matokeo ya utafi ti wa viashiria vya vvu/ukimwi na malaria ...utafi ti wa viashiria vya vvu/ukimwi...

2
Utafiti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania (THMIS) wa mwaka 2011-12, ulitathmini mikakati ya kuzuia malaria, tiba ya malaria, kiwango cha malaria na upungufu wa damu mwilini. Katika kaya zote nchini Tanzania, 91% zinamiliki angalau chandarua kimoja kilichotiwa dawa. Umiliki wa chandarua chenye dawa ni mdogo zaidi Mkoa wa Mjini Magharibi (67%) na ni mkubwa zaidi katika Mkoa wa Lindi (96%). Kwa nchi nzima, 14% tu ya kaya ndizo zilizokuwa zimepulizia dawa ndani ya nyumba miezi 12 kabla ya utafiti, lakini 87% ya kaya Zanzibar zilikuwa zimepuliziwa dawa miezi 12 kabla ya utafiti. Upungufu wa damu ni dalili kubwa ya malaria. Nchini Tanzania, 6% ya watoto chini ya miaka mitano wana upungufu wa damu kiasi hadi upungufu mkubwa wa damu, ambao ni chini ya haemoglobin 8.0/dl. Kwa ujumla, kiwango cha upungufu wa damu wa wastani hadi mkubwa kinapungua sambamba na kuongezeka kwa umri. Watoto na wajawazito ndio waathirika wakubwa wa malaria. Mwaka 2011-12, 72% ya watoto chini ya miaka mitano na 75% ya wajawazito walilala kwenye chandarua chenye dawa usiku wa kuamkia siku ya utafiti. Matumizi ya chandarua kwa wanakaya, watoto chini ya miaka mitano na wajawazito yameongezeka kwa kiasi kikubwa tangu mwaka 2004-05. Kaya 9 kati ya 10 zina angalau chandarua kimoja kilichowekwa dawa. Robo-tatu ya wakazi katika kaya wangeweza kulala kwenye chandarua chenye dawa ikiwa kila chandarua kimoja chenye dawa katika kaya kingetumiwa na watu wawili. Kwa ujumla, 68% ya watu katika kaya walilala katika chandarua chenye dawa usiku wa kuamkia siku ya utafiti. Nchini Tanzania, 9% ya watoto chini ya miaka mitano walikutwa na malaria walipofanyiwa kipimo cha papo kwa hapo (Rapid Diagnostic Test - RDT). Maambukizi ya malaria yanaongezeka kadri umri unavyoongezeka. Umiliki, Upatikanaji na Utumiaji wa Chandarua chenye Dawa 75 Wenye angalau chandarua 1 chenye dawa Waliokuwa wamelala katika chandarua chenye dawa 91 Asilimia ya: 56 68 Wenye vyandarua vyenye dawa vya kutosha kwa kaya nzima* Wanaotumia chandarua chenye dawa katika kaya* *Kwa makadirio ya chandarua kimoja kwa watu 2 Kaya Wanakaya Umiliki wa Chandarua Kilichotiwa Dawa na Upuliziaji Dawa 92 14 91 Kaya zenye angalau chandarua kimoja chenye dawa Kaya zilizopulizia dawa ndani angalau miezi 12 iliyopita Kaya zenye angalau chandarua 1 chenye dawa na/au zilizopuliziwa dawa angalau miezi 12 iliyopita Asilimia ya: Kiwango cha Upungufu wa Wastani hadi Mkubwa wa Damu kwa Watoto 9 7 9 7 6 Umri kwa miezi Asilimia ya watoto wa umri wa miezi 6-59 wenye upungufu wa damu mwilini wa kiwango cha wastani hadi wa kiwango cha juu (haemoglobin <8.0 g/dl) 6-8 9-11 12-17 18-23 24-35 36-47 48-59 4 3 Jumla 6-59 6 Zaidi ya 90% ya wanawake na wanaume wa miaka 15- 49 wanafahamu kwamba kuna njia za kujikinga dhidi ya malaria. Njia iliyotajwa na watu wengi ya kuepuka malaria ni kulala kwenye chandarua. Mwenendo wa Utumiaji wa Chandarua Chenye Dawa 15 20 16 27 Wanakaya wote Asilimia ya waliolala kwenye chandarua chenye dawa usiku wa kuamkia siku ya utafiti 45 68 57 75 Watoto chini ya miaka 5 2010 TDHS 2011-12 THMIS 2007-08 THMIS 2004-05 TDHS Wajawazito 15-49 16 26 64 72 Malaria kwa Watoto 4 5 6 9 10 Umri kwa miezi Asilimia ya watoto wenye miezi 6-59 waliopimwa na kukutwa na malaria kwa kipimo cha papo kwa hapo (RDT) 6-8 9-11 12-17 18-23 24-35 36-47 48-59 11 12 Jumla 6-59 9 Matokeo ya Utafiti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania 2011-2012 Malaria kwa Watoto (kwa Mikoa) Asilimia ya watoto wenye miezi 6-59 walioonekana kuwa na malaria baada ya kufanyiwa kipimo cha papo kwa hapo (RDT). Tanzania 9% Unguja <1% Kagera 8% Mara 25% Simiyu 3% Mwanza 19% Geita 32% Shinyanga 7% Tabora 9% Kigoma 26% Katavi 5% Rukwa 5% Mbeya 1% Singida <1% Dodoma 3% Manyara 1% Arusha <1% Kilimanjaro <1% Tanga 6% Morogoro 13% Pwani 10% Iringa <1% Njombe 2% Lindi 26% Ruvuma 12% Mtwara 17% Dar es Salaam 4% Pemba <1% Kiwango cha malaria kinatofautiana sana baina ya mikoa. Kiwango cha malaria kiko juu zaidi katika mikoa ya Geita, Kigoma na Lindi.

