fataawa za wanachuoni (34)

34
1 علماء ال فتاوىFataawa Za Wanachuoni [34] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

Upload: wanachuoni

Post on 13-Apr-2015

239 views

Category:

Documents


11 download

DESCRIPTION

Fataawa Za Wanachuoni (34)

TRANSCRIPT

Page 1: Fataawa Za Wanachuoni (34)

1

فتاوى العلماءFataawa Za Wanachuoni

[34]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Wanachuoni (34)

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 3: Fataawa Za Wanachuoni (34)

3

Fataawa zilizomo:

1) Je Kuna Du´aa Maalum Ya Kumuombea Mtoto Wa Kuwaliza?

2) Inajuzu Kumuadhinia Mtoto Anapozaliwa?

3) Hukumu Ya Kumlipa Mtu Deni Msikitini

4) Ameapa Kutojichua Sehemu Za Siri Ila Kafanya, Alipe Kafara?

5) Ni Kipi Chakula Cha Majini Wa Kiislamu?

6) Mtu Akivua Soksi Alizopaka Juu Yake, Wudhuu Unatenguka?

7) Kusikiliza Qur-aan Na Kusoma Adhkaar Kwa Mwenye Janaba

8) Je Inajuzu Kutoa Zakaatul-Fitwr Pesa?

9) Inajuzu Kumpa Mtoto Jina La "Iynaas"?

10) Nasaha Za Shaykh Zayd Kwa Wale Wenye Kuangalia Filamu Za Ngono

11) Hukumu Ya Kulala Na Janaba

12) Aanze Na Swalah Ya Janaza Au ´Aswr Na Jamaa´ah Ya Pili?

13) Mama Kashika Tupu Ya Mtoto Hali Kishatawadha

14) Kundi Limechelewa Siku Ya Ijumaa, Waswali Ijumaa Au Dhuhr?

15) Je Hadiyth Dhaifu Hutumiwa Katika Fadhwaail al-A´amaal?

16) Inajuzu Kubusu Msahafu?

17) Hukumu Ya Kujitibu Kwa Tumbaku

18) Inafaa Kuwa Na Isbaal Kwa Mwenye Kuwa Na Kilemba?

19) Kijana Kila Anapotubia Anarudi Kufanya Dhambi Tena

20) Kafunga Mwezi Mzima Wa Muharram, Kapatia?

21) Kipigo Cha Kutia Adabu Kinachoruhusu

22) Kafunga Sunnah Kisha Baadae Kaamua Kula

23) Imamu Kakumbuka Kuwa Nguo Yake Ina Madhiy Ndani Ya Swalah

24) Ewe Kaka Wa Kiislamu, Mtume Wako Akuamrisha Kufuga Ndevu

25) Imamu Na Muadhini Hawatakiwi Wawe Watu Wa Bid´ah; Kama Suufiy,

Ash´ariy, Mu´taziliy, Jahmiy

26) Twawaaf Ya Kuaga Ni Wajibu Katika ´Umrah

27) Baba Hataki Kuwaozesha Mabinti Zake Kwa Kukhofia Riziki Zao

28) Hukumu Ya Kubaki Macho Baada Ya Swalah Ya ´Ishaa

29) Kuuza Katika Maeneo Ya Msikitini Kama Bustani La Msikitini

30) Mtu Anataka Kulipa Deni Katika Pesa Za Zakaah

31) Mwanaume Anaruhusiwa Kuvaa Pete?

32) Du´aa Nzuri Wakati Mwanamke Anataka Kuzaa

33) Hadiyth Ya Waislamu Kupeana Zawadi Ili Wapendane

34) Kuswali Swalah Za Sunanh Kabla Ya Swalah Ya Ijumaa

35) Mtoto Akipita Mbele Ya Mwenye Kuswali Swalah Yaharibika

36) Mwanamke Mgonjwa Anastanji Na Kujiosha Kwa Maji Ya Zamzam

37) Talaka Inatokana Na Alivyokusudia (Nia) Ya Mume

Page 4: Fataawa Za Wanachuoni (34)

4

38) Dada Anataka Kubadilisha Rangi Ya Nywele Zake Nyeusi

39) Hukumu Ya Unyevu (Majimaji, Utoko) Umtokao Mwanamke

40) Kuna Muda Maalumu Wa Mtu Kufanya Kijicho?

41) Mwanamke Anatokwa Na Upepo Kwenye Tupu Ya Mbele, Hukumu Ya

Swalah Yake

42) Baadhi Ya Sifa Zinazopasa Kuwa Na Mke Mtarajiwa

43) Hukumu Ya Kupuuza Swalah Mpaka Ukaondoka Wakati Wake

44) Hukumu Ya Kubusu Msahafu Na Kuuweka Chini

45) Hukumu Ya Kula Daku Baada Ya Adhaana Ya Pili Ya Fajr

46) Hukumu Ya Kupuuza Swalah Mpaka Ukaondoka Wakati Wake

47) Hukumu Ya Mume Kamwambia Mke Wake Wewe Ni Kama Mamangu

48) Imefika Ramadhaan Na Ana Deni La Ramahaan Ingine

49) Inafaa Kwa Kwenye Kukaa Eda Kuangalia Jua, Mwezi, Nyota, Mbingu,

Kupika, Ndugu Zake?

50) Je Mkaaji Eda Haruhusiwi Kutoka Nyumbani Kabisa?

51) Je Salaf Waliwahi Kutofautiana Katika ´Aqiydah?

52) Kajiapiza Kutofanya Kitu Fulani Kisha Akamtaliki Mke Wake

Wanachuoni waliomo:

1) ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

2) ´Allaamah Zayd bin Haadiy al-Madkhaliy

3) ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Waswaabiy

Page 5: Fataawa Za Wanachuoni (34)

5

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1) Je Kuna Du´aa Maalum Ya Kumuombea Mtoto Wa Kuwaliza?

