mwongozo wa mwezeshaji utangulizi wa mikutano ya elimu ya ... · mpango wa kuinua ubora wa elimu...

55
Mwongozo wa Mwezeshaji Utangulizi wa Mikutano ya Elimu ya Wilaya

Upload: others

Post on 18-Feb-2020

46 views

Category:

Documents


1 download

TRANSCRIPT

Mwongozo wa Mwezeshaji

Utangulizi wa Mikutano

ya Elimu ya Wilaya

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

2

Yaliyomo

Mwongozo wa Mwezeshaji ....................................................................................................... 3

Siku ya 1 Mkutano wa Elimu wa Wilaya ........................... Error! Bookmark not defined.

Kipindi cha 1 Utangulizi wa mafunzo na Mkutano wa Elimu wa Wilaya ........................... 6

Kipindi cha 2 Malengo ya Mkutano wa Elimu wa Wilaya ................................................ 10

Kipindi cha 3 Kupanga na kuandaa Mkutano wa Elimu wa Wilaya ................................. 13

Kipindi cha 4 Umuhimu wa Mada za majadiliano na Mwongozo wa mada za mwaka ... 16

Siku ya 2 Kuandaa na Kuendesha mikutano ya MEW ...................................................... 20

Kipindi cha 5 Matarajio ya Maafisa Elimu Kata na kujenga uwezo wao wa kitaaluma .. 21

Kipindi cha 6 Ufuatiliaj, Msaada na Mapitio ya Mkutano wa Elimu wa Wilaya ............. 25

Kipindi cha 7 Kupanga Mkutano wa Elimu wa Wilaya ..................................................... 30

Kipindi cha 8 Kukutokea nini baada ya mafunzo? ........................................................... 32

Viambatisho

Kiambatisho A Majukumu ya Kamati ya Maandalizi naWajibu wa Mwakilishi wa MEW..35

Kiambatisho B Kiolezo cha Mikutano ya MEW .................................................................... 36

Kiambatisho C Kipindi cha 1 Manufaa ya MEW ................................................................... 37

Kiambatisho D Kipindi cha 2 Mapitio ya Mpango wa Maendeleo ya Shule ........................ 41

Kiambatisho E Kipindi cha 3 Ziara za Afisa Elimu Kata na Uandishi mzuri wa ripoti........... 44

Kiambatisho F Mfano wa Mwongozo wa mada za Mwaka .................................................. 47

Kiambatisho G Ufafanuzi wa Kazi ya Afisa Elimu Kata ........................................................ 49

Kiambatisho H Waraka juu ya namna ya kuandika taarifa nzuri ........................................ 50

Kiambatisho I Mpangokazi kwa ajili ya mikutano ya MEW ....................................................... 53

Kiambatisho J Mjukumuna Taratibu za utoaji taarifa za mkutanoa wa Elimu was Mkoa na

Wilaya...................................................................................................................54.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

3

Mwongozo wa Wawezeshaji Wawezeshaji wanaandaaje semina zao.

Wagawanye washiriki katika makundi ili kila Mwezeshaji apewe jukumu la kuwezesha kundi moja (kwa mfano, ikiwa kuna Wawezeshaji wa 3 na jumla ya washiriki ni 60, kila Mwezeshaji atafanya kazi na kundi la Washiriki 20).

Maandalizi ya Wawezeshaji kabla ya Semina kuanza: • Kusoma mwongozo huu wa mwezeshaji kwa kila kipindi • Kuandaa kila kipindi mapema na kuhakikisha kuwa una nakala za kutosha za:

Kitini cha mshiriki Miongozo ya mikutano ya MEW Karatasi za bango kitita zenye maelezo, vielelezo, n.k zilizoandaliwa mapema Mabangokitita yasiyoandikwa, kalamu rashasha, madaftari ya kuandikia kumbukumbu,

na kalamu Kompyuta, projekta-mashine ya kurusha picha/maandishi ukutani, kisitiri na waya wa

kuunganishia umeme kwa siku ya kwanza.

Wawezeshaji wanaandaaje kazi za vikundi: Hakikisha kwamba washiriki wanaelewa vyema kazi yao, Muda na jinsi ya kutoa Mrejesho kabla ya kuanza kufanya kazi katika vikundi:

Kazi: Hakikisha washiriki wanaelewa vyema kile wanachopaswa kufanya (hii ni "LAZIMA" wakati washiriki wanafanya kazi ya kikundi);

Muda: Hakikisha washiriki wanajua wazi wana muda gani. Hakikisha kila kikundi kinateua mtunza muda ili kuhakikisha vikundi vinazingatia muda;

Mrejesho: Hakikisha kila kikundi kinateua mwandishi/mtoa taarifa. Hakikisha washiriki wanajua ni mambo gani wanapaswa kuyatolea taarifa kwa ujumla. Waambie kwamba kuna ukomo wa muda kwa kila mrejesho.

Vidokezo na mbinu za Mwezeshaji: Tumia ujuzi na uzoefu wa washiriki kama hatua ya kuanzia:

Waalimu wakuu na Maafisa Elimu Kata tayari wanayajua haya kwa kiwango kikubwa, na changamoto yako wewe kama Mwezeshaji ni kuyachota haya kutoka kwao na kuwaongezea dhana na mawazo mapya ambayo hawana.

Hakikisha washiriki wote wanashiriki kikamilifu muda wote wa Semina: kuanzia wakati wa utangulizi, vipindi vya pamoja, wakati wa kazi za vikundi, na wakati washiriki wanafanya kazi katika jozi kwa kutumia:

o Vipindi vya majadiliano katikati ya maelezo ya pamoja. Waombe washiriki wageukiane na wenza wao na wajadili uzoefu au uelewa wao katika suala fulani. Majadiliano haya ni mafupi, na mrejesho unafanywa katika majadiliano mafupi ya pamoja yanayoongozwa na Mwezeshaji.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

4

o Vipindi vya bungua bongo hivi ni vipindi ambavyo makundi makubwa ya washiriki hufikiria juu ya mada au suala fulani na kujaribu kuibua masuala kadhaa au uzoefu wao kuhusiana na suala hilo.

Tazamana na washiriki mara kwa mara na jaribu kujifunza na kutumia majina yao

Washiriki wanapokuwa wanafanya kazi katika vikundi, tembelea kila kikundi. Ingilia majadiliano yao ikiwa tu utagundua kwamba wanakikundi husika hawaelewi wanachofanya au kama wamekwama na hawajui jinsi ya kuendelea.

Wakati mwingine washiriki huomba kupewa tafsiri au ufafanuzi zaidi (kwa mfano, maana ya "kusikiliza vizuri au vibaya", au maana ya "lengo" na "kusudi") kabla ya zoezi hilo kuanza. Usiwape ufafanuzi bali waambie washiriki kuwa watapata majibu ya maswali yao kwa kufanya zoezi lao na wakati wa majumuisho.

Wakati wa kutoa majumuisho, usielezee wala kufundisha. Badala yake, tumia "pointi kusisitiza" na kuuliza maswali zaidi (kudadisi) ili kuwafanya washiriki wafikiri wenyewe.

Usiogope unapoona hali ya ukimya baada ya kuuliza swali. Wapatie washiriki muda wa kufikiria na kutoa majibu ("hesabu hadi kumi").

Kiti cha Kusikilizia: Wakati washiriki wanafanya kazi katika vikundi, ikiwa samani za kutosha zinapatikana, weka kiti cha ziada kwenye kikundi na ungana nao kusikiliza bila kuvuruga sana majadiliano yao. Njia hii ni ya kiungwana zaidi kuliko kusimama karibu na kikundi.

Usisahau kuwapatia washiriki karatasi ya tathimini ili waweze kujaza/kuandika kwa namna gani mafunzo yalivyo fanyika.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

5

Siku ya 1: Mkutano wa Elimu wa Wilaya

Muda Shughuli Mbinu na maudhui Rasilimali

01:30-02:00 Usajili wa Washiriki

02:00-03:45 Kipindi cha 1 Ukaribisho, Utangulizi Kuchangamkiana/ vunja ukimya Mkutano wa Elimu wa Wilaya

1. Ukaribisho na Utangulizi Maneno ya kufungua Afsa Elimu wa Mkoa na Kiongozi wa EQUIP mkoa(RTL). 2. Kuchangamshana 3. Hali ya sasa kwa ajili ya Maboresho ya shule (kazi ya kikundi) 4. Mreojesho wote

Nakala za kutosha za vitabu vya mshiriki Karatasi za Bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe Karatasi ya A4, kalamu

03:45-04:15

04:15-06:00 Kipindi cha 2 Malengo ya Mkutano wa Elimu wa Wilaya

5. Habari za MEW mpaka sasa – ‘PowerPoint’ 6 Manufaa za MEW 7. Mreojesho wote 8. Kipindi cha Majumuisho

Nakala za kutosha za Kiambatisho A. Bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe Karatasi ya A4, kalamu Projekta, kisitiri, kompyuta

06:00-07:00

07:00-08:45 Kipindi cha 3

Kupanga na kuandaa Mkutano wa Elimu wa Wilaya

9.Kamati ya maandalizi na Wajibu wa Mwakilishi wa MEW 10. Mfano wa MEW na kupanga Mkutano 11. Mfano wa mipango ya Mikutano ya mwazo 12. Uwezeshaji na mbinu shirikishi 13. Majumuisho ya wote na majadiliano

Nakala za kutosha za Mipango ya Mkutano zilizoandaliwa (Kiambatisho B, C, D na E) Karatasi za bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe Karatasi ya A4, na kalamu

08:45-09:15

09:15-11:00 Kipindi cha 4 Umuhimu wa Mada za majadiliano na Mwongozo wa mada za mwaka

14. Mada zipi zinafaa 15. Tengeneza orodha ya Mada 16. Mrejesho wa wote 17. Tafakuri juu ya umuhimu wa kuchagua mada 18. Kupiga kura ili kuchagua Mada 10 bora zaidi 19.Kushirikishana mwongozo wa Mada za mwaka 20 Kuhitimisha siku

Karatasi za bango kitita zilizoandikwa kwa ajili ya kazi ya 17 Mfano wa Mwongozo –Kiambatisho F Karatasi ya ukubwa wa bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

6

Kipindi cha 1

Utangulizi wa mafunzo na Mkutano wa Elimu wa Wilaya (MEW) Kama ‘Jamil

Inayojifunza”

Muda: Saa 1 na dakika 45 (dakika 105) Lengo la Kipindi:

Kukuza uelewa wa washiriki juu ya Mikutano ya Elimu ya Wilaya na malengo yake ya kusaidia uboreshaji wa shule.

Kuelewa ni kwa jinsi gani Mikutano ya Elimu ya Wilaya (MEW) inaendana na jamii nyingine inayojifunza.

Matokeo ya kujifunza: Mwishoni mwa kipindi washiriki wataweza kuelezea: Jinsi Mkutano wa Elimu wa Wilaya unavyohusika na “Jamii inayojifunza” Mkutano wa Elimu wa Wilaya ni nini, na tofuati yake na mikutano inayofanyika sasa Wawezeshaji watakiwa kuwa wameandaa:

Mpangilio wa namna ya kukaa ukumbini: hakikisha washiriki wote wanaweza kumuona Mkufunzi

Nakala za kutosha za vitabu vya washiriki

Karatasi ya bango kitita kama inavyoonekana katika kielelezo hapa chini.

_____________________________________________________________________________ Maelezo ya Kipindi

1. Kukaribisha washiriki na kutoa utangulizi (dakika 20)

Pitia kijitabu na ueleze kuw:

Wakaribishe washiriki kwenye warsha na ueleze kwa ufupi malengo ya warsha. Eleza kuwa utaongoza na kuwezesha mchakato na kwamba washiriki watashiriki ipasavyo wakati wa vipindi vya semina (kama vile katika mafunzo ya Usimamizi wa Utendaji wa shule (SPMM). Tangaza na weka wazi taratibu zote za ndani ya ukumbi ikiwa ni pamoja na muda wa vipindi na uandike hayo kwenye karatasi ya bango kitita:

Muda gani tunaanza (2:00 asubuhi), kupumzika, kupata chakula cha mchana, na mwisho (11:00 jioni)

Mbinu, kufanya kazi katika jozi, na katika vikundi

Umuhimu wa kuteua mwandishi wa taarifa kwa ajili ya vipindi vya mrejesho Waulize washiriki ni kanuni gani au taratibu zipi za ndani ya ukumbi wangependa ziwepo na uziandike kwenye bango kitita. Hakikisha kuwa karatasi ya bango kitita itabaki imebandikwa ukutani kwa muda wote wa semina.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

7

Elezea Nii kwa jinsi gani mafunzo haya kuhusu MEW ni Jamii nyingine Inayojifunza na inavyohusiana na Mikutano ya Kila wiki ya Shule na Mikutano kati ya Waalimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata inayojadili kuhusu Usimamizi wa Utendaji wa Shule.

English Swahili

Communities of learning Jamii zinazojifunza

PTP+School Committee+Village Government UWW+Kamati ya Shule+Kamati ya Kijiji

District Education Meeting Mkutano wa Elimu wa Wilaya

Zonal Kikanda

Region-District-Ward-School Mkoa-Wilaya-Kata-Shule

Community Jamii

Score card IdadiAlama

QA Mthibiti wa Ubora SIS Mfumo wa Taarifa za Shule

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

8

Afisa Elimu Kata anahusika katika kila mafunzo ya jamii inayojifunza. Hii inamfanya yeye kuwa muhimu sana katika mambo yote ya uboreshaji wa shule.

