tekeleza kwa

307
i YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI .................................................................................. 1 2.0 HALI YA SEKTA YA MAJI NCHINI.............................................. 4 2.1 RASILIMALI ZA MAJI..................................................................... 5 2.2 HUDUMA YA MAJI VIJIJINI .......................................................... 9 2.3 HUDUMA YA MAJI MIJINI........................................................... 10 2.4 KUJENGA UWEZO WA KITAASISI ............................................ 14 3.0 UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2014/2015 NA MALENGO KWA MWAKA 2015/2016....................................... 15 3.1 RASILIMALI ZA MAJI................................................................... 15 3.1.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji .............. 15 3.1.2 Ubora na Usafi wa Maji ....................................................... 34 3.2 HUDUMA YA MAJI VIJIJINI ........................................................ 44 3.2.1 Mpango wa “Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa” (Big Results Now – BRN) .................................................. 44 3.2.2 Utekelezaji wa BRN kwa Miradi ya Maji Vijijini.................. 46 3.2.3 Mpango wa BRN kwa mwaka 2015/2016.......................... 48 3.2.4 Hali ya Utekelezaji wa Miradi ya Maji Vijijini..................... 48 3.3 HUDUMA YA MAJI MIJINI........................................................... 63 3.3.1 Kuboresha Huduma za Maji Mijini...................................... 63 3.3.2 Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji ya Mpanda, Njombe na Bariadi.............................................................. 82 3.3.3 Usanifu wa Miradi ya Maji katika Miji Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo.......................................................................... 84 3.3.4 Miradi ya Kutoa Maji kutoka Ziwa Victoria Kupeleka Miji Mbalimbali ........................................................................... 86 3.3.5 Miradi katika Jiji la Dar es Salaam ..................................... 88 3.3.6 Huduma ya Maji katika Miji Mikuu ya Wilaya, Miji Midogo na Miradi ya Kitaifa............................................................. 96 3.3.7 Miradi ya Maji ya Kitaifa ..................................................... 105 3.3.9 Kuzijengea Uwezo Mamlaka za Maji Mijini ...................... 110 3.4 TAASISI ZA WIZARA YA MAJI ..................................................113 3.4.1 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ...........................................................................113 3.4.2 Chuo cha Maendeleo na Usimamizi wa Maji ................... 117

Upload: phungkiet

Post on 30-Dec-2016

943 views

Category:

Documents


45 download

TRANSCRIPT

Page 1: Tekeleza kwa

i

YALIYOMO

1.0 UTANGULIZI .................................................................................. 1

2.0 HALI YA SEKTA YA MAJI NCHINI.............................................. 4

2.1 RASILIMALI ZA MAJI ..................................................................... 5 2.2 HUDUMA YA MAJI VIJIJINI .......................................................... 9 2.3 HUDUMA YA MAJI MIJINI ........................................................... 10 2.4 KUJENGA UWEZO WA KITAASISI ............................................ 14

3.0 UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2014/2015 NA MALENGO KWA MWAKA 2015/2016 ....................................... 15

3.1 RASILIMALI ZA MAJI ................................................................... 15 3.1.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji .............. 15 3.1.2 Ubora na Usafi wa Maji ....................................................... 34

3.2 HUDUMA YA MAJI VIJIJINI ........................................................ 44 3.2.1 Mpango wa “Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa”

(Big Results Now – BRN) .................................................. 44 3.2.2 Utekelezaji wa BRN kwa Miradi ya Maji Vijijini .................. 46 3.2.3 Mpango wa BRN kwa mwaka 2015/2016.......................... 48 3.2.4 Hali ya Utekelezaji wa Miradi ya Maji Vijijini ..................... 48

3.3 HUDUMA YA MAJI MIJINI ........................................................... 63 3.3.1 Kuboresha Huduma za Maji Mijini...................................... 63 3.3.2 Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji ya Mpanda,

Njombe na Bariadi .............................................................. 82 3.3.3 Usanifu wa Miradi ya Maji katika Miji Mikuu ya Wilaya na

Miji Midogo .......................................................................... 84 3.3.4 Miradi ya Kutoa Maji kutoka Ziwa Victoria Kupeleka Miji

Mbalimbali ........................................................................... 86 3.3.5 Miradi katika Jiji la Dar es Salaam ..................................... 88 3.3.6 Huduma ya Maji katika Miji Mikuu ya Wilaya, Miji Midogo

na Miradi ya Kitaifa ............................................................. 96 3.3.7 Miradi ya Maji ya Kitaifa .....................................................105 3.3.9 Kuzijengea Uwezo Mamlaka za Maji Mijini ......................110

3.4 TAASISI ZA WIZARA YA MAJI ..................................................113 3.4.1 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji

(EWURA) ...........................................................................113 3.4.2 Chuo cha Maendeleo na Usimamizi wa Maji ...................117

Page 2: Tekeleza kwa

ii

3.4.3 Wakala wa Uchimbaji Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA)...............................................................................118

3.4.4 Bohari Kuu ya Maji .............................................................120 3.5 MASUALA MTAMBUKA .............................................................121

3.5.1 Sheria ..................................................................................121 3.5.2 Habari, Elimu na Mawasiliano ...........................................123 3.5.3 Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ...............................124 3.5.4 Jinsia ...................................................................................125 3.5.5 UKIMWI ...............................................................................126 3.5.6 Maendeleo ya Rasilimali Watu ..........................................127 3.5.7 Mapambano Dhidi ya Rushwa ..........................................129 3.5.8 Uratibu wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji....129

3.6 CHANGAMOTO NA HATUA ZINAZOCHUKULIWA .................133

4.0 SHUKRANI ..................................................................................141

5.0 MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2015/2016 .....................144

Page 3: Tekeleza kwa

1

HOTUBA YA WAZIRI WA MAJI MHE. PROF. JUMANNE ABDALLAH MAGHEMBE (MB)

AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA MAJI

KWA MWAKA 2015/2016 1.0 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu, baada ya kupokea taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mheshimiwa Profesa Peter Mahamudu Msolla, Mbunge wa Kilolo, ambayo ilichambua bajeti ya Wizara ya Maji; naomba sasa Bunge lako likubali kupokea, kujadili na kupitisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2015/2016. 2. Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kuwashukuru Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa ushauri, maoni na ushirikiano mkubwa walioutoa wakati wa uchambuzi wa taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2014/2015 pamoja na mpango na bajeti ya Wizara yangu kwa mwaka 2015/2016. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba maoni, ushauri na mapendekezo yaliyotolewa na Kamati yamezingatiwa katika bajeti hii. 3. Mheshimiwa Spika, kipekee kabisa naomba kumpongeza Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuteuliwa na Bw. Ban Ki Moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, kuwa Mwenyekiti wa Jopo la Ngazi ya Juu kuhusu Mwitikio wa Kimataifa wa Majanga ya Afya (High-Level Panel on Global Responses to Health Crisis). Vilevile, nampongeza kwa

Page 4: Tekeleza kwa

2

kukabidhiwa Uenyekiti wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Tanzania. Kukabidhiwa kwake majukumu haya makubwa kunaonesha uongozi wake mahiri na madhubuti katika nyanja mbalimbali kitaifa na kimataifa.

Vilevile, napenda kukupongeza Mheshimiwa Spika, kwa kazi nzuri unayoifanya katika kuliwakilisha vizuri Bunge letu Tukufu kitaifa na kimataifa. Nichukue fursa hii kukupongeza kwa kuchaguliwa kwako mwezi Novemba, 2014 kuwa Rais wa Bunge la SADC kwa kipindi cha miaka miwili. Nakuombea kila la kheri na mafanikio katika kutekeleza majukumu hayo. 4. Mheshimiwa Spika, nawapongeza Waheshimiwa Wabunge walioteuliwa kuwa Mawaziri na Manaibu Waziri ili kuziongoza Wizara mbalimbali. Vilevile, nawapongeza Wenyeviti wapya wa Kamati mbalimbali za Kudumu za Bunge waliochaguliwa wakiwemo Mhe. Amina Mohamed Mwidau, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali; Mhe. Festus Bulugu Limbu, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti na Mhe. Richard Mganga Ndassa, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini. Ni mategemeo yangu kuwa katika kipindi hiki kilichobaki tutashirikiana kwa karibu katika kufanikisha majukumu yaliyo mbele ya Bunge letu. 5. Mheshimiwa Spika, vilevile, nichukue fursa hii kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wapya Mhe. Dkt. Grace Khwaya Puja na Mhe. Dkt. Innocent Sebba walioteuliwa na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujiunga na Bunge lako

Page 5: Tekeleza kwa

3

Tukufu. Nawatakia heri na mafanikio katika kazi yao hiyo mpya. 6. Mheshimiwa Spika, nawashukuru na kuwapongeza Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mb), Waziri Mkuu na Mhe. Mary Michael Nagu (Mb), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Uhusiano na Uratibu, kwa hotuba zao ambazo zimetoa mwelekeo wa bajeti na uchumi kwa mwaka 2015/2016 pamoja na utekelezaji wa kazi za Serikali kwa mwaka 2014/2015. Nawapongeza pia, Mawaziri wenzangu wote walionitangulia kuwasilisha hoja zao. 7. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu ilipokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa, taarifa ya kifo cha kipenzi chetu, marehemu Kapteni John Damiano Komba aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi. Nachukua nafasi hii kutoa pole kwako wewe Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu, familia ya marehemu, ndugu na wananchi wa jimbo la Mbinga Magharibi pamoja na Watanzania wote kwa msiba huo mkubwa. Marehemu pamoja na ubunge wake, alikuwa msanii mahiri ambaye Taifa litamkumbuka daima. Vilevile, natoa pole za dhati kwa wananchi waliopoteza ndugu zao na mali kutokana na matukio ya ajali za barabarani, maafa ya mafuriko na mvua kubwa katika maeneo mbalimbali nchini. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu wote mahali pema peponi. Amin. 8. Mheshimiwa Spika, napenda sasa kuchukua fursa hii kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara yangu ambayo inatoa taarifa ya hali ya Sekta nchini; utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2014/2015 na malengo ya mwaka 2015/2016; na maombi ya fedha kwa mwaka 2015/2016.

Page 6: Tekeleza kwa

4

2.0 HALI YA SEKTA YA MAJI NCHINI 9. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatekeleza mipango ya Serikali kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025; Malengo ya Maendeleo ya Milenia 2015; Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA II); Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015; Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/2012 - 2015/2016); Mpango wa “Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa” (Big Results Now - BRN) na Ahadi za Serikali. Aidha, Wizara inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maji chini ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kwa mujibu wa Sera ya Maji ya mwaka 2002; Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Maji (2006 – 2015); pamoja na Sheria za Maji na Kanuni zake. 10. Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali inatekeleza miradi ya maji vijijini kupitia mpango wa BRN ambapo Sekta ya Maji ni moja ya sekta sita zilizopewa kipaumbele katika mpango huo. Awamu ya kwanza ya mpango huo wa miaka mitatu (2013/2014 – 2015/2016) ilianza kutekelezwa mwezi Julai, 2013. Katika awamu hiyo, jumla ya miradi 1,810 inatarajiwa kujengwa na itakapokamilika jumla ya vituo 56,981 vya kuchotea maji vitajengwa na wananchi wapatao milioni 15.4 zaidi watanufaika hivyo kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji vijijini kufikia asilimia 74. Kutokana na mpango huo kuonesha mafanikio katika kutekeleza miradi ya maji vijijini, nimeziagiza Idara zote pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara yangu kuanza kutekeleza majukumu yao kupitia mpango wa “Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa”. 11. Mheshimiwa Spika, Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji inatekelezwa katika vipindi vya miaka mitano kuanzia mwaka 2006/2007 hadi mwaka 2024/2025. Hadi

Page 7: Tekeleza kwa

5

sasa, hali halisi ya utekelezaji katika Sekta ya Maji imefikia hatua mbalimbali kama ifuatavyo:- 2.1 RASILIMALI ZA MAJI 12. Mheshimiwa Spika, Rasilimali za maji zilizopo Tanzania kwa sasa zinakadiriwa kuwa kilomita za ujazo 87 juu ya ardhi na kilomita za ujazo 38 chini ya ardhi. Rasilimali hizo zinatumika kwa matumizi mbalimbali ikiwemo majumbani, kilimo cha umwagiliaji, uzalishaji wa nishati, mifugo, uvuvi, viwanda, uchimbaji wa madini, usafirishaji, utalii na ujenzi. Hata hivyo, mtawanyiko na upatikanaji wa rasilimali hizo nchini hauko sawa katika maeneo yote kutokana na tofauti za kijiografia, kijiolojia na mabadiliko ya hali ya hewa. Vilevile, rasilimali za maji zinatumika kwa ajili ya kuhifadhi bioanuai na kupokea majitaka yaliyosafishwa na kufikia viwango vinavyokubalika baada ya matumizi. Usimamizi wa vyanzo vya maji nchini unaendelea kutekelezwa na Bodi za Maji za Mabonde yote tisa kwa kufuata kanuni za usimamizi wa rasilimali za maji. 13. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa kihaidrolojia unaoanzia mwezi Novemba 2013 hadi Oktoba 2014, maeneo mengi nchini yalipata mvua za kuridhisha na kuongeza kiasi cha maji katika mito na mabwawa. Hata hivyo, hali ya upatikanaji wa mvua katika mabonde ya maji nchini ilitofautiana kulingana na tabia za hali ya hewa. Wastani wa viwango vya mvua katika mabonde yote tisa nchini vilikuwa kama ifuatavyo:- Bonde la Pangani milimita 817 ikilinganishwa na milimita 720 kwa mwaka wa kihaidrolojia uliopita; Bonde la Rufiji milimita 1,271 ikilinganishwa na milimita 1,144; Bonde la Wami/Ruvu milimita 2,306 ikilinganishwa na milimita 979; Bonde la Ziwa Nyasa milimita 1,643 ikilinganishwa na milimita 1,356; Bonde la

Page 8: Tekeleza kwa

6

Ziwa Victoria milimita 1,450 ikilinganishwa na milimita 968; Bonde la Kati milimita 774 ikilinganishwa na milimita 825 ya mwaka uliopita, katika Bonde la Ziwa Rukwa milimita 900 ikilinganishwa na milimita 844; Bonde la Ziwa Tanganyika milimita 1,116 ikilinganishwa na milimita 917 na katika Bonde la Ruvuma na Pwani ya Kusini wastani wa milimita 801 ikilinganishwa na milimita 835 mwaka uliopita. Jedwali Na.1 linaonesha mwenendo wa viwango vya mvua katika mabonde tisa nchini kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia Novemba, 2011 hadi Oktoba, 2014. 14. Mheshimiwa Spika, kutokana na takwimu zilizokusanywa, wastani wa viwango vya maji katika mito na mabwawa viliongezeka katika maeneo mengi ikilinganishwa na msimu wa mvua wa mwaka uliopita. Viwango vya mtiririko wa maji katika baadhi ya mito nchini vilikuwa kama ifuatavyo:- Mto Kiwira ulioko Bonde la Ziwa Nyasa ulikuwa na wastani wa mita za ujazo 61.88 kwa sekunde ikilinganishwa na mita za ujazo 25.89 kwa sekunde; Mto Wami mita za ujazo 56.82 kwa sekunde ikilinganishwa na mita za ujazo 18.69 kwa sekunde; Mto Ruvu mita za ujazo 48.92 kwa sekunde, ikilinganishwa na wastani wa mita za ujazo 36.21 kwa sekunde; Mto Ruaha Mkuu mita za ujazo 42.72 kwa sekunde ikilinganishwa na wastani wa mita za ujazo 9.91, Mto Kihansi mita za ujazo 18.43 kwa sekunde ikilinganishwa na mita za ujazo 14.35; Mto Kikuletwa katika Bonde la Pangani ulikuwa na mita za ujazo 20.16 kwa sekunde ikilinganishwa na kiasi cha mita za ujazo 14.66 kwa sekunde; Mto Ruvuma mita za ujazo 11.13 kwa sekunde ikilinganishwa na wastani wa mita za ujazo 8.31 kwa sekunde mwaka uliopita; Mto Kagera mita za ujazo 265.93 kwa sekunde ikilinganishwa na mita za ujazo 368.7 kwa sekunde; na Mto Mara mita za ujazo 31.75 kwa sekunde ikilinganishwa na mita za ujazo 56.06 kwa mwaka uliopita.

Page 9: Tekeleza kwa

7

15. Mheshimiwa Spika, kutokana na ongezeko la mvua katika kipindi cha mwaka huo, wastani wa vina vya maji kwenye mabwawa umeongezeka ikilinganishwa na mwaka uliopita. Takwimu za ongezeko hilo katika baadhi ya mabwawa ni kama ifuatavyo:- Bwawa la Nyumba ya Mungu usawa wa maji ulikuwa mita 684.81 juu ya usawa wa bahari, ikilinganishwa na mita 683.94 mwaka uliopita; bwawa la Mtera mita 691.685 ikilinganishwa na mita 691.18, Kidatu mita 448.87 ikilinganishwa na mita 446.33, Kihansi mita 1173.16 ikilinganishwa na mita 1,144.64; na bwawa la Mindu ni mita 507.30 juu ya usawa wa bahari ikilinganishwa na mita 506.45 mwaka uliopita. 16. Mheshimiwa Spika, vilevile, usawa wa maji katika Ziwa Victoria ulikuwa wastani wa mita 1,133.41 juu ya usawa wa bahari ikilinganishwa na mita 1,133.22 mwaka uliopita, Ziwa Tanganyika mita 775.2 ikilinganishwa na mita 775.0, na Ziwa Nyasa lilikuwa na wastani wa mita 475.92 ikilinganishwa na mita 474.48 juu ya usawa wa bahari kwa mwaka uliopita. Kulingana na takwimu hizo, hali ya maji iliimarika ikilinganishwa na mwaka wa kihaidrolojia uliopita.

17. Mheshimiwa Spika, hata hivyo, katika mwaka wa kihaidrolojia ulioanza mwezi Novemba 2014, hali ya upatikanaji wa mvua ilionesha kuwa chini ya wastani na hivyo kuathiri mtiririko wa maji kwenye mito na vina katika mabwawa na maziwa. Vilevile, baadhi ya maeneo yameendelea kuathirika na uhaba wa maji kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupungua kwa uwezo wa ardhi kuhifadhi maji; athari za mabadiliko ya tabianchi; ongezeko la shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ya vyanzo vya maji; na kasi kubwa ya ongezeko la watu. Pamoja na changamoto hizo, mvua zinazoendelea kunyesha kwa sasa zinatarajiwa

Page 10: Tekeleza kwa

8

kuongeza wingi wa maji kwenye mito, mabwawa na maziwa na hivyo kuimarisha upatikanaji wa maji katika maeneo mengi nchini. 18. Mheshimiwa Spika, takwimu za kitaifa za rasilimali za maji zilizopo zinaonesha kuwa kiasi cha maji kwa sasa kwa kila Mtanzania ni wastani wa mita za ujazo 1,952 kwa mwaka. Kutokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu nchini, kiasi hicho kinatarajiwa kupungua hadi kufikia mita za ujazo 883 ifikapo mwaka 2035. Kiwango cha chini cha mahitaji ya maji kwa kila mtu kwa mwaka kinachokubalika kimataifa ni mita za ujazo 1,700. Hali hiyo inaashiria kwamba, hatua madhubuti zinahitajika kuchukuliwa katika utunzaji wa vyanzo vya maji, kujenga miundombinu ya kuongeza upatikanaji maji na kuboresha ufanisi katika matumizi yake. Wizara yangu kwa kushirikiana na wadau wa Sekta ya Maji inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na hali hiyo ili nchi yetu isifikie kiwango hicho cha upatikanaji wa maji kwa kila Mtanzania.

Page 11: Tekeleza kwa

9

2.2 HUDUMA YA MAJI VIJIJINI 19. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha huduma ya maji vijijini kwa kujenga miradi mipya, kupanua, na kukarabati miundombinu ya maji. Uboreshaji huo unatekelezwa kwa kuwashirikisha wananchi katika hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupanga, kusanifu, kujenga, kusimamia na kuendesha miradi hiyo kulingana na Sera ya Maji ya mwaka 2002. Vilevile, Wizara yangu inaendelea na jukumu lake la kutafuta fedha, kuandaa miongozo ya utekelezaji na kutoa ushauri wa kitaalam ambapo Sekretarieti za Mikoa husimamia na kutoa ushauri wa kiufundi kwa Halmashauri katika kutekeleza miradi ya maji vijijini. Jitihada hizo hufanyika kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo, Serikali za Mitaa, wananchi, Sekta Binafsi na wadau wengine. 20. Mheshimiwa Spika, tathmini ya utekelezaji wa BRN kwa sekta zote sita imeonesha mafanikio makubwa ambapo Sekta ya Maji imeweza kufikia malengo yaliyowekwa kwa kiwango kikubwa. Mafanikio yaliyopatikana kutokana na mpango huo ni pamoja na kuongezeka kwa idadi ya wananchi wanaopata huduma ya maji kutoka wananchi 15,200,000 sawa na asilimia 40 mwezi Juni, 2013 hadi kufikia wananchi 20,957,855 sawa na asilimia 55.9 mwezi Aprili 2015, likiwa ni ongezeko la wananchi milioni 5.76 wanaoishi vijijini. 21. Mheshimiwa Spika, naomba nichukue nafasi hii kuwashukuru wadau wote hususan Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Sekretarieti za Mikoa, Halmashauri na Washirika wa Maendeleo tulioshirikiana nao katika kufikia malengo hayo. Kazi hiyo ilikuwa kubwa na yenye changamoto nyingi, hivyo

Page 12: Tekeleza kwa

10

nawaomba tuendelee kushirikiana katika kutekeleza miradi ya Sekta ya Maji ili kufikia azma ya Serikali ya kuwapatia wananchi huduma ya maji safi na salama. 2.3 HUDUMA YA MAJI MIJINI 22. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika maeneo ya mijini kupitia Mamlaka za Maji kwenye Miji Mikuu ya Mikoa 23 pamoja na Dar es Salaam; Miji Mikuu ya Wilaya 99, Miji Midogo 14; na Miradi 8 ya kitaifa. Kwa sasa takribani watu milioni 7 wanapata huduma ya maji safi na salama kwa upande wa Miji Mikuu ya Mikoa, Miji Mikuu ya Wilaya, Miji Midogo pamoja na huduma inayotolewa na miradi ya kitaifa. Vilevile, wakazi wapatao milioni 3 kwa upande wa Jiji la Dar es Salaam na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani wanapata huduma hiyo. 2.3.1 Huduma ya Majisafi katika Miji Mikuu ya Mikoa na

Jiji la Dar es Salaam (a) Miji Mikuu ya Mikoa 23. Mheshimiwa Spika, jukumu la Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira za Miji Mikuu ya Mikoa ni kutoa huduma ya maji safi na salama pamoja na uondoaji wa majitaka katika miji hiyo. Hadi mwezi Aprili 2015, mahitaji ya maji katika Miji Mikuu ya Mikoa ni lita milioni 619 kwa siku ikilinganishwa na uzalishaji wa lita milioni 385 kwa siku. Wastani wa wakazi wanaopata huduma ya maji katika miji hiyo kwa sasa ni asilimia 86 kwa wastani wa saa 17 kwa siku. Idadi ya wateja waliounganishwa na huduma ya maji imeongezeka kutoka 336,898 mwezi Machi, 2014 hadi

Page 13: Tekeleza kwa

11

wateja 362,953 mwezi Aprili, 2015. Asilimia 96 ya wateja waliounganishwa na huduma hiyo wamefungiwa dira za maji. 24. Mheshimiwa Spika, wastani wa upotevu wa maji kwenye miundombinu ya usambazaji maji katika miji mikuu ya mikoa umefikia asilimia 35 ikilinganishwa na asilimia 38 mwezi Machi, 2014. Upotevu huo wa maji unatokana na uchakavu wa miundombinu ya usambazaji wa maji, uharibifu wa miundombinu, pamoja na wizi wa maji unaofanywa na wateja wasio waaminifu. Wizara yangu inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kukabiliana na upotevu wa maji ikiwemo kuzifanyia marekebisho Sheria zake ili kuzipa nguvu zaidi kwa watakaobainika na wizi wa maji pamoja na vifaa na uharibifu wa miundombinu ya maji. Vilevile, katika utekelezaji wa Mpango wa Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), upotevu wa maji umepewa kipaumbele cha kwanza katika viashiria vya kupima utendaji (KPIs) wa Mamlaka za Maji Mijini ili kuzihamasisha Mamlaka hizo kutambua umuhimu wa kupunguza upotevu wa maji ili kuongeza makusanyo ya maduhuli katika Mamlaka zao. 25. Mheshimiwa Spika, moja ya majukumu ya Bodi za Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini ni kuandaa mikakati ya ukusanyaji wa maduhuli yanayotokana na ankara za matumizi ya maji. Hadi mwezi Aprili, 2015, makusanyo ya maduhuli kwa mwezi yameongezeka na kufikia shilingi bilioni 7.28 ikilinganishwa na shilingi bilioni 6.36 mwezi Machi, 2014. Ongezeko hilo linatokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa maji, wateja, mabadiliko ya bei za maji, kupungua kwa upotevu wa maji na juhudi za Mamlaka katika kukusanya madeni kutoka kwa wateja kwa kutumia teknolojia za mawasiliano. Vilevile, mapato hayo yameziwezesha Mamlaka kuboresha huduma zinazotolewa kwa wateja ikiwa ni pamoja na kukarabati miundombinu na kugharamia

Page 14: Tekeleza kwa

12

shughuli za uendeshaji. Aidha, kupitia mpango wa “Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa” (BRN), Wizara imetoa viashiria vya utendaji kazi (Key Performance Indicators) kwa kila Mamlaka ya Maji na kukubaliana viwango na malengo ya utekelezaji yakiwemo kuongeza uzalishaji, kuongeza idadi ya wateja, kupunguza upotevu wa maji na kuongeza makusanyo ya maduhuli. (b) Jiji la Dar es Salaam

26. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2015, mahitaji ya maji katika Jiji la Dar es Salaam na Miji ya Kibaha na Bagamoyo ni lita milioni 450 kwa siku ikilinganishwa na uwezo wa mitambo wa kuzalisha maji wa lita milioni 300 kwa siku ambazo ni sawa na asilimia 77 ya mahitaji. Wastani wa asilimia 68 ya wakazi wa Jiji wanapata huduma ya maji kwa wastani wa saa 8 kwa siku. Wakazi wanaobaki hupata huduma ya maji kupitia visima, magati na huduma ya magari (water bowsers). Aidha, idadi ya wateja waliounganishwa na huduma ya maji ni 126,405 na kati ya hao, asilimia 97 wamefungiwa dira za maji. Makusanyo ya maduhuli kwa mwezi ni shilingi bilioni 3.31 na kiwango cha upotevu wa maji ni asilimia 57. Upotevu huo unatokana na wizi wa maji, uvujaji wa mabomba, uharibifu unaotokea wakati wa ukarabati wa miundombinu ya barabara pamoja na uchakavu wa miundombinu. Serikali inaendelea kukabiliana na changamoto hizo na kuzipatia ufumbuzi hatua kwa hatua. 2.3.2 Huduma ya Majisafi katika Miradi ya Kitaifa, Miji

Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo 27. Mheshimiwa Spika, hadi sasa kuna Mamlaka za Maji 99 za Miji Mikuu ya Wilaya na 14 za Miji Midogo ambazo

Page 15: Tekeleza kwa

13

hutoa huduma ya maji katika miji hiyo. Mamlaka hizo husimamiwa na Bodi za Wakurugenzi zinazoteuliwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu na uendeshaji wa Mamlaka hizo uko chini ya Halmashauri za Miji husika. Aidha, kuna miradi 8 ya maji ya kitaifa ambayo Bodi zake huteuliwa na Waziri wa Maji akishirikiana na Sekretarieti ya Mkoa husika. 28. Mheshimiwa Spika, mahitaji ya maji katika Miji Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo kwa sasa ni lita milioni 244.2 kwa siku ikilinganishwa na uzalishaji wa lita milioni 99.2 kwa siku. Upatikanaji wa huduma ya maji ni asilimia 60 ya wakazi wa miji hiyo ambapo wastani wa upatikanaji wa huduma ni saa 9 kwa siku. Idadi ya wateja waliounganishwa na huduma hiyo ni 107,313 na kati ya wateja hao asilimia 58 wamefungiwa dira za maji. Kwa upande wa miradi ya kitaifa mahitaji ya maji ni lita milioni 104.6 kwa siku ikilinganishwa na uzalishaji wa lita milioni 51.6 kwa siku. Upatikanaji wa huduma ya maji ni asilimia 60 ya wakazi wanaohudumiwa na miradi hiyo ambapo wastani wa upatikanaji wa huduma ni saa 9 kwa siku. Idadi ya wateja waliounganishwa ni 16,995 na kati ya hao, asilimia 60 wamefungiwa dira za maji. 29. Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Miji Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo hairidhishi. Hivyo, Wizara yangu kwa kushirikiana na TAMISEMI inaendelea kuwekeza katika miundombinu ya maji na kuzijengea uwezo Mamlaka hizo ili kuongeza upatikanaji wa huduma ya majisafi katika miji hiyo. Lengo ni kuongeza ufanisi na kuziwezesha Mamlaka hizo kujiendesha kibiashara na kupunguza mzigo kwa Serikali.

Page 16: Tekeleza kwa

14

2.3.3 Uondoaji wa Majitaka Mijini 30. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili, 2015 huduma ya uondoaji majitaka katika Miji ya Arusha, Moshi, Tanga, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Songea, Tabora, Morogoro na Dar es Salaam imefikia asilimia 20. Idadi ya wateja waliounganishwa kwenye mtandao wa majitaka katika miji hiyo imeongezeka kutoka 22,976 mwezi Machi, 2014 hadi kufikia wateja 24,346 mwezi Aprili, 2015. Hali ya uondoaji wa majitaka bado ni ya kiwango cha chini kutokana na mwamko mdogo wa wananchi kujiunga kwenye mtandao wa majitaka, miundombinu chakavu ya majitaka kwa baadhi ya miji inayohudumia maeneo machache, ongezeko kubwa la watu mijini pamoja na miji mingine kutokuwa na miundombinu ya majitaka. 2.4 KUJENGA UWEZO WA KITAASISI 31. Mheshimiwa Spika, katika hotuba yangu ya mwaka jana nililiarifu Bunge lako Tukufu kuwa Wizara inahitaji wataalam 8,749 kwa kipindi chote cha utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (2007-2025), ili kutekeleza majukumu kwa ufanisi na kufikia malengo yaliyokusudiwa. Wizara iliwasiliana na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na kwa kuanzia, kupata kibali cha kuajiri wataalam 475. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya wataalam 318 kati ya wataalam 475 wameajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi. Kati ya wataalam hao walioajiriwa, Wahandisi ni 96 na Mafundi Sanifu ni 222. Ongezeko hilo limeifanya Sekta ya Maji kuwa na jumla ya wataalam 1,856 wanaosimamia na kutekeleza Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji.

Page 17: Tekeleza kwa

15

3.0 UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2014/2015 NA MALENGO KWA MWAKA 2015/2016

32. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa bajeti kwa mwaka 2014/2015 na malengo ya mwaka 2015/2016 kwa Sekta ya Maji umejikita katika usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji, huduma ya majisafi na usafi wa mazingira vijijini na mijini na masuala mtambuka. Taarifa ya mapitio ya utekelezaji wa bajeti na malengo ya mwaka ujao imechambuliwa kwa undani katika aya zifuatazo. 3.1 RASILIMALI ZA MAJI 33. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Bodi za Maji za Mabonde ina wajibu wa kusimamia na kuendeleza rasilimali za maji nchini. Usimamizi na uendelezaji huo unahusu kuchunguza, kutathmini na kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji ikiwa ni pamoja na rasilimali za maji shirikishi (transboundary water resources). Ili kuziwezesha Bodi za Maji kutekeleza majukumu yao, Wizara inazijengea uwezo na kuziimarisha. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na kuandaa mipango shirikishi ya usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji, kusanifu na kusimamia ujenzi wa miundombinu ya kipaumbele.

3.1.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji (a) Mwenendo wa Rasilimali za Maji 34. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliimarisha vituo vya kupima wingi na ubora wa rasilimali za maji juu na chini ya ardhi kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa takwimu na taarifa sahihi. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa vituo tisa katika

Page 18: Tekeleza kwa

16

mabonde ya Rufiji, Ruvuma na Pwani ya Kusini pamoja na Ziwa Victoria. Aidha, jumla ya vituo 118 vimekarabatiwa katika Mabonde ya Ziwa Rukwa vituo 16, Ziwa Nyasa (4), Ziwa Victoria (3), Ziwa Tanganyika (1), Pangani (69), Rufiji (22) na Wami-Ruvu vituo vitatu. Kwa hiyo, hadi mwezi Aprili, 2015 kuna jumla ya vituo 633 vya kupima mwenendo wa rasilimali za maji na kati ya hivyo, vituo 321 ni vya kupima mtiririko wa maji mtoni, vituo 196 vya kupima wingi wa mvua, vituo 93 vya hali ya hewa na vituo 23 vya kupima usawa wa maji kwenye maziwa na mabwawa katika mabonde ya maji nchini. 35. Mheshimiwa Spika, kati ya vituo hivyo 633, vituo 515 vinafanya kazi vizuri na kutumika kukusanya takwimu. Lengo ni kupata takwimu sahihi za hali ya maji nchini. Taarifa zinazopatikana kutokana na uchambuzi wa takwimu zinatumika katika utafiti wa masuala mbalimbali kwa ajili ya maandalizi ya miradi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Katika mwaka 2015/2016, vituo vipya 90 vya kuchunguza mwenendo wa rasilimali za maji vitajengwa na vingine kukarabatiwa kwenye maeneo mbalimbali. Jedwali Na. 2 linaonesha idadi ya vituo vya kuchunguza mwenendo wa maji katika Mabonde. (b) Kuhifadhi Mazingira na Vyanzo vya Maji 36. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatekeleza Mpango Maalum wa Miaka Mitano wa Kuhifadhi na Kutunza Vyanzo vya Maji. Mpango huo ulianza kutekelezwa kwa kuhakikisha vyanzo vilivyobainishwa vinawekewa mipaka, kutengenezewa ramani na kuandaa taratibu za fidia ili wahusika waweze kulipwa na maeneo hayo kutangazwa katika Gazeti la Serikali. Katika kutekeleza mpango huo, vyanzo saba vya maji katika Bonde la Ziwa Rukwa

Page 19: Tekeleza kwa

17

vilitangazwa kuwa maeneo tengefu. Hadi mwezi Aprili 2015, vyanzo 31 vimewekewa mipaka tayari kwa ajili ya kutangazwa na vyanzo 28 vipo katika hatua mbalimbali za upimaji, uwekaji mipaka na kutengeneza ramani. Aidha, elimu inaendelea kutolewa kwa jamii kuhusu umuhimu wa utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji, madhara ya uharibifu wa vyanzo vya maji, na elimu ya Sheria na Kanuni mbalimbali za usimamizi wa rasilimali za maji. Jedwali Na. 3 linaonesha vyanzo vilivyowekewa mipaka (demarcated water sources) na vilivyo katika hatua mbalimbali za kuwekewa mipaka. 37. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu imepanga kutangaza maeneo 18 ya vyanzo vya maji kuwa maeneo tengefu. Vilevile, Wizara itaendelea kubaini maeneo zaidi ya vyanzo vya maji na kuweka mipaka kwenye maeneo yaliyoainishwa ili kuyakinga dhidi ya uharibifu wa mazingira. Lengo ni kuhakikisha usalama wa vyanzo na upatikanaji wa uhakika wa maji kwa maendeleo endelevu. 38. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea kuunda na kuziimarisha Jumuiya za Watumia Maji ili ziweze kusimamia rasilimali za maji katika ngazi ya watumia maji. Hadi mwezi Aprili 2015, Jumuiya 25 ziliundwa na kujengewa uwezo katika mabonde ya Ziwa Victoria, Ziwa Rukwa, Rufiji, Ruvuma na Pwani ya Kusini, Wami-Ruvu, na Pangani ili ziweze kushiriki katika kulinda, kutunza na kusimamia rasilimali za maji katika mabonde hayo. Vilevile, Wizara imetangaza maeneo matatu kuwa mabonde madogo ya maji (catchments) ili maeneo hayo yaweze kuanzisha Ofisi za Mabonde Madogo na kuunda Kamati. Maeneo hayo ni Umba-Zigi na Kikuletwa katika Bonde la Pangani na Ruaha Mkuu katika Bonde la Rufiji.

Page 20: Tekeleza kwa

18

Kamati ya Bonde Dogo la Ruaha Mkuu tayari imeshaundwa. Kamati hizo zitasimamia rasilimali za maji katika ngazi ya mabonde madogo na kuweza kuzisimamia Jumuiya za Watumia Maji zitakazokuwa chini yao. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu imepanga kuunda Jumuiya za Watumiaji Maji 33 na Kamati za Mabonde Madogo 18 pamoja na kuzijengea uwezo Jumuiya 91. 39. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza Sheria Na. 20 ya Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake, Wizara yangu ilifanya tathmini za athari kwa mazingira na kijamii kwa mabwawa sita ya Itobo, Nkiniziwa, Uchama, Enguikument I, Enguikument II na Leken yaliyopo katika Bonde la Kati. Mabwawa matano yalipata vibali vya mazingira ili ujenzi wa mabwawa hayo uanze. Bwawa la Uchama halikupata kibali cha mazingira kwa sababu eneo la chanzo cha bwawa hilo limejengwa makazi ya watu. Hata hivyo, ujenzi wa Bwawa la Leken umeanza chini ya usimamizi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli. Hadi mwezi Aprili 2015, mabwawa manne yaliyobaki yalikuwa yamefanyiwa usanifu upya na makabrasha ya zabuni yameandaliwa kwa ajili ya kupata Mkandarasi wa ujenzi unaotarajiwa kuanza mwaka ujao wa fedha. Aidha, rasimu za taarifa ya tathmini za athari kwa mazingira na jamii kwa ajili ya miradi ya mabwawa ya Farkwa na Ndembera na barabara inayoelekea eneo litakapojengwa Bwawa la Kidunda zimewasilishwa NEMC kwa hatua zaidi. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu imepanga kukarabati mabwawa manane ya ukubwa wa kati katika maeneo kame nchini. (c) Kudhibiti Uchafuzi wa Vyanzo vya Maji 40. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza jukumu la kudhibiti uchafuzi wa vyanzo vya maji, jumla ya sampuli 381

Page 21: Tekeleza kwa

19

za maji zilichukuliwa na kupimwa kwenye maabara katika mabonde ya Wami-Ruvu, Ziwa Nyasa, Ziwa Victoria na Rufiji. Vilevile, jumla ya viwanda 40 vilikaguliwa ili kuangalia utekelezaji wa Sheria na Kanuni zinazosimamia mazingira na rasilimali za maji katika mabonde ya Pangani na Wami-Ruvu. Ukaguzi huo ulibaini kuwa mifumo ya kusafisha majitaka katika baadhi ya viwanda haifanyi kazi vizuri na viwanda vingine vinatiririsha majitaka bila kuyatibu na kusababisha uchafuzi wa vyanzo vya maji. 41. Mheshimiwa Spika, hatua stahiki zimechukuliwa kwa viwanda vyenye mifumo mibovu ya majitaka na kutakiwa kuikarabati na kwa viwanda visivyo na mifumo hiyo kuhakikisha vinaijenga. Vilevile, viwanda hivyo vimeagizwa kutathmini athari za kimazingira na kijamii ili kuwa na mipango mikakati ya utunzaji wa vyanzo hivyo. Aidha, katika kuimarisha udhibiti wa uchafuzi wa vyanzo vya maji, maeneo 210 yanayoweza kuleta uchafuzi katika vyanzo vya maji (pollution hotspots) yalitambuliwa katika mabonde ya Ruvuma na Pwani ya Kusini, Wami-Ruvu, Ziwa Nyasa na Pangani na hatua mbalimbali kuchukuliwa. Katika mwaka 2015/2016, Wizara itaendelea kuhakikisha uchafuzi wa vyanzo vya maji unadhibitiwa na Sheria na Kanuni zinafuatwa ili kulinda vyanzo hivyo. (d) Kutafuta Vyanzo Vipya vya Maji 42. Mheshimiwa Spika, katika juhudi za Wizara yangu za kuongeza upatikanaji wa maji, vyanzo mbalimbali vya maji viliendelea kuainishwa, kufanyiwa tathmini na usanifu kwa ajili ya kuhifadhiwa na kutunzwa. Katika mwaka 2014/2015, jumla ya vyanzo vya maji 114 vilitambuliwa kwenye mabonde ya Ziwa Rukwa vyanzo 94, Ziwa Nyasa (17), Rufiji (1), Wami-Ruvu (1) na Ziwa Tanganyika (1) kwa ajili ya

Page 22: Tekeleza kwa

20

kuvihifadhi na kuvilinda. Aidha, maeneo 413 yalifanyiwa utafiti wa maji chini ya ardhi ili kubaini maeneo yanayofaa kwa ajili ya uchimbaji wa visima. Kwa mwaka 2015/2016, Serikali itaendelea kutafiti maji chini ya ardhi katika maeneo mengine zaidi. Vilevile, kazi za upembuzi yakinifu, uchunguzi wa kina wa miamba, usanifu na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa ya Farkwa na Ndembera zitaendelea. Katika mwaka 2015/2016, Wizara imepanga kuchimba visima 20 na kukarabati visima 30 vya kuchunguza mwenendo wa maji chini ya ardhi, pamoja na kuendelea na taratibu za kutafuta fedha ili kuajiri Wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa vyanzo vipya vya maji. 43. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara yangu imeendelea kutafuta vyanzo vya maji katika maeneo mbalimbali nchini kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Serikali ya Misri. Katika mwaka 2014/2015, Wizara kwa kushirikiana na Serikali ya China imekamilisha uchimbaji wa visima 55 katika Wilaya za Kisarawe visima 30 na Kilosa visima 25 Vilevile, utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi wa uchimbaji wa visima 30 kwa kushirikiana na Serikali ya Misri unaendelea. Hadi mwezi Aprili 2015, uchimbaji wa visima 11 katika Wilaya za Mwanga kisima kimoja, Same (8) na Kiteto (2) umekamilika na uchimbaji wa visima vingine 8 Wilayani Kiteto unaendelea. Katika mwaka 2015/2016, visima 11 vilivyobaki vitachimbwa katika Wilaya za Bariadi visima (2) na Itilima (9). 44. Mheshimiwa Spika, Wizara inahakikisha kuwa taratibu za kitaalam za utafiti wa maji chini ya ardhi na uchimbaji wa visima unafanywa kwa umakini ili visima vinavyochimbwa viwe na ubora unaostahili kwa matumizi endelevu. Hadi mwezi Aprili 2015, Wizara yangu ilitoa leseni saba kwa kampuni za uchimbaji visima vya maji na leseni

Page 23: Tekeleza kwa

21

moja kwa kampuni ya utafiti wa maji chini ya ardhi. Leseni hizo zimeanza kutolewa upya kuanzia mwezi Julai 2014 kutokana na kuanza kutumika kwa Kanuni za utafiti wa maji chini ya ardhi na uchimbaji wa visima ambazo zilifuta vibali vyote vilivyotolewa awali. Kulingana na hali hiyo, nazihimiza kampuni zote kuomba upya leseni ili wafanye kazi zao kwa mujibu wa Sheria. Aidha, hadi mwezi Machi 2015, jumla ya visima vya maji 570 vilichimbwa na kusajiliwa katika maeneo mbalimbali nchini. Kati ya hivyo, visima 233 vilichimbwa na Wakala wa Uchimbaji Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA) na visima 337 vilichimbwa na kampuni binafsi. Katika mwaka 2015/2016, Serikali itaendelea kusimamia watafiti na wachimbaji visima wote ili kupata takwimu za uchimbaji wa visima nchini. Kwa kuwa uzoefu umeonesha maji chini ya ardhi yanaweza kuwa na kemikali ambazo ni sumu kwa binadamu, lazima maji yatokanayo na uchimbaji wa visima yapimwe kwanza kabla ya kutumiwa. 45. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Uingereza kupitia Idara yake ya Maendeleo ya Kimataifa (DFID), inatekeleza Mradi wa Kufanikisha Uhakika wa Maji (Achieving Water Security) kwenye eneo la Uendelezaji Kilimo Ukanda wa Kusini Tanzania - Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania (SAGCOT). Mradi huo utakaogharimu kiasi cha Paundi za Uingereza milioni 5, unasimamiwa na Bodi ya Maji ya Bonde la Rufiji na umepangwa kutekelezwa kwa miaka mitatu kuanzia mwezi Machi 2013 hadi Machi, 2016. Aidha, mradi huo utaimarisha shughuli za usimamizi wa rasilimali za maji kwa ajili ya kukusanya takwimu zitakazowezesha kufanya maamuzi ya kutumia rasilimali hiyo kwenye eneo la SAGCOT. Vilevile, mradi utaunda Jumuiya za Watumiaji Maji na kutoa mafunzo mbalimbali kuhusu usimamizi na utunzaji wa rasilimali za maji.

Page 24: Tekeleza kwa

22

(e) Matumizi Bora ya Rasilimali za Maji 46. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi za Maji za Mabonde ina wajibu wa kusimamia matumizi bora ya maji kwa kutoa vibali vya kutumia maji na kutiririsha majitaka kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya vibali vipya 421 vya kutumia maji vilitolewa katika mabonde ya Ruvuma na Pwani ya Kusini (15), Pangani (34), Rufiji (191), Wami-Ruvu (44), Ziwa Victoria (13), Ziwa Rukwa (51) na Ziwa Tanganyika (73). Aidha, jumla ya vibali 10 vya kutiririsha majitaka vilitolewa katika mabonde ya maji ya Wami-Ruvu (3), Ziwa Victoria (6) na Pangani (1). Vilevile, zoezi la kuwatambua watumiaji maji kwa matumizi mbalimbali lilifanyika. Katika zoezi hilo, jumla ya watumiaji maji 67 walitambuliwa na kubainika kuwa hawana vibali katika mabonde ya Ziwa Victoria, Ziwa Rukwa, Ziwa Nyasa na Bonde la Kati. Elimu kuhusu taratibu za kisheria za matumizi endelevu ya maji ilitolewa kwa wahusika wasio na vibali na kuagizwa kuomba vibali vya kutumia maji hayo. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu imepanga kutoa vibali 600 vya watumiaji maji katika vyanzo mbalimbali vya maji nchini. (f) Mipango Shirikishi ya Usimamizi na Uendelezaji

wa Rasilimali za Maji 47. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea na uandaaji wa Mipango Shirikishi ya Kusimamia na Kuendeleza Rasilimali za Maji (Integrated Water Resources Management and Development Plans – IWRM&D) katika mabonde yote tisa nchini. Hadi mwezi Aprili 2015, mipango hiyo katika mabonde ya Ruvuma na Pwani ya Kusini, na Bonde la Kati imekamilika. Utayarishaji wa Mipango Shirikishi katika mabonde ya Ziwa Tanganyika,

Page 25: Tekeleza kwa

23

Ziwa Nyasa, Ziwa Rukwa na Rufiji unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2015. Katika mwaka 2015/2016, Mtaalam Mshauri anayeandaa Mpango Shirikishi katika Bonde la Wami-Ruvu anatarajiwa kuanza kazi mwezi Julai, 2015 na kukamilisha mwezi Desemba, 2015. Mpango huo utatayarishwa kwa kutumia Tathmini ya Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji iliyofanywa na JICA katika Bonde hilo. (g) Kuimarisha Bodi za Maji za Mabonde 48. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha hali ya utendaji kazi wa Bodi za Maji za Mabonde, Wizara yangu imeendelea kuzijengea uwezo Bodi hizo kwa kutoa mafunzo kwa watumishi, kujenga ofisi, kununua vitendea kazi na kufanya tafiti mbalimbali. Lengo ni kuhakikisha kuwa Bodi hizo zinaongeza ufanisi katika kutekeleza majukumu yake ya kusimamia, kutunza, kuhifadhi na kuendeleza rasilimali za maji nchini. 49. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, watumishi 203 wa mabonde yote tisa walipatiwa mafunzo ya muda mfupi na semina mbalimbali kama ifuatavyo; Bonde la Pangani watumishi 12, Rufiji (52), Ruvuma na Pwani ya Kusini (21), Ziwa Victoria (21), Bonde la Kati (28), Ziwa Tanganyika (10), Ziwa Nyasa (15), Ziwa Rukwa (25) na watumishi 19 kutoka Bonde la Wami-Ruvu. Mafunzo hayo yalihusu usimamizi wa mikataba ya kimataifa katika rasilimali za maji; ukaguzi wa mazingira; usalama wa mabwawa; uhasibu; ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (Public Private Partnership-PPP); na mifumo ya kielektroniki kuhusu utunzaji na uhifadhi wa rasilimali za maji.

Page 26: Tekeleza kwa

24

50. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2015, ujenzi wa Ofisi za Bodi za Maji za Mabonde uliendelea na umefikia katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Katika Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Victoria ujenzi umefikia asilimia 90, Ziwa Tanganyika asilimia 60, Bonde la Kati asilimia 60 na ujenzi wa Ofisi ya Bonde Dogo la Kilombero iliyopo Ifakara katika Bonde la Rufiji umekamilika. Ujenzi wa Ofisi hizo unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2015 kwa Bonde la Ziwa Victoria na mwezi Septemba 2015 katika mabonde ya Ziwa Tanganyika na Bonde la Kati. Kwa mabonde ya Wami – Ruvu na Pangani, usanifu wa kina wa ujenzi wa ofisi za mabonde hayo unaendelea. Mchakato wa kuwapata Wakandarasi wa ujenzi wa ofisi unaendelea katika Mabonde manne ambayo ni Bonde la Ziwa Nyasa kwenye miji ya Songea na Njombe; Bonde la Ruvuma na Pwani ya Kusini (Mtwara, Lindi, Tunduru na ofisi ya watumia maji-Likonde); Bonde la Rufiji (Iringa, na ofisi za Watumia maji Kimani na Mkoji); na katika Bonde la Ziwa Rukwa (Mbeya na Sumbawanga). Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaajiri wakandarasi na kuanza ujenzi wa ofisi hizo. 51. Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara yangu imeendelea kuzijengea uwezo Bodi za Maji za Mabonde katika kufanya utafiti mbalimbali katika rasilimali za maji nchini. Katika mwaka 2014/2015, utafiti umefanywa katika mabonde ya Wami-Ruvu, Ziwa Rukwa na Bonde la Kati. Utafiti huo unahusu upotevu wa maji katika Mto Ruvu kwenye eneo kati ya Kidunda na Ruvu Darajani; pamoja na utafiti kuhusu uwiano wa maji (water balance) katika maziwa ya Rukwa na Manyara. Katika mwaka 2015/2016, utafiti huo unatarajiwa kukamilika na kuanza utafiti mwingine utakaohusu kiwango cha kujaa kwa mchanga/udongo na usafirishaji wake (Sediment yield and transport modeling) kwenye Mto Mbwemkuru katika Bonde la Ruvuma na Pwani ya Kusini.

Page 27: Tekeleza kwa

25

(h) Ukusanyaji wa Maduhuli

52. Mheshimiwa Spika, jukumu mojawapo la Bodi za Maji za Mabonde ni kuweka malengo, kuandaa na kutekeleza mikakati ya ukusanyaji wa maduhuli yanayotokana na ada za matumizi ya maji. Mapato hayo hutumika katika usimamizi, utunzaji na uendelezaji wa rasilimali za maji nchini. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya shilingi bilioni 2. 15 zilikusanywa sawa na asilimia 84 ya lengo la shilingi bilioni 2.6 zilizopangwa kukusanywa katika mwaka 2014/2015. Katika mwaka 2015/2016, Bodi za Maji za Mabonde zimelenga kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 3.02 kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato. Jedwali Na. 4 linaonesha makusanyo ya maduhuli mwaka 2014/2015 na makadirio ya makusanyo kutoka Bodi za Maji za Mabonde kwa mwaka 2015/2016. (i) Udhibiti wa Migogoro katika Matumizi ya Maji 53. Mheshimiwa Spika, ni jukumu la Bodi za Maji za Mabonde kuhakikisha kuwa rasilimali za maji zinatumika katika uwiano sahihi kwa watumiaji kufuatana na sheria, taratibu na kanuni zilizopo. Migogoro inayojitokeza katika matumizi ya maji husuluhishwa na Bodi za Maji za Mabonde kwa kushirikiana na Jumuiya za Watumiaji Maji. Usuluhishi unaposhindikana katika ngazi hiyo, vyombo vya kisheria hutumika kutatua migogoro hiyo. Katika mwaka 2014/2015, migogoro 17 ya watumiaji maji ilijitokeza na kutatuliwa kwenye Mabonde ya Maji ya Pangani, Wami-Ruvu, Bonde la Kati na Rufiji. Katika mwaka 2015/2016, Serikali itaendelea kutoa elimu ya ugawaji na utunzaji wa rasilimali za maji ili kupunguza migogoro baina ya watumiaji maji.

Page 28: Tekeleza kwa

26

(j) Usimamizi wa Rasilimali za Maji Shirikishi 54. Mheshimiwa Spika, nchi yetu ina jumla ya mabonde tisa na kati ya hayo, mabonde saba yanavuka mipaka ya nchi yetu na hivyo kuwa na ulazima wa kushirikiana na nchi nyingine 17 kwa kuunda vyombo vya pamoja vya kusimamia matumizi endelevu ya rasilimali za maji. Nchi hizo ni Angola, Botswana, Burundi, Ethiopia, Eritrea, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Malawi, Misri, Msumbiji, Namibia, Rwanda, Sudan, Sudani Kusini, Uganda, Zambia na Zimbabwe. Ushirikiano wa kitaasisi na nchi hizo umeendelea kutekelezwa kama ifuatavyo:-

(i) Bonde la Mto Nile 55. Mheshimiwa Spika, Umoja wa Ushirikiano wa Nchi za Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative - NBI) unaundwa na jumla ya nchi 11 ambazo ni Burundi, Ethiopia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Misri, Rwanda, Sudan, Sudani Kusini, Uganda na Tanzania. Katika umoja huo nchi ya Eritrea ni mtazamaji (observer). Umoja huo ni chombo cha mpito kuelekea kwenye uundwaji wa Kamisheni ya Bonde la Mto Nile. Madhumuni ya kuanzishwa kwa umoja huo ni kusimamia matumizi ya maji yenye uwiano na haki baina ya nchi wanachama, kusimamia utekelezaji wa miradi ya kuhifadhi Bonde la Mto Nile, mazingira, nishati, kilimo, mafunzo na kujenga uwezo kwa taasisi zilizopo katika nchi husika. 56. Mheshimiwa Spika, katika kufikia malengo hayo nchi shiriki sita za Burundi, Ethiopia, Rwanda, Uganda, Kenya, na Tanzania zilisaini Mkataba wa Msingi wa Ushirikiano (CFA) katika Bonde la Mto Nile na hivyo kukidhi matakwa ya kuingia hatua ya kuridhia (ratification) mkataba huo.

Page 29: Tekeleza kwa

27

Ninapenda kuchukua fursa hii kulishukuru Bunge lako Tukufu kwa kupitia na kujadili mkataba huo ambao uliwasilishwa katika Bunge la 19 na hatimaye kuridhiwa tarehe 26/03/2015. Tanzania imekuwa nchi ya tatu kuridhia baada ya nchi za Ethiopia na Rwanda. Kamisheni ya Bonde la Mto Nile itaundwa pindi nchi sita zitakaporidhia mkataba huo. Katika mwaka 2015/2016, Tanzania itaendelea kuzishawishi nchi za Burundi, Uganda, Sudani Kusini, Kenya na Sudan ziridhie ili Kamisheni iundwe.