Swali:

Je kuna Du´aa maalum ya kumuombea mtoto mpya wa kuzaliwa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Sijui kama kuna Du´aa makhsus. Ila atamuomba Allaah (´Azza wa Jalla)

Amjaalie kuwa mtoto mwema na mtiifu kwa wazazi wawili, awe ni mwenye

kumtii Allaah (´Azza wa Jalla) na mwenye kufuata Sunnah za Mtume wa

Mtume wa Allaah (´alayhis-Salaam). Na Allaah Atampokelea Du´aa yake.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2301

2) Inajuzu Kumuadhinia Mtoto Anapozaliwa?

Swali:

Ipi hukumu ya kumtolea adhaana katika masikio ya mtoto mwenye kuzaliwa?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Hadiyth hii ni dhaifu. Haadhiniwi katika sikio lake la kulia wala hakimiwi

Swalah katika sikio lake la kushoto.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4870

Page 6: Fataawa Za Wanachuoni (34)

6

3) Hukumu Ya Kumlipa Mtu Deni Msikitini

Swali:

Ipi hukumu ya kurudisha (lipa) deni Msikitini?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hakuna ubaya, kwa kuwa hili si kununua wala kuuza. Ni amana ya watu

aliokuwa nayo anairudisha kwa mmiliki. Hakuna ubaya. Lakini wasirefushe

sana hesabu na maongezi kuhusu kununua na kuuza ambayo ndio ilikuwa

sababu ya deni hili. Iwe ni kama amana alichukua sasa anamrudishia mmiliki

kisha aende zake. Hakuna ubaya kwa hilo.

Chanzo: http://youtu.be/lEhpBOGDmJE

4) Ameapa Kutojichua Sehemu Za Siri Ila Kafanya, Alipe Kafara?

Swali:

Aliapa kuwa hatojichua sehemu za siri (kupiga punyeto), halafu baadae

akafanya. Anauliza je anawajibika kutoa kafiri?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ndio. Utatoa kafara kumuadhimisha Allaah (´Azza wa Jalla) kwa kuwa

uliapa Kwake na hukuchunga ulichokiapia. Na umuombe Allaah (´Azza wa

Jalla) kwa kufanya kwako maasi haya. Ni Haramu. Ni ni juu yako kupigana

Jihaad na nafsi yako. Usijiachie kwa Shaytwaan wala kwa maasi. Ni Haramu

Haramu, na upigane Jihaad kwa hili. Huku ukifanya sababu, kama kuoa ni

katika sababu. Mwenye ada ya kufanya kitendo hiki kichafu. Kufunga pia ni

katika sababu za kuacha kitendo hiki kichafu. Tangamana na watu wema na

ukae nao, tafuta elimu pia yote haya ni katika sababu. Jitahidi kusahau

Page 7: Fataawa Za Wanachuoni (34)

7

mambo haya na kutojishughulisha kabisa, ni katika sababu. Ama kulifikiria

sana, hii ni katika sababu ya kupelekea ukalifanya tena.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5419

5) Ni Kipi Chakula Cha Majini Wa Kiislamu?

Swali:

Je ni sahihi kuwa majini ya Kiislamu yanakula mifupa ambayo ilitajiwa Jina la

Allaah wakati wa kuitupa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Bila shaka, kumepokelewa (Hadiyth) kuhusiana na hili Hadiyth.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2291

6) Mtu Akivua Soksi Alizopaka Juu Yake, Wudhuu Unatenguka?

Swali:

Je Wudhuu utatenguka ikiwa aliyezivaa atazivua baada ya kupaka juu yake?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ndio akivua soksi kwa muda maalumu, kwa mkazi ni siku (mchana) moja na

usiku wake, msafiri siku tatu - akivua soksi Twahara yake imebatilika na ni

juu yake kutawadha upya na azivae kwa Twahara kamili.

Page 8: Fataawa Za Wanachuoni (34)

8

Chanzo: http://youtu.be/K4C8vy4Pw18

7) Kusikiliza Qur-aan Na Kusoma Adhkaar Kwa Mwenye Janaba

Swali:

Ipi hukumu ya kusikiliza Qur-aa na kusoma Adhkaar naye yuko katika

janaba?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Kusikiliza Qur-aan na kusom Adhkaar hakuna ubaya inajuzu. Ila Qur-aan

asiisome naye yuko katika janaba.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4863

8) Je Inajuzu Kutoa Zakaatul-Fitwr Pesa?

Swali:

Muulizaji kutoka Ubelgiji, je inajuzu kutoa Zakaatul-Fitwr pesa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hapana, imethibiti kutoa Zakaatul-Fitwr chakula. Na pesa zilikuwepo wakati

wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ila hakutoa yeyote katika

Maswahabah wake Zakaah pesa. Hata kama baadhi ya wanachuoni

wamejuzisha hilo, ila maneno yao yanarudishwa kwa kuwa yanakhalifu

Sunnah. Sunnah ni kutoa chakula ambacho kinapatikana katika mji huo, wala

mtu asitoe pesa.

Page 9: Fataawa Za Wanachuoni (34)

9

Chanzo: http://youtu.be/ki4SAYRjDrI

9) Inajuzu Kumpa Mtoto Jina La "Iynaas"?