Upload: others

Post on 21-Jan-2021

5 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: Matokeo ya Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria ...Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania (THMIS) wa mwaka 2011-12, ulitathmini mikakati ya kuzuia malaria,

Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania (THMIS) wa mwaka 2011-12, ulitathmini mikakati ya kuzuia malaria, tiba ya malaria, kiwango cha malaria na upungufu wa damu mwilini.

Katika kaya zote nchini Tanzania, 91% zinamiliki angalau chandarua kimoja kilichotiwa dawa. Umiliki wa chandarua chenye dawa ni mdogo zaidi Mkoa wa Mjini Magharibi (67%) na ni mkubwa zaidi katika Mkoa wa Lindi (96%). Kwa nchi nzima, 14% tu ya kaya ndizo zilizokuwa zimepulizia dawa ndani ya nyumba miezi 12 kabla ya utafi ti, lakini 87% ya kaya Zanzibar zilikuwa zimepuliziwa dawa miezi 12 kabla ya utafi ti.

Upungufu wa damu ni dalili kubwa ya malaria. Nchini Tanzania, 6% ya watoto chini ya miaka mitano wana upungufu wa damu kiasi hadi upungufu mkubwa wa damu, ambao ni chini ya haemoglobin 8.0/dl. Kwa ujumla, kiwango cha upungufu wa damu wa wastani hadi mkubwa kinapungua sambamba na kuongezeka kwa umri.

Watoto na wajawazito ndio waathirika wakubwa wa malaria. Mwaka 2011-12, 72% ya watoto chini ya miaka mitano na 75% ya wajawazito walilala kwenye chandarua chenye dawa usiku wa kuamkia siku ya utafi ti. Matumizi ya chandarua kwa wanakaya, watoto chini ya miaka mitano na wajawazito yameongezeka kwa kiasi kikubwa tangu mwaka 2004-05.

Kaya 9 kati ya 10 zina angalau chandarua kimoja kilichowekwa dawa. Robo-tatu ya wakazi katika kaya wangeweza kulala kwenye chandarua chenye dawa ikiwa kila chandarua kimoja chenye dawa katika kaya kingetumiwa na watu wawili. Kwa ujumla, 68% ya watu katika kaya walilala katika chandarua chenye dawa usiku wa kuamkia siku ya utafi ti.