(ii) Kuhifadhi Mazingira ya Ziwa Victoria 57. Mheshimiwa Spika, madhumuni ya utekelezaji wa Mradi wa Usimamizi na Hifadhi ya Mazingira ya Ziwa Victoria (Lake Victoria Environmental Management Project - LVEMP) ni kuimarisha usimamizi wa pamoja wa rasilimali za Bonde la Ziwa Victoria kwa kudhibiti uharibifu wa mazingira katika ziwa hilo. Nchi shiriki katika usimamizi wa bonde hilo ni Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda na Tanzania. Kwa upande wa Tanzania, mradi huo umeimarisha taasisi zinazohusika na hifadhi ya maji na samaki; kukarabati mifumo ya kusafisha majitaka katika miji ya Mwanza, Musoma na Bukoba; pamoja na miradi midogo ya kijamii katika Halmashauri za Wilaya zinazozunguka ziwa hilo. Halmashauri hizo ambazo zimeingizwa kwenye Awamu ya Pili ya utekelezaji wa mradi huo ni Maswa, Itilima, Busega, Bariadi, Magu, Meatu, Kwimba, Sengerema, Geita, Chato, Muleba, Karagwe, Kyerwa na Misenyi. 58. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili, 2015 katika kutekeleza Awamu ya Pili ya mradi huo, miradi midogo 341 ya kijamii (Co – Development Driven Interventions) yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 8.3 imefikia hatua mbalimbali za utekelezaji na kati ya miradi hiyo, 116

Page 30: Tekeleza kwa

28

imekamilika na ipo tayari kukabidhiwa kwa jamii. Aidha, miradi mingine 24 ya kijamii yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 5.7 inatekelezwa katika Wilaya za Musoma Mjini, Bukoba Mjini, Maswa, Bariadi, Itilima, Meatu, Kwimba, Magu, Ukerewe, Misenyi, Misungwi, Ilemela na Nyamagana. Miradi hiyo 24 inajumuisha uhifadhi wa maeneo ya mita 60 kutoka kwenye kingo za Mto Simiyu na Mto Duma katika Halmashauri za Wilaya za Busega, Magu, Kwimba, Bariadi, Meatu na Maswa pamoja na uendelezaji wa teknolojia ya majiko sanifu na banifu katika Wilaya ya Maswa. Miradi iliyotajwa katika Halmashauri hizo sita imekamilika. 59. Mheshimiwa Spika, miradi minne inayohusisha miundombinu ya usafishaji majitaka yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 3.5 imeanza kutekelezwa. Mradi wa kusafisha na kutupa majitaka (Sludge Disposal Facility) katika Manispaa ya Bukoba umekamilika. Miradi mingine inayoendelea ni ya uunganishaji wa mfumo wa majitaka ya majumbani kwenye mtandao mkuu wa majitaka Jijini Mwanza; mradi wa ujenzi wa mabwawa ya majitaka katika eneo la Bweri, Manispaa ya Musoma; na ukarabati wa mfumo wa kusafisha majitaka katika machinjio ya Jiji la Mwanza. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kukamilisha miradi iliyobaki na kuikabidhi kwa jamii.

(iii) Bonde la Mto Mara 60. Mheshimiwa Spika, Bonde la Mto Mara ni eneo muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi pamoja na bayoanuai zilizopo. Bonde hilo linahusisha nchi mbili za Kenya na Tanzania na miradi mbalimbali ya pamoja inatekelezwa chini ya uratibu wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (Lake Victoria Basin Commission - LVBC). Katika mwaka

Page 31: Tekeleza kwa

29

2014/2015, Wizara yangu iliendelea kushiriki katika utekelezaji wa Mradi wa Masuala ya Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Planning for Resilience in East Africa through Policy, Adaptation, Research and Economic Development-PREPARED). Vilevile, Hati ya Makubaliano (MoU) kwa ajili ya usimamizi shirikishi wa rasilimali za maji katika Bonde la Mto Mara chini ya uratibu wa Lake Victoria Basin Commission ipo katika hatua za mwisho kukamilika. Aidha, utekelezaji wa mradi wa Bwawa la Borenga litakalotumika kwa shughuli za binadamu; mifugo; uzalishaji wa nishati ya umeme; na kilimo cha umwagiliaji katika vijiji 16 kwenye Wilaya za Butiama, Serengeti na Tarime unaendelea. Hadi sasa, upembuzi yakinifu na usanifu wa bwawa hilo umekamilika na taratibu za kupata fedha na kuajiri Mkandarasi wa ujenzi zimeanza. Mradi huo pamoja na mingine unaratibiwa na Nile Equatorial Lakes Subsidiary Action Plan (NELSAP) chini ya Nile Basin Initiative, NBI. 61. Mheshimiwa Spika, chini ya uratibu wa NELSAP maandalizi ya Mipango ya Usimamizi wa Hifadhi ya Maji katika sehemu ya Bonde la Mto Mara (Sub-Catchment Management Plans) kwenye maeneo ya Tobora (kilomita za mraba 364) na Somonche (kilomita za mraba 682); pamoja na uainishaji na upimaji wa maeneo ya mfano unaendelea. Vilevile, mikutano na wananchi kwa kuzingatia jinsia ili kupata maoni mbalimbali kuhusu utunzaji wa mabonde madogo katika maeneo hayo ilifanyika. Aidha, Serikali za Tanzania, Kenya pamoja na NELSAP zitasaini Hati ya Makubaliano ya kutekeleza miradi iliyopangwa.

(iv) Bonde la Mto Songwe 62. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Malawi inatekeleza Awamu ya Pili

Page 32: Tekeleza kwa

30

ya Programu ya Kuendeleza Bonde la Mto Songwe. Awamu hiyo inahusu kazi za usanifu wa kina wa miundombinu ya rasilimali za maji na maandalizi ya uwekezaji. Miundombinu hiyo ni kwa ajili ya kuzuia mafuriko, kuzalisha umeme, kilimo cha umwagiliaji, matumizi ya maji majumbani, ufugaji samaki na uwekezaji katika Sekta ya Utalii. Vilevile, umeme utakaozalishwa utaunganishwa kwenye gridi ya Taifa ya nchi za Malawi na Tanzania na kusambazwa kwenye vijiji vilivyo ndani ya eneo la Bonde. Aidha, chini ya awamu hiyo, maandalizi ya awali ya kuanzisha Kamisheni ya Pamoja ya Kusimamia Programu na kujenga uwezo kwa watekelezaji wa programu katika ngazi za Halmashauri hadi Taifa yako tayari. 63. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2015, kazi zilizotekelezwa ni pamoja na kukamilisha Dira ya Maendeleo ya Bonde la Mto Songwe inayolenga mwaka 2050; mapitio ya upembuzi yakinifu wa mwaka 2003; na Tathmini ya Kimkakati ya Athari za Kimazingira na Kijamii (SESA-Strategic Environmental and Social Impact Assessment). Aidha, rasimu ya mwisho ya Mfumo wa Kitaasisi (Convention on establishment of Songwe River Commission) kwa ajili ya kuanzisha Kamisheni ya Pamoja ya kusimamia Programu ya kuendeleza Bonde la Mto Songwe imekamilika na itawasilishwa Bungeni kwa kufuata taratibu zilizopo kwa ajili ya kuridhiwa. Vilevile, Mtaalam Mshauri amewasilisha rasimu za Programu ya miaka 10 ya Kuendeleza Bonde la Mto Songwe; Mpango Biashara wa Kamisheni ya Kuendeleza Bonde la Mto Songwe (Songwe River Basin Commission Business Plan); Tathmini ya Athari za Kimazingira na Kijamii; na rasimu ya Mpango Kazi wa Kuwahamisha na Kuwalipa Fidia waathirika wa mradi (Resettlement Action Plan). Rasimu hizo zimepitiwa na kutolewa maoni na wadau kwa ajili ya maboresho.

Page 33: Tekeleza kwa

31

64. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na usanifu wa kina kwa miradi ya kipaumbele katika uwekezaji ambayo ni Bwawa la Songwe Chini (Lower Songwe dam) linaloambatana na miundombinu ya kuzalisha umeme megawati 180.2; skimu mbili za kilimo cha umwagiliaji zenye jumla ya hekta 6,200 (hekta 3,050 upande wa Malawi na hekta 3,150 nchini Tanzania); miundombinu ya usafirishaji umeme; na maandalizi ya nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo. Pamoja na mafanikio hayo, kazi ya usanifu wa miundombinu kwa ajili ya kudhibitiwa mkondo wa Mto Songwe; na usanifu wa miradi ya maji ya kunywa kwa ajili ya miji midogo ya Songwe nchini Malawi na Kasumulu kwa upande wa Tanzania zinaendelea. Kazi hizo zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2015. 65. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Serikali itakamilisha taratibu za kuridhia Azimio la kuanzisha Kamisheni ya Pamoja ya Kusimamia Bonde la Mto Songwe. Vilevile, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Malawi itaendelea kutafuta wafadhili mbalimbali ili kutekeleza Awamu ya tatu ya mradi huo na kuunda Sekretarieti ya mpito ya Kamisheni kwa ajili ya kuanza kusimamia utekelezaji wa miradi ya awali. Miradi hiyo inahusu mradi wa maji ya kunywa kwa vijiji vilivyopo kwenye Bonde la Mto Songwe ambao unalenga kuwapatia huduma ya maji safi na salama wastani wa asilimia 22.5 ya wakazi wa bonde hilo kwa upande wa Malawi na asilimia 18.7 kwa upande wa Tanzania. Mradi huo unakadiriwa kugharimu Dola za Marekani milioni 1.5. Mradi mwingine ni wa kuandaa mfumo wa kuratibu haidrolojia katika bonde (Hydrological Monitoring System) ambao unakadiriwa kugharimu Dola za Marekani 425,000.

Page 34: Tekeleza kwa

32

(v) Ziwa Tanganyika 66. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea na usimamizi wa pamoja na uendelezaji wa rasilimali za maji ya Ziwa Tanganyika kwa kushirikiana na nchi za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Zambia. Ziwa Tanganyika linaendelea kukumbwa na changamoto ya kupungua kwa kina cha maji kama inavyojidhihirisha katika bandari za Kigoma upande wa Tanzania; na Kalemie, Uvira na Moba kwa upande wa DRC hivyo, kuathiri matumizi ya bandari hizo. Miongoni mwa sababu zinazochangia tatizo la kupungua kwa kina cha maji ni kubomoka kwa banio la Mto Lukuga uliopo DRC unaotoa maji kutoka Ziwa Tanganyika kupeleka Mto Kongo. 67. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hizo na kwa kuwa waathirika wakuu ni Tanzania na DRC, nchi ambazo zinamiliki kwa pamoja asilimia 86 ya Ziwa hilo, Marais wa Serikali zote mbili walitoa maelekezo kwa Mawaziri wa Maji wa Tanzania na DRC kukutana ili kujadili na kupata ufumbuzi wa changamoto husika. Mkutano wa kwanza wa Mawaziri ulifanyika tarehe 16/04/2014, Mjini Dodoma ambapo tulikubaliana kushirikiana katika maeneo yanayohusu usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji za Bonde la Ziwa Tanganyika.

68. Mheshimiwa Spika, kabla ya kuanza utekelezaji wa makubaliano hayo, ililazimu masuala muhimu yafanyike ili kuweka msingi wa utekelezaji, ambapo kila nchi ilitakiwa kuteua wataalam watakaounda kamati ya pamoja ya kushughulikia mradi wa ujenzi wa banio la Mto Lukuga pamoja na masuala ya usimamizi wa rasilimali za maji. Aidha, ilikubalika kwamba mkutano wa pili ufanyike Kalemie DRC ambapo Mawaziri wangezindua Kamati hiyo ya pamoja.

Page 35: Tekeleza kwa

33

Mkutano huo ulifanyika tarehe 16-17 Agosti, 2014 na ulimalizika kwa kutoa azimio la pamoja (Ministerial Declaration) lenye makubaliano ya msingi yafuatayo:-

(i) Kuendeleza ushirikiano wa dhati wa kikanda na kati ya nchi zetu mbili kwa kuzingatia yaliyomo kwenye mkataba wa kuanzisha Mamlaka ya Ziwa Tanganyika;

(ii) Kuimarisha na kuendeleza jitihada na mikakati ya pamoja ya kushughulikia kwa ujumla wake, tatizo la kupungua kwa kina cha maji ya Ziwa Tanganyika; na

(iii) Kuandaa Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya nchi zetu mbili kwa kuzingatia maeneo ya ushirikiano tuliyokubaliana wakati wa mikutano ya Mawaziri iliyofanyika Dodoma na Kalemie.

69. Mheshimiwa Spika, kamati ya pamoja ya wataalam ilifanya kikao chake cha pili Jijini Dar es Salaam tarehe 16-18 Februari, 2015 kwa lengo la kukamilisha rasimu ya pamoja ya Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano wa pamoja wa usimamizi wa rasilimali za maji ya Bonde la Ziwa Tanganyika na ujenzi wa banio kwenye Mto Lukuga. Kila nchi iliwasilisha rasimu hiyo kwa mamlaka husika kupata maoni kwa ajili ya kuiboresha kabla ya kusainiwa. Baada ya taratibu zote za kisheria katika kila nchi kukamilika, hati hiyo ilisainiwa tarehe 07/05/2015, Jijini Kinshasa-DRC. Katika mwaka 2015/2016, Serikali ya Tanzania itaendelea kutekeleza shughuli zilizoainishwa kwenye MoU na pia kushirikiana kwa karibu na nchi za Burundi, Zambia na Sekretarieti ya Mamlaka ya Ziwa Tanganyika.

Page 36: Tekeleza kwa

34

3.1.2 Ubora na Usafi wa Maji 70. Mheshimiwa Spika, Sera ya Maji (2002), Sheria za Usimamizi wa Rasilimali za Maji Na. 11 na Huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Na.12 za mwaka 2009, zinaelekeza mamlaka zote za kiutawala na kiutendaji nchini kuhakikisha maji yanayotumiwa na wananchi kwa shughuli za kiuchumi na kijamii yanafikia viwango vya ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa. Maji safi na salama ni msingi muhimu katika kulinda afya za wananchi dhidi ya magonjwa yatokanayo na maji. Katika kutekeleza matakwa ya Sera kuhusiana na vyanzo na ubora wa maji, Wizara yangu kupitia mtandao wa Maabara za Ubora wa Maji za Kanda na Mikoa iliendelea kuhakiki ubora wa maji katika vyanzo na mitandao ya kusambaza maji. 71. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya sampuli 4,442 zilikusanywa na kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara wa kemikali na makrobaolojia kati ya sampuli za maji 8,000 zilizopangwa kuchunguzwa kwa mwaka 2014/2015. Hali ya ubora wa maji kwa matumizi mbalimbali ni kama ifuatavyo:- (a) Ubora wa Maji kwa Matumizi ya Majumbani 72. Mheshimiwa Spika, Wizara ilihakiki hali ya ubora wa maji katika vyanzo kwenye Halmashauri, mitandao ya maji mijini, taasisi na vyanzo vya maji vya watu binafsi ambapo jumla ya sampuli 3,882 zilichunguzwa. Matokeo ya uchunguzi yalionesha sampuli 3,175 sawa na asilimia 82 zilikuwa na viwango vinavyokubalika kitaifa. Sampuli 707 hazikukidhi viwango kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha chumvi pamoja na vimelea vya wadudu hususan, kwenye visima vifupi na maji juu ya ardhi. Aidha, maji ya

Page 37: Tekeleza kwa

35

visima hivyo yalitibiwa kwa kuwekewa dawa ya kuua vimelea na visima vinaendelea kutumika. (b) Ubora wa Maji kwa Matumizi ya Viwanda 73. Mheshimiwa Spika, katika kufuatilia hali ya ubora wa maji yanayotumiwa viwandani, jumla ya sampuli 364 kutoka viwanda vya samaki vya Kagera, Mwanza, Mara, Dar es Salaam na kiwanda cha sukari cha Kagera zilichunguzwa. Matokeo ya uchunguzi huo yalibainisha kuwa maji yanayotumiwa na viwanda hivyo yanakidhi viwango vinavyokubalika kitaifa na kimataifa. Wizara itaendelea kuchukua tahadhari ya kuhakikisha kuwa maji yanayotumika katika viwanda vya usindikaji vyakula yanakidhi viwango vya ubora wa maji unaokubalika ili kulinda afya ya mlaji. (c) Mwenendo wa Ubora wa Maji katika Vyanzo 74. Mheshimiwa Spika, usafi na usalama wa maji hutegemea hali ya mazingira yanayozunguka vyanzo. Katika kudhibiti vyanzo visichafuliwe inabidi kufuatilia mwenendo wa ubora wa maji katika vyanzo. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya sampuli za maji 322 kutoka katika vyanzo mbalimbali zilichunguzwa na matokeo yalionesha kuwa maji katika vyanzo hivyo yana ubora unaokubalika kwa matumizi ya kijamii na kiuchumi pamoja na ustawi wa mfumo wa ikolojia. (d) Ubora wa Maji kwa ajili ya Ujenzi na Utafiti 75. Mheshimiwa Spika, usalama na uimara wa miundombinu ya Sekta ya Ujenzi ikiwemo barabara na majengo unategemea kiwango cha kemikali kwenye maji yanayotumika. Kwa kuzingatia hilo, jumla ya sampuli 22 za maji kwa ajili ya matumizi ya ujenzi kutoka kwa Wakandarasi

Page 38: Tekeleza kwa

36

mbalimbali wa majengo na barabara zilichunguzwa ubora wake. Uchunguzi huo ulibaini kuwa baadhi ya sampuli hizo zina kiwango kikubwa cha madini ya sulphate yanayoweza kuathiri muunganiko wa saruji, kokoto na mchanga na hivyo, kudhoofisha uimara wa barabara na majengo. Ushauri wa kitaalam kuhusu uchanganyaji wa maji (blending) ili kupata kiwango sahihi cha madini kwenye maji yanayotumika kwenye ujenzi ulitolewa kwa Wakandarasi hao. 76. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kwa kushirikiana na Chuo cha Utafiti wa Uvuvi (Tanzania Fisheries Research Institute-TAFIRI) ilifuatilia mwenendo wa ubora wa maji katika Rasi ya Nyegezi kwenye Ziwa Victoria ambapo sampuli za maji 13 zilichunguzwa. Matokeo ya uchunguzi yalibaini kuendelea kuongezeka kwa kiwango cha madini ya phosphorus na nitrate. Ongezeko hilo linasababisha kuwepo kwa mwani (algae) ambao unaathiri mazalia ya samaki. Hivyo, Wizara yangu inaendelea kushirikiana na taasisi na watu binafsi katika kulinda na kuhifadhi mazingira ya Ziwa Victoria. (e) Ubora wa Majitaka 77. Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza hapo awali, vyanzo vya maji vinaweza kuathiriwa na shughuli za kibinadamu ikiwemo utiririshaji wa majitaka kutoka majumbani na viwandani kwenye maeneo ya vyanzo vya maji. Katika kutathmini ubora wa majitaka yanayotiririshwa, sampuli 524 zilichunguzwa kati ya sampuli 1,000 zilizopangwa kwa mwaka 2014/2015. Vielelezo ambavyo vinazingatiwa kwa kipimo cha lita moja ya majitaka ni Biological Oxygen Demand (BOD) ambayo haitakiwi kuzidi miligramu 30, Chemical Oxygen Demand (COD) miligramu 60, Nitrates miligramu 20 na Phosphorous miligramu 6.

Page 39: Tekeleza kwa

37

Matokeo ya uchunguzi yalionesha asilimia 93 ya sampuli zilikidhi viwango vya kurudishwa kwenye mazingira. Wizara inaendelea kukagua na kutoa ushauri wa kitaalam kuhusu uboreshaji wa mabwawa na mifumo ya kutibu majitaka kwa mamlaka husika ili kulinda mazingira dhidi ya uchafuzi. (f) Ubora wa Madawa ya Kusafisha na Kutibu Maji 78. Mheshimiwa Spika, Mamlaka za Maji na vyombo vya usambazaji maji vijijini vinalazimika kutumia madawa ya kutibu maji yanayozalishwa na kusambazwa kwa matumizi ya majumbani. Viwango vya ubora wa madawa yanayotumika hutakiwa kuthibitishwa kabla ya matumizi husika kwa lengo la kulinda afya za wananchi na usalama wa maji kwa ujumla. Katika mwaka 2014/2015, jumla ya sampuli 24 za madawa mbalimbali ya kusafisha na kutibu maji zilichunguzwa na kukidhi viwango. Madawa hayo ni pamoja na Calcium hypochlorite, Aluminium Sulphate, Poly-Aluminium Chlorite, Soda Ash, Magna floc na Algal Floc. Wizara imeendelea kuzishauri taasisi za umma na binafsi kuhakiki ubora wa madawa ya kusafisha na kutibu maji kabla ya kununuliwa, kwa lengo la kunusuru rasilimali fedha inayoweza kupotea kwa kununua madawa yasiyofaa kwa matumizi yaliyolengwa. (g) Juhudi za Kuondoa Madini ya Fluoride katika Maji

ya Kunywa na Matumizi ya Nyumbani 79. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, maandalizi ya kupata benki ya takwimu na kuchora ramani inayoonesha maeneo yaliyoathiriwa na uwepo wa madini ya fluoride kwa wingi katika maji imeendelea kufanyika ili kuandaa ramani inayoonesha ukanda wa fluoride (fluoride belt) hapa nchini. Kazi iliyofanyika ni kutambua vyanzo vyote

Page 40: Tekeleza kwa

38

vya maji katika Halmashauri za Wilaya za Arusha Mjini, Karatu, Arumeru, Longido, Monduli na Ngorongoro Mkoani Arusha; Wilaya za Simanjiro, Hanang, Babati, Mbulu na Kiteto Mkoani Manyara. Katika kutekeleza kazi hiyo, jumla ya vyanzo vya maji 954 vimekaguliwa na maji kufanyiwa uchunguzi wa kemikali na kuangalia uwepo wa madini ya fluoride. Zoezi la kuhakiki takwimu zilizopatikana linaendelea ili kupata takwimu sahihi zitakazowekwa kwenye ramani hiyo na vilevile kupata benki ya takwimu ya madini ya fluoride (fluoride database) hapa nchini. 80. Mheshimiwa Spika, katika kupanua wigo wa upatikanaji wa teknolojia ya uondoaji wa madini ya fluoride, kituo cha utafiti wa kemikali ndani ya maji cha Ngurdoto kimeanza utafiti kwenye maeneo yenye madini ya phosphate yanayowezesha kutengeneza artificial hydroxyl apatite inayotumika katika uondoaji wa madini ya fluoride kama zilivyo chengachenga za mifupa ya ng’ombe. Maeneo yaliyoanza kufanyiwa utafiti wa ubora wa udongo wenye madini ya phosphate ni Matombo Mkoani Morogoro, Mlima Panda (Mbeya) na Minjingu Mkoani Arusha. Vilevile, elimu kuhusu uondoaji madini ya fluoride kwa kutumia chengachenga za mifupa ya ng’ombe imeendelea kutolewa kwa jamii kupitia warsha, makongamano na maadhimisho ya Wiki ya Maji. 81. Mheshimiwa Spika, Wizara imepokea mtambo wa majaribio wa kusafisha na kutibu maji kutoka Kampuni ya Marekani (International Water Company). Mtambo huo umefanyiwa majaribio ya awali na umeonesha kuwa na uwezo wa kuondoa madini ya fluoride. Chanzo cha maji chenye madini ya fluoride ya kiwango cha miligramu 20 kwa kila lita moja ya maji kilifanyiwa majaribio, ambapo mtambo huo umeweza kupunguza kiwango hicho hadi kufikia kiasi

Page 41: Tekeleza kwa

39

cha miligramu 0.06. Mtambo huo wa kisasa unatumia nishati ya jua, upepo na umeme wa kawaida hivyo, unaweza kutumika katika ngazi ya jamii kwa maeneo ya vijijini na mijini. Kwa sasa majaribio ya ziada yanaendelea ili kujua uwezo wa chujio (filter media) ina uwezo wa kusafisha maji kwa kiwango gani kabla ya chujio hilo kubadilishwa. Matokeo ya majaribio hayo yatatoa mwelekeo kwa Wizara kuweza kutoa mwongozo juu ya matumizi ya teknolojia hiyo mpya kwa Halmashauri na Mamlaka za Maji zilizo kwenye maeneo yaliyoathiriwa na madini ya fluoride. 82. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kutekeleza mkakati wa kuondoa madini ya fluoride katika maji ya kunywa na kupikia kwa kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya kuondoa fluoride katika ngazi ya kaya na mitambo 1,000 ya kuondoa madini ya fluoride kwenye maji itasambazwa. Katika ngazi ya jamii mitambo itajengwa kulingana na mahitaji. Kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali, utafiti wa kupata mitambo ya kisasa yenye gharama nafuu utaendelea. Aidha, kazi ya kubaini vyanzo vya maji vilivyoathirika na madini ya fluoride itaendelea katika mikoa iliyopo kwenye ukanda wa fluoride. (h) Maabara za Maji kupata Ithibati (Accreditation) 83. Mheshimiwa Spika, katika hotuba yangu ya mwaka jana, nililiarifu Bunge lako Tukufu kuwa Maabara ya Maji Jijini Mwanza ilikuwa imefikia hatua nzuri ya kupata ithibati. Napenda kuliarifu Bunge lako kuwa, tarehe 30/03/2015, Maabara hiyo imepata ithibati. Mafanikio hayo yametokana na Bodi ya Taasisi inayotoa ithibati katika nchi za Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community Accreditation Services - SADCAS) kuthibitisha kuwa Maabara imetimiza vigezo vyote vya kiutawala na kiutendaji

Page 42: Tekeleza kwa

40

vilivyotakiwa. Aidha maabara ya Mwanza imekabidhiwa rasmi cheti cha ithibati tarehe 15/05/2015 na kupewa namba maalum “TEST – 50011” ikianisha uwezo wa kuweza kupima viashiria 15 vya kemikali katika maji (Chemical Analysis to ISO/IEC17025:2005). Hivyo, kufanikiwa kupata kwa ithibati kunatoa fursa nyingi kwani kwa sasa kazi zake zinatambulika kitaifa na kimataifa. Vilevile, kuanzia mwezi Juni 2015, Maabara ya Mwanza itaanza kuonekana kwenye tovuti ya SADCAS ambayo ni www.sadcas.org. 84. Mheshimiwa Spika, kupatikana ithibati kwa Maabara ya Mwanza, kumeongeza ari kwa maabara nyingine kuanza mchakato unaolenga kukidhi viwango vya kitaifa na kimataifa. Katika kutekeleza hayo, Maabara za Maji za Dar es Salaam na Iringa zimeanza mafunzo ya uandaaji wa miongozo ya usimamizi (Quality Management Systems) ambayo ni kigezo kikubwa cha maabara kupata ithibati. Aidha, kwa kutumia uzoefu uliopatikana katika mchakato mzima wa kupata ithibati kwa Maabara ya Mwanza, maabara nyingine zote zitaendelea na ushiriki wa mazoezi ya kujipima kiutendaji kwa kuchunguza sampuli kitaifa na kimataifa (Proficiency Testing) ili matokeo hayo yaendelee kubaini maeneo muhimu zaidi ya kufanyia maboresho katika maabara hizo. (i) Utekelezaji wa Mpango wa Usalama wa Maji 85. Mheshimiwa Spika, usalama wa maji unahitaji kuwa na mpango wa usimamizi na ufuatiliaji kuanzia kwenye chanzo hadi kwa mtumiaji. Wizara yangu imeanza kutekeleza Mpango wa Usalama wa Maji (Water Safety Plan) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Shirika la Afya Duniani ili uweze kutumika katika mamlaka zinazotoa huduma za usambazaji maji. Majaribio

Page 43: Tekeleza kwa

41

ya mpango huo yanafanyika katika Mamlaka ya Maji Kigoma na Chombo cha Watumia Maji cha Mbande–Kongwa. Wataalam wa kada mbalimbali katika mamlaka hizo wamepata mafunzo yaliyohusisha Washauri wa Maji wa Mikoa, Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutoka katika maeneo ya majaribio. 86. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Maji (International Water Association – IWA) ilitoa mafunzo kuhusu uandaaji wa Mipango ya Usalama wa Maji kwa wataalam 35 kutoka Maabara za Ubora wa Maji; Mamlaka za Maji za Mtwara, Iringa, Kigoma; pamoja na Mradi wa Kitaifa wa Masasi-Nachingwea. Mafunzo hayo yaliwezesha wataalam kubaini njia mbalimbali zinazoweza kuathiri usalama wa maji siyo kwenye chanzo cha maji pekee, bali hata ndani ya mifumo ya kutibu na kusambaza maji. Wataalam hao watashirikiana na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini pamoja na Vyombo vya Watumiaji Maji katika kuandaa mipango ya usalama wa maji kwa taasisi hizo. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kushirikiana na taasisi na mashirika mbalimbali ili kuboresha hali ya usalama wa maji kwa ajili ya kulinda afya za wananchi. Katika kutekeleza hayo, Wizara itaandaa miongozo ya utekelezaji wa Mipango ya Usalama wa Maji katika ngazi za Mamlaka za Maji na Vyombo vya Watumia Maji Vijijini (COWSOs). (j) Mafunzo kwa Watumishi wa Maabara 87. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa watumishi wa kada ya uchunguzi wa ubora wa maji wanaendelea kutoa huduma stahiki kwa wananchi, watumishi 90 walipata mafunzo katika nyanja mbalimbali.

Page 44: Tekeleza kwa

42

Mafunzo hayo yalihusisha Global Information System (GIS), Good Laboratory Practies (GLP), ISO 17025:2005, Best Microbiology Practice for laboratory accreditation na Laboratory Information Management System. Katika mwaka 2015/2016, Wizara itaendelea kuwajengea uwezo watumishi ili waendelee kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi. (k) Ujenzi na Ukarabati wa Maabara za Maji 88. Mheshimiwa Spika, katika juhudi za Wizara yangu kuboresha na kusogeza karibu zaidi huduma za ubora wa maji kwa wananchi, Wizara inakarabati na kujenga maabara mpya za maji katika mikoa mbalimbali. Hadi mwezi Aprili 2015, ujenzi wa Maabara ya Kigoma umefikia asilimia 65, Singida asilimia 55; ukarabati wa Maabara ya Bukoba umefikia asilimia 65, na Shinyanga asilimia 60. Vilevile, zabuni za kujenga maabara za Mtwara na Mbeya pamoja na ukarabati wa majengo ya maabara katika Miji ya Songea na Sumbawanga zilitangazwa mwezi Februari, 2015. Mapitio ya michoro (architectural and structural drawings) kwa ajili ya ujenzi wa maabara za Morogoro, Tanga na Arusha yamefanyika mwezi Machi, 2015 na zabuni za ujenzi wa maabara hizo zitatangazwa baada ya taratibu za kifedha kukamilika. Aidha, mkataba kwa ajili ya upanuzi na ukarabati wa jengo la Maabara Kuu ya Maji Dar es Salaam upo katika hatua za mwisho kusainiwa. 89. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kuzijengea uwezo maabara za maji nchini kwa kuzipatia vifaa vya kisasa vya kufanyia uchunguzi na hivyo kuongeza tija. Vilevile, mazingira ya kufanyia kazi za kiuchunguzi yataboreshwa zaidi ili kuongeza ari ya utendaji kazi na kulinda afya za watumishi. Aidha, Wizara yangu itaendelea kutekeleza mkakati wa usimamizi wa ubora

Page 45: Tekeleza kwa

43

wa maji na kudhibiti uchafuzi kwa kuchunguza sampuli 10,000 kutoka vyanzo mbalimbali vya maji na sampuli 1,500 za majitaka zitahakikiwa ubora wake kabla ya kutiririshwa kwenye vyanzo vya maji. Vilevile, elimu kuhusu ubora wa maji na ushauri wa kitaalam utatolewa kwa taasisi na vyombo vinavyotoa huduma ya usambazaji maji safi na salama vijijini na mijini.

Page 46: Tekeleza kwa

44

3.2 HUDUMA YA MAJI VIJIJINI 3.2.1 Mpango wa “Tekeleza kwa Matokeo Makubwa

Sasa” (Big Results Now – BRN) 90. Mheshimiwa Spika, Serikali iliandaa mpango mkubwa wa kupeleka maji safi na salama vijijini chini ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (Water Sector Development Programme) iliyoanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2007/2008. Programu hiyo iligubikwa na urasimu mkubwa katika utekelezaji wake uliosababishwa na masharti yaliyowekwa kabla ya kuanza kwa mradi ikiwa ni pamoja na:-

(i) Kupata kibali (No Objection) cha Benki ya Dunia katika uteuzi wa Wahandisi Washauri (Wasimamizi) wa kila mradi kabla ya kuanza ujenzi;

(ii) Kupata kibali cha Wizara ya Maji katika kuteua

Wakandarasi wa ujenzi wa kila mradi;

(iii) Kupata michango ya wananchi wanaonufaika na mradi inayofikia asilimia 5 ya thamani ya mradi kabla ya ujenzi kuanza;

(iv) Kuhitajika kwa Halmashauri kutoa elimu, kuanzisha na

kusajili Vyombo vya Watumiaji Maji (COWSOs) katika kila eneo la mradi kabla ya ujenzi wa mradi wowote kuanza; na

(v) Baadhi ya Halmashauri kutaka kupokea fedha zote

zinazotosha kujenga mradi kabla ya mradi husika kuanza kujengwa.

Page 47: Tekeleza kwa

45

91. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Juni, 2012, Wilaya 12 tu kati ya 132 zilikuwa zimetimiza masharti hayo na kuanza utekelezaji. Kutokana na hali hiyo, kuanzia mwezi Julai, 2013, Wizara kupitia Mpango wa Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) iliondoa urasimu huo ili kuharakisha uandaaji na utekelezaji wa miradi ya maji vijijini. Katika kutekeleza mpango huo, madaraka yote ya kubuni, kuandaa, kutekeleza na kusimamia miradi ya maji vijijini yalikasimiwa kwa Halmashauri za Wilaya ili kuwa na miradi na huduma endelevu. Vilevile, bajeti ilitengwa katika Sekretarieti za Mikoa kwa ajili ya kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa kazi za ujenzi wa miradi. Aidha, Wizara inaendelea kutekeleza majukumu yake ya kutafuta fedha, kuandaa miongozo, kutoa utaalam unaohitajika na kuzijengea uwezo Halmashauri kwa kuzipatia wataalam wa nyanja mbalimbali wakiwemo wahandisi na mafundi sanifu. 92. Mheshimiwa Spika, kabla ya kuanza kutekeleza mpango wa BRN, idadi ya wakazi wa vijijini waliokuwa wananufaika na huduma ya maji safi ni wastani wa watu 200,000 hadi 400,000 kwa mwaka. Baada ya kuondolewa kwa urasimu na kuanza kutekelezwa kwa mpango wa BRN, jumla ya miradi ya maji 248 kwenye Halmashauri 98 ilijengwa kwa kipindi cha mwaka mmoja. Utekelezaji huo uliongeza idadi ya wakazi wa vijijini wanaopata huduma ya maji safi na salama kutoka wakazi milioni 15.2 mwezi Julai, 2013 hadi wakazi milioni 17.8 mwezi Juni 2014, sawa na ongezeko la wakazi milioni 2.6. 93. Mheshimiwa Spika, mpango wa BRN kwa Sekta ya Maji umejielekeza katika utoaji wa huduma ya usambazaji maji na usafi wa mazingira vijijini kwa kutekeleza kazi za ujenzi wa miradi mipya; ukarabati wa miundombinu chakavu; upanuzi wa miradi iliyopo; na uendeshaji na matengenezo

Page 48: Tekeleza kwa

46

(operation and maintenance). Ujenzi wa miradi mipya unahusisha miradi ya vijiji 10 kwa kila Halmashauri na miradi ya kimkakati. Miradi ya upanuzi na ukarabati inahusisha utekelezaji wa miradi ya matokeo ya haraka kwa kujenga miundombinu kutoka kwenye vyanzo vikiwemo mabwawa, visima virefu na chemichemi. Vilevile, uendeshaji na matengenezo unahusu kuvijengea uwezo Vyombo vya Watumiaji Maji na ukusanyaji wa taarifa za utekelezaji. 3.2.2 Utekelezaji wa BRN kwa Miradi ya Maji Vijijini 94. Mheshimiwa Spika, baada ya Serikali kutekeleza mpango wa BRN kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia mwezi Julai 2013 mpaka mwezi Juni 2014, iliona umuhimu wa kujitathmini kwa kuajiri Mtaalam Mshauri kupima utekelezaji wa mpango huo kwa sekta zote sita zilizoanza kutekeleza BRN. Kazi hiyo ilifanywa na Kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PwC) na kuthibitishwa na Kamati ya Watu Mashuhuri Duniani (Committee of Emminent Persons) mwezi Januari, 2015. Matokeo ya tathmini hiyo yameonesha mafanikio makubwa kwa upande wa Sekta ya Maji ambapo imeweza kufikia asilimia 80 ya malengo yaliyowekwa na kuongoza kwa kiwango cha juu kati ya Sekta zilizoanza kutekeleza mpango wa BRN. 95. Mheshimiwa Spika, mafanikio yaliyopatikana kutokana na mpango wa BRN ni pamoja na kuongezeka kwa idadi ya wananchi wanaopata huduma ya maji vijijini kutoka wananchi 15,200,000 sawa na asilimia 40 mwezi Juni, 2013 hadi kufikia wananchi 20,957,855 sawa na asilimia 55.9 mwezi Aprili, 2015. Hili likiwa ni ongezeko la zaidi ya wananchi milioni 5.76 wanaopata huduma ya maji katika kipindi hicho cha utekelezaji wa mpango huo. Lengo ni kufikia asilimia 74 ifikapo mwezi Juni, 2016.

Page 49: Tekeleza kwa

47

96. Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia malengo ya BRN ya kuhakikisha miradi ya maji vijijini inatekelezwa kitaalam kwa ufanisi na haraka, Wizara yangu imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kufanikisha utekelezaji wa mpango huo. Hatua hizo ni pamoja na kuajiri wataalam ambao wamepangiwa vituo vya kazi katika ngazi za Wizara, Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya wataalam 318 wa fani mbalimbali za kiufundi waliajiriwa. Hatua nyingine zilizochukuliwa ni kupunguza muda wa ununuzi wa Wataalam Washauri na Wakandarasi kutoka siku 210 hadi siku 97 kwa kuondoa vibali visivyo vya lazima; na kuendelea na ujenzi wa miradi ya maji hata kama michango ya wananchi haijakamilika. Aidha, Wizara imeendelea kuwahamasisha wananchi kutoa michango itakayotumika kwa ajili ya uendeshaji na matengenezo ya miradi hiyo baada ya ujenzi kukamilika. 97. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilitengewa shilingi bilioni 270.98 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji vijijini. Hadi mwezi Aprili 2015, kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 76.52 sawa na asilimia 28 zilitolewa na kutumwa kwenye Halmashauri na Sekretarieti za Mikoa. Matumizi ya fedha hizo, kiasi cha shilingi bilioni 73.09 yalilenga utekelezaji na usimamizi wa miradi ya maji ya vijiji 10 kwa kila Halmashauri; na shilingi bilioni 3.43 zilizobaki zilielekezwa kwenye miradi mingine ya maji vijijini ambayo inahusisha miradi yenye kuleta matokeo ya haraka, ujenzi wa mabwawa na gharama za ziada (incremental cost) za usimamizi na ufuatiliaji wa miradi. Vilevile, kiasi kingine cha shilingi bilioni 6.71 kilikasimiwa kupitia Mafungu ya Mikoa kwenda kwenye Halmashauri, OWM-TAMISEMI na Wizara zinazoshiriki katika kutekeleza Kampeni ya Kitaifa ya Usafi wa Mazingira Vijijini.

Page 50: Tekeleza kwa

48

3.2.3 Mpango wa BRN kwa mwaka 2015/2016 98. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kujenga, kupanua na kukarabati miundombinu ya maji vijijini chini ya mpango wa BRN. Jumla ya shilingi bilioni 269.57 zimepangwa kutumika, na kati ya hizo shilingi bilioni 167.82 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 101.75 ni fedha za nje. Katika kutekeleza miradi hiyo, vijiji 534 vitanufaika kwa kupatiwa miradi ya maji ambapo vituo 9,757 vya kuchotea maji vitajengwa na kuhudumia jumla ya wakazi 2,439,462 waishio vijijini. Majedwali Na. 5a na 5b yanaonesha mgawo wa fedha zitakazotumwa katika Halmashauri na Sekretarieti za Mikoa kutekeleza miradi ya maji vijijini na kwa ajili ya usimamizi wa miradi ya maji katika ofisi ya mkoa kwa mwaka 2015/2016. 3.2.4 Hali ya Utekelezaji wa Miradi ya Maji Vijijini 99. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza jumla ya miradi 1,814 ya maji vijijini katika Halmashauri zote nchini. Miradi hiyo inahusu ujenzi wa miradi ya vijiji 10, miradi ya kimkakati, miradi ya upanuzi na ukarabati pamoja na miradi inayofadhiliwa na wadau mbalimbali. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya miradi ya maji 975 katika vijiji 1,206 yenye jumla ya vituo 24,129 vya kuchotea maji imekamilika kwenye Halmashauri 148. Utekelezaji huo umewanufaisha wakazi milioni 5.75 waishio vijijini na kuongeza idadi ya watu wanaopata huduma ya majisafi vijijini kufikia 20,957,855 sawa na asilimia 55.9. Jedwali Na. 6 linaonesha orodha ya vijiji 1,206 vilivyopata huduma kutoka kwenye miradi iliyokamilika chini ya mpango wa BRN pamoja na wakazi walionufaika na miradi hiyo.

Page 51: Tekeleza kwa

49

100. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea kutekeleza miradi 839 iliyobaki katika vijiji 1,115 inayohitaji jumla ya shilingi bilioni 234.6 kuikamilisha. Miradi hiyo imefikia hatua mbalimbali za utekelezaji na ikikamilika itahudumia watu 5,594,493. Kati ya miradi hiyo, utekelezaji wa miradi 262 kwenye vijiji 311 upo kati ya asilimia 71 hadi asilimia 95, na jumla ya shilingi bilioni 40.14 zinahitajika kuikamilisha miradi hiyo itakayohudumia watu 1,732,800. Kufanikiwa kwa lengo hilo kutategemea upatikanaji wa fedha zilizopangwa kwa wakati. Jedwali Na. 7 linaonesha miradi 262 ambayo utekelezaji wake upo kati ya asilimia 71 na asilimia 95. (a) Ujenzi wa Miradi Mipya (i) Miradi ya Kimkakati Mradi wa Maji Tabora 101. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Japan inatekeleza mradi wa maji katika vijiji 19 kwenye Wilaya zote saba za Mkoa wa Tabora. Mradi unatekelezwa katika awamu mbili; Awamu ya Kwanza ilianza mwezi Septemba, 2009 na kukamilika mwezi Mei, 2011 kwa kukarabati visima virefu na vifupi 46; kuandaa Mpango Mahsusi wa Maji Vijijini kwa Mkoa; kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa miradi ya maji katika vijiji 19; na kuandaa makadirio ya gharama za ujenzi na makabrasha ya zabuni. 102. Mheshimiwa Spika, Awamu ya Pili ya mradi huo inayogharimu Yeni za Kijapani bilioni 1.56 sawa na shilingi bilioni 25.2 imeanza kutekelezwa mwezi Aprili, 2014. Utekelezaji unahusu uchimbaji wa visima virefu, ujenzi wa matanki ya maji, ujenzi wa nyumba ya pampu na ulazaji wa

Page 52: Tekeleza kwa

50

mabomba katika vijiji 19 kwenye Wilaya zote za Mkoa wa Tabora. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya visima 38 vimekamilika na kupata maji safi katika Halmashauri za Wilaya za Sikonge, Kaliua,Uyui,Nzega,Urambo, Igunga na Manispaa ya Tabora. Vilevile, kazi ya ujenzi wa matanki ya maji; ujenzi wa nyumba ya pampu; na ulazaji wa mabomba katika vijiji vya Mabama (Wilaya ya Uyui) na Kakola (Manispaa ya Tabora) kwa pamoja umefikia wastani wa asilimia 70. Aidha, vifaa vya kisasa vya kutafiti maji chini ya ardhi vyenye thamani ya shilingi milioni 615.39 vimenunuliwa na kukabidhiwa ofisi ndogo ya Tabora katika Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Tanganyika. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2016 na utawanufaisha zaidi ya wakazi 40,352 wa Wilaya hizo. Mradi wa Maji Bungu - Korogwe 103. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la World Vision inatekeleza mradi wa Maji wa Bungu uliopo katika Wilaya ya Korogwe. Mradi huo unahusu upanuzi na ukarabati. Utekelezaji wa mradi huo umeendelea katika vijiji vya Msasa, Bungu, Bungu-Msiga na Manka na hadi sasa wakazi 9,306 wameanza kunufaika na huduma ya maji safi. Katika mwaka 2014/2015, kazi zilizotekelezwa na kukamilika ni ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 90,000 katika Kitongoji cha Sinai-Kwebago kijiji cha Bungu; ulazaji wa mabomba urefu wa Kilomita 5.3 kutoka tanki la Gare hadi Kijiji cha Bungu-Msiga; pamoja na kujenga vituo vitano vya kuchotea maji. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itakamilisha miradi ya maji katika vijiji vilivyobaki vya Mlungui, Kwemshai na Ngulu. Kukamilika kwa miradi hiyo, wakazi 18,460 wa vijiji saba vya Bungu, Bungu-Msiga, Kwemshai, Ngulu, Mlungui, Msasa na Manka watanufaika na huduma ya maji safi na salama.

Page 53: Tekeleza kwa

51

Mradi wa Maji wa Same – Mwanga – Korogwe 104. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wa maeneo ya Wilaya za Same, Mwanga na Korogwe wanapata huduma ya maji safi, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) na Mfuko wa Maendeleo wa Nchi Zinazozalisha Mafuta (OFID) inatekeleza mradi wa Same-Mwanga-Korogwe. Mkataba wa ujenzi wa Fungu la Kwanza la Mradi (Contract Package I) kwa Awamu ya Kwanza, umesainiwa tarehe 20/11/2014 kati ya Wizara na Mkandarasi kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 41.36. Katika kutekeleza mradi huo, Serikali itachangia Dola za Marekani milioni 19.36, mchango wa BADEA ni Dola za Marekani milioni 10 na OFID itachangia Dola za Marekani milioni 12. 105. Mheshimiwa Spika, Mkandarasi wa Awamu ya Kwanza ya mradi ameshaanza kazi na atatekeleza mradi huo kwa kipindi cha miezi 31. Mradi utakamilika mwezi Juni, 2017. Kazi zitakazotekelezwa ni kujenga choteo la maji (intake) katika Bwawa la Nyumba ya Mungu; mtambo wa kutibu maji eneo la Njia Panda; kulaza bomba kuu lenye kipenyo cha milimita 1,000 umbali wa kilomita 2.5 kutoka kwenye choteo la maji hadi mtambo wa kutibu maji; na kulaza bomba lenye kipenyo cha milimita 900 umbali wa kilomita 10.3 kutoka kwenye mtambo wa kutibu maji hadi matanki ya kituo cha kusukuma maji Kisangara. 106. Mheshimiwa Spika, katika hatua ya maandalizi ya Awamu ya Pili ya mradi, mikataba ya mkopo wa fedha (Loan Agreements) imesainiwa kati ya mwezi Oktoba na Desemba, 2014 ambapo BADEA itatoa Dola za Marekani milioni 12, Kuwait Fund Dola za Marekani milioni 34 na Saudi Fund itachangia Dola za Marekani milioni 25. Mkataba wa mkopo

Page 54: Tekeleza kwa

52

wa fedha kutoka OFID wa Dola za Marekani milioni 15 umesainiwa tarehe 08/04/2015. 107. Mheshimiwa Spika, kazi zitazotekelezwa katika Awamu ya Pili ya mradi ni ujenzi wa mtambo wa kusukuma maji na ulazaji wa bomba kuu kutoka eneo la Kisangara hadi tanki la Kiverenge; ujenzi wa matanki mawili yenye ujazo wa lita milioni 7.5 kila moja eneo la Kiverenge na kulaza mabomba ya kupeleka maji kutoka Kiverenge hadi miji ya Mwanga na Same; ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita milioni 6 katika Mji wa Mwanga na tanki lenye ujazo wa lita milioni 9 katika Mji wa Same; pamoja na kulaza mabomba ya kusambaza maji katika Miji ya Same na Mwanga. Aidha, Serikali inaendelea na taratibu za kumwajiri Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa Awamu ya pili ya Mradi. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza mwezi Septemba, 2015 baada ya kumpata Mkandarasi. Mradi utakapokamilika utahudumia jumla wakazi 456,931 wa Miji ya Same na Mwanga. Awamu ya tatu ya utekelezaji wa mradi huo itahusisha jumla ya vijiji 38 vya Wilaya za Same vijiji 16, Mwanga (17) na Korogwe (5). Mradi wa Maji Masoko - Rungwe 108. Mheshimiwa Spika, mradi wa Masoko ulianza kutekelezwa mwezi Septemba, 2010 na kutegemewa kukamilika mwezi Novemba, 2011 kulingana na mkataba. Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ilisitisha mkataba na Mkandarasi kwa kushindwa kutekeleza kazi kulingana na viwango vya usanifu. Hata hivyo, Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe inaendelea na taratibu za usuluhishi na kutafuta Mkandarasi wa kukamilisha mradi huo. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu imetenga jumla ya shilingi bilioni

Page 55: Tekeleza kwa

53

1.76 kwa ajili ya kumalizia kazi zilizobaki ili kuharakisha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa Masoko. Mradi wa Maji Mkoani Kigoma 109. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ubelgiji inatekeleza miradi ya maji katika vijiji vya Halmashauri za Mkoa wa Kigoma (Water and Sanitation Kigoma Region Projects - WaSKiP). Miradi hiyo itagharimu shilingi bilioni 20.6, kati ya fedha hizo shilingi bilioni 18.13 sawa na Euro milioni 8 zitatolewa na Serikali ya Ubelgiji na shilingi bilioni 2.44 zitatolewa na Serikali ya Tanzania. Hadi mwezi Aprili 2015, mpango wa utekelezaji wa miradi hiyo umeanza kwa kubainisha jumla ya vijiji 26 vya kipaumbele katika Halmashauri zote za Mkoa wa Kigoma. Mpango huo umeonesha kuwa jumla ya wakazi 200,000 watanufaika na huduma ya maji. Mradi huo unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano, kuanzia mwaka 2014/2015. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 1.04 sawa na Euro 650,000 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa mradi huo. Jedwali Na. 8 linaonesha orodha ya vijiji 26 vya kipaumbele katika Halmashauri zote mkoani Kigoma. (ii) Miradi yenye Kuleta Matokeo ya Haraka

(quickwins) Mradi wa Maji kwa Vijiji 100 Vinavyopitiwa na Bomba Kuu kutoka Ziwa Victoria hadi Kahama-Shinyanga 110. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa maji wa vijiji 100 vilivyopo pembezoni mwa bomba kuu la maji kutoka Ziwa Victoria hadi Miji ya Kahama na Shinyanga. Mradi huo unahusu uboreshaji wa huduma ya upatikanaji wa maji kwenye vijiji 40 vya awali

Page 56: Tekeleza kwa

54

vilivyotambuliwa katika Halmashauri za Misungwi, Kwimba, Shinyanga na Msalala. 111. Mheshimiwa Spika, mradi huo umeanza kutekelezwa na hadi mwezi Aprili 2015, upimaji na usanifu ulikamilika katika vijiji 31 kati ya vijiji 40 kwenye Halmashauri za Msalala na Shinyanga. Vijiji tisa vinavyobaki vitatekelezwa katika mwaka 2015/2016. Gharama ya ujenzi wa mradi kwenye vijiji hivyo 31 ni shilingi bilioni 2.59 na utekelezaji wake upo katika hatua mbalimbali kama ifuatavyo: Ujenzi wa vituo 16 vya kuchotea maji na mabirika manne ya kunyweshea mifugo katika vijiji vinne vya Magobeko, Nyashimbi, Kakulu na Butegwa kwenye Halmashauri ya Msalala umekamilika; ujenzi wa vituo tisa vya kuchotea maji na mabirika mawili ya kunyweshea mifugo katika vijiji vingine sita vilivyopo Halmashauri ya Shinyanga utakamilika ifikapo mwezi Juni, 2015; na ujenzi wa vituo nane vya kuchotea maji na mabirika mawili ya kunyweshea mifugo katika vijiji viwili vya Mwasekagi na Mwakatolya katika Halmashauri ya Shinyanga umeanza na utakamilika mwezi Oktoba, 2015. Mradi wa Maji wa Ntomoko 112. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea kutekeleza mradi wa maji wa Ntomoko uliolenga kuhudumia vijiji 18 katika Halmashauri za Kondoa na Chemba. Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wakazi katika vijiji vinavyokusudiwa kuhudumiwa na mradi huo ikilinganishwa na uwezo wa chanzo kilichopo, iliamuliwa kuwa vijiji vitakavyohudumiwa viwe 10 ambapo ukarabati wa mtandao wa mabomba ya usambazaji maji kwa sasa umefikia asilimia 40. Vijiji hivyo ni Makirinya, Kirere cha Ng’ombe, Lusangi, Hamai, Songolo, Madaha, Churuku, Kimkima, Jinjo na Jangalo. Kwa vijiji vinane vilivyobaki iliamuliwa vichimbwe

Page 57: Tekeleza kwa

55

visima na utekelezaji wake upo katika hatua mbalimbali. Hadi mwezi Aprili 2015, ujenzi wa miundombinu katika vijiji vya Jenjeluse na Goima umefikia asilimia 98; Kijiji cha Mtakuja asilimia 95 na Kijiji cha Mlongia asilimia 80. Uchimbaji wa visima katika vijiji vya Mapango na Chandama umekamilika na vimepata maji, utafiti wa kina unaendelea katika vijiji vya Igunga na Itolwa ili kupata maeneo bora ya kuchimba visima. Katika mwaka 2015/2016, Wizara imetenga jumla ya shilingi bilioni 1.6 kwa ajili ya kumalizia kazi zilizobaki ili huduma ya maji ipatikane kwa wananchi wa vijiji hivyo. Mradi wa Maji Chiwambo - Masasi 113. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa maji Chiwambo unaendelea na hadi mwezi Aprili, 2015 ulazaji wa mabomba kwa umbali wa kilomita 24.8 umekamilika; ujenzi wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 50,000 kila moja katika vijiji vya Nagaga–Mitesa na Chiungutwa unaendelea, ukarabati wa matanki manne yenye ujazo wa lita 25,000 kila moja umekamilika kwenye vijiji vya Luatala, Nagaga, Mpeta na Namalenga; ukarabati wa tanki moja lenye ujazo wa lita 75,000 na kichoteo (sump) katika Kijiji cha Mitesa umefikia asilimia 70. Vilevile, kazi nyingine zinazoendelea ni pamoja na kukarabati nyumba ya mtambo wa kusukuma maji (pump house) ambayo utekelezaji wake umefikia asilimia 50 na ujenzi wa vituo 36 vya kuchotea maji umefikia asilimia 90. Katika mwaka 2015/2016, Wizara itakamilisha kazi zilizobaki ili kuweza kuwapatia huduma ya maji wakazi wapatao 84,082 wa Kata saba za Lulindi, Lupumbulu, Namalenga, Chiungutwa, Sindano, Mchauru na Mbuyuni.

Page 58: Tekeleza kwa

56

(iii) Usambazaji wa Maji kutoka Visima Virefu na Vyanzo vya Maji Juu ya Ardhi

114. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili, 2015 jumla ya shilingi bilioni 2.28 zilitumika kwa ajili ya kuendelea kutekeleza miradi ya kuleta matokeo ya haraka. Miradi hiyo ilihusisha ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji kutoka kwenye visima virefu na vyanzo vingine juu ya ardhi. Katika mwaka 2015/2016, jumla ya shilingi bilioni 93.58 zitatumika kutekeleza miradi ya kuleta matokeo ya haraka. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 75.4 zitatumika kwa ajili ya kuendeleza miradi ya maji ya visima virefu na vyanzo vingine vya maji juu ya ardhi. Vilevile, shilingi bilioni 18.18 zitatumika kutekeleza miradi ya usambazaji maji kutoka kwenye mabwawa. Jumla ya vituo 9,123 vya kuchotea maji vitajengwa katika vijiji 376 ambapo wananchi 2,280,893 watanufaika na huduma ya maji safi. (iv) Upanuzi na Ukarabati wa Miradi ya Kitaifa 115. Mheshimiwa Spika, upanuzi na ukarabati wa miradi ya kitaifa iliyoainishwa katika Mpango wa BRN, unahusu miradi mitatu ya kitaifa ya Makonde, Wanging’ombe na Handeni Trunk Main (HTM). Upanuzi na Ukarabati wa Mradi wa Kitaifa Makonde 116. Mheshimiwa Spika, kazi zinazotekelezwa zinahusu upanuzi na ukarabati wa miundombinu ya maji kutoka Mradi wa Kitaifa wa Makonde hadi kwenye vijiji vilivyomo pembezoni mwa mradi. Upembuzi yakinifu wa miundombinu chakavu umekamilika kwenye vijiji vilivyopo katika Halmashauri za Wilaya za Newala, Tandahimba na Mtwara Vijijini. Upembuzi huo ulibainisha kazi zote zinazotakiwa kufanyika ili kuboresha huduma ya maji katika eneo la mradi.