Swali:

Je inajuzu kumpa mtoto jina la "Iynaas"?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa hakuna ubaya In Shaa Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4866

10) Nasaha Za Shaykh Zayd Kwa Wale Wenye Kuangalia Filamu Za

Ngono

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kuingia tovuti chafu za ngono kwenye Intanet, na

anaangalia Aliyoharamisha Allaah. Ipi nasaha yako kwao?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hukumu yake ni kwamba anafanya dhambi kubwa na itamfanya nafsi yake

kuwa chafu. Allaah Anamwangalia na yeye yuko katika maasi. Ni wajibu

kwake kuwa na aibu kwa Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala) ambaye Humzidishia

mtu mwema kwa Ihsaan Zake na Humzidishia kwa fadhila Zake, na Humlipa

mtenda dhambi kutokana na ´amali yake ilivyo, kutokana na Hekima na

Uadilifu Wake. Ni juu ya watu hawa wanaotumia njia kama hizi kwa kufanya

ya Haramu na maasi, wamche Allaah. Hakika Allaah (´Azza wa Jalla) hata

Page 10: Fataawa Za Wanachuoni (34)

10

kama bado anawaacha hajashindwa kuwakamata. Ni bora kwao kukimbilia

kuomba Tawbah maadamu roho bado ingali mwilini, waache matendo

machafu na waazimie kuacha kabisa na wasiyarudi.

Chanzo: http://youtu.be/LAnhy8aBVk4

11) Hukumu Ya Kulala Na Janaba

Swali:

Ipi hukumu ya kusikiliza Qur-aa na kusoma Adhkaar naye yuko katika

janaba?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Kusikiliza Qur-aan na kusom Adhkaar hakuna ubaya inajuzu. Ila Qur-aan

asiisome naye yuko katika janaba.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4863

12) Aanze Na Swalah Ya Janaza Au ´Aswr Na Jamaa´ah Ya Pili?

Swali:

Kuna mtu aliingia Msikitini na Swalah ya Jamaa´ah imeshampita,

wakasimama watu kuswali Swalah ya janaza. Je aswali ´Aswr na Jamaa´ah ya

pili au aswali Swalah ya janaza?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Page 11: Fataawa Za Wanachuoni (34)

11

Aanze kwanza na Swalah ya maiti kisha ndo aswali faradhi iliyompita.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5187

13) Mama Kashika Tupu Ya Mtoto Hali Kishatawadha

Swali:

Je mama atawadhe tena ikiwa atashika tupu ya mtoto wake?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni ndio, atawadhe tena.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4874

14) Kundi Limechelewa Siku Ya Ijumaa, Waswali Ijumaa Au Dhuhr?

Swali:

Likiingia kundi siku ya Ijumaa na Imamu amekwishaswali. Je, waswali Ijumaa

au waswali Dhuhr?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa wataswali Dhuhr. Ila tu ikiwa watamkuta Imamu bado yu wima

katika Rakaa ya pili, hapo wataswali Ijumaa. Ama ikiwa kishainuka kutoka

katika Rukuu katika Rakaa ya pili, wataswali Dhuhr.

Page 12: Fataawa Za Wanachuoni (34)

12

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5179

15) Je Hadiyth Dhaifu Hutumiwa Katika Fadhwaail al-A´amaal?

Swali:

Je wamekubaliana wanachuoni kutumia Hadiyth dhaifu katika "Fadhwaail al-

A´amaal" kama alivyosema hilo an-Nawawiy?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni hapana, hawakukubaliana. Kauli yenye nguvu ni kuwa Hadiyth dhaifu

haitumiwi. Asli ni kuegemea katika yaliyothibiti kutoka kwa Mtume wa

Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4873

16) Inajuzu Kubusu Msahafu?

Swali:

Ipi hukumu ya kubusu msahafu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Haijulikani kwa Salaf suala la kubusu msahafu. Msahafu mapenzi yake ni

ndani ya moyo na si kwa kubusu. Hatujui kwa Salaf kuwa walikuwa

wakibusu msahafu. Mtu asiubusu msahafu.

Chanzo: http://youtu.be/pUoYt3FEtzE

Page 13: Fataawa Za Wanachuoni (34)

13

17) Hukumu Ya Kujitibu Kwa Tumbaku

Swali:

Ipi hukumu ya kujitibu kwa tumbaku?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Tumbaku nakunasihi kujiepusha nayo. Na mada yako mengi mbali na hii

tumbaku, sehemu za madawa. Pia asali ni dawa, Habbat sawdah In Shaa

Allaah na kadhalika.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4861

18) Inafaa Kuwa Na Isbaal Kwa Mwenye Kuwa Na Kilemba?

Swali:

Je kilemba kina Isbaal?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa imekuja hii pia katika Hadiyth, Isbaal katika kanzu, kikoi na

kilemba.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=5209

Page 14: Fataawa Za Wanachuoni (34)

14

19) Kijana Kila Anapotubia Anarudi Kufanya Dhambi Tena

Swali:

Mimi ni kijana nimefanya dhambi nikatubia, kisha nikatubia kwa Allaah

lakini nikarejea tena katika dhambi hii, ipi nasaha zako kwangu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Rejea uombe tena Tawbah yakweli na wala usikate tamaa kwa Rahmah ya

Allaah. Lakini rejea uombe Tawbah yakweli na uwe mkweli kwa Allaah

(´Azza wa Jalla). Atakusamehe Allaah dhambi yako na Ataifanya kuwa mema.

Lakini kuwa mkweli katika Tawbah yako na Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala).

Chanzo: http://youtu.be/e7huH83HlvU

20) Kafunga Mwezi Mzima Wa Muharram, Kapatia?

Swali:

Atakayefunga mwezi wa Muharram wote au baadhi ya siku chache, je kitendo

chake hiki kapatia?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ndio ni sahihi. Muulizaji anasema kwa kuwa nimesikia katika Hadiyth:

"Swawm bora kwa Allaah baada ya Ramadhaan ni Swawm ya mwezi wa

Allaah Muharram."