1. Mikutano mipya ya kila wiki ngazi ya shule ni kwa ajili ya Mwalimu mkuu na Walimu yenye lengo la kuboresha kiwango cha ufaulu shuleni

2. Mikutano ya jamii inahusisha wazazi na jamii katika kuleta maendeleo ya shule na kuwasaidia wanafunzi 3. Mkutano wa kata wa Walimu wakuu ni kwa ajili ya kushirikishana uzoefu na kuwajengea uwezo walimu wakuu,

kujadili changamoto na mambo yanayohusu maendeleo ya shule 4. MEW ni jukwaa la Wathibiti Ubora wa Shule, Maafisa Elimu Wilaya na Waratibu Elimu Kata linalotoa fursa ya

kushirikishana masuala mbalimbali yanayohusu elimu katika wilaya ili kuboresha shule. Unatoa msaada maalumu kwa Maafisa Elimu Kata kwenye kutekeleza kazi zao

Mkutano wa Elimu wa Wilaya ni Mkutano wa kila mwezi unaowahusisha Maafisa Elimu wa Wilaya, Wathibiti Ubora na Maafisa Elimu Kata. MEW unawezesha kutenga muda ili;

Kushughulikia masuala yanayohusu ufundishaji na ujifunzaji yanapoibuka --> ni lengo la MEW

Kushirikishana na kuimarisha jitihada za uboreshaji elimu katika wilaya

Kuwezesha mawasiliano kuwa mazuri zaidi.

MEW ni mkutano rasmi wa Wilaya unaotambulika na wizara i, kama vile Ofisi ya ya Rais – TAMISEMI na Wizara ya Elimu, wenye lengo la kuteta mawazo ya pamoja, katika kusaidia kuboresha maendeleo ya shule.

2. Kuvunja ukimya, zoezi la kuchangamsha mwili (dakika 25)

Wagawanye washiriki katika makundi matatu; Kundi la 1 litajifanya kuwa Maafisa Elimu Kata, kundi la 2 litajifanya kuwa la Wadhibiti Ubora na kundi la 3 litakuwa la Maafisa Elimu. Wapatie kila kundi karatasi ya bango kitita na kalamu rashasha.

Waambie kila kundi wajadili ni kwa jinsi gani wanachangia katika kuboresha shule, na waandike mawazo yao kwenye bango kitita. Kundi la kwanza kumaliza litaita kwa sauti "BINGO". Kundi hili litabandika bango kitita ukutani. Endelea kufanya hivyo hivyo hadi makundi yote 3 yakamilishe.

Ni mambo gani muhumu mliyo yakuta katika majadiliano?

Tutayaangalia/jadili mambo hayo katika siku hizi mbili za mafunzo. 3. Kazi ya kikundi: Wajibu wa sasa katika kuboresha shule katika Wilaya (dakika 35) Hakikisha kila kundi lina bango kitita na kalamu rashasha. Yakumbushe makundi kwamba wanapaswa kuchagua mtu mmoja ambaye atachukua maelezo na kuwasilisha wakati wa majumuisho.

Waambie washiriki wajadili ni kwa namna gani shule zinasimamiwa kwa sasa. Lengo la zoezi hili ni kupata maoni ya washiriki juu ya wajibu wao wa kuboresha shule Wilayani. 4. Majumuisho ya Mrejesho (dakika 25) Kila kundi libandike bango kitita ukutani. Waambie washiriki wasome orodha ya majukumu ya kila kikundi.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

9

Mwezeshaji sasa anaongoza mjadala wa majumuisho ya mrejesho kwa kutumia maswali yafuatayo:

• Ni zipi kati ya kazi zenu zinasaidia sana kuboresha shule? • Je, mnatumia muda mwingi zaidi kwenye kazi zipi ? • Ni majukumu gani na kazi zipi vinawasaidia kutekeleza uboreshaji wa shule yenu?

Mambo muhimu ya kusisitiza:

Kupitia mafunzo haya ya jamii inayojifunza Wilaya zinahakikisha kwamba:

Ufundishaji na ujifunzaji unaboreshwa

Viwango vya ufaulu wa wanafunzi vinaboreshwa

Shule zinawajibika

Ubunifu mpya unatolewa kwa wengine na unafanyiwa majaribio

Jamii zinashiriki na kujishughulisha na masuala ya shule zao

Taarifa zinapokelewa na kusambazwa

Masuala ya fedha yanajadiliwa, kama vile ruzuku ya IGA

Hili ni jukumu la pamoja!

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

10

Kipindi cha 2 Lengo la Mkutano wa Elimu wa Wilaya

Muda: Saa 1 na dakika 45 (dakika 105)

Malengo ya Kipindi:

Kuelezea malengo ya siku ya 2 ya mafunzo kuhushu MEW

Kuwawezesha washiriki kuelewa madhumuni ya Mkutano wa Elimu wa Wilaya

Kuonesha kuwa Mkutano wa Elimu wa Wilaya ni chombo muhimu cha kusaidia kuboresha maendeleo ya shule>

Kuhusianisha MEW na fursa nyingine za kujifunza

Matokeo ya mafunzo: Hadi kufikia mwisho wa kipindi washiriki wa kipindi hiki wataweza:

• Kuelezea ni kwa jinsi gani Mkutano wa Elimu wa Wilaya unasaidia kuboresha shule • Kuelewa tofauti iliyopo kati ya mikutano ya Wilaya ya sasa na MEW

Wawezeshaji wameandaa:

Mahali pa kuweka kompyuta, projekta na skrini, na zana za kuunganishia umeme

Mpangilio mzuri wa ukumbi wa mafunzo ili washiriki wote waweze kuona vyema kwenye skrini

Karatasi za bango kitita za kutosha, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu

_________________________________________________________________________ Maelezo ya Kipindi 5. Uwasilishaji kwa kutumia “PowerPoint” (dakika 40) Kushirikishana malengo ya mafunzo na taarifa za mkutano wa majaribio wa MEW uliofanyika Mkoa wa Tabora. Tumia maswali na majibu kutoka kwa washiriki. 6. Kazi ya kikundi: Faida za Mkutano (dakika 20) Hakikisha kila kikundi kina karatasi ya bango kitita na kalamu rashasha. Wakumbushe washiriki kuwa wanapaswa kuchagua mtu mmoja ambaye atachukua maelezo na kuwasilisha waliyojadili wakati wa majumuisho.

Kuna manufaa gani kwa Wathibiti Ubora, Maafisa Elimu Kata na Maafisa wa Wilaya kukutana kila mwezi kujadili mbinu za kuinua ubora wa elimu katika Wilaya?

Kwa jinsi gani MEW unatofautiana na mikutano ya sasa?

7. Mrejesho wa wote (Uwasilishaji) (dakika 30)

Waombe washiriki wa kila kikundi wakwambie majibu yao (yasizidi majibu 2). Kisha endelea kwa mzunguuko huohuo mpaka wametoa majibu yao yote. Yaombe makundi yasirudie ambacho kimesemwa na kundi kingine.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

11

Andika mambo muhimu (siyo neno kwa neno) kutoka kwa washiriki kwenye bango kitita.

Faida za mikutano ya MEW: Mambo muhimu ya kusisitiza:

Uelewa wa pamoja kuhusu mchango wa kila mmoja na kushirikishana mawazo

Kufikia makubaliano ya kuchukua hatua za pamoja za kuboresha shule wilayani

Kuthamini na kujenga uwezo wa washiriki wote kwenye mkutano, hasa Maafisa Elimu Kata

Kushirikishana mafanikio na mawazo mapya

Kuboresha utendaji wa shule ni jukumu la pamoja!

Kipi cha tofauti kuhusu Mikutano ya Elimu ya Wilaya (MEW)? Mikutano ya Maafisa Elimu wa Wilaya na Maafisa Elimu Kata imelenga mambo mengi, yakiwemo yafuatayo:

Kazi za kiutawala kwa kuzingatia miongozo ya Wizara

Kuwataarifu wafanyakazi kuhusu nyaraka na maagizo ya Wizara

Kujadili kuhusu ufaulu wa wanafunzi

MEW ni chombo cha kusaidia kuboresha utendaji wa shule:

Mijadala inalenga njia za kuboresha elimu wilayani

Maamuzi yanatolewa kwa pamoja kama ‘jamii inayojifunza’

Ufumbuzi unapatikana, licha ya changamoto, kwa ushirikiano wa Maafisa Elimu Kata, Wathibiti Ubora na Maafisa Elimu kwa kufanya kazi pamoja

Jitihada na wajibu wa kuboresha shule vinafanywa kwa kushirikishana na kukubaliana, pamoja na ufuatiliaji

Ni fursa kwa Wathibiti Ubora na Maafisa Elimu ya kuwajengea uwezo wa kitaaluma Maafisa Elimu Kata.

Maafisa Elimu Kata wanabeba jukumu la kuhakikisha ufumbuzi unapatikana

8. Majumuisho ya Kipindi (dakika 15) Elezea kwa ufupi jinsi tunavyoiona mikutano ya MEW:

Kujenga uelewa wa pamoja na njia za kuinua viwango na ubora wa elimu katika wilaya:

o Kwa Wathibiti ubora wa Shule waweze kuchangia utaalamu wao, na Maafisa Elimu

Kata waweze kuwapa taarifa muhimu za shule katika wilaya zao.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

12

o Kwa Halmashauri kuweza kupokea taarifa za kuiwezesha kuandaa mipango yao kwa

ajili ya kusaidia, kufundisha na kuhamasisha shule kufanya vizuri, vile vile kuweka

vipaumbele kwenye mipango yao ya kuboresha na kugharamia elimu.

o Kwa kusaidia upatikanaji wa taarifa kati ya Wathibiti Ubora wa Shule, Maafisa Elimu wa

Wilaya na Maafisa Elimu Kata kuhusu shughuli zao za mwezi uliopita na na za mwezi

unaofuata.

Kufanya mapitio ya mikakati ya wilaya na kupata mrejesho kuhusu progamu mbalimbali

Kujikita kwenye masuala muhimu yanayoinua ubora wa elimu wilayani, kupanga shughuli

za mafunzo na kusaidia maendeeo ya shule kwa ujumla.

Kutoa fursa kwa Maafisa Elimu Kata, Wathibiti Ubora wa Shule na Maafisa Elimu

wengine ngazi ya wilaya kuwa na Mikutano “Jamii inayojifunza” ya kila mwezi, ili kupata

mawazo mapya na kutafuta njia za kutatua changamoto za uboreshaji wa maendeleo ya

shule.

MEW ni tofauti na mikutano mingine ya sasa:

• Katika ,MEW masuala pekee yanayojadiliwa yanayohusiana moja kwa moja na Uboreshaji

wa shule.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

13

Kipindi cha 3 Maandalizi na Kupanga Mkutano wa Elimu wa Wilaya

Muda: saa 1 na dakika 45 (dakika 105) Lengo la kipindi: Lengo la kipindi ni kuwapatia washiriki fursa ya kuelewa umuhimu wa kupanga na kuandaa Mkutano wa Elimu wa Wilaya. Matokeo ya kujifunza: Hadi mwisho wa kipindi hiki washiriki watakuwa na uwezo mkubwa wa:

Kujua kuhusu umuhimu wa kupanga na kuandaa Mkutano wa Elimu wa Wilaya

Kuelewa wajibu wa Kamati ya Maandalizi na jukumu la Mwakilishi wa Mkutano wa Elimu wa Wilaya

Kuelewa umuhimu wa kuwezesha na mbinu shirikishi

Kuangalia mipango mitatu iliyoandaliwa kwa ajili ya mikutano ya awali ya huko Tabora

Kubuni muundo wa Mkutano wa Elimu wa Wilaya Wawezeshaji waandae:

Nakala za viambatisho A, B, C, D na E kwa ajili ya washiriki wote

Idadi ya kutosha ya karatasi za bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu

______________________________________________________________________________ Maelezo ya Kipindi 9. Majukumu ya Timu ya Maandalizi na Wajibu wa Mwakilishi wa MEW (dakika 20) Soma na kupitia Majukumu ya Kamati ya Maandalizi na Wajibu wa Mwakilishi wa MEW Kiambatisho A: Elezea jukumu la Mwakilishi wa MEW kuwa ni mtu anayeratibu mkutano na mwenendo wa Kamati ya MEW. Mwakilishi wa MEW mara nyingi ni Afisa Elimu Taaluma / Afisa Elimu Vifaa na Takwimu na Afisa wa EQUIP-T kwa kuwa majadiliano mara nyingi hurejea mafunzo yaliyopita. Angalia ajenda na vifaa Soma na kupitia malengo makuu ya Mkutano

Hakikisha washiriki wanaelewa kuwa malengo makuu ya Kuandaa na Kupanga Mkutano wa Elimu wa Wilaya ni:

Wathibiti bora, Maafisa Elimu Kata na Maafisa Elimu kwa pamoja ni timu ya kuandaa mkutano

Kutazama mafanikio ya mkutano wa mwisho wa MEW na kushirikishana mawazo ambayo yaliyofanikiwa vizuri

Kuamua kwa pamoja ni hatua gani ambazo watachukua ili kuboresha

Kuangalia ni nini kinapaswa kufuatiliwa kutokana na mikutano ya awali

Kuandaa ajenda na mada kuu kwa ajili ya mkutano ujao

Kutafuta wawezeshaji na kuandaa mbinu shirikishi Kukutana kila mwezi

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

14

10. Kiolezo cha mkutano wa MEW kilichotumika Tabora (dakika 15) Soma na kushirikishana Kiolezo cha MEW kwa pamoja. Kiambatisho B Muda Tarehe na muda wa MEW unapangwa kulingana na ratiba ya wilaya husika. Katika baadhi ya wilaya tarehe za mwaka mzima zimekwishapangwa kabisa. Chakula/Chai Eleza kuwa chai inaweza inaweza kuwepo au kutokuwepo kulingana na bajeti ya wilaya husika na utoe mifano halisi kutoka mkoa wa Tabora. Wengine wanapata chai, wengine chakula cha mchana, kwa wengine ni soda na biskuti, na wengine hawapati kitu chochote. Kila Wilaya inapaswa kuzingatia na kuamua kuhusu chakula kulingana na bajeti yake. Hata hivyo, muda wa mkutano utategemea mipangilio na upatikanaji wa viburudisho. Uwezeshaji na Mbinu Shirikishi Uwezeshaji na Mbinu Shirikishi ni muhimu kwa jinsi MEW unavyofanya kazi. Ili majadiliano yafanikiwe tunahitaji kutumia masomo tuliyojifunza kutoka kwenye Mafunzo kuhusu Usimamizi wa Utendaji wa Shule (SPMM) kuhusu mawasiliano bora - kuwa ni mawasiliano shirikishi yanayozingatia tabia ya 'Twiga'. Taratibu nyingine Mpango unapaswa kuonesha nani atakayewezesha wakati wa kipindi na vifaa vinavyotakiwa. 11. Elezea kwa ufupi kupitia mipango ya sampuli ya MEW 1, 2 na 3 ya huko Tabora (dakika 10) Mpango wa 1 ni mkutano wa kwanza: Kutambulisha MEW na kuangalia faida zake Kiambatisho C Mpango wa 2 ni mapitio ya Mpango wa Maendeleo ya Shule Kiambatisho D Mpango wa 3 unaangalia taarifaza Maafisa Elimu Kata na Ziara za Shule Kiambatisho E & H

12. Kazi kubwa ya kikundi: Uwezeshaji wa Mkutano (dakika 30) Wagawanye washiriki katika makundi matatu: kundi la1 wafanye mapitio ya Mpango wa 1, kundi la 2 mapitio ya Mpango wa 2 na kundi la 3 mapitio ya Mpango wa 3. Hakikisha kila kundi lina karatasi ya bango kitita na kalamu rashasha. Yakumbushe makundi kwamba wanapaswa kuchagua mtu mmoja ambaye atachukua maelezo na kuwasilisha wakati wa majumuisho. Waambie washiriki wajadili kuhusu mkutano:

Njia gani zimetumika kuwezesha mkutano huu?