Page 59: Tekeleza kwa

57

Kazi hizo ni ununuzi na ufungaji wa vifaa vya mfumo wa umeme, viungio vya mabomba ya maji pamoja na vipuri vya mitambo ya kusukuma maji. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga shilingi milioni 800 kwa ajili ya kutekeleza kazi hizo. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Uingereza kupitia Idara yake ya Maendeleo ya Kimataifa (DFID) imekamilisha upembuzi yakinifu wa kubaini gharama za kutekeleza mradi wa kutoa maji kutoka katika chanzo cha Mkunya kwenda katika Vijiji vya Chihanga, Mapili, Chikwedu, Chiunjira na Mpilipili vyenye wakazi wapatao 7,659 watakaonufaika na mradi huo. Ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2015/2016. Upanuzi wa Mradi wa Kitaifa Wanging’ombe 117. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa kazi katika mradi huo utahusisha kusambaza maji kwenye vijiji vilivyopo pembezoni mwa bomba kuu kutoka vyanzo vya maji vya Mbukwa na Mtitafu hadi Wilayani Mbarali, Mkoa wa Mbeya. Upanuzi wa mradi huo wa kitaifa utafanyika baada ya kukamilika kwa ukarabati wa bomba kuu. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga shilingi milioni 300 kwa ajili ya upanuzi wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji kwenda katika vijiji hivyo. Upanuzi na Ukarabati wa Mradi wa Kitaifa Handeni (Handeni Trunk Main - HTM) 118. Mheshimiwa Spika, upanuzi na ukarabati wa mradi huo unaendelea kwenye vijiji mbalimbali katika Halmashauri za Wilaya za Handeni, Korogwe na Kilindi. Hadi mwezi Aprili 2015, kazi zilizofanyika ni pamoja na ukarabati wa mabomba na valvu kutoka banio la Mandera hadi mtambo wa kutibu maji wa Tabora; kutoka mtambo wa kutibu maji wa Tabora hadi kituo cha kusukuma maji cha Kwamatuku; kutoka

Page 60: Tekeleza kwa

58

Kwamatuku hadi kwenye tanki la maji la Bongi; kutoka tanki la Bongi hadi Kwamkono; na njiapanda ya bomba kuu hadi tanki la maji la Komsala. Kukamilika kwa kazi hizo kumewanufaisha wakazi 50,000 kupata huduma ya maji katika Vijiji vya Vibaoni, Kwamasaka, Kwamgondi, Bangala, Kiva, Kibindu, Magamba, Bogolwa, Kwankonje na Kwachaga. 119. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya kumalizia kazi zilizobaki. Kazi hizo ni pamoja na kuchimba mtaro wa kulaza bomba; kubadilisha mabomba na valvu maeneo ya tanki la Komsala hadi Michungwani; kubadilisha mabomba na valvu kutoka tanki la Bongi kwenda kwenye nyumba ya mitambo ya Sindeni; na kununua mabomba, viungio, dira za maji na vifaa vingine vya matengenezo. 3.2.5 Ujenzi wa Miradi Mingine ya Maji Vijijini 120. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuboresha hali ya upatikanaji wa maji vijijini, hususan katika maeneo kame, Serikali imeendelea kushirikiana na taasisi, mashirika na asasi mbalimbali katika kujenga miradi ya maji, ikiwemo ukarabati wa mabwawa yaliyopo, ujenzi wa mabwawa mapya na uvunaji wa maji ya mvua. (a) Ukarabati na Ujenzi wa Mabwawa 121. Mheshimiwa Spika, uwepo wa mabwawa ya maji ni ufumbuzi wa kero ya uhaba wa maji, hasa katika maeneo kame na kwenye vyanzo vyenye uwezo mdogo wa kutoa maji. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali imeendelea kukarabati mabwawa yaliyopo na kukamilisha ujenzi wa mabwawa katika maeneo mbalimbali nchini

Page 61: Tekeleza kwa

59

yakiwemo bwawa la Sasajila lililopo katika Wilaya ya Chamwino, Mkoani Dodoma; bwawa la Iguluba (Iringa Vijijini); bwawa la Habiya (Itilima - Simiyu); bwawa la Sekeididi (Kishapu – Shinyanga); bwawa la Matwiga (Chunya – Mbeya); bwawa la Kawa (Nkasi – Rukwa); bwawa la Wegero (Butiama – Mara); bwawa la Mwanjoro (Meatu – Simiyu); na bwawa la Kidete (Kilosa – Morogoro). Utekelezaji wa kazi hizo umefikia hatua mbalimbali na katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 8 ili kukamilisha kazi hizo. 122. Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada nilizozieleza hapo juu, Serikali imepanga kujenga mabwawa mengine kwenye maeneo kame hasa vijijini ili kupunguza kero ya uhaba wa maji unaoendelea kuwakabili wananchi wa maeneo hayo. Katika mwaka 2015/2016, Serikali itaanza kutekeleza miradi hiyo kwa kufanya upembuzi yakinifu kwenye maeneo kame na kubaini maeneo yanayofaa kujenga mabwawa hayo. (b) Uvunaji wa Maji ya Mvua 123. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa utekelezaji wa miradi ya uvunaji wa maji ya mvua kupitia mapaa ya majengo, Wizara yangu imetoa miongozo kwa kila Halmashauri kutunga Sheria ndogo zenye kuzitaka Taasisi, Asasi na watu binafsi kujenga miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua kwenye majengo yao. Vilevile, Sheria hizo zinalenga kuhakikisha kuwa michoro ya majengo yote yanayojengwa inajumuisha mifumo ya kuvuna maji ya mvua kabla ya ujenzi wa majengo hayo kuidhinishwa. Katika kutekeleza agizo hilo, Halmashauri 28 zimetunga Sheria ndogo kuhusu uvunaji wa maji ya mvua kutoka kwenye mapaa na Halmashauri zilizobaki zinaendelea na mchakato

Page 62: Tekeleza kwa

60

wa kutekeleza agizo hilo. Hadi mwezi Aprili 2015, matanki 800 ya lita 1,000 hadi 5,000 yamejengwa kwenye maeneo mbalimbali kama shule, zahanati na taasisi nyingine katika Halmashauri zote nchini. 3.2.6 Uendeshaji na Matengenezo (a) Takwimu za Vituo vya Kuchotea Maji

(Water Point Mapping System) 124. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea kutekeleza kazi ya kuainisha vituo vya kuchotea maji katika maeneo ya vijijini kwa kutumia mfumo wa kompyuta uitwao Water Point Mapping System-WPMS. Kuainishwa kwa vituo hivyo, kumewezesha kufahamu kwa urahisi na usahihi takwimu za uendeshaji wa miundombinu ya maji na kuandaa ramani za vituo vya maji. Takwimu zinazopatikana huwezesha Halmashauri kufahamu hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika vijiji. Aidha, takwimu hizo zinapatikana kwenye tovuti ya Wizara ya Maji www.maji.go.tz na kuangalia WPMS. 125. Mheshimiwa Spika, zoezi hilo ni endelevu na limesaidia kupata takwimu sahihi na zilizoboreshwa kwa baadhi ya maeneo nchini. Hivyo, kupata taarifa sahihi za vituo vinavyotoa maji na visivyotoa maji kwa wakati husika. Kwa kuzingatia umuhimu wa upatikanaji wa takwimu sahihi, mwezi Machi 2015, Wizara yangu iliendesha zoezi la kuboresha taarifa hizo kwa kushirikiana na Wahandisi wa Halmashauri katika Halmashauri 67 kutoka Mikoa 10 ya Mwanza, Geita, Simiyu, Tabora, Singida, Kagera, Shinyanga, Dodoma, Kigoma na Mara. Matokeo yalibaini idadi ya vituo vipya 6,228 vya kuchotea maji na kufanya jumla ya vituo vilivyopo kwenye mikoa hiyo kufikia 33,082

Page 63: Tekeleza kwa

61

kwa sasa. Katika mwaka 2015/2016, Wizara itaendelea kuboresha takwimu za vituo vya kuchotea maji katika Halmashauri zilizobaki. 126. Mheshimiwa Spika, mkutano mkuu wa kikanda Barani Afrika kuhusu matumizi ya mfumo wa Water Point Mapping (WPMS) ulifanyika mwezi Februari, 2014 katika Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach, jijini Dar es Salaam. Washiriki wa Mkutano huo walikuwa ni Wataalam wa Sekta ya Maji pamoja na Wadau kutoka ndani na nje ya nchi. Lengo la mkutano huo lilikuwa ni kujadili changamoto zinazoukabili mfumo huo katika ukusanyaji wa takwimu na utoaji wa taarifa kwa wakati kuhusu upatikanaji wa huduma ya maji vijijini. Katika kufikia lengo hilo, Mkutano ulitoa maazimio ya utekelezaji yanayojumuisha hatua nne zifuatazo:-

(i) Kutoa mafunzo stahiki kwa wakusanyaji wa takwimu

katika ngazi za Wilaya na kukusanya takwimu za vituo vya kuchotea maji katika maeneo ambayo yalikuwa hayafikiwi ili kuhuisha taarifa kwenye mfumo;

(ii) Kurasimisha matumizi ya mfumo wa WPMS ili kuhakikisha taasisi za watendaji katika Sekta ya Maji zinawasilisha taarifa katika kila kipindi cha robo mwaka kama ilivyo katika mifumo mingine;

(iii) Kutoa taarifa ya hali halisi ya vituo vya kuchotea maji ikiwa ni pamoja na ubora wa maji na upatikanaji wake; na

(iv) Kuoanisha mfumo huo na mifumo mingine ya kielektroniki kama PLANREP, EPICOR, MIS ili taarifa

Page 64: Tekeleza kwa

62

hizo ziwe zinapatikana kwa haraka na kwa gharama nafuu.

(b) Vyombo vya Watumiaji Maji 127. Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka sheria, kanuni na taratibu zitakazohakikisha kuwa miradi ya maji iliyokamilika inakuwa endelevu kwa kuunda Vyombo vya Watumiaji Maji (COWSOs) kwa ajili ya kusimamia miradi hiyo. Kulingana na Kifungu Na. 31 cha Sheria Na. 12 ya mwaka 2009 ya Huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira, Halmashauri zinaelekezwa kusajili COWSOs kwa mujibu wa sheria ili uendeshaji na usimamizi wa miradi hiyo kuwa endelevu. Wizara yangu, imetoa miongozo ya usajili ikiwemo uteuzi wa Wasajili katika Halmashauri na namna vyombo vitakavyoendeshwa; kuongeza idadi ya wataalam kwenye miradi; na kutoa mafunzo kwa wasimamizi wa skimu za miradi. Vilevile, Wizara imeandaa Mkakati wa Uendelevu wa Miradi ya Maji Vijijini (National Rural Water Supply Sustainability Strategy) ambao utekelezaji wake utaanza katika mwaka wa fedha 2015/2016. 128. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili, 2015, idadi ya vyombo vya watumiaji maji vilivyosajiliwa kisheria imefikia 909 kutoka vyombo 373 mwezi Juni, 2014. Katika mwaka 2015/2016, Serikali itaendelea kutoa mafunzo kwa viongozi wa vyombo hivyo, kuhimiza uundwaji zaidi wa vyombo vya watumiaji maji na kusisitiza wasajili kuongeza kasi ya usajili kwa miradi iliyopo na mingine itakayojengwa. Vilevile, Halmashauri zinatakiwa ziandae mipango kazi ya kutoa elimu kwa wananchi. Elimu hiyo inahusu usajili wa vyombo hivyo na uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa mipango hiyo kila robo mwaka.

Page 65: Tekeleza kwa

63

3.3 HUDUMA YA MAJI MIJINI 129. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea kutekeleza Programu ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini kwa kujenga, kupanua na kukarabati mifumo ya majisafi na uondoaji majitaka pamoja na kuzijengea uwezo Mamlaka zote za maji za Miji Mikuu ya Mikoa na Jiji la Dar es Salaam; Miji Mikuu ya Wilaya; Miji Midogo na Miradi ya Kitaifa. Lengo ni kuwapatia wananchi wengi zaidi huduma ya maji safi na salama pamoja na huduma ya usafi wa mazingira katika maeneo yao. Vilevile, katika kutekeleza Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kupitia mfumo wa “Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa" (BRN), nimesaini mikataba ya matarajio ya kazi na viashiria vya utendaji (Key Performance Indicators – KPIs) na kila Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Mamlaka za Majisafi za Miji Mikuu ya Mikoa yote likiwemo Jiji la Dar es Salaam na Miradi ya Kitaifa ili kupima ufanisi wa utoaji wa huduma katika maeneo yao. 3.3.1 Kuboresha Huduma za Maji Mijini (a) Miradi ya Maji katika Miji Saba

130. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali iliendelea kutekeleza miradi ya kukidhi mahitaji ya huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika miji saba ya Bukoba, Musoma, Lindi, Kigoma, Sumbawanga, Mtwara na Babati. Utekelezaji huo unashirikisha Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Serikali ya Ujerumani kupitia Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) na Umoja wa Ulaya.

Page 66: Tekeleza kwa

64

(i) Manispaa za Musoma na Bukoba 131. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa miradi ya majisafi kwa Manispaa za Musoma na Bukoba, unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD). Utekelezaji huo unahusu ujenzi wa mitambo ya kusafisha na kusukuma maji pamoja na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji katika miji hiyo. 132. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili, 2015 utekelezaji wa mradi wa Bukoba unaogharimu shilingi bilioni 27.54 umefikia asilimia 85. Aidha, kwa upande wa Manispaa ya Musoma, mradi huo unagharimu shilingi bilioni 40.62 na utekelezaji wake umefikia asilimia 80. Mnamo tarehe 22/03/2015, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliweka jiwe la msingi kwenye Mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Musoma. Miradi hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2015.

(ii) Manispaa za Lindi, Kigoma na Sumbawanga 133. Mheshimiwa Spika, kwa Manispaa za Lindi, Kigoma na Sumbawanga, ujenzi wa miradi ya maji na usafi wa mazingira inatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya. Ujenzi wa miradi hiyo unagharimu kiasi cha Euro milioni 62.59 na unahusu uchimbaji wa visima; ujenzi wa mabanio, chujio, matanki na vituo vya kuchotea maji; ulazaji wa bomba kuu na mabomba ya usambazaji maji.

Page 67: Tekeleza kwa

65

Manispaa ya Lindi 134. Mheshimiwa Spika, Serikali katika kuboresha huduma za maji Lindi Mjini ilitekeleza kazi za muda wa kati kwa kukarabati na kupanua miundombinu ya maji ya katika Manispaa hiyo kwa gharama ya shilingi bilioni 4.7. Kazi zilizotekelezwa na kukamilika ni pamoja na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji ya umbali wa kilomita 47; ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 680,000; uunganishaji wa umeme kwenye vyanzo vya visima virefu vya Kitunda umbali wa kilomita 25; kufunga booster pumps mbili katika kituo cha kusukuma maji cha Kawawa Road; na ufungaji wa dira za maji 2,030. Mradi huo ulizinduliwa na Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Maji Kitaifa tarehe 23/3/2013. Kukamilika kwa mradi huo kumeongeza uzalishaji wa maji kutoka lita 1,163,000 hadi lita 2,400,000 kwa siku. 135. Mheshimiwa Spika, katika mipango ya muda mrefu, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya inatekeleza mradi wa ujenzi wa miundombinu ya majisafi katika Manispaa ya Lindi kwa gharama ya Euro Milioni 11.91. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na uchimbaji wa visima virefu 10; ujenzi wa chujio la maji; ujenzi wa matanki mawili ya maji ya ujazo wa lita milioni 3 na milioni 2; ulazaji wa bomba kuu la maji umbali wa kilomita 11.5; mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 27; ujenzi wa vituo 85 vya kuchotea maji; ujenzi wa mabwawa mawili ya kutibu majitaka; na ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka. Hadi mwezi Aprili 2015, uchimbaji wa visima umekamilika na utekelezaji wa mradi kwa ujumla umefikia asilimia 48. Mradi huo utakamilika mwezi Novemba, 2015

Page 68: Tekeleza kwa

66

na utaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 2.4 kwa siku hadi lita milioni 7.1 kwa siku. Manispaa ya Kigoma 136. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya inatekeleza mradi wa ujenzi wa miundombinu ya majisafi katika Manispaa ya Kigoma kwa gharama ya Euro Milioni 15.16. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa kichoteo cha maji; ujenzi wa kituo cha kusukumia maji; ujenzi wa matanki sita ya maji ya ujazo wa lita milioni 2 kila moja na tanki moja la ujazo wa lita 500,000; ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 16.9 na mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 122.8; ujenzi wa vituo 200 vya kuchotea maji; ujenzi wa mabwawa mawili ya kutibu majitaka; na ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka. Hadi mwezi Aprili 2015, utekelezaji wa kazi hizo umefikia asilimia 31. Mradi huo utakamilika mwezi Novemba, 2015 na utaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 12 kwa siku hadi lita milioni 26 kwa siku na kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji hadi mwaka 2020. Manispaa ya Sumbawanga 137. Mheshimiwa Spika, Serikali ilitekeleza mradi wa upanuzi wa miundombinu ya maji katika Manispaa ya Sumbawanga (immediate works) kwa gharama ya shilingi bilioni 5.31. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ukarabati wa mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 46; uchimbaji wa visima virefu vinane vyenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 4 kwa siku; ulazaji wa bomba kuu la umbali wa kilomita 9; kununua na kufunga pampu nne na kuunganisha umeme kwenye chanzo pamoja na ujenzi wa

Page 69: Tekeleza kwa

67

collector tank la ujazo wa lita 500,000. Kazi hizo zilikamilika na kuongeza upatikanaji maji kutoka asilimia 62 hadi asilimia 70 ya wakazi wa Manispaa ya Sumbawanga. 138. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya, kwa sasa inatekeleza mradi wa ujenzi wa miundombinu ya majisafi katika Manispaa ya Sumbawanga kwa gharama ya Euro Milioni 14.99. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na kuchimba visima virefu 17 na kufunga pampu; kulaza bomba kuu umbali wa kilomita 16; ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 68; kujenga booster station mbili; ujenzi wa mtambo wa kusafisha na kutibu maji; ujenzi wa matanki sita ya maji yenye ujazo wa jumla ya lita milioni 7; upanuzi wa mtambo wa kusafisha maji kwa kujenga chujio; ujenzi wa vituo 56 vya kuchotea maji; kujenga mabwawa mawili ya kutibu majitaka na kununua magari matatu ya uondoshaji wa majitaka. Utekelezaji wa kazi hizo upo kwenye hatua mbalimbali na kwa ujumla utekelezaji umefikia asilimia 43. Mradi ukikamilika, utaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 5.4 kwa siku kwa sasa hadi lita milioni 19 kwa siku.

(iii) Manispaa za Mtwara na Babati 139. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa mradi wa majisafi na usafi wa mazingira katika Miji ya Mtwara na Babati unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani chini ya Programu ya Millennium Development Goals Initiative (MDGI-EU). Jumla ya Euro milioni 8.72 zilitengwa na Serikali ya Ujerumani kupitia KfW kwa ajili ya utekelezaji wa mradi katika miji hiyo. Wizara yangu iliajiri Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kupitia taarifa ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali pamoja na kuainisha kazi

Page 70: Tekeleza kwa

68

zitakazotekelezwa kulingana na kiasi hicho cha fedha. Kwa sasa Mtaalam huyo anakamilisha mapitio ya usanifu na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni. Kazi hiyo itakamilika mwezi Juni, 2015 na ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2015. (b) Miradi ya Maji ya Kukidhi Mahitaji ya Muda Mrefu (i) Mradi wa Maji Tabora 140. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Uswisi kupitia Shirika lake la Maendeleo (SECO) imekamilisha mradi wa ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya maji katika Manispaa ya Tabora. Mradi huo uligharimu Dola za Marekani milioni 4.84 na kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ukarabati wa mtandao wa maji mjini Tabora kwa kilomita 27; ulazaji wa bomba kuu lenye urefu wa kilomita 2.7; ununuzi wa pampu mbili za kusukuma maji pamoja na transfoma mbili; ujenzi wa matanki matatu yenye ujazo wa lita 750,000 kila moja; ununuzi wa dira za maji 5,000; upanuzi wa chanzo; na kujenga kituo cha kutibu maji (post chlorination). Kukamilika kwa mradi huo kumeongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 9.6 hadi lita milioni 15 na kuwanufaisha wakazi 171,526 wa Manispaa ya Tabora. 141. Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji inaendelea kutekeleza mradi wa ukarabati na upanuzi wa chujio la maji katika kituo cha Igombe Mjini Tabora, unaogharimu Dola za Marekani milioni 4.74. Mradi huo unalenga kuzalisha lita milioni 30 kwa siku na utakapokamilika utawapatia huduma ya maji ya kutosheleza mahitaji ya wakazi wa Manispaa ya Tabora hadi kufikia mwaka 2032. Uzalishaji kwa sasa ni lita milioni 15 na

Page 71: Tekeleza kwa

69

mahitaji halisi ya sasa ni lita milioni 24.5 kwa siku. Kazi zinazoendelea kutekelezwa ni pamoja na kufunga pampu kubwa tatu; na kulaza bomba lenye urefu wa mita 240 na kipenyo cha milimita 400 kutoka bwawani hadi kwenye machujio. Hadi mwezi Aprili 2015, ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 40 na utakamilika mwezi Agosti, 2015. (ii) Mradi wa Maji Mjini Dodoma 142. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na uondoaji wa majitaka katika Chuo Kikuu cha Dodoma unaogharimu shilingi bilioni 27.7. Kazi zinazoendelea kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa matanki makubwa matatu yenye jumla ya lita milioni 12 ya kuhifadhi maji katika maeneo ya Chimwaga lita milioni 4.5, Luangu (lita milioni 4.5) na Informatics (lita milioni 3); na kulaza mabomba makubwa yenye urefu wa kilomita 12.2 na mabomba ya kusambaza maji urefu wa kilomita 9.6. Vilevile, ujenzi utaendelea katika kituo cha kusukuma maji eneo la Makulu na uunganishaji wa umeme; kujenga mtandao wa majitaka wenye urefu wa kilomita 18.05 kwa bomba kuu na kilomita 8 za mabomba ya kukusanya majitaka; pamoja na ujenzi wa mabwawa ya kutibu majitaka katika eneo la wastani wa hekta 108. 143. Mheshimiwa Spika, mradi huo uliwekwa jiwe la msingi tarehe 22/03/2014 na Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Maji. Hadi mwezi Aprili 2015, utekelezaji wa kazi hizo umefikia asilimia 94 na mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2015. Mradi huo utakapokamilika, jumla ya wakazi 100,000 kwenye maeneo ya mradi watapata huduma bora ya

Page 72: Tekeleza kwa

70

majisafi na uondoaji wa majitaka na hivyo, kuondoa kero ya upatikanaji wa huduma hizo. 144. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Korea Kusini inatekeleza mradi wa uboreshaji wa huduma ya majisafi katika Mji wa Dodoma kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 49.62. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na uchimbaji wa visima vitatu na ukarabati wa visima 21 katika eneo la Mzakwe. Kazi hizo zitakapokamilika uwezo wa kuzalisha na kusafirisha maji utaongezeka kutoka lita milioni 32 kwa siku za sasa hadi kufikia lita milioni 61.5 kwa siku. Hadi mwezi Aprili 2015, jumla ya visima 17 vimekarabatiwa na uchimbaji wa visima viwili umekamilika. 145. Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zinazotekelezwa ni ujenzi wa mtandao wenye urefu wa kilomita 6.5; ujenzi wa barabara ya urefu wa kilomita 5 kwenda kwenye visima; ulazaji wa bomba kuu lenye urefu wa kilomita 31.2 kutoka Mzakwe hadi Mjini Dodoma ambapo jumla ya kilomita 22.2 zimekamilika; ujenzi wa tanki eneo la Imagi lenye uwezo wa lita milioni 7 na eneo la Itega lenye uwezo wa lita milioni 5.5; ukarabati wa mitambo ya kusukuma maji; ujenzi wa booster station eneo la Mailimbili; ununuzi wa mitambo/vifaa vya kisasa vya kutibu maji; na kujenga maabara ya kisasa ya kupima ubora wa majisafi na majitaka. Utekelezaji wa mradi kwa ujumla umefikia asilimia 95 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2015. Kukamilika kwa mradi huo kutaongeza kiwango cha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa Mjini Dodoma kutoka asilimia 87 hadi asilimia 95. Mradi huo uliwekewa jiwe la msingi na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 01/09/2014 katika eneo la tanki la Itega.

Page 73: Tekeleza kwa

71

(iii) Mradi wa Maji Jijini Arusha 146. Mheshimiwa Spika, mradi wa maji wa Moshono Jijini Arusha, umelenga kuboresha huduma ya maji kwa wakazi wa Kata za Moshono na Engutoto ambao idadi yao ni 28,124. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni uchimbaji wa kisima kirefu ambacho ujenzi wake umekamilika. Kazi nyingine ni uboreshaji wa chanzo cha maji ya chemichemi ya Machare; ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita milioni 2.5; kulaza bomba kuu la kupeleka maji kutoka kwenye kisima hadi kwenye tanki; na kulaza mabomba ya kusambaza maji kwenye mitaa yote ya Kata ya Moshono. Kazi hizo hazikufanyika kutokana na wananchi wanaolima ndani ya eneo la chanzo cha maji Machare kugoma kupisha uboreshaji wa chanzo na ujenzi wa tanki kwenye eneo la Kilima lenye upana wa mita 35 na urefu mita 35. Katika kutafuta ufumbuzi wa suala hilo, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha inaendelea kujadili suala hilo na viongozi wa ngazi ya Kata hadi Mkoa pamoja na kutumia Sheria zilizopo ili kuweza kutatua tatizo hilo na mradi uweze kutekelezwa. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 2.78 ili kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Arusha. 147. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na AfDB imepanga kuboresha huduma ya upatikanaji wa majisafi na usafi wa mazingira katika Jiji la Arusha. Mradi huo utagharimu Dola za Marekani milioni 218. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji ya Mto Malala; Uchimbaji wa visima virefu vipatavyo 18; ujenzi wa mtambo wa kutibu maji; ulazaji wa bomba za kusambaza maji umbali wa kilomita 200; ujenzi wa matanki 17 ya kuhifadhia maji ya ujazo tofauti; ukarabati na upanuzi wa mfumo wa majitaka; ujenzi wa mabwawa 14 mapya ya

Page 74: Tekeleza kwa

72

kutibu majitaka; ujenzi wa maabara ya maji; na kujenga uwezo wa taasisi na watumishi. Mradi huo unatarajiwa kuanza kutekelezwa katika mwaka 2015/2016 na kukamilika mwaka 2020. Kukamilika kwa mradi huo kutaboresha huduma ya maji katika Jiji la Arusha kwa kuongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 46.87 kwa siku hadi lita milioni 86.24 kwa siku, sawa na ongezeko la asilimia 86. Aidha, huduma ya uondoaji majitaka itaboreshwa kutoka asilimia 7.6 ya eneo la Jiji kwa sasa hadi asilimia 30. (iv) Mradi wa Maji Mjini Singida 148. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya majisafi katika Mji wa Singida umekamilika na ulikabidhiwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Singida tarehe 31/07/2014. Mradi huo umefadhiliwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kiarabu (BADEA) pamoja na Mfuko wa Maendeleo wa Nchi zinazozalisha Mafuta (OPEC Fund for International Development-OFID) kwa gharama ya shilingi bilioni 32.53. Ujenzi huo ulihusu uchimbaji wa visima saba kati ya hivyo, visima viwili maeneo ya Mwankoko na visima vitano katika maeneo ya Irao; ujenzi wa matanki mawili katika maeneo ya Airport; kulaza bomba kuu la maji hadi kwenye matanki; na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji katika eneo la Mandewa. Hadi mwezi Aprili 2015, kazi za kuunganisha mabomba madogo kwenye bomba kuu katika maeneo ya Unyankindi, Mitunduruni, Itungukia, Minga, Misuna, Kibaoni na Kindai; na uunganishaji wateja 1,000 kwenye mtandao wa maji katika maeneo hayo zimekamilika. Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa chemba na ufungaji wa control valves kwenye mtandao huo na zitakamilika mwezi Juni, 2015.

Page 75: Tekeleza kwa

73

(v) Mradi wa Maji Morogoro Mjini 149. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la MCC la Marekani ilikamilisha mradi wa kupanua na kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi katika Manispaa ya Morogoro kwa gharama ya shilingi bilioni 10. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na kukarabati matanki matatu; ulazaji wa bomba kuu la maji la urefu wa kilomita 1.8; kupanua chujio la maji la Mafiga; na kujenga mtambo wa kusafisha maji wa Mambogo. Mradi huo ulizinduliwa rasmi tarehe 22/08/2014 na Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kukamilika kwa mradi huo kumewezesha kuongezeka kwa wakazi wanaopata huduma ya maji safi na salama kutoka asilimia 75.4 kabla ya mradi hadi asilimia 85 kwa sasa. (vi) Mradi wa Maji Songea Mjini 150. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea na mradi wa kukarabati chanzo cha Mto Ruhila Mjini Songea kwa kujenga banio la maji (weir) ili kukabiliana na upungufu wa maji wakati wa kiangazi. Utekelezaji wa mradi huo unagharimu shilingi bilioni 2.6 na fedha hizo zinatolewa na Serikali. Utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 42 na unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2015 na kuwanufaisha wakazi 164,162 wa Mji wa Songea. (vii) Huduma ya Maji Mjini Mtwara

Kuboresha Upatikanaji wa Maji Mjini Mtwara 151. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani chini ya Programu ya Millennium

Page 76: Tekeleza kwa

74

Development Goals Initiative (MDGI-EU) inatekeleza ujenzi wa mradi wa muda kati (Intermediate works) wa kuboresha huduma ya majisafi kwa Mji wa Mtwara. Hadi mwezi Aprili 2015, Mtaalam Mshauri anaendelea kukamilisha mapitio ya usanifu na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni, kazi ambayo itakamilika mwezi Juni, 2015 na ujenzi wa mradi utaanza mwezi Agosti, 2015. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2016 na kuongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 9 kwa siku za sasa hadi lita milioni 14 kwa siku. Vilevile, upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa Mji wa Mtwara utaongezeka kutoka asilimia 81 kwa sasa hadi asilimia 90. Mradi wa Kutoa Maji Mto Ruvuma Kupeleka Mtwara-Mikindani 152. Mheshimiwa Spika, katika mipango ya muda mrefu ya kuboresha huduma ya maji Mjini Mtwara-Mikindani, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa kutoa maji kutoka Mto Ruvuma kupeleka Mtwara-Mikindani na vijiji 26 pamoja na vitongoji vitakavyopitiwa na bomba kuu ndani ya kilomita 12. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa chanzo kutoka Mto Ruvuma, chujio la kutibu maji, nyumba ya mtambo wa kusukuma maji, matanki 26, tanki kuu la ujazo wa lita milioni 30 ambalo litajengwa eneo la Mangamba, vituo vya kuchotea maji 234; na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 63. Hadi mwezi Aprili 2015, Mtaalam Mshauri amekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali na anaendelea na usanifu wa kina, kuandaa michoro pamoja na makabrasha ya zabuni. Kazi hizo zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2015. Aidha, Serikali kupitia Wizara ya Fedha, tayari imewasilisha maombi kwenda Serikali ya China kupitia China Development Bank kwa ajili ya kupata fedha za kutekeleza ujenzi wa mradi huo.

Page 77: Tekeleza kwa

75

Kukamilika kwa mradi huo kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 9 kwa siku za sasa hadi lita milioni 120 kwa siku. Ongezeko hilo litatosheleza mahitaji ya watu pamoja na kasi ya viwanda vinavyoendelea kujengwa vikiwemo vya saruji na gesi katika Mji wa Mtwara. (c) Mradi wa Maji katika Miji ya Geita, Sengerema na

Nansio 153. Mheshimiwa Spika, mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Ziwa Victoria (LVWATSAN II) unatekelezwa katika Miji ya Geita, Sengerema na Nansio kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 30.4. Mradi huo unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na unasimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza. Kazi zinazotekelezwa zimegawanyika katika vipindi vya muda mfupi na muda mrefu. Kazi za muda mfupi zimekamilika. Kazi hizo ni ununuzi wa vifaa kama magari, pikipiki, trekta, tela, magari makubwa na madogo ya majitaka, vifaa vya kukusanyia taka ngumu; uchimbaji wa visima vipya vitatu; na kusafisha visima vitano vya zamani. 154. Mheshimiwa Spika, kazi za muda mrefu zinazoendelea ni kujenga na kuboresha miundombinu ya majisafi, mifumo ya utoaji wa huduma ya usafi wa mazingira na mitaro ya maji ya mvua. Utekelezaji wa kazi hizo katika Miji ya Sengerema, Nansio na Geita ni kama ifuatavyo:- (i) Mji wa Sengerema 155. Mheshimiwa Spika, kazi ya ujenzi wa miundombinu ya majisafi na mradi wa usafi wa mazingira ilianza mwezi Oktoba, 2014 kwa gharama ya shilingi bilioni 20.06. Kazi zinazotekelezwa ni ujenzi wa chanzo kipya cha Nyamazugo

Page 78: Tekeleza kwa

76

cha kutoa maji kutoka Ziwa Victoria na ujenzi wa matanki matano ya kuhifadhi maji kwenye maeneo ya Ibondo (lita 150,000); Igogo (lita milioni 1.5); Kilabela (lita 100,000); Mwabaluhi (lita 500,000) na Bukala (lita 350,000) na kulaza mabomba yenye umbali wa kilomita 71.3. Mradi utakamilika mwezi Februari, 2016 na utaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 2.34 za sasa kwa siku hadi lita milioni 6.02 na hivyo kuongeza upatikanaji wa huduma ya majisafi kutoka asilimia 33 hadi asilimia 85. Kwa upande wa mradi wa usafi wa mazingira, kazi zinazotekelezwa ni ujenzi wa mabwawa ya kutibu majitaka eneo la Iyogelo; kujenga vyoo kwenye shule tatu za msingi za Ibondo, Ngweli na Mwabaluhi na kujenga dampo la kisasa kwa ajili ya kutupa taka ngumu eneo la Ibondo. (ii) Mji wa Nansio 156. Mheshimiwa Spika, miradi inayotekelezwa ni ya kuimarisha huduma ya majisafi na kuboresha usafi wa mazingira. Miradi hiyo ilianza kutekelezwa mwezi Februari, 2015 kwa gharama ya shilingi bilioni 10.9. Kazi zinazofanyika kwa upande wa uimarishaji wa huduma ya majisafi ni kujenga chanzo kipya cha maji kutoka Ziwa Victoria; kujenga kituo cha kusukuma maji chenye uwezo wa kusuma maji lita 270,000 kwa saa; kujenga kituo cha kutibu maji chenye uwezo wa lita milioni 6.45 kwa siku; kufunga pampu zenye uwezo wa kusukuma maji lita 270,000 kwa saa; kujenga matanki mawili katika maeneo ya Nebuye (lita 350,000) na Malegeya (lita milioni 3) na kulaza bomba za chuma umbali wa kilomita 5.6 na mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilomita 14. Mradi utakamilika mwezi Februari, 2016 na kunufaisha wakazi 60,000 ikilinganishwa na wakazi 30,000 kabla ya mradi. Vilevile, kwa upande wa uboreshaji wa huduma za usafi wa mazingira, kazi

Page 79: Tekeleza kwa

77

zinazotekelezwa ni ujenzi wa mabwawa ya kutibu majitaka eneo la Bukongo yenye uwezo wa lita 50,000, kujenga vyoo viwili kwenye shule za msingi za Nansio na Nakoza na kujenga dampo la kisasa la kutupia taka ngumu eneo la Bukongo. (iii) Mji wa Geita 157. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia programu ya LV-WATSAN inatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji safi na usafi wa mazingira katika Mji wa Geita. Hadi mwezi Aprili 2015, taarifa ya tathmini ya zabuni ya kumpata Mkandarasi imeidhinishwa na AfDB tarehe 09/04/2015. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 6.67. Mkataba wa ujenzi utasainiwa mwishoni mwa mwezi Mei, 2015 na ujenzi utaanza mwezi Julai, 2015. Kazi zitakazotekelezwa kwa upande wa mradi wa kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi ni pamoja na uchimbaji wa visima virefu vitatu; kufunga pampu; kuvuta umeme kwenye kila kisima; kujenga nyumba ya mtambo wa kusukuma maji kwenye kila kisima; kujenga matanki manne ya kuhifadhi maji kwenye maeneo ya Kagera A (lita 500,000); Buhalahala (lita 135,000); Shule ya Msingi Waja (lita 135,000), na Kituo cha Mabasi (lita 45,000); na kulaza bomba kuu umbali wa kilomita 3 na mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 17.5. Aidha, kwa upande wa mradi wa kuboresha huduma za usafi wa mazingira, kazi zitakazotekelezwa ni kujenga mabwawa ya kutibu majitaka eneo la Usindakwe yenye uwezo wa lita 50,000; vyoo viwili kwenye Shule za Msingi za Mbugani na Nyankumbu; na dampo la kisasa la kutupa taka ngumu eneo la Usindakwe.

Page 80: Tekeleza kwa

78

(d) Mradi wa Maji Geita kutoka Ziwa Victoria:- Uwekezaji wa Serikali na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML)

158. Mheshimiwa Spika, Hati ya Makubaliano (Limited Distribution Network Agreement) ya kuanza kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria hadi Mji wa Geita ambao unagharamiwa na Serikali kwa kushirikiana na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (Geita Gold Mining Limited – GGML) ilisainiwa tarehe 31/05/2014. Mchango wa Serikali ni Dola za Marekani 400,000 na GGML ni Dola za Marekani milioni moja. Mradi huo unahusu ujenzi wa mtandao wa majisafi wenye urefu wa kilomita 35; vituo 15 vya kuchotea maji; na magati (water kiosks) matano. Mkandarasi alianza kazi mwezi Desemba, 2014 na hadi mwezi Aprili 2015, mradi huo umefikia asilimia 70 ya utekelezaji. Mradi huo utakamilika mwezi Julai, 2015 na utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji katika mji wa Geita kutoka asilimia 12.5 za sasa hadi asilimia 56. (e) Mradi wa Maji katika Miji ya Muleba, Mutukula na

Kamachumu (i) Mji wa Muleba 159. Mheshimiwa Spika Wizara inatekeleza Awamu ya Pili ya miradi ya usambazaji wa maji kwenye maeneo ya Muleba Mjini ambayo hayapati huduma ya maji safi. Maeneo hayo ni Omundangara, Kamanengo National Housing (maeneo ya Magereza), Bukono na Bujumbi. Katika mwaka 2015/2016, kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na uchimbaji wa kisima kirefu, kufunga pampu na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji yenye urefu wa kilomita 21.5. Kukamilika kwa kazi hiyo kutaongeza uzalishaji wa maji kwa mji wa

Page 81: Tekeleza kwa

79

Muleba kutoka lita 560,000 kwa siku hadi lita milioni 1.7. Kwa sasa mradi unahudumia wakazi 11,563, ambao kati ya hao wakazi 10,063 ni wa Mji wa Muleba na 1,500 ni wa Vijiji vya Bwata, Kamishango, Kabare na Katanga. Mradi utakapokamilika utawanufaisha zaidi ya wakazi 29,000. (ii) Mji wa Mutukula 160. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Bukoba imeendela kusimamia kazi za ukarabati wa miundombinu ya maji katika Mji wa Mutukula ili kuhakikisha mji huo unapata huduma ya maji. Kazi zilizopangwa kutekelezwa katika mwaka huo ni pamoja na:- usafishaji wa visima viwili na kuvifanyia majaribio; ufungaji wa umeme kwenye kisima cha Kasharu; kubadilisha bomba kuu kutoka kwenye kisima hadi tanki lenye uwezo wa lita 900,000; ununuzi wa vifaa vya umeme kwa ajili ya pampu; na kurekebisha mfumo wa usambazaji maji kutoka kwenye tanki hadi kwenye magati. Hadi mwezi Aprili 2015, usafishaji wa visima viwili umekamilika, ufungaji wa umeme unaendelea ambapo nguzo 16 zimejengwa na ufungaji wa nyaya za umeme upo kwenye hatua za mwisho. Mradi huo utakamilika mwezi Juni, 2015. (iii) Mji wa Kamachumu 161. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Muleba inatekeleza miradi ya maji katika Mji wa Kamachumu chini ya mpango wa quickwins. Usanifu wa mradi huo umekamilika na gharama za ujenzi zinakadiriwa kuwa shilingi bilioni 1.5. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa vyanzo viwili vya maji; ulazaji wa bomba la umbali wa kilomita 27; ujenzi wa

Page 82: Tekeleza kwa

80

matanki mawili ya kuhifadhia maji ya ujazo wa lita 135,000 na lita 90,000; na ujenzi wa vituo 31 vya kuchotea maji. Halmashauri inaendelea na taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi na mradi utaanza katika mwaka 2015/2016 na utakapokamilika utawanufaisha wakazi wapatao 23,289. (f) Miradi Mipya katika Eneo la Ziwa Victoria 162. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imeanza utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa huduma ya majisafi katika Jiji la Mwanza na Miji ya Magu, Misungwi na Lamadi pamoja na mradi wa uondoaji wa majitaka katika Miji ya Bukoba na Musoma. Miradi hiyo inatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank-EIB) na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (French Development Agency-AFD) kwa gharama ya Euro milioni 104.5. Mchango wa Serikali ni Euro milioni 14.5, na EIB pamoja na AFD watachangia jumla ya Euro milioni 90. Mtaalam Mshauri ameanza kazi ya upembuzi yakinifu, usanifu na uandaaji wa makabrasha ya zabuni kwa upande wa mradi wa uboreshaji wa huduma ya majisafi na kazi hizo zitakamilika mwezi Aprili, 2016 na ujenzi utaanza mwaka 2016/2017. 163. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea kutekeleza miradi ya majitaka kwa Miji ya Bukoba na Musoma. Katika Mji wa Bukoba utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mabwawa ya kusafisha majitaka kupitia Mradi wa Usimamizi wa Mazingira ya Ziwa Victoria (Lake Victoria Environmental Management Project - LVEMP) umekamilika mwezi Desemba, 2014 kwa gharama ya shilingi bilioni 2.54. Kukamilika kwa mradi huo kumeboresha huduma ya uondoaji majitaka katika Mji wa Bukoba. Kazi zinazotekelezwa katika Mji wa Musoma

Page 83: Tekeleza kwa

81

zinagharamiwa na Serikali kwa kushirikiana na AFD. Kazi hizo ni pamoja na ujenzi wa mabwawa ya kumwaga majitaka (sludge digester) katika eneo la Bweri ambao umefikia asilimia 70 na utakamilika mwezi Julai 2015. Vilevile, taratibu za ununuzi wa magari mawili ya kuondoa majitaka zinaendelea na magari hayo yanatarajiwa kupatikana mwaka 2015/2016. (g) Miradi ya Maji katika Miji ya Ziwa Tanganyika 164. Mheshimiwa Spika, Serikali ikishirikiana na nchi za Zambia, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda zinatekeleza Mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika eneo la Ziwa Tanganyika (LT-WATSAN) unaosimamiwa na Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa (UN-HABITAT). Mradi huo ulifanyiwa upembuzi yakinifu mwaka 2011 katika Miji ya Kigoma, Kasulu, Mpanda, Namanyere, Uvinza na Kasanga. Kazi zinazotarajiwa kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa mitandao ya majisafi na usafi wa mazingira, ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua na uondoaji wa taka ngumu pamoja na kuzijengea uwezo taasisi husika. Hata hivyo, utekelezaji wake haukuanza kutokana na kutopatikana kwa fedha. Serikali inaendelea na jitahada za kutafuta fedha ili kuweza kutekeleza mradi huo na kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika miji hiyo. 165. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa mradi wa maji wa Mji wa Kigoma unaotekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na AfDB kwa gharama ya Euro 170,000 upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki la ujazo wa lita 150,000 ambalo limefikia asilimia 98; ununuzi wa mabomba ya umbali wa kilomita 6; Kazi zilizokamilika ni ununuzi wa mabomba ya

Page 84: Tekeleza kwa

82

umbali wa kilomita 1, dira za maji 692 pamoja na ufungaji wa kifaa cha kudhibiti matumizi ya umeme (power factor correction). 3.3.2 Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji ya Mpanda,

Njombe na Bariadi 166. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji, inaendelea kutekeleza miradi ya huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika miji ya Mpanda, Njombe na Bariadi. Miji hiyo ni makao makuu ya Mikoa mipya ya Katavi, Njombe na Simiyu ambayo hali ya upatikanaji wa huduma na miundombinu ya maji bado ipo chini. Utekelezaji wa miradi ya maji katika miji hiyo ni kama ifuatavyo:- (a) Mji wa Mpanda 167. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilituma shilingi milioni 550 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji katika Mji wa Mpanda ili kukabiliana na uhaba wa maji. Kazi zilizokamilika ni ujenzi wa tanki la maji la Kazima lenye uwezo wa lita milioni moja; nyumba mbili za watumishi na kufunga solar panel nne katika maeneo ya Kazima na Ikolongo; ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilomita 48; kulaza bomba kuu umbali wa kilomita 13.6 kwenye eneo la Ikolongo; kununua na kufunga pampu moja; na kununua dira za maji 4,000. 168. Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa kazi hizo kumeongeza uzalishaji wa maji hadi lita milioni 5 kwa siku ikilinganishwa na lita milioni 3.4 kabla ya kutekeleza mradi huo. Vilevile, muda wa upatikanaji wa maji umeongezeka

Page 85: Tekeleza kwa

83

kutoka saa sita mara mbili kwa wiki hadi saa sita kwa siku. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 4 ili kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Mji wa Mpanda. 169. Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara yangu inaendelea na mazungumzo na Kampuni ya Ostap ya nchini Austria ambayo imeonesha nia ya kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Mpanda. Hadi sasa Kampuni hiyo imeelekezwa kuwasilisha Andiko la Mradi (Project Proposal) pamoja na mpangokazi (workplan) kwa ajili ya kupitiwa na kuwasilishwa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango kwa hatua zaidi. (b) Mji wa Njombe 170. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/2015, Wizara yangu imetuma shilingi bilioni 1.38 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa maji katika Mji wa Njombe. Kazi zinazotekelezwa ni ujenzi wa chanzo cha Mto Nyenga; ulazaji wa bomba kubwa umbali wa kilomita 14.3; ujenzi wa matanki 3 yenye ujazo wa lita 135,000 kila moja katika maeneo ya Magereza, Airport na Nazareti; ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 16.58 katika maeneo ya Airport, Kambarage, Igeleke na Nzengelendete na ununuzi wa dira 1,000. Hadi mwezi Aprili 2015, mradi huo umefikia asilimia 81 na utakamilika mwezi Julai, 2015. Mradi huo utakapokamilika hali ya upatikanaji wa huduma ya maji itaongezeka kutoka asilimia 43 hadi asilimia 81. Katika mwaka wa fedha 2015/2016, Serikali imetenga shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Njombe.

Page 86: Tekeleza kwa

84

(c) Mji wa Bariadi 171. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea kukamilisha miradi ya maji katika Mji wa Bariadi. Kazi zilizokamilika ni uchimbaji wa visima vitano na kuweka umeme kwenye visima vitatu; kuongeza mtandao wa mabomba umbali wa kilomita 5.76; na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 50,000 eneo la Kidinda. Katika mwaka wa fedha 2015/2016, Serikali itaendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa kumalizia kazi za kuunganisha visima vipya vitano kwenye mtandao wa maji; kujenga matanki mawili ya maji yenye ujazo wa lita 135,000 katika eneo la Somanda na lita 680,000 eneo la Sima. Vilevile, kazi nyingine ni pamoja na kuongeza mtandao wa mabomba umbali wa kilomita 9.65 katika maeneo ya Sima, Malambo na Somanda; kujenga nyumba ya mtambo wa kusukuma maji na kulaza bomba kuu la kupandisha maji kwenye matanki; ujenzi wa kituo cha kuchotea maji; na kufunga dira za maji kwa wateja 400. Mradi huo utakapokamilika, utaboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 30 hadi asilimia 50. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani kupitia KfW imepanga kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Bariadi. Hadi mwezi Aprili 2015, Mtaalam Mshauri anaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu, usanifu na kuandaa makabrasha ya zabuni na utakamilika mwezi Januari, 2016. 3.3.3 Usanifu wa Miradi ya Maji katika Miji Mikuu ya

Wilaya na Miji Midogo 172. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imeendelea na kazi za kuajiri Wataalam Washauri ili kufanya upembuzi yakinifu, usanifu na kuandaa makabrasha ya zabuni katika Miji Mikuu ya Wilaya na Miji

Page 87: Tekeleza kwa

85

Midogo. Hadi mwezi Aprili 2015, Mtaalam Mshauri amewasilisha taarifa ya upembuzi yakinifu kwa Miji ya Biharamulo, Muleba, Ngara, Karagwe, Chato na Bunazi (Kagera) na anaendelea na usanifu wa kina pamoja na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni katika Miji ya Namanyere, Chala, Matai na Laela (Rukwa); Inyonga na Mpanda (Katavi). Mtaalam Mshauri amesaini Mkataba tarehe 19/03/2015 na kazi hizo zitakamilika mwezi Januari, 2016. Kwa upande wa Miji ya Manyoni na Kiomboi mkoani Singida, Mtaalam Mshauri amekamilisha kazi ya usanifu kwa Mji wa Manyoni, na kwa Mji wa Kiomboi usanifu utakamilika mwezi Juni, 2015. 173. Mheshimiwa Spika, taratibu za kuwapata Wataalam Washauri kwa ajili ya kufanya kazi ya upembuzi yakinifu, usanifu na kuandaa makabrasha ya zabuni zinaendelea kwa Miji ya Mombo, Songe, Lushoto, Kasela, Mkinga, Korogwe na mradi wa kitaifa wa Handeni Trunk Main - HTM katika Mkoa wa Tanga; Mji wa Kakonko mkoani Kigoma; mradi wa maji kutoka Mto Ugala hadi Miji ya Urambo na Kaliua (Tabora); Miji ya Mangaka, Ruangwa na Liwale (Lindi); Miji ya Kibaya, Mbulu, Magugu, Galapo, Dareda na Bashnet (Manyara); Miji ya Mahenge, Ifakara, Dakawa na Mikumi (Morogoro); na Miji ya Chamwino, Bahi na Kondoa mkoani Dodoma. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea na juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa miradi ya maji kwa miji ambayo usanifu umekamilika.

Page 88: Tekeleza kwa

86

3.3.4 Miradi ya Kutoa Maji kutoka Ziwa Victoria Kupeleka Miji Mbalimbali

(a) Miji ya Bariadi, Lagangabilili, Mwanhuzi, Sumve na

Malya

174. Mheshimiwa Spika, Serikali imeajiri Mtaalam Mshauri wa kufanya usanifu na uandaaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya mradi wa majisafi kutoka Ziwa Victoria kwenda Miji ya Bariadi, Lagangabilili na Mwanhuzi. Mtaalam Mshauri amewasilisha taarifa ya awali (Inception report) mwezi Machi, 2015. Ujenzi wa mradi huo utaanza katika mwaka wa fedha 2015/2016. Mradi huo utakapokamilika utanufaisha wakazi wa miji hiyo pamoja na vijiji 40 vilivyopo umbali wa kilomita 12 kandokando ya bomba kuu kutoka kwenye Ziwa Victoria. Aidha, Wizara imeagiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza kufanya upembuzi yakinifu ili kubaini chanzo mbadala cha kupeleka maji katika miji midogo ya Sumve na Malya kutoka Magu au Ngudu. Baada ya kazi hiyo kukamilika usanifu wa kina utafanyika na ujenzi kuanza. (b) Mji wa Ngudu

175. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilikamilisha mradi wa upanuzi wa mtandao wa maji kutoka tanki la Mhalo kwenda Mji wa Ngudu. Mradi huo ulizinduliwa rasmi tarehe 11/10/2014 na Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kukamilika kwa mradi huo kumewanufaisha wakazi wapatao 36,417 wanaoishi katika Mji wa Ngudu na vitongoji vyake pamoja na wakazi wa vijiji linapopita bomba kuu la maji.