Jibu ni ndio, Hadiyth hii ni sahihi.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4708

Page 15: Fataawa Za Wanachuoni (34)

15

21) Kipigo Cha Kutia Adabu Kinachoruhusu

Swali:

Mwalimu anaweza kumpiga mwanafunzi kumuogopeshe ili arejee kufanya

jambo fulani au kuacha jambo fulani, je hili pia linangia katika tishio [la

dhuluma]?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kipigo cha kumuweka [kumtia] adabu mwalimu mnasihiaji kwa mwanafunzi,

kipigo cha kumuweka adabu kidogo halaumiwi kutokana na maslahi kwake

[mwanafunzi] na kumkinga na yatayomdhuru katika uhai wake na Mustaqbal

wake. Pia kipigo cha baba kwa mtoto wake, na kwa mleaji - kama mtu

mkubwa kwa mdogo, hali kadhalika mume kwa mke wake katika baadhi ya

hali kama jinsi Allaah Alivyotoa idhini hio. Hichi huitwa kipigo cha kuweka

adabu na kutengeneza. Atakayefanya hana makosa wala haingii katika

kufanya dhuluma. Lakini ikiwa atachupa mipaka katika kupiga, hapo

atachukuliwa amefanya dhuluma. Na ikiwa atapiga bila ya haki hata kama

kitakuwa ni kipigo kidogo, atachukuliwa ni dhalimu na siku ya Qiyaamah

Allaah naye Atamlipiza.

Chanzo: http://youtu.be/e0PZUe5gE3A

22) Kafunga Sunnah Kisha Baadae Kaamua Kula

Swali:

Kuna kanuia kufunga Swawm ya Naafil, akala wala hakutimiza Swawm yake.

Je huku ni kuharibu ´amali na kunaingia katika Kauli Yake Allaah:

أعمالكمااتبطلوااولا

Page 16: Fataawa Za Wanachuoni (34)

16

"Wala msiviharibu vitendo vyenu." (47:33)

´Allaamah al-Waswaabiy:

Imekuja katika Hadiyth, anasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Mwenye kufunga Swawm ya Sunnah na msafiri wanakhiari, wakitaka

watafunga na wakitaka watakula."

Hakuna ubaya akila na lau angelitimiza Swawm yake ingelikuwa bora.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4701

23) Imamu Kakumbuka Kuwa Nguo Yake Ina Madhiy Ndani Ya Swalah

Swali:

Akikumbuka Imamu kuwa katika nguo yake kuna madhiy, atoke katika

Swalah au aitimize?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa madhiy ni najisi. Akiweza kuvua nguo hii aivue na aendelee na

Swalah. Na akiwa hawezi atoke [ndani ya Swalah] na paingie nafasi yake mtu

mwingine.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=283

24) Ewe Kaka Wa Kiislamu, Mtume Wako Akuamrisha Kufuga Ndevu

Swali:

Page 17: Fataawa Za Wanachuoni (34)

17

Hukumu ya kunyoa ndevu au kutoa kitu humo?

´Allaamah al-Waaswabiy:

Kufuga ndevu ni wajibu. Na kuzinyoa au kutoa kitu humo ni Haramu. Kwa

kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Kuweni kinyume na washirikina; fugeni ndevu kwa wingi na punguzeni

masharubu." [Muttafaq, Ibn ´Umar]

Mtume (´alayhis-salaam) anakuamrisha kufuga ndevu. Wewe zifuge na wala

usitoe humo kitu. Na anakuamrisha kuacha masharubu, usiyafanye marefu

wala usiyatoe yote.

Na Allaah Anasema:

أليم ااعذاب اايصيبهمااأواافتنة ااتصيبهمااأناأمرهااعناايخالفونااالذيناافليحذرا

"Basi nawatahadhari wanaokhalifu amri yake, usije ukawapatamsiba au

ikawapata adhabu chungu." (24:63)

Usijiamini. Kumbuka yule mtu aliyekuwa anakula kwa Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa mkono wake wakushoto, akamwambia:

"Kula kwa mkono wakulia!". Akasema: "Siwezi". Akamwambia: "Hutoweza

kamwe."

Hakuna kilichomzuia ila ni kiburi. Hakika Mtume alimuamrisha kula kwa

mkono wakulia, akasema hapana siwezi. Akamuombea Du´aa kumwambia

"Hutoweza." Wewe pia usijiamini. Akikuamrisha Allaah au Mtume Wake

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) basi tekeleza. Na akikukataza Allaah au

Mtume Wake kwa kitu, basi jitenge nacho.

سولااآتاكمااوما قواافانتهوااعنهاانهاكمااوماافخذوهااالر ااوات ااإنااللا العقابااديداشااللا "

"Na anachokupeni Mtume chukueni, na anachokukatazeni jiepusheni nacho.

Na mcheni Allaah. Hakika Allaah ni Mkali wa kuadhibu." (59:07)

Page 18: Fataawa Za Wanachuoni (34)

18

Chanzo:

http://www.olamayemen.net/default_ar.aspx?id=283&Name=%D8%A7%D9%

84%D9%81%D8%AA%D8%A7%D9%88%D9%89

25) Imamu Na Muadhini Hawatakiwi Wawe Watu Wa Bid´ah; Kama

Suufiy, Ash´ariy, Mu´taziliy, Jahmiy

Swali:

Muulizaji kutoka UK. Hakuna katika Msikiti wetu muadhini, vipi

tutamchangua muadhini na kwa kitu gani tutaangalia kwa mwenye kufaa

kutoa adhaana?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kwa hakika ni kwamba ni lazima kwa waliohai kuwa na Msikiti, na ni lazima

kwa Msikiti kuwepo na Imamu na muadhini, ili watu wahifadhi wakati na

waswali Jamaa´ah. Kwa Imamu anashurutishwa awe mtu mwenye ´Aqiydah

sahihi na mjuzi. Na muadhini anashurutishwa awe mtu mwenye ´Aqiydah

sahihi, iliyo salama; Asiwe Suufiy, Ash´ariy, Mu´taziliy, Jahmiy wala asiwe

mwenye ´Aqiydah (Itikadi) potofu. Bali anatakiwa awe katika Manhaj ya Ahl-

us-Sunnah wal-Jamaa´ah na awe na ´Aqiydah yao katika mlango wa Majina

na Sifa za Allaah na yanayofanana na hayo katika mambo makubwa kuhusu

´Aqiydah na Tawhiyd. Awe ni mtu mwenye kuhifadhi wakati [wa Swalah],

mtu anajua Fiqh - katika Twahara yake, usomaji wake, Swalah yake kiasi

ambacho akikwama Imamu muadhini asimame nafasi yake na aswalishe

Jamaa´ah.

Chanzo: http://youtu.be/r5C3RBFSMfY

26) Twawaaf Ya Kuaga Ni Wajibu Katika ´Umrah

Page 19: Fataawa Za Wanachuoni (34)

19

Swali:

Twawaaf ya kuaga katika ´Umrah ni wajibu au ni Mustahaba?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ni Mustahaba. Yaani katika Hajj ni wajibu na katika ´Umrah ni Mustahaba.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4237

27) Baba Hataki Kuwaozesha Mabinti Zake Kwa Kukhofia Riziki Zao

Swali:

Ipi hukumu ya baba ambaye hataki kuwaozesha mabanati zake kwa ajili ya

riziki zao?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Huchukuliwa kuwa ni dhalimu. Na Allaah Hawapendi madhalimu. Anasema

Allaah:

الميناوا أليمااعذاباالهمااأعداالظ

"Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu." (76:31)

Riziki yao iko kwa Allaah. Akimuozesha binti yake riziki yake iko kwa Allaah.

Ajitahidi kumuozesha kwa mwanamume mwema ambaye atamsaidia katika

Dini na dunia yake. Haijuzu kwake kumkatalia kwa kitu Alichomhalalishia

Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4706

Page 20: Fataawa Za Wanachuoni (34)

20

28) Hukumu Ya Kubaki Macho Baada Ya Swalah Ya ´Ishaa

Swali:

Je inajuzu kutoka kwenda kutembea na familia baada ya [Swalah ya] ´Ishaa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kuwa macho baada ya ´Ishaa hairuhusiwi ila kwa msafiri au mwenye

kuswali, au mtafutaji elimu (mwanafunzi), au kusaidia kidogo katika mambo

ya Waislamu. Kama kwa mwenye wilaya katika wilaya ya Waislamu sawa

iwe kwa jumla au khaswa. Mbali na hayo kuwa macho inadhuru na huenda

ikawa sababu ya kukosa Swalah ya Jamaa´ah, bali hata Swalah kwa wakati

wake.

Chanzo: http://youtu.be/iYe1w1bYuvY

29) Kuuza Katika Maeneo Ya Msikitini Kama Bustani La Msikitini

Swali:

Hukumu ya kuuza katika maeneo ya Msikitini?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Pale ambapo ni maeneo ya Msikitini haijuzu kuuza, kutokana na ujumla wa

Hadiyth [inayokataza kuuza Msikitini].

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4712

Page 21: Fataawa Za Wanachuoni (34)

21

30) Mtu Anataka Kulipa Deni Katika Pesa Za Zakaah

Swali:

Mtu ambaye mali yake imeeneza niswaab, na yeye ana madeni kwa baadhi ya

watu. Je, anaweza kulipa madeni hayo kwa kulipa Zakaah?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Fatwa za wanachuoni zinasema kuwa jambo hili halijuzu, kwa kuwa

anajihami mali yake kwa kutoa Zakaah. Lakini ampe fakiri Zakaah. Na fakiri

ikiwa ndio huyo aliyekuwa akimdai hakuna ubaya. Kwa sharti isiwe

alikubaliana naye kabla, mimi nakukopa na wewe utanirudishia. Hii ni

khiyana haijuzu.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4714

31) Mwanaume Anaruhusiwa Kuvaa Pete?

Swali:

Hukumu ya kuvaa pete kwa kijana?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Hakuna tofauti kati ya kijana wala mzee, hukumu yao ni moja. Na pete

hakubainisha ni pete ipi, ikiwa ni ya dhahabu ni Haramu kwa wanaume.

Ikiwa ni ya fedha ni Sunnah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4713

Page 22: Fataawa Za Wanachuoni (34)

22

32) Du´aa Nzuri Wakati Mwanamke Anataka Kuzaa

Swali:

Dada kutoka Ubelgiji anauliza. Ni Du´aa ipi ambayo mwanamke anaweza

kuomba wakati wa kuzaa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Amuombe Allaah Amuweke wepesi. Na Du´aa iliyojumuisha mengi ni yeye

aseme: "Allaahumma anta Rabbiy, laa ilaaha illa Anta. Khalaqtaniy wa ana

´abduka, wa anna ´alaa ahdika wa wa´adika mastatwa´at. A´udhubika min-

sharri maaswanaytu. Abu-ulaka bi ni´imatika 'alayyah wa abu-u bidhambi,

faghfirliy innahu laa yaghfiruu dhunuuba illa anta."