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

15

Ni nani anayehusika na kuongoza mkutano?

Ni faida gani kuu za mkutano huu? 13. Mrejesho wa wote na Mjadala (dakika 30) Kila kikundi kibandike bango kitita ukutani. Kisha waambie wasome.

Nini maoni yako?

Kuna kitu gani kingine cha ziada ambacho umekiona? Mwezeshaji sasa anaongoza majumuisho ya mrejesho kwa kusisitiza vipengele vifuatavyo

Vipengele muhimu vya kusisitiza: Mbinu za Uwezeshaji zilizotumika ni: Majadiliano, bungua bongo ya kikundi, mrejesho, igizo dhima, uchambuzi wa Mpango wa Maendeleo ya Shule, kwa kutumia vigezo vya pamoja Wajibu wa kuongoza mkutano Ni jukumu la pamoja. Katika mikutano ya baadaye Maafisa Elimu Kata watachukua nafasi ya utendaji katika mikutano. Faida za Mkutano

Uelewa wa pamoja wa michango kutoka kwa kila mtu na kushirikishana mawazo.

Kufikia makubaliano ya kuchukua hatua za pamoja za kuboresha shule wilayani

Kuthamini na kujenga uwezo wa washiriki wote katika mkutano hasa Maafisa Elimu Kata.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

16

Kipindi cha 4 Umuhimu wa Kujadalii mada na Mwongozo wa Mada za MEW kwa Mwaka Muda: saa 1 na dakika 45 (dakika 105) Malengo ya kipindi:

Kukuza uelewa wa wawashiriki kuhusu wigo na upana wa mikutano ya MEW kwa kuangalia mada za mwaka

Kukuza uelewa wa washiriki kuhusu changamoto zinazoweza kujitokeza kwenye kufikia elimu bora

Matokeo ya kujifunza: Mwisho wa kipindi washiriki wataweza:

Kuelewa umuhimu wa mada kwa kila MEW

kutoa orodha ya mada zitakazo endesha mikutano ya .MEW

Kupanga mpango wa kuwezesha mada moja

Wawezeshaji waandae:

Karatasi za bango kitita za kutosha, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu

Karatasi za bango kitita zilizo na maswali yaliyoandikwa kwa ajili ya kutafakari mada katika Kazi ya 17.

watu wa 2 wa kuhesabu kura wakati wa kupiga kura katika Kazi ya 18.

Nakala za Mwongozo wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Kiambatisho F

Mambo muhimu ya kusisitiza:

Mkutano una lengo la kuboresha maendeleo ya shule na kuinua viwango vya wanafunzi

Mkutano ni kwa ajili ya kuboresha uelewa wa maswala muhimu au mada ambazo zinahitaji ufafanuzi

Mkutano ni kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi na kujua nini cha kufanya

Mkutano unapaswa kusababisha maboresho ya kazi ya wadau wote Mada zilizochaguliwa inapaswa kuwa ni zile ambazo MEW unaweza kuzitekeleza na kupata matokeo chanya, hasa mada zinazolenga katika ufundishaji na ujifunzaji Jaribu kupata urari wa mada za mwaka ikiwa ni pamoja na: Jamii, Kufundisha na Kujifunza, Usimamizi wa Shule, Ufuatiliaji na Tathmini Mada zinaweza kurudiwa mara kadhaa katika miaka mingine. Mkutano sio kwa ajili ya kujadili masuala ya utawala au kuwafundisha Maafisa Elimu Kata. Majadiliano kuhusu piki piki, posho, miundombinu au ukosefu wa walimu sio mambo ambayo mkutano huu unaweza kuyabadilisha hivyo masuala haya inapaswa yasipewe nafasi ya kujadiliwa sana.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

17

14. Ni mada gani ambazo zinaweza kuingizwa katika MEW ? (Dakika 5)

Mwezeshaji anaanzisha somo kwa kugawana baadhi ya mada zilizochaguliwa kwenye mkutano wa MEW Mkoani Tabora:

• Kufanya kazi na walimu wakuu wenye changamoto • Kuelewa Mtaala Mpya • Kuboresha Mahudhurio ya Mwalimu Darasani • Uchambuzi wa ubora wa Mipango ya Maendeleo ya Shule • Uchambuzi wa ubora wa taarifa za Maafisa Elimu Kata na ziara za kutembelea shule

Mada zinapaswa:

Kupelekea maboresho kwa maendeleo bora ya shule na kuinua viwango vya wanafunzi

Kusaidia kupata ufumbuzi na kujua nini cha kufanya Mada hazipaswi:

Kuwa za masuala ya utawala na kutoa maelekezo kwa Maafisa Elimu Kata

Kuwa za kuhusu piki piki, posho, miundombinu au ukosefu wa walimu

15. Kazi ya vikundi: Andaa orodha ya Mada (dakika 15) Wagawe washiriki katika makundi 6 Hakikisha kila kundi lina karatasi za bango kitita na kalamu rashasha. Wakumbushe kwamba wanapaswa kuchagua mtu mmoja ambaye ataandika maelezo na kutoa mrejesho wakati wa majumuisho. Waambie washiriki waorodheshe mada ambazo zinaweza kufanyiwa kazi kwenye MEW Bandika mara moja orodha hizo ukutani na omba kila kikundi wasimame karibu na karatasi yao wakiwa na kalamu.

16. Mrejesgo wa wote kuhusu orodha ya mada (dakika 15)

Kikundi cha 1 watoe mrejesho na kama mada tajwa imerudiwa na vikundi vingine wanapaswa kuifuta. Kisha vikundi vingine watoe mrejesho wao pia.

17. Kazi ya mtu mmoja mmoja na vikundi vidogo; Kutafakari juu ya mada zilizotajwa (Dakika 30)

Mwezeshaji anasoma swali na kuelezea umuhimu wa kila mada katika kuchagua mada za MEW

Ni mada gani zinafaa zaidi?

Ni mada zipi zitaleta matokeo chanya zaidi katika ufundishaji na ujifunzaji?

Ni mada gani zina changamoto zaidi katika kuleta mabadiliko?

Ni mada zipi ambazo zitasababisha kupanda kwa viwango vya ufaulu shuleni?

Ni mada gani zinaweza kuchaguliwa ili kupata mada bora zaidi za mwaka?

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

18

Kila mtu anafikiria juu ya maswali haya na kuandika sababu za majibu yao (dakika 5) Kisha kujadili katika vikundi maoni yao na maelezo ya uchaguzi wao. (dakika 15) Mwezeshaji anaongoza majadiliano ya kundi zima (dakika 10):

Je, kuna kikundi chochote kilikubaliana juu ya maswali yoyote / majibu? Haishangazi kwa kikundi kutokubaliana maana hakuna majibu sahihi na wote tutakuwa na machaguo tofauti tofauti.

Je, kuna mtu yeyote amepata shida kuelewa au kujibu maswali yoyote?

Vipengele muhimu vya kusisitiza: Mkutano una lengo la kuboresha maendeleo ya shule na kuinua viwango vya wanafunzi Mkutano ni kwa ajili ya kuboresha uelewa wa masuala muhimu au mada ambazo zinahitaji ufafanuzi Mkutano ni kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi na kujua nini cha kufanya Mkutano unapaswa kusaidia maboresho ya kazi ya wadau wote Mada zilizochaguliwa inapaswa kuwa ambazo MEW inaweza kuzitekeleza na kupata matokeo chanya, hasa mada zinazolenga katika ufundishaji na ujifunzaji Jaribu kupata mada kwenye masuala tofuati tofauti za mwaka ikiwa ni pamoja na: Jamii, Kufundisha na Kujifunza, Usimamizi wa Shule, Ufuatiliaji na Tathmini Mada zinaweza kurudiwa mara kadhaa katika miaka mingine. Mkutano siyo kwa ajili ya kujadili masuala ya utawala au kuwafundisha Maafisa Elimu Kata. Majadiliano kuhusu piki piki, posho, miundombinu au ukosefu wa walimu sio mambo ambayo mkutano huu unaweza kuyabadilisha hivyo masuala haya inapaswa yasipewe nafasi ya kujadiliwa sana.

18. Kupiga kura kuchagua Mada 10 bora zaidi (dakika 20) Mwezeshaji anaelezea kuwa sasa tunakwenda kuchagua mada 10. Kila mtu anaweza kupiga kura mara 3 tu. "Unaweza kuchagua mada tatu tu za kupigia kura. Unaruhusiwa kupiga kura mara tatu tu. Nitasoma orodha ya mada. Katika kila mada wale wanaotaka kuipigia kura mada hiyo wanaweza kuinua mikono yao juu na wenzangu watahesabu jumla ya kura hizo." Soma orodha na kuwaomba washiriki wanaochagua wainue mikono kila wakati na uandike kwa kila mada jumla ya kura zilizohesabiwa kwa mada hiyo. Endelea kufanya hivyo kwa haraka ili zoezi hili lisichoshe.

Baada ya kupiga kura, weka alama ya nyota kwenye mada 10 zenye kura nyingi zaidi. Mwezeshaji anawauliza washiriki "je zoezi hili limetupa orodha nzuri ya mada za mwaka mmoja? Je, kuna mada zinazohusu: • Jamii • Kufundisha na Kujifunza • Uongozi na Usimamizi • Ufuatiliaji na Tathmini? "

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

19

19. Kushirikishana Mwongozo wa Mwaka (dakika 10) Kazi ya kupiga kura kuchagua mada ilikamilishwa katika DEM nyingi huko Tabora. Maafisa Elimu Kata, Maafisa Elimu na Wathibiti Ubora walipiga kura na kuamua mada za mwaka nzima. Mada hizo ndizo zilizoandikwa kwenye Mwongozo. Mwongozo huu ni mojawapo kati ya miongozo ya kutumia. Kusoma na kushirikishana Mwongozo wa Wilaya ya Nzega. Kiambatisho F Je, kuna usawa mada za mwaka?

Jamii

Kufundisha na Kujifunza

Uongozi na Usimamizi

Mafunzo Mada zitarudiwa mara kadhaa kwa miaka mingi ijayo ili kuimarisha, kuboresha na ili kuwasaidia wadau wapya. 20. Majumuisho ya huhitimisha Siku (dakika 5) "Leo tumeangalia kuhusu MEW, malengo ya Mkutano na upangaji mipango kwa ajili ya MEWna Kuandaa Mwongozo wa Mada za mwaka. Kesho tunatakiwa kufika hapa saa 1.30 asubuhi kujisajili na saa 02.00 tutaanza kipindi. Tutaangalia juu ya kuendeleza utaalamu wa Maafisa Elimu Kata na kufanya maandalizi kwa ajili ya MEW katika Mkoa huu." Maliza kwa Wimbo Kabla ya kuondoka hakikisha endapo kila Wilaya imeleta mifano 5 ya ripoti za Maafisa Elimu Kata kutoka katika Wilaya yao.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

20

Siku ya 2: Kuandaa na kutekeleza mkutano wa MEW

Muda Kazi Mbinu na Maudhui Zana

02:00-3:45

Kipindi cha 5 Matarajio ya Maafisa Elimu Kata na kujenga uwezo wao wa kitaaluma

21. Utangulizi na ufupisho wa mada za siku ya 1 22. Wajibu wa Maafisa Elimu Kata 23. Kujenga uwezo wa Maafisa Elimu Kata 24. Matembezi kuona majibu na Mrejesho 25. Uhusiano wa kazi za Maafisa Elimu Kata na Wathibiti Ubora wa shule

Karatasi za bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu Mpira Yaliyoandikwa kwa ajili ya Kazi ya 23 Ufafanuzi wa Kazi ya Afisa Elimu Kata-Kiambatisho G

03:45-04:15

04:15-06:00

Kipindi cha 6 Ufuatiliaji, Msaada, na Mapitio ya Mkutano wa Elimu wa Wilaya

26. Kuchangamshana na tafakari 27. Ufuatiliaji, Msaada na mrejesho wa MEW 28. Mjadala wa wote 29. Taarifa za Maafisa Elimu Kata 30. Kushirikishana taarifa bora zaidi za Maafisa Elimu Kata.