Nchini Tanzania, 9% ya watoto chini ya miaka mitano walikutwa na malaria walipofanyiwa kipimo cha papo kwa hapo (Rapid Diagnostic Test - RDT). Maambukizi ya malaria yanaongezeka kadri umri unavyoongezeka.

Umiliki, Upatikanaji na Utumiaji wa Chandarua chenye Dawa

75

Wenye angalau chandarua 1 chenye dawa

Waliokuwa wamelala katika

chandarua chenye dawa

91

Asilimia ya:

5668

Wenye vyandarua vyenye dawa vya

kutosha kwa kaya nzima*

Wanaotumia chandarua

chenye dawa katika kaya*

*Kwa makadirio ya chandarua kimoja kwa watu 2

Kaya Wanakaya

Umiliki wa Chandarua Kilichotiwa Dawa na Upuliziaji Dawa

92

14

91Kaya zenye angalau chandarua kimoja chenye dawa

Kaya zilizopulizia dawa ndani angalau miezi 12 iliyopita

Kaya zenye angalau chandarua 1 chenye dawa na/au zilizopuliziwa dawa

angalau miezi 12 iliyopita

Asilimia ya:

Kiwango cha Upungufu wa Wastani hadi Mkubwa wa Damu kwa Watoto

97

97 6

Umri kwa miezi

Asilimia ya watoto wa umri wa miezi 6-59 wenye upungufu wa damu mwilini wa kiwango cha

wastani hadi wa kiwango cha juu (haemoglobin <8.0 g/dl)

6-8 9-11 12-17 18-23 24-35 36-47 48-59

43

Jumla6-59

6

Zaidi ya 90% ya wanawake na wanaume wa miaka 15-49 wanafahamu kwamba kuna njia za kujikinga dhidi ya malaria. Njia iliyotajwa na watu wengi ya kuepuka

malaria ni kulala kwenye chandarua.

Mwenendo wa Utumiaji wa Chandarua Chenye Dawa

15 20 1627

Wanakayawote

Asilimia ya waliolala kwenye chandarua chenye dawa usiku wa kuamkia siku ya utafiti

45

6857

75

Watoto chini ya miaka 5

2010 TDHS

2011-12 THMIS

2007-08 THMIS

2004-05 TDHS

Wajawazito 15-49

1626

6472

Malaria kwa Watoto

45 6

9 10

Umri kwa miezi

Asilimia ya watoto wenye miezi 6-59 waliopimwa na kukutwa na malaria kwa kipimo cha papo kwa hapo (RDT)

6-8 9-11 12-17 18-23 24-35 36-47 48-59

11 12

Jumla6-59

9

Matokeo ya Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania 2011-2012

Malaria kwa Watoto (kwa Mikoa)Asilimia ya watoto wenye miezi 6-59 walioonekana

kuwa na malaria baada ya kufanyiwa kipimo cha papo kwa hapo (RDT).

Tanzania9%

Unguja<1%

Kagera8%

Mara25%

Simiyu3%

Mwanza19%

Geita32%

Shinyanga7%

Tabora9%

Kigoma26%

Katavi5%

Rukwa5% Mbeya

1%

Singida<1% Dodoma

3%

Manyara1%

Arusha<1% Kilimanjaro

<1%

Tanga6%

Morogoro13% Pwani

10%Iringa<1%

Njombe2%

Lindi26%

Ruvuma12% Mtwara

17%

Dar es Salaam4%

Pemba<1%

Kiwango cha malaria kinatofautiana sana baina ya mikoa. Kiwango cha malaria kiko juu zaidi katika mikoa ya Geita, Kigoma na Lindi.

