya kutafuta kemikali.

C.1. Sodium Hydroxide

Inauzwa kwa kiasi kidogokidogo katika maduka makubwa kwa ajili ya kusafishia

mifereji na mabomba lakini hakikisha kuwa hakuna kemikali yeyote iliyoongezwa

ndani yake. Kwa kiasi kikubwa uliza kwenye viwanda vya pombe, au jaribu kununua

moja kwa moja toka kwenye kiwanda cha sabuni.

C.2. Kileo (Alcohol): Unaweza kutengeneza kimiminika chenye kama 10% ya kileo (angalia: divai ya asali,

sura 4:8). Mvinyo (gongo) ya mahindi inayotengenezwa vijijini inaweza kuwa na

30% hadi 40% ya kileo, lakini kwa sababu za kiusalama, itumie kwa matumizi ya nje

tu. Ili kupata hadi 70% ya kileo kutoka katika mvinyo ya mahindi unatakiwa

kuichemsha na kupata mvuke wake na kisha kuugeuza kuwa kimiminika tena. Itumie

hii kwa dawa za maji kwa matumizi ya nje ya mwili pekee au kwa dawa ya kusafisha

na kuua vijidudu . Unaweza kupata 95% ya kileo katika mapipa; mfano, kutoka

katika viwanda vya sukari.

C.3. Nta

Ukihitaji kiasi kidogo tumia mishumaa. Nunua kiasi kikubwa kutoka makampuni ya

petroli. Yanauza nta katika mifuko ya kilo 50. Hii ni nta ya kiwandani, lakini

tulipoitumia hakuna aliyedai kupata madhara ya ngozi.

Vinginevyo tumia masega ya nyuki (kwa kuyavuna na kuyatayarisha angalia sura

6:31).Yatumie kwa kutengeneza dawa za mafuta, karatasi zenye nta, mishumaa, rangi

za kupaka, dawa za viatu, varnish.

Nta ya nyuki huondolewa rangi kwa kusambazwa kwenye kipande cha nguo na

kisha kuiweka juani; kwa kufuata mtindo wa kiwandani, ni kwa kutumia chloride of

lime au potassium permanganate lakini sisi huwa hatuiondolei rangi hata mara moja.

Hakuna kabisa haja ya kuiondolea rangi!

kutoka Ukraine:

Mgeni wa kizungu akisaidiwa na tabibu wa kiafrika

Page 149: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

149

SURA YA 8

KAMA WEWE NI DAKTARI AU MUUGUZI: Tafadhali angalia uwezo wa tiba

yako kwa kutumia darobini na vifaa vya maabara vilivyopo.

KAMA WEWE NI MGANGA WA JADI: Shirikiana na hospitali ili kuthibitisha

matokeo.

KAMA WEWE NI MGONJWA: Kwa baadhi ya magonjwa, matumizi ya dawa za

mimea yanaweza kukutibu; katika baadhi ya magonjwa, matumizi ziada ya mimea

yanaweza kukusaidia; mtarifu mganga wako juu ya suala hili.

Kwa magonjwa katili kama kifua kikuu, UKIMWI, kansa, magonjwa ya ngono, ni

muhimu kumuona daktari! Tiba bora daima hutolewa kwanza ikifuatwa na tiba ya muhimu zaidi, na kuendelea.

Agitation Mziwaziwa 5.11; raurolfia 6.41; na 7.4b

Arteriosclerosis (arteri

kuvimba na kuwa ngumu)

Kitunguu swaumu 5.1; karoti 6.21

Arthritis Pilipili 5.4; mbafu 6.10; dawam mchuzi 6.19.

Athlete’s foot Kitunguu swaumu 5.1; mwarobaini 5.3.

Baridi yabisi (Rheumatism) Pilipili 5.4; mbafu 6.10; mkaratusi 5.10

Bawasiri Artemisia 5.2; Mwingajini 5.7; embe 5.12; pilipili

5.4; michaichai 5.9 (mafuta ya dawa 4.4)

Bilious troubles Dawam mchuzi 6.19; mfuta 6.25.

