fataawa za wanachuoni (32)

36
1 علماء ال فتاوىFataawa Za Wanachuoni [32] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

Upload: wanachuoni

Post on 13-Apr-2015

324 views

Category:

Documents


20 download

DESCRIPTION

Fataawa Za Wanachuoni (32)

TRANSCRIPT

Page 1: Fataawa Za Wanachuoni (32)

1

فتاوى العلماءFataawa Za Wanachuoni

[32]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Wanachuoni (32)

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 3: Fataawa Za Wanachuoni (32)

3

Fataawa zilizo:

1) Lini Mtu Anaomba Du´aa Ya Istikhaarah?

2) Kutoka Katika I´tikaaf Na Kwenda Kuswali Tarawiyh Msikiti Mwingine

3) Kuinua Kidole Wakati Wa Kusema "Laa ilaaha Illaa Allaah"

4) Inafaa Kumuuliza Mtu, Vipi Imani Yako?

5) Yule Asiyewafanyia Tabdiy´ Watu Wa Bid´ah

6) Vijana Wanavyowekwa Mtegoni Kwa Mawaidha Ya Visa

7) Wale Wanaosema Kuwa Shaykh al-Albaaniy Ni Murji´iy

8) Uwajibu Wa al-Ikhwaan al-Muslimuun Na Jamaa´at-ut-Tabliygh

9) Mume Anataka Mke Avae Suruwali

10) Mtoto Wa Baba Mdogo Ni Mahram?

11) Mbinu Za Hizbiyyuun Kumbadiy´ Imaam Ibn Hajar Na an-Nawawiy

12) Makatazo Ya Kumuacha Mke Na Mtumishi Mwanamume

13) Majumba Yaliyojengwa Kwenye Makaburi Ya Mawalii

14) Kuuza Manukato Ambayo Yana Alcohol

15) Kusoma al-Mu´awidhaat Mchana Wakati Wa Kulala

16) Kusikiliza Mikanda Ya ´Aa´idh al-Qarniy Na Twaariq as-Swaydaan

17) Kusherehekea Mwaka Wa Hijriyah Na Kuzaliwa Na Kupeana Pongezi

18) Kumkosoa Mtawala Juu Ya Minbar

19) Kujumuisha Swalah Wakati Wa Mvua, Upepo Na Barafu

20) Je Kuna Kundi Linaitwa Jaamiyyah? Na Ni Nani Shaykh Muhammad al-Jaamiy?

21) Ipi Tofauti Kati Ya ´Aqiydah Na Manhaj?

22) Inajuzu Kula Samaki Maiti Ambayo Haikuchinjwa?

23) Hukumu Ya Mwenye Kumtukana Allaah Na Mtume Wake

24) Shaykh Fawzaan Kuhusu Radd Kwa Sayyid Qutwub

25) Umuhimu Wa Kuhifadhi Swalah Ya Dhuhaa

26) Kabla Ya Kutumwa Mtume Watu Walikuwa Katika Dini Ya Nani?

27) Je Sigara Inavunja Wudhuu? Na Ipi Hukumu Ya Sigara Na Bangi?

28) Nasaha Kwa Dada Wapya Waliyoingia Katika Uislamu -1-

29) Nifuturu Nyumbani Kwangu Au Msikitini Nikaapo I´tikaaf?

30) Nasaha Kwa Dada Wapya Waliyoingia Katika Uislamu -2-

31) Mume Kamlaani Mke Wake, Je Mke Katalikika?

32) Mavazi Yenye Picha Za Watu Na Minyama Na Maneno Mabaya

33) Kuna Aina Tatu Kwa Wenye Kuyatembelea Makaburi

34) Kutabaruku Kwa Mabaki Ya Mtume ( وسلم عليه هللا صلى )

35) Jinsi Ya Kuweka Nia Unapotaka Kuanza Kukaa I´tikaaf

36) Inajuzu Mume Kumkabili Mke Wake Usoni?

37) Hukumu Ya Mtu Mwenye Kuitukana Dini

38) Inajuzu Kwa Mwanamke Kufanya Kazi Ya Uuguzi Katika Mji Wa Kikafiri?

39) Muislamu Kupenda Nchi Ya Kikafiri

40) Mambo Gani Yanayofanya Mwanamke Akawa Na Msimamo Katika Dini?

41) Kuwa Na Subira Katika Da´wah Kwa Kupewa Mitihani

42) Kuna Mpaka Wa Mtu Kukaa Itikaaf Msikitini?

Page 4: Fataawa Za Wanachuoni (32)

4

43) Ipi Faradhi Ya Kwanza Kubwa?

44) Hukumu Ya Kuhudhuria Janaza Na Kuwasalia Watu Wa Bid´ah

45) Amevaa Soksi Kisha Akazivua, Vipi Wudhuu Wake?

Wanachuoni waliomo:

1) ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy

2) ´Allaamah ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad

3) ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy

4) ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

5) ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy

6) ´Allaamah Zayd bin Haadiy al-Madkhaliy

7) ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Waswaabiy

8) Shaykh ´Ubayd bin ´Abdillaah al-Jaabiriy

Page 5: Fataawa Za Wanachuoni (32)

5

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1) Lini Mtu Anaomba Du´aa Ya Istikhaarah?

Swali:

Lini mtu anasoma Du´aa ya Istikhaarah, je inasemwa ndani ya Swalah au

baada ya Swalah?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni baada ya kutoa Salaam.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5485

2) Kutoka Katika I´tikaaf Na Kwenda Kuswali Tarawiyh Msikiti

Mwingine

Swali:

Nataka kukaa I´tikaaf kwa sharti niswali Tarawiyh katika Msikiti mwingine

kutokana na kisomo cha Imamu huyo, je inajuzu kwangu kufanya hivyo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Inajuzu kwako, ila kuacha ni bora zaidi. Bora kwako ni wewe kuswali

Tarawiyh katika Msikiti ambao unafanyia I´tikaaf. Hili ndo bora ili ubakie

Msikitini ambapo wewe unafanyia I´tikaaf.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2658

Page 6: Fataawa Za Wanachuoni (32)

6

3) Kuinua Kidole Wakati Wa Kusema "Laa ilaaha Illaa Allaah"

Swali:

Je kunyanyua (kuinua) kidole cha Shahadah wakati wa kusema "laa ilaaha illa

Allaah" ni katika Sunnah?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kumepokelewa katika hili Athaar, kunyanyua kidole wakati wa Tashahhud

na kukitikisa kumepokelewa Hadiyth hata kama [baadhi yazo] ni dhaifu. Ama

kukitikisa ni wakati wa Du´aa. Atakayeshahidilia laa ilaaha illa Allaah na

akapandisha kidole hakuna ubaya kwake.

Chanzo: http://youtu.be/Ey6xPqior08

4) Inafaa Kumuuliza Mtu, Vipi Imani Yako?

