mwongozo wa lugha rahisi wa ripoti ya mwaka ya utekelezaji ... · ipoti ya mwaka ya utekelezaji wa...

48
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007

Upload: others

Post on 17-Jan-2020

20 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Mwongozo wa Lugha Rahisi wa

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa

MKUKUTA 2006/07

Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi.

Desemba 2007

ii

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA (MAIR) ni moja ya matokeo ya Mfumo wa

Ufuatiliaji wa MKUKUTA. Hivyo ripoti hii ni sehemu ya muundo wa jumla wa utoaji wa

taarifa za wadau mbalimbali wanaojihusisha na utekelezaji wa MKUKUTA. Wadau hao ni

pamoja na Wizara, Idara, na Wakala wa Serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa,na Asasi Zisizo za

Kiserikali.

Ripoti hii inatokana na uchambuzi wa utekelezaji wa kila lengo la MKUKUTA na inatoa picha

ya mafanikio yaliyofikiwa, changamoto, mambo ya kujifunza, na hatua zinazopaswa kuchukuliwa

kwa kila nguzo ya MKUKUTA. Pia ripoti hii inajumuisha hatua iliyopigwa katika michakato na

maboresho mengine, na kuonyesha jinsi yanavyochangia katika kufikiwa kwa matokeo ya MKUKUTA

yanayotarajiwa.

Lengo la ripoti hii ni kuwafahamisha wadau kuhusu maendeleo ya utekelezaji wa MKUKUTA sanjari

na michakato inayohusiana, ikiwa na lengo la kuchochea mijadala juu ya masuala muhimu, na kusaidia

kuboresha michakato ya mipango, bajeti na utekelezaji.

Msingi wa wazo la kuandaa chapisho hili la lugha rahisi ni lengo la jumla la MAIR 2006/07 liliotajwa

hapo juu. Ili kuwezesha ushiriki wa wadau wengi zaidi wa kada mbali mbali, ilionekana ni lazima

kuandaa chapisho hili kwa lengo la kujenga ufahamu wa pamoja juu ya maendeleo ya utekelezaji wa

MKUKUTA.

Dibaji

iii

Dibaji ............................................................................................................................................. ii Yaliyomo ...................................................................................................................................... iii Ujue MKUKUTA .......................................................................................................................iv Vifupisho .......................................................................................................................................v Utangulizi ......................................................................................................................................vi 1. Ijue MAIR ........................................................................................................................... 1 Masuala Makuu ya MAIR, Madhumuni, Malengo na Matumizi .......................................... 1 Uoanishaji na Kuhusianisha Michakato ya Kitaifa ................................................................... 2 Ripoti Ilivyoandaliwa .................................................................................................................... 2 Mapana ya MAIR ......................................................................................................................... 3 Mapana na Mapungufu ya Mwongozo huu wa Lugha Rahisi ................................................. 3 2. Changamoto za Nguzo na Hatua za Kuchukua ................................................................... 5 Nguzo ya Kwanza – Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini wa Kipato ........................ 5 Nguzo ya Pili –Uboreshaji wa Maisha na Ustawi wa Jamii .................................................... 9 Nguzo ya Tatu – Utawala Bora na Uwajibikaji ....................................................................... 13 3. Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA .............................................................................. 18 Chimbuko la Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA ........................................................... 18 Sekretarieti ya MKUKUTA ..................................................................................................... 19 Makundi Matatu ya Kiufundi .................................................................................................. 21 Uoanishaji wa Shughuli ............................................................................................................. 22 Shughuli Zinazoendelea ............................................................................................................ 23 Changamoto na Mambo Tuliyojifunza .................................................................................... 24 Hatua za Kuchukua.................................................................................................................... 25 4. Ugharamiaji ....................................................................................................................... 26 Utafutaji na Upangiliaji wa Fedha ............................................................................................ 26 MKUKUTA na Bajeti ya Taifa ................................................................................................. 28 Kuboresha Michakato ya Bajeti na Ugharamiaji ..................................................................... 29 Njia za Kuripoti Bajeti ............................................................................................................... 30 Mapana ya Ripoti ya Bajeti ........................................................................................................ 31 Sera Nyingine Zinazohusiana na Bajeti .................................................................................. 31 5. Muhtasari wa Masuala Makuu na Hatua za Kuchukua ...................................................... 33 6. Viambatisho ...................................................................................................................... 36 Kiambatisho 1: Muundo wa Utekelezaji wa MKUKUTA.................................................... 36 Kiambatisho 2: Mchakato wa Mapitio ya Kisekta .................................................................. 37 Kiambatisho 3: Viunganishi muhimu vya intaneti ................................................................. 38 7. Maana za Maneno Makuu Yaliyotumika (Faharasa) .......................................................... 39 8. Shukrani ........................................................................................................................... 41

Yaliyomo

iv

� Ni Mkakati wa Kitaifa wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini kwa kipindi cha kuanzia

2005/2006 hadi 2009/2010

� Ni uzao wa pili wa Waraka wa Mkakati wa Upunguzaji Umaskini. Uliandaliwa kufuatia mapitio ya

Mkakati wa kwanza wa Upunguzaji Umaskini wa mwaka 2000 yaliyohusisha mashauriano ya wadau

mbali mbali nchini.

� Uliandaliwa na unatekelezwa kwa njia ya mashaurino endelevu yanayohusisha ushiriki mpana wa

wadau wengi.

� Umekusudiwa kuwa muundo wenye kuoanisha mipango, bajeti, utekelezaji, ufuatiliaji na taarifa za

wadau wengi.

� Hupitiwa na Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA ambao huongozwa na Mpango Mkuu wa

Ufuatiliaji wa MKUKUTA.

� Huongozwa na Kamati ya Ufundi. Husimamiwa na Sekretarieti. Huendeshwa na makundi matatu

ya Kitaalamu ‘Utafiti na Uchambuzi’, ‘Tafiti na Takwimu za kila siku’ na ‘Mawasiliano’

� Unagharamiwa na Serikali, fedha za ndani na msaada wa Wabia wa Maendeleo sanjari na wadau

wengine wa MKUKUTA.

� Umejikita katika nguzo tatu zenye kulenga matokeo badala ya kuzingatia sekta (Tazama jedwali

lifuatalo kwa maelezo zaidi)

Nguzo ya kwanza: Kukuza Uchumi

na Kupunguza Umaskini wa Kipato

Nguzo ya pili: Uboreshaji wa Maisha

na Ustawi wa Jamii

Nguzo ya tatu: Utawala Bora na

Uwajibikaji

Matokeo ya Jumla Matokeo ya Jumla Matokeo ya Jumla

Ukuaji wa uchumi wenye msingi mpa-na na unaozingatia usawa unafikiwa na kuendelezwa

Kuboreka kwa maisha na ustawi wa jamii msisitizo wa kipekee ukiwa kwa watu maskini zaidi pamoja na wale walio katika mazingira hatarishi.

Kupungua kwa tofauti ya kimatokeo (mfano; elimu, na afya) kwa kuzingatia maeneo ya kijiografia, kipato, umri, jinsia, na makundi mengine

Utawala bora na Utawala wa Sheria

Uwajibikaji wa Viongozi na watumishi wa umma,

Demokrasia na uvumilivu wa kisiasa na kijamii,

Amani, Utulivu wa kisiasa, umoja wa kitaifa na mshikamano wa kijamii.

Malengo Malengo Malengo

Kuhakikisha kunakuwapo usimamizi mzuri wa uchumi

Kuchochea ukuaji wenye msingi mpana na endelevu

Kuongeza upatikanaji wa chakula

Kupunguza umaskini wa kipato kwa wanaume na wanawake vijijini

Kuhakikisha upatikanaji sawa wa elimu bora ya msingi na sekondari kwa wavulana na wasichana, elimu ya kufuta ujinga miongoni mwa wanaume na wanawake, na upanuzi wa elimu ya juu, ufundi na ufundi stadi

Kuboresha maisha, afya na ustawi wa watoto wote na wanawake hususan makundi yaliyo katika maazingira hatarishi

Kuhakikisha kuwa miundo na mifumo ya utawala pamoja na utawala wa sheria ni vya kidemokrasia, shirikishi, uwakilishi, uwajibikaji na ujumuishaji.

Kuhakikisha ugawaji sawa wa rasili-mali za umma – pamoja na kushughu-likia rushwa ipasavyo.

Ujue MKUKUTA

v

Malengo Malengo Malengo

Kupunguza umaskini wa kipato kwa wanaume na wanawake mjiniKutoa nishati ya kuaminika na rahisi kwa watumiaji.

Kuongeza upatikanaji wa maji safi, salama nay a gharama nafuu, usafi, malazi mazuri, na mazingira salama na endelevu; na hivyo kupunguza uathirikaji utokanao na hatari za mazingira.

Kuhakikisha kunakuwapo hifadhi ya uhakika ya kijamii na utoaji wa mahitaji na huduma za msingi kwa wahitaji na walio katika maazingira hatarishi.Kuhakikisha kunakuwepo mfumo wenye ufanisi unaotoa fursa sawa kwa watu wote kupata na kumudu huduma bora za umma.

Kuweka mfumo wa huduma za umma unaofaa kama msingi wa kuboresha utoaji wa huduma na kupunguza umaskini.

Kuhakikisha kwamba haki za maskini na vikundi vilivyo katika mzingira hatarishi zinalindwa na kukuzwa katika mfumo wa haki.

Kupunguza kutengwa na kutovumiliana kisiasa na kijamii.

Kuboresha usalama binafsi na wa mali, kupunguza uhalifu na kuondoa unyanyasaji wa kijinsia na unyanyasaji majumbani.

Kuendeleza na kuimarisha utamaduni wa watu kama utambulisho wa kitaifa.

VifupishoAZISE Asasi Zisizo za Serikali

JAST Mkakati wa Pamoja wa Misaada ( Joint Assistance Strategy for Tanzania)

MAIR Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji MKUKUTA

(MKUKUTA Annual Implementation Report)

MKUKUTA Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini

NACSAP II Mkakati na Mpango Kazi wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa

PHDR Ripoti ya Umaskini na Maendeleo ya Watu (Poverty and Human Development Report)

PIMA Kadi ya Jamii ya kukusanyia taarifa (Community score cards)

PlanRep Programu ya Kompyuta ya kuandalia mipango na Kutoa taarifa inayotumika

kwenye Serikali za Mitaa. (Planning and Reporting Takwimubase for

local authorities )

RIMKU Ripoti ya Utekelezaji ya MKUKUTA (Programu ya Kompyuta)

SBAS Mfumo wa Bajeti wa Upangiliaji Fedha Kimkakati

(Strategic Budget Allocation System)

UKIMWI Upungufu wa Kinga Mwilini

VVU Virusi Vya UKIMWI

vi

Kijitabu hiki kinaelezea Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA (MAIR) 2006/07

kwa lugha rahisi. Kifupisho MAIR, kinachotokana na maneno ya Kiingereza MKUKUTA

Annual Implementation Report kitatumika kumaanisha ripoti hii.

MKUKUTA uliandaliwa mwaka 2005. MKUKUTA ni Mkakati wa Kitaifa wa Kukuza Uchumi na

Kupunguza Umaskini. Ulikuwa ni matokeo ya ufuatiliaji uliohusisha marudio na mapitio makubwa ya

Waraka wa Mkakati wa Kupunguza Umaskini wa mwaka 2000. MKUKUTA ni Mkakati utakaodumu

kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2005/06 hadi 2009/10.

MKUKUTA umejengwa kwenye nguzo kuu tatu za mikakati. Nguzo ya “Kukuza Uchumi na

Kupunguza umaskini wa Kipato” inahusiana kwa karibu na nguzo ya “ Kuboresha Maisha na Ustawi wa

Jamii” ambapo zote kwa pamoja zinajengwa kwenye msingi wa “Utawala Bora na Uwajibikaji”.

Hata hivyo mafanikio ya utekelezaji wa MKUKUTA hayategemei kuwepo kwa sera nzuri zinazokubalika

na zenye malengo na shabaha zinazoeleweka pekee. Pia unahitajika mfumo bora na wenye ufanisi wa

kufuatilia na kutathmini utekelezaji. Kwa hiyo Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA umebuniwa ili

kuubadili mfumo wa awali wa Ufuatiliaji wa Umaskini. Maelezo ya kina ya Mfumo wa Ufuatiliaji wa

MKUKUTA yamebainishwa kwenye Mpango Mkuu wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA.

MAIR ni mojawapo ya matokeo yaliyopendekezwa kwenye Mpango Mkuu wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA.

Lengo kuu ni kuleta pamoja na kuchambua aina mbali mbali za taarifa za ufuatiliaji kwa makusudi ya (a)

kutoa taarifa juu ya kazi zinazofanyika (au kutofanyika) (b) kubainisha changamoto na mambo muhimu

ya kujifunza kutokana na utekelezaji (c) kupendekeza hatua za kuchukua katika siku zijazo. Wazo la

msingi ni kuifanya MAIR iweze kuwafikia wadau wengi ili kuwahimiza na kuwahamasisha wadau hao

kufanya mijadala na midahalo. Hii itasaidia kuboresha michakato ya mipango na utungaji sera kwa siku

zijazo katika maeneo mbali mbali ya kiutawala. Hata hivyo, katika muundo wake, MAIR ni kitabu

kikubwa na kilichoandikwa kitaalam sana kiasi kwamba wasomaji wengi watashindwa kuelewa, hata

kama kingetafsiriwa kwa Kiswahili. Ni kwasababu hiyo ndiyo maana tumeandaa kijitabu hiki cha lugha

rahisi.

Utangulizi

1

Kwenye sura hii tunaeleza kwa ufupi juu ya masuala makuu ya MAIR, madhumuni na

malengo yake na jinsi MAIR ilivyoandaliwa. Kisha tunaelezea mapana ya MAIR na mapana

na mapungufu ya mwongozo huu wa lugha rahisi.

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA (MAIR) ni moja ya matokeo ya Mfumo wa Ufuatiliaji

wa MKUKUTA. Hivyo ripoti hii ni sehemu ya muundo wa jumla wa utoaji wa taarifa za wadau

mbalimbali wanaojihusisha na utekelezaji wa MKUKUTA. Wadau hao ni pamoja na Wizara, Idara, na

Wakala wa serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa,na Asasi Zisizo za kiserikali.

Masuala makuu ya MAIR ni:• MAIR imejikita zaidi kwenye uchambuzi wa maendeleo ya utekelezaji wa kila lengo, kwa kuzingatia

malengo ya MKUKUTA na kutoa picha halisi ya utekelezaji, changamoto, mambo ya kujifunza na

hatua za kuchukua katika siku zijazo kwa kila nguzo ya MKUKUTA

• MAIR huzingatia kwa karibu uhusiano baina ya makundi makuu ya MKUKUTA

• Inajumuisha maendeleo ya michakato na maboresho yaliyofanywa na Wizara, Serikali za Mitaa na

AZISE na kubainisha mchango wa kila moja katika kufikia matokeo ya MKUKUTA.

• Inatambua kwamba licha ya mchango wa AZISE kutowekwa bayana mara nyingi, sekta hii ina

mchango mkubwa.

• Katika maeneo mengi uandaaji na utoaji wa taarifa hutegemea taarifa na takwimu za malengo ya

utekelezaji. Taarifa hizi zinaweza kuwa za kitakwimu zaidi ama za maelezo kutegemeana na upatikanaji

wa takwimu.

• Utekelezaji wa masuala mtambuka umejumuishwa katika uchambuzi wote wa mafanikio

yaliyopatikana.

1. Ijue MAIR

2

MAIR ina Madhumuni Makuu Mawili• Kuwafahamisha Watanzania na wadau wote kuhusu mafanikio yaliyofikiwa katika utekelezaji wa

MKUKUTA pamoja na michakato inayohusika. Hili linaweza kufanyika moja kwa moja ama kupitia

wawakilishi wa wadau au wananchi kama vile Wabunge.

• Kuchochea mijadala katika masuala ya msingi, na hivyo kusaidia kuhabarisha, kushawishi na

kuboresha mipango, bajeti na utekelezaji wake

Malengo makuu na matumizi ya MAIR• Kupima mafanikio ya vipaumbele vya Serikali kwa ajili ya ukuaji wa uchumi na upunguzaji wa

umaskini kama vilivyoainishwa kwenye MKUKUTA

• Kuwezesha upatikanaji wa taarifa zitakazosaidia kubaini vipaumbele katika sekta mbali mbali na

kubuni mikakati thabiti na endelevu.