Chanzo: http://youtu.be/rKDnt34ZKX8

33) Hadiyth Ya Waislamu Kupeana Zawadi Ili Wapendane

Swali:

Hadiyth (ombeaneni Du´aa mtapendana), je makusudio yake ni watu kupeana

zawadi au ni uongofu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ni watu kupeana zawadi. Kumpa ndugu yako Muislamu zawadi, naye

akakurudishia zawadi. Zawadi inasababisha mapenzi, kama kutoleana Salaam

baina ya Waislamu pia yasababisha mapenzi baina yao.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4858

Page 23: Fataawa Za Wanachuoni (34)

23

34) Kuswali Swalah Za Sunanh Kabla Ya Swalah Ya Ijumaa

Swali:

Je inajuzu kwa mtu kuswali kabla ya Swalah ya Ijumaa Nawaafil [Swalah za

Sunnah] kadhaa? Na je ni sahihi kuwa masuala haya yana khilafu kwa

wanachuoni, na ipi kauli yenye nguvu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Kasema hili Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika taaliki yake katika

Subul-us-Salaam na pamoja na maneno ya Swan´aaniy pia katika Subul-us-

Salaam kuwa:

"Hakuna ubaya kwa Muislamu kuswali kabla ya Swalah ya Ijumaa katika

Naafil au Swalah ya Dhwuhaa apendacho."

Na Ijumaa huwa haina Sunnah za kabla, bali Sunnah zake ni baada. Kwa hiyo

anaweza kuswali kabla ya Ijumaa Swalah za Naafil, kadiri na Allaah

Atavyomuwezesha. Hakuna ubaya In Shaa Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4238

35) Mtoto Akipita Mbele Ya Mwenye Kuswali Swalah Yaharibika

Swali:

Mwalimu anaweza kumpiga mwanafunzi kumuogopeshe ili arejee kufanya

jambo fulani au kuacha jambo fulani, je hili pia linangia katika tishio

[dhuluma]?

Page 24: Fataawa Za Wanachuoni (34)

24

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kipigo cha kumuweka [kumtia] adabu mwalimu mnasihiaji mukhlisw kwa

mwanafunzi, kipigo cha kumuweka adabu kidogo halaumiwi kutokana na

maslahi kwake [mwanafunzi] na kumkinga na yatayomdhuru katika uhai

wake na mustaqbal wake. Pia kipigo cha baba kwa mtoto wake, na kwa mleaji

- kama mtu mkubwa kwa mdogo, hali kadhalika mume kwa mke wake katika

baadhi ya hali kama jinsi Allaah Alivyotoa idhini hio. Hichi huitwa kipigo cha

kuweka adabu na kutengeneza. Ataekifanya hana makosa wala haingii katika

kufanya dhuluma. Lakini ikiwa atachupa mipaka katika kupiga, hapo

atachukuliwa amefanya dhuluma. Na ikiwa atapiga bila ya haki hata kama

kitakuwa ni kipigo kidogo, atachukuliwa ni dhalimu na siku ya Qiyaamah

Allaah naye Atamlipiza.

Chanzo: http://youtu.be/ydnNQuD5zVw

36) Mwanamke Mgonjwa Anastanji Na Kujiosha Kwa Maji Ya Zamzam

Swali:

Mwanamke ni mgonjwa, anajiosha kwa maji ya zamzam bafuni na anastanji

nayo. Je hili linajuzu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ikiwa anajitibu kwa hili hakuna ubaya. Kwa kuwa kustanji kunachukuliwa ni

dawa. Hakuna ubaya In Shaa Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4856

Page 25: Fataawa Za Wanachuoni (34)

25

37) Talaka Inatokana Na Alivyokusudia (Nia) Ya Mume

Swali:

Ipi hukumu mume kamwambia mke wake "Nikirudi kwenye ghala mimi si

mumewe tena", kisha akajirudi?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Hili itatokana na nia yake. Je, makusudio yake ni Talaka kwa hili? Hili

itatokana na nia yake. Ikiwa makusudio yake ni Talaka atakuwa kamtaliki. Na

ikiwa hakukusudia Talaka, itakuwa si Talaka. Kasema Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam):

"Vitendo vinategemea (vinalipwa kwa) nia na kila mtu atapata kwa mujibu wa

kile alichokusudia."

(Akimwambia) wewe si mke wangu, wewe si mke wangu mwema, au

nimridhiae. Itatokana na anachokusudia (nia yake).

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4700

38) Dada Anataka Kubadilisha Rangi Ya Nywele Zake Nyeusi

Swali:

Dada anauliza kuhusu kubadilisha rangi ya nywele nyeusi kichwani?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ikiwa nywele za kichwani ni nyeusi hakuhitajiki kuzibadili. Tayari ziko katika

asili yake rangi nyeusi. Haifai kupoteza muda na mali katika mambo

yasiyokuwa na faida. Zinazobadilishwa ni nywele zenye rangi nyeupe (mvi),

kwa kuwa zimebadilika zilikuwa nyeusi. Mtu anabalidisha kwa rangi yoyote

Page 26: Fataawa Za Wanachuoni (34)

26

isipokuwa nyeusi tu. Rangi nyeusi haijuzu mtu kujibadilisha kwayo.

Kutokana na Hadiyth inayokataza hilo.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4698

39) Hukumu Ya Unyevu (Majimaji, Utoko) Umtokao Mwanamke

Swali:

Anauliza kuhusu unyevunyevu (majimaji/utoko) umtokao mwanamke?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Fatwa za wanachuoni zinasema kuwa unatengua Wudhuu. Pia Fatwa ya al-

Lajnah ad-Daa´imah inasema hali kadhalika - Fatwa ya Shaykh Ibn Baaz.

Anatakiwa kustanji na aoshe sehemu ilipopatwa nguo yake na unyevu huo,

kisha atawadhe.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4857

40) Kuna Muda Maalumu Wa Mtu Kufanya Kijicho?

