morogoro - jica...jarida la afya morogoro – na.5 5 kwa miaka 4 iliyopita tayari usugu wa ugonjwa...

12
JARIDA LA MOROGORO M MA AE E L LE EZ ZO O Y YA A U UJ J U UM ML LA A Y YA A T T A AT TH HM MI I N NI I Y YA A M MW WI I S S H HO O Y YA A P P A AM MO OJ J A A M MR R A AD DI I W WA A A AF F Y YA A M MO OR RO OG GO OR RO O asomaji Wapendwa, HONGERA!! Baada ya Taarifa ya Tathmini ya Mwisho ya Pamoja hapo Oktoba 2005 Mradi wetu wa Afya Morogoro umefanikiwa kukubaliwa na Shirika la Ushirikiano la Kimataifa la Japan (“JICA”) kuongeza muda wa mwaka mmoja; hadi 2007 Machi. Mradi wa Afya Morogoro (“MHP”), unaofadhiliwa na Japan ulipokea Timu ya Tathmini ya Mwisho ya Pamoja kati ya Tanzania na Japan (ikiongozwa na Bibi Harumi Kitabayashi, Makao Makuu ya JICA, Tokyo, Japan) kwa kusudi la kupitia maendeleo ya mradi tangu uanze 2001 Aprili. Kwa kuwa hapo awali mradi ulipangwa kumalizika baada ya miaka 5 ya utekelezaji, yaani 2006 Machi, huu ni wakati muafaka kufikiria mradi utaendeshwaje siku zijazo. Timu ya Tathmini, iliyokuwa na Bingwa wa nje wa kujitegemea kutoka Makao Makuu JICA, Japan, aitwaye Bibi Minako Nakatani na wawakilishi 2 kutoka Makao Makuu Wizara ya Afya, Tanzania, ilipitia mafanikio ya Mradi. Walifanya hivyo kwa njia ya mahojiano ya kina, kutumia dodoso (questionnaire) kwa watendaji wa Kitanzania (Counterparts), wao wenyewe kutembelea wilaya (zote) kusikofungamana na upande wowote, na kwa kuhudhuria mikutano mbalimbali muhimu iliyofanyika wakati wa tathmini hapo 2 Oktoba hadi 23 Oktoba2005: kwa mfano “Project Final Internal Evaluation Workshop”, “Morogoro Health Stakeholders Conference” na “Tanzania – JICA Project Review Workshop”. Mwishoni Timu ya Tathmini ilijadili taarifa ya tathimini kwa pamoja na mamlaka za ngazi ya juu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Sekretariati ya Mkoa na Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Morogoro.Katika majadiliano hayo walifikia muafaka kuwa mafanikio ya mradi katika kujenga uwezo wa uendeshaji kiafya na baadhi ya matokeo katika utoaji na utumiaji wa huduma za afya ni yale ambayo yangetazamiwa kupatikana kutegemea hali halisi katika Mkoa wa Morogoro. Tathmini hiyo ilihitimisha kwa kusema, “Wakati wa kazi ya kutathmini mabadiliko mbalimbali ya mwenendo wa wajumbe wa Timu za Afya za Uendesahji ya Mkoa na za Wilaya yalitambuliwa kuwa yanaelekea katika uendeshaji wenye ushahidi . Mabadiliko hayo yana thamani katika kusaidia W ISSN 0856-9517 Toleo Na.5 Desemba 2005 Picha ya pamoja ya washiriki wa Tathmini ya Mwisho ya Mradi wa Afya Morogoro

Upload: others

Post on 11-Jan-2020

17 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

JARIDA LA

MOROGORO

MMAAEELLEEZZOO YYAA UUJJUUMMLLAA YYAA TTAATTHHMMIINNII YYAA MMWWIISSHHOO YYAA PPAAMMOOJJAA MMRRAADDII WWAA AAFFYYAA MMOORROOGGOORROO

asomaji Wapendwa,

HONGERA!!

Baada ya Taarifa ya Tathmini ya Mwisho ya Pamoja

hapo Oktoba 2005 Mradi wetu wa Afya Morogoro

umefanikiwa kukubaliwa na Shirika la Ushirikiano la

Kimataifa la Japan (“JICA”) kuongeza muda wa

mwaka mmoja; hadi 2007 Machi.

Mradi wa Afya Morogoro (“MHP”), unaofadhiliwa

na Japan ulipokea Timu ya Tathmini ya Mwisho ya

Pamoja kati ya Tanzania na Japan (ikiongozwa na Bibi

Harumi Kitabayashi, Makao Makuu ya JICA, Tokyo,

Japan) kwa kusudi la kupitia maendeleo ya mradi

tangu uanze 2001 Aprili. Kwa kuwa hapo awali mradi

ulipangwa kumalizika baada ya miaka 5 ya utekelezaji,

yaani 2006 Machi, huu ni wakati muafaka kufikiria

mradi utaendeshwaje siku zijazo.

Timu ya Tathmini, iliyokuwa na Bingwa wa nje wa

kujitegemea kutoka Makao Makuu JICA, Japan,

aitwaye Bibi Minako Nakatani na wawakilishi 2

kutoka Makao Makuu Wizara ya Afya, Tanzania,

ilipitia mafanikio ya Mradi. Walifanya hivyo kwa njia

ya mahojiano ya kina, kutumia dodoso (questionnaire)

kwa watendaji wa Kitanzania (Counterparts), wao

wenyewe kutembelea wilaya (zote) kusikofungamana

na upande wowote, na kwa kuhudhuria mikutano

mbalimbali muhimu iliyofanyika wakati wa tathmini

hapo 2 Oktoba hadi 23 Oktoba2005: kwa mfano

“Project Final Internal Evaluation Workshop”,

“Morogoro Health Stakeholders Conference” na

“Tanzania – JICA Project Review Workshop”.

Mwishoni Timu ya Tathmini ilijadili taarifa ya

tathimini kwa pamoja na mamlaka za ngazi ya juu

kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za

Mitaa, Sekretariati ya Mkoa na Halmashauri za

Wilaya za Mkoa wa Morogoro.Katika majadiliano

hayo walifikia muafaka kuwa mafanikio ya mradi

katika kujenga uwezo wa uendeshaji kiafya na baadhi

ya matokeo katika utoaji na utumiaji wa huduma za

afya ni yale ambayo yangetazamiwa kupatikana

kutegemea hali halisi katika Mkoa wa Morogoro.

