tathmini ya mahusiano baina ya watu na tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 muhtasari tulifanya...

23
Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na Uwanda wa Magharibi wa Mapori ya Akiba ya Rungwa-Kizigo-Muhesi Septemba 2016

Upload: others

Post on 24-Jan-2021

4 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na Uwanda wa Magharibi wa Mapori ya Akiba ya Rungwa-Kizigo-Muhesi

Septemba 2016

Page 2: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

1

Mawasiliano Southern Tanzania Elephant Program S.L.P 2494, Iringa www.stzelephants.org [email protected] Waandishi Josephine Smit Dr. Trevor Jones Rehema John

Uchoraji ramani Frank Lihwa Rehema John

Ukusanyaji wa takwimu Kephania Mwaviko Rehema John

Nakala ya ripoti hii Ripoti hii kwa lugha ya kiswahili na kiingereza linapatikana katika tovuti: www.stzelephants.org/publications-news/articles-reports. Nukuu Southern Tanzania Elephant Program. 2016. Tathmini ya mahusiano baina ya watu na tembo karibu na uwanda wa Magharibi wa Mapori ya Akiba ya Rungwa-Kizigo-Muhesi. Ripoti ya kiufundi. Ufadhili Ripoti hii inawezeshwa kwa msaada mkubwa wa watu wa Marekani kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), kupitia ufadhili mdogo kutoka Wildlife Conservation Society’s Southern Highlands and Ruaha-Katavi Protection Program (SHARPP). Yaliyomo ni wajibu wa waandishi na si lazima kutafakari maoni ya USAID au Serikali ya Marekani. Shukrani Tunaishukuru taasisi ya utafiti ya Tanzania (Tanzania Wildlife Research Institute-TAWIRI) na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa ajili ya kutoa ruhusa ya kufanya utafiti huu, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Singida na Mkuu wa Wilaya ya Manyoni kwa ushirikiano wao. Tunawashukuru viongozi wote wa vijiji na wakulima walioshiriki katika utafiti huu, na tunatarajia kupitia ripoti hii itawafaidisha wale wanaoishi na tembo. Kuhusu Southern Tanzania Elephant Program STEP ni taasisi isiyo ya kiserikali inayohusika na uhifadhi wa tembo iliyosajiliwa mwaka 2014 na makao makuu yake yapo kusisni mwa Tanzania. Kazi za STEP zimegawanyika katika makundi makuu manne: Ulinzi wa tembo, utafiti na ufuatiliaji, kuimarisha mahusiano baina ya tembo na watu kupitia miradi ya uhifadhi ya jamii, na utetezi na elimu.

Kuhusu Southern Highlands na Ruaha-Katavi Protection Program (SHARP)

SHARPP ni programu ya miaka mitano inayofadhiliwa na Shirika la Marekani kwa ajili ya Maendeleo ya Kimataifa (USAID) ambao unatekelezwa na Shirika la Uhifadhi wa Wanyamapori (Wildlife Conservation Society – WCS)kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania, taasisi binafsi za ndani, na wanajamii. SHARPP inalenga maeneo makuu manne, ambayo ni: maeneo ya usimamizi wa wanyamapori (WMAs); maisha; usimamizi wa mazingira; na ufuatiliaji na ulinzi wa tembo. Tathmini hii ya muingiliano baina ya tembo na watu kuzunguka Mapori ya Akiba ya Rungwa, Kizigo na Muhesi ina lengo la kuwajulisha jitihada za kuongeza mshikamano baina ya tembo na watu kuzunguka hifadhi hizi muhimu.

Page 3: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

2

Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana na Mapori la Akiba ya Rungwa, Kizigo na Muhesi kati ya Agosti na Septemba 2016. Aina kuu za madhara ya tembo ilikuwa ni upotevu wa mazao, na mazao makuu yaliyolioathiriwa yalikuwa ni mahindi, viazi, na mtama. Pia, tembo ilisemekana kuvunjwa kwa maghala ya vyakula, paa za nyumba, na vyanzo vya maji, na kusababisha ushindani wa maji na chakula kwa mifugo. Maeneo makuu yenye athari za tembo ni vijiji vya Rungwa na Dorotto, na kwa kiwango cha chini Kintanula na Itagata. Juhudi za kukabiliana na athari hizo kwa sasa zipo kwa kiwango kidogo hadi cha kati, na huhusisha mbinu za jadi kama vile kelele, moto, na kulinda mashamba. Kwa mitazamo ya wahojiwa, Wizara ya Maliasili na Utalii, Serikali Kuu, na Mamlaka ya Mapori ya Akiba (katika mfuatano huo) zilionekana kuwa na majukumu yaa kusimamia kukubaliana na athari za tembo. Mitazamo ya wahojiwa ilionyesha utendaji wa mashirika hayo katika kusimamia athari za tembo kwa ujumla ilionekana kutokidhi. Wengi wa wahojiwa walidhani ilikuwa ni muhimu sana kuboresha mahusiano baina ya jamii na tembo. Mahusiano baina ya jamii na mamlaka ya Mapori ya Akiba kwa ujumla ilionekana kuwa mazuri sana.

1. Utangulizi Mshikamano baina ya watu na tembo ni changamoto kubwa katika uhifadhi nchini Tanzania, na katika maeneo mengi ya Tembo wa Afrika. Tembo ni aina ya viumbe vyenye kipaumbele katika uhifadhi nchini Tanzania, hutambuliwa kwa mchango wao katika uchumi wa Taifa kupitia utalii wa wanyamapori,na wamekuwa hatarini kutoweka kutokana na ujangili kwa ajili ya meno yao ambao umepunguza idadi ya tembo kitaifa kutoka 109,000 mwaka 2009 hadi kufikia takribani tembo 50,0001 mwaka 2015. Hata hivyo, tembo wanaweza pia kuwa na athari juu ya watu na maisha, hasa katika jamii ambazo hushirikiana na tembo katika maeneo na rasilimali. Hivyo, kuhakikisha mshikamano wa muda mrefu baina ya tembo na watu, Tanzania inahitaji hatua za kukabiliana na athari za tembo kwa watu na kuongeza msaada kwa jamii mzima kuhusiana na uhifadhi wa tembo.

Lengo la tathimini hii ilikuwa ni kuelewa muingiliano baina ya tembo na watu katika mwambao wa Magharibi wa Mapori ya Akiba ya Rungwa-Kizigo-Muhesi, na kuwapatia wadau taarifa na mapendekezo kwa ajili ya kusaidia kusimamia migogoro baina ya watu na tembo.

Utafiti uliopita (Wilbright 2016) wa muingiliano baina ya tembo na watu katika vijiji sita karibu na Pori la Akiba la Rungwa ulionyesha kuwa umbali wa eneo la hifadhi ulikuwa ishara kubwa ya upotevu wa mazao, ambapo vijiji vilivyokuwa karibu na hifadhi viliathirika zaidi kuliko vijiji vilivyoko mbali na hifadhi. Utafiti huu pia uliweza kutambua uhamiaji wa wafugaji wa kabila la wasukuma kama moja ya sababu zinazopelekea migogoro baina ya watu na tembo, kwa sababu wahamiaji (ambao walikuwa wakilima jirani na mipaka ya Mapori ya Akiba) walikuwa katika hatari zaidi ya mazao yao kuliwa na tembo kuliko wenyeji (Wilbright 2016).