Swali:

Je kuna muda maalumu katika Kitabu na Sunnah ambao hutoka kijicho kwa

wale wenye vijicho?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Page 27: Fataawa Za Wanachuoni (34)

27

Elimu ya jambo hili iko kwa Allaah (´Azza wa Jalla), Allaah Hufanya

Atakacho. Wewe ni juu yako kujitibu nafsi yako kwa kufanya Ruqyah ya

Kishari´ah na Allaah Hufanya Atakacho. Na haya ni kama maradhi mengine

yote. Ujitibu kwa yale Aliyokuruhusu Allaah na lini maradhi yataisha, elimu

ya hili ni kwa Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4710

41) Mwanamke Anatokwa Na Upepo Kwenye Tupu Ya Mbele, Hukumu

Ya Swalah Yake

Swali:

Mwanamke katawadha kisha anatokwa na upepo wakati wa kuswali

anapoenda kwenye Rukuu na Sujuud, akaamua kuswali hali ya kuwa amekaa

ili asitokwe na upepo.

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ikiwa Swalah ni ya faradhi kusimama ni nguzo [yaani lazima]. Na ikiwa ni

Swalah ya Naafilah [Swalah ya Sunnah], akiswali hali ya kuwa amekaa

hakuna ubaya. Na kutokwa na upepo katika tupu ya mwanamke hakutengui

Wudhuu. Kitenguacho Wudhuu ni kutokwa na upepo katika tupu ya nyuma.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4855

42) Baadhi Ya Sifa Zinazopasa Kuwa Na Mke Mtarajiwa

Swali:

Page 28: Fataawa Za Wanachuoni (34)

28

Ipi nasaha zako kwa anayeoa kwa wale wasiyo katika jamii yake ambapo

anaishi, [mwanamke] kutoka magharibi kwa mfano?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ndugu yetu anatakiwa kuoa mwanamke Muislamu, mwema, mtiifu, mwenye

msimamo, atakayekusaidia katika mambo ya Dini yako.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=567

43) Hukumu Ya Kupuuza Swalah Mpaka Ukaondoka Wakati Wake

Swali:

Kuna mtu alisikia adhaana ya Swalah na wala hakwenda kuswali na akaswali

baada ya wakati kuondoka, ipi hukumu?

´Allaamah a-Waswaabiy:

Anasem Allaah (´Azza wa Jalla):

الةااإنا وقوتااكتابااالمؤمنينااعلىاكانتااالص م

“Hakika Swalah kwa Waumini ni faradhi iliyo wekewa nyakati maalumu.”

(04:103)

Kila faradhi ina wakati wake maalumu na mwanzo wake na mwisho wake.

Haijuzu kupuuza swalah, hakika Allaah Anasema:

ساهونااصالتهمااعناهمااالذينااللمصليناافويل ا

“Basi, ole wao wanao swali, Ambao wanapuuza Swalah zao.” (107:04-05)

Kuacha swalah ya jama´ah inachukuliwa ni katika madhambi makubwa,

mwenye kuacha swalah mpaka wakati wake ukaondoka huchukuliwa ni

Page 29: Fataawa Za Wanachuoni (34)

29

dhambi ingine kubwa; Bali huchukuliwa ni ukafiri. Kwa kauli ya Mtume

(´alayhis-Salaam):

"Ahadi iliopo baina yetu sisi na wao ni swalah, ataeiacha basi kakufuru."

Kuiacha yaani mpaka ukaondoka wakati wake naye kakusudia hilo. Ni wajibu

kwake kufanya tawbah na istighfaar, na ahifadhi swalah tano kwa wakati

wake tena pamoja na jama´ah. Na azidishe nawaafiyl [sunnah], nawaafiyl za

´Ibaadah kwa kuwa Allaah Anasema:

ـيئاتاايذهبنااالحسناتااإنا الس

“Hakika mema huondoa maovu.” (11:114)

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1910

44) Hukumu Ya Kubusu Msahafu Na Kuuweka Chini

Swali:

Ipi hukumu ya kuubusu msahafu na kuuweka mahala katika ardhi ambapo ni

pasafi?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Kubusu msahafu kama ilivyo katika Fatwa ya al-Lajnah ad-Daa´imah ni

kwamba ni jambo halina dalili. Na kuuweka katika ardhi ikiwa ni safi hakuna

ubaya, ila bora zaidi uwe juu ya kitu kama kiti n.k.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1979

45) Hukumu Ya Kula Daku Baada Ya Adhaana Ya Pili Ya Fajr

Page 30: Fataawa Za Wanachuoni (34)

30

Swali:

Kuna mtu kaamka kula daku katika Ramadhaan, akala na kunywa akidhani

kuwa adhaana ya pili haijafika wakati wake, na ghafla wanakimu Swalah. Ipi

hukumu ya Swalah yake?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa anachukuliwa kala siku hii. Afanye Istighfaar kwa Allaah (´Azza

wa Jalla) na ajizuie siku nzima iliobaki na juu yake ana deni [kulipa siku hii].

Ilikuwa juu yake kuharakisha wakati [wa daku].

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1909

46) Hukumu Ya Kupuuza Swalah Mpaka Ukaondoka Wakati Wake

Swali:

Mtu kasalisha watu Tarawiyh na baada ya kuwasalisha anataka kusimama

usiku kuswali, afanye nini?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Kwa kuwa aliwaongoza katika Tarawiyh, akisimama baada ya hapo [usiku]

na akaswali Rakaa mbili mbili [hakuna neno], asiswali tena Witr kwa kuwa

kishaiswali. Na katika Hadiyth:

"Hakuna [kuswali] Witr mbili katika usiku mmoja."