Page 89: Tekeleza kwa

87

(c) Miji ya Isaka, Kagongwa, Tinde, Kishapu, Kolandoto, Maganzo na Mwadui

176. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliiagiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama-Shinyanga (KASHWASA) kufanya usanifu na kuandaa gharama za utekelezaji wa mradi wa kutoa maji kutoka Ziwa Victoria kupeleka katika Miji ya Isaka, Kagongwa na Tinde. Hadi sasa kazi ya usanifu inaendelea na ujenzi wa mradi huo utatekelezwa na KASHWASA chini ya usimamizi wa Wizara kama ilivyofanyika kwa mradi wa majisafi wa Wilaya ya Ngudu. Vilevile, KASHWASA inaendelea kutekeleza mradi wa kupeleka maji katika Miji ya Kishapu, Kolandoto, Maganzo na Mgodi wa Almasi wa Mwadui. Mradi huo uko katika hatua za awali za ujenzi ambapo uchimbaji wa mtaro na ulazaji wa mabomba unaendelea. Mradi utakapokamilika utawanufaisha wakazi wapatao 58,155 wanaoishi katika miji hiyo pamoja na wakazi wa vijiji vilivyopo pembezoni mwa bomba kuu la maji. (d) Miji ya Tabora, Igunga, Nzega, Sikonge, Urambo

na vijiji vya Wilaya ya Uyui 177. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Serikali itaanza upanuzi wa mradi wa maji wa Ziwa Victoria kutoka katika Kijiji cha Solwa hadi Miji ya Tabora, Igunga, Nzega na vijiji vilivyomo ndani ya kilomita 12 kila upande vinavyopitiwa na bomba kuu. Vilevile, mradi utahudumia baadhi ya vijiji vya Wilaya ya Uyui, Miji ya Sikonge na Urambo. Mradi huo utahusisha ujenzi wa matanki, ulazaji wa mabomba na ukarabati wa mitandao ya usambazaji maji katika miji hiyo. Hadi mwezi Aprili, 2015 upembuzi yakinifu umekamilika. Kwa sasa, Mtaalam Mshauri anakamilisha usanifu wa kina, michoro na uandaaji wa makabrasha ya

Page 90: Tekeleza kwa

88

zabuni. Kiasi cha Dola za Marekani Milioni 268.35 kimepatikana kutoka Serikali ya India na Mkataba wa Makubaliano ya Kifedha utasainiwa mwezi Juni, 2015, na ujenzi utaanza katika mwaka wa fedha 2015/2016. 3.3.5 Miradi katika Jiji la Dar es Salaam 178. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inaendelea kutekeleza miradi ya kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa Jiji la Dar es Salaam, na miji ya Kibaha na Bagamoyo ili kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi, salama na ya kutosha. Hadi mwezi Aprili, 2015 miradi inayoendelea kutekelezwa ni kama ifuatavyo:- (a) Ujenzi wa Bwawa la Kidunda 179. Mheshimiwa Spika, Mtaalam Mshauri amekamilisha kazi ya tathmini ya athari za kimazingira na kijamii (ESIA) ya bwawa na barabara inayounganisha barabara kuu ya Dar-Morogoro na eneo la ujenzi wa bwawa hilo. Tathmini hiyo imewasilishwa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa ajili ya uhakiki na kutolewa kibali cha ujenzi. Aidha, taratibu za kuandaa zabuni kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo zinatarajiwa kuanza mara baada ya kupata kibali kutoka NEMC. 180. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, ulipaji wa fidia kwa ajili ya watakaohamishwa kupisha ujenzi wa bwawa na barabara inayoelekea katika eneo la ujenzi, ulifanyika kati ya mwezi Agosti na Septemba 2014. Jumla ya shilingi bilioni 7.3 zilitumika kulipa fidia kwa wananchi 2,603. Hata hivyo, baadhi yao wamelalamikia viwango vya fidia waliyopata. Katika kukabiliana na changamoto hiyo,

Page 91: Tekeleza kwa

89

Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) imeanzisha dawati la kupokea malalamiko. Hadi mwezi Aprili 2015, uhakiki ulifanyika kwa wakazi ambao wamelipwa fidia. Uhakiki huo ulibaini kuwa fidia kwa wakazi 341 zilikuwa na kasoro. Kwa sasa, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro inaboresha takwimu za fidia kwa wakazi hao ili watakaostahili waweze kulipwa fidia stahiki. Hivi sasa utaratibu wa kuwagawia viwanja wananchi watakaoathirika na ujenzi wa bwawa unaendelea pamoja na ujenzi wa shule, ofisi ya walimu, ofisi ya kijiji na zahanati umeanza kwa kutumia kampuni ya Jeshi la Wananchi-Mzinga. 181. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia DAWASA iliingia makubaliano (MoU) na Kampuni ya M/s AVIC ya China tarehe 23/6/2014 ya kushirikiana katika kujenga bwawa la Kidunda. Makubaliano hayo yalihusu kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ujenzi wa bwawa la Kidunda na tukio la uwekaji saini makubaliano hayo lilishuhudiwa na Makamu wa Rais wa China wakati wa ziara yake hapa nchini. Mradi wa ujenzi wa Bwawa la Kidunda utahusu pia ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme cha megawati 20, njia ya kusafirisha umeme kutoka Kidunda hadi Chalinze na barabara yenye kilomita 75 kutoka Ngerengere hadi Kidunda. Serikali inaendelea na majadiliano na Serikali ya Watu wa China ili kupata fedha za kutekeleza mradi huo ambao unakadiriwa kugharimu shilingi bilioni 473. (b) Visima Virefu vya Kimbiji na Mpera 182. Mheshimiwa Spika, kazi ya uchimbaji wa visima virefu 20 vya uzalishaji maji vya Kimbiji na Mpera ilipangwa kukamilika mwezi Novemba, 2014. Hata hivyo, kazi hiyo ilichelewa kukamilika kutokana na kuchelewa kuwasili kwa mabomba ya kujengea visima (casings and screens) kutoka

Page 92: Tekeleza kwa

90

nje ya nchi. Wizara yangu kupitia DAWASA ilimwandikia Mkandarasi kuhusu uamuzi wa kumtoza gharama za kuchelewesha mradi (liquidated damages) kuanzia tarehe 3/11/2014. Hadi mwezi Aprili 2015, Mkandarasi amekamilisha kuchimba visima vinne. Mradi huo utakamilika mwezi Desemba, 2015 na utahudumia wakazi wa maeneo ya Mkuranga, Kongowe, Chanika, Ukonga, Pugu, Kinyerezi, Mbagala, Kigamboni, Kurasini, Mtoni na Kisarawe. 183. Mheshimiwa Spika, aidha, Mkandarasi wa kuchimba visima vinane vya uchunguzi wa mwenendo wa maji chini ya ardhi amekamilisha uchimbaji wa visima saba kati ya vinane vilivyopangwa kuchimbwa katika maeneo ya Mwasonga, Mkuranga, Kibada, Buyuni, Changani, Chanika na Nzasa-Chanika. Mradi huo utakamilika mwezi Juni, 2015. (c) Upanuzi wa Mtambo wa Ruvu Juu na Ulazaji wa

Bomba Kuu kutoka Mlandizi hadi Kimara 184. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatekeleza mradi wa upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu na ulazaji wa bomba kuu kutoka Mlandizi hadi Kimara. Hadi mwezi Aprili 2015, ujenzi wa upanuzi wa Mtambo wa Ruvu Juu unaogharimu Dola za Marekani milioni 39.7 umefikia asilimia 70 na utakamilika mwezi Agosti, 2015. Kukamilika kwa upanuzi wa mtambo huo, kutaongeza uwezo wa kuzalisha maji kutoka lita milioni 82 kwa siku hadi lita milioni 196 kwa siku. Aidha, mradi wa ujenzi wa bomba kuu kutoka Mlandizi hadi Kimara unaogharimu Dola za Marekani milioni 59.3, umefikia asilimia 45 ya utekelezaji wake na utakamilika mwezi Septemba, 2015. Kukamilika kwa ujenzi huo kutapunguza kero ya uhaba wa maji katika Miji ya Mlandizi na Kibaha pamoja na maeneo ya Kiluvya, Kibamba, Changanyikeni, Mbezi, Kimara, Kibangu, Makuburi, Tabata,

Page 93: Tekeleza kwa

91

Segerea, Vingunguti, Airport, Ukonga na Kipawa katika Jiji la Dar es Salaam ambayo yana uhaba mkubwa wa maji. (d) Upanuzi wa Mradi wa Maji Ruvu Chini 185. Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa mradi wa upanuzi wa chanzo cha maji cha Ruvu Chini na mtambo wa kusafisha maji (Treatment Plant) kumeongeza uwezo wa mtambo wa kuzalisha maji kutoka lita milioni 180 hadi lita milioni 270 kwa siku. Kazi inayoendelea ni ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 55.93 ambapo hadi mwezi Aprili, 2015 ulazaji wa bomba hilo umekamilika kwa kilomita 53. Utekelezaji wa mradi kwa ujumla umefikia asilimia 97. Mradi huo umechelewa kukamilika kutokana na vikwazo katika njia ya bomba kama vile nyaya za mawasiliano, nguzo za umeme na kesi zilizopo mahakamani zinazowahusu waliojenga juu ya bomba. Mradi huo utakamilika mwezi Juni, 2015 na kupunguza kero ya maji kwa wakazi wote wanaotumia maji kutoka wa Ruvu Chini unaohusisha maeneo ya Bagamoyo na vitongoji vyake, Bunju, Mabwepande, Boko, Tegeta, Kunduchi, Mbezi Beach, Mbezi Juu, Salasala, Kawe, Makongo, Chuo Kikuu, Mikocheni, Msasani, Masaki, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Sinza, Manzese, Ubungo, Mabibo, Kigogo, Buguruni, Ilala, maeneo yote ya katikati ya jiji la Dar es Salaam pamoja na Kurasini na Bandarini. Aidha, Serikali imekamilisha ukarabati wa matanki ya kuhifadhia maji yaliyopo Chuo Kikuu cha Ardhi. Kukamilika kwa miradi ya Ruvu Juu na Ruvu Chini kutawezesha maeneo yote ambayo yana mabomba ya kusambaza maji, maarufu kama “mabomba ya mchina” ambayo hayapati maji, kuanza kutoa maji.

Page 94: Tekeleza kwa

92

(e) Ukarabati na Upanuzi wa Mfumo wa Kusambaza Majisafi

186. Mheshimiwa Spika, Serikali ilimwajiri Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu wa mradi wa kusambaza maji na kuunganisha wateja kwenye maeneo kutoka Mbezi hadi Kiluvya; na Tegeta hadi Bagamoyo. Usanifu huo ulikamilika katika mwaka 2013/2014. Kutokana na gharama kubwa ya mradi iliyoainishwa katika taarifa ya usanifu, Wizara yangu ilimwelekeza Mtaalam Mshauri huyo kupitia upya makadirio ya mradi kwa lengo la kupunguza gharama ili iwiane na bajeti iliyopo. Mtaalam Mshauri aliwasilisha rasimu ya pili ya makabrasha ya zabuni mwezi Januari, 2015 ambayo yalitumika kutangaza zabuni ya ujenzi. Zabuni zilipokelewa tarehe 6/5/2015 na uchambuzi unaendelea. Mradi utatekelezwa katika mwaka wa fedha 2015/2016. Aidha, Wizara yangu inamtafuta Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu wa mabomba ya usambazaji maji kwenye maeneo mengine ya Jiji ambayo hayana mfumo wa kusambaza maji kwa sasa. Majadiliano ya kimkataba yanaendelea, matarajio ni kuanza kazi ya usanifu mwezi Julai, 2015. 187. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa Jiji la Dar es Salaam, Wizara yangu kupitia DAWASA iliingia makubaliano (MoU) na Kampuni ya Power China Kunming kwa madhumuni ya kutafuta fedha kutoka Benki ya Exim ya nchini China. Fedha hizo ni kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kulaza mabomba ya kusambaza maji katika Jiji la Dar es Salaam. Kampuni ya Power China Kunming ilianza kazi ya upembuzi yakinifu ya mradi huo; na hadi mwezi Aprili 2015, Kampuni hiyo imewasilisha rasimu ya pili ya upembuzi yakinifu na mradi

Page 95: Tekeleza kwa

93

huo unatarajiwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2015/2016 kwa gharama ya shilingi bilioni 316. (f) Kuboresha Mfumo wa Uondoaji Majitaka 188. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa uondoaji wa majitaka katika Jiji la Dar es salaam ili kuongeza upatikanaji wa huduma hiyo kutoka asilimia 10 ya wakazi kwa sasa kufikia asilimia 30 ifikapo mwaka 2017. Utaratibu wa kupata Mtaalam Mshauri atakayesanifu mradi huo umekamilika na mkataba utasainiwa mwezi Juni, 2015. Kwa sasa Serikali inaendelea na majadiliano na Washirika wa Maendeleo walioonesha nia ya kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Vilevile, Serikali ilisaini Makubaliano ya Kisera (Policy Dialogue) na Serikali ya Korea Kusini tarehe 05/03/2015 ambapo Serikali ya Korea Kusini imekubali kutoa Dola za Marekani milioni 89, sawa na shilingi bilioni 160.2 kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa mradi huo. Makubaliano ya awali ya mpango wa utekelezaji wa Mkataba wa Kifedha (Financial Agreement) yalisainiwa tarehe 25/03/2015. Aidha, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Korea Kusini pamoja na Benki ya Dunia itatekeleza mradi wa uondoshaji majitaka pamoja na ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya uondoaji wa maji ya mvua katika Jiji la Dar es salaam. Hatua za majadiliano zinaendelea kati ya Serikali na taasisi nyingine zinazohusika na ujenzi wa miundombinu ya barabara pamoja na Manispaa zote za Jiji la Dar es Salaam. Vikao vya majadiliano vinaendelea baina ya wataalam kutoka taasisi husika ikiwa ni pamoja na Wizara ya Maji, OWM-TAMISEMI, DAWASA, DAWASCO, Mradi wa DART, TANROADS na Manispaa zote za Mkoa wa Dar es Salaam. Lengo la vikao hivyo ni kupitia na kuoanisha michoro ya

Page 96: Tekeleza kwa

94

ujenzi wa miundombinu ya majitaka na uondoaji maji ya mvua katika Jiji la Dar es Salaam. 189. Mheshimiwa Spika, mradi unatarajiwa kuanza kutekelezwa mwaka 2016, na kazi zitakazofanyika ni pamoja na upanuzi wa mfumo wa majitaka katika maeneo ya katikati ya Jiji; na ujenzi wa mifumo mipya ya majitaka maeneo ya Ilala, Magomeni hadi Ubungo, Sinza, Kinondoni, Mwananyamala, Oysterbay, Masaki, Msasani, Kawe, Mbezi Beach, Kurasini, Keko, Chang‘ombe na Temeke. Vilevile, mradi huo utahusu ujenzi wa mitambo mitatu ya kisasa ya kusafisha majitaka katika maeneo ya Jangwani, Kurasini na Mbezi Beach. (g) Miradi Mingine ya Maji Jijini Dar es Salaam 190. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, Wizara yangu kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ubelgiji (BTC) na Umoja wa Nchi za Ulaya imekamilisha miradi sita iliyobaki kati ya miradi 15 iliyopangwa kutekelezwa ya kujenga mifumo ya usambazaji maji katika maeneo hayo. Kazi zilizotekelezwa ni uchimbaji wa visima, ujenzi wa matanki na vituo vya kuchotea maji katika maeneo ya Tabata Darajani, Minazi Mirefu, Kinyerezi, Mwanamtoti, Yombo Dovya-Msakala na Tandale. Majedwali Na. 9a, 9b na 9c yanaonesha utekelezaji wa miradi 15 katika maeneo mbalimbali katika Wilaya za Jiji la Dar es Salaam. 191. Mheshimiwa Spika, vilevile katika kupunguza kero ya maji kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake, hadi mwezi Aprili 2015, DAWASA imechimba visima 49 katika maeneo mbalimbali ya Jiji. Kati ya visima hivyo, visima 23 vimekamilika na kuanza kutumika. Visima vilivyokamilika

Page 97: Tekeleza kwa

95

ni pamoja na visima saba vilivyopo Kimara katika maeneo ya Mavurunza A, Kilungule A, Kilungule B, King’ongo I, King'ongo III, Saranga I na Saranga II; visima vitano vipo Keko/Chang’ombe katika maeneo ya Keko-Magurumbasi, Keko-Mwanga, Chang’ombe A, Unubini na Chang’ombe-Toroli; visima vitatu vipo Sandali katika maeneo ya Sandali, Mpogo na Mwembeladu; visima vitatu vipo Mburahati maeneo ya National Housing, Shebe na Shule ya Msingi Muungano; visima viwili katika maeneo ya Mwaninga-Kigamboni na Kisarawe II; na visima vitatu katika maeneo ya Kipunguni, FFU na Mongo la Ndege yaliyoko Ukonga. Vilevile, ukamilishaji wa ujenzi wa visima tisa unaendelea katika maeneo ya Kisarawe visima vinne, Segerea visima vitatu, Chanika kisima kimoja na Mbagala Mwembe Pacha kisima kimoja. Visima vilivyobaki vimebainika kuwa na maji kidogo na vingine kuwa na kiwango kikubwa cha chumvi. (h) Mradi wa Maji wa Mloganzila-Chuo Kikuu cha Afya

Muhimbili 192. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji ya bomba kwenda eneo la hospitali mpya ya Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili inayojengwa Mloganzila. Wizara imenunua na kufunga booster pump, kulaza bomba kutoka Kibamba mpaka Mloganzila urefu wa kilomita 3.5, kukarabati sump well ya ujazo wa lita 20,000, kujenga mnara wa tanki la lita 10,000 na kuweka transfoma mpya. Mradi huo umefanyiwa majaribio na maji yameweza kufika kwenye tanki lililopo eneo la Chuo Kikuu cha Muhimbili-Mloganzila. Kwa sasa mradi unafanya kazi.

Page 98: Tekeleza kwa

96

3.3.6 Huduma ya Maji katika Miji Mikuu ya Wilaya, Miji Midogo na Miradi ya Kitaifa

(a) Miji ya Kilosa, Turiani, Mahenge, Mvomero na

Gairo 193. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2015, utekelezaji wa miradi ya maji katika Miji ya Kilosa imefikia asilimia 80, Turiani (77), Mahenge (77), Mvomero (81) na Gairo (86). Miradi hiyo ilisimama kutekelezwa kutokana na kuchelewa kwa upatikanaji wa fedha za kulipa madeni ya Wakandarasi na hivyo kusababisha waondoke kwenye maeneo ya miradi. Wizara yangu imefanya majadiliano na Wakandarasi ili warudi katika maeneo ya kazi. Majadiliano hayo yamefanikiwa na Wakandarasi hao wamekubali kuendelea na kazi. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itakamilisha ujenzi wa miradi katika miji hiyo. (b) Mji wa Bunda 194. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu iliendelea kutekeleza mradi wa maji katika Mji wa Bunda. Mradi huo uliwekewa jiwe la msingi na Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 20/03/2015 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Maji Mkoani Mara. Kazi zinazoendelea kwa sasa ni kukamilisha ulazaji wa bomba umbali wa kilomita 25.4 ambapo kwa sasa umefikia asilimia 98; ujenzi wa kichoteo ambao umefikia asilimia 65; bomba la maji kutoka Ziwani ambalo limejengwa kwa asilimia 60; pamoja na ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji uliofikia asilimia 45. Vilevile, kazi ya kulaza mabomba ya kusambaza maji Mjini Bunda imeanza kwa uchimbaji wa mtaro wa umbali

Page 99: Tekeleza kwa

97

wa kilomita 2 pamoja na ununuzi wa mabomba. Kazi hizo zitakamilika mwezi Juni, 2015. (c) Mji wa Orkesumet 195. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na kero ya uhaba wa maji katika Mji wa Orkesumet, Serikali kwa kushirikiana na BADEA na OFID itajenga mradi wa majisafi utakaohudumia wakazi wa Mji huo. Mradi huo utagharimu Dola za Marekani milioni 18.4, kati ya fedha hizo BADEA imetoa Dola za Marekani milioni 8, OFID Dola za Marekani milioni 8 na Serikali itatoa Dola za Marekani milioni 2.4. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 44; mabomba ya usambazaji maji kilomita 52; ujenzi wa matanki manne yenye uwezo wa lita milioni 1.6, lita 150,000, lita 225,000 na lita 50,000; ujenzi wa magati 10 na vituo vinane vya kuchotea maji. Hadi mwezi Aprili, 2015 Mtaalam Mshauri amekamilisha mapitio na kuwasilisha rasimu ya makabrasha ya zabuni kwa ajili ya kumwajiri Mkandarasi wa ujenzi. Wizara imeomba kibali BADEA na OFID kwa ajili ya kumpata Mkandarasi. Ujenzi utaanza katika mwaka wa fedha 2015/2016 na jumla ya shilingi bilioni 1.8 zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 800 ni fedha za ndani. (d) Mji wa Muheza 196. Mheshimiwa Spika, Serikali imeandaa mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Muheza. Mradi huo utatoa maji kutoka Mto Zigi kwenye milima ya Amani hadi Muheza umbali wa kilomita 22.7. Kazi za usanifu wa kina na tathmini ya athari za kimazingira na kijamii (ESIA) zimekamilika mwezi Machi, 2015. Aidha, Wizara yangu

Page 100: Tekeleza kwa

98

imejadiliana na Kampuni ya EUROFINSA ya Hispania kwa ajili ya kutekeleza mradi huo. Kampuni hiyo imewasilisha andiko la mradi kwa kutumia taratibu za Engineering Procurement and Construction (EPC). Wizara imeridhika na andiko hilo na kuliwasilisha Ofisi ya Rais-Tume ya Mipango kwa ajili ya kuridhiwa na hatimaye kuwasilishwa Wizara ya Fedha. Mradi unatarajiwa kuanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2015/2016 kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 26.63. Mradi utakapokamilika utakuwa ndiyo ufumbuzi wa kudumu wa kero ya maji safi na salama kwa wakazi wapatao 30,384 wa Mji wa Muheza. (e) Mji wa Karatu 197. Mheshimiwa Spika, mradi wa maji Mjini Karatu ulizinduliwa rasmi tarehe 22/04/2014 na Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mradi huo umeongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 1.2 kwa siku hadi lita milioni 1.92 kwa siku, sawa na asilimia 41 ya mahitaji ya maji ya lita milioni 4.7 kwa siku. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kutekeleza kazi zilizobaki ambazo ni kukamilisha ujenzi wa visima viwili katika maeneo ya Bwawani na Kwa-Tom; ujenzi wa tanki moja lenye ujazo wa lita 225,000; ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilomita 3.8; ujenzi wa vioski 13; ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 5; na kusambaza mabomba ya maji umbali wa kilomita 8 katika eneo la G – Lambo. (f) Miradi ya Maji ya Miji Mikuu ya Wilaya na Miji

Midogo 198. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imetuma kiasi cha shilingi bilioni 4.26 kwa

Page 101: Tekeleza kwa

99

ajili ya kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Miji Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo. Miji hiyo ni pamoja na Ifakara, Ludewa, Mkuranga, Kondoa, Gairo, Namanyere, Chamwino, Dakawa, Vwawa, Mpwapwa, Mwanga, Mlowo, Igunga, Lamadi, Misungwi, Magu, Ilula, Chunya, Bunda, Tinde na Mutukula. Fedha hizo zimeziwezesha Mamlaka za Maji katika miji hiyo kuongeza wastani wa upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 57 mwaka 2013/2014 hadi kufikia asilimia 60 mwaka 2014/2015. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga shilingi bilioni 20 kwa ajili ya kuendelea na kazi za kukarabati na kupanua miundombinu ya maji katika miji hiyo. Jedwali Na. 10 linaonesha mchanganuo wa fedha zitakazotumwa kwenye Mamlaka za Miji Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo kwa mwaka 2015/2016. Utekelezaji wa miradi hiyo kwa mwaka 2014/2015 ni kama ifuatavyo:-

(i) Mji wa Namanyere 199. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara ilituma Shilingi milioni 650 kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Namanyere. Kazi zinazoendelea kutekelezwa ni ukarabati na upanuzi wa bwawa la maji la Mfili, ununuzi wa pampu na kuzifunga katika visima vinne vilivyochimbwa, ununuzi wa madawa ya kutibu maji na kukamilisha ulazaji wa bomba la usambazaji maji umbali wa kilomita 2.7 kutoka Bwawa la Mfili hadi kwenye matanki ya maji.

(ii) Mji Mdogo wa Lamadi 200. Mheshimiwa Spika, kwa Mji Mdogo wa Lamadi, Wizara imetuma shilingi milioni 195.8 kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika mji huo. Kazi

Page 102: Tekeleza kwa

100

zinazoendelea kutekelezwa ni ulazaji wa bomba kuu kutoka Ziwa Victoria lenye urefu wa mita 156, ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusukuma maji na sump tank, ulazaji wa bomba la usambazaji maji umbali wa kilomita 14, ujenzi wa vioski 17 na ununuzi wa matanki manane yenye ujazo wa lita 10,000 kila moja. Kukamilika kwa kazi hizo kutaongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi katika mji huo na kuwanufaisha wakazi wapatao 15,000. Hadi mwezi Aprili 2015, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 70 na utakamilika mwezi Juni, 2015.

(iii) Mji wa Kilwa Masoko 201. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Mji wa Kilwa Masoko ulipatiwa shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji. Kazi zinazoendelea kutekelezwa ni ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilomita 3.18, ukarabati wa tanki la maji la ujazo wa lita 250,000 katika cha kitongoji cha Mpara pamoja na ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 2.8 ili kuwezesha maji kufika katika tanki lililoko Mji wa Kilwa Masoko. Kukamilika kwa kazi hizo, wananchi zaidi ya 5,000 wa vitongoji vya Mpara, Mkwanyule, Kisangi, na Miina watapata huduma ya maji ya uhakika na endelevu.

(iv) Mji Mdogo wa Ilula 202. Mheshimiwa Spika, katika Mji mdogo wa Ilula, kwa kipindi cha mwaka 2013/2014 na 2014/2015, Serikali imetuma shilingi milioni 616 kwa ajili ya kutekeleza kazi zifuatazo; kukarabati eneo la kuchotea maji (intake) katika mto Idemule chenye uwezo wa kuzalisha lita 940,000 kwa siku; ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilomita 21.3, kubadilisha mabomba ya zamani kwa umbali

Page 103: Tekeleza kwa

101

wa kilomita 6.21 na kukarabati tanki la Mazombe la ujazo wa lita 45,000. Kazi hizo zimekamilika na kuongeza uzalishaji wa maji kutoka lita 600,000 kwa siku hadi lita 940,000 kwa siku. Aidha, Wizara yangu inaendelea na mazungumzo na Kampuni ya Ostap ya nchini Austria ambayo imeonesha nia ya kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Ilula. Kampuni hiyo imeelekezwa kuwasilisha Andiko la Mradi (Project Proposal) pamoja na mpangokazi (workplan) kwa ajili ya kupitiwa na kuwasilishwa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango kwa hatua zaidi.

(v) Mji Mdogo wa Tinde 203. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara ilituma shilingi milioni 100, kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika Mji Mdogo wa Tinde. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni uchimbaji wa kisima kirefu, ujenzi wa magati, nyumba ya mtambo wa kusukuma maji na ununuzi wa tanki la plastiki. Hadi mwezi Aprili 2015, kazi ya uchimbaji wa kisima imekamilika na kazi zinazoendelea ni ujenzi wa magati matatu, nyumba ya mtambo kusukuma maji, usanifu wa mtandao wa kusambaza maji na ununuzi wa mabomba na tanki la maji. Kazi hizo zitakamilika mwezi Julai, 2015 na kukamilika kwake kutawanufaisha wakazi 6,316 wa mji huo. (vi) Miji ya Mugumu, Tarime na Sirari Miji ya Mugumu na Tarime 204. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma ya maji katika Miji ya Mugumu na Tarime, Wizara ilituma jumla ya shilingi milioni 900 kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo ya

Page 104: Tekeleza kwa

102

maji. Kwa upande wa Mji wa Mugumu, kiasi cha shilingi milioni 350 kilitumwa kwa ajili ya ujenzi wa mtambo wa kusafisha maji na ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 40. Aidha, katika Mji wa Tarime, shilingi milioni 550 zilitumwa kwa ajili ya kutekeleza kazi za ujenzi wa nyumba tatu za mitambo ya kusukuma maji, ujenzi wa tanki la ujazo wa lita 100,000, ulazaji wa bomba kuu kwa umbali wa kilomita 2.91 na ujenzi wa vituo vinne vya kuchotea maji. Mradi huo umefikia asilimia 75 na wananchi wameanza kupata huduma ya maji kupitia vituo vitatu. Kazi zinazoendelea ni ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji. Miradi katika miji hiyo, itakamilika katika mwaka 2015/2016.

Mji wa Sirari 205. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na AfDB chini ya LV-WATSAN inatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Sirari. Kazi zitakazohusika ni pamoja na kulaza bomba kuu umbali wa kilomita 4.5 kutoka Isibania, Kenya hadi Sirari; ujenzi wa intake kutoka Mto Hibwa; na tanki la ujazo wa lita 250,000 litakalojengwa Sirari. Mradi unatarajiwa kugharimu shilingi milioni 340. Utekelezaji wa mradi umeanza kwa upande wa Kenya na kwa Tanzania, Mkandarasi ameajiriwa na ataanza kazi mara baada ya Halmashauri ya Tarime kukamilisha ulipaji wa fidia kwenye eneo la kujenga tanki. Kwa upande wa Tanzania, ujenzi huo utasimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Musoma. Kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wakazi 16,000 wa Mji wa Sirari.

(vii) Mji wa Chamwino 206. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imetuma jumla ya shilingi milioni 250 kwa

Page 105: Tekeleza kwa

103

ajili ya kutekeleza kazi za ukarabati wa mabomba kutoka Chamwino Ikulu hadi Bwigiri umbali wa kilomita 6; ukarabati wa mabomba kutoka Chamwino hadi Msanga umbali wa kilomita 6; ununuzi wa dira za maji 770 pamoja na viungio vyake; kuunganisha wateja 300 kwenye mfumo mpya wa mabomba baada ya kuwaondoa kwenye mabomba yaliyochakaa. Hadi mwezi Aprili 2015, kwa ujumla kazi hizo zimetekelezwa kwa wastani wa asilimia 40 na zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2015 ambapo jumla ya wananchi 8,518 Mji wa Chamwino watanufaika na huduma ya majisafi. Mipango ya baadaye ni kutekeleza mipango ya muda wa kati na muda mrefu. Katika mipango ya muda wa kati, Wizara imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:- ukarabati wa tanki la maji la Bwigiri la ujazo wa lita 400,000 pamoja na kufufua visima viwili vya maji vilivyopo Chamwino. Kwa upande wa mipango ya muda mrefu, Mtaalam Mshauri kupitia Awamu ya pili ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji atafanya upembuzi yakinifu na usanifu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika Miji ya Chamwino na Bahi. Katika mwaka 2015/2016, taratibu za kumwajiri Mtaalam Mshauri zitaendelea.

(viii) Miji ya Gairo, Dakawa na Ifakara 207. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara ilituma kiasi cha shilingi milioni 880 katika Miji ya Gairo (milioni 500), Dakawa (milioni 300) na Ifakara (milioni 80) kwa ajili ya kutekeleza kazi mbalimbali za kuboresha hali ya huduma ya maji katika miji hiyo. Kwa mji wa Gairo kazi zilizotekelezwa ni ulazaji wa bomba kuu na bomba la usambazaji yenye urefu wa kilomita 8.46, uchimbaji wa visima vitatu na ujenzi wa vituo vinane vya kuchotea maji na utekelezaji wa kazi hizo kwa sasa umefikia asilimia 60. Kwa upande wa Mji wa Dakawa, kazi

Page 106: Tekeleza kwa

104

zilizotekelezwa ni ulazaji wa bomba kuu na bomba la usambazaji lenye urefu wa kilomita 8.15, ujenzi wa vituo vitatu vya kuchotea maji na ununuzi wa dira za maji. Utekelezaji wa kazi hizo umefikia asilimia 85. Vilevile, katika Mji wa Ifakara kazi za ulazaji wa bomba kuu na bomba la kusambaza maji lenye urefu wa kilomita 2.4 zimekamilika na ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusukuma maji unaendelea.

(ix) Mji wa Mkuranga 208. Mheshimiwa Spika, ili kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Mkuranga, Wizara ilituma kiasi cha shilingi millioni 100. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na uchimbaji wa kisima, ulazaji wa bomba kuu kilomita 2 kutoka katika visima hadi kwenye matanki, mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 7.2, kununua pamoja na kufunga pampu mbili. Kazi hizo zinatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2015.

(x) Mji wa Longido 209. Mheshimiwa Spika, katika kutatua tatizo la maji kwenye Mji wa Longido, Wizara yangu imefanya utafiti wa kina na kubaini kuwa chanzo pekee ambacho kitatosheleza mahitaji ya maji ni Mto Simba kilichopo Mlima Kilimanjaro, Wilaya ya Siha Mkoani Kilimanjaro. Mradi huo utahudumia wakazi wa Mji wa Longido na Vijiji vya Oltepes, Orbomba na Engikaret. Hadi mwezi Aprili 2015, usanifu wa kina na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni umekamilika. Katika mwaka 2015/2016, ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza baada ya kuajiri Mkandarasi na Wizara imetenga shilingi bilioni 2 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo.

Page 107: Tekeleza kwa

105

3.3.7 Miradi ya Maji ya Kitaifa 210. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika miji na vijiji vinavyohudumiwa na Miradi ya Kitaifa. Katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilituma fedha kwenye miradi hiyo kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji na utekelezaji wa miradi hiyo kwa mwaka huo na kazi zinazoendelea ni kama ifuatavyo:-

(i) Mradi wa Maji Chalinze 211. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali kwa kushirikiana na BADEA, Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Mfuko wa Pamoja wa Sekta ya Maji (Basket Fund), iliendelea kutekeleza Awamu ya Pili ya mradi wa maji Chalinze. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa matanki 40; ujenzi wa vituo 372 vya kuchotea maji; ulazaji wa bomba kuu lenye umbali wa kilomita 335 na mabomba ya kusambaza maji (kilomita 127) katika vijiji 47 pamoja na Kambi 3 za Jeshi. Awamu hiyo imegawanywa katika vipande tisa ambavyo ni: Lot 1, Lot 2, Lot 3, Lot 4, Lot 5, Lot 6, Package F, Package H na Package J. 212. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2015, miradi katika Lot 1, Lot 2, Lot 4, Lot 5, Lot 6 na Package J imekamilika na wananchi katika vijiji 32 na Kambi 3 za Jeshi wanapata maji. Vijiji vilivyonufaika ni pamoja na Mkange, Mihuga, Mandamazingara, Masimbani, Kweikonje, Masuguru, Madesa, Pongwe-Msungura, Kiwangwa, Fukayosi, Kidomole, Makurunge, Mkenge, Msinune, Vigwaza, Buyuni, Visezi, Chamakweza, Chahua, Gwata, Gumba, Magindu, Lukenge, Kwaruhombo, Kifuleta, Pongwe-Kiona, Kwang’andu, Kidugalo, Ngerengere, Sinyaulime,

Page 108: Tekeleza kwa

106

Bwawani-Gwata, Kinonko, pamoja na Kambi za Jeshi za Sangasanga, Kizuka na Kinonko. Aidha, kwa upande wa Lot 3, mradi umelenga kuboresha huduma ya maji katika vijiji 7 ambapo utekelezaji wa mradi huo umekamilika katika vijiji 6 na wananchi wa vijiji hivyo wanapata maji. Vijiji vilivyonufaika ni Kinzagu, Makombe, Talwanda, Msigi, Kisanga na Mindukeni. Kazi ya ulazaji bomba katika kijiji cha Malivundo inaendelea na itakamilika mwezi Julai, 2015. 213. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa Package H, unaohusisha vijiji 8 unaendelea na kwa sasa vijiji vitatu vya Msolwa, Mdaula na Matuli vinapata maji. Vijiji vitano vilivyobaki vya Mwidu, Visakazi, Tukamisasa, Kaloleni na Ubenazomozi utekelezaji wake umefikia asilimia 95 na ujenzi utakamilika mwezi Juni, 2015. Kwa upande wa Package F, ujenzi unaendelea na hadi mwezi Aprili 2015, kazi zilizokamilika ni kufunga pampu 2 Mbwewe na Mkandarasi anaendelea na ujenzi wa vituo vya kusukuma maji; kufanya majaribio ya pampu 4 za Ubenazomozi na kufunga mtambo kwenye chujio la Wami. Kazi hizo zitakamilika mwezi Julai, 2015. Mradi utakapokamilika, utawanufaisha wakazi 197,684 wa Wilaya tatu za Bagamoyo, Kibaha na Morogoro Vijijini. Jedwali Na. 11 linaonesha vijiji vilivyonufaika kwa kila kipande cha mradi. 214. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2015, Mkandarasi wa utekelezaji wa Awamu ya Tatu ya mradi wa maji wa Chalinze amepatikana na gharama ya mradi ni Dola za Marekani milioni 60. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na kukarabati wa chanzo; kujenga tanki kubwa la kuhifadhi maji lenye uwezo wa lita milioni 2 katika Mlima Mazizi; kujenga matanki 18 ya kuhifadhi maji yenye jumla ya lita milioni 2.75; kupanua mitandao ya kusambaza maji; kufunga pampu za kusukuma maji kutoka Wami hadi kwenye

Page 109: Tekeleza kwa

107

tanki la Mlima Mazizi; kufunga pampu kwenye kituo cha Mbwewe ili kusukuma maji kwenda katika kijiji cha Manga Wilayani Handeni; pamoja na kujenga vituo 210 vya kuchotea maji katika maeneo ambayo hayakufikiwa na ujenzi wa Awamu ya Kwanza na ya Pili. Mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi Juni, 2015 na utachukuwa muda wa miezi 15 hadi kukamilika. Mradi ukikamilika utaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 7.2 za sasa hadi lita milioni 11 kwa siku. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga shilingi bilioni 3 kwa kuanza utekelezaji wa mradi wa Awamu ya Tatu.

(ii) Mradi wa Mugango-Kiabakari

215. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali ilituma shilingi milioni 100 kwa ajili ya ukarabati wa bomba kuu la maji kutoka kwenye chanzo hadi Kiabakari na kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Butiama. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) na Mfuko wa Maendeleo wa Saudia (Saudi Fund for Development-SFD) imeanza mpango wa kutekeleza mradi wa maji wa Mugango–Kiabakari. Mradi huo unakadiriwa kugharimu Dola za Marekani milioni 30.69. Kazi zitakazotekelezwa ni ujenzi wa chanzo; ujenzi wa mtambo wa kusafisha na kusukuma maji; kujenga matanki matatu; kulaza mabomba kutoka eneo la Mugango kupitia Kiabakari hadi Butiama umbali wa kilomita 32; kukarabati mitambo ya kusukuma maji ya Kiabakari; na kulaza mabomba ya mtandao wa usambazaji maji kutoka Butiama hadi Bisalye. 216. Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wakazi wapatao 80,000 waliopo eneo la mradi pamoja na vijiji vilivyopo umbali wa kilomita 12

Page 110: Tekeleza kwa

108

pembezoni mwa bomba kuu. Wizara imeomba kibali (No Objection) BADEA na Saudi Fund kwa ajili ya kumpata Mtaalam Mshauri wa kufanya mapitio ya usanifu na usanifu wa mradi wa miundombinu ya maji na mkataba umesainiwa tarehe 11/05/2015 na kazi ya mapitio itaanza mwezi Juni, 2015. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga shilingi milioni 300, fedha za ndani kwa ajili ya kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji katika eneo la mradi wakati matayarisho ya ujenzi wa mradi mpya yanaendelea.

(iii) Mradi wa Makonde

217. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali ilituma shilingi milioni 226 kwa ajili ya kuboresha hali ya upatikanaji wa maji katika vijiji na miji katika Mradi wa Kitaifa wa Makonde. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Uingereza kupitia Idara yake ya Maendeleo ya Kimataifa (DFID) itakarabati visima virefu sita katika chanzo cha Mitema. Kazi hiyo inatarajiwa kuanza mwezi Juni, 2015 na kukamilika mwezi Septemba, 2015. Mahitaji ya maji kwa sasa ni lita milioni 14.2 kwa siku ambapo, kukamilika kwa kazi hiyo kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 7.4 za sasa hadi lita milioni 14.8 kwa siku na kuweza kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji katika maeneo yanayohudumiwa na mradi huo. Katika mwaka 2015/2016, jumla ya shilingi bilioni 1.8 zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza kazi hizo. Aidha, Wizara yangu inaendelea na majadiliano na Kampuni ya Ostap ya nchini Austria ambayo imeonesha nia ya kutekeleza kazi za kuboresha huduma ya maji katika Mradi wa Kitaifa wa Makonde. Hadi sasa Kampuni hiyo imeelekezwa kuwasilisha Andiko la Mradi (Project Proposal) pamoja na mpangokazi kwa ajili ya kupitiwa na kuwasilishwa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango kwa hatua zaidi.

Page 111: Tekeleza kwa

109

(iv) Mradi wa Handeni Trunk Main (HTM) 218. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilituma shilingi milioni 150 kwa ajili ya kuboresha hali ya upatikanaji wa maji katika miji na vijiiji vinavyohudumiwa na mradi wa Kitaifa wa HTM. Aidha, Wizara yangu inaendelea na majadiliano na Kampuni ya BAM International ya nchini Uholanzi pamoja na AfDB kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika maeneo yanayohudumiwa na mradi wa kitaifa wa HTM. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga fedha za ndani shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji katika eneo la mradi wakati matayarisho ya mradi mpya yanaendelea.

(v) Mradi wa Wanging’ombe 219. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/2015, Serikali yangu ilituma shilingi milioni 180 kwa ajili ya kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika miji na vijiji vinavyohudumiwa na Mradi wa Kitaifa wa Wanging’ombe. Aidha, Wizara yangu imejadiliana na Kampuni ya EUROFINSA ya Hispania kwa ajili ya kutekeleza mradi huo. Kampuni hiyo imewasilisha andiko la mradi kwa kutumia taratibu za Engineering Procurement and Construction (EPC). Wizara imeridhika na andiko hilo na kuliwasilisha Ofisi ya Rais-Tume ya Mipango kwa ajili ya kuridhiwa na hatimaye kuwasilishwa Wizara ya Fedha. Mradi unatarajiwa kuanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2015/2016 kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 64.69. Vilevile, Serikali imetenga shilingi milioni 800 fedha za ndani kwa ajili ya kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kabla ya kuanza kutekeleza mradi mpya.

Page 112: Tekeleza kwa

110

(vi) Mradi wa Masasi-Nachingwea 220. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilituma shilingi milioni 84 kwa Mamlaka ya Maji Mtwara ambayo ilikuwa ni msimamizi wa ujenzi wa mradi wa maji wa Masasi-Nachingwea kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi waliopisha ulazaji wa bomba kuu la maji katika vijiji vya Chinongwe na Likwachu Wilayani Ruangwa; na vijiji vya Chiumbati na Tunduru-ya-Leo katika Wilaya ya Nachingwea. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga fedha za ndani shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuimarisha huduma ya maji kwenye maeneo ya Mradi wa Kitaifa wa Maji wa Masasi-Nachingwea.

(vii) Mradi wa Maswa 221. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilituma shilingi milioni 50 kwa Mamlaka ya Mradi wa Kitaifa Maswa, kwa ajili ya kulipia sehemu ya gharama za umeme wa mitambo ya kusukuma maji. Katika mwaka 2015/2016, Serikali imetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika maeneo yanayohudumiwa na mradi huo. 3.3.9 Kuzijengea Uwezo Mamlaka za Maji Mijini (a) Ujenzi wa Ofisi za Mamlaka 222. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuzijengea uwezo Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini kwa kujenga na kukarabati ofisi za mamlaka. Hadi mwezi Aprili 2015, ujenzi wa ofisi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Babati umefikia asilimia 92. Katika Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Tunduma, ujenzi wa

Page 113: Tekeleza kwa

111

ofisi umefikia asilimia 70. Aidha, Wizara yangu imezielekeza Mamlaka za Maji za Miji ya Geita na Mpanda kuwasilisha michoro ya ofisi na makadirio ya gharama za ujenzi kwa ajili ya kuhakikiwa ili ujenzi uanze. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itakamilisha ujenzi wa ofisi za Mamlaka za Maji za Babati na Tunduma, na kuanza ujenzi wa ofisi za Mamlaka za Geita na Mpanda. Vilevile, ukarabati wa ofisi za mamlaka za majisafi na usafi wa mazingira katika Miji Mikuu ya Wilaya, Miji Midogo na Miradi ya Kitaifa utafanyika. (b) Mafunzo kwa Watumishi 223. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali ikishirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) imeendelea kuzijengea uwezo Mamlaka za Miji ya Wilaya na Miji Midogo pamoja na Miradi ya Kitaifa kwa kutoa mafunzo. Mafunzo yaliyotolewa yalihusu nyanja za kiufundi; uongozi na utawala; biashara; na usimamizi wa fedha. Faida zilizopatikana kwa watumishi wa Mamlaka hizo ni kuongezeka kwa ufanisi wa utendaji kazi za kila siku na kuendelea kuwapatia huduma bora wananchi. Katika mwaka 2015/2016, Wizara kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji itaendelea kuisimamia miradi inayotekelezwa kwenye mamlaka za maji mijini ili iweze kukamilika na kuweza kutoa matokeo yaliyotarajiwa. Vilevile, Wizara yangu itaziimarisha Mamlaka za Maji Mijini kwa kuzipatia ofisi vitendea kazi, mafunzo na watumishi wa kutosha ili ziongeze ufanisi katika utoaji wa huduma ya maji kwenye maeneo yao. (c) Malipo ya Umeme 224. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea kuchangia gharama ya sehemu ya ankara za umeme kwa Mamlaka za Maji Mijini za Daraja C pamoja na Miradi ya

Page 114: Tekeleza kwa

112

Kitaifa. Katika mwaka 2014/2015, jumla ya shilingi milioni 506 zimetumwa kwenye Mamlaka za Miradi ya Maji ya Kitaifa kwa ajili ya kulipia sehemu ya ankara za umeme wa mitambo ya kuzalisha maji. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kuziimarisha Mamlaka hizo ili hatimaye ziweze kujiendesha kibiashara na hivyo, kuipunguzia Serikali mzigo.

Page 115: Tekeleza kwa

113

3.4 TAASISI ZA WIZARA YA MAJI 3.4.1 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji

(EWURA) 225. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuisimamia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ili iweze kutekeleza majukumu yake ya kutoa leseni, kusimamia utekelezaji wa masharti ya leseni, kudhibiti ubora na ufanisi wa utoaji huduma, kutathmini na kupitisha bei za huduma na kutatua migogoro baina ya watoa huduma na wateja wao. EWURA inatekeleza majukumu hayo kulingana na Kifungu Na. 414 cha Sheria Na.11 ya EWURA ya mwaka 2001; ambapo Sheria hiyo inaitaka EWURA kudhibiti utoaji wa huduma kwenye Sekta za umeme, mafuta ya petroli, gesi asilia, majisafi na usafi wa mazingira nchini. Katika mwaka 2014/2015, kwa upande wa Sekta ya Maji, EWURA imeendelea na udhibiti wa huduma za upatikanaji wa maji na uondoaji majitaka katika Mamlaka 146 za majisafi na usafi wa mazingira nchini. Kati ya hizo, Mamlaka 23 ni za Miji Mikuu ya Mikoa; Mamlaka 113 za Miji Mikuu ya Wilaya na Miji midogo; DAWASA; DAWASCO; na Mamlaka za Miradi nane ya maji ya Kitaifa. 226. Mheshimiwa Spika, EWURA ilipokea maombi ya kubadilisha bei za majisafi na majitaka kutoka Mamlaka 13 za majisafi na usafi wa mazingira na ilitathmini na kuidhinisha bei za Mamlaka saba za Mtwara, Tanga, Tabora, Dodoma, Singida, Kahama na Korogwe. Aidha, EWURA inaendelea kutathmini bei za maji za Mamlaka sita za Shinyanga, Ngudu, Moshi, Kiomboi, KASHWASA na DAWASA. Sababu za maombi ya mabadiliko ya bei ni kutokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji na kuziwezesha Mamlaka kutekeleza mipango yao ya

Page 116: Tekeleza kwa

114

kibiashara. Vilevile, EWURA ilitoa maoni katika Mipango ya Kibiashara (Business Plans) ya miaka mitatu kutoka Mamlaka za Maji za Arusha, Babati, Dodoma, Geita, Iringa, Moshi, Mtwara, Mwanza, Shinyanga, Singida, Tanga, Tabora, Njombe, Mbinga, KASHWASA, MANAWASA na Ngudu. Mamlaka zilizobaki zinaendelea kutekeleza mipango yao ya kibiashara. 227. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, EWURA ilikagua miundombinu inayotoa huduma ya majisafi na majitaka katika Mamlaka mbalimbali za maji mijini ili kuhakiki viwango vya huduma vinavyotolewa na Mamlaka hizo, kupima ubora wa maji, kufuatilia utekelezaji wa mipango ya kibiashara na utekelezaji wa maagizo ya EWURA. Mamlaka 61 zilikaguliwa ambazo ni:- Arusha, Babati, Bariadi, Bukoba, DAWASCO/DAWASA, Dodoma, Geita, Iringa, Kigoma, Lindi, Mbeya, Morogoro, Moshi, Mpanda, Mtwara, Musoma, Mwanza, Njombe, Shinyanga, Singida, Songea, Sumbawanga, Tabora, Tanga, Bunda, Chunya, Gairo, Igunga, Ilula, Itumba-Isongole, Kahama, Kondoa, Karagwe, Katesh, Kilwa-Masoko, Korogwe, Ludewa, Mafinga, Makete, Mbalizi, Mbulu, Mkuranga, Mpwapwa, Monduli, Nzega, Ngudu, Pangani, Orkesumet, Rujewa, Songe, Tukuyu, Tunduma, Tunduru, Utete, Vwawa, Chalinze, HTM, KASHWASA, Makonde, Wanging’ombe na MANAWASA. Ukaguzi na uhakiki huo unatumika kutoa maelekezo maalum kwa Mamlaka ili kuboresha kasoro zilizobainika na kuandaa taarifa ya utendaji wa Mamlaka za majisafi na usafi wa mazingira mijini kila mwaka. 228. Mheshimiwa Spika, taarifa ya utendaji wa Mamlaka kwa kipindi cha mwaka 2013/2014 iliyotayarishwa na EWURA, inaonesha kuwa Mamlaka za maji zimepiga hatua katika ufungaji wa dira za maji, kuongezeka kwa idadi ya

Page 117: Tekeleza kwa

115

wateja wa majisafi na majitaka, kuongezeka kwa wastani wa saa za upatikanaji wa huduma ya maji na ukusanyaji wa maduhuli. Vilevile, EWURA ilipokea jumla ya malalamiko saba yaliyohusu ankara za majisafi na majitaka zilizokosewa, ukosefu wa maji, kukatiwa huduma ya maji kimakosa na huduma hafifu kwa wateja. Kati ya malalamiko hayo, sita yamepatiwa ufumbuzi na moja lililobaki liko katika hatua ya utatuzi. 229. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Sekta Ndogo za Umeme, Petroli na Gesi Asilia, EWURA imeendelea kusimamia Sekta ndogo hizo ili kuhakikisha uwepo, ubora na usalama wa huduma hizo kwa kuandaa kanuni na taratibu zinazovutia uwekezaji. EWURA imetoa leseni mbili kwa wawekezaji wa miradi midogo ya umeme isiyozidi Megawati 10 (makampuni ya Mapembasi ya Njombe na Bwelui ya Mbeya); leseni mpya 125 za Petroli na kati ya hizo, leseni saba ni kwa ajili ya wauzaji wa jumla wa mafuta ya petroli, leseni 110 kwa ajili ya vituo vya mafuta, leseni moja kwa ajili ya uagizaji wa jumla wa vilainishi, leseni tatu za uagizaji wa jumla wa gesi ya kupikia inayotokana na mafuta ya petroli, leseni moja kwa ajili ya kuuza mafuta kwenye meli (bunkering), na leseni tatu kwa viwanda vyenye miundombinu ya mafuta kwa ajili ya matumizi binafsi (Consumer Installation Licence). Vilevile, EWURA imeendelea kupanga bei kikomo za mafuta ya petroli yanayouzwa kwenye vituo vya mafuta na kusimamia kuhakikisha mlaji hauziwi zaidi ya bei kikomo. Aidha, EWURA imeidhinisha ombi la TPDC la tozo la kuchakata na kusafirisha gesi asilia na imeendelea kukagua miundombinu ya kuchakata, kusafirisha na kusambaza gesi asilia na kubainika kuwa ni salama kwa matumizi na mazingira.

Page 118: Tekeleza kwa

116

230. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, EWURA imelenga kuzingatia vipaumbele vifuatavyo katika kuimarisha udhibiti wa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira nchini.

(i) Uandaaji wa miongozo ya uwekezaji na ya utoaji wa huduma ya maji kwa kuishirikisha Sekta Binafsi katika utoaji wa huduma za majisafi na majitaka;

(ii) Kufuatilia utendaji wa mamlaka za maji mijini kwa kuchambua na kuhakiki taarifa za utendaji kazi wa Mamlaka za maji nchini kwa kukagua miundombinu na utendaji wa mamlaka za maji;

(iii) Ufuatiliaji wa utekelezaji wa miongozo ya viwango vya

ubora wa huduma zinazotolewa na mamlaka za maji;

(iv) Kuendelea kufuatilia utekelezaji wa mipango ya kibiashara (Business Plans) ya mamlaka kwa kuzingatia mwongozo uliotolewa na EWURA; na

(v) Kuhakikisha kuwa viwango vya ubora wa huduma na

viashiria vya utendaji vilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Utendaji Kazi (Performance Agreement) vinazingatiwa na mamlaka.

231. Mheshimiwa Spika, EWURA ni mamlaka ya udhibiti wa Sekta kuu mbili za Nishati na Maji. Ili kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi, nimeiagiza EWURA iendeleze ushirikiano wa karibu na kupokea na kutekeleza miongozo inayotolewa na Wizara zinazosimamia Sekta hizo kulingana na sheria, kanuni na taratibu zilizopo.

Page 119: Tekeleza kwa

117

3.4.2 Chuo cha Maendeleo na Usimamizi wa Maji 232. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Chuo kilidahili wanafunzi 383 wa stashahada (Water Technicians) na wanafunzi 119 wa shahada ya kwanza ya uhandisi wa rasilimali za maji na umwagiliaji (Bachelor of Engineering in Water Resources and Irrigation). Kwa sasa Chuo kina jumla ya wanafunzi 1,117. Katika jitihada za kuongeza idadi ya wanafunzi wa kike katika masomo ya sayansi, Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ilifadhili wanafunzi wa kike 41 katika kozi ya kuwawezesha kujiunga na masomo ya stashahada (Access Course). Ufadhili huo umeongeza udahili wa wanafunzi wa kike kutoka 138 mwaka 2013/2014 hadi 224 katika mwaka 2014/2015. Vilevile, jumla ya wanafunzi 217 walihitimu mafunzo yao mwezi Novemba 2014 katika fani mbalimbali zinazohusu Sekta ya Maji. Katika kutekeleza jukumu la utoaji wa ushauri katika masuala ya maji, Chuo kilifanya utafiti wa maji chini ya ardhi katika Halmashauri za Songea Vijijini, Mwanga, Korogwe, Mvomero na Iringa Mjini. 233. Mheshimiwa Spika, Wizara iliendelea na mpango wa kukijengea uwezo Chuo cha Maendeleo na Usimamizi wa Maji ambapo jumla ya watumishi 13 waligharamiwa mafunzo ya muda mrefu, watumishi watano mafunzo ya muda mfupi na watumishi wapya 17 waliajiriwa. Aidha, maabara ya kupima mwenendo wa maji (Hydraulics Laboratory) ilikarabatiwa na imeanza kutumika. Maabara nyingine za kufundishia ziliboreshwa kwa kuwekewa vifaa mbalimbali vikiwemo vifaa vya uchunguzi wa ubora wa maji, hali ya hewa, haidrolojia, usambazaji maji na upimaji ardhi pamoja na ununuzi na ufungaji wa viti 800 katika madarasa. Aidha, Wizara ilikamilisha ukarabati wa majengo ya chuo mwezi Desemba, 2014; na kuajiri Mtaalam Mshauri kwa ajili ya

Page 120: Tekeleza kwa

118

kufanya usanifu wa jengo la ghorofa sita lenye madarasa, maabara, kumbi za mikutano na maktaba. 234. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali ilitenga jumla ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya Mfuko wa Mafundi Sanifu (Water Technician Fund) ambapo jumla ya wanafunzi 212 wamenufaika kwa kupata mkopo kutoka kwenye mfuko huo. Wizara yangu itaendelea kuchangia katika mfuko huo kiasi cha shilingi milioni 300 kila mwaka ili wanafunzi wengi zaidi waweze kunufaika na mkopo huo. Katika mwaka 2015/2016, Chuo kitaongeza idadi ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanaodahiliwa kwa mwaka kutoka 502 ya sasa na kufikia 920. Vilevile, Wizara itagharamia mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi kwa watumishi 20 katika fani mbalimbali, na kuanza ujenzi wa jengo la ghorofa sita pamoja na kukarabati madarasa, mabweni pamoja na nyumba za walimu. Aidha, Chuo kimepanga kufanya tafiti mbalimbali ikiwemo uwepo wa maji chini ya ardhi kwenye maeneo 100, uendelezaji wa miradi ya maji vijijini ikiwemo Mfumo wa Water Point Mapping na teknolojia ya uvunaji wa maji ya mvua; pamoja na mbinu za kupunguza upotevu wa maji mijini. 3.4.3 Wakala wa Uchimbaji Visima na Ujenzi wa

Mabwawa (DDCA) 235. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu kupitia Wakala wa Uchimbaji Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA) iliendelea na jukumu lake la kuongeza vyanzo vya maji kwa kuchimba visima maeneo mbalimbali nchini. Hadi mwezi Aprili 2015, DDCA imefanya uchunguzi wa maji chini ya ardhi kwenye maeneo 154 kwa ajili ya uchimbaji wa visima virefu na ifikapo mwezi Juni 2015, maeneo 214 yatakuwa yamechunguzwa. Vilevile, Wakala

Page 121: Tekeleza kwa

119

ulichimba visima virefu 233 na ifikapo mwezi Juni, 2015 kulingana na malengo, visima 300 vitakuwa vimechimbwa. Jedwali Na. 12 linaonesha orodha ya visima vilivyochimbwa hadi mwezi Aprili, 2015. 236. Mheshimiwa Spika, Wakala umekamilisha miradi ya ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji katika jengo la Benki Kuu ya Tanzania na eneo la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Kibada-Kigamboni. Aidha, upembuzi yakinifu wa miradi ya mabwawa katika maeneo ya Msomela na Mtunduzi yaliyopo Handeni ulikamilika. Hadi mwezi Aprili 2015, ujenzi wa mabwawa ya Aviv katika Halmashauri ya Songea na Tulia (Mbinga) pamoja na ukarabati wa mabwawa ya Olypasei katika Halmashauri ya Kiteto, Mbangala (Chunya), Kwamaligwa (Kilindi), Habiya (Itilima), Matwiga (Chunya) na Sekeididi (Kishapu) unaendelea na utakamilika katika mwaka 2015/2016. 237. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kujenga uwezo wa Wakala kwa kununua mitambo kwa ajili ya uchimbaji visima, ujenzi wa mabwawa na vifaa vya uchunguzi wa maji chini ya ardhi. Vilevile, ukarabati wa karakana, mitambo na majengo unaendelea. Katika mwaka 2014/2015, Wizara imenunua mtambo kwa ajili ya uchimbaji visima yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 6.8 ikijumuisha seti 8 za mitambo ya kuchimbia visima (drill rigs); mitambo 7 ya kufua upepo (compressors); mitambo mitano ya kupimia wingi wa maji (pumping test units); karakana moja inayohamishika (mobile workshop); kamera moja ya kisima (borehole camera); na nyenzo za kazi. Jitihada hizo, zitauwezesha Wakala kuchimba visima virefu 450, kufanya utafiti kwenye maeneo 300, kujenga mabwawa makubwa mawili, ya ukubwa wa kati manne na mabwawa madogo 10 kwa mwaka. Vilevile, uchunguzi wa ubora wa udongo kwa

Page 122: Tekeleza kwa

120

ajili ya mahitaji mbalimbali ya kimaendeleo pamoja na usanifu wa maeneo 16 ya ujenzi wa mabwawa utafanyika. 3.4.4 Bohari Kuu ya Maji 238. Mheshimiwa Spika, Bohari Kuu ya Maji imeendelea kuhakikisha kuwa vifaa na nyenzo zenye ubora unaotakiwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji nchini vinawafikia watekelezaji wa miradi hiyo kulingana na mahitaji na kwa wakati. Hadi mwezi Aprili 2015, Wizara kupitia Bohari Kuu ya Maji, imesambaza mabomba yenye vipenyo mbalimbali na urefu wa kilomita 80,000; viungio vyake (fittings); na dira za maji 10,000. Vifaa hivyo vilipelekwa kwenye miradi ya maji inayotekelezwa katika Mamlaka za Maji za Singida, Babati, Wanging’ombe, Chalinze, Chamwino, Tanga, Mtwara, Dodoma, Kondoa, Namanyere, Makonde, Igunga, Kigoma, KASHWASA na kwenye Halmashauri za Wilaya mbalimbali nchini. 239. Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maagizo niliyotoa katika hotuba yangu ya mwaka jana, Bohari Kuu ya Maji imeanza kushirikiana na wadau mbalimbali kutoka Sekta Binafsi katika kutekeleza Sera ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (Public Private Partnership-PPP). Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kusambaza vifaa na nyenzo mbalimbali kwa ajili ya kuhakikisha miradi ya maji inatekelezwa kwa ufanisi. Vilevile, Bohari hiyo itaendelea kuwashawishi wawekezaji zaidi ili kuingia nao ubia, kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma na hivyo kupunguza utegemezi kwa Serikali Kuu.