Tathmini hii hujenga juu ya kazi ya awali ya kutoa ufahamu zaidi juu ya madhara ya tembo katika vijiji vinavyopakana na mipaka ya Pori la Akiba ili kuwajulisha mikakati ya kupunguza athari zinazosababishwa na tembo. Ni matumaini yetu kuwa ripoti hii itahamasisha kwa kiasi kikubwa ushirikiano kati ya jamii zinazoishi kando ya Mapori ya Akiba ya Rungwa, Kizigo na Muhesi, Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori, Serikali ya Wilaya na ya Mkoa, na mashirika ya uhifadhi katika kufanya kazi ili kufanikisha mshikamano baina ya watu na tembo katika mazingira ya Rungwa.

1.1 Malengo

1. Kutambua aina na mgawanyo wa muingiliano baina ya watu na tembo 2. Kutambua maeneo yanayopata migogoro kwa kiasi kikubwa 3. Kuelewa jinsi uongozi wa kijiji na wakulima wanavyosimamia muingiliano baina ya tembo na watu. 4. Kukusanya taarifa kuhusu shoroba na mapito ya tembo. 5. Kupata ufahamu juu ya maoni ya jamii kuhusu tembo na mamlaka ya mapori ya akiba. 6. Kutoa mapendekezo juu ya usimamizi wa muingiliano baina ya watu na tembo

Page 4: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

3

1.2 Maeneo yaliyofanyiwa utafiti

Utafiti huu ulifanywa katika vijiji tisa ndani ya wilaya ya Manyoni (mkoa wa Singida) vilivyoko kando ya mpaka wa magharibi wa Mapori ya Akiba ya Rungwa, Kizigo na Muhesi (Jedwali 1). Hifadhi hizi ni sehemu ya eneo la mfumo wa ikolojia wa Ruaha-Rungwa (wenye eneo lipatalo 45,000 km2), ambapo mwaka 2015 iliofanyika sensa ya Tembo na kupata idadi inayookadiriwa kuwa 15,000, na hii ni kufuatia kushuka kwa idadi hiyo kutoka Tembo 36,000 mwaka 2006 kutokana na ujangili kwaajili ya meno ya Tembo (TAWIRI 2015). Pori la Akiba la Rungwa lilianzishwa mwaka 1951 na lina ukubwa wa kilomita za mraba 9,000. Hifadhi hii inaundwa na vilima vilivyochanganyikana na maeneo machache ya misitu kandokando ya mito katika bonde la Mto Mpera. Pori la Akiba la Kizigo lilianzishwa mwaka 1982 na lina ukubwa wa kilomita za mraba 4,000. Pori la Akiba la Muhesi lina ukubwa wa kilomita za mraba 2000 na lilianzishwa mwaka 1994. Mapori ya Akiba ya Kizigo na Muhesi yana uoto wa miombo, pamoja na nyasi, miamba iliyojitokeza, na mabonde ya kandokando ya mito. Mapori ya Akiba ya Rungwa, Kizigo na Muhesi yanasimamiwa na Idara ya Wanyamapori (Wildlife Division). Vikwazo vikuu katika hifadhi hizi ni pamoja na kuvamiwa na watu, matumizi mabaya ya maji, moto usiosimamiwa, malisho yasiyokuwa na udhibiti, uwindaji haramu na migogoro baina ya watu na wanyamapori (Coppolillo 2004, Wilbright 2016).

Ramani ya vijiji vilivyofanyiwa tafiti

Page 5: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

4

Sensa ya Tanzania ya mwaka 2012 ilionyesha kuwa wilaya ya Manyoni ilikuwa na idadi ya watu 296,763

kutoka katika kabila sita tofauti ikiwa ni pamoja na Nyiramba, Nyaturu, Sukuma, Mang'ati, Barabaig na

Hadzabe. Utafiti wetu juu ya viongozi wa vijiji ulionyesha kuwa vijiji vingi vinajikita katika kilimo na

ufugaji, pamoja na ukusanyaji wa asali. Mazao makuu yanayolimwa ni pamoja na mahindi, alizeti,

tumbaku, karanga, viazi, mchele, karanga, tikiti maji na mtama (Singida Region Socio-economic Profile

1997). Asilimia ya kaya wanazoishi chini ya kiwango cha umaskini katika mkoa wa Singida ni asilimia 49

(URT 2005).

Jedwali 1. Idadi ya watu katika vijiji mbalimbali vilivyofanyiwa utafiti kuzunguka Mapori ya Akiba ya

Rungwa-Kizigo-Muhesi (chanzo: mahojiano na viongozi wa vijijii)

Jina la kijiji Idadi ya watu

mwaka 2016

Kayui 17560

Makale 3077

Dorotto 12849

Itagata 4916

Mitundu 23000

Kalangali 2050

Rungwa 6300/6400

Kintanula 3089

Mwamagembe 17568

2. Mbinu Zilizotumika Dodoso za tafiti zilifanyika ndani ya vijiji tisa mnamo tarehe 25 mwezi wa nane hadi tarehe 2 mwezi wa

tisa mwaka 2016 (Jedwali 2). Chaguzi za vijiji zilitolewa taarifa na Meneja Mkuu wa Pori la Akiba ya

Rungwa Bwana S. Kabanda ambaye aliainisha sehemu hatarishi zenye migogoro baina ya watu na tembo.

Barua ya ruhusa ya kufanya tafiti za dodoso ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Kutoka Ofisi ya

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni. Kopi ilitolewa kwa viongozi wa vijiji.

Jedwali 2. Vijiji vilivyofanyiwa tafiti

Kijiji Tarehe ya Tafiti Pori la Akiba la jirani Idadi ya Dodoso

Dorotto 26/08/2016 Muhesi 11

Itagata 27/08/2016 Muhesi 9

Kayui 25/08/2016 Muhesi 6

Makale 25/08/2016 Muhesi 7

Mitundu 27/08/2016 Muhesi 8

Kalangali 01/09/2016 Kizigo 8

Mwamagembe 31/08/2016 Kizigo/Rungwa 11

Kintanula 30/08/2016 Rungwa 12

Rungwa 29/08/2016, 02/09/2016

Rungwa 23

Page 6: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

5

Aina mbili za dodoso zilitumika, moja kwa viongozi wa vijiji na ya pili kwa wakulima. Jumla ya wahojiwa

95 walihojiwa, ikiwemo viongozi wa vijiji 12 (wenyeviti wa vijiji, vitongoji na watendaji wa vijiji) na

wakulima 83 ndani ya vijiji tisa (kiiambatinisho 1). Angalau kiongozi mmoja wa kijiji na wakulima sita

walihojiwa kila kijiji. Kwa wastani wa dodoso kumi zilifanyika kwa kila kijiji.

Dodoso (ambazo zinapatikana kwa maombi) zilizofanyika kutadhimini muingiliano baina ya watu na

tembo na mitazamo ya watu kuhusu mahusiano baina ya watu na tembo. Wahojiwa waliulizwa maswali

kuainisha aina tofauti za madhara ya tembo yanayotokea. Dodoso pia zilijumuishwa maswali kuhusu ni

kwa namna gani kwa sasa viongozi wa vijiji na wakulima wanadhibiti madhara ya tembo. Pia dodoso

ilikuwa na maswali kuhusu ufugaji wa nyuki na masoko ya asali. Vipengele vingine vya dodoso ni pamoja

na maswali kuhusu misafara ya tembo na maeneo ya mapito ya tembo, na mawazo ya jamii kuhusu

tembo na maeneo ya uhifadhi.