Tathmini hiyo ilihitimisha kwa kusema, “Wakati wa

kazi ya kutathmini mabadiliko mbalimbali ya

mwenendo wa wajumbe wa Timu za Afya za

Uendesahji ya Mkoa na za Wilaya yalitambuliwa

kuwa yanaelekea katika uendeshaji wenye ushahidi .

Mabadiliko hayo yana thamani katika kusaidia

W

ISSN 0856-9517 Toleo Na.5 Desemba 2005

Picha ya pamoja ya washiriki wa Tathmini ya Mwisho

ya Mradi wa Afya Morogoro

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

2

mchakato wa kuondoa madararka toka ngazi za juu

kuyapeleka chini kwa jamii kwa mujibu wa

Mabadiliko Katika Serikali za Mitaa na Mabadiliko

Katika Sekta ya Afya, na yana umuhimu katika

kuhakikisha ubora wa huduma za afya wilayani.

Kwa manufaa ya watoa huduma walio mstari wa

mbele na mwishowe kwa watumiaji huduma za afya

Mkoa wa Morogoro ni lazima katika siku zijazo

juhudi zifanywe na wadau wote, ili kuimarisha

mabadiliko hayo ya mwenendo katika uwezo wa

uendeshaji wa wajumbe wa Timu za Afya za

Uendeshaji ya Mkoa na za Wilaya” – (Ikumbukwe

kuwa hakuna tafsiri yeyote ya Kiswahili ya Taarifa ya

Tathmini inayoelezewa hapa: hii ni tafsiri ya

mwandishi tu, ya nakili ya Kiingereza).

Ili kuimarisha mafanikio ya Mradi katika Timu za

Afya za Uendeshaji ya Mkoa na za Wilaya na kueneza

uzoefu na masomo yatokanayo na Mradi kwa mikoa

mingine, Timu ya Tathmini ya Mwisho ilipendekeza

kuwa kipindi cha mradi kiongezwe kwa mwaka

mmoja; kutoka Aprili 2006 hadi 2007 Machi na JICA

itoe msaada kamili. Katika siku zijazo mradi unaweza

kuwa mfano wa kujenga uwezo wa uendeshaji katika

mifumo ya afya Tanzania. Tanzania na Japan hazina

budi kufanya kazi zaidi kwa pamoja ili kuleta ubora

na usawa katika huduma za afya Tanzania.

Mradi wa Afya Morogoro ungependa kuwashukuru

Wadau wote kwa juhudi endelevu na unaridhia

kutenda zaidi ndani ya Mradi.

Ukitaka taarifa zaidi kuhusu Taarifa ya Mwisho ya

Tathmini inapatikana ofisi ya Mradi wa Afya

Morogoro, Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa na Ofisi

za Waganga Wakuu wa Wilaya Mkoa wa Morogoro.

Asanteni sana kwa ushirikiano na kujali kwenu.

Hatuna budi kutumikia ili tufikie maisha mazuri kwa

Watanzania wakati ujao.

Dk. T. Sugishita

Mshauri Mkuu

Mradi wa Afya Morogoro

- Yaliyomo -

Tathmini ya Mwisho ya Pamoja Mradi wa Afya Morogoro 1 Tahariri 3 Tabia na Mila Zinazodhuru Meno 4 Dawa Mpya ya Kutibu Malaria 4 Wachuuzi wa Chakula: Taarifa Utafiti 6 Kuboresha Mazingira kwa Kuhusisha Jamii 7 Huduma ya Wagonjwa Nyumbani 8 Utafiti wa Kiafya Kiutendaji Unavyoendeshwa 9 Matukio Muhimu : Agosti - Desemba 2005 11 Vichekesho 12

BODI YA UHARIRI

Mwenyekiti:

Bw. N. Masaoe Afisa Afya Mkoa

Katibu:

Bi. C. Maro Mratibu wa Huduma za Afya ya

Uzazi na Mtoto Wilaya Morogoro

Msaidizi wa Katibu:

Bi. N. Ahmed Afisa Muuguzi Manispaa Morogoro

Wajumbe:

Bw. J. Mankambila Katibu wa Afya Mkoa

Dk. G. Mtey Mganga Mkuu Manispaa Morogoro

Dk. O. Mbena Mganga wa Meno Wilaya Mvomero

Bw. J. Bundu Afisa Afya Wilaya Kilosa

Bw. D. Dia Katibu wa Afya Wilaya Kilombero

Bw. W. Mkessey Afisa Afya Wilaya Ulanga

Bi. M. Tsuda Mshauri, MHP*

Mshauri Mkuu:

Dk. M. Massi Mganga Mkuu Mkoa

Mjumbe Mshiriki:

Dk. F. Fupi Mshauri, MHP*

Kamati ya Ushauri:

Bw. H. Mohamed Mhadhiri, Chuo Kikuu cha Sokoine cha

Kilimo, Morogoro

*MHP: Mradi wa Afya Morogoro (Morogoro Health Project),

JICA

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

3

JARIDA LA AFYA MOROGORO Wasomaji wetu wapendwa,

Kwa niaba ya bodi ya uhariri ya hili jarida,

napenda kuwakaribisha kwa Toleo la tano la hili

jarida.

Leo napenda kukazia mambo mbalimbali. Jamii

inatakiwa kufahamu kwamba, ugonjwa wa Malaria

ambao ni tatizo linaloongoza katika afya ya jamii,

sasa hautibiki kikamilifu na dawa aina ya

Sulfadoxine - Pyrimethamine (SP). Tiba mseto ya

huu ugonjwa itaanza kutolewa mwaka 2006. Jamii

inashauriwa kuweka kwa pamoja mikakati ya mseto

ya kupambana na mbu wanaoeneza Malaria kwa:

kila mtu kutumia chandarua chenye viuatilifu,

kuharibu mazalia yote ya mbu katika makazi,

kuweka nyavu za kuzuia mbu kwenye nyumba,

kuwa na silka ya kutafuta tiba mapema na kadhalika.