Karatasi za bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu Kadi kubwa yenye namba 0, 5 & 10. Ripoti ya 5 za Maafisa Elimu Kata kutoka kila Wilaya Nakala iliyoandikwa kwa vikundi 3 kwa ajili ya Kazi ya 27 Nakala za Kiambatisho E & H Orodha ya Machaguo ya lazima

06:00-07:00

07:00-08:45

Kipindi cha7 Kupanga Mkutano wa Elimu wa Wilaya

31. Utangulizi 32. Kupanga na kuandaa Mkutano wa MEW 33. Mjadala wa wote 34. Maswali na Majibu, hitimisho

Karatasi za bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu Nakala za kiolezo cha MEW Kiambatisho A Orodha ya Mada kutoka Kipindi cha 4

08:45-09:15

09:15-11:00

Kipindi cha 8 Kutatokea nini baada ya mafunzo? Kuhitimisha

35. Ufupisho wa mada za MEW 36. Maswali na Majibu, Hitimisho 37. Nini cha kufanya baada ya mafunzo? 38. Muhtasari wa siku 2 za mafunzo 39. Maneno ya kuhitimisha na kuagana

Miongozo ya mikutano ya kila wiki ya Walimu wakuu, nakala moja kwa kila mshiriki Fomu za Tathmini Nakala na Chati ya Kazi ya 37

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

21

Kipindi cha 5 Matarajio ya Maafisa Elimu Kata na kujenga uwezo wao wa kitaaluma

Muda: saa 1 na dakika 45 (dakika 105)

Malengo ya kipindi:

Kuinua uelewa na umuhimu wa MEW wa kuongeza uwezo wa kitaaluma wa Maafisa Elimu Kata

Kuamsha ujuzi wa washiriki kuhusu Wajibu wa Maafisa Elimu Kata

Kuonyesha uhusiano uliopo kati ya kazi za Maafisa Elimu Kata na Wathibi Ubora

Matokeo ya kujifunza: Hadi mwisho wa kipindi hiki washiriki wataweza:

Kueleza matokeo chanya ambayo Maafisa Elimu Kata wanaweza kuchangia katika kuinua viwango vya shule

Kueleza jinsi MEW unaweza kuwasaidia Maafisa Elimu Kata kuboresha utendaji wao

Kueleza uhusiano na mwingiliano uliopo kati ya kazi ya Maafisa Elimu Kata na Wathibiti Ubora

Wawezeshaji waandae: Mpira wa kutumia kuchangamsha mwili

Swali kuhusu kazi ya Maafisa Elimu Kata katika Kazi ya 23 litakuwa tayari limeandikwa kwenye karatasi ya bango kitita

Nakala za kutosha za Maelezo ya majukumu ya Maafisa Elimu Kata - Kiambatisho G

Mabango kitita na kalamu rashasha

_____________________________________________________________________________ Maelezo ya Kipindi 21. Utangulizi na Muhtasari wa Siku ya 1 (dakika 10) Anza siku na wimbo kwa kuwaomba washiriki wasimame kwa jinsi ya mduara. Rusha mpira kwenye mduara ili warushiane wao kwa wao. Kila anayedaka mpira anajitambulisha na kusema anachokumbuka kuhusu mafunzo ya jana. 22. Majukumu ya Maafisa Elimu Kata (dakika 15) Waombe washiriki waketi katika vikundi. Waambie washiriki kuwa asubuhi hii watatazama kuhusu majukumu ya Mafisa Elimu Kata na jinsi mkutano wa MEW unaweza kujenga uwezo wao wa kitaaluma. Maafisa Elimu Kata ni wasaidizi kwanza wa shule, na hivyo wanaweza kuleta matokeo muhimu sana kwenye maendeleo ya shule. Kwa haraka soma maelezo ya kazi ya Maafisa Elimu Kata Kiambatisho G

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

22

23. Kujenga uwezo wa Maafisa Elimu Kata (dakika 25)

Hakikisha kila kikundi kina karatasi ya bango kitita na kalamu rashasha. Wakumbushe kwamba wanapaswa kuchagua mtu mmoja ambaye atachukua maelezo ya majadiliano yao na kutoa mrejesho wakati wa majumuisho.

Ni uboreshaji gani wa kitaaluma tunaotaka kuboresha utendaji wa Maafisa Elimu Kata?

Ni kwa jinsi gani Maafisa Elimu Kata wanaweza kuinua viwango vya shule?

Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia Maafisa Elimu Kata kuboresha utendaji wao?

Toa mifano ya Maafisa Elimu Kata wanaofanya kazi vizuri ambao wanaweza kushirikishana uzoefu wao na wengine 24. Kuzunguka kuona kazi na mrejesho (dakika 40) Waombe washiriki wabandike karatasi zao ukutani. Wapatie dakika kumi za kila mshiriki kutembea tembea ili kusoma kazi za vikundi vingine. Wahimize washiriki kuandika maoni / maswali yoyote waliyo nayo, au nyongeza yoyote wanayopenda kuongeza.

Baada ya dakika kumi, endesha mjadala wa majumuisho juu ya masuala ambayo wameibua kwa ajili ya MEW na kwa nini hayo. Wapeni washiriki fursa ya kuuliza maswali yao nk. Andika mambo muhimu kwenye bango kitita. Sisitiza kuwa kwa mikutano ya MEW, masuala yanayoibuliwa yanapaswa kuwa yanahusiana na yale ambayo Maafisa Elimu Kata wanaweza kufanya ili kuboresha utendaji wao au masuala ambayo Maafisa Elimu Kata wanaweza kushawishi kwa namna isiyo ya moja kwa moja.

25. Uhusiano uliopo kati ya kazi ya Maafisa Elimu Kata na Wathibiti Ubora (dakika 15) Elezea Imezoeleka Wathibiti wa Ubora wamekuwa wakifahamika kama Wakaguzi wa Shule na jukumu lao kuu ilikuwa ni kufanya ukaguzi wa shule, jukumu ambalo kimsingi linabeba dhana ya kuhukumu au kukosoa. Hili lilifuatiwa na utoaji wa mrejesho wa papo kwa papo na taarifa ya maandishi. Hata hivyo, kutokana na mabadiliko yanayoendelea katika Idara ya Ukaguzi, kwa sasa Wakaguzi wanafahamika kama Wathibiti Ubora wa shule. Wakaguzi wa Shule sasa ni Wasimamizi wa Shule wa nje. Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inaandaa mwongozo mpya wa Uthibiti Ubora wa Shule unaompa majukumu mengi zaidi Afisa Elimu Kata kama Afisa kwenye ngazi ya kata. Majukumu makuu ya Maafisa Elimu kata ni: - (i) Kumshauri Afisa Mthibiti Ubora wa elimu wa Wilaya kuhusu ubora wa elimu katika kata (ii) Kusaidia na kufanya mapitio ya Mpango wa Maendeleo ya Shule, na mchakato wa Tathmini ya ndani ya Shule na utekelezaji wake (iii) Kumwezesha mwalimu mkuu kama msimamizi wa ndani katika shule husika Uthibiti Ubora wa Ndani Mwalimu Mkuu anatarajiwa kuwa msimamizi wa ndani wa shule. Mwalimu mkuu anawajibika kuandaa Tathmini ya ndani ya Shule inayo tazama kwa kina masuala ya shule ili kuboresha zaidi hali ya utendaji wa

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

23

shule. Imekuwa ni jambo muhimu sana kwa sasa kukubali na kuhamasisha kufanyika kwa Tathmini ya ndani ya Shule kama njia muhimu ya kuinua viwango vya mafanikio shuleni. Jambo hili linaenda sambamba na mchakato wa Mpango wa Maendeleo ya Shule na Kikao cha Jamii inayojifunza cha kila wiki. Afisa Elimu Kata atahakikisha haya yote yanatekelezwa.

English Swahili QA led with support from WEO Mthibiti Ubora anaongoza akisaidiwa na Afisa Elimu Kata Follow up WEO and School Community Ufuatiliaji wa Afisa Elimu Kata na Jumuiya ya Shule Input from WEO and School Community

Mchango kutoka kwa Afisa Elimu Kata na Jumuiya ya Shule

Periodic Quality Assurance inspection of school

Uthibiti ubora wa mara kwa mara wa ukaguzi wa shule

Monthly review of progress against plan and amendments

Mapitio ya kila mwezi kuangalia maendeleo dhidi ya mpango na kufanya marekebisho

Implementation of plan Utekelezaji wa Mpango School Development Plan-based on self assessment and previous QA reports

Mpango wa Maendeleo ya Shule – Kutokana na tathmini ya ndani ya shule na ripoti za nyuma za Uthibiti Ubora

School self assessment Tathmini ya ndani ya shule Mchakato wa Nje wa Uthibiti Ubora Afisa Elimu Kata anatoa usimamizi wa nje wa mara kwa mara karibu mara mbili au zaidi kwa mwezi. Afisa Elimu Kata humsaidia mwalimu mkuu katika kufanya mapitio ya ndani, na anaweza kumsaidia kufanya maandalizi ya taarifa ya maandishi kwa ajili ya maandalizi ya ukaguzi. Afisa Elimu Kata pia anajukumu la kumsaidia Afisa Mthibiti Ubora wa Wilaya anayehusika na masuala ya Uthibiti Ubora wa shule kwenye kata yake.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

24

English Swahili Report to region/zone/national Taarifa kwenda mkoani/kanda/Taifa QA able to prioritise follow up on the most necessary cases

Mthibiti Ubora anaweza kuweka vipaumbele kufuatilia masuala ambayo ni ya muhimu zaidi

Annual/biannual Quality Assurance Visit to School and report

Ziara za kutembelea shule kwa mwaka/kila nusu mwaka za Uthibiti Ubora na kuandaa taarifa

Monthly WEO/QA (LGA) discussion of progress

Majadiliano ya maendeleo ya kila mwezi ya Afisa Elimu Kata/Mthibiti Ubora/ Afisa Elimu

Monthly WEO follow up at school level-support implementation of improvements

Ufuatiliaji wa kila mwezi wa Afisa Elimu Kata katika ngazi ya Shule-Kusaidia utekelezaji wa maboresho

Mfano wa mabadiliko ambayo yanatokea sasa Waratibu Elimu Kata wawili hadi watatu wamekuwa wakiungana na kushirikiana kutembelea shule zao na kukusanya taaarifa katika mambo muhimu yanayohusu uboreshaji wa shule. Wamekusanya matokeo ya ziara zao zote na kuyawasilisha kwenye mkutano wa Elimu wa wilaya(MEW), wakionesha maeneo mbalimbali yanayohitaji maboresho. Maeneo haya yaliunda mwongozo wa mada kwa ajili ya mikutano yao ya MEW ya miezi ijayo, kwa msaada maalum uliotolewa na Wathibiti Ubora.

Mambo yatakayoathiri majukumu na utendaji wa Mratibu Elimu Kata siku zijazo: Mfumo wa ukaguzi unabadilika na kuwa wa kimaendeleo zaidi

Shule zinatakiwa kukamilisha tathmini ya ndani ya maendeleo ya shule na hatua zinazochukuliwa kwa ajili ya maboresho ya shule.

Maafisa Elimu Kata wanatakiwa kumsaidia Mwalimu Mkuu kujitathmini na kuisaidia shule kujiandaa na ukaguzi.

Maafisa Elimu Kata na Wathibiti Ubora wanatakiwa kufanya kazi kwa ukaribu ili kujiridhisha na mchakato wa tathmini ya ndani na namna inavyoendana na ukaguzi.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

25

Kipindi cha 6 Msaada wa Ufuatiliaji na Mapitio ya mikutano ya MEW

Muda saa 1 na dakika 45 (dakika 105)

Malengo ya kipindi:

Kukuza uelewa wa washiriki kuhusu umuhimu wa kufuatilia na kuunga mkono MEW.

Kukuza uelewa wa washiriki kuhusu umuhimu wa kuchunguza na kufuatilia matokeo ya mikutano hii.

Ili kukubaliana juu ya mifumo ya kufanya hili.

Kufahamu umuhimu wa ripoti ya Maafisa Elimu Kata. Matokeo ya kujifunza: Hadi mwisho wa kipindi washiriki wataweza:

Kueleza jinsi ya kuunga mkono MEW

Kueleza mfumo wa kufuatilia mikutano

Kuhimiza maboresho ya ripoti ya Afisa Elimu Kata

Wawezeshaji waandae: Namba O, 5 na 10 kwa ajili ya zoezi la Machaguo ya lazima. Weka 0 na 10 mwisho wa

chumba na 5 katikati. Unataka watu wasikie maoni na maelezo ya wengine, hivyo ruhusu hii kwa umbali kati ya 0 hadi 10.

Orodha ya Machaguo ya lazima kwa ajili ya kazi ya 26

Hakikisha Maafisa wote wa Wilaya wanakuwa na ripoti zao 5 za Maafisa Elimu Kata.

Kadi 3 zilizoandaliwa hapo awali kwa ajili ya makundi 3 kwenye kazi ya 27

Nakala za Kiambatisho E-Mpango wa MEW na Kiambatisho H-Ziara za Maafisa Elimu Kata na Uandishi wa Ripoti.