Page 123: Tekeleza kwa

121

3.5 MASUALA MTAMBUKA 3.5.1 Sheria 240. Mheshimiwa Spika, ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa Sheria za maji, Wizara yangu imeendelea kutoa elimu kuhusu Sheria Na.11 ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji na Sheria Na. 12 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira za mwaka 2009, kwa Halmashauri, Bodi za Maji za Mabonde, Mamlaka za maji na wadau wengine wa Sekta ya Maji pamoja na jamii kwa ujumla. Elimu hiyo hutolewa kupitia warsha, mikutano, semina na makongamano. Vilevile, Wizara inaendelea kutoa ushauri wa kisheria kuhusu utekelezaji wa Sheria hizo na kwa mwaka 2014/2015, jumla ya nakala 5,200 za Sheria za Maji na Kanuni zake zimesambazwa kwa wadau. 241. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara imekamilisha kuandaa Matamko matatu ya kutambua maeneo ya mabonde madogo ya maji katika vyanzo na kuyatangaza kwenye Gazeti la Serikali la tarehe 19/09/2014. Vyanzo vya maji ambavyo mabonde madogo yametangazwa ni chanzo cha maji cha Kikuletwa/Ruvu [The Water Resources Management (Designation and Declaration of Kikuletwa/Ruvu Water Catchment Area) Order 2014]; chanzo cha maji cha Umba/Zigi [Water Resources Management (Designation and Declaration of Umba/Zigi Water Catchment Area) Order, 2014]; na chanzo cha maji cha Mto Ruaha Mkuu [The Water Resources Management (Designation and Declaration of Great Ruaha Water Catchment Area) Order, 2014]. 242. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, maoni, ushauri na mapendekezo ya wadau kuhusu Kanuni nne

Page 124: Tekeleza kwa

122

yamekusanywa, kufanyiwa kazi na kanuni hizo zipo kwenye utaratibu wa kutangazwa katika Gazeti la Serikali. Kanuni hizo ni The Water Resources Management (Transfer of water use, discharge and groundwater permits) Regulations 2015; The Water Resources Management (Control and Management of Storm Water) Regulations 2015; The Water Supply and Sanitation (Provision and Management of Sewage and Waste Water Services) Regulations 2015; na The Water Supply and Sanitation (Delegation of Powers by the Minister to Local Government Authorities) Notice 2015. 243. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imeendelea na mchakato wa kurekebisha Sheria Na.11 ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji na Sheria Na. 12 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira za mwaka 2009 pamoja na Sheria Na. 273 ya DAWASA ya mwaka 2001. Maoni, ushauri na mapendekezo ya wadau yaliyotolewa kwenye mkutano wa mapitio ya sheria hizo uliofanyika mwezi Februari, 2015 yanaendelea kufanyiwa kazi. Vilevile, Wizara imekamilisha rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Maji na kuijadili rasimu hiyo na wadau kwenye vikao vilivyofanyika mwezi Novemba, 2014 na Machi, 2015. Maoni, ushauri na mapendekezo yaliyotolewa na wadau yamefanyiwa kazi na kwa sasa Wizara inaendelea na taratibu za kuwasilisha mapendekezo ya kutunga sheria hiyo kwenye Baraza la Mawaziri. 244. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kukamilisha utayarishaji wa Kanuni za Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji na Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira kutegemeana na uhitaji, upatikanaji wa rasilimali fedha pamoja na ukamilishaji wa tafiti. Vilevile, kukamilisha marekebisho ya Sheria za Maji, utayarishaji wa rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mfuko

Page 125: Tekeleza kwa

123

wa Maji na kuendelea kutoa ushauri kuhusu Sheria za maji kwa wadau wote wa Sekta. 3.5.2 Habari, Elimu na Mawasiliano 245. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea kutoa elimu na taarifa mbalimbali zinazohusu Sekta ya Maji, hii inatokana na umuhimu wake kwa jamii kama njia mojawapo ya kuelezea masuala ya usimamizi wa rasilimali za maji na uendelezaji wa miradi ya maji nchini. Mnamo mwezi Juni 2014, Wizara yangu ilishiriki kikamilifu katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kitaifa Mkoani Dar es Salaam. Katika maonesho hayo, Wizara ilishika nafasi ya kwanza kwa ubunifu kwenye utendaji kazi wake kupitia teknolojia ya kuondoa madini ya fluoride kwenye maji kwa kutumia chengachenga za mifupa ya ng’ombe. 246. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara iliendelea kutoa elimu kwa wananchi kupitia maonesho, warsha, tovuti na vyombo mbalimbali vya habari. Maadhimisho ya Wiki ya Maji yalifanyika kitaifa mkoani Mara mwezi Machi 2015. Wakati wa maadhimisho hayo, miradi ya maji ilizinduliwa na kuwekwa mawe ya msingi katika maeneo mbalimbali nchini. Mkoani Mara Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Musoma na Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji Bunda. Vilevile, Wizara yangu ilishiriki maonesho ya Kilimo ya Nanenane yaliyofanyika mwezi Agosti, 2014 katika viwanja vya Ngongo Mjini Lindi. Aidha, jumla ya machapisho 3,000 yalisambazwa kwa wadau; na vipindi vitano vya luninga na vipindi vitatu vya redio vilirushwa hewani katika kipindi cha maadhimisho hayo. Pamoja na vipindi hivyo; Idara, vitengo,

Page 126: Tekeleza kwa

124

taasisi za Wizara na wadau mbalimbali wa sekta hutumia maadhimisho hayo kuelimisha umma kuhusu kazi mbalimbali zinazotekelezwa katika Sekta ya Maji. 247. Mheshimiwa Spika, vilevile, katika mwaka 2014/ 2015, Wizara yangu ilitoa vipindi maalum katika redio na luninga, pamoja na makala kwenye magazeti yaliyolenga kufafanua na kuelimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali ya Sekta ya Maji. Aidha, Wizara imefanikisha kuboresha tovuti na hivyo kuifanya kuwa rafiki zaidi kwa watumiaji. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kuelimisha wananchi na kutoa taarifa mbalimbali zinazohusu Sekta ya Maji pamoja na kuandaa na kutangaza vipindi kwenye luninga na redio. 3.5.3 Teknolojia ya Habari na Mawasiliano 248. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea na juhudi za Serikali za utekelezaji wa mpango wa Serikali Mtandao ili kuboresha utoaji wa huduma zinazohusiana na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA). Katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imeboresha mfumo wa kielektroniki wa takwimu na taarifa (www.mowimis.go.tz) ili kusaidia masuala ya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji. Vilevile, mafunzo kuhusu matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa takwimu na taarifa yametolewa kwa watumishi 30 wa Makao Makuu ya Wizara. Aidha, Wizara imepanga kuwapatia mafunzo hayo watumishi wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira, Bodi za Maji za Mabonde, Mikoa mipya na Halmashauri za Wilaya ifikapo mwezi Julai 2015. 249. Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara imeendelea kutekeleza Mpango wa Uendeshaji wa Serikali kwa Uwazi

Page 127: Tekeleza kwa

125

(Open Government Partnership) kwa kuiboresha tovuti yake (www.maji.go.tz) na kushiriki katika matumizi ya Tovuti ya Takwimu Huria (www.opendata.go.tz). Lengo ni kurahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali za Sekta ya Maji kwa uwazi ndani na nje ya nchi. Aidha, Wizara imeanza kutumia mfumo wa Barua Pepe ya Serikali (Government Mailing System) katika mawasiliano ya kiserikali badala ya kutumia anuani za barua pepe binafsi kama vile yahoomail, gmail, n.k; na pia, Wizara imeunganishwa kwenye Mkonga wa Taifa ili kuboresha urahisi wa mawasiliano kwa njia ya TEHAMA. 250. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itatekeleza kazi zifuatazo: kuandaa mpango mkakati wa TEHAMA wa Sekta ya Maji (Water Sector ICT Strategy) na miongozo ya matumizi ya TEHAMA; kuimarisha zaidi mfumo wa kielektroniki katika ukusanyaji wa takwimu, uchambuzi, na utayarishaji wa ramani za vituo vya kuchotea maji vijijini (Water Point Mapping System); kupanua mfumo wa kielektroniki wa Menejimenti ya Takwimu na Taarifa (Management Information System) na kuoanisha na mifumo mingine iliyopo; kutekeleza mpango wa ‘Open Data’; na kujenga uwezo wa Wizara na Taasisi zake katika matumizi ya TEHAMA kwa kununua vifaa vya kisasa na kutoa mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu kwa wataalam. 3.5.4 Jinsia 251. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea kuhamasisha uwepo wa uwiano wa kijinsia baina ya wanawake na wanaume kama inavyoelekezwa katika Sera ya Maji (2002) pamoja na Sheria za Maji za mwaka 2009. Uwiano huo unazingatiwa kwenye maeneo ya vyombo vya maamuzi makubwa katika usimamizi, uendeshaji na matumizi kwenye utekelezaji wa miradi ya maji. Katika

Page 128: Tekeleza kwa

126

mwaka 2014/2015, Wizara yangu ilishiriki katika Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani lililofanyika kitaifa tarehe 06-08/03/2015 mkoani Morogoro. Vilevile, Wizara inazingatia suala la kurithishana madaraka (succession plan) kwa kuangalia sifa za miundo na kuweka kipaumbele hasa kwa wanawake wenye sifa; na imeendelea kuhamasisha wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

252. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) imeendelea kuandaa Mkakati na Mwongozo wa masuala ya jinsia. Nyaraka hizo zitatumika katika kupanga mipango madhubuti na kubaini changamoto zinazohusu jinsia mahala pa kazi na kuzipatia ufumbuzi. Katika mwaka 2015/2016, Wizara itaendelea na mpango wa kuwa na uwiano/usawa katika uongozi kwa kuzingatia sifa, taaluma na uadilifu. Vilevile, Wizara itakamilisha maandalizi ya benki ya takwimu ya masuala ya jinsia kwa lengo la kuwa na takwimu sahihi za ushiriki unaozingatia jinsia katika mipango, ufuatiliaji na usimamizi wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji. 3.5.5 UKIMWI 253. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea kutoa elimu kuhusu UKIMWI kwa watumishi wake, na tarehe 16/12/2014, Wizara kwa kushirikiana na GIZ iliadhimisha siku ya UKIMWI duniani kwa watumishi wote kwa kuendesha kongamano katika viwanja vya Makao Makuu ya Wizara. Katika kongamano hilo watumishi wapatao 600 walishiriki na kati ya hao, watumishi 141 walipata ushauri nasaha na kukubali kupima VVU kwa hiari yao. Matokeo ya upimaji huo yalibaini watumishi watatu kuwa na maambukizi ya VVU. Vilevile, Dawati la UKIMWI la Wizara lilishiriki katika

Page 129: Tekeleza kwa

127

maonesho ya Wiki ya Maji yaliyofanyika kitaifa Mkoani Mara tarehe 16-22/3/2015 kwa kutoa elimu, ushauri nasaha pamoja na upimaji wa hiari kwa jamii na washiriki walionesha mwitikio mkubwa. 254. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu imeendelea kutoa posho maalum ya chakula na dawa kwa watumishi wake 10 waliojiweka wazi kuwa wanaishi na VVU ili kupata lishe bora. Vilevile, Kamati ya UKIMWI ya Wizara imeundwa na Mpango wa UKIMWI Mahali pa Kazi umeandaliwa tayari kwa utekelezaji. Aidha, Wizara itaendelea kutenga bajeti ya masuala ya UKIMWI; kuandaa mpango wa mafunzo utakaoonesha aina ya mafunzo yatakayotolewa; na kuzingatia mahitaji halisi ya watumishi wanaoishi na VVU kama yalivyoainishwa katika Sheria ya Kazi na Mwongozo wa Utumishi wa Umma. 3.5.6 Maendeleo ya Rasilimali Watu 255. Mheshimiwa Spika, katika hotuba yangu ya mwaka jana nililiarifu Bunge lako Tukufu kuwa Wizara inahitaji wataalam 8,749 kwa kipindi chote cha utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (2007-2025), ili kutekeleza majukumu kwa ufanisi na kufikia malengo yaliyokusudiwa. Katika kutekeleza suala hilo Wizara iliwasiliana na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na kufanikiwa kupata kibali cha kuajiri wataalam 475. Kibali hicho kilielekeza waajiriwe Wahandisi 125, Mafundi Sanifu 150 wa Daraja la II na Mafundi Sanifu Wasaidizi 200. Hadi mwezi Aprili, 2015 jumla ya wataalam 318 kati ya wataalam 475 wameajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi. 256. Mheshimiwa Spika, ajira ya wataalam hao kutoka Sekretarieti ya Ajira ilifanyika kwa awamu mbili. Awamu ya

Page 130: Tekeleza kwa

128

kwanza waliajiriwa wataalam 41 kati ya hao 29 ni Wahandisi na 12 ni Mafundi Sanifu. Wataalam walioajiriwa katika awamu ya kwanza walipangiwa vituo vya kazi kwenye Idara za Wizara ili kupunguza uhaba wa watalaam. Katika awamu ya pili, Wizara ilipokea wataalam 277 ambao kati ya hao Wahandisi ni 67, Mafundi Sanifu 210. Watumishi hao wote walipangwa kwenye Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri za Wilaya. Hadi sasa Sekta ya Maji ina jumla ya wataalam 1,856 wanaosimamia na kutekeleza Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji. 257. Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha mpango wa mafunzo kwa watumishi wa kuwajengea uwezo watumishi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Aidha, viongozi saba wamehudhuria mafunzo ya usimamizi wa fedha (Financial Management and Disbursement Course); viongozi 34 wamehudhuria mafunzo ya kuboresha utendaji (Strengthening Leadership Performance); viongozi wanane wamehudhuria mafunzo ya utatuzi wa migogoro, usimamizi wa mikataba na utawala bora; na watumishi 15 wamehudhuria mafunzo ya PPP. Vilevile, watumishi 210 wa Sekta ya Maji wamehudhuria mafunzo ya kutumia mifumo ya kielektroniki ya Management Information System (MIS) na Water Point Mapping (WPM); watumishi 20 wanaendelea na mafunzo ya muda mrefu ndani na nje ya nchi; na watumishi 85 wa fani ya haidrolojia kutoka Makao Makuu na Ofisi zote za Bodi za Maji za Mabonde wamepata mafunzo ya namna bora ya kukusanya takwimu kutoka kwenye vituo vya maji kwa kufuata taratibu za kimataifa za World Metrological Organization.

Page 131: Tekeleza kwa

129

3.5.7 Mapambano Dhidi ya Rushwa 258. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu katika mwaka 2014/2015, imeendelea na harakati za kupambana na vitendo vya rushwa kwenye maeneo yote ya kazi. Katika kutekeleza harakati hizo, Dawati la Malalamiko limeendelea kusimamia kwa karibu ambapo jumla ya malalamiko matano yalipokelewa na kupatiwa ufumbuzi. Aidha, baada ya kupokea mrejesho wa wadau kuhusu Mkataba wa Huduma kwa Mteja, Wizara itaufanyia mapitio Mkataba huo ili ulingane na hali halisi ya mahitaji ya sasa katika kutoa huduma na kupunguza mianya ya rushwa. 3.5.8 Uratibu wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya

Maji 259. Mheshimiwa Spika, Serikali katika azma yake ya kuendeleza Sekta ya Maji nchini, imeweka mfumo endelevu wa kusimamia na kuendeleza rasilimali za maji. Kupitia mfumo huo, Serikali imeandaa na kutekeleza Sera ya Maji ya Mwaka 2002, Mkakati wa Maendeleo ya Sekta ya Maji (2006-2015) na Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (2006-2025). Vilevile, Mfumo huo unaandaa na kutekeleza taratibu za kisheria na kuweka muundo wa kitaasisi wenye uwezo wa kutekeleza Sera ya Maji. Muundo huo unahusisha ushirikishwaji wa Wadau wa Sekta ya Maji katika hatua mbalimbali za utekelezaji kuanzia uibuaji, usanifu, upangaji, ujenzi, usimamizi, uendeshaji hadi matengenezo ya miradi ya maji pamoja na kuchangia gharama za huduma ya maji. 260. Mheshimiwa Spika, Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (Water Sector Development Programme – WSDP) ya mwaka 2007 – 2025 inaendelea kutekelezwa nchini kote. Utekelezaji wa Progamu hiyo upo katika Awamu

Page 132: Tekeleza kwa

130

ya Pili baada ya Awamu ya kwanza kukamilika mwezi Juni, 2014. Programu hiyo inatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo. Kulingana na Hati ya Makubaliano kati ya Serikali na Washirika wa Maendeleo, Wizara yangu inaratibu programu hiyo kwa kushirikiana na OWM-TAMISEMI, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Wizara ya Fedha. Lengo ni kuhakikisha kuwa viwango na kasi ya utekelezaji wa programu vinazingatia thamani ya fedha iliyowekezwa (value for money). Hadi mwezi Aprili 2015, vikao vya pamoja vya mashauriano kutoka ngazi ya wataalam hadi ngazi ya makatibu wakuu vilifanyika, na mkutano wa mwaka wa wadau wa Sekta ya Maji (Joint Water Sector Review Meeting) uliandaliwa na kufanyika kwa mafanikio tarehe 15 – 16 Novemba 2014 ambapo maamuzi kuhusu utekelezaji wa programu yalitolewa. Vilevile, ziara za ukaguzi (Joint Supervision Missions) zimefanyika pamoja na utayarishaji wa taarifa mbalimbali za utekelezaji. Uratibu huo unafanyika kulingana na matakwa ya Hati ya Makubaliano ya programu. Katika mwaka 2015/2016, Wizara yangu itaendelea kuratibu programu hiyo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha majadiliano baina ya wadau wa sekta yanafanikiwa na kutoa taarifa mbalimbali za utekelezaji wa programu. Awamu ya Pili ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji 261. Mheshimiwa Spika, katika kikao kilichopita cha Bunge la bajeti, nililitaarifu Bunge lako Tukufu juu ya maandalizi ya Awamu ya Pili ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji yaliyohusisha tathmini ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya programu iliyofanyika mwezi Februari hadi Mei, 2013. Tathmini hiyo ilipitia maeneo yote yanayohitaji maboresho kwa ajili ya Awamu ya Pili ya

Page 133: Tekeleza kwa

131

Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (2014/2015 – 2018/2019). Maeneo hayo ni pamoja na utekelezaji wa Mipango Shirikishi ya Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji; mipango ya ujenzi wa miradi ya maji vijijini inayohusisha ukarabati, upanuzi, ujenzi wa miradi mipya na uendeshaji na matengenezo ya miradi katika Halmashauri; mipango ya ujenzi wa miradi ya maji katika Miji Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo, kuboresha huduma za maji katika Miji Mikuu ya Mikoa likiwemo Jiji la Dar es Salaam; na mipango ya kuzijengea uwezo taasisi zinazotekeleza Programu ikiwa ni pamoja na kuongeza wigo wa Kampeni ya Kitaifa ya Usafi wa Mazingira. Hivi sasa, Wizara inaendelea na utekelezaji wa kipindi cha mpito kwa kukamilisha kazi za Awamu ya Kwanza ya programu. 262. Mheshimiwa Spika, Awamu ya Pili ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji itakuwa haina tofauti kubwa kimuundo na awamu iliyopita, na inakadiriwa kuwa na bajeti ya Dola za Marekani bilioni 3.3. Awamu hiyo itatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano hadi mwaka 2018/2019. Katika awamu hiyo, Sekta ya Maji itatekeleza mpango wa kuboresha huduma za maji vijijini na mijini pamoja na usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji. Mpango huo unalenga kujenga, kukarabati na kupanua jumla ya vituo 76,334 vya kuchotea maji vyenye uwezo wa kuhudumia watu 19,080,000 vijijini na kufikisha vituo 155,934 vitakavyohudumia jumla ya watu 38,475,697 sawa na asilimia 80 ifikapo mwaka 2020. 263. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa huduma ya maji mijini, miradi mikubwa inayoendelea kutekelezwa katika Jiji la Dar es Salaam, inalenga maunganisho ya maji 500,000 majumbani, viwandani, Taasisi za Umma na shughuli za biashara ili kuongeza wastani wa upatikanaji wa huduma ya

Page 134: Tekeleza kwa

132

maji kutoka asilimia 68 za sasa hadi asilimia 95 ifikapo mwaka 2020. Vilevile, utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ikiwa ni pamoja na udhibiti wa wizi wa maji utapunguza upotevu wa maji kutoka asilimia 57 za sasa hadi asilimia 25 ifikapo mwaka 2020. 264. Mheshimiwa Spika, kwa Miji Mikuu 23 ya Mikoa; mpango unalenga maunganisho ya maji 200,000 ya majumbani yatakayohudumia watu 2,000,000 ifikapo mwaka 2020; kupunguza upotevu wa maji kutoka asilimia 35 za sasa hadi asilimia 25 kwa kipindi hicho; na hivyo, kuongeza wastani wa upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 86 za sasa hadi asilimia 98 ifikapo mwaka 2020. Aidha, katika Miji Mikuu ya Wilaya, Miji Midogo na maeneo yanayohudumiwa na Miradi ya Kitaifa; miradi iliyopangwa kutekelezwa inalenga maunganisho ya maji 110,000 ya majumbani yatakayohudumia jumla ya watu 1,100,000; hivyo kuongeza wastani wa upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 60 za sasa hadi asilimia 65 ifikapo mwaka 2020. 265. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa rasilimali za maji, hatua zitakazochukuliwa na Ofisi za Bodi za Maji za Mabonde nchini ni pamoja na kuyatambua, kuyatenga na kuyatangaza maeneo yote ya vyanzo vya maji kuwa hifadhi kisheria; kujenga mabwawa na visima virefu hasa kwenye maeneo kame; kuboresha utendaji wa maabara za maji ili kudhibiti viwango vya majisafi na majitaka; kuboresha mfumo wa utoaji wa vibali vya kutumia maji kwa shughuli za kijamii na kiuchumi kwenye mabonde yote; na kuboresha menejimenti ya takwimu za wingi na ubora wa maji kwenye mabonde yote.

Page 135: Tekeleza kwa

133

3.6 CHANGAMOTO NA HATUA ZINAZOCHUKULIWA 266. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Sekta ya Maji imekuwa na mafanikio hasa kwa upande wa utekelezaji wa miradi ya maji vijijini kupitia mpango wa BRN. Pamoja na mafanikio hayo, Sekta imeendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali. Maelezo kuhusu changamoto hizo pamoja na hatua zinazochukuliwa ni kama ifuatavyo:- 3.6.1 Uwekezaji mdogo kwenye miundombinu ya maji

ikilinganishwa na mahitaji ya kijamii na kiuchumi 267. Mheshimiwa Spika, Sekta ya Maji inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa huduma ya maji unaosababishwa na uwekezaji mdogo kwenye miundombinu ya maji ikilinganishwa na mahitaji ya kijamii na kiuchumi katika maeneo ya vijijini na mijini. Miji inakua kwa kasi kutokana na ongezeko la idadi ya watu, na kasi kubwa ya uwekezaji katika viwanda, biashara na ujenzi wa makazi. Vilevile, maeneo mengi ya miji mikuu ya wilaya, miji midogo na vijijini yanakua kwa kasi na idadi ya watu kuongezeka wakati huduma ya maji haitoshelezi. Ongezeko la watu mijini kitaifa ni wastani wa asilimia 4.5 kwa mwaka tofauti na maeneo ya vijijini ambapo wastani wa ongezeko la watu ni asilimia 2.3 kwa mwaka. Kwa Jiji la Dar es Salaam, ambalo linakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji lina ongezeko kubwa la watu la asilimia 6 kwa mwaka. Kasi kubwa ya ongezeko la idadi ya watu mijini na vijijini isiyowiana na uwekezaji kwenye miundombinu ya maji kumesababisha kuongezeka kwa mahitaji makubwa ya huduma ya maji nchini. Sababu zinazochangia changamoto ya uwekezaji mdogo usiolingana na mahitaji pamoja na hatua zinazochukuliwa zimefafanuliwa katika aya zifuatazo:-

Page 136: Tekeleza kwa

134

(a) Upatikanaji Mdogo wa Fedha kulinganisha na Bajeti

268. Mheshimiwa Spika, bajeti inayokasimiwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji haikidhi mahitaji halisi ya utekelezaji wa miradi. Vilevile, kiasi cha fedha kinachotolewa ni chini ya kiwango kilichokasimiwa. Kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo, fedha za maendeleo za ndani zilizotolewa zilikuwa ni kidogo ikilinganishwa na fedha zilizokasimiwa. Katika mwaka 2012/2013, jumla ya shilingi 140,015,967,000 zilikasimiwa ambapo fedha zilizotolewa zilikuwa ni shilingi 104,000,000,000 sawa na upungufu wa asilimia 25.7; kwa mwaka 2013/2014, kiasi cha shilingi 312,066,164,000 zilikasimiwa na kiasi kilichotolewa ni shilingi 166,000,000,000 sawa na upungufu wa asilimia 53.2. Katika mwaka 2014/2015, fedha zilizokasimiwa ni shilingi 312,066,164,000 na hadi mwezi Aprili, 2015 kiasi cha shilingi 82,390,507,067 zimetolewa sawa na asilimia 26.4. 269. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto ya upatikanaji mdogo wa fedha, Wizara yangu imeendelea kuwahamasisha Washirika wa Maendeleo wanaochangia Mfuko wa Pamoja wa Sekta ya Maji kuongeza michango yao. Vilevile, Wizara inaendelea kuwashawishi washirika wengine wa maendeleo kuchangia katika Sekta ya Maji ili kuongeza fedha kwenye bajeti ndogo inayoelekezwa kwa Sekta. Washirika hao ni pamoja na Serikali ya Watu wa China, Serikali ya India, na Mifuko ya Kimataifa ya Maendeleo kama Saudi Fund for Development na OFID, ambao wamechangia katika ujenzi wa Bwawa la Kidunda na mradi wa maji wa Same-Mwanga-Korogwe. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Maendeleo ya Kimataifa kama KfW na DFID inakamilisha taratibu za kuanza kupata fedha za kukamilisha miradi kupitia Mipango ya Output-

Page 137: Tekeleza kwa

135

Based Arrangement Funding kwa Mamlaka za Maji Mijini na Payments by Results Program kutekeleza miradi ya maji vijijini. Aidha, Serikali ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya Sheria ya Mfuko wa Maji itakayotumika kusimamia mfuko huo ambao ulianza kutekelezwa mwaka 2013/2014 lakini kukosa chombo cha usimamizi wake. (b) Ushiriki Hafifu wa Sekta Binafsi katika Sekta ya

Maji 270. Mheshimiwa Spika, ushiriki wa Sekta Binafsi umejikita zaidi katika ujenzi wa miundombinu ya maji na suala la uendeshaji na usimamizi wa miradi umebaki kwenye Mamlaka za Maji, Halmashauri na Vyombo vya Watumiaji Maji. Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuiwezesha Sekta Binafsi kuongeza ushiriki wake katika uendeshaji wa miradi ya maji vijijini na mijini kupitia Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (Public Private Partnership –PPP). Hatua hizo ni pamoja na kutunga Sera ya Taifa ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ya mwaka 2009, Sheria ya Ubia ya mwaka 2010 na Kanuni zake. Pamoja na jitihada za Serikali kuweka misingi hiyo, Sekta Binafsi bado haijahamasika vya kutosha katika kushiriki kwenye kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo miradi ya maji. 271. Mheshimiwa Spika, Wizara imeamua kuchukua juhudi za makusudi za kuhakikisha Sekta Binafsi inashiriki kikamilifu katika kubuni, kujenga, kusimamia na kuendesha miradi ya maji. Ili kutimiza azma hiyo, Mamlaka za Maji zitajengewa uwezo wa kuandaa miradi ya maji itakayoendeshwa na Sekta Binafsi. Vilevile, Wizara itawajengea uwezo wataalam wake kwa kuwapatia mafunzo yanayohusu Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi

Page 138: Tekeleza kwa

136

na uwekezaji. Katika mwaka 2015/2016, Wizara itaendelea kushirikiana na Washirika wa Maendeleo, Taasisi na Asasi mbalimbali ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira kupitia PPP. 3.6.2 Kupungua kwa Rasilimali za Maji 272. Mheshimiwa Spika, pamoja na nchi yetu kuwa na rasilimali za maji katika maeneo mengi, rasilimali hiyo imeendelea kupungua siku hadi siku na kusababisha uhaba wa maji kwa matumizi salama ya majumbani pamoja na shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Upungufu huo unasababishwa na uchafuzi wa vyanzo vya maji, uvamizi katika vyanzo vya maji kwa ajili ya shughuli za kibinadamu, matumizi holela ya maji na mabadiliko ya tabianchi. Uchafuzi wa vyanzo vya maji umekithiri hasa kutokana na utiririshaji majitaka kutoka viwandani, shughuli za uchimbaji madini na kilimo cha umwagiliaji. 273. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto ya kupungua kwa rasilimali za maji, Wizara yangu kwa kushirikiana na wadau wengine hususan NEMC imekuwa ikifanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maeneo ya viwanda, migodi na mabwawa ya kutibu majitaka ili kuhakikisha utupaji majitaka unafanyika kulingana na sheria, kanuni na taratibu za utunzaji mazingira ili kuvinusuru vyanzo vyetu visiendelee kuathiriwa. Vilevile, Wizara imeanza kutekeleza mpango wa kutunza na kuhifadhi vyanzo vya maji, kwa kubainisha na kuainisha vyanzo vilivyo katika hatari ya kuharibiwa ili maeneo hayo yawekewe mipaka na hatimaye kutangazwa kuwa maeneo tengefu. Hadi sasa jumla ya maeneo tisa yametangazwa kuwa maeneo tengefu na maeneo 31 yapo katika hatua za kutangazwa.

Page 139: Tekeleza kwa

137

274. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea kutoa elimu kwa watumiaji maji kuhusu Sheria ya Rasilimali za Maji na Kanuni zake zinazosimamia matumizi ya maji kwa lengo la kudhibiti matumizi holela. Kanuni hizo ni Regulations Regarding Water Abstraction, Use and Discharge Permits; na Ground Water (Exploration and Drilling) Licensing Regulations. Aidha, vyombo vya usimamizi wa rasilimali za maji vilivyosajiliwa kisheria vimeendelea kuimarishwa ili kuhakikisha rasilimali za maji zinagawanywa na kutumiwa kwa mujibu wa Sheria. 275. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali zikiwemo kujenga mabwawa madogo na makubwa kwa ajili ya kuhifadhi maji kwa matumizi mbalimbali; kuimarisha ukusanyaji wa takwimu zinazohusu rasilimali za maji na mabadiliko ya tabianchi; kutoa mafunzo kwa wataalam na kuelimisha umma ili kuongeza weledi kuhusu mabadiliko ya tabianchi; kutumia utaalam asilia (Indigenous knowledge) katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi; na kushirikiana na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali zinazofanya utafiti kuhusu mabadiliko ya tabianchi kwa lengo la kufanya utafiti wa pamoja na kutathmini matokeo ya tafiti hizo. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo inaandaa mipango itakayozingatia masuala ya athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo ni pamoja na;

(i) Mipango Shirikishi ya Uendelezaji na Usimamizi wa

Rasilimali za Maji (IWRM&DPs); na

(ii) Jukwaa la Majadiliano ya Athari za Mabadiliko ya Tabianchi katika Sekta ya Maji (Water Sector Climate Change Coordination Mechanism Dialogue Forum).

Page 140: Tekeleza kwa

138

3.6.3 Uendelevu wa Miradi ya Maji Vijijini 276. Mheshimiwa Spika, tathmini ya jumla ya miradi ya maji vijijini iliyofanyika mwaka 2013 kupitia mpango wa BRN, ilibaini kuwa vituo 14,800 vya kuchotea maji sawa na asilimia 40 ya vituo 37,000 vilivyojengwa zaidi ya miaka 20 iliyopita, vilikuwa havifanyi kazi. Vituo hivyo vilikuwa vihudumie jumla ya watu milioni 5.3 ya wakazi waishio vijijini. Sababu za vituo hivyo kutofanya kazi ni pamoja na:-

(i) Kukosekana kwa mipango ya uendeshaji na matengenezo wakati wa kuandaa miradi ya maji vijijini;

(ii) Uteuzi wa aina ya teknolojia sahihi kuendeleza

chanzo cha maji; (iii) Kutokupatikana kwa wakati kwa vipuri vya miradi ya

maji; (iv) Kiwango cha chini cha ufuatiliaji wa masuala ya

kiufundi; na

(v) Usimamizi hafifu wa makusanyo ya fedha za miradi. Kutokana na upungufu huo, Wizara yangu imeandaa Mkakati wa Uendelevu wa miradi ya maji vijijini (National Rural Water Supply Sustainability Strategy) ambao utekelezaji wake utaanza katika mwaka wa fedha 2015/2016. Mkakati huo unasisitiza yafuatayo:-

Page 141: Tekeleza kwa

139

(i) Kuunda Vyombo vya Watumiaji Maji (COWSOs) na kuhimiza wasajili kuongeza kasi ya usajili wa miradi iliyopo na mingine itakayojengwa;

(ii) Kuimarisha ukusanyaji wa takwimu sahihi za vituo vinavyotoa maji na visivyotoa maji kupitia mfumo wa kompyuta (Water Point Mapping System-WPMS);

(iii) Kusaidia matengenezo makubwa ambayo yapo nje ya uwezo wa Vyombo vya Watumiaji Maji (COWSOs); na

(iv) Kuwezesha kuwepo kwa maghala ya kuhifadhi vifaa na vipuri vya maji katika maeneo mbalimbali nchini pamoja na kuhakikisha uwepo wa wataalam na ushauri wa kitaalam katika maeneo ya vijijini.

3.6.4 Upotevu wa Maji 277. Mheshimiwa Spika, uendeshaji wa miradi ya maji umeendelea kuathirika kutokana na upotevu mkubwa wa maji ambao hadi sasa ni wastani wa asilimia 35 ya maji yanayozalishwa kwa Miji Mikuu ya Mikoa 23 na kwa upande wa Dar es Salaam upotevu huo ni asilimia 57. Kiwango cha upotevu wa maji kinachokubalika kimataifa ni asilimia 20. Upotevu huo husababishwa na hujuma kwenye miundombinu ya maji, wizi wa maji na miundombinu chakavu. Hali hiyo imesababisha Mamlaka hizo 23 za Maji Mijini kupoteza kila mwezi jumla ya shilingi bilioni 1.83 za mauzo ya maji na kwa Jiji la Dar es Salaam, jumla ya shilingi bilioni 2.64 hupotea kila mwezi. Upotevu huo wa mapato umesababisha Mamlaka za Maji Mijini kushindwa kulipia gharama za uendeshaji na matengenezo ya miundombinu na hivyo, Serikali kulazimika kubeba mzigo

Page 142: Tekeleza kwa

140

huo ili kuondoa kero ya uhaba wa maji kwenye maeneo mbalimbali nchini. 278. Mheshimiwa Spika, hatua zinazochukuliwa za udhibiti wa maji yanayopotea bila kulipiwa ni kwa Mamlaka za Maji Mijini kufunga dira za maji kwa wateja wote waliounganishiwa huduma ili kubaini matumizi yao halisi. Upotevu wa maji ni kiashiria kimojawapo kwenye Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa tarehe 02/02/2015 kati yangu na Wenyeviti wa Bodi za Mamlaka za Maji Mijini katika kutekeleza mpango wa BRN kwa maji mijini. Vilevile, Wizara imekamilisha rasimu ya mapitio ya Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Na. 11 na Sheria ya Huduma za Majisafi na Usafi wa Mazingira Na. 12 ili kuzipa nguvu zaidi za kukabiliana na watakaobainika kuhusika na wizi wa maji, vifaa na uharibifu wa miundombinu ya maji. Uboreshaji wa sheria hizo uko kwenye hatua za mwisho na utakapokamilika, miswada ya sheria hizo itawasilishwa kwenye Bunge lako Tukufu. 279. Mheshimiwa Spika, kwa Jiji la Dar es Salaam, Kikosi Maalum cha Wataalam wa Wizara na vyombo mbalimbali vya Dola, kiliundwa ili kubaini wezi wa maji na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria. Hadi mwezi Aprili 2015, kuna jumla ya kesi 163 zilizopo mahakamani na watuhumiwa 23 wa kesi hizo wamepewa adhabu mbalimbali zikiwemo kutumikia kifungo au kulipa faini na kesi zilizobaki zinaendelea.

Page 143: Tekeleza kwa

141

4.0 SHUKRANI 280. Mheshimiwa Spika, napenda sasa kuchukua fursa hii kuwashukuru wale wote waliochangia kuiwezesha Wizara yangu kufanikisha majukumu yake. Nakiri kwamba mafanikio yaliyopatikana katika mwaka 2014/2015 ni kutokana na jitihada za pamoja, ushirikiano na misaada ya kifedha na kitaalam kutoka kwa Wadau mbalimbali. Wadau hao ni pamoja na nchi wahisani, mashirika ya maendeleo ya kimataifa, taasisi zisizo za kiserikali, mashirika ya kidini, na taasisi za kifedha. Napenda kuzishukuru nchi rafiki zikiwemo Serikali za Ujerumani, Uholanzi, Uingereza, Marekani, Japan, Hispania, Ufaransa, China, Uswisi, Ubeligiji, Ireland, Korea Kusini, Sweden, Denmark, Norway, India, Misri, Saudi Arabia na Kuwait. 281. Mheshimiwa Spika, vilevile, natoa shukrani kwa taasisi za fedha za kimataifa na mashirika ya kimaendeleo kwa misaada ya fedha na ushirikiano wa kitaalam katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu na malengo ya Wizara yangu. Taasisi hizo ni pamoja na:- Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW), Benki ya Maendeleo ya Ufaransa (AFD), Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EIB), Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), Mfuko wa Maendeleo wa Nchi Zinazozalisha Mafuta (OPEC Fund for International Development-OFID), Mfuko wa Maendeleo wa Saudia (SFD), Umoja wa Ulaya (EU), Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Shirika la Misaada ya Maendeleo la Norway (NORAD), Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID), Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ), Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo (UNDP), Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA), Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Makazi

Page 144: Tekeleza kwa

142

Duniani (UN HABITAT), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Shirika la Misaada ya Maendeleo la Sweden (SIDA), Shirika la Misaada ya Maendeleo la Canada (CIDA), Shirika la Misaada ya Maendeleo la Denmark (DANIDA) na Shirika la Misaada la Marekani (USAID). 282. Mheshimiwa Spika, aidha, michango ya mashirika ya kidini imeongeza hamasa katika kuyafikia malengo tuliyojiwekea. Hivyo, napenda kuyashukuru mashirika hayo ya kidini ya World Islamic League, Shirika la Ahmadiya Muslim Jamaat Tanzania, Islamic Foundation, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Kanisa la Kilutheri la Ujerumani, Baraza Kuu la Waislam Tanzania, Kanisa Katoliki Tanzania, Kanisa la Kianglikana Tanzania, Catholic Agency for Overseas Aid and Development (CARITAS), Adventist Development Relief Agency (ADRA), Norwegian Church Aid na Livingwater International. Pia, nazishukuru taasisi zisizo za kiserikali za Tanzania Water and Sanitation Network (TAWASANET); Wahamasishaji wa Maji, Maendeleo na Afya (WAMMA); Southern Highlands Participatory Organizasition (SHIPO); WaterAid; World Vision; Plan International; Concern Worldwide; Netherlands Volunteers Services (SNV); Shirika la Kimataifa la Kuhifadhi Uasili na Mali Asili (IUCN); World Wide Fund for Nature (WWF); African Medical Research Foundation (AMREF); Clinton HIV Aids Initiative (CHAI); Bill and Melinda Gates Foundation; na wale wote ambao wameendelea kuisaidia Wizara ya Maji kufanikisha malengo yake. 283. Mheshimiwa Spika, pia, naomba nimshukuru Bw. Phillipe Dongier, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Burundi, Uganda na Tanzania anayemaliza muda wake. Kuwepo kwake nchini tangu mwaka 2012 hadi

Page 145: Tekeleza kwa

143

atakapomaliza rasmi muda wake tarehe 30/06/2015 kumewezesha Sekta ya Maji kupata mafanikio makubwa katika kuwapatia wananchi huduma ya maji vijijini na mijini. Napenda kumtakia heri na fanaka katika kituo chake kipya cha kazi. Aidha, nachukua fursa hii kumkaribisha Mkurugenzi Mkazi mpya, Bi. Bella Bird atakayeanza rasmi kazi tarehe 01/07/2015. Tunamuahidi kumpatia ushirikiano wa kutosha utakaozidi kuongeza chachu kwenye harakati za maendeleo ya nchi yetu. 284. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya kipekee kabisa naomba nitumie fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mhe. Amos Gabriel Makalla (Mb), Naibu Waziri wa Maji; Mhandisi Mbogo Futakamba, Katibu Mkuu; Wakurugenzi wote, Wakuu wa Vitengo, Wataalam na Watumishi wote wa Wizara; na Maafisa Watendaji Wakuu wa Mashirika, Wakala na Taasisi zilizo chini ya Wizara yangu kwa ushirikiano wanaonipatia pamoja na kujituma kwao kwa kusimamia utekelezaji wa majukumu yao kwenye Sekta ya Maji kwa kiwango cha hali ya juu. Napenda pia, nimshukuru aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Bashir Juma Mrindoko ambaye amestaafu kwa heshima. Ni matumaini yangu kuwa huko aliko kwa sasa anaendelea kuwa balozi mzuri wa Sekta ya Maji. 285. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya kipekee nachukua fursa hii kuishukuru sana familia yangu, akiwemo mke wangu mpenzi Kudra Maghembe na watoto wetu Dkt. Ngwaru Maghembe, Dkt. Mwanamkuu Maghembe, Namcheja na Namvumo Maghembe kwa upendo, ushirikiano pamoja na msaada wao katika kipindi chote na kuniwezesha kutekeleza majukumu yangu kwa ufanisi uliohitajika. Familia yangu inaendelea kuwa nguzo muhimu katika maisha yangu.

Page 146: Tekeleza kwa

144

286. Mheshimiwa Spika, vilevile, ninayo furaha kubwa kuendelea kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Mwanga ambao wamekuwa nami bega kwa bega katika kipindi chote cha miaka mitano iliyopita. Natumaini tutaendelea kushirikiana katika kipindi kijacho ili kuiletea maendeleo Wilaya yetu na Taifa kwa ujumla. Napenda kuwahakikishia kuwa nitaongeza nguvu zaidi ili Wilaya yetu ya Mwanga iwe moja ya Wilaya bora nchini. 5.0 MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2015/2016 287. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, naomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya shilingi 458,900,981,000 kwa ajili ya matumizi ya Wizara yangu kwa mwaka 2015/2016, ili Wizara iweze kutekeleza majukumu na malengo yaliyoelezwa katika hotuba hii. Kati ya fedha hizo, Matumizi ya Kawaida ni shilingi 31,643,077,000 ambapo shilingi 13,682,361,000 sawa na asilimia 43.3 ni kwa ajili ya kugharamia Matumizi Mengineyo (OC) na shilingi 17,960,716,000 sawa na asilimia 56.7 ni kwa ajili ya kulipa mishahara (PE) ya watumishi wa Wizara na Chuo cha Maji. Jumla ya bajeti ya maendeleo ni shilingi 427,257,904,000 ambapo kati ya fedha hizo shilingi 315,000,000,000 sawa na asilimia 74 ni fedha za ndani na shilingi 112,257,904,000 sawa na asilimia 26 ni fedha za nje. 288. Mheshimiwa Spika, naomba tena nitoe shukrani zangu kwako na kwa Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza. Hotuba hii pia inapatikana katika Tovuti ya Wizara kwa anwani: www.maji.go.tz. 289. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

Page 147: Tekeleza kwa

145

Jedwali Na. 1: Mwenendo wa Viwango vya Mvua katika

Mabonde Tisa Nchini kwa Kipindi cha Miaka Mitatu kuanzia Novemba, 2011 hadi Oktoba, 2014

Na Bonde

Kiwango cha Mvua (millimita) Novemba

2011-Oktoba

2012

Novemba 2012-

Oktoba 2013

Novemba 2013-

Oktoba 2014

1 Bonde la Pangani 782 720 817 2 Bonde la Rufiji 846 1,144 1,271

3 Bonde la Wami Ruvu 1,150 979 2,306

4 Bonde la Ziwa Tanganyika 705 917 1,116

5 Bonde la Ziwa Victoria 1,175 968 1,450

6 Bonde la Ruvuma na Pwani ya Kusini 917 835 801

7 Bonde la Ziwa Nyasa 1,356 1,643

8 Bonde la Kati 825 774

9 Bonde la Ziwa Rukwa 844 900

Page 148: Tekeleza kwa

146

Jedwali Na. 2: Vituo vya Kupima Mwenendo wa Maji

Bonde Aina ya Kituo

Vipy

a Vi

livyo

jeng

wa

Viliv

yoka

raba

tiwa

Vina

vyo

fany

a ka

zi

Vibo

vu

Jum

la

Rufiji Vya Mtoni 1 21 53 5 58 Maziwa/Mabwawa 0 0 0 0 3 Mvua 0 1 8 3 11 Hali ya Hewa 2 10 3 13

Pangani Vya Mtoni 0 54 54 0 54 Maziwa/Mabwawa 0 2 2 0 2 Mvua 0 5 31 0 36 Hali ya Hewa 0 8 8 0 8

Nyasa Vya Mtoni 0 4 31 3 34 Maziwa/Mabwawa 0 0 3 0 3 Mvua 0 0 14 0 14 Hali ya Hewa 0 0 5 1 6

Bonde la Kati Vya Mtoni 0 0 14 22 36 Maziwa/Mabwawa 0 0 2 2 4 Mvua 0 0 10 0 10 Hali ya Hewa 0 0 8 0 8

Rukwa Vya Mtoni 0 16 23 1 24 Maziwa/Mabwawa 0 0 2 0 2 Mvua 0 0 9 2 11

Page 149: Tekeleza kwa

147

Bonde Aina ya Kituo

Vipy

a Vi

livyo

jeng

wa

Viliv

yoka

raba

tiwa

Vina

vyo

fany

a ka

zi

Vibo

vu

Jum

la

Hali ya Hewa 0 0 5 1 6 Ruvuma Vya Mtoni 0 0 18 3 21

Maziwa/Mabwawa 0 0 0 0 0 Mvua 0 0 4 0 4 Hali ya Hewa 0 0 8 2 10

Tanganyika Vya Mtoni 0 0 23 6 29 Maziwa/Mabwawa 0 0 3 0 3 Mvua 0 0 15 7 22 Hali ya Hewa 0 1 6 7 14

Lake Victoria Vya Mtoni 0 2 16 7 23 Maziwa/Mabwawa 0 0 2 3 5 Mvua 0 0 33 5 37 Hali ya Hewa 2 1 12 5 17

Wami/Ruvu Vya Mtoni 0 3 28 14 42 Maziwa/Mabwawa 0 0 1 0 1 Mvua 0 0 49 2 51 Hali ya Hewa 0 0 5 6 11

JUMLA 5 118 515 110 633

Page 150: Tekeleza kwa

148

Jedwali Na. 3: Vyanzo Vilivyowekewa Mipaka (Demarcated Water Sources) na Vilivyo Katika Hatua Mbalimbali za Kuwekewa Mipaka

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

Rufiji 1 Bwawa la Mtera

Kwa Matumizi ya uzalishaji umeme

Iringa, Chamwino na Mpwapwa

Nguzo za zege

Umbali wa kilomita 155.3

Bado

Rukwa 2 Mto Katandala

Bwawa la Kawa

Rukwa, Nkasi

Nguzo za zege (sio za kudumu)

Mita za mraba 2,200,000

Bado

3 Mto Kausi Bwawa la Milala

Katavi, Mpanda

Fito (sio za kudumu zenye urefu wa mita 1.5) kuzunguka chanzo

Mita za mraba 2,300,000

Limetangazwa

Page 151: Tekeleza kwa

149

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

4 Kisima cha Chokaa

Mji wa Chunya

Mbeya, Chunya

Fito (sio za kudumu zenye urefu wa mita 1.5)

Mita za mraba 95,928

Kimetangazwa

5 Kisima cha Kidole

Mji wa Chunya

Chunya Fito (sio za kudumu zenye urefu wa mita 1.5)

Mita za mraba 13,084

Kimetangazwa

6 Kisima cha Kiswaga

Mji wa Chunya

Chunya Fito (sio za kudumu zenye urefu wa mita 1.5)

Mita za mraba 29,831

Kimetangazwa

7 Kisima cha Matundasi A

Kijiji cha Matundasi

Mbeya, Chunya

Fito (sio za kudumu zenye urefu wa mita 1.5)

Mita za mraba 7,794

Kimetangazwa

Page 152: Tekeleza kwa

150

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

8 Kisima cha Matundasi B

Kijiji cha Matundasi

Mbeya, Chunya

Fito (sio za kudumu zenye urefu wa mita 1.5)

Mita za mraba 12,047

Kimetangazwa

9 Kisima cha Mkola

Kijiji cha Makongolosi

Mbeya/Chunya

Fito (sio za kudumu zenye urefu wa mita 1.5) kuzunguka kisima

Mita za mraba 200,000

Kimetangazwa

10 Mto Halewa/Swaya

Mji wa Mbeya

Mwasanga Mbeya mjini

Beacon na kupanda miti

Mita za mraba 16,226

Bado

11 Mto Mfwizimo/Iziwa

Mji wa Mbeya

Iziwa, Mbeya peak, Mbeya mjini na

Beacon na kupanda miti

Mita za mraba 11,572

Bado

Page 153: Tekeleza kwa

151

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

kijiji cha Mpomu Mbeya vijijini

12 Mto Nzovwe Mji wa Mbeya

Kata ya Mwakibete, Mbeya Mjini

Beacon na kupanda miti kuzunguka eneo

Mita za mraba 260,000

Bado Chanzo kmetunzwa

13 Mto Ivumwe Mji wa Mbeya

Kata ya Mwakibete mtaa wa Ivumwe Mbeya mjini

Beacon za kudumu, kupanda miti eneo la chanzo

Mita za mraba 118,000

Bado Chanzo kimetunzwa vizuri

14 Mto Imeta Mji wa Mbeya

Kata ya Mwansekwa Mbeya mjini

Beacon za kudumu, kupanda miti eneo la

Mita za mraba 178,000

Bado Shughuli za kibinadamu zinaendelea sehemu za juu

Page 154: Tekeleza kwa

152

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

chanzo za chanzo

15 Mto Hanzya Mji wa Mbeya

Kata ya Nsoho Mbeya mjini

Beacon za kudumu, kupanda miti eneo la chanzo

Mita za mraba 279,000

Bado

16 Mto Mfwizimo/Lunji

Mji wa Mbeya

Iziwa Mbeya Mjini

Beacon za kudumu, kupanda miti eneo la chanzo

Mita za mraba 82,653

Bado

17 Mto Sisimba Mji wa Mbeya

Kijiji cha Iganzo Mbeya Mjini

Beacon za kudumu, kupanda miti eneo la chanzo

Mita za mraba 104,000

Bado Shughuli za kibinadamu zinaendelea sehemu za juu za chanzo

Page 155: Tekeleza kwa

153

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

Pangani 18 Chemichemi ya Miwaleni

Moshi Vijijini

Kahe na Kiruavunjo Kusini

Kupanda miti

Upimaji Unaendelea

Bado Shughuli za kibinadamu za kilimo na ufugaji zinaendelea

19 Chemichemi ya Kinamiri

Wilaya ya Hai

Kata za Lyamungo na Masama

Kupanda miti na beacons

Upimaji unaendelea

Bado Shughuli za kibinadamu za kilimo na ufugaji. Beacons zimetolewa

20 Chemichemi ya Soko

Moshi Vijijini

Moshi Vijijini

Kupanda miti

Upimaji unaendelea

Bado Shughuli za kibinadamu za kilimo na ufugaji zinaendelea

21 Chemichemi ya Shiri

Wilaya ya Hai

Wilaya ya Hai

Kupanda miti na kuzungushia uzio wa

Upimaji unaendelea

Bado

Page 156: Tekeleza kwa

154

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

senyenge

22 Chemichemi ya Nsere

Wilaya ya Hai

Wilaya ya Hai

Kupanda miti na kuzungushia uzio wa senyenge

Upimaji unaendelea

Bado

23 Chemichemi ya Saaki

Wilaya ya Hai

Wilaya ya Hai

Kupanda miti

Upimaji unaendelea

Bado

24 Eneo la unyevu la Boloti swamp

Wilaya ya Hai

Wilaya ya Hai

Kupanda miti

Upimaji unaendelea

Bado Shughuli za kibinadamu za kilimo na ufugaji. Beacons zimetolewa

Page 157: Tekeleza kwa

155

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

25 Eneo la unyevu Kwalesengui swamp

Wilaya ya Siha

Wilaya ya Siha

Nguzo za zege (Beacons)

Upimaji unaendelea

Bado Shughuli za kibinadamu za kilimo na ufugaji. Beacons zimetolewa

26 Eneo la kuchimba visima

Wilaya ya Same

Wilaya ya Same

Nguzo za zege (Beacons)

Upimaji unaendelea

Bado

27 Mawoi Wilaya ya Hai

Kijiji cha Roo

Kupanda miti

Upimaji unaendelea

Bado Shughuli za kibinadamu za kilimo na ufugaji. Beacons zimetolewa kwa baadhi ya vijiji

Page 158: Tekeleza kwa

156

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

28 Eneo oevu la Kiamboni

Wilaya ya Hai

Kijiji cha Roo

Kupanda miti

Upimaji Unaendelea

Bado

29 Eneo oevu la Chago

Same Kata ya Chome, Kijiji cha Gwan’ga

Kupanda miti na Kuzungushia uzio wa senyenge

Upimaji Unaendelea

Bado

30 Eneo oevu la Nkwatuma

Wilaya ya Hai

Kijiji cha Roo

Kupanda miti 10,000

Upimaji Unaendelea

Bado Uharibifu umepungua na wananchi wanafanya kilimo cha ufugaji nyuki

31 Chemichemi ya Mtakuro

Wilaya ya Hai

Wilaya ya Hai

kupanda miti 500

Upimaji Unaendelea

Bado Uharibifu umepungua na wananchi wanafanya kilimo cha ufugaji nyuki

Page 159: Tekeleza kwa

157

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

32 Mto Kihuhwi Muheza Kijiji cha Bombani

kupanda miti

Upimaji Unaendelea

Bado

33 Mto Kwemdimu

Muheza Kijiji cha Kwemdimu

kupanda miti

Upimaji Unaendelea

Bado

34 Mto Zigi Muheza Kijiji cha Mangugu

kupanda miti

Upimaji Unaendelea

Bado Utumiaji wa sumu katika kuvua samaki(dawa ya kuogeshea ng’ombe na mmea aina ya belesi vinatumika)

35 Mto Zigi Muheza Kijiji cha Kiwanda

kupanda miti

Upimaji unaendelea

Bado Utumiaji wa sumu katika kuvua samaki(dawa ya kuogeshea ng’ombe na

Page 160: Tekeleza kwa

158

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

mmea aina ya belesi vinatumika)

36 Mto Sengele Muheza Kijiji cha IBC na Magoda

kupanda miti

Upimaji unaendelea

Bado

37 Mto Mkulumuzi

Tanga Kijiji cha Kiomoni

kupanda miti

Upimaji unaendelea

Bado

38 Eneo la kuchimba visima la Mwankoko

Mji wa Singida

Singida Nguzo za zege (Beacons)

Kilomita za mraba 7.5

Bado hatua za kulipa fidia zinafuata

Page 161: Tekeleza kwa

159

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

Bonde la Kati

39 Eneo la kuchimba visima la Maisaka

Mji wa Babati

Babati Nguzo za zege (Beacons)

Kilomita za mraba 0.242

Bado Wananchi walifungua kesi mahakamani Fedha za Fidia kwa baadhi ya Wananchi zimelipwa

40 Chemichemi ya Ndengu

Kijiji cha Kiheleketi

Mbinga eneo limeanishwa kwa ajili ya kuwekewa mipaka hivi karibuni

Hekta 16 Bado

Nyasa 41 Mkele na Lupembe A,B,C,and D

Vijiji vya Kihulila, na Tukuzi

Mbinga miti 20,000 ya kupanda

Hekta 700 Bado

42 Mito ya Toze na Mnyoro

Vijiji 15, Njombe

Nguzo za zege

Kilomita za maraba 10

Bado

Page 162: Tekeleza kwa

160

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

43 Chemichemi ya Mbwinji

Miji ya Masasi na Nachingwea

Vijiji vya Newala (Makonde Plateau) na vijiji vya Masasi

Beacons za zege na mabango ya chuma yamewekwa

Kilomita za mraba 169

Bado Eneo limeunganisha chemichemi za Nahinga na Mwena na kuna wananchi wanadai fidia ambayo ilitolewa ahadi na serikali toka miaka ya themanini kabla Bonde halijaweka mipaka hiyo

Ruvuma

44 Eneo la kuchimba visima la Mitema

Mji wa Newala na baadhi ya Vijiji vyake

Kitangari - Mitema

Beacons za zege

Mita za mraba 10,000

Bado Eneo la chanzo lilikua makazi ya watu kabla ya maji chini ya

Page 163: Tekeleza kwa

161

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

ardhi hayajapanda juu ya ardhi na kutengeneza chemichemi iliyopo sasa hivyo maeneo mengi yana mazao ya kudumu hasa mikorosho ambayo inahitaji fidia kwa wananchi

45 Chemichemi ya Chipwapwa

Lindi Vijijini

Kijiji cha Chipwapwa

Beacons za zege

Upimaji unaendelea

Bado Maeneo yana wakulima wakubwa wa nyanya

46 Mto Liwale Mji wa Liwale

Jumla ya vijiji (16)

Beacons za zege na

Upimaji unaendelea

Bado Asilimia zaidi ya 90 ya

Page 164: Tekeleza kwa

162

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

kuanzia Kijiji cha Mpigamiti (UPS) hadi kijiji cha Kikulyungu (DNS)

mabango ya chuma yamewekwa

maeneo yaliyowekewa beacons na signboards yanahitaji idadi kubwa sana ya miche kwa ajili ya kuhakikisha maeneo hayo yaliyoharibiwa yanarudi katika hali yake ya zamani ya uoto wa asili

47 Chanzo cha maji Kapripoint

Mji wa Mwanza, Wilaya za NyamaganaIlemela

Wilaya ya Nyamagana eneo la Capri-point

Fensi ya miti ya kupanda

Kilomita za mraba 30

Bado

Page 165: Tekeleza kwa

163

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

na Misungwi

Ziwa Viktoria

48 Eneo la kuchukilia maji ziwani la Bunena na custom

Manispaa ya Bukoba

Kata ya Bukoba mitaa ya Bunena, na Kafuti

Fensi ya miti ya kupanda

Upimaji unaendelea

Bado

49 Chemichemi ya Nyakanasi na Kisindi

Manispaa ya Bukoba

Nyakanasi na Kisindi

Fensi ya miti ya kupanda

Upimaji unaendelea

Bado

50 Eneo la kuchukilia maji ziwani la Mkinyelelo, New Bukanga

Manispaa ya Musoma

Kata za Mwisenge na Makoko

Fensi ya miti ya kupanda

Kilomita za mraba 8.4 Mkinyelelo na Kilomita za mraba 14.4 Bukanga

Bado

51 Mto Simiyu Wilaya za Vijiji 100 Kupanda Kilomita za Bado Kazi hii

Page 166: Tekeleza kwa

164

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

Meatu, Maswa, Bariadi, Itilima, Busega na Magu

katika wilaya za Meatu, Maswa, Bariadi, Itilima, Busega na Magu

miti kuzunguka eneo la mita 60 kutoka kingo za mito pamoja na kupanda katani na kuweka beacons za zege

mraba 21.6 imefanyika chini ya Mradi wa LVEMP. Shughuli za kilimo na ufugaji na utashi wa wanasiasa vimekuwa changamoto kubwa

Page 167: Tekeleza kwa

165

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

52 Eneo la kuchukilia maji ziwani la Ihelele

Mji wa Shinyanga, Wilaya za Kahama na Misungwi na vijiji kando kndo ya Mtandao wa bombakuu

Ihelele Upandaji miti

Bado uchimbaji madini, kilimo na ufugaji vinaendelea

53 Eneo la kuchimba visima la Kwimba (well fields)

Mji wa Ngudu

Kupanda miti, beacons za zege

Upimaji unaendelea

Bado uvamizi kwa ajili ya makazi, kilimo na ufugaji vinaendelea

Page 168: Tekeleza kwa

166

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

54 Mto Kizinga Mipaka imewekwa katika baadhi ya sehemu za mto – mita 60 kutoka kingo za mito

Upimaji unaendelea

Bado

Page 169: Tekeleza kwa

167

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

Wami/ Ruvu

55 Mto Mlali (unaingiza maji katika Bwawa la Mindu)

Bwawa la Mindu

Wilaya ya Mvomero

Mimea ya katani imepandwa umbali wa mita 60 kutoka kingo za Mto, miti ya mbao 1500, na miti ya matunda 400 imepandwa umbali wa mita 30 kutoka kingo za mto Mlali

Upimaji unaendelea

Bado Maeneo mengine ya mito inayoingiza maji katika bwawa la Mindu yanatakiwa kuwekewa mipaka. Miti mingine ya mbao 1600 na ya matunda 400 imenunuliwa itapandwa baada ya kutambua idadi ya wakulima

Page 170: Tekeleza kwa

168

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

wenye mashamba ndani ya mita 60 kutoka kingo za mto.