Bodi ya Uhariri inapongeza kwa dhati kwa

uongozi wa Serikali Kuu na halmashauri zote za

mkoa wa Morogoro kwa kuthamini hili jarida na

hivyo kutenga, katika bajeti za mwaka, fedha za

kuchapisha hili jarida. Moyo huu umefurahisha sana

Shirka la JICA ambao ndio wafadhili wa Mradi wa

Afya Morogoro (“MHP”), kwa kuwa ni dhahiri

kwamba jarida litakuwa endelevu, hata baada ya

Ufadhili wa Mradi kuhitimishwa.

Wajumbe tisa wa hii Bodi wamepatiwa mafunzo

ya “type setting” na “computer skills” ya siku nne

katika Chuo Kikuu Mzumbe. Mafunzo yalikuwa

muhimu na hii ni hatua ya maana katika kujenga

uwezo wa bodi kumudu shughuli za kitaalamu za

kuhariri na kuchapisha hili jarida. Bodi inatoa

shukrani kwa Mradi wa Afya uliolipia haya

mafunzo.

Kikundi cha wataalamu 4 wa nje: Ms. Harumi

Kitabayashi, Prof. Ichiro Okubo, Mr. Ikuo Takizawa

na Ms. Minako Nakatani waliofanya Tathmini ya

Mwisho ya Mradi wa Afya Morogoro tarehe

1-10-2005 hadi 23-10-2005; walitembelea

halmashauri zote sita za mkoa huu. Katika vituo vya

huduma ya afya walivyotembelea, walikuta makala

za hili jarida. Baadhi ya watoa huduma walitumia

makala ya jarida hili kutoka elimu ya afya. Hili

limewafurahisha sana. Bodi inawapongeza sana

wale wote wanaosoma na kutumia hili jarida

kuelimisha umma. Wengine wanashauriwa kuiga.

Timu ya Tathmini iliridhika na utehelezaji wa

Mradi na iliona kuwa makusudio ya “MHP” ya

kujenga uwezo wa uendeshaji wa Timu za Afya

Mkoani Morogoro yamefanikiwa kwa kiasi

ambacho kilitazamiwa kutegemea hali halisi.

Bodi inazidi kuomba wasomaji wa hili jarida

kutuma habari na maoni ya kuchapishwa, ili kukidhi

adhma ya kuanzishwa kwa jarida hili, yaani

kubadilishana uzoefu na maoni baina yawatendaji

wa afya na jamii kwa ujumla.

Nachukua nafasi hii kuwaarifu wasomaji wetu

kwamba, mwaka 2006 katikati ya Januari nitastaafu

rasmi na hivyo, uenyekiti wangu kwa Bodi unafika

ukingoni 2005 kati ya Desemba. Namtakia

mwenyekiti ajae Dk. G. Mtey kazi na afya njema na

kumuahidi msaada na kujitolea thabiti kwa

maendeleo ya hili Jarida.

Aidha nashukuru wajumbe wote wa Bodi ya

Uhariri na wasomaji kwa ushirikiano, msaada na

kujituma kwao, kuliowezesha kufanikisha malengo

ya hili jarida. Tutaonana Mungu akipenda.

Nawatakia wasomaji wote Krismasi njema na

Mwaka Mpya.

Bw. N. Masaoe

Mwenye Kiti

Bodi ya Uhariri

Bw. N. MasaoeMwenyekiti

Bodi ya Uhariri

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

4

TTAABBIIAA NNAA MMIILLAA ZZIINNAAZZOODDHHUURRUU MMEENNOO

Meno ya binadamu ni kiungo muhimu katika

mwili wake, yanaweka uzuri wa uso, ulinzi hasa

kama silaha na kutafuna vyakula na matunda.

Hivyo yanatakiwa kutunzwa yasiharibike kwa

kutibiwa na kukaguliwa maramara.

Walakini baadhi ya watu wamekuwa wakifanyiwa

urembo wa meno wa kimila katika baadhi ya nchi,

kulingana na tamaduni. Urembo huo umefaywa

maarufu na mataifa mengi. Katika karne kadhaa

zilizopita. Urembo wa meno kimila ulikuwa na

maana mbalimbali ikiwemo alama wakati wa vita na

sifa hasa kwa wanawake.

Meno pia yalikuwa yanatolewa kwa manufaa ya

tiba kuondoa maumivu. Wakati mwingi ilikuwa ni

tiba ya imani tu na mara chache ilikuwa tiba sahihi.

Urembo wowote ule wa meno unaharibu kinywa na

meno yenyewe.

Siku hizi urembo hauna faida kwa Mtanzania.

Hatuna budi kusisitiza kuwa watu wasirembe meno

au kuyang’oa bila sababu ya kufaa.

Baadhi ya mila na desturi zinazostahili kupingwa

ni:

• Kuchonga au kukwangua meno. Hii inaondoa

ganda la juu linalolinda jino.

• Kung’oa meno ya chini ya mbele.

• Kutoa meno ya juu na kutoboa mdomo wa juu

na kuweka “ndonya” (kitu mviringo) ambacho

ni alama ya urembo kwa wanawake wazima.

• Kung’oa meno ya utotoni mara yanapoanza

kulegea huumiza mtoto na kuchelewesha kuota

meno ya kudumu. Uvumi wa meno ya “plastic”

au “nylon” si kweli.

• Kutumia meno kufungulia vizibo vya chupa,

kukata kamba, kutafuna mifupa na kunyanyua

vitu vizito.

• Kukwangua meno kwa kutoa rangi iliyoganda

kwa mfano “fluorine”.

Hasara ya kuchonga meno:

• Kuumwa kwa jino wakati wa kula kitu moto au

baridi.

• Kufanya jino lioze kwa urahisi.

• Meno kulegea kwa urahisi na hatimaye

kungoka.

Kwa hiyo tuzingatie masharti ya miongozo ya

kulinda meno kwa afya njema.