• Kuchochea mazungumzo na midahalo zaidi miongoni mwa wadau juu ya masuala muhimu ya

kimkakati ikiwemo (a) kuweka na kupanga vipaumbele na utafutaji raslimali; na (b) namna bora ya

kutumia michakato ya mijadala siku za baadaye 1

• Kubaini masuala muhimu pamoja na fursa zilizopo kwa ajili ya kuinua uwekezaji ili kufikia malengo

ya MKUKUTA

• Kuwezesha upatikanaji wa taarifa zitakazosaidia kuboresha mchakato wa kitaifa wa uandaaji wa

bajeti.

Uoanishaji na upangiliaji wa michakato ya kitaifa Pamoja na wadau wakuu, serikali imefanyakazi ya kuoanisha na kupangilia michakato mikuu ya (a)

mipango ya sera na bajeti (b) ufuatiliaji na utoaji taarifa, na (c) kuoanisha mtiririko wa raslimali fedha

kutoka nje ya nchi na malengo na vipaumbele vya Maendeleo ya taifa. Kanuni za kuoanisha na kupangilia

masuala ya ubia kuhusiana na misaada zimeelezwa kwenye nyaraka nyingi 2 . MAIR inazingatia uoanishaji

wa ajenda na hatua iliyokwisha pigwa, changamoto na fursa zilizopo mbele ya safari.

Jinsi ripoti ilivyoandaliwaMaandalizi ya MAIR yamekuwa na changamoto kubwa kutokana na kubadilika kutoka utaratibu wa

kuzingatia sekta wa mfumo wa awali wa Ufuatiliaji wa Umaskini kwenda kwenye utaratibu unaozingatia

matokeo wa Mfumo mpya wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA (. Mabadiliko haya yameongeza mipaka ya

ripoti kwa kiasi kikubwa. Hali kadhalika wadau wanaohusika wameongezeka.

Idara ya Kuondoa Umaskini Wizara ya Fedha na Uchumi inaratibu maandalizi ya MAIR kwa kushirikiana

na wadau wengine wengi. Kamati ya Kiufundi ya MKUKUTA3 inawajibika na kusimamia uandaaji.

Kazi ya kuandaa MAIR ilihusisha kukusanya taarifa kutoka vyanzo mbali mbali (tazama kisanduku 1).

Taarifa hizi zilitoa picha ya jumla, jinsi raslimali zilivyotumika, matokeo, na maendeleo katika masuala

mtambuka.

3

Izingatiwe kuwa ni nchi chache zinazoweza

kuandaa ripoti ya kitaifa inayotoa taarifa za

jumla zinazohsu serikali nzima. Ripoti za

aina hiyo zitakuwa kubwa sana na utakuwa

ni ufujaji mkubwa wa raslimali za umma.

Badala yake ripoti nyingi huzingatia kutoa

taarifa za matokeo. Taarifa hizi zinaelezea

juu ya mabadiliko makubwa na mienendo ya

hali na huwa zinatumika kutoa mwanga na mwelekeo katika uandaaji wa mipango na sera na uwekaji wa

vipaumbele. Inafahamika kwamba hatua muhimu inayofuata nchini Tanzania ni kuimarisha uhusiano

baina ya utengaji wa raslimali, matumizi na utoaji wa taarifa za matokeo.

Mapana ya MAIRTangu ilipoanza, MAIR imekuwa na kiu kubwa ya kutaka kutoa taarifa za utekelezaji wa shughuli

zilizopangwa, matumizi pamoja na matunda yake kwenye matokeo. Hii ingehusisha utoaji wa taarifa za

kina kuhusu mambo ambayo serikali ilipanga kufanya, kiasi cha raslimali kilichopangwa na kutumika,

shughuli zilizotekelezwa na hatua zipi zilichukuliwa. Hata hivyo, MAIR 2007 haijakidhi matarajio yote

haya kutokana na sababu zifuatazo:

• Licha ya bajeti za Wizara, Idara, Wakala na Serikali za Mitaa kufungamanishwa na MKUKUTA

kwa kiasi kikubwa, njia ya sasa ya utoaji ripoti juu ya namna bajeti inavyotumika haijafungamanishwa

kikamilifu na malengo ya kimkakati na matokeo ya MKUKUTA.

• Kukosekana kwa takwimu kwa baadhi ya viashiria ambapo taarifa hazizalishwi mara kwa mara.

• Kwa baadhi ya maeneo kama vile utamaduni, mfumo wa ufuatiliaji bado haujaweka viashiria vya

matokeo. Hata hivyo, kila inapowezekana, shughuli na michakato inayohusika kwenye maeneo hayo

imeripotiwa.

Mapana na Mapungufu ya Mwongozo huu wa Lugha RahisiMAIR huwasilisha muhtasari wa taarifa zilizotolewa kwenye ripoti nyingine nyingi. Nyingi ya

hizi hutolewa kama takwimu zinazothibitisha kiwango cha kufikiwa au kutofikiwa kwa shabaha za

MKUKUTA. Takwimu hizi hutumika kuzalisha na kuhalalisha orodha ya changamoto, mambo ya

kujifunza na mapendekezo kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa.

Mwongozo huu haujaribu kuufupisha takwimu bali unachukulia kwamba takwimu hizo ni sahihi na

kwamba msomaji mwenye kutaka kujua undani wa takwimu hizo anaweza kuzipata kwenye MAIR (au

chanzo kingine ambako MAIR imechukua takwimu hizo).

Mwongozo huu umejikita kwenye orodha ya changamoto, mambo ya kujifunza na mapendekezo ya

hatua zinazopaswa kuchukuliwa. Katika sura inayofuata ya kijitabu hiki, taarifa hizi zimewasilishwa kwa

kila nguzo ya MKUKUTA na katika sura mbili zinazofuata zimewasilishwa kulingana na mfumo wa

kwanza wa ufuatiliaji na tathmini, na kisha masuala ya ugharamiaji.

Kisanduku 1: Vyanzo vya Taarifa za MAIR

• Ripoti ya Umaskini na Maendeleo ya Watu (PHDR)

• Ripoti za Mapitio ya Matumizi ya Umma (PER)

• Taarifa ya Hali ya MKUKUTA (2006)

• Tafiti za Kiuchumi

• Mapitio ya Sekta

• Ripoti za Wizara mbali mbali

4

Sura ya mwisho hujumuisha na kutoa muhtasari wa mawazo kutoka kwenye sura zilizotangulia.

Izingatiwe kwamba mwongozo huu wa lugha rahisi unatoa vidokezo vingi kwa wasomaji wenye kutaka

kufahamu masuala husika kwa kina zaidi. Vidokezo hivi ni pamoja na visanduku vya maelezo, ambavyo

vinatoa maelezo ya kina zaidi kwa baadhi ya mada zinazotajwa kwenye kijitabu hiki.

5

Katika sura hii tunafanya mapitio ya mahitimisho makuu kuhusu changamoto zilizobainishwa,

mambo ya kujifunza na mapendekezo ya hatua za kuchukua kwenye nguzo kuu tatu za

MKUKUTA. Kwa kila nguzo tunaanza kwa kuelezea sehemu za nguzo hiyo. Hii itamsaidia

msomaji kuona kiwango na ugumu wa muundo wa MKUKUTA. Kisha tunaendelea kutazama

changamoto kuu zilizojitokeza na mambo ya kujifunza yaliyoonekana. Kila sehemu inahitimishwa kwa

kueleza mapendekezo ya hatua za kuchukua. Kwa ujumla Maendeleo ya utekelezaji wa MKUKUTA

yamechanganyika. Kuna matokeo mazuri katika baadhi ya maeneo, matokeo mabaya katika maeneo

mengine wakati masuala mengine yamebaki kama yalivyokuwa. Izingatiwe kwamba kumekuwepo tofauti

kati ya mijini na vijijini na baina ya maeneo mbali mbali ya nchi. Watu mbali mbali kutoka sehemu mbali

mbali watakuwa na vipaumbele tofauti. Ziko changamoto nyingi zaidi katika hatua za kuchukua kwa

siku zijazo!

Nguzo ya kwanza – Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini

wa Kipato

Katika sehemu hii kwanza tunaelezea matokeo makuu na malengo ya nguzo halafu tunazungumzia

kwa ufupi juu ya sehemu nyingine za nguzo hii. Hii itasaidia msomaji kupata mapana na mipaka ya

nguzo hii. Kwa vile huu ni mwongozo wa lugha rahisi hatufanyi mapitio ya takwimu ‘kavukavu’ ila

tonasonga mbele na kudokeza juu ya changamnoto kuu zilizojitokeza na mapendekezo ya hatua za

kuchukuliwa.

2. Changamoto za Nguzo na Hatua za Kuchukua

6

Sehemu za Nguzo ya KwanzaNguzo ya kwanza hujumuisha shughuli zinazolenga kukuza uchumi na kupunguza umaskini wa kipato.

Matokeo ya jumla ni kuhakikisha kuwa “Ukuaji wa uchumi mpana na unaozingatia usawa unafikiwa na

kuendelezwa “

Malengo sita ya nguzo ni haya yafuatayo:

• Kuhakikisha kuwa kunakuwapo na usimamizi mzuri wa uchumi

• Kuchochea ukuaji wa uchumi wenye msingi mpana na endelevu

• Kuongeza upatikanaji wa chakula

• Kupunguza umaskini wa kipato kwa wanaume na wanawake vijijini

• Kupunguza umaskini wa kipato kwa wanaume na wanawake mjini

• Kutoa nishati ya uhakika na rahisi kwa watumiaji.

Changamoto Kuu Nane za Nguzo ya KwanzaPamoja na kuwepo Maendeleo mazuri katika kufikia na kuendeleza ukuaji wa Uchumi mpana na wenye

kuzingatia usawa katika miaka miwili iliyopita, bado zimekuwepo changamoto nyingi. Sehemu hii

inaelezea changamoto kuu nane.

Kuharakisha Ukuaji wa UchumiKasi ya ukuaji wa uchumi bado iko chini ya shabaha iliyowekwa kwenye MKUKUTA. Kasi ya sasa ya

ukuaji wa uchumi haiwezi kupunguza umaskini, hususan kwa kuzingatia kasi ya sasa ya ongezeko la

idadi ya watu ya asilimia 3 kwa mwaka. Uharakishaji wa ukuaji wa uchumi unahitajika ili kuongeza wigo

wa raslimali za ndani ya nchi na kuongeza uwezo wa serikali kutoa huduma za umma.

Mahusiano Bora Zaidi ya Uchumi Mkubwa na Ule wa Ngazi za Chini ili Ukuaji Uweze Kuwanufaisha Zaidi Watu Maskini. Changamoto kubwa ni kuona mafanikio katika Uchumi mkuu yakileta Maendeleo endelevu katika ngazi

za chini za jamii. Swali muhimu ni namna gani faida itokanayo na ukuaji inaweza kusambazwa kwa kaya

za watu maskini. Hii itahusisha kutafakari upya mifumo (kama vile sera, ya kisheria, taasisi n.k.) katika

ngazi ya kati, kwa mfano ya serikali za Mitaa (kama halmashauri za wilaya) ili ziweze kuhudumia ngazi

za chini zaidi kama vile ngazi ya jamii.

Uoanishaji Bora Zaidi wa SeraUoanishaji bado unakosekana miongoni na baina ya sekta. Mifano yaweza kuwa Ajira dhidi ya Biashara,

Kazi dhidi ya Ubinafsishaji, Elimu, Uwekezaji, Fedha, na Sera zenye kulenga kuwavutia wawekezaji zaidi

wa kigeni. Ipo haja ya kuzifanyia mapitio sera hizi na nyingine nyingi, sambamba na sheria zinazohusiana

na sera hizo ili ziweze kuoana badala ya kukinzana.

Uongezaji wa Mauzo ya Bidhaa Nje ya NchiUchumi wa Tanzania bado unategemea kiasi kidogo cha bidhaa zinazouzwa nje ya nchi; na mapato

yanayotokana na mauzo ya bidhaa nje ya nchi hayajaongezeka kwa kiwango cha kuridhisha. Hii inaweza

7

kuelezwa kuwa imetokana na kushindwa kubaini fursa zilizoko kwenye soko la kimataifa. Fursa zilizoko

katika soko la nje hazijaweza kutumika ipasavyo. Kwa hiyo serikali inafanya jitihada za kuongeza wigo

wa bidhaa za kuuza nje ya nchi zenye kukidhi viwango vya soko la kimataifa.

Kuna changamoto mahsusi katika kuboresha uuzaji nje wa huduma mbali mbali. Hii inahitaji upanuzi

wa vivutio vya kitalii sanjari na uboreshaji wa miundombinu inayohusika, kama vile viwanja vya ndege,

barabara na reli.

Kiwango kidogo cha mauzo ya bidhaa nje ya nchi na kiwango kikubwa cha bidhaa zinazoingizwa kutoka

nje ya nchi vimesababisha kukosekana kwa mizania ya kibiashara nchini.

Upatikanaji Bora wa NishatiKatika miaka miwili iliyopita Tanzania imekumbwa na uhaba na kutotabirika kwa upatikanaji wa nishati

itokanayo na nguvu ya maji. Kwa hiyo kuna umuhimu wa Kupunguza utegemezi katika nishati itokanayo

na nguvu ya maji kwa kuendeleza vyanzo mbadala vya umeme. Changamoto inayohusiana na hii ni ile ya

kufikisha nishati katika maeneo ya vijijini kwa gharama nafuu.

Kuboresha Zaidi Maendeleo ya Vijijini na Katika KilimoChangamoto ya ukuaji katika Uchumi wa maeneo ya vijijini zina uhusiano wa karibu na zile za sekta ya

kilimo. Hizi ni pamoja na:

• Uzalishaji mdogo wa ardhi na nguvu kazi

• Utegemezi katika maji ya mvua

• Kutoendelezwa kwa fursa za umwagiliaji

• Mtaji mdogo na kutopatikana kwa huduma za kifedha

• Huduma zisizotosheleza za utaalamu wa kilimo

• Miundombinu hafifu ya vijijini ambayo hukwamisha ufanisi wa uhusiiano wa Mjini na vijijini.

• Maambukizi na milipuko ya magonjwa ya mazao na wadudu na magonjwa ya wanyama

• Mmomonyoko wa raslimali asilia sanjari na uharibifu wa mazingira

• Vyama dhaifu vya wazalishaji sambamba na uratibu dhaifu na uhaba wa teknolojia sahihi na rahisi

Mipangilio Mizuri Zaidi ya Soko la AjiraSoko la ajira linakabiliwa na changamoto kutokana na (a) uhuria unaotarajiwa katika ajira kwa nchi

za Afrika Mashariki, na (b) kuwepo kwa utandawazi. Utafiti zaidi unahitajika katika masuala ya ajira,

likiwemo suala la uhaba wa ajira miongoni mwa vijana.

Matumizi Bora na Endelevu ya MaliasiliHayajapatikana mafanikio ya kuridhisha katika utunzaji wa mazingira na maliasili katika maeneo ya

nyanda za juu kusini, misitu ya miombo huko Tabora, na kusini mwa Tanzania kuliko katika maeneo

mengine ya nchi.

8

Matokeo ya Maendeleo ya viwanda vinavyohusisha mazao ya misitu na uendelevu wa maisha si wa

kuridhisha. Hii kwa sehemu imesababishwa na kukosekana kwa fedha za kutosha kunakohusisha

kushindwa kwa kuchochea sekta binafsi kuchangia utekelezaji wa Programu ya Taifa ya Misitu.

Imebainishwa pia kwamba ongezeko la mapato kutokana na sekta ya maliasili kunatokana na utaifishaji

na uuzaji wa mazao haramu ya maliasili yanayokamatwa.

Hatua za KuchukuliwaHatua zinazopaswa kuchukuliwa zinahusisha kukabiliana na changamoto zilizotajwa hapo juu. Sehemu

hii inaorodhesha baadhi ya hatua muhimu zinazopaswa kuchukuliwa:

Kilimo Sera ya kilimo haina budi kuwa na malengo ya aina mbili. Lengo moja likijikita katika kuinua uzalishaji

mdogo wa kilimo kama sehemu ya mkakati wa kupunguza umaskini. Hii itahusisha kuanzisha shughuli

za mashamba madogo madhubuti, na za muda wote zikijumuisha uzalishaji wa kujikimu na kwa ajili ya

kukidhi soko.