Page 171: Tekeleza kwa

169

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

56 Mto Morogoro

Mambogo Manispaa ya Morogoro

Mabango ya makatazo manne yamesimikwa kandokando ya Mto Morogoro kuzuia shughuli za kibinadamu zisifanyike ndani ya mita 60

Upimaji unaendelea

Bado Mipaka ya kudumu inatakiwa kuwekwa ili kuonyesha umbali wa mita 60

57 Bwawa la Mindu

Bwawa la Mindu

Manispaa ya Morogoro

Beacons zimewekwa umbali wa mita 500 kutoka

Upimaji unaendelea

Bado Utashi wa wanasiasa unazuia zoezi la kufufua beacons, Eneo

Page 172: Tekeleza kwa

170

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

ujazo wa Bwawa kuonyesha mpaka, mimea ya katani imepandwa kuzunguka nusu ya eneo la hifadhi

lingine oevu juu ya Bwawa linatakiwa kuongezwa katika eneo la awali la hifadhi

58 Mto Wami Mto Wami Wilaya Kilosa–Wami Dakawa

Miti ya mbao 3000 imepandwa kandoni mwa Mto Wami ndani ya mita 60 kutoka kingo za

Upimaji unaendelea

Bado Upandaji wa miti unaendelea na miti zaidi inatakiwa

Page 173: Tekeleza kwa

171

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

Mto katika eneo la Wami/Dakawa. Mabango ya makatazo sita yamesimikwa katika eneo la Rudewa kuzuia shughuli za kibinadamu kandokando ya Mto Wami

Page 174: Tekeleza kwa

172

Bonde Na.

Jina la Chanzo

Chanzo cha Maji

kwa matumizi/

eneo/ mji/kijiji

Maeneo yaliyozungushiwa

Aina ya mipaka

Eneo la chanzo

lililowekwa mipaka

Kutangazwa eneo kweye

gazeti Maoni/

Changamoto

59 Makutopora well field

Maji chini ya ardhi-Mzakwe

Mzakwe, Mamba, Mchemwa na Gawaye

Kuweka nguzo (beacons) 1,700 katika eneo la kilomita za mraba 85.

Kilomita za mraba 85

Limetangazwa

Page 175: Tekeleza kwa

173

Jedwali Na. 4 : Makusanyo ya Maduhuli mwaka 2014/2015 na Makadirio ya Makusanyo kutoka Bodi za Maji za Mabonde kwa Mwaka 2015/2016

Na. Bonde Makusanyo 2014/2015

Makadirio 2015/2016

1 Pangani 301,267,150 370,000,000 2 Wami/Ruvu 130,027,729 320,000,000 3 Rufiji 599,694,080 723,000,000 4 Ruvuma 154,858,685 170,000,000 5 Ziwa Nyasa 140,989,162 350,000,000 6 Bonde la Kati 167,884,807 300,000,000 7 Ziwa Rukwa 215,309,410 350,000,000 8 Ziwa Tanganyika 63,068,557 90,000,000 9 Ziwa Victoria 240,725,106 350,000,000

Jumla 2,013,824,685 3,023,000,000

Page 176: Tekeleza kwa

174

Jedwali Na. 5a:- Mgawo wa Fedha zitakazotumwa katika Halmashauri za Wilaya Nchini katika mwaka 2015/2016 kutekeleza Miradi ya Maji Vijijini

Miradi ya Vijiji 10

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

Arusha

1 Arusha MC 394,730,921 117,963,555 512,694,476 2 Arusha DC 481,314,116 175,097,941 656,412,057 3 Karatu DC 315,157,650 202,055,525 517,213,175 4 Longido DC 312,347,823 148,805,222 461,153,045 5 Meru DC 482,038,297 245,036,659 727,074,956 6 Monduli DC 589,219,705 199,933,487 789,153,192 7 Ngorongoro DC 200,123,455 251,443,553 451,567,008

Jumla ndogo 2,774,931,968 1,340,335,942 4,115,267,910

Dar es Salaam

8 Ilala MC 355,940,831 103,414,762 459,355,593 9 Kinondoni MC 258,855,292 172,337,184 431,192,476 10 Temeke MC 570,893,843 172,342,323 743,236,166

Jumla ndogo 1,185,689,966 448,094,269 1,633,784,235

Dodoma

11 Bahi DC 346,222,222 125,799,134 472,021,356 12. Chamwino DC 380,889,666 219,491,319 600,380,985 13 Chemba DC 207,834,244 245,991,230 14 Dodoma MC 317,340,000 99,883,453 417,223,453 15 Kondoa DC 470,940,469 209,307,891 680,248,360 16 Kongwa DC 380,000,000 282,239,284 662,239,284

Page 177: Tekeleza kwa

175

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

17 Mpwapwa DC 444,882,932 173,495,423 618,378,355 Jumla ndogo 2,548,109,533 1,356,207,734 3,904,317,267

Geita

18 Bukombe DC 95,789,000 302,564,037 398,353,037 19 Chato DC 623,456,782 332,277,227 955,734,009 20 Geita DC 648,288,305 289,019,281 937,307,586 21 Geita TC 236,572,648 216,143,550 452,716,198 22 Mbogwe DC 476,666,221 362,134,780 838,801,001 23 Nyang'wale DC 422,245,644 332,305,101 754,550,745

Jumla ndogo 2,503,018,600 1,834,443,976 4,337,462,576

Iringa

24 Iringa DC 370,000,000 259,355,221 629,355,221 25 Iringa MC 167,744,221 190,548,562 358,292,783 26 Kilolo DC 249,000,000 299,959,374 548,959,374 27 Mufindi DC 155,566,778 252,145,772 407,712,550

Jumla ndogo 942,310,999 1,002,008,929 1,944,319,928

Kagera

28 Biharamulo DC 259,877,827 246,506,325 506,384,152 29 Bukoba DC 439,161,855 384,555,873 823,717,728 30 Bukoba MC 92,848,729 83,296,377 176,145,106 31 Karagwe DC 368,540,232 375,205,468 743,745,700 32 Kyerwa DC 177,855,533 353,076,391 530,931,924 33 Misenyi DC 367,889,000 270,165,899 638,054,899 34 Muleba DC 119,792,535 349,695,150 469,487,685 35 Ngara DC 323,240,176 137,194,914 460,435,090

Jumla ndogo 2,149,205,886 2,199,696,397 4,348,902,283

Page 178: Tekeleza kwa

176

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

Katavi

36 Mlele DC 422,848,166 399,533,811 822,381,977 37 Mpanda DC - 385,922,762 385,922,762 38 Mpanda TC - 174,215,324 174,215,324 39 Nsimbo DC 556,716,064 306,618,971 863,335,035

Jumla ndogo 979,564,230

1,266,290,868

2,245,855,098

Kigoma

40 Buhigwe DC 133,346,780 390,358,470 523,705,250 41 Kakonko DC 401,003,998 290,358,874 691,362,872 42 Kasulu DC 594,655,018 298,419,930 893,074,948 43 Kibondo DC 567,349,184 305,187,730 872,536,914 44 Kigoma DC 257,327,509 317,855,799 575,183,308 45 Kigoma/Ujiji MC 78,135,747 77,533,709 155,669,456 46 Uvinza DC 264,762,423 343,784,907 608,547,330

Jumla ndogo 2,296,580,659 2,023,499,419 4,320,080,078

Kilimanjaro

47 Hai DC 296,000,000 198,509,650 494,509,650 48 Moshi DC 170,000,000 261,038,248 431,038,248 49 Moshi MC 334,000,600 169,686,130 503,686,730 50 Mwanga DC 300,667,800 357,109,376 657,777,176 51 Rombo DC 300,982,256 356,136,011 657,118,267 52 Same DC 411,706,693 250,403,878 662,110,571 53 Siha DC 213,463,753 138,356,539 351,820,292

Jumla ndogo 2,026,821,102 1,731,239,832 3,758,060,934 Lindi 54 Kilwa DC 40,730,288 383,056,711 423,786,999

Page 179: Tekeleza kwa

177

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

55 Lindi DC 406,736,556 361,907,613 768,644,169 56 Lindi TC 92,445,907 109,170,613 201,616,520 57 Liwale DC 125,319,607 315,202,424 440,522,031 58 Nachingwea DC 145,990,432 379,106,538 525,096,970 59 Ruangwa DC 340,000,000 39,445,662 779,445,662

Jumla ndogo 1,151,222,790 1,987,889,561 3,139,112,351

Manyara

60 Babati DC 111,577,009 230,920,157 342,497,166 61 Babati TC 80,211,938 88,269,098 168,481,036 62 Hanang DC 233,677,897 411,544,636 645,222,533 63 Kiteto DC 273,334,422 368,152,853 641,487,275 64 Mbulu DC 151,106,370 356,053,490 507,159,860 65 Simanjiro DC 300,000,005 441,401,876 741,401,881

Jumla ndogo 1,149,907,641 1,896,342,110 3,046,249,751

Mara

66 Bunda DC 293,799,607 450,613,499 744,413,106 67 Butiama DC 377,880,004 260,161,551 638,041,555 68 Musoma DC 383,732,738 351,465,380 735,198,118 69 Musoma MC - - - 70 Rorya DC 270,903,068 184,321,028 455,224,096 71 Serengeti DC 204,829,602 154,009,415 358,839,017 72 Tarime DC 347,788,006 244,034,238 591,822,244 73 Tarime TC 81,200,003 197,444,034 278,644,037

Jumla ndogo 1,960,133,029 1,842,049,145 3,802,182,174 Mbeya 74 Busokelo DC 449,392,456 194,888,069 644,280,525

Page 180: Tekeleza kwa

178

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

75 Chunya DC 526,384,762 186,753,302 713,138,064 76 Ileje DC 473,675,792 308,940,534 782,616,326 77 Kyela DC 352,803,815 144,974,825 497,778,640 78 Mbarali DC 211,556,808 245,529,350 457,086,158 79 Mbeya CC 80,339,971 172,009,001 252,348,972 80 Mbeya DC 442,486,416 277,135,552 719,621,968 81 Mbozi DC 298,690,755 151,632,817 450,323,572 82 Momba DC 416,691,691 245,991,230 662,682,921 83 Rungwe DC 477,889,900 252,338,816 730,228,716 84 Tunduma TC 77,032,131 148,019,349 225,051,480

Jumla ndogo 3,806,944,496 2,328,212,845 6,135,157,341

Morogoro

85 Gairo DC 213,555,778 221,200,264 434,756,042 86 Kilombero DC 302,638,472 258,316,136 560,954,608 87 Kilosa DC 427,367,579 272,396,468 699,764,047 88 Morogoro MC 78,038,140 117,081,941 195,120,081 89 Morogoro DC 432,111,660 367,388,414 799,500,074 90 Mvomero DC 303,339,971 377,230,866 680,570,837 91 Ulanga DC 264,248,641 336,669,048 600,917,689

Jumla ndogo 2,021,300,241 1,950,283,137 3,971,583,378

Mtwara

92 Masasi DC 416,691,691 197,444,034 614,135,725 93 Masasi TC 79,222,555 199,232,218 278,454,773 94 Mtwara DC 307,032,131 183,846,349 490,878,480 95 Mtwara MC 93,615,157 360,034,148 453,649,305

Page 181: Tekeleza kwa

179

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

96 Nanyumbu DC 565,281,213 103,914,954 669,196,167 97 Newala DC 140,000,000 251,906,905 391,906,905 98 Tandahimba DC 131,000,000 332,332,068 463,332,068

Jumla ndogo 1,732,842,747 1,628,710,676 3,361,553,423

Mwanza

99 Ilemela MC 411,093,972 371,985,013 783,078,985 100 Kwimba DC 459,422,623 122,173,211 581,595,834 101 Magu DC 550,857,812 302,997,760 853,855,572 102 Misungwi DC 352,853,748 176,654,743 529,508,491 103 Mwanza CC 104,342,643 345,436,059 449,778,702 104 Sengerema DC 312,431,726 225,866,851 538,298,577 105 Ukerewe DC 466,509,417 132,385,815 598,895,232

Jumla ndogo 2,657,511,941 1,677,499,452 4,335,011,393

Njombe

106 Ludewa DC 248,824,075 245,991,230 494,815,305 107 Makambako TC 430,000,000 80,836,627 510,836,627 108 Makete DC 382,211,000 201,884,499 584,095,499 109 Njombe DC 473,334,588 370,296,072 843,630,660 110 Njombe TC 564,117,277 218,232,922 782,350,199 111 Wangingombe DC 100,087,442 289,466,529 389,553,971

Jumla ndogo 2,198,574,382 1,406,707,879 3,605,282,261

Pwani

112 Bagamoyo DC 222,556,009 370,820,373 593,376,382 113 Kibaha DC 375,000,000 170,863,214 545,863,214 114 Kibaha TC 375,000,000 147,912,456 522,912,456 115 Kisarawe DC 109,936,240 314,114,572 424,050,812

Page 182: Tekeleza kwa

180

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

116 Mafia DC 267,755,080 283,343,799 551,098,879 117 Mkuranga DC 370,000,000 184,641,201 554,641,201 118 Rufiji DC 400,000,000 212,193,054 612,193,054

Jumla ndogo 2,120,247,329 1,683,888,669 3,804,135,998

Rukwa

119 Kalambo DC 443,234,500 116,162,972 559,397,472 120 Nkasi DC 300,000,000 157,110,306 457,110,306 121 Sumbawanga DC 520,000,000 181,300,485 701,300,485 122 Sumbawanga MC 250,000,000 172,230,090 422,230,090

Jumla ndogo 1,513,234,500 626,803,853 2,140,038,353

Ruvuma

123 Mbinga DC 354,395,714 218,383,556 572,779,270 124 Namtumbo DC 233,498,550 245,991,230 479,489,780 125 Nyasa DC 164,280,300 265,106,463 429,386,763 126 Songea DC 412,424,860 186,670,119 599,094,979 127 Songea MC 78,555,322 181,219,977 259,775,299 128 Tunduru DC 277,640,004 220,102,120 497,742,124

Jumla ndogo 1,520,794,750 1,317,473,465 2,838,268,215

Shinyanga

129 Kahama TC 80,665,220 177,097,667 257,762,887 130 Kishapu DC 327,600,000 271,426,264 599,026,264 131 Msalala DC 211,889,000 215,793,504 427,682,504 132 Ushetu DC 261,989,821 286,661,649 548,651,470 133 Shinyanga DC 285,957,329 184,784,791 470,742,120 134 Shinyanga MC 207,741,722 245,586,599 453,328,321

Page 183: Tekeleza kwa

181

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

Jumla ndogo 2,896,637,843 1,381,350,474 4,277,988,317

Simiyu

135 Bariadi TC 89,444,425 118,621,642 208,066,067 136 Bariadi DC 302,716,416 171,659,359 474,375,775 137 Busega DC 312,426,609 172,151,228 484,577,837 138 Itilima DC 220,097,444 117,932,885 338,030,329 139 Maswa DC 140,206,182 199,973,109 340,179,291 140 Meatu DC 351,526,021 219,081,364 570,607,385

Jumla ndogo 1,416,417,096 999,419,587 2,415,836,683

Singida

141 Ikungi DC 300,056,668 185,075,688 485,132,356 142 Iramba DC 329,242,041 187,442,090 516,684,131 143 Manyoni DC - 150,459,627 150,459,627 144 Mkalama DC 206,700,009 128,298,153 334,998,162 145 Singida DC 249,864,740 74,331,872 324,196,612 146 Singida MC 362,376,329 245,766,140 608,142,469

Jumla ndogo 2,864,656,883 971,373,570 3,836,030,453

Tabora

147 Igunga DC 545,889,000 122,762,521 668,651,521 148 Kaliua DC 223,079,643 107,495,197 330,574,840 149 Nzega DC 311,453,153 273,577,828 585,030,981 150 Sikonge DC 281,530,930 283,623,356 565,154,286 151 Tabora MC 82,111,229 152,930,920 235,042,149 152 Urambo DC 207,330,000 174,598,144 381,928,144 153 Uyui/Tabora DC 111,000,876 297,338,726 408,339,602

Jumla ndogo 1,762,394,830 1,412,326,692 3,174,721,522

Page 184: Tekeleza kwa

182

Mkoa Na. Halmashauri Aina Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

Tanga

154 Bumbuli DC 290,000,000 246,357,513 536,357,513 155 Handeni DC 203,343,832 297,011,497 500,355,329 156 Handeni TC 83,567,880 233,000,301 316,568,181 157 Kilindi DC 165,000,000 193,019,369 358,019,369 158 Korogwe DC 211,000,444 288,875,059 499,875,503 159 Korogwe TC 90,000,000 261,245,038 351,245,038 160 Lushoto DC 290,000,000 234,934,829 524,934,829 161 Mkinga DC 166,778,000 200,509,192 367,287,192 162 Muheza DC 208,897,766 180,092,232 388,989,998 163 Pangani DC 309,999,805 276,229,110 586,228,915 164 Tanga CC 83,343,832 276,577,379 359,921,211

Jumla ndogo 2,101,931,559 2,687,851,519 4,789,783,078 Jumla kwa Halmashauri 50,280,985,000 39,000,000,000 89,280,985,000

Page 185: Tekeleza kwa

183

Jedwali Na. 5b:- Mgawo wa Fedha zitakazotumwa katika Sekretarieti za Mikoa Nchini katika mwaka 2015/2016 kwa ajili ya Usimamizi wa Miradi ya Maji Vijijini

S/N Mkoa Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

1 Arusha 20,378,933 40,757,866 61,136,798 2 Dar es Salaam 15,888,786 31,777,573 47,666,359 3 Dodoma 19,564,322 39,128,643 58,692,965 4 Geita 19,987,419 39,974,837 59,962,256 5 Iringa 18,704,465 37,408,931 56,113,396 6 Kagera 20,704,465 41,408,931 62,113,396 7 Katavi 18,787,419 37,574,837 56,362,256 8 Kigoma 18,787,419 37,574,837 56,362,256 9 Kilimanjaro 18,787,419 37,574,837 56,362,256 10 Lindi 18,787,419 37,574,837 56,362,256 11 Manyara 19,787,419 39,574,837 59,362,256 12 Mara 18,685,419 37,370,837 56,056,256 13 Mbeya 22,704,465 45,408,931 68,113,396 14 Morogoro 22,643,265 45,286,531 67,929,796

Page 186: Tekeleza kwa

184

S/N Mkoa Fedha za Ndani Fedha za Nje Jumla

15 Mtwara 21,787,419 43,574,837 65,362,256 16 Mwanza 20,704,465 41,408,931 62,113,396 17 Njombe 18,787,419 37,574,837 56,362,256 18 Pwani 20,704,465 41,408,931 62,113,396 19 Rukwa 18,787,419 37,574,837 56,362,256 20 Ruvuma 18,787,419 37,574,837 56,362,256 21 Shinyanga 22,704,465 45,408,931 68,113,396 22 Simiyu 18,787,419 37,574,837 56,362,256 23 Singida 18,787,419 37,574,837 56,362,256 24 Tabora 23,000,045 46,000,091 69,000,136 25 Tanga 22,963,415 45,926,831 68,890,246 Jumla kwa Sekretarieti za Mikoa 500,000,000 1,000,000,000 1,500,000,000

Page 187: Tekeleza kwa

185

Jedwali Na. 6: Orodha ya Miradi 975 iliyokamilika katika Vijiji 1,206 vinavyopata Huduma ya Maji chini ya Mpango wa BRN

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

ARUSHA Arusha MC 1 Sinoni, Sokon, Mkonoo & Nadosoito

1 Sinoni,

144 35,444 ARUSHA Arusha MC 2 Sokon,

ARUSHA Arusha MC 3 Mkonoo

ARUSHA Arusha MC 4 Nadosoito

ARUSHA Arusha DC 2 Ilkirevi 5 Ilkirevi 11 4,207

ARUSHA Arusha DC 3 Oloigeruno 6 Oloigeruno 11 5,550

ARUSHA Karatu 4 Getamock 7 Getamock 96 23,199

ARUSHA Karatu 5 Endanaghan/Mik

ocheni 8 Endanagha

n 55 13,229 ARUSHA Karatu 9 Mikocheni

ARUSHA Longido 6 Longido 10 Longido 87 21,158

ARUSHA Monduli 7 Lolkisale 11 Lolkisale 25 5,852

ARUSHA Monduli 8 Engaruka Juu 12 Engaruka Juu 41 9,557

Page 188: Tekeleza kwa

186

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

ARUSHA Monduli 9 Mbaash 13 Mbaash 17 3,901

ARUSHA Monduli 10 Lepurko 14 Lepurko 4 1,000

ARUSHA Meru 11 Ambureni Moivaro 15 Ambureni

Moivaro 57 13,658

ARUSHA Meru 12 Kikuletwa 16 Kikuletwa 41 9,800

ARUSHA Meru 13 Nkoasenga 17 Nkoasenga 15 3,522

ARUSHA Meru 14 Leguruki 18 Leguruki 20 4,669

ARUSHA Meru 15 Miririnyi 19 Miririnyi 13 3,097

ARUSHA Meru 16 Maruvano 20 Maruvano 18 4,179

ARUSHA Meru 17 King'ori 21 King'ori 22 5,263

ARUSHA Meru 18 Nsengony 22 Nsengony 21 5,040

ARUSHA Meru 19 Ngajisosia 23 Ngajisosia 15 3,582

ARUSHA Meru 20 Kolila 24 Kolila 17 3,970

ARUSHA Meru 21 Malula 25 Malula 17 3,903

ARUSHA Meru 22 Mareu 26 Mareu 16 3,830

ARUSHA Meru 23 Imbaseny 27 Imbaseny 55 13,433

Page 189: Tekeleza kwa

187

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

ARUSHA Meru 24 Shishton 28 Shishton 17 3,917

ARUSHA Ngorongoro 25 Bulati 29 Bulati 6 6,263

ARUSHA Ngorongoro 26 Engaresero 30 Engaresero 2 2,641

ARUSHA Ngorongoro 27 Mugholo 31 Mugholo 9 1,979

ARUSHA Ngorongoro 28 Soitsambu 32 Soitsambu 7 4,342

DAR ES SALAAM Temeke MC

29 Toangoma

33 Goroka

74 18,253 DAR ES SALAAM Temeke MC 34 Dalla-

Mvuha DAR ES SALAAM Temeke MC 35 Changa

DAR ES SALAAM Temeke MC 36 Korelo

DAR ES SALAAM Temeke MC 30 Minyinya 37 Minyinya 19 7,904

DAR ES SALAAM Temeke MC 31 Muhange 38 Muhange 25 11,300

DAR ES SALAAM Temeke MC 32 Nyagwijima 39 Nyagwijima 16 7,931

DAR ES SALAAM Temeke MC 33 Kibingo 40 Kibingo 15 5,687

DAR ES SALAAM Temeke MC 34 Nyabitaka 41 Nyabitaka 16 8,709

DAR ES SALAAM Temeke MC 35 Mianzini 42 Mianzini 120 29,736

DAR ES SALAAM Temeke MC 36 Kilamba 43 Kilamba 8 2,197

Page 190: Tekeleza kwa

188

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

DAR ES SALAAM Temeke MC 37 Kijichi 44 Mtoni kijichi 79 19,424

DAR ES SALAAM Temeke MC 38 Kijichi 45 Mgeninani 61 14,970

DAR ES SALAAM Temeke MC 39 Kijichi 46 Butiama 81 20,194

DAR ES SALAAM Temeke MC 40 Kizuiani 47 Kizuiani 33 8,236

DAR ES SALAAM Temeke MC 41 Makuka 48 Makuka 56 14,110

DAR ES SALAAM Temeke MC 42 Mbagala kuu 49 Mbagala kuu 106 26,311

DAR ES SALAAM Temeke MC 43 Kichemchem 50 Kichemchem 59 14,486

DAR ES SALAAM Temeke MC 44 Kibondemaji B 51 Kibondemaji B 81 19,994

DAR ES SALAAM Temeke MC 45 Uwazi 52 Uwazi 38 9,300

DAR ES SALAAM Temeke MC 46 Dovya 53 Dovya 60 14,791

DAR ES SALAAM Temeke MC 47 Msakala 54 Msakala 89 22,012

DAR ES SALAAM Ilala 48 Pugu solar demonstration 55 Pugu sub

village 13 3,000

DAR ES SALAAM Ilala 49 Chanika 56 Chanika 11 2,500

DAR ES SALAAM Ilala 50 Mongolandege 57 Mongolandege 16 3,750

Page 191: Tekeleza kwa

189

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

DAR ES SALAAM Ilala 51 Mwembe mdafu 58 Mwembe mdafu

DAR ES SALAAM Ilala 52 Mazizini 59 Mazizini

DAR ES SALAAM Ilala 53 Kinyerezi 60 Kinyerezi 1 1,317

DAR ES SALAAM Ilala 54 Mwanagati 61 Mwanagati 1 1,175

DAR ES SALAAM Ilala 55 TabataMsimbazi 62 TabataMsimbazi 1 258

DAR ES SALAAM Ilala

56 Pugu

63 Kinyamwezi 38 9,393

DAR ES SALAAM Ilala 64 Kigogo fresh 41 10,268

DAR ES SALAAM Ilala 65 Bombani 53 13,256

DAR ES SALAAM Ilala 66 Kichangani 24 6,112

DAR ES SALAAM Ilala 67 Pugu station 34 8,540

DAR ES SALAAM Ilala 57 Kivule Machimbo 68 Kivule Machimbo 160 40,064

DAR ES SALAAM Kinondoni 58 Mburahati 69 Mburahati 32 8,000

DAR ES SALAAM Kinondoni 59 Kwembe 70 Kwembe 10 2,500

DAR ES SALAAM Kinondoni 60 Hondogo/Kibweg 71 Hondogo 25 6,000

Page 192: Tekeleza kwa

190

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

DAR ES SALAAM Kinondoni ere 72 Kibwegere 49 12,081

DAR ES SALAAM Kinondoni 61 Mpiji Magohe 73 Mpiji Magohe 26 6,647

DAR ES SALAAM Kinondoni 62 Magomeni Idrisa 74 Magomeni Idrisa 8 1,785

DAR ES SALAAM Kinondoni 63 King'azi 75 King'azi 37 9,067

DAR ES SALAAM Kinondoni 64 Hananasif 76 Hananasif 68 16,756

DAR ES SALAAM Kinondoni 65 Makoka 77 Makoka 42 10,148

DAR ES SALAAM Kinondoni 66 Ndugumbi 78 Ndugumbi 168 40,965

DAR ES SALAAM Kinondoni 67 Salasala 79 Salasala 69 16,949

DAR ES SALAAM Kinondoni 68 Kilimahewa 80 Kilimahewa 77 19,089

DAR ES SALAAM Kinondoni 69 Magomeni Dosi 81 Magomeni Dosi 11 2,545

DAR ES SALAAM Kinondoni 70 Mzimuni 82 Mzimuni 92 22,851

DAR ES SALAAM Kinondoni 71 Boka chama 83 Boka chama 64 15,794

DAR ES SALAAM Kinondoni 72 Msigani 84 Msigani 70 17,259

DAR ES SALAAM Kinondoni 73 Madale Kisauke 85 Madala Kisauke 50 12,164

Page 193: Tekeleza kwa

191

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

DAR ES SALAAM Kinondoni 74 Manzese Mvuleni 86 Manzese

Mvuleni 35 8,605

DAR ES SALAAM Kinondoni 75 Manzese Midizini 87 Manzese Midizini 32 7,639

DAR ES SALAAM Kinondoni 76 Makurumla ward 88 Makurumla ward 283 70,443

DAR ES SALAAM Kinondoni 77 Mburahati Barafu 89 Mburahati Barafu 72 17,693

DAR ES SALAAM Kinondoni 78 Mbuyuni 90 Mbuyuni 60 14,629

DAR ES SALAAM Kinondoni 79 Mzimuni 91 Mzimuni 6 1,250

DODOMA Dodoma MC 80 Chididimo 92 Chididimo 38 8,913

DODOMA Dodoma MC 81 Mkonze 93 Mkonze 62 15,036

DODOMA Dodoma MC 82 Ngo'ngonha 94 Ngo'ngonha 21 4,729

DODOMA Bahi DC 83 Nondwa 95 Nondwa 23 5,058

DODOMA Bahi DC 84 Mchito 96 Mchito 11 2,400

DODOMA Bahi DC 85 Mindola 97 Mindola 11 2,301

DODOMA Bahi DC 86 Nholi 98 Nholi 11 2,157

DODOMA Kondoa DC 87 Choka 99 Choka 34 7,893

Page 194: Tekeleza kwa

192

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

DODOMA Kondoa DC 88 Magasa 100 Magasa 17 3,811

DODOMA Kondoa DC 89 Kwadelo 101 Kwadelo 19 4,229

DODOMA Kondoa DC 90 Gonga 102 Gonga 5 2,112

DODOMA Kondoa DC 91 Madisa 103 Madisa 13 2,729

DODOMA Kondoa DC 92 Mwaikisabe 104 Mwaikisabe 23 6,986

DODOMA Kondoa DC 93 Soera 105 Soera 7 846

DODOMA Kondoa DC 94 Kelema kuu 106 Kelema kuu 13 3,900

DODOMA Kondoa DC 95 Olboroti 107 Olboroti 23 7,862

DODOMA Kondoa DC 96 Mlongia 108 Mlongia 15 3,426

DODOMA Chemba 97 Jenjeluse 109 Jenjeluse 7 1,743

DODOMA Chemba 98 Soera 110 Soera 13 846

DODOMA Chemba 99 Olboroti 111 Olboroti 23 7,862

DODOMA Chemba 100 Mtakuja 112 Mtakuja 13 846

DODOMA Chemba 101 Mlongia 113 Mlongia 11 7,862

DODOMA Chemba 102 Waida 114 Waida 6 2,622

DODOMA Chamwino 103 Mvumi makulu 115 Mvumi makulu 31 7,229

Page 195: Tekeleza kwa

193

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

DODOMA Chamwino 104 Itiso 116 Itiso 42 9,933

DODOMA Chamwino 105 Mvumi Mission 117 Mvumi Mission 37 8,729

DODOMA Kongwa 106 Mkoka 118 Mkoka 25 13,307

DODOMA Kongwa 107 Nghumbi 119 Nghumbi 31 25,498

DODOMA Kongwa 108 Mlali ( A & B)

120 Mlali A) 54 28,667

DODOMA Kongwa 121 Mlali B

DODOMA Mpwapwa 109 Chinyanhuku 122 Chinyanhuku 25 5,729

DODOMA Mpwapwa 110 Chunyu 123 Chunyu 31 7,229

DODOMA Mpwapwa 111 Kimagai 124 Kimagai 14 3,670

GEITA Nyang'hwale

112 Kayenze,

125 Kayenze, 2 545

GEITA Nyang'hwale 126 Kakora, 2 562

GEITA Nyang'hwale 127 Ikangara 2 446

GEITA Nyang'hwale 128 Kharumwa 2 422

GEITA Nyang'hwale 113 Nyamtukuza 129 Nyamtukuza 13 5,721

GEITA Nyang'hwale 114 Kharumwa 130 Kharumwa 1 294

Page 196: Tekeleza kwa

194

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

GEITA Chato DC 115 Ichwankima, 131

Ichwankimab Imalabupina Rubambangwe

7 1,260

GEITA Chato DC 116 Kikumbaitale 132 Kikumbaitale 23 5,729

GEITA Chato DC 117 Rubambangwe 133 Rubambangwe 7 3,358

GEITA Chato DC 118 Muungano 134 Muungano

28

1,446

GEITA Chato DC 119 Chato Kati 135 Chato Kati 6,129

GEITA Chato DC 120 Kitela 136 Kitela 6,487

GEITA Chato DC 121 Mbuye 137 Mbuye 11

3,044

GEITA Chato DC 122 Bwina 138 Bwina 3,052

GEITA Bukombe 123 Bukombe 139 Bukombe 34 7,893

GEITA Bukombe 124 Ibambilo 140 Ibambilo 8 4,830

GEITA Bukombe 125 Ikuzi 141 Ikuzi 19 4,229

GEITA Bukombe 126 Uyovu 142 Uyovu 93 22,616

Page 197: Tekeleza kwa

195

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

GEITA Bukombe 127 Bulega 143 Bulega 25 5,729

GEITA Mbogwe 128 Bulugala 144 Bulugala 42 9,933

GEITA Mbogwe 129 Shinyanga A &B

145 Shinyanga A 107 12,729

GEITA Mbogwe 146 Shinyanga B

GEITA Mbogwe 130 Shenda

147 Shenda 38 8,913

GEITA Mbogwe 148 Masumbwe

GEITA Mbogwe 131 Lulembela 149 Lulembela 34 7,893

GEITA Geita 132 Ruhuha 150 Ruhuha 13 3,326

GEITA Geita 133 Nyakagomba 151 Nyakagomba 17 4,377

GEITA Geita 134 Inyala 152 Inyala 44 10,266

GEITA Geita 135 Katoro, 153 Katoro, 6 1,229

GEITA Geita 136 Chikobe 154 Chikobe 1 367

GEITA Geita 137 Chankolongo 155 Chankolongo 1 133

GEITA Geita 138 Inyala

156 Inyala 6 1,229

GEITA Geita 157 Kharumwa 5 979

Page 198: Tekeleza kwa

196

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

IRINGA Iringa MC

139 Mawelewele Group

158 Mawelewele

70 17,076 IRINGA Iringa MC 159 Mkoga

IRINGA Iringa MC 160 Kitasengwa

IRINGA Iringa MC 140 Nduli & Mgongo

161 Nduli 23 5,579

IRINGA Iringa MC 162 Mgongo

IRINGA Iringa MC 141 Kigonzile 163 Kigonzile 29 7,000

IRINGA Iringa MC 142 Kigungawe &

Ulonge 164 Kigungawe 3 623

IRINGA Iringa MC 165 Ulonge 11 907

IRINGA Kilolo DC

143 Kipaduka

166 Kipaduka 11 2,890

IRINGA Kilolo DC 167 Vitono 11 1,767

IRINGA Kilolo DC 168 Ikuka 12 3,323

IRINGA IRINGA DC 144 Igangidung’u 169 Igangidung’u 16 3,288

IRINGA IRINGA DC 145 Malinzanga 170 Malinzanga 61 9,000

IRINGA IRINGA DC 146 Weru 171 Weru 21 5,000

IRINGA Mufindi DC 147 Igomaa 172 Igomaa 22 2,226

Page 199: Tekeleza kwa

197

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

IRINGA Mufindi DC 148 Kiponda 173 Kiponda 4 1,735

IRINGA Mufindi DC 149 Mapanda 174 Mapanda 21 3,475

KAGERA Bukoba MC 150 Kagondo 175 Kagondokaluguru 42 10,204

KAGERA Bukoba MC 151 Kagondo 176 Kyamuzinga 9 2,000

KAGERA Bukoba MC 152 Ijuganyondo

177 Ijuganyondo A 11 2,500

KAGERA Bukoba MC 178 Ijuganyondo B 13 3,000

KAGERA Bukoba MC 153 Bulibata 179 Bulibata 42 10,000

KAGERA Bukoba MC 154 Kyamyosi 180 Kyamyosi 7 1,777

KAGERA Bukoba MC 155 Bunkango 181 Bunkango 7 1,141

KAGERA Bukoba MC 156 Rwazi 182 Rwazi 7 1,311

KAGERA Bukoba DC 157 Mashule 183 Mashule 79 19,409

KAGERA Bukoba DC 158 Kyamulaile 184 Kyamulaile 21 8,331

KAGERA Bukoba DC 159 Kitahya 185 Kitahya 21 3,456

KAGERA Bukoba DC 160 Itongo 186 Itongo 20 3,006

Page 200: Tekeleza kwa

198

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KAGERA Bukoba DC 161 Rukoma 187 Rukoma 1 450

KAGERA Bukoba DC 162 Kibirizi 188 Kibirizi 1 702

KAGERA Bukoba DC 163 Omumbweya 189 Omumbweya 1 355

KAGERA Bukoba DC 164 Bundaza 190 Bundaza 12 2,565

KAGERA Bukoba DC 165 Mikoni 191 Mikoni 11 2,224

KAGERA Muleba DC 166 Kyota, Ruteme na Kagulamo 192 Kyota,

29 9,626 KAGERA Muleba DC 167 Kyota, Ruteme na Kagulamo 193 Ruteme

KAGERA Muleba DC 168 Kyota, Ruteme na Kagulamo 194 Kagulamo

KAGERA Muleba DC 169 Kabare 195 Kabare 29 4,853

KAGERA Biharamulo DC 170 Kagondo 196 Kagondo 58 14,346

KAGERA Biharamulo DC

171 Mabare -Mihongora

197 Mabare

177 30,095 KAGERA Biharamulo DC 198 Mihongora

KAGERA Biharamulo DC 199 ngaralambe

KAGERA Biharamulo DC 200 nyakuhula

KAGERA Biharamulo DC 172 Kagondo 201 Kagondo 7 9,677

Page 201: Tekeleza kwa

199

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KAGERA Biharamulo DC 173 Kasato 202 Kasato 11 7,722

KAGERA Biharamulo DC 174 Kabindi,Kagondo,Rwekubo na Nemba

203 Kabindi

31 7,500

KAGERA Biharamulo DC

175 Kabindi,Kagondo,Rwekubo na Nemba

204 Rwekubo

KAGERA Biharamulo DC 205 kisuma,

KAGERA Biharamulo DC 206 Runazi,

KAGERA Biharamulo DC 207 Mbindi,

KAGERA Biharamulo DC 208 Nyantakara,

KAGERA Biharamulo DC 209 Kasilo

KAGERA Biharamulo DC 210 Kaniha

KAGERA Biharamulo DC 211 Mubaba

KAGERA Biharamulo DC 212 Mavota

KAGERA Biharamulo DC 213 Kasato

KAGERA Biharamulo DC 214 Ruganzu

KAGERA Biharamulo DC 176 Kabindi,Kagondo,Rwekubo na Nemba

215 Nemba

Page 202: Tekeleza kwa

200

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KAGERA Ngara DC 177 Rulenge 216 Rulenge 103 25,531

KAGERA Ngara DC 178 Ngundusi 217 Ngundusi 46 11,225

KAGERA Ngara DC 179 Munjebwe 218 Munjebwe 31 4,456

KAGERA Ngara DC 180 Mukibogoye 219 Mukibogoye 25 8,658

KAGERA Ngara DC 181 Kabanga /Murukukumbo 220 Kabanga

32 7,872 KAGERA Ngara DC 182 Kabanga

/Murukukumbo 221 Murukukumbo

KAGERA Ngara DC 183 K9 222 K9 18 4,756

KAGERA Ngara DC 184 Rusumo 223 Rusumo 33 7,972

KAGERA Ngara DC 185 Murusagamba 224 Murusagamba 22 5,367

KAGERA Ngara DC 186 Benako 225 Benako 20 3,865

KAGERA Karagwe DC 187 Nyaishozi 226 Nyaishozi 42 10,204

KAGERA Kyerwa DC 188 kibingo 227 kibingo 47 11,500

KAGERA Kyerwa DC 189 Rwabikagati 228 Rwabikagati 41 9,614

KAGERA Misenyi 190 Kilimilile 229 Kilimilile 31 7,500

Page 203: Tekeleza kwa

201

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KAGERA Misenyi

191 Kanyigo/Kashenye

230 Bugombe,

44 10,750 KAGERA Misenyi 231 Kikukwe,

KAGERA Misenyi 232 Kashenye,

KAGERA Misenyi 233 Kigarama,

KAGERA Misenyi 192 Nkenge 234 Mbale 31 7,500

KAGERA Misenyi

193 Mshasha/Bwanjai/Kashaba/kyazi /Bulembo

235 Mshasha

7 1,750

KAGERA Misenyi 236 Bwanja

KAGERA Misenyi 237 Kashaba

KAGERA Misenyi 238 kyazi

KAGERA Misenyi 239 Bulembo

KAGERA Misenyi 194 Mutukula 240 Mutukula 33 8,145

KATAVI Mlele 195 Kibaoni 241 Kibaoni 26 5,979

KATAVI Mlele 196 Usevya 242 Usevya 26 4,229

KATAVI Mlele 197 Mamba 243 Mamba 22 4,979

KATAVI Mlele 198 Mbede 244 Mbede 14 2,979

KATAVI Mlele 199 Kanoge A 245 Kanoge A 86 11,590

Page 204: Tekeleza kwa

202

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KATAVI Mlele 200 Kanoge B 246 Kanoge B

KATAVI Mlele 201 Nduwi, 247 Nduwi,

8 1,750 KATAVI Mlele 202 Mnyaki A 248 Mnyaki A

KATAVI Mlele 203 Mnyaki B 249 Mnyaki B

KATAVI Mlele 204 Mishamo 250 Mishamo 56 13,750

KATAVI Mlele 205 Mirumba 251 Mirumba 2 500

KATAVI Mpanda DC 206 Ikola 252 Ikola 29 7,000

KATAVI Mpanda TC

207 Ikorongo

253 Ilembo,

95 23,578

KATAVI Mpanda TC 254 Kasimba,

KATAVI Mpanda TC 255 Kazima,

KATAVI Mpanda TC 256 Kigamboni,

KATAVI Mpanda TC 257 Kivukoni,

KATAVI Mpanda TC 258 Migazini,

KATAVI Mpanda TC 259 Milupwa,

KATAVI Mpanda TC 260 Msufini,

KATAVI Mpanda TC 261 Misunkumilo

Page 205: Tekeleza kwa

203

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KATAVI Mpanda TC 262 Nsemulwa

KATAVI Nsimbo

208 Kaminula

263 Nduwi,

8 1,750 KATAVI Nsimbo 264 Mnyaki A

KATAVI Nsimbo 265 Mnyaki B

KATAVI Nsimbo 209 Mishamo 266 Mishamo 56 13,750

KIGOMA Kasulu 210 Mubanga 267 Mubanga 47 11,229

KIGOMA Kasulu 211 Nyumbigwa 268 Nyumbigwa 39 9,229

KIGOMA Kasulu 212 Munzeze 269 Munzeze 53 12,340

KIGOMA Kibondo 213 Minyinya 270 Minyinya 37 8,630

KIGOMA Kibondo 214 Nyagwijima 271 Nyagwijima 31 7,328

KIGOMA Kibondo 215 Nyabitaka 272 Nyabitaka 33 7,729

KIGOMA Kibondo 216 Kibingo 273 Kibingo 29 6,729

KIGOMA Kibondo 217 Kiga 274 Kiga 29 6,714

KIGOMA Kibondo 218 Nabuhima 275 Nabuhima 11 2,149

KIGOMA Kibondo 219 Kumwambu 276 Kumwambu 17 3,745

KIGOMA Kibondo 220 Rusohoko 277 Rusohoko 33 7,787

Page 206: Tekeleza kwa

204

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KIGOMA Kibondo 221 Kifura 278 Kifura 47 11,110

KIGOMA Kibondo 222 Kichananga 279 Kichananga 22 4,968

KIGOMA Kibondo 223 Kigaga 280 Kigaga 24 5,684

KIGOMA Kibondo 224 Mukabuye 281 Mukabuye 3 1,650

KIGOMA Kibondo 225 Mabamba 282 Mabamba 6 1,478

KIGOMA Kibondo 226 Nyakasanda 283 Nyakasanda 22 5,168

KIGOMA Kibondo 227 Nyarugusu 284 Nyarugusu 2 483

KIGOMA Kibondo 228 Kigina 285 Kigina 4 1,022

KIGOMA Kibondo 229 Maglama 286 Maglama 2 469

KIGOMA Kibondo 230 Kichembeka 287 Kichembeka 2 548

KIGOMA Kibondo 231 Kumshwabure 288 Kumshwabure 4 971

KIGOMA Kibondo 232 Kumhama 289 Kumhama 3 719

KIGOMA Kibondo 233 Magarama 290 Magarama 26 5,868

KIGOMA Kibondo 234 Nyarulanga 291 Nyarulanga 3 523

KIGOMA Kibondo 235 Kumkuyu 292 Kumkuyu 2 736

Page 207: Tekeleza kwa

205

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KIGOMA Kibondo 236 Kigendeka 293 Kigendeka 25 5,969

KIGOMA Kibondo 237 Nyange 294 Nyange 13 2,996

KIGOMA Kibondo 238 Mkarazi 295 Mkarazi 3 503

KIGOMA Kibondo 239 Bitare 296 Bitare 3 509

KIGOMA Kibondo 240 Kumkugwa 297 Kumkugwa 2 519

KIGOMA Kibondo 241 Samvura 298 Samvura 2 472

KIGOMA Kibondo 242 Muhange 299 Muhange 49 11,029

KIGOMA Kigoma 243 Nyarubanda 300 Nyarubanda 28 14,794

KIGOMA Kigoma 244 Kagongo 301 Kagongo 36 9,450

KIGOMA Kigoma 245 Nkungwe 302 Nkungwe 63 15,500

KIGOMA Kigoma 246 Kandaga 303 Kandaga 45 11,000

KIGOMA Kigoma 247 Rukoma 304 Rukoma 63 15,500

KIGOMA Kigoma MC 248 Kagera 305 Kagera 31 17,654

KILIMANJARO Same 249 Mwembe / Mteke

306 Mteke 31 7,307

KILIMANJARO Same 307 Mwembe 39 9,156

KILIMANJARO Same 250 Myombo 308 Myombo 47 11,130

Page 208: Tekeleza kwa

206

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KILIMANJARO Same /Sambweni 309 Sambweni 39 9,328

KILIMANJARO Same 251 Kisesa 310 Kisesa -Mseke 24 1,703

KILIMANJARO Siha 252 Magadini-

Makiwaru 311 Wiri,

116 28,399 KILIMANJARO Siha 312 Namwai

KILIMANJARO Siha

253 North-West Kilimanjaro

313 Miti mirefu,

197 48,710 KILIMANJARO Siha 314 Matadi,

KILIMANJARO Siha 315 Namwai

KILIMANJARO Hai

254 Lyamungo-Umbwe

316 Mbatakero 58 14,015

KILIMANJARO Hai 317 Ngosero 91 22,179

KILIMANJARO Hai 318 Kimashuku 25 5,852

KILIMANJARO Hai 319 Kwasadala 9 1,980

KILIMANJARO Hai 320 Kwatito 9 1,770

KILIMANJARO Hai 255 Sanyastation/Tin

digan 321 Sanyastatio

n, 21 4,729 KILIMANJARO Hai 322 Tindigani

KILIMANJARO Hai 256 Mungwamae 323 Mungwamae 21 5,000

Page 209: Tekeleza kwa

207

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KILIMANJARO Hai 257 Somali 324 Somali