Swali:

Je ibara hi ni nzuri "Vipi Imani yako"? Na je ni katika Sunnah?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kutasaahul huku hakuna faida, [kumuuliza mtu] "vipi Imani yako?" Imani

anaijua Allaah (´Azza wa Jalla) ndani ya moyo, [kinachotakiwa] ni

kunasihiana. Wakikutana Waislamu wawili, kinachojulikana ni kila mmoja

kumpa nasaha mwenziwe kwa kuwa na subira katika Dini na kuwa na

uthabiti na kuwalingania watu kwayo. Na imepokelewa kuwa Salaf

(Maswahabah) walikuwa hawaachani wanapokutana mpaka wasome kwanza

Suurat al-´Aswr:

Page 7: Fataawa Za Wanachuoni (32)

7

"Naapa kwa Zama! Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara, Ila

wale walioamini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na

wakausiana kusubiri.” (103:1-03)

Chanzo: http://youtu.be/8XzIxfQ3TDI

5) Yule Asiyewafanyia Tabdiy´ Watu Wa Bid´ah

Swali:

Ulisema jana kuwa yule ambaye hambadiy´ mtu wa Bid´ah haingii katika

mkumbo wa watu wa Bid´ah na si lazima amfuate yule anayembadiy´. Na

baadhi ya wanachuoni wanasema yule ambaye hambadiy´ mtu wa Bid´ah

anaingia katika mkumbo wao. Je, tofauti katika hili ni ya lafdhi tu?

´Allaamah ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad:

Kuna watu wa Bid´ah ambao Bid´ah zao na mambo yao yako wazi. Wako

mbali kabisa na Ahl-us-Sunnah na si hata katika Ahl-us-Sunnah bali

wanaiharibu hata Sunnah. Sunnah iko huko na wao wako kule. Watu hawa

yule asiyewabadiy´ bila shaka naye ni Mubtadiy´. Ama watu ambao ni katika

Ahl-us-Sunnah na wakaanguka katika kitu kama kosa au ufahamu wa

makosa, watu hawa si kama wale wa kwanza. Hapa mtu hawezi kusema yule

asiyemfanyia Tabdiy´ huyu ni Mubtadiy´.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127855

6) Vijana Wanavyowekwa Mtegoni Kwa Mawaidha Ya Visa

Swali:

Page 8: Fataawa Za Wanachuoni (32)

8

Ipi nasaha yako kwa vijana wengi ambao wamejishughulisha sana kusambaza

mikanda ya wapiga visa na watoa mawaidha na wanapuuza kusambaza

mikanda ya kielimu (ya wanachuoni)?

´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy:

Yule anayejishughulisha na mikanda hii, mikanda ya watoa mawaidha ambao

naamini wamewawekea daraja watu wa Bid´ah na mapote... Watu wa Bid´ah

na mapote wanapata nguvu kwa sura ya watu hawa. Wanawawinda vijana.

Wanaanza kwa mawaidha, kulia, unyenyekevu. Wanajidhihirisha namna hii

mbele ya vijana. Pindi wanapojisikia salama na hakika kwao, wanawaweka

katika nafsi zao utata na wanawatuma kwa hao ambao wamewapa kazi hio ya

kuwawinda [hawa] vijana. Na ndo maana utaona hawa watoa mawaidha

wamejidhatiti ima kwa pote potofu au makundi maangamivu. Hukuti Salafiy

humo, na wala hawana uhusiano na Salafiyyuun. Bali wanawafanyia shere na

hila Salafiyyuun na wanatahadharisha kupita njia yao. Wanasema wanakaza

sana, matusi na kadhalika. Na wanawasahilishia watu kutumbukia na watu

wa Bid´ah.

Mimi ninawanasihi vijana Masalafiy kujishughulisha na elimu sahihi na

Manhaj ya Salaf sahihi. Ikiwa wanataka mawaidha, yapo katika Kitabu cha

Allaah, kama wanataka elimu ipo katika Kitabu cha Allaah na Sunnah za

Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kama mlivosikia katika

Hadiyth ya al-´Irbaadh Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa

anapotoa mawaidha, nyoyo zinatetemeka na macho yanatiririka machozi. Na

wakati mwingine walikuwa wakilia sana. Atakayesoma kwa mfano Riyaadh-

us-Swaalihiyn ataona kuwa kuna yakutosheleza katika Sunnah za Mtume wa

Allaah ili mtu asiwe na haja ya kuwasikiliza watu kama hawa.Na mawaidha

yao unakuta yamejaa Bid´ah, ukhurafi na Hadiyth dhaifu na za kuundwa.

Yote ni kwa kuwa hawa Madu´aat si maulamaa. Na Salaf walikuwa

wakiwadharau hawa wapiga visa, wakitahadharisha watu dhidi yao na uongo

wao. Kwa masikitiko makubwa ni hivyo! Kwa hali yoyote Manhaj ya Salaf iko

wazi. Na tunawanasihi vijana kama kweli wanataka mawaidha na mafunzo,

yapo ya kutosha katika Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume wa Allaah

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Page 9: Fataawa Za Wanachuoni (32)

9

Aliulizwa Abuu Haatim kuhusu vitabu vya al-Haarith al-Muhaasibiy.

Alikuwa ni mjuzi, mchaji Allaah kuliko watu hawa watoa mawaidha. Na

alikuwa mbali kabisa na Bid´ah kuliko watu hawa. Kulipatikana katika vitabu

vyake kitu kama Taswawwuf ambayo haiwezi kukosa katika mawaidha ya

watu hawa.

Aliulizwa Abuu Zur´ah, Imaam mkubwa wa Sunnah kuhusu vitabu vya al-

Haarith.

Akasema: "Viacheni. Ni vitabu vya upotofu na Bid´ah." Wakasema vina

mafunzo.

Akasema: "Yule ambaye hakupata mafunzo katika Kitabu cha Allaah, hawezi

kamwe kupata mafunzo kwa hivyo."

Ndugu! Hii ndo Manhaj ya Salaf! Walikuwa wakitahadharisha vitabu vya

watu wa Bid´ah na mtu kuviangalia. Na walikuwa wakitahadharisha falsafa

kwa kuwa ni Bid´ah na upotofu. Shikamaneni na Kitabu cha Allaah na Sunnah

za Mtume Wake na Manhaj ya Salaf-us-Swaalih. Wallaahi naapa yule ambaye

kaanguka kwa watu hawa atakuja kupotea. Na mwenye kufaulu ni yule

mwenye kuchukua funzo kwa makosa ya wengine. Chukueni funzo kwa

vijana waliopotea waliokuwa katika Manhaj ya Salaf. Mwisho wao uliishia na

taawili potofu na propaganda za batili mpaka hapo walikuja kuwa maadui

wakubwa wa Ahl-us-Sunnah.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=123813

7) Wale Wanaosema Kuwa Shaykh al-Albaaniy Ni Murji´iy

Swali:

Kuna baadhi ya watu wanasema kuwa Shaykh al-Albaaniy ni Murji´iy.

Unasema nini kuhusu hili?