Bronchitis Mkaratusi 5.10; michaichai 5.9; limau 5.8; embe

5.12; chumvi 6.33

Chawa kichwani (Mafuta 4.3.F); mwarobaini 5.3.

Choo kufunga Mwingajini 5.7; ringworm bush 5.6; karoti 6.21;

embe 5.12

. tatizo kubwa Mbono 6.43.

Colitis Artemisia 5.2.

Eczema Kabeji 6.8; mwarobaini 5.3; chamomile 6.29;

maharagwe 6.39

Elimu ya afya Sabuni 4.1

Filaria Mafuta ya scabies (upele) 4.3.F

Flatulence Mkaratusi 5.10; pilipili 5.4; dawam mchuzi 6.19.

Gastritis Mperapera 5.14; mshubili 6.3; viazi vitamu 6.26.

Goiter (Mchanganyiko 4.10j)

Guinea worm Papai 5.5

Hedhi

kutokuingia (Amenorrhea)

Nanasi 6.5

maumivu wakati wa hedhi Tururu 6.44

Hepatitis Papai 5.5

CHAGUO LA KWANZA KATIKA TUKIO LA UGONJWA

Page 150: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

150

Herpes labialis Limau 5.8; chungwa 6.14.

Hofu (Anxiety) Mziwaziwa 5.11; passion 6.37.

Homa Michaichai 5.9; mkaratusi 5.10; kurimbais 6.35;

mbuyu 6.1 (ushauri 7.3)

Homa ya manjano Papai 5.5.

Homa ya matumbo

(Typhoid)

Kitunguu saumu 5.1; ORS 4.6.

Impetigo Rejea magonjwa ya ngozi

Insect repellant Michaichai 5.9; mkaratusi 5.10

Insecticide Mwarobaini 5.3; mbaazi 6.46; tumbaku 6.34 (ushauri

4.11.I)

Jaundice Papai 5.5

Jipu Papai 5.5; kitunguu maji 6.2

Kansa (Ushauri, vinka 6.49)

Kichefuchefu Tangawizi 5.15; kahawa 6.16

Kichocho (Bilharzia) Artemisia 5.2

Kichwa kuumwa Rejea homa au migraine

Kifaduro Tururu 6.44

Kifua kikuu Mkaratusi 5.10 (supportive)

Kikohozi Mkaratusi 5.10; kitunguu saumu 5.1; limau 5.8;

tangawizi 5.15; kitunguu maji 6.2; ovakado 6.38;

elixir 4.9.

Kisonono (Ushauri 7.1)

Kisukari Mhindi 6.50; kitunguu maji 6.2; kitunguu saumu 5.1;

maharagwe 6.39; Mpira 5.14 kama hakuna mimea

mingine, vinka 6.49.

Kuhara damu:

Light cases: Kitunguu saumu 5.1; Mpira 5.14; tangawizi 5.15;

mwarobaini 5.3.

Bacillary: Mziwaziwa 5.11; vinka 6.49.

Kuhara kwa ameba

Kuharisha kidogo na

kuzuia:

Papai 5.5; Mpera 5.14; Embe 5.12

Kuharisha sana: Mziwaziwa 5.11

Kuharisha Watu wazima Mkaa 4.5; ORS 4.6; Mpira 5.14; mziwaziwa 5.11.

embe 5.12; mwarobaini 5.3

Kuharisha Watoto ORS 4.6; pera 5.14; karoti 6.21; juisi ya nazi 6.15.

Kukosa usingizi Karanga 6.6; passion flower 6.37.

Kupungua uzito (Ushauri 7.1)

Kuumwa na nyoka Jiwe jeusi 4.7.

Kuumwa na wadudu Mranaa 6.20

Kuungua Mshubili 6.3; chumvi 6.33; kiretemete 6.27; kitunguu

maji 6.2; papai 5.5.