Na lengo la pili ni kutia msukumo na nguvu mpya katika sekta ya kilimo cha kibiashara ili kukuza

uzalishaji. Hii moja kwa moja itaongeza ajira na kupunguza umaskini wa vijijini kwa kuajiri nguvu kazi

na kupitia viwanda vya usindikaji vinavyohusiana na mazao ya kilimo.

Njia nyingine za kuinua uzalishaji wa sekta ya kilimo ni pamoja na kuongeza upatikanaji wa taarifa za

masoko ya bidhaa za kilimo na kuongeza kasi ya mwitikio wa sekta binafsi katika kuzitumia taarifa

hizo.

Juhudi za maksudi zitahitajika katika kuboresha upatikanaji, usambazaji, na wananchi kumudu pembejeo

za kilimo, huduma za ugani, na huduma za kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa. Juhudi pia hazina

budi kuelekezwa katika kuboresha uzalishaji wa mazao ya sekta ya mifugo na kuhakikisha kwamba

kunakuwepo na masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi kwa mazao ya mifugo.

Shughuli Zisizo za Shamba VijijiniShughuli za vijijini zisizo za mashambani hususan kwenye usindikaji na utoaji huduma, hazina budi

kukuzwa kwani ni fursa muhimu katika kuongeza ajira maeneo ya vijijini. Mkakati wa aina hii unaweza

kufanikiwa katika maeneo yenye barabara nzuri, umeme na mawasiliano ya kuaminika.hii inamaanisha

kwamba maeneo yenye sifa hizo ndiko viwanda na masoko ya bidhaa kuweza kuwa na ufanisi na gharama

za uzalishaji zitakuwa chini zaidi.

Viwango vizuri vya elimu na miundombinu ya msingi ndivyo vichocheo muhimu katika kukuza shughuli

za kiuchumi zisizo za mashambani kwenye maeneo ya vijijini. Hivyo serikali haina budi kuhakikisha

kuwa mambo hayo yanaboreshwa.

9

Huduma za FedhaSerikali inapaswa kuongeza kasi ya utekelezaji wa awamu ya pili ya Maboresho ya Sekta ya Fedha. Sekta

hii itaendelea kuchochea ukuaji wa uchumi kwa kutoa huduma za kifedha za kutosha za kna ambazo

watu wengi wanaweza kuzimudu.

NishatiKuna umuhimu wa kuwa na vyanzo mbadala vya nishati. Hili linaweza kufanikishwa kwa kukuza

ushirikiano wa kikanda katika sekta ya nishati, na kwa kutekeleza Mpango Mkuu wa Sekta ya Nishati.

Ajira Kuna uhitaji mkubwa wa kutekeleza Sera ya Maendeleo ya Vijana, Sera ya Ajira ya Taifa, na Sera ya Taifa

ya Hifadhi ya Jamii. Utekelezaji wa sera hizi utasaidia kuongeza fursa za ajira sambamba na kuandaa

mazingira bora zaidi kwa ajili ya ajira binafsi.

Fedha za UmmaHapana budi kuwapo msisitizo (a) katika kufikia na kudumisha kiwango cha kuridhisha cha usimamizi

bora wa fedha na uwajibikaji na (b) kuboresha ukusanyaji, upangiliaji na utumiaji wa raslimali.

Katika ngazi ya kimataifa, kuna umuhimu wa kuhimiza diplomasia ya kiuchumi kwa lengo la (a) kuvutia

masoko na wawekezaji wa nje ya nchi (b) kujadiliana na wahisani juu ya mikopo yenye riba nafuu pamoja

na kushawishi kufutiwa madeni.

Maliasili na MazingiraJuhudi zinahitajika ili:

• Kuboresha usimamizi katika sekta hii

• Kuongeza jitihada za upandaji miti

• Kutekeleza malengo ya ukusanyaji wa maduhuli (mapato)

• Kuimarisha Kitengo cha Usimamizi wa Misitu

• Kuzuia uvunaji haramu wa maliasili

Msaada zaidi unahitajika katika kuwezesha ukusanyaji na uchanganuzi wa taarifa kwa kuzingatia

uendelevu wa mchango wa maliasili kwa

Maendeleo ya Taifa.

Nguzo ya Pili – Uboreshaji wa Maisha na Ustawi wa Jamii

Katika sehemu hii kwanza tunaelezea matokeo makuu na malengo ya nguzo halafu tunazungumzia kwa

ufupi juu ya sehemu nyingine za nguzo hii. Hii itasaidia msomaji kupata mapana na mipaka ya nguzo hii.

Kwa vile huu ni mwongozo wa lugha rahisi hatufanyi mapitio ya takwimu ‘kavukavu’ ila tunasonga mbele

na kudokeza juu ya changamnoto kuu zilizojitokeza na mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa.

10

Sehemu za Nguzo HiiNguzo ya pili ya MKUKUTA inahusu shughuli zinazochochea “Uboreshaji wa Maisha na Ustawi wa

Jamii” . Matokeo ya jumla yatakuwa (a) Kuboreka kwa maisha na ustawi wa jamii msisitizo wa kipekee

ukiwa kwa watu maskini zaidi pamoja na wale walio katika mazingira hatarishi. (b) kupungua kwa tofauti

ya kimatokeo (mfano; elimu, kiwango cha kuishi na afya) kwa kuzingatia maeneo ya kijiografia, kipato,

umri, jinsia, na makundi mengine Malengo matano ya nguzo hii ni:

• Kuhakikisha upatikanaji sawa wa elimu bora ya msingi na sekondari kwa wavulana na wasichana,

elimu ya kufuta ujinga miongoni mwa wanaume na wanawake, na upanuzi wa elimu ya juu, ufundi na

ufundi stadi.

• Kuboresha maisha, afya na ustawi wa watoto wote na wanawake na hasa makundi yaliyo katika

mazingira hatarishi.

• Kuongeza upatikanaji wa maji safi, salama na ya gharama nafuu, usafi, malazi mazuri, na mazingira

salama na endelevu; na hivyo kupunguza uathirikaji utokanao na hatari za mazingira.

• Kuhakikisha kunakuwapo hifadhi ya uhakika ya kijamii na utoaji wa mahitaji na huduma za msingi

kwa wahitaji na walio kwenye mazingira hatarishi.

• Kuhakikisha kunakuwepo na mfumo mzuri kuwezesha upatikanaji wa huduma safi za umma na

zenye gharama nafuu kwa wote

Changamoto kuu sita za nguzo ya piliLicha ya kuwepo Maendeleo mazuri katika kufikia na kuendeleza uboreshaji wa maisha na ustawi

wa jamii katika miaka miwili iliyopita, bado zimekuwepo changamoto nyingi. Sehemu hii inaelezea

changamoto kuu sita.

11

Ubora na Upanuzi wa ElimuNi muhimu kuhakikisha kunakuwa na elimu yenye ubora wa kiwango cha juu katika ngazi zote kadri

mfumo unavyozidi kupanuka. Upanuzi wa elimu unajumuisha kuwepo kwa vyumba vingi zaidi vya

madarasa ili kukabili tatizo la msongamano wa wanafunzi, vifaa na zana za kufundishia, nyumba za

walimu, vyoo, na uwiano unaokubalika wa walimu wenye sifa na wanafunzi.

Jinsia na ElimuBado iko tofauti katika uandikishaji wa wanafunzi katika shule za sekondari na taasisi za elimu ya

juu. Katika hili changamoto kubwa ni kuhakikisha wanafunzi wa kike wanaoandikishwa wanaendelea

na masomo hadi kuhitimu na kuinua viwango vya ufaulu kwa wanafunzi wa kike. Hali hii inaweza

kusababishwa na kukosa uwezo wa kumudu gharama, mahitaji ya soko la ajira na mimba na watoto

wa kike kulazimishwa kuolewa mapema. Sababu hizi huchangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi wa kike

kuacha shule katika maeneo ya mijini na vijijini

AfyaJuhudi zinahitajika (a) kuendeleza chanjo ya Donda koo, Pepopunda, na Homa ya Ini na kuifikia mikoa

yote (b) Kuhakikisha maambukizi mapya ya Kifua Kikuu yanapungua, na (c) kufanya ushauri na upimaji

wa VVU na UKIMWI kuwa endelevu.

Maji na Usafi wa MazingiraKuna umuhimu wa kukarabati, kupanua na kujenga mitandao ya mifumo ya miundombinu ya maji na

usafi wa mazingira. Juhudi za maksudi zinahitajika katika kuhimiza matumizi sahihi ya vyoo na mifumo

ya utupaji wa taka, sambamba na uboreshaji wa makazi holela.

Makundi Yaliyo katika Mazingira HatarishiKunahitajika juhudi katika kushughulikia ongezeko la makundi maalum ya watu walio katika hatari

zaidi ya kuathirika yanayosababishwa na matatizo ya kiafya kama vile magonjwa yanayoenezwa kwa

ngono. Ni muhimu kulenga katika (a) hali ngumu ya maisha inayosababishwa na VVU na UKIMWI

(b) matatizo mahsusi ya familia zinazoongozwa na watoto na wazee.

Wafanyakazi Wenye SifaSekta za elimu , afya na kwenye serikali za Mitaa kuna upungufu wa wafanyakazi wenye ujuzi unaohitajika.

Wafanyakazi wengi waliopo hawajapewa motisha wa kutosha – hususan wale wanaofanyakazi maeneo

ya vijijini na maeneo yasiyokuwa na vivutio vingi.

Mambo TuliyojifunzaMtazamo wa MKUKUTA wa kuzingatia matokeo unawezesha kubainisha mwelekeo mtambuka wa

juhudi nyingi za kimaendeleo

12

Elimu Kuongeza idadi ya walimu wenye sifa zinazotakiwa ni sharti muhimu la kukuza ubora wa elimu.

Hata hivyo sharti hili peke yake halijitoshelezi.

AfyaKumekuwepo na mafanikio katika kupunguza utapiamlo, vifo vya watoto wachanga na walio chini ya

umri wa miaka mitano, na kudumaa. Mafanikio haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na utoaji wa

chanjo, sanjari na uboreshaji wa lishe.

Maji na NishatiUpatikanaji duni wa huduma za jamii kama vile maji na vyanzo mbadala vya nishati hukwamisha juhudi

za upatikanaji wa elimu katika ngazi ya familia, hususan kwa wanawake. Muda mwingi unaotumika

katika kuchota maji na kutafuta nishati kama vile kuni ungeweza kutumika kwa shughuli nyingine.

Wafanyakazi Wenye SifaMaeneo mengi ya vijijini na yasiyokuwa na vivutio hayana huduma nzuri kwa watumishi, ikiwa ni pamoja

na nyumba za kuishi. Hali hii inawakatisha tamaa wafanyakazi katika sekta ya huduma za jamii wenye

sifa kufanya kazi katika maeneo hayo.

Ushiriki wa JamiiBila ushiriki wa wananchi malengo mengi ya Nguzo ya pili hayatafikiwa. Mchango wa ushiriki wao

katika kupanga, kutoa mchango wa hali na mali katika miradi ya maendeleo ni muhimu sana hivyo

taratibu zinapaswa kuwekwa ili kuongeza ushiriki wao.

Hatua za KuchukuliwaHatua zinazopaswa kuchukuliwa zinahusu namna ya kukabiliana na changamoto zilizotajwa hapo juu.

Sehemu hii inaorodhesha baadhi ya hatua muhimu zinazopaswa kuchukuliwa:

Ushiriki wa Wadau Changamoto zilizoibuliwa kwenye nguzo hii zinaashiria kuhitajika kwa juhudi za maksudi kwa wadau

wote kuchukua hatua zitakazowezesha kufikiwa kwa malengo ya MKUKUTA.

ElimuSerikali itaendelea kuboresha na kupanua elimu kupitia programu zinazolenga kuongeza idadi ya walimu

wenye sifa, na kuongeza ubora wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia ili kuboresha mazingira ya shule.

Pia juhudi hazina budi kuelekezwa katika kuondoa tofauti za kijinsia katika ngazi zote za elimu.

Watumishi Wenye SifaUjengaji uwezo kwa watumishi wa serikali za Mitaa utaendelea kama njia ya kuimarisha usimamizi wa

raslimali za umma katika ngazi hiyo. Kutakuwa na mafunzo kwa njia ya masafa kwa watumishi wa sekta

ya huduma za jamii, hususan wale walioko vijijini na maeneo mengine yasiyokuwa na vivutio.

13

Afya Juhudi za maksudi zinahitajika miongoni mwa wadau wa afya ili kukomesha tatizo la vifo vya kinamama

wazazi. Hii itahusisha (a) Muundo wa Kitaifa wa VVU na UKIMWI unaohusisha sekta nyingi (b)

kupanua utoaji wa dawa za kurefusha maisha

Makundi ya Watu Walio katika Mazingira HatarishiMiongozo na mifumo ya kuyafanya masuala ya watoto yatima na wale walio katika mazingira hatarishi

kuwa mtambuka haina budi kuandaliwa. Miongozo na mifumo hii itapaswa kutumiwa na Wizara, Idara,

Wakala wa Serikali na Wadau wasiokuwa wa Kiserikali. Miongozo hiyo inapaswa kuhusisha ujengaji wa

uwezo wa maofisa husika katika kushughulikia masuala ya watu wenye ulemavu na wazee.

Ugharamiaji wa Huduma za Jamii. Kutakuwa namwendelezo wa juhudi za kuongeza upanuzi na uboreshaji wa huduma za jamii kupitia

ubia wa sekta ya umma na ya binafsi .

Hifadhi ya JamiiKuna umuhimu mkubwa wa kuboresha mipango ya hifadhi ya kijamii kwa makundi yaliyo katika

mazingira hatarishi.

Mazingira Kampeni za utunzaji wa mazingira zinapaswa kupanuliwa ili kuongeza ufahamu wa wadau juu ya hifadhi

ya mazingira.

Nguzo ya Tatu –Utawala Bora na Uwajibikaji

Katika sehemu hii kwanza tunaelezea matokeo makuu na malengo ya nguzo, halafu tunazungumzia kwa

ufupi juu ya sehemu nyingine za nguzo hii. Hii itasaidia msomaji kupata mapana na mipaka ya nguzo hii.

Kwa vile huu ni mwongozo wa lugha rahisi hatufanyi mapitio ya takwimu ‘kavukavu’ ila tunasonga mbele

na kudokeza juu ya changamnoto kuu zilizojitokeza na mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa.

Sehemu za Nguzo HiiNguzo ya tatu ya MKUKUTA inahusu shughuli zinazo lenga kukuza, “ Utawala Bora na Uwajibikaji”.

Matokeo ya jumla ni (a) Utawala bora na Utawala wa Sheria (b) Uwajibikaji wa Viongozi na watumishi

wa umma, (c) Demokrasia na uvumilivu wa kisiasa na kijamii, na (d) Amani, Utulivu wa kisiasa, umoja

wa kitaifa na mshikamano wa kijamii.

Malengo saba kwa nguzo hii ni haya yafuatayo:

• Kuhakikisha kuwa miundo na mifumo ya utawala pamoja na utawala wa sheria ni vya kidemokrasia,

shirikishi, uwakilishi, uwajibikaji na jumuishi

• Kuhakikisha ugawaji sawa wa rasilimali za umma – pamoja na kushughulikia ipasavyo suala la

rushwa

14

• Kuweka mfumo wa huduma za umma unaofaa kama msingi wa kuboresha utoaji wa huduma na

kupunguza umaskini

• Kuhakikisha kwamba haki za maskini na makundi yaliyo katika mazingira hatarishi zinalindwa na

kukuzwa katika mfumo wa haki

• Kupunguza hali ya baadhi ya watu kutengwa na kutovumiliana kisiasa na kijamii

• Kuboresha usalama binafsi na wa mali, kupunguza uhalifu na kuondoa unyanyasaji wa kijinsia na

unyanyasaji majumbani

• Kuendeleza na kuimarisha utamaduni wa watu kama utambulisho wa kitaifa.

Changamoto Kuu Saba za Nguzo ya TatuLicha ya kuwepo mafanikio kuelekea kuboreka kwa utawala na uwajibikaji katika kipindi cha miaka

miwili iliyopita, bado tunakabiliwa na changamoto nyingi. Sehemu ifuatayo inazungumzia changamoto

kuu saba zilizojitokeza.