Dodoso zilifanyika na watafiati wawili kutoka STEP: Bwana Kephania Mwaviko na Bi. Rehema John. Timu

hii inauzoefu mzuri wa tafiti za kijamii na ujuzi wakufanya mahojiano, pamoja na jinsi ya kuhakikisha

ridhaa ya watu, kuhudhulia bila malipo na kufanya mahojiano bila Kuchukua majina ya wahojiwa,

kuelezea malengo ya tafiti, kuongeza dodoso. Wahojiwa walichaguliwa kwa kufanya matembezi kwa

kutumia taratibu za sampuli, wahojiwa kuanzia mwisho mwa kijiji na kutembea kurudi nyuma, na

kuchagua kila baada ya nyumba ya tatu kwa mahojiano. Mahojiano yote yalifanyika kwa Kiswahili na

majibu yaliandikwa kwenye karatasi ya dodoso. Uingizaji taarifa na uchambuzi ulifanywa kwakutumia

mfumo wa takwimu wa Sayansi ya Jamii (SPSS-21) Software na Microsoft Excel. Watafiti walipima

kiwango cha ushiriki na uelewa wa dodoso kwa wahojiwa katika vipimo vya 1 mpaka 5 (1 ikiwa kiwango

kidogo cha kushiriki/kuelewa, na 5 ikiwa ni kiwango kikubwa cha kushiriki). Kiwango cha ushiriki kutoka

kwa viongozi wa kijiji na wakulima kilifika wastani wa 4 na 3.8, na ilikuwa ni kiwango kizuri. Kiwango cha

uelewa cha wastani wa 4.1 kwa viongozi wa kijiji na 3.7 kwa wakulima, pia kilikuwa ni kizuri.

3. Matokeo 3.1 Mgawanyiko na Aina Mbalimbali za Athari za Tembo

Vijiji vitatu (Rungwa, Dorotto, na Kintanula) viliripotiwa kuwa na kiwango kikubwa cha upotevu wa

mazao kutokana na wanyamapori (Jedwali 3) na athari za mara kwa mara za tembo (Jedwali 4). Kijiji

kimoja (Itagata) kililipotiwa kuwa na athari za tembo za kiwango cha chini. Vijiji vitano viliripotiwa kuwa

kiasi cha wanyamapori kusababisha upotevu wa mazao na athari za tembo ambazo zilionekana kwa kiasi

kidogo. Vijiji vya Rungwa na Dorotto vilitoa ripoti ya namba kubwa ya matukio ya upotevu wa mazao na

misafara ya mara kwa mara ya tembo (Jedwali 5). Kuvunjwa kwa maghala ya kuhifadhi mazao iliripotiwa

kwa kijiji cha Rungwa pekee. Watu kujeruhiwa na vifo vitokanavyo na tembo iliripotiwa na vijiji viwili

(Itagata na Dorotto), lakini ilitokea mara chache. Hakuna kijiji kilitoa taarifa ya matukio ya mauaji ya

mifugo inayosababishwa na tembo, wala tembo kuuawa. Viongozi wa vijiji Dorotto, Rungwa na Itagata

walitoa taarifa za athari za tembo kwa wafugaji ndani ya vijiji vyao. Walielezea kwamba watu na tembo

wanashindania malisho ya mifugo na vyanzo vya maji ndani ya eneo la kijiji (visima). Wafugaji pia

wameripotiwa kuwa wamehamisha makazi yao kwa kuofia kuathiriwa na tembo.

Page 7: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

6

Jedwali 3. Ni kwa kiasi gani upotevu wa mazao unatokea kutoka na wanyama pori ndani ya kijiji?

Kijiji Hakuna tatizo

Kwa kiasi kidogo

Sifahamu Kwa kiasi kikubwa

Kwa kiasi kikubwa sana

Makale 0 75 0 25 0

Mitundu 0 75 0 25 0

Kalangali 0 75 13 0 13

Itagata 0 44 0 33 22

Mwamagembe 0 45 0 27 27

Kayui 17 33 0 17 33

Dorotto 9 0 0 18 73

Kintanula 0 0 0 25 75

Rungwa 0 0 0 0 100

Jedwali 4. Ni kwa jinsi gani migogoro ya watu na tembo ipo ndani ya kijiji? (majibu kwa %)

Kijiji Hakuna tatizo

Kwa kiasi kidogo

Sifahamu Kwa kiasi kikubwa

Kwa kiasi kikubwa sana

Kalangali 50 50 0 0 0

Kayui 50 33 0 17 0

Makale 0 88 0 13 0

Mitundu 0 88 0 13 0

Mwamagembe 36 45 0 9 9

Itagata 0 33 0 33 33

Kintanula 0 33 0 17 50

Dorotto 0 0 0 9 91

Rungwa 0 0 0 0 100

Jedwali 5. Aina za madhara ya tembo na mzunguko wake (majibu yaliyotolewa na wahojiwa wengi)

Kijiji Misafara ya tembo

Upotevu wa mazao

Kuvunjwa kwa maghala ya chakula

Watu kujeruhiwa/ vifo

Mauaji ya mifugo

Tembo kuuawa/ kujeruhiwa

Rungwa > Mara 5 kwa mwaka

> Mara 5 kwa mwaka

> Mara 5 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Dorotto > Mara 5 kwa mwaka

> Mara 5 kwa mwaka

Mara 5 kwa mwaka

<Mara 1 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Kintanula Mara 1-5 kwa mwaka

Mara 1-5 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Itagata Mara 1-5 kwa mwaka

> Mara 5 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

< Mara 1 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijulikani

Mwamagembe Mara 1-5 kwa mwaka

< Mara 1 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Mitundu < Mara 1 kwa mwaka

< Mara 1 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Kayui Mara1-5 kwa mwaka

Mara 1-5 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Page 8: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

7

Kijiji Misafara ya tembo

Upotevu wa mazao

Upotevu wa maghala ya chakula

Watu kujeruhiwa/ vifo

Mauaji ya mifugo

Tembo kuuawa/ kujeruhiwa

Kalangali < Mara 1 kwa mwaka

< Mara 1 kwa mwaka

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Makale Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Haijawahi kutokea

Upotevu wa tembo kwenye maghala ya kuhifadhi mazao na kuvunjwa kwa paa za nyumba ndani ya kijiji

cha Rungwa, mwezi wa tisa 2016 (Picha na K. Mwaviko)