Nakala of Annex J Majukumu na Taratibu za utoaji taarifa mkutano wa Elimu wa Mkoa na Wilaya

Mambo muhimu ya kusisitiza: Kwamba msaada utahitajika mwanzoni hasa kutoka EQUIP -T na kwa Afisa Elimu Wilaya Kwamba ripoti ya Afisa Elimu Kata ni muhimu. Rejea kwenye Kiambatisho E-Mpango wa MEW na Kiambatisho H-Ziara za Maafisa Elimu Kata na Uandishi wa Ripoti Washiriki wanajua nini cha kufanya baada ya mkutano kwa ajili ya kusaidia na kufuatilia MEW

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

26

26. Zoezi la Machaguo ya Lazima (dakika 15)

Sifuri upande mmoja hadi 10 upande mwingine, 5 iwe katikati. Eleza kwamba utasoma sentensi/kauli na wanapaswa wajiweka kwenye mstari kutoka 0 hadi 10 kulingana na jinsi wanavyokubaliana au hawakubaliana na sentensi/kauli hiyo. 10 ina maana ya kukubaliana kabisa 0 inamaanisha hawakubaliani kabisa Basi utaisoma sentensi/kauli ya kwanza na baada ya washiriki kuwa wamesimama kwenye nafasi zao waombe baadhi yao waeleze sababu yao ya kuchagua nafasi hiyo katika chumba. Wakati mwingine unaweza kuwauliza ikiwa wanataka kubadilisha msimamo wao kwa sasa baada ya kuwa wamesikia maelezo kutoka kwa wengine. Baada ya majadiliano mafupi, endelea na sentensi/kauli inayofuata. Sentensi/Kauli • Tanzania inatoa elimu bure • Elimu katika mkoa imeboreshwa kwa wanafunzi wengi zaidi • Nadhani MEW itakuwa muhimu • Nadhani MEW inapaswa kuwa ya lazima • Nadhani MEW inapaswa kufanyika kila mwezi, bila kujali chochote kinachoendelea • Nadhani MEW inapaswa kuingizwa inapofaa kufanya hivyo • Nadhani kuna manufaa yatokanayo na MEW kwa kila mtu • Nadhani Maafisa Elimu Kata watafaidika na MEW • Nadhani Wilaya inaweza kutoa fedha kugharamia vifaa vya MEW • Nadhani Wilaya inaweza kutoa fedha kwa ajili ya chakula wakati wa MEW

27. Msaada wa Ufuatiliaji na Mrejesho (dakika 25)

Utangulizi Mwezeshaji anaelezea haja ya kupata msaada kiasi fulani. Kutokana na uzoefu wetu huko Tabora, MEW, kama ilivyo katika programu nyingine nyingi, inahitaji msaada.

Mikutano bora ya MEW ni ile ambayo Afisa Elimu wa Wilaya anahuhudhuria baadhi au sehemu ya mikutano hiyo

Kutoa msaada kwa Kamati ya Mipango

Kuhamasisha mikutano ifanyike

Kusaidia na kushirikisha taarifa

Kuchukua malalamiko kama vile mabadiliko ya mjumbe muhimu wa Kamati ya Mipango ya MEW

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

27

Mwezeshaji ataelezea haja ya kupata Mrejesho kutoka MEW

Kuna haja ya kushirikishana maswala mbalimbali na maamuzi yaliyotolewa katika Mkutano wa MEW

Kuna haja ya kujua ya mafanikio na changamoto za MEW

Kuna haja kwa wengine kuelewa na kuchangia kikamilifu kwenye MEW.

Kazi ya Kikundi Wagawe washiriki katika vikundi 3. Hakikisha makundi yana idadi sawa ya washiriki, lakini

Kikundi cha 1 ni cha wafanyakazi wote wa Mkoa na Kanda pamoja na washiriki wengine

Kikundi cha 2 ni Afisa Elimu Wilaya na ADQA na washiriki wengine

Kikundi cha 3 ni wafanyakazi wote wa EQUIP-T na washiriki wengine Hakikisha kila kikundi kina karatasi ya bango kitita na kalamu rashasha. Wakumbushe kwamba wanapaswa kuchagua mtu mmoja ambaye ataandika maelezo na kutoa mrejesho wakati wa majumuisho. Kila kikundi kina orodha yake ya maswali kulingana na uhusika wao.

Kundi la 1 Wote ni wafanyakazi wa Kanda na Mkoa pamoja na washiriki wengine.

Ni taarifa gani Afisa Elimu wa Mkoa na Wafanyakazi wa kanda wanahitaji kutoka MEW?

Ni mabadiliko gani Afisa Elimu wa Mkoa na Wafanyakazi wa kanda wanatarajia kutokana

na mikutano hii?

Watajuaje kuhusu maendeleo na majadiliano ya Maafisa Elimu Kata?

Watajuaje kuhusu mafanikio na changamoto?

Wanaisaidiaje Halmashauri kuwajibika kwenye mikutano na mrejesho wa taarifa ya

Maafisa Elimu Kata?

Ni msaada gani Wathibiti Ubora na Halmashauri wanahitaji kutoka kwa Maafisa wa mkoa

na kanda ili kuendeleza mikutano hii?

Ni msaada gani unaweza kutolewa ili kufanikisha mikutano hii?

Kundi la 2 Linajumuisha Maafisa Elimu, na Wadhibiti Ubora wa Wilaya pamoja na washiriki wengine.

Ni taarifa zipi Afisa Elimu Wilaya na Mthibiti Ubora wanahitaji kutoka kwenye mikutano

hii?

Ni mabadiliko gani Afisa Elimu Wilaya na Mthibiti Ubora wanatarajia kutokana na

mikutano hii?

Watajuaje kuhusu maendeleo na majadiliano ya Elimu Kata?

Watajuaje kuhusu mafanikio na changamoto?

Wanasaidiaje kuhakikisha kuna ushiriki mzuri kwenye mikutano na kutoa mrejesho wa

taarifa za Maafisa Elimu Kata?

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

28

Ni msaada gani Wafanyakazi wa Mkoa na Kanda wanahitaji kutoka kwa Wathibiti Ubora

na Halmashauri ili kuendeleza mikutano hii?

Ni msaada gani unaweza kutolewa ili kufanikisha mikutano hii?

Kundi la 3 Linajumuisha wafanyakazi wa EQUIP-T na washiriki wengine

Ni taarifa zipi EQUIP-T inazihitaji kutoka kwenye mikutano hii?

Ni mabadiliko gani wafanyakazi wa EQUIP-T wanatarajia kutokana na mikutano hii?

Watajuaje kuhusu maendeleo na majadiliano ya Maafisa Elimu Kata?

Watajuaje kuhusu mafanikio na changamoto?

Wanaisaidiaje kupata mrejesho wa ripoti za mikutano ya MEW na ya Maafisa Elimu Kata?

Ni msaada gani unaweza kutolewa ili kuendeleza mikutano hii?

28. Majumuisho (dakika 30) Vikundi vitatu vinatoa mrejesho kimoja kimoja na kufafanua pointi zilizopatikana. Mwendeshaji anapaswa kuuliza mwishoni:

Je, kuna uwiano kati ya vikundi hivi 3 kwa taarifa na mrejesho?

Ikiwa jibu ni hapana, je, tofauti zilizopo zinaweza kutatuliwa?

Je, kuna masuala mengine zaidi ya kuzingatiwa?

Fafanua ili kwamba washiriki wote wajue nini cha kufanya baada ya mkutano kwa ajili kusaidia na kufuatilia MEW.

Afisa Elimu Mkoa, Kanda, Afisa Mthibiti Ubora na Afisa Elimu wa Wilaya wanatakiwa

kuonesha dhamira na utayari wao kwenye MEW:

Kuwaonesha Maafisa Elimu Kata na Wawezeshaji kwamba MEW inathaminiwa

Kuwapa msaada Kamati ya Mipango

Kuhamasisha mikutano ifanyike

Kuunga mkono na kushirikishana taarifa mbalimbali

Kuchukua na kuyafanyia kazi mambo yaliyoibuliwa kwenye mkutano

Kusaidia mabadiliko ya kubadili mjumbe muhimu wa Kamati ya Mipango ya MEW

Kuweka wazi mambo mbalimbali na maamuzi yaliyofanyika wakati wa MEW kwa maendeleo ya Wilaya

Kujua mafanikio na changamo za MEW

Kushiriki mara kwa mara na kutoa mchango stahiki kwenye MEW

Kwa kusoma taarifa ya Afisa Elimu Kata, kuielewa na kutoa msaada kwa Maafisa Elimu Kata na Kata zao

Kusoma yatokanayo na MEW Kutoa mrejesho na taarifa muhimu

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

29

29. Ripoti za Afisa Elimu Kata (dakika 20) Mwezeshaji awaombe washiriki waketi katika vikundi vya Kiwilaya.

"Mtakuwa katika makundi haya kwa siku nzima ya leo, hivyo jipangeni ili mkae vizuri."

Utangulizi

Mwezeshaji anafafanua kuwa, Ripoti ya Afisa Elimu Kata ni muhimu sana kwa sababu inatoa

mrejesho kuhusu shule.

Kila wilaya imeleta ripoti 5 za mfano ambazo tutakwenda kuzipitia na mwishoni tutachukua

ripoti iliyo bora zaidi.

30. Kushirikishana Ripoti bora zaidi ya Afisa Elimu Kata (dakika 15)

Kwa ufupi kila kikundi kinashirikisha ripoti bora zaidi waliyoichagua na kuelezea kwa nini wameichagua. Mwezeshaji anaweka pamoja mawazo ya jumla.

Taarifa nzuri itaeleza yafuatayo Ni sababu zipi zimekufanya kutembelea hilo eneo Ni maamuzi gani mmeyafanya kutokana na mabadiliko Katika ufuatiliaji wenu ni vitu gani vinahitajika ili kuweza kuboreshaji

Onyesha kwamba wanaweza kutumia Kiambatisho E - Mpango wa MEW kwa ajili ya Kuboresha

Ziara za kutembelea Shule za Afisa Elimu Kata na Taarifa za Maandishi kwa msaada wa

Kiambatisho H.

Washukuru maafisa kwa kuleta ripoti za Maafisa Elimu Kata kwa ajili ya kipindi hiki.

Maafisa Elimu Kata wanapaswa kupata mrejesho mwezi kuhusu ubora a wa ripoti zao na juu ya ufuatiliaji wa maendeleo ya maboresho ya shule yaliyofikiwa tangu ripoti ya itolewe.

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

30

Kipindi cha 7 Uandaaji wa Mkutano wa Elimu wa Wilaya Muda: saa 1 na dakika 45 (dakika 105) Lengo la kipindi: Kutoa fursa kwa washiriki ya kujizoeza kuandaa mpango na kuandaa MEW. Matokeo ya kujifunza: Hadi mwisho wa kipindi washiriki watakuwa na uwezo wa: • Kuthamini kamba wanafanya kazi kama timu ya kuandaa na kupanga mpango wa MEW • Kutengeneza mpango wao wenyewe Wawezeshaji wameandaa: • Karatasi za bango kitita zenye orodha ya mada kutoka Siku ya kwanza • Kiolezo cha Mpango wa MEW (Kiambatisho C) • Idadi ya kutosha ya karatasi za bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu

____________________________________________________________________________ Maelezo ya Kipindi 31. Utangulizi (dakika 15) Anza na wimbo au changamsha mwili Mwezeshaji anafafanua kwamba watakwenda kubungua bongo kwa kuhusu ajenda za Mkutano wa Maandalizi ya MEW. Kamati ya Mipango Kamati ya mipango inakutana kupanga mikutano ya MEW

Afisa Mwakilishi wa MEW-ndiyo Mwenyekiti. Wajumbe ni: Afisa Elimu Wilaya, Afisa Elimu Watu wazima / Afisa Elimu Takwimu wanaohusika na EQUIP-T au Maafisa wengine. Wawakilishi wawili wa Wathibiti Ubora Maafisa Elimu Kata 2

Agenda

Kuamua na kupitisha mada

Kufuatilia jambo lolote muhimu lililojitokeza katika mkutano uliopita

Kuhakikisha uwezeshaji wa mada utakaohusisha njia shirikishi unaandaliwa

Kukubaliana nani atakuwa Mwezeshaji kwa kila sehemu ya mkutano

Kupanga vifaa vitakavyotumika

Kupanga na kuandaa ukumbi

Kuandaa mpangilio wa ukaaji

Kupanga kuhusu chai/chakula cha mchana kama bajeti inaruhusu

Kuweka wazi majukumu ya kila mhusika kwa ajili ya MEW ijao

Kuchagua mtu atakayeandika yatokanayo na mkutano na kuwasambazia wengine

Kuchagua mtu atakaye wataarifu Maafisa Elimu Kata, Wathibiti Ubora, na Maafisa wengine kuhusu tarehe na muda wa mkutano

nye karatasi nyingine tofauti bungua bongo kuhusu mbinu za uwezeshaji: Tafakuri

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

31

Bungua bongo

Igizo dhima

Fikiri, jozisha, shirikisha

Mijadala ya vikundi na mrejesho

Maswali na Majibu

Mambo muhimu Kupanga tarehe na muda wa mkutano. Ikiwezekana pangeni haya mwanzoni mwa kila mwaka. Kwa mfano, Ijumaa ya kwanza ya mwezi Kuwepo ukumbini kuwakaribisha wengine wanapofika

32. Maandalizi na Kupanga Mipango ya MEW (dakika 40)

Washiriki watafanya kazi katika vikundi vya Wilaya. Waombe washiriki kuchagua watu watakaoshika nafasi hizi:

• Afisa Mwakilishi wa MEW ambaye atakuwa Mwenyekiti • Afisa Elimu Taaluma / Afisa Elimu Vifaa na Takwimu anayehusika na EQUIP-T • Wathibiti Ubora • Maafisa Elimu Kata 2

Eleza kuwa sasa wana Mkutano wa Mipango na Maandalizi ya MEW.

Kwa hiyo watapanga MEW wa mwezi ujao.

Watahitaji kuchagua mada kutoka kwenye orodha ya mada zilizochaguliwa jana.

Wanahitaji kuhakikisha kwamba wanatumia mbinu shirikishi za uwezeshaji

Watahitaji kuhakikisha wamekamilisha vipengele vyote vilivyoorodheshwa kwenye ajenda

Kiolezo cha MEW Kiambatisho B kinaweza kuwa cha msaada

33. Majumuisho ya majadiliano (dakika 40) Waombe washiriki kushirikishana mipango yao, hasa maelezo ya kina ya uwezeshaji wa mada, kundi moja baada ya jingine. 34.Maswali na majibu, kuhitimisha (dakika 10) Waulize washiriki wana maswali gani au wasiwasi wao kuhusu kujiandaa kwa ajili ya Mkutano wa .

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

32

Kipindi cha 8 Nini kitafuata baada ya mafunzo?