Majeraha ya kuungua

yenye vijidudu

Mwarobaini 5.3; papai 5.5.

Page 151: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

151

Kuvimbewa Paipai 5.5; nanasi 6.5; kechu 6.40; dawam mchuzi

6.19.

Lactation (kuongeza

maziwa ya mama)

Boga 6.18

Low blood pressure Kahawa 6.16

Lumbago Rejea maumivu ya kuvimba kwa viungo (Baridi

yabisi/ Rheumatism)

Maambukizi ya figo Mahindi 6.50; mziwaziwa 5.11.

Macho mekundu

(Conjunctivitis)

Chamomile 6.29; mshubili 6.3; Artemisia 5.2.

Madawa ya mifugo (Ushauri na michanganyiko 4.10)

Mafua Kitunguu saumu 5.1; limau 5.8; michaichai 5.9;

Artemisia 5.2; mkaratusi 5.10.

Magonjwa ya kusambaa

kwa kujamiiana

Tumia antibiotics. Saidia tiba hii kwa papai 5.5;

mshubili 6.3; mziwaziwa 5.11; (Ushauri 7.1.11)

Magonjwa ya njia ya mkojo Papai 5.5; mziwaziwa 5.11; kitunguu maji 6.2;

Mkaratusi 5.10; vinka 6.49.

Malaria (Ushauri 7.3) kwa mujibu wa homa;

katika joto lolote: Michaichai 5.9; kitunguu saumu5.1)

Hadi 37.5°C Tangawizi 5.15; Mpera 5.14

Hadi 38°C Papai 5.5

Hadi 38.5°C Mwarobaini 5.3; mtukutu 6.48

Hadi 40°C Artemisia 5.2; cinchoma 6.13

Mammary gland infection Tururu 6.44

Matatizo ya tumbo Mpera 5.14

Maumivu ya kunyonga

(Cramps)

Passion 6.37; mziwaziwa 5.11; mramaa 6.20.

Mba (Fungal infection) Kitunguu saumu 5.1; ringworm bush 5.6; papai 5.5;

kitunguu maji 6.2; kabeji 6.8

Meno - kuoza (Caries) Poda ya meno 4.5; mwarobaini 5.3.

kusafisha meno Mwarobaini 5.3; mkaratusi 5.10; (ushauri na

mchanganyiko 7.1d)

Migraine Kahawa 6.16; mgagolia 6.17; chungwa 6.14; mranaa

6.20.

Minyoo, intestinal Papai 5.5; mziwaziwa 5.11; boga 5.19; embe 5.12;

lesena 6.28.

Mkanda wa jeshi (Herpes

zoster)

Pilipili 5.4

Mtando mweupe mdomono

(Candidiasis) Asali na kitunguu saumu 5.1; Artemisia 5.2.

Ngozi kuwasha Kitunguu maji 6.2; kabeji 6.8; mranaa 6.20.

Ngozi – ulinzi (Skin care) Mafuta ya watoto 4.3; mafuta ya dawa ya watoto 4.4.

Nywele kutoka Mshubili 6.3; pilipili 5.4.

Oedema Mahindi 6.50; mwingajini 5.7; nanasi 6.5.

Oral mucous membrane

Page 152: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

152

infection Embe 5.12

Parkinson’s disease Mranaa 6.20.

Poisoning Mkaa 4.5B; mbono 6.42; mranaa 6.20.

Prostatitis Boga 6.18; karoti 6.21.

Psoriasis Mwarobaini 5.3; ringworm bush 5.6.

Pumu (Asthma) Mziwaziwa 5.11; mkaratusi 5.10; papai 5.5.

Ringworm Ringworm bush 5.6; Mwarobaini 5.3.

Roundworm Tazama minyoo, intestinal

Safura (Hookworm) Tazama minyoo

Sciatica Pilipili 5.4

Shingles Rejea Herpes zoster

Shinikizo la damu Kitunguu saumu 5.1; mahindi 6.50; kitunguu maji

6.2; vinka 6.49.