3.2 Kiwango cha Upotevu wa Mazao Unaosababishwa na Tembo na Misafara ya Tembo

Aina ya wanyamapori wanne wakuu waliainishwa kuhusika na upotevu wa mazao katika eneo la utafiti ni tembo, nguruwe pori, nyani na tumbili. Jumla ya spishi 14 yaliainishwa kusababisha upotevu wa mazao. Upotevu wa mazao kutokana na tembo ilionekana kuathiri zaidi zao la mahindi, ikifuatiwa na viazi pamoja na ulezi. Katika eneo la utafiti, asilimia 56% ya wahojiwa walitoa taarifa kuwa upotevu wa mazao kutokana na tembo unatokea kipindi cha masika na kipindi cha mavuno, wakati asilimia 36% ya wahojiwa walitoa taarifa kuwa upotevu wa mazao unatokea kipindi cha kiangazi na masika. Vijiji vya Rungwa na Dorotto vilionekana kuwa tembo ni mnyama namba moja anayesababisha upotevu wa mazao, uzoefu unaonesha watu wanakutana na tembo mara nyingi. Wahojiwa walitoa taarifa kuwa upotevu wa mazao kutokana na tembo ulianza miaka kumi iliyopita, na kiwango cha upotevu kinazidi kuongezeka. Vijiji hivi vilitoa taarifa ya upotevu wa mazao unaosababishwa na tembo kutoka 2015 na 2016, na ni zaidi ya matukio matano ya upotevu wa mazao na ndani ya kijiji kwa mwaka (Jedwali 5). Kiukweli, wahojiwa wengi ndani ya kijiji walitoa taarifa kuwa upotevu wa mazao kutokana na tembo yanatokea mara nyingi kwa mwaka (Jedwali 8). Vijiji vya Kintanula na Itagata pia vilimuweka tembo kama ni aina la wanyama linalosababisha upotevu wa mazao, lakini uzoefu unaonesha sio mara nyingi ukilinganisha vijiji vya Rungwa na Dorotto. Vijiji hivi pia vilitoa taarifa ya upotevu wa mazao kuanza kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita, na matukio ya upotevu wa mazao kati ya mwaka 2015 na 2016. Wahojiwa wengi walitoa taarifa kuwa idadi ya matukio ya upotevu wa mazao inaongezeka. Wahojiwa walikadilria kuwa na misafara ya tembo 4.3 (Kintanula) na 3 (Itagata) kwa mwaka, inachukuliwa ni ndogo kuliko Rungwa na Dorotto. Mwamagembe, Mitundi na

Page 9: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

8

Kayui walimuweka tembo kama ni mnyama namba tatu au ya nne yanayosababisha upotevu wa mazao. Mitundi na Kayui havikutoa taarifa yeyote ya misafara ya tembo ndani ya mwaka 2016, na kilitoa taarifa ya wastani ya misafara mmoja kwa mwaka. Mwamagembe kilitoa taarifa ya upotevu wa mazao ndani ya mwaka 2016 (misafara 1.3) na mwaka 2015 (1.7), na wastani mdogo isiyozidi misafara tatu ya tembo kwa mwaka. Vijiji vya Kalangali na Makale kwaujumla havijazulika na tembo na havikuambatanishwa kwenye Jedwali 8. Jedwali 6. Kwa jinsi gani Tembo amewekwa kiwango tofauti na wanyama wengine wanayosababisha upotevu wa mazao (kwa eneo lote la utafiti)

Kiwango Aina la mnyama

1 Tembo

2 Nguruwe pori

3 Tumbili

4 Kudu

5 Pofu

6 Ndege

7 Pundamilia

8 Nungunungu

9 Kicheche

10 Kakakuona

11 Nyati

12 Ngiri

13 Swala pala

14 Ngiri

Jedwali 7. Mazao makuu yanayoathiriwa na tembo (kwa eneo lote la utafiti)

Kiwango Mazao

1 Mahindi

2 Viazi

3 Ulezi

4 Karanga

5 Alizeti

6 Miwa

7 Maboga

8 Mpunga

9 Mihogo

10 Nyanya

11 Tikiti

12 Dengu

13 Ndizi

14 Mtama

15 Nyanya

Page 10: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

9

Jedwali 8. Kiwango cha mfululizo wa tembo kusababisha upotevu wa mazao

1. Kiwango cha upotevu wa mazao kinachosababishwa na tembo tofauti na aina nyingine ya wanyamapori

Kijiji Kiwango cha tembo1

Lini upotevu wa mazao ulianza

Misafara ya mwisho ya tembo

Kipindi cha upotevu wa mazao

Kiwango cha upotevu wa mazao

Idadi ya misafara ya tembo kwa mwaka (wastani)

Misafara ya tembo 2016 (wastani)

Misafara ya tembo 2015 (wastani)

chanzo

Rungwa 1 > Miaka 10 iliyopita 2016 Kipindi cha mavuno

Imeongezeka sana Kila siku Kila siku Kila siku Pori la Akiba

Dorotto 1 > Miaka 10 iliyopita 2016 Kipindi cha mavuno

Imeongezeka kidogo Kila siku Kila siku Kila siku Pori la Akiba

Kintanula 1 > Miaka 10 iliyopita 2016

Kipindi cha masika na mavuno

Imeongezeka sana 4.3 3.25 3.7 Pori la Akiba

Itagata 1 > Miaka 10 iliyopita 2016 Kipindi cha masika Haijulikani 3.4 2.2 2.9 Pori la Akiba

Mwamagembe 4 > Miaka 10 iliyopita 2016 Kipindi cha masika

Imeongezeka kidogo 2.9 1.3 1.7 Pori la Akiba

Mitundu 3 Miaka 0-10 iliyopita 2015 Kipindi cha masika

Imepungua sana 1 0 1

Pori la Akiba Sikonge-Tabora

Kayui 3 Miaka 0-5 iliyopita Haijulikani Kipindi cha masika

Imepungua sana 1.3 0 4 Pori la Akiba

Page 11: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

10

Ramani inayoonyesha vijiji ambavyo vinahitaji kipaumbele kwenye jitihada za kukabaliana na athari za

tembo

3.3 Usimamizi na Uzuiaji

Kwa ujumla, mitazamo ya wahojiwa ni kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii, Serikali Kuu na Mapori ya

Akiba wanawajibika na tembo na kuzuia madhara hasi ya tembo (Jedwali 9). Ni wahojiwa wachache

waliona Serikali za vijiji na jamii wanawajibu wa kuwalinda tembo na kuzuia madhara hasi yatokanayo na

tembo. Miongoni mwa wahojiwa wengi waliona vitengo hivi havikuwajibika vizuri zaidi (Jedwali 10)

katika kuwasimamia tembo na madhara yao. Hata hivyo, wahojiwa walitoa taarifa kwamba mahusiano

kati ya jamii na Pori la akiba yalikuwa mazuri sana (Jedwali 11)

Jedwali 9. Ni akina nani wanawajibika na tembo?

Kiwango Wakala

1 Wizara ya Maliasili na Utalii

2 Serikali Kuu

3 Mapori ya Akiba

4 Wanakijiji

5 Serikali ya Kijiji

Page 12: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

11

Jedwali 10. Ni kwa jinsi gani Mamlaka zinazohusika zinafanya kazi?