Mapungufu katika mfumo wa kisheriaChangamoto zinazoukabili mfumo wa kisheria ni pamoja na:

• upungufu wa miundombinu (yaani Ofisi, vifaa vya ofisini, nyumba, vifaa vya mawasiliano) kwa vyombo

vya utekelezaji wa sheria ( yaani jeshi la Polisi, Magereza, Mahakama)

• mishahara isiyokidhi mahitaji jambo linalowafanya wasimamizi wa utekelezaji wa sheria kutumbukia

katika kuchukua rushwa

• uchache wa raslimali watu na ujengaji wa uwezo katika kufanya yale yanayopaswa kufanyika

• kukosekana kwa upanuzi wa magereza na hivyo kusababisha msongamano wa wafungwa

15

• Teknolojia duni katika kupambana na uhalifu mkubwa kama ule wa kimataifa (kama ugaidi, fedha

haramu, Biashara ya dawa za kulevya, uhamiaji haramu, n.k)

Maboresho ya Sekta ya SheriaLicha ya kuwepo mafanikio katika maboresho ya sekta ya sheria bado ziko changamoto katika kuboresha

mfumo wa mahakama. Hizi ni pamoja na:

• Kutafakari upya na kuwianisha ngazi za mishahara kwa watumishi wa sekta ya sheria

• Kuongeza kasi ya mfumo wa uendeshaji wa kesi

• Kuongeza uhuru wa mahakama

• Kuongeza utolewaji wa taarifa kwa wananchi wa kawaida kuhusu muundo na kazi za mfumo wa

mahakama.

Usimamizi wa Upelekaji wa Madaraka, Majukumu na Raslimali kwa WananchiInaziwia vigumu Serikali za Mitaa kumudu usimamizi wa ongezeko la fedha lililosababishwa na

maboresho ya serikali za Mitaa ambapo raslimali nyingi zinapaswa kupelekwa moja kwa moja kwenye

mamlaka za serikali za Mitaa.

Kuna hitaji la haraka kuwianisha upelekaji wa madaraka, majukumu na raslimali kwa wananchi dhidi ya

programu za kuzijengea uwezo mamlaka husika za serikali za mitaa. Hii inapaswa kuhusisha kuongeza

uelewa miongoni mwa watumishi wa serikali kuu na serikali za mitaa kuhusu dhana ya ‘‘Upelekaji wa

Madaraka, Majukumu na Raslimali kwa Wananchi”

Kumekuwepo na uhaba mkubwa wa raslimali katika kufanya ukaguzi wa mahesabu ya fedha za umma.

Maeneo ya vijijini zaidi yameathirka zaidi na uhaba huu kwa vile wakaguzi wa mahesabu wenye sifa

wamekuwa wakigoma kwenda maeneo hayo pale wanapopangiwa kufanya kazi huko.

Usimamizi wa MaliasiliKumekuwa na udhaifu katika kanuni na ushiriki wa wananchi katika kusimamia matumizi ya maliasili.

Hali hii imesababisha kuongeza kwa vitendo vya rushwa. Juhudi zaidi zinahitajika katika kuzishirikisha

asasi zisizo za serikali katika kutekeleza NACSAP II . Suala lenye umuhimu wa kipekee ni utendaji wa

bodi za zabuni chini ya sheria mpya ya manunuzi.

Haki za BinadamuIpo haja ya kujenga uwezo wa watumishi wa haki za binadamu pamoja na kufanya ufuatiliaji wa mara

kwa mara. Wazo la kutumia ubia wa serikali na sekta binafsi linaleta changamoto ya kubainisha AZISE

zinazoaminika katika ngazi ya wilaya. Pia kumekuwepo na ukosefu wa takwimu za kitaifa zinazohusu

masuala ya unyanyasaji wa kijinsia na ukatili wa majumbani.

Mbao za MatangazoKubandika taarifa kwenye mbao za matangazo hakutoshelezi kwa vile hakuwasukumi wananchi katika

ngazi ya jamii kusoma na kuzichambua taarifa hizo. Mojawapo ya sababu ya hali hii ni mbao nyingi za

16

matangazo kutofikiwa na wananchi walio wengi kwani zinapatikana kwenye makao makuu ya wilaya na

siyo vijijini.

Teknolojia ya Habari na MawasilianoTeknolojia ya kisasa inaweza kutumika vizuri zaidi katika kusambaza taarifa na kuwahamasisha wadau

kuhusiana na jambo Fulani. Maeneo ambako huduma hii inahitajika zaidi ni pamoja na magerezani na

kwenye makambi ya wakimbizi.

Mambo TuliyojifunzaMatumizi hafifu ya taarifa za umma

Wizara, Idara, Wakala wa Serikali na Serikali za Mitaa hutoa taarifa kwa umma lakini bado kumekuwapo

na hamasa ndogo miongoni mwa wananchi katika ngazi ya jamii katika kuzitumia taarifa hizo. Hili

linajidhihirisha zaidi kutokana na taarifa zinazotolewa kwa umma na Serikali za Mitaa. Kuna haja ya

kuzirahisisha zaidi taarifa hizi ili ziweze kueleweka kirahisi.

Mambo ambayo jamii inapenda kupatiwa taarifa ni mengi ikiwa ni pamoja na:

• Watu wenye hati za kimila za umiliki wa ardhi katika ngazi ya kaya kwa kuzingatia jinsia

• Mazingira ya kazi ya watumishi wa vyombo vya dola

Vita Dhidi ya RushwaHatua za kuchukuliwa ili kupunguza rushwa zinapaswa kuhusisha:

• Uhamasishaji unaolenga kubadili mitazamo ya watumishi wa umma

• Kuimarisha shughuli za ukaguzi wa taasisi za umma ili kupunguza matumizi mabaya ya raslimali

• Kuimarisha uwezo na utayari wa wananchi kuwa makini katika kufuatilia michakato ya uwajibikaji wa

ofisi za umma

Uoanishaji Masuala yanayohitaji kuoanishwa ni pamoja na:

• Mchakato wa kupeleka madaraka, majukumu na raslimali kwa wananchi ili kuhakikisha uthabiti,

uendelevu na utekelezaji wenye ufanisi.

• Uratibu rasmi wa maboresho mbalimbali (Sekta ya Sheria, Sekta ya Utumishi wa Umma na Programu

za Maboresho ya Serikali za Mitaa n.k.)

• Migongano ya sheria za kisekta

Hatua Zinazopendekezwa KuchukuliwaHatua zinazopaswa kuchukuliwa zinahusisha namna ya kukabiliana na changamoto zilizotajwa hapo

juu. Sehemu hii inaorodhesha baadhi ya hatua muhimu zinazopaswa kuchukuliwa:

Serikali kwa ushirikiano na wadau wengine watapaswa;

• Kuongeza shughuli za uhamasishaji wa jamii juu ya umuhimu na matumizi ya taarifa za umma.

• Kutoa mafunzo zaidi juu ya maadili na uaminifu kwa wataalamu ili kuimarisha utawala bora na

uwajibikaji

17

• Kufanya utafiti wa awali wa viashiria vikuu vya utendaji ili kusaidia ufuatiliaji na tathmini za baadaye

• Kuboresha mazingira na miundombinu ya kazi

• Kushirikisha wadau wasiokuwa wa kiserikali katika kuimarisha uwajibikaji ikiwemo kupitia matumizi

ya mbao za matangazo

• Kuajiri wafanyakazi wapya na kuwapatia mafunzo kazini kila inapohitajika

• Kupunguza mrundikano wa kesi mahakamani

• Kuboresha miundombinu ya mawasiliano

• Kuweka mfumo uanaoeleweka wa utawala bora, uwajibikaji na uwakilishi.

• Kushirikisha zaidi jamii katika kusimamia maliasili

• Kujenga uwezo wa watumishi wa Serikali za Mitaa katika kusimamia raslimali na utoaji wa huduma.

• Kupanua na kuboresha magereza na kuweka mfumo wa uwekaji wa taarifa za wahalifu

• Kupanua mifumo katika kudhibiti na kufuatilia mipaka ya nchi

• Kupanua na kuimarisha Programu ya Huduma za Jamii na ya Zima moto na Uokoaji katika mikoa

yote

18

Katika sura hii kwanza tunaangalia chimbuko la MKUKUTA kwenye mapitio ya Mfumo wa

awali wa Ufuatiliaji wa Umaskini. Kisha kwa ufupi tunatazama kazi za sasa za Sekretarieti ya

MKUKUTA na Makundi matatu ya Kiufundi. Hii itatupeleka katika kutafakari maendeleo

ya uoanishaji wa shughuli mbalimbali. Sura hii inahitimishwa kwa kutoa fikra juu ya changamoto

zilizobainishwa, mambo ya kujifunza na mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa.

Chimbuko la Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA

Mwaka 2001, Serikali iliandaa Mfumo wa Ufuatiliaji Umaskini kwa ajili ya Mkakati wa Kupunguza

Umaskini. Mfumo huo ulipitiwa na kuboreshwa mwaka 2005/06 ili uweze kutumika kufuatilia

MKUKUTA ambao ni mkakati mpana zaidi na wenye kuzingatia matokeo zaidi kuliko Mkakati wa awali

wa Kupunguza Umaskini. Mfumo wa ufuatiliaji uliopitiwa na kuboreshwa uliidhinishwa mwaka 2006

na unajulikana kama Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA.Mabadiliko makubwa yaliyojumuishwa

kwenye mfumo mpya ni pamoja na:

• Kuunganishwa kwa kamati za awali za utendaji na kamati ya ufundi na kuwa Kamati moja ya Kiufundi

ya MKUKUTA . Kazi za kamati hii ni (a) kuhakikisha utendaji mzuri wa Mfumo wa Ufuatiliaji wa

MKUKUTA na uandaaji wa taarifa kutoka kwenye Makundi ya Kiufundi (b) kuarifu ngazi mbali

mbali za uwakilishi za serikali (yaani Kamati ya kiufundi ya Makatibu Wakuu wa Wizara, Baraza

3. Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA

19

la Mawaziri na Bunge) kuhusu hatua

zinazopigwa pamoja na masuala ya sera

yanayoibuka kutokana na mfumo wa

ufuatiliaji.

• Kubadilika kutoka Makundi manne ya

Kiufundi na kuwa Makundi matatu.

Makundi ya Kiufundi ya ‘utafiti na sensa’

na ‘ Taarifa za kawaida za kila siku za

kiutawala’ yameunganishwa kufuatia

kutambuliwa kwa mchango wa Ofisi ya

Takwimu ya Taifa katika kuhakikisha

kuwa takwimu rasmi zinakuwa bora. Kundi hilo hivi sasa linaitwa ‘Kundi la Kiufundi la Utafiti na

Takwimu za Kawaida za Kila Siku za kiutawala’. Makundi ya Kiufundi ya ‘Utafiti na Uchambuzi’ na

ya ‘Mawasiliano’ yamebakia kama yalivyokuwa, lakini ili kuleta urahisi zaidi, kundi la Mawasiliano

limebatizwa jina jipya la ‘Uenezaji, Uhamasishaji na Ushawishi’

• Kuimarishwa kwa uwianishaji na uhusiano baina ya (a) Matokeo ya ufuatiliaji katika ngazi ya kitaifa

na tathmini (b) Mipango mikakati ya serikali, Bajeti na mifumo ya utoaji ripoti.

Sekretarieti ya MKUKUTA

Sekretarieti ya MKUKUTA ina malengo ya (a) kuhakikisha utendaji mzuri wa jumla wa Mfumo wa

Ufuatiliaji wa MKUKUTA (b) Kuhudumia Kamati ya Kiufundi, Makundi ya Kiufundi, na Kamati

ya Ushauri wa Ufuatiliiaji, na (c) kutumia muundo wa MKUKUTA Kuboresha uhusiano na uratibu

baina ya michakato ya serikali ikiwemo ya upangaji wa mipango, utoaji wa taarifa na uandaaji wa bajeti

ya Wizara, Idara, Wakala wa Serikali na Serikali za Mitaa. Shughuli za hivi karibuni vya Sekretarieti ya

MKUKUTA ni pamoja na kufanya mapitio, uratibu na mashauriano.

Mapitio Mwaka 2005/06, Sekretarieti ya MKUKUTA ilifanya mapitio ya Mfumo wa awali wa Ufuatiliaji wa

Umaskini, na kuandaa Mfumo mpya wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA. Mchakato wa mapitio ulihusisha

mashauriano baina na miongoni mwa wadau wengi wanaohusika na mfumo wa ufuatiliaji.

Kama sehemu ya mchakato huu, Viashiria vya kitaifa pia vilifanyiwa mapitio ili kupanua wigo wake

kutoka kulenga sekta za kipaumbele kwenye Mkakati wa Kupunguza Umaskini, na kuzingatia nguzo

tatu za MKUKUTA. Mchakato huu ulihusisha zaidi mashauriano na Wizara, Idara na Wakala wa

serikali sambamba na wadau wengine. Orodha ya mwisho yenye viashiria 84 katika ngazi ya kitaifa kwa

kiasi kikubwa vinazingatia sekta mbali mbali na vinatambua kuwepo kwa viashiria vingi zaidi kwenye

nyingi ya Wizara, Idara na Wakala wa serikali. Changamoto iliyopo sasa ni kuimarisha usimamizi wa

mfumo wa taarifa za Wizara, Idara, Wakala wa serikali pamoja na Serikali za Mitaa kwa lengo la kuinua

ubora wa taarifa na upatikanaji wa mara kwa mara wa taarifa hizo.

Kisanduku 2: Hali ya Utekelezaji wa Mfumo wa

Ufuatiliaji wa MKUKUTA

Hali ya autekelezaji wa mfumo wa ufuatiliaji wa

MKUKUTA inahusu kipindi cha mwaka 2005/06

na 2006/07. hii ni kwasababu mwaka 2005/06

ulikuwa wa mpito ambapo mfumo wenyewe ulikuwa

ukifanyiwa mapitio; kwa hiyo mambo mengi

yaliyofanyika hayakutolewa taarifa.

20

Uratibu Sekretarieti ya MKUKUTA ilisimamia kupangwa kwa kazi za Makundi matatu ya Kiufundi pamoja

na Kamati ya Ufundi. Kalenda ya mwaka ya mikutano ya kamati zote pamoja na Makundi ya Kiufundi

ilipitishwa mapema mwaka 2006. Sekretarieti ilifanya kazi kwa karibu sana na Makundi ya Kiufundi

ili kuhakikisha kwamba (a) Mikutano ilifanyika, (b) mipango kazi ilikuwa na ubora unaokubalika na (c)

ripoti za utekelezaji zinaandaliwa kwa wakati. Zaidi ya haya, Sekretarieti ilihakikisha fedha kwa ajili ya

Makundi ya Kiufundi zinapatikana na kutumika vizuri.

Mafanikio mengine ni pamoja na kuimarishwa kwa mawasiliano na mitandao baina ya Sekretarieti

na wadau wengine. Jarida lilopo kwenye tovuti www.povertymonitoring.go.tz limesaidia kuimarisha

mawasiliano baina ya sekretarieti na wadau wengine .

Sekretarieti kwa ushirikiano na wizara mbali mbali, zimejumuishwa katika ajenda ya kuoanisha upangaji

wa mipango, upangaji wa bajeti na utoaji wa taarifa kwenye michakato mbali mbali ya serikali. Matokeo

muhimu ya uoanishaji ni pamoja na Mwongozo wa Upangaji wa Kimkakati wa Mipango ya Muda

wa Kati, Uandaaji wa Bajeti na Utoaji wa Taarifa. Mwongozo huu unafafanua uhusiano uliopo kati

ya MKUKUTA, Sera za Kisekta, Mipango Mikakati, Muundo wa Mipango ya Matumizi ya Muda wa

Kati, na kuzisaidia taasisi mbali mbali kupanga, kuandaa bajeti, kufanya ufuatiliaji, na kutoa taarifa kwa

kuzingatia MKUKUTA.

Matrix ya MKUKUTA ilifanyiwa mapitio ili kuimarisha usahihi wa upangaji mipango katika ngazi za

Wizara, Idara na Wakala wa serikali. Mfumo wa Bajeti wa Upangiliaji Fedha Kimkakati (SBAS) pia

ulifanyiwa mapitio ili kwenda sambamba na mfumo mpya uliobainishwa na mwongozo wa mipango,

pamoja na kujumuisha Mikakati ya Nguzo za MKUKUTA. Hii imezirahisishia Wizara, Idara, Wakala

na Serikali za Mitaa kuhusisha hatua mbali mbali zinazochukua na malengo ya MKUKUTA kupitia

mchakato wa uandaaaji wa bajeti.

Ili kuziwezesha taasisi kutoa ripoti za MKUKUTA, programu ya kompyuta ijulikanayo kama RIMKU,

yaani Ripoti ya Utekelezaji wa MKUKUTA ilitengenezwa. Juhudi zinafanyika kuiboresha na kuioanisha

programu hii na programu nyingine za kompyuta za serikali na hivyo kupunguza sana gharama

zinazohusiana na utoaji wa taarifa.

Shabaha nyingine muhimu inayoratibiwa na sekretarieti ni Zoezi la Kukadiria gharama za

MKUKUTA. Hatua muhimu za kuchukuliwa kwenye sekta za msingi za afya, elimu, maji, barabara,

kilimo, ardhi, nishati na nguvu kazi tayari zimefanyiwa ukadiriaji. Zoezi hili linatarajiwa kufanya

ukadiriaji wa gharama kwa kila mwaka katika kipindi cha zaidi ya miaka mitano.

MashaurianoSekretarieti ya MKUKUTA pia imekuwa ikiratibu maandalizi ya Muundo wa Hifadhi ya Jamii wa

sekta Mbalimbali. Mchakato wa kuandaa muundo huu ni shirikishi ambapo unahusisha wadau wengi

katika maeneo matatu tofauti ya kiutawala.

21

Mapendekezo ya rasimu yalitarajiwa kutumika kama rejea katika hatua ya mwisho ya mashauriano

yaliyopangwa kufanyika kati ya Oktoba na Novemba 2007.

Makundi Matatu ya Kiufundi

Makundi ya Kiufundi ni msingi wa uzalishaji wa taarifa, uchambuzi na mawasiliano ya taarifa kwa

wadau. Makundi haya ni kiungo kati ya utoaji taarifa za jumla wa Serikali za Mitaa na wizara, Idara na

Wakala, na uchambuzi wa matokeo unaotolewa kwenye nyaraka kuu kama vile Ripoti ya Umaskini na

Maendeleo ya Watu, Ripoti ya Hali Halisi na dondoo za Sera .

Kundi la Kiufundi la Utafiti na UchambuziKundi hili linawajibika na uchambuzi wa takwimu na kuratibu matokeo ya tafiti za kitaifa ambazo hutoa

taarifa kwa ajili ya watunga sera na wadau wengine.

Matunda makuu ya kundi hili kwa mwaka 2005 – 07 ni toleo la tatu la Ripoti ya Umaskini na Maendeleo

ya Watu, ambalo lilijumuisha dondoo/vidokezo vya Sera kwa lugha za Kiingereza na Kiswahili . Ripoti

hii ilitoa uchambuzi wa viashiria vikuu katika ngazi ya wilaya kwa mara ya kwanza. Hili liliwezekana

kupitia njia ya kuuchambua Umaskini kupitia taarifa za sensa ya kitaifa na utafiti wa bajeti ya kaya. Kwa

nyongeza, Ripoti ya Umaskini na Maendeleo ya Watu ilitoa picha ya Maendeleo kwa viashiria pamoja na

uchambuzi wa ukuaji wa Uchumi kwa maeneo ya vijijini.

Mwaka 2006, iliandaliwa ripoti ya kwanza ya hali halisi iliyopewa jina la Ripoti ya Halihalisi (2006) .

Ripoti hii iliandaliwa kwa kuzingatia viashiria vya MKUKUTA vilivyoboreshwa. Mafanikio mengine

ni pamoja na uratibu wa Utafiti wa Maoni ya Watu na midahalo ya wazi inayohusu sera ambapo wadau

wanapata fursa ya kujadili matokeo ya tafiti mbali mbali. Tafiti hizi mbali mbali zinafanyika kwa lengo la

kusaidia kuboresha mchakato wa utungaji sera nchini.

Kundi la Kiufundi la Utafiti na Takwimu za Kawaida za Kila Siku za Kiutawala Kundi hili linawajibika na ukusanyaji na uchambuzi wa takwimu zitokanazo na tafiti za kitaifa na

zitokanazo na utendaji wa kila siku wa serikali.

Mwaka 2005/06, makundi mawili ya kitaalam yaliunganishwa ili kuweka majukumu ya usimamizi wa

takwimu chini ya udhibiti wa Ofisi ya Takwimu ya Taifa kama Sekretarieti. Hivi sasa chini ya Kundi

hili kuna makundi madogo mawili: utafiti na takwimu za kawaida za kila siku. Ofisi ya Waziri Mkuu-

TAMISEMI ni mwenyekiti mwenza wa kundi dogo la takwimu za kila siku kutokana na ukweli kwamba

utawala wa serikali za Mitaa ndio unaozozalisha nyingi ya takwimu hizi.

Kundi Dogo la Takwimu za Kila Siku za KiutawalaKabla ya kuunganishwa na kundi la tafiti, majukumu ya kundi la takwimu za kila siku yalilenga katika

uelimishaji juu ya mfumo wa ufuatiliaji hususan kuhusu takwimu za kila siku. Mchakato huu ulihusisha

kuendesha warsha za kanda na kuendesha mashauriano ya kisekta. Matokeo ya michakato hii yalitumika

22

kuandaa Waraka wa Mkakati wa Mfumo wa Takwimu za Kila Siku. Majukumu mengine ya kundi hili

yaliahirishwa kusubiri uboreshwaji wa makundi ya Kiufundi uliofanyika mapema mwaka 2006.

Kundi la Kiufundi la MawasilianoKundi hili linaongozwa na Idara ya Kuondoa Umaskini na Uwezeshaji katika Wizara ya Fedha na Uchumi

Linajumusha Maafisa Habari kutoka Wizara Mama, Sekta binafsi, Wakala za Wabia wa Maendeleo na

wadau wengine wa sekta ya habari. Hii inachochea mijadala na midahalo miongoni mwa wadau na hivyo

kusaidia utekelezaji wa MKUKUTA.

Kundi hili linatumia mbinu mbali mbali katika kufikisha taarifa kwa wadau wengi. Usambazaji mpana

zaidi wa Mpango Mkuu wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA ulifanyika. Taarifa ya Hali halisi ya Utekelezaji

wa MKUKUTA (2006) ilisambazwa kwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

pamoja na wadau wengine. Machapisho mbali mbali yanayohusu Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA

yalisambazwa sana wakati wa Maadhimisho ya Miaka 45 ya Uhuru wa Tanganyika.

Ili kufikia wadau wengi zaidi, hususan maeneo ya vijijini, vipindi vya radio na televisheni viliandaliwa ili

kufikisha ujumbe wa MKUKUTA na Malengo ya Millenia ya Maendeleo. Shughuli nyingine ni pamoja

na kusambazwa kwa kalenda za MKUKUTA, na semina kwa Wabunge. Kundi hili pia lilishirikiana kwa

karibu na kundi la Utafiti na Uchambuzi katika kuandaa Utafiti wa Kukusanya Maoni ya Watu.

Uoanishaji wa Kazi

MKUKUTA unaozingatia Nguzo, mtazamo wa matokeo hutegemea mchango wa washiriki kutoka sekta

mbali mbali katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini. Maboresho katika baadhi ya michakato

inayoendelea (hususan Mapitio ya Matumizi ya Umma) hayana budi kufanyika ili kuhakikisha kuwa

juhudi za watu na wadau mbalimbali (hususan Wizara, Idara, Wakala na serikali za Mitaa) zinaratibiwa

na kuoanishwa. Mpangilio mzuri na kwa wakati muafaka wa shughuli na matukio ni muhimu sana.

Mwaka 2006/07 kiliundwa Kikundi Maalumu

Kinachohusisha Wizara mbali mbali kwa ajili

ya Mipango, Bajeti na Utoaji taarifa. Lengo la

kikundi hiki lilikuwa ni kuoanisha taratibu za

serikali za utoaji taarifa, ufuatiliaji na tathmini.

Mafanikio ya kuridhisha yamepatikana katika

ajenda ya uoanishaji wa michakato ya mipango,

bajeti, ufuatiliaji na utoaji taarifa na katika

kuandaa mifumo ya mijadala na midahalo. Mwongozo wa lugha rahisi uliandaliwa na serikali mwaka

2005. Mwongozo huu unaitwa Mwongozo wa Upangaji wa Kimkakati wa Mipango ya Muda wa Kati,

Uandaaji wa Bajeti na Utoaji wa Taarifa. Taratibu za upangaji wa mipango, kuandaa bajeti, kufanya

ufuatiliaji na kutoa taarifa zimebainishwa kwa kina kwenye chapisho hili.

Kisanduku 3: Kikundi Maalumu cha Maofisa

kutoka Wizara mbali mbali cha Mipango, Bajeti

na Taarifa Kinahusisha watumishi kutoka:

• Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na

Serikali za Mitaa

• Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa

Umma.

• Wizara ya Fedha na Uchumi

23

Kikundi hiki maalumu pia kimeandaa mahitaji ya utendaji katika utoaji ripoti ambayo yamejumuishwa

kwenye Miongozo ya Mipango na Bajeti ya mwaka 2007/08. Mahitaji hayo yanabainisha mlolongo wa

ripoti zilizochambuliwa zaidi, na zinazoeleweka vizuri zaidi na watumiaji, na zisizokinzana na mfumo

wa utoaji taarifa wa MKUKUTA na mifumo mingine ya kitaifa.

Ajenda ya uoanishaji na upangiliaji ina msukumo wa aina tatu:

Kwanza kuandaa na kutumia muundo mmoja kwa ajili ya malipo, mahesabu, utoaji taarifa na tathmini ya

utendaji. Muundo huu unazingatia mifumo iliyopo ya serikali. Lengo ni kuboresha uwazi na kutabirika

kwa misaada kutoka kwa wadau wa maendeleo. Pia mfumo unalenga kuboresha uhakika wa kiwango na

muda wa upatikanaji wa mchango wa wafadhili

Pili ni kushughulikia suala la kukosekana kwa muunganiko baina ya Mipango ya Maendeleo ya Kisekta

na MKUKUTA. Hii inamaanisha kwamba Mipango na Mikakati ya Maendeleo ya Kisekta haina budi

kufanyiwa mapitio ili kuhakikisha (a) inaendana na MKUKUTA, na (b) kunakuwepo muunganiko wa

kimkakati wa upangiliaji wa raslimali na MKUKUTA.

Tatu ni kuoanisha michakato ya kitaifa hususan Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA, Mapitio ya

Matumizi ya Umma, na Muundo wa Mipango ya Matumizi ya Muda wa Kati/Miongozo ya Bajeti. Vile

vile ni muhimu kuhusisha Misaada ya Bajeti, Mfuko wa Kusaidia Upunguzaji wa Umaskini, na Juhudi za

Sekta binafsi (PSI). hii haina budi kufanywa kuwa michakato ya kitaifa badala ya sasa inavyojitegemea

na kuonekana kama michakato midogo.

Izingatiwe pia kwamba ili kuwezesha ubadilishanaji mpana zaidi wa taarifa baina na miongoni mwa

nguzo za MKUKUTA, hapana budi kuandaliwa muundo mpya wa mijadala na midahalo. Muundo

huu mpya utaleta pamoja michakato iliyochini ya Misaada ya Bajeti, Mapitio ya Matumizi ya Umma na

MKUKUTA. Sekretarieti mbali mbali zimekuwa zikishirikiana kwa karibu katika kufanikisha ajenda

ya uoanishaji. Matukio muhimu kama ya mikutano ya mashauri ya Mapito ya Matumizi ya Umma na

Wiki ya Sera ya Umaskini hivi sasa yanapangwa na kuandaliwa kwa pamoja.

Shughuli Zinazoendelea

Mwongozo wa Upangaji wa Kimkakati wa Mipango ya Muda wa Kati, Uandaaji wa Bajeti na Utoaji

wa Taarifa unabainisha wazi wazi kazi ya utoaji taarifa za MKUKUTA. Mwongozo huu unaziweka

pamoja taarifa binafsi za utendaji kutoka kwenye Wizara, Idara, Wakala na Serikali za Mitaa huku

zikitoshelezwa na matokeo ya tafiti zinazojitegemea na kazi za uchambuzi mbali mbali. Utoaji wa ripoti

unapaswa kufanywa kwa (a) Ripoti ya Utekelezaji wa MKUKUTA, yaani MAIR itolewayo kila mwaka

(b) Ripoti ya Umaskini na Maendeleo ya Binadamu na Ripoti ya Hali Halisi itolewayo kila baada ya

mwaka mmoja.

Ofisi za serikali zinatoa taarifa za utekelezaji za robo mwaka. Taarifa hizi sasa zitahusishwa na matokeo

ya kila nguzo ya MKUKUTA kupitia Mfumo Mpya wa Utoaji Ripoti za Utekelezaji MKUKUTA

24

(RIMKU), na pia kupitia Mapitio ya Kisekta, Mapitio ya Matumizi ya Umma na Taarifa za ukaguzi wa

mahesabu ya Wizara, Idara, Wakala na serikali za Mitaa.

Serikali imedhamiria kuoanisha mifumo mbali mbali ya utoaji taarifa ili kuimarisha uhusisano wa jumla

na MKUKUTA na baina ya Mipango, Bajeti na mifumo ya utoaji taarifa.

Kuna utafiti unaojitegemea unaoendelea kuhusu Ufuatiliaji na Tathmini kwenye wizara, idara, na wakala

27. Pamoja na mambo mengine utafiti huu (a) utatoa mwanga juu ya hali ya ufuatiliaji na tathmini

kwenye wizara, idara na wakala kuhusiana na upatikanaji wa vitendea kazi na watumishi wenye ujuzi

unaohitajika (b) utawasaidia watoa maamuzi juu ya namna bora ya kuandaa mfumo wa kisheria wa

ufuatiliaji na tathmini.

Muundo mpya wa mijadala umebuniwa ili kuwezesha mawasiliano miongoni mwa wadau wa nguzo ya

MKUKUTA inayohusika. Hii inaleta pamoja michakato iliyochini ya Misaada ya Bajeti, Mapitio ya

Matumizi ya Umma na MKUKUTA. Sekretarieti tatu zinashirikiana kwa karibu katika kufanikisha

ajenda ya uoanishaji. Matukio muhimu kama ya mikutano ya mashauri ya Mapitio ya Matumizi ya

Umma na Wiki ya Sera ya Umaskini hivi sasa yanapangwa na kuandaliwa kwa pamoja.

Changamoto na Mambo Tuliyojifunza

• Mabadiliko kutoka mfumo wa awali wa Ufuatiliaji wa Umaskini kwenda mfumo mpya wa Ufuatiliaji

wa MKUKUTA yamepanua ajenda ya ufuatiliaji katika (a) ukusanyaji wa taarifa, uchambuzi na

usambazaji wa taarifa (b) raslimali zinazohitajika (miundombinu, fedha na watumishi) (c) usimamizi

wa mfumo.

• Kupanuka kwa viashiria kutoka 84 vya awali kunamaanisha kwamba kazi kubwa na yenye kupangiliwa

vizuri zaidi inapaswa kufanyika.

• Mfumo wa MKUKUTA unaozingatia matokeo unahusisha watu na taasisi nyingi zaidi kuliko

Mkakati wa awali wa Upunguzaji Umaskini. Kwa hali hiyo; unahitajika (a) mfumo madhubuti zaidi

wa Ufuatiliaji na Utoaji taarifa (b) Muunganiko bayana kati ya serikali na wadau wengine muhimu, na

(c) Uimarishaji wa michakato ya uwajibikaji.

• Muunganiko kati ya Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA na shughuli nyingine za ufuatiliaji

zinazofanywa na serikali na wadau wengine bado ni dhaifu. Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA

haujapata mafanikio makubwa katika kuimarisha mifumo ya takwimu za kila siku na tafiti mbali

mbali katika ngazi ya wizara, idara, wakala na serikali za Mitaa. Bado kuna tofauti kati ya viashiria

vinavyotumika kwa shughuli za MKUKUTA, na pale vinapokuwepo, katika muundo wa utendaji wa

serikali.

• Pamoja na mafanikio hayo makubwa ya Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA, bado fedha za

utekelezaji wake unategemea msaada kutoka kwa Wabia wa Maendeleo kupitia mfuko wa pamoja wa

fedha. Hali hii inatishia uendelevu wa mfumo huu.

• Makundi Mahsusi ya Kitaalam yaliundwa upya Aprili 2006. Mafunzo ya utambulisho kwa wajumbe

wa makundi haya yalipangwa na kalenda ya mwaka ya vikao vya makundi haya iliandaliwa na

25

kukubaliwa. Pamoja na haya yote, vikao vinavyopangwa vimekosa mahudhurio ya kuridhisha na hii

imeathiri utekelezaji wa shughuli zilizopangwa. Moja ya sababu za mahudhurio hafifu ni kwamba

kazi za makundi hayo hazikujumuishwa kwenye kazi za kawaida za taasisi wanakotoka wajumbe.

Ilibainika pia kwamba wajumbe wengi wa makundi ya Kiufundi wanaona kazi yao kama ya ushauri

zaidi na siyo utendaji; wanadhani kuwa Sekretarieti itafanya kazi zote. Hali hii imezalisha matarajio

ambayo hayawezi kufikiwa. Inapendekezwa kuwa wajumbe wa makundi haya washirikishwe katika

utendaji wa baadhi ya kazi badala ya kuwa washauri.

Hatua za Kuchukua

• Juhudi zitaendelea kufanyika kuoanisha mfumo wa Ufuatiliaji na tathmini kwenye taasisi za serikali

ili kuhakikisha utoaji taarifa wa kiwango cha juu na utoaji maamuzi ulio bora zaidi

• Kazi za Ufuatiliaji na Tathmini kwenye wizara, idara, wakala wa serikali na serikali za Mitaa

zitabainishwa ili kuzioanisha na Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA. Hii itahusisha uandaaji wa

sera ya Ufuatiliaji na Tathmini sanjari na ujengaji uwezo katika ngazi zote.

• Utafiti umefanyika ili kuondoa Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA kutoka kwenye utegemezi

wa Mfuko wa Ufadhili na badala yake kuujumlisha kwenye Bajeti ya kitaifa. Serikali itatekeleza

mapendekezo ya utafiti huo hatua kwa hatua.

• Kamati maalum ya pamoja baina ya Serikali na Wabia wa Maendeleo imeundwa ili kubaini masuala

muhimu ikiwa ni pamoja na ugharamiaji na uimarishaji wa Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA.

Masuala haya yatashughulikiwa katika kipindi cha mpito ambacho kinaisha mwaka 2012.

26

MKUKUTA unapaswa kugharamiwa na hauna budi kuonekana kwenye bajeti za wadau ili

kuhakikisha kuwa utoaji wa fedha unatabirika na kufanyika kwa wakati. Kwenye sura hii

kwanza tunaangalia (a) namna fedha zinavyopatikana, kupangiliwa kwa ajili ya nguzo mbali

mbali za MKUKUTA (b) jinsi MKUKUTA unavyopatana na bajeti kuu ya kitaifa. Hii inatupeleka

kwenye baadhi ya mawazo kuhusu jinsi michakato ya ugharamiaji na uandaaji bajeti inavyoweza

kuboreshwa. Kisha tunaangalia baadhi ya changamoto kwenye taratibu za kutoa taarifa za bajeti. Sura

hii inahitimishwa kwa kuufanyia mapitio kwa ufupi Mkakati wa pamoja wa Misaada kwa Tanzania na

Sera ya mishahara ya utumishi wa umma.

Utafutaji na Upangiliaji wa Fedha

MKUKUTA unatekelezwa na kugharamiwa na serikali pamoja na wadau wengine nje ya serikali. Si kazi

rahisi kupata taarifa kuhusu michango ya wadau wasiokuwa wa kiserikali, kwa hiyo ripoti hii inajikita

zaidi kwenye hatua zilizochuliwa na serikali.

Mfumo wa bajeti ya Mkakati wa awali wa Upunguzaji Umaskini ulitenga fedha kwa sekta chache tu

za kipaumbele. Bali Mfumo mpya wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA unatambua kwamba wizara, idara,

wakala wa serikali na serikali za Mitaa kwenye sekta zote zinachangia katika juhudi za kukuza uchumi

na kupunguza umaskini. Hali hii imefanya mfumo huu mpya kuwa na mwelekeo wa kutegemea

matokeo ambao unachangiwa na wadau wengi na imechochea hatua za kuwepo kwa juhudi nyingine

zinazokamilishana kama vile Mkakati wa pamoja wa misaada kwa Tanzania. Hii inalenga kufikia

malengo ya MKUKUTA kwa gharama nafuu zaidi.

Kumekuwepo na Maendeleo ya kuridhisha kupitia Mkakati wa pamoja wa Misaada kwa Tanzania

katika kuoanisha misaada ya wahisani na Kupunguza gharama. Michakato ya Kusaidia Bajeti ya jumla

na mapitio ya matumizi ya umma imesaidia kuratibu juhudi za serikali na wadau wa maendeleo katika

kuunga mkono upunguzaji umaskini.

Miongoni mwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa misaada ya Wabia wa

Maendeleo kwenye bajeti ya kitaifa , na kuongezeka kwa ukusanyaji wa mapato . Ongezeko hili linatokana

na (a) maboresho makubwa yaliyofanywa katika taasisi zinazokusanya mapato ya ndani (b) kuboreka

kwa usimamizi wa fedha. Hali hii imeongeza imani ya Wabia wa Maendeleo kwa Tanzania.

Serikali inaboresha mchakato wa usimamizi wa bajeti (uandaaji na utekelezaji wa bajeti). Kila mwaka

uhusiano baina ya vipaumbele vya MKUKUTA na migawo ya fedha inaboreshwa na kuimarishwa.

Matumizi yanapangiliwa kufuatana na vipaumbele vya nguzo za MKUKUTA. Hii inafanyika kupitia

Mfumo wa Bajeti wa Upangiliaji Fedha Kimkakati (SBAS) katika ngazi ya serikali kuu na kupitia

programu dada ya kompyuta ya Upangaji Mipango na utoaji Ripoti (PlanRep) kwa serikali za Mitaa.

Mfumo wa Bajeti wa Upangiliaji Fedha Kimkakati uilitumika kwenye Sekretarieti za Mikoa wakati wa

4. Mipango ya Ugharamiaji

27

maandalizi ya bajeti ya mwaka 2006/07 . Mifumo hii kwa pamoja inawezesha utengaji wa raslimali kwa

kuzingatia MKUKUTA kwa serikali nzima.

Hatua hii pia imesaidiwa na zoezi la ukadiriaji wa gharama za MKUKUTA na Malengo ya Millenia

ya Maendeleo. Matokeo ya mwanzo ya zoezi hili pamoja na takwimu zinazotokana na nguzo za

MKUKUTA kwa ajili ya mashauriano ya Mapitio ya Matumizi ya Umma, yamesaidia katika kuamua

maeneo ya kutengewa raslimali.

Kukamilika kwa zoezi la ukadiriaji wa gharama za MKUKUTA kutaimarisha juhudi za serikali katika

kuweka vipaumbele na kuunganisha utengaji wa raslimali na MKUKUTA. Sekta nane ambazo tayari

zimekamilisha ukadiriaji wa gharama ni pamoja na afya, elimu, maji, barabara, kilimo, ardhi, kazi na

nishati.

Hata hivyo, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, bado changamoto kadhaa zimebakia:

• Kuna umuhimu wa kupima na kujumuisha mchango wa Wadau Wasiokuwa wa Kiserikali kwenye

juhudi za Kupunguza Umaskini. Raslimali za umma zinaweza kutumika vizuri zaidi kwa kujumuisha

hatua zinazochukuliwa na sekta binafsi na asasi za kiraia kwenye mchakato wa uandaaji wa mipango.

Wadau mbali mbali kama vile sekta binafsi, asasi za kiraia, na Wabia wa Maendeleo watahamasishwa

kushirikiana taarifa kuhusu harakati zao za Kupunguza Umaskini wakati wa kuandaa Ripoti ya

Mwaka ya Utekelezaji MKUKUTA itakayofuata. Hii itakuwa hatua ya mwanzo ya ujumuishaji kamili

wa taarifa hizi kwenye mipango ya sekta mbali mbali.

28

• Hakuna raslimali za kutosheleza utekelezaji wa mambo yote yanayopaswa kufanyika. Ukusanyaji

wa raslimali ni suala muhimu sana katika mchakato wa upunguzaji Umaskini. Serikali inapaswa

(a) kutafuta njia za kuongeza mapato ya ndani yatokanayo na kodi na yasiyotokana na kodi (b)

kuwashawishi wadau wa Maendeleo ili waongeze mchango wao kulingana na ahadi zao za kimataifa na

za ndani ya nchi (c) kuongeza kasi ya Kukuza Ubia baina ya Serikali na Sekta binafsi (d) kuhakikisha

kwamba vyanzo vipya vya mapato vinabuniwa.

Ipo haja ya:

• Kuimarisha kutabirika kwa upatikanaji wa raslimali kutoka nje ya nchi

• Kutoa miongozo kuhusiana na vikwazo vya raslimali – hii itapunguza, kama si kuondoa kabisa

maombi yasiyotekelezeka kutoka wizara, idara na wakala wa serikali.

• Kutoa miongozo juu ya kiwango cha maelezo ya kina kinachotakiwa kutolewa na wizara, idara na

wakala wa serikali kwenye mapendekezo ya awali ya bajeti – hii itaepusha kutolewa kwa maelezo ya

kina sana ambayo mara nyingi hukosa muundo wa kimkakati.

• Kuboresha (a) uhusiano baina ya bajeti na nyaraka za programu mbali mbali, na (b) uratibu na

mamlaka kati ya maofisa wa bajeti na programu ndani ya wizara, idara na wakala husika.

MKUKUTA na Bajeti ya Taifa

MKUKUTA unatambua kwamba sekta

zote na wizara, idara na wakala wa serikali

zinachangia katika mchakato wa Kukuza

uchumi na kupunguza Umaskini. Kwa

vile Ukuaji wa Uchumi na Upunguzaji wa

Umaskini vimekuwa nguzo muhimu katika

upangaji wa mipango ya serikali, bajeti

nzima ya serikali inaweza kuelezwa kwamba

ni kwa ajili ya utekelezaji wa MKUKUTA.

Hata hivyo kwa makusudi ya uchambuzi

na upangaji mipango, ni matumizi yale tu

yanayohusiana moja kwa moja na mikakati

ya nguzo za MKUKUTA yanayoainishwa

kuwa matumizi ya MKUKUTA.

Ndani ya Mfumo wa Bajeti wa Upangiliaji Fedha Kimkakati, bajeti iliyopitishwa kutekeleza MKUKUTA

mwaka 2006/07 ilikuwa ni asilimia 48 ya bajeti yote. Asilimia 52 iliyobakia ilikuwa kwa ajili ya miradi na

programu zisizo na uhusiano wa moja kwa moja na MKUKUTA. Mgawanyo wa bajeti iliyotengwa kwa

ajili ya MKUKUTA ulikuwa asilimia 46 kwa nguzo ya kwanza, asilimia 36 nguzo ya pili, na asilimia 18

kwa nguzo ya tatu. mgawanyo huu unashabihiana na lengo la kukuza uchumi na kuongeza kipato cha

watu maskini zaidi.

Kisanduku 4: Machaguo ya Sekta

Matumizi ya kijamii (mfano kwenye elimu na afya)

yanaweza kutazamwa kama uwekezaji kwenye raslimali

watu ambayo ni ya msingi sana katika kuchochea

ukuaji wa Uchumi. Hata hivyo, mapato yanayotokana

na uwekezaji huo siyo ya moja kwa moja na ni ya muda

mrefu. Uchaguzi wa kimkakati hauna budi kufanyika

baina kuelekeza raslimali kwenye sekta za kijamii na

sekta za kiuchumi (mfano fedha na kilimo) ambazo

matunda yake ni ya moja kwa moja na kwa muda

mfupi.

29

Serikali inaendelea kuandaa matumizi halisi kwa mwaka 2006/07. Uchambuzi wa awali unaonyesha

kwamba ugharamiaji wa shughuli za MKUKUTA ulikuwa wa kutosheleza licha ya kuwepo mchepuko

kutoka mafungu yaliyotengwa kwenye bajeti

ya awali. Mchepuko huu ulisababishwa kwa

kiasi kikubwa na serikali kulazimika kupanga

upya mafungu ya fedha ili kukabiliana na

tatizo la umeme katika nusu ya kwanza

ya mwaka wa fedha wa 2o06/07, uhaba

wa chakula, kupanda kwa bei ya mafuta,

kuongezeka kwa riba ya deni la ndani.

Kwa kipindi cha muda wa kati, mkazo utabaki katika kuweka vipaumbele na kutekeleza shughuli za

MKUKUTA zenye matokeo mengi moja baada ya nyingine. Ili kudumisha uthabiti katika vigezo

muhimu vya kiuchumi, bajeti itatenga raslimali zaidi kwa ajili ya shughuli zenye kukuza uchumi wenye

kujali watu maskini zaidi.

Kwa hiyo tunaweza kutegemea bajeti kubwa zaidi kwa ajili ya maendeleo ya miundombinu kwa uwiano

wa ongezeko kwenye huduma za jamii. Tunaweza pia kutarajia mikakati yenye kulenga kupunguza

tofauti baina ya mikoa na yenye kujumuisha masuala mtambuka.

Kuboresha Michakato ya Bajeti na Ugharamiaji Tunahitaji Mkakati mzuri wa kugharamia shughuli za MKUKUTA. Ni muhimu kutenga na kutoa

fedha kwa wakati. Ili kufanikisha hili michakato ya utoaji wa mafungu ya fedha haina budi kuboreshwa.

Hivi sasa shabaha za MKUKUTA zinaweza kufikiwa kwa vile raslimali za kutosha zinatolewa na ipo

mifumo ya kudhibiti ufujaji wa raslimali hizo. Kwa ajili ya shabaha nyingine, kama tulivyoona hapo

juu, serikali itachukua hatua kukusanya raslimali zaidi; na hizi zitatumika kwa busara zaidi kwa ajili ya

malengo yaliyokusudiwa.

Kiwango cha mapato kwa mwaka 2006/07 kiliendana na shabaha za bajeti kwa kiasi kikubwa. Ukusanyaji

mzuri zaidi wa mapato ya ndani ulifanyika sambamba na mambo mengine, kutosheleza utekelezaji wa

hatua za kodi kwa mwaka wa fedha 2006/07.

Kiwango cha matumizi kwa mwaka 2006/07 vile vile kiliendana na shabaha za bajeti. Jumla ya

matumizi kwa mwaka 2006/07 yalikuwa sh. 4,761,700 milioni sawa na asilimia 98 ya makadirio ya

sh. 4,850,588 million, ikilinganishwa na asilimia 94.4 kwa mwaka 2005/06. jumla ya matumizi

kwa uwiano wa pato la ndani lilipungua kutoka asilimia 26.1 mwaka 2005/06, hadi asilimia 25.5

mwaka 2006/07, lakini hii ilibaki kuwa ndani ya mfiko wa shabaha za MKUKUTA. Sababu kubwa

za kushuka huku ni upungufu katika mbinu za kupima msaada wa wahisani uliotolewa moja kwa

moja kwenye miradi.

Kwa vile Ukuaji wa Uchumi na Upunguzaji wa

Umaskini vimekuwa nguzo muhimu katika upangaji

wa mipango ya serikali, bajeti nzima ya serikali

inaweza kuelezwa kwamba ni kwa ajili ya utekelezaji

wa MKUKUTA.

- MAIR (2007)

30

Bado kuna matatizo katika namna mafungu ya fedha yanavyotolewa kwenda kwenye wizara, idara na

wakala wa serikali kwa mwaka. Mpangilio wa utoaji mafungu unatofautiana kati ya wizara na wizara,

kutegemeana na mahitaji na upatikanaji wa raslimali.

Wizara ya fedha imekuwa ikitoa fedha kwenda wizara, idara na wakala wa serikali kila mwezi kwa

kutegemea (a) mpango wa mtiririko wa fedha wa wizara, idara na wakala wa serikali (b) fedha ziliopo

Hazina. Kulikuwa na utoaji mdogo wa fedha ikilinganishwa na makadirio ya mtiririko wa fedha katika

robo ya kwanza ya mwaka 2006/07. Hii ilisababishwa na (a) mapungufu ya Wizara, Idara na Wakala

wa Serikali katika kupanga mtiririko wa

fedha, na (b) uingiaji hafifu wa raslimali

kwenda hazina. Sehemu kubwa ya Bajeti

ya Maendeleo inagharamiwa na Wabia wa

Maendeleo. Makadirio yanaidhinishwa

mapema lakini changamoto inabaki katika

kukabili ucheleweshaji wa na kutotabirika

kwa utoaji wa fedha hizo (tazama kisanduku 5)

Changamoto ya kukadiria uhusiano baina

ya matumizi ya fedha na matokeo halisi

katika ngazi ya jamii. Changamoto hii

inazidi kuwa kubwa inapotokea kuwa

zaidi ya mwaka mmoja unahitajika mpaka

matokeo kuanza kuonekana. Hili ni tatizo

kubwa kwa viashiria vingi vya MKUKUTA

na halina budi kuzingatiwa.

Njia za Kuripoti BajetiUtoaji wa ripoti za bajeti na za uwazi vimekuwa vikiboreka kwa muda sasa nchini Tanzania.

Bajeti ya taifa huzingatia viwango vya Kimataifa vya Takwimu za za Fedha za Serikali. Mahitaji ya utoaji

taarifa yaliwekwa kwenye Sheria ya Fedha za Umma ya mwaka 2001. hii husaidiwa na miongozo ya

taratibu za mahesabu ya fedha za serikali.

MKUKUTA hutumia Mfumo wa Bajeti wa Upangiliaji Fedha Kimkakati (SBAS) katika kubainisha

namna unavyotumia raslimali. Hii inamaanisha kwamba takwimu za bajeti za MKUKUTA zinapaswa

kubadilishwa ili kuendana na mfumo wa kimataifa wa Takwimu za Fedha za Serikali. Ili kurahisisha

mambo, serikali inaandaa mfumo wa MKUKUTA wa uchambuzi wa matokeo ya utekelezaji wa bajeti.

Hii itaripotiwa kupitia Mapitio ya Utekelezaji wa Bajeti .

Hivi sasa uhusiano wa sera na utekelezaji wa bajeti hupimwa kwa (a) kulinganisha migawo ya SBAS na

matumizi halisi (b) kwa kuangalia matokeo yake kwenye umaskini kwa kutumia Mfumo wa Ufuatiliaji

wa MKUKUTA. Njia nyingine za kuripoti zinazotumika ni pamoja na:

Kisanduku 5: Utolewaji Usio wa Uhakika wa

Mafungu ya Fedha

Mwaka 2005/06 Wizara ya Kilimo, na Usalama wa

Chakula na Ushirika ilipokea asilimia 47 tu ya bajeti

yote ya Maendeleo, asilimia 12 kati ya hiyo ilitolewa

kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka.

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa upande

mwingine ilipokea asilimia 32 kwa mwaka huo huo,

asilimia 22 kati ya kiasi hicho kilikuwa kwa kipindi

cha nusu ya kwanza ya mwaka.

Hata hivyo Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii

mafungu yaliyopokelewa yalikuwa asilimia 81 ya bajeti

yote iliyoidhinishwa kwa mwaka huo na asilimia43

ilitolewa katika nusu ya kwanza ya mwaka.

31

• Ripoti ya utekelezaji ya robo mwaka inayochapishwa kwenye tovuti ya Wizara ya Fedha . Ripoti hizi

hutoa muundo wa jumla wa kifedha.

• Wizara pia hutoa ripoti za kila mwezi kwa kutumia Mfumo wa jumuishi wa Usimamizi wa Fedha.

Ripoti hizi huwa na taarifa kuhusu fedha zilizoahidiwa na kutolewa.

Pamoja na taarifa hizi kutolewa kwa wakati, kufikika, kueleweka na kuwa zenye manufaa, bado hazina

budi kurekebishwa ili kutoa mtazamo wa programu na muundo wa MKUKUTA.

Mapana ya Ripoti ya BajetiMapitio ya Utekelezaji wa Bajeti yanahusisha fedha za serikali kwa misingi ya fedha taslimu, lakini

(a) hayahusishi fedha zinazopelekwa na Wabia wa Maendeleo moja kwa moja kwenye miradi (b)

yanachukulia fedha zinazopelekwa kwenye serikali za Mitaa kama matumizi. Mfumo wa sasa unashindwa

kushughulikia ugumu uliopo katika ngazi ya wilaya kutokana na kuwepo vyanzo mbali mbali vya

ugharamiaji wa programu katika ngazi hiyo.

Ugumu huu kwenye mchakato wa bajeti unahitaji marekebisho katika mtiririko wa fedha na kuhakikisha

kuwa mfumo unabaki kuwa wa uwazi. Kwa hiyo, katika mwaka unaofuata wa utekelezaji wa MKUKUTA,

mifumo ya uainishaji na utoaji taarifa itaanzishwa ili kurahisisha ukusanyaji na utoaji taarifa jumuishi

za fedha.

Ili kufanikisha mchakato huu, wadau mbali mbali hususan wabia wa maendeleo na taasisi zinazonufaika

zitapaswa kuanza kutumia mifumo jumuishi ya ugharamiaji na utoaji wa taarifa.

Serikali inatambua umuhimu wa kuripoti matumizi ya MKUKUTA kila wakati. Kwa ushirikiano wa

karibu na wadau wengine, serikali inaandaa mwongozo utakaotumika na Wizara, Idara na Wakala wa

Serikali kwa kutoa ripoti za (a) MKUKUTA (b) uhusiano wa Mfumo Jumuishi wa Usimamizi wa Fedha

na Mfumo wa Bajeti wa upangiliaji fedha Kimkakati.

Changamoto kubwa ni kupanga na kusimamia utoaji ripoti juu ya nguzo za MKUKUTA pamoja na

shabaha zake. Takwimu zinapatikana kwenye mfumo jumuishi wa usimamizi wa fedha, lakini kuzihusisha

takwimu hizi na Mfumo wa Bajeti wa upangiliaji fedha Kimkakati unabaki kuwa changamoto. Serikali

inaandaa njia itakayo: (a) wezesha ubadilishanaji wa taarifa wenye ufanisi zaidi baina ya zana, na (b)

uchambuzi wa matokeo ya utekelezaji wa bajeti kufanyika kwa wakati.

Sera Nyingine Zinazohusiana na BajetiSerikali ya Tanzania ilianza kutumia Mkakati wa Pamoja wa Misaada ( JAST) mwezi Desemba 2006.

kwa kuzingatia Mkakati huu, Wabia wa Maendeleo wanaohusika kwa kushirikiana kwa karibu na

serikali wameandaa Mwongozo wa Pamoja wa uandaaji wa Programu ambao umefungamana kikamilifu

na malengo ya MKUKUTA.

32

Kwa kuzingatia Mkakati wa Pamoja wa

Misaada kwa Tanzania na Mwongozo wa

Pamoja wa Uandaaji wa Programu, serikali

itashughulikia tatizo la kutotabirika kwa

misaada kutoka nje ya nchi. Itafanya hili

kwa kufanya uchambuzi wa pamoja na

Wabia wa Maendeleo kuhusu njia mbadala

za matumizi na fedha kutoka nje ya nchi.

Hii italeta maafikiano ya wazi juu mkakati

wa muda wa kati na mipango ya matumizi

kabla ya mzunguko wa bajeti ya 2008/09

. hatua hii itachochea kuongezeka kwa

misaada na hivyo kuharakisha ukuaji wa

uchumi na kupungua kwa umaskini.

Tume ya Rais ya Mishahara ya Watumishi wa Umma ilikabidhi ripoti yake Desemba 2006. hii ililenga

kwenye sera ya serikali ya muda wa kati kuhusu kiwango cha ajira ya serikali na uhusiano wake na

bajeti. Serikali inayapitia mapendekezo ya tume kwa kulinganisha na vipaumbele vya utekelezaji wa

MKUKUTA na uwezekano wa kuyatekeleza kwa kuzingatia hali halisi ya bajeti. Matokeo yake itakuwa

ni kutungwa kwa sera ya muda wa kati kuhusu mishahara ya watumishi wa Umma.

Kisanduku 6: Mkakati wa Pamoja wa Misaada kwa

Tanzania (JAST)

JAST ni matokeo ya mashauriano yenye wigo mpana

yaliyoongozwa na serikali kati ya wabia wa maendeleo

na taasisi zisizo za kiserikali. Mkakati huu una

akisi nafasi ya serikali katika kuoanisha msaada wa

wahisani. Malengo makuu ya JAST ni (a) kupunguza

zaidi gharama za uhamishaji fedha (b) kukuza umiliki

wa kitaifa na nafasi ya serikali katika kuongoza ajenda

ya maendeleo.

33

Kwa ufupi, hatua zinazopendekezwa na MAIR zinalenga katika mchakato. Wito wa MAIR ni

juu ya kuwepo kwa mawasiliano bora zaidi yatakayowezesha kuwepo kwa uratibu ulio mzuri

zaidi. Hali hii itathibitisha uhalali wa ongezeko la raslimali kwa ajili ya MKUKUTA.

• Mawasiliano bora zaidi yanahitaji mfumo bora wa ubadilishanaji taarifa na kuwepo kwa mijadala

miongoni na baina ya wadau. Pia inamaanisha kuwepo kwa ushiriki bora zaidi wa asasi zisizo za

kiserikali katika hatua mbali mbali za mchakato wa maendeleo.

• Uratibu mzuri zaidi wa kazi utatokana na kuwepo kwa mawasiliano mazuri zaidi. Kazi iliyo mbele ni

kuhakikisha kuwa wadau wote wanafanya kazi kwa kulingana na muundo wa MKUKUTA wa bajeti,

mipango, ufuatiliaji na utoaji wa taarifa. Mchakato huu utatekelezwa na makundi madhubuti ya kila

nguzo ya MKUKUTA na yale yanayojumuisha wadau kutoka nguzo zote tatu katika ngazi mbalimbali

nchini. Hali kadhalika, mifumo mbali mbali ya takwimu za kompyuta itasaidia kuwezesha mchakato

huu. Kazi muhimu ya usimamizi itafanywa na Kamati maalumu ya Mipango, Bajeti, na Utoaji Taarifa

inayoundwa na wajumbe kutoka Wizara mbali mbali.

• Kuongeza raslimali kwa ajili ya MKUKUTA kutahalalishwa na kuhimizwa na kuwepo kwa uratibu

na ulinganifu mzuri zaidi wa mfumo wa utendaji kazi. Michango mingi ya Wabia wa Maendeleo

itaweza kushabihiana na taratibu za sasa za bajeti ya serikali.Ushiriki wa sekta binafsi utahimizwa

zaidi (hususan kupitia Ubia baina ya Sekta ya Umma na sekta Binafsi)

Sehemu fupi fupi zifuatazo zinatazama hatua zilizopendekezwa kuchukuliwa kwa ajili ya nguzo tatu

za MKUKUTA na kisha masuala ya ugharamiaji, ufuatiliaji na tathmini. Sehemu Hii inajaribu kujazia

nyama kwenye mifupa hapo juu.

5. Muhtasari wa Masuala Makuu na Hatua za Kuchukua

34

Nguzo ya Kwanza: Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini

Hatua za kuchukuliwa katika nguzo hii ni pamoja na:

• Miundombinu ya kiuchumi inaweza kuwa kigezo muhimu zaidi katika kuchochea ukuaji wa uchumi.

Inapunguza gharama za uzalishaji, hususan kwa wazalishaji wadogo na wa kati na wasindikaji wa

bidhaa za kilimo. Katika kuongeza misaada, uwekezaji katika miundombinu huchukua nafasi kubwa

zaidi.

• Kuna umuhimu mkubwa wa kuongeza uzalishaji katika kilimo na kukuza zaidi usindikaji wa mazao

ya kilimo. Hili litahusisha kupunguza au kuondosha vikwazo kama vile upatikanaji hafifu wa huduma

za mikopo na fedha.

• Tatizo la uhaba wa nishati lililolikumba taifa hivi karibuni limethibitisha umuhimu wa nishati kwa

maendeleo. Ni muhimu kutafiti na kubaini vyanzo mbadala vya nishati – kulingana na lengo la sita la

MKUKUTA.

• Juhudi za kuboresha mtandao wa barabara za vijijini si za kuridhisha. Juhudi za kuongeza raslimali na

utekelezaji hazina budi kuwa sehemu ya mchakato wa mjadala wa sekta wa kila mwaka.

• Mishtuko na majanga kama ukame na kupanda kwa bei ya mafuta ulimwenguni hivi karibuni

yamethibitisha kuwa uchumi bado uko katika hali tete. Mbadala wa vyanzo vya nishati, na mazao ya

kuuza nje na akiba ya kutosha ya chakula ni masuala muhimu katika kuimarisha uchumi ili uweze

kuhimili vishindo hivyo.

Nguzo ya Pili: Uboreshaji wa Maisha na Ustawi wa Jamii

Hatua za kuchukuliwa katika nguzo hii ni pamoja na:

• Tatizo la VVU na UKIMWI limerudisha nyuma mafanikio kwenye viashiria vinavyohusiana na

sekta ya afya kama vile kupungua kwa vifo vya kina mama wakati wa kujifungua. Pamoja na juhudi

kubwa iliyofanywa bado vifo hivi vimeongezeka kutoka 529 hadi 578 kwa kila vizazi hai 1000. Hii ni

changamoto ambayo haiwezi kupuuzwa. Ili kuikabili changamoto hii, hatuna budi kuongeza juhudi

na kubuni mikakati mipya.

• Mahusiano yasiyofaa baina ya marika yameleta changamoto kubwa pia.. Kuna haja ya kuongeza

hatua zinazochukuliwa kuwalinda na kuwatunza watu na makundi ya watu walio katika mazingira

hatarishi.

• Makazi holela, hususan maeneo ya mijini yamekuwa ni tishio kwa mazingira. Hali hii inaibua haja

ya kubuni hatua za haraka za kulikabili tatizo hili ikiwa ni pamoja na kuyaboresha na kuyahalalisha

makazi hayo yasiyopangwa.

• Kumekuwepo na ongezeko la mzigo kwa wazee na pia ongezeko kubwa la watoto yatima sambamba

na watoto kutoka katika familia fukara zaidi. Makundi haya yanahitaji namna fulani ya hifadhi ya

kijamii. Mahitaji ya fedha kwa makundi haya ni makubwa kwa hiyo ipo haja ya kubainisha walengwa.

Tafiti zinahitajika ili kusaidia kufahamu uwezo na ufanisi wa hatua za hifadhi ya kijamii.

• Maendeleo ya baadaye ya taifa yatategemea sana uwepo wa wasomi waliofuzu vizuri katika fani mbali

mbali (hususan katika elimu na afya). Changamoto kubwa hapa ni ugharamiaji wa maendeleo ya

raslimali watu inayohitajika ili kuboresha huduma za jamii. Hili siyo tu kwamba linalazimisha kuwepo

35

kwa mfumo endelevu wa ulipaji kodi, bali pia linaleta msukumo wa madai ya ongezeko la mishahara

ya watumishi wa umma.

Nguzo ya Tatu: Utawala Bora na Uwajibikaji

Hatua za kuchukuliwa katika nguzo hii ni pamoja na:

• Uwezo mdogo wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa kutenga mafungu, na kusimamia matumizi ya

raslimali, unalazimu hatua zaidi za kuimarisha uwezo wake.

• Ukaguzi wa mahesabu chini ya serikali za mitaa unahitaji kujengewa uwezo na kuimarishwa zaidi.

Hitaji hili linazidi kuwa muhimu kufuatia hatua za hivi karibuni za upelekaji wa madaraka, majukumu

na raslimali kwa wananchi.

• Hakuna uhakika kwamba uwekaji wa taarifa kwenye mbao za matangazo unaofanywa na serikali za

mitaa katika ngazi mbali mbali umeweza kuongeza ubora wa upatikanaji na matumizi ya taarifa hizo

miongoni mwa jamii.

Ufuatiliaji wa MKUKUTA

Hatua za kuchukuliwa katika nguzo hii ni pamoja na:

• Kuna haja ya kuboresha mfumo wa taarifa za utendaji kwenye Wizara, Idara na Wakala wa serikali

pamoja na sekta nyinginezo.

• Wadau wote wanapaswa kufanya juhudi za maksudi kubuni mfumo ulioratibiwa vizuri wa ukusanyaji,

uchambuzi na utumiaji wa taarifa

Ugharamiaji wa MKUKUTA

Hatua za kuchukuliwa katika nguzo hii ni pamoja na:

• Kuna umuhimu wa kuoanisha mipango mikakati ya Wizara, Idara na Wakala wa serikali na

MKUKUTA ili raslimali ziweze kuelekezwa kulingana na mipango iliyowekwa.

• Raslimali za kugharamia MKUKUTA hazitoshelezi. Hii inailazimu serikali (a) Kuongeza mapato ya

ndani (b) Wabia wa Maendeleo kuongeza na kulinganisha utoaji wa misaada

• Kuna umuhimu wa kuwepo ufanisi katika (a) kuhusianisha raslimali na matokeo yanayotarajiwa (b)

utoaji wa taarifa za matokeo. Hii inahitaji uboreshaji zaidi wa mfumo wa utoaji taarifa.

• Bado kuna changamoto katika kuwashirikisha wadau wengi katika mchakato wa kuandaa Ripoti ya

Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA.

36

Kiambatisho 1: Muundo wa Utekelezaji wa MKUKUTA

Kiambatisho 2 kwa “Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji MKUKUTA 2006/07” Kinahusu “Hali ya

Utekelezaji wa Muundo wa MKUKUTA”. Kinaorodhesha shughuli 16 (tazama hapa chini). Kila moja

ya shughuli hizi imeambatana na kiashiria cha matokeo na jedwali dogo lenye safu za (a) matokeo (b)

malengo (c) hatua zilizochukuliwa (d) Mapendekezo ya hatua za kuchukua. Kiambatisho hiki kinaeleza

kwa mpangilio na kwa kifupi kazi mbali mbali zinazoendelea na kuonyesha kwa ufupi nini kinapaswa

kufanyika ili kufanikiwa katika siku zijazo.

Muundo wa Utekelezaji wa MKUKUTA – Majukumu Makuu

1 Kuoanisha Mipango/Mikakati ya Kisekta na ya Serikali za Mitaa na MKUKUTA

2 Kuoanisha MKUKUTA na Bajeti na Mapitio ya Matumizi ya Umma

3 Imarisha Uwajibikaji na Utoaji Taarifa kwa Sekta na serikali za Mitaa

4 (hakuna)

5 Jumuisha masuala mtambuka kwenye programu na mipango ya Wizara, Idara, Wakala wa Serikali

na Serikali za Mitaa

6 Pitia na kuimarisha Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA, na ufuatialiaji na tathmini ya Sekta na

Serikali za Mitaa.

7 Jumuisha MKUKUTA kwenye sera, programu na mipango ya Wadau wasiokuwa wa kiserikali

8 Saidia uoanishaji wa michakato mikuu ya Maendeleo ya kitaifa ( Mapitio ya Matumizi ya Umma,

Muundo wa Matumizi ya Muda wa Kati, MKUKUTA, Mkakati wa Misaada Tanzania, n. k )

9 Tekeleza Mkakati wa Mawasiliano wa MKUKUTA

10 Chukua hatua kuhakikisha kunakuwepo ushirikiano baina ya sekta katika utekelezaji wa

MKUKUTA

11 Fanya mapitio ya Maboresho makuu (Maboresho ya kitaasisi na ya Kimuundo ) na programu mbali

mbali

12 Andaa Mkakati wa Hifadhi ya Jamii na fanya uchambuzi zaidi wa Haki za binadamu, ambacho ni

kiungo muhimu katika umaskini

13 Ongeza utekelezaji wa Nguzo ya ukuaji wa Uchumi

14 Ongeza kasi ya utekelezaji wa MKUKUTA

15 Imarisha Mfumo wa Utoaji Taarifa za MKUKUTA

16 Imarisha Raslimali Watu inayohitajika kwa ajili ya utekelezaji wa MKUKUTA

LGA = Mamlaka ya Serikali za MitaaM&E = ufuatiliaji na TathminiMDA = Wizara, Idara na wakala wa serikaliMMS = Mfumo wa Ufuatiliaji wa MKUKUTAMTEF = Muundo wa Matumizi ya Muda wa KatiNSA = Wadau wasiokuwa wa Kiserikali PER = Mapitio ya Matumizi ya UmmaTAS = Mkakati wa Misaada wa Tanzania

6. Viambatisho

37

Kiambatisho 2: Mchakato wa Mapitio ya Kisekta

Mapitio ya kisekta yalibuniwa ili kusaidia kuhakikisha kwamba sekta zinakuwa na sera, mikakati na

mipango sahihi na kwamba inatekelezwa kwa njia bora zaidi.

Kama sehemu ya mchakato wa MKUKUTA, mapitio ya kisekta hivi sasa yanalenga kupata matokeo

yanayohusiana na ukuaji wa Uchumi na Kupunguza Umaskini. MKUKUTA unatambua umuhimu wa

maboresho na mikakati ya Maendeleo iliyopo ya kisekta. Matokeo ya mapitio ya kisekta yamekuwa

chanzo muhimu sana cha Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji MKUKUTA – MAIR (2007)

Mapitio ya Kisekta yanashughulika na maboresho yanayofanywa na serikali ambapo yanahusisha

wigo mpana wa wadau. Wazo la msingi ni kwamba uwazi, na njia zinazotabirika na kukubalika ndizo

zinazopaswa kutumika katika kuweka malengo ya usimamizi na mifumo ya uwajibikaji. Hii itasaidia

kuibua ushahidi unaohitajika katika kutathmini mafanikio ya sekta husika na kubuni mipango mizuri ya

Maendeleo ya sekta hiyo katika siku zijazo. Mapitio haya hutoa taarifa zinazohitajika kuongoza uwekaji

wa vipaumbele na kuboresha ufanisi na umadhubuti katika kutumia raslimali.

Malengo mahsusi ya mapitio ya kisekta ni pamoja na:

• Kujenga uelewa wa kina juu ya uhusiano maridhawa uliopo baina ya sera, mikakati, mipango, sheria na

kanuni za sekta ndogo mbali mbali

• Kubainisha mafanikio makuu, mapungufu yaliyojitokeza, na changamoto zinazotishia kukwamisha

kufikiwa kwa mabadiliko yaliyotarajiwa katika sekta hiyo

• Kulenga kwenye matatizo na matokeo yake katika upangaji wa mipango na uandaaji wa bajeti kwa

sekta husika na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa.

• Kujadili namna wadau mbali mbali wanavyoweza kuchangia kwenye mijadala ya ufanisi wa sera na

serikali.

• Kujadili jinsi hatua za Maendeleo zinazofikiwa kwenye sekta mbali mbali zinavyoweza kufuatiliwa

kikamilifu sambamba na mwelekeo wa kimatokeo wa MKUKUTA

• Kuwa taarifa zitakazoongoza uandaaji wa miongozo mahsusi ya sera za kisekta na mipango mikakati

Mapitio ya kisekta na programu za maboresho zilizotumika kama chanzo cha MAIR (2007) :

Nguzo ya kwanza: Nguzo ya pili: Nguzo ya tatu:

Ukuaji wa Uchumi Uboreshaji wa Maisha Utawala Bora

na Upunguzaji na Ustawi wa Jamii na Uwajibikaji

wa Umaskini• Mapitio ya sekta ya Usafirishaji

• Mapitio ya sekta ya Nishati

• Mapitio ya sekta ya Kilimo

• Programu ya Maboresho ya Sekta ya Sheria

• Programu ya Maboresho ya Utumishi wa

Umma

• Programu ya Maboresho ya Serikali za Mitaa

• Programu ya Maboresho ya Usimamizi wa

Fedha

• Mkakati wa Taifa wa Mapambano dhidi ya

Rushwa na Mpango kazi

• Mapitio ya sekta ya Mazingira

• Mapitio ya sekta ya Elimu

• Mapitio ya sekta ya Maji

• Mapitio ya sekta ya Afya

38

Kiambatisho 3: Viunganishi Muhimu vya Intaneti

zingatia: [PV] inamaanisha kwamba mwongozo wa lugha rahisi unapatikana kwenye tovuti ya Hakikazi

Catalyst http://www.hakikazi.org/plain_language.htm

Machapisho Mbali Mbali ya Sera Muhimu za Kitaifa ni Pamoja na:Mkakati wa Taifa wa Kuondoa Umaskini (NPES) 1997

www.tzonline.org/pdf/thenationalpovertyeradicationstrategy.pdf

Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025 (1999)

www.tanzania.go.tz/vission_2025f.html

Mkakati wa Misaada wa Tanzania [PV]

www.tzonline.org/pdf/Tanzaniaassistancestrategy.pdf

Waraka wa Mkakati wa Upunguzaji Umaskini (2000) [PV]

www.tzonline.org/pdf/FinalPRSP25.pdf

Mpango Mkuu wa Ufuatiliaji wa Umaskini [PV]

www.tzonline.org/pdf/povertymonitoringmasterplan.pdf

Mkakati wa Taifa wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (2005) [PV]

www.povertymonitoring.go.tz/downloads/new/nsgrptext.pdf

Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (2005) (Kiambatisho)

www.povertymonitoring.go.tz/downloads/new/nsgrpmatrix.pdf

Mpango Mkuu wa Ufuatiliaji wa MKUKUTA & Taarifa za Viashiria (Sehemu ya 1 &2) (2006)

www.povertymonitoring.go.tz/documents/mkukutamasterplan.pdf

Baadhi ya Ripoti Zinazohusu Ufuatiliaji wa Umaskini:Ripoti ya Maendeleo ya Waraka wa Mkakati wa Upunguzaji Umaskini (PV 2001)

www.mof.go.tz/index.php?option=com_content&task=view&id=172&Itemid=169

Tathmini Shirikishi ya Umaskini Tanzania (PV)

www.repoa.or.tz/content/blogcategory/35/67/

Ripoti ya Umaskini na Maendeleo ya Watu, Ripoti za Hali halisi na dondoo ya Sera

www.repoa.or.tz/content/blogcategory/35/67/

Mawasilisho ya mada mbali mbali za Wiki la Umaskini 2007

www.povertymonitoring.go.tz/Communications_reports.asp

Matokeo ya tafiti na sensa mbali mbali www.nbs.go.tz

Msaada wa Bajeti kwa ajili ya Kupunguza Umaskini (PRBS) www.tzdpg.or.tz/index.php?id=34

Mkakati wa Pamoja wa Misaada kwa Tanzania ( JAST) www.tzdpg.or.tz/index.php?id=8

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA (MAIR)(2007) www.xxx

39

Tovuti Zenye Taarifa Zinazohusu Ufuatiliaji wa UmaskiniTovuti ya Ufuatiliaji wa Umaskini –ina habari mbali mbali kuhusu hatua za Maendeleo zilizofikiwa na

matokeo ya Mikakati ya Kupunguza Umaskini nchini na Mfumo wa Ufuatiliaji wa Umaskini

www.povertymonitoring.go.tz

Tanzania Mtandaoni -inatoa taarifa nyingi kuhusu masuala mbali mbali ya Maendeleo nchini Tanzania.

www.tzonline.org/

Lango kuu la Maendeleo Tanzania – husambaza taarifa, kubadilishana taarifa, Majadiliano ya kwenye

mtandao www.tanzaniagateway.org/

Taarifa za Kiuchumi na Kijamii – unaweza kupata taarifa sahihi kuhusu masuala mbali mbali ya viashiria

vya Uchumi na kijamii kwa lugha rahisi. www.tsed.org

Maana za Maneno Makuu Yaliyotumika (Faharasa)

Asasi za Kiraia Ma shirika, vyama, taasisi za kijamii, na mitandao mbali mbali kati ya familia na ngazi

ya taifa. Zinahusisha vikundi vya kujitolea na vya hisani, jumuiya za wazazi, vikundi vya wazee, vilabu

vya michezo, vikundi vya sanaa na utamaduni, vyama vya kitaaluma na kitaalamu, taasisi za kidini, vyama

na vikundi vya wafanyakazi

Hifadhi ya jamii ni huduma za ustawi wa jamii zenye kulenga kuwalinda dhidi ya matatizo ya kijamii

kama vile umaskini, uzee, ulemavu, na ukosefu wa ajira. Pia tembelea http://en.wikipedia.org/wiki/

Social_Protection

Huduma za jamii hizi ni huduma zinazotolewa na serikali kwa wananchi, ama moja kwa moja (kupitia

sekta ya umma) au kwa kufadhili sekta binafsi ili iweze kutoa huduma. Miongoni mwa huduma za jamii

ni pamoja na elimu, umeme, afya, majeshi, polisi, usafiri wa umma, simu, mipango miji, maji na huduma

za usafi. Kwa maelezo zaidi tazama http://en.wikipedia.org/wiki/Public_services

Huduma za kifedha ni huduma zinazotolewa na tasnia ya fedha zinazohusisha taasisi nyingi za

usimamizi wa fedha. Miongoni mwa taasisi hizo ni benki, makampuni ya bima, makampuni ya uuzaji wa

hisa, na baadhi ya kampuni za biashara zinazodhaminiwa na serikali.

Masuala mtambuka ni masuala yanayoweza kuathiri na kuathiriwa na sekta mbalimbali. Baadhi ya

masuala mtambuka makuu ni utawala bora, jinsia, mazingira, VVU/UKIMWI, hifadhi ya jamii kwa

makundi ya watu walio katika mazingira hatarishi. Unaweza kupata taarifa zaidi kwenye tovuti http://

www.agriculture.go.tz/Projects/ASDP/Cross-sectoral-issues.htm

Mdau ni mtu anayeweza kuathiri au kuathiriwa na kitendo fulani. Ufanyaji maamuzi mzuri unapaswa

kuzingatia mchango wa wadau wote.

Miundombinu ni pamoja na mifumo ya usafirishaji na mawasiliano, mitandao ya maji na umeme, taasisi

za umma kama shule, posta, na magereza.

Msaada wa Bajeti Ni aina ya msaada ambapo fedha zinatolewa na Wabia wa Maendeleo kusaidia

programu za serikali zikilenga ukuaji wa Uchumi na upunguzaji wa Umaskini. Fedha zinatolewa kwa

serikali husika na kutumika kwa kufuata mifumo yake ya usimamizi wa fedha na uwajibikaji.

Wabia wa Maendeleo Hawa ni wadau wa Maendeleo ya taifa, mbali ya serikali. Mara nyingi msamiati

huu hutumika kumaanisha mashirika ya kimataifa yanayotoa misaada, mikopo, uwekezaji na msaada wa

kiufundi.

40

Ubia baina ya sekta ya umma na ya binafsi (PPP) ni huduma inayoendeshwa na serikali au sekta binafsi

ikigharamiwa kwa ubia wa serikali na kampuni binafsi moja au zaidi. Wakati fulani mapato ya kodi

hutumika kama mtaji wa uwekezaji kwa shughuli zinazofanywa kwa ubia wa serikali na sekta binafsi au

kwa mkataba. Kwa namna nyingine mtaji wa uwekezaji hutolewa na sekta binafsi kwa kupewa msukumo

na serikali chini ya mkataba wa sekta binafsi kutoa huduma husika. Mchango wa serikali kwenye ubia wa

aina hii unaweza kuwa wa hali (kwa kuhamisha raslimali iliyopo)

Ukaguzi wa mahesabu Mchakato wa kutathmini kumbukumbu au mahesabu.

Ukuaji Mpana wa uchumi Ukuaji wa Uchumi ambao unamnufaisha kila mtu (Pia unajulikana kama

ukuaji unaojali watu maskini au ukuaji wa Uchumi wenye kujali usawa)

Uoanishaji wadau hukaa pamoja na kukukubaliana juu ya nadharia na vitendo vya kanuni zinazosimamia

ukuzaji wa uchumi na upunguzaji wa umaskini

Utawala bora unahusisha Uwazi, taasisi zinazowajibika, taratibu za haki za ufanyaji maamuzi,mifumo

ya kidemokrasia ya siasa na mahakama na uwezpo wa asasi hai na huru za kiraia.

Wadau wasio wa Kiserikali ni pamoja na Wabia wa Maendeleo, mashirika ya kijamii, (CBOs), Mashirika

yasiyo ya Kiserikali (NGOs), Taasisi za Kidini (FBOs), Taasisi za Kitaaluma, vyama vya wafanyakazi,

na sekta binafsi

41

ShukuraniWizara ya Fedha na Uchumi inatoa shukrani kwa mchango uliotolewa na wadau waliohusika katika

kutayarisha mwongozo huu wa lugha rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji MKUKUTA

2006/07.

.Michango ya watu na taasisi mbali mbali inatambuliwa, lakini shukrani za pekee ziende kwa timu

ya maofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi. Maofisa hawa walifanya kazi kubwa ya kuwezesha utoaji

wa kijitabu kwa kukipitia mara kwa mara na kutoa maoni ya kina ili kuhakikisha kuwa ni sahihi na

kamilifu.

Pia shukrani za pekee ziende kwa asasi ya kiraia ya Hakikazi Catalyst ambayo

ilijihusisha na utaalamu wa kutayarisha na kuwezesha toleo hili katika lugha za Kiingereza na

Kiswahili.

Kadhalika shukrani ziende kwa Nathan Mpangala kwa katuni zake zinazosisimua. Na kwa kazi ya

usanifu na uchapishaji shukrani ziwaendee Colour Print Tanzania Ltd.

42