Muda: Saa 1 na dakika 45 (dakika 105) Malengo ya kipindi.

Kutoa fursa kwa washiriki kufikiri, kushirikishana na kutoa mawazo yao juu ya jinsi ya kuanzisha mikutano ya MEW kwenye Wilaya zao.

Kukubaliana mpangokazi kwa ajili ya kuanzisha MEW watakaporudi kwenye Wilaya zao. Matokeo ya kujifunza: Hadi mwishoni mwa kipindi washiriki watakuwa na mpango unaoonyesha nini cha kufanya baada ya mafunzo na ambao unaweza kuwasaidia kupata msaada inapobidi.

Wawezeshaji waandae: • Fomu ya tathmini, fomu moja kwa kila mshiriki • Idadi ya kutosha ya karatasi za bango kitita, kalamu rashasha, gundi utepe, karatasi za A4, na kalamu ______________________________________________________________________________ Maelezo ya Kipindi 35. Muhtasari wa Majumuisho ya MEW; kazi ya kikundi (dakika 25) Waombe washiriki kujadili katika vikundi yale waliyojifunza kuhusu "lini", "kwa muda gani", "madhumuni ya MEW", "jukumu la timu", "taratibu za MEW", "umuhimu wa Mada na uwezeshaji wake "na" jukumu la mwakilishi wa MEW" kuhusiana na MEW. 36. Maswali na Majibu, Kufunga (dakika 15) Washiriki wana nafasi ya kuuliza maswali mengine zaidi 37. Kupanga "nini cha kufanya baada ya mafunzo" Kimabatisho I (dakika 45) Waambie washiriki kwamba wataanza kuandaa MEW baada ya kurudi katika Wilaya zao. Wataanza pia kufuatilia kuhusu MEW. Wakiwa katika vikundi vya Wilaya wajadili: • Tunakwenda kufanya nini sasa, baada ya mafunzo haya? • Je, ni ujuzi gani na zana zipi tutakazotumia? • Tukiwa na shida yoyote katika kuandaa au kuwezesha MEW, ni nani tunaweza kumuomba msaada? • Tutaanza lini MEW katika Wilaya yetu? • Tukiwa na matatizo katika kufuatilia MEW, ni nani tunaweza kumuomba msaada?

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

33

Baada ya

mafunzo haya

nini tunapaswa

kufanya?

Tutafanya nini

na wakati gani?

Tutajiandaaje na

kuendeshaje

MEW? Zana zipi

tutatumia?

Tunatakiwa

kufanya nini

baada ya MEW,

kusaidia na

kufuatilia?

Nani

atatusaidia?

Wataarifu

Maafisa Elimu

Kata kuhusu

MEW

Mkubaliane

tarehe na muda

38. Muhtasari wa mada za siku 2 (dakika 15) Jumuisha kwa ufupi siku 2 za mafunzo, sisitiza kuwa mikutano ya MEW ni zana za usimamizi wa Wilaya za kuboresha shule. Waulize washiriki wanajisikiaje kwa sasa ikilinganishwa na siku ya kwanza? Hitimisha kwa kupokea maswali yoyote ambayo washiriki wanaweza kuwa nayo. Waulize kama kuna maswali yoyote, ufafanuzi, malalamiko, au changamoto nyingine ambazo wangependa kuuliza au kushirikishana. Washukuru washiriki wote kwa michango yao na kuwatakia kila la heri katika kuanzisha na kuwezesha mikutano ya MEW na ufuatiliaji, na mawasiliano yenye ufanisi. Usisahau kuwapa washiriki fomu ya tathmini ili wajaze 39. Maneno ya kuhitimisha na kuagana (dakika 10)

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

34

VIAMBATISHO

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

35

KIAMBATISHO A Majukumu ya Kamati ya Maandalizi na Wajibu wa Mwakilishi wa MEW Mwakilishi wa MEW anawajibu kwa kuhakikisha kuwa mikutano ya MEW inafanyika na vigezo vyote vya mkutano vinatekelezwa. Hata hivyo, jukumu hili wamepewa Wathibiti Ubora, Maafisa Elimu na Maafisa Elimu Kata wanaohudhuria Kamati ya mipango. Hili ni jukumu la pamoja. Mwakilishi wa MEW Ataitisha mkutano wa Kamati na kuuongoza mkutano wa maandalizi kama mwenyekiti kila mkutano wa mwezi wa MEW. Mkutano wa maandalizi au MEW usifanyike bila uwepo wa watajwa hapo juu isipokuwa kwasababu maalumu. Atamwalika Afisa Elimu Wilaya kuhudhuria MEW angalau mara 4 kwa mwaka. Atatoa taarifa muhimu zote kuhusu mikutano ya MEW kila inapotakiwa kufanya hivyo kwa wafanyakazi wote, Maafisa Elimu, Wathibiti Ubora na Maafisa Elimu Kata. Atawakaribisha na kuwashirikisha wafanyakazi wapya kwenye mikutano. Kwa pamoja Kamati itafanya yafuatayo Itaandaa agenda kwa ajili ya MEW ujao

Itafanya mapitio ya Mafanikio ya MEW iliyopita na kushirikishana mambo yaliyofanikiwa vizuri

Itathibitisha kwa pamoja hatua zilizochukuliwa kuboresha Itaangalia mambo gani yanapaswa kufuatiliwa kutokana na mkutano uliopita Itafafanua Mada za Mkutano Itapanga Uwezeshaji wa mada kwa kutumia mbinu shirikishi Itakubaliana kuhusu wawezeshaji wa vipengele vya mkutano Itaandaa upatikanaji wa zana mbalimbali Itapanga tarehe na muda wa mkutano Itapanga na kuandaa ukumbi Itapanga jinsi ya kukaa katika makundi au duara ukutani wakitazamana Itakuwepo ukumbini mapema ili kuwakaribisha Waratibu Elimu Kata wanapofika

Itaandaa utaratibu wa kupata chai / chakula cha mchana kama inavyotakiwa kulingana na bajeti

Itaweka wazi majukumu ya nani atafanya nini wakati wa MEW ujao Mwakilishi wa MEW atakuwa na jukumu la kupokea na kushughulikia jambo lolote litakalojitokeza baada ya mkutano. Wanakamati wanapaswa kumtaarifu mwawakilishi jambo lolote ambalo linaweza kuathiri mkutano ujao Mwishoni mwa mwaka kamati itafanya yafuatayo Itafanya tathimini ya mwaka ya mada zilizofanyiwa kazi Itabainisha mafanikio na changamoto zilizojitokeza Itaandaa mwongozo wa mada kwa ajili ya mwaka ujao

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

36

KIAMBATISHO B

MKUTANO WA MAAFISA ELIMU, WATHIBITI UBORA NA WARATIBU ELIMU KATA

MWONGOZO WA RATIBA ULIOPENDEKEZWA

Vifaa: Matumizi ya bango kitita na kalamu rashasha

MUDA SHUGHULI MWEZESHAJI

2.30 Kuwasili na kujisajili

3.00 Kufungua Mkutano na kuelezea malengo ya mkutano Afisa Elimu (W)

3.30

Kuelezea/Kuwezesha mada inayohusu mkutano husika

Mthibiti Ubora

5.00 Chai

5.30

Kujadili utekelezaji wa shughuli fulani kutokana na maazimio ya

mkutano au mikutano iliyopita

Afisa Elimu /

Mthibiti Ubora

6.30 Mrejesho kutoka kwa Maafisa Elimu na Wathibiti Ubora kuhusu

taarifa mbalimbali za Waratibu Elimu Kata

Maafisa Elimu na

Wathibiti Ubora

7. 30

Maandalizi kwa ajili ya mkutano ujao

Maafisa Elimu na

Wathibiti Ubora

7.45 Matangazo mbalimbali

Afisa Elimu (W)

8.00 Kuagana

Afisa Elimu (W)

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

37

KIAMBATISHO C MKUTANO WA KWANZA WA MWEZI WA MAAFISA ELIMU, WARATIBU ELIMU KATA NA WATHIBITI UBORA-MANUFAA YA MKUTANO KATI YA AFISA ELIMU, WARATIBU ELIMU KATA NA WATHIBITI UBORA

Vifaa: Karatasi kubwa ya bango kitita na kalamu rashasha

MUDA SHUGHULI MWEZESHAJI

2.30 - Kuwasili na kujisajili

3.00

Kipindi cha Ufunguzi: Maneno ya ufunguzi ya Afisa Elimu na Utangulizi

Kuwasilisha malengo

Mkutano wa Elimu wa Wilaya ni mkutano mpya

unaowakutanisha Maafisa Elimu wa wilaya, Wathibiti Ubora, na

Waratibu Elimu Kata.

Hauhusiki na masuala ya fedha, Pikipiki au posho

Mkutano huu unahusu uboreshaji wa Elimu kwa wanafunzi

madarasani katika Wilaya zetu na kwenye jamii

Malengo ya Mkutano huu ni kuangalia faida kwa kila mshiriki wa

mkutano

AFISA ELIMU

WILAYA

4.00

Kipingi cha 1: Wagawanye washiriki katika makundi 3

Kundi la 1, Watasimama kama Waratibu Elimu Kata

Kundi la 2. Watasimama kama Wathibiti Ubora

Kundi la 3. Watakuwa Maafisa Elimu

Wapatie kila kundi Karatasi ya bango kitita na Kalamu

rashasha. Waambie kila kundi wajadili yafuatayo

Wanachangiaje katika kuboresha shule?

Wanaonaje umuhimu wa mkutano huu kwenye kazi zao

kama Halmashauri, Wathibiti Ubora, na Waratibu Elimu

Kata?

Andika mawazo yao kwenye karatasi ya bango kitita. Kundi

litakalokuwa la kwanza kumaliza litasema kwa sauti "BINGO". Kundi

hilo waambie wabandike bango kitita lao ukutani. Fanya hivyo hadi

makundi yote 3 yamalize. Zipi ni hoja muhimu?

Mjadala wa wote

Hoja muhimu ni zipi?

Ni zipi kati ya kazi zao zinasaidia zaidi katika kuboresha shule?

ADQA

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

38

Ni kwenye kazi gani hasa mnatumia muda wenu mwingi?

Kazi na jukumu gani vinawasaidia kutekeleza uboreshaji wa shule?

Mambo ya msingi ya kusisitiza

Kwa kupitia Jamii inayojifunza Wilaya ihakikishe kwamba;

Ufundishaji na Ujifunzaji unaboreshwa

Viwango vya wanafunzi vinaboreshwa

Shule zinawajibika

Changamoto za fedha zinajadiliwa kama vile ruzuku za IGA

Jamii zinawajibika na kushiriki kwenye masuala yanayohusu shule zao

Taarifa zinapokelewa na kusambazwa kwa kupitia ripoti

Hili ni jukumu la pamoja

Ili kufanya kazi pamoja lazima pawepo muda maalumu uliotengwa,

unaitwa mkutano wa MEW ili:

Kushughulikia masuala yanayohusu ufundishaji na ujifunzaji yanapotokea

Kushirikishana na kuimarisha uboreshaji wa elimu katika wilaya

Kuwezesha mawasiliano yawe imara zaidi

5.00 Chai

5.30

Kipindi cha 2 : Katika vikundi 6 vyenye watu saba saba

Faida za MEW ni nini? Dakika 20

Hakikisha kila kikundi kina bango kitita na kalamu rashasha.

Wakumbushe wanakikundi wachague mtu mmoja kati yao

atakayekuwa anaandika wanayoyajadili na atatoa mrejesho wakati wa

majumuisho.

Kuna manufaa gani kwa Wathibiti Ubora, Waratibu Elimu Kata, na Maafisa Elimu kukutana kila mwezi kujadili namna ya kuboresha elimu katika wilaya?

Kuna kipi cha tofauti kuhusu MEW?

Mrejesho wa wote Dakika 40

Omba kila kundi liwasilishe majibu ya vipengele walivyojadili (yasizidi

majibu 2 kwa kila kipengele). Kisha rudia kwa mzunguko uleule mpaka

Afisa Vifaa na

takwimu/Afisa

Taaluma

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

39

majibu ya vipengele vyote yakamilike. Waombe washiriki wasirudie

majibu ambayo yamekwishatolewa na kikundi kingine.

Mambo ya kusisitiza

Uelewa wa pamoja wa michango ya kila mshiriki na kushirikishana mawazo mbalimbali

Makubaliano ya hatua za kuchukua kwa ajili ya kuboresha shule Wilayani

Kuthamini na kuwajengea uwezo washiriki wote kwenye mkutano, hasa Waratibu Elimu Kata

Mafanikio ya pamoja na mawazo mapya

Umuhimu wa mahusiano ya MEW na ‘Jamii nyingine zinazojifunzaji’

Umuhimu wa kushirikishana taarifa za mikutano ya “Jamii inayojifunza”

Uboreshaji wa utendaji wa shule ni jukumu la pamoja!

Mkutamno wa MEW Una tofauti gani na program nyingine?