Kiwango cha utendaji kwa mamlaka % Mwitikio

Mbaya sana 32

Mbaya 43

Kotekote 5

Mzuri 18

Mzuri sana 1

Jedwali 11. Mitazamo juu ya mahusiano kati ya Kijiji na Mamlaka ya Pori la Akiba

Mahusiano na Pori la Akiba % Mwitikio

Mabaya sana 17

Mabaya 4

kotekote 5

Mazuri 14

Mazuri sana 57

Sifahamu 2

Wahojiwa wengi (64%) walionyesha kuwa juhudi za kuzuia zililenga kupunguza upotevu wa mazao, kwa wakulima kuanzia chini kwenda kati (Jedwali 12). Pia kwenye vijiji hivyo kuna vijiji vilivyoathiriwa na migogoro ya watu na tembo (Rungwa na Dorotto) mawazo juu ya kiwango cha jiitihada ziligawanywa, kwa makadirio sawa ya idadi ya wahojiwa walitoa taarifa ya juhudi hafifu kama walivotoa taarifa za kati kwenda jiitihada za juu. Sababu kuu mbili kwa jiitihada za chini za kuzuia upotevu wa mazao, ni mkwamva watu walikuwa na hofu juu ya tembo na ufahamu kidogo kuhusiana na njia sahihi za uzuiaji. Njia kuu zinazotumika kwa sasa ni kupiga kelele, moto na ulinzi wakati wa usiku (Jedwali 13). Jedwali 12. Juhudi za wakulima za kuzuia upotevu wa mazao

Juhudi za kuzuia % Mwitikio

Hakuna jitihada 26

Jiitihada kidogo 32

Jiitihada za kati 32

Jiitihada kubwa 11

Jedwali 13. Njia zinazotumika na wakulima kukabiliana na tembo

Njia % Mwitikio

Kelele 84

Moto 56

Kulinda mashamba 56

Kutoa taarifa kwa mamlaka 11

Fensi 4

Page 13: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

12

Wengi wao wa wahojiwa (66%) waliona kuna umuhimu mkubwa kuboresha mahusiano kati ya watu na tembo ndani ya kijiji chao (Jedwali 14). Wazo hili lilitamkwa kwa mkazo mkubwa vijiji vya Rungwa, Dorotto, na Itagata. Kwa ujumla, kuna hisia chanya kwamba migogoro ya watu na tembo inaweza kushughulikiwa (Jedwali 15), na 62% ya wahojiwa walisema kwamba kuzuia migogoro ya tembo na watu inawezekana. Mawazo yaliyojirudia kwaajili ya njia za uzuiaji miongoni mwao wahojiwa ilikuwa ni ulinzi wa mashamba na mipaka ya Mapori ya Akiba, kuwatumia maaskari kuwafukuza tembo, kujenga fensi na vizuizi vingine kunzunguka mashamba, na Serikali kuchukua hatua (Jedwali 16). Jedwali 14. Maoni juu ya kama migogoro dhidi ya watu na tembo inaweza kushughulikiwa

Je ni muhimu kushughulikia migogoro ya tembo na watu? % Mwitikio

Sio muhimu 4

Muhimu kidogo 3

Sifahamu 3

Muhimu 25

Muhimu sana 66

Jedwali 15. Imani juu ya uwezekano wa kukabiliana na migogoro kati ya watu na tembo

Je inawezekana kukabiliana na migogoro baina ya tembo na watu? % Mwitikio

Haiwezekani kabisa 22

Inawezekani kwa kiasi 7

Sifahamu 9

Mara nyingi inawezekana 13

Inawezekana sana 49

Jedwali 16. Njia zilizo pendekezwa kutumika kukabiliana na tatizo

Njia za kukabiliana % Mwitikio

Kulinda mashamba na Mipaka ya Mapori ya Akiba 23

Askari kuwafukuzia tembo 19

Fensi na vizingiti vingine 18

Serikali kuchukua hatua 11

Elimu ya uhifadhi 9

Sifahamu 9

Askari kuwaua tembo 4

Kutoa taarifa kwenye mamlaka husika 3

Kuwapa uwezo wanakijiji kuwafukuzia mbali tembo 3

Shoroba ya tembo kuachwa wazi 1

Page 14: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

13

3.4 Maoni Juu ya Tembo na Mwingiliano Baina ya Watu na Tembo

Wahojiwa waliulizwa kuhusu ukubwa wa madhara tofauti ya tembo (Jedwali 17). Wahojiwa wengi (60%)

walisema misafara ya tembo ndani ya kijiji mbali na makazi halikuwa tatizo. Zaidi ya theluthi mbili ya

wahojiwa walisema upotevu wa mazao unaosababishwa na tembo, kuvunjwa kwa maghala ya chakula,

na misafara ya tembo kupita karibu na makazi ya watu lilikuwa ni tatizo kubwa sana. Kwa kuongezea,

73% ya wahojiwa walifikiri kwamba kuwaua tembo kwa ajili ya upotevu wa mazao lilikuwa ni tatizo

kubwa sana.

Jedwali 17. Mtazamo juu ya ukubwa wa athari za tembo

Sio tatizo

Ni tatizo kidogo Kotekote

Ni tatizo kubwa

Ni tatizo kubwa sana Sifahamu

Tembo kupita ndani ya kijiji mbali na makazi ya watu 60 5 1 12 22 0 Tembo kupita ndani ya kijiji jirani na makazi ya watu 2 4 0 24 67 1

Tembo kuharibu mazao 1 1 0 20 77 0 Tembo kuharibu maghala ya chakula 2 1 0 21 69 5 Kuuwa tembo wakati wanapovamia mazao 5 2 7 26 47 11

Kwa ujumla, wahojiwa wengi walidhani kwa sasa idadi ya tembo kwenye aridhi ya kijiji inazidi kuongezeka, wakati wahojiwa waliowengi hawakuwa na ufahamu wa idadi ya tembo kwenye Mapori ya Akiba na Tanzania kwa ujumla. Waliulizwa kuhusu idadi inayohitajika ya tembo, na 73% ya wahojiwa walisema wangehitaji tembo wapungue kwa kiasi kikubwa kwenye aridhi ya kijiji. Kwa heshima ya Mapori ya Akiba na nchi nzima kwa ujumla, 78% na 83% ya wahojiwa walihitaji namba ya tembo kuongezeka.

Jedwali 18. Mtazamo juu ya idadi ya sasa ya tembo

Mwenendo wa idadi ya tembo

Aridhi ya Kijiji

Pori la Akiba

Nchi

Inapungua sana 21 11 25

Inapungua kidogo 6 5 1

Imara 16 2 0

Inaongezeka kidogo 11 2 4

Inaongezeka sana 38 34 20

Sifahamu 8 46 48

Jedwali 19. Mtazamo juu ya idadi ya tembo inayotakiwa

Idadi inayohitajika Aridhi ya kijiji

Pori la Akiba

Nchi

Ipungue sana 73 12 6

Ipungue kidogo 1 2 0

Ibaki iliyopo 6 0 1

Iongezeke kidogo 4 1 1

Iongezeke sana 11 77 82

Sifahamu 5 7 8

Page 15: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

14

Japokuwa kuna wastani wa juu wa migogoro kati ya watu na tembo, mitazamo ya jamii kuhusu tembo

bado ni mtazamo chanya. Karibia ya theluthi mbili ya wahojiwa walikubali kuwa tembo ni mnyama mzuri.

Pia 56% ya wahojiwa walikubali kwa kuunga mkono kuwa tembo ni wa muhimu kwenye mazingira, na

93% walikubali na kuunga mkono kuwa tembo wanaongeza pato la Taifa kwa kupitia utalii. Utafiti wa

vijiji sita vinavyokaribiana na Pori la Akiba la Rungwa (Wilbright 2016) vilevile ilionyesha kwamba watu

wengi walikuwa na uelewa wa faida za uhifadhi, hasa mapato yatokanayo na utalii wa kuwinda

yanayofanyika kwenye Mapori ya Akiba. Kati ya mwaka wa fedha 2011/2012 na 2014/2015, Wilaya ya

Manyoni imeweza kupata Shilingi za Kitanzania 324,962,413 (ambazo ni sawa na Dola za Kimarekani

147,710) kutoka kwenye mapato ya uwindaji kwenda kufadhili mahitaji ya jamii (Wilbright 2016). Kwa

kuongezea, 87% ya wahojiwa walikubali kuwa kuna umuhimu wa kuwahifadhi tembo. Hata hivyo, 71% ya

wahojiwa walikubali kuunga mkono kuwa tembo wanawapa watu gharama, wakati 55% walikubaliana

kuwa tembo wanawapa watu binafsi faida. Zaidi ya nusu ya wahojiwa walikataa kuwa mahusiano kati ya

tembo na watu kuwa ni mazuri ndani ya kijiji.