Aswali Rakaa mbili mbili. Pia imethibiti kutoka kwa Mtume (´alayhis-Salaam)

aliswali Witr na akaswali baada ya hapo Rakaa mbili kama ilivyo katika

Swahiyh Muslim. Ni dalili ya kuonesha katika kauli yake:

"Ifanyeni Swalah yenu ya mwisho usiku iwe Witr."

Page 31: Fataawa Za Wanachuoni (34)

31

Imependekezwa na si wajibu.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1911

47) Hukumu Ya Mume Kamwambia Mke Wake Wewe Ni Kama

Mamangu

Swali:

Kuna mtu kamwambia mke wake "Wewe kwangu ni kama mama yangu au

binti yangu". Je, hii huchukuliwa ni talaka au Dhwihaar?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa hii ni Dhwihaar. Anawajibika kutoa kafara ya Dhwihaar, sawa

kama alisema "wewe ni kama mama yangu", au "kama binti yangu" au

mwanamke yeyote katika Mahaarim (asiyeweza kuwaoa). Na kafara ya

Dhwihaar ni kuacha mtumwa huru kabla ya kumgusa, yaani kabla ya

kumjamii (kumuingilia). Ambaye hakupata (hawezi) afunge miezi miwili

mfululizo kabla ya kumgusa; na ambaye hawezi alishe masikini sitini, pia

kabla ya kumgusa.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1973

48) Imefika Ramadhaan Na Ana Deni La Ramahaan Ingine

Swali:

Mtu ana deni la Ramadhaan, ikaingia Ramadhaan ingine na hakulipa. Afanye

nini?

Page 32: Fataawa Za Wanachuoni (34)

32

´Allaamah al-Waswaabiy:

Atafunga Ramadhaan iliyohudhuria na baada ya Ramadhaan atalipa

Ramadhaan ya kwanza pamoja na kulipa kafara ya kulisha masikini mmoja

kwa kila siku moja ikiwa alichelewesha bila ya udhuru. Ama ikiwa

alichelewesha kwa udhuru, atalipa [atafunga] tu [bila ya kulipa kafara].

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1912

49) Inafaa Kwa Kwenye Kukaa Eda Kuangalia Jua, Mwezi, Nyota,

Mbingu, Kupika, Ndugu Zake?

Swali:

Je inajuzu kwa mwanamke aliyekufa mume katika hali ya eda yake kuangalia

mwezi na kujidhihirisha kwa Mahaarim na ndugu zake?

´Allaama al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa inajuzu kwake kuangalia mwezi nae yuko katika eda, pia

kuangalia jua, nyota, mbingu, ardhi, moto. Inajuzu kwake kupika chakula kwa

moto, inajuzu kwake kufanya usafi nyumbani, inajuzu kwake kuvaa nguo

zake nzuri [asitoke nazo nyumbani]. Huu ni uzushi na yanayosemwa na

wajinga wasiojua kitu. Ama kuhusu kumuangalia Mahram wake na ndugu

inajuzu, na ambaye ni ndugu lakini si Mahram usimuangalie.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1981

50) Je Mkaaji Eda Haruhusiwi Kutoka Nyumbani Kabisa?

Swali:

Page 33: Fataawa Za Wanachuoni (34)

33

Je kwa mwenye kukaa eda kwa kufa mume wake anaweza kutoka nje ya

nyumba na mmoja katika jamaa zake?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Hakuna neno kukitokea haja [dharurah], kama kumzuru jirani yako, au katika

jamaa zako. Ila hutakiwi kubaki isipokuwa katika nyumba ya mume wako.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=570

51) Je Salaf Waliwahi Kutofautiana Katika ´Aqiydah?

Swali:

Wanasema baadhi ya watu kwamba Salaf walitofautiana katika baadhi ya

masuala ya ´Aqiydah, kwa mfano "je alimuona Mtume wa Allaah ( اعليهاللااصلى

Mola Wake Usiku wa Mi´iraaj?", na kuwa hili lilitokea zama za (وسلم

Maswahabah. Je, maneno haya ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hawakutofautiana katika masuala ya ´Aqiydah ewe ndugu. Masuala ya

´Aqiydah ni kuonekana Allaah Peponi. Ni kwamba waumini watamuona

Peponi. Ama duniani hakuna yeyote atayemuona. Hakuna yeyote

atayemuona, hata Mtume ( وسلماعليهاللااصلى ) hakumuona, wala hakumuona

Muusa (´alayhis-Salaam). Alisema:

ترانيالناقالااإليكااأنظرااأرنياربااقالا

"Nionyeshe nikutazame." Allaah Akasema: "Hutoniona." (07:143)

Hili ni hapa duniani. Hawana tofauti katika ´Aqiydah. Hii ni ikhtilafu je

alimuona yeyote duniani au haikutokea. Hii sio ikhtilafu katika ´Aqiydah.

Kuonekana Allaah Peponi hili wamekubaliana wote Ahl-us-Sunnah wal-

Jamaa´ah wala hawatofautiani.

Page 34: Fataawa Za Wanachuoni (34)

34

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2750

52) Kajiapiza Kutofanya Kitu Fulani Kisha Akamtaliki Mke Wake

Swali:

Kuna mtu alijiharamishia na akataliki, na akaapa kuwa hatofanya kitu fulani;

kisha akafanya kitu hicho, analazimika kufanya nini?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Itarejea katika nia yake. Ikiwa nia yake [makusudio yake] ilikuwa ni Talaka,

itachukuliwa kuwa kamtaliki Talaka ya kwanza. Na ikiwa alikuwa hakusudii

Talaka bali ni yamini, hivyo atalipa kafara ya yamini ambayo

tumekwishaitaja.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1971

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.