Mikutano ya Afisa Elimu wa Wilaya na Waratibu Elimu Kata inalenga mambo mengi ikiwa ni pamoja na yafuatayo:

Kazi za kiutawala kwa kuzingatia muongozo wa wizara

Kuwataarifu wafanyakazi kuhusiana na nyaraka na maelekezo ya wizara

Kujadili kuhusu ufaulu wa wanafunzi

6.30

Majumuisho kwa ufupi

Kwa ufupi elezea juu ya mkutano wa MEW:

Kujenga uelewana wa pamoja na mbinu za kuinua viwango na ubora wa elimu katika Wilaya

o Ili Wathibiti Ubora waweze kushirikisha utaalamu wao na

Waratibu Elimu Kata waweze kutoa taarifa juu ya shule

zao katika wilaya

o Ili Halmashauri iweze kupokea taarifa za kuiwezesha

kuandaa mipango yao kwa ajili ya kusaidia, kufundisha na

kuhamasisha na pia kuweka kipaumbele cha mipango

yake kwa ajili ya kuboresha na kugharamia elimu

o Ili kusaidia upatikanaji wa taarifa kati ya Wathibiti Ubora

, Maafisa Elimu wa Wilaya, na Waratibu Elimu Kata

kuhusu shughuli zao za mwezi uliopita na kazi za mwezi

unaofuata

ADQA

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

40

Kufanya mapitio ya miradi ya wilaya na kupata mrejesho

Kuangalia masuala muhimu kwa ajili ya kuinua ubora wa elimu

katika wilaya; kupanga shughuli za mafunzo na kusaidia

maendeleo ya shule kwa ujumla

Kutoa fursa kwa Waratibu Elimu Kata,Wathibiti Ubora na

Maafisa Elimu kuwa na Mkutano “Jamii Inayojifunzaji” wa kila

mwezi, ili kupata mawazo mapya na kutafuta njia za kutatua

changamoto za uboreshaji wa maendeleo ya shule

7. 00

Maandalizi ya Mkutano ujao

Kamati ya mipango: Afisa Elimu Wilaya, 2 Afisa Elimu , 2 Maafisa Elimu

Kata wa 2, na Wathibiti Ubora wa

Wafanyakazi wa EQUIP-T

Watakutana kupeana taarifa na tarehe

Chagua Maafisa Elimu Kata 2 watakaoungana na Kamati ya mipango

7.20 KUPANGA MADA ZA MKUTANO UJAO

Mpango wa Maendeleo ya Shule ni moja ya nyaraka muhimu sana za

shule

Maafisa Elimu Kata waje na nakala za Mipango ya Maendeleo ya Shule

kutoka katika Kata zao

Watafanya mapitio ya Mwongozo wa Mafunzo ya Mpango wa

Maendeleo ya Shule hasa zana za uchambuzi. SWOC, Mti wa matatizo,

Kuhusisha Wadau na uwekaji vipaumbele.

7.30 Matangazo kuhusu matukio ya kazi nyingine

Maoni na kuhitimisha

8.00 Kuagana

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

41

KIAMBATISHO D MKUTANO WA PILI WA MAAFISA ELIMU WILAYA, WARATIBU ELIMU KATA NA WATHIBITI

UBORA -KUCHAMBUA NA KUBORESHA MPANGO WA MAENDELEO YA SHULE

Vifaa: Karatasi ya bango kitita na kalamu rashasha

Maafisa Elimu Kata waliombwa kuja na nakala za Mpango wa Maendeleo ya shule

MUDA SHUGHULI MWEZESHAJI

2.30 Kuwasili na Kujisajili Wote

3.00 Kufungua kipindi cha 1

Maneno ya ukaribisho na utangulizi toka kwa Afisa Elimu Wilaya

Kujikumbusha malengo ya Mkutano

Malengo ya Mkutano wetu wa leo

1 Kushirikishana mambo yanayofanya ziara ya kutembelea shule

iwe yenye mafanikio

2 Kushirikishana changamoto zinazoweza kufanya ziara ya

kutembelea shule isifanikiwe

3 Kutaja mada tunazoweza kuzijadili kwenye mkutano yetu

4 Kufanya mapitio juu ya mafaniko ya Mpango wa Maendeleo ya

Shule

5 Kufanya mapitio ya taarifa za Waratibu Elimu Kata

Afisa Elimu

Wilaya

3.15

Kipindi cha 2

Unda makundi 6 mchanganyiko, angalau awepo Mthibiti Ubora 1,

na Afisa Elimu 1 katika kila kikundi

Dakika 5 katika jozi

Sisi sote huwa tunatembelea shule. Tushirikishane mifano ya ziara

zenye mafanikio ambazo unajua mchango wako umechangia katika

kuboresha shule uliyotembelea.

Je, ulifanya nini kuongeza ubora?

Kipindi cha 2 kinaendelea

Dakika 20 za kushirikishana katika vikundi

Je, kuna mafanikio yanayojirudia?

Je, una uhakika ni juhudi zako zilizoleta mafanikio hayo?

Tumia bango kitita na kalamu rashasha

Dakika 20 Kufanya majumuisho ya pamoja ya mkutano

ADQA

4.00

Kipindi cha 3: katika vikundi vilevile

Dakika 30

Mambo gani yanakwamisha jitihada za kuboresha ziara zako

shuleni?

DAO/DSLO

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

42

Unafanya nini kutatua changamoto hizo?

Mambo gani yanakuwepo shuleni yanayosaidia ziara ifanikiwe?

Tumia bango kitita na kalamu rashasha

Dakika 20 za majumuisho ya awali ya mkutano

5.10 Chai WOTE

5.45

Kipindi cha 4: Kufanya mapitio ya Mpango wa Maendeleo ya Shule

Vikundi vyenye watu 6, Wathibiti Ubora na Waratibu Elimu Kata

waungane na Maafisa Elimu katika vikundi

Katika mkutano uliopita Waratibu Elimu Kata waliombwa waleta

nakala za Mpango wa Maendeleo ya shule kutoka katani kwao, na

kila mmoja aliambiwa kufanya mapitio ya Mwongozo wa Mafunzo

ya Mpango wa Maendeleo ya Shule.

Kazi ya vikundi Dakika 40

Pitia Mpango wa Maendeleo ya Shule kwa kuzingatia yafuatayo

Je, malengo yote matano yapo?

Rasilimali za shule na fedha

Ufundishaji na Ujifunzaji

Mazingira Chanya yanayozingatia jinsia

Maboresho ya shule

Ushiriki wa jamii

Je, kila lengo angalau limeonekana kuwa na shabaha 2 zenye

uhalisia?

Je, kila lengo limepata angalau mambo 3 ya kufanyia kazi?

Je, malengo, shabaha, na kazi zake vinaendana?

Je, muda wa utekelezaji una uhalisia?

Je, imewekwa bayana ni nani atawajibika kwa kila kazi?

Je, kuna ushahidi unaothibitisha kwamba zana za uchambuzi

zilitumika?

SWOC, Mti wa matatizo, Kuhusisha Wadau na uwekaji vipaumbele.

Je, kuna ushahidi kwamba wadau wote walishirikishwa?

Chagua Mpango wa Maendeleo ya Shule ulio bora zaidi

Dakika 30: Mjadala wa wote

ADQA

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

43

7.00 -

7.45

Kipindi cha 5. Mada za Mkutano Ujao

Mkutano ujao utahusisha kushirikishana ripoti za utekelezaji wa

Mratibu Elimu Kata.

Waratibu Elimu Kata watatakiwa waje na nakala za mifano ya ripoti

kwenye mkutano ujao

Wazingatie mambo yanayofanya ripoti iwe nzuri

DAO/DSLO

7.45 -

8.00

Taarifa kuhusu matukio ya kazi nyingine

Mkutano mwingine wa mipango utafanyika.......

Mkutano kamili ujao utafanyika........

Maoni na kuhitimisha

Mambo mengine ya kufanya

Kikao cha maandalizi kitakuwa ………………..

Kikao kitakuwa ……..

Mengineyo

Afisa Elimu

Wilaya

8.00 Kuagana WOTE

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

44

KIAMBATISHO E

MKUTANO WA TATU WA KILA MWEZI WA MAAFISA WA WILAYA, WARATIBU ELIMU KATA, NA

WATHIBITI UBORA – NINI KINAFANYA TAARIFA YA AFISA ELIMU KATA IWE BORA?

Zana

Bango kitita na Kalamu rashasha

Waratibu Elimu Kata waliombwa kuleta nakala za Ripoti zao kwa Afisa Elimu Wilaya

Nakala moja kwa kila mshiriki ya Kiambatisho H “NINI HUFANYA RIPOTI YA MRATIBU ELIMU

KATA IWE BORA” KIAMBATISHO H

MUDA SHUGHULI MWEZESHAJI

2.30 - Kuwasili na kujisajili Wote

3.00

1 Kufungua kipindi – Maneno ya ukaribisho na Utambulisho

Lengo la Mkutano -

2 Kuangalia na kujadili mambo yanayofanya uandishi mzuri wa

ripoti

Afisa Elimu

3.30

Tumia

bango kitita

na kalamu

rashasha

Kipindi cha 1. Kupitia matarajio ya ripoti za Maafisa Elimu Kata

Dakika 30

Mpatie kila mtu na upitie kusoma Kiambatisho H “NINI

KINAFANYA RIPOTI YA MRATIBU ELIMU KATA IWE BORA”

1. Kuna maelezo na ripoti zilizoandaliwa kwa kila ziara ya

kutembelea shule

1. 2. Mratibu Elimu Kata huandika kwenye Kitabu Cha Wageni (log book)kila anapotembelea shule

2. 3. Kuna ripoti ya kila mwezi ya Mratibu Elimu Kata kwa Afisa Elimu wa Wilaya imbayo;

Inabainisha masuala kadha wa kadha ya shule husika Inalinganisha masuala ya shule Inalenga maeneo muhimu yanayohitaji msaada

4 Halmashauri hupokea ripoti hizo na kufuatilia ubora wa taarifa

za Mratibu Elimu Kata

Huhakikisha mambo muhimu yanayoibuliwa katika ripoti

yanajadiliwa

Hufanya uchambuzi na kuchukua hatua dhidi ya utendaji wa

shule

Hatua zilizoafikiwa hutekelezwa kwa kutengewa muda

maalum

Dakika 30

ADQA Kwa

kutumia

maelezo ya

Kiambatisho

H

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

45

Majadiliano ya wazi na maswali

4.30 Chai

5.00

Kipindi cha 2- Katika vikundi mchanganyiko

Kila igizo dhima la kikundi ni mahojiano kati ya Mratibu Elimu Kata

na mwalimu mkuu, fanya igizo dhima moja moja. Baada ya kila

igizo dhima waulize washiriki wamegundua nini na mjadiliane kwa

pamoja ili kupata ufumbuzi wa changamoto zilizoibuliwa. Ni

mahojiano gani mazuri unapokutana na mwalimu mkuu?

Igizo dhima 1

1 Mwalimu mkuu hasikilizi na amevurugwa. Mwalimu mkuu anaongea na simu, na kushughulika na kazi za kuandika kwenye makaratasi, mtoto yuko mlangoni. Je, MEK atalishughulikiaje hili?

Igizo dhima 2

2 MEK anatoa taarifa ambazo ni siri juu ya shule nyingine na Mwalimu mkuu? Igizo dhima 3

3 MEK anazungumza muda wote na Mwalimu Mkuu mwenye wasiwasi hana nafasi ya kuzungumza kuhusu matokeo ya hivi karibuni ya mitihani ya shule ambayo yanaonesha shule imeboresha sana.

Igizo dhima 4

4 Mahojiano hayana malengo ya wazi kuhusu shule. Yamejikita kuongelea kuhusu Magufuli na matatizo yao binafsi.

Igizo dhima 5

5 MEK anazungumza na Mwalimu mkuu kuhusu mafunzo ya walimu ngazi ya shule(INSET). Hajui majibu lakini anajaribu, hata hivyo majibu yake hayaeleweki kabisa kama alivyoelekezwa kwenye kozi aliyohudhuria. MEK atafanya nini?

Igizodhima 6

6 MEK anataka taarifa kuhusu UWW ya shule na wadau. Mwalimu mkuu anatoa ushirikiano mdogo kwao. Je, MEK anawezaje kumshauri na kumsaidia Mwalimu mkuu kujenga mahusiano m azuri na wadau?

Mjadala wa wote – Je, mkutano mzuri una sifa zipi?

DAO/DSLO

6.00

Kipindi cha 3. Kushirikishana RIPOTI ZA MRATIBU ELIMU KATA

katika vikundi.

Dakika 30

ADQA

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

46

Kushirikishana katika vikundi ripoti ya Mratibu Elimu Kata na

kuichunguza kwa kuangalia vigezo vifuatavyo.

Tumia bango kitita na Kalamu rashasha kuandika jambo lolote

linaloibuliwa kwenye majadaliano

Je, sentensi zinaeleweka bayana?

Je, unajua mambo ambayo Mratibu alifuatilia tangu mkutano wa

mwisho, wiki 2 kabla?

Je, unajua mambo gani muhimu yaliyopo shuleni?

Je, unajua Mratibu alisema alifanya nini wakati wa ziara yake?

Je, unajua majukumu waliyokubaliana kufanya ili kuboresha

shule?

Dakika 30

Majumuisho

7. 00

Maandalizi ya Mkutano ujao wa 4

Kwenye mkutano ujao tunatarajia kuangalia kazi za Afisa Elimu

Kata na Jamii /UWW na Kamati ya shule.

1. Zingatia hali ya wadau katika shule yako

2. Tafadhali kumbuka kuleta jambo lolote linalohusu miradi ya

IGA

7.45 Taarifa kuhusu matukio ya kazi nyingine

Maoni na Hitimisho

8.00 Kuangana

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

47

KIAMBATISHO F Mfano wa Mwongozo wa mada wa MEW kwa mwaka 2017

MEW- 2017

Mapitio/Ufuatiliaji

MADA/LENGO Mwezeshaji

JAN Hakuna

FEB 14

Mwongozo wa mada 2017 Mapitio ya Mpango wa Maendeleo ya Shule wa mwaka 2017 Mipango na taarifa za hivi karibuni Taarifa

ADQA DAO/MEW REP

MACH 17

Angalia 25% ya MMS iliyobora zaidi ya 2017

Mapitio ya Uandishi wa Taarifa ya Mratibu Elimu Kata kwa kutumia mwongozo wa mwaka 2016 Simulizi za mabadiliko Klabu za Juu IGA

DEO ADQA DAO/MEW REP RES

APR 21

Uboreshaji wa ushiriki wa jamii katika masuala ya Elimu shuleni.