Jedwali 20. Mitazamo juu ya kauli mbalimbali kuhusu tembo na mshikamano

Haikubaliki kabisa

Haikubaliki Sifungamani na upande wowote

Inakubalika Inakubalika sana

Sifahamu

Tembo ni mnyama mzuri 24 3 1 31 33 7

Tembo wananipa hasara 17 7 0 25 46 3

Tembo wananipa faida 32 4 0 29 26 7 Tembo ni muhimu kwa uhifadhi wa mazingira 23 2 0 28 38 7 Tembo wana faida kwa watu kwasababu ni kivutio cha utalii 1 0 0 38 55 2 Ni muhimu kuwahifadhi tembo 4 2 0 42 45 5 Mahusiano kati ya tembo na watu ndani ya kijiji ni mazuri 49 5 3 13 17 11

3.5 Shoroba na Misafara ya Tembo

Kulingana na wahojiwa 71%, tembo wanaokuja mara kwa mara kwenye kijiji chao wanatoka Mapori ya Akiba ya Rungwa, Kizigo na Muhesi. Kiasi kidogo cha wahojiwa walisema kwamba tembo walikuwa wakitoka upande wa Tabora (Wilaya ya Sikonge, vijiji vya Kilumbi na Kihombe).

Jedwali 21. Mahali ambapo tembo ilisemekana wanatoka

Chanzo % Wahojiwa

Pori la Akiba la Rungwa-Kizigo-Muhesi 71

Vijiji vya jirani 3

Wilaya ya Sikonge, Tabora 1

Vijiji vya Kilumbi na Kihombo (Tabora) 1

Rungwa North Open Area 1

Page 16: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

15

Ndani ya vijiji saba, zaidi ya nusu ya wahojiwa wanafahamu eneo la shoroba au njia za tembo, na wanafikiri kwa sasa bado zinatumika na tembo (Jedwali 22-23). Wahojiwa ndani ya vijiji vitano vinaonyesha kwamba matumizi ya hivi karibuni ya nji za tembo ni mwaka 2016, na ndani ya mwaka 2015 ndani ya vijiji viwili (Jedwali 24). Kila kijiji kilitoa maelezo ya mdomo ya njia za tembo na shoroba (Jedwali 25). Jedwali 22. Je unafahamu njia zinazotumika na tembo karibu na kijiji chako? (% majibu)

Kijiji namba Ndiyo Sifahamu

Dorotto 0 91 9

Itagata 33 44 22

Kalangali 50 50 0

Kayui 33 67 0

Kintanula 25 67 8

Makale 71 29 0

Mitundu 25 75 0

Mwamagembe 36 55 9

Rungwa 9 74 17

Jedwali 23. Njia hizi kwa sasa bado zinatumika na tembo?

Kijiji Namba Ndiyo Sifahamu

Dorotto 0 100 0

Itagata 0 100 0

Kalangali 0 50 50

Kayui 0 50 50

Kintanula 0 100 0

Makale 0 100 0

Mitundu 0 83 17

Mwamagembe 0 100 0

Rungwa 0 100 0

Jedwali 24. Ni lini ilikuwa mara ya mwisho misafara ya tembo kupita katika njia hizi?

Kijiji 2014 2015 2016

Dorotto 0 0 100

Itagata 0 25 75

Kalangali 50 0 50

Kayui 0 67 33

Kintanula 0 0 100

Makale 0 0 100

Mitundu 17 50 33

Mwamagembe 17 17 67

Rungwa 0 0 100

Page 17: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

16

Jedwali 25. Maelezo kuhusu njia na shoroba za tembo

Dorotto

Legeza mwendo, charcoaling camp (kambi ya mkaa)

Dalabeta-Msimbehe-Mkwegi-Ipunguli

Damweru-Kahomwe-Dorotto katikati-Msisi-Mwakitanda-Mkwegi-Ipunguli

Ipunguli, Mwakitanda

Ipunguli, Kenyekenye, Dorotto

Misisi, Kahomwee

Simbanguru-Chikola-Kiula-Mugandu-Dorotto katikati mwa upande wa kaskazini

Itagata

Italia-Mwakita-Muhesi

Mkwegi, charcoaling camp (kambi ya mkaa)

Pori la Akiba-Itagata-Tabora Reserve

Pori la Akiba Muhesi-Itagata-Ukimbu

Kalangali

Balabala ya Salada

Kati ya Kintanula na Tandamilomo

Tabora -Kalangali

Kayui

Isanzu na Mihama

Njarumono-Lulanga-Chaya

Njarumono -Chang'ombe-Kigoma-Mkwira

Njarumono-Itagata-Chaya

Kintanula

Itaga-mabonde-Miungu

Mwinuko wa Mkolole, Matumaini

Mpanda, Miungu, Kintanulayazamani

Pori la akiba -Mkolole (kanda)- Sehemu ya wazi kusini mwa Rungwa

Pori la Akiba -Mwabhuki-Kintanula

Pori la akiba-Mwauki (Kanda)- Sehemu ya wazi Kusini mwa Rungwa

Makale

Kaselya, Misonge

Matagata-Misiu-pori la akiba

Mitundu

Makale, Ipanduka

Pori la akiba-Mahinya-Makuga-Mitundu-Nzinge – Hifadhi

Pori la akiba-Itandamilo-Mitundu

Kati ya Makale na Mitundu

Mwamagembe

Pori la Akiba - Mikese (Shoroba) – Mwamagembe

Page 18: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

17

Rungwa

Pori la akiba- Cemetery (Makaburini) – Kijiji cha Rungwa

Pori la Akiba- Daraja la mkola A – Kijiji cha Rungwa

Itaga –Shule ya sekondari mkola

Itaga, Itangalala

Karibu na kanisa, Mkola B

Mimalaupene-Mansega

Msufini

Mkola A, Mahikwi

Station Useli

Njia ya tembo, kijiji cha Rungwa

Page 19: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

18

4. Mapendekezo

4.1 Maeneo ya Kipawombele Kufanyiwa Jitihada

Uchaguzi wa maeneo sahihi ya kukabiliana nayo na mbinu ni sanjari na historia ya hivi karibuni na ukubwa wa athari za tembo, ukaribu wa njia za tembo, upokeaji wa jamii kushirikiana kama wahojiwa kufanya kazi ya uhifadhi ni mzuri. Kwa kuzingatia uchunguzi wa upotevu wa mazao unaosababishwa na tembo na misafara ya tembo, tunapendekeza vijiji vinne ambavyo ni muhimu kukabiliana na migogoro ya watu na tembo:

Kipawombele namba 1: Rungwa na Dorotto

Kipawombele namba 2: Kintanula na Itagata

4.2 Mwingiliano Baina ya Watu na Tembo Kijiji cha Rungwa

Kulingana na matokeo ya tafiti hii na majadiliano yaliyofanyika kati ya WCS pamoja na uongozi wa Pori la

Akiba la Rungwa, STEP ilipendekeza kuelekeza jitihada zakupunguza athari za tembo ndani ya kijiji cha

Rungwa, ambacho kimepakana na Makao Makuu ya Pori la Akiba la Rungwa.