´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy:

Page 10: Fataawa Za Wanachuoni (32)

10

al-Albaaniy ni mwanachuoni katika maulamaa wa Sunnah, na Imaam

mkubwa katika maimamu wa Sunnah. Katumia maisha yote kulingania katika

Sunnah. Katumia zaidi ya miaka sitini kwa kutumikia Sunnah za Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ana vitabu kuhusu ´Aqiydah, na ana

vitabu vinavyosafisha Sunnah za Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) katika Hadiyth dhaifu na zilizoundwa. Ni nyingi sana. Na ana

vitabu vya Hadiyth Swahiyh na ni mijaladi mikubwa. Pia katumikia Sunnah

kwa njia zingine. Isitoshe alihakiki vitabu vingi vya Salafiyyah. Ana vitabu

kuhusu ´Aqiydah, [kwa mfano] "Tahdhiyr-us-Saajid min Ittikhaadh-il-Qubuur

Masaajid, "at-Tawassul-Anwaa´uh wa Ahkaamuh", "al-Aayaat al-Bayyinaat"

na sherehe na taaliki zake katika al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah". Alihakiki

vitabu vingi vya Iymaan, kama kitabu cha Imaam Abu ´Ubayd al-Qaasim bin

Sallaam, Ibn Abi Shaybah na Ibn Taymiyyah (Rahimahumu Allaah).

Kaitumikia Sunnah kwa kitabu "Manzilat-us-Sunnah Fiyl-Islaam", "Difaa´

´anal-Hadiyth an-Nabawiy" na "al-Hadiyth Hujjah fiyl Nafsih fiyl´-´Aqaa´id

wal-Ahkaam". Ni Radd kwa watu wa Bid´ah. Katika vitabu hivi kuna Ruduud

kwa Murji-ah na wengineo. Alikufa baada ya kuupiga vita Uirjaa´ na Murji-

ah. Yule anayesema kuwa ni Murji´iy, yeye ndo Khaarijiy mpotofu. Wamche

Allaah watu hawa na waseme ukweli. Waache kumsema vibaya mtu huyu na

mfano wake. Wahifadhi ndimi zao. Ni katika maimamu wa Sunnah. Sijawahi

kuona yeyote katika karne hizi za mwisho akipigana na Bid´ah kama yeye.

Vitabu vyake vingi kama "Swifah Swalat-in-Nabiyy" na "Hajjat-un-Nabiyy" na

vinginevyo, anahitimu kwa kuwashambulia watu wa Bid´ah. Kweli mtu

anaweza kusema kama huyu mtu ni wa Bid´ah na Murji´iy? Kamwe maishani.

Chanzo:

http://www.sahab.net/forums/index.php?s=912150d01f48950f1dec3ef1af7c98ab

&showtopic=127805

8) Uwajibu Wa al-Ikhwaan al-Muslimuun Na Jamaa´at-ut-Tabliygh

Swali:

Page 11: Fataawa Za Wanachuoni (32)

11

Ulisema katika darsa iliopita kuwa kundi la al-Ikhwaan al-Muslimuun na

Jamaa´at-ut-Tabliygh si katika makafiri, bali ni katika Ahl-ul-Bid´ah. Je, ni

katika makundi mapotofu yatayoangamia kama ilivyokuja katika Hadiyth ya

mgawanyiko?

´Allaamah al-Fawzaan:

Sikumbuki kama nilisema kauli hii, ila maana yake [kauli hii] ni sahihi. Si

makafiri In Shaa Allaah. Lakini wako na wanaenda kinyume kutokana na

Manhaj ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Da´wah, wako na

mambo wanaenda kinyume. Ni wajibu kwao kusahihisha makosa yao na

wawe katika Manhaj sahihi - Manhaj ya Da´wah na walinganie katika

Tawhiyd na wakataze Shirki. Huu ndo wajibu. Lakini hatujawahi kusikia

wakikataza Shirki, na wala hatujawahi kusikia wakilingania [watu] katika

Tawhiyd. Huu ni upungufu mkubwa na Da´wah haiwezi kuwa sahihi kwa

mfumo huu.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127630

9) Mume Anataka Mke Avae Suruwali

Swali:

Ipi hukumu ya kuvaa suruwali mbele ya mume kwa lengo la kumpambia tu

na si [kwa lengo] la kujifananisha [na makafiri]?

Shaykh Dr. ´Ubayd bin ´Abdillaah al-Jaabiriy:

Haya ni maneno yako wewe. Makusudio hayahalalishi kilichokatazwa. Kuvaa

suruwali mbele ya mume au wengine, huku ni kujifananisha na makafiri.

Isitoshe si hata nzuri kwa kuwa inadhihirisha uchi wa mwanamke au nusu ya

uchi wake, jambo ambalo ni baya. Na si katika ada ya wanawake wa Kiislamu,

si wa mama wa Waislamu wala baada yao kutokana na tunayojua. Na wala

Page 12: Fataawa Za Wanachuoni (32)

12

sijasoma kama kuna mwanachuoni katoa Fatwa ya kujuzisha hilo. Mwanamke

anatakiwa kuvaa vazi la wasaa. Ni kweli mbele ya mume hahitaji kuwa na

mtandio, hahitaji Jilbaab. Anaweza kudhihirisha baadhi ya ´Awrah

anapokwenda huku na kule. Hili si katika mapambo hata kama baadhi ya

watu wajinga watamtaka asifanye hivyo, ima kwa ujinga au kwa Taqliyd kwa

baadhi ya watu wamakosa ambao wanafuata kichwa wana-askari wa kikafiri

wa mashariki na magharibi. Sisi tunawanasihi mabanati wetu wa kiislamu

wajifananishe na Waislamu wa kwanza katika wamama wa Waislamu (wake

za Mitume), Maswahabah wa kike, waliokuja baada yao na wa baada yao. Iwe

kwenu, kwetu na katika kila kona ya Kiislamu hata walioko nje kuwa na

wanawake wazuri wanaoelewa Sunnah na waipende. Hivyo wasije kuwaiga

makafiri.

Muulizaji:

Shaykh ikiwa mume atamuomba hili, na kuwa jambo hili analichukulia

pambo kwake [mume].

Shaykh Dr. ´Ubayd al-Jaabiriy:

Huyu kageuzwa nyuma na mbele. Huyu kapinda na ni mjinga. Na nadhani ya

kwamba kakuzwa kwa musalsalaat (series) na programu za uchi

zinazorushwa kwenye Video na nyinginezo. Mimi namnasihi amche Allaah

(´Azza wa Jalla) kwa mke wake na amsaidie kwa kumcha Allaah. Wala

asimtii. Kwa kuwa hakuna utiifu kwa kiumbe kwa kumuasi Muumba.

Kujifananisha na makafiri ni jambo limekatazwa.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127839

10) Mtoto Wa Baba Mdogo Ni Mahram?

Swali:

Page 13: Fataawa Za Wanachuoni (32)

13

Je, mtoto wa mama yangu mdogo ni katika Mahram wangu, na inajuzu

kukabiliana naye uso?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ndio, kwa kuwa ni katika Mahram wako. Maadamu ni Mahram wa baba yake

basi atakuwa Mahram wake [huyo mwanaume pia].