Dk. O. Mbena

DDO Mvomero

DDAAWWAA MMPPYYAA YYAA KKUUTTIIBBUU MMAALLAARRIIAA

Malaria bado ndiyo ugonjwa hatari kupita yote

katika Dunia ya Tatu. Malaria inaongoza kwa maana

ya kuugua na vifo, hasa kwa watoto chini ya umri wa

miaka mitano na akina mama wajawazito. Serikali

imetoa mwongozo wa ugunduaji na tiba ya ugonjwa

wa Malaria ili kuwa na utabibu unaofanana nchi

nzima. Msingi wa mwongozo wa sera ya dawa ya

Malaria ni kuongeza usalama, ufaaji, ubora, gharama

nafuu, upatikanaji, kukubalika kwa tiba ya Malaria na

kupunguza ustawi wa usugu wa dawa.

Hapo Agosti 2001 nchi yetu ilibadilisha mwongozo

wa sera ya tiba ya Malaria kutoka tiba moja ya

“Chloroquine” kwenda “Sulfadoxine – Pyrimethamine

(SP)” tiba ya mchanganyiko kama tiba ya dawa ya

mstari wa kwanza kwa ugonjwa wa Malaria. Walakini

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

5

kwa miaka 4 iliyopita tayari usugu wa ugonjwa wa

Malaria kwa kutumia dawa aina ya SP umeripotiwa

kuongezeka. Tafiti zilizofanyika nchini Tanzania hivi

karibuni (2004) zimeonyesha kuwa tiba ya SP

imeshindikana kwa wastani wa asilimia 25.5 %.

Usugu wa SP (molecular markers) umeonyesha

kiwango kikubwa cha viini vya Malaria kubadilika

(mutation). Tiba ya “Amodiaquine”, iliyokuwa mstari

wa 2 kwa tiba ya Malaria, iliyoonyesha kushindwa

kwa wastani wa asilimia 12 %. Matokeo haya yana

onyesha kuwa kuna haja ya kubadili mwongozo wa

tiba.

Kutokana na hatari ya kuongezeka usugu wa

wadudu wa Malaria kwa dawa moja. Hivi sasa duniani

kote kuna mwelekeo wa kutumia tiba ya dawa

mchanganyiko. Sababu nyingine ni kwamba dawa

mchanganyiko zina faa zaidi na kuna uwezekano wa

kuchelewesha ueneaji wa usugu wa dawa.

Tiba iliyopendekezwa:

• Mchanganyiko ulipendekezwa ni dawa aina ya

“ARTEMETHER / LUMEFANTRINE (ALU)”

kama tiba ya mstari wa kwanza kwa ugonjwa wa

Malaria. (Tazama Jedwali-1)

• Endapo ALU ikishindwa kutibu au kwa sababu

yeyote mgonjwa atumie dawa iliyopo mstari wa

pili ambayo ni “Quinine”.

• Dawa iliyopendekezwa kwa tiba ya Malaria kali

ni Quinine.

• Hata hivyo dawa iliyo katika mstari wa kwanza

kwa tiba ya Malaria kwa wanawake na watoto

chini ya uzito wa kg 5 (chini ya miezi miwili) ni

Quinine.

• Dawa aina ya SP itaendelea kutumika tu kwa

akina mama wajawazito kwa kuzuia Malaria

(Intermittent Presumptive Treatment – IPT). Dozi

ya kwanza pale wanapokuwa na ujauzito wa wiki

20 - 24 na dozi ya pili (IPT) wanapokuwa na

wiki 28 - 32.

Utumiaji wa SP kwa mama wote wajawazito

utazuia hatari ya vimelea kwenye damu na vimelea wa

Malaria kwenye kondo la nyuma; kwa sababu vimelea

vilivyo kwa mama mjamzito mara nyingi havionyeshi

dalili mapema.

Dawa ya SP hupewa mama wajawazito na kumeza

mbele ya wahudumu afya (“DOT”) katika clinic zao.

Ridhaa ya mgonjwa kutumia sahihi dawa aina ya

ALU ni muhimu sana kwa sababu ALU siyo dozi

moja. Maelezo sahihi kuhusu dawa ni muhimu sana

kwa wateja. Mama wajawazito wote wanahimizwa

kutumia vyandarua vyenye dawa (ITNs) licha ya tiba

ya kuzuia (IPT).

Kitabu cha: Rejea Malaria namba 10

Bi. C. Maro

DRCHCo Morogoro

Jedwali-1 Utaratibu wa dozi za ALU – Dozi ya vidonge Artemether 20 mg & Lumefatrine 120 mg (ALU)

Uzito (Kgm)

Umri Siku 1 Siku 2 Siku 3 Msimbo

Dozi 1 2 3 4 5 6 Masaa 0(“) 8 24 36 48 60 vidonge vidonge vidonge vidonge vidonge vidonge 5-14 Miezi 3 hadi

Miaka 3 1 1 1 1 1 1 Njano

15-24 Miaka 3 hadi Miaka 7

2 2 2 2 2 2 Buluu

25-34 Miaka 7 hadi Miaka 12

3 3 3 3 3 3 Nyekundu

35 na zaidi

Miaka 12 na zaidi

4 4 4 4 4 4 Kijani

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

6

WWAACCHHUUUUZZII WWAA CCHHAAKKUULLAA:: TTAAAARRIIFFAA UUTTAAFFIITTII WWAA EELLIIMMUU NNIIAA NNAA DDEESSTTUURRII

Biashara ya uuzaji vyakula inayofanywa na

wachuuzi wa chakula, inashamiri haraka mijini na

kando ya miji. Hii biashara inayofahamika kwa jina

la fumbo (nick name) kama “mama/baba lishe” licha

ya kupatia chakula wateja kwa bei nafuu, imepatia

ajira akina mama na baba wengi wa umri wa kati na

wengineo. Vikundi vingine hutoa huduma ya

chakula katika sherehe kama harusi mazishi nk.

ambapo watu wengi hushiriki kula.

Usindikaji wa matunda, achali, na hata mvinyo

kwa matumizi ya binadamu hutayarishwa na baadhi

ya hivi vikundi.

Usafi wa hawa “mama/baba lishe” (food vendors)

siyo wa kuridhisha. Hivyo watumiaji wa hivi

vyakula huwa katika hatari isiyojulikana ya kupata

maradhi yanayotokana na chakula kilichochafuliwa.