Rungwa ni kijiji kilichopo kwenye uwanda wa magharibi mwa mipaka ya Pori la Akiba la Rungwa. Baada

ya kumaliza tathimini, STEP walifanya mikutano na wananchi wa vitongoji vya Mkola, Stesheni na Itaga

mnamo tarehe 15 mpaka tarehe 17 ya mwezi wa kumi mwaka 2016. Lengo kuu la mikutano hiyo ilikuwa

ni kuwasilisha majibu ya tathimini iliyofanyika na kujifunza zaidi juu ya kiwango cha mwingiliano baina ya

watu na tembo ndani ya vitongoji hivyo vinavyo pakana na Pori la Akiba la Rungwa. Kijiji cha Rungwa kina

jumla ya idadi ya wakazi wapatao elfu sita, na idadi ya kaya ikiwa ni 1200. Upotevu wa mazao na upotevu

wa maghala kutokana na tembo ulitolewa taarifa ndani ya kijiji wakati wa mikutano. Mazao makuu

yakiwa ni mahindi, viazi vitamu, karanga, na ulezi. Tembo pia waliripotiwa kuvunjwa maghala ya chakula

na kuvunjwa paa za nyumba, na kushindania malisho na maji pamoja na mifugo. Kwa sasa, juhudi dhidi

ya uhifadhi wa mazao dhidi ya tembo ni kubwa, na wakulima wanatumia njia kama vile kupiga kelele,

moto, na wakulima kuyalinda mashamba yao nyakati za usiku, na kupiga mayowe. Hata hivyo, njia hizo

zimeonekana kushindwa kuzuia na kumaliza tatizo la tembo, na sababu kubwa ikiwa watu kuogopa

tembo, na ukosefu wa elimu juu ya njia sahihi za kumzuia tembo kuharibu mazao. Japokuwa Rungwa

kuna ukosefu na uhaba mkubwa wa maji, lakini ni sehemu muhimu sana ya ufugaji wa nyuki, na hii

inaonyesha kwamba njia ya utumiaji wa fensi ya mizinga ya nyuki kutumika kuzuia upotevu wa mazao na

maghala inaweza kuwa njia sahii, kama mizinga itakuwa na nyuki na fensi kutunzwa na kuhifadhiwa

vizuri.

Page 20: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

19

Chemchem na visima vya maji vinavyotumiwa na binadamu pamoja na tembo

Kitongoji cha Mkola

Kitongoji hiki kipo jirani sana na Pori la Akiba la Rungwa. Kitongoji kilitoa taarifa ya kiwango kikubwa cha

upotevu wa mazao, misafara mingi ya tembo kwa mwaka, upotevu wa maghala ya chakula na upotevu

wa paa za nyumba. Upotevu wa mazao unaosababishwa na tembo unatokea mwanzoni mwa kipindi cha

masika na kipindi cha kiangazi. Ndani ya mwaka 2016 zaidi ya kaya 30 waliathiriwa na upotevu wa

mazao, na maghala tisa kuvunjwa na tembo. Kukiwa hakuna matukio ya binadamu kujeruhiwa wala vifo

vya mifugo vinavyosababishwa na tembo. Sababu kuu ya misafara ya tembo kutoka kwenye Pori la Akiba

na kuingia kwenye aridhi ya kijiji ni uhaba ya maji na chakula kipindi cha kiangazi. Njia za kuzuia upotevu

zilizopendekeezwa na jamii wakati wa mikutano ni kama vile kuendelea kulinda mashamba, kuendlea

kupata msaada kwa maaskari wa Rungwa kufukuza tembo, pamoja na matumizi ya fensi.

Kitongoji cha Stesheni

Ndani ya Kitongoji hiki mwingiliano baina ya tembo na binadamu inazidi kuongezeka kutokana na ukaribu

wa Kitongoji na Pori la akiba la Rungwa, na kwa sababu hii inaonyesha umbali wa kiuhifadhi eneo

limekuwa ni tatizo la kuzuia upotevu wa mazao na uhaharibifu wa maghala ya chakula ndani ya kijiji

kutokana na ukaribu na watu wanaathiriwa zaidi ukilinganisha na watu wanaoishi mbali zaidi. Washiriki

walielezea kuwa upotevu wa mazao unatokea zaidi kipindi cha masika mpaka kipindi cha kiangazi kipindi

cha mavuno, na zaidi ya familia 37 ziliathiriwa na upotevu wa mazao. Ndani ya mwaka 2016 maghala

matatu yalivunjwa na tembo. Kukiwa hakuna matukio ya kujeruhiwa binadamu wala vifo

vilivyosababishwa na pasipo mifugo kupotea uhai kwa kusababishwa na tembo. Kwa sasa jitihada za

kuzuia upotevu wa mazao ni hafifu zinazojihusishwa na utumiaji wa njia za kimila zisizofanya kazi

kiusahihi kama vile kupiga kelele, moto na kuyalinda mashamba nyakati za usiku. Sababu kubwa ni watu

wanahofu juu ya tembo na ukosefu wa elimu kuhusu njia sahihi za kuzuia upotevu wa mazao.

Kitongoji cha Itaga

Kitongoji hiki kina sifa ya kuwa na makazi zilizoachana umbali mpaka kaya nyingine kutokana na kabila

kuu la Wasukuma ambao ni wafugaji na ni jamii inayohamahama. Katika Kitongoji hiki pia taarifa

zimeripotiwa kuwa na kiwango kikubwa cha upotevu wa mazao unaosababishwa na wanyama pori

akiwemo tembo na migogoro mingi kati ya binadamu na tembo ilianza mnamo mwaka 2012 mpaka sasa.

Familia zipatazo 15 zimeathiriwa na tembo kwa kuharibiwa mazao, kaya 3 kubomolewa, na maghala 9

kuvunjwa kabisa na mazao kuliwa mwaka 2016. Miitikio hii ilijionyesha dhahiri wakati wa mikutano

Page 21: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

20

iliyofanyika ndani ya Kitongoji, athari za mara kwa mara na kijiji kutoa taarifa ya namba kubwa ya

upotevu wa wa mazao na misafara ya tembo kwa mwaka, kuvunjwa kwa maghala na paa. Ikiwa hakuna

taarifa za binadamu kuuawa au kujeruhiwa na tembo, na hakuna vifo vilivyosababishwa na tembo na

wala hakuna mifugo iliyopotea kwa kusababishwa na tembo. Pia viongozi wa vijiji walitoa taarifa ya watu

na tembo kugombania maji (visima) na malisho ya mifugo. Wafugaji wamekuwa wakihamisha makazi yao

kwa hofu ya kukutana na tembo. Kwa kawaida upotevu wa mazao unaanza kutokea kipindi cha masika

mwezi wa pili mpaka kipindi cha kiangazi muda wa mavuno (kati ya mwezi wa pili na mwezi wa tatu

mpaka mwezi wa kumi na moja).