KILIMANJARO Hai 258 Somali PRT 325 Somali PRT

KILIMANJARO Hai 259 Mtakuja 326 Mtakuja 31 7,500

KILIMANJARO Hai 260 Chemka 327 Chemka 25 6,000

KILIMANJARO Moshi DC 261 Korini

328 Korini-Juu, 189 46,669

KILIMANJARO Moshi DC 329 Korini-Chini

KILIMANJARO Mwanga DC 262 Msangeni 330 Msangeni 69 16,700

KILIMANJARO Mwanga DC 263 Shighatini 331 Shighatini 65 15,758

KILIMANJARO Mwanga DC 264 Kisangara 332 Kisangara 81 19,698

KILIMANJARO Mwanga DC 265 Butu 333 Butu 33 7,760

KILIMANJARO Mwanga DC 266 Kisanjuni 334 Kisanjuni 65 15,729

KILIMANJARO Mwanga DC 267 Lomwe 335 Lomwe 26 2,800

KILIMANJARO Mwanga DC 268 Vuagha 336 Vuagha 19 3,300

KILIMANJARO Rombo DC 269 Ngoyoni 337 Ngoyoni 17 3,811

KILIMANJARO Rombo DC 270 Mahorosha 338 Mahorosha 9 2,178

Page 210: Tekeleza kwa

208

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

KILIMANJARO Rombo DC 271 Kiraeni 339 Kiraeni 13 2,800

KILIMANJARO Rombo DC 272 Msaranga 340 Msaranga 13 2,789

KILIMANJARO Moshi MC 273 Longuo A 341 Longuo A 12 7,157

LINDI Kilwa 274 Kandawale 342 Kandawale 10 3,200

LINDI Kilwa 275 Haga 343 Haga 23 2,300

LINDI Kilwa 276 Mtandi 344 Mtandi 9 1,729

LINDI Kilwa 277 Njinjo 345 Njinjo 23 4,120

LINDI Kilwa 278 Nanjirinji 346 Nanjirinji 31 4,475

LINDI Kilwa 279 Ngea 347 Ngea 5 268

LINDI Kilwa 280 Chumo 348 Chumo 38 9,470

LINDI Lindi DC 281 Rondo 349 Rondo 21 4,936

LINDI Lindi DC 282 Namkongo 350 Namkongo 9 2,061

LINDI Lindi DC 283 Kiwawa 351 Kiwawa 2 510

LINDI Lindi DC 284 Namangale 352 Namangale 29 4,825

LINDI Lindi DC 285 Likwaya 353 Likwaya 4 605

LINDI Nachingwea 286 Rweje 354 Rweje 1 470

Page 211: Tekeleza kwa

209

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

LINDI Nachingwea 287 Mituguru 355 Mituguru 11 669

LINDI Nachingwea 288 Farm 8 356 Farm 8 1 241

LINDI Nachingwea 289 Mkoka 357 Mkoka 17 2,120

LINDI Nachingwea 290 Ikungu 358 Ikungu 9 2,039

LINDI Nachingwea 291 Libea 359 Libea 1 189

LINDI Nachingwea 292 Namatula 360 Namatula 1 489

LINDI Nachingwea 293 Muungano 361 Muungano 1 360

LINDI Nachingwea 294 Maziwa 362 Maziwa 1 160

LINDI Nachingwea 295 Mbondo 363 Mbondo 1 172

LINDI Nachingwea 296 Ilolo 364 Ilolo 1 194

LINDI Nachingwea 297 Nditi 365 Nditi 1 347

LINDI Nachingwea 298 Likwela 366 Likwela 1 381

LINDI Nachingwea 299 Nalung;ombe 367 Nalung;ombe 1 153

LINDI Nachingwea 300 Namauni 368 Namauni 1 217

LINDI Nachingwea 301 Kingunduliu 369 Kingunduliu 1 145

LINDI Nachingwea 302 Mtimbo 370 Mtimbo 1 120

Page 212: Tekeleza kwa

210

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

LINDI Nachingwea 303 Ntepeche 371 Ntepeche 1 280

LINDI Nachingwea 304 Nambalapala 372 Nambalapala 1 302

LINDI Nachingwea 305 Mwandila 373 Mwandila 1 185

LINDI Nachingwea 306 Mbote 374 Mbote 1 201

LINDI Nachingwea 307 Likongongowele 375 Likongongowele 1 144

LINDI Nachingwea 308 Mpiluka 376 Mpiluka 7 1,730

LINDI Nachingwea 309 Mkotokuyana 377 Mkotokuyana 3 770

LINDI Nachingwea 310 Ndomondo 378 Ndomondo 1 317

LINDI Nachingwea 311 Makitikiti 379 Makitikiti 1 198

LINDI Nachingwea 312 Mgangani 380 Mgangani 1 352

LINDI Nachingwea 313 Farm 17 381 Farm 19 2 408

LINDI Nachingwea 314 Namanja 382 Namanja 1 246

LINDI Nachingwea 315 Namkoka 383 Namkoka 1 243

LINDI Nachingwea 316 Luponda 384 Luponda 1 289

LINDI Nachingwea 317 Ndomole 385 Ndomole 1 318

Page 213: Tekeleza kwa

211

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

LINDI Nachingwea 318 Nang'ondo 386 Nang'ondo 1 282

LINDI Nachingwea 319 Kihue 387 Kihue 1 203

LINDI Nachingwea 320 Mkumba 388 Mkumba 2 438

LINDI Nachingwea 321 Marambo 389 Marambo 2 603

LINDI Nachingwea 322 Mchonda 390 Mchonda 1 185

LINDI Nachingwea 323 Mnero Miembeni 391 Mnero Miembeni 1 218

LINDI Nachingwea 324 Naipingo 392 Naipingo 1 232

LINDI Nachingwea 325 Luponda 393 Luponda 2 473

LINDI Nachingwea 326 Stesheni 394 Stesheni 1 181

LINDI Nachingwea 327 Chiumbati Miembeni 395 Chiumbati

Miembeni 1 289

LINDI Nachingwea 328 Naitingo 396 Naitingo 1 328

LINDI Nachingwea 329 Naipanga 397 Naipanga 1 197

LINDI Nachingwea 330 Ikungu 398 Ikungu 14 3,181

LINDI Ruangwa 331 Luchelegwa 399 Luchelegwa

19 2,541

Page 214: Tekeleza kwa

212

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

LINDI Ruangwa 332 Chimbila 'B' 400 Chimbila 'B' 1 250

LINDI Ruangwa

333 Nandagala

401 Nandagala A

45 8,654 LINDI Ruangwa 402 Nandagala B

LINDI Ruangwa 403 Ng'au

LINDI Ruangwa 334 Mpumbe 404 Mpumbe 2 460

LINDI Ruangwa 335 Mibure 405 Mibure 2 540

LINDI Liwale 336 Tulieni 406 Tulieni 8 2,456

LINDI Liwale 337 Barikiwa 407 Barikiwa 21 5,122

LINDI Liwale 338 Mpigamiti 408 Mpigamiti 12 2,729

LINDI Liwale 339 Namihu 409 Namihu 11 751

LINDI Liwale 340 Namakololo/Mita

wa 410

Namakololo 17 4,000 LINDI Liwale 411 Mitawa

LINDI Liwale 341 Nabuya 412 Nabuya 2 500

LINDI Lindi MC 342 Tulieni

413 Tulieni 7 2,185

LINDI Lindi MC 414 Mitumbati

Page 215: Tekeleza kwa

213

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

LINDI Lindi MC

343 Mingoyo

415 Mingoyo

41 9,888 LINDI Lindi MC 416

Mnazimmoja

LINDI Lindi MC 417 Mawasiliano

LINDI Lindi MC 344 Chikonji

418 Chikonji kusini

25 5,976 LINDI Lindi MC 419 Chikonji

kaskazini

LINDI Lindi MC

345 Kitumbikwela

420 Kitumbikwela,

25 5,941 LINDI Lindi MC 421

Nachingwea

LINDI Lindi MC 422 Kitunda

LINDI Lindi MC 346 Mtange 423 Mtange 15 2,164

LINDI Lindi MC 347 Kineng'ene

424 Mchocholo, 21 4,514

LINDI Lindi MC 425 Nanembo

Page 216: Tekeleza kwa

214

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

LINDI Lindi MC 426 Mmukule

MANYARA Hanang 348 Getasam 427 Getasam 23 5,852

MANYARA Hanang 349 Ng’alda 428 Ng’alda 21 4,860

MANYARA Hanang 350 Gidagharbu 429 Gidagharbu 21 4,802

MANYARA Hanang 351 Ishponga 430 Ishponga 21 4,831

MANYARA Hanang 352 Simbay 431 Simbay 74 18,097

MANYARA Hanang 353 Galangal 432 Galangal 24 4,700

MANYARA Hanang 354 Garawja 433 Garawja 29 5,560

MANYARA Mbulu 355 Masieda 434 Masieda 30 6,872

MANYARA Mbulu 356 Dongobesh 435 Dongobesh 132 32,383

MANYARA Mbulu 357 Maretadu Chini 436 Maretadu Chini 2 456

MANYARA Mbulu 358 Endamasak 437 Endamasak 2 592

MANYARA Babati DC 359 Endagile

438 Endagile 66 16,056

MANYARA Babati DC 439 Mamire

MANYARA Babati DC 360 Gedamar

440 Gedamar 123 30,342

MANYARA Babati DC 441 Hallu

Page 217: Tekeleza kwa

215

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MANYARA Babati DC

361 Managha

442 Managha,

107 26,260 MANYARA Babati DC 443 Duduye

MANYARA Babati DC 444 Arritsaayo

MANYARA Babati DC 362 Riroda 445 Riroda 66 16,056

MANYARA Babati DC

363 Darakuta Minjingu

446 Mwada,

132 32,383

MANYARA Babati DC 447 Mayomayoka,

MANYARA Babati DC 448 Minjingu,

MANYARA Babati DC 449 Olasiti

MANYARA Babati DC 450 Ngoley

MANYARA Babati DC 364 Seloto 451 Seloto 21 12,430

MANYARA Babati DC 365 Seloto 452 Loto

MANYARA Babati DC 366 Tsamasi 453 Tsamasi 25 5,754

MANYARA Babati DC 367 Err 454 Err 21 6,888

MANYARA Babati TC 368 Mutuka 455 Mutuka 74 18,097

MANYARA Babati TC 369 Chemchem 456 chemchem 19 1,416

MANYARA Babati TC 370 Himiti 457 Himiti 28 5,762

Page 218: Tekeleza kwa

216

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MANYARA Babati TC 371 Kiongozi 458 Kiongozi 21 5,000

MANYARA Babati TC 372 Managhat 459 Managhat 20 3,388

MANYARA Kiteto DC 373 Mwanya 460 Mwanya 34 7,893

MANYARA Kiteto DC 374 Ndorkon 461 Ndorkon 21 4,831

MANYARA Kiteto DC 375 Njiapanda 462 Njiapanda 2 512

MANYARA Kiteto DC 376 Eseki 463 Esekii 17 3,811

MANYARA Kiteto DC 377 Kona 464 Kona 5 2,807

MANYARA Kiteto DC 378 Loolera 465 Loolera 6 1,443

MANYARA Simanjiro 379 Loswaki 466 Loswaki 9 1,915

MARA Butiama 380 Kitaramanka 467 Kitaramanka 62 15,307

MARA Butiama 381 Nyagisya 468 Nyagisya 34 8,164

MARA Butiama 382 Magunga 469 Magunga 25 5,260

MARA Butiama 383 Kamugendi 470 Kamugendi 11 2,816

MARA Butiama 384 Bukabwa 471 Bukabwa 29 3,127

MARA Bunda 385 Nyang'aranga 472 Nyang'aranga 111 27,552

Page 219: Tekeleza kwa

217

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MARA Bunda 473 Mugeta

MARA Bunda 386 Nyamatoke 474 Nyamatoke 58 14,286

MARA Bunda 387 Karukekere 475 Karukekere 83 20,409

MARA Bunda 388 Kung'ombe 476 Kungombe 33 7,729

MARA Bunda 389 Mumagunga 477 Mumagunga 13 1,164

MARA Serengeti 390 Natta Mbiso 478 Natta Mbiso 13 2,729

MARA Serengeti 391 Motukeri 479 Motukeri 12 2,479

MARA Serengeti 392 Park Nyigoti 480 Park Nyigoti 42 10,204

MARA Serengeti 393 Masangura 481 Masangura 25 6,123

MARA Serengeti 394 Mbalibali 482 Mbalibali 58 14,286

MARA Serengeti 395 Nyansurumuti 483 Nyansurumuti 8 1,332

MARA Musoma DC

396 Musanja

484 Musanja 25 5,729

MARA Musoma DC 485 Wanyere 1 356

MARA Musoma DC 486 Mikuyu 1 521

MARA Tarime 397 Gibaso 487 Gibaso 18 3,978

Page 220: Tekeleza kwa

218

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MARA Tarime 398 Nyagisya 488 Nyagisya 18 3,980

MARA Tarime 399 Korotambe/

Sirari 489 Korotambe

9 2,000 MARA Tarime 490 Sirari

MARA Tarime 400 Kebweye 491 Kebweye 11 2,500

MARA Tarime 401 Nyarwana 492 Nyarwana 16 4,000

MARA Tarime 402 Muriba 493 Muriba 9 1,500

MARA Rorya

403 Komuge

494 Komuge, 14 3,198

MARA Rorya 495 Kyamwami 9 2,121

MARA Rorya 496 Irienyi, 19 4,547

MARA Rorya 497 Baraki, 18 4,352

MARA Rorya 498 Kuruya 20 4,729

MARA Rorya 499 Bitiryo 20 4,671

MARA Rorya

404 Masonga

500 Masonga 15 3,419

MARA Rorya 501 Shirati 19 4,511

MARA Rorya 502 Raranya 20 4,774

MARA Rorya 503 Nyahera 13 3,072

Page 221: Tekeleza kwa

219

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MARA Rorya 504 Nyamagongo 10 2,370

MBEYA Rungwe 405 Mbambo 505 Mbambo 62 15,307

MBEYA Rungwe 406 Kikuba 506 Kikuba 54 13,266

MBEYA Rungwe 407 Kyimo 507 Kyimo 18 4,250

MBEYA Rungwe 408 Syukula 508 Syukula 22 5,250

MBEYA Rungwe 409 Itete na Kapugi

509 Itete 32 7,750

MBEYA Rungwe 510 Kapugi

MBEYA Chunya 410 Namkukwe 511 Namkukwe 19 4,229

MBEYA Chunya 411 Udinde 512 Udinde 9 3,492

MBEYA Chunya 412 Mwambani 513 Mwambani 15 3,373

MBEYA Chunya 413 Mbuyuni 514 Mbuyuni 33 7,800

MBEYA Chunya 414 Chang'ombe 515 Chang'ombe 31 4,754

MBEYA Kyela 415 Ikombe 516 Ikombe 66 16,056

MBEYA Kyela 416 Masoko 517 Masoko 34 7,893

MBEYA Kyela 417 Busoka 518 Busoka 7 1,529

Page 222: Tekeleza kwa

220

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MBEYA Kyela 418 Lubaga 519 Lubaga 16 2,380

MBEYA Mbarali 419 Ubaruku 520 Ubaruku 36 8,497

MBEYA Mbarali 420 Ubaruku 521 Mpakani

MBEYA Mbarali 421 Chimala 522 Chimala 50 11,974

MBEYA Mbarali 422 Simike 523 Simike 29 3,813

MBEYA Mbarali 423 Udindilwa 524 Udindilwa 7 1,520

MBEYA Mbarali 424 Mkunywa 525 Mkunywa 38 9,221

MBEYA Mbarali 425 Igurusi 526 Igurusi 19 4,419

MBEYA Mbarali 426 Ilanga/Shitete/Ikumbilo 527 Ilanga 4 924

MBEYA Mbarali 427 Ilanga/Shitete/Ikumbilo 528 Shitete 8 1,637

MBEYA Mbarali 428 Ilanga/Shitete/Ikumbilo 529 Ikumbilo 16 3,868

MBEYA Mbarali 429 Kalembo 530 Kalembo 16 1,392

MBEYA Mbarali 430 Malangali 531 Malangali 12 2,861

MBEYA Mbarali 431 Mtula 532 Mtula 12 2,304

MBEYA Mbarali 432 Shikunga/Ibaba 533 Ibaba 8 1,696

Page 223: Tekeleza kwa

221

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MBEYA Mbarali 433 Shikunga/Ibaba 534 Shikunga 9 1,978

MBEYA Mbarali 434 Igava 535 Igava 14 3,158

MBEYA Mbozi DC 435 Maninga 536 Maninga 19 2,187

MBEYA Mbozi DC 436 Lungwa 537 Lungwa 50 11,974

MBEYA Mbozi DC 437 Utambalila 538 Utambalila 20 4,460

MBEYA Mbozi DC 438 Lungwa 539 Lungwa 11 2,524

MBEYA Mbozi DC 439 Hezya/Haraka/Namwangwa 540 Hezya 14 3,221

MBEYA Mbozi DC 440 Hezya/Haraka/Namwangwa 541 Haraka 17 3,901

MBEYA Mbozi DC 441 Hezya/Haraka/Namwangwa 542 Namwangw

a 6 1,313

MBEYA Mbozi DC 442 Kamsamba 543 Kamsamba 27 6,546

MBEYA Busokelo DC 443 Kipapa 544 Kipapa 27 6,500

MBEYA Busokelo DC 444 Mbambo 545 Mbambo 16 3,750

MBEYA Busokelo DC 445 Kikuba 546 Kikuba 14 3,250

MBEYA Busokelo DC 446 Mpanda 547 Mpanda 31 7,500

MBEYA Ileje 447 Mbebe 548 Mbebe 21 5,000

Page 224: Tekeleza kwa

222

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MBEYA Ileje 448 Luswisi 549 Luswisi 27 3,123

MBEYA Ileje 449 Ilanga/Shitete/Ikumbilo 550 Ilanga 4 924

MBEYA Ileje 450 Ilanga/Shitete/Ikumbilo 551 Chitete 7 1,637

MBEYA Ileje 451 Ilanga/Shitete/Ikumbilo 552 Ikumbilo 16 3,868

MBEYA Ileje 452 Kalembo 553 Kalembo 7 1,392

MBEYA Ileje 453 Malangali 554 Malangali 12 2,861

MBEYA Ileje 454 Mtula 555 Mtula 10 2,304

MBEYA Ileje 455 Shikunga/Ibaba 556 Shikunga 10 1,696

MBEYA Ileje 456 Shikunga/Ibaba 557 Ibaba 9 1,978

MBEYA Ileje 457 Ilondo 558 Ilondo 7 1,442

MBEYA Kyela 458 Ikombe 559 Ikombe 17 4,000

MBEYA Kyela 459 Masoko 560 Masoko 17 4,000

MBEYA Kyela 460 Busoka 561 Busoka 13 3,000

MBEYA Kyela 461 Lubaga 562 Lubaga 16 3,750

MBEYA Kyela 462 Ngonga 563 Ngonga 16 1,715

Page 225: Tekeleza kwa

223

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MBEYA Momba 463 Itumbula 564 Itumbula 13 3,184

MBEYA Momba 464 Namtambalala 565 Namtambalala 9 1,966

MBEYA Mbeya DC 465 Iwalanje 566 Iwalanje 29 6,729

MBEYA Mbeya DC 466 Shongo and

Igale 567 Shongo

57 14,000 MBEYA Mbeya DC 568 Igale

MBEYA Mbeya DC 467 Mleje 569 Mleje 12 2,654

MBEYA Mbeya DC 468 Idimi/Haporoto, 570 Idimi 12 2,867

MBEYA Mbeya DC 469 Idimi/Haporoto, 571 Haporoto, 8 1,862

MBEYA Mbeya DC 470 Swaya/Lupeta, 572 Swaya 16 3,667

MBEYA Mbeya DC 471 Swaya/Lupeta, 573 Lupeta, 6 1,372

MBEYA Mbeya DC 472 Galijembe, 574 Galijembe, 13 2,944

MBEYA Mbeya DC 473 Mbawi/Jojo 575 Mbawi 7 1,482

MBEYA Mbeya DC 474 Mbawi/Jojo 576 Jojo 14 3,238

MBEYA Mbeya CC 475 Ilomba, 577 Ilomba, 21 5,042

MBEYA Mbeya CC 476 Nsoho, 578 Nsoho, 2 623

MBEYA Mbeya CC 477 Iziwa, 579 Iziwa, 15 3,532

Page 226: Tekeleza kwa

224

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MBEYA Mbeya CC 478 Mwasanga/Tembela, 580 Mwasanga 10 2,175

MBEYA Mbeya CC 479 Mwasanga/Tembela, 581 Tembela, 48 11,840

MBEYA Mbeya CC 480 Mwansekwa 582 Mwansekwa 9 2,005

MBEYA Mbeya CC 481 Itagano 583 Itagano 6 1,271

MOROGORO Morogoro MC 482 Kiegea A 584 Kiegea A 3 5,229

MOROGORO Morogoro MC 483 Kauzeni 585 Kauzeni 9 1,770

MOROGORO Morogoro MC 484 Boma

586 Kibwe 31 3502

MOROGORO Morogoro MC 587 Visole

MOROGORO Morogoro MC 485 Lugala 588 Lugala 23 1,790

MOROGORO Morogoro MC 486 Mkoya 589 Mkoya 21 1,415

MOROGORO Ulanga 487 Lupiro 590 Lupiro 41 9,729

MOROGORO Ulanga 488 Igota/ Kichangani

591 Igota 13 5470

MOROGORO Ulanga 592 Kichangani

MOROGORO Ulanga 489 Gombe 593 Gombe 13 1,653

MOROGORO Ulanga 490 Mgolo 594 Mgolo 23 2,125

Page 227: Tekeleza kwa

225

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MOROGORO Kilombero 491 Mlimba

595 Mlimba A 165 12,729

MOROGORO Kilombero 596 Mlimba B.

MOROGORO Kilombero 492 Viwanja 60 597 Viwanja 60 22 5,827

MOROGORO Kilombero 493 Katurukila 598 Katurukila 23 5,000

MOROGORO Kilombero 494 Msufini 599 Msufini 25 6,000

MOROGORO Kilombero 495 Tanganyika 600 Tanganyika 26 6,500

MOROGORO Kilombero 496 Kamwene 601 Kamwene 25 6,000

MOROGORO Kilombero 497 Mbasa 602 Mbasa 3 750

MOROGORO Kilombero 498 Kibaoni 603 Kibaoni 5 1,250

MOROGORO Kilombero 499 Namwawala 604 Namwawala 6 1,500

MOROGORO Kilombero 500 Lungongole 605 Lungongole 3 824

MOROGORO Kilombero 501 Sagamaganga 606 Sagamaganga 3 676

MOROGORO Kilombero 502 Mlabani 607 Mlabani 5 1,250

MOROGORO Kilombero 503 Katindiuka 608 Katindiuka 3 750

MOROGORO Kilombero 504 Lipangalala 609 Lipangalala 5 1,250

Page 228: Tekeleza kwa

226

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MOROGORO Kilombero 505 Idete 610 Idete 3 750

MOROGORO Kilombero 506 Michenga 611 Michenga 3 671

MOROGORO Kilombero 507 Machipi 612 Machipi 3 829

MOROGORO Kilombero 508 Kining’ina 613 Kining’ina 5 1,250

MOROGORO Kilombero 509 Lumemo 614 Lumemo 5 1,250

MOROGORO Kilombero 510 Ihanga 615 Ihanga 2 500

MOROGORO Kilombero 511 Mbingu 616 Mbingu 3 750

MOROGORO Kilombero 512 Mofu 617 Mofu 5 1,250

MOROGORO Kilombero 513 Ipinde 618 Ipinde 2 500

MOROGORO Kilombero 514 Taweta 619 Taweta 3 750

MOROGORO Kilombero 515 Mpanga 620 Mpanga 5 1,250

MOROGORO Kilombero 516 Ngalimila 621 Ngalimila 3 750

MOROGORO Kilombero 517 Kisawasawa 622 Kisawasawa 3 750

MOROGORO Kilombero 518 Kiberege 623 Kiberege 5 1,250

MOROGORO Kilombero 519 Kisegese 624 Kisegese 3 750

MOROGORO Kilombero 520 Mgudeni 625 Mgudeni 3 750

Page 229: Tekeleza kwa

227

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MOROGORO Kilombero 521 Msalise 626 Msalise 3 750

MOROGORO Kilombero 522 Kanyenja 627 Kanyenja 4 1,000

MOROGORO Kilombero 523 Msolwa station 628 Msolwa station 3 750

MOROGORO Kilombero 524 V/60 Mlimba 629 V/60 Mlimba 2 492

MOROGORO Kilombero 525 Matema 630 Matema 2 508

MOROGORO Kilombero 526 Miembeni 631 Miembeni 3 749

MOROGORO Kilombero 527 Kalengakelu 632 Kalengakelu 4 1,000

MOROGORO Kilombero 528 Chisano 633 Chisano 5 1,250

MOROGORO Kilombero 529 Mgugwe 634 Mgugwe 3 751

MOROGORO Kilombero 530 V/60 Ifakara 635 V/60 Ifakara 5 1,250

MOROGORO Kilombero 531 Mhelule 636 Mhelule 3 790

MOROGORO Kilombero 532 Igima 637 Igima 3 750

MOROGORO Kilombero 533 Njage 638 Njage 3 710

MOROGORO Kilombero 534 Mkangawalo 639 Mkangawalo 5 1,250

MOROGORO Kilombero 535 Merera 640 Merera 3 750

Page 230: Tekeleza kwa

228

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MOROGORO Kilombero 536 Chita 641 Chita 5 1,250

MOROGORO Kilombero 537 Udagaji 642 Udagaji 4 1,000

MOROGORO Kilombero 538 Lukolongo 643 Lukolongo 5 1,250

MOROGORO Kilombero 539 Ikule 644 Ikule 3 750

MOROGORO Kilombero 540 Mngeta 645 Mngeta 5 1,250

MOROGORO Kilombero 541 Mang'ula A 646 Mang'ula A 50 12,250

MOROGORO Kilombero 542 Mang'ula B 647 Mang'ula B

MOROGORO Kilombero 543 Mchombe 648 Mchombe 5 1,250

MOROGORO Morogoro DC 544 Ngerengre 649 Ngerengre 33 8,000

MOROGORO Morogoro DC 545 Mkambarani 650 Mkambarani 35 8,500

MOROGORO Morogoro DC 546 Kolero 651 Kolero 31 7,500

MOROGORO Morogoro DC 547 Kalundwa 652 Kalundwa 23 5,500

MOROGORO Morogoro DC 548 Changa 653 Changa 11 2,500

MOROGORO Kilosa 549 Zombo

654 Zombo 25 3,876

MOROGORO Kilosa 655 Lumbo

MOROGORO Kilosa 550 Tundu 656 Tundu 36 12,225

Page 231: Tekeleza kwa

229

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MOROGORO Kilosa 551 Msowelo, 657 Msowelo,

MOROGORO Kilosa 552 Iwemba, 658 Iwemba,

MOROGORO Kilosa 553 Kifinga 659 Kifinga

MOROGORO Mvomero 554 Kigugu 660 Kigugu 25 4,713

MOROGORO Mvomero 555 Kwa Doli 661 Kwa Doli 19 3,446

MOROGORO Mvomero 556 Doma 662 Doma 15 4,321

MOROGORO Mvomero 557 Bumu 663 Bumu 10 1,551

MTWARA Masasi DC 558 Sindano 664 Sindano 17 3,811

MTWARA Masasi DC 559 Mtakuja 665 Mtakuja 30 6,794

MTWARA Masasi DC 560 Nambawala 666 Nambawala 30 6,950

MTWARA Masasi DC

561 Chiwambo

667 Lulindi,

218 54,150

MTWARA Masasi DC 668 Nkaseka,

MTWARA Masasi DC 669 Chiwambo,

MTWARA Masasi DC 670 Luhagara,

MTWARA Masasi DC 671 Ndwika

MTWARA Masasi DC 672 Chini,

Page 232: Tekeleza kwa

230

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MTWARA Masasi DC 673 Muungano,

MTWARA Masasi DC 674 Mnopwe,

MTWARA Masasi DC 675 Kivukoni,

MTWARA Masasi DC 676 Matogoro,

MTWARA Masasi DC 677 Mbuyuni,

MTWARA Masasi DC 678 Mitonji,

MTWARA Masasi DC 679 Ndibwa,

MTWARA Masasi DC 680 Mkangaura,

MTWARA Masasi DC 681 Nagaga,

MTWARA Masasi DC 682 Namalenga,

MTWARA Masasi DC 683 Mvita,

MTWARA Masasi DC 684 Chigawe,

MTWARA Masasi DC 685 Msokosela,

MTWARA Masasi DC 686 Chiungutwa

Page 233: Tekeleza kwa

231

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MTWARA Masasi DC 562 Lilala 687 Lilala 13 3,000

MTWARA Masasi DC 563 Lupaso 688 Lupaso 1 320

MTWARA Masasi DC 564 Chiwale 689 Chiwale 9 2,000

MTWARA Masasi DC 565 Namichi 690 Namichi 1 217

MTWARA Masasi DC 566 Mraushi 691 Mraushi 1 319

MTWARA Masasi DC 567 Mpanyani 692 Mpanyani 1 289

MTWARA Masasi DC 568 Makong'onda 693 Makong'onda 12 3,000

MTWARA Masasi DC 569 Nanyindwa 694 Nanyindwa 10 2,367

MTWARA Mtwara DC

570 Nanyamba

695 Nanyamba

188 46,600

MTWARA Mtwara DC 696 Namkuku

MTWARA Mtwara DC 697 Dinyecha

MTWARA Mtwara DC 698 Mnyawi Sokoni

MTWARA Mtwara DC 699 Mnyahi

MTWARA Mtwara DC 700 Mkumbwanana

MTWARA Mtwara DC 701 Mitangani

Page 234: Tekeleza kwa

232

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MTWARA Mtwara DC 702 Chikwaya

MTWARA Mtwara DC 703 Milangominne

MTWARA Mtwara DC 704 Mnyawi shuleni

MTWARA Mtwara DC 705 Mnyawi Barabarni

MTWARA Mtwara DC 706 Namtumbuka

MTWARA Mtwara DC 707 Namtumbuka shuleni

MTWARA Mtwara DC 708 Mnongodi

MTWARA Mtwara DC 571 Naumbu 709 Naumbu 9 1,487

MTWARA Mtwara DC 572 Mahurunga 710 Mahurunga 11 1,888

MTWARA Mtwara DC 573 Kitere 711 Kitere 46 10,709

MTWARA Mtwara DC 574 Miule 712 Miule 8 1,176

MTWARA Mtwara DC 575 Libobe 713 Libobe 5 469

MTWARA Mtwara DC 576 Nanguruwe 714 Nanguruwe 15 2,967

MTWARA Mtwara DC 577 Dihimba 715 Dihimba 9 158

Page 235: Tekeleza kwa

233

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MTWARA Mtwara DC 578 Tangazo 716 Tangazo 12 2,131

MTWARA Mtwara DC 579 Kihimika 717 Kihimika 7 1,033

MTWARA Mtwara DC 580 Mbuo 718 Mbuo 9 1,538

MTWARA Mtwara MC 581 Mjimwema 719 Mjimwema 8 1,229

MTWARA Mtwara MC 582 Rwelu 720 Rwelu 9 1,969

MTWARA Mtwara MC 583 Mbae 721 Mbae 8 1,637

MTWARA Mtwara MC 584 Haikata 722 Haikata 7 615

MTWARA Mtwara MC 585 Mkangala 723 Mkangala 10 2,672

MTWARA Nanyumbu DC 586 Lukula 724 Lukula 24 5,229

MTWARA Nanyumbu DC 587 Ndwika 725 Ndwika 28 6,229

MTWARA Nanyumbu DC 588 Nandembo 726 Nandembo 44 10,229

MTWARA Nanyumbu DC 589 Chipuputa 727 Chipuputa 22 4,729

MTWARA Nanyumbu DC 590 Chivirikiti 728 Chivirikiti 38 2,514

MTWARA Nanyumbu DC

591 Sengenya, Mara & Ngalinje

729 Sengenya

28 3,998 MTWARA Nanyumbu DC 730 Mara

MTWARA Nanyumbu DC 731 Ngalinje

Page 236: Tekeleza kwa

234

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MTWARA Nanyumbu DC 592 Ndechela 732 Ndechela 1 149

MTWARA Nanyumbu DC 593 Holola 733 Holola 10 2,514

MTWARA Nanyumbu DC 594 Ulanga 734 Ulanga 12 1,830

MTWARA Nanyumbu DC 595 Mangaka 735 Mangaka 12 2,428

MTWARA Newala DC 596 Mdimba 736 Mdimba 22 4,831

MTWARA Newala DC 597 Malatu juu

737 Malatu juu 23 4,979

MTWARA Newala DC 738 Malatu chini

MTWARA Newala DC

598 Chikalule/Mnauya/Mmulunga

739 Chikalule 22 4,479

MTWARA Newala DC 740 Mnauya 17 3,750

MTWARA Newala DC 741 Mmulunga MTWARA Tandahimba DC 599 Matogoro 742 Matogoro 34 7,729 MTWARA Tandahimba DC

600 Mkupete,

743 Mkupete,

22 6,269 MTWARA Tandahimba DC 744 Chikongola,

MTWARA Tandahimba DC 745 Mahuta mjini,

Page 237: Tekeleza kwa

235

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MTWARA Tandahimba DC 746 Mahuta Bondeni

MTWARA Tandahimba DC 747 Lilande

MTWARA Tandahimba DC 601 Likolombe 748 Likolombe 12 2,977

MTWARA Tandahimba DC

602 Mkonjowano,

749 Mkonjowano,

96 23,229

MTWARA Tandahimba DC 750 Chaume,

MTWARA Tandahimba DC 751 Mweru,

MTWARA Tandahimba DC 752 Chiwonda

MTWARA Tandahimba DC 753 Chimbuko

MTWARA Tandahimba DC 603 Mihambwe 754 Mihambwe 15 3,283

MTWARA Tandahimba DC 604 Malamba 755 Malamba 8 1,619

Page 238: Tekeleza kwa

236

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MTWARA Tandahimba DC 605 Litehu 756 Litehu

39 7,544 MTWARA Tandahimba DC 606 Libobe 757 Libobe

MTWARA Tandahimba DC 607 Mkola chini 758 Mkola chini

MWANZA Kwimba DC 608 Ishingisha 759 Ishingisha 66 16,327

MWANZA Kwimba DC 609 Mwabilanda 760 Mwabilanda 42 10,204

MWANZA Kwimba DC 610 Nyambiti 761 Nyambiti 50 12,245

MWANZA Kwimba DC

611 Ngudu

762 Ngudu 120 29,655

MWANZA Kwimba DC 763 Chibuji 20 4,800

MWANZA Kwimba DC 764 Ndami 11 2,400

MWANZA Kwimba DC 765 Nyahonge 15 3,600

MWANZA Kwimba DC 766 Igumagodo 17 3,900

MWANZA Kwimba DC 767 Lumele 13 3,000

MWANZA Kwimba DC 768 Igunghya 32 7,800

MWANZA Kwimba DC 612 Gatuli 769 Gatuli 13 3,000

Page 239: Tekeleza kwa

237

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MWANZA Kwimba DC 613 Maro 770 Maro 13 3,600

MWANZA Kwimba DC 614 Sasalawe 771 Sasalawe 20 4,800

MWANZA Kwimba DC 615 Mwarujo 772 Mwarujo 23 5,400

MWANZA Kwimba DC 616 Milyungu 773 Milyungu 27 6,600

MWANZA Kwimba DC 617 Kawekamo 774 Kawekamo 18 4,200

MWANZA Kwimba DC 618 Sanga 775 Sanga 25 6,000

MWANZA Kwimba DC 619 Butigiti 776 Butigiti 11 2,400

MWANZA Kwimba DC 620 Malya 777 Malya 1 2,500

MWANZA Sengerema DC 621 Nyamtelela

778 Nyamtelela 100 24,741

MWANZA Sengerema DC 779 Katunguru

MWANZA Sengerema DC 622 Kalebezo 780 Kalebezo

48 11,750

MWANZA Sengerema DC 623 Nyehunge 781 Nyehunge

MWANZA Sengerema DC 624 Lwenge, 782 Lwenge,

MWANZA Sengerema DC 625 Butonga, 783 Butonga,

MWANZA Sengerema DC 626 Kanyelele, 784 Kanyelele,

MWANZA Sengerema DC 627 Igwanzozu, 785 Igwanzozu,

Page 240: Tekeleza kwa

238

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MWANZA Sengerema DC 628 Kagunga, 786 Kagunga,

MWANZA Sengerema DC 629 Mwabaluhi 787 Mwabaluhi

MWANZA Sengerema DC 630 Buzilasoga 788 Buzilasoga

MWANZA Misungwi DC 631 Fella 789 Fella 59 14,286

MWANZA Misungwi DC 632 Isesa 790 Isesa 50 12,245

MWANZA Misungwi DC 633 Inonelwa 791 Inonelwa 4 1,020

MWANZA Misungwi DC 634 Ngudama 792 Ngudama 1 248

MWANZA Misungwi DC 635 Nyamatala 793 Nyamatala 1 456

MWANZA Misungwi DC 636 Kabale 794 Kabale 1 359

MWANZA Misungwi DC 637 Igenge 795 Igenge 1 235

MWANZA Misungwi DC 638 Mwasonge 796 Mwasonge 1 307

MWANZA Magu 639 Ilula 797 Ilula 1 279

MWANZA Magu 640 Lugeye 798 Lugeye 1 308

MWANZA Magu 641 Budilya 799 Budilya 1 412

MWANZA Magu 642 Mwaniga 800 Mwaniga 1 332

MWANZA Magu 643 Isangijo 801 Isangijo 1 432

Page 241: Tekeleza kwa

239

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

MWANZA Magu 644 Nyanguge - Muda 802 Nyanguge

30 7,250 MWANZA Magu 645 Nyanguge -

Muda 803 Muda

MWANZA Magu 646 kahagala-lutale 804 kahagala 11 2,393

MWANZA Magu 647 kahagala-lutale 805 lutale

MWANZA Ilemela 648 Kayenze 806 Kayenze 4 9,865

NJOMBE Njombe DC 649 Image 807 Image 29 2,519

NJOMBE Njombe DC 650 Ihang'ana 808 Ihang'ana 14 1,200

NJOMBE Njombe DC 651 Tagamenda 809 Tagamenda 4 1,500

NJOMBE Njombe DC 652 Welela 810 Welela 2 650

NJOMBE Njombe DC 653 Ibumila 811 Ibumila 35 4,599

NJOMBE Njombe DC 654 Itambo 812 Itambo 4 935

NJOMBE Njombe TC 655 Limage 813 Limage 16 1,672

NJOMBE Njombe TC 656 Igominyi 814 Igominyi 9 1,100

NJOMBE Wanging'ombe DC 657 Masaulwa 815 Masaulwa 83 20,409

Page 242: Tekeleza kwa

240

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

NJOMBE Wanging'ombe DC 658 Tagamenda 816 Tagamend

a 4 1,500

NJOMBE Wanging'ombe DC 659 Welela 817 Welela 2 500

NJOMBE Ludewa DC 660 Mbwila 818 Mbwila 50 12,245

NJOMBE Ludewa DC 661 Ilininda 819 Ilininda 50 12,245

NJOMBE Ludewa DC 662 Lifua 820 Lifua 21 5,000

NJOMBE Ludewa DC 663 Lihagule 821 Lihagule 9 2,000

NJOMBE Makete DC 664 Ubiluko 822 Ubiluko

30 6,872 NJOMBE Makete DC

665 Mpangala

823 Mpangala

NJOMBE Makete DC 824 Matamba

NJOMBE Makete DC 825 Mbela 62 15,307

NJOMBE Makete DC 826 Mlondwe 9 2,088

NJOMBE Makete DC 666 Tagamenda 827 Tagamenda 4 1,500

NJOMBE Makete DC 667 Welela 828 Welela 2 500

NJOMBE Makete DC 668 Ibumila 829 Ibumila 35 4,599

Page 243: Tekeleza kwa

241

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

NJOMBE Makambako TC 669 Kifumbe 830 Kifumbe 39 4,454

PWANI Bagamoyo DC 670 Kiharaka 831 Kiharaka 21 4,729

PWANI Bagamoyo DC 671 Milo 832 Milo 9 1,000

PWANI Bagamoyo DC 672 Mataya 833 Mataya 29 3,500

PWANI Bagamoyo DC 673 Yombo 834 Yombo 31 3,750

PWANI Bagamoyo DC 674 Kidogozero-Kitonga 835 Kidogozero

-Kitonga 23 2,750

PWANI Bagamoyo DC 675 Sadani 836 Sadani 10 2,000

PWANI Kibaha TC 676 Mwanalugali 837 Mwanalugali 23 5,230

PWANI Kibaha TC

677 ZOJOSA

838 Zogowale,

17 3,728 PWANI Kibaha TC 839 Saeni

PWANI Kibaha TC 840 Jonhgha

PWANI Kibaha TC 678 Vikawe

841 Shule 31 7,229

PWANI Kibaha TC 842 Bondeni

PWANI Kibaha TC 679 Viziwaziwa/Sagal

e 843 Viziwaziwa

17 3,731 PWANI Kibaha TC 844 Sagale

Page 244: Tekeleza kwa

242

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

PWANI Kibaha DC 680 Ngeta 845 Ngeta 21 4,727

PWANI Kibaha DC 681 Msongola 846 Msongola 19 4,008

PWANI Kibaha DC 682 Kipangege 847 Kipangege 5 772

PWANI Kibaha DC 683 Lupunga

848 Lupunga 29 6,732

PWANI Kibaha DC 849 Kikongo

PWANI Kibaha DC 684 Mwanabwito, 850 Mwanabwito,

33 7,726 PWANI Kibaha DC 685 Kisabi 851 Kisabi

PWANI Kibaha DC 686 Madimala 852 Madimala

PWANI Kibaha DC 687 Vikuruti 853 Vikuruti 11 2,618

PWANI Kibaha DC 688 Bokomnemela 854 Bokomnemela 21 4,907

PWANI Kibaha DC 689 Dutumi 855 Dutumi 10 2,225

PWANI Mafia DC 690 Chunguruma 856 Chunguruma 22 10,224

PWANI Mafia DC 691 Jimbo 857 Jimbo

PWANI Mafia DC 692 Kanga 858 Kanga 13 2,723

PWANI Mafia DC 693 Mlongo 859 Mlongo 7 1,874

Page 245: Tekeleza kwa

243

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

PWANI Mafia DC 694 Kungwi 860 Kungwi 17 2,868

PWANI Rufiji DC 695 Uponda 861 Uponda 29 6,710

PWANI Rufiji DC 696 Kiwanga 862 Kiwanga 13 2,720

PWANI Rufiji DC 697 Ngorongo 863 Ngorongo 23 5,213

PWANI Rufiji DC 698 Mbwara 864 Mbwara 23 5,214

PWANI Rufiji DC 699 Muyuyu 865 Muyuyu 13 2,719

PWANI Rufiji DC 700 Hanga 866 Hanga 13 2,729

PWANI Rufiji DC 701 Mkenda/Kivinja B

867 Mkenda 17 1343

PWANI Rufiji DC 868 Kivinja B

PWANI Mkuranga DC 702 Kilamba 869 Kilamba 13 2,678

PWANI Mkuranga DC

703 Kilimahewa

870 Kilimahewa

39 9,229 PWANI Mkuranga DC 871 Kusini

PWANI Mkuranga DC 872 Mvuleni

PWANI Mkuranga DC 704 Mandimkongo 873 Mandimkongo 1 302

PWANI Mkuranga DC 705 Mandimpera 874 Mandimpera 1 195

Page 246: Tekeleza kwa

244

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

PWANI Mkuranga DC 706 Tundu 875 Tundu 1 253

PWANI Mkuranga DC 707 Tipo 876 Tipo 19 4,147

PWANI Mkuranga DC 708 Nyanduturu 877 Nyanduturu 15 3,311

PWANI Mkuranga DC 709 Bupu 878 Bupu 15 3,128

PWANI Kisarawe 710 Kibuta 879 Kibuta 13 2,830

PWANI Kisarawe 711 Kihare 880 Kihare 11 2,309

PWANI Kisarawe 712 Chakenge 881 Chakenge 11 2,149

PWANI Kisarawe 713 Msanga 882 Msanga 8 3,089

PWANI Kisarawe 714 Mafizi 883 Mafizi 9 2,088

RUKWA Sumbawanga MC 715 Kanondo 884 Kanondo 54 11,456

RUKWA Sumbawanga MC 716 Chelenganya 885 Chelengan

ya 25 5,658

RUKWA Sumbawanga MC 717 Kilyamatundu 886 Kilyamatun

du 27 6,300

RUKWA Sumbawanga MC 718 Malonje 887 Malonje 29 6,760

Page 247: Tekeleza kwa

245

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

RUKWA Sumbawanga MC 719 Mlanda 888 Mlanda 65 16,000

RUKWA Sumbawanga MC

720 Pito/Malagano/Tamasenga

889 Pitoga

125 31,000 RUKWA Sumbawanga MC 890 Malagano

RUKWA Sumbawanga MC 891 Tamasen

RUKWA Sumbawanga MC

721

Mponda 892 Mponda 31 4,427

RUKWA Nkasi DC Chala B 893 Chala B 29 6,698

RUKWA Nkasi DC Chala A 894 Chala A 54 13,290

RUKWA Nkasi DC 722 Chala C 895 Chala C

RUKWA Nkasi DC 723 King'ombe 896 King'ombe 19 4,500

RUKWA Nkasi DC 724 Matala 897 Matala 23 4096

RUKWA Kalambo 725 Matai/Kisungamil

e

898 Matai 25 10,514

RUKWA Kalambo 899 Kisungamile

RUKWA Kalambo 726 Mwimbi 900 Mwimbi 33 7,029

Page 248: Tekeleza kwa

246

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

RUKWA Kalambo 727 Matai

901 Matai 49 11,785

RUKWA Kalambo 902 Kisungamile

RUKWA Sumbawanga DC 728 Nankanga 903 Nankanga 16 8,004

RUKWA Sumbawanga DC 729 Kinambo 904 Kinambo 14 4,507

RUKWA Sumbawanga DC 730 Solola 905 Solola 13 1,932

RUKWA Sumbawanga DC 731 Laela 906 Laela 19 21,068

RUKWA Sumbawanga DC 732 Kamnyazya 907 Kamnyazya 25 16,625

RUVUMA Songea MC 733 Mahilo 908 Mahilo 17 4,082

RUVUMA Songea MC 734 Chandarua

909 Chandarua shuleni

8 1,501 RUVUMA Songea MC 910 Chandarua

Jeshini RUVUMA Songea MC 735 Mahinya 911 Mahinya 9 1,570

RUVUMA Songea MC 736 Tanga 912 Tanga 1 250

Page 249: Tekeleza kwa

247

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

RUVUMA Songea MC 737 Mletele 913 Mletele 1 250

RUVUMA Namtumbo DC 738 Ulamboni 914 Ulamboni 21 4,831

RUVUMA Namtumbo DC 738 Nakawale

&Mwangaza 915 Nakawale

71 17,229 RUVUMA Namtumbo DC 916 Mwangaza

RUVUMA Mbinga DC 739 Kigonsera 917 Kigonsera 39 9,229

RUVUMA Mbinga DC 740 Litumbakuhamba 918 Litumbakuhamba 12 2,109

RUVUMA Mbinga DC

741 Mango group

919 Kihagara

199 49,500

RUVUMA Mbinga DC 920 Tumbi

RUVUMA Mbinga DC 921 Mango

RUVUMA Mbinga DC 922 Luli

RUVUMA Mbinga DC 923 Puulu

RUVUMA Mbinga DC 924 Nkalachi

RUVUMA Mbinga DC 925 Hongi

RUVUMA Mbinga DC 926 Mkali

RUVUMA Mbinga DC 742 Mahande 927 Mahande 25 1,182

Page 250: Tekeleza kwa

248

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

RUVUMA Songea DC 743 Liweta 928 Liweta 7 1,229

RUVUMA Songea DC 744 Masigira 929 Masigira 10 1,865

RUVUMA Songea DC 745 Likyufusi 930 Likyufusi 13 2,775

RUVUMA Songea DC 746 Mkongotema/Ma

gingo 931 Mkongotem

a 26 5,841 RUVUMA Songea DC 932 Magingo

RUVUMA Songea DC 747 Mgazini 933 Mgazini 41 9,852

RUVUMA Tunduru

748 Nandembo

934 Nandembo

23 6,515 RUVUMA Tunduru 935 Amka

RUVUMA Tunduru 936 Nangunguru

RUVUMA Tunduru

749 Nalasi

937 Nalasi

38 13,909 RUVUMA Tunduru 938 Lipepo

RUVUMA Tunduru 939 Chilundundu

RUVUMA Tunduru 750 Tinginya 940 Tinginya 35 8,750

RUVUMA Tunduru 751 Lukumbo 941 Lukumbo 7 1,500

RUVUMA Nyasa 752 Ukuli-Kingerikiti 942 Ukuli 73 17,729

Page 251: Tekeleza kwa

249

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

RUVUMA Nyasa 943 Kingerikiti

RUVUMA Nyasa 753 Lundu 944 Lundu 43 10,500

RUVUMA Nyasa

754 Lituhi Group

945 Lituhi

51 12,500

RUVUMA Nyasa 946 Ngingama

RUVUMA Nyasa 947 Kihuru

RUVUMA Nyasa 948 Nkaya

RUVUMA Nyasa 949 Mwerampya

RUVUMA Nyasa

755 Ndengele-Chinula Group

950 Ndengele

37 8,500 RUVUMA Nyasa 951 Chinula

RUVUMA Nyasa 952 Mbuyula

RUVUMA Nyasa 756 Lundo-Lipingo

group 953 Lundo

36 9,000 RUVUMA Nyasa 954 Lipingo

RUVUMA Nyasa 757 Mitomoni 955 Mitomoni 4 1,000

RUVUMA Nyasa 758 Tingi 956 Tingi 31 14,500

RUVUMA Nyasa 759 Mtipwili 957 Mtipwili 30 7,500

RUVUMA Nyasa 760 Chimte group 958 Chimte 25 6,000

Page 252: Tekeleza kwa

250

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

RUVUMA Nyasa 959 Kwambe

RUVUMA Nyasa 960 Matenje

RUVUMA Nyasa

761 Lunyele group

961 Lunyele

33 8,000 RUVUMA Nyasa 962 Songea pori

RUVUMA Nyasa 963 Tanzania one

RUVUMA Nyasa 762 Ng'ombo 964 Ng'ombo 47 11,500

RUVUMA Nyasa 763 Nangombo 965 Nangombo 73 18,000

RUVUMA Nyasa 764 Liparamba 966 Liparamba 4 1,000

RUVUMA Nyasa

765 Kilosa

967 Kilosa

137 34,000 RUVUMA Nyasa 968 Likwilu

RUVUMA Nyasa 969 Ruhekei

RUVUMA Nyasa 766 Litindoasili-

Lumecha 970 Litindoasili

57 14,000 RUVUMA Nyasa 971 Lumecha

RUVUMA Nyasa 767 Ngindo 972 Ngindo 9 2,000

RUVUMA Nyasa 768 Mbamba Bay group 973 Mbamba

Bay 179 44,500

Page 253: Tekeleza kwa

251

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

RUVUMA Nyasa 974 Ndesule

SHINYANGA Kahama 769 Segese 975 Segese 168 41,838

SHINYANGA Kahama 770 Bulige 976 Bulige 83 20,409

SHINYANGA Kahama 771 Chela 977 Chela 58 14,286

SHINYANGA Kahama 772 Kagongwa 978 Kagongwa 22 8,162

SHINYANGA Ushetu 773 Nyamilangano 979 Nyamilangano 27 6,167

SHINYANGA Ushetu 774 Shaka 980 Shaka 37 3,723

SHINYANGA Kishapu 775 Mwamashimba 981 Mwamashimba 95 23,470

SHINYANGA Kishapu 776 Mwigumbi 982 Mwigumbi 62 15,307

SHINYANGA Kishapu 777 Nyenze/Sekeididi

/ 983 Nyenze

11 2,607 SHINYANGA Kishapu 984 Sekeididi

SHINYANGA Kishapu 778 Iboja/Bulekela

985 Iboja

SHINYANGA Kishapu 986 Bulekela

SHINYANGA Kishapu 779 Mwamadulu 987 Mwamadulu 16 2,145

SHINYANGA Kishapu 780 Bubinza 988 Bubinza 17 1,893

Page 254: Tekeleza kwa

252

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

SHINYANGA Kishapu 781 Buganika 989 Buganika 1 390

SHINYANGA Kishapu 782 Idukilo 990 Idukilo 1 382

SHINYANGA Kishapu 783 Bulima 991 Bulima 1 354

SHINYANGA Kishapu 784 Ilula 992 Ilula 1 158

SHINYANGA Shinyanga DC 785 Sayu 993 Sayu 45 11,225

SHINYANGA Shinyanga DC 786 Kazuni 994 Kazuni 53 13,266

SHINYANGA Shinyanga DC 787 Bunonga 995 Bunonga 41 10,204

SHINYANGA Shinyanga DC 788 Mishepo 996 Mishepo 18 2,473

SHINYANGA Shinyanga DC 789 Didia 997 Didia 24 6,000

SHINYANGA Shinyanga MC 790 Ndembezi 998 Ndembezi 33 8,164

SHINYANGA Shinyanga MC 791 Mwamalili/sesek

o 999 Mwamalili

86 21,429 SHINYANGA Shinyanga MC 1000 Seseko

SHINYANGA Shinyanga MC 792 Mwagala 1001 Mwagala 38 9,184

SHINYANGA Shinyanga MC 793 Mwamagunguli 1002 Mwamagunguli 42 10,204

SHINYANGA Shinyanga MC 794 Bugimbagu 1003 Bugimbagu 27 5,102

SHINYANGA Shinyanga MC 795 Mwamashele 1004 Mwamashe 30 7,143

Page 255: Tekeleza kwa

253

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

le

SHINYANGA Shinyanga MC 796 Bushola 1005 Bushola 15 2,438

SHINYANGA Msalala 797 Magombe 1006 Magombe 14 3,216

SHINYANGA Msalala 798 Kakuru 1007 Kakuru 11 2,457

SHINYANGA Msalala 799 Nyashimbi 1008 Nyashimbi 19 2,509

SHINYANGA Msalala 800 Butegwa 1009 Butegwa 12 1,482

SHINYANGA Msalala 801 Buganzo 1010 Buganzo 1 423

SHINYANGA Msalala 802 Kalagwa(Ngelela) 1011 Kalagwa(N

gelela) 1 367

SHINYANGA Msalala 803 Kalagwa(Jamida) 1012 Kalagwa(Jamida) 1 321

SHINYANGA Msalala 804 Mhandu 1013 Mhandu 1 271

SHINYANGA Msalala 805 Bukwangu 1014 Bukwangu 1 437

SHINYANGA Msalala 806 Gulla 1015 Gulla 1 609

SHINYANGA Msalala 807 Ntobo sekondari 1016 Ntobo sekondari 1 572

SHINYANGA Msalala 808 Wichamike 1017 Wichamike 1 306

Page 256: Tekeleza kwa

254

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

SHINYANGA Msalala 809 Masabi 1018 Masabi 1 265

SHINYANGA Msalala 810 Igwamanoni 1019 Igwamanoni 1 450

SHINYANGA Msalala 811 Buyange 1020 Buyange 1 227

SHINYANGA Msalala 812 Bushing’we 1021 Bushing’we 1 204

SHINYANGA Msalala 813 Bushing’we A 1022 Bushing’we A 1 284

SHINYANGA Msalala 814 Bushing’we B 1023 Bushing’we B 1 267

SHINYANGA Msalala 815 Bushing’we kati 1024 Bushing’we kati 1 279

SHINYANGA Msalala 816 Mkolani 1025 Mkolani 1 580

SHINYANGA Msalala 817 Kakola 1026 Kakola 1 439

SHINYANGA Msalala 818 Kabale 1027 Kabale 1 480

SHINYANGA Msalala 819 Rwabakanga 1028 Rwabakanga 1 479

SHINYANGA Msalala 820 Buyange 1029 Buyange 1 269

SHINYANGA Msalala 821 Bugarama 1030 Bugarama 1 356

SHINYANGA Msalala 822 Kakola 1031 Kakola 1 421

Page 257: Tekeleza kwa

255

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

SHINYANGA Msalala 823 Bushing’we B 1032 Bushing’we B 1 392

SHINYANGA Msalala 824 Kakola Na.9 1033 Kakola Na.11 1 202

SHINYANGA Msalala 825 Buganzo 1034 Buganzo 1 478

SHINYANGA Msalala 826 Gula 1035 Gula 1 512

SHINYANGA Msalala 827 Chela 1036 Chela 1 430

SHINYANGA Msalala 828 Mwazimba 1037 Mwazimba 1 398

SHINYANGA Msalala 829 Ntobo A 1038 Ntobo A 1 349

SHINYANGA Msalala 830 Buganzo 1039 Buganzo 1 292

SHINYANGA Msalala 831 Gula 1040 Gula 1 342

SHINYANGA Msalala 832 Kalagwa 1041 Kalagwa 1 690

SHINYANGA Msalala 833 Kalagwa 1042 Kalagwa 1 523

SHINYANGA Msalala 834 Mhandu 1043 Mhandu 1 346

SIMIYU Maswa 835 Malampaka 1044 Malampaka 53 13,056

SIMIYU Maswa 836 Mwasayi 1045 Mwasayi 42 9,800

SIMIYU Maswa 837 Sayusayu 1046 Sayusayu 10 5,410

Page 258: Tekeleza kwa

256

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

SIMIYU Maswa 838 Njiapanda 1047 Njiapanda 11 4,300

SIMIYU Meatu 839 Sakasaka 1048 Sakasaka 58 14,286

SIMIYU Meatu 840 Mwang'humbi 1049 Mwang'humbi 30 7,143

SIMIYU Busega 841 Nyangili 1050 Nyangili 54 13,266

SIMIYU Busega 842 Mwamanyili 1051 Mwamanyili 13 3,500

SIMIYU Busega 843 Bukabile 1052 Bukabile 4 1,000

SIMIYU Busega 844 Bulima 1053 Bulima

SIMIYU Bariadi 845 Luguru 1054 Zanzui 63 13,815

SIMIYU Bariadi 846 Luguru 1055 Luguru

SINGIDA Iramba DC 847 Nguvumali 1056 Nguvumali 87 21,158

SINGIDA Iramba DC 848 Mkalama 1057 Mkalama 50 11,974

SINGIDA Iramba DC 849 Mingela 1058 Mingela 54 12,995

SINGIDA Iramba DC 850 Ng'ang'uli 1059 Ng'ang'uli 42 10,204

SINGIDA Iramba DC 851 Kidarafa 1060 Kidarafa 16 9,023

SINGIDA Iramba DC 852 Mampanta 1061 Mampanta 23 5,500

SINGIDA Manyoni 853 Majiri 1062 Majiri 34 7,893

Page 259: Tekeleza kwa

257

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

SINGIDA Manyoni 854 Solya/Kilimatinde

1063 Solya 49 11,974

SINGIDA Manyoni 1064 Kilimatinde

SINGIDA Manyoni 855 Rungwa 1065 Rungwa 21 4,831

SINGIDA Manyoni 856 Londoni 1066 Londoni 23 7,896

SINGIDA Singida DC 857 Siuyu 1067 Siuyu 46 10,954

SINGIDA Singida DC 858 Nkhoiree 1068 Nkhoiree 34 7,893

SINGIDA Singida DC 859 Puma 1069 Puma 38 8,913

SINGIDA Singida DC 860 Ughandi 'A' 1070 Ughandi 'A' 54 12,995

SINGIDA Singida DC 861 Mjughuda 1071 Mjughuda

38 8,913 SINGIDA Singida DC 862 Mgungira 1072 Mgungira

SINGIDA Singida DC 863 Laghanida 1073 Laghanida

SINGIDA Singida DC 864 Mipilo 1074 Mipilo

SINGIDA Singida DC 865 Sefunga 1075 Sefunga 25 6,000

SINGIDA Singida DC 866 Nkuhi 1076 Nkuhi 29 7,000

SINGIDA Singida MC 867 Ititi 1077 Ititi. 58 14,015

SINGIDA Singida MC 868 Mwankoko A 1078 Mwankoko A. 54 12,995

Page 260: Tekeleza kwa

258

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

SINGIDA Singida MC 869 Kisasi 1079 Kisasi 32 3,387

TABORA Tabora MC

870 Uyui, Itonjanda, Imalamihayo,Inala na Ndevelwa

1080 Uyui,

21 4,831

TABORA Tabora MC 1081 Itonjanda,

TABORA Tabora MC 1082 Imalamihayo

TABORA Tabora MC 1083 ,Inala

TABORA Tabora MC 1084 Ndevelwa

TABORA Tabora MC 871 Kabila 1085 Kabila 18 3,979

TABORA Tabora MC 872 Kalunde

1086 Kalunde 43 5,199

TABORA Tabora MC 1087 Igombe

TABORA Nzega DC 873 Uhemeli 1088 Uhemeli 99 24,306

TABORA Nzega DC 874 Mahene/Ikindwa 1089 Mahene 25 5,662

TABORA Nzega DC 875 Mahene/Ikindwa 1090 Ikindwa 14 2,491

TABORA Nzega DC 876 Buhondo/Sigili/Nawa 1091 Buhondo

39 9,750 TABORA Nzega DC 877 Buhondo/Sigili/Nawa 1092 Sigili

TABORA Nzega DC 878 Buhondo/Sigili/Nawa 1093 Nawa

Page 261: Tekeleza kwa

259

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TABORA Nzega DC 879 Nata 1094 Nata 33 7,529