Sinusitis Michaichai 5.9; Artemisia 5.2; kitunguu saumu 5.1.

Spasm, intestinal Passion flower 6.37; mranaa 6.20

Sprains Pilipili 5.4

Travel sickness Tangawizi 5.15

Uchungu wa kuzaa Pilipili 5.4

Ugonjwa wa masikio (Otitis) Kinetenete 6.27; kitunguu maji 6.2.

Ugonjwa wa fizi Embe 5.12; mshubili 6.3

UKIMWI (Ushauri 7.1)

Ukosefu wa hamu ya kula Ngongolia 6.17; anchona 6.13

Ulcers Mshubili 6.3.

Upele (Scabies) Mafuta 4.3f; mafuta ya dawa 4.4; ringworm bush 5.6;

mwarobaini 5.3; rauwolfia 6.41.

Upungufu wa damu Jamii ya mchicha 6.4; chuma 4.10; Folic acid 4.10

Upungufu wa Vitamin C Mchicha 6.4; nanasi 6.5; limau 5.8; chungwa 6.4;

mwembe 5.12; matunda damu 6.37; Mpera 5.14

Utapiamlo Mlongelonge 5.13; (ushauri 7.10)

Vidonda Asali 6.30; chumvi 6.33; kinetenete 6.27; papai 5.5;

annatto 6.7; mafuta ya dawa 4.4.D)

Vidonda koo (Tonsillitis) Mkaratusi 5.10; mwembe 5.12

Vidonda vyenye usaha Papai 5.5; kitunguu saumu 5.1; kitunguu maji 6.2.

Warts Kitunguu saumu 5.1; mwarobaini 5.3; mziwaziwa

5.11

Page 153: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

153

Abscess (jipu) Mkusanyiko wa usaha chini ya ngozi uliozungukwa na tissue

zilizovimba.

Allergen (Pia huitwa antigen) kitu cha nje ambacho husababisha mzio,

hasa mbelewele, vumbi la ndani ya nyumba na moshi wa sigara

Mzio (allergy) inayosababishwa na allergen. Baadhi ya matukio ya mzio

hutokea hapo hapo, na mengine baadaye.

Amenorrhea Kukosekana kwa hedhi kwa wanawake.

Amoeba dysentery Kuharisha kunakosababishwa na kimelea Entamoeba –

histolytica, ni wa pili kwa malaria ambayo imeenea katika nchi

za tropiki.

Anaemia Upungufu wa chembechembe nyekundu za damu, mgonjwa

hupauka na kuwa dhaifu.

Anaesthetic Dawa ambayo inasababisha kutokuhisi maumivu.

Analgesic Kitu ambacho hupunguza maumivu.

Antiseptic Ni kitu ambacho huzuia maambukizi kwa kuua bacteria.

Anti-spasmodic Kitu ambacho hulegeza maumivu ya kunyonga (cramps).

Arthritis Kuvimba kwa viungo.

Ajurveda Mfumo wa jadi wa dawa za kihindi ambao una maana

“Ufahamu wa namna ya kuishi.”

Bacillary dysentery Pia huitwa shigellosis, ugonjwa mkali wa matumbo ambao

husababisha kuharisha. Husababishwa na kula kinyesi cha

mgonjwa katika vyakula au maji.

Bacillus Jamii ya bacteria ambao huzalisha vijidudu katika familia ya

bacillaceae. Katika aina 33, tatu husababisha ugonjwa.

Beri-beri Ugonjwa wa mishipa ya fahamu ya mikono na miguu

husababishwa na upungufu wa thiamine.

Bile (nyongo) (Pia huitwa gall) Majimaji yanayotolewa na ini, yana rangi

njano-kijani na machungu. Nyongo huhifadhiwa katika kifuko

cha nyongo, na hutolewa wakati mafuta yanapoingia sehemu

ya kwanza ya tumbo mdogo (duodenum), kusaidia katika

uyeyushaji wa mafuta.