4.3 Mbinu za Kukabiliana na Athari za Tembo

Vizuuizi vya tembo vyenye msingi yake mashambani na nyumbani Kwenye maeneo yenye matukio mengi ya upotevu wa mazao, tunashauuri kuwawezesha wakulima kuzuia upotevu wa mazao kwa kutumia njia zenye misingi yake mashambani kama fensi za mizinga ya nyuki, ambapo kwa uzoefu wa STEP ni njia yenye ufanisi mkubwa wa kupunguza upotevu wa mazao ambapo mizinga itakuwa na nyuki na fensi kutunzwa vizuri.Fensi ya mizinga ya nyuki inafaida zaidi na kipato kinachotokana na asali,na ushiriki wa wakulima kwenye miradi ya fensi ya mizinga ya nyuki inaweza kuongeza Uvumilivu dhidi ya tembo.Mazingira ya Rugwa yenye misitu aina ya miombo ni bora kwa ufugaji wa nyuki ,na vijiji vingi vilivyofanyiwa tafiti Rungwa ikiwemo tayari kuna sekta za ufugaji wa nyuki kwa kutumia mizinga ya kienyeji.Ufugaji wa nyuki pia unahamasisha ulinzi wa mazingira na vyanzo vya maji,kwakuwa nyuki wanahitaji maji na chakula ili kujiimarisha na kustawi.

Fensi ya mizinga ya nyuki Mang’ula, Udzungwa (kushoto); Mizinga ya kienyeji kijiji cha Rungwa (kulia)

Njia nyingine ya kawaida ya kuzuia tembo ni fensi ya pilipili. Kufuatana na Semina zilizotolewa na Pori la Akiba la Rungwa kuhusu matumizi ya fensi ya pilipili, fensi ya pilipili mwanzoni ilifanyiwa majaribio na wakulima wachache ndani ya kijiji cha Rungwa. Fensi hiyo ya pilipili haikuweza kuzuia tembo kuingia mashambani, na wakulima walisitisha kuitumia.

Mashamba na nyumba zinaweza kulindwa dhidi ya madhara ya tembo kwa kutumia kinyesi cha tembo kilichochanganywa na pilipili na kisha kukaushwa na kuchomwa ambapo huweza kuzalisha moshi ndani ya masaa 8 na kuzuia tembo kwa moshi unaozalishwa wenye pilipili. Matofali haya ya pilipili na kinyesi cha tembo kwa sasa yamefanyiwa majaribio na mradi wa Eco-Exit nchini Botswana. Pia, uvunjwaji wa maghala ya chakula unaweza kupunguzwa kwa kujenga maghala ya kuzuia tembo kwenye kaya. Maghala haya yanamuundo imara ambapo tembo hawataweza kuyafikia mazao kiurahisi, na pia inapunguza harufu ya chakula kutoka nnje ambayo itawavutia tembo. Maghala haya yakuzuia tembo kwasasa yamefanyiwa majaribio na Mradi wa South Luangwa Conservation Society nchini Zambia na kunaonyesha kiasi kikubwa cha mafanikio andapo maghala yatatunzwa vizuri.

Page 22: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

21

Ghara la kuzuia tembo (kushoto); matofali ya kutengenezwa na pilipili pamoja na kinyesi cha tembo

(kulia)

Ufuatiliaji wa tembo kwa jamii

Utaratibu wa utoaji taarifa za misafara ya tembo na upotevu wa mazao utatathimiwa kwa kufuatilia

mwingiliano wa watu na tembo kwa muda mrefu, na pia kwa ajili ya kuamua maeneo ambayo ni muhimu

kuchukuliwa hatua zaidi.

Njia mbadala ya Tembo kuwapa Maji

Ukosefu wa maji kipindi cha kiangazi ndani ya eneo la Pori la Akiba la Rungwa karibu na kijiji cha Rungwa

(iliripotiwa kuwa chanzo cha maji kilicho jirani ilikuwa ni umbali wa kilometa 40) inawezekana ikawa

sababu inayopelekea tembo kutoka ndani ya hifadhi, na kwakuwa tembo wanahitaji maji kilasiku.

Kuwepo kwa njia mbadala ya vyanzo vya maji kwaajili ya tembo kupata maji ndani ya Pori la Akiba

inaweza kupunguza misafara ya tembo kwenda kwenye chem chem na visima vya kijiji kwaajili ya

kujipatia maji. Bwawa au sdimbwi la maji lakutengenezwa linaweza kujengwa ndani ya Pori la Akiba

kwamadhumuni hayo. Bwawa la maji mwanzoni lilikuwepo karibu na makao makuu ya poli mnamo

mwaka 1990 na iliripotiwa kuwa lilitumika na tembo pamoja na wanyamapori wengine, lakini bwawa hili

lilikauka baada ya mto Rungwa kubadili mkondo wake (mazungumzo binafsi na S. Kabanda). Mradi huu

utakuwa wamafanikio zaidi kama utafanikiwa kusambaza maji ya kuaminika ndani ya kijiji cha Rungwa.

Matumizi ya aridhi na mipango ya kuunganishwa na kujenga uhusiano Aidha, tunaamini kwamba mshikamano wa mda mrefu baina ya watu na tembo unapaswa kushirikisha

zaidi mipango ya matumizi ya aridhi na uudwaji wa shoroba za wanyama pori. Kusimamia misafara ya

tembo nje ya maeneo ya uhifadhi ili kupunguza upotevu wa mazao utokanao na kusambaa kwa tembo

na uhamiaji, vijiji vinaweza kuzingatia kuacha sehemu ya aridhi inayotenganisha maeneo ya uhifadhi na

maeneo ya kijiji kwaajili ya misafara ya tembo katika maeneo ambayo yako mbali na makazi ya watu na

mashamba ya watu.

Page 23: Tathmini ya Mahusiano Baina ya Watu na Tembo karibu na … · 2020. 3. 6. · 2 Muhtasari Tulifanya utafiti juu ya mahusiano baina ya watu na tembo katika vijiji tisa vinavyopakana

22

5. Marejeo

Coppolillo, P. (2004). A preliminary situation analysis for the Rungwa-Ruaha landscape, Tanzania. A

report to WWF International “Improving Conservation and Development within Ecoregions Programme.”

<http://www.coppolillo.com/uploads/1/1/2/3/11231708/wwf-report-situationanalysis30sep04.pdf>

Accessed 01/10/2016.

The Planning Commission of Dar es Salaam and Regional Commissioner’s Office Singida (1997) Socio-

Economic Profile of Singida Region http://www.tzonline.org/pdf/singida1.pdf Accessed 04/10/2016.

Research and Analysis Working Group (2005). Poverty and Human Development Report 2005. Poverty

Monitoring System of the Government of Tanzania. Dar es Salaam, Tanzania.

<http://www.repoa.or.tz/documents/PHDR_2005_Prelim.pdf> Accessed 01/10/2016.

Thouless CR, Dublin HT, Blanc JJ, Skinner DP, Daniel TE, Taylor RD, Maisels F, Frederick HL, Bouché PJC.

(2016). African Elephant Status Report 2016: an Update from the African Elephant Database. Occasional

Paper Series of the IUCN Species Survival Commission, No. 60 IUCN/SSC Africa Elephant Specialist Group,

IUCN, Gland, Switzerland. Vs + 309 pp.

Munuo, W. (2016) Distribution Patterns of Human Elephant Conflict in Areas Adjacent to Rungwa Game

Reserve, Tanzania. MSc Thesis submitted to the Norwegian University of Science and Technology,

Norway.