Kutokana na hali hii, utafiti wa Elimu, Nia na

Desturi wa “mama/baba lishe” umeendeshwa katika

Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Matokeo, hitimisho na Ushauri wa huu utafiti unafaa

sana kwa uimarishaji wa biashara ya mama/baba

lishe nchini kote.

Washiri 175 walidodoswa kwa dodoso la

maandishi katika eneo lililofanyiwa utafiti.

Walio dodoswa walikuwa na sifa zifuatazo:

• Umri kati miaka 18 hadi 48.

• Jinsi: 154 [88%] wanawake, 21 [12%]

wanaume.

• Elimu: 150 [86%] msingi, 13 [7%]

sekondari/ufundi na 12 [7%] hawana darasa.

• 172 [98%] wamepata mafunzo kuhusu usalama

wa chakula na 3 [2%] hawakuwa na ufahamu.

Mazingira chakula kilipoandaliwa na kuuzwa:

• Mabaki ya vyakula na plastiki zilizotumika

zimezagaa ovyo.

• Vyombo vya kulia vichafu, huhifadhiwa kwa

mifuko ya plastiki iliyotumika.

• Hakuna dawa za kutakasa ama sabuni ya

kunawa mikono.

• Uondoshaji mbaya wa maji taka na taka

ngumu.

• Baadhi ya vibanda ni chakavu, vibovu sana na

havina huduma muhimu kama: maji, sehemu ya

kujisaidia, [vyoo] vifaa vya kuzolea taka

ngumu na majitaka.

Mambo mazuri yaliyoonekana:

• Chakula kuuzwa kingali cha moto kwa wateja

wa awali.

• Bei wanazimudu wateja.

• Maji moto kwa kuoshea vyombo na kunawia

mikono, yapo katika baadhi ya sehemu.

Desturi mbaya kwa mama/baba lishe wengi

wakiwa kazini:

• Kuzungumuza.

• Kuchokonoa puani ama meno kwa vidole.

• Kujikuna mwili.

• Kupiga chafya bila tahadhari.

• Kukohoa ovyo.

• Kuvuta sigara wakipika au kupakua chakula.

• Kutopimwa afya zao kabisa au kupimwa bila

utaratibu.

• Kutokuwa na sare na zana za kujikinga.

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

7

Hitimisho na mapendekezo:

Shughuli za wachuuzi wa chakula inakua haraka

na kutoa ajira kwa akina mama na baba wa umri

mbalimbali. Wateja wengi hujipatia mlo kwa bei

nafuu.

Mamlaka husika ina wajibu wa kusimamia na

kuidhibiti kwa mujibu wa sheria zilizopo kwa:

• Kutambua, kusaili na kutoa vibali kwa mama

na baba lishe wote.

• Kutambua uongozi wao na kuwa na mdahalo

na mikutano mara kwa mara ya kuboresha

shughuli zao.

• Kuwahusisha wadau wote katika kuweka

viwango vinavyokubalika.

• Kuwapatia mafunzo na mafunzo rejea kuhusu

usalama wa chakula. Mafunzo yangeweza

kulipiwa kutoka Mipango Kabambe ya Afya ya

Halmashauri (CCHP).

• Kuwasaidia kupata mikopo ya kuimarisha

shughuli zao.

• Kuwa na ratiba ya kuchunguza afya zao.

• Kuhakikisha kila mama na baba lishe anavaa

sare na zana za kujikinga awapo kazini.

• Kuto waweka watoto wadogo/wachanga karibu

na maeneo ya biashara.

Bi. L. F. Temu

Afisa Afya [Mazoezini]

Morogoro

KKUUBBOORREESSHHAA MMAAZZIINNGGIIRRAA KKWWAA KKUUHHUUSSIISSHHAA JJAAMMIIII MMAANNIIPPAAAA YYAA MMOORROOGGOORROO

Manispaa ya Morogoro ni kati ya Manispaa zenye

mandhari na mazingira yanayovutia ya milima ya

Uluguru na mito mingi inayotiririka. Uzuri huu

umekuwa ukiporomoka kila mwaka kutokana

sababu zifuatazo:

• Wakazi wengi hawathamini usafi. Hawashiriki

kikamilifu katika mikakati ya kusafisha

Manispaa yao.

• Taka ngumu na taka mimina hulundikana

kwenye makazi bila kuondolewa.

• Baadhi ya nyumba za kuishi hazina:

○ Vyoo vinavyokubalika

○ Mashimo ya maji machafu ya kufaa

○ Karo za kuoshea vyombo na kufulia

○ Vifaa vya kuhifadhia taka za nyumbani

• Chupa za plastiki na mifuko iliyotumika

huzagaa ovyo kwenye maeneo yote ya

Manispaa.

• Baadhi ya wakazi hufugia kwenye maeneo ya

watu wengi, hivyo kusababisha kero na adha

kubwa kwa majirani.

Manispaa ya Morogoro kwa mara tatu mfululizo

imekuwa ya 12 kati ya Manispaa 13 za Tanzania

bara, katika mashindano ya usafi wa mazingira

yanayoendeshwa na Wizara ya Afya. Kutokana

sababu zilizotajwa na nyingine kama: machinjio na

chakavu, makaburi yasio na uzio, soko kuu

lisilokarabatiwa, barabara mbaya, mifereji ya maji

ya mvua isiyotunzwa na kuwepo kwa makazi mengi

yasiyopimwa (squarters).

Wakazi wa Manispaa wanatakiwa kuwajibika

kikamilifu kwa afya na usafi wa manispaa yao, kwa

kuingia ubia na uongozi ya Manispaa ili kubadili

hali hii.

Mwaka 2003, Manispaa kwa msaada toka Ubalozi

wa Denmark kupitia shirika la DANIDA wamebuni

mkakati mpya kwa kuanzishwa kwa mpango

endelevu wa “Sustainable Morogoro Project”

(SUMO). Mpango huo ukiungwa mkono utakuwa

Daima sisitiza uuziwe chakula cha moto, kilichoandaliwa kwa usafi

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

8

sehemu ya utatuzi wa tatizo hili.

Mojawapo ya malengo ya SUMO ni

kushughulikia tatizo la taka ngumu katika manispaa

kwa mbinu shirikishi inayotekelezeka na makini

kwa kutupa taka ngumu unaofahamika kama

“Sustainable Solid Wastes Program” ambao

umeanza kutekelezwa tangu Julai 2005. Programu

hiyo inatekelezwa na jamii ikishirikisha akina mama

na vijana “Community Based Organizations”

(CBOs) wanaoondoa taka ngumu wakishirikiana na

manispaa.

Huu mpango unatarajiwa, licha ya kuwapa CBOs

sauti ya kuumiliki pia unawawezesha kiuchumi na

hivyo kuchangia katika Mpango wa Kupunguza

Umaskini (MKUKUTA).

Hawa CBOs wanatarajiwa kukusanya malipo ya

uzoaji taka ngumu toka kwa makazi na kuendeleza

usafi wa mitaa na mitaro ya maji machafu na

maeneo ya wazi. Pia kuwasaidia Maafisa Afya

katika kutekeleza kanuni za afya katika maeneo yao.

Watazolea taka kwa mapipa maalumu “Skip Bucket”

na kulipa kwa manispaa gharama za kusafirisha

hayo mapipa maalumu hadi “dampo”. Akaunti

maalumu itafungliwa ili kufanya huu mpango kuwa

endelevu kwa kugharamia utunzaji wa “dampo” la

manispaa na ununuzi wa vifaa vipya.

CBOs watachaguliwa kwa nia ya zabuni katika

ngazi ya kata, kwa kupitia Kamati ya Maendeleo ya

Kata (WDC). Watakaofanikiwa, wataidhinishwa na

kamati ya zabuni ya “Manispaa Council Tender

Board”, wataazima vifaa muhimu vya kuanzia kazi.

Usimamizi na ufuatiliaji utafanyika katika ngazi

ya kata yaani WDC. Katika ngazi ya Manispaa, hili

litafanyika katika Kata na mfuko wa kusafirisha

“Skip Bucket”.

Habari hii inalenga kuamsha hamasa kwa wadau

wote ili kupata ushirikiano wao katika utekelezaji

wa huu mpango, na pia mchango wa maoni wa

kuboresha mpango wenyewe.

Imani yetu ni kwamba “Tunaweza kuleta

mabadiliko tukiiunga na pamoja”.

CHMT

Manispaa ya Morogoro

HHUUDDUUMMAA YYAA WWAAGGOONNJJWWAA NNYYUUMMBBAANNII WWIILLAAYYAA YYAA KKIILLOOSSAA

Wilaya ya Kilosa imeanzisha mpango wa huduma

ya wagonjwa nyumbani kwa wanaoishi na virus vya

UKIMWI na wenye magonjwa ya kusendeka.

Magonjwa hayo ni:

UKIMWI, Kisukari, Kifafa, Saratani, Kifua kikuu,

Magonjwa ya akili na Magonjwa ya moyo.

Sababu za kuanzisha huduma hii ni:

• Kuongezeka kwa magonjwa ya UKIMWI na ya

kusendeka. Asili mia 50 – 60% ya vitanda vya

hospitali hutumiwa na wagonjwa wa UKIMWI

na ya kusendeka.

• Kuwawezesha Wafanyakazi wa Afya kusaidia

kufundisha Familia zenye wagonjwa wa

UKIMWI pamoja na magonjwa sugu kuweza

kuwahudumia wagonjwa wao nyumbani.

Malengo mahususi ya huu mpango ni:

• Kupunguza maumivu sugu kwa wagonjwa

wanaoishi na virus vya UKIMWI.

• Kuelimisha na kusaidia wanaohudumia

Saidia magonjwa ya akili katika jamii kwa huduma ya nyumbani

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

9

wagonjwa wanaoshi na virus vya UKIMWI au

UKIMWI na magonjwa sugu ili aweze kutoa

huduma ya kitaalam kwa wagonjwa wao

nyumbani.

• Kutoa ushauri nasaha kwa wagonjwa pamoja na

ndugu zao jinsi ya kupunguza maumivu, msongo

unaotokana na UKIMWI na magonjwa sugu.

• Kusambaza vifaa vya kitaalamu, dawa na

vitendea kazi kwa wahudumu wa huduma ya

wagonjwa nyumbani.

• Kuelimisha jamii na kushauri kuanzisha huduma

hii na kuelewa kuwa njia hii itawasaidia.

• Kuelimisha jamii jinsi ya kujikinga na

maambukuzi na namna ya kuhudumia wenye

magonjwa ya kusendeka nyumbani.

Maafisa tabibu 14 na Wauguzi wa afya ya jamii 28

walipatiwa mafunzo ya siku 21, kuhusu huduma ya

wagonjwa nyumbani. Hawa walianza kutekeleza huu

mpango katika vituo vyao vya kazi.

Wizara ya Afya kupitia Tume ya Kudhibiti Ukimwi,

imetoa baiskeli 14 kwa watoa huduma hii, na pia

kununua dawa kwa vituo 14 vya huduma, ikiwepo

hospitali moja, vituo vya afya 5 na zhanati 8. Fedha

zilipokelewa pia za kununua chakula (unga na sukari)

kwa hivyo vituo 14 vinavyo tekeleza huu mpango.

Faida zitakazotokana na huduma hii ni pamoja na:

• Jamii inahamasika hivyo kutowanyanyapaa

wanaoihi na virus vya UKIMWI.

• Itapunguza wingi wa wagonjwa wanaolazwa

hospitalini.

• Itapunguza maambukizo mapya ya virus vya

UKIMWI kwa jamii.

• Wanaotunza wagonjwa kwa huu utaratibu

watapata nafasi ya kufanya shughuli nyingine za

kuzalisha kipato.

Huduma hii itamsaidia mgonjwa vitu vifuatavyo:

• Kuzuia magonjwa nyemelezi kwa kutoa

matibabu.

• Kuwapatia huduma muhimu km. vyakula vyenye

virutubisho na nyumba zene mwanga wa

kutosha.

• Kuendeleza usafi wa mwili na usafi wa

mazingira.

• Kuwapatia mazoezi mara kwa mara.

• Kujenga uwezo wa wahudumu wa huduma ya

wagonjwa nyumbani.

• Kuwapatia burudani na michezo.

• Huduma za kiroho.

• Msaada wa kisheria.

• Msaada wa kifedha.

• Kuelimisha jamii kuhusu matumizi ya dawa za

kurefusha maisha kwa wenye UKIMWI.

Kwa kupitia huu utaratibu wa “Home Based Care”

(HBC) wagonjwa wa UKIMWI hupatiwa

Antiretroviral (ARV) kufuatana na mwongozo wa

World Health Organization (WHO). Wilaya inalenga

kusambaza hii huduma kwa vtuo 49 vya huduma ya

afya vilivyobaki katika miaka mitatu ijayo.

Dk. W. Munuo

Mratibu wa magonjwa ya kusendeka nyumbani

Kilosa

MMAAEELLEEZZOO YYAA UUJJUUMMLLAA KKUUHHUUSSUU UUTTAAFFIITTII WWAA KKIIAAFFYYAA KKIIUUTTEENNDDAAJJII UUNNAAVVYYOOEENNDDEESSHHWWAA KKWWAA

PPAAMMOOJJAA TTAANNZZAANNIIAA NNAA JJAAPPAANN KKAATTIIKKAA MMRRAADDII WWAA AAFFYYAA MMOORROOGGOORROO

Hivi karibuni Mkusanyo (Corpus) wa Kwanza wa

Taarifa za Utafiti wa Kiafya Kiutendaji (“Health

Operational Research”) ulitolewa ukiwa ni matokeo

ya mafunzo ya vitendo kwa Timu za Afya za

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

10

Uendeshaji (Health Management Teams - CHMTs), ya

Mkoa na za Halmashauri za Wilaya, Mkoani

Morogoro. Mafunzo hayo yameendeshwa na Mradi

wa Afya Morogoro (“Morogoro Health Project -

MHP”) ambao kusudi lake kubwa ni kuboresha uwezo

wa kuendesha huduma za afya za wilaya Mkoa wa

Morogoro.

Uanzishwaji wa Mabadiliko Katika Sekta ya Afya,

Tanzania, unawataka mameneja wa afya kufuata

mipango yenye misingi ya ushahidi. Mipango ya

namna hiyo huhitaji michakato (processes) ya

kutambua na kuchambua matatizo ya kiafya ya mahali

husika na kuyaingiza katika Mipango Kabambe ya

Afya ya Halmashauri ya Wilaya (Comprehensive

Council Health Plans - CCHPs). Kutokana na hali

hiyo ufanyaji wa “Operational Research (OPR)” kwa

kusudi la kupata ushahidi umekuwa ni shughuli ya

pekee lakini muhimu inayofanywa na hizo Timu za

Afya za Uendeshaji. Mtindo na fikira zinazozingatia

uchambuzi (“analytical attitude and thinking”),

ambazo zinaweza kujengeka kwa njia ya uendeshaji

“OPR”, ni vitu vya lazima kwa mameneja wa afya ili

waweze kuyamudu mazingira mageni

yanayotazamiwa katika Mabadiliko ya Jamii kwa

Ujumla (Public Sector Reforms - PSR) yanayofanywa

na Serikali.

Kwa sababu ya madai thabiti kutoka kwa mameneja

wa afya “MHP” umesaidia, tangu Septemba 2004,

uendeshaji wa “OPR” halisi unaofanywa na Timu za

Afya za Uendeshaji za Halmashauri na ya Mkoa

katika wilaya husika. Zaidi ya hayo Mradi unatoa

ujuzi stadi muhimu kwa mameneja hao wa Wilaya na

Mkoa; mradi unahusisha pia jamii na wafanyakazi wa

afya walio mstari wa mbele. Baada ya matokeo ya

utafiti (“OPR”) mipango ilifanywa (pale

panapohusika) na kuingizwa kwenye “CCHPs”.

Topiki (“Topics”), (timu husika katika mabano)

hizo, na mipango hiyo kwa mwaka 2005/6 ni kama

ifuatavyo:

1) Vifo vingi vya Watoto wachanga Manispaa ya

Morogoro (Timu Mkoa) - Mipango: Kuimarisha

Wodi ya watoto wachanga ya mfano

2) Mambo yanayoshawishi utumiaji wa vyandarua

vilivyowekwa dawa miongoni mwa watoto chini ya

miaka 5 Morogoro Mjini (Timu Manisipaa)

- Mipango: Mikutano ya uhamasishaji viongozi wa

vitongoji

3) Uchunguzi wa mkondo wa huduma za afya

zinavyotumiwa na mama wajawazito wakati wa

kujifungua wilaya ya Morogoro (Timu Morogoro)

- Mipango: Kuelekeza watoa huduma wa mstari wa

mbele kuweka mkazo katika uzingatiaji wa huduma

salama kwa wajawazito kabla ya kujifungua

4) Mambo yanayoleta usambazaji duni wa

vyandarua vyenye dawa katika udhibiti wa

malaria Wilaya ya Mvomero (Timu Mvomero)

- Mipango: Uhamasishaji wa Sekta Binafsi kuuza

vyandarua vyenye dawa

5) Uchunguzi wa i sababu zinazolleta mlipuko wa

magonjwa ya kuhara miongoni mwa familia katika

Tarafa 3 Wilaya ya Kilosa (Timu Kilosa)

- Mipango: Uhamasishaji wa jamii kuhusu udhibiti wa

kipindupindu

6) Kuchunguza utendaji wa Mipango ya Afya

katika kudhibiti milipuko ya kipindupindu Tarafa

ya Ifakara Wilaya ya Kilombero (Timu Kilombero)

- Mipango: Kutoa mafunzo ya “Participatory Hygiene

and Sanitation Transformation (PHAST)” kwa jamii

na wasaidizi wa afya

7) Uchunguzi wa mambo yanayoleta uwingi wa

kuugua na vifo kwa watoto chini ya miaka 5 katika

Tarafa ya Mwaya, Wilaya ya Ulanga (Timu

Ulanga) - Mipango: Mafunzo juu ya “Intergrated

Management of Childhood Illness (IMCI)” kwa Jamii

Hapo Novemba 2004 “MHP” ilianzisha Kundi la

Kazi (“Working Group - WG”), lililoundwa kutokana

na mjumbe mkutanishi (contact person) kutoka kila

Timu ya Afya ya Uendeshaji ya Wilaya na ya Mkoa.

Kwa njia ya majadiliano ya kina mara kwa mara

katika mikutano ya “WG” wajumbe wamejijengea

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

11

uelewano (“rapport”) miongoni mwao na kukubali

mapendekezo na ukosoaji wa kujenga kutoka kwa

watu wengine kwa nia ya kuboresha usahihi wa utafiti.

Kutokana na hali hiyo wajumbe wanaboresha ujuzi

wao wa mawasiliano na wa kufanya kazi kama timu,

ambao moja kwa moja unatumiwa na kila Timu ya

Afya ya Uendeshaji anapotoka mjumbe wa “WG”.

Wajumbe wa “WG” ndio chombo muhimu cha

kuchochea uendeshaji wa utafiti.

Kwa kifupi, uendeshaji wa “OPR” umejenga,

miongoni mwa mameneja wa afya, hali ya “kujiamini”,

ambayo ni muhimu katika kufanikisha kukabiliana na

changamoto ya kazi yao ya uendeshaji kwa kutumia

ujuzi unaotakiwa. Mwisho Tunaweza kuhitimisha kwa

kusema kuwa uendeshaji wa “OPR” ni miongoni mwa

njia zinazofaa kuimarisha uwezo wa uendeshaji wa

mameneja wa afya mkoani na wilayani katika

mchakato wa kuipelekea jamii madaraka utokanao na

Mabadiliko ya Jumla Katika Sekta ya Jamii (PSR),

Tanzania.

Kutokana na umuhimu wa kufahamishana matokeo

ya utafiti miongoni mwa mamlaka mbalimbali ngazi

husika ili kuufaidi vizuri utafiti, Timu za Afya za

Uendeshaji Mkoa na Wilaya zimeamua, kwa

kushirikiana na wadau, kupanga shughuli za kueneza

taarifa za matokeo ya utafiti kwa kutumia njia

zinazofaa kikamilifu katika kila wilaya husika. Kundi

la Kazi la Utafiti (OPR WG) linatambua kuwa Jarida

la Afya Morogoro ni mojawapo ya njia zinazofaa

kikamilifu kueneza taarifa na linashukuru kupewa

nafasi katika jarida hili kwa shughuli za utafiti.

Shukrani zinatolewa kwa wafuatao. Timu za Afya

za Uendeshaji Mkoa na Wilaya kwa kujitolea kwao,

mamlaka za Utawala ngazi ya Mkoa na Wilaya kwa

msaada na ushirikiano wakati wote wa zoezi la utafiti,

kwa wafanyakazi wa afya wa mstari wa mbele na

jamii katika wilaya zote kwa ushirikiano wakati wa

ukusanyaji takwimu.

Inaamainiwa kuwa mameneja wa afya Mkoa wa

Morogoro wataendelea kustawisha uwezo wao wa

uendeshaji kwa kuendeleza utekelezaji wa “OPR”

ambao utaleta matokeo mazuri kwa njia mbalimbali

kadiri inavyowezekana, ili kufanikisha kikweli

huduma bora zaidi na hivyo kuleta hali ya afya bora

zaidi kwa watu wa Mkoa wa Morogoro na kwa

Watanzania kwa ujumla.

Bi. E. Fukushi

Mtaalamu Mshauri na Kundi la Kazi La Utafiti

Mradi wa Afya Morogoro

MATUKIO MUHIMU : Agosti - Desemba 2005 AGOSTI 1 - 5, 2005 Mkutano wa Waganga Wakuu wa Mkoa

Kauli mbiu: “Magonjwa yasiyo ya kuambukiza: changamoto ya Watanzania” Mahali: Mtwara

AGOSTI 8, 2005 Nane Nane (Siku ya Wakulima)

Kauli mbiu: “Kilimo bora ni nyenzo muhimhu ya kuondoa aina zote za umaskini”

Mahali: Mbeya (Kitaifa) na Morogoro (Kikanda)

OKTOBA 2 - 23, 2005 Tathmini ya Mwisho ya Mradi wa Afya Morogoro (“MHP”) Taarifa ilionyesha mafanikio mazuri; Mradi umeongezewa kipindi cha mwaka mmoja hadi 2007 Machi

OKTOBA 14, 2005 Siku ya Nyerere NOVEMBA 18, 2005 Ufunguzi wa Maktaba ya Afya Kilosa DESEMBA 1, 2005 Siku ya UKIMWI Duniani Kauli mbiu: “Tokomeza UKIMWI: timiza ahadi” Mahali: Songea, Ruvuma

DESEMBA 9, 2005 Siku ya Uhuru DESEMBA 14, 2005 Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Jarida La Afya Morogoro – Na.5

12

VICHEKESHO Umuhimu wa Usalama wa Chakula kwa Jamii Mtungaji/Mchoraji : Bw. N. Masaoe & Bw. J. Bundu

Makala au barua za maoni zitumwe kwa anuani zifuatazo:-

Mhariri, Jarida la Afya Morogoro S.L.P. 110, MOROGORO au, S.L.P. 1193, MOROGORO FAX 023 - 2614148

Au

Yapelekwe kwenye ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya husika:-

S.L.P. 166, Morogoro Manispaa S.L.P. 1862, Morogoro S.L.P. 14, Kilosa S.L.P. 47, Ifakara, Kilombero S.L.P. 4, Mahenge, Ulanga

• Tunawaomba wasomaji wetu watoe maoni yao kuhusu jina litakalofaa kuitwajarida hili.

• Aidha tunaomba wasomaji wetu watume makala za kuchapisha kwenye toleo la Julai 2006: zenye maneno yasiyozidi 400, zinazohusiana na afya ama maonikuhusu huduma za afya zinazotolewa katika mkoa wa Morogoro.

LIMECHAPISHWA NA BODI YA UHARIRI JARIDA LA AFYA MOROGORO

S.L.P. 110, MOROGORO

M H P

Morogoro Health Project

Chakula ni cha leoleo tena cha moto.

Mbona unapenda kula chakula kwa mamantilie, pesa yako ndogo nini? Hapo ndiyo tatizo …

Unakula kila kitu.

Je usafi wake vipi?