Bilharzia (kichocho) Pia huitwa Schistosomiasis. Ugonjwa wa minyo

ohusababishwa na vimelea (schistosoma); mtu anaweza

akaugua kwa kuogelea katika mito au maziwa, yenye vimelea,

au kwa kunywa maji yenye vimelea.

Black water fever Ni madhara makubwa ya kutumia quinine kutibu malaria.

Boil (jipu) Uvimbe wenye usaha chini ya ngozi.

Bronchitis Inflammation of the mucous membrane ya mirija ya hewa

kwenye mapafu.

ORODHA YA MANENEO YA KISAYANSI NA

MAELEZO YAKE

Page 154: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

154

Candida Fungus nyeupe ambazo wakati mwingine hutokea midomoni

mwa watoto. Kwa watu wazima ambao wana kinga ndogo

inaweza ikashindikana kudhibitiwa, hivyo kupelekea utando

mweupe mdomoni, ukeni, njia ya chakula au kwenye ngozi.

Carminative Dawa ambayo hutibu msokoto wa tumbo na tumbo kujaa hewa.

Cold sores Malengelenge madogomadogo yanayowasha yaliyo na

majimaji (wakati mwingine husababishwa na virusi vya

herpes).

Colic Maumivu makali ndani ya utumbo.

Colitis Mwako (inflammation) katika utumbo mkubwa (bowel)

Conjunctivitis Kuvimba kwa mucous membrane ya jicho.

Contagious disease Ugonjwa unaoenezwa kutoka mtu mwenye ugonjwa kwenda

kwa mtu mwingine.

Cramp Maumivu ya kunyonga

Delirium Hali ya kuchanganyikiwa kiakili (hasa husababishwa na dawa

au homa kali).

Dermatitis Kuvimba na kuuma kwa ngozi.

Dehydration Upungufu mkubwa wa maji mwilini.

Diabetes (kisukari) Ugonjwa wa kongosho ambao huzuia sukari na wanga

kufyonzwa inavyotakiwa.

Diarrhea (kuharisha) Kinyesi cha mara kwa mara cha majimaji husababishwa na

hofu, wadudu (microbes) au sumu.

Digestion Mchakato wa kuyeyusha chakula kuwa kidogo ambacho

kinaweza kufyonzwa.

Diuretic Kitu ambacho kinaongeza utokaji wa mkojo.

Dysentery Mwako (inflammation) wa utumbo, ambao husababisha

kuharisha sana.

Dysmenorrhea Maumivu wakati wa hedhi

Ebola virus disease Ugonjwa mkali wa virus na wenye homa kali ya ghafla na

kutokwa damu sehemu mbalimbai za mwili, yakiwemo macho.

Unaambukizwa kupitia damu au majimaji ya mgonjwa.

Eczema Ugonjwa wa ngozi unaosababisha wekundu, maumivu makali

na ngozi kuwa na magamba.

Emetic Dawa inayofanya mtu kutapika.

Enema Maji yanayoingizwa kupita njia ya haja kubwa kwa lengo la

kusafisha utumbo.

Enteritis Kuvimba kwa matumbo

Enzyme Protin inayoundwa katika chembechembe hai ambayo husaidia

mabadiliko ya kikemikali.

Expectorant Ni kitu ambacho humsaidia mgonjwa kukohoa makohozi

(mucous) na majimaji mengine kutoka kwenye mapafu.

Filariasis Ugonjwa unaosababishwa na filarial, thread worms wanaoishi

kama vimelea kwa binadamu, wanyama na mimea.

Flavonoid Rangi ya njano kwenye mimea

Furunculosis Ugonjwa mkali wa ngozi unaosababisha majipu majipu.

Page 155: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

155

Galenics Ni Sayansi ya kubadilisha kemikali kuwa dawa.

Gall Rejea bile (nyongo).

Gangrene Kuoza na kufa kwa tissue za mwili wakati upelekwaji wa damu

unapokuwa umekatwa.

Gastric Yenye kuhusiana na tumbo.

Genital Yenye kuhusiana na uzazi.

Gonorrhea Ugonjwa wa ngono unaosababishwa na bacteria Neisseria

gonorrhea.

Guinea worm Threadworm hadi meta 1 urefu, huishi chini ya ngozi.

Haemostatic Kitu ambacho huzuia kuvuja damu

Haemorrhoids

(bawasiri)

“Piles” kuungua (kuvimba) kwa mishipa ya damu

inayozunguka njia ya haja kubwa.

Hepatic Yenye kuhusiana na ini.

Hepatitis Kuvimba kwa ini, husababisha ngozi kuwa njano, ini kuwa

kubwa, kukosa hamu ya kula, tumbo kuvurugika, choo chenye

rangi ya mfinyanzi na mkojo kuwa na rangi ya njano sana.

Herpes Ugonjwa unaoletwa na virus; husababisha cold sores kwenye

ngozi na mucous membrane. Aina mbalimbali za virus

hushambulia maeneo ya pua na midomo (herpes labialis), kati

ya kiuno na mapaja (herpes zoster or shingles) na kuzunguka

sehemu za uzazi (herpes genitalis)

Insecticide Inayoua wadudu

Insectifuge Inayofukuza wadudu

Jaundice Ngozi kuwa njano, mucous membrane na

macho,kunasababishwa na bilirubine kuwa nyingi sana

(sehemu ya nyongo) katika damu.

Kwashiorkor Aina ya Utapiamlo unaosababishwa na upungufu wa protein

kwenye chakula

Lactagogue Dawa inayochochea maziwa ya mama kuzalishwa.

Lactation Utokaji wa Maziwa ya mama baada ya kujifungua.

Laxative Dawa inayochochea choo kutoka (kuharisha).

Lesions Vidonda vinavyosababishwa na ugonjwa fulani, mfano candida

au herpes.

Murasmus Kunyong’onyea na kukonda, aina ya Utapiamlo.

Menstrual Yenye kuhusiana na hedhi (utokaji wa damu ya uterine mucous

membrane)

Nephritis Kuvimba kwa figo.

Neuralgia Kutokea na kutoweka kwa maumivu makali kwenye mishipa

ya fahamu, kawaida kichwani au usoni.

Oedema Kuvimba kwa tissue kwa kuwa na majimaji

Oral rehydration “Kurudisha” maji ya mwilini yaliyopotea kwa kunywa

mchanganyiko maalum.

Paralysis Kukosa nguvu katika misuli kwa sababu ya jeraha au ugonjwa

katika mishipa ya fahamu.

Page 156: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

156

Parasite Mnyama au mmea ambao huishi kwenye au ndani ya mnyama

au mmea mwingine na kupata chakula chake kutokana na

mnyama huyo.

Pectoral Yenye kuhusiana na kifua au matiti.

Placental retention Kondo la nyuma kushindwa kutoka baada ya kujifungua

Prostatitis Kuvimba kwa tezi za kiume (tezi za kiume ambazo huzunguka

shingo ya kibofu na mfereji wa mkojo)

Psoriasis Ugonjwa wa ngozi unaosababisha ukurutu na ngozi kama

magamba ya samaki

Purgative Kitu kinachofanya utumbo kutoa uchafu.

Pyrogene Kitu cha kibacteria ambacho husababisha homa.

Renal Yenye kuhusiana na figo.

Rheumatism Ugonjwa mkali ambao utaufahamu kwa kuvimba na maumivu

makali kwa kiungo kimoja au zaidi.

Rickettsia Wadudu wadogo ambao sura yao inaunganisha sura ya bacteria

na virusi

Scabies Ugonjwa wa kuambukiza ambao husababisha vigaga na

maumivu. Husababishwa na vijidudu (mites) vidogo.

Schistosomiasis Rejea Bilharzia (kichocho)

Scurvy Ugonjwa unaosababishwa na upungufu wa vitamin C.

Sedative Dawa ya nguvu ya kutuliza.

Shingles Rejea herpes zoster (mkanda wa jeshi)

Sores Vidonda, majeraha au kidonda chochote kilichowazi.

Spasmodic Inahusiana na spasms, mishituko mikali ya vipindi.

Syphilis

(Kaswende)

Ugonjwa unaoletwa na kujamiiana; husababishwa na

Treponema palladium.

Tuberculosis

(Kifua kikuu)

Ugonjwa unaoathiri mapafu na wakati mwingine mifupa,

husababishwa na bacillus, mycobacterium tuberculosis.

Typhoid (Homa ya

matumbo)

Ugonjwa wa gastro-intestinal. Husababishwa na salmonella

typhi, huambukizwa kutokana na maji yasiyo safi.

Typhus Ugonjwa ambao husababishwa na aina ya Rickettsia,

huchukuliwa kutoka wanyama kwenda kwa watu kwa kuumwa

na chawa, viroboto, papasi au vidudu vidogovidogo.

Hujulikana kwa homa kali na mgonjwa kuonekana kuwa

mwenye huzuni kubwa.

Venereal disease Ugonjwa unaoambukizwa kwa njia ya kufanya tendo la ngono.

Vermifuge Dawa ambayo hufukuza parasitic worms.

Volatile oils Mafuta yenye harufu nzuri ambayo hutoweka kwa mvuke

katika hewa.

Page 157: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

157

Matoleo mengine ya vitabu vya anamed

“Dawa za asili katika nchi za joto.

I: Mimea ya nchi za joto kama chanzo cha ulinzi wa afya.” Na Hans – Martin Hirt na Bindanda M`Pia.

Kitabu hiki kinapatikana katika Kkiingereza “Natural Medicine in the Tropics”, Kijerumani:

“Natuerliche Medizin in den Tropen,” Kifaransa: “La Médecine Naturelle Tropicale”, Spanish:

“Medicina Natural” and Ukranian.

“Dawa za asili katika nchi za joto II: Uzoefu” Na Hans – Martin Hirt na Keith Lindsay

Kijitabu chenye kurasa 48 kinachoelezea magonjwa ya kawaida na jinsi ya kuyatibu, na maelezo ya

kina ya mimea mitano.

Kitabu muhimu kwa semina ya kwanza katika mada wa asili:

Kinapatikana katika kiingereza, kifaransa kireno na Kisualuli.

Tafsiri katika Lugha nyingine zinaendelea kutayarishwa.

Bango la “Mimea inayoponya katika nchi za joto.” Linapatikana katika kiingereza, kifaransa na kijerumani.

Tumia Water Hyacinth!

Kitabu cha mwongozo wa matumizi ya magugu maji kutoka dunia nzima. Na Keith Lindsay na Hans – Martin Hirt.

Magugu maji ni janga katika nchi zote za joto. Kitabu hiki kinaelezea jinsi Water Hyacinth

inavyoweza kuonekana kama malighafi inayopatikana daima na bure, na inatumika kwa mambo

mengi. Ikiwa ni pamoja na mbolea , chakula cha wanyama, ufundi, samamni, karatasi, usafishaji

maji na kwa nishati. Pia ndani yake kuna mpango wa mtengenezaji wa jiko la jua na ULOG.

Linapatikana katika Kiingereza.

Vikorokoro vya programu ya malaria wa anamed (AMP). Mbegu na taarifa zote unazohitaji ili kupanda na kustawisha Artemisia annua anamed (A3),

kutayarisha chai ya Artemisia na matumizi yake kwa wagonjwa wa malaria. Habari nyingi za

kisayansi juu ya mmea huu zinatolewa pia.

Fomu zinatolewa kwa ajili yako ili kutoa taarifa ya uzoefu wako – kwa anamed.

Nyaraka juu ya mpango wa malaria wa Anamed. Vifurushi vinapatikana katika lugha za kiingereza, kijerumani na kifaransa.

Sabuni zenye zebaki (Mecury): Aibu ya siku hizi. Taarifa inaelezea tatizo la kutumia sabuni na vipodozi vyenye zebaki kwa lengo la kung’arisha

ngozi. Kurasa 15 za taarifa kuu zimefuatiwa na kurasa nyingine 27 zenye taarifa kutoka magazetini,

taarifa za kisayansi na taarifa nyingine muhimu. Anamed inatafuta kuondoa sheria inayoruhusu

uuzaji wa bidhaa za sumu kama hizo dunia nzima.

Kwa taarifa kuhusu bei, au kuagizwa, tafadhali angalia katika toviti yetu , au andika kwa anamed,

Schafweide 77, 71364 Winnenden, Germany.

Page 158: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

158

Bindanda M’Pia alizaliwa July, 27, 1963 huko

Matamba – Solo, Zaire.Tangu 1983 hadi 1986

alikuwa mwalimu wa sekondari. Tangu 1986 hadi

1991 aliajiriwa na Kitengo cha Shirikisho la Kitabu

cha Kanisa la Kiprotestanti huko Kwango,

Zaire, ambako alifanya mikutano mbalimbali na

waganga wa kienyeji. Alibadilisha mimea mingi ya

asili kuwa madawa ambayo kwa sasa yanajulikana

sana huko Zaire katika hospitali, kwa kuitikia wito

mbalimbali amekuwa akiwatia moyo na

kuwafundisha watu wengi katika nchi za tropiki jinsi

ya kutengeneza dawa zao wenyewe, na hivyo

kutunza na kushughulikia afya zao wenyewe. Tangu 1991 hadi 1993 alipata

masomo zaidi huko Ufaransa. Kwa wakati huu anajishughulisha na “program

ya madawa ya asili” katika jimbo la Bandundu katika Jamhuri ya

Kidemokrasia ya Kongo.

Hans – Martin Hirt alizaliwa huko Winnenden,

Ujerumaji 25 January, 1951. Kufuatia masomo ya

Ufamasia katika Chuo Kikuu cha Heidelberg

alitunukiwa “The Doctor of Pharmacy,”kwa kusomea

“Uimarishaji wa asili wa mfumo wa kinga mwilini,”

kwenye kituo cha Ujerumani cha “Cancer Research

Center”(Utafiti juu ya Saratani) – ambapo katika somo

hilo amekwisha

toa matoleo zaidi ya 30 juu ya uchunguzi wake

kisayansi.

Tangu 1976 hadi 1985 alikuwa Mkuu wa Idara ya

Uchunguzi na Utengenezaji madawa kwenye kituo kikuu cha Ufamasia cha

Wilaya ya Heilbronn. Mwaka 1985 alifanya ziara kwenye mahospitali nchini

Peru, Nepal na India. Tangu 1985 hadi 1991 alikuwa mshauri wa mambo ya

madawa huko Matamba – Solo, Zaire, na tangu 1992 hadi 1994 alikuwa

mshauri wa Kanisa la Kiprotestanti la Ujerumani kwa shughuli za nchi za nje

nchini Zaire. Mwaka 1991 alianzisha “anamed” (Action for Natural Medicines)

ambayo kwayo anaongoza semina juu ya madawa ya asili huko nyumbani na

nchi za nje, ameanzisha vikundi vya anamed katika nchi kadhaa.

Page 159: MADAWA YA ASILI...MADAWA YA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI Dr. Hans Martin Hirt Bindanda M’pia 1. Mimea ya tropiki kama chanzo cha ulinzi wa afya. Uzalishaji wa madawa na vipodozi

159

HATARI KUBWA ZAIDI KATIKA NCHI ZA TROPIKI NI KUPOTEZA

UFAHAMU WA UTAMADUNI WAO.