ADQA DAO/MEW REP

MEI 19

Kuwasaidia walimu wakuu kutathmini maandalio ya masomo ya walimu

DAO/MEW REP ADQA na VSO

JUNI 16

Mtaala mpya

ADQA DAO/MEW REP

JULAI 21

Kuboresha mahudhurio ya walimu shuleni na darasani

DAO/MEW REP ADQA

AGOS Kuzisaidia shule kupata zana za kufundishia na kutumia vyema zilizopo

DAO/MEWREP

SEPT Kushirikishana vigezo vya ukaguzi? & Jinsi Waratibu Elimu Kata wanavyoweza kusaidia?

ADQA

OKT 20

Kuzisaidia shule zenye uhitaji wa miundombinu bora zaidi ya vyumba vya madarasa, vyoo, vyumba vya madarasa ya walimu

DEO & DSLO

NOV 17

Mapitio ya Mipango ya Mpango wa

Kufuatilia uhamisho wa wanafunzi wa Vituo vya Utayari(SRP) kwa ajili ya kuendelea na maboresho wanavyoingia shuleni

Mwakilishi wa SRP

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

48

Maendeleo ya Shule 2017

Mapitio ya Mwongozo wa mada za MEW 2017 Kuamua na kupitisha Mwongozo wa mada wa mwaka 2018

DES 15

Mapitio ya malengo ya utendaji wa shule na kupanga malengo mengine kwa ajili ya mwaka ujao

DAO

Mada nyingine zilizochaguliwa kwa ajili ya mwaka 2018 Ufundishaji wa madarasa makubwa Kufanya kazi na walimu wakuu wenye matatizo Kusaidia Elimu jumuishi kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum Changamoto na mafanikio ya kufanya kazi na shule shikizi Masuala ya mipaka ya shule Mipango ya uzalishaji mali na utekelezaji wake Kusaidia Elimu ya watoto wa kike Kuwezesha Mikutano ya shule kwa kutoa dondoo za mbinu za uwezeshaji

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

49

KIAMBATISHO G Ufafanuzi wa kazi ya Afisa Elimu Kata

Kutoka chuo cha ADEM

Atawajibika na masuala ya elimu ndani ya kata yake

Kusimamia elimu ya awali, shule za msingi, sekondari na elimu ya watu wazima katika kata yake

Kuhakikisha kuwa sera na nyaraka za mtaala zinapatikana na kuzingatiwa pamoja marekebisho

ya sera za nyaraka za serikali

Kufanya usimamizi wa mara kwa mara wa elimu katika shule za kata yake

Kufanya tathmini ya walimu ili kuhakikisha wanafundisha vizuri

Kutoa ushauri kwa walimu

Kuandaa Mafunzo ya Walimu – Mafunzo ya Walimu ngazi ya Shule (INSET), Kufanya uchunguzi

wa vipindi vya masomo darasani, semina na warsha za mafunzo

Kuanzisha jamii zinazojifunza ili walimu waweze kujiendeleza wenyewe

Kuwa daraja kati ya walimu na jamii

Kutoa taarifa za shule katika kata yake kwa wadau wote kama vile kwa Afisa Elimu Wilaya,

Wathibiti Ubora, Wazazi na Jamii.

Mada za Ziada kutoka EQUIP-T

Kufuatilia na kusaidia kuongeza ufaulu wa wanafunzi shuleni katika mitihani yao na majaribio

Kufuatilia ustawi wa watoto, watoto wenye ulemavu, ulinzi wa Mtoto, vilabu vya shule.

Kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi na walimu – watoto wasioandikishwa shule, walioacha

shule, walimu n.k

Kufuatilia upangaji mipango kimkakati katika shule- Mpango wa Maendeleo ya Shule - MMS

Kusaidia utunzaji na usimamizi wa fedha na rasilimali za shule – ruzuku na zana za darasani,

Kuhakikisha kuna utawala bora shuleni-kamati za shule

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

50

KIAMBATISHO H

MAMBO GANI YANAFANYA RIPOTI YA MRATIBU ELIMU KATA IWE NZURI?

RIPOTI ZIPI NA MATARAJIO

1. Ripoti ya WEO ya mikutano ya Shule

Hii ni ripoti inayoandikwa baada ya kila ziara ya shughuli za shule kufuatilia Utendaji wa Shule.

Ripoti hii itaandikwa baada ya kila ziara ya kutembelea shule. Maelezo ya kila ziara pia

huandikwa kwenye batli (logbook) ya shule.

Kila ziara zinapaswa kuwa na lengo mahususi na ijikite kwenye suala fulani. Ripoti inahitaji

kurekodi lengo hili na sual lilifuatiliwa na matokeo yake. Inarekodi ushauri wa pamoja na mambo

ya kufanya waliyokubaliana ili yaweze kukaguliwa wakati wa ziara zinazofuata.

Mfano wa suala la kujikita

Ukusanyaji wa data za mfumo wa taarifa za shule (SIS). Kusaidia uboreshaji na usimamizi wa

Shule.

Takwimu tofauti tofauti hukusanywa na kuripotiwa kwa mzunguko tofauti kulingana na sababu

ya ziara ya kutembelea shule na taarifa zozote zinazotakiwa na Halmashauri.

Fuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mambo waliyokubaliana wakati wa ziara ya mwisho

Fuatilia utekelezaji wa MMS.

Kuna matokeo gani yaliyoonekana kutokana na mafunzo ya walimu ngazi ya shule na mikutano

ya walimu (Pata ushahidi).

Fuatilia na pitia mafunzo au kozi yoyote ilifanyika nje ya shule. Kama vile kozi/mafunzo ya EQUIP-

Tanzania

Chunguza kwa kina uandaaji mipango, kazi za wanafunzi, maandalio ya kazi na ushauri

uliotolewa

Tunashauri huu uwe utaratibu endelevu wa kutoa taarifa utakaojazwa kwa kila shule

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

51

RIPOTI YA MIKUTANO YA SHULE

Tarehe ya 1

Ripoti iliyoandikwa ……….………………………………………

………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………

Tarehe ya 2

Ripoti iliyoandikwa ……..………………………………………

………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………

2. Ripoti ya Mwezi ya MEK ya kata iliyounganishwa

Hii ni ripoti iliyounganisha taarifa za Mkutano ya kila shule na kuunda ripoti ya kila mwezi ya

WEO. Ripoti inapaswa:

Ibainishe masuala ya kata nzima yanayotokana na taarifa za mikutano ya kila shule

Ioneshe kwa kina takwimu za shule

Ifanye ulinganisho kati ya shule na shule. Ichambue maendeleo ya shule tofauti

Ibainishe maeneo ya shule yanayohitaji msaada na hatua za kushughulikia

o Itoe taarifa juu ya matokeo ya mafunzo na mafunzo ya walimu ngazi ya shule

o Itoe taarifa juu shughuli zilizofanyika kama vile kukagua kazi, yaliyoonekana

Fomu ya kuomba fedha za ruzuku ya mwezi

Ripoti ya fedha za ruzuku ya mwezi/robo mwaka

Shughuli za Ruzuku ya UWW na fedha kama vile za Miradi ya kuingizia shule kipato (IGA)

3 Halmashauri inawajibu wa kupokea Ripoti za Mratibu Elimu Kata na kufuatilia ubora wa

Ripoti zake

Huweka takwimu hizo kwenye Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa wa Halmashauri

Huhakikisha masuala muhimu yaliyoibuliwa katika ripoti yanajadiliwa

Huchambua na kuchukua hatua juu ya maendeleo ya shule

Hatua zilizoafikiwa zinatekelezwa kwa wakati

RIPOTI NZURI NI IPI?

Mrejesho wa ana kwa ana unaofuatiwa na ripoti ya maandishi

Haifuati muundo maalum lakini inagusa maeneo muhimu ya ziara

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

52

Rahisi kusoma, ina lugha rahisi, maelezo mafupi

Maudhui yake yanabeba picha halisi ya masuala yaliyochunguzwa wakati wa ziara

Inarekodi maendeleo yaliyofikiwa tangu ziara ya mwisho

Mawazo yanapangwa kwa mtiririko mzuri, kwa ufupi na kwa ufasaha

Pointi za msingi sana na zile dhaifu zinaelezwa kwa uwazi na kwa kifupi

Hakuna utata

Inaonesha ushauri na mapendekezo ya kusaidia masuala yaliyoibuliwa

Imeandikwa katika muundo wa aya na kila aya ina taarifa kamili

Ina uwazi

Inaangalia uboreshaji wa taaluma

Inarekodi maendeleo ya ujifunzaji wa wanafunzi tangu ziara ya mwisho ilipofanyika

Inarekodi maendeleo ya ubora wa ufundishaji tangu ziara ya mwisho

Inarekodi maendeleo ya UWW na Kamati za shule tangu ziara ya mwisho

Inarekodi ushauri na msaada uliotolewa

Inarekodi hatua zinazopaswa kuchukuliwa, na nani wa kuchukua hatua

KUFANYA ZIARA NZURI ZA SHULE Ripoti nzuri inatokana na ziara iliyoandaliwa vizuri na yenye

malengo maalum

Weka wazi malengo ya ziara ya kutembelea shule, kama vile;

Kukusanya takwimu za shule

Kusaidia shule kukabiliana na changamoto zinazotokana na mabadiliko ya mtaala na mbinu mpya

za ufundiji

Kuhakikisha kuna utekelezaji wa sera za Elimu

Kusaidia kuainisha mahitaji na kutoa msaada kwa wanafunzi, walimu, walimu wakuu na

wafanyakazi wengine

Kutoa ushauri juu ya jinsi ya kuboresha usimamizi wa shule kwa ujumla

Kupitia na kusaidia katika masuala ya Mpango wa Maendeleo ya Shule na Utekelezaji wake

Kufuatilia na kuangalia maendeleo ya shule tangu ilivyotembelewa mara ya mwisho

Mwenendo mzuri wenye maadili ya kitaaluma

Dumisha mahusiano ya kikazi na kitaaluma

Onesha mfano

Heshimu wengine

Uwe mwaminifu na muwazi katika kutekeleza majukumu

Linda usiri

Baki kwenye lengo

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

53

KIAMBATISHO I NINI CHA KUFANYA BAADA YA MAFUNZO

Baada ya

mafunzo haya

nini tunapaswa

kufanya?

Tutafanya nini

na wakati gani?

Tutaandaaje na

kuwezesha

MEW? Vifaa vipi

tutatumia?

Tunatakiwa

kufanya nini

baada ya

mkutano wa

MEW, kusaidia

na kufuatilia?

Nani

atatusaidia?

Wa taarifu

Waratibu Elimu

Kata kuhusu

MEW

Mkubaliane

tarehe na muda

KIAMBATISHO J

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

54

MAJUKUMU NA TARATIBU ZA UTOAJI TAARIFA ZA MKUTANO WA ELIMU WA MKOA NA

WILAYA

AFISA ELIMU MKOA NA KANDA

Majukumu

Afisa Elimu Mkoa atagawa majukumu kati ya ofisi ya elimu ya kanda na mkoa

Kufuatilia kuhakikisha kwamba mikutano ya Halmashauri inafanyika na kuendeshwa vizuri na kutoa msaada kwa kupiga simu mara kwa mara

• Kuhudhuria MEW mara kwa mara na kuwasaidia maafisa elimu wa Halmashauri na Wathibiti Ubora

• Kupokea Mwongozo wa mada za mwaka kutoka Halmashauri mwezi Januari kila mwaka • Kujaza idadi ya mikutano na mada zilifanyiwa kazi • Kujaza mahudhurio ya maafisa elimu wa Halmashauri na Wadhibiti Ubora • Kuchangia kuendesha mada na kuzitawanya kwenye Halmashauri nyingine • Kutunza na kuboresha orodha ya namba za mawasiliano

Kutoa taarifa

• Kupokea Mwongozo wa mada za mwaka mwezi Januari kila mwaka • Kudai taarifa za MEW kama sehemu ya ripoti ya Afisa Elimu Wilaya • Kumbukumbu za mikutano ya MEW • Kutoa mrejesho kwa Halmashauri

Halmashauri

Majukumu

• Afisa Elimu Wilaya atateua Mwakilishi/Mratibu wa MEW • Halmashauri kuonesha nia na uwajibikaji wa kusimamia mikutano ya MEW na Jamii

inayojifunza • Kushirikishana na kuisaidia Kamati ya Maandalizi ya MEW • Wilaya zote kuboresha mrejesho unaotolewa kwa Waratibu Elimu Kata kuhusu ripoti zao • Kufuata na kutekeleza mambo yaliyopitishwa wakati wa MEW • Wilaya kutenga bajeti na kuhakikisha mikutano ya MEW inaendelea kufanyika

Utoaji wa taarifa

• Afisa Elimu Wilaya atatoa taarifa kuhusu MEW kwenye ripoti yake ya maendeleo ya kila mwezi kwa Afisa Elimu Mkoa, kada na EQUIP-Tanzania

• Kumbukumbu za mikutano ya MEW zitasambazwa kwenda EQUIP-T, kwa Afisa Elimu Mkoa na Mthibiti Ubora wa Kanda

• Kupokea Mrejesho na taarifa za kufuatiliaji kutoka mkoani kuhusu kupokea yatokanayo na MEW na ripoti ya maendeleo ya Afisa Elimu Wilaya

WARATIBU ELIMU KATA

Majukumu

• Afisa Elimu Kata kuonesha nia na uwajibikaji wa kusimamia mikutano ya MEW na Jamii inayojifunza

• Kufuata na kutekeleza makubaliano yaliyopitishwa wakati wa MEW • Kushirikishana na kuisaidia Kamati ya Maandalizi ya MEW

Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-Tanzania)

Uongozi na Usimamizi wa Shule

55

Kutoa wa taarifa

• Kuandika na kusambaza taarifa za mkutano wa MEW kwa ADQA, Afisa Elimu wa Wilaya, Afisa Elimu Mkoa, Mthibiti Ubora wa Kanda, na EQUIP-T

• Kuboresha taarifa za kila mwezi ya Afisa Elimu kata • Kupokea mrejesho na kufuatiliaji kutoka Halmashauri baada ya kupokea ripoti za Afisa

Elimu Kata