Chanzo: http://youtu.be/lha0R_pgG7M

11) Mbinu Za Hizbiyyuun Kumbadiy´ Imaam Ibn Hajar Na an-Nawawiy

Swali:

Hizbiyyuun wanasema, kwa nini mnatahadharisha watu dhidi ya vitabu vya

Qutbiyyuun na Suruuriyyuun na hamtahadharishi dhidi ya vitabu vya Ibn

Hajar na an-Nawawiy kwa kuwa nao walikosea katika masuala ya ´Aqiydah?

´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy:

Maneno ya ajabu kabisa ya kuchekesha. Ni kweli enyi ndugu. Hivi kweli

tunaweza kulinganisha vitabu vya Sayyid Qutwub, au Muhammad Suruuriy

na mtu kama Imaam an-Nawawiy, Ibn Hajar? Kamwe maishani! Hawa ni

wapotofu masikini, na wale ni maimamu wakubwa wenye hadhi kabisa na

waaminifu. Ibn Hajar ni mwanachuoni wa Hadiyth na sidhani kama kutakuja

baada yake ambaye anaweza kuchukua nafasi yake. Hali kadhalika an-

Nawawiy ambaye ni mwanachuoni katika Fiqh na ana ufahamu mkubwa sana

fani hii. Ahl-us-Sunnah walibainisha makosa ya Ibn Hajar na an-Nawawiy

katika vitabu maalum, Allaah Awajaze maulamaa wetu kheri. Ama nyinyi

hamna hadhi hio ya watu kujishughulisha na vitabu vyenu. Ni kina nani

nyinyi? Karibu Uhizbiyyah utaisha hivi punde.

Page 14: Fataawa Za Wanachuoni (32)

14

Chanzo: http://aloloom.net/show_sound.php?id=8677

12) Makatazo Ya Kumuacha Mke Na Mtumishi Mwanamume

Swali:

Ikiwa [mume] siniko nyumbani na kuko mke wangu na watoto wake wadogo,

inajuzu kwa mtumishi kuingia nyumbani kwa ajili ya kufanya usafi

nyumbani?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Nyumba ikiwa imejaa wanawake hakuna ubaya kuingia. Ama ikiwa ni baina

yake [mtumishi] na huyo mwanamke haijuzu kwake kuingia. Haijuzu kwa

mume kuridhia hili.

Muulizaji:

Mke wangu yuko nyumbani na watoto wadogo.

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Sio Mahaarim wake [hao watoto wadogo].

Chanzo: http://youtu.be/DQt3tcsOIyY

13) Majumba Yaliyojengwa Kwenye Makaburi Ya Mawalii

Swali:

Page 15: Fataawa Za Wanachuoni (32)

15

Katika mji wetu kuna majumba ambayo yamejengwa kwenye makaburi ya

mawalii. Lakini hakuna anayeswali hapo wala kufanya chochote,

yamefungwa. Miaka kadhaa ya nyuma walikuwa wakiyafanyia ziara, ila kwa

sasa imesimama. Je, ni wajibu kuyabomoa au kuyaacha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni wajibu kuyabomoa na wala haijuzu kuyaacha, lakini wasiyabomoe ila

wenye mamlaka, mtawala. Haijuzu kwa watu wa kawaida kuyabomoa, kwa

kuwa hili litapekelea katika fitina na shari. Yabomolewe na mtawala wa

Waislamu baada ya mashauriano na wanachuoni.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127695

14) Kuuza Manukato Ambayo Yana Alcohol

Swali:

Ipi hukumu ya kuuza (manukato yaitwayo) "Kaaloniyaa" kwa ajili ya

kuitumia wakati wa kunyoa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Tumeshataja Hadiyth kuhusiana na kaaloniyaa na kwamba inakuwa na

chembe za pombe, hivyo haijuzu kuuza pombe kwa hali yoyote. Na ni juu ya

mtu kujiepusha na vitu vyote vya Haramu na afanye yale ambayo ni Halali

yako wazi, na ajiepushe na mambo yenye utata.

Chanzo: http://youtu.be/yVNbbDlRRd4

Page 16: Fataawa Za Wanachuoni (32)

16

15) Kusoma al-Mu´awidhaat Mchana Wakati Wa Kulala

Swali:

Je mtu anasoma al-Mu´awidhaat (al-Ikhlasw, al-Falaq na an-Naas) wakati wa

kulala tu usiku au wakati wowote anapolala mtu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Akisoma mtu wakati wa kulala kwake mchana, hakuna ubaya kwako kwa

kuwa ni kinga kwa Allaah kutokana na Mashaytwaan wa kijini na wa

kibinaadamu. Na ni jambo zuri kwa Muislamu.

Chanzo: http://youtu.be/ymlV774xPpU

16) Kusikiliza Mikanda Ya ´Aa´idh al-Qarniy Na Twaariq as-Swaydaan

Swali:

Yapi maoni yako kusikiliza mikanda yote ya ´Aa´idh al-Qarniy na Twaariq as-

Swaydaan?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Sionelei na wala siwezi kumpa Fatwa yoyote ya kujuzisha kusikiliza mikanda

ya ´Aa´idh al-Qarniy wala Twaariq as-Swaydaan.

Chanzo: http://youtu.be/SqjXLIElqQs

17) Kusherehekea Mwaka Wa Hijriyah Na Kuzaliwa Na Kupeana

Pongezi

Page 17: Fataawa Za Wanachuoni (32)

17

Swali:

Ipi hukumu ya kusherehekea sikukuu za mwaka mpya wa Kiislamu na

sherehe za kuzaliwa?

´Allaamah Zayd al-Madhkhaliy:

Sikukuu hizi hazina asili katika Shari´ah ya Kiislamu. Bali katika Shari´ah ya

Kiislamu kuna sikukuu (´Iyd) mbili, ´Iydi al-Fitwr na ´Iyd al-Adhwhaa.

Sikukuu zisizokuwa hizo hazina asili bali ni katika Bid´ah, kutahadharishwe

kwazo na Muislamu atahadhari kutozishiriki.

Muulizaji:

Hukumu ya kupeana pongezi kwa kuzaliwa na kwa mwaka mpya?

´Allaamah Zayd al-Madhkhaliy:

Hapana, wasipeane watu pongezi ila tu kwa ´Iyd al-Adhwhaa na ´Iyd al-

Fitwr.

Chanzo: http://youtu.be/-emr5Gww6cY

18) Kumkosoa Mtawala Juu Ya Minbar

Swali:

Je ni katika Manhaj ya Salaf kumhukumu mtawala, kusema makosa yake na

kumsengenya katika mimbar? Ni vipi Manhaj Salaf katika kuwanasihi

watawala, na inakuweje?

Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz:

Page 18: Fataawa Za Wanachuoni (32)

18

Swali hili limeulizwa zaidi ya mara moja. Si katika Manhaj ya Salaf kutaja

makosa ya mtawala katika minbar. Kwa kuwa hili linapelekea katika migomo

na watu kuacha kutii katika mambo mema. Hili linapelekea katika madhara

na halinufaishi. Njia ya Manhaj ya Salaf ni kumnasihi kisiri, kumwandikia au

unawasiliane na maulamaa kisha watamwasilia hivyo ili wamuelekeze katika

kheri. Madhambi yatajwe bila ya kumtaja mtendaji. Zinaa, pombe na Ribaa

vikatazwe bila ya kumtaja mtendaji, maasi yakatazwe bila ya kumtaja

mtendaji - bila kujali sawa ni mtawala au mwingine yeyote. Fitina ilipopamba

moto wakati wa ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anhu), walisema baadhi ya

watu kumwambia Usaamah bin Zayd (Radhiya Allaahu ´anhu):

"Je humkatazi ´Uthmaan?" Akasema [Usaamah]: "Nimkataze mbele ya watu?

Nitamkataza kisiri baina yangu mimi na yeye bila ya kufungua mlango wa

shari kwa watu."

Jambo ambalo lilipelekea katika fitina baina ya ´Aliy na Mu´aawiyah.

´Uthmaan na ´Aliy waliuawa kwa sababu hiyo. Maswahabah wengi (Radhiya

Allaahu ´anhum) na watu wengi waliuawa kwa sababu hili la kuhukumiana

hadharani. Lilipelekea watu kumchukia mtawala wao mpaka wakumuua.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127880

19) Kujumuisha Swalah Wakati Wa Mvua, Upepo Na Barafu

Swali:

Muulizaji kutoka Amerika anauliza. Kwetu kuna mvua [kali] na barafu, je

tunaweza kujumuisha Swalah?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Mvua ikinyesha wakati wa Swalah ya Maghrib na ´Ishaa, wanaweza

kujumuisha katika hali hii mvua na barafu na upepo mkali wenye baridi.

Wanaweza kujumuisha baina ya Maghrib na ´Ishaa ili isiwapite Jamaa´ah.

Page 19: Fataawa Za Wanachuoni (32)

19

Ama ikiwa mtu kujumuisha Swalah ndo ada yake, au kwa mvua ndogo tu ni

wajibu kuswali Swalah kwa wakati wake tena Msikitini.

Muulizaji:

Kipi kipimo cha kujumuisha, yaani kujumuisha kuna muda maalumu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hapana hakuna muda maalumu maadamu udhuru wa kufanya hilo upo. Mtu

atajumuisha maadamu udhuru upo, mvua nyingi ya kulowanisha nguo,

barafu nyingi mtu hawezi kutembea katika giza, ni sahihi kwao kujumuisha

na waswali Jamaa´ah. Wajumuishe tu bila ya kufupisha. Baina ya Maghrib na

´Ishaa na ´Aswr na Dhuhr.

Chanzo: http://youtu.be/8ttnGcH4-pE

20) Je Kuna Kundi Linaitwa Jaamiyyah? Na Ni Nani Shaykh Muhammad

al-Jaamiy?

Swali:

Tumesikia kundi la Jaamiyyah ulilotahadharisha dhidi yalo, je kundi hili kweli

lipo na ni nani Shaykh Muhammad (Amaan) al-Jaamiy?

´Allaamah al-Fawzaan:

Muhammad al-Jaamiy ni ndugu yetu na kipenzi chetu, alihatimu katika Chuo

Kikuu hiki (Madiynah) na akaenda kuwa mwalimu katika Chuo kikuu cha

Kiislamu na (mwalimu) katika Msikiti wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) na alikuwa ni mlinganiaji katika njia ya Allaah (Subhaanahu wa

Ta´ala). Hatujui kwake ila kheri tu. Na hakuna kundi linaloitwa Jaamiyyah,

hili ni uongo na udanganyifu. Haya ndo tunayoyajua kwa Shaykh

Page 20: Fataawa Za Wanachuoni (32)

20

Muhamamd Amaan al-Jaamiy (Rahimahu Allaah). Lakini kwa kuwa alikuwa

akilingania katika Tawhiyd na akikemea Bid´ah na fikra za kipotofu, hivyo

(watu wa Bid´ah) wakawa wanamjengea uadui na kumpachika majina ya

bandia kama haya.

Chanzo: http://youtu.be/s9JIRTSAF9s

21) Ipi Tofauti Kati Ya ´Aqiydah Na Manhaj?

Swali:

Ipi tofauti baina ya ´Aqiydah (itikadi) na Manhaj (mfumo)?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

´Aqiydah na Manhaj vinaenda sambamba, tofauti tu ni katika matendo.

´Aqiydah ni ibara ya Imani, mtu kuamini nguzo zake sita (za Imani). Na

Manhaj ni yale matendo ya Kiislamu, kutekeleza wazi zile nguzo tano za

Kiislamu. Navyo ni vitu viwili vinaenda sambamba. Ni lazima Muislamu awe

na ´Aqiydah sahihi na Manhaj Sahihi. Viendane sambamba kama ilivyo katika

Manhaj ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Hawatofautishi kati ya ´Aqiydah na

Manhaj katika matendo.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2632

22) Inajuzu Kula Samaki Maiti Ambayo Haikuchinjwa?

Swali:

Muulizaji kutoka Ireland anauliza, je inajuzu kula nyama ya samaki ikiwa ni

maiti?

Page 21: Fataawa Za Wanachuoni (32)

21

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Maiti ya baharini inajuzu, ama maiti ya bara ni lazima kwanza kuichinja ima

kwa mfano bunduki na mfano wa hayo.

Chanzo: http://youtu.be/W_2CK1vmbQg

23) Hukumu Ya Mwenye Kumtukana Allaah Na Mtume Wake

Swali:

Je atatakiwa atubie yule mwenye kumtukana Allaah na akamtukana Mtume

Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), na kuna tofauti baina ya haya

mawili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Maulamaa wamesema kuwa atauawa wala hakuna cha kutakiwa kutubia.

Mwenye kumtukana Allaah na Mtume atauawa wala hatatakiwa kutubia, kwa

kuwa hii ndo adhabu yake inayofaa kumpa.

Chanzo: http://youtu.be/olZtrSblZ6s

24) Shaykh Fawzaan Kuhusu Radd Kwa Sayyid Qutwub

´Allaamah al-Fawzaan:

Sayyid Qutwub ni mjinga hana elimu wala maarifa. Wala hana dalili kwa

ayasemayo. Kumlinganisha Imaam Ahmad [bin Hanbal] na Sayyid Qutwub ni

dhuluma.

Page 22: Fataawa Za Wanachuoni (32)

22

Chanzo: http://youtu.be/z3A6nSGyclg

25) Umuhimu Wa Kuhifadhi Swalah Ya Dhuhaa

Swali:

Je, kuna Hadiyth inayosema mwenye kuhifadhi Swalah ya dhuhaa,

atasalimishwa na khofu kubwa [ya siku ya Qiyaamah]?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa mimi sijui hili, lakini mtu huyo atakuwa katika al-Awwaabiyn,

yaani wenye kutubia, wenye kurejea kwa Allaah (´Azza wa Jalla).

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5210

26) Kabla Ya Kutumwa Mtume Watu Walikuwa Katika Dini Ya Nani?

Swali:

Je, dini sahihi kabla ya kutumwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni

Haniyfiyyah Dini ya Ibraahiym au ni Shari´ah ya ´Iysa (´alayhis-Salaam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa nisba ya waarabu ni Dini ya baba yake na Ismaa´iyl, Dini ya Ibraahiym.

Ama kwa nisba ya mayahudi na manaswara, walikuwa katika Dini ya Muusa

na ´Iysa. Na kuna miongoni mwa waarabu walioathirika na Uyahudi na

Unaswara, wakifuata Dini ya Ibraahiym.

Page 23: Fataawa Za Wanachuoni (32)

23

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2734

27) Je Sigara Inavunja Wudhuu? Na Ipi Hukumu Ya Sigara Na Bangi?

Swali:

Je kuvuta bangi kunavunja Wudhuu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa haivunji Wudhuu, lakini ni Haramu. Inachukuliwa ni katika

madhambi makubwa. Kuvuta sigara, bangi ni katika madhambi makubwa.

Kwa kuwa yanasababisha kujiua mwenyewe na kuua wengine walioko karibu

nawe, uuaji wa kidogo kidogo. Tunamuomba Allaah afya na usalama. Ni

wajibu kwa Muislamu kujiepusha na kuvuta sigara, bangi na aina zote za

sigara. Na ajiepushe na yote yanayompelekea kumuua. Hakika ni katika

uchafu, madhara yenye kuua na kuangamiza.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5207

28) Nasaha Kwa Dada Wapya Waliyoingia Katika Uislamu -1-

Swali:

Tunamuomba Shaykh kuwapa nasaha ya kijumla wanawake ambao ni wapya

wameingia katika Uislamu, huenda Allaah Akawafaa kwa hilo.

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Page 24: Fataawa Za Wanachuoni (32)

24

Kwanza tunawapa hongera dada zetu wa Kiislamu ambao kawakirimu Allaah

(Tabaaraka wa Ta´ala) kuingia kwao katika Uislamu na kuacha dini zenye

kwenda kinyume, ni kuokoka kutoka katika moto kwa uwezo na nguvu za

Allaah. Na wale waliong´ang´ana kubaki katika dini zao batili na wakafa

katika dini hizo hawana kwa Allaah isipokuwa Moto tu na ni makazi mabaya

sana na hawatotoka humo. Ama kwa wale Aliowakirimu Allaah katika

wanaume na wanawake, hakika hii ni katika Tawfiyq ya Allaah kwa wote.

Ni juu ya aliyeingia katika Uislamu akimbilie kujifunza nguzo za Uislamu,

kwanza aanze kuisafisha ´Aqiydah, ampwekeshe Allaah (´azza wa Jalla)

katika Uluuhiyyah - hivyo asiwe ni mwenye kumuabudu yeyote zaidi ya

Allaah Pekee. Na katika Rubuubiyyah - awe mwenye kukiri kuwa Allaah

ndiye Muumba, Mwenye kuruzu daima, Mwenye kuendesha yote. Na katika

Sifa Zake - Mwenye Kusamehe, Kurehemu, Kusikia, Kuona, Kujua, Mwenye

Hekima na mengine yote katika Majina Mazuri na Sifa Zake Kuu. Aamini yote

hayo, na atekeleze faradhi zilizofaradhishwa; kama Swalah tano - kwa jumla

kama nguzo za Uislamu tano na nguzo za Imani sita na nguzo ya Ihsaan. Na

ajitahidi kujua Halali na Haramu. Na ajilazimishe kuwa na adabu za Kiislamu

na aendelee kujifunza daima mpaka awe imara mwanaume na mwanamke

katika kuhakikisha Uislamu sahihi ambao Kawachagulia Allaah (Tabaaraka

wa Ta´ala) kwa watu wote binaadamu na majini. Kinachotakiwa ni kuendelea

baada ya Uislamu kujifunza nguzo zingine zote za Kiislamu.

Chanzo: http://youtu.be/p275UYtTbPg

29) Nifuturu Nyumbani Kwangu Au Msikitini Nikaapo I´tikaaf?

Swali:

Nyumba yangu iko karibu na Msikiti ambao nataka kukaa I´tikaaf. Je, ni bora

kwangu wakati wa futari nikafuturu nyumbani kwangu halafu nioge wakati

wa haja au ni bora kwangu kuhudhuria [kwa ajili ya futari] katika Msikiti

ambao uko karibu nami?

Page 25: Fataawa Za Wanachuoni (32)

25

´Allaamah al-Fawzaan:

Bora ni wewe kubakia mahali ulipo, futuru Msikitini na usiende nyumbani.

Kwa kuwa hili si dharurah, na tumesema mtu anatoka tu kama kuna haja

dharurah, kama kutatua haja fulani, kutawadha. Ama hili kufuturu nyumbani

kwako si dharurah, futuru Msikitini na hili ndo bora kwako. Kwa kuwa futari

ni ´Ibaadah na ikiwa Msikitini ndo bora zaidi.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2662

30) Nasaha Kwa Dada Wapya Waliyoingia Katika Uislamu -2-

Swali:

Dada kaingia katika Uislamu naye anataka nasaha kutoka kwa Shaykh

kuhusiana na jinsi atatangamana na mamake kafiri ambaye alikata

mawasiliano naye kwa kuingia kwake Uislamu kwa kuwa [mamake]

anamfanyia kejeli kwa Hijaab yake ya Kishari´ah?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Huyu [dada yetu] tunampa hongera kwa kuingia kwake katika Uislamu,

hakika Allaah Atamuepusha na Moto ikiwa atakuwa thabiti na akafa katika

Uislamu na Imani, ambao Allaah Kawaahidi Pepo Yake yenye neema.

Tunamnasihi kuwa na ufahamu (kuielewa) Dini, nguzo za Uislamu tano,

vigawanyo vya Tawhiyd vitatu, nguzo za Imani sita, Ihsaan, kujua Halali na

Haramu, kuelewa yale mambo ambayo ni wajibu kwake na aliyoharamishiwa.

Ama mama yake atangamane nae muamala mzuri huku akimlingania kuingia

katika Uislamu, amuwekee mtumishi na aongee nae vizuri lakini amchukie

ndani ya moyo maadamu bado angali katika ukafiri wake. Na Allaah (´Azza

wa Jalla) Anasema:

نيا في وصاحبهما بع معروفا الد إلي أناب من سبيل وات

Page 26: Fataawa Za Wanachuoni (32)

26

"Lakini kaa nao kwa wema duniani, nawe ishike njia ya anayeelekea

Kwangu." (31:15)

Wala usimtii kwa kitu ambacho ni Haramu. Na uendelee kumlingania huenda

Allaah Akamtoa katika ukafiri, sawa ikiwa [yuko katika dini] ya kinaswara,

kiyahudi, kiwathaniyyah; Atamuokoa kwa kumuingiza Kwake katika

Uislamu. Fanya sababu.

Chanzo: http://youtu.be/VhhE9FDNjL4

31) Mume Kamlaani Mke Wake, Je Mke Katalikika?

Swali:

Mwenye kumlaani mke wake ni kama vile kampa Talaka?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hapana, si kama aliyemtaliki. Ila akidhihirisha kuwa kakusudia kumtaliki

[itakuwa imepita]. Kumlaani ni Haramu kwake [mume], kumlaani ni Haramu

kwake.

Chanzo: http://youtu.be/l_SxS32XeMA

32) Mavazi Yenye Picha Za Watu Na Minyama Na Maneno Mabaya

Swali:

Anauliza kuhusu mavazi ya watoto ambayo yanakuwa na mapicha ya

minyama na watu?

Page 27: Fataawa Za Wanachuoni (32)

27

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa haijuzu kununua mavazi kama haya, sawa ikiwa ni mavazi ya

watoto, wanaume au wanawake. Lazima ziwe hazina picha zenye viumve

vyenye roho na maneno mabaya.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5486

33) Kuna Aina Tatu Kwa Wenye Kuyatembelea Makaburi

Swali:

Kwetu kuna wanaoenda kuzuru makaburi na wanaamini kuwa yananufaisha

na kudhuru. Je, watu hawa ni washirikina au ni lazima kwanza

kuwasimamishia hoja?

´Allaamah Zady al-Madkhaliy:

Kuzu makaburi kumegawanyika sehemu tatu:

- Ziara ya Kishari´ah Nayo ni pale mwenye kuzuru anaenda kuzuru kwa nia

ya kuwasalimia. Atawasalimia kisha aende, atasema: "Salaamun ´alaykum

daara qaumil mu-uminiyn, wa inna In Shaa Allaahu bikum lahaaikun,

yarhamu Allaahu mustaqdimiyna minna wa minkum wal mustaakhiriyn."

Kisha anasema: "Allaahumma laa tuhrimaa ajrahum." Kisha ende. Hii ndio

ziara ya Kishari´ah."

- Na kuna ziara ya Shirki. Nayo ni pale mtu anazuru makaburi ya watu wema;

atafuta Shafaa´ah kutoka kwao, awachinjie huku akiamini wananufaisha na

kuzuia madhara. Anawaomba wafikishe haja zake kwa Allaah (´Azza wa

Jalla), huku akiamini wananufaisha au kuzuia madhara. Hii ni ziara ya

kishirki, mwenye kufanya hivi kafanya Shirki kubwa. Kwa kuwa kachinja

kwa asiyekuwa Allaah, na kawaomba maiti wamtatulie haja zake, hivyo

katumbukia katika Shirki kubwa.

Page 28: Fataawa Za Wanachuoni (32)

28

- Na kuna ziara za Bid´ah. Nazo ni pale mtu anapomzuru aliyemo ndani ya

kaburi, kisha amuombe Allaah hapo kwenye kaburi huku akiitakidi kuwa

mahala hapo kuna baraka. Anatafuta baraka sehemu hio anamuomba Allaah

kwa mtu huyo aliyemo ndani ya kaburi akiitakidi baraka. Ni juu ya Muislamu

kutofautisha baina ya aina hizi tatu; ziara za Shirki, ziara za Bid´ah na ziara za

Sunnah.

Chanzo: http://youtu.be/WLQm_MM4wyU

34) Kutabaruku Kwa Mabaki Ya Mtume ( وسلم عليه هللا صلى )

Swali:

Muulizaji kutoka Spain, je inajuzu kutabaruku (kuitakidi baraka) kwa athari

ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya kufa kwake?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Athari imegawanyika sehemu mbili, inayojuzu kutafuta kwayo baraka na

isiyojuzu.

- Yanayojuzu kutafuta kwayo baraka ni yale yaliyothibiti kuwa ni katika

mabaki yake; kama damu yake, nguo na yote yanayohusiana na yeye. Haya

inajuzu kutabaruku kwavyo.

- Ama yaliyokatazwa ni kutabaruku kwa kumuomba, kutawassul kwa jaha

yake. Haya hayajuzu kwa hali yoyote. Kukipatikana nywele, damu n.k. vya

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) inajuzu kutabaruku kwavyo, kwa

kuwa hilo limethibiti wakati wa uhai wake. Yasiyokuwa hayo katika

kutabaruku kwa jaha yake, kumuomba Allaah kwa jaha yake (Mtume) na

makubwa kuliko hayo - kumuomba na kumchinjia ni Shirki kubwa inayomtoa

mtu katika Uislamu ikiwa mfanyaji ni Muislamu.

Chanzo: http://youtu.be/BSz34STSOzUp

Page 29: Fataawa Za Wanachuoni (32)

29

35) Jinsi Ya Kuweka Nia Unapotaka Kuanza Kukaa I´tikaaf

Swali:

Je ni lazima kuitamka nia pindi mtu anapotaka kufanya I´tikaaf, au inatosha

nia ndani ya moyo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Inatosha nia yako ndani ya moyo. Anasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam):

"Vitendo vinategemea [vinalipwa kwa] nia na kila mtu atapata kwa mujibu wa

kile alichokusudia."

Akinuia kukaa I´tikaaf na akanuia kutoka kwa baadhi ya mambo [wakati wa

dharurah], hii ndo sharti hata kama hakuyatamka. Na Allaah Anajua

yaliyomo ndani ya moyo na Anajua nia yako na makusudio yako hata kama

hukuyatamka.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2661

36) Inajuzu Mume Kumkabili Mke Wake Usoni?

Swali:

Je mume akimkabili mke wake uso anapata dhambi?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa hapati dhambi, mlango uliopo baina ya mume na mke ni mpana.

Page 30: Fataawa Za Wanachuoni (32)

30

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5194

37) Hukumu Ya Mtu Mwenye Kuitukana Dini

Swali:

Ipi hukumu ya kuitukana Dini katika Shari´ah ya Kiislamu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Laa hawla walaa Quwwata illa biLlaah. Kuitukana Dini ni ukafiri na kuritadi,

mwenye kuitukana Dini ya Kiislamu basi huyo karitadi katika Uislamu.

Anatakiwa kuingia [upya] katika Uislamu. Akiafikishwa na kurejea - akaomba

Tawbah ya kweli kabisa, atakubaliwa. Na ikiwa atakufa na yeye ni mwenye

kuutukana Uislamu atakuwa kafiri aliyeritadi.

Chanzo: http://youtu.be/8oWf0rFVDVg

38) Inajuzu Kwa Mwanamke Kufanya Kazi Ya Uuguzi Katika Mji Wa

Kikafiri?

Swali:

Muulizaji kutoka Spain, je inajuzu kwa mwanamke wa Kiislamu kufanya kazi

ya muuguzi (nurse) Hospitali katika mji wa kikafiri?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ikiwa atajisitiri vizuri kwa Hijaab, na akawa anawauguza wanawake tu,

kutakuwa hakuna neno. Kwa kuwa Hospitalini ni sehemu pa mchanganyiko

Page 31: Fataawa Za Wanachuoni (32)

31

baina ya wanaume na wanawake. Kwa sharti hizi inajuzu, awe amejisitiri

vizuri kwa Hijaab na awe sehemu ya wanawake tu.

Chanzo: http://youtu.be/24d59c38gSk

39) Muislamu Kupenda Nchi Ya Kikafiri

Swali:

Muulizaji kutoka Spain, inajuzu kwa Muislamu kupenda nchi yake ya

kikafiri?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Muislamu nchi ya kikafiri sio nchi yake, bali nchi ya Kiislamu ndio nchi yake.

Ni juu yake kufanya juhudi kuhama katika nchi ya Kiislamu, ama nchi ya

kikafiri sio yake. Alihama Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na

Muhajiruun katika Maswahabah na wakaiacha Makkah na wakapenda

kuhamia Madiynah na hawakurejea Makkah ila baada ya al-Fath (kutekwa

kwa Makkah na Waislamu).

Chanzo: http://youtu.be/W8s3uitAGCs

40) Mambo Gani Yanayofanya Mwanamke Akawa Na Msimamo Katika

Dini?

Swali:

Ni mambo gani yanayomthibitisha (yanampa msimamo) mwanamke katika

Dini ya Allaah?

Page 32: Fataawa Za Wanachuoni (32)

32

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Amuogope Allaah (´Azza wa Jalla) na Imani ya kuwa Allaah Kamuumba kwa

ajili amuabudu na atamuhesabu kwa hilo. Akiyajua mambo haya hivyo

ajitahidi katika kumtii Allaah na kuacha maasi na ajikurubishe kwa Allaah

(´Azza wa Jalla) kwa yatakayomfaa katika Dini na dunia yake.

Chanzo: http://youtu.be/rXSou8HREOI

41) Kuwa Na Subira Katika Da´wah Kwa Kupewa Mitihani

Swali:

Kuna watu wanaomsema Shaykh Muhammad bin Haadiy [al-Madkhaliy] na

Shaykh ´Abdullaah al-Bukhaariy?

´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy:

Kusemwa Mashaykh sio tu Shaykh Muhammad bin Haadiy na Shaykh

´Abdullaah al-Bukhaariy. Mitume nao walisemwa. Waliwatuhumu kwa

uchawi, ukuhani, uongo na kadhalika. Wamewapiga vita maimamu wa

Uislamu kwa hila na chuki zao, hii ni Sunnah ya Allaah. Hii ni Sunnah ya

Allaah kwa waja wake yule ambaye atashikamana na njia ya haki na akapita

njia iliyonyooka, lazima apate maadui na Shaytwaan anawachochea watu

kama hawa na kuwaita waje kuipiga vita haki na watu wake. Mitume

(´alayhimus-Salaam) waliudhiwa, waliambiwa:

"Nyinyi si chochote ila ni wanaadamu kama sisi." (14:10)

"Mitume wao wakawaambia: "Sisi kweli si chochote ilani wanaadamu kama

nyinyi. Lakini Allaah Humfanyia hisani amtakaye katika waja wake." (14:11)

Kuna nini akitukanwa Muhammad bin Haadiy, Bukhaariy, Rabiy´ na

wengineo? Watu wamezowea kuongea kwa batili, dhuluma na uongo.

Page 33: Fataawa Za Wanachuoni (32)

33

Hawakumsalimisha Muhammad bin Hanbal, Ibn Taymiyyah, [Muhammad

bin] ´Abdil-Wahhaab na wengineo katika maimamu wa Uislamu. Vipi kweli

mnaweza kusahau haya mpaka mkauliza swali kama hili? Sisi tunawanasihi

watu hawa wanaomzungumzia fulani na fulani, wamche Allaah katika nafsi

zao. Watu hawa wanaomtukana Muhammad bin Haadiy, al-Bukhaariy

wanadai Salafiyyah, nao wako mbali na Salafiyyah na msingi wake na mfumo

wake. Na wanajificha nyuma ya pazia la Salafiyyah ili wapate kupoteza waja

wa Allaah (Tabaakara wa Ta´ala) na wawapoteza katika njia ya Allaah iliyo

nyooka.

Chanzo: http://youtu.be/BIxUv8f1owg

42) Kuna Mpaka Wa Mtu Kukaa Itikaaf Msikitini?

Swali:

Je uchache wa kukaa I´tikaaf ni usiku mbili au siku moja kama ilivokuja katika

Hadiyth ya ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhu)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna mpaka. Wanachuoni wanasema mtu anaweza kukaa hata saa moja

kwa kuwa hapakuja mpaka katika Shari´ah.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2651

43) Ipi Faradhi Ya Kwanza Kubwa?

Swali:

Faradhi ipi kubwa aliyokuja nayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

Page 34: Fataawa Za Wanachuoni (32)

34

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Faradhi kubwa ni kumpwekesha Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala) - Tawhiyd na

kuacha kumshirikisha. Nayo ndio Da´wah ya kila Mtume na Nabii. Na ndio

faradhi ya kwanza kubwa na iliyofaradhishwa.

Chanzo: http://youtu.be/6QPuhsXXHVw

44) Hukumu Ya Kuhudhuria Janaza Na Kuwasalia Watu Wa Bid´ah

Swali:

Ipi hukumu ya kuhudhuria janaza kukikithiri Bid´ah?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Watu wa Bid´ah wanasuswa sawa waliohai na waliokufa, na wala

hawahukumiwi ukafiri ila tu ikiwa Bid´ah zao ni za kukufurisha. Kama wale

wanaoabudu makaburi, na wale wanaowaomba maiti na kuwaomba msaada,

hizi ni katika Bid´ah za kukufurisha. Muislamu asishuhudie janaza zao na

wala asiwasalie bali wao ni katika watu wa Motoni. Ama Bid´ah chini ya

ukafiri na Shirki, hawahukumiwi wanaozifanya kwa ukafiri. Bali tu Salaf-us-

Swaalih walikuwa hawawaswalii kabisa watu wa Bid´ah wala hawahudhurii

katika janaza yao kwa ajili watu wachukue funzo kwa kutoka katika Bid´ah

walizoangukia humo.

Chanzo: http://youtu.be/UB_nHlso_AY

45) Amevaa Soksi Kisha Akazivua, Vipi Wudhuu Wake?

Page 35: Fataawa Za Wanachuoni (32)

35

Swali:

Nikipaka juu ya soksi halafu nikazivua na kuvaa soksi zingine bila kuweka

Wudhuu upya, je Wudhuu wangu utatenguka?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ndio akizivua utatenguka, akivua moja au mbili upakaji utakuwa

umebatilika. Na ni juu yake kutawadha upya na azivae kwa Twahara kamili.

Chanzo: http://youtu.be/wcVPthHGelA

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 36: Fataawa Za Wanachuoni (32)

36