Page 2: Matokeo ya Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria ...Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania (THMIS) wa mwaka 2011-12, ulitathmini mikakati ya kuzuia malaria,

Mwitikio na mfumo wa utafi ti: Watoto wote wenye miezi 6-59 wanaoishi katika kaya zilizochaguliwa walistahili kupima malaria na kiwango cha damu. Upimaji wa malaria ulifanywa kwa kutumia kipimo cha papo kwa hapo pamoja na kipimo cha kawaida cha kutumia darubini. Upimaji wa kiwango cha damu ulifanywa kwa kutumia kifaa kinachoitwa HemoCue. Kati ya watoto 8,119 waliostahili kuingia katika zoezi hilo, 95% walitoa damu kwa ajili ya kipimo cha kiwango cha damu, 94% kwa ajili ya kipimo cha malaria cha papo kwa hapo na 92% kwa kipimo cha malaria cha darubini.

Kwa taarifa zaidi kuhusu matokeo ya Utafi ti wa Viashiria vya VVU/

UKIMWI na Malaria Tanzania 2011-12, tafadhali wasiliana na:

Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania 2011-12

(THMIS) ulifanywa na Ofi si ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana

na Ofi si ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali- Zanzibar (OCGS-Zanzibar)

kuanzia Desemba 16, 2011 hadi Mei 24, 2012. Tume ya Kudhibiti

UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Tume ya Kudhibiti UKIMWI

Zanzibar (ZAC) zilitoa idhini ya kufanyika kwa utafi ti huu. Utafi ti huu

ulifadhiliwa na Shirika la Misaada ya Maendeleo la Watu wa Marekani

(USAID), TACAIDS na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (MoHSW).

ICF International ilisaidia kufanyika kwa utafi ti huu kupitia mradi wa

MEASURE DHS unaofadhiliwa na USAID. Mradi wa MEASURE DHS

unatoa msaada wa kiufundi na fedha kwa tafi ti za demografi a na afya

katika nchi mbalimbali duniani.

Nchini USA:ICF International

11785 Beltsville Drive

Calverton, MD 20705 USA

Simu: 301-572-0200; Nukushi: 301-572-0999

www.measuredhs.com

www.statcompiler.com

Nchini Tanzania:Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS)

P.O Box. 76987, Dar es Salaam, Tanzania

Simu: 255 22 212 2651; Nukushi: 255 22 212 2427

www.tacaids.go.tz

Ofi si ya Taifa ya Takwimu (NBS)

PO. Box 796, Dar es Salaam, Tanzania

Simu: 255 22 212 2722; Nukushi: 255 22 213 0852

www.nbs.go.tz

TANZANIANS AND AMERICANSIN PARTNERSHIP TO FIGHT HIV/AIDS

Kuzuia malaria, wajawazito wanapaswa kupatiwa dozi mbili au zaidi za SP/Fansidar wanapokwenda kliniki. Karibu theluthi-moja (32%) ya wajawazito walipata tiba hii ya kuzuia malaria (IPTp) walipokwenda kliniki, idadi hii imeongezeka kidogo kutoka 26% katika utafi ti wa TDHS wa 2010.

Tiba ya Kinga ya Malaria

Mwenendo wa Tiba ya Kinga ya Malaria kwa Wajawazito

5057

2130

Walimeza aina yoyote ya SP/Fansidar walipokwenda

kliniki

Asilimia ya wanawake waliokuwa wajawazito miaka miwili kabla ya utafiti, kwa uzazi wao wa mwisho, ambao:

61 60

26 32

Walipata dozi 2+ za SP/Fansidar

walipokwenda kliniki

2010 TDHS

2011-12 THMIS

2007-08 THMIS

2004-05 TDHS

Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania (THMIS) 2011-12

MalariaMatibabu ya Homa kwa Watoto

54Walitumia dawa za malaria

25Walitolewa damu kwa ajili ya kupima malaria

77Walipata ushauri au tiba kutoka kituo cha huduma za afya, mtoa huduma za afya au duka la dawa

Miongoni mwa watoto chini ya miaka mitano waliopata homa wiki mbili kabla ya utafiti, asilimia ya wale ambao:

Zaidi ya nusu (54%) ya watoto waliokuwa wamepata homa walipata dawa za malaria. Miongoni mwa watoto waliokuwa wamepata homa ambao walitumia dawa za malaria, 61% walitumia ACT (dawa mseto ya malaria) – tiba inayopendekezwa.