TABORA Nzega DC 880 Itobo 1095 Itobo 24 4,890

TABORA Nzega DC 881 Bulambuka 1096 Bulambuka 1 355

TABORA Nzega DC 882 Upambo 1097 Upambo 1 472

TABORA Nzega DC 883 Lububu 1098 Lububu 1 1356

TABORA Igunga DC 884 Matinje 1099 Matinje 41 5,105

TABORA Igunga DC 885 Mwandihimiji 1100 Mwandihimiji 33 5,363

TABORA Igunga DC 886 Bulumbela 1101 Bulumbela 51 5,009

TABORA Igunga DC 887 Mwalala 1102 Mwalala 17 6,729

TABORA Igunga DC 888 Mgongoro 1103 Mgongoro 15 3,938

TABORA Uyui DC 889 Mwakashindye 1104 Mwakashindye 13 2,729

TABORA Uyui DC 890 Msimba 1105 Msimba 42 9,933

TABORA Uyui DC 891 Malongwe 1106 Malongwe 24 5,852

TABORA Uyui DC 892 Kizengi 1107 Kizengi 2 500

TABORA Uyui DC 893 Malongwe 1108 Malongwe 13 2,729

Page 262: Tekeleza kwa

260

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TABORA Uyui DC 894 Miswaki 1109 Miswaki 1 367

TABORA Uyui DC 895 Lutona 1110 Lutona 1 303

TABORA Uyui DC 896 Mwakadala 1111 Mwakadala 1 378

TABORA Uyui DC 897 Isimu 1112 Isimu 1 1,278

TABORA Uyui DC 898 Kilungu 1113 Kilungu 1 534

TABORA Uyui DC 899 Imalauduki 1114 Imalauduki 1 324

TABORA Sikonge DC

900 Mibono

1115 Kiloleli 79 1,911

TABORA Sikonge DC 1116 Kanyamsenga 30 6,872

TABORA Sikonge DC 1117 Ukondamoyo 17 3,729

TABORA Sikonge DC 1118 Lembeli 19 4,500

TABORA Sikonge DC 1119 Imalampaka 20 4,750

TABORA Sikonge DC 1120 Mtakuja 23 5,500

TABORA Sikonge DC 901 Majojoro 1121 Majojoro 8 2,262

TABORA Sikonge DC 902 Kilumbi 1122 Kilumbi 1 1279

TABORA Sikonge DC 903 Tumbili 1123 Tumbili 1 1303

Page 263: Tekeleza kwa

261

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TABORA Urambo DC 904 Ukondamoyo 1124 Ukondamoyo 21 342

TABORA Urambo DC 905 Songambele 1125 Songambele 29 3,946

TABORA Kaliua 906 Uhindi 1126 Uhindi 17 4,000

TABORA Kaliua 907 Ushokola 1127 Ushokola 1 342

TABORA Kaliua 908 Imalamihayo. 1128 Imalamihayo. 1 67

TANGA Kilindi DC 909 Kikunde 1129 Kikunde 31 11,974

TANGA Kilindi DC 910 Negero 1130 Negero 30 6,872

TANGA Kilindi DC 911 Chamtui 1131 Chamtui

35 7,729 TANGA Kilindi DC 912 Chamtui 1132 Nyamaleni

TANGA Kilindi DC 913 Chamtui 1133 Mtakuja

TANGA Kilindi DC 914 Kwekivu 1134 Kwekivu 13 3,229

TANGA Kilindi DC 915 Kwedboma 1135 Kwedboma 49 11,729

TANGA Kilindi DC 916 Negero 1136 Negero 13 3,229

TANGA Korogwe D C 917 Vugiri 1137 Vugiri 21 4,729

TANGA Korogwe D C 918 Kwashemshi 1138 Kwashemshi 23 5,229

Page 264: Tekeleza kwa

262

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TANGA Korogwe D C 919 Bungu 1139 Bungu 12 2,503

TANGA Korogwe D C 920 Bungu 1140 Bungu Msiga 9 1,822

TANGA Korogwe D C 921 Bungu 1141 Msasa 6 960

TANGA Korogwe D C 922 Bungu 1142 Manka 11 2,424

TANGA Korogwe D C 923 Foroforo 1143 Foroforo 8 1,407

TANGA Korogwe D C 924 Bagamoyo 1144 Bagamoyo 4 691

TANGA Korogwe D C 925 Mlalo 1145 Mlalo 3 478

TANGA Korogwe D C 926 Makweli 1146 Makweli 8 1,282

TANGA Korogwe D C 927 Mali 1147 Mali 13 2,676

TANGA Korogwe D C 928 Lewa 1148 Lewa 6 1,057

TANGA Korogwe D C 929 Welei 1149 Welei 11 2,412

TANGA Korogwe D C 930 Magamba Kwalukong 1150 Magamba

Kwalukong 1 421

TANGA Korogwe D C 931 Kijango 1151 Kijango 1 467

TANGA Korogwe D C 932 Kwamhaya 1152 Kwamhaya 2 574

TANGA Korogwe D C 933 Kwalukonge 1153 Kwalukonge 13 3,113

Page 265: Tekeleza kwa

263

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TANGA Korogwe D C 934 Makumba 1154 Makumba 19 4,029

TANGA Korogwe D C 935 Mnyuzi 1155 Mnyuzi 11 2,334

TANGA Korogwe TC 936 Kwamndolwa/Kw

ameta 1156 Kwamndol

wa 24 5,479 TANGA Korogwe TC 1157 Kwameta

TANGA Korogwe TC 937 Kwasemangube 1158 Kwasemangube 33 7,729

TANGA Korogwe TC 938 Msambiazi 1159 Msambiazi 2 656

TANGA Korogwe TC 939 Lwengera Relini 1160 Lwengera Relini 2 578

TANGA Korogwe TC 940 Mgambo na Mgombezi 1161 Mgambo

22 5,346 TANGA Korogwe TC 941 Mgambo na

Mgombezi 1162 Mgombezi

TANGA Bumbuli 942 Bumbuli

1163 Bumbuli Kaya 99 24,220

TANGA Bumbuli 1164 Bumbuli Mission

TANGA Bumbuli 943 Kweminyasa

1165 Kweminyasa, 48 11,576

TANGA Bumbuli 1166 Mhange

Page 266: Tekeleza kwa

264

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TANGA Bumbuli 1167 Mponde

TANGA Lushoto DC 944 Irente

1168 Irente 54 12,995

TANGA Lushoto DC 1169 Muhelo TANGA Lushoto DC 945 Kivingo 1170 Kivingo 29 2,350

TANGA Lushoto DC 946 Mwangoi -Mlalo 1171 Dule juu,

55 14,525

TANGA Lushoto DC 947 Mwangoi -Mlalo 1172 Mlesa,

TANGA Lushoto DC 948 Mwangoi -Mlalo 1173 Dule chini,

TANGA Lushoto DC 949 Mwangoi -Mlalo 1174 Handei,

TANGA Lushoto DC 950 Mwangoi -Mlalo 1175 Ngazi,

TANGA Lushoto DC 951 Mwangoi -Mlalo 1176 Mlalo,

TANGA Lushoto DC 952 Mwangoi -Mlalo 1177 Mhelo,

TANGA Lushoto DC 953 Mwangoi -Mlalo 1178 Kwemshasha,

TANGA Lushoto DC 954 Mwangoi -Mlalo 1179 Mwangoi

TANGA Lushoto DC 955 Mwangoi -Mlalo 1180 Majulai

TANGA Mkinga DC 956 Daluni Kibaoni 1181 Daluni Kibaoni 36 8,391

Page 267: Tekeleza kwa

265

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TANGA Mkinga DC 1182 Mtoni Bombo

TANGA Mkinga DC 1183 Ng'ombeni

TANGA Mkinga DC 957 Mtibwani 1184 Mtibwani 9 1,882

TANGA Mkinga DC 958 Boma 1185 Boma 7 1,424

TANGA Muheza DC

959 Ubembe -kwemhosi

1186 Ubembe 30 6,872

TANGA Muheza DC 1187 Kisiwani Nkumba 34 7,893

TANGA Muheza DC 1188 Kibanda Nkumba 30 6,872

TANGA Muheza DC 1189 Kwemhosi 50 11,974

TANGA Muheza DC 1190 Misongeni 34 7,893

TANGA Muheza DC 960 Ubembe -kwemhosi 1191 Mikwamba 29 6,729

TANGA Muheza DC 961 Kigongomawe 1192 Kigongomawe 11 2,229

TANGA Pangani DC 962 Madanga 1193 Madanga 42 9,933

TANGA Pangani DC 963 Madanga 1194 Jaira

TANGA Pangani DC 964 Bweni 1195 Bweni 34 7,893

Page 268: Tekeleza kwa

266

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

JUMLA YA VITUO

IDADI YA WANANCHI

WANAOPATA MAJI

TANGA Pangani DC 965 Kwakibuyu 1196 Kwakibuyu 37 5,729

TANGA Pangani DC 966 Mzambarauni 1197 Mzambarauni 3 750

TANGA Pangani DC 967 Mwembeni 1198 Mwembeni 5 1,076

TANGA Pangani DC 968 Msaraza 1199 Msaraza 6 1,158

TANGA Pangani DC 969 Kimang'a 1200 Kimang'a 9 1,971

TANGA Pangani DC 970 Mkalamo 1201 Mkalamo 19 4,547

TANGA Pangani DC 971 Lingoni 1202 Lingoni 5 973

TANGA Pangani DC 972 Ushongo 1203 Ushongo 5 881

TANGA Pangani DC 973 Mkwaja 1204 Mkwaja 6 1,324

TANGA Handeni DC 974 Misima 1205 Misima 15 3,578

TANGA Handeni DC 975 Suwa 1206 Suwa 24 5,692

JUMLA KUU 24,129 5,757,855

Page 269: Tekeleza kwa

267

Jedwali Na. 7: Miradi 262 ambayo Utekelezaji upo kati ya Asilimia 71 na Asilimia 95

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

ARUSHA Monduli 1 Engaruka juu 1 Engaruka juu 76 66 15,313 894,029,387

ARUSHA Monduli 2 Eluai 2 Eluai 78 10 2,412 60,903,000

ARUSHA Monduli 3 Emairete 3 Emairete 90 16 3,699 93,399,750

ARUSHA Monduli 4 Moita Bwawani 4 Moita Bwawani

83 44 10,207 257,726,750

ARUSHA Meru DC 5 Nshupu 5 Nshupu 75 24 5,682 87,394,848

ARUSHA Arusha CC 6 Baraa 6 Baraa 76 62 14,525 366,756,250

ARUSHA Karatu 7 Makhoromba 7 Makhoromba 76 16 3,640 91,910,000

ARUSHA Longido 8 Mairouwa 8 Mairouwa 76 63 14,800 373,700,000

ARUSHA Longido 9 Irkaswa 9 Irkaswa 74 69 16,056 405,414,000

ARUSHA Ngorongoro 10 Oldonyosambu 10 Oldonyosambu

78 18 4,225 106,681,250

ARUSHA Arusha DC 11 Nduruma 11 Nduruma 92 38 8,858 400,609,812

ARUSHA Arusha DC 12 Ngaramtoni 12 Ngaramtoni 90 67 15,650 268,680,590

Page 270: Tekeleza kwa

268

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

ARUSHA Arusha DC 13 Likamba 13 Likamba 89 85 19,766 499,091,500

DAR ES SALAAM

Ilala District 14 Pugu Kajiungeni

14 Pugu Kajiungeni

90 116 27,000 184,147,550

DAR ES SALAAM

Ilala District 15 Kipunguni B 90 109 25,380 640,845,000

DAR ES SALAAM

Ilala District 16 Mji mpya 90

DAR ES SALAAM

Ilala District 15 Ugombolwa - Segerea

17 Ugombolwa - Segerea

87 37 8,628 217,857,000

DAR ES SALAAM

Ilala District 16 Kivule 18 Majohe 80 69 16,200 681,668,891

DAR ES SALAAM

Ilala District 17 Amani - Segerea

19 Amani - Segerea

76 35 8,205 207,176,250

DAR ES SALAAM

Ilala District 18 Kidole-Msongola

20 Kidole-Msongola

76 30 7,034 177,608,500

DAR ES SALAAM

Ilala District 19 Yongwe - Msongola

21 Yongwe - Msongola

76 10 2,316 58,479,000

DAR ES SALAAM

Temeke MC 20 Mbagala kuu 22 Kizuiani 89 155 36,161 913,052,625

DAR ES SALAAM

Temeke MC 21 Mianzini 23 Mianzini 90 127 29,736 288,960,000

Page 271: Tekeleza kwa

269

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

DAR ES SALAAM

Temeke MC 22 Pemba Mnazi 24 Chambewa 78 27 6,344 160,173,375

DAR ES SALAAM

Kinondoni MC 23 Mpiji Magohe 25 Mpiji Magohe 87 28 6,647 378,991,192

DODOMA Kondoa 24 Gonga 26 Gonga 87 20 4,574 207,400,950

DODOMA Kondoa 25 Jenjeluse 27 Jenjeluse 90 9 2,014 50,853,500

DODOMA Kondoa 26 Goima 28 Goima 90 15 3,433 86,683,250

DODOMA Kondoa 27 Mlongia 29 Mlongia 90 15 3,426 86,506,500

DODOMA Kondoa 28 Kinkima 30 Kinkima 89 14 3,255 82,188,750

DODOMA Kondoa 29 Kiteo 31 Marumba 89 25 6,220 * * DODOMA Kondoa 30 Lusangi 32 Lusangi 78 2 400 10,100,000

DODOMA Kondoa 31 Songolo 33 Songolo 78 29 6,880 173,720,000

DODOMA Kondoa 32 Churuku 34 Churuku 80 15 3,514 88,728,500

DODOMA Kondoa 33 Jinjo 35 Jinjo 76 9 2,046 51,661,500

DODOMA Kondoa 34 Jangalo 36 Jangalo 78 16 3,657 92,339,250

DODOMA Kondoa 35 Masange 37 Masange 76 33 7,696 194,336,302

Page 272: Tekeleza kwa

270

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

DODOMA Kondoa 36 Kinyasi 38 Kinyasi 76 35 8,132 205,335,117

DODOMA Kondoa 37 Kirere cha Ng'ombe

39 Kirere cha Ng'ombe

76 5 1,080 27,270,000

DODOMA Kondoa 38 Kelema kuu 40 Kelema kuu 79 8 1,763 52,983,989

DODOMA Kongwa District 39 Ibwaga 41 Ibwaga 89 27 6,348 279,836,120

DODOMA Chamwino District

40 Chanhumba 42 Chanhumba 80 16 3,764 170,947,270

DODOMA Chamwino District

41 Mvumi Mission 43 Mvumi Mission 76 70 16,229 687,496,870

DODOMA Mpwapwa District

42 Chunyu 44 Chunyu 76 27 6,393 280,655,920

DODOMA Mpwapwa District

43 Mitenzela 45 Mitenzela 79 16 3,750 171,130,000

DODOMA Chemba 44 Madaha 46 Madaha 89 17 3,934 99,322,127

IRINGA Iringa DC 45 Kikombwe 47 Kikombwe 92 19 4,464 112,716,000

IRINGA Iringa DC 46 Migoli -Mtera 48 Migoli -Mtera 84 19 4,500 113,625,000

IRINGA Iringa DC 47 Malinzanga 49 Malinzanga 74 21 4,854 122,563,500

IRINGA Iringa DC 48 Itengulinyi 50 Lumuli 74 32 7,500 189,375,000

Page 273: Tekeleza kwa

271

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

IRINGA Iringa DC 49 Izazi-Mnadani 51 Izazi-Mnadani 80 15 3,526 89,031,500

IRINGA Iringa MC 50 Ulonge 52 Ulonge 71 15 3,559 89,864,750

IRINGA Iringa MC 51 Kigonzile 53 Kigonzile 78 4 890 22,472,500

IRINGA Kilolo DC 52 Ng'uruhe 54 Ng'uruhe 74 20 4,605 116,276,250

IRINGA Kilolo DC 53 Ihimbo 55 Ihimbo 76 11 2,497 63,049,250

KAGERA Bukoba MC 54 Kibeta 56 Kibeta 87 11 2,456 62,014,000

KAGERA Bukoba MC 55 Kitendaguro 57 Kitendaguro 90 15 3,413 86,178,250

KAGERA Bukoba MC 56 Ihyoro 58 Ihyoro 76 8 1,777 44,869,250

KAGERA Bukoba MC 57 Kyamyosi 59 Kyamyosi 75 18 4,233 106,883,250

KAGERA Bukoba DC 58 Kibona 60 Kibona 89 17 4,035 101,883,750

KAGERA Bukoba DC 59 Kibirizi 61 kibirizi 91 11 2,608 65,852,000

KAGERA Bukoba DC 60 Katale 62 katale 76 27 6,340 160,085,000

KAGERA Muleba 61 Katembe 63 Katembe 84 11 2,560 64,640,000

KAGERA Muleba 62 Kinagi 64 kinagi 85 14 3,245 81,936,250

KAGERA Muleba 63 Kangaza 65 Kangaza 73 10 2,349 59,312,250

Page 274: Tekeleza kwa

272

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

KAGERA Muleba 64 Muyenje 66 Muyenje 72 12 2,771 133,795,663

KAGERA Ngara DC 65 Rwinyana 67 Rwinyana 89 25 5,721 144,455,250

KAGERA Ngara DC 66 Muruvyagila 68 Muruvyagila 87 34 7,986 201,646,500

KAGERA Ngara DC 67 Kanazi/kabalenzi

69 Kanazi/kabalenzi

90 30 7,111 179,552,750

KAGERA Biharamulo DC 68 Katoke 70 Katoke 73 21 4,976 125,644,000

KAGERA Biharamulo DC 69 Kasozibakaya 71 Kasozibakaya 78 26 6,077 153,444,250

KAGERA Karagwe DC 70 chabuhora 72 chabuhora 75 18 4,086 103,171,500

KAGERA Karagwe DC 71 kayungu 73 kayungu 76 14 3,293 83,148,250

KAGERA Misenyi 72 Kibeo 74 Kibeo 72 10 1,158 * * KATAVI Mpanda District 73 Karema 75 Karema 94 27 6,362 21,454,191

KATAVI Mkalalama DC 74 Sepuka Water Supply

76 Sepuka 98 18 4,146 104,686,500

KATAVI Mkalalama DC 75 Makiungu /Unyaghumpi

77 Unyaghumpi 78 20 4,654 117,513,500

KATAVI Mkalalama DC 76 Irisya shallow wells.

78 Mwasutianga. 78 17 3,967 100,166,750

Page 275: Tekeleza kwa

273

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

KATAVI Mlele 77 Mamba 79 Mamba 72 45 10,538 266,084,500

KATAVI Nsimbo 78 Mtamkumbuka 80 Mtamkumbuka 73 30 7,104 179,376,000

KATAVI Nsimbo 79 Isinde 81 Isinde 74 78 18,166 458,691,500

KIGOMA Kibondo 80 Kiduduye 82 Kiduduye 88 21 4,953 44,577,000

KIGOMA Kibondo DC 81 Kiga 83 Kiga 87 22 5,101 128,800,250

KIGOMA Kibondo DC 82 Minyinya 84 Minyinya 78 34 7,931 200,257,750

KIGOMA Kibondo DC 83 Nyankwi 85 Nyankwi 92 65 15,078 380,719,500

KIGOMA Kigoma DC 84 Rukoma 86 Rukoma 74 68 15,810 399,202,500

KIGOMA Kigoma MC 85 Kibirizi 87 Kibirizi, 75 49 31,345

* * KIGOMA Kigoma MC 88 Buhanda 76

KIGOMA Kigoma MC 89 Bushabani, 91

KIGOMA Kigoma MC 90 Buronge, 93

KILIMANJARO

Moshi DC 86 East Scheme 92 Mawanjeni, 90 14 3,250 82,062,500

KILIMANJARO

Moshi DC 93 Kilimo/ 89

Page 276: Tekeleza kwa

274

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

KILIMANJARO

Moshi DC 94 Makami- Chini 76

KILIMANJARO

Moshi DC 95 Makuyuni 78

KILIMANJARO

Moshi DC 87 Makame juu 96 Makame juu 75 11 2,669 55,594,816

KILIMANJARO

Moshi MC 88 Mwenge/Longuo

91 Longuo B 87 46 10,801 272,725,250

KILIMANJARO

Mwanga 89 Vuagha 97 Vuagha 87 11 2,500 63,125,000

KILIMANJARO

Mwanga 90 Kisanjuni 98 Kisanjuni 72 13 2,957 142,713,426

KILIMANJARO

Mwanga 91 Lomwe 99 Lomwe 84 14 3,378 118,378,127

KILIMANJARO

Same 92 Hedaru 100 Hedaru 75 92 21,375 445,321,042

KILIMANJARO

Same 93 Karamba 101 Karamba 92 7 1,703 43,000,750

KILIMANJARO

Hai 94 Losaa 102 Sanyastation, Tindigani

75 10 5,159 * *

KILIMANJARO

Siha 95 Lekrimuni, 103 Orkolili, 91 11 9,354 * *

Page 277: Tekeleza kwa

275

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

KILIMANJARO

Siha 104 Mwasiliano 78

KILIMANJARO

Siha 96 Donyomuruak 105 Naibilie, 91 12 6,174

* * KILIMANJARO

Siha 106 Kishisha 83

KILIMANJARO

Rombo DC 97 Kahe 107 Kahe 71 32 7,763 * *

KILIMANJARO

Rombo DC 98 Urauri 108 Urauri 73 22 5,199 131,274,750

LINDI Lindi DC 99 Hingawali 109 Hingawali 90 13 3,000 75,750,000

LINDI Lindi DC 100 Litipu, 110 Litipu, 83 31 7,232 116,150,000

LINDI Lindi DC 111 Nyangamara 73

LINDI Lindi Dc 101 Kilolambwani 112 Kilolambwani 75 5 1,226 25,531,740

LINDI Lindi MC 102 Likotwa 113 Likotwa 86 13 2,929 73,957,250

LINDI Lindi MC 103 Kitumbikwera 114 Kitumbikwera 75 8 1,929 40,188,271

LINDI Lindi MC 104 Namakololo 115 Mitawa 73 8 710 * * LINDI Kilwa District 105 Nainokwe 116 Nainokwe 75 5 1,209 25,187,983

Page 278: Tekeleza kwa

276

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

LINDI Ruangwa 106 Mchichili 117 Mtondo 76 12 1,918 * * LINDI Ruangwa 107 Madawa chini, 118 Madawa chini, 80 31 7,249 183,037,250

MANYARA Babati 108 Erri 119 Erri 86 27 6,200 67,882,440

MANYARA Simanjiro DC 109 Lorokare 120 Lorokare 74 11 2,500 63,125,000

MANYARA Simanjiro DC 110 Olchoronyori 121 Olchoronyori 80 6 1,469 37,092,250

MANYARA Simanjiro DC 111 Naisinyai 122 Naisinyai 73 30 7,047 177,936,750

MARA Rorya 112 Nyihara 123 Nyihara 90 40 9,261 233,840,250

MARA Rorya 113 Kisumwa 124 Kisumwa 75 15 3,390 70,626,355

MARA Rorya 114 Ng’ope 125 Ng’ope 81 15 3,546 89,536,500

MARA Rorya 115 Komuge 126 Komuge, 90 72 24,978

* *

MARA Rorya 127 Kyamwami 91

MARA Rorya 128 Irienyi, 89

MARA Rorya 129 Baraki, 87

MARA Rorya 130 Kuruya 89

MBEYA Ileje 116 Malangali 131 Malangali 91 11 2,638 66,609,500

Page 279: Tekeleza kwa

277

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

MBEYA Ileje 117 Kalembo 132 Kalembo 82 10 2,327 58,756,750

MBEYA Ileje 118 Mtula 133 Mtula 94 10 2,328 58,782,000

MBEYA Ileje 119 Luswisi 134 Luswisi 73 13 3,123 178,855,750

MBEYA Ileje 120 Ilanga, Chitete na Ikumbilo

135 Ikumbilo 78 14 3,499 * *

MBEYA Kyela 121 Lugombo 136 Lugombo 87 11 2,508 63,327,000

MBEYA Kyela 122 Kiingili 137 Kiingili 73 8 1,851 98,991,677

MBEYA Kyela 123 Kagogo 138 Kagogo 78 4 844 21,311,000

MBEYA Mbarali 124 Luduga - Mawindi

139 Matemela, 90 10 2,665

* * MBEYA Mbarali 140 Ipwani, 87 10 2,108

MBEYA Mbarali 141 Itipinging 80 7 2,062

MBEYA Mbarali 142 Manienga 76 16 2,695

MBEYA Mbarali 125 Simike 143 Simike 76 16 3,813 96,278,250

MBEYA Mbeya DC 126 Izumbwe/Iwindi

144 Mwampalala 82 19 1,892 * *

MBEYA Mbeya DC 127 Galijembe 145 Galijembe 94 17 4,046 102,161,500

Page 280: Tekeleza kwa

278

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

MBEYA Mbeya DC 128 Swaya /Lupeta 146 Lupeta 87 29 6,761 170,715,250

MBEYA Mbeya DC 129 Idimi /Haporoto 147 Haporoto 92 41 9,505 240,001,250

MBEYA Mbeya DC 148 Idimi 76

MBEYA Rungwe 130 Itet/ Kapungi 149 Itete 87 19 4,336 109,486,048

MBEYA Chunya 131 Kiwanja, 150 Kiwanja, 76 54 12,594 317,998,500

MBEYA Chunya 132 Matwiga dam 151 Lupa mwiji, 76 205 47,803 1,207,025,750 MBEYA Chunya 152 matwiga, 90

MBEYA Chunya 133 Mkola 153 Mkola 87 19 4,372 * * MOROGORO

Morogoro (W) 134 Kikundi 154 Kikundi 87 48 11,291 285,101,481

MOROGORO

Morogoro (W) 135 Kolero 155 Kolero 76 20 4,640 117,150,718

MOROGORO

Morogoro (W) 136 Kizinga, 156 Kizinga, 76 18 4,222 106,600,928

MOROGORO

Morogoro (W) 137 Mfumbwe 157 Mfumbwe 79 22 5,156 130,190,199

MOROGORO

Morogoro (W) 138 Dalla-Mvuha 158 Dalla-Mvuha 76 31 7,181 181,326,949

Page 281: Tekeleza kwa

279

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

MOROGORO

Morogoro (W) 139 Kiroka Kiziwa 159 Kiroka Kiziwa 76 33 7,781 196,466,272

MOROGORO

Morogoro (W) 140 Singisa 160 Singisa 78 17 4,010 101,241,280

MOROGORO

Morogoro (W) 141 Kibwaya 161 Kibwaya 77 18 4,313 108,904,376

MOROGORO

Morogoro (W) 142 Mlilingwa, 162 Mlilingwa, 74 12 2,726 68,823,610

MOROGORO

Kilosa 143 Mikumi 163 Mikumi 86 83 19,415 490,228,750

MOROGORO

Kilosa 144 Ngoheranga 164 Ngoheranga 76 14 3,294 83,173,500

MOROGORO

Mvomero 145 Mlali 165 Mlali 78 47 11,047 278,936,750

MOROGORO

Mvomero 146 Kipera 166 Kipera 76 53 12,368 312,292,000

MOROGORO

Mvomero 147 Bunduki 167 Bunduki 76 53 12,456 314,514,000

MOROGORO

Kilombero 148 Idandu 168 Idandu 78 6 1,503 * *

MOROGORO

Kilombero 149 Bomanzinga, 169 Bomanzinga, 76 6 1,822 * *

Page 282: Tekeleza kwa

280

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

MOROGORO

Kilombero 150 Udagaji 170 Udagaji 80 12 3,254 * *

MOROGORO

Kilombero 151 Chita Sekondari,

171 Chita Sekondari,

90 3 712 * *

MOROGORO

Kilombero 152 Mangwale 172 Mangwale 89 5 2,111 * *

MTWARA Nanyumbu 153 Ndechela 173 Ndechela 75 3 612 12,750,245

MTWARA Mtwara Mc 154 Mkangala 174 Mkangala 75 6 1,364 28,406,795

MTWARA Masasi DC 155 Mkaliwata 175 Chipingo, 87 34 8,031 502,782,750

MTWARA Masasi DC 176 Mkaliwata 87

MTWARA Masasi DC 177 Mnavira 76

MTWARA Masasi DC 156 Mpindimbi 178 Kanyimbi 76 9 2,260 * * MTWARA Masasi DC 157 Mkululu 179 Mkululu A, 76 47 10,960 576,740,000

MTWARA Masasi DC 180 Mkululu B, 87

MTWARA Masasi DC 181 Syenjela, 78

MTWARA Masasi DC 182 Chipunda, 80

MTWARA Masasi DC 183 Majembe 76

Page 283: Tekeleza kwa

281

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

MTWARA Mtwara DC 158 Msanga Mkuu 185 Majengo 90 8 1,725

* * MTWARA Mtwara DC 186 Nambeleketela 87 4 1,189

MTWARA Mtwara DC 187 Msakala 78 4 1,773

MTWARA Mtwara DC 188 Ziwani (Mnawene)

76 4 798

MTWARA Mtwara DC 159 Mayaya 184 Mayaya 75 8 1,766 36,781,956

MTWARA Mtwara DC 160 Mbembaleo, 189 Mbembaleo, 73 26 6,125 254,656,250

MTWARA Newala DC 161 Mnauya / Mmulunga

190 Mnauya 78 44 10,300 541,867,450

MTWARA Newala DC 191 Mmulunga 90

MTWARA Newala DC 162 Mnima 192 Mnima 78 46 10,852 474,013,000

MTWARA Newala DC 163 Mahoha 193 Mahoha 80 8 1,969 * * MTWARA Newala Dc 164 Miyuyu 194 Miyuyu 75 6 1,332 27,750,532

MTWARA Tandahimba DC 165 Nannala, 195 Nannala, 78 9 2,171 64,817,520

MTWARA Tandahimba DC 166 Chidede, 196 Chidede, 79 6 1,359 84,325,827

MWANZA Kwimba 167 Igumangobo 197 Igumangobo 87 34 8,000 202,000,000

Page 284: Tekeleza kwa

282

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

MWANZA Magu DC 168 Nyanguge-Muda

198 Muda. 89 16 3,639 91,884,750

MWANZA Ukerewe 169 Kazirankanda 199 Namagondo 89 14 3,345 84,461,250

MWANZA Ukerewe 200 Busunda 90 26 6,025 152,131,250

MWANZA Ukerewe 201 Malegea 87 14 3,371 85,117,750

MWANZA Ukerewe 202 Buhima 89 43 10,143 256,110,750

MWANZA Ukerewe 203 Lutare 78 31 7,184 181,396,000

MWANZA Misungwi 170 Mabuki 204 Mabuki 90 18 4,172 105,343,000

MWANZA Misungwi 171 Isakamawe 205 Isakamawe 87 27 6,229 157,282,250

MWANZA Misungwi 172 Kasololo/Igongwa

206 Kasololo/Igongwa

90 18 4,191 105,822,750

MWANZA Misungwi 173 kabale 207 kabale 87 12 2,726 68,831,500

MWANZA Misungwi 174 Mwasonge 208 Inonelwa 86 15 3,500 88,375,000

MWANZA Misungwi 175 Usagara 209 Usagara 78 107 25,000 631,250,000

MWANZA Sengerema DC 176 Nyakaliro-Bukokwa

210 Nyakaliro, 76 25 5,686 * * MWANZA Sengerema DC 211 Lugasa, 76

Page 285: Tekeleza kwa

283

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

MWANZA Sengerema DC 212 Itumbili 78 6 4,762

MWANZA Sengerema DC 177 Kalebezo-Nyehunge

213 Kasela, 90 5 2,620 * * MWANZA Sengerema DC 214 Mwangika, 87 7 2,943 * * MWANZA Sengerema DC 178 Buyagu,

Kalangalala na Bitoto

215 Bitoto 90 15 5,241 452,500,000

MWANZA Sengerema DC 179 Nyakaliro-Bukokwa

216 Lumeya, 87 15 11,948 * *

NJOMBE Njombe (W), Wanging'ombe (W) na Makambako (M)

180 Kinenulo 217 Kinenulo 87 6 1,500 37,875,000

NJOMBE Njombe (W), Wanging'ombe (W) na Makambako (M)

181 Tagamenda Shallow Wells

218 Tagamenda 90 20 4,599 116,124,750

NJOMBE Njombe (W), Wanging'ombe (W) na Makambako (M)

182 Ibumila pumping

219 Ibumila 76 24 5,564 140,486,178

Page 286: Tekeleza kwa

284

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

NJOMBE Wanging'ombe (W)

183 Isimike - Igenge- Idenyimembe

220 Isimike 71 19 4,454 112,463,500

NJOMBE Njombe (W), 184 Ikuna 221 Ikuna 76 18 1,660 * * NJOMBE Njombe (M) 185 Lugenge –

Kisilo-Utalingolo

222 Kisilo 98 12 2,859 72,189,750

NJOMBE Njombe (M) 226 Lugenge 78 4 974 24,593,500

NJOMBE Njombe (M) 227 Utalingolo 78 13 3,018 76,204,500

NJOMBE Njombe (M) 186 Igongwi Group Scheme

223 Kitulila 90 8 1,764 44,541,000

NJOMBE Njombe (M) 224 Madobole 89 19 4,531 114,407,750

NJOMBE Njombe (M) 228 Njoomlole 80 6 1,426 36,006,500

NJOMBE Njombe (M) 229 Luponde 78 23 5,413 136,678,250

NJOMBE Njombe (M) 230 Uwemba 76 14 3,166 79,941,500

NJOMBE Njombe (M) 187 Peruhanda 225 Peruhanda 72 8 1,835 46,333,750

NJOMBE Ludewa (W) 188 Lugarawa 231 Lugarawa 89 5 1,214 30,653,500

NJOMBE Ludewa (W) 189 Mapogoro 232 Mapogoro 90 6 1,304 32,926,000

NJOMBE Ludewa (W) 190 Kipangala 233 Kipangala 91 5 1,271 32,092,750

Page 287: Tekeleza kwa

285

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

NJOMBE Ludewa (W) 191 Lumbila 234 Lumbila 76 14 3,244 81,911,000

NJOMBE Ludewa (W) 192 Kingole 235 Kingole 78 6 1,328 33,532,000

NJOMBE Ludewa (W) 193 Lihagule 236 Lihagule 76 7 1,600 67,832,165

NJOMBE Makete (W) 194 Mpangala - Matamba - Mbela

237 Ng'onde 89 11 2,483 62,695,750

NJOMBE Makete (W) 238 Matamba 87 6 1,516 38,279,000

NJOMBE Makete (W) 239 Mpangala 90 6 1,304 32,926,000

NJOMBE Makete (W) 240 Mlondwe 78 7 1,522 38,430,500

NJOMBE Makete (W) 195 Ivilikinge 241 Ivilikinge 76 9 2,202 55,602,160

NJOMBE Makete (W) 196 Ikovo 242 Ikovo 78 2 578 14,606,550

NJOMBE Makambako (M) 197 Manga 243 Manga 74 6 1,428 36,057,000

PWANI Mafia District 198 Kungwi 244 Kungwi 75 17 3,852 108,809,650

PWANI Rufiji District 199 Mkenda 245 Kivinja B 76 14 1,964 * * PWANI Rufiji DC 200 Mbwara 246 Mbwara 78 20 4,650 117,412,500

PWANI Mkuranga DC 201 Mvuleni 247 Mvuleni 78 18 4,245 107,186,250

PWANI Mkuranga DC 202 Bupu 248 Bupu 76 10 2,287 57,746,750

Page 288: Tekeleza kwa

286

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

PWANI Bagamoyo District

203 Saadani 249 Saadani 86 9 2,000 85,004,045

RUKWA Sumbawanga MC

204 Kanondo 250 Kanondo 90 16 3,689 93,147,250

RUKWA Sumbawanga MC

205 Chelenganya 251 Chelenganya 89 19 4,427 111,781,750

RUKWA Sumbawanga MC

206 Malonje 252 Malonje 87 90 21,068 531,967,000

RUKWA Sumbawanga MC

207 Azimio/ Nambogo

253 Nambogo 76 36 8,330 210,332,500

RUKWA Sumbawanga DC

208 Kizumbi 254 Kizumbi 90 15 3,443 1,237,899

RUKWA Sumbawanga DC

209 Laela 255 Laela 91 102 23,729 978,900

RUKWA Sumbawanga DC

210 Solola 256 Solola 78 16 3,779 95,419,750

RUKWA Sumbawanga DC

211 Mfinga 257 Mfinga 76 71 16,625 419,781,250

RUKWA Sumbawanga DC

212 Ndelema 258 Ndelema 76 15 3,567 90,066,750

RUKWA Kalambo DC 213 Mwazye 259 Mwazye 76 7 1,548 39,087,000

Page 289: Tekeleza kwa

287

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

RUKWA Kalambo DC 214 Kasanga 260 Kasanga, 76 30 6,892 374,014,004

RUVUMA Songea DC 215 Lilondo 261 Lilondo 90 22 5,063 127,840,750

RUVUMA Songea DC 216 Liula 262 Liula 87 18 4,246 107,211,500

RUVUMA Songea DC 217 Luyelela 263 Peramiho B 81 9 1,997 50,424,250

RUVUMA Songea DC 218 Maweso 264 Maweso 78 25 5,919 149,454,750

RUVUMA Songea DC 219 Luyelela 265 Maposeni 72 29 6,868 173,417,000

RUVUMA SONGEA MC 220 Chandarua 268 Chandarua 89 10 2,447 61,786,750

RUVUMA SONGEA MC 221 Ruhuwiko-Kanisani

269 Ruhuwiko-Kanisani

90 4 991 25,022,750

RUVUMA SONGEA MC 222 Muungano 270 Muungano 89 5 1,080 27,270,000

RUVUMA SONGEA MC 223 Ruhila-Kati 271 Ruhila-Kati 78 11 2,567 64,816,750

RUVUMA TUNDURU 224 Matemanga 272 Changarawe 87 33 7,680 193,920,000

RUVUMA TUNDURU 225 Mtina 273 Muungano 76 33 8,815 * * RUVUMA TUNDURU 226 Mchoteka 274 Kitani 76 37 8,634 218,008,500

RUVUMA TUNDURU 227 Amani/ Chiungo/

275 Chiungo 78 40 10,993 * *

Page 290: Tekeleza kwa

288

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

Meamtwaro

RUVUMA TUNDURU 228 Lukumbule 276 Lukumbule 73 30 6,437 * * RUVUMA MBINGA 229 Mkako 277 Mkako 78 14 3,206 80,951,500

RUVUMA NAMTUMBO DC

230 Hanga/ Mawa/Msindo

278 Hanga, 78 61 14,291 476,823,458

RUVUMA NAMTUMBO DC

231 Naikesi /Luhimbalilo

279 Luhimbalilo 76 35 8,266 208,716,500

RUVUMA NAMTUMBO DC

232 Mkongo Gulioni / Nahimba

280 Mkongogulioni 78 44 8,266 * *

RUVUMA NAMTUMBO DC

233 Njalamatata/ upper Nakawal

281 Njalamatata 78 31 6,037 * *

RUVUMA NAMTUMBO DC

282 Upper Nakawale

76 8 1,772 44,743,000

RUVUMA NAMTUMBO DC

234 Magazini 266 Magazini 89 21 4,988 125,947,000

RUVUMA NAMTUMBO DC

235 Milonji 267 Milonji 90 34 7,916 199,879,000

SHINYANGA

Ushetu 236 Iboja 283 Iboja 76 23 5,400 136,350,000

Page 291: Tekeleza kwa

289

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

SHINYANGA

Kishapu 237 Mendo 284 Mendo 76 10 2,306 58,226,500

SHINYANGA

Kishapu 238 Nyashimbi 285 Nyashimbi 74 15 3,844 97,061,000

SHINYANGA

Kishapu 239 Manyada 286 Manyada 73 30 7,112 179,578,000

SHINYANGA

Kishapu 240 Mwamadilana 287 Mwamadilana 87 8 1,969 49,717,250

SHINYANGA

Kishapu 241 Nyashimbi 288 Nyashimbi 76 10 2,438 61,559,500

SHINYANGA

Shinyanga MC 242 Mwamagunguli 289 Mwamagunguli 71 7 1,629 41,132,250

SHINYANGA

Shinyanga MC 243 Galamba 290 Galamba 76 6 1,311 33,102,750

SIMIYU Bariadi TC 244 Zanzui / Luguru

291 Luguru 78 11 2,634 66,508,500

SIMIYU Maswa 245 Jija 292 Jija 76 12 2,850 71,962,500

SIMIYU Maswa 246 Mwanegele 293 Mwanegele 73 21 4,918 124,179,500

SIMIYU Busega 247 Kalemela-Mkula

294 Mwamjulila, 76 10 1,333 * *

Page 292: Tekeleza kwa

290

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

TABORA Tabora MC 248 Kalunde, Igombe na Tumbi

295 Igombe 82 17 4,000 101,000,000

TABORA Tabora MC 296 Tumbi 76 27 6,276 158,469,000

TABORA Igunga DC 249 Bulangamilwa 297 Bulangamilwa 87 17 4,047 102,186,750

TABORA Nzega 250 Nata 298 Nata 89 24 5,646 142,561,500

TABORA Nzega 251 Nkiniziwa 300 Nkiniziwa 76 105 24,500 618,625,000

TABORA Kaliua 252 Uhindi. 299 Uhindi 89 16 3,750 94,687,500

TABORA Sikonge DC 253 Tutuo 301 Tutuo 76 35 8,720 * * TABORA Uyui District 254 Kilungu 302 Kilungu 75 10 2,222 46,282,138

TABORA Uyui District 255 Isimu 303 Isimu 75 5 1,070 22,281,677

TANGA Handeni DC 256 Kwamsangazi 304 Kwamsangazi 89 15 3,602 90,950,500

TANGA Handeni DC 257 Kwaluwala 305 Kwaluwala 87 15 3,408 86,052,000

TANGA Handeni DC 258 Kilimilang'ombe

306 Kilimilang'ombe

90 14 3,244 81,911,000

TANGA Handeni DC 259 Malezi 307 Malezi 87 32 7,570 191,142,500

TANGA Handeni DC 260 Mkata 308 Mkata 78 89 20,597 520,074,250

Page 293: Tekeleza kwa

291

MKOA HALMASHAURI Na. JINA LA MRADI Na. JINA LA KIJIJI

ASI

LIM

IA Y

A

UTE

KEL

EZA

JI

IDA

DI Y

A

VITU

O V

YA

KU

CH

OTE

A

MA

JI

IDA

DI Y

A

WA

NA

NC

HI

WA

TAK

AO

-N

UFA

IKA

FED

HA

ZI

NA

ZOH

I-TA

JIK

A

TANGA Lushoto DC 261 Shume- Madala

309 Shume, 89 144 33,703 851,000,750

TANGA Lushoto DC 310 Madala 90

TANGA Korogwe DC 262 Vugiri 311 Vugiri 78 14 3,175 80,168,750

JUMLA KUU 7,212 1,732,800 40,142,823,674

Angalizo ; * * - Kijiji/Vijiji ambavyo vipo katika Mradi wa vijiji vingi ambavyo fedha zake zimejumuishwa pamoja katika utekelezaji uliopo chini ya asilimia 70.

Page 294: Tekeleza kwa

292

Jedwali Na. 8: Orodha ya Vijiji 26 vya Kipaumbele katika Halmashauri zote Mkoani Kigoma

S/N HALMASHAURI MAJINA YA VIJIJI IDADI YA

VIJIJI IDADI YA WATU

1. Kakonko DC Kanonko

8 28,008

Mugaza Mbizi Kiziguzigu Kabingo Mugaza Kiyobera Ruyenzi

2. Kigoma DC Kiganza

7 50,186

Kibingo Bitare Mkongoro Kizenga Nyamhonza Mwandiga

3. Kasulu Nyantare

4 29,895 Kigongo Kidyama Nyansha

Page 295: Tekeleza kwa

293

S/N HALMASHAURI MAJINA YA VIJIJI IDADI YA VIJIJI IDADI YA WATU

4. Uvinza Kazuramimba 3 37,910 Nyanganga

Zeze 5. Buhigwe Mnamila

3 27,648 Mwaya Nkatanga

6. Kibondo Kifura 1 10,005 JUMLA 26 183,652

Page 296: Tekeleza kwa

294

Jedwali Na. 9 :Utekelezaji wa Miradi 15 Katika Maeneo Mbalimbali ya Jijini Dar es Salaam.

Jedwali Na. 9a: Manispaa ya Ilala

JINA LA MRADI WA MAJI

TAARIFA TABATA DARAJANI

MINAZI MIREFU KINYEREZI

GONGO LA MBOTO,

GULUKAKWALALA, ULONGONI

UGOMBOLWA

Chanzo cha maji Kisima Kisima Kisima Kisima Kisima Idadi ya walengwa

960 192 512 640 42

Idadi ya vituo vya jumuiya (DP)

13 8 9 23 4

Kiwango cha juu cha maungio binafsi (private conection)

1,300 250 680 850 0

Ujazo wa tanki (m3)

200 90 680 135 10

Gharama ya 609,000,000 287,000,000 245,000,000 244,000,000 68,000,000

Page 297: Tekeleza kwa

295

JINA LA MRADI WA MAJI

TAARIFA TABATA DARAJANI

MINAZI MIREFU KINYEREZI

GONGO LA MBOTO,

GULUKAKWALALA, ULONGONI

UGOMBOLWA

mradi (Tshs)

Jedwali Na. 9b: Manispaa ya Kinondoni

JINA LA MRADI WA MAJI

TAARIFA TANDALE MBURAHATI BARAFU KWEMBE

HONDOGO, DELINI,

KIBWEGERE Chanzo cha maji Visima 2 Kisima DAWASCO

(pump) DAWASCO

(gravity) Idadi ya walengwa (population) 41,000 6,200 12,500 12,500 Idadi ya vituo vya jumuiya (DP) 21 12 12 12 Kiwango cha juu cha maungio binafsi (Maximum private connection)

2,100 320 650 650

Ujazo wa tanki (m3) 270 90 90 135 Gharama ya mradi (Investment cost (Tsh)

1,174,000,000 223,000,000 232,000,000 223,000,000

Page 298: Tekeleza kwa

296

Jedwali Na. 9c: Manispaa ya Temeke

JINA LA MRADI WA MAJI

TAARIFA MBAGALA KUU-

MGENINANI-KICHEMCHEM

MTONI KIJICHI -MISHENI

MWANA MTOTI

KIBONDEMAJI B- KICHEMCHEM

YOMBO DOVYA –UWAZI-

MSAKALA KINGUGI

Chanzo cha maji Kisima Kisima Kisima Kisima Kisima Kisima Idadi ya walengwa (population)

16,400 16,400 6,600 4,500 16,400 13,100

Idadi ya vituo vya jumuiya (DP)

23 12 9 11 12 13

Kiwango cha juu cha maungio binafsi (private conection)

850 1,300 340 290 850 230

Ujazo wa tanki (m3) 135 135 90 50 90 40 Gharama ya mradi (investment) costs)(Tshs)

802,000,000 710,000,000 324,000,000 182,000,000 460,000,000 88,000,000

Page 299: Tekeleza kwa

297

Jedwali Na. 10:- Mgawanyo wa Fedha Zilizotengwa kwa ajili ya Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji Midogo (Quickwins) katika mwaka 2015/2016

NA JINA LA MKOA JINA LA MJI MAKADIRIO KAZI ZITAKAZOFANYWA

1. Arusha Karatu 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

2. Arusha Loliondo 400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

3. Arusha Longido 2,000,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

4. Dodoma Bahi 1,400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

5. Dodoma Chamwino 300,000,000 Kukamilisha ujenzi wa mradi

6. Dodoma Kondoa 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

7. Dodoma Kongwa 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

8. Geita Katoro/Buseresere 500,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

Page 300: Tekeleza kwa

298

NA JINA LA MKOA JINA LA MJI MAKADIRIO KAZI ZITAKAZOFANYWA

9. Geita Nyarugusu 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

10. Iringa Kilolo 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

11. Iringa Mafinga 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

12. Kagera Kyerwa 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

13. Kagera Muleba 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

14. Kigoma Uvinza 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

15. Kigoma Kakonko 500,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

16. Lindi Kilwa Masoko 500,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

17. Lindi Liwale 400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

Page 301: Tekeleza kwa

299

NA JINA LA MKOA JINA LA MJI MAKADIRIO KAZI ZITAKAZOFANYWA

18. Lindi Ruangwa 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

19. Manyara Mbulu 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

20. Manyara Kibaya 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

21. Mara Shirati 200,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

22. Mara Mugumu 1,000,000,000 Kukamilisha ukarabati wa chujio la maji

23. Mara Tarime 500,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

24. Mbeya Ileje 400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

25. Mbeya Kyela 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

26. Mbeya Mbarali 400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

Page 302: Tekeleza kwa

300

NA JINA LA MKOA JINA LA MJI MAKADIRIO KAZI ZITAKAZOFANYWA

27. Mbeya Mlowo 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

28. Mbeya Tukuyu 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

29. Mbeya Tunduma 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

30. Mbeya Vwawa 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

31. Morogoro Dakawa 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

32. Morogoro Gairo 200,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

33. Morogoro Ifakara 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

34. Morogoro Mahenge 500,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

35. Morogoro Mikumi 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

Page 303: Tekeleza kwa

301

NA JINA LA MKOA JINA LA MJI MAKADIRIO KAZI ZITAKAZOFANYWA

36. Mwanza Malya 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

37. Njombe Ludewa 400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

38. Pwani Kilindoni 400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

39. Pwani Mkuranga 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

40. Rukwa Inyonga 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

41. Ruvuma Namtumbo 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

42. Simiyu Mwanhuzi 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

43. Simiyu Itilima 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

44. Simiyu Mwandonya 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

Page 304: Tekeleza kwa

302

NA JINA LA MKOA JINA LA MJI MAKADIRIO KAZI ZITAKAZOFANYWA

45. Tabora Sikonge 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

46. Tanga Kasera 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

47. Tanga Kilindi 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

48. Tanga Korogwe 400,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

49. Tanga Mkata 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

50. Tanga Mombo 300,000,000 Kupanua mfumo wa maji mjini

JUMLA 20,000,000,000

Page 305: Tekeleza kwa

303

Jedwali Na. 11: Orodha ya Utekelezaji kwa kila Kipande cha Mradi wa Chalinze na Vijiji Vinavyonufaika na Mradi

KIPANDE MAELEZO UTEKELEZAJI HADI APRILI, 2015

(Lot 1)

Katika kipande hiki jumla ya wakazi 11,936 wanapata huduma ya maji katika Vijiji vya Mihuga, Masimbani, Kweikonje, Mandamazingara na Mkange.

umekamilika

(Lot 2)

Katika kipande hiki jumla ya wakazi 26,282 watapata huduma ya maji katika Vijiji vya Masuguru/Mwetemo, Kiwangwa/Mwavi, Fukayosi, Kidomole, Mkenge, Msinune, Pongwe Msungura, Madesa na Makurunge.

umekamilika

(Lot 3)

Katika kipande hiki jumla ya wakazi 14,308 watapata huduma ya maji katika Vijiji vya Kinzagu, Makombe, Talawanda, Malivundo, Msigi, Kisanga na Mindukeni.

95%

(Lot 4)

Katika kipande hiki jumla ya wakazi 16,416 watapata huduma ya maji katika Vijiji vya Chamakweza, Vigwaza, Buyuni na Visezi.Mkandarasi hakuweza kufikia malengo hayo.

umekamilika

(Lot 5)

Katika kipande hiki jumla ya wakazi 13,291 watapata huduma ya maji katika Vijiji vya Chahua, Gwata, Gumba, Magindu na Lukenge.

umekamilika

Page 306: Tekeleza kwa

304

KIPANDE MAELEZO UTEKELEZAJI HADI APRILI, 2015

(Lot 6)

Katika kipande hiki jumla ya wakazi 14,396 watapata huduma ya maji katika vijiji vya Kwan’gandu, Pongwe Kiona, Kifuleta Na Kwaruhombo.

umekamilika

F

Ujenzi wa vituo viwili vya kusukuma maji utawezesha vijiji vya kipande J chenye wakazi 31,772, Lot 6 chenye wakazi 14,396 na baadhi ya wakazi wa kipande H kupata chanzo cha maji baada ya ujenzi kukamilika.

90%

H Katika kipande hiki jumla ya wakazi 31,158 watapata huduma ya maji katika Vijiji vya Msolwa, Mdaula, Matuli, Ubenazomozi, Mwidu, Visakazi, Kaloleni na Tukamisasa Mradi utakapokamilika.

95%

J Katika kipande hiki jumla ya wakazi 31,772 watapata huduma ya maji katika Vijiji vya Kidugalo, Ngerengere, Sinyaulime, Bwawani, Gwata, Kinonko pamoja na maeneo ya Sangasanga, Kizuka na Kinonko

umekamilika

Page 307: Tekeleza kwa

305

Jedwali Na. 12:- Orodha ya Visima vilivyochimbwa na Wakala (DDCA) hadi mwezi Aprili mwaka 2014/2015

Na. Mkoa Visima 1. Arusha 2 2. Pwani 26 3. Dodoma 10 4. Dar es Salaam 78 5. Feita 1 6. Iringa 8 7. Kigoma 3 8. Kilimanjaro 9 9. Lindi 6

10. Manyara 1 11. Mbeya 2 12. Morogoro 25 13. Mtwara 5 14. Mwanza 2 15. Njombe 7 16. Ruvuma 2 17. Shinyanga 5 18. Singida 1 19. Tabora 22 20. Tanga 17 21. Zanzibar 